Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to supplementary Questions by Hon. Dr. Tulia Ackson (1 total)

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza niishukuru sana Wizara ya Maji kwa sababu Jimbo letu la Temeke maji yamefika karibu kila kata. Tatizo letu kubwa ni kwamba bomba lile kubwa limepita katika barabara kubwa lakini kuvuta maji kwenda ndani ya nyumba zetu ambapo miundombinu siyo mizuri sana kwenye Kata za Buza na Kilakala na nyumba ziko mbali. Niombe Wizara ya Maji tunapoomba kuvutiwa maji ndani ya nyumba zetu, fedha ile ambayo tunatakiwa kuilipa kidogo ni kubwa, sasa mfikirie tuweze kuvuta kwa nusu ya bei halafu muendelee kutudai ndani ya malipo ya kila mwezi kama vile tunavyofanya luku ili tuweze kuona kila mmoja sasa anapata maji ndani ya nyumba yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
NAIBU SPIKA: Hilo ni ombi, nadhani utakuwa umeliandika Mheshimiwa Waziri.