Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Questions to the Prime Minister from Hon. Kenneth Ernest Nollo (1 total)

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Spika, nchi nyingi duniani zimerusha satellite angani kwa matumizi mbalimbali ikiwemo kupata takwimu sahihi za hali ya hewa. Katika anga la Afrika kwa sasa tuna satellite 41 na kati ya hizo 41 mbili zinatoka katika mataifa ya Afrika Mashariki. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuanza na programu ya kutengeneza satellite na baadaye tuweze kuirusha katika anga letu?
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kenneth Nollo, Mbunge wa Bahi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa anahitaji kujua maendeleo ya teknolojia kwenye mawasiliano. Ameeleza kwamba nchi nyingine tayari zimejitegemea katika kununu mitambo inayowezesha nchi husika kuboresha mawasiliano yake. Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zinaendelea kwa kasi katika maboresho ya TEHAMA, na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kazi moja kubwa aliyoifanya ni kuanzisha Wizara ya Sayansi, Mawasiliano na Teknolojia ambayo pia ina habari mawasiliano na teknolojia ya habari ambayo pia inaendelea kufanya ufuatiliji wa maeneo ambayo tayari tunayo na maeneo ambayo bado hayapo kwa lengo la kufanya maboresho. Na Wizara, kama ambavyo inaendelea kufanya kazi yake na imeshapitishiwa bajeti yake, na Waziri hapa ameeleza maboresho makubwa yaliyofanywa nchini. Lengo hii teknolojia kufikisha kwa Watanzania mpaka vijijini. Tumeanza na teknolojia ambayo inawezesha kufanya mawasiliano maeneo yote, na tunapanua wigo huu mpaka kwenye ngazi za kimataifa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka nikuhakikishie kwamba maeneo yote ambayo nchini sasa hayapo ambayo yanahitajika katika kuboreshwa mfumo mzima wa mawasiliano Serikali itafanya maboresho kutafuta fedha zaidi kwa ajili ya kuhakikisha kwamba teknolojia tunaipandisha na teknolojia inawafikia wananchi wote mpaka kule vijiji, ahsante. (Makofi)