Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to supplementary Questions by Hon. David Mwakiposa Kihenzile (20 total)

MHE. SALIM MUSSA OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza kabisa nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali yenye kutia matumaini, lakini nimuulize swali la nyongeza.

Je, haoni kama ipo sababu ya kuweza kuweka kipaumbele au Wizara yake iko tayari kutoa kipaumbele kwa hili jambo ili kuweza kutatuliwa kwa haraka sana, kwa sababu Wapemba wanalaghaiwa na issue hii imekuwa kubwa sana. Sasa hivi ili Wapemba waweze kukupa dua ili uweze kutoboa katika mikeka ijayo?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Salim Mussa Omar kwamba Serikali inafahamu na inatambua uzito mkubwa na umuhimu wa kupeleka ndege hiyo Pemba na ndiyo maana imeshaanza mchakato. Alichokifanya ni kutukumbusha, nasi tutajitahidi kuongeza kasi zaidi ili angalau ndugu zetu Wapemba waweze kusafiri kama inavyotakiwa. (Makofi)
MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Waziri, swali la kwanza; kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amesema kwamba uko mdaki mmoja utafungwa katika eneo la Azam Sea Link, tunataka kujua, ni lini mdaki huu utakwenda kufungwa ili kuondoa adha kwa wananchi wanaotumia eneo hili?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa vilevile Mheshimiwa Waziri amesema kwenye bajeti ya mwaka huu, wametenga fedha kwa ajili ya kununua midaki mingine. Je, ni midaki mingapi itakwenda kunuliwa kwa ajili ya eneo la Azam Sea Link ili kuendelea kuboresha eneo hili? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza kuhusu lini, ni ndani ya Mwaka huu wa Fedha 2023/2024.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusu ni midaki mingapi itajengwa kwenye eneo hili ni kwamba hakuna mpango wa kuongeza kwenye eneo la Azam Link kwa sababu tayari umeshapatikana mmoja na kama kutakuwa na uhitaji tutakwenda kwenye maeneo mengine yenye uhitaji mkubwa.
MHE. ASHA ABDULLAH JUMA : Mheshimiwa Spika, ahsante sana na nashukuru kwa majibu mazuri ila nina maswali mawili.

Je, ni kwa nini Serikali haifanyi utafiti wa suala la bei wa safari za ndege za ndani ya nchi kutokana na bei hizo kuwa kubwa sana, kwa mfano Dodoma - Dar es Salaam 200,000 na zaidi mpaka 500,000 kwa safari ya mara moja?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, Serikali haioni hatari ya kupoteza soko la ndani endapo yakajitokeza mashirika mengine yakafanya biashara hii kwa mfano Flight-Link inafanya safari hiyo kwa dola 180 sawa na shilingi 450,000 kwa safari ya kwenda na kurudi Dodoma - Dar es Salaam na ni fixed. Kwa nini hamuoni mfanye bidii ili kuliokoa Shirika la Ndege Tanzania lisije likazama? Kwa nini hamjiongezi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Asha Abdullah Juma kama alivyoeleza.

Mheshimiwa Spika, moja kuhusu tafiti, Shirika letu kwanza, mashirika ya ndege sio moja yako mengi kama alivyosema Mheshimiwa Spika, lakini kwa kuwa amegusia kwenye ATCL specific, ni kwamba tafiti zinafanyika lakini kwa kuwa jukumu la Bunge ni kushauri Serikali tutaongeza pengine utafiti zaidi ili kwenda sambamba na hoja yake.

Mheshimiwa Spika, kuhusu hoja namba mbili ya kwamba je, hatuoni hatari ya kupoteza soko, nadhani ni jambo ambalo pia linazungumzika kupitia utafiti huo ambao tunaenda nao ambao ameusema kama alivyoshauri tutaendelea kujipima, lakini kwa sasa hivi ATCL haijapoteza soko kwa sababu ipo kwenye ushindani na viwango vilivyowekwa ni kwa mujibu wa ushindani kama nilivyosema kwenye jibu la msingi. (Makofi)
MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba tunapata ndege za moja kwa moja kutoka Dodoma kwenda Kilimanjaro na Arusha au muda mfupi wa kuunganisha kwa kupitia Dar es Salaam?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, tumepokea ushauri wa Mheshimiwa Priscus Tarimo kuhusiana na kuanzisha route inayokwenda Kilimanjaro, nafikiri Serikali itakapokuwa tayari basi ataweza kuarifiwa. (Makofi)
MHE. ASYA SHARIF OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Serikali nashukuru kwa majibu mazuri, lakini nina swali moja la nyongeza.

