Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Khadija Shaaban Taya (14 total)

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020
MHE. HADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa nafasi hii. Ikiwa leo ni siku ya kwanza nazungumza katika Bunge lako hili tukufu naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu sana, mwingi wa rehema na mwenye kurehemu amenijalia mimi kuwa hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia naomba kumshukuru Mheshimiwa Rais na chama chake, Chama Cha Mapinduzi, Wajumbe wa Baraza wa Dodoma hii Mkoa, Wajumbe wa Baraza wa Taifa, Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Ndugu Heri James na Umoja wa Vijana na Wazazi wote ahsante sana, muda hautoshi kushukuru wote, lakini naomba niishukuru familia yangu sana kwa support kubwa ambayo wamenionesha mpaka sasa kufikia hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ikiwa leo ni siku saratani duniani, mimi kama mtu mwenye ualbino nimeomba niongee leo ili niwaambie umma kwamba Mheshimiwa Rais amefanya kazi nzuri sana kwa watu wenye ulemavu au watu wenye ualbino, amefanya kazi nzuri sana. Amenunua mashine ambazo zinasaidia kuondoa tatizo la saratani. Hizi mashine ziko saba katika mikoa ya Singida, Iringa, Mara, Lindi, Zanzibar na kwingineko, lakini naomba nimuombe Mheshimiwa Rais kwa huruma yake, kwa uwezo wake, kwa kupenda kwake wanyonge, aongeze hizi mashine zitapakae mikoa yote kwa sababu hizi mashine mimi ni shuhuda wa hizi mashine. Nilikuwa na alama hapa shingoni kwangu ambayo ingeweza kunisababishia kupata saratani, hii mashine imenisaidia mimi kupona leo hii ninavyozungumza hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia naomba Serikali yako tukufu, Serikali ya Chama Cha Mapinduzi, naomba kwa sababu ni sikivu sana, iongeze idadi ya lotions kwa watu wenye ualbino. Hizi lotions zinatusaidia sana kuondoa tatizo la kupata mionzi ya jua, hili tatizo ambalo linatufanya sisi tusiishi kwa amani tupate saratani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, natamani kila Mbunge aliyekuwepo hapa aende Ocean Road aone jinsi gani saratani ya ngozi inavyotumaliza na namna gani saratani ya ngozi inavyotuua. Na hata life span yetu ni miaka 35. Hapa nipo nina miaka 33 naingia miaka 34 tarehe 7 Februari, keshokutwa nashukuru Mungu kwa sababu familia yangu imeweza kunitunza na labda pia wamekuwa na uwezo kwa muda mrefu kunipa haya mafuta, lakini si kila familia ina uwezo wa kupata haya mafuta. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pamoja na yote haya naomba nimshukuru Rais mara ya mwisho kabisa. Nimwambie Mheshimiwa Rais ahsante sana kwa miaka mitano aliyoingia yeye ameondoa lile janga kubwa lililokuwa linaumiza Watanzania, lililokuwa linawaumiza na kuwaliza, lilimliza Waziri wetu Mkuu katika Bunge hili tukufu, janga la kuwauwa watu wenye ualbino. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, imani ile potofu imeondoka na sasa hivi tunaishi kwa raha, tunaishi kwa amani, tunajidai.

Ahsante sana Mheshimiwa Rais, lakini naomba nikwambie tena umejali sana watu wenye ulemavu, sasa hivi kila shule inajengwa kwa kuzingatia mazingira mazuri kwa watu wenye ulemavu kupita, lakini Mheshimiwa Rais pia nakuomba uboreshe mazingira ya vyoo kwa ajili ya afya. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. HADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba niunge hoja, naungana na hoja, ahsante sana. (Makofi)

SPIKA: Nimepata taabu kukatiza Mheshimiwa Keisha.

MHE. HADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, basi naomba niendelee.

SPIKA: Hapana, basi tena. Siku nyingine nitakufikiria leo muda umebana kidogo. (Kicheko)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022
MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kupata fursa hii leo kuchangia taarifa ya Kamati yetu ya Katiba na Sheria. Kwanza kabisa naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu ambaye amenipa uhai mpaka sasa, na jana nimeongeza mwaka mwingine, mwaka ambao mwaka umeinifanya nitafakari mambo mengi sana, leo hii nataka nizungumze na Bunge hili Tukufu lakini na Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu fika kwamba Tanzania yetu inachukua hatua mbali mbali za kusaidia watu wenye ulemavu. Nafahamu fika Serikali imeleta mwongozo mzuri juu ya kuimarisha, kusaidia hali ya watoto ya watu wenye ulemavu. Hata hivyo, naomba niliambie Bunge hili Tukufu hali ya watu wenye ulemavu ni ngumu zaidi kuliko tunavyofikiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika likizo ya ya mwezi wa 11 na wa 12, nilipata kufanya ziara kwenda katika vituo mbalimbali vya watu wenye ulemavu. Mambo niliyoyaona kule ni magumu sana hata kuayelezea. Mfano tu mzuri nichukue hapa Kongwa nilenda katika Kituo cha Mlali, nimekuta kuna watoto wenye ulemavu wa viungo wako pale wanalelewa na Kanisa Katoliki la pale Mlali. Hali niliyokuta pale inatia huruma sana sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watoto wamepelekwa pale kwa ajili ya kupata huduma ya afya ya kunyooshwa viungo mbalimbali lakini pia kupata huduma ile ambayo kuna madaktari wa KCMC na madaktari wengine kutoka nje ya nchi wanakuja pale kwa ajili ya kusaidia au wanajitoa. Wazazi wamekuwa wakipeleka watoto wao pale lakini wazazi wengine wameshindwa kwenda kuwaona watoto wao katika vile vituo kwa sababu kile kituo kina chaji shilingi 130,000 kwa ajili ya mtoto kupata huduma katika eneo lile. Sasa najiuliza, kwa Mtanzania wa kawaida anaweza kumudu hii shilingi 130,000 kwa ajili ya mtoto wake kupata huduma katika kituo kile? Mtanzania wa kawaida kila mwezi, 130,000 anaweza? Hilo ni swali la kujiuliza sisi Wabunge humu ndani ambapo katika maeneo yetu vituo kama hivi vipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuangalia tu, mzazi anayeshindwa kulipia hiyo anamwacha mtoto wake pale anaondoka harudi tena kumwona, watoto wanatelekezwa katika vituo vile kwa sababu huyu mzazi anaona fika kabisa kwamba mimi sina hii fedha, naendaje pale. Nitakabidhiwa huyu mtoto, nitawezaje kumhudumia? Ningeomba sana Serikali iangalie hili jambo kwa upande wa pili waone kabisa zaidi. Wazazi wanaozaa watoto, wenye watoto wenye ulemavu wanapata shida ngumu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka mama yangu aliwahi kuniambia wakati nazaliwa, kabla baba yangu hajaja kuniona hospitali. Kuna mtu aliwahi kumuuliza kwamba hivi, unafikiri Shabani ataweza kumpokea huyu mtoto? Atamkubali kweli? Hii ni changamoto ambayo wazazi wengi wanakutana nayo, lakini cha kushangaza baba yangu aliponiona alinifurahia na kunikumbatia na leo hii nimefika hapa nilipo. Kwa sababu familia yangu iliweza kunikubali na kunilea na leo hii mimi sijioni kama ni mtu mwenye ulemavu; na watu wengi humu ndani wananiambia kwamba wewe mbona siyo mlemavu? Ni kwa sabau nimelelewa vizuri na familia ambayo ilinikubali na changamoto zangu na kunilea hadi nilipofika hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tuangalie, ni familia ngapi zinamudu? Akina mama wengi wamekuwa wakitelekezwa na mababa kwa ajili ya kuzaa watoto wenye ulemavu na wanabaki na watoto wale wanawalea wenyewe. Wanapata shida nyingi mno. Leo hii Bunge hili, hapa akija mtu mwenye ulemavu wanatoa huduma ya msaidizi, kwa sababu wanafahamu fika kabisa huyu mtu mwenye ulemavua ana changamoto, hawezi kujihudumia mwenyewe lazima apate msaidizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tujiulize, yule mzazi ambaye yupo nyumbani, amezaa mtoto mwenye ulemavu, ni msaidizi gani, ni familia gani au ni ndugu ugani ambaye anaweza akakaa na huyu mtoto ambaye ana ulemavu atakulelea wewe? Ina maana huyu mzazi hana budi akae nyumbani, aweze kumlea huyu mtoto, amhudumie mwingine hawezi hata kujilisha mwenyewe. Hawezi hata kuoga mwenyewe. Je, Serikali inamfikiria vipi huyu mama ambaye hawezi kufanya shughuli nyingine zaidi ya kumlea mtoto wake?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilikuwa naona kabisa Serikali ione namna na haja ya kuona fika kabisa kwamba waone hawa wazazi either watafutiwe wasaidizi, kwamba Serikali ichukue jukumu la kulea au watafute namna ya kuwawezesha hawa wazazi waweze kupata fedha kupitia zile asilimia mbili. Asilimia mbili ile isaidie akina mama ambao wana watoto wenye changamoto ya ulemavu waweze kujikwamua kiuchumi ili tuone namna gani tuweze kuona hawa watu waweze kulea watoto wao, waone fika kabisa na wao ni part ya Tanzania hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mzuri upo pale katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Mtu mwenye ulemavu akifika pale anapata msaidizi kwa siku analipiwa shilingi 10,000. Anapata bajaji ya kwenda kumpeleka sehemu moja kwenda sehemu nyingine. Hivi vitu vyote tunafanya juu huku. Bunge linafanya, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kinafanya; lakini vipi huku chini kwenye ngazi ya familia? Kwa sababu kama huyu mzazi ameweza kutelekezwa na mwanaume kwa ajili ya kulea, ndugu pia wanaweza kuona kwamba huu ni mkosi kwenye familia yetu. Analeaje huyu mtoto?

Mheshimiwa Mwenyekiti, jamani, Bunge hili naamini kabisa, watu wote sidhani kama kuna mtu ambaye hajawahi kufuatwa na shida za watu wenye ulemavu; na ukiangalia fedha ya jimbo haiangalii kusaidia watu wenye ulemavu. Watu wanaingia kwenye mifuko yao kusaidia watu wenye ulemavu. Juzi tumepata takwimu ya sensa lakini bado majibu hatujayapata ya kujua idadi gani ya watu wenye ulemavu ambao wapo katika hii nchi ili Serikali sasa iweze kusaidia. Sasa tunahitaji zile takwimu ili tujue katika kila jimbo kuna watu wangapi wenye watoto wenye ulemavu wanawalea ili sasa Serikali ione haja na Bunge hili lishauri namna gani ya kusaidia hawa wazazi wenye hawa Watoto?

