Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Eng. Ezra John Chiwelesa (37 total)

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, kwanza na mimi nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye amenijaalia kuwa sehemu ya Bunge hili la Kumi na Mbili. Lakini pia nichukue fursa hii kuwashukuru wananchi wa Biharamulo walioniamini na kunichagua kwa kura nyingi za kishindo niwe muwakilishi wao katika Bunge hili, lakini bila kumsahau mke wangu mpenzi Engineer Ebzenia kwa support kubwa ambayo amenipa na watoto wangu wawili Isack na Ebenezer. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa haraka haraka mimi ningependa kuchangia kwa sababu ya muda nimekuwa katika viwanda kwa muda mrefu kidogo takriban miaka 14 nimekuwa nafanyakazi katika viwanda kama engineer, kwa hiyo ningependa nijikite hapa zaidi. Nimejaribu kuangalia tumetengeneza ajira takribani 480,000 katika viwanda 8,447 ambavyo tumevizalisha katika muda huu wa miaka mitano. Sasa nikijaribu kuangalia average ni sawasawa na kila kiwanda kimetengeneza ajira 56, sasa najaribu kuangalia tuna-target ya kutengeneza ajira milioni nane na tukisikiliza au kupitia hotuba ya Rais aliyoitoa hapa focus kubwa tuna target kuangalia integration ya mazao ya kilimo yaweze ku- integrate na viwanda ili tuone sasa mambo ambayo tunayachakata hapa katika kilimo, mifugo na uvuvi ambao umeajiri Watanzania wengi ndiyo viweze kuwa vyanzo vikubwa vya ku-integrate ajira hizi katika viwanda.

Sasa nilikuwa najaribu kupiga hesabu let’s say tunataka ku-create ajira milioni mbili tu kutoka katika viwanda maana yake tunahitaji tutengeneze viwanda takribani 33,000 tukienda na mwendo huu viwanda vile vya kawaida. Sasa ninachojaribu kukichangia hapa ni nini au maoni yangu ambayo ninayo ni nini? Tujaribu kujikita zaidi katika kuwezesha watu wenye viwanda ambao wanaviwanda tayari.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano Breweries wana-import ngano hapa na tumeangalia hotuba ya Rais inasema tunaingiza ngano takriban tani 800,000 kwa mwaka. Sasa tukiongea na Breweries tukajipanga tukawapa mashamba wao kwanza wawe ndiyo watu wa kwanza wa kulima kama wanavyofanya watu wa miwa na watu wengine yeye mwenyewe azalishe raw material kwa ajili ya ku-feed viwanda vyake huyo atatutengenezea ajira, ataajiri vijana wetu ambao wanasoma katika vyuo kwa mfano SUA na sehemu nyingine hiyo tu ni ajira tosha kwanza itazuia importation ya ngano, lakini vilevile itatengeneza ajira kwaajili ya vijana.

Mimi nimekuwa katika viwanda vya sukari nimekuwa naona kwa mfano kiwanda kimoja unakuta kimeajiri takribani Watanzania 10,000 wanaofanyakazi katika kiwanda cha Kagera au Mtibwa, ni watu wengi sana hawa ambao wamekuwa wameajiriwa huko. Kwa hiyo nikawa nasema same applies kwenye alizeti, niko katika Kamati ya Viwanda na Biashara, Mheshimiwa Waziri uliongelea suala la Kiwanda cha Singida kwamba kina-operate katika 35% of installed capacity sasa kiwanda ambacho kinafanyakazi katika 35% of installed capacity, kama tungekiwezesha kwanza kiwanda chenyewe tukakipa eneo la kulima kama kiwanda, kikalima alizeti yake yenyewe maana yake kiwanda kile kingeajiri Watanzania katika mashamba yake ya alizeti watu wengine pia wangeweza kulima na kuuza katika kiwanda kile maana yake kiwanda tungeweza ku-boost production yake ikapanda zaidi kwa sababu raw material ipo na kiwanda hakifanyi kazi katika installed capacity kwa sababu malighafi ya ku-supply katika kiwanda kile huenda ina scarcity yake pia. Same applies kwenye sehemu kama za kwetu…

SPIKA: Engineer Ezra mbegu ya alizeti hakuna, mbegu ya alizeti iko wapi? Endelea tu.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, najua mbegu ya alizeti hakuna ndiyo tunapohitaji sasa Wizara ya Kilimo ijikite katika hili kwa sababu kama tunategemea ajira ya Watanzania wengi iko katika kilimo tukasema mbegu ya alizeti hamna, halikadhalika tutasema na mbegu ya michikichi Kigoma hamna na bado tunaagiza mafuta it’s a shame kwa nchi kama hii juzi meli ya mafuta inakuja hapa Waziri anashangilia anasema meli ya mafuta imekuja hapa wakati wale watu kule bado tunaweza tukaongea nao hata wao wenyewe wanachokifanya kule tukaweza kuki-copy hapa tulete wawekezaji kule wanaozalisha mafuta ya mchikichi tuwaleta Kigoma pale, tuwaambie na sisi tuna michikichi hapa hebu waweke kiwanda Kigoma halafu tuwahimize watu wao wenyewe wenye kiwanda kwanza watalima mashamba yao, wataajiri jirani zangu wa Kigoma, halikadhalika walio na mashamba ya michikichi pale wataweza kuuza kwenye kiwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata mimi nina maeneo makubwa, Biharamulo tuna mapori ambayo yamekuwa yanateka Watanzania wanaumia kwa muda mrefu tunaweza kulima alizeti pale au tukaweka mwekezaji akalima alizeti ndugu zangu wa Biharamulo pale wakaweza kuajiriwa. (Makofi)

Lakini ajira tunapoipata ile maana yake tunabeba wakulima watu wa chini kabisa ambao wanashida ni wakulima hata mimi mtu atalima heka moja, atalima heka mbili, kwa sababu anajua kiwanda kiko pale ataweza kuuza kwenye kiwanda.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, naona muda hautoshi naomba kuunga hoja 100% nadhani nitaongea kwenye mipango pia. (Makofi)
Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mimi nami pia nichukue fursa hii kumpongeza Waziri wa Fedha na Mipango, kwa Presentation nzuri ya Mpango huu wa Maendeleo wa Miaka mitano lakini pia Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti kwa presentation nzuri pia.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo nimpongeze Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti na timu yake nzima kwa kuliona suala la Bandari ya Bagamoyo ambayo hata Mheshimiwa Spika ameliwekea msisitizo hapa. Labda kwa haraka, nadhani mpango unao maeneo matano makubwa ambayo Waziri ame - present hapa lakini kwasababu ya muda mimi nitaongelea mbili tu. Nitaongelea kwenye kuimarisha uwezo wa Viwanda na utoaji wa huduma, lakini pia kukuza uwekezaji na biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani mara ya kwanza kabisa niliposiamama wakati nachangia nilisema kwamba nimekuwa katika viwanda kwa takribani miaka 14 nikifanya kazi kama engineer, kwa hiyo nina uzoefu mkubwa kidogo katika suala la viwanda; na bahati nzuri nipo kwenye Kamati ya Viwanda na Biashara kwa hiyo sana naongea kwa experience yangu ambayo ninajua nimeiishi kama kazi lakini pia yale ambayo nimekuwa ninayaona huko.

Mheshimiwa Naibu Spika, ila labda tu niweke angalizo. Tunapokuwa tunachangia hapa sio kusema tumetumwa labda na mabosi zetu wa zamani au tunakuja kumsemea mtu yeyote hapa. Tunachangia kwababu tunahakika na tunajua kila ambacho tunakifanya ni sehemu ya expertism yetu. Kwasababu ninakumbuka mara ya mwisho hapa kuna mtu aliniambia au hao wafanyabiashara wanawatuma mje kuwasemea, na hawapo humu by the way kwa hiyo tupo hapa kwa ajili ya kuwasemea kwababu tunajaribu kuangalia mianya ya kutengeneza kodi, mianya ya kukusanya fedha ili zile fedha ambazo Waziri hapa amewasilisha Trilioni 40 kwa miaka mitano tuweze kuzipata; tutazipata huko kwenye private sector.

Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani mmemsikia mchangiaji aliyepita Abbas Tarimba. Jana nimeona we are proud kwamba kuona Mtanzania sasa anakuwa recognize na nchi kubwa ambayo imeendelea kiviwanda kama South Africa. Kwa hiyo lazima tujue tunazo hazina hapa, kwa hiyo sasa ni jukumu la Mheshimiwa Waziri kuwaangalia wafanyabiashara wakubwa walioko kwenye nchi hii aweze kuwatumia. Maana najua ameweka mpango wa trilioni 40 kutoka sekta binafsi, anataka atengeneze ajira milioni nane kwa muda wa miaka mitano, mpaka 2026. Hizi ajira milioni nane hataweza kuzipata kama hatatafuta hawa watu wenye viwanda huko nje. Watu kama akina Dewji hawa na wafanyabiashara wengine wakubwa. awatafute akae nao na tuje na hii mipango mikubwa ambayo tunayo hapa, maana tunataka tutengeneze ajira, tunataka tukuze uchumi lakini huu uchumi hatutaweza kukukuza kama wenzetu huko nje hawajui mipango yetu sisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa hiyo nikuombe Mheshimiwa Waziri wa Fedha tafuta muda wa kukaa na wafanyabiashara wakubwa na ni sisitizo usikae nao kupitia kwenye taasisi zao zile, kaa nao mmoja mmoja, mtafute mmoja baada ya mwingine, mwite, mwambie tuna mpango huu, unaweza ukawekeza kwenye nini.

Mheshimiwa Naibu Spika, maana niko huku kwetu kwenye Kamati ya Viwanda na Biashara tunahangaika kutafuta wawekezaji kutoka nje tuwalete hapa, lakini bado wapo wawekezaji wa Kitanzania wakubwa ambao wanaweza wakafanya biashara kutokaea hapa kuliko hata kumtafuta mtu wa nje ukamtumia mfanyabiashara wa Kitanzania aliyekuwepo hapa hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa hili ambalo ameliona, hasa suala la Kodi maana mimi last time tumefanya ziara EPZA pale Ubungo niliumia sana, kwamba pale kuna Mtanzania ambaye anafunga kiwanda chake anakipeleka Uganda. Sasa nikawa nafikiria unapofunga kiwanda, leo sasa tunatafuta wawekezaji wa kuja kuwekeza hapa ila Mtanzania ambaye alikuwa ameweka mle ndani, anaondoa anakipeleka kiwanda kwenye nchi Jirani. Maana yake ni nini, obvious unapoenda kule watakuuliza kuna nini huko.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini haya mazingira ambayo Rais amesema mwende mkakae na wawekezaji. Ninaomba uyafanyie kazi haraka ili Watanzania ambao ndio watu wa kwanza kuwaleta watu wa nje kuja kuwekeza hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina experience kidogo, nilikuwa natoa mfano. Ukienda katika nchi ya Egypt, kuna sehemu ile ya ukanda wa Suez nimetembelea pale, mimi nikaona, yaani lile eneo utafikiri ni kama nchi ya China imehamia pale. Walichokifanya cha kwanza ni kwamba ili uweze kumvutia mwekezaji aje pale lazima uwe na Bandari. Ile Bandari ya Black Sea pale ndiyo inayotumika. Wachina wameletwa pale wakapewa eneo, bandari imejengwa wamejenga viwanda vingi sana maeneo yale. Kwa hiyo wanachokifanya wanaleta vitu vyao wanafanya process pale Bandari ipo wana-export kwenda Europe.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa hiyo badala ya kuchukua mzigo kutoka China uusafirishe kwenda Europe kutoka Egypt kuushusha mzigo Ulaya inakuwa rahisi Zaidi, ndiyo kazi kubwa wanayoifanya hapa, sasa na sisi kama Kamati ya Bajeti ilivyo-suggest, tunayo nafasi kubwa zaidi ya kutumia Bandari ya Bagamoyo, kwasababu lile eneo la Bagamoyo ambayo tayari tulishalitenga na lilishalipiwa fidia takriban bilioni 27 zimewekwa pale. Hatuwezi kusema kwamba tuitelekeze.

Mheshimiwa Naibu Spika, na ukiweka pale na umwambie mfanya biashara atoke Dar es salaam anatoa mzigo Bandari ya Dar es Salaam anausafirisha mpaka Bagamoyo, aanze kuzalisha pale akimaliza kuzalisha ausafirishe tena kuurudisha Bandari ya Dar es Salaam afanye export, huo muda haupo, maana ni cost ya transportation ya kuja na kurudi, lakini vile vile na logistic inakuwa ngumu. Kwa hiyo nishukuru na niomba Waziri wa Fedha pigana unavyoweza bandari ile inyanyuke pale ili sasa fidia zile ambazo tumezifanya na uwekezaji mkubwa tunaotaka kuufanya Bagamoyo uweze kufanyika pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa kilimo, kwababu tunaongelea viwanda vinavyoweza kuzalisha mazao haya ya kilimo mazao ya mifugo na pia uvuvi na madini. Labda upande wa kilimo Mheshimiwa Waziri kwa kushirikiana na Waziri wa Viwanda Waziri wa Killimo na hali kadhalika Waziri wa Fedha, mjaribu kutuangalizia njia sahihi ya kufanya. Wakulima wa nchi hii wanahangaika sana. Mimi ninaweza nikatolea wakulima wa upande huu wa Kagera; nilikuwa ninajaribu kufuatilia. Nchi ya Ecuador ndio nchi ambayo inaongoza kwa ku-export banana, ndizi hizi, 3.3 billion dollar per year, ina-export ndizi, hiyo ni hela nyingi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika lakini sisi tupo pale, tulihamasishwa ndizi, watu wa Kagera mnaelewa, tumelima ndizi sasa hivi ndizi za mtwishe si zipo kule zimekaa hatuna hata watu wa kuwauzia tena? Maana unalima ndizi, Mkungu ambao hata hauwezi kuunyanyua shilingi 5,000 hatupati mteja tena. Sasa Mtusaidie. Maana nilikuwa ninaangalia hapa kwa Tanzania tume- export kwa mwaka tani 258. Tani 258 ukipiga kwa bei ya tani moja dola 300 katika World Market unaongelea dola elfu 75. Yaani mtu ana – export ndizi kwa dola 3.3 bilioni wewe hata dola laki moja haifiki, na bado tuna wakulima wanalima ndizi hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Unaongelea nchi kama Egypt, nimekuwa Egypt. Ukitoka Egypt, kama unatoka Cairo unaenda Alexander ile njia yote unapotembea imejaa zabibu, imejaa migomba na vitu vingine; nikawa najiuliza hawa watu wanafanyaje hawana maji hawana chochote kile. Wanachofanya zile ndizi wanatumia Irrigation.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa unashangaa mtu hana mvua ana irrigate ndizi zile, ana export ndizi anapeleka Dubai ndilo soko lao kubwa. Sasa mimi hapa nina m vua ya Mungu ndizi zinaozea kule mtusaidie ili sasa tuweze kufanya biashara na tuweze ku-export ili ndizi hizi ambazo tunazilima katika kanda hizi ziweze kutusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, najua wako Mbeya wako Kilimanjaro Mzee Mheshimiwa Dkt. Kimei amekuwa anaongea sana suala la ndizi kwa hiyo, haya ni mambo ambayo Serikali ikiingia kati ikaangalia jinsi ya kutusaidia itatutoa hapa tulipo itusogeze mbele maana hatuwezi kuongelea pamba tu hatuwezi kuongelea vitu vingine nadhani mmesikia hapa bei inashuka na kuongezeka. Lakini bado tunazo fursa nyingine za kupeleka matunda huko nje na vitu vingine vikaweza kutusaidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, bado dakika tano suala lingine niongelee suala la Liganga na Mchuchuma Mheshimiwa Waziri nimefika kule kwenye ziara yetu ya Kibunge lile eneo ni pori maana mwanzoni nilikuwa nawaza labda kuna hata majumba kuna hata nini ukifika kule mambo yale yanashangaza lakini umeiweka kwenye mpango humu vipaumbele sita ambavyo inabidi tuende navyo Liganga na Mchuchuma imo humu na mbaya zaidi Serikali tayari imeshaanza kuwekeza fedha nadhani mnajua tunajenga barabara ya zege tusingeweza kujenga barabara ya zege ya kilomita 50 sasa ya kuruhusu magari yaende kule kwenye ile migodi ile ni pesa nyingi sana ambayo tumeweka pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niombe nadhani kuna mambo ya kimkataba au mambo mengine ambayo yamekuwepo hapa biashara ni maelewano lazima ifikie stage ushuke ukae chini. Nimewahi kutoa mfano siku moja nimekuja kufuatilia biashara nimekuwa nafanyakazi kama Sales Manager kwa muda mrefu saa nyingine unaenda mpaka usiku hunywi pombe unakaa na mtu bar hapo unatafuta biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna siku nimeenda siku moja mchina mmoja anavuta sigara akipuliza moshi unaniingia puani lakini siwezi kumwambia usipulize maana nimekuja kutafuta biashara. Kwa hiyo, saa nyingine mkubali kushuka chini wafanyabiashara hawa tunapokuwa tunawatafuta kubalini kushuka chini twende tukae chini na hawa wachina, maana unashangaa hivi Mungu huyu aliwaza nini kipindi anakileta hiki kitu kwamba hapa kuna makaa ya mawe na hapa kuna mlima wa chuma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mwenyezi Mungu ametuletea kitu cha kufanya sasa niombe hiki kitu tuondoke sasa hivi Mheshimiwa Waziri jaribu kupigana waiteni hawa watu tukae nao chini tuongee kama huu mradi kweli una faida kubwa kama hiyo ni lazima huyu mwekezaji hawezi kuja kushindwa kuwekeza hiki kitu hapa ili tuondoke sasa kwenye hii stori ya Liganga na Mchuchuma ambayo tumeisoma tangu Shule ya Msingi mpaka leo watu tunapata mvi na haijawahi kufanyakazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikuombe Mheshimiwa Waziri hili suala lichukulie serious ili sasa itutoe hapa maana matatizo mengine madogo madogo tunayoyasema yatakwisha na yatakwisha kabisa yatamalizika. Maana najua tunawekeza hela nyingi sana kwenye bwana la Mwalimu Nyerere lakini ile ni megawati 2115 hapo unaongelea megawati 650 almost 1/3 tu sasa 1/3 tunashindwa kukomboa pale maana ni vitu vingi tutapata chuma tutapata umeme, tutapata makaa ya mawe vitu vyote vitamalizika pale na bado Serikali itapata pesa ya kuweza kutusaidia kufanya miradi kwa hiyo niombe na hilo uweze kutusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia suala la kumalizia niombe viwanda nimekuwa naongea hilo jambo hata kwenye kamati Mheshimiwa Waziri ukijaribu kuangalia wenzetu ningeomba mfanye kitu kimoja kama Serikali na kama Wizara tunazungukwa na nchi tisa hapa ambazo zinatumia Bandari ya Dar es Salaam leo hatuna haja ya kuacha Toyota wana-assemble magari Japan halafu Toyota wana export magari ambayo yako assembled wanayaleta hapa? Why don’t we sit down na Toyota tujaribu kuangalia Serikali ni mteja mkubwa wa Toyota tuangalie tuongee na Toyota tunavyokuja kutengeneza sehemu hii ya Bagamoyo special economic zone, tumuombe Toyota aje aweke hapa akiweka plant yake yaku-assemble tu maana yake ni kwamba nchi zote Jirani ambazo zinatumia magari ya Toyota tutapata advantage magari yanakuwa assembled hapa kutoka kwenye bandari yetu wanakuja wanachukua hapa kiwanda kinakuwa cha kwake analeta watu wake lakini tunapata ajira pia na uzoefu wa kuweza kujifunza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, maana nimeona hiyo sehemu nyingi hata Nairobi leo tukiongelea pump za KSB Waziri wa Maji yuko hapa nimalizie hiyo dakika moja Waziri wa Maji yuko hapa pump za KSB the needing company ni Wajerumani wale lakini leo assembly inafanyika Nairobi ilikuwa inafanyika South Africa lakini leo assembly inafanyika Nairobi wenzetu wamefanya bidii ya kwenda ku-lob kule hatimae ikaja hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niombe brand kubwa ambazo wengi wana export kwa kutumia bandari ya Dar es Salaam Mheshimiwa Waziri angalia Serikali muangalie kama tunaweza kuonana na hawa watu waje waweke viwanda vyao hapa wafanye assembly hapa vitu vitakuwa vinatoka vimekamilika vinaenda kwa wenzetu naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi ya kuchangia katika Wizara hii ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Pia nimpongeze waziri kwa hotuba nzuri ambayo ame-present hapa na timu yake kwa ujumla. Sitakuwa mbali na wachangiaji wenzangu waliotangulia, ningependa nijikite katika suala la TARURA pia, ila sitajikita zaidi katika kulalamikia mazingira nataka kutoa ushauri. Nitoe ushauri hasa kwenye mgawanyo wa fedha kama Waziri ama Serikali ipo hapa itatusikia, itakuwa vizuri zaidi maana nimekuwa najaribu kupitia.

Mheshimiwa Spika, ukijaribu kuangalia network ya barabara ambayo ipo chini ya TANROADS naambiwa ipo chini ya TARURA, TARURA wanahudumia barabara nyingi zaidi. Hata hivyo, kuhudumia barabara nyingi zaidi si sababu tu, ni kwamba pesa kubwa inayoelekezwa TANROADS ku- maintain barabara ambazo zimejengwa kwa gharama kubwa zaidi ambazo tunajua ziko durable zaidi, naona haina uwiano halisi na fedha zinazoelekezwa TARURA ku-maintain barabara za vumbi, barabara za changarawe na barabara za udongo kwa sababu nadhani wana kilokita 78,000 za barabara za undogo. Sasa barabara ya udongo always mvua inaponyesha, barabara ile sio barabara tena inakuwa tope na uharibifu unaanzia hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili, TARURA wanahudumia sehemu ambayo wengi wa wapiga kura na watu ambao wametuchagua kutuleta hapa wanaishi huko kwenye hayo mazingira. Kwa sababu ni barabara ambazo ziko kwenye Serikali za Mitaa, ahadi tulizozunguka tukaliliwa barabara na wananchi, hawakuwa wanatulilia barabara za lami zile kubwa hapana, sehemu kubwa ya nchi imeshaunganishwa. Walikuwa wanalia na barabara za vijijini, barabara zile ambazo wakulima wapo kule wanalima lakini wanashindwa kutoa mazao na watu wanaumwa wanashindwa kufika kwenye hospitali. Hizo ndizo barabara ambazo hata sisi wakati wa kampeni walio wengi humu, tumeletwa hapa na wananchi walituuliza tukasema tutazishughulikia. Sasa niiombe Serikali, kama hawataweza kutusaidia kwenye suala hili, wakajaribu kuangalia mgawanyo mpya, aidha kama wanaona ule mgawanyo uendelee kubaki TANROAD, basi waje na alternative ya kupata fedha ili tuweze kupata fungu kubwa kwenye upande wa TARURA ili iweze kutusaidia sisi kama Wabunge na hasa wananchi ambao wako kule vijijini.

Mheshimiwa Spika, lipo jambo kwa upande wangu nilikuwa najaribu kuliangalia kwenye wilaya yangu. Nilivyozunguka kwenye kampeni na sehemu kubwa kitu ambacho nilikiona, wananchi hasa wa upande wa vijijini, naomba Serikali wajikite kwenye kujenga madaraja. Huko vijijini wananchi wanachokwama zaidi ni madaraja, maana utakuta mvua imenyesha, mtu anaumwa, kuna bodaboda ndio usafiri, vijijini hawatumii magari kwa sehemu kubwa, labda nyie kwenye wilaya zenu, lakini kwangu sehemu kubwa za vijijini wanatumia bodaboda, wanatumia miguu na baiskeli. Kwa hiyo, mvua zinaponyesha kwenye msimu huu, kuna sehemu madaraja hayapitiki kabisa, unakuta daraja limefunga kata mbili, limefunga vijiji sita, limefunga vitu vingapi, kwa hiyo wajaribu kutusaidia. Fedha nyingi ya TARURA ielekezwe kwenye ku-maintain madaraja.

Mheshimiwa Spika, kujenga madaraja sio kitu kigumu, kuna makampuni hapa yanatengeneza mabomba yale makubwa, bomba linaenda mpaka three meters, hata kama ni kina kikubwa sana, wapo Pipe industries, wapo PLASCO tunajua. Ukienda hata Ngorongoro Craters kule chini, mabomba yanayotumika sasa hivi kutengeneza madaraja kule mbugani ni mabomba ya plastiki. Kwa hiyo wangeweza kwenda kununua, lile halihitaji mkandarasi, mtu tu wa kawaida, a normal technician anaweza kufanya ile kazi kule kijijini. Kwa sababu atachimba na wananchi, wataingiza lile bomba pale na watafukia, watajengea cement huku na huku basi kitu kinaenda. Ile Force Account wanayoitumia huko TARURA kwenye madaraja vijijini inaweza ikatusaidia zaidi tukaweza kupunguza gharama lakini tukasaidia watu wengi zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, nataka niongelee suala la shule. Niipongeze Serikali kwa kazi kubwa ambayo wanazidi kuifanya. Nadhani kwa record kubwa tuna kikosi kukubwa sana ambacho tunategemea tutaanza kukipokea kwenye shule za sekondari, nadhani miaka miwili au mitatu, maana mazao ya elimu bure ile sasa ambayo Mheshimiwa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli aliianzisha, tunaanza kuipata nadhani miaka miwili au mitatu ijayo. Wale ambao waliingia darasa la kwanza bure, nadhani sasa hivi wako darasa la sita, either wengine wanaelekea la tano, kwa hiyo ule wingi mkubwa tunaanza kuuona huko. Sasa naomba Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, tunaomba waje na mpango mkakati wa miaka hii miwili au mitatu inayokuja, ili waweze kutusaidia, maana Watoto kule vijijini ni wengi na wale watoto wana akili watafaulu, kwa hiyo tunachotegemea, wasifaulu wakaishia kubaki vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nasema hivi kwa sababu sisi kama wawakilishi tutakuja na kazi nyingine ya kurudi kwa mzazi anayekwambia mimi bwana mtoto wangu amefanya vizuri lakini amekosa shule. Mimi Mbunge siwezi kujenga shule, lakini Serikali inaweza kujenga shule, kwa hiyo watusaidie. Nataka nitoe mfano hapa, kwenye jimbo langu kuna shule moja ya msingi kwenye Kata ya Nemba, shule nzima ina wanafunzi 4,819, ila ina vyumba tisa vya madarasa. Kuna maboma matatu sasa hivi wananchi wanahangaika ndio wanayanyanyua matatu mengine, Wizara ingeweze kutusaidia kuyaezeka sasa angalau wawe navyo 12.

Mheshimiwa Spika, lakini nilipokuwa napitia hii shule, ni shule ya kata. Darasa la saba sasa hivi wako 276, la sita wale wako 703 kwenye shule moja tu. Hii shule inahudumiwa na shule moja ya sekondari ambapo shule moja ya sekondari ukiangalia watoto walioko darasa la sita maana yake walioko form three leo wanavyoondoka kumaliza form four wao ndiyo watapisha room kwa ajili ya watoto walioko darasa la sita. Sasa form three wako 999 hawafiki hata 100 lakini shule hii ita-release watoto zaidi ya 700 wanaingia sekondari. Of course, hata wakifeli labda haiwezi kuwa chini ya asilimia 90 maana kwa Kagera Biharamulo sisi hatujapungua chini ya asilimia 95 kwneye ufaulu wa primary.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nina uhakika watoto si chini ya 600 kutoka kwenye shule moja tu wanatakiwa waende sekondari. Sasa wanaendaje sekondari kwenye shule ambayo leo inatoa wanafunzi 99 inapokea zaidi ya 600. Na hawa 600 ni kwenye shule moja ya msingi na hii shule ya sekondari inahudumia shule za msingi takriban nne. Kwa hiyo, ninategemea hawa watoto zaidi ya 1,000 watakuwa wanafaulu kwenda form one. Sasa shule hii mjaribu kutusaidia. Kwa hiyo ningeomba sasa Mheshimiwa Waziri mje na kikosi maalum cha kuzunguka kwenye kata. Shule hizi za kata tulizozianzisha za haraka haraka hizi zinaenda kuzaa matunda. Zisizae matunda watoto hawa wakabaki mtaani maana wengine ni darasa la saba akimaliza kabaki mtaani anafanya nini? Hatuna vyuo vya ufundi sehemu hizo maana ziko kwenye kata bado. Kwa hiyo, mtusaidie kwenye hilo ili watoto hawa tuwatoe hapa walipo tuweze kuwasogeza mbele zaidi na wao wayafikie malengo ya kuwa madaktari, wahandisi, walimu, maaskari, wanasheria na kada nyingine ambazo wanategemea wazifanye. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pili wakati wa kampeni mwaka jana kuna jambo lilijitokeza. Huenda lilikuwa nchi nzima au lilikuwa kwenye wilaya yangu ya Biharamulo lakini naongelea kwa experience yangu. Suala la vitambulisho vya wajasiriamali. Suala la vitambulisho vya wajasiriamali mwaka jana lilileta saga sana Biharamulo. Watu wakawa wanaona sasa wanalazimishwa kuwa na vitambulisho vile, vurugu zikawa kubwa sana lakini baadaye kwa busara yale mambo yakaja yakatulia. Sasa juzi wiki iliyopita wenzetu waislamu wameanza mfungo siku ya Jumatano. Biharamulo tuna gulio siku mbili, tuna gulio siku ya Alhamisi na tuna gulio siku ya Jumapili sehemu ile ambayo sasa hata wakulima na yeyote yule anayejisikia kuuza anakuja sokoni kuuza.

Mheshimiwa Spika, ningeomba sasa maelekezo mahsusi yatolewe. Tutofautishe wakulima wa kawaida na wafanyabiashara wadogo wadogo. Kuna mama yangu kule kijijini anabeba ndizi, shilingi 5,000 ukipeleka ndizi sokoni na basically unachoenda kukifanya sokoni ni barter trade. Mtu analeta mkungu wa ndizi shilingi 5,000… (Makofi)

SPIKA: Engineer muda sasa.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, nimalizie dakika moja. Mtu analeta mkungu wan dizi shilingi 5,000. Anavyofikisha mkungu wa ndizi shilingi 5,000 akimaliza kuuza anaondoka na chumvi, sukari, habaki hata na shilingi ya hela. Lakini mtu anataka yule mtu awe na kitambulisho cha 20,000. Ndugu zangu tuliozaliwa vijijini tunajua, kuna watu huko unamuuliza leo ni mzee, hajawahi kuwa hata na shilingi 5,000 mfukoni. Ukimuambia atafute shilingi 20,000 na kukata kitambulisho ili alete ndizi sokoni tunamuumiza. Kwa hiyo ningeomba hilo jambo tuliangalie tuweze ku-harmonize hao watu ili situation irudi kawaida na hakika Serikali hii ni Sikivu mtaweza kutusaidia ili wananchi wetu huko waweze kufanya kazi anayeuza auze, anayelima alime lakini wafanye kazi kwenye mazingira mazuri. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maji
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia kwenye hotuba hii ya Wizara ya Maji. Kwanza, nichukue nafasi hii kumpongeza Waziri kijana na machachari ambaye amedhihirisha umwamba wake katika Wizara hii ya Maji. Nadhani ukiona mpaka Mheshimiwa Rais ananukuu yale unayoyafanya maana yake unahakikisha unayasimamia kwelikweli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimkushukuru kwa miradi ambayo imeainishwa kwa ajili ya wakazi wa Biharamulo. Nikushukuru kwa mradi ule wa Maziwa Mkuu, nimeona Biharamulo imetwaja; ni mradi wa shilingi bilioni karibu 750 ambayo itahudumia miji inayozunguka Ziwa Victoria na Biharamulo ipo na vijiji vyake, kwahiyo nakushukuru kwa ajili ya hilo. Pia ukurasa wa 149 nimeona miradi ambayo nimetengewa kwa ajili ya Wilaya ya Biharamulo nishukuru, itatutoa hapa tulipo na kutusogeza mbele zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nizidi kukumbushia tu nadhani nilim-consult kwa ajili ya ahadi ya Rais; mradi mkubwa wa kuleta maji katika Mji wa Biharamulo kutoka Ziwa Victoria. Naomba azidi kuukumbuka hata kama bajeti imebana ili shida ile ambayo imekuwepo kwa muda mrefu iweze kumalizika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nimpongeze kwa nia thabiti ya kutusaidia kwa sababu nilishamuona ameniahidi baada ya bajeti mimi kama Mhandisi na yeye kama mzoefu twende pale tuangalie chanzo ambacho kinatuhudumia sasa hivi ili tuweze kuanza mwanzo mwisho ikiwezekana tupate treatment plant ya kuanzi sasa hivi kipindi ananiandalia mradi mkubwa. Nazidi kukushukuru kwa ajili ya hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kutoa shukrani niweze kuongea mambo machache mengine yatakuwa yangu ya ufuatiliaji kwa ajili ya eneo langu ila kwa sababu ninao uzoefu mkubwa katika sekta hii kwa hiyo napenda kuongea juu ya yale ambayo nayajua na yale ambayo nadhani tukishauri Serikali ikayabeba na wakayafanyia kazi yataweza kweli kutusaidia. Cha kwanza, niipongeze Serikali kwa uanzishaji wa RUWASA. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ile ambayo Mheshimiwa Waziri amekuwa akiita ni kichefuchefu; mpaka anawaambiwa watu wachezee vitambi lakini sio miradi, nakumbuka iliyo mingi ni ya BRN (Big Results Now), ndiyo ilifeli wakati ule tukitumia wakandarasi na Halmashauri mkaona solution ni kuja na RUWASA. Kweli RUWASA imetusaidia kwa sababu wakati ule nakumbuka unakuta mkandarasi hajui chochote, mwingine ana stationary na kadhalika na miradi mingi ilikuwa ni ya viongozi hao hao waliokuwa kwenye halmalshauri zile; mainjinia na watu wengine ndio maana ilifeli. Kwa hiyo, tuhuma zile za nyuma tuziache tuku-support tuanzie hapa na RUWASA ili twende mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimejaribu kufuatilia utendaji wa RUWASA, wanafanya kazi vizuri, wote tunajua. Development partners wanatoa pesa kusaidia miradi ya maji vijijini, lakini based on performance. Nimefuatilia nimeona DFID, sasa hivi imetoka shilingi bilioni 23 imeenda mpaka shilingi bilioni 79. Maana yake RUWASA wamefanya vizuri, wame-qualify kwenye vigezo na fedha imeongezeka. Nimeona hata ya World Bank ilikuwa shilingi bilioni 118 nadhani safari hii inaenda mpaka shilingi bilioni 186, hii ni good performance kwa sababu wanafanya wanavyofanya, mkienda kuchujwa kwenye viegezo, inaonekana mme- qualify mmeenda mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Mheshimiwa Waziri, baada ya kuyaona haya yote na kwamba RUWASA inaaminiwa, ili lisiwe bomu baadaye, maana mwanzo wakandarasi waliharibu. Maana unapoongelea miradi ya maji is purely engineering practice. Huwezi kufanya engineering project bila kuwa na ma-consultant, na watu ambao wanahausika. Hata ukijenga nyumba yako wewe mwenyewe unaita fundi. Wewe sio mjenzi, lakini kuna kipindi unapitia nyumba unamwambia fundi hapa ulivyopiga ripu siyo. Wewe sio engineer wala nini, lakini unaona.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba turudishe practice ile ya ma-engineer. Nimefuatilia nikaona kwamba mpango wa kuchuja wakandarasi unaendelea na ni hatua nzuri sana ambayo inafanywa na RUWASA, kufanya shortlisting ya wakandarasi mkajua kama wana vigezo then twende hatua ya pili ya kuwaamini wakandarasi hawa tuwarudishe kwenye miradi watusaidie.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii miradi ni mingi, hatuwezi kuifanya kwa kutumia force account tu. Ni lazima tu-employ wakandarasi. Kwanza watatengeneza ajira kwa vijana wa Kitanzania na miradi itafanyika haraka kwa sababu wananchi hawa wanachohitaji ni maji. Tukienda kwenye process hii ya muda mrefu, kesho na kesho kutwa tutakwama tena. Maana ni bajeti hii, mwakani utakuja na bajeti nyingine na bajeti nyingine. RUWASA ni mtoto mdogo ambaye mmemzaa hata miaka miwili hajafikisha, kaanza 2019. Mwezi wa Saba ndiyo anaenda mwaka wa pili. Tumwezeshe pia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu utakuwa enginee; wote jiografia ya mazingira yetu tunaijua. Hata magari, kuna baadhi ya sehemu hawana magari bado. Kuna baadhi ya sehemu bado hawajaruhusiwa kuajiri. Ni wafanyakazi wale wale waliotoka nao Halmashauri, leo ndiyo wale wale ambao tunawategemea wafanye miradi hii. Sasa tuhakikishe kwamba kwenye bajeti hii tunawasaidia mtafute magari, vijana hawa wakafanye kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumepiga kelele sana ya TARURA hapa, lakini miradi haifanyiki mjini. Ni bora sasa hata TARURA tunawafuata wananchi kwenye sehemu ambazo wamelima wenyewe. Wote tunajua, vyanzo vya maji viko maporini, tunatoa maji kwenye mapori tunayatiririsha yanakuja kwenye vijiji au miji. Sasa kama hawana vitendeakazi hawa watu watakwama sehemu. Baadaye tutarudi hapa kuwahukumu, tutaona RUWASA haina maana, tutaazimia kuivunja. Sasa tuwawezeshe. Tukishawawezesha nia hii waliyonayo ni nzuri itaweza kutusaidia.

Mheshimwia Naibu Spika, kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Waziri with due respect, mimi nimekuwa na uzoefu na nimejaribu kufuatilia hususan kwenye suala la maji. Yapo makampuni ambayo yapo tayari kutusaidia kuhakikisha kwamba tunapata vifaa. Kwa sababu almost asilimia 60 ya miradi ya maji iko kwenye mabomba na viungio, lakini viwanda viwanda vya Kitanzania viko hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumesema tu-engage private companies. Private companies twende tukaongee nao wakubali kutoa mabomba kwa wakandarasi ambao leo tutawaleta hapa. Wakishakubali kutoa mabomba kwa wakandarasi, wakandarasi wafanye miradi ili nyie sasa mtakapoipata fedha mlipe kwenye viwanda moja kwa moja kwa niaba ya wakandarasi. Viwanda vitatoa mabomba hapa na miradi itakimbia. Maana na best practice najua, nawe mwenyewe unajua nimekuwa nafuatilia hayo kwako.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukiweza kufanya hivi, kelele kubwa ni vifaa. Mabomba yakishafika site, hamna shida tena. Shida imekuwa kubwa kwa sababu kazi ya kuchimba mitaro na kufukia siyo issue. Mkandarasi anaweza akawa na fedha, lakini kazi ya kununua mabomba pale; unaenda kwenye kiwanda mtu anaambiwa shilingi bilioni 700 au shilingibilioni 800. Wakandarasi wa Kitanzania tunajua, walio wengi wamekuwa wanaandika paper works tu. Ukienda kwenye reality vile vitu havipo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili tuwanyanyue tuwarudishe kwenye mstari wale waliokuwa wameanguka, tukubali kufanya commitment ya Serikali kwamba viwanda vikubali kutoa mabomba, Wizara na RUWASA wasimamie. Mabomba yale yakishaletwa, kateni pesa za viwanda muwalipe waweze kukopesha wengine i-rotate kule miradi hii itakimbia. Hakuna Mbunge hapa atakayekuja kulalamika kwa sababu kila mahali mlipopeleka mkandarasi, ataanza kufanya kazi kwa sababu mabomba yatakuwepo, viungio vitakuwepo, kazi yake ni kuchimba mitaro na kulaza mabomba. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuyasema hayo, kuna jambo lingine ambalo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Ni kengele ya kwanza eh!

MBUNGE FULANI: Ndiyo.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, kuna jambo lingine ambalo nimekuwa nalo kwa experience yangu. Nilichokuwa naomba, tujaribu pia kuangalia uendeshaji wa hizi taasisi tulizonazo. Nilikuwa natamani RUWASA iendeshwe kama inavyoendeshwa TANROADS. Ikiwezekana muwape target. Yaani I believe in targets kwa sababu private companies kwa sehemu kubwa tunafanya kazi kwa target. Nimekuwa Nairobi National Water, nimekuwa Uganda National Water nimeona, yaani Mamlaka ya Maji iko responsible kwa Bodi na wana target. Kwa sababu nimekuwa kwenye hii biashara kwa muda, kwa hiyo, nilikuwa nafuatilia sehemu zote. Nimekuwa Uganda na Nairobi, nimeona wanavyoendesha.

