Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Sixtus Raphael Mapunda (17 total)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la Morogoro Kusini Mashariki linafanana na tatizo la Mbinga Mjini, hasa maeneo ya Mbinga „A‟, Mbinga „B‟, Ruwiko, Bethlehemu na kadhalika; ile 5% inayotolewa kwa ajili ya vijana, pamoja na kwamba inaonekana inawasaidia vijana na maeneo mengine haiwafikii, bado inaonekana ni hela ndogo sana ukilinganisha na mahitaji ya vijana na hasa ukizingatia mabenki yetu hayajawa marafiki kwa vijana.
Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza, ukiondoa ile 5% inayotoka kwenye Halmashauri, Serikali Kuu kutengeneza fungu maalum kwa ajili ya kuwasaidia vijana, hususan vijana wa Mbinga? (Makofi)
NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, swali la Mbinga kwa vijana, nadhani mnafahamu. Katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambapo wananchi wote wameipa ridhaa Serikali ya Chama cha Mapinduzi, imeonesha kwamba kwa kila kijiji kitatengewa shilingi milioni 50. Lengo kubwa ni kwa ajili ya kuwawezesha vijana na akina mama katika vikundi waliojiunga katika SACCOS.
Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba ndugu yangu Mheshimiwa Sixtus Mapunda, najua ni mpiganaji sana wa Mbinga. Tushirikiane katika hili tuhakikishe hizi collection zinapatikana, lakini twende huko tukazisimamie, mwisho wa siku vijana wapate mahitaji yao kwa ajili ya kukuza uchumi wao.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, naomba niulize swali moja la nyongeza. Mradi unaokusudiwa kujengwa au kukamilishwa Mbinga ni mradi mkubwa; na fedha zilizoainishwa ambazo zinatafutwa, Dola milioni 11.86 ni nyingi, zinaweza zisikamilike kwa wakati:-
Je, Serikali haioni sasa kuna haja ya kutengeneza mpanga wa dharura kwa kukarabati miundombinu ya maji ulioko sasa ili watu wa maeneo ya Frasto, Kipika, Masumuni, Lusonga, Mbambi, Bethlehemu, Luiko na Misheni waweze kupata maji safi na salama?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimwambie Mheshimiwa Mbunge, kwamba Serikali tayari imeendelea na ujenzi wa miradi ya vijiji 10 katika Jimbo la Mbinga ambapo mpaka sasa kuna mradi mmoja wa Kigonsela ambao umekamilika na watu wanapata huduma ya maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, kuna miradi ambayo inaendelea ikiwepo Kingirikiti, Mkako, Kihongo, na Litoha. Pia katika bajeti ya mwaka wa fedha tunaoanza tarehe moja mwezi wa saba, tumetenga shilingi bilioni 1.7 ambazo yeye mwenye Mheshimiwa Mbunge akirishikiana na Halmashauri yake, basi watapanga kuangalia vipaumbele maeneo yale ambayo ameyataja ili yaweze kupata huduma ya maji.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuvishirikisha Vyama vya Msingi na AMCOS kwenye hiyo contract farming badala ya ku-deal na wafanyabiashara binafsi ambao wale hawamgusi moja kwa moja mkulima, wao wako zaidi kwa ajili ya ununuzi wa kahawa siyo uzalishaji wa kahawa.
Mheshimiwa Waziri huoni sasa ni wakati muafaka kwa ile AMCOS ya Kimuli ya kule Utili sasa ishirikishwe na zile „AMCOS’ nyingine za Miyangayanga, Utili na sehemu nyingine?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, kama alivyosema, ni kweli kwamba kama AMCOS zingekuwa zinashirikishwa ingeweza ikawa na manufaa kwa wakulima wengi. Nimweleze tu Mheshimiwa Mbunge kuwa, kwa kutambua umuhimu wa kushirikisha wakulima katika contract farming, tayari Wizara kwa kushirikiana na Bodi ya Kahawa ilishaifanyia marekebisho Sheria ya Kahawa ya mwaka 2001 pamoja na Kanuni zake za mwaka 2012, ili kuweka utaratibu kwa yeyote yule ambaye anataka kuingia katika kilimo cha mkataba katika maana ya contract farming aweze kuingia katika namna ambayo haitamnyonya wala kumuumiza mzalishaji mdogo.