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii naamini kabisa jambo lolote likija whether kwa kukatwa tozo, whether kwa kukatwa mishahara yetu sidhani kama kuna mtu humu ndani ataweza kuwa na sauti ya kusema kwamba jambo hili hapana, wananchi watakasirika kwa ajili hawataki kuhudumia watu wenye ulemavu. Sasa hivi tumeona kabisa watu wanatafuta namna ya kujikwamua kiuchumi wanatumia watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kuna tamthiliya ya Juakali. Ukiangalia mazingira ya ile tamthiliya mule ndani Mtu ana NGO yake anaita watu wenye ulemavu anatengeneza story apate fedha halafu anajinufaisha yeye na familia yake. Yale ndiyo maisha halisi ya huku nchini, siyo tamthiliya ile. Kuna mzazi mwingine ana mtoto wake mwenye ulemavu amemficha ndani, anashindwa namna ya kutoka kwenye jamii, anaona ni aibu, anaona ni mikosi. Hivi vitu si kwenye tamthilia, ni maisha halisi ya Watanzania. Sasa Bunge hili lione namna halisi ya kusaidia watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi namshukuru sana Mheshimiwa Rais. Amekuja na huu mwongozo, ni mwanzo mzuri mno, Serikali mmeanza vizuri mno. Sasa kwa Serikali hii mama, kama Mheshimiwa Rais unanisikia, ninakuomba usije kuondoka katika Serikali hii kama haujatatua shida za watu wenye ulemavu kuona namna gani ya kusaidia. Kwa sababu ukiangalia idadi ya watu wenye ulemavu katika nchi hii ni wachache mno na Serikali hii ikiipa kipaumbele, hatushindwi kitu. Kuna kampuni nyingi tu ambazo zinafanya kazi katika nchi hii. Kuna fedha nyingi wanazo, CSR sijui nini na nini. Mfuko wa watu wenye ulemavu ni muhimu kulea watoto wenye ulemavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba Bunge hili Tukufu, endapo sheria hii itakuja muiunge mkono, kwa sababu naamini kila mtu hapa ni mlemavu mtarajiwa. Kwa sababu naamini kuna Wabunge humu ndani wamekuja wakiwa wazima na sasa hivi ni watu wenye ulemavu na leo hii sisi tuna watu tunawazaa humu ndani, tutazaa watoto wenye ulemavu. Leo hii tukitengeneza msingi mzuri au tathmini nzuri ya watu wenye ulemavu kuishi vizuri, tunajitengenezea sisi wenyewe na kizazi chetu cha baadaye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kusema hayo naunga mkono hoja nashukuru sana. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2021 (Toleo la Kiingereza)
MHE. HADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kupata nafasi hii ya kuzungumza leo mara ya pili.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikupe pole wewe pamoja na Bunge lako Tukufu na Wabunge wote kwa kuondokewa na kipenzi chetu, rafiki yetu, Mheshimiwa Nditiye.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesimama hapa mbele kuzungumza juu ya hii sheria ambayo imekuja kuhusu kutumia Kiswahili katika Mahakama zetu. Mimi naona umuhimu wa hili. Nitashangazwa sana kama kuna mtu ataona hakuna umuhimu katika hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimekuwa msanii kwa muda mrefu sana na katika tasnia ya sanaa, kikubwa sana kilichokuwa kinatufanya tupoteze haki zetu ni kwa sababu ya kutokujua lugha ya Kiingereza ambayo ndiyo ilikuwa inaandikwa katika mikataba yetu mingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, wengi sana wamepoteza haki zao, wengi sana wamepoteza uwezo, mpaka sasa ambapo tumeweza kuwa na uwezo wa kumiliki Wanasheria. Kwa muda huo tulikuwa hatuna uwezo wa kuwa na Mwanasheria, fedha hizo tulikuwa hatuna. Kwa hiyo, nafahamu umuhimu wa kutumia Kiswahili katika hizi Mahakama zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongee jambo lingine kwamba tulipopata safari ya kwenda China kupata mafunzo ya Chama cha Mapinduzi, nilipendezwa sana na tabia za Wachina. Vile vikao vilikuwa vinaendeshwa kwa lugha ya Kichina japokuwa wanajua kuzungumza Kiingereza. Wanazungumza Kichina, anatokea mkalimani anazungumza Kiingereza, halafu sisi mwenzetu anazungumza Kiingereza halafu anatafsiri kwa Kiswahili. (Makofi)

