Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Additional Questions to the Prime Minister from Hon. Joseph George Kakunda (1 total)

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba nimwulize Mheshimiwa Waziri Mkuu, ni lini atakuwa tayari kutembea Tabora ili nako ajionee migogoro hasa katika Wilaya ya Sikonge?
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu kwamba, nimeamua kufanya ziara katika Mkoa wa Tabora baada tu ya Bunge hili kwa sababu mbili. Moja, kufanya hilo, lakini pili nakuja kuongea na wadau wa zao la tumbaku; nakuja kufanya mapitio ya zao la tumbaku ambalo limekuwa kero kubwa. Nakuja kuongea na wakulima wenyewe, Viongozi wa Vyama vyao vya Msingi, kuongea na wafanyabiashara na wenye viwanda ili tubaini tatizo liko wapi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, mkakati ambao tumeufanya kwenye zao la korosho, tunahamia kwenye tumbaku na baadaye tunakwenda kwenye pamba, tutakwenda na kwenye kahawa vile vile, kwa lengo la kuwapa tija wananchi waone kabisa kwamba sasa ni wakati wao wa kupata tija ya mazao wanayoyalima ili waweze kupata manufaa.