Mheshimiwa Spika, kwa maana hiyo, zile AMCOS ambazo zinataka kuingia katika mkataba wa kilimo na wazalishaji wakubwa, tayari kuna utaratibu wa kufanya hivyo. Kwa hiyo, ni suala la wenyewe kujiweka sawa na Bodi ya Kahawa itawahakikishia kwamba wanaingia katika mikataba ambayo haitawanyonya.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa tatizo la Kata ya Rasbura linafanana na tatizo lililoko Kata la Lusonga Jimbo la Mbinga Mjini ambapo Halmashauri ilitwaa eneo ambalo lilikuwa linamilikiwa na wananchi kwa malengo ya kupima viwanja na kuliboresha eneo lile lakini mpaka sasa fidia bado haijalipwa na viwanja bado vinaendelea kugawanywa kwa watu wengine. Serikali haioni sasa hiyo formula inayotumika kule Lindi ikatumike na Mbinga yaani kulirudia tena kulipima upya na wale wananchi wa Lusonga wapate haki yao?
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, wazo lake ni zuri, nami nalikubali kama Wizara. Kikubwa ambacho nataka kusema ni kwamba, kabla ya utoaji wa ardhi katika maeneo yoyote, tuwaombe sana Halmashauri zinazohusika lazima wahusishe Ofisi ya Mthamini Mkuu ili waweze kuona kwamba tathmini itakayofanyika haimpunji mtu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa sababu anasema kule kwake kuna tatizo, namwomba sana, kwa sababu hatujapata kwa maandishi kwamba kuna matatizo hayo, ashirikiane na Kanda yetu ya Ardhi kule kwa maana ya Kamishna ili waweze kuliangalia suala hili. Kama kuna malalamiko ambayo yapo, basi ofisi itakuwa tayari kuyasikiliza na kuweza kuipitia upya. Kwa sababu hatujalipokea, siwezi kulitolea jibu la moja kwa moja, isipokuwa ni kushirikiana na Kamishna wa Kanda katika Kanda ambayo Mheshimiwa anatoka.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kibamba na Ubungo katika ujumla wake ni Mji unaokua kwa kasi sana na ongezeko kubwa la watu linalohatarisha usalama wa mali na raia kitu ambacho Kituo cha Kibamba kinapochelewa kujengwa kinahatarisha usalama wa eneo hili. Serikali haioni umuhimu wa kulichukulia hili jambo katika udharura wake ili kituo kijengwe kwa haraka?
Pili, kwa kuwa tatizo la maslahi ya askari wa Kibamba na maeneo mengine hayatofautiani na yale ya Mbinga, Nyasa, Songea Vijijini, Namtumbo Tunduru na Madaba; haoni kuna ulazima sasa kwa Serikali kuboresha maslahi ya watumishi katika maeneo niliyoyataja ikihusisha fedha maalum kwa ajili ya operation za ulinzi na usalama pamoja na kuboresha makazi yao hususan maeneo ya kulala ili kusitiri utu wao?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA (K.n.y. NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI): Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza kuhusu Serikali haioni udharura wa kujenga? Kama nilivyosema ni kwamba Serikali inatambua sana umuhimu wa kuboresha hicho Kituo cha Polisi cha Kibamba.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwamba, tayari tumewaongezea gari la pili kwa kuzingatia umuhimu huo huo na nikasema kwamba wakati wowote ule, Serikali inatafuta fedha sasa hivi kwa ajili ya kuanza kujenga vituo vya polisi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa tukijibu hapa mara kwa mara kwamba sasa hivi tuna mpango kabambe wa kujenga nyumba za watumishi 4,136, ambazo zitaenda sambamba na ujenzi wa vituo vya polisi. Kwa hiyo, namuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali tayari imeshachukuwa udharura wa suala hili na tutahakikisha kwamba tunajenga haraka sana iwezekanavyo ili kuweza kuimarisha ulinzi na usalama katika maeneo hayo ambayo yametajwa na Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge na concern ya Wabunge wengi sana ni kusikia maslahi ya Polisi wetu, Askari wetu; Serikali imekuwa ikifanya jitihada nyingi sana za kuhakikisha kwamba maslahi ya polisi yameimarishwa. La kwanza, askari ambao hawana nyumba tumekuwa tukiwapatia allowances za pango za nyumba ili waweze kulipia gharama hizo ambazo ni asilimia 15 ya mishahara yao kwa ajili ya kulipia pango.