Mheshimiwa naibu Spika, kwa hiyo, tunatakiwa tutambue umuhimu wa hii lugha kwa sababu itatuletea heshima kama Watanzania. Watanzania wengi wanakwenda China wanafanya biashara na Wachina wengi wanakuja Tanzania wanafanya biashara pamoja na kutokujua lugha lakini wanafanya biashara. Kwa hiyo, naomba Bunge hili Tukufu liunge mkono hoja hii kwa kutambua umuhimu wa uzalendo wa nchi yetu na Mheshimiwa Rais ameonyesha uzalendo wa nchi yetu kwa kuzungumza Kiswahili katika vikao vyake vyote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hii hatua ambayo tunakwenda kutumia Kiswahili katika Mahakama zetu ni heshima kubwa sana kwa Tanzania. Kama kuna mtu ambaye hawezi kufahamu hili, namshangaa kwa nini amekuja kuwa Mbunge kwa ajili ya kuwawakilisha wananchi wake ambao wanazungumza Kiswahili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lugha ambayo tunatumia hapa Bungeni ni Kiswahili, nasi ndiyo watunzi wa hizi sheria. Kwa hiyo, nashangaa kwa nini mtu hawezi kuona umuhimu wa kutumia sheria ya Kiswahili au kutumia Kiswahili katika Mahakama zetu kwa ajili ya kutoa haki? Hatujakataza kutumia Kiingereza, endapo kutakuwa na uhitaji wa kutumia Kiingereza watatumia, lakini bado itatafsiriwa kwa Kiswahili ili iweze kutusaidia baadaye kwa ajili ya records. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naunga mkono hoja hii iliyoletwa na Mheshimiwa Waziri, kama Mwanakamati wa Katiba na Sheria na Mwanasheria mpya sasa. Nashukuru sana kwa kuchangia leo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Awali ya yote, naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu, Mola wa viumbe wote ambaye ametufikisha hapa leo tukiwa na afya njema na uhai ambao ametupa.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo napenda nijikite katika mambo mawili, matatu. Mojawapo nataka nizungumze juu ya watu wenye ulemavu na ajira. Katika kusoma na kufuatilia hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu nimegundua kwamba ni msikivu sana, amefanya kazi nzuri sana, amefanya kazi ambayo Mungu anamtaka yeye afanye. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati yetu ilishauri mambo kadhaa wa kadha lakini nashukuru moja ambalo umesema unaenda kulitekeleza ni hili la kuleta data kamili ya watu wenye ulemavu. Data kamili ya watu wenye ulemavu itatusaidia katika utekelezaji wa majukumu ya watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hiyo data kamili ya watu wenye ulemavu, kutakuwa na wasomi, wafanyakazi, watoto wadogo na wagonjwa ambao tutawatambua ili kutekeleza kwa urahisi kabisa malengo ambayo tumejiwekea kwa watu wenye ulemavu. Naomba niseme kwamba hali ya watu wenye ulemavu ni ngumu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niweke msisitizo katika suala la ajira. Namshukuru sana Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, ameendeleza yote mazuri yaliyofanywa na Awamu ya Tano. Katika kuchagua na kujali Makatibu Wakuu na Manaibu Makatibu Wakuu, amechagua watu watano katika Baraza la Makatibu Wakuu, hii pekee inaonesha dhahiri anatuamini sisi watu wenye ulemavu. Naomba Serikali iangalie suala hili kuanzia hapo, kwamba tumejaliwa watu watano wenye ulemavu basi ishuke mpaka chini kwenye watumishi ili tuweze kuonekana na kuonesha uwezo wetu ambapo tunaamini kabisa uwezo tunao.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia tuangalie lile suala la asilimia tatu, je, limetimizwa na kwa ukubwa gani? Kwa sababu nikiangalia private sector, hata humu ndani tu kuna Wabunge wana makampuni makubwa, je, wametimiza ule wajibu wa asilimia tatu? Hili suala tulifuatilie, tusiwe tunaweka sheria ambazo hatuwezi kuzifuatilia kama zinatekelezeka. Tuweke sheria ambazo tunaweza tukazifuatilia tukajua kabisa hii idadi ya watu wenye ulemavu ya asilimia tatu inatekelezwa Serikalini pamoja na private sectors. Kwa private sector, mtu amewekeza pale akiamini mtu mwenye ulemavu hawezi, basi tuangalie namna gani ya kuwapa hawa watu motivation au kuangalia namna yoyote ile hata ya kuwapunguzia kodi fulani hivi ambayo inaweza wao kuwafanya waendelee kuajiri watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nayasema haya kwa sababu nafahamu watu wanaoniomba kazi na wanataka ada ya shule na kadhalika. Kwa hiyo, hizi data zitatusaidia sana, nawaomba ushirikiano katika hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia naomba nishukuru baadhi ya Wabunge ambao tayari wameendelea kuzungumzia watu wenye ulemavu na wale ambao wameendelea kujitoa katika majimbo yao kama kutoa miguu kwa watu wenye ulemavu wa viungo, kwa mfano, namshukuru sana Mheshimiwa Antony Mavunde. Kwa hiyo, naomba Serikali iangalie watu wenye ulemavu kwa jicho pana zaidi. Kwanza, tupo wachache sana na sidhani kama Serikali hii chini ya Mheshimiwa mama Samia Suluhu Hassan itashindwa kulisimamia suala hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine nizungumze juu ya Jiji la Dodoma au Makao Makuu ya Dodoma. Sote humu ndani tunafahamu kwamba Bunge la Kumi na Moja liliazimia kuweka Sheria ya Makao Makuu, basi hii sheria isiwe tu kwenye makaratasi iendane na utekelezaji wake. Utekelezaji wake ni kuendelea kufufua vitu ambavyo vitaonyesha kweli hii ni Makao Makuu. Tuangalie Uwanja wa Msalato, ring road, upatikanaji wa maji. Hili la upatikanaji wa maji ni shida sana, kuna maeneo ambapo siku nne hakuna maji, tunaishije hapa na sasa hivi tuna kiwango kikubwa sana cha watu. Kwa hiyo, naomba sana Serikali hii itambue na iendeleze lile wazo la Mwalimu Julius Nyerere la kuhamia Dodoma ambalo lilitekelezwa Awamu ya Tano, tuendelee kutekeleza yale yote ambayo waasisi wetu wametuwekea katika mipango yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia niwashukuru Watanzania wote ambao wamejitokeza kwa wingi kuomboleza msiba wa kipenzi chetu. Hii imetuonesha kabisa kwamba Rais wetu alikuwa anakubalika, amefanya kazi kubwa kwa ajili wa Watanzania na kweli alikuwa ni Rais wa wanyonge. Kwa kuangalia hilo, naamini Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan Rais wetu mpendwa ataendeleza yote kwa sababu ni mwanamke shupavu na jasiri. Naomba wanawake wote tumsaidie kusimamia yale yote ambayo tumejiwekea katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa haya machache niliyozungumza, naunga mkono hoja hii ya Waziri Mkuu. Ahsante sana. (Makofi)
The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No. 3) Bill, 2023
MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii kuchangia Muswada huu. Kwanza naomba niungane na wenzangu kuwapongeza Mawaziri wote walioteuliwa, sana sana Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu. Lakini vilevile nimshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuzidi kuwaamiani vijana katika majukumu makubwa kabisa ya nchi hii. Hii inaongeza chachu lakini inatupa moyo sana vijana, pia inatuamsha kuona kwamba tunaweza kushika nafasi kubwa especially ukimtaja Mheshimiwa Juduth Kapinga, kwa kweli hongera sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama unavyofahamu tuko hapa kwa ajili ya kubadilisha sheria tukiamini kwamba hizi sheria zinaenda kufanya kazi. Kwa hiyo kama sheria haitoweza kwenda kufanya kazi maana yake lengo kuu lazima tubadilishe au turekebishe ili tuweze kusaidia wananchi au tusaidie jamii yetu. Mheshimiwa Rais ameona fika kabisa, na juzi amebadilisha Mawaziri na ameweza kubadilisha Wizara na kutengeneza Wizara mpya ambayo ni Wizara ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji. Hii Wizara imepewa majukumu makubwa sana ya kufanya. Lakini kama unavyoweza kuona kwamba kuna baadhi ya majukumu yalikuwa yamebakia katika Wizara ya Viwanda na Biashara sasa leo hii wameona kuna umuhimu wa kubadilisha kuona EPZ ihamie kwenye Wizara ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu sote kwamba EPZ ni sheria ya uwekezaji ya masuala ya mauzo ya nje ya nchi. Kwa hiyo Mheshimiwa Rais anauwezo wa kuipeleka hii sehemu yoyote, na ndio maana lengo la Sheria hii kubadilishwa ni ili iweze kwenda katika Wizara nyingine yoyote. Kama leo hii EPZ ikiamua kwenda Wizara ya Viwanda na Biashara basi iweze kufanya kazi, ndilo lengo kuu la mabadiliko ya sheria hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba sana nimpongeze Mheshimiwa Rais, na pia niipongeze Serikali kwa kutuletea sheria hii ambayo inatupa flexibility, kwamba hatutakuwa tunabadili mara kwa mara; leo hii EPZ imeenda Wizara nyingine basi tubadilishe sheria kupeleka Wizara nyingine, lakini inatupa uwanja mpana wa kusema sasa EPZ ipo wizara fulani basi sheria hii iweze kwenda vizuri na iweze kwenda kufanya kazi katika Wizara yoyote ile.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kwa mabadiliko hayo tunaomba tuipongeze Serikali lakini tupongeze pia Kamati, kwa sababu Kamati katika mchango wake iliona pia kuna pengo la Katibu Mkuu kutokuwepo katika Kamati hii ya EPZ Katibu Mkuu wa Wizara rasmi, hivyo basi Serikali imetuahidi kwamba itaweza kuleta marekebisho mengine ambayo haya marekebisho yataweza kuja kusaidia ili Katibu Mkuu wa Wizara hii ambaye ndio permanent secretary wa Waziri aweze kujua vizuri masuala yote ya EPZ kuliko kwenda kumchukua Mheshimiwa Waziri awe kila siku anampelekea taarifa ya kikao cha Kamati ambayo mambo ambayo yameelezewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa kusema hayo nashukuru kwa kutoa mchango wangu huu, ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Awali ya yote naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu, Mola wa viumbe wote ambaye amenipa uhai wa leo hii kusimama leo na kuzungumza sekta yangu na sekta ya maisha yangu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii naomba nizungumze na umma huu wa Wabunge pamoja na Taifa hili. Sanaa ni maisha yetu vijana na kama Serikali ina mpango mzuri wa kuongeza ajira kwa vijana basi sanaa ni sehemu nzuri sana ya kuongeza ajira. Msanii kama msanii anayeimba, kuna anaye-produce, kuna director, kuna mpiga picha, kuna kila aina ya kazi, sasa hivi hadi mabaunsa wamekuwa wanaajiriwa kupitia sehemu ya sanaa. Kwa hiyo sanaa ni jambo muhimu sana na tukilizungumza hapa tuzungumzie kwa u-serious wake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende moja kwa moja kwenye upande wa mirabaha; mirabaha kwa wasanii ni jambo la muhimu sana, leo hii Keisha nitazeeka, siasa nitastaafu, lakini kupitia hii mirabaha tutaweza kupata pesa mpaka tunakufa na watoto wetu wataendelea kula hela, kama ambavyo mimi sasa hivi bado naendelea kula hela ya muziki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hii hela ya muziki tunayokula, tunakula kupitia caller tune, ringtones, lakini tunataka COSOTA wasimamie mirabaha. Hii mirahaba itatusaidia sisi ku-generate lot of money, yaani pesa nyingi sana ambazo hizi pesa zitatusaidia sisi wasanii kutengeneza kazi zenye ubora ili tuweze kushindina kimataifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mirabaha ninayoizungumiza hapa kuna sehemu za starehe nyingi sana ambazo wewe huwezi kwenda kwenye starehe kama hauwezi kusikiliza muziki, kwa hiyo mirabaha hii tunayoizungumza sehemu za starehe, sehemu za mabasi, sehemu za hotels hawawezi kupiga muziki wetu bila kulipia pesa, ina maana tunapata pesa nyingi sana, lakini vilevile na Serikali inakusanya mapato mengi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kuna mapato mengi ambayo yanakosekana kwa Serikali kwa sababu ya kutokusimamia vizuri mirabaha ya wasanii katika hii nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine naomba nizungumze juu ya masuala ya maadili, mimi ni mfuasi mzuri sana wa maadili ya wasanii. Ni mfuasi mzuri sana na ni mfano mzuri sana kwa maadili ya wasanii. Leo hii mimi nisingefika hapa kama ningekuwa sina maadili, lakini maadili gani tunayozungumza hapa, maadili ya kufungia nyimbo za wasanii bila kujua hawa wasanii wanatakiwa waimbe nini?(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ningeomba Wizara iwaite hawa wasanaii, ikae nao, iseme wanataka nini katika hizi kazi, lakini siyo wasanii peke yao hata hivi vyombo vya televisions, media zote wawaite, media ziambiwe ni nyimbo gani na nyimbo gani zinatakiwa kupigwa kwa muda gani, kwa sababu kuna muda ambao Watoto wamelala, hawasikilizi nyimbo zingine, lakini kuna hata kwa hawa watu wa filamu wanaigiza filamu na zinawekwa masharti pale chini ya miaka 13 hapaswi kuangalia hii filamu, chini ya miaka 18 anapaswa kuangalia, hivyo, kwa hiyo tuweke utaratibu ambao hawa wasanii watajua ni namna gani wao wanapaswa kuongoza kazi yao ili waweze kufanya kazi zao za sanaa kwa uhuru vizuri. Kwa sababu mwisho wa siku utamfungia huyu msanii ana familia yake, ana maisha yake, ana ndugu zake wanamtegemea hebu tuangalie hili suala kama Wizara ione namna gani ya ku-deal na wasanii katika masuala haya especially masuala haya ya maadili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimefurahi sana kuona kwamba katika hii hotuba ya Waziri imezungumza kuhusu masuala ya tuzo. Tuzo ni muhimu sana, mimi nimekuwa msanii kwa kipindi cha muda mrefu na nimekuwa nimeshika tuzo mbili za mwanamuziki bora wa kike Tanzania, lakini nimeshika tuzo ya albamu bora ya Zuku. Hizi tuzo zilinifanya mimi niwe motivated kufanya kazi sana. Kwa hiyo leo hii kama Wizara imeona umuhimu wa kuanzisha tuzo hizi basi ione umuhimu wa kuruhusu tuzo zingine za watu wengine kuendelea kufanya kazi kuliko kuwawekea vizingiti vingi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii mtu akianzisha tuzo anaambiwa kipengele fulani usiseme, kipengele fulani usiseme, sasa hizi tuzo zitaendeshwaje, hizi tuzo mnataka ziwe nyingi ili zi-motivate wasanii wetu. Wasanii wapo kila sehemu na wanafanya vizuri na kila msanii ana ubora wake na katika kazi yake.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikwambie jambo moja ambalo wasanii wanahangaika, wasanii wamepata bima za afya, lakini wasanii wanataka bima ya maisha. Tunashukuru sana Wizara, wameweza kutuwezesha kupata bima za afya, lakini wanataka bima za maisha ili wajihakikishie maisha yao hawa wasanii, tunaomba sana sana hili jambo liendelee, liwekwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile naomba pia nizungumze juu ya masuala ya maadili ya mavazi, hili suala jamani naomba sasa Serikali ituambie ni mavazi gani msanii anapaswa avae. Je, akienda kufanya video kwenye swimming pool anatakiwa avae baibui au nikabu? (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, tujiulize ni mavazi gani haya ambayo yanahitajika kwa wasanii wavae? Je, tuangalie asili ya Mtanzania vazi lake ni nini? Turudi tena huko kwenye tamaduni zetu, tuangalie Mtanzania anapaswa kuvaa nguo ya aina gani, ili akifikisha ujumbe ajue anafikisha ujumbe kwa namna gani. Wenzetu tunawaona nje wanavaa swimming costumes kwenye swimming pool kwa sababu ndivyo utamaduni wao unavyosema. Basi na sisi tuangalie kwenye swimming pool tuvae nini, tuvae nikabu au tuvae skin tight au tuvae nguo gani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili ni suala la uhalisia, leo hii tutawalaumu wasanii wanaenda kurekodi nje South Africa wapi, kwa sababu wanafuata facilities, hizi facilities zinawasaidia wao kuonesha uhalisia katika kazi zao. Sasa leo hii kama facilities hapa Tanzania haturuhusiwi kutumia nguo za polisi, haturuhusiwi kutumia sijui mahakama, sasa tutafanyaje kazi kama wasanii? Uhalisia utatoka wapi? Tutashindana vipi kitaifa na kimataifa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunamshukuru sana Diamond kusema kweli, Diamond anatuwakilisha vizuri sasa hivi Diamond anagombea tuzo ya BET. Ningeomba Wabunge wote hapa wam-support Diamond kwenye ma- group yao ya maeneo yao wapige kura kwa ajili ya Tanzania. Diamond hayuko pale kwa sababu ya Diamond au kwa ajili ya Wasafi au kwa sababu ya Babu Tale hapana, Diamond yuko pale kwa ajili ya Watanzania na anawawakilisha Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, basi naomba Bunge hili wahamasishe wananchi wao huko wanakoenda, wampigie kura Diamond aweze kuleta tuzo hii Tanzania proudly kabisa na sisi tuone kwamba tumepata hii tuzo ya mwanamuziki ambaye anaiwakilisha vizuri Tanzania hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kusema hayo machache na Bunge lako hili Tukufu, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Lakini naomba niunge mkono hoja endapo haya mambo yatatekelezeka, lakini nilisahau jambo moja la mwisho samahani kweli muda wangu haujaisha. Kuna suala hili la arena. (Makofi/Kicheko)

NAIBU SPIKA: Kengele imeshagonga

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, arena arena arena, Babu Tale umesahau kuwaambia kwamba…

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Keisha muda wako umekwisha.

