Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Ali Salim Khamis (4 total)

MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri amesema hapa kwamba shida ni watu ambao wamewasababishia wafanyakazi hawa ambao wanafanya kazi zao kwa nia ya dhati ya kuitumikia nchi yao. Naomba Waziri atoe commitment ni lini wafanyakazi wote hasa wa Idara ya Uhamiaji ambao wameanza kazi zaidi ya miezi mitano sasa, hawajalipwa mshahara hata mwezi mmoja, , watalipwa malimbikizo yao ya mishahara mara moja?
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba commitment ya Serikali. Ahsante.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwanza kabisa niunge mkono majibu ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Sasa hivi inapotokea ajira mpya siyo kwamba hawajalipwa kwa miezi minne.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyoeleza; kulikuwa na ajira mpya za Maafisa Uhamiaji 297, Maafisa wa Utumishi wa Idara ya Uhamiaji ni lazima wafanye higher action katika mfumo wetu wa taarifa za kiutumishi na mishahara, walikuwa hawajafanya. Kwa hiyo, ingekuwa ni vigumu wao kuweza kulipwa. Kwa mwezi huu tayari tunaendelea vizuri watakuwa wameshalipwa. Pia kuhusiana na masuala ya malimbikizo mara tu Maafisa Utumishi wa Uhamiaji watakapokuwa wamefanya hizo higher action na pending salaries arrears automatically katika mfumo wataweza kulipwa mara moja.
MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa katika umiliki wa Benki Kuu ya Tanzania, Zanzibar imeainishwa wazi kwamba inamiliki asilimia 12, ni vipi leo Waziri anatuambia Shirika hili la Jamhuri ya Muungano kati ya Zanzibar na Tanzania Bara au Tanganyika, haikuainishwa asilimia za umiliki wa Shirika hili. Je, siyo njia ile ile ya kuendelea kuinyonya Zanzibar na kuinyang‟anya haki zake?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili…
SPIKA: Mheshimiwa kabla maswali yako hayajaendelea, una chanzo cha hizo asilimia zinazonyonywa, una reference yoyote au ni mawazo yako wewe?
MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Spika, amesema Naibu Waziri hapa kwamba Shirika linamilikiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano kwa asilimia 100, Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano, lazima tujue asilimia zinazomilikiwa na Serikali ya Zanzibar, tujue Wazanzibari haki zetu zi zipi, kama ilivyoainishwa katika Benki Kuu kwamba Zanzibar inamiliki Benki Kuu kwa asilimia 12.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo swali langu namwomba Waziri asikwepe hili suala, atuainishie hisa za Zanzibar ni kiasi gani katika ATCL kwa sababu hapo mwanzo Shirika hili lilikuwa ni ATC na wamiliki walikuwa ni hao hao Serikali, kwa hiyo imetoka Serikali halafu ikajibinafsishia Serikali… (Makofi)
SPIKA: Swali la pili!
MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Spika, swali la pili, Naibu Waziri amesema kwamba deni la kutua kwa ndege ya ATCL, kwa muktadha ule ule wa kuinyang‟anya Zanzibar haki zake, ndege hii inatua katika viwanja vya ndege vya Zanzibar na hailipi kodi na hapa Mheshimiwa Naibu Waziri ametaja deni ambalo lipo, lakini bado anatuambia kwamba mpaka CAG alihakiki wakati wanajua kwamba walikuwa wanatua Zanzibar na hawalipi kodi…
SPIKA: Swali ni nini?
MHE. ALI SALIM KHAMIS: Ni lini deni hili litalipwa kwa Serikali ya Zanzibar haraka iwezekanavyo, kwa sababu deni hili ni la siku nyingi? Ahsante
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, siyo Serikali ya Tanganyika. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ina uwezo wa kumiliki na ndiyo maana inamiliki hisa asilimia 100 za ATCL ambayo tuliibinafsisha huko nyuma na sasa tumeirudisha na tunataka kuirekebisha zaidi.
Mheshimiwa Spika, kuhusu deni, tumelitaja, haya madeni ni ya siku nyingi, ni ya Shirika ambalo lilishakufa, ATC, sasa tuko kwenye kampuni ATCL, lakini tunasema deni hili likishahakikiwa, litalipwa na ndege za ATCL zitakapoendelea kutua landing fee ya kila kiwanja italipwa.
MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Ni lini Wizara itakuja Wilaya ya Mkalama kutugawia ramani mpya Wabunge na viongozi husika na kutuonyesha mipaka ya Wilaya kwa Wilaya ili kuepusha migogoro inayoendelea sasa na inayosababisha uvunjifu wa amani kama ambavyo imejitokeza katika Jiji la Dar es Salaam?
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimwa Allan ametaka kujua ni lini Wizara itagawa ramani kama ilivyofanya Dar es Salaam ili kuweza kuepusha uvamizi katika maeneo hayo? Naomba nirudie tena kusema kwamba zoezi hili limefanywa na Wizara kwa kuanzia Dar es Salaam lakini lengo la kufanya kwa kila Mkoa na kila Halmashauri inao wajibu wa kutoa ramani hizi kwa Wenyeviti wake ili waweze kulinda maeneo yao siyo kwamba Wizara itakwenda katika kila Halmashauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nirudie tena kusema kupitia katika Bunge lako hili kwamba Halmashauri zote zinatakiwa kusimamia zoezi hili na hasa katika maeneo ambayo migogoro imekuwa mingi katika maeneo ya mjini ambapo viwanja vimevamiwa ovyo ovyo ili waweze kuona ni jinsi gani wataweza kutawanya ramani hizo ili watu waweze kulinda maeneo yao. Kama kuna tatizo pengine katika uelimishaji wa kusoma zile ramani basi Wizara inaweza ikasaidia kutoa wataalam kwenda kushirikiana na Halmashauri kuwafanya hawa watu waweze kusoma ramani vizuri na kuweza kuyalinda maeneo yao. Kwa hiyo, nizitake tu Halmashauri ziweze kufanya kazi hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, anasema ni lini tutakwenda kwa ajili ya kubainisha mipaka ambayo ipo…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, swali la nyongeza lazima liwe moja, kama yalikuwa mawili, basi umeshamaliza kujibu hilo moja. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Ndiyo Mheshimiwa Naibu Spika.
MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nimuulize Waziri maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyosema Waziri kwamba mfumo wa vyama vingi ni mfumo wa kidemokrasia. Kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa Tanzania inaelezwa kwamba ni haki ya kila chama kufanya kazi zake za kisiasa wakati wote kwa kutumia sheria na kanuni ambazo zimewekwa. Je, ni kwa nini Serikali imezuia harakati na mikutano ya kisiasa ili vyama visifanye kazi yake?
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ni kwa nini Msajili anaingilia mwenendo wa vyama vya siasa hali ya kuwa vinafanya kazi zake kikanuni, kikatiba kwa kufanya maamuzi kupitia Ofisi ya Msajili na kukataa maamuzi ya vikao halali vya vyama vya siasa kama vile Chama cha Wananchi (CUF). Naomba Mheshimiwa Waziri atuambie ni sheria ipi ambayo inampa mamlaka hayo Msajili ya kutengua vikao halali vya chama ambavyo vimefanywa kwa mujibu wa kanuni na katiba na sheria za nchi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA, NA AJIRA (MHE. ANTONY P. MAVUNDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na la kwanza, si kweli kwamba Serikali imezuia harakati za kisiasa. Kama ambavyo yamekuwa yakijibiwa humu ndani bungeni, umewekwa utaratibu maalum wa kufanya siasa kutokana na sheria mbalimbali hasa ambazo zinaongoza utaratibu wa vyama vya siasa kushughulika katika shughuli za kisiasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme tu kwamba Serikali haijakataza vyama kufanya harakati za kisiasa lakini zimeruhusu vyama kufanya harakati za kisiasa kwa mujibu wa taratibu na sheria ambazo zimewekwa katika nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, Msajili wa Vyama vya Siasa kwa mujibu wa sheria; ukisoma Sheria ya Vyama vya Siasa Sura namba 258 iliyorejewa mwaka 2002 na sheria ya vyama vya siasa iliyofanyiwa mabadiliko namba 7 ya mwaka 2009 inampa mamlaka Msajili kama mlezi wa vyama vya siasa kuhakikisha anavilea vyama vya siasa na pale panapotokea matatizo awe sehemu ya kusaidia kurudisha harmony katika vyama vya siasa akiwa kama mlezi wa vyama vya siasa.