Mheshimiwa Naibu Spika la pili, tumekuwa tukiwalipia kwa mfano, utalaam maalum, professional allowances. Mtu ana utalaam maalum; ni askari, lakini dereva. Tunamlipa vilevile posho ya asilimia 15 ya mshahara wake, lakini vilevile kwa mfano, unakuwa Polisi umeajiriwa leo, lakini wewe labda ni Doctor of Medicine, tayari umeshakuwa daktari, lakini umeajiriwa polisi na una cheo cha chini, unapewa mshahara sawa na wa daktari kama kawaida bila kujali cheo chako. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, kuna hardship allowance kwa wale ambao wanafanya kazi ngumu mnawajua ninyi, FFU, ambao kila mwezi nao tunawapa allowances ya shilingi 100,000.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Bima ya Afya, askari anapomaliza tu mafunzo yake anakatiwa Bima ya Afya asilimia 100 na Serikali. Pia kuna suala lingine ambalo tumekuwa tukiwadhamini; wanapotaka mikopo kwenye taasisi za fedha pamoja na SACCOS, yote haya yamekuwa yakifanywa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hili la mwisho ambapo Serikali imeboresha maslahi ya Polisi kuyapandisha kuyatoa kwa maana ya ration allowance ilikuwa shilingi 180,000 sasa ni shilingi 300,000. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge wanaweza kuona jinsi Serikali ambavyo inazidi kuboresha maslahi ya askari wetu ili wajisikie kwamba wanafanya kazi nzuri ya ulinzi wa Taifa lao.
Sasa ameuliza, mambo mengine ya kupata fedha kwa ajili ya ulinzi…

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri hasa eneo la kutoa milioni 50 kwa ajili ya wodi ya watoto, nina maswali madogo mawili ya nyongeza. Swali la kwanza ni lini Serikali itaboresha wodi ya akinamama wajawazito pamoja na sehemu ya kujifungulia hasa ukizingatia hali ya sasa pale hospitalini, akinamama wanakaa katika mazingira magumu na wanalala watatu watatu? (Makofi)
Swali la pili la nyongeza; kama nilivyoeleza kwenye swali la msingi, Hospitali ya Wilaya ya Mbinga inahudumia Halmashauri nne, yaani Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa, Mbinga Vijijini, Mbinga Mjini na sehemu ya Halmashauri ya Songea Vijijini. Gari ambalo limetolewa na waterreed liko kwa ajili ya kitengo cha UKIMWI na linawasaidia wale wagonjwa wa UKIMWI tu, maeneo kama ya Mpepai kwenye zahanati na vituo vya afya Kihungu, Kilimani, Kigonsera, Mkumbi ambao hao wakipata mazingira magumu katika maeneo yao wanahitaji kuletwa katika hospitali ya Wilaya. Ni lini Serikali itatuletea gari la wagonjwa kwa sababu hilo lililosemwa hapa haliko kwa ajili ya kuwasafirisha wagonjwa wa hali ya kawaida, ni wale tu kwenye kitengo cha UKIMWI?