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kupata nafasi hii kuchangia leo katika Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Kwanza kabla ya yote naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu kutujaalia uhai.

NAIBU SPIKA: Ndiyo wewe au?

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya, leo hii nimesimama hapa kuchangia masuala ya elimu juu ya watu wangu ambao wamenileta hapa Bungeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Rais, sana sana. Mama jana tumekusikia umezungumza kama Mama tena Mama yule ambaye ana viakiba vyake yupo tayari watoto wake wale hata ugali na mlenda kuliko kushinda na njaa. Kwa hiyo, tayari tumeona namna gani Mama anaguswa na Watanzania na wanyonge na tunakupongeza sana Mama, tunakupongeza sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie leo kwenye hii Elimu, Sayansi na Teknolojia juu ya masuala ya vipaji. Mimi ni muumini wa vipaji, kwa sababu nimepata kipaji changu, nilikuwa na kipaji changu lakini nimeendelezwa kupitia Shule ya Msingi. Nimefanya bands, nimefanya kwanya, nimeimba na nimefanya vitu vingi sana mashindano ya kwaya, bendi yakanijengea uwezo. Kwa hiyo ninaamini kabisa Wizara ya Elimu ikiangalia namna hii ya kuweza kukuza vipaji vya watu, leo hii tusingewaponda akina Diamond na wengine kwa sababu shamra shamra za shuleni za mashuleni zile za mashindano ya waimbani na vitu kama hivyo.

Kwa hiyo, naamini kabisa, Wizara ya Elimu ikiangalia namna hii ya kuweza kukuza vipaji vya watu, leo hii tusingewapata akina Diamond akina nani kwa sababu ya ile shamra shamra za shuleni zile za mashindano ya waimbaji ya nini na vitu kama hivyo. Kwa hiyo, naamini sio kipaji kimoja tu tunaweza tukakipata shuleni vipaji vingi tu tunaweza tukatengeneza watu wengi tu wacheza mpira, michezo, everywhere, kila sehemu tunaweza tukapata watu wa kuweza kuwakilisha hii nchi, lakini pia kuinua uchumi wa hii nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ni muumini wa vipaji kwa sababu pia itaacha haya mambo ya kukaa vijiweni kuvuta bangi, kuvuta unga na panya road. Vipaji vitakuzwa kimaadili zaidi, tutaona kabisa umuhimu wa vile vipaji ambavyo tunavitengeneza kuanzia chini mpaka kwenda juu. Kwa hiyo, naiomba Wizara hii iangalie hilo kurudisha mambo ya muziki shuleni, mambo ya mpira michezo na vitu kama hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, cha pili naomba nichangie juu ya masuala ya lugha ya alama mashuleni. Juzi nimesema tunahitaji lugha ya alama mashuleni, ni muhimu sana. Tunafahamu kabisa lugha ni mojawapo ya sehemu ya mawasiliano, hatuwezi kuelewana kama hatutumii lugha ambayo tunaweza tukaelewana. Naomba tu niwaulize Wabunge leo hii Wabunge nyinyi humu ndani mnawawakilisha wananchi, watu wenye ulemavu huko chini katika Majimbo yenu, hivi ni wangapi humu ndani wanafahamu lugha ya alama ya kuwasiliana na viziwi? Wangapi?

