Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Questions to the Prime Minister from Hon. Cosato David Chumi (3 total)

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii, nami niweze kumwuliza Mheshimiwa Waziri Mkuu swali ambalo nimeona kuna umuhimu wa kuliuliza kwa sababu jana nilisikia ufafanuzi kutoka kwa Mheshimiwa Rais, lakini bado nimeendelea kupokea message kutoka kwa watu mbalimbali wakiuliza kuhusu swali hilo. Suala hilo ni kwamba, kumekuwepo na taarifa katika mitandao ya kijamii na mitaani kwamba Serikali imefuta ajira hali ambayo imesababisha tahamaki na taharuki miongozi mwa wahitimu mbalimbali waliokuwa wanatarajia kuajiriwa na Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia, taarifa hizo za mitandaoni na mitaani zinasema pia kwamba Serikali haitafanya tena promotion wala kupandisha madaraja, hali ambayo pia inawafanya Watumishi wa Umma kwa namna fulani morali yao kushuka.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa napenda kusikia ukweli halisi ni upi katika suala hili. Je, ni kweli kwamba Serikali haitaajiri tena? Ni kweli haitapandisha madaraja tena? Nakushukuru.
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimejibu swali la Mheshimiwa Mbogo, ni kwamba sasa hivi kuna watu wengi hupenda kusema maneno ambayo siyo sahihi na hili pia napenda nikanushe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa bahati nzuri sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, jana kwenye hotuba yake ya Maadhimisho ya Miaka 50 ya Benki Kuu, ametoa ufafanuzi mzuri sana. Nami nataka nitumie nafasi hii kurudia tu yale ambayo Mheshimiwa Rais ameyasema kwa kuwahakikishia Watumishi wa Umma na wale ambao wanatarajia kuajiriwa kwamba Serikali haijasitisha ajira. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imesimamisha kwa muda kuajiri kwa sababu tunaendelea na zoezi la uhakiki wa watumishi hewa. Kazi hii ilishaanza, sasa hivi tunaikamilisha. Katika ukamilishaji huu, tunataka tujue sasa watumishi hewa ni akina nani kwa kila idara na kila sekta na watumishi walioko sasa kazini ni akina nani; ili tuweze kujua idadi ya watumishi waliobaki na pengo yaliyopo ndipo sasa tuweze kuajiri kwa ajili ya kusheheneza mahitaji ya watumishi kwenye maeneo hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia Serikali inafanya mapitio ya Miundo ya Utumishi kwa lengo la kuboresha. Tunaposema kuboresha, maana yake sasa tunataka tupate tija zaidi kwa watumishi. Kwa hiyo, naomba niwasihi Watumishi wote wa Umma kwamba zoezi hili halilengi kuwakandamiza watumishi; kazi hii hailengi kuathiri utumishi wao na madaraja yao, bali kuboresha watumishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niwahakikishie Watumishi wa Umma kwamba Serikali hii inawapenda sana na inajali mchango mkubwa ambao watumishi mnautoa kwa Serikali hii. Ili tuweze kufanya kazi kwa motisha, Serikali hii imeona ni muhimu sasa kuboresha zaidi miundo mbalimbali na maslahi mbalimbali, lakini pia kuona idadi ya watumshi tuweze kutumia fedha inayotakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka muwe na amani kwamba kazi hii inayoendelea ni ya muda mfupi sana. Itakapokamilika, ajira zote ikiwemo na elimu, afya, majeshi, ambazo pia zilikuwa tayari zianze karibuni, zote zitarudishwa na watu watapelekwa kwenye vituo vya kazi kwenda kuanza kazi zao na madaraja mapya yatakuwa yameshatolewa.
MHE. COSATO D. CHUMI:
