Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Shamsi Vuai Nahodha (1 total)

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Wilaya ya Lushoto inatumia x-ray ya zamani na pia ni ndogo haina uwezo. Je, ni lini Serikali itapeleka x-ray ya kisasa (digital x- ray) ili kuondoa adha wanayoipata wagonjwa?
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuboresha huduma za x-ray. Kama alivyokuwa amesema katika swali lake la msingi, ni kweli tulikuwa na x- ray pale lakini katika mkataba huu ambao tunao na Philips lengo letu sasa ni kuziondoa zile x-ray za zamani na kuweka x-ray mpya; na tutalizingatia hilo kwamba mgao huu mpya utakapokuja basi na Hospitali ya Lushoto nayo iweze kuwa katika sehemu zile ambazo zitapata.

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa swali lako la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ina mkataba wa utoaji wa huduma za x-ray nchi nzima kwa kupitia kampuni hii ya Philips.