Mheshimiwa Naibu Spika, ni wachache sana, kama wapo basi ni mmoja, wawili au watatu, mimi mwenyewe sifahamu lugha ya alama na huwa najisikia vibaya sana. Kwa hiyo, ningeomba Wizara pia ilete semina hata ya wiki moja tufahamu tujifunze lugha ya alama, tujue numbers tujue vitu basic ambavyo vinaweza vikatusaidia kuwasiliana na hawa watu wasijione kama wanatengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo mpiga kura wako akija kwako anataka kuzungumza na wewe hawezi kuzungumza naye. Gharama za mkalimani ni kubwa sana, hawezi kumudu muda wote akawa anatembea na mkalimali ili akuelezee shida zake. Kwa hiyo, tunaamini kabisa watoto wetu mashuleni wakianza kujifunza lugha ya alama ina maana hata watu ambao wamezaliwa wana ulemavu wa kutokusikia, tayari itawasaidia wao. Kwa hiyo, naomba Serikali iangalie hili ni muhimu mno mno, ni muhimu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, cha mwisho, naomba nichangie juu ya masuala ya elimu jumuishi, tunafahamu tuna Walimu katika mashule ya elimu jumuishi. Tunafahamu kwamba hawa Walimu wengine ni wachache mno, lakini wengine pia wame-specialize kwenye area moja lakini sasa kwa sababu tu ni walimu wa elimu jumuishi, wanakwenda mashuleni wanafundisha kila mtoto ambaye ana matatizo ya ulemavu, hapana. Tunatakiwa tujue kabisa huyu mwalimu ame-specialize kwenye viziwi peke yake, huyu mwalimu ame- specialize kwenye ulemavu wa akili, huyu mwalimu ame- specialize kwenye area hii na hii na hii. Kwa hiyo, tujue namna gani hawa watu wanaweza wakatusaidia tuongeze Walimu ambao wamebobea katika sehemu mbalimbali ili tuweze kuwafundisha hawa watu na vile vile kuwatengenezea mazingira mazuri ya wao kuishi katika hii dunia.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpongeze mama katika area moja. Ameongeza vyuo vya watu wenye ulemavu sasa hivi vimeongezeka. Katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, amesema vyuo vilivyoongezeka kule Singida kesho kutwa tunakwenda kuzindua Tanga. Hii tayari ni hatua nzuri sana ambayo Serikali imefikia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi vyuo tuvitumie hivi vyuo viende kuamsha/kuondoa umasikini wa watu wenye ulemavu tuwatengenezee elimu, lakini pia tuwape nyanja tofauti tofauti tuwatengenezee ubora na uwezo ambao wanaweza wakafanya. Hivi leo hii wanaonaje Serikali wakawafundisha hawa watu wenye ulemavu ambaye yeye labda hawezi kutembea, tukamfundisha kutengeneza bahasha tu hizi, halafu leo tender za hizi bahasha tukazichukua kwa watu wenye ulemavu, ndio tukawa tunawalipa wale watu wenye ulemavu, hatuoni kama tutakuwa tumewasaidia hawa watu wenye ulemavu? Kwa hiyo, naomba Serikali itafute namna gani ya kuondoa umaskini wa watu wenye ulemavu, watu wenye ulemavu ni maskini sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumze, hawa watu ni masikini sana, kwa sababu kama mtu tu ana miguu yake na mikono yake na maisha ni magumu, fikiria mtu ambaye hana miguu, hana mikono, hawezi kusikia, ni namna gani ambavyo anaishi au na wale pia familia ambayo inawalea wanashindwa kuwalea vizuri. Kwa hiyo, naomba Serikali inapokuwa inafikiria mambo yake ya kimaendeleo, mambo ya kielimu, iangalie sana kundi hili ni muhimu mno. Mmii ni sauti ya watu wenye ulemavu hapa Bungeni, nitazungumza kila siku na mtanichoka lakini naomba Serikali iangalie namna gani ya kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kusema hayo machache naunga mkono hoja na nashukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Afya
MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kupata nafasi hii tena katika Wizara ya Afya kuchangia mambo mbalimbali. Kwanza naomba nikupongeze sana dada Ummy, Mheshimiwa Ummy anafanya kazi kubwa sana ndio maana leo hii Mheshimiwa Rais amemrudisha hapo, ameona kazi ambayo ameifanya. Leo hii anawasikia Wabunge wengi wakiomba vifaa tiba kwa sababu tayari kuna majengo, kwa hiyo Mheshimiwa Rais pamoja na Mheshimiwa Waziri wamefanya kazi kubwa sana kuleta fedha za UVIKO kujenga vituo vya afya vingi na ndio maana leo hii tunaomba vifaa tiba kwa sababu tunayo tayari majengo ambayo yanaenda kufanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitakuwa mchoyo sana wa fadhila leo hii kama sitomshukuru Mheshimiwa Rais, kwa sababu Mheshimiwa Rais ni msikivu mno, mwaka jana nilisimama hapa ndani nilizungumza sana kuhusu masuala ya mafuta kwa ajili ya watu wenye ulemavu. Leo hii nasimama hapa kwa kujidai kwamba Mheshimiwa Rais amesikia kile kilio chetu. Aliwaita watu wenye ulemavu Ikulu na akaelekeza Wizara ya Mheshimiwa Ndalichako kwa ajili ya kutenga bajeti ya watu wenye ulemavu, ya kununua mafuta Sh.60,000,000. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naamini hii bajeti ya Sh.60,000,000 kwa mwaka 2022/2023, itaongezeka kutokana na idadi tutakayopata kutokana na sensa. Tukishafanya sensa tutajua idadi kamili ya watu wenye ulemavu wa ngozi ili tuweze kupata mafuta yanayotosheleza kabisa, lakini kwa kianzio tumeanza vizuri, Sh.60,000,000 imetengwa na utaratibu mzuri sana utafanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia naomba nimshukuru Mheshimiwa Rais kwa kufanya mabadiliko ya MSD. MSD leo hii tumepata kiongozi mwingine mpya na leo hii kila mtu anasifia MSD, lakini naomba niwaambie MSD jambo moja, wasijisahau na hizi sifa. Hawa hawa watu leo hii wanaowasifia kesho watawasema humu ndani mtawashangaa. Kwa hiyo, kwa makosa ya huko nyuma waangalie kitu gani wenzao walikosea na wao wajitengeneze kwa namna gani ili waweze kuboresha. Tunawaamini sana MSD na sisi, wao ni kimbilio letu kwa sababu sisi tunawawakilisha wananchi, kwa hiyo wao ni kimbilio letu sisi. Kwa hiyo, tunawaomba sana sana katika jambo hili waangalie sana maslahi ya wananchi zaidi.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo hii pia nina maombi kadhaa kwa Wizara hii ya Afya; leo namwomba Mheshimiwa Ummy, kuna jambo hili la mashine kwa ajili ya kuzuia kansa. Wanasema kinga ni bora kuliko tiba. Nawaambia kweli humu ndani Wabunge hawajawahi kuona mgonjwa wa kansa mtu mwenye ulemavu wa ngozi au mtu mwenye ualbino na kama wakitoka hapa wakaenda ocean road wakaona wagonjwa wa kansa watanielewa kwa nini kila siku nikisimama hapa nazungumzia suala la kansa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hivyo, basi naomba hizi mashine zilizopo ziongezwe zipo kwenye mikoa saba, basi tuone namna gani ya kuongeza hizi mashine ili kila mkoa wapate hizi mashine, wasiweze kusafiri kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine kwa ajili ya kuzuia saratani ya ngozi. Pia naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Ummy amefanya kazi nzuri sana. Leo hii nimefurahi mno, nimefurahi sana sana kwa kuona kwamba kitengo cha mionzi kinahamia Dodoma. Kwa hiyo sasa Dar es Salaam pale ocean road kipo kitengo cha mionzi, lakini pia Mwanza pale kipo na sasa hivi Dodoma kipo, ina maana itawasaidia watu wanaotoka Singida, Manyara, Arusha hawatoenda mbali sasa hivi watakuja hapa Dodoma kwa ajili ya kupata mionzi kwa ajili ya saratani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimwombe pia jambo lingine Mheshimiwa Ummy, namwomba sana kitengo cha afya, huduma za afya kwa watu wenye ulemavu namwomba sana, leo hii tunazungumza kuhusu suala la afya ya akili, sisi walemavu mimi mwenyewe nawezakana sina afya ya akili, kwa sababu tukiudhiwa tunakasirika haraka sana, tuna mambo mengi sana ambayo yametuzonga, hiki kitengo kitatusaidia sana kwa huduma zake kwa ajili ya kushauri. Kwa hiyo naomba huduma ya utengemao ili iweze kutusaidia sisi tuweze kufanya majukumu yetu vizuri. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hayo machache, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo
MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata fursa hii kuchangia katika Wizara hii ambayo na-declare interest kwamba nahusika, mimi ni mdau mkubwa wa hii Wizara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa sababu katika Wizara ambayo anaonyesha mapenzi ya dhati kabisa, kuwapenda kabisa ni Wizara hii. Ndiyo maana sasa hivi naona hamasa kubwa katika hii Wizara, tayari ameishaonesha dira kabisa kwamba hii Wizara ni watoto wangu, wanahitaji kulelewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tayari Mheshimiwa Rais ameshaonesha dhamira ya dhati katika Wizara hii, Mheshimiwa Waziri na Waheshimiwa Wabunge waanze kuangalia Wizara hii kwa mnajili mpya kabisa, tukianzia hasa kwenye masuala ya bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri. Kusema kweli, mimi ni kati ya watu ambao nilishangaa kumwona Bakhresa amekuja kwenye hii Wizara, Mama ana jicho la mbali sana, lakini naanza kuona sasa namna gani umeanza ku-cope vizuri na wanasanii na wanamichezo. Tayari tunaanza sasa kuona siku ile kwenye Tuzo tulikuwa tunacheza sana pale, tunaanza kuona sasa Wizara imempata mtu ambaye anaweza akaifanyia kazi vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumpongeze Mheshimiwa Rais pia kwa kumchagua kaka yangu Kipenzi Mheshimiwa Hamis Mwinjuma tayari huyu ambaye ana-idea anajua kabisa, anajua shida na chnagamoto za Wizara hii naamini kabisa kwa sababu yeye ni mwanamichezo lakini pia ni mwanamuziki ataenda kuleta ukombozi katika wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumzie suala la bajeti. Kwa kuangalia zamani wakati nasoma tulifundishwa basic needs katika maisha na wakawa wanasema kwamba malazi, mavazi, usafiri ikawa ni kitu kama luxury sasa hivi usafiri siyo luxury tena ni lazima. Leo hii katika hii wizara tunaangalia kama entertainment kwamba hii Wizara ni kwa ajili ya entertainment hapana siyo kweli. Hii Wizara inaenda kuwa mkombozi mkubwa wa kupunguza ajira katika nchi hii. Kwa namna gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii Wizara ikiweka mikakati mizuri kama ambavyo alivyoweka mikakati kaka yangu Bashe katika BBT. Hii Wizara italeta heshima ya kupata bajeti kubwa sana na kuweza kuendeleza Wizara hii katika uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu niambie Waheshimiwa Mawaziri hao wawili ambao tayari wamepewa dhamna katika wizara hii muhimu sana katika nchi yetu waangalie namna gani ya kuja kuwa–convince wabunge hawa waangalie mikakati gani waipange katika nchi hii, ili iweze kuondoa hii isuue ya bajeti. Leo hii bilioni 35 ni bajeti ndogo sana, ni bajeti ya aibu najisikia vibaya kwa sababu hii wizara ambayo inanihusu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi Mheshimiwa Rais Wizara hii imeweza kutoa mikopo kwa badhi ya wasanii mnaweza kuona namna gani Mheshimiwa Rais anaipenda hii wizara, lakini leo hii Wizara ina bajeti ya bilioni 35, nazungumza hapa wasanii wakiwepo pale, nazungumza hapa wanamichezo wako humu ndani bilioni 35 inaenda kusaidia kitu gani katika hii Wizara? Tuangalie namna nyingine ya kufanya uwekezaji katika Wizara hii ili iweze kusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine Mheshimiwa Waziri mimi ni mmoja ya watu ambao tulikuja kwenye tuzo za wanamuziki pale the The Dom Masaki. Mheshimiwa Waziri na Wizara yako naomba niwapongeze sana mwaka jana hii shughuli imeanza na sasa hivi mwaka huu mmefanya kazi nzuri sana, lakini naomba niulize au niwaambie ni namna gani ya kufanya kwa namna moja ama nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri umewaandalia wasanii tuzo. Wasanii hawa ambao wameandaliwa tuzo. Tuzo zinatangazwa pale kwa ajili ya wasanii kupewa tuzo hawapo na wengine hawajaandaa hata wapokeaji wa tuzo hizi sasa unajiuliza ni kwamba lack of coordination ama ni shida iko wapi? Je, wasanii hawajazipokea hizi tuzo ama Mheshimiwa Waziri na jopo lako hamjaweza kuzitangaza hizi tuzo vizuri au kuwapa tarehe nzuri ya kujua tuzo ni tarehe fulani na wasanii wote wanapaswa kuwepo. Mimi sijawahi kuona huko nje kina Beyonce wakakosa kwenye tuzo, sijawahi kuona kina Rihanna wakakosa kwenye tuzo, kwa sababu ndiyo sehemu pekee ya kuonesha appreciation ya kazi yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii unaenda pale unakuta nusu ya wasanii ambao wanaenda kupewa tuzo hawapo hii inaondoa hamasa na Ladha ya tuzo zetu za Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri tafuta namna ya kukaa na wasanii wako. Wasanii ni wasikivu na wanakuheshimu, wanaheshimu Serikali ya Mama Dkt. Samia Suluhu Hassan. Fanya warsha mbalimbali, fanya semina mbalimbali, waelimishe mambo ambayo unataka kuwafanyia, waoneshe njia waoneshe upendo. Nina uhakika hao wasanii wako watakuwa wanashiriki kila tukio ambalo wewe na Wizara yako inaandaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu mimi nilijisikia vibaya naona hadi wasanii ambao juzi tu wametoka eti na yeye hayupo. Ukiuliza yuko wapi? hujui. Yaani haijulikani yuko wapi nasema sasa hii tuzo ameandaliwa nani? Kama siyo wasanii. Kwa hiyo, tuangalie either kama shida iko kwa wasanii basi zungumzeni nao, lakini kama shida iko kwene menejimenti ya Wizara basi fuatilieni hili jambo mjue namna gani ya kuweza kwenda kusaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu nataka nizungumze kuhusu mmomonyoko wa madili. Naisema huku kwa sababu wizara hii au tasnia hii ni sehemu mojawapo ya mmomonyoko wa maadli katika Tanzania yetu. Nasema hivi kwa sababu nimetokea huko nafahamu vizuri jinsi gani mtu anaona kwa namna moja au nyingine kwamba ili mimi niwe msanii lazima nivute bangi, ili niwe msanii lazima ninywe madawa ya kulevya, ili niwe msanii lazima ninywe pombe, ili niwe msanii lazima nicheze uchi yaani kuna vitu vingi sana katika wizara hii ambavyo Mheshimiwa Waziri kwa weledi wako, kwa muonekano wako, kwa namna yako na uzoefu wako utawaweza Kwenda kuvifanyia kazi, ili hii wizara au hivi vipaji wazazi huko nyumbani waweze kuruhusu watoto wao kutaka kuwa wasanii tulinde utamaduni wetu. Tulinde asili yetu tulinde utanzania wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la utamaduni unaweza ukaona sasa hivi dunia ilivyo badilika masuala ya utandawazi mambo yamebadilika. Watu tumepita kwenye phases za kubadilisha nywele, phases za kuweka kope za kujichubua…

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. KHADIJA S. TAYA: …lakini sasa hivi kuna phases ambayo ni mbaya sana ya kubadilisha maumbile.

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. KHADIJA S. TAYA: Tunabadilisha maumbile yetu leo hii huyu mtu mwembamba hana shape lo hii kesho kutwa unamuona ana shape kubwa sana.

MWENYEKITI: Ahsante muda wako…

MHE. KHADIJA S. TAYA: Kwa hiyo naamini hii Wizara ya kuelimisha vijana wetu, watu wetu…

MWENYEKITI: Muda wako umeisha Mheshimiwa Khadija, ahsante sana.