Je, Serikali ina mkakati gani wa chuo hichi cha usafirishaji kuongeza wanafunzi wa kigeni? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asya kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Chuo cha Usafirishaji ambacho kiko pale Dar es Salaam kina wanafunzi 14,464 na katika wanafunzi hao asilimia 99.2 ni wanafunzi wa Kitanzania na asilimia 0.8 ni wanafunzi wa nje.

Mheshimiwa Spika, chuo kimeendelea na programu mbalimbali za kuhakikisha kinaongeza wanafunzi wengi kama ambavyo imeulizwa na Mheshimiwa Mbunge ikiwa ni kwa ajili ya kuhakikisha tunaongeza forex, lakini pia kwa ajili ya kuongeza experience kwa wanafunzi wetu.

Mheshimiwa Spika, programu mbalimbali zimefanyika katika chuo hicho ikiwa ni pamoja na kushirikiana na Balozi zetu za nje kukitangaza chuo chetu kimataifa. Vile vile tumeshiriki katika mikutano mbalimbali mingine imefanyika Nchini Rwanda kwa ajili ya kuongeza na kutangaza chuo chetu.

Mheshimiwa Spika, kama hilo halitoshi, chuo chetu kwa sasa kinaandaa mkutano mkubwa tarehe 18 mpaka tarehe 20 mwezi ujao ambao ni First International Conference on Transport and Logistics and Management ili kuleta wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi kuhakikisha kwamba pengine tunaweza kujitangaza zaidi na kupata wanafunzi wengi zaidi, ahsante.
MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri yenye kutia moyo. Pia, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Nyasa na jirani zao tunapenda kushukuru sana na kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay. Baada ya hapo naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Bandari ya Mbamba Bay itakuwa ni kubwa na ya kisasa na itahitaji mzigo mkubwa kwa ajili ya kuhudumia Tanzania pamoja na nchi za jirani. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha sasa reli ya kutoka Mtwara mpaka Mbamba Bay inajengwa ili kuhakikisha kwamba bandari hii inatumika kiukamilifu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa Bandari ya Mbamba Bay inategemeana sana mizigo yake na bandari ndogondogo zilizopo Kando ya Ziwa Nyasa. Bandari kama Liuli, Njambe, Lipingu na kule Manda katika Wilaya ya Ludewa. Nini mpango wa Serikali kuboresha bandari hizi ili ziweze kusaidia na kuhakikisha kwamba mizigo yote inachukuliwa vizuri?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, kwanza kwa niaba ya Serikali nipokee pongezi za dhati za Mheshimiwa Manyanya kwa sababu ni kwa muda mrefu Wananchi wa Ruvuma na mikoa ya jirani wamekuwa wakitamani kuona bandari hii inafanyiwa uboreshaji na tayari Serikali ya Awamu ya Sita imeshaanza utekelezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake pili anauliza kuhusu bandari ndogondogo kama za Liuli, Njambe na maeneo mengine. Hizi bandari zote zimejumuishwa katika mpango kabambe ambao ni The Updated National Proposed Master Plan 2022/2023 mpaka 2026/2027 ambazo zipo kwenye mpango wa kuboreshwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye swali la kwanza ambalo ndio swali kubwa linaulizwa na Wabunge karibu wote wa Nyanda za Juu Kusini pamoja na Kusini. Kwamba ni lini sasa reli ya SGR ya kutoka Mtwara mpaka Mbamba Bay itaanza kujengwa na pengine reli hii wengine wanakwenda mbele zaidi wanataka kufahamu kuunganisha mpaka Liganga na Mchuchuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pengine nieleze kwa ufupi tu kwamba, Serikali inao mpango kwamba inatambua umuhimu na ukubwa wa mradi huu wa SGR ya Southern Corridor ambao ndani yake una miradi zaidi ya sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja reli hii ikijengwa ya kilometa 1,000 kutoka Mtwara kwenda mpaka Mbamba Bay kwenda mpaka Liganga na Mchuchuma utawezesha kusafirisha makaa ya mawe ambapo Mungu ametujalia zaidi ya metric tons milioni 400 na yaligundulika zaidi ya miaka pengine mia moja iliyopita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili itatusaidia makaa ya mawe yale yakishatengenezwa yataanza kuzalisha umeme zaidi ya megawati 600; nusu yake yakayeyushe chuma pale Liganga, nusu yake yaingie kwenye Gridi ya Taifa lakini kama haitoshi meli hii pia inakwenda kutoa ajira na inakwenda kutoa pia chuma ambacho kinakwenda kutengenezea magari na vitu mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninyi mnafahamu Watanzania kwamba kwa sehemu kubwa zaidi ya asilimia 100 tunaagiza chuma kutoka nje jambo ambalo linachukua fedha zetu nyingi zaidi. Hivyo basi, Serikali kwa kutumbua umuhimu huo mkubwa; moja, imeshaanza kutengeneza uboreshaji mkubwa wa Bandari ya Mtwara ili mzigo upatikane kwa wingi zaidi; lakini pili, inaongeza bandari nyingine ya pili ya kisiwa mgao ili bidhaa chafu zote kwa maana ya makaa ya mawe, simenti na kadhalika ipitie pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ipo kwenye mpango wa kuhuisha stadi iliyofanyika miaka ya nyuma kwa maana ya kutafuta mshauri mwelekezi kuhuisha ile reli ili tuweze kujua mahitaji yake ni yapi. Mara tu baada ya kukamiliisha tunategemea kuanza kuijenga kwa mfumo wa PPP na hatimaye tunaamini likikamilika hili ni moja kati ya mambo ambayo Mheshimiwa Rais wetu anayapigania na kwa msaada wa Mwenyezi Mungu atakayakamilisha na hivyo kwenda kufufua uchumi wetu kwa kiasi kikubwa zaidi.
MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, ukanda wa Ziwa Tanganyika yaani Mkoa wa Kigoma, Rukwa na Katavi tumesubiri kwa muda mrefu ukarabati wa meli ya MV Liemba. Je, ni lini Serikali itakamilisha ukarabati wa meli ya MV Liemba ili kunusuru usafiri huo?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, Serikali ya awamu ya sita imejipambanua katika kutenda. MV Liemba ni kiungio kubwa la Ziwa Tanganyika na wananchi wote wanaotumia ziwa hilo. Tumekwishasaini mkataba mwaka jana mwezi Novemba na ndani ya mwaka mmoja tutakuwa tumeshakamilisha ukarabati na ili Wananchi wa Kigoma na maeneo jirani wasubiri kwa hamu tunakwenda kukamilisha meli yao.
MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kuna agenda ya Mtwara Corridor na tunapozungumza Mtwara Corridor tunazungumza bandari, tunazungumza Airport pia tunazungumza reli ya Liganga na Mchuchuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umekuwa ni wimbo toka mwaka 2020 mpaka leo hii Serikali kila ikija hapa wanasema ipo kwenye mpango. Tunataka sasa tufahamu ni lini sasa ujenzi wa reli hii ya Liganga na Mchuchuma.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, nafikiri Mheshimiwa Mtenga anataka kupata pengine ufafanuzi wa ziada. Nimekwishasema na naomba nirejee. Tulishaanza SGR ya kutoka Dar es Salaam kwenda mpaka Isaka, tumekwishaenda na SGR kutoka Dar es Salaam tumekwenda mpaka Kigoma sasa tunakwenda mpaka Msongati Burundi. Awamu inayofuatia Serikali ya Awamu ya Sita imejipambanua na imejiwekea malengo ya kwenda SGR Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimtoe mashaka uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita unakwenda kujenga reli ya SGR ya kusini ambayo ni Mtwara Corridor kama nilivyosema. Hii inakwenda kuungana pamoja na uboreshaji mkubwa wa Airport kama nilivyosema sambamba na uboreshaji mkubwa wa maeneo ambayo nimeyaeleza pale awali, kwa hiyo, nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge.
MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Serikali imekuwa ikitoa ahadi ya kujenga meli kwa ajili ya abiria na mizigo katika Ziwa Tanganyika ili kutatua changamoto ya usafiri katika Mikoa ya Kigoma, Katavi na Rukwa. Je, ujenzi huo utatekelezwa lini?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, siyo tu meli ya mizigo na abiria kama alivyouliza Mheshimiwa Mbunge. Serikali imesaini tayari mkataba, tumeanza kujenga kiwanda cha kutengeneza meli nyingi nyingi katika Ziwa Tanganyika. Ambapo kiwanda hicho kitahusika na kutengeneza meli za mizigo na abiria na kukarabati zilizopo, hili linakwenda sambamba na uboreshaji mkubwa wa meli ambazo zipo za akina Mwongozo, Sangala pamoja na kina Liemba kama ilivyoulizwa na Mheshimiwa Sylvia pale awali.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza niwapongeze Serikali kwa kujenga reli ya kisasa ambayo ya SGR kutoka Makutupora Tabora. Reli ile mpaka sasa hivi wamefukua makaburi ya watu wa Igalula, watu wa Goweko, Tula hamjawalipa mpaka leo. Je, ni lini mtawalipa fedha ambazo mliwarudishia msiba mpaka leo hamjawalipa kwa sababu reli inataka ipite?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, hii hoja ya Mheshimiwa Venant naomba niichukue tuifatilie halafu tuifanyie kazi baada ya kupata taarifa zake za kina.
MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bandari ya Tanga ilifanya vizuri sana miaka ya 1980 na sababu kubwa ilikuliwa ni uwepo wa viwanda vingi ambavyo asilimia 90 sasa vimeshakufa. Kwa kuwa, meli kubwa na nyingi haziwezi kwenda mahali ambako zitapeleka tu mzigo bila kuchukua, yaani ile exchange of containers hakuna meli kubwa ambayo itakwenda bila kukutana na hali hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, tunamini kabisa bandari ndiyo uti wa mgongo wa Taifa hili; Je, Wizara hii ya Uchukuzi haioni haja ya kushirikiana kwa karibu na Wizara zingine kuhakikisha kwamba meli kubwa zinakuja kwa kufufua viwanda ambavyo Tanga vimekufa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, Bandari ya Mwambani ilipangwa kuendeshwa kwa ubia lakini kikwazo ilikuwa ni Sheria ya Ubia ambayo sasa imekwishafanyiwa marekebisho. Sasa Serikali itueleze wazi, mpaka sasa imeshachukua hatua gani kuhakikisha mpango ule wa kuendesha Bandari ya Mwambani kwa ubia unatekelezeka?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Eng. Mwanaisha kwa kazi yake kubwa anayofanya ya kufuatilia mchakato wa miundombinu katika Mkoa wa Tanga. Serikali imeshaanza kufanya mambo mengi katika eneo hilo, mojawapo ni ukarabati wa hiyo Bandari ya Tanga lakini pia uwepo wa fursa kama bomba la mafuta ni hatua muhimu kwenye kuelekea Tanga kuwa eneo muhimu sana la kiuwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ameuliza kama je, tuko tayari kushirikiana na Wizara nyingine, ni kweli, tuko tayari kushirikiana na sekta nyingine ikiwemo Wizara ya Viwanda na Biashara kuhakikisha kwamba viwanda vilivyokuwa vimefungwa na vimefanya vizuri miaka ya 1990 na huko nyuma vinafufuliwa ili angalau bandari hiyo iweze kupata mizigo. Mojawapo ya mambo ambayo tunayafanya ni pamoja na kufufua pia uwanja wa ndege wa Tanga ili ndege kubwa na za kati ziweze pengine kuanza kutumia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ameuliza kuhusu Bandari ya Mwambani, kwenye mpango wetu mkakati wa mwaka 2045 hiyo ni moja kati ya maeneo ambayo tunatazama kwa jicho la karibu zaidi. Kwa sasa hivi, moja tumeshakamilisha mabadiliko ya sheria ya PPP na hivyo tunakaribisha mtu yeyote anayetaka kuja kushirikiana nasi katika kuendeleza bandari hiyo ili kwa pamoja tuweze kuhakikisha kwamba Bandari ya Mwambani inafanya vizuri zaidi. Ahsante. (Makofi)
MHE. PROF. PALAMAGAMBA J. A. M. KABUDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ambayo yanatia moyo wa kuanza kufufuliwa kwa reli hii muhimu kwa uchumi wa Tanzania. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Moja, ningependa kujua ni lini hasa mchakato wote huu utakamilika (timeframe) ili wananchi wa Kilosa lakini Wananchi wa Mikumi na wananchi wa Kilombero wajue ni lini reli hii itaanza kukarabatiwa?

Swali langu la Pili la nyongeza; kwa kuzingatia kwamba Mji wa Kilosa sasa utaunganisha reli tatu, yaani reli ya sasa ya MGR, reli ya SGR na kwa sababu kutoka Kilosa mpaka Kidatu inaanza reli ya TAZARA Kidatu mpaka Mlimba. Maana yake sasa Mji wa Kilosa utaunganisha reli tatu.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuifanya sasa Kilosa kuwa ndiyo logistic hub kubwa katika nchi yetu inayounganisha reli hizi tatu, ukichukua reli ya TAZARA ina uwezo mpaka wa kufika Zimbabwe, Zambia, Afrika ya Kusini na Namibia ili mizigo katika reli hizi iweze kuhamishwa na makontena kwa urahisi katika Mji wa Kilosa ambao sasa una stesheni kubwa mbili ya MGR na SGR na uwezo wa kuungana na reli ya TAZARA. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Profesa kwa sababu swali lake linagusa sehemu kubwa sana ya maeneo ya Mashariki na Kati mwa Tanzania. Kwa kuwa reli hii ilikuwa ni muhimu sana miaka ya nyuma kwa nchi za SADC kuanzia nchi za South Africa mpaka Uganda, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Jemedari Dkt. Samia Suluhu Hassan inao mkakati madhubuti wa kufanyia kazi jambo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ameuliza ni lini, jibu ni Mwaka huu wa Fedha 2023/2024, tumekwishaanza mchakato wa kimanunuzi na pengine ifikapo mwezi Februari tayari tutakuwa kwenye hatua kubwa zaidi.

Swali la pili anauliza ni upi mkakati wa Serikali wa kuifanya Kilosa kuwa logistic hub, kwa sababu tayari reli ya MGR, SGR na TAZARA zinaungana, kwanza nataka kumhakikishie kupitia SGR na MGR, tutajenga kituo kikubwa cha mizigo katika eneo hilo la Kilosa na tayari tumeshaanza upembuzi yakinifu katika kuhakikisha tunatimiza jambo hilo na hivyo kuifanya Kilosa kuwa ni Logistic hub kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameuliza hapo awali kwenye swali lake la nyongeza.
MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa kuna malalamiko kwamba hata kazi ndogo ndogo kama za usafi, kufyeka na ulinzi, mkandarasi anatoa wafanyakazi maeneo ya mbali badala ya maeneo ya Seke, Malampaka na Malya. Je, Serikali inamshauri nini mkandarasi huyu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa pia kuna malalamiko kwamba mkandarasi ambaye ndiyo mwajiri hapeleki au anapeleka michango kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa kusuasua, je Serikali inasemaje juu ya malalmiko haya? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mashimba Mashauri Ndaki.

Mheshimiwa Spika, la kwanza, amezungumzia kuhusiana na watu wengi kutoka nje ya eneo la mradi. Moja, nimetoa takwimu ya watu ambao wameajiriwa kutoka kwenye eneo hilo katika Mkoa wake wa Shinyanga.

Pili, nimkumbushe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba mradi huu ni wa Kitaifa. Hata hivyo, Serikali itaendelea kumsimamiwa na kumsisitiza kwamba, anatafuta kwanza wafanyakazi kwenye eneo husika kabla hajepeleka kipaumbele kwenye maeneo mengine ya nje ya eneo husika.

Mheshimiwa Spika, hoja yake pili ni kuhusiana na michango ya NSSF, kwamba pengine mkandarasi anasuasua. Tunafahamu Sheria ya NSSF (The National Social Security Act) Revised ya 2018 Cap. 50, inamtaka mkandarasi au mwajiri kuhakikisha kwamba anapeleka makato hayo NSSF mapema iwezekanavyo.

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba kuna changamoto kubwa sana kwenye upande wa mkandarasi huyu kwa sasa. Tayari tumeshaanza vikao kupitia wenzetu Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa ajili ya kukaa naye na kuweka commitment, mara tu anapolipwa fedha aweze kupeleka michango hiyo kwenye Mifuko ya Hifadhi za Jamii. Pia, aweze kuwalipa na wazabuni mbalimbali wa ndani. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, naona umesimama.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri, napenda tu kuongezea kwenye kile kipengele cha mkandarasi kutopeleka michango kwenye Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Mheshimiwa Spika, nakiri kweli kuna madai ambayo mkandarasi anadaiwa na Mfuko umekuwa ukifatilia madai hayo na kuna makubaliano ambayo NSSF imeweka na mkandarasi ambapo tunataka madeni haya yakamilike ndani ya mwaka mmoja.

Mheshimiwa Spika, nimesimama pia kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, kuna utaratibu ambao umewekwa kati ya NSSF na mkandarasi kwa wale ambao wanatakiwa kulipwa mafao yao sasa, kuna utaratibu maalum wa fedha zao kupatikana ili wasiathirike na malipo hayo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nikuhakikishie kwamba, kama Wizara ambayo tunasimamia mifuko ya hifadhi ya jamii, tutahakikisha kwamba madeni haya tunayafatilia ili haki za wafanyakazi zisipotee. Ahsante sana.
MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri yenye kutia moyo. Pia, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Nyasa na jirani zao tunapenda kushukuru sana na kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay. Baada ya hapo naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Bandari ya Mbamba Bay itakuwa ni kubwa na ya kisasa na itahitaji mzigo mkubwa kwa ajili ya kuhudumia Tanzania pamoja na nchi za jirani. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha sasa reli ya kutoka Mtwara mpaka Mbamba Bay inajengwa ili kuhakikisha kwamba bandari hii inatumika kiukamilifu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa Bandari ya Mbamba Bay inategemeana sana mizigo yake na bandari ndogondogo zilizopo Kando ya Ziwa Nyasa. Bandari kama Liuli, Njambe, Lipingu na kule Manda katika Wilaya ya Ludewa. Nini mpango wa Serikali kuboresha bandari hizi ili ziweze kusaidia na kuhakikisha kwamba mizigo yote inachukuliwa vizuri?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, kwanza kwa niaba ya Serikali nipokee pongezi za dhati za Mheshimiwa Manyanya kwa sababu ni kwa muda mrefu Wananchi wa Ruvuma na mikoa ya jirani wamekuwa wakitamani kuona bandari hii inafanyiwa uboreshaji na tayari Serikali ya Awamu ya Sita imeshaanza utekelezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake pili anauliza kuhusu bandari ndogondogo kama za Liuli, Njambe na maeneo mengine. Hizi bandari zote zimejumuishwa katika mpango kabambe ambao ni The Updated National Proposed Master Plan 2022/2023 mpaka 2026/2027 ambazo zipo kwenye mpango wa kuboreshwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye swali la kwanza ambalo ndio swali kubwa linaulizwa na Wabunge karibu wote wa Nyanda za Juu Kusini pamoja na Kusini. Kwamba ni lini sasa reli ya SGR ya kutoka Mtwara mpaka Mbamba Bay itaanza kujengwa na pengine reli hii wengine wanakwenda mbele zaidi wanataka kufahamu kuunganisha mpaka Liganga na Mchuchuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pengine nieleze kwa ufupi tu kwamba, Serikali inao mpango kwamba inatambua umuhimu na ukubwa wa mradi huu wa SGR ya Southern Corridor ambao ndani yake una miradi zaidi ya sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja reli hii ikijengwa ya kilometa 1,000 kutoka Mtwara kwenda mpaka Mbamba Bay kwenda mpaka Liganga na Mchuchuma utawezesha kusafirisha makaa ya mawe ambapo Mungu ametujalia zaidi ya metric tons milioni 400 na yaligundulika zaidi ya miaka pengine mia moja iliyopita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili itatusaidia makaa ya mawe yale yakishatengenezwa yataanza kuzalisha umeme zaidi ya megawati 600; nusu yake yakayeyushe chuma pale Liganga, nusu yake yaingie kwenye Gridi ya Taifa lakini kama haitoshi meli hii pia inakwenda kutoa ajira na inakwenda kutoa pia chuma ambacho kinakwenda kutengenezea magari na vitu mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninyi mnafahamu Watanzania kwamba kwa sehemu kubwa zaidi ya asilimia 100 tunaagiza chuma kutoka nje jambo ambalo linachukua fedha zetu nyingi zaidi. Hivyo basi, Serikali kwa kutumbua umuhimu huo mkubwa; moja, imeshaanza kutengeneza uboreshaji mkubwa wa Bandari ya Mtwara ili mzigo upatikane kwa wingi zaidi; lakini pili, inaongeza bandari nyingine ya pili ya kisiwa mgao ili bidhaa chafu zote kwa maana ya makaa ya mawe, simenti na kadhalika ipitie pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ipo kwenye mpango wa kuhuisha stadi iliyofanyika miaka ya nyuma kwa maana ya kutafuta mshauri mwelekezi kuhuisha ile reli ili tuweze kujua mahitaji yake ni yapi. Mara tu baada ya kukamiliisha tunategemea kuanza kuijenga kwa mfumo wa PPP na hatimaye tunaamini likikamilika hili ni moja kati ya mambo ambayo Mheshimiwa Rais wetu anayapigania na kwa msaada wa Mwenyezi Mungu atakayakamilisha na hivyo kwenda kufufua uchumi wetu kwa kiasi kikubwa zaidi.
MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, ukanda wa Ziwa Tanganyika yaani Mkoa wa Kigoma, Rukwa na Katavi tumesubiri kwa muda mrefu ukarabati wa meli ya MV Liemba. Je, ni lini Serikali itakamilisha ukarabati wa meli ya MV Liemba ili kunusuru usafiri huo?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, Serikali ya awamu ya sita imejipambanua katika kutenda. MV Liemba ni kiungio kubwa la Ziwa Tanganyika na wananchi wote wanaotumia ziwa hilo. Tumekwishasaini mkataba mwaka jana mwezi Novemba na ndani ya mwaka mmoja tutakuwa tumeshakamilisha ukarabati na ili Wananchi wa Kigoma na maeneo jirani wasubiri kwa hamu tunakwenda kukamilisha meli yao.
MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kuna agenda ya Mtwara Corridor na tunapozungumza Mtwara Corridor tunazungumza bandari, tunazungumza Airport pia tunazungumza reli ya Liganga na Mchuchuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umekuwa ni wimbo toka mwaka 2020 mpaka leo hii Serikali kila ikija hapa wanasema ipo kwenye mpango. Tunataka sasa tufahamu ni lini sasa ujenzi wa reli hii ya Liganga na Mchuchuma.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, nafikiri Mheshimiwa Mtenga anataka kupata pengine ufafanuzi wa ziada. Nimekwishasema na naomba nirejee. Tulishaanza SGR ya kutoka Dar es Salaam kwenda mpaka Isaka, tumekwishaenda na SGR kutoka Dar es Salaam tumekwenda mpaka Kigoma sasa tunakwenda mpaka Msongati Burundi. Awamu inayofuatia Serikali ya Awamu ya Sita imejipambanua na imejiwekea malengo ya kwenda SGR Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimtoe mashaka uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita unakwenda kujenga reli ya SGR ya kusini ambayo ni Mtwara Corridor kama nilivyosema. Hii inakwenda kuungana pamoja na uboreshaji mkubwa wa Airport kama nilivyosema sambamba na uboreshaji mkubwa wa maeneo ambayo nimeyaeleza pale awali, kwa hiyo, nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge.
MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Serikali imekuwa ikitoa ahadi ya kujenga meli kwa ajili ya abiria na mizigo katika Ziwa Tanganyika ili kutatua changamoto ya usafiri katika Mikoa ya Kigoma, Katavi na Rukwa. Je, ujenzi huo utatekelezwa lini?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, siyo tu meli ya mizigo na abiria kama alivyouliza Mheshimiwa Mbunge. Serikali imesaini tayari mkataba, tumeanza kujenga kiwanda cha kutengeneza meli nyingi nyingi katika Ziwa Tanganyika. Ambapo kiwanda hicho kitahusika na kutengeneza meli za mizigo na abiria na kukarabati zilizopo, hili linakwenda sambamba na uboreshaji mkubwa wa meli ambazo zipo za akina Mwongozo, Sangala pamoja na kina Liemba kama ilivyoulizwa na Mheshimiwa Sylvia pale awali.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza niwapongeze Serikali kwa kujenga reli ya kisasa ambayo ya SGR kutoka Makutupora Tabora. Reli ile mpaka sasa hivi wamefukua makaburi ya watu wa Igalula, watu wa Goweko, Tula hamjawalipa mpaka leo. Je, ni lini mtawalipa fedha ambazo mliwarudishia msiba mpaka leo hamjawalipa kwa sababu reli inataka ipite?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, hii hoja ya Mheshimiwa Venant naomba niichukue tuifatilie halafu tuifanyie kazi baada ya kupata taarifa zake za kina.
MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali na nina maswali mawili ya nyongeza. Mchakato wa uboreshaji na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege Kilwa Masoko ni wa muda mrefu sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; nataka Mheshimiwa Naibu Waziri, awahakikishie Watanzania, Wanakilwa na Bunge hili, je, mpango wa Serikali wa uboreshaji na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kilwa Masoko bado uko pale pale?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Mheshimiwa Naibu Waziri amefika Kilwa Masoko mara kadhaa. Alifika mwezi Juni akiwa Mwenyekiti wa Kamati na akafika mwezi Agosti akiwa Naibu Waziri katika Sekta hii ya Uchukuzi na alikuja mahususi kwa ajili ya masuala haya ya kiwanja cha ndege.

Mheshimiwa Naibu Spika, pale kuna changamoto kadhaa, kwa wananchi wangu hawa 438 mpaka sasa bado hawajalipwa fidia. Je, yuko tayari sasa baada ya Bunge hili kwenda Kilwa Masoko akiambatana nami ili kwenda kusikiliza kero za hawa wananchi wangu 438?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. DAVID M. KIHENZILE): Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimpe uhakika Mheshimiwa Mbunge wa Kilwa Kusini kwamba, Serikali ya Awamu ya Sita inayo dhamira ya dhati ya kuboresha Uwanja wa Ndege wa Kilwa Masoko. Pia, hiyo inakwenda sambamba na uwekezaji mkubwa unaofanyika pale wa kujenga bandari kubwa kwa ajili ya uvuvi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namhakikishia kwamba mpango wa Serikali uko pale pale, mara baada ya wenzetu wa Wizara ya Fedha kukamilisha taratibu za ndani, fidia hiyo kwa wananchi hao itaanza kulipwa. Hilo moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili anauliza je, niko tayari kuambatana naye baada ya kumaliza Bunge hili. Amekiri mwenyewe nilikwenda pale pamoja na wenzangu nikiwa Mwenyekiti wa Kamati Kilimo na Mifugo. Vile vile, nimekwenda hapo juzi kukagua bandari hiyo na uwanja huo. Niko tayari kwenda pamoja naye ili tukawape uhakika wananchi hao ambao wanamwamini Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ili waendelee kujenga imani naye.
MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri mwenyewe kwamba, upembuzi yakinifu utakamilika Desemba, je, ni lini ujenzi utaanza rasmi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; je, ujenzi huo utazingatia kwa kiasi gani kuweka vifaa vya kisasa ili abiria wasikaguliwe na mbwa kama inavyofanyika sasa?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. DAVID M. KIHENZILE): Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kumhakikishia Mheshimiwa Ramadhan Suleiman Ramadhan kama nilivyosema hapo awali. Hatua ya kwanza ambayo Serikali inafanya ni kufanya uthamini au upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ambao utaweza kutusaidia kujua nini kinapaswa kufanyika. Pia, mara baada ya kukamilisha hatua hiyo, hatua itakayofuatia itakuwa ni kuanza kufikiria au kuanza mchakato kwa ajili ya ujenzi. Kwa sababu, Serikali imeendelea kufanya maboresho makubwa sana kwenye bandari zetu nchini ikiongozwa na Bandari yetu kubwa ya pale Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, namba mbili; kama nilivyojibu swali la kwanza, katika usanifu huu unaoendelea kwa ajili ya ghati letu jipya la Dar es Salaam, utaambatana pamoja na ufungaji wa mashine ya ukaguzi wa kisasa ambao utatumia teknolojia ya kisasa ya ukaguzi kwa ajili ya abiria na mizigo.