Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Abdullah Ali Mwinyi (17 total)

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa zawadi hii. Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu, Muumba wa Mbingu na Ardhi kwa kutujalia uhai, afya na ustawi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa hii ni mara yangu ya kwanza toka tulivyoingia Bungeni kuongea ndani ya Bunge hili Tukufu, napenda vilevile kuwashukuru wannachi wa Jimbo la Mahonda pamoja na chama changu cha CCM kwa kunipa ridhaa na kuniingiza hapa mjengoni niwe mwakilishi wao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, napenda kumshukuru Mheshimiwa Rais, Mwenyekiti wetu wa Taifa, kwa uamuzi, ujasiri na umahiri wake mkubwa katika kuongoza nchi hii kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita. Sina haja ya kuyazungumza yote aliyoyafanya, walionitangulia, Mheshimiwa Askofu Gwajima na Mheshimiwa Polepole wameyasema yote ya msingi kabisa ambayo yamefanyika katika hii miaka mitano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijikite katika maeneo matatu. Eneo la kwanza huu Mpango umekamilika na umefanyika kwa kiwango cha hali ya juu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda tu kugusia maeneo ambayo nahisi hayajawekewa mkazo mkubwa ambayo ni haya matatu. La kwanza, mchango wa diaspora katika uchumi wetu; la pili, dhana ya Tanzania kuwa logistics na transit hub; na la tatu, ushiriki wa Watanzania kwenye uwekezaji wa rasilimali zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, diaspora ina mchango mkubwa sana katika chumi za nchi. Kuna study ambayo nimeitazama ya mwaka 2018, katika nchi nne; Nigeria, Kenya, Uganda na sisi Tanzania. Mwaka 2018, fedha zinazotoka kwenye diaspora kuingia Nigeria, zilikuwa Dola bilioni 23.6 sawa na asilimia 6.1 ya GDP ya Nigeria. Kwa ule mwaka diaspora ili-contribute fedha nyingi kushinda export ya mafuta. Nigeria ndiyo nchi ya nne ulimwenguni kwa ku-export mafuta. Hata hivyo, Wanaijeria waliokuwa nje wameleta fedha zaidi ya mara mbili ya export yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kenya mwaka 2018, contribution ya diaspora ni Dola bilioni 2.72 sawa na 3% ya GDP yao. Uganda mwaka 2018 imeingiza Dola bilioni 1.24 sawa na asilimia 4.5 ya GDP ya Uganda. Mwaka huo huo Tanzania tumeingiza Dola milioni 430, sawa na 0.8% ya GDP yetu. Bayana kabisa, sisi kama Tanzania hatujalea hii sekta muhimu ambayo inaweza kuwa mchango mkubwa sana katika maendeleo yetu na katika Mpango wetu wa Miaka Mitano. Hii sekta ni lazima ilelewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna haki fulani fulani ambazo zinakuwa vichochezi. Kwa mfano, Mkenya mwenye passport ya nchi nyingine hadhibitiwi kununua ardhi. Halikadhalika na Uganda, lakini Tanzania huwezi. Sasa naiomba Serikali iyatazame haya, tuweze kuwapa hawa incentives ili sekta hii, hawa watu, Watanzania wameamua kuishi nje, washiriki na watusaidie katika mchango wa uchumi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, tumejenga miundombinu mikubwa sana katika sekta ya transport; SGR, barabara nyingi, tumeboresha bandari na nyingine tunaziongeza; dhamira yetu siyo tu kuiendesha Tanzania bali kusaidia nchi zilizokuwa jirani. Tanzania inapakana na nchi tisa. Mbili tu kati ya hizo tisa zina access ya bahari ya hindi. Mbili tu; Kenya na Msumbiji. Saba hazina; na zote hizo saba, kuna advantage kubwa sana kwa wao kupitisha mizigo yao kwetu. Uganda, Rwanda, Burundi, Congo, Malawi, Zambia, wote wana advantage kubwa na ndiyo distance fupi, hupiti katika nchi nyingine. Ikitoka baharini inapita Tanzania, inaingia kwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, advantages zote strategically tunazo. Kwa nini hawazitumii? Mambo magumu yote Serikali ya Awamu ya Tano imeyafanya. Upungufu wetu ni katika yale mambo mepesi (soft skills). Yapi hayo? Customer service; urasimu. Civil service kwa kijeshijeshi badala ya kuwa kirafiki na kibiashara. Haya mambo mepesi lakini thamani yake ni kubwa mno. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwashauri Mawaziri wa sekta, hilo jambo walitazame kwa macho makini ili tukuze uchumi na mpango wetu utimie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, ni ushiriki wa Watanzania kwenye uwekezaji. Serikali hii kwa nia njema kabisa inataka Watanzania tumiliki rasilimali zetu zilizokuwa kubwa. Sheria zilizopitishwa kwenye Extractive Industry; madini, oil and gas, sasa Tanzania ina hisa asilimia 16 katika kila investment kubwa ya namna hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna vitu vinaitwa mutual farms au collective investment schemes. Hii ni mifuko tu; maneno makubwa tu haya ya Kiingereza, lakini ni mifuko ya kuwachangisha sekta binafsi washiriki kwenye miradi ya mkakati. Kunakuwa na mfuko maalum, mnasema pengine Kabanga Nickel, mahesabu yake haya; Kabanga Nickel tunajua ina idadi gani? Faida yake ni hii. Nyie mnaotaka kuchangia na mkawa na hisa, karibuni. Hiyo ndiyo njia sahihi ya kuongeza ownership.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa badala ya 16 tu ile ya Serikali peke yake, Watanzania sisi katika sekta binafsi, pamoja na wale wa diaspora walioko nje, wanaweza waka-invest tuka-own zaidi na ile fedha ya faida ikawa repatriated kwenda nje ikabaki hapa hapa.

MWENYEKITI: Ahsante sana.

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. ningependa kuanza mchango wangu kwa kutoa salamu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, hivi karibuni tumepoteza Rais wetu, amefariki Rais wetu wakati yeye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Jambo hili halina rejea ndani ya nchi yetu katika historia ya nchi yetu na si jambo jepesi kwa Rais kufariki katika nchi changa kama hii ambayo wapinzani wetu wanasema hatuna mfumo wa utawala bora, lakini amefariki Rais.

Ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa Serikali pamoja na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kwa kuhakikisha Katiba na mfumo mzima wa utawala bora unasimamiwa na hali yetu mpaka Rais wetu mwingine aliyekuja akashika wadhifa bila matatizo yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nchi nyingi wamepata changamoto kama hizi na ikasababisha machafuko. Hili si bure, haya ni ukomavu wetu wa Serikali yetu chini ya Chama chetu Cha Mapinduzi ambayo imewezesha utaratibu na kuonesha dunia nzima kwamba, sisi ni wakomavu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimeupitia mpango pamoja na kusikiliza hotuba za hivi karibuni za Mheshimiwa Rais. Na mambo ya msingi ambayo ningependa kuyachangia ni matatu, la kwanza ukimsikiliza Mheshimiwa Rais vipaumbele vyake ni vitatu cha kwanza ni kurekebisha mfumo wa biashara. La pili ni kuimarisha zaidi mahusiano kikanda na ya kimataifa na cha tatu ni kuhakikisha miradi yetu ya mkakati inakamilika. Hayo mambo mawili ya mwanzo yakifanyika vizuri ndio yatahakikisha hili jambo la tatu, miradi ya mkakati, itakamilika kwa salama na amani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa kwasababu muda si rafiki mimi ningependa kugusia suala la kwanza kuboresha mfumo wa biashara. Ukiungalia mpango mzima na section kubwa ya kuhusu business environment utaambiwa tumepitia kitu kinaitwa blue print; kila uki-question jamani tumefika wapi, tunafanya nini, blue print implementation imefika wapi?

Mheshimiwa Spika, utaambiwa ikikamilika mambo yote hayo unayoya-raise yatakuwa sawa. Sasa wenzangu humu ndani ya Bunge walilizungumzia suala la monitoring na evaluation. Ili tuweze kurekebisha yale matatizo tuliyokuwanayo lazima tuwe na taasisi rasmi ama hapa Bungeni chini ya kamati moja au Serikalini na sehemu bora zaidi ni chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwasababu, yeye ndio kiongozi wetu katika shughuli za kila siku za Serikali. Lazima tuwe na taasisi ambayo inahakikisha quarterly tunafanya monitoring na evaluation kwa yale ambayo tumeyapanga. Bila kuboresha mfumo mzima wa kibiashara revenue hazitakuja zile ambazo tunategemea, biashara haitakua, uwekezaji hautaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa sehemu hii ni sehemu ambayo ni nyeti sana ambayo ningependa kuunga hoja za miongoni mwa wenzetu ambao wamezungumzia kwamba, ama tufanye sehemu mbili Bunge liwe lina-monitor pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu kuhakikisha kwamba, yale ya
kimkakati, reforms tangible kwasababu, kuna projects ambazo unaona kama kitu kimejengwa hakijajengwa, lakini kuna mfumo wenyewe inabidi ubadilishwe uwe rafiki zaidi kwa ajili ya kukaribisha uwekezaji. Kwa hayo machache ningependa kushukuru kwa fursa hii na napenda kuunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia hidaya hii nami kusema maneno machache, cha msingi ningependa kuzungumza kuhusu mambo mawili; mchango wangu hautakuwa specific, mchango wangu ningependa uwe general. Na mambo makuu mawili ningependa kuyazungumza la kwanza ni amani, la pili ni utawala bora. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, amani hii ambayo tunajivunia sisi na kuna baadhi ya wenzetu ambao wanatuhusudu na amani yetu haikuja kwa bahati mbaya, imelelewa, ikatunzwa na hatimaye ikastawi mpaka hapa hii leo tukawa tunajivunia. Mwanzilishi wetu Baba wa Taifa aliitunza na kuilea hii amani kwa msingi mmoja mkuu msingi huo ni msingi wa utaifa. Baba wa Taifa kwa kipindi kikubwa sana cha awamu yake ya kwanza, nguvu nyingi sana za kifikra, za kifedha, aliziwekeza katika kujenga utaifa (national unit and cohesion) na alijenga hivyo kwa kufanya yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kuhakikisha Serikali Kuu; pili, Serikali za Mitaa na tatu, Taasisi na Asasi za Kiserikali zina sura ya kiutaifa. Hili jambo kwa kweli hatuwezi kulichukulia wepesi wa aina yoyote, ni zito mno, tukilega hapo hii amani ambayo tunajivunia inaweza ikapeperuka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Askofu Bagonza anasema; amani ni tunda la haki, na haki hii aliyoitenda Baba wa Taifa kuhakikisha kwamba taasisi zote, Serikali yenyewe ipo na sura ya kiutaifa ndio zao lake hii amani. (Makofi)

Mheshimiwa Waziri naomba nikukumbushe hili somo la kihistoria na sina shaka yoyote utalichukua kwa umakini na katika uboreshaji wenu wa taasisi zote za ndani mtazingatia sura ya kitaifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nina maana gani sura ya Kitaifa? Mheshimiwa baba wa Taifa alichukia ukabila, alichukia udini na alihakikisha taasisi za Kimuungano zina sura ya Kimuungano (national cohesion). Hili ni jambo la msingi sana hili amani idumu na itamalaki kama hivi leo.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili ningependa kuzungumzia suala la utawala bora. Tumejichagulia sisi kama nchi kuendesha nchi yetu kwa misingi ya kidemokrasia, Serikali ya watu, kwa ajili yao na inayowatumikia wao (Government of the people, by the people, for the people) huu ndio mfumo wetu. Sisi tulibahatika kuwa viongozi tunadhamana hii ya muda mfupi tu na tupo hapa kwa ajili yao, tumejiwekea misingi ya utawala bora pasiwe na uonevu wa aina yoyote, tuwe tunalinda hii misingi iwalinde watu, hii misingi ilinde mali zao na misingi hii ilinde utu wao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mantiki hiyo basi ningependa kuona sheria ambazo zimetoka nje ya mlolongo huu, nje ya mfumo wa utawala bora ziletwe na tuzirekebishe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wale...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, imefika dakika saba?

NAIBU SPIKA: Tayari ahsante sana.

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Napenda kuanza mchango wangu kwa kutoa shukrani na kwa kuwapongeza sana Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kwa kazi nzuri na kwa uwasilishaji mzuri wa report hii ndani ya Bunge hili.

Mheshimiwa Spika, pili, ningependa vilevile kumpongeza Mheshimiwa Mhagama kwa uwasilishaji wake wa Report ya Kamati. Ameweka mambo vizuri kabisa, sina shaka yoyote kwamba, kuna mambo mengine makubwa zaidi yanakuja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Soud amenifilisi kidogo katika mchango wake sasa mimi nitajikita katika jambo moja, moja ameshalizungumza kwa kina na nisingependa kulirudia na yeye amekuwa mahiri zaidi katika sekta yake hiyo ya masuala ya mazingira.

Mheshimiwa Spika, ningependa kujikita katika masuala ya yale mambo ambayo tunaita kero za muungano. Kero za Muungano imekuwa jambo la msingi kabisa ambalo hata Mheshimiwa Rais amelizungumzia mara mbili, tatu na kukabidhi kwa Mheshimiwa Makamu wa Rais, masuala ambayo bado hayajafanyiwa kazi yafanyiwe kazi kwa kipaumbele. Hata hivyo, ningependa kuzungumzia jambo moja ambalo lilishatafutiwa ufumbuzi, suala la mafuta na gesi, extractive industry.

Mheshimiwa Spika, mnapo mwaka 2014 mpaka 2015 suala hili lilikuwa moto sana na tukatolea maamuzi kwamba, suala la mafuta na gesi lisiwe suala la Muungano, kila upande ujitegemee. Jambo hili ni jema katika uendelezaji wa tasnia hii na hivi karibuni kwa bahati mbaya Ndugu zetu wa Msumbiji Total imejitoa, imetangaza juzi wamejitoa kuwekeza Msumbiji kwenye project ya LNG. Bahati mbaya kwa Ndugu zetu kwa sababu ule mradi ulikuwa mkubwa ndio unasemekana ndio ulikuwa mradi mkubwa kabisa ambao ungeweza kutokea katika Sub Saharan Africa katika miaka yote iliyopita, lakini kwa sababu ya matatizo ya machafuko na ugaidi wameamua kujitoa na investment hiyo haitaendelea.

Mheshimiwa Spika, sasa msiba wa wenzetu ni faraja kwetu, lakini kuna changamoto moja ambayo lazima tuitazame. Ukiangalia yale makubaliano yetu ya ndani tuliyokubaliana kwamba, tasnia hii sio sekta ya Muungano na taasisi na sheria na asasi zikaundwa, huku upande wa bara zipo TPDC, PURA na mengineyo na Zanzibar zikafanywa hivyohivyo na sheria ikaundwa na kuna watu ambao tayari wameshaingia katika kufanya utafiti, lakini kuna changamoto moja.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia Katiba yetu ukurasa wa 128 inazungumza, Mambo ya Muungano, jambo la 15. Naomba ninukuu kwa ruhusa yako, inasema ifuatavyo; “15. Maliasili ya mafuta pamoja na mafuta yasiyochujwa na ya motokaa na mafuta ya aina ya petroli na aina nyinginezo za mafuta au bidhaa na gesi asilia.”

Mheshimiwa Spika, hiyo ni mojawapo ya vitu ambavyo vipo katika orodha ya muungano, Kikatiba, japokuwa sisi wenyewe tumekubaliana kwamba kila upande unajitegemea. Sasa suala la mafuta na gesi ni suala linalohusisha fedha nyingi sana, Mabilioni ya dola yanawekwa pale ili kuyatoa hayo mafuta na gesi.

Mheshimiwa Spika, japo kuwa sisi wenyewe tumekubaliana kwamba kila upande unajitegemea, sasa suala la mafuta ya gesi ni suala linalohusisha fedha nyingi sana, Mabilioni ya dola yanawekwa pale ili kuyatoa hayo mafuta na gesi.

Mheshmiwa Spika, jambo la kwanza mwekezaji yeyote atakayefanya kama ataweka mabilioni yake anafanya legislative review anatazama Sheria, Katiba na Mikataba yote kuangalia anawezaje kufanya hivyo. Na mtu mwekezaji wa Kimataifa ambaye anataka kuweka mabilioni hata fanya hivyo kama kuna kuwa kuna tatizo kama hili. Kwasababu ukiangalia kikatiba suala hili bado ni la Muungano. Sheria zipo zinazosema kwamba inaruhusu upande wa pili na makubaliano ya Kiserikali mambo ya pili yaendelee.

Mheshimiwa Spika, sasa kuna mgongano hapo bila huu mgongano kuurejebisha hakuna mwekezaji wa fedha nyingi atakayeweza kuweka fedha upande wa pili wa Muungano wa Zanzibar. Huku ipo bayana upande wa pili itashindikana, ningependa tu kumuomba Mheshimiwa Waziri alitazame hili hasa katika kipindi hiki ambacho fursa hii itakuwa moto, alitazame ajue jinsi gani tutalifanyia ufumbuzi suala hili kwa haraka iwezekanavyo ili uwekezaji mkubwa ule ambao tunautaka uweze kufanyika upande wa pili wa Muungano. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hayo machache ningependa tu kumshukuru tena Mheshimiwa Waziri kwa uwasilishaji mzuri na ningependa atoe maelezo katika hili ambalo nimeliweka hapa hadharani, ahsante sana. (Makofi)
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Awali ya yote nami napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri na wataalam wote wa Wizara ya Fedha kwa kutupatia na kufanya kazi kubwa sana ili kuikamilisha hii bajeti ambayo tunaijadili kipindi hiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile muda siyo rafiki napenda kuingia moja kwa moja katika mchango wangu. Napenda kuzungumzia mambo mawili; la kwanza ni uchumi kwa ujumla wake na la pili suala la ubunifu na ajira, kwa sababu sehemu nyingi wenzangu ambao wamenitangulia wamezigusia na kwa kweli sina haja ya kuyarudia.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na janga kubwa la Uviko 19 lililokabidili dunia nzima Tanzania imebahatika; na siyo bahati, kwa mkakati na kwa mpango mzuri tumejaaliwa uchumi wetu kukua kwa asilimia 4.8.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia nchi ambazo zinatuzunguka Kusini mwa Jangwa la Sahara nchi zote kwa wastani chumi zao zimepungua, zimekuwa hasi, zimepungua kwa asilimia 1.9. Na kwa ulimwengu kwa ujumla wake chumi zimepungua kwa asilimia 3.3.

Mheshimiwa Naibu Spika, hakika kabisa, na iko bayana kabisa, kuna jambo ambalo sisi tumeweza kulifanya vizuri katika Janga hili la UVIKO-19 na ikatuwezesha uchumi wetu kukua kulinganisha na chumi nyingine zote za ulimwenguni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nimechukua fursa ya kutazama makampuni yetu makubwa yameendeleaje katika kipindi hiki. Nimechagua kampuni zifuatazo; TBL, TCC, Vodacom, Tigo na Puma Energy, kwa makusudi kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiziangalia hizo kampuni, ndizo kampuni ambazo zinatupa kodi kwa wingi; TBL, TCC, Vodacom na Tigo pamoja na Puma. Kuangalia taswira ya kibiashara inakwendaje. Ukiangalia kampuni zote hizo tano, hasa hizo nne za mwanzo, zote mapato yao yamepungua kwa kipindi cha miaka miwili mpaka mitatu sasa na kipindi cha mwaka uliopita mapato (revenue) yamepungua.

Mheshimiwa Naibu Spika, Vodacom quarter ya mwisho imepata hasara. Sasa ukiangalia huu uchumi umekuwa katika sekta gani, wakati ukiangalia makampuni haya makubwa mengi yameathirika. Sekta zilizotuwesha uchumi wetu sisi kukua ni ujenzi, madini, mawasiliano, uchukuzi, kilimo na viwanda. Ujenzi asilimia 13, madini asilimia tisa; hayo ndiyo maeneo ambayo yamekuza uchumi wetu. Eneo la hospitality; mahoteli, migahawa na utalii, yamepungua kwa asilimia karibu 14. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ukiipitia ripoti ya BoT ya Desemba, 2020, inaonesha bayana kwamba eneo kubwa la ukuzi wa uchumi ni ujenzi, asilimia 42.6 na kilimo, asilimia 24.6. Theluthi mbili ya uchumi wetu umeshikwa katika hayo maeneo mawili.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nimetoa haya kama muhtasari. Ili kuitathmini bajeti lazima tuelewe uchumi wetu uko wapi na unakwendaje na bajeti yetu iendane na hali halisi ya huu uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, asilimia 42.6 katika ujenzi imekuwa kwa sababu ya ile miradi ya kimkakati. Fedha nyingi zimepelekwa kwenye SGR, fedha nyingi zimepelekwa kwenye Bwawa la Mwalimu Nyerere, fedha nyingi zitapelekwa kwenye bomba la mafuta la kutoka Uganda. Kwa takribani miaka mitano mpaka kumi sekta hiyo itaendelea kukua.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pato kubwa, asilimia 24.6, katika kilimo ndiyo imetoka hapo. Lakini ukiiangalia bajeti inachangia chini ya asilimia moja. Chini ya asilimia moja inakwenda sehemu ambayo inatupa robo ya pato letu la nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wangu kwa Waziri wa Fedha ni kwamba bajeti zijazo lazima tuongeze uwekezaji katika sekta hii ili izidi kustawi na izidi kutupa tija. Kama chini ya asilimia moja inatupa robo basi tukiweka asilimia kumi, kama Maputo Protocol, hakika uchumi wetu na bajeti yetu na mapato yetu yatakuwa makubwa zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ni kuhusu ubunifu na ajira nilisema ninataka kugusia. Tatizo la ajira Tanzania ni kubwa. Asilimia 70 ya Watanzania wana umri chini ya miaka 35. Tulisikilize vizuri; asilimia 70 wana umri wa chini ya miaka 35. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, humu ndani sisi Wabunge kwa demography hiyo hatuwawakilishi wananchi wetu, sisi ni wazee wote kwa takwimu na kwa mfano wa hiyo demography. Maana yake wachache sana hapa wako chini ya miaka 35, lakini asilimia 70 ndio hao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hiyo inaonekana dhahiri kwamba ajira itakuwa changamoto na itakuwa agenda yetu kubwa sana. Tunafanyaje kukabili tatizo la ajira? Maeneo ni haya mawili; la kwanza, kwa Tanzania ni kilimo, la pili ni ubunifu ambao upo kwenye teknolojia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hapo sasa ndiyo ninataka nipagusie zaidi. Mwaka 2005 wanafunzi wa Nairobi University, Kitivo cha Computer Science walibuni solution ambayo hii leo ni mobile money; mwaka 2005. Ukiangalia uchumi, siyo tu wa Tanzania, wa Afrika Mashariki yote, umetokana kwa sehemu kubwa na mchango huo. Ukiangalia sasa hivi katika mawasiliano mobile money inachangia fedha nyingi sana katika kodi zetu, Afrika Mashariki yote na Tanzania yenyewe. Hilo limetokana na ubunifu wa wanafunzi vijana. Na haikuwa bahati mbaya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kipindi hichi TCRA ilikuwa inaongozwa na Profesa Mkoma na BoT Gavana alikuwa Prof. Ndulu. Hawa maprofesa wawili walikuwa na imani ya kukuza vipaji na ubunifu kabla ya kuongeza mfumo wa kupata fedha Kiserikali. Waliuacha huu ukastawi halafu ndiyo wakawekea mfumo wa regulation. Haikuwa bahati mbaya, imefanywa kwa makusudi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu kwa Mheshimiwa Waziri wa Fedha katika sekta hiyo ni kwamba lazima turuhusu ubunifu ustawi na tuulee. Tusifanye kama yule bata anayezaa yai la dhahabu kila siku tukamkaba yule mpaka lile yai asilizae. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sekta hiyo – kama angalizo – kwa Tanzania ukilinganisha na wenzetu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ndiyo sekta ambayo ina kodi kubwa. Ukilinganisha na Uganda, kodi yake ni ndogo, ukilinganisha na Kenya, kodi yake ni ndogo, Tanzania kodi yake ni kubwa. Na kwa safari hii tunaelewa kwa nini imebidi kuiongeza, lakini hilo ni angalizo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sekta ya ubunifu lazima ilelewe istawi ndiyo tuweze kupata tija. Sasa eneo kubwa ambalo sisi tunategemea kuwapa ajira vijana wetu ni maeneo mawili kwa bahati mbaya bajeti hii haiyapi support ya hali ya juu; kilimo na sekta ya ubunifu. Sekta zote hizo zipo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Kama tutaiwekea kipaumbele na tutafanya mazingira ya ustawi ili ikue itupe tija zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hakika kwa hayo machache, ninapenda kuunga mkono hoja na ahsante sana.
Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana nami kupata fursa hii na kuchangia katika hoja hii ya Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika
(Agreement Establishing the African Continental Free Trade Area).

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hakika siku ya leo ni siku ya kihistoria ambayo, kama dada yangu Mheshimiwa Pindi Chana alivyosema, ni siku ambayo ndiyo chanzo cha ndoto za Baba wa Taifa mwanzilishi wetu kufika sehemu ya kuwa na Afrika moja. Siku zote nchi kuungana zinatakiwa ziwe na chachu na chachu kuu ya muunganiko ulimwengu mzima ni biashara na uchumi. Kuanza kufanya biashara kwa pamoja mkawa na soko moja ndiyo chachu kuu ya kuunganisha nchi au mabara kote ulimwenguni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndoto ya Baba wa Taifa ilikuwa Afrika iwe moja, na ndoto yakeni tofauti na Kwame Nkrumah, fikra zake ilikuwa Afrika iwe moja kwa kupitia building blocks. Kwame Nkrumah yeye alisema tuwe wamoja kuanzia siku ya kwanza, kama Muammar Gaddafi alivyokuwa anafikiria.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Baba wa Taifa alisema through building blocks ya Afrika Mashariki, ya SADC, COMESA na Building blocks nyingine. Na huu mkataba chanzo chake ndiyo hivyo, mazungumzo ya mkataba huu yalikuwa mazungumzo ya viongozi wa Secretary General wa East African Community, kipindi kile alikuwa Balozi Mwapachu, SADC na ECOWAS ndio chanzo, inakwenda sambamba na ile ndoto ya Baba wa Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa wasiwasi mwingi mkumbwa niliousikia leo ni kama Tanzania tupo tayari au la; na kama tumejipanga na kama tuna kasoro zozote. Kasoro hazikosekani kila nchi ina mapungufu yake. Lakini Tanzania na mfumo huu wa soko tayari sisi tumeshajifunza na tupo daraja la juu kabisa kulinganisha na nchi nyingi hizi za ndani ya Afrika, tofauti na tunavyojifikiria. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Jumuiya ya Afrika Mashariki ni jumuiya ya mambo mazito kabisa. Kwanza, Umoja wa Forodha, pili, Soko Huria ndani ya nchi hizi tano, tatu, Umoja wa Kifedha. Kwa sehemu kubwa Umoja wa Forodha tayari umeshakamilika, na kwa kipindi ambacho sisi tupo toka mwaka 1999 mpaka leo; wakati tunaanza hofu kubwa ya Tanzania ilikuwa kuwa soko la Kenya kwa sababu kulikuwa kuna dhana ya kwamba Kenya ina uchumi mkubwa, ambao ni sahihi, na sisi kwa sababu uchumi wetu ni mdogo tutakuwa tu na watu wengi, tutakuwa tu soko la Kenya; lakini ukweli uliothabitika ni tofauti na hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kipindi cha zaidi ya miaka sita mpaka saba leo Tanzania ina positive balance of trade. Maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba inauza zaidi katika masoko ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kushinda tunachokinunua. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naona kuna kimya hivi kana kwamba hamuamini, angalieni takwimu. Tanzania inauza bidhaa yenye thamani kubwa Kenya kushinda inachonunua kutoka Kenya kuja Tanzania kwa zaidi ya miaka sita. Hali kadhalika Tanzania tunauza vitu vingi Uganda kushinda tunachonunua. The same Rwanda, na Burundi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ki ukweli kama Mheshimiwa hapa mmoja aliyezungumza hatuna tatizo lolote na wajasiliamali na wafanyabiashara wetu. Tatizo muda hadi muda tunawafunga minyororo wanashindwa kufanya kazi vizuri zaidi, lakini juu ya hivyo tuna mifano ya kampuni za kitanzania ambao wanafanya biashara nchi zaidi ya kumi na mbili na nyingine kumi na nane na zina-compete vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitakupa mfano; Azam ipo ndani ya Afrika inafanya biashara nchi 15, MeTL nchi 18, export trading nchi 12, MM Steel Intergrated nchi 13, wamekwenda huko wanaendesha viwanda vikubwa na wanaweza ku-compete. Sasa huu umoja umuhimu wake ni soko, soko ni watu. Ukiangalia nchi ambazo zimeendelea kwa haraka sana kama vile China, India, Brazil, Marekani, nchi zote hizi zina kitu kimoja, zina watu wengi. Jumuiya Afrika Mashariki ina watu zaidi ya milioni 200, hili eneo lote hili litakuwa na watu zaidi ya bilioni moja, hii ni fursa adhimu sana kwa Tanzania kujipambanua na kuuza nje ya soko. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nini tunachokiuza kikubwa Kenya na ndani ya Jumuiya Afrika Mashariki ni mazao, Tanzania inalisha Afrika Mashariki katika kuzalisha, na tunalisha mpunga, vitunguu, machungwa na mananasi. Kimsingi tunaweza ku-compete.

Mheshimiwa Naibu Spika, wiki iliyopita, nikimalizia, nilikuwa naangalia You Tube kupitia Internet kuangalia katika sekta ya muziki, kwa sababu nimekaa na kaka yangu hapa naona niigusie, sekta ya muziki. Nikaangalia katika You Tube, ni miziki gani inasikilizwa Nairobi kwenye ile top ten ya You Tube. Katika top ten wana muziki saba wa Tanzania wakiongozwa na Diamond Platinums.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini nazungumzia hilo, vijana wetu hawana hofu ya kupambana wakati sisi tunafunguka Music Industry Nairobi ilikuwa imefika daraja kubwa kushinda sisi, lakini wale vijana hawakuwa na hofu. Leo hii Afrika Mashariki yote vijana wetu wana dominate. Hii ni message positive kwamba Tanzania mapungufu tunayo, tunajua matatizo yetu yapo wapi, lakini tunauwezo mkubwa sana wa kupambana na kushindana na kupata manufaa makubwa katika hili eneo huria la biashara. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana.

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Natoa shukrani zangu za dhati kwa kunipatia wasaa kuchangia huu Mpango kwa dakika chache ambazo tunazo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uhai na uzima na kuwepo leo hii. Pili, kuwashukuru Kamati kwa uchambuzi wao mzuri na kuainisha yale ambayo sisi kama Wabunge tuyatazame.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati nzuri au mbaya Mheshimiwa Nape Nnauye na wewe mwenyewe kwa sehemu kubwa mmenifilisi yale ambayo nataka kuyazungumza, lakini nitagusia mambo fulani fulani kuzungumza kiini cha nini tunachotaka kukifanya na katika kilimo tutazame maeneo gani ili tuboreshe Mpango na tuboreshe maisha ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, athari za UVIKO-19 ni mtambuka. UVIKO-19 umetuathiri kiafya, kiuchumi na kijamii. Maisha ya walimwengu yamebadilika kama vile usafiri wa anga ulivyobadilika baada ya matukio ya Osama Bin Laden, usafiri wa anga umebadilika kabisa na UVIKO-19 maisha yetu ndani ya ulimwengu huu tuliokuwa nao hayawezi kurudi kama yalivyokuwa mwanzo. Athari zake zimekuwa kubwa ulimwengu mzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sayansi inatuambia kwamba UVIKO-19 ni janga ambalo ni la kibaguzi, linaathiri rika tofauti, linaathiri watu wenye maradhi sugu tofauti, linaathiri maskini tofauti. Kwa hiyo lazima janga hili na utaratibu wetu wote huu tuliokuwa nao tuuangalie kwa utofauti wake ambao unaathiri sehemu mbalimbali. Kwa mantiki hiyo basi, tiba ya janga la UVIKO-19 ambayo ndiyo maudhui yetu yote haya ya hizi fedha tulizopewa, lazima ziangaliwe kwa maeneo ambayo limetuathiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mpango huu kwa ujumla maneno yote yanayozungumzwa; mpango wetu na mipango yetu yote imepangwa na imelenga kutatua mambo makuu matatu. Mambo hayo makuu matatu ambayo Mwasisi wetu wa Tanzania hii amepambana nayo na sisi tunaendelea kupambana nayo; mambo makuu matatu ni yapi? Adui ujinga, adui maradhi na adui umaskini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mpango huu ukiutazama umelenga kutatua na umepambana na maadui wawili tu; adui ujinga na adui maradhi. Ukiangalia kipaumbele katika afya, kuna intervention kubwa sana kwenye afya. Ukiangalia kwenye afya kuna intervention kubwa, lakini umaskini haujaguswa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umaskini kwa Tanzania ni nini? Umaskini ni kilimo. Mheshimiwa Nape amezungumza vizuri katika hilo, lakini ningependa tu kugusia kilimo katika maeneo gani. Wajumbe wengi hapa wamezungumzia kilimo katika sehemu moja, lakini kilimo ukikiangalia na athari zake ni sehemu kuu tatu. Kilimo awali, sehemu ya kwanza ya kilimo ni mbolea, mbegu bora, maji ya kumwagilia na kupanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu kuu ya kilimo ya pili ni, Waingereza wanasema post-harvest losses, athari inayotokea baada ya kupata mazao yao. Asilimia 40 ya hasara yetu katika kilimo inapatikana baada ya kupata mazao na sehemu kuu ya tatu ni masoko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ili tuweze kuhimili hili janga la umaskini, ili tupambane na adui maskini kwa kupitia njia ya kilimo tuna mambo ya msingi matatu ya kufanya. Na hayo lazima Serikali kupitia mpango huu iwekeze katika hayo makuu matatu ili kupata tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka iliyopita kabla ya mapinduzi yaliyotokea ya kisera, nitayasema Zimbabwe, hakuna nchi ulimwenguni ambayo ilikuwa inafanya vizuri katika sekta ya kilimo kama Zimbabwe. Nasema ulimwenguni, kwa nini? Zimbabwe ndiyo nchi pekee ambayo haikuweka ruzuku katika sekta ya kilimo. Kilimo chao kilikuwa kinakwenda kibiashara, mazao yakawa rahisi, faida ikawa kubwa. Nini wamekifanya Zimbabwe ambacho sisi tunaweza kuiga tukafika huko walikofika wao? Hilo ndilo jambo la kwanza la kutazama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo kubwa walilolifanya Zimbabwe, unajua Nchi yetu ya Tanzania kwanza imejipanga vizuri zaidi kushinda Zimbabwe, kwa sababu kuna maeneo ambayo yako juu kama Nyanda za Juu Kusini, halafu kuna mabonde yanatiririka mpaka kwenye bahari na mito mingi inakwenda mpaka kwenye bahari. Jambo kuu ambalo Zimbabwe waliweza kufanya ni kuweka mabwawa. Kwa hiyo, focus iwe kuweka mabwawa ili tuweze kuwa na maji ya kufanya irrigation. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kisayansi imethibitishwa na hiyo ndiyo njia rahisi zaidi kuathiri sekta ya kilimo; mabwawa. Zimbabwe watu waliobahatika kufika Zimbabwe, utabiri wa hali ya hewa kila siku asubuhi na jioni mtaambiwa leo kutakuwa kuna mvua, lakini bwawa hili liko asilimia 50 limejaa, bwawa lile asilimia 75 limejaa, bwawa lile kule asilimia 100. Ilikuwa sehemu ya msingi kabisa katika uhai wa Nchi ya Zimbabwe. Sisi pia tujikite kwenye mabwawa zaidi kushinda visima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, post-harvest losses, tatizo lake nini? Ni maghala. Tuweke maghala, tuweke cold storage. Kwa sababu haya yatafanya mambo mawili makuu; kwanza tutaokoa yale mazao ambayo tumeshayavuna, lakini pili, maghala ndiyo center ya mauzo, ita-solve tatizo la tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale kwenye maghala kutakuwa kuna wataalam wa vipimo, wanasema bwana mpunga wetu huu ni wa grade hii, unawekwa kwenye mtandao ili mnunuzi asipate taabu.

Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wabunge, hakuna tatizo la soko, tatizo la soko halipo, kila kitu kinahitajika. Tatizo lililopo ni ufikishaji sokoni. Teknolojia tunayo ambayo inaweza kuondoa hilo tatizo kabisa. Teknolojia ipo, tunaweza kulipa kimtandao; teknolojia ipo ambayo tunaweza kununua na ku-grade kila kitu kimtandao. Sasa tuta-solve mambo makuu mawili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa napenda kuishauri Wizara ya Fedha kutazama upya, kama wengi walivyosema, suala la kilimo, lakini maeneo makuu ambayo tunapenda yaangaliwe na yatiliwe mkazo mkubwa kabisa ni mabwawa ya maji ndani ya nchi yetu, ghala na cold storage investment ndani ya nchi yetu na mtandao wa kuwezesha sisi kuuza na kuhakikisha watu wote na sekta hii inaboreshwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na nashukuru sana. (Makofi)
Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Kuongeza Mamlaka ya Mahakama ya Afrika Mashariki
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nami naomba kutoa shukrani ya dhati kwa kunijaalia wasaa huu kuleta mchango wangu juu ya Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Kuongeza Mamlaka ya Mahakama ya Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwanzo kabisa napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza wawasilishaji, Mheshimiwa Waziri pamoja na Mheshimiwa Khadija Shaaban Taya ambaye amewasilisha report kwa niaba ya Kamati, kwa hakika uwasilishaji ulikuwa mahiri sana na wameeleweka. Tutajitahidi na sisi kuchangia vema ili tuende na mlolongo wao waliouanzisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakika tumechelewa kuipitisha hii Itifaki. Itifaki hii ina umuhimu mkubwa sana katika ustawi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Ili nieleweke inabidi niweke kwa muhtasari Jumuiya ya Afrika Mashariki ni nini na mihimili yake ili watu watuelewe na kwa nini Itifaki hii ni muhimu sana iridhiwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jumuiya ya Afrika Mashariki ina mihimili Minne. Mhimili wa kwanza ni Umoja wa Forodha (Customs Union), mhimili wa pili ni Soko Huria (Common Market), mhimili wa tatu ni Sarafu Moja (Monitory Union) na mhimili wa nne ni Umoja wa Kisiasa (Political Federation) lakini kwa sasa hivi tunazungumzia Political Confederation.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchukua wasaa kidogo nigusie kwa muhtasari haya. Customs Union (Umoja wa Forodha), hivi Umoja wa Forodha maana yake nini? Haya maneno yanazungumzwa sana lakini bila kuyatambua na kuyafahamu ni vigumu kwa Waheshimiwa Wabunge na Bunge lako Tukufu kujadili vema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Umoja wa Forodha ni jambo jepesi sana. Umoja wa Forodha ni mfumo ambao ndani ya hizi nchi Tano au Sita za Jumuiya ya Afrika Mashariki tukafanya tukawa na kitu kinaitwa common external tariff. Common external tariff ni nini? Kila nchi ikiagizia vitu kutoka nje ya nchi kuna vipengele vya kulipia kodi, Tanzania tuna vipengele vitatu. Chochote utakachoagiziwa nje ama utalipa zero percent ya kodi au asilimia 25 au asilimia 35. Vitu vyote vya nje vikiingia ndani lazima vilipiwe ushuru kwa vigezo hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa common external tariff baina ya zile nchi tano, hivi vigezo vyote vinakuwa sawia katika hizo nchi zote tano. Yaani ukiagiza kishikwambi chako kutoka China au Mkenya akiagiza kishikwambi chake kutoka China au Mganda au Mnyarwanda au Mkongo kodi itakayolipwa ni ileile. Sasa common external tariff inatengeneza single customs territory. Eneo zima lile linakuwa na umoja wa forodha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mgogoro ukitokea nani awe msuluhishi? Ndiyo hoja tunayoizungumzia hapa. Msuluhishi hapa tunasema iwe East African Court of Justice wale ndiyo wataalam ambao wanaelewa taratibu na sheria na itifaki kwa undani ili wao ndiyo warekebishe, hilo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, kila nchi kupitia Mahakama zake za nchi wanachama kuna uwezekano mkubwa sana tukapata maamuzi tofauti. High Court ya Tanzania ikaamua vyake, High Court ya Kenya ikaamua vyake, High Court ya Rwanda ikaamua vyake, kwa kweli kwa uhakika tutajivuruga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mhilimi wa pili, Common Market (Soko Huria) watu wanapenda kusema soko la pamoja, Hapana ni soko huria (free market). Ndani ya Jumuiya hii ya Afrika Mashariki soko liko wazi. Tumekubaliana sisi Itifaki hii ya mwaka 2004, vitu vitakavyotengenezwa ndani ya Jumuiya vikihama kutoka sehemu moja kwenda nyingine havina kodi. Utakachokitengeneza Tanzania ukakipeleka Kenya, Uganda, Rwanda hakuna kodi. Hali kadhalika utakachokitengeneza Rwanda, DRC, South Sudan ukikileta Tanzania hakina kodi, soko huria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa soko huria linatoa haki fulanifulani na hizo ni muhimu tuzielewe. Soko huria linatoa haki ya kwanza ya free movement of goods (bidhaa ziko huru), free movement of person maana yake nini? Maana yake uhuru wa wananchi kwenda popote ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Haki ya tatu, haki ya kuishi. Mwanaafrika Mashariki ana haki ya kuishi kokote ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki maadamu ana shughuli ya msingi ya kufanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uhuru wa kufanya kazi sehemu yoyote, uhuru wa kusafirisha mitaji na uwekezaji sehemu yoyote, uhuru wa kufanya biashara ya huduma. Sasa, kukiwa na mkanganyiko baina ya nchi moja au nyingine juu ya uhuru au huru hizo, nani ahukumu? Itifaki hii inatuambia The East African Court of Justice ambao Majaji wake wanatoka kila nchi mwanachama, Watanzania wapo, Wakenya wapo, Majaji ambao wanazo sifa na uwelewa wa kuhukumu masuala hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mhimili wa tatu, Monitoring Union. Monitoring Union kidogo ina utaalam na ni kitu kikubwa kidogo. Monitoring Union ili tuwe tuna sarafu moja, chumi za hizi nchi Sita kwa pamoja lazima ziunganishwe ziwe moja (marketing integration). Unafanyaje chumi hizi kutoka kuwa sita iwe moja? Kuna vigezo tumejiwekea. Vigezo hivyo vinaitwaje? Maneno complicated lakini ni simple. Inaitwa macroeconomic convergence criteria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo vitu ni vitu gani? vitu vichache ni kama vifuatavyo: -


(i) Kila nchi mwanachama lazima inflation rate yao wai-control isizidi asilimia nane. Kiwango cha juu cha mfumuko wa bei usizidi eight percent.

(ii) Nakisi ya bajeti baada ya kujumuisha misaada isizidi asilimia tatu ya GDP ya Pato la Taifa.

(iii) Deni la Taifa lisilozidi asilimia 50 ya Pato la Taifa.

(iv) Akiba ya fedha za kigeni isiyopungua mahitaji ya miezi minne na nusu.

(v) Nchi wanachama lazima waweze kuweka hivi vigezo kwa miaka mitatu mfululizo ili waweze kuingia kwenye sarafu moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo ndiyo tutapata marketing integration. Eneo lote lile likawa kama sehemu moja na tukaweza kuwa na sarafu moja. Sasa, mtazamaji ni nani wa kusema bwana nchi fulani kidogo hapa imelegalega? Lazima kuwe na taasisi moja ya kuhakikisha haya yote yako sawa. Kama kuna mgogoro lazima taasisi hiyo moja ya katikati itatue huo mgogoro. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakika Jumuiya ya Afrika Mashariki ni jambo nyeti sana. tunalichukulia poa lakini siyo poa. Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa upana wake ina dhamira ya kutufanya sisi, chini Kusini mwa Jangwa la Afrika kuna chumi kuu mbili, wengine wote wadandiaji tuu. Chumi kuu mbili, Nigeria in West Africa na South Africa Kusini kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Jumuiya ya Afrika Mashariki mawanda yake mapana ni kutengeneza chumi kuu Tatu. Nigeria na wenzake ECOWAS kule, South Afrika na wenzake Kusini, Tanzania na Afrika Mashariki. Major geopolitical purpose tunataka kuwa katika miongoni mwa nchi Kusini mwa jangwa la Afrika ambao tuna chumi kubwa kuendeleza maendeleo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hayo kuyagusia, mwisho kabisa napenda sana kuunga mkono hii hoja na napenda kuwaomba Wabunge wenzangu waiunge mkono hii hoja bila ukakasi wa aina yoyote, kwa sababu ya maslahi mapana ya Tanzania ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii ya kuchangia katika mjadala huu muhimu na adhimu. Awali ya yote ningependa kuchukua fursa hii kutoa shukrani na pongezi zangu za dhati kwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa maendeleo makubwa sana toka alivyoingia madarakani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nyanja nyingi zimeendelea lakini kama tutakuwa tunachambua, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Sera ya Nje ni miongoni mwa vitu ambavyo Mheshimiwa Rais na timu yake imefanya kwa weledi mkubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile pongezi zangu ziende kwa Waziri Mheshimiwa Tax na aliyemtangulia Mheshimiwa Mulamula kwa kazi kubwa waliyoifanya. Naomba nichukue fursa hii kumtakia Mheshimiwa Mulamula kila la kheri katika nia yake ya kuwania nafasi ya General Secretary wa Commonwealth kila la kheri Mheshimiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kuzungumzia mambo matatu na nitajitahidi yote niyagusie kwa sababu ya msingi na ya dhati. Nimefarijika mno kumsikia Mheshimiwa Waziri kwamba ameyagusia mambo yote ambayo ningependa kuyachangia. Ningependa kuzungumzia diaspora, Sera ya Diplomasia ya Uchumi na suala la uraia pacha au hadhi maalum yote ya msingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, diaspora maana yake nini? Diaspora ni neno la Kigiriki ambalo maana yake ni kutawanyika ulimwenguni. Watu ambao wametoka sehemu yao ya asili wakatawanyika ulimwenguni, ndio maana ya diaspora. Watu hutawanyika ulimwenguni kwa sababu mbalimbali kuna wengine inawabidi wahame kwa sababu ya vita, mauaji ya kimbali, kwa sababu ya njaa kali (famine), na wengine wanakwenda tu kwenye masomo na wengine tu kuwania maisha na kutafuta riziki zao za kheri na watoto wao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna ubaya kwa mtu kuhama na kwenda sehemu yoyote kujitafutia riziki yake, yote hiyo ni ruhusa. Tafiti zinaonesha kwamba diaspora inachangia katika nchi ya asili mambo makuu matatu mpaka manne. La kwanza, kijamii; la pili, kisiasa; na la tatu, kiuchumi au kimaendeleo. Hayo ndio maeneo ya msingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kijamii, wale ambao wako huko pengine wanajifunza ubunifu na kufanya mambo tofauti, wakirudi makwao wanafanya hivyo na kutuendeleza katika gurudumu la maendeleo. Anaweza mtu akawa Israel akawa mkulima mzuri kule, una teknolojia au njia ya kulima vyema, anarudi kwetu anatusaidia katika hilo. Huo ni mchango chanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili katika kisiasa, kuna nchi ambazo zimeingia kwenye machafuko nyingi tu, mfano Iraq, Libya, Burundi, Somalia hata Kenya katika machafuko ya 2007. Diaspora wa nchi hizo walichangia mchango mkubwa sana katika kupata amani. Sasa nao huo ni mchango vile vile na wanachangia maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho na la msingi zaidi ambalo nilitaka kujikita zaidi ni kiuchumi. Kiuchumi, wana-diaspora wanaweza kuchangia nchini mwetu kwa njia kuu mbili ya kwanza ni remittances ambazo zimezungumzwa na Mheshimiwa Profesa Kitila Mkumbo na ya pili ni investment. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, remittances ni zile fedha ambazo wana-diaspora wanawapa ndugu zao huku kuwasaidia kujikimu katika maisha yao na hizo zinapimwa. Nimefanya tafiti kidogo kwa nchi nne; Nigeria mwaka 2021/2022 remittances kutoka katika diaspora kwenda Nigeria zilikuwa dola bilioni 20, ndani ya mwaka mmoja. Ni fedha nyingi zaidi kushinda their largest export ya mafuta. Mafuta yanayouzwa nje yana thamani ndogo kushinda Wanaijeria waliopo nje wakileta kwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kenya Wana-diaspora wapo milioni tatu, wamechangia mwaka 2021/2022 dola bilioni nne. Uganda wapo laki sita, wamechangia dola biloni 1.4. Sisi tumechangia mwaka huo huo dola bilioni 1.1 na bilioni 1.1 imeongezeka kwa kasi kubwa sana kulinganisha na mwaka uliopita ilikuwa milioni mia tano na kitu na ukiangalia cha msingi kabisa ni jinsi gani wana-diaspora wanajiona wanathaminika ndani ya nchi yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli nitoe pongezi kwa hatua ya kwanza ambayo imetuwezesha sisi kuongeza lakini ukiangalia wana-diaspora wa Uganda wako laki sita sisi tupo milioni 1.5. Wao wanachangia nchini mwao zaidi kuzidi sisi kwa nini? Hilo ndio swali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nchi yetu inajikita katika Diplomasia ya Uchumi. Diplomasia ya Uchumi shamba lake kubwa ipo kwenye diaspora. Tukiweza kuwapa incentives wana-diaspora, tunaweza tukavuna mabilioni ya fedha mengi zaidi kushinda export yoyote ambayo tutaifanya hapa Tanzania.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Mheshimiwa ahsante sana.

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, napenda kumalizia jambo moja tafadhali. Suala la uraia pacha na hadhi maalum. Uraia pacha tunaouzungumzia hapa Mheshimiwa Rais Nyerere kama msingi wa msimamo wetu. Tuna ahadi za Wanachama wa TANU au sasa CCM. Tuna ahadi mbili ambazo ni relevant katika hili ya kwanza binadamu wote ni ndugu na Afrika ni moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, msingi huu ulitumika kuwa-nationalize wakimbizi 200,000 wa Burundi Tanzania awamu ya kwanza, wakimbizi hamsini elfu wa Somalia awamu ya pili. Sasa ahadi ya pili ya mwanachama sote sisi tunaijua, nitatumikia nchi yangu na watu wake wote, narudia tena nitatumikia nchi yangu na watu wake wote. Wana-diaspora ni watu wetu, lazima tuwatizame tuwajengee hoja, tuwasaidie, kama sio uraia pacha, hadhi maalum. Tofauti yake ni ndogo, sio tofauti kubwa. Hadhi maalum inategemea unawapa haki gani, uraia pacha unaweza kuzuia mambo makuu mawili masuala ya siasa wasiweze kushiriki katika siasa na wasiweze kufanya kazi katika vyombo vya ulinzi na usalama. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa ahsante sana umeeleweka sana.

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga hoja mkono, ahsante sana. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2021 (Toleo la Kiingereza)
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Awali ya yote ninapenda na mimi kutoa pole zangu kwa wafiwa wa Mheshimiwa Nditiye na tunawaombea wapendwa wake wote subira katika kipindi hiki kigumu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa wasaa huu nami kuchangia mawili/matatu katika mada hii muhimu na nyeti sana. Walionitangulia hasa Mheshimiwa Olelekaita na Mheshimiwa Tadayo, wameyazungumza mengi ambayo kwa kiasi kikubwa wamenifilisi yale ambayo nilitaka kuyasema, lakini ninapenda tu kusema hakuna mtu yeyote mwenye akili timamu anayeweza kubisha umuhimu wa mchakato wa kutoa haki kuwa katika lugha ambayo wengi wetu ndani ya nchi wanaifahamu. Hilo halina mjadala wa aina yoyote. Sasa lazima tuseme hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kumetokea kidogo hofu katika tasnia ya sheria kwa wale ambao walishazoea na walishapata mafunzo kwa lugha ya Kiingereza. Mabadiliko ya aina yoyote lazima yatakuwa yana ugumu wake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 1973 sisi kama Tanzania tuliamua kufanya Dodoma uwe Mji Mkuu. Tukachukua hatua za awamu hadi awamu lakini ile azma yenyewe haikufika ikatokea Awamu ya Tano na Rais, Dkt. Magufuli, akafanya maamuzi ya kuhamisha mji kufika Dodoma; tuko hapa. Tulilalamika hivi hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hali kadhalika katika lugha ya Kiswahili katika mihula yote miwili na sehemu kubwa huu muhula wa mahakama Kiswahili kinatumika. Lakini kuna hofu ya kwamba tukifanya kwa haraka pengine tutaleta athari ikatufanya sisi kama kisiwa. Hiyo hofu ipo lakini msiwe na wasiwasi. Sheria hii imegusia hayo, imeweka bayana kwamba lugha ya Mahakama ni lugha ya Kiswahili, lakini pale haki itakapohitajika kutendeka kwa kutumia lugha nyingine ruksa. Sasa msiwe na wasiwasi. (Makofi)

Mheshimiwa Salome ana wasiwasi huo, jurisprudence sijui kwa Kiswahili itakuwaje, nadhani itakuwa jurisprudensi, itajijenga upya kwa lugha ya Kiswahili na tutatafsiri na Jumuiya ya Madola itatuelewa. Lakini umuhimu wa kwanza ni kwa wananchi wetu na umuhimu wa kwanza wa misingi ya haki za binadamu na utawala bora inatulazimisha sisi kuhakikisha lugha ya kutoa haki ni lugha ile ambayo wengi wetu wanaielewa. (Makofi)

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Naibu Spika, Taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mchengerwa kwa kifupi.

T A A R I F A

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpe taarifa msemaji kwamba kamusi ya kwanza iliyotafsiri lugha ya kisheria kutoka lugha ya kisheria ya Kiingereza kuwa lugha ya sheria ya Kiswahili ilisainiwa na aliyekuwa Waziri Mkuu, Mzee wetu Kawawa mwaka 1968 na iliandaliwa na Kitivo cha Sheria Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Abdullah Mwinyi, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, naipokea tena kwa shangwe kubwa sana. Inaonesha bayana kwamba huu mchakato haukuanza leo, toka mwaka 1962 ulikuwepo na hatua hadi hatua mpaka tumefika kilele hiki cha leo cha kutunga hii sheria. (Makofi)

Sasa sheria hii na mabadiliko haya yamezingatia mambo yote ambayo ni ya msingi na ninapenda kuwaomba wenzangu kuiunga mkono na mimi pia naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na 2) wa Mwaka 2021 (Toleo la Kiingereza)
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Awali ya yote napenda kuchukua fursa hii kwanza kabisa kumshukuru Mheshimiwa Mwenyekiti wetu kwa uwasilisho mzuri kabisa kama kawaida yake. Pili, napenda kuchukua fursa hii kumshukuru sana na kwa dhati Mwanasheria Mkuu wa Serikali na timu yake yote pamoja na Waziri na CPD kwa kurahisisha kazi yetu katika Kamati na kuifanya kuwa nyepesi kabisa.

Mheshimiwa Spika, hakika napenda kuchukua fursa hii kuishukuru Serikali kwa ujumla wake, kwa kufanya kazi kuwa nyepesi kwa sababu hakukuwa na mvutano wa aina yoyote. Ukipendekeza vizuri, Serikali imekuwa sikivu na inapokea mapendekezo na kwa kweli tumefarijika sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimefilisiwa na watangulizi wangu kwa sehemu kubwa na vile vile tumefilisiwa na Serikali kwa sababu sehemu kubwa nadhani sehemu zote za mapendekezo yetu Serikali imepokea. Sasa kazi yangu itakuwa tu ni kuongeza msisitizo na kujenga hoja za ziada kidogo ili Bunge lituelewe zaidi kwa nini tumefanya haya mapendekezo na waridhie haya mapendekezo kwa minajili mizima ya kuboresha hii sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika suala la mawakili, Wakili Msomi Olelekaita amelizungumza vizuri na kwa kina, lakini napenda tu kuongeza jambo moja la msingi. Kuna msingi mmoja unasema, the power to appoint, pre-supposes the power to disappoint or to remove. Mamlaka ambayo inatoa wadhifa lazima iwe hiyo hiyo mamlaka ya kuondoa ule wadhifa. Huo ni msingi kwenye administration, msingi wa kisheria. Japokuwa hii Sheria ya Mawakili ya Sura 341 (Advocates Act, Cap. 341) kupeleka Kamati za Kinidhamu mikoani ni jambo zuri sana na kuna viwango vya nidhamu, kile kiwango cha mwisho kabisa tumeona akirudi Taifani kwa sababu ya msingi huu mmojawapo, pamoja na misingi mingine ambayo Wakili Msomi mwenzangu amezungumza.

Mheshimiwa Spika, kuhusu masuala ya vizazi na vifo kama Mwenyekiti wetu wa Kamati alivyosema, mjadala huu ulikuwa mkubwa na yamezuka mambo mengi na kwamba dada yangu Mheshimiwa Salome amezungumzia kuhusu hati za vifo zaidi ya kimoja, kwa kweli kiutaratibu kwanza cheti cha kifo kinamsaidia mtu kitu gani? Hilo lazima tujue, tuweke wazi. Pili, cheti cha kifo hakiwezi kuwa zaidi ya kimoja. Tunaweza tukawa tuna utaratibu wa kuwa na nakala
kwamba watu wenye haki ya kupata hivi vyeti wawe zaidi ya mtu mmoja, basi original kikatoka kimoja na nakala kwa mwingine yeyote ambaye anaweza kuwa na hiyo haki ili mradi awe nacho.

Mheshimiwa Spika, kiukweli cheti cha kifo ni ithibati ya kuonyesha kama fulani amefariki, hakikuzidishii zaidi ya hapo. Hakuna kingine cha ziada ila watu wengi wamezungumza na ingefanyika kama kungekuwa kuna muhtasari wa kifamilia. Familia mnakaa mnaandika muhtasari wenu na pengine watu wote wana haki; huenda kuna mtoto mmoja mtundu tu, japokuwa ana haki ya kwenda kuchukua hicho cheti na familia isitake yule aende, tukawa na muhtasari wetu, tukakubaliana mtu mmoja akaenda kuchukua kwa niaba ya familia. Sasa hayo ni mambo ya ki-administration na sidhani kwamba ni busara kuyaweka katika sheria, kutakuwa na utaratibu mwingine wa kuiweka huko mbele.

Mheshimiwa Spika, suala la Sheria za Kampuni, nataka nigusie tu kidogo, hiki kipengele ambacho Mheshimiwa Mbatia nacho alikigusa akasema ni cha hatari sana, kwa kweli inabidi nami nikubali na Kamati imekubali kwamba kipengele hiki ni kidogo cha hatari. Katika Ibara ya 30 inayopendekezwa Marekebisho ya Kifungu cha 3 cha Sheria…

SPIKA: Ni Salome Makamba.

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, Salome Makamba kumradhi. Naomba radhi. Mheshimiwa Makamba naomba radhi.

Mheshimiwa Spika, katika Ibara ya 30 inayopendekeza Marekebisho ya Kifungu cha 3 cha Sheria katika kifungu kidogo cha (5) kufuta maneno “associated with instances of”, naomba niseme, hili ni hatari zaidi kuliko lile alilolizungumza Mheshimiwa. Alilozungumza Mheshimiwa ni mtu ambaye tayari ameshahukumiwa akakatazwa, nami naungana naye mkono, kwa hiyo haifai. Amefanya makosa, jamii imeshamhukumu, aendelee na maisha yake ya kupata ujira wake. Hii inayosema “associated with instances of” hata kama hujahukumiwa ukishukiwa shukiwa hivi, usiweze kufungua Kampuni. Hii ni hatari. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna principle ya kisheria inasema, “innocent to proven guilty.” Huwezi ukapewa majukumu; kwanza wewe ni innocent, umeshukiwa tu ukazuiwa kufanya biashara. Hili tumeliona kwenye Kamati na tumelizungumza na tumekitoa hicho kipengele na Serikali imekubali. Sasa kwa ufupi, mengi ambayo tumeyaona na tumeyagusia hapa, Serikali wameyapokea na tunaomba Bunge lako Tukufu liridhie hayo mapendekezo ya Kamati ambapo masuala mengi yamekaa vizuri.

Mheshimiwa Spika, naomba sana kwa hayo machache niunge mkono hoja na niwasihi Wabunge wenzangu kuipokea ripoti yetu ya Kamati ili kuboresha hii sheria na ikakaa vizuri.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)
THE WRITTEN LAWS (MISCELLANEOUS AMENDMENTS) (NO. 5) ACT, 2021
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, kidogo nimeshtuka kwa sababu nilikuwa sijajipanga kuchangia lakini kwa sababu umeninyanyua nitasema mawili matatu.

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Mwenyekiti kwa ripoti yake nzuri na Mheshimiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa uwasilishaji wake mzuri sana. Kwa kuwa mimi ni mjumbe wa Kamati hii sitaweza kukosa mawili, matatu ya kuzungumza.

Mheshimiwa Spika, Muswada huu umegusia sheria 9, napenda tu kugusia maneno mawili, matatu katika sheria zifuatazo. Ya kwanza ni Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu, Sura ya 432; Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Sura ya 95; Sheria ya Utumishi wa Jeshi la Polisi, Idara ya Uhamiaji na Jeshi la Magereza, Sura ya 241; na mwisho napenda tu kugusia Sheria ya Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori, Sura 260. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Sheria ya The Anti-Trafficking in Persons Act, Sura 432 kwa kweli ni sheria ya msingi sana. Ulinzi na usalama ni jukumu letu sote Tanzania nzima sio tu jukumu la vyombo vya ulinzi na usalama pekee.

Mheshimiwa Spika, mabadiliko katika Sura 432 yamegusia masuala mbalimbali na kuwapa mamlaka wananchi kadhaa kuweza kudhibiti biashara hii haramu. Napenda kuzungumzia kifungu cha 9 kinachozungumzia kuhusu whistle-blowers, wale ambao wanaona uharamia unatokea na wakaripoti ili kuhakikisha kwamba uharamia ule unadhibitiwa. Pia kifungu cha 12 nacho kinathibitisha tena kwa ziada private citizens arrest, wananchi tukiona kuna matatizo yanatokea, tumepewa mamlaka ya kuhamasishana na kuhakikisha ule uharamia wa namna hiyo hauendelei. Kwa kweli, sisi kama Kamati tumeridhia na ni masuala mazuri kabisa yameletwa kwa ajili ya kuyarekebisha.

Mheshimiwa Spika, Sura inayofuata ya 95, Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, napenda tu kugusia jambo moja la msingi. Kipengele kipya cha 15 na 15A kinazungumzia masuala ya mirungi na bangi na kuweka mipaka na uzito wa kosa hilo kulingana na uzito wa mihadarati yenyewe.

Mheshimiwa Spika, katika jambo hili, kwa kweli nimekubaliana na proposal ya Serikali lakini nitoe tahadhari. Suala la mirungi japokuwa nchini kwetu ni haramu lakini tunapakana na nchi za ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na nyingi za SADC ambazo suala la mirungi lenyewe si haramu. Sasa udhibiti wake utakuwa una matatizo makubwa sana.

Mheshimiwa Spika, kwa vile sisi tuko ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Kenya pale zinarushwa ndege kama zile ndege za minofu za pale Mwanza zinaruka kutoka Nairobi zimejaa mirungi kupeleka Ulaya hali kadhalika Uganda. Sasa hili suala katika territory yetu ndani ya Tanzania ni haramu na lina penalty kubwa lakini wenzetu wanaotuzunguka wote wamelihalalisha. Sasa ama tulitazame kwa ujumla wetu wote, tuwashawishi wenzetu liwe haramu kote au tuliwekee misingi fulani fulani ambayo inaweza ikaruhusu hii biashara ikaendelea la udhibiti wake utakuwa una matatizo makubwa. Haikuwa maudhui ya mabadiliko ya sheria hii lakini hilo ni angalizo kwa Serikali, tulitazame siku zijazo kwa sababu udhibiti wake utakuwa una matatizo ilhali wote wanaotuzunguka mirungi kwao ni halali isipokuwa sisi hapa kwetu.

Mheshimiwa Spika, suala la Uhamiaji ambalo limezungumziwa kwa ari kubwa mpaka sasa hivi, sheria na Katiba vinaguswa katika masuala haya. Kiukweli vipengele vimesomwa hapa kwa pupa sana bila kuwaruhusu watu kujenga hoja halafu tukazitumia zile hoja ili kuelekezana vizuri.

Mheshimiwa Spika, ibara sahihi ya kwanza kwa kuanzia ni Ibara ya Katiba ya 147(2), naomba nipewe wasaa kidogo niitafute katika kishkwambi hapa, niipate kuisoma vizuri nitiririke vizuri. (Makofi)

SPIKA: Kama huioni tukusomee.

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, Ibara 147(2) inasema: “Majeshi ya Ulinzi.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano yaweza, kwa mujibu wa sheria, kuunda na kuweka Tanzania majeshi ya aina mbalimbali kwa ajili ya ulinzi na usalama wa nchi na wananchi wa Tanzania”.

Mheshimiwa Spika, Ibara ya 147(4) inasema: “Kwa madhumuni ya ibara hii, “mwanajeshi” maana yake ni askari aliyeajiriwa kwa masharti ya muda au ya kudumu katika Jeshi la Ulinzi, Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza au Jeshi la Kujenga Taifa”.

Mheshimiwa Spika, hii katiba ni ya mwaka 1977, kipindi hicho wakati hii Katiba inakuwa formulated haya ndiyo yalikuwa majeshi. Mwaka 1977 haya ndiyo yalikuwa majeshi lakini walitazamia kabisa kwamba siku za usoni kwa sababu mbalimbali nyingine kunawezekana kuwe na sababu ya kufanya tuwe na majeshi ya ziada. Ndiyo maana Ibara ya 147(2) inasema, kwa mujibu wa sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Ibara ya 151 inazungumzia maana ya jeshi. Jeshi maana yake nini? Maana ya jeshi, ni lolote kati ya majeshi ya ulinzi na ni pamoja na jeshi lolote lingine lililoundwa na Katiba hii au kwa mujibu wa sheria na iliyotawaliwa na Amiri Jeshi Mkuu au kwa mujibu wa sheria. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja. Naomba kuishia hapa, ahsante. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Usimamizi wa Maafa, 2022
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia fursa hii nami kusema machache juu ya Muswada huu ambao ni wa muhimu na umeletwa kwa wakati muafaka kabisa. Awali ya yote, naomba kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uhai na uzima na kutujalia kufika hii leo na kusema machache mbele ya Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Spika, mwanzo kabisa ningependa kuchukua fursa hii kutoa salamu zetu za rambirambi kwa familia ya Malkia Elizabeth wa pili aliyefariki, yeye ni kama Rais, Malkia ni head of state wa United Kingdom kwa familia yake na Serikali ya Uingereza kwa wananchi wa Jumuiya za Madola na wote wale ambao wameguswa na msiba huo. Tunapenda kusema poleni sana, Mwenyezi Mungu awajalie subira wote waliofikwa na huo msiba mkubwa.

Mheshimiwa Spika, pili, ningependa vilevile kuzungumzia Muswada huu kwa ujumla wake. Maafa ni jambo ambao linaweza kutokea wakati wowote na suala mtambuka. Mara nyingi tukizungumza tunafikiria nini kinaweza kuleta maafa, lakini kuna maeneo mengi tu. Maeneo ambayo yanaweza yakasabishwa na sisi na maeneo ambayo yanaweza yakatokea tu kwa kudra za Mwenyezi Mungu, lakini maafa yanatabirika, siyo yote lakini sehemu kubwa ya maafa yanatabirika.

Mheshimiwa Spika, sasa wenzetu wa nchi za kimataifa wana mifumo ambayo inawasaidia kuwa na early warning mechanisms. Sasa sijui tutatafsiri vipi hiyo lakini ni taarifa za awali za mapema ambavyo ni viashiria pengine maafa yanaweza yakatokea. Climate change tunajua mnaweza mkawa hampati mvua, mkaanza kuona wanyama wanafariki, ukame na athari zake. Migogoro ya kivita inaweza ikawa sio nchini kwenu lakini vita ikitokea jirani mauaji ya kimbari jirani hapa sisi kama Tanzania tumeyaona yote hayo.

Mheshimiwa Spika, sasa yote haya yanahitaji mambo makuu manne; mipango, uhakika wa utekelezaji, fedha, resource mobilization yaani jinsi mbadala na mtambuka wa kuzitafuta hizo fedha kutusaidia katika hayo maafa na wakati mwingine utaalam ambao pengine sisi tusiokuwa nao katika sekta fulani au katika maafa fulani.

Mheshimiwa Spika, sasa yote haya yanahitaji mambo makuu manne; mipango, uhakika wa utekelezaji, fedha, resource mobilization, yaani jinsi mbadala na mtambuka wa kuzitafuta hizo fedha kutusaidia katika hayo maafa. Wakati mwingine utaalam ambao pengine sisi tusiokuwa nao katika sekta fulani au katika maafa fulani. Ukiangalia hii sheria inagusia mambo yote hayo. Inaweka mfumo ambao tutakuwa tuna mpango yakitokea maafa tunajipanga vipi. Pili, nani anahusika kutekeleza na kukabili yale maafa ambayo yametokea. Resource mobilization kuna watu, ukiangalia Wizara ya Fedha - Treasury ipo lakini haizuii taasisi za nje ambazo zipo tayari kusaidia vilevile kwa sababu mfumo huo upo.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia hii sheria katika ngazi zote, kuanzia ngazi ya juu kabisa Kitaifa, Mkoa, Wilaya mpaka chini, inatoa fursa ya kuleta wataalam wa sehemu mbalimbali au wa sekta mbalimbali kuja kuleta mchango wao ili kutusaidia katika tatizo au janga ambalo limetukuta.

Mheshimiwa Spika, kwa ufupi, Muswada huu umekuja kwa wakati, tunawashukuru Serikali kwa kuwa wazi kwa kuchukua maoni tofauti, kwa sehemu kubwa Kamati imeweza kutoa maoni sehemu kubwa ya haya maoni yamepokelewa na Serikali na yamefanyiwa kazi hadi kupata Muswada huu ambao sina shaka yoyote unakidhi vigezo kwa Karne hii ya 21.

Mheshimiwa Spika, kwa hayo machache, naomba kuchangia hoja na kuiunga mkono. (Makofi)
The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (no. 2) Act, 2022
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nami nitoe shukrani zangu za dhati kwa kunipa wasaa huu wa kuchangia huu Muswada wa Sheria wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 2 wa Mwaka 2022 ambao umelenga kurekebisha Sheria Tatu. Sheria ya kwanza ni Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu, Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Madawa ya Kulevya na Sheria ya Kanuni ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Mheshimiwa Spika, hakika wenzangu wengi wameyazungumza na kwa kiasi kikubwa wamenifilisi yale ambayo ningependa kuyachangia lakini ningependa tu kusisitiza na kuwekea mkazo maeneo machache ili kuongeza uelewa na kwa nini Bunge hili Tukufu liunge mkono sheria hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika Kamati sheria yoyote ambayo inayoletwa lazima iwe na sababu ya kwenda kurekebishwa. Sheria ni kitu hai kama binadamu kama vitu hai vingine vyovyote ambavyo vikiendelea katika mchakato wa utekelezaji wake mapungufu yanaonekana na watu wanakaa wanaamini wapi tuende kurekebisha ili azma yetu ile ambayo tumeipanga iweze kutekelezeka vizuri. Katika haya yamekuwa vilevile.

Mheshimiwa Spika, ningependa kuzungumzia zaidi hii Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Madawa za Kulevya. Ndani ya Kamati baada ya kupokea maelezo mazuri ya awali ya Serikali, Wajumbe wengi walikuwa wanafikiria mambo makuu matatu katika mabadiliko ya aina yoyote. Kwanza ni haki za binadamu, pili ni rasilimali watu na rasilimali fedha ambazo zitatumika kisawia na la tatu, utekelezaji wake utaleta ufanisi au la. Kwa vigezo vyote hivyo vitatu tumeona bayana kabisa kwamba taasisi hii imeletwa kwa sababu za msingi kabisa.

Mheshimiwa Spika, huko tulikotoka kesi zinazohusiana na masuala ya madawa ya kulevya nyingi sana zinashindwa Mahakamani kwa sababu kama Mheshimiwa Zainab Katimba alivyosema doctrine of chain of custody, ili uweze kushinda kukusanya ushahidi kwa ufanisi mkubwa lazima taasisi moja toka mwanzo mpaka unavyofikisha kesi Mahakamani iwe in control, iwe imedhibiti maeneo yote. Hiyo ndiyo sababu kubwa kabisa ya kuingiza na kuipa mamlaka hii taasisi ya kuwa na mahabusu, hawakuamua tu kuwa na mahabusu bila ya sababu, sababu hii ni ya msingi kabisa ambayo itawezesha Serikali kushinda hizi kesi. Hawa watu wa madawa ya kulevya ni watu wenye rasilimali fedha kubwa sana ambao wanaweza kuleta ushawishi na kuwarubuni watu wengi katika taasisi mbalimbali, lakini mkiwa na mlolongo mmoja kutoka mwanzo mpaka mwisho inasaidia hizi kesi kuzishinda Mahakamani, hilo ndiyo jambo la msingi na kubwa pamoja na mengine yote ambayo wenzangu wameyachangia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ningependa kuzungumza la ujumla hapa sheria hizi mbili ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu na Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Madawa na Kulevya zote zinagusia eneo moja la masuala ya ulinzi na usalama. Haya yote ni masuala ya jinai, haya yote ni masuala ya ulinzi na usalama wa Taifa na yanapaswa yaguswe pande zote mbili za Muungano.

Mheshimiwa Spika, Sheria moja hii ya Kudhibiti Madawa ya Kulevya ni Sheria ya Tanzania Bara tu, wakati Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu ni Sheria ya Muungano. Hapa kuna jambo ambalo tungependa tulitazame kwa ujumla wake. Masuala ya madawa ya kulevya ukiyazungumza na ukiyajadili na wataalam wanavyotuambia ni kwamba yanapita sehemu zote. Sehemu ya Zanzibar yanapita, sehemu ya Bara yanapita na kuwa kuna taasisi mbili ambazo haziingiliani, ufanisi wake wa utekelezaji wa kazi inabidi taasisi zote mbili zizungumze badala ya kuwa na taasisi moja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ningependa tuone kama kuna uwezekano ama Kamati zetu za Katiba na Sheria au Bunge au uongozi wa juu pande mbili zote za Muungano zikae ziyajadili haya mambo tujue jinsi gani ya kuleta sheria ambazo kimsingi zinatakiwa ziwe za Muungano na zile ambazo kila mtu anaweza akazileta kwa upande wake kwa mujibu wa mfumo mzima wa Katiba yetu na Sheria za Muungano na ambazo siyo za Muungano. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hayo machache ninapenda kuwasihi wenzangu tuunge mkono marekebisho haya ya sheria na nashukuru sana.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 3) wa Mwaka 2022
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Napenda kuanza kwa kukushukuru kwa dhati kwa kunipatia nafasi ili kuchangia machache kwenye Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na.3) wa 2022.

Mheshimiwa Spika, kwa hakika ningependa kuanza kwa kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mwanasheria Mkuu pamoja na Serikali na Wizara za Sekta ambazo kwa kipindi ambacho tupo kwenye Kamati tulikuwa tunajadiliana kwa kina. Kwa hakika wametupa ushirikiano mkubwa sana na kazi kubwa ya Muswada huu, imefanyika na ikakamilika ndani ya Kamati. Mambo mengi tuliyokuwa tumeyashauri yalipokelewa na wenzangu hawa walionitangulia leo wamezungumza kwa msingi kwa yale ambayo yalikuwa yana utata kidogo, lakini kwa ujumla wake tumekubaliana na tumepata ushirikiano mkubwa na wamepokea mapendekezo yetu. Kwa hiyo nimefilisika, sina mengi sana ya kuzungumza ndio Muswada huu ilaningependa kuzungumza kwa ujumla katika sekta hizi ambazo zimeathirika na zimeguswa na hizi sheria.

Mheshimiwa Spika, eneo kubwa la uwekezaji katika hizi sheria limegusa Sheria ya Madini na ningependa mazungumzo yangu yagusie hapo. Uwekezaji kwa ujumla wake katika nchi yoyote unapenda stability (utulivu), certainty (uhakika) hasa maeneo ambayo uwekezaji wake unagusia fedha nyingi sana. Sekta ya Madini unawekeza na ina-contribute katika uchumi wetu na inawekezwa fedha nyingi sana, mabilioni ya dola. Wawekezaji ambao wanawekeza fedha nyingi sana wana mambo ya msingi ambayo yanawavutia. La kwanza miongoni mwao, ni sera ambayo ina utulivu na la pili ni sheria ambazo zinadumu kwa muda. Ukiona eneo linabadilishabadilisha sera au kuna marekebisho ya mara kwa mara ya sheria ina viashiria vikuu viwili: -

Mheshimiwa Spika, kiashiria cha kwanza, inaonesha ushirikishwaji haukuwa mkubwa na la pili ile dira ya awali pengine haikukaa sawa. Sasa yangu ilikuwa tu kutoa tahadhari, tuangalie sheria zetu hasa katika maeneo ambayo uwekezaji ni wa fedha nyingi. Policy certainty and legislative stability ni vitu vya msingi sana katika kukuza uwekezaji katika sekta hizi kubwa zinazogusia fedha nyingi, kwa mfano, Sekta ya Madini.

Mheshimiwa Spika, kiashiria cha pili ni business environment, uwekezaji unataka business environment ambayo ni nzuri. Kuna suala mtambuka la blueprint, ni mfumo mzima wa kuboresha business environment ili tuwalete wawekezaji. Limewekwa bayana, limezungumzwa lakini kwa bahati mbaya utekelezaji wake ambao unatakiwa utekelezwe kisekta pamoja na Sekta hii ya Madini umekuwa hafifu, kwa hakika inabidi tujitahidi tutafute jinsi ya kuhakikisha business environment katika hizi aekta inakaa sawa, inatulia na inaondoa vikwazo vidogovidogo ambavyo vinaweza kuleta ukakasi katika investment.

Mheshimiwa Spika, la tatu kama ushauri, ikibidi mabadiliko ya sheria yafanyike au mabadiliko ya sera yafanyike basi tuwe tunazingatia mambo kama matatu makuu. La kwanza, ni usimamizi wa utawala bora, mabadiliko yaendane na mfumo wa utawala bora. La pili, kuna extensive consultation yaani ushirikishwaji wa sekta husika ambao wa uhakika na la tatu clear communication, yale maamuzi na mabadiliko yanayofanyika yazungumzwe na yajadiliwe kwa uwazi ila sekta yenyewe itulie.

Mheshimiwa Spika, nazungumza hivi kwa sababu uwekezaji mkubwa katika sekta yoyote unatokana na fedha ambazo ni za kukopa katika masoko ya fedha ya kimataifa. Perception ndogo ya mabadiliko inaathiri sana uwekezaji na investment environment yetu ambayo tungependa iboreke ili tupate huo uwekezaji. Mheshimiwa Rais alitupa na aliwapa ya Madini challenge ya kuhakikisha Sekta ya Madini inachangia GDP yetu kwa 10% ya kipato chetu. Sasa kwa minajiri hiyo lazima tuwe makini sana katika ubadilishaji wa sera na hasa katika ubadilishaji wa sheria.

Mheshimiwa Spika, kwa hayo ya ujumla haya specific ambayo tumeyapitia, tumeyazugumza kwa kina na maboresho yetu yalikuwa katika mazingatio hayo ambayo nimeyazungumza kwa mapana yake na kwa hakika tumepata ushirikiano mkubwa wa Serikali pamoja na Attorney General.

Mheshimiwa Spika, ningependa kuunga mkono hii hoja na kuwaasa wenzangu kuiunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Tume ya Mipango wa Mwaka 2023.
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nami napenda kutoa shukurani za dhati kwa kunijalia wasaa kusema machache, kujadili Miswada hii nyeti kabisa ambayo iko hapa mbele yetu.

Mheshimiwa Spika, napenda kwanza kutoa shukurani zangu za dhati kwa Serikali ikiongozwa na Mawaziri wote watatu ambao wanakwenda kwenye maudhui ya Miswada hii, kwa ushirikiano wao mkubwa sana. Hakika kipindi hiki tulikuwa na kazi nyingi sana, tumepitia sheria nyingi mno, lakini kazi zetu zimekuwa nyepesi kwa sababu ya ushirikiano mkubwa. Nasemea Kamati kwa ujumla kwamba, responsiveness ya Serikali na usikivu mkubwa wa Serikali umefanya kazi yetu kuwa nyepesi, tumeimaliza na tumefikia muafaka katika sheria zote ambazo tunazijadili.

Mheshimiwa Spika, napenda kuweka maoni yangu katika sheria zote, lakini sina hakika kama muda utaniruhusu. Napenda kuanza na Sheria ya TISS. Kwa ujumla wake Sheria hii ukiitazama kwa mawanda mapanda, inarasimisha kazi ambazo tayari zilikuwa zinafanyika katika Idara ya TISS. Kwa mapana yake, hakuna mambo mapya ambayo yanafanyika katika sheria hii, imerasimisha yale ambayo tayari yamekuwa yakifanyika. Kila jambo likifanyika hivyo, linawekewa framework ya jinsi gani utendaji kazi unakwenda.

Mheshimiwa Spika, kimsingi kuna mambo makuu matano ambayo napenda kuyagusia kwa sababu yamekuwa yakigusa hisia za wadau. Pia, kama mwenzangu alivyosema, ili uifahamu vizuri sheria hii, lazima uzisome sheria mbili; hii ya leo na ile ya mwaka 1996, zina-inform. Kuna maeneo ambayo bila kuangalia sehemu zote mbili inaweza ikaja kukuvuruga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni nini ambacho kilikuwa cha msingi na kinazungumzwa sana na watu kuwa na hofu ambapo kwa haki hakuna sababu ya kuwa na hiyo hofu? Kwanza ni kwamba, unyeti wa taasisi hii ni wa msingi mno kwa ajili ya usalama na ustawi wa Taifa letu. Haiwezekani usalama wa Taifa ukawepo bila taasisi hii kuwa na majukumu hayo.

Mheshimiwa Spika, kwanza taasisi hii kupitia sheria hii, kwanza imerasimisha kazi zake; pili, iko chini ya Ofisi ya Rais moja kwa moja. Sasa, mambo yapi ambayo ningependa kuyagusia moja baada ya lingine ambayo yamewekwa bayana na yako vizuri katika sheria hii? La kwanza linalozungumzika, kuhusu usimamizi na oversight ya taasisi hii.

Mheshimiwa Spika, Taasisi ya TISS kwa unyeti wake ina oversight function ya sehemu mbalimbali. Kwanza ni hii Kamati yetu. Katika masuala ya sera na bajeti ambayo amekabidiwa kwa Mheshimiwa Waziri, yatapita kwenye Kamati ya Utawala, Katiba na Sheria. Pili, sehemu kubwa ya oversight katika sheria hii imeweka bayana, ni Rais mwenyewe na Tassisi ya Urais yenyewe. Tatu, ni Katibu Mkuu Kiongozi, naye sheria hii imeainisha sehemu yake ya kazi.

Mheshimiwa Spika, kwa sehemu kubwa, eneo la oversight na kwa sababu ya unyeti na mambo mengi yanayoendelea, Waheshimiwa Wabunge lazima tujue kuna siri na kuna mambo nyeti ya Taifa na Mataifa yote ambayo hayawezi yakawa wazi. Hata hivyo, katika section ya oversight ukiangalia sheria, Rais, Katibu Mkuu Kiongozi, DGIS yeye mwenyewe na Kamati hii, oversight function ipo.

Mheshimiwa Spika, lingine, kulikuwa na mazungumzo kuhusu security of tenure ya DGIS kwamba akiingia hatoki. Siyo kweli. Sheria inasema bayana, DGIS (Director General of Intelligence) ata-serve at the pleasure of the President. Hiyo iko wazi. Hilo nalo halipo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tatu. Kuhusu suala la immunity from Criminal prosecution. Ukiipitia sheria yote hii hakuna sehemu yoyote ambayo inasema hivyo. Kuna mistakes done in action and omissions in good faith, ambayo professional yoyote Tanzania, hiyo omission anayo. Ukienda kwa Daktari ipo, kwa Mwanasheria ipo, ukienda kwenye taasisi za kawaida omission hiyo ipo. Sasa hofu hiyo tusiwe nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu ripoti za CAG, zimezungumzwa vile vile. CAG Act ndiyo ina-decide kitu gani kitafanyiwa ukaguzi wa CAG. Hakuna sheria yoyote ambayo inasema lazima taasisi hii ikaguliwe na CAG. Sheria ya CAG iko bayana, anaweza kukagua Serikali nzima na kwa utaratibu gani, itajulikana huku. Tusiwe na wasiwasi, sheria hii imepitiwa, tumeijadili kwa kina, maoni mengi ya wadau ambayo yalikuwa na mashaka yamewekwa wazi na sheria hii iko salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda kuwaambia ndugu zangu kwamba, kwa mazungumzo ya Kamati na Serikali, tumepata muafaka na sheria hii iko salama.

Mheshimiwa Spika, vilevile napenda kuzungumzia suala la Tume ya Mipango. Niguse tu kwa muhtasari. Nimekuwa nikimsikiliza ndugu yangu Mheshimiwa Askofu Gwajima akizungumza sana kuhusu mipango iwe endelevu. Sheria hii kwa mawanda yake tena mapana, imefanya mipango yetu kwanza iwe specialized kwamba kuwe na utaalam, na pili, iwe endelevu. Hakuna kitu katika nchi ambacho kinaweza kikafungwa kisibadilike milele. Vilevile sheria hii imefanya mipango isiwe rahisi kubadilishwa kwa wakati wowote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kimsingi hicho ndicho kilikuwa kilio chetu kikubwa sana ndani ya Bunge hili, kwamba mipango inatumia gharama kubwa, inatumia watu wengi na muda mrefu sana, lakini inaweza ikabadilishwa haraka. Sheria hii ndiyo mwarobaini wa hilo tatizo. Inaweza kubadilishwa lakini kwa hatua ambazo zimewekwa bayana kwenye Katiba na Sheria hii kama alivyozungumza Mheshimiwa Kisau. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kweli napenda kutumia fursa hii kuishukuru Serikali kwa maono hayo yaliyotuletea hii Sheria. Napenda kuwaambia Wabunge tuiunge mkono hii sheria.

Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa, katika Sheria ya Urekebu kulikuwa kuna sheria ambayo tuliipitisha kwenye Bunge hili ambayo ilifanya sheria zetu zisomeke na ziandikwe kwa lugha ya Kiswahili. Katika mazungumzo yetu huko kwenye Kamati, tulikubaliana kwamba sheria hizi zote zisomeke kwa lugha zote mbili; Kiingereza na Kiswahili. Tanzania ni nchi ya lugha mbili; Kiswahili na Kiingereza. Hapa Bungeni tunaweza ku-debate kwa lugha ya Kiingereza au Kiswahili, kanuni ziko wazi. Mashuleni kwetu tunasomeshwa Primary Kiswahili, Sekondari na Vyuo Vikuu Kiingereza na mfumo wetun a mitaala yetu yote iko hivyo.

Mheshimiwa Spika, sasa nashukuru katika Sheria hiyo ya Urekebu imesahihishwa kwamba sheria zetu zote lazima ziwe published kwa lugha mbili (Kiswahili na Kiingereza). Tuipongeze sana Serikali kwa hilo. Sababu kuu ya hilo ni kwamba sisi ni nchi ambayo tuko katika sehemu ya nchi za Jumuiya ya Madola. Nchi za Jumuiya ya Madola tunafuatilia masuala ya kisheria ya Commonwealth.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, nimekuona na ninakushukuru kwa kunipa wasaa wa ziada. Naunga mkono hii hoja. Napenda kuwaambia wenzangu wote kwamba sheria zote ziko salama, tumezichambua kwa kina na tuziunge mkono, ahsante sana. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Yatokanayo na Urekebu wa Sheria wa Mwaka 2023 .
MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nami napenda kutoa shukurani za dhati kwa kunijalia wasaa kusema machache, kujadili Miswada hii nyeti kabisa ambayo iko hapa mbele yetu.

Mheshimiwa Spika, napenda kwanza kutoa shukurani zangu za dhati kwa Serikali ikiongozwa na Mawaziri wote watatu ambao wanakwenda kwenye maudhui ya Miswada hii, kwa ushirikiano wao mkubwa sana. Hakika kipindi hiki tulikuwa na kazi nyingi sana, tumepitia sheria nyingi mno, lakini kazi zetu zimekuwa nyepesi kwa sababu ya ushirikiano mkubwa. Nasemea Kamati kwa ujumla kwamba, responsiveness ya Serikali na usikivu mkubwa wa Serikali umefanya kazi yetu kuwa nyepesi, tumeimaliza na tumefikia muafaka katika sheria zote ambazo tunazijadili.

Mheshimiwa Spika, napenda kuweka maoni yangu katika sheria zote, lakini sina hakika kama muda utaniruhusu. Napenda kuanza na Sheria ya TISS. Kwa ujumla wake Sheria hii ukiitazama kwa mawanda mapanda, inarasimisha kazi ambazo tayari zilikuwa zinafanyika katika Idara ya TISS. Kwa mapana yake, hakuna mambo mapya ambayo yanafanyika katika sheria hii, imerasimisha yale ambayo tayari yamekuwa yakifanyika. Kila jambo likifanyika hivyo, linawekewa framework ya jinsi gani utendaji kazi unakwenda.

Mheshimiwa Spika, kimsingi kuna mambo makuu matano ambayo napenda kuyagusia kwa sababu yamekuwa yakigusa hisia za wadau. Pia, kama mwenzangu alivyosema, ili uifahamu vizuri sheria hii, lazima uzisome sheria mbili; hii ya leo na ile ya mwaka 1996, zina-inform. Kuna maeneo ambayo bila kuangalia sehemu zote mbili inaweza ikaja kukuvuruga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni nini ambacho kilikuwa cha msingi na kinazungumzwa sana na watu kuwa na hofu ambapo kwa haki hakuna sababu ya kuwa na hiyo hofu? Kwanza ni kwamba, unyeti wa taasisi hii ni wa msingi mno kwa ajili ya usalama na ustawi wa Taifa letu. Haiwezekani usalama wa Taifa ukawepo bila taasisi hii kuwa na majukumu hayo.

Mheshimiwa Spika, kwanza taasisi hii kupitia sheria hii, kwanza imerasimisha kazi zake; pili, iko chini ya Ofisi ya Rais moja kwa moja. Sasa, mambo yapi ambayo ningependa kuyagusia moja baada ya lingine ambayo yamewekwa bayana na yako vizuri katika sheria hii? La kwanza linalozungumzika, kuhusu usimamizi na oversight ya taasisi hii.

Mheshimiwa Spika, Taasisi ya TISS kwa unyeti wake ina oversight function ya sehemu mbalimbali. Kwanza ni hii Kamati yetu. Katika masuala ya sera na bajeti ambayo amekabidiwa kwa Mheshimiwa Waziri, yatapita kwenye Kamati ya Utawala, Katiba na Sheria. Pili, sehemu kubwa ya oversight katika sheria hii imeweka bayana, ni Rais mwenyewe na Tassisi ya Urais yenyewe. Tatu, ni Katibu Mkuu Kiongozi, naye sheria hii imeainisha sehemu yake ya kazi.

Mheshimiwa Spika, kwa sehemu kubwa, eneo la oversight na kwa sababu ya unyeti na mambo mengi yanayoendelea, Waheshimiwa Wabunge lazima tujue kuna siri na kuna mambo nyeti ya Taifa na Mataifa yote ambayo hayawezi yakawa wazi. Hata hivyo, katika section ya oversight ukiangalia sheria, Rais, Katibu Mkuu Kiongozi, DGIS yeye mwenyewe na Kamati hii, oversight function ipo.

Mheshimiwa Spika, lingine, kulikuwa na mazungumzo kuhusu security of tenure ya DGIS kwamba akiingia hatoki. Siyo kweli. Sheria inasema bayana, DGIS (Director General of Intelligence) ata-serve at the pleasure of the President. Hiyo iko wazi. Hilo nalo halipo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tatu. Kuhusu suala la immunity from Criminal prosecution. Ukiipitia sheria yote hii hakuna sehemu yoyote ambayo inasema hivyo. Kuna mistakes done in action and omissions in good faith, ambayo professional yoyote Tanzania, hiyo omission anayo. Ukienda kwa Daktari ipo, kwa Mwanasheria ipo, ukienda kwenye taasisi za kawaida omission hiyo ipo. Sasa hofu hiyo tusiwe nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu ripoti za CAG, zimezungumzwa vile vile. CAG Act ndiyo ina-decide kitu gani kitafanyiwa ukaguzi wa CAG. Hakuna sheria yoyote ambayo inasema lazima taasisi hii ikaguliwe na CAG. Sheria ya CAG iko bayana, anaweza kukagua Serikali nzima na kwa utaratibu gani, itajulikana huku. Tusiwe na wasiwasi, sheria hii imepitiwa, tumeijadili kwa kina, maoni mengi ya wadau ambayo yalikuwa na mashaka yamewekwa wazi na sheria hii iko salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda kuwaambia ndugu zangu kwamba, kwa mazungumzo ya Kamati na Serikali, tumepata muafaka na sheria hii iko salama.

Mheshimiwa Spika, vilevile napenda kuzungumzia suala la Tume ya Mipango. Niguse tu kwa muhtasari. Nimekuwa nikimsikiliza ndugu yangu Mheshimiwa Askofu Gwajima akizungumza sana kuhusu mipango iwe endelevu. Sheria hii kwa mawanda yake tena mapana, imefanya mipango yetu kwanza iwe specialized kwamba kuwe na utaalam, na pili, iwe endelevu. Hakuna kitu katika nchi ambacho kinaweza kikafungwa kisibadilike milele. Vilevile sheria hii imefanya mipango isiwe rahisi kubadilishwa kwa wakati wowote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kimsingi hicho ndicho kilikuwa kilio chetu kikubwa sana ndani ya Bunge hili, kwamba mipango inatumia gharama kubwa, inatumia watu wengi na muda mrefu sana, lakini inaweza ikabadilishwa haraka. Sheria hii ndiyo mwarobaini wa hilo tatizo. Inaweza kubadilishwa lakini kwa hatua ambazo zimewekwa bayana kwenye Katiba na Sheria hii kama alivyozungumza Mheshimiwa Kisau. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kweli napenda kutumia fursa hii kuishukuru Serikali kwa maono hayo yaliyotuletea hii Sheria. Napenda kuwaambia Wabunge tuiunge mkono hii sheria.

Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa, katika Sheria ya Urekebu kulikuwa kuna sheria ambayo tuliipitisha kwenye Bunge hili ambayo ilifanya sheria zetu zisomeke na ziandikwe kwa lugha ya Kiswahili. Katika mazungumzo yetu huko kwenye Kamati, tulikubaliana kwamba sheria hizi zote zisomeke kwa lugha zote mbili; Kiingereza na Kiswahili. Tanzania ni nchi ya lugha mbili; Kiswahili na Kiingereza. Hapa Bungeni tunaweza ku-debate kwa lugha ya Kiingereza au Kiswahili, kanuni ziko wazi. Mashuleni kwetu tunasomeshwa Primary Kiswahili, Sekondari na Vyuo Vikuu Kiingereza na mfumo wetun a mitaala yetu yote iko hivyo.

Mheshimiwa Spika, sasa nashukuru katika Sheria hiyo ya Urekebu imesahihishwa kwamba sheria zetu zote lazima ziwe published kwa lugha mbili (Kiswahili na Kiingereza). Tuipongeze sana Serikali kwa hilo. Sababu kuu ya hilo ni kwamba sisi ni nchi ambayo tuko katika sehemu ya nchi za Jumuiya ya Madola. Nchi za Jumuiya ya Madola tunafuatilia masuala ya kisheria ya Commonwealth.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, nimekuona na ninakushukuru kwa kunipa wasaa wa ziada. Naunga mkono hii hoja. Napenda kuwaambia wenzangu wote kwamba sheria zote ziko salama, tumezichambua kwa kina na tuziunge mkono, ahsante sana. (Makofi)