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa fursa hii lakini Serikali iangalie namna gani ya kusaidia vizazi vyetu Tanzania inaenda kunagamia kwa namna hii. Ahsante sana nashukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo
MHE. KHADIJA S. TAYA: Bismillah Rahman Rahim.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kupata nafasi hii. Kwanza naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu ambaye amenipa leo afya njema ya kusimama katika Bunge lako tukufu kuzungumza masuala ambayo yanaenda kustawisha maisha ya vijana wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Rais sana na siyo kinafiki. Tuzungumze ukweli, Royal Tour siyo kitu ambacho kinaenda kunufaisha utalii peke yake, Royal Tour inaenda kunufaisha wasanii wa Tanzania hii. Mama alipoenda Marekani, alitembelea Paramount Studio. Katika hii studio amezungumza na watu masuala ya kuwekeza Tanzania kupitia hiyo hiyo Royal Tour.

Mheshimiwa Naibu Spika, mama alipoenda Los Angeles amekutana na wadau zaidi ya 15. Hawa wadau wamejadili mambo tofauti tofauti, wanakuja hapa Tanzania na amezungumza nao kabisa kuhusu fursa zinazopatikana hapa nchini. Leo hii mama anatuletea wasanii wakubwa ambao wanaweza kutuletea maendeleo katika hii nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiachana na hayo, mama pia katika mtu ambaye ametengeneza hii Royal Tour anaitwa John, yule jamaa Producer, amekuja Tanzania, amezungumza na wasanii, amefanya kikao na wasanii tarehe 29 Aprili, ameona changamoto gani ambazo wanapitia na kadhalika ili waboreshe kazi zao katika maeneo tofauti tofauti. Mama anaupiga mwingi sana. Jiulizeni sisi tunaupiga wapi? Umeuliza swali zuri sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuipongeza timu ya Serengeti Girls na pia niipongeze timu ya Tembo Warriors. Pia naomba niwaambie kwamba tunahitaji timu za makundi maalum ziendelezwe vizuri. Tunahitaji timu hizi za makundi maalum waanze kuwa na maslahi mazuri, kwa sababu katika upeo wangu sasa hivi naanza kuona hizi timu ndiyo zinazotutangazia nchi yetu vizuri, na sasa hivi tumesaini mkataba wa masuala ya usawa wa kijinsia. Tunaomba maslahi ya hawa wanatimu ambao wanaenda kwenye kutuwakilisha katika nchi nyingine huko, maslahi yawe sawa na hizi timu za wanaume ili tuweze kutimiza masuala ya usawa wa kijinsia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakienda kwenye hotels, wasifikie huko uchochoroni, Hapana. Waende kwenye hoteli, kama ni Four Stars au Serengeti Boys au Taifa Stars nao pia waende huko. Kuwe na bajeti nzuri ambayo itasaidia hawa vijana, kwani watajitoa sana na wanaumia sana. Kwa hiyo, naomba Serikali iangalie suala hili sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kuna timu hizi za watu wenye ulemavu, tunazisaidia vipi? Naomba nimwambie leo Waziri, kuna timu imekuja hapa Tembo Warriors tayari wanaenda kuwakilisha Kombe la Dunia, lakini kuna timu ya Albinism Sports Club ambao nao wanaenda Kenya keshokutwa hapa kwa ajili ya kuwakilisha nchi. Sasa tunazisaidiaje hizi timu? Tutafute namna yoyote ile ambayo Wizara na Bunge lako Tukufu zisaidie hizi timu ili ziweze kwenda kuwakilisha michezo hii ili tuweze kukuza hii nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumze kuhusu masuala ya muziki pia leo. Kaka yangu hapa Mheshimiwa Babu Tale amezungumza sana kuhusu BASATA na COSOTA. Naomba niwaambie jambo moja, msanii mpaka mnamwona amefika pale, amepitia mambo mengi sana; anapitia changamoto nyingi sana. Ukizingatia kwamba huyu msanii hana pesa, hana capital ambayo inamwezesha kufanya hizi kazi zake. Kwa hiyo, wanapitia kwenye changamoto nyingi hapa katikati kiasi kwamba zinaondoa yale maadili ya Kitanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa leo hii msanii ameshakuwa hivyo: Je, Serikali mnafanya nini? Kazi yenu kubwa ni kutoa elimu siku hadi siku ili hawa watu tuweze kuwa-shape, wajue sasa kwamba wanaenda kuwakilisha nchi. Tuwa-shape wawe wasanii wazuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii ukisema tu msanii amekosea, amevaa vibaya, hujamtengeneza au hujamkuza vizuri au hujamlea vizuri, hujampa elimu vizuri, unamfungia kazi yake. Hivi mnafahamu tunatumia gharama kiasi gani kutengeneza hizi video? Hivi mnafahamu tunatumia muda kiasi gani ku-invest kwenye hizi videos? Hivi mnafahamu vyote hivi? Hamfahamu! Sisi ndio tunafahamu ndiyo maana leo hii tulipambana kuja humu Bungeni tuwazungumzie wananchi wetu waliotuleta humu Bungeni, lakini tuzungumze juu ya masuala ya sanaa ya nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii umemsikia pale Mheshimiwa Riziki Lulida hajaniita Mheshimiwa Khadija, ameniita Mheshimiwa Keisha. Hilo ndiyo jina ambalo linatambulika katika nchi hii. Hili jina halikuja hivi hivi tu, limekuja kwa juhudi.

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Taarifa.

T A A R I F A

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, natoa taarifa kwa mwongeaji kwamba mambo yote yanayotokea, kwa kweli wanatakiwa Wizara hii pamoja na yote waelezee kwamba wameshawatafutia masoko ya kazi zao wasanii hawa katika maeneo au nchi ngapi? Watupe idadi. Ahsante.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Taarifa hiyo.

MHE. KHADIJA S. TAYA: Sijaielewa taarifa. (Kicheko)

NAIBU SPIKA: Haya tuendelee. (Makofi)

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninachotaka kusema hapa ni kwamba wasanii tunatumia muda mwingi sana kutengeneza majina yetu ili tufike pale tunapopataka. Tunatumia investment ambazo hatujui hata namna ya kuzipata lakini tunazipata. Sijui mnanielewa! Hatujui hata namna tunavyozipata, lakini tunazipata.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa kutumia hizi changamoto tunazopitia, sometimes tunakuwa frustrated, tunahitaji elimu, tunahitaji semina nyingi, nyingi. Kwa hiyo, naomba hii Wizara ikiwezekana, mwakani mwongeze bajeti ya kuwaelimisha wasanii, na sio wasanii kubwa peke yake, mwende Tanzania nzima kutoa elimu kwa wasanii ili wajue namna gani wanazifanya kazi zao vizuri katika maadili ya Kitanzania ili tuweze kutangaza nchi yetu Kimataifa vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu leo hii kuna wasanii jamani wanafanya kazi. Hii ni kazi kama kazi nyingine. Mfahamu hilo, hizi ni kazi kama kazi nyingine. Kuna wasanii wamesoma katika hii nchi. Kuna wasanii wamesoma; Nanji amesoma, Billnass amesoma, Zuchu amesoma India Advance Diploma ya Business, Saraphina amesoma Petroleum Chemistry Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na leo hii ni msanii pale amesimama, Mwana FA ana Masters ya Uingereza, ana Degree ya pale IFM, mimi nina degree ya pale CBE. Tumesoma, msitudharau. Msione kama vile katika hii nchi hatuna mchango wowote. Tuna mchango mkubwa sana, na leo hii tunazungumzia kila siku hapa masuala ya ajira, sijui ajira ndogo, ajira nini! Tukiweza kutengeneza vijana vizuri vijana humu ndani, nawambieni suala la ajira litakuwa ni historia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kila nyumba kuna msanii mmoja, katika kila nyumba, kuna wanamichezo, tunataka nini tena? (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante, kengele ya pili.

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na 2) wa Mwaka 2021 (Toleo la Kiingereza)
MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa nafasi hii ambayo nimeipata leo ya kuchangia Muswada huu ambao tumeletewa, Muswada Na.2.

Mheshimiwa Spika, naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Rais, kwa namna ambavyo anafanya kazi yake vizuri, anaongoza Taifa letu vizuri, anaonyesha ukomavu wa kisiasa na vile vile anaona kabisa namna gani ya ku-deal na masuala mbalimbali ya kitaifa ambayo kwa namna moja ama nyingine yeye anaona kwamba ni busara kunyamaza kimya na kufanya au kuachia vyombo vyake vifanye kazi.

Mheshimiwa Spika, nikupongeze pia kwa namna ambavyo unaendesha Bunge letu na kufuata Sheria zote na Kanuni zote za Bunge lako Tukufu ambalo leo hii sisi tunakuangalia kama kioo chetu na tunaangalia kama mfano mzuri wa uongozi, especially sisi vijana. Pia nikupe pole kwa changamoto ambazo unakutana nazo kwa sisi vijana ambao tumekuwa na mihemko ambayo tunaona kabisa haituletei afya kabisa katika Bunge letu na Taifa letu kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, leo hii nimekuja kuchangia mada tofauti tofauti ambazo kuna Sheria hii ya Mawakili, hii Sheria ya Mawakili katika Kamati yetu, tuliona kabisa Mawakili wanaapishwa na Jaji Mkuu wa Serikali. Tukaona kabisa kwa namna ambavyo sheria hii inatutaka tuwaweke hawa wawe wanajajiwa au wanatolewa na Mamlaka za Mkoa na si Taifa, hii ni kuondoa ile namna ya usomi wao au ni dharau kwao kwa kuona kwamba, yaani waondolewe kwa mamlaka ya chini wakati wao wameapishwa na mamlaka ya juu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Kamati iliona kabisa kwamba kuna busara ya wao kuamuliwa na Kamati ya Kitaifa, lakini siyo Kamati ya Maadili ya Mkoa. Kwa hiyo naomba nikuhakikishie Kamati yako ipo makini sana na inafanya kazi kwa weledi na uamunifu wa hali ya juu.

Mheshimiwa Spika, kuna jambo lingine hili la masuala ya Sheria za Usajili wa Vizazi na Vifo; tuliona kwamba kwenye familia kuna mambo mengi sana ambayo yanatokea especially pale mtu anapofariki. Tumeona ni namna gani ambavyo famili zinakuwa na mkanganyiko. Watu wengi wanadhulumiwa mali zao na yote kwa sababu labda ya cheti na tukaona kabisa kwamba tuone namna wazazi I mean watoto wa familia au mwenza wa familia na au kama hao wote hawapo basi ndugu wapate hiki cheti ili kiweze kuwasaidia katika majukumu yao mengine.