Mheshimiwa Naibu Spika, tujaribu kuwapa target, they have to perform based on targets kwa sababu mtu anapokuwa anafanya kazi na hana target, ndiyo kesho na keshokutwa unakuja kukuta uzembe mdogo mdogo wa mtu mmoja unakuletea kashfa wewe Waziri ambaye unapigana, unamletea kashfa Mkurugenzi Mkuu, lakini kwa sababu tu ya watu wachache ambao wako huko. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, muundo huu wa kuunda hii taasisi ni mzuri, lakini twende mbele na turudi nyuma, ni lazima iwe performance based. Tuifanye kama Taasisi separate, tusiifanye kama sehemu ya Wizara, iwe performance based, Bodi ipo, iwajibishe watu wanaoleta uzembe. Kabla ya Rais kukuwajibisha wewe, hebu wewe uanze kuwawajibisha hao watu. Maana nimeona hapa ukurasa wa 29 wa hotuba ya Rais, mambo aliyoyataja kwenye upande wa maji. Usimamizi ametaja mara mbili. Nilikuwa nafuatilia hapa ukurasa wa 79. Usimamizi mbaya na huku kaja tena kwamba, ili kuimarisha usimamizi, atafanya mabadiliko moja mbili, tatu, nne kama alivyotaja hapa. Kwa hiyo, sehemu kubwa ambayo inatukwamisha, ni usimamizi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ninachoomba ili msimamizi asitafute sababu yoyote ya kukwepa, hebu tuwawezeshe. Tuwape magari na vifaa. Baada ya hapa, usimamizi ule sasa ambao unautaka wewe kupitia RUWASA kwenye Bodi, kupitia RUWASA kwenye Management uende ukatekelezeke huku mtu akiwa hana sababu yoyote ile. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine cha kumalizia, wako watu ambao wakati wa nyuma walipata shida kidogo kwenye miradi hii ya maji. Maana wakati ule miradi mingi sana ilikuwa imekwama kama ulivyosema. Miradi karibu 177 mmekuta ikiwa imekwama kabisa kabisa, lakini leo mmetekeleza almost miradi 85 inatoa maji. Sasa unavyoona kazi hiyo kubwa imefanyika kwa muda mfupi na miradi iliyokuwa kichefu chefu, sina budi kukupongeza. Maana nisipokupongeza wewe Mheshimiwa Waziri na RUWASA nitakuwa siwatendei haki. Hotuba nimeipitia, kazi mliyofanya ni kubwa. Tunaojua maji, tunajua miradi ilivyokuwa imekwama.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nampongeza Mheshimiwa Waziri na wasaidizi wake; nampongeza Naibu Waziri maana amekuwa kila anapoitwa anakubali kufika, kwangu ameshatembelea. Nampongeza pia Katibu Mkuu kwa sababu amekuwa msikivu, unapoenda kumwona yupo tayari kusaidia na Naibu Katibu Mkuu. Kwa hiyo, ni Wizara ambayo kwetu ambao tunajaribu kufanya ufuatiliaji, mmekuwa tayari kutusikiliza na kutuhudumia. Kwa hiyo, haya ambayo yanafanyika hapa na especially kazi ngumu ya kukwamua miradi iliyokuwa imekwama, mnastahili sifa ya pekee. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Bunge tuwaunge mkono kwenye bajeti hii tuweze kuipitisha sasa ili yale ambayo wananchi wanayategemea hasa kwenye maji, maana kilio cha Watanzania ni maji; maji ni uhai na bila maji, uhai wetu hautastawi; na tusipopata maji huko tunakoelekea majimboni mnajua. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na ninaunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii pia niweze kuchangia kwenye hotuba hii ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, nadhani nianze kwanza kwa kuipongeza Wizara kwa hotuba nzuri ambayo wameitoa, lakini pia niseme tu jambo moja, nitapenda zaidi kujikita kwenye sehemu ya mifugo hasa kwenye masuala ya ng’ombe kwa sababu mwenyewe historia yangu nimezaliwa kwa wafugaji, nimechunga sana ng’ombe nikiwa mdogo, kwa hiyo, kidogo ni kitu ambacho nakielewa na nimekiishi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa haraka kuna jambo moja ambalo nimekuwa najiuliza alichangia mwenzangu bwana Maganga hapa tangu zamani hata kabla sijaingia kwenye siasa nimekuwa najiuliza kuhusu wafugaji wa Tanzania. Yaani wafugaji wa Tanzania wamekuwa kama yatima always ni watu ambao ni watu wa kufukuzwa fukuzwa, ni watu ambao wanaonekana wanakosea kosea kwenye vitu vyao vingi wanavyovifanya, sasa nikawa niwaza Wizara ya Mifugo mnajua kwamba mna mtoto ambaye ni mfugaji na bado anakimbikizwa kimbizwa, lakini bado hamchukui hatua ya kum-protect? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayasema haya kwa sababu wafugaji hawa sijui wanamakosa gani, kwa mfano kwa upande wa Biharamulo ni eneo ambalo tuna mifugo mingi sana na baada ya kuingia hasa wakati wa kampeni nimekuwa nikiuliza maelekezo ilikuwa ni kwamba tuna-ranch zimetengwa Karagwe, ranch zimetengwa Misenyi sasa nikawa najiuliza Mkoa mzima wa Kagera tutaenda kufugia Karagwe na Misenyi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba labda tusaidiane kwenye jambo moja, wafugaji wetu wa Kata ya Kaniha kuna Kijiji pale kinaitwa Kijiji cha Mpago, wiki mbili zilizopita bwana mmoja wamemkamata ng’ombe wake akatozwa faini shilingi milioni saba, mwingine naye akatozwa faini ya shilingi milioni tano, reason ng’ombe wameingia kwenye hifadhi ya TFS.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nikawa najiuliza swali moja wewe ni mfugaji, let say ni mfugaji, nafuga kule kwa sababu tumehamasishwa kufuga, nipo Bungeni hapa sasa hivi vijana wanaochunga ng’ombe wapo karibu na hifadhi ng’ombe wameingia mle, mtanzania yule anatozwa shilingi milioni saba at per kama hajatoa milioni saba ng’ombe wote sabini wanaondoka najiuliza hata Waheshimiwa Wabunge tumo ndani leo tukimnyanyua mtu milioni saba ambayo haikutegemea papo aitoe hapa sidhani kama kuna mtu yupo hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ikumbukwe wale watu wapo maskini, wapo vijijini kule ni maskini kabisa, faini ya kumtoza mtu shilingi milioni saba mtu ambaye juzi Kijiji cha Mpago kamati iliyoundwa wamesogeza mipaka, hawajaweka alama TFS, lakini wafugaji wetu wameshaanza kukamatwa wanatozwa hela yote hiyo, lakini hawa ni Watanzania tunahamasisha kwamba ufugaji uendelee, mnalenga leo kutengeneza maziwa kutoka lita bilioni 2.7 mpaka lita bilioni 4.5 yatatoka wapi kama hawa watu wapo disturbed kiasi hiki na hawana sehemu ya kulishia ng’ombe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ilani ya CCM imeahidi ukurasa wa 51 kwamba tunataka tuongeze malisho, sehemu ya kulishia kutoka hekta milioni 2.7 mpaka hekta milioni sita. Sasa hizi hekta milioni 2.7 na hekta milioni sita kutoka hapo hiyo range tunaipata wapi? sisi wananchi tunaipata wapi kama siyo Wizara ya Mifugo ndiyo itabidi ifanye kazi hiyo ya kuitafuta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hayo maeneo ambayo mnataka muyaongeze nani anayamiliki, tungekuwa tunamiliki wananchi wenyewe tungepeana, lakini yanamilikiwa na Serikali kupitia TFS. Sasa tunachowaomba ndugu zangu wa mifugo, ninachowaomba kwa niaba ya wananchi wangu sisi tuna eneo kubwa sana Kata ya Nyantakara pale tunaomba mfunge safari mje Biharamulo muwaambie wafugaji wa Biharamulo kwamba eneo lipo hapa kaeni na TFS, maana Biharamulo kwa sehemu kubwa tumezungukwa na mapori, kwa nyuma huku tumezungukwa na hifadhi ya Burigi Chato ambayo off course tunashukuru Mungu watalii wataanza kuja tutapata fedha za kigeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo mengine yamehifadhiwa wananchi hatuwezi kwenda kuomba TFS hawatatuelewa ila wewe custodian wa mifugo ni kazi yako kuwatafutia wafugaji wako maeneo. Nyie mwende mkaongee na Serikali maana Serikali kwa Serikali mnashindwanaje? Ila wananchi huku wanaumia, nayaongea haya kwa uchungu kwa sababu wakazi wa Biharamulo tunajua tulivyoteseka na haya mapori. Sasa mnavyoyaacha mnataka wale jamaa warudi tena waanze kutuimbisha mtaji wa maskini nguvu zake mweyewe, tumeteseka mno tulikuwa tunashushwa kwenye magari usiku tunapigwa viboko, leo tumeshakaa vizuri sasa maeneo haya iyambieni TFS nyie watu wa mifugo wawakatie maeneo wafugaji wa Biharamulo wapate eneo la kufugia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sina haja ya kushika shilingi, lakini ninachoomba sasa nyanyukeni mkae na wenzenu wa maliasili kwa sababu maliasili hatuwezi kuomba sisi, waombeni nyie watenge maeneo ili wakazi wa Biharamulo wapate maeneo ya kufugia, nina wafugaji wengi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa imekuwa ina-prompt watu maliasili wapo hapa, mwezi wa pili nadhani walikuja wakamfukuza mkuu wa TFS pale na viongozi wengine, wafugaji wa Biharamulo wamekuwa wanalipa pesa, wanachanga, pesa nyingi mpaka milioni 50 wanawalipa viongozi, viongozi halafu wanawaruhusu wanaingiza ng’ombe, angalia mfugaji huyu anavyodhulumika, kwamba hana eneo la kuchungia inabidi amlipe mtu wa TFS amruhusu aingie yaani Mtanzania mwenyewe hata eneo la kuchungia ng’ombe unanunua, lakini bado Serikali ipo hapa inasema inataka ikuze ufugaji, kwa hiyo naomba hili jambo mliangalie nyanyukeni mkatusaidie na hapo. Sina haja ya kuendelea sana kwenye masuala hayo nadhani mmenielewa, rafiki yangu Mheshimiwa Ulega unaniangalia umenielewa vizuri njoo unisadie ili wakazi hawa wa Biharamulo wapate eneo la kufugia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lipo jambo moja nimekuwa naliangalia kuhusu ufugaji wa Samaki, kwangu kule mwanzo watu walihamasishwa wafuge samaki, watu wengi sana wamechimba mabwawa kwa ajili ya kufuga samaki mabwawa yale yamekauka hayana maji na watu wengi sana wamepata hasara, sasa ameongea sana bwana Mheshimiwa Mwijage hapa asubuhi Mheshimiwa Mwijage ni mtaalam sana wa mambo ya samaki kwa sababu mpaka anaandaa na vyakula issue ya kufuga kwa kutumia cage, lakini si kila mtu yupo karibu na ziwa, kutoka kwangu Biharamulo mpaka nifike Chato ziwani ni kilometa 50 siwezi kuwaambia wakazi wote wa Biharamulo sasa washuke Chato kwenda kufuga cage fifty kilometers unaenda ukaweke cage pale ukatafute eneo its difficult.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba sana Serikali mnisikilize katika hili bado tunaingiza Samaki all most fifty-eight billion tunaingiza value, lakini kwenye Ilani ya CCM ukurasa wa 55 tumesema tunataka tuongeze idadi ya vifaranga vinavyofugwa katika vituo vyenu vile vinne vya Ruvuma, Iringa, Morogoro na Tabora ifike vifaranga milioni tatu, sasa hao vifaranga milioni tatu tunamuuzia nani kama watu wanajenga mabwawa, wakishajenga mabwawa maua yanakauka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilichokuwa naomba nataka nitolee mfano, kwa mfano Biharamulo tulikuwa na mradi mkubwa wa maji ambao umekuwa design kwa ajili ya kutuhudumia pale kwa sababu tupo mbali na ziwa na hatuna access ya maji. Mwanzoni walikuwa wame-design wachimbe bwawa kubwa ambalo bwawa litakuwa linakusanya maji ya mvua kwa mwaka mzima, lakini bahati nzuri tutapata maji ya maziwa ambayo yatakuja kama Ilani ilivyoahidi, kwa hiyo mpango wa bwawa umeisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ikaja na hii idea; Don Consult ndiyo wali-design ile kitu. Sasa nilitaka mfanye pilot project kwa kuanzia kwangu. Mje mwombe pesa, ongeeni na Don mchimbe lile bwawa pale kwetu Biharamulo. Bwawa lile litumike kwa ufugaji. Watu waliokuwa wanataka kufuga kwa kutumia vizimba sasa kule ziwani waje wafugie pale, then you will be charging them. Kwa sababu, kukuza wale vifaranga mnakosema, mtapata wateja pale. Is a business mind, mnaweza mkaja pale mkachimba lile bwawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkishachimba bwawa, maji yanaingia pale; watu wa kufuga kwa cage waje, lakini mtawa-charge kadri mnavyowakatia maeneo. Watafuga pale, mtakapokusanya fedha mnahamia sehemu nyingine, mnatengeneza bwawa lingine, maana yake tunatengeneza samaki fresh, hata mtu asiyekuwa karibu na ziwa aweze kupata samaki fresh, siyo wa kwenye friji. Maana samaki wanasaidia hata kukuza brain za watoto. Wote ni mashahidi hapa, kwa wenzangu wanaotoka Ukerewe kwa Kanda ya Ziwa, waliozaliwa mle visiwani, huwa tunasema kwa Kanda ya Ziwa watu wa Ukerewe wana ma-professor wengi sana. Kwa sababu gani? Samaki wanaoishi nao mle ziwani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba hili jambo mliangalie, mtusaidie, mje mjenge mabwawa. Mabwawa muwakodishe wafugaji, ambao watafuga na watakuwa wanalipa as time goes on huku mkikusanya fedha mnapeleka sehemu nyingine. Tunafungua watu kibiashara na vile vile tunapunguza fedha ambazo tunaagiza sato na samaki wengine kuwatoa nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema hayo, kwa sasa yalikuwa ni hayo mawili, niseme kwamba naunga mkono hoja. Nategemea haya ambayo nimeyasema, tutapata majibu sahihi na ya uhakika ili wananchi hawa walioniagiza mambo ya ufugaji wapate solution kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na naunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia katika Wizara hii ya Viwanda na Biashara. Kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza sana Waziri wetu wa Viwanda na Biashara, Naibu Waziri na watendaji wote maana kazi kubwa wameifanya na hotuba nzuri imesomwa hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda nadhani nina dakika saba tu na vitu ni vingi nadhani niweze kwenda haraka haraka. Jambo langu la kwanza ambalo ninalo tuna hii issue ya Special Economic Zone, nilikuwa najaribu kupita nimeona tulijiandaa ni karibu kila mkoa uweze kutengeneza kongani kwa ajili ya viwanda, lakini sasa nikawa nawaza jambo moja, nimejaribu kuangalia katika research zangu nikawa naona viwanda vingi sana ambavyo vimejengwa katika wakati uliopita vimejengwa Mikoa ya Pwani na Mikoa ya Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikawaza nikasema kwanini viwanda vingi sana vimejengwa Pwani na Dar es Salaam wakati sikusema labda malighafi nyingi sana ziko pale, lakini kitu ambacho nimekiona viwanda vingi vilivyojengwa ni viwanda vya process, unakuta mtu analeta raw material kutoka nje ya nchi ana i-process akimaliza ku-process inakuwa product ambayo tunaitaka anaweza kuiuza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikawa nawaza sisi wa Mkoa wa Kagera, kilometa 1,400 kutoka bandari ya Dar es Salaam, watu wa Mara Kigoma kilometa 1500, tutakapo jenga viwanda ambapo tunaleta malighafi kutoka nje ya nchi tukaenda kujenga vile viwanda kwetu Kigoma, kwetu Kagera, sidhani kama tutaweza kuwa competitvetuweze kushindana na watu ambao wanajenga vile viwanda maeneo ya Pwani. Kwa sababu hakuna mfanyabiashara ambaye hatakuwa tayari kuja ku-invest Kagera na Kigoma at is the same incentiveambayo na mtu wa Dar es Salaam anapata na mtu wa Pwani anapata yeye aongeze kilometa zile aende kule aweke kiwanda, halafu kesho wakati wa kuuza mtu yule akashindane na mtu aliopo Dar es Salaam. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, umeshaongeza cost of transportation container moja mpaka ulifikishe Kagera la forty feets ni milioni sita, ufikishe Kigoma ni milioni sita, kuja na kurudi kama ile product utakayouza Dar es Salaam ni milioni sita unaongea forty feets imeshaongeza milioni 12, wakati aliopo Dar es Salaam ka-clear kwa 350,000, mzigo unaingia sokoni. Sasa nilichokuwa naomba kwa Wizara ya Viwanda tujaribu kuweka mkakati maalumu wa kuona na sisi maeneo yetu ya huku tuweze kuweka uwekezaji yaani tuweze kuweka vivutio kwa ajili ya uwekezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama na sisi tunasema watu wakawekeze Kagera, wakawekeze Kigoma, wakawekeze mikoa mingine ya pembeni huku tuwe na incentive ambayo Serikali inatoa, waone kuna unafuu fulani kwao ili hata kama tukiwaambia wakaweke viwanda kule waweze kuja kuweka viwanda unless otherwise sasa viwanda hivi vitaendelea kubaki Dar es Salaam na Pwani tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kitu kimoja cha muhimu ambacho ninacho, mimi nina declear kwamba niko kwenye Kamati ya Viwanda na Biashara tulitembelea Ubungo pale EPZA, kuna watu pale wanazalisha jeans wanapeleka Marekani, lakini kitu ambacho niliona wakati wa ziara wanatoa material kutoka Pakistan wanaleta garments kabisa ambayo iko tayari kwa ajili ya kushona kinachofanyika pale ni kama fundi cherehani wanashona tu zile nguo, alafu wana export kwamba zimetoka hapa alafu wanapeleka Marekani, maana analeta under Special Economic Zone halipi kodi anamaliza pale tena ana export halipi kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nilichokuwa naomba ni kitu kimoja, amemaliza kuongea Mheshimiwa Nyongo hapa, mimi natoka Kanda ya ziwa katika Jimbo langu la Biharamulo tunalima pamba pia, wakulima wa pamba wako wengi sana hapa ni aibu kuona pamba inatolewa hapa, tuna export pamba inaenda nje ya nchi, wale jamaa wanaenda wana process wanatangeneza garments za kutengenezea jeans Pakistan halafu the same pamba ambayo tulipeleka sisi inatoka Pakistan inakuja Ubungo inashona, inamaliza kushona inapeleka Marekani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilichokuwa nasema ni nini, viwanda hivi vya kimkakati ambavyo tunavyovipanga, tupange viwanda vya kimkakati ambavyo vitatumia raw materials ambazo ziko kwenye sehemu zetu. Sidhani kama kile kitu kinachofanyika Pakistan kinashindwa kufanyika hapa, maana tuna viwanda vingi ambavyo vina process vitu hapa na tumeonesha kwamba tunaweza kufanya vitu ambavyo vinafanyika nje vikaweza kufanyikia hapa. Nilichokuwa naomba kwa upande wa Wizara ya Viwanda sasa, maana ninyi ndiyo custodian wa suala la biashara na vitu vingine hapa, muende mkatusaidie mkae na TIC, mtusaidie, wawekezaji wanapokuja washaurini wawekezaji kwa sababu tayari tuna client anayetengeneza jeans hapa na ana export jeans nyingi sana. Sasa kwa sababu tuna client anaye export jeans hapa na pamba tunayo tutafute wawekezaji wa kwenda kuweka viwanda Kanda ya Ziwa tunapolima pamba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakishaweka viwanda Kanda ya ziwa tutowe pamba sisi kwanza tukishatengeneza vile tutapata mashudu kwenye pamba, tutapata mafuta haya tunayo import kutoka nje, kutakuwa na advantage nyingi. Yule mtu akishamaliza kutengeneza garment tutoe pale tulete Ubungo pale tukamuuzie. Najua ipo shida maana katika maongezi na mtu mmoja aliniambia hatuna capacity hiyo, hakuna mtu ambaye yuko tayari kulima pamba hapa kwa shilingi 1,000; akakope pesa benki alafu pesa ifie kule wauze assets zake. Lakini kama soko liko pale Ubungo tuna hakika kwamba watu watalima pamba na kinachotakiwa anayekuja kuwekeza kwenye kile kiwanda hakishakuwa na shamba lake yeye mwenyewe la kulima pamba ni kwamba hata kile kiwanda chake hakitakufa, maana tumekuwa na shida moja sana Watanzania, unakuta mimi nimwekeza kwenye kiwanda, unapowekeza kwenye kiwanda hata kwa wenzetu wanachokifanya huwezi kutengeneza excavator tunaona caterpillar yale barabarani, kuna anaye muuzia engine, kuna anayemuuzia vitu vingine, kuna anayemuuzia ticks, inakuwa combination kiasi kwamba kabla ya kiwanda chako wewe kufa unayetengeneza caterpillar kuna stakeholders wengi sana huku nyuma yako wana feel uchungu kabla ya wewe kuweza kuathirika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa shida yetu sisi utakuja kukuta kiwanda unacho wewe tu, raw material unatoa nje kwa hiyo hata kesho kiwanda kinakufa hakuna mtu anayeumia hapa, lakini tukiweza kutengeneza viwanda ambavyo ni feeders wa viwanda vingine ambavyo vipo hapa nina hakika hata vile viwanda vikubwa havitaweza kufa kwa sababu tayari kuna mtu ananufaika navyo pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kitu kingine ambacho ninacho kwenda kwa Serikali, kuna jambo moja ambalo nimekuwa najiuliza sana, mimi nimekuwa nafanya kazi ya sales naweza ni-declare interest, kitu kimoja ambacho watu tumehusika na maunzo sehemu nyingi tulipo, lazima usimame katikati, unasimama katikati kwa client na unasimama katikati kwa kampuni, unaangalia maslahi both sides. Sasa sehemu kubwa sana ya viwanda wafanyabiashara wamekuwa wanaachwa kama yatima, ninachoomba kwa Serikali hasa kupitia Wizara ya Viwanda wa Biashara tunapolia humu tukawa tunasema viwanda, viwanda, kazi yenu nyie kubwa ni mambo ya viwanda na wafanyabiashara. Simameni na wafanyabiashara maana mfanyabiashara anapokufa hebu feel kwamba kuna kitu mimi nimepoteza kwenye sehemu yangu ya kazi maana hawa watu wanakuwa wanalia kodi.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka kipindi cha nyuma niliwahi kuelezea hapa tulivyoenda pale Ubungo mtu mmoja amefunga kiwanda anapeleka Uganda, wakati tunaongea pale tunaambiwa TRA. Sasa nikawa najiuliza hivi TRA ni nani? Maana mimi nakumbuka wakati nafanya kazi nilikuwa nagombana sana na wahasibu unaleta mteja pale mhasibu akija naye anakubalikia wakati unatafuta mteja mhasibu hayupo, lakini siku unamfikisha pale anasisimama anataka hiki anataka hiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mimi nikuombe Mheshimiwa Waziri hii kazi ya kutafuta wateja ni yako tunachotaka utuhakikishie kwamba unapoangaika kutafuta wateja huyu TRA wanajua unatumia nguvu kuwatafuta, sasa msimalize kuwapata watu wanajenga viwanda hapa, kesho mtu mwingine anaweka kikwazo hivi viwanda vinafungwa itakuwa ni aibu kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nina hakika direction yetu ni nzuri, tumemsikiliza Rais hapa alivyosema, kwa hiyo, nina hakika tukiji-tune katika kuhakikisha tunajenga mazingira mazuri ya kuwasikiliza wafanyabiashara, haiwezekani mtu akaweka bilioni 250 hapa halafu wewe huwezi kwenda kukaa naye mezani ukamuuliza ana matatizo gani? Akaweka bilioni 300 hapa huwezi kwenda kukaa naye mezani ukajua anamatatizo gani? Hizo atazipeleka Uganda, atazipeleka Kenya, atazipeleka Zambia na sehemu nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nadhani baada ya hayo kwa sababu ya muda nilitaka niongee issue ya Liganga na Mchuchuma lakini wenzangu wameshaongea ni sehemu ambayo itatusaidia sana sana, maana kama unaagiza mzigo China, ukiomba quotation ya product yoyote ya chuma China hawawezi kukupa quotation ya thirty days kwenda nje, sana sana ya siku kumi/siku saba kwa sababu bei ya chuma inabadilika kila wakati. Sasa suala la Linganga na Mchuchuma tulichukulie serious ni sehemu itakayotunyanyua sisi hapa maana product za chuma hata tunavyoziagiza huko nje ni very expensive na bei zinapanda kila siku. Nyote ni mashahidi kama kuna mtu anafanya biashara hapa tumesikia China juzi wameongeza 13 percent kwenye export zote. Kwa hiyo, kama hata kuna mzigo ulikuwa umeagiza China leo umeongezeka kwa asilimia 13 kwa sababu bei ya chuma ilivyo fractuate. (Makofi)

Kwa hiyo, niombe suala la Liganga na Mchuchuma Serikali ilichukulie serious ili sasa liweze kututoa hapa, tuunze chuma hapa kwa majirani zetu kama sisi tutashindwa kutumia hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema hayo naomba niunge mkono hoja, ahsante sana.(Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Nishati
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi pia niweze kuchangia mchango wangu katika hotuba ya Wizara yetu ya Nishati, kwanza nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa hotuba nzuri ambayo ameitoa na Naibu Waziri pamoja na Watendaji wote wa Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, lakini pia nitoe shukrani kwa Wizara hawa kwa Waziri na Naibu Waziri nakumbuka mwezi Desemba na mwingine mwezi Januari mlifanya ziara Biharamulo mkatutembelea sehemu kubwa mkilenga katika kituo chetu cha kupoozea umeme cha Nyakanazi ambacho kinajengwa kwa hiyo niwashukuru sana kwa visit ile ambayo mmeifanya na sehemu zote ambazo tulitembelea na ahadi nzuri ambazo zilitolewa base done contract ambayo ilikuwepo pale ambayo tunategemea itamalizika tarehe 30 mwezi wa tatu kama ulivyosema wakati tumetembelea Nyakanazi pale. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kwa bahati mbaya mpaka sasa contract ile haijamalizia na wale wakandarasi bado wapo site. Labda niseme jambo moja tu tumekuwa na tatizo kubwa sala la kukatika umeme sehemu za Biharamula na Ngara na halikadhalika na Chato, lakini Chato nadhani kuna unafuu ila kwangu kwa sehemu ya Biharamulo tatizo kubwa tupo kwenye low voltage umeme unaotoka geita kuja Chato substation unakuja kwenye 34 Kv lakini kutoka pale nadhani kuja Biharamulo unakuja uko chini sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa umeme ule hauwezi kufanya kazi na sasa hivi tuna shinda kubwa watu hata fridge kwenye supermarket pale ice-cream zinayeyuka napigiwa simu Mbunge, maji sasa hivi tunamgao wa maji Biharamulo maji yenyewe hatuna lakini hata yale machache tuliyonayo Biharamulo tupo kwenye mgao tupo kwenye mgao kwasababu umeme uliopo ni mdogo kwa hiyo pampu zetu pale Kagango haziwezi kupampu yale maji hatimaye tukaweza kupata maji vizuri pale mjini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini baada ya kufuatilia yote haya maana nimejaribu kufanya follow up ya issue ya Nyakanazi, Nyakanazi imeahidiwa kwenye Ilani ya CCM na pia tulishaenda pale tukatembea kwamba tulikuwa inabidi tupate umeme wa Msongo wa Kilo Volt 220 kutoka Geita uje pale. Nimepita pale juzi ujenzi unaendelea vizuri, lakini lipo tatizo ambalo labda sasa kwasababu na Waziri Mkuu yupo hapa ningependa kujua tuna transfoma mbili ambazo inabidi zije kufungwa pale Nyakanazi. Tangu tarehe 20 Desemba transfoma zile zipo Bandarini hapa, tarehe 20 Desemba as we are talking sasa inaenda sasa ni miezi sita. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini shida iliyopo pale ni kwamba TANROADS na TANESCO wanashindwa kuelewana jinsi gani watalipana kwenye surcharge amount ili waweze ku- release zile transforma zile pale Nyakanazi. Lakini kipindi yote haya yanafanyika sisi pale kwetu bado ni shida ndugu zangu, maeneo ya Nyakanazi pale hata kuchaji simu wananchi wananipigia simu hawawezi kuchaji simu umeme upo chini lakini kuna watu wa Serikali hii hii ambayo inatekeleza Ilani ya CCM watu wa Serikali hii hii ambao wameapa kumsaidia Rais wanashindwa kukaa chini na kuelewana kwa vitu vidogo hivi wananchi wanatesema. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa nilikuwa naomba tunapo windup nipate kauli ya Serikali hizo transfoma zinatoka lini Serikali ni hii hii moja, maana hata mkizizuia pale mwisho wa siku zitatoka tu hata zikikaa mwaka mzima zitatoa tu sasa kinachoshindikana ni nini hizo transfoma zikatoka leo zikafungwa pale, mambo yenu ya kulipana mnatoa mfuko wa kushoto mnaingiza mfuko wa kulia mtayafanya baadaye kipindi hicho wananchi wanyonge walioko huko vijijini wanapata umeme.

Mheshimiwa Spika, naomba TANESCO tuwasaidie maana sasa TANESCO nia yetu nyie ni nzuri mlishakuja pale mkasema, lakini 2.3 bilion per one transforma hiyo fedha mnaitoa wapi? Ukiongeza 4.6 bilion umlipe TANROADS hiyo fedha si ingeenda kufanya miradi mingine ya umeme pale! Kwa hiyo, ninadhani kuna vitu vingine nadhani mkae wenyewe humo ndani muelewane lakini sisi tunachohitaji tuone zile transfoma zimefungwa pale wananchi wa Biharamulo waondokane na tatizo la kukatika katika umeme hata wenye viwanda vidogo vidogo pale Nyakanazi waweze kufanya kazi maana leo tuna viwanda lakini hakuna anayeweza kufanya kazi kwasababu umeme una run under low voltage. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hilo jambo naomba niliweke wazi kama hatutapata majibu ndugu yangu Mheshimiwa Kalemani najua tuna-share ma-generator ya pale Biharamulo otherwise sasa itabidi unipe permission Biharamulo tuanze kuwasha Generator kwa kutumia mafuta ya Diesel kipindi wewe unapata ya kutoka Geita nipate ya Biharamulo kwa kutumia mafuta ya diesel mpaka pale mtakapopata zile transforma tuweze ku-balance tukae pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini baada ya kulisema hilo lipo jambo jingine moja ambalo nilipenda pia niliongelee Biharamulo tunao mgodi wa STAMIGOLD last week nadhani kama wiki mbili nimetembelea mgodini pale. Imeletwa line ya umeme kutoka Geita Special line mpaka Mgonini STAMIGOLD lakini cha ajabu ile line ipo pale umeme bado haujaingizwa ndani na wale watu wa mgodi wa STAMIGOLD mgodi wetu wa Serikali ambao hata CSR tu wanashindwa kunisaidia vitu vidogo pale mtaani wale watu wanalipwa 1.2 bilion kila mwezi kwa ajili ya mafuta ya diesel ule mgodi ni wa Serikali ungeniambia ni GGM wanalipa hata Bilioni ngapi I don’t care kwa sababu ni fedha yao labda mna process nyingine ya kuwarudishia lakini ile ni fedha ya Serikali ule mgodi ni wetu sisi na TANESCO nyie mkishawaingizia umeme kule your assured kupata more than seven hundred million per month nyie ndio mtakuwa the large users wa umeme ukiondoa Kagera sugar kwa Mkoa mzima wa Kagera .

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niwaombe hilo jambo mliangalie ili tatizo limalizika na hata wakati wa ku-wind up pia nipate majibu maana sisi tuna mgodi lakini mgodi unaoshindwa hata kunisaidi barabara pale Kaniha huo mgodi ni wa nini? Mgodi unaoshindwa kunisaidia hata kujenga zahanati pale ule mgodi ni wa nini. Lakini kwa sababu wana run under high cost kama hizi za kununua mafuta maana wakikulipa wewe Milioni 700 TANESCO wanabaki na Milioni 500 itaweza hata kutusaidia na sisi tukiomba CSR watusaidie kusaidia jamii iliyozunguka mgodi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kuja jambo jingine Mheshimiwa Waziri ulipotembelea Biharamulo wakati ule kuna kata kama tano ambazo bado hazijapata umeme kata ya Kalenge lakini najua Kalenge watapata umeme kutoka kwenye hii substation ya Nyakanazi pindi unaenda Kigoma kati ya vile vijiji thelathini na ngapi ambavyo vimetajwa, lakini kuna Kata ya Kaniha na pia kuna Kata ya Nyantakara kuna Kata ya Nyanza. Lakini hii Kata ya Kaniha na Nyantakara ulipokuja kuna mkandarasi pale ana umeme wake anawauzia wananchi Power Janne. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ulitoa maelekezo specific kwamba umeme ni shilingi 100 per unit huyu mtu tukakaa kwenye Baraza la Madiwani tunakuelekeza Meneja wa TANESCO na Mkuu wa Wilaya wakati ule tulikuwa pamoja leo karudi tena anawaambia watu anawachaji shilingi 2,000 TANESCO mmemruhusu, sasa nashindwa kuelewa, yaani Waziri unatoa order kuna mtu mwingine nyuma yako naye anatoa barua ingine, mwenye madaraka ni nani hapo?

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nilikuwa naomba pia hili jambo la power Janne tupate majibu humu ndani maana Diwani wa Kalenga anashinda mjini pale anahangaika kila siku, wale watu wamegoma kuwasha umeme na wamesema wanataka shilingi 2000 na wewe ulishaagiza ni shilingi mia moja, nimemuuliza Naibu Waziri, nimekuuliza wewe mwenyewe umeniambia shilingi mia moja. Kwa hiyo nilikuwa nipate majibu ya Serikali wananchi wa Kalenga wasikie, walioko Mavota wasikie na sehemu nyingine kwamba ni shilingi mia moja ile ile iliyoagizwa na Waziri ndiyo hiyo inayofanyika pale. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho nilitaka niongee kwasababu ya muda kuhusu issue ya bomba la mafuta hili la kutoka Uganda. Niishukuru sana Serikali na hasa nimpongeze Rais kwa kusaini contract hii na hatimaye sasa neema hii kubwa inakuja kwenye nchi yetu. Lakini nilikuwa nawaza katika angle ya tofauti kidogo, sehemu kubwa ya lile bomba itakuwa ni project ile ya mabomba yenyewe yanayolazwa.

Mheshimiwa Spika, sasa nikawa naomba Mheshimiwa Waziri na Serikali, kama mnaweza mkaongea na contractor najua kutengenezea bomba huko watakapozitengeneza akazisafirisha zile bomba kilomita 1000 azifikishe transportation cost tu ile anatosha kuja ku-setup kiwanda hapa, I am sure tukiangalia cost ya ku-transport bomba za kilomita 1000 yule mtu akabeba mashine Europe akaja hapa mkampa eneo na watu wake nilicho na uhakika nacho kutakuwa na transfer of technology lazima yule mtu baada ya kuondoka hapa watu wetu watakuwa wamejifunza kwa sababu tuna vijana ma-engineer tuna watu ambao wamesoma wataajiriwa kwenye kile kiwanda, kwake ni rahisi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukishampa site akaweka hapa ni rahisi kwasababu anafanya serving kwa sababu bomba atazizalishia hapa na the good thing ni kwamba badala ya kuleta meli nzima imejaa mabomba, ukakodi truck zaidi ya 600 zaidi ya 800 zikaanza kusafirisha mabomba kuelekea Uganda unampa site hapa, kila siku truck kumi anatoa zinaenda site zinashusha mabomba, truck ngapi anatoa kwake logistically itakuwa imekaa vizuri. Kama mtaturuhusu tunaolewa hivi vitu tunaweza tukawasaidia hata kama atakuja hapa ili sasa tushawishi yule mtu kwamba hatukuelekezi boma uje uzalishie hapa leta material, fanya kila kitu leta watu wako, leta mashine tumekupa site hii hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nina hakika baada ya project ile yule mtu zile mashine hatazing’oa hapa na sisi tunafanya research ya mafuta kesho na kutwa kama vijana wetu wamejifunza watatumika wao, we are sure leo tumejenga flying over pale niliwahi kusema, vijana ma-engineer wa Kitanzania waliohusika na flying over ya Ubungo leo wanahusika na kwingine baada ya muda hatutahitaji wageni vijana hawa hawa wa Kitanzania watajenga vile vitu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo niombe hilo wazo ni zuri kibiashara ni wazo zuri kwa manufaa ya nchi kama mtaweza mshawishini huyu mtu anaweza aka-set up hata sehemu mbili au tatu za kuja kutusaidia.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya muda nashukuru sana na naunga mkono hoja ahsante. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Fedha na Mipango
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nikushukuru kwa kunipatia nafasi hii ili niweze kuchangia katika hotuba hii ya Wizara ya Fedha na Mipango.

Mheshimiwa Spika, kwanza, nichukue nafasi hii kumpongeza Waziri na timu yake yote kwa hotuba nzuri ambayo ameitoa. Pia na wasaidizi wake wote katika ofisi yake kwa kazi nzuri ambayo wamekuwa wanaifanya wakitusaidia katika kutekeleza Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi maana kwa sehemu kubwa wao ndio wawezeshaji wakubwa ambao wanatupatia pesa ili tuweze kutekeleza miradi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi nimesimama hapa kwa mambo kama mawili; jambo la kwanza ni ku-share experience katika kitu ambacho nataka nichangie nikikiita protection ya local industries au viwanda vyetu vya ndani. Maana nimejaribu kupitia katika baadhi ya details nikaona kwamba iko haja ya kupanua wigo wa kodi kwa sababu nakumbuka siku Rais anahutubia Bunge alitamka hapa akasema tujaribu kupanua wigo wa kodi. Sasa najaribu kuangalia vyanzo vipya vya kodi ambavyo vinaweza vikatusaidia ili hatimaye tuweze kuongeza mapato kule ambapo tunahisi kwamba mapato yalikuwa hayakusanywi vizuri ili haya ambayo tumeyapanga kuyafanya yaweze kufanyika kwa wakati na pesa zikiwepo.

Mheshimiwa Spika, cha kwanza, nilijaribu kuangalia trend ya biashara katika nchi hii. Nikawa najaribu kuangalia viwanda vya ndani na tozo za kodi mbalimbali, hasa importation ya vitu ambavyo vinatolewa nje na tunavyoviingiza hapa kuna kitu tunaita import duty, nikawa najaribu kuangalia duties ya baadhi ya vitu na experience yangu ya shughuli zangu za nyuma nikaona liko jambo la kufanya.

Mheshimiwa Spika, cha kwanza, nilikuwa napitia manufactures wa trailers, haya ma-trailers ambayo tunatengeneza. Nadhani kuna Kiwanda cha Super Doll, Simba Trailers na M Trailers nilijaribu kufanya research pale nikawa naona trend yao ya uzalishaji nikaona kwamba as time goes on trend imekuwa inashuka haipandi na employment so far ni kama ime-stuck, lakini ina stuck kwa sababu kumekuwa na unfair competition kwenye importers wa trailers na manufacturers wa trailers.

Mheshimiwa Spika, nataka niliseme jambo hili kwa sababu kwanza nilijaribu kuangalia kitu kimoja nikawa nawaza aliyeleta sera ya kwamba tupitishe sheria trailer linatozwa 10% ya buying price halafu gari tu la kawaida IST ambalo unajua hapa hamna mtengenezaji wa IST nikileta hapa la kwangu la kutumia ni mstaafu ni nini, natozwa import duty 25%. Sasa nikawa naona tunapotafuta kulinda viwanda vya ndani, maana nimejaribu kufanya research si hapo na sehemu nyingine nitaelezea, wenzetu kwa mfano Uturuki na China unapofanya export ya trailer lolote lile kuna export levy wanapewa na nchi zao; 17% mpaka 20%.

Mheshimiwa Spika, sasa mtu ambaye ana-export akapewa levy ya 17% na 20% maana yake huyo mtu tayari ana kitu anachoki-save kwa asilimia 17 mpaka 20. Unapo- save asilimia 17 mpaka 20 ukaja hapa Tanzania bado unalipa kodi import duty kwa asilimia 10. Already yule mtu kuna kama asilimia 10 ambayo ameshai-save kule anaponunua. Tukumbuke materials nyingi ya hivi vitu tunaagiza kutoka kule nje. Sasa tumekuwa tunajikuta kwamba tunasaidia kutengeneza biashara na kujenga viwanda vya nchi nyingine wakati tukisahau ku-protect watu wa kwetu hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, watu wa kwetu hapa tuna faida gani tunapojenga viwanda? Hiki kitu nimekuwa nakisema mara zote, cha kwanza kikubwa ambacho tunakuwa nacho ni transfer of technology yaani tunachokililia hapa ni watu wetu wapate ujuzi wa kuvifanya vitu vile. Hii ni kwa sababu vyuo vyetu vya Tanzania kwa sehemu kubwa tunasoma theories na practical kidogo ile ya miezi mingapi tunayoenda field kule tunarudi sasa tunapopata viwanda tukakaa kwenye viwanda na sisi tukaweza kujifunza maana yake tuna advantage kubwa zaidi ya kuja kugundua vitu vingine ambavyo vinafanyika kule nje, tukiweza kuvifanya hapa vitapunguza importation hatimaye tuweze kujenga ajira hapa. Tuna vijana wa Kitanzania tunapowatengenezea ajira wale vijana maana yake wanalipa Pay as You Earn, SDL na halikadhalika pesa inayopatikana inabaki hapahapa. Kwa sababu tunapeleka dola kununua vitu nje na wao hawaji kununua vitu hapa, hatu-export vitu vingi hivyo maana yake balance ya Mheshimiwa Waziri kwa sehemu kubwa tutakuja kujikuta kwamba tuna pesa nyingi za kigeni ambazo zimeenda nje huku stock yetu inakuwa ndogo baadaye tunapata shida. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba chanzo kipya cha kodi, kama mtajaribu kuliangalia hili jambo, tuongeze kwenye upande wa importers wa trailers ili tulinde viwanda vya ndani. Nilikuwa nawaza tukiongeza hata yenyewe ikawa 25% kuna shida gani? Mtu anayeona kwamba ni ngumu kununua hapa ina maana atatuongezea 15% kwenye kodi ambayo tunaililia hapa. Kama hataongeza ile atanunulia hapa kwa sababu bado kuna Watanzania wengine wananunua haya ma-trailers hapahapa na wanayatumia. Sasa anayeenda kutoa kule nje kwa sababu anapata unafuu wa bei na haji kulipa kodi kubwa hapa ndiyo maana anafanya hivyo. Kwa hiyo, hili jambo nilikuwa naliomba ili kuweza kulinda viwanda vya ndani.

Mheshimiwa Spika, kitu kingine nilikuwa najaribu kupitia kwenye miradi ya maji Mheshimiwa Waziri. Kuna mambo ambayo yamekuwa yanafanyika hapa, kwa mfano nakumbuka Hayati Rais Magufuli aliwahi kuuliza kwa nini tuna- design miradi ya maji kwa kutumia vifaa ambavyo haviko kwenye nchi hii? Hilo jambo mimi ni shahidi, unakuta mtu ana- design Ductile Iron Pipe, unajiuliza bomba la DI linapatikana India na China lakini tuna kiwanda pale Ubungo kinatengeneza mabomba ya chuma. Hakuna kitu ambacho kinafanywa na DI hakiwezi kufanywa na bomba la chuma la kawaida, lakini kwa sababu ya mtu na interest zake yeye mwenyewe ana-design kitu ambacho hakipo hapa.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba hata hayo mabomba kwa sababu yamekuwa na 10% tuyaongezee yapate 25% tuone kama kuna mtu ataya-design hapa. Kwa sababu tunavyoyatoa kule India au China yatashindwa ku- compete na mabomba ya hapa maana yake mabomba ya hapa yatakuwa cheaper kuliko yale kwa sababu tumeongeza kodi. Matokeo yake ni kwamba watu wata-opt kununua ya hapa, atakayeamua kuyaleta atatulipa 25% again tumeongeza kodi. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri hili jambo mliangalie.

Mheshimiwa Spika, lakini kuna jambo moja mimi niende nalo mbali. Last time nilikuwa Zambia wale watu wanakuuliza unachotaka kukiuza hapa kwetu hakipo? Yaani the first thing uwaambie kwamba ulichoendanacho kama unafanya mauzo kwao hakipo? Kama kwao hakipo watakusikiliza lakini kama kipo inakuwa ngumu. Same applies hata Uganda, Uganda wana sera yao wazi kabisa wanakwambia buy Uganda build Uganda. Hicho kitu Waganda wanacho kabisa yaani anakwambia lazima anunue kitu cha kwao ili aweze kuijenga nchi yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niombe hata sisi kama kuna uwezekano tuje na sera ya ku-protect vitu vya kwetu hapa. Tutamke Watanzania wajue akinunua kanga ya Tanzania anaijenga Tanzania. Watanzania wajue wakivaa vitenge vya Tanzania wanajenga Tanzania. Tusigombane hapa kwamba ma-container ya vitenge yame-park bandarini wameshindwa kuyatoa wakati tungekuwa tumewahamasisha Watanzania wakanunua vitenge ambavyo vinatengenezewa hapa kuna faida fulani, kwanza wangependa vya kwao lakini pili kuna saving tunaifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kwa kumalizia harakaharaka kwa sababu ya muda, mimi naomba ni-declare interest nina jambo moja hapa. Mimi nimekuwa staff wa Air Tanzania nikifanya kazi kama cabin crew pale na baada ya kumaliza chuo nilirudi Air Tanzania kama Development Engineer. Nakumbuka niliondoka pale mwaka 2012 lakini kuna jambo moja ambalo limekuwepo pale kwa sehemu kubwa limewaumiza sana waliokuwa wafanyakazi wa Air Tanzania.

