Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Godbless Jonathan Lema (2 total)

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kikwazo kikubwa sana cha biashara kuendelea katika Taifa letu ni riba kubwa inayotolewa na mabenki ya biashara ambayo sababu yake ni kiwango kilichowekwa na Benki Kuu ya Tanzania.
Je, Serikali ina mpango gani dhidi ya kusaidia wafanyabiashara dhidi ya riba kuwa inayotolewa na mabenki, kikwazo hicho ambacho BOT ndiyo imekuwa msingi mkubwa ili kuwezesha watu wengi kufanya biashara zenye sura ya miradi na siyo biashara za uchuuzi?
WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Benki Kuu itaendelea kusimamia sekta ya fedha ili kuhakikisha kwamba riba zinapungua na ndiyo maana katika mapendekezo ya Mpango tulioleta, moja ya hatua ambazo Serikali inachukua ni kuhakikisha kwamba, taasisi za umma sasa zinafungua akaunti Benki Kuu ili tuhakikishe kwamba fedha nyingi ambazo zilikuwa zinatumika na mabenki kwa ajili ya kufanya bashara, fedha za Serikali bila Serikali yenyewe kupata faida, sasa zinaweza zikatumika ili hayo mabenki sasa yaende huko kwa kupeleka huduma kwa wananchi vijijini. Hii ni hatua mojawapo ya kusaidia kupunguza riba ili wananchi wetu waweze kunufaika zaidi.
MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, ripoti ya UNDP inatahadharisha kwamba vita nyingine ya ulimwengu katika siku zinazokuja itakuwa ni maji, pamoja na chakula na kwa sababu, umeme unaotumia mionzi ya jua umethibitika kote ulimwenguni kwamba ni umeme muafaka, ni kwa nini Serikali sasa isi-concentrate kwenye umeme huu, ambao katika Taifa letu la maeneo mengi sana, ambao ni almost…

MWENYEKITI: Swali Mheshimiwa Lema.

MHE. GODBLESS J. LEMA: Swali langu ni kwa nini Serikali isi-concentrate sasa, kwenye umeme huu na ikaachana na umeme wa maji ambao sehemu kubwa inakwenda kuleta uharibifu wa mazingira.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Godbless Lema kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake, amejielekeza, kwa nini Serikali isijielekeze zaidi kwenye umeme huu, unaotokana na jua, kwenye jibu letu la msingi tumeainisha jitihada ambazo Serikali imefanya. Tumesema kutokana na Power System Master Plan yetu kwamba tunatakiwa tuzalishe zaidi ya MW 350 kwenye Power System Master Plan na nikaeleza kwamba hata kazi yenyewe imeanza, TANESCO wametangaza Tender kwa ajili ya MW zaidi ya 200 kwenye upepo na 150 kwenye jua, lakini ukiacha mradi huu wa Kishapu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, Serikali imejielekeza kuhakikisha kwamba nishati jadidifu ina mchango mkubwa katika kuzalisha umeme, licha tu ya kwamba umeme wa jua, lakini kuna umeme wa makaa ya mawe ambao tumetangaza wa MW 600, licha ya huo pia umeme unaotokana na jotoardhi, tunatarajia kuzalisha MW 200, katika kipindi hiki, hii Power System Master Plan.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile amesemea kwenye miradi ya maji, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, tafiti zimefanyika za kina kuainisha sustainability ya miradi yote ya umeme inayotokana na miradi ya maji, lakini kwa kutambua miradi ya umeme, inayozalishwa kwa maji na gharama nafuu, zaidi zinatumika shilingi 36 kulinganisha na umeme wa upepo ambao ni shilingi 103; umeme wa jua, shilingi 103 kwa per unit kilowatts; lakini pia umeme unaotokana na makaa ya mawe 108. Kwa hiyo masuala haya ni zaidi kulinganisha gharama kwa sababu nia ya Serikali ni kumpatia Mtanzania umeme wa gharama nafuu na wa uhakika. Ahsante sana.