Mheshimiwa Spika, hii Kamati yako haipo legelege kama watu wanavyofikiria, hii Kamati ya Katiba na Sheria ipo makini kuliko mnavyoweza kufikiria, kuna mambo ambayo yanaletwa katika Kamati yetu tunayarudisha kwenye Serikali na tunataka kuiomba Serikali iwe inaangalia mambo ya msingi ya kutuletea huku kwa maslahi ya Taifa letu. Nakupa tu mfano mzuri; tuliletewa issue ya Makatibu kwamba waendelee kufanya kazi endapo Bodi zinavunjwa.

Mheshimiwa Spika, sasa kitu kama hiki kwa maslahi ya Taifa mtu mmoja akaamua maamuzi ya wengi ambao hawa wengi walikuwa kwa ajili ya maslahi ya Taifa, sasa mtu mmoja kwa muda wa mwaka mmoja na zaidi ambao wao walikuwa wanataka tuwaongezee, tuwaongezee miezi mingine 12. Kwa kweli Kamati iliamua kwa pamoja kuondoa hii sheria, tukairudisha Serikalini. Kwa nilitaka kukuonyesha kwamba namna gani Kamati hii ipo makini na inajali maslahi ya Taifa lake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa yote ambayo tumeyapitisha hapo, naunga mkono hoja kwa kuona kabisa kwamba kila kitu tulichofanya tulifikiria mara mbili kwa kuangalia kwamba namna gani tunaweza kusaidia Taifa letu kupitia hizi sheria kwa sababu tunatengeneza sheria kwa ajili ya kutatua matatizo, hatutengenezi sheria kwa ajili ya kuendeleza matatizo ambayo yanatukuta katika jamii yetu.

Mheshimiwa Spika, kwa kusema haya machache, nashukuru sana na Bunge lako hili Tukufu na Mwenyezi Mungu akujaalie uendelee kuwa na busara siku zote na hata pale utakapokuja kuombwa msamaha basi Mwenyezi Mungu busara ikuongoze na Mwenyezi Mungu akuongeze basi, uendelee kuwa na moyo huo huo wa kusamehe. Ahsante sana. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Khadija Shaabani Taya.

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 7) wa Mwaka 2021
MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kupata nafasi hii ya kuchangia masuala haya ya sheria. Nami naweza kusema siku hizi naanza kuwa mwanasheria kidogo kupitia hii Kamati ya Katiba na Sheria wananifundisha mambo mawili matatu.

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba niungane na wenzangu wote kumpongeza Rais na Kamati Kuu kukuleta wewe kuwa Spika wetu. Tunakuamini sana na tunafahamu uwezo wako, kwa hiyo, tunakupenda sana na tunaamini kabisa utaleta mabadiliko mengi katika Bunge hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili, naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Rais na Serikali yake, imekuwa ni Serikali sikivu mno, ambayo inaleta tija. Mambo mengi sana ambayo tunayaomba, yanakuja. Leo hii nitawathibitishia Umma kwa namna moja ama nyingine kwamba mambo ambayo tunayasukuma kwenye Kamati, tunawasumbua Mawaziri, wameamua kuleta marekebisho leo.

Mheshimiwa Spika, leo hii ni siku ambayo watu wasioona wanapata ukombozi wa kupata elimu ambayo itawawezesha wao kujitambua na kujielewa vizuri zaidi. Leo hii tuna sheria ambayo ni ya Copyright and Neighboring Rights Act. Hii sheria inaruhusu Serikali kuweza kuchapisha vitabu ambavyo vitaweza kuwasaidia watu wasioona. Jambo hili ni kubwa mno katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata juzi niliuliza swali juu ya masuala ya vitabu vya nukta nundu. Leo hii Serikali inaenda kupata nafasi ya kwenda kuchapisha vitabu vyovyote vile ambavyo vinaletwa na watu, au vinachapishwa na watu. Kwa hiyo, ni mkombozi mkubwa sana kwa watu wenye ulemavu. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kutambua na kujali sana watu wenye ulemavu kwa kutuletea hii sheria.

Mheshimiwa Spika, katika hii sheria Ibara ya 20, pia tumeona kabisa kwamba wanaenda kudhibiti maudhui au vitu ambavyo vitaingia katika nchi hii ambavyo vinapingana mila na desturi zetu. Kwa hiyo, tayari tupo vizuri katika masuala ya desturi na tamaduni zetu, yaani Tanzania inaenda chini ya Mheshimiwa Mama Samia, tuko vizuri sana. Mama yetu anaupiga mwingi mno na we real appreciate. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sheria ya pili ni hii ya National Sports, mambo ya betting. Wapendwa hii sheria ni nzuri sana kwa sababu inaenda kidogo ku-discourage haka kamchezo kwa kutoa tozo kwa hii sports betting. Jamani vijana wengi sana wamejiingiza katika haya mambo. Naamini kabisa gharama inaenda kuwa kubwa kidogo ambapo watu wengi wataanza kufanya kazi. Mimi naamini kabisa vijana wanaenda kuanza sasa kufanyakazi zaidi na siyo ku-bett zaidi. Najua ni mambo ambayo mnapenda, lakini kidogo tu- discourage hivi vitu ili tuweze kuwa na Taifa zuri au vijana ambao wanaenda kufanya kazi nzuri.

Mheshimiwa Spika, pia kingine, katika Kamati tumeshauri walete sheria nyingine ambazo zinaenda kuangalia kupata mapato sehemu nyingine pia. Siyo mchezo wa Sports Betting peke yake, basi hata michezo mingine au sehemu nyingine ambazo tunaona kabisa katika michezo, tutaweza kwenda kutengeneza michezo yetu na kulinda michezo yetu na kuimarisha michezo yetu.

Mheshimiwa Spika, kingine naomba pia nimpongeze Mheshimiwa Mchengerwa pale ambapo ameingia tu na masuala ya tuzo na masuala ya mirabaha; japo mimi mrabaha wangu sijapata, nashangaa sana kwa sababu Tanzania nzima inafahamu nyimbo zangu zimekuwa zikipigwa sehemu nyingi na tofauti tofauti. Ila naamini kabisa mwanzo ni mzuri, mmefanya kazi nzuri, tunaamini kabisa mnaenda kufanya mapinduzi ya hizi tuzo na hizi tuzo tunaambiwa kabisa hazitopendelea.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tayari tunaenda kutengeneza michezo yetu, sanaa yetu na utamaduni wetu. Kwa hiyo, tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais na Serikali yake na tunashukuru pia kwa usikivu wa mambo na kuona namna gani ya kubadilisha sheria ambazo zinashindwa kutekelezeka zinakuja kubadilishwa ili ziweze kutekelezeka kwa urahisi zaidi. Hilo ndiyo lengo letu kuu la kubadilisha hizi sheria.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naishukuru sana Serikali na nakushukuru pia wewe kwa kunipa nafasi hii, japo nilisahaulika katika orodha, lakini umeni-consider ndiyo maana nasema unafaa sana na unaupiga mwingi sana. Ahsante sana. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Tume ya Mipango wa Mwaka 2023.
MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kupata fursa hii ya kuchangia siku hii ya leo.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu muumba wa viumbe vyote ambaye amenipa uzima leo nasimama hapa mbele kuchangia Miswada muhimu mitatu katika nchi yetu, ambayo hii miswada inaenda kuleta mapinduzi makubwa katika Taifa letu katika nyanja ya maendeleo na uchumi kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, naomba nimpongeze Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan sana kwa kufikiria kuleta Miswada ya aina hii ambayo sasa ameona ni namna gani inaweza kwenda kuchangia, kuchechemua maendeleo ya nchi yetu, lakini pia naomba nimpongeze kwa namna ambavyo anavyotembea usiku na mchana kwa ajili ya kutetea Taifa letu kuleta maendeleo na kusaidia jamii yake ya Tanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, pia naomba nikupongeze wewe kwa kuliongoza Bunge hili vizuri sana na kutupa sifa nzuri sana na keshokutwa hapo unaenda kuwa Rais, tunakuombea Mwenyezi Mungu akujalie uende kuwa Rais wa Bunge la Dunia. Tunakuombea kwa Mwenyezi Mungu tunaamini uwezo wako, tunaamini kabisa umaridadi wako, tunaamini kabisa weledi wako, kwa hiyo tunaamini kabisa unaenda kuwa Rais mzuri sana wa Bunge la Dunia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nianze kuchangia Muswada wa Tume ya Mipango. Katika jambo ambalo Bunge hili tunapaswa ku-support leo hii ni hii Tume. Haya yamekuwa malalamiko ya muda mrefu sana kwa Wabunge wengi ambao mimi nimesikia michango yao humu ndani. Wanasema uratibu hakuna kwenye Serikali, wanasema juu ya mipango, leo hii tunaweza tukajenga shule lakini shule haina labda madawati, shule haina walimu, shule haina vitendeakazi vingi tu, Muswada huu unaenda kusaidia tatizo hilo.

Mheshimiwa Spika, Muswada huu unaenda kusaidia tatizo la kukosa vifaa vya hospitalini. Leo hii tunajenga majengo lakini hatuna vifaa ni kwa sababu tunakosa mipango thabiti katika nchi yetu. Leo hii Tume hii inaenda kusaidia upatikanaji wa vifaa vya hospitalini na upatikanaji wa vifaa vyote.

Mheshimiwa Spika, wakati mimi nasoma tulikuwa tunaambiwa sehemu ambayo tunataka tupeleke maendeleo, tupate mawasiliano, tupate maji, tupate umeme, tupate barabara nzuri. Nakumbuka tulikuwa tuna point zinasema lack of infrastructure, lack of transportation vitu vingi sana ambavyo tulikuwa tunajifunza mashuleni. Leo hii Tume hii inaenda kupanga mkakati mzuri sana. Tumeona barabara zetu watu wanajenga barabara baadae wanaenda kubomoa kwa ajili ya kupitisha mabomba ya maji. Tume hii inaenda kutatua tatizo hilo.

Mheshimiwa Spika, hii Tume imechelewa kuja kwa sababu tunaamini kabisa chini ya Mheshimiwa Rais hakuna Waziri atashindwa kupanga mpango mzuri wa watu wenye ulemavu. Tume hii inaenda kusaidia masuala yote ya watu wenye ulemavu. Tume hii inaenda kupanga mkakati mzuri wa watu wenye ulemavu wasaidiwe kwa namna gani katika nyanja ya elimu, katika nyanja ya afya, katika nyanja tofauti tofauti ya maendeleo na masuala mengine ya kimsingi.

