Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Additional Questions to the Prime Minister from Hon. Jaku Hashim Ayoub (1 total)

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na mimi niendelee kumshukuru Waziri Mkuu kwa umakini wake wa hali ya juu kujibu suala hili nililomuuliza. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini Mheshimiwa Waziri Mkuu hii imekuwa kama miongo ya mvua za masika. Ni sababu gani hasa Serikali kuwa haijajipanga kuonekana tatizo hili likafika pahala likamaliza kabisa suala la sukari?
Baada ya miezi mitatu, sita atakuja kiongozi mwingine atasahau kuhusu suala hili, kwa hiyo, Serikali ikajipange na suala hili, wananchi ndio muhimu na mlikuwa mkipiga kelele kuwa mtawajali wananchi, Serikali haiogopi hasara kwa ajili ya wananchi wake ni hilo tu Mheshimiwa.
SPIKA: Mimi naona kilichotolewa ni ushauri tu, lakini kwamba haijajipanga tusubiri ripoti ni ushauri tu.