Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Questions from Hon. Abdi Hija Mkasha (1 total)

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza:-

Je, lini Kituo cha Polisi Micheweni kitakarabatiwa ili kiendane na hadhi ya Wilaya?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abdi Hija Mkasha, Mbunge wa Micheweni, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Polisi ilifanya tathmini kwa ajili ya kubaini kiwango cha uchakavu na gharama za ukarabati wa jengo la Kituo cha Polisi Micheweni na kubaini kuwa jumla ya shilingi milioni 65 zinahitajika kwa ajili ya ukarabati huo. Fedha hizo zimetengwa kupitia Mfuko wa Tuzo na Tozo katika mwaka wa fedha 2023/2024. Mara fedha hizo zitakapopokelewa, zitatumwa katika kituo hicho ili ukarabati wake uanze kufanyika, nashukuru.