Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to supplementary Questions by Hon. Dr. Selemani Said Jafo (780 total)

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Pamoja na majibu mazuri yenye kutia matumaini ya Naibu Waziri, naomba niulize swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa muda mfupi wa kuwapatia japo huduma ya visima virefu wakazi wa vijiji vya Maseleka, Madala na Tema wakati wanasubiri utekelezaji wa mradi huu mkubwa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kwanza Mheshimiwa Shangazi nadhani ni Mbunge kijana na ni mara yake ya kwanza ameingia Bungeni lakini ameonesha ni wazi kwamba kuingia kwake moja kwa moja ameenda katika ajenda kubwa ya suala zima la matatizo ya wananchi kuhusu suala la maji.

Mheshimiwa Spika, kutokana na ajenda hiyo naomba Serikali ichukue wazo hili, naomba tuangalie kwamba ni jinsi gani tutafanyakazi kwa pamoja ili wananchi wa Mlalo waweze kupata huduma hii ya maji. Naomba nichukue jambo hilo na naomba nimuahidi kwamba Ofisi yetu, Mheshimiwa Waziri wangu nadhani ataniruhusu nitafika kule Mlalo, licha ya ajenda ya maji nadhani ana changamoto nyingi kama Mbunge kijana lazima tumsaidie ili Jimbo lake liende vizuri.
MHE. AZZA H. HAMAD: Mheshimiwa Spika, nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa mradi huu wa kisima kirefu cha maji Mji Mdogo wa Tinde gharama yake halisi iliyotolewa na SHIWASA ilikuwa ni milioni 400 na mpaka sasa hivi Serikali imeshatoa milioni 300 kwa awamu.

Je, ni lini Serikali itakamilisha kutoa milioni 100 ili kukamilisha mradi huo?

Swali la pili, mradi huu wa maji, unategemewa kuhudumia zaidi ya watu 10,000 katika Mji mdogo wa Tinde. Vituo vilivyowekwa vya kuchotea maji havitoshelezi kabisa ukilinganisha na idadi iliyopo.

Je, Serikali haioni kuna umuhimu mkubwa wa kuongeza vituo vya kuchotea maji ili wananchi waweze kuchota maji hayo bila bugudha?
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nikiri kwamba katika Bunge lililopita hapa la Bajeti, kwa kumbukumbu zangu Mheshimiwa Azza alishika mshahara wa Mheshimiwa Waziri kwa ajili ya tatizo la maji. Kwa hiyo, hapa ninakiri kwamba Mheshimiwa Azza amekuwa akipigania jambo hili kwa muda mrefu sana, hilo suala la kwanza.

Mheshimiwa Spika, suala zima la mradi huu bajeti yake ni shilingi milioni 400, lakini mpaka sasa tumepeleka milioni 300. Nadhani hata Mbunge atakiri hapa wazi kwamba upelekaji wa milioni 100 za awamu ya kwanza, upelekaji wa milioni 200 ambao umefanyika mwezi Novemba, bado milioni 100. Suala hili nadhani kila Mbunge hapa atasimama na kusema mradi wake hapa haujakamilika.

Mheshimiwa Spika, jambo kubwa ni kwamba upelekaji wa fedha hivi sasa Serikali imejipanga, na ninyi wote ni mashahidi kwamba katika kipindi hiki mchakato wa kukusanya mapato ya Serikali umekuwa mkubwa sana lengo lake ni kwamba kuhakikisha viporo vya miradi vyote inatekelezeka ndani ya muda.

Mheshimiwa Spika, naomba nikuambie Mheshimiwa Mbunge, kwamba Serikali imejipanga lengo kubwa ni kwamba commitment ya Serikali na Mheshimiwa Rais aliyoitoa kwa Tanzania kumwondoa ndoo kichwani mwanamama, hii ni ajenda kubwa tutaendelea kuifanya. Naomba uiamini Serikali yako itaenda kufanya mchakato mpana ili mradi huu ukamilike na wananchi wapate huduma.

Mheshimiwa Spika, swali lingine la pili, ni jinsi gani mradi ulikuwa na vituo vinne lakini population ni kubwa, naomba niseme kwamba Mamlaka ya Maji sasa iangalie ni jinsi gani ya kutatua kwa sababu population imeongezeka. Hali kadhalika, watu wa Tinde, hata huyu Mheshimiwa Mbunge alikuwa ana changamoto kubwa sana wakati wa kampeni, hali ilikuwa ni tete pale Tinde. Lakini ukija kuangalia sasa hata huo mradi ukikamilika ukiweka vituo vinne bado changamoto ya maji katika Mji wa Tinde kwa sababu ya population itakuwa ni kubwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ajenda kubwa hapa ni kama nilivyosema ni lazima kama Wabunge tushikamane tukusanye mapato ya Serikali ili mapato yale yasaidie hata ule mradi mkubwa wa kutoa maji kutoka katika Mji wa Kahama pale, yanakuja Tinde yanaenda Nzega, yanaenda Igunga mpaka Tabora. Ni mkakati mpana kusaidia ukanda ule wote uondokane na tatizo la maji. Kwa hiyo, tumesikia hiki kilio Serikali itaifanyia kazi. (Makofi)
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini naomba niulize maswali madogo mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa Serikali imekiri kuwa kuna upungufu wa nyumba 1,183 za kuishi walimu na sasa tayari wananchi wa Wilaya ya Magu wameshajenga maboma 27 yapo tayari kukamilishwa; je, Serikali inaweza kutusadia fedha za kukamilisha ili walimu waingie kwenye nyumba hizo kupunguza uhaba wa nyumba za walimu?
Swali la pili, kwa kuwa nyumba hazitoshi, je, Serikali inaonaje kuwasaidia walimu ambao wanapanga nje mitaani kuwaongeza mishahara kidogo ili waweze kumudu upangaji wa nyumba mitaani? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA) Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza napenda kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi hii kubwa anayoifanya katika Jimbo lake na kwa sababu wamejenga maboma 27, hii inaonyesha ni commitment, jinsi gani watu wa Magu wameendelea kujitahidi kuhakikisha kwamba Walimu wanapata fursa ya kuishi katika nyumba bora.
Mheshimiwa Spika, kwa sababu request imesema ni jinsi gani Serikali itaweza ku-top up hiyo amount? Nasema, ni lazima tuangalie, tufanye ile resource mobilization kutoka katika pande zote.
Mheshimiwa Spika, napenda kumshauri Mheshimiwa Mbunge kwamba katika allocation ya own sources katika Halmashauri zetu, tuangalie ni jinsi gani tutafanya kupitia vyanzo mbalimbali katika Halmashauri; na bahati nzuri sasa hivi tumefanya uboreshaji mkubwa sana katika ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri zetu. Nakiri kwamba Halmashauri zimefanya kazi kubwa sana baada ya kuwapa commitment wahakikishe wanakusanya own source kwa kutumia electronic devices na hili wamelifanya.
Mheshimiwa Spika, nina mategemeo makubwa sana kwamba Halmashauri ya Magu hivi sasa, maana yake mapato yake yataongezeka kwa kasi. Naomba nimwambie kwamba Serikali kupitia TAMISEMI, itashirikiana na Halmashauri ya Magu kuona jinsi gani tutayafanya mpaka maboma hayo yaweze kukamlika. Lengo ni kwamba walimu wetu waishi katika mazingira salama na wapate motisha ya kufundisha.
Mheshimiwa Spika, katika sehemu (b) ya swali lake linasema, jinsi gani kama kutakuwa na topping allowance ilimradi walimu waweze kupata jinsi gani watakapokuwa mitaani waweze kulipia lile suala la pango.
Mheshimiwa Spika, naomba nikiri kwamba ni kweli tuna wafanyakazi mbalimbali ambao wanaishi katika mazingira magumu; acha walimu, acha sekta ya afya, acha mabwana shamba, wote wapo katika mazingira mbalimbali. Hili Serikali imeliona, ndiyo maana katika jibu langu la msingi mwanzo nilisema kwamba lazima tuhakikishe kwamba mishahara inaboreshwa ili mwisho wa siku hata mwalimu akikaa mtaani aweze kuwa na ile purchasing power ya kulipia nyumba. Ahsante.
SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na swali linalofuata. Tuko Wizara hiyo hiyo ya TAMISEMI; swali la Mheshimiwa Omary Tebweta Mgumba, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki.
MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini niseme Serikali inaonekana haiko serious katika hizi Halmashauri mpya ambazo tumekuwa tukizianzisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2014/2015 Halmashauri ya Wilaya ya Momba tuliomba shilingi bilioni mbili fedha maalum, maombi maalum, kwa ajili ya kuanzisha ujenzi wa Makao Mkuu yaani kwa maana ya kujenga boma na nyumba za watumishi ili watumishi watoke katika Halmashauri mama ya Mbozi kwenda Momba eneo la Chitete wakaanze kazi maalum. Mwaka 2014/2015 ukiangalia hapa hapa Serikali haijatenga kitu chochote, ni kwa nini Serikali inakuwa haiko serious inapoanzisha Wilaya mpya kwa ajili ya maandalizi ya watu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali (b), Halmashauri ya Momba ipo katika Mkoa mpya wa Songwe ambao na wenyewe umeanzishwa hauna Mkuu wa Mkoa, hauna ofisi, hauna chochote. Ni kwa nini Serikali imekuwa ikianzisha jambo la msingi lakini utekelezaji imekuwa ikishindwa?
Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka kupata majibu lini Mkoa Mpya wa Songwe utapelekewa Mkuu wa Mkoa na ofisi itakuwepo pamoja na Halmashauri ya Mombo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Silinde anasema kwamba Serikali haina nia ya dhati. Kikubwa zaidi naomba kwanza Bunge lako hili, tukiri kwamba miongoni mwa mambo ambayo Watanzania wametendewa haki na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni pale ambapo maombi yamepelekwa ya Mikoa, Halmashauri na Wilaya mpya na Serikali ikaamua kutekeleza hili ili mradi suala la kuleta huduma kwa wananchi, naomba tukiri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo ukija kuangalia katika ujenzi wa Ofisi za Wilaya peke yake, takribani Serikali ilitenga ujenzi wake kupitia TBA zaidi ya bilioni 12.9. Katika mchakato huo zaidi ya bilioni 5.6 zimepelekwa na mchakato mwingine unaendelea. Naomba tukiri kwamba rasilimali fedha ndiyo lilikuwa tatizo, lakini Serikali inajitahidi kuhakikisha kwamba, Halmashauri na Wilaya zilizojengwa na Mikoa iweze kufanikiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima hususan la Mkoa wa Songwe, Serikali imejipanga itajitahidi kwa kadri iwezekanavyo na ukija kuangalia hivi sasa, tuna Mikoa hii mipya iliyoanzishwa na lengo kubwa ni kukusanya mapato. Mwisho wa siku ni kwamba ofisi hizi na hasa masuala ya kiutawala, ngazi za utawala ziweze kukamilika ilimradi wananchi waweze kupata huduma, lakini Serikali imejidhatiti katika hilo kwa ajili ya kuleta huduma kwa wananchi.

MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE - WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri aliyoyatoa. Pengine bila kurudia yale aliyoyasema, nimesimama ili tu niongezee jibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Silinde anasema Mkoa wa Songwe umeanzishwa, mchakato wa Mkoa wa Songwe kuanzishwa haujakamilika kwa sababu hadi sasa hatuja-gazette. Kwa hivyo, huwezi ukaanza kumhudumia mtoto kabla hajazaliwa, unamnunulia nguo za kwenda shule.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutakachofanya kwa sasa baada ya muda tutatoa tamko rasmi la Serikali na tamko la Serikali huwa lipo kwa mujibu wa sheria. Kwa hiyo, tukishaipa GN, tutatamka kwamba Rais ameuanzisha huo Mkoa. Naomba uvumilie, lakini napongeza pia, najua una hamu kweli kuanza kuingia katika Mkoa wa Songwe, lakini taarifa hiyo uliyoitoa ni kwamba bado hatujauanzisha rasmi Mkoa wa Songwe, subiri tutatamka wakati wowote Serikali itakapokuwa tayari imemaliza mchakato wake. (Makofi)
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa akina mama hao wanatoka mbali na wanaamka usiku wa manane na kwa kuwa wanahatarisha ndoa zao kama katika Kijiji cha Mtambo, Kariakoo, Iwimbi na wako karibu na hifadhi na mara nyingi wanakutana na wanyama wakali kama simba, je, Serikali ina mikakati gani ya kuwasaidia hawa akina mama ili waweze kupata maji karibu na makazi yao kwa sababu wanapata shida sana?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa Mto Ugala upo karibu sana na Katumba, ni kilometa 20 tu na wananchi wa maeneo hayo wapo takribani 100,000, je, Serikali ina mikakati gani ya kuwasaidia wananchi hao kwa vile wako wengi ili waweze kupata maji kwa urahisi na wepesi zaidi?
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa haraka wa Serikali, nadhani jana Mheshimiwa Waziri wa Maji alitoa ufafanuzi wakati wa mjadala wa hotuba ya Mheshimiwa Rais kwamba ni kweli changamoto ya maji imeonekana kuwa kubwa. Mheshimiwa Mama Anna naomba nikupongeze sana katika hili maana mara ulipoingia katika nafasi yako umeona kipaumbele cha kwanza ni kushughulikia tatizo la maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, amesema katika Kijiji cha Mtambo wananchi wanapita katika hifadhi kubwa hivyo lazima wapate huduma ya maji ya haraka. Naomba niseme jambo moja, juzijuzi tulikuwa na semina kubwa na tuliambiwa tulikuwa na awamu ya kwanza ya maji sasa tunaingia katika awamu ya pili ambayo inaanza Januari hii. Mheshimiwa Waziri wa Maji jana alisema katika awamu hii tutaangalia jinsi gani tuweze kutatua matatizo kwenye sehemu zile zenye changamoto kubwa sana ya maji. Mheshimiwa Anna naomba nikuambie Waziri atakapokuja kufanya majumuisho ya Mpango katika suala zima la maji atazungumzia kiuwazi sehemu zenye changamoto tutafanyaje ili mradi tuweze kutatua tatizo la maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini umezungumzia matumizi ya Mto Ugala, kama Ofisi ya Rais (TAMISEMI) naomba tulichukue ili kuweka mpango mkakati hata ikiwezekana kwa kutumia wataalam wa Halmashauri na Wizara ya Maji tukishirikiana na TAMISEMI kufanya upembuzi yakinifu kuangalia ni jinsi gani mto huu unaweza kutumika kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa eneo hilo la Ugala, ahsante.
MHE. KATANI A. KATANI: Naitwa Katani Ahmad Katani, Mbunge wa Jimbo la Tandahimba.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Wilaya ya Tandahimba ina vyanzo vingi vya maji ukiwepo Mto Ruvuma na Mahuta lakini bado wananchi wake wanapata tatizo kubwa la maji.
Je, Wizara ina utaratibu gani wa kuhakikisha inaleta mashine ikafunga pale watu wake wakapata maji ya kutosha?
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli pale Tandahimba kuna mto na ni kweli wana changamoto ya maji. Kama nilivyosema pale mwanzo kila jambo lazima tuwe na mchakato wa upatikanaji wa fedha.
Kwa suala hili katika kikao chetu cha juzi tulifanya maamuzi tukasema lazima Wizara ya Maji na TAMISEMI utendaji wetu wa kazi uwe wa karibu sana. Katika haya nini cha kufanya?
Mheshimiwa Naibu Spika, tumesema kila Halmashauri kwanza angalau itenge bajeti ya kuanza kushughulikia yale mambo ya awali mfano kufanya upembuzi yakinifu sehemu ambayo chanzo cha maji kinaweza kupatikana. Hali kadhalika katika mchakato wa bajeti, naomba nizielekeze Halmashauri zote zihakikishe katika bajeti zao ajenda ya maji ni ya msingi sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba ajenda kubwa ya Serikali ni kuhakikisha inatatua tatizo la maji kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Katani hili ulilolizungumzia Serikali imesikia na inalichukua na lengo kubwa la Mheshimiwa Rais wetu amesema ni lazima tuhakikishe tunamtua ndoo mama, suala hili tutakwenda kulifanyia kazi.
MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wetu wa Katavi kijiografia upo pembezoni lakini inapotokea shida ya barabara, shida ya huduma za afya inaufanya mkoa kuendelea kuwa pembezoni. Ninavyofahamu mimi, huduma ya afya kwa maana ya hospitali ni hitaji muhimu. Je, Serikali imejipangaje kulifanya jambo hili kwa haraka ili kunusuru nguvu kazi iliyoko kule kwa kuiepusha na maradhi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, fungu linalotengwa kwa ajili ya uendeshaji wa Hospitali ya Wilaya ni dogo, wananchi wote wa Wilaya ile ya Mpanda ambayo kwa sasa hivi ni mkoa, wanategemea Hospitali hiyo ya Wilaya. Je, Serikali inaisadiaje hospitali ile kwa maana ya kuiongezea bajeti?
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ameuliza Serikali imejipanga vipi kuhakikisha jambo hili linafanyika kwa haraka?
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kama nilivyosema awali, Serikali imetenga shilingi bilioni moja katika bajeti ya mwaka huu, tunachosubiri sasa hivi ni kibali cha Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili mradi kazi hiyo ianze maana huo ndiyo mwanzo. Kazi yoyote haiwezi kufanyika lazima mshauri afanye kazi yake na kibali hicho kitakapotolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali nadhani kazi hii itaanza rasmi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naomba nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mchakato wa bajeti unaondelea sasa katika Ofisi ya Mkoa, kwa mwaka wa fedha 2016/2017 matarajio ni kwamba hospitali hii itatengewa shilingi bilioni 1.8 ili kuhakikisha watu wa Mkoa huu wa Katavi wanapata huduma ya afya. Umesema miundombinu ya barabara ina changamoto kubwa sana, endapo Hospitali ya Mkoa itakamilika tutawasaidia akina mama. Jambo hili ni la kipaumbele sana katika Serikali hii ya Awamu ya Tano. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala zima la hospitali yetu ya Mpanda ambayo kutokana na jiografia ilivyo inahudumia wananchi wengi wanaotoka maeneo mbalimbali. Pia inaonekana wazi hata dawa zikipelekwa pale hazitoshelezi na vifaa tiba vina changamoto kubwa. Namshukuru Mheshimiwa Waziri ameweza kupita katika maeneo mbalimbali, ni imani yangu tunakwenda kushughulikia jambo hili. Isipokuwa nawaagiza wataalamu wetu, mara nyingi wamekuwa na kigugumizi kikubwa sana cha kuandaa data za wagonjwa wanaotibiwa katika hospitali zao. Niwaagize zile data sheet za kusema hospitali inatibu wagonjwa wangapi zikusanywe vizuri. Mwisho wa siku ndiyo hizo data sheet ndiyo itakuwa taarifa elekezi ya jinsi gani Hospitali hii ya Mpanda iweze kusaidiwa ili mradi wananchi wapate huduma bora katika maeneo yao.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa niaba ya Waziri wa Nchi (TAMISEMI), napenda kujibu sehemu ya pili ya swali, je, Serikali inaisaidiaje Hospitali ya Wilaya ya Katavi katika kuongeza bajeti?
Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyosema Naibu Waziri, afya ndiyo kipaumbele cha juu katika Serikali ya Awamu ya Tano, kwa hiyo, tutaongeza bajeti katika fedha zinazotoka moja kwa moja Serikalini. Hata hivyo, nimesimama kusisitiza jambo moja, ni lazima tuhakikishe mapato yanayopatikana kutokana na uchangiaji wa wananchi katika kupata huduma za afya yanatumika pia kwa ajili ya kuboresha huduma za afya. Tuwahimize Wanakatavi na wananchi wote wajiunge bima ya afya kwa sababu kadri wananchi wengi wanavyojiunga katika Mfuko wa Bima ya Afya au CHF, ndivyo mnavyopata fedha za kuweza kutatua changamoto za bajeti. Tumetoa mwongozo asilimia 60 ya fedha zinazopatikana kutokana na uchangiaji zirudishwe kwa ajili ya kuboresha huduma kama vile kununua dawa, vifaa na vifaa tiba. Kwa hiyo, bajeti haitatosha kwa sababu kasungura siku zote kitakuwa kadogo. Tutumie fedha za makusanyo za Bima ya Afya na CHF ili kuweza kutatua tatizo la bajeti ndogo.
MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Hospitali ya Kwangwa ya Mkoa wa Mara iliyopo Musoma Mjini imekuwa ni ya historia kila siku tunaisikia ipo tokea hatujazaliwa hadi leo; na kwa kuwa wanawake na watoto wanapata shida sana na vifo vingi vinasababishwa na umbali wa kutoka Hospitali ya Musoma hadi Mwanza, je, Serikali inaonaje sasa kwa sababu imeshaitengea bajeti Hospitali ya Kwangwa kumalizia suala hilo au kuipa kipaumbele Hospitali ya Kwangwa?
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali imepokea suala zima la Hospitali ya Kwangwa. Maelekezo yetu ni kuhakikisha Hospitali za Wilaya na Mikoa zinafanya vizuri na zile ambazo zina changamoto kama vile miundombinu haijakamilika, changamoto za kibajeti zilizojitokeza katika kipindi cha nyuma kwamba bajeti zimetengwa lakini hazikufika, tunaenda kusisitiza suala zima la ukusanyaji wa mapato, huduma ya afya tumesema ni jambo la msingi ili kila mwananchi apate huduma bora ya afya. Kwa hiyo, Mheshimiwa Marwa, Serikali imejipanga na katika kipindi hiki tutaangalia bajeti inasemaje katika hospitali hii. Lengo letu ni kuipa nguvu wananchi wa eneo hilo wapate huduma kwa manufaa ya Serikali yao.
MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, lakini siyo kweli kwamba katika Wilaya ya Kilwa kuna wakulima wanaingilia maeneo ya wafugaji na kama hivyo ndivyo, Mheshimiwa Waziri anao uwezo wa kunitajia vijiji vitano ambavyo kuna migogoro ya wakulima kuingilia maeneo ya wafugaji, hiyo ni moja.
Mbili, kwa kuwa, mpango wa matumizi bora ya ardhi katika Kijiji cha Ngea haukutenga eneo kwa ajili ya wafugaji na kwa kuwa, Mkutano Mkuu wa Kijiji cha Ngea, ulishaamua wafugaji waondoke na kupata baraka za uongozi wa Wilaya. Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuongozana na mimi kwenda kuona athari ambazo wakulima wamezipata lakini athari za hifadhi za misitu pamoja na Bwawa la Maliwe?
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kusema kwamba hizi ni taarifa ambazo tumezipata, nikuhakikishie ndugu yangu Ngombale mimi niko tayari kwanza kufika Kilwa. Katika sehemu yako na pili naomba nikuhakikishie kwamba, nitafika Kilwa, siyo kwa ajenda hii tu ya wakulima na wafugaji peke yake hapana! Kuna mambo mengi ya kimsingi ya kuweza kuyafuatilia kule Kilwa ambapo ofisi yangu ina kila jukumu la kufanya hivyo ili wananchi waweze kupata huduma.
Mheshimiwa Spika, lakini suala zima la vijiji nikutaarifu kwamba, katika miaka ya nyuma kulikuwa na Mkuu mmoja wa Wilaya pale alikuwa anaitwa Nurdin Babu, katika hiki Kijiji cha Ngea ulichokizungumza japokuwa mwanzo wafugaji walikataliwa lakini baadaye Mkuu wa Wilaya alipokwenda kufuatilia baadhi ya wananchi walisema hapana, tunahitaji wafugaji waendelee kuwepo.
Kwa hiyo, kwanza kuna changamoto kidogo katika maeneo yetu, lakini kubwa zaidi haya yanatokea ni nini mara nyingi sana wakati mwingine hata hawa Viongozi wetu wa Vijiji inakuwa ni tatizo, mwanzo wafugaji walikataliwa walipoingia pale, lakini baada ya kukaa muda fulani tayari sasa kukawa na mgogoro mpaka Mkuu wa Wilaya pale aliingia site na wananchi wamesema bwana sisi hapa hatuna matatizo kwa sababu wafugaji wamechimba kisima hapa, sisi tunaishi vizuri, Mkuu wa Wilaya nenda, leo hii suala hili limekuja! Hata hivyo, nimesema ngoja niyachukue haya kwa sababu lengo letu kubwa ni kuhakikisha kwamba Watanzania wanaishi katika hali ya usalama. Hii migogoro mwisho wa siku inahatarisha maisha ya wananchi wetu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Spika, hivyo nayafanyia kazi ndugu yangu, wala usipate hofu.
MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nianze kwa kuishukuru Serikali kwa kupeleka hizo fedha kwa ajili ya kukamilisha miradi. Hata hivyo, wananchi wa Busanda wangependa kujua kwamba ni lini sasa miradi hii itakamilika, maana imekuwa ni miradi ya muda mrefu sana na utekelezaji wa miradi hii ya Benki ya Dunia imekuwa ni ya muda mrefu sana?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa, Jimbo la Busanda linagusa Ziwa Viktoria katika maeneo ya Bukondo na sehemu zingine, ningependa kujua sasa mkakati wa Serikali, ni lini mtahakikisha wananchi wanapata maji ya uhakika kwa kuvuta maji kutoka Ziwa Viktoria?
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kwa suala la lini naomba nizungumze wazi, bahati nzuri tumeshapeleka fedha nilivyozungumza pale awali, shilingi bilioni 1.144. na hili naomba nimuagize Mkurugenzi wa Halmashauri husika kuhakikisha katika Mwaka huu wa Fedha, kwa sababu fedha zimeshafika hakuna sababu ya wananchi kuendelea kupata shida.
Hili Mheshimiwa Mbunge naomba nikwambie, nadhani tulikuwa pamoja katika kuzindua mradi mkubwa wa maji pale Geita. Katika hili nasema kwamba, tutarudi tena kule Geita kuangalia tatizo hili la maji, kama pesa zimefika nitashangaa sana kuwaona Wataalam wetu wanashindwa kuzitumia fedha hizi vizuri ili wananchi wapate huduma ya maji.
Mheshimiwa Spika, lakini ajenda ya pili, ni kwa nini sasa tusitumie suala la Ziwa Viktoria, nadhani siku ile ya Mkutano Mkubwa tulisema wazi kwamba wale wananchi wote wanaopakana na Ziwa Victoria, Serikali katika awamu ya pili itaangalia ni jinsi gani ya kufanya badala ya wakati mwingine kuchimba bore hole, twende sasa kutumia hii rasilimali adimu tuliyokuwanayo ya Maziwa yetu.
Mheshimiwa Lolesia nikwambie kwamba, Serikali katika huu mpango wa maji wa awamu ya pili ambao ulianza Januari iliyopita, tunajipanga kuhakikisha kuwa tutafanya matumizi mazuri ya Ziwa Victoria, siyo Busanda peke yake bali vijiji vyote na maeneo yote yanayozunguka Ziwa Viktoria, wakiwepo ndugu zangu wa Magu ambao mwezi uliopita nilikuwa kule.
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri na naipongeza pia Serikali kwa kutambua umuhimu wa kuipandisha hadhi Hospitali ya Kibena kuwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.
Swali langu la nyongeza, Mheshimiwa Naibu Waziri, Serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa kujenga Hospitali ya Wilaya mpya ndani ya Wilaya ya Wanging‟ombe, ukizingatia kwamba Wilaya hii ni mpya na iko ndani ya Mkoa mpya?
Vilevile swali la pili la nyongeza, Serikali haioni kwamba tatizo la ukosefu wa madawa na uchakavu wa majengo ya Hospitali lipo pia katika Wilaya ya Ludewa na lini Serikali itatafutia ufumbuzi suala hilo.
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, hoja ya Mheshimiwa Mbunge ni kwamba Hospitali ile ilikuwa ya Wilaya ya Njombe, sasa maana yake itaenda kupandishwa kuwa hospitali ya Mkoa, watakuwa hawana hospitali ya Wilaya, hiyo ndiyo hoja ya Mheshimiwa Mbunge. Naomba tulichukue hili, kwanza, kwa sababu matatizo makubwa ya hospitali hii hivi sasa ya Kibena imekuwa ni kwa sababu mwanzo ilikuwa ni hospitali ya Wilaya na kwa vile ni hospitali ya Wilaya hata ule mgao wake unaenda kiwilaya Wilaya, ndiyo maana Serikali imeona sasa ni vema hospitali hii kuipandisha daraja kuwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa.
Mheshimiwa Spika, kitendo cha kuifanya kuwa hospitali ya Mkoa, maana hata catchment area yake inakuwa tofauti na hivi sasa ilivyo. Maana yake ni nini, wananchi wa Mkoa wa Njombe watakuwa na fursa kubwa ya kupata matibabu mazuri zaidi kulinganisha na pale mwanzo.
Mheshimiwa Spika, kwa nini sasa tusihakikishe tunajenga hospitali ya Wilaya nyingine mpya, hili kama Ofisi ya TAMISEMI kwa kushirikiana na halmashauri husikia tutafanya hiyo kazi. Naomba niseme kwamba hapa sasa hivi ukiangalia hata kwa ndani kuna mgogoro, ukiangalia wale wanaosema kwamba hii hospitali yetu ikiwa ya Mkoa tutakuwa hatuna hospitali ya Wilaya. Nadhani sasa hivi tushikamane kwa pamoja tupate Hospitali ya Mkoa, mikakati mingine mipana iende katika suala zima la upataji wa hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Spika, naomba nilichukue hili Suala la Ludewa kwa sababu yote ni maeneo ambayo yanatakiwa yatafanyiwa kazi na wewe najua ni Mbunge wa Viti maalum wa Mkoa wa Njombe tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo. Mkoa wa Njombe ni Mkoa mpya, wananchi wake waweze kunufaika na huduma za afya ya Serikali yao, asante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini Wilaya ya Morogoro Kusini mpaka hivi sasa, hata hivyo vikundi alivyovizungumzia hapa; na kwa kuwa, Wilaya hiyo haina Makao Makuu ya Wilaya, wanaripoti Morogoro Mjini, kwa hiyo, inakuwa ngumu vijana hawa kufuatilia hizo fedha anazosema; na kutokana na idadi na umasikini wa wananchi wa Morogoro Vijijini, kwa kweli, kasi ya Serikali katika kuwawezesha vijana imekuwa ndogo sana kutokana na ukubwa wa Wilaya hiyo ambapo haina Ofisi ya Wilaya.
Je, Serikali ni lini sasa itaweka Ofisi ya Halmashauri ndani ya Wilaya ya Morogoro Vijijini ili vijana hao waache kuhangaika na kufuatilia masuala yao ndani ya Wilaya yao badala ya kukimbilia Morogoro Mjini ambako ni mbali na Wilaya yao? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kwa kuwa matatizo ya vijana Wilaya ya Morogoro Mjini na Wilaya ya kilombero, hususan Jimbo la Mlimba yanalingana; mara nyingi katika hii Mifuko ya Vijana ukitaka kuangalia ufuatiliaji wake, kwanza Halmashauri hazipeleki hizo hela. Mara nyingi Wabunge wengi ndani ya Bunge hili wamelalamika kwamba pesa hizo haziwafikii vijana.
Je, Serikali ina mpango gani sasa kwa kusudio la kuhakikisha hela zinazotengwa kwa ajili ya vijana ambapo hazitengwi na Wakurugenzi kuweka kipindi maalum kulipa madeni ya nyuma na kuendelea kutoa zile asilimia ili vijana wengi wapate kujiajiri wenyewe katika awamu hii?
NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, agenda ya kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro haina Ofisi ni kweli. Swali hili nadhani nimelijibu wiki iliyopita hapa na nimetoa ufafanuzi wa kina kuhusu swali hili; na tumesema mchakato hivi sasa unaendelea wa ujenzi kule. Lengo kubwa, ni kweli watu wanaotoka maeneo ya mbali kabisa; kwa mfano mimi mwenyewe nilienda Morogoro Vijijini yapata karibuni mwezi uliopita, ukitoka maeneo ya Mvuha mpaka kufika mjini changamoto kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeshatoa maelekezo kwamba mchakato ufanyike kwa haraka ilimradi wananchi wale wa Morogoro Vijijini kama Swali la Msingi alilouliza Mheshimiwa Tebweta, wiki iliyopita nilivyokuwa nikilifafanua.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala zima la uwezeshaji wa vijana, ni kweli, nanyi mnakumbuka hapa mwaka 2015 katika mchakato wetu tulipitisha mpaka Baraza la Vijana. Lengo kubwa ni kuona jinsi gani vijana waweze kufanyiwa kazi. Katika Bajeti ya mwaka huu wa fedha, ninyi Waheshimiwa Wabunge mnakumbuka, katika kikao chetu kilichopita cha Bajeti, tulitenga mafungu katika maeneo matatu tofauti.
Katika Wizara ya Habari na Vijana, kipindi kile tulitenga karibu shilingi bilioni moja katika bajeti, halikadhalika Waziri wa Utumishi alipokuja hapa eneo kubwa la concentration jinsi gani vijana wanaomaliza vyuo wanakosa ajira, Serikali ilitenga takribani bilioni 233, lengo likiwa ni kuajiri waajiriwa wapya wapatao 71,408.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hili nini kimefanyika hivi sasa? Siku mbili zilizopita hapa, Mheshimiwa Angellah Kairuki alizungumzia kwamba sekta ya afya peke yake itaajiri takriban wafanyakazi wapatao 10,870. Katika changamoto ya kuajiri walimu wapya, tunatarajia kuajiri walimu wapatao 40,000 ambao idadi katika bajeti ile ya shilingi bilioni 233, lengo kuwa ni kuwaajiri wafanyakazi wapya ambao ni vijana wapatao 71,408. Hii ni ajenda kubwa sana ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaambie ndugu zangu, tatizo hasa la kukosa 5% kwa vijana na akinamama, changamoto hii inatukabili sisi Wabunge. Kwa sababu own source inajadiliwa katika vikao vya Mabaraza ya Madiwani na sisi ni miongoni mwa Wajumbe katika Mabaraza ya Madiwani. Own source haiji TAMISEMI wala haiji Wizara ya Fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kinachofanyika nini? Collection imefanyika ndani ya Halmashauri; Kamati ya Huduma za Jamii na Kamati ya Uchumi inakaa, baadaye Kamati ya Fedha; ninyi mnajua mwezi huu tumekusanya shilingi milioni 100 na wewe Mbunge upo na unafanya decision. Naomba niwaambie ndugu zangu, Taarifa ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali, katika report yake aliyo-submit mwezi wa nne imeonesha kwamba takriban shilingi bilioni 38.7 ambazo zinawagusa akina mama na vijana hazijapelekwa katika makundi hayo, lakini sisi ndio wa kufanya maamuzi hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwape changamoto ndugu zangu, hili jukumu ni la kwetu sisi sote. Kila Mbunge katika Kamati ya Fedha aende akasimame, own source zinazokusanywa ahakikishe 5% kwa vijana na akina mama inakwenda kwa ajili ya kuokoa uchumi wa vijana wetu. Katika hili tutawekeza ajira pana sana ya vijana wetu kwa sababu. Kwa sababu shilingi bilioni 38; sasa hivi tuna Halmashauri 181, takriban kila Halmashauri ikitoa shilingi milioni 100 ambayo collection ikiwasilishwa shilingi bilioni moja kwa mwaka, maana yake nini? Kwa Halmashauri 181 maana yake kuna shilingi bilioni 181 ilibidi ziende kwa vijana na akinamama.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwasihi Wabunge wenzangu, sasa tufanye mabadiliko ya kweli kuwakomboa Watanzania. Mabadiliko haya yataanza na sisi na Wenyeviti wetu wa Halmashauri na Madiwani wetu kuhakikisha own source ya 5% kwa vijana na akina mama inakwenda kwa ajili ya mustakabali wa nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la Morogoro Kusini Mashariki linafanana na tatizo la Mbinga Mjini, hasa maeneo ya Mbinga „A‟, Mbinga „B‟, Ruwiko, Bethlehemu na kadhalika; ile 5% inayotolewa kwa ajili ya vijana, pamoja na kwamba inaonekana inawasaidia vijana na maeneo mengine haiwafikii, bado inaonekana ni hela ndogo sana ukilinganisha na mahitaji ya vijana na hasa ukizingatia mabenki yetu hayajawa marafiki kwa vijana.
Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza, ukiondoa ile 5% inayotoka kwenye Halmashauri, Serikali Kuu kutengeneza fungu maalum kwa ajili ya kuwasaidia vijana, hususan vijana wa Mbinga? (Makofi)
NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, swali la Mbinga kwa vijana, nadhani mnafahamu. Katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambapo wananchi wote wameipa ridhaa Serikali ya Chama cha Mapinduzi, imeonesha kwamba kwa kila kijiji kitatengewa shilingi milioni 50. Lengo kubwa ni kwa ajili ya kuwawezesha vijana na akina mama katika vikundi waliojiunga katika SACCOS.
Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba ndugu yangu Mheshimiwa Sixtus Mapunda, najua ni mpiganaji sana wa Mbinga. Tushirikiane katika hili tuhakikishe hizi collection zinapatikana, lakini twende huko tukazisimamie, mwisho wa siku vijana wapate mahitaji yao kwa ajili ya kukuza uchumi wao.
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, asante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini kwa mujibu wa swali nilivyouliza pamoja na majibu ambayo yametolewa ni dhahiri kwamba kwa vijiji ama Kata ambazo amezisema mimi mwenyewe ni shahidi kwamba kuna hela ambazo hazijafika hadi sasa hivi na katika jibu lake la msingi amesema zimefika. Kwa mfano Kata ya Mpata, nimepeleka mabomba zaidi ya milioni 10 lakini Serikali mpaka sasa hivi haijatoa chochote. Mheshimiwa Waziri unaweza ukathibitishia wananchi wa Mpata kwamba hizo fedha zimefika kule? Hilo ni swali la kwanza.
Swali la pili, kuna baadhi ya Kata ya Ntaba, kijiji cha Ilamba wananchi pamoja na wakazi wa eneo la pale wananyang’anyana maji, wananchi na mamba, na zaidi ya wananchi kumi na moja wameshauawa na mamba ama kuliwa na mamba kwa sababu ya kutafuta maji, je, Serikali inatoa tamko gani kwa ajili ya wananchi hawa na ikizingatiwa kwamba kuna mradi ambao umeshafanyiwa upembezi yakinifu tangu mwaka 2008 hadi leo hii kwa thamani ya shilingi milioni 100, haikufanya kitu chochote.
NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, asante.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwa taarifa aliyosema kwamba fedha hazijafika ni kwamba ngoja nita-cross check vizuri katika Ofisi yangu nijue ni nini kilichotokea lakini kikubwa ni nini? Ni kwamba kuna changamoto ya upelekaji wa fedha, siyo mradi huo tu isipokuwa maeneo mengi sana, fedha zimeenda kwa kusuasua na hivi karibuni ndiyo maana Waziri wa Maji juzi juzi alikuwa anazungumza kwamba kutokana na kusuasua kwa kupeleka fedha katika miradi ya maji na miradi hii mingi sasa mingine ilikuwa imesimama, sasa Serikali iliamua kwamba ile outstanding payment ambazo zilikuwa zinakaribia karibuni bilioni 28, kwamba fedha hizi sasa zipelekwe katika maeneo mbalimbali ilimradi wale Wakandarasi walio-demise mitambo waweze kuendelea.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba nikuambia kwamba nitazifuatilia kwa karibu ilimradi kwamba huu mradi lengo letu liweze kufanikiwa na wananchi waweze kupata huduma ya maji.
Lakini sehemu ya (b) ni kwamba kuna changamoto ya wananchi wanakamatwa na Mamba. Kwanza nitoe masikitiko yangu sana katika eneo hilo, kwa sababu kama watu wanaliwa na mamba ina maana kwamba ni changamoto kubwa, tunapoteza jamii ya Watanzania.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba nikiri kwamba nimesikia hili na nakumbuka tulifanya discussion juzi juzi kwamba katika ziara yangu nitakapokuwa nimeenda katika Mkoa wa Mbeya nimesema kipambele katika Jimbo lako la Busokelo litakuwa ni sehemu mojawapo ambayo nitaenda kutembelea ilimradi mambo haya yote kwa ujumla wake tuweze kuyatazama vizuri tukiwa site na kuweze kupanga mipango mizuri, mwisho wa siku wananchi wa Jimbo hili waweze kupata huduma ya maji, kila mtu aweze kujiona ana faraja na nchi yake.
MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, Naitwa Willy Qambalo Mbunge wa Jimbo la Karatu.
Kwa kuwa, matatizo ya maji yaliyoko Busekelo yanafanana kabisa na matatizo ya maji yanayoukumba Mji wa Karatu na vijiji vinavyouzunguka. Na kwa kuwa Mji wa Karatu unakua sana kutokana na shughuli za utalii zinazoendelea katika maeneo ya jirani. Je, ni lini Serikali itamaliza kabisa matatizo ya maji katika Mji wa Karatu na vijiji vinavyozunguka?
NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, ndugu yangu huyu tukiri kwanza Busokelo haifanani na Karatu kwa sababu kule Busokelo kuna mamba, na naamini Karatu hakuna mamba. Lakini kubwa zaidi ni jinsi gani kama Serikali itajielekeza kuhakikisha Mji wa Karatu unapata maji kwanza nikiri kwamba miongoni mwa Miji ambayo Tanzania tunaitegemea katika suala zima la uchumi ni Mji wa Karatu, kwa sababu ni center kubwa sana ya utalii katika nchi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kwamba Serikali kupitia Wizara ya maji katika programu ya pili tunayoenda nayo ambayo imeanza hii Januari, tumeweka kipaumbele katika Mji Mikakati yote ambayo kwanza ina vivutio vya Kitalii, lakini ni source kubwa sana ya uchumi wa nchi yetu kuipa kipaumbele katika suala zima la huduma ya maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikiri wazi kwamba katika suala zima la utalii kama nilivyosema awali, Karatu ni Mji tunaoutegemea sana. Kwa hiyo suala hili tunalilchukua kwa ujumla wake, Wizara ya Maji halikadhalika Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, tutahakikisha jinsi gani tutaipa kipaumbele. Ile miradi ambayo imeanza Singida haijakamilika vizuri, au ni jinsi gani tutumie vyanzo vingine ili mradi tupate maji katika Mji wa Karatu, wananchi wa Karatu waweze kupata manufaa katika nchi yao.
MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, asante sana. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, ningependa kuuliza maswali mado mawili.
Moja ya kero inayowakuta wafugaji wanapokuwa minadani, inatokea mahali mtu amekwenda kuuza bahati mbaya akiwa pale mnadani hajauza mfugo wake, na anapotoka pale anadaiwa ushuru wakati hajapata hiyo fedha. Sasa nilitaka nifahamu kauli ya Serikali juu ya wale wote ambao wanashindwa kuuza mazao ama mifugo yao katika maeneo hayo?
Swali la pili, je, ni kiwango gani ambacho mtu anapaswa kulipa, kwa sababu kuna watu wanatoka mashambani labda ana mahindi wanakwenda nyumbani kwao kuyatunza. Sasa wakikutana na kizuizi, mtu ana gunia mbili, gunia tatu anaambiwa lazima alipe ushuru hata kwenye yale mahindi ya kutumia.
Je, ipi ni kauli ya Serikali juu ya hili jambo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika mazoea ya kawaida watu wengine wanapeleka mazao yao sokoni, lakini kwa bahati mbaya wakifika pale wanakosa kuyauza. Ina maana na concept ya ushuru wa mazao, maana inataka mtu akishauza, yule mnunuzi sasa maana yake anatakiwa alipia ule ushuru. Lakini kama hajauza ukimwambia kwamba yule mkulima sasa aweze kutoa ushuru maana yake unambana mkulima. Na kauli ya Mheshimiwa Rais alipokuwa katika kampeni alizungumza wazi kwanza lengo lake ni kutoa huu usumbufu wa ushuru mdogo mdogo ambao unamkabili mwananchi wa kawaida.
Mheshimiwa Naibu Spika, kikubwa zaidi nawahimiza Watendaji wetu hasa katika Halmashauri, jinsi gani wabainishe kwamba katika maeneo yao kuna watu hawa wa kawaida ambao wanaenda kuuza. Kuna mfanya biashara mkubwa ambaye anakuja kuchukuwa mazao pale site, akishachukua lazima alipie ushuru. Lakini yule mtu anayefanya kazi ya kuchuuza kwa ajili ya maisha yake tu hili ni jambo ambalo ni suala zima kuwaelekeza watendaji wetu katika Halmashauri zetu watafanya vipi kuondoa kero hii kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ni kwa kiwango gani, nadhani suala la pili sikulipata vizuri lakini kikubwa zaidi ni nini. Ni kwamba mifugo yote inayopelekwa pale eneo la mnada, ndiyo maana nimesema sijalipata vizuri swali la pili, tuangalie kwamba kwa sababu sheria ndiyo inaelekeza kati asilimia tatu mpaka asilimia tano, sasa mtu anapoenda kuuza mfano ana ng’ombe wake mmoja, ng’ombe wake wawili, ndiyo nimesema hapa utaratibu mkubwa unaotakiwa ni katika Halmashauri husika. Kwa sababu tunajua Halmashauri nyingine zinategemea asilimia karibuni 70 ya mapato yake katika ushuru wa mazao.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jinsi gani kama Baraza la Madiwani pamoja na Watendaji wao watafanya kuangalia mazingira ya kijiografia katika eneo husika ili kuwasaidia wananchi hali kadhalika kuongeza uchumi katika Halmashauri zao.
MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninamuomba awahakikishie wananchi wa Kata hizo kwa sababu siyo wote ni wakimbizi, ni lini zoezi hilo la naturalization litakamilika ili kusudi nao wapate kutimiza haki yao ya kidemokrasia?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, mchakato pale ulikuwa ni mpana sana, kama alivyosema pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba zoezi lile lilikamilika na kuhakikisha Kata zinapatikana lakini ilikuwa ni baada ya uchaguzi, baada ya hapo kuna zoezi kubwa la integration ambalo linafanyika ambalo lina-involve pesa na awali mchakato uliokuwa unaendelea ni suala zima la kupata fedha kutoka Benki ya Dunia.
Mheshimiwa Spika, lakini kwa sababu Serikali ime-invest vya kutosha kuhakikisha wakimbizi hawa wanakuwepo maeneo haya kipindi chote, maana yake Serikali ya Tanzania ilitumia jukumu kubwa la kiutu na kiubinadamu na resources nyingi sana kuhakikisha wakimbizi hawa wanakuwepo, lakini suala la kuhakikisha unajenga miundombinu ni jambo lina-involve pesa.
Kwa hiyo, Serikali iko katika mchakato kuangalia jinsi gani tutafanya, suala la kujenga structure zikamilike baadaye basi uchaguzi uweze kufanyika, kwamba sasa eneo lile uchaguzi ufanyike rasmi baada ya kuwa na muundo rasmi wa Serikali za Mitaa. Ahsante.
SPIKA: Ahsante sana, tunaendelea na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, swali linaulizwa na Mheshimiwa Mwita Mwikabe Waitara, Mbunge wa Ukonga, kwa niaba yake tafadhali endelea.
MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Naibu Waziri.
Mheshimiwa Spika, ninataka kujua hii Hospitali ya Wilaya ambayo inajengwa hapo Kivule inagharimu kiasi gani kwa sababu mpaka sasa hivi anasema zimeshatoka shilingi milioni 1.9?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, Mkoa wa Dar es Salaam kwa ujumla una idadi kubwa sana ya wananchi na hospitali nyingi zimepandishwa hadhi. Kwa mfano, Hospitali ya Amana - Ilala ambapo wananchi wa Kivule wanakwenda pale, lakini mpaka leo huduma za afya bado ni mbovu sana.
Je, sasa Serikali ina utaratibu gani wa kuhakikisha kwamba hospitali hizi zinazopandishwa hadhi ikiwemo na hii inayojengwa, inakidhi mahitaji ili wananchi waweze kupata huduma ya afya ambayo ni haki yao ya msingi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, ahsante.
Kama alivyosema ni kweli sehemu ya Kivule ina changamoto kubwa sana, ndiyo maana tumeamua ujenzi wa ile hospitali ya Wilaya na kwa miundombinu yote mpaka inakamilika, hospitali ya Wilaya inagharimu takriban bilioni 24, lakini katika zoezi la kwanza ambapo katika bajeti niliyosema kwamba kumetengwa shilingi milioni 900 ya kwanza, na mkandarasai yuko site na ameshaanza stage ya foundation. Mkataba uliosainiwa na Skol Building Contractors Limited utagharimu karibu shilingi bilioni moja na milioni 19.
Mheshimiwa Spika, huu ujenzi maana yake utafanikisha sasa angalau sehemu ya OPD ianze kukamilika, katika sehemu ya pili ni kwamba Hospitali ya Amana imepandishwa hadhi ni kweli, lakini ukiangalia Manispaa ya Ilala ni eneo lina changamoto kubwa sana na ndiyo maana tunajenga Hospitali ya Kivule. Sambamba na hilo kwa sababu Jimbo la Ilala ni pana, kulikuwa na harakati ya kujenga sehemu maalum ya akina mama na watoto katika eneo la Chanika katika kituo cha afya cha Chanika.
Mheshimiwa Spika, tunaishukuru Wizara ya Afya na Serikali kwa ujumla kwamba ni nini kimefanya katika maeneo hayo ni kupandisha vituo viwili vya Pugu pamoja na Chanika, sambamba na hilo maana yake jambo linalofanyika maeneo ya kati ya Ilala ambayo imetanuka kuna zahanati nyingi ambazo nimezisema pale awali ambazo zinafanyiwa ukarabati na zingingine kuhakikisha kwamba vituo vyake vya afya vinafanya kazi vizuri.
Mheshimiwa Spika, kwa nini sasa hii hospitali ikipandishwa hadhi itaweza kufanyakazi vizuri, ndiyo maana katika bajeti ya mchakato wa mwaka huu mtaona kwamba bajeti ya Wizara ya Afya itakuwa imejielekeza kwa kiwango kikubwa kuhakikisha kwamba bajeti ya dawa inaongezeka kwa kiwango kikubwa kukidhi hili ongezeko la watu na ongezeko la mahitaji ya wananchi katika sekta ya afya.
MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kutokana na majibu ya Mheshimiwa Waziri, ni masuala yale yale kwamba tupo kwenye mchakato. Naomba kupata majibu katika maswali yangu mawili.
(a) Ni lini sasa TAMISEMI itakamilisha mchakato wa marekebisho ya sheria hiyo ili Halmashauri zetu ziweze kujipatia mapato yake stahiki?
(b) Ni lini kikao hicho cha wadau kitakwenda kufanyika ili tuweze kuokoa mapato mengi yanayopotea katika sekta hii? Asante.
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kwamba ni kweli kumekuwa na kero kwa Waheshimiwa Wabunge wote katika Majimbo yote kwa sababu minara imeenea maeneo yote.
Mheshimiwa Spika, kila mtu katika Jimbo lake ana mnara na kila mtu anatarajia kukusanya kodi. Lengo ni kuhakikisha Halmashauri zinapata mapato, ndiyo maana ofisi yetu imeona, kwa sababu suala hili linagusa Halmashauri zote, lazima tuwe na mfumo ambao utakuwa muafaka kuhakikisha kwamba fedha zinakusanywa hali kadhalika Halmashauri zinapata fursa ya kukusanya hayo mapato vizuri na ndiyo maana mchakato huo umeshaenda.
Mheshimiwa Spika, bahati nzuri sana kikao cha wadau kimeshakamilika, na jukumu linalofanyika ni kwamba paper itaondoka katika Baraza za Mawaziri, itajadiliwa na itakuja huko. Hata hivyo, tumeenda mbali katika marekebisho ya sheria hii, tunaenda kuangalia suala zima la crop cess, watu wanajua ushuru wa mazao umekuwa ni changamoto kubwa sana.
Kwa hiyo, sheria hii inakutanisha mambo mengi ili mradi Sheria ya Fedha Sura Namba 290 itakapokuja hapa Bungeni, basi iweze kukidhi mahitaji ya Waheshimiwa Wabunge wote katika Halmashauri zao, fedha ziweze kukusanywa na wananchi wapate huduma bora. Asante.
MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri, lakini pamoja na majibu yake Naibu Waziri kwamba hili gari kwenye bajeti ya mwaka 2013/2014 na swali la msingi niliuliza mwezi wa Tisa na kwenye bajeti walisema kwamba wametenga milioni 150 kwa ajili ya ununuzi wa hili gari la wagonjwa wa kule Mgololo, mpaka leo hili gari halijapelekwa. Niliwahi kumuuliza Waziri wa Afya akaniambia kwamba kuna magari matano yamenunuliwa mojawapo litapelekwa kule, lakini mpaka leo halijakwenda. Je, bajeti ya mwaka uliopita ambayo ilitengwa kwa ajili ya hilo gari, hiyo fedha ya shilingi milioni 150 ilikwenda wapi?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, hii gari ni ya msingi sana, kwa sababu itahudumia Kata tatu, kuna ya Kiyowela, Kata ya Idete na Kata ya Makungu. Kule kuna watu wanakaribia karibu 120,000 hivi, akinamama wanapata taabu sana kuna milima, jiografia ya kule ni ngumu sana. Sasa naomba Mheshimiwa Naibu Waziri anithibitishie kwa sababu hii pesa ya Halmashauri haina uhakika, ni lini hii gari hili la wagonjwa litapelekwa Mufindi?
NAIBU WAZIRI WA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikiri wazi kwamba nilifika Mufindi katika Jimbo la Mheshimiwa Mbunge mpaka Mgogolo. Hili ni miongoni mwa Jimbo ambalo lina changamoto kubwa kutokana na jiografia yake ilivyo. Hata hivyo, nipende kumshukuru pia kwa juhudi kubwa anayofanya katika kuhakikisha mambo yanakwenda katika Jimbo lake kwa sababu katika miaka mitano iliyopita alikuwa akipigania mambo mbalimbali katika maeneo yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala la msingi la kwanza aliposema bajeti ya mwaka ilitengwa lakini haikupatikana ni kweli, na nyinyi mnafahamu sio bajeti ya ambulance peke yake, isipokuwa miradi mingi sana ya maendeleo katika kipindi kilichopita, imekumbwa na changamoto kubwa sana hasa ya upelekaji wa fedha. Maombi haya yalikuwa ni katika maombi maalum, hivyo ni imani yangu kwamba katika bajeti ya mwaka huu sasa kwa vile jiografia yake inajulikana, Ofisi ya Rais - TAMISEMI tutaweka kipaumbele kuhakikisha gari hilo linapatikana. Kikubwa zaidi katika hayo yote maana yake maombi maalum wakati mwingine yana changamoto kubwa sana na sana sana zinalenga katika collection ya mapato.
Mheshimiwa Naibu Spika, basi niwaombe Waheshimiwa Wabunge wote tushikamane kwa pamoja kuisaidia nchi yetu ili tupate mapato ya kutosha, yale maombi maalum yote tuliyoyapeleka, Serikali iweze kuona ni jinsi gani yatayafanyiwa kazi.
Sehemu ya pili, ni kwamba ni lini gari litapatikana, nimesema kwamba, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa sababu tunaguswa na hili, katika uongozi wetu wa sasa tutapambana kwa kadri iwezekanavyo. Ndugu yangu wa Mufindi tujitahidi kwa pamoja Mungu akijalia tutapata gari, naomba amini Ofisi yako.
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pia nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nasikitika kwamba, pesa hizi ni za bajeti ambayo tunakwenda kumalizia, naomba nijue ni lini pesa hizi zitatoka ziende zikafanye kazi hiyo kwa wananchi?
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali langu la pili, kwa uzoefu unavyojionesha pesa hizi zinaweza zikatoka mwisho wa bajeti yaani Juni 30. Je, pesa hizi zinapotoka zinakwenda wapi?
NAIBU WAZIRI WA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, pesa hizi ni za bajeti ya mwaka huu 2015/2016, lakini kama nilivyojibu awali, miradi mingi sana ya maji katika kipindi hiki toka tunapotoka katika mwaka wa uchaguzi mpaka hivi sasa, ni miradi mingi sana siyo katika Jimbo la Kavuu peke yake, isipokuwa miradi mingi sana imekuwa ikisuasua kutokana na upelekaji wa fedha. Hata hivyo Serikali imefanya juhudi kubwa sana mara baada ya kukusanya mapato makubwa Serikalini kuhakikisha kwamba maeneo mbalimbali ambayo miradi ilikuwa imesimama sasa ianze kufanya kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri kwamba Wizara ya Maji kwa kupitia Wizara ya Fedha, maeneo mbalimbali ambayo miradi mingine ilikwama sasa hivi imeshaanza kufanya kazi. Imani yangu kubwa iliyoko ni kwamba Ndugu yangu Mbunge ambaye najua siku zote ulikuwa ukipambana Jimboni kwako katika maeneo haya, kwa kipindi hiki tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo, Serikali iweze kupeleka maeneo yote ambayo miradi ilisimama ilimradi, miradi ikamilike katika mwaka huu wa fedha,
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, hata katika ripoti za Mkaguzi wa Serikali kuna miradi mingine inakwama kwa sababu fedha zinafika mwishoni. Kwa hiyo, niwaombe hasa ma-engineer wetu kule site kwamba, wajipange vizuri kiasi kwamba pesa hii itakapofika wahakikishe usimamizi unakwenda kwa haraka ilimradi wananchi wa Jimbo la Kavuu waweze kupata huduma za maji katika maeneo yao.
MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Niliuliza swali kwa niaba ya Mheshimiwa Obama mimi mwenyewe naitwa Dkt. Hadji Mponda.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunashukuru Serikali kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
La kwanza, kwa kuwa mkataba kati ya Halmashauri ya Buhigwe na ile Hospitali ya Mission umesitishwa kwa sababu ya fedha, sasa ni nini Serikali wana njia mbadala ya kutoa huduma za afya bure kwa makundi haya ya wazee na watoto?
Swali la pili, mkataba kama huo huo uliofanyika Buhigwe na mwaka 2011 - 2013 ulifanyika katika Wilaya ya Ulanga ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga waliingia mkataba na Hospitali ya Lugala, ni Hospitali ya Mission, lakini mkataba ule ulidumu kwa muda wa miezi sita mpaka leo umesitishwa. Sasa swali langu ni lini Halmashauri hiyo ya Malinyi pamoja na TAMISEMI wataufufua mkataba ule kwa kurudisha huduma hizi bure kwa makundi haya mawili ya wajawazito na watoto chini ya miaka mitano?
NAIBU WAZIRI WA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza katika sehemu ya (a) ni kwamba nilivyosema katika majibu yangu ya msingi, mkataba huu haujasitishwa, kilichotokea ni kwamba kuna fedha za quarter ya kwanza ambayo imekuja mpaka mwezi Disemba ambapo tunarajia sasa kuna pesa zingine zitakuja mpaka hivi sasa na nimesema pale mwanzo kwamba matarajio zile pesa zikishafika Halmashauri, basi lazima zielekezwe katika sehemu hizi tatu ilimradi wananchi waendelee kupata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ya pili, kwa sababu hili ni suala la Hospitali ya Lugala Mission sijakuwa na taarifa nayo za kutosha, lakini nina imani kwamba mikataba yote kilichozingatiwa ni kwamba, inakwenda kutekelezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwezekano ni kwamba naomba nishauri hasa Baraza la Madiwani hasa katika vikao vyao vya Kamati ya Fedha. Lazima fedha zinapokuja, wasimamie fedha hizi maelekezo yake ni wapi, kwa sababu sehemu zingine inawezekana fedha zikapita lakini watu katika kufanya maamuzi wakaelekeza pesa sehemu ambazo siyo muafaka mwisho wake wakati mwingine mikataba inavunjika wakati kumbe kuna watu hawajatimiza majukumu yao. Imani yangu ni kwamba, kila mtu atatimiza wajibu wake ilimradi wananchi wetu waweze kupata huduma bora kwa ajili ya kuhakikisha afya ya mama na mtoto inaimarika katika nchi yetu.
MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, katika Kituo cha Afya cha Nzela ambacho kimekuwa kikihudumia wananchi wa Jimbo la Geita na ni kikubwa na tayari kimekwishafanyiwa maamuzi na Halmashauri ya Wilaya. Je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kuambatana na Mheshimiwa Mbunge kwenda katika kituo hicho na kuona kama kinafaa kufanywa kuwa Hospitali ya Wilaya?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, baada ya Hospitali ya Geita ambayo ndiyo ilikuwa Hospitali ya Wilaya kuwa Hospitali ya Mkoa, hivi sasa kuna vifaa vingi ambavyo zimeletwa na Mkoa lakini hakuna Madaktari na watumishi mbalimbali. Je, lini Mheshimiwa Waziri atapeleka watumishi na watalaam katika Hospitali ya Wilaya ya Geita?
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, nipende kuwapongeza Wabunge wote wa Geita kwa kazi kubwa waliyoifanya kwa kushirikiana na Geita Gold Mine (GGM) kwa kuhakikisha kwamba Hospitali yao ya Wilaya ya Geita imekuwa na structure ambayo inarahisisha sasa kufanya hospitali hiyo kuweza kutoa huduma bora. Nishukuru sana kwa sababu tulikuwa na Makamu wa Rais pale na Waziri mwenye dhamana wa sekta ya afya na kushuhudia hospitali ile kukabidhiwa vile vifaa kwa kweli tunawapongeza sana kwa kazi kubwa mliyoifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, jinsi gani ya kuambatana nami, naomba nikiri wazi mchakato huu wa Bunge la Bajeti ukiisha nilikuwa na ziara maalum ya Mkoa wa Geita, hili litakuwa ni miongoni mwa eneo moja ambalo tutakwenda kulifanyia kazi kwa pamoja. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, suala zima la kupatiwa wataalam, naomba niwajulishe ndugu zangu si muda mrefu mtasikia sasa Wizara ya Afya inatoa idadi ya waajiriwa katika sekta hiyo na Hospitali yetu ya Geita itakuwa ni kipaumbele kwa sababu ina hadhi ya kutosha ili wananchi wa Mkoa wa Geita wapate fursa kubwa ya kupata matibabu katika Mkoa wao.
MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Nina swali moja dogo tu. Wilaya nyingi mpya za Tanzania hazina Hospitali za Wilaya ikiwemo Wilaya ya Chemba ninakotoka mimi. Je, Serikali itatuhakikishia ndani ya Bunge hili kwamba katika bajeti inayokuja wametenga fedha kujenga hospitali mpya katika Wilaya zote mpya Tanzania?
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, ni kweli na naifahamu Chemba, kaka yangu Mheshimiwa Nkamia tumeshaongea sana kufika Chemba pale kuangalia siyo suala zima la afya, lakini na mambo mengine. Ninavyojua ni kwamba katika bajeti ya mwaka huu ambayo tutakuja kuisoma wiki ijayo ina mikakati mbalimbali katika halmashauri mbalmbali. Halmashauri zingine wamejielekeza katika kuboresha vituo vya afya, wengine wamejielekeza katika Hospitali zetu za Wilaya, lakini wengine wamejielekeza katika Hospitali za Mkoa.
Mheshimiwa Spika, katika hili ninavyojua wazi kwamba michakato yote aidha ya ujenzi wa zahanati, Hospitali ya Wilaya au ya Mkoa, vikao husika kwanza vinaanza na mchakato huo. Imani yangu kwamba na wenzetu katika Jimbo la Chemba jambo hilo watakuwa wameliangalia kwa jicho la upana zaidi. Katika haya maana yake Serikali sasa itafanya juhudi kubwa kupeleka resources kutokana na mipango iliyopangwa kutoka katika Halmashauri ili mradi wananchi wetu waweze kupata huduma katika maeneo hayo.
MHE. SALMA M. MWASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini nina swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na mazoea ya kuchelewa kurekebishwa kwa sheria hizi ndogo ndogo na Serikali Kuu na badala yake kwa zile Halmashauri ambazo zinajitahidi zenyewe hasa zikiwemo za mijini, zinakuwa zinanyang’anywa mamlaka yake na Serikali Kuu. Kwa mfano, Kodi ya Majengo (Property Tax) kupelekwa TRA na tume-prove kwa miaka miwili ya nyuma TRA ilishindwa kabisa kukusanywa kodi hii; na sasa tunaambiwa kodi hii inaenda tena TRA. Je, ni lini hasa Serikali Kuu itaacha kuingilia mamlaka au kunyang’anya mamlaka ya Serikali za Mitaa ili ziweze kujitegema?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli wakati mwingine Marekebisho ya Sheria yanachelewa lakini mara nyingi sana yanafanyika mara baada ya mahitaji mahususi yanapotokea. Kwa sababu tuelewe kwanza katika suala zima la Serikali za Mitaa kuna maeneo matatu; kuna Sura Namba 287, 288 na 290. Sura ya 290 ndiyo inalenga hasa katika ukusanywaji wa kodi na ushuru mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, ajenda ya kusema kwamba ni lini sasa Serikali itaanza kuzuia suala zima la kunyang’anya mamlaka ya Serikali za Mitaa, kutoa kodi kwa mfano katika kodi ya majengo; Serikali sasa hivi tuko katika Serikali ya Awamu ya Tano, naamini Bunge hili ndiyo Bunge ambalo mara ya kwanza tunajadili bajeti yetu katika kipindi hiki cha Awamu ya Tano na ninaamini kwamba mjadala huu wa bajeti utakapofika katika suala zima la Wizara ya Fedha, mwisho katika Wizara ya Fedha kuna ile Sheria ya Fedha ya mwisho pale ndio tutapata way forward tunapokwenda ni wapi. Lengo kubwa la Serikali ni kuhakikisha mapato yanakusanywa katika Serikali yake ili mradi mambo yaweze kuendelea vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwahiyo, nina imani tutakapofika katika suala zima la Sheria ya Kodi ambayo mwisho wa siku Waziri wa Fedha ata-table hapa mezani, tutakuwa tumefika mahali muafaka na kupewa maelekezo ya kutosha nini tunataka tufanye. Lengo kubwa ni kwamba Serikali iweze kukusanya kodi ya kutosha na miradi ya maendeleo iweze kufanikiwa.
MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, lakini ni aibu kwa Serikali ya Chama cha Mapinduzi. Majibu hayo ni ya Arumeru na siyo ya Mkoa wa Rukwa. Halafu mnajiita Serikali ya kazi tu, hapa! Swali hili sijaleta jana, lakini kwa sababu madai ya walimu yako nchi nzima, nitauliza maswali madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, Serikali ina mkakati gani wa kuwalipa madeni kwa wakati walimu ambao wamekuwa wakilia kila siku na ni malalamiko ya kila siku!
Swali la pili, mpaka sasa walimu wanadai fedha walizosahihisha mitihani ya mwaka 2015 ya kidato cha nne, ni lini Serikali itawalipa walimu hawa na kuwatendea haki kama wafanyakazi wengine wa nchi hii?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba niweke wazi, katika mchakato wa madeni ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI pale ina maswali zaidi ya takriban 15 ambayo yote moja kwa moja yanalenga katika suala zima la madai ya walimu na yote yanafanana fanana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwahiyo, kwa concern ya Mheshimiwa Mbunge siyo kwamba Serikali haiko makini, isipokuwa jambo hili limekuwa ni kilio karibuni kwa Wabunge wote. Kwa hiyo, suala la msingi ni jinsi gani tutafanya kutatua tatizo hili tuweze kulimaliza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati uliopo, nilisema Serikali kwa awamu ya kwanza ilishalipa haya madeni, lakini naomba niwambie, katika madeni haya katika sehemu nyingine ni fake. Tunafahamu sasa hivi hata katika suala zima la mishahara hewa, mmeona jinsi ambavyo kuna matatizo makubwa, wengine wanaingiza ilimradi waweze kupata pesa. Kwa hiyo, Serikali imejipanga na ndiyo maana uhakiki umefanyika. Katika jibu langu la msingi nimesema kwamba kuna madeni yameshaanza kulipwa na ndiyo maana tulichokifanya ni kuelekeza Halmashauri zote zifanye uhakiki kwa haraka ilimradi walimu waweze kulipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tukiri kwamba madeni haya hata tukilipa lazima yataendelea kwasababu kila siku walimu wanahama na kila siku walimu wanaenda likizo. Jambo la msingi ni kwamba madeni yanapojitokeza, inapaswa sasa watu waweze kulipwa haki zao wanazostahili.
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, tunatambua kwamba Serikali ina mzigo mkubwa sana kuhusiana na masuala ya madai ya walimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuuliza kwamba kuna zaidi ya 3,000 ambao wamestaafu mwaka 2014 na mwaka 2015, mpaka sasa hivi hawajalipwa mafao yao. Je, ni lini Serikali angalau mafao ya watu ambao wameshastaafu tayari wanahitaji walipwe warudi majumbani kwao watalipwa pesa hizi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna Walimu wamestaafu, nami naomba nikiri kwamba hata katika Ofisi yangu kuna baadhi ya walimu walifika pale moja kwa moja kuleta madai yao. Kwa mfano, kuna mwalimu mmoja alikuwa akifundisha pale Bahi. Walimu wengi waliokuwa na changamoto, walikuwa katika Mfuko wa PSPF.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, Serikali imetoa maelekezo katika Mfuko wa PSPF kwamba haraka iwezekanavyo walimu wote waliokuwa wanadai, wahakikishe stahili zao zimelipwa, kwa sababu Serikali imefanya mchakato mkubwa sana kuiwezesha PSPF katika madeni iliyokuwa inadai kwamba iweze kupata mafungu ya kutosha ilimradi PSPF iendelee kulipa madeni na Serikali imetimiza hilo.
Sasa naomba nitoe agizo kwamba Mamlaka zinazohusika katika hii mifuko zihakikishe kwamba Walimu wote ambao waliokuwa wanadai waweze kupata stahili yao. Siyo jambo jema kutokuwalipa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe mfano, mwalimu mmoja kutoka pale Morogoro alizimia kabisa kwa kudondoka kwasababu hakupata mafao yake. Ndiyo maana tumetoa maelekezo mazito na ni imani yangu kwamba Mfuko wa PSPF kwa sababu umeshaanza kupata mafungu yale yaliyokuwa yanadai Serikalini, iwalipe walimu wetu ilimradi waendelee kuishi maisha mazuri.
MHE. EMMANUEL P. JOHN: Naomba kuuliza ni lini tunaweza kupata fedha za nyongeza kwa ajili ya mafuta ili watu hawa waweze kupata huduma ya kliniki kwenye maeneo hayo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama nilisema katika jibu langu la msingi kwamba, ni kweli Halmashauri ya Kiteto ina changamoto kubwa sana kijiografia na hili tunakiri wazi na ndiyo maana hata bajeti ukiipeleka wakati mwingine inakutana na changomoto kubwa sana! Kwa hiyo, maelekezo yetu kama Ofisi ya Rais TAMISEMI ni kwamba niwashauru wananchi wa Kiteto hasa ndugu zetu wa Halmashauri Wakurugenzi na timu yake wahakikishe kwamba wanaweka mkazo wa kutosha katika kipindi hiki cha mpito kabla hatuaanza mwaka mpya wa bajeti. Wafanye udhibiti wa kutosha katika own source ili wakikusanya mapato ya ndani, japo kipindi hiki kilichobakia cha kumaliza mwaka wahakikishe kwamba wanakusanya fedha nyingi ili gari muda wote ziweze kufanya kazi na akina mama waweze kupata huduma. Lakini nikiri ni kweli Halmashauri ya Kiteto ni moja ya Halmashauri ambazo tunatakiwa tuziangaliye karibu. Ahsante!
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuuliza swali la nyongeza, kwa kuwa Kituo cha Afya cha Mlalo ndiyo kituo pekee kinachofanya huduma ya upasuaji katika Jimbo la Mlalo.
Je, ni lini Serikali itakipatia kituo hiki gari la wagonjwa ili pale ambapo upasuaji unakwama waweze kupelekwa Hospitali ya Wilaya ya Lushoto? Ahsante!
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshmiwa Naibu Spika, ni kweli Kituo cha Afya cha Mlalo kina changamoto ya gari. Lakini wiki iliyopita nilizungumza kwamba wakati mwingine hizi changamoto ni kweli, naomba ikiwezekana tuweke priority katika mchakato wa bajeti. Mheshimiwa Shangazi kwa sababu najua ni mfuatiliaji sana katika maeneo yako haya, tukiri kwamba mwaka huu Mlalo hawajapanga hii bajeti kwa ajili ya ununuzi wa gari, lakini naomba niwasisitize kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI itakuwa nanyi kwa karibu kuhakikisha katika bajeti ya mwaka wa fedha unaokuja Mlalo inapewa kipaumbele au tukipata fursa yoyote ya upatikanaji wa gari basi Mlalo iwe kipaumbele kwa sababu eneo lake na jiografia yake mpaka kuja huku Mjini changamoto yake ni kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba tulichukue hilo kama Ofisi ya Rais TAMISEMI tukishirikiana nanyi kwa pamoja kuhakikisha watu wa Mlalo baadaye wapate gari la wagonjwa ili akina mama na watoto waweze kupata huduma ya kutosha.
MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba nimuulize swali dogo tu la nyongeza. Kwa kuwa, watumishi wetu hawa inawalazimu kuishi Wilaya nyingine ya Bariadi ambapo kuna umbali wa Kilometa 100 kwenda na kurudi kila siku.
Je, Serikali haioni kuna umuhimu wa kuharakisha makazi haya ili watumishi hawa waishi katika maeneo husika?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali inaona hilo, ndiyo maana hata Halmashauri yenyewe ya Itilima katika mkataba wao waliosaini na National Housing, bahati mbaya mkataba ule ulikuwa haujahusisha Ofisi ya Rais -TAMISEMI wala Ofisi ya Mkuu wa Mkoa pale katika Ofisi ya RAS na ndiyo maana Ofisi ya Rais - TAMISEMI iliona kwamba licha ya mapungufu yaliyokuwepo lakini ofisi iweze kutoa kile kibali kwa mkataba ule. Hivi sasa Ofisi ya Rais - TAMISEMI imeshatoa kibali, na kwa sababu fedha tayari ninazo na kibali kimeshapatikana, imani yangu ni kwamba ujenzi kupitia Shirika la Nyumba utakamilika haraka iwezekanavyo ili kuondoa kero ya watumishi ambao wanapata taabu kutoka katika Halmashauri moja kwenda Halmashauri nyingine.
MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Wilaya ya Bukoba Vijijini wanategemea Wilaya yao iliyoko Bukoba Mjini na ina umbali mkubwa sana, kata zake ziko mbali sana kuja kufika Bukoba Mjini, ni lini Serikali itaona umuhimu wa watu wa Bukoba Vijijini kupata Wilaya yao karibu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika hili tumelichukua, lakini mchakato wa Wilaya, mchakato wa Halmashauri upo na una taratibu zake. Mimi naomba niwahimize ndugu zangu wa Bukoba na Mheshimiwa Mbunge hapa nadhani katika hili atakuwa amejipnga vyema, tufuate ule mchakato wa kawaida, tupitishe katika Halmashauri zetu, tupitishe katika vikao vya DCC, RCC, mwisho wa siku ikifika katika Ofisi ya Rais -TAMISEMI jukumu letu kubwa ni kuweza kuangalia matakwa ya jamii na kuangalia mahitaji ya msingi yakiwa yamekamilika basi tutamalizia hilo zoezi. Ahsante sana.
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.
Kwa kuwa Wilaya ya Kilolo ilipata kuwa hadhi ya Wilaya toka mwaka 2002 lakini majengo mengi katika Wilaya bado hayajakamilika, kama Hospitali ya Wilaya bado wanatumia Hopitali ya Mission, Makao Makuu ya Polisi bado hayajajengwa kwenye Wilaya yake na vilevile Mahakama bado hakuna…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa naomba uulize swali!
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, je, huwa vigezo gani vinatumika katika kuweka mipango kujenga hizi Wilaya? Kwa sababu Wilaya za zamani bado hazijatimiziwa majengo yote na zinaanzishwa Wilaya mpya, nilitaka nijue vigezo gani vinatumika?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwamba miundombinu ya Wilaya ya Kilolo bado haijakamilika, siyo Wilaya ya Kilolo peke yake isipokuwa ni Wilaya mbalimbali, vipaumbele vinavyotumika kwanza mazoezi yote yanaanza katika mchakato wa bajeti, na ndiyo maana mwaka huu ukiangalia tuna karibu Wilaya zipatazo 44, hizi ni Halmashauri na Wilaya mpya mbalimbali ambazo tumezipa fedha.
Hali kadhalika tunaangalia upungufu katika maeneo mbalimbali. Imani yangu kubwa ni kwamba suala la Kilolo limesikika na kwa sababu tuna Wilaya mpya na Halmashauri nyingine tunaendelea katika ujenzi wa miundombinu, tukifika katika mafungu yetu ya Mikoa utakuja kubainisha kwamba jinsi gani kila Mkoa katika mafungu yake yameweza kuelekezwa. Ile sehemu ambapo miundombinu haijakamilika lakini Wilaya ambazo ni mpya tunaanza kuziasisi tena upya, jinsi gani tume-allocate funds katika mwaka huu wa fedha ili tuweke hali halisi ya kuhakikisha kwamba wafanyakazi katika maeneo hayo waweze kufanyakazi katika mazingira rafiki.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA(MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE): Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana yaliyotolewa na Naibu Waziri Jafo, nilitaka tuelewane kwenye jambo hili la uanzishaji wa maeneo mapya ya utawala.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili ni gumu na sote hapa tunafahamu kwamba maombi haya ya kuanzisha haya maeneo yanatokana na mahitaji ya wananchi. Lakini ni sisi wenyewe kwenye maeneo yetu ndiyo huwa tunaanzisha haya. Kwa kuwa maombi haya yanakuja mengi na wakati mwingine Serikali siyo rahisi sana kupata fedha kwa mara moja kujenga mahitaji yote ya Makao Makuu ya Halmashauri au Wilaya ni lazima tuvumiliane. Ni lazima tuvumiliane twende kidogo kidogo na ndiyo maana Serikali imekuwa ikitenga milioni 500, tunaamini tukifanya hivyo kwa miaka mitano, miaka minne, tunaweza tukakamilisha majengo yote.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuvumiliane kwa sababu Wabunge wengi wanakuja kuniona wakiwa na maombi mapya ya maeneo mengine ya utawala, sasa tukianza kuulizwa maswali kama kwa nini tunakuwa hatujajipanga na tunayaanzisha, kuna wengine hapa mmeahidi huko mlikotoka kwamba sisi tutahakikisha hapa panakuwa Mji Mdogo, sisi tutahakikisha tunakuwa na Halmashauri, sisi tutahakikisha tunakuwa na Wilaya.
Sasa tuvumiliane na tuende pamoja na tuamini kwamba kadri Serikali itakapopata uwezo tutakuwa tunafanya, lakini jambo hili ni gumu.
MHE ABDALLAH N. MAFTAHA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
(a) Kwa kuwa Mtwara Mjini kila kipindi cha masika maji huwa yanajaa na mafuriko yanatokea na Serikali inatoa kilo 16 za unga, je, Serikali iko tayari hivi sasa kusema tarehe ngapi itaanza ujenzi wa miundombinu Mtwara Mjini?
(b) Kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri kadanganywa katika jibu lake nililiouliza kwamba Barabara ya Mikindani- Lwelu itajengwa lini kwa kiwango cha lami, yuko tayari hivi sasa kufuatana na mimi kama Mbunge ili aweze kujionea mwenyewe kwamba kadanganywa? Ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la lini barabara hii itajengwa nadhani katika jibu langu la msingi nimesema. Katika Mradi ule wa Strategic City ambapo lengo lake kubwa ni kuhakikisha kwamba tuna maeneo mbalimbali ya miji ambayo imejengwa miradi hii, hata ukiangalia pale Tanga, ukiangalia Mbeya ukiangalia Arusha, huu ndiyo mpango mkakati, hivi sasa tunakwenda hata katika Jiji la Dar es Salaam. Eneo hili nimesema kwamba mchakato wake sasa uko katika hali ya manunuzi, lengo ni kwamba bajeti hii sasa mchakato utakapokamilika maana yake miundombinu inakwenda kujengwa. Lakini kusema kwamba nimedanganywa au vipi nitafika kule Mtwara, naomba nikwambie Mheshimiwa Mbunge, siyo Mtwara peke yake, nitahakikisha maeneo yote, ikiwemo na Mtwara niende nikakague maeneo ya field, hii ndiyo kazi kubwa tumekuwa tukiifanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu ni kuweza kufika kila maeneo kubaini changamoto mbalimbali na hasa katika kipindi hiki mvua inanyesha, maeneo mengi sasa hivi yameharibika. Taarifa ya habari pale ukiangalia jana Kyela, ukiangalia Morogoro na maeneo mbalimbali yameharibika. Kwa hiyo, ni jukumu la Ofisi hii, kufika kila mahali kubaini uhalisia wa eneo lile wananchi waweze kupata huduma inayokusudiwa na Serikali yao.
MHE.ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, asilimia 20 ni fedha ndogo sana inayopelekwa kijijini na kama wataamua kumlipa Mwenyekiti wa Kijiji, Serikali ya Kijiji haitafanya kitu chochote kingine. Je, Serikali haioni sasa ni muda muafaka wa kubeba jukumu hili la kuwalipa Wenyeviti wa Vijiji?
Swali langu la pili, kutokana na umuhimu sasa wa kundi hili na malalamiko yaliyopo kila kona nchini Serikali sasa haioni ni muda muafaka wa kutoa waraka maalum ambao utatoa maelekezo kwa mamlaka ya Serikali za Mitaa kuhusu malipo ya Wenyeviti hawa na kuweka kiwango cha chini cha posho hiyo, badala ya kila Halmashauri kutekeleza jinsi wanavyoona wao inafaa.
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ukiangalia kwa tathmini, maeneo mbalimbali posho hizi huwa hazilipwi na hoja ya Mbunge ni kwamba asilimia 20 ni ndogo. Ina maana ukiirejesha Kijijini, ikimlipa Mwenyekiti wa Kijiji mwisho wa siku ni kwamba fedha ile haitatosheleza hata kufanya kazi zingine za vijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu Serikali za Mitaa safari hii ndiyo maana tumeweka Specification katika bajeti ya mwaka huu. kila Halmashauri wakati ikipitia mchakato wa bajeti tuione inakidhi jinsi gani itahakikisha mapato yake ya ndani kwa kupitia vyanzo mbalimbali ili mwisho wa siku iweze kuhakikisha kwamba inapeleka fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana tumesisitiza kuanzia Julai Mosi lengo letu kubwa ni kuhakikisha kwamba hili jambo tunalolifanya, jinsi gani kila Halmashauri iweze kukusanya pesa za kutosha. Lengo ni kwamba Wenyeviti wa Vijiji waweze kupata posho, hali kadhalika pesa nyingine iende katika shughuli zingine za Maendeleo ya Kijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili juu ya kupanga kiwango maalum, ni kweli. Sehemu zingine wanalipa sh. 20,000, sehemu nyingine wanalipa sh. 10,000, tutaangalia lakini, tutafanya utafiti wa kutosha kuona jinsi gani hii hali iende sawasawa. Kwa sababu tunajua wazi kwamba kila mtu hapa katika Bunge hili anategemea kazi ya Mwenyekiti wa Kijiji au Mwenyekiti wa Mtaa katika kufanikisha shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwa ni sambamba na mikutano yetu ambayo tunaenda kuifanya katika Jumuiya hizo.
MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri wa TAMISEMI kuhusu swali langu, nina swali la nyongeza.
Pamoja na jitihada na changamoto walizonazo na kuhakikisha kwamba masomo haya yanapatikana katika maeneo yetu ya Rukwa na hasa katika Mikoa yetu ya pembezoni. Kwa kuwa tumechelewa kupata elimu hii na speed ambayo wanakwenda nayo naona kana kwamba haitaweza kuleta mafanikio mazuri kwa mikoa yetu ya pembezoni. Swali langu dogo napenda kuuliza kwa niaba ya Mkoa wa Rukwa, ni lini sasa Wilaya ya Nkasi na Wilaya ya Kalambo masomo hayo yatafikishwa kwani Makao Makuu ya Wilaya hizi umeme umekwishafika?
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tukiri kwamba suala la kompyuta sasa hivi na elimu ya TEHAMA ni jambo la msingi sana kama tunataka twende katika maendeleo ya kasi. Tumejielekeza sasa hivi, kama jibu langu la msingi lilivyosema kwamba, tutatumia kila liwezekanalo kuhakikisha tunawezesha vijana katika shule hizi kupata elimu hii ya kompyuta.
Suala la Nkasi na Kalambo ni kweli, katika maeneo mbalimbali ambayo tunataka tuyape nguvu hasa ukiangalia mkoa huu una changamoto kubwa sana, jambo hili hata Mheshimiwa Keissy na Mbunge wa Viti Maalum huwa eanalizungumzia sana, siyo hilo tu na mambo mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, naomba nieleze wazi katika michakato ambayo tutaifanya Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kwa sababu Mkoa wa Rukwa ni Mkoa wenye changamoto kubwa sana, tunaita mikoa ya pembeni, tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo katika program zetu Wilaya hizi tuwape kipaumbele, kwa sababu maeneo mengine ya mijini kama vile Dar es Salaam, Arusha na Mikoa mingine ni rahisi zaidi vijana ku-access mambo ya kompyuta kuliko mikoa ya pembezoni. Kwa hiyo, Ofisi ya Rais, TAMISEMI itaupa kipaumbele Mkoa wa Rukwa na hasa katika Wilaya ya Nkasi na Wilaya ya Kalambo.
MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jibu zuri alilotoa. Pamoja na jibu hilo, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Kwanza, Hanang ni Wilaya ya pili kuwa na CHF iliyoboreshwa na CHF hii iliyoboreshwa haitaweza kunufaisha wananchi kama hakutakuwa na dawa za uhakika. Je, Serikali haioni ni vizuri pamoja na CHF iliyoboreshwa kuwe na duka la MSD?
Pili, Wilaya ya Hanang ina upungufu wa Wodi za akina mama na watoto na nimeshukuru sana kuona kwamba wodi ambayo italaza wanawake 16 inajengwa, lakini Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri kwamba ni wanawake 200. Je, kuwa na wodi itakayolaza wanawake 16 itatosheleza mahitaji hayo?
Pamoja na hivyo, naomba Serikali ione umuhimu wa Wilaya ya Hanang ambayo imezungukwa na Wilaya nyingi kuwa na wodi za kutosheleza akina mama kulazwa.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, kwanza siyo CHF peke yake iliyoboreshwa kwa Halmashauri ya Hanang, lakini kubwa zaidi napenda kumpongeza Mbunge huyu kwa sababu katika michakato yao ya kuhakikisha kwamba huduma ya afya inaimarika huko Hanang kwamba japo wana vituo vya afya vinne, lakini sasa hivi wanaendelea na ujenzi wa vituo vya afya sita. Kwa hiyo, naomba nimpongeze sana katika hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kweli tumesema kwamba sasa hivi dawa zinapatikana kule Kilimanjaro na lengo ni kwamba kuhakikisha maduka ya dawa haya yanapatikana kila eneo; nilisema pale awali, tatizo kubwa ni changamoto ya bajeti, lakini nadhani kwa kadri tunavyokwenda, tutaangalia jinsi gani tutafanya kila maeneo maduka ya madawa haya yaweze kupatikana ilimradi kuwapelekea wananchi huduma kwa karibu zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la wodi ya wazazi, ni kweli kwamba ile haitoshelezi, lakini watu wanasema angalau tuna sehemu tumeanza. Sasa hivi kuna wodi ya wazazi ndani ya kipindi hiki cha mwaka 2016 na wodi ile itakamilika ambayo itakuwa ina uwezo wa kuchukua akina mama 16.
Lengo la Serikali ni kwamba tunatafuta fursa zote zinazowezekana ili mradi eneo lile ambalo population yake ni kubwa zaidi, kuhakikisha kwamba tunapata fursa mbalimbali za kuongeza nguvu angalau kuhakikisha wodi hizi zinaongezeka. Siyo Hanang peke yake, isipokuwa Tanzania nzima changamoto za wodi zimekuwa ni kubwa, lakini ni jukumu la Serikali kuangalia tunafanya vipi sasa ili mradi huduma ya afya iweze kuimarika na hususan tukiangalia Bajeti ya mwaka huu ya Wizara ya Afya ambayo itakuja, Waziri atakuja hapa kuelezea jinsi gani bajeti imejielekeza sasa katika miradi ya maendeleo kwa kiwango kikubwa sana ukilinganisha na pale awali.
MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitoe masikitiko yangu kwamba Serikali haina takwimu sahihi ili kuweka kumbukumbu vizuri, Ukerewe tuna zahanati 29 na vituo vya afya vitatu. Kwa kuwa, suala la kupatikana kwa wataalam kwenye kituo cha afya cha Bwisya limekuwa ni la muda mrefu, niiombe sasa Wizara au Serikali kwa ujumla itoe commitment kwa sababu akinamama wengi sana wanapoteza maisha kwenye eneo lile, lini hasa ufumbuzi wa tatizo hilo utapatikana na kituo hiki kianze kutoa huduma kwa wananchi wa Ukerewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Halmashauri miaka miwili iliyopita ilijitahidi kujenga kituo cha afya cha Nakatunguru ili kupunguza msongamano wa wagonjwa kwenye hospitali ya Wilaya ya Ukerewe, lakini kituo hiki bado hakijaanza. Je, Serikali sasa iko tayari kutoa vifaa na wataalam ili kituo hiki kiweze kuanza kutoa huduma na kwa maana hiyo kupunguza msongamano wa wagonjwa kwenye hospitali ya Wilaya ya Ukerewe?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni wazi tunaelewa jiografia ya Ukerewe kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge na kama nilivyosema katika jibu langu la awali ni kweli, jiografia ya Ukerewe ina changamoto kubwa sana na Ukerewe tunaifananisha na Rufiji ambapo kuna deltas mbalimbali kiasi kwamba huduma za kijamii zinakuwa ni ngumu. Mheshimiwa Mbunge najua kwamba, siyo huduma ya afya peke yake, hata huduma ya elimu ina changamoto kubwa katika visiwa vile. Kwa hiyo, Serikali ina kila sababu ya kuangalia ni jinsi gani tunaweka kipaumbele katika visiwa vya Ukerewe ili hali ya kiafya iendelee vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala la upatikanaji wa wataalam, naomba nikwambie kwamba sasa hivi tuko katika mchakato na siyo muda mrefu sana tutaajiri wataalam. Niwashukuru sana watu wa Ukerewe. Katika ile hospitali ya Nansio kuna vijana watano pale ambao ni Madaktari graduates wanajitolea na baada ya mawasiliano wameonesha wazi kwamba wale vijana wanataka kubaki kule.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikuhakikishie hili kwanza, kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Afya tutakapokwenda katika mchakato wa kuwapeleka wale Madaktari watano tutahakikisha wanabaki kule Ukerewe kwa ajili ya huduma ya afya. Kwa hiyo, mchakato wa upatikanaji wa Madaktari tunaufanya kabla hatujatoka katika Bunge hili, wataalam hao watakuwa wameshakwenda siyo Ukerewe peke yake, isipokuwa na maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia amesema kuna changamoto katika zahanati inayojengwa Nyakatungu. Naomba nimwambie kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI, nitakuwa na hamu sana mara baada ya Bunge hili, niweze kufika Ukerewe nijue jiografia ya Ukerewe na kupanga mikakati tukiwa field kule, kuona tutafanyaje kutatua tatizo la afya la watu wa Ukerewe. Itanipa faida kubwa zaidi siyo afya peke yake, nitaangalia hata sekta ya elimu ambayo siku moja nimeona katika TV watoto wanavuka na boti kwenda sehemu nyingine kwa ajili ya kupata huduma ya elimu.
MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake, lakini vile vile Ileje ina changamoto kubwa sana ya shule ya sekondari ya bweni ya wasichana. In fact hakuna shule ya bweni ya wasichana peke yake, hii inaleta changamoto kubwa kwa watoto kusafiri kwenda Wilaya nyingine au Mikoa mingine na ni gharama kubwa kwa wazazi na inaleta usumbufu. Watoto wengine wameshindwa hata kumaliza masomo yao. Je, Serikali iko tayari kutusaidia kujenga shule ya bweni ya wasichana kwa kuchangia nguvu na wananchi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Ileje vile vile ni katika wilaya ambazo hazina vyuo vya ufundi vya aina yoyote. Tumejitahidi sana, tumepata mfadhili ametujengea VETA, hivi sasa karibu imalizike. Je, Serikali iko tayari kuchukua ile VETA kuiendesha, kuiwekea vifaa na kuwalipa Walimu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kukosekana kwa shule ya wasichana; tukiri wazi, ni katika miongoni mwa changamoto kubwa sana inayoikabili nchi yetu na kusababisha tatizo la ujauzito kwa vijana wetu ambao kwa njia moja au nyingine wanaposafiri kutoka majumbani mwao kwenda shuleni, katikati huwa wanakumbana na changamoto kubwa sana za ushawishi. Hili nimpongeze Mbunge huyu kwa kuona kwamba kuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba wasichana wanatengenezewa eneo maalum kwa ajili ya elimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri wazi kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa sababu watu wa Ileje wameshaanza hili na sisi kwa njia moja au nyingine, tutashirikiana nao kwa pamoja ili kuhakikisha kwamba tunapata wasichana wengi ambao kesho na keshokutwa watakuwa viongozi wa nchi yetu. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge tutashirikiana na Jimbo lako na Wilaya yako katika eneo hilo ili kuhakikisha kwamba wasichana wanathaminiwa na kupata elimu bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia niwapongeze ninyi kwa kufanya harakati kubwa na kupata wadau mbalimbali walioshiriki mpaka kujenga hiki chuo cha VETA. Ofisi ya Rais kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu tutaangalia jinsi gani tutafanya ili kuangalia jinsi gani chuo hicho kiweze kutumika kwa upana wake ili kuwafanya Watanzania hasa watoto wa Ileje na maeneo jirani waweze kupata elimu hiyo. Naomba tulichukue hilo kwa ajili ya kulifanyia kazi ofisini kwetu na Wizara ya Elimu.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, TAMISEMI, nataka kumthibitishia Mheshimiwa Mbene na Waheshimiwa Wabunge wote na Watanzania, Serikali ya Awamu ya Tano itawachukulia hatua za kisheria wanaume wote wanaowapa ujauzito watoto wa shule. Hatutakuwa na msalie Mtume, wanawake wamejaa mitaani ambao siyo wanafunzi, kwa hiyo hatutacheka na mwanaume yeyote ambae anawapa ujauzito watoto wa shule.
Mheshimiwa Naibu Spika, nawaagiza Maafisa Maendeleo ya Jamii na Maafisa Ustawi wa Jamii wa Wilaya, Kata na Mikoa kuwafuatilia wanaume wote hao na kuhakikisha wanafikishwa Mahakamani haraka iwezekanavyo.