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MTAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kujali afya za akinamama na watoto katika eneo hilo, nikiri wazi kwamba kwa umahiri wako nadhani tutafika vizuri. Naomba nimhakikishie katika suala la wodi ya akinamama na watoto kipaumbele cha Serikali hivi sasa ni kuimarisha afya za jamii hasa akinamama na watoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kumbukumbu yangu siyo muda mrefu tulikuwa na mkutano mkubwa sana hapa wa Madaktari wa Mikoa na Wilaya na bahati nzuri mkutano ule alikuwepo Makamu wa Rais wetu kama mgeni rasmi, mambo makubwa sana yameahidiwa pale. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mchakato wa bajeti wa mwaka huu unaokuja tutaangalia jinsi gani tutashirikiana nao kuhakikisha kwamba tunaweka kipaumbele katika wodi ya wazazi katika hospitali yetu ya Mbinga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika suala la gari la wagonjwa, ni kweli nafahamu katika hospitali mbalimbali siyo ya kwake peke yake isipokuwa hospitali nyingi sana changamoto za gari za wagonjwa zimekuwa ni kubwa. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Ofisi yangu itashirikiana naye kutafuta uwezekano wa aina yoyote japokuwa siwezi kuwaahidi hapa sasa, kwa sababu najua jambo kubwa sana linalotukwamisha ni ukomo wa bajeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango mkakati mpana ambao tunauandaa hivi sasa naomba tujadiliane kwa karibu zaidi jinsi gani tutafanya, lengo kubwa ni kuwasaidia wale watu ambao catchment area yake ni kubwa zaidi, tutafanya vipi kama Serikali, tukishirikiana na Mbunge na wadau mbalimbali kuwawezesha wananchi wa eneo hili kufika sehemu za referral ambazo zimekusudiwa katika eneo lake. Ahsante sana
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tatizo linaloikabili Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe linafanana na linaloikabili
Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, lakini tofauti iliyoko kati ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe na ile ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga imekwishakujengwa takribani zaidi ya miaka mitano iliyopita, imekwisha kuezekwa, isipokuwa mpaka sasa haijamalizika kwa kutopakwa rangi, haijawekwa madirisha, haijawekwa mfumo wa wiring pamoja na milango na madirisha ambapo thamani ya umaliziaji huo inakadiriwa kuwa 300,000,000. Waziri anawahakikishiaje wananchi wa Wilaya ya Mbinga kwamba mwaka huu hautaisha mpaka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga inakamilika? Kwa sababu inapozidi kukaa zaidi ya miaka mitano inazidi kupoteza ubora, inakuwa ni nyumba ya popo, bundi na kadhalika ambayo siyo malengo ya ujenzi wa ile ofisi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nilijibu swali la msingi, na bahati nzuri nyumba anayoongelea ina uhusiano wa moja kwa moja na swali la msingi, kwamba
mwaka ujao wa fedha 2017/2018 TBA imeahidiwa kupata fedha kutosha na itakamilisha majengo ambayo imeyaanza.