Mheshimiwa Spika, Tume hii inaenda pia kusaidia kuna Sheria ya PPRA ya Manunuzi katika nchi hii, Wabunge wengi hawaifahamu hii sheria na hata watendaji wengine pia hawaifahamu hii sheria. Asilimia 30 ya manunuzi ya taasisi zote inatakiwa iende kwa makundi maalum. Sasa Sheria hii inaenda kusaidia utekelezaji wake wa hii Sheria, pia kusimamia Watendaji waweze kujua hii Sheria inapaswa kutekelezwa kwa namna gani. Kwa hiyo tunaenda kutengeneza mifumo mizuri ya utekelezaji, mifumo mizuri ya utendaji, kwa hiyo hii Sheria nawaomba Wabunge wenzangu leo hii tuipitishe kwa sababu ina umuhimu mwingi sana.

Mheshimiwa Spika, hii Sheria jamani inaenda kusimamiwa na Mheshimiwa Rais na Mawaziri wawili ambao ni Waziri wa Fedha na Waziri wa Mipango. Leo hii, hii sheria inaenda kuwa na tija kwa namna moja ama nyingine katika jamii yetu katika Taifa letu la Tanzania.

Mheshimiwa Spika, pia naomba nichangie juu ya Sheria ya Usalama wa Taifa. Katika pita pita zetu huko mitandaoni kuna watu wanasema kwamba kwa nini hii Sheria watu wanaenda kulindwa, wale wagombea Urais. Serikali imejipanga vizuri kulinda amani ya Taifa hili. Hii amani tunayojivunia ni kwa sababu Usalama wetu wa Taifa wanatusaidia sana. Sasa leo hii Wagombea wa Urais wanaenda kuomba nafasi ya Urais walindwe na nani? Je, leo hii wakipata shida yoyote huoni kama italeta machafuko katika nchi yetu? Kwa hiyo Sheria hii inaenda kuleta wapate mamlaka ya kwenda kusimamia viongozi wote ambao wanaomba nafasi ya Urais ili waweze kulindwa, kushauriwa namna ya kujilinda na namna ya kulinda na wajumbe wao ambao wanaenda kuwapigia kura.

Mheshimiwa Spika, vilevile kuna mtu alikuwa ananiambia kwamba hii Sheria inakwenda kuondoa madaraka ya Mheshimiwa Rais. Guys hii sheria inaenda kuongeza madaraka ya Mheshimiwa Rais. Ni nani ambaye anaweza kupinga mamlaka ya Mheshimiwa Rais wakati katika vitabu vyote vya dini vinatambua mamlaka za nchi, sasa ni nani ambaye anaweza kuondoa mamlaka ya Mheshimiwa Rais?

Mheshimiwa Spika, hii sheria inaenda kuongeza uwezo wa Mheshimiwa Rais kuchanganua mambo kuweza kulinda nchi yake vizuri, kuwasaidia Usalama wa Taifa vizuri, na Usalama wa Taifa wanaenda kumsaidia Mheshimiwa Rais katika mambo ya usalama wa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo kwa kusema hayo, naomba Bunge lako hili na Wabunge wako hawa, waweze kupitisha Sheria hizi tatu pamoja na Sheria ya Urekebu ambayo hii sheria ni muda mrefu sana miaka kadhaa haijafanyiwa marekebisho na leo hii tunaenda kufanya marekebisho ya Sheria hii ambayo inaenda kuleta mapinduzi ya kubadilisha Sheria mbalimbali za nchi hii.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo kwa kusema hayo machache naomba niunge mkono hoja wa Miswada hii mitatu. Ahsante sana. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Yatokanayo na Urekebu wa Sheria wa Mwaka 2023 .
MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kupata fursa hii ya kuchangia siku hii ya leo.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu muumba wa viumbe vyote ambaye amenipa uzima leo nasimama hapa mbele kuchangia Miswada muhimu mitatu katika nchi yetu, ambayo hii miswada inaenda kuleta mapinduzi makubwa katika Taifa letu katika nyanja ya maendeleo na uchumi kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, naomba nimpongeze Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan sana kwa kufikiria kuleta Miswada ya aina hii ambayo sasa ameona ni namna gani inaweza kwenda kuchangia, kuchechemua maendeleo ya nchi yetu, lakini pia naomba nimpongeze kwa namna ambavyo anavyotembea usiku na mchana kwa ajili ya kutetea Taifa letu kuleta maendeleo na kusaidia jamii yake ya Tanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, pia naomba nikupongeze wewe kwa kuliongoza Bunge hili vizuri sana na kutupa sifa nzuri sana na keshokutwa hapo unaenda kuwa Rais, tunakuombea Mwenyezi Mungu akujalie uende kuwa Rais wa Bunge la Dunia. Tunakuombea kwa Mwenyezi Mungu tunaamini uwezo wako, tunaamini kabisa umaridadi wako, tunaamini kabisa weledi wako, kwa hiyo tunaamini kabisa unaenda kuwa Rais mzuri sana wa Bunge la Dunia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nianze kuchangia Muswada wa Tume ya Mipango. Katika jambo ambalo Bunge hili tunapaswa ku-support leo hii ni hii Tume. Haya yamekuwa malalamiko ya muda mrefu sana kwa Wabunge wengi ambao mimi nimesikia michango yao humu ndani. Wanasema uratibu hakuna kwenye Serikali, wanasema juu ya mipango, leo hii tunaweza tukajenga shule lakini shule haina labda madawati, shule haina walimu, shule haina vitendeakazi vingi tu, Muswada huu unaenda kusaidia tatizo hilo.

Mheshimiwa Spika, Muswada huu unaenda kusaidia tatizo la kukosa vifaa vya hospitalini. Leo hii tunajenga majengo lakini hatuna vifaa ni kwa sababu tunakosa mipango thabiti katika nchi yetu. Leo hii Tume hii inaenda kusaidia upatikanaji wa vifaa vya hospitalini na upatikanaji wa vifaa vyote.

Mheshimiwa Spika, wakati mimi nasoma tulikuwa tunaambiwa sehemu ambayo tunataka tupeleke maendeleo, tupate mawasiliano, tupate maji, tupate umeme, tupate barabara nzuri. Nakumbuka tulikuwa tuna point zinasema lack of infrastructure, lack of transportation vitu vingi sana ambavyo tulikuwa tunajifunza mashuleni. Leo hii Tume hii inaenda kupanga mkakati mzuri sana. Tumeona barabara zetu watu wanajenga barabara baadae wanaenda kubomoa kwa ajili ya kupitisha mabomba ya maji. Tume hii inaenda kutatua tatizo hilo.

Mheshimiwa Spika, hii Tume imechelewa kuja kwa sababu tunaamini kabisa chini ya Mheshimiwa Rais hakuna Waziri atashindwa kupanga mpango mzuri wa watu wenye ulemavu. Tume hii inaenda kusaidia masuala yote ya watu wenye ulemavu. Tume hii inaenda kupanga mkakati mzuri wa watu wenye ulemavu wasaidiwe kwa namna gani katika nyanja ya elimu, katika nyanja ya afya, katika nyanja tofauti tofauti ya maendeleo na masuala mengine ya kimsingi.

Mheshimiwa Spika, Tume hii inaenda pia kusaidia kuna Sheria ya PPRA ya Manunuzi katika nchi hii, Wabunge wengi hawaifahamu hii sheria na hata watendaji wengine pia hawaifahamu hii sheria. Asilimia 30 ya manunuzi ya taasisi zote inatakiwa iende kwa makundi maalum. Sasa Sheria hii inaenda kusaidia utekelezaji wake wa hii Sheria, pia kusimamia Watendaji waweze kujua hii Sheria inapaswa kutekelezwa kwa namna gani. Kwa hiyo tunaenda kutengeneza mifumo mizuri ya utekelezaji, mifumo mizuri ya utendaji, kwa hiyo hii Sheria nawaomba Wabunge wenzangu leo hii tuipitishe kwa sababu ina umuhimu mwingi sana.

Mheshimiwa Spika, hii Sheria jamani inaenda kusimamiwa na Mheshimiwa Rais na Mawaziri wawili ambao ni Waziri wa Fedha na Waziri wa Mipango. Leo hii, hii sheria inaenda kuwa na tija kwa namna moja ama nyingine katika jamii yetu katika Taifa letu la Tanzania.

Mheshimiwa Spika, pia naomba nichangie juu ya Sheria ya Usalama wa Taifa. Katika pita pita zetu huko mitandaoni kuna watu wanasema kwamba kwa nini hii Sheria watu wanaenda kulindwa, wale wagombea Urais. Serikali imejipanga vizuri kulinda amani ya Taifa hili. Hii amani tunayojivunia ni kwa sababu Usalama wetu wa Taifa wanatusaidia sana. Sasa leo hii Wagombea wa Urais wanaenda kuomba nafasi ya Urais walindwe na nani? Je, leo hii wakipata shida yoyote huoni kama italeta machafuko katika nchi yetu? Kwa hiyo Sheria hii inaenda kuleta wapate mamlaka ya kwenda kusimamia viongozi wote ambao wanaomba nafasi ya Urais ili waweze kulindwa, kushauriwa namna ya kujilinda na namna ya kulinda na wajumbe wao ambao wanaenda kuwapigia kura.

Mheshimiwa Spika, vilevile kuna mtu alikuwa ananiambia kwamba hii Sheria inakwenda kuondoa madaraka ya Mheshimiwa Rais. Guys hii sheria inaenda kuongeza madaraka ya Mheshimiwa Rais. Ni nani ambaye anaweza kupinga mamlaka ya Mheshimiwa Rais wakati katika vitabu vyote vya dini vinatambua mamlaka za nchi, sasa ni nani ambaye anaweza kuondoa mamlaka ya Mheshimiwa Rais?

Mheshimiwa Spika, hii sheria inaenda kuongeza uwezo wa Mheshimiwa Rais kuchanganua mambo kuweza kulinda nchi yake vizuri, kuwasaidia Usalama wa Taifa vizuri, na Usalama wa Taifa wanaenda kumsaidia Mheshimiwa Rais katika mambo ya usalama wa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo kwa kusema hayo, naomba Bunge lako hili na Wabunge wako hawa, waweze kupitisha Sheria hizi tatu pamoja na Sheria ya Urekebu ambayo hii sheria ni muda mrefu sana miaka kadhaa haijafanyiwa marekebisho na leo hii tunaenda kufanya marekebisho ya Sheria hii ambayo inaenda kuleta mapinduzi ya kubadilisha Sheria mbalimbali za nchi hii.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo kwa kusema hayo machache naomba niunge mkono hoja wa Miswada hii mitatu. Ahsante sana. (Makofi)