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UFUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri aliyoyatoa Mheshimiwa Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba niongeze jibu la swali linalohusiana na VETA kwa Mheshimiwa Janet Mbene kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba wananchi hao wana majengo mazuri ambayo yalijengwa kwa kushirikiana na wafadhili wa JICA lakini hata kwa kuwatumia VETA walishakwenda wakakagua na wakaona yanakidhi viwango, isipokuwa sasa baada ya kutuandikia na kuona kwamba tuweze kukichukua, tulichowafahamisha kupitia Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya, Ndugu Rosemary Staki Senyamule wanachotakiwa ni kwanza eneo hilo lipimwe na kwa kuwa kile chuo kilikuwa kinamilikiwa na NGO, tunawaomba wakabidhi rasmi kwa Halmashauri. Halmashauri kupitia vikao vyake vya kisheria viridhie na kupitia kwenye RCC ili sasa hati hiyo ikishakuwa tayari ambayo pia ni pamoja na kuongeza kidogo eneo la chuo hicho, tutakuwa tayari kukichukua na kukifanya kiwe chuo cha Wilaya ya Ileje. Tunampongeza sana Mheshimiwa Janet Mbene kwa jitihada anazozifanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza, nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jinsi anavyomudu nafasi yake na anavyochanganua majibu mbalimbali. Hata hivyo, nataka kumshauri aiangalie sana ofisi yake inayotoa majibu ya maswali, ni jipu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ameelekeza taratibu tunazotakiwa kuzifuata na Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ilishazifuata, Mikutano ya Vijiji, Mikutano ya Madiwani, Mikutano ya DCC, Mikutano ya RCC na vigezo vipo na Bunge linajua hivyo na tulishaomba. Nataka aniambie ni lini wananchi wale watapata Wilaya mpya? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, haoni kwamba kitendo cha kuunganisha Wilaya, Sumbawanga Mji na Sumbawanga Vijijini ambazo jiografia zake ni ngumu kunamfanya Mkuu wa Wilaya asiweze kumudu nafasi yake na hatimaye wananchi wa Wilaya wa Sumbawanga Vijijini kucheleweshwa kimaendeleo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kumbukumbu zetu za kitakwimu zinatuonesha Halmashauri ya Wilaya hii ambayo anazungumzia Mheshimiwa Mbunge, ukiiachia Sumbawanga Mjini kwa vigezo vya kijiografia kwa ukubwa wake ina square meter 1,300 ambapo kwa Wilaya inatakiwa iwe na square meter 5,000 lakini halmashauti iliyobakia ina square meter 8,000. Kwa hiyo, ukizi-combine maana yake hapa unapata equivalent ya Wilaya mbili.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hili naomba nikiri wazi, Wabunge wengi sana wanasema wengine wamewasilisha taarifa, ndiyo maana wiki mbili zilizopita nimeagiza, baada ya Mheshimiwa Shangazi kuja ofisini kwangu kwa ajili ya Jimbo lake la Mlalo kuhusiana na suala hili, nikasema nimewaagiza wataalam wangu kuniletea orodha za halmashauri na wilaya zote ambazo zimeleta mapendekezo yao. Nia yangu ni tuweze kubaini ni wilaya ngapi zilipeleka maombi ili kama hazijakidhi vigezo vile tuweze kuwapa marejesho ni mambo gani wanatakiwa kuyarekebisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Malocha aniamini kwa sababu amesema wameshawasilisha haya yote, nitakwenda kufuatilia kwenye orodha ambayo nimeagiza. Tukiona kwamba kila kitu kiko sawa au kama kuna marekebisho ambayo yanatakiwa yafanyike tutawasiliana kwa sababu wananchi lengo lao kubwa ni kupata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini suala hili litatekelezwa. Naomba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba, tukishajua hatua iliyofikiwa, tutaona jinsi gani tutafanya kuhusiana na suala hili la Sumbawanga Mjini na Vijijini. Bahati nzuri ofisi yetu iko chini ya Mheshimiwa Rais mwenyewe, tutamshauri ipasavyo kwamba watu wa Sumbawanga kwa jiografia yao ilivyokuwa ngumu, Wabunge wanapata shida sana kutoa uwakilishi mzuri katika maeneo yao, basi Sumbawanga wapate maeneo ya kiutawala.
MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa Naibu Waziri amejibu kwamba kuna uwezekano mkubwa kabisa wa kupata halmashauri ndani ya Wilaya moja na kwa kuwa mchakato wa wilaya ni mrefu kidogo na mchakato wa kupata halmashauri uko ndani ya uwezo wake na kwa kuwa Jimbo la Mlimba lina kata 16 na urefu wa kilometa 265 kutoka Jimboni mpaka Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero, ni lini Wizara italipa hadhi ya kiwango cha halmashauri Jimbo la Mlimba ili angalau tuanze sasa kujitegemea wenyewe kwa sababu vigezo vyote tunavyo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, amezungumzia Jimbo la Mlimba nadhani akiwa na maana pamoja na Ifakara kwamba eneo lake ni kubwa. Kuanzisha halmashauri kwa mujibu wa vigezo vyetu lazima iwe na kata 15, hicho ndiyo kigezo cha kwanza. Kwa hiyo, kama mna kata 16 maana yake tulitarajia kwamba angalau kata ziongezeke. Tukiachia vigezo hivyo, kuna vigezo vingine vya jiografia maana kuna maeneo mengine kata zinaweza kuwa chache lakini mtawanyiko wa jiografia yake unakuwa ni mkubwa zaidi kama kwa akina Mheshimiwa Keissy kule ndiyo malalamiko ambayo kila siku wanayazungumza hapa.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu ni kwamba, kama mtakuwa mmekidhi vigezo tutafanya mchakato, lakini mwisho wa siku, wataalam wetu lazima watakuja field ku-assess uhalisia wa maeneo hayo yakoje. Lengo letu ni nini kama Serikali? Lengo letu ni kwamba katika maeneo ambayo wananchi wanatakiwa wapate huduma waweze kupata huduma. Kwa hiyo, thibitisho langu kwako ni kwamba, kama mtakuwa mmekidhi vigezo na wataalam wakija ku-verify wakiona kwamba vigezo hivi vimetimizwa na matakwa ya kisheria na taratibu zote zikishakamilika, basi Ofisi ya Rais, TAMISEMI haitosita kufanya maamuzi sahihi kwa ajili ya wananchi wa Mlimba.
Mheshimiwa Naibu Spika, siyo hapo tu, kutokana na jiografia ya Mkoa wa Morogoro hata watu wa Morogoro Kaskazini wana-issue kama hiyo hiyo. Kwa hiyo, naamini kwamba maeneo yote ambayo yataonekana kwamba yana kila haja ya kugawanywa, basi Serikali itaangalia, lakini wakati huo huo tutaangalia suala zima la kibajeti jinsi gani Serikali itaweza kuzihudumia hizi mamlaka mpya ambazo tutakwenda kuzianzisha.
MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu yako Mheshimiwa Waziri, kwangu naona hayajitoshelezi. Nilitegemea ungenipa ni kiasi gani pesa zilitolewa kwenye hivi vikundi vya akinamama kila Wilaya.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kumekuwa na urasimu mkubwa sana wa utoaji wa hizi pesa kwa akinamama especially kwa Wilaya zangu za Mufindi, Iringa Mjini, Kilolo na Iringa Vijijini: je, huoni umuhimu wa kutoa tamko rasmi kwa Wakurugenzi ambao watakwenda kinyume na utaratibu wa utoaji wa pesa hizi? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, je, huoni wakati sasa umefika kwa Wabunge wa Viti Maalum kusimamia zoezi zima la utoaji wa pesa hizi kwenye vikundi vya akinamama? After all, wao ndio wametuchagua sisi kuwa wawakilishi wao. Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kumpongeza dada yangu Mheshimiwa Rose Tweve kwa ajenda yake na swali lake. Ni kweli, katika analysis, maana yake nilizungumza jinsi gani wanawake na vijana wamefikiwa. Nilichambua mchanganuo mbalimbali katika kila Halmashauri. Kwa figure halisi ni kwamba wanawake walipata sh. 339,487,000/= wakati vijana walipatana shilingi milioni 98. Hapa kuna mchanganuo mdogo wa kila Halmashauri kuona ni jinsi gani ilishiriki katika vile vikundi ambavyo i nimevibainisha awali kwamba vilipewa zile fedha.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, katika Mkoa wa Iringa ni kwamba, kila Halmashauri, kama nilivyosema, kwa figure, akinamama walipata karibu shilingi milioni 339 na vijana milioni 98. Kwa suala zima la kutoa maagizo kwa Wakurugenzi, hili lilikuwa ni jambo langu la msingi zaidi. Nilizungumza siku tulipohitimisha bajeti yetu hapa, tukasema kwa sababu mwaka huu karibu takriban shilingi bilioni 56 zitakwenda kwenye vikundi vya akinamama na vijana, katika ule mgao wa asilimia tano tano. Nilisema katika bajeti yetu kwamba Wakurugenzi wote wa Halmashauri wana kila sababu kuhakikisha wanatekeleza hili.
Pia niliainisha tena, nikasema kwa sababu pesa za ndani maamuzi yake yanafanyika ndani ya Halmashauri, baada ya kupokea kwamba ni kiasi gani kimekusanywa, Kamati ya Fedha sasa inaweza kuhakikisha kwamba katika mwezi ule ule inatoa ule mgawanyo wa asilimia tano kwa tano kwa vijana na kwa akinamama.
Kwa hiyo, niliwahimiza Wabunge wote, kwa sababu sisi ni Wajumbe katika hizo Halmashauri zetu, tuhakikishe tunapokusanya own source tuwe wa kwanza kuhakikisha kwamba tunazielekeza pale pale, kwa sababu pesa hizi haziendi Hazina wala haziendi TAMISEMI, zinaishia katika Halmashauri zetu.
Mheshimiwa Spika, nitoe wito kwa Wakurugenzi wetu kwamba waende wakalisimamie hili. Vile vile niseme tena, Madiwani wote wanaingia katika Kamati ya Fedha na yale Mabaraza yetu ya Madiwani wahakikishe fedha hizi tano kwa tano zinakwenda kwa mujibu wa taratibu tulizojiwekea.
Mheshimiwa Spika, kuhusu Wabunge Wanawake kusimamia jambo hili kwa karibu; naomba niwaambie, hili ni jukumu letu sisi sote. Akinamama, vijana na Wabunge wote humu tuna jukumu hilo. Mimi lengo langu ni nini? Ni kwamba kila Mbunge ataona kwamba jambo hili ni la kwake. Mama akinufaika katika Jimbo hilo, maana yake unakuza uchumi wa watu katika eneo hilo.
Mheshimiwa Spika, hali kadhalika, vijana wakinufaika, maana yake unakuza uchumi wa vijana katika eneo hilo. Kwa hiyo, ni jukumu letu sisi sote, twende sasa tukalisimamie hili kwa nguvu kubwa kwa ajili ya mustakabali wa uchumi wa nchi yetu.
MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa vita ya Majimaji au harakati za awali za kudai uhuru wa Tanganyika zilitokana na chokochoko na misingi imara ya kukataa kuonewa na kudai uhuru kulikofanywa na majemedari wetu wakati wa vita vya Majimaji. Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga barabara hii ili kuwawezesha Watanzania kwenda katika eneo hilo wakajifunze namna gani nchi yetu ilivyojengwa katika misingi ya kudai haki? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, kwa kuwa barabara hii haipitiki kabisa Serikali ina mpango gani wa kuweka lami katika sehemu korofi kwa mfano mlima Ndundu, Mlima Ngoge pale Chumo, Mlima Kinywanyu na Mlima Karapina pale Kipatimu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi kwamba umuhimu wa barabara hii na Mheshimiwa Mbunge amesema kwamba sehemu hii ndiyo chemichemi za harakati ya ukombozi wa nchi yetu. Naomba nikiri kwamba, kuna maeneo mengi sana ya kijiografia ambayo wakati wa uhuru kama Tanzania tulipokuwa tunaenda katika mchakato walishiriki kwa kiwango kikubwa sana katika kufanikisha uhuru wa nchi yetu, nawapongeza sana ndugu zetu wa Kilwa katika hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakiri wazi kwamba kwa sababu umuhimu wa barabara hii kama nilivyosema awali katika jibu langu, tukirejea tena marejeo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi, lengo lake kubwa ni kuhakikisha wananchi wanafikiwa wa maeneo mbalimbali. Mheshimiwa Ngombale tutafanya juhudi siyo hapo Kilwa tu, isipokuwa maeneo mbalimbali. Ndiyo maana Ofisi ya Rais, TAMISEMI ilikuwa ikifanya mikakati katika maeneo mbalimbali, tulianza hasa katika miji tumeenda katika halmashauri, lengo letu ni kwamba maeneo mbalimbali yaweze kufikika chini ya miradi yetu ambayo sasa hivi tuna mradi wa TSP Project ambayo inahusisha ujenzi wa miundombinu ya barabara za lami katika maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hili litakuwa katika mpango wetu, mkakati mpana wa kuhakikisha Halmashauri nyingi zinafikiwa na haya ni mambo ambayo tunayafikiria, ndiyo maana hata ukiangalia bajeti yetu ya mwaka huu tuna bajeti takribani ya bilioni 43 kwa ajili ya kuondoa vikwazo, lakini bilioni zaidi ya 200 kwa ajili ya kuhakikisha Halmashauri ziweze kufikiwa vizuri. Kwa hiyo, ni mambo ambayo Serikali yetu inayaangalia na ndani ya miaka mitano tuna imani tutafanya mambo makubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini lile la kuhusu sasa vile vipande korofi ikiwezekana viwekewe lami na najua Halmashauri ya Kilwa jinsi gani jiografia yake ilivyo na wakati mwingine malori yanashindwa kupanda. Tutawaelekeza wenzetu wa TANROAD ambao tunashirikiana nao kwa karibu zaidi na barabara takribani kilomita 48 zinahudumiwa na TANROAD, tutahakikisha Serikali inayapa kipaumbele yale maeneo korofi ambayo mvua ikinyesha barabara hazipitiki kwa kuyafikiria kwa jicho la karibu zaidi.
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Pamoja na mikakati ya Serikali kujenga barabara za lami, lakini kuna ahadi ya Mheshimiwa Rais ambayo aliitoa katika maeneo yetu wakati anaomba kura, ya ujenzi wa barabara za lami. Katika Bunge hili tuliomba tupatiwe time frame kwamba ni muda gani hizi ahadi zinatekelezwa. Nataka kufahamu ni lini Mheshimiwa Waziri atatuletea ratiba ya ujenzi wa barabara hizo za lami kwa ahadi ya Rais ili tufuatilie kwa karibu ikiwemo Jimbo langu la Babati Mjini kilomita ishirini za lami?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ni lini, kifupi time frame ya ujenzi wa utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi, imeainishwa ndani ya miaka mitano 2015-2020. Jukumu letu kubwa ni kuhakikisha ndani ya kipindi hiki zile ahadi ambazo tumeahidi kwa kadri ilani yetu ilivyojielekeza, tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo, ili mwisho wa siku tuone kwamba ilani yetu imetekelezwa kwa ajili ya kuwapatia wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania maendeleo ya kutosha na siyo Babati peke yake, isipokuwa kwa Tanzania nzima kwa mujibu wa Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi.
MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Nataka kufahamu pia kuhusiana na mgogoro wa wafanyakazi uliopo katika Hospitali ya Ndanda. Serikali iliahidi itaajiri wafanyakazi 85 na wale Wamisionari sasa hivi wameamua kupunguza wafanyakazi 59 kwa sababu Serikali haijatekeleza ahadi yake toka mwaka 2012 hali inayotishia kuifanya Hospitali ya Ndanda isiwe tena Hospitali ya Rufaa katika eneo la Kusini. Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kutekeleza ahadi yake ya kupeleka pesa kwa ajili ya wafanyakazi wa Ndanda Hospitali?
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kufahamu pia ni lini Serikali italipa pesa za fidia katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi kwa vile katika vitu vilivyoharibika ni pamoja na gari la wagonjwa la hospitali ya Chiwale ili waweze kujinunulia wenyewe tena lile gari liweze kusaidia baada ya kujenga wodi ya akinamama katika eneo lile? Ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala la changamoto ya watumishi ni kwamba Serikali tumelichukua. Sasa hivi tuna mchakato wa kuajiri watumishi mbalimbali katika Halmashauri zetu na Wizara ya Afya ina-finalize stage hiyo. Nina imani kwamba siyo muda mrefu ndani ya mwezi huu wa Mei na Juni tutaenda kupunguza hii gape ya watumishi, lakini changamoto ya Ndanda tutakwenda kuifanyia kazi. Naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakwenda kulifanyia kazi kwa karibu zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la ambulance zilizoungua, ni kweli na mimi mwenyewe nimefika pale. Pale kuna ambulance tatu zilichomwa moto na kwa njia moja au nyingine siyo kwamba Serikali ni ya kulaumiwa. Katika hili, naomba nitoe maelekezo kwa wananchi, inawezekana kwa jazba zetu tunaharibu vitu ambavyo vilikuwa kwa maslahi ya wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kipindi kile pale Mtwara watu walienda kuchoma ambulance ambazo zinabeba akinamama na watoto. Fikiria mtu anachukua kibiriti na petrol anakwenda kuchoma ambulance tatu mpya, unategemea nini katika mazingira hayo? Kwa kweli ni jambo lenye kuhuzunisha na ndiyo maana nilipofika pale Masasi nilienda kutembelea maeneo yake, kwa kweli ni jambo la kuhuzunisha, lakini Ofisi ya Rais, TAMISEMI tutaangalia jinsi gani tutafanya kwa sababu mwisho wa siku ni wananchi na akinamama ndiyo wanaopata shida zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunalichukua hili kwa upana wake lakini kwa kweli kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI tumesikitika sana kwa sababu ile ni fursa ambapo wananchi walikuwa wanapata huduma kila siku. Naomba nitoe onyo kwa watu wote, tusichukue jazba zetu mbalimbali tukazielekeza katika vitu ambavyo vinawasaidia wana jamii kupata huduma bora katika maisha yao.
MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, Halmashauri zinatofautiana kimapato na Kituo cha Afya cha Nyambiti hakina gari, ni utaratibu gani sasa utumike ili kituo hiki kiweze kupata gari kwa sababu uwezo ni mdogo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala zima la upatikanaji wa gari katika vituo vya afya, tulipokuwa tunapitia mchakato wa bajeti yetu ya mwaka huu 2016/2017, tulikuwa tukifanya analysis ya halmashauri mbalimbali katika suala zima la sekta ya afya, kila halmashauri iliweka kipaumbele chake. Kuna wengine waliweka kipaumbele cha ujenzi wa miundombinu, kwa mfano kwa ndugu yangu pale zahanati aliyosema ya Chiwale, wametenga karibuni milioni 287 kwa ajili ya kituo kile cha afya. Wengine kipaumbele chao walichoweka ni ununuzi wa gari la wagonjwa. Kwa hiyo, vipaumbele hivi vinatofautiana kati ya zahanati na zahanati.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumjulisha Mheshimiwa Ndassa kwa sababu sijajua kipaumbele walichoweka katika eneo hili, sisi na wenzetu wa Wizara ya Afya tutaangalia katika bajeti ya mwaka huu tumegusa vipi katika eneo hilo. Mwisho wa siku ni kwamba, lazima kwa umoja wetu wote tuangalie jinsi gani tutafanya maeneo kama hayo ambayo wananchi wanapata shida waweze kupata fursa za kuwa na gari la wagonjwa ili mama akipata matatizo aweze kupelekwa hospitali ya karibu kupata huduma. Kwa hiyo, Mheshimiwa Ndassa naomba tulichukue hili tujadiliane kwa pamoja na kuangalia bajeti yenu ya halmashauri mlipanga vipi kama vipaumbele vyenu vya awali.
MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza hasa kwa kuwa majibu hayakutosheleza haja.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunarudi pale pale kwenye kutoa huduma stahiki na kuajiri wahudumu stahiki, siyo suala la kuajiri wengi bali waajiriwe Wakunga ambao wanaendana na mila na desturi zetu na wale ambao wanakidhi haja. Je, Mheshimiwa Waziri atakubaliana na mimi kwamba Serikali hii ya CCM imekuwa inafanya mambo yake kanyaga twende tu na siyo kwa kufuata taratibu maalum?
Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali hii ya CCM itakubaliana na mimi nikisema kwamba haiendani na matamko yake? Leo hii gazeti linaandika kuboresha huduma za uzazi lakini wanatuambia wataendelea kutuwekea Wakunga wanaume kwa kuwahudumia wanawake. Naomba majibu.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Serikali ya Chama cha Mapinduzi haifanyi mambo yake ya kanyaga twende. Hapa nilizungumzia sheria inasemaje kwa sababu kama Majaji Naibu Spika mna taratibu na sheria zenu. Nimeshangaa sana, kuna sehemu nyingine sasa hivi hata ukiangalia kuna ma-gyno wengi sana akinamama lakini siku nyingine wanaenda kwa ma-gyno wa pande zote mbili. Niseme kwamba siku zote Serikali inalenga kuona ni jinsi gani itawasaidia wanajamii kupata huduma bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusiana na dhana nzima ya kusema kwamba tuwe tunaajiri watumishi wa kike na wa kiume, nimesema kwamba tutaendelea kuajiri na ndiyo maana nimesema jamii zetu zinatofautiana. Kuna maeneo mengine ambayo inaonekana kwa mila na desturi zao itabidi tuweke watu wa aina fulani na sisi tutafanya hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge katika Mkutano uliopita aliuliza swali hili hili na nilitoa maelekezo. Bahati nzuri hapa tumepata takwimu wataalam wangu wa afya na RMO wetu wa Mkoa baada ya agizo lile waliweza kufanya mchakato katika kila zahanati takribani nane wameweza kubadilisha wale wataalam kutokana na swali lako mama la msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimepata taarifa hizo lakini nitaenda kufanya verification mwenyewe kuona hali ikoje, lakini taarifa nilizozipata toka wiki iliyopita ni kwamba walifanya mchakato huo na zile zahanati ambazo mwanzo zilikuwa na wataalam wa kiume peke yake sasa hivi wamepeleka na wataalam wa kike lengo likiwa ni kuwasaidia akinamama.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa Wilaya ya Mafia, napenda kuwashukuru sana kwa mchakato mlioufanya wa kupata mashine mbalimbali. Tulikuwa na tatizo la X-ray na Utra-sound machine, Mbunge wao Mheshimiwa Dau amefanya harakati watapata Ultra-sound na X-ray machine mpya, zimeshafika Dar es Salaam sasa hivi wanaendelea na taratibu za kuzisafirisha kwenda Mafia. Kwa hiyo, tutaendelea kuenzi juhudi kubwa zinazofanyika lakini Serikali itajitahidi kwa kadiri iwezekanavyo wananchi wapate huduma bora.
MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jibu lake la msingi Mheshimiwa Waziri amesema kwamba vikundi 39 vya vijana na akina mama wamepata shilingi 23,800,000. Nataka kujua je, fedha hizi ni kwa muda wa fedha wa miaka mingapi?
Swali la pili; fedha hizi shilingi 23,800,000 zimekwenda katika Vijiji vipi na vikundi vipi katika Halmashauri ya Morogoro vijijini? Ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza linasema pesa hizi zimeenda kwa vikundi vingapi. Ninaomba nifanye mrejeo swali hili nadhani nilijibu katika Bunge lililopita. Niliainisha vikundi hivi na nilikiri wazi nikasema kwamba pesa hizi zilizotengwa kwa Halmashauri ya Morogoro Kusini ni chache sana ukilinganisha na mahitaji halisi yaliyotakiwa kupelekwa. Nikatoa msisitizo hata katika wind up ya bajeti yetu ya Wizara ya TAMISEMI, nikasema ndugu zangu hizi pesa own source Wabunge ndiyo wenye jukumu ya kwenda kuzisimamia. Kwa sababu pesa hizi haziendi kwa Waziri wa Fedha wala haziji TAMISEMI, pesa hizi zinabakia katika Halmashauri na vikao vya Kamati ya Fedha za Halmashauri ndiyo vinavyopanga maamuzi ya mgawanyo wa pesa hizo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana katika bajeti yetu ya mwaka huu tukasema Halmashauri yoyote haiwezi ikapitishwa bajeti yake lazima kuonyesha mchanganuo kwa sababu hata hizi zilizopelekwa ni chache hazitoshelezi. Kipindi kilichopita nimesema hata Mkaguzi wa Hesabu za Serikali outstanding payment ambayo wapeleke karibu shilingi bilioni 39 hazijakwenda kwa wanawake na vijana. Mwaka huu peke yake tunatarajia kwamba kutokana na bajeti ya mwaka huu tumepisha shilingi bilioni 64.12 zinatakiwa ziende katika mgawanyiko huo. Lengo langu ni nini? Ni kwamba kila mwananchi, kila Mbunge atahakikisha kwamba hizo bilioni 64 tukija kujihakiki mwaka unapita katika Jimbo lake amesimamia katika vikao vyake pesa hizo zimewafikia wananchi wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ni vikundi vingapi kwamba nivitaje kwa jina naomba niseme kwamba kwa takwimu nitampatia ile orodha ya mchanganuo wote wa vikundi vyote katika Jimbo la Morogoro Kusini.
MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kwa kuwa tatizo hili limeikumba pia hospitali ya Namanyele - Nkasi Kusini na kwa bahati nzuri Serikali imejenga majengo ya wodi. Je, ni lini sasa Serikali itakabidhi na kufungua majengo haya?
Swali la pili, azma ya Serikali ni kuwa kila kata kuwa na kituo cha afya na kila kijiji kuwa na zahanati, je, ni lini vijiji hivi vinavyotegemea hospitali ya Kirando vitapatiwa zahanati?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nipende kushukuru kama facilities zimekamilika, sasa bado kuweza kufunguliwa nadhani kikubwa zaidi tutawasiliana na uongozi wa mkoa kuangalia utaratibu tukishirikiana na wenzetu wa Wizara ya Afya, vifaa hivyo vikishakamilika basi hospitali hiyo iweze kufunguliwa. Hilo ni jambo ambalo tunasema kama Serikali tunalichukua kwa ajili ya kwenda kulifanyia kazi ili wananchi waweze kupata huduma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ajenda ya pili ni jinsi mchakato wa ujenzi wa vituo vya afya ya zahanati ni kweli sasa hivi tuna karibuni ya kata 3390, lakini vituo vya afya tulivyonavyo ni vituo 484 maana yake tuna gap kubwa sana ya kufanya. Ndiyo maana leo hii Waziri wa Afya ata-table bajeti yake hapa ikionyesha mikakati mipana kwa ajili ya kufikia maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukijua wazi kwamba katika hao wenzetu wa eneo hili wanachagamoto kubwa sana na nikifanya rejea ya Mheshimiwa Keissy hapa alishasema mara nyingi sana. Hiki hasa kituo chako cha Kirando na yeye alikuwa akiomba ikiwezekana iwe Hospitali ya Wilaya kwa mtazamo wake. Lakini alikuwa akifanya hivi ni kwa sababu wenzetu wa kule wa pembezoni wakati mwingine wanapata wagonjwa wengine mpaka kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Congo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo Serikali naomba tuseme wazi kwamba tutashirikiana vya kutosha na mimi naomba nikiri kwamba katika maeneo yangu ya mchakato wa kuanza kutembelea nina mpango baada ya Bunge hili la Bajeti kutembelea katika mkoa huu ili kuangalia changamoto zinazowakabili ili kwa pamoja tuweze kuzitatua tukiwa katika ground pale tuone ni lipi linalowakabili wananchi wetu.
MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru naitwa Bobali, Mbunge wa Mchinga.
Kwa kuwa matatizo yaliyopo katika Mkoa wa Katavi yanafanana kabisa na matatizo ya kituo cha afya ya Chalutamba katika Jimbo la Mchinga kumekuwa na kuharibika mara kwa mara kwa gari ya kituo kile.
Je, Wizara haioni kwamba kuna haja sasa ya yale magari yaliyochakaa kuya-compensate katika vituo vyote ambavyo vina magari yaliyochakaa wakapewa magari mapya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumelisikia suala la Mheshimiwa Bobali, lakini mimi nikijua kwamba hapa tulivyokuwa tunapitisha bajeti tuliona vipaumbele vya kila Halmashauri, wengine walitenga gari, wengine wakatenga vituo vya afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwa sababu yale magari yamechakaa lakini nadhani tutaangalia jambo kubwa ni kwamba kama Halmashauri tunapokaa katika priority zake katika mpango wa bajeti ni vema zaidi kuona kwamba kama gari limechaka basi tutenge bajeti maalum kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunapata gari jipya ili kuondoa gharama za matengenezo ya kila siku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Serikali tumelisikia hilo, niwahamasishe sasa katika maeneo ya vipaumbele tuangalie lipi hasa ni kipaumbele cha wananchi katika eneo letu husika ili wananchi wapate huduma bora.
MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naitwa Chikambo siyo Chikabo.
Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba ikumbuke kwamba Wilaya ya Tunduru tumeendelea kukiamini Chama cha Mapinduzi kwa kutoa kura nyingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ikumbuke kwamba wakati wa ziara ya Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete mwaka 2014 alitoa ahadi za kutoa magari ya ambulance katika vituo vya afya vya Nalarasi,Nakapanya na Matemanga. Kwa hali ile ile ya kuendelea kukiamini Chama cha Mapinduzi. Naomba Mheshimiwa Naibu Waziri aniambie ni lini sasa ahadi hiyo itatekelezwa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba ahadi hii imetolewa na Mheshimiwa Rais aliyepita na ahadi hii ni ahadi ya Serikali na ndiyo maana nimesema katika mchakato huu sasa hivi kuna gari la wagonjwa, bajeti imetengwa kwa ajili ya kupelekwa. Umesema maeneo mbalimbali ambayo Mheshimiwa Rais mstaafu alitoa ahadi hiyo, hii ni ahadi ya Serikali na ninajua wazi katika mkoa ule kwa sababu una vipaumbele vingi sana. Siyo ahadi hiyo peke yake, Mheshimiwa Mbunge ameniambia kwamba mpaka walikuwa na ahadi ya Mkoa mpya wa Selous tunayajua hii kama Ofisi ya Rais TAMISEMI.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa sababu maeneo haya yana vipaumbele maalum naomba nikwambie kwamba ahadi ya Serikali iko palepale katika mchakato tulioondoka nao tutahakikisha kwamba ahadi ya Mheshimiwa Rais inatekeleza ili mradi wananchi wapate huduma bora.
MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante, kwa kuwa tatizo la Tunduru huko linalingana kabisa na Korogwe Mjini. Ni lini Serikali itaifanya Hospitali ya Magunga iwe Hospitali Teule?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Hospitali ya Korogwe Mjini, juzi nilipita pale katika ziara yangu wakati naenda Arusha nilitembelea Hospitali ile na nikaona kwamba congestion ya watu wa pale na mahitaji yake na kwamba Wilaya iko barabarani, bahati nzuri Naibu Waziri wa Afya juzi alifika pale hali kadhalika Waziri wa Afya alifika pale, naona kwamba haya yote nimeona ni kipaumbele hospitali ile kuwa Hospitali yetu ya Rufaa ya Mkoa ili mradi kufanya hivyo. Ninaamini mchakato unaohitajika ukikamilika na mahitaji yote hasa yanayotakiwa kwamba kuifanya hospitali ya Mkoa kukamilika basi nadhani Serikali haitosita kuhakikisha hospitalki ile inakuwa Hospitali ya Mkoa kwa vigezo vitakavyokamilika na kutokana na maelekezo kutoka Wizara ya Afya.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri Jafo nataka kuongezea kwenye suala la muundo na mgawanyo na set up kwa kuzingatia maeneo katika utoaji wa huduma ya afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeongea na Waziri wa Afya, tumeona liko tatizo la catchment areas namna zilivyowekwa na uwiano wa vituo vya afya, hospitali za Wilaya, hospitali za Mikoa na ziko nyingine ambazo maombi yako mengi sana wakiomba zipandishwe madaraja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ingawa utaratibu unaanzia huko chini kuanzia kwenye Kata, kwenye Wilaya, kwa maana ya Halmashauri, hata hivyo tunaona haja ya Serikali kukaa na kufanya sensa maalum ya kuweka mfumo wa utaratibu mzuri ili tuende kwa utekelezaji ambao utastahiki. Kwa mfano, haiwezekani ukakuta catchment area ya kata karibu nne kukawa hakuna kituo cha afya, lakini kituo cha afya kimeelekea upande mmoja. (Makofi)
Kwa kuwa tuna uchache wa rasilimali lakini iko haja ya kufanya sensa hiyo ili baadaye tuje na mpango kazi maalum kwa kushirikiana na Wizara ya Afya tutakapopanga mpangilio mzuri wa vituo vya afya, Hospitali za Wilaya na Hospitali za Mikoa kulingana na mahitaji ya wananchi.
MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Mheshimwia Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kwa kuwa amejibu kwamba ni jukumu la Mkurugenzi kuandika na kuomba shule hii iwe ya bweni; ni lini sasa ofisi yake itamuagiza Mkurugenzi huyo ambaye anaonekana hafahamu kama yeye ndiyo anawajibika ili aweze kuandika barua na kuomba? (Makofi)
Swali la pili, kwa kuwa mwezi huu au mwisho wa mwezi ujao, Serikali itaajiri walimu wapya na uchunguzi wangu shule nyingi za Jimbo la Geita za Vijijini hazina walimu; ni maagizo gani Serikali itatoa kwa walimu wapya ili waelekezwe zaidi Vijijini badala ya Mjini? Nashukuru.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini nitamwagiza Mkurugenzi, nadhani huu mchakato unaanza kwenu ninyi katika Baraza la Halmashauri, kwa sababau hii ni need ambayo ninyi mnahitaji. Kama Baraza la Madiwani mtaona kwamba ninyi mnahitaji hilo, baadaye Mkurugenzi ataandika barua, akishaandika barua maana yake ikifika katika Wizara ya Elimu, Wizara ya Elimu inatuma wataalamu chini ya Kamishna wake, wataenda kufanya uhakiki, baadaye vigezo vikishapita ndiyo shule hiyo itasajiliwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niliache suala hili katika Baraza lenu la Madiwani, maana inawezekana Mkurugenzi akaandika halafu Madiwani wakamgeukia kwa nini umegeuza shule hii kwa mahitaji yako bila kutaka maelekezo kutoka katika Baraza la Madiwani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba niache jambo hili katika mchakato wa Baraza la Madiwani litaamua kumwelekeza Mkurugenzi aweze kufanya haraka kupeleka Wizara ya Elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo kuhusu suala la upelekaji wa walimu. Ni kweli hivi sasa tupo katika mchakato siyo muda mrefu sana tutaajiri walimu wapya. Katika kuajiri, kuna Mikoa ambayo inabidi ipewe kipaumbele, tuna Mikoa takribani sita ambayo ina changamoto kubwa sana ya walimu ikiwepo ni pamoja na Mkoa wa Kigoma, Rukwa, Katavi na Geita. Kwa hiyo, katika maeneo hayo yote tutaangalia walimu watakaopatikana basi tutawapa maelekezo maalum. Wakifika pale lazima waende maeneo ambayo wananchi wanataka huduma, bahati mbaya wakati mwingine inajitokeza walimu tukiwaajiri, tukiwapeleka kule inawezekena wengine sisi Waheshimiwa tunapeleka vi-memo ili yule mwalimu arudi mjini, tunasababisha maeneo ya vijijini yanakosa walimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Ofisi ya Rais TAMISEMI tunaelekeza walimu watakaopangwa lazima waende kufanya kazi katika maeneo husika.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi hii.
Kwa kuwa, hili suala la Geita linafanana sana na tatizo lililoko Wilaya ya Kakonko, Jimbo la Buyungu kutokuwa na sekondari kabisa ya A-level na tunayo shule moja ya sekondari Kakonko ambayo ikiwekewa miundombinu mizuri yafaa kuwa na A-level.
Je, Waziri yuko tayari kuweka kipaumbele katika shule ya sekondari Kakonko ili ipewe hadhi ya kuwa na A-level itakayokuwa ya kwanza katika Wilaya ya Kakonko?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba Serikali kutoa kipaumbele, nadhani hili tumetoa maagizo katika maeneo mbalimbali, kwa sababu tuna shule nyingi sana za kata. Shule hizi za kata watoto wakifaulu lazima waende Advance Level. Tunapokuwa na shule za kata wanafunzi wanishia form four maana yake wakikosa nafasi za kwenda advance, shule zikiwa chache vijana inawezekana wakafaulu lakini wakakosa nafasi.
Kwa hiyo, haya ni maelelekezo ya maeneo yote, ndiyo maana mwaka huu hata ukiangalia bajeti yetu tumezungumza, tunakarabati zile shule kongwe, hali kadhalika kuhamasisha maeneo mbalimbali kujenga shule. Kwa sababu tunajua eneo lile jiografia yake ni ngumu tutaangalia jinsi gani ya kufanya maeneo ambayo hayana shule za Kata tuyape msukumo shule za advance level ili kwamba watoto wakifaulu katika shule a O level waende advance level katika maeneo husika.
RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba kuuliza maswali madogo mawili.
Kwa kuwa Wilaya ya Kilolo imezungukwa na mito ya Ruaha, Mto Rukosi; ni kwa nini Serikali isivute maji kutoka katika mito hiyo kuliko kuchimba visima ambavyo vimekuwa vikichimbwa, lakini havitoi maji?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa visima…
SPIKA: Hilo, swali la kwanza ulilouliza ni kwa niaba ya kaka au? (Kicheko)
Mheshimiwa endelea!
MHE. RITTA E. KABATI: Swali la pili, kwa kuwa visima virefu huwa havina uhakika sana wa kutoa maji na mara nyingi vimekuwa vikiharibika! Ni kwa nini Serikali isielekeze nguvu kwenye kuchimba mabwawa badala ya kutumia fedha nyingi sana katika kuchimba hivi visima ambavyo mara nyingi vimekuwa havina uhakika?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKAL ZA MITAA): Mheshimiwa Spika, swali la kwanza lilikuwa ni kwa nini sasa tusitumie fursa za mito ambayo inapita katika Jimbo la Kilolo badala ya kwenda kuchimba visima virefu. Katika utekelezaji wa miradi ya maji, kwanza wataalam wanaangalia au wanafanya analysis, ni chanzo gani cha maji ambacho kitaweza kusaidia, lakini utafiti huo vilevile unaendana na bajeti.
Mheshimiwa Spika, kuna maeneo mbalimbali ambayo yamebainika kwamba kumeenda kuchimbwa visima virefu, lakini sehemu zingine kuna fursa za maji. Hili naomba nikiri hapa wazi kwamba, watu wengi mbalimbali hasa wa kutoka maeneo mbalimbali ambayo kuna mito mirefu au maziwa, kama watu wa Kanda ya Ziwa wanasema kwa nini tuchimbiwe visima badala ya kutumia vyanzo vilivyopo. Naamini katika Programu ya Maji ya Awamu ya Pili ambayo sasa inaanza, Watalaam wetu, wataangalia katika sehemu ambayo kuna fursa ya vyanzo vikubwa vya maji hasa mito viweze kutumika vizuri kutokana na bajeti iliyopo.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba nimthibitishie Mbunge kwamba katika Awamu ya Pili ya Mradi wa Maji, watalaam wetu wataenda mbali zaidi kuangalia fursa. Ndiyo maana tulisema pale awali kwamba maeneo yote yanayozungukwa na vyanzo vikubwa vya maji, basi watalaam itabidi wajielekeze huko kuona jinsi gani ya kufanya ilimradi kupata maji ya uhakika na kuhakikisha fedha inatumika vizuri.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, ni kwa nini sasa kuchimba visima virefu badala ya kuchimba mabwawa. Mara nyingi sana watalaam wanazungumza kwamba maji ya kisima kirefu, kitaaluma au kitalaam, ukiyatoa yanakuwa maji safi na bora, kwa sababu yanakuwa hayana contamination, lakini maji ya bwawa maana yake yanataka ufanye treatment.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, imeonekana wazi, sehemu zingine visima virefu kweli vimechimbwa, lakini hatukupata maji. Kwa sababu uhitaji wa maji ni mkubwa na sehemu zingine water table inasumbua sana, naamini sasa, ndiyo maana katika mkutano wetu wa pili tuliofanya tathmini pale Dar es Salaam, tulielekeza kila Halmashauri, ikiwezekana kila mwaka twende katika uelekeo wa mabwawa kwa sababu maeneo mengi mbalimbali tuliyochimba visima virefu ni kweli wakati mwingine tulikosa maji na wakati mwingine miradi hii inaharibika. Vitu hivi vyote vitakwenda sambamba kwa pamoja kuangalia engineering specifications ya maji inasemaje kwa ajili ya kuelekeza wananchi wapate maji bora na salama.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Naomba niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Waziri, Korogwe ilikuwa na mradi wa World Bank ambapo ilikamilisha miradi yake Kwa Msisi, Ngombezi na Kwa Mndolwa na ikabakiza mradi wa Rwengela Relini, Rwengela Darajani na Msambiazi. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha miradi hiyo ambayo imebakia?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Spika, ni kweli Korogwe kuna mradi wa maji, lakini naomba nitoe maelezo kwamba si Korogwe peke yake isipokuwa kuna miradi ya maji mingi sana hivi sasa, hata Wabunge wengi wanaweza wakasimama. Miradi hii ni kwamba mingi ambayo wakandarasi walikuwa site, lakini baadaye wakafanya mpaka waka-demobilize vifaa kutokana na kushindwa kulipwa fedha. Nadhani hata mradi wa Korogwe ndiyo tulipata changamoto hiyo, lakini siyo mradi wa Korogwe peke yake isipokuwa ni miradi mingi.
Mheshimiwa Spika, ndiyo maana, tulipoanza katika Serikali ya Awamu ya Tano jukumu lake kubwa, lilikuwa ni kuangalia jinsi gani itakusanya fedha za kutosha. Wakati tunaingia tulikuwa na outstanding payment ambapo deni tunalodaiwa lilikuwa karibu bilioni 28, lakini kutoka na makusanyo mazuri yaliyofanywa hivi sasa deni lile lote limeshalipwa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naamini sasa hivi ukiangalia hata Waziri wa Fedha hapa atakapokuja katika bajeti yake ataeleza kwamba hivi sasa tuna uwezo hata certificate zikija watu wakaweza kulipwa. Kwa hiyo, mradi wa Korogwe sawasawa na miradi mingine ambayo imesimama. Naamini Halmashauri zingine hivi sasa watasema bado hawajapokea fedha, lakini mchakato huu sasa nawasisitiza Wakurugenzi wote na ma-engineer wote wa Wilaya, wale wakandarasi ambao certificate zao hazijapelekwa, haraka zipelekwe Wizara ya Maji ilimradi kuhakikisha kwamba, wakandarasi wanarudi site kazi ziweze kufanyika. Hii ni kutokana na umakini uliyofanyika katika ukusanyaji wa kodi. Hapa naomba niwasistize ndugu zangu Wabunge, wote tushikamane na Serikali yetu ili kodi ziweze kulipwa, miradi iweze kutekelezeka.
MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.
(i) Naomba niiulize Serikali ni lini sasa madai ya hawa watumishi 65 waliosalia yatalipwa?
(ii) Kwa kuwa posho za kujikimu na posho ya usumbufu ni halali ya mtumishi, ni lini sasa Serikali itakuwa tayari kuwa inawalipa watumishi inapowahamisha malipo hayo kwa wakati?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni lini fedha hizi zitalipwa, nimesema katika jibu langu la msingi, kwamba ni kweli pale kuna watumishi ambao wamehamia katika Halmashauri mpya. Katika kuliona hilo sasa tukaona ni vema sasa hii fedha itengwe katika bajeti ya mwaka wa fedha huu ili watumishi waweze kulipwa.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ndungu yangu Masele naomba uwe na subira tu, kwa sababu katika Bajeti yetu tulivyopitisha tulizungumza mchakato mkubwa katika suala zima la Halmashauri mpya kwa hiyo katika suala hili la ujenzi wa miundombinu lazima uende sambamba na malipo ya madeni ya watumishi mbalimbali. Kwa hiyo, jambo hili tutakwenda kulifanya kwa kadri iwezekanavyo ili watumishi wale wapate utulivu, wafanye kazi yao kwa ubora zaidi.
Mheshimiwa Spika, ni jinsi gani tutafanya Halmashauri zinapoanzishwa madai ya watumishi yaweze kulipwa kwanza, hili tutaliwekea maanani. Lakini Waheshimiwa Wabunge tukumbuke kwamba sasa hivi kuna Halmashauri mpya nyingi sana, ofisini kwangu mpaka sasa hivi nimeaandaa matrix form ya kuona Halmashauri ina Wilaya mpya ambazo Wabunge mbalimbali wameenda kupeleka maombi Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa ajili ya kuweza kuanzishwa. Kwa hiyo, jukumu letu kubwa tutakuwanalo ni kuona ni jinsi gani haya matakwa ya wananchi katika maeneo husika yaweze kufikiwa, lakini hatuwezi kuzuia Halmashauri kuanzishwa kwa sababu posho bado hazijapatikana.
Mheshimiwa Spika, tukifanya hivyo tutakuwa tumezuia maendeleo ya wananchi katika maeneo husika, hata ninyi Wabunge hamtoridhika katika hilo. Kwa hiyo, tumechukua ushauri huo wote, lengo kubwa ni mipango yote iende sambamba, Halmashauri zinapoanzishwa na fedha ziweze kulipwa.
Vinguguti ina wakazi wengi na mpaka sasa hivi Kata ya Vinguguti haina zahanati yoyote.
Swali la Pili, kwa kuwa Kata ya Kipawa, Kata ya Minazi mirefu, Kata ya Kiwalani pamoja na Kata ya Kisukuru na Kimanga zina matatizo kama haya haya. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba inashirikiana na Manispaa ya Ilala ili Kata hizi ziweze kuwa na zahanati lakini pia tuweze kuwa na vituo vya afya ili kuondoa msongamano katika Hospitali ya Amana?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, Vinguguti kweli ni eneo ambalo lina wakazi wengi sana na kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge ni kweli kwamba eneo hili lazima lipatiwe kipaumbele. Lakini naomba nimwombe Mheshimiwa Mbunge japokuwa juhudi kubwa zinafanyika needs assessment wakati mwingine zinaanza katika Mabaraza yetu ya Madiwani.
Kwa hiyo, kwa sababu nia yako ni njema na Serikali tutakuunga mkono katika eneo hilo. Lakini kikubwa zaidi tutaweka nguvu zaidi katika lile eneo letu la Kituo cha Afya cha Mnyamani, kwa sababu ni eneo ambalo wenzetu wa Plan International walifanya juhudi kubwa sana kujenga kituo kile, jukumu letu kubwa ni kwamba kwanza kuwekeza vya kutosha kituo kile angalau kiweze kua-accommodate hii demand iliyokuwepo hivi sasa, wakati huo tukiangalia mtazamo wa mbali jinsi gani tutafanya, eneo lile la Vinguguti tuwe na sehemu ya kujenga zahanati kubwa na siyo zahanati kwa hadhi ya Vingunguti, kujenga moja kwa moja kituo cha afya kutokana na mahitaji ya idadi ya watu waliokuwa katika maeneo yale.
Mheshimwa Spika, eneo la Kipawa, Kiwalani na maeneo haya ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyasema ni kweli, ukiangalia yana sifa zinazofanana na maeneo ya Vingunguti kwamba watu ni wengi.
Mheshimiwa Spika, naomba nisema kwamba mimi nipo radhi kabisa kukutana na Mheshimiwa Mbunge kubadilishane mawazo, kwamba tutafanya vipi na kwa sababu nikijua Halmashauri ya Manispaa ya Ilala wana mikakati mikubwa sana ya ujenzi wa sekta afya ukiangalia demand ya sasa hivi iliyokuwepo hivi sasa hospitali yetu ya Amana inazidiwa, hata Hospitali ya Taifa ya Muhimbili idadi ya wagonjwa imekuwa wengi, ni kwa sababu katika ngazi ya chini tunakosa facilities za kuwasaidai wananchi kiasi kwamba kila mngojwa anaona kwanza aende Hospitali ya Taifa.
Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI jukumu letu kubwa ni kwamba katika mpango unaokuja tuhakikishe tufanye kila liwezekanalo. Huduma ya afya tuipeleke chini zaidi kupunguza ile referral system inayoenda juu ili kuhakikisha hospitali zetu za ngazi za juu ziweze kupata fursa nzuri zaidi.
Mheshimiwa Spika, hili kwa sababu Waziri wa Afya kesho ata-table bajeti yake hapa, tutaona mipango mipana katika Wizara Afya ambayo ina lenga moja kwa moja kutatua tatizo la suala la afya katika jamii yetu.
changamoto kubwa ya zahanati hizi katika Jimbo la Segerea na Manispaa ya Ilala ni maeneo lakini wapo watu wanaoishi jirani na maeneo hayo, wapo tayari kutoa maeneo yao kwa ajili upanuzi wa maeneo ya zahanati hizi.
Je, Serikali ipo tayari kusaidiana na Halmashauri ya Ilala kulipa fidia kwa ajili ya kuongeza ukubwa wa maeneo ili kupata zahanati na vituo vikubwa vya afya katika maeneo ya Jimbo la Segerea na Manispaa ya Ilala kwa ujumla?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kama nilivyosema katika jibu letu la awali, mahitaji ya afya hapa yamekuwa ni changamoto kubwa sana, nilipofanya reference tulipokuwa na Mbunge wa Segerea kipindi kilichopita, alipokuwa na timu iliyoenda eneo la Vingunguti katika machinjio yale, vilevile akaja katika ofisi yangu kuona jinsi gani tutafanya, licha ya suala la machinjio lakini wananchi wana changamoto ya afya.
Mheshimiwa Spika, mimi naamini hayo mawazo ni mazuri, tutakaa vizuri kubadilishana mawazo ili tuone ni jinsi gani tutafanya ujenzi wa zahanati au kituo cha afya maeneo yaweze kupatikana. Lengo kubwa ni kwamba kina mama na watoto wa maeneo yale waweze kupata huduma kama wengine.
Mheshimiwa Spika, ajenda yetu kubwa ni kuhakikisha kwamba hospitali zetu za rufaa sasa tupunguze idadi ya wagonjwa siyo mtu anaumwa mguu mpaka aende Muhimibili au Amana haiwezekani hata kidogo. Lazima tuhakikishe mfumo mzuri unatengenezwa katika sekta ya afya katika ngazi za chini kusaidia sekta za juu ziweze kufanya huduma kubwa zinazohitajika.
MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya ndugu yangu Naibu Waziri.
Je, Serikali haioni kila sababu ya kupeleka visima vya maringi kwa kuanzia katika maeneo hayo ya Delta?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba niweke rekodi sawa katika harakati za kutekeleza miradi mimi naomba nimsifu huyu Mbunge maana siku zote anakuja pale ofisini kwangu na amekuwa akifanya juhudi kubwa kwa Jimbo lake, wakati mwingine anatumia hata resource zake mwenyewe kwa ajili ya Jimbo lake. Lakini mahitaji yake ni jinsi gani tutafanya visima vya ringi viweze kujengwa, naomba niseme ngoja tulichukue hili.
Lakini kwa ukubwa wake zaidi lazima tuseme kwamba maeneo ya Delta yote yana shida kubwa sana, nikisema suala la Delta halikadhalika hata juzi nilikuwa najibu swali la ndugu yangu Mbunge wa Jimbo la kule Mwanza, ni kwamba maeneo haya yenye delta yana matatizo makubwa sana siyo maji peke yake hata huduma nyingine za afya na elimu.
Kwa hiyo, nikuombe ndugu yangu kwamba tutajitahidi kufanya kila liwezekanalo ikiwezekana ni kwamba maeneo haya tuweze kuyapatia huduma ya maji ili wananchi wa Kibiti na wao wajisikie kama sawa na wananchi wengine.
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, katika Jimbo la Bunda Mjini tangu nikiwa Mbunge wa Viti Maalum nilikuwa nazungumzia mradi wa maji wa kutoka Nyabeu kuja Bunda Mjini. Huo mradi una miaka nane, sasa niulize hivi ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa mradi ule, wananchi wa Bunda ambao hawajawahi kupata maji safi na salama tangu uhuru waone na wenyewe ni wananchi wa Tanzania na ndiyo liwe swali la mwisho kuuliza katika Bunge hili Tukufu.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, na mimi naomba nikiri wazi kwamba Mheshimiwa Ester toka tukiwa katika timu moja alikuwa akiuliza swali hili, naomba niseme.
Mheshimiwa Spika, lakini najua kabisa katika mpango wa maji ambao nadhani Wizara ya Maji watakapokuja ku-table bajeti yao hapa watazungumzia jinsi gani wana programu kuhakikisha maeneo haya miradi yote ya maji inaenda kukamilika. Ukiangalia jinsi gani watazungumza katika bajeti yao ya Wizara ya Maji, sitaki kuwazungumzia sasa. Lakini nikijua kwamba Wizara ya Maji na TAMISEMI ni Wizara pacha, tunahusiana Wizara ya Maji, TAMISEMI, Kilimo halikadhalika na Wizara ya Afya. Mambo yetu yanaingiliana yote kwa pamoja kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi. Ninajua kabisa katika mpango wa maji wa sekta ya maji namba mbili imeweka mipango ya kumalizia miradi yote ya muda mrefu. Mimi ninaamini wananchi wa Bunda kipindi hiki sasa ule mradi wa maji kama Serikali ilivyokusudia utaweza kukamilika katika kipindi hiki.
MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza:
Mheshimiwa Naibu Spika, Naibu Waziri amesema mwaka huu Serikali imetenga shilingi milioni 50. Hizi hela ni hela za Halmashauri, own source ya Halmashauri na mimi Mbunge nitachangia katika hela hizo. Mimi ninalosema Serikali kutoka Makao Makuu iwe Wizara ya Afya au TAMISEMI watachangia kiasi gani kwenye hospitali hiyo ambayo ni ya wananchi wa Wilaya ya Chunya hilo la kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Bunge lililopita la Kumi Serikali ilianzisha mpango wa kukarabati hospitali za Wilaya kumi, kuziinua kiwango ziweze kutibu maradhi yote ili kupunguza congestion kwenye hospitali ya rufaa na Chunya ilikuwa mojawapo katika hospitali hizo kumi katika Tanzania.
Je, huo mpango umefia wapi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli safari hii imetengwa shilingi milioni 50 na tunapofanya mobilization of resources mara nyingi sana kuna vipaumbele, najua wazi kwamba pesa hizi ni own source. Lakini siyo kusema kwamba kwa vile ni own source basi Serikali maana yake haina jicho lake ndiyo maana mchakato wa bajeti kuna pesa nyingine zinatoka katika Serikali za Mitaa na nyingine zinatoka katika Serikali Kuu. Wakati mwingine kipaumbele cha baadhi ya vipengele inaenda katika miradi mingine. Kwa hiyo, lengo kubwa ni Serikali kupeleka mchakato huo mpana na mwisho wa siku ni kwamba wananchi kuweza kupata huduma.
Mheshimiwa Mwambalaswa naomba nikuhakikishie kwamba hela hii ni own source na ninajua kwamba na ninyi mmefanya harakati na wewe mwenyewe ulikuwa ukisimamia ile harakati ya harambee. Mimi naomba niwapongeze kwa sababu miongoni mwa watu ambao wamefanya wenyewe kuhakikisha kwamba wanafanya harambee tena ikiongezewa na Mbunge Mwambalaswa nikupongeze katika hilo. Naomba nikuhakikishie kwamba katika mchakato wetu najua hii itakapokuwa imekamilika lazima kutakuwa na mapungufu mengine yatakuwa yanajitokeza katika kuhakikisha hospitali ile inaweze kufanya kazi. Jukumu la Serikali mwisho wa siku ni kwamba hospitali ile ya Chunya iweze kuwa na hadhi sasa kama nyingine, naomba nikuhakikishie kwamba tutakuunga mkono kwa nguvu zote kwa vile umekuwa ukipigania katika hili tutashirikiana kwa jinsi zote.
Suala zima la ukarabati kama ulivyosema kulikuwa na mchakato wa ukarabati ni kweli, na maeneo mbalimbali ukarabati huu ulikuwa unaendelea. Lakini bado tukiri wazi tatizo hili bado ni kubwa sana ukiachia ukarabati; hata niliposema wiki iliyopita, kwamba ukiacha ukarabati halikadhalika kuna majengo mengine ambayo hayajakamilika. Ndiyo maana tumetoa maelekezo wiki iliyopita nimesema Halmashauri zote hata Mheshimiwa Mwambalaswa tulikuuliza kule Chunya kuwa Mkurugenzi atakuwa amepata waraka kutoka TAMISEMI, lengo letu ni nini, najua kuna mambo tumeyafanya lakini bado mapungufu yapo makubwa zaidi, tuweze kubainisha hizo changamoto tuzipangie mkakati wa pamoja sasa jinsi gani tutafanya kurekebisha matatizo haya hasa ya magofu ambayo hayajakamilika lakini kuhakikisha hadhi za hospitali zetu za zahanati ziwe sawa sawa. Nadhani mchakato huu utakuwa mpana sana ili kukidhi matakwa ya ilani ya Chama Cha Mapinduzi kama tulivyoahidi wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimuahidi Mheshimiwa Mwambalaswa kwamba tutakuunga mkono katika juhudi kubwa ulizozifanya katika Jimbo lako la Chunya na Halmashauri yako ya Chunya.
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Nkasi leo ina miaka 40 tangu ilipoanzishwa, lakini haina hospitali ya Wilaya, wala Serikali haina mpango wa kujenga hospitali ya Wilaya. Ni lini Serikali yetu itakuwa na azimio la kujenga hospitali ya Wilaya hasa katika Makao Makuu ya Wilaya katika Mji wetu wa Namanyere?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ninamfahamu Mheshimiwa Keissy kuhusu suala la tatizo la afya. Miongoni mwa mambo ambayo ninayakumbuka Mheshimiwa Keissy alipendekeza kituo kimoja kile cha afya kukipandisha grade kuwa hospitali ya Wilaya kama sikosei. Alizungumza hapa Bungeni kwamba kituo kile cha afya licha ya kuwahudumia wananchi wa Jimbo lake, wengine wanatoka katika nchi mpaka ya Congo. Hili nilisema siku ile kwamba Mheshimiwa Keissy jambo hili tumelichukua, katika mpango wa pili wa afya kila Halmashauri kuwa na hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Keissy naomba niseme tu kwamba tutaungana pamoja katika mipango kwa sababu tunajua Wilaya yako ipo pembezoni na ina changamoto nyingi. Tutajitahidi kwanza kuhakikisha kile kituo cha afya tunakiangalia na mimi nimekiri wazi kwamba nikija kwako lazima nikitembelee kituo cha afya, tutashawishi wenzetu wa Wizara ya Afya wakiangalie kama kimefikia vigezo kipandishwe kuwa hospitali ya Wilaya, tutakuunga mkono ili wananchi wa eneo lako lazima wapate afya. Jambo hili umelipigia kelele sana toka Waziri Mkuu wa mwanzo Mheshimiwa Peter Pinda nilikusikia ukilizungumza, nasema kwamba tupo pamoja katika hili.
MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru kwa kuniona na mimi naomba niulize swali moja tu dogo la nyongeza;
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Wilaya hii ya Chunya ni mojawapo ya Wilaya kongwe sana Tanzania, lakini hospitali hii haina vifaa tiba wala matibabu ni kweli. Pia akina mama kwenye wodi ya wazazi wanapata shida mpaka wanajifungulia chini, naomba kujua Serikali ina mkakati gani kuiangalia jicho la ziada Wilaya hii kongwe nchini
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ya vifaa tiba na siyo vifaa tiba tu maana yake kuna changamoto nyingi, ukienda kwenye vifaa tiba utakuta changamoto ya madawa, ndiyo maana katika mpango wetu wa sasa ninawashukuru sana wenzetu wa Wizara ya Afya ukiangalia mpango mkubwa tunaondoka nao, suala zima la vifaa tiba, madawa katika bajeti ya mwaka huu imeji-reflect kabisa ni jinsi gani tutafanya hasa hospitali zetu za Wilaya ziweze kuwezeshwa. Maelekezo makubwa tumeona hospitali nyingi sana mara nyingi zinasuasua katika suala la madawa na vifaa tiba na ndiyo maana mpango wetu mkakati sasa hivi ni kuhakikisha kwamba tunafanya collection ya kutosha, mara nyingi pesa zilikuwa zinakusanywa lakini siyo zile zinakusanywa zinaingia katika Halmashauri na hospitali, nyingi zilikuwa zinapotea.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana tumeasisi hii mifumo ya ki-electronic, hata mwanzo pesa zikikusanywa zilikuwa hazitumiki zote kwa matumizi ya hospitali, mengine watu walikuwa wanatumia kwa ajili ya kulipana per diem mwisho wa siku ni kwamba hata dawa na vifaa tiba vinakosekana. Kwa hiyo kutokana na mwongozo tumesema kwamba pesa zote zinazokusanywa katika hospitali za Wilaya ukiachia na mafungu mengine, lengo letu kubwa kwamba hii mifumo ya electronic tutakusanya fedha lakini lazima mwongozo ufuatwe. Je, asilimia ngapi inaenda katika vifaa tiba na asilimia ngapi inaenda katika dawa, mwisho wa siku tuweze kutatua tatizo la dawa na vifaa tiba katika hospitali zetu.
Hili Mheshimiwa Mwanjelwa tutaenda kulisimamia katika mwaka huu wa fedha ili kuongeze ufanisi katika hospitali zetu za Wilaya na hospitali zetu mbalimbali wananchi waweze kupata huduma.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi nina swali dogo la nyongeza;
Kwa kuwa, wananchi wa Kijiji cha Majami, Kibolianana, Mlembule na Mgoma tayari wameshaonesha juhudi ya kujenga majengo ya zahanati, kilichobaki ni Serikali kusadia. Lakini Igodi Kusini, Isalanza jengo lipo tayari limekamilika pamoja na Igodi Kaskazini.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri utakuwa tayari kuwapelekea watu wa Igoji Kaskazini na Kusini huduma ya madawa na kusaidia hawa ambao tayari wameonesha nguvu za kujenga zahanati?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesikia kilio hiki na bahati nzuri Mheshimiwa Lubeleje kama ukifanya reference mwenyewe hili ni miongoni mwa maswali mengi sana aliyouliza katika sekta ya afya, Mheshimiwa Lubeleje nikuhakikishie kwamba katika eneo hilo kwanza ahadi zetu zile za kwanza ni lazima tutazitembelea zahanati hizi kuziangalia kama kuna changamoto tuweze kuzitatua; hali kadhalika tutafanya utaratibu jinsi ya upatikanaji wa dawa, kwa sababu nikijia Jimbo lako ni kubwa, maeneo yako ni makubwa. Nimefika katika sehemu wanaita Makutupa, kutoka Makutupa mpaka mtu anaenda kufuata huduma ya afya ni mbali sana. Kwa hiyo Mheshimiwa Lubeleje juhudi unayoenda kufanya endelea kuifanya, tutaunga mkono lakini lazima tu-visit tuangalie kama kuna changamoto nyingine tuweze kurekebisha, tuwaambie wataalamu wetu tuweze kufanya hata allocation ya wataalamu wa ndani na madawa tutafanya ili vituo hivi viweze kufanya kazi na wananchi waweze kupata huduma.
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na commitment ya Serikali kutoa shilingi milioni 50 kwa ajili ya sekondari ya Bulunde na kutoa fedha kwa ajili ya sekondari ya Chief Itinginya. Nataka nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri swali dogo moja;
Kwa kuwa, jitihada za wananchi na Mbunge wa Jimbo la Nzega ni kumalizaS ya Bulunde ili tuwe na high school, na kwa kuwa, mahitaji ya fedha yaliyotengwa na Serikali kwa ajili ya shule ya Chief Itinginya hayatoweza kumaliza ujenzi wa shule ile kuwa na high school katika sekondari ya Chief ya Itinginya, mahitaji halisi ni shilingi milioni 250.
Je, Serikali iko tayari kuongeza fedha kwa ajili ya ujenzi wa sekondari ya Chief Itinginya, ili katika Halmashauri ya Mji wa Nzega tuwe na shule mbili za A-level ?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba niseme wazi kwamba, Mheshimiwa Bashe kama nilivyosema pale mwanzo, ninajua una juhudi kubwa sana unaendelea kuifanya pale Nzega na umekuwa kila wakati ukija pale ofisini siyo kwa suala hilo tu, hata suala zima la kukuza uchumi wa maeneo yako ya vibanda pale, lengo ni kwamba mpate mapato muweze kuelekeza katika huduma za kijamii, kwa hiyo lazima tu-recognize juhudi kubwa unayoifanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Serikali kwa sababu mchakato wa bajeti wa mwaka huu umeshapita na bajeti ya mwakani tunaona ni jinsi gani tutafanya. Lengo ni kusukuma nguvu kuwasaidia watu wa Nzega. Ni kweli haiingii akilini eneo kama lile ambapo population ni kubwa, watoto wengi wanafaulu lakini wanakosa fursa ya kusoma.
Kwa hiyo, Serikali tutashirikiana nanyi kwa pamoja, Halmashauri na Ofisi ya Rais, TAMISEMI tutaangalia jinsi gani tutafanya kuiboresha Nzega sasa iwe na thamani hiyo ya ukuaji wake wa Mji na Mji wa kihistoria tokea enzi za madini ya almasi, basi watu waone mwisho wa siku wananchi wa Nzega waweze kunufaika.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikuhakikishie kwamba, juhudi ya Serikali tutakaa pamoja tutajadiliana nini kinatakiwa kifanyike na katika muda gani na kuangalia resource zilizokuwepo tuweze kusukuma watu wa Nzega waweze kupata fursa ya elimu.
MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo hili la kuanzisha shule za kidato cha tano katika nchi yetu linafanana kabisa na tatizo ambalo liko kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Halmashauri ambayo ni kongwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatuna hata high school moja kwenye hiyo Halmashauri yetu ya Wilaya ya Bunda. Wananchi katika miaka mitano tumewahamasisha, tumejenga mabweni na mabwalo lakini tumeshindwa kukamilisha kwa sababu ya fedha na Serikali tumekuwa tukiitaka itusaidie.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri uko tayari kuambatana na mimi na Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere ili twende kwenye Halmashauri yetu ukajionee juhudi za wananchi ili muweze kutusaidia?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kiufupi Mheshimiwa Kangi Lugola ndugu yangu nikuambie kwamba, mimi niko tayari kuambatana na wewe na Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere ambaye ni jirani nyuma yangu hapa. Tutajitahidi tuende pamoja siyo kwa suala hilo la shule tu inawezekana tukabaini mambo mengi sana kwa ajili ya wananchi wa eneo hilo.
MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
Kwa kuwa, tatizo lililoko Halmashauri ya Nzega linafanana kabisa na Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, haina Sekondari ya kidato cha tano na sita. Kwa kuwa, Serikali ilitupa ukomo wa bajeti bilioni 14 na tumeshindwa, tumekatwa fedha nyingi za maendeleo.
Je, Ofisi ya Rais TAMISEMI, iko tayari kututafutia fedha kwenye vyanzo vingine ili tuweze kujenga sekondari ya kidato cha tano na sita katika Halmashauri yetu ya Wilaya ya Nsimbo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli najua kwamba, mwaka huu kulikuwa na suala zima la ukomo wa bajeti lakini ndiyo mwaka pekee ambao bajeti yake imevuka tumeenda karibuni kutoka bajeti ya maendeleo ya asilimia 27 mpaka asilimia 40, kwa hiyo kuna kazi kubwa imefanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa siwezi kusema kwamba, mwaka huu kuna fedha zingine zitaingia kwa sababu mchakato wa bajeti umeshapita. Lengo kubwa ni nini! Nina imani kwamba, katika mwaka mwingine wa fedha unaokuja hii itakuwa ni kipaumbele kwa sababu tunajua wazi kwamba, tumejenga shule nyingi za Kata vijana wengi wanafaulu. Kwa mfano, mwaka huu tuna vijana karibuni zaidi ya elfu tisini, lakini ukiangalia capacity yetu inaenda karibuni vijana zaidi ya elfu hamsini, maana yake inaonekana tuna tatizo kubwa sana la kuhakikisha tunaweka miundombinu kuwa-accommodate vijana wa form five na form six.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Richard Mbogo katika mchakato wa bajeti wa mwakani tuweze kuliangalia kwa pamoja zaidi. Hata ikiwezekana kwa sababu mambo haya tumesema kwamba, hata shule zingine za Kata ambazo ziko vizuri tunaweza tukazi-upgrade zile baadhi ya shule kuziongezea miundombinu kuweza kuwa shule za form five na form six.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwahiyo katika mwaka wa fedha unaokuja tutaangalia kwa pamoja ni jinsi gani tutatanya Nsimbo tupate high school moja kwa ajili ya vijana wetu.
MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa, matatizo yaliyopo Nzega yanafanana kabisa na Halmashauri ya Morogoro hatuna high school hata moja katika Halmashauri yetu ya Morogoro Vijijini.
Je, Serikali ina mpango gani wa kutusaidia ambao ukizingatia juhudi za wananchi tumejitahidi tumejenga ile Sekondari ya Nelson Mandela. Je, Serikali ina mpango gani wa kutuongezea nguvu ili kuimalizie shule ile angalau Halmashauri hii iwe na shule hata moja ya sekondari?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nilifika kwa Mheshimiwa Mbunge, ukitoka pale Morogoro Mjini pale kwa mfano unatoka Ngerengere pale, ukienda mpaka kule mwisho unaenda Kidunda halafu mpaka kule mbali zaidi wananchi wanapata shida.
Mheshimiwa Naibu Spika, mfano mtoto akitoka pale maana yake changamoto yake ni kubwa. Ni vizuri zaidi tungepata shule moja ya form five pale, kwa hiyo naomba nikuambie kwa mwaka huu kwa sababu bajeti imeshapita, imani yangu ni kwamba kwa mwaka wa fedha unaokuja 2017/2018 anzeni kuweka maoteo ya bajeti zenu katika Halmashauri, then na sisi huko Ofisi ya Rais TAMISEMI tutaona hicho ni kipaumbele kikubwa ili eneo lile sasa la Mandela tuweze kupata shule ya form five na form six angalau tupate high school moja katika maeneo hayo na Wizara ya Elimu ikija ikiona kwamba, vigezo vimefikiwa basi shule ile itapandishwa kuwa ya form five na form six.
Mheshimiwa Mbunge, naomba nikupongeze kwa juhudi kubwa tutashirikiana kwa pamoja, naomba lianze hilo wazo kwenu then Ofisi ya Rais TAMISEMI katika mchakato wa bajeti itaona siyo mbaya sasa kuipa kipaumbele eneo hili kupata shule ya form five na form six kwa ajili ya vijana wetu.
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la Mchinga linafanana sana na tatizo la Halmashauri ya Tandahimba iliyopo Mkoani Mtwara, je, Serikali ina mpango gani sasa wa kugawanya Halmashauri ya Tandahimba ili kuwe na Halmashauri mbili?
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili, Wilaya ya Mtwara sasa hivi ina Halmashauri tatu, Mtwara Manispaa, Halmashauri ya Mtwara na Halmashauri ya Mji wa Nanyamba, je, Serikali ina mpango gani kumpunguzia mzigo Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, ili kuanzisha Wilaya mpya ya Nanyamba?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA:Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema awali katika jibu langu la msingi ni kwamba mgawanyo huu wa Halmashauri na halikadhalika uanzishaji wa kata mpya, uanzishwaji wa vijiji halikadhalika uanzishwaji wa Wilaya una taratibu zake. Na nilizungumzia kwamba, kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 145 Ibara ya 146 inayoanzisha Mamlaka ya Serikali za Mitaa, lakini kwa mujibu wa Sheria ya 287 inaainisha jinsi gani mchakato huu unaenda.
Sasa kwa Wilaya, Halmashauri ya Tandahimba, kwa mujibu wa Mheshimiwa Mbunge alivyoshauri ni kwamba mimi ninamshauri kwa sababu najua Mheshimiwa Chikota ni Mtaalamu mkubwa sana wa Serikali za Mitaa, tukimkumbuka katika reference yake alipokuwa katika ngazi ya mkoa hapo awali. Kwa hiyo, naona kwamba yeye awe chachu kubwa ya kutosha na mimi naona jambo hili halitamshinda. Mchakato ule utakapokamilika katika maeneo yake akija katika Ofisi ya Rais – TAMISEMI sisi hatutasita kufanya maamuzi sahihi kulingana na vigezo vitakavyokuwa vimefikiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika suala zima la hizi Halmashauri sasa kupata Wilaya Mpya ya Nanyamba ni kama nilivyosema awali. Nakuomba Mheshimiwa Chikota fanya utaratibu huo, wataalam watakuja site, wata-survey kuangalia vigezo vinafikiwa vipi; na mimi najua Kanda ile ukiangalia eneo lake ni kubwa sana siku nilipokuwa natoka Songea kwenda mpaka Masasi hapa katikati jiografia ya maeneo yale unaona kwamba, jinsi gani maeneo ya kiutawala mengine yako makubwa sana. Kwa hiyo, fanyeni hayo, baadae sasa Ofisi ya TAMISEMI itafanya tathmini na kuona kufanya maamuzi sahihi.
MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ilishatuma maombi ya kugawa Halmashauri ambayo iliambatana na maombi ya Wilaya, Jimbo na kupitia vikao vyote kuanzia Vijiji, WDC, DCC, RCC na kuonekana kwamba, ina vigezo vyote na hata watawala ambao wametawala maeneo hayo wanaujua ukweli huo; kwa mfano Mheshimiwa Manyanya, Mheshimiwa Mkuchika, hata baadhi ya Wabunge ndani humu, hata Waziri Mkuu aliyepita alishashuhudia ndani ya Bunge. Je, ni lini wananchi hawa watapata haki yao ya kugawanya Halmashauri?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika kumbukumbu yangu Mheshimiwa Malocha ndiye alinisababisha mpaka nikaanda database ya kuona kwamba Halmashauri zilizoleta matakwa ya kugawanywa Halmashauri halikadhalika Mikoa. Nikiri wazi kwamba Mheshimiwa Malocha alikuja mpaka ofisini kwangu tukalijadili suala hili na ndio maana nikawatuma wataalam wangu waandae database hiyo ikiwemo pamoja na uanzishwaji wa mji mpya kwa kaka yangu hapa kukata maeneo ya Korogwe ilikuwa yote pamoja katika mchakato huo, Mheshimiwa Profesa Maji Marefu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, na lile ndio maana tumepata muongozo sasa hivi kama viongozi wapya katika eneo hilo. Tumewatuma wataalam wetu sasa hivi wanaandaa kikosi kazi kwa ajili ya kutembelea maeneo yote ya Tanzania ili kubainisha yale maombi yaliyokuja waliofikia vigezo, kama ndugu yangu Mheshimiwa Malocha anavyosema huko, waliofikia vigezo kwamba waweze kupata hizi halmashauri na Wilaya mpya au halikadhalika Mikoa mipya ambayo imependekezwa. Basi haya yakifanyika, naomba nikuahidi Mheshimiwa Malocha kwamba timu itafika kule site kufanya final finishing, kumalizia zoezi la mwisho la kuhakiki na nikijua kwamba, eneo lako kweli ni eneo kubwa na umekuwa ukililalamikia kwa muda mrefu. Kwa hiyo kikosi kazi kitafika kule site kama maelekezo tuliyopeana pale ofisini kwangu.
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi. Wilaya ya Tanganyika ni Wilaya mpya ambayo ina Jimbo moja tu la Uchaguzi la Mpanda Vijijini. Eneo hili la kiutawala ni kubwa mno, lina uwezo wa kutoa mgawanyo wa halmashauri mbili, kwa maana ya Ukanda wa Ziwa, Halmashauri ya Karema na ukanda wa huku juu eneo la makazi mapya ya Mishamo. Je, ni lini Serikali itafikiria kutoa mamlaka ya kugawa maeneo haya, ili yaweze kuwasaidia wananchi wa Mpanda kwa ujumla?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba, Wilaya ya Mpya ya Tanganyika, lakini pale awali nadhani tulikuwa katika mchakato ulikuwa hatuna Wilaya hii, lakini baadaye mchakato ukafanyika tukapata Wilaya, lakini bado changamoto ni kubwa sana ya Halmashauri hii. Kwa hiyo, naomba niseme tena vilevile Mheshimiwa Kakoso kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi ya awali kwamba mimi naomba Mheshimiwa Mbunge kwa sababu najua eneo lenu nalo limegawanyika sana hapa katikati, Halmashauri nyingi zimepatikana katika eneo hilo, lakini bado kijiografia eneo bado ni kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nipende tena nitoe maelezo yaleyale kama niliyotoa mwanzo ni kwamba, andaeni tena ule mchakato upite katika vigezo vyote, katika vijiji, WDC, Halmashauri, RCC, halafu ikifika katika Ofisi ya Rais – TAMISEMI kama nilivyosema ni kwamba, tutafanya maamuzi sahihi kutokana na vigezo vitakavyokuwa vimefikiwa katika eneo hilo.
MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa mazingira ya Mchinga yanafanana kabisa na Wilaya ya Tunduru yenye kilometa za mraba 18,776; na kwa kuwa tayari kuna majimbo mawili na taratibu zote za kuigawa Wilaya ile zilishafanyika siku za nyuma; na kwa kuwa zilitolewa ahadi za viongozi wa Awamu ya Nne kuigawa Wilaya ile na Mkoa kwa ujumla. Je, ni lini taratibu za kuigawa Wilaya ile na Mkoa mpya wa Selous zitafanyika?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika kumbukumbu zangu nilizokuwanazo ni kwamba eneo analozungumzia Mheshimiwa Mpakate ni kweli jambo hili liko ofisini, lakini nadhani kuna baadhi ya vitu vingi zaidi ya hapo hata kuna suggestion ya kugawa kupata Mkoa mpya wa Selous, kama sikosei katika eneo hilo! Na Mheshimiwa Ngonyani alikuwa akizungumza jambo hilo na hata Mheshimiwa Ramo Makani alikuwa katika mchakato huo wa pamoja kuhakikisha kwamba maeneo hayo, kutokana na jiografia yake, tunapata Mkoa mpya wa Selous.
Kwa hiyo, sasa kama Ofisi ya TAMISEMI itafanya uhakiki jinsi gani, aidha hizo Wilaya, Halmashauri au Mkoa mpya, mwisho wa siku tutakuja na majibu sahihi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo kubwa ni kwamba kupeleka utawala katika eneo hilo kwa sababu, ni kweli, kuna wananchi wengine saa nyingine ukitoka huku Tunduru kwenda hata kule Ruvuma kuna changamoto, lakini uko karibu hapa karibu na Masasi. Kwa hiyo, walikuwa na maombi mengi kwa pamoja na viongozi waliopita walitoa ahadi mbalimbali.Ofisi ya TAMISEMI italifanyia kazi na mwisho wa siku ni kwamba, eneo hilo ki-jiografia litagawanywa vizuri kwa suala zima la kiutawala ilimradi wananchi wapate huduma ya karibu katika maeneo yao
pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini pamoja na changamoto kubwa ya maji katika kata nilizoainisha lakini tumekuwa na tatizo sugu katika suala la maji katika Mji wetu Mkuu wa Pangani, na mpaka sasa nioneshe masikitiko yangu kutokana na changamoto hii ya maji, fedha zilizokuwa zimeidhinishwa katika bajeti iliyopita kiasi cha shilingi milioni 200 mpaka sasa nazungumza hazijafika.
Je, ni nini commitment ya Waziri kuhakikisha kwamba fedha zile zilizoainishwa kwa ajili ya kwenda kutatua tatizo la maji mjini, na ni lini zinapelekwa na wakati bajeti inafikia ukingoni? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali langu la pili; Wilaya yetu ya Pangani imejaliwa kuwa na Mto Pangani ambao unatiririsha maji baharini. Ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba inautumia mto huu kwa kuanzisha mradi mkubwa wa maji ambao utaweza kutatua suala zima la maji kwa Wilaya yetu ya Pangani na Wilaya za jirani kwa maana ya Muheza na Tanga Mjini?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kilio cha Mheshimiwa Mbunge ni kweli kilio sahihi, kwa reference ni kwamba miaka miwili iliyopita nilienda na nililala mpaka katika ule Mji wa Mwera pale. Nimeweza kubaini tatizo la maji katika Mji wa Pangani, lakini kama hiyo haitoshi nikaenda mpaka Redio Pangani nikawa nina kipindi cha moja kwa moja cha kuongea na maswali ya wananchi pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninawashukuru wananchi wa Pangani wengi walipiga simu kusikia Mbunge wa Pangani yuko eneo lile na miongoni mwa shida ambayo waliizungumza ilikuwa ni shida ya maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, na ni kweli, ule Mradi wa Pangani nadhani ulianzishwa takribani pale Pangani Mjini kati ya mwaka 1963 au 1973, miundombinu yake kweli kwa idadi ya watu waliokuwa wanahudumiwa kipindi hicho kwanza imechakaa, lakini population kipindi hicho ilikuwa ni ndogo. Ndio maana katika Ofisi ya Mheshimiwa Mbunge harakati zilizofanyika ni kwamba Ofisi ya Mkurugenzi walipeleka maombi maalum katika Wizara ya Maji, walitaka shilingi milioni 400 ikiwezekana kwamba waweze kupata bajeti ya kukarabati miundombinu ile.
Mheshimiwa Naibu Spika, walipata awamu ya kwanza shilingi milioni 200 kutoka Wizara ya Maji, lakini hata hivyo wanasubiria kwamba kwa sababu ule mradi wa milioni 200 umepelekwa pale Pangani Mashariki, lakini kuna maeneo mengine bado ukarabati haujafanyika ikiwemo sambamba na ukarabati wa tenki. Kwa hiyo, ni kwamba Serikali imesikia hiki kilio na inalifanyia kazi ndio maana nimezungumza haya yote.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sambamba na hilo ni program kubwa ni kweli, haiwezekani hata kidogo eneo la Pangani ambalo Mto Pangani ni mkubwa unapoteza maji baharini, halafu wananchi wa Pangani hawapati maji! Na hili ndio maana leo hii niliongea na Mkurugenzi wa Pangani pale na ameniambia sasahivi yuko Mahakamani kuna kesi za uchaguzi zinazoendelea; nikamwambia, nini programu yake anayotaka kuhakikisha Mto Pangani unatumika?
Mheshimiwa Naibu Spika, amekiri kwamba, sasahivi wanafanya utafiti na inaonekena gharama ya shilingi bilioni 10 nadhani itahitajika kwenye mradi ule, lakini bado iko katika suala zima la tathmini, lakini hili niseme ni nini! Ni kwamba Wizara ya Maji nayo ilisema kwamba sasa wataenda kutumia kama Serikali tutaenda kutumia vyanzo vyote vinavyowezesha kutumia maji. Imani yangu ni kwamba Mto Pangani tunaweza kuutumia katika sekta ya maji hasa Programu ya Awamu ya Pili ya Maji ambayo tunaenda kuibua suala zima la kutatua tatizo la maji kwa wananchi wetu wa Tanzania.
MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Katika Jimbo la Korogwe Vijijini kulitokea kampuni ambayo sio mali ya Serikali, UNDP, ilinipa milioni 243 nikachimba visima tisa. Baada ya kuchimba visima hivyo walikuja wataalamu wa Serikali wakasema sehemu hizi tukichimba tutapata maji safi, lakini cha kusikitisha baada ya kuchimbwa maji yale yalivyokwenda Serikalini kuleta majibu nikaambiwa maji yale hayafai kutumika kwa binadamu na hela tayari zimeshatumika shilingi milioni 243.
Je, hii hasara ambayo wameipata wananchi wa Jimbo la Korogwe Vijijini italipwa na nani?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani Naibu Waziri Wizara ya Maji siku ile kama mtaalam wa maji, amezungumza hapa kwamba, mara nyingi sana taaluma zetu hizi za maji wakati mwingine unaweza kufanya survey, lakini hujui kiwango gani cha maji utakipata! Lakini sio kiwango cha maji, hata ule ubora wa maji wa kiasi gani!
Mheshimiwa Naibu Spika, na ndio maana ukiangalia, kwa mfano katikati tulikuwa na mradi kutoka China, tulipata visima kwa Wilaya ya Kilosa na Wilaya ya Kisarawe. Katika visima vilivyochimbwa ikaonekana kwamba kiwango cha madini ya chuma yako mengi zaidi ya madini ya aina mbalimbali maji yale hayafai kunywa! Halikadhalika katika eneo lako, kwanza nikupongeze kwa sababu umefanya initiative ya kupata watu ambao wanakusaidia kuchimba maji, maji yamechimbwa, lakini ubora wa maji bado hauko sawasawa! Naomba nikwambie itakuwa ni jambo la ajabu kusema kwamba gharama ile italipwa na nani!
Mheshimiwa Naibu Spika, itakuwa ni jambo la ajabu ni kwa sababu, maji yamepatikana, lakini mtaalamu wa maji hata anavyofanya survey hawezi kusema maji haya nikiyatoa hapa yatakuwa matamu au ya chumvi! Jambo hilo bado ni gumu na wataalam wote wanakiri hivyo. Kwa hiyo, nini cha kufanya; cha kufanya ni kwamba kwa sababu visima vile maji hayajawa na ubora uliokusudiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni jukumu la Serikali sasa tuweke mipango mipana jinsi gani tutawasaida wananchi wa Jimbo lako waweze kupata huduma huduma ya maji kama sera ya maji inavyoelekeza hivi sasa kwamba wananchi waweze kupata maji. Mbunge nakujua kama ni mpiganaji na hili litawezekana katika maeneo yetu.
MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante. Ni kweli kama alivyosema Naibu Waziri kwamba Serikali itaendelea kutekeleza ahadi za Serikali ya Awamu ya Tano. Naomba nimuulize kama anafahamu pia kwamba kuna mradi wa barabara kutoka Singida – Irongero – Mtinko - Meria mpaka inaungana na Mkoa wa Manyara ambayo pia ilikuwa ni ahadi ya Rais aliyemaliza muda wake. Je, yuko tayari pia kuiingiza barabara hii katika mchakato wa kuikamilisha mapema ili wananchi wale wasiendelee kusubiri kwa muda mrefu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martha Mlata kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, anachosema Mheshimiwa Mlata ni kweli na juzi nilikuwa katika Mkoa wa Singida na hiyo barabara ni miongoni mwa barabara ambazo nimeziona. Jambo la kufurahisha zaidi katika barabara hiyo, Waziri mweye dhamana ya Miundombinu alipita na kuna daraja la Sibiti ambapo amesema katika bajeti ya mwaka huu mchakato wa lile daraja tayari umeshatengewa fedha kuona ni jinsi gani litaweza kujengwa. Kwa hiyo, commitment ya Serikali ni kuhakikisha kwamba barabara ile inajengwa na tukijua wazi kwamba kwa watu wanaoenda kwa mfano katika Mkoa wa Simiyu, kitendo cha kupita Nzega ni changamoto kubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mlata kwamba jambo hili liko katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi. Kwa hiyo, ni commitment ya Serikali kuangalia katika miaka mitano tutafanya vipi ili mradi wananchi waweze kupata fursa za maendeleo.
MHE. HASSAN S. KAUNJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wa eneo hili la bahari unaendana na shughuli za wavuvi na Lindi kuna wavuvi. Nilipenda niulize nini msimamo wa Serikali kuwasaidia wavuvi wa Lindi kuhusiana na kodi mbalimbali ambazo ni kero kwao? Vilevile wana mpango gani wa kuwasaidia zana za uvuvi ili waweze kuleza pato katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi?
NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kaunje, Mbunge wa Lindi Mjini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli watu wa Lindi shughuli zao kubwa sana hasa wale wa ukanda ni uvuvi na siyo watu wa Lindi peke yake isipokuwa hata Kanda ya Ziwa na maeneo mbalimbali ambao wanaguswa na vyanzo vya maji. Wengi wao wana tatizo kubwa za tozo za kodi za aina mbalimbali ambazo zinawakabili kiasi kwamba shughuli zao zinakwama. Ndiyo maana katika nyakati mbalimbali hapa nimekuwa niki-refer aliyekuwa Waziri wa Mifugo na Kilimo aliyezungumzia suala la kupitia hizi kodi mbalimbali, lengo kubwa ni kupunguza hizi tozo mwisho wa siku wananchi wa kawaida ambao wavuvi wa Lindi waweze kupata fursa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namuomba Mheshimiwa Mbunge tuwe na subira, Serikali inafanya mchakato huu mpana katika suala zima la kilimo, mifugo na uvuvi ambapo inaonekana kwamba mvuvi mwingine akitoka halmashauri moja kwenda halmashauri nyingine anatakiwa alipe kodi. Kwa hiyo, Serikali inaangalia haya yote kwa kina lengo kubwa ni kuliboresha eneo hili mwisho wa siku wananchi wa eneo lako la Lindi wataweza kupata fursa sana katika suala zima la shughuli zao za uvuvi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini eneo la pili la jinsi gani ya kuboresha suala zima la uvuvi, niki-refer tena katika Wizara ya Kilimo na Mifugo, wakati waki-submit hapa bajeti yao mwaka huu, walizungumzia wazi mkakati wao mpana wa kuwasaidia wavuvi hasa wale wa kandokando ya bahari na katika maziwa kwa kuangalia jinsi gani watapewa nyenzo ambazo zitasaidia katika suala zima la uvuvi. Hata hivyo, tulipopitisha bajeti ya TAMISEMI tulisema kuna zile asilimia tano za vijana na akina mama, katika maeneo mengine hasa ya uvuvi, halmashauri katika mipango yao iweze kuona jinsi gani ya kutumia five percent ya vijana na akina mama kuwasaidia wavuvi wa maeneo hayo ili waweze kushiriki katika shughuli za kujenga uchumi wa nchi yao.
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Mamlaka za Maji Mijini ndiyo vyombo vyenye dhamana ya kuhakikisha upatikanaji wa maji mijini na kwa kuwa Halmashauri ya Mji wa Nanyamba imeanzishwa kisheria mwaka 2015, je, Serikali ina mpango gani wa kuharakisha uundwaji wa Bodi ya Mamlaka ya Maji ya Mji wa Nanyamba ili kuhakikisha maji katika Mji wa Nanyamba yapatikana kwa kirahisi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Chikota, Mbunge wa Nanyamba kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, suala analolizungumzia Mheshimiwa Chikota ni jambo la msingi na hizi Bodi za Mamlaka za Maji za Halmashauri ziko chini ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI, mwanzo Ofisi hii ilikuwa chini ya Waziri Mkuu. Tulichokifanya ni nini? Mwezi mmoja uliopita tulikuwa na mkutano mkubwa wa wadau mbalimbali kuhusiana na suala la uundwaji wa Bodi za Mamlaka za Maji ili ifike wakati halmashauri ziweze kuhudumiwa vizuri. Sasa Ofisi yetu inafanya uratibu kutokana na mabadiliko ya Serikali yetu kwamba sasa iko chini ya Ofisi ya Rais na tunafanya mchakato mpana, siyo kwa Bodi ya Mamlaka ya Maji ya Nanyamba peke yake isipokuwa ni Bodi za Mamlaka za Maji za halmashauri mbalimbali ambapo nyingi sana hatujaziunda, si muda mrefu sana zoezi hili litakamilika na Nanyamba Mamlaka yenu itakuwa rasmi.
MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza. Tunaposukuma uanzishwaji wa mamlaka hizi, tunataka kuharakisha maendeleo kwa wananchi. Mji wa Namanyere umekuwa na maombi haya muda mrefu na majibu yamekuwa ya namna hii hii, tangu Bunge lililopita majibu yamekuwa ni haya ya kusema kuna timu ya wataalam watakwenda kuhakiki ili majibu ya kuanzisha yapatikane. Nataka kujua kama Serikali inaweza ikatoa hasa tarehe maalum au time frame ili wananchi wajue hasa ni lini zoezi hili litakamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, miji midogo mingi hapa nchini inaendelea kukuwa ikiwepo ile ya Chala, Kate ambako ni Makao Makuu ya Jimbo, Wampembe, Kipande na kwingineko, lakini mpangilio wake umekuwa si mzuri sana kutokana na Halmashauri kukosa fedha za kufanya utaratibu wa mipango ya uendelezaji wa miji hiyo. Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya ukuaji huu wa miji usioridhisha hapa nchini?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mipata, anataka time frame ya lini jambo hili litakamilika. Mheshimiwa Mipata amekuja ofisini kwangu si chini ya mara mbili katika jambo hili na siyo Mipata peke yake na wadau mbalimbali wengine kutoka Lushoto, wengine kutoka maeneo mbalimbali kwa ajili ya jambo hili. Ndiyo maana nilisema hapa siku zilizopita kwamba, jambo hili kwa sababu limekuwa ni kilio cha Wabunge wengi, mpaka Waziri wangu akaagiza kwamba tulete database ya status ya kila maombi haya yamefikia wapi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nieleze, naweza nika-table hii status ya database mpaka kwa kaka yangu pale Ilula, mpaka kwa kaka yangu Profesa Majimarefu wote maombi yao yapo katika hili na hii chati yote iko hapa wataalam wetu tumewaagiza sasa jinsi gani watakwenda kufanya assessment.
Mheshimiwa Naibu Spika, hili naomba niseme, hapa katikati tumepata matatizo, kuna Halmashauri zingine zinaanzishwa kwa presha hata zile GN namba zinapotajwa zile code zinakosewa, zinapokosewa maana yake unaingilia katika mipaka ya Halmashauri nyingine. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mipata avute subira, sitaki kusema ni lini inaanza, lakini lengo letu kubwa ni kwamba, ndani ya kipindi hiki cha mwaka huu wa fedha tunapoanza, imani yangu kwamba, hii kazi itakwenda kwa kasi kwa sababu hata mimi sipendi kila siku kusimama hapa kujibu swali hilo hilo. Kwa hiyo, imani yangu ni kwamba, jambo hili tutafikia mwisho, wenye kukidhi vigezo watakidhi na wale ambao watakuwa na upungufu wataambiwa wapi warekebishe ili mradi wapate mamlaka. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mipata avute subira.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine alizungumzia suala zima la mipangilio mibaya ya miji. Ni kweli sasa hivi ukiangalia hasa miji mingi inayokua, maeneo mbalimbali yanajengwa kiholela sana. Hata hii miji midogo, kwa mfano, ukienda hata pale Kibaigwa, eneo la karibu tu hapa, ukienda kuna ujenzi kama unatengeneza kachumbari vile, kitunguu, nyanya kila kitu yaani miji imekuwa hovyo hovyo kabisa. Ndiyo maana tunapopita katika Halmashauri zetu tumewaelekeza Maafisa wa Mipango Miji na Maafisa Ardhi, jukumu lao kubwa sio kuchukua mshahara wa Serikali tu na kukaa ofisini, japokuwa resource ni ndogo lakini wakitumia taaluma zao, tutafanikiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, haiwezekani Afisa Mipango Miji au Afisa Ardhi yuko ofisini pale, nje ya Halmashauri palepale, lakini watu wanaendelea kujenga kiholela katika maeneo yasiyokuwa sawasawa. Tumetoa maelekezo kwamba Maafisa Mipango Miji na Maafisa Ardhi watumie own source zilizokuwepo, kuona jinsi gani watatumia taaluma yao kufanya mipango rafiki ya kijamii, angalau wananchi wetu waishi katika mipango bora. Kwa sababu ukitegemea kwamba utapata bilioni mbili (2) kwa wakati mmoja kupanga mipango miji, inawezekana itakuwa changamoto kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba nimwambie Mheshimiwa Mipata kwamba, tumeliona hili na tumeendelea kutoa maelekezo na kwa kutumia platform hii ya leo naomba niwaagize Maafisa Mipango Miji wote na nilishawaagiza Afisa Mipango Miji wa Bahi na Magu nilikopita kwamba, wahakikishe maeneo yao yote wanapokuwa Ofisini, yanakuwa maeneo rafiki yaliyopangwa vizuri kwa kutumia taaluma zao.
MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kama ilivyo Mji Mdogo wa Namanyere, katika Wilaya ya Geita kuna Mji Mdogo wa Katoro ambao una hadhi na umetimiza vigezo vyote. Napenda kujua sasa ni lini Mamlaka ya Mji Mdogo huu wa Katoro utapandishwa kuwa Mamlaka ya Mji?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kweli Mji wa Katoro unakua sana hasa katika eneo lile la Mkoa wa Geita. Kutokana na suala la Sekta ya Madini, hali ya miji imekuwa ikikua kwa kasi sana ukiwemo na mji wa Katoro. Kwa hiyo, nipendekeze tu kwa sababu katika database yangu hapa nikiangalia Mji wa Katoro siuoni, kwa hiyo Mheshimiwa Lolesia, kama walishaleta Ofisi ya Rais, TAMISEMI nitakwenda ku-cross check, lakini kama bado hawajaanza huo mchakato, naomba nielekeze sasa jinsi gani tutafanya katika eneo la Halmashauri yao, wahakikishe kwamba wanaanza mchakato wa kawaida kwanza katika Vijiji, katika u-DC, Baraza la Madiwani na baadaye RCC, yale maombi yaje Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutayatathmini, mwisho wa siku ni kwamba, eneo hili litapandishwa kwa vigezo vitakavyokuwa vimefikiwa.
MHE. ALLY M. KEISSY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Mheshimiwa Naibu Waziri katika swali lake la kwanza alisema kwamba ana ziara ya Iringa, Mbeya na Songwe. Je, yuko tayari sasa katika hiyo ziara kuunganisha mpaka Wilaya ya Nkasi akajionee mwenyewe matatizo ya Afya, Elimu na Barabara katika Wilaya yetu ya Nkasi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ziara yangu inaanzia Mkoa wa Iringa, nitakwenda Mkoa wa Njombe, Mbeya, Rukwa, nikitoka hapo nitakwenda Mkoa wa Kigoma halafu namalizia Mkoa wa Tabora, hiyo ni phase namba moja. Baadaye nitakwenda Mkoa wa Mara, Geita, Mwanza, Kagera, halafu nitarudia katika Kanda ya Mashariki. Kwa hiyo, Mheshimiwa Keissy mpo katika awamu ya kwanza ya ziara yetu kubaini changamoto ili kuona jinsi gani Ofisi ya Rais TAMISEMI, tutafanya kuwahudumia wananchi wa Tanzania.
MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa hali ya kukamilika kwa vigezo vya kupandisha hadhi miji yetu kule Namanyere iko sawa sawa na kule Maramba ambapo tumetimiza vigezo vya kupata mji mdogo tangu kabla Mkinga haijawa Wilaya. Je, ni lini Mji wa Maramba utapewa hadhi ya kuwa Mji Mdogo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli hawa wenzetu walikuwa na maombi yanayogusa sehemu mbili; walikuwa wanaomba hii Maramba iwe mji mdogo, lakini walikuwa wanaomba eneo hili la Mkinga. Naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge, nadhani maombi haya yamepita muda mrefu sana. Sasa nimwombe na nimwagize Mkurugenzi na timu yake kule Halmashauri wakishirikiana naye kwa sababu kulikuwa na maombi haya na muda mrefu sana umepita, waanze huu mchakato vizuri ilimradi itufikie Ofisi ya Rais, TAMISEMI, mwisho wa siku vile vigezo vikiwa vimefikiwa hatutosita kuhakikisha eneo hili linapandishwa hadhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimwagize Mheshimiwa Mbunge na wengine wote, maana yeye ni rafiki yangu tupo humu ndani. Namwambia Mkurugenzi na timu yake yote waanze huu mchakato sasa vizuri ilimradi hili jambo lifike Ofisi ya Rais, TAMISEMI na wataalam wetu waende kuhakiki kwa ajili ya vigezo hivyo
MHE. DKT. RAPHAEL M.CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na kwa kuwa Mkoa wa Simiyu ni moja ya mikoa mipya, tuna tatizo kubwa sana la kutokuwa na Hospitali ya Rufaa. Kwa vile Mheshimiwa Nyongo alikuwa ameomba kwamba, Hospitali ya Maswa ipewe hadhi hiyo ya kuwa hospitali ya rufaa, lakini Mkoa wa Simiyu tuliamua kwamba Bariadi ndiyo inafaa kuwa Hospitali ya Rufaa. Sasa kwa kuwa Serikali imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo, ni lini ujenzi huu wa kukamilisha Hospitali ya Rufaa kwa Mkoa wa Simiyu na mikoa mingine mipya ikiwemo Mikoa ya Songwe, Mkoa wa Katavi, Mkoa wa Geita pamoja na Simiyu yenyewe, lini hii mikoa mipya itasaidiwa kupata hospitali za rufaa? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa katika Wilaya mpya vilevile ndani ya mikoa hii mipya ikiwemo na Wilaya ya Usega, tuna tatizo la kutokuwa na Hospitali za Wilaya na sisi katika Wilaya ya Busega tumeiteua Hospitali ya Mkula kwa mkataba wa miaka miwili kuwa hospitali teule ili iweze kutoa huduma kwa wananchi wa Wilaya ya Busega waweze kupata huduma za Kiwilaya. Lini mchakato huu wa Serikali utakamilika? Tumeshapeleka maombi Wizarani sasa ni muda mrefu lakini hatujapata majibu. Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kukiri wazi kwamba, kwa mtazamo wake wa Hospitali ya Bariadi ambayo Serikali mwaka huu tunajielekeza kupeleka 1.4 billion kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Mkoa. Hapa maana yake, ule ujenzi uendelee na ni mtazamo mzuri, hata wao kule wanaona kwamba inastahili iwe Hospitali ya Kanda. Kwa hiyo, kikubwa zaidi tutaendelea kuipa nguvu hiyo Hospitali ya Bariadi, lengo kubwa ni kuwa hospitali inaweza kuhudumia ukanda wote ule. Pia suala zima la ujenzi wa Hospitali ya Mkoa, huu ni mpango mkakati wa Serikali yetu ya Awamu ya Tano kwa sababu tunajua tuna mikoa mipya ambayo, tumeianzisha kama alivyosema kuna Songwe na mikoa mingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nini kinachohitajika kufanyika? Ni kwamba katika mwaka wa fedha, kwa sababu huu ndiyo mwaka wa kwanza wa Serikali ya Awamu ya Tano, imani yangu ni kwamba katika mwaka wa fedha unaokuja niwaombe sasa Waheshimiwa Wabunge, kwa umoja wetu na katika vikao vyetu vile vya kisheria, vikao vyetu vya Madiwani, hali kadhalika vikao vyetu vya RCC, jambo hili liwe kipaumbele ili mradi mwisho wa siku na sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI tutakuwa tunakusanya mikakati yote ya mikoa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali za mikoa. Hata hivyo, katika hili hatutosita kwa sababu lengo letu kubwa ni kuhakikisha kwamba, kila mkoa unakuwa na hospitali yake ya mkoa na baadaye tunakuwa na hospitali za Kanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo katika swali la pili kwamba Busega hamna hospitali ya Wilaya, ni kweli na kwamba wanatumia hospitali ya Mkula kama ni hospitali teule, lakini bahati mbaya kibali bado hakijapatikana. Hivyo, tutawasiliana na wenzetu wa Wizara ya Afya, lengo kubwa ni kupata kibali, lakini hata hivyo mpango mkakati wa Serikali ni kuhakikisha kwamba kila wilaya inapata hospitali ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumekwenda mbali zaidi, kwa sababu sehemu zingine coverage ya Wilaya ndani yake kuna Halmashauri kadhaa. Sasa tunasema kwamba, ikiwezekana kila Halmashauri iwe na hospitali yake, kwa hiyo huo ndio mpango wa Serikali. Imani yangu kubwa ni kwamba, tutaungana na mpango huu wote kwa pamoja kusukuma juhudi za ukusanyaji wa kodi ili tupate fedha za kutosha, mwisho wa siku maamuzi yetu ya ujenzi wa Hospitali za Wilaya na Mikoa yaweze kufikiwa. Hivyo, Mheshimiwa Chegeni endelea na spidi hiyo hiyo, nadhani kila kitu kitakuwa sawasawa.