Aidha, nikupongeze, maana sikutengemea utarudia tena kuliuliza hapa wakati ulishakuja ofisini na tukaongea kwa
kirefu.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nami nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, tatizo linalolikabili Jimbo la Kalenga linafanana vilevile na Kijiji cha Ruvuma chini, Kijiji cha Kihungu, Kijiji cha Mpepai, hao nao wanapata shida kubwa ya mawasiliano. Je, ni lini Serikali itahakikisha vijiji hivi navyo vinawekwa katika mpango na mwaka huu usipite wapate mawasiliano kama wanavyopata Watanzania wengine?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji hivyo alivyovitaja vya Ruvuma chini, Mpepai na eneo lote lile la ukanda wa Ziwa Nyasa pamoja na Mto Ruvuma, maeneo hayo yameingizwa katika mpango wa UCSAF, tunachohitaji ni kupata fedha ili tuweze kuyatekeleza hayo maeneo na nimhakikishie tutaendelea kufuatilia kama ambavyo Waziri wangu alimuahidi ofisini wakati alipokuwa akifuatilia hili suala.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie kwamba tutalifuatilia hadi tunakamilisha mawasiliano katika maeneo hayo ili watu wetu wasiwe wanapata matatizo na mawasiliano ya nchi jirani na wakashindwa kuwasiliana kwa upande wa Tanzania.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri na yenye matumaini kutoka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa muda mrefu unaosemwa na Serikali, umesemwa kwa miaka mingi sana. Hata mwaka 2015, Rais wetu mpendwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli katika kampeni zake alisema hakuna zao lenye tozo na kodi za ajabu ambazo hazi-exist duniani kama zao la kahawa, alisema lina kodi 26. Mwaka jana ametoa kodi moja tu ya usindikaji wa kahawa dola 250, bado kuna kodi 25, hatuoni commitment ya Serikali kwenye hili. Mbona tumefanikiwa kwenye korosho mwaka jana imefuta kodi zote na wananchi wakulima wa korosho wanaishi vizuri? Naiomba Serikali iji-commit kwenye hili mwaka huu iondoshe hizo kodi zote kwa sababu haya matumaini tumeyachoka.
NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI:
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge kwamba suala la tozo, kodi, limekuwa likizungumziwa kwa muda mrefu na ni kweli vilevile kwamba Mheshimiwa Rais wakati wa ziara yake ya kampeni ni moja kati ya masuala ambayo aliahidi kwamba atayafanyia kazi. Sisi kama Wizara tumeendelea kutekeleza sio katika zao la kahawa tu lakini katika mazao yote ya biashara.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Sixtus Mapunda kwamba tarehe 22 Mei, tutakuja na mapendekezo ya kufuta tozo mbalimbali katika mazao ya biashara. Katika hili nimuahidi kwamba tutavuka mategemeo yake. Siku hiyo ya tarehe 22 mimi mwenyewe nitahakikisha namwita aje Bungeni kusikiliza. Katika hili tutaleta, sisi tunasema mapinduzi makubwa, tutaondoa tozo nyingi sana sio katika kahawa pekee bali katika mazao yote ya biashara.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa uzito unaoikabili Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma ni uzito ule ule unaoikabili Hospitali ya Wilaya ya Mbinga hasa ikizingatiwa Wilaya ile inahudumia Halmashauri kubwa tatu, yaani Halmashauri ya Nyasa, Halmashauri ya Mbinga Mjini na Halmashauri ya Mbinga Vijijini, lakini vile vile sehemu ya Halmashauri ya Songea Vijijini: Mheshimiwa Waziri haoni sasa kuna haja ya kutimiza ile ahadi yake aliyoiahidi ya kuiboresha ile hospitali ili kuweza kupunguza mzigo mkubwa kwenda Hospitali ya Mkoa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa Mbunge anakumbuka kwamba tulikuwepo kule Mbinga na tumebaini hizo changamoto, ndiyo maana katika mipango yetu ya sasa, tumeamua kwamba Kituo cha Afya cha Kalembo ambacho ukiangalia mahitaji, sasa yamekuwa makubwa.
Kwanza tuboreshe Kituo cha Afya cha Kalembo ambacho siyo muda mrefu sana tutaenda kufanya ukarabati mkubwa sana wa theater na wodi ya watoto pale; lengo kubwa ni kwamba huduma ziweze kupatikana vizuri zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, ndiyo maana wenzetu kule wa Nyasa tume-cite Kituo cha Afya cha Mkiri ambacho tunaenda kufanyia huduma hiyo hiyo vilevile. Lengo letu kubwa ni katika maeneo hayo mawili, Nyasa na pale Mbinga, tukiweka huduma za kutosha zitasaidia wananchi wa eneo hilo waweze kupata huduma vizuri.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana nami kupata fursa hii ya mwisho ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa mazingira ya kusini katika maana ya Ruaha, Rufiji mpaka Kilwa yanafanana kabisa na Hifadhi ya Msitu wa Liparamba unaounganisha upande wa Nyasa, Mbinga Mjini na upande wa Msumbiji. Ni lini Hifadhi ya Liparamba itapata hadhi inayostahili ili iwe kivutio cha utalii kwa center ya Kusini, hususan tunaunganisha nchi mbili za Msumbiji na nchi ya Malawi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kweli kwamba Hifadhi ya Liparamba iliyopo mkoani Ruvuma ni mojawapo kati ya maeneo ya hifadhi ya wanyamapori machache sana kwa Mkoa wa Ruvuma, lakini tajiri kwa wanyamapori na ambayo inastahili kabisa kuwa kwenye viwango vya Kimataifa vya kuwa mojawapo ya maeneo yenye vivutio vya utalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli pia kwamba katika siku za nyuma, mkazo wa kuweka mipango na mikakati ya kuweza kuboresha utalii katika hifadhi hiyo, hapo nyuma hakukuwa na mipango madhubuti kwa sababu hatukuwa na utaratibu wa kuweza kuboresha utalii upande wa kusini mwa nchi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema hapo awali kwamba katika Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano, tumezungumzia juu ya ku-diversify au kuweka utaratibu wa kuwa na mtawanyiko wa vivutio kwa maana ya vivutio vyenyewe; aina za vivutio, pia mahali vivutio vilipo hapa nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, chini ya mpango huo, tutakwenda kuboresha utalii kusini na Hifadhi ya Liparamba ni mojawapo kati ya hifadhi ambazo zinaenda kuwekwa katika kipaumbele ili kuhakikisha kwamba sasa watalii hawaendi tu Arusha, Moshi, Kilimanjaro na maeneo ya Kaskazini, pia waweze kwenda Mbeya, Songea, Mtwara na maeneo mengine ya Kusini.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Mbunge atupe nafasi tuweze kukamilisha mipango iliyopo kwa ajili ya kutekeleza sehemu ya mpango wa miaka mitano ili tuweze kuona sasa tunaboresha utalii upande wa kusini.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa na mimi nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, naomba niulize swali dogo tu la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, moja kati ya matatizo yaliyosababisha wakulima wapate shida sana na zao la kahawa kuporomoka ni utendaji mbovu wa hivyo Vyama vya Msingi na Vyama vya Ushirika. Mwaka huu tunakwenda kwa mara ya kwanza kwa kuwa na Chama Kikuu cha Ushirika na Mkoa ambacho kitanunua kahawa kwa niaba ya wakulima.
Je, Serikali imejiandaa vipi kuwaandaa Watendaji Wakuu wa Vyama vya Msingi kwa sababu tumebakiwa na muda mchache na uwezo wao unaweza ukawa ni mdogo huko nyuma walishatuletea hasara, kwa mfano, Mbinga, hoteli ya Mbiku, ma-godown, viwanja na majengo yote yako kwa Msajili wa Hazina….
