Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Additional Questions to the Prime Minister from Hon. Lucy Simon Magereli (1 total)

MHE. LUCY S. MAGERELI:
Mheshimiwa Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Waziri Mkuu, nilichotamani kusikia kutoka kwako ni tamko lako kama Serikali kuziagiza Halmashauri kutoa ushirikiano kwa
GS1 lakini TFDA, TBS na washirika wengine ikiwemo Wasajili wa Viwanda wa Makampuni kwa sababu hiyo ni timu inayofanya kazi pamoja. Changamoto hiyo imekuwa kubwa kwa sababu ya kupata
resistance kutoka kwa Halmashauri, lengo mlilolianzisha lilikuwa jema lakini Halmashauri hazitoi ushirikiano na kutotoa ushirikiano zinawanyima fursa wazalishaji na wafungashaji wadogo kupata fursa hiyo.
WAZIRI MKUU:
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, nimekusikia kwa namna ambavyo ume-experience
huko ambako umeona kwamba Halmashauri zetu hazitekelezi maagizo yetu ambayo tunayatoa na inawezekana siyo Halmashauri tu ziko pia nyingine ambazo pia zinafanya jambo hilo hilo. Kwa hiyo, nilichukue jambo lako baada ya kikao hiki nitawasiliana na Waziri wa TAMISEMI kuhakikisha kwamba maagizo yetu ya Serikali yanatekelezwa na wazalishaji wetu wadogo wanapata nafasi.
Lakini pia Wizara ya Kilimo nayo pia ilichukue hili kwa sababu tunayo
Maonesho ya Kilimo ambayo sasa tumeyaanzisha katika kanda mbalimbali, hawa wajasiriamali wadogo wapate nafasi za kwenda kuonyesha bidhaa zao kwenye maonyesho yale ili pia waweze kutangaza soko lao, waonyeshe ubora wao na sasa Halmashauri zisimamie wajasiriamali wadogo hao kwenda kwenye maonyesho hayo ili uonyesha kazi zao ziweze kuleta tija zaidi huo ndiyo msisitizo wa Serikali.
(Makofi)