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda tu kuongezea majibu ya nyongeza kuhusu swali la pili la kibali cha Hospitali ya Mkula, kuwa district designated hospital, kwa ajili ya Wilaya ya Busega. Tayari Mheshimiwa Raphael Chegeni, Mbunge wa Jimbo hilo amewasilisha jambo hili Wizarani kwetu na amenikabidhi barua zake mimi mwenyewe hapa Bungeni juzi tu, hata siku tatu hazijapita, ili niweze kufuatilia suala hili. Namwahidi kwamba nitawakabidhi wataalam suala hili, ili waweze kufika maeneo ya pale Mkula, bahati nzuri napafahamu vizuri, wakafanye ukaguzi, wajiridhishe kama inakidhi vigezo na hatimaye Wizara ya Afya iweze kuipa kibali cha kuwa Hospitali Teule ya Wilaya.
MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Kwa kuwa tatizo la Maswa linafanana kwa ukaribu kabisa na tatizo la Wilaya ya Momba, kwa sababu Wilaya ya Momba haina hospitali ya Wilaya. Kipindi cha kampeni Mheshimiwa Rais alituahidi kutupatia majengo ya pale Chipaka yatumike kama hospitali ya Wilaya. Nataka kujua, je, Serikali ina mpango gani wa kutupatia majengo yale ili yatumike kama Hospitali ya Wilaya ya Momba?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Momba hatuna hospitali ya wilaya pale na siyo hospitali ya wilaya hata zile infrastructure za wilaya yenyewe, halmashauri hatujakaa vizuri. Momba kwa sababu ni eneo jipya, mkakati wetu ni kuweza kuimarisha, lakini kwa sababu kuna majengo tayari, kikubwa zaidi ni kwamba wataalam watatakiwa kufika pale kufanya assessment ya hayo majengo.
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri katika ziara yangu ambayo nitaanzia Mkoa wa Iringa kuanzia tarehe 17 vilevile nitafika na maeneo ya Momba. Nikifika Momba, nitaomba wanifikishe katika yale majengo. Lengo letu ni nini? Tubainishe jinsi gani wananchi wataweza kupata huduma hizi. Kwa hiyo, namshukuru sana Mheshimiwa Juliana Shonza kwa juhudi kubwa anayofanya kwa ajili ya wananchi wa Momba.
MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa Hospitali ya Wilaya ya Maswa ina majengo mazuri na yamekamilika, mojawapo ni jengo la upasuaji, lakini hakuna vifaa kwa ajili ya kazi hiyo ya upasuaji na wataalam; na kwa kuwa Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alifika hapo akaahidi kwamba vifaa vitakuja na wataalam Madaktari wawili wataletwa kwenye Wilaya ya Maswa. Sasa Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ahadi hiyo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, baba mwenye nyumba akisema maana yake hiyo hoja imekwisha. Kama Rais amekuja ameshatoa ahadi hiyo, ndiyo maana nimesema jukumu kubwa ni kwa jinsi gani tutafanya katika utekelezaji. Sasa katika hili, nini tunachotaka kufanya? Tunataka kuangalia jinsi gani tutatumia fursa zote kwamba hospitali hii iweze kupata huduma. Hata hivyo, naomba niwaambie ndugu Watanzania kwa ujumla kwamba, sasa hivi Wizara ya Afya tuna mradi mmoja mkubwa sana, ambao sisi Watanzania tunashirikiana na wenzetu wa Uholanzi, mradi wa shilingi bilioni zisizopungua 44.
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu kazi yake kubwa itakuwa kuweka vifaa tiba katika hospitali zetu za kanda na hospitali za mikoa na kwa sababu Maswa kuna kipaumbele maalum, tutaangalia jinsi gani tutafanya eneo hili lipate vifaa tiba. Sambamba na kuweka kwamba wataalam waweze kupatikana ili mradi wananchi wapate huduma za upasuaji katika Hospitali ya Maswa.
MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuru. Kiu ya wananchi wa Maswa ya kupandishiwa hadhi hospitali yao, kiu hiyo hiyo iko kwa wananchi wa Bukombe hasa wa Kata ya Uyovu, ambao kituo chao cha afya ni kikubwa sana na kinahudumia watu kutoka Wilaya za Chato, Biharamulo pamoja na Bukombe. Kinahudumia watu wengi zaidi kuliko hata Hospitali ya wilaya, kwa sababu chenyewe kinahudumia watu zaidi ya 82,000 wakati hospitali ya wilaya inahudumia watu 68,000 tu. Namwomba Mheshimiwa Naibu Waziri atusaidie wananchi wa Bukombe, atuambie tuna uwezo wa kupandisha Kituo cha Afya cha Uyovu ili kiwe hospitali?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Biteko anafahamu, tulikuwa pamoja pale Geita katika uzinduzi wa hospitali na kuweka vifaa katika Hospitali ya Geita pale. Bahati nzuri nilipita katika eneo lake, jiografia yake kweli ina changamoto kubwa na wananchi lazima wapate huduma na kituo hiki cha afya anachokizungumzia amesema kinahudumia watu wengi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimwombe Mheshimiwa Mbunge sasa kwa uhodari wake uleule wa kutetea wananchi wake katika suala zima la maliasili ambapo namsikia mara nyingi zaidi na uhodari wake wa kutetea wananchi katika sekta ya afya na nakumbuka kwamba alileta malalamiko mpaka wataalam wake walihamishwa katika eneo la Jimbo lako na akasema Madaktari wamehama.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nimwombe kupitia vile vikao husika vya mchakato wa upandishaji vituo vya afya kuwa hospitali ya Wilaya kuanzia katika Ward C, Baraza la Madiwani, halafu mwisho wa siku naamini ikienda katika Wizara ya Afya ambao wao kazi yao ni kuangalai, kama vigezo vikikidhi, hospitali hiyo inapandishwa. Nadhani hawatosita, namwamini Mheshimiwa Dkt. Kigwangala na dada yangu Ummy Mwalimu watakuwa tayari kuhakikisha kwamba, watu wa Bukombe wanapata hospitali yao kwa mujibu wa vigezo vitakavyokuwa vimefikiwa.
MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kumuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa shule zilizoko pembezoni katika Wilaya ya Ilemela huwa zinasahaulika katika mgao wa madawati. Mfano wa shule hizo ambazo ziko pembezoni mwa Wilaya ya Ilemela ni Shule ya Bugogwa, Igombe, Isanzu, Kisuni, Kilabela, Kabangaja na zinginezo. Katika shule hizo ambazo ziko pembezoni wanafunzi ambao wanakaa chini ni wa kuanzia darasa la kwanza mpaka la tatu. Je, Serikali inatoa tamko gani kuwa madawati yanapokuwa yamegawiwa, kwa mfano nikiangalia hapa katika majibu yake inaonekana pesa iliyotengwa yatapatikana madawati 4,000 kwa bei ya Sh.50,000 kwa kila dawati, je, Serikali inanihakikishia vipi kwamba shule hizi za pembezoni zitapata mgao huo wa madawati?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili…
SPIKA: Mheshimiwa umeshauliza mawili tayari.
MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimeuliza moja. Swali la pili, je...
SPIKA: Mheshimiwa Kiteto samahani. Mheshimiwa Waziri kati ya hayo mawili utachagua moja la kujibu, haya endelea na swali la pili.
MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Je, Serikali haioni sasa kwamba ni wakati wa kuruhusu Halmashauri za Mkoa wa Mwanza kutumia msitu wa Buhindi ambao haujavunwa kwa muda mrefu sasa, miti ivunwe kwa ajili ya kutengeneza madawati ili kukidhi tatizo hili sugu la madawati katika Mkoa wa Mwanza? Nashukuru.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Koshuma amezungumza agenda muhimu sana hapa, upelekaji wa madawati katika maeneo ya pembeni. Kwa uzoefu wangu nilipotembelea maeneo mbalimbali siyo madawati peke yake, hata Walimu tunaowapeleka katika migao mbalimbali wengi sana wanaishia maeneo ya mijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama mlikuwa mnafuatilia vyombo vya habari juzi juzi nimetembelea shule moja ya Manispaa ya Dodoma iliyoko pembezoni hata mgao wa madawati haufiki kule na nikatoa maelekezo sasa shule hiyo ina madawati ya kutosha. Kwa hiyo, natoa maelekezo kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri wahakikishe madawati yanafika maeneo ya pembezoni hasa tukizingatia kwamba shule za pembezoni huwa zinasahaulika.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika ziara zangu nitakazozifanya utaratibu wangu utakuwa uleule, sitatoa taarifa ni shule gani nakwenda kuitembelea na Mkurugenzi ambaye nitafika katika Halmashauri yake, niki-pick shule nikikuta hakuna madawati maana yake ameshindwa kukidhi vigezo na maelekezo ya Serikali za Mitaa. Kwa hiyo, naomba nitoe onyo kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni kuhusu kutumia msitu, kuna misitu ya vijiji na mingine ni ya Serikali Kuu. Nadhani Ofisi ya Mkuu wa Wilaya itaangalia utaratibu na kuona tunafanyaje na kama kuna uwezekano msitu huo uweze kutumika. Vilevile nizishauri Halmashauri, wakati mwingine mbao zinakamatwa badala ya kukaa mpaka zinachakaa wakati Halmashauri ina shida ya madawati, tuangalie namna ya kufanya mbao zile ziweze kutumika kwa ajili ya kuondoa tatizo la madawati katika shule zetu.
MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kunipatia nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo wote tunajua kuna tatizo kubwa sana la madawati na Halmashauri nyingi sasa hivi zinatengeneza madawati. Swali langu la msingi ni kwamba, je, ni nani anayedhibiti ubora wa madawati hayo? Kwa sababu yawezekana kabisa mbao hizo wakati mwingine zinaweza zikawa hazijakauka vizuri na maana yake ni kwamba hayo madawati hayatadumu. Swali langu ni nani anayedhibiti kuhakikisha kwamba mbao zinazotengeneza madawati hayo ni bora na zimekauka ili isiwe tunafanya kazi ya zimamoto? Nashukuru.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la quality control (ubora wa madawati) ndiyo maana Ofisi ya Rais, TAMISEMI, imegawanyika katika Halmashauri na Mikoa na huko tuna watu tunaita wahandisi au mainjinia ambao jukumu lao kubwa kwa kila kitu kinachotengenezwa sio madawati peke yake hata majengo, kuhakikisha wanazingatia viwango vya ubora ili tupate vitu katika ubora unaokusudiwa. Kwa hiyo, tuliowapa dhamana hii ni Wahandisi wa Halmashauri wetu kuhakikisha kwanza madawati hayo yanakidhi vigezo siyo kwa ajili ya uvyevunyevu peke yake hata mbao ya aina gani inatumika ili tupate madawati siyo ya kutumika mwaka mmoja bali ya muda mrefu.
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, anasema tusiweke karakana kwenye shule za msingi lakini kuna vituo vya shule za msingi ambavyo vina ufundi, watoto huwa wanachaguliwa darasa la saba wengine wanakwenda sekondari wengine ufundi na vituo hivi vipo kwenye shule za msingi na vina fani za useremala. Je, Serikali iko tayari kusaidia kituo kama cha Shule ya Msingi Uwemba ili kusudi kiweze kutengeneza madawati kwa ajili ya Jimbo la Njombe Mjini?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna shule zingine zina karakana na hii nadhani ni kutokana na maelekezo kwamba tuwafunze wanafunzi wetu masomo ya ufundi. Kama shule ina kiwanda cha ufundi maana yake hata kiwanda chake kimewekwa kwa minajili kwamba hakitaathiri mazingira ya shule. Miongoni mwa zile shule ambazo tutazibainisha ni shule ambazo ndani yake zina karakana. Ofisi ya Rais, TAMISEMI ni jukumu lake kubwa kuangalia shule hizi sasa zinashiriki vipi, siyo kuziwezesha peke yake, isipokuwa kuona kwamba programu hii inakuwa endelevu ili vijana watakaotoka hapo wawe na ufundi bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimweleze Mheshimiwa Mbunge kwamba na mimi nitatamani sana nikifika Jimboni kwake anipeleke katika shule hiyo ili kwa pamoja tubadilishane mawazo kuhusu kuisaidia shule hiyo. Lengo likiwa ni kuongeza stadi za kazi kwa wanafunzi wetu lakini kurahisisha mambo mengine ambayo yanaweza kufanyika katika Halmashauri husika yaweze kwenda vizuri.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Sambamba na suala la madawati, wananchi wameitikia wito wa uandikishaji wa watoto shule za awali pamoja na darasa la kwanza. Je, Serikali iko tayari sasa kupeleka Walimu wa madarasa haya ya awali kwa sababu madarasa hayo hayana Walimu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba tuweke rekodi sawa, katika utekelezaji wa ahadi ya Chama cha Mapinduzi na Ilani yake lakini azimio la Mheshimiwa Rais kuhakikisha watu wote wanakwenda shuleni, tumepata mafanikio makubwa sana na ni kweli tumepata ongezeko la wanafunzi na shule zingine zime-burst. Shule ambayo ilikuwa inatarajia kusajili wanafunzi 500 wamesajili mpaka wanafunzi 1,000, haya ni mafanikio makubwa katika Taifa letu hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa utaratibu uliopo sasa Walimu wote wanaosoma ngazi ya certificate wanakuwa na component ya elimu ya awali. Kwa hiyo, imani yangu kubwa ni kwamba katika ajira ambazo tunatarajia kuzitoa mwaka huu ambapo siyo muda mrefu ujao, suala hilo la kuzingatia Walimu ambao watakwenda kufundisha masomo ya awali litapewa kipaumbele bila mashaka ya aina yoyote.
MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, TAMISEMI, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, jana wakati Wizara ya Afya ina wind-up, wameendelea kusisitiza kwamba Serikali itaajiri watumishi wa kada za afya wanaozidi 10,000 lakini katika jibu la Mheshimiwa Naibu Waziri katika uhaba wa watumishi 95 anasema tutapewa watumishi 18. Haoni umuhimu wa kuongeza idadi hiyo ikafika angalau watumishi 50 kwa sababu tutaajiri watumishi 10,000?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kutarajia michango kutoka CHF ni jambo zuri lakini wote tumeona Wabunge hapa katika michango yao mbalimbali wameelezea ambavyo jambo hili linaendelea kuwa gumu kwa sababu ya kipato duni, lakini pia kutokana na ukosefu wa elimu ya uhamasishaji. Sasa kutarajia fedha kutoka CHF ni kama vile tunaota tu ndoto ambayo inaweza isiwe ya kweli. Kwa hali hiyo, kutokana na mazingira ya hospitali hiyo ambayo nimeshayaeleza, hii fedha iliyotengwa shilingi milioni 90, haitoshi hata on call allowance kwa muda wa miezi mitatu, je, Serikali haioni sababu kwa mazingira hayo ambayo nimeelezea kwamba, Hospitali ya Mafinga iko along the highway, ikaongeza kiwango hicho japo hata theluthi moja ya fedha hizo? Ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika hotuba yetu ya jana Mheshimiwa Waziri wangu wa Afya na Waziri wa Utumishi walielezea suala hili la watumishi ambapo taarifa inaonesha watumishi takribani 10,000 wataajiriwa na maombi ya awali ya kibali kutoka Mafinga yalikuwa yanahitaji watumishi 18. Kwa hiyo, katika mgawanyo wa watumishi hawa 10,000 Halmashauri hii ilikuwa na watumishi 18. Hata hivyo kwa sababu mahitaji ni makubwa tutaangalia tutafanya vipi ili kuondoa matatizo ya wananchi katika sekta ya afya. Kwa hiyo, concern kwamba watumishi 18 watakuwa ni wachache hili tutaliangalia, lakini hayo ndiyo maombi ambayo yametoka katika Halmashauri ya Mafinga.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala zima la ukosefu wa uhamasishaji na kwamba hizi fedha ni ndogo, naomba niwaambie ndugu zangu katika maelekezo yetu mbalimbali tulisema sasa hivi jambo muhimu katika sekta ya afya, ukiachia CHF na mifumo mingine, ni ukusanyaji wa mapato. Nimesema tulivyofanya mazoezi ya kukusanya mapato kwa njia ya electronic mapato yamebadilika sana na jana Waziri wa Afya alikuwa akitoa mifano katika Hospitali ya Mbeya badala ya kukusanya shilingi milioni 70 kwa mwezi sasa inakusanya mpaka shilingi milioni 500. Hospitali ya Sekou Toure pale Mwanza badala ya kukusanya shilingi milioni 150,000 mpaka milioni 200,000 kwa mwezi sasa inakusanya shilingi milioni 3.5 kwa siku. Nenda kule Tumbi badala ya kukusanya shilingi milioni 200,000 kwa siku sasa tunakusanya shilingi milioni nne kwa siku, haya ni mabadiliko makubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hili ndiyo maana tunatoa msisitizo kwamba Wabunge tuhakikishe, katika hospitali zote mifumo ya electronic iwe imefungwa ili fedha ziweze kukusanywa na ziende katika mgao sahihi wa kununua vifaa tiba na madawa mwisho wa siku mtaona kila kitu kinaenda vizuri. Tusipozingatia haya, hata tukipeleka fedha bado tutakuwa na matatizo. Kwa hiyo, ajenda yetu kubwa ni kwamba, tutumie mifumo sahihi ya electronic kwa ukusanyaji wa mapato kwa ajili ya huduma ya afya.
MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa matatizo yanayoikumba Mafinga yanafanana kabisa na yale yanayoikumba Hospitali ya Mji wa Kondoa kwa maana ya kwamba Kondoa inahudumia Halmashauri tatu za Kondoa Mjini, Kondoa Vijijini pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Chemba. Je, Serikali ina mpango gani na inafikiria nini katika kuongeza rasilimali fedha na rasilimali watu ili kukidhi mahitaji?
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli hospitali ya Kondoa demand yake imekuwa kubwa na kama nilivyosema awali ajenda yetu kubwa ni kuongeza rasilimali watu pale Kondoa. Concern ya kaka yangu Mheshimiwa Nkamia, Mbunge wa Chemba ni kujenga Hospitali ya Wilaya Chemba ili kupunguza population. Juzi juzi tulivyokuwa tunafungua Hospitali yetu ya Mkoa hapa, Mheshimiwa Nkamia alipeleka ombi maalum kwa Mfuko wa Bima ya Afya Taifa kuangalia uwezekano wa kujenga Hospitali ya Chemba ili kupunguza ile population.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, katika suala la rasilimali watu tutajitahidi kadri iwezekanavyo kwa huu mgao unaokuja tuangalie Hospitali ya Kondoa tunaisukuma vipi. Hali kadhalika katika suala la rasilimali fedha kama nilivyosema ukiachia hii bajeti ambayo tumeitenga ni lazima sasa twende tukasimamie makusanyo ya mapato kwa nguvu zote. Mifumo hii ya kielektroniki ikitumika vizuri katika sekta ya afya mafanikio yake ni makubwa sana na tutaondoa kero nyingi sana za wananchi katika kupata huduma za afya.
MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naomba niulize swali dogo. Kwa kuwa Mkoa wa Singida tumejenga Hospitali ya Rufaa na mpaka sasa haijaanza kufanya kazi, je, Serikali iko tayari sasa kuhakikisha hospitali ile inaanza kazi kwa kupeleka vifaa tiba?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kweli na katika ziara yangu hospitali hiyo ni miongoni mwa hospitali nilizozitembelea wakati wa ziara zangu mikoani na siku ile tulikuwa na Mheshimiwa Mbunge, miongoni mwa majengo makubwa sana yaliyojengwa ni lile pale Singida Mjini. Nilitoa maelekezo kwa Mkuu wa Mkoa aliyekuwepo kipindi kile na kwa Mganga Mkuu wa Mkoa kuhakikisha hospitali ile inafanya kazi. Ukiangalia inawezekana ikawa Hospitali ya Kanda kutokana na ukubwa wake kwa sababu kuna center kubwa ya akinamama kujifungulia.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kusikitisha jana nilipata taarifa kwamba kuna watu wanataka kutoa vile vitanda kurudisha mjini, natoa agizo hakuna kuondoa kitanda au kitu chochote katika hospitali ile. Wiki ijayo nitakwenda Singida nataka niikute Hospitali ya Singida inafanya kazi. Sitaki kusikia hospitali ambayo uwekezaji wake ni mkubwa na wa mfano, watu wanatoa vitanda kupeleka sehemu zingine, tutawashugulikia watu wote wanaotaka kufanya ubadhirifu katika sekta ya afya.
MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa watumishi hawa wanaohamishwa katika sekta ya afya wanacheleweshewa mafao yao huko wanakopelekwa. Je, Serikali itahakikishaje wanapata stahiki zao kwa wakati muafaka?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la malipo ya watumishi, nadhani kama tulivyozungumza awali tutaendelea kuyashughulikia malipo haya hasa kulipa madeni ya watumishi, lakini siyo watumishi pekee hata madeni ya wazabuni mbalimbali ambao wanadai Halmashauri zetu, suala hili tutalifanya kwa pamoja. Lengo kubwa ni kuhakikisha kwamba tunalipa madeni yote ya watoa huduma aidha watumishi au wale wanaotoa huduma za zabuni katika hospitali zetu na center mbalimbali ili isije kufika muda tukawafunga mikono wakashindwa kufanya kazi zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kuna jambo tulizungumzia katika maeneo mbalimbali kwamba kuna pesa ambazo zitakuwa zinatumika kwa ajili ya kulipa madeni ya watumishi. Hata hivyo, naomba kusema kwamba kama hakuna ulazima wa kuhamisha watumishi, tusifanye hivyo kwa sababu tutakuwa tunakuza madeni ya watumishi bila sababu ya msingi.
MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali ya nyongeza na nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa sababu kuu za ufaulu duni ni miundombinu mibovu ya ufundishaji na kujifunza. Je, Serikali imeweka mkakati gani kwa shule za Njombe?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa waathirika wakuu ni wasichana, kwa sababu wanapewa kazi nyingi na wazazi wao majumbani, je, Serikali ina mkakati gani kumsaidia mtoto huyu wa kike?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la miundombinu mibovu, hili ni kama tulivyosema katika bajeti yetu ya mwaka huu wa fedha kwamba tumeelekeza katika maeneo mbalimbali ili angalau kuongeza speed kwenye hii changamoto tuliyo nayo hivi sasa ya wanafunzi wengi sana tuliowasajili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo vilevile kuwafanya walimu wafundishe katika mazingira rafiki. Ndiyo maana katika bajeti ya mwaka huu mkoa wa Njombe peke yake tumetenga kiwango cha fedha cha kutosha ili kuhakikisha maeneo mbalimbali yanaweza kufikiwa. Ndiyo maana tukifanya rejea ya bajeti yetu tuliyopitisha hapa hapa, siwezi kukupa takwimu halisi, lakini tumeugusa Mkoa wa Njombe kuangalia kipaumbele hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala zima la miundombinu Mheshimiwa Mbunge nadhani na wewe ni mpiganaji mzuri katika eneo hilo. Ukiachia miundombinu, vilevile miongoni mwa mambo ambayo yanachangia sana ni suala zima la malezi. Wakati mwingine wazazi wanakuwa irresponsible, hawawajibiki vya kutosha kuhakikisha watoto wao wanawasimamia kwa karibu.
Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie wakati napita pita maeneo mbalimbali, kuna maeneo mengine utakuta madarasa yapo ya kutosha, hali kadhalika walimu wa kutosha lakini shule zile tulizozipitia hakuna hata mwanafunzi aliyepata division one au division two. Kwa bahati mbaya zaidi unaweza kukuta walimu wengi wa sayansi hakuna lakini wa arts wapo na bado huwezi ukaona “C” moja au “B” moja ya Kiswahili wala ya civics; ni kwamba concentration ya watoto imekuwa chini. Kwa hiyo, jukumu letu kubwa sambamba na kuongeza miundombinu tuna changamoto kubwa ya kuwahamasisha wazazi kusimamia suala zima la taaluma za watoto wao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuwaokoa vijana wetu wa kike. Ni kweli suala la mimba kwa watoto wa kike limekuwa kubwa, ndiyo maana mchakato wetu sasa hivi ni tunajielekeza katika ujenzi wa shule za sekondari za bweni hasa kwa upande wa wanawake. Lengo letu ni kuhakikisha zile changamoto zinawapata watoto wanapokwenda shuleni ziweze kupungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wa Afya wiki iliyopita alisema kwamba wale mabaradhuli wanaohakikisha wanaharibu watoto wa watu, tuhakikishe wanachukuliwa hatua kali ili hawa watoto wa kike waweze kupata elimu yao kama ilivyokusudiwa.
MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kumekuwa na tabia ya walimu kuto-report kwenye mikoa ambayo inaitwa mikoa ya pembezoni kama Mkoa wetu wa Lindi. Je, kuna mkakati gani mwaka huu wa kuhakikisha kwamba walimu watakaopangwa watakwenda Lindi kutatua tatizo kubwa la walimu lililopo kwenye shule zetu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, wiki iliyopita nilisema kwamba kuna tatizo, si mkoa wa Lindi peke yake, ukienda Katavi, Kigoma, Mara, Sumbawanga na maeneo mengine. Tumesema mwaka huu tu tunaajiri walimu wapatao 35,000, lakini walimu wengine wakipelekwa kule hawaendi; na kwa bahati mbaya wengine wakienda wanataka kuishia pale pale mjini. Na ndiyo maana tumetoa maelekezo mwaka huu kwamba walimu wote watakaokwenda ku-report wahakikishe wanafika vituoni.
Naomba kutoa rai, mwaka huu tumepeta maombi mengi sana ya walimu ambao ndani ya miaka mitatu, minne walishindwa ku-report wakaenda private schools, sasa hivi private schools hali imekuwa mbaya, wanakuja kuomba tena ajira Serikalini.
Tuombe kutoa maelekezo; kwamba walimu watakaoshindwa kufika katika vituo vyao wasitarajie kuja kuomba mwakani baada ya kuona kwamba wamekosa nafasi katika private schools. Hili ni agizo letu na tutaenda kulisimamia kwa nguvu zote.
MHE. KEMILEMBE J. LWOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante kwa majibu ya Mheshimiwa waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tatizo kubwa la vifaa hivyo kwenye Hospitali hii ya Wilaya ya Nyamagana, na ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais ya mwaka 2013. Sasa je, ni lini vifaa hivi vitaletwa kwenye hospitali ya Wilaya ya Nyamagana?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana inahudumia wananchi zaidi ya 300,000 kwa hiyo inaelemewa na Halmashauri ya Jiji la Mwanza inafika mahala inashindwa kutoa huduma stahiki. Pamoja na hayo, Halmashauri ya Jiji imejitahidi na kuongeza jengo la wodi ya wanaume na watoto ambayo hazikuwepo. Je, Wizara inampango gani wa kutusaidia ili wodi hizi ziweze kukamilika? Ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nadhani ni mara ya pili Mheshimiwa Kemi anauliza swali la sekta ya afya katika Mkoa wa Mwanza, kwa hiyo nimpongeze sana kwa kuona kwamba suala la afya ni muhimu sana. Lakini katika suala zima la ni lini x-ray italetwa, nimesema hapa kwamba kila kitu ni budgeting na bajeti ya mwaka huu tumetenga karibuni milioni 133. Lengo kubwa ni kwamba x-ray iweze kununuliwa na iweze kufika. Jukumu letu kubwa Ofisi ya Rais - TAMISEMI ni kuhakikisha kwamba pesa hizo mwaka huu wa fedha zinapatikana ili ahadi aliyoweka Mheshimiwa Rais iweze kutimia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kujengwa kwa wodi pale, nipende kusema kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI itashirikiana na ninyi watu wa Mwanza kuhakikisha wodi ile inafanya kazi. Sambamba na hilo nipende kuwashukuru wenzetu wa Vodacom ambapo juzi kupitia vyombo vya habari nimeona wanafanya usaidizi mkubwa sana katika hospitali ya Sekou Toure pale Mwanza. Lengo letu ni kwamba wadau wanaoshiriki kama kama hivi na sisi Serikali tunasaidia kwa kiwango kikubwa kupeleka huduma za afya kwa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Kemi kwamba Serikali itaungana na watu wa Mwanza, itaungana na Bwana Mabula, Mbunge wa Nyamagana na ninyi Wabunge wa Mwanza wote kuhakikisha suala la afya katika mkoa wa Mwanza, kwa sababu ni Jiji kubwa inaimarika vizuri kutokana na population kubwa iliyokuwepo katika eneo hilo.
MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa tatizo hili la kifaa cha x- ray katika Hospitali ya Nyamagana ambalo Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI amelijibu na sisi katika Hospitali yetu ya Wilaya ya Mkuranga linatusumbua; je, Serikali inaweza kutuhakikishia kwamba katika mgao huo wa vifaa tiba hivi hospitali ya Wilaya ya Mkuranga itakuwa ni miongoni mwa hospitali zitakazopata kifaa hiki cha x-ray ili kuwaondoa wana Mkuranga na adha ya kusafiri umbali mrefu mpaka Dar es Salaam katika Hospitali ya Temeke? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Hospitali ya Mkuranga haina x-ray, hali kadhalika na Hospitali ya Mafia na maeneo mengine yote. Lakini katika harakati zilizofanyika sasa hivi wenzetu wa Mafia angalau kupitia Mbunge Mheshimiwa Dau sasa wamepata x-ray, nadhani wiki iliyopita walinijulisha kwamba Mafia inapata x-ray.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la Mkuranga vilevile tunajua kweli hakuna. Nimuombe Mheshimiwa Mbunge tukae pamoja, kwa sababu katika bajeti ya mwaka huu nadhani haikutengwa, lakini tutakaa kwa mikakati ya pamoja tuangalie jinsi gani tutafanya kuwashirikisha wadau mbalimbali ambao katika njia moja au nyingine wanaweza kutusaidia kupata x-ray kwa sababu kifaa hiki ni muhimu sana ukiangalia au ukizingatia suala zima la ajali za pikipiki zinazotokea maeneo mbalimbali ambapo lazima mtu apimwe aangaliwe jinsi gani amepata majeruhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile nilipenda kuongezea yale majibu, kwamba vile vifaa havijafunguliwa katika hospitali nyingine. Kweli mimi nimepita maeneo mbalimbali, nilipita mpaka Bukene kwa rafiki yangu Mheshimiwa Zedi kuona center ambazo hazijafunguliwa; na tumetoa maagizo, ndiyo maana hata juzi hapa nimezungumza kwa ukali sana juu ya suala zima la Hospitali ya Singida. Lakini nimesikia, na leo nimekutana na Mbunge wa Singida amesema lile jambo limeshashughulikiwa sasa, hata vile vitanda havihami kutoka katika Hospitali ya Rufaa ya Singida.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, katika ziara zangu ambazo natarajia kuzifanya, lengo langu ni kufika katika Nyanda za Juu Kusini kuhakikisha kwamba kwa sababu tunapeleka madaktari wapya maeneo mbalimbali hizi zahanati ambazo hazijafunguliwa; ambapo tunawashukuru sana wenzetu wa Mkapa Foundation, wamefanya kazi kubwa sana; center hizi zinafunguliwa ili wananchi wapate huduma katika maeneo yao ya karibu zaidi.

