Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Suleiman Masoud Nchambi (9 total)

MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, wabheja sana. Kwa kuwa Jimbo la Kishapu halikupata mgao wa magari mapya ya polisi katika awamu hii na Jimbo hili lenye watu sharp na askari wanaofanya kazi zao kwa u-sharp, lina magari mawili mabovu yenye umri wa zaidi ya miaka mitano.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, nilipata ahadi kuwa mwezi wa pili tutapata magari mapya ya polisi, uko tayari kunihakikishia Jimbo sharp litapata magari mapya ili Wananchi waweze kupata huduma hasa za kiusalama wanapohitaji kuliko hivi sasa polisi wangu wa Kishapu wanavyohangaika? Wabheja
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Nchambi kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano ya hapa kazi tu huwa haina desturi za kutoa ahadi ambazo hazitekelezeki. Kwa hiyo, kama ni ahadi ambayo imetolewa, basi nitaifuatilia hiyo ahadi yenyewe halafu tuone hatua zilizofikiwa zimefikiwaje na kama imekwama imekwama vipi, halafu tutaonana mimi na yeye tuone ni jinsi gani ya kufanya.
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, wabheja sana. kwa niaba ya wananchi sharp wa Jimbo Sharp, namwomba Mheshimiwa Naibu Waziri, Jimbo la Kishapu limekamilisha ujenzi wa hospitali ya kisasa kabisa ya Wilaya, tena ni hospitali ya mfano na kujivunia ambayo Serikali ya Chama cha Mapinduzi, imeijenga kwa kushirikiana na wananchi wa Jimbo la Kishapu pamoja na Wawekezaji.
Kwa kuwa, hospitali hiyo ina upungufu mchache, imekamilika takribani kwa asilima 78 na upungufu huo katika swali la nyongeza hauwezi kunoga kuueleza, nimwombe Naibu Waziri, yuko tayari kufuatana na Mbunge sharp, kwenda kwa wananchi sharp, kuiona hospitali sharp, inayotoa huduma sharp sharp, ili mambo yaendelee kuwa sharp wakati wowote atakapotamka kwamba yuko tayari? Wabheja Sana.
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa majibu sharp, kwa Mbunge sharp wa wananchi sharp wa Kishapu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa na mimi ni Naibu Waziri sharp, namuahidi Mbunge sharp kwamba nitakuwa sharp, kuandamana naye ili tufanye safari ya sharp sharp, kwenda Kishapu kwa ajili ya kuwahudumia wananchi sharp wa Kishapu.
Mheshimiwa Naibu Spika, weekend ijayo baada ya hii, namuahidi Mheshimiwa Suleiman Nchambi kuandamana naye kwenda Kishapu kwenda kuitembelea hospitali hii na naomba Waheshimiwa Wabunge wengine wawe sharp kutekeleza mambo sharp sharp kwa ajili ya wananchi wao kama Mbunge wa Kishapu.
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Namuomba sasa Mheshimiwa Mwiguli na Naibu wake Mawaziri hawa shapu wanaofanya mambo kwa ushapu watumie neema hiyo kwa kutengeneza mabwawa kwa ajili ya umwagiliaji wa mazao ambayo yatawakomboa wana Kishapu.
WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunalipokea wazo la Mbunge shapu wa Jimbo shapu la Kishapu, ambaye kwa kweli kwa ushapu wake ndiyo maana amekuwa akichaguliwa. Tayari tumeshaandika barua kwa Waziri pacha ambaye kwa leo yupo na heshima kubwa.
Kwa hiyo tutatengeneza hilo ili tuweze kutumia mabwawa hayo.
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa tatizo hili la pembejeo hasa mbegu bora ni tatizo ambalo kwa kweli linatakiwa sasa lishughulikiwe kwa kina na kwa kuwa Mungu ameijalia Wizara hii ya Kilimo kupata Waziri na Naibu Waziri ambao ni wachapa kazi na ni mahodari, je, kutokana na uhaba wa mvua, Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Wizara wapo tayari kuharakisha tafiti za mbegu ambazo zitaendana na mazingira ya sasa
NAIBU WAZIRI KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, tunatambua wazi kwamba changamoto ambazo tunazipata katika kilimo chetu ni pamoja na mabadiliko ya tabia nchi na hivyo kuhitaji mbinu za kisasa za kuweza kupata pembejeo na hasa mbegu ambazo zinaendana na hali halisi ya mvua ambayo tunapata. Taasisi yetu ya Taifa ya Mbegu (ASA) imejikita sana sasa katika kufanya utafiti wa mbegu ambazo zinaendana na mazingira yetu na hali halisi ya mvua ambayo tunapata.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari Serikali imewekeza sana katika utafiti wa mbegu, kwa hiyo, tunaamini kwamba kadiri muda unavyokwenda tutapata mbegu ambazo zinaendana na mazingira yetu. Vilevile nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa pamoja na changamoto kubwa tuliyonayo kwa sasa ambayo takribani asilimia 60 ya mbegu zote zinazotumika nchini zinatoka nje, tumeelekeza nguvu nyingi katika kuzalisha mbegu ndani ya nchi na tunashirikiana na sekta binafsi katika shughuli hii. Nashukuru sana.
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wabeja sana. Kwa niaba ya wananchi Shapu wa Jimbo la Kishapu, kwanza naomba nitoe shukrani za dhati kwa Wizara kwa kutekeleza mradi kabambe wa maji ya ziwa victori katika Jimbo la Kishapu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, naomba nije na scenario tofauti baada ya mradi huo kufika katika Mji Mdogo wa Muhunze, Mbunge wa Kishapu kushirikiana na viongozi wa Kishapu tumeshafanya mkakati kabambe wa kutafuta mkandarasi ambaye anaweza kutupatia fedha kwa vigezo vile ambavyo Serikali inaweza ikaridhia. Je, Mheshimiwa Waziri je, yuko tayari kukaa na uongozi wa Kishapu ukiongozwa na Mbunge wa Kishapu ili tumweleze kuwa tumeshapata fedha ambazo zinaweza zikayasambaza maji katika Jimbo lote la Kishapu katika vitongoji vyote vya Kishapu iwapo utaridhia tena kwa masharti yale ambayo Serikali inaya…(Makofi)
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inakubaliana naye kama kuna mwekezaji ambaye anataka kuja kuwekeza katika sekta ya maji na iko ndani ya sera yetu ya maji, maji ni shirikishi ni Serikali pamoja na washirika wa maendeleo mbalimbali. Kwa hiyo, sisi tunamkaribisha yeye aje tuzungumze tuweze kuona namna gani tunaweza kwenda naye katika jambo hili.
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, wabheja sana.
Kwa kuwa Jimbo la Kishapu lenye watu shapu na Mbunge shapu, ni moja ya Majimbo ama Jimbo lililotekeleza kwa kiwango cha juu sana mpango wa huduma za afya. Tunayo hospitali ya kisasa kabisa katika Wilaya yetu ya Kishapu, tuna vituo vinne vya afya vya kisasa kabisa ambavyo vimekamilika na vinatoa huduma bora katika Jimbo la Kishapu, lakini katika vijiji 118, takribani asilimia 50 mpango wa zahanati katika Jimbo la Kishapu unaendelea vizuri na miongoni mwa vituo hivyo vya zahanati vinatoa huduma bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu je, ndugu yangu, wajina Mheshimiwa Suleiman Jafo na dada yangu Mheshimiwa Ummy, kutokana na malumbano ama tatizo kubwa la mpango wa afya ambalo ni dhahiri limeelezeka na wewe umekiri kuwa watu wengi wanahitaji kuuliza maswali katika jambo hili la afya na kwa kuwa Kishapu tumekwishajitahidi tumepiga hatua…
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Kwa kuwa Kishapu tumepiga hatua kubwa, je, Wizara ya Afya na Ofisi ya TAMISEMI kwa maana ya Wizara hawaoni sasa watoe kipaumbele kwa Jimbo la Kishapu ili kuiweka kuwa ni ajenda maalum na kipaumbele cha kumaliza tatizo hili ili Kishapu iwe mfano katika Wilaya zote nchini kwa kumaliza kabisa tatizo hili kwa kutuongezea michango?
AZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge Nchambi kwa kazi kubwa ya ujenzi wa vituo vya afya na zahanati na shughuli kubwa wanayofanya ya uhamasishaji katika eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mbunge kwamba tutamuunga mkono na ajenda ya kwanza ni kwamba Ofisi yangu itafanya utaratibu wa ziara maalum kama ya kiheshima kwenda kule Kishapu ku-recognize juhudi kubwa inayofanywa kule. Baadaye tutaangalia way forward tunafanyaje kwa pamoja kwa lengo kubwa la kuwasaidia wananchi wa Kishapu kwa juhudi hiyo waliyoifanya.
MHE. SULEIMAN S. MURAD: Mheshimiwa Mwenyekiti, na yeye apewe maelekezo afike kwenye kaya zote. Na Mheshimiwa Naibu Waziri nakukaribisha Mvomero karibu sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Murad kwa swali lake la nyongeza na kazi anazoendelea kufanya za kufuatilia miradi ya umeme. Nakubaliana na yeye kwamba, huyu Mkandarasi MDH kwa kweli hakufanya vizuri na hakuwa mkandarasi katika mkoa wake tu, lakini alikuwa mkandarasi pia katika Mkoa wa Pwani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo sisi tumetoa maelekezo kwa REA kwa sababu, wakandarasi wote wa Miradi ya REA Awamu ya Pili ni Mikoa miwili tu Tanga na Arusha ambao wametimiza vigezo na wamemaliza kipindi cha uangalizi. Kwa hiyo mikoa mingi ina changamoto, Singida, Mbeya, Mikoa ya Kanda ya Ziwa. Kwa hiyo, tumetoa maelekezo na tumewataka REA wafanye tathmini na tutachukua hatua na kwamba, maelekezo ni kwamba, awamu ya tatu isiruke kitongoji chochote wala taasisi ya umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niliahidi Bunge lako Tukufu kwamba, nimesema tangu awali kwamba, upungufu wa awamu ya pili tumeubaini, tathmini imefanyika, awamu ya tatu tumejipanga vizuri kuhakikisha kwamba, umeme huu au miradi hii inatimiza lengo lililotarajiwa na maelekezo ya Serikali kwamba, kila kitongoji kisirukwe. Ahsante sana.
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wabheja sana. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Jimbo la Kishapu lina zahanati 45 zilizokamilika na zinafanya kazi, vituo vya afya vinne vimekamilika vinafanya kazi na viwili tayari tunasubiri vianze kufanya kazi hivi karibuni na tuna hospitali kubwa ya kisasa ambayo inafanya kazi vizuri. Kwa kuwa tumekwishaleta maombi ya upungufu wa baadhi ya madaktari, wauguzi na watumishi wa kada ya afya, je, Mheshimiwa Naibu Waziri, uko tayari kukaa na mimi hata leo tupitie maombi hayo uone namna ambavyo utasaidia jitihada za watu wa Kishapu? Mheshimiwa Mwenyekiti, wabheja sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabla ya kujibu kama niko tayari au siko tayari, naomba niwapongeze kwa jitihada ambazo zimefanyika za kuweza kuhakikisha kwamba huduma za afya zinapatikana kwa kiwango kikubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, niko tayari kabisa, kabisa. (Makofi)
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya wananchi shapu wa Jimbo la Kishapu, naomba nitoe pongezi kwa Wizara kwa kazi nzuri manayoifanya, lakini nina swali la nyongeza kwakuwa bararaba ya Kolandoto kwenda Kishapu ni muhimu kwa kuwekwa lami kwa sababu za kiuchumi na mambo mengine. Je ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hiyo ya lami kutoka angalau Kolandoto kwenda Kishapu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nchambi, Mbunge shapu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba eneo hili kutoka Kolandoto kwenda Mwangongo na bararaba hii inaenda kuunganisha kupita Sibiti na maeneo ya mikoa mingine. Kwa hiyo, tutakapopata fedha tutaanza kujenga barabara hii muhimu.