Mheshimiwa Spika, nakumbuka kipindi kile kipindi shirika limekwama pesa za mishahara zilikuwa zinatoka Serikalini, lakini pale Air Tanzania tulikuwa na SACCOS yetu inaitwa Wanahewa SACCOS, tunakatwa mishahara kwa sababu ya SACCOS, lakini pia pesa yao ya pension. Nadhani Mheshimiwa Waziri analielewa na Serikali iko hapa inalielewa. Ningeomba basi, kwa heshima maana watu hawa nimefanya nao kazi na wamekuwa wananililia, wananiambia kijana wetu na wewe upo Bungeni kama mwakilishi na wewe jambo linakuhusu. Naomba muwaangalie wazee wale, wengi sana wamekufa, wazee wapo kwenye tabu, lakini fedha yao ipo kule. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali ilisikie hili jambo kupitia kiti chako, tuwaokoe wazee hawa kwa sababu wamelitumikia Taifa, fedha zao zilikatwa kama pension lakini hazikupelekwa, fedha zao zilikatwa kwa SACCOS ya Wanahewa lakini hazikupelekwa. Leo wamestaafu lakini hawana chochote na mbaya zaidi nyote tunajua, Watanzania wengi wanavyokuwa wanafanya kazi wanakuwa wapo kwenye bima, wanalipiwa bima. Wakishamaliza miaka 60 akastaafu hata bima tu hana, tena labda hata tuje tena na sera hata ya kuwa-protect hawa kwamba kama alikuwa mtumishi aendelee kulipiwa bima mpaka anakufa angalau hata tuweze kuwasaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nasema hivi kwa sababu leo wanalalamika, fedha zao zimezuiliwa hawajazipata na matokeo yake hata wanaoumwa tu hawawezi kujitibia. Naomba sana kupitia kiti chako tuliangalie hili ili wazee hawa ambao wametoka kwenye hili shirika kwa shida kabisa, tuweze kuwasaidia na mimi mwenyewe nikiwemo humo, najua za kwangu nazo bado zipo ili hata mimi niweze kupata haki yangu kupitia huko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, kwa leo ni hayo machache, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi pia na mimi niweze kuchangia katika hotuba ya Waziri wa Fedha na Mipango, hasa kwenye bajeti hii kuu ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukuwe nafasi hii kumpongeza sana Waziri na timu yake kwa kazi kubwa ambayo wameifanya, aliongea Mheshimiwa Jerry hapa juzi kwamba umeupiga mwingi sana kama wa Morrison, nadhani na staili ya kuupiga ndiyo staili vijana wanaitumia zaidi, hata jana Mama aliyoyafanya Mwanza kule vijana wanapo- comment wanasema Mama anaupiga mwingi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tuseme kwa kweli kutoka ndani ya kilindi cha moyo wangu nikupongeze sana Mheshimiwa Waziri na Wasaidizi wako kazi mliyoifanya ni kubwa, bahati mbaya siku inasomwa bajeti sikuwepo nilikuwa na msiba kwa hiyo nikawa niko kwenye mazishi ya Babu yangu Biharamulo lakini nilipokuwa njiani narudi nikawa napitia comments nyingi sana kuna watu waliitisha press conference. Ukiona mtu anaitisha press conference anakosa kitu cha kukosoa humu kwenye bajeti anaishia kusema bajeti haijaongelea Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchuguzi uelewe kwamba umemaliza kila kitu. (Makofi)

Kwa hiyo niwapongeze juu ya hilo kazi iliyofanyika ni kubwa sana, pia nimpongeze Mama kwa kazi kubwa ambayo ameifanya tangu ameingiea madarakani ni muda mfupi lakini watu tunaona matokeo chanya kabisa kabisa hasa kwa niaba ya wananchi wa Biharamulo nishukuru kwa milioni 500 za ujenzi wa barabara ambazo zinaingia kupitia TARURA na tayari tumeshakubaliana tuongeze kilometa moja ya lami pale hili tuweze kuchochea maendeleo haraka zaidi. Hali kadhalika na suala la shule ya sekondari, kuna shule sasa tumekubaliana inaenda kujengwa pale Nyakaula pale ni eneo ambalo lilikuwa na wanafunzi wengi zaidi kwa hivyo tutaongezea shule ya pili ili maendeleo haya ambayo Mama anayasema kwa vitendo na wao wayapokee haraka zaidi ili waweze kuunga mkono juhudi kubwa ambazo zinafanywa na Serikali ya Awamu ya Sita. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema haya labda lipo jambo moja ambalo mimi ningependa nijikite nalo, mimi ni mdau wa viwanda kwa hiyo nadhani mchango wangu kwa sehemu kubwa una- base zaidi katika masuala ya viwanda, mpango wetu wa maendeleo wa miaka mitano ijayo 2021/2022 - 2025/2026 dhima yake kubwa inasema ni kujenga uchumi shindani na viwanda kwa maendeleo ya watu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi tangu nimeanza kuchangia mara nyingi sana nimekuwa ninagusa masuala ya viwanda kwa sababu ni area yangu ambayo nimekuwa nikitumika kwa muda mrefu kwa hiyo napenda nichangie kitu ambacho nina experience. Kwanza ni Mjumbe wa Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira, kwa hiyo nichukuwe pia nafasi hii sana kumpongeza Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama yetu, Mama Samia Suluhu Hassan kwa maelekezo ambayo aliyatoa juzi hasa suala la Liganga na Mchuchuma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niko kwenye Kamati na bahati nzuri tumefanikiwa kufika site pale kwenye ziara ya Kamati, mradi huu ni mradi ambao unaenda kuliinua Taifa hili na kutupeleka mbele zaidi. Ukipitia ripoti zote ripoti ya NDC inasema, lakini pia jambo moja ambalo nimekuwa nikiliona kwa upande wangu na upande profession yangu tunachokikosa hapa mpaka mradi huu unachelewa ni technology tu! Technology ndiyo inayotutesa leo tungelikuwa na uwezo tuna wataalam wa Kitanzania pale tungeshatia timu na hii kazi ingekuwa inafanyika leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ukiangalia ripoti NDC, total investment cost ambayo huyu Mchina anakuja kuweka pale ni three billion US Dollars. Sasa ukiangalia three billion US Dollars, tunajenga reli leo inatumia thamani kiasi gani? Wakati ule ni mradi wa kibiashara kwa sababu anaweka three billion USD, na income per year – hii ni ripoti ya NDC – income per year itakuwa ni 1.736 billion USD.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani anaweka bilioni tatu mtaji, baada ya mwaka mapato ni 1.736 billion USD. Kwa hiyo baada ya miaka miwili tu alichokiwekeza pale kashakipata na kila kitu kinakwenda sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo unaweza kuona kwamba kinachotutesa pale mpaka leo ni transfer of technology. Ndiyo maana mimi kwenye michango yangu mingi sana nimekuwa naomba, tujaribu kusikiliza jinsi ya kulinda viwanda vya ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapojaribu kulinda viwanda vya ndani hatulindi tu kwa sababu tunazuia wale watu wasilete au wasifanye nini, tunawawezesha vijana wetu wa Kitanzania kupata knowledge ya how they can work on these industries ili waweze wao wenyewe kesho na kesho kutwa kutumia experience waliyoipata kwenye viwanda watusaidie kujenga viwanda vingine hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, sasa niombe, na nadhani hapa tuko sawa, kwamba kuna watu wameweza kuelezea sana suala la importation. Nilichangia juzi nikielezea suala la importation of traders, sitaki sana kurudia kule, lakini tumeona kwamba viwanda vilivyokuwepo hapa vingi vilikufa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tutakapokwenda kuvinyanyua viwanda hivi maana yake tuna-transfer technology hata kwa vijana wetu wanaosomea mechanical engineering katika vyuo vyetu, vijana ambao wanasoma VETA, maana tunafungua vyuo vya VETA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unafungua vyuo vya VETA tuna-invest billions and billions kwenye VETA halafu hatuna viwanda, hawa watoto tunawapeleka wapi baada ya hapa? Investment tuliyoifanya kwenye vyuo vya VETA tunaipeleka wapi baada ya hapa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunachoomba ni kwamba tujikite zaidi kwenye kuwezesha viwanda vya ndani. Kwanza niwashukuru na kuwapongeza, kwa mfano ishu ya tiles tunajua wengi sana wakienda madukani wanataka Spanish tiles. Sasa ili kulinda viwanda hivi ambavyo vimejengwa kwenye Mkoa wa Pwani, mmeona, mmeongeza asilimia 35, kwamba sasa import duty iwe 35%; unampa mtu chance ya kuchagua premium.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tajiri anayesema anataka akajenge kwa Spanish tiles maana yake anatuongezea asilimia kwenye import duty. Anavyoleta hapa zile tiles ili waweze kuzinunua hapa Serikali inapata kodi ya kufanya vitu vingine, lakini huku tukiendelea kuvilinda viwanda hivyo ambavyo vimejengwa hapa kwa ajili ya kuwaajiri Watanzania na kutumia malighafi za Kitanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niombe sambamba na hilo, ninakumbuka hata ishu ya REA. Nilikuwa napitia ripoti ya REA hapa, wakati mnaanza miaka mitano iliyopita, wakati tunaanza kufanya miradi hii ya umeme nakumbuka walio wengi walikuwa na wasiwasi kwamba je, tutapata capacity? Tutakuwa na uwezo wa kuzalisha hivi vitu hapa nchini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini unapoweka sera nzuri kinachotokea ni nini? Hili likishakuwa soko la tajiri fulani ambaye ana viwanda kule nje, anapoona soko lake halifanyi kazi, anachojaribu kukifanya lazima alifuate soko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu ambaye amesha-invest na anajua soko lake ni Tanzania, amekuwa anapata bilioni 50 au 30 kutoka Tanzania anapofanya biashara, yule mtu ukimwambia tumezuia importation au importation anaona inakuwa kubwa anashindwa ku-compete, anachokifanya anatoka kwenye nchi yake anakuja kuwekeza hapa. Akishawekeza hapa tayari anatutengenezea biashara kwa sababu anataka alinde soko lake ambalo amelipata Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunachoomba, lazima tujaribu kuangalia, mtusaidie kwenye hili. Lakini kipindi mnatusaidia kwenye hili, kwamba sasa tujaribu kuvutia wawekezaji na kuweka conditions ambazo zitalinda viwanda vya ndani, lakini vilevile twende step moja mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilijaribu kuchangia hapa last time nikasema hatuwezi kujenga viwanda vyote Mkoa wa Pwani. Pwani haitaenea. Maana bada ya hapa na sisi vilevile huko mikoani tunahitaji viwanda viwepo. Tunapotamka viwanda hatutatakuja kila siku tunalia viwanda vijengwe Chalinze au Dar es Salaam wakati hata mimi huko Biharamulo, Kigoma na wapi, na sisi tunataka viwanda hivi. Ili sasa mwekezaji atoke aje kuwekeza Kigoma, Biharamulo, Arusha, Mtwara au Mbeya lazima tuoneshe kwamba kuna incentive fulani tunampa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, jana Mheshimiwa Mavunde kaongelea hapa suala la income tax. Tujaribu kuona, huyu mtu anapata advantage gani akija Kigoma? Maana atoe kontena Dar es Salaam, alipeleke Kigoma halafu amalize arudishe tena kuuza Dar es Salaam. Anafanya double kwenye transportation, hataweza kushindana na mtu aliyeko Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tujaribu kuona jinsi ya kuweza kuwasaidia. Hata kama ni income tax, mpe grace period. Mwambie labda akiwekeza Bukoba au Buharamulo mnampa chance ya kutokulipa income tax kwa miaka mitano au mingapi, au vinginevyo mpunguzie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yule mtu ataangalia, atapiga hesabu na benki yake then atajua aende akawekeze wapi. Hapo tutakuwa tunatanua uchumi na kusambaza viwanda kwa ajili ya watu wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nilikuwa najaribu kulipitia hapa ni mazingira mazuri ya uwekezaji ili watu waweze kuwekeza. Hilo jambo mmeliahidi, Mheshimiwa Waziri ninaomba mkalisimamie maana kipindi cha nyuma kilio kilikuwa kikubwa. Lakini kwa sababu bajeti yako imesema na bajeti imesema mawazo ya Wabunge kwa kweli mimi sina budi kushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hata Wabunge tunaondoka hapa kifua mbele kwa sababu miezi mitatu tuliyokaa Dodoma tunaishauri Serikali, kwa sehemu kubwa mambo mengi yametekelezwa na mambo mengi yamekuwa incorporated hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo hata sisi tunaporudi huko nyuma, kesho na keshokutwa hata tunaporudi kwenye Bunge lingine tuna uhakika kwamba tunachokishauri hapa Serikali inasikia. Na hii ndiyo kazi yetu sisi, kuwashauri ninyi, ili ninyi msikie wananchi waliyotutuma muende mkayafanyie kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, kwa kumalizia, niliongelea suala la trailers, naomba hili jambo ulichukulie serious kwa sababu nina experience nalo. Tumeongea, si mimi tu, naona watu wengi, nililianzisha lakini watu wengi sana wameweza kuliongelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, import duty, unajaribu kuangalia magari yanazalishwa hapa, trailers hizi. Tunachojaribu kuangalia, tuvute wawekezaji waje, hata HOWO trucks. Tumeona HOWO ziko nyingi sana hapa. Ongeeni na yule mtu mwenye HOWO kule. Kwa sababu hii ni bandari ambayo ina-serve nchi zaidi ya tisa, tukimwambia aje awekeze hapa akaja na spea, akajenga kiwanda hapa cha kufanya assembling, kama leo wanavyo-assemble magari pale Kibaha, wana-assemble mabasi yameanza kutoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yake ataajiri Watanzania. Tunahitaji ajira kwa ajili ya Watanzania maana wanalipa SDL, wanalipa PAYE, wanalipa vitu vingi zaidi. Lakini chanzo kikubwa cha kutengeneza ajira milioni nane, tutazipata tutakapovutia wawekezaji wakaja hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niombe hilo jambo uliangalia, suala la duty kwa ajili ya trucks, hizi trailers, tuone jinsi tunavyoweza kuzipandisha nazo ili wawe competitive na waweze kushindana na watu wengine hapa. Maana huna haja ya kuichaji IST asilimia 25 halafu mtu anayeleta gari kubwa lenye thamani kubwa ya kutupa kodi kubwa bado anachajiwa asilimia kumi. Hili jambo naomba milaingalie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwapongeze. Mimi sina jambo la kuongezea zaidi ya kushukuru kwa hotuba nzuri na yote ambayo mmeyaweka ambayo tumeyachangia hapa. Mungu awabariki sasa tunapokwenda kuyatekeleza ili sasa kwa sababu ninyi ndio wenye pesa, kuna mambo mengine ambayo tumeyasema hapa yanahitaji pesa, mkaweza kuzitoa hizi pesa kwa haraka zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, kwa kumalizia; TBS tumewapa kazi nyingi sana. TBS leo ndio anayekagua magari, kazi iliyokuwa inafanyika Japan; TBS leo ameacha mkataba na SGR ndiye anayekagua pre-export verification anafanya yeye; TBS tumempa vinasaba ndiye anaanza kuweka vinasaba kwenye mafuta ya petroli. Kwa hiyo kwenye Bunge hili tumempa kazi nyingi sana TBS.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ninachoomba, ili TBS asituangushe kwa sababu hizi kazi ni continuous, atahitaji bajeti ya manpower, atahitaji bajeti ya kununua vifaa. Ninaomba mtenge pesa na TBS apatiwe hizi pesa haraka ili isije ikawepo sababu sasa kwamba TBS tulimpa kazi na ameshindwa kufanya kazi huku akiwa anakwamishwa na ninyi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema hayo, naunga mkono hoja na ahsante sana. (Makofi)
Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kukushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuchangia katika Mpango huu wa Tatu wa Maendeleo lakini pia nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa nafasi hii. Kwanza kabisa, nimpongeze Rais kwa usimamizi mzuri wa miaka mitano hii kwa ambacho kimefanyika, ni very impressive. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda nataka nijikite kwenye suala la mchango wa sekta binafsi. Nimejaribu kupitia hapa Mpango, naona sekta binafsi tunategemea ichangie almost 40.6 trillion shillings na nikafanya average kwa mwaka ni 8.12 trillion, huo sio mchango mdogo sana kwa sekta binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kitu ambacho nimekuwa najiuliza, nimekaa sekta binafsi kwa muda mrefu, labda kwa upande mwingine ningeomba Serikali pia ihusike kwenye ku-support sekta binafsi. Kwa nini nasema hivi? Ni kwa sababu unapoiweka sekta binafsi kwenye Mpango halafu huishirikishi mipango kidogo inakuwa gumu maana tunawaacha wanakuwa separate halafu baadaye tunaenda kukamua maziwa pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nayasema haya? Sasa hivi nimetoka kwenye Kamati tulikuwa na semina nikajaribu kuuliza swali kwa watu wa TANTRADE kwamba nyie kazi yenu kwa sehemu kubwa ni kuhakikisha mnatafuta masoko na mnashauri. How many times mmechukua muda wa kwenda kushauri sekta binafsi, maana nitaenda nitamkuta Mheshimiwa Musukuma na biashara yake ya mabasi naanza kuchukua kodi pale, lakini Mheshimiwa Musukuma amekuwa anaongea humu anasema darasa la saba ndiyo matajiri au ndiyo mabilionea tunaweza kuona kama anafurahisha lakini reality ipo kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kitu kimoja kifanyike, ni lazima Serikali ijikite kwenye kuhakikisha tunashirikisha sekta binafsi kwenye mipango yetu, maana wapo matajiri au wafanyabiashara ambao leo hawajui hata Ilani ya CCM inalenga nini lakini wapo kule. Wale watu wanakopesheka kwenye mabenki na wana uzoefu wa biashara, kwa hiyo, tukiwatumia vizuri wanaweza wakatusaidia kwenye kukuza uchumi. Maana hapa basically tunachojaribu kukiangalia ni nini? Tunajaribu kuangalia possibility ya ku-raise pesa kutoka sekta binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ambacho nashauri ni kitu kimoja, tuangalie Serikali iweze kuwatafuta hawa watu, tusiwatafute kwenye makundi maana wafanyabiashara wa Tanzania kwa sehemu kubwa kila mmoja anaficha mambo yake, hakuna mtu ambaye yuko tayari kufunguka. Ukiita semina ya wafanyabiashara hapa hakuna ambaye yupo tayari kufunguka, lakini tukijaribu ku-identify labda wafanyabiashara kumi potential, tukaangalia huyu mtu uwezo wake ni mkubwa katika industry fulani na bado benki anaweza akakopesheka. Huku mfanyabiashara kupata bilioni 300, bilioni 400 benki unampelekea idea ya biashara maana tunahangaika na viwanda hapa, kuna mwingine yupo kwenye mabasi lakini anaweza akajenga viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itafute kupitia TANTRADE, iende imshauri, tuwatembelee hawa watu tusikutane nao tu wakati tunatafuta kodi maana haya mambo hata kwenye halmashauri zetu huko yaani Afisa Biashara ni kama Polisi, yeye atatembelea duka lako, atatembelea sehemu yako ya biashara anakagua leseni au anakagua vitu vingine. Wapate muda wa kuwatembelea watu hawa, ujue huyu mtu ana shida gani, sometimes mtoe hata out maana private ukijaribu kuangalia wanaotu-train private aliongea mtu mmoja aliyekuwa anachangia asubuhi, kwamba investment hata kwenye Makampuni ya Simu na Serikalini huku ni tofauti, yaani unayemweka am-audit mtu wa private, mtu wa private anajua zaidi kwa sababu wale watu wame-invest hela nyingi Zaidi, sisi tumekuwa tunasafirishwa tufanye kazi private, tunasafirishwa sana na makampuni nje, sio kusema yule mtu hakusafirishi tu bila manufaa, anataka uelewe ili kurudi umfanyie kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hali kadhalika hata watumishi wetu umma watafute muda wa kukaa na watu wa private, wawaulize matatizo yao ni nini. Wawatembelee hata ofisini, wawatoe hata out jioni wakae sehemu waongee hizi bajeti ziwepo, maana hawa watu washirika, mtu wa kukuchangia trilioni 40 kwa miaka mitano huwezi tu kuwa unakuta naye kwenye tax collection, hapana lazima tuwatafute tushirikiane nao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo limekuwepo, watu wengi sana wameongelea habari ya TRA, niombe Serikali. Nimekuwa kwenye biashara, tunafanya kazi na Serikali, una-supply mzigo au contractor anafanya kazi, baada ya hapo kuna raise certificate, ipelekwe wizarani, baadaye iombewe hela hazina ije ilipwe, inachukua almost miezi miwili au miezi mitatu ndio hela inakuja. Hela inafika kuna maelekezo sasa hivi kwamba kabla ya kumlipa mkandarasi au supplier yoyote yule, uanze kwanza kuwauliza TRA kwamba huyu mtu anadaiwa. Sasa hata yule niliyefanya naye biashara taasisi ya umma naye amegeuka tax collector, leo hanilipi hela yangu kwamba kama nadaiwa ile hela anaihamisha moja kwa moja inaenda TRA. Jamani nafanya kazi na wewe, ni mfanyabiashara unajua ofisi yangu, nilipe kwanza maana sisi tunakopa kwenye mabenki, hawa ndio partners, sasa leo ukichukua bilioni yote na mtu wa TRA anakwambia unadaiwa, sometimes anakwambia ile ilipe kwanza, ikishalipwa kwanza tutakuja tuta-negotiate, hela haiwezi kuingia kule ikarudi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ninachoomba, TRA wasiwe Polisi, hawa ni partners, ni watu wa kufanya nao biashara, tuwashirikishe lakini tushirikiane nao maana wako registered, kila mfanyabiashara tunajua alipo na hizi trilioni 40 ndio hao wanaotakiwa wazichangie lakini tusiwa- discourage kwenye biashara. Nasema hili kwa sababu haya mambo yanatokea sana hawa watu wanakata tamaa kuendelea kuwekeza hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka nije nalo, kwa sababu ya muda nilikuwa najaribu kupitia, nikaangalia historia ya Northern Ireland, wale watu wakati wanataka kuanzisha viwanda…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Muda umekwisha Mheshimiwa, lakini unaruhusiwa kupeleka mchango wa maandishi, kwa hiyo usiwe na wasiwasi.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. (Makofi)
Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nichukue nafasi hii kukushukuru kwa kunipa nafasi ya kuwa mchangiaji katika Azimio la Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika. Pia naomba ku-declare interest, mimi ni Mbunge wa Kamati hii ya Viwanda, Biashara na Mazingira, kwa hiyo nitachangia maoni yangu binafsi nikijaribu kukazia kwenye yale ambayo yamewasilishwa na Kamati.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba vile vile nimpongeze Waziri na niipongeze Serikali kwa kuchukua hatua hii muhimu ya kuungana na nchi nyingine 41 za Afrika ambazo tayari zilisharidhia Azimio hili na tayari zenyewe zinaendelea. Hii ni decision ya kishujaa kwa sababu nchi hii ni kubwa, sasa wenzetu wanapokuwa wamefanya jambo la kuendelea, halafu sisi tukabaki nyuma, kwangu niliona ni kama kitu kilikuwa kinaturudisha nyuma kidogo. Kwa hiyo, niipongeze Serikali kwa hatua hii muhimu, lakini niseme yapo maeneo ambayo nimeyaona na nilipenda zaidi kuyaongelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani tumemaliza discussion ya mambo ya mahindi hapa, ni kitu ambacho nimejiandaa kuongea hasa masuala ya kilimo, maana tunayo fursa ya kufanya biashara hasa kwenye mazao ya kilimo, lakini nadhani yameongelewa mengi sana hapa, kwa hiyo nisingependa niingie sana huko. Hata hivyo, kwenye research zangu ambazo nilikuwa nimezifanya kwa siku mbili hizi wakati najiandaa, nilijaribu kuona eneo la tija, kwa sababu kilimo chetu tunapokwenda kuingia sasa katika ushindani mkubwa wa takribani nchi 42 au 41 za Afrika zile ambazo zimeshaingia, ni lazima tujaribu kuangalia sisi tumejipangaje hasa kwenye issue ya tija.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa tunalima sawa, tunafanya shughuli zetu sawa, lakini ile yield tunachokipata labda kutoka kwenye heka moja unachokipata comparing na wenzetu ambacho wanapata tumekuwa tuko nyuma sana. Sasa ukija ukaangalia cost of production, kwetu inapokuwa kubwa zaidi na tunaingia kwenye ushindani huu mkubwa, wenzetu watatulazimisha tushushe bei ya mazao ili waweze kuuza hapa au na sisi tutakapojaribu kwenda kuuza nje itakuja kuwa shida kidogo. Kwa hiyo, naomba tujikite zaidi kwenye suala hili kwa sababu nilikuwa naangalia average production katika tani moja ya mahindi, kwa mfano, kwa Tanzania, heka moja ya mahindi tumekuwa tunapata karibu gunia sita za kilo mia moja, mia moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ukija ukaangalia kwa wenzetu kwa mfano Zambia, kwa sababu tunaongelea ukanda huu wa kusini ndio unaolima mahindi sana, kwa Zambia ni double, tunaongea kwamba kwa hekta sio heka, kwa hekta moja kwa Tanzania ni 1.5 tons wakati kwa Zambia ni three tons kwa same hector. Ukija ukaangalia kwa South Africa inaenda karibu six. Sasa hawa ni wenzetu ambao ndio tunaoenda kushindana nao kwenye hili soko hasa uzalishaji wa mahindi. Sasa tukijaribu kuangalia competition yetu hasa kwenye bei itakuja kuwa ndogo zaidi, kwa sababu wenzetu watalima kidogo watavuna mengi. Wakishamaliza kuvuna mengi tunaingia kwenye soko moja la kushindana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo unakuja kukuta mbolea aliyoiweka kila kitu alichokiweka kwenye kuandaa shamba ni gharama zile zile sawa na wewe, lakini yeye amevuna magunia mengi zaidi, kwa hiyo atakuwa na uhuru zaidi wa kuuza kwa bei ya chini zaidi. Kwa hiyo hili jambo ningeomba tuliangalie ili tunavyokwenda kwenye ushindani kesho na kesho kutwa soko letu lisipotee, tuhakikishe kwamba hata na Wizara ya Kilimo inatusaidia tuweze kupata mazao mazuri zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine kikubwa liko suala la haya mazao ya GMO, hatuwezi kwenda mbali na dunia inapoelekea. Leo tunaingia kwenye ushindani, wenzetu wanalima pamba, tumekuwa tunasikia hapa Kanda ya Ziwa, watu wapo wanalima pamba, lakini pamba ambayo wenzetu leo wanalima ambapo wameshakwenda kwenye GMO technology ni tofauti. Yeye atalima heka moja, hapo unaongelea labda kwenye heka moja utavuna labda tani tano au tani 10, mwenzako labda yuko zaidi ya mara mbili kwa sababu wako kwenye GMO.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nilikuwa naomba kipindi tunaingia kwenye ushindani, kwa sababu nchi nyingine zimesha-advance kwenye teknologia hii, Serikali ijaribu kuangalia kwamba teknologia ya GMO bado tuna wasiwasi, tunajua labda ni genetic modified, tuna wasiwasi bado, lakini kwenye mazao ambayo siyo consumables kama vyakula, mazao yale ambayo tunaenda kushindana na wenzetu kama pamba na vitu vingine hivi vya kuuza kule, hebu tujaribu kuona kama tunaweza tuka-adapt hiyo teknolojia, tuanze kuruhusu baadhi ya vitu tukatumia teknolojia ya GMO. Kesi kubwa hapa ni kuwafanya Watanzania wanaofanya kilimo, kilimo chao kiwe cha tija, kiweze kuwaletea majawabu ambayo watawafanya wapate pesa kwenye rotation yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwenye suala la masoko, tuna hakika kwamba sisi tuna mifugo hapa, tuna maziwa na uvuvi. Kwa hiyo, kwa sehemu kubwa mkataba huu utaenda kusaidia zaidi vijana wa Kitanzania na hasa Watanzania kuweza ku-embark sasa kwenda kuuza katika nchi za jirani na hatimaye tuweze kujipatia kipato kizuri zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ipo habari ya viwanda. Nadhani sasa hili ni soko ambalo tumekuwa tuna-trade labda sisi wenyewe na watu wa East Africa, hatuzidi watu milioni
200. Leo hii tunaingia kwenye soko la zaidi ya watu bilioni 1.2 iko fursa kubwa zaidi ya kuweza ku-trade na wenzetu, lakini ni lazima Serikali tuweke mguu chini; maana siku hizi vijana wanasema tuweke mguu chini. Maana ya kuweka mguu chini ni nini? Lazima ifikie hatua tujue tunaingia kwenye biashara. Kama tunaingia kwenye biashara, tufanye politics lakini huku tukijua kwamba tunaenda kwenye biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, biashara ni ushindani. The moment umefungua, watamwagika Wanaigeria hapa, watamwagika Wakenya hapa; sasa siyo kesho umefungulia, halafu keshokutwa unaanza kulalamika. Tutakuwa na miaka mitano ya kufanya changes, lakini hamtawafukuza kwa sababu watakuwa wamesha-invest.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunachoomba, kesi kubwa ambayo tumekuwa tunaipata upande wa Serikali, ni lazima tuhakikishe tunawa-fever hawa watu wanaofanyabiashara hapa. Tusione mfanyabiashara kama adui. Hiki ndicho kitu ambacho naomba zaidi upande wa Serikali ituangalie. Kodi na tozo zimekuwa nyingi mno kwenye biashara. Hatutaweza kushindana na wenzetu kama kodi na tozo zinaenda kuwa nyingi kiasi hicho. Kwa hiyo, hivi ni vitu ambavyo lazima tujaribu kuangalia. Tunapoingia kwenye uhuru wa soko hili la Afrika, kwa sababu ni market tunayoifungua, una wateja wengi, ukubali kushusha bei, kuondoa baadhi ya tozo, kuzalisha kwa wingi zaidi, kuuza kwa wingi zaidi, ndiyo tutakapopata faida, kuliko kuzalisha kidogo, ukataka kuuza kwa bei kubwa kwa sababu mna tozo nyingi zaidi, hatimaye ukajikuta kwamba umekwama na wenzenu ndiyo wakaanza kuingiza hapo, kwa sababu wao watakuwa wako free.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nilichokuwa naomba kwa upande wa Serikali, tuliangalie sana hili. Wafanyabiashara tusiwaone kama maadui, tuwaone kama partners. Ni lazima kwa upande wetu, hasa Serikali yetu ya Tanzania, Wizara ya Viwanda na Biashara muwe tayari kuwa-support wafanyabiashara wa Kitanzania, pale watakapotaka kwenda nje, watakapotaka kubaki hapa, waone kwamba Serikali iko nyuma yao. Kwa sababu tunavyoingia kwenye hili soko, wenzetu lazima Serikali zao zitakuwa zinawa-support.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninao mfano hapa nilikuwa najaribu kupitia, kuna tangazo la NEMC walilitoa tarehe 7, this one here, nimelitoa kwenye Citizen leo, linasema, “NEMC hits Lake Oil with 3.3 billion Fine” ya vituo 66 vya mafuta. Sasa Waziri wa Viwanda na Biashara uko hapa, Lake Oil wana vituo 66 nchi hii. Leo NEMC anawatangazia kwamba anawapiga faini ya shilingi bilioni 3.3; huyu ni mfanyabiashara ambaye yuko hapa ame-invest kwenye vituo vyote hivyo, anampiga faini ya shilingi bilioni 3.3, over sudden tu anamwambia ndani ya siku 14 alipe. Kesi ni nini? Ni kwamba amefanya vituo vyake hivyo bila kufanya Environmental Impact Assessment. Unajiuliza, mpaka mtu anafungua vituo 66, Serikali ilikuwa wapi? NEMC walikuwa wapi? Au kuna kitu gani ambacho walielewana na NEMC, sasa leo kimeshindikana hapo katikati, wanawageuzia kibao? This is the very big shame! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo ukiongelea vituo 66, Serikali itapoteza fedha kiasi gani? Yule mtu akisema leo hana, ikaamuliwa vifungwe, Serikali itapoteza pesa kiasi gani? Ajira ngapi za Watanzania zitapotea na vilevile ni scandal. Kwa hiyo, nilikuwa naomba, vitu kama hivi, kama kunakuwa na cases kama hizi; sasa leo unavyotuambia Lake Oil hawana hiyo Environmental Impact Assessment mnawafungia, vituo vingine waliokuwa wanalipa ambao wamefuata taratibu kihalali, wenyewe mliwafunguliaje? Yaani huyu mtu mpaka anajenga vituo 66 alikuwa anajificha wapi mpaka vikamilike 66 ugundue leo? Hivi ni vitu vidogo tu ambavyo baadaye vinam-discourage mtu.

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Ezra Chiwelesa kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Ngassa.

T A A R I F A

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumpa taarifa mzungumzaji; ili uweze kipata kibali cha kujenga Kituo cha Mafuta, lazima uwe na certificate kutoka NEMC, ipelekwe Ewura, Ewura ndiyo wakupe kibali. Ili upate kibali cha NEMC, ni lazima uwe umesajili kile Kituo cha Mafuta uweze kufanya hiyo Environment Impact Assessment. Maana yake, anachokiongea Mheshimiwa pale, kutakuwa kuna shida kule ambayo ndiyo imeleta hili tatizo kubwa. Kwa hiyo, hata Serikali waweze kuliangalia. Ahsante.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Ezra Chiwelesa, unapokea taarifa hiyo?

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, naipokea. Hili ni jambo moja tu ambalo nimesema kwamba ni discouragement upande wa biashara. Ndiyo maana nikasema, Wizara ya Viwanda na Biashara na hasa upande wa Serikali, tuangalie; tunapoingia kwenye ushindani mkubwa namna hii tunakuja kuleta giants hapa, tutaleta giants kwa sababu sisi advantage tuliyonayo hapa, lazima wenzetu watakuja ku-invest tu hapa kwa sababu tuna ardhi nzuri, tuna vitu vingi, tuko kwenye ukanda huu wa bahari, lazima tutapata watu wa kuja ku-invest hapa. Ila kipindi wale investors tunajaribu kuwavuta, ni lazima tujaribu kuangalia kwamba vitu vidogo na vya kukwaza kama hivi visiweze kutuharibia.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono azimio. Ahsante sana. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii kwanza kukushukuru kwa kunipa nami nafasi ya kuchangia katika hoja zetu tatu hizi ambazo zinaendelea mezani, hoja ya Kamati ya PIC, PAC na Kamati ya LAAC. Nitajikita kwenye mambo mawili.

Mheshimiwa Spika, jambo la kwanza nitajikita kwenye Kamati hii yetu ya PAC juu ya ukaguzi na hasara ambayo tumeipata kutokana na matumizi mabaya ya fedha za umma ninayo ripoti hapa ya Kamati kuanzia ukurasa wa 10 mpaka ukurasa wa 11 kipengele 2, 5, 1 kuhusu riba kuchelesha malipo inayotokana na kuchelewa kulipa wakandarasi katika Wakala wa Barabara TANROADs Billion 68.7.

Mheshimiwa Spika, nataka nijikite hapa, kutokana na taarifa ya Kamati inasema sharti la Kifungu cha 54 ya jumla ya mkataba wa ujenzi GCC kinatamkwa kwamba Mwajiri atamlipa Mkandarasi kiasi kilichothibitishwa na Meneja wa Mradi ndani ya siku 28 tangu tarehe ya kila hati ya malipo (Mikata ya Kimataifa ni siku Hamsini na Sita (56) kwa msingi huo Mwajiri akichelewesha malipo Mkandarasi atalipwa riba ya kuchelewa malipo katika hati ya malipo inayofuata.

Mheshimiwa Spika, sasa nikipitia hapa tunaona kwamba TANROADS wanetusababishia matumizi mabaya ya Fedha ya Umma kwa takribani billion 68.73 katika Mwaka huu wa Fedha 2021. Nimejaribu kupitia baadhi ya miradi nikawa najaribu kuangalia nikaona kwamba yapo matatizo na hususan ambao tumetokea kwenye ukandarasi huko tunajua. Kumekuwa na shida kubwa sana ya kupoteza fedha za umma lakini fedha hizi zinapotea kwa mipangilio mibaya tu. Sasa kama wanakubaliana au wanakosea kwa kutokujua sasa ndiyo nataka leo tuangalie hapa.

Mheshimiwa Spika, pesa zote hizi ambazo tunaziongelea hapa tunao uzoefu kwamba hakuna Mkandarasi wa ndani ambaye huwa analipwa hizi pesa, mara nyingi Mkandarasi wa ndani ukidai tu penalty kwamba umecheleweshewa malipo mradi unaofuata sehemu hiyo hutopewa mradi hata siku moja, experience tunayo lakini pesa zote hizi wanapewa watu wa nje, kwa sababu kwenye mkataba kuna sehemu ya kulipa riba lakini kuna sehemu ya kukata liquidated damage.

Mheshimiwa Spika, haiwezekani ripoti ya CAG inatuonesha kwamba TANROADs wamesababisha hasara hii kwakulipa riba lakini nowhere tunaoneshwa kwamba hata wao liquidated damage walikata wapi? Serikali peke yake ndiyo wanaokosea, lakini Mkandarasi katika Wakandarasi wote waliowalipa kwa sababu kulikuwa na miradi ya takribani zaidi ya Billion 600 ambazo walikuwa wanadaiwa lakini there is nowhere tunapooneshwa kwamba na upande wa Mkandarasi napo huwa kuna makosa. Kwa sababu kipengele cha kumtoza faini Mkandarasi kama liquidated damage kipo, kwamba na yeye anapochelewesha mradi unaanza kumkata baada ya siku kadhaa mpaka pale mradi utakapoisha au amount ile ya security ambayo ameiweka, lakini we don’t see that ila tunachokiona ni sehemu ile tu ambayo upande wa Serikali wanakosea.

Mheshimiwa Spika, kwa nini inafikia hatua hii? Kwanza iko tabia na mazoea yale ambayo tunayo sisi hapa, hakuna Mkandarasi anayefanya makosa. Mkandarasi akishaona tu muda wake wa ku-expire umefika kwamba mkataba unafika mwisho Mkandarasi anaandika barua ya kuomba extension, lakini upande wa Serikali hata humu ndani kuna Waheshimiwa Wabunge mnafanya biashara mnajua. Ukishampelekea certificate ya malipo wewe tena ndiyo unayetakiwa kugeukwa kuwa mtumwa kila siku kwenda kumbembeleza kama vile ile hela ni ya kwakwe mfukoni anakupa wewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa wenzetu wa nje hawafanyi hivyo. Wenzetu wa nje kwa sababu sisi tunapenda nchi yetu, tunapata kazi hapa lakini tunapenda nchi yetu hatutaki ugomvi wa kugombana na Serikali. Wakati wenzetu wa nje wakishapeleka certificate hatakupigia simu wala hakufuati yeye anakaa siku 56 zimeisha anasubiri, sasa mambo mengi tumeyaona ikitokea ziara ya Kiongozi wa Kitaifa hapo ndipo utakaposhangaa Mkandarasi anatafutwa kwa nguvu zote maana wanaona hela inaelekea huku, hata ile hela ambayo ulikuwa umeomba certificate haijaja mtu yuko tayari kukutumia hela leo halafu Kiongozi anaingia keshokutwa, matokeo yake akifika pale Wakandarasi wazawa tunaonekana kwamba tunalipwa pesa na hatufanyi kazi! lakini jiulize ile pesa imelipwa lini?

Mheshimiwa Spika, ndio maana mimi kuna rafiki yangu mmoja nakumbuka aliwahi kuwaambia hata pesa wasimuwekee kwenye akaunti maana aliogopa, unaletewe hela leo halafu Kiongozi anaingia keshokutwa, akiingia keshokutwa wewe ukikubali kwamba hela umeipokea kwenye akaunti kinachotokea ni nini? Anayesoma ripoti atasema Mkandarasi tumemlipa mpaka hapa lakini kazi haionekani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa naongea hii generally tujaribu kuangalia jinsi ya kuondokana na haya. Tukikumbuka TANROADS wamekuwa na na tabia ya kutangaza miradi yao yote mwezi wa Julai, tunapoanza tu mwaka mpya wa fedha wanatangaza miradi yao yote, lakini tujiulize chanzo cha pesa za TANROADS ni nini? Tunazo pesa za Road Fund, tuna pesa za Hazina - Mfuko Mkuu wa Serikali na tunazo pesa za donors saa nyingine. Sasa unapotangaza miradi yote mwezi Julai kwa pamoja, miradi ya mwaka mzima, kinachokuja kutokea ni nini? Cash flow haiji kwa pamoja!

Mheshimiwa Spika, wale watu ukishawapeleka site kila mmoja anafanyakazi bila kumuuliza mwenzake umefikia wapi? Sasa unajikuta certificate zinafika mwisho kila mmoja ana madai na pesa ile haijapatikana au haijaonekana. Kwa hiyo the proper planning ambayo inabidi tufanye kama Bunge kuielekeza ni kwamba ili tuondokane na hizo hasara, kwa sababu Billion 68 siyo hela ndogo, hapo ungejenga kilometa 68 zingine. Unaongelea vituo vya afya zaidi ya 120, hii si pesa ndogo wanaenda kulipwa watu interest!

Mheshimiwa Spika, mbaya zaidi ukijaribu kuangalia pesa ya nje huwezi kuilipia interest tutalipa kwa kutumia pesa ya ndani, maana yake ni nini? Pesa yetu ile ambayo tumeikusanya kwa kodi na kwa taabu badala ingetusaidia hapa tunachukua kama penalty tunapeleka nje tena kwa Wakandarasi ambao wametoka huko nje waonatudai hizi penalty. Kwa hiyo, niombe Bunge tutoe maelekezo mahsusi, ni bora wakagawanya in quarterly basis, miradi wakaigawanya kama wana miradi mia mbili, ukafanya miradi hamsini ianze Mwezi wa Saba na miradi 50 ianze Mwezi wa Tisa, miradi hii iendane, iwe inapishana utakapoanza kupokea pesa, kwa sababu una uhakika hakuna Mkandarasi wa barabara ambae atafanya mobilizations afanye vitu vyote hivyo ndani ya mwezi mmoja au miezi miwili awe ameanza kudai certificate. Kwa hiyo, tukifanya hivi itatusaidia ku-save hizi pesa. Hivyo, mipango mibovu ya TANROADS imetufikisha hapa leo kutusababishia hasara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninapoendelea kuyasema haya mipango mibovu ni pamoja na management nzuri. Tumeangalia hapa kwenye ripoti ya Kamati yako hii ya PAC ukurasa wa 22 inasema hivi, Taasisi kutokuwa na Bodi za Wakurugenzi. Tunajua TANROADS hawana Bodi ya Wakurugenzi leo ni takribani mwaka wa pili. Sasa jiulize taasisi hii tunaiendeshaje na haina Bodi ya Wakurugenzi? Imesemwa hapa kwamba complains hizi tunazozitoa hapa, ushauri tunautoa hapa unampelekea nani? Bado TANROADS huyu amerundikiwa majukumu mengi, tumesikikia jana hapa Waziri Mambo ya Viwanja vya Ndege baada ya watu kuongea hapa tangu juzi, akasema ooh! tutafanya adjustment! Unajiuliza kasema uwanja wa Msalato utaendelea kubaki chini ya TANROADS, nilikuwa najiuliza jambo moja hapa, Shule ya Msingi tukiwa tunasoma, tulikuwa tunafundishwa Wakala wa Barabara TANROADS, kazi yake nini? Kujenga barabara. Wakala wa Viwanja wa Ndege? TAA, Wakala sijui wa mambo ya Reli? TRL. Sasa tukianza kuchanganya haya mambo leo mtoto kesho na kesho kutwa miaka imepita, kwa sababu hivi vitu haviondoki.

Mheshimiwa Spika, nimeingia tu kwenye website uki- type pale Bajeti ya Mwaka gani unapata. Leo tuko na mtoto mmoja pendwa katika Wizara hii ambapo wote wapo chini ya Wizara moja. Lakini kuna mtoto mmoja ana mapenzi makubwa mpaka anapewa kazi za wenzake, bado tupo humu ndani ya Bunge tunaambiwa kwamba ataendelea na Kiwanja cha Msalato, sasa unajiuliza huyu mtoto mzuri namna hii kama Baba ni huyohuyo mmoja, kwa nini asiwaelekeze na wenzake wazuri wakafanya kazi zao? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwangu mimi ninachokiona tusichanganye mambo haya. Hili Bunge limejaa wasomi, wewe mwenyewe ni msomi wa Degree Tatu za Sheria, hebu tuende sawa tunapofanya maamuzi kama Bunge tuweke legacy na heshima ya Bunge hili. Tuelekeze TANROADS waachie miradi ya Viwanja vya Ndege, iende chini ya TAA, kama kuna matatizo ya management Waziri ni yuleyule. Hata hivyo, kwa kukumbuka hapa Bodi ya TANROADS ninavyojua na ambavyo jinsi nilivyofuatilia hii ni advisory board siyo executive board, ndiyo maana wanaweza hata kupeleka vitu huko wakaingilia fanya kazi ya fulani, ikakubali fanya kazi ya fulani ikakubali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, unapoongelea Uwanja wa Ndege, unapokuwa unajenga uwanja wa ndege huongelei runway, runway ndiyo barabara. Uwanja wa ndege una vitu vingi, una majengo pale, ina watu wa umeme na nini, sasa unajiuliza TANROADS ni Mkandarasi ndani ya ile Wizara anayetakiwa afanye kazi za wenzake au TANROADS ni nani ndani ya ile Wizara?