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa majibu ya nyongeza kwenye maswali yote yanayohusu vifaa tiba kama x-ray hapa nchini kwamba Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaendesha mradi mkubwa wa vifaa tiba unaoitwa ORIO. Mradi huu utahusisha ununuzi wa vifaa mbalimbali vya kufanyia uchunguzi wa magonjwa kama MRI, CT Scan, x-ray, ultrasound na vifaa vingine na kuvitawanya nchi nzima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati nzuri Hospitali ya Mkuranga kwa mujibu wa kumbukumbu zangu ni mojawapo ya vituo ambavyo vitapatiwa mashine ya x-ray.
MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Kwanza nichukue nafasi hii kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Buhigwe, kupongeza Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi. Kwanza pongezi zimuendee Mheshimiwa Rais mwenyewe, Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa kuikazania barabara hii alipokuwa Waziri wa ujenzi. Lakini niendelee kupongeza Wizara ya TAMISEMI, nayo imechukua juhudi hiyo ili iweze kujengwa. Lakini naomba nimpongeze tena Waziri wa Fedha na Mipango kwa kuiweka kwenye mpango barabara hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali moja dogo la nyongeza. Mheshimiwa Naibu Waziri kwenye Jimbo letu na Wilaya yetu ya Buhigwe makao makuu ya Wilaya yamebadilika kutoka Kasulu kwenda Buhigwe lakini tunazo barabara nyingine ndani ya Halmashauri yetu ambazo inabidi zichongwe kwa ajili ya kufika makao makuu na kupunguza urefu wa kuzunguka. Tunazo barabara kama nane ambazo zinahitaji kama shilingi milioni 950. Naomba ushauri wako.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tukiweka rekodi sawa, Mheshimwa Obama toka kipindi chote cha miaka mitano ambapo alikuwa kama partner wangu wa karibu zaidi alikuwa akizungumzia maeneo haya ya barabara zake na amefanikiwa kuhakikisha kwamba wamehamisha makao makuu. Lakini nikijua wazi kwamba Sera ya Barabara tunaanza kipaombele katika zile barabara za kwanza zilizokuwa bora zaidi. Maana sera ya barabara ndiyo ilivyo hivyo; zile barabara ambazo hazijafunguliwa zinapewa kipaumbele cha mwisho zaidi.
Mheshimiwa Mweyekiti, sasa kwa sababu barabara hii kwa jinsi Mheshimiwa Mbunge alivyouliza ni barabara mpya, lengo ni ku-connect vizuri, kurahisisha ule umbali uwe mfupi zaidi. Nimsihi Mheshimiwa Mbunge, hili ni jambo jema, wananchi lazima wapate huduma, lakini nipende kuwahamasisha Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo mumuunge mkono Mbunge huyu sasa katika vile vipaumbele vya kufungua barabara hizo mpya; kwa sababu hii ni barabara ya ndani ya Halmashauri, jambo hili katika Kamati ya Uchumi hali kadhalika katika Kamati ya Fedha na Baraza la Madiwani muangalie jinsi gani sasa mtatumia own source japo angalau kuanza kulifungua. Ofisi ya Rais TAMISEMI katika suala zima la kufungua barabara zake za vikwazo tutaangalia jinsi gani kwa njia moja au nyingine zile Halmashauri za pembezoni zote ambazo zina changamoto kubwa za miundombinu ya barabara tutaziangalia kwa jicho la karibu ili wananchi waweze kupata huduma za kijamii katika maeneo yao.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa sera zinaelekeza kwamba barabara zinazounganisha mikoa zitajengwa kwa kiwango cha lami na kuna barabara inayotoka Mbulu kuja Karatu kwa maana inaunganisha Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Manyara, ni barabara ya siku nyingi; ni lini itajengwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera zetu nimezieleza wazi, sera hizo zinatafsiriwa vizuri katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Na Ilani ya Chama cha Mapinduzi imesema itawafikia wananchi wote hasa kuunganisha hii mikoa. Kama eneo hili linaunganisha Mkoa kwa Mkoa, Waziri wa Miundombinu akifika katika hotuba yake hapa nadhani atatuelezea mchanganuo wa mambo mengi zaidi. Kikubwa zaidi ni kwamba katika utekelezaji wa Ilani, maeneo yote yaliyoainishwa kwamba yatafikiwa, kwa mujibu wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi, jambo hilo litafanyika.

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kesho tuna bajeti yetu, na barabara zote ambazo zitajengwa kwa kiwango cha lami tutaeleza kwa kina kesho. Naomba Waheshimiwa Wabunge muwe wavumilivu mpaka kesho mtasikia mambo yote. Ahsanteni.
MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Nimesikia majibu ya Serikali kwa upande wa jinsi Serikali zitakavyoshughulika na hawa watu ambao wanaleta matatizo, lakini kuna matatizo ambayo yanasababishwa na Serikali. Kwa mfano kule Moshi Vijijini katika Kata ya TPC
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
17
watoto wa kike wanatembea kilometa kumi, saba kutoka eneo linaitwa Chemchem kwenda kutafuta shule iliko, na haya ni mashamba ya miwa ambapo kuna mambo membo mengi sana yanaweza kutokea hapo katikati, kuomba lift na vitu kama hivyo. Sasa Serikali inaweza kutuambia nini kuhusiana na hali kama hiyo; labda kujenga mabweni kwenye shule za aina hiyo ambazo ziko mbali kiasi hicho?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA:Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majibu yangu ya mwanza nilizungumzia suala ambalo Mheshimiwa Komu amelisema na hili linanipa faraja kubwa sana, kuona kila Mbunge hapa anasimama katika ajenda ya kumuokoa mtoto wa kike, hili naomba nishukuru sana. Na katika hili naomba niwaambie Wabunge tutaendelea kwa kadiri iwezekanavyo kuhakikisha kwamba tunasimika mabweni maeneo ya jirani, lakini sio mabweni peke yake, tutahakikisha kwamba jinsi gani tunafanya nguvu ya pamoja kwa ajili ya kuleta solidarity hata kwa wazazi; kwa sababu kuna maeneo mengine mabweni yamejengwa lakini watoto wanapenda kukaa uswahilini au kutembea mbali zaidi kwa sababu kuna mambo yao yale ya ku-discuss zaidi wanayoyapenda.
Kwa hiyo, sisi tutahakikisha kwamba tunasimamia na kuhamasisha wazazi wote; lakini kama Ofisi ya TAMISEMI inaliona hilo kwa sababu Wizara ya Afya imejielekeza vya kutosha katika kumuokoa mtoto wa kike na Wabunge wote, mimi naamini jambo hili tutafanikiwa kwa karibu zaidi.
MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa hii niweze kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, nianze kuipongeza Serikali kwa kutupelekea madaktari wawili kwenda kusoma waje kuwa Madaktari Bingwa kwa sababu hiyo ndiyo njia pekee ya kutusaidia sisi ambao tuko mikoa ya pembezoni. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile nimhakikishie Mheshimiwa Waziri wale ma-volunteer wa Kichina watano anaosema ni Madaktari Bingwa, wanaingia hospitali saa 5.00 na kutoka saa 7.00. Kwa maana hiyo, hawatusaidii ile ni Hospitali ya Rufaa, wagonjwa wanaingia ndani ya masaa 24. Kwa hiyo, wale Madaktari wa Kichina watano anaowasema hawatusaidii ipasavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimekuwa nikisema Bungeni hapa toka 2011 nikidai Madaktari Bingwa wa Mkoa wa Tabora, akina mama wanapata vifo vingi vya uzazi, watoto wetu wanakufa kwa sababu hatuna Madaktari Bingwa, vijana wetu madereva wa bodaboda wanavunjika miguu, hatuna Madaktari Bingwa wa Mifupa. Hii imekuwa kero kubwa kwetu sisi Wabunge ndani ya Mkoa wa Tabora na nimekuwa nikilisemea hilo kwa muda mrefu toka 2011 naingia hapa Bungeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Naibu Waziri hajanijibu vizuri, ana mkakati gani wa kutuletea Madaktari Bingwa ndani ya Mkoa wa Tabora?
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeomba vibali miaka 10 iliyopita lakini hatujapewa kibali cha kuajiri Madaktari hao. Naomba anijibu ana mkakati gani wa kutuletea Madaktari Bingwa katika Mkoa wa Tabora kwa sababu watu wanakufa? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ni kuhusiana na vifaa. Niipongeze Serikali kwa mkakati wake mzuri wa kusema kwamba Bima ya Afya itatukopesha na tupate vifaa ndani ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora. Hospitali ni ya siku nyingi, haina vifaa vyovyote, watu wanaendelea kufa. Hata hivyo, nimesema hatuna huduma ya ICU pale Tabora…
Mheshimiwa Naibu Waziri, yuko tayari kufuatana nami kwenda Tabora kuangalia changamoto zilizopo katika Hospitali ya Rufaa?
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, usimuone Mheshimiwa Munde ana-rap sana ni kwamba ameguswa na jambo hilo na ndiyo maana nimesema kwamba Serikali imepeleka madaktari kwa ajili ya kwenda kubobea katika maeneo hayo na lengo kubwa na mahsusi ni kwa ajili ya Mkoa wa Tabora, hili ni jambo moja kubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nafahamu fika, wiki chache zilizopita nilifika Mkoani Tabora pale. Nilienda katika Kituo cha Afya cha Bukene na Itobo, kote kuna vifaa vya upasuaji vinataka wataalam. Hata katika kipaumbele chetu tumesema suala la Mkoa wa Tabora lazima liwe kipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwaombe sana wataalam wetu, mara nyingi sana hospitali zilizoko pembeni madaktari wanaona ni tabu sana kwenda kwenye maeneo hayo. Sisi sasa hivi tumejipanga, lengo letu ni kuelekeza wataalam kwenye maeneo yote ya pembezoni na kuhakikisha kwamba wataalam wanaosomeshwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanaenda kuwahudumia Watanzania.
Suala la vifaa nimesema pale mwanzo na Waziri wa Afya na yeye analizungumza mara nyingi sana kwamba suala la vifaa kuna utaratibu maalum. Naomba niwaambie, kuna mchakato mkubwa sana wa hivi vifaa mwisho wa siku Hospitali zote za Kanda na Mikoa zifungiwe vifaa maalum ili mradi akina mama na wagonjwa mbalimbali waweze kuhudumiwa. Huu ni mpango mkakati wa Serikali na unaanza mwaka huu. Kwa hiyo, dada yangu Munde usihofu, mimi mtani wako umesema tuongozane, nitaongozana na wewe Mungu akijalia. (Makofi/Kicheko)


WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi (TAMISEMI), napenda kuongeza kidogo ufafanuzi katika suala la uhaba wa watumishi especially Madaktari Bingwa, nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kuwathibitishia Waheshimiwa Wabunge kwamba tumefanya tathmini ya uhaba wa watumishi katika sekta ya afya, especially Madaktari na Madaktari Bingwa. Tumebaini mikoa tisa ina uhaba mkubwa ikiwemo Tabora, Simiyu, Katavi, Geita, Shinyanga, Rukwa na Singida.
Kwa hiyo, kipaumbele cha ajira za Madaktari Bingwa katika mwaka huu tunatoa katika mikoa hiyo tisa. Kwa hiyo, Mheshimiwa Munde na Waheshimiwa Wabunge wengine wote ambao mnatoka katika hiyo mikoa tisa tutawapa kipaumbele kwa sababu mnao uhaba wa wataalam chini ya 52%. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia tumekusudia kufanya zoezi moja kugumu sana. Tunataka kuondoa tatizo la Madaktari Bingwa wataalam kurundikana katika mkoa mmoja na kuiacha mikoa ya pembezoni, kwa hiyo, tunataka kuangalia mgawanyo.
Waheshimiwa Wabunge mtuvumilie tutakapoendesha zoezi hili gumu mkasema huyu naomba umbakize, mwanamke wa Rukwa, Katavi, Njombe, Simiyu, ana haki ya kupata huduma za Daktari Bingwa kama mwanamke wa Dar es Salaam. Kwa hiyo, tunataka kuendesha zoezi la redistribution, tuwatawanye madaktari waende mikoani wakatoe huduma ili wanawake wa huko wapate huduma nzuri kama wanawake wa Dar es Salaam, Arusha na Kilimanjaro.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. (Makofi)
MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
Kwa kuwa matatizo ya ukosefu wa huduma katika Hospitali za Mkoa wa Morogoro hayana tofauti na matatizo ya Mkoa wa Tabora. Mkoa wa Morogoro una Hospitali ya Rufaa ambayo inatoa huduma katika wilaya zake zote lakini cha kusikitisha hospitali hiyo haina huduma ya X-ray. Huduma ya X-ray iliyopo ni ya zaidi ya miaka 20 iliyopita hali ambayo inawalazimu wagonjwa waliolazwa hata wodini kwenda kupata huduma za X-ray nje ya hospitali hiyo katika Hospitali za Mzinga. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha inapeleka huduma hizo za X-ray katika Hospitali hii muhimu ya Rufaa ambayo inategemewa na wananchi wa Mkoa wa Morogoro?
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, hiki kilio tumekisikia na tunajua Morogoro ni center. Ukisema huduma ya X-ray pale Morogoro hakuna wakati tukijua Morogoro ni muungano wa barabara mbili, inayotokea Dodoma na ile inayotokea Iringa, na katika njia moja au nyingine kama kesi za ajali za magari lazima mgonjwa moja kwa moja atapelekwa katika Hospitali ya Mkoa. Sasa kama changamoto hii ni kubwa kiasi hiki, naomba niseme katika zoezi letu la kupeleka vifaa vya upimaji tutahakikisha Morogoro inapewa kipaumbele. Naomba aiamini Serikali yake itaenda kufanya kazi hiyo haraka iwezekanavyo.
MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kutoa masahihisho, Naibu Waziri wakati anajibu aliniita Malopo naitwa Malapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu hayo ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, je, Serikali iko tayari sasa kuwaambia wananchi kuwa haiko tayari kutekeleza Sera ya Elimu Bure kwa maana halisi ya Kiswahili ya neno bure isipokuwa elimu inayotolewa sasa ni ya kuchangia gharama? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, nini wito wa Serikali kwa wananchi kuhusu sera hii ili kuwawezesha walimu kufanya kazi yao bila kero kutoka kwa wazazi wanaofikiri hawawajibiki kulipa pesa yoyote kwa ajili ya elimu hiyo kwa watoto wao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, asante. Kwanza naomba radhi kwa kukosea jina la Mheshimiwa Mbunge ni Malapo na nakushukuru sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala kwamba Serikali iseme haina nia ya dhati katika suala zima la elimu bure, ndugu zangu naomba niwaambie, kama sisi ni mashahidi wa kweli vijana wengi waliokuwa wanaenda sekondari walikuwa wanashindwa kulipa hizi gharama za kawaida. Hata wale waliokuwa wanaanza elimu ya msingi mnafahamu wazazi wengi sana wanashindwa kulipa zile gharama za awali ili mtoto wake aweze kujiunga na shule na ninyi wenyewe ni mashahidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, juzi juzi kupitia vyombo vya habari wazazi wanakiri kabisa kwamba suala hili limewasaidia kwa kiwango kikubwa vijana wao kwenda shule. Hata turn over katika shule zetu imekuwaje? Hata madarasa wakati mwingine shule zinahemewa kwa sababu wazazi wote ambao mwanzo walikuwa wanakwazika na gharama hizi sasa wanapata fursa ya kuwapeleka watoto wao shule. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tukiri kwamba Serikali katika hili imefanya juhudi kubwa sana. Naamini jambo lolote lazima lina changamoto zake, hizi changamoto ndogo-ndogo ni kwa ajili ya kuboresha ili mradi mpango uende vizuri lakini dhana ya Serikali imekamilika na inaenda vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika sehemu ya pili, wito wa Serikali Walimu wasibughudhi wazazi, nadhani tumeshasema wazi na Waziri wangu jana alilisema wazi kwamba jambo kubwa elimu hii ni bure. Hatutarajii mwalimu awazuie watoto kwenda shule kwa kuzusha mchango wake mwenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hili tumesema tutakuwa wakali sana kwani lengo kubwa ni mtoto wa Kitanzania aweze kupata elimu ya shule ya msingi na ya sekondari mpaka form four. Lengo ni kwamba kila mwanafunzi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania apate fursa ya uongozi na mikakati ya Serikali ya Awamu ya Tano.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuongezea majibu mazuri yaliyotolewa na Naibu Waziri wa TAMISEMI kutokana na maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Malapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali imefanya jitihada kubwa katika suala hili la elimu bure, lakini inasikitishwa kwamba wenzetu walihoji fedha hizi zimetoka wapi kwenye bajeti na leo fedha hii iliyotolewa kwa ajili ya kusaidia jamii maskini watoto wao waende shule wanahoji tena hiyo bure gani, ni mkanganyiko ambao haueleweki. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, mimi niseme tu, katika kila shule za msingi za kutwa tutapeleka kila mwezi shilingi 600/= kwa kila mtoto kwa ajili ya uendeshaji. Kwa shule za sekondari za kutwa tunapeleka kwa kila mwezi shilingi 3,540.57/= kwa kila mtoto kwa ajili ya uendeshaji wa shule. Kwa wale wa bweni tunapeleka shilingi 7,243.39/= kwa kila mwezi. Fedha hizi zikijumlishwa uwezekano wa kuendesha elimu upo pamoja na changamoto zilizopo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo ninavyozungumza kutokana na mpango huu wa elimu msingi bila malipo pale ambapo tulitegemea wajiandikishwe watoto 80 kuanza darasa la kwanza wamejiandikisha 240; pale tulipotaka wajiandikishe watoto 180 wamejiandikisha karibu 700 na hiyo ni Dar es Salaam tu.
Mheshimiwa Naibu Spika, yako baadhi ya maeneo uwezekano tu wa kuwapokea watoto hawa ni mgumu kwa sababu wazazi maskini wameona mpango huu ni muhimu kwao na umewasaidia sana.
Kwa hiyo, kuubezabeza hapa ni kwenda kinyume kabisa na wananchi ambao wanaona mpango huu umewasaidia na kwa hakika kusema kweli unalisaidia Taifa. Tupingane katika mengine lakini kwenye jambo zuri tutiane moyo kama Watanzania. (Makofi)
MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, asante sana. Kwa kuwa walimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi walisimamia mtihani wa kidato cha Nne mwaka jana 2015 hawajalipwa fedha zao. Je, Serikali haioni ni mwendelezo wa kuwanyanyasa walimu na kuwaonea?
NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika asante. Mheshimiwa Pascal juzi wakati anajadili hapa nadhani alizungumzia suala la Mbozi, na ofisi yetu inalifanyia kazi kushirikiana na Hazina na katika mchakato tunaoondoka nao walimu wote ambao malipo yao yalikuwa bado hayajakamilika basi yataweza kusawazishwa na jambo hili likaweza kukaa vizuri, Serikali inafanyia kazi jambo hilo.
MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuiuliza Serikali, je, katika maeneo ambapo sisi kama wananchi na viongozi tumejitahidi, kwa mfano, Kituo cha Afya Magugu tumeweza kuwekeza vifaa mbalimbali ambavyo ngazi hiyo haina mpango au kwa mpango wa Serikali haipeleki wataalam wa aina hiyo, kwa mfano, tuna ultra-sound na vifaa vya macho. Je, Serikali itakuwa tayari mahali ambapo sisi wananchi tumewekeza vifaa mbalimbali ituletee wataalam wa ngazi hiyo? Kwa mfano, Kituo cha Afya Magugu watuletee Madaktari wa Upasuaji wa Macho na wa Ultra-sound kwa sababu vifaa vyote tunavyo na havitumiki. Inabidi tuombe wataalam kutoka mkoani wawe wanakuja mara moja kwa wiki kutusaidia. Je, Serikali itakuwa tayari kutusaidia wataalam hawa?
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nikiri miongoni mwa Wabunge ambao wanafanya kazi kubwa ni Mheshimiwa Jitu Soni. Mwaka juzi nilikuwa ni shahidi Detros Group ya Arusha imesaidia vifaa vyote kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Magugu. Kwa hiyo, juhudi hii amefanya Mbunge akashirikiana na wadau wenzake kutoka Arusha lakini kusaidia Mkoa wa Manyara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikiri katika mgao wa mwaka huu zoezi kubwa tunalokwenda kufanya, juzi nilijibu swali hapa kwamba mwaka huu mkakati wa Serikali ni kuajiri watumishi wapya wa afya 10,780. Katika watumishi hao wapya ambao tunakwenda kuwaajiri, naomba nikuambie Mheshimiwa Jitu Soni; Kituo cha Afya cha Magugu kitapewa kipaumbele kwa sababu wananchi wa Manyara, Babati Vijijini mmefanya kazi kubwa, lengo letu akinamama wapate huduma bora pale. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi nitoe tu majibu ya ziada kwamba Wizara ya Afya na Maendeleo ya Jami ipo kwenye mchakato wa kutengeneza utaratibu wa kuwasainisha mikataba maalum watumishi wote ambao wataajiriwa kuanzia sasa kwa kipindi maalum, kama miaka mitatu ama miaka mitano ili wasiondoke kwenye maeneo ya pembezoni kama ilivyo kwenye Kituo cha Afya cha Magugu.
MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na kwa niaba ya wananchi wa Mafia niulize maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kutoa majibu ambayo hayatoshelezi sana, namuuliza Mheshimiwa Waziri kama ataichukulia kesi ya Mafia kuwa ni special case ambayo inahitaji kushughulikiwa kwa haraka? Hili liko katika zahanati ya Chemchem ambapo zahanati imepewa jukumu la kuwa kituo cha afya kwa maana ya kushughulikia vijiji zaidi ya kimoja lakini ina mhudumu wa afya badala ya tabibu ambaye anahudumia wananchi. Je, analichukulia jambo hili kuwa ni suala la dharura na kwa hiyo atupatie tabibu haraka iwezekanavyo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ataichukulia pia kama ni special case Zahanati ya Chunguruma ambapo pamoja na kumuweka Mkunga mwenye sifa lakini ni mwanaume. Je, atatupelekea haraka Mkunga mwanamke katika Zahati ya Chunguruma ili wanawake wa Mafia wapewe huduma stahiki? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeisikia changamoto hii na umezungumzia Zahanati ya Chechem na Chunguruma. Kama nilivyosema pale awali, ni kweli, ukiangalia Mafia ina Hospitali ya Wilaya na tuna zahanati takriban 16. Changamoto yake ni kwamba zinazo-function vizuri ni zahanati tano. Kwa hiyo, tuna upungufu mkubwa zaidi katika zahanati zipatazo 11.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili nini cha kufanya sasa, ndiyo maana Wilaya ya Mafia sasa hivi imepewa kibali cha kuajiri watumishi wapatao 18 lakini katika hilo kipaumbele cha awali ni kuajiri Clinical Officers ili ku-cover maeneo yale ambayo tunaona kuna watu ambao hawastahili kufanya hizo kazi lakini kutokana na changamoto iliyopo wanafanya kazi ambazo ziko nje ya kada yao. Kwa hiyo, tunalifanyia kazi hilo suala hilo na tunaishukuru Ofisi ya Utumishi imeshatupatia kibali. Si muda mrefu sana baada ya ajira hiyo watumishi hao wataweza kufika katika zahanati hizo ili waweze kutoa huduma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile katika hili tumejielekeza, asubuhi tulikuwa tunawasiliana na RAS wetu wa Mkoa wa Pwani. Changamoto ya jiografia ya Mafia utakuta watumishi wengi sana wakipangwa wengine wanasuasua kufika. Tumeelekezana na RAS wa Mkoa wa Pwani kuhakikisha watumishi wote wanaotakiwa kufika Mafia hasa katika sekta ya afya waweze kufika ili wananchi wote wanaotakiwa kupata huduma waweze kupata huduma. Lengo letu kama Serikali ni kuhakikisha afya hasa ya mama na mtoto inalindwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya kwamba mhudumu mwanaume ndiye anayetoa hiyo service, tumelichukua hili. Nadhani ni angalizo kwa sisi watu wa Serikali japokuwa watu wa afya hasa Madaktari kazi zao wanafanya sehemu zote lakini tunatoa kipaumbele kwa akinamama. Inawezekana magonjwa mengine anapohudumiwa na baba inakuwa ni changamoto kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tulichukue hili na nimwelekeze RAS wetu wa Mkoa wa Pwani kuhakikisha kwa haraka anafanya juhudi iwezekanavyo kupeleka Madaktari au wahudumu wanawake katika zahanati hii ambayo inaonekana ina changamoto kubwa ili hata mtu akienda katika zahanati ile akiwa mwanamama aone kwamba sitara yake imesitirika. Nashukuru sana.
MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ningependa kujua ushirikishwaji wa vikao vya Wilaya ya Maswa, kwa sababu jibu lake la mwanzo ameeleza kwamba vijiji vilishirikishwa, lakini nina hakika kabisa ushirikishwaji wa vijiji hivi na Kamati hizi zilizoorodheshwa hapa sina hakika navyo. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuniridhisha kwa kunionesha vikao hivi vilifanyika lini na wapi ili watu wa Maswa waweze kulitambua hilo?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa Mwenyekiti wa RCC ni Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Mkoa wa wakati ule alikuwa ni Dkt. Balele ambaye naye anatokea Bariadi, huoni naye alikuwa labda ni sehemu ya kufanya Serikali iingie kwenye matumizi makubwa, kupeleka sehemu ambapo hakuna majengo mengi ikilinganishwa na Maswa ambayo ni Wilaya kongwe iliyozaa Bariadi na Meatu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika majibu yangu ya awali, kwa sababu suala la michakato ya kuanzisha Wilaya, kuanzisha Halmashauri, kuanzisha Mkoa mpya yote haya hayaanzii katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI, haya ni maoni ya wadau ambao wameona kwamba kuna haja ya kufanya hivyo, wanakaa katika vikao halali na kufanya maamuzi.
Mheshimiwa Spika, nimesema pale awali kwamba kikao hiki kilipitishwa na wajumbe, tarehe 10 Mei, ndiyo walifanya maamuzi hayo. Sasa nikisema nirejee kuthibitisha vikao kwa sababu suala hili nadhani DCC zote kabla hujafika katika maeneo mbalimbali; kuna vikao vya Mabaraza ya Madiwani, kuna Vikao vya Ushauri vya Wilaya, then kuna Vikao vya Ushauri vya Mkoa.
Kwa hiyo, nasema kwamba tukitaka kupata reference vizuri, tunapokutana katika RCC yetu inayokuja hapo tuitishe mihtasari ambayo ilipitisha, haya naamini tutayaona na ninyi ni wajumbe wa Kamati ya RCC. Kwa hiyo nadhani hili halina shaka.
Mheshimiwa Spika, suala la kusema kwamba Mwenyekiti wa Kikao hicho ambaye alikuwa Mkuu wa Mkoa lakini asili yake alikuwa anatokea Bariadi. Naomba niwaambie ndugu zangu, tunapofanya maamuzi siku zote tusisukumwe na maamuzi ya mtu mmoja. Mimi kwa akili yangu siamini kama mtu mmoja ataburuza Kamati yote ya RCC na Wilaya yote na yakafuatwa maamuzi yake. Kikubwa zaidi tunapojipambanua katika mikutano yetu ni lazima tuwe imara kujenga hoja kujua jambo hilo linafanyika vipi.
Naamini kama kulikuwa na upungufu RCC yenu mtakaa na kufanya maamuzi sasa kwa mujibu wa sheria. Jambo hili bahati nzuri watu walileta pingamizi, lakini kutokana na vigezo vilivyoletwa, pingamizi lile baadaye ikaonekana kwamba kwa sababu maamuzi hayo yalifanyika halali kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 145, kurudisha madaraka kwa wananchi, ikaonekana ni halali. Ndipo jambo hili limekuja na Ofisi ya Rais, TAMISEMI ikaona kwamba ni sawa.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge najua kwamba hoja yake ina msingi, lakini inawezekana wakati huo yeye hukuwepo katika RCC, lakini wenzake waliokuwepo kipindi hicho waliona kwamba jambo hilo lifanyike hivyo. Ahsante sana.
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Migogoro ya ardhi hasa ya WMA imekuwa ya muda mrefu katika nchi yetu. Jimboni kwangu vipo vijiji ambavyo vina migogoro ya WMA wakati vijiji hivyo ardhi hiyo ni mali yao, lakini kumekuwa na tatizo la wakulima kusumbuliwa, kufukuzwa, kuchomewa nyumba kwenye maeneo yao. Je, ni lini Serikali itakomesha tabia hii ya kuwachomea wananchi kwenye Vijiji husika vya Kabage, Sibwesa, Kapanga na eneo la Kagobole?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, tukifanya rejea ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi katika majibu yake alipokuwa akijibu swali la Mheshimiwa Juma Nkamia, alisema kwamba ni maeneo mbalimbali. Hata hivyo, katika suala la kutaka Wabunge kuuliza swali la nyongeza, Wajumbe wengi wamesimama kuonesha kwamba jambo hilo linagusa siyo sehemu ya Mheshimiwa Kakoso peke yake au sehemu ya Mheshimiwa Nkamia peke yake isipokuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Spika, tukifanya rejea, Waziri Mkuu alipokuwa akitembelea katika Mkoa wa Kigoma na mikoa mingine katika Kanda ya Ziwa, alipofika kule Geita miongoni mwa matatizo yalikuwa ni ya wakulima na wafugaji hasa sehemu za hifadhi.
Mheshimiwa Spika, Waziri Mkuu alitoa maelekezo katika Wizara ambazo kwa njia moja au nyingine zinashirikiana hasa Wizara ya Ardhi, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Maliasili na Utalii hali kadhalika na TAMISEMI.
Mheshimiwa Spika, naomba, Mheshimiwa Kakoso, sitaki kuweka commitment hapa ambayo maelekezo Mheshimiwa Waziri Mkuu ameshayatoa ni kwamba, timu itaundwa kuangalia maeneo yote ya mgogoro na kuangalia mbinu gani ya kuweza kutatua case by case kutoka na hali halisi ya mgogoro husika.
Mheshimiwa Spika, jambo hili Mheshimiwa Kakoso tumelisikia kama Serikali, ni miongoni mwa maeneo ambayo yatajumuishwa kufanyiwa kazi kwa pamoja kuondoa migogoro hii katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naongezea majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Ni kweli kuna matatizo mengi sana katika WMAs nyingi, siyo hii tu anayotoka Mheshimiwa Kakoso. WMAs zimeanzishwa kwa mujibu wa Sheria, ni maeneo ya hifadhi ambayo yanamilikiwa na wanavijiji, kandokando mwa hifadhi za Serikali, lakini WMAs hizi zimepewa mipaka na zimepewa majukumu na mamlaka ya kumiliki maeneo haya.
Mheshimiwa Spika, nadhani Wilaya au kwa makusudi au kwa kutokujua wanaingilia mipaka hiyo. Kwa sababu wanaotakiwa kusimamia kuweka mipaka ya WMAs hizi ni Viongozi wa Wilaya. Sasa nitashangaa Viongozi wa Wilaya kuingia kuchoma! Hata hivyo, kinachotakiwa Mheshimiwa Kakoso hapa, kila WMA iweke matumizi bora ya ardhi katika eneo lake wanalomiliki ili ijulikane wazi sehemu ya kilimo ni ipi na sehemu ya mifugo ni ipi na mipaka hiyo na ramani hizo zinasajiliwa kwenye ngazi zote kuanzia Wilaya, Mikoa na Wizara ya Maliasili.
Mheshimiwa Spika, nadhani Mheshimiwa Kakoso arudi kule akaangalie je, mipaka hii ya WMAs imesajiliwa katika ngazi zote hizo na mipango ya matumizi bora ya ardhi imefanyika? Kwa sababu ikifanyika mipango ya matumizi bora ya ardhi na wanaofanya ni watalaam wa ardhi na viongozi wa Wilaya haitatokea hata siku moja kuwa na contradiction kati ya Viongozi wa Wilaya na WMAs.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri, tumekusudia kama Serikali wote kwa pamoja, Wizara ya Ardhi, Wizara ya TAMISEMI, Maliasili na watumiaji wakubwa wa ardhi kilimo na mifugo, kukaa pamoja, kuainisha migogoro yote hii hata hiyo migogoro ambayo inasababishwa na hifadhi, wafugaji na wakulima ili kwa pamoja tukae tuweze kuitatua migogoro hii.
Mheshimiwa Spika, najua hapa wakisimama, kila mmoja ameguswa na migogoro kama hii. Kwa hiyo, ni kweli kwamba tumeamua kama Serikali tutakaa pamoja na nitaleta kwenye bajeti yangu sehemu ya migogoro kwa uchokozi, ambayo mmeshatuletea Waheshimiwa Wabunge, kama bado mingine ipo tutaendelea kujazilizia ili Wizara hizi zote zinazohusika tuweke utaratibu wa namna ya kupitia mgogoro mmoja baada ya mwingine ili tuweze kuitatua.
MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri Jafo mpaka sasa tunavyoongea baadhi ya shule za sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ikiwemo Shule ya Sekondari Magindu, Shule ya Ruvu Station na Shule ya Dosa Aziz katika kutii agizo la Serikali Kuu la kujenga maabara katika shule zetu za sekondari inakabiliwa na madeni makubwa ya wazabuni pamoja na mafundi. Swali langu la kwanza, ninaomba kauli ya Serikali, je, itakuwa tayari ku-clear madeni hayo ili kutua mzigo Halmashauri zetu?
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, ni lini sasa Serikali Kuu itaacha kubebesha mizigo Halmashauri kwa kutoa maagizo nje kabisa ya bajeti ya Halmashauri ya kuzitaka zitekeleza maagizo ya Serikali kuu ikiwemo hili agizo jipya la kila mtoto kukalia dawati pasipo kuwatengea fungu maalum. Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alitoa agizo la ujenzi wa maabara na agizo lile lilikuwa ni agizo la kimkakati. Kwa sababu shule nyingi sana katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hasa hizi shule za kata zilikuwa zina upungufu wa maabara. Sambamba na hiyo watoto walikuwa wakienda shuleni wanakosa fursa ya kupata masomo ya sayansi, kwa mtazamo ulio makini ndiyo maana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
16
alitoa agizo hilo. Lakini naomba niseme wazi kwamba agizo lile limeleta manufaa makubwa sana kwa watoto wetu wanaosoma shule za kata. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, hili niwapongeze Watanzania wote kwa ujumla wamejitahidi katika kila eneo moja kufanya fursa, hata Halmashauri ya Kibaha najua walikuwa na mchakato wa kujenga takribani maabara nane, changamoto iliyokuwepo ni upatikanaji wa fedha ilikuwa ni changamoto kubwa kwa sababu Kibaha peke yake walichanga shilingi milioni 218. 6 lakini bahati mbaya upelekaji wa fedha haukuwa vizuri.
Mheshimiwa Spika, naomba niwaambie suala la upelekaji wa fedha lilikuwa sio suala la sekta ya elimu peke yake, mnakumbuka hata miradi ya maji ilisimama ndiyo maana ajenda kubwa ya Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliposhika madaraka aliazimia kuhakikisha kwamba kodi inakusanywa ili mradi kulipa madeni ya wakandarasi wa aina mbalimbali. Hili naomba niseme pale kuna wakandarasi wanadai na niseme Serikali inalitambua hilo na juhudi ya Serikali itaendelea kukusanya kodi ili mradi kulipa madeni ya wakandarasi kwa kadri iwezekanavyo kuweza kutatua tatizo hilo.
Mheshimiwa Spika, suala lingine ni lini Serikali sasa itaacha kutoa maelekezo haya. Naomba niwaambie ndugu zangu, Serikali inapima nini kifanyike katika muda gani na hivi sasa mnakumbuka kuna maagizo mbalimbali yametoka lakini lengo lake kubwa ni kuisaidia jamii.
Kwa hiyo, naamini maagizo yote yaliyotolewa na Serikali ni maagizo na kuona ni uhitaji wa kiasi gani uweze kufanyika kwa ajili ya kutatua matatizo ya Watanzania. Lakini hili nililosikia kwamba kila mtoto achangie dawati, hili nadhani ngoja tutalifanyia kazi kwa sababu maagizo yetu ya Serikali kama watu watachangia ni wadau wenyewe katika maeneo husika wanajihamasisha kama tunavyoona hivi sasa, na juzi nishukuru nilikabidhi madawati hapa Dodoma. Watu/wadau waliamua kuchangia madawati lakini siamini kama kuna watu wanalazimishwa kuchangia madawati kwa sababu hizo ndiyo miongoni mwa kero tuliamua kuzitatua katika Jamhuri ya Muungano ya Tanzana ili mradi mwananchi wa kawaida aweze ku-access elimu ya mtoto wake. Ahsante.
MHE. FREEMAN H. MBOWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kumuuliza swali Mheshimiwa Waziri.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
17
Maadam Mheshimiwa Waziri ameeleza kwamba maelekezo ambayo Serikali Kuu inatoa kwa Serikali za Mitaa yanasimamiwa ama yanasimamia msingi wa nia njema na kwa sababu tunakubaliana katika utawala wa nchi, nia njema haiwezi ikazidi utaratibu uliowekwa kwa sheria, kanuni na taratibu za kiutawala na kwa sababu kumekuwepo na tatizo kubwa sana la muingiliano wa maelekezo hususan kwenye zile Hamlashauri za Wilaya ama Manispaa ambazo zinaongozwa na vyama tofauti na Chama cha Mapinduzi.
Je, ili kuweka utawala wa sheria, unaoheshimu mifumo yetu ya kiutawala iliyowekwa na sheria, Waziri haoni kwamba ni muhimu na busara sana Serikali ikatoa tamko katika Bunge hili kwamba viongozi katika ngazi ya Wilaya kwa maana ya Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa waache kuingilia majukumu ya Halmashauri za Wilaya na Manispaa ili kuruhusu maamuzi ya vikao vya Madiwani na wengine kufanya kazi kwa mujibu wa taratibu za sheria?
Mheshimiwa Spika, kwanza naomba tuweke kumbukumbu sawa sawa, lengo letu Serikali za Mitaa zimewekwa kwa mujibu wa Katiba Ibara 145 na utekelezaji wake unaelezewa katika Ibara 146; kwa hiyo, maana yake ni chombo halali ambacho kiko kwa mujibu wa sheria. Nimesema pale awali maelekezo hasa ya kutoka Serikali Kuu, maana yake kikubwa zaidi yanania njema kama Mheshimiwa Mbowe ulivyorejea hapa. Lakini anasema jinsi gani Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wasiingilie maamuzi, kinachofanyika ni kwamba Wakuu wa Mikoa na Wilaya sio wanaingilia, wanachokifanya ni nini? Kinachotakiwa hasa cha msingi ni kuona kama utaratibu unakiukwa pale Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya ana haki ya kuweza kuliingilia hilo jambo lisiharibike kwa ajili ya maslahi ya umma. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nina imani haiwezekani kikao halali cha baadhi ya Madiwani kimefanya ambayo hakuna utaratibu wowote uliokiukwa Mkuu wa Mkoa au Wilaya atakuwa ameingilia. Lakini kama kuna jambo linaenda kinyume na Mkuu wa Mkoa yupo, naye anaona jambo linaharibika kwa makusudi mbele yake ni lazima aingilie hapo ilimradi kuweka mambo sawasawa. Kwa sababu mwisho wa siku ni kwamba watu wanatarajia kwamba Serikali hiyo iliyowekwa kwa mujibu wa sheria basi itatimiza majukumu yake kama wananchi walivyoipa ridhaa itawaongoza katika kipindi hicho mambo yanayohitajika yaweze kufikiwa na yaweze kufahanikiwa. Kwa sababu sasa hivi Tanzania tunaongozwa kwa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 - 2020.
Mheshimiwa Spika, lengo kubwa ni kwamba kuanglia kama Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya aharibu utaratibu wa Baraza la Madiwani lakini wanahakikisha kwamba utekelezaji wa Ilani unakamilika kama ilivyokusudiwa na wananchi walioichagua Serikali hiyo.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa hospitali zetu mbalimbali nchini zina upungufu mkubwa wa dawa, je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha dawa za uhakika zinapatikana katika hospitali zetu nchini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali dogo la pili, kwa kuwa MSD pia inaidai Serikali fedha nyingi, je, ni lini Serikali itahakikisha inalipa deni la MSD?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Cecilia Paresso kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tulivyoeleza hapa katika vipindi tofauti, jukumu kubwa la Serikali ni kuhakikisha tunaondoa upungufu wa dawa na vifaa tiba. Katika swali la kwanza linalosema Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba dawa zinapatikana, ni kama tulivyoeleza hapo awali kwamba jukumu letu kubwa hivi sasa ni kuhakikisha kwanza tunajielekeza zaidi katika ukusanyaji wa mapato.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vipindi tofauti nimesema kwamba ukusanyaji wa mapato kwa kutumia mifumo ya kielektroniki ni kuongeza ukusanyaji wa fedha katika hospitali, zahanati na vituo vyetu vya afya. Tutakapofanya hili kwa upana wake maana yake ni kwamba vituo vya afya vitakuwa na dawa za kutosha kwa sababu mwongozo unasema jinsi gani pesa zinazopatikana zitaenda kwenye ununuzi wa dawa na vifaa tiba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala la deni la MSD Waziri wa Afya alipokuwa aki-table bajeti yake na katika mijadala mipana iliyojitokeza imejielekeza kuhakikisha deni la MSD linalipwa lengo likiwa ni MSD kuwa na uwezo wake wa kusambaza dawa. Waziri wa Afya alielezea suala hili kwa upana sana na Wizara ya Fedha ilichukua commitment ya kuhakikisha kwamba MSD deni lake linalipwa ili mwisho wa siku MSD iweze kusambaza dawa katika hospitali, zahanati hali kadhalika vituo vya afya na hospitali za mkoa.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa swali la msingi lilikuwa linahusu kuhusu kupandisha vituo vya afya; na kwa kuwa Wilaya ya Kilolo toka ilipoanzishwa mwaka 2000 haijawahi kuwa na hospitali ya Wilaya, imekuwa na Kituo cha Afya cha Dabaga na hivyo imepelekea ili wananachi kufuata huduma za hospitali inabidi waende Ilula kilometa zaidi ya 120.
Je, Serikali sasa haioni kuna umuhimu wa kupandisha hadhi kituo hicho cha Dabaga kuwa hospitali ya wilaya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwamoto, Mbunge wa Kilolo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba tupokee huo mtazamo kwamba Kilolo hakuna Hospitali ya Wilaya kwa hiyo ina maana lazima watu waende Ilula kwa ajili ya kupata matibabu. Nilieleza hapa katika vipindi tofauti kwamba mchakato wa kupandisha ama Zahanati kuwa Kituo cha Afya au Kituo cha Afya kuwa Hospitali ya Wilaya kuna utaratibu wake muhimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu wake unaanzia kwenye WDC kwa maana ya Mabaraza ya Madiwani mwisho wa siku unafika Wizara ya Afya ambao ndiyo wenye dhamana. Wizara wakishafanya uhakiki kwamba kituo hicho kimekidhi kuwa hospitali ya wilaya basi inapandishwa moja kwa moja kama nilivyozungumzia katika suala la wenzetu wa Nanyumbu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maelezo haya, naomba nimuelekeze Mheshimiwa Mbunge kwa sababu najua yupo makini sana katika Kamati ya TAMISEMI, ahakikishe kwamba ule mchakato wa awali unaenda na kuangalia vigezo vinafikiwa mwisho wa siku na sisi TAMISEMI tutaweka nguvu na Wizara ya Afya wataangalia vigezo vikikubalika kituo hicho cha afya kitapandishwa hadhi lengo kubwa likiwa ni kuwafikia wananchi kwa karibu zaidi. Ni kweli haiwezekani wala haiingii akilini mwananchi kutembea kilometa 100, ni umbali mkubwa sana.
Kwa hiyo, hili ni jambo la msingi na naomba mchakato uendelee kwa kufuata utaratibu unaoelekezwa, nadhani Serikali italiangalia kwa jicho la karibu zaidi.
MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru majibu mazuri ya Waziri ya kutununulia baadhi ya vifaa vya upasuaji ili tupate huduma hii. Kama nilivyosema vifaa hivi vimekaa tu haviwezi kufanya kazi, ni sawa na mifugo umechukua majike umeyaweka hujapeleka madume hakuna kitu ambacho kitaendelea pale. Serikali haioni sasa uko umuhimu wa kupeleka kwa mfano hizi dawa za usingizi ili shughuli za upasuaji ziweze kuanza? (Makofi)
Mheshimiwa mwenyekiti, la pili, Mheshimiwa Rais alipopita pale aliahidi kuwaondolea kero wananchi wa Makambako ili wasiende kufanyiwa upasuaji Njombe na Kibena kama nilivyouliza kwenye swali la msingi. Hawaoni sasa iko haja ya kuchukua fedha za dharura kununua vifaa hivi pamoja na vile vilivyopelekwa ili shughuli za upasuaji zianze?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Deo Sanga kama ifuatavyo:-
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
13
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nikiri nilifika pale Makambako na nikaenda mpaka Hospitali ya Kibena wakati nilipotembelea Makambako mpaka Njombe. Kihistoria ni kwamba watu wa Makambako walikuwa wakitibiwa katika Hospitali ya Kibena na ni kweli Hospitali hii inakabiliwa na changamoto kubwa sana na nimshukuru Mbunge kwa kweli lazima niweke wazi, ni miongoni mwa Wabunge ambao kwa kweli wanafanya kazi kubwa sana na nilitembelea mpaka miundombinu ambayo yeye mwenyewe alishirikiana na halmashauri yake kuiweka sambamba na miundombinu ya elimu. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge tunakupongeza kwa hilo kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kwamba vifaa viko pale havifanyi kazi ni kweli na ndiyo maana katika jibu langu la msingi nimesema vifaa vile havifanyi kazi. Pia hata lile jengo nadhani ukarabati ulianza kufanyika na hata mfumo wa maji zile koki zenyewe zilikuwa hazifanyi kazi vizuri. Kulikuwa kunatakiwa koki maalum ambazo unagonga kwa mkono inafunguka badala ya kushika ku-avoid contamination. Zoezi hilo limeenda vizuri ikiwa ni pamoja na urekebishaji wa mitaro, lakini changamoto kubwa pale imekuwa ni fedha. Jukumu letu kubwa ni kuhakikisha ile bajeti iliyotengwa iweze kufika angalau lile jengo lifanye kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia amesema wazi Mheshimiwa Rais alipita kule wakati wa kampeni na aliahidi kushughulikia hospitali ile ya Makambako ili ifanye kazi vizuri. Kuhusu kutenga pesa za dharura, mimi nasema jukumu letu kubwa katika kipindi hiki cha mwaka wa fedha tunaoenda nao ile bajeti ambayo ilielekezwa kwenda pale ambayo kwa bahati mbaya haijafika vizuri basi tutawasiliana ndani ya Serikali yetu ili iweze kwenda. Sasa hivi tumesema tumeongeza sana ukusanyaji wa mapato tutahakikisha yale mapato yanayokusanywa kwa zile bajeti zilizopangwa ambazo pesa hazijapelekwa ziweze kupelekwa ili miradi iweze kutekelezeka na wananchi wapate huduma.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mzee Deo Sanga naomba nikiri kwamba tutakuwa pamoja kuhakikisha kwamba wananchi wa Makambako hasa tukijua ni center kubwa sana kwa watu wa Mbeya na Songea, tutasaidia eneo lile liweze kupata huduma bora za afya.
MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tatizo la afya au linalohusiana na zahanati kwa ujumla linagusa maeneo mengi katika nchi hii ya Tanzania. Mojawapo ni Zahanati ya Nduruma iliyopo katika Kata ya Nduruma, Wilaya ya Arumeru. Zahanati hii imepandishwa hadhi na kuwa Kituo cha Afya lakini hakuna jengo la upasuaji, hakuna vifaa na inahudumia vijiji karibia kumi. Je, Waziri anatuambia nini kuhusiana na kituo hiki cha afya ambacho hakina vifaa na wananchi wanalazimika kwenda Hospitali ya Mount Meru iliyoko mkoani Arusha?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Mollel, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, wiki moja iliyopita Mheshimiwa Amina Mollel aliniambia kuhusu zahanati hiyo ambayo imepandishwa hadhi kuwa Kituo cha Afya na mimi nilimpa ahadi kwamba tutafanya kila liwezekanalo, huenda kabla Bunge hili halijaisha tutafika pale Arusha kuangalia zahanati hii. Pia ameniambia mambo mengine zaidi kwamba wataalam wengine wameondoka na zahanati ile haifanyi kazi. Naomba nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge kwamba kwanza safari yetu itakuwa palepale mimi na yeye, tutaenda pale Nduruma kuona changamoto za zahanati ile kwa karibu zaidi. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wale kutoka pale kwenda Mount Meru na Arusha ni jiji linalokuwa na population inaongezeka. Ni lazima maeneo ya pembeni tuyaimarishe ili kupunguza ile referral system kwamba siyo kila mtu ugonjwa mdogo aende katika Hospitali ya Wilaya. Serikali kupitia TAMISEMI na tutakapokwenda pamoja tutahakikisha ule upungufu tunaubaini na kupanga mpango mkakati wa jinsi gani tutafanya ili kituo hiki cha afya kiwe na vifaa tiba na wataalam kiweze kutoa huduma katika maeneo hayo na kata zinazokizunguka.
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika jibu la msingi napenda kwanza kumshukuru ameweza kueleza kwamba kuna fedha ilitengwa kwa kipindi cha mwaka 2015/2016 ambayo bajeti yake inakwisha mwezi wa Sita tarehe 30; na hizi fedha amesema Serikali imepanga kufanya matengenezo ya kilometa 42 kwa kiwango cha changarawe ambapo fedha zilizotengwa kwa ajili ya kazi hiyo ni shilingi milioni 246. Swali langu, je, fedha hizo zitatoka kabla ya Juni 30 mwaka huu? Hilo ni swali la kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, pamoja na kufahamu changamoto za barabara zilizoko katika Majimbo yetu hasa katika mikoa yetu hiyo ya pembezoni, tatizo siyo barabara anayoniambia ambayo imetengewa fedha ya kutoka Kibaoni kupitia Majimoto mpaka Kasansa na kwenda Inyonga.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la barabara nilizokuwa nikisema ni ambazo ziko chini ya Halmashauri na concern yangu na ya wananchi ni kwamba Halmashauri hizi mpya zikiwemo na mikoa mingine mipya ya Simiyu, Geita pamoja na Katavi kwamba hazina bado uwezo wa kuwa na hizo barabara. Swali langu la msingi hapa ni kwamba Serikali iangalie sasa namna ya kutafuta fungu la dharura kwenye barabara zilizoko ndani ya Halmashauri. Kwa mfano, kwangu, barabara ya kutoka Mamba…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kikwembe, naomba ufupishe tafadhali.
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Kwa mfano, kule kwangu, barabara ya kutoka Mamba kwenda Kabunde, barabara ya kwenda mpaka Maimba, barabara ya kutoka Lunguya mpaka Majimoto; barabara hizi hazipo kabisa. Naomba Serikali iangalie namna ya kupata fungu la ziada kuweza kutoa hiyo kwa ajili ya kutengeneza. Naomba kupata majibu ya maswali hayo, lini fedha hizo zitapatikana na ningependa zitakapopatikana tupewe taarifa.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru Mheshimiwa Mbunge anayezungumza hapa, ni Makamu Mwenyekiti wangu wa Kamati yetu ya TAMISEMI na Utawala Bora. Kwa hiyo, najua kwamba anajua wazi namshukuru sana, ameshiriki kwa kiwango kikubwa katika mchakato wa bajeti.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la fedha kwamba lini zitakwenda? Hili hata jana nililisema; nikasema, miradi mingi sana kwa kipindi kilichopita ilisuasua. Jana nilifanya reference siyo kwa miradi ya barabara peke yake isipokuwa hata miradi ya maji na miradi mbalimbali ya elimu, miundombinu ya madarasa, yote ilikwama kwa sababu makusanyo ya fedha yalikuwa siyo mazuri. Nilisema pia kwamba kutokana na Serikali ya Awamu ya Tano ilivyojipanga, ndiyo maana tunaona kila mwezi makusanyo ya mapato yameongezeka. Sasa hivi mradi mingi sana iliyokuwa imesimama, inaanza kutengewa fedha za kuanza kufanya kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni imani yangu kwamba katika kipindi hiki Mheshimiwa Kikwembe kabla hatujamaliza, basi mafungu hayo na wenzetu wa Hazina watatuhakikishia kwamba wanapeleka fedha zinazokusudiwa ili mradi wananchi waweze kupata huduma hii ya barabara. Kwa hiyo, nakiri kweli fedha hazijafika, lakini Ofisi ya Rais (TAMISEMI) inaendelea kufanya harakati na Ofisi ya Wizara ya Fedha ilimradi fedha zile kama zimetengwa katika bajeti ya fedha mwaka huu unaomalizika, iweze kupatikana na miradi iweze kuendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Halmashauri mpya ni kweli; na kweli Jimbo lako ni Halmashauri mpya pale na siyo hilo isipokuwa ni Halmashauri mbalimbali. Ndiyo maana katika bajeti yetu ya mwaka huu mtaona tumetenga karibu shilingi bilioni 240 plus. Lengo kubwa ni kuhakikisha kwamba tunazifikia Halmashauri katika miundombinu ya barabara. Bajeti zile tumetenga kwa sababu sehemu nyingine kuna barabara korofi na barabara zenye vikwazo, bajeti yake nayo tumeitenga hivyo hivyo karibu shilingi bilioni 45. Lengo letu kubwa ni kuangalia jinsi gani tutafanya kwenye Halmashauri ambazo ziko katika changamoto kubwa ili tuweze kuzitatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, siwezi kusema kwamba hapa kuna fedha za dharura; kesho na kesho kutwa zitatoka, isipokuwa, kama Serikali, tunachukua ombi hili na lengo ni Mikoa ya Pembezoni yote, siyo Jimbo la Mheshimiwa Kikwembe peke yake bali Mikoa yote ya Pembezoni imekuwa na changamoto kubwa sana, lazima Serikali tuliangalie kwa jicho la karibu ili kuweza kutatua matatizo ya wananchi.
MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuuliza swali la nyongeza. Tatizo la barabara hasa katika Halmashauri zetu ni kubwa sana ikiwemo hata Halmashauri ya Wilaya ya Geita na wananchi wanashindwa kwenda sehemu mbalimbali, wanashindwa kusafirisha mazao yao kwa sababu tatizo la barabara ni kubwa sana. Napenda kupata kauli ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba mnasemaje sasa kuhusu kupeleka fedha hizi ili barabara ziweze kutengenezwa kwa wakati?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema awali, nakiri wazi kwamba barabara nyingi sana ziko katika hali mbaya na nakiri wazi kwamba mvua iliyonyesha sasa hivi, zile barabara ambazo zilikuwa katika hali mbaya, sasa hivi hali imekuwa ni mbaya zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana nimesema pale awali wakati nilipokuwa najibu swali la Mheshimiwa Pudenciana kwamba jukumu letu kubwa ni kujielekeza sisi kama Serikali. Haya makusanyo ambayo sasa hivi yanakusanyika, basi katika bajeti ya fedha ambayo mwaka huu tunaondoka nayo, ziweze kufika Majimboni.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu ni kwamba, tunaposukuma fedha hizi, japokuwa ni kipindi kifupi kilichobakia, lakini zitasaidia hasa kukwamua barabara zenye changamoto kubwa. Nakiri wazi kwamba kweli barabara hali yake siyo nzuri na Mheshimiwa Lolesia nakiri kwamba nami nimeshafika kule Jimboni kwake kipindi naenda kuzindua mradi wa maji. Nimetembelea na nimeona barabara zile jinsi gani zilivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naahidi tutashirikiana ilimradi kinachopatikana siyo katika Jimbo lake peke yake isipokuwa katika maeneo mbalimbali ambayo yana changamoto kubwa, kama nilivyosema jana katika swali la msingi. Tutajitahidi ili hizi fedha ziweze kwenda na miradi iweze kutekelezeka.
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa shule hii ni siku nyingi sana imezungumzwa na Serikali kwamba itapandishwa hadhi kuwa shule ya Kidato cha Tano na Kidato cha Sita, lakini siyo kweli kwamba hii shule ina upungufu wa matundu ya vyoo, mimi shule hii naifahamu sana. Mwaka jana yamejengwa matundu 16, tatizo ni mabweni.
Swali langu la kwanza; je, Serikali ipo tayari hivi sasa kutenga bajeti ya kutosha ili shule hii ya Mchinga Sekondari waweze kujenga mabweni kwa ajili ya kupokea wanafunzi wa Kidato cha Tano na cha Sita? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, amezungumza hapa Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba shule ya Kidato cha Tano na cha Sita, mwanafunzi kutoka Lindi na maeneo mengine anaweza kupangiwa mkoa wowote, lakini shule hizi za Kidato cha Tano na cha Sita Tanzania zina matatizo mengi ya chakula na wanafunzi wanakula milo ambayo siyo kamili, wanakula maharage ya kuoza maeneo mengi. Swali langu; Serikali iko tayari hivi sasa kuhakikisha kwamba inapeleka bajeti ya kutosha ili wanafunzi wa Kidato cha Tano na cha Sita Tanzania waweze kupata milo kamili?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza suala la kutenga fedha za kutosha, naomba nikiri kwamba katika mchakato wetu wa bajeti tulivyokuwa tunazungumza hapa, nilitaja miongoni mwa vipaumbele katika bajeti zetu. Vipaumbele vile viliji-reflect katika kila Halmashauri ilitenga nini. Tulikuwa na mpango mkakati mkubwa wa kuhudumia shule kongwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, jambo hili nadhani mchakato wake tulishaupitisha katika suala zima la mchakato wa bajeti. Halikadhalika Mkoa wa Lindi na vipaumbele vyake vimewekwa. Lengo kubwa ni nini? Kwa sababu ilikuwa ni maelekezo na Halmashauri ya Lindi ilishatenga baadhi ya fedha kwa ajili ya ku-facilitate hilo jambo. Lengo kubwa ni fedha zipatikane ziweze kupelekwa ilimradi kazi ile iweze kukamilika vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala la kwamba shule hizi chakula chake, mgao wake hauendi vizuri; naomba niwaambie ndugu zangu, ni kwamba hili kama Serikali tumeliona na ndiyo maana kila wakati sasa hivi tunafanya rejea hata ya viwango vya posho ya kila siku ya chakula. Lengo letu ni kwamba, tufike muda tu-realize kwamba unit cost ya mwanafunzi kwa sasa ni kiasi gani, ili tunapokwenda katika mpango mpana kabisa wa kuhakikisha tunaboresha elimu Tanzania tuboreshe kwa ukubwa wake.
Naomba nikiri wazi kwamba Serikali inafanya kila liwezekanalo sasa hivi ili kutatua na kuongeza kiwango cha Walimu. Najua mpango huu mpana unapouanzisha ni lazima una changamoto yake kubwa. Sasa zile changamoto zinatupa sisi jinsi gani tutafanya tuweze kwenda vizuri zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana nimesema katika majibu yangu ya kwanza katika lile swali lake la kwanza la nyongeza kwamba ukiangalia sasa, zile shule kongwe tunaanza kuzibadilisha, tunakwenda kuziwekea miundombinu, lakini kuangalia ni jinsi gani watoto watakapokuwa katika mazingira ya shule waweze kupata elimu bora. Sambamba na hilo upatikanaji wa elimu bora unatokana na jinsi gani mtoto anapata lishe ya kutosha pale shuleni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Serikali inafanya utaratibu wote wa kina ili mwisho wa siku tuone elimu yetu Tanzania tunaipeleka wapi ilimradi tuweze ku-compete katika nchi nyingine za wenzetu za East Africa.
MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Tatizo la shule hasa Kidato cha Tano na cha Sita ni la Kitaifa na hii inatokana na azma ya Serikali ya kuongeza Shule za Kata ambazo zilianzia Kidato cha Kwanza mpaka cha Nne. Nimeshangaa sana Naibu Waziri alipozugumzia kwamba hizi Shule za Kidato cha Tano na cha Sita ni za Kitaifa lakini hapo hapo anazungumzia habari ya Halmashauri kuendelea kujenga shule hizi. Je, anaweza akatuambia baada ya shule hizi za Kata, kuanzia Kidato cha Kwanza mpaka cha Nne, Serikali imeshajenga shule ngapi za Kidato cha Tano na cha Sita?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mwalimu Suzan Lyimo anafahamu, unapozungumzia Minaki, Tabora, Ilboru, Mzumbe zote ni Shule za Kitaifa hizo. Kwa hiyo, nilikuwa na maana kwamba huo ni msingi wa Shule za Kitaifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile tulielezea, kwa sababu tulikuwa na mchango mkubwa sana katika ujenzi wa shule za Kata na kila Halmashauri ilielekezwa kwa sababu watoto wengi watafaulu katika elimu ya Form Four, lakini idadi yetu ya shule zitakuwa ni chache kuwa-accommodate hao wanafunzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana kila Halmashauri imeelekezwa kufanya kila liwezekanalo miongoni mwa shule zao kubainisha miongoni mwa shule nyingine ziweze kuchukua advanced level, Form Five na Form Six. Hata hivyo, haikatazi, japokuwa wamekuza; mfano Shule ya Mchinga itakapokuwa Form Five na Form Six haitakataza mtoto kutoka Wanging‟ombe kwenda kule Mchinga, maana yake itakuwa ni room hiyo, watu kwenda maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ajenda yetu kubwa ni nini? Ni watu kupata elimu kadri iwezekanavyo. Amesema idadi ya takwimu, hata ukiangalia katika kanuni, nitampa takwimu, idadi halisi ya jinsi gani mchakato umekwenda. Sitaki kukupa jibu ambalo halitakuwa sawasawa hapa.
MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa Sera ya Afya inasema, kila Kijiji kijenge Zahanati na kila Kata ijenge Kituo cha Afya; nakumbuka mwaka 2007 tulikuwa na program ya kujenga sekondari kwa kila Kata na kulikuwa na uhaba mkubwa sana wa watumishi; tulikuwa tunasema ni Vodacom ama Voda faster kwa sababu tu walikuwa wanamaliza Form Six na kwenda kufanya kazi. Je, Serikali imejipangaje ukizingatia hii ni afya kwa ajili ya watumishi watakaoajiriwa kwa vituo ama vijiji 12,000 na kitu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Halmashauri ya Busokelo ni changa sana; tuna Hospitali moja tu, nayo hiyo Hospitali ni CDH kwa maana ya kwamba ni Council Designated Hospital; na tuna Kituo kimoja tu cha Afya. Je, Serikali ipo tayari sasa kushirikiana na wananchi nguvu kazi tunazozifanya ili iweze ku-upgrade Kituo cha Kambasegela, Kituo cha Afya Isange pamoja na Kanyerere?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli sera ya afya ni kwamba kila Kijiji kiwe na Zahanati na kila Kata iwe na Kituo cha Afya. Suala la watumishi ni kweli kuna changamoto, lakini tulivyokuwa katika bajeti yetu ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI), hali kadhalika wiki iliyopita tulikuwa na bajeti ya Wizara ya Afya; na Waziri wa Afya alisema wazi kuhusu mkakati wa kuajiri watumishi takriban 10,000 kwa kipindi hiki ili mradi kwenda kuziba zile gap.
Mheshimiwa Naibu Spika, hili liko katika utaratibu na naamini kwamba, wale watumishi watakapoajiriwa, nimwambie Mheshimiwa Atupele kwamba, tutalipa kipaumbele Jimbo lake ili mradi ile changamoto ambayo inalikabili sasa hivi ya upungufu wa watumishi tuweze kupunguza ile kasi yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, tunahimiza hata vyuo vyetu vile vile kuongeza idadi ya watumishi, ili mwisho wa siku ile needs assessment tukiweza kuifanya, watu waweze kupatikana, basi katika soko, wawepo watu wa kutosha kuwapeleka katika hivi Vituo vya Afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kushirikiana na watu wa Jimboni kwa Mheshimiwa Mbunge, kwanza namsifu sana, kwani ni miongoni wa Wabunge aliyenipa proposal mkononi, kwamba mimi nina proposal yangu ya Sekta ya Afya katika Jimbo langu. Kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na hilo, naomba nikiri wazi kwamba Ofisi ya Rais, (TAMISEMI) itashirikiana naye, kuhakikisha kwamba changamoto zilizoko katika Jimbo hili, tuone tutazifanyaje kwa pamoja. Najua Jimbo hili hata Profesa alikuwa huko zamani. Kwa hiyo, tutashirikiana kwa pamoja kuona jinsi gani tutafanya ili mradi watu wa Jimboni kwake waweze kupata huduma ya afya hususan katika suala zima la kuongeza miundombinu.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa jibu zuri. Swali langu ni kwamba, kuna maeneo ya Wilaya ambayo hata Hospitali za Wilaya hakuna. Je, Serikali inasemaje?
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kufika maeneo kama ya Kilolo, kuja kuona anafanyaje ili kuhakikisha angalau vile Vituo vya Afya na Zahanati ambazo zimeanzishwa na wananchi, kuzipa msukumo ili angalau wapate matibabu na wao wajue kwamba ilani yao wanaitekeleza vizuri?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri kwamba niko tayari na bahati nzuri Mheshimiwa Mwamoto Jimboni kwake wanakuja hapa Ihula karibu kilometa 100. Kwa hiyo, wana changamoto kubwa na matatizo haya tunayafahamu vizuri sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri wazi, Mheshimiwa Mwamoto kwamba tutajitahidi kwa kadiri iwezekanavyo. Tutafika, tukiangalia tutapata jawabu kwa pamoja. Kama kuna Vituo vya Afya ambavyo vime-advance vizuri zaidi, tutaangalia jinsi gani tuvipe nguvu vile Vituo vya Afya, ili mradi wataalam kutoka Wizara ya Afya wakija kukagua, vituo vile viweze kupanda, basi viweze kutoa huduma kwa wananchi kwa hadhi ya Hospitali; kwa kadri itakavyoonekana kama mahitaji ya kuwahamisha kutoka katika Kituo cha Afya, kwenda Hospitali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mwamoto naomba nikiri wazi, nitafika Jimboni kwakE tutabadilishana mawazo na wananchi wakE, lengo ni kuboresha huduma ya afya katika nchi yetu.
MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Matatizo ya ukosefu wa Zahanati na Vituo vya Afya yapo kila sehemu. Jimbo la Pangani ni moja kati ya Majimbo ambayo yana Kituo cha Afya kimoja tu, lakini kituo chenyewe pia hakina wahudumu wa kutosha, hakina vifaa vya kutosha. Je, Serikali ina mpango gani, kuhakikisha Kituo kile cha Afya kinaboreshwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama sikosei amesema Pangani na bahati nzuri nilifika Pangani pale na kuona mahitaji, japokuwa sikwenda katika zoezi la kufanya assessment ya Sekta ya Afya. Bahati nzuri Mbunge wa Pangani ndugu yangu pale alikuwa kila siku ananikorofisha katika hili; na nikijua kwamba watu wa Pangani wana changamoto hii, kwa hiyo, naomba nikiri wazi kwamba, lengo letu kubwa ni kwamba, kwa watu wa Pangani siyo afya peke yake, Jimbo la Pangani ukiangalia lina changamoto kubwa hata ya miundombinu yake ya barabara.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa pamoja mimi nitakwenda na Waheshimiwa Wabunge huko, tutashirikiana kwa pamoja kubaini sasa nini tutafanya kwa pamoja? Kwa sababu jambo hili lazima tushirikiane kwa pamoja, lazima tubaini pamoja, halafu tuweke vipaumbele. Ndiyo maana jana nilimwita mtaalam wangu pale TAMISEMI aniandikie special proposal, lengo langu ni kwamba, mwakani inawezekana tukaja na sura nyingine hasa kutatua tatizo la afya. Nikawaambia waandike proposal maalum tutafanyaje kutatua tatizo la Zahanati na Vituo vya Afya na Hospitali za Wilaya, kama special project ya five years kuangalia tutafanya vipi, tuje na mtazamo mpya.
Mheshimiwa Naibu Spika, tukisema kwamba tunatenga Halmashauri peke yake, lakini centrally kama Ofisi ya Rais (TAMISEMI), tunafanyaje kuhakikisha ili tunakuwa na global program ya kupambana kwenye suala la afya katika Tanzania yetu hii. Kwa hiyo ,Mheshimiwa Mbunge nimelichukua hilo suala, tutapanga kwa pamoja kuona ni jinsi gani tutafanya ili mradi kuboresha maisha ya wananchi.
MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa Serikali ilianzisha mpango huu wa MMAM miaka kadhaa iliyopita na ukizingatia kwamba wanawake wajawazito na watoto ndio waathirika wakubwa; nataka kujua, nini mkakati wa Serikali katika kutoa vifaa tiba kwa akinamama wajawazito na watoto hususan katika suala zima la misoprostol wakati wa PPH? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikifahamu Mheshimiwa Mary Mwanjelwa ni Daktari, kwa hiyo, najua anaguswa sana katika hilo. Vile vile mkakati uliopo, kwanza niseme lazima sisi Watanzania tujipe faraja wenyewe, kwa sababu jana kama wale watu walikuwa wanafuatilia katika mitandao ya kijamii, walimwona Rais Mstaafu Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa katika harakati mbalimbali za watu wanaomtunuku kwamba ameshughulikia suala kubwa sana la vifo vya akinamama na watoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama Watanzania lazima tujivunie kwa kazi kubwa aliyoifanya Rais wetu mstaafu. Harakati za sasa ni nini? Maana yake ni kujielekeza katika kila eneo katika kuboresha Sekta ya Afya. Ndiyo maana hapa nimezungumza mara kadhaa, kwamba sasa hivi tunakwenda kuhakikisha tunatekeleza mradi mkubwa na wenzetu wa kutoka Uholanzi, kuhakikisha mradi karibuni wa shilingi bilioni zipatazo 46. Katika hili maana yake nini? Tutakwenda kufanya mapinduzi makubwa katika Sekta ya Afya, hasa katika Hospitali yetu ya Kanda kuipatia vifaa tiba, lengo kubwa ni kupunguza vifo vya akinamama na watoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mkakati wa Serikali ni huo kwa upana, kushirikisha the own source, kushirikisha income ambazo ziko ndani ya nchi, lakini halikadhalika fursa kutoka maeneo mbalimbali. Lengo kubwa ni kwamba Tanzania iwe ni icon kuhakikisha tunapambana na vifo vya akinamama na watoto katika Bara la Afrika.
MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kweli sijaridhishwa na majibu niliyopewa. Ukikaa ukiangalia, kwa mfano kule Kisorya mpaka Mheshimiwa Waziri Jenista Mhagama alikuja, wale watu walipewa amboni tatu tu na hawana makazi. Naomba Mheshimiwa Waziri husika anielezee kwamba atawasaidiaje wananchi wale, kwa sababu hawana sehemu za kukaa? Pia toka walivyopewa chakula na mazao yote yaliharibiwa: Je, Serikali ina mpango gani kuwasaidia wale wananchi pia kupata chakula?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni kwa nini Serikali inasubiri linapotokea janga, ndiyo wanaanza sasa kutuma wataalam wao kwenda kuwapa wananchi elimu ya mazingira? Kwa nini wasiwe wanatoa kabla? Ahsante, naomba majibu.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kwa mujibu wa taarifa kutoka kwenye Kamati ya Ulinzi na Usalama, kama nilivyoeleza kwamba tumekuwa tukishirikiana nao na kuona namna majanga haya yanapojitokeza na kuweza kuwahudumia wananchi hawa waliopatwa na majanga.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa msisitizo ambao Mheshimiwa Mbunge anasema kwamba hawa wananchi sasa hawana makazi kwa muda mrefu na kwamba hawana chakula; nitafanya ziara kwenda kuona eneo analolizungumzia Mheshimiwa Mbunge ili tuweze kuona namna ya kuwasaidia hawa wananchi ambao wanateseka bila chakula na bila sehemu ya kuishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nijbu hili swali lake analosema kwamba Serikali inasubiri; Serikali hatusubiri, ndiyo maana muda wote, saa zote tumekuwa tukisisitiza wananchi kutokujenga mabondeni, tumekuwa tukisisitiza wananchi kutokujenga kandokando ya mito na tumesisitiza wananchi waliojenga na kuziba mifereji na kusababisha mafuriko kutokufanya hivyo. Kwa hiyo, kila siku tuko katika jambo hili katika kuhakikisha kwamba wananchi hawajengi kwenye mabonde kwenye kingo za mito wala bahari, wala maziwa ili kuepukana na maafa haya.
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile, tumekuwa tukiwaondoa wananchi wanaoishi kwenye mabonde na sehemu hizo. Pia tunaweka msisitizo mkubwa wa kuhakikisha kwamba katika miradi yetu ya kimazingira, maeneo mengine ambayo yanatuama maji tunatengeneza mifereji na tunatengeneza mabwawa ya kuweza kuya-contain hayo maji ili sasa tuweze kuyapunguza mafuriko haya katika namna hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, siyo kweli kwamba Serikali inangojea tatizo litokee, Serikali iko makini na tutaendelea kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha kwamba mambo haya hayajitokezi tena.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya yetu ya Kondoa haina ultra sound na kuna Kata zaidi ya 30, lakini wanawake wanapopata shida, wanaletwa Dodoma Mjini. Kituo cha Afya cha Chamwino lkulu, kiko katika geti la Ikulu pale Chamwino hakina ultra sound, na wanawake wanatoka kilometa 50, 80, 90 wakija Dodoma Mjini,kwa ajili ya matibabu.
Je, Serikali iko tayari sasa kuongea na Bima ya Afya ili tupate mkopo huo wa shilingi milioni 72 kwa haraka?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, Serikali iko tayari kuisaidia Hospitali ya Kondoa, ambayo pia haina kifaa tiba hicho; na wanawake wengi wa Kondoa, wanabebwa kilometa 150 kuja Dodoma Mjini kwa ajili ya ultra sound. Je, wako tayari kuisaidia hospitali hii ya Kondoa wakapata kifaa hicho?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tarehe 24 Februari katika ziara yangu katika Wilaya ya Chamwino niliweza kufika Chamwino soko la Bwigiri na kuangalia ujenzi wa Halmashauri ya Chamwino. Nilipofika pale kweli nilitembelea majengo yote na kuangalia kituo cha afya kile kikoje, na kwakweli na mimi sikuridhika, ndiyo maana nikatoa maelekezo siku ile ile, kwamba kinachotakiwa sasa tuangalie jinsi gani kituo kile kitapata ultra sound. Na bahati mbaya wakati ule bajeti ilikuwa haijaanza, na niliwaelekeza kwamba ikiwezekana waangalie kupitia mfuko wa Bima ya Afya, hali kadhalika katika mpango wao wa bajeti. Lakini kwa bahati mbaya kutokana na ukomo wa bajeti walishindwa kungiza katika bajeti yao.
Mheshimia Naibu Spika, lakini hata hivyo katika maagizo yangu niliyoyatoa nimshukuru sana DMO wa Chamwino na timu yake ya Mkurugenzi kwamba waliweza kufanya utaratibu wa kuwahusisha wenzetu wa NHIF. Na mchakato huu upo mbioni na mimi nina imani kwamba ombi lako Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iko tayari, ni kwamba tulishakuwa tayari ndiyo maana nikaagiza. Kwa hiyo, jukumu letu kubwa ni kuendelea kupambana ili wenzetu wa NHIF waweze kusaidia Kituo cha Afya Chamwino.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala zima la Kondoa; ni kweli kutoka Kondoa mpaka hapa ni mbali; na pale ultra sound hakuna, kama Serikali tumeliona hili. Lakini vilevile naomba nisisitize jambo hili jamani; kwamba mambo haya wakati mwingine yote lazima yaanze katika mchakato wetu wa bajeti. Kama bajeti katika vipaumbele inawezekana hatukuweka ultra sound inaonekana kwamba sisi wenyewe tumedhulumu vityo hivyo. Kwa hiyo, jukumu langu kubwa mimi ni kuwasisitiza ndugu zangu Wabunge, tunapoweka katika mchkato wa bajeti tuangalie kipi kipaumbele cha zaidi? Tupunguze yale mambo mengine ambayo hayana maana tuweke katika sehemu ambayo moja kwa moja tunaenda kumsaidia mama na mtoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kama Serikali tumelisikia hili na kwamba tutawahusisha wenzetu wa NHIF ili kama itawezekana waangalie ni jinsi gani waipe kipaumbele Hospitali ya Kondoa. Mheshimiwa Naibu Spika, natambua kuwa Mheshimiwa Mbunge yuko makini katika hili, najua tutashirikiana na wenzetu wa NHIF. Na siku ile alizungumza pale katika Hospitali yetu ya General, wenzetu watalisikia hili watatupa kipaumbele pale Kondoa.
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Matatizo yaliyopo kwenye Kituo cha Afya cha Chamwino ni sawa sawa na matatizo yaliyopo kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Tarime ambayo inahudumia takribani wananchi zaidi ya 500,000, hawana kifaa cha ultra sound. Ningependa kujua sasa ni lini Serikali itaona kuna umuhimu wa dhati kabisa wa kuleta huduma hii ya kifaa cha ultra sound kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Tarime ili kuondoa hizi adha kwa wananchi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nimemsikia Mheshimiwa Esther, lakini katika jibu langu la msingi alishasikia pale awali. Mimi naamini kwamba ni kweli changamoto hii ni kubwa na ndiyo maana katika mwaka huu ukiangalia katika bajeti yetu ya TAMISEMI, development budget karibuni ni shilingi bilioni 182.5.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hiyo kuna sehemu zingine watu wameweka vipaumbele vya vifaa tiba, wengine wameweka magari ya wagonjwa, wengine wameweka miundombinu kujenga wodi za wazazi. Kwahiyo, japokuwa hii ni changamoto iliyopo pale Tarime naomba vilevile Waheshimiwa Wabunge tutumie fursa zinazowezekana katika mchakato wa bajeti.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto kubwa ni kwamba mchakato wa bajeti wa mwaka huu ulivyokuja Wabunge wengi sana tulikuwa katika vikao vingine vya Kamati, inawezekana hiyo ndio ndo ikawa miongoni mwa changamoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini huko mbeleni tunapokwenda tuangalie jinsi gani tufanye ili michakato ya bajeti itakavyoendelea sisi Wabunge tuwe mbele kuwa main stakeholders katika ile budget process. Hii itasaidia vile vipaumbele ambavyo sisi kama Wabunge wa majimbo tunaona kwamba ni jambo la msingi kuwa katika bajeti yetu viweze kufanyiwa kazi.
Hata hivyo Mheshimiwa Esther Matiko nimelisikia jambo hili, tutawaambia wadau mbalimbali kuona ni jinsi gani wanaweza wakatusaidia. Lengo letu kubwa ni kwamba mwananchi katika kila angle katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aweze kupata huduma bora na mama aweze kunusurika katika suala zima la uzazi.
kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa ukosefu wa vifaa tiba katika Wilaya ya Chamwino ni sawasawa kabisa na ukosefu vifaa tiba uliopo katika Wilaya ya Kasulu. Wilaya ya Kasulu haina ultra sound, lakini mpaka sasa hivi ninavyoongea Wilaya ya Kasulu haina vifaa-tiba vya kupimia sukari (test strips), na hili linasababisha wagonjwa kuweza kupoteza maisha kwa sababu wanapopima vipimo kinakosekana kipimo cha sukari wakati mwingine wanaweza kupoteza maisha kwa sababu wanapima…
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo. Sasa ni lini Serikali itahakikisha inapeleka ultra sound Kasulu lakini sambamba na vifaa vya kupimia sukari? Ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Gezabuke, Mbunge Viti Maaalum kutoka Mkoa wa Kigoma, ambaye amerudi tena baada ya wananchi kumpa ridhaa kama ifauatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Kigoma kuna changamoto hiyo kama alivyosema Mbunge. Lakini jibu langu lile litakuwa vilevile kama jibu la awali. Mkoa wa Kigoma ni Mkoa ambao upo pembezoni zaidi, kwa hiyo hata kufanya ile referral system ni changamoto kubwa sana. Sisi kama Serikali naomba tuseme kwamba eneo la Mkoa wa Kigoma tutalipa kipaumbele maalum katika kipindi hiki na naomba nikwambie kwamba jukumu langu kubwa baada ya Bunge la Bajeti miongoni mwa mikoa ambayo natarajia kuitembelea ni Mkoa wa Kigoma.
Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu kubwa tutakalolifanya ni kuwahimiza watu katika suala zima la ukusanyaji wa mapato.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu kubwa ni kwamba tutakapokusanya mapato vizuri, kama nilivyoelekeza katika maeneo mablimbali, kwamba tukitumia mifumo ya electronic zile collection zetu zitakuwa kubwa, na zitatuwezesha kununua vifaa tiba. Lakini kwa Mkoa wa Kigoma kuwa Mkoa wa pembezoni kama Serikali tutaupa kipaumbele. Mheshimiwa Genzabuke kwa sababu wewe ni mwakilishi wa wakina mama na watoto, naomba nikwambie kwamba tumesikia lakini tutaangalia jinsi ya kufanya ili Kigoma ipewe kipaumbele cha msingi. (Makofi)
MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.
Kwa kuwa Waziri amepotoshwa kwenye jibu (b) sehemu ya kwanza ya swali langu na hivyo kuwapotosha wananchi wa Mji Mdogo wa Mbalizi na pia kulipotosha Bunge; je, Waziri atachukua hatua gani kwa Afisa huyo aliyempotosha?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ndani ya Mji Mdogo wa Mbalizi kuna ardhi ya zaidi ya ekari 5,000 iliyokuwa Tanganyika Packers, na haijaendelezwa kwa zaidi ya miaka 30 sasa na kwa kuwa Halmashauri ya Mbeya imetenga eneo mahsusi kwa kunenepesha mfugo na kwa ajili ya kiwanda cha nyama, je, ni lini Serikali itarudisha ardhi hiyo kwa Halmasahuri ya Mbeya kwa madhumuni ya makazi bora na huduma za jamii? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Sasa naomba nitoe msisitizo katika eneo la kwanza ni kwamba Ofisi ya Rais - TAMISEMI tunapofanya hizi kazi tunahakikisha kwamba coordination inakamilika vizuri. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge kama unaona kwamba kuna mapungufu, naomba u-clarify ni eneo gani ambalo linaonekana halijakuwa sawasawa, ili mimi kama Naibu Waziri, Ofisi ya Rais TAMISEMI nijue kwamba eneo gani ambalo halikukaa vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la opotoshaji limekuwa la jumla, lakini hili tulilielekeza katika ofisi zote za mikoa, kwamba ma-RAS wote wako responsible katika majibu yote yanayojibiwa na TAMISEMI. Kwa hiyo, nilitaka angalau ungenipa ufafanuzi ni eneo gani uliona kwamba lilikuwa na mapungufu tuweze kulifanyia kazi kubwa, kwa sababu lengo kubwa ni kujenga, kwamba ni jinsi gani majibu yawe sawasawa kwa ajili ya kuboresha mahitaji ya wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika eneo la pili…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri amesema hivi swali lake kipengele (b) hakijajibiwa kabisa kwa maana hiyo, kwa sababu umepotoshwa majibu ya kipengele chote.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kuhusu swali la ni lini Serikali itarudisha eneo hili kwa ajili ya wananchi, mimi nilifika pale Mbeya nilipokwenda kutembelea Iyunga lakini nikafika katika Jimbo la Mheshimiwa. Mimi naipongeza Serikali kwa sababu kuna juhudi kubwa imefanyika, sasa pale kuna machinjio ya kisasa kwa ajili ya uchinjaji wa nyama tena wa kisasa katika eneo hilo la Mbeya. Lakini kwamba kuna eneo kubwa sasa eneo hili jinsi gani litafanyiwa kutwaliwa kurudishwa kwa wananchi kwa ajili ya makazi, nadhani sasa jambo hili ni jambo la mchakato, si jambo la kutoa maelekezo tu hapa, nini kifanyike haraka haraka.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu lazima tufanye tathimini ni kitu gani kilichokuwepo hapo, kwa sababu inawezekana ukienda ndani kuna migogoro mingine ya ziada. Kwa hiyo, naomba niseme kwamba hilo ni suala zima la mchakato, naamini kwamba Baraza la Madiwani likikaa litafanya maamuzi litapeleka mapendekezo halafu vyombo husika vitakuja kufanya tathimini. Vitakaporidhika TAMISEMI - Ofisi ya Ardhi tutafanya tathimini ya kinakuona kama eneo hilo linaweza likarudishwa kwa ajili ya maslahi ya wananchi ili wananchi wapate huduma ambayo inahitajika katika maeneo yao.
MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto zilizoko wenye Mji Mdogo wa Mbalizi unafanana kabisa na changamoto zinazopatika kwenye Mji Mdogo wa Namanyere ambao pia ni Makao Makuu ya Wilaya ya Nkasi. Mamlaka hii ya Mji Mdogo wa Namanyere inahudumiwa na Mamlaka Ndogo ya Mji wa Namanyere. Mamlaka hii imeshindwa kuhudumia Mji huu kutokana na kupanuka zaidi kwa Mji wenyewe. Na kwa kuliangalia hilo Halmashauri imeshapitisha katika vikao vyake maombi ya kupata mamlaka ya Mji wa Namanyere. Je, ni lini Serikali itazingatia maombi haya ili kukidhi huduma zinazohitajika sana kwenye Mji huu wa Namanyere? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tumesikia ombi hili. Mheshimiwa Mbunge alifika ofisini kwangu na walinisaidia sana kuandaa database ya kuangalia maombi yote ya Miji Midogo katika Halmashauri zote za Miji mipya na Halmashauri ya Mkoa. Tunachokifanya hivi sasa ni kwamba wataalam katika Ofisi ya Rais - TAMISEMI wataenda katika maeneo mbalimbali; na nilishasema mara kadhaa; baada ya kupata ile database, kujua nani wamefikia hatua gani, waliokidhi vigezo, na ambao hawajakidhi vigezo. Hivi tutavipata hasa baada ya wataalamu kufika site.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Mheshimiwa Mipata, naomba nikuhakikishie kwamba, watu wetu watafika Namanyere, watafika maeneo ya yote Sumbawanga na maeneo yale yote ambako kuna matatizo haya ya wananchi kutaka maeneo yao aidha yawe Miji Midogo, kupata Halmashauri mpya, au kupata Wilaya mpya. Wataalam wakishakamilisha lile zoezi tutakavyoangalia, pale vigezo vitakapokuwa vimefikiwa naamini Ofisi ya Rais - TAMISEMI haitosita kuipa mamlaka hii kuwa Mji Mdogo rasmi.
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kutuangalia sisi kambi mbadala.
Mheshimiwa Naibu Spika, kituo cha afya cha Lupilo ndiyo kama Hospitali ya rufaa katika kata tano za Ilagua, Lupilo, Kichangani na Milola. Je, ni lini serikali itaifanyia ukarabati kituo hiki cha afya maana kina hali mbaya ya majengo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze kwa sababu ni kweli kwamba Mbunge amekuja amejipanga kweli katika Bunge hili na mimi naomba nikuhakikishie, naelewa wazi kwamba ukarabati unaanza pale Baraza la Madiwani linapoweka vipaumbele. Na mimi nilivyopitia katika database wakati wa mchakato wa bajeti ya mwaka huu niligundua kwamba hata eneo lako la Ulanga ni kweli kuna mahitaji, isipokuwa tatizo kubwa lilikuwa katika budget ceiling.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kikubwa zaidi naomba nikuhakikishie, ni kwamba sasa hivi ukiwasiliana na Mkurugenzi wako; kama nilivyosema siku mbili zilizopita hapa; kwamba tumewaagiza wabainishe magofu yote na maeneo yote katika eneo la afya yanayotakiwa kufanyiwa ukarabati ili Ofisi ya Rais - TAMISEMI tuangali tunapeleka wapi nguvu. Katika hilo naamini kwamba eneo lako la Ulanga katika kituo hicho cha afya ni miongoni mwa takwimu ambazo zitakuja tuweze kuzifanyia kazi. Na nikuhakikishie kwamba zitakapofika ofisini kwetu tutapanga mpango mkakati kuweza kukusaidia ili uendelee kuleta heshima katika Jimbo la Ulanga kama ilivyokuwa toka zamani.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na nazidi kumpongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kadri anavyochapa kazi kuhakikisha kwamba anatoa majibu yanayoridhisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, wa kuwa zahanati hizi wananchi walizijenga, Nyang‟hanga, Salongwe, Bundilya, Nsola, Nyamahanga, Nyashigwe, Chabula, Ikengele, Isangijo, Langi na Lutale; na ziko hatua za kukamilisha ili waweze kupata huduma; na kwa kuwa bajeti ya mwaka 2015/2016 inaelekea mwisho; je, Serikali inaweza kutupatia fedha hizi kwa haraka ili tuweze kukamilisha miradi hii na wanachi wapate huduma?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi inasema kila kijiji kiwe na zahanati, na wananchi wetu wamekuwa wakiwahi kutimiza wajibu wao kwa maana ya kujenga maboma haya.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuharakisha utekelezaji wa ilani hii ili wananchi waweze kupata huduma hiyo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuweka kumbukumbu sawa, miongoni mwa maswali mengi niliyoyapata yalikuwa ni maswali kutoka Jimbo la Magu na miongoni mwa ziara yangu ya kwanza katika nafasi yangu Mheshimiwa Rais aliyonipa nilianza Jimbo la Magu kwa Mheshimiwa Kiswaga. Kwa hiyo. nimpongeze sana kwa kazi kubwa anayofanya na katika ziara hiyo niliona miradi mbalimbali ukiwemo mradi wa ujenzi huu wa zahanati. Naomba nikiri wazi, ni kweli fedha hazijaenda. Lakini Serikali kama tulivyosema, kwamba tumejipanga.
Mheshimiwa Naibu Spika, watu wate mnafahamu kwamba mara baada ya uchaguzi miradi mingi ilikuwa imesimama, lakini mchakato mkubwa uliofanyika kuanzia mwezi Januari mpaka tunapozungumza hivi, angalau fedha nyingi zimeenda katika miradi mbalimbali. Wakati napita kwa Mheshimiwa Kiswaga miradi mingi ilikuwa imesimama. Katika kipindi hichi Jimbo la Magu limepatiwa karibuni shilingi bilioni 4.9 baada ya msukumo mkubwa wa Serikali katika miradi mingine ya maendeleo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo najua Serikali itaendelea ku-push kuhakikisha kwamba mambo yanakwenda. Najua katika zahanati fedha hazijaenda, lakini hata zile fedha za maji mlizokuwa mmeomba Serikali imeweza kuzipeleka kule. Hii inamaana kwamba Serikali inawajali watu wa Magu. Kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kufanya juhudi zilezile.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la mpango mpana wa jinsi gani maboma haya yatamaliziwa nimesema hapa mara kadhaa. Ni kwamba ni kweli jukumu letu ni kumalizia maboma. Lakini katika ajenda ya sera ya Serikali na Ilani ya Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi tumejielekeza kwenye vituo vya afya katika kila kata na zahanati katika kila kijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana Waziri wangu mwenye dhamna hapa hata jana alisema mpango wetu mpana sasa hivi ni kuhakikisha angalau kila mwaka katika Halmashauri zote tujenge kituo kimoja cha afya, lakini halikadhalika ujenzi wa zahanati na kumalizia yale maboma. Imani yangu kubwa ni kwamba kwa sababu tuna Halmashauri 181 tukijenga kituo kimoja cha afya, maana yake tulikuwa tumejenga kwa mwaka mmoja vituo vya afya 181, ni mapinduzi makubwa kwa mwaka mmoja peke yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu ndani ya miaka mitano tutafanya mabadiliko makubwa, na mwisho wa siku ni kwamba Sera na Ilani ya Chama cha Mapinduzi itatekelezeka kwa mipango hii tunaifanya pamoja baina ya TAMISEMI, Wizara ya Afya na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Kamati ya Bajeti.
MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze na mimi kuuliza swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimwia Naibu Spika, kwa kuwa changamoto zinazowakabili wananchi wa Jimbo la Magu zinafanana sana na changamoto zinazolikabili Jimbo la Mbogwe, ambapo wananchi katika Kata za Ikunguigazi, Lolangulu, Ikobe na Bukwande wamejenga majengo yao ya maboma kwa ajili ya vituo vya afya lakini nguvu zao zikawa zimepelea. Je, Serikali iko tayari sasa kuwaunga mkono ili kuweza kukamlisha vituo hivyo vya afya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumjibu Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele mjukuu wa Mzee Ulega kuwa tumeliongelea suala la zahanati na tukiwa pale Geita wakati Mheshimiwa Mama Suluhu Hassan alipokuwa akizindua hospitali kubwa ya Geita. Nimesema hapa katika majibu yangu ya msingi, kwamba mambo makubwa tunaenda kuyafanya. Sasa hivi tunafanya tathimini ili tuangalie jinsi ya gani ya kufanya.
Kwa hiyo nikuhakikishie Mheshimiwa Augustino kwamba tutakupa kipaumbele kikubwa zaidi na kwa sababu katika ratiba ambayo nimeitengeneza leo, katika ziara yangu miongoni mwa maeneo nitakayopita Jimbo lako nimeliweka kutokana na kunisukumasukuma sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani tukifika kule tunaweza kuangali hata structure ya majengo yenyewe na kukupa kipaumbe ili wanchi wako wa Jimbo la Mbogwe kupata huduma ya afya.
MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, kwa sababu kazi ya ujenzi wa zahanati ni kazi nyingine, ujenzi wa vituo vya afya ni kazi nyingine, upelekaji wa tiba ni kazi nyingine. Je, Serikali kwa sababu inajua kwamba upo upungufu mkubwa sana wa wataalam katika ngazi zote, imejipanga namna gani kuhakikisha kwamba zahanati na vituo vyote vile vinakuwa na waganga wa kutosha?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, juu ya mpango wa Serikali tumezungumza hapa. Ni kweli tunajenga structures hizi lakini lazima tupeleke vifaa tiba, dawa na wataalam. Hili tumelizungumza na mlikuwa mnajua tulikuwa na mchakato katika suala zima la ajira, lakini kutokana na changamoto ya watumishi hewa, maelekezo yametoka ya kumaliza kufanya analysis ya kuangalia watumishi hewa na baadaye tutaendelea na mchakato wa kupata ajira mpya na vijana wetu watapata kazi katika maeneo ya site.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninamuomba Mheshimiwa Ndassa, tuwe na subira, jambo hili linakwenda vizuri, kwa sababu vijana wanaopakuliwa kutoka vyuoni, utaratibu wa Serikali utakapokaa vizuri sasa watapelekwa maeneo husika baada ya kupata ajira ili wakawapatie wananchi huduma ya afya.
MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyo katika swali la msingi, Wilaya ya Igunga nayo ina zahanati kama Jogohya, Mbutu, Mwazizi na Kalangale ambazo hazijakamilishwa. Je, Serikali nayo itaelekeza jicho lake huko kwenye Wilaya ya Igunga pia?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Dalaly Peter Kafumu kwamba eneo lako pale, mpaka Jimbo la Manonga kwa Mheshimiwa Gulamali kuwa ni miongoni mwa eneo ambayo nimepanga kuyatembelea. Kwa sababu licha ya suala zima la umaliziaji wa zile zahanati, lakini pia kuna vituo vya afya ambavyo vimejengwa ambavyo hata upatikanaji wa vifaa vyake inaonekana kuna uchakachuaji umefanyika. Na ndio maana nimepanga ziara maalum kwa Wilaya yako ya Igunga licha ya kuangalia namna ya kumaliza zile structure, lakini pia kuangalia juu ya habari niliyoipata ya ubadhirifu uliofanyika katika baadhi ya maeneo. Kwa hiyo lazima nifike site kuja kupambana na hayo yaliyotokea.
Mheshimiwa Naibu Spika, na naomba nikuhakikishie kwamba wale wote ambao inaonekana wamefanya ubadhirifu katika majengo ya afya tutawachukulia hatua. Uwe na amani ya kutosha, Serikali iko kwa ajili ya kupambana na mambo ya maendeleo katika nchi yetu.
MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwanza nimpongeze kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia suala la afya kwa Jimbo langu la Busokelo, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, je, ni lini hasa hospitali hii itaanza kujengwa ikizingatia kuwa wananchi wa Jimbo la Busokelo pamoja na Mbunge wao tupo tayari kushirikiana na Serikali kujenga hospitali hii?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, pamoja na kwamba hizi shilingi bilioni mbili ambazo zimetamkwa kwenye jibu la msingi yalikuwa ni maombi maalum, je, Mheshimiwa Naibu Waziri unaweza ukawathibitishia wananchi wa Jimbo la Busokelo kwamba hizi fedha sasa na maombi yao yamekubaliwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, juu ya lini hospitali hii itajengwa, nimesema hapa.
Kwanza mimi naomba niwapongeze hawa Wabunge wote unaowaona humu. Wabunge unaowaona humu jana wamefanya tukio kubwa sana la kupitisha Bajeti ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Bajeti ile sasa inatupa uwezo wa kwenda kutekeleza matatizo ya wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikwambie sisi Mawaziri tutakuwa serious kuhakikisha kuwa hawa Wabunge kutokana na kelele na juhudi kubwa wanayoifanya tunawahudimia kwa nguvu zetu zote. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimueleze Mheshimiwa Mwakibete kwamba kwa sababu pesa imetengwa; na nilikuambia kwamba bajeti ya Serikali hapa imeshapitishwa, na kwamba inafanyiwa kazi; kama swali lako linavyosema fedha hii imetengwa kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya yako. Jukumu letu kubwa sisi sasa ni kuweza kusimamia ili wananchi wako wapate huduma na hatimaye wa- appreciate kwamba wamepata Mbunge kijana wa kuwatumikia. Kwa hiyo ondoa hofu katika hilo.
MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa vile swali la msingi la Busokelo linafanana na la Wilaya yangu mpya ya Itilima. Kwa vile Halmashauri ya Wilaya ya Itilima ishatenga eneo la hekari 40 na tayari mipango yote inaendelea. Je, Serikali iko tayari kusaidia baadaye watakapokamilisha mpango huo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, wameshatenga eneo ekari 40, Serikali inasemaje katika hili? Serikali inachokisema ni kwamba mkimaliza mipango yenu wekeni katika Mpango wa Bajeti ya 2017/2018 kama kipaumbele cha ujenzi wa hospitali. Na ninaomba nikwambie itakapofika katika mchakato huu wa bajeti, kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kwa sababu sera yetu kubwa ni kujenga hospitali kila Halmashauri badala hata ya kujenga Hospitali kila Wilaya. Kwa hiyo kwa huu mpango mkiuanza sisi kazi yetu ni kusukuma tu.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba uondoe hofu, ni kwamba wekeni katika mpango, nia yetu ndani ya miaka mitano watu waone kwamba, Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga kuleta mabadiliko katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, matatizo ya kiafya yanayoikabili Wilaya ya Busokelo yanafanana na Wilaya ya Karagwe, haina Hospitali ya Wilaya, inayo Hospitali Teule ya Nyakahanga inayotoa huduma za tiba kwa Wilaya mbili, Karagwe na Kyerwa. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya ili kuboresha huduma za afya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Karagwe hawana hospitali, lakini naomba niwapongeze kwamba wanafanya juhudi kubwa na ndiyo maana pale tumempeleka kijana mmoja anaitwa Dkt. Sobo, daktari mzuri sana wa upasuaji kama DMO. Ni kweli changamoto hizi, ninapata taarifa kutoka kule kila siku kwamba hakuna Hospitali ya Wilaya. Maeneo haya ni miongoni mwa maeneo tuyoyawekea kipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge kwa sababu tunajua kwamba kule mnatengeneza kikosi kazi cha kuweza kuhudumia maeneo yale, naomba katika bajeti ya mwaka unaokuja sasa wekeni kipaumbele chenu ili tuhakikishe sasa Karagwe badala ya kutumia hospitali ya DDH, tutumie Hospitali zetu za Wilaya kwa kuhakikisha kwamba tunaweka nguvu.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naomba, ikiwezekana kama kuna kituo cha afya ambacho mnatumia pale kipewe nguvu ili baadaye kipandishwe kuwa hata Hospitali ya Wilaya kwa kuanzia linaweza likawa jambo jema. Lakini naomba nikwambie kwamba, Serikali itaunga mkono juhudi zote za wana-Karagwe na watu wa Mkoa wa Kagera.
MHE. AZZA H. HAMAD: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa matatizo ya Busokelo yanafanana kabisa na matatizo yaliyoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Vijijini, na kwa kuwa, wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Vijijini tumeanzisha kwa nguvu zetu wenyewe ujenzi wa Hospitali ya Wilaya toka mwaka 2007, na mapato ya Halmashauri ni kidogo, Halmashauri imekuwa ikijenga kidogo kidogo kwa kushirikiana na wananchi wake, lakini ukamilishaji wa hospitali hii umekuwa ni mgumu.
Je, Serikali iko tayari sasa kuipa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Vijijini ombi maalum la fedha ilizoomba kwa ajili ya ukamilishaji wa hospitali hii?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Azza nakumbuka mwaka 2015 alitaka kushika shilingi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, kuhusiana na suala zima la mambo ya maendeleo katika Mkoa wa Shinyanga. Na nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba mwaka huu ulikuwa na kilio kikubwa sana cha suala zima la ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Shinyanga.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kwamba, Serikali imesikia kilio hiki, tutajitahidi kwa kadiri iwezekanavyo. Lengo kubwa ni kwamba, juhudi unazozifanya kwa wana-Shinyanga, kama Mbunge wao wa Viti Maalum, naomba niseme tutakuunga mkono.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ninakumbuka kuna lile ombi maalum Serikali imesikia hili. Jambo kubwa ni kwamba, tushikamane kwa pamoja tukusanye mapato, Serikali iwe na nguvu, miradi tuliyoipanga na maombi tuliyoyapeleka yote yaweze kufanikiwa.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Azza ondoa hofu, Serikali yako, na mimi mweyewe niseme na Waziri wangu mwenye dhamana, tuko tayari kuhakikisha kwamba Wanashinyanga wanapata huduma bora ya afya katika eneo lao.
MHE. AZZA H. HAMAD: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI kwa majibu yake lakini nitumie fursa hii kumpa pole kwa ajali aliyoipata jana, hakika Mwenyezi Mungu ni muweza wa yote.
Mheshimiwa Spika, sasa naomba nimuulize maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya gharama zake ni kubwa sana na kwa kutegemea bajeti ya Halmashauri inaonesha wazi Hospitali hii haitakamilika kwa wakati. Toka ujenzi huu umeanza ni takribani miaka saba leo na Hospitali haijaanza kufanya kazi. Je, ni lini Serikali itaipa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ombi la fedha maalum kwa ajili ya ukamilishaji wa hospitali hii?
Swali la pili, kwa kuwa Naibu Waziri amefika Shinyanga na akajionea hal halisi ya matatizo ya huduma ya afya na katika Mkoa mzima wa Shinyanga ni Wilaya moja tu ambayo inatoa huduma za Hospitali ya Wilaya, je, ni lini sasa Serikali itahakikisha kwamba inausaidia Mkoa wa Shinyanga na kuhakikisha Hospital ya Wilaya ya Shinyanga na Hospitali ya Wilaya ya Kishapu zinapewa kipaumbele kwa kuanza kutoa huduma kwa majengo yaliyokamilika na kuwapa watumishi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli tarehe 11 mwezi Agosti nilikuwa pale Shinyanga na miongoni mwa ajenda, miradi tuliyotembelea ilikuwa ni miradi ya afya, hospitali yetu ya Mkoa na Hospitali yetu ya Rufaa inaendelea kujengwa.
Mheshimiwa Spika, suala zima la ombi maalum ni kweli, mwaka huu walileta ombi maalum la shilingi bilioni tatu lakini katika mchakato wa bajeti ombi lile maana yake halikupewa kipaumbele, lakini ni imani yangu kwamba kwasababu lengo kubwa la Serikali hii ni kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma ya afya na nilieleza katika vikao vilivyopita kwamba lengo letu ni kwamba kila Halmashauri ipate Hospitali ya Wilaya na kwa sababu Serikali imejielekeza katika ukusanyaji wa mapato; mimi imani yangu ni kwamba wananchi wa Shinyanga itapewa kipaumbele katika mwaka wa fedha ili mradi hospitali hiyo iweze kufanya kazi iweze kukamilika wananchi wa Shinyanga wapate huduma hiyo.
Mheshimiwa Spika, lakini suala la pili lililkuwa ni suala zima la Hospitali ya Shinyanga na Hospitali ya Kishapu ni kama nilivyosema awali, lengo kubwa ni kuboresha huduma ya afya na mimi nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa sababu tulifika pale na tulitembelea maeneo yote mpaka ile Hospitali ya Mkoa ambayo ya Rufaa mmefanya kazi kubwa sana, mmetumia pesa ni chache, lakini miundombinu iliyojengwa pale ni miundombinu nimetembelea ni hali ya juu sana. Mimi naamini Serikali yetu iko mbioni katik ahilo na mimi nalichukua hili kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI lakini Serikali ikijua kwamba jinsi gani tutafanya kuhusu kero za wananchi hasa katika sekta ya afya. Ahsante.
MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa uwiano kati ya walimu na wafunzi limekuwa tatizo sugu, katika shule zetu hasa kwamadarasa ya awali hususani Mkoa wa Rukwa, Serikali ina mkakati gani wa kuweza kukamilisha au kuweka uwiano sana ili kuweka ufanisi wa ufundishaji na uelewa wa watoto wetu?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa walimu hawa walipokuwa wakiwafundisha watoto walikuwa wanatumia mikakati mbalimbali ikiwepo nyimbo, michezo pamoja na kuwapatia uji ili wapende elimu. Toka Serikali imetangaza elimu bure mpaka sasa imetoa kiasi gani kuweza kukidhi mambo hayo ili watotowaendele kupenda shule? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kweli uwiano ni tatizo lakini kilichofanyika ni nini? Mwaka jana tumepeleka walimu katika Chuo chetu cha UDOM, lengo kubwa ni kuhakikisha walimu wale ambao wengine walikuwa hawana zile skills za kufundisha watoto wa awali waweze kupata mafunz hayo na hili hivi sasa limefanyika karibuni nchi nzima na hata jana wakati narudi safari yangu nilikuwa pale Chuo cha Tukuyu ambapo tuna takribani walimu 22,995 ambao tunawaka skills za uchopekaji katika ufundishaji.
Lengo kubwa ni kwamba katika yale mafunzo yale ya uchopekaji maana nadhani lugha ngumu hii, walimu wanaifahamu kwamba integration katika masomo haya kwamba sasa itasaidia katika huu mtaala mpya unaoboreshwa walimu wote watakuwa na mbinu kubwa kuhakikisha kwamba suala zima la ufundishaji watoto wanaomaliza darasa la saba wakijua kusoma na kuandika.
Kwa hiyo katika suala hili lote kwamba ni walimu wangapi ni kwamba tumefundisha walimu takriban 22,000 na sasa hivi katika hii dhana mpya tumefundisha 22,995 tegemeo letu ni kwamba walimu wale wakisharudi shuleni kufundisha walimu wenzao vilevile, lakini katika masomo hayo watu wanaimba nyimbo na mambo mbalimbali ndiyo maana nimesema ni dhana mpya ya uchopekaji ambayo ninaomba sana Waheshimiwa Wabunge muanze kujua dhana hiyo mkienda huko site msishangae mtu anasema sasa naenda kuchopeka darasani, hii ni dhana mpya katika ufundishaji lengo ni watoto waweze kuelewa vizuri.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa Jimbo la Chilonwa na Jimbo la Mpwapwa yanapakana, na kwa kuwa matatizo ya barabara ya Jimbo la Chilonwa ni sawa kabisa na matatizo ya Jimbo la Mpwapwa, Kibakwe na Kongwa.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri utatusaidiaje wananchi wa Jimbo la Mpwapwa kuhusu barabara ya kutoka Lupeta - Bumila - Makutupa kwenda Mbori - Mang‟weta - Mlali mpaka Pandambili. Barabara hii iko chini ya TANROADS, lakini ni muda mrefu sasa haijatengenezwa, pamoja na barabara ya Mkanana – Majami pamoja na Nana. Nakuomba Mheshimiwa Naibu Waziri Serikali itoe tamko kuhusu barabara hii, ni lini itaanza kuzikarabati?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema wiki iliyopita kwamba greda ni la zamani lakini makali yale yale.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii anayosemea Mheshimiwa Mbunge ni kwamba ukitoka huku baada ya kuvuka Kibaigwa unafika sehemu inaitwa Pandambili, unapita ile barabara ambayo ni ndefu sana, inapita Mlali, inapita Cha Mkoroma, inapita Makutupa, katikati inapitia Mang‟weta mpaka unafika pale Mpwapwa Mjini ni barabara ndefu kwa kweli. Kijiografia ni barabara ambayo watu hawa zamani walikuwa wakipitia barabara ya Kibaigwa kuzunguka huku walikuwa na tatizo kubwa sana, kufunguka kwa barabara ile kwa kiwango kikubwa imesaidia sana watu wa eneo hilo. Barabara ile takribani mwezi uliopita niliipita mimi mwenyewe kwa gari yangu, nimeiona na kiufasaha ni kwamba ukiangalia katika vitabu yenyewe imejiainisha katika barabara za TANROADS kwamba ni miongoni mwa barabara zitakazofanyiwa matengenezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu kubwa ni kwamba Mheshimiwa Lubeleje, barabara hiyo itaendelea kutengezwa ili watu wa maeneo yale ambao najua suala zima la uchumi wa eneo lile unakua kutokana na ujenzi wa barabara ile, basi naamini kabisa Serikali kwa sababu imetenga katika bajeti ya mwaka huu wa fedha ukarabati wa barabara ile, ukarabati huo utaendelea kufanyika kama ilivyokusudiwa.
MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kama ilivyo kwenye vijiji vya Msanga, Kawawa na kadhalika katika Jimbo la Chilonwa, ndivyo ilivyo katika Wilaya ya Mkalama kwenye kata ya Msingi pamoja na kata ya Kinyangiri, vijiji vya Ishinsi pamoja na Kidi na Lelembo, vijiji hivi mvua inaponyesha vinakuwa ni kama kisiwa kwa sababu vimezungukwa na mito ambayo haina madaraja, hivyo wagonjwa wanapougua wakibebwa kwenye machela hawawezi kuvuka na matokeo yake wengine wanaweza wakapoteza maisha.
Je, Serikali inasemaje kuhusu kuwawekea madaraja ya kuvuka wakati wote vijiji hivi nilivyovitaja? Ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kwamba kwanza tumelipokea ombi hili, bahati nzuri ni kwamba siku ya tarehe 25 Juni, Mbunge wa Mkalama amenialika kwenda Jimboni kwake kwa ajili ya kukabidhi madawati.
Mheshimiwa Naibu Spika, hii maana yake ninazungumza ni Jumamosi hii inayokuja, nitakapofika kule Mkalama, miongoni mwa maeneo ya kuyatembelea baada ya kuhakikisha tunazindua baadhi ya ile miradi ambayo Mbunge amekusudia ikiwepo madawati na mambo mengine, lakini tutakwenda kutembelea maeneo haya ikiwezekana tuweze kubaini nini kinatakiwa kifanyike ili wananchi wa Jimbo la Mkalama waendelee kupata huduma.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nataka kuuliza swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa Wizara ya TAMISEMI pamoja na Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano ni Wizara ambazo zinashabihiana katika utekelezaji kwenye maeneo ya Wilaya yetu; na kwa kuwa kuna baadhi ya maeneo ambayo hakuna barabara wala hakuna mawasiliano. Kwa mfano, Kata ya Mahenge katika Kijiji cha Ilindi Namagana, Kata ya Ruaha Mbuyuni katika Kijiji cha Ikula na Kata ya Nyanzwa katika Kijiji cha Nyanzwa hakuna mawasiliano, hakuna barabara, sasa Serikali inasemaje kuboresha maeneo hayo ili wale wananchi nao wahisi kwamba wapo Tanzania?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, analozungumzia Mheshimiwa Mwamoto ni jambo la msingi, na kama Serikali naomba niseme kwamba ni haki ya Serikali kusikiliza kwanza, nikijua kwamba ujenzi wa barabara una vipaumbele vyake kutokana na Sera za Barabara.
Mheshimiwa Naibu Spika, watu wengine wanaweza wakashangaa kwa nini barabara kutoka Airport kila wakati inakarabatiwa ni kwa sababu barabara ikiwa bora lazima ikarabatiwe kwanza, lakini barabara ikiwa korofi inawekwa kipaumbele cha mwisho.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ambayo haijafunguliwa maana yake inakuwa kipaumbele cha mwisho kabisa. Kwa hiyo jambo la msingi ukiangalia hata Mfuko wa Barabara maana yake hautoelekeza katika kufungua hizo barabara mpya. Ni lazima tubuni mipango mikakati mingine jinsi gani tutafungua barabara hii.
Mheshimiwa Mwamoto najua kwamba tarehe 18 Julai, nitakuwa Jimboni kwako kutembelea, naomba tufike maeneo hayo tubainishe kwa pamoja. Katika ziara yangu naanzia Mkoa wa Iringa katika Jimbo la Kilolo, tutakaa pamoja kama nilivyokuahidi, tutatembelea kubaini nini tufanye kwa pamoja, ni mkakati gani tutafanya ili wananchi wa maeneo hayo waweze kupata huduma inayokusudiwa, na kwamba wakiri kwamba Mwamoto aliyekuwa DC sasa ni Mheshimiwa Mbunge katika Jimbo la Kilolo anafanyakazi.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipatia muda wa kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa Hospitali ya Haydom inahudumia Mikoa ambayo umeitaja ya Singida, Simiyu, Arusha, Dodoma na Mara; na nashukuru Serikali kwa kutoa fedha na kupanga kiwango hiki cha shilingi milioni 570.
Je, kwa kuwa Serikali sasa imesema haya na hela iliyopelekwa ni kidogo, haioni sasa ni muda wa kuongeza ruzuku hii ili hospitali hii ikaweza kutoa huduma nzuri kwa watu wanaozunguka?
Swali la pili, kwa kuwa tumeleta maombi ya hospitali hii kupandishwa hadhi kuwa hospitali ya Kikanda na kwa kuwa Wabunge wanaozunguka hospitali hii na Mikoa niliyoitaja tumeomba namna hiyo.
Je, ni lini sasa Serikali itajibu maombi haya ya kuipandisha Hospitali ya Haydom kuwa Hospitali ya Kanda?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ya Mheshimiwa Mbunge anasema kwamba hospitali hiyo ikiwezeana iongezewe ruzuku; kwanza naomba niwapongeze watu wote wa Mkoa wa Manyara kuanzia wewe, Mheshimiwa Jitu Soni, Kaka yangu pale, wote mnafanya juhudi kubwa kwa ajili ya Mkoa wenu wa Manyara, lazima niwapongeze. Mara nyingi mmefika katika ofisi yangu suala la kutaka madaktari, kutaka nini, inaonekana mnajali shida za wananchi wenu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na hilo ndiyo maana nimesema Serikali iko katika mchakato wa kuweka mkataba vizuri, kwa sababu hospitali hii sasa hivi huduma kubwa ilikuwa inatokea Kiwilaya, lakini sasa hivi ruzuku ya mishahara zaidi ya shilingi milioni 500 kwa sasa, na zile za madawa zaidi ya shilingi milioni 134, na kwa mwaka huu wa fedha ambao tunaendelea nao, tutawapatia ruzuku ya shilingi milioni 714 mishahara peke yake, vivyo hivyo katika dawa kutoka shilingi milioni 130 tunakwenda mpaka zaidi ya shilingi milioni 300, maana yake tunazungumza suala la shilingi bilioni moja. Hivyo, Serikali imeshaona jinsi gani sasa Hospitali hii ya Haydom inatakiwa ipewe kipaumbele, kwa hiyo tumeshaiweka katika mikakati. Tunachokifanya sasa hivi ni kusubiri suala ule mkataba ufanyiwe vetting utaratibu ukishakamilika basi nadhani suala zima la ruzuku litakwenda vizuri kama linavyokusudiwa Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kupandisha hadhi, naamini kwa sababu suala la kupandisha hadhi ni mchakato mzuri na naamini katika kikao cha RCC nitamaliza hilo lipo katika Ofisi ya Waziri wa Afya, litapitiwa. Mwisho wa siku suala la Hospitali ya Haydom kuwa Hospitali ya Kanda itafanyiwa hivyo. Serikali lengo lake kubwa ni kuboresha maisha ya wananchi wake na hususan kuboresha sekta ya afya. Kwa hiyo, kwa sababu mchakato huu wote ulishakamilika na Wizara ya Afya, mwisho wa siku tutapata majibu halisia kwa ajili ya kuhakikisha wananchi wa Manyara wanapata huduma bora.
MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Kwa kuwa, fedha za own source hazitoshi wakati mwingine kulipa hata posho za Madiwani, ni kwa nini sasa Serikali isione umuhimu wa kupandisha hadhi Kituo cha Afya cha Dongobesh ili kuondoa msururu mkubwa katika Hospitali ya Haydom kwa ajili ya wananchi wa Mbulu Mjini na Mbulu Vijijini?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kupandisha Kituo cha Afya cha Dongobesh sisi hatuna matatizo, provided kwamba vigezo vimefikiwa. Ule mchakato Mheshimiwa Ester ninakuamini kwa sababu umenisaidia sana, hata Mzee pale alinisaidia sana, miongoni mwa watu walioshiriki nilivyokwenda katika Shule ya Kisimani pale katika Jiji la Arusha. Kwa hiyo najua ni mpiganaji na unapambana katika mambo mbalimbali. Na mchakato huu mkimaliza mchakato katika vikao vyenu, katika ule utaratibu wa kawaida, maana kuna hilo, lakini ukienda kwa Mheshimiwa Jitu Soni pale, kituo cha Afya cha Magugu na wao wanaomba ipandishwe ifike katika hadhi inayokusudiwa.
Naomba maombi haya sasa yaende pamoja Wizara ya Afya, yakifika Wizara ya Afya naamini Dada yangu, Mheshimiwa Ummy Mwalimu, kwa sababu anajali sana haki na matatizo ya akina mama na watoto jambo hili ataliangalia kwa jicho la karibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo haya, vituo vya afya vinavyotaka vipandishwe viwe katika hadhi inayokusudiwa au katika zahanati kupandishwa kuwa vituo vya afya, provided kwamba vigezo zimefikiwa Serikali haitoshindwa kufanya hivyo. Kwa hiyo, naomba niwasisitize kwamba vile vikao vya awali vikishakaa lazima mchakato uende kama unavyokusudiwa katika Wizara ya Afya na mwisho wa siku Serikali itafanya maamuzi sahihi kwa ajili ya wananchi wake.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Wilaya ya Mbulu yenye majimbo mawili, tuna vituo vya afya ambavyo havijakamilika takribani vituo vitano. Kwa mfano, Tarafa ya Nambisi ina kituo cha afya ambacho hakina hadhi, Tarafa ya Daudi na Tarafa ya Dongobesh.
Je, ni kwa nini Serikali isichukue hatua za makusudi kukagua vituo vyote vya afya, na kwa kuwa Waheshimiwa Madiwani katika bajeti ya Halmashauri hawawezi kupitisha bajeti ikaenda kwenye kituo kimoja ili Serikali itenge fedha za kutosha kwa kila Halmashauri, kwa kila mwaka walau kuwa na kituo cha afya kitakachotengewa fedha kutoka Hazina, nje ya bajeti ya Halmashauri? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, miongoni mwa hoja muhimu sana ambayo ni muhimu sana imesaidia kuibua mambo mbalimbali, Mheshimiwa Zacharia alikuja pale ofisini, na alizungumzia suala zima la maboma ambayo yapo katika Jimbo lake ambayo hayajakamilika.
Ninakushukuru Mheshimiwa Mbunge, ulivyokuja pale ofisini siku ile na Mheshimiwa Jitu na Mheshimiwa Issaay pamoja, katika suala zima la maboma pia suala zima la watendaji, miongoni mwa hoja ambazo mmenisaidia ni kuweza kuangalia tutafanya vipi sasa tuweze kumaliza maboma.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili nimezungumza wiki iliyopita tumeelekeza Halmashauri zote zibaini yale majengo yote ambayo hayajakamilika, tunayapangia mpango mkakati maalum kama Serikali, nimesema tulikaa katika utatu, Wizara ya Afya, TAMISEMI pamoja na Kamati ya Bunge ya Bajeti kubaini maboma yote na tumeshatoa maelekezo kwa Wakurugenzi wote huo ndiyo mkono wa Serikali sasa, maboma yote yatabainika, lakini tunachotaka kufanya ni angalau kila Halmashauri kwa kila mwaka japo angalau tujenge kituo cha afya kimoja kilichokamilika. Lakini sambamba na hilo, jinsi gani tutafanya kuimarisha zahanati yetu, mwisho wa siku tunakwenda katika utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi kama ulivyokusudia kupeleka huduma kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge, nikwambie kwamba ni mpango wa Serikali na tunaendelea nao na hili litaendelea kufanikiwa ndani ya kipindi chetu cha bajeti ya miaka mitano hii.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Naibu Waziri Mheshimiwa Jafo nilitaka niongezee kidogo juu ya jambo hili la huduma ya afya ya msingi kwa namna ambavyo linaulizwa mara nyingi na imekuwa concern kubwa sana ya Waheshimiwa Wabunge wote.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema wakati tunajumuisha Bajeti ya Serikali juzi, ni kweli kwamba tuna vituo vya afya vichache, tangu tumepata uhuru tumeweza kujenga vituo vya afya vya Serikali takribani 470 tu. Lakini maeneo ya utawala yamekuwa yakiongezeka Wilaya zimeongezeka Halmashauri zimeongezeka, Mikoa imeongezeka na hivyo ni lazima tufanye utafiti, tufanye tathmini ya namna catchment zilivyokaa ili tuweze kuja na mpango mzuri sana ambao utajibu maswali mengi sana ya Waheshimiwa Wabunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hali ilivyo sasa waridhike na Waheshimiwa Wabunge watuamini tunaendelea kufanya mchakato huo wakufanya tathmini tukishirikiana na Wizara ya Afya na kama nilivyosema juzi kwamba tukiamua kwa Halmashauri 181 tulizonazo nchini, tukasema kila mwaka tujenge kituo kimoja, kwa miaka mitatu tutakuwa tumejenga vituo 543, vituo 543 ni zaidi ya vituo tulivyovijenga vya afya toka tupate uhuru ambavyo ni 470.
Kwa hiyo, nasema Waheshimiwa Wabunge hili tunalichukua pamoja na uchache wa fedha kama mnavyosema lakini kwenye mpango huo tunaokubaliana Wizara ya Afya tutakuwa pia tuna-package ya Serikali ya kuhakikisha kwamba tuna-fund siyo tu kwa maana ya ujenzi lakini pia kwa maana ya vifaa tiba, pia na wataalam.
Waheshimiwa Wabunge, hivyo, niwaombe sana tuvumiliane tuende kwa style hiyo ninaamini baada ya miaka mitano mtakuwa na kitu cha kusema kwa wananchi waliowachagua.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Wilaya ya Korogwe ina Halmashauri mbili na Halmashauri ya Mji wa Korogwe haina hospitali, wananchi wake asilimia 60 wanatibiwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya na kusababisha msongamano mkubwa katika hospitali hiyo. Halmashauri ya Mji tuna zahanati ipo Kata ya Majengo ambayo vilevile inalaza akina mama wajawazito wanajifungulia pale.
Je, Serikali sasa kwa maana ya Wizara ya Afya hasa ikizingatiwa kwamba hatuna hospitali itakuwa tayari kutusaidia kujenga jengo la upasuaji ili kusudi wa kina mama wale wajawazito wasiende kule kwenye hospitali ya Magunga ambako kuna msongamano mkubwa?
NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika kumbukumbu zangu kama sikosei na Mama Mary Chatanda atanisahihisha, mwezi wa Machi tulikuwa pamoja kutembelea Hospitali ya Korogwe pale, lakini tulivyoenda pale nilichokishuhudia ni umati mkubwa wa watu waliojaa katika hospitali ile, sikujua kwamba umati ule ni kutokana na congestion kutoka katika hizi Halmashauri mbili.
Nimshukuru Mbunge kwa sababu siku ile tulivyoondoka nimekuta kwa mara ya kwanza mashuka yaliyowekwa katika makabati siku hiyo wametandika katika vitanda, Mbunge alinisaidia sana tukatoa maagizo mazito kuhakikisha kwamba makabati wataalamu suala la shuka ziwekwe katika vitanda siyo watu walalie vitenge vyao. Kwa hiyo Mbunge nikushukuru katika lile. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu wana hiki kituo cha afya naomba niseme wazi umati mkubwa tuliouona pale naomba kwa sababu bajeti ya mwaka huu tumeshaipanga, katika bajeti inayokuja naomba tuweke mkakati wa pamoja katika kikao chetu cha Baraza la Madwani. Tutenge bajeti na Ofisi ya TAMISEMI itasimamia hilo kuhakikisha tunajenga theater ili hiki kituo cha afya tukipandishe tukipandishe hifikie hadhi inayokusudiwa, mwisho wa siku ni kwamba katika hii Korogwe Mji iwe na Hospitali yao inayojitegemea kupunguza umati wa watu katika Hospitali ya Halmashauri ya Korogwe.
MHE. FREEMAN A. MBOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu kuwepo na mabweni katika shule kwa ajili ya kidato cha tano na sita ni jambo muhimu ama sharti muhimu la kupata nafasi ya kuwa na shule ya kidato cha tano na sita, na kwa sababu kazi ya ujenzi wa mabweni katika maeneo mengi imeweza kufanywa na wananchi wenyewe na Serikali ikaongezea nguvu zake; na kwa sababu vilevile sera ya Serikali katika ujenzi wa kidato cha tano na sita ni kupata wananfunzi kutoka maeneo mbalimbali ya nchi ili wachanganyikane, jambo ambalo ni jambo jema.
Serikali haioni kwamba kwa wale wananchi ambao wapo tayari kujenga mabweni ya kidato cha tano na sita; maeneo kama hayo yanapojitokeza wapewe kipaumbele katika kupata nafasi zaidi katika shule hizo? Japo na nafasi nyingine itolewe kwa wananchi katika Mikoa mingine? (Makofi)
NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS TAMISEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli na tunashukuru kwanza wananchi kwa dhati kabisa. Katika maeneo mbalimbali na hata katika pitapita yangu karibuni wananchi wengi sana wameamua ku-invest sana katika suala zima la kuhakikisha kwamba wanaboresha shule zao. Na hili limetusaidia sana kwa sababu shule nyingi katika kipindi hiki cha kati tumeweza kupata shule za kidato cha tano na kidato cha sita lakini nguvu kubwa katika upande wa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na hili naomba nikiri wazi kwamba sisi kama Serikali tutapenda kuweka kipaumbele cha kutosha kabisa jinsi gani tutafanya kuweka nguvu zaidi katika maeneo hayo; lengo kubwa ni kwamba Watanzania hawa na vijana wetu wanaofaulu kidato cha nne waweze kupata fursa. Kwa sababu mwaka huu ukiangalia kuna maeneo mbalimbali tulipata wanafunzi walifaulu zaidi hata ukilinganisha na idadi ya shule tuziokuwa nazo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbowe swali lako ni jambo la msingi na Serikali hii tutaipa jicho la karibu zaidi; lengo kubwa ni kwamba vijana wa Tanzania waweze kupata fursa ya elimu katika nchi yao.
MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kutokana na mwamko ambao umejitokeza hivi sasa kwa watoto wengi kuhudhuria shule kutokana na elimu bure, lakini vilevile kumekuwepo na changamoto mbalimbali yakiwemo pia malalamiko kutoka kwa wananchi.
Je, Serikali inajipanga vipi kuhakikisha kwamba changamato hizi inaziondoa ili watoto wote waweze kupata elimu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, watoto wenye mahitaji maalum bado wao wanakabiliwa na changamoto nyingi; je, Serikali ili kuendana na kasi hii, inajipangaje kuhakikisha watoto wenye ulemavu ambao jamii imekuwa ikiwaficha na wao pia wanapata nafasi ya kupata elimu bure na kuifurahia nchi yao?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika sehemu ya kwanza ni changamoto zinazozikabili shule zetu. Ni kweli mara baada ya mchakato wa Serikali yetu ya Awamu ya Tano, ilipojielekeza kwamba elimu kuanzia shule ya awali mpaka form four kuwa ya bure, tumegundua kuna mambo mengi sana yamejitokeza.
Jambo la kwanza ni kitendo cha watoto wengi waliokuwa wakibaki mitaani kwa kukosa fursa ya kujiunga na shule, hivi sasa wanaende shule. Baada ya hilo kilichotokea ni kwamba tumekuwa na tatizo kubwa la upungufu wa madawati na mambo mbalimbali. Katika hili ndiyo maana Waziri wangu wa Nchi sambamba na Waziri Mkuu walitoa maelekezo kwamba ikifika 30 Juni, madawati yote yawe yameweza kupatikana maeneo ili kuondoa changamoto ya watoto wanaokaa chini. Hata hivyo, Serikali imejielekeza kuhakikisha kwamba tunajitahidi katika ujenzi wa miundombinu ikiwemo madarasa lengo likiwa watoto wote wanaofika shuleni waweze kupata elimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo kuna swali la pili linalohusu watoto wenye ulemavu. Ni kweli mimi mwenyewe nikiri kwamba nimetembelea shule kadhaa za watoto wenye ulemavu, kule Mufindi hali kadhalika pale Dar es Salaam, maeneo hayo nilioyatembelea ni kweli watoto hao wana changamoto mbalimbali, lakini nimeweza kutoa maelekezo mbalimbali kwa Wakurugenzi wa Halmashauri, wahakikishe kwanza watoto hao wenye ulemavu wanapewa kipaumbele. Ndiyo maana katika bajeti yetu ya TAMISEMI mwaka huu tumejielekeza wazi jinsi gani tumejipanga katika suala zima la watu wenye ulemavu ili kwamba watoto wote wanaoenda shuleni kutokana na hali zao wote waweze kupata elimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Amina Mollel, najua kwamba wewe ni mwakilishi halisi na makini sana wa walemavu, tutahakikisha ombi lako hili linafanyiwa kazi katika Serikali hii ya Awamu ya Tano kwa nguvu zote.
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri, ni kwa nini sasa katika yale madarasa ya awali ukiangalia fungu lile la elimu bure wanapotoa ile fedha, wale watoto wa madarasa ya awali hawapati ile fedha na inawafanya wazazi waendelee kuchangia yale madarasa ya awali.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema katika majibu yangu ya msingi, ukija kuangalia maeneo mbalimbali ambapo watoto wale wa awali waliokuwa wakienda shuleni, mara nyingi sana walimu waliokuwa wanafundisha utakukuta ni walimu waliokuwa wanachukuliwa mtaani, waliomaliza form four, darasa la saba ambaye anaweza akafundisha. Katika maelekezo ya utaratibu wetu wa elimu, wale watu wote wanaomaliza grade „A‟ wanakuwa na component ya elimu ya awali. Kwa hiyo, utakuja kuona kwamba, wakati mwingine watoto walikuwa wakienda shule wanalazimishwa walipie fedha kwa ajili ya mwalimu wa awali, jambo lile tumesema kwamba, walimu wote sasa hivi wanaomaliza grade „A‟ walimu wale wanaopelekwa mashuleni, kuna mwalimu anayefundisha darasa la awali.
Mheshimiwa Naibu Spika, maelezo yetu kama Ofisi ya Rais – TAMISEMI, ni kuhakikisha Wakurugenzi, wanahakikisha katika allocation ya wale walimu katika shule mbalimbali, wawapeleke walimu ili kusaidia kuondoa ule utaratibu wa wazazi kuwa wanachanga kwa ajili ya kumchukua mtu mtaani kuja kufundisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, hili tumeenda mbali zaidi, ndiyo maana watu walioshudia mwaka jana hapa katika Chuo chetu cha UDOM, tulipeleke takribani walimu wapatao 17,000 katika somo la KKK. Lengo ni kuwawezesha watoto wanapoingia shuleni kuanzia awali na watoto wa darasa la kwanza waweze kujua kusoma na kuandika.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge ni kweli Serikali tunajua changamoto ni nyingi kutokana na suala la elimu bure, lakini Serikali inaangalia jinsi gani tutatatua matatizo mbalimbali. Mara baada ya kufanya jambo hili tumegundua jambo changamoto nyingi zimeweza kujitokeza, changamoto hizi ni kutokana na hii fursa sasa, Serikali ya Awamu ya Tano iliweza kufungua sasa na kupitia hizi changamoto, ndiyo tunaenda kuhakikisha kwamba tunalijenga Taifa la kupata elimu bora. Changamoto hizi, tutakuwa tunazitatua awamu kwa awamu.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri Jafo, ninataka kuongezea kwenye swali alilokuwa analijibu hivi punde kwamba, isichukuliwe kwamba watoto wanaojiunga kwa darasa la awali ni tofauti na watoto wanaoanzia darasa la kwanza mpaka la saba. Wote ni wanafunzi isipokuwa tu wale wana special treatment, lakini fedha inayopelekwa kwa ajili ya uendeshaji wa shule, ndiyo hiyo itumike katika kuendesha na mahitaji ya wale watoto wa awali.
Mheshimiwa Naibu Spika, ingawa tunafahamu Serikali kwamba mahitaji ya watoto wa awali ni maalum sana. Jitihada kubwa itakayokuwa inafanyika ni kuona namna gani tutaongeza hii bajeti, pia kutafuta facilities kwa ajili ya watoto hawa wa awali kwa sababu namna yao ufundishwaji ni tofauti na hawa wengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii tu kuwaomba Walimu Wakuu wa shule na Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya kuhakikisha kwamba hawatenganishi zionekane kwamba kuna shule ya awali na shule ya msingi inayoanzia darasa la kwanza. Hii shule ni moja na ndiyo maana hata walimu wake ni walewale, kwa sababu wale walimu wanaomaliza grade „A‟ wanakuwa wana component ambayo wamefundhishwa namna ya kufundisha watoto hawa wa madarasa ya awali.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, mara kwa mara umekuwepo usumbufu wa walimu wa awali kupata mishahara yao kwa wakati.
Je, kuna mkakati gani wa kuwapatia mishahara yao kwa wakati?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri Mheshimiwa Waziri hapa amelizungumza punde kwamba walimu wa awali ni walewale ambao wapo katika utaratibu wa walimu walioajiriwa. Kwa hiyo, ina maana kwamba, hatutarajii mshahara wa mwalimu wa awali uchelewe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, walimu wote wanapata mishahara yao katika utaratibu ule wa kawaida sambamba na walimu wengine katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Isipokuwa inawezekana kama nilivyosema awali katika majibu yangu ya msingi ya mwanzo kwamba inawezekana katika maeneo mengine watu walikuwa wanawachukua walimu kutoka mtaani, kutoka katika mfumo usiokuwa rasmi, ambao wazazi walikuwa wanachangia. Kwa sababu jukumu letu kubwa sasa tumepeleka walimu wengi wa grade „A‟, ili sasa waweze kufundisha yale madarasa ya awali kama ilivyokusudiwa kwa sababu wamepewa ile package ya kufundisha watoto wa awali ili mradi matatizo hayo yote Mheshimiwa Ishengoma yatakuwa hayapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimeona, swali lako lilikuwa makini lakini huo ndiyo utaratibu, ambao tunaenda nao. Lengo letu ni kwamba, watoto wetu wapate elimu bora katika shule zetu.
MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza naishukuru sana Serikali kwa kutenga bajeti ya daraja hili la Ruhembe kwenye bajeti ya mwaka 2016/2017. Hata hivyo, kutokana na kilio na mateso makali pamoja na vifo vya watu wa Ruhembe ambao wamekuwa wakilia kwa muda mrefu, Serikali ipo tayari kuleta pesa hizi kule Mikumi katika robo ya kwanza ya mwaka 2016/2017?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nimesema hapa tumetenga shilingi milioni 700 na hii milioni 700 Mheshimiwa Joseph Haule anachosema ni kweli, katika lile daraja tumepoteza watu wengi sana, takribani watu wanane hivi kwa mujibu wa takwimu nilizozipata na mtu mmoja ambaye tumempoteza pale ni mtumishi wa Serikali katika Ofisi yetu ya TAMISEMI.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kwamba, jambo hili sisi wengine tunalifuatilia na tunalijua vizuri sana. Ndiyo maana tumeona katika suala zima la bajeti, mwaka jana waliomba shilingi milioni 600, lakini kilichopitishwa Hazina ilikuwa ni shilingi milioni 300 na ilikuja milioni 100 peke yake. Katika msisitizo mwaka huu tukaona ile milioni 700 lazima irudi katika bajeti kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili linatugusa sana kwa sababu, wananchi pale wakitaka kuvuka kufika ng‟ambo ya pili ni mpaka watembee au wazunguke karibu kilometa 20. Tatizo ni kubwa, ndiyo maana ofisi yetu sasa imefanya harakati za kutosha kuhakikisha tunawasiliana na wenzetu wa TANROAD na hivi sasa nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tunapewa daraja la mudam lile la chuma kupitia ofisi ya TANROAD, si muda mrefu sana angalau liweze kufungwa wakati tukisubiri mpango mrefu kuhakikisha daraja lile linajengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kufanya hivyo sasa angalau tutapunguza kilio cha watu wa eneo lile na imani yangu kubwa ni kwamba, watu wa TANROAD kuanzia wiki hii sasa muda wowote watakwenda kulifunga ili kuondoa tatizo kwa wananchi wa eneo lile.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali ya nyongeza. Kwa kuwa katika kipindi hiki cha mvua barabara nyingi sana zimeharibika, mfano, Wilaya ya Mpwapwa; Kata za Matomondo, Lembule, Mlima, Bereje, Mkanana, Londo, Chamanda, Majami mpaka Nana kule. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari sasa kutenga fungu la kutosha kwa ajili ya ukarabati wa barabara hizo kwa sababu zinapitika kwa shida?
NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAMISEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi na Mheshimiwa Lubeleje hivi karibuni tumekwenda Wilaya ya Mpwapwa pale kutembelea kuangalia baadhi ya huduma zikiwemo huduma za afya, huduma ya shule, takribani wiki mbili na nusu zilizopita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nimeona changamoto ya barabara katika maeneo yale, lakini nimesema katika kila mgawanyo wa halmashauri una fungu lake. Jukumu letu kubwa ni hii bajeti iliyotengwa, ikishapatikana basi iende kuweka miundombinu, kwa sababu utengaji wa bajeti ni jambo moja na utekelezaji wa bajeti ni jambo lingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sasa hivi Ofisi ya Rais, TAMISEMI tutajielekeza kuhakikisha pesa yote iliyotengwa angalau iweze kufika katika maeneo kwa ajili ya kuhakikisha miundombinu inarekebishwa. Kwa hiyo, Mheshimwa Lubeleje kwa sababu na mimi nilifika kule nimeona hali jinsi gani ilivyo naomba tushirikiane kwa pamoja kuangalia kile kitakachowezekana tuweze kukifanya ili mradi wananchi wa Mpwapwa waweze kupata huduma ya miundombinu ya barabara.
MHE. RASHID M. CHUACHUA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali ya nyongeza.
Swali la kwanza, namuomba Mheshimiwa Waziri anipe specific time, kwa sababu wanafunzi hawa hawafundishwi masomo ya sayansi, ni lini mpango wa Serikali wa kuwaajiri walimu hawa utatimizwa?
Swali la pili; naomba Mheshimiwa Naibu Waziri anieleze ni lini Serikali itatenga pesa kwa ajili ya kukamilisha maabara kumi ambazo zipo katika mchakato wa kujengwa na vifaa katika maabara 14 za shule za sekondari? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikiri miongoni mwa matatizo makubwa sana tunayokabiliana nayo ni ukosefu wa walimu wa sayansi katika shule zetu za sekondari. Katika hili, ndiyo maana Serikali tumesema pale wazi kwamba tunachokifanya ni nini, tunajipanga kwa kadri iwezekanavyo, walimu wanavyopatikana baada ya udahili ule, watoto wanapohitimu masomo yao tunawaelekeza katika shule zile za sekondari. Inawezekana mwaka huu tukaja na approach nyingine tofauti, kwa sababu imeonekana maeneo mengine walimu wakipelekwa katika Halmashauri husika, walimu wale wengi wanaishia maeneo ya mijini. Sasa mwaka huu inawezekana tukawapeleka walimu moja kwa moja katika shule husika ili kuondoa tatizo la walimu katika maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, time frame, tulisema hapa kwamba katika michakato yetu ya ajira hapo itakapokamilika, ni kwamba walimu tunatarajia kuwaajiri ambao lengo ni kuweza kuwapeleka, kwa hiyo ni suala zima la utaratibu ambao unaendelea hivi sasa. Ndiyo maana mwaka huu tumejielekeza kwamba ikiwezekana kuna walimu wengine takribani 2,000 ambao tunaona kwamba walikuwa wana uwezo wa kufundisha sayansi, Serikali inaona kwamba itaweza kuwachukua walimu wale kwa mkataba maalum, ili kuwaingiza katika suala zima la ajira kupunguza tatizo kubwa la walimu wetu hawa ambao imekuwa kero sana kwa walimu wa sayansi. Sambamba na hiyo, tunafanya harakati nyingi sana, lengo letu ni kuboresha vijana wetu ili tupate walimu wengi wa sayansi katika maeneo yetu ili watoto waweze kufuzu masomo ya sayansi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la ujenzi wa maabara kukamilika, ndugu zangu nimesema haya juzi tu, tena tumetoka katika mchakato wa bajeti. Nimesema haya mambo kila Halmashauri ina vipaumbele vyake na kila Halmashauri itenge vipaumbele kama tumejenga maabara kuna upungufu wa vifaa, lengo letu iwe ni kutenga vifaa. Naomba niwapongeze kwanza Wabunge wote na viongozi wote, tumesimamia vya kutosha katika ujenzi wa maabara katika Halmashauri zetu. Kwa mara ya kwanza tumefanya mapinduzi makubwa kama nchi ya Tanzania kuhakikisha tumejenga maabara katika kila shule ya Kata, hili ni jambo kubwa tena ni jambo la kujipongeza. Ujenzi huu ni lazima utakumbana na changamoto mbalimbali kama suala la upungufu wa vifaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimuelekeze Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu najua uko makini na asubuhi tulikuwa tunaongea hapa katika suala la Halmashauri yako, kuhakikisha kwamba katika own source inayowezekana hivi sasa, kama kuna baadhi ya vifaa vinavyohitajika ili maabara zile ziweze kufanya kazi, muweze kuzitenga kusaida vijana wetu. Serikali pia vilevile tuko mbioni kuhakikisha kwamba tunaboresha shule zote ziweze kutoa elimu bora kwa wanafunzi wetu hasa elimu ya sayansi.
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Napenda kuuliza swali moja.
Katika hii Mikoa na Wilaya mpya, nyingi zina matatizo ya kutokuwa na shule za kidato cha tano na sita. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuzisaidia hizi Wilaya mpya ikiwepo Busega, ambayo mpaka leo hii hatuna shule ya A-Level? Mheshimiwa Waziri anaweza kunipa mkakati gani wa Serikali kusaidia hizi Wilaya na Mikoa mipya?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba yapo baadhi ya maeneo makubwa hadi Wilaya nzima ambako hakuna shule ya kidato cha tano na sita, lakini nilisema hapa kwamba sekta ya elimu imekuwa decentralized na kwa hiyo maana ya decentralization ni kwamba mipango yote inapangwa kuanzia kule chini na ikiletwa kwetu ni kwa ajili ya kuona tu kwamba tunaipokea na kukubaliana na wadau kama ambavyo tunavyosema kwamba Halmashauri ndizo zinazomiliki shule hizi na kwa kufanya hivyo tunaamini kwamba ndiyo sera ile ya D by D inapokuwa imetekelezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ninamsihi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kama wao wataanzisha jambo hili wakalikamilisha, wakileta kwetu hatuna pingamizi kama watakuwa wameziteua shule watakazodhani zinaweza zikawa ni rahisi kuzifanya ziwe high school.
MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Spika, ahsante. Awali ya yote napenda nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa kauli yake ya kuruhusu wafanyabiashara ndogo ndogo wafanye biashara bila kubughudhiwa. Sasa naomba nijikite katika maswali yangu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza kutokana na majibu ya swali la msingi; naomba Serikali iniambie mama lishe na wafanyabiashara ndogo ndogo wangapi ambao walikamatwa na bidhaa zao zikaharibiwa au kuchukuliwa ambao tayari wamepewa fidia?
Mheshimiwa Spika, pia niambiwe askari mgambo wangapi, kutokana na sheria ambayo ametueleza Mheshimiwa Naibu Waziri, wameshakamatwa, wamehukumiwa au bado wako wanaendelea na kifungo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwanza Mheshimiwa Rais ametoa maelekezo ambayo haya ni lazima yazingatiwe na kila mmoja wetu katika maeneo yetu. Lakini pia kwa mujibu wa sheria hii ni kweli wafanyabisahara ambao wengine kwa kweli ni jambo baya, utakuta mtu amechukua mkopo, ameenda kufanya biashara yake, lakini kwa makusudi mtu mwingine, hata hawa mgambo wanalichukua hizi bidhaa nyingine, waliamua kuchukua na wakazitumia kwa maslahi yao binafsi hata bila kuzi-report katika Halmashauri zetu, hili limekuwa ni tatizo kubwa sana.
Mheshimiwa Spika, sasa hivi siwezi kutoa takwimu ni wangapi waliokamatwa, lakini katika maeneo hayo na maeneo mbalimbali, maana yake nchi nzima hii, tukizungumzia Dar es Salaam, Arusha, Mwanza, Mbeya, hili limejitokeza katika maeneo mbalimbali na hata hivyo maeneo mengine hatua zimeshachuliwa. Kwa mfano ukienda katika Jiji la Arusha kwa rafiki yangu Mheshimiwa Lema, kuna baadhi ya wafanyabiashara ambao bidhaa zao zilichukuliwa na baadhi ya mgambo waliohusika kwenye hilo wameshapelekwa kwenye vyombo vya sheria. Mheshimiwa Spika, na juzi juzi kule Mwanza ambako tukio kama hilo limetokea, na ninashukuru sana dada yangu Angelina Mabula naye alikuwepo kule site, kuna kazi kubwa ambayo imefanyika. Wale wote ambao wameonekana kwamba wamedhulumu mali za watu, kukatakata mapanga mapapai pamoja na matikiti hivi sasa wanachukuliwa hatua zile za kisheria.
Mheshimiwa Spika, na ni kwamba katika eneo la pili ni askari mgambo wangapi ambao hivi sasa wamefikishwa; niseme hili ni suala la kitakwimu. Jukumu letu kubwa ni kusimamia sheria. Wale ambao watakiuka sheria ambazo zimewekwa ni lazima tuwachukulie hatua za kisheria. Lengo kubwa ni kwamba mwananchi wetu aweze kushiriki katika yale mazingira halali yaliyotengwa na Serikali. Ahsante.
MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Nashukuru pia kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na pia nashukuru kwa juhudi za misaada ya UNICEF kwa kuboresha elimu kwenye Halmashauri ya Mbeya na sehemu nyingine za nchi yetu.
Mheshimiwa Spika, pamoja na juhudi hizo, changamoto nyingi, hasa kwa shule za vijijini ni miundombinu. Ukichukulia mfano wa Jimbo langu la Mbeya Vijijini, Shule ya Msingi Ipwizi ya ina walimu wawili na wanafunzi wanaozidi 200; Shule za Iyanga, Shule za Ivwanga hazina hata mwalimu na hizo ziko karibu sana na Jiji la Mbeya.
Mheshimiwa Spika, shule nyingine kama za Kitusi na Ivwanga wanafunzi wanatembea zaidi ya kilometakumi kwenda Mkoa mpya wa Songwe kwa ajili ya kujipatia elimu.
Je, ni kwa nini misaada hii haijalenga kwenye changamoto muhimu za miundombinu katika shule zetu za vijijini? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli hili jambo analolisema Mheshimiwa Mbunge lipo na juzi tarehe tano tulipokuwa katika Mkutano wa Programu ya Walimu ya Mpango wa KKK pale Rungwe miongoni mwa changamoto ambayo niliiona ni kwamba kuna mshiriki mmoja alishindwa kuhudhuria mafunzo yale kwa sababu idadi ya walimu ni chache katika shule yao. Na ndiyo maana juzi tulikubaliana kwamba RAS Mkoa wa Mbeya anaweza kupitia michakato ya mgawanyo wa walimu katika shule zote kwa sababu imebainika kwamba kuna baadhi ya walimu wamelundikwa katika baadhi ya maeneo na maeneo mengine wamekosa walimu.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa hili jambo unalosema sio jambo la uongo.
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwa Mkoa wa Mbeya jambo hilo lipo na RAS Mkoa wa Mbeya Mama yangu Mariam Mtunguja, amelibeba hili na tumekubaliana ndani ya mwezi huu atafanya reallocation vizuri ya walimu katika Mkoa wake wa Mbeya.
Mheshimiwa Spika, lakini suala zima la ajenda ya miundombinu ni kweli naomba tuendelee kushirikiana. Lakini wakati mwingine hii misaada inayotoka kwa wafadhili, inawezekana wao wana malengo yao maalum katika eneo lao.
Mheshimiwa Spika sisi kwanza tunapenda kuwashukuru sana wenzetu wa UNICEF kwa kazi kubwa wanayofanya, na tutajitahidi vile vile kuwashawishi wadau mbalimbali katika baadhi ya misaada, japokuwa itakuwa na capacity building, basi tutatafuta wengine ambao wataweza kutusaidia katika suala zima la infrastructure, jinsi gani tutawekeza miundombinu katika maeneo yetu, lengo kubwa ni kupunguza kero kwa wananchi wetu na hasa watoto wetu wanaotembea umbali mrefu.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, maombi ya kuanzisha Mji huo sasa hivi ni miaka tisa, tangu mwaka 2007. Nataka Mheshimiwa Waziri anihakikishie; ni lini, wataalam wake wa kwenda kuhakiki watafika Muheza?
Swali la pili, Jimbo la Muheza linaweza kuwa ni kubwa kuliko Majimbo yote hapa mjengoni, lina kata 37, vijiji 135, vitongoji 530 unafikiria ni lini Jimbo hilo linaweza kugawiwa? Ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kumbukumbu halali tulizokuwa nazo, ni kwamba kikao cha RCC kilikaa Novemba 2013; na mchakato huu maana yake ulienda kuja katika Ofisi ya Rais, lakini kipindi hicho ikiwa Ofisi ya Waziri Mkuu. Ndiyo maana hapa juzi juzi Waziri wangu mwenye dhamana, Mheshimiwa George Simbachawene, aliwaambia wataalam wetu kuleta analysis ya kila Halmashauri na kila Mkoa. Nadhani wameomba na wanaangalia iko katika status gani?
Mheshimiwa Naibu Spika, katika maeneo haya ya Jimbo lako Mheshimiwa Adadi, ni kwamba wataalamu wetu katika kipindi hiki cha hivi sasa, bajeti wanayoshughulika nayo ni kwamba maeneo ya kipaumbele cha kwanza, itakuwa kuja kwako Muheza lakini hali kadhalika kwenda katika Mji huu wa Mombo ambapo maeneo haya maombi yao yote yameletwa pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Adadi Rajab usiwe na mashaka, hata ndugu yangu hapa Mheshimiwa Profesa Maji Marefu mambo yenu yote yakiwa yako jikoni yanaendelea kufanyiwa vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kugawanya Kata ili Jimbo la Muheza kuwa katika Majimbo mawili, naomba niseme kwamba kwa sababu jambo hili haliko kwetu, TAMISEMI, liko katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi; ambapo ikiona kama inafaa kwa vigezo, basi labda Jimbo hili linawezekana litaweza kugawa kama Majimbo mengine yalivyogawiwa.
Kwa hiyo, nina imani Tume ya Taifa ya Uchaguzi, wataangalia kufanya analysis, kuangalia ukubwa wa Jimbo hili, kwa sababu kuna Kata 37 na vijiji zaidi ya 135 wataangalia kwamba katika uchaguzi ujao, inawezekana saa nyingine wao watakavyoona inatosha, watafanya maamuzi sahihi katika eneo hilo.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, na mimi niulize swali moja dogo tu. Kwa kuwa vijiji vya Chipogolo, Mima, Pwaga, Kibakwe, Berege, Mbori na Chunyu vina idadi ya watu wengi sana, ni trading centers ambazo ni kubwa sana na kuna wafanyabiashara wengi.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, atakubaliana nami kwamba sasa ipo haja kwenda kufanya utafiti kuona kwamba vinaweza kupewa hadhi ya kuwa Miji Midogo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikiri wazi kuwa juzi nilikwenda pale Mpwapwa, katika kuangalia ule mfumo wa maji kama vijana wa sekondari ya Mpwapwa wanapata maji na kuangalia huduma ya afya kama wanatumia mifumo ya electronic katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Wilaya ile ina Majimbo mawili, Jimbo la Kibakwe na Jimbo la Mpwapwa, lakini jiografia yake ni kubwa zaidi; na kwa sababu najua utaratibu wa kuomba maeneo hayo sasa kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo, maana yake mchakato wake unaanza katika ngazi za chini, kuanzia ngazi za vijiji, katika mikutano ya Baraza la Madiwani, halikadhalika katika WDC na Baraza la Madiwani.
Mheshimiwa Naibu Spika, mtakavyoona kuwa hiyo nafasi inatosha, basi nadhani michakato hiyo itaanza na Ofisi ya Rais, TAMISEMI itafanya tathmini kuangalia kwamba, basi kama kuna hadhi ya kuipa mamlaka ya Miji Midogo hatutasita kufanya hivyo. Kuhusu kuangalia kama vile vigezo vitakuwa vimefikiwa.
Kwa hiyo, kwa kushirikiana na Mheshimiwa George Simbachawene ambaye ni Waziri wa Nchi yuko eneo hilo, halikadhalika Mheshimiwa Lubeleje ambaye ni Mbunge wa Mpwapwa aliyeleta concern hii, nadhani tunaweza kufanya mchakato huo, basi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, haitasita ikiona kwamba pale mahitaji yanayotakiwa yaweze kufanyiwa hivyo.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Wilaya ya Kilolo inafanana kabisa na matatizo ambayo yako hapo, na ni katika Majimbo makubwa, takriban lina kilometa za mraba takribani 21,000; na kwa kuzingatia hilo, Serikali iliamua kutoa Mji Mdogo wa Ilula, sasa ni muda mrefu.
Je, haioni sasa ni muda muafaka wa kupewa hadhi ya kuwa Halmashauri kamili?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika kumbukumbu zangu pale kuna barua ya tarehe 2 Juni, 2015 imetoka Kilolo iliyokuwa ikiomba uanzishaji wa Halmashauri hii. Katika maeneo ambayo Ofisi ya Rais, TAMISEMI itaenda kufanya uhakiki, eneo la Kilolo litakuwa mojawapo. Kwa hiyo, tufanye subira katika hilo.
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto ina Majimbo mawili; Mlalo na Lushoto, na tunalo ombi katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI la kupata Halmashauri ya Mlalo.
Je, ni lini sasa Serikali itatupatia Jimbo la Mlalo Halmashauri kamili?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika kumbukumbu zetu, namshukuru Mheshimiwa Mbunge alishawahi kufika mpaka ofisini na katika kufanya rejea katika documents zetu, tumeona kwamba kuna vitu fulani vilikuwa bado havijakidhi vigezo kule Mlalo; na maelekezo tuliyoyatoa ni kwamba, wafanye ule mchakato kuangalia vile vigezo viweze kukamilika, halafu maombi yale yawasilishwe rasmi katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ilimradi eneo hilo sasa wataalam watakapokuja kufanya uhakiki; ikionekana eneo hilo sasa linatosha kuanzisha Halmashauri mpya, basi hakuna shaka, Ofisi ya Rais, TAMISEMI haitosita kufanya hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeshatoa maelekezo katika suala zima la Mlalo na Mheshimiwa Shangazi amekuwa akilifuatilia kwa ukaribu sana suala hili. Sasa naomba nitoe msukumo katika maeneo husika, ule mchakato na vile vigezo mwanzo vilikuwa havijakamilika vizuri, tuweze kuvikamilisha na maombi hayo sasa yawasilishwe katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa ufanisi wa hali ya juu katika maeneo hayo.
MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri na nina maswali mawili ya nyongeza.
Moja, kwa kuwa zoezi hili limeleta malalamiko na kwa kuwa baadhi ya waliochangia utaratibu huu kwenda vibaya na kuandikisha kaya ambazo hazikustahili kupata mgao huu wa TASAF; je, Serikali inawachukulia hatua gani watumishi ambao wamefanya makosa haya na kuwakosesha haki yao ya msingi wale waliostahili kupata mgawanyo huu wa TASAF?
Swali la pili, kwa kuwa baadhi ya walionufaika wanadai kwamba kiasi hiki ni kidogo; je, Serikali haioni kwamba kuna haja ya kuongeza kiasi cha fedha ili kiwanufaishe walengwa? Ahsante.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kutambua kwamba kumetokea udanganyifu kama nilivyosema katika jibu langu la msingi na kwamba takribani kaya 25,446 ni zile ambazo hazikuwa zinakidhi vigezo vilivyoelezwa vya kiwango cha umaskini, lakini wakawekwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tumechukua hatua mbalimbali za kinidhamu hasa kwa watumishi wale ambao ni wa Halmashauri, kwa sababu kwa kiasi kikubwa zoezi hili linafanywa kwa ushirikiano kati ya Wizara hii na Wizara ya TAMISEMI kwa maana ya watumishi wa Halmashauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwa wale viongozi wa kuchaguliwa, tutaona hatua nzuri zinazofaa kwao, kwa sababu udanganyifu huu umefanywa mahali pengine ni kwa makusudi na mahali pengine siyo kwa makusudi, ni kwa kukosa vielelezo vya kutosha juu ya hao wanaotakiwa kunufaika na utaratibu huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kiasi hiki anachodai Mheshimiwa Mbunge kwamba ni kidogo na je, hatuoni haja ya kuongeza? Msingi wa kiwango hiki ni kwamba lengo letu ni kuzisaidia, not permanently kaya hizi maskini ili ziweze ku-gain mahali ambapo sasa zinaweza zikajiendesha zenyewe. Vigezo vinavyotumika kama nilivyosema, kwanza kabisa unaangalia kama familia hiyo ina watoto, lakini cha pili, ni kwamba je, hata kama ina watoto je, watoto hao wanaenda shule au wanaenda kliniki?
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana katika mpango huu, baadhi ya maeneo wameamua kuzisaidia hizi familia kuwalipia CHF yaani Mfuko wa Afya ya Jamii ili waweze kuwa na uhakika wa kupata matibabu. Hili tunalitia moyo sana, kwa sababu moja kati ya vitu vinavyoumiza familia masikini ni kutokupata matibabu stahiki. Sasa hili la shule na lishe ni jambo ambalo tumeweka kama vigezo. Sasa kama haya nia yake ni kuikuza familia itoke pale na ifike mahali ambapo itajitegemea, ikiwa ni pamoja na shughuli nyingine za kiuchumi, basi fedha hizi kwa kiwango tulichopanga, tumezingatia hali ya kutosha kwake na hivyo watajenga uwezo kidogo kidogo na baadaye wataweza kujitegemea.
Mheshimiwa Naibu Spika, natoa wito tu kwa watu wanaonufaika na mpango huu kuwa na dhamira ya kujenga kujitegemea na siyo kuendelea kusaidiwa ili baada ya programu hii kuisha, wawe wameshajenga huo uwezo.
MHE. DANIEL N. NSANZUGWAKO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Naomba niulize swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, muuliza swali msingi wake ulikuwa ni udanganyifu mkubwa uliotokea katika Mkoa wa Kigoma hasa katika Mfuko huu wa TASAF, sasa nilikuwa naomba Waziri anipe comfort hapa kwamba je, haoni kwamba kuna haja ya kufanya uhakiki maalum kwa Mkoa wa Kigoma kama ambavyo Mheshimiwa Sabreena alijielekeza kwenye swali lake?
Mheshimiwa Naibu Spika, udanganyifu kwa Mkoa wa Kigoma ulikuwa ni mkubwa sana katika Wilaya ya Kasulu na Kibondo katika Mfuko huu wa TASAF.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba ni kweli kwamba msingi wa swali ilikuwa hasa ni kujua udanganyifu uliotekea Kigoma; na tunapojibu swali hapa kwa sababu linagusa karibu programu hii ambayo ni ya Wilaya ambapo tumeanza kwa Tanzania Bara karibu Wilaya 151, ni dhahiri kwamba tungepata maswali mengi na ndiyo maana tumekuja na jibu la jumla kwamba yale yaliyotokea Kigoma yametokea pia na maeneo mengine; na udanganyifu umekuwepo na hatua hizo hizo zitakazochukuliwa Kigoma ndizo zitakazochukuliwa na huko sehemu nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa taarifa tu ni kwamba kwa utafiti tuliofanya Kigoma ni kwamba kaya ambazo zinaonekana zimefanyiwa udanganyifu ni takribani kaya 1,020 na hizo tumeshaziondoa kwenye orodha na wale watumishi waliofanya udanganyifu huo wanaendelea kuchukuliwa hatua, lakini pia kuna wale wengine ambao ni wa kuchaguliwa maana unavyojua lile zoezi linashirikisha wale Wenyeviti wa Vijiji pale, Mtaa na nini na nini. Sasa unamkuta Mwenyekiti wa Kijiji au Mwenyekiti wa Kitongoji amemweka mke wake au unamkuta mwingine ni mtumishi, ni mwalimu naye yupo kwenye mpango huu. Hao wote tumewaondoa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kama ni kuchua hatua za kinidhamu dhidi yao pamoja na ile benefit of doubt ya watu kutokufahamu; wengine wamefanya siyo kwa makusudi, lakini kwa wale waliofanya makusudi kusema ukweli hatua zitachukuliwa na kazi hiyo kwa maana ya Mkoa wa Kigoma, tumeifanya vizuri labda tu hapa tuendelee kuchukua hatua ili jambo hili lisijirudie tena. (Makofi)
NAIBU SPIKA: Tunaendelea. Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mheshimiwa Hawa Abdulrahman Ghasia, Mbunge wa Mtwara Vijijini, swali lake litaulizwa na Mheshimiwa Abdallah Chikota.
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali madogo mawili. Kwa kuwa Chama cha Mapinduzi kinaongoza kwa kuwa na utaratibu unaoeleweka na wa kidemokrasia ndani ya chama chake tofauti na baadhi ya vyama ambavyo vimekuwa havina uongozi wa demokrasia iliyoshamiri. Je, Serikali kupitia kwa Msajili wa Vyama anaweka utaratibu gani ili kuhakikisha demokrasia ndani ya vyama inatekelezwa?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa nchi yetu iko kwenye vyama vingi na baadhi ya wanasiasa wanagomea mijadala ndani ya Bunge kitu ambacho ni kuwanyima haki wananchi ambao wamewachagua ili waje kuwawakilisha ndani ya Bunge. Je, Bunge hili linazidi kuchukua hatua gani dhidi ya kitendo hiki cha kutowatendea haki wananchi hawa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza limeulizwa, Serikali kupitia Msajili wa Vyama vya Siasa inahakikisha vipi demokrasia inakuwepo katika vyama vya siasa. Vyama vya siasa vipo kwa mujibu wa sheria ambayo imevianzisha lakini vilevile vyama hivi vinasimamiwa na Msajili wa Vyama ambaye kazi yake kubwa ni kuratibu shughuli zote za vyama na amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba vyama vyote vinatii sheria ambayo imeviunda lakini na Katiba ya nchi ambayo inaelekeza masuala mbalimbali ya kiuongozi katika vyama hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kwa nafasi ya Msajili wa Vyama vya Siasa yeye siku zote ndiye amekuwa mlezi wa vyama hivi na popote pale ambapo kumekuwa kuna shida ya masuala ya kidemokrasia ndani ya vyama amekuwa akichukua hatua stahiki kwa maana ya kukutana na wadau na kuweka mambo sawasawa katika vyama hivi. Kwa hiyo, tunaendelea kuamini kwamba kwa nafasi ya Msajili ataendelea kuvilea vyama hivi na kuhakikisha demokrasia inakuwepo katika vyama vya siasa kama ambavyo vimeanzishwa kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili limeulizwa kwamba kama Serikali tunachukua hatua gani sasa kwa namna ambavyo hali inaendelea hapa Bungeni ambapo baadhi ya wenzetu wanatoka nje na hivyo wananchi kukosa uwakilishi kupitia uongozi wao humu ndani. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari jambo hili lilishatolewa ufafanuzi mara nyingi sana na wewe Naibu Spika ulishatoa maelekezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nisirudie maneno mazuri ambayo umekwishayatoa, lakini msimamo unafahamika kwamba wote tumeingia humu ndani kwa ajili ya kutetea na kuwasilisha maslahi ya watu wetu. Kwa hiyo, ndugu zangu Watanzania wenzetu huko nje wanaona ambao wamebaki kutetea maslahi yao na ambao wametoka.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa kuwa nafasi za Wakuu wa Mikoa na Wakuu Wilaya zipo kisheria na zipo ndani ya Katiba, Serikali inasemaje kwa baadhi ya vyama ambavyo vimekuwa vikiwapuuza, vikiwadharau na kutotii amri zao pale wanapotakiwa kufanya hivyo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Katiba yetu na sheria mbalimbali zimeunda nafasi ya Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya. Katika utaratibu wa Katiba yetu ukisoma katika Ibara ya 64 inaelekeza wazi kabisa kwamba Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya ni wawakilishi wa Serikali katika eneo husika kwa maana ya Rais. Kwa hiyo, wako pale kwa niaba ya Serikali na ndiyo maana kazi yao kubwa ni kuhakikisha wanasimamia na kuelekeza yale matakwa na mambo yote ambayo Serikali imekuwa ikiyataka yafanyike katika maeneo husika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa mujibu wa Sheria ya Utawala wa Mikoa, Sura ya 97, katika kifungu kile cha 14(1)-(3) imeelezea wazi pia kazi ya Wakuu wa Wilaya. Kwa hiyo, niwaombe tu wanasiasa wenzangu ikifika masuala ya utendaji, viongozi hawa wako kwa mujibu wa sheria na Katiba hawajajiweka wenyewe. Kwa hiyo, amri zao, maelekezo yao ni lazima yazingatiwe kwa sababu wako pale kwa niaba ya Mheshimiwa Rais na kwa niaba ya Serikali.
MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniruhusu niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa uwezo wa kifedha wa Halmashauri ya Tabora ni mdogo sana na haiwezi kununua nyumba hizo zote kwa ajili ya mahitaji ya wafanyakazi wake. Je, Serikali inaweza kuidhamini Halmashauri ya Uyui ili iweze kukopa kwa muda mrefu kutoka Shirika la Nyumba?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Halmashauri ya Uyui ni mpya bado na ina changamoto nyingi sana, je, Serikali haioni umuhimu wa kuibeba Halmashauri hii ili iweze kutatua matatizo yake au changamoto ambazo zinaikabili na hasa tatizo hili la nyumba?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Shirika la Nyumba limejenga pale nyumba za kutosha takribani nyumba 49 kama sikosei na katika bajeti ya mwaka huu wameweza kutoa gharama za ujenzi wa nyumba tatu. Suala la kuidhamini, kwa sababu Serikali ikidhamini lazima kuwe na utaratibu wa kurejesha na Mheshimiwa Mbunge alifika ofisini kwangu na timu yake na kwa analysis ya mapato yao ya ndani hata kama wakikopa zile nyumba watahitaji siyo miaka mitatu takribani miaka 10 ili kurejesha mkopo huo, kwa hiyo, hili ni suala la negotiation kati ya Halmashauri na Shirika la nyumba.
Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika la Nyumba lilikuwa linasema kwamba, ni lazima iwe ndani ya miaka mitatu lakini ukiangalia uwezo wa Halmashauri ya Uyui kulipa katika miaka mitatu haiwezekani unless otherwise wakubaliane kulipa ndani ya miaka kumi. Kama wakikubaliana ndani ya miaka kumi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI haitosita kuangalia jinsi gani itafanya ili watumishi wale waweze kupata nyumba. Hata hivyo, lazima Halmashauri hii iangalie jinsi gani itaweza kulipa lakini ndani ya miaka mitatu kwa Uyui hawawezi kulipa lile deni.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala zima la kuibeba Halmashauri hii, naomba niseme wazi, jukumu letu kubwa ni kuhakikisha Halmashauri zote zinafanya kazi vizuri. Japo changamoto ya bajeti ni kubwa lakini tunaendelea na harakati mbalimbali za kukamilisha majengo yaliyokuwepo pale Uyui ili Halmashauri mpya ya Uyui ifike muda sasa isimame vizuri, watumishi wote wapate mazingira rafiki ya kufanya kazi na wananchi wapate huduma.
MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili na mimi niweze kuuliza swali moja dogo la nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa matatizo ya nyumba za watumishi katika Makao Makuu ya Wilaya ya Uyui yanafanana kabisa na yale matatizo ya watumishi wa Wilaya ya Mbogwe na tayari Serikali imeshatoa shilingi milioni 45 kwa ajili ya kujenga nyumba za watumishi lakini nyumba hizo mpaka sasa hivi hazijakamilika. Je, Serikali iko tayari sasa kuongezea pesa ili nyumba za watumishi hao ziweze kukamilika?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala la Mbogwe alilolisema, nadhani wiki iliyopita nilikuwa natoa tathmini ya Halmashauri mbalimbali mpya zilizopatiwa mgao wa shilingi bilioni mbili, milioni mia moja na arobaini kila moja, zingine zilipatiwa kati ya shilingi milioni mia tano mpaka shilingi milioni mia nane na hamsini na katika mchakato ule Mbogwe ipo.
Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu letu kubwa ni nini? Kwa sababu bajeti imeshatengwa, jukumu la Serikali katika mwaka huu wa fedha ni kuhakikisha kwamba tunakusanya mapato ya kutosha kama tunavyofanya sasa ili mradi bajeti tulizozitenga tuweze kuzielekeza maeneo husika ili maeneo hayo ujenzi uweze kufanyika na likiwemo eneo lake la Mbogwe. Kwa hiyo, eneo lake la Mbogwe tumelishalizungumza katika bajeti yetu ya mwaka huu wa fedha.
MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante. Wilaya mpya ya Mkalama pamoja na kwamba ilitengewa fedha kwa ajili ya kujenga Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya hiyo, fedha hizo zimeonekana hazitoshi kwa sababu nyingi zimeenda kulipa tu fidia na hivyo kushindwa kuendelea kujenga ofisi hiyo. Naomba Mheshimiwa Naibu Waziri atuambie wako tayari sasa kuiongezea fedha Halmashauri hiyo ili iondokane na adha ya kupanga majengo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya mpya ya Mkalama katika orodha yangu ya zile Halmashauri nilizozizungumza ni miongoni mwa Halmashauri ambayo imo kwenye orodha. Jukumu letu sisi Wabunge kwa umoja wetu tuhakikishe bajeti ya Serikali inapita na tutaiomba sasa Wizara ya Fedha bajeti tuliyoipanga mwaka huu iweze kupatikana ili Mkalama kama tulivyoipangia bajeti katika mwaka huu iweze kupata fedha, ujenzi uweze kuendelea ile Halmashauri iweze kusimama vizuri. Kwa hiyo, Mkalama ni miongoni mwa Wilaya ambazo tunaenda kuzifanyia kazi katika mwaka huu wa fedha.
MHE. RASHID M. CHUACHUA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo. Swali la kwanza, mwaka 2014 baadhi ya watumishi wa hospitali ya Mkomaindo walifanya ubadhirifu wa shilingi milioni 29 za dawa. Je, Serikali imechukua hatua gani mpaka sasa?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Jimbo la Masasi linakabiliwa na uhaba mkubwa sana wa watumishi wa huduma ya afya takribani watumishi 400. Je, Serikali haioni kwamba suala hili linapaswa kuchukuliwa kuwa ni la dharura ili watumishi hawa wapelekwe haraka iwezekanavyo katika Jimbo la Masasi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri wazi miongoni mwa maeneo ambayo nilitembelea ilikuwa ni Masasi nikiwa na Mbunge huyu na pale nilibaini changamoto kubwa na nilitoa maagizo mbalimbali. Hata hivyo, hivi sasa Ofisi yetu ya Rais, TAMISEMI, inafanya mchakato mpana siyo kuhusu suala la madaktari peke yake au idara ya afya peke yake kwa sababu kuna tatizo kubwa katika maeneo mengi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeunda timu hapa si muda mrefu itakuwa kule site vizuri ili kubaini upungufu wote siyo Masasi Mjini hali kadhalika na Masasi Vijijji. Tuna ripoti inayoonesha kwamba hali ya afya ya pale siyo sawasawa hasa kutokana na baadhi ya Wakuu wa Idara kushindwa kutimiza wajibu wao. Kwa hiyo, naomba nimweleze Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hili tumekuwa serious nalo na tunaenda kulifanyia kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, siku tutakayokuja kuwachukulia hatua baadhi ya watendaji wazembe, tunaomba sana Waheshimiwa Wabunge waache kuleta vi-memo kwamba yule ni ndugu yangu, tutakwenda kuwashughulikia wale wanaoharibu fedha za Serikali na kwa hili tuko serious sana na wala hatuna masihara. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala la watumishi, Waziri wa Afya alishasema hapa mchakato unaendelea. Nimelisema jibu hili mara kadhaa, eneo hili la Masasi nimefika na nimeona mwenyewe Hospitali yetu ya Mkomaindo pale changamoto ni kubwa ikiwa ni pamoja na zahanati zetu, tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo katika watu ambao wanaajiriwa hivi sasa, Masasi itapewa kipaumbele kupunguza tatizo hili kubwa la watumishi katika eneo hilo.
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Jimbo la Mpanda Vijijini ni jimbo ambalo lina kata 16, kati ya hizo tatu tu ndizo ambazo zina vituo vya afya. Napenda kumuuliza swali Naibu Waziri, ni lini itajenga vituo vya afya katika Kata ya Mnyagala, Kasekese, Mpanda Ndogo, Tongwe, Bulamata, Ilangu, Ipwaga na Katuma?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Jimbo la Mheshimiwa Kakoso lina tatizo kubwa sana na ukiangalia ni jimbo ambalo zamani lilikuwa likigawanyika na bahati mbaya resources zao zimekuwa ni changamoto kubwa. Siyo tatizo la zahanati tu lakini hata suala zima la ambulance wana tatizo, hilo nalifahamu vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mchakato wetu hivi sasa na Wabunge ni mashahidi, wafanye reference kutoka katika Halmashauri zao, tumetuma barua kutoka TAMISEMI kuwaelekeza wabainishe changamoto za miundombinu hasa katika zahanati na vituo vya afya na kuwapa maelekezo jinsi Serikali inavyojipanga katika mkakati mpana wa kutatua tatizo la afya hasa katika suala zima la ujenzi wa zahanati.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu kubwa ni kwamba Mkurugenzi wa Jimbo la Mheshimiwa Kakoso na Madiwani watakuwa wanafanya harakati hizo kubainisha ili Serikali iweze kujipanga kwa kuwa na mpango mpana wa kutatua tatizo la ukosefu wa vituo vya afya katika nchi yetu. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Kakoso kwamba sasa hivi yuko Bungeni lakini waraka uko kule na watu wako site hivi sasa kubainisha changamoto hizo kwa ajili ya mpango mpana wa Serikali ili kutatua tatizo hilo.
MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwa kuwa tatizo la Masasi linafanana na Jimbo la Nsimbo na sasa hivi taasisi nyingi za Serikali zina masalia ya fedha, mojawapo ikiwa ni Tume ya Taifa ya Uchaguzi imerudisha shilingi bilioni 12. Je, Serikali ina mpango gani wa hizi fedha zinazobakia katika bajeti hii ya 2015/2016 katika moja ya Majimbo kutuletea kujenga vituo vya afya na zahanati kama Jimbo la Nsimbo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mpango wa Serikali kuhusu pesa zinazobakia, kwanza naomba nimjulishe kwamba hizi pesa kubakia ni kutokana na uongozi mzuri wa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Kwa mara ya kwanza tunaona fedha zinarudishwa Serikalini kutatua matatizo ya wananchi. Naomba nilipongeze na Bunge lako hili kuhakikisha zile pesa zinarudi Serikalini na sisi Wabunge wote tutapata madawati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, siwezi kusema kwamba pesa zilizorudi zitaenda Nsimbo, isipokuwa kwa mtazamo mpana wa Mheshimiwa Rais ataangalia jinsi gani ya kutatua changamoto za wananchi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hasa katika ajenda kubwa ya kubana matumizi na kuwapelekea wananchi huduma ya msingi. Kwa hiyo, nadhani tunaangalia kwa ukubwa wake, lakini Rais ataelekeza vizuri nini cha kufanya katika nchi yetu, kipaumbele ni nini ili wananchi wapate huduma bora.
MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Naomba nimuulize swali dogo tu Mheshimiwa Waziri. Kwa kuwa swali la msingi linafanana sana na Jimbo langu la Manyoni Magharibi ambapo kuna zahanati tatu tu. Je, ni lini Serikali itaanza kujenga vituo vya afya katika Kata za Idodyandole, Aghondi, Sanjaranda, Majengo, Tambuka Reli, Kitaraka, Mgandu, Kalangali, Mwamagembe na Ipande?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu Jimbo la Mheshimiwa Mbunge ni sehemu ambazo zimegawanyika na wana changamoto ya resources lakini suala la ujenzi wa hizi zahanati kama nilivyosema ajenda yetu ileile. Bahati mbaya mwaka huu tulikuwa na mchakato mpana wa vikao vyetu vya Bunge na vikao vya bajeti vya Halmashauri havijaenda vizuri, lakini niwaombe tunapoanza Bunge hili la Awamu ya Tano sisi Wabunge tuwe ndiyo wa kwanza kubainisha vipaumbele vya maeneo yetu na ujenzi huu wa zahanati maana yake unaanzia kwetu sisi, Mbunge unaangalia priority yako iko katika maeneo gani.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu kubwa ni kwamba, michakato ile itakapoanza katika vikao vyetu ikifika Ofisi ya Rais, TAMISEMI, jukumu letu ni kusukuma sasa mambo haya yaweze kwenda vizuri. Najua wazi kwamba Mheshimiwa Mbunge wangu wa Manyoni ni kweli ana changamoto kubwa, lakini namuahidi kwamba mwaka huu ni wa kwanza tulikuwa na changamoto kubwa sana lakini mwaka unaokuja tutakaa pamoja; kama Wabunge tutakuwa katika mikutano yetu katika Halmashauri na sisi Ofisi ya TAMISEMI tutashirikiana vizuri zaidi kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya afya hususani kupata zahanati na vituo vya afya katika maeneo hayo aliyoyaeleza.
MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba niipongeze Serikali kwa kupeleka fedha hizi kwenye shule za bweni zilizoko kwenye Wilaya ya Hanang. Pamoja na hatua hiyo nzuri na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nilikuwa naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Swali la kwanza, kwa kuwa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kwa kushirikiana na Mbunge wao wamefanya kazi kubwa sana ya kujenga shule pamoja na hosteli kwenye shule za Isaka, Baloha, Mwalimu Nyerere, Lunguya pamoja na Busangi. Lakini shule hizi au hosteli hizi hazitambuliki kabisa na Serikali kwa maana ya kutolewa au kupewa msaada wa aina yoyote kama inavyofanyika kwa wenzao wa Hanang. Je, Serikali inaweza sasa ikaziingiza shule hizi kwenye mpango wa kupatiwa huduma ya chakula kama ilivyofanyika kwenye maeneo mengine nchini?
Swali la pili, kwa kuwa tatizo la mabweni kwenye shule nyingi za sekondari za kata ni kubwa sana hasa kwenye shule zilizoko kwenye maeneo ya wafugaji ambao wengi wao wanaishi kwenye maeneo ya pembezoni na yenye mazingira magumu, na kwa kutambua mazingira hayo wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kwa kushirikiana na Mbunge wao wameanza juhudi au wanaendelea na juhudi za kujenga hosteli kwenye shule ambazo bado hazijapata ikiwemo shule za sekondari za Isakajana, shule za sekondari za Ngaya pamoja na zingine.
Je, Serikali inaweza ikachangia namna gani au ikaunga mkono namna gani juhudi hizi nzuri za wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala pamoja na Mbunge wa eneo hilo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Mbunge huyu pamoja na wananchi wake kuhakikisha kwamba wamejenga hosteli katika shule hizo za kata, lengo kubwa ni kuhakikisha kwamba vijana especially wa kike au wanafunzi wa kike waweze kusoma katika mazingira rafiki. Mheshimiwa Maige nakumbuka kwamba tulikuwa pamoja katika gari yangu tukisafiri kutoka Msalala pale Mjini tukaenda mpaka kule Bulyanhulu, kwa hiyo ninalijua vizuri jiografia ya eneo lako. Naomba nikupongeze katika harakati kubwa ulizofanya na wenzako wa kule Msalala.
Mheshimiwa Naibu Spika, ombi lako katika eneo la kwanza ulikuwa unaomba kwamba ikiwezekana shule hizi sasa ziingizwe katika utaratibu mwingine wa Kiserikali sasa vijana wa maeneo haya waweze kupewa chakula.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mchakato wetu mpana tulioufanya na hili nimezungumza katika vipindi tofauti kwamba lengo kubwa lilikuwa kwanza programu ya kwanza ni ujenzi wa shule za kata, lakini suala lingine la pili inaonekana kwamba vijana wengi wanaoenda shule za kata wanapata ushawishi mkubwa sana kurubuniwa katikati tumejikuta kwamba vijana wengi wanapata ujauzito.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeelekeza maeneo mbalimbali kwamba zile shule za Kata zilizojengwa angalau ikiwezekana wazazi waone kama kutakuwa na utaratibu wa ujenzi wa mabweni ili kuweza kuwa- accomodate vijana katika mazingira ya karibu zaidi na shule. Jambo hili naomba nishukuru karibu Tanzania nzima limefanyika kwa upana mkubwa zaidi, lakini kuna shule maalum za bweni ambazo zinatambuliwa na Serikali, lakini kuna zile zingine hosteli zimejengwa na wananchi wenyewe. Tunachokifanya sasa hivi Serikali ni kumebainisha zile shule ambazo ziko katika mkakati wa Kiserikali kama tunavyozijua zile shule za Kitaifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hivi sasa siwezi kuzungumza wazi kwamba kusema kwamba shule zote ambazo mabweni yamejengwa kwamba zitapewa chakula jambo hilo litakuwa ni jambo la uongo. Isipokuwa Serikali tunaangalia jambo hili kwa uzito wake na kufanya tathmini ya kina basi hapo baadaye kama tulivyoenda na programu ya elimu bure katika analysis ya kutosha hapo baadaye kuzibainisha baadhi ya shule tuzi - upgrade ziwe special shule za hosteli jambo hili Serikali hatutosita kuliangalia lakini jambo kubwa hilo tutafanya analysis kwa nchi nzima tutafanyaje kazi kuhakikisha mazingira bora yanatengenezwa kwa vijana wetu wasichana.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika sehemu ya pili ni kwamba kuna baadhi shule zingine bado hazijapata hosteli, naomba nikuunge mkono tena kwamba endelea na juhudi ile ile. Lakini naomba nikuahidi kwamba katika mipango yenu ya Halmashauri ikiwezekana ninavyofanya mchakato wa bajeti za Halmashauri wekeni vipaumbele hivyo na Ofisi ya Rais, TAMISEMI nia yake itakuwa ni kuweza kusukuma juhudi hizi za wananchi ifike muda kwamba shule zote ambazo zina changamoto kubwa tuweze kusaidia zipate mabweni.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema awali lengo kubwa ni kwamba vijana wetu hasa wasichana watakuwa wanakwepa hivi vishawishi ambavyo vimekuwa ni tatizo kubwa sana na likiwagharimu vijana wengi kupata ujauzito.
MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, shule hizi za bweni zimekuwa zikipelekewa fedha shilingi 1,500 kwa siku kwa mwanafunzi. Je, nilitaka kujua ni lini Serikali itaongeza hizi fedha ili shule zetu za bweni zisifungwe mapema na kuchelewa kufunguliwa ili watoto wapate muda mwingi wa kusoma wakiwa shuleni? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, anachozungumzia ni unit cost ya chakula kwa mwanafunzi, na concern hii nadhani Wabunge wengi walikuwa wameelezea kusema na hii rate ya shilingi 1,500 ni ndogo. Unit cost siyo kwa ajili ya chakula peke yake isipokuwa kwa ajili ya mchakato mzima wa elimu, jambo hili watalamu wetu sasa hivi wanalifanyia kazi pale litakapokamilika tutaangalia ni jinsi gani kama kuna uwezekano kupandisha gharama hii kidogo ili mtoto apate lishe ya kutosha ya kuweza kumfanikisha aweze kupata masomo vizuri. Kwa sababu tunajua kwamba suala la lishe ni jambo la msingi sana kujenga akili ya mtoto.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge ni kwamba jambo hili tunalifanyia kazi sasa hivi kuangalia unit cost kwa shilingi 1,500 ni kweli tutafanyaje sasa na iende mpaka kiasi gani kwa kuangalia uwezo wa Serikali kwa muda muafaka.
MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi hii.
Kwa kuwa, Wilaya ya Hanang ni Wilaya ya wafugaji, na wananchi wamejitahidi sana kujenga hosteli kama ya shule ya Mreru, Mulbadau, Endasak na kwa kufuatia suala hilo; je, Serikali ipo tayari kusaidiana na wananchi, kuona kwamba zile hosteli na mabweni yaliyokuwepo toka wakati wa uhuru, tunaimarisha na kuboresha miundombinu ambayo ipo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge senior katika Bunge hili amesema jinsi gani Serikali itaboresha hizi shule, ni kweli shule ambazo zimejengwa muda mrefu lazima tuangalie ni jinsi gani tutaboresha miundombinu.
Mheshimiwa Naibu Spika, juzi nilikuwa katika Chuo cha Kigurunyembe, nimepitia shule mbalimbali. Kuna baadhi ya shule zamani zilikuwa zinafanya vizuri zaidi, lakini kutokana na uchakavu wa miundombinu ufanisi wake umekuwa chini sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilipotembelea shule ya Iyunga kule Mbeya ambayo bweni lake liliungua, nilivyoangalia nikaona ni kwa nini sasa shule nyingi ambazo zamani zilikuwa ni shule za vipaji lakini sasa hivi uwezo wake umekuwa chini, bunsen banner iliyokuwa inatumika mwaka 1980, ndiyo inayotumika mpaka mwaka 2017; jambo hili haliwezekani.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba nikuhakikishie kwamba, jukumu letu kubwa ikiwezekana katika Halmashauri tubainishe katika vipaumbele kwa sababu tumekuwa na tatizo kubwa sana la kufanya ukarabati katika shule zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuungane kwa pamoja, tubainishe shule zilizochakaa katika mipango yetu ya Halmashauri katika bajeti tuliweke hili mapema, Ofisi ya Rais TAMISEMI itaweka nguvu kuhakikisha kwamba shule hizi sasa zinakuwa na ubora ili wanafunzi waweze kupata taaluma inayokusudiwa na shule zetu za Serikali ziwe shindani sawa na shule nyingine za private katika Jamhuri wa Muungano wa Tanzania..
MHE. COSATO D. CHUMI: Nashukuru Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuniona, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, na mimi naomba kuuliza swali dogo la nyongeza, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mafinga Mjini.
Katika Jimbo la Mafinga Mjini tuna shule mbili za sekondari za bweni, mojawapo ni shule ya sekondari ya bweni ya Changarawe. Katika kutekeleza majukumu kama wananchi, bodi ya shule kwa kushirikiana na wazazi imeanza na inaendeleza jitihada za kujenga jiko la kudumu na bwalo la chakula kwa ajili ya wanafunzi hao. (Makofi)
Je, Serikali kwa kilio changu kile kwamba hii ni Halmashauri mpya ipo tayari kwa kutuongezea nguvu ili kukamilisha jiko hilo la kudumu na bwalo la chakula kwa ajili ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Changarawe?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anasema ujenzi wa bweni pamoja na jiko katika Shule ya Sekondari ya Changarawe, naomba niseme kwamba nimelisikia hili jambo, Mheshimiwa Cosato Chumi tumezungumza mambo mengi, ukiachia miradi yake ya maji iliyokuwa imekwama amepambana, na hili naomba niseme kwa sababu hapa siwezi kusema kuna bajeti special kwa ajili ya bweni hili, lakini katika mchakato wetu, kama tulivyoahidiana kwamba mara baada ya Bunge tutapitia, nitakwenda kukagua Shule ya Sekondari ya Iyunga ambayo ujenzi wa mabweni unaendelea, tutapita kuangalia kwa pamoja, mikakati gani tuifanye ili bweni likikamilika na jiko likikamilika, watoto watakula na kuishi sehemu rafiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali hatuoni tatizo katika eneo hilo, lakini ni lazima tushirikishane kwa pamoja tuangalie ni mkakati gani wa haraka utaweza kusaidia katika eneo hili la Shule ya Sekondari ya Changarawe. Mheshimiwa Mbunge, naomba niseme kwamba jambo hili nimelipokea tutakapokuwa pale field tutapanga mikakati ya pamoja lengo ni kuwasaidia vijana wetu.
MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kwa kuwa asilimia kumi iliyopo sasa hivi imepitwa na wakati, na wanawake na vijana wanakuwa kwenye makundi ya watu watano, watano, wanagawana hiyo asilimia 10 wanagawana shilingi laki moja, pesa ambayo haiwezi kukidhi matakwa ya mahitaji yao. Je, serikali ina mpango gani wa kuongeza asilimia kumi iliyoko sasa hivi? (Makofi)
Swali la pili, kwa kuwa asilimia kumi iliyoko sasa hivi haitoki kwa wakati na wakati mwingine inasubiri matukio muhimu kama vile Mwenge. Je, ni lini Serikali itafanya sasa asilimia hii itoke kwa wakati?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Bupe, kwa sababu nimeona akiguswa sana na kinamama na vijana katika maeneo yake. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge hiyo ni credit kwako, kwa sababu naona unawatumikia wananchi wako wa Mkoa wa Rukwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema awali asilimia kumi ni mgao katika mapato ya ndani, na asilimia kumi hii inatofautiana kutoka Halmashauri moja na kwenda Halmashauri nyingine. Kwa mfano, Halmashauri ambayo collection yake kwa mwezi ni shilingi milioni 200, unapozungumzia asilimia kumi maana yake unazungumzia shilingi milioni 20. Lakini tujue kwamba kiwamba kiwango hiki ni (own source) mapato ya ndani ya Halmashauri, na katika yale mapato ya ndani kuna mgawanyiko wa aina mbalimbali kutoka mapato ya ndani, kuna mingine kutoka miradi ya maendeleo, kuna vitu mbalimbali. Kwa hiyo, hii asilimia kumi kiundani ni asilimia yenye kutosha kabisa katika mchakato wa own source, kwa sababu ile pesa ya ndani bado kuna mahitaji mengine ya miradi ya maendeleo inatakiwa ifanyike katika Halmashauri.
Kwa hiyo, hii asilimia kumi siyo ndogo, isipokuwa lengo kubwa ni kila Halmashauri iweze kujipanga ikusanye mapato ya kutosha kutoka katika vyanzo vya ndani. Kuna Halmashauri zingine kwa mwezi wanakusanya shilingi milioni 500, asilimia kumi ni shilingi milioni 50; ni imani yangu kubwa kama kila Halmashauri imejipanga vizuri wanapofanya collection zao mfano hata shilingi milioni100, asilimia kumi yake ni shilingi milioni kumi, wakiamua kuzigawa zile vizuri, wakipanga mpango mkakati vizuri, zitawasaidia kina mama na vijana katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo letu kubwa lilikuwa pesa tulizozipanga katika own source ten percent ilikuwa haiendi kwa akina mama na vijana, na ndiyo maana katika Kikao cha Bunge kilichopita nilisema kwamba kipindi kilichopita own source peke yake ambazo hazikupelekwa kwa kina mama na vijana zaidi ya shilingi bilioni 39; maana yake ni kwamba Madiwani na sisi tulivyokuwa katika Kamati ya Fedha hatukutimiza wajibu…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, tafadhali naomba ufupishe majibu, tafadhali! (Makofi/Kicheko)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka angalau kidogo tuelezane hili, suala la asilimia kumi halitoki, nilikuwa nakuja asilimia kumi kutoka maana yake ni maamuzi ya wenyewe Wabunge na Madiwani, ndiyo tunakaa katika Kamati ya Fedha tunapanga kwamba asilimia kumi zitoke. Ina maana sisi tukishindwa kutimiza wajibu wetu, zitakuwa bado haziwafikii vijana, kwa sababu ten percent inafanywa katika Kamati ya Fedha ya Halmashauri husika.
MHE. SUKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ifahamike kwamba pesa hizi zinatengwa kwa ajili ya kusaidia vikundi vya wanawake na vijana na hasa wale wanaojiunga kupitia makundi mbalimbali. Kwa bahati nzuri nimekuwa Diwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru vipindi vinne. Pesa hizi hata kama zikitengwa katika Halmashauri nyingi nchini, kunapojitokeza jambo la dharura kwenye Halmashauri, pesa hizi zimekuwa zikitumika.
Mheshimiwa Naibu Spika, niiombe sasa Serikali itoe tamko kupitia Halmashauri zetu nchini, kunapojitokeza Halmashauri imekiuka utaratibu wa kutekeleza pesa hizi kuwafikia akina mama ni hatu gani sasa zitachukuliwa kwa Halmashauri ambazo zitashindwa kutekeleza? Ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naomba kiufupi tu niseme ifuatavyo; sasa hivi ni marufuku kwa Halmashauri yoyote asilimia kumi iliyotengwa kutowafikia vijana na kina mama na ninasema hivi sitanii.
Katika bajeti ya mwaka huu kila Halmashauri imepitishwa bajeti yake mara baada ya kutenga ile asilimia kumi; kwa hiyo Mkurugenzi yeyote na Kamati ya Fedha watakaposhindwa kutimiza wajibu huu wa Serikali, tutahakikisha Halmashauri yao tutaiwajibisha kwa sababu imeshindwa kutimiza matakwa halisi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo tumepitisha katika bajeti ya mwaka huu wa fedha.
MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na mazingira ya baadhi ya Halmashauri kuwa upya na changa kama ilivyo Halmashauri ya Mji wa Kondoa, vyanzo vya mapato ya ndani, huwa ni vidogo sana na hafifu; je, Serikali haioni umuhimu kupitia Wizara zake husika zenye dhamana kwa vijana na akina mama kuweka walau ruzuku fulani kufikia ukomo ili iweze kukidhi mahitaji ya vijana na akina mama?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tumesema kwanza hii asilimia kumi siyo peke yake ndiyo inayowagusa vijana, katika Ofisi ya Waziri Mkuu, kuna Mfuko wa Uwezeshaji wa Vijana, kwa hiyo, tunachokifanya na lengo mi kwamba vijana na kina mama weweze kupata fursa kutoka maeneo mbalimbali, ninajua Halmashauri nyingine ni changa kama ulivyosema Mheshimiwa kwenye Wilaya yako ya Kondoa, Serikali imejipanga ukiacha own souce ya ten percent, kuna Mfuko wa Vijana kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, hali kadhalika kwa mujibu wa Serikali ya Chama cha Mapinduzi, katika Ilani yake imezungumza kwamba kutakuwa na mgao wa shilingi milioni 50, lengo kubwa ni kwenda kusukuma nguvu zile za vijana na kina mama katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya shughuli za uchumi.
Kwa hiyo, nadhani kwamba mpango wa Serikali utaendelea kuboresha ili vijana na akina mama waweze kupata nguvu za kujenga uchumi katika nchi yao.
MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali moja tu dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninaipongeza sana Serikali kwa kutenga asilimia kumi kwa ajili ya wanawake na vijana. Serikali sasa hivi haioni kwamba kuna umuhimu kuhakikisha inawashirikisha Wabunge wa Viti Maalum katika Halmashauri zetu, kwa kuzingatia kwamba mara nyingi pesa hizi haziwafikii walengwa. Washirikishwe kisheria na ikiwezekana washirikiane na Maofisa Maendeleo wa Miji pamoja na Kamati ya Fedha, naomba Serikali itoe tamko. Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani tukifanya reference wiki hii nilijibu swali hili siku ya Jumatatu, ushiriki wa Wabunge wa Viti Maalum katika Kamati ya Fedha, na nilizungumza kwa upana kwa ku-qoute sheria na vifungu vya kanuni. Nilitoa mifano mbalimbali katika maeneo hayo nikasema wadau watakaa wataona kama inafaa basi tuboreshe sheria zetu na kanuni zetu, hili jambo nililiongelea juzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine kwa sababu nimejua kwamba Mheshimwa Waziri wangu wa Afya alitaka ku-top up katika eneo hilo nadhani aongezee katika kipande hicho.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nataka tu kuongeza majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba sambamba na Halmashauri kutakiwa kutenga asilimia tano kwa ajili ya Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake; Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, imetenga shilingi bilioni moja katika bajeti ya 2016/2017 kwa ajili pia ya kuwakopesha wanawake. Kwa hiyo, fedha hizi tutazipeleka katika zile Halmashauri ambazo kwanza zimefanya vizuri, kwa hiyo kigezo ni Halmashauri kutenga za kwako, halafu Wizara yangu itaongeza zaidi ya zile ambazo zimetengwa na Halmashauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, kupitia Benki ya Wanawake Wizara pia imetenga shilingi milioni 900 ambazo tutazikopesha kwa wanawake wajasiriamali katika Halmashauri mbalimbali nchini
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Tukiachana na hayo ya huko Ndembela, naomba sasa maswali ya nyongeza nielekeze Njombe kwa maana hii nafasi ni fursa kwangu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imesema kwamba, Shule zote za Kata ambazo zinakidhi vigezo vya kuwa shule za bweni iko tayari kuzichukua na kuzifanya kuwa shule za bweni. Je, baada ya kuzichukua hizi shule kuwa za bweni zitakuwa zinachukua wanafunzi kutoka ndani ya eneo la kata kama ilivyo sasa ama zitachukua kama shule za Kitaifa? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, Serikali iko tayari kutuma wakaguzi kwenda kukagua Shule ya Sekondari Uwemba na Shule ya Sekondari Matola zilizoko ndani ya Jimbo la Njombe Mjini ili ziweze kuwa shule za Kitaifa na kupata hiyo keki ya Taifa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika harakati za ujenzi wa miundombinu ya shule za sekondari toka ilipoanza Awamu ya Nne changamoto kubwa ilikuwa ni suala zima la kuwasaidia vijana jinsi gani waweze kufikia elimu ya sekondari. Mchakato huu umefanyika kwa jitihada kubwa sana ndiyo maana tunaona shule nyingi za sekondari za kata zimejengwa. Baada hapo, tumekuja kugundua kuna changamoto kwamba vijana wa sekondari za kata wanakosa kwenda Form Five and Six kwa kuwa idadi kubwa ya wanafunzi wanafaulu lakini nafasi ni chache. Sasa tumetoa maelekezo kwamba shule hizi sasa zipanue wigo na kuzifanya sekondari hizi kuwa na mabweni ili baadaye ziwe na Form Five na Form Six.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali lake specific lilikuwa linasema ni jinsi gani zile shule za sekondari za kata zilizokuwa na mabweni zitahuishwa rasmi ili ziwe sekondari za bweni za kitaifa. Naomba nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa shule ambazo zitakidhi vigezo zitajadiliwa katika vikao husika vya Halmashauri na kupelekwa Wizara ya Elimu. Wizara ya Elimu itafanya tathmini ya kina ili kuona kama shule husika ina hadhi ya kupandishwa daraja na ikijiridhisha itapandishwa daraja rasmi na kuwa shule ya sekondari ya bweni. Hata hivyo, naomba niseme kwamba Serikali haiwezi kupandisha shule zote za kata kwa mara moja kuwa sekondari za bweni kwa sababu jambo hili vilevile lina changamoto ya kibajeti.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili aliuliza ni jinsi gani hizi shule mbili za Uwemba pamoja na nyingine aliyoitaja zitapandishwa rasmi daraja. Kama nilivyosema katika majibu yangu ya awali kwamba tufanye mchakato ule wa kawaida baada ya mchakato huo, Wizara ya Elimu itaangalia na wataalam watafika watafanya tathmini kama vigezo vitakuwa vimefikiwa Serikali itaona jinsi gani ya kufanya.
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa niweze kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la Shule ya Sekondari Ndembela linaendana sana na tatizo la Shule Sekondari ya Kandete Wilayani Rungwe ambapo sasa tumeanza kujenga ili iwe ya wasichana pekee. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza akawadhibitishia wananchi wa Busokelo kwamba Serikali itashiriki kikamilifu ili ianze mapema mwakani?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge amesema kwamba kama ikiwezekana Serikali ianzishe mchakato wa kuifanya Shule ya Sekondari ya Kandete ili kuwa sekondari ya bweni. Nimerudia hapa mara kadhaa kwamba tumekuwa na changamoto kubwa ya vijana wetu wasichana kupata mimba na nikasema tumetoa kipaumbele sana katika ujenzi wa shule za bweni. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Halmshauri yake ikianza na sisi Ofisi ya Rais – TAMISEMI lazima tutaweka nguvu ya kutosha kwa sababu ajenda kubwa ni jinsi gani tutamsaidia msichana aweze kupata elimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama Mheshimiwa Mbunge watakuwa wameanza juhudi hizo basi, naomba nimuambie kwamba na sisi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, kwa vile watakuwa wameweka katika bajeti yao tutahakikisha bajeti hizo zinapitishwa ili sekondari hiyo ambayo inatarajiwa kubadilishwa kuwa sekondari ya wasichana iweze kuwa sekondari ya wasichana vijana waweze kumaliza vizuri, waweze kupata elimu na hapo baadaye tuwe na viongozi wengi wasichana kutoka maeneo hayo.
MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza. Shule ya Sekondari ya Kuryo, iliyoko Wilayani Chemba ina historia ndefu sana. Shule hii inamilikiwa na Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Chama cha Mapinduzi kupitia Jumuiya ya Wazazi kimeshindwa kuiendesha shule hii na sasa hivi imefungwa na ina miundombinu yote, je, Serikali iko tayari sasa kuichukua shule hii kutoka mikononi mwa Chama cha Mapinduzi na kuikabidhi Halmashauri ya Chemba ili iweze kufanya kazi yake vizuri?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Nkamia amezungumzia Shule ya Sekondari ya Kuryo ambayo inamilikiwa na Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi. Kwa sababu hii ni mali ya Chama sitaki kuleta ugomvi kati ya Mheshimiwa Mbunge na Mheshimiwa Bulembo ambaye ni Mwenyekiti wa Wazazi Taifa. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, najua lengo kubwa la Mheshimiwa Mbunge ni vijana wale waende shule wakapate elimu kwa sababu majengo yapo na yana miundombinu mizuri. Mimi nimshauri Mheshimiwa Nkamia kwa sababu katika ahadi yetu tulipanga twende Chemba, siku tukienda Chemba, hata wiki ijayo, tufike angalau tukaione shule hiyo, tufanye ushawishi na Jumuiya ya Wazazi ili shule hii iweze kutumika na hivyo iwasaidie vijana wa Chemba kupata elimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini wazo la Mheshimiwa Mbunge ni zuri nadhani linataka consultation meeting kati ya watu wa Chemba na Jumuiya ya Wazazi. Kwa sababu Ilani ya Chama cha Mapinduzi ina lengo la kuhakikisha vijana wanapata elimu nadhani jambo hili litafikia mahali pazuri katika kuhakikisha vijana wa Chemba wanapata elimu.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi hii.
Kwa kuwa suala la wakimbizi ambalo linaathiri Wilaya ya Kibondo, vilevile limeathiri Wilaya ya Kakonko, Jimbo la Buyungu.
Je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kuwashauri watu wa UNHCR kutoa huduma za afya katika Kituo cha Afya Wilaya ya Kakonko?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba kuzungumza wazi kwamba tuwashukuru wenzetu wa UNHCR katika maeneo mbalimbali. Kwa mfano mwezi uliopita nilikuwa katika Mkoa wa Katavi. Miongoni mwa kazi kubwa sana waliyoifanya kule licha ya kusaidia katika miundombinu, lakini nimeona wamesaidia ambulance katika maeneo yale.
Kwa hiyo, ni imani yangu kwamba kwa suala analolizungumza Mheshimiwa Mbunge, nadhani hili ni wadau wetu wa karibu sana, ofisi yetu ya Mkoa kule itafanya utaratibu kuangalia ni jinsi gani tutafanya; na kwa Mkoa wa Kigoma kwenda kutoa juhudi hizo especially katika sehemu ya afya. Mwisho wa siku tunahitaji wananchi wetu katika eneo lile waweze kupata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni wazo zuri sana, nadhani katika Serikali tunalichukua hili kwa ajili ya kuleta ule msisitizo tu wa makubaliano ya karibu kwamba lile linalowezekana basi liweze kufanyika, wananchi wa eneo lile waweze kupata huduma vizuri.
MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba yake kwa sababu hayupo, yupo safari.
Pamoja na majibu ya Naibu Waziri; jambo hili limechukua muda mrefu na kama nchi ilivyokwishaamua kwamba inakwenda kwenye mpango wa viwanda na uchumi wa kati, jambo hili ni muhimu sana. Sasa nataka kujua:-
(i) Ni lini sasa huo mchakato utakamilika ili jambo hili liweze kuanza?
(ii) Napenda kujua vilevile kutoka kwenye Serikali, ni mambo gani hayo hasa ambayo yamepelekea huo mchakato kurejeshwa tena kwenye kufanyiwa marekebisho na vitu kama hivyo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kama nilivyosema kwamba tukifanya rejea Bunge lililopita, nilisema kuna timu ya TAMISEMI itapita maeneo mbalimbali; na lengo kubwa ni kubaini kwamba yale maombi yaliyoletwa kutoka katika Ofisi za Mikoa baada ya vikao vya RCC kukaa, kwamba maombi yale sasa wataalam wakienda kufanya tathmini wataona jambo lipi limekamilika na jambo lipi halijakamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri naomba nikujulishe kwamba ofisi yetu imeshatuma timu katika maeneo hayo yote na kazi hiyo wameshamaliza. Hivi sasa wana-compile ripoti yao baadaye kuweza kutushauri vizuri jinsi gani ya kufanya. Kwa hiyo, Mheshimiwa Komu vuta subira jambo hili litaenda vizuri zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la pili kwamba mambo gani mwanzo yalikuwa hayajakamilika; ni kwamba ukiangalia Mji wa Moshi, square kilometer karibu 58 peke yake, yaani ni eneo dogo sana kuwa Jiji. Ndiyo maana walidhani kama ingewezekana ni kuongeza eneo lile la utawala na ndiyo maana nadhani wameona maeneo waliyokubaliana katika muhtasari wa mwisho, eneo limeongezeka mpaka maeneo ya Hai na maeneo mengine. Ina maana kwamba eneo limevuka kutoka zile square kilometer 58 imeenda mpaka karibu 142.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kulikuwa na mambo mengine hasa yanayohusu master plan. Kwa hiyo, vitu hivi vyote vilileta mrejesho, walipelekewa mrejesho watu wa Moshi kule kwenda kuvifanyia kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu ni kwamba marekebisho yale yameshafanyika, sasa wahakiki wetu walivyoenda kuangalia kule site, watajua ni jinsi gani vile vilivyoelekezwa vimeweza kufikiwa vizuri na baadaye Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana atafanya maamuzi. Naomba tusiwe na hofu, kila kitu kitaenda kwa utaratibu ambao umepangwa katika ofisi.
MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Mamlaka ya Mji Mdogo wa Namanyere ni moja ya mamlaka iliyotembelewa na timu ya uhakiki kutoka Serikali za Mitaa na kwa taarifa tulizozipokea ni kwamba mamlaka hiyo ilikuwa imetimiza vigezo vyote na kwamba kulikuwa na dosari ndogo ndogo ambazo kwa kweli wataalam wetu wameshaleta ripoti na kukamilisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua ni lini hasa wananchi wa Namanyere wategemee kupata hicho walichokiomba kuwa Mamlaka ya Mji kamili wa Halmashauri ya Mji?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakumbuka katika Bunge lilipita nilijibu swali la Mheshimiwa Mipata na kaka yangu Mheshimiwa Malocha pale, walipokuwa wanazungumza suala zima la Namanyere na sehemu ya Sumbawanga. Ndiyo maana kati ya tarehe 14 na 15, nilikuwa Rukwa na Katavi na niliweza kufika mpaka Namanyere. Hata hivyo, timu yetu ya wataalam ilifika Namanyere kufanya uhakiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema awali kwamba zoezi hili sasa litakuwa lipo katika stage ambayo ni muafaka sana, mambo yatakapokamilika.
Naomba Mheshimiwa Mbunge asiwe na hofu, ni kwamba yale maamuzi sahihi yatafikiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sio yeye peke yake, hata akina Profesa Maji Marefu hapa, mpaka Mzee wangu hapa wa Mpwapwa, wote wana masuala hayo hayo. Kwa hiyo, tuondoe hofu, ofisi yetu inafanya kazi, tutapata mrejesho muda siyo mrefu sana. (Makofi)
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa Dodoma ni Makao Makuu ya nchi; na kwa kuwa Manispaa ya Dodoma imekamilisha vigezo vyote vya kupata hadhi ya kuwa Jiji; na kwa kuwa majengo ya Manispaa ya Dodoma yamejengwa kitaalam, yamefuata master plan, hakuna squatters. Ni lini Serikali sasa itatangaza Mji wa Dodoma kuwa Halmashauri ya Jiji? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani Mheshimiwa Lubeleje anafanya rejea ya siku alipokuwa akiniambia suala la Jiji la Dodoma; lakini nadhani ombi lake alivyokuwa anazungumza vile tukiwa barabarani, Mungu amelitilia tunu juu yake kiasi kwamba sasa hivi naona Serikali yote kiukubwa wake yote inahamia Dodoma. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili nadhani halina mashaka, ni taratibu tu zitakamilika hapa na kwa sababu michakato mipana inakwenda na Serikali yote inahamia Dodoma, uwanja wa ndege unaimarishwa, basi nadhani vikao sahihi vitakaa na kufanya mapendekezo haya. Ofisi ya Rais - TAMISEMI haitasita kwa sababu nchi kwa ujumla wake sasa, Serikali yote inahamia Dodoma.
Kwa hiyo, ni mambo ya kimchakato tu, Mheshimiwa Lubeleje avute subira na tunavyoendelea kuliimarisha Jiji letu la Dodoma, nadhani itakuwa ni sehemu ya fahari ya Tanzania. (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nataka kuongezea kwenye swali lililouliza kwamba je, ni lini Dodoma itatangazwa kuwa Jiji?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tu Dodoma sasa ndiyo tunafanya jitihada za kuhamia kwa sababu tayari imeshaamuliwa kuwa ndiyo Makao Makuu ya nchi yetu, kwa kawaida na kwa utaratibu ni lazima iwe Mamlaka ya Jiji. Kwa hiyo, utaratibu huu utakwenda sambamba na hii jitihada inayofanyika, lakini pia Dodoma ina faida kubwa kwamba walipokuwa wanatenga na kuitengenezea ramani yake, walitenga mipaka mikubwa, ina square kilometer zaidi ya 250,000. Kwa hiyo, ni eneo kubwa sana na linafaa na lina sifa zote kuwa Jiji. (Makofi)
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, Asante sana. Pamoja
na jibu zuri la Naibu Waziri. Sasa lini Serikali itatoa kero kwa hizi kodi ndogo
ndogo za akina mama hasa wakinamama wauza vitumbua, wauza mchicha,
wauza dagaa, wauza nyanya ili kutoa kero kwa wananchi wetu wasiendelee
kudhulumiwa na kuteswa na hawa wakusanya kodi na hawa Wanamgambo,
imekuwa kero na Serikali kila mara ilitangaza hapa kwamba kodi ndogondogo
hizi ni kero lini Serikali itatangaza Halmashauri zote ziache mara moja kutoza
akina mama kwenye masoko madogo madogo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tukifanya rejea wakati wa kampeni ya uchaguzi ya mwaka 2015. Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akijinadi kwa wananchi ni suala zima la mchakato wa kuondoa hizi kero ndogo ndogo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mheshimiwa Keissy, nimefanya ziara katika maeneo mbalimbali hata pale maeneo ya Ilala pale katika soko letu la Ilala, soko la Feri, Sokola Pugu Kajungeni na maeneo mbalimbali, soko la Mwanjelwa kule Mbeya. Hizi ni miongoni kwa concern lakini siyo hivyo utakuta mtu wa kawaida analipishwa risiti isiyokuwa sawasawa ndio maana tumezielekeza Halmashauri zote. Sambamba na hilo tukaona sasa lazima tubainishe ipi ni kero ambayo itaweza sasa ikashughulikiwa vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndio maana sasa kwa mujibu wa utaratibu wetu tumeandaa sheria sasa inakuja hapa Bungeni, ambayo sheria ile itaainisha sasa sheria ambayo marekebisho ya Sheria ya Mambo ya Tozo na Ushuru Sura ya namba 290 itakuja hapa na sisi Wabunge wote tutashiriki, na nina imani kwamba Mungu akijalia huenda Mkutano ujao wa Bunge inawezekana sheria hiyo itaweza kufika mara baada ya wadau wakishashiriki vya kutosha.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaziagiza Halmashauri zote kwamba yale mambo ambayo unaona kwamba hili ni kero, kwa sababu hili suala Mameya wote, Wenyeviti wa Halmashauri wanajua kwamba sehemu hizo wamepewa kura na wananchi wao. Jambo ambalo naona kwamba jambo hili halina tija kwa wananchi wetu wa kawaida, naomba tulifanyie kazi, lakini jambo ambalo mmeona mmeliweka kwa mujibu wa sheria basi mlisamize kwa utaratibu bora, siyo kwenda kutoa kapu la mama anauza vitunguu barabarani au anauza nyanya barabarani hilo jambo litakuwa siyo sawasawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nazielekeza Halmashauri zote hasa Mameya na Wenyeviti wa Halmashauri waweze kukaa pamoja na Kamati zao za Fedha, wabainishe ipi ni kero kwa sasa kabla sheria hii haijakuja hapa Bungeni ili mradi kuweza kuondoa kero kuwafurahisha wananchi waishi katika maisha ya utaratibu wa kujenga uchumi wa nchi yao.
MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata nafasi hii, kwa kuwa Halmashauri ya Mji wa Mafinga na maeneo mengi ya mijini kumekuwa na kero kubwa kama hii ambayo imeelezwa kwenye swali la msingi iikiwa ni pamoja na timua timua ya wafanyabiashara ndogo ndogo. Sasa kwa kuwa Halmashauri ya Mji wa Mafinga ni Halmashauri mpya bado haijakuwa na uwezo wa kutenga maeneo kwa maana ya kwamba kifedha, kwa ajili ya wafanyabiashara ndogo ndogo. Je, Serikali iko tayari kutusaidia sisi kama Halmashauri mpya japo kusudi kutuwezesha kutenga maeneo hayo na hivyo wafanyabiashara kuwapunguzia bugudha bugudha wamama wauza vitumbua, wauza matunda, vijana wachoma mahindi na wote wanaofanya shughuli za namna hiyo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, si muda mrefu nilifika pale Mafinga nilifika Jimboni kwake Mheshimiwa na nilienda mpaka katika kituo kile cha watoto walemavu pale, lakini kwa maelekezo ya Mheshimiwa Mbunge mwenyewe. Ni kweli Halmashauri ile ni mpya, naomba niseme sisi tutakupa ushirikiano mkubwa kama Serikali kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Lakini suala zima la utengaji wa eneo naomba niwasihi Waheshimiwa Wabunge jambo hili linaanza kwetu sisi wenyewe, kwa sababu sisi ndio tunajua wapi eneo la wazi lipo nini kifanyike.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vile vile atuelekezi watu waende wakapange biashara katika maeneo ya barabara, hilo jambo halikubaliki. Kwa hiyo, naomba nikusihi Mheshimiwa Mbunge ninyi pale kama Baraza la Madiwani naomba anzeni, kwa sababu mnanza kufanya mambo mazuri zaidi. Na sisi Ofisi ya Rais – TAMISEMI tutashauri vizuri nini kifanyike ili mradi wananchi wa Mafinga pale wapate huduma bora hasa ya suala zima ya ujasiriamali kufanya biashara katika maeneo yao.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri sana, hata hivyo kwa namna kero ya askari hawa mgambo walioajiriwa na mamlaka zetu za Serikali za Mitaa na hasa za Mijini ni kero kubwa na inaleta usumbufu mkubwa na miongoni mwa mambo ambayo husababisha na pengine kupelekea hata Serikali kuchukiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sekta yetu binafsi nchini haijarasimishwa sana na kwa hivyo wananchi wetu wanahangaika kufanya shughuli mbalimbali ili wapate kipato na kwa hakika ndio wanaojenga uchumi wa nchi yetu. Lazima tuwe na staha katika kushughulika nao, maana hata hivyo hatujaweza kuwatengea maeneo ya kufanyia shughuli zao rasmi lakini hatuna mfumo rasmi sana wa mitaji na kwa hivyo kitendo cha askari mgambo kuvuruga biashara zao, kukamata na kutaifisha mali zao kitendo hiki hakikubaliki na Serikali kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kuziomba mamlaka zote na hasa za Mijini zinazounda majeshi haya kwa maana ya mgambo chini ya Sheria ile ya Jeshi la Akiba linalosaidiana na Polisi, kuhakikisha kwamba kila operation wanayoifanya basi inakuwa na makubaliano maalum katika mamlaka husika kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, na baada ya pale operation yeyote inayofanyika, lazima isimamiwe vizuri, haiwezekani mgambo wa Jiji wakawa wanakamata pikipiki, wanakamata bodaboda, wanakamata yaani ni vurugu tupu. Kwa hiyo, hili jambo halikubaliki nafahamu na nafikiri iko haja tukafanya mapitio ya Jeshi la Mgambo ambalo linaundwa kwenye hizi Mamlaka za Mijini na kuona kama kuna haja ya kuja na mwongozo na utaratibu mpya pamoja na kwamba tunafahamu kwamba iko sheria hili jambo hili liweze kukomeshwa kwa sababu wanaleta mateso na vilio vingi katika familia ambazo zinataifishiwa mali zao.
MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza napenda kujua usanifu huu wa kina umeanza lini na utaisha lini?
Swali la pili ningependa kujua kwa sababu nimefuatilia kwa muda mrefu ahadi hii ya Mheshimiwa Rais kumekuwa na mkanganyiko wa kutokujua, kwamba fedha za ujenzi wa barabara hizi kilometa tatu zitatoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa au zitatoka katika Serikali Kuu? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema katika jibu langu la msingi kwamba bajeti ya fedha hii imetengwa katika mwaka huu wa fedha 2016/2017 ambayo bajeti tumepitisha si muda mrefu sana katika Ofisi ya Rais TAMISEMI. Lengo kubwa ni kwamba fedha zile sasa zitatoka ilimradi detailed design iweze kukamilika, mara baada ya hapo sasa tutajua gharama halisi ya ujenzi wa barabara hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namuomba Mheshimiwa Stanslaus avutea subira tu na kwa sababu unajua kwamba ofisi yetu, imejielekeza sasa imejipanga jinsi gani tutafanya kutatua tatizo la miundombinu katika Halmashauri mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, jambo la kwamba hizi fedha zitatoka wapi aidha Halmashauri au zitatoka wapi hii ni ahadi ya Mheshimiwa Rais ambaye ni mstaafu regardless hizo fedha kama zitatoka Halmashauri lakini lengo kubwa ni kwamba kazi hii lazima itekelezwe. Na ndio maana hata kama ukifanya rejea bajeti yetu ya mwaka huu tumetenga takribani bilioni 245 na bilioni hizi maana yake kulikuwa na mgawanyiko wa maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna takribani shilingi bilioni 43 kwa ajili ya miradi ile ya kuondoa vikwazo maeneo mbalimbali zingine ni kwa ajili katika Halmashauri mbalimbali. Lakini ukifanya rejea sana katika hiki kipindi cha miaka mitano, kupitia mradi wetu wa uboreshaji wa miji mbalimbali, unaona Miji mingi sasa hivi imebadiika, lakini tunaenda hivyo maana yake tunaenda katika hatua sasa za Halmashauri. Lengo langu na jukumu letu kubwa ni nini kama Serikali, tutahakikisha miradi hii ambayo ni kipaumbele ambayo imetolewa ahadi na viongozi wetu wakuu wa nchi tutahakikisha kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI inasimamia na miradi hii iweze kutekelezeka. Kwa sababu lazima tulinde imani ya viongozi wetu wameifanya na jambo hili tumejipambanua wazi kwamba ahadi zote zilizopangwa lazima tuzitekeleze kwa kadri tulivyowaahidi.
MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Tatizo la Maswa Mashariki linalingana kabisa na tatizo la Mji wa Mombo, katika Halmashauri ya Korogwe Vijijini. Rais wa Awamu ya Nne aliaahidi kwamba atajenga kiwango cha lami barabara kilometa 1.5 na Rais wa Awamu ya Tano alivyokuja vilevile alitoa ahadi hiyo kwamba atatekeleza ahadi ya ambayo imeachwa na Rais Mstaafu. Lakini mpaka leo hii hakujafanyika kitu cha aina yoyote, je, Serikali inasemaje kuhusiana na Mji wa Mombo ambao wananchi wake wanategemea sana mpaka sasa hivi kungekuwa na barabara ya lami lakini hakuna kinachoendelea
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ahadi hii ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais lakini tunaona kulikuwa na faraja kubwa sana, wakati Rais Mstaafu anatoa ahadi hiyo Waziri wake wa Ujenzi ni Dkt. John Pombe Magufuli. Then katika uchaguzi wa mwaka huu sasa yule aliyekuwa ni Waziri wa Ujenzi sasa hivi ndio Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama tukisema ndugu zetu wa Korogwe Vijijini ni watu ambao mmelamba dume katika mchezo wa karata. Naomba nikuambie hii ahadi ya Rais itakuwepo pale pale na ndio maana ukiangalia katika harakati hizo juzi juzi nilipita Korogwe kwa mama yangu, jinsi ujenzi wa kituo kikubwa cha mabasi kinavyofanyika. Maana yake ni kazi kubwa inafanyika na siyo kituo cha mabasi maana yake ni suala zima la ujenzi wa miundombinu ya barabara ya lami. Maana yake mambo haya yote katika Mkoa wa Tanga kama ilivyoahidiwa na Mheshimiwa Rais kwa kweli yatatekelezwa tufanye subira tu.
MHE ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyo kwenye Mji mdogo wa Maswa tuna tatizo kama hilo kwa Mji wetu Mdogo wa Mbalizi, ambapo Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliahidi kumalizia kipande kidogo cha barabara ya kilometa moja na pia aliahidi kumalizia ujenzi wa stand pale Mbalizi lakini mpaka leo hakuna chochote kinachofanyika labda ningepena Waziri ajaribu kutoa ufafanuzi ni lini ujenzi huo utaanza? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI YA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Ujenzi kwanza naomba tukiri wazi kwamba bajeti katika kipindi ambacho Dkt. John Pombe Magufuli anaahidi bajeti yake ndio kwanza hii tunaanza bajeti ya kwanza na baadaye tuna miaka mitano. Lakini ameahidi stand na amewaahidi barabara ya kilomita moja. Mheshimiwa Mbunge, naomba nikwambie kwamba, ahadi ya Rais itakuwepo palepale na kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu kazi hii na sisi tuliopewa dhamana ya kuisimamia, tutaisimamia kwa karibu zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutaisimamia kwa karibu zaidi, lengo ni kwamba, ahadi ya Rais aliyoitoa, ujenzi wa stand, ujenzi wa barabara ya kilometa moja itafanyika na muweze kuona kwamba, maeneo mbalimbali sasa hivi stand zinajengwa kupitia miradi yetu sio stand tu, kuna ma-dampo, kuna barabara. Kwa hiyo, nikwambie Mheshimiwa Mbunge ni kwamba, katika maeneo ya Mbalizi ni kwamba, watu wawe na subira hii ndio bajeti yetu ya kwanza imeanza. Imani yangu ni kwamba, maeneo ya Mbalizi, kama Mheshimiwa Rais alivyoahidi, suala lile litatekelezwa.
MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.
Nataka kuuliza swali la nyongeza. Katika ziara ya Mheshimiwa Rais, alipita katika Kijiji cha Budarabujiga aliyeko madarakani Mabasabi na Ikindilo, aliahidi kivuko pamoja na barabara hiyo, ni lini itatekelezwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahadi ya kivuko, ahadi kama ya barabara, ahadi zote kama nilivyosema awali na ninajua na nyie watani zangu huko Wasukuma mambo mengi sana mmeahidiwa huko hasa katika suala zima la maboti na maeneo mbalimbali.
Mimi imani yangu kubwa ni kwamba, Dkt. John Pombe Magufuli ndani ya miaka hii mitano atafanya mambo ya mfano sana ambayo hatujawahi kuyaona. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, na haya yanajielekeza jinsi gani amejipanga Serikali yake katika ukusanyaji wa mapato, kwa mara ya kwanza mnaona rekodi kubwa katika ukusanyaji wa mapato kutoka kukusanya kwanza bilioni 600 mpaka bilioni 800, sasa tunaanza kukusanya one point something trillion, sio jambo la mchezo! Na mnaona jinsi gani pesa wakandarasi waliokuwa wamesimamisha miradi yao sasa wakandarasi wako site wanaanza kufanya kazi kwa ajili ya umakini wa ukusanyaji wa kodi.
Kwa hiyo, naomba niwaambie, mkakati huu unaoenda wa kukusanya fedha katika Serikali maana yake utaenda sambamba na kuhakikisha zile ahadi zote na miundombinu iliyokusudiwa inaweza kutekelezwa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, Kata ya Litapunga, Halmashauri ya Nsimbo, vijiji vingi havina maji. Je, ni lini Serikali itapeleka miradi Kata ya Itapunga, ili akinamama wale waweze kupata unafuu wa maisha?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Nsimbo maana yake Jimbo liko pana najua na vijiji viko vingi. Na Katika bajeti zetu za TAMISEMI tulielezea baadhi ya miradi ya maji, lakini na wenzetu wa Wizara ya Maji wameelezea mipango yao katika ujenzi wa maji. Na ni kwamba tulikuwa na programu ya maji ya awamu ya kwanza sasa tunaingia katika programu ya maji ya awamu ya pili.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika program ya maji ya awamu ya kwanza kuna maeneo mengine maji tulikosa, visima vilichimbwa, lakini maji hayakupatikana! Katika programu ya Awamu ya II tunaenda mbali zaidi, maana yake maeneo ambayo yalikosa maji yaweze kupata maji. Maeneo yaliyokuwa hayana maji maana yake hawana miradi ile ya maji ni lazima kujielekeza kuweka miradi ya maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, na lengo kubwa ni nini? Tulichokipanga katika kipindi hiki lengo kubwa tulikuwa na ile, principal yetu ni kwamba, lazima tumuondoe mama ndoo kichwani. Nikijua kwamba Nsimbo ina changamoto kubwa sana kama ilivyokuwa Korogwe, Kisarawe, Bahi na kama ilivyokuwa maeneo mengine yote, jukumu letu kubwa ni kwamba, sisi tutafanya analysis jinsi gani tutafanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo uliyoyazungumza tutaangalia kwa pamoja kwamba kuna miradi gani ambayo imetengwa kwa sasa hivi, lakini ni jijsi gani tutafanya tuyafikie maeneo ya watu mbalimbali kwa sababu lengo letu kubwa ni kumuondoa mama ndoo kichwani, kutumia fursa mbalimbali, kama visima vilikuwa vinachimbwa, na vilikuwa vimepatikana basi tunaangalia alternative way, kama kutumia malambo au kutumia chanzo kingine cha karibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nikuahidi Mheshimiwa Mbunge na bahati nzuri mnafanya ushirikiano mzuri wewe na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo pale na yeye tulikuwa na kikao mpaka hata kesho tulipanga kuweza kuonanan katika mambo mengine ya ukusanyaji wa mapato. Lakini hayo ni miongoni mwa mambo mengine ambayo tutaenda kuyaangalia; lengo kubwa ni kwamba kuwapatia wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania maji kwa hiyo, tumelichukua swali lako kwenda kulifanyia kazi.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Kwa kuwa Naibu Waziri umeshatembelea Wilaya ya Mpwapwa na Wilaya ya Mpwapwa kuna vijiji ambavyo vina matatizo makubwa sana ya maji; kwa mfano Kijiji cha Tibwetangula, Lupeta, Bumila, Makutupa, Nana, Chimai, Salaza, Iyoma, Ngalamilo, Chamanga na Majami.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri utatembelea maeneo hayo, ili uone shida ya maji wanayopata wananchi wa Jimbo la Mpwapwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimshukuru Mbunge huyu, tulifanya ziara ya pamoja pale katika sekondari yetu ya Mpwapwa tukabaini wanafunzi wanashindwa hata kufanya mitihani vizuri kwa sababu, maji hawapati. Reason behind kuna connection ya maji ya shilingi milioni nne tu! Tumeshirikiananae kwa pamoja, juzi hapa nimekwenda, sasa vijana wa sekondari ya Mpwapwa wanapata maji. Kwa hiyo, Mheshimiwa Lubeleje nakushukuru kwa uongozi wako mzuri, mradi ule umekamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sambamba na hilo kweli, ukiangalia katika jimbo lake lile, ni pana! Jimbo lile sasa hivi na Jimbo la Kibwakwe lote linafanya Halmashauri ya Mpwapwa. Na nilipotembelea nikuhakikishie Mheshimiwa Lubeleje, nilifika mpaka katika Kijiji cha Makutupa, pale hata ukitokea msiba pale kupata maji maana yake wananchi wanaenda kuyapata maji mbali zaidi. Lakini Jimbo lako Mheshimiwa Lubeleje ni kwamba ukiliangalia jiografia yake lina tatizo kubwa sana, lakini hata nikapita maeneo mengine ya Chamkoroma kule watu msitu wamekata wote, maana yake hata vyanzo vya maji vya mtiririko maana yake vimepotea. Sasa nini tutafanya? Ulichoniomba nitembelee kule, lakini nakwambia nimeshatembelea in advance mpaka maeneo ya kambi kule ndani nikavuka na ule mto! Tutaendelea kufanya hivyo tena, lengo kubwa ni kubaini hizo changamoto kwa pamoja, tujadili kwa pamoja, tuondoe matatizo ya wananchi wetu.
MHE. GODFREY W. MGIMWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Tatizo ambalo lipo katika Jimbo la Mheshimiwa Mendrad Lutengano, ni sawasawa na tatizo ambalo liko katika Jimbo langu la Kalenga. Ningeomba kujua Miradi ya Maji ya Weru, Itengulinyi, Supilo, itakamilika lini kwa sababu wakandarasi wamekuwa wakipiga makelele na kudai pesa zao za malipo?
Ningependa kujua kutoka kwa Mheshimiwa Waziri, ni lini sasa Wakandarasi hawa watalipwa, ili kwamba, miradi iweze kuendelea na wananchi wangu waweze kupata maji? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna miradi ya maji mingi sana ilisimama. Wakandarasi wali-demobilize mitambo kutoka maeneo ya miradi na sababu kubwa ilifanya kwamba, flow ya fedha, wakandarasi walifanya kazi walikuwa hawajalipwa, certificates zilienda Wizarani, lakini watu walikuwa hawajalipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu letu kubwa tulilofanya ni kuhakikisha pesa zinakusanywa kama nilivyosema awali. Hivi sasa nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge wakandarasi wote karibuni sasa hivi kila Halmashauri pesa sasa zimeshapelekwa, ilimradi wakandarasi waweze kurudi site.
Mheshimiwa Naibu Spika, juzi nilikuwa na Naibu Waziri wa Maji hapa tukifanya mjadala katika hayo, imeonekana sasa hivi hali imeenda vizuri zaidi. Kama tutafanya analysis kama huko Makete kama watu hawajaanza kurudi site, lakini ni kwamba kweli wakandarasi walitoa mitambo mwanzo, lakini fedha sasa hivi baada ya makusanyo mazuri tumeshapeleka site huko ilimradi wakandarasi walipwe, kazi iweze kuendelea. Tutaangalia kama huku katika Jimbo lako kama kuna matatizo kidogo bado yapo, tutaangalia jinsi gani tutafanya kuyatatua kwa pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sambamba na hili niweze kuzungumzia hata pale kwa ndugu yangu wa Mufindi pale, ndugu yangu Mheshimiwa Chumi, kulikuwa na suala la pampu pale, tumefanya harakati, hivi sasa ile pampu inafungwa baada ya kupata uhakiki wa kutosha. Lengo letu ni kwamba, miradi yote ikamilike na wananchi waweze kupata maji.