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii, nami niweze kumwuliza Mheshimiwa Waziri Mkuu swali ambalo nimeona kuna umuhimu wa kuliuliza kwa sababu jana nilisikia ufafanuzi kutoka kwa Mheshimiwa Rais, lakini bado nimeendelea kupokea
message kutoka kwa watu mbalimbali wakiuliza kuhusu swali hilo. Suala hilo ni kwamba, kumekuwepo na taarifa katika mitandao ya kijamii na mitaani kwamba Serikali imefuta ajira hali ambayo imesababisha tahamaki na taharuki miongozi mwa wahitimu mbalimbali waliokuwa wanatarajia kuajiriwa na Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia, taarifa hizo za mitandaoni na mitaani zinasema pia kwamba Serikali haitafanya tena promotion wala kupandisha madaraja, hali ambayo pia inawafanya Watumishi wa Umma kwa namna fulani morali yao kushuka.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa napenda kusikia ukweli halisi ni upi katika suala hili. Je, ni kweli kwamba Serikali haitaajiri tena? Ni kweli haitapandisha madaraja tena? Nakushukuru.
WAZIRI MKUU:
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimejibu swali la Mheshimiwa Mbogo, ni kwamba sasa hivi kuna watu wengi hupenda kusema maneno ambayo siyo sahihi na hili pia napenda nikanushe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa bahati nzuri sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, jana kwenye hotuba yake ya Maadhimisho ya Miaka 50 ya Benki Kuu, ametoa ufafanuzi mzuri sana. Nami nataka nitumie nafasi hii kurudia tu yale ambayo Mheshimiwa Rais ameyasema kwa kuwahakikishia Watumishi wa Umma na wale ambao wanatarajia kuajiriwa kwamba Serikali haijasitisha ajira.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imesimamisha kwa muda kuajiri kwa sababu tunaendelea na zoezi la uhakiki wa watumishi hewa. Kazi hii ilishaanza, sasa hivi tunaikamilisha. Katika ukamilishaji huu, tunataka tujue sasa watumishi hewa ni akina nani kwa kila idara na kila sekta na watumishi walioko sasa kazini ni akina nani; ili tuweze kujua idadi ya watumishi waliobaki na pengo yaliyopo ndipo sasa tuweze kuajiri kwa ajili ya kusheheneza mahitaji ya watumishi kwenye maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia Serikali inafanya mapitio ya Miundo ya Utumishi kwa lengo la kuboresha. Tunaposema kuboresha, maana yake sasa tunataka tupate tija zaidi kwa watumishi. Kwa hiyo, naomba niwasihi Watumishi wote wa Umma kwamba zoezi hili halilengi kuwakandamiza watumishi; kazi hii hailengi kuathiri utumishi wao na madaraja yao, bali kuboresha watumishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niwahakikishie Watumishi wa Umma kwamba Serikali hii inawapenda sana na inajali mchango mkubwa ambao watumishi mnautoa kwa Serikali h
ii. Ili tuweze kufanya kazi kwa motisha, Serikali hii imeona ni muhimu sasa kuboresha zaidi miundo mbalimbali na maslahi mbalimbali, lakini pia kuona idadi ya watumshi tuweze kutumia fedha inayotakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka muwe na amani kwamba kazi hii inayoendelea ni ya muda mfupi sana. Itakapokamilika, ajira zote ikiwemo na elimu, afya, majeshi, ambazo pia zilikuwa tayari zianze karibuni, zote zitarudishwa na watu watapelekwa kwenye vituo vya kazi kwenda kuanza kazi zao na madaraja mapya yatakuwa yameshatolewa.
MHE. CASATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kupata nafasi ili niweze kumuhuliza Mheshimiwa Waziri Mkuu swali, katika siku za karibuni dunia imekumbana na majanga makubwa mawili; la kwanza ni ule ugonjwa ambao uko rafiki ya China unausababishwa na virus wa aina ya corona.

