Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to supplementary Questions by Hon. CAN.RTD Ali Khamis Masoud (1 total)

MHE. ZITO Z. KABWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati mchakato wa bajeti mpya ya Serikali ya Mwaka 2018/2019 unaendelea, kumekuwa na taarifa kwamba Serikali sasa inajiondoa katika mfumo wa conditional cash transfer, yaani kwenda kuwapa fedha wananchi na inaanzisha mfumo tofauti. Baadhi ya mikataba ambayo Wizara ya Fedha ilikuwa iingie na baadhi ya nchi wafadhili ikiwemo Benki ya Dunia, Wizara ya Fedha imesitisha kusaini kwa sababu Serikali haitaki tena kuendelea kutoa hizi conditional cash transfer. Tunaomba taarifa rasmi ya Serikali ndani ya Bunge kuhusiana na jambo hili.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kama Waziri mwenye dhamana ya TASAF sina taarifa ya Serikali sasa hivi kujiondoa katika kuwapelekea hizi fedha. Taarifa nilizonazo ni kwamba sasa hivi tunafanya utafiti wa hizi fedha. Badala ya watu kwenda kupanga foleni pale wilayani kila siku tunaangalia uwezekano wa kupekea fedha zao kwa njia ya simu ili kuwaondolea usumbufu wa kwenda wilayani. Hilo ambalo anasema Mheshimiwa Zitto Kabwe kama analisema liko njiani, lakini halijafika mezani kwa Waziri mwenye dhamana ya TASAF. (Makofi)