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri – TAMISEMI, kuhusu Jimbo la Kalenga tayari nimeshaongea na Mheshimiwa Mbunge na tumeangalia vitabu, tumeshapeleka shilingi milioni 365. Nikawa nimemuomba Mheshimiwa amfahamishe Mkurugenzi kwamba, kama kuna certificate zozote walizonazo mezani watuletee, ili tuweze kukamilisha malipo Wakandarasi waendelee na kazi.
MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Serikali imekuwa ikijali sana wanafunzi wa vyuo kwa kuwapa mikopo na allowance mbalimbali, lakini hivi karibuni kumekuwa na fununu za kucheleweshwa kwa hizi fedha. Sasa je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba fedha zinaenda kwa wakati na kama zinachelewa taarifa inaenda kwa viongozi husika, ili kuondoa hali ya sintofahamu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (K.n.y. WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli wakati mwingine huwa kunakuwa na ucheleweshaji wa fedha, lakini lazima niregiste kwamba, kazi kubwa wanayofanya Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hasa Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lazima tuwe wakweli, wakati mwingine unasema kwamba, kuna mtu anazungumza jambo lakini hatekelezi. Wabunge hawa unaowaona humu ni waadilifu wa hali ya juu, siku zote wanalia suala la wanafunzi wanaokosa mikopo. Lakini wengine wanasema wanafunzi wanakosa mikopo ilimradi watengeneze umaarufu wa kisiasa tu, ikiletwa bajeti hapa kupitisha wanasema hapana. Lakini Wabunge hawa wanajadili kuhakikisha kwamba bajeti hizo kila mwaka zinapita. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikwambie, waliweza ku-raise budget kuanzia shilingi bilioni 56 mwaka 2006 mpaka 2007, leo hii tunazungumzia bajeti ya shilingi 480,000,000,073 watoto wanapata mikopo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, lazima tukiri kwamba, kuna kazi kubwa imefanywa na Wabunge hawa kwa ajili ya kuhakikisha wanafunzi wanapata mikopo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini isitoshe ni kweli wakati mwingine changamoto zinajitokeza. Na juzi-juzi nimesikia kwamba, Chuo cha Dar es Salaam kuna wanafunzi walitaka kugoma. Ni jukumu la Serikali kuhakikisha pesa zinapelekwa na pesa zimeshapelekwa katika vyuo mbalimbali. Kuna baadhi ya vyuo vichache ambavyo bado uhakiki unafanyika, especially Chuo cha UDOM na baadhi ya vyuo vingine. Na uhakiki huu unafanyika kwa sababu imebainika kuna wanafunzi wengine ni wanafunzi hewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba ndugu zangu tuwe na subira kidogo ni kwamba, mchakato huu unafanyika katika baadhi ya vyuo, vyuo vingine tayari ilitokea mpaka jana nafanya analysis, baadhi ya vyuo vingine wameshapelekewa cheque zao jana, wengine wamepelekewa cheque zao juzi kwa ajili ya vyakula vya wanafunzi. Jukumu letu kubwa kama Serikali ni kuwahudumia wanafunzi hao kwa sababu, tunajua kwamba kuweka bajeti ya shilingi karibuni bilioni mia nne na zaidi kwa ajili ya wanafunzi sio jambo dogo ni jambo ambalo lina utashi wa kisiasa.
NAIBU SPIKA: Waheshimiwa tuendelee. Mheshimiwa Naibu Waziri alikuwa anajibu kwa niaba. Tunaendelea, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Musa Rashid Ntimizi, Mbunge wa Igalula, sasa aulize swali lake.
MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, fedha zote za Serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya wananchi vijijini zinapita kwenye Halmashauri za Wilaya na katika vikao vya Halmashauri za Wilaya hasa Kamati hiyo ya Fedha na Mipango Wabunge wa Viti Maalum hawashiriki na ndiyo watu wenye dhamana na maendeleo ya wanawake.
Kwa kuwa sheria hiyo iliyotungwa ambayo inawakataza Wabunge wa Viti Maalum kuingia kwenye Kamati hizo ilitungwa zamani sana kabla hata utaratibu wa Ubunge wa Viti Maalum haujaanza bali kulikuwa na Wabunge wa Majimbo na Wabunge wa Kuteuliwa na Rais; na kwa kuwa mwaka jana kwenye Bunge la Kumi, Mheshimiwa Mwanri aliyekuwa Naibu Waziri alipokuwa anajibu swali hapa Bungeni, alitueleza kwamba sheria hiyo ni kandamizi na tunahitaji kuileta hapa Bungeni ili tuirekebishe Wabunge wa Viti Maalum washiriki.
Je, Serikali italeta lini hiyo sheria ili Wabunge wa Viti Maalum waweze kushiriki katika Kamati hii muhimu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Halmashauri zetu za Wilaya hasa kwa Mkoa wetu wa Manyara zinatenga asilimia kumi za fedha kwa ajili ya miradi ya wanawake. Utaratibu na mfumo wa utoaji wa fedha hizo kwa ajili ya miradi ya wanawake hauko vizuri na kuna upotevu mkubwa sana wa fedha hizo za Serikali.
Je, ni kwa nini Madiwani wa Viti Maalum wakisaidiana na Wabunge wao wasisimamie kikamilifu utoaji na urejeshaji wa fedha hizo ili ziweze kuwafikia walengwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Martha kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema awali kila kitu kipo kwa mujibu wa sheria na kanuni zake. Katika jibu langu la msingi katika eneo la pili nikasema mchakato unaweza ukaendeshwa kwa kuwashirikisha wadau. Hili la kuwashirikisha wadau kama nilivyosema lina umuhimu mkubwa sana. Katika maeneo mengine kwa mfano nikichukua Jimbo langu mimi la Kisarawe, Mbunge wangu wa Viti Maalum anaingia katika Kamati ya Fedha na sehemu zingine wanaingia katika Kamati hii, ina maana hivi sasa katika zile nafasi mbili Mwenyekiti anaweza akateua Mbunge wa Viti Maalum kuweza kuingia pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kusimamia fedha ni wajibu wa Madiwani na Wabunge wahusika katika eneo hilo. Kwa upana wa jambo hili, ndiyo maana nimesema wadau lazima washirikishwe. Kuna baadhi ya Majimbo, mfano Jimbo la Ilala, lina Wabunge wa Majimbo watatu, lina Madiwani wa Viti Maalum wasiopungua watano, kwa hiyo ukiangalia hapo, ndiyo maana nasema lazima wadau washirikishwe kuona jambo hilo linakaajekaaje na kuangalia ni jinsi gani tutafanya Kamati ya Fedha iweze kufanya vizuri. Kwa mfano, kwa hali ya sasa hivi ukisema Jimbo la Ilala Wabunge wote wa Viti Maalum waingie katika Kamati ya Fedha mtapata sura hapo, ndiyo maana nasema lazima sheria hiyo tuitazame kwa upana na wadau washiriki kila mmoja katika eneo lake kuangalia jinsi gani tutafanya, hilo ni jambo la msingi lakini kwa sasa hivi sheria inasimama hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusu asilimia tano ya akina mama na siyo ya akina mama peke yake, ni ya vijana na akina mama. Jambo hili nililisema katika vikao mbalimbali kwamba jukumu la Kamati ya Fedha ni kuhakikisha kwamba fedha zinazokusanywa kutoka own source ziweze kuyafikia yale makundi ya akina mama na vijana. Kwa bahati mbaya hata katika kaguzi mbalimbali zilizopita hili ni miongoni mwa eneo lenye changamoto kubwa na ndiyo maana tumetoa maelekezo kuhusu suala hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nasema agenda ya kuhakikisha akina mama na vijana wanapata fedha hii ni yetu sote. Ndiyo maana bajeti ya mwaka huu criteria tuliyotumia kuhakikisha Halmashauri zote zinatengewa bajeti ni kuhakikisha kwamba wanatenga asilimia tano ya vijana na akina mama na walemavu watakuwa katika mchakato huo. Kwa hiyo, hili ni agizo la jumla kwamba kwa vile bajeti tumeipitisha basi kila Halmashauri ihakikishe inasimamia asilimia tano za akina mama na tano za vijana ziweze kuwafikia walengwa.
MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri lakini naomba niulize maswali ya nyongeza mawili kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu swali langu la msingi nimeelezea namna ambavyo wananchi wa Kata ya Saja, Kijiji cha Nyigo na Mtewele namna wanavyopata tabu kwani huduma zote zinapatikana Makambako na kwenda kwenye Halmashauri yao kutoka Saja kwenda Wanging‘ombe ni kilometa 88 na kwenda Makambako ni kilometa 20 na kutoka Mtewele ni kilometa tano na Waziri amekiri ni kweli katika suala la upatikanaji wa huduma ni mbali. Kwa nini Waziri asiagize shughuli hii ya vikao ianze kufanyika? Siku za nyuma vilishafanyika na kupelekwa kwenye vikao vinavyohusika vya mkoa na hivi juzi tu tulikaa kwenye kikao na mkoa tayari walianza kushughulikia. Niombe Waziri sasa ashughulikie suala hili na kuagiza kwamba waweze kukaa vikao ili wananchi hawa wapate huduma jirani.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika Kijiji cha Nyigo, GN ambayo iko katika Halmashauri ya Makambako inaonyesha Kijiji cha Ngigo mpaka wake mwisho ni barabara ya zamani ya Mgololo. Hata hivyo, uongozi wa Iringa umewahi kwenda pale na kutaka kupotosha ukweli. Niombe sasa Waziri asimamie na afuatane na mimi ili tukaone ile GN ambayo tulipewa Halmashauri ya Mji wa Makambako ili wananchi wale waweze kupata huduma jirani na Mji wa Makambako. Nakushukuru.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna suala zito kama linalohusu mipaka. Mimi namuelewa sana Mheshimiwa Sanga katika concern yake hiyo, wananchi wanahitaji kweli kwenda eneo hilo lakini kwa sababu maeneo ya mipaka yameshaainishwa itakuwa ni vigumu leo niagize kufanya jambo fulani. Isipokuwa nifanye jambo moja, endapo haya mahitaji yanaonekana ni ya msingi, kama nilivyosema katika jibu langu la awali, Mheshimiwa Deo Sanga najua una ushawishi mzuri sana katika maeneo yale na ukizingatia kwamba ulikuwa Mwenyekiti wa Chama wa Mkoa kwa hiyo kauli yako inasikika vizuri sana, nadhani mchakato ukianza kama nilivyoeleza katika vikao vyetu vya vijiji vya WDC, DCC na RCC jambo hili litaisha vizuri. Jambo hili linaenda hadi kubadilisha zile coordinates katika GN, ndiyo maana nasema lazima liwe shirikishi, watu wa maeneo hayo wakubaliane kwa pamoja ni jinsi gani tutafanya kama tunataka kubadilisha mipaka. Kwa mujibu wa Sheria Sura 287, kifungu cha 10 mpaka 11 vimempa mamlaka Waziri mwenye dhamana kubadilisha mipaka lakini ni endapo itaonekana ninyi mmemaliza mchakato huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Kijiji cha Nyigo kwamba GN zimebadilishwa yaani haziko sawasawa, naomba niseme kwamba katika hilo niko radhi kutembelea kijiji hicho. Katika safari zangu za Nyanda ya Juu Kusini nitamshirikisha na nitamuomba tushirikiane kama tulivyoshirikiana katika ziara yangu iliyopita lengo kubwa likiwa ni kuleta mtengamano mzuri katika maeneo yetu.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, pamoja na kutenga shilingi milioni 15 kwa ajili ya ukamilishaji wa Kituo cha Mima na shilingi milioni 35 kwa ajili ya kukamilisha Kituo cha Afya cha Mbori, je, Mheshimiwa Waziri haoni fedha hizi zilizotengwa ni kidogo kiasi kwamba vituo hivi vitachukua zaidi ya miaka mitano kukamilika?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa kuna majengo ya zahanati ya Kijiji cha Igoji Kaskazini na Igoji Kusini Salaze yamekamilika na kinachohitajika sasa ni huduma za dawa.
Je, yuko tayari sasa majengo haya yakaanza kutumika kwa ajili ya huduma za dawa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Lubeleje, kama nilivyosema wiki iliyopita kwamba yeye ni greda za zamani lakini makali yale yale. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Kituo cha Mima kimetengewa shilingi milioni 15 na Mbori shilingi milioni 35, Mbunge anasema fedha hizi hazitoshi. Hata hivyo, katika mchakato wa bajeti tulikuwa tunapokea mapendekezo mbalimbali ambapo wahandisi wetu walifanya analysis ya kila jengo linahitaji kiasi gani ili liweze kukamilika. Kama fedha hizi hazitoshi basi tutaangalia nini cha kufanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika jibu langu la swali la msingi la wiki iliyopita nilisema, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Wizara ya Afya na Kamati ya Bunge tulifanya zoezi moja ambalo tunaendelea kulifanya mpaka hivi sasa na tumeshapeleka maelekezo mbalimbali kwa Wakurugenzi wetu wa Halmashauri, wabainishe miradi yote ambayo haijakamilika halafu tuifanyie analysis tuone ni jinsi gani tutafanya ili mradi miradi hiyo yote iweze kukamilika. Kwa sababu ukiachia kwa Mheshimiwa Lubeleje sambamba na hilo kuna maeneo mbalimbali miradi mingi sana iliyojengwa miaka ya nyuma bado haijakamilika. Kwa hiyo, ndiyo maana Ofisi yetu ikaamua ni vyema tubainishe miradi yote na tuifanyie tathmini ya kina ili tujue tunahitaji pesa kiasi gani ili iweze kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimuahidi Mheshimiwa Lubeleje kwamba lengo letu ni kukamilisha maeneo haya nikijua wazi kwamba Halmashauri ya Mpwapwa na Jimbo lake la Mpwapwa na Kibakwe ambapo kijiografia ni eneo kubwa sana, wananchi wake lazima wapatiwe huduma. Kwa hiyo, tuna kila sababu kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuhakikisha huduma za wananchi hasa huduma za afya zinapatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kwamba vituo vya afya vimekamilika lakini kuna tatizo kubwa la ukosefu wa dawa na vifaa tiba, naomba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge, kama nilivyofanya siku chache zilizopita kutembelea Jimbo lake na kubaini huduma na changamoto mbalimbali, tutajitahidi kadiri iwezekanavyo vituo hivi viweze kufanya kazi ili wananchi wapate huduma.
MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa hospitali inayotegemewa na wananchi wa Loliondo, Mkoani Arusha ni Hospitali ya Misheni ya Waso ingawa hospitali hii ina changamoto nyingi sana; na kwa kuwa hatuna Hospitali ya Wilaya ya Ngorongoro, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kujenga Hospitali ya Wilaya ili wakazi wa maeneo yale wapate huduma ya matibabu ipasavyo maana wakazi wengi wa maeneo yale ni wafugaji?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue ombi hili kutoka kwa Mheshimiwa Catherine Magige kwamba Ngorongoro ijengwe Hospitali ya Wilaya na nikitambua kwamba katika maeneo haya kuna changamoto kubwa sana. Juzi juzi nilikuwa na Mbunge wa eneo hilo akishirikiana na wananchi wake na Madiwani ambapo walikuja ofisini kwangu kuelezea changamoto zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.
Kwa hiyo, jambo kubwa kama nilivyosema katika miradi kama hii, naomba Mheshimiwa Mbunge kwa sababu yeye ni wa mkoa mzima ashirikiane na Mbunge wa Jimbo na najua ni mpambanaji mkubwa sana katika sekta ya afya, wafanye mchakato mpana wa kuliibua vizuri jambo hili ili badala ya kutumia Hospitali ya DDH ambayo ni ya Misheni tuhakikishe wananchi tunawapatia Hospitali yao ya Wilaya ili mradi na wao waweze kunufaika na huduma ya afya katika nchi yao.
MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa Wilaya ya Lushoto ina majimbo matatu na Hospitali ya Wilaya ni moja. Je, ni lini sasa Serikali itapanua hospitali ile hasa wodi ya akinamama wajawazito?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri kwamba si chini ya wiki tatu au nne Mheshimiwa Shekilindi na Mheshimiwa Shangazi walikuja ofisini kwangu. Lengo la kuja ofisini kwangu ilikuwa ni ajenda ya barabara halikadhalika huduma ya afya katika maeneo yao. Licha ya ajenda ya kuhakikisha tunapanua hospitali ile lakini miongoni mwa ajenda walizokujanazo ni kuimarisha vile vituo vyao vya afya viweze kufanya kazi vizuri. Kwa hiyo, kama nilivyomuahidi Mheshimiwa Shekilindi alivyokuja ofisini, jukumu letu kubwa ni kubainisha na aliniambia nipite route tofauti nione jiografia ya eneo lake, nikija naomba anipitishe niione vizuri lakini tupange mikakati ya pamoja kuwasaidia wananchi wetu.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, napenda kuongeza majibu kwenye swali la Mheshimiwa Shekilindi, Mbunge wa Lushoto kwamba katika sera ya afya sasa hivi tunataka kuondoka kwenye Hospitali ya Wilaya twende kwenye Hospitali za Halmashauri.
Kwa hiyo, nataka kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge wote ambao Wilaya zao zina Halmashauri zaidi ya mbili, tatu, sasa hivi kisera tunapendekeza kila Halmashauri iwe na hospitali yake badala ya kuwa na Hospitali ya Wilaya. Kwa kufanya hivi tunaamini tutaweza kutatua mlundikano wa wagonjwa katika hospitali mbalimbali za Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutatoa maelekezo rasmi ya kisera katika Halmashauri mbalimbali.
MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba nimuulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la ukosefu wa nyumba za kuishi watumishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale ni kubwa sana; watumishi hawa hulazimika kutembea umbali wa kilometa 50 mpaka 80, lakini wengine wanaishi Mkoani kabisa Geita ambako ni umbali wa kilometa 100. (Makofi)
Je, Serikali haioni kuna haja sasa ya kuharakisha majengo haya ili watumishi hawa waweze kuishi karibu na ofisi zao?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tumekisikia kilio hiki, ndiyo maana mwaka huu tumetenga bajeti ya shilingi milioni 850.
Nawapongeza kwa sababu mshauri ameshaanza zile kazi za awali; ramani imeshapatikana na bajeti iliyolipwa pale kwa shilingi milioni 177, pesa iliyobakia inaonekana mkandarasi aliyepatikana hawezi kuanza kufanya kazi. Ndiyo maana tumesema kwamba mwaka huu tumetenga shilingi milioni 850, lengo letu kubwa ni kwamba tukichanganya na zile za mwanzo sasa, mkandarasi aweze kuingia site na hii kazi iende kwa haraka.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mchakato huu wa bajeti tutaharakisha fedha hizi ziende mapema ili mradi ujenzi uweze kuanza kwa wakati ili kuondoa kero kwa watumishi hawa ambao wanasafiri katika umbali mrefu.
MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Tatizo la nyumba na ofisi katika Halmashauri mpya ya Wilaya ya Nyang’hwale ni sambamba na matatizo katika Halmashauri nyingi zilizoanzishwa hapa nchini ambazo ni mpya. Sasa napenda kujua, je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha inatenga fedha za kutosha kwa ajili ya kujenga ofisi mpya na nyumba mpya katika Halmashauri zote nchini zilizoanzishwa ikiwemo na Halmashuri ya Butiama ambako ndiko alikotoka Baba wa Taifa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa mama yangu na wamama wa Tanzania, Mheshimiwa Mama Amina Makilagi kama ifuatavyo:- (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali hili ni lazima nilijibu taratibu sana kwanza. Kweli hoja aliyoitoa Mheshimiwa Mama Makilagi ni ya msingi sana, ndiyo maana siku tulipokuwa tukihitimisha bajeti yetu ya TAMISEMI nilisema kwamba Halmashauri zile mpya lazima tuhakikishe tunaweka miundombinu na ni lazima nyumba zijengwe. Ndiyo maana katika kipaumbele chetu sisi cha TAMISEMI katika bajeti yetu ya mwaka huu, tuliziorodhesha zile Halmashauri ambazo ujenzi unaanza, lakini Halmashauri nyingine mpya hata ujenzi haujaanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu swali hili ni kubwa na zito na limetolewa na Mbunge mzito, niseme yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuliona hili tunaweka kipaumbele; kuna Halmashuri mpya zipatazo 20 tumezitengea kila moja shilingi bilioni 2,140,000,000 kila Halmashuri moja! Halmashauri hizo ni Buchosa, Bunda TC, Chalinze DC, Handeni TC, Ifakara TC, Itigi DC, Kasulu TC, Kibiti DC, Kondoa TC, Madaba DC, Mafinga TC, Malinyi DC, Mbinga TC, Mbulu TC, Mpimwa TC, Nanyamba TC, Newala TC, Nzega TC, Songwe DC na Tunduma TC. Hizi kila moja tumezitengea shilingi bilioni 2,140,000,000.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, kuna Halmashauri zipatazo 44 tumezitengea kati ya shilingi milioni 500 na shilingi milioni 850. Hii maana yake ni nini? Wajumbe mbalimbali inawezekana wakasimama hapa kutaka kujua juu ya hoja hiyo.
Nakala hii iko hapa, mtu anaweza akafanya reference katika Halmashauri yoyote ambapo mwaka huu tumeweka kipaumbele, lazima Ofisi ya Rais, TAMISEMI ihakikishe inajenga miundombinu katika maeneo hayo, ili mradi wafanyakazi waweze kupata huduma bora na waweze kupata mazingira rafiki ya kufanyia kazi.
MHE. HUSSEIN N. AMAR: Hussein Nassor Amar, Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Naibu Waziri wa TAMISEMI kwa majibu yake mazuri ya kwamba tumetengewa shilingi milioni 850 katika Halmashauri ya Nyang’hwale. Namuomba Mheshimiwa Waziri kwamba kwa kuwa kuna pesa ambayo imetengwa, shilingi milioni 80 kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi wenye eneo lile. Naomba amuagize Mkurugenzi zoezi hilo la kuwalipa wananchi lifanyike haraka ili ujenzi huo uanze kujengwa mara moja. Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, anayezungumza hapa ni Mbunge wa Jimbo hilo, maana yake yeye anayajua ya huko yalivyo na hizo pesa wameshatenga tayari. Hizo pesa kama zipo sasa, nadhani tusifanye ajizi. Namuomba Mkurugenzi haraka sana, kama vigezo vyote vimetimia, hakuna sababu kuwacheleweshea ulipaji wa fidia. Tunachotaka ni kwamba fidia ilipwe, ujenzi uendelee.
Mheshimiwa Naibu spika, kwa hiyo, moja kwa moja Mheshimiwa Mbunge ni kwamba tunamwelekeza Mkurugenzi wa Nyang’hwale ahakikishe kwamba kama kuna hiyo fedha imetengwa na ipo, watu walipwe fedha zao ili mradi hii kazi hii isiendelee kuchelewa tena kwa sababu ina maslahi mapana kwa wananchi wa Nyang’hwale.
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante sana. Napenda nishukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwa kuwa muuliza swali ametoka Bungeni humu na ameliacha swali hili, mimi naomba niulize kama ifuatavyo:- (Makofi)
Mheshimiwa Waziri, kwa kuwa wananchi wa Luchelele wamekuwa kwa muda mrefu sana wakiahidiwa kuhusu suala la fidia; na pale Luchelele kulikuwa na mpango mpaka kujenga kiwanja cha golf ambacho mpaka leo hii imekuwa ni hadithi; na hii mara kwa mara tunaambiwa kuna fidia italipwa, imechukua muda mrefu. Sasa Serikali imefikia wapi kwa suala la fidia ili kweli wananchi wa Luchelele walipwe fidia yao na Serikali iendelee na mpango wake wa Luchelele kama ilivyopangilia?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Wilaya ya Nyamagana inapanuka kuelekea sehemu za Luchelele na kwa kuwa mipango mingi kule inafanyika. Je, Serikali kupitia Wizara yako, ina mkakati gani kuhakikisha kwamba ile Luchelele na St. Augustine yote inaendelezwa kwa mpango na masharti ya Mpango Mji wa Jiji la Mwanza?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika majibu yangu ya awali nilisema kwamba wananchi hawa watalipwa fidia na taarifa zilizopo kama nilivyosema ni kwamba kuna mkopo kutoka CRDB. Status ya mkopo huo ni nini na tumefikia wapi mpaka sasa? Ni kwamba walipoleta ile request, katika ile shilingi bilioni sita, CRDB walikuwa wameweka commitment yao kuwakopesha shilingi bilioni 5.5. Kwa hiyo, ilivyokuja ile request TAMISEMI, ikaonekana kwamba deni linalodaiwa ni tofauti na mkopo watakaoweza kupata.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ikatakiwa clarification, ni jinsi gani pesa nyingine itaweza kupatikana hapo? Wakaandikiwa tena barua, Mkurugenzi wa Nyamagana ambayo ni barua ya tarehe 5 Mei, 2016 kumwambia kwamba alete mchanganuo huo sasa, ile tofauti ya shilingi bilioni 2.5 ambayo inatakiwa ku-top up na ile ambayo inatoka CRDB, kuona italipwa vipi na utaratibu wake utakuwaje?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, wakaleta hiyo feedback tena katika Ofisi ya TAMISEMI lakini hawakuambatanisha ule muhtasari wa vikao vilivyokubaliana hilo. Kwa hiyo, ofisi yetu imepeleka hiyo barua tena. Lengo ni kuleta zile attachments za makubaliano ya kikao ili mradi ofisi ya Rais, TAMISEMI iendelee na process ya kuhakikisha jambo hili linakamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili kuhusu mikakati ya kuendeleza Wilaya ya Nyamagana; kama nilivyosema watu wa Nyamagana mpango wao mkubwa ni kuhakikisha maeneo hayo yanapimwa. Tunajua wazi kwamba Jiji la Mwanza ni kubwa sana, ndiyo maana katika suala zima la uendelezaji wake, tunaelekeza hizi Halmashauri na Manispaa zetu ziweze kuweka utaratibu mzuri wa mipango miji.
Mheshimiwa Naibu Spika, nawashukuru sana watu wa Jiji la Mwanza, kwa sasabu kwa utashi wao mzuri na mawasiliano mazuri wamesababisha Jiji la Mwanza libadilike. Kwa kushirikiana na LAPF wametengeneza center nzuri sana ya kibiashara. Ni imani yangu kubwa sana kwamba mpango ule walioufanya LAPF na mikakati yao ya upimaji katika eneo la Nyamagana kuelekea maeneo haya ya Luchelele itaendelea. Lengo kubwa ni kulibadilisha Jiji la Mwanza liendelee kuwa bora, katika suala zima la kuendeleza Kanda ya Ziwa ya nchi yetu.

