Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Questions to the Prime Minister from Hon. Venance Methusalah Mwamoto (5 total)

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Serikali ya utawala wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ilitimiza malengo yake ya kusaidia kupigania uhuru nchi za Afrika na hivyo kupelekea nchi zote kupata uhuru; nchi hizo wakati zikiwa hapa zilijenga makambi ambayo yalitumika kwa ajili yao katika sehemu tofauti; na kwa kuwa makambi hayo yametumika baada ya kuondoka kama Vyuo na Sekondari na pia kufanya wao waendelee kukumbuka kwa yale ambayo tumeenzi:-
Ni lini Serikali sasa, itabadilisha makambi ya wapigania uhuru hawa ambayo yametumika kama Magereza na matumizi mengine yasiyofaa, ili waendelee kukumbuka sehemu ambazo walikaa kwa ajili ya kupigania uhuru wetu?
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la kwanza kabisa la Mheshimiwa Mwamoto, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba nchi yetu ilishiriki sana kuwakaribisha wapigania uhuru wa nchi mbalimbali, kuendesha harakati zao za kisiasa hapa nchini. Maeneo yote waliyokuwa wamekaa, waliweza kujenga miundombinu mbalimbali na yanatambulika kama makambi ya wapigania uhuru.
Katika kumbukumbu zangu, Morogoro kuna eneo linaitwa Dakawa ambalo sisi tunatumia kama Sekondari, lakini pia Mazimbu pale kwenye Compus ya SUA na maeneo mengine, nakumbuka kule Nachingwea kuna eneo la Matekwe na eneo lile lililotumika ni kama vile Pashule; na kuna eneo pale Msata, hapa jirani Chalinze pale ambako jeshi linatumia sana kama sehemu ya mazoezi. Pia kuna makambi mengine, nakumbuka nikiwa Naibu Waziri nilikuja kwako Kilolo, eneo moja kati ya maeneo ya makambi pale Kilolo ndiyo wanatumia kama Magereza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa maeneo haya baada ya kuwa shughuli za wapigania uhuru kumaliza kazi zao, Serikali ilifanya maamuzi kutumia miundombinu ile kwa shughuli mbalimbali ikiwemo elimu. Eneo lingine kama hilo la Msata, Jeshi na pale Kilolo, Magereza. Maeneo hayo yote, kutokana na nature ya miundombinu iliyopo, maamuzi haya yalifanywa ili kutumia kwa umuhimu wa mahitaji ya nchi. Kwa hiyo basi, eneo kama Kilolo ambalo limetumika kama Magereza, suala la Magereza siyo suala la matumizi yasiyokuwa muhimu, ni muhimu pia kwa sababu ni sisi wenyewe ndio tunaenda kuishi pale na ni maeneo ya mafunzo, lakini pia ni eneo ambalo tunawahifadhi wale ambao wamepatikana na hatia kadhaa na kwenda kutunzwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, pale ambako tumetumia miundombinu ile kwa shughuli nyingine nje ya elimu, basi napenda kutumia nafasi hii kuwasihi Halmashauri za Wilaya, pamoja na wananchi kujenga miundombinu mingine kwa ajili ya kutumia kwa matumizi ya elimu na haya maeneo mengine yanayotumika kwa elimu yataendelea kutumika kama ambavyo imepangwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kumbukumbu hizi sasa ukiangalia kwa sehemu kubwa, makambi yale yote yaliyotumika, mengi sana yanatumika ni kwa matumizi ya elimu zaidi na maeneo machache ndiyo kama hayo mawili niliyoyataja, kule Msata na Kilolo ndipo ambako yanatumika kwa Jeshi pamoja na Magereza. Yote haya ni mambo muhimu kwetu sisi, ni lazima tutumie miundombinu ile ili pia badala ya kuwa tumeyaacha tu, bora yatumike ili huduma mbalimbali ziweze kutolewa katika maeneo hayo.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO:
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Serikali ya utawala wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ilitimiza malengo yake ya kusaidia kupigania uhuru nchi za Afrika na hivyo kupelekea nchi zote kupata uhuru; nchi hizo wakati zikiwa hapa zilijenga makambi ambayo yalitumika kwa ajili yao katika sehemu tofauti; na kwa kuwa makambi hayo yametumika baada ya kuondoka kama Vyuo na Sekondari na pia kufanya wao waendelee kukumbuka kwa yale ambayo tumeenzi:-
Ni lini Serikali sasa, itabadilisha makambi ya wapigania uhuru hawa ambayo yametumika kama Magereza na matumizi mengine yasiyofaa, ili waendelee kukumbuka sehemu ambazo walikaa kwa ajili ya kupigania uhuru wetu?
WAZIRI MKUU:
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la kwanza kabisa la Mheshimiwa Mwamoto, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba nchi yetu ilishiriki sana kuwakaribisha wapigania uhuru wa nchi mbalimbali, kuendesha harakati zao za kisiasa hapa nchini. Maeneo yote waliyokuwa wamekaa, waliweza kujenga miundombinu mbalimbali na yanatambulika kama makambi ya wapigania uhuru.
Katika kumbukumbu zangu, Morogoro kuna eneo linaitwa Dakawa ambalo sisi tunatumia kama Sekondari, lakini pia Mazimbu pale kwenye Compus ya SUA na maeneo mengine, nakumbuka kule Nachingwea kuna eneo la Matekwe na eneo lile lililotumika ni kama vile Pashule; na kuna eneo pale Msata, hapa jirani Chalinze pale ambako jeshi linatumia sana kama sehemu ya mazoezi. Pia kuna makambi mengine, nakumbuka nikiwa Naibu Waziri nilikuja kwako Kilolo, eneo moja kati ya maeneo ya makambi pale Kilolo ndiyo wanatumia kama Magereza.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa maeneo haya baada ya kuwa shughuli za wapigania uhuru kumaliza kazi zao, Serikali ilifanya maamuzi kutumia miundombinu ile kwa shughuli mbalimbali ikiwemo elimu. Eneo lingine kama hilo la Msata, Jeshi na pale Kilolo, Magereza. Maeneo hayo yote, kutokana na nature ya miundombinu iliyopo, maamuzi haya yalifanywa ili kutumia kwa umuhimu wa mahitaji ya nchi. Kwa hiyo basi, eneo kama Kilolo ambalo
limetumika kama Magereza, suala la Magereza siyo suala la matumizi yasiyokuwa muhimu, ni muhimu pia kwa sababu ni sisi wenyewe ndio tunaenda kuishi pale na ni maeneo ya mafunzo, lakini pia ni eneo ambalo tunawahifadhi wale ambao wamepatikana na hatia kadhaa na kwenda kutunzwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, pale ambako tumetumia miundombinu ile kwa shughuli nyingine nje ya elimu, basi napenda kutumia nafasi hii kuwasihi Halmashauri za Wilaya, pamoja na wananchi kujenga miundombinu mingine kwa ajili ya kutumia kwa matumizi ya elimu na haya maeneo mengine yanayotumika kwa elimu yataendelea kutumika kama ambavyo imepangwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kumbukumbu hizi sasa ukiangalia kwa sehemu kubwa, makambi yale yote yaliyotumika, mengi sana yanatumika ni kwa matumizi ya elimu zaidi na maeneo machache ndiyo kama hayo mawili niliyoyataja, kule Msata na Kilolo ndipo ambako yanatumika kwa Jeshi pamoja na Magereza. Yote haya ni mambo muhimu kwetu sisi, ni lazima tutumie miundombinu ile ili pia badala ya kuwa tumeyaacha tu, bora yatumike ili huduma mbalimbali ziweze kutolewa katika maeneo hayo.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Spika, nami naomba nimuulize swali Mheshimiwa Waziri Mkuu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa moja ya sababu ambazo zilipelekea wananchi wengi kutoa ridhaa kwa Serikali ya Chama cha Mapinduzi kuongoza ilikuwa ni ahadi nzuri ambazo zilitolewa. Pamoja na kuwa ahadi hizo nyingi zimeanza kutekelezwa lakini kulikuwa kuna kilio kikubwa sana cha wafanyakazi kwa ujumla kutokana na malimbikizo ya madeni na mishahara yao na hasa walimu. Serikali inasemaje kuhusu suala hili ili waweze kupata moyo wa kuona kweli zile ahadi ambazo walipewa na mgombea wa Chama cha Mapinduzi zimetekelezwa?
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Venance Mwamoto Mbunge wa Kilolo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali tunao watumishi wengi walimu wakiwemo na kama watumishi kwa sababu wanafanya kazi zao za kila siku na nyingine zinahitaji kulipwa malipo ya ziada mbali na malipo ya mshahara, nikiri kwamba tunadaiwa na watumishi wetu ikiwemo na walimu pia. Hata hivyo, Serikali yetu imeahidi kumaliza kwa kiasi kikubwa kero hii ya madeni kutoka kwa watumishi wetu wa Serikali walimu wakiwemo. Hatua ya awali ambayo tumeichukua ni kufanya mapitio ya madeni yetu yote tunayodaiwa na watumishi ikiwemo na walimu.
Mheshimiwa Spika, madeni ya walimu yote yalishakusanywa na yalihakikiwa kwanza na Wakaguzi wa Ndani wa kila Halmashauri mahali walipo lakini madeni yale pia yameendelea kuhakikiwa na Mkaguzi Mkuu wa Serikali kwa maana ya timu ambayo imeundwa pamoja na Wizara ya Fedha ili kuona uhalali wa madeni hayo baada ya kuwa tumegundua kuwa baadhi ya madeni yamepandishwa kwa kiasi kikubwa ambayo sio halali. Kwa hiyo, kila hatua tunayoifikia ya kukusanya madeni na kuyahakiki tukishapata kiwango tunaendelea kulipa. Kwa hiyo, Serikali imeendelea kulipa madeni ya wafanyakazi na inataka iwahakikishie wafanyakazi kwamba madeni yao yatalipwa na hiyo ndiyo stahili yao na kwa sababu tumeanza kulipa, tunaendelea kulipa kadri ambavyo tunamaliza kuhakiki ili tuweze kuondokana na madeni haya. Pia Serikali haijaishia hapo. Tumeweka utaratibu wa kudhibiti uzalishaji wa madeni kwa watumishi wetu na kusisitiza watu wafuate Kanuni na taratibu za eneo linazozalisha madeni ili tuweze kuondoa madeni ambayo sio muhimu wakati mwingine. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini nataka nitumie nafasi hii pia kusema kwamba baadhi ya madeni ambayo hayana viwango vikubwa yanaweza kulipwa kwenye Halmashauri zenyewe mbali ya kulipwa na Serikali Kuu. Lazima nimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Arusha ambaye kupitia mapato yake ya ndani na kupitia Baraza lake la Madiwani waliweza kulipa madeni ya watumishi wao hasa walimu ya zaidi ya shilingi milioni mia moja na zaidi. Kwa hiyo, mfano huu ni mzuri kwa Wakurugenzi wengine kwenye Halmashauri nyingine ili kuondoa kero kwenye maeneo yao. Wanaweza kutenga fedha kupitia mapato yao ya ndani kulipa watumishi wao wakiwemo walimu ili kuondokana na ule mlolongo ambao tunatakiwa tuuhakiki. Wakishahakiki wakijiridhisha na hasa baada ya kuwa tumedhibiti madeni na wao wanaweza kuruhusu kazi fulani zifanywe, wazitengenezee bajeti ili waweze kulipa moja kwa moja kuondokana na kero zinazoweza kupatikana kwa wafanyakazi.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Spika, naomba niulize swali moja. Nchi yetu imepata bahati ya kuandaa Mashindano ya Vijana ya Afrika (AFCON). Kwa sababu kutakuwa na wageni wengi akiwemo Rais wa Mpira wa Dunia na wageni tofauti ambao wanakuja kuangalia wachezaji wa nchi mbalimbali, kwa hiyo, tutakuwa na ugeni wa kutosha, nilitaka kujua tumehusishaje mashindano haya na utalii wa nchi yetu ili kuutangaza na kuwafanya wageni hao wawe mabalozi watakaporudi kwao? Pia mmehusishaje na Wizara ya Mambo ya Ndani kuhakikisha kwamba…

SPIKA: Swali moja tu.

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Kuhakikisha kwamba usalama unakuwepo? Naomba nijibiwe swali hilo.
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwamoto, Kocha wa Timu yetu ya Bunge, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza, nataka nitumie nafsi hii kuipongeza Wizara ya Habari, Utamaduni, Michezo na Sanaa, kwa kazi nzuri waliyofanya ya ushawishi kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani ili kuleta mashindano haya kwetu nchini Tanzania. Pongezi hizi pia zifikie chombo chetu au Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania kwa jitihada zake za kuratibu vizuri jambo hili kutoka tulipopata dhamana hiyo mpaka hatua tuliyoifikia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Tanzania kupitia Serikali hii ya Awamu ya Tano imeridhia mashindano hayo kufanyika hapa Tanzania na yanafanyika mwaka huu wa 2019. Katika mashindano hayo vijana wetu wanapata fursa ya kushiriki kutoka ngazi ya awali mpaka fainali kama timu zetu zitafika fainali na ndiyo tunaomba taimu yetu ifike fainali ili sisi kama mwenyeji tuweze kufika kwenye fainali na ikiwezekana pia tuchukue kombe la dunia. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Serikali imejiandaa kupokea wageni wote wanaokuja kushiriki mashindano haya hapa nchini na inaendelea na maandalizi hayo kwa kushawishi sekta zote zitakazonufaika na uwepo wa wageni hao kuja hapa nchini kujiandaa. Vikao mbalimbali vinafanywa na Wizara pamoja na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania na wadau mbalimbali wanashirikishwa na Serikali tunajua kazi kubwa inayoendelea kufanywa na tunatambua kwamba tutapokea wageni wengi akiwemo Rais wa FIFA hapa nchini na tunaendelea kujenga mazingira kuwapokea wageni wengi zaidi kadri watakavyopatikana. Huduma tunazo, tunazo hoteli, maeneo ya kutoa vyakula lakini pia usafiri wa ndani tunao, kwa hiyo, ni maeneo ambayo tumeendelea kuimarisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia kupitia mashindano haya tumehamasisha mikoa ya jirani na maeneo ambako viwanja vitatumika na tunaambiwa viwanja vitatu vitatumika wakati wote wa mashindano Dar es Salaam na maeneo mengine, Shirikisho la Mpira litatupa taarifa baada ya kuwa wamekamilisha maandalizi, kwa hiyo, pia na mikoa hiyo nayo itaweza kunufaika. Kwa hiyo, maandalizi ya maeneo yote hayo yanaendelea kufanywa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kupitia swali la Mheshimiwa Mbunge niwahakikishie Watanzania kwamba ujio huu kwetu ni muhimu sana. Kwa hiyo, sote tunatakiwa tushirikiane kuhakikisha kwamba tunapata mafanikio kwa wageni hawa kuingia, kuishi hapa na kurudi makwao wakiwa salama. Kwa hiyo, ni jukumu letu kuhakikisha kwamba tuko salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia Shirikisho la Soka Tanzania liendelee kuimarisha maandalizi ya timu yetu ambayo itashiriki kwenye mashindano haya ili hatimaye tuweze kuibuka kidedea. Sisi Watanzania wote tunawajibika sasa kuonesha uzalendo kwa timu yetu itakayofanikiwa kuingia ili kuipa moyo. Kwa hiyo, mchango wa kila mmoja wa namna yoyote ile unahitajika katika suala hili. Kwa hiyo, niwahakikishie Watanzania kwamba mashindano tunayapokea, tuko tayari kuwapokea wageni wake na tutaendelea kushindana kwa sababu na sisi tuna timu ambayo itashindana na naamini tutafanikiwa. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Spika, hivi karibuni nchi yetu ilipata heshima kubwa ya kuandaa mashindano ya AFCON, lililotokea Watanzania wote wameshuhudia lakini tumejifunza mambo mengi. Sasa kwa kuwa tumepata heshima nyingine tena ya kuandaa mashindano ya watu wenye ulemavu ya Afrika Mashariki. Je, Serikali sasa inasemaje ili watuondoe kimasomaso?
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Venance Mwamoto, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba nchi yetu sasa tumeanza kushuhudia na kuona mwamko wa Watanzania kushiriki katika michezo mbalimbali. Pamoja na mwamko huu tuliokuwa nao tumeanza kuona pia hata mashirikisho mbalimbali duniani na Afrika wanaendelea kututambua Watanzania na kutupa heshima ya kuendesha mashindano mbalimbali. Leo hii nchini tunayo mashindano ya vijana wetu wa umri chini ya miaka 17 yanaendelea nchini na sisi tulipelekea timu yetu, hatujafanya vizuri lakini tumejifunza mambo mengi kupitia mashindano haya.

Mheshimiwa Spika, pia nafurahi kusikia kwamba nchi yetu pia imepata heshima ya kuendesha Mashindano ya Walemavu ya Afrika Mashariki. Jambo hili kwetu kama Tanzania ni tunu kwa sababu tunaanza kuona mashirikisho mbalimbali ya michezo duniani na Afrika yakitupa hadhi ya kusimamia mashindano hayo, maana yake ni nini? Maana yake nchi yetu inatambulika au kwa upande wa usalama au uwezo wa kusimamia pia inatutengenezea fursa kwa Watanzania kutumia mashindano hayo kuboresha pia masuala ya uchumi. Hili litatufanya pia na sisi sasa tuondoke hapa tulipo kimichezo katika michezo mbalimbali na tuweze kufikia hatua nzuri ya kuweza kushindana mpaka ngazi ya dunia.

Mheshimiwa Spika, mashindano ambayo yanaendelea na hayo ambayo yatakuja, tutaendelea kujifunza na kuandaa vizuri timu zetu za ndani zinapokwenda kushiriki zipate kombe lililotarajiwa na ambalo tumeletewa hapa nchini ili tuweze kuboresha. Vile vile Serikali sasa tumeanza kusimamia michezo hii ikichezwa kutoka umri mdogo kwenye shule za msingi na sekondari, kwenye vyuo ili kuweza kupata kuunda timu za Kitaifa ambazo sasa tunaanza kuona mwelekeo huo mkubwa. Hiyo ndiyo ilifanya hata mashindano haya ya vijana wa umri chini ya miaka 17 kuruhusu vijana wote wa shule za msingi, sekondari walioko likizo na Watanzania wote kuingia bure kwenda kushuhudia michezo inayochezwa kwa lengo la kujifunza zaidi kwenye michezo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo hadhi na heshima ambayo tunaipata Serikali ni pamoja na kupata fursa za kuongeza uchumi, kutangaza nchi, kuboresha sekta ya utalii na kila mmoja hasa watoa huduma kupata fursa ya kuweza kutoa huduma. Nitoe wito kwa Watanzania, tuanze sasa kuona michezo kuwa ni fursa kwetu na tuendelee kuungana pamoja kuhakikisha kwamba michezo inachezwa katika maeneo yote na michezo yote, tuunde vilabu, tuvisimamie vizuri, viingie kwenye mashindano na kila shirikisho la kila mchezo lishawishi kwenye ngazi yake ya Afrika, ngazi ya Dunia michezo iweze kuchezwa hapa ili fursa zile sasa ziwewe kunufaisha Watanzania. Kwa hiyo kwa kupitia michezo sasa Serikali na Watanzania tunaweza kunufaika zaidi. Ahadi ya Serikali kwenye hili ni kusimamia michezo. Ahsante sana.