Mheshimiwa Spika, la pili ni baa la Nzige ambao tayari wameshafika katika baadhi ya nchi jirani na hasa za Afrika Mashariki. Nilikuwa napenda kufahamu, Serikali imejipangaje katika kukabiliana na kudhibiti masuala haya mawili ambayo kwa namna moja ama nyingine yasipodhibitiwa yanaweza yakaadhiri ukuaji wa maendeleo ya taifa letu na wananchi wetu na hasa ukizingatia kwamba kuna biashara kubwa kati ya nchi yetu na China?

Vilevile ukizingatia kwamba kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki wenzetu jirani wameshakubwa na baa la Nzige?
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Chumi Mbunge wa Mafinga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba nchini China kuna ugonjwa unaosababishwa na virusi vya corona ambao unapoteza maisha ya watu; na sasa tumeanza kuona hata nchi za jirani yake nazo pia zimepata maambukizi hayo. Lakini pia hili la pili la nzige tumepata taarifa kupitia mitandao na vyombo vya habari kwamba hapa nchi jirani ya Kenya mazao yao yanashambuliwa na hao nzige.

Mheshimiwa Spika, sasa tuanze na hili la corona, corona iliyopo nchini China, China ni nchi rafiki na Tanzania, Watanzania wengi wapo China, lakini pia wapo wachina walioko nchini Tanzania. Tunayo maingiliano mengi kati ya Tanzania na China. Wakati huu wa uongonjwa huu, kwanza tumewahakikishia Watanzania kwamba Tanzania haina tatizo hilo la corona; na jana Waziri wa afya pamoja na Naibu Waziri wa afya wametoa taarifa kwa Watanzania, na nimeona leo kwenye gazeti limetoka hili, sasa jukumu letu ni kuwa na taadhari tusije tukapata tatizo hilo.

Mheshimiwa Spika, sasa kwenye tahadhari Serikali imejipanga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja tumeimarisha mawasiliano na Balozi yetu iliyoko China kujua hali huko China inaendeleaje; na Mheshimiwa Mbelwa Kairuki anafanya kazi hiyo ya kutupa mrejesho kila siku na hali iliyoko kule. Baalozi Mbelwa anaendelea kazi nzuri ya kuendelea kutoa elimu kwa Watanzania kwanza ametafuta madaktari wa Kitanzania ambao wamejifunza ugonjwa huo na kuendelea kuwaelimisha Watanzania walioko nchini China namna ya kujikinga.

Mheshimiwa Spika, na balozi kule kwa Tanzania walioko China amewakanya watanzania wasiwe na mizunguko mingi sana kwa sababu ugonjwa huo maambukizi yake ni pale ambapo watu wanakutana. Hiyo moja.

Mheshimiwa Spika, lakini pia tumewataka Watanzania wale wanapohitaji labda kurudi Tanzania, na kwa sababu watatakiwa kusafiri kwenye ma treni, mabasi wafanye mawasiliano na Balozi juu ya namna nzuri ya kusafiri. Wasisafiri kwenda ubalozini Beijing ulipo Ubalozi na badala yake watumie mawasiliano ya kimtandao kupata ridhaa hiyo na kuambiwa hali ikoje ili wapate vibali vya kurudi.

Ndugu Watanzania tunatambua kuna wazazi wana watoto wetu wanasoma nchini China, na wengine wamesharudi likizo. Tunawasihi watoto hawa wasiende kwanza nchini China mpaka hapo tutakapopata taarifa za kidiplomasia.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Mambo ya Nje Tanzania inaendelea kufanya mawasiliano na Balozi zote mbili, Balozi ya China Nchini Tanzania na Balozi Tanzania Nchini China kuona mwenendo wa ugonjwa huo. Pale ambapo Serikali itaridhika kwamba kule hali imepungua tutatoa tamko kwa Watanzania walioko likizo hapa kurudi nchini China kuendelea na masomo, na vinginevyo ikiendelea sana basi Serikali itatafuta utaratibu mwingine.

Mheshimiwa Spika, kwahiyo, nitowe wito kwa Watanzania kama ambavyo Wizara imetoa kwamba kila Mtanzania awe makini na wageni wanaoingia mpakani na hasa wale wote ambao tumewaweka mpakani kuhakiki wanaongia nchini kupitia vifaa vyetu ambavyo vinaweza kutambua magonjwa mbalimbali kuvitumia vifaa hivyo kikamilifu ili kubaini hao ambao wana dalili ya magonjwa hayo ili kudhibiti kuingizwa ugonjwa huu wa corona hapa nchini Tanzania.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la nzige, kama ambavyo nimesema majirani zetu mazao yanaharibiwa. Nzige ni wadudu hatari sana, wakiingia hapa watamaliza mazao yetu. Tumechukuwa taadhari, Wizara yetu ya Kilimo inaendelea kuwasiliana na Wizara ya Kilimo nchini Kenya kuona mwenendo na ukuwaji wa tatizo hilo, na sisi huku tunajipanga kwa namna ambavyo tunaweza kushiriki kikamilifu; lakini Serikali yetu inashiriki pia kusaidia nchini Kenya kupoteza wadudu hao ili wasiongezeke tatizo hili likawa kubwa nchini Kenya lakini pia lisije likaamia huku nchini kwetu.

Mheshimiwa Spika, sasa bado nitowe wito kwa mikoa na wilaya na vijiji vilivyoko mpakani kuwa makini na hao wadudu nzige.Pale ambapo watawaona wakiingia watowe taarifa haraka sana kwenye mamlaka zao ili hatua kamili iweze kuchukuliwa.

Sisi tumejipanga kudhibiti hali hiyo na tutaendelea kudhibiti hali hiyo ili tusije tukapata tatizo hilo la kuwa na nzige hapa nchini kwetu. Ahsante sana.