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nilitaka kuongezea tu katika majibu yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la uendelezaji wa Mji wa Mwanza kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameuliza, Jiji la Mwanza pamoja na Majiji mengine kama 14 yako kwenye utaratibu wa kupanga Miji yao kwa maana ya kuwa na master plan; na Jiji la Mwanza ni mojawapo na master plan yake inaandaliwa na wameshirikishwa vizuri. Kwa hiyo, hata hawa ambao wako Luchelele wamekuwa considered katika ile master plan ambayo iko katika process ambayo inaandaliwa. Baada ya muda mfupi nadhani kwenye mwezi Juni hii itakuwa imekamilika na watakuwa katika utaratibu mzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia katika suala la fidia siyo Luchelele peke yake, ni maeneo mengi labda kwa kutumia fursa hii pia niseme Wizara imejipanga katika kuhakikisha tunawakumbusha wale wote ambao Mashirika na Taasisi mbalimbali ambazo zinadaiwa wakimewo wenzetu wa Airport Dar es Salaam na maeneo mengine na hata yale yaliyochukuliwa na Jeshi. Tunawaandikia ili kuwakumbusha zile fidia waweze kuzilipa kwa sababu zimekuwa za muda mrefu na kadri zinavyokaa ndivyo jinsi gharama ya Serikali inavyokuwa kubwa hasa katika kupitia katika Mashirika yenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutalizingatia na tutaendelea kulifuatilia na watu wa Mwanza, Luchelele na maeneo mengine watafidiwa.
MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimwa Naibu Spika, hoja yangu bado iko pale pale kwamba pamoja na majibu mazuri ya Serikali na utaratibu mzima ambao Jiji la Mwanza unao sasa wa master plan ya miaka 20 ijayo lakini kama tunavyofahamu, pamoja na master plan bado kuna suala la fidia. Luchelele sasa ni takriban miaka kumi tangu wamethaminishwa na fidia wanaambiwa kila leo.
Mheshimiwa Naibu Spika, imefika hatua sehemu wananchi wanachoka. Sasa ukopaji wa fedha hizi umeanza muda mrefu; ulianzia TIB ukashindikana; umehamia CRDB; lakini ili fedha ziweze kupatikana CRDB ni lazima kibali cha Serikali kutoka TAMISEMI kipatikane. Sasa lazima tuliweke vizuri, ni lini Serikali itakuwa tayari kutoa kibali cha fedha ili Halmashauri ipate fedha iende kulipa fidia na mipango inayotarajiwa hata ya master plan ifikie kwenye wakati wake na ikubalike vizuri na wananchi? Nakushukuru sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, hapa ninayo barua ya tarehe 5 Mei, 2016. Barua hii inataka ufafanuzi kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Nyamagana. Lengo kubwa ni kwamba akisha-meet haya maelezo ambayo yameandikwa humu, tofauti yake ni nini? CRDB kama nilivyosema awali, walikuwa na uwezo wa kutoa mkopo wa shilingi bilioni 5.5. Kulikuwa na tofauti pale kidogo ambapo kulikuwa na maelezo ambayo yalitaka ufafanuzi zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya TAMISEMI tarehe 5 Mei ikaandika barua kwa ajili ya hayo maelezo, ambapo kwa mujibu wa barua hii, yenye kumbukumbu Na. CE.214/237/01/31 imani yangu kwamba Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza ataweza ku-meet hivi vigezo vya barua hiyo. Halafu mwisho wa siku ni kwamba Waziri mwenye dhamana ataipitia ile document. Lengo ni kwamba wananchi wa eneo hili ambao wanadai fidia, fidia yao iweze kufika.
Mheshimiwa Naibu Spika, najua ni kweli jambo hili la muda mrefu, lakini naamini kwamba vigezo hivi vikipita na vikifika kwa Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana, basi atalitolea maamuzi sahihi.
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Naomba niulize maswali mawili tu ya nyongeza. Kwa kuwa Mkoa wa Iringa hasa katika Wilaya za Kilolo, Iringa Vijijini, Isimani, Kalenga na Mufindi, miradi mingi sana ya maji imekuwa haikamiliki kwa wakati na kusababisha wanawake wengi sana hata ndoa zao zimekuwa hatiani kwa sababu ya baridi; wamekuwa wakiamka asubuhi sana kwenda kutafuta maji. Je, ni lini sasa miradi ile iliyopo katika Mkoa wetu wa Iringa, Serikali itafanya kwa uharaka zaidi, pamoja na kuponya ndoa za wanawake wa Iringa? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Wakandarasi wengi sana wamekuwa wakikamilisha miradi, lakini Serikali imekuwa haiwalipi madai yao kwa wakati. Je, ni mkakati gani umewekwa na Serikali kuhakikisha Wakandarasi hawa wanalipwa kwa wakati ili hii miradi iweze kukamilika kwa wakati?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote naomba kutoa pole sana kwa wale ambao ndoa zao zimeingia hatiani, mashakani kwa hiyo changamoto ya maji. Naomba niwasihi akinababa kwamba hawa akinamama msiwahukumu katika hilo kwa sababu wanachokifanya ni kuwatafutia maji watoto na ninyi akinababa wenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la kwanza ni kwamba lini miradi hii itakamilika? Katika vipindi mbalimbali nimeelezea hapa, ni kweli miradi mingi ya maji imechelewa kukamilika kwa muda na watu mnafahamu ile miradi ya World Bank hasa tuliyokuwa tukiitekeleza katika kipindi kilichopita ambayo mpaka sasa tunaendelea nayo, ni kwamba miradi mingi Wakandarasi waliweza kutoa vifaa kutoka site, ni kwa sababu Wakandarasi wengi sana wali-raise certificate lakini walikuwa hawajalipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto kubwa kama nilivyosema awali, ni kwamba, kwa sababu mwaka uliopita ulikuwa ni wenye changamoto kubwa sana, kwani fedha za miradi hazikwenda vizuri. Kama nilivyosema, katika Serikali hii ya Awamu ya Tano jukumu lake kubwa lilikuwa ni kukusanya kodi na mnafahamu kwamba tokea mwezi wa 12 mpaka hivi sasa, makusanyo ya kodi kila mwezi tumevunja rekodi ukilinganisha na kipindi kilichopita.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana certificate zote zilizokwenda katika Wizara ya Maji, zimelipwa na hata Naibu Waziri wa Maji juzi juzi hapa alikuwa anasema kwamba Mkandarasi yeyote mwenye certificate ambaye anatakiwa alipwe, afikishe haraka Wizara ya Maji pesa hizo zitalipwa. Ndiyo maana wale Wakandarasi wote waliokuwa hawajalipwa mwanzo, sasa hivi wote wamelipwa. Imani yetu kubwa ni kwamba sasa miradi hiyo itakwisha kwa sababu Wakandarasi wote wako site.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu madai yao kwamba ni lini yatalipwa? Ndicho nilichokisema hapa katika majibu yangu ya awali, kwamba sasa pesa zote za Wakandarasi wote zimeshapelekwa katika Halmashauri. Tunachohitaji ni kwamba zile certificate ambazo Wakandarasi wamelipa, Wakurugenzi wa Halmashauri wafanye haraka waweze kulipwa pesa zao ilimradi kwamba ile miradi iweze kukamilika na wananchi wetu waweze kupata huduma ya maji.
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Swali; je, wale Wakandarasi au Halmashauri zilizolipa pesa kwa Wakandarasi hewa, mtachukua hatua gani? Kuna miradi kadhaa katika Wilaya ya Nkasi ambayo pesa zililipwa lakini hakuna kilichofanyika.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA Mheshimiwa Naibu Spika, kama Mkandarasi amelipwa lakini kazi hajafanya, maana yake huo ni wizi; jambo la kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaambie na hili tumelisema katika vipindi mbalimbali, Wakandarasi wowote ambao kwa njia moja au nyingine wamechukua fedha na kazi wametelekeza, tutahakikisha, nami nitawaomba Wakurugenzi wote waweze kuwabainisha; hasa wale Wakandarasi wa maji waliotekeleza miradi katika maeneo yao. Kwa sababu tukirejea katika Bunge lililopita, Waziri wa Maji hapa alisema wazi kwamba Wakandarasi ambao watashindwa kutekeleza wajibu wao watafutiwa hata suala la kupata tenda katika nchi yetu. (Makofi)
Kwa hiyo, Mheshimiwa Keissy, naomba tukitoka hapa unipe rejea ya hao Wakandarasi ili mradi tuweze kuwafanyia kazi. Lengo kubwa ni kwamba, wananchi wetu waweze kupata huduma ya maji.