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia sana katika suala zima la Vyama vya Ushirika hususan katika Jimbo lake la huko Mbinga.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Jimbo la Mbinga na lenyewe limekuwa likilima sana zao hili la biashara la kimkakati la kahawa na ni kweli naomba nikiri kwamba vyama vingine vya ushirika vimekuwa havifanyi vizuri. Lakini kama nilivyomjibu Mheshimiwa Mbunge Stanslaus Mabula, katika maswali yake mawili ya nyongeza ni kwamba Serikali imejipanga sawasawa kufanya total transformation katika suala zima la Vyama vya Ushirika na tumejipanga kuingia kwa miguu miwili. Tutakuwa tunafanya mafunzo ya mahesabu na vilevile kuhakikisha kwamba ukaguzi utakuwa unafanyika kwa kina ili tuweze kupata mazao bora ambayo pia yatakuwa yanatupatia bei nzuri. (Makofi)
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa, tatizo la Hospitali Teule ya Muheza linafanana na tatizo la Hospitali ya Wilaya ya Mbinga Mjini, mapema mwaka huu Waziri Mkuu alipofanya ziara yake Mkoa wa Ruvuma aliahidi kwamba Hospitali ya Wilaya ya Mbinga itaboreshwa katika maana ya theatre, nyumba ya kuhifadhia marehemu pamoja na kuhakikisha kwamba Madaktari wanaongezeka na gari ya wagonjwa. Ni lini ofisi yako itahakikisha hizo ahadi za Waziri Mkuu zinatekelezwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Pius Mapunda kwanza kwa kushiriki pamoja na Waziri Mkuu katika ziara yake, vilevile kwa sababu Waziri Mkuu ameshatoa ahadi hii haina negotiation, kinachotakiwa ni kwamba katika mpango wa fedha kwa sababu sasa hivi bajeti imeshapita na Waziri Mkuu lengo lake ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika ofisi yetu ya Rais, TAMISEMI tutahakikisha mchakato wa mwaka wa fedha wa 2017/2018 vipaumbele ambavyo Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuja pale aliviona, lazima tuviweke kama ni vipaumbele vya awali. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge katika mipango yao ya Bajeti kule wanapoanzisha lazima ionekane wazi na ikifika katika ofisi yetu nitaweza kuipa nguvu ili mambo haya yaweze kutekelezeka na wananchi katika eneo lake waweze kupata huduma kama Mheshimiwa Waziri Mkuu alivyokusudia.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niipongeze Serikali kwa kutenga hiyo milioni 250 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya. Kutenga fedha ni jambo moja na kulipeleka ni jambo lingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ikumbukwe kwamba mwaka wetu wa bajeti unaanza mwezi Julai, unaisha mwezi Juni, kuchelewa kuipeleka hiyo pesa kwa namna yoyote ile kutaathiri ujenzi wa hilo jengo hasa ikizingatiwa gharama zinaweza zikabadilika.
Je, Serikali inawahakikishia vipi wananchi wa Mbinga kwamba pesa hii itakwenda kwa wakati na ndani ya mwaka wa bajeti wa 2017/2018 jengo likatakamilika? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge mwenyewe na wananchi wa Mbinga, kwa sababu Mbunge unakumbuka ulikuja mpaka ofisini kwangu kwa shida kubwa sana za Jimbo lako na eneo lako. Mwaka huu umepambana mpaka umepata shilingi milioni 250 ambayo kutokana na maombi yako tumeiweka katika bajeti ya mwaka huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni commitment ya Serikali, kwamba tutakapofika mwezi wa Saba mpaka kipindi ambacho tutakachoenda nacho hicho sasa nikuhakikishe kwamba Serikali itajitahidi kwa kadri iwezekanavyo In Shaa Allah, tutajitahidi fedha zitaenda na nikuombe kwamba usimamizi uwe karibu kama ulivyokuwa makini jengo hilo liweze kukamilika kwa ajili ya wananchi wa Mbinga.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana nami kupata fursa hii ya mwisho ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa mazingira ya kusini katika maana ya Ruaha, Rufiji mpaka Kilwa yanafanana kabisa na Hifadhi ya Msitu wa Liparamba unaounganisha upande wa Nyasa, Mbinga Mjini na upande wa Msumbiji. Ni lini Hifadhi ya Liparamba itapata hadhi inayostahili ili iwe kivutio cha utalii kwa center ya Kusini, hususan tunaunganisha nchi mbili za Msumbiji na nchi ya Malawi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kweli kwamba Hifadhi ya Liparamba iliyopo mkoani Ruvuma ni mojawapo kati ya maeneo ya hifadhi ya wanyamapori machache sana kwa Mkoa wa Ruvuma, lakini tajiri kwa wanyamapori na ambayo inastahili kabisa kuwa kwenye viwango vya Kimataifa vya kuwa mojawapo ya maeneo yenye vivutio vya utalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli pia kwamba katika siku za nyuma, mkazo wa kuweka mipango na mikakati ya kuweza kuboresha utalii katika hifadhi hiyo, hapo nyuma hakukuwa na mipango madhubuti kwa sababu hatukuwa na utaratibu wa kuweza kuboresha utalii upande wa kusini mwa nchi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema hapo awali kwamba katika Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano, tumezungumzia juu ya ku-diversify au kuweka utaratibu wa kuwa na mtawanyiko wa vivutio kwa maana ya vivutio vyenyewe; aina za vivutio, pia mahali vivutio vilipo hapa nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, chini ya mpango huo, tutakwenda kuboresha utalii kusini na Hifadhi ya Liparamba ni mojawapo kati ya hifadhi ambazo zinaenda kuwekwa katika kipaumbele ili kuhakikisha kwamba sasa watalii hawaendi tu Arusha, Moshi, Kilimanjaro na maeneo ya Kaskazini, pia waweze kwenda Mbeya, Songea, Mtwara na maeneo mengine ya Kusini.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Mbunge atupe nafasi tuweze kukamilisha mipango iliyopo kwa ajili ya kutekeleza sehemu ya mpango wa miaka mitano ili tuweze kuona sasa tunaboresha utalii upande wa kusini.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na mimi kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa mazingira ya Mitaa ya Matogolo, Ndilimalitembo, Lizaboni na Bombambili kwa upande wa Songea Mjini, yanafanana kabisa na matatizo ya Mitaa ya Luwiko, Lusaka, Bethlehemu, Misheni, Mbinga A, Mbinga B, na Lusonga kwa upande wa Mbinga Mjini ni lini Serikali italeta neema ile ile inayotaka kuipeleka Songea Mjini kwa upande wa Mbinga Mjini?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, neema inakuja tunamsubiri Mheshimiwa Waziri wa Fedha, akamilishe finance agreement ya milioni 500 kutoka India ambayo sehemu ya fedha hiyo pia na Jimbo la Mheshimiwa Mbunge litafaidika na huo msaada. Tayari sasa hivi tupo katika hatua ya kuwapata Consultants ambao watafanya study kwa muda mfupi sana tutangaze tenda. Mheshimiwa Mbunge nimhakikishie kwamba Jimbo lake na Mji wake wa Mbinga utapata maji safi na salama baada ya muda mfupi. (Makofi)
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa chanzo cha umeme cha maji cha Tulila kipo katika Kata ya Mpepai na miundombinu yake inapitia katika Kitongoji cha elfu mbili na vijiji vya Kata za Mapendano kuelekea Songea, Serikali haioni umuhimu wa kuvipatia Vijiji vya Kata za Mpepai na Kihungu umeme kwanza kabla ya vijiji vingine hasa ukizingatia vijiji hivyo hulinda na kuitunza miundombinu hiyo na hivyo kuwafanya wananchi wa Mpepai kupata hisia za kuwa wametengwa na kubaguliwa kwenye huduma hiyo ya umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ni kweli miundombinu ya umeme kutoka katika chanzo cha maji cha Tulila inapita katika Kata za Mpepai na Kihungu. Katika Kata ya Kihungu kuna Vijiji vya Pachasita na Kihungu ambavyo tayari vimeunganishwa na huduma ya umeme. Kijiji kimoja cha Lipembe kitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA III unaoendelea.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika jibu la msingi kuwa kupitia utekelezaji wa mradi wa REA III, Mzunguko wa pili, vijiji vyote vya Kata ya Mpepai ambavyo ni Lipilipili, Luhangai, Mtua, Mpepai na Ruvuma chini vitapatiwa umeme.