Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Abdi Hija Mkasha (1 total)

MHE. ABDI HIJA MKASHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina swali moja la nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni muda gani tangu Jeshi la Polisi lifanye tathmini ya ukarabati wa kituo hicho?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tathmini ilifanyika mwaka jana, 2023. Nami nimhakikishie Mheshimiwa Mkasha, kwa sababu, liko kwenye bajeti ya 2023/2024, mara fedha hizo ambazo tayari zimeombwa Hazina zitakapotoka, kituo hiki kitaanza kukarabatiwa. (Makofi)