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, TAMISEMI, hoja ya Mheshimiwa Keissy ndiyo tumeshaanza kuifanyia kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Maji na Umwagiliaji tumeamua kuchukua hatua kwamba hatuwezi kupeleka hela kwenye Halmashauri mpaka walete certificate. Tumefikia hili kwa sababu hela zilikuwa zinapelekwa, halafu zinatumika, lakini ukienda kule hakuna kilichofanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyozungumza huko nyuma katika Bunge hili, ni kwamba tunakwenda kuunda Kamati ya Wataalam. Utaleta certificate yako kabla hatujailipa, tutatuma wataalam kwenye eneo twende tukaangalie kama hiyo kazi imefanyika ili tuweze kupambana na hili suala ambalo lilitaka kutupeleka pabaya.
MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini naomba niulize maswali madogo ya nyongeza. Kwa kuwa mfumo wa ugatuaji wa madaraka ulikuwa na lengo la kuwapa madaraka wananchi kuweza kuwa na maamuzi yao na kutekeleza masuala yao yanayohusiana kufuatana na mazingira yaliyopo; na kwa kuwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wamekuwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu hayo katika maeneo husika: Je, Serikali haioni haja ya kuupitia upya huu mfumo ili Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya ndio wabaki badala ya kuwa na Wenyeviti wa Halmashauri za Miji, Halmashauri za Wilaya pamoja na Wenyeviti wa Halmashauri za Majiji ambao kidogo wamekuwa wakiongeza gharama kwenye Serikali?
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili; kwa kuwa Ofisi za Wakuu wa Wilaya sasa hivi zimekuwa zikikabiliwa na upungufu mkubwa sana wa mapato na kwa sababu Serikali kuu imekuwa haina fedha za kutosha kuweza kuzipatia hizo Wilaya. Je, Serikali haioni haja kwamba Wakuu wa Wilaya sasa iwe ni sehemu ya kutegemea mapato yanayotokana na hizo Halmashauri ili waweze kuendesha majukumu yao na kusimamia sera vizuri katika maeneo husika?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimeelezea pale awali maeneo haya mawili; nafasi za Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kwa mujibu wa Katiba, Ibara ya 61 na ile ya Serikali za Mitaa Ibara ya 145 na 146.
Mheshimiwa Naibu Spika, wazo la Mheshimiwa Mbunge ni kwamba ikiwezekana basi hizi nafasi nyingine zitolewe. Kutokana na Katiba hiyo sasa zimekwenda kutungwa sheria. Kuna Sura namba 287 na 288, ambapo 287 inaelekeza katika Halmashauri, kuonyesha structure, jinsi gani kama Mwenyekiti wa Halmashauri, Diwani na kiongozi wa ngazi ya Kijiji anayechaguliwa ndiyo maana ya ile dhana kubwa ya D by D kushusha madaraka kwa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukisema uondoe hilo, maana yake umetoa dhana ya D by D. Kwa hiyo, maana yake ni Katiba sasa imetupeleka katika utengenezaji wa sheria ambapo leo hii kijiji kinahakikisha kina Mwenyekiti wake wa Kijiji na Mwenyekiti wake wa Vitongoji, wanafanya maamuzi katika maeneo haya.
Mheshimiwa Naibu Spika, hawa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya, jukumu lao kubwa ni kusimamia utaratibu na kanuni kuhakikisha kwamba unaendelea kama ilivyo. Kwa hiyo, kitendo cha kuondoa kimojawapo, maana yake, kwanza utakuwa umevunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini Sheria za Bunge ambazo zimewekwa humu kwa mujibu wa sheria itakuwa inaonekana hatuko sawasawa. Naamini kwamba mfumo tuliokuwa nao hivi sasa uko sawasawa. Kama kutakuwa na mawazo mengine, basi tutaendelea kuboresha kwa kadri siku zinavyoendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala hili la Wakuu wa Wilaya kwamba hawana mapato na mapato yao ikiwezekana yanayotoka kwenye Halmashauri ndiyo yangeweza kuwasaidia kufanya kazi zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo kubwa ni kwamba, tunajua Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa wakati mwingine wanakuwa na changamoto kubwa sana kwenye OC. Jukumu letu kubwa sisi kama Ofisi ya Rais ni kuhakikisha tunaziwezesha ofisi hizi. Kitendo cha mfano, hata hatukipendi sana, saa nyingine kitendo cha Mkuu wa Wilaya kwenda kuomba kwa Mkurugenzi kupewa pesa ya mafuta, mwisho wa siku anashindwa hata kuisimamia Halmashauri husika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hili ni jukumu la Serikali Kuu na sisi tutajitahidi, ndiyo maana tunasema kwamba tufanye collection ya mapato. Serikali Kuu inavyopata fedha za kutosha zitasaidia ku-facilitate kazi zake kwa Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa ziweze kufanya kazi vizuri.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Jafo, nataka niongezee majibu hayo katika swali lililoulizwa na Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga, Mbunge wa Vwava kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, amesema yeye angependekeza kwamba hawa Wenyeviti wa Halmashauri waondoke na badala yake, kazi zile kwa sababu zinafanywa kwa pamoja katika dhana ya ugatuaji wa madaraka kwenye Halmashauri, basi Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya hawa wachukue nafasi ile. Nataka tu niseme kwamba kusema ukweli hapa itakuwa imekiuka dhana ya checks and balances kwa sababu Wenyeviti ni Wawakilishi wa wananchi na wao ndiyo political figures kwenye maeneo yale, kwa maana ya uwakilishi wa wananchi per se.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya ni Wawakilishi wa Serikali Kuu. Kazi yao, pamoja na kazi nyingine ni kuziangalia hizi Halmashauri kama zinafuata sera, sheria za nchi, kanuni, taratibu na maagizo mbalimbali ya Serikali Kuu, pale chini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa wanamwangalia nani? Wanamwangalia huyu Mwakilishi wa wananchi ambaye yuko pale na wataalam wake hawa kuanzia Mkurugenzi na wataalam wengine kama wanafanya vizuri. Ndiyo maana tunasema, hakuna mwingiliano kwa sababu mwingiliano ni pale ambapo Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya anaingilia jambo ambalo linakwenda vizuri. Huo ni mwingiliano; lakini anapofanya intervention ya jambo linalokwenda vibaya ili sheria izingatiwe, hii inaruhusiwa kwa sababu ndiyo kazi yake iliyomweka pale. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka niongezee majibu haya na niwahakikishie kwamba mfumo wetu sisi Watanzania wa ugatuaji wa madaraka ni mfumo mzuri ambao nchi nyingi za Kiafrika zinakuja kujifunza hapa kwa sababu ni mfumo uliokaa vizuri na unasababisha amani na utulivu katika nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani tuendelee nao huu hadi hapo baadaye ingawa tunakubali kwamba huwa kuna reforms zimekuwa zikifanyika kuanzia mwaka 1982, mwaka 1992, mwaka 1998, lakini ipo haja ya kuendelea kuboresha lakini siyo katika eneo hili la checks and balances. Tutaharibu system nzima ilivyokaa.
MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naitwa Nkamia, ahsante. Najua umenikosea kwa sababu leo niko tofauti kidogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri nina swali moja tu la nyongeza. Wala sina tatizo lolote na Wakuu wa Wilaya, lakini kama Serikali Kuu inashindwa kumhudumia Mkuu wa Wilaya, anakwenda kuomba Halmashauri ambayo inaongozwa na Mkurugenzi, hiyo checks and balances inatoka wapi? Haoni kwamba Wakuu wengi wa Wilaya watakuwa ni ombaomba sasa kwa sababu OC wanazopata ni kidogo na matokeo yake wanaishi kwa kutegemea fadhila za Wakurugenzi?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kumekuwa kuna maelezo kwa baadhi ya maeneo kwamba Wakuu wa Wilaya wanawaomba mafuta Wakurugenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi formally yaani kupata taarifa rasmi kwa maana ya kwamba hilo linatokea na kwamba limekubalika, kweli jambo hilo halipo. Kwa hiyo, kama linatokea pengine ni kwa kesi fulani fulani tu, lakini kusema ukweli kwanza hatulikubali na haliruhusiwi kwa mujibu wa sheria. Pia kama linafanyika, linakiuka sheria. Kwa hiyo, niseme tu, siwezi kuridhia udhaifu huu mpaka tufanye utafiti tujue kweli hili jambo linatokea? Kama linatokea, nini tufanye kwa kuzingatia hili linalosemwa na Mheshimiwa Mbunge?
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani jambo hili siyo maeneo yote tuka-generalise kwamba sehemu zote inatokea, siyo kweli. Pia kama linatokea, linakiuka taratibu, kanuni na sheria za mgawanyo wa madaraka na majukumu na the principle of checks and balances.
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa zana ya D by D inaonekana bado haieleweki hata kwa sisi Wabunge; je, Serikali ina mpango gani wa kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ikiwemo sisi Wabunge na Madiwani?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli hii dhana imekuwa ni dhana ngeni, japo imeanza muda mrefu; lakini hata ukifanya rejea, wakati mijadala yetu katika bajeti mbalimbali za sekta unaona kwamba hata Waheshimiwa Wabunge, ile concept nzima ya D by D bado haijakaa vizuri. Leo hii tulivyokuwa tukijadili katika Wizara ya Elimu, tulivyokuwa tukijadili katika Wizara ya Afya, ukiangalia michango ya Wajumbe wengi sana dhana ya D by D haijakaa vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ndiyo maana hata katika kikao chetu tulivyokuwa tukifanya na Wizara ya Afya, Wataalam na sisi Viongozi Wakuu tulivyokuwa tukibadilishana mawazo tukasema ni vyema sasa dhana hii kwanza ikiwezekana iingie hata kwa watu walioajiriwa wa Serikali, wajue falsafa halisi ya dhana ya D by D. Maana yake katika Mpango huu imetupa changamoto pana.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tutaangalia jinsi gani tutafanya ili mradi hata Wabunge na Waheshimiwa Madiwani wote kwa pamoja na Watumishi wote wa Serikali wajue nini concept ya D by D? Nini maana ya dhana ya kurudisha madaraka kwa wananchi?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hoja yake ni ya msingi, nadhani tutaifanyia kazi kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba uelewa siyo mzuri sana kwenye dhana hii ya ugatuaji wa madaraka, nami napendekeza tu kwa sababu dhana hii ina maudhui makubwa sana katika msingi wa utawala wa nchi yetu. Inapokuwa haieleweki, inasababisha hata mijadala wakati mwingine kutoka nje ya context na pengine siyo kawaida kuonekana pengine mjadala huo anayetoa kwenye context ni mtu ambaye ana nafasi kubwa na kwamba jambo hili lipo kikatiba sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa napendekeza na pengine naomba kwa kupitia swali hili tuone utaratibu kwa sisi Serikali na Bunge; namna ya kufanya kwanza semina hata kwa Wabunge wote kabisa kwenye jambo hili. Mfanye semina na ikibidi kile Chuo chetu cha Uongozi ndiyo kije kituwezeshe katika jambo hili na kama tuna Wataalam ndani ya Serikali tunaweza tukatoa Watalaam, lakini kama kuna wataalam ndani ya Bunge, tutoe. Kwa sababu jambo hili kwa mimi ambaye ni mwanataaluma wa eneo hilo, napata nalo shida sana. Kusema ukweli context imepotea kabisa kwa sababu watu wanatafuta hata kwa upungufu fulani wanafikiri solution ni ku-centralize tena badala ya ku-decentralize. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nadhani tuone namna bora ya kuweza kufanya semina kubwa nzuri ya watu kupata uelewa juu ya jambo hili.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Kwa kuwa Wakuu wa Wilaya ndiyo Watendaji Wakuu ambao wanakutana na wananchi kwa karibu zaidi. Je, Waziri anaweza sasa kufanya mabadiliko badala ya kupeleka OC kwa RAS wakapeleka moja kwa moja kwa DAS ili kusudi waweze kufanya kazi zao vizuri zaidi?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba jambo hili tumeliona na pengine liko dhahiri sana. Kwa sababu kule kuna Mkuu wa Utawala katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya. Pia kuna Mkuu wa Utawala katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambaye ndiye RAS na huku anaitwa DAS ambao kazi yao na majukumu tofauti ni maeneo tu. Kwa hiyo, sidhani kama kuna ubaya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nilisema wakati wa majumuisho yangu siku ya bajeti yangu kwamba tunaangalia namna ya kuhakikisha kwamba OC hizi kwenye Wilaya zinapelekwa moja kwa moja, nasi tumekubaliana. Katika utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2016/2017, OC hizi kwenye Wilaya zitapelekwa moja kwa moja kwenye Ofisi za Ma-DAS ili na wenyewe waweze ku-manage pale kama wanavyoafanya Mkoani. Kusema ukweli tunalichukua wazo hili, ni zuri nasi tulishawekea mkakati wake, tutalitekeleza, ni jambo zuri sana.
MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nami pia niungane na Serikali kwanza kuwapongeza wananchi wa Kata za Mkumbi, Kata za Kipololo na Ukata ambao walikubali kupisha mradi huu kwa ustawi wa uchumi wa Wilaya yetu. Hata hivyo nitakuwa na maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa upana wa barabara hii, barabara hii inaanzia Mbinga Mjini inapita Litowo lakini pia inaunganisha na Wilaya ya Nyasa. Mfadhili amekubali kujenga kutoka Longa hadi Litoho; kuna kipande cha kilomita 15 kutoka Mbinga Mjini haji Kijiji cha Longa. Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kutumia nguvu zetu za ndani ili kukamilisha kipande hiki cha kutoka Mbinga Mjini hadi Longa chenye umbali wa kilomita 15?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, barabara yetu inayotoka Mbinga Mjini kwenda Hospitali ya Litembo kupitia Kijiji cha Tanga – Uyangayanga - Kindimba - Mundeki ni muhimu sana kwa vile Hospitali hii inatumika kama Hospitali yetu ya Rufaa. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuijenga barabara hii inayoelekea Hospitali ya Rufaa ya Litembo ili kurahisisha huduma za afya katika eneo hilo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nami nawapongeza sana wananchi hawa kwa sababu barabara hii ina Euro karibu milioni nne ambayo ukipiga mahesabu inaenda karibu shilingi bilioni kumi na eneo lile nadhani Mheshimiwa Mbunge anafahamu, kwanza kuna changamoto kubwa sana ya milima; lakini tumepata ufadhili mkubwa, kwa hiyo, hata zao la kahawa sasa watu watakuwa na fursa ya kuweza kusafirisha vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, ombi lake ni kwamba hiki kipande cha katikati cha kutoka Mbinga Mjini mpaka Longa ambacho kina kilomita 15 ni jinsi gani tutafanya sasa kipande hiki kiweze kuunganishwa? Mheshimiwa Mbunge, tumelisikia hili, lakini naomba michakato hii sasa ianze katika bajeti kuonyesha kwamba kuna uhitaji kutoka Halmashauri husika, nasi tutaangalia kwa pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, najua kwamba barabara hii, hiki kipande cha kilomita 15 bajeti yake itakuwa ni kubwa, lakini nadhani kwanza muanze kuangalia jinsi ya kufanya kwamba Halmashauri ionyeshe kipaumbele katika eneo hilo. Katika mchakato wa bajeti, Serikali itaangalia namna ya kufanya ili eneo hilo sasa liweze kupewa kipaumbele, angalau kipande cha lami kiweze kuunganishwa na mwisho Nyasa na Mbinga iweze kuunganika vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kusema kutoka Mbinga Mjini mpaka Kihesa ambako kuna Hospitali, wananchi wanapata huduma pale, vilevile naomba nirejee katika jibu langu la kwanza kwamba tuweke kipaumbele na Serikali haitasita kuona kwamba kwa sababu ni maeneo ambayo wananchi wanapata huduma hasa ya afya, nasema kipaumbele hiki lazima tukifanyie kazi.
Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi ile anayoendelea kuifanya na Madiwani wake, waweke katika mpango, Serikali itaujadili kwa kina na sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI hatutasita kushirikiana na Halmashauri ya Mbinga kuhakikisha maeneo haya yanapata huduma kama maeneo mengine.
MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Suala la fidia ambalo linawakabili wananchi wa Mbinga Vijijini katika kupisha ujenzi wa barabara ya lami, ndilo pia linalowakabili wananchi wa Jimbo la Mwibara ambako kuna barabara ya lami ya Nyamuswa – Bunda - Kisolia - Nansio inajengwa kilomita 50 kutoka Bulamba kwenda Kisolia.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri alitembelea ujenzi wa barabara ile akaahidi kwamba wananchi wale watalipwa fidia. Sasa nataka kupata majibu ya Serikali, wananchi wa Mwibara wategemee lini wataweza kulipwa fidia zao kwa nyumba zilizobomolewa na mashamba yaliyopitiwa na barabara ya lami? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikiri, kaka yangu Mheshimiwa Lugola amechomekea hapa vizuri sana. Kwa sababu barabara hizi zina sura tofauti. Hii barabara anayosema Mheshimiwa Kangi Lugola iko chini ya Wizara ya Miundombinu na huku tunazungumzia barabara ya Halmashauri ambayo ilipata ufadhili maalum.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikifanya rejea, siku ya Wizara ya Miundombinu, swali hili liliulizwa vizuri sana na Waheshimiwa Wabunge huko. Nadhani lilitolewa ufafanuzi kwamba Serikali itahangaika kutafuta fedha, pale itakapokuwa mambo yamekamilika, wananchi watalipwa fidia; kwa mujibu wa rejea ninayoifanya ya siku hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nina imani kwamba maswali yale au majibu yale yaliyokuwa yanafanyiwa rejea siku ya Wizara ya Miundombinu, yatabaki vilevile. Naomba nikiri wazi, Kangi Lugola kwa sababu ni mpiganaji mzuri sana, kilio chake kitakuwa kimesikika vizuri na Serikali.
MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, naitwa Alex Raphael Gashaza, ni Mbunge wa Jimbo la Ngara.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa barabara ya Murugarama Lulenge mpaka Mzani kilomita 85 iliahidiwa na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne mwaka 2012, lakini barabara hiyo imeahidiwa tena na Rais wa Awamu ya Tano wakati wa Kampeni mwaka 2015 na ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi, lakini katika bajeti hii ya 2016/2017 haipo kwenye bajeti, naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri, ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge tumeongea naye kwa muda mrefu, tulikutana na Waziri wa Ujenzi na baadaye tukaomba twende tukakutane na Katibu Mkuu. Kwa kweli anafuatilia sana ujenzi wa hii barabara. Namshukuru sana na naomba aendelee na juhudi hizo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kitu ambacho tulikuwa tumemwambia na naomba kurudia ni kwamba ahadi zote za Mheshimiwa Rais na ahadi za Viongozi wengine wote zilizotolewa na zile ambazo zimewekwa katika Kitabu cha Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa mwaka 2015 hadi 2020, Serikali hii ya Awamu ya Tano itazitekeleza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kilichotekea, kwa nini mwaka huu fedha hazikutengwa, ni kwa sababu tu tulitoa kipaumbele kwa zile barabara ambazo zilishaanza kujengwa na Wakandarasi wako site na Serikali inapoteza fedha kuwalipa watu ambao hawafanyi kazi. Tulitaka barabara hizi kwanza zikamilike, halafu kuanzia mwaka ujao wa fedha tutaanza kuingia katika maeneo mapya ambayo viongozi wetu wakuu waliahidi.
MHE. AMINA S. MOLELL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona na kunipa nafasi nami niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya kutoka Mkoa wa Arusha kwenda Chuo cha Mandela na hatimaye katika Vijiji vya Mlangarini, Nduruma na mpaka Bwawani Lusi ni barabara ambayo kwa muda mrefu imekuwa na kero. Tangu enzi za Elisa Molell akiwa Mbunge, Hatimaye Goodlucky Ole-Medeye mpaka sasa barabara hii kilio chake bado hakijasikikika. Je, Waziri anawaeleza nini wakazi wa vijiji hivi vya Mlangarini, Nduruma, Bwawani pamoja na Lusi kwamba barabara hii wataifikiria na kuweza kuijenga katika kiwango cha lami na hasa ukizingatia Chuo hiki cha Nelson Mandela ni Chuo cha Kimataifa na kinatarajiwa kupokea wanafunzi wengi kutoka nchi mbalimbali? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikiri wazi kwamba tumesikia kilio cha Mheshimiwa Amina Molell na Chama cha Mapinduzi kwa utaratibu wake, Mkoa wa Arusha ni miongoni mwa mikoa ambayo tumefanya intervention kubwa sana katika mradi wetu wa CSP Project ambao unafadhiliwa na World Bank. Sasa hivi Mji wa Arusha, Mbeya na baadhi ya miji, tumefanya vizuri zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii anayoizungumza Mheshimiwa Amina Molell, naomba niseme kwamba tumeisikia kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI na kwa kuwa pale kuna chuo kikubwa sana na vile vile hii ni ahadi yetu kwa wananchi hawa na lengo ni kuhakikisha lazima tunawahudumia. Serikali imesikia kilio hicho.
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; kuhusu uboreshaji wa elimu lazima tuzingatie mafunzo kazini kwa walimu. Sasa nataka niulize, Wizara ina mpango gani wa kufufua Vituo vya Walimu ambavyo vilianzishwa huko nyuma chini ya Mpango wa Kuboresha Elimu Ngazi ya Wilaya (District Based Support to Education(DBSPE) ambavyo kwa sasa hivi havitumiki. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili morale kwa Walimu ni muhimu sana katika kuhakikisha kwamba, dhana hii ya elimu bure inafanikiwa. Kwa hiyo, sasa nataka kujua kwamba, Serikali ina mpango gani kuhakikisha madeni kwa Walimu hayajirudii pamoja na kwamba, tupo kwenye sera ya kubana matumizi?
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba majibu ya maswali haya ya nyongeza.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunazo Teachers Resource Centers ambazo ni kweli zimekuwa zikisaidia sana katika harakati za kuanza kuwajengea Walimu taaluma ya kutosha katika kuhakikisha kwamba, wanafundisha masomo yao vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimwambie Mheshimiwa Chikota, kwamba Serikali katika mpango wake mpana wa sasa hivi; licha ya kufanya ukarabati wa maeneo mbalimbali katika shule kongwe pia itahakikisha kwamba vile vituo vinakuwa centers nzuri kama ilivyokula pale awali.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo kubwa ni kuhakikisha kwamba, vituo vile vinasaidia kuweka mbinu bora. Kwenye hii Sera mpya ya Elimu tutaweka mbinu bora kwa Walimu. Kwa hiyo, vituo vile vitaendelea kutumika vizuri zaidi, lakini vile vile TAMISEMI na Wizara ya Elimu tuna mpango mpana katika kuhakikisha kwamba, wanafundisha vijana wetu katika mazingira mazuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la morale kwa wafanyakazi hasa Walimu, suala la malimbikizo ya madeni, ni kweli na tumesema hapa, hata Waziri wa Elimu siku ile alipokuwa anahitimisha hoja yake alizungumzia jinsi gani madeni yaliyokuwepo mwanzo na madeni yaliyolipwa na madeni gani ambayo yako sasa yanahakikiwa ili waweze kulipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naomba nikiri wazi kwamba, madeni ya Walimu hayawezi kwisha kwa sababu kila siku ya Mungu lazima kuna Walimu wanakwenda likizo na lazima kuna Walimu ambao wakati mwingine wanahama kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, suala la dhana ya kulipa madeni mpaka ibaki sifuri kabisa, jambo hilo litakuwa gumu kwa sababu kila siku lazima kutakuwa na watu wanaendelea kudai. Jambo la msingi ni kwamba, ni lazima madai yanapojitokeza tulipe. Tukiri wazi kwamba Serikali ilijitahidi kwa kadri iwezekanavyo kuhakikisha Walimu hawa wanalipwa madeni yao.
Mheshimiwa Naibu Spika, si kulipa madeni tu, hali kadhalika sasa hivi tunapambana katika kuboresha mazingira ya Walimu wanaofanyia kazi hususani ujenzi wa nyumba ili Walimu hawa wajisikie wako katika mazingira rafiki ya kufanya kazi.
MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipatia fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa katika majibu ya msingi ya Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusiana na suala la elimu bure na changamoto ambazo zinakabiliana na suala hili, katika Wilaya ya Kigamboni, Wilaya ya Temeke na naamini katika Wilaya nyingi Tanzania, kuna changamoto kubwa sana ya Walimu hususani upande wa sayansi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Walimu hawa walikuwa wanagharamiwa kwa michango ambayo ilikuwa inakusanywa pale shuleni ambayo ilikuwa inalipia hawa Walimu wa part time. Serikali imesema imetoa mwongozo wa jinsi ya kusimamia suala hili, je, Serikali itakuwa tayari sasa kutoa maelezo ya mwongozo huo kwa Waheshimiwa Wabunge ili na sisi twende kuwasimamia zoezi hili kwa ukamilifu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama alivyosema kwamba, dhana ya elimu bure imekumbana na changamoto nyingi, lakini changamoto hizi ni changamoto za mafanikio. Kwa sababu kama mwanzo kulikuwa na suala la ulipiaji wa Walimu, vijana waliokwenda sekondari wanashindwa kwenda kusoma kwa sababu ya ada au michango mbalimbali. Nimeshuhudia sehemu mbalimbali zilizopita miongoni mwa vijana hao wengine walikuwa madereva wa bodaboda.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii na Wabunge ni mashahidi; naamini Wabunge wengi walishakopwa na kuombwa sana na wananchi wao kuwalipia watoto ambao matokeo yao hawakuweza kuyapata kwa sababu ya ada ya mitihani.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali baada ya kuyachukua madeni na katika mpango wake mkakati, hasa kama ulivyojielekeza kwa Walimu wa sayansi, ni kwamba mwaka huu katika suala zima la ajira; Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora siku ile ilivyozungumza, kwamba katika Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2015/2016 kulikuwa na tengeo kwa ajili ya Walimu ambao tulikuwa tunatakiwa tuwaajiri na kipaumbele kikiwa ni kuwaajiri Walimu wa sayansi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tukaenda mbali zaidi, kwa upande wa Walimu wa sayansi kuna wengine ambao wako nje ya system, lakini wana uwezo Serikali itaangalia kwa ukaribu zaidi namna ya kufanya ili Walimu wale waweze kutumika pamoja na wale ambao wamestaafu lakini wana uwezo wa kufundisha masomo ya sayansi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo tunaweza kuangalia vilevile vijana wetu waliosoma Bachelor of Science in Chemistry, Bachelor of Science in Physics, Statistics, au Bachelor of Science in Mathematics. Watu hawa hawaitwi walimu, ni watu waliosomea fani nyingine lakini akienda shuleni anaweza kufundisha. Ndiyo maana tumesema kwamba watu hawa tutawabainisha vilevile. Vijana hawa wengine wametembea mpaka soli za viatu zote zimekatika, hawaitwi Walimu lakini ni wataalam wazuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunakwenda katika mpango wetu mpana kabisa wa kuhakikisha jinsi tutakavyowaingiza vijana hawa katika utaratibu mzuri angalau wapewe hata short course ya teaching skills ili tuongeze idadi ya Walimu wa Sayansi na kuondoa tatizo hilo, kwa sababu tumejenga maabara nyingi hivyo lazima tupate Wataalam ambao watafundisha maeneo hayo. Nadhani hayo ndiyo maeneo ya kuweka msisitizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeipeleka katika Halmashauri zote miongozo yote ya Sera ya Elimu, kwamba kila eneo ada kiasi gani, gharama za ukarabati kiasi gani. Miongozo hii tumepeleka katika Halmashauri zote ili watu wapate ufahamu ile pesa inayopelekwa inaenda katika kipengele gani kwa sababu kila kipengele kimewekwa asilimia yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ningependa kuuliza swali dogo tu la nyongeza kwa Mheshimiwa Waziri. Kwa kuwa hapo nyuma, shule nyingi zilikuwa zinategemea sana michango ya wazazi ili iwasaidie katika kuweza kutoa mafunzo hasa katika zile fani ambazo hazikuwa na Walimu wa kutosha. Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza fungu maalum kwa ajili ya wale Walimu ambao watakuwa wanatoa mafunzo hasa ya masaa ya ziada baada ya ule muda wa kazi kukamilika?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwamba tutafanyaje katika kuongeza fungu maalum kwa ajili ya Walimu?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tunaanza, maana tumepata mahali pa kuanzia. Kama nilivyosema kwamba mgawanyiko wa fedha unapelekwa katika jinsi gani kugharamia elimu hii na naamini kama nilivyosema kwamba kila jambo lina changamoto yake. Jambo hili limekuwa na mafanikio makubwa sana na ndiyo maana kwa kadri tunavyoenda tunafanya tathmini vile vile ili kuangalia na changamoto zilizojitokeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, basi tutaangalia jinsi gani tutafanya, lakini lengo kubwa ni kuweza kuwaajiri Walimu ili waweze kutatua tatizo la upungufu wa Walimu hasa Walimu wa sayansi katika maeneo yetu.
MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nataka kujua, kwa kuwa sekondari nyingi sasa zina maabara na baadhi ya sekondari hizo kata zake zimekwishapitiwa na umeme, lakini Sekondari hazina umeme ni jukumu la Wizara au ni nani mwenye jukumu la kuingiza umeme kwenye shule hizo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge juu ya mchakato wa shule hizi za sekondari ambazo zina maabara. Ni kwamba katika mchakato wa utengenezaji wa bajeti za Halmashauri, Halmashauri inatakiwa itenge bajeti ya kutosha kwa ajili ya uwekaji wa umeme katika shule hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hata hivyo Waziri wa Nishati na Madini wiki iliyopita alizungumza wazi kwamba tutaweka kipaumbele kwa kupitia Wizara ya Nishati na Madini, kuhakikisha kwamba Halmashauri zinafanya hivyo. Pia Wizara ya Nishati na Madini itaweka kipaumbele ili shule hizi zote ziwe na umeme katika nchi yetu.
MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Raphael Michael, Mbunge wa Moshi Mjini ametoka nje, naomba nitumie nafasi hii kwa sababu swali alilouliza linafanana kabisa na suala ambalo liko Tabora katika Hospitali yetu ya Mkoa ya Kitete, naomba niulize swali kwa Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, Hospitali yetu ya Mkoa wa Tabora ya Kitete ina tatizo lile lile la mlundikano wa wagonjwa kama ambavyo iko Moshi Mjini. Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Hospitali ya Wilaya inajengwa Tabora ili kuweza kupunguza huu mlundikano wa wagonjwa?
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, Hospitali ya Mkoa wa Tabora ya Kitete ina upungufu mkubwa sana wa Madaktari, tuna Daktari Bingwa mmoja tu. Serikali inajipanga vipi kuhakikisha Hospitali ya Mkoa wa Tabora ya Kitete inapata Madaktari Bingwa wa kutosha?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, watu wanasema hata katika mpira vilevile, ikitokea mpira unapigwa golini halafu mtu kaondoka wewe piga goli tu. Kwa hiyo, naomba nimpongeze kwa hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Tabora ya Kitete aliyoizungumzia kwamba kwa sababu changamoto ni nyingi tuna mpango gani wa kuanzisha Hospitali ya Wilaya. Katika hili naomba nielekeze, tuweke vipaumbele katika Manispaa zetu kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Serikali iko tayari kabisa kushirikiana na wananchi wa Tabora ili kuhakikisha wananchi wa Tabora wanapata afya njema.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, napenda kuwashukuru wana Tabora kwa ujumla wao, kwa sababu nilipopita kule Tabora nimeona shughuli mbalimbali za kusimamia miradi. Nilitembelea Kituo cha Afya cha Itobo na kile kingine cha Bukene nimeona vifaa vya upasuaji vimewekwa kwa ajili ya akinamama. Kwa hiyo, juhudi zile wakati tukifanya mpango wa pamoja sasa kuimarisha Mkoa wa Tabora, kwa sababu tukiangalia sehemu ile hata watu kutoka Kigoma watakaopata matatizo wanaweza wakaja pale, ni vema kabisa tukaendelea kuweka nguvu. Katika mpango wetu mkakati wa Serikali kuimarisha Hospitali za Mikoa kupitia ule mradi mkubwa, nadhani tutaelekezana hapo baadaye jinsi gani tutafanya na Tabora ipewe kipaumbele kikubwa zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala la watumishi kwamba hatuna Madaktari Bingwa, bahati nzuri katika mchakato tutakaoufanya ni pamoja na kuhakikisha Madaktari Bingwa wanafika katika kanda mbalimbali. Imeonekana mara nyingi sana Madaktari Bingwa wanaishia katika maeneo ya miji mikubwa sana hasa Dar es Salaam. Katika maeneo ya pembezoni Madaktari Bingwa hasa madaktari wa magonjwa ya akinamama (gyno) wanakosekana.
Mheshimiwa Naibu Spika, hili nililigundua hata nilipofika katika Mkoa wa Singida, kuna hospitali nzuri lakini Madaktari Bingwa wamekosekana na hata nilivyofika Songea jambo hili nililiona. Mpango wetu ni kwamba kupitia Wizara ya Afya vilevile tutafanya mkakati sasa kuweka mipango vizuri ili Madaktari Bingwa waweze kufika maeneo mbalimbali ikiwemo na Tabora, lengo kubwa wananchi wetu wapate huduma bora.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, TAMISEMI, napenda kumthibitishia Mheshimiwa Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini kwamba, Tabora ni mojawapo ya mikoa tisa ambayo Wizara ya Afya imeifanyia tathmini kwamba inayo uhaba mkubwa wa Madaktari Bingwa pamoja na Mikoa ya Kigoma, Mara, Katavi, Rukwa na Simiyu. Kwa hiyo, tutakapopanga Madaktari kwa mwaka huu wa fedha, tutatoa kipaumbele kwa Mkoa wa Tabora na mikoa mingine nane.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niombe Madaktari wote na wataalamu wa afya ambao mnatarajia kuomba kazi Serikalini kwamba tutawapanga katika mikoa hiyo tisa ndiyo kipaumbele chetu. Kwa hiyo, kama wanataka kukaa Dar es Salaam wajue hatutachukua daktari ambaye anataka kukaa Dar es Salaam. Nakushukuru.
MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwa niaba ya wananchi wa Lupembe.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo lililopo Moshi Mjini na maeneo mengine ndilo ambalo lipo katika Jimbo la Lupembe, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Naomba kujua ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Lupembe kwa kuwa hatuna hospitali katika jimbo na halmashauri ile. Tuna vituo vya afya viwili tu na wananchi wengi wanasafiri umbali mrefu zaidi ya kilomita 80 kwenda kutafuta hospitali. Kwa hiyo, ni lini sasa Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya katika eneo la Matembwe?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, analozungumza Mbunge ni kweli, ule Mkoa wa Njombe ni mpya na nilipofika pale katika Hospitali ya Kibena nimekuta changamoto nyingi kwa sababu watu wote wanakuja katika Hospitali ya Kibena hata wa kutoka maeneo ya Mheshimiwa Mbunge ambapo imekuwa ni kero kubwa sana na nashukuru na Wizara ya Afya vilevile kupitia viongozi wake wakuu walifika pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kufanya katika eneo lile kunakuwa na Hospitali ya Wilaya, nadhani sisi kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI tumelisikia hili lakini nimsihi Mheshimiwa Mbunge mchakato wa ujenzi wa Hospitali hiyo ya Wilaya uanzie kwao kwa sababu kuna suala la kutenga eneo na kuweka kipaumbele hiki cha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Tukifanya hivyo na sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI hatutasita kushirikiana na wananchi na viongozi katika eneo hilo kuhakikisha wananchi wanapata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana jana Kamati ya Bajeti ilikutana na Wizara yetu na Wizara ya Afya, lengo kubwa ni kuweka mipango kabambe ya kusaidia suala hili ili wananchi wote wapate huduma nzuri. Katika mipango hii kabambe inayokuja sasa naamini kwamba Mheshimiwa Mbunge akijipanga vizuri katika Jimbo lake na najua kwamba amejipanga vizuri sana, tutahakikisha kwamba hii mipango ya pamoja inakwenda vizuri zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, jana Ofisi ya Rais, TAMISEMI tumetoa maelekezo kupitia kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri 181 katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, waainishe maboma ambayo hayajamaliziwa na changamoto mbalimbali ili Bunge hili lije katika mpango mkakati wa huduma ya afya katika ujenzi wa miundombinu. Kwa hiyo, namshauri Mheshimiwa Mbunge waanze kufanya ile needs analysis na kutenga eneo kwa ajili hiyo na tutaona ni jinsi gani tutashirikiana katika ujenzi wa hospitali hiyo.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa niliwahi kumlalamikia Mheshimiwa Naibu Waziri wakati tunakwenda Mpwapwa kwamba kuna vituo viwili vya afya ambavyo havijakamilika sasa ni miaka 10, Kituo cha Afya cha Mima na Kituo cha Afya cha Mbori na bajeti haijatengwa zaidi ya miaka 10. Je, unawaeleza nini wananchi wa maeneo hayo ya Mima na Mbori na kwamba vituo hivyo vitakamilika lini?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, siku tulipokwenda pale Mpwapwa nilipokuwa na Mzee Lubeleje nikawaambia watu wa Mpwapwa, Mzee Lubeleje huyu nimemwita kama greda la zamani lakini makali yaleyale, alikuwepo na sasa amerudi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nlipofika pale Mpwapwa tulitoa maelekezo kwamba licha ya hivyo vituo anavyozungumza lakini Hospitali yao ya Wilaya walikuwa hawajaanza kutumia mifumo ya electronic. Siku nne zilizopita nimekwenda Hospitali ya Mpwapwa na mimi mwenyewe nilikuwa mteja wa kwanza kukata risiti ya mfumo wa electronic. Kwa hiyo, Mzee Lubeleje namuunga mkono kwanza katika hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo nini tumefanya? Ndiyo maana nimeeleza toka mwanzo tuna maboma mengi yamekaa muda mrefu, mengine yamekaa miaka saba, mengine miaka nane, wananchi wameshafanya juhudi ya awali, ndiyo maana nimesema hapa jana Kamati ya Bajeti ya Bunge hili ilikaa na Ofisi ya Rais, TAMISEMI na Wizara ya Afya na jana tumeshatoa maelekezo kwenda kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri 181 waainishe maboma yote yamefikia hatua kiasi gani na yanahitaji fedha kiasi gani, lengo ni maboma yote haya yaweze kwisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, tukimaliza maboma yote tutakuwa tumepiga hatua moja kubwa sana. Imani yangu ni kwamba, haya maeneo mawili ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyasema ni miongoni mwa mambo ambayo tunaenda kuyafanyia kazi katika ule mpango mkakati mkubwa. Kwa hiyo, naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imejipanga katika hili na tunajipanga siyo Wizara ya Afya peke yake, siyo TAMISEMI peke yake halikadhalika Kamati ya Bunge ya Bajeti jana kikao hicho kilifanyika.
MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante.
Kwa kuwa bajeti ya 2015/2016 Serikali imeweza kupeleka asilimia 61.5 katika Wilaya ya Itilima; je, kulingana na makusanyo ya Serikali hivi sasa tunavyoona ina kasi kubwa ya kukusanya fedha nyingi, iko tayari kufidia asilimia 38.5 ya fedha ili kukamilisha miradi iliyobakia kwa 2015/2016? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa bajeti ya mwaka 2016/2017 ya Wilaya ya Itilima ina shilingi bilioni 10, hadi sasa Serikali inaweza ikaniambia katika quarter hii ya kwanza imepeka kiasi gani? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema pale awali kwamba katika Wilaya ya Itilima, Halmashauri ya Itilima katika kipindi kilichopita imepelekewa asilimia 61 na hili ni kutokana na hali mbalimbali tulipotoka katika kipindi cha mwaka wa fedha uliopita.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo naomba nikuhakikishie kwamba Serikali itahakikisha kwamba inasukuma juhudi kubwa sana, fedha zinazokusanywa zinapelekwa kwa wananchi ndiyo maana hivi sasa ukiangalia kwamba hata kuna miradi ile ambayo ilikuwa imepitiliza mwaka especially miradi ya maji Serikali imekuwa ikitoa nguvu ya kutosha kupeleka fedha katika maeneo hayo lengo kubwa ni kutekeleza miradi hiyo.
Mheshimiwa Spika, ni kweli katika bajeti ya mwaka wa fedha mwaka huu kwa mfano, wenzetu wa Itilima bajeti yao ya mwaka sasa hivi ni shilingi bilioni 10.2 lakini nikiri wazi kwamba katika katika hii bajeti ya maendeleo bado hakuna fedha yoyote ya maendeleo iliyoenda isipokuwa ni fedha za OC tu ambazo kiujumla wake katika Halmashauri mbalimbali tumepeleka hivi sasa karibuni shiingi bilioni 6.2 na Halmashauri ya Wilaya ya Itilima kwa OC ya mwezi wa Julai imepelekwa milioni 39, lakini lengo kubwa la Serikali kuhakikisha fedha iliyokusanywa iweze kupelekwa katika miradi ya maendeleo ili kukidhi yale makisio ya bajeti ya mwaka huu wa fedha yaweze kutekelezeka vizuri.
MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi hii. Kwa kuwa tatizo la kutokupelekewa fedha kwenye Halmashauri linajitokeza sana hasa Wilaya ya Bukombe na hasa fedha za barabara. Mji wa Bukombe, barabara zake nyingi zimekatika na tunaelekea kwenye msimu wa mvua.
Je, Waziri anawaambia nini wananchi wa Bukombe juu ya barabara hizi ambazo wakati wa msimu wa mvua tuna uhakika hazitapitika kama fedha hazitapelekwa kwa dharura?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli na naomba nikiri wazi kwanza siku zipatazo kama mbili Mheshimiwa Doto Biteko aliniletea request katika Halmashauri yake ikionesha miundombinu ya barabara hivi sasa ilivyoharibika kule katika eneo lake.
Mheshimiwa Spika, niseme wazi kwamba sasa hivi lengo letu kubwa ni Kuhakikisha kwamba yale maeneo ambayo yamekuwa korofi kwa sababu makusanyo yanaendelea kukusanywa tutaenda kuyafanyia kazi. Mheshimiwa Doto Biteko, naomba niseme kwamba lengo la Serikali na bahati nzuri hivi sasa unaona jinsi gani Serikali inakusanya misuli yake kwa ajili ya ukusanyaji wa mapato. Naamini katika bajeti ya mwaka huu tutaipa vipaumbele hasa katika suala zima la miundombinu ya barabara kwa sababu tunajua ndiyo itachochea uchumi wa wananchi wetu kuweza kusafirisha mazao yao kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine, kwa hiyo naamini kwamba katika jambo hili tutalipa kipaumbele katika Ofisi yetu ya Rais, TAMISEMI.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Tano imekuwa ikitoa taarifa za makusanyo kila mwezi na imekuwa ikijisifia kwamba makusanyo yameongezeka kwa kiasi kukubwa. Lakini ni ukweli kwamba katika Halmashauri zetu fedha hazifiki na hazipo kabisa.
Je, ni kwa nini Serikali haioni umuhimu wa hizo fedha ambazo mmekuwa mkisema mkizikusanya kwa wingi zikafika kwenye Halmashauri zetu nchini kwa sababu kule ndiko kwenye watu, ndiko ambako huduma inatakiwa kutolewa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba niseme wazi kwamba Serikali imekuwa na tumekuwa tukitoa taarifa kila mwezi kwamba kwa kipindi cha sasa Serikali katika makusanyo yake imejitahidi kwa kiwango kikubwa sana kukusanya fedha na makusanyo hayo ya fedha lengo lake mnakumbuka mwaka huu tuna bajeti takribani ya shilingi trilioni 29.54 na hii maana yake lazima fedha zikusanywe ili kwamba miradi iweze kutekelezeka.
Kwa hiyo, hayo makusanyo ya fedha yanayoendelea hivi sasa, imani yangu kubwa sasa hivi Serikali inajipanga kuna vipaumbele vingi ndiyo maana katika suala zima la awali kuna ile miradi ya maji ilikuwa inaendelea na wakandarasi wali-mobilise vifaa kutoka site na ndiyo maana kwamba katika eneo la kwanza la kipaumbele ukiangalia miradi mingi ya maji ambayo ilikuwa inaendelea, hivi sasa mingi inatekelezeka. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ukienda katika sekta ya miundombinu ya barabara, ninyi mnafahamu ni mashahidi, wale wanaotoka kule maeneo ya Tunduru wanakuta barabara kutoka Songea mpaka kule Mtwara kwenda Masasi pale, zamani mitambo ili-stuck pale ilikuwa haifanyi kazi, lakini Serikali imepeleka pesa hizi. Sisi watu wa Dodoma na watu wa Manyara wanafahamu, barabara kutoka Dodoma kwenda Manyara pale, hapa katikati kipindi kilichopita, Wabunge walikuwa wanalalamika, kazi ilikuwa imesimama, sasa hivi ukiangalia karibuni zote zinaenda. Serikali inakusanya hizi nguvu na nina amini miradi yote iliyopangwa katika mwaka wa fedha mwaka huu tutahakikisha inatekelezeka kwa sababu ni commitment ya Serikali ya Awamu ya Tano katika kipindi hiki cha bajeti.(Makofi)
MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Naibu Waziri na hasa wazo la ku-design nyumba moja ambayo itaweza ku-accommodate Walimu sita kwa maana familia sita. Sasa swali langu ni kwamba je, Serikali haioni sasa kwamba kuna umuhimu wa kusambaza hii ramani ya design hii ambayo nyumba moja inaweza ika-accommodate Walimu sita kwa Halmashauri zote na maelekezo maalum ili shule ambazo zipo vijiji sana Halmashauri ziweze kutumia ramani hii na kujenga nyumba? Kwa sababu ukiweza kujenga nyumba mbili tu maana yake tayari ume-accommodate Walimu 12?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikiri katika Jimbo analozungumza Mheshimiwa Mbunge na mimi nilikuwa kule. Aliponiagiza yeye mwenyewe nitembelee Jimbo lake; nikatembelea miradi ya afya na kuona mambo mengine na changamoto za miundombinu. Naomba niseme ushauri huu tumeshaufanyia kazi Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuhakikisha ramani hizi zinakwenda kila Halmashauri. Tunachokifanya ni kuhakikisha tunaweka mkazo sasa, bajeti yoyote inayopatikana lazima tuelekeze katika mfumo wa ramani mpya ambayo kwa kiwango kikubwa ina tija sana katika Halmashauri zetu kuhusu suala la kupunguza tatizo la upungufu wa nyumba za Walimu katika Halmashauri zetu.
MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa wananchi wengi wamejitolea kujenga maboma ambayo wamejitolea kujenga zahanati, nyumba za Walimu na mpaka sasa halmashauri hazijaweza kukamilisha. Je, ni lini sasa Halmashauri zitakamilisha miradi ambayo ni viporo ambavyo wananchi wameweza kujenga? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli maboma ni mengi na kumbukumbu yangu kati ya tarehe 12 na 13 nilikuwa kule Tabora katika Mkoa wako na nishukuru sana ushirikiano wako japokuwa ulikuwa na changamoto za kuuguliwa. Katika kupita huko huko katika Mkoa wa Tabora lakini na mikoa mingine tatizo la maboma limekuwa ni kubwa ndiyo maana katika maelekezo yetu tumeagiza kwanza lazima tumalize vile viporo vya mwanzo. Kama maboma ya ujenzi wa zahanati, nyumba za Walimu lazima tumalize hilo kwanza.
Waheshimiwa Wabunge, ndiyo maana mtaona katika maelekeo ya bajeti yetu itakayokuja ya mwaka mwingine wa fedha unaokuja, tutahakikisha suala zima la maboma sio suala katika sekta ya elimu peke yake hali kadhalika katika sekta ya afya tumalize hayo halafu ndiyo tuweze kuanza upya. Haiwezekani wananchi wamefanya nguvu kubwa za kutosha halafu nguvu zikapotea bure; Serikali imeliona hilo na ndio maana tuna mpango mkakati mpana sana kuondoa kero hiyo katika Jamhuri yote ya Tanzania.
MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Naomba kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kufanya bidii yote ya kutengeneza madawati kwa ajili ya watoto wa shule na kwa sababu madarasa hayatoshelezi kuna hatari ya madawati hayo kuharibika. Je, wakati haujafika sasa kuwa na mpango mzuri kama ulivyokuwa wa madawati kutengeneza madarasa hasa pale ambapo tunazingatia wananchi wameshajitolea kwa kiasi kikubwa? Je, ni mpango gani ambao Serikali unaweza ukaufanya ili tuwe na madarasa ya kutosha kuweka madawati ambayo tumeyatengeneza wote? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, kwanza naomba tuongeze juhudi kubwa za Watanzania; Mheshimiwa Rais alipotoa maelekezo kwamba tuondoe tatizo la kero wanafunzi kukaa chini na wengine kukaa katika mawe sasa watanzania tushirikiane kwa pamoja kutengeneza madawati.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri kwamba zoezi hili limefanikiwa kwa kiwango kikubwa sana lakini tulipongeze na Bunge lako hili kuhakikisha kwamba limeweza kutoa mgao wa madawati kwa Majimbo mbalimbali ili kuweza kupunguza ile kero ya madawati katika maeneo yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tatizo la kwanza ukipunguza maana yake tumetoa tatizo la wanaokosa shuleni, watoto elimu bure tumepata changamoto, tumepata madawati. Lakini sasa hivi tuna tatizo la vyumba vya madarasa hali kadhalika na vyoo, ndiyo maana katika mpango mkakati uliokuwepo hivi sasa katika bajeti hii ya mwaka wa fedha tunaoondoka nao tunaona kwamba kutakuwa na ujenzi wa madarasa katika maeneo mbalimbali na ujenzi wa matundu ya vyoo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, naomba niwahimize Watanzania wote, japokuwa Serikali itakuwa na mpango mpana sana kuhakikisha kwamba tunaondoa kero ya vyoo na kero ya vyumba vya madarasa hali kadhalika nyumba za Walimu kama nilivyosema awali, lakini niwaombe Watanzania tuendelee kushirikiana kwa pamoja vile vile kama tulivyofanya katika madawati, basi tufanye tena katika nyumba za Walimu na madarasa. Mwisho wa siku tukipata elimu bora, itakuwa ni kwa maslahi mapana ya nchi yetu. Ahsante sana.
MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Mji wa Sirari, Mji wa Nyamwaga na Mji wa Nyamongo, kwanza Mji wa Sirari una wakazi zaidi ya 40,000, Mji wa Nyamongo una wakazi zaidi ya 32,000, Mji wa Nyamwaga una wakazi zaidi ya 25,000 na hii ni miji ambayo imekua, ni mikubwa sasa kuna nyumba mpaka za milioni 600 pale, lakini kwa sababu tu haijakuwa surveyed wananchi hawawezi kutumia zile nyumba kukopa kama collateral ili waweze kuendesha biashara zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano Mji wa Sirari ulitamkwa kwamba ni Mamlaka ya Mji, hakuna Mkurugenzi, bado ni vijiji kwa kifupi tu na miji yote hii, sasa ni lini Serikali itaifanya ile miji iwe Mamlaka za Miji ili iweze kupanga hii miji na kuipima ili wananchi watumie nyumba zao kukopa benki waweze kukwamua maisha yao?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; sisi tunaishi mpakani mwa Kenya na Tanzania, upande wa pili tu pale mtu ana kiwanja square meters 2,000 anakwenda benki anakopa pesa anaendesha maisha, upande wa Tanzania mtu ana eka 20, 30, hawezi kukopa kwa sababu vijiji vyote havijapimwa. Ni lini Serikali itapima vijiji vyote vya Jimbo la Tarime wapatiwe hati za kimila ili waweze kutumia kwenye mabenki kuendesha maisha yao?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la kwanza kwamba ni lini sasa tutafanya mamlaka ya mji. Nakumbuka katika wiki hii nilijibu swali kwamba mchakato ule wa maeneo mbalimbali ambao vikao vya Madiwani na vikao vingine vya kisheria vimekaa na kufika katika RCC na kuja katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tulituma timu ya uhakiki katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu, kwa sababu Mji wa Sirari kama mapendekezo yake yalishafika maana yake ni sehemu mojawapo tunayokwenda kufanyia uhakiki. Kwa hiyo, nithibitishe kwamba ni mchakato unakwenda kwa sababu sija-specify katika eneo lako, lakini tumefanya zoezi hili kwa Tanzania nzima, lengo letu ni nini? Yale maeneo ambayo yanatakiwa kupandishwa hadhi sasa yatapandishwa hadhi kwa kufikia vile vigezo vyao vilivyofikiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala zima la upimaji. Ni kweli unaposema kwamba huku Sirari ni changamoto lakini upande wa pili imepimwa vizuri, ndiyo maana katika hili tumetoa maelekezo mbalimbali katika halmashauri zetu, waweke mipango mikakati mipana ya kuhakikisha kwamba wanapima maeneo yao. Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, hatukuishia hapo, tulichokifanya sasa hivi ni kuhakikisha kwamba tunatafuta funds kutoka maeneo mbalimbali, kupitia DFID sasa hivi katika maeneo yote ya mipakani, lengo letu ni kuweza kuyaboresha yawe mazingira rafiki yakiwemo maeneo ya Sirari. Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili litakapokamilika kupitia mradi huu mpana tutayaboresha na kuyapandisha hadhi maeneo yetu, maana yake ni nini, hata thamani ya ardhi katika maeneo yetu itakua na wananchi wetu wataweza kuhakikisha mazingira yao yanakuwa mazingira rafiki hata zile hati zitapatikana, maana yake hata investment ya huku Tanzania itafanana kuwa na investment shindani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa ndugu yangu Mheshimiwa Heche, naomba niseme kwamba tunaomba ushirikiano wa kutosha, pindi zoezi hili litakapokuja basi niombe halmashauri zote tutoe ushirikiano wa kutosha lengo kubwa ni kwamba tuki-invest pesa hizi pesa ziweze kuleta matunda mazuri. Kwa hiyo tufanye subira tu katika mchakato huu unaokuja kupitia DFID.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana na nimpongeze Naibu Waziri kwa maelezo ya swali la msingi. Tatizo la ujenzi holela wa miji katika Tanzania yetu inakumbwa na changamoto mbalimbali ikiwemo fedha, watumishi kwa maana ya Maafisa Mipango miji.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu takribani miaka sita tulikuwa tunatafuta fedha kwa ajili ya kuandaa mpango kabambe wa Master Plan ya Mji wa Mbulu na hatimaye kushindikana, hivyo ni kwa nini Serikali isifanye mapitio upya kuona rasilimali watumishi kwa maana ya wataalam wa Mipango Miji, fedha za kuhakikisha kwamba miji midogo na miji mikubwa inayopanuka inafanyiwa utaratibu wa mipango miji ili nchi yetu isikumbwe mara nyingi na bomoabomoa zinazojirudia mara nyingi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli na ndiyo maana hapa mwanzo nimezungumzia hii programu kubwa ambayo kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI tunaanza nayo hivi sasa na hii maana yake haitogusa maeneo yale ya pembezoni, isipokuwa yale maeneo ya mipakani kwanza ndiyo yatakuwa kipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunafanya hivi kwa nini, ni kwamba ukipita nchi mbalimbali, maeneo yaliyopangwa yatafurahisha hata unaposhuka katika ndege unapoona jinsi gani mji umepangwa vizuri na bahati mbaya sana katika maeneo yetu mbalimbali miji yetu imekuwa ikijengwa katika squatter na ndiyo maana tumetoa maelekezo hasa kwa Maafisa Mipango Miji wa maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, itakuwa haipendezi, kwa mfano, eneo kama la Kibaigwa ndiyo kwanza linakua na Afisa Mipango Miji yupo pale, anaacha tu ujenzi unaendelea, ndiyo sababu tumetoa maelekezo kwamba kila Afisa Mipango Miji ahakikishe kwamba kupimwa kazi yake na Wakurugenzi tumewaagiza hili, katika zile performance appraisal za Maafisa Mipango Miji wahakikishe jinsi gani wametumia taaluma zao kuhakikisha miji yetu inayokua inapangwa vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Serikali imejipanga tutatafuta funds, lakini vilevile tutatumia human resources tulizonazo kuhakikisha kwamba watu wetu wanawajibika. Hata hivyo, tunakiri kwamba Maafisa Mipango Miji bado wapo wachache tutajitahidi kutafuta uwezekano wa kadri iwezekanavyo kuongeza nguvu kazi hii ilimradi maeneo yetu yaweze kuwa maeneo rafiki kama nchi ya Tanzania ambayo inakwenda katika Awamu ya Tano ambayo inakwenda kwa kasi zaidi.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwa maeneo ambayo ameyataja, kwa mfano Iyoma, Mzase na Bumila kwamba kazi inaendelea. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari kufuatana na mimi kuona kama kazi hiyo imeanza? Hilo swali la kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Mji wa Mpwapwa ni mji wa zamani sana, una zaidi ya miaka 100 sasa tangu mwaka 1905 lakini vyanzo vya maji ni vilevile, kuna maji baridi na kuna maji ya chumvi, na kuna maeneo ambayo wanaweza wakachimba visima vya maji tukapata maji baridi ili wananchi wa Mpwapwa waweze kupata maji baridi. Je, Serikali iko tayari kutuma watafiti waende waanze kufanya utafiti ili kuongezea visima vya maji kwa Mji wa Mpwapwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Lubeleje, ambaye mimi namwita greda la zamani lakini makali yale yale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niko tayari, tena hata kipindi hiki cha Bunge tunaweza tukatoka Mpwapwa ni karibu hapa tukaenda kutembelea hapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, katika suala zima la kufanya utafiti, ni kweli, ukiangalia Mji wa Mpwapwa siku ile tumekwenda pamoja Mheshimiwa Mbunge, chanzo cha maji sasa hivi kimeelemewa na hata ile changamoto kubwa ni kwamba uharibifu wa mazingira ndiyo umekuwa ukiathiri sana suala zima la maji yanayopatikana katika Mji wa Mpwapwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, hivi sasa kuna watu wako site wanafanya utafiti maeneo mbalimbali lakini kwa uzoefu wako uliokuwa nao na kwa kushirikiana na watafiti hawa kuangalia jinsi gani tutafanya kwa pamoja kama Serikali, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Lubeleje, katika safari yetu ya pamoja tutaangalia, tutaonana na wataalam wa maji katika ofisi yangu kama sehemu ya awali. Mwisho wa siku ni kwamba watu wa Jimbo lako la Mpwapwa, lakini Halmashauri yote ya Mpwapwa kwa ujumla waweze kupata fursa ya maji kama Mbunge wao anavyowapigania.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa Jimbo la Mpwapwa linafanana kabisa na Jimbo la Mbulu Vijijini kwa ukosefu wa maji kwa eneo kubwa mno, je, ni lini Serikali itakuwa tayari kuja kuviangalia hivi vijiji na kata za Labay, Bisigeta, Maretadu, Endamilay, Endahagichan, Bashnet na Dinamu, ili kuzipatia visima virefu na wananchi wa Jimbo la Mbulu Vijijini kupata maji?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme wazi, nilifika kwa Mheshimiwa Mbunge takribani wiki nne zilizopita kutembelea katika jimbo lake. Nipende kumpongeza kwa harakati kubwa sana anazozifanya na mwezake Mbunge wa Mbulu Mjini. Naomba nikiri wazi kwamba kweli kuna changamoto ya maji na kwa sababu mpango wetu wa Serikali sasa hivi ndani ya miaka mitano kujielekeza tunahakikisha kwamba Mpango wa Maji katika Awamu ya Pili unafanyika vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili naomba niseme kwamba tutafanya kila liwezekanalo kutumia wadau mbalimbali kupitia bajeti hizi tulizokuwa nazo lakini kutumia fursa nyingine mbalimbali tunazozipata, lengo kubwa na ushahidi niliyouona nilivyofika site nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutashirikiana kwa pamoja kwa kadri iwezekanavyo kwa ajili ya wananchi wa Mbulu Vijijini.
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa tatizo la maji lililopo Jimbo la Mpwapwa linaonesha uhalisia wa ukosefu wa maji Tanzania nzima likiwepo Jimbo la Tarime Mjini, na kwa kuwa maji safi na salama ni muhimu kwa afya za binadamu; ni lini sasa Serikali ya Chama cha Mapinduzi itaona kuna umuhimu wa kuwapatia maji wananchi wa Jimbo la Tarime Mjini maji safi na salama kwa kutekeleza bajeti ambayo tuliipitisha hapa, ambayo bado hamjaanza kuitekeleza mpaka sasa hivi, ili wananchi wa Tarime Mjini na Tanzania kwa ujumla waweze kupata maji safi na salama?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, anachokisema ni kweli, tatizo la maji sio Tarime tu, ni nchi nzima, na ndiyo maana katika mipango ya Serikali tumejielekeza jinsi gani tutafanya kuhakikisha tatizo la maji tuweze kulipunguza. Hata sasa hivi katika halmashauri zetu ukiangalia, takribani shilingi bilioni 25 zimepelekwa ili miradi ya maji iweze kufanyika katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie kwamba sisi dhamira yetu ya dhati ni kuhakikisha katika bajeti ta mwaka huu ambayo Serikali inafanya mpango, utaratibu mzuri wa kupeleka hizi fedha, utafikia mahali pazuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Matiko asiwe na hofu katika hili, tutasimamia bajeti za Halmashauri, lengo letu ni kwamba ile bajeti ya karibu halmashauri zote na TAMISEMI, zaidi ya shilingi trilioni 6.4 ziweze kutekelezeka katika mwaka huu wa fedha. Na hili ni wazi kwa sababu mchakato wa ukusanyaji wa mapato unavyoendelea Serikali tuta-pump hizo pesa lakini sisi tuliopewa dhamana ya kusimamia tutahakikisha tunasimamia wananchi waweze kupata huduma ya maji.
MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ina vituo vya afya vitano ambavyo havina magari ambavyo ni Laela, Kayengeza, Msanadamungano, Mpuwi na Milepa, na Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga imejitahidi sana katika kuweka bajeti kwa mwaka 2013/2014, 2014/2015 ili kukabiliana na adha hii lakini Serikali haijatoa fedha ili halmashauri iweze kununua magari hayo. Sasa Serikali inaithibitishiaje halmashauri kwamba ikitenga fedha inaweza kuipatia ili iweze kununua magari kukabiliana na tatizo hilo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Mheshimiwa Naibu Waziri amezungumzia tatizo la msongamano wa wingi wa wagonjwa katika Kituo cha Afya Laela, na amezungumzia utatuzi wa tatizo hilo kwa mpango wa muda mrefu, wakati kwa sasa tatizo hilo ndiyo lipo na ni kubwa sana kutokana na wingi wa watu na kupanuka kwa mji mdogo. Nataka Serikali inieleze, kwa sasa inafanyaje mpango wa dharura ili kuokoa wananchi wanaosongamana katika kituo cha afya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mchakato wa bajeti unaokuja, naomba ninyi anzeni tu ule mchakato wa awali wa kuhakikisha kwamba mnatenga ile bajeti halafu sisi tutasimamia jinsi gani katika Bajeti ya mwaka 2017/2018 hilo gari liweze kupatikana, yaliyopita si ndweli tugange yajayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa msongamano wa sasa tulionao katika hospitali, nakumbuka Mheshimiwa Mbunge tulikuwa pamoja pale katika eneo lako. Kwanza wasiofahamu jimbo la Mheshimiwa Malocha, liko kama mbalamwezi hivi ambao mwezi mchanga, ambayo kuna watu wengine wanatoka maeneo ya Pembe mbali sana kuja katika Hospitali ya Sumbawanga. Kwa hiyo, mwenyewe nime-verify lile tatizo, ni tatizo la msingi na hili naomba nimwelekeze RAS wetu wa Mkoa wa Rukwa kwamba aangalie jinsi gani kwanza kama mpango wa haraka kuhakikisha eneo hili linapata angalau huduma katika sekta ya afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ni kweli, wananchi wa Mheshimiwa Malocha pale wakitoka kule Pembe mpaka kufika hapa kama mgonjwa anaweza akafariki. Kwa hiyo, naomba nikwambie ofisi yetu itawasiliana na ofisi ya mkoa pale tuangalie mipango mikakati ya haraka kuwasaidia wananchi wa eneo lako ilimradi waweze kupata huduma ya afya kama ilivyokusudiwa na Watanzania wengine.
MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Kwa kuwa swali la msingi hapa ni kituo cha afya; na kwenye Jimbo la Vunjo, Kata ya Marangu Magharibi yenye vijiji saba haina kituo cha afya wala zahanati hata moja, na mpaka sasa Mbunge kwa kushirikiana na wananchi wa kijiji cha Kitowo na Kiraracha tumeweza kufanikisha shilingi milioni 20, na KINAPA wanatupatia shilingi milioni 53 na tunategemea kujenga kwa shilingi milioni 200, commitment ya Serikali itatoa mchango gani ili Kata ya Marangu Magharibi, hasa Kijiji cha Kiraracha waweze kupata huduma ya afya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niwapongeze kwa ile initial stage ya wananchi wako, mmefanya resource mobilization pale mmeweza kupata karibu shilingi milioni hiyo ishirini na kwa ajili ya jambo hilo, nililizungumza katika vipindi mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumesema kwanza tumefanya tathmini ya nguvu za wananchi katika maeneo mbalimbali, kuna maboma mengi sana yamejengwa lakini yamefika katikati hayajakamilishwa, ndiyo maana tumewaagiza Wakurugenzi wote wa maeneo mbalimbali kuangalia zile juhudi ambazo wamefanya katika eneo lao, ili mradi katika bajeti hii ya mwaka wa fedha inayokuja tuhakikishe kwamba ajenda ya kwanza ni kukamilisha maboma na maeneo yote. Tukifanya hivi yale maboma ambayo yapo katika stage mbalimbali tutakuwa tumesaidia sana kuwapa support wananchi, lakini hali kadhalika tutakuwa tumejenga vituo vingi vya afya na zahanati tutapunguza tatizo la afya katika maeneo mbalimbali. Kwa hiyo nikushukuru katika hilo. Serikali commitment yetu ni kwamba tumeshafanya hilo zoezi liko katika ground linaendelea na katika mchakato wa bajeti hiyo ni priority yetu katika mpango wa fedha wa mwaka 2017/2018.
MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, katika jibu la Mheshimiwa Naibu Waziri suala zima la miundombinu; Mheshimiwa Rais alivyokuwa na ziara Mkoani Geita alitoa ahadi kwa wananchi wa Kasamwa kwa ajili ya kuwachangia pesa kujenga bwawa au lambo kama tunavyoweza kuliita. Lakini kazi iliyofanyika ni chini kabisa ya viwango na maji yale ni machafu, wananchi hawawezi kuyatumia. Na katika majibu yako pia katika hizi pesa ambazo zimetajwa hapa tumepata taarifa katika Kamati zetu kwamba Serikali haina pesa ya kutoa kwa ajili ya miradi ya maji katika sehemu nyingi hapa nchini.
Sasa naomba Serikali itoe tamko kwa wananchi ambao wana wasikiliza leo kwamba Serikali hii ina mkakati gani wa kuhakikishia wananchi kwamba wanapata maji safi na salama ambao wananchi wengi ambao ni wanyonge shida yao ni maji na sio bombardier? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali pili Mheshimiwa Rais Magufuli aliweza kutoa ahadi kwa wananchi wa Geita kuweza kuwapatia magwangala, lakini katika eneo la Nyarugusu ni kati ya maeneo ambayo yameathirika sana kutokana na uchenjuaji wa dhahabu na wananchi katika maeneo hayo hawana maji salama kutokana kwamba vyanzo vingi vimeathiriwa na mercury.
Serikali inatoa tamko gani kwamba pamoja na shughuli za magwangala ambazo Rais amezitoa kwamba wananchi wa Geita watapata maji salama ili waweze kuendelea na maisha yao? Ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, amesema kwamba Mheshimiwa Rais ametoa ahadi pale, lakini kazi inaendelea chini ya kiwango. Naomba nikuhakikishie kwamba tarehe 27/08 nilikuwa katika Mkoa wa Geita na nilifanya harambee kubwa pale tulipata karibuni 1.4 billion kwa ajili ya madawati katika Mkoa wa Geita. Hata hivyo, katika sekta ya maji kwa sababu ni kipaumbele changu, nilitembelea maeneo mbalimbali ikiwepo Chato na mradi mwingine nikazindua lakini na mradi mwingine ambao ulikuwa watu wamefanya mambo ya ovyo na kuunda kamati. Na hivi sasa tutaenda kuchukua hatua stahiki kwa wale watu wote waliokiuka utaratibu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nikwambie ni commitment ya Serikali kama sehemu ambayo umefanya ubadhirifu na mambo ya hovyo tutaenda kuyasimamia. Nikwambie kama kamati sasa hivi timu niliyounda tayari taarifa ipo mezani kwangu tunaenda kuchukua hatua stahiki kwa ajili ya wananchi. Kuna mradi mmoja wa Changolongo ambao umefanyika mambo ya ovyo, watu hawakufanya mambo sawasawa hata hiyo tunaenda ku-cross check. Lengo letu ni kwa wananchi wa Mkoa wa Geita na Mikoa na mingine waweze kupata huduma ya maji na hatutokuwa na masihara hata kidogo kwa watu ambao wanachezea kwa makusudi nguvu yoyote ya Serikali inayopelekwa halafu watu wakafanye mambo ya ovyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimwambie commitment yetu ipo hapo na Mkoa wa Geita tunaenda kuchukua hatua, lakini naomba niwaombe radhi sana kwa wale watu ambao hata wakiwa ndugu zenu tukiwachukulia hatua tunaacha sasa naomba tusileteane vi-memo tunaenda kuwachukulia hatua watu waliokiuka taratibu za manunuzi katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili; suala la kwamba kuna mercury wananchi wa Nyarugusu wanahakikishiwa vipi? Ni kwamba ni commitment ya Serikali na ndio maana hata nilipofika kule niliwaambia wataalam wetu wajiongeze. Haiwezekani Mkoa wa Geita ambao kuna Ziwa Victoria kila sehemu unakoenda unakuta maji wananchi wanakosa fursa ya maji. Tukawaambia kwamba waje na mpango jinsi gani tutafanya Mkoa mzima wa Geita kutumia fursa ya Ziwa Victoria badala ya kuchimba borehole, tupate vyanzo vya maji mbadala kutumia Ziwa Victoria na hili niliwaagiza watalaam wetu na hilo wanalifanyia kazi. Na nimewaambia nataka tulione katika mpango wa bajeti wa mwaka huu wa fedha unaokuja, lengo kubwa wananchi wapate fursa ya maji katika maeneo yao.
MHE. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Ni dhahiri kama Mheshimiwa Naibu Waziri alivyosema kuna shule 29 za sekondari ambazo ni nyingi kwa shule moja ya form five na six. Hiyo shule moja ya form five na six sasa hivi haipo tena, baada ya tetemeko la ardhi imeharibika kabisa na imefungwa. Sasa Serikali haioni kwamba umuhimu umeongezeka baada ya shule hii kuharibika kabisa kuharibiwa na tetemeko la ardhi, kwamba juhudi zifanywe za ziada kujenga shule ya form five na six?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa vile shule ya namna hii ni shule ya Kitaifa kwa nini jambo hili wanaachiwa halmashauri ndio washughulike nalo kutafuta fedha, kujenga wenyewe na isijengwe na Serikali Kuu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunajua kwamba, pale hali imekuwa ni mbaya na hasa katika ile shule ambayo imeporomoka zaidi, na hata hii Shule ya Lubale karibu nyumba mbili zimehaibika pamoja na baadhi ya madarasa. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali italiwekea hili kipaumbele. Na ndiyo maana katika Mfuko huu wa Maafa ya Mkoa wa Kagera maeneo ya elimu tumeyapa kipaumbele cha kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, ile shule iliyoharibika tutaijenga upya yote, lakini halikadhalika hii shule ya Lubale tutaweka nguvu kubwa sana kuhakikisha kwamba majengo yanarudi katika hali yake nzuri, ili vijana ambao wanasoma wapate elimu. Vile vile juhudi za Serikali kwenye janga hili ambalo limeupata Mkoa wa Kagera zitakuwa ni kupeleka nguvu za kutosha katika taasisi zote zilizopata uharibifu mkubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake linalohusu shule hizi kuwa ni shule za kitaifa na kwamba kwa nini inaachiwa Halmashauri? Ni kweli na ndiyo maana tumetoa maelekezo kwamba kila halmashauri ifanye hivyo kwa sababu wote tunaunga mkono nguvu moja nguvu ya Kitaifa na ndiyo maana hata mpango wa Serikali wa uwezeshaji wa shule mbalimbali mwaka huu ni kuhakikisha tunaboresha zile shule za Kitaifa, lakini pia kuongeza nguvu kwenye zile za wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo naomba nimpongeze sana ndugu yangu Mheshimiwa Rweikiza kwa juhudi kubwa anayoifanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika kwa upekee niwapongeze wananchi wa Mkuranga, nimpongeze Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Mkuu wa Mkoa wa Pwani pamoja na Mbunge wa Mkuranga kwa kuwahamasisha vijana wapatao 53 watengenezaji wa matofali mapya karibu 45,000. Naomba niwasihi Wakuu wote wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya, mambo haya ni mambo ya kuigwa tufanye hayo kwa ajili ya maslahi ya Taifa letu.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, Mheshimiwa Jafo nilipenda niongezee kwenye eneo lifuatalo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kisera kila Kata inakuwa na shule ya sekondari ya kidato cha kwanza mpaka cha nne, lakini kwa kidato cha tano na cha sita, shule hizi zina umaalum wake na ni lazima ziwe na vigezo ambavyo vimeelezwa kwa mujibu wa sheria na si lazima kila eneo kuwa na shule yake ya kidato cha tano na cha sita, Kwa sababu hakuna mtoto aliyefaulu kwenda kidato cha tano ambaye atakosa nafasi kwa shule zetu tulizonazo nchini; kubwa hapa ni ubora wa shule hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme tu kwamba Mheshimiwa Rweikiza kama wao wana mpango wa kujenga shule ya kidato cha tano na cha sita waje tutawapa vigezo vinavyotakiwa ili tusirudi kwenye makosa yaliyopita ili tuweze kujenga shule zenye sifa zinazostahili kwa ajili ya kidato cha tano na cha sita, kwa sababu hata tulizoanza nazo nyingine bado zina changamoto nyingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwa Waheshimiwa Wabunge na wawakilishi wa maeneo yote kuhakikisha kwamba tunapotaka kuanzisha shule ya kidato cha tano na cha sita basi vigezo vyote vile vya msingi vizingatiwe ikiwepo kwanza uwepo wa umeme, uwepo wa maji maeneo husika, majengo yanayostahili lakini na mazingira yanayoweza ku-accommodate masomo ya watoto wa kidato cha tano na cha sita.
MHE. AHMED A. SALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nashukuru sana kwa majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri yenye matumaini kwa wananchi wa Jimbo la Solwa na hasa Hospitali yetu ya Wilaya katika Kata hii ya Salamagazi, Makao Makuu ya Wilaya yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, hospitali hii imechukua muda mrefu, sasa imefika miaka karibu sita na nguvu ya Halmashauri yetu ilifika mahali ikawa haiwezekani kuikamilisha; na kwa kuwa tumeomba fedha hizi kwa muda mrefu; na kwa kuwa Serikali sasa imeahidi kulikamilisha: Je, fedha tunazozihitaji tunaweza tukazipata zote katika bajeti hii inayokuja ya 2017/2018? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Mheshimiwa Naibu Waziri, Jafo mdogo wangu, namwamini, naiamini Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Magufuli, yeye mwenyewe na Serikali yake yote kwa ujumla, anaweza akawa tayari kuja kutembelea hospitali hii akajionea hatua na nguvu ya Halmashauri yetu tuliyoiweka na kwa nini tunaomba fedha hizo ili Hospitali yetu ya Wilaya iweze kukamilika na kutoa huduma kwa wananchi wetu wa Jimbo la Solwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Ahmed kwa sababu amekuwa akizungumzia sana hospitali hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme wazi kwamba nami nilifika katika Mkoa wa Shinyanga, nimebaini changamoto zinazoukabili mkoa huu, hasa ukiangalia kwanza pale tuna Hospitali ya Mkoa, lakini ukiangalia katika eneo hili la Shinyanga Vijijini hakuna hospitali ambayo itaweza ku-accommodate idadi kubwa sana ya watu. Kwa hiyo, kinachotokea ni kwamba, wagonjwa wengi sana wanakwenda pale katika hospