Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Livingstone Joseph Lusinde (36 total)

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mungu kwa kupata muda, lakini mimi siyo wa kuzungumza dakika chache ila nitajitahidi maana mara nyingi huwa napiga hapa nusu saa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Dkt. Mpango kwa kuleta taarifa nzuri. Nianze na suala la viwanda mimi nizungumzie kilimo cha biashara. Ni vema Serikali ikajikita kwenye kuanzisha viwanda vidogo ili wakulima hasa wa matunda, badala ya makampuni yanayotuuzia juice kununua juice nje ya nchi, yanunue matunda yetu ya ndani. Tukifanya hivyo tutakuza na tutakuwa na kilimo cha biashara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niseme watu wamekuwa wakizungumza sana humu ndani ya Bunge, wanazungumza kuhusu Polisi kuingia humu ndani. Nataka leo nisimame kuwatetea Polisi kwa sababu wao hawawezi kuja humu. Polisi ukimwona mahali popote kaenda kama Field Force, ujue ameitwa na watu wa eneo hilo. Wabunge, tuache tabia ya kuwaita Polisi, ukifanya fujo unawaita Polisi, na Polisi wameshaingia Kanisani wakati wa mgogoro ule wa Dayosisi ya Pare, Polisi wameshaingia Msikitini wakati wa fujo, Polisi wameshaingia Bungeni baada ya Wabunge wa Upinzani kuanzisha fujo. (Makofi)
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ukimwona Polisi kaingia mahali ujue kaitwa, na kama ninyi ni wageni hamuelewi utaratibu wa humu ukianzisha fujo umeita Polisi. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua kuna watu wamekuja hapa bado hawajapigwa semina, kwa hiyo ngoja leo niwaelimishe. Mmesema vizuri na mfano uliotolewa na Mheshimiwa Heche hapa mdogo wangu ambaye mimi nimemfundisha siasa, kwamba eti anataka kulinganisha Chama hiki na kina Hitler, lakini leo nawaambia Chama chochote cha Upinzani duniani kikishindwa kushinda uchaguzi katika vipindi vitatu, kinageuka kuwa chama cha kigaidi, ndiko wanakoelekea hawa. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa ndipo wanapoekelea, maana kinakuwa chama sugu, kinakuwa Chama cha Upinzani sugu, tulikubaliana wakati ule, kwamba ili kuthamini haki za binadamu walau kila chama kitakachoshinda basi kilete mtu mmoja walau mwenye ulemavu wa ngozi. Yupo wapi albino wao hawa? Wabaguzi hawa na inawezekana hata wakati ule wa mauaji wako inawezekana walikuwa wanahusika hawa, yuko wapi? CUF waliwahi kuleta hapa alikuwepo Mheshimiwa Barwany, CCM yule pale wa kwao yupo wapi hawa? (Makofi).
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumze hapa, kwamba usiwaone wanazungumza hivi na nataka nichukue fursa hii kumpongeza sana, nimpongeze sana Mzee Lowassa, Lowassa aligundua hawa wamemchafua sana akaamua kwenda kwao wamsafishe. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mzee Lowasa aligundua walimwita fisadi, walimwita fisadi papa, Edward Lowasa ana akili sana. Mchawi mpe mtoto amlee, akajua nakwenda kwao wanisafishe. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna Mtanzania mwenye akili atakayewasikiliza tena hawa, hivi wewe unakaa na jirani yako mwanaume anakuja anakwambia mke wako malaya, mke wako mhuni unamuacha, asubuhi anamuoa utamwamini tena? Hawa hawaaminiki, hakuna kitu watakachokieleza wakaaminiwa duniani. Kwa sababu wana ndimi mbili kama za nyoka hawa. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanachokisema leo kesho watakibadilisha hawa, ndimi mbili za nyoka…
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana mnawaona leo wanasema hiki, leo wanageuka hivi, nataka nichukue fursa hii kumpongeza Jecha, kwa utaratibu huu wa kila Mzanzibar kuwa Tume ya uchaguzi, Jecha alikuwa sahihi kufuta yale matokeo. (Makofi)
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kila mtu anajifanya Tume, wenyewe unaowaona hapa wameletwa baada ya Tume ya Uchaguzi kuwatangaza ila Mheshimiwa Seif wanamtangaza wao, hawa ni wanafiki wakubwa.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Lusinde, nakushukuru. Muda wako umekwisha.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kawaida yangu, nataka nimshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunijalia zawadi ya uhai, kunipa afya bora ili niweze tena kusimama kwenye Bunge lako na niweze kutoa mchango.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niweke sawa kumbukumbu, katika Bunge hili kuna Wizara tatu zinachangiwa kwa mfumo wa aina yoyote mchangiaji anayotaka. Wizara ya kwanza ni Ofisi ya Waziri Mkuu, unachangia kwa hoja zozote unazojisikia Mbunge. Wizara ya pili ni TAMISEMI, unapiga kokote Mbunge unakotaka kupiga; na ya tatu ni Finance Bill, kwa hiyo, kama mtu huelewi, Mbunge ukisimama Wizara hizo, usiache kitu! Kula moto, tema madini, watu watakusikiliza. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kumpongeza Waziri Mkuu, amefanya kazi kubwa tangu ameteuliwa kuwa Waziri Mkuu. Tuna uhakika kwamba Rais hajakosea kukupa kiti hicho Mheshimiwa Majaliwa na wala sisi Wabunge hatujakosea kukuidhinisha. Nakuomba sana Mheshimiwa Waziri Mkuu, katika Majimbo ya Waheshimiwa Wabunge wengi hapa Tanzania likiwepo la Mtera, kuna baadhi ya miradi imekuwa ya muda mrefu, imekuwa miradi sugu. Tufanye utaratibu wa kila Mbunge akuandikie ni mradi gani umechukua muda mrefu haujatekelezwa, tukuletee ili kuwe na bajeti maalum ya kuondoa viporo vya miradi iliyopita. Tukifanya hivyo, tutakufanya uanze sasa kutekeleza miradi mipya wakati umekamilisha ile miradi ya zamani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nilisema kwenye Bunge hili kwamba, ndugu zangu hawa wamechanganya mayai yote kwenye kapu moja, tupige. Nilizungumza nikiwa mahali hapa! Leo tumepiga, si mnaona biashara imekwisha?
Kwa hiyo, niwaambie tunampongeza sana Mheshimiwa Rais, kuna wengine wanasema anatafuta umaarufu; hivi ukimshinda mtu anayesema mafuriko hayazuiwi kwa mikono, wewe ukayazuia, unataka umaarufu gani tena? Mheshimiwa Dkt. Magufuli anatafuta umaarufu upi kama amekuwa binadamu wa kwanza duniani kuzuia mafuriko kwa mikono? Anatafuta umaarufu upi? Tuliwaeleza hawa na leo nataka niwathibitishie, nataka niseme na nchi, nataka niwaambie Watanzania kwamba hawa jamaa mliowapigia kelele, leo hii wameonesha wamefeli, hawana uwezo wowote hata ndani ya Bunge hawa! (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Rais. Leo wanasimama hapa, watu wa Dar es Salaam mnisikilize. Anasimama hapa Kiongozi wa Upinzani anasema, Rais anafanya makosa kuamrisha pesa zilizokuwa ziende kwenye sherehe zijenge barabara ya Morocco. Wapinzani wanasema ni makosa. Hivi watu wa Dar es Salaam mnawapendea nini hawa? Hawa watu hawataki maendeleo! Wanataka domo! Mnawaona, wanataka waonekane kwenye TV wanasema bajeti ile na hela za kutengenezea barabara ya Mwanza, wanataka tukupe Mheshimiwa Nape halafu urushe live TBC ili waonekane hawa. Kutengeneza barabara na kuonekana kwenye TV lipi bora jamani?
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme hapa na nazungumzia hapa kwenye ukurasa wa 11, 17 kipengele kinachohusu demokrasia. Someni hapo! Mheshimiwa Waziri Mkuu huwezi kukuza demokrasia kama una Wapinzani wa jinsi hii. Haiwezekani! Utakuzaje demokrasia katika nchi kama Wapinzani ulionao ni wa aina hii?
TAARIFA
MBUNGE FULANI: Taarifa Mwenyekiti! Mwenyekiti taarifa!
MWENYEKITI: Mheshimiwa Lusinde kaa!..
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka kumwonya mzungumzaji anayezungumza. Mimi ni Mbunge senior na mwenye jina kubwa kuliko wewe. Unaposema kwenye Bunge hili, unamtolea mtu taarifa; wewe kama unaweza kusema umeambiwa, sema; kama hujafukuzwa Chama! Simama useme humu! (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumzia kukua kwa demokrasia. Mimi hapa nataka leo nitoboe ndiyo maana nimesema leo najitoa muhanga. Katika maisha yangu nimewahi kuwa Kiongozi; Mjumbe wa Baraza Kuu la Uongozi la CHADEMA. Kule ndani kulikuwa na siri kubwa! Tulikuwa tumepanga siri wakati huo, niliyoikataa mimi, mpaka nikahama Chama hiki ya kuua Vyama vingine. CHADEMA wamefanikiwa kuua Vyama vyote hapa Tanzania.
Kwa hiyo, tunapozungumzia kukuza demokrasia tujue kwamba NCCR-Mageuzi ilikuwa na Wabunge watano na sasa ina Mbunge mmoja tu. Sijui ni maendeleo gani hayo? Wanaviua Vyama! Hawa wako kwa ajili ya kuua Vyama vingine! CUF walikuwa na Wabunge chungu nzima, sasa hivi Zanzibar sifuri. Hawa! Hawa wanaua Vyama vingine. Wanataka kubaki peke yao.
Kwa hiyo, nakuomba Msajili wa Vyama vya Siasa, endelea kusajili Vyama, ukifanya mchezo nchi hii demokrasia itakufa kwasababu kuna Chama kinataka kuhodhi Vyama vingine vyote viwe ndani yake. Hawa wanataka kufanya hivyo! (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, CCM huko nyuma tulikuwa na zidumu fikra za Mwenyekiti. Tumetoka, hawa wameingia huko. Hawa sasa hivi zidumu fikra za Mwenyekiti, ndiyo maana unaona kila wakiambiwa kitu, wanafanya. Jambo la aibu sana! Unasimama kwenye Bunge hili, unasema Serikali imevunja Katiba, haiko Kikatiba, Serikali hii imekosea, kwa hiyo, hatutasema, lakini posho wanachukua, hawa! Yaani kama ni Waislamu; kama una Muislamu anasema hali nguruwe, anakula maini tu, ndiyo hawa! Wanasema Serikali hii imekosea, haiko Kikatiba, lakini mishahara na posho wanachukua hawa. Hawako tayari kusema! (Kicheko/Makofi)
Kwa hiyo, nakuomba Mheshimiwa Waziri Mkuu, sasa nimegundua siyo tu tuna wafanyakazi hewa, tuna Wabunge hewa; hawa! Bunge hili lina Wabunge hewa! Nataka nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Nape. Wizara yako Mheshimiwa Nape ilikuwa haijawahi kuchangia maendeleo yoyote vijijini zaidi ya habari, tunasikia michezo lakini kwa mara ya kwanza, pesa ulizozizuia ambazo mmeshauri, sasa zinaelekea kuchimba visima vya maji. Tunakupongeza sana Mheshimiwa Waziri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wanataka maji, hawataki kumwona Mbunge kwenye TV. Tunafahamu wamepata political mileage sana kwa sababu ya kusema mambo ya hovyo, watu wanayasikia, lakini kwa sasa watatakiwa kwenda kufanya kazi na kutoka jasho ili wananchi wawakubali. Ofisi ya Waziri Mkuu inashughulika na TASAF. Kwenye TASAF kuna malipo hewa. Wako watu wamekufa, lakini wanaendelea kupokea zile hela kama ambavyo tuna Wabunge wamekufa, hawazungumzi Bungeni, lakini wanapokea hela. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wafanyakazi hewa wako wengi sana kwenye nchi hii, tuwashughulikie. Kuna watu hapo wanazungumza habari ya kumponda Rais kwamba anakurupuka kuchukua maamuzi. Rais, watu wote anaowafukuza na wanaosimamishwa ni kweli majipu. Kwa mfano, mchukulie ndugu yangu Kabwe. Mbunge wa Upinzani alisimama hapa, Mheshimiwa Wenje akasema Kabwe ni jipu hafai atolewe na hawa wakampigia makofi. Leo kasimamishwa, hawa wanasema anaonewa. Huwezi kuwaelewa hawa! (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu zangu wana-CCM pamoja na Waheshimiwa Mawaziri, kwa Baraza hili aliloliunda Mheshimiwa Rais, kule Mheshimiwa Majaliwa, pembeni Mheshimiwa Nape, kule kuna Mzee Handsome boy, hapa Mheshimiwa Mavunde, Mheshimiwa Jenista Mhagama; hawa hawachomoki, ndiyo maana mnaona wanapiga kelele! Mnawaona wanapiga kelele hawa, anazungumza habari ya shule wakati CHADEMA ilimsimamisha Rajabu Jumbe kugombea Umakamu wa Rais akiwa darasa la saba, wewe umesahau? Sasa kama ninyi mlitaka kuleta Makamu wa Rais darasa la saba, itakuwa Mbunge! (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaipongeza sana Serikali. Nataka niwaambieni, katika siasa duniani, mimi ni Mwanafalsafa, nikija kufa ndiyo mtaelewa kwamba yule mtu alikuwa wa namna gani. Katika watu ambao wanajua siasa na wamefanya, nawaambieni Tanzania hatuwezi kusonga mbele. Wana-CCM tujigawe; wawepo Wabunge wa Upinzani kutoka CCM, tuisaidie Serikali. Hawa tuachane nao! Hakuna kitu wanachokifanya hawa! Tukiendelea kuwaamini hawa, tutapoteza point nyingi sana. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, duniani kote, Chama cha Upinzani kinakuwa na hoja moja tu. ANC wameshinda uchaguzi pale, hoja yao ilikuwa Ubaguzi; lakini hawa umeme, barabara, maji nini, hawa Wapinzani wa wapi? Hakuna Wapinzani wa namna hiyo! Mpinzani anakuwa na hoja moja tu. Anaijenga na anaaminika kwa watu. Hawa hawaaminiki, wanazungumza kila kitu! (Kicheko/Makofi)
Nakuomba Mheshimiwa Waziri Mkuu, maendeleo katika nchi yetu kuna mikoa imechelewa kupata maendeleo kwa sababu resources zetu kuwa ndogo, igeukieni hiyo, acheni mikoa ambayo wananchi wameshiba, wanachagua Mbunge kuja kunyamaza tu Bungeni, achaneni nayo! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunaomba Mheshimiwa Waziri Mkuu, wakati wa kutekeleza hoja hii, fanyeni kazi kwa Waheshimiwa Wabunge waliochangia shida zao; hawa walionyamaza achaneni nao, hawana shida hawa. Mbunge anatoka nyumbani anakuja kukaa hivi, hasemi shida yoyote halafu baadaye wanakuja kwenye viti vya Mawaziri kunong’ona; Waziri mtu mzuri. Unafiki wa namna hiyo haukubaliki! Tunataka waseme wazi. Wakisimama hapa, wanakashifu Mawaziri, wanawatukaneni, halafu wanakuja kwenye kiti, naomba umeme. Tunataka maombi wanayoyaleta mezani kwenu, wayaseme wazi. (Makofi)
Mheshimiwa Waziri wa Fedha, tunakufahamu, wewe ni mtaalam; umekuwa Bwana Mpango, umeongoza maeneo mengi. Tunataka safari hii, Serikali ya Awamu ya Tano, mipango yenu yote mliyoipanga na mkatupa asilimia 41 ya pesa, zishuke kwa wananchi ili maendeleo yapatikane, tuwakate mdomo hawa. Sasa hivi tutafanya!
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuhakikishie, tutatengeneza umoja wa kutembea Jimbo kwa Jimbo kuwaambia hawa wasichaguliwe tena 2020. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuzungumzie barabara. Ukitoka hapa kwenda Iringa, kuna kipande cha barabara ambacho Mheshimiwa Rais ameshakiahidi kutoka barabara ya lami inayokwenda Iringa ipite barabara ya lami mpaka Hospitlai Teule ya Mvumi. Naomba kipande hicho mkikamilishe ili mimi niwe Mbunge wa maisha wa Jimbo lile. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuhakikishie, katika wanasiasa wanaoniuma; nazungumzia demokrasia, lazima niwe mkweli; ananiuma sana kaka yangu Mheshimiwa James Mbatia. Mheshimiwa Mbatia ni mwanasiasa wa siku nyingi kuliko Mheshimiwa Mbowe. Sijui kalishwa nini, siku hizi anaambiwa na Mheshimiwa Mbowe, nyamaza! Naye ananyamaza kweli! Ananyamaza! Yaani sielewi kilichotokea!
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mbatia ni Mwanasiasa wa siku nyingi, Chama chake kilikuwa na Wabunge watano. Akanambia yeye amesoma, mimi sijasoma, sasa anakwenda mbele. Kutoka watano kuja mmoja! (Kicheko)
MWENYEKITI: Mheshimiwa Lusinde inatosha kwa leo, muda wako umemalizika!
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Kweli hata mimi ambaye sijasoma siwezi kufanya ujinga kama huo! Hata mimi ambaye sijaenda shule, siwezi kufanya kitu cha namna hiyo. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Hawa tunawamudu, hamna kitu na tutahakikisha tunawafagia. Ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nakushukuru kwa kunipa nafasi jioni ya leo na mimi niweze kusema mambo machache ya muhimu kuhusu hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kaka yangu Mheshimiwa George Boniface Simbachawene. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nachukua fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais. Mheshimiwa Rais ameonesha namna gani anataka kuirudisha Tanzania kwenye msimamo hasa wa nidhamu, uwajibikaji na uadilifu. Kwa sisi Wagogo tuna usemi unasema; mdabula nhili mwana na kalanga ganyina mmeso. Ukitaka kuonja uji wa mtoto, mtazame kwanza mama yake usoni. Ukimwona namna alivyokaa, unaweza ukaamua aidha, uonje au usionje. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais Magufuli ameonesha yuko makini na mkali sana kwenye matumizi ya hovyo hovyo. Nataka niseme haya mnayoyaona wengine kushindwa kumwelewa ni kwa sababu Rais Magufuli amewashangaza wengi katika utendaji wake wa kazi. Ndiyo maana mtasikia mengi! Mtasikia Katiba imevunjwa, mtasikia nini! Kwa sababu wengine hawana namna ya kusema, inabidi waseme hivyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Waziri, tunakufahamu kwa msimamo wako Mheshimiwa Simbachawene. Tuna hakika utaitendea haki kama ambavyo umeonesha tangu mwanzo Wizara hiyo, ni Wizara kubwa, tuna hakika mkijipanga vizuri na Jafo kama mlivyokaa, mna uwezo wa kuhakikisha nchi yetu inasonga mbele. Tunawapa big up, tunawaomba mwendelee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme maneno machache hapa. Tunapozungumzia pengine kuna mtu hapa ameshindwa kuelewa anasema Mwanasheria Mkuu wa Serikali anatafsiri mambo ki-CCM. Ndugu zangu, nchi hii Ilani inayotekelezwa ni ya CCM. Nchi hii hakuna Sera ya Serikali peke yake tu inayojiendesha! Mlikataa wakati wa Bunge la Katiba. Tulipowaambia tuwe na Sera ya Serikali tuachane na Sera za Vyama, mkakataa! Leo tumeenda kuuza sera kwa wananchi; CHADEMA walikwenda nayo, CUF walikwenda nayo na CCM walikwenda nayo. Wananchi wamechagua ya CCM. Sasa mtu anaposema unaongea ki-CCM hata wewe Mbunge unatekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM. Tuelewane hapo! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wala tusitake kuzungumza hapa vitu kama vile tunaimbiana mapambio. Upinzani watakuwa wanafanya kazi kama vile ambavyo tunaweza tukasema, wanafanya kazi waki-support kazi ya shetani, kwamba unapinga lakini wenzako wanaotawala wanafanya kazi ya Mungu. Wakati unaeleza upungufu, kwanza unashukuru kwa vichache vilivyotolewa. Hawa kazi yao ni kuponda, halafu baadaye wanaomba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kazi yetu ni kusifu baadaye tunaomba. Wote kazi yetu ni moja, lakini utajiuliza mwenyewe, je, wa kuponda anafurahisha? Maana kwanza anaponda, halafu baadaye anapiga mzinga. Sisi tunasifu baadaye tunapiga mzinga. Kwa hiyo, tunafanya kazi ya Kimungu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa namwomba Mungu sana, anipe uwezo watu wanielewe. Sitaki kuingia kule kwenye siasa ambazo watu wamepanga; anasema tu kwa sababu Lusinde tumemwona, yeye anataka kuhamisha vita kutoka kwa Mawaziri kuja kwake; tutampakazia! Wewe useme kwamba Lusinde amepigiwa simu ya Mheshimiwa Rais, kaambiwa asiwatetee. Mimi Wakili? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi siyo Wakili, sifanyi kazi ya Mahakama na wala simtetei mtu yeyote katika Mahakama yoyote ya nchi hii. Kwa hiyo, unaweza ukaona; na mimi nataka niwaambieni mkitaka kuleta siasa za uzushi mimi ndiyo natisha kwenye upande huo. (Makofi)
Nirudie tena kuwaonya, mimi mtu kunitaja namruhusu kwasababu hili jina kubwa na nimelitengeneza kwa gharama kubwa. Kwa hiyo, kuna watu watajitahidi kutaka kulifikia jina hili, lakini ni kazi ngumu sana. Waitara nimemfundisha siasa akiwa CCM, leo tena yuko CHADEMA nitaendelea kumsaidia taratibu lakini asifikie huko; Rais ni matawi mengine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, humu ndani tunafanya kazi mbili tofauti. Wako Wabunge ambao kazi yao tangu anasimama mwanzo, ataponda halafu mwishoni anakuja kwenye kiti, nisaidie maji. Yupo Mbunge atasimama, atasifu halafu baadaye atatoa shida zake. Ndiyo tofauti! Ninyi Mawaziri mtapima, yupi anayezungumza vitu vya msingi? Mtapima maana mimi siamini, hata kutafuta mchumba umkute msichana wa watu, umwambie dada una sura mbaya, lakini naomba nikuoe. Akikubali, ujue huyo hana akili. Hana akili huyo! Lazima umsifu kwanza! (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimewaeleza juzi kwa uchungu sana, nikasema nchi yetu tunajenga demokrasia, tuangalie kwa umakini sana. Hii nchi inapita kwenye mawimbi makubwa ya kujengwa demokrasia. Tunapojenga demokrasia, ni lazima hivi vyama tuvipe uhuru mkubwa wa kufanya mambo yao kama ambavyo tunafanya. Ndiyo maana nikawashtua wenzangu, Chama cha CUF, nikawashtua NCCR Mageuzi; siamini kwamba katika ndoa waliyonayo wanajenga demokrasia. Naamini wanakwenda kuuawa! (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunaweza kumwona Mheshimiwa Zitto hana akili, yuko peke yake, lakini nawaambia katika miaka ijayo, pengine chama chake ndiyo kitakuwa maarufu kuliko vyama vingine hivyo. Maana kinapata muda wa kufanya siasa. Leo kuna watu wanazuiwa na Mwenyekiti, usiseme; wanakaa kimya. Sema, wanasema! Watu wa namna hii ni watu wanaoendeshwa kwa remote, hawawezi kuwa wanasiasa. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaambia Tanzania ina Chama cha Upinzani pengine kimoja tu, ACT, vingine vyote ni vyama shindikizo. Ni Vyama vinavyokwenda na hoja. Meli ikizama, wanahamia kwenye meli; ikitokea kashfa, wanahamia kwenye kashfa. Serikali hii inaziba kila kitu. Wamehamia kwenye tv live. Hebu ngoja nizungumze kidogo hapa! (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninyi wasomi mnasema nchi ina Executive, Parliament na Judiciary, hebu tujiulize; mbona Executive mambo yao hayaoneshwi live kila siku? Nayo ndiyo Executive inayoongoza nchi! Mbona hatuoni live kila siku mambo ya Ikulu? Mbona hatuoni Mahakimu wakiendesha kesi live kila siku na wao ni mhimili? Mbona hatuoni Majaji Mahakamani wakiamua mashauri wakiwa live na wao ni mhimili? Iweje watu wang’ang’anie mhimili mmoja? Huku ni kufilisika! Watu wamefilisika, hawana nafasi, wanataka kwenda kujitangaza kwa njia hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikasema leo nitoe somo. Katika nchi yenye mfumo wa vyama vingi tuangalie hivi vyama, tuangalie hata aina ya Wabunge. Mimi nawaambia tutakwenda mahali tutajikuta tunatumia resource kubwa, kupoteza muda hapa, hatuisaidii Serikali. Kwa hiyo, naomba niwaambie Waheshimiwa Mawaziri, tunapokuja kuwaambia shida zetu na juzi nilisema, hapa mnatukanwa, mnadharauliwa, halafu wakija wanasema naomba maji. Leo nchi ielewe hakuna Jimbo lolote la mpinzani linalopelekwa maendeleo. Maendeleo katika Majimbo yao tunapeleka sisi CCM.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi ndio tunakubali bajeti itekelezwe. Leo tunamwomba Waziri wa maji apeleke maji Moshi, Arusha; Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa huo wanakataa. Mwisho wa siku wanasema tumeleta maendeleo. Unaleta maendeleo kwa kusema hapana? Haiwezekani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi ifahamu maendeleo yanaletwa na Wabunge wa Chama cha Mapinduzi.
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Aah, niendelee! Niliona Mheshimiwa Mch. Msigwa amesimama nami namheshimu kwa sababu nimeoa kwao. Unajua mimi nimeoa Iringa. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, watu waelewe hata barabara zilizojengwa Iringa Mjini aliposimama Mheshimiwa Msigwa, mimi nilitetea humu ndani ya Bunge. Maana mke wangu anatoka pale.
KUHUSU UTARATIBU.......
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nakushukuru na nimshukuru hata Mheshimiwa Mch. Msigwa. Mheshimiwa Msigwa na mimi hatujawahi kupingana, sijui leo kimemkuta nini? Mimi juzi nimemwacha ameongea propaganda zake hapa, lakini leo yeye kashindwa kuvumilia. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba sana Mheshimiwa George Simbachawene, Mheshimiwa Waziri kupitia Bunge hili, aitazame Halmashauri mpya. Tumezungumza kuhusu mgawanyo wa nchi yetu. Tumeomba Halmashauri mpya ya Mtera, lakini atazame hata jina la Jimbo la Mtera. Kata ya Mtera iko kwako, Kijiji cha Mtera kiko kwako, mimi naitwaje Jimbo la Mtera? Haiwezekani!
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana nikasema Mheshimiwa George hakuna sababu ya Jimbo langu kuitwa Jimbo la Mtera. Unanipa jina la utumwani. Mimi ningependa Jimbo langu liitwe Jimbo la Mvumi ambako anatoka Chifu Mazengo. Kwa hiyo, naomba Halmashauri yetu uitazame, Jimbo letu libadilishwe jina, lisiitwe jina la kijiji kilichoko kwako, kwa sababu sisi hatuwezi kuitika kwako. Watu wengi wanafikiri sisi tuko Mtera; Mtera ni ya George Simbachawene. Sielewi mzee alipoiita, aliita kwa sababu gani.
Mheshimiwa Mweyekiti, naomba kwenye Bunge hili uturudishie majina ya kwetu ya asili. Sisi pale tuna Mvumi karibu ziko 20. Kwa hiyo, ungetuita Jimbo la Mvumi ungekuwa umetutendea haki zaidi kuliko kutuita Jimbo la Mtera ambalo liko kwako wewe Mheshimiwa Simbachawene.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine tunaloliomba, kuna barabara za TANROADS na kuna barabara za Halmashauri. Halmashauri nyingi hazina uwezo wa kujenga barabara ndefu.
Kwa hiyo, naomba kwa niaba ya Wabunge wenzangu, angalia kila Jimbo lenye barabara ndefu, badala ya kuiachia Halmashauri ambayo haina uwezo, zipandishwe hadhi ziende TANROADS ili ziweze kutengenezwa vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumza hivi kwasababu tuna uzoefu; kuna barabara nyingine Halmashauri hazina mapato ya kuweza kutengeneza urefu wa hizo barabara, lakini mkiwapa TANROADS wana uwezo. Kwa mfano, chukulia barabara inayotoka Dodoma Mjini. Kuna barabara inatoka Dodoma Mjini, inapita moja kwa moja kwenye Jimbo la Bahi kwa Mheshimiwa Badwel, inaenda moja kwa moja tena kwenye Jimbo langu la Mtera, halafu ndiyo inaenda kupakana ng’ambo kule kwa Mheshimiwa Waziri wa Ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba ile barabara tuipandishe hadhi iwe barabara ya Mkoa kwasababu inapita kwenye Manispaa na kwenye Halmashauri mbili. Ukipata hela Chamwino ukitengeneza kipande, wenzako Bahi wanakosa, panabaki mashimo; kunakuwa hakuna mtengenezaji. Kwa hiyo, naomba kupitia Wizara yako, barabara tulizoziombea zipandishwe hadhi, mzipandishe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tuangalie, kuna Halmashauri nyingine, kata nne Halmashauri; kata tatu Halmashauri; hebu tuangalie, sisi tuna Jimbo lina kata 22. Tumeomba tugawanywe Wilaya, mkasema hapana tutawapa Halmashauri. Tupeni Halmashauri ili tuweze kusukuma maendeleo mbele. Tunataka kuendelea kufanya kazi!
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana tulisema…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)
Aaah, naendelea, ahsante sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naunga mkono hoja. Naona jamaa wanasema umemaliza. Ahsanteni, nimemaliza.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunipa nafasi hii kubwa, kunipa zawadi ya uhai ili nami nisimame leo kuchangia katika Bajeti ya Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge wengi sana wamekupongeza kwa umahiri wako wa ufanyaji kazi, lakini nataka nifafanue kidogo. Kuna kipindi watu wanachanganya sana hizi mada. Wapinzani walipotaka kuelezea kutoridhishwa kwao na Naibu Spika, kwanza walianza kuzungumzia habari ya uteuzi wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, siyo Mbunge wa kwanza kuteuliwa na Rais wa nchi yetu. Katika Bunge lililopita Mheshimiwa James Mbatia alikuwa Mbunge wa kuteuliwa na Rais na hapo ndipo alipopatia na mtaji wa kugombea Ubunge; lakini siku zote tulikuwa tunamwita Mheshimiwa Mbunge na Wapinzani walikuwa wanamwita Mheshimiwa Mbunge Mbatia. Hakuna mtu aliyemwita ndugu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo wamekuja na hoja nyingine tena; imekuwaje umetoka kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ghafla, umeingia na kuchaguliwa kuwa Naibu Spika? Nikawaambia tu, ndugu zangu, mbona Mheshimiwa Tulia alishaoneshwa njia na Mzee Lowassa? Mheshimiwa Lowassa Jumatano katoka CCM, kahama; Alhamisi ni Mgombea Urais CHADEMA. Mheshimiwa Tulia naye alitumia ile ile! Amechomoka kwenye Unaibu Mwanasheria Mkuu, amezama Bungeni – Naibu Spika wa Bunge.
Tena kwa kupigiwa kura, wala siyo kwa kuteuliwa. Wewe tumekuchagua sisi. Mheshimiwa Rais alikuteua kuwa Mbunge, lakini nafasi hiyo tumekupa sisi Wabunge. Siyo kwamba Rais amesema Mheshimiwa Dkt. Tulia awe Naibu Spika, aah, tumesema sisi kwa kukuamini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niseme jambo lingine ambalo watu wengi wamelisahau. Tanzania imezalisha viongozi wanawake wengi mahiri. Akina mama Mongella tunakumbuka, walikuwepo akina Bibi Titi Mohamed, wapo sasa hivi akina Samia Suluhu Hassan, akina mama Magreth Sitta; wamefanya kazi kubwa kwenye nchi hii. Leo nataka niwaambie msifikiri Wapinzani wanakimbia tu, kushindana na kiongozi shupavu mwanamke siyo kazi rahisi. Ni kazi ngumu sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuliwaambia wakajifanya mahiri wa kujenga hoja za kisheria, sijui wana uwezo mkubwa; huyu ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, yaani amebobea kwenye nafasi hiyo. Kwa hiyo, walipoona yameshindikana, ndiyo unaona wanachomoka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, duniani wanaume ndio tumeshika nafasi kubwa ya kuwa viongozi mahali pengi, lakini ikitokea mwanamke akapata nafasi, ogopa! Angalia akina Magraret Thatcher, amekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza pale. Mwangalie Indira Gandhi, amekuwa Waziri Mkuu wa India pale; mwangalie Golda Meir, amekuwa Waziri Mkuu wa Israel. Hawa ni akinamama wachache waliofanya mambo makubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka nikuhakikishie kwamba unakoelekea ni kuzuri. Komaa, endelea kufanya kazi nasi tunakuunga mkono. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie Bajeti ya Serikali. Waheshimiwa Wabunge wamesema kwa uchungu sana, tunakuomba Mheshimiwa Waziri; tumefikia kipindi ambacho makusanyo sasa ni makubwa. Impact ya makusanyo yenu yatakuwa na maana sana kama yatashuka kwa wananchi wa chini maskini. Vinginevyo, hata mkijisifu kukusanya itakuwa haina maana. Ndiyo maana Mheshimiwa Rais anabana matumizi, Serikali nzima inabana matumizi, lakini mategemeo yetu ni kuona bajeti hiyo ni kwa namna gani itashuka kumaliza matatizo ya wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge wamesema habari ya kujichanganya kwenu hapa. Amesimama Mheshimiwa Waziri hapa anasema amefuta ushuru. Hao vijana mnaotaka tuwainue kiuchumi, mwaka huu ndio wamelima ufuta na alizeti. Leo bado kuna mageti ya vijana kuchangishwa kutoka kwenye kilimo chao duni walicholima, siyo sawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ufuta umeshuka bei, alizeti haina bei, halafu mageti ya kuwachangisha ushuru mkubwa. Hili mlitazame, linatupaka madoa Waheshimiwa Wabunge tuliotoka kwenye Majimbo ya vijana wakulima. Watu wanataka kuinuka kiuchumi. Kwa hiyo, naomba Serikali wakati wa kutoa majibu ilisemee hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tumezungumzia habari za Zahanati hasa za Vijijini, zinahitaji pesa. Akinamama wengi wanaojifungua wanapoteza maisha yao kwa kukosa vyumba vya kufanyia upasuaji kwenye hospitali zetu za Kata. Tumesema tuwe na Vituo vya Afya kwenye kila Kata. Vituo vile havina theatre maalum ya kuwafanyia upasuaji akinamama wajawazito.
Mheshimiwa Naibu Soika, kwa hiyo, inatupa shida na Kata nyingine zina kilometa ndefu sana kutoka Kata moja kwenda Kata nyingine. Kwa hiyo, tunamwomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha, asukume fedha kwenye Wizara muhimu; Wizara ya Afya na Wizara ya Maji ili kuweza kuwapunguzia usumbufu wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mchezo wa kuigiza unaofanyika kwenye nchi yetu ni wa ajabu sana. Mwaka 2015 tulikuwa na mashindano ya kisiasa ya nchi nzima. Kila mwanasiasa maneno aliyokuwa nayo aliyasema. Wananchi wamepiga kura, siasa zimehamia Bungeni. Haiwezekani tena ukakimbia Bungeni ukaenda kuwaambia wananchi yanayoendelea Bungeni, wamekutuma kazi hiyo? Hili lazima niweke sawa! Serikali haiwezi kuleta maendeleo kama nchi haina utulivu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nchi lazima iwe na utulivu, iwe na amani yake ili hayo makusanyo ya Serikali yanayotafutwa yaweze kuwafikia wananchi. Kwa hiyo, hiki kiini macho kinachotumiwa na Wapinzani kwamba tunaenda kuwaambia wananchi yanayotokea Bungeni, tuko Wabunge wa Majimbo, hiyo tutaenda kuwaambia wananchi wetu waliotutuma! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka kila Mbunge akafanye kazi kwenye Jimbo lake. Hivi, Mbowe anavyosema anaenda Kahama, Kahama kuna Mbunge wa CHADEMA? Kwa nini asiende kuwaambia wananchi wa Hai? Aende akawaambie wananchi wa Jimbo lake; lakini kwenda Kahama ambako hakuna Mbunge wa CHADEMA, ni uchokozi na ni kuwapotezea muda wananchi wa Kahama wasifanye kazi yao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niseme kuhusu udikteta. Hili sitaki kuficha, moja ya viongozi madikteta kwenye nchi hii ni pamoja na Mheshimiwa Mbowe. Anawatoa Wabunge kwa nguvu. Waheshimiwa Wabunge wako hapo kwenye chai, wamenituma nije niwasemee humu ndani. Wameniomba, wamesema, Lusinde, kuna mambo sisi hatuwezi kumwambia Mbowe, nenda kamwambie.
Mheshimiwa Naibu Spika, natumia fursa hii kumwambia Mheshimiwa Mbowe warudishe Wabunge ndani ya Bunge! Usiwanyanyase! Anawapigia simu wakae kwenye chai badala ya kuingia Bungeni. Tabia gani hiyo? Hiyo ni kutumia Uenyekiti vibaya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, haya siyo maamuzi ya Chama ndugu zangu, tusiwalaumu. Hawa wamepigiwa simu, wamekatazwa; atakayeingia atapewa adhabu. Kwa hiyo, wako kwenye chai, wameniomba; nenda katusemee Bungeni, sisi hatuwezi kusema. Najua huko waliko wananipigia makofi kwa sababu natekeleza agizo walilonituma. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tukiendeleza siasa uchwara za kufanya fujo wakati Serikali imeshapatikana, tutamnyima fursa Mheshimiwa Dkt. Magufuli ya kuwahudumia Watanzania. Tumpe nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndugu zangu, wengi hapa mnajua mpira; mpira una sheria zake. Hivi mchezaji wa Simba au wa Yanga anapewa kadi nyekundu kwenye mchezo wa mpira, Wanayanga wanaweza kuandamana nchi nzima kupinga? Haiwezekani! Mbunge akipewa kadi nyekundu ndani ya Bunge, ni kwa kufuata kanuni za ndani ya Bunge, siyo nje ya Bunge. Haiwahusu wananchi hiyo. Hiyo inatuhusu wenyewe; tumewekeana sheria, tumewekeana kanuni; Mbunge akifanya kosa hili, red card, anatoka nje. Hiyo huwezi ukaandamana nchi nzima kwenda kuwaambia ooh, demokrasia inaminywa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna demokrasia isiyo na mipaka. Demokrasia isiyo na mipaka ni fujo. Tunaitaka Serikali isimamie amani, Serikali idumishe utulivu ili pesa zinazokusanywa ziende ziwahudumie wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunazungumzia habari ya usambazaji wa umeme. Mkisambaza umeme kwenye vijiji, mnainua uchumi na mnapunguza msongamano mijini. Leo kama kila kijiji kitakuwa na umeme; kila kijiji wananchi watakuwa wamejiwekea pale miundombinu ya kujiletea maendeleo, wana sababu gani ya kwenda Dar es Salaam? Hawana sababu. Kwa hiyo, hata ile foleni ya Dar es Salaam itapungua na hayo yote yatafanyika kama nchi ina utulivu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ni mjumbe wa Kamati ya PAC, hapa nataka ku-declare interest. Naiomba Serikali badala ya kupeleka bajeti ya shilingi bilioni 72 kwa TAKUKURU, waitazame Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali. Leo unawapa shilingi bilioni 34 na point ngapi sijui, siyo sawa. Huyu ndio Mkaguzi. Huyu ndiye anayekwenda kuwaonesha TAKUKURU hapa kuna wezi. Huyu ndiye anayekwenda kuonesha ubadhirifu, ndio jicho la Bunge. Kwa hiyo, naomba, sisi Wabunge kwa kulithamini jicho letu, tunaomba jicho lisafishwe, liwekewe dawa, liwekewe miwani ili likawaone wabadhirifu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana Serikali iwe makini kwenye ushauri wa Waheshimiwa Wabunge. Waheshimiwa Wabunge tunapoomba, Serikali itusikilize; Ofisi ya CAG ni Ofisi kubwa. Ndiyo Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali; akikosa pesa hawezi kufanya kazi hiyo.
Kwa hiyo, tunawaomba waongezewe pesa ili wakafanye ukaguzi ili hata hiyo Mahakama ya Mafisadi iende na ushahidi. Hawa wasipofanya kazi yao vizuri, wote mtakaowashtaki watashinda kesi kwa sababu kutakuwa hakuna ushahidi wa kuaminika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niseme, kwenye Bunge, tunapokutana Waheshimiwa Wabunge, yanakutana Majimbo yote kuzungumzia maendeleo ya nchi nzima. Wabunge wa CCM tunao wajibu; sisi ndio tumepewa dhamana na wananchi wa Tanzania kuongoza nchi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata Wabunge wao wanapokosa hoja za msingi, tusimame kutetea Majimbo yale kwa sababu yana wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tutakapofika, wananchi watagundua, wananchi sio wajinga, watagundua kwamba amekuja Mheshimiwa Rais, anafanya mabadiliko ya vitendo; Mheshimiwa Rais anapozungumza, unamwona mpaka macho yanalenga lenga machozi kwa uchungu alionao. Watu wanamwona, wamemwamini, leo hawa wamekosa hoja wanapokimbia nje kutekeleza kauli ya Mheshimiwa Mbowe, inawauma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, sisi Waheshimiwa Wabunge wa CCM tuzibe lile pengo kuhakikisha kwamba tunayasemea Majimbo yao, wananchi watusikilize kwamba Iringa ipelekewe maji, kwamba Kigoma ipelekewe maji na miundombinu ijengwe na Moshi Mjini pale patekelezewe miradi yao. Hiyo ndiyo kazi tuliyonyo Wabunge wa CCM maana sisi ndio mama, sisi ndio baba, sisi ndiyo tumeaminiwa na wananchi wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie kweye miradi ya maendeleo. Kwa mara ya kwanza, Serikali imetenga asilimia 40 kwenye bajeti ya maendeleo. Miaka yote Wapinzani wamekuwa wakilalamika, bajeti ya maendeleo ndogo, hakuna pesa zilizotengwa; lakini mwaka huu Mheshimiwa Dkt. Magufuli na Serikali yake amekuja na asilimia 40 ya maendeleo…
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na namshukuru sana Mheshimiwa Kanyasu kwa kuniongezea dakika zake tano kwa niaba ya nchi hii, nami naendelea sasa kupiga dawa taratibu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tujifunze. Kama nchi inataka kufanya siasa za ustaarabu, tufanye siasa za ustaarabu. Tusiige kila kinachofanywa na watu wengine na sisi tukakileta hapa Tanzania, haiwezekani. Hata mashindano ya ma-miss tu, yakiisha, hakuna ugomvi tena. Hakuna mtu anapita kujitangaza kwamba yeye mzuri kuliko aliyechaguliwa, hakuna! Wanakuwa wamemaliza. Siasa za Tanzania ni siasa gani ambazo hazina muda? Lazima tuwe na muda wa kampeni, ukiisha tumwachie Rais atekeleze kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nalisema hili kwa sababu tukiendeleza tabia hii, nataka niwaambie, itakuwa ndiyo Taifa peke yake ambalo watu hawafanyi kazi, wanafanya siasa muda wote. Haiwezekani! Lazima tuwe tunajitenga. Tukimaliza kampeni, viongozi wamechaguliwa, tunawapa fursa ya kutekeleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Rais aliyeko wa Awamu ya Tano, slogan yake na msimamo wake ni Hapa Kazi Tu! Anachotaka ni watu wafanye kazi. Watu tufanye kazi, siyo turudi kwenye majukwaa tena sijui ooh, Dkt. Tulia kafanyaje! Haiwezekani. Mheshimiwa Dkt. Tulia hawezi kuwa msingi wa Wapinzani kutoka; wamekimbia kwa sababu hoja haipo. Mheshimiwa Mbowe ametumia nafasi hiyo vibaya kuwaambia sasa tokeni, kaeni kwenye chai mpaka mtakaponisikiliza. Huo ndiyo uongozi bora? Siyo uongozi bora! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunapozungumzia uongozi bora, tunazungumza kwa wote sisi, ndiyo kodi yetu inatumika kulipa Upinzani, kulipa Chama kinachotawala na kuleta maendeleo ya nchi. Kwa hiyo, mchango unapokosekana, lazima CCM tuzibe lile pengo, kama ambavyo imetokea Kambi Mbadala. Huo ndiyo wajibu wetu na tuwaambie wananchi kwamba kinachofanywa na Wapinzani siyo kweli, siyo sahihi. Hata viongozi wa dini wanajua, akishachaguliwa Mufti, hakuna uchaguzi mwingine tena. Anaachiwa Mufti aongoze. Akichaguliwa Askofu, hakuna uchaguzi mwingine wa Askofu. Anaachiwa aliyechaguliwa afanye kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kinachotaka kufanyika kupitia upinzani, ile ni fujo; kuiweka nchi katika fujo za maandamano yasiyo na msingi. Haiwezekani! Serikali isimamie amani, isimamie haki, isimamie maendeleo kwa nchi nzima. Mbunge anayejisikia kwenda kuwaambia wananchi wake kaonewa Bungeni, akafanye kwenye Jimbo lake, siyo kwenye Jimbo la Mbunge mwingine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mbunge yeyote akitoka hapa Bungeni naye ataenda kueleza nini tumepata, nini Serikali itafanya katika miaka mitano. Hatuhitaji msaada toka kwa Mheshimiwa Mbowe wala kwa mtu mwingine yeyote. Pale Kahama yuko Kishimba wamemchagua, atakwenda kuwaeleza yanayotokea hapa. Hatuhitaji msaada wa mtu mwingine. Hatuwezi kufanya siasa muda wote, haiwezekani. Tunafanya siasa, tukishamaliza, siasa zinahamia Bungeni, wananchi wanachapa kazi kuleta maendeleo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kuzungumza kidogo kuhusu kiinua mgongo. Waheshimiwa Wabunge, naomba mnisikilize. Naamua nijitoe muhanga kwenye jambo hili. Kujitoa kwangu muhanga ni hivi, hili jambo Serikali imesema kama yatakuwepo hayo makato, yatakatwa 2020. Sisi tunahoji kwamba kwa nini hoja hiyo muilete saa hizi? Sisi hatuitaki saa hizi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninachotaka niwaambie Waheshimiwa Wabunge, jambo hili tukae wote. Serikali hii ni ya kwetu na sisi ni Wabunge tunaoongoza nchi hii. Wananchi wasije wakatuelewa vibaya wakafikiri sisi hatutaki kuchangia maendeleo, hapana. Moyo wa kuchangia maendeleo na sisi tunao. Tunachosema, jambo hili linahitaji mazungumzo, twende tukae, tukubaliane, utaratibu gani utumike ili kuweza kusonga mbele, wala siyo la kubishania hapa. Wala hatuwezi kusema hatutaki, haiwezekani. Huu ni ushauri wa Serikali na sisi hatuwezi tukailazaimisha Serikali kwa nguvu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunawashaurini kwamba jambo hili linahitaji mjadala wa pande zote mbili. Waheshimiwa Wabunge, tunalipa kodi, tunakatwa kwenye mishahara yetu. Kama mnataka kuendelea mbele kukata tena gratuity, tuzungumze, tuone impact yake, maendeleo yatakavyosukumwa, wala siyo jambo la kubishania hapa. Jambo hili ni zuri. Isije ikachukuliwa kwamba Waheshimiwa Wabunge wote wanapinga kukatwa hela zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niwaambie, kuna waandishi wanasema, Waheshimiwa Wabunge wa CCM, imewauma kusikia wanakatwa hela. Mimi haijaniuma, niko tayari hela yangu ikatwe, lakini kwa mazungumzo. Tuone hiyo hela inakatwa kuelekea wapi na utaratibu gani utatumika ku-balance jambo hili ili liweze kuleta afya badala ya malumbano hapa Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nchi hii ni yetu wote. Siyo kazi yetu kuwashtaki wengine kwamba viongozi wote wa kisiasa lazima wakatwe. Hiyo siyo kazi yetu. Kazi yetu sisi ni kuangalia kitakachopatikana. Kama hakitoshi, ndiyo tutashauri Serikali sasa iangalie na viongozi wengine ili kuongeza mfuko, maendeleo yaweze kupatikana. Tusikae tunabishania hapa, tunabishania kitu gani? Kwa sababu juzi hapa tumeondoa matangazo live ili pesa itakayopatikana iende kuwahudumia wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tulikuwa na hoja za msingi hapa, tukasema anayetaka kurusha live, hata harusi siku hizi watu wanarusha live; kalipie mwenyewe. Nenda lipia pale TBC, mtakapopewa dakika 15, rusheni live wananchi wako wakuone. Mbona tulipitisha na tukakubaliana? Hili lisilete ugomvi. Hili ni jambo dogo sana. Tunahitaji muda wa kuzungumza na Serikali kukubaliana juu ya jambo hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna Mbunge anayepinga Bungeni, sijui kumekucha, sijui Waheshimiwa Wabunge wameamua kumkatalia Mheshimiwa Dkt. Magufuli. Mheshimiwa Dkt. Magufuli tumemchagua sisi, ni Rais wetu, tutamuunga mkono kwa hoja yoyote atakayoileta humu ndani, tukiwa na imani kwamba Rais hakosei. Rais hawezi kukosea. Nia yake ni njema katika kuitumikia nchi hii. Anataka Waheshimiwa Wabunge pamoja na wananchi wote turudi katika mstari sawa. Kama Mheshimiwa Mbunge ulikuwa unakunywa bia kumi, kunywa moja ili tuweze kusonga mbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi kuna mwezi Mtukufu huu, Waislamu wamefunga, wanaweza kuombea nchi hii watu wakaachana kabisa na ulevi. Nawahakikishieni kabisa, tutapata maendeleo makubwa ya kusonga mbele. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka kuwatia moyo sana Waheshimiwa Mawaziri, Dkt. Mpango na dada yangu pale, fanyeni kazi. Tuna imani na nyie. Mheshimiwa Rais anawaamini na sisi Waheshimiwa Wabunge tunawaamini. Tutafanya kazi kwa mshikamano kuhakikisha nchi hii inasonga mbele bila mikwaruzano, bila nini.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na naunga mkono hoja.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza nimshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa ajili ya kutuzawadia uhai na kwa huruma yake tuko salama na tuko ndani ya Bunge hili kwa sababu ya kujadili Mpango wa Maendeleo wa Serikali 2016/2017 na 2017/2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza, nataka nichukue fursa hii ndugu zangu kwa unyenyekevu mkubwa sana kutoa pole kwa wananchi wenzangu watatu watafiti kutoka Chuo cha Seliani waliouawa katika Kijiji cha Iringa-Mvumi, katika Wilaya ya Chamwino, nawapa pole sana familia. Vilevile nitoe pole sana kwa wananchi kadhaa wa Kijiji cha Mvumi Mission pamoja na Kata ya Manda na Kijiji chenyewe cha Iringa-Mvumi kwa familia ya Tatu ambaye naye pia aliuawa wiki moja kabla ya wale watafiti kukumbwa na kadhia hiyo. Naomba Mungu azipumzishe roho za marehemu wote mahali pema peponi, lakini niitake Serikali kuchukua hatua madhubuti kuwatafuta watu waliokimbia ambao kwa kweli kwa kiasi kikubwa wanatajwa kuhusika na mambo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya utangulizi huo, nina mambo machache ya kuzungumza. Jambo la kwanza, naomba niipongeze sana Serikali kwa kazi nzuri. Ndugu zangu nataka nirudie tena maneno ambayo nimekuwa nikiyasema mara nyingi kwamba katika kazi rahisi duniani, hakuna kazi rahisi kuliko kupinga, kupinga jambo lolote ni kufanya kazi rahisi sana. Maana mtu anajenga nyumba kwa gharama kubwa wewe unatumia dakika mbili tu kumwambia nyumba yako mbovu. Kwa hiyo, unaweza kuona namna ambavyo kupinga ni kazi rahisi sana na inayoweza kufanywa na mtu yeyote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe Waziri, Mheshimiwa Dkt. Mpango, maneno mengi mazuri ameyaandika katika kitabu chake, mojawapo ni kukua kwa uchumi ambapo sasa hivi umekua kwa 5.7% na unategemewa kukua kwa 5.9%. Tatizo tulilo nalo Dkt. Mpango ni namna gani tunahusianisha kati ya ukuaji wa uchumi kwenye vitabu na hali halisi kwa wananchi wenyewe. Hapa ndiyo inatakiwa sasa mtusaidie ku-link kwa sababu tunavyoelewa ni kwamba uchumi unapokua ni lazima uguse baadhi ya wananchi au pengine wananchi wengi zaidi hasa wanaoishi maeneo ya vijijini. Huko bado tuna matatizo makubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumzia viwanda vidogo vidogo, nashauri Serikali tujikite zaidi kwenye viwanda ambavyo vitainua kilimo. Tujikite kwenye viwanda vya mazao yanayolimwa na wananchi. Kwa mfano, kwa Mkoa wa Dodoma ukianzisha kiwanda kwa ajili ya kuinua zao la zabibu utakuwa umetusaidia zaidi kuliko tukiwa tunazungumza ukuaji wa uchumi wa point za kwenye karatasi ambao hauakisi wananchi wenyewe wanainukaje kimaendeleo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niyaseme haya maana imeonekana kwamba Wabunge wa CCM tuna uoga wa kumshauri Rais, lakini leo nataka nitamke kwenye Bunge hili, Rais anafanya kazi nzuri sana na aendelee kuifanya. Bahati nzuri tumekuwa na Rais kama Mbunge mwenzetu kwa miaka 20, anatujua Wabunge, anaijua nchi, anajua namna ambavyo tuna tabia za kuzusha, hawezi kubabaishwa na maneno yanayotoka humu. Katika nchi yetu kwa miaka mingi sana tumekuwa na malalamiko kwamba Serikali yetu inalindana, mtu anaharibu hapa anahamishiwa hapa, mtu anaharibu hapa anapelekwa hapa, tunataka mabadiliko, amekuja Rais wa mabadiliko, ukiharibu unakwenda kupumzika nyumbani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ndugu zangu nataka niwaambie wala hakuna mtu anayetisha wala hakuna mtu anayeshindwa kumshauri. Ila nataka niwapongeze sana, mimi mara chache sana huwa nawapongeza Wabunge wa Upinzani lakini safari hii nataka niwapongeze, nawapongeza kwa sababu wamejitoa mhanga. Wanaposimama kusema Serikali imefilisika msifikiri wanaisema Serikali, hapana, wana sehemu wanayolenga kwa sababu ili ujue kwamba huyu mtu amefilisika kuna vielelezo. Cha kwanza, lazima ashindwe kulipa madeni, mtu akishindwa kulipa madeni ujue amefilisika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Wabunge wa Upinzani acheni uoga, badala ya kusema Serikali imefilisika, Serikali inayolipa mishahara, Serikali inayowalipa nyie, Serikali inayosomesha watoto bure, tamkeni wazi kwamba Mbowe umefilisika maana umeshindwa kulipa madeni. Tamkeni wazi, hakuna sababu ya kuzungukazunguka unapiga kona ooh mimi nitakamatwa, sasa unatuambia sisi tuje tukuwekee dhamana, ukikamatwa ni kwa makosa yako. (Makofi/Vigelegele)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais ameteua Wakuu wa Mikoa wengi wazuri, lakini wachache nitawataja hapa, wa kwanza Mrisho Gambo, nampongeza sana. Wa pili Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rugimbana Jordan nampongeza sana. Wa tatu, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, nampongeza sana Mongella anafanya kazi nzuri. Rais anawajua watu wake, anapowapanga anajua kabisa nani anaweza kufanya kazi wapi. Big up sana Dkt. Magufuli, endelea kufanya kazi ukiamini kwamba nyuma yako wako watu wanaokuombea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwaambie msamiati mgumu sana. Ni bora mtu ufe mawazo yako yabaki hai kuliko mtu uwe hai halafu mawazo yako yawe yamekufa, ujue wewe umepotea kabisa. Hatuwezi kuogopa kuchukua hatua. Leo hii tunasimama ndani ya Bunge hili tunasema utumishi ni uti wa mgongo, kwenye utumishi haitakiwi kuingiza siasa inakuwaje mtu aliyefikia level ya kuwa mtu mkubwa mpaka Katibu Mkuu leo Mbunge wa CHADEMA, alianza lini? Lazima alianza akiwa huko huko katika Utumishi, ndiyo maana lazima tufukue kila sehemu kuangalia tunao watumishi au tunao watu wanaopiga porojo za siasa badala ya kufanya kazi, lazima tusimamie nidhamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kuna mtu anafikiria kwamba eti tutakuwa na Taifa ambalo halina mabadiliko, haiwezekani! Tumeyaomba sana mabadiliko, tumelala tunasisitiza kwamba tunataka mtu atakayekuja kubadilisha. Kama kuna mfanyakazi anaenda kazini akiwa hana hakika kwamba ajira yake ipo, sawasawa, yeye akachape kazi. Kazi peke yake ndiyo itasababisha ajira yako iendelee kuwepo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tusidanganyane hapa. Tunasimama hapa na kuanza kusema ooh kwenye kikao cha chama cha Wabunge wa CCM wamepewa hela, aaah, wamepewa hela na nani? Mbona ninyi mnachangishwa kila siku hapa? Wabunge wanachangishwa kila siku milioni moja moja, wengine wanakuja wanalia wanasema Lusinde angalia meseji hii tunatakiwa tutoe milioni moja moja kwa ajili ya kesi, mbona sisi hatuyasemi yenu? Sisi tupewe pesa na nani? Wabunge wote tulipewa fursa ya kwenda kukopa, kila Mbunge kakopa, wengine wamekopa 200, wengine 300, leo hii uje upewe milioni 10 ili iweje, ni kutudhalilisha tu.
Msichukue fursa hiyo kutudhalilisha, Wabunge wa nchi hii wote wa Upinzani, wa CCM tulipewa fursa, tumekopa hela nyingi, hakuna Mbunge wa kuhongwa milioni 10 wala wa kupewa milioni moja. Ndiyo maana nyie mnachukua hela zenu kukichangia chama chenu, hakuna mtu anayewazungumza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri sana wakati huu ambapo tunazungumzia mpango, baada ya kuwa nimeshawapa dawa kidogo, ni vyema tukajikita kwenye sekta binafsi. Serikali imeambiwa uti wa mgongo ni sekta binafsi. Rais amekwenda kufungua kiwanda kuna watu wanapiga kelele tena, mnaenda kwa Bakhresa, katika sekta binafsi kuna mtu mjasiriamali jamani katika nchi hii anayemfikia Bakhresa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bakhresa akimuita au akimuomba Rais kwenda kufungua kiwanda chake, uharamu wake uko wapi? Au Bakhresa kuacha kuwachangia wapinzani ndiyo imekuwa nongwa? Maana nashangaa unaanza kumlaumu eti kwa nini Rais kaenda kufungua kiwanda cha Bakhresa kampa na ardhi, kuna vivutio vya kuwafanya wawekezaji wa ndani nao waweze kuwekeza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe Mheshimiwa Waziri Mpango kelele anazozisikia uchumi wa ndani una booster yake. Booster yake ni kuwalipa wadeni wa ndani, ukiweza kuwalipa wadeni wa ndani hela itaonekana mtaani na hizo kelele zitapungua. Mnapokumbuka madeni ya nje ni sawa, lakini kumbukeni na madeni ya ndani. Kuna wazabuni mbalimbali waliofanya kazi kwenye Serikali, hawa wakipata pesa mzunguko wa pesa ndani ya nchi nao utaonekana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunawashauri Serikali muangalie pande zote. Mnaposomesha bure tunaona, mnaponunua ndege tunaona, tunajua yatasemwa mengi lakini endeleeni kufanya kazi kwa sababu hata Mungu angeleta majadiliano na wananchi hicho kikao kisingekwisha. Ndiyo maana ukaona akakaa mbali akaamrisha kama ni mvua, mvua, kama jua, jua. Mwambie Rais tunamuunga mkono, kazi anayofanya ni njema, tumepata Rais wa kunyooka, akinyooka na jambo linaenda kama alivyopanga na ndicho tunachokitaka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu wanalalamika hapa ooh Rais anafanya kazi yeye mwenyewe. Halafu mimi nashangaa hawa jamaa wanasema halafu wanajijibu wenyewe. Wananikumbusha Sauli kwenye Biblia alipokutana na kibano cha Mungu Sauli alisema, ni nani wewe Bwana? Yaani aliuliza swali halafu akajibu kwamba huyu ni Bwana, ndiyo hawa! Huku unasema Rais anafanya kazi zote, huku tena unabadilika unasema Rais anawatisha watumishi. Mtu anayewafanyia kazi zote atawatishaje sasa wakati kazi zote anafanya yeye mwenyewe. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka Rais ananyooshe hii nchi na tuna uhakika Magufuli nchi hii atainyoosha kutoka pale ilipokuwa imeishia kwenda mbele zaidi. Nawaambia moja ya vitu ambavyo nataka Watanzania watusaidie 2020 nchi zetu za ulimwengu wa tatu hizi kuwahi kila kitu nalo ni tatizo, hata kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi tuliwahi ndiyo maana mnaona hoja zenyewe…..
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Nimalize? Sasa unaingiaje Bungeni kujadili kaptura ya Mfalme wa Morocco hiyo ina uhusiano gani na matatizo ya wananchi? (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba nikushukuru sana kwa kunipa fursa hii ili na mimi nichangie kuhusu hizi Wizara mbili. Wabunge wengi wamepongeza na mimi nawaunga mkono kwa pongezi walizotoa kwa Waheshimiwa Mawaziri kwa uchapakazi na hata zile tahadhari zilizotolewa kuhusu namna gani wanatakiwa kukaza buti kwa ajili ya kuhakikisha Taifa linasonga mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hizi ni Wizara nyeti sana na zimepewa watu barabara kabisa ambao wanafanya kazi kwa ufanisi na weledi mkubwa. Kazi yetu siis kama Wabunge ni kujaribu kuonesha ni maeneo gani Serikali iyatilie mkazo na ni maeneo gani yanahitaji uangalifu mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni Mbunge kutoka jimbo la Mtera na ni jimbo la vijijini, naiomba Serikali itazame kwa jicho la huruma sana majimbo ya vijijini. Hata hili ongezeko la watu mijini tunalolisema linatokana na vijijini kukosa huduma nyingi za msingi, huduma nyingi za msingi zikipatikana vijijini, nataka niwahakikishie mlundikano wa watu mijini utapungua kwa kiwango kikubwa. Tukizungumzia maji safi tunazungumzia mjini, tukizungumzia umeme wa uhakika, tunazungumzia mjini na tukizungumzia matibabu ya uhakika tunazungumzia mjini. Vijijini watu hawatakaa, watakimbilia mijini ili waje wapate huduma hizo muhimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namuomba sana Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI, suala la kuhakikisha kila kata, hata ikiwezekana kila tarafa ipate kituo cha afya cha uhakika, gari la kubeba wagonjwa la uhakika, hii itasababisha watu wabaki vijijini na wasukume mbele gurudumu la maendeleo. Tukiweka bajeti kubwa za maji mijini, tukaweka bajeti kubwa za afya mijini, watu wa vijijini hakuna namna yoyote ya kuwaacha wao wakae vijijini wasije huko mjini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie barabara. Barabara za vijijini Halmashauri nyingi hazina uwezo wa kuzitengeneza. Uharibifu wa barabara ni mkubwa! Kuna majimbo ni makubwa mno. Kwa mfano, Jimbo langu mimi, ukitoka hapa ilipodondoka treni wakati ule, ukatoka Igandu mpaka mwisho Ilanga kuna kilometa zaidi ya 220; haiwezekani ambulance ziwe mbili au moja, inachakaa haraka kabla ya muda, kwa sababu inapita kwenye barabara mbovu halafu hazitoshi ambulance zenyewe. Kwa hiyo, naiomba Wizara ya TAMISEMI ihakikishe inatoa msukumo mkubwa kwenye bajeti za kutengeneza barabara za ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumezungumza na Waheshimiwa Wabunge hapa, wamesema sana kuhusu Halmashauri zetu, kwa Waheshimiwa Madiwani. Tunawapozungumzia Waheshimiwa Madiwani kuna baadhi ya Halmashauri Madiwani wana hali mbaya, hata posho zao zile stahili zao hawapati, sembuse hiyo ya kuongeza! Hawapati hata zile za ndani za kwao. Wanakopwa kuendesha vikao, kwa sababu ya ugumu wa Halmashauri; katika vyanzo vya mapato wengine wanategemea kilimo; ukame umekuja, hawawezi kukusanya mapato ya ndani. Kwa hiyo, hata hiyo asilimia 10 tunazosema wapewe akina mama na vijana haziwezi kupatikana kwa sababu Halmashauri hazina makusanyo ya kutosha. Zile kodi za kero zilizofutwa, hakikisheni Serikali mnazifidia kuzilipa Halmashauri ili zipate uwezo wa kujiendesha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nazungumza sana kuhusu mapato ya Madiwani, tukiyaboresha Diwani ndio anayezika, anauguza, anasomesha. Akibaki na mapato yake madogo Diwani anakimbilia kwa Mbunge, anamkuta vilevile naye yupo taabani, inakuwa shida kubwa sana kuendesha majimbo. Kwa hiyo, naomba sana Waheshimiwa Madiwani wapewe uangalizi mkubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumzia maji. Miradi ya maji inasuasua sana. Ukienda unakuta hela ipo. Nauzungumzia mradi wa Kata ya Manzase, umechukua muda mrefu sana. Tumempeleka Katibu Mkuu wa CCM, tumempeleka Waziri Mkuu, Mzee Pinda na ndio alikuwa aufungue, imeshindikana. Leo ukienda anakwambia BOQ imefanyaje; ukienda wanakwambia mkandarasi sijui amefanyaje, wananchi hawataki kusikia maneno, wanataka kuona wanapata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, imefika wakati mpaka wananchi wanakata tama. Mheshimiwa Jafo kaenda pale kasukuma akaweka na tarehe, lakini bado. Wanakwambia sijui tutangaze tenda upya, tubadili kutoka mfumo wa diesel kwenda solar, maneno hayatusaidii, tunataka maji katika katika Kata ya Manzase, hatutaki maneno. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumze kwa utulivu sana kwenye suala la ulinzi na usalama; nadhani juzi sikupata muda wa kutosha. Nashauri Serikali iunde dawati kwenye Wizara ya Mambo ya Ndani au Wizara yoyote, ambalo wananchi watakwenda kuripoti pale juu ya ndugu zao waliopotea. Tusizungumze pale anapopotea mtu maarufu tu, Watanzania wengi sana wamepotea katika mazingira ambayo watu wengi hawajui wako wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tengenezeni dawati halafu mruhusu wananchi waje watoe taarifa za upotevu wa ndugu zao, mtashangaa idadi ya watu waliopotea bila taarifa.

Kwa hiyo, nashauri Serikali badala ya kulaumiana sisi wenyewe sijui kuna kikundi kinafanya nini, nilisema juzi mimi mwenyewe ni muhanga, nina mjomba wangu anaitwa Nikanoli, aliondoka mwaka 1980 mpaka leo hatujui yuko wapi. Wala siyo maarufu, wala hakuwa Balozi wa Nyumba Kumi useme ametekwa; aliondoka akapotea. Yupo mwingine alikuwa anaitwa Yoel, ameondoka tangu miaka ya 1970, hata kumjua watu hawamjui. Kwa hiyo, ukienda kwa kila Mbunge inawezekana ukakutana na taarifa za upotevu wa watu kwenye majimbo mengi sana, kama siyo yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naiomba Serikali, badala ya kuanza kushutumiana sijui nani anafanya nini, tutengeneze dawati watu wapeleke habari za upotevu wa ndugu zao, za upotevu wa jamaa zao ili waweze kutafutwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge hapa tunazungumzia juu ya heshima na Daktari tena kazungumza vizuri sana. Daktari akasema tubadilishe fikra na huu ni mchango wake karibu wa pili anatushauri tubadilishe fikra kwamba tuwe na mtazamo mpya. Sina hakika kama yeye anao, lakini anasema katika huo mtazamo mpya, tuache kushughulika na watu wadogo wanaomtukana Mheshimiwa Rais. Ila Daktari huyo huyo anayetaka tubadilishe fikra, anasema Kiongozi wa Upinzani aheshimiwe ni mtu mkubwa. Mheshimiwa Rais atukanwe, Mheshimiwa Mbowe aheshimiwe, hatuwezi kwenda hivyo! (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunataka heshima, turudi kwenye Katiba inayosema kila mtu anastahili heshima, bila kuangalia cheo chake. Watanzania wanastahili heshima, Mheshimiwa Rais anastahili heshima, Kiongozi wa Upinzani anastahili heshima, Mbunge anastahili heshima, Diwani anastahili heshima. Tutaheshimiana na tutaona kuendesha nchi ni kazi rahisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukibadili fikra zetu tukaacha eti watu wadogo wadogo wanamtukana Mheshimiwa Rais kwenye simu, hao tusishuhulike nao, ila tushughulike na viongozi waliotengeneza, aaah, sidhani kama ni sawa sawa!

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nalishauri Bunge hili, kama tunataka kutoka hapa tulipo, kwanza kuna baadhi ya mazoea tuyaache. Pale tunaposema tunahitaji mabadiliko kwenye nyanja fulani, nina hakika kabisa Mheshimiwa Rais anafanya kazi nzuri kabisa ya kubadilisha mfumo wa nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi yetu kubwa badala ya kumrudisha nyuma tumpe moyo, tumtie nguvu, Mawaziri tuwape moyo, tuwatie nguvu wasukume gurudumu mbele. Nani asiyejua maeneo mengi yaliyokuwa yamesimama? Wizara kama ya Ardhi ilikuwa na matatizo chungu nzima! Tulikuwa na kesi chungu nzima, lakini sasa hivi zinatatuliwa kwa speed kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwaombe sana, tunapozungumzia heshima tuzungumze pande zote mbili. Nataka niseme kwamba, jana ilitolewa hoja hapa, watu wameidharau na wengine wakaona kama inachomekwa. Nasikia ninyi mna vyombo hapa mnaweza kutuambia, kuna Mbunge amekamatwa na konyagi anaingia nayo Bungeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi juzi hapa Serikali imemwajibisha Kitwanga kwa kudhaniwa tu amelewa, akawajibishwa. Leo Mbunge anaingia na konyagi ndani ya Ukumbi wa Bunge, huko amekamatwa. Tunataka tuone na ninyi meno yenu yako wapi katika kumwajibisha huyo Mbunge, kama mtaweza! Maana kazi yenu ni kusema tu, siyo kutenda. Bahati nzuri Mbunge mwenyewe anatoka upande huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka tuone mtakuwa wakali kwa kiwango gani kwa Mbunge anayeingia amelewa, halafu ana chupa ya konyagi ndani ya eneo la uzio wa Bunge! Sisi tumeshaonyesha njia, Mheshimiwa Waziri amekuja anatikisika, hana chupa, hana nini, mkasema ooh, amelewa sijui nini na Uwaziri kaupoteza. Ninyi sasa tuone sasa mtachukua hatua gani ili...(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, na mimi naungana na Waheshimiwa Wabunge wote, ambao wamemshukuru Mungu kwa ajili ya afya yako tunaendelea kukuombea. Inawezekana hata sisi wenyewe tuna matatizo lakini bado hatujapimwa sawasawa. Kwa hiyo, kwa kweli tunakuombea Mheshimiwa Spika uendelee kuimarika ili uweze kuwatumikia wananchi wako wa Jimbo la Kongwa lakini na sisi Wabunge wenzako.

Mheshimiwa Spika, pongezi zangu za pili zinakwenda kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu pamoja na Mawaziri wanaomsaidia kazi. Hotuba ni nzuri, wameiwasilisha vizuri lakini imegusa maeneo mengi muhimu. Isipokuwa kuna baadhi ya maeneo Waheshimiwa Wabunge tutawakumbusha ili nanyi muweze kuongeza nguvu kwenye maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, tunamshukuru Mungu sana kwa sisi wakazi wa Mkoa wa Dodoma kutupatia mvua za kutosha mwaka huu ingawa baadhi wa maeneo zimeleta majanga makubwa sana, kama uharibifu wa barabara inayotoka Dodoma Mjini kwenda Ilangali. Pale daraja limesombwa kwa hiyo, tuna uhakika kwamba Serikali watafuatilia kulitengeneza haraka ili kuweza kuwanusuru wananchi wa ukanda ule wa Tarafa ile ya Mpwayungu ili mazao yao ya biashara yaweze kufika kwa wakati hapa Dodoma ambapo kwa kweli ndiko kwenye soko kubwa tunalolitegemea.

Mheshimiwa Spika, yamezungumzwa mengi nami naomba nitoe mchango wangu kidogo katika baadhi ya masuala ambayo yamezunguzwa mahali hapa.

Mheshimiwa Spika, tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais. Mheshimiwa Rais amefanya kazi kubwa, kuna mambo ambayo yamefanyika kwa miaka miwili na nusu unaweza kusema ni miujiza. Kwa sababu matukio makubwa na ya kutisha tumeyaona yakifunguliwa na haya yote yakikamilika, reli ikakamilika, umeme wa maji ukakamilika, barabara zetu zimekamilika nina hakika kabisa kwamba yatachagiza maendeleo kwa kiwango kikubwa. Kwa hiyo tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais na tunamwomba Mungu aendelee kumlinda.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ununuzi wa ndege; nataka niwakumbeshe baadhi ya watu wanaweza kuwa aidha wadogo au wamesahau. Uamuzi wa kulifufua shirika la ndege sio mara ya kwanza, baada ya iliyokuwa Jumuiya ya East Africa kufa na ndege nyingi kubakishwa nchini Kenya na sisi tukapata moja. Mwalimu Nyerere mwaka 1977 alifufua shirika lile kwa kununua ndege zinazokadiriwa kufikia kama nne au tano kwa wale watu wazima kama mimi mnaweza kukumbuka.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Mheshimiwa Rais anachokifanya sasa anafufua shirika la ndege, ni kama vile una debe moja la mbegu unajiuliza ukaange ule au uende ukapande zizae ili waweze kutumia wengi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa wengine wamezungumza kwa dharau sana. Mtu anasema eti watu wanaenda kupiga picha kwenye ndege, watu wanashangilia ndege. Hapa wako Wabunge hapa wako humu ndani kwa sababu wameletwa na ndege. Wengine helicopter zilipokuwa zikikusanya watu ndiyo wakachaguliwa kuingia humu ndani ya Bunge wamesahau.

Mheshimiwa Spika, kuna chama hapa hakina ofisi ya mkoa, hakina ofisi ya wilaya, kimepata ruzuku zaidi ya mabilioni ya pesa, lakini huwa wanakodia ndege wakati wa uchaguzi ili Wabunge wao waweze kushinda. Wamesahau wanaingia humu ndani kutukana ndege maskini wa Mungu. Hivi kama kweli isingekuwa helicopter zinawasaidia, si tungeona mmejenga hata ofisi ya Mkoa?

Mheshimiwa Spika, tumeona NCCR Mageuzi mahali pengine wana ofisi, tuwameona CUF wana ofisi ya kueleweka lakini kuna chama kina kaofisi squatter pale Kinondoni wanapiga kelele kila siku hapa.

Mheshimiwa Spika, unashindwa kuwaelewa kabisa kwa nini msioneshe hayo maendeleo kwenye chama chenu kwa ruzuku mlizopewa? Mbona mnakodia helicopter hizo hizo? Kwa hiyo, kununua ndege Mheshimiwa Rais mimi naona ni jambo jema kwa sababu tutapanda sisi, watapanda Watanzania na lile shirika litaleta maendeleo makubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, dharau kwenye viwanda vidogo si njema. Tunadharau mafundi cherehani, hivi hapa Waheshimiwa Wabunge bila mafundi cherehani si tungekuwa uchi tu hapa. Wengi tunashona tunashona nguo huko. Leo nataka niwaambie kiko kiwanda ambacho kinatusaidia sana juzi tu ndiyo nimekiona. Kiwanda cha Saloon jamani kumbe Wabunge tunalindwa sana na saloon. Kuna Mbunge mmoja amekosa kwenda Saloon siku tatu, sura yake imebadilika kabisa, wala siyo yeye.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunataka tuwashukuru sana hata watu wa saloon; akinadada wa saloon, akinababa wa saloon kumbe mnatuweka vizuri mpaka tunaonekana watu wa maana mbele za watu. Kwa hiyo hivi ni viwanda vidogo ambavyo Watanzania vinatuletea maendeleo lakini na sisi vinatuletea heshima fulani. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Spika, nataka nikubaliane, Waheshimiwa Wabunge wameongea vizuri sana hapa kuhusu gharama za uchaguzi, hili nataka niwaunge mkono. Kuna gharama kubwa sana kurudia chaguzi ndogo, lakini ambao wanaweza kutusaidia kwa kweli wanaweza kutusaidia Wapinzani, kwa sababu Serikali imeshaundwa Wabunge wengi wa CCM una uhakika Mbunge wa Upinzani hata akishinda haendi kubadili Serikali. Kwa nini mnaweka wagombea msiweke ili kunusuru mapesa hayo yaende kwenye maendeleo. Hakuna sababu maana hata ukishinda kiti kimoja, kilo moja ya sukari haiwezi kwenda kukolea kwenye pipa la maji.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo hakuna sababu ya vyama vya upinzani kuweka wagombea kwenye uchaguzi mdogo, maana tayari umeshafahamika aliyeshinda kafahamika kuna sababu gani za kuweka mgombea kwenda kupoteza hela za nchi. Kwa hiyo ni vema wakatuunga mkono, kuanzia sasa hivi kukitokea uchaguzi mdogo hakuna sababu ya wao kuweka mgombea na sisi tutapita bila kupingwa, hakutakuwa na gharama pesa zote zitaenda kwenye maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna Waheshimiwa Wabunge wamezungumza sana leo hapa, wamezungumza kwa uchungu mkubwa sana. Mbunge mmoja wa CHADEMA amezungumza sana kuhusu Rais kutoka Kanda ya Ziwa na kwamba ni aibu sana Kanda ya Ziwa kukosa maji. Akasimama ndugu yangu Nape akasema Waziri Mkuu anatoka Kusini ni aibu kukosa maendeleo. Sasa najiuliza tuna Waziri Mkuu wa Kusini, tuna Rais wa Kanda ya Ziwa? Tuna Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jamani. Hatuna Rais wa Kanda, tuna Waziri Mkuu wa Jamhuri Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, tusiwafanye viongozi wetu wakawa viongozi wa Kanda haiwezekani na mtakuwa hamtutendei haki. Hivi na sisi ambao Spika unatoka Dodoma mbona unawaruhusu wao kusema, kwa nini usituruhusu sisi wa Dodoma tuseme sana ili shida zetu zisikilizwe. Haitawezekana!

Mheshimiwa Spika, hili jambo lazima tujue Viongozi wakishakuwa wa Kitaifa, wanaongoza Taifa la Tanzania na sio sehemu walikotoka. Kwa hiyo kama Rais anahakikisha kwamba kwao hakuna maji lakini wengine wamepata huyo ndio Rais bora analitazama Taifa, hatazami upande wake. Kama Mheshimiwa Waziri Mkuu anaelekea sehemu zingine za Tanzania anazunguka kuhakikisha maendeleo yanapatikana huyo ndio Waziri Mkuu bora.

Mheshimiwa Spika, sikutegemea kwamba tuanze kuwagawa viongozi wetu kwa namna ya wanakotoka haiwezekani. Tusimame katikati tuishauri Serikali mambo ya msingi yafanyike ili nchi nzima ipate maendeleo. Nchi hii ni kubwa ndugu zangu, nchi hii changanya Uganda, Kenya, Rwanda, Burundi ndipo unaweza ukaikaribia ukubwa wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, huwezi ukapeleka maendeleo kwa haraka na maeneo yote yakaridhika ndugu zangu, twendeni taratibu. Twendeni taratibu, twendeni awamu kwa awamu. Sehemu zingine ukipeleka sehemu zingine wanasubiria, sehemu zingine ukipeleka sehemu zingine wanasubiria, tutafika tu mahali na nchi nzima itapata maendeleo. Kwa hiyo nawaombeni sana Waheshimiwa Wabunge tuvute subira, viongozi wanahitaji kuungwa mkono.

Mheshimiwa Spika, watu wanazungumzia habari ya usalama…

T A A R I F A . . .

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, naipokea taarifa yako Mheshimiwa Musukuma. Bahati mbaya tu mwenyewe hayupo maana na mimi nilitaka asikie lakini atakusikia. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tunaomba sana sisi kama Taifa kama nchi, viongozi wetu wagawanye rasilimali za nchi kwa usawa maeneo yote. Hata yale ambayo haya vivutio vikubwa vinavyokusanya hela nayo wayatazame. Kwa mfano tunaelewa sisi Dodoma hapa tuna zao la zabibu. Zao la zabibu hili likifunguliwa viwanda vya kutosha tutanufaika, watu wetu watapata pesa, watalima, watauza.

Mheshimiwa Spika, kuhusu mifugo, sisi tumepata kiwanda kizuri kabisa cha kuandaa ngozi pale katika Kijiji cha Idipu, namwomba sana Mheshimiwa Waziri Mkuu umeme upelekwe kwenye kile kiwanda. Kile kiwanda hakiishi kwa wakati kwa sababu umeme wenye nguvu kubwa haujafika pale kiwandani.

Mheshimiwa Spika, umeme ukiweza kufika na sisi ni wafugaji, tuna ng’ombe wengi wanachinjwa kwenye minada, ngozi nyingi zinapelekwa pale, wananchi wa jimbo la Mtera nao watapata maendeleo makubwa. Tutanufaika na hii hoja ya uanzishwaji wa viwanda maana kiwanda tayari kinajengwa.

Mheshimiwa Spika, naomba tuitazame Tanzania katika yale maeneo ambayo yamesahaulika kwa muda mrefu tuyatupie macho. Maana kuna mwingine ana maji ana barabara nzuri akija hapa kupiga porojo ni sawa, lakini kuna wengine vitu vyote vitatu hawana, tuangalie kimoja wapate. Watu ambao wanaishi kijijini; tunapoteza akinamama wengi sana wakati wa kujifungua, kwa sababu unaweza kukuta wakati wa kujifungua njia imefunga, maji yamekata barabara, gari haliwezi kufika.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa kupata ambulance, lakini kuna mahali ambulance hazipiti kwa sababu barabara ni mbovu. Tumeondoa barabara kutoka Halmashauri tumezipeleka TARURA, lakini ukitazama uwezo wa TARURA na bajeti yao bado ndogo bado hai-reflect maendeleo ya barabara za vijiji. Kwa hiyo, tunaomba waongezewe pesa, ziwe nyingi ili waweze kutengeneza zile barabara kwa kiwango kinachotakiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tuwatazame sana! Watu tumejenga sekondari za Kata, tumejenga mashule vijijini, lakini bado namna ya kuwachagiza wananchi wa vijijini ni umeme ufike kwa wakati. Kuna baadhi ya maeneo hayana umeme Tarafa nzima ya Mkwayungu haina umeme. Tukiwapelekea umeme watu wa Mkwayungu baadhi ya mambo yao mengi watafanyia kule, watakamua alizeti zao kule, hawana haja ya kuzileta Dodoma Mjini. Dodoma Mjini wataleta mafuta. Kwa hiyo viwanda vidogo vitaanzishwa Mkwayungu.

Mheshimiwa Spika, nakuomba sana tunaposimama hapa na sisi lengo letu ni kuwaunga mkono na kuwatia moyo Waheshimiwa Mawaziri. Ukilitazama Baraza hili ni dogo kuliko lililopita, lakini Mawaziri wake wanafika kila kona ya Tanzania, lazima tuwapongeze na kuwatia moyo. Hawa ni binadamu usiku kucha wanasafiri wanafika kwenye majimbo yetu wanaongea na wananchi, lazima na sisi tuwaunge mkono.

Kwamba Waheshimiwa Mawaziri tunatambua kazi kubwa mnayoifanya sisi kama Wabunge wenzenu tunawaungeni mkono, endeleeni kuchapa kazi ili Taifa hili liweze kusogea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, watu wamezungumza hapa kuhusu amani. Amani na utulivu ipo lakini ipo kwa sababu na wahalifu nao wapo. Tuwaombe Serikali waendelee kuwasaka wahalifu kwenye kila nyanja ya uhalifu unavyotokea. Tusiichafue Serikali kwa sababu ya kosa moja.

Mheshimiwa Spika, ikitokea kiongozi mmoja wa dini amekengeuka pengine amezini Mungu aepushe mbali hatuwezi kulaumu dini nzima, haiwezekani. Tunamlaumu huyo huyo kwa kufanya hilo kosa. Kwa hiyo lazima tukubaliane, kwamba uhalifu upo lakini tuitake Serikali kupambana na uhalifu kama inavyofanya siku zote.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana na naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali Wizara ya Maji na Umwagiliaji 2018/2019
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, namshukuru Mungu kupata nafasi asubuhi hii ili nami niweze kuchangia Wizara hii ya Maji ambayo nyeti na muhimu kwa maendeleo ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili na mimi kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mtera niweze kueleza machache kwa ajili ya Wizara hii ya Maji.

Mheshimiwa Spika, ni maneno mazuri sana yanazungumzwa na Waheshimiwa Wabunge tangu jana mpaka asubuhi hii na wengine wanashauri sasa Serikali hii itolewe ingiizwe Serikali ambayo hamna kitu wala ofisi haina, halafu ilete maji. Vitu vya ajabu sana! Hata aliyeanzisha benki alihakikisha jengo zuri, imara, wahudumu wazuri ili kuweka imani ya watu kuweka hela zao. Lakini hiyo benki nyingine mtu aende akaweke huko, benki ya makuti, ofisi hakuna, matete, haiwezekani. Nadhani alikuwa anajifurahisha, haiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya hilo, kama alivyotoa utangulizi aliyezungumza, na mimi naingia kwenye Wizara ya Maji. Namshukuru sana Mheshimiwa Waziri na Naibu wake, wanafanya kazi nzuri. Hata katika umri alionao Engineer tunamwona namna anavyohangaika kwenye Majimbo na mpaka Mheshimiwa Aweso anazidi kutoka kipara kwa kujitwisha ndoo za maji, pamoja na Katibu Mkuu Profesa Kitila Mkumbo, tunawashukuru sana.

Mheshimiwa Spika, Wizara na Maji ni Wizara muhimu sana na kama ikifanikiwa, kwa kiasi kikubwa itapunguza bajeti za Wizara nyingine, maana Wizara hii ni mtambuka, inaweza kusaidia Wizara ya Afya, inaweza kusaidia hata ongezeko la watu mijini. Hivi kwa sisi Wabunge wa vijijini, kwenye vijiji kule hakuna maji, hakuna barabara, hakuna afya, watu wataachaje kuja mjini kuzifuata huduma hizo?

Kwa hiyo, Wizara hii ikiweza kufanya kazi zake sawa sawa, watu wakapata maji safi na salama, baadhi ya magonjwa kama ya matumbo yanafutika kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa nataka niishauri Serikali, wakati mwingine ijifunze kupitia vitu vidogo. Nataka nichukue nafasi hii kuwashukuru sana watu wa WFP chini ya uongozi wa dada Neema Sitta kwa kazi nzuri waliyoifanya kwenye Jimbo la Mtera.

Mheshimiwa Spika, hapa Mheshimiwa Waziri akinisikiliza vizuri, anaweza kuona namna ambavyo Serikali wakati mwingine inashindwa kusimamia matumizi mazuri tu. Ikisimamia matumizi mazuri, value for money ikazingatiwa, tutapata maji mengi na kwa uhakika.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano watu wa WFP wametupa shilingi milioni 799 kwenye Jimbo la Mtera. Katika milioni hizo hizo 799 tumepata matenki makubwa matatu ya lita 800,000, tumepata visima 18, tumepata mashamba heka 300 kwa ajili ya umwagiliaji, tumepata visima12 vilivyofungwa solar power kwa ajili ya wananchi kupata maji.

Mheshimiwa Spika, hebu angalia matumizi haya ya shilingi milioni 800 tu hizi kasoro moja yameweza kuleta vitu hivyo vikubwa ambavyo wananchi leo hii wananufaika. Ukija kwenye Serikali, hamna kitu. Inatolewa shilingi bilioni moja pale Mkwayungu kwa ajili ya kujenga bwawa la umwagiliaji, bwawa halijakamilika, hakuna miundombinu na shilingi bilioni moja imeliwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, unaweza ukaona matumizi mabaya kwenye miradi ya maji kwa upande wa Serikali yanatuletea matatizo makubwa. Hawa wameweza kutoa shilingi milioni 800 zimetengeneza mambo ambayo ni maajabu kabisa. Mheshimiwa Waziri na Katibu Mkuu na Naibu Waziri piteni mwone kwa macho namna ambavyo pesa ikisimamiwa hata ikiwa kidogo inaweza kufanya vitu vikubwa.

Mheshimiwa Spika, watu wamepata maji ya kunywa, wamepata irrigation wanamwagilia na maisha yao yako safi. Ukienda kwenye Kata ya Fufu katika Vijiji vya Suri, Chibori na Fufu yenyewe, WFP wametufanyia mambo makubwa kwa pesa kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukienda mahali pengi kwenye miradi ya Serikali, hela nyingi zimetumika, zaidi ya shilingi bilioni moja imeliwa pale Mkwayungu na maji hakuna. Kwa hiyo, nakuomba sana, hebu twende tuangalie wenzetu hawa wamewezaje? Wamefanikiwaje? Wamefunga solar system katika visima vyote. Hakuna mwananchi anayehangaika kutafuta bill ya umeme, kutafuta nini na pampu za kisasa, zinazomwagilia mashamba kwa uhakika.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naishauri Serikali, tumepata Makao Makuu ya Nchi, haitakuwa na maana kama Mkoa wa Dodoma hautakuwa scheme za umwagiliaji. Vijana wakiweza kumwagilia huko kwenye Majimbo ya vijijini waleta bidhaa zao hapa mjini, zitakuja kuwanufaisha na wao na watoto wao. (Makofi)

Msheshimiwa Spika, Wizara ya Maji ikijitahidi kusimamia resource kidogo iliyopo, nina uhakika inaweza kutosha kutusukuma mbele. Kwa mfano, nimekuja hapa kuomba maji kwa ajili ya vijiji vyangu; Kijiji cha Loji hakina maji, Kijiji cha Ng’aheleze hakina maji, kijiji cha Handali hakina maji. Hivi ni vijiji vikubwa mnoo! Kijiji cha Ng’ng’i leo hii kina wakazi karibu 8,000 lakini hakina maji ya uhakika. Halafu Halmashauri baadhi ya visima vya zamani vikiharibika vinashindwa kuvitengeneza. Kwa hiyo, utakuta kuna matatizo ya visima vya zamani na kuna matatizo ya visima vipya, havipatikani.

Mheshimiwa Spika, naomba sana, Mheshimiwa Waziri atakapokuja hapa kujibu, atupatie maji katika Jimbo la Mtera na atupatie maji katika Kijiji cha Muheme.

T A A R I F A . . .

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, taarifa yake wala siwezi kuikataa, naipokea. Naipokea kwa maana ya kwamba akasimamie na pesa alizosema CAG zimeliwa kwenye chama chake, kama anao uwezo huo akasimamie ili ziweze kuleta maendeleo. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilijua tu, ukisikia kelele ujue tayari tiba. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba Mkoa wa Dodoma ambao hamna mito inayotiririka maji kwa msimu mzima, uangaliwe kwa makini hususan katika uchimbaji wa mabwawa. Sisi maji yetu yanapita tu, mvua ikinyesha, yanapita yanaondoka moja kwa moja. Hatuna mito inayotiririsha maji msimu mzima. Kwa hiyo, tunaiomba Wizara ilitazame hilo kama eneo mahususi tukipata mabwawa ya kutosha, tuna uwezo mkubwa sana wa kuzalisha, tuna uwezo mkubwa sana kwa kulima kilimo cha kisasa, tuna uwezo mkubwa sana wa kujisimamia. Tunachotaka Serikali mtuangalie muwe mnafanya research basi, kuna Mkoa huu tofauti yake na Mkoa huu.

Mheshimiwa Spika, WFP wameleta hela kidogo lakini zimefanya mambo makubwa, zimejenga mpaka matanki ya maji ya shule za msingi, hela kidogo hii! Ndiyo maana namwomba Mheshimiwa Waziri na Katibu Mkuu na Naibu Waziri watembelee wakaone, siyo vibaya kuona kwa macho na kuja kusimamia pesa zenu mlizonazo ili ziweze kutusogeza mbele. Hata mabwawa ya zamani yaliyochimbwa enzi za Mwalimu Nyerere, leo hii yapo; mengine yameshajifukia. Liko bwawa la Mkulabi hapa Dodoma Mjini, lipo Bwawa Mlowa Bwawani pale. Mwalimu alichimba mabwawa makubwa lakini leo hii hayana maana yoyote.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba sana atakaposimama Mheshimiwa Waziri atusaidie sana kupata maji katika vijiji nilivyovitaja vya Jimbo la Mtera na kuhakikisha kwamba tunapata kilimo cha umwagiliaji. Mbona nimewaomba sana kwenda Mkwayungu kuona ule mradi ambao Serikali imetumbukiza shilingi bilioni moja, lakini hamna kitu chochote? Mbona hamuendi? Twendeni mkaone kwa macho ili mfananishe yale yaliyofanyika pale Mkwayungu na ambayo wenzenu wanaweza kufanya.

Mheshimiwa Spika, tukifanya namna hiyo tutakuwa tunazuia ulaji, tutakuwa tunazuia wizi na umangimeza na nina uhakika Serikali ya Awamu ya Tano itazuia mambo hayo na ndiyo maana nawasihi mfike mwone ufisadi uliofanyika, mchukue hatua ili wananchi wa Kijiji cha Mkwayungu waweze kupata maendeleo kwa kilimo cha umwagiliaji ambacho kilikusudiwa kufanyika eneo lile.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema maneno hayo, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na naipongeza sana Serikali kwa kazi nzuri mnayoifanya. Wizara hii lazima iwe na kelele kwa sababu maji ni muhimu sana. Tunataka kuwatua ndoo kichwani akina mama. Tusiwatue wa mijini tu, hebu tazameni na Majimbo ya vijijini jamani. Vijijini nako kuna akina mama wengi wanaoteseka, wanatoa maji mbali, wanachelewa kufanya kazi zao za kujiletea maendeleo.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri anafanya ziara mwenyewe anakutana na hiyo hali, tusaidieni na sisi Wabunge wa vijijini. Hawa wa mjini ambao wana lami, wana hospitali nzuri na nini, nao kwa maji wangesubiri kidogo, geukieni upande mwingine.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, ahsante na ninaunga mokono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kutuzawadia tena pumzi yake leo bure ili tuweze kukaa kwenye Bunge lako Tukufu na tuweze kuchangia hoja za Wizara mbili; ile ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na ile ya Utawala Bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wengi wamesema juu ya Waheshimiwa Watendaji Wakuu wa Wizara hizi; nami nachukua fursa hii kuwapongea sana ndugu yangu Mheshimiwa Selemani Jafo, Waziri; pamoja na Mheshimiwa George Huruma Mkuchika, Waziri; pamoja na Waheshimiwa Manaibu Waziri, Mheshimiwa Dkt. Mary Mwanjelwa; pamoja na ndugu yangu Mheshimiwa Waitara na Naibu Waziri mwenzake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mawaziri hawa wanafanya kazi kubwa sana. Tunaona namna wanavyopambana na shida za watu wetu, siyo vizuri sana kuwavunja moyo, wakati mwingine tuwapongeze kwa kazi nzuri wanazozifanya. Mheshimiwa Jafo pamoja na timu yake ya Watendaji wametusaidia sana sisi wa Jimbo la Mtera kutuletea pesa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Mpwayungu. Wametupa shilingi milioni 700 pale, wakatupa shilingi bilioni 1,500,000,000/= kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya; vilevile wametusaidia miradi ya maji yenye thamani karibu ya shilingi bilioni mbili hivi na ushee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunawashukuru sana ingawa nina ombi maalum kwa ajili ya ambulance ya Tarafa ya Mpwayungu, ilipata ajali na ikachakaa kabisa, lakini tunamshukuru Mungu haikuua. Tunaomba tusaidiwe kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Tarafa ya Mvumi, kile Kituo cha Handali ili kwa kushirikiana na Kituo cha Mpwayungu, hospitali ya wilaya iweze kupumua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile timu ya ukaguzi wa zahanati, naomba Mheshimiwa Jafo hii aitilie maanani sana. Huko vijijini kuna zahanati nyingine hazina sifa hata za kung’oa meno, lakini wanang’oa meno. Hatujui vile vifaa kama viko katika hali ya ubora. Kuna magonjwa mengi sana ya kuambukiza ambayo ni hatari sana kama zahanati zile hazikugaliwa sawasawa hasa kwenye upande wa tiba ya kinywa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maneno mengi yemezungumzwa, nami bahati nzuri nimepewa kazi ya kupiga penalty ya mwisho. Unapopiga penalty ya mwisho lazima uwe umetulia. Ndugu zangu tunapozungumzia habari ya utawala bora kwanza tukubaliane mambo ya msingi. Utawala Bora, vyama vya siasa vinashindana kwa sera. Kila chama kinapeleke sera kwa wananchi kwenda kuomba kichaguliwe. Uchaguzi Mkuu umepita, chama kilichochaguliwa ni CCM, ndiyo kimechaguliwa kwa wingi. Chama hiki hakichaguliwi kwa rangi zake tu, kinachaguliwa pamoja na ubora wa sera zake. CCM ndiyo inapewa nafasi Serikali itafsiri ilani yake kwa miaka mitano bila kujali kwamba Jimbo hili la CHADEMA wala Jimbo hili la NSSR, wala Jimbo hili la chama gani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ilani inayotekelezwa pale ni ilani ya mshindi wa ujumla. Wapinzani wanapewa kazi ya ku- oppose, kuleta sera mbadala kama wanazo, lakini wetu hawa kwa sababu hawana, ndiyo maana mnasikia madudu haya. Kama wangekuwa na sera mbadala, wangekuwa wanaeleza kwa hoja. Unasikia hoja, hivi ni Serikali gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi namwombea sana Mheshimiwa Rais, Mungu ambariki aendelee kutumia hekima. Nyie Mawaziri, mwendelee kutumia hekima. Hivi ni Waziri gani anatukanwa, anasemwa vibaya halafu tena anatakiwa apeleke maendeleo kwenye Jimbo la huyo anayemtukana? Hii iko Tanzania tu. Ndiyo maana mnaona tunapata tatizo kwa sababu uchaguzi ukiisha, wale walio shinda ndio wanakuwa na kazi ya kutafsiri ilani yao ya uchaguzi kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa leo upinzani wa Tanzania mnaona wanapiga kelele, wanataka kufaidi kwenye kushindwa. Mimi sijawahi kuona. Ninyi mmeshindwa, mnataka kufaidi nini? Mmeshindwa, lazima m-face problem, lazima m-face utulivu, lazima mkae muwaache walioshinda watekeleze ilani ya uchaguzi. Sasa leo eti timu imefungwa bao tatu bila, hiyo hiyo inataka ishangilie. Nyie mbona mnachekesha! Mimi sijawahi kuiona hii. Hii naiona Tanzania tu. Mtu anasimama anasema, ohoo, tunanyimwa hiki, tunanyimwa hiki. Si mmeshindwa, mtulie. Lazima... (Makofi)

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Bwege kaa chini, Mheshimiwa Lusinde endelea.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ndiyo maana unaona kunaundwa Kambi ya Serikali na Kambi Rasmi ya Upinzani na wanaundwa Mawaziri wa Serikali na Mawaziri Kivuli. Leo wanaona aibu hata kutaja Wizara zao, kwamba huyu ni Waziri Kivuli. Hawasemi, kwa sababu wanajua kivuIi hakiaminiki. Nani ataamini kivuli? Wanajua kivuli saa sita kiko sawa na mtu, saa saba kinaanza kuwa kirefu, saa 12 kivuli ni kirefu kuliko mtu, wanajua. Wewe uliwahi kuona wapi Mbunge unasimama unampangia Mheshimiwa Rais kitu cha kufanya? (Kicheko/Makofi)

Jamani hii nchi mbona hatuna heshima, unampangia Rais kwamba akija kwangu afanye moja, mbili, tatu, hivi nyumbani kwako hata baba yako mzazi unaweza kumpangia wewe kwamba, leo baba tule hiki, inawezekana? Haiwezekani, kwanza hamjasoma vizuri Katiba ya nchi, Rais wa nchi ni mkuu wa nchi, Rais wa nchi ana madaraka makubwa ambayo hata kikatiba hajayatumia, mnapiga kelele; Rais hayo madaraka yake akiyatumia hamponi ninyi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndio maana mimi sasa nawaomba Watanzania hebu mwakani tukubaliane, unajua wakati mwingine kuwahi sana nalo ni tatizo, kuwahi sana nayo ni shida.

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaambiwa kwamba, kuwahi sana ni tatizo. Tunaambiwa hata mtoto wa kike wakati mwingine asubiri akomae via vyake vya uzazi ndio abebe ujauzito, kinyume cha hapo ataugua. Upinzani wa Tanzania uliwahi sana, kwa hiyo, nahisi umepata matatizo, uliwahi sana. Kwa hiyo, sishangai kuwaona Kambi nzima ya Upinzani badala ya kujenga hoja za kisiasa zenye muelekeo wa kusisimua Serikali mnaleta hoja za udumavu; angalia upinzani ulivyodumaa kwa sababu ya kuwahi, wamewahi sana kabla ya wakati wao wamejikuta wamedumaa. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, natangaza kwenye Bunge hili, tatizo tulilonalo tuna upinzani mdumavu. Wamedumaa kisiasa, wamefika mahali hawawezi kujenga hoja mbadala, kazi yao ni kulalamika na kupiga kelele kama unavyowasikia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri nchi yetu Mheshimiwa George Mkuchika kwenye utawala bora ashikilie hapohapo. Hakuna nchi yenye utawala bora usio na mipaka, haipo duniani. Wameng’ang’ana wanataka kufanya maandamano ya nini? Mbona mazoezi asubuhi hawaendi sembuse maandamano? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna Serikali ya namna hiyo duniani, uruhusu watu wafanye fujo tu. Eti mtu anasema ooh, mimi nataka niende nikahutubie mkutano, wewe jimbo lile umeshindwa ukahutubie kitu gani? Utaeleza nini? Huna sera, huna ilani, huna kazi unayoifanya pale unataka ukahutubie ueleze nini? Kama sio kufanya kampeni kabla ya wakati? Ninyi mnataka mpate ruhusa ya kwenda kufanya kampeni kabla ya wakati, sisi ndio washindi jamani tunashindwa hata na Miss Tanzania? Kachaguliwa mrembo mmoja, wengine wote wamekaa kimya, wamekaa kimya, lakini hawa wanashindwa; sisi ndio washindi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakasikia kadada kamoja kanasema Lusinde nakupenda, tulia dawa iingie. Mimi nina mke na watoto watano, tukikutana nao kwenye chai wanaongea maneno ya unafiki kabisa, ooh tunaunga mkono, mnachapa kazi vizuri, tunaunga mkono. Tukija humu ndani wanajifanya ooh, Mwenyekiti patachimbika, pachimbike kwa hawa? Hakuna kitu cha kuchimbika hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naiomba Serikali ishikilie hapohapo. Angalia kuna watoto wanawaona wanavyozomea, wanawaona ni watu wamechanganyikiwa kabisa. Humu ndani ya Bunge kuna watu wanakuja kujifunza uendeshaji bora wa Bunge, wao wameongea sisi tumenyamaza…

MBUNGE FULANI: Umechanganyikiwa wewe.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: …sisi tunawapa dawa, ooh, ooh. Watoto wadogo hawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nakusihi, tunaomba Serikali kwenye kusimamia sheria isiangalie huyu mpinzani, isiangalie huyu CCM, wote kula kichwa, wakivuruga amani weka ndani, hizo siku 120 walizosema ni kidogo. Kwa hiyo, nataka nikwambie dawa yake ukitaka nchi inyoke, sheria zifanye kazi asiwepo mtu wa kubembelezwa. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hiyo dawa kuingia naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, nimshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya asubuhi ya leo ili na mimi niweze kuchangia hili Fungu 28 la Wizara ya Mambo ya Ndani.

Mheshimiwa Spika, Wabunge wengi wamempongeza sana Mheshimiwa Waziri Kangi Lugola pamoja na Naibu wake Masauni pamoja na Katibu Mkuu na watendaji wote wa vyombo vya ulinzi na usalama walioko chini ya Wizara hiyo wanafanya kazi nzuri sana. Mimi niwe shuhuda tu kuthibitisha kwamba Jeshi la Polisi, Magereza na Uhamiaji ni miongoni mwa vyombo muhimu sana kwa ajili ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, wakati tunajadili leo, kuna tofauti kubwa sana kati ya mjadala wa leo na mjadala wa jana Waheshimiwa Wabunge mtakubaliana nami. Jana tulifikia mahali hata kuambiwa kwa nini mnawapa pole Polisi ya kung’atwa na mbu wakati ni kazi yao. Sasa mimi nikawa napata taabu sana, hii ni kazi ya kizalendo, si tu kazi yao kazi wanayoifanya ni ya kizalendo ambayo ina mazingira magumu yanayohitaji kupongezwa.

Mheshimiwa Spika, aliyesema maneno hayo akasema ninyi wengine hamjawahi kulala hata ndani ninyi, wewe si umelala ndani kwa kujitakia mwenyewe? Kwani ukiwa hutaki kulala ndani utalala ndani jamani! Siyo rahisi, maana Polisi wanashughulika na watu waovunja sheria. Polisi hawashughuliki na kila mtu barabarani hapa, ingekuwa kila mtu basi kakamatwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nature ya chombo chenyewe tunachokijadili, kwanza ni chombo chenye mafunzo, lakini chombo kina watu wanahenya, kuna watu wanasoma na kuhenya juu.

Mheshimiwa Spika, unajua hapa Wabunge, Bunge lililopita muliamua wewe na Mheshimiwa Spika Anna Makinda, tukaenda JKT, tulikwenda na mdogo wangu Mheshimiwa Neema hapa, nadhani tulijifunza kidogo utofauti wa hivi vyombo, kwa hiyo, nataka nikupongeze Mheshimiwa Neema kwa ajili ya ukakamavu, kumaliza. Jamani counter ya jeshi la polisi haiwezi kufananishwa na counter ya hoteli, haiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, counter ya polisi lazima umkute mtu ana sura ya jiwe, ametulia, anakusikiliza umasema nini, ya hoteli utamkuta mtu anatabasabu, karibu, chumba kipo, hiyo ni ya hoteli, siyo polisi! (Makofi/Vicheko)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, polisi lazima wawe wakakamavu, siyo kitu cha mchezo.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Tena ndiye ninayemtaka huyo.

SPIKA: Wewe unampa taarifa Lusinde, haya toa taarifa. (Kicheko)

T A A R I F A

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, mzungumzaji anayezungumza, ni vizuri tukaweka rekodi sawa hapa, anayesema hajanitaja lakini najua ananisema kwa hiyo, lazima niweke rekodi sawasawa. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, na ni rafiki yangu, hoja niliyozungumza jana kwamba polisi wanatimiza majukumu yao, Serikali huwa inatoa nafasi za kazi, mtu yeyote anapokwenda kuomba kazi yoyote huwa wanajua consequences zake, anajua polisi wana kazi gani, Askari wana kazi gani.

Mheshimiwa Spika, hata wewe hapo unafanya kazi ya kizalendo, tunategemeana kama Taifa. Tulichokizungumza jana, na nilivyosema jana wengine hamjalala polisi, na nimetoa ushahidi kwamba nimesingiziwa nimelala kwa makosa. Kwa hiyo, ninachotaka kusema, kufanya kazi ngumu kisiwe kisingizio cha kuvunja sheria, hiyo ndiyo hoja tunayoizungumza, lakini siyo kwamba tunadhalilisha kazi ya polisi.

MWENYEKITI: Mbona unahutubia sasa si taarifa iwe fupi!

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, ndiyo hiyo.

SPIKA: Mchungaji ahsante sana, Mheshimiwa Lusinde unapokea taarifa!

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, ukipenda kachumbali upende na pilipili. Watu wote, wanaofanya upinzani kwenye maeneo yao, wote wanaingia kwenye matatizo! Mheshimiwa Zitto alijaribu kufanya upinzani ndani ya CHADEMA, kumpinga Mheshimiwa Mbowe, yupo CHADEMA? Amemalizwa, ameondoka, alijaribu Kafulila, yupo salama CHADEMA! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, muelewe kazi mnayoifanya ina hatari yake, ndiyo ninachotaka kukwambia ukweli hapa, yaani huwezi ukajiita upinzani, yuko wapi, Mheshimiwa Komu alijaribu juzi kumteta Mwenyekiti na mwenzake, wako wapi! Kwa hiyo, ninachotaka kusema, hamuwezi kuwa wapinzani, halafu mkawa salama tu, haiwezekani! (Makofi/Vicheko)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka niwasaidie, kwamba kazi wanayoifanya ni kazi inayoweza kuwapa matatizo wakati wowote! (Makofi/Vicheko)

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, nitulie kaka yangu kasimama amua.

SPIKA: Mheshimiwa Komu, nini tena rafiki yangu! (Kicheko)

T A A R I F A

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Haya, dakika moja bwana maana yake tunakaribia mwisho.

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Spika, nataka kumpa taarifa Mheshimiwa Lusinde, ambaye tuna historia nzuri sana na yeye kwa sababu tumemkuza sisi na anajua. Sasa nipo, na sijazurika, sijateteleka, nipo, maana yake yeye amesema yuko wapi, nipo hapa. (Makofi)

SPIKA: Ila jambo moja tu, hajakanusha kama alimteta Mwenyekiti wake. (Makofi/Vicheko)

Mheshimiwa Lusinde, endelea!

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, nilichotaka kusema, kwanza namheshimu sana kaka Komu na ni mmoja wa watu waaminifu sana na alichokuwa anakisema Komu kwa kweli, naweza nikakiamini kwa upande wangu, kwamba kweli kuna matumizi mabaya ya ruzuku mle ndani. Na yeye ndiye aliyekuwa mhasibu wa chama, kwa hiyo, hata, alichofanyiwa alisema ameonewa. Nilitaka kumuonyesha Mheshimiwa Msigwa, kwamba wanaoonewa hawako huku tu, hata ndani ya chama chenu mnaonea watu, mmojawapo mmemuonea Mheshimiwa Komu! Mheshimiwa Komu amesema, kuna matumizi mabaya ya ruzuku, amevuliwa nafasi zake zote, ameonywa, yuko kwenye uangalizi hapo alipo. Sasa hii siyo sawa na Mheshimiwa Kubenea, (Makofi/Vicheko)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, jeshi la polisi linafanya kazi nzuri sana. Niombe Waziri wa Mambo ya Ndani, nichukue fursa hii kumpongeza sana Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Mroto. (Makofi/Vigelegele)

Mroto anafanya kazi nzuri, jeshi la polisi ni beat, huwezi kucheka na waharifu, kwamba hapa kuna Bunge, Wabunge wanavaa cheni za dhahabu kama unavyowaona wengine humu, halafu Mroto acheze na maandamano maandamano hapa, Wabunge mtaporwa hizo cheni. (Kicheko)

Kwa hiyo, Mroto anaposema hataki mchezo watu watachakaa, yuko sahihi kwa ajili ya kuwalinda ninyi. (Makofi/ Vigelele)

Mheshimiwa Spika, jeshi la polisi kazi zake nyingi, kazi za operation, kwa hiyo, tunaomba Makao Makuu yamehamia hapa Dodoma na jeshi la polisi liimarishwe hapa Dodoma! Wapeni magari ya kufanyia kazi, njia nzima ya kutoka Dodoma kwenda Iringa, kuna vituo viwili tu vya polisi navyo vyote havina gari na wanapita Wabunge wengi, wanapata matatizo huko, kwa hiyo, wapeni, wapeni magari waweze kufanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Mtera tuna Tarafa tatu, tumeomba pikipiki tatu tu Mheshimiwa Kangi, mpaka leo! Tusaidieni, ili wale polisi waweze ku-move kwenda sehemu moja hadi nyingine. Majuzi hapa kuna mtu alijinyonga, ilichukua karibu siku nzima, mtu kuweza kufika pale, polisi hana pikipiki, hana nini mpaka Mbunge nimetoa gari kwa ajili ya kwenda ku-rescue hiyo situation. Kwa hiyo, sisi tunaomba jeshi la polisi liimarishwe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini jambo lingine ambalo limezungumzwa hapa, mikutano ya hadhara, kuna mikutano ya hadhara kama mtakumbuka Waheshimiwa Wabunge, kila mkutano ulikuwa unasababisha mauaji! Iringa alikufa mtu, Morogoro alikufa mtu, Singida alikufa mtu, ni mikutano gani hiyo, Arusha, mikutano hiyo imetuletea matatizo. Kwa hiyo, jeshi la polisi wakati mwingine linapima, hivi kama Bungeni tu tunaongea kwa mihemko hivi, Mbunge anaongea mpaka anasema rubbish, jana hapa. Sasa unajiuliza huyo Mbunge akiwa kwenye mkutano wa hadhara wa kwake binafsi ataongea maneno gani huyu! Lazima jeshi la polisi lipige marufuku, jamani uchaguzi ukishakwisha siasa zinahamia humu, nje tuache watu wachape kazi, tutakutana 2020! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimewaambia siku zote nazidi, unajua wakati mwingine huwa natema madini sijui kama huwa mnasikiliza, uchaguzi ukiisha, mnaachia washindi wafanye kazi waliochaguliwa, na washindi ni Chama cha Mapinduzi. Wapeni nafasi watekeleze Ilani, maswali mtatuuliza mwakani kama yapo, na nina uhakika yatakuwa hayapo, vituo vya afya vinajengwa, maji yanapatikana, sasa kutakuwa na maswali gani tena, hakuna! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nasema, baadhi ya Askari wachache ambao wametajwa, kwamba siyo waaminifu, hao waendelee kuchukuliwa hatua, kama sheria inavyosema, lakini tusiliharibu jeshi la polisi lote kwa sababu ya mtu mmoja kakosea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jamani ikitokea bahati mbaya Padre, au Shekhe kakamatwa ugoni, siyo dini mbaya, haiwezekani, ni huyo huyo aliyeshikwa, dini inaendelea kuaminika, dhehebu linaendelea kuaminika ila yeye aliyevunja masharti ya imani yake huyo ndiye anayechukuliwa hatua. Tusiwatukane Askari wote kwamba wote hawafai, wote wanakosea, hapana, lakini kuna mambo yamezungumzwa.

Mheshimiwa Spika, jana kilizungumzwa kitu hapa na nataka nikiseme, kwenye taarifa ya CAG iliguswa hapa jana kwamba, Mbunge wa CHADEMA alikopeshwa fedha za kununua gari. Nasema, jambo lile lina harufu ya ukwepaji wa kodi, kwa nini nasema hivyo, Wabunge tuna exemption, leo CCM wakinitumia kununua gari la chama, maana yake CCM wanataka kukwepa kodi, kwa sababu wanajua mimi nitasamehewa kodi fulani, lakini ukiniambia kwamba eti alikopeshwa na chama, halafu ameshindwa kulipa chama kimemnyang’anya, si kweli, hapo CHADEMA msikwepe mlitaka kuwepa kodi! (Makofi)

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Spika, kuhusu utaratibu.

SPIKA: Nini tena Chief Whip!

KUHUSU UTARATIBU

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Spika, jambo analolizungumza rafiki yangu anayeongea sasa hivi, Mheshimiwa Chenge akiwa kwenye Kiti chako, alishatolea uamuzi na hiyo hoja anayoisema haiko kwenye taarifa ya CAG! (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Selasini ni hoja gani.

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Spika, ni suala la Mbunge wa CHADEMA kukwepa kodi. Sasa CAG hakuliweka hivyo, hoja ni kwamba kuna gari lilinunuliwa kwa mkopo kutoka CHADEMA na ile gari iko kwa jina la mwanachama, haliko kwenye jina la Baraza la Wadhamini la chama. Kwa hiyo, agizo ni kwamba lile jina liondoke kutoka kwenye jina la mwanachama liende kwenye jina la Baraza la Wadhamini na siyo kukwepa kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na Mheshimiwa Chenge akiwa kwenye kiti chako alitoa hiyo ruling.

SPIKA: Hivi huyo mwanachana ni nani!...

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, huyu mwanachama hatajwi, huyu mwanachama ni Mbunge, Mbunge, siyo mwanachama wa kawaida, na CHADEMA ituambie kabla ya mwaka huu, au mwaka gani iliwahi kumkopesha mtu fedha ya kununua gari, wakati Wabunge wote tunakopeshwa hapa! Jamani kuna harufu ya kukwepa kodi, ndicho ninachosema na niko wazi, niiteni popote hata kwenye maadili niiteni nithibitisha, nyie mnataka kukwepa kodi kwa kumtumia Mbunge mwenye exemption! Ninyi siyo watu wasafiki kiasi hicho! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka nizungumze kuhusu mauaji, jeshi la polisi…

SPIKA: Mheshimiwa malizia.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, jeshi la polisi tunaliomba sana. Kuna watu wengi tu, siyo wale wanaotajwa maarufu, kwamba wameuawa taarifa zao hazipo, wako wengi, nina mjomba wangu anaitwa Nikanoli, amepotea tangu mwaka 1979 mpaka leo. (Kicheko)

Tunaomba jeshi la polisi lipewe vifaa vya kisasa vyenye weledi ili viwasaidie katika uchunguzi hasa wa mauaji, hasa wa mauaji. Watanzania wengi, siyo hawa tu wanaotajwa, wako wengi ambao wamepotea wengine wameuliwa, bila sisi kujua wala bila familia zao kuelewa.

Mheshimiwa Spika, lakini la mwisho kabisa, niombe suala la uraia limezungumzwa sana, hili suala halijawahi kujadiliwa humu Bungeni, lakini kwa kuwa limeanza kusemwa humu, tuombe mamlaka za Serikali zilifanyie kazi. Watu wamezungumza sana kuhusu wafanyabiashara maarufu, kuna siku hapa ametajwa Vedagri wa Mwanza ni mfanyabiashara mkubwa amewekeza sijui Mafya, wapi, Mwanza, hawa watu wote ambao wengine siyo maarufu wakulima ambao wanataka kuhamia nchi hii wapewe huo uraia, kama ni haki yao na kama kuna matatizo vyombo vichunguze, viangalie ubaya wao, viwakatalie kama ambavyo wengine wamewahi kukataliwa bila kusemwa Bungeni na wengine wamewahi kupewa bila kusemwa Bungeni, Serikali iendelee kuchapa kazi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja, ahsante sana kwa kunisikiliza. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimshukuru Mungu sana kwa kupata fursa hii ya kuchangia Wizara ya Nishati, lakini zaidi sana nikushukuru wewe kwa kunipa nafasi hii ili niweze kutoa mchango.

Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kukupongeza sana, unapokaa kwenye kiti chako Bunge linaendeshwa kisayansi na linaendeshwa kwa utulivu mkubwa sana. Wabunge tunaheshimiana na kuthamini kila mchango wa Mbunge anayesimama na hivi ndivyo inavyotakiwa iwe hata kwa wenzako wengine wote unaowaachia nafasi ya kiti wanatakiwa kwa kweli kulinda heshima ya Bunge na hasa pale Mbunge anaposimama na kutoa mawazo yake ambayo pengine wewe unaona kwako hayakufurahishi lakini ni lazima umpe nafasi ya kumsikiliza na zogo la Bunge la juzi halikuwa jambo zuri sana.

Mheshimiwa Spika, nitoe pongezi sana kwa Mheshimiwa Waziri Dkt. Mendrard Chanancha Matogolo Kalemani pamoja na Naibu wake Mheshimiwa Subira Mgalu pamoja na Katibu Mkuu na timu nzima ya Wizara. Watu hawa wanafanya kazi kubwa ya kuzunguka nchi nzima, lakini kubwa zaidi kwao hawa wawili ni mahusiano mazuri na Waheshimiwa Wabunge. Hili ni jambo zuri sana, lazima kujenga PR ya pamoja maana hii kazi ni ngumu, kazi inahitaji ushirikishwaji na ushirikiano wa karibu.

Mheshimiwa Spika, vilevile spidi ya Mheshimiwa Waziri na Naibu wake naiona ni kubwa kuliko spidi ya makandarasi, yaani Waziri anagawa umeme kwa spidi sana kuliko wajenzi, kama ni forward wakati mwingine unasema inaweza ikaingia kwenye nyavu yenyewe ikaacha mpira nje, sasa kidogo hapo inatupa mazingira magumu sana.

Mheshimiwa Spika, nizungumzie Jimbo la Mtera katika tarafa zangu tatu, Tarafa ya Mvumi Mission, Tarafa ya Makangwa na Tarafa ya Mpwayungu. Tunavyo vijiji ambavyo bado havijafikiwa umeme, lakini kama unavyojua ukijua kulaumu ujue na kushukuru. Nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa kufikisha umeme kwa mara ya kwanza katika Tarafa ya Mpwayungu katika Kijiji cha Nagulo na Kijiji cha Mpwayungu chenyewe.

Nimwombe sana vile vitongoji anavyovitaja, vijiji anavyovitaja kwamba umeme hautamruka mtu, wale watu wanaorukwa wote kimbilio lao ni kwa Mbunge. Kwa hiyo unajikuta Mbunge anafanya kazi kubwa sana baada ya Waziri kuondoka, wakisema mbona Waziri alisema tusirukwe, sasa kwa nini tunarukwa. Kwa hiyo nimwombe sana Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu wake na timu nzima washughulike kwa namna ya pekee kuhakikisha kwamba yale maeneo waliyoagiza maagizo yao yanatekelezwa.

Mheshimiwa Spika, ukisoma ilani za hivi vyama ambavyo vina Wabunge humu unaweza ukacheka sana. Nimepitia ilani ya CHADEMA hapa sioni mahali wameahidi megawati 18,000 alizokuwa anazisema mzungumzaji wa CHADEMA, kwa hiyo unaweza ukaona wakati mwingine maneno haya yanayozungumzwa ni maneno ya kufurahisha tu Bunge. Unajua faida kwenye uongozi wa nchi wakati mwingine haionekani moja kwa moja…

T A A R I F A

SPIKA: Taarifa Mheshimiwa Esther.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nataka kumpa Mheshimiwa Lusinde taarifa kwamba wakati Mheshimiwa Silinde anachangia alisema trilioni sita ambazo zinatarajiwa kujenga Stiegler’s Gorge zikilinganishwa na extension one ya Kinyerezi ambayo inajengwa kwa bilioni ambazo ni megawati 185 equivalent yake ni ya kujenga megawati 18,500, hakusema inatokana na Ilani ya CHADEMA.

SPIKA: Mzungumzaji pia hajasema hivyo kama inatokana ameuliza tu kwenye ilani yenu hakuona. Endelea Mheshimiwa Lusinde.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, shemeji yangu Matiko nataka nimsaidie tu kwamba unajua wakati mwingine faida kwenye shughuli za Serikali haifananishwi na faida ya genge la nyanya au pengine mgahawa. Huwezi ukaiona moja kwa moja wakati mwingine unaona MSD wananunua dawa nyingi mpaka zile za ugonjwa wa Ebola, sio mpaka wasubiri ugonjwa uwepo ndio wanunue.

Kwa hiyo, wakati mwingine tunasema kwa nini dawa zina-expire zina-expire kwa sababu zilikuwepo na ugonjwa haukutokea, sasa huwezi ukangoja mpaka utokee ndio uanze kununua. Kwa hiyo kuongoza Serikali tunawafundisha tu, ni mambo makubwa sana, huwezi kufananisha na biashara ya genge au mama ntilie, kwa hiyo kuna faida unaweza ukazitafuta kwa macho usizione.

Mheshimiwa Spika, nimezungumzia sana kuhusu kuwabana wakandarasi ili waendelee kusambaza umeme katika vijiji vyote. Tumeona namna ambavyo…

T A A R I F A

SPIKA: Mheshimiwa Lusinde unapewa taarifa na Mheshimiwa Getere.

MHE.BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, naomba kumpa taarifa mzungumzaji anayeongea kwamba CHADEMA katika miaka ijayo itakapokuwa kwenye madaraka tutahakikisha tunafanya utafiti wa kina kuhusu vyanzo mbalimbali vya nishati hatimaye kutunga sera ya kupata nishati hizo. Kwa taarifa kamili ni kwamba mpaka leo CHADEMA haina chanzo cha nishati, kwa hiyo anachosema Silinde ni sawa tu.

SPIKA: Mheshimiwa Lusinde, tafadhali.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, nimesema kuongoza nchi faida zake ni wananchi kunufaika. Sisi Rais wetu na Serikali ya Awamu ya Tano imeamua kujitoa muhanga kujenga kinu cha kufua umeme katika maporomoko ya Rufiji. Haya ni maamuzi makubwa ambayo impact yake itaonekana wakati Watanzania watakapoanza kunufaika na ndio maana hakuna Mbunge humu ndani anayesimama na kusema umeme huo nisipewe humwoni. Kwa hiyo ni kweli kwamba Serikali imepatia na iendelee kujenga huo umeme ambao utatunufaisha sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nchi yetu sasa kwenye vijiji ambavyo vilikuwa vimesahaulika kabisa, tumeona mawaziri wetu wakiwasha umeme mpaka kwenye nyumba za nyasi, nyumba za tembe, kule waliko Watanzania, hili ni jambo jema. Tumeona umeme unawashwa mpaka Loliondo, kwa babu wa kikombe, hili ni jambo jema. Kwa hiyo nataka nimsihi sana Mheshimiwa Waziri aendelee.

Mheshimiwa Spika, nimeachiwa hapa taarifa na jirani yangu na mimi ni mtu muungwana Mheshimiwa Mwamoto amesema nizungumzie habari ya Kata ya Image. Kwa bahati nzuri naomba ku-declare interest, Kata ya Image ndiko nilikoolea mimi, Waziri apeleke umeme kwa wakwe zangu pale Image katika Jimbo la Kilolo na wakwe zangu nao kule wafurahie waseme na mzee alitaja ili mtoto wao aendelee kubaki mikono ni mwangu. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo kwenye suala la kuongoza nchi ni suala ambalo hata wenzetu wameonyesha kwamba kuna kipindi unahesabu faida, ukiona faida ni kubwa unachukua huo huo uamuzi. Tumeona CHADEMA ni chama cha kidemokrasia na maendeleo lakini tumeona demokrasia hawaitendi, wana Mwenyekiti ana miaka 20 kwa sababu gani, pengine wanaona kuna faida kubwa kuendelea na huyo Mwenyekiti. Kwa hiyo wakati mwingine huwezi kuona faida ya moja kwa moja mpaka watu wakuelimishe kwamba hapa sasa unatoka kwenye reli. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika,Jambo lingine ambalo naliona hapa naona hapa tunazungumzia madeni ya TANESCO. Mheshimiwa Waziri hapa nataka anisikilize kwa makini sana. TANESCO imekuwa na madeni makubwa sana…

SPIKA: Mbona hakuna anayesimama upande huu huo msumari. (Kicheko)

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, TANESCO ina madeni makubwa sana na madeni haya yanatokana na capacity charge za makampuni, makampuni haya matatu yanaipa mzigo mkubwa sana TANESCO. Kuna IPTL, kuna Aggreko, kuna Symbion, haya makapuni kila kampuni moja kwa mwaka linaitia deni TANESCO karibu bilioni 635, sasa hii si sawa. Serikali iondoe haya makampuni, iondoe mitambo yao, wanaipa TANESCO madeni makubwa sana, wanaagiza mafuta, wanaagiza vitu gani, matokeo yake ni kwamba tunapoteza fedha nyingi na tunaipa TANESCO mzigo mkubwa sana wa madeni.

Mheshimiwa Spika, vilevile ukiangalia kwa hesabu tu za shule ya msingi ukiondoa mitambo ya haya makampuni matatu utaokoa karibu trilioni mbili, maana ni trilioni moja na bilioni 930 na kitu, kwa hiyo utakuwa umeokoa karibu trilioni mbili. Hii itasaidia sana kuboresha uendeshaji wa TANESCO na wao watafika mahali watafanya kazi zao vizuri.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo nimeona linatupa tabu, umeme ukikatika kutokana na mvua inawachukua muda mrefu TANESCO kwenda kushughulikia kwa sababu tuna umeme sehemu nyingi vitendea kazi vichache, magari machache ya TANESCO, mafundi wachache sasa wanachukua muda mrefu na kupoteza muda mrefu na kupoteza fedha nyingi, maana hivyo vijiji vina wateja tayari.

Mheshimiwa Spika, nimeona kuna kipindi Ndebo walikosa umeme, Mvumi Mission walikosa umeme inachukua mpaka wiki moja na nusu sasa hii si sawa, tuwarahisishie, aidha kwenye maeneo ambayo wanaona udongo wake haustamili sana wakati wa mvua wapitishe umeme chini au wanaweza kutumia umeme wa nguzo za zege, ukitumia umeme wa nguzo za zege ukazipitisha umeme juu maana yake eneo hilo hata kama mvua ikinyesha zege lile linazidi kujiimarisha.

Mheshimiwa Spika, tunaishukuru sana Serikali ya Awamu ya Tano, haya maamuzi wanayoyafanya ni maamuzi ya utekelezaji wa Ilani ya Chama chetu. Hatuwezi kurudi nyuma kwa sababu tuliwaahidi Watanzania na wenzetu hawa ambao wanatupinga nao ni maamuzi ya chama chao, lakini hakuna mmoja hapa anayesema hataki umeme, sisi tuendelee kuwahudumia na wao kwenye majimbo yao tuwahudumie. Tunapopitisha hii bajeti tunapitisha pamoja na kusaidia majimbo ya Upinzani wa nchi hii kwa sababu kule kuna Watanzania, tunawahudumia Watanzania.

Mheshimiwa Spika, tuwahudumie wananchi wote kwa sababu mwakani nataka nikuhakikishieni kutakuwa na mabadiliko makubwa sana kupitia hii Wizara ya Nishati, Watanzania wamewashiwa umeme mpaka vijijini kitu ambacho kilikuwa ni ndoto, mwakani wanakwenda kuitunza Serikali hii ya Awamu ya Tano kwa kuipigia kura ambazo hazijawahi kupigwa kwenye Bunge hili, ambazo hazijawahi kupigwa kwenye nchi hii kwa sababu kazi iliyofanyika. Umeme uzuri wake ni kitu kinachoonekana kwa macho, kwa hiyo kila wanapokwenda akina Mheshimiwa Subira tunawaona na wananchi wanavyowapokea tunawaona, hawawezi kuwashangilia vile halafu kesho wakatunyima kura, haiwezekani! Kwa hiyo wanatufanyia kazi njema sana, wanatupa hoja za kwenda kuyasemea hata majimbo yao kwa sababu wanawasikia wanavyokataa bajeti wanawasikia, wanavyokataa umeme wanawasikia, lakini sisi wana CCM kwa sababu tumebeba dhima ya kuongoza Taifa hili tunapeleka umeme nchi nzima bila kujali Mbunge wa Jimbo hilo kasema nini humu ndani ya Bunge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niombe sana kazi ya kusambaza umeme iongezeke nguvu, vinginevyo kama Waziri atatuhakikishia kwamba anayo awamu nyingine ya nne, lakini kama ni awamu zile zile tatu maana yake hii ndio finally. Sasa kwenye finally kusiwe tena na kulegalega maana wametuambia kuna REA awamu ya kwanza, awamu ya pili na ya tatu, hatuna REA awamu ya nne. Kwa hiyo speed yao lazima iwe kubwa kuhakikisha kuwa mambo yanafanyika na yanafanikiwa ili kutupa hoja za kwenda kuwaambia wananchi umeme upo au haupo, wanasema upo, piga kura kwa Magufuli, shughuli imekwisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimesema gharama za kuendesha nchi ni kubwa, umeme wa maji utatuletea punguzo kubwa sana la gharama na hivyo kuifanya nchi yetu iweze kusonga mbele. Kwa hiyo naomba sana Mheshimiwa Waziri atakaposimama hapa vijiji vyangu avikumbuke; nimeomba umeme Kijiji cha Huzi, Kijiji cha Manda, Kijiji cha Ciifukulo, Kijiji cha Muheme, Kijiji cha Mpwayungu umalizike pale na Mvumi Mission tuhakikishe maeneo yote Chihembe yanapata umeme na kule nilikozaliwa mimi ili wananchi wenzangu waweze kupata maendeleo.

Mheshimiwa Spika, leo tumeona saluni zinafunguliwa vijijini, tumeona watu wanachomelea madirisha vijijini, tunaona vijana wanajiajiri kwa kupitia sekta hii ya umeme. Kwa hiyo niombe sana Mheshimiwa Waziri atakaposimama atuhakikishie kumalizika kwa REA III itakuwa ni lini ili vijiji vyote viweze kupata umeme na mambo yaweze kwenda.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nichukue fursa hii kumshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai na afya ili niweze kuchangia katika mchango unaoendelea sasa wa Wizara ya Fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Dkt. Mpango pamoja na dada yangu, Mheshimiwa Dkt. Ashatu ambaye ni Mbunge wa Mkoa huu wa Dodoma, wanafanya kazi nzuri sana, kazi yao ni njema na tumeona Mheshimiwa Rais akionesha njia kwa kukutana na wafanyabiashara pale Dar es Salaam watano toka kila wilaya na wafanyabiashara wakamwambia mambo mengi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina hakika wakuu wa mikoa na Waziri mwenye dhamana ya Wizara hiyo watakuwa wamepata mwongozo kutoka kwa Mheshimiwa Rais wa namna ya kukutana zaidi na wafanyabiashara wengine wengi zaidi, isiishie pale tu alipoishia Rais, Rais yeye ameonesha njia wao sasa wachukue nafasi hiyo kuendeleza ambayo Mheshimiwa Rais ameyafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kitabu cha Mheshimiwa Dkt. Mpango kinaonesha uchumi unakuwa takribani kwa asilimia saba. Na kila siku nimekwa nikisisitiza sana kwamba hesabu hizi wakati mwingine tuwe tunazihusisha na maisha ya kawaida ya raia wa nchi yetu, tukifanya hivyo tutauona uchumi namna unavyokuwa. Tuwe tuna sample ya pengine wilaya iliyokuwa maskini mwaka jana au mwaka juzi hali yao kwa sasa ikoje, tukifanya hivyo tunaweza tukapata picha ya moja kwa moja namna ambavyo uchumi wa nchi yetu unakuwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeona safari hii TRA wakiondoa kodi kwa biashara mpya. Kitendo hiki kitachagiza sana wafanyabiashara hawa kuweza kujua katika miezi sita amezalisha kiasi gani na anaweza kutozwa kodi kiasi gani. Mwanzoni yalikuwa ni maajabu kabisa, unamkamua ng’ombe halafu ndiyo unakwenda kumlisha, yaani biashara inaanza leo na kodi unaanza sasa. Kwa kweli pale haikuwa sawasawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, na ndiyo maana nikawa natafakari, wakati mwingine maafisa wetu wa kutoza kodi hawa ingekuwa kama zamani ambapo viongozi tulikuwa tunasisitizwa unapotaka kuhamaisha kilimo na wewe uwe na heka yako moja ya kilimo, kwa hiyo, unaweza ukawaonesha wananchi kwa vitendo kwamba wewe unalimaje na unfuataje taratibu za kilimo. Na maafisa wetu watoza kodi hawa na wao wangekuwa walau na biashara, walau duka, anauza ili na yeye tuje tumuone katika miezi sita atakuwa amepata faida kiasi gani.

Mheshimiwa Naibu Spika, unajua ukitaka kupima adha anazopata mlemavu wa macho hebu funga kitambaa cheusi halafu nenda sokoni, ukikoswa na bodaboda ya kwanza tu utakitoa kile kitambaa. Kwa hiyo, kwa kweli wakati mwingine tunafanya vitu kwa sababu sisi hatuishi maisha hayo. Kwa hiyo, rai yangu kwa watu wa TRA ni yaleyale maelekezo ya Mkuu wa Nchi kwamba wawe rafiki na wafanyabiashara badala ya kuleta lugha ambazo zitakuwa zinaudhi baadhi ya wafanyabiashara na kuwakatisha tamaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo nachangia vitabu vyote viwili; kitabu cha Mheshimiwa Dkt. Mpango na kitabu cha Kambi Rasmi ya Upinzani. Na kwa kweli sikusudii kukichana hata kidogo, labda pengine ntakichana kwa hoja tu. Kuna watu wanajaribu kuzalisha hoja kwamba Serikali, Mawaziri, sijui wanahofia maelezo ya Kambi Rasmi ya Upinzani, si kweli.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikinukuu katika hotuba yao ukurasa wa kwanza anasema, namnukuu Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani:-

“Mheshimiwa Spika, kama mkakati ndiyo huo wa kudhoofisha Upinzani Bungeni kwa kuwafukuza Wabunge wa Upinzani. Napenda kulithibitishia Bunge lako kwamba mkakati huo umeshindwa kabla hata haujaanza kutekelezwa. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni iko imara zaidi leo kuliko jana ndiyo maana kila wakati tunapowasilisha maoni yetu hapa Serikali yote inahaha kutujibu”. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, haya maneno si ya kweli nataka nieleze hapa kwamba kama ikitokea Mwalimu Nyerere akarudi hapa akiwa na rafiki yake Bob Makani, hawa watu wawili wote watakuwa na mshangao mkubwa sana. Mwalimu Nyerere kuna mambo yatamshangaza na Bob Makani kuna mambo yatamshangaza. Bob Makani alikuwa Mwasisi wa CHADEMA, Mwalimu Nyerere Mwasisi wa CCM, hawa wawili wanatashangaa!

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati Mwalimu akifika Lumumba atashangaa kukuta ofisi ya ghorofa ambayo hakuiacha, Bob Makani atashangaa kukuta ule mgahawa bado upo pale. Yaani nataka niwaambie hawa watu watashangaa sana. Bob Makani kila atakapojaribu kwenda Kinondoni atakuta hata rangi zilizopakwa za CHADEMA bado ni zilezile, hazijawekwa mpya, atashangaa sana Bob Makani, kwamba hawa watu ndio walikuwa wa maendeleo hawa?

Mheshimiwa Naibu Spika, kubwa zaidi Mwalimu atakapokuja atakwenda Chimwaga akidhani ndiyo Ukumbu wa CCM, ataambiwa ni chuo kikuu, atashangaa Mwalimu kwamba hii kazi imefanywa. Atapotea atakuwa anakwenda Kizota anafikiri bado tunafanyia mikutano Kizota, ataambiwa hapana, shuka hapo katikati kwenye daraja, Mwalimu atashangaa sana, atakuta mabadiliko ni makubwa ambayo Bob Mnyanga Makani hatayaona CHADEMA. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Bob Makani kuna kitu atataka kujiuliza, atasema labda niende sasa kwenye demokrasia maana ndiyo jina la chama chetu, hebu niulize demokrasia inatendekaje ndani ya CHADEMA, atakuta Mwenyekiti ni yuleyule, atashangaa sana Bob Makani. Hawa watu ndiyo mnasema eti sisi tunawahofia, hawa, ambao hata Bob akija leo atawashangaa. Atauliza Mwenyekiti wa chama nani, ataambiwa yuleyule uliyemuacha, wakati huku Mwalimu ataambiwa Mkapa alimaliza, akaja kijana wako Kikwete kamaliza sasa yuko Magufuli, Mwalimu atashangaa kukuta demokrasia inatekelezwa ndani ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka niseme kweli kwamba hawa jamani hata mzee wa paka huwa anapokea, hawa ndio mnasema tuwaogope? Hatuwezi kuwaogopa hawa. Mwalimu Nyerere atauliza chama changu vipi mfumo wake wa Viti Maalum unafanya kazi, ataambiwa wapo, Wabunge wa Viti Maalum wapo. Bob Makani akiuliza CHADEMA atasema wapo lakini wanapangishwa chama, milioni moja na laki tano kila mwezi wanalipia chama. Kwa hiyo atashangaa sana, hawa watu siyo wa kututisha sie. Pia kila atakapokuwa akiuliza, ataambiwa basi chama kingine ataambiwa, cha Cheyo Mwenyekiti bado Cheyo; cha Mrema, Mwenyekiti bado Mrema, NCCR Mageuzi ataambiwa bado Mbatia; hawa ndio waje watutishe sisi? Hawa? Akiuliza ataambiwa na Dovutwa bado anaendelea, akiuliza ataambiwa na Lipumba naye ni Mwenyekiti; kwa kweli Mwalimu atashangaa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nataka niwasihi Watanzania kwamba sisi hatuko hapa kwa ajili ya kushughulika na hawa, hawa wameshajifia jamani, hakuna upinzani nchi hii, wamejifia wao wenyewe kutokana na tabia zao na maisha yao, wamefika mahali wamejiua wamegonga ukuta. Kwa hiyo tusisumbuke kabisa na watu hawa na wala viongozi wa Serikali msihangaike na watu hawa, wameshajiua. Mtu kama anakufa kwa asali huna sababu ya kumtilia sumu jamani, unamuacha tu anajifia mwenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna vichaa walikuwa wamekubaliana watoroke hospitali. Wakakubaliana kwamba wafike getini wamnyonge mlinzi halafu watoroke. Vichaa wale walipofika getini wamkakuta mlinzi hayupo wakasema dili limeharibika turudi; dili limeharibika turudi.

Mheshimiwa Naibu Spika, unaweza ukaona namna ambavyo tunafanya siasa za ajabu. Tumeona Serikali ya Awamu ya Tano ikifanya kazi kubwa; inajenga hospitali kila wilaya inajenga vituo vya afya kila jimbo; Wizara ya Maji imeboresha mfumo wake tunaona maji yanapatikana. Kazi yetu sisi ni kuwatieni moyo tu ili muendelee. Migogoro ya ardhi sasa hivi ukifika kila kona ya nchi yetu inaondolewa. Mimi nasema hivi hakuna sababu ya kuwavunja moyo Waheshimiwa Mawaziri pigeni kazi; Dkt. Mpango pamoja na mwenzako pigeni kazi ili uchumi wa nchi hii uweze kukua na wananchi wapate maendeleo. Hizi rabsha rabsha chache mnazozisikia hizi zisiwapotezee muda; hawa Wabunge mnaowaona humu ndani wamepangishwa chama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na kwneye hili nataka nimwambie Dkt. Mpango, kuna kodi mpya hutozi hapa, hapa lazima TRA watoze kodi mpya. Ni kwamba, Wabunge wa Viti Maalum wa CHADEMA wanalipishwa kodi ya upangaji kwenye chama 1,500,000 kila Mbunge kwa mwezi, kasoro Wabunge wateule wachache tu kama wawili, watatu ambao nao wakiniudhi nitawataja siku moja hapa, hao hawalipi na sababu mimi nazijua, nao nawaweka kiporo; lakini wengine wote ni wapangaji hawa, wamepanga kwenye chama, wanalipishwa kodi hawa na wasipolipa wanafukuzwa chama. Wabishe si wako hapa mimi naongea vitu vya ukweli, hawa ni wapangaji. Hapa hatuna Wabunge; hapa tunawapangaji wamepangishwa, sasa na sisi tutoze kodi mpya ya mapato ambayo aliyewapangisha anapata ili walipie.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza kabisa nimshukuru Mungu kwa kunipa nafasi na kunijalia zawadi ya uhai ili niweze kusimama kwenye Bunge lako Tukufu niweze kutoa mchango wangu kwa Wizara hii ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Kikanda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza hii ni kwa ajili kuweka rekodi vizuri tu, nataka nichukue nafasi hii kuwapongeza sana wananchi wa Iringa na hasa makanda wa Chama cha Mapinduzi wa pale Iringa Mjini. Kumbe walifanya kazi nzuri sana ya kumkaba mpinzani wao mpaka leo anaonesha kwenye Bunge hili kwamba ushindi wake ni ajabu sana hakuutegemea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma taarifa hii ya Kambi Rasmi ya Upindani, unaona kuna vitu vimeandikwa kijinga kabisa. Moja ya kitu kulichoandikwa kijinga neno Mungu anaandikwa kwa herufi ndogo mimi sijawahi kuona mahali popote pale, ukitaka kutaja Mungu lazima uandike kwa herufi kubwa. Kwa hiyo, uchungaji wa Msigwa unanitia mashaka makubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuzungumzia Chuo cha Diplomasia. Chuo cha Diplomasia ni chuo kinachofanya kazi kubwa sana ya kuwaelimisha, kuwafundisha, watu, wananchi wanaoteuliwa kuwa mabalozi, wake wa viongozi, Wakuu wa Nchi, ili kuweza kujua diplomasia inafanyaje kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niiombe Serikali itenge fedha ya kutosha kwa chuo hiki ili kiweze kufanyakazi yake kwa ufanisi na nimuombe Waziri atakaposimama hapa kutoa majibu atueleze ni fedha kiasi gani zimetengwa kwa ajili ya chuo hiki ili kiweze kufanya kazi yake kwa ufanisi.
Tunasemwa maneno mabaya lakini tunavumilia mpaka wasemaji wamalize, lakini sisi tukitaka kujibu kidogo unasikia kelele za kuwashwa washwa upande wa pili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme moja ya diplomasia kubwa iliyojengwa katika nchi yetu ni kuwa na upinzani japo kwamba upinzani wenyewe ni dhaifu. Tunao upinzani lakini ni dhaifu hata kwenye kujenga hoja. Mtu anasimama hapa kuzungumzia habari ya Mabalozi hawafanyi kazi, anasimama hapa kuzungumzia habari ya Rais haendi nje. Tulikuwa na Rais Kikwete, anasafiri kila siku. Hawa walisimama Bungeni hapa kusema kwamba Rais anasafiri sana, Rais anatumia fedha nyingi, leo tumempata Dkt. Magufuli, Rais anabana matumizi, fedha zinaelekezwa kwenye maendeleo, hawa wanasimama kupinga, watu gani hawa. (Makofi/Vigelele)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanataka tufanye nini, leo nataka niwaambie ndugu zangu kweli kazi kubwa ya upinzani ni kupinga lakini sio huu, huu ni upinzani hewa kwa sababu hakuna wanachopinga, wao wenyewe wanaingia wanasaini wanaondoka bila kufanya kazi, leo hii wanataka kusema kwamba nchi hii haina demokrasia wangekuwepo hawa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo upinzani wa Tanzania naufananisha kama mtoto mchanga tumboni. Mtoto mchanga tumboni haelewi ukubwa wa dunia. Kwa hiyo, anafikiria eneo la tumbo la mama yake ni eneo kubwa linalostahili hata kucheza. Hajui kwamba akitoka duniani kuna eneo kubwa mno, kuna eneo la kukimbia atachoka, kuna eneo la kucheza atachoka, kuna eneo la kulima atachoka, kuna eneo la kutembea atachoka. Hawa wanafikiria kama mtoto mchanga tumboni anayefikiria eneo la tumbo ni eneo kubwa sana. Leo unamkosoa Balozi eti kwamba tunao Mabalozi wenye hadhi ya nyumba kumi, haya ni matusi wa Mabalozi wetu. Mabalozi wetu ni Mabalozi waliochunjwa, wameiva, ukiwepo Balozi Mahiga, nani asiyejua kwamba Mahiga ni moja ya watu waliobobea katika masuala ya kidiplomasia ya kimataifa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii wanasimama hapa kutuambia as if kwamba sisi ni watoto wadogo. Hivi ingekuwa Watanzania wote au viongozi wote wa nchi hii wanatakiwa kusafiri nje ya nchi kwenda kuwasilisha masuala ya nchi hii wao wangekuwa Wabunge hapa. Si kila mwananchi wa Jimbo lao angekuja hapa Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani wananchi wote kuja kwenye jengo hili ndio maana tumekuchagua Msigwa, ndio maana tumekuchagua Januari, ndio maana umechaguliwa Lusinde, kwa sababu wana nchi wa Jimbo zima hawawezi kuhudhuria katika kikao hiki. Sasa leo wanataka nchi nzima kila mtu akajiwakilishe kule, katika kimataifa aende akazungumzie matatizo ya nchi, haiwezekani ndio maana kuna Mabalozi wameteuliwa. Jifunzeni ninyi! Kwa hiyo, nataka niwaambie, anazungumza pale mwisho, anasema nchi ya kifisadi kama hii wakati fisadi mkuu mnaye nyie. (Makofi/Vigelele)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunao upinzani ambao unachosema haukielewi, wanachopinga hawakielewi, walichosema mwaka jana mwaka huu wanakuja wanajijibu. Walichokataa mwaka juzi, mwaka huu wanakuja wanakikubali. Nataka nimpongeze Rais Magufuli, amewafanya wapinzani wa nchi hii hawana hoja, ndio maana mnawaona wakisimama humu hakuna lolote la msingi wanalolisema. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Dkt. Magufuli, amewafanya wapinzani wa nchi hii hawana hoja ya msingi, sasa imekuwa moto ukiwaka wanatoka nje ya Bunge, daladala ikiungua wanatoka nje ya Bunge kwa sababu hoja ya msingi hawana maana Rais anafanya kazi vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuhakikishe Rais akienda kwa speed hii kufika mwaka 2020 hawa watakuwa hawapo ndani ya Bunge hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaitumia diplomasia ya nje kuhakikisha kwamba nchi hiii inapata uchumi mkubwa utakaowafanya wananchi wanufaike, na utakaowafanya wapinzani wa nchi hii waondolewe na wananchi kwenye Bunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuhakikishie, nina uzoefu wa kuongeza na hawa, nina uzoefu nao, unapowaona wanapiga kelele jua sindano zinaingia ndio maana unaona wanapiga kelele. Huwezi ukasimama kwenye Bunge hili ukiita Tanzania ni nchi ya kifisadi wakati fisadi mkuu mmemchukua, na itafika mahali nataka nikuambie, hata Mheshimiwa Mahiga hawa wakubeze vipi, siku ukijiunga kwao utakuwa mgombea Urais wa chama hicho, za kwao hawa ni kuokoteza tu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namtia moyo Mheshimiwa Waziri na Naibu wako, Katibu Mkuu na Mabalozi wote wakilisheni nchi kama Rais alivyowaamini, watanzania tunawaamini, na ndio maana tuko nyuma yenu tunawaunga mkono.Chapeni kazi na hiyo kazi italeta manufaa hata kwenye Majimbo ya hawa wanaopiga kelele leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuhakikishie, nina uzoefu wa kuongeza na hawa, nina uzoefu nao, unapowaona wanapiga kelele jua sindano zinaingia ndio maana unaona wanapiga kelele. Huwezi ukasimama kwenye Bunge hili ukiita Tanzania ni nchi ya kifisadi wakati fisadi mkuu mmemchukua, na itafika mahali nataka nikuambie, hata Mheshimiwa Mahiga hawa wakubeze vipi, siku ukijiunga kwao utakuwa mgombea Urais wa chama hicho, za kwao hawa ni kuokoteza tu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namtia moyo Mheshimiwa Waziri na Naibu wako, Katibu Mkuu na Mabalozi wote wakilisheni nchi kama Rais alivyowaamini, watanzania tunawaamini, na ndio maana tuko nyuma yenu tunawaunga mkono.Chapeni kazi na hiyo kazi italeta manufaa hata kwenye Majimbo ya hawa wanaopiga kelele leo.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, nimshukuru Mungu sana kunipa wasaa huu wa kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, lakini nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri Mkuu pamoja na wasaidizi wake, Waheshimiwa Mawaziri Mheshimiwa Jenista pamoja na Mheshimiwa Angela Kairuki; Manaibu, Mheshimiwa Ikupa pamoja na Mheshimiwa Mavunde, lakini Makatibu Wakuu Ndugu Nzunda, Ndugu Massawe pamoja na Dada Doroth. Tunawapongeza sana kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya kumsaidia Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Spika, Chama Cha Mapinduzi ni kweli kinalea watu vizuri. Ukitazama wakati ule anatoka Mheshimiwa Mizengo Pinda na anaingia Mheshimiwa Majaliwa alikuwa mtu mpole, mtulivu, mwanamichezo tena alikutwa uwanjani; watu wengi hatukufikiri kwamba, Mheshimiwa Majaliwa angeweza kukimudu kiatu cha Mzee Pinda, lakini leo ninapochangia hotuba ya mwisho ya Mheshimiwa Waziri Mkuu nataka nichukue fursa hii kukupongeza sana Mheshimiwa Kassim Majaliwa, kiatu umekivaa kimetosha, lakini umekuwa Mheshimiwa Majaliwa yuleyule. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mtakubaliana nami kwamba, Mheshimiwa Majaliwa cheo hakijamvaa, amebaki kuwa Mheshimiwa Majaliwa, mtu mpole, mtu anayeheshimu kila mtu, mtu anayefanya kazi zake kwa utaratibu mzuri. Mheshimiwa Majaliwa tunakupongeza sana na kweli Chama Cha Mapinduzi ni msitu, kinatoa viongozi wakutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mengine unayowasikia watu wanajaribu kuamsha tu moral ya wapiganaji ili waingie kwenye uchaguzi walao wakiwa na moral, lakini nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Rais timu aliyoipanga, hili Baraza la Mawaziri linalofanya kazi wakati mwingine mpaka usiku wa manane limeiweka CCM katika hali nzuri ya kuingia kwenye uchaguzi tukiwa na ushindi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, chama chetu kingepwaya kama ninyi msingepambana, lakini Waheshimiwa Mawaziri, Manaibu Mawaziri mmepambana katika sekta zote; sekta ya afya, sekta ya ardhi, sekta ya madini, sekta ya uwekezaji, yaani mmetuweka katika mazingira mazuri ambayo wapinzani wetu sasa hoja hawana wanakimbilia kwenye vitu vidogovidogo kama kutafuta refa awe huru, refa awe nini, ukishaona timu inakimbilia kwa refa, jua jiyo timu tayari iko taabani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nikuhakikishie kwamba, uchaguzi tu joto la uchaguzi ndio linalosababisha unaona tume sasa inaitwa sio huru. Sijui utawapata wapi, juzi tumeona kiongozi mkubwa kabisa tena anayeongoza upinzani Bungeni akiteuwa watu anasema nimekuteuwa kuwa Katibu Mkuu na watu wanapiga makofi. Anasema nimekuteuwa Mheshimiwa Heche kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu na mziki unafuata, “Mbowe tubebe”, wala hakukuwa na tume, alikuwa mwanaume mmoja anafanya uteuzi na watu wote wanapata nafasi. Aah! Sasa leo hii wanazungumza kitu gani? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, maana tumeona. Maana hivi vitu sio siri unaona wazi…

SPIKA: Mheshimiwa Lusinde na hapa Bungeni wanashukuru kuteuliwa.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, naona kabisa na uteuzi umekuwa mzuri kwa sababu Wabunge wanaume hawaaminiki sasa Mheshimiwa Mbowe karudi kwa wanawake ambao naamini kwamba, hawa wanaaminika kuliko hawa wanaume walioachwa kwa hiyo, amefanya vizuri kwa kweli. Nakubaliananaye kwamba, hawaaminiki kwa sababu, hata kwenye chai ukikutananao kuna wengine wana mpango wa kuhama mwishoni kwa hiyo, Mheshimiwa Mbowe yuko sawa kabisa kuwaacha hawa wanaume na kufuata akinamama, yuko sahihi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nasema kwamba, jambo zuri wangelifanya baadhi ya Wabunge wa upinzani kama alivyofanya Profesa. Profesa ameonesha, unajua kama unaona maji mazito aga, jamani tumieni Bunge hili kuaga kuweni wastaarabu; hivi saa hizi unaomba lami kweli jamani, Bunge hili unaomba lami? Hiyo game imeisha hiyo, game imeshaisha hapa tunajadili uchaguzi, keshokutwa Rais anakuja anasema Bunge limevunjwa, wewe unaomba lami kilometa 70, taabani hapa. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka niwashauri tutumie haki ya kidemokrasia wakati mwingine kuaga. Ukiona maji yamezidi unasema jamani eeh!, kama alivyosema mama kwamba, jamani naomba niwashukuruni safari ijayo sitakuwepo na wewe tumia zile dakika tatu ambazo umemuachia nina hakika huyo Mbunge atatumia kuaga badala ya kuendelea hata kuzungumza mambo mengine.

MHE. PROF. ANNA K. TIBAIJUKA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Taarifa Mama Anna, Profesa Tibaijuka.

T A A R I F A

MHE. PROF. ANNA K. TIBAIJUKA: Mheshimiwa Spika, asante sana, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Lusinde kwamba, mimi sikuaga kwa kuwa maji ni marefu, kule Muleba Kusini niko imara kabisa, nimeaga kwa sababu ninang’atuka, naomba kuwasilisha. (Makofi)

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mhshimiwa Spika, mama maji kule mazuri si tuko CCM mama, nazungumza ambao hawako kwenye chama hicho ndio ambao maji yanazama mama yangu, sizungumzii wewe Profesa. Wewe ungepita bila kupingwa. (Makofi/kicheko)

Mheshimiwa Spika, nimeona hapa Wabunge wanazungumza kwamba, ooh, magereza wanapiga wanawake. Jamani magereza hawawezi kupiga wanawake, Jeshi letu la Magereza haliwezi kupiga wanawake hata siku moja, Jeshi la Magereza linashughulika na wahalifu sio jinsia, halishughuliki na jinsia ya mtu. Kwa hiyo, akiwa mhalifu mwanamke wanachukua, akiwa mhalifu mwanaume wanachukua, yaani wao hawashughuliki na jinsia wanashughulika na matatizo kwa hiyo, nataka niwapongeze sana Serikali hii kwa kufanya kazi vizuri.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tumeona namna ambavyo mwaka huu mvua imekuwa kubwa na Ofisi ya Waziri Mkuu ndio inashughulikia maafa. Barabara nyingi za Wabunge, hasa zile za vijijini, barabara zimegeuka mito kwa hiyo, tunaomba muiwezeshe TARURA kwa haraka ili itengeneze barabara za kwenda kukusanya kura maana hizi kura tutazifuata vijijini kwa hiyo, barabara zitengenezwe ili watu waweze kufika, wafike Manda, wafike kule Mvumi Mission lile daraja litengenezwe, wafike kule chini Loje kule tukusanye kura za Mzee Magufuli, habari ya uchaguzi na hoja mnaziona hapa hazipo.

Mheshimiwa Spika, tunashukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa kusimamia ukusanyaji wa mapato na nidhamu ya matumizi ya fedha, maana kukusanya kitu kingine, lakini nidhamu jambo jingine. Tumeona namna ambavyo kwa kutumia pesa zetu za ndani kila kijiji kinapata umeme kwa sababu, ya nidhamu ya mapato na nidhamu ya matumizi. Tumeona namna ambavyo migogoro ya ardhi inashughulikiwa na Mawaziri mpaka usiku wa manane kwa sababu ya nidhamu ya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa watu waliofanya, nataka niseme, CCM haiwezi kujisifu kwamba, inapendwa ila vitendo vinavyofanywa na viongozi wa Serikali vinaonesha chama hiki kinapendwa. Chama Cha Mapinduzi kadiri mtakavyotenda mema ninyi Mawaziri mnaturahisishia kazi, tunakaa kwenye mserereko wa kuingia moja kwa moja, yaani kama ni meli iko kwenye chetezo inaingia tu baharini. Sasa hapa tunashindana na nani jamani hii hali mnavyoiona hivi? Hamna kitu na ninataka niwaambie wakati mwingine watu wasiseme tunafuta demkrasia, hatufuti, timu ya mpira wa miguu inajifuta yenyewe kwa kufungwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tulikuwa na timu hapa inaitwa Zimanimoto, iko wapi? Tulikuwa na timu inaitwa CDA, imefungwa na ndivyo ambavyo hawa mwezi wa 10 tunakwenda kuwafungilia kwa mbali na kuwashusha daraja, wala sio kwamba, kwa kufuta demokrasia ni nguvu tu; kazi imefanyika Watanzania wameamini, wamekiamini Chama Cha Mapinduzi wanakwenda kukichagua Chama Cha Mpinduzi, sio suala, lazima tuwambie hapa wazungu. Hatufuti…

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge pamoja na mchango mzuri wa Mheshimiwa Lusinde nafikiri tutakubaliana kwamba, mkimuona ile suti yake ilivyokaa kwa kweli, ni kiwango. (Makofi/kicheko)

Ilikuwa ni kengele ya kwanza tu Mheshimiwa bado unaendelea na dakika zako, malizia. (Makofi)

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, tunakushukuru wewe kwa kuongoza Bunge vizuri, Bunge limeongozwa kisayansi. Ule upinzani wakukurupukia hoja ndogondogo hizi oooh! Ufisadi, haupo sasa kwa sababu, nidhamu iko Serikalini kwa hiyo, maana yake nini?

Mheshimiwa Spika, maana yake Watanzania sasa wanakwenda kufanya uchaguzi mwepesi ndio maana mnaona sasa inalalamikiwa tume. Hoja iliyopo sasa sio CCM mafisadi, hoja iliyoko sasa sio CCM kuna wizi wa fedha, hoja iliyoko sasa sio CCM wameshindwa kumaliza migogoro, aah aa, hoja iliyoko ya refa, wanataka refa, sasa huyu refa anatoka wapi? Atatoka nchi gani refa atakayesimamia uchaguzi? Mbona kwenye chama chao hawatuoneshi namna ambavyo wanafanya uchaguzi? Tunaona tu mwanaume mmoja kwenye clip anasema nimekuteuwa kuwa Katibu Mkuu, nimekuteuwa kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu, nimekuteuwa, halafu na kanyimbo kanamsindikiza; mbona hawabishi kule wanakujaje kubisha huku?

Mheshimiwa Spika, Tena huku hakuna uteuzi, huku ni shughuli tu. Unaenda kuomba kura, unapewa kura shughuli zinaisha. Kwa hiyo, nataka nikuombe Bunge lako hili tujipange kuhakikisha kwamba, mambo yanakwenda vizuri.

Mheshimiwa Spika, habari ya corona imezungumzwa hapa, ninachotaka mtusaidie tu, maana mnaposema kila mnayemuhisi ana corona mnampeleka kwenye kambi na wagonjwa wako kwenye kambi. Sasa hapa watusaidie maana kuhisiwa sio kuugua, unaweza ukahisiwa una corona halafu ukapelekwa kwenye kambi yenye wagonjwa wa corona, sasa pale unakuwa tena umepelekwa kupata corona au umepelekwa kusaidiwa?

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ingekuwa vizuri Serikali ikatuonesha kambi tofauti kwamba, kambi fulani iwe kwa ajili ya wanaohisiwa tu, haina mgonjwa. Kambi fulani hii ni kwa ajili ya wagonjwa tu, haina mtu anayehisiwa na kambi fulani wanapelekwa hotelini wale waliotoka nje, lakini mkisema tu kila mnayemuhisi, Mloganzila, wagonjwa Mloganzila, eeh ee!

Mheshimiwa Spika, sasa tunapata shida hapa. Ni lazima kuwe na tofauti ya mtu anayehisiwa na mtu anayeugua, ili tusije tukachukua watu tunaowahisi tukawapeleka kwenda kuugua badala ya kuwasaidia.

Mheshimiwa Spika, lakini jambo la mwisho nakushukuru sana, umefanya kazi kubwa, umeliongoza Bunge kisayansi. Na hata wale ambao walikuwa na mashaka na wewe wakati unaingia mashaka wameondoa, wamegundua kwamba, Mzee Ndugai ni mzee wa viwango. Anaweza kulibadilisha Bunge hata akina Lusinde sasa tunabofya tu, maana mwanzoni tulikuwa tunaonekana mimi na Bwege labda tutapata shida katika kubofya, lakini watu wako wametusaidia mpaka mimi na Bwege sasa tunabofya na tunaingia humu ndani na mambo yanakwenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)
Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru sana Mungu kwa kutupa nafasi nzuri kabisa ya kujadili juu ya huu Mkataba wa EPA. Vilevile sina budi nichukue fursa hii katika Bunge hili kumpongeza sana Profesa Kabudi kwa namna alivyotufumbua macho. Profesa Kabudi ni moja ya Watanzania wenye uwezo wa walichonacho kuwasaidia na wengine waweze kuelewa. Hilo ni jambo zuri sana na kwa kweli tunajivunia sana kwamba elimu yako inawafaa wengi na inaifaa nchi. Hongera sana Profesa Kabudi.
Mheshimiwa Spika, ni ngumu sana kusimama hapa kuutetea huu mkataba na ndiyo maana unaweza kuona kuna baadhi wanaojaribu wanapata shida sana. Hauna namna yoyote ya kuuzungumzia uzuri wa Mkataba huu, hata kama umeandaliwa au umejiandaa; ni jambo gumu sana. Ndiyo maana umeona hata waliojaribu kufanya hivyo, wamejikuta wao wenyewe wakipata shida sana. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Spika, nataka nimpongeze sana Mheshimiwa Khatib, ameonyesha kwamba isiyo kongwe haivushi, kwamba ukongwe wa CCM ni jambo zuri na inaendelea kuvusha nchi hii. Amesema chama hiki ni kikongwe. Ukishasema kikongwe, maana yake hicho ndicho chenye uwezo wa kuvusha baadhi ya mambo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kama umewasikiliza wazungumzaji wachache waliotangulia, nataka niungane nao kwamba hata kuchukua muda mwingi kuujadili mkataba huu ni kutumia tu fedha za Watanzania vibaya, huu mkataba haukustahili hata kufika huku. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, huu ni moja ya mikataba mibovu kabisa ambao pengine nimsaidie hata mzungumzaji aliyepita, kwa nini Kenya wamesaini? Wamesaini bila kuutafakari kwa makini. Wangetafakari kwa makini; na nikubaliane na Mhesimiwa Zitto kwamba wamesaini kwa ajili ya kufanya biashara ya maua, siyo kwa ajili ya usalama wa mkataba wenyewe. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kifungu cha 140, hakiruhusu nchi moja kujitoa baada ya kuingia. Mimi nataka niseme, Jumuiya yetu ya East Africa, kama kuna jambo mmetuangusha ni katika jambo hili. Kwa nini msingekaa wenyewe kwanza mkaupitia huu mkataba? Secretariat ya Jumuiya ya East Africa mkakaa mkausoma kwa pamoja kabla ya kuruhusu nchi moja moja kwenda kujisainia yenyewe? Kwa hiyo, hapa tunaanza kona kuna problem kwenye Jumuiya yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lazima Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki iwe inakaa pamoja kwenye mambo ya muhimu na mazito kama haya, leo tusingeona aibu ya Kenya kutangulia kusaini kama mngekaa pamoja mkashauriana, kwamba jamani hivi unaingiaje kwenye mkataba ambao unakuchagulia rafiki? Unaingiaje kwenye mkataba ambao unakulazimisha kushirikiana na adui? Huu mkataba kadri unavyousoma, kuna sehemu unakuchagulia rafiki wa kufanya naye biashara na kuna sehemu unakulazimisha kukaribiana na mtu ambaye wakati huo humhitaji.
Mheshimiwa Spika, ukitazama kwa makini mkataba huu wa EPA, ni sawa sawa na mzee wangu pale kijijini kwenda kupelekewa zawadi ya kuku halafu akachukuliwa ng‟ombe wake kumi; kitu ambacho hakiwezi kukubalika!
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni moja ya mikataba mibovu kabisa. Nasi tunapoukataa mkataba huu na kuitaka Serikali, isiusaini, tunaukataa ili kuwaonesha Jumuiya ya Ulaya kwamba Afrika sasa inao wataalam, wanajitambua na wanaweza kufanya biashara huria na mtu yeyote. Sisi sio watu wa kupangiwa na kuletewa mikataba ya namna hii. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka niishauri Serikali; kwa mkutadha huu, huu mkataba haufai kusainiwa hata kidogo kwa sababu una vipengele vingi vinavyodhalilisha Afrika.
TAARIFA...
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, namshukuru na namheshimu sana Mheshimiwa Millya, lakini ni mmoja wa watu wachache ambao wamerubuniwa na wazungu. Hawa wazungu waliokuja wamemwona Millya. Maana hapa hatutakiwi kutafuna maneno; kuna baadhi ya Wabunge wamewaona, inawezekana na Mheshimiwa Millya akawa ni mmojawapo kati ya waliowaona. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kama hukatazwi, unawezaje kutoa notice halafu mwaka mzima ukaendelea kubaki mle? Unabaki humo kwa sababu zipi? Khah, maana wewe mwenyewe unasoma, halafu unajijibu. Bahati nzuri wewe mwanasheria na pengine unaelewa zaidi, lakini umepata majibu kwamba ukishatoa notice, mwaka mzima unaendelea kubaki mle. Ukifanya nini kama unao uhuru wa kutoka moja kwa moja? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nirudie, hili ni jambo letu wote kama Bunge, tusianze kushindana humu. Tukubaliane kwamba mkataba huu haufai, maana ndani una vi-package vya ushoga, una vitu vya ovyo ovyo vimefichwa humo, Watanzania watatushangaa sana.
Mheshimiwa Spika, sisi hatuwezi kuburuzwa na nchi yoyote, sisi ni Taifa huru! Iwe wamasaini nchi nyingine ambazo pengine wao wanavutiwa na ushoga, sisi hatuvutiwi nao. Kwa hiyo, hatuko tayari kukubaliana na jambo hili.
TAARIFA...
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, hiyo itakuwa imetusaidia wote, lakini zaidi sana, Mheshimiwa Millya ameelewa kwamba ni ile block ndiyo inatakiwa kuomba kutoka lakini siyo nchi moja ambayo imezuiwa na mkataba huu.
Mheshimiwa Spika, tuseme tu kwa kifupi, mkataba huu haufai. East Africa wawe makini na mikataba ya namna hii, waipitie wao wenyewe kama Sekretatieti na wao na uchungu na nchi zao kabla ya kuangalia manufaa watakayopata. Kwa sababu wakati mwingine kuna hadithi moja; watu waliwahi kushangilia kwenda kufanya kazi kwa Mfalme, wakati huo huo kulikuwa kuna agizo kwamba ili ukafanye kazi kwa Mfalme, ni lazima uhasiwe kwanza ndiyo uruhusiwe kufanya kazi kwa Mfalme. Kuna watu wakashangilia, walipofika pale kukuta masharti, yakawa magumu kwao. Kwa hiyo, kila mikataba ya kimataifa inapokuja, tuwe na Sekretarieti zinazotazama kwa makini, siyo kukurupuka! Tutakuja tuingie kwenye matatizo makubwa na tuziingize kwenye shida kubwa. Tutakuja kupata adhabu ambazo hazina msingi. Maana kadri unavyousoma unakutana na sehemu inasema EU inaweza kuchukulia hatua.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, unaweza kuona ambayo tunaweza tukaingia kwenye matatizo makubwa ya kuchukuliwa hatua na uhuru wa nchi zetu ukawa unatekwa bila sisi wenyewe kuelewa.
Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naunga mkono mkataba usisainiwe.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kupata nafasi hii ya kufungua dimba. Namshukuru sana Mungu kwa ajili ya vipawa na vipaji vingi alivyotujalia. Awali ya yote, nitoe pole kwa familia ya Mheshimiwa Hayati Dkt. Magufuli, Mama Janeth pamoja na Watoto; Joseph, Michael pamoja na Jesca. Tunawapa pole sana. Vile vile tumpe pole Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kweli tukupe pole na wewe kwa sababu ulishindwa hata kuchukua hela yako ya utani kwa namna ambavyo ulikuwa umeguswa, maana yule ni mtani wako, ulitakiwa pale uzuie shughuli zisiendelee mpaka upewe chochote; lakini kwa sababu alikuwa mtu wako wa karibu ukashindwa kufanya hata utani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunamshukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi kubwa ya kusimamia msiba wa Kitaifa. Mheshimiwa Waziri Mkuu pamoja na Waziri Jenista Mhagama na timu yako akiwepo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, tumeona namna ambavyo Kamati yenu imefanya kazi kubwa sana; na kwa kweli tutakuwa wachoyo wa fadhila tusipokushukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kusimamia msiba ule ambao umetupa heshima kubwa kama Taifa kwa namna ambavyo tumemzika Kiongozi wetu kwa heshima kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tutoe pole kwa yule Bwana aliyepoteza mke na watoto pale Dar es Salaam kwa kukanyagwa kwa ajili ya wingi wa watu waliofika kushuhudia msiba ule. Tunawapa pole sana Watanzania wote kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu imejaa mambo mengi. Imesheheni vitu vikubwa sana, imesheheni tulikotoka, tuliko na tunakokwenda na hatuna mashaka kwa usimamizi thabiti wa Rais aliyepo sasa Mheshimiwa Samia pamoja na timu aliyoipanga kwamba mambo haya yanakwenda kufanyika. Kazi tuliyonayo, Bunge lako ni kuendelea kuwashauri, kuwatia moyo na kuwaunga mkono kuhakikisha kwamba haya yaliyokusudiwa yanafanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, rai yangu ni kwamba, tungetengeneza vijitabu vichache, siyo Ilani mpya, lakini vya kukumbusha zile ahadi za Waheshimiwa Viongozi walikopita. Ziwe katika kitabu kimoja cha Kitaifa, alikopita Mheshimiwa Mama Samia aliahidi, alikopita Mheshimiwa Hayati Dkt. Magufuli aliahidi, sasa badala ya kila Mbunge kuwa anasimama anakumbusha ahadi ya Rais, ni vyema zikawekwa kwenye kitabu kimoja tukajua kwamba, ahadi za Viongozi wa Kitaifa ni hizi. Kuna mahali waliahidi barabara kama Mvumi pale, kuna mahali waliahidi madaraja, kuna mahali waliahidi kuchimba mabwawa; tukifanya hivyo, tutarahisisha Wabunge wote kwa pamoja tutakuwa tunadai tu ahadi za viongozi zitekelezwe ambazo ziko kwenye kitabu kimoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikishukuru Chama cha Mapinduzi, kimefanya kazi kubwa sana kwenye uchaguzi uliopita. Hiki Chama hakina mashaka kwamba ndiyo chama pekee kilichobaki kwenye eneo la ukanda huu kinachotetea maslahi mapana ya wananchi wa nchi yake. Kwa kweli bila uchoyo, nataka nimshukuru sana Katibu Mkuu, Mheshimiwa Dkt. Bashiru, tunakushukuru sana kwa kazi kubwa ambayo uliifanya. Jamani mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Spika, jambo kubwa ambalo Mheshimiwa Waziri Mkuu amelisema hapa ni kuhakikisha kwamba Serikali inaendelea kusimamia amani na utulivu wa nchi yetu. Amani na utulivu haviwezi kuwepo kama kuna baadhi ya Watanzania na baadhi ya Wabunge wanamsema vibaya Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli, haiwezi kuwepo amani na utulivu. Haiwezekani! Kwa hiyo, leo nataka kujitoa muhanga hapa. Haiwezekani tuwe na viongozi ambao wanajaribu kupinga mambo mazuri aliyoyafanya Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli, haiwezekani. Hatuwezi kuwavumilia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hawa wanaomsema vibaya leo Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli, watamsema vibaya Mheshimiwa Samia. Hii ni tabia! Jamani Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli amefanya kazi kubwa sana kwenye nchi hii. Maana lazima tukubaliane, unajua kuna wengine wanafikiri labda Mheshimiwa Samia alikuwa bench akaingia kucheza mpira, hapana. Mheshimiwa Samia alikuwa anacheza pamoja na Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, aliyemtaja Mheshimiwa Samia ni Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli mwenyewe. Siku zote Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli amekuwa akisema, kama akijitabiria kifo chake; kila hotuba yake alikuwa akisema siku moja nitakufa. Kwa hiyo, alikuwa anajua, akiondoka yuko Mheshimiwa Samia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunataka watu wamheshimu. Huwezi kuondoa legacy ya Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli kwenye nchi hii na kwenye Bara la Afrika, haiwezekani. Haiwezekani, haiwezekani! Hatuwezi kuwavumilia watu wa namna hiyo. Nasi kama viongozi ambao tumelelewa, hivi leo Mbunge gani hapa hakutetewa na Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli? Tuko humu ndani kwa sababu ya Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli na Mheshimiwa Samia. Kila sehemu walipita.

Mheshimiwa Spika, kuna watu hapa walikuwa hata hawachaguliki, Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli na Mheshimiwa Samia wakipita wanasema, tupeni huyu, tutafanya naye kazi, tutamrekebisha. Kwa sababu yao, watu wakachaguliwa. Leo wasemwe vibaya sisi tupo! Leo Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli asemwe vibaya hata arobaini haijaisha! Hili jambo halikubaliki. Hawa watu washike adabu na adabu ziwashike, hatutaki warudie tena mambo ya kipuuzi kama haya. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Spika, anasimama mtu anasema eti mradi ule wa maji tuuache! Unajua mimi nina hakika kwamba, hata mle ndani inawezekana hata kaburi la Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli lilitikisika! Tuuache mradi ule wa Mwalimu Nyerere? Ule mradi una faida kibao! Pale ametuambia hapa Mheshimiwa Majaliwa kwamba tumetumbukiza shilingi trilioni mbili; tuziache ziteketee? Kwa sababu gani? Ule mradi kwa taarifa yenu, mimi sio Profesa Professor, mimi ni wa Darasa la Saba, lakini ngoja niwape faida za ziada za ule mradi. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, ngojeni niwape faida za ziada za ule mradi. Lile bwawa linalochimbwa pale, upana wake peke yake ni kilometa 25, lakini urefu wa maji yatakayokuwa pale ni kilometa 100; hapa na Kibaigwa. Hilo ni bwawa au ziwa? Pale linazaliwa ziwa! Hii nchi itabidi wachoraji wa ramani mbadilishe, msitaje maziwa yale tuliyonayo, mwongeze na Ziwa la Magufuli linalozaliwa pale. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye lile ziwa, pembeni kutajengwa hoteli za utalii, pale patawekwa samaki watu watavua, lakini ziwa lile linagusa Wilaya tano. Hivi jamani elimu ya Tanzania kweli inatusaidia? Kama wa Darasa la Saba naelewa, halafu Profesa huelewi, inakuwaje? Inakuwaje? Inakuwaje? (Makofi/Kicheko/Vigelegele)

Mheshimiwa Spika, haiwezekani, ni lazima tusome na vile vile tuwaeleze watu vitu vya kweli. Tusiwadanganye wananchi. Amesema hapa Mheshimiwa Waziri Kalemani, umeme wa maji ndiyo umeme wa bei rahisi kuliko umeme wowote. Kwa nini tunawadanganya Watanzania? Kama tuna madili yetu tuyaeleze, lakini tusiingize kuanza kuharibu image ya Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli kwa wananchi wakati tegemeo lao kubwa ni Mheshimiwa Samia kutekeleza mambo waliyoyapanga na ndugu yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kila sehemu watu wana matumaini makubwa sana na Mheshimiwa Rais Samia. Kazi yetu sisi Wabunge ni kumtia moyo, siyo kuanza kumrudisha nyuma, siyo kuanza kuzungumza kana kwamba Mheshimiwa Samia ni mtu mwingine na Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli ni mtu mwingine, haiwezekani. Haiwezekani! Haiwezekani! Nasi Wabunge tuko humu, haiwezekani!

Mheshimiwa Spika, Samia ni Magufuli na Magufuli ni Samia. Wamefanya kazi kubwa na sasa Samia anaelekea kwenda kuitendea Tanzania jambo la ajabu, kukamilisha ile miradi waliyokubaliana na Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli na siyo hivyo tu, na kuongeza mingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nchi hii Rais anayetawala, anatekeleza Ilani na vile vile anakuja na maono yake. Tusianze kumtangulia Rais. Rais ana maono yake. Mnaposikia huko watu wanafanya Ibada Makanisani na Misikitini wanamwombea, pale busara zinaongezeka, anawaza mambo mengine makubwa ya kuitendea nchi. Nani asiyejua kwamba ziwa la mama ndiyo linalolea mtoto? Sisi tuna Imani kubwa na Rais aliyepo, kwa hiyo, tusianze kumzongazonga na kuanza kumfananisha sijui Magufuli na Samia, sijui Samia bora kuliko Magufuli, inatoka wapi hiyo? Hawa wote ni kitu kimoja, wamechezea timu moja, wote wamezaliwa na Chama cha Mapinduzi. Huyu ni kada wa Chama chetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika na Waheshimiwa Wabunge, nimesema mimi najitoa muhanga eti kwa sababu nagombea NEC, sijui mtaninyima kura. Mkininyima hiari yenu, lakini leo napasuka hapa. (Makofi/Kicheko)

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge! (Kicheko)

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika,…

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge wa CCM, naomba kuwahoji, Mheshimiwa Lusinde amepita NEC? (Kicheko/ Makofi)

WABUNGE FULANI: Amepita! (Kicheko/Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa umepita bwana. (Makofi/ Kicheko)

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, watu wengi wanataka kuliharibu suala ambalo umelisema. Suala la ujenzi wa bandari, Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli alieleza mabaya yaliyoko kwenye mkataba. Kazi tuliyonayo sisi ambao tumebaki hai, kama upo uwezekano, tufanye mapitio upya ya ule mkataba. Wewe hujasema ijengwe kama ilivyo; na ulikuwa msimamo wako wa siku zote hata Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli akiwepo. (Makofi)

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, ngoja nataka niseme hapo.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Haya, Mheshimiwa Kingu.

T A A R I F A

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Nataka nimpe taarifa mzungumzaji anayesema kwamba hata watu ambao wanaendelea kumshambulia na kutaka kumchafua Spika wetu kuhusiana na Mradi wa Bagamoyo ni vile hawajui kwamba alichokuwa amekisema Spika hata kwenye Bunge la mwaka 2020 alikuwa amemaanisha kwamba kama kuna upungufu kwenye mradi wa Bagamoyo, kama nchi tuyatoe na mazuri tuyapokee, tuendeleze mradi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ninatoa rai kwamba sisi kama Bunge, nampa taarifa msemaji, tusikubali kuona image yoyote ya kutaka kumdhalilisha Spika wetu kwenye hilo jambo.

Mheshimiwa Spika, nina imani kaka yangu ataipokea taarifa yangu. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Lusinde, unaipokea taarifa?

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, naipokea taarifa ya Kingu. Hauwezi ukachoma nyumba moto kwa sababu ndani ya nyumba kumeingia panya, haiwezekani. Tunachofanya pale, yale maovu tunayaondoa, kinachobaki kinaletwa hapa Bungeni, wananchi wanaelimishwa kwamba ubora wa bandari ya Bagamoyo ni huu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hakuna kitu chochote kilichokosewa. Nimesimama hapa kufungua dimba…

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Taarifa ya Mheshimiwa Musukuma.

T A A R I F A

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Napenda kumpa taarifa tu mzungumzaji kwamba, mawazo yanayotolewa na Senior Lusinde, Darasa la Saba ni mawazo… (Kicheko)

Waheshimiwa Wabunge, msicheke, ni mawazo ambayo kama alivyosema, humu ndani kuna watu watu ni Maprofesa na ma-Ph.D yenu hamna hayo mawazo.

Mheshimiwa Spika, sasa kiti chako, haya mawazo tukiwa tunayaacha yanapoteapotea, hayawezi kuwa na kumbukumbu kwenye Taifa letu. Unaonaje watu kama hawa ukawatunukia hata Udaktari wa heshima ili hata... (Makofi/ Kicheko)

SPIKA: Mheshimiwa Lusinde, unapokea taarifa?

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, napokea kwa mikono miwili kwa sababu mtathmini naye ana elimu kama yangu. Kwa hiyo, napokea taarifa. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, nataka nipige mabomu ya ndani na ya masafa marefu. Kabla ya uchaguzi uliopita, tuliwaasa baadhi ya viongozi, tujenge tabia ya ustaarabu; ukiongoza chama, ukiongoza timu ya mpira, tusishindwe na makocha? Juzi tumemwona Kocha wa Timu ya Taifa Etienne Ndayiragija; timu imefungwa, kajiuzulu katoka.

Mheshimiwa Spika, tunashangaa wako wanasiasa ving’ang’anizi; kaongoza chama, kilikuwa na Wabunge 100, sasa hivi kina Mbunge mmoja; bado naye anasimma kuzungumza eti Mwenyekiti wa chama. Mwenyekiti wa chama gani? Unasema vitu vya uongo, eti akaunti yangu ilifungwa. Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli alikuwa anafanya kazi BoT? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, Nani asijejua kuna utaratibu wa kibenki? Kama una madeni, una vitu vingine, akaunti yako ikafungwa, ni mambo ya BoT na benki ambayo umefungua akaunti. Hayo yanamhusu nini Rais? Kwa hiyo, tunataka kuwaambia Watanzania, utamaduni wa kitu kikifanywa vibaya unajiuzulu, kisiishie kwenye CCM. Vyama vyote viige. Umeongoza chama kikiwa na Wabunge 100, umepigwa uchaguzi, kimepata Mbunge mmoja toka. Onyesha ustaarabu kwamba jamani nimepigwa. Baba bata yule yupo tu; watoto wametumbukia naye mwenyewe katumbukia, bado ana haki ya kusimama. Unasimama kuzungumza nini wakati hapa kijana mdogo tu kamtoa nishai? (Kicheko/ Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, wanasiasa wa namna hii hatuna haja nao. Kuna mmoja nataka nimtumie kombora yuko Ubelgiji, aendelee kukaa huko huko, asitubabaishe. Wamwache Mheshimiwa Samia afanye kazi ya nchi. Asije mtu akamtangulia Rais ooh, Mheshimiwa Rais huyu nataka nikae naye. Ukae naye uzungumze naye kitu gani? Sisi tuko hapa kumtetea Mheshimiwa Samia na tuko hapa kumpigania Mheshimiwa Samia.

Mheshimiwa Spika, Serikali anayoiongoza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ina Wabunge wa kutosha, tutasimama imara kuhakikisha nchi yetu inakwenda. Watanzania wanataka maendeleo, hawataki maneno mengine. Ndiyo maana slogan ya Mheshimiwa Rais sijui kama watu wameielewa vizuri!

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Samia hajasema kuna mabadiliko, kasema kazi iendelee. Maana yake wale walioko kazini waendelee. Anachokisema Mheshimiwa Rais Samia, nidhamu ya wafanyakazi iendelee, nidhamu ya uadilifu kwenye mapato na matumizi iendelee, nidhamu ya uchapa kazi iendelee, reli ijengwe, viwanja vya ndege vijengwe, maji yapatikane, bwawa lijengwe, umeme upatikane, kazi iendelee. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi/Vicheko/Vigelegele)
Taarifa za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Kamati ya Kudumu Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu shughuli za Kamati hizo kwa Mwaka 2021
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, nami namshukuru Mungu sana kupata nafasi hii ya kuzungumza katika hii hoja ya Kamati mbili. Hoja yangu kwanza nitajikita kwenye Kamati ambayo imevuta hisia za watu wengi, Kamati ya Maliasili.

Mheshimiwa Spika, sitaki kuchukua muda mwingi kwa pongezi. Umeshapongezwa sana, nami nakupongeza wewe pamoja na wote waliochaguliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna mambo mengi sana yamezungumzwa hapa na Waheshimiwa Wabunge, lakini kama mtakumbuka siku Mheshimiwa Rais anawaapisha Makatibu Wakuu, alisema tuchague jambo moja kati ya mambo mawili; au tuache Hifadhi ya Ngorongoro ife iwe makazi ya watu moja kwa moja au tuihuishe ile hifadhi iendelee kuishi kwa manufaa yetu na ya vizazi vyetu. Hii ni kauli nzito sana kutoka kwa mkuu wa nchi. Mheshimiwa Rais anataka sisi Watanzania tuchakate halafu tuishauri Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa ushauri wangu ni huu; Waheshimiwa Wabunge, wamesema hapa lakini kwa bahati mbaya sana ukweli huwezi kuufunika. Ukitazama maudhui ya kuwaruhusu wale watu 8,000 waishi mle na wanyama, kulikuwa na masharti yake; usijenge nyumba ya kudumu, jenga nyumba za kimila, ambazo zitawavutia watalii watakapokuja. Sasa ghorofa ni nyumba ya kimila? Siyo nyumba ya kimila!

Mheshimiwa Spika, sasa unapojenga nyumba za kudumu, kwanza wale watu upande mwingine tumewatia umasikini, kwa sababu mle ndani ya hifadhi mtu hamilikishwi ardhi, siyo yake. Sasa kwa nini Wizara isiweke utaratibu mzuri kuwatafutia eneo zuri wale wafugaji na kuwamilikisha? Wapeni hati ili siku nyingine msije mkawafukuza huko watakapoenda. Wapeni hati za kumiliki ardhi yao pale. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wapewe hati ili siku nyingine wasije kufukuzwa hapo watakapokwenda, wapewe hati za kumiliki ardhi yao pale na huu utaratibu wa kusema kuna watu maskini wamepewa mifugo, sio tu wa kabila la Kimasai, hata sisi Wagogo na makabila mengi ya Wasukuma. Sisi tunaita Ng’ozwa, mtu anakuwa hana kitu anapelekewa ng’ombe 200, yeye pale anafaidi maziwa kidogo, lakini anakula nyama mpaka ng’ombe afe, sio kwamba achinje hapana, mpaka afe na ngozi anakuwekea tajiri.

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Ukija tajiri anakuja kukuonyesha ng’ombe wako fulani alikufa, hao ndio wanaishi mle. (Makofi)

T A A R I F A

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Munde Tambwe Abdallah.

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba nimpe mwongeaji taarifa kwamba, amesema wale watu Serikali inaweza kuwajengea nyumba sehemu nyingine na kuwahamisha. Nakubaliana naye kwa kumpa taarifa kwamba, wale watu wanatumia shilingi bilioni tatu kwa mwaka kwa ajili ya chakula.

Kwa hiyo, fedha hizo zikienda kujenga nyumba zao wakamilikishwa ardhi, wakajengewa shule hospitali na kadhalika, inawezekana. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Kweli.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, hilo nimelipokea na ndio maana nilitaka nijenge hoja yangu… (Kicheko)

SPIKA: Mheshimiwa Lusinde subiri kidogo. Naona unafanya haraka sana, lazima nikuite tena ndio uzungumze. Mheshimiwa Lusinde.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana tuna Spika wa viwango. Hebu mpigieni makofi Spika haraka sana. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, ndio maana nilitaka nijenge hoja yangu hivi katika nchi nzima ambayo watu wote sisi tunaishi kwa usawa, leo unakuwa na Tarafa moja ambayo ukifuga humo ndani ya hiyo Tarafa hao wote wanaoishi humo watanunuliwa chakula bure. Hao watu wanaoishi humo madawa ya mifugo yote watapata bure, hao watu wanaoishi humo watoto wao watasomeshwa mpaka Chuo Kikuu bure. Nani atakataa kwenda kuishi kwenye hiyo Tarafa? Sisi wenyewe tuna mpango hapa wa kuhamia huko. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, maana yake kuzuri kuna kila kitu ambacho unapewa bure. Kwa hiyo, nataka kusema hivi kama tumefuatilia mitandao na tumeona zile picha, kama za uongo Serikali wasimamie hili jambo ili kutenda haki. Mle ndani wameonekana mbwa kama yule mbwa wa Wema Sepetu anaitwa Nunu, wako kule Ngorongoro, wako. Kuna mbwa German Shepherd wako mle Ngorongoro. Sasa tunajiuliza hivi mbwa kama yule atakaaje na wanyama wa kawaida? Ndio maana wanyama wanakimbia wanawaacha watu. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, nikwambie kengele ile ya kufunga ng’ombe shingoni ile sisi tunaita chidodolo kwa sisi Wagogo. Ile kengele ikilia paaaa mara moja hivi, faru anakwenda kusimama Morogoro speed yake. Sasa niambie huyo faru atarudi saa ngapi mpaka mtalii aje amwone? Kwa hiyo, ndugu zangu tukubaliane kwamba haiwezekani, kwa hali tuliyonayo sasa kuchanganya kati ya watu pamoja na hifadhi kuishi mule ndani haiwezekani. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, ukitaka upime kwamba utajiri sasa unaanza kutuondolea utu. Tumepata taarifa mle kuna vijana watatu wameliwa na simba na picha zao zimeonyeshwa. Umeona hata mtu mmoja hata Mbunge wa eneo hilo au wahusika wa eneo hilo wametoa hata pole? Jamani maisha gani haya, haya ni maisha gani? Nataka niwape pole familia ambazo kwa namna moja au nyingine wamewahi kudhurika na wanyama. Tuwape pole wenzetu ambao wamepoteza watoto wao kwa nyakati fulani kwa kuliwa na simba. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Spika, hatuwezi tukaishi maisha hayo yaani mali inatuondolea hata utu wa kushindwa kuthamini kwamba wenzetu wanaishi mule wengine wanajeruhiwa. Haiwezekani, vinginevyo watuambie kwamba ule ni uongo na wachukuliwe hatua. Hata hivyo, kama unaweza ukafuga mbwa mle hatari kabisa, mbwa wakubwa kama wale, niwaombe matajiri wachache ambao wananufaika na ile mifugo na Serikali twende tukafanye sensa. Serikali ikitaka ku- prove hilo wafanye sensa, wale kondoo wamewekwa mpaka bei. Kondoo mmoja anauzwa Shilingi laki tano halafu mimi nibaki masikini, nani kakudanganya? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni wazi huyo kondoo sio wake. Kwa hiyo, watu wanafuga kondoo wakubwa mle kwa sababu huduma zote ni za bure, halafu wanakwenda kuuza wanapata fedha wananunua VX, yule mchungaji yuko mule anabaki na umasikini wake. Asikudanganye mtu zile familia za wale wanaochunga haziwezi kusoma, kwa sababu baba hachungi kila siku, siku ya pili anaachia watoto. Wanaacha kwenda shule anasema mkafanye kazi ya tajiri, ndio wale watoto ambao tunaona picha zao zinarushwa kwenye mitandao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka ni-conclude, sio kwamba naunganisha kama Waziri, lakini nataka niseme hivi, naunga mkono hoja hii. Serikali naomba niwashauri wale watu watafute namna ya kuwaondoa mle kwa namna mbili; wanaotaka kuondoka kihiari waondoke kihiari kuanzia sasa. Wakajipange waorodhoshe watu wanaotaka kuhama, wahame, wwaape kifuta jasho chao, watafute eneo la kuwapeleka. Wanaotaka kuondoka kwa sheria, Serikali ilete sheria tubadilishe waondoke kwa sheria. Yote hayo mawili yafanyike, (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba yote mawili yafanyike; anayetaka kuhama kwa hiari ahame kwa hiari, anayetaka kuhama kwa sheria, sheria sio msahafu, iletwe hapa tuibadili, sisi ndio watunga sheria, aondoke kisheria. Yote hayo yanawezekana nchi si ya kwetu jamani? Wataondoka kwa sheria, kama kuna mafao walipwe waende na huko wanakokwenda wapewe hati za kumiliki ardhi. Tusiwapeleke tena kwenye eneo la kuwapangisha. Maisha yao yakishaanza kuwa mazuri tutasema tena hapo hameni hapana. Tuwatengenezee structure nzuri ya shule. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka 2018 wote kulikuwa na kipindupindu kwa mwaka mzima hakikuondoka. Leo hii tunashindwa kuhurumia hawa watu jamani? Mtu anawezaje kukaa na kipindupindu kwa mwaka mzima watu wangapi wamepotea pale? Watu wangapi wamedhurika pale? Lazima tuangalie maisha ya watu. Pia mle ndani kuna minada, jana nimeona kwenye gazeti limeandika. Kuna minada miwili kila wiki, minada unajua inavyokusanya watu wengi, magari mengi, sasa mnyama gani atastahimili hiyo hali jamani? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono Serikali Waziri alete hapa habari wanaohama kwa hiari waorodheshwe, wahamishwe, Serikali ikafanye sensa. Kila mtu asimame na mifugo yake utashangaa hali za wale watu na mifugo wanayomiliki pale. Hapo ndio tutajua akina nani wanafugia pale na inawezekana, hata wale wanaochunga ile mifugo hawalipwi hata fedha. Anaambiwa kunywa maziwa tu, ng’ombe hizi ni za bwana mkubwa. Hii haiwezekani katika nchi yetu, mtu unaishi unawafanya wenzako kama watumwa, katika nchi ambayo tumedai uhuru na tumepigania uhuru wa nchi hii. Hilo jambo haliwezekani.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niiombe Serikali ije na tamko rasmi wanaohama waanze kuhama mara moja sio suala la kuchelewa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naendelea kuishauri Serikali ifanye mambo mawili. Ilete hapa orodha ya wananchi wanaotaka kuhama kwa hiari, iwasaidie kuhama. Wasije kuwa wanatishwa, wengine wanakaa mule kwa nguvu kwa sababu, kuna mabwana wakubwa wana mabavu wanawatishia. Wanaotaka kuhama kwa hiari Serikali iweke wazi orodha yao na waondoke eneo lile. Wanaotaka kuhama kwa mujibu wa sheria Serikali ilete sheria tubadilishe, wahame kwa mujibu wa sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa mwaka 2022/2023. Vilevile nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri Mkuu na Amiri Jeshi Mkuu Mheshimiwa Rais, Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa ambayo wamekuwa wakiifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nianzie ukurasa wa 18 Ibara ya 26 ya hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu anazungumzia habari ya kufanya mapitio ya sera ya uwekezaji. Tanzania tuna Wizara ya Uwekezaji na Ukuzaji wa Mitaji kwa Umma. Ukiitazama bajeti ya Wizara hiyo na kama Wizara hiyo itaamua sasa kuihamishia bajeti hiyo kwenye kukuza mitaji ya wananchi wenzetu tutasogea mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nini nataka kusema hapa. Badala ya kila siku kusema Wizara inashughulika na sera, hapana! Wizara sasa iende ikuze mitaji ya watu na ituletee orodha ya wananchi ambao mitaji yao imekuzwa. Hivyo ndivyo tutakavyotengeneza mabilionea wa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tusiwe na Wizara za kisera tu, sasa una Wizara ya Uwekezaji na Ukuzaji wa Mitaji ya Umma halafu huna mtu hata mmoja wa kutolea mfano kwamba mtaji wake umekuzwa, hiyo inasaidia nini? Haisaidia chochote!

Mheshimiwa Mweyekiti, kwa hiyo ninataka niishauri Serikali kama kweli tuna Wizara ya Uwekezaji na Ukuzaji wa Mitaji ya Umma basi mwakani watuletee hapa orodha ya wafanyabiashara waliokuwa na mitaji midogo, mitaji yao imekuzwa nakufikia hatua ya juu. Vinginevyo tutakuwa na Wizara inatamkwa vizuri lakini kazi inayofanyika haionekani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumzia habari ya mfumuko wa bei. Juzi hapa tulipata maoni mengi sana kutoka kwa Waheshimiwa Wabunge. Tulimsikia Mheshimiwa Shabiby akisema, tukamsikia Profesa Kitila Mkumbo akisema, tukamsikia Mheshimiwa Tabasam akisema. Nini nataka kusema hapa, ili tuwe na uelewa wa pamoja tunaomba Wizara pamoja na taasisi zake ikiwemo EWURA waje hapa Bungeni watupe semina ya pamoja tenda zinatolewaje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiwa na uelewa wa pamoja Wabunge ni rahisi sana kuishauri Serikali vizuri kuliko kila Mbunge akiwa na uelewa wake. Huyu anasema tenda zinatolewa kimagumashi, huyu anasema watu wanne ndiyo wanaopanga, haya mambo yanaumiza sana watu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwaambie nchi yetu tusisahau kwamba ni nchi maskini na Wabunge hata nikiwemo ninayezungumza natokana na familia maskini. Kuna watu leo wanashindwa kula, wanakula mlo mmoja, hali ni mbaya sana mtaani hatuwezi kufanya kama hatuoni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali wakati wa njaa kubwa ikitokea hapa, tunaona Serikali inafungua maghala ya Serikali inashusha bei ili kupunguza makali. Vipi Serikali haifungui maghala ya mafuta ya Serikali? Kama haina kwa nini? Kwa nini tusianze mchakato wa kutengeneza maghala tuwe na mafuta ya Serikali ikitokea bei kubwa kama hii Serikali inafungua maghala yake inashusha bei ina-regulate, mambo yanakaa sawa. (Makofi)

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Mwenyekiti taarifa!

MWENYEKITI: Taarifa kutoka wapi?

T A A R I F A

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimweleze mchangiaji kwamba Serikali inayo maghala, inayo maghala TIPER, Oryx ana 49 na Serikali ina 51, Serikali ina maghala mengine tena kama BP, kule BP ambapo sasa hivi ni PUMA tuna zaidi ya Milioni 80 ya kuhifadhi mafuta. Endelea mchangiaji.

MWENYEKITI: Unaipokea taarifa Mheshimiwa. Haya endelea.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naipokea taarifa yako Mheshimiwa Tabasam. Ninaiomba Serikali ifungue maghala kama yapo. Ndugu zangu mnakumbuka Waheshimiwa Wabunge wote wakati wa shida ya chakula Serikali hufungua maghala yake na kushusha bei ya mahindi. Ikishusha bei ya mahindi tunaona wafanyabiashara nao wanashusha. Kama Serikali ina maghala na ina mafuta iyafungue sasa ili bei ya mafuta ishuke. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani tuwe tunazungumza tu yatapanda tena. Lakini vilevile Mheshimiwa Mwenyekiti hebu ninaomba nisaidie muda wangu huo. (Makofi)

MWENYEKITI: Unazungumza na kiti, endelea.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe Serikali…

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa!

MWENYEKITI: Taarifa kutoka wapi? Mheshimiwa Shangazi aah! umesimama hapo. Mheshimiwa Shangazi taarifa. (Makofi)

T A A R I F A

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza pamoja na mchango mzuri wa mzungumzaji lakini ninataka tu nitoe taarifa kwamba Serikali ina zile facility lakini stock iliyoko kwenye maghala yale siyo ya Serikali. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Lusinde unapokea taarifa?

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama taarifa ya Mheshimiwa Shangazi ni ya kweli basi tuna mtihani mkubwa sana. (Makofi/Kicheko)

MWENYEKITI: Endelea Mheshimiwa Lusinde.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna mtihani mkubwa kwa sababu jambo kubwa kama hili ndugu zangu hivi hata kweli ndio imetokea shida purukushani hayo mafuta tunayatoa wapi? Hili ni jambo kubwa sana ni suala la usalama wa nchi. Kweli kabisa Taifa hili likose maghala ya Serikali ya kutunza mafuta? Hii ni hatari. Hatari kubwa sana hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo ninakuomba Serikali kama kweli hakuna, hili tatizo ni kubwa wala siyo jambo la kufumbia macho, tuende tupange bajeti tuanze kutengeneza maghala ya kutunza mafuta ili tuwe na hifadhi ya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine mimi nakushuru sana.

MHE. CHARLES J. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa!

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mwijage taarifa.

T A A R I F A

MHE. CHARLES J. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nimpe taarifa mzungumzaji kwamba pamoja na Serikali haina mafuta kwenye maghala yale ya kwake lakini kutokana na location advantage na mfumo wa kudhibiti mafuta Tanzania nchi yetu iko salama na ina mafuta ya kutosha. (Makofi)

MWENYEKITI: Unapokea taarifa Mheshimiwa Lusinde?

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani sasa tena Mwijage unataka kunipiga siasa hata mimi Mbunge mwenzako bwana? Hili jambo ni zito. Jamani eeh! hili jambo ni kubwa. Hili jambo tusiliongelee kwa lugha hiyo. Tusipige siasa kwenye mambo ya hatari. (Makofi)

MWENYEKITI: Waheshimiwa Wajumbe muacheni Mbunge achangie; endelea Mheshimiwa Lusinde.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi kufika mahala inakosa akiba ya mafuta ya Serikali halafu tunasema nchi iko salama! tunasema hali ni nzuri! Hii jamani tutakuwa tunajifungia humu ndani tunajidanga. Hapana, hapana, hapana! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima tuwe na utaratibu mzuri na nataka nikwambie, nisikilize. Sisi hali hii siyo ya kwanza, alizungumza hapa Profesa. Sisi vita imeshapigana kwenye eneo ambako ndiko tunanunua mafuta. Ishapigana na Uajemi vita lakini hali yetu haikufikia kama hii ambayo vita inapigana Urusi ambako ni mbali. Sasa hebu niambie kama hali hii vita wanapigana Urusi na Ukraine. Je ingepigana hapa OPEC ambako ndiko tunanunua mafuta tungeishi hapa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii kuna watu wanashindwa kufikisha wagonjwa hospitalini wanakufa. Ndugu zangu kukodi pikipiki gharama imeongezeka mara kumi. Vijijini huko lita moja ya petrol inauzwa Shilingi Elfu Nne, nani atakubali kumsafirisha mgonjwa wako kumkimbiza? Ambulance za Watanzania ni pikipiki za vijijini!

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mambo lazima tuyazungumze katika ukubwa wake tusiweke mambo ya siasa kwenye jambo hili, hapana tumsaidie mama kwenye jambo hii. (Makofi) Kwa hiyo, mimi ninasema hapa hii itasaidia kushusha mfumuko wa bei.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna miaka 60 ya kuongoza hili Taifa, tunashindwaje kuwa na hifadhi ya mafuta ya kwetu, tunashindwaje? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya naona alikuwa amesimama Waziri wa Fedha.

MWENYEKITI: Nimemuona Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango.

T A A R I F A

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitambue mchango wa mchangiaji na jambo analochangia ni jambo la msingi na ni jambo kubwa, kitu ambacho ninataka kukisema ni kwamba sambamba na mchango wake na dira hiyo anayoisema, Serikali inalifuatilia kwa umakini mkubwa sana jambo hili na siyo tu kwa maana ya hivi vita vinavyoendelea pamoja na majanga mengine yanayojitokeza lakini Wizara imeendelea na dira hiyo hiyo ya kufufua Tanzania iwe na akiba ya kutosha na siyo tu yakutosha kwa maana na majanga lakini iwe focal point kwa sababu ni entry ya nchi nyingi za ukanda huu hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo tunaenda kuwa na akiba ya kutosha siyo tu kwa ajili ya majira haya ya sasa ya vita, lakini tutakuwa na utaratibu tu wa kuwa na mafuta ya kutosha na actualy tuta-supply na kwenye nchi majirani kwa sababu lango la mafuta haya katika ukanda huu linapitia kwetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuhusu hiki kinachoendelea ambacho ni cha sasa hivi, tumesema hata jana tumetoa kauli ambayo tumewaambia wananchi kwamba tunaenda kuangalia baadhi ya maeneo ambayo hayagusi Development Budget yanayogusa Other Charges matumizi ambayo yanaenda kwa njia ya makato kwenye TBS, EWURA na maeneo mengine TPA, customs tunaenda kuyaangalia yale ili tuweze kuchomoa ili kuweka unafuu kwa wananchi na wakati ule ule Hazina iweze kuzisaidia zile taasisi zilizokuwa zinachukua kwenye mafuta. Maana yake tutoe unafuu kwa wananchi lakini Hazina na taasisi zingine ambazo zilikuwa zinachukua kwenye eneo lile tuweze kuangalia namna ya uendeshaji ndani ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo hili ni jambo ambalo linafanyiwa kazi na liko kwenye vipaumbele vya Mheshimiwa Rais na viko kwenye dira ya Wizara na Serikali inaipa umuhimu mkuwa kwa sababu mafuta ni injini ya uchumi wa nchi yoyote ile.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Lusinde.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, bado narudia kwanza tukubaliane kwamba ni lazima tuwe na hifadhi ya mafuta ya kwetu kama nchi, kama Taifa. Mafuta ya Serikali kuacha hivi visheli vya Serikali magari yanapita Mawaziri kuweka mafuta. Tuwe na hifadhi ya mafuta ya nchi, sisi kama Taifa ili hata ikitokea huko duniani kuna shida, sisi tunakuwa nayo. Jamani tunashindwaje kutunza? Watu wa kawaida tu wanatunza chakula wakati wa njaa anaenda anafumua watoto wanaishi, hayo ndiyo ninayoyataka maono yetu yawe hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni lazima inapotokea crisis kubwa kama hii tuiangalie jamii. Tuangalie maisha ya watu mtaani tunayafanyaje? Haiwezekani tuwe tunaendelea kupanga. Tunapanga maendeleo, tunapanga matumizi makubwa kana kwamba hakuna tatizo. Hiyo haiwezekani! Tukijifungia humu tuelewe kwamba Watanzania wana wakati mgumu sana kutokana na hii hali iliyopo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nihame hapo niende kwenye kilimo. Hebu niwaombe Serikali Maprofesa wale wa SUA pale watutengenezee mtaala wa kilimo ufundishwe kuanzia shule ya msingi mpaka sekondari. Kwa kufanya hivyo tutakuwa na wataalam wa kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu anayeishia Darasa la Saba atakuwa anajua kilimo kwa kiwango fulani. Anayeishia Sekondari atakuwa anajua kilimo kwa kiwango fulani. Kwa utaratibu huo watu watalima kilimo siyo cha chakula tu. Tutakuwa na kilimo cha biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani Taifa kama hili tunazungumzia habari ya kumpa leo mtu pikipiki, kumpa Afisa Ugani kipimo. Yale yote tukiyafundisha shuleni tutakuwa na Maafisa Ugani wa kiwango hicho nchi nzima. Lazima watu wetu wafundishwe namna ya kutunza chakula. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa Kilimo Bashe, anafanya kazi vizuri sana lakini tumuongezee nguvu kwa kutengeneza mtaala wa elimu ya kilimo ufundishwe mashuleni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nataka kuzungumza ni kuhusu ahadi za viongozi. Hivi ndugu zangu akiahidi Rais kwa Watanzania nitafanya jambo Fulani, halafu nyinyi watu wa Wizara hiyo hamtekelezi, ndiyo maana mwaka jana nilisema na leo narudia, tuweke kwenye kitabu kimoja ahadi za Marais, ziandikwe kwenye kitabu cha peke yake ili mwakani anaposimama hapa Waziri Mkuu anatueleza katika ahadi za Marais walizoahidi sehemu fulani imetekelezwa hii, imetekelezwa hii, imetekelezwa hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa utaratibu huu wa kwenda pamoja hivi tutakuwa tunatoka kwenye reli. Wananchi wanashangaa Rais anaahidije jambo lisitekelezwe? Sasa wasubiri nani aahidi? Rais alishaahidi kutengeneza barabara ya Mvumi kwa lami. Alishaahidi kujenga pale barabara ya Mvumi kwenda kuunganisha na barabara ya Iringa, leo ni hii mwaka wa 10 huu ni Mbunge nazungumzia ahadi ya Rais. Sasa watu wanauliza hivi akisema Rais kuna nani mwingine tena mkubwa wa kuzuia? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivyo Marais wameahidi kwa Wabunge karibu wote. Tutengenezeeni kitabu hata Ilani, tutengenezeeni kitabu cha ahadi za Marais waliopita na zilivyotekelezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la MSD Rais alishalitolea maamuzi suala hili. Rais ameagiza kwamba MSD ifanyiwe overhauling, sasa Wabunge kuanza kueleza nani alikuwa anafanya kazi vizuri. Nani aaah! siyo kazi ya Bunge, tusubiri hiyo overhauling inafanyikaje, tumuache Rais atengeneze pale ili utaratibu uweze kwenda. Rais amesema haraka kwa hiyo nina hakika kabisa soon mambo yatakaa sawa pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie jambo kidogo hapa, kuna maneno yanazungumzwa mitaani kuhusu Mheshimiwa Waziri Nape kuzunguka kwenda kuhamasisha anuani za makazi. Hapa ndipo panatuonesha wapi lipo tatizo. Tatizo lilipo siyo kwa Nape. Mheshimiwa Nape ameona kazi iliyofanyika mpaka sasa hivi ni asilimia 68 bado asilimia 32 na muda umeisha. Nategemea kwamba baada ya kumaliza ziara Mheshimiwa Nape hili jambo tutakuwa tumelikamilisha kwa asilimia 100. Kuna viungo vyetu havifanyi kazi sawa sawa. Tuna Wakurugenzi, tuna Wenyeviti, tuna Watendaji, tuna Ma-DC kwa hiyo, tuna uhakika akirudi hapa atatuambia wapi panavuja ili tuweze kusukuma nchi iweze kwenda. Kwa hiyo tusilaumu tu. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi nichangie hotuba ya Mheshimiwa Waziri Jenista Mhagama kutoka Wizara ya Utumishi na ambao kwa kweli wapo chini ya Mheshimiwa Rais mwenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwanza na TASAF niigusie kidogo ili baadae sabufa ikifunguka nisije nikasahau jambo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Waziri nilimuomba watu wa TASAF pale Mvumi kuna kitendo kibaya sana kilifanywa pale, walengwa wa TASAF wanagawiwa fedha zao halafu mgambo wakasimama dirisha la pili, halafu wakaanza kuwachangisha mchango kwamba nishike mkono wanachangia elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili jambo nimemlalamikia Mheshimiwa Waziri na Naibu wake bahati nzuri nawashukuru sana wamelifanyia kazi na nimeona barua kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa TASAF kwamba zile pesa zirudishwe kwa wale walengwa wa Kijiji cha Mvumi Mission na walengwa wote wa Wilaya ya Chamwino ambao walikatwa fedha zao kwa mchango ule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli nilitaka kushangaa sana mgonjwa badala ya kupewa drip halafu kuna watu wengine wenyewe ndiyo wanamtoa maji sasa. Sasa niombe Mheshimiwa Waziri tamko liwe la haraka utakapojibu hapa, hebu jambo hili lifanyike haraka ili wale walengwa warudishiwe pesa zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa nina mambo machache sana, moja ni mgawanyo wa ajira. Tukisema tutegemee mtandao peke yake jamani nataka niwaambie sijui kuna nini kinatokea hata kwenye mtandao, mtandao wakati mwingine unaruka watu maskini, huwezi kuamini mimi nitakupa ushahidi hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa kuna mgao wa net, yaani pale Mvumi mission wote wenye uwezo wa kati majina yao kwenye mtandao yamesomwa nikiwepo Mbunge kupata net ya bure lakini vipofu na wasioona wote hawamo mtandao umewaruka. Sasa hili la ajira tukisema tuombe online kuna vijana wafamilia maskini hawatakaa wapate. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishauri, kwa sababu Taifa hili tunafahamiana, hizi ajira zitolewe kiwilaya au zitolewe kijimbo. Ukizishusha kama zilivyo ukasema Jimbo fulani limepata ajira nane Mbunge na watu wake pale na sifa wanazo, wataajiriwa watu ambao tunawafahamu, lakini kila zikitoka ajira watu unaowajua kwenye Jimbo lako hawamo na wenye sifa hawamo. Jamani nina mashaka na mtandao unakwepa watu maskini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ninalotaka kulizungumza, tukiwa mgawango wa ajira kiwilaya au kijimbo tutamaliza hayo matatizo kwa sababu nchi nzima itaajiriwa mara moja utakuwa umewapata watu kutoka nchi nzima.

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Dah, kaka yangu yaani leo niko vibaya. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Lusinde, Kanuni inasema kwa idhini ya Spika atatoa taarifa, kwa hiyo sijaidhinisha bado.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, haya naendelea, ndiyo nimesema aniache kidogo leo nina mambo mazito, Mheshimiwa Tabasam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ninalotaka kulizungumza hapa, kipaumbele cha ajira wapewe wale ambao wanaojitolea. Kuna watu wanajitolewa, wana miaka mingi wanafanya kazi ya kujitolea kwenye kila Idara, hao ndiyo wapewe kipaumbele cha kuajiriwa kwanza, lakini tukiwaweka kwenye kapu moja, wanaojitolea wanakosa wanapata watu wengine. Nchi yetu ina wastaafu... (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Tabasam.

T A A R I F A

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe taarifa mchangiaji, mtandao wenyewe leo ni siku ya tatu umezimwa, unapatikana mijini tu.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Lusinde, endelea.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Sasa niwaombe watoa taarifa wengine watulie, nataka kuzungumza mambo makubwa ya nchi.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Lusinde.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepokea.

MWENYEKITI: Unaipokea, ahsante, endelea.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sana, watu wanaofanya kazi ya kujitolea ndiyo wapewe kipaumbele cha kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu ina wastaafu aina nyingi sana, ina wastaafu ambao wametumikia Serikali, lakini bahati mbaya sana ina wastaafu ambao hawajawahi kufanya kazi popote, yaani yeye anazaliwa, anatakiwa ajifundishe kilimo anaingia kazini, anaingia kusoma, akishamaliza kusoma anaomba kazi hapati, kila akiomba kazi hapati, kwa hiyo kilimo hajui, kuchunga hajui na kazi aliyosomea hana. Huyu tunamweka kwenye kundi gani? Hawa katika uzee ndio tunashauri wapewe kiinua mgongo cha wazee ili waweze kuishi, kwa sababu Tanzania ni ya kwao na sisi ndiyo tumewanyima hiyo ajira. Qualifications anazo lakini mpaka anazeeka hajawahi kuzitumia mahali popote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nataka niende kwenye suala la Utawala Bora. Nchi yetu imeweka vizuri sana masuala ya Utawala Bora kisheria lakini kuna baadhi ya vyama, kwa mfano pale Zanzibar ACT-Wazalendo tunashirikiana nacho kwenye Utawala Bora, sisi tuna Rais, tuna Serikali, wao wana Makamu wa Kwanza wa Rais, lakini nimemsikia Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo Zitto, anamnanga Mheshimiwa Magufuli kana kwamba Zitto hashiriki kwenye Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili nataka niliseme, Mheshimiwa Magufuli aheshimiwe, Zitto aelewe kwamba suala la kufiwa ni suala kubwa. Haiwezekani tuache kwenye utawala bora kulizungumza suala la Magufuli kusemwa vibaya na mimi sitaacha. Mheshimiwa Zitto anatutaka tunaompenda Mheshimiwa Magufuli tukazikwe naye. Zitto ndugu zangu amewahi kufiwa na mama yake, mimi sitaki kuingia huko, mama wa Zitto ni mama yangu mimi, ametangulia, mimi nimewahi kufiwa na baba yangu, lakini ACT wamewahi kufiwa na Makamu wa Kwanza wa Rais, Zitto analazimisha sisi tumseme vibaya Maalim Seif, hatuwezi, hatuwezi! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii ninapoongea hapa Waislam mmefunga, dini inakataza kuwasema vibaya marehemu, Zitto ni Muislam anajua. Zitto ametukosea sana Watanzania, Zitto atuombe radhi Watanzania, Zitto amemkosea sana mama Magufuli, Zitto ameikosea sana familia ya Magufuli. Hili jambo siyo sawa. Ndugu zangu tusifikiri kwamba kumsema vibaya Magufuli kutatusaidia, hawezi kujibu, hayupo. Kama ulikuwa na tatizo naye maliza utakuja kukutana naye kwa Mwenyezi Mungu. Mtu akishatangulia, kitabu chake kinafungwa tunamwachia Mwenyezi Mungu kuja kutoa hukumu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, inakuwaje watu mnakuwa waoga Viongozi wakiwepo hamsemi, wakiondoka ndiyo mnasema, huu ni uoga uliyopitiliza. Mtu mmoja tu alisema kwa vitendo kwamba yeye hawezi kufanya kazi na Magufuli, Nyalandu aliachia ubunge hapa akaondoka, lakini wote tuliobaki hapa ni watu wa Magufuli na tumefanya naye kazi na tulikuwa tunamsifu. Hivyo ndivyo ambavyo tunatakiwa tumsifu Mheshimiwa Samia na ndiyo kazi tunayofanya hapa, tusiweke unafiki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwaambie, hawa watu ambao sasa hivi wanamsema vibaya Mheshimiwa Magufuli na kumsifu Mheshimiwa Samia ni wanafiki wakubwa. Mheshimiwa Samia akiondoka watamsema vibaya hivyo hivyo, hivyo hivyo, ni bora mimi Lusinde ambaye niko wazi na siwezi kuacha, haiwezekani!

Kwa hiyo nchi yetu ili iendelee na utawala bora hawa watu tunashirikiana nao, Viongozi waliokufa wale ni watu wazito, Maalim Seif amefanya kazi kubwa, Mheshimiwa Magufuli amefanya kazi kubwa. Sasa ukisema kwamba wanaompenda Mheshimiwa Magufuli wakazikwe na Mheshimiwa Magufuli maana yake nini? Hii ni kashfa kubwa sana. Zitto aliombe radhi Taifa hili, awaombe radhi familia ya Magufuli na asirudie tena kufanya mambo ya kipuuzi kama hayo. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Lusinde.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ngoma imeisha, sasa sabufa ndiyo lilikuwa limefunguka.

MWENYEKITI: Hitimisha hoja yako kwa dakika moja, dakika zako zimeshakwisha.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kupata nafasi ya kufungua dimba asubuhi ya leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mungu sana kwa ajili ya kutuzawadia zawadi ya uhai.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nishukuru kupata nafasi ya kuchangia Hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, ambayo imewasilishwa mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, tunampelekea shukrani zetu kutoka kwa wananchi wa Jimbo la Mvumi, kwa kazi kubwa anazozifanya. Majuzi hapa tulimsikia Mheshimiwa mama Kilango akipiga hesabu ya fedha zilizokwenda jimboni kwake. Kila Mbunge ukimsimamisha hapa atazungumzia pesa zilizokwenda kwenye jimbo lake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Jimbo la Mvumi Mheshimiwa Rais Dkt. Samia majuzi tu ametuteremshia shilingi bilioni tatu na milioni 700 kwa ajili ya ujenzi wa chuo cha VETA lakini hapo kabla tulishapata pesa kwa ajili ya mradi wa booster, pesa chungu mzima, karibu bilioni sita ukijumlisha, zote zimeingia kwenye Jimbo la Mvumi; haya ni maajabu. Lazima tumshukuru Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayotufanyia Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepata miradi ya maji katika Jimbo la Mvumi, karibu ya bilioni mbili inaendelea kujengwa katika Kata ya Mvumi Mission pamoja na Kata ya Handali; hii tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kazi njema anayotufanyia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo kubwa ambalo limezungumzwa katika bajeti ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Nataka niende kwenye suala la amani na utulivu, amani na utulivu ndio msingi wa kuendesha Tanzania. Lakini Mheshimiwa Rais ameidumisha amani na utulivu kwa kuileta nchi pamoja; amekusanya makundi yote kukaa mezani pamoja ili tuzungumze namna gani tutatoka hapa tulipo kuisogeza nchi pamoja; hongera sana Dkt. Samia Suluhu Hassan. Hili siyo jambo dogo, hili ni jambo kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumemuona Rais namna anavyohangaika kutafuta pesa. Waheshimiwa Wabunge ambao tumekaa hapa muda mrefu mtakubaliana nami, sasa hivi mimi ni kipindi cha tatu hapa; bajeti ya mwaka 2021/2022 tulipitisha hapa bajeti Mheshimiwa Rais akaenda kutafuta fedha mpaka zikapita ile bajeti; sijawahi kuona tangu tumekuwa Wabunge humu, wote, akina Mheshimiwa Ole- Sendeka mko hapa. Tumepata pesa zinazovuka bajeti kwa mara ya kwanza. Rais Dkt. Samia anafanya kazi kubwa, tusimkatishe tamaa, lazima tumsaidie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata ninyi Waheshimiwa Mawaziri, Tanzania tumebahatika kupata Rais anayewapa uhuru mkubwa wa kufanya kazi; fanyeni kazi ya kumsaidia Rais. Rais anatafuta pesa, mnataka yeye mwenyewe aingie tena kupiga hesabu; haiwezekani. Lazima muwasimamie watu wetu. Tuwasimamie Makatibu Wakuu, tuwasimamie wahasibu, ili waweze kujibu hoja kabla hazijaletwa hapa Bungeni. Tunachokifanya hatumtendei haki Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Mawaziri, si sawa, hili jambo Mheshimiwa Waziri Mkuu, si sawa. Tunataka Rais afanye kazi ya kutafuta fedha za ujumla lakini haya mambo madogo madogo myamalize ninyi. Tumalize kero za wananchi, tumalize matatizo ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna vihoja vidogovidogo tunashindwa kuvijibu. Unashindwaje kumaliza tatizo katika Wizara yako wakati unajua kabisa CAG anapokuja anakuja kuhoji watu wako; wasimamie. Hizi hoja nyingine zinajibika kabisa, ndiyo maana unaona Bunge sasa tunatolewa kwenye mstari tunapelekwa sehemu kujadili hoja kabla ya wakati, kitu ambacho siyo sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka kupitisha bajeti ya nchi, tunataka kupitisha bajeti ya wananchi wa Tanzania. Hili ni jambo kubwa, lakini kwa sababu kuna baadhi ya Wizara zilizembea kushughulika na hoja za Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali, ndiyo maana mnaona sasa Bunge linasukumwa pembeni tuanze kujadili kabla ya wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, taratibu zinafahamika kwamba ile ripoti ikishapokelewa na Mheshimiwa Spika inakabidhiwa kwa Kamati ya PAC (Hesabu za Serikali), Kamati ya PAC inakwenda kuchakata kwa kuwaita wote. Tunaliita jicho, wataitwa na watu wanaotuhumiwa watatoa majibu, halafu ndio Wabunge tunakuja kuamua. Sasa tukianza kuamua mapema, huo mwezi Novemba wakati PAC wamechakata tutatoa uamuzi gani tena? Tutakuwa tunajikanyaga wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu zangu, kwa hiyo, tusifanye jambo kwa mihemko. Tuna Spika mzuri, mwanasheria, anatuongoza vizuri, kwa hiyo, nina uhakika kabisa Bunge hili litaamua sawasawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema; Mheshimiwa Rais ametoa uwazi mkubwa. Unajua hata hii ripoti yenyewe kama Rais angekuwa hataki itoke, ingetoka? Ni Rais ndio anataka, Rais ameweka mambo kwa uwazi, hataki kificho, anataka sisi tumsaidie wapi panavuja, wapi tuzibe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutapata wapi Rais kama huyu ambaye anaiongezea bajeti Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali; utampata wapi? Ili aweze kukagua kila kona. Rais anataka nchi yetu tuwe wawazi ili tuweze kujua wapi kuna tatizo tusughulike nalo; wapi kuna shida tushughulike nayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Waheshimiwa Mawaziri, tusimamie kwenye Wizara zetu. Mnafanya kazi vizuri, msinyongee, hakuna Waziri ametajwa mahali popote katika hii ripoti. Wasiwasi wenu uko wapi? Chapeni kazi za maendeleo ya wananchi. Tusimamie barabara, tusimamie maji, tusimamie maendeleo kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, angalia kwenye kada ya afya, juzi Mheshimiwa Rais amefanya kufuru hapa; ameleta magari ya kuchimba visima vya maji karibu nchi nzima. Kwa hiyo, sasa hivi maana yake kila jimbo likipangiwa ratibu vitatobolewa visima virefu vya maji na kuondoa matatizo yote ya maji; hii ni kazi inayofanywa na Mheshimiwa Dkt. Samia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi tumeona madarasa yalivyojengwa nchi nzima, kila jimbo limeguswa. Zamani kabla ya Mheshimiwa Samia, wananchi wetu tulichangishana mpaka wengine wangefungwa; uongo kweli? Kuna watu wangekimbia kwenye majimbo. Lakini Mheshimiwa Samia akasema hapana, tutatafuta fedha tuwapunguzie mzigo wananchi ili watu waweze kusoma shule, na sasa hivi tuna tatizo la kupeleka wanafunzi, siyo tena madawati. Madawati yapo, madarasa yapo, ila sasa watoto hawataki kwenda shule. Tumpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa kazi hii nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nawaomba sana tunapomuunga mkono Mheshimiwa Rais tumuunge kwa vitendo. Mawaziri fanyeni kazi sisi Wabunge tupo. Ukifika wakati wa kujadili Taarifa ya CAG tutaijadili kwa nguvu zote. Lakini kwa sasa tupitishe bajeti ya Serikali ambayo iko mbele yetu. (Makofi)

MHE. CHRISTOPHER O. OLE-SENDEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa Mheshimiwa Ole-Sendeka.

T A A R I F A

MHE. CHRISTOPHER O. OLE-SENDEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kutumia nafasi hii kutoa taarifa kwa Mheshimiwa Mbunge, rafiki yangu Lusinde. Kusema kwamba jambo hili liendelee kusubiri mpaka wakati mwingine kwa maana ya kufuata ratiba mpaka Novemba ilihali mnaujua upepo uliopo nje, Watanzania wamekerwa na hatua hii ya ufisadi uliokithiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitendo chochote cha kuchelewesha uchukuaji wa hatua dhidi ya wahusika wa ufisadi huu wa matrilioni, mabilioni ya fedha, na bila Bunge lako kuchukua hatua ya kuunda Kamati teule au kufanya maamuzi kwa ripoti iliyokamilika ni kuchelewesha kutoa haki kwa Watanzania na huko ni kufifisha jitihada za kumuunga mkono Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anayofanya ya kukusanya fedha na kwamba hata hasira yake Bunge hili litakuwa halijamtendea haki Samia wala Watanzania kama hamtachukua hatua sasa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Lusinde, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, siipokei kwa sababu anachangia kwenye hotuba yangu. Nilichosema ni kwamba tufuate taratibu, taratibu ni taratibu. Tumejipangia taratibu na sheria zimepangwa. Jamani eh, kuku anatotoa baada ya siku 21. Sasa Mheshimiwa Mzee Ole- Sendeka anataka atotoe kesho, yaani mayai atage leo, atotoe kesho; itawezekana jamani? Wabunge tusijidanganye, tusifikiri kwamba hapo ndiyo tunamsaidia Rais, kumsaidia Rais kwa kuvunja sheria, kwa kuvunja Bunge, kwa kuvunja kanuni itakuwa siyo sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi maafisa masuhuli wote wako pale, wamekuja kuleta bajeti. Utawaitaje? PAC itawaitaje kwenda kushughulikia mambo yao? Kwa hiyo, ninashauri sisi wakati tunajadili hukatazwi kuligusa kaka, lakini lazima lifuate ratiba ya Kibunge. Na likifuata ratiba ya Kibunge ndiyo litakuwa na majibu sahihi ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nakushukuru sana; ahsante sana. naunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na kwa namna ya pekee nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge aliyeketi kwa kutoa mchango mzuri ambao hauna unafiki wala ubabaishaji.
Ameeleza vizuri kuhusu utawala bora na Wabunge wa namna hii ndiyo wanaotakiwa ili kuijenga Tanzania kwa pamoja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa hotuba nzuri iliyofafanua mambo mengi ya msingi kuhusu kilimo, afya, maji na maendeleo mbalimbali ya nchi yetu. Hata hivyo, Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa upande wa afya mmefanya kazi kubwa lakini bado zipo changamoto nyingi sana. Changamoto kwenye majimbo ya vijijini ni kubwa mno. Tukija mijini huku tunawakuta madaktari bingwa wa akinamama na magonjwa mbalimbali lakini vijijini tunakuwa na daktari mmoja halafu huyo ndiyo bingwa wa magonjwa yote. Kwa
hiyo, nataka nichukue fursa hii kuwapongeza sana madaktari wanao-save katika vijiji vyetu, wanafanya kazi kubwa sana kwa sababu magonjwa ya akinamama ni yao, ya watoto ni yao na ya akinababa ni yao. Hawa ndiyo ambao nataka kuwatambua leo kwenye Bunge kwamba ni madaktari bingwa kwelikweli kwa sababu wanashughulika na matatizo makubwa sana ya wananchi vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niipongeze sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa uamuzi sahihi wa kuamua kujenga baadhi ya vituo vya afya kwenye maeneo yaliyotengwa sana na maeneo makubwa ya kupata huduma nzuri za afya. Kwa mfano, ukitazama Tarafa yangu ya Mpwayungu, pale usiponipa kituo kikubwa cha afya ni hatari sana kwa akinamama wajawazito, kwa sababu kutoka Mpwayungu mpaka kuja Hospitali Teule ya Wilaya pana kilometa kama 85 niambie barabara ya vumbi, mama mjamzito anafikaje hapo kuja kuwahi operesheni. Kwa hiyo, naipongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa uamuzi wenu sahihi na nina hakika hili mtaliangalia kwa jicho la huruma kwenye majimbo mengi ya vijijini hasa yaliyokosa huduma za msingi za kiwango hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumzia habari ya Wizara ya ujenzi, itazame vilevile barabara za vijijini.
Tunazungumza sana ujenzi wa barabara za mijini lakini za vijijini tunaacha. Barabara za vijijini zikipitika kwa kiwango kizuri zitarahisisha sana huduma za maendeleo kwa wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumie kwa haraka haraka Wizara ya Maji. Maji ni Wizara mtambuka. Tukipata maji safi na salama tutapunguza kwa kiasi kikubwa sana matumizi kwenye Wizara ya afya kwa sababu magonjwa mbalimbali ambayo yanaweza kutibika kwa
kupata maji safi na salama yatakuwa yameji-solve yenyewe na kuruhusu wananchi wafanye shughuli zingine za maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, pamoja na pongezi zangu kwa Wizara zote ambazo Mheshimiwa Waziri Mkuu ameziwasilisha katika hotuba yake hii, nataka nizungumzie vile vile suala la ulinzi na usalama. Suala la ulinzi na usalama limezungumzwa hapa kwa mapana na marefu lakini nataka nizungumze kwenye kipengele kimoja. Nichukue fursa hii kusema watu wanaotuhumiwa, unajua Wabunge tunachanganya kuna wengine wanasema kuna kikundi kidogo ndani ya Usalama wa Taifa wengine wanasema Usalama wa Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwapongeze sana watu wanaofanya kazi kwenye idara hiyo. Idara ya Usalama wa Taifa inafanya kazi kubwa sana, inafanya kazi nyeti sana na kuna baadhi ya watu nitawataja hapa bila kuwepo ulinzi na usalama kwenye maeneo yao wasingekuwepo hapa.
Mnakumbuka wakati wa msiba wa Chacha Zakayo Wangwe, ni watu wa Usalama wa Taifa ndiyo walimuokoa Mbowe pale Tarime nani hajui? Kwa hiyo, wakati mwingine tusiwe tunawalaumu tu pale wanapofanya vizuri tuwasifie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme habari ya kupotea watu mimi mwenyewe ni mhanga, wako ndugu zangu walishapotea siku nyingi wengine walipotea mwaka 1980 na hwakuwa wanasiasa. Tanzania hii hata ukitaka kila Mbunge aorodheshe watu waliowahi kupotea wapo.
Hawapotei kwa sababu kuna kikundi kinapoteza watu, hapana! Kupotea kwa wananchi ni jambo la kawaida ila tunaitaka Serikali
iendelee kutafuta wananchi waliopotea hata wale ambao hawana majina. Kwa sababu nchi hii tusiseme tu akipotea mtu fulani maarufu ndiyo tunaanza kuzungumza. Upotevu wa wananchi ni jambo la siku nyingi. Kwa hiyo, tuitake Serikali, Idara ya Upelelezi ifanyie kazi mambo haya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mnazungumza mnasema eti ooh kuna Mkuu wa Mkoa alisema mtu fulani aliyepotea ataonekana kesho mbona Kubenea alisema kwamba huyu Saanane anafahamika na kila siku anaonekana, mbona hamumhoji Kubenea? Kubenea si huyu hapa mhojini? Mbona alisema kwamba Saanane yupo anatafuta kiki tu? Kwa nini msianze na Kubenea mnaanza kuisakama Serikali? Anzeni na Kubenea atuoneshe Saanane yuko wapi, Kubenea anajua.
Taarifa...
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Wabunge wengi
hawana ofisi. Tunaitaka Ofisi ya Waziri Mkuu kukamilisha ujenzi
wa ofisi za Wabunge ili Wabunge waweze kufanya kazi zao
kwa ufanisi. Tunaitaka Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia TAMISEMI
isimamie ujenzi wa Ofisi za Wabunge ili Wabunge waweze
kupata Ofisi zao na waweze kufanya kazi zao kwa uhakika,
waweze kuheshimika kwenye majimbo yao tofauti na sasa
ambapo Wabunge wengi wanafanyia kazi zao nyumbani,
hili haliwezekani. Ofisi zimejengwa hazijakamilika, kuna
maeneo fulani mpaka frame zinaanza kung’olewa, kuna
maeneo fulani majumba yanaoza kabla hayajamalizika,
tunaitaka Serikali ikamilishe ujenzi wa Ofisi za Wabunge ili
Wabunge wafanye kazi zao kama sheria inavyotaka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimpongeze sana
Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa kipindi cha mwaka mmoja
mmefanya kazi kubwa sana. Mheshimiwa Rais amesimamia
maadili, nidhamu na uwajibikaji. Leo tunapozungumza hapa
Rais anazindua ujenzi wa reli ya standard gauge ambayo
itatumia saa moja kufika Morogoro na baadaye
watakamilisha Dodoma na kuelekea Mikoa ya Kanda ya
Ziwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano imefanya kazi kubwa sana kwa vitendo na tunamwomba Rais aendelee kusimamia nidhamu ya uwajibikaji, nidhamu ya mapato na matumizi, aendelee kusimamaia amani ya nchi yetu ili watu tuweze kuishi kwa amani na tufanye kazi kwa bidii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
Muswada wa Sheria ya Upatikanaji wa Habari wa Mwaka 2016
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda nimshukuru Mungu kwa kunijalia zawadi ya uhai na afya njema ili na mimi niweze kusema machache juu ya mchango wangu kuhusu Muswada wa Upatikanaji wa Taarifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nichukue fursa hii kuipongeza sana Serikali kwa kuuleta Muswada huu. Kabla ya Muswada huu, suala la kutoa taarifa halikuwa la lazima. Mtu angetaka kutoa anatoa; hataki, anakaa hivyo hivyo; lakini leo kwenye Muswada huu Afisa analazimishwa kutoa taarifa kama sheria tutakavyoipitisha. Kwa hiyo, tunaipongeza sana Serikali kwa uamuzi wake wa kuleta Muswada huu Bungeni ili watu wasitafute habari kwa kuomba, wasitafute habari kwa hisani, bali wazitafute habari kisheria. Hili ni jambo zuri sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo mengi yanazungumzwa humu ndani kwamba Katiba inatoa haki, ndugu zangu, Waheshimiwa Wabunge, Katiba haifanyi kazi ya utendaji wanaotenda ni watu sio Katiba yenyewe ndiyo inayotekeleza. Leo Katiba inasema kila Mtanzania ana haki ya kuishi popote, lakini Rais au Waziri mwenye dhamana ya makazi ana uwezo wa kusema watu watoke hapa kuna mafuriko wakati Katiba haisemi hivyo. Kwa hiyo, tusiishi kama tumejifungia; maana yake kila mtu hapa anasema Katiba, Katiba. Katiba haitekelezi, Katiba ni sheria mama ya nchi. Zinatungwa sheria kutafsiri Katiba na ndiyo kazi ambayo tunataka kufanya hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nasikitika sana ninapoona watu wanakimbilia kujificha kwenye Katiba. Katiba haitekelezi, wanatekeleza watu na hao watu wanaweza kutekeleza kitu ambacho kiko kwenye Katiba. Leo hii hapa tuna jengo la Bunge, lakini pakipita mafuriko litahama, hata kama imeandikwa hivyo kwenye sheria kwamba jengo la Bunge liwe hapa. Kwa hiyo, watu waelewe tu kwamba hapa tunatunga Sheria ya Upatikanaji wa Taarifa na hakuna sehemu tunapokwenda kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hakuna sehemu tunapokwenda kinyume.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona Waheshimiwa Wabunge wanajaribu kuwatisha baadhi ya Mawaziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, hivi kumbe ninyi mngeshinda nchi mngetunga sheria ambazo zingewa-favour akina Lowassa? Sheria ni msumeno, inatakiwa ikate kote kote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo kama kuna mtu alikuwa Waziri akaivunja sheria amefungwa ni sawasawa. Hatutungi sheria kwa ajili ya wananchi tu; tunatunga sheria kwa ajili ya Watanzania wote na sisi wenyewe. Sasa naona kuna mtu anasimama anasema, shauri yenu, akina Mramba walikuwa hapo, leo wamefungwa. Hata ninyi mtafungwa, hata sisi Wabunge tutafungwa, hata mimi nitafungwa. Sheria inataka kila mtu aitekeleze.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumbe wenzetu wangepata Serikali hawa, wangetunga sheria za kukandamiza wananchi, wao zisingewahusu. Ndiyo maana mnaona kila wakisimama hapa, wanajaribu kukutisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali, wanajaribu kukwambia eti leo hii Lowassa anapigwa mabomu, angepigwa mabomu angekuepo? Amepigwa gesi za kutolea machozi, siyo bomu. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tusidanganyane hapa! Watu wanaowazungumza, hata kukimbia hatua tano hawawezi, apigwe bomu ataweza kuvumilia yule? Acheni mambo ya kudanganya kwenye Bunge hapa. Tusidanganyane! Watanzania lazima tuelewe, tunapotunga sheria na Wabunge tuelewe, hatuwatungii watu, tunajitungia na sisi wenyewe, hili ndiyo nataka lieleweke.
Kwa hiyo, isije ikafikiriwa kwamba kuna kundi tu tunalolilenga, hapana. Kumbe wenzetu wametupongeza kwamba Serikali ya CCM inatenda haki, inatunga sheria zinazowalamba mpaka Mawaziri, wametupongeza. Hizi tuzichukulie kama pongezi kabisa, kwa sababu leo hii kila kitu wanataka kiandikwe kwenye Katiba. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii kuna Chama kimoja, Mwenyekiti wao anadaiwa, walikutana kikao kujadili deni, kwenye Katiba yao imeandiwa wapi? Imeandikwa wapi? Wapi kwenye Katiba yao imeandikwa Mwenyekiti akidaiwa mtaacha shughuli zote mkutane kwenye kikao kujadili deni? Kwa hiyo, kuna mambo mengine ya utekelezaji yanafanyika nje ya hizo Katiba kwa sababu ya hali halisi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa namna unavyoliendesha Bunge kisayansi na linavyokwenda. Nataka niseme leo, tajiri hanuniwi! Ukimnunia tajiri, inakula kwako. Kwa hiyo, hizi siku mbili mnazowaona watu wana uhuru fulani wanazungumza humu ndani, ndiyo uhuru umepatikana hivyo. Kwa hiyo, tuendelee kuwavumilia, tutakwenda nao vizuri tu hawa wa kwetu. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya adhabu; hakuna sheria inayoweza kutekelezwa kama haitoi adhabu. Haiwezekani. Sheria yoyote ili itekelezwe, ni lazima iwe na adhabu. Kwa hiyo, kama kwenye sheria hii kuna mtu ataikosea sheria, atakwenda jela miaka mitano, iko sawa. Kumbe tutatungaje sheria bila kuweka adhabu? Hiyo sheria itatekelezwaje sasa? Sheria ili itekelezwe ni lazima iwe na upande wa kuadhibu ili watu tuogope; ili watu waogope. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kusimama hapa na kusema upatikanaji wa habari ni haki ya Kikatiba. Kweli ni haki ya Kikatiba, lakini kwa mfano, kama mtu nyumbani kwake hajanunua redio, hana betri, anapataje habari? Hawa watu wa ajabu sana! Ni haki kweli, lakini kuna haki ambazo ni lazima uzigharamie. Leo upatikanaji wa habari, huna TV, huna umeme unapataje hiyo habari? Wenzetu wanalazimisha, ooh, ni haki ya Kikatiba, haki ya Kikatiba, sasa Serikali igawe TV nchi nzima, Serikali igawe redio nchi nzima, igawe betri nchi nzima? Kwa hiyo, kuna vipande kwa vipande. Kuna haki na kuna wajibu. Uko wajibu! Ukitaka habari, ni lazima uwe na wajibu. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tusitake kutumia fursa hii kudanganya. Zipo haki zimetajwa kwenye Katiba, lakini uko wajibu. Kila Mtanzania ana haki ya kuishi, lakini ana wajibu wa kulima ili apate chakula kitakachomfanya aishi. Sasa kama hafanyi kazi, hapiki chakula, anaishije? (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tusidanganye watu kwa kutumia kisingizio cha Katiba, inatoa haki, Katiba inaminywa. Katiba inatoa haki na Katiba hiyo hiyo inatoa fursa. Mwanasheria Mkuu wa Serikali, watu wakikusonga sana, jua uko sahihi. Kwa hiyo, wewe endelea kufanya kazi zako, ndiyo maana unaona wanasimama wanakushutumu. Mawaziri endeleeni kupiga kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi kila mtu akisimama hapa, mnataka kupotosha watu kwamba Mheshimiwa Rais amekataza kufanya mikutano!
Hakuna mahali Mheshimiwa Rais amekataza kufanya mikutano. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kila Mbunge anatakwa kufanya Mkutano kwenye Jimbo lake. Kilichokatazwa ni kuendelea na kampeni kwa tabia ambayo tulikuwa tumezoea. Uchaguzi unaisha, watu wanaendelea na kampeni miaka mitano, hiyo ndiyo haikubaliki. Mbunge gani, wa Jimbo gani, kaenda kufanya mkutano kwenye Jimbo lake akakatazwa? Nani? Hakuna mahali. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa walikuwa wameshazoea. Watanzania kwa sasa hivi hawana nafasi ya kupokea tena maneno, wanataka kupokea maendeleo, siyo maneno. Maneno mengi yameshazungumzwa, maneno mengi yameshasemwa, nyimbo nyingi zimeimbwa mpaka nyingine zimezuiwa kuimbwa, sasa hivi ni wakati wa kufanya kazi, siyo wakati wa maneno kama walivyokuwa wamezoea hawa.
Kwa hiyo, mkisikia wanalaumu, ooh, Mheshimiwa Rais ametukataza kufanya mkutano; wewe Jimbo lako la Tarime, nani kakukataza kufanya mkutano? Nenda kahutubie wananchi wako waliokuchagua, isipokuwa kutoka Tarime unafunga safari kwenda Mpwapwa; Mpwapwa wana kiongozi wao waliomchagua, acheni afanye kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ambacho leo nataka nikiseme, kauli ya Mheshimiwa Rais imewaumiza baadhi ya watu. Walikuwa wanatumia ruzuku vibaya, wakati huo wanajifanya kuna operesheni sijui nini; sijui operesheni ndorobo; sijui operesheni nini, kumbe wanakula hela za wananchi kwa kutumia mgongo wa operesheni. Sasa hiyo hakuna. Hakuna nafasi hiyo, kila Mbunge afanye mikutano kwenye Jimbo lake, ahamasishe maendeleo, shughuli za maendeleo zifanikiwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kuja kumsingizia Mheshimiwa Rais kwamba kazuia mikutano, siyo sahihi, lazima tuliweke vizuri jambo hili. Ulaji wa ruzuku kupitia vyama vya siasa umezuiwa, ndiyo maana mnaona kelele. Maana ilikuwa saa hizi unaona maspika yamefungwa, bendera zimefungwa; wapi? Mtera, kufanya nini? Mtera kuna Mbunge wake, mnakwenda kufanya nini? Miezi mitatu imepita tumefanya uchaguzi, leo hii tuendelee tena kuwajaza watu maneno? (Makofi)
Ukisikia kelele, ujue tayari!
MWENYEKITI: Ahsante. Ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kuchukua fursa hii kumshukuru Mungu kwa kupata nafasi hii, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara ya Maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri ya kusimamia na kuliongoza Taifa hili kwa speed inayotakiwa. Nimshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa uteuzi wa Profesa Kitila Mkumbo, ninahakika akiungana na wenzake pale wanaweza kufanya kazi kubwa sana ya kusukuma nchi hii mbele pamoja na vijana wadogo wakina Luhemeja ambao sasa hivi wamepata nafasi ya kushughulikia matatizo ya maji katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ambayo wanaifanya Wizara ni kazi nzuri sana, lakini kuna baadhi ya mambo wanakutana hapa na upinzani mkubwa hasa wa takwimu zao, mimi nadhani wanatakiwa vilevile kufanya vile vile kazi ya RITA ya kusajili vizazi na vifo. Wanatakiwa wasajili visima vilivyokufa na vilivyo hai. Pengine kwenye orodha, wana orodha ya visima lakini vimeshapigwa radi siku nyingi vingine vimepigwa tetemeko wao kwenye vitabu wameandika kwamba visima vinatoa maji. Watajikuta wanapata matatizo makubwa bila sababu za msingi, sajilini takwimu za visima ambavyo havifanyi kazi na vinavyofanya kazi, mtapata kwa uhakika kwamba maji yapo kwa kiasi gani si kuleta tu kwamba kuna visima kadhaa na maeneo kadhaa yanapata maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata visima vya zamani ambavyo vimekufa Halmashauri hazina uwezo wa kuvifufua. Kuna baadhi ya maeneo walikuwa na maji sasa hivi hawana maji. Kwa mfano ukija kutazama kwenye Jimbo la Mtera kuna Kata kadhaa zinahangaika kupata maji. Kata ya Handali, ukienda kutembelea Idifu, ukienda kutembelea Mlowa Bwawani wote hawana maji lakini ukija hapa unakuta takwimu vijijini ni 72. Kwa hiyo, nina uhakika wakisajili visima vilivyo hai na vilivyokufa wanaweza wakaja na mahesabu ya uhakika. Lakini nchi hii tuigawe kwenye vipande, kuna baadhi ya maeneo yanasubiri muda mrefu sana kupata huduma hii, tujue tu kwamba tutapata lini, nayo tukijua hiyo inaweza kutusaidia. Tumeona kuna ongezeko kubwa sana la huduma za maji mijini tumekubali na sisi tunayaona lakini kuna baadhi ya maeneo hata wananchi waelewe tu kwamba mwaka gani basi hii huduma muhimu ya maji itawafikia vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Maji ni Wizara mtambuka sana, na nashangaa tunapoijadili Wizara hii halafu Wizara ya Fedha haina Waziri wala Naibu Waziri humu ndani ya Bunge, hii si sawa. Ndiyo maana Mheshimiwa Rais aliwaweka wawili mmoja akiwa hayupo mwingine yupo, hii ni dharau kubwa sana kwa Bunge lako Tukufu. Kwa hiyo, tungependa, tunapojadili Wizara muhimu kama hizi Mawaziri wa fedha wawepo, Bunge maana yake karibu ni Wizara tatu tu; ni kiti cha Spika, Waziri Mkuu na Waziri wa Fedha maana humu tunazungumzia hela sasa tukiwa tunazungumzia pesa wahusika wa fedha hawamo kidogo inatupa matatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna vitu hapa vinazungumzwa, jana kulikuwa na Mbunge mmoja alikuwa anaicheka Serikali na kuibeza kwanini Rais ameanza na ndege asianze na maji. Jamani, nataka leo nitoe somo kidogo hapa. Ndege ni sawa sawa na mkulima mwenye kilo moja ya mahindi ndani hana chakula na mvua zimeanza kunyesha, anatakiwa achague akaange ile kilo moja afe au apande apate mahindi mengi ili aweze kuishi? Mheshimiwa Rais alipoleta ndege ameleta biashara ili izalishe tupate hela za kutengeneza maji mengi zaidi, kwa hiyo, badala ya kumbeza tumuunge mkono,Waheshimiwa Wabunge tumuunge mkono Mheshimiwa Rais, nchi haiendeshwi kwa hapana.

Nataka niwambie, kwamba duniani kuna aina tatu za upinzani; uko uoinzani shinikizo wanashinikiza hoja, upo upinzani kioo na uko upinzani serious, huu wa Tanzania ni upinzani kioo. Kama hujachana wanakwambia hujachana kesi inaisha unaendelea na shughuli zako. Kwa hiyo, Serikali msiwe na wasiwasi tuendelee kujipanga kufanya kazi za maendeleo ya nchi hii, tusishughulike na upinzani kioo ambao kaa hawajachana wanakwambia umechana kasoro Zitto tu ndiyo anajitahidi na kwa sababu yuko peke yake. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi umeona walivyomuabisha Makamu Mwenyekiti wa Chama, amekuja Profesa Safari kugombea hapa amepewa kura 30 na hawa, hawamtaki Makamu Mwenyekiti wa Chama chao awe kiongozi, hawa ndiyo wanaweza kupewa Serikali, haiwezekani watu ambao hawaheshimiani, haiwezekani. Kwa hiyo, nakushukuru sana, mimi naunga mkono hoja, lakini nawaambia Serikali msihofu upinzani tufanye kazi. Ahsante.
Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua anazochukua kukabiliana na Upotevu wa Mapato ya Serikali katika Sekta ya Madini
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nakushukuru kwa kunipa dakika tatu za kuunga mkono Azimio la Bunge kwa ajili ya kumpongeza Rais kwa hatua madhubuti alizochukua kuhakikisha kwamba nchi yetu inanufaika kikamilifu na uchimbaji wa madini hapa nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli viongozi wote waliotangulia, naomba unyamaze usiniite, nitakutakana halafu nitaonekana sina maana. Eeh kwa sababu wewe unaniita jina la nini mimi mume wako niache nichangie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli viongozi wote waliotangulia waliunda Tume na ni kweli wakati ule sheria zetu zilikuwa zina wa-favour sana wawekezaji kwa wakati ule wa 1977, 1979, tulihitaji wawekezaji waje wawekeze kwenye sekta ya madini ambapo hawakuwepo wawekezaji wakubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tume zile zilizoundwa zilifanya kazi zake lakini Tume ya Mheshimiwa Magufuli kwa nini tunaipongeza, imefanya kazi na yeye mwenyewe ameenda mbele zaidi. Ameweka wazi ripoti za hizi Tume tena hadharani na kila mtu amezisikia tofauti na Tume zilizoundwa hapo kabla. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunampongeza Mheshimiwa Rais kwa hatua hii kubwa kwa sababu haiwezekani Taifa lisimpongeze kiongozi wake anapochukua hatua zinazoonekana kwa macho. Hapa nilisema na leo tumegawana, ukishindwa kupongeza, utapongeza wale wanaotuibia na imekuja hiyo wazi kabisa kwenye Bunge hili, umeona ripoti za Maprofesa, wataalam zinaitwa za upuuzi kwa sababu kuna watu wanaunga mkono upande mwingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sisi ambao tuko kwenye Bunge hili ambao tunaona kazi nzuri iliyofanywa na Rais, nataka niwaambie tu, siyo msemaji wake lakini nimeona kuna clip Mzee Lowassa naye kampongeza Rais. Sasa sijui hawa ambao wanakataa kumpongeza Rais wanaitoa wapi, kwa sababu hata Sumaye amempongeza Rais na ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA. Kwa hiyo, ndiyo maana tunasema Bunge zima lina wajibu wa kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa hatua kubwa alizozichukua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kurekebisha sheria, hivi kwenye Bunge la Bajeti hili, umeletwa Muswada wa kurekebisha sheria ya madini? Labda uelewa wangu mdogo, kwa sababu haiwezekani ulete Muswada sasa hivi turekebishe hizo sheria wakati tuko kwenye Bunge la Bajeti. Hapa tunachukua hatua ya kumpongeza Mheshimiwa Rais halafu tuitake Serikali ilete haraka Miswada ya kurekebisha.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mungu kupata nafasi hii ya kuchangia hoja za Wenyeviti wa Kamati walizoziwasilisha mbele yetu. Nami nitoe pole kwa familia ya Ndugu Kingunge Ngombale-Mwiru, Mwanasiasa Mkongwe wa nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini wakati mwingine Bunge zinapokuja hoja za msingi kama hizi tatu kwa pamoja zinaletwa na Kamati halafu sisi wenyewe Wabunge tunajinyima tena nafasi ya kuzichangia, kidogo hapo Bunge tunakuwa ni kama vile hatujitendei haki. Ukiangalia hoja hizi ni za Kamati zetu na wachangiaji ni sisi Wabunge, kuna sababu gani ya kujipa dakika saba wakati uamuzi ni wa Bunge lenyewe? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema maneno hayo, nataka kwa haraka haraka nichambue baadhi ya mambo machache, nikijikita zaidi kwenye hoja ya Kamati ya Viwanda na Biashara. Kuna tofauti kubwa kati ya kujenga uchumi wa viwanda na kujenga viwanda vyenyewe. Unapotaka kujenga uchumi wa viwanda hasa kwa sisi Wabunge wa Vijijini ni vyema viwanda hivyo vikawa na chain. Kama vinahusu kilimo vikajipanga katika mpango ambao utawafanya wakulima wanufaike moja kwa moja na uwepo wa viwanda hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, unapokuwa na viwanda vya mazao ya mifugo, halafu kukawa na viwanda vya mbolea ambavyo vinagusa moja kwa moja wakulima, kutaifanya nchi yetu ipate kodi ya kutosha kwa wakulima na wakulima wenyewe wakajiletea maendeleo makubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna tatizo kubwa sana la mwingiliano wa Taasisi za Serikali. Kwa mfano, ukiangalia kazi zinazofanywa na TFDA na TBS unaona ni kazi ileile moja, mfanyabiashara anaweza kupata certificate ya TFDA lakini TBS wakamkatalia. Kwa hiyo, unaweza kuona jinsi vyombo Serikali vinavyokuwa kikwazo cha kuhakikisha wanapata kodi ya kutosha na kupata maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wakati Kamati ya Viwanda na Biashara iliwahi kutembelewa na watu wa konyagi, wakaleta aina 32 za viroba na zikaonekana ni hatari Serikali ikazipiga marufuku, lakini leo viroba vinarudi tena kwa mlango wa uani, watu wanavipaki kwenye chupa, havina
stika za ubora za TBS, hazina stika za TRA wanakwepa kodi lakini vinauzwa. Wale wafanyabiashara ambao wanafuata utaratibu wanatozwa kodi kubwa wanajikuta wenzao wanauza kwa bei ya chini wao wanauza kwa bei ya juu, hawapati wateja, matokeo yake Serikali inashindwa kukusanya fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi mtu anayeuza kinywaji kikali kwenye chupa ya plastiki, haina nembo zozote za Serikali, nani atajua ubora wa kinywaji hicho? Matokeo yake bado tunaendelea kuwaangamiza vijana wetu kutokana na uwepo wa viroba kwa njia ya uani. Tunaomba leo Mheshimiwa Mwenyekiti utakapokuwa ukipitia tupate majibu ya kutosha kwenye jambo hili.

Mheshimiwa mwenyekiti, unajua Mungu akikupa kilema anakupa na mwendo wa kukitembelea, hawezi akakupa kilema akakunyima mwendo. Nataka niweke usahihi kidogo tu, ukitazama makusanyo ya kodi, walipokuwa wakikusanya Halmashauri, 2014/2015 walikusanya shilingi bilioni 18.9. Baada ya Serikali Kuu kuchukua na kuanza kukusanya wenyewe kupitia TRA kwa mara ya kwanza mwaka 2015/2016 walikusanya shilingi bilioni 28.2. Mwaka uliofuata, 2016/2017, Serikali walikusanya shilingi bilioni 34.9 maana yake kuna ongezeko hapo. Mwaka wa 2017/2018, kwa robo mwaka wamekusanya shilingi bilioni 16.6.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo langu mimi siyo kukusanya ila ni namna gani zinarudi kwenye Halmashauri ili ziweze kujitegemea. Ni kweli mmekusanya sana kuliko walipokuwa wanakusanya Halmashauri wenyewe lakini ni namna gani zinarudi ili ziweze kuleta maendeleo kwenye Halmashauri zenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo lingine kubwa linaloleta mgongano kati ya Kamati ya Bajeti na Wizara ya Fedha. Kwenye Halmashauri kunakuwa na bajeti ndogo za Halmashauri, wanapitisha vyanzo vyao vya ndani, wanapitisha namna ya kukusanya, inapokuja kwenye bajeti

kuu, vile vyanzo vinafutwa halafu hakuna namna ya kuvifidia. Kwa hiyo, tunajikuta tunakuwa na bajeti za Halmashauri ambazo zimefelishwa na kutokuwepo na vikao vya mwanzoni kati ya Kamati ya Bajeti na Wizara ya Fedha. Mkiweza kukutana mapema mkaondoa mkanganyiko huu, maana yake Halmashauri haziwezi kupanga bajeti ambazo huko mbele ya safari zitakuja kukataliwa na Serikali Kuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba kuwe kuna vikao vya kutazama bajeti vya mapema, tunashindwa nini? Kwa sababu leo hata zile tozo za kero ambazo tulizifuta, bado hazirudishwi kwenye Halmashauri. Kwa hiyo, Halmashauri zinashindwa kujiendesha, zinakosa mapato ya kutosha kuweza kuwaletea maendeleo wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, narudia kuwaomba sana, Wizara ya Viwanda na Biashara hebu tuleteeni orodha kati ya vile viwanda 130 na kitu vilivyobinafsishwa vingapi vinafanya kazi na vinafanya kazi kwa ufanisi gani? Leteni hapa orodha ili Waheshimiwa Wabunge tujue kumbe tangu tumeanza kuongelea viwanda kuna viwanda kadhaa vimeanza kufanya kazi na viwanda kadhaa bado vipo kwenye maandalizi ya kuhakikisha vinaendelea kufanya kazi. Vinginevyo tutakuwa tunapiga kelele hapa ya viwanda, viwanda kumbe hakuna kiwanda hata kimoja ambacho kinafanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie habari ya namna gani tunaweza kuzisaidia Halmashauri zetu. Halmashauri zinaweza kujiendesha zenyewe lakini pale ambapo vyanzo vyake vya makusanyo ya ndani vinaheshimiwa na Serikali Kuu. Tusiwe tunakuja tunafuta halafu baadaye tunazitaka zijiendeshe, hawataweza! Waheshimiwa Madiwani wamepitisha vizuri makusanyo yao ya ndani, wameyatungia sheria ndogo tunapokuja sisi kukataza huku juu maana yake tunawaweka katika mazingira magumu sana ya kuhakikisha wanapata mapato ya kuendelea kujiendesha wao wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, niombe sana Serikali na Wenyeviti wa Kamati watakapokuwa wanayapitia haya wayatilie maanani sana ili tuweze kusonga mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia hoja hiyo hapo juu hasa nijikite katika masuala ya miundombinu ya barabara zote za Jimbo la Mtera zilizopo TARURA. Mwaka huu 2018 mvua zimeharibu sana barabara zote, naomba Mheshimiwa Waziri atusaidie kupata fungu la matengenezo ya uhakika wa barabara hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri atupatie majibu ya uhakika kuhusu ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka barabara kuu ya kwenda Iringa pale Mlowo barabarani mpaka Mvumi Mission Hospital kama ambavyo Mheshimiwa Waziri aliwaahidi wananchi wa Jimbo la Mtera mwaka 2015. Naomba kujua ni lini barabara hiyo itajengwa? Ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maji
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara ya Maji. Na nimshukuru Mungu sana kwa ajili ya zawadi ya uhai pamoja na afya njema aliyonipatia.

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri Aweso, pamoja na Naibu Waziri, Mheshimiwa Eng. Maryprisca Mahundi na Katibu Mkuu, Eng. Sanga, kwa namna ambavyo Rais amewaamini kuendelea kuhudumu katika Wizara hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukitazama namna ambavyo Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amepanga uongozi kwenye Wizara hii utagundua kwamba ana matarajio makubwa sana ya safu yake hii kumletea ushindi katika mapambano ya kumtua ndoo mama kichwani. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa ajili ya kuwaamini hawa na kwa ajili ya msukumo anaoufanya ili wananchi waweze kupata maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Maji ni Wizara mtambuka, ni Wizara ambayo ikifanya vizuri inaweza kupunguza bajeti ya Wizara ya Afya kwa kiwango kikubwa sana. Kwasababu Wizara ya Afya wakati mwingine magonjwa mengi yaliyopo ni ya mlipuko yanayosababishwa na watu kukosa maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Wizara ya Maji mkijitahidi mkafikia tu malengo yenu, bajeti ya Wizara ya Afya itashuka chini badala ya kuendelea kupanda. Sio jambo zuri sana kuona kila mwaka Wizara ya Afya bajeti inapanda, maana yake ni kwamba matatizo ni mengi kuliko mafanikio.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi mingi ya Wizara ya Maji ni ya zamani, ni chakavu. Kwa hiyo, tunahitaji nguvu kubwa sana kuweza kuifufua hii miradi na kutengeneza mipya. Mheshimiwa Aweso, wakati mwingine nasema wazi; nchi yetu tusiijenge yote kwa mara moja. Kuna majimbo hayana barabara wala zahanati na maji hakuna, sasa tuwe tunaangalia basi, tufanye sensa ya kutosha tuone hivi maji yako mengi upande gani na upande gani unahitaji, unaweza kuona namna nzuri kabisa ya ku-solve tatizo la maji vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Aweso, sisi Wabunge wa vijijini tuna matatizo makubwa sana ya maji. Visima vyetu vimekuwa visima chakavu, lakini nenda uangalie, hata ongezeko la watu limeongezeka. Chukulia Jimbo la Mvumi; tuna Tarafa tatu za Makang’wa, Mvumi na Mkwayungu. Hizi tarafa zimekuwa miji mikubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninashauri tu hata kama tutakwenda kila mwaka, mwaka mmoja Tarafa ya Mvumi tujenge tanki kubwa la lita laki mbili, mwaka unafuata Tarafa ya Makang’wa tujenge tanki kubwa la lita laki mbili, mwaka unaofuata tumalizie Mkwayungu tanki kubwa la lita laki mbili. Tutakuwa tayari tumeondoa matatizo makubwa sana ya namna ya kupata maji. Kwasababu matanki yetu ni ya zamani mno, yana lita 40,000, lita 50,000; hazitoshelezi kutokana na ongezeko kubwa la watu katika maeneo haya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ambali ninataka kuishauri Wizara; hivi vile visima kumi vifuatilieni; vimefikia wapi? Maana mwanzoni tulikuwa na visima kumi, pesa zikatolewa visima vikachimbwa baadhi ya maeneo maji yakapatikana, vimefukiwa. Kwa hiyo, wananchi wanaambiwa tu kuna kisima pale lakini maji hakuna. Twende tuwaondolee matatizo kwa sababu kama visima vimechimbwa kusambaza maji kuna gharama gani?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna baadhi ya maeneo yana maji machungu, yana maji ya chumvi nyingi. Chukua maeneo kama Mlodaa, pale kila tukichimba kisima lazima tukute maji makali sana; Manzase; hivi kama tumeweza kutoa maji Ziwa Victoria tunashindwa nini kuchukua maji Mlowa barabarani kuyapeleka Mlodaa ambapo ni kilometa saba tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, na Mlowa barabarani ina maji mengi, tumechimba Ng’wenda tumekosa maji, tumekwenda hadi mita 150 tumekosa maji, tunashindwa nini kuchukua maji Lowa barabarani au Mlowa bwawani kuyapeleka Ng’wenda, mahali ambapo ni karibu? Tunashindwaje kuchimba maji katika Kata ya Nini kupeleka Ng’wenda; tunashindwaje kutoa maji katika Kata ya Mlowa kuyapeleka Manzase na barabara ni ileile moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, siyo lazima watu wanywe maji ya palepale, maji yatoke sehemu nyingine, yaende yahudumie wananchi sehemu nyingine ili wananchi wetu waweze kupata huduma bora ya maji safi na salama.


Mheshimiwa Naibu Spika, hatuna sababu kama sehemu hiyo tuna-drill tunakuta maji ya chumvi, tunaendelea kuchimba tena eneo lilelile; ni kupoteza resources. Tuangalie kijiji gani kiko Jirani kina maji safi na salama tuchimbe halafu tuyapeleke kwa wale wananchi waweze kupata maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Aweso, kwa hiyo, nakushukuru sana. Najua mmejipanga vizuri na mnafanya kazi vizuri na Wizara yako itakuwa Wizara ya kelele kwa sababu hakuna mbadala wa maji, maji ni ibada, maji ni afya, maji ni kila kitu. Kwa hiyo tutaendelea kukuhimiza lakini lengo letu ni kukushauri na sisi Wabunge tutakuunga mkono kuhakikisha kwamba unafanya kazi vizuri, wale wezi wa maji tunayo kazi ya kuhakikisha nao vilevile wanapatikana.

Mheshimiwa Naibu Spika, upotevu wa maji; tuweke utaratibu mzuri wa kutoa taarifa. Hivi bomba linavuja kutwa nzima na Watanzania wanapita eneo hilo; hii si sawa. Kwa hiyo endeleeni kuzitangaza namba zile za kutoa taarifa za uvujifu a maji, lakini vilevile raia wema watoe taarifa kwa wizi wa maji ili wananchi wote waweze kupata huduma hii ambayo wote tunaitarajia.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja; ahsante sana kwa kunisikiliza. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa uongozi wako na Mungu aendelee kukujalia kwa namna unavyotenda haki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana hapa kuna Waheshimiwa Wabunge walikuwa wanataka kubomoka lakini leo nataka kusema ukweli sasa, maana yake Tanzania ukweli watu hawaupendi, nami nataka leo niseme ukweli halafu nitatumia kauli ya mdogo wangu Mwenyekiti wa Vijana wa CCM Ndugu Kheri James kuwaomba wanipigie makofi kwa kusema ukweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI pamoja na Waziri mzoefu Kaka yangu Kapt. George Mkuchika. Nawapongeza sana Waheshimiwa Naibu Mawaziri wa TAMISEMI, Katibu Mkuu, Mhandisi Iyombe pamoja na timu yako mnafanya kazi nzuri. Wakati nikiwapongeza niwashukuru kwa kunipatia milioni 700 kwa ajili ya kujenga kituo cha afya pale Mpwayungu, milioni 400 kwa ajili ya ujenzi na 300 kwa ajili ya vifaa. Hii itasaidia sana wakazi wa Tarafa ya Mpwayungu kupata huduma za afya kwa urahisi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe tu watu wa TARURA watengeneze daraja lile la Manda limevunjika kwa mvua, hii inatupa shida sana ambulance kupita pale kuleta wagonjwa kwenye kituo cha afya cha Mpwayungu. Kama ambavyo Wabunge wengi wameeleza tunaomba bajeti ya TARURA na utendaji wao wa kazi uwe wazi ili Wabunge waweze kuasaidiana nao kuhakikisha kwamba maendeleo yanakwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka nilitolee ufafanuzi kabla sijaingia kwenye utawala bora, nizungumzie kuna baadhi ya Wabunge walikuwa na mashaka juu ya kugawana mali za Chama. Wengine wanafikiri kwamba mali ambazo walizijenga kabla hawajahama CCM wana haki nazo. Ndugu zangu hata Maaskofu hilo mkiwauliza watawasaidieni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiwa Muislam ukachangia matofali siku utakayokuwa Mkristo yale matofali ya Msikiti hayatakuhusu tena, wala huwezi kuyadai tena, ukiwa Mkristo ukachangia matofali ya kujenga Kanisa siku utakayohama kwenda kuwa Muislam matofali yale ukidai ni ugomvi. Kwa hiyo, ndugu zangu muelewe tu kwamba ile michango mliyoitoa wakati wa Chama kimoja kuijenga CCM mkitaka kufaidi rudini CCM ili muweze kufaidi vizuri. Hata kwenye harusi tu, michango ya harusi inaishia mlangoni huingii chumbani kwa maharusi kwa sababu ya mchango uliotoa. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema hayo sasa ninukuu tu kwenye Biblia huo mstari siukumbuki. Kuna mstari unasema toa kwanza boriti jichoni mwako ndipo uone vema kibanzi kilicho kwenye jicho la mwenzako. Wapinzani wa nchi hii, tuoeni kwanza boriti iliyomo kwenye macho yenu kabla hamjaona boriti iliyopo kwenye Serikali ya CCM. Nasema hivi kwa sababu nataka niingie sasa kwenye ukweli mtupu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma kwenye ripoti ya CAG ukurasa 266 nanukuu “mkopo ambao haukuthibitishwa mapokezi ndani ya Chama cha CHADEMA, mnamo tarehe 11 Aprili, Menejimenti ya CHADEMA (Mkopaji) iliingia makubaliano na mwanachama wake (Mkopeshaji) kuhusu kukopeshwa kiasi cha bilioni mbili.” Mnisikilize hapo, wanakopa hewa yaani deni hewa hilo. Mkopo waliingia makubaliano na mwanachama wake mkopeshaji kuhusu kukopeshwa shilingi bilioni mbili kwa shughuli za Chama. Hakuna nyaraka zinazoonesha kuwa kiasi cha mkopo walichokubaliana kilitolewa na kupokelewa na Chama husika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, CAG anaendelea tarehe 26 Agosti, kiasi cha shilingi milioni 866 kililipwa kwa mwanachama kwa niaba ya Chama kwa ajili ya mabango ya matangazo yaliyotolewa na kampuni ya MS Milestone International Company Limited nje ya deni hilo. Kiasi cha shilingi milioni 715 kililipwa kwa mwanachama kama marejesho ya fedha iliyokopwa kulipia ununuzi wa mabango bila ya kuambatanisha makubaliano ya kisheria. Wajinga ndio waliwao, mmeng’ang’ania maandamano mnaacha wenzenu wanapiga hela. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukaguzi wangu wa taarifa ya makusanyo ya Chama umebaini kiasi cha Sh. 2,302,305,500 kilikusanywa bila kuingizwa kwenye akaunti ya Wadhamini.” Angalia mambo hayo! Hazikupelekwa benki na matumizi yake hayakutolewa kwa ajili ya ukaguzi. Kutokupeleka makusanyo benki kunaonesha Chama kutokuwa na mfumo mzuri wa udhibiti wa fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, manunuzi yaliyofanyika, nimebaini kuwa CHADEMA kimefanya manunuzi ya bidhaa na huduma zenye thamani ya Sh.24,216,625,309 bila kufuata utaratibu.” Wajinga ndio waliwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wajinga ndio waliwao kuna Kwaya imeimba. Badala ya kushughulikia matatizo makubwa ya ufisadi ndani ya Chama chao wameng’ang’ana kila siku kukosoa Serikali, kukosoa Chama chenye Serikali. Ndugu zangu ndani ya Chama chenu kuna wizi na ubadhirifu mkubwa wa pesa, watu wanakula hela na ninyi mpo hapo! Madeni hewa yanatengenezwa, helcopter hewa zinakodiwa ninyi mmekaa hapa mnang’ang’ania CCM, toeni kwanza boriti kwenye macho yenu ndiyo muone vibanzi vilivyopo kwenye Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka Watanzania waelewe kwamba ufisadi mkubwa upo kwenye Chama kinacholalamikia ufisadi kumbe wao ndani hawajikagui. Kwa mara ya kwanza ipo humu na ndiyo maana nasema hakuna mtu atapinga kwa sababu haya ni mawe ya uhakika. Nipigieni makofi kwa ukweli ninaowapa. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ni ukweli mtupu, ndugu zangu mkienda mkajisimamia mkawa wakweli kwenye mambo yanayowagusa ninyi mtakuwa na haki ya kutukosoa, lakini kama ninyi wenyewe mnakumbatia ufisadi na wizi wa mabilioni ya pesa yanakusanywa kwa wanachama yanaingia kwenye Chama chenu, watu wanagawana wanakula, michango ya Wabunge inaliwa, mmekaa hapo mmenyamaza kazi yenu kukosoa hii! Nawaambia hamtakaa mfike popote. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana nimewaambia huu ni ukweli mchungu, nimesema natumia maneno ya Kheri Denice James kwamba ifike mahali kama tunataka kutengeneza Upinzani tutengeneze Upinzani wenye kusema kweli. Ukianza kumulika nyoka anzia kwenye miguu yako ndipo uanze kumulika kule. Niliwaambia hata juzi mna Chama kilichopokea ruzuku zaidi ya bilioni 10 hakina Ofisi hata moja wilayani, hakina ofisi hata moja mikoani, mnataka kufanana na Chama cha Zitto! (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mnazungumzia utawala bora nataka niwaambie, Mheshimiwa Zitto yupo peke yake anahangaika. Wapo Wapinzani Wazalendo, mimi nataka niseme kwenye Bunge hili mtakuja kunikumbuka, Mheshimiwa Zitto wewe ni hazina lakini badili Chama, njoo CCM uje ufanye kazi ya wananchi, kubaki huko unapoteza muda bure, tutakukosa mtu mzuri kwa sababu ya muda na huko unakopoteza muda. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwambie hivi tangu CHADEMA imesajiliwa, nazungumzia utawala bora, tangu CHADEMA imesajiliwa imezaa vyama viwili. SAU imevunjika kutoka CHADEMA, ACT imevunjika kutoka CHADEMA, sasa Chama hiki kingekuwa na Serikali si kingekuwa kimeleta vita kubwa sana ndani ya nchi? Kingeleta vita kubwa ndani ya nchi. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, tunapozungumzia utawala bora tuanze kujitazama sisi wanasiasa, tutazame miongozo na mienendo ya Viongozi wetu. Kuna Vyama hapa vina Mwenyekiti wa kudumu, kila unapokuja uchaguzi Mwenyekiti wa kudumu, Chama cha namna hiyo hakiwezi kujenga demokrasia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie Bunge lako Tukufu kuwaomba Waheshimiwa Wabunge, tukikosoa tuanze kujikosoa wenyewe ndipo tuende tuwakosoe watu wengine tunaotaka kuwakosoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hotuba hizi zote mbili na naunga mkono kwa asilimia mia moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na namshukuru Mungu kupata nafasi hii ya kuzungumzia taarifa mbili za Kamati. Nitaanza kuzungumzia taarifa inayohusiana na kilimo.

Mheshimiwa Spika, mimi ni Mbunge ninayetokana na wazazi maskini kabisa kwenye Taifa hili. Ukitaja watu maskini wa nchi hii unataja wakulima. Kama kweli tumedhamiria kuwainua wakulima basi ni lazima Serikali ijielekeze walau tuwe na kiwanda hata kimoja cha zana za kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni jambo la aibu sana panga tunaagiza kutoka nje, shoka tunaagiza kutoka nje, jembe tunaagiza kutoka nje, hivi huyu mkulima ambaye tunataka kumuinua tutamsaidiaje kwa karibu kama hatuna uzalishaji wa zana hizo ndani ya nchi? Kwa hiyo, ningeshauri kwamba walau tufufue kile kiwanda cha zana za kilimo Mbeya au tujenge kingine kipya ili mradi uzalishaji wa hizi zana za kilimo upatikane ndani ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini nimekuwa nikisema mara nyingi sana kuhusu zao la zabibu. Bahati mbaya sana kila majibu yanapotolewa wanasema zabibu iko katika Bodi ya Mazao Mchanganyiko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, zabibu ni zao la kipekee kwa hapa Tanzania linalimwa katika Mkoa wa Dodoma na halilimwi Dodoma yote. Unajua kuna watu hawaelewi wanafikiri Dodoma nzima ukipanda zabibu zinakubali, hapana, zabibu zinalimwa eneo kidogo la Kongwa, baadhi ya maeneo ya Dodoma Mjini, baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Chamwino na Wilaya ya Bahi. Kwa hiyo, unaweza kuona ni muhimu sana hata kutambuliwa tu yale maeneo ambayo zao hilo linastawi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo tumekuwa Makao Makuu ya Nchi unaweza kukuta ardhi ileile inayostawi zabibu watu wakaenda kulima na wakaweka vitu vingine tukajikuta hata maeneo tunayotegemea kuzalisha zabibu yakakosekana. Kwa hiyo, kutambua tu peke yake kwamba eneo hili linaweza kustawi zao hili na eneo hili linaweza kustawi zao hili ni jambo zuri na litasababisha wakulima wetu waweze kuinuka na kuendelea kupata uchumi mzuri. (Makofi)

T A A R I F A

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Juma Selemani Nkamia, mdogo wangu kwa siku mbili kwa kuzaliwa. Nikimtangulia mimi kwa siku mbili zinazofuata yeye, taarifa nimeipokea.

Mheshimiwa Spika, haya ndiyo mambo ambayo tunayaelekeza. Mwanzoni kila ukanda ulikuwa una zao lake la biashara, huku wanalima pamba, huku wanalima korosho, huku wanalima kahawa, ule utaratibu ulikuwa mzuri sana kwa sababu wananchi walikuwa wanaangalia ardhi na mazao yanayostawi kwenye ardhi yao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lazima tukubaliane dunia nzima ina vitu vikubwa viwili, kuna nuru na kuna giza. Kama unataka kufanya vizuri lazima uvitambue sio kwa sababu humu ndani tuna upande wa Chama Tawala na upande wa Upinzani ndiyo upinge kila kitu. Hivi Mheshimiwa Rais analetewa na Wizara juu ya mchakato wa kufuta shamba fulani ambalo limemilikiwa kwa miaka mingi, watu maskini wa eneo hilo wamekosa maeneo ya kulima, Rais anafuta, leo Mbunge unasimama kutetea kwamba Rais asifute. Mimi sielewi hapa tunatoa wapi hoja hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wabunge wanaokataa maskini wa nchi hii wasipewe ardhi hebu wajitambulishe kwa majina yao na majimbo yao ili wananchi wapate kuwafahamu. Tunaposema Rais anatetea wanyonge tunamaanisha na Mheshimiwa Rais hizi Wizara zote zilizotajwa katika hizi taarifa ni Wizara ambazo zinaweza kumsaidia sana katika vita hii ya uchumi. Maana tunapozungumzia vita hatuzungumzii ya kuuwana moja kwa moja kuna vita ya uchumi sasa, kilimo kikifanya vizuri, viwanda vikafanya vizuri, utalii ukafanya vizuri, maisha ya Watanzania hayatategemea tena wafadhili, tutakuwa huru hata kujitungia sheria zetu wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, juzijuzi mmeona umaskini mbaya sana, tunalazimishwa tukubaliane na sheria ambazo zinakiuka hata mila na desturi yetu kwa sababu tu tunasaidiwa. Mambo mengine hata ukiyatazama kwao hao walioendelea kidemokrasia hayapo.

Mheshimiwa Spika, juzi nilikuwa na-Google kama Mheshimiwa Musukuma rafiki yangu kuangalia tangu Uchaguzi Mkuu wa Marekani umepita Hillary Clinton hajafanya mkutano hata mmoja wa kushukuru wananchi lakini ndiyo haohao wa kwanza kusema sisi hatuna demokrasia. Mbona Marekani walioshindwa hawazunguki kufanya mikutano ili kuwashukuru wananchi? Haya mambo unayona kwetu tu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kitu kingine, Trump, Rais wa Marekani, hataki ushoga, hakuna mtu anamuuliza, hakuna mtu anampinga, watu wamenyamaza kimya, lakini sisi kwa sababu ya umaskini wetu kila kitu kibaya wanataka kutuletea. Kwa hiyo, Serikali ikijikita kuinua wakulima, kukuza sekta ya utalii tunaweza kupata pesa nyingi ambazo zitasababisha tupange maendeleo yetu wenyewe bila kufuatwafuatwa na mtu mwingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hivi leo hii Wabunge tunazungumzia umeme wa Stiegler’s Gorge wakati tayari saini zimeshawekwa, huu ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu sana. Saini zimeshawekwa, mikataba imeingiwa, halafu sisi tunataka kuonesha kwamba eti kuna tatizo, tatizo liko wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumeelimishwa…

SPIKA: Tena Mheshimiwa Lusinde na Spika nilialikwa nikashuhudia kwa niaba yenu wote. (Makofi)

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Kwa niaba ya Bunge hili. Maana popote anapoalikwa Spika anaalikwa kwa niaba ya Bunge. Kwa hiyo, Bunge lilishuhudia utiaji saini na ujenzi unaanza, tunaanza kuzungumzia eti inawezekana kuna matatizo, jamani tumetumwa au ni akili yetu sisi wenyewe? Mbona tunazungumza kama Bunge la Ujerumani hivi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nawashukuru sana Wizara ya Maliasili na Utalii mmeboresha mazingira. Jimboni kwangu kule tembo wameongezeka mpaka juzijuzi walikunywa pombe za wananchi. Kulikuwa na mnada pale tembo wawili wakakuta wananchi wangu wanakunywa, wananchi wakakimbia tembo wakanywa pombe, ilikuwa shughuli. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa sijawahi kushuhudia tembo akilewa balaa lake ni kubwa. Kwa hiyo, tunachokiomba walau Serikali sasa kupitia KDU itengeneze ulinzi wa kuzuia wanyama waharibifu ili wasiwafikie wananchi na kuchukua pombe yao. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru sana Mungu kwa kunipa nafasi ya kuchangia leo katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kunipa afya na kutuwezesha sisi Wabunge kuweza kukutana mahali hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge wengi wamempongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu na watendaji wote wanaofanya kazi kwenye ofisi yake na mimi nichukue fursa hii kukubaliana nao. Nampongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi kubwa anazozifanya za kiutendaji lakini tumeona yeye na watendaji wake wakuu wote wakitembea na kuzunguka taifa zima ili kuchagiza maendeleo kwenye nchi yetu, tunasema hongereni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, shukrani za pekee zimuendee Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Joseph Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya kuiongoza Serikali hii ya Awamu ya Tano ambayo imejielekeza kabisa kwenye kuondoa changamoto zilizokuwa zikiwakabili wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi punde kuna Mbunge ametoka kuchangia hapa akiisifu Serikali ya Awamu ya Nne kwa kazi kubwa ilizofanya. Nina hakika Wabunge wengine watakuja kuisifu Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi nzuri inazofanya kwa sababu siyo wote tutaona mara moja, wengine wataona baadaye. Kwa hiyo, nina uhakika hata haya yanayofanyika sasa hivi baadaye watakuja kuyaona na kuyapongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nisimame kama shuhuda kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mtera kuishukuru Serikali ya Awamu ya Tano imefanya kazi kubwa kutuletea pesa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Mpwayungu. Wametuletea Sh.1,500,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya pale Mlowa Barabarani njia ya kwenda Iringa. Vilevile upande wa maji wamefanya kazi kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona Prof. Kitilya Mkumbo akitembea hata yeye kuangalia miradi kadhaa ya maji na kuikamilisha pamoja na Waziri na Naibu Waziri wamefanya kazi kubwa sana kuhakikisha Watanzania wanaondokana na dhiki ya maji. Kwa hiyo, mimi kama Mbunge ninayeongoza wananchi ambao wamechanganyika maskini wengi kuliko pengine matajiri, nachukua fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa anayofanya kuhakikisha kwamba nchi yetu inapata maendeleo makubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuendelee kuomba mjielekeze zaidi kwenye kumaliza miradi ya maji ambayo haijakamilika. Vilevile kuanzisha visima vipya na kuna maeneo mengine visima vya zamani vimekauka tuweze kuvifufua ili akina mama wasipate adha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo niliamua wakati napewa nafasi hii kwamba nataka kusema na Waheshimiwa Wabunge wote kwa ujumla. Tumekuwa tukipokea misaada mingi sana, mingine kutoka nje lakini sisi wenyewe pengine Bunge hili lilishawahi lenyewe kujinyima fursa halafu likachukua pesa zake za Bunge tukaenda kununua madawati. Napongeza sana Bunge kwa uamuzi ule ambao tulijinyima tukasema tuchukue hizi pesa twende tukanunue madawati ya watoto wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema maneno haya? Nasema maneno haya kwa sababu tumepata misaada mingi sana ya kusaidia jamii yetu lakini sasa naomba Taifa hili hebu na sisi tujinyime jambo moja ili tuweze kutoa msaada mkubwa sana kwa nchi yetu. Jambo lenyewe ni hili, ukisoma kwenye ukurasa wa 7 utaona kuna mafanikio lakini ukienda kwenye hotuba ya Waziri Mkuu ukurasa wa 17 kuna habari za Tume ya Taifa ya Uchaguzi inategemea kuongeza vituo 858, hivi vituo vinavyoongezeka bado tunaongeza gharama kubwa kwa wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nini nachotaka kushauri? Tumeona uchaguzi mwingine tunaoufanya na wenzetu wamelalamika sana kwamba wakati mwingine tunaingia gharama kubwa bila sababu, naomba Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote hivi kwa nini mwakani tusifanye uchaguzi wa Diwani na Mbunge tu Rais tukaacha apite bila kupingwa? Kwa nini tusifanye hivyo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tutakuwa tumeokoa fedha nyingi wakati Rais anaapishwa tumkabidhi cheque ambayo Taifa hili limeokoa ili Rais aende akatumie hizo fedha kuondoa matatizo ya maji na barabara vijijini. Kuna faida gani kwenda kupoteza pesa chungu zima kwa uchaguzi wa Rais, Rais ambaye hana mpinzani? Hii ni kwa sababu tumeona hata mshindi wa pili aliyepata kura 6,000 ameunganishwa na 8,000. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ndugu zangu nataka niwashauri, naomba mitandao yote na wanazuoni wote hoja hii naiweka mezani tuangalie faida ambayo tunaipata na hasara zake tupime. Jamani sisi ni Wabunge tuliotokana na familia maskini, tusijisahau tunaongoza watu maskini; watu maskini wakati mwingine huwa wanajadili katika milo mitatu ambayo ni haki yake anaamua kukata milo miwili anakula mlo mmoja, sisi kwa nini tusile mlo mmoja? Tule mlo wa Udiwani na Ubunge, kwenye Urais tumuache Mzee Magufuli apite bila kupingwa. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi aliyoifanya Rais ni kubwa, Taifa hili sasa na lenyewe lijinyime kwenye upande huo badala ya kupoteza pesa bila faida tumkabidhi Mheshimiwa Rais pesa ambazo zilikuwa zimetengwa kwa ajili ya uchaguzi wake tumwambie Rais kamata cheque hii ondoa shida ya maji kwa Watanzania. Mshindi namba mbili Ulipo Tupo tayari tayari yupo kule kule na Walipo Tupo wamemfuata huko huko, hivi kweli kuna chama nchi hii kinaweza kutengeneza mgombea Urais kwa miezi tisa (9) akamshinda Magufuli jamani? Ukweli tuuseme, haiwezekani! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, badala ya kupoteza muda mimi nawakaribisha tuje tushindane kwenye Ubunge na Udiwani, kwenye nafasi ya Urais tumpe heshima huyu mtu amefanya kazi kubwa. Ameonyesha kwamba yupo tayari kuondoa changamoto za Watanzania, kusimamia pesa za Watanzania na kuhakikisha mambo yanakwenda.

WABUNGE FULANI: Katiba.

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Hiyo Katiba ni ya kwetu sasa tuangalie faida ya Katiba na umaskini wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua kuna Wabunge wengine humu wanapiga kelele Katiba, kwa sababu Majimbo wanayoongoza hayana watu maskini lakini sisi ambao tunaongoza watu maskini ukiwauliza, ndiyo maana nimesema tujadiliane, naomba tujadiliane hasara na faida ya kufanya huo uchaguzi kwa sababu kwa vyovyote vile hakuna mtu atakayeweza kusimama 2020. Mimi naweka wosia kwenye Bunge hili siyo tu akamshinda, akamtikisa Mzee Magufuli, hayupo! (Makofi)

(Hapa baadhi ya Waheshimiwa Wabunge waliongea bila utaratibu)

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa sababu hiyo hatuna sababu ya kutumia mabilioni ya pesa kwenda kupoteza muda na kitu ambacho tuna uhakika. Katiba ni yetu, matatizo na changamoto ni zetu, tupime kama Watanzania. Ndiyo maana nimesema naruhusu mjadala huu na naomba Wabunge mtulie nasema makubwa sana hapa, mnaweza mkapata matatizo wengine hapa. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumza na nchi, tuangalie kwa namna nchi yetu ilivyo, ufadhili tunaopokea, na sisi tutoe ufadhili kwa nchi yetu. Tutakumbukwa kwa kitendo hicho kuliko kwenda kupoteza pesa bila sababu yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Waziri Mkuu lakini nilikuwa nataka kuweka hoja hii mezani Watanzania waijadili waone faida na hasara zake halafu waamue kuniunga mkono au wasiunge mkono. Naunga mkono hoja hii asilimia mia. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana kunipa muda huu mfupi ili nichangie katika hii Wizara ya Maliasili na Utalii.

Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge wengi wamezungumza, wametoa pongezi zao nyingi sana kwa Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri na mimi bila kupoteza muda nawapongeza sana kwa kazi nzuri wanayofanya na kwa kweli mimi nawakaribisha Jimboni kwangu ili tuweze kutembelea vivutio vipya vya utalii. Kama Waziri hatakuwa na nafasi basi naweza kwenda na Naibu Waziri na kwa sababu kule barabara ni mbovu, wakati mwingine tunaweza tukalala huko huko kutokana na ubovu wa barabara. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama Wizara zitachukua ushauri japo nusu tu wa Waheshimiwa Wabunge, zitakuja na kitu kizuri sana. Wabunge wameshauri kwa ufasaha na kwa ufundi mkubwa sana. Wasiwasi wangu tusije kuwa tunatwanga maji kwenye kinu, wanayachukua hapa lakini hawaendi kuyafanyia kazi. Hebu tujifunze kufanyia kazi ushauri wa Waheshimiwa Wabunge. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukija kwenye vivutio vipya, tuna tatizo la kugundua na kuvivumbua vivutio vipya vya utalii. Hapa Dodoma Mjini, katikati ya Tanzania wameweka pale Jiwe na wameweka alama pale, hakuna shughuli zozote za utalii zinaendelea pale. Pale tungeweza kujenga hoteli, tungeweza kupika vyakula vya makabila yote ya Tanzania. Mtu akitembea hapa anaenda anatalii katikati ya nchi ya Tanzania, lakini hatuvumbui! Ukisikia jina la Dodoma kuna mahali tembo alizama hapa karibu na St. John, ndiyo Mgogo akasema tembo idodomela, ndiyo ikaanza Dodoma, Mzungu akashindwa kutamka. Hakuna shughuli zozote zinafanyika pale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nenda katika Jimbo la Kibakwe, hapo Pwaga, kuna ndege ambao dunia nzima hawapo wako kwa Mheshimiwa Simbachawene, tena Mheshimiwa Simbachawene ni rafiki mkubwa wa Waziri lakini hajawahi kumkaribisha akaangalie. Kwa hiyo, ningeshauri tuendelee kuvumbua vivutio vipya vya utalii. Tunajenga uwanja mkubwa wa ndege hapa Msalato. Hivi mtalii atashuka Msalato, aende Iringa kilometa 274 halafu ndiyo aende kuzitafuta tena kilometa 160 na kitu wakati tuna barabara kati hapa ambayo ni njia fupi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa barabara hii ukitoka hapa unaenda Mpunguzi, ukitoka Mpunguzi unaenda Mwitikila, ukitoka Mwitikila unaenda Nagulo, ukitoka Nagulo unaenda Uzi, ukitoka Uzi unaenda Manda, unavuka mto Kizigo tayari umeshaingia Ruaha National Park kwa kilometa 125 tu. Badala ya kutembea kilometa 300, ukikatiza hii njia ya kati unafika kwenye maeneo ya utalii kwa urahisi Zaidi, tuimarishe. Kwa hiyo, sio lazima watalii wazunguke mbali, kilometa nyingi wanaenda kutafuta wanyama wakati ukikatiza hapa katikati unafika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tuna vivutio vingi sana. Ukija kwenye jimbo langu mimi kuna mapango yako hapo Kata ya Ilolo. Ukitembea hapo unaenda unakuta mapango mazuri, watu huwa wanaenda pale wakati mwingine wanaomba na mvua inanyesha hapo hapo, hata kama jua ni kali. Kuna jiwe moja kubwa sana liko Mloda pale, nawakaribisha Wizara waende wakaangalie, kuna vivutio vingi, vingi vingi, vinaweza kutusaidia nchi hii kusonga mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna kitu kimoja nataka nishauri hapa. Suala sio kwamba wanyamapori wameongezeka kuvamia mashamba yetu, hapana. Sisi tunachoshauri kingine ni uharaka wa kuwafukuza. Mnyama anaingia, anashinda humo analala mpaka siku tatu. Hivi, tunasema eti oh! Hakuna silaha, hakuna watu, hawawahi mbona Bunge linawahi hapa Tanzania? Bunge halijawahi kuchelewa, saa tatu kamili limeanza. Mbona Bunge halichelewi? Kwa hiyo, Taasisi kubwa kama hii lazima tuipongeze, hakuna siku Bunge limechelewa hata dakika moja. Bunge ni saa tatu kamili kila siku na saa tatu kamili Bunge liko hewani. Mbona sisi tunawahi? Taasisi zingine za Serikali zinashindwa wapi?

Mheshimiwa Naibu Spika, tumewafundisha vijana ulinzi shirikishi. Hivi kwa nini wale vijana tuliowafundisha ulinzi shirikishi kwenye kila kijiji kama pale Handali wapo vijana wazuri sana. Manda kuna vijana wazuri sana. Ukienda Chiluhuru kuna vijana wazuri sana wamefundishwa na nyie. Kwa nini wale vijana wasipewe silaha ili wawafukuze wanyama wakifika? Wanawaaminije kuingia mpaka hadi kwenye hifadhi wawafukuze majangili lakini hawawaamini kwenye kulinda mali zao? Kila Kijiji kingeweza kununua silaha, sio kusema kwamba wanaua wanyama, wazitumie kufukuza wanyama kwa sababu wamewaelimisha wao na Askari walio nao ni wachache.

Mheshimiwa Naibu Spika, vijana wale ambao tumeshawafundisha, tuwafundishe vile vile kujilinda kwa sababu kujilinda ni haki ya mtu. Mbona jambazi akiingia ndani mtu anamuua jamani na wala hashtakiwi na mtu yeyote? Sasa tembo anaingiaje kwenye shamba la mtu anakula, anamaliza, anakula anamaliza tunakuja hapa tunajadili habari ya kifuta machozi, kifuta jasho, wakati tungesema vijiji vyote vinavyopakana na wanyamapori na ambavyo vimesajiliwa, kila kijiji kimiliki silaha kwa ajili ya kufukuza wanyama hatari wanapoingia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nimshukuru Mungu sana kwa kutupa uhai ili leo tuweze kuzungumza machache kuhusu Wizara ya Fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niwape pole sana vijana wa timu ya Mwadui kwa namna walivyoonewa jana na lile goli la offside, kwa kweli lile goli halikuwa goli, Yanga walibebwa sana, lakini Insha Allah tutawalipia tarehe 3 Mungu akipenda. Vijana wasilie, wanyamaze tutawalipia tarehe 3. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunampongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan kwa uteuzi wa Mheshimiwa Mwigulu Lameck Nchemba pamoja na Engineer Masauni Masauni kukaa kwenye Hazina Kuu ya Nchi kwenye Wizara ya Fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kitendo cha kuaminiwa tu na Mheshimiwa Rais, nasi hatuna mashaka na uelewa na uchapakazi wa Mheshimiwa Dkt. Mwigulu pamoja na Mheshimiwa Eng. Masauni, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha pamoja na watendaji wengine wote. Mimi ni miongoni mwa Wabunge wanaotoka kwenye familia masikini. Kitendo alichokifanya Mheshimiwa Rais cha kutupa Shule ya Sekondari kila jimbo, cha kutupa shilingi milioni 500 kila Jimbo, kimetugusa masikini wengi wa nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais amegusa nyoyo za watu masikini wa nchi hii kwa sababu maeneo anayoyagusa ni yale yatakayoinua sana uwezo wa watu masikini wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Shule moja ya Sekondari itazalisha watoto wengi sana kwenda kwenye ufaulu wa kati na kwenda kwenye kujitegemea na kupata ajira. Kwa hiyo, Mheshimiwa Rais amepanda mbegu njema kwenye mioyo yetu, tunamshukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wengine watasema tuna Shule za Sekondari kila Kata; kweli, chukulia mfano katika Kata yangu ya Mvumi Mission, watoto waliopo Darasa la Saba mwaka huu ambao ndio wanategemewa kwenda Kidato cha Kwanza mwakani wapo 450. Utawapeleka shule gani hata kama una shule? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kitendo cha Rais kutupa tu shule moja hii, popote tutakapoiweka itasaidia sana wakazi wa Jimbo la Mvumi kuweza kupata elimu bora na kuendelea, lakini watu hawajaelewa sawa sawa, hii shilingi milioni 500 ilizungumzwa vizuri sana na Mheshimiwa Mama Kilango pamoja na Waheshimiwa Wabunge wengine. Mwaka 2020 tulipata mvua nyingi sana. Mmvua zile ziliharibu sana barabara za vijijini. Sasa Mheshimiwa Rais kuliona hili na kutupatia hii fedha, sisi hatusemi kidogo. Asiyeshukuru kwa kidogo hata kwa kikubwa hawezi kushukuru. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa tendo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba tu wenzetu wa TARURA, zikatengenezwe barabara za kiwango cha Mheshimiwa Mama Samia. Tumemwona, mama hacheki katika mambo mabaya. Likitokea jambo ambalo halimfurahishi, hapo hapo anakula kichwa cha mtu. Kwa hiyo, tusije tukaanza kushuhudia maumivu. Tusifikiri ametoa tu kama zawadi, atataka baadaye aone kazi iliyofanywa kutokana na fedha hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba tuishauri Serikali kuendelea kutanua wigo wa walipa kodi. Hili jambo ni jema sana. Unajua tunawezaje kuwapata walipa kodi wapya? Kama tutaboresha kilimo chetu kwa nchi nzima, tutatengeneza wakulima wa chini kupanda kuwa wakulima wa kati na hivyo kilimo chao kuwa kilimo cha biashara. Hapo tutapata walipa kodi wapya tusiendelee na wale wale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine jipya, tumekuwa tukishauri sana Mheshimiwa Dkt. Mwigulu. Dodoma tukitengeneza bandari kavu hapa tutapunguza mafoleni yote kuelekea Dar es Salaam, mizigo mingi inayokwenda kanda ya ziwa inayokwenda nchi za Kongo, Burundi na Rwanda itatokea Dodoma badala ya kutokea Dar es Salaam. Kwa hiyo, tunashauri tu kwamba mkitengeneza bandari kavu hapa Dodoma, mtarahisisha sana uchumi wa hapa Dodoma pamoja na Kanda nzima ya Ziwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza sana Serikali kwa kupunguza kodi ya pikipiki, lakini kuja jambo wamelisahau pale. Siyo pikipiki pekee inayobeba abiria mmoja, hata taxi inabeba abiria mmoja, lakini bado faini yake ni shilingi 30,000. Vile vile taxi zimebanwa sana, ujio wa bodaboda pamoja na bajaji umeua kabisa madereva taxi wengi, hali zao ni mbaya. Sasa tukiwaacha na faini kuwa ile ile shilingi 30,000, kwani taxi inabeba watu wangapi jamani? Taxi siyo daladala, inabeba mtu mmoja anayekodi, akipigwa faini ni ile ile shilingi 30,000. Kwa hiyo, Waziri alitazame hilo nalo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu ina maeneo mengi ambayo yanategemewa kuzalisha. Tumesikia hapa watu wanazungumza habari ya biashara katika Soko Kuu la Kariakoo, kwamba imepooza. Ni kazi ya Serikali kwenda harmonize biashara pale, kwa sababu pale tulikuwa tunapokea wageni wengi. Nchi nyingi wamekuwa wakija Kariakoo pale wanalala kwenye hoteli zetu, wananunua bidhaa hapa kwetu. Sasa tuiangalie ile kodi ya wafanyabiashara, ikiweza kupunguzwa kufikia kiwango ambacho wafanyabiashara wengi watalipa, itasababisha Serikali ikusanye mapato ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi sina mashaka na Mchumi daraja la kwanza Mheshimiwa Dkt. Mwigulu pamoja na Engineer, hebu nendeni mkae mwangalie namna ya kulifanya lile soko lirudie ubora wake kama ambavyo lilikuwa Dubai ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, nimeona na nimpongeze sana kwa habari ya kuweka kodi kwenye michezo ya kubahatisha, hizi betting. Ushauri wangu Mheshimiwa Dkt. Mwigulu, kwanza niwapongeze sana Sports Pesa wamekuwa wakidhamini timu ya Simba, Yanga na Namungo. Taasisi nyingine nazo zichukue, tuweke walau hata sheria ya lazima, hawa wanaoendesha michezo hii nao wadhamini club nyingine ili hizi clubs ziweze kupata wadhamini, ziweze kucheza michezo ya kibiashara na baadaye kukuza mpira wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tunaona soko kubwa, tuna wachezaji wa nje hapa wanalipwa fedha nyingi sana na wachezaji wetu wa ndani viwango vyao vimeongezeka. Unaweza kuona katika ukanda huu wa East Africa sasa hivi hakuna forward kama John Raphael Boko. Sasa tukizalisha akina Boko wa kutosha, maana yake ni nini? Maana yake Tanzania nayo itauza wachezaji nje, tutanufaika na uchumi wa michezo.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Halafu mimi nikichangia huwa kengele inawahi. (Kicheko)

Mhehsimiwa Naibu Spika, kazi tuliyonayo nimesema kwanza ni kuhakikisha kwamba tunamuunga mkono Mheshimiwa Rais katika kazi njema anayoifanya katika nchi hii, lakini tuelewe kwamba Rais anaandika historia yake na kuna vitu vya tofauti huko mbele ya safari vitatokea ambavyo havikuwahi kutokea katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, kuna wengine hawalitazami, sisi tumekuwa tuna uchaguzi tofauti kati ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwenye chama chetu, uchaguzi unatangulia wa Zanzibar, halafu baadaye tunakuja Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mungu akimpa uhai, akaendelea mpaka miaka
10 ijayo Mheshimiwa Samia, atakutanisha Uchaguzi wa Zanzibar na Uchaguzi wa Jamhuri, vyote vitakutana pamoja chini ya uongozi wa Samia. Sasa tumuache huyu mama aandike historia hiyo, yaani atakuwa Mwenyekiti wa Chama
2030 anayetafuta Rais wa Zanzibar na wakati huo huo anatafuta Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hili ni jambo jipya kabisa halijawahi kutokea, lakini litatokea 2030. Kwa hiyo, hapa katikati mimi sioni kama kuna mtu yeyote katika nchi hii ambaye atasema anaweza kushindana na mama. Katika jambo gani? Maana mama anapiga hii mitano, anapiga mitano ya mwisho, halafu anaunganisha pande zote mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara ya Maji. Ninaomba nikupongeze sana kwa namna ambavyo, unajua watu wengi wanafikiri tunakupongeza kwa kuendesha Bunge, kwa namna unavyotuongoza sisi Wabunge ndani ya Bunge na nje ya Bunge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge wengi wameshazungumza, tumetoa pongezi na ahsante nyingi kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa namna ambavyo anamwaga pesa kwenye miradi mbalimbali, hususan kwenye miradi ya maji.

Mheshimiwa Spika, ukitazama hata namna ambavyo Mheshimiwa Rais anaipanga kiuongozi Wizara ya Maji unaona nia ya Rais ni kuongeza speed ya utendaji katika Wizara hiyo. Tumeona juzi hapa Mheshimiwa Rais amemteua Eng. Luhemeja kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji. Tunaona nia nzuri ya Rais ya kuifanya Wizara iwe imara katika utendaji. Waziri amekaa sawasawa, Naibu yuko sawa, sasa mnaongezewa nguvu, Katibu Mkuu amekuja ili mtoke pale alipoishia Eng. Sanga kwenda mbele kwa spidi zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wabunge wamepiga kelele sana kuhusu maji kwa sababu maji hayana mbadala. Hata wale ambao hawakupata nafasi ya kuzungumza bado ungewasimamisha wote wangetaka maji kwenye Majimbo yao. Kwa hiyo, tunamuomba sana Mheshimiwa Waziri kuigawanya rasilimali maji.

Mheshimiwa Spika, unajua tumemaliza sensa juzi. Sensa itupeleke kuona wingi wa watu na namna ya kujenga matenki makubwa, tuondoke tena kwenye yale matenki madogo ya lita 50,000, lita 60,000. Tuanze sasa kujenga lita 200,000 na kuendelea ili yaweze kusaidia kusukuma maji kwa wingi katika vijiji.

Mheshimiwa Spika, leo kuna miji imekua. Ukiangalia sasa hivi kwa mujibu wa sensa iliyopita Kijiji kama cha Mkwayungu katika Jimbo langu, kina watu 19,000, Mvumi Mission kuna watu 19,000, ukienda Mlowa kuna watu 18,000. Hapa huwezi kutengeneza tena tenki la lita 50,000 likatosha.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo rai yangu kwa Wizara, ikiwezekana tubadili sasa ujenzi wa matenki tuende tujenge matenki makubwa kwenye vijiji vyote ambayo mengine yatabaki kama reserve. Kama kijiji kina watu wachache, watakapoongezeka tenki tusijenge tena kwa sababu lipo la kutosheleza kusukuma maji kwa ajili ya kijiji hicho. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hapa Dodoma tunapongeza sana uongozi wa maji wa Mkoa wa Dodoma, wanajitahidi sana. Nanyi Wabunge ni mashahidi na wengi muda mrefu tuko hapa. Lakini tunaona bado maji hayatutoshi. Kulikuwa kuna mpango wa kuyachukua maji kutoka Mtera kuyaleta hapa Dodoma Mjini. Nataka kupata majibu ya Mheshimiwa Waziri mmefikia wapi? Kwa sababu maji yale yakichukuliwa kwenye Bwawa la Mtera kuyaleta hapa Dodoma yatanufaisha vijiji vyangu vingi kule njiani yatakakopita. Kwanza tutambue kwamba kuna vijiji kuanzia kwenye Jimbo la Kibakwe kwa Mheshimiwa Simbachawene, ukanda ule wote, vijiji vile vina maji ya chumvi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ukitupitishia maji kutoka Bwawa la Mtera maana yake Vijiji kuanzia Fufu, Isima kwa Mheshimiwa Simbachawene, Chipogoro kwa Mheshimiwa Simbachawene, ukija kwangu Manzase, ukija Mlodaa, Mlowa, Ng’wenda, wote watapata maji safi na salama. Kwa hiyo, naomba majibu utakaposimama Mheshimiwa Waziri utusaidie. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna vijiji tumefanya utafiti na kuchimba maji hayapatikani. Kijiji kama Chinoje tumechimba zaidi ya mara tatu maji yako mbali. Tumechimba maji kwenye Kijiji cha Ng’wenda, zaidi ya mara tano, maji hayapatikani. Ni nia yangu kuiomba Wizara tutoe maji kwenye vijiji jirani kupeleka huduma ya maji. Kumbe wale wananchi wahame wote, waende wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine ambalo nataka kuiomba Wizara ni ukamilishaji wa miradi mikubwa ambayo imeanza kujengwa mingi imesimama kwa sababu ya kukosa pesa. Pale Mvumi Mission tunao mradi wa milioni 988. Mkandarasi ameshajenga, ame-raise certificate Wizarani ya milioni 522 mpaka sasa hivi hamjampatia, matokeo yake mradi umesimama.

Mheshimiwa Spika, vilevile ukienda Handali kuna tatizo pale. Mkandarasi yule pale tangu mmempa ile kazi ameweka mabomba halafu ameingia mitini. Mtusaidie, hii miradi kadri inavyochelewa inaongeza gharama ya utendaji. Ukienda Mlowa Bwawani pale tulikuwa tunatengeneza tenki, mifuko 200 ya simenti imekauka. Kwa hiy,o tunapata gharama inakuwa kubwa inazidi ile ya mwanzo ambayo mlikuwa mmeikisia kwa ajili ya kujenga mradi.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Chamwino ndiyo Wilaya yenye Ikulu. Nikuombe sana Mheshimiwa Waziri utupatie gari, meneja wetu pale hana gari. Na ile Wilaya ndiyo Wilaya ya kimkakati wewe unajua na Mama anakaa pale. Mimi sitaki kuwasemea kwa Mama, hebu tupatieni gari jipya ili yule Meneja aweze kukimbia kwenye Majimbo yote mawili kwa wakati muafaka na aweze kutupatia maji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu bei ya maji. Wakati mwingine wanakurupuka tu watu wanajipangia bei ya maji. Maji siyo biashara, maji ni huduma. Kwa hiyo tumuombe Mheshimiwa Waziri, hebu elekeza mameneja wako hawa bei ya uhakika ya maji ni ipi, kwa sababu maji ni huduma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukienda huku unit ni shilingi 2,000, kwingine unit ni shilingi 2,500, kwingine unit ni shilingi 3,000, haiwezekani! Tuwe na bei moja maana maji ni ibada, maji ni uhai. Yakiwepo maji ya kutosha, safi na salama, yatapunguza hata bajeti ya baadhi ya Wizara, magonjwa ya maji haya kama typhoid yote yatatoweka tukiwa na maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia akina mama ukiwapunguzia muda wanaopotoza wa kutafuta maji, nikuhakikishie kwamba uchumi wa nchi yetu utakua kwa sababu akina mama ni jeshi kubwa, likishiriki kwenye maendeleo na kuacha kupoteza muda kwenye maji, mambo yetu yatakwenda kwa speed sana kwenye kuiendeleza nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninaomba sana Mheshimiwa Waziri wataalam wakuletee idadi ya visima vya maji vya zamani ambavyo mitambo yake ni chakavu ili muweze kutu-boost kama mlivyofanya kwenye elimu. Umesema kwenye hotuba yako kwamba tunataka tutengeneze utaratibu wa kuvuna maji. Hebu tuanze na Serikali, kwanza hapa Bungeni tunavuna maji kutoka wapi kuja hapa? Bunge hili linavuna maji kutoka wapi?

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo miundombinu ianzie Serikalini, majengo yote ya shule yawe na namna ya kuvuna maji. Kwenye Wizara zenu tukija tukute mifumo ya kuvuna maji, halafu wananchi ndiyo wataiga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini mkituambia tu sisi tutengeneze structures za kuvuna maji wakati tukienda kwenye Wizara zenu, kwa Mheshimiwa Jenista pale, hakuna mfumo wa kuvuna maji, ndiyo wanaanza kuweka juzi hapa. Tukienda kwa Mheshimiwa Doto pale, hakuna mfumo wa kuvuna maji, kwa Mheshimiwa Simbachawene hakuna, sasa tunajifunza wapi? Tuanzie kwenu, ninyi muanze kuonesha njia ili sisi tufuate. Majengo yote ya Serikali yatengenezewe mfumo wa kuvuna maji halafu sisi wananchi tutaiga. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, baada ya kuyasema hayo, naunga mkono hoja, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara hii. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na nimshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kutupa afya. Mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Miundombinu, kwa hiyo, kwa kuwa, ni Mjumbe wa Kamati ya Miundombinu, la kwanza kabisa niunge mkono hoja ya Wizara hii ya Ujenzi na Uchukuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukipita nje hapo unaona limeandikwa Bunge la Tanzania, kwa hiyo, Wabunge kutoka majimbo mbalimbali tukiingia humu tunakuwa Wabunge wa Taifa. Serikali inaposhauriwa na Waheshimiwa Wabunge ichukulie kwamba, Bunge linaishauri Serikali ili kuweza kuleta maendeleo ya wananchi wa Tanzania kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, michango mingi imezungumzwa na Waheshimiwa Wabunge hapa, wamezungumza kwa kishindo sana kuhusu barabara, lakini kwa kuwa na mimi ni mmoja wa Wabunge wa Taifa, nataka nianze na wastaafu wa ATCL. Kuna watu wameshafariki hawajalipwa pesa zao, kuna watu wako kitandani hawajalipwa pesa zao, kuna watu wana mazingira magumu, Mheshimiwa Waziri atakaposimama hapa atupatie majibu hawa wastaafu watalipwa lini? Maana deni lao lilishafanyiwa uhakiki, upembuzi yakinifu ulishafanyika kwa hiyo, tupate majibu kwamba, lini watalipwa pesa zao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo la pili, nataka nizungumzie Barabara ya Ntyuka Junction - Mvumi Makulu - Mvumi Mission - Handali kwenda Kikombo. Barabara hii ina wakandarasi wawili, kuna mkandarasi ameanzia mjini na mwingine ameanzia Kikombo. Nataka Mheshimiwa Waziri anihakikishie kwamba, hawa wakandarasi wanakwenda kutuacha sisi kama kisiwa au wanaenda kumaliza kazi ya kutuunganisha Makao Makuu ya Jimbo la Mvumi pamoja na Mji wa Dodoma na Mji wa Chamwino wa Kiserikali? Majibu hayo yatakuwa majibu mujarabu sana kwa ajili ya wananchi wa Jimbo la Mvumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo nataka kulizungumzia hapa, kwa suala la kipande maana hatuzungumzi kubinafsisha bandari yote, tunazungumza kipande ambacho walikuwa wanafanya kazi TICTS. Mimi huwa nafananisha na mtu amenunua lori lake, amenunua semi, matairi yameisha, propeller imekatika, huna uwezo umeli-park nje, sasa kazi yako ni kuonesha wajukuu gari la kwangu hili, lakini wajukuu hawana chakula, wamefukuzwa ada, wewe kazi yako kuonesha lile gari bovu, gari hili langu bwana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunachofanya hapa, tunaiomba Serikali itafute mwekezaji wa kuja kutia matairi mapya, kununua propeller jipya, ili mtoto wetu sisi awe tingo, wakusanye pesa, maisha yaendelee. Kwa hiyo, eneo hilo tunaomba Serikali ikatafute mwekezaji mwenye uwezo mkubwa, lakini wakati wakitafuta mwekezaji mwenye uwezo wahakikishe jambo la kwanza wanalinda ajira za Watanzania walioko katika eneo lile. Tusije tukaanza tena kuathirika, watoto wetu wakafukuzwa kazi, hapana, tunataka mwendo mkubwa zaidi kutoka pale walipoishia TICTS kwenda mbele, ili tuweze kujiletea maendeleo ya Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukishabinafsisha bandari katika kipande hicho kidogo tutapata tija kutoka makusanyo tunayokusanya sasa yataongezeka zaidi, lakini na uharaka. Juzi tumeona wafanyabiashara namna ambavyo wamelalamikia suala la uharaka, tunaambiwa meli moja kila siku moja tunayoichelewesha tunalazimika kuilipa Dola 25,000. Sasa hebu niambie na pale kuna meli kibao zinasubiri ziko foleni, tuweke mwekezaji ambaye atatuondoa kwenye deni lile, tuweke mwekezaji ambaye speed yake ya kutoa ma-container itakuwa kubwa ili kuondosha ile gharama ambayo tunaipata pale.

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa Mheshimiwa Lusinde, Taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Songe.

TAARIFA

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimpe Taarifa Mchangiaji kwamba, zile gharama ambazo anazisema za ucheleweshaji kwa siku dola 25,000, mwisho wa siku analipa mlaji wa mwisho. Kwa hiyo, tunaongeza gharama kwa vitu vyetu bila sababu ya msingi.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Lusinde, Taarifa unaipokea?

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea maana inatoka kwa Mbunge kijana kabisa, mtu smart, nawezaje kuikataa Taarifa ya kijana wangu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa yake ni njema, yote hayo ndio tunayoyazungumza sisi kama Wabunge, kuishauri Serikali kwamba, itupunguzie hizo gharama kwa sababu, gharama mwisho wa siku zinakuja kwa anayetumia. Unaweza kuona hata bidhaa hizo ambazo zilitakiwa ziuzwe hapa kwa bei ya chini zaidi zinauzwa bei ya chini Zambia, zinauzwa bei ya chini Kongo, halafu zinaturudia tena sisi hapa. Kwa hiyo, soko letu linakuwa gumu, lakini tukiweza kuboresha hiyo, bidhaa zetu zitakuwa za bei ya chini na hapo wageni wengi watakuja kununua hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo nataka nilizungumze. Namshukuru sana Mheshimiwa Rais ametupatia pesa milioni 500 kujenga Daraja la Mloa Barabarani kuunganisha na Makang’wa na ile ni barabara ya lami ambayo baadaye inakuja kujengwa kuja tena kuunganisha Mvumi. Vilevile connection ya watalii tunapata uwanja mkubwa wa ndege hapa Dodoma Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huu uwanja utakuwa na faida kama tutafungua barabara mpya kutoka hapa Dodoma Mjini, kupitia Nagwelo, kwenda Huzi, kwenda Manda, kwenda Ilangali, iingie ndani ya hifadhi kwa njia ya mkato. Badala ya watalii kuzunguka kupita Iringa watakuwa wanakatiza hapa tu taratibu wameshaingia kwenye Ruaha Game Reserve na baadaye wanaingia kwenye National Park ya Ruaha kwa ajili ya kuona wanyama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mambo ya barabara yamezungumzwa kwa umakini. Kuna barabara ambazo zinajengwa Dodoma za mzunguko, lakini barabara nyingine za mzunguko ambazo Wizara izifikirie ni Barabara ya Mpwapwa inayotokea Kibakwe kwa Mheshimiwa Simbachawene. Hii barabara ni ya muhimu sana, badala ya mtu akitoka Iringa kuja moja kwa moja anaweza kuingilia pale Kibakwe akaja kuunganisha Kongwa kwa Mheshimiwa Mzee Ndugai, tayari tumepata barabara nyingine ya lami inayotokea Kiteto, moja kwa moja anakwenda Arusha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni muhimu sana ujenzi wa Dodoma ukatuondolea adha ambazo wanapata sasa hivi Dar-es-Salaam. Tunapozungumza jiji tusiseme tu Dar-es-Salaam maji yakijaa kuna shida, hata Dodoma mvua ikinyesha kuna shida. Nje ya Bunge hapa kunakuwa na foleni kubwa kabisa. Kwa hiyo, tuangalie majiji yote, modal ya Dar-es-Salaam ya kuondoa matatizo ya mvua hiyo hiyo itumike kwa Dar-es-Salaam, Arusha, Mwanza, Mbeya na Dodoma, tusiseme leo tunazungumzia Dar-es-Salaam halafu kesho Dodoma inapata shida, tunaanza kusema, aah, na Dodoma, hapana. Wasomi wetu lazima waiangalie sasa nchi namna inavyokuwa na namna ya kuondoa misongamano ya magari pamoja na maji mvua ikinyesha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kama nilivyosema. Sina shida na Mheshimiwa Waziri pamoja na timu yake. Sina shida na watendaji wote wa taasisi zake wamejipanga vizuri, ni matarajio yetu kwamba, watakwenda kwa kasi zaidi kuweza kuondoa matatizo yanayolikabili Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii nami nichangie katika Bajeti hii ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi. Awali ya yote niunge mkono hoja ya bajeti hii kwamba tuipitishe.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile leo naweza nikawa siyo katika kiwango kikubwa sana kwa sababu leo mimi ni zamu yangu ya kuhudumu katika Kanisa letu la hapa Bungeni. Kwa hiyo, Roho wa Bwana ameniatamia tangu asubuhi. Sasa naomba niwakaribishe baadaye saa saba kwenye Ibada hapo Basement, kwa sababu watu watakuwa wengi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiitazama Sura ya Viongozi wa Wizara hii unaweza kuona namna ambavyo Mheshimiwa Rais aliteua watu watulivu. Ukimtazama Waziri, tazama wasaidizi wake, Katibu Mkuu, unaweza kuona nini Rais anataka kwenye Wizara hii. Anataka umakini, anataka utulivu, nami nitakuwa Mbunge wa ajabu sana kuwaondolea utulivu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunawapongeza sana na tunawaunga mkono, lakini tunataka wazidishe zaidi kusimamia taasisi ambazo ziko chini yao. Ukitazama taasisi ambazo ziko chini yao nazo ni kubwa. Unaweza kuona bandari, Mkurugenzi wa Bandari tunampongeza sana Ndugu yangu Erick Hamisi, pia Masanja Kadogosa tunampongeza kwa kazi nzuri. Hata ule wizi wa kijinga jinga ulikuwa pale wa kuibaiba sijui redio za magari bandarini siku hizi ni hadithi. Kwa hiyo, unaweza ukaona namna ambavyo jamaa wako serious.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na Mkurugenzi wa ATCL tunampongeza sana Eng.Matinde, lakini yeye kwa kweli amelemewa sana na madeni. Mimi nilikuwa nashauri Serikali ingeyachukua haya madeni, tungeweza kuona ufanisi wa ATCL.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikiwa nje hapo wakati naingia nimepewa message na mama mmoja mtu mzima sana, aitwa Sauda Fundi, unajua mimi ni Mbunge wa Taifa, siyo wa Jimbo peke yake; huyu mama amestaafu kazi mwaka 2015, amefanya kazi miaka 32, mpaka sasa hivi hajalipwa mafao yake. Kwa hiyo, mwangalie wastaafu wa ATCL, wanapata taabu sana, ni watu wazima, ukimwona huyo Bi. Mkubwa yuko hapo nje, hebu angalieni maslahi yao ili nao waweze kuishi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapozungumza habari ya barabara, Wabunge wanajitahidi sana kuzungumza pengine thamani ya barabara inayoelekea sehemu fulani, lakini ukweli ukimsikiliza Hayati Mwalimu Nyerere, namnukuu, anasema: “Kwa kuwa sisi ni viongozi wa watu, basi isiwepo shida yoyote ya watu tunayoweza kusema shida hiyo haituhusu.” Yaani tunapotaja barabara, ni barabara kwenda kwa watu, kwenda kwa wananchi, hakuna barabara ambayo siyo muhimu. Barabara zote zinazoenda kwa wananchi ni za muhimu. Kinachotofautiana hapa ni ufundi tu wa namna ya kusema Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tuiombe Serikali iongeze kasi ya kutafuta fedha ya kujenga barabara za lami kwenda kwa Watanzania kama Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi inavyosema. Kwa mfano, chukulia barabara ya Dodoma Mjini – Ntyuka - Mvumi Makulu - Mvumi Mission inakuja kutokea Handali, inakuja kutokea Kikombo Makao Makuu ya Jeshi, inaunganisha na Ikulu. Hii barabara imezungumzwa sana na mwaka huu tumeiweka kwenye Ilani ya Uchaguzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Wizara hii lazima iwe na vipaumbele. Mwanzo nimesema kuna barabara za service na za investment. Kwa sasa hivi zianze barabara za investment, hasa ukanda wa mwambao wa Ziwa Tanganyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeitaja Bandari ya Kabwe. Bandari ya Kabwe ndio inakuja kubeba uchumi wa Bonde la Rukwa kwa Mheshimiwa Geofrey Pinda, Mkoa wa Rukwa, kupeleka soko Congo. Bandari zote zimejengwa kwa lengo la kufanya fursa ya uwekezaji kwa nchi jirani Rwanda, Burundi, Zambia na Congo. Kwa hiyo, namshauri Mheshimiwa Waziri na Wizara nzima ije na mpango mkakati wa barabara zitakazojengwa na TANROADS. Kupitia Wizara barabara zijengwe kwa ajili ya kuelekea ukanda wa Ziwa Tanganyika ambako ndio kuna uchumi, kwa hiyo, maziwa yote mawili tutakuwa tunalisha Congo kutokana na juhudi za Mheshimiwa Rais za kufungua fursa kupitia diplomasia ya uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa wa Mwaka 2018
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru sana Mungu kupata nafasi hii, ya kutoa mchango kwa ajili ya Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa. Nikushukuru kwa sababu nilikuwa miongoni mwa wajumbe wa hiyo Kamati ambayo walichakatachakata kidogo na ndio maana unaona hata namna yangu ya kuzungumza sasa ni ya Kisheria zaidi kuliko ambavyo siku zote huwa nazungumza kwa verse za kisiasa zaidi. Kwa hiyo, leo nitajikita kwenye kuongea kwa Kisheria na kushawishi Wajumbe, Waheshimiwa Wabunge, waiunge mkono hoja hii kwa ufasaha wake. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru sana Serikali kwa kuleta Muswada huu kwa wakati huu muafaka kabisa, Muswada umelenga kuviimarisha zaidi Vyama vya Siasa, kutoka kwenye vingine kuwa Vyama shinikisho kuwa Vyama vinavyotetea hoja ndogondogo na kwenda kuwa Vyama vya Kisiasa kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu, tunaishukuru sana Serikali kwa kuleta Muswada huu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ujio wa Muswada huu, na namna ambavyo tulisaidiana sana na Wanasheria kama Kaka yangu Mheshimiwa Ally Saleh alikuwepo hapo, walikuja wakina Mheshimiwa Zitto Kabwe na wote tulitoka mle tukiwa tumekubaliana kwamba Muswada huu sasa uende kama ulivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa nini nasema hivi, kuna vipengele hapa ukiondoa kimoja unaharibu maudhui yote ya Muswada mzima, kwa hiyo, ndio maana tunasema Muswada huu upite kama ulivyo kwa sababu vipengele vinabebana na kuleta maana kulingana na umuhimu wa Muswada. Na hii maana yake nini? Wanasiasa Watanzania sasa tukomae, tufahamu kwamba nchi hii ina Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wazee wetu wametetea uhuru wa nchi hii na Sheria peke yake zinatungwa ndani ya Bunge, sio kwenye korido za Mabalozi tusiende kuwapotezea muda Waheshimiwa Mabalozi tukafikiri labda kwenye korido zao ndio zinatungwa Sheria, hapana, Sheria ya nchi hii inatungwa ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilitaka niwakumbushe tu, maana kuna wengine mpaka viatu vilishaisha soli kila siku Ubalozi huu, Ubalozi huu kuzungumzia Muswada huu. Huu Muswada sasa unataka Vyama Misaada yote ambavyo Vyama vitapata, Serikali ijue Misaada hii ina lenga kuimarisha nini kwenye Chama hiki. Maana yake nini? maana yake Muswada huu sasa unakiimarisha Chama, unajua anayetunza mara nyingi kwenye ngoma ndio anachagua wimbo, sasa ukiacha Vyama vipewe pesa, bila Serikali kujua maana yake wale wanaotoa pesa ndio watachagua nyimbo za kuimbwa na hivyo Vyama, Muswada huu unakataa hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Muswada huu unavitaka Vyama kutambua nembo za Kitaifa, hivi kuna ubaya gani? Waheshimiwa, utambue Mwenge wa Uhuru, utambue Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, huu Muswada watu wanauzungumzia juu juu hawajaingia ndani, huu Muswada unakwenda kuviimarisha Vyama vya Siasa Tanzania, kuzungumzia mambo ya msingi ya Kitaifa. Ndio maana nimesema vipengele vyake vyote vilivyomo humu vipitishwe kama vilivyo, Muswada huu unakwenda kumpa nguvu Msajili sasa, Msajii alikuwa akihudhuria Mikutano Mikuu ya Vyama vya Siasa kama mwalikwa tu, lakini Sheria haimtambui. Sasa anahudhuria na kusimamia demokrasia kuona inafanyika ndani ya Vyama hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajabu sana, Watu wanasema oooohh! Muswada huu unampa Mamlaka makubwa Msajili ya kumbana Mwanachama mmoja mmoja, jamani, kama Shirikisho la Mpira tu Duniani linaweza, mpira una adhabu zake, una kadi ya njano, una kadi nyekundu lakini mpira huo huo, unakufungiwa maisha, kwa hiyo shabiki ambaye atakuwa anakiuka mambo yaliyowekwa kwa ajili ya kuhakikisha mchezo wa mpira wa mguu unafanyika salama, sasa itakuwa sembuse kwenye Chama cha Siasa! Chama cha Siasa lazima kiwe na Sheria ambayo inawatazama Wanachama, na sasa Watu wajue uhuni tena kwenye kufanya mambo ya siasa haupo, sasa tufanye kwa ukomavu huku tukijua kwamba kuna Sheria inayo tu-guide kuhakikisha kwamba tunatekeleza mambo haya kwa kufuata utaratibu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka nishukuru sana, kwa namna ambavyo Muswada umeletwa na namna ambavyo vipengele muhimu vimewekwa kama ulinzi na usalama, Watu wanapotosha wanafikiri Muswada huu unakataza Mtu kulindwa, hapana mlinzi wa kwako binafsi wa kumuajiri kutoka group four ukamlipa Mshahara kitambulisho kikapelekwa kwenye Wizara ya Kazi kwamba nimemuajiri mlinzi Muswada haukatazi, haukatazi, hakuna mahali Muswada huu unakataza mlinzi binafsi, tusipotoshe, huu Muswada unakataza vikundi vya Kijeshi vya Ulinzi, ambavyo vilikuwa vinapewa mafunzo porini tunavijua kwa hiyo tunasema Muswada huu haujamkataza Mtanzania kulindwa. Naomba utulie, tulia, mama watoto tulia, tulia, mimi nakujua, huyu ni mama watoto wangu kwa hiyo achana naye. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, eehe! Jamani mambo ya mapenzi hayaingii kwenye Chama jamani.

Mheshimiwa Spika, ulinzi binafsi mtu akatazwi, anaruhusiwa kujilinda, yeye mwenyewe kwa kuajiri mlinzi lakini sio chama, kianzishe kundi la vijana kiliite Kundi la ulinzi hiyo Muswada huu umekataza, kwa hiyo mimi nimesimama hapa kusema mambo ya msingi kwanza Muswada huu umetambua nembo za Kitaifa, Mwenge wa Uhuru pamoja na Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilitaka Muswada huu uspite bila kusema, kwamba Sheria sasa zinatungwa, sisi ni nchi huru jamani na wote diplomasia waliokuwa kwenye nchi yetu watuheshimu kwamba hili ni Taifa huru linajifanyia mambo yake lenyewe na hatujawahi kuingilia nchi yoyote kwenye kutunga Sheria za nchi zao, nilitaka niseme kwa sababu
wenyewe wapo, wasikie kwamba Mbunge amesisitiza watuachie uhuru wetu na sisi tutaheshimu uhuru wa nchi zao, na Waheshimiwa Wabunge wajue Sheria zinatungwa ndani ya Bunge sio kwa Mabalozi, hayo nilitaka yaeleweke vizuri halafu mambo ya vifungu sasa nawaachia Wanasheria asante sana.

Mheshimiwa Spika, naunga Mkono hoja. (Makofi/ Kicheko)