Mheshimiwa Spika, hivyo ninaomba kama TANROADS ana cheti cha ukandarasi tukakutane naye site tushindane naye, lakini kama hana cheti cha ukandarasi, miradi ya viwanja vya ndege irudishwe TAA, kwa sababu hii Miradi inafanywa kwa standard. International Civil Aviation Organization wametoa standard za kujenga viwanja vya ndege. Sasa sielewi TANROADS ya Tanzania yenyewe mpaka inajua, kesho tutawakuta na kwenye reli hawa kama hatutangalia hapa, tutakuja kuambiwa TRL hawafanyi vizuri SGR ipelekwe TANROADS tena. Kwa hiyo, ninachoomba tusimame kwenye standard. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hili ni Bunge la Wananchi wa Tanzania, kama ni Bunge la Wananchi wa Tanzania kila mmoja afanye kazi zake kwa mujibu wa Sheria maana hizi Organizations au hizi Taasisi zimetundwa kwa Sheria ya Bunge, tusizibadilishie matumizi kwa mtu mmoja kukaa na kuamua anavyotaka wakati vitu hivi vimetungiwa na Sheria na Bunge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nilikuwa naomba juu ya hayo tuyaangalie ili yaweze kutusaidia, kesho na keshokutwa tutakapokuwa tunakimbizana na hasara kama hizi, huyu unayempelekea mpaka na viwanja vya ndege ametusababishia hasara namna hii na bado tunazidi kumrundikia kazi. Kwa hiyo, ningeomba tuliangalie hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kumalizia najaribu kupitia hapa tena kwenye suala la miradi ambayo baadhi ya Wakandarasi wamepewa. Kuna Wakandarasi wametutoza penalty huko kwenye ile Billion 68, yet tumeenda na tumewapa na kazi nyingine kubwa tu wamesaini hivi karibuni na wanaendelea nazo. Sasa unajiuliza hawa Wakandarasi wa nje wana mapenzi gani na sisi? Wanatutoza penalty tunawalipa na bado tunawapa kazi nyingine wanaendelea nazo. Naomba tutoe kauli kwamba miradi hii ikae chini ya taasisi na hatimae iweze kufanyika, hata Watanzania wanapokosea au wanapocheleweshewa malipo na wenyewe pia walipe penalty kama hizi. Kwa sababu haiwezekani mtu anayetoka nje ya nchi tunampa pesa halafu wa ndani ya nchi tunamnyima.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana naunga mkono hoja. (Makofi)
Azimio la Bunge la Kutambua na Kuenzi Mchango wa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kwa Utumishi wake Uliotukuka Pamoja na Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nami niungane na Watanzania wenzangu kutoa pole kwa Mheshimiwa Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan, Mheshimiwa Spika wa Bunge na wewe mwenyewe kwa sababu Rais aliyetangulia alikuwa sehemu ya Bunge. Pia nitoe pole kwa wakazi wa Chato na Biharamulo kwa ujumla sababu sisi ndiyo wenyeji zaidi pale kwa hiyo, msiba ule ulikuwa nyumbani na nawashukuru wote walioungana nasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye kuchangia ninayo mambo mawili ya kumuelezea Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Cha kwanza kila binadamu anapozaliwa ana mambo mawili makubwa katika dunia hii. Incident mbili kubwa katika dunia kwa mwanadamu, kwanza ni kuzaliwa na pili kugundua kwa nini umezaliwa. Watu wengi tunaishi hatujui kwa nini tumezaliwa au kwa nini tupo hapa duniani.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa kesi ya Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aligundua purpose ya Mungu kumleta duniani. Nakumbuka mwaka 1990 nikiwa mdogo akiwa anagombea Ubunge kwa mara ya kwanza Biharamulo kila alichokuwa anakifanya au statement yake kila mmoja alikuwa anamuelezea. Tukiwa wadogo tunaambiwa kuna mtu anaitwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli that time yuko Chato mimi niko Biharamulo.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuwa Mbunge kwa mara ya kwanza mwaka 1995 nyote ni mashahidi, Naibu Waziri wa Ujenzi kila alichokigusa aliacha alama. Hakuna sehemu Raisi Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amepita hakuacha alama. Mmemsikia Rais Jakaya Kikwete juzi kwenye suala la ujenzi, ardhi, uvuvi na hata alipomrudisha ujenzi. Hatimaye Watanzania na Chama cha Mapinduzi kikaona na kumuweka kuwa Rais. Alipokuwa Rais alama ile aliyoiweka katika maisha yake kwamba kila anachokabidhiwa kufanya lazima akifanye kwa hundred percent haikukoma. Watanzania wote ni mashahidi ujasiri wa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika kuamua mambo, ujasiri wa katika kuipigania nchi hii haukuanza akiwa Rais umeanza back-and-forth na alipokuwa Rais mambo aliyoyafanya ni makubwa mmeyasikia hatuna haja ya kuyarudia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo moja kubwa ambalo nilimuuliza Mungu wakati ule napokea taarifa hizi, nikasema why God, kwa sababu niliumia sana nikajiuliza kwa nini uruhusu hili jambo katika wakati kama huu? Ila nikarudi katika Maandiko Matakatifu nikamkumbuka Musa alivyopigana na wana wa Israel, najua safari ilikuwa ngumu hata safari ya Dkt. John Pombe Joseph Magufuli imekuwa ngumu kwa sababu kipindi anaenda hivi kuna wengine walitaka kurudi nyuma na wengi wamekuwa wanapigana kurudi nyuma lakini hakukata tamaa. Nikakumbuka Musa alipopandishwa katika mlima ule na akaoneshwa nchi ya ahadi kule lakini akaambiwa kazi yako imeishia hapa na hautarudi huko na wala hutaiona. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka kuwaambia ni nini? Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliletwa na Mungu kwa ajili ya kazi maalum katika nchi hii, amemaliza kazi ile ambayo Mungu alimleta aifanye, tuendelee kumuombea na kuyaishi yale aliyofanya. Ninachotaka kuwasihi Watanzania na Wabunge wenzangu baba huyu aliletwa kwa purpose, akagundua purpose iliyomleta hapa, kafanya sehemu yake na amemaliza. Hata sisi sasa tunachotakiwa tumuenzi nacho kila mmoja ajitafakari ajue purpose yangu mimi kuwa duniani ni nini na purpose ya wananchi walioniamini kunileta Bungeni ni nini. Tukiyajua hayo basi tukaisimamie Ilani ya Chama cha Mapinduzi ili maendeleo haya ambayo Rais wetu alitamani kuyaona aweze kuyaona yakifanyika na Watanzania waweze kuyapokea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninachotaka kuwasihi Watanzania na Waheshimiwa wabunge wenzangu, baba huyu aliletwa kwa purpose akagundua purpose iliyomleta hapa kafanya sehemu yake amemaliza. Hata sisi, tunachotakiwa tumuenzi nacho, kila mmoja ajitafakari ajue purpose yangu mimi kuwa duniani ni nini? Purpose ya wananchi walioniamini kunileta Bungeni ni nini? Ili tukiyajua hayo tukaisimamia Ilani ya Chama cha Mapinduzi, ili maendeleo haya ambayo Rais wetu alitamani kuyaona aweze kuyaona yakifanyika na Watanzania waweze kuyapokea.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hapo labda, nirudi kwenye suala mama pia, kumpongeza mama yetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme neno moja tu; watu wote wameongea katika habari ya wanawake, lakini mimi niseme hakupewa nafasi ya Makamu wa Rais kwa sababu ni mwanamke, alipewa nafasi ya Makamu wa Rais kwasababu ame-demonstrate na ameonesha uwezo wa kupata nafasi ile. Kwa hiyo tunaposimama hapa, tusimame hapa tukijua tunaye Rais mwenye uwezo ambaye aliaminiwa na Chama mwaka 2015 kipindi Magufuli anaingia, akiwa hajulikani kama atayafanya haya halikadhalika Mama Samia aliingia akiwa hajulikani kama atayafanya haya. Lakini chini ya uongozi imara, chini ya Ilani ya CCM wakayasimamia wakatufikisha hapa walipotufikisha. (Makofi)

Labda neno moja tu la biblia ambalo nataka niliseme kwa ajili ya Mheshimiwa Rais, nikikaribia kukaa, maana najua wote tumeshaongea mengi. Tuki-refer katika Kitabu cha Ezra 10:4 inasema “Inuka maana kazi hii inakuhusu wewe. Na sisi tu pamoja nawe, uwe na moyo mkuu ukaifanye”.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme kwamba Wabunge tuko na Rais wetu, Watanzania wako na Rais wetu, ameambiwa ainuke na maandiko hayo tuko pamoja naye, awe na moyo mkuu akaifanye. Tunachotakiwa ni kumuombea ule moyo mkuu ambao umesemwa, uwe juu yake akaifanye. Nina uhakika itafanyika vizuri na tunashukuru Mungu kwa sababu ya Dkt. Philip Mpango ambaye ameteuliwa leo, Mungu awasaidie watufikishe katika nchi ya maziwa na asali ambayo ilikuwa tamanio la Rais wetu Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana na niseme ninaunga mkono hoja hizi ambazo zimetolewa hapa. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, nai pia nikushukuru kwa nafasi hii. Nichukue nafasi hii pia kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa ambayo ameifanya ya kututangazia ajira hizi ambazo zinajaribu kutupunguzia gape la watu walioko mtaani na hatimaye kutusaidia kwenye ujenzi wa uchumi na halikadhalika kuwapa fursa Watanzania ya kushiriki ujenzi wa Taifa lao.

Mheshimiwa Spika, nadhani nimemsikiliza sana Mheshimiwa Waziri kwenye Hotuba, lakini vile vile taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari wiki hii iliyopita. Nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri na msaidizi wake kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya. Vile vile niipongeze Serikali kwa ajira hizi mpya kwa sababu tumeona kwamba ajira hizi takribani 32,604 kwa mujibu wa taarifa zinaenda kuigharimu Serikali takribani milioni 26.297 na kwa mwaka ni bilioni 315. Hii ni hela nyingi sana ambayo sasa Serikali inaitoa irudi kwa wananchi na hatimaye isaidie mzunguko huko mtaani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tunachokiona ni kwamba itatusaidia kupunguza ukali wa maisha na hatimaye vijana wetu ambao wamekuwa stranded kwa muda mrefu wataweza kupata ahueni halikadhalika waweze kwenda mbele zaidi.

Mheshimiwa Spika, nimpongeze pia Mheshimiwa Waziri hasa kwa tamko ambalo amelitoa kuhusu mpango mzuri wa kufanya usaili katika Mwaka huu wa Fedha ambao unakuja hasa suala lile la kuweza kufanya usaili kutokea kwenye maeneo yale yale ambayo wananchi wapo kule. Nayasema haya Mheshimiwa Waziri kwa sababu vijana wetu wamekuwa wanapata shida sana sana kupita kiasi, maana ilikuwa inafikia hatua mtu unajiuliza ni mwakilishi wa wananchi na mbaya zaidi hata hizi interview zimekuwa zinafanyika mara nyingi kipindi Wabunge tuko majumbani hatuko hapa. Walau hata tungekuwa hapa tungeweza kui-feel ile pinch ya kwamba vijana wako hapa. Unaita vijana 3,000 kuja kuwafanyisha interview hapa Dodoma ya kutafuta watu 400 au watu 600. Vijana ambao wamekaa miaka mitano bila ajira, vijana wamekaa miaka minne bila ajira, ila anapoitwa anaona matumaini yanakuja anaingia kwenye mikopo ya pesa, wengine wanauza mali walizonazo wanasafiri kuja Dodoma. Anafika hapa kati ya 4,000 uliowaita ni 300 tu ndiyo watakaochukuliwa au ni 400 ndiyo watakaochukuliwa. Wale vijana wengine 4,600 wanarudi wapi?

Mheshimiwa Spika, wamekuwa wanarudi na masononeko makubwa na mioyo yao inauma kwa sababu wanajiona kwamba hawana bahati, kusoma kwao ni kwa bure. Kwa hiyo ile hali pamoja na kwamba tunao ukali wa maisha ambao tulikuwa tunaendelea nao, ila ile hali ilikuwa inaleta manung’uniko huko mitaani na kuzidi kuleta chuki hata kuzidi kuichukia Serikali. Kwa hiyo mfumo huu ambao tunasema tunauleta leo, vijana wafanyiwe usahili huko kwao itatusaidia kutupunguzia vurugu nyingine ambazo zilikuwa zinatuletea kero kwa vijana wetu. Kwa sababu kama usahili utafanyika na mtu yuko Biharamulo, akafanyiwa usahili pale pale kwake alipo, haingii gharama kubwa sana kwa sababu bado ataendelea na shughuli zake ambazo anahangaika nazo na majibu yakija amekosa atakuwa na matumaini ya kujaribu tena next time.

Mheshimiwa Spika, nimekuwa najiuliza, kama tunaweza kupeleka mitihani ya darasa la saba, tukapeleka mitihani ya kidato cha nne, tukapeleka mitihani ya kidato cha sita, wakaisimamia kule hatimaye ikarudishwa huku ikasahihishwa. Unamsafirisha mtu hapa ambaye hana ajira muda mrefu, aje tu hapa kufanya written examination haikuwa sawa kabisa. Kwa hiyo tumpongeze Waziri kwa hatua hiyo nzuri ambayo sasa inaenda kutengeneza platform nzuri kwa vijana wetu ili sasa waweze kutoka kwenye maumivu yale ambayo walikuwa nayo, hatimaye waweze kusogea mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na haya yote yanayotokea, tungeomba sasa watu wa Sekretarieti ya Ajira wajitahidi zaidi, pamoja na kwamba watakuwa wanafanya huu mchujo hebu haki itendeke. Haki itendeke kwa sababu nyie nyote ni Wabunge humu ndani. Tuko Wabunge zaidi ya 390, kila Mbunge anawapiga kura hapa. Hata kama hamsemi lakini lazima meseji za vijana wetu tunazo na vijana wanalalamika. Wengine wanakwambia Mheshimiwa jaribu kutusaidia, ukimwambia kuna mfumo sasa guvu hivi, anakwambia hamna mbona wenzetu wamepitia sehemu Fulani na wamepata. Kwa hiyo kama kuna Wabunge special humu wanao uwezo wa kupita huko tujulishane ili na sisi tuje, lakini kama kuna platform ya haki kwa Wabunge wote, tunaomba huu mchakato ufanyike kwa haki ili vijana wajue kwamba tuko kwa ajili ya kuwawakilisha lakini hatuingilii mchakato wa usaili huko. Kwa hiyo tulikuwa tunaomba hilo jambo lijaribu kufanyika hivyo ili muweze kutusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini vile vile tumieni ya first in first out, FIFO itumike Mheshimiwa Waziri. Kwa sababu kuna mtu mwingine kamaliza miaka mitano iliyopita unakuja unaajiri mtu aliyemaliza mwaka jana, kozi ile ile, kwa kigezo gani unamwacha yule kule aliyekuwa amemaliza kipindi cha nyuma? Wakati yule aliyekuwa amemaliza nyuma, hakupenda kutoku-apply ajira ni kwamba Serikali haikuwa imetoa ajira, kwa hiyo alikuwa hana pakwenda. Kwa hiyo fursa inapopatikana leo tumpe aliyekuwa ametangulia nafasi tuendelee kujipanga kwa ajili ya wale ambao wanakuja leo. Kwa sababu umri wa kuajiriwa Serikalini nao unapita. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu tumeona sasa hivi vigezo vingi sana, tumekuwa na vigezo vya miaka 18 mpaka 25 na hili jambo naomba tuliweke wazi hapa. Leo tuseme conditions nyingine ambazo zinawanyima fursa Watanzania tuziache. Katiba ya nchi hii inampa kila mtu haki ya kutokubaguliwa hasa anapotaka kushiriki shughuli za maendeleo za Taifa hili. Sasa unapokuja unatangaza nafasi ya kazi. Mimi nina document hapa, nina tangazo la kazi, hii ni Public Service Recruitment Secretariat tarehe 14 Aprili. Hizi wametangaza nafasi za Ngorongoro Conservation nyingi sana nafasi ziko hapa. Wametangaza madereva, wametangaza na wengine, huku chini sasa kwenye condition; general conditions all applicants must be citizens of Tanzania with age between 18 and 25 years old for certificate and diploma, age 18 and 30 years for bachelor degree holders.

Mheshimiwa Spika, hii sikatai wameweka condition hii, lakini nimerudi kwenye tangazo hapa, hii hapa Pasiansi Chuo cha Wanyamapori. Hiki Chuo ni cha Wizara ya Maliasili na Utalii, age waliyoweka hapa applications za mwaka jana ambao hawa wako shule leo wameweka mtu anayetakiwa aingie chuo miaka 18 mpaka 24. Sasa unajiuliza mtu aliyeingia chuo na miaka 24 labda na miezi 11 au miaka 24 na miezi 10 anamaliza chuo akiwa tayari na miaka 25. Halafu condition ya ajira, wewe huyo huyo unayemiliki Wizara unampa condition ya ajira kwamba huyu mtu asizidi miaka 25. Unajiuliza wewe mwenye chuo unayempa condition huyu umeongea na Wizara kwamba hili darasa lote mtaliajiri muda ule utakaokuwa umeisha? Huna hiyo condition, matokeo yake unaweka condition ambayo inazidi kuongeza maumivu kwa Watanzania.

Mheshimiwa Spika, kitu kibaya zaidi hii hapa wazazi wanalipa, ada milioni tatu, ada milioni nne, mzazi amejihimu kapeleka mtoto pale Chuo cha Wanyamapori. Mtoto anamaliza unamwambia kazidi umri. Chuo kina conditions zake, anayeajiri ana conditions zake. Hili jambo naomba tuliache. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni lazima tuwatendee haki Watanzania na tuwape fursa ya kuajiriwa. Kwa sababu hapa wangelikuwa wanafanya vizuri kama wanataka haya masharti ya miaka na nini, wawachukue fresh from school, wawasomeshe wenyewe kwenye kile chuo, wawapeleke tayari, hiyo hawatakuwa na kigezo kingine, lakini wasiache mzazi anapeleka mtoto wake pale, mtoto hujampa condition hiyo, anamaliza chuo, yuko mtaani unaanza kumwambia miaka 25. Miaka 25 anaitoa wapi? Miaka minne hujaajiri. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Ezra kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Esther Matiko.

T A A R I F A

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nataka nimpe Mheshimiwa Engineer Ezra anachokizungumza ni kweli, siyo tu kwenye maliasili, ajira zote ambazo Serikali inatangaza inaweka vigezo ambavyo vinaengu Watanzania wengi wasiweze kuajiriwa bila kuangalia uhalisia wa umri na lini anamaliza chuo. Siyo kwenye maliasili tu, ni sekta zote ambazo wanatangaza hata kwenye majeshi. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Mhandisi Ezra Chiwelesa, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, naipokea.

Mheshimiwa Spika, labda sasa kwa kumalizia kwenye hili eneo ningeomba kama Bunge, sisi ndiyo tuna nafasi ya kuwasemea vijana hawa wa Kitanzania na wazazi hawa ambao wamepeleka watoto wao. Hii condition naomba tuiangalie upya, ifutike kama ni kusaili waite hata watu 10,000, watafute wawili lakini hawa wawili wanaowataka wawape fursa, kila mtu ajue kwamba nili-apply sikuzuiliwa kuliko hiki kinachofanyika leo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na hali nyingine pia tumeiona. Recently, kazi nyingi ambazo zimekuwa zinatangazwa Magereza, Polisi, Uhamiaji, condition mtu awe amepita JKT. Ni lini Taifa hili liliweka kigezo cha kupita JKT? Au ililetwa humu tukakubaliana kwamba sasa JKT kama JKT ndiyo condition turuhusu vijana wetu walioko mtaani waanze kwenda JKT na Serikali itupe nafasi ya kwamba vijana wote walioko mtaani, wataweza kuwabeba kweli? Tukiruhusu vijana wote waliomaliza form four waje wajiunge na JKT tutaweza kuwabeba? Hatutaweza. Kwa hiyo hizi conditions nyingine tujaribu kuzitoa ili tutengeneze fursa sawa kwa vijana ambao wako huko kila mmoja aone na aweze kuitumia nafasi yake kushiriki kwenye kuleta maendeleo ya nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa nafasi hii. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana kwa nafasi ya kuchangia, lakini pia nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa wasilisho zuri na ushirikiano mzuri ambao amekuwa anautoa kwetu.

Mimi na declare kwamba ni Mjumbe wa Kamati ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji; ndiyo maana nampongeza waziri kwa sababu tangu ameingia kwenye Wizara hii kwa kweli amejitaji kwa kiasi kikubwa kutoa ushirikiano kwa Kamati, lakini pia kuyapokea mawazo ya Wabunge na ushauri ambao tumekuwa tunautoa. Kwa hiyo, tumshukuru sana yeye na msaidizi wake na Katibu Mkuu na wengine wote ambao wanahusika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi leo nitajikita kwenye jambo moja tu, suala la mafuta ya kula ndiyo nitakaloliongelea tu kwa leo, maana masuala ya Liganga na Mchuchuma nimeongea sana hapa mpaka nikafikia stage ya kuchumba chima (kuchimba chuma), kwa hiyo leo naomba niiache twende kwenye suala la mafuta ya kula. (Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, jana tumesimama hapa kwa jambo la dhalura tukijadili suala la mafuta ya petrol, diesel na mafuta ya taa. Lakini tukirudi huko mtaani suala la mafuta ya kula bado ni kero kubwa na ni mzigo mkubwa kwa Watanzania, bei zime-shoot sana almost more than 100% increment ukilinganisha na wakati uliopita.

Sasa nikirejea katika Ilani ya CCM, ilani yetu inasema ambayo tunaitekeleza kwamba tuhamasishe ujenzi wa viwanda lakini viwanda ambavyo vitaajiri watu wengi na watu wengi wakitoka katika kilimo, mifugo na uvuvi. Lakini Mpango wetu wa Tatu wa Maendeleo unasema kwamba ni ujenzi wa uchumi shindani na viwanda kwa maendeleo ya watu. Sasa tukirejea huko kote nimekuwa nikipitia baadhi ya papers, nina journal hapa ambayo imeandikwa na Bwana Mgeni Nampenda wa Department of Trade and Investment College of Economic and Business Study, Sokoine University; inauliza Can Sub-Saharan Africa become food safe sufficient? Analyzing the market demand for sunflower edible oil in Tanzania. Lakini ikaja nyingine ninayo hapa ambayo nimekuwa nazipitia investment analysis of sunflower farming and prospect of raising household income in Iramba District Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimechukulia hizi case study mbili nikajaribu kupitia demand yetu ya mafuta, katika kupitia ni kwamba tumekuwa tuna annual demand ya almost tani 570,000 kwa mwaka. Uwezo wetu wa ndani wa kuzalisha ni tani 205,000 kwa record ambazo nimekuwa nazipata. Kwa hiyo, tumekuwa na shortage ya takriban tani 365 na almost more that 90 something percent tunaagiza haya mafuta kutoka Malaysia na spending yetu ilikuwa ni zaidi ya bilioni 443 tukiagiza haya mafuta.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ukijaribu kuangalia si kusema Watanzania hawataki kuweka viwanda vya kuzalisha mafuta haya ya alizeti, viwanda vipo lakini shida kubwa imekuwa ni upatikanaji wa alizeti yenyewe ambayo inabidi ikamuliwe ili iweze kutengeza mafuta. Sasa baada ya kupitia kwa muda mrefu nikijaribu kusoma huku na huku, nimejaribu kuangalia demand, ukijaribu kufuata Ripoti ya Shirika la Chakula Duniani - FAO; average yield ya sunflower per hectare ni kilo 979 ukilima hekta moja unaweza ukapata kilo 979.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile kilo moja ya mafuta inayo ujazo wa lita 1.1 na kwa hekta moja tunaweza kuvuna lita zaidi ya 700. Sasa ukijaribu kuangalia ile demand yetu ya takribani tani 365,000 ambazo zimepungua, tunajikuta kwamba tunahitaji takribani lita 401,500,000 ili tuweze ku- cover lile gap. Sasa hizi lita 401,500,000 tukijaribu kuangalia uzito wa mbegu ya alizeti ambayo tunahitaji ili kuweza kuzikamua ni takribani tani 287,196. Tukirudi nyuma huku kwenye hii ambayo nimeisema kuhusu kuzalisha tunajikuta kwamba ili tuweze kupata mbegu hizi tani 289,196 tunahitaji tuwe na hekta 290,000 average. Sasa hekta 290,000 tukirudi hata kwenye maandiko ya dini nilikuwa najaribu ku-refer hapa mimi ni Mkristo, Mathayo 6:20-21 unasema; “Jiwekeeni hazina Mbinguni ambako nondo na kutu hawawezi kuharibu wala wezi hawaingii maana pale ilipo hazina yako ndipo pia utakapokuwa moyo wako.” (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba nianze kuchangia, tunapopanga kufanya maendeleo ya viwanda ni lazima tuelewe, huwezi kumwambia mtu leo tumeshaongelea hapa tani zaidi ya 290,000 inabidi zilimwe alizeti. Unamwambia mtu aliyekaa Dar es Salaam abebe shilingi bilioni 50 akazifiche Biharamulo au kwenye mapori kule yeye kakaa kule, hazina iko kule moyo hautakuwepo. Desire ya mfanyabiashara yeyote yule ni apate profit anapowekeza sehemu kwa hiyo, kama hili jambo hatutalichukua kama Serikali hakuna anayeweza kuwekeza huku. Kwa sababu tunahitaji mbegu za alizeti ili tukamue mafuta. Sasa tunachoweza kukifanya hapa, baada ya kuangalia hizi mbegu tani hizi zinaweza zikazalishwa kwa fedha kiasi gani ni almost shilingi bilioni 190. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tukiweza kuibeba hii kitu kama Serikali tuka-invest almost shillings 200 billion, tunao vijana wengi sana ambao hawana ajira kwa sababu tani 190,000 ni kwamba hii nchi tutailima alizeti karibu kila sehemu. Sio tunazunguka hapa mapori yote yameshikiliwa na TFS, kila unapozunguka ni mapori, tunapozunguka ni mapori. Sasa ifikie hatua Serikali ibebe jukumu la kulima. Ikishabeba jukumu la kulima kwa kuwaweka vijana wakazunguka vijana wamemaliza form four, imagine lile darasa lenye wanafunzi 100 wanaofaulu ni nusu, nusu wanabaki tunawapeleka wapi wale vijana? Tubebe JKT, tuwape maeneo, tuwape fedha, wabebe vijana wa Kitanzania, tukalime haya mapori tukishamaliza kulima, mavuno yatakayopatikana kama tunavyofanya kwenye NFRA wakati wa mahindi yakahifadhiwe pale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mtu mwenye kiwanda sasa anayeweza kuhamasishwa akajenge kiwanda cha shilingi milioni 200, shilingi milioni 300, shilingi milioni 400, shilingi milioni
500 hata sisi Wabunge tutaweza kufanya. Yule mtu ataondoka atakwenda atanunua mbegu kwenye ghala la Serikali, atasaga kwa muda wake kila mwezi anaweza kufanya. Kwa sababu kilimo cha alizeti ni zao la miezi minne tu sasa hata wenye viwanda wanapata shida. Maana mimi wakulima wamelima miezi minne hii, mimi natakiwa nifanye production mwaka mzima kinachonitokea ni nini, inabidi ninunue alizeti ya kusaga mwaka mzima ila benki wanani- charge for something that I am just keeping it in my stock.

Kwa hiyo, tungeweza kufanya hiki kitu kikafanywa na Serikali, Serikali ni sawa na inavyotuuzia mahindi ihifadhi alizeti wenye viwanda watakuwa wanakwenda wananunua, in monthly consumption two months, three months or wherever, waweze kuzalisha mafuta. Tutakapokuwa tumebeba hawa vijana tukawaweka after four months wanarudi mtaani wameshajifunza kilimo, lakini pia na wao wamepata fedha watakwenda hata wao wataanzisha kilimo. Kesho na kesho kutwa tunakuwa kwenye position hata ya kuwalisha majirani zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, maana nimekuwa najiuliza what if Malaysia kesho watasema hawatuuzii sisi wanapeleka Marekani? Maana yake hapa hatutakuwa na mafuta. Huwezi kuendesha nchi kwa kutegemea mtu mwingine akuletee mafuta more than 90 something percent. (Makofi)

Kwa hiyo, tuweze kuiona hii kama focus mpya Serikali iichukue sawa na tulivyo-approve shilingi bilioni 50 hapa mwaka jana tukapeleka kwenye mahindi, hebu tuone hii ili Waziri huyu anapohangaika na watu wenye viwanda kuja kuwekeza hapa mbegu za alizeti wazikute.

Mimi ninakuhakikishia kama tutalifanya hili kwa study ambazo nimezifanya kama tutalifanya hili in two or three years, nakuhakikishia hatutakuwa na shida ya mafuta ya kula hapa tunaweza tukaanza kuwalisha na majirani zetu. Kwa sababu maeneo tunayo kinachohitajika ni nia tu, tukiweza kuweka nia chini tutatoka hapa tulipo tutasogea mbele zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu shida ya mafuta ya kula ni kubwa, wananchi mitaani wanalalamika yanazidi kupanda, sasa hatutegemei baada ya hapa yataelekea wapi. Kwa sababu as long as anai-control mtu mwingine hatuna ubavu nayo tutakwenda kununua ndio maana umeona idea inayokuja sasa hivi tunakuja na kuondoa duty tunataka duty irudi zero kwenye importation ya mafuta ya kula, maana yake ni nini, tunaleta tu mafuta ili tule tuishi Taifa halitapata faida yoyote kwa sababu mafuta yanazalishwa na Malaysia watatuletea hapa with zero duty, nchi haipati chochote kile ila tunachofanya tunaji-sustain ili tuweze kuendelea kuishi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuyasema haya mimi nimesema naongelea mafuta ya kula tu leo, ili kuwahi kengele na muda naomba niishie hapa, naunga mkono hoja, ahsante. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maji
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi pia niweze kuchangia kwenye Bajeti hii ya Wizara ya Maji. Kwanza nianze kwa kumshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mradi wa UVIKO ambao tuliupata Biharamulo Mjini. Mradi unaendelea vizuri tumetandaza mabomba pale kwa takribani kilomita 20 na tunajenga tenki kubwa tu kwa ajili ya kutusaidia pale Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri, pale ambapo mtu anastahili heshima na anastahili pongezi ni lazima tumpe. Mheshimiwa Waziri wakati unasoma Bajeti yako hapa, nadhani Wabunge wengi walikuwa in vibrant mood wamepiga makofi, wakashangilia, wakakushukuru lakini wanakushukuru kwa sababu ya mahusiano uliyonayo na Wabunge humu ndani. Yawezekana wanashida ya maji kwao, yawezekana wana matatizo mengine lakini matumaini wanayo kwa sababu life style yako humu ndani inakuunganisha na Wabunge karibu wote. Kwa hiyo, hilo tunaomba tukushukuru, maana kila tunapokufuata mtu unamwambia twende DUWASA. Saa nne kamili uko pale. Muda mwingi tunakuta foleni lakini mara nyingi unahudumia Wabunge. Kwa hiyo, bwana kwenye hilo naomba nikupongeze. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini si wewe tu pamoja na msaidizi wako Mheshimiwa Injinia Maryprisca nakupongeza pia. Ulinitembelea Biharamulo, tukaenda Mubaba, tukaenda Kabindi maji sasa hivi maeneo yale tuliyotembelea mambo yanaenda vizuri. Lakini siwezi kuwapongeza ninyi wawili bila kujua kwamba kuna Watendaji nyuma yenu. Mhandisi Anthony Sanga, tumpongeze pia lakini pia na Nadhifa Kemikimba Injinia naye anastahili pongezi kwa sababu wamefanya kazi kubwa. Wote tunajua tulichonacho ndio hichi tunagawana kidogo kidogo lakini wanafanya kazi kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikirudi upande wa RUWASA kwa kweli siwezi kumsahau Injinia Kivegaro kwa kazi kubwa ambayo ameifanya yeye na Taasisi yake ya RUWASA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati nachangia kwenye Bajeti iliyopita nilisoma kwa uzoefu wangu, bahati nzuri nimekuwa karibu sana na hii Wizara kabla ya kuingia humu Bungeni. Kero kubwa ilikuwa ni miradi ambayo ilikuwa imekwama kwa muda mrefu. Tumesikia wote Bajeti iliyopita na Bajeti hii pia. Kitendo cha kukwamua kutoka miradi 177 kichefuchefu na leo imebaki 57 tunaamini tunakoelekea ni kuzuri zaidi kuliko kule ambako tulikuwa tumekwama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini wakati wa uchangiaji mwaka jana nilieleza kitu kimoja ambacho kilikuwa ni concern yangu. Kama Mhandisi kilio changu kikubwa ni kuhakikisha kwamba tunatengeneza fursa kwa ajili ya watu wetu hasa ambao ninajua kwamba wamesoma course kama za kwetu hizi waweze kupata nafasi ya kufanya kazi na hatimaye watengeneze kipato kwa familia zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipindi kilichopita miradi mingi tulikuwa tunafanya kwa Force Account ikafikia stage watu wamesoma course zetu hizi walifungua kampuni zao lakini hawakuwa na ajira. Bajeti iliyopita mmerudisha wakandarasi kufanya miradi ya maji. Kwa hiyo, kwenye hilo naomba niwapongeze. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia kulikuwa na issue ya vifaa vinavyotumika kwenye miradi ya maji. Tumeona miradi mingi sasa hivi inayosimamiwa na Wizara ya Maji. Miradi ya RUWASA na hata miradi ya UVIKO ambayo imetokea pale material mengi yaliyotumika kwenye kufanya hizi kazi ni material yanayozalishwa ndani ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kitendo cha miradi ya maji kutumia mabomba na kutumia viungio na vitu vingine ambavyo vinatoka ndani ya nchi hapa ni fursa kwa wawekezaji wa ndani lakini vilevile ni fursa kwa vijana wa kitanzania ambao wameajiriwa kwenye haya makampuni. Kwa hiyo, kwa sehemu kubwa mmetubeba na mmesaidia ile adhma na hali ya kutengeneza ajira kwa ajili ya vijana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kitu kizuri ambacho nimefurahia napenda nikipongeze kabla ya kurejea kwenye miradi sasa ambayo inaelekea Jimboni kwangu. Mheshimiwa Waziri kama Mhandisi kuna kitu nilikuwa najiuliza, mnajenga Kituo cha Afya cha shilingi milioni 550 au milioni 500 kinakuwa na watu wa kukisimamia pale kila kitu. Ila unapeleka mradi wa maji wa milioni 700 unawaachia wanakijiji tu pale hawana Technician hawana nini. Kwa hiyo, hii ambayo mmekuja nayo sasa ya kuweka Technicians na Wahasibu maana yake hata Vyuo vyetu vya VETA ambavyo tunajenga kila sehemu wale vijana wanaenda kupata ajira za kuwa wasimamizi. Wengine wanaotoka kwenye Chuo chetu cha Maji wanaenda kusimamia pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwangu naona mmetu-boost lakini vilevile ile miradi itadumu kwa sababu ina watu wataalam ambao wanaelewa nini maana ya mradi wa maji. Kwa hiyo, nawapongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sasa nikirejea kwenye miradi ambayo inaendelea Jimboni kwangu, Mheshimiwa Waziri kwanza naomba nikupongeze. Ninalo eneo moja linaitwa Nyakanazi. Nyakanazi ni Mji unaopanuka sana na ni Mji mkubwa sana pale Biharamulo ni center kubwa kwa kweli kwenye Wilaya yetu ya Biharamulo. Kitendo cha kupata sasa kwamba signing ya Mkandarasi ambaye anaenda kutekeleza mradi mkubwa wa maji Nyakanazi nimeambiwa muda wowote watasaini Mkataba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwangu nishukuru kwa sababu ilikuwa ni kilio cha wanabiharamulo na hawa watu wa Nyakanazi wapate maji waweze kufungua pale fursa za kiuchumi na shughuli nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nishukuru kwa miradi inayoendelea kwenye Kata ya Nyabusosi eneo la Mbindi, Nyamigele, Mavota tunajenga tenki pale lakini Mheshimiwa Waziri alikuja pale maeneo ya Mubaba Sekondari, Naibu Waziri ulikuja, tunamalizia ule mradi pale lakini kuna miradi mipya pia ambayo naona nimeipata huku kwenye Bajeti hii ambayo imesomwa leo. Nina mradi wa Nemba, nina mradi wa Kikomanabusili, nina mradi wa Nyamigogo, Songambele na Kagoma, nina mradi wa Migango. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hii naomba niwashukuru. Lakini mwaka jana mwezi wa kumi tulipita eneo la Nyakahula na Mheshimiwa Waziri Mkuu. Nadhani pale kesi kubwa ilikuwa ni maji na baada ya kuwepo pale tulikuwa na taarifa kwamba tunaenda kufanya design pale ya mradi mkubwa wa maji wa kuhudumia lile eneo. Mwanzo tulitegemea kutumia mto lakini kwa sababu ya jiografia ya Biharamulo visima ukitaka kuchimba lazima vinakauka, viwe vya muda mfupi.

Kwa hiyo, tumeona sasa kwenye Bajeti hii imetengwa pesa kwa ajili ya kwenda kufanya upembuzi yakinifu na design ili tuweze kupata mtu wa kutekeleza mradi mkubwa wa maji ambayo utaondoa tatizo la Nyakahula.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimshukuru Katibu Mkuu, tukiwa pale na Waziri Mkuu baada ya ile ziara nilim- contact tukaletewa pesa ya pampu mbili za kilowati 22 pale, zimeshafungwa na kazi inaendelea. Lakini sasa kikubwa ambacho kipo, lile bwawa la Nyakahula ni bwawa ambalo limejengwa tangu wakati wa Mkoloni. Limeshajaa tope sana, sasa kwa taarifa nilizonazo tulishaleta maombi hapa ya pesa milioni 148 kwa ajili ya kwenda kusafisha lile bwawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nikuombe Mheshimiwa Waziri kesho utakapokuwa unahitimisha nipate majibu sasa zile pampu tulizozifunga pale kwa pesa nyingi zisivute udongo impeller zikaharibika, tukanunua tena pampu nyingine. Kwa sababu uwekezaji umefanyika ni vizuri tukamalizia ili kazi ya kuwapatia maji wananchi wa Biharamulo hususan Kata ya Nyakahula iweze kumalizika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kitu kikubwa kabisa kabisa ambacho ninacho leo napenda nishukuru kampuni au Shirika la CBHCC hawa ni wadau wa maendeleo wametusaidia sana maeneo yetu ya Biharamulo kwa kutekeleza miradi katika Kijiji cha Kasiro na Kijiji cha Luganzu wametusaidia kujenga miradi ya maji pale. Lakini vilevile tuna tunatarajia kwamba katika Mwaka huu wa Fedha wametuahidi watachimba visima 12 katika maeneo mbalimbali ya Biharamulo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia wana ujenzi ambao unaendelea katika maeneo ya Ntumagu na Lusenga. Kwa hiyo, lazima niwashukuru kwa sababu ni wadau wa maendeleo ambao wanatuunga mkono kwa sehemu kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nikirejea jambo langu la mwisho wakati namalizia. Mheshimiwa Waziri naomba nikushukuru. Naomba nikushukuru kwa sababu Biharamulo ni sehemu ambayo tumekuwa na kilio kikubwa sana cha muda mrefu cha maji. Ziwa Victoria liko hapo umbali wa kilomita 50 tu kutoka Biharamulo. Tumekuwa tunajiuliza yaani maji yanaenda sehemu nyingine, Biharamulo hatuna chanzo cha kudumu cha maji. Mwaka juzi wakati wa kampeni aliyekuwa mgombea wa Chama cha Mapinduzi aliahidi mradi mkubwa wa maji wa kuondoa kero ya maji ya muda mrefu kwa Wilaya ya Biharamulo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nikushukuru kwa sababu kwa meeting ambayo tumefanya nadhani jana na juzi mmenihakikishia na mkamwambia Meneja kwamba asiondoke Dodoma bila kupata barua ya kwenda kutangaza ule mradi. Kwa hiyo, kwa niaba ya wananchi wa Biharamulo walionituma hapa, sina budi kukushukuru, nakupongeza sana lakini zaidi nimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sababu mnafanya kazi ya kumuwakilisha humu ndani na kilio chetu watu wa Biharamulo kimesikika. Tufikishieni salamu kwa sababu sasa mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria unaenda kuingia katika Wilaya ya Biharamulo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hata sisi kwa mara ya kwanza tunayaona maji ya ziwa pale ambapo tulikuwa tunakutana nayo huku tukisafiri wakati ziwa lilikuwa karibu na sisi pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema hayo Mheshimiwa Waziri nadhani nina ombi moja maalum. Tumekuwa na kijana huyu Meneja wa RUWASA ni Injinia mwenzangu, Injinia Matina amekaimu muda mrefu sana. Sasa hata kukaimu kwenyewe inafikia stage unakata tamaa. Kijana huyu anashinda maporini kule, anashinda anahangaika mkizingatia maeneo yetu kule, hebu basi mtoeni kwenye kukaimu mu-approve sasa awe Meneja wa Wilaya. Hilo tu ndiyo ombi langu nikuombe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini namshukuru sana Meneja wa Mkoa, Injinia Sanya amekuwa msaada mkubwa hata katika miradi midogo midogo kwa sababu mara nyingine tumekuwa tunashauriana kitaalam. Anapokuja ni mwepesi hata wa kufika Biharamulo, ukimpigia simu anafika anatutendea haki. Kwa hiyo, ninaomba ombi langu Meneja wa Wilaya naomba Mheshimiwa Waziri kesho tamka neno ili roho yangu ipone na roho ipone. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kukushukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia hotuba hii ya bajeti ya Waziri Mkuu. Kwanza kabisa nachukua nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa fedha nyingi sana ambazo zimeletwa katika Wilaya yetu ya Biharamulo, lakini pia ziara mbili alizozifanya mwaka jana 2022 mwezi wa Sita na mwezi wa Kumi katika Wilaya yetu ya Biharamulo na akapata nafasi ya kuongea na wananchi katika maeneo ya Biharamulo Mjini na Nyakanazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitajikita kwenye mambo mawili siku ya leo. Jambo la kwanza ni mipango bora ya matumizi ya ardhi, ili kuondoa migogoro kati ya wafugaji na hifadhi zetu za Taifa, halikadhalika wafugaji na wakulima; na wakulima na hifadhi. Jambo la pili, nataka niongelee habari au njia bora ya kuzuia wizi au ubadhirifu kwenye miradi ya umma au miradi yetu inayotekelezwa na Serikali. Ni mambo mawili nataka niyaongelee kwa haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianza na suala la mipango bora ya matumizi ya ardhi; kwa muda mrefu sana wakulima wa nchi hii au wafugaji wa nchi hii wamekuwa kama watu ambao hawana sehemu ya kukaa. Sasa tulizoea ugomvi kati ya wafugaji na wakulima, lakini leo hii tunashuhudia ugomvi kati ya wafugaji na Serikali yao kupitia TANAPA au kupitia TFS.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunaotoka maeneo haya yenye hifadhi wafugaji wa nchi hii wanapata tabu sana. Wafugaji wengi sana wamefilisiwa. Kila ng’ombe anapokamatwa anatozwa shilingi 100,000 kwenye yale maeneo. Mimi si-support watu kuingiza ng’ombe mle, lakini wafugaji hawa wamedhalilika na wamefilisiwa kwa sababu Serikali haijawawekea mpango bora wa kujua wanafugia wapi? Hii ndio shida. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunaotoka maeneo kama ya Biharamulo, kwa sehemu kubwa; mimi naongea na wananchi wangu na wananipigia simu; na mara nyingi nimekuwa nawauliza, kwa nini mnaendelea kuweka ng’ombe huko wanakamatwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, makundi makubwa ya ng’ombe kutoka nchi jirani yamewekwa kwenye Hifadhi ya Burigi. Sasa wananchi wetu wanapoingiza ng’ombe mle, wanakamatwa, lakini ng’ombe wa wageni wako mle. Hii ni aibu na udhalilishaji wa wafugaji wa nchi hii. Ninachoomba, kama Bunge ni lazima tupate hatua nzuri ya kuwasaidia wafugaji wa nchi hii. Hatuwa-support kuingiza mifugo kwenye hifadhi, lakini tuje na mpango bora wa kuwasaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati nzuri wewe ni Mwenyekiti wa Kamati yangu ambayo ninatoka na Kamati ya Mifugo iko chini yako. Tulipata ripoti kutoka kwa Waziri wa Mifugo, a very good report kwamba wanao mpango wa kuleta majani kutoka nje ya nchi waanze kuotesha kwa ajili ya kuwasaidia wafugaji wa nchi hii, lakini wanasaidia wafugaji wangapi? Anayejua ng’ombe wa Biharamulo ni wangapi? Ng’ombe Mufindi ni wangapi? Hatujafanya sensa ya kujua idadi ya mifugo kwenye nchi hii. Sasa naomba hili jambo lifanyike, tujue idadi ya ng’ombe kila eneo na Serikali itusaidie kutenga maeneo kwa ajili ya wafugaji. Halikadhalika, hata ng’ombe ambao tunasema, ni nani anayeweza kuwa-identify?

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tumeanza mnada wa kuuza ng’ombe live. Huko ng’ombe wanakopelekwa, ng’ombe wetu hawana alama wala hawana identification. Tulijaribu kuongelea issue ya alama hapa ya kuwawekea sijui imepotelea wapi? Matokeo yake tutaenda kwenye mnada wa dunia unapeleka ng’ombe kule, wenzetu tunawajua, hata maparachichi yalivyokuwa yanakuwa mabovu kule watasema yametoka Tanzania. Kesho utapeleka ng’ombe pale anaonekana ana ugonjwa katoka sehemu nyingine, kwa sababu hawana alama, watasukumia, watasema ametoka Tanzania. Kwa hiyo, kesho na keshokutwa, hata kizuri ambacho tunakifanya kwenye soko kitaharibika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba hilo tusaidiwe, ng’ombe wafanyiwe identification, pia maeneo yatengwe, na hayo majani yatakapokuja, watu tuwe tunajua, tunapata majosho mangapi kwenye maeneo yetu? Tunapata mabwawa mangapi ya kunyweshea ng’ombe? Halikadhalika, hata hayo majani yaje yaoteshwe. Wafugaji wako tayari kutoa hata pesa kuliko kuhangaika na makundi ya ng’ombe watoke Biharamulo wayapeleke Sumbawanga. Wako tayari kutoa pesa hata hayo majani yakioteshwa ili waweze kuyapata kwenye maeneo yao. Kwa hiyo, nilikuwa naomba hilo liangaliwe kwa ajili ya kulinda wafugaji na kulinda hii mifugo tunayoiuza nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 18/09/2021 Mheshimiwa Waziri Mkuu alitembelea Biharamulo, akafanya mkutano pale kwangu Nyakanazi. Nakumbuka kwenye mkutano ule wananchi wa Nyakanazi walimwomba Mheshimiwa Waziri Mkuu eneo la kulima. Kuna Swamp pale kwenye eneo la TFS, wakawa wameomba na Waziri Mkuu akatoa maelekezo kwamba, Waziri wa Maliasili, aliyekuwepo wakati ule aje, nami nikamjulisha, lakini as I am speaking today, hakuna Waziri aliyekanyaga Biharamulo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba, kuheshimu maelekezo aliyotoa Waziri Mkuu tarehe 18/09/2021, naomba Waziri wa Maliasili na Utalii afike Biharamulo, aongee na wananchi wale wa Nyakanazi awaambie lile eneo linapatikana au halipatikani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kibaya sana, kitu kibaya mno, Maaskari wa TFS walioko maeneo ya Nyakanazi kwenye ule msitu wetu pale, wamekuwa wanawalaghai wananchi wa Biharamulo, wanawalipa pesa, wanaenda wanalima kwenye hifadhi, muda wa kufanya mavuno unapofika, wale Maaskari wanawakamata wale wananchi na yale mavuno wanayachukua. Huo ni udhulumishi na udhalilishaji wa ajabu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kabla ya kumaliza bajeti hii, Waziri Mkuu atakapokuwa ana-wind up tupate majibu.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ulinde muda wangu. Maana nadhani Mawaziri wanayo nafasi ya kujibu hoja zetu.

MWENYEKITI: Taarifa.

T A A R I F A

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba tu nimpe Taarifa Mheshimiwa Mbunge wa Biharamulo kwamba, Wizara ya Maliasili na Utalii na Utalii imekasimiwa madaraka na Serikali kusimamia maeneo yote yaliyohifadhiwa. Kazi kubwa kwetu ni kulinda na kuyahifadhi hayo maeneo. Linapofika suala la kuomba eneo, tunawaomba wananchi wanaandaa vikao, wanakuja wanaleta-proposal yao, tunaiangalia kama itawezekana. Kwa sababu, tunapolinda tunaangalia mambo mengi, kuna masuala ya shoroba, kuna masuala ya maeneo ya mtawanyiko, kuna mandhari ambazo tunazitunza kwa ajili ya faida ya wananchi wao wenyewe walioko katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, unapoomba usitarajie wakati wowote utapata. Ni pale ambapo tutaona: Je, kuna umuhimu wa kulitoa hilo eneo ama la?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, maeneo tunayoyahifadhi sisi ni kwa ajili ya faida ya wananchi wenyewe pamoja na Watanzania wote na siyo ya maliasili na watumishi wake peke yake.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Engineer Ezra unapokea Taarifa?

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa siipokei. Mimi nawakilisha wananchi wa Biharamulo, ningeomba nisikilizwe hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sipingani na Serikali, na sijasema wananchi waingize ng’ombe au wafanye kazi kwenye hifadhi. Nilichokisema hapa, kitendo cha askari kuwaambia wananchi wakalime kwenye hifadhi, wakampa pesa akawaruhusu wakalima, kesho wakati anaenda kuvuna wakamkamata, that is insubordination kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi hawana maeneo. Tunapoomba maeneo kwa Serikali hapa, Waziri umekaa hapa, watakuletea taarifa walioko kule site. Aliyeko site kama anafanya bishara ya kuwakodisha wananchi pale, anawadhulumu ardhi, kesho utamwuliza akupe ushirikiano? Hicho ndicho ninachokitaka. Sitaki wananchi wakalime mle bila kibali, lakini ninachotaka, wananchi watendewe haki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeomba ardhi, Mheshimiwa Rais tarehe 16 akiwa Nyakanazi nilisimama nikaomba, tumeshawasilisha, Mkoa wa Kagera umeleta, Serikali inafanyia mchakacho, lakini kipindi inafanya mchakato wananchi hawa wasiumizwe na watu wenye uchu kwa kuwadanganya halafu baadaye wanawadhulumu ardhi yao. Hicho ndicho ninachokisema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ameniwahi, sijasema wananchi wakafanye…

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ezra, unaweza kukaa pale tu nikiruhusu taarifa. Taarifa hizi zinakula muda wako. Kwa hiyo, endelea kuchangia mpaka itakaponipendeza. (Kicheko)

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Anyway, sasa hilo la hifadhi nadhani limesikika, limeeleweka, naomba mlifanyie kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu ya pili, naomba unilinde muda wangu maana nimekalishwa mara nyingi hapa. Sehemu ya pili, nilikuwa nataka kuongelea njia bora ya kuzuia wizi na ubadhirifu katika miradi ya umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe ni shahidi, tumesema tusiongelee habari ya Ripoti ya CAG hapa kwa sababu muda bado, lakini ukweli ni kwamba, wananchi wa nchi hii kinachoendelea kila mmoja anakijua. Kwenye vijiwe, kwenye mitandao na kila maeneo, kila mmoja anajua yaliyofanyika na kila mmoja anajua yanayoendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wangu nilitaka niseme jambo moja, kidogo nina uzoefu kwenye hii miradi. Kinachofanyika hapa kwenye Ripoti ya CAG…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Naomba uhitimishe Mheshimiwa Ezra, dakika zako zimeisha.

MHE. ENG. EZRA J CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kengele ya kwanza.

MWENYEKITI: Haya, nakuongeza dakika moja nyingine.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, haitanitosha, naomba nihitimishe.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi pia nichukue nafasi hii kukushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika bajeti hii ya Wizara ya Ulinzi na nichukue nafasi hii kumpongeza Waziri wa Ulinzi kwa hotuba nzuri ambayo ameitoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninayo machache ya kuchangia kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Biharamulo nadhani taarifa zangu nilishakaa na Waziri pia lakini ningeomba jambo hili niliweke sawa kwa ajili ya records na kwa ajli ya wale ambao wamenituma, maana nilikuwa Jimboni juzi na jana kelele kubwa ni kwa ajili ya mgogoro wa muda mrefu kati ya Kikosi cha 23KJ na wananchi wa Kata ya Nyarubungo katika Vijiji vya Rusabya na Kata ya Ruziba vilevile katika vijiji vya Ruziba lakini na kata ya Biharamulo mjini sehemu ya ng’ambo Lukoma.

Mheshimiwa Naibu Spika, mnamo mwaka 1984 wakati kambi ya jeshi inaletwa pale Biharamulo tayari wananchi walikuwa wanaishi katika vijiji hivi na ikafanyika tathmini, ilipofanyika tathmini wananchi wakaamuliwa wasifanye maendelezo yoyote yale kwa sababu tayari ilikuwa ni sehemu ambayo imetengwa kwa ajili ya kufanya mazoezi ya kikosi cha 23KJ na hivyo wananchi wakabaki stranded kwa sababu hawakutakiwa kuendeleza nyumba wala kulima au kufanya chochote kile. Lakini tangu mwaka 1984 wananchi wale hawakulipwa wala hawakufikiwa chochote kile. Kwa hiyo ninavyosimama kuongea ni miaka 37 tangu wakati ule, wanachi wamekuwa katika sintofahamu ya muda mrefu na zaidi wakiendelea kuilaumu Serikali kwa kitu hiki ambacho kilifanyika, lakini pia mwaka 1998 iliundwa kamati nyingine ndogo iliyohusika viongozi wa kijiji, ilihusisha viongozi wa Wilaya pale, Afisa Ardhi na watu wengine wakapitia tena upya.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ninasema sio mgogoro ila ni changamoto ambayo imekuwepo kwasababu hata jeshi lenyewe ambalo llimechukua eneo lile ni eneo ambalo lipo ndani perimeter ya kilometa tano kutoka katikati ya mji wa Biharamulo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo hata jeshi lenyewe ni kwamba haliwezi kutumia eneo lile ambalo limetengwa kwa sababu ni eneo ambalo lilitengwa kwa ajili ya kufanyia mazoezi, lakini kwa sababu wananchi wale hawakulipwa inaonekana sio mali halali ya jeshi kwa sababu jeshi haliwezi kusema kwamba ni male yake kwa sababu bado halijawalipa wananchi, lakini wananchi waliamuliwa wasiendelee kufanya kazi yoyote. Kwa hiyo kumekuwa na mvutano mdogo mdogo ambao unaendelea. Wananchi wale wanachoka kwasababu sasa ni eneo la mjini unapomtoa pale na ukampeleka sehemu nyingine ni kwamba wamekosa sehemu za kufanyika kazi, maana hata maeneo yale ambayo ilibidi wakimbilie wamekimbilia kwenye kata moja ya Nyamahanga eneo moja linaitwa Kibale lakini hata kule walipo bado ni maeneo ambayo wameenda na kuwakuta watu wengine kwa hiyo wameenda kuanzisha mgogoro na watu wengine tena pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nilichokuwa naomba kipindi Waziri ana-wind up tuje na majibu sasa tujue wananchi hawa ambao wamekaa kwa miaka 37 wakisubiria kujua hatima yao ni nini kinaendelea, maana kabla ya mimi kuingia Bungeni niliambiwa kwamba mwaka jana kuna Tume ziliundwa na Mawaziri nadhani wakazunguka kupitia maeneo ambayo yalikuwa na migogoro, lakini kwa Biharamulo hawakufika na maswali ambayo nimekumbana nayo sana na wananchi wale bado wanalalamika kwasababu wanasikia watu walienda sehemu nyingine Biharamulo hawakufika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nilikuwa ninaomba Serikali itupe majibu ya kina na ya ufasaha ili wakazi hao ambao wameachia maeneo yao, maeneo ya Rubasya, maeneo ya Ruziba, maeneo ya Ng’ambo ili wajue hatma yao ni nini (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu hata jeshi nalo pia haliwezi kuyatumia maeneo yale kwasababu kuna kipindi katika kufanya range walipiga risasi wakati wanajeshi wanafanya majaribio pale wananchi wakaja kuokota maganda wakaleta complain nyingi sana kwamba ni kama vile wameshambuliwa na nini. Kwa hiyo, nilikuwa ninaomba hili jambo liangaliwe kwa sababu ninachoelewa kazi kubwa ambalo jeshi linayo pale ni kazi ya kuhamasisha, kuelimisha wananchi juu ya masuala ya ulinzi wa nchi yetu ili waweze kushiriki katika kulinda mipaka ile na mkizingatia sisi tupo mipakani kule. Sasa wananchi wale ambao inabidi muwaelimishe na watusaidie kulinda mipaka ile, wanapokuwa wana-feel kwamba kama wameonewa au wamedhulumiwa eneo lao sidhani kama watakuwa walinzi wazuri wa mipaka kule.

Mheshimiwa Naibu Spika, nyote ni mashahidi kwamba sisi ambao tupo maeneo yale wenzetu wa nchi jirani wakati mwingine wanaingia na ndio hao wanatumika, lakini mlinzi wa kwanza ambae anawatambua wale kabla ya Serikali au vyombo vya ulinzi na usalama mlinzi wa kwanza lazima awe mwananchi. Kwa hiyo kama mwananchi ameshirikishwa vizuri ataweza kutusaidia kulinda maeneo yetu ya mpakani kule.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nilichokuwa ninaomba mimi sina maneno mengi sana kwa ajili ya ku-save muda lillilonisimamisha hapa kwenye Wizara hii ni hilo moja ya kwamba sasa tupate majibu ya uhakika ya Serikali mkwamo huu wa tangu mwaka 1984 ambao ume-consume miaka 37 leo tunaumalizaje ndani ya Bunge hili iliwananchi hawa wa Biharamulo waweze kupata haki yao na hatimaye jeshi pia liweze kuwa free kuyatumia maeneo yale kwa ajili ya kufanyia mazoezi wanajeshi. (Makofi)

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Ameshamalizia kuchangia.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba niunge mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia katika bajeti hii ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa niwapongeze Mheshimiwa Waziri na msaidizi wake kwa hotuba nzuri waliyoitoa. Lakini pia nimpongeze mtangulizi wake aliyekuwepo, Mheshimiwa Jenista, kwa kuyachukua mengi tuliyoyachangia katika Bunge la Bajeti lililopita. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini yako baadhi ambayo hayajafanyiwa kazi. Sasa nilitaka kipindi tunaendelea kwanza nipongeze nafasi nyingi sana za ajira ambazo zimetoka, hasa hizi nafasi 21,200. Tumpongeze Mheshimiwa Rais kwa nafasi hizo, walau zinapunguza joto ingawa joto bado ni kubwa, lakini at least zinapunguza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana wakati nachangia bajeti hii ya Utumishi specifically niliongelea

jambo moja linalohusu watoto waliomaliza katika vyuo vya maliasili lakini wakanyimwa ajira kwa sababu umri wao umevuka miaka 25. Nililisema hapa na ninaomba nilirudie kwa sababu ni kama halikufanyiwa kazi na bado halijafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati tunapewa majibu humu ndani tuliambiwa sheria za Jeshi haziruhusu kuajiri mtu aliyevuka miaka 25. Nikasema sawa. Lakini vijana hawa wengi ambao tunasema wametoka kwenye vyuo vyao wamekuwa trained Kijeshi na tayari wanavyo vyeti. Sasa unaposema huwezi kumuajiri wakati ana cheti na umem-train Kijeshi na yuko mtaani, sidhani kama ni fair. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe, kwa sababu vyuo hivi ni vya Serikali, wazazi wamelipia kuwapeleka watoto wao wakaenda kusoma pale, tunaomba Serikali itumie busara ione vijana hawa ambao hawakuajiriwa kati ya 2015 mpaka 2022 waone jinsi ya kusaidiwa ili na wao jasho lao walilolitoa kujifunza mafunzo haya ya Kijeshi waone kwamba kuna sehemu wanakwenda.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu kuendelea kuwaacha mtaani ni kuwaonea. Maana mtu amesomeshwa na mzazi kwa ada ya milioni nne mpaka nane, leo anamaliza pale unamwacha mtaani unamwambia umri umevuka, na hakukataa kujiajiri, ni kwa sababu hatukuwa na nafasi za kuwaajiri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini huku tunapotoka kila siku tunalalamika tembo wanatoka wanajeruhi wananchi, wanafanya nini. Hawa vijana wako mtaani, tuone jinsi ya kuwachukua kwa sababu bado nafasi za kuwaajiri zipo; hilo ndiyo ninaomba. Mlichukue hivyo, Serikali ilione ili iweze kutusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mchango wangu wa mwaka jana niliongelea pia habari ya nafasi zinazotoka kwa kigezo cha JKT. Wote ni mashahidi; kambi zetu tulizonazo za ku-hold watoto katika JKT hazitoshi wala haziwezi kuenea watoto wote walio mtaani. Lakini inashangaza kwamba nafasi bado zinatoka kwa kigezo cha kwamba mtu awe amepita JKT. Na humu ndani tulisema na Serikali ikasema imesikia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninao mfano; nafasi za Uhamiaji zilizotoka ilikuwa ni miaka 18 mpaka 25 kigezo cha kwanza, kinachofuata, awe amehitimu JKT. Lakini ni vijana wangapi wamekuwa denied nafasi ya kwenda JKT? Unamnyima kwenda JKT, wakati wa kutafuta ajira umetangaza ajira unamwambia awe ametoka JKT. Inaumiza kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hili naomba niliseme kwa niaba ya vijana walioko mtaani. Tumeona habari za Uhamiaji, tumeona nafasi za Magereza. Leo nilikuwa nasoma kwenye website ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Jeshi ambalo tunasema kwamba labda ndiyo basic; hakuna hiyo condition ya kwamba mtu awe ametoka JKT. Wameandika tu miaka 18 mpaka 25, awe Mtanzania aliyemaliza kidato cha nne, wao hawaweki kigezo cha JKT.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tunaomba haya Majeshi mengine ambayo yanafuata hapa wajaribu kuona, mpe nafasi huyu Mtanzania aje kwenye interview. Kama anafeli afeli kwa kigezo hicho cha kufeli baadaye mrudishe nyumbani, kuliko kum-deny kabisa hata nafasi ya kufanya interview. Watoto hawa wanaonewa, naomba hilo liangaliwe ili tuweze kuwasaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, liko suala lingine ambalo nataka niliongelee. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI, jana ametutolea ufafanuzi mzuri sana hapa kuhusu hizi ajira, maana simu zimeelemewa huku; meseji ni nyingi, watu bado wanaendelea kutuma, pamoja na ufafanuzi wako wa jana meseji zinaendelea; wazazi, watoto na kila mmoja anaendelea kutuma. Lakini ninaomba nitoe suggestion moja; kuna mtu aliyeongea jana hapa kuhusu allocation ya hizi nafasi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndugu zangu, wote hapa tulikwenda kuomba kura kwa wananchi. Wakati tunaomba kura kwa wananchi tuliinadi Ilani ya CCM. Ilani ya CCM imeweka specific kabisa kwamba tunataka kutengeneza ajira milioni nane. Ni aibu kwa Mbunge ninayesimama hapa leo, sijui hata watu ambao katika hizo nafasi 21,000 zilizotoka, leo hata jimboni kwangu naulizwa wametoka watu wangapi, sijui. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wewe ni Mbunge mwenzetu, unawawakilisha wananchi, na humu ndani hakuna mtu anayegombea kwamba hizi nafasi anazipeleka kwenye familia yake. Lakini tunachoomba ni kwamba pale tunaposhauri mawazo yetu ni mawazo ya wananchi, tunawasikiliza wananchi huko mtaani wanavyosema. Wanatoa mawazo kwamba kwa nini hata hizi nafasi zisigawanywe kwa kila jimbo?

Mheshimiwa Naibu Spika, kama mnatugawia pesa sawa ya miradi ya barabara, mnatugawia pesa sawa miradi ya maji, mbona kwenye ajira kunakuwa na kigugumizi? Tukigusia tu ajira mnaanza kusema ubaguzi. Tunachotaka ni kwamba nafasi zimetoka 21,200, hatutaki kumpangia Waziri nafasi zile amuweke nani au afanye nini, tunachotaka iwekwe equality. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimepiga hesabu, nafasi 21,200, ukigawanya kwa halmashauri 184 za nchi hii wote wako sawa, kila halmashauri iko sawa, hakuna halmashauri kubwa wala ndogo hapa. Nawawakilisha wananchi na Wabunge wenzangu wanawakilisha wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukigawanya maana yake kila halmashauri itapewa nafasi 115 katika ajira hizi. Twende kwenye ile system yetu, system si unai-feed tu? Iwe ni system ya JAVA au kama ni C++ programming, unai-feed information, ielekeze, kwamba choose watu 140 kutoka wilaya hii itakupa, choose watu 140 kutoka wilaya nyingine watakuwepo pale, mkabidhi Waziri wa TAMISEMI mwambie watu wako 21,200 hawa hapa. Yeye awapange anavyotaka, lakini ajira hizi zisambae nchi nzima. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, haiwezekani sisi tunakaa hapa tunawawakilisha wananchi unatoka hapa wananchi kila mtu anatuma meseji, wewe unakuwa unamwambia mfumo. Wakati unaomba kura ulimwambia tutawasaidia kupata ajira, tutaleta maendeleo, leo unamwambia mfumo. Hiyo haikubaliki, tusaidiane. Najua bado deadline haijafika, mnaweza kwenda kwenye mfumo – Utumishi mko hapa – tukakubaliana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri zaidi tunaye Mheshimiwa Bashe ni mfano tosha hapa kwenye Mradi wa BBT. Waliomba nchi nzima lakini kila wilaya imepata, tumeona, na yakatoka matangazo. Hakuna malalamiko tena. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wanaouliza tunawaambia kwamba nafasi ya pili ya BBT inakuja, subiri. Iko wazi inaonekana. Ajira hazipo lakini zikitoka chache tukawaambia wilayani kwetu tumepata ajira 50, subirini raundi ijayo, wananchi wanaelewa na wanaelewa hali ilivyo. Kuliko unakwenda sehemu mtu anakuuliza huna hata jibu la kumpa. Ninaomba hilo tulizingatie. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, kuna kitu nimekuwa najiuliza. Ajira tunazoziona hapa; ualimu, huduma ya afya, hivi ajira za TRA huwa mnazitangazia wapi; ajira za BoT mnazitangazia wapi? We want to see them. Ajira za TANESCO mnazitangazia wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka hata zile ajira kubwa tuone watoto wa maskini wakienda huko kwa sababu wamesoma. Kelele zilizoko huko ni kwamba wanahisi zile ajira ni za watoto wa viongozi, siyo za kwao. Tuone zikitangazwa wazi, huo mfumo uwekwe kwa uwazi kama ni kugawanya tugawanye equally, nchi nzima.

Mheshimiwa Naibu Spika, hatutaki tuone watu wa TRA ukienda unakuta watu wa kabila fulani tu na watu wa eneo fulani. Tunataka uende ukute Muha, Mhaya, Mchagga, ukute nchi nzima tumeenea kule, that is what we want. Kwa sababu hii ni keki ya Taifa, tuigawane equally ili kila mmoja aweze kupata haki ya kutumika katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho kwa kumalizia, ninachoomba, taasisi hii ya Sekretarieti ya Ajira, tulikuwa tunaomba kama inawezekana ajira zote zipitie huko, tui- empower hii Sekretarieti ya Ajira. Kwa sababu ndiyo usalama wa Taifa letu wenyewe ulipo, tuwaajiri watu tunaowajua watachujwa kwa vigezo wataonekana kwa merits na qualifications zao ili iweze kutusaidia hata kuulinda usalama wa nchi hii. Siyo sasa kila taasisi inaachiwa inaajiri yenyewe tukitoka hapo baadaye tunakuja tunataja mfumo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuyasema hayo, nishukuru sana kwa nafasi. Lakini pia tuzidi kuangalia, tuzidi kumuomba Mheshimiwa Rais atusaidie ajira nyingine ziweze kuongezeka kwa sababu kweli kiuhalisia madarasa ni mengi, vituo vya afya ni vingi, watumishi wanahitajika na bado wengi wako mtaani.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunisikiliza, nashukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi pia na mimi niweze kuchangia katika hotuba hii ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kwa kuaminiwa na Mheshimiwa Rais kwa ajili ya kushuika nafasi hii. Naamini nyie ni vijana, Mheshimiwa Rais anaelewa kazi ya ufugaji iko vijijini na sio vijijini tu, maporini na ndiyo maana amewateua nyie vijana ili mweze kufika huko kuonana na wafugaji. Baada ya kuyasema haya; mimi ni Mjumbe wa Kamati kwa hiyo kuna mambo ambayo tuliyaona hasa kwenye ziara na nilikuwa natamani kuishauri Wizara na ikiwezekana Bunge tuweze kusaidia Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetembelea miradi, hasa ule mradi wa mabwawa ya kunyweshea mifugo. Tulitembelea Bwawa la Matekwe Nachingwea. Mmpaka ufike Nachingwea kwanza ni safari ndefu sana ambayo kwa kweli unafika umechoka, lakini kutoka Nachingwea penyewe mjini kwenda huko Matekwe kwenye hilo bwawa ni kilometa 154. Kwa hiyo unaweza uka imagine ni kiasi gani Kamati iliingia ndani na iliingia ndani kweli kweli maporini. Kwa nini nayasema haya, jana wakati nawasilisha taarifa ya Kamati, nadhani mtakua mlisikia nyote, kwamba thamani ya bwawa tuliyoikuta kule ilikuwa haiendani na uwekezaji ambao tuliambiwa. Sababu kubwa ambayo tuliiona kama Kamati; engineers wapo wawili, sijui watatu nchi hii, wazunguke wao kushughulikia miradi yote hii ni, ngumu kufanya hicho kitu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi wote ni mashahidi, tunao ma- engineers kwenye majimbo yetu au Wilayani lakini bado hawajaweza kufika sehemu zote hizo, sasa Engineer mmoja kuweza ku manage miradi ambayo inapitishwa na Wizara hapa ni ngumu, na ndiyo maana tukaja na pendekezo kama Kamati jana. Kwamba, tunaomba iwekwe taasisi maalumu inayo-deal na mifugo, na pia iwekwe taasisi maalumu inayo-deal na uvuvi, sawa na ambavyo tumeanzisha Wakala wa Umeme Vijijini, tumeanzisha wakala wa barabara na vitu vingine kama hivyo; tuanzishe wakala atakay-deal na mifugo na atakaye-deal na uvuvi, itatusaidia miradi ile ambayo tunaipeleka huko vijijini tuweze kuwa na monitoring. Ni aibu kupeleka mradi wa milioni 405 mna uweka porini baada ya hapo mmeaga na salama ndio mmeondoka na mradi ukishazinduliwa umekabidhiwa kwa wananchi umepotea. Kesho hata kama kuna tatizo linalotokea hakuna mtaalam kule. Kwa hiyo mradi mnauweka baada ya muda value for money haionekani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini unajenga mradi wa maji hata wa milioni 20, milioni 30 kuna watu wanaufanyia monitoring na ma engineer wapo. Kwa hiyo tulikuwa tunaomba taasisi maalumu ya ku-deal na mifugo na uvuvi iundwe ndani ya Bunge hili iweze kusaidia fedha hizi zinazopelekwa huko. Ni mabilioni ya shilingi yanapelekwa lakini hayaonekani thamani yake kwa sababu hakuna anayefatilia. Mwaka mwingine unaofuata Waziri anakuja na kitu kipya, tukishapitisha unaofuata anakuja na kitu kingine, hivyo hivyo. Kwa hiyo fedha hii inaenda lakini hakuna anayeonekana kuisemea. Nilikuwa nataka niliweka hilo.

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ezra kuna taarifa naomba…

TAARIFA

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi, naomba kumpa taarifa Mheshimiwa mzungumzaji kwamba maeneo haya sio yapo mbali tuna mjini kama alivyotolea mfano wa Jimbo la Nachingwea ambako mimi ni Mbunge bali hata monitoring yake kama halmashauri hatuelewi chochote kwa sababu Mkandarasi anatoka moja kwa moja Wizarani na kama halmashauri hatuna namna ya kwenda kumsimamia na kukagua huo mradi.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ezra, taarifa hiyo unaipokea.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea, ni nyama tosha kabisa hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niachane na huko; cha kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mkuu, Alhamisi alitoa hotuba hapa yenye mwelekeo mzuri; lakini kama Wabunge wengine walivyosema. Wizara ya Mifugo nimesema ninyi ni vijana tunaomba mtusaidie. Kuna kipindi tunagombana na watu wa maliasili hapa ninyi mkiwa mmekaa kimya; we want you to speak out. Kwa sababu Waziri wa Maliasili amekuwa na wivu mkubwa hapa. Unamuuliza kati ya tembo na binadamu anayeuawa mwenye thamani ni nani anawaambia wanamfuata tembo, unaweza ukaona; lakini nyie wafugaji wetu wananyanyasika kweli kweli.

Mheshimiwa Mwenyekiti,nina ushahidi hapa kwenye simu ninaweza nikatoa. Juzi Alhamisi Mheshimiwa Waziri Mkuu alisimama, hapa ameelezea reconciliation ambayo inabidi ifanyike na akasema hata haya mambo sasa ya watu kukaa karibu na hifadhi wanachukua wananyama na wakati mwingine wanawaingiza ndani wanasema wamekamatwa, Jumamosi mwenyekiti wangu wa halmashauri, na message ninazo hapa, huyu si mtu mdogo ndiye anayesimamia halmashauri yetu, na haina hati chafu. Kwenye kata yake akanitumia ujumbe wafugaji wawili, mmoja katozwa milioni tano mwingine katozwa milioni 11 hawajapelekwa sehemu, pesa imetolewa cash hakuna risiti hakuna; wafugaji wananyanyasika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siku mbili baada ya Waziri Mkuu kuhutubia Bunge mambo yanafanyika kule sisi tukiwa hapa. Kwa hiyo tunaomba Wizara ya Mifugo mchukue hatua vinginevyo sasa utakuja kuanza ugomvi kule wale wahifadhi na wakulima na sisi sasa tutaingilia kati. Lakini tumechoka, hatuwezi kuja hapa kila siku wafugaji wetu wananyanyaswa kila ng’ombe shilingi laki moja Wizara iko hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti,tunaomba mtusaidie, wafugaji ni Watanzania. Ni lazima, kama mnasema Pato la Tanzania linaingia kwa asilimia 7.8 hawa watu hii nchi ni yao, lazima ifikie hatua na wao waone thamani ya kuwa hapa, wasinyanyaswe tuna watu. Kwa hiyo tunaomba hilo mlione mje na strategy nzuri ya kutusaidia ili wafugaji ambao wanafuga ng’ombe kule na wao wajione kama Watanzania. Nimelisema mara nyingi hili suala sasa inafikia stage tunachoka, tunaomba hilo mtusaidie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nishukuru pia na nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mkuu, nadhani tumeona wote video na hotuba jana kipindi anapita kwenye mabanda. Ameelekeza suala la utambuzi wa wanyama lianze upya, hususan suala la herein, ameelezea jana pale. Kwa hiyo kama Waziri Mkuu tumepokea lakini tunachoomba tunaomba Wizara tuwashauri. Wafugaji hawa mlikuja na habari ya chapa ng’ombe wakachapishwa ng’ombe wakaumia ngozi matokeo yake hatukuona kilichoendelea, na baada ya miaka mitatu mnahamisha mnapeleka kwenye heleni sasa mimi nilikuwa na ushauri…

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ezra kuna taarifa kutoka kwa Nusrat Shaaban Hanje.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mngeniacha nichangie, muda umeisha.

TAARIFA

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimpe taarifa mzungumzaji kuhusiana na suala la identification ya mifugo, kwamba si suala la utashi wa viongozi kwa sababu ni sheria ambayo ilitungwa na Bunge hili, Sheria ya Usajili, ufatiliaji na utambuzi wa mifugo mwaka 2010, ambapo kifungu cha saba, cha nane mpaka cha tisa vina elezea devices. Kwa hiyo ni jambo la kisheria si jambo la utashi.

MWENYEKITI: Mheshimiwa taarifa unaipokea?

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea ila sasa naomba unilindie muda wangu maana na mimi hapa nahesabu. Taarifa nazipokea jamani tungevumiliana tumalize maana muda unaenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ninachoomba, cha kwanza tuna ranchi zetu za taifa, kwenye zile ranch kuna watu wanapewa nafasi ambao si wafugaji. Kwa hiyo tunachoomba, kwa kuanzia, mifugo yote ambayo iko kwenye ranch za taifa, achana na hawa wafugaji ambao wanafuga wao kama wao. Wewe umekodisha mtu anakwambia ana mifugo kwenye eneo lako; mifugo ni mingapi hatujui anamifugo mingapi. Kwa hiyo tunachoomba process ya kuweka heleni ianze na ng’ombe wote walioko kwenye Ranchi ya Taifa, tuwajue. Tukishaanza na ng’ombe walioko kwenye Ranchi ya Taifa hapa ndipo tutakapoujua ukweli kwa sababu kuna watu wameshikiria maeneo kwenye ranch na hawana ng’ombe pale wanatukodisha sisi; hilo ni la kwanza ambalo watakuwa wametusaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili kwa wafugaji wale ambao dawa ni yake, malisho ni yake kila kitu ni chake hamjawatengea chochote wanapouza ng’ombe si wanatozwa kwenye minada, hawa watu wananunua madawa tunapata, hebu tufumbeni macho basi wafugaji hao muwasaidie kwa kwenda kuvalisha heleni. First process mfanye nyie the second one itakapotokea itakuwa sasa kila ng’ombe anayezaliwa anazaliwa mfugaji anaruhusiwa kulipia heleni; hiyo itaweza kutusaidia. Lakini leo ukimwambia mtu mwenye ng’ombe 200, 300 hadi 400 akalipe hereni kwa mkupuo itawaumiza sana wafugaji. Kwa hiyo tuombe, walio kwenye ranch kwa sababu ni wakodishaji wenu cha kwanza mtakijua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili, Wizara walituahidi habari ya malisho. Kwamba kuna majani maalum wanataka kuja kuotesha nchi nzima na yale majani yatatusaidia hasa upande wa kiangazi kuzuia ng’ombe wasitoke sehemu moja kwenda sehemu nyingine…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ezra ahsante sana.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie muda wangu umeliwa sana dakika moja, nimalizie.

MWENYEKITI: Mheshimiwa sekundee moja.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, okay, sekunde haitatosha. Sasa Mheshimiwa Waziri tunakuomba fanya identification ya maeneo na hasa uanzie kwangu kwa sababu kuna mifugo mingi ili tutengewe maeneo na yale majani yaoteshwe, wananchi wa Biharamulo waweze kupata majani wakati wa kiangazi wasihangaike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na ninaunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi pia na mimi ya kuchangia, na nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri na wasaidizi wake kwa hotuba nzuri ambayo ameitoa. Lakini kwa kwenda haraka nipongeze pia juhudi kubwa ambazo zimekuwa zinafanyika hasa kwenye kukuza diplomasia ya uchumi kwa sababu kazi kubwa imefanyika, nyote ni mashahidi; Mheshimiwa Rais amezunguka huku na huku akijaribu kuvutia wawekezaji. Kwa hiyo pongezi kubwa ziende kwako Mheshimiwa Waziri kwa sababu iko chini ya wizara yako.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipindi unahitimisha nilitaka kujua pia, miongoni mwa vitu ambavyo nilitaka nijue nisije, nikakushikia shilingi shemeji yangu. Tumeona mkisafiri huku na huku tuna register wakandarasi zinafanyiwa memorandum nyingi sana. Tunataka kujua, katika zile memorandum of understanding ambazo zimesainiwa ni kampuni ngapi zimesharipoti hapa na zimeshaanza kufanya biashara au zimeajiri Watanzania; muweze kutusaidia ili zile fedha ambazo mnakuwa mnazitamka kule at least tuone kwamba zimeshaanza kuingia nchini na zinafanya kazi, hilo moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu ya pili sehemu yetu kubwa ambayo ni Wizara ya Madini halijaribiwi kuongelewa kwa kirefu kabisa ni issue ya Liganga na Mchuchuma. Hili jambo tumeliongea kwa muda mrefu sana kama Kamati. Lakini nichukue nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Waziri lakini pia Mheshimiwa Rais, kwa sababu kwa taarifa ambazo tunazo na hotuba ambayo imetolewa ulituahidi mwezi wa nne fedha itakuwa imetoka lakini huu ni mwezi wa tano; na kwenye hotuba yako uliyotoa ni kwamba tayari pesa ile bilioni 15.4 iko kwenye process nzuri, kwa hiyo wale wananchi wa Ludewa wanaenda kulipwa pesa yao na haitima ya matatizo haya ambayo yamekuwepo kwa muda mrefu tunahakika yatamalizika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini tunasema tunauhakika yatamalizika, Serikali haikuwa imefanya commitment yote ile pale ndiyo maana Kamati tulikuwa tunapiga kelele. Kwamba tunataka tuone mkono wa Serikali pia. Kwa sababu tunavyosema mkandarasi alikuja tukakubaliana hivi ilhali Serikali haijawekeza hata shilingi ilikuwa inakuwa ngumu kwetu. Ndiyo maana tukaomba kwamba basi hata fidia tulipe sisi kama Serikali, na baada ya hapo ndipo turudi nyuma tuanze kutafakari ni wapi tunaenda au ni nini tunafanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa baada ya kulipa fidia kwa sababu tuna uhakikia ni bilioni 15.9 za walipa kodi wa Tanzania zitakuwa zimewekwa pale sidhani kama kutakuwa na kurudi nyuma. Ni lazima tuone majibu na tuone mradi huu mkubwa wa liganga na mchuchuma ukinyanyuka na hatimaye uweze kutupa matokeo yale ambayo tunayahitaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeongea mara nyingi na nimekuwa najiuliza huyu bwana ambaye tulikuwa tumeingia naye mkataba nadhani niliwahi kutoa taarifa kwenye Kamati hawa watu kiongozi wao ambaye alikuwa ni mwenyekiti wa group yao alinyongwa tarehe 09 Februari kwenye nchi yao, kwa makosa ya rushwa na kujihusisha na vikosi vya mafia na vurugu nyingine ambazo zilikuwa zinaendelea huko. Since then, kumekuwa na hali ya sintofahamu. Kwa sabau kula wakati tukiuliza Mheshimiwa Waziri tunambana sana na kweli sometimes alikuwa anatoa majibu lakini unaona alikuwa anafikia hatua unaona anajibu lakini inafikia stage hawezi kuendelea tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu ambacho kipo ni kimoja; mimi niombe tena, hata kama tunarudi kwenye meza ya majadiliano, maana kunakuwa na tetesi kwamba huyo mtu kuna Serikali inataka imchukue halafu yenyewe irudi kwenye meza badala yake. Lakini ukijaribu kuangalia huyu mtu kwenye makubaliano yetu alikuwa anakuja na Dola za Kimarekani milioni 600 halafu tunaunda kampuni ya ubia. Tukiunda kampuni ya ubia huyu mtu anaenda kukopa bilioni 2.4 dola kwa kutumia mtaji wa eneo llile ambalo tumempa na hati zetu. Na huyu mtu amekwamisha mradi huu kwa muda mrefu kwa sababu anadai vivutio vya ziada.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa unajiuliza fedha yenyewe ni dola milioni 600 hujaja nayo, bado tunaunda kampuni ya ubia ya kukusaidia kukopa hutaki kwenda, pili unataka vivutio vya ziada ilhali hata shilingi hujaweka. Sasa mimi nimekuwa na wasiwasi sana; lakini Mheshimiwa Waziri nikawa najiuliza, maana kuna tetesi nyingine zipo, kwamba CEO wa hii kampuni ni mtanzania mwenzetu, hivyo ninaomba wakati una wind up utujibu. Huenda hii kampuni inasemekana ipo china kumbe ipo hapahapa, tunazungushana na wenzetu. Kwa hiyo nilikuwa naomba hili pia tupate majibu ili tuweze kuondoka hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo jingine ambalo limeongelewa na watu wengi sana hapa, na mimi sitaki kuwa mbali ya hili, ningependa niligusie pia. Issue ya utoaji wa Kampuni ya Tanga Cement ikichukuliwa na Twiga Cement. Mimi sina shida sana na issue ya take over lakini kwa sababu jambo hili limeleta taharuki, jambo hili limelalamikiwa na watu wengi sana; Mheshimiwa Waziri nikuombe, kwa busara. Jana Mheshimiwa Ulega hapa wakati anamaliza alisema jambo moja kwamba Mheshimiwa Rais asingependa aone manung’uniko na vurugu zile. Ndugu zangu wa Kigoma waliokuwa pale wakashangilia,
Mbunge mwenzangu wa Kigoma aliyekuwa hapa mbele yangu akaanza kupiga simu jimboni kwamba mambo yamemalizika nikasikia na wananchi wanashangilia kwenye TV. Maana yake ni kwamba jambo hili lilikuwa na shida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tusingependa twende na mambo ambayo yanatuletea shida. Mimi kwangu ukiniambia mtu anamiliki share hundred percent, kama antulipa kodi na ameajiri Watanzania its fine, acha amiliki. Kwa sababu at the end of the day hatutegemei kwamba kiwanda hiki cha Twiga kitashindwa ku-expand au Kiwanda cha Tanga kitashindwa ku-expand kwa sababu tu kina limit. Lakini tunachokisema, sheria yenu mliyojiwekea wenyewe ikoje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni Bunge hatuwezi kutunga sheria halafu tukakanyaga sheria sisi wenyewe, hapo ndipo utata unapokuja. Ndiyo maana tunaomba, kama kweli sheria ilitungwa na iko hivyo tuheshimu sheria tulizojitungia wenyewe, maana kama hatutazijali hizi sheria kesho zitatuletea shida hapa hilo ndilo tunaloliomba. Maana kweli FCC ipo chini ya Wizara, hii FCT ipo chini ya Wizara hii. Haiwezekani tukawa na taasisi mbili chini ya wizara moja zinasimamiwa na Waziri mmoja; huyu anasema hivi na huyu anasema hivi halafu sisi tukaamua ku-side na taasisi moja wapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima tukubali turudi nyuma kama kuna irregularities zilizofanyika wakati wa take over hii tuzifute tutangaze upya. Kukiwa open kila mmoja akaona tutaweza kwenda mbele. Maana ilisomwa habari hapa, kuna kampuni gani ambayo sijui imefutiwa usajiri, walisema ni Chalinze au whatever, nimesikia, kwamba ilifutiwa usajiri. Lakini kama ilikuwa na usajiri mpaka mwaka jana inafungua kesi mtawafikia BRELLA huko; lakini yenyewe bado ni sehemu ya ile kesi kwa sababu tayari walishakuwa na usajiri kipindi jambo linaanza na kama halipi, hakuna anaye mtetea asilipe. Na kama ana fedha huyu mtu mnasema kampuni ya mfukoni…

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: … na kama ni kampuni ya mfukoni tayari mnasema ana fedha, hii fedha anaitoa wapi na ni kampuni ya mfukoni? Kwa hiyo ningependa tusiende sana kujiuliza huko kutaja kampuni au kufanya nini; tunachotaka tuone procedure yetu iko sawa ili tuweze….

MWENYEKITI: Mheshimiwa Engineer Ezra naomba upokee taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Msukuma.

TAARIFA

MHE. JOSEPH K. MSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru napenda kumpa taarifa mzungumzaji. Nilivyochangia mchana nilisema kampuni hii ni kampuni ya briefcase ambayo haijukani inakotokea. Sikutaka kwenda mbali kwa sababu muda wangu wa kuchangia ulikuwa mchache; lakini tunao ushahidi na uthibitisho ambao unaonesha kuwa kampuni hii ni hewa haijulikani ilikotoka address fake, kiwanda kiko kwenye plot Kinondoni na wenye kiwanda ninazo picha zao hapa ukitaka tukabidhi tukabidhi. Tuachana na hizo biashara ya matapeli Bungeni.

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Ezra Chiwelesa unapokea taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Msukuma?

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napokea taarifa, maana kama kampuni ilisajiliwa na Serikali halafu tunaita ni kampuni fake, kwamba ni za kwenye briefcase means kampuni nyingi ziko hapa mnatuambia tuna makampuni yamesajiliwa kumbe hayapo basi Serikali irudi nyuma ikayaangalie kama yapo mengine yafutwe sawa na hiyo Kamapuni ya Chalinze ilivyofutwa. Napokea taarifa ya kaka yangu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa kumalizia, nime- experience kidogo na haya mambo, naomba ni share experience yangu. Nimefanya kazi Air Tanzania mwaka 2020, that time nilikuwa najihusisha kama cabbing crew. Kilichokuwa kinafanyika; hizi take over ni nzuri sometimes take over ni mbaya. Unakatiwa tiketi Air Tanzania ndani inasema Air Tanzania cover juu limeandikwa South African Airways. Kilichokuwa kinatokea ukishasoma kesho una haja ya kwenda Air Tanzania, si utakata moja kwa moja kwa msafirishaji mwenyewe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo sometimes take over ni nzuri lakini intention ya yule anaye-take over unaijua? Huyu bwana Tanga anazalisha clinker kwa sehemu kubwa, Twiga Cement akishakaa na Tanga Cement wakaanza kushirikiana na shareholder ni mmoja huyu anahitaji material kutoka kwa mwenzake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, achana na mambo ya sukari ile ni miwa, huwezi kutoa muwa Kagera ukaupeleka Bukoba kwenda kuzalisha ukaupeleka Morogoro kwenda kuzalisha, hautakulipa. Huyu bwana akichukua clinker Tanga kwa bei ambayo wanajuana wao akaongeza tu bei ya transport, kwamba transportation cost yangu mimi kutoka Tanga kwenda Dar es salaam ni kadhaa maana yake production cost yake itakuwa kubwa, twiga pale. Production cost ikiwa kubwa ata-declare low profit aki-declare low profit maana yake kodi tutapata ndogo.

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kodi tukipata ndogo huku Tanga akapunguza production ya clinker maana yake huyu anaweza akafanya biashara tukapata kiwanda kipya kinazalisha lakini hatupati faida na kodi kwa Serikali.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ezra…

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ungeacha nimalizie tu.

MWENYEKITI:…naomba upokee taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Mhagama.

TAARIFA

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimuongezee taarifa Mheshimiwa Engineer Ezra kwamba Teknolojia ya Twiga ni ya viwango vya juu sana ukilinganisha na teknolojia ya Tanga Cement maana yake nini? Maana yake uwezekano wa Tanga Cement na asset zilizopo pale Tanga Cement pamoja na resources zilizopo pale zikawa zinatumika kusafirishwa zaidi kwenda kuzalisha Dar es salaam kuliko kuendeleza kiwanda cha Tanga.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Chiwelesa unaipokea taarifa?

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipokea na unilindie muda kidogo kuna jambo nilikuwa namalizia. Kwa hiyo ninachosema ni kwamba, tunaweza tukaendelea na production ya cement Tanga, its fine, itaendelea kuwepo pale, lakini wakazalisha kwa kiwango kidogo halafu Dar es salaam wakaongeza huku waki-declare kwamba cost of production kwa Dar es salaam ni kubwa kwa sababu watakuwa wanaunua raw material pale. Kiwanda kile kitazalisha less tutakiua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi Wabunge wa Kanda ya Ziwa cement tunayotumia kwa sehemu kubwa ni cement ya Simba. Leo hata mkisema kwamba cement inazunguka nchi nzima leo tunaona mfuko 24,000, cement ukiitoa Mtwara ukaifikisha Biharamulo utauza mfuko kwa shilingi ngapi? Cost of production ni ileile transportation cost itakuwa kubwa; ndiyo maana kama hilio jambo tunalisema hapa Serikali itusikilize.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mambo hata ya Liganga na mambo mengine Waheshimiwa Wabunge walipata nafasi ya kusema, sasa msiposikiliza tuangalie mbele siyo leo take over ya leo ni nzuri kwa sababu amekaa na fulani ameongea lakini baada ya miaka mitano miaka kumi miaka 20 tunaoongea sisi hatutakuwepo, hata Wabunge tunaoongea humu ndani ya bunge labda watakuwa wamebaki asilimia 30 au 20, sasa where are we going baadaye? Turudi hapa tena kubadilisha sheria? Turudi hapa kulaumiana? Ni bora tunapowashauri leo msikilize kuliko kusubiri mambo yaharibike baada ya miaka 10 miaka 20 warudi hapa watu kuja kubadilisha sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yangu ni hayo nashukuru kwa nafasi na ninaunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi pia nichangie kwenye hotuba ya Wizara ya Nishati.

Kwanza kabisa nichukue nafasi hii kama watangulizi wangu waliopita Wabunge wengine waliochangia kumshukuru sana Mheshimiwa Rais, kwa kazi kubwa ambayo inafanyika katika Wizara hii ya Nishati, hususani kwa niaba ya watu wa Biharamulo uzinduzi wa substation ya Nyakanazi ambayo sasa inatuondoa katika shida ya umeme tuliyokuwa tumeipata ya ku - run katika low voltage, licha ya hiyo inaingiza Mkoa wa Kagera kwenye gridi bada ya kuunganisha na Rusumo nadhani hata ndugu zangu na majirani zangu wa Kigoma, wote ni mashahidi sasa hivi wananufaika kutokea Biharamulo, kwa hiyo nishukuru sana kwa ajili ya hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ninampongeza Mheshimiwa Waziri na Msaidizi wake na Watendaji wote katika Wizara hii, kwa kazi kubwa ambayo mnaifanya, ninazidi kuwashukuru tayari mgodi wetu wa Biharamulo STAMIGOLD tumepokea umeme. Hasara ile ya mafuta zaidi ya bilioni 1.2 yaliyokuwa yanatumika pale mgodini tuna umeme tayari, kwa hiyo ni hatua kubwa na mapinduzi katika Wilaya yetu ya Biharamulo, nina hakika mgodi ule kwa sababu ulikuwa unajiendesha kwa hasara sasa wataanza kufanya kazi kwa faida na hatimae hata CSR ambayo tumekuwa tunapambana nayo pale tunaweza kuipata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawashukuru pamoja na kubanana huko wamenisaidia juzi kwenye ujenzi wa shule ya sekondari ya Mavota, wamejenga vyumba viwili vya madarsa, ofisi, vyoo. Kwa hiyo, nina uhakika baada ya kuanza kupata umeme watafanya vingine vikubwa zaidi ili Biharamulo iweze kusonga mbele kwa kasi sawa na maeneo mengine yanayoendelea kukimbizwa chini ya utendaji wa Mheshimiwa wetu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wangu nilitaka kuongelea miradi ya REA kidogo, kabla ya kwenda kwenye mambo mengine ya Kitaifa. Ninayo ripoti hapa mimi kwangu nilikuwa na vijiji 25 so far ni vijiji Saba tu ambavyo vimeunganishwa na umeme. Sasa ukijaribu kuangalia kasi ya uunganishaji ni ndogo sana na sisi tunapokuwa tunazunguka kwenye ziara ukishawaambia wananchi Mkandarasi amepita hapa, wao hawajui kaunganisha kijiji gani? Kila mwananchi anataka apate umeme kwenye Kijiji chake, huwezi kwenda kwenye Kijiji ‘A’ ukamwambia Mkandarasi ameshaunganisha ‘B’ yeye akendelea kusubiria, kwa sababu umeme ni demand ya kila mwananchi hasa kwenye Jimbo langu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilikuwa nina ushauri kama inawezekana as long as Mheshimiwa Waziri amekiri mwenyewe kwamba wanatafuta mbinu mbadala ya kutafuta Wakandarasi wa REA, hebu liangalieni hili kumpa mkandarasi mmoja Mkoa mzima it was a very big mistake, ni mzigo mzito mno, ninapopiga mimi wa Biharamulo anaondoa timu anapeleka Ngara, akipiga wa Ngara anaondoa timu anapeleka Kyerwa ndivyo hivyo inavyofanyika, kwa hiyo tulikuwa tunaomba kama inawezekana tafuteni Mkandarasi kwa kila Wilaya, bora wakimaliza wataenda hivyo hivyo, hata kama wana miradi miwili, lakini wakimbize haraka hii kazi umalizike maana wananchi wamechoka kusubiri wanataka waone umeme sawa na kule walikowasha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kwenye miradi hii kumekuwa na maelekezo yale ya taasisi zipate umeme kwanza, sasa unakuta taasisi wanataka umeme na wananchi wanataka umeme. Sisi sote ni mashahidi, ujenzi wa Taasisi za Umma una vigezo vyake. Kigezo cha kwanza ni pamoja na taasisi kuwa na eneo kubwa ambalo wanaweza wakafanya miradi mingi, sasa unapoongelea ekari 20 za kujenga kituo cha afya, ukiongelea ekari 20 za kujenga shule automatically haziwezi kuwa kwenye center ya kile Kijiji. Kwa hiyo wengi wamejenga shule pembeni, kwa hiyo tunachoomba sasa, nilikuwa naomba nikuombe Mheshimiwa Waziri ulione hili pia andaa programu maalumu ya kupeleka umeme kwenye taasisi, achana na mambo yaani REA peleka umeme kwenye vijiji, lakini taasisi ambazo ziko pembeni pia utusaidie pia umeme ufike tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwangu nina shule ya sekondari kwa mfano shule ya sekondari Ruziba, shule ya sekondari Lusahunga, shule ya sekondari Nyakanazi ni shule kubwa lakini hazina umeme kabisa. Kwa hiyo, tulikuwa tunaomba siyo kwangu tu, huenda na maeneo mengine yapo vitu kama vituo vya afya, vitu kama shule ya sekondari, hebu iandalie package yake peke yake. Wapelekewe umeme wao separate tofauti na kwenye vijiji, maana ukienda kwenye ziara wanakijiji wanasema umeme hauko kwenye taasisi hawa wanasema umeme ubaki kijijini, kwa hiyo kidogo inaleta confusion hata kwa Mbunge uwaambie nini wale watu unaowawakilisha au wakutume nini? hilo nilikuwa naomba ulione ili uweze kutuisaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri nilikuwa napitia na andiko hapa pia. Mimi ni mdau wa mambo ya gesi kwa sababu kidogo ni idara ambazo tumezipitia pitia huko hata kwenye masomo yetu. Kwanza ni pongezi, nitakuwa mnafiki na nitakuwa mtu ambaye kweli sitawatendea haki kwa uamuzi huu mkubwa ambao mmeufanya wa kulitoa Taifa letu hapa na kulipeleka mbele. Niyaaseme haya, walio wengi tumekuwa tuna - deal na nchi kama China na vitu vingine kama hivyo, nchi kubwa China na India.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunaposimama hapa China kwa mara ya kwanza hata sisi tunaeza tukasema ndani ya Bunge hili tutaanza kum - supply gesi, kwa sababu China hana LNG anaagiza, India hawana LNG wanaangiza, yale mataifa makubwa ambayo yanatumia hii gesi kwa wingi lakini hawana wanachokifanya wanaagiza. Sehemu kama China leo wana nchi zaidi ya 20 ambazo wana - import ile gesi pale ya LNG. Zaidi ya hiyo hata bei China nilikuwa naangalia mwezi uliopita tani moja ya LNG inaenda dola 808, kwa hiyo unaweza ukaona soko kubwa tulilonalo kwenye hilo eneo, mimi siongelei uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwekezaji ni investment ambayo tunaenda kufanya pale ya zaidi ya trilioni 8.7 hiyo tuiache, lakini baada ya hapo Taifa linapata nini baada ya uwekezaji. Tuko na ajira za kutosha tuko na power yaku - supply kwenye viwanda, tuko na gesi ya ku - supply kwenye magari. Kwa sababu dunia inapoenda leo tunaenda kwenye clean energy. Unapoongelea clean energy, LNG hata kwenye EACOP nadhani kwenye mkutano, LNG leo wanavyochoma kwenye gari au ukachoma sehemu nyingine ina 40 percent gas ya carbon dioxide tofauti na diesel au tofauti na petroli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo unapoongelea hapo ina less than 35 percent ya Sulphur oxide, zile ni gesi mbaya na ni gesi ambazo zinaua, lakini leo tunapoingia kwenye project kubwa kama hii ya Kitaifa. Siyo tu kwamba tunaenda kujulikana duniani lakini tunaenda kutoa kitu cha maana, kitu ambacho kitaitangaza hii nchi kwa miaka na miaka nenda rudi. Nilikuwa naandika hapa na nilikuwa napitia, umeongelea gesi hii for more than 500 years wanansema stock tuliyonayo au reserve ya gesi tuliyonayo ni more than 500 years tunaweza kuitumia hiyo gesi at current rate. Kwa hiyo, unaona ni mradi mkubwa ambao unaenda kulipeleka hili Taifa miaka na miaka na miaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawapongeza zaidi uamuzi wenu wa kumfanya TPDC akawa mbia, maana tumekuwa tunafanya miradi hii unaweza ukaleta Mkandarasi lakini leo chochote kitakachotokea as long as mradi huu umeanza we are the owners, sisi ni wa wabia tutakaopata faida na zaidi ya kupata faida tutapata kodi kwenye hizi bidhaa. Kwa hiyo, kitu kikubwa ambacho mmekifanya leo kwa ajili ya kulinyanyua Taifa hili history ya nchi hii itawakumbuka lakini zaidi uwekezaji mkubwa ambao anaufanya Mheshimiwa Rais kuzunguka huku na huku na hatimae maongezi haya akawa ameyakamlisha ni lazima tumpe sifa na ni lazima tumpongeze kwa juhudi kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu kama hili jambo limeenda muda mrefu halikufanyika ni kwamba kuna imani ambayo watu wameijenga mpaka wakaamua kuja hapa. Unapoongelea kampuni kubwa kama Shell leo unaingia nao mkataba wa ku - run LNG project siyo kampuni ndogo. Ina visima 12 vya gesi duniani ambavyo inachimba leo, ina visima vingine vitatu ambavyo inajenga kwenye nchi mbalimbali, ina maana na Tanzania tunaingia kwenye ramani ya kufanya kazi na kampuni kubwa kama Shell. Kwa hiyo, kitendo cha kuingia kwenye ramani hii haitatutangaza tu kwenye upande wa gesi, inaenda kututangaza pia kwa investors wengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unapokuwa unatafuta watu wa kuwekeza lazima kuna watu wengine wataanza kujiuliza Tanzania kuna nini? Kwa hiyo, kama wanajiuliza Tanzania kuna nini maana yake miradi na uwekezaji mkubwa utakuja hapa. Kwa hiyo hilo jambo nilitaka niligusie. Niwapongeze sana kwa bidii kubwa naamini Mungu atatutangulia sawa na hiyo mikataba ambayo mmesema imeandaliwa ya Inter Governmental vilevile mkataba wa operation iende ikafanikiwe salama kwa maslahi ya Taifa hili, lakini kikubwa katika kupitia nimeona hata gawio kwamba tutakuwa tunagawana 50 per cent ya mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kweli leo mtu ana - invest katika kiwango kikubwa kama hicho, mnaenda kugawana faida kubwa kiasi hicho, jamani tunataka nini zaidi ya kumshukuru Mungu aliyetupa hili Taifa. Kwa sababu unavyoongelea gesi leo ya LNG, upande huu wa ukanda huu wetu wote huu, soko kubwa ni China, soko kubwa ni India. Maana yake meli zitakuwa zinakuja hapa zinabeba gesi zinapeleka kule. Hii siyo gesi ya mabomba labda tuelezee kwa sababu huenda mtu mwingine anaweza akaanza kuwaza kwamba utalaza pipe hapa mpaka India, hapana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, gesi hii inakuwa compressed. Ni gesi inachimbwa inakandamizwa kwa moja ya mia sita, yaani tumezoea moja ya mbili, moja ya tatu lakini unaongelea kwamba volume inayochimbwa inakandamizwa kwa moja ya mia sita ya original volume. Kwa hiyo, baadae ikitiwa kwenye meli zile zinazoondoka itaenda kuuzwa kule, kwa hiyo itauzwa sehemu yoyote ile duniani. Siyo gesi ya kutumia mabomba kwa sababu LPG ndiyo wanapampu kwenye bomba lakini hii itaenda direct kuuzwa kwenye maeneo hayo ya nchi hizo ambapo itauingizia faida lakini zaidi ya kutuingizia faida inatuletea pia kutangaza pia hili Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapomalizia nikiondokana na gesi. Tulihudhuria utiaji wa saini za mikataba ile ya kuimarisha gridi ya Taifa au gridi imara Ikulu pale. Ninakupongeza sana Mheshimiwa Waziri zaidi ninampongeza Mheshimiwa Rais, ambaye amekubali kuwekeza zaidi ya trilioni 4.42 kwa ajili ya kuimarisha gridi yetu ya Taifa. Kwa nini nasema hayo, Ndugu zangu umeme una-stage ya kuuzalisha, Wahandisi wanaelewa. Unakuwa na sehemu ya production lazima uanze kuzalisha umeme kabla ya kufanyia transmission, sasa wote ni mashahidi hata engine ya gari ukichukua gari lililotengenezwa mwaka 2023, ukachukua gari the same type na same engine iliyotengenezwa mwaka 2010 au labda 1995 ulaji wake wa mafuta unakuwa tofauti, efficiency inapungua kadri linavyoendelea kubaki. Kwa hiyo, investment mnayoifanya leo ukiunganisha na mradi wa Mwalimu Nyerere maana yake mnatuweka kwenye sehemu nzuri hata wawekezaji mnaowaleta hapa wataweza kuja na watakubali kuja kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ilikuwa ni aibu unaona mtu anataka aje awekeze kwa matrilioni ya shilingi, halafu mtu huyohuyo anatakiwa aje na pesa ya kununua generator megawatt moja, megawatt mbili, megawatt tatu, lakini yote haya tunavyofanya stabilization ya gridi ya Taifa maana yake hali ya kukatikakatika kwa umeme haitakuwepo. Kwa hiyo, investor anachokuja anakiwaza ni kuja kufanya biashara, kuzalisha na kupata faida na hatimae aweze kuajiri Watanzania walio wengi. Siyo aanze kuwaza ku-run generator kwa sababu, generator la megawatt moja unaweza ukajua linakula mafuta kiasi gani, kwa hiyo, walio wengi at the end of the day anakuwa amewekeza, lakini hawezi kuzalisha kwa sababu, aki-invest kwenye mafuta hataweza kuuza akashindana na watu wengine wanaozalisha kwenye soko katika umeme ule wa maji au umeme wa gesi ambao tunautumia leo kwa asilimia 60.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema hayo ninakushukuru kwa mara nyingine, lakini niwapongeze Mheshimiwa Byabato, Mheshimiwa Makamba, kwa kazi kubwa mnayoifanya. Mungu awatangulie, haya tunayoshauri Wabunge leo myachukue, hasa kwenye upande wa REA mkatusaidie wananchi wapate umeme, hapo ndiyo tutakapokuja hapa tukaanza kuimba wimbo mmoja na wimbo wa parapanda tutauimba kipindi tunaelekea huko mbele. Asanteni sana nawashukuru. (Makofi)
Azimio la Bunge Kuhusu Pendekezo la Kuridhiwa Mkataba Baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Dubai kwa Lengo la Kuanzisha Ushirikiano wa Kiuchumi na Kijamii katika Uendelezaji wa Maeneo ya Bandari Nchini
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, na mimi pia nichukue nafasi hii nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia maoni yangu kwenye Azimio hili la Bunge ambalo tunategemea kulipitisha muda mchache unaokuja.

Mheshimiwa Spika, labda mimi nianze pia kama wengine waliochnagia kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa anayoifanaya ya uwekezaji. Nakumbuka mwaka jana kwenye Dubai Expo ilisainiwa Memorandum of Understanding takribani 35 yenye thamani ya trilioni 17.5. Zimesaini Wizara nyingi tu, Wizara ya Nishati ilisaini na Wizara nyinyine. Sasa tunapoona mikataba hii inatekelezwa na ilisainiwa Watanzania tukajulishwa tukafurahi halafu wananyanyuka wengine wanaanza kusema imekosewa nadhani iko haja ya kuelimishana vizuri zaidi.

Mheshimiwa Spika, lakini pia nichukue nafasi hii kuomba sana Watanzania, hili Bunge ni Bunge lao, wametutuma humu kwa ajili ya kuwawakilisha, yapo mambo mengi sana yamesemwa huko nje tumeyasikia na wamesikilizwa kwenye mitandao na sehemu nyingine. Tuwasihi watupe nafasi na sisi pia, maana kama wametuamini kama wawakilishi wao kwenye kupitisha miradi ya maendeleo, kwenye kufanya uwakilishi ambao wamekuwa wanategemea tunaufanya vuizuri na kwenye hili pia watupe nafasi ya kutusikiliza na kutuamini. Siyo pale tunapochangia mitandao iko macho, Bunge la CCM, Bunge la hivi hapana, Bunge la CCM hili limejenga madarasa, limefanya shughuli nyingine zote ambazo zinaendelea watupe nafasi tutoe ushauri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya haya, mimi kwa upande wangu ni engineer kwa hiyo nitaenda zaidi kwenye vitu vyangu vya kihandisi ambavyo vinahusu bandari, mambo haya mengine ya mikataba wengi mmeongea sana kwa kiasi kikubwa mimi nataka nuiongelee stage hii ya engineering na hasa mambo haya ya uhandisi ambayo yanafanyika pale.

Mheshimiwa Spika, wengi kwanza wameuliza kile kiambatanisho au appendix number one. Naielezea appendix number one tu kwa haraka ya maeneo yale ya kimkakati ambayo uki–refer article namba tano right to develop, manage or operate. Kwa hiyo, kuna mojawapo kati ya hao yanaweza yakafanyika. Wameelezea appendix namba moja na specifically phase one. Kwa hiyo, ukiangalia scope ilitaja appendix yote, lakini development inataja phase one ya appendix ile. Kwa hiyo, phase two ukija kuisoma ni pale TPA atakapoamua ndio maana kule mwisho ukisoma phase two kwa mwisho, mambo ya maziwa mambo ya nini endapo TPA mwenyewe ataamua atawashirikisha. Kwa hiyo, siyo sehemu ya scope. Kwa hiyo, tukienda namba tano hii ndiyo inayoelezea maeneo ambayo tutashirikiana ambayo amepewa haki yeye ya kwamba amepewa ile exclusive kwa phase one for twelve months, sasa wengi walikuwa wanauliza hapa.

Mheshimiwa Spika, kwanza ukiongelea phase one ni sehemu ambayo nchi hii tumewekeza kwa kiasi kikubwa pale, lakini ukweli uliopo ni kwamba hatukuwa na vifaa kwenye bandari hii. Tumechimba kina cha bandari yetu imefika mita 15 leo kina kilipo unaweza ukashindana na Mombasa. Mombasa nao wana mita 15, tulikuwa na mita 11 sasa tumeenda mita 15. Gati Namba 8 mapaka 11bado lina mita 11. Mwekezaji huyu Gati Namba 8 mpaka 11 kuna vifaa vilivyokuwa na mwekezaji yule aliyepita, huwezi kumleta mtu ukamuweka kwenye sehemu ambayo tayari una vifaa, lakini kwa sababu sisi upande wa kwetu pamoja na kwamba tulikuwa na kina cha mita 11 tulikuwa tuna-miss vifaa vingi sana.

Mheshimiwa Spika, mimi nikiongea hapa sehemu hii tunahitaji tuwe na ship to shore gantry crane sita, lakini tulikuwepo nayo moja na gantry crane moja inauzwa shilingi bilioni 42 za Kitanzania. Tulitakiwa tuwe na rubber tag, gantry crane ziko 20 tulizotakiwa tuwe nazo, tunazo mbili tu. Vifaa vyote nilikuwa nimepiga hapa hesabu na moja inauzwa bilioni saba. Ukienda kwenye mobile harbor crane zinatakiwa ziwe 11 tulikuwa nazo sita, moja inauzwa shilingi bilioni 15 kwa haraka na hesabu za kawaida tu za haraka haraka tunahitahji uwekezaji wa vifaa vya shilingi bilioni 435 sehemu hii tu ambayo mmempa huyu mtu aje kuwekeza.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo sehemu hii ilikuwa muhimu mpe yeye aje na vifaa aje awekeze. Hatuwezi kwenda benki kuchukua shilingi bilioni 435 unaenda kuweka pale halafu unampa mtu aende kwenye kina kifupi. Kina hiki cha mita 15 leo tuko kwenye position ya kushindana na Bandari ya Mombasa. Meli kubwa zilizokuwa haziwezi kuja hapa zinashusha Mombasa zitaanza kuja hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo cha kwanza efficiency ya bandari yetu inakwenda kuongezeka kwa hili tu. Nadhani niliweke sawa hilo ndio maana nikasema ile exclusivity tunayosema kwanza ni ya twelve months ndugu zangu. Tangu kusainiwa mkataba huu, tuliposimama hapa exclusivity ya phase one kwao imebaki ikifika tarehe 28 Oktoba ule uhalali wa kwao wa kutoa phase one walioi-operate wao utakuwa umeisha endapo hatujakubaliana. Kwa hiyo itakuwa wazi kwa TPA kuweza kutafuta wawekezaji wengine au yeye mwenyewe aombe, lakini bila exclusivity, liko wazi hili.

Mheshimiwa Spika, sasa sielewe wanasheria wanakwama wapi wanatafsiri vitu vingine ambavyo havipo. Kwa hiyo mimi niombe Watanzania wanaotusikiliza huko nje muelewe Bunge hili lina wanasheria, Bunge hili lina wahandisi, Bunge hili lina madaktari, hatuwezi kwenda kupeleka nchi sehemu ambayo sisi wengine bado ni vijana wadogo tunataka tuone Taifa hili likisonga huku tuki-enjoy na watoto wetu na vizazi vyetu vikiwa vinaenda mbele. (Makofi)

Kwa hiyo tuombe hili tuwe na imani na Bunge hili tuwe na imani na Serikali yetu, kuna wengine wamenda mbali zaidi anasema mkataba huu huwezi kujitoa, lakini vifungu hivi viko wazi.

Mheshimiwa Spika, mkataba huu umeelezewa kabisa kwamba duration and determination iko hapa namba 23 imeeleza; subject to paragraph two ukienda namba two hii the expiration of all HGAs and all projects agreements subject to any additional or extension, ikisha-expire hii mikataba midogo tunayosaini huu mkataba mkubwa, hii agreement hii kubwa haina kazi tena it is obvious na iko hapa, sasa hatuelewi hawa watu haya mambo wanayatoa wapi na tumeenda mbali zaidi mtu anasema huu mkataba huwezi kujitoa mkataba mpaka umekupa room ya kufanya amendment article 22 kwamba kama kuna jambo hata leo kama limeshapita bado states wanaweza wakakaa wakafanya amendments ya baadhi ya mambo, ipo hapa.

Mheshimiwa Spika, tukienda article 23 namba nne ambayo imeongelewa sana na watu wengi, mimi siyo mwanasheria lakini usisome ukaishia hapa tu, kulikuwa na kipengele kimeendelea; notwithstanding the foregoing, any dispute between State Parties in respect of such circumstances shall be dealt with in accordance with the requirements of Article 20 of this Agreement. Unarudi nyuma article 20 inasemaje; kutakuwa na mazungumzo kati ya viongozi wetu endapo tutashindwana kwenye hiyo article 20 ndio twende kwenye arbitration. Sasa kwa nini mtu anasema mkataba huu ni kifungo hauwezi kutoka? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi tu sasa niongee with experience pia. Kwa nini tumeenda Dubai? Hilo ndiyo jambo la muhimu pia wananchi wajue why Dubai today?

Mheshimiwa Spika, wote mnajua mizigo inayokuja kwenye Bandari ya Dar es Salaam, wafanyabiashara wanajua, sehemu kubwa ya mizigo yetu unapoongelea kutoa kontena moja Shanghai, China kuja Dar es Salaam, 20 feet kontena inaenda dola 2,500 mpaka dola 2,800 na kontena la 40 feet mpaka inaenda dola 4,500. Unapoongelea kutoa mzigo ule ule kuja Mombasa 20 feet dola 1,200 wao kati ya 20 feet na 40 feet kontena, zinatofautiana kati ya dola 300 na dola 400; hawafikishi kontena hata la 40 feet kwa dola 2,000; utashindana vipi mtu anayepeleka mzigo Congo atakubali kuleta Dar es Salaam hapa?

Mheshimiwa Spika, ndugu zangu kama tunaipenda hii nchi tuache siasa, mimi siyo mwanasiasa, mimi ni mhandisi mambo yangu yamenyooka hivi. Mbili jumlisha mbili ni nne haibadiliki. Tukitaka kwenda mbele tuache siasa, tukileta siasa kwenye masuala makubwa kama ya Taifa hili, ndugu zangu Taifa hili tunaliangamiza, unapoenda mbele kwa nini mizigo yetu imekuwa inachelewa kwa sababu cha kwanza mfanyabiashara anachotaka other than saving cost anachotaka na mzigo aupate kwa uharaka zaidi. Wote ni mashahidi trans-shipment ya mizigo ya Tanznaia ni Jebel Ali Dubai. Mizigo mingi inayotoka Bara la Asia, inayotoka Ulaya mingi inapita Dubai Jebel Ali, ikishafika Jebel Ali ndio wanai–consolidate kutafuta meli ya kuileta huku kwetu. Mizigo imekuwa ikichelewa Jebel Ali not less than three to two weeks sometimes. Mfanyabiashara ambaye ameagiza mgigo mwenzake ameshapokea Kenya yeye yuko Congo anasubiira mzigo umekaa Dubai wiki mbili unauleta Dar es Salaam, utoke Dar es Salaam uje huku, nani atapitishia mizigo kwenye bandari hii?

Mheshimiwa Spika, no wonder ukisema wenzetu wale majirani zetu kwenye nchi wanazozihudumia mpaka wameweka kwamba na Tanzania wanaihudumia, sasa unaposoma profile ya mwenzetu mwenye bandari kama sisi, competitor wetu, anasema anatuhudumia na sisi kama Taifa na sisi ndiyo tuna bandari maana yake ni nini? Anatuondolea baishara, sometimes tusiingie kwneye mkumbo.

Mheshimiwa Spika, ameongea vizuri sana Mheshimiwa Jerry pale, sisi tunaowakilisha hii nchi kwenye Mabunge ya nje tunajua upinzani tulionao na wenzetu wa jirani. Ni lazima kama Taifa ifikie stage tusimame, hawezi kuja mtu anayeongea lafudhi ya nchi jirani, mnamuita mmbobezi na mtaalamu wa sheria, mlitaka Bunge tujadili kitu kabla ya kuja humu? Leo kimekuja, Serikali imesema, Wabunge tumeona kazi imeishia hapa leo, tusingeweza kwenda kwenye mitandao Wabunge na Serikali tukaanza kujibu kule. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa mimi kwa kuomba tunapoenda kumalizia hasa kwenye utekelezaji, nimefika katika bandari ya Suez nchini Misri mwaka 2019 pale kwenye Suez Special Economic Zone. Wale watu wamefanya uwekezaji mkubwa sana, pale kazi anayofanya anafanya APM, hii kazi anakuja kufanya DP World hapa Suez anafanya APM. APM ni kampuni ya Uholanzi kutoka Maersk Group, wao walichokifanya...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa Muda wa Mzungumzaji)

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, namalizia; wao wamekodisha miaka 45 kwenye upande ule wa makubaliano, sasa mimi nilikuwa nataka niweke maoni. Maoni yangu ni mawili; cha kwanza, kwenye contracts ambazo mnaenda kuingia kati ya TPA na DP World tunaomba tupate specific time, nilikuwa na suggest not more than 25 years kwa kuanzia na mikataba iwe revisited after every five years.

SPIKA: Mheshimiwa muda wako umeisha, ahsante sana.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kukushukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi niwe miongoni mwa wachangiaji katika hotuba hii ya bajeti Kuu ya Serikali. Kwanza kabisa nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa ambayo ameifaya, hasa tuki-refer ukurasa wa 29 wa Bajeti ya Serikali, tumeona kwamba wanafunzi wanaochaguliwa kujiunga na vyuo vya kati vya ufundi wakitokea Kidato cha Nne wameondolewa ada, chuo cha DIT, Chuo cha Arusha Tech na Mbeya Tech, kwa hiyo hii inatupatia ma-technician na watu wengine wakati wa kuweza kusaidia hasa miradi hii mikubwa inayoendelea katika nchi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuanzisha program maalum ya mikopo kwa wanafunzi waliochaguliwa kwenda kusomea Vyuo vya Afya na Sayansi, Ufundi na Ualimu. Ni maendeleo makubwa kwa sababu wote Waheshimiwa Wabunge mnaelewa hali ambayo wananchi wamekuwa wanaipitia, ulikuwa ni usumbufu mkubwa sana lakini hii itatusaidia kupiga hatua mbele ili kipindi tunapata wale wa kada ya juu na hata kada ya kati pia waweze kwenda na sisi tuweze kwenda pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema haya ninataka nichangie eneo moja, niki-refer ukurasa wa 80 wa hotuba ya Mheshimiwa Waziri, amesema kwamba acheni Watanzania walipwe pesa nyingi acheni Watanzania watajirike. Nataka nianze na statement hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati nzuri niko kwenye Kamati ya Viwanda Biashara, Kilimo na Mifugo na wewe ni Mwenyekiti wangu wa Kamati, tunapotaja biashara sehemu kubwa tumekuwa tuna-refer hasa biashara ambayo inafanywa na wazawa. Mimi leo nataka nisimame kwenye habari ya wakandarasi wanaofanya miradi ya ndani. Kwenye hotuba ya CAG 2021 nakumbuka kulikuwa na riba zilizolipwa takribani bilioni 68.7 na wakati nachangia nilisema riba nyingi zinazolipwa, zinalipwa kwa wakandarasi wa nje, kwa sababu wakandarasi wa ndani huwa hatutozi riba. The moment mkandarasi wa ndani ametaka kudai riba kinachofuata kesho yake anapoomba kazi hatapewa. Ni haki yake kudai, lakini wale wanaompa kazi wanaona kama anawasababishia hasara, ingawa yeye kwa upande wake anapata hasara kwa sababu mabenki yanamdai na malipo yanavyochelewa analipa interest kwenye mabenki lakini anapotaka kudai yeye inaonekana si haki yake. Lakini wanapodai watu wa nje tunahangaika kuwalipa zaidi kwa sababu wao hawahofii kwamba utawanyima kazi kwa sababu wana sehemu nyingine za kupata kazi ila Mtanzania hana sehemu nyingine ya kupata kazi ispokuwa humu humu ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nilikuwa naomba kipindi tunatangaza miradi mizuri hii ambayo inakuja na bajeti kubwa ya trilioni 44, bajeti ambayo ina miradi mingi sana ya maendeleo na tukitegemea kwamba Watanzania wanaenda kunufaika huko, na ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais pia alishasema wakandarasi wa ndani wawe considered kwenye kazi na kwenye malipo. Sasa tuombe Mheshimiwa Waziri wa Fedha wakumbuke vijana wenzako wa Kitanzania, watu wengi sana wamechukua mikopo kwenye mabenki, kwa riba za juu sana asilimia 20 mpaka 22, lakini malipo ya wakandarasi wengi hayajalipwa kwa muda mrefu sana. Sasa wakandarasi wengi wanalalamika, Wabunge wengine wako humu ni wakandarasi na tuko humu tunafanya kazi hizi hali kadhalika tuna madeni makubwa tunadai hatujalipwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunachoomba Mheshimiwa Waziri hili liangalie, kwa sababu kipindi hii miradi unaileta, wenzetu wanafilisika kwenye mabenki, hakuna benki inayouza nyumba unachofanya kila wakati unaomba extension ukimwambia hujalipwa na yeye anajua hujalipwa, yeye ana-extend lakini yeye anavyo-extend interest ya benki haisimami, utajiukuta mtu amefanya mradi wa bilioni moja bilioni mbili au bilioni tatu matokeo yake interest benki ameshalipa karibu milioni 500 hana faida tena. Kwa hiyo, tunaomba hili uliangalie ili uweze kuwasaidia wakandarasi wa ndani hatimaye waondokane na tatizo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kitu kingine ambacho Mheshimiwa Waziri nataka nishauri, kama inawezekana kuondoa adha hii inayofilisi wakandarasi wa ndani na pia kujikuta tunalipa pesa nyingi sana kwa wakandarasi wa nje kwenye issue ya riba. Kwa nini kusiwe na utaratibu maalum wa kuomba vibali kwako wewe kwenye Wizara ya Fedha? Mtu anapotaka kutangaza miradi mikubwa aombe kibali Wizara ya Fedha, mmhakikishie kwamba fedha ipo. Siyo Wizara inatangaza pesa halafu pesa ni mradi ambao unakuja kuomba pesa hazina, matokeo yake anapoomba pesa hazina unajikuta kwamba ile pesa kwako haipo au hujaikusanya, matokeo yake tunaanza kukulaumu wewe, kumbe na wewe hukuwa umetarifiwa wakati ile miradi inatangazwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tuombe kama inawezekana iwepo procedure maalum ya kukuomba wewe kibali, utakapo ruhusu Wizara au Taasisi kutangaza maana yake pesa una uhakika nayo ili tusitoze riba kwa wakandarasi wa nje wanaotutoza lakini hali kadhalika wakandarasi wa ndani wasiumie, hilo naomba nimalizie hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unakumbuka wiki mbili zilizopita Kamati yako ya Viwanda na Biashara na Kamati ya Bajeti tulikutana kwenye eneo la Wizara ya Kilimo pale, tukiwa na Waziri Bashe na hali kadhalika Waziri wa Viwanda. TBL walikuwa wametukaribisha pale wakiwa wanatangaza ufunguzi wa kiwanda chao kipya cha Kilimanjaro Breweries. Kiwanda ambacho wamehakikisha kwamba kitatumia shayiri ya ndani kwa asilimia mia kwa ajili ya kufanya uzalishaji wa bia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kushangaza mwaka 2021 hapa ndani ya Bunge lako, tulipitisha kushusha exercise duty kwa bia ambayo inazalishwa kwa kutumia shayiri ya ndani kwa asilimia 20 tukashusha kutoka 765 kwa lita ikaenda 620. TBL wakawa attracted kuwekeza kama siku ile ulivyosikia pale, hali kadhalika Waziri Bashe aka-attract watu kuwekeza kwenye ngano. Kwa hiyo, tulichokuwa tunategemea ni kwamba TBL wangesaidiwa ili ngano hii ambayo wamesema inakwenda kulimwa Makete, ngano inayoenda kulimwa Babati iweze kuwanufaisha Watanzania walio wengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matokeo yake tunachokiona hapa, ile shayiri ya ndani huyu mtu amemaliza kuwekeza hajaanza kuzalisha anaanza mwakani imeongezeka tena 20 percent na shayiri ya nje imeongezewa tena 20 percent, inazidi kupanda lakini kwenye kuingiza ngano kutoka nje tunaona ngano ya nje inashushwa by 35 percent ninaenda 25 percent, sasa maana yake ni nini? Huyu aliyekuwa anataka azalishe kwa ngano ya ndani umempandishia halafu anayetoa nje umemshushia, tunaenda kuua hata hawa wakulima ambao juzi tuliambiwa wananufaika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mimi naomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha hili jambo aliangalie. Unajua unapoongeza wigo hasa kwa watu wanaoweza kuzalishia kwa ndani; kinachotusaidia ni kwamba, tutengeneze ajira za Watanzania walio wengi. Sasa huyu mtu kawekeza, kamaliza hapa tena, kodi zinaongezeka, extra duty inaongezeka, halafu import duty kwenye ngano ya nje inapungua. Tutakuwa hatujengi, ila tunabomoa. Kwa hiyo, naomba hilo mweze kuliangalia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumalizia, Mheshimiwa Waziri siku nachangia Wizara yako ya Fedha niliongea habari ya ETS, mimi ni mwaka wa tatu sasa unaenda niko kwenye Kamati ya Viwanda na Biashara, Mwenyekiti wetu huyu hapa anaongoza kikao hiki, hakuna siku wafanyabiashara wamekuatana na sisi bila kuongelea habari ya ETS.

Mheshimiwa Mwenyekiti, narudia tena, naomba kwa mara nyingine, Mheshimiwa Waziri aangalie jinsi ya ku-rectify hili tatizo. Hatusemi yule aliyepo aondoke, kwa sababu tayari ameshawekeza muda mrefu, lakini kaa naye uone kama anaweza aka-adjust price. Kwa sababu leo ameenda kwenye sukari, ameenda kwenye cement. Ina maana tayari wigo wake wa kukuonesha kwamba mapato unayapata wapi, ni mkubwa. Angalia basi, wafanyabiashara wa ndani wasiendelee kulalamika kila wakati, inawaumiza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, it is very bad, wafanyabiashara wanapokuja wanategemea Bunge liwasaidie na Bunge ni la kwao, lakini wanaona Bunge haliwasaidii, wameenda kwenye Kamati ya Bajeti hawasaidiwi, wamekuja kwenye Kamati ya Viwanda na Biashara hawasaidiwi, basi tulilete kwa Mheshimiwa Waziri atafute jinsi ya kuwasaidia watu hawa ili tuwe na balanced state ambayo itaweza kusababisha wafanyabiashara wafanye vizuri na naye akusanye kodi yake vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua Mheshimiwa Waziri amekuwa muumini wa kusema kwamba unapokuwa na watu wachache uliowabana kwenye kodi haisadii zaidi ya kwamba wao wanaumia. Atengeneze wigo mpana. Wigo mpana ni pamoja na kuwa na hawa watu. Wasipolalamika, watawekeza zaidi, watapanua wigo wa kukusanya kodi, kuliko leo unapokuwa na walipakodi wachache huku ukiwakaba mashati mpaka damu ya mwisho wanaitoa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa muda na kwa nafasi hii, naunga mkono hoja. Nina uhakika kwamba Mheshimiwa Waziri kwa sababu ni msikivu, haya ameyasikia, atayafanyia kazi, hatimaye walipakodi katika mwaka wa 2023/2024 watalipa kodi huku wakiwa wanatabasamu, hatimaye tupate mapato haya ya kufanya miradi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, nashukuru. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii nami pia niweze kuchangia kwenye hotuba ya Wizara hii ya Maliasili na Utalii. Kwanza kabisa, nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kwa kazi kubwa na nzuri ambayo wanaifanya, hasa Mheshimiwa Naibu Waziri ulishanitembelea Biharamulo, nashukuru sana kwa sababu ulifanya ziara pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nampongeza Mtendaji Mkuu wa TANAPA ambaye pia ndio Katibu Mkuu wa Wizara hii kwa response kubwa ambayo amekuwa anaifanya pale ambapo nimekuwa nikijaribu kuwasiliana naye juu ya mambo ambayo yanaendelea kwetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa haraka kwa sababu ya muda pia; na kwa sababu ndiyo nachangia Wizara hii kwa mara ya kwanza tangu nimeingia humu kama Mbunge wa Biharamulo; na tukiwa na Hifadhi ya Burigi Chato; nachukua nafasi hii pia kutambua juhudi kubwa za Hayati Rais wa Tano, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ambaye alihakikisha anatutoa katika pori hili la Burigi, pori ambalo limetumika katika utekaji na kuwanyanyasa watu wa Biharamulo kwa muda mrefu sana na hatimaye leo ni sehemu tunayojivunia tuki-anticipate tunaanza kupokea wageni muda siyo mrefu, hasa baada ya haya ambayo tunayatarajia kwenye bajeti hii yatakapokuwa yamefanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninayo mambo kama matatu ya haraka haraka ya kwenda nayo kwa sababu ya muda. Jambo la kwanza, hifadhi hii imekuwa na kelele kidogo hasa kwa wakazi wa Biharamulo. Nadhani suala hili nimeshalifikisha kwa Waziri, lakini kikubwa ambacho kimekuwepo ni jina la hifadhi. Maana kwetu sisi wakati hii hifadhi inaundwa, imechukua sehemu ya Chato na sehemu ya Biharamulo ukiunganisha wilaya mbili kama hifadhi moja. Kwa upande wa Biharamulo kwa sababu pori lilikuwa linaitwa Burigi, wakazi wa Biharamulo walipoona sasa pori linaundwa hifadhi, linabaki jina Burigi na huku linabaki jina Chato, wakahisi kama vile sasa ni kwamba pori limesomeka chini ya Chato. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hali hii imeleta kelele na Mheshimiwa Waziri nilimwambia, wakati wa kampeni ilikuwa ni saga kubwa sana. Hata leo nilikuwa na kipindi Star TV asubuhi. Siongelei hili suala kabisa, ni suala lingine, lakini miongoni mwa mada zilizokuja ilikuwa ni mada ya jina.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba kwa sababu mbuga hii inaunganisha wilaya mbili; tuna Wilaya ya Biharamulo na Wilaya ya Chato, nilikuwa naomba pale penye neno “Burigi” mridhie kubadilisha neno “Burigi” likae jina “Biharamulo.” Mbuga isomeke “Biharamulo Chato National Park” ili wakazi wa Biharamulo ambao wanabeba sehemu kubwa ya hili pori waone kwamba juhudi kubwa ya kuwatoa katika mateso na unyang’anyi wa watekaji wale, inaleta faida kwao.

Mheshimiwa Naibu Spika, hilo nilikuwa naliomba Mheshimiwa Waziri alichukue kwa niaba ya wakazi wa Biharamulo, wakubali ku-amend jina, kwa sababu kinachoonekana Tourist Board wakati wanaanzisha hiki kitu ni kwamba hawakutoa elimu ya kutosha kwa ajili ya wakati wa Biharamulo. Nasema hawakutoa elimu kwa sababu hata geti tu la kuingilia mbugani, uwanja mkubwa ambao tuna- anticipate kuutumia utakuwa ni uwanja wa Chato; kutoka Chato mpaka Biharamulo kama watalii wametua pale ni takribani kilometa 50. Unapofika Biharamulo huingii mjini, kwa sababu Mji wa Biharamulo barabara kubwa inatoka inaeleke Nyakahura na hatimaye inaelekea Rwanda na Burundi. Sasa mjini hutaingia kama unakwenda mbugani kule; na geti linalofuata liko kilometa 82 kutoka Biharamulo Mjini upande wa Nyakahura kule karibu unaelekea Rwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa unafikiria, mgeni yupi ambaye utamtoa Chato Airport, kilometa 50 umtembeze, afike aone Mji wa Biharamulo kulia, unamkatisha mbuga kilometa 82 yule mgeni ndio anakwenda kuingia kwenye hifadhi kupitia Geti la Nyungwe, halafu tena aanze kutembea kurudi nyuma ya Biharamulo. Kwasababu Basically, hata Naibu Waziri alipokuja Biaharamulo tulimweleza, Central Burigi lilipo, lile Ziwa Burigi ambalo linaunganisha Karagwe na Mulega, lipo nyuma ya Biharamulo pale; ni takriban kilometa 10 tu, ukipitia kati ya Ruziba, Kijiji cha Kitochembogo na Kitongoji cha Muungano, unatokea kwenye hifadhi, katikati kabisa kwenye ziwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tulikuwa tunaomba, najua mtaongeza mageti, nilishaambiwa kuwa kuna haja ya kuongeza geti na niliomba geti liongezwe. Sasa ninachoomba, geti litakaloongezwa this time litokee pale pale Biharamulo ili wageni hawa sasa wasizunguke umbali mrefu. Maana mgeni anapokwenda sehemu anataka aone Wanyama. Sasa ukianza kumtembeza kule na bado miundombinu haipo, itakuwa haisaidii. Kwetu sisi kwa wakazi wa Biharamulo tunataka mbuga hii tuituimie kutangaza utalii na vile vile ku-brand wilaya yetu, maana imekuwa ni nyuma sana. Hii wilaya imekuwepo tangu mkoloni, lakini haijulikani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tulikuwa tunaomba fursa hii na geographical location ambayo Mwenyezi Mungu ametupatia pale iweze kutunufaisha. Mheshimiwa Waziri nikienda haraka haraka, nimeona hapa mnao mpango wa kujenga hoteli pia. Sasa nilikuwa naiomba Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii watusaidie kwenye plan ya kujenga hoteli hata sisi tupate angalau hoteli moja pale. Tukipata hoteli moja itatusaidia. Pia nimeona kwenye bajeti mna mpango wa kujenga barabara kilometa 2,256 pia sehemu ambayo mna madaraja takribani 18 na culvert 157.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nilikuwa naomba kwa sababu mbuga hii haina miundombinu kabisa kabisa. Tunaomba mtusaidie, wakazi wa Biharamulo watakapojua kwamba kilometa ngapi zimetengwa kwa ajili ya hii ya kwetu Burigi, Chato itatusaidia sasa hata sisi kujipanga ku-grab hizo opportunities. Maana najua kama ni ujenzi wa barabara hamtafanya nyie, nami nahitaji watu wangu kwa sababu mbuga ipo kwao, watumike na washiriki kwenye kujenga barabara na kuchukua opportunities za kufanya kazi hizo ili waweze kujinufaisha kimapato. Kwa sababu basically tunachokiangalia ni kwamba hii mbuga iwanufaishe wao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba haya yazingaiwe kwa haraka kwa sababu ya muda. Ili haya yote yaweze kufanyika, lipo jambo moja. Tumekuwa tunaona kwamba mapato yote yanayokusanywa na TANAPA siku hizi yanakwenda TRA. Sasa hawa watu mvua inaponyesha na kwenye hifadhi hizi, maana tunazo taarifa kwamba mbuga zetu za Tanzania barabara zimeharibika kweli kweli, hata huduma zipo chini sana. Kwa sababu wanapoomba fedha ya miradi ya maendeleo kutoka Hazina mpaka irudi inachukua muda mrefu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hizi mbuga basically lazima zijiendeshe kibiashara, kwa sababu zinajiendesha kibiashara na tuna-competition na jirani zetu wa Kenya au watu wengine wanaotuzunguka, tunaomba kosa moja la mtendaji mmoja au watendaji wawili la kuharibu au kutapanya zile fedha isiwe adhabu ya kuharibu biashara ya utalii. Tunaomba Serikali ifikirie ku-amend hii sheria, fedha irudi TANAPA, waikusanye, muweke usimamizi maalum, ili sasa watakapohitaji fedha ya kutengeneza barabara kule, tusianze wote kuomba kwenye kapu moja, kwa sababu hii ni sehemu ya biashara. Tunaporudi kuomba kwenye kapu moja, inakuja kutuchelewesha na inashindwa kufanya maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu ya muda, naomba kuunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru pia kwa kunipa nafasi ya kuchangia nadhani niende moja kwa moja kwenye hoja na hasa tunapojadili mapendekezo haya ya mpango. Kwa sababu kauli mbinu yetu ya miaka mitano hii ya Mpango wa Maendeleo tunasema kujenga uchumi shindani na viwanda kwa maendeleo ya watu. Nita-base kidogo kwenye viwanda zaidi sasa nimejaribu kupitia Mpango na Taarifa ya Kamati niwapongeze sana watu wa Kamati ya Bajeti kwa kazi kubwa na nzuri ambayo wameifanya ya kuishauri Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia kwa upande wangu nilikuwa nataka kujikita kwenye viwanda kama nilivyosema na hasa kwa kuangalia kwenye Ilani yetu ya chama tumesema kwamba tunataka kutengeneza ajira na ajira nyingi zaidi ziko vijijini na viwanda siku zote tumekuwa tunasema hapa kaulimbiu yetu ni kuhakikisha tunakuwa na viwanda vitakavyotumia mazao ya kilimo, mazao ya mifugo uvuvi kwenye madini na sehemu nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa sababu ya athari za UVIKO nimejaribu kuwa nafuatilia trend ya biashara inavyoenda kwenye dunia kwa sababu sisi tuko na wenzetu na tunafanya kazi na mataifa mengine duniani na hasa kwa sasa tunaona kwa sababu ya effect ya Amerika kujifungia na kufanya nini tumeona kwamba gharama kubwa za usafirishaji wa bidhaa nyingi duniani zimepanda kwa sababu demand and supply imekuwa kubwa sana hasa kwa USA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tukirejea hata kwa upande wetu bidhaa nyingi ambazo tunatoa nje. Kwa mfano kusafirisha Kontena moja ya bidhaa ya 20 ft kutoka China, ilikuwa ni dollar 2100, dollar 2000 mpaka dollar 1900 as we speak juzi nadhani Jumatatu nilikuwa najaribu kufuatilia baadhi ya sehemu sasa hivi kontena moja ya 20 ft imefika dollar 4900 kuitoa China kuileta hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda kwenye 40 ft inaenda dola 9800 mpaka dola 10000. Sasa zote hizi zina effect kwenye upande mmoja hasa kwenye upande wa biashara hasa viwanda wanapokuwa wanaagiza malighafi za kuleta hapa zinakuja kuleta shida sana kwa sababu cost of production itaongezeka kwa sababu ya ile transportation ambayo ipo hapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tukiangalia kwenye upande wa kilimo tumekuwa na kelele nyingi sana za mbolea hapa wote mnaelewa lakini mbolea haikupanda kwa sababu ya Tanzania imepanda kwa sababu ya hii hali ambayo inaendelea na hasa usafirishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nikawa nawaza kitu kimoja wakati tunaongelea ule mpango wa kutengeneza eneo huru la biashara la Afrika niliongelea kwamba wenzetu ambao tupo nao kwenye sehemu moja hii ya biashara wapo tayari kwenye GMO products. GMO products ambazo zinatumika kwenye viwanda na baadhi ya sehemu nyingi hasa mazao kama pamba na vitu vingine wenzetu wameshatoka kwenye teknolojia ya kawaida huko wapo kwenye teknolojia ya mbele zaidi. Kwa sababu wote tunajua advantage ya zile product, leo tunasema kwamba tunaingia kwenye ukame tuna- expect mvua zinaweza zikawa zimepungua, lakini unapokuwa kwenye upungufu wa mvua ukawa na products zile za GMO mbegu zile kinachosaidia ni nini, kwamba ile mbegu inaweza ikavumilia ukame, lakini mbegu ile haihitaji mbolea nyingi kama leo ambavyo tunahangaika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana nasema kwamba katika Mpango Serikali ijaribu kuangalia pia kwa sababu tunaongelea jambo la 2022 kwenda 2023 tuone hii hali ya sasa hivi kwenye bajeti ya sasa hivi tumeshaiacha, lakini tunapoenda mbele tujaribu kuona kama Serikali can we adopt this technology? Maana hii teknolojia itatusaidia kwanza kuwa competitive na pia kuweza kuhimili hali ya hewa kama hii ambayo inabadilika badilika kwa sababu hatujui baada ya hapa kitakachotokea nini. Kwa hiyo, niliomba hili jambo tuliangalie ili tusiathiri viwanda vyetu hivi ambavyo vina-deal na mazao ya kilimo na ambavyo vimeajiri watu wengi na watanzania wengi zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika Mpango kuna jambo moja nilikuwa naliangalia tumewekeza fedha nyingi sana kwenye miradi mingi ambayo inaendelea. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa pesa ambayo imepatikana kuna pesa nyingi zimeenda kwenye miradi ya maji na nyingine zinaendelea kutoka kwenye bajeti yetu, lakini nimekuwa najaribu kuangalia trend kila ukiangalia milioni 500, milioni 400, milioni 500, milioni 400 fedha ambazo zinapelekwa kwenye miradi ya maji, nikawa najiuliza katika best engineering practice hakuna kitu ambacho unakifanya bila kuwa na plan ya kuki- maintain baada ya pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana kwenye upande wa barabara tumekuwa tunatenga pesa kupitia road fund lami hizi hizi ambazo tumezijenga kwa hela nyingi bado ipo pesa ya kuendelea kuzi- maintain nikajiuliza what is the plan hasa kuhusu miradi ya maji mikubwa ambayo tumeifanya kwenye maeneo ya vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema haya kwa sababu unajenga kituo cha afya cha milioni 250 yupo Daktari pale na wapo watu wanaendelea kuki-maintain kile kituo. Ukijenga madarasa Walimu wapo pale wanaendelea kuya- maintain, lakini miradi ya maji ambayo inatumia pesa nyingi za Watanzania wote ni mashahidi hakuna watu ambao ni technical or qualified people ambao wana technical knowledge wanaosimamia ile miradi ya maji. Zaidi ya kuunda ma-group tunasema ma-group ya watumiaji wa maji, vyama vya watumiaji wa maji unakuta pale ni Mwenyekiti wa Kijiji na Mtendaji wa Kijiji ndiyo wanaosimamia, technically hawajui kile kitu, kinachokuja kujitokeza ni nini miradi hii itakuja kututoa jasho baada ya miaka mitano baada ya miaka sita miradi itakufa tutaanza kuwekeza pesa nyingine tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa sababu tumejenga vyuo vingi sana vya VETA kila anayesimama hapa anaomba chuo cha VETA kwenye Jimbo lake, kila anayesimama anaomba chuo cha VETA kwenye Jimbo lake tunao vijana wale, wale vijana gharama yao siyo kubwa, wanaweza wakafanya kazi katika mazingira yale ya chini kwa sababu ndiyo kada ya chini kabisa kwenye ufundi ambayo inaweza ikafanya zile kazi.

Sasa tuombe Serikali mjikite kwenye kufikiria ajira za vijana hawa ambao tunawatengeneza kupitia vyuo vyetu vya VETA tuwapeleke vijijini wakakae kule wao ndiyo wawe mafundi wa ngazi ya chini wa kusaidia miradi ile maji ambao tunaweka hela nyingi wailinde na waweze kui-maintain. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimezunguka kwenye Jimbo langu kuna baadhi ya sehemu vilichimbwa visima, pesa nyingi imetumika baada ya miaka mitatu kisima kimekauka. Lakini kama una mtu ambaye is a technical qualified person yule mtu ange-inspect kwamba hapa kuna shida akajaribu kujulisha hata kama maji yanapungua usiunguze hata ile pampu vile visima havifanyiwi service, pampu ile ukiichimbia kule chini mpaka siku ikiharibika ndiyo unakuja kuangalia baada ya muda inaharibika na ina-cost hela nyingi. Pampu ambayo inakuja ku-cost shilingi milioni mbili, milioni tatu, milioni nne, tungeweza kui-maintain kwa shilingi laki moja, laki mbili tukaitoa tukaipeleka sehemu tukasafisha tukairudisha. Lakini yote hiyo ni lazima kuwe na a best plan ya kuhakikisha vitu hivi tunavyovifanya pesa tunazowekeza ziwe na watu wa kuzifuatilia na kuzisimamia na by the way ni sehemu ya kutengeneza ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mimi yangu yalikuwa hayo nilitaka tuone mpango mzuri kwenye hasa upande wa maji wakusimamia hii miradi mizuri ambayo tunaifanya baadae miradi hii isije ikatutokea puani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema hayo naomba kuunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na mimi nichukue nafasi hii kukupongeza sawa na watangulizi waliopita kwa nafasi hii muhimu na nyeti katika Bunge letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa nijikite kwenye suala la Liganga na Mchuchuma maana ni jambo ambalo limekuwa kizunguzungu kwenye Kamati yetu, tunaona tangu tumeingia ni hadithi zimekuwa nyingi, sasa nikasema nijaribu kufanya utafiti wangu kidogo ili nijue ni nini kinakwamisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika miradi ya kimkakati ambayo imetajwa katika mpango wetu wa mwaka huu 2021/ 2022 ambao uliwasilishwa mwezi Machi, 2021 miongoni mwa miradi muhimu ambayo ilitajwa ilikuwa ni mradi wa Liganga na Mchuchuma, lakini mpaka leo ni miezi sita imepita, tunategemea kupokea mpango mwingine mwezi wa Machi mwaka huu lakini ninachosema ni kwamba hatuna kilichofanyika mpaka sasa, siyo pesa ni hadithi tu vitu vyote vimebaki kama vilivyokuwa vimewasilishwa pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima tujaribu kujikita kuona tatizo ni nini, maana huu mgodi umeongelewa kwa muda mrefu na ni mgodi wenye manufaa sana katika nchi hii lakini hakuna ambacho kinafanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuangalia hii kampuni ya Sichuan Hongda ambayo ndiyo mkandarasi, nimejaribu kufuatilia nikajua hawa watu wanachokwama ni nini. Katika ripoti ambayo tumepewa na NDC inaonekana hata teknolojia yenyewe ya kuchenjua madini haya kwa sababu madini ya chuma yapo na vanadium, yapo na titanium, teknolojia yenyewe kaja nayo huyu Mkandarasi ambaye tumepewa. Kwa hiyo kwa upande mkubwa hata Taifa hatukuwa tumejiandaa kwa sababu hatukujua hata uchenjuaji hata hiyo process itafanyika vipi.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuangalia zaidi, huyu Sichuan Hongda anachokifanya ana-deal na Zinc, Zinc Oxide products ana-deal na mbolea na vitu vingine, he has never done any product on ferrous metal kabisa! Anavyo- deal navyo ni non-ferrous metal, ambapo tutakuta titanium, tutakuta na vanadium lakini chuma ambayo ndiyo product hakuna profile inayoonesha kwamba huyu mtu amefanya. Sasa huenda anashindwa kuendelea na huu mradi kwa sababu uwezo hana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu ambao ninataka tuende nao, process hii as a chemistry process ambayo ni ya kawaida kabisa maana kuna study zimefanyika, wenzetu South Africa wanachimba chuma, Egypt wanachimba chuma, Libya wanachimba chuma, hizi ni nchi ambazo tumekuwa na ushirikiano nazo mkubwa, tungeweza hata kwenda kujifunza tukajua mtu huyu tunayemkabidhi mradi ana uwezo au hana uwezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukijaribu kuangalia, mradi wa bilioni tatu investment kwa mwaka mmoja tunategemea tupate bilioni 1.736; kwa hiyo mwaka wa pili ile investment yote ya bilioni 3 itakuwa imerudi kwa sababu tutakuwa na 3.4 bilion, lakini mradi huu umekwama. Ungekuwa ni mradi mtu anauweza huyu mtu angeshakuja kuufanya, jambo ambalo inabidi tujiulize ni nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, China ndiyo nchi inayoongoza kwa production ya steel hapa duniani, mtu huyu anatoka China, je, kama kuna ucheleweshaji kama sehemu ya hujuma ili huu mradi usiendelee wao waendelee kufanya biashara hii? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuishauri Serikali, kwanza kwa sababu ya muda inabidi niende haraka haraka, huu mradi contract yake kwanza iwe terminated, huyu mtu hawezi na ameshindwa kufanya hii, kwa sababu hata uwezo wa vitu anavyovifanya hauendani na chuma ambayo tumeitafuta wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine tumeona upande wa TPDC, tumeona na sehemu nyingine wanapeleka vijana wao kusoma, leo tuna watalaam wa gesi hapa, tuna watalaam wa petroli hapa, lakini tunapokuja kwenye chuma hata tukiwauliza watu ile content yenyewe ya hii chuma ya Liganga na Mchuchuma kuna nini? Chuma ni asilimia ngapi, hiki ni asilimia ngapi, mtachenjua vipi? Wanakuambia yule mwekezaji ndiye anayekuja kuangalia njia ya kuchenjua. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama inawezekana Serikali ijikite kuwezesha vijana wa Kitanzania sawa na tulivyowekeza kwenye petroli, sawa na tulivyowekeza kwenye gesi, tuwekeza kwa vijana wa Kitanzania wakasome material specifically kwa ajili ya material, wakirudi hapa watakuwa wanajua hata hizo process za uchenjuaji ni chemistry ya form two, lakini watu wetu hawajawezeshwa! Kama hawajawezeshwa huyu mtu anatupiga chenga kila siku, kwa hiyo kwa sababu ya muda ninapenda niishie hapo na ninaunga mkono hoja kwamba huyu mtu aondolewe tutafute mwekezaji mwingine ambaye atalisaidia Taifa. Ahsante sana. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nichukue nafasi hii kukushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niwe miongoni mwa wachangiaji katika taarifa zetu hizi mbili ambazo zimewasilishwa na Kamati. Kipekee niwapongeze sana Wenyeviti wetu wote wawili kwa uwasilishaji mzuri kwa niaba ya Kamati zao lakini pia nipongeze Mawaziri na Watendaji wote kwa kazi nzuri ambazo wanaendelea kuzifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipekee mimi nitajikita kwenye upande wa Wizara ya TAMISEMI na kwa sababu ya muda, nitaenda moja kwa moja kwenye sehemu ya TARURA. Tukiangalia ukurasa wa 37 wa taarifa ya Kamati, imejaribu kutupa kwa kina mchanganuo wa barabara ambazo zinahudumiwa katika nchi hii; barabara za lami, barabara za changarawe na barabara za udongo. Sasa tunaona asilimia zaidi ya 69 ya barabara katika nchi hii zinazohudumiwa na TARURA bado ni barabara za udongo, lami ni asilimia 2.23; na changarawe ni asilimia 28.46.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ukijaribu kuangalia hali zetu mnazijua, tunaposema udongo, udongo hata ukimwaga maji tu ya kawaida ule udongo unaondoka. Sasa unaweza uka-imagine hali ya mvua kama hii ambayo tumekuwepo nayo katika kipindi hiki na ni mateso kiasi gani wananchi wa nchi hii wanapata shida. Kama barabara za lami zinaharibika udongo ukoje? Kwa hiyo picha tunayoondoka nayo hapa, kwa sababu mvua inanyesha nchi nzima maana yake ni kwamba zaidi ya asilimia 70 ya miundombinu ya nchi hii ipo taabani na iko katika hali mbaya, kwa sababu taarifa yenyewe inasema zaidi ya asilimia 69 ni udongo. Maana yake maeneo yote yenye barabara za udongo leo hayaingiliki wala hayafikiki na nyote ni mashahidi tuko hapa wananchi wetu tunajua yanayoendelea majimboni huko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kidogo nilitaka tujikite hapa tujaribu kuchambua na kuona ni jinsi gani tunaweza tukawatoa wananchi hawa wa Tanzania katika lindi hili kubwa ambalo limewakwamisha na zaidi linawarudisha nyuma. Linawarudisha nyuma kwa sababu bila miundombinu mizuri no matter what you are doing, mimi kama siwezi kutoka nyumbani leo, umejenga kituo cha afya lakini mvua imenyesha hamna daraja, nafia ndani kwa sababu sintoweza kuvuka kwenda kwenye kituo cha afya. Umejenga shule watoto hawawezi kwenda shule kwa sababu ya miundombinu mibovu. Umejenga masoko na vitu vingine vyote vizuri watashindwa kusafirisha mazao toka mashambani wayafikishe kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo unapokuwa huna miundombinu maana yake unakwama completely na unabaki kule chini. Kwa hiyo cha kwanza focus yetu kubwa kupitia Wizara hii ya TAMISEMI ni lazima tuangalie jinsi tunaweza tukawasaidia TARURA wafanye kazi zao na kazi hazifanyiki bila pesa, maana kazi hizi za ujenzi ni pesa, mafuta yanahitajika kwenye mashine ni pesa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikiliza ripoti hapa tunasema wakandarasi wanasuasua wengine hawana mitambo, wengine hawana nini; akini nikwambie wakandarasi wa nchi hii ni wazalendo na Wabunge ingebidi tuwapigie makofi kuwapongeza. Kwa sababu wanafanya kazi kubwa na wanamadeni mengi sana ambayo hawajalipwa ni lazima tusema tu, tusipowasemea sisi nani atawasemea? Kwa sababu kama leo ndani ya Bunge ripoti inasema zaidi ya kazi ambazo zimefanyika ni zaidi ya bilioni 339 exchequer imekuja zaidi ya bilioni 339 lakini barabara tunachojua kwa TARURA walishatangaza mpaka asilimia 80 ya barabara zote walikuwa wametangaza ilibaki asilimia 20.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nina uhakika asilimia 80 ya zile barabara zilizotangazwa wakandarasi wako site na wanaendelea na kazi lakini kama watu wamefanya kazi kwa asilimia 80 au hawajafikisha bado wanaendelea, wewe pesa uliyoleta ikawafikia na asilimia 12, leo huyo mkandarasi huyo unamlaumu na nini? Wakandarasi wamekopa kwenye mabenki, ni benki gani itakupa pesa kama hurejeshi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, pamoja na mpango mzuri wa kuja na hiyo Samia Infrastructure Bond lakini kama hatutapanga mpango mzuri wa kuwalipa wakandarasi, mimi nakwambia ukweli watashika hizo barabara lakini barabara zitaishia njiani. Sasa tuombe, tuiombe Serikali hasa Wizara ya Fedha yaani leo unapofanya prioritization yako wewe ukifanya vipaumbele vyako wewe, huwezi kufanya vipaumbele ukasahau miundombinu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Wabunge tunaondoka hapa tunarudi majimboni, inabidi turudi tukafanye ziara tuwaambie wananchi ni vitu gani tunarudi navyo, tukakusanye mawazo yao kwa ajili ya Bunge la Bajeti. Unafikaje huko? Kila mwananchi anakwambia barabara haifikiki, ukirudi leo jimboni unaenda kuongea nini? Ukirudi jimboni unaitisha mkutano watu hawawezi kufika, madaraja hamna barabara zote zimeharibika unawaambia nini? Na ukifika hapo, wakandarasi tena wanaodai huwezi kuwaita kwa sababu wao bado wanakudai pesa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tulikuwa tunaomba Wizara ya Fedha, katika maazimio ambayo tunayo kabla ya Ijumaa tunapoondoka hapa, hili jambo siyo la kusubiria tuje tupewe taarifa mwakani, kwa sababu ni jambo la kibajeti, tulipitisha hapa tukaongezewa milioni 350. Tukaondoka tukaenda majimboni tukawaambia wananchi, Mheshimiwa Rais kaongeza pesa bilioni 350 kwa kila jimbo tulikuwa tunategemea tupate milioni mia tano, mia tano. Tukachagua na barabara za kwenda kujengwa tukasema kwenye mikutano tukimtaja Rais kwa maendeleo haya na pesa aliyoiongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo pesa hiyo bilioni 350 haijaja hata moja, Wabunge hatujaulizwa barabara, tumejaribu kukaa na mameneja wetu tukapanga zikija tutafanya hivi. Tumeenda tumefanya mikutano tukawaambia wananchi, tukachagua na barabara tulizotaka zikajengwe kwa hiyo milioni 500, unarudije leo ukiwa imebaki miezi minne kwa wananchi kuwaambia ile nilikuambia habari njema ya bilioni 350 haipo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachonganishwa na Mheshimiwa Rais anachonganishwa kama tunafanya hivi, if that money wasn’t there ingebidi watuambie haipo lakini hatuwezi kuondoka hapa katika Bunge, tumekaa hapa tumepitisha bajeti tunaenda tunawaambia wananchi kuna pesa imeongezeka yet mpaka leo hatuambiwi ni barabara gani zinajengwa, hatuambiwi pesa inakuja lini? This is not fair, siyo fair kwa Mheshimiwa Rais lakini si fair kwa wananchi ambao tunawawakilisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilikua naomba hili tulione…

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, katika maazimio ambayo tunataka tuondoke nayo…

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nina wazo, nina wazo la kusaidia TARURA. Ukijaribu kuangalia barabara nyingi za vijijini zinajengwa kwa upana.

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Engineer Ezra, kuna taarifa.

Waheshimiwa Wabunge niwakumbushe taarifa ni sehemu ya mchangiaji lakini pia inatolewa kwa idhini ya kiti, kwa hiyo Mheshimiwa Tarimba taarifa kuwa ufupi.

TAARIFA

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ufupi sana, nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa mchango wake mzuri sana. Nilitaka nimuongezee tu katika mchango wake kwamba kuomba barabara siyo hisani, barabara ina mkono wa moja kwa moja na uchumi wa Nchi hii. Siyo tu kwamba inakwenda kutusaidia sisi majimboni lakini inasaidia uchumi wa Tanzania ilivyo hivyo Serikali haina hiari kusema ipeleke fedha ama isipeleke mathalan Bunge hili lilitangaza na kutoa maamuzi kwamba fedha ziende basi Serikali ipeleke, ahsante sana. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa, taarifa ilitakiwa iwe fupi; Mheshimiwa Engineer Ezra taarifa unaipokea?

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeipokea hiyo ni nyama kabisa nyongeza nzuri nimeipokea. Sasa nataka nitoe ushauri wa kitaalamu. Barabara zote za nchi hii especially upande wa TARURA zinajengwa kwa upana wa mita 6.5 hadi mita saba lakini standard ya magari katika dunia na utengenezaji; gari dogo kabisa lina upana wa mita 1.8, zile gari kubwa semi zina 2.4 meters.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa unajiuliza huko kijijini unajenga barabara ya mita saba, barabara ya mita sita matokeo yake tairi zinakuwa zinapita tu pale katikati ya barabara huku pembeni majani yameota na huku pembeni majani yameota. Umejenga daraja la upana wa mita saba huko kijijini ni la nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka TARURA waende kwenye standard zinazoendana na mahitaji ya wananchi kule vijijini. Waweke upana wa barabara 4.5 meters au five meters na daraja likiwa vile tutajenga madaraja mengi na barabara zitakuwa ndefu zaidi. Ina maana hii plan ya kwenda kufika mbele zaidi itaweza kufikiwa kwa haraka zaidi, kuliko leo unajenga barabara pana baada ya muda majani yameota huku, yameota huku wakati eneo lote lile lililipiwa. Hiyo nayo bado ni hasara ambayo tunaipata. Kwa hiyo wa-review ili waweze kuona kwamba twende kwa barabara finyu lakini zinazoweza kwenda mbele zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimeomba kwenye hili. Tunachoomba wakati tunamalizia hapa Ijumaa kwenye maazimio ambayo Bunge linaleta hapa tupate majibu ya shilingi bilioni 350 za nyongeza na tupate majibu ya fedha yetu ya bajeti hii ambayo imeenda asilimia 12. Hizi fedha zinatolewa lini na hiyo iwe ndani ya maazimio ya Bunge Serikali itujibu hapa siku ya Ijumaa wakati Bunge linahitimishwa ili tunaporudi majimboni tukawaambie wananchi nini kinafanyika kwa habari ya barabara kabla ya mwezi wa saba.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru ahsante sana kwa nafasi na ninaunga mkono hoja. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa na Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha uliuoishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishi tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezajiwa wa Mitaji ya Umma kuhusu uwekezaji wa mitaji ya umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti na mimi nachukua nafasi hii kukushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika taarifa ya Kamati hizi tatu PAC, LAAC na PIC. Napenda pia niungane na Wabunge wenzangu kupongeza Kamati hizi tatu kwa taarifa nzuri ambazo wameziwasilisha. Summary nzuri hata kama una usingizi unasoma utaelewa. Kwa hiyo, nawapongeza sana Wanakamati kwa kazi hii kubwa mliyoifanya kwa niaba ya sisi Wabunge wenzenu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwenda haraka, mimi naomba tu kwanza nijaribu kuongea na Wabunge wenzetu ambao wameaminiwa wakaenda Serikali, maana nimeona jana hapa mtifuano ulikuwa mkubwa sana. Napenda tu niwaambie Waheshimiwa Mawaziri, sisi ni wenzenu. Kuna wengine walikuwa huku sasa hivi wamerudi tuko nao huku, labda wengine watatoka wataenda huko. Tunawapenda zaidi kuliko hao the so called wataalam wanaojaribu kuwaambia sometimes tunasema jambo hapa, unasema wataalam waliniambia hivi na sisi kabla ya kuja humu Bungeni tulikuwa wataalam. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo simaanishi kwamba tulivyoingia Bungeni humu akili zetu tulizokuwa nazo huko nje zimeisha, sasa hivi tumebaki dull kama hatujui chochote. Kuna Madaktari wengi sana humu, kuna Maprofesa wengi sana humu, kuna Mainjiania, kwa hiyo, tunaposhauri tunaomba mtupe nafasi ya kutusikiliza na ushauri wetu muupokee. Kwa sababu, ushauri huu ni wa kuisaida nchi. Tuko huko tunapambana na mambo haya yanapotokea, sisi ndiyo tunarudi Majimboni kwenda ku-defend Serikali yetu ya Chama Cha Mapinduzi, bila kujali yaliyofanyika huku, tunaenda kuwaambia wananchi nini kimefanyika. Ndiyo maana halisi ya taarifa hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa hii haiji kusifia. Ukiangalia ukurasa wa tatu wa taarifa hii inasema, “Kushughulikia maeneo yenye matumizi mabaya ya fedha.” Kwa hiyo, ndugu zetu tunayoyasema haya ni matumizi mabaya ya fedha, myasikie hata kama yanaumiza, ndiyo haya! Ndiyo kazi ya taarifa hii.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema haya mwaka jana wakati nachangia taarifa hii, TANROADS walikuwa wamesababisha hasara ya riba shilingi bilioni 68 na tukasema hapa. Mwaka huu shilingi bilioni 36, in two years shilingi bilioni 104. Zaidi ya bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara. Hizo ni riba tu zinaondoka. Hatuwezi kwenda namna hii! Ifikie hatua pale tunaposhauri msikie na mkafanyie kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wa bajeti nilishauri hapa mwaka huu, nikasema haiwezekani mtu anatangaza bajeti na tender anaanza kutangaza, Wizara ya Fedha haijatoa kibali. Maana wewe unamaliza kitangaza kwenye Wizara ya Kisekta, umeshatangaza watu wamefanya kazi unanyanyuka na certificate kwa Mheshimiwa Mwigulu, Mheshimiwa Mwigulu unafika pale anakwambia, nimelipia SGR sina hela, zinaanza ku-count huku! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunayoona ni upande wa TANROADS tu, wapo watu wanafanya miradi ya maji hapa hawajalipwa zaidi ya miezi 12. Jana Waziri wa Ujenzi ameongelea Wakandarasi kulipwa kulipwa hiyo shilingi bilioni sabini, sabini, anaongea wanaofanya kazi TANROADS na Wakandarasi wengi wa Kitanzania maskini hawa, wako kwenye miradi ya maji na huko kwenye miradi mingine. Kwa hiyo, pesa wanazodai ni nyingi sana. Tujaribu kusaidia Watanzania hali kadhalika tuokoe hizi pesa. Kwa sababu, uhakika nilionao, kwenye hizi shilingi bilioni 68 na shilingi bilioni 38, hakuna mkandarasi wa Kitanzania hata mmoja anayelipwa riba! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata mimi ni Mkandarasi, sijawahi kulipwa riba, nadai hela zangu huko. Hizi pesa zinaenda kwa Wakandarasi wa kigeni! Sasa, Watanzania ambao mnaona ni wengi wanafanya kazi hizi, wako wanaumizwa lakini wageni tena wakija wanachukua hizi pesa wanaondoka nazo. Kwa hiyo, naomba hili tuliangalie sana tuweze kuwasaidia hawa watu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo nataka kuongelea, nilikuwa napitia hii ripoti kidogo ukurasa wa 21. Kuna hawa watu wanaitwa TANOIL, yaani mtu anaamua tu kutoa discount, anaamua kuweka bei tofauti na EWURA, hawana uchungu na hivi vitu! Anajua hata tukipiga kelele humu na sasa hivi wanatuangalia, hii si ya mwaka 2021/2022? Bajeti tuliyopitisha mwezi wa sita, leo si ni mwezi wa 11 huu? Miezi minne imeshapita, hawa jamaa wanatuangalia tu hata huko nje. Wanajua watapiga kelele baada ya hapa ngoma imefungwa inaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, CAG akija kukagua, miaka mitatu minne ndiyo tunaelekea kwenye uchaguzi, wanatuangalia tu. Sasa, mimi naomba Bunge hili tutoke na maazimio yenye maana zaidi. Maazimio ya kusaidia nchi hii. Kazi ya CAG ni kudhibiti na kukagua lakini nafasi ya udhibiti anakuwa nayo? Kama huwezi kufanya real time auditing, leo tunajadili kitu kilichotokea mwaka 2021/2022 hawa watu walishajenga majumba, walishahamisha hizi hela ziko huko nje, wengine walishaondoka, unawatoa wapi? Mwingine kahamishwa Wizara kaenda huko, unawatoa wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba, kwa sababu ripoti hii kwa sehemu kubwa inachokisema ni kwenye Mashirika ya Umma, mimi nitakuja na proposal hapa kama utaipokea. Kwa sababu, nimeona hata huyu wa TANOIL alikuwa anakiri kabisa. Ni kweli EWURA hawakuturuhusu, ni kweli hatukufanya hivi. Kwa hiyo, unaona ni mtu yuko comfortable, yaani anafanya anavyotaka kama vile hili ni shirika lake nyumbani, hata nyumbani huko saa nyingine unakuwa na bodi kama una shirika lako, iweze kukusaidia kuendesha, lakini hapa hamna kinachofanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pendekezo jingine, nimepitia ripoti ya SGR ukurasa wa 46. Mwaka jana wakati wa bajeti nilionya hapa, maana Waziri wa Fedha alitamka kiasi ambacho kinaenda kutumika kwenye lot six, kutokea Tabora kwenda Kigoma. Waziri wa Fedha akatamka 2.1 billion dollar. Nikasema 2.1 billion-dollar ukii-convert kwenye rate ya wakati ule, ilikuwa inakua kama 4.8 trillion shillings. Nikamwambia lakini ukiingia kwenye TANePS, huyu mtu ambae anapewa kwa single source alikuwa amewasilisha pendekezo la 6.6 trillion shillings. Nikasema, ni zaidi ya shilingi trilioni 1.84, ongezeko linaloongezeka kutoka kwenye kile alichokisema Waziri na kile ambacho kinafanyika kwenye TANePS.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilijibiwa hapa kwamba, watakaa naye yule mtu apunguze zaidi ya asilimia 38 na bado abaki na faida. Mkataba ulisainiwa kwa ile ile 6.6 trillion shillings. Sasa, tunapokuwa tunashauri tusikilizwe. Tunapata muda wa kusoma na sisi tunauelewa. Hilo ndilo tunaloliomba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona hapa mabadiliko, mtu anakwambia ana justification ya kwamba ile 1.3 million dollar inayoongezeka kwa kila kilometa, ni kwa sababu kumekuwa na fluctuation ya bei na vitu vingine na miaka imeongezeka. Ndugu zangu tuko hapa, TANROADS wako hapa na Waziri wa Ujenzi yuko hapa, mimi ni Engineer naelewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara kilometa moja ya double surface inajengwa kati ya shilingi bilioni 1.5 mpaka shilingi bilioni 1.8. Mbona hizo kwenye barabara haziongezeki ikawa shilingi bilioni 3? Huku kwenye reli peke yake ndiyo zinaongezeka? Kwani reli hazijengwi na madaraja? Lami haibadiliki bei? Sasa, vitu hivi mkija kufanya hapa muelewe na sisi wengine tuna akili tunasoma, msitufanye hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ambacho ninacho, mimi naomba nitoe ushauri sasa kwa kumalizia ili muda usiishe. Tangu mimi niko huko nje, kila ripoti ya CAG inaposomwa hapa, wizi, wizi, Mawaziri hawa watafukuzwa mpaka lini? Kuna Mawaziri wengine hata hawakuwepo wakati ule, walikuwa huku nyuma, wameshaenda huko mbele mambo haya yanaendelea. Hawa Watumishi wa Umma wamekuwa na comfort zone ambayo wanahangaika nayo, hamtakuja mkae muwaguse hata siku moja. Kwa sababu yeye ana uhakika Waziri ataondoka yeye atakuwepo pale! Kama Katibu Mkuu atahamishwa, yeye atakuwepo pale! Sisi tunakuja kwa kuchaguliwa. Ni kwa nini Wabunge mnakuwa committed kufanya kazi zenu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo wananchi wanatu-monitor huko nyuma. Ni kwa sababu tuna timeframe ya five years. In five years umechemsha wananchi wanakusubiri huko nje wakakupe adhabu yako. Ni kwa nini Watumishi wa Umma nchi hii tumewaacha waka-relax kiasi kwamba wao ndiyo wamiliki wa hii nchi? Tunaenda kuomba kura kwa wananchi tunawaahidi kufanya. Tunakuja hapa watumishi wanatuangusha. Ni kwa nini iwe hivyo? Chama cha Mapinduzi kinasemwa, viongozi wanasemwa, tutarudi huko nje tukahukumiwe lakini kuna watu wamekaa maofisini. Wako nyuma hawajawahi kuonekana. Wao ndiyo wanaotufanya tukaenda vibaya kwenye hii nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima ifikie hatua Watumishi wote wa Umma kuanzia ngazi ya Wakurugenzi, wapewe mikataba ya miaka mitano mitano, isizidi hapo. Kazi zitangazwe watu waombe. Sijawahi kusikia kampuni ya mtu binafsi hata siku moja kila siku inapata hasara, akawacha watu waendelee kuwepo. Wakina Bakhressa wanakua leo, kwa nini wanakua? Umepewa job descriptions, umepewa mkataba, umefeli wanakuondoa wanaleta mtu mwingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaona leo akina Rostam wanakua mpaka wanafungua viwanda huko nje, hawajakua kwa sababu waliwabeba watu, There is no permanent employment ukatengeneza faida, kuwe na proper job descriptions, kazi zile zionekane, waambiwe kabisa ukikosea hapa miaka mitano unaondoka. (Makofi)

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ezra, kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Nusrat Hanje.

TAARIFA

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimpe taarifa mzungumzaji, anachokizungumza nakubaliana naye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi mwizi ni mwizi tu, ameiba na suti, ameiba na system, ameiba na begi, kaiba na jeans, mwizi ni mwizi. Tunajua ya kwamba mwizi anatakiwa afanyiwe nini. Mimi nafikiri tuwe realistic kidogo. Tumekuwa tunazungumza sana kuhusu ripoti za CAG na anachokizungumza pia ni ushauri mzuri, lakini kwenda kusema tunyongwe na vitu vingine, nafikiri tuwe realistic. Kwanza, hawa ambao wanatajwa wametajwa wanajulikana, ripoti zimeandikwa, tuwaone angalau kuna kesi zinaendelea Mahakamani, mchakato unaendelea Mahakamani ili wengine wawe wamefungwa, tuache kwenda mbali sana, tuangalie hawa, kwa sababu tunawaweza na kweli inaumiza sana. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ezra muda wako ulikuwa umeisha, basi malizia tu, muda wako umeisha. Taarifa hiyo unaipokea?

MHE. ENG. EZRA J. CHILEWESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napokea taarifa. Kwa kumalizia naomba kitu kimoja ambacho nataka nishauri tufanye kama Bunge na tutoke na maazimio.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ezra kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais.

TAARIFA

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisimama tu niliona alignment ya anachokisema Mheshimiwa Chiwelesa na walichokisema Wabunge wengine juu ya hatua zinazochukuliwa au zinazopaswa kuchukuliwa, pia, ameongea Mheshimiwa hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa vile hatupendi kuingilia michango ya Waheshimiwa Wabunge, ninataka niwahakikishie kwamba tunavyo vyombo very competent katika nchi, vinachukua hatua na sisi sote tunaona taarifa na ripoti za vyombo hivi huwa zinaletwa humu Bungeni. Waheshimiwa Wabunge zile ripoti za vyombo vinavyofanya kazi zake hasa kwa mfano TAKUKURU, tuwe tunazisoma, tuwe tunazipitia. Tungeweza kujua hata angalau kwa hatu gani tumepiga hatua katika kushughulikia changamoto mbalimbali za uadilifu lakini za uaminifu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, itafika wakati wa sisi Mawaziri tuta-respond. Tunaogopa sana kuwaingilia Waheshimiwa Wabunge, kwa hiyo, tunapoongea, ongeeni kwa kiasi kwa sababu, tusiboboe sana, siyo kwamba hatuna nchi, siyo kwamba hatuna system. Kazi zinafanyika na tutatoa ripoti hapa kesho kama zamu yetu itafika, Mawaziri tutasema kazi gani zimefanyika.

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Mwenyekiti taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mulugo, hakuna taarifa juu ya taarifa. Mheshimiwa Chiwelesa malizia mchango wako. (Kicheko)

MHE. ENG. EZRA J. CHILEWESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa naipokea. Kwanza labda nimwambie tu Mheshimiwa Waziri nina 10 minutes tu ya kuongea hapa. Nikianza kuchambua tu huku ninao uwezo wa kuongea dakika ngapi na nikatoa maelezo yangu ambayo naona ni mawazo yangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, Bunge linapomaliza hapa likaielekeza Serikali, Seriakali siyo kusema haichukui hatua, mkishachukua hatua TAKUKURU mmempeleka mtu Mahakamani, maana yake Bunge na Serikali mnakaa pembeni, yule mtu kapelekwa Mahakamani ni Muhimili mwingine hamtaingilia kule. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wale watu ndiyo maana tukishawatoa hapa hatuwagusi kule, wanaenda kwenye haki wanapambana na wanasheria, wakishinda keshi wanakuwa huru. Ndiyo maana nasema, we have to give them three years contract, five years contract, akichemka terms zake ziko pale mnapambana naye huko, ameshatoka kwenye mfumo wa ajira ili Watanzania wengine waliosubiria huko nje wasio na kazi waje hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu wana uwezo, wako huko nje, mtu anashikilia nafasi mpaka anastaafu miaka 60! Wewe leo unateua Bodi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA Mheshimiwa Mwenyekiti namalizia. Unataka tufanye biashara sawa, unateua Bodi mtu kastaafu, unaenda unamwambia aongoze Bodi, Katibu wa Bodi ndiyo Mkurugenzi pale, kuna nini hapo? (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ezra, ahsante.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na naunga mkono hoja.
Hoja ya Dharura kuhusu Mikopo ya Elimu ya Juu Nchini
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, nashukuru, kwanza nichukue nafasi hii kukupongeza kwa kukubali jambo hili na kunipa nafasi ya kuwasilisha hoja yangu hii ya Bodi ya Mikopo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni juzi tu tulimwona Waziri wa Elimu katika vyombo vya habari akisema kwamba aliunda tume maalum ya kuchunguza Bodi ya Mikopo, lakini Waziri akawa analalamika kwamba ile tume aliyoiunda imeshindwa kupata ushirikiano. Kwa hiyo, maana yake Bodi na Serikali haviko pamoja ndiyo maana Waziri ameunda tume na tume haijaweza kutoa ushirikiano kwa Serikali. Kwa hiyo jambo lile likanishtua kidogo.

Mheshimiwa Spika, lakini weekend yote hii baada ya majina kutoka na wanafunzi kuanza kudahiliwa na wengine kuripoti mimi nimepokea simu nyingi sana kutoka jimboni kwangu, wazazi wengi wanafunzi wao wamekosa mikopo, wote wanakimbilia kwa Mbunge. Sasa solution hata mimi nikawa naona nikirudi kwa Waziri yule ambaye nilimwona kwenye vyombo vya habari analalamikia tume, sidhani kama ningeweza kupata jibu la haraka, ndiyo maana nikasema Bunge ndicho chombo cha wananchi hivyo nilete hoja katika Bunge ili Bunge liweze kujadili hatimaye tupate majibu na tutoke na maazimio ya Bunge ili tuweze kuielekeza Serikali nini ifanye kuweza kuwakwamua watoto hawa ambao wamekwama katika maeneo haya. (Makofi!)

Mheshimiwa Spika, niki-refer ukurasa wa 49 wa hotuba ya Waziri wa Elimu aliyoitoa humu Bungeni, tumeona alikuwa anasema kwamba katika mwaka huu uliopita wa fedha, tumetoa mikopo ya takribani Shilingi bilioni 569. Tukaona ni jambo zuri, na katika mwaka huu wa fedha ambao tunaendelea nao wa 2022/2023 tulikuwa tunategemea kwamba fedha ilikuwa inaongezeka. Alikuja pia na shilingi bilioni 200 kutoka NMB ambazo zingeenda kukopesha wafanyakazi na watu wengine ambao wanao uwezo wa kukopesheka kutokea huko, mpaka na watu wa diploma waweze kupata huo mkopo.

Mheshimiwa Spika, jambo la kushangaza, niko na fomu hapa ya mtoto wa mkulima ambaye ameandika, mama ni farmer na baba ni farmer. Mtoto huyu ni miongoni mwa watoto reference katika Taifa hili ambaye amepata division 1.7 O’level, Msalato Sekondari (shule ya Serikali). Akiwa na “A” saba mtoto wa kike, form five na form six akabaki Msalato palepale. Mtoto huyu wa kike akapata division 1.7 tena. Mtoto huyu amechaguliwa kwenda kusomea udaktari Chuo cha KCMC. Ajabu ni kwamba alichokipata, anapewa ile fedha ya kujikimu lakini hajapewa ada.

Mheshimiwa Spika, ada ni shilingi 5,600,000. Mtoto wa mkulima ambae amesoma Msalato miaka yote sita, anapata wapi ada hii ya kuweza kusomea udaktari? Maana yake tunachokiona ni nini? Hata watoto wadogo walioko pale waliomwona kama role model wao aliyepata division one ya pointi saba watakata tamaa ya kusoma maana ndoto zao zinakatizwa kwa sababu hawana uwezo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kigezo ambacho nashindwa kukielewa kipindi wanachambua. Katika masharti yaliyowekwa humu kwenye Loan Board hapa, kipo kigezo ambacho, baada ya viongozi wa Serikali ya kijiji kusaini fomu ya mtu huyu, tumeambiwa kwamba endapo itakuwa wametaja taarifa za uongo, watatozwa faini ya shilingi milioni moja na nusu au kifungo cha miezi sita jela au vyote kwa pamoja. Sasa tunajiuliza, kama watu wanasaini fomu na zinapita kwa viongozi na sheria mmeweka, sijasikia kama kuna kiongozi wa kijiji hata mmoja ambaye amepelekwa mahakamani kwamba alijaza fomu za uongo na akashtakiwa, that means taarifa za watoto hawa ni sahihi lakini watoto hawa wananyimwa mikopo.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba kutoa hoja sasa kwamba Bunge lako lipokee hoja yangu na lijadili hili jambo ili tuone jinsi ya kuwakwamua hawa watoto ambao wamekwama na wengine bado wako majumbani na hata walioripoti vyuoni bado hawajapewa fedha hiyo pia bado wanahangaika mtaani.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja. (Makofi)

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika naafiki.
Hoja ya Dharura kuhusu Mikopo ya Elimu ya Juu Nchini
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kukushukuru sana kwa kukubali hoja hii iwasilishwe hapa.

Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kuwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge. Wamechangia jumla ya wachangiaji 16, nadhani sitaweza kuwataja kwa majina kwa sababu ya muda, lakini niwashukuru sana kwa sababu mmeeleza kwa kina, Watanzania wamesikia kwa sababu Bunge hili ni la Watanzania na hii ndiyo sehemu yao wanapoweza kusikiliza maoni yenu kwa niaba yao.

Mheshimiwa Spika, lakini pia hata wale ambao wamekosa mikopo wamesikia, kwa hiyo sina haja ya kuyarudia yote ambayo Waheshimiwa Wabunge mmeongea kwa sababu ni dhahiri yameeleweka, kila mmoja ameyasikia. Ila sasa kwa sababu ya ku-save muda mimi ninaomba niende kwenye maazimio, kwa sababu tumesikia mengi hapa. Nina maazimio matatu ambayo nataka kuyawasilisha kwako. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, cha kwanza, kwa sababu tayari vyuo vimeshafunguliwa na watoto hawa wako majumbani wanahangaika, hawakupenda wawe nyumbani leo, ni kwa sababu wamekosa mikopo, tunaomba Serikali itoe tamko hapa la kuruhusu watoto hawa warudi vyuoni wakaungane na wenzao kipindi inatafutwa solution ili wasichelewe masomo kwa makosa ambayo siyo ya kwao. (Makofi)

Kwa hiyo, naomba tupitishe kama azimio ili wanafunzi hao, wale ambao wana vigezo na vinajulikana, lakini hawapo vyuoni kwa sababu pesa haijapatikana, kwa hiyo, Serikali itoe tamko na kama Bunge tuazimie ili sasa watoto hawa warudi shuleni, wakaungane na wenzao wakati solution inatafutwa.

Mheshimiwa Spika, azimio la pili,…

SPIKA: Kabla hujaenda kwenye azimio la pili; kwenye hilo la kwanza, ili Bunge lijue linahojiwa nini, kama umeliandika hebu ulisome maana umeenda na maelezo mengine ya ziada, kwa hiyo, hatutajua tunaazimia kwenye kitu gani? Kama unayo sentensi ya kuisema moja, mbili, tatu ili Bunge linapohojiwa, basi lijue linahojiwa nini? Kama unalo, lisome; kama huna, basi itabidi uandike.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, Azimio la kwanza; Kwa kuwa vyuo vimefunguliwa na baadhi ya watoto wameripoti vyuoni;

Na kwa kuwa wanafunzi hao wanavyo vigezo lakini wamekosa mikopo;

Hivyo Basi, waruhusiwe kuripoti vyuoni huku Serikali kwa kushirikiana na Bodi ya Mikopo wakitafuta fedha za haraka ili kukidhi uhitaji wa watoto hao. (Makofi)

SPIKA: Endelea na la pili.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, Azimio la pili; Kwa kuwa inaonekana shida kubwa hapa ni fedha;

Hivyo basi, Serikali ilete budget review hapa ili tuweze kujadili na hatimaye watoto hao ambao wamekosa fedha tuweze kupitisha kama Bunge ili fedha hiyo ipatikane kwa ajili ya kufanya nyongeza ya bajeti. (Makofi)

Sasa sijui ina….

SPIKA: Endelea tu, mimi nakusikiliza.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, Azimio la tatu; Kwa kuwa kutokana na michango ya Wabunge na hali iliyoko huko nje, malalamiko mengi yanailenga Bodi;

Na kwa kuwa tumeshindwa kupata majibu kwa muda mrefu;

Hivyo Basi, iundwe Tume Maalum ya Kibunge, ambacho ndicho chombo cha uwakilishi wa wananchi, ikapitie maoni ya Wabunge wote ambayo wameyataja hapa, pia iende Bodi ikachunguze nini kinaendelea huko kwa sababu inaonekana Serikali imeshindwa kuichunguza Bodi na hatimaye irudishe majibu ndani ya Bunge ili tuweze kufanya maamuzi kwa niaba ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mapendekezo ni hayo matatu.

SPIKA: Sawa. Azimio la kwanza na la tatu nimeyapata vizuri, hebu rejea la pili.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, la pili; Kwa kuwa inaonekana shida kubwa ni bajeti (fedha) ndiyo imefanya watoto wengi wasipate mikopo;

Hivyo Basi, Serikali ilete budget review ili kama Bunge tupitie na kutoa mapendekezo hatimaye tuweze ku-approve nyongeza ya bajeti kwa ajili ya Loan Board ili waweze kukopesha watoto wengi hao waliobaki huko bila fedha. (Makofi)

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, hilo ni la tatu. Ulisema yapo matatu?

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ni matatu tu.

SPIKA: Haya hitimisha.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge likubali maazimio haya kwa ajili ya kuyapitisha.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja. (Makofi)

(Hoja ilitolewa Iamuliwe)

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, naafiki.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi pia na mimi niweze kuchangia kwenye hotuba hii ya Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nami niungane na wenzangu waliotangulia kumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa miradi mikubwa ambayo inaendelea kwenye Majimbo yetu, miradi ya barabara inaendelea vizuri, miradi ya maji na ujenzi wa vyumba vya madarasa ambao umepita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa ziara ambayo aliifanya Mkoa wa Kagera tarehe 29 mwezi uliopita, ziara ambayo imetoa ufumbuzi wa kilio cha muda mrefu cha wakulima wa kahawa katika Mkoa wa Kagera, kutuondolea tozo 42 kati ya tozo 47 ambazo zilikuwa zinatunyonya na kututesa sasa tumebaki na tozo tano ambazo zimeleta unafuu wa kuweza kuendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya nitaongelea sehemu kama tatu. Sehemu ya kwanza ni mfumuko wa bei, sehemu ya pili itakuwa ni issue ya ajira na kama nitapata muda kidogo nitaongelea habari ya TARURA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukirudi kwenye habari ya mfumuko wa bei nimekuwa najiuliza kitu kikubwa kimoja ambacho nimekuwa nacho. Kwanza tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwamba hili Taifa wakati wa janga la Corona limeipiga dunia Taifa hili tulisimama na Mungu kama tulivyosema na mambo yetu yalienda vizuri hatukuwa na lockdown, hatukuwa na nini na kila kitu kiliendelea kwenda sawa, hatukuona changamoto yoyote ile katika shughuli zetu za kiuchumi, lakini sasa baada ya hili janga kuwa limetukumba wenzetu walipokuwa wamejifungia baada ya kurejea kwenye shughuli za kawaida kunakuwa na uhaba sasa, supply and demand inaongezeka kwamba vitu vingi vinahitajika kwa wakati mmoja kwa wakati huo huo kwa hiyo, wafanyabiashara wanachukua advantage ya kupandisha baadhi ya bei ili waweze kujinufaisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii haianzii hapa tu inaanzia duniani huko imeshuka mpaka sasa imekuja imetukumbuka. Kitu kimoja ambacho nimekuwa najiuliza, kwa hali ya nchi sasa leo hapa tunaposimama huko nje ni mbaya sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge wengine wameshatangulia kusema hali ya wananchi ni mbaya mno, vitu vimepanda bei sana kupita kiasi. Statement ya nyanya kupanda bei, vitunguu kupanda bei, tukaanza kusema ni vita ya Ukraine mimi hiki kitu sikubaliani nacho! Nadhani tunakosa control kwenye nchi, kama Taifa ni lazima ifikie stage tujue jinsi ya kufanya control ya bei kwenye nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kuwa na Taifa ambalo watu wanajiamulia kupanga bei wanavyojua wao kwa kisingizio cha vitu vingine hakuna mtu anayeenda kuuliza, halafu tunakuja kuishauri Serikali kwamba tutafute hela ya kukopa na ku-inject kule, uta-inject mara ngapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona kwenye pesa ya UVIKO, Mama ameleta hapa 1.3 trilioni lakini matokeo yake mabati yalipanda bei, cement ilipanda bei, vitu vingi vilipanda bei, lakini baada ya vitu vile kupanda bei hakuna mtu ambaye amerudi nyuma akawaambia wale watu washushe bei.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Biharamulo bati linaenda Shilingi 38,000 la gauge 28, limeshafikia Shilingi 38,000 lakini kabla ya ujenzi ule mabati yalikuwa yapo chini ya Shilingi 35,000. Sasa unaweza ukaona kwamba tabia ya wafanyabiashara wa nchi hii kila wanapopata fursa ya kupandisha bei hata yale mambo yakimalizika bei huwa hazirudi nyuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, jambo la kwanza lazima kama Taifa tusimame tujue jinsi ya kujikwamua kutoka hapa, tusikubali ongezeko la bei kwenye kitu chochote kile, hiyo ndiyo itakayoweza kusaidia wananchi, kwa sababu tutakapokuja na wazo la kukopa na ku-inject pesa mzunguko unakopa anaelipa ni nani? Ni Watanzania walewale hakuna unafuu ambao unao wasababishia, kwa sababu watalipa kwenye kodi hakuna mfanyakazi ameongezewa mshahara, tunajua tarehe 01 Mwezi wa Tano kilio cha wafanyakazi Mama anatakiwa ajibu, sasa Mama atajibu mambo mangapi? Anatakiwa aongeze mshahara huku tukiwa tunalia na vitu vingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, idea ambayo mimi ninayo, maoni yangu mimi ni lazima…

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa kutoka wapi, aah! Mheshimiwa Mtemvu.

T A A R I F A

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampa taarifa mzungumzaji kwamba asishangae bidhaa nyingine kupanda bei ilihali ni eneo moja tu analoliona yeye malighafi ya mafuta kupanda bei. Malighafi ya mafuta inasababisha multiplayer effect katika maeneo yote. Hoja kubwa hapo ni kuendelea kumuomba sana Waziri Mkuu anayeisimamia Serikali kuendelea kusimamia matumizi ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi sasa wanalia huko barabarani wanalia kwenye vyombo vya mitandao kwamba matumizi ni makubwa sana yanayoendelea kwa Viongozi wetu wa Serikali.

MWENYEKITI: Ahsante, Mheshimiwa Chiwelesa, Injinia, unapokea taarifa?

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa naipokea na huko ndiko nilikokuwa naelekea kwenye solution, kwa sababu kazi yangu ni kuongea tatizo halafu baadae tuende kwenye kutafuta ufumbuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, idea ambayo ninayo ni moja, hii ni ripoti ya BOT kwenye issue ya Treasury Bond, tulipokuwa tunapewa ripoti hapa kipindi kilichopita tulipewa ripoti, tulikuwa tunaanza kuuza bond mwezi huu nadhani kesho zilikuwa zinauzwa. Kesho tulikuwa tunauza bond ya 20 years kwa asilimia 15.4, BOT wameshusha leo ipo asilimia 12.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 27 tulikuwa tunauza bond ya seven years kwa asilimia 9.48 leo wameshusha imeenda asilimia 10 na nyingine asilimia 10 leo wameshusha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kimoja ambacho ninacho, unilindie muda wangu. Kitu kimoja ambacho ninacho ni kwamba ni lazima sasa kama Serikali imejitafakari upande wa BOT tumeanza kushusha hizi hisa na interest ambazo zipo ni lazima turudi nyuma tukae na mabenki, unajua unapotaka wafanyabiashara washushe bei, mfanyabiashara yupo tayari ku-adjust kwenye faida yake, lakini wafanyabiashara wengi wamechukua working capital kutoka kwenye mabenki na wakati wote wa CORONA mabenki yaliendelea kutoza interest ileile na wafanyabiashara wameendelea kufanya biashara katika interest zilezile zinatoka kwenye mabenki.

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Msongozi, taarifa.

T A A R I F A

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. ninampa taarifa mchangiaji anayechangia sasa, kwenye suala ambalo analifanya la kuishauri Serikali juu ya masuala ya uchumi. Mheshimiwa Mbunge anachokiongea ni sahihi kabisa na hata Bunge lililopita tumemsikia Mheshimiwa Mbunge akitekeleza majukumu yake alipokuwa anashauri namna ambavyo wenzetu wa Egypt wanachimba chima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

MWENYEKITI: Endelea Mheshimiwa Ezra.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilindie muda wangu. Nilichokuwa nasema ni kwamba, hatuwezi kuwa na Taifa ambalo kila mmoja anajipangia vitu anavyovitaka. Tukumbuke tumetoka katika athari ya uchumi sasa wakati ule wa lockdown, vitu vingi sana vilisimama lakini katika Taifa letu mambo yalienda vizuri. Kwa hiyo ushauri wangu kwa upande wa Serikali, Serikali irudi nyuma, kwanza iongee na Commercial Banks zishushe riba kwa ajili ya wafanyabiashara ambao wamekopa mikopo ya kibiashara. Benki zikishashusha riba turudi sasa kwa wafanyabiasha tukawaambie kwamba, kwa sababu Serikali imewa-favor kwenye upande wa biashara iweze kushusha riba hali kadhalika wafanyabishara watengeneze faida ndogo lakini ile faida ndogo iweze kushusha bei ya bidhaa vinginevyo hali itakuwa mbaya na uchumi wetu unaenda kuathirika kwa sehemu kubwa.

MWENYEKITI: Ahsante sana, kengele yako ya pili imepigwa Mheshimiwa Ezra.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nina dakika 10 hapa nilizihesabu sidhani kama zimetimia au umenichanganya na wa dakika tano?
Hoja ya Dharura (Changamoto ya Kupanda kwa bei za Mafuta ya Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa)
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami pia. Ni-declare tu kwamba naunga mkono hoja na ninampongeza sana mtoa hoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nadhani kwa sababu mengi yameshaongelewa, nitaongea kwenye mambo kama mawili au matatu. Cha kwanza ni tozo. Nimejaribu kupitia huku na hoja yangu ilikuwa tozo zisifutwe, lakini tujaribu kuona jinsi ya kuzipunguza, kwa sababu haiwezekani nchi iko kwenye crisis, mwezi wa Kumi na Moja mwaka 2021 au mwezi wa Kumi au wherever huko nyuma TBS walikuwa wanapata Shilingi moja au Shilingi mbili na sasa wanaendelea kupata pesa ile ile. Kwa hiyo, nilikuwa naomba kwanza tupunguze even by 50%. Tukiweza ku-cut down by 50% watu waelewe kwamba nchi iko kwenye crisis, wananchi wanaumia, nchi inaumia, Mheshimiwa Rais naye anahangaika; kwa hiyo, tukiweza kushusha even by 50% kwenye zile tozo, zitaweza kutusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili, nimejaribu kupitia ile calculation; najua hata Taifa limepitia wakati mgumu sana. Tunatoka kwenye post impact ya Corona, leo tunakuja kwenye mafuta pia. Hawa wanaotuletea mafuta hapa in bulk procurement wana fixed profit, kwamba wakati wa Corona, kipindi dunia imefungwa watu wamejifungia, wao waliendelea kupata faida kwenye nchi hii kwa sababu shughuli zetu zliendelea, leo dunia inahangaika mafuta yanapanda bei, yeye bado anapata fixed profit ile ile. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kuna haja ya ku-revisit hizi profit zao, kwa sababu kuna financial overhead hapa, kwa sababu kulikuwa na financial cost. Yeye kama amekopa, financial cost imekuwa calculated hapa. Kwa hiyo, tunachohitaji, tuongeenao pia, kwamba wewe mwaka 2021 umepata faida ya Shilingi 123 kwa lita, sasa hivi hata wewe kubali kushuka kwa sababu Taifa hili haliwezi kuendelea kuangamia huku wewe ukiwa unatengeneza faida ile ile. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, turudi hata kwao hawa, kipindi tunayaangalia haya, kurudi kwa hawa wafanyabisahara pia, twende sasa kwenye upande wa Serikali. Najua iko miradi ambayo tunakusanya, tunalipa, tunakusanya tunalipa. Kama tutaogopa kugusa kwenye sehemu kama za REA, tutaogopa kugusa kwenye sehemu za maji; hivi vitu vitapanda bei, kwa sababu mafuta yanapopanda bei, costs zikianza kubadilika, tutakuwa na variation kubwa. Serikali itaenda kuwalipa tena wafanyabiashara…

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Chiwelesa, kuna Taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Godwin Kunambi.

T A A R I F A

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tozo zinaathiri moja kwa moja bei ya kupanda kwa mafuta, lakini kuna ushindani wa soko. Ushindani wa soko pia unaathiri moja kwa moja kwenye kushuka kwa bei. Hivyo, nadhani ni vyema sasa Serikali ikaruhusu kuwe na uhuru wa kuagiza mafuta na bila ya shaka naamini bei itashuka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Ezra Chiwelesa, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, tumesimamisha Bunge kwa hoja ya dharura. Hayo mambo ni ya baadaye, we are talking about now. Hizo idea tutazitoa baadaye huko, mambo ya kuanza kuagiza; hii ni dharura. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunapoongea leo, mimi kwangu Biharamulo mafuta ni shilingi 3,370. Naongelea Biharamulo mjini. Kutoka Biharamulo Mjini kuna wananchi wako kwenye kata ambazo zinaenda kilometa 70 kutoka mjini, yule mwananchi leo mafuta yako shilingi 4,000 yanaelekea shilingi 5,000; bodaboda ndiyo ambulance yao, bodaboda ndiyo usafiri wao. Tunapoongea hapa, tuongee hili jambo kama dharura. Hizo ideas Serikali itupe nafasi tutatoa mawazo huko baadaye jinsi ya kufanya, lakini for now it is an emergency.

Mheshimiwa Spika, tunapoongelea emergency, yaani tunataka Serikali isikie leo, kesho jioni au leo jioni tuje na majibu, kwamba tumesikia na tumeondoa shilingi 200 mafuta yashuke leo. Tukitaka kwenda mwisho wa mwezi, it won’t help us, huenda huko vita itakuwa imeisha, mafuta yatakuwa yameshuka pia. Hicho ndiyo tunachoendeleanacho. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ninachosema ni kwamba, twende kwenye hali ya udharura, tuone tunafinya wapi, bei zishuke, wananchi wakiamka kesho waamke na tabasamu.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naunga mkono hoja. (Makofi)
Azimio la Bunge la kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuimarisha demokrasia nchini na kukuza diplomasia ya uchumi
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kukushukuru na kushukuru Waheshimiwa Wabunge wote waliopata nafasi ya kuchangia. Wamechangia takribani Waheshimiwa Wabunge 16 na michango yao karibu yote ilijikita kwenye yale maazimio yetu matatu ambayo niliyasoma hapa mwishoni. Kwa hiyo, nawashukuru sana kwa michango ambayo mmeitoa ya kumpongeza Mheshimiwa Rais katika maazimio haya matatu ambayo nimeyasoma hapa, ni michango mikubwa sana.

Mheshimiwa Spika, nadhani Watanzania ambao tunawawakilisha katika Bunge hili, sisi kama Wawakilishi wao ni mashahidi. Haya ambayo Waheshimiwa Wabunge wameyasema ni dhahiri Mheshimiwa Rais anayaishi na wao wanayaona kwa vitendo.

Mheshimiwa Spika, labda nigusie tu kidogo kwa wale waliochangia katika habari ya kudumisha demokrasia. Nadhani karibu wote wameogelea hii nyanja ya demokrasia na wote ni mashahidi tunaona, shughuli za siasa zimeanza na zinaendelea. Hali kadhalika vile vikosi vya maridhiano ambavyo vinaendelea na kazi, vyote vinaenda vizuri. Kwa hiyo, tumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa hiki alichokianzisha. Maana kama wasingempa ushirikiano wale watu, tusingekuwa tumefika hapa.

Mheshimiwa Spika, pia ipo habari ya kukuza diplomasia ya kiuchumi. Hili jambo ni nyeti sana, wote tumesikia jinsi Waheshimiwa Wabunge wamechangia. Kuvutia wawekezaji kama Wabunge walivyosema, kama mazingira kwako siyo mazuri; na pia unapotafuta wawekezaji kwenye biashara, unaponyanyuka kuna baadhi ya watu utakutana nao unapata confidence ya kuja huku, kwa sababu mataifa mengi ya Afrika hayajulikani. Kwa hiyo, kazi kubwa anayoifanya Mheshimiwa Rais ya kuzunguka huku na huku, ndiyo tunaona matunda kama haya.

Mheshimiwa Spika, wote ni mashahidi, mwaka jana 2022 kwenye Dubai Expo mikataba iliyosainiwa pale mbele yake ilikuwa ni mingi na mizunguko yote ambayo amekuwa akiifanya tumekuwa tunaendelea kupokea neema kama hizo, na kama tulivyosema kwenye maelezo, hata ujio wa Makamu wa Rais wa Marekani pia umetufungulia fursa nyingine kwa vipengele ambavyo nimevitaja.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, pia hiyo ni sehemu na ni juhudi kubwa sana za Mheshimiwa Rais ambazo amezifanya, lakini kwenye sehemu ya tatu au sehemu C ambayo niliisema, kulikuwa na habari ya kumuunga mkono Mheshimiwa Rais. Sasa nadhani wale wote ambao wameongelea Ripoti ya CAG, wote ambao wameongelea yale mambo yanayoendelea hapa sasa, hatumuungi mkono tu atekeleze, ni pamoja na kumlinda. Sasa kazi kubwa ambayo anayoifanya Mheshimiwa Rais kama haitapata protection ya Bunge kama ambavyo mmesikia Wabunge wanaongea, kesho na keshokutwa inaweza isionekane. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nawashukuru Wabunge wote ambao wamechangia wakipaza sauti zao kwamba sasa kupitia Bunge hili tupate nafasi ya kuyalinda mazuri yote haya ambayo anayafanya Mheshimiwa Rais. Mazuri haya tutaweza kuyalinda kwa kuhakikisha kwamba yale yote ambayo yanapitishwa ndani ya Bunge yanasimamiwa na yanatekelezwa.

Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha, kwa dhahiri kabisa amesema yeye mwenyewe kwamba hata Bajeti ya CAG imeongezeka na bajeti ya ukaguzi wa ndani imeongezeka. Sasa kazi kubwa ambayo anaifanya Mheshimiwa Rais, Bunge tunapopitisha bajeti ambayo imeongezeka kama hivyo, maana yake inampa freedom CAG na wakaguzi wa ndani kuweza kufanya ukaguzi mzuri wa hizi fedha ambazo tunazipitisha kwa niaba ya Watanzania na fedha ambazo Mheshimiwa Rais anazihangaikia usiku na mchana ziweze kuja kuwasaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa kumalizia, niwashukuru Wabunge wote ambao wamechangia, ninaamini mengine sasa yanabaki mezani kwako kwa ajili ya utekelezaji kwa sababu ni Maazimio ya Bunge. Yale yote ambayo yameombwa na baadhi ya Wabunge nadhani umeyasikia, muda ukiwadia, kwa sababu Ripoti ya CAG bado haijaja humu, ndiyo maana sikuiongelea katika azimio hili.

Itakapofika, ikishapokelewa ikawa mali ya umma ikapita ndani ya Bunge, nadhani Kiongozi wetu wa Mhimili atajua jinsi gani ataenda nayo.

Mheshimiwa Spika, baada ya kuyasema haya, naomba kutoa hoja.

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, naafiki. (Makofi)
Azimio la Bunge la kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuimarisha demokrasia nchini na kukuza diplomasia ya uchumi
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni ya 61(1) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Februari, 2023, naomba kuwasilisha hoja kwamba Bunge lako Tukufu lijadili na kupitisha Azimio la Bunge la kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuimarisha demokrasia nchini na kukuza diplomasia ya uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, awali ya yote, nichukue nafasi hii kukushukuru wewe binafsi kwa kuruhusu na kunipa fursa hii adhimu ya kuwasilisha hoja hii ya azimio hili. Naomba pia kutumia nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uongozi bora na thabiti aliyouonesha kwa taifa letu tangu alipoingia madarakani. Nawaomba Watanzania wenzangu tuzidi kumwombea kwa Mwenyezi Mungu aendelee kumpa afya njema ili aweze kutekeleza majukumu haya ipasavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sote tulishuhudia katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hali ya demokrasia na utawala bora imeendelea kuimarika nchini.

Miongoni mwa mambo muhimu yaliyochangia kuimarika kwa demokrasia ni pamoja na haya yafuatayo: -

(1) Uamuzi wa kuruhusu shughuli za siasa hasa mikutano ya hadhara kufanyika nchini kote; uamuzi huu umefufua na kuimarisha shughuli za siasa nchini, kwani vyama vya siasa vimepata fursa ya kunadi sera zao na kutoa mawazo mbadala ambayo yatasaidia Serikali kutekeleza huduma za kijamiii na kiuchumi hususan masuala yanayogusa maendeleo ya wananchi;

(2) Kuanzisha vikao vya maridhiano ya kisiasa miongoni mwa vyama vya siasa nchini ili kuhakikisha kunakuwepo mahusiano mema miongoni mwa makundi ya kisiasa yaliyokuwa yanahasimiana;

(3) Kuanzisha mchakato wa kufanya marekebisho ya kimfumo na kisheria yanayoongoza shughuli za kisiasa na kudumisha misingi ya amani na mshikamano miongoni mwa Watanzania; na

(4) Kuridhia kuundwa kwa kikosi kazi cha kufanyia kazi masuala yananyohusu demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini ambapo lengo kubwa la kikosi kazi hicho ilikuwa ni kupendekeza namna bora ya kutekeleza haki ya vyama vya siasa ikiwemo kuwepo na uwanja sawa wa kufanya shughuli za kisiasa bila kukiuka sheria na maadili ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tumeshuhudia ukuaji mkubwa wa diplomasia ya uchumi ambapo Mheshimiwa Rais mwenyewe amekuwa chachu ya mafanikio hayo kwa kuwa mwanadiplomasia mahiri. Katika kipindi hicho, tumeshuhudia nchi yetu ikipitia mafanikio haya yafuatayo: -

(1) Kuongezeka kwa masoko ya bidhaa zinazozalishwa nchini katika masoko ya nje;

(2) Kuimarika kwa mahusiano ya kimkakati na makampuni ya kimataifa yanayolenga kuwekeza katika sekta za uzalishaji ili kuchochea uchumi wa nchi yetu;

(3) Kuwezesha upatikanaji wa misaada na mikopo ya masharti nafuu kutoka kwenye taasisi za fedha duniani ambapo kwa kiasi kikubwa imesaidia kuboresha shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo elimu, miundombinu, afya na maji.

(4) Kukua kwa shughuli za uwekezaji na kuongezeka kwa idadi ya wawekezaji wapya nchini kutoka nje ya nchi, baada ya kufanyika maboresho ya mazingira ya kufanya biashara nchini;

(5) Kupitia filamu maarufu ya Tanzania The Royal Tour amefanikiwa kutangaza vivutio vilivyoko nchini na hivyo kukuza sekta ya utalii ambapo tumeshuhudia watalii maelfu kwa maelfu wakiingia nchini na hivyo kuongeza pato la Taifa; na

(6) Kuimarika kwa mahusiano na mataifa mengine na taasisi za kimataifa kutokana na ziara mbalimbali ambazo Mheshimiwa Rais amezifanya nje ya nchi ambazo zimezaa matunda makubwa. Mathalan, hivi karibuni nchi yetu imepokea ugeni mkubwa wa Mheshimiwa Kamala Harris, Makamu wa Rais wa Marekani. Kupitia ziara hiyo, Serikali ya Marekani imeahidi kuimarisha ushirikiano na Tanzania kwenye sekta mbalimbali ikiwemo miundombinu, viwanda, usalama wa mitandao, TEHAMA, afya usafirishaji na usalama wa chakula.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naomba sasa niwasilishe Azimio la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuimamrisha demokrasia nchini na kukuza diplomasia ya uchumi kama ifuatavyo: -

Kwa kuwa, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameonesha wazi nia yake ya kuifanya Tanzania kuwa moja, salama na bila kundi lolote kuwa nyuma katika kufurahia demokrasia ya kweli;

Na kwa kuwa, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa mstari wa mbele katika kukuza na kuimarisha diplomasia ya uchumi ambayo imelenga kuiletea Taifa letu maendeleo;

Kwa hiyo basi, Bunge hili katika Mkutano wake wa Kumi na Moja, Kikao cha Kwanza, tarehe 4 Aprili, 2023, linaazimia kwa dhati na kauli moja haya yafuatayo:-

(a) Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuimarisha demokrasia nchini; (Makofi)

(b) Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kukuza demokrasia ya uchumi; na (Makofi)

(c) Kumuunga mkono Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika majukumu yake ya kazi ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, kumwombea afya njema, baraka na ulinzi wa Mwenyezi Mungu katika kutekeleza majukumu yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja. (Makofi)

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Spika, naafiki.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Kilimo
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Nashukuru kwa kunipa nafasi namimi pia niungane na wachangiaji waliyopita kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kunyanyua kilimo cha nchi hii. Maana tunajua vipaumbele ni vingi lakini unapoona umeamua kuelekeza pesa polini ukakate mapoli hatimaye upate chakula na urudi mijini watu wafurahie ni uamuzi wa busara na ni uamuzi wa kijasiri lakini pia nimpongeze Mheshimiwa Bashe na msaidizi wake na Watendaji wote wa Wizara hii kwa maono makubwa ambayo Bashe amekuwepo nayo maana amejipambanua kama Mkulima na maono haya yanatimia kwa sababu amepata Mheshimiwa Rais kumshika mkono na tunaona mambo yanaenda na pesa hizi ambazo zinatoka na zinaendelea kwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile pia niishukuru Serikali hata sisi Biharamulo kwa mara ya kwanza katika historia tumeenda kujengewa skimu ya irrigation siyo jambo dogo hili kwa hiyo neema hii na sisi imetuangukia. Ukurasa wa 207 wa Hotuba yako Mheshimiwa Waziri, tutajengewa Mradi wa Mwiruzi hekta karibu karibu 1,300 kwa hiyo hili jambo kubwa kwa wakazi wa Biharamulo tukushukuru. Hata hivyo sasa baada ya hayo nijikite mimi kwenye mambo mawili au matatu, mawili kama muda utapatikana yatakuwa matatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huwezi kutaja zao la kahawa bila kuitaja Kagera kwa sababu history inaonyesha mnamo karne ya 16 wenyeji wa Mkoa wa Kagera ndiyo waliyoingiza kahawa Tanzania wakitokea Ethiopia. Kahawa aina wa robusta na kwenye mauzo mpaka sasa kwenye andiko hili nililonalo la Tanzania coffee industry development strategy ya 21 – 25 la Bodi ya kahawa ukurasa wa 19 nimepitia nikawa naangali uzalishaji wa kahawa na trend ilivyo. Kahawa aina ya robusta kwa sehemu kubwa inazalishwa Kagera na percentage ya uzalishaji ya asilimia 44 so far kati ya asilimia 100 sasa tukija kuangalia expansion na project hii ambayo inafanyika kuna habari ya kugawa miche ya kahawa. Tumeona watu wa robusta tulicho pangiwa katika miche milioni 20 tumepangiwa kuwa tunapewa miche milioni tano tano sasa unajiuliza wewe unaezalisha 44 percent unapewa five million mwenye fifty six anapewa fifteen million sasa hiyo unajiuliza nikuirudisha Kagera chini au kuinyanyua Kagera ili iweze kuendelee kufanya kazi kama kweli unataka kuturudisha kwenye zao la kahawa kama vinara wa kahawa ebu hata miche inayopangwa tupewe forty four percent kama share yetu ambayo tunamiliki katika soko ili hiyo iwasaidie wakazi wa Kagera waweze kunyanyuka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo ukiangialia gharama ya uzalishaji wa hii miche ni kubwa sasa Mheshimiwa Waziri mimi nilitaka nikuombe na nitoe ushauri, wenzetu ya Uganda wanachokifanya wanatumia tissue culture. Tuko kwenye volume mass production ya miche ya kahawa ndiyo inabidi twende nayo. Mheshimiwa Waziri sasa tukuombe najua wewe ni mbunifu, umekuwa kinara wa ubunifu kama ulivyoanzisha BBT rudi maabara nyanyuka na tissue culture hii tukimbizane na wenzetu Waganda itatusaidi kututoa hapa tulipo. Pesa kubwa unayotengwa cha kwanza haitokuwa na magonjwa ya kahawa kwa hiyo itatusaidia tutapata mass production ya miche lakini hakutakuwa na ugonjwa hata tunapo otesha hii miche itastawi na itakuwa kwa ajili ya manufaa ya hao wananchi hilo nikuombe uliangalie halafu tupewe share yetu ya forty four percent ukishamaliza kuzalisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile pili hata migomba Mheshimiwa Waziri. Migomba ya Kagera tumeta ugonjwa sana wa mnayauko rudini maabara ulitupeleka Kibaha maabara nzuri sana pale iliyojengwa rudi pale weka tissue culture hata kwenye habari ya migomba ili iweze kutusaidia kwa hayo nikuombe uweze kutusaiodia ili sasa Kagera turudi kwenye hadhi yetu ya kahawa na migomba hatimaye uchumi huu ambao Mama Samia anaunyanyua na sisi uweze kutugusa. Iko habari ya Tumbaku Mheshimiwa Waziri, niliongea hapa kwa ajili ya wakulima wa tumbaku wa Biharamulo tunapeleka tumbaku kilomita 250 kwenda kuuza kwenye Mkoa wa Kitumba wa Kahama. Tunakuomba wakulima wa Biharamulo wana wasiwasi kwanza kama vile kuwapeleka Kahama wanaanza kuwa na wasi wasi kama wanaenda kuibiwa. Kwa sababu wanasema ikishafika pale akapangua grade hawezi kuibeba airudishe nyakaura au airudishe Kalenga au airudishe Nyanza matokeo yake anakubaliana na bei pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti sasa nimuombe Mheshimiwa Waziri atakapokuwa anamaliza naomba tumbaku ya Biharamulo inunuliwe Baharamulo isitoke nje ya Wilaya yetu. Hilo nakuomba utusaidie na uweze kuisimamia lakini Mheshimiwa Waziri niliomba pia habari ya mbolea ya ruzuku ya tumbaku najua World Bank na IMF wanapinga hiyo hasa kwenye mbolea ya NPK tusaidie tafuta jinsi ya kusaidia maana wakulima wote ni wa kwako. Tafuta jinsi ambavyo unaweza najua wewe ni intelligence sina haja ya kukufundisha lakini naamini liko jambo unaweza ukafanya hata wakulima wa tumbaku wakanufaika hujawahi kushindwa jambo Mheshimiwa Bashe, hilo naomba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tuliomba pia kwenye habari ya mbolea wamesema hapa wenzangu mbolea isiyo na ubora. Tangu Serikali ya Awamu ya Nne kumekuwa na malalamiko makubwa sana juu ya quality ya mbolea inayozalishwa hapa nchini sina haja ya kutaja kiwanda. Sasa nikuombe hata wewe mwenyewe at some extent nimekusikia ukiongelea habari ya mbolea isiyo na ubora mpaka ukaifutia ruzuku, sasa tuombe huwezi kufikia huko mtaani hili ni Bunge wananchi wale waliyopelekewa mbolea isiyo na ubora wamepata hasara na ile mbolea wameilipia. Utakapokuwa una wind up tusikie kauli ya Serikali juu ya mwenendo mbovu uliyopigiwa kelele wa kiwanda hiki tupate kauli humu ndani. Wananchi wa Tanzania wanaopewa mbolea feki au mbolea mbovu isiyo na quality waendelee kuumia au mbadilishe mtafute jinsi ya kuwasaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile pia katika kitu kingine ambacho niliomba na nilijibiwa kwenye Bunge la mwezi wa pili tunaomba mbolea isogezwe karibu. Mimi nina watu leo wako Kalenge kilomita 70 na unamwambia aje Biharamulo Mjini kuchukua mbolea mifuko miwili au mifuko mitatu kwa sababu mlitujibu kwamba mnapeleka katika ngazi ya AMCOS tunaomba mbolea safari hii zifike vijijini na wananchi wazipokee kulekule kwao hiyo itawasaidia wananchi wasihangaike na hatimaye tutawapunuguzia hata uchovu na usumbufu mwingine wa pesa ambao wanakuwa wanaupata pale wanapoenda kuchukua mbolea mjini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema hayo na kwa sababu ya muda naomba kuunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunisikiliza. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Fedha na Mipango
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza na mimi niungane na wengine kukupongeza Mheshimiwa Waziri na msaidizi wako kwa hotuba nzuri lakini kipekee kama Mjumbe wa Kamati ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo nisimame hapa kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tukio kubwa na la kihistoria linaloendelea Mkoa wa Njombe. Kwa ulipwaji wa fidia uliozinduliwa leo kwenye miradi ya Liganga na Mchuchuma, kama kamati tunafarijika na hasa mimi ambaye nimekuwa kinara wa jambo hili ninapoona hatua hii kubwa ya ku-inject shilingi bilioni 15 kwa ajili ya wananchi maana yake tunaona mradi mkubwa wa kimkakati wa kulinyanyua Taifa hili wa uchimbaji wa chuma Liganga na makaa ya mawe Mchuchuma sasa unaenda kufanya kazi. Tumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia upande wangu mimi wa kuchangia, kama nilivyosema mimi ni Mjumbe wa Kamati na kwenye kamati yetu tangu tumefika kumekuwa na habari ya zile risiti za electronic au ambazo zimekuwa zinafanywa na Kampuni ya SICPA. Sasa nilikuwa naomba nijielekeze hapa kwenye habari ya risiti za ETS ili walau na mimi niweze kupata nafasi ya kuchangia jambo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, wafanyabiashara wametufuata sana kwenye Kamati nadhani tangu miaka hii miwili yote iliyopita na hata juzi walikuwa hapa wanaendelea na jambo hili. Hili Bunge ni la wananchi, wafanyabiashara kila wanapohisi kwamba wanahitaji msaada wamekuwa wanakimbilia katika Bunge. Sasa mimi kama mjumbe tumekaa miaka yote hii lakini bado hatujapata majibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nikawa nimekuja leo, naomba nitoe ushauri tu kwa Waziri wa Fedha, nadhani anakumbuka vikao tulishafanya mpaka Kamati ya Uongozi wa Bunge na wewe mwenyewe ukiwemo, maofisa wa TRA; wafanyabiashara wanayo hoja na hoja ambayo lazima isikilizwe. Hii ni kwa sababu hawa ndiyo wanaolipa kodi, ni wazalishaji wakubwa wameajiri Watanzania. Kwa hiyo hatuwezi kuendelea kufanya nao bisahara huku wakiwa wana sononeka.

Mheshimiwa Naibu Spika, point yao kubwa ni kwamba gharama ziko juu sana ukilinganisha na nchi nyingine; na wao wanasema mwanzo walivyoanza zilikuwa kampuni karibu tisa na huyu muwekezaji akasema amewekeza mtaji. Kwa hiyo angetakiwa ku-recuperate ile capital yake ambayo ameweka na akawa anawachaji juu akitegemea kwamba baada ya muda ingeshuka. Sasa kutoka kampuni tisa zilizoanza sasa tuna kampuni zaidi ya 200 sasa. Kwa hiyo wafanyabiashara wanahisi zile gharama inabidi zishuke ili na wao waweze kuji-tune na wafanye biashara katika unafuu zaidi waweze kuajiri Watanzania wengi na kupanua wigo wa biashara zao; nadhani ameongelea Mheshimiwa Vuma hapo

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu jambo moja Mheshimiwa Waziri. Tumeliongea sana kwenye kamati hili lione. Ongea na mwekezaji huyo aliyepo ambaye anafanya kazi hii ili ashushe gharama hizi ili kwa pamoja wafanyabiashara pia waweze kuridhika. Na kwa sababu wao wamekuwa wanakuja kwenye Kamati na wewe hujawahi kukaa nao, sasa, andaa kikao awepo mzabuni, wawepo wafanyabiashara na wewe mwenyewe ikiwezekana na Kamati tukae hili jambo tujadili kwa pamoja. Kwa sababu haiwezekani tukawa tunafanya biashara na watu ambao wana lalamika. Mwwekezaji kawekeza mtaji wake na hivyo ni lazima tujue amewekeza fedha lakini aone pia jinsi ya kupunguza ili iwe justifiable kwa sababu hiki kitu watu wanaona. Dunia ni kijiji, wewe mwenyewe katika bajeti hii ulituhubiria kwamba tutaenda kufanya biashara yaani tutaendesha Serikali kidijitali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo leo kila kitu kiko wazi. Kila kinachofanyika sehemu yoyote kiko wazi watu wanaona. Kwa hiyo tuombe hili ulichukue wafanyabiashara wakapatiwe unafuu ili waweze kufaidika na kile kidogo wanachokizalisha na Watanzania waweze kupata ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nikitoka kwenye habari ya SICPA au kwenye stempu hizi za ETS, mimi ni mjumbe kama nilivyosema, kilimo kiko kwetu. Mheshimiwa Waziri mme-inject fedha nyingi sana kwenye Mradi wa BBT, nyote ni mashahidi. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa project hiyo ambayo inaenda kuinua vijana na wakina mama; lakini iko habari ya Benki yetu ya Kilimo (Tanzania Agricultural Development Bank). Hii benki kwenye Azimio la Bunge la mwaka jana mwezi Novemba kwenye Ripoti ya PAC walisema kabisa kwamba benki ilipewa mtaji wa bilioni 208 na kukawa na ahadi ya Serikali kuiongezea mtaji mpaka ifike shilingi bilioni 760 lakini hatujapata ripoti kujua kazi hii ilifanywa vipi na so far mmeongeza nini na mwaka wa fedha unaisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tunachoomba ahadi ilikuwa kufikisha mtaji wa benki hii iwe shilingi bilioni 760. Mheshimiwa Waziri hatuwezi…

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa taarifa.

TAARIFA

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpe taarifa mzungumzaji Serikali ingeipa Benki ya TADB bilioni 100 ingelikuwa na mtaji wa zaidi ya shilingi bilioni 760, ingewakopesha wakulima wengi, ingekopesha vyama vya ushirika vingi na ingeleta mapinduzi makubwa kwenye hii sekta ya kilimo nchini. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Ezra taarifa?

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa naipokea na ndipo hapo nilikuwa naendelea; kwamba maelekezo au Azimio la Bunge tuwe tunatoa shilingi bilioni 100 kila mwaka. Kwahiyo tunachoomba azimio lile ambalo Bunge lako lilipitisha mwaka jana Novemba hebu liweze kufanyiwa kazi. Kwa sababu kwa sisi tunaotoka vijijini siyo kila mtu yuko kwenye BBT, wala siyo kila mtu anaweza kukopesheka benki, wengine hawana dhamana kwenye benki za biashara. Benki yetu hii riba ni ndogo, asilimia tisa hadi asilimia kumi na mbili, si kila benki inaweza kutoa hivyo. Kwa hiyo tunachoomba mtaji uongezwe ili wakulima wetu huko vijijini waweze kupata nafasi ya kuweza kushiriki uchumi na hasa fedha hizi ambazo Mama Samia anazitoa sehemu nyingi na anavyozidi kuifungua nchi kiuchumi hata sisi huko vijijini waweze kushiriki kufanya uchumi wa nchi hii hatimaye waweze kupata maendeleo; niliombe hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia Mheshimiwa Waziri wa Fedha najua mikopo ile ya asilimia 10 imesitishwa. Niombe kwenye hili, kipindi mnajaribu kuangalia kanuni na ukopeshaji mpya, kundi la vijana ni kundi linalokua. Unapoweka kijana wa miaka 35, these guys are still teenagers. Walio wengi hawajajua hata thamani ya ile fedha, mnawapa hii fedha baadaye wanaanza kusumbuana na halmashauri. Ongezeni umri at least miaka 45 na wenyewe bado ni vijana. Waende huko wapewe watu ambao kidogo wako matured hizi fedha watazipata watafanyia biashara, watawaajiri wale vijana wenye miaka 18, 20 waweze kufanya nao kazi huku fedha iki-rotate na kurudi; kuliko leo ambavyo unampa fedha mtu kijana wa miaka 18 au 25 haendi, hajui aitumiaje. Lakini kwa sababu ameambiwa fedha ipo anachukua na hatimaye anashindwa kuirejesha na thamani ya ile fedha inashindwa kuonekana…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante.

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, nashukuru. (Makofi)