Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Shabani Hamisi Taletale (18 total)

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza samahani, kwa kuwa leo ni siku yangu ya kwanza na mara yangu ya kwanza kuongea, napenda niwashukuru ndugu zangu wa Morogoro Kusini Mashariki. Pia nishukuru familia yangu, mama yangu mzazi na marehemu mke wangu popote alipo, Mungu amlaze mahali pema.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa majibu ya Serikali na kwa kutambua ufinyu wa bajeti na kuzingatia umuhimu wa barabara hii, je, Serikali iko tayari kushirikiana nami kutafuta mkandarasi wa building and finance? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamisi Shabani Taletale, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nimemuelewa vizuri kwamba Serikali itashirikiana naye kutafuta mkandarasi, utaratibu wa kutafuta wakandarasi ni utaratibu ambao uko kisheria na ni utaratibu ambao unatekelezwa na Serikali kupitia mamlaka husika.

Mheshimiwa Maibu Spika, kwa kuwa tumeahidi katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi na Mheshimiwa Rais katika hotuba yake barabara anayoizungumzia ameiahidi, hivyo, nimhakikishie tu kwamba itajengwa na kukamilika katika kipindi hiki cha miaka mitano ambayo Ilani hii itakuwa inatekelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano, Dkt. John Pombe Magufuli, alipopita kwenye Jimbo letu la Morogoro Kusini Mashariki alituahidi barabara ya Bigwa – Kisaki. Naomba kuiuliza Serikali barabara hii itaanza lini kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Babu Tale, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alipotembelea Mkoa wa Morogoro, moja ya ahadi alizotoa na ilikuwa ni maagizo kwamba barabara hii ijengwe haraka kwa kiwango cha lami. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Babu Tale, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki na wananchi anaowaongoza wa Jimbo lake kwamba barabara hii kwa maelekezo ya Mheshimiwa Waziri itajengwa kwa kiwango cha lami kuanzia kilometa 50. Kama navyoongea naye mara kwa mara, nimhakikishie kwamba barabara hii itakuwa ni kati ya barabara ambazo zitatangazwa muda si mrefu kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya swali dogo la nyongeza. Naomba kuuliza, Serikali iliahidi kutangaza tender ya ujenzi wa barabara ya Bigwa – Kisaki.

Je, ni lini Serikali itatangaza barabara hii?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ni kweli kwamba kwa sasa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ipo kwenye hatua mbalimbali za kutangaza baadhi ya barabara ili ziweze kujengwa kwa hatua mbalimbali, nyingine kwa kiwango cha lami na mengine ni madaraja ya kujengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira na maelezo mengine ya ziada yatatolewa kwenye bajeti yetu ambayo inatarajiwa kusomwa Jumatatu ijayo tarehe 17 na tarehe 18. Ahsante.
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujua barabara yetu ya Ubena Zomozi-Ngerengere ya kilometa 10?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Taletale Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Mbena Zomozi imeshapata kibali kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami hizo kilomita alizozisema. Ahsante.
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nauliza Serikali, je, ni lini itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Bigwa – Kisaki ya kilometa 78?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamisi Taletale, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Bigwa – Kisaki (kilometa 78) ilishapata kibali na taratibu za kukamilisha zabuni hizo ilitangazwa, lakini itatangazwa tena kwa ajili ya kupata mkandarasi. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa kibali kilishatolewa, kwa hiyo ni taratibu tu za manunuzi ambazo zinaendelea ili ianze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kuiuliza Serikali; je, ni lini barabara yetu ya Bigwa - Kisaki ya kilometa 78 itaanza matengenezo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Taletale, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara hii ilitangazwa, lakini kilometa zilikuwa chache na sasa barabara hii tunategemea kuitangaza muda wowote kuijenga kwa kiwango cha lami na tuko kwenye hatua za mwisho za manunuzi na barabara hii nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge itatangazwa mwaka huu wa fedha na itaanza kujengwa hizo kilometa 78, ahsante.
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza Serikali ni lini itaanza kujenga barabara yetu ya Bigwa
– Kisaki?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Taletale Mbunge wa Morogoro Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Bigwa – Kisaki ni kati ya barabara 22 ambazo ziko kwenye taratibu mbalimbali za manunuzi ili ujenzi wa barabara hii muhimu ya kutoka Bigwa – Kisaki, kwenda Bwawa la Nyerere uanze. Kwa hiyo, muda wowote taratibu zikikamilika, barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami. (Makofi)
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba Serikali barabara yetu Bigwa na barabara yetu Ngerengere, Matuli, Matulazi:-

Je, lini Serikali itatuangalia?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamisi Taletale, Mbunge wa Morogoro Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Ngerengere kwenda Matulazi ni moja ya barabara muhimu na ya kipaumbele. Moja ya kazi kubwa ambayo tunaifanya sasa hivi, ni kufanya usanifu ili sasa tuiweke katika mipango yetu ya kufanyiwa kazi haraka iwezekanavyo. Ahsante sana.
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Moja ya changamoto kubwa ya wananchi wa Morogoro Kusini Mashariki na Morogoro Vijijini kwa ujumla ni ukosefu wa mitaji. Je, Serikali ina uratatibu gani wa kutuletea mitaji wana Morogoro Vijijini?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Hamisi Shabani Taletale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la mitaji kwa wakulima ni suala ambalo tunalipa kipaumbele Serikali, tupo tayari kukaa na Mheshimiwa Mbunge pamoja na ushirika wa wakulima hawa ili tuangalie fursa ambayo wanaweza kuipata kuimarisha mitaji yao.
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kuiuliza Serikali; je, ni lini italeta mradi wa maji kwenye Tarafa ya Ngerengere?
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Taletale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Ngerengere ipo kwenye mpango wa Wizara, Mheshimiwa Waziri alishapita maeneo hayo. Mheshimiwa Mbunge tuko mbioni kuleta mradi huu wa maji tutatumia Mradi wa Chalinze ama Morong’anya kuhakikisha maji yanafika Ngerengere.
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante, je, ni lini Serikali itaenda kujenga barabara ya Bigwa – Kisaki ya kilometa 78 kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Taletale, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba barabara ilishatangazwa kwa ajili ya kuijenga na kwa hiyo sasa hivi ipo kwenye hatua ya manunuzi kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, ni lini Serikali italeta mawasiliano katika Kata ya Gwata, Tununguo na Tomondo?
NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hamisi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Kata ya Gwata ipo katika utekelezaji na tusubiri Mheshimiwa Mbunge mradi huu ambapo ukiwa unaendelea kutekelezwa ndani ya kipindi cha mkataba, tunaamini Kata ya Gwata itakuwa imefikishiwa huduma ya mawasiliano, ahsante sana.

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza Serikali Bunge lililopita iliahidi kujenga na kusaini barabara ya Bigwa – Kisaki hadi sasa ipo kimya; je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Bigwa – Kisaki?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, barabara hiyo imeshapata mkandarasi na sasa hivi kinachoandaliwa tu ni taratibu za kuisaini hiyo barabara. Kwa hiyo tuna barabara kama 16 ambazo zinaandaliwa utaratibu mzuri wa kuzisaini ili Wakandarasi waanze kazi, ikiwepo na hiyo barabara ya Bigwa – Kisaki.

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kuuliza, je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya maji katika Tarafa ya Ngerengere?
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamisi Taletale, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Tarafa ya Ngerengere tayari tuna miradi ambayo ipo kwenye utekelezaji, lakini tuna mipango thabiti ya kuona kwamba eneo hili nalo linaenda kupata huduma ya maji safi na salama mwaka ujao wa fedha Mheshimiwa Mbunge atashuhudia shughuli nyingi sana zikifanyika katika Tarafa hii.
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kituo cha afya cha Kata ya Mkuyuni kinachangamoto ya gari la wagonjwa; je, na sisi lini tutaletewa gari la wagonjwa?

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamisi Taletale, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, magari haya yatakayo kuja yatapelekwa kwenye vituo vyetu vikiwemo vya Morogoro ambavyo vitakidhi vigezo. Kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutawasiliana tuone namna ya kufanya tathimini kwenye kituo hiki kama kinakidhi vigezo hivyo, ahsante.
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, kutokana na ahadi ya Serikali barabara yetu ya Ubena Zomozi – Ngerengere je, lini itaanza kujengwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Taletale Mbunge wa Morogoro Kaskazini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara iliyotajwa imetengewa fedha katika bajeti hii kuianza kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama yote hayo wanayafahamu, sasa ni zaidi ya mwaka wa tatu tumesimama hapa kuomba Kituo cha Afya cha Ngerengere, hakina jengo la Huduma ya Mama na Mtoto, Mortuary hakuna. Wakazi wa Kata ya Ngerengere ni 15,000, Kata ya jirani ya Kidugalo ni 8,000, leo hii Mheshimiwa Waziri anajibu majibu ambayo anafahamu tatizo liko wapi, mpaka nashindwa kuelewa. Naomba kumwuliza swali Mheshimiwa Waziri; je, ni lini mtakwenda kutatua hili tatizo? Siyo kwamba majibu mnayo na utatuzi hakuna, ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamisi Shabani Taletale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wa upanuzi wa Kituo cha Afya cha Ngerengere. Nasi kama Serikali, taarifa hii tunaifahamu na ndiyo maana tulitoa maelekezo kwa Mkurugenzi, kuongeza eneo la ujenzi wa Kituo cha Afya, ekari 4 na nusu hazitoshi kujenga Kituo cha Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya hiki kilikuwa ni cha Mission, kwa hiyo, kilichukuliwa na Serikali kikiwa tayari kinatoka Mission. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba mara hili eneo la ekari mbili la Posta ambalo halijaendelezwa, ambalo liko mkabala kabisa na Kituo hiki, likishachukuliwa na kuwa na ekari sita na nusu, basi mapema iwezekanavyo tutatafuta fedha kwa ajili ya kuongeza majengo haya ambayo yanapungua katika Kituo cha Afya cha Ngerengere, ahsante. (Makofi)
MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama yote hayo wanayafahamu, sasa ni zaidi ya mwaka wa tatu tumesimama hapa kuomba Kituo cha Afya cha Ngerengere, hakina jengo la Huduma ya Mama na Mtoto, Mortuary hakuna. Wakazi wa Kata ya Ngerengere ni 15,000, Kata ya jirani ya Kidugalo ni 8,000, leo hii Mheshimiwa Waziri anajibu majibu ambayo anafahamu tatizo liko wapi, mpaka nashindwa kuelewa. Naomba kumwuliza swali Mheshimiwa Waziri; je, ni lini mtakwenda kutatua hili tatizo? Siyo kwamba majibu mnayo na utatuzi hakuna, ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamisi Shabani Taletale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wa upanuzi wa Kituo cha Afya cha Ngerengere. Nasi kama Serikali, taarifa hii tunaifahamu na ndiyo maana tulitoa maelekezo kwa Mkurugenzi, kuongeza eneo la ujenzi wa Kituo cha Afya, ekari 4 na nusu hazitoshi kujenga Kituo cha Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya hiki kilikuwa ni cha Mission, kwa hiyo, kilichukuliwa na Serikali kikiwa tayari kinatoka Mission. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba mara hili eneo la ekari mbili la Posta ambalo halijaendelezwa, ambalo liko mkabala kabisa na Kituo hiki, likishachukuliwa na kuwa na ekari sita na nusu, basi mapema iwezekanavyo tutatafuta fedha kwa ajili ya kuongeza majengo haya ambayo yanapungua katika Kituo cha Afya cha Ngerengere, ahsante. (Makofi)