Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Additional Questions to the Prime Minister from Hon. Hamida Mohamedi Abdallah (2 total)

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa majibu yake mazuri, lakini ningependa kujua sasa, eneo hili la watumishi kupitia Halmashauri zetu, wamejipangaje kwa suala zima la mapokeo haya ya mabadiliko ya kuendelea kutaka kuleta maendeleo zaidi? Kwa sababu kuna maeneo mengine tuna Makaimu Wakurugenzi na Makaimu Watendaji mbalimbali. Sasa napenda kujua Serikali imejipanga vipi katika eneo hili la Watendaji wetu? Ahsante.
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwa namna gani tumejipanga kuhakikisha fedha hizi zinapokelewa na watu stahiki, kwa maana wenye mamlaka kamili; kama ambavyo mnajua, Mheshimiwa Rais anaendelea kuunda Serikali kwa kuteua watumishi mbalimbali katika kada mbalimbali. Najua hatua iliyobaki sasa ni ya Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wenye dhamana. Wakurugenzi watashirikiana na Wakuu wa Idara na watumishi wote kwenye Halmashauri zetu.
Kwa hiyo, moja kati ya mikakati ya kuhakikisha kwamba tunapeleka fedha kwa wahusika ni kwa kukamilisha uundaji wa Serikali kwenye ngazi ya mamlaka ya Serikali za Mitaa na Halmashauri za Wilaya jambo ambalo litatokea pindi Mheshimiwa Rais atakapofanya maamuzi ya kusoma orodha ya Wakuu wa Wilaya na Wakarugenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, muhimu zaidi, ni kwamba mtumishi yeyote atakayekuwa kwenye eneo hilo na fedha zimefika na anawajibika kuzipokea ili aende kuzisimamia, anao wajibu wa kuzisimamia. Kwa sababu jukumu hili la kila mtumishi wa mamlaka ya Serikali za Mitaa, inaweza kuwa Mkurugenzi au Mkuu wa Idara na Mkuu wa Idara huyo kwa idara yake, anawajibika kupeleka fedha kwenye ngazi ya vijiji kwa ajili ya utekelezaji wa miradi anawajibika kufanya hilo na Serikali haitasita kuchukua hatua kali kwa yeyote ambaye atahusika kwa ubadhirifu wa fedha ambazo tutazipeleka kwenye shughuli za maendeleo kwenye ngazi zetu za Vijiji na Kata.
MHE. HAMIDA M. ABDALLAH:
Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa majibu yake mazuri, lakini ningependa kujua sasa, eneo hili la watumishi kupitia Halmashauri zetu, wamejipangaje kwa suala zima la mapo
keo haya ya mabadiliko ya kuendelea kutaka kuleta maendeleo zaidi? Kwa sababu kuna maeneo mengine tuna Makaimu Wakurugenzi na Makaimu Watendaji mbalimbali. Sasa napenda kujua Serikali imejipanga vipi katika eneo hili la Watendaji wetu? Ahsante.
WAZIRI MKUU:
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwa namna gani tumejipanga kuhakikisha fedha hizi zinapokelewa na watu stahiki, kwa maana wenye
mamlaka kamili; kama ambavyo mnajua, Mheshimiwa Rais anaendelea kuunda Serikali kwa kuteua watumishi mbalimbali katika kada mbalimbali.
Najua hatua iliyobaki sasa ni ya Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wenye dhamana. Wakurugenzi watashirikiana na Wakuu wa Idara na watumishi wote kwenye Halmashauri zetu.
Kwa hiyo, moja kati ya mikakati ya kuhakikisha kwamba tunapeleka
fedha kwa wahusika ni kwa kukamilisha uundaji wa Serikali kwenye ngazi ya mamlaka ya Serikali za Mitaa na Halmashauri za Wilaya jambo ambalo litatokea pindi Mheshimiwa Rais atakapofanya maamuzi ya kusoma orodha ya Wakuu wa Wilaya na Wakarugenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, muhimu zaidi, ni kwamba mtumishi yeyote
atakayekuwa kwenye eneo hilo na fedha zimefika na anawajibika kuzipokea ili aende kuzisimamia, anao wajibu wa kuzisimamia. Kwa sababu jukumu hili la kila mtumishi wa mamlaka ya Serikali za Mitaa, inaweza kuwa Mkurugenzi au Mkuu wa Idara na Mkuu wa Idara huyo kwa idara yake, anawajibika kupeleka fedha kwenye ngazi ya vijiji kwa ajili ya utekelezaji wa miradi anawajibika kufanya hilo na Serikali haitasita kuchukua hatua kali kwa yeyote ambaye atahusika kwa ubadhirifu wa fedha ambazo tutazipeleka kwenye shughuli za maendeleo kwenye ngazi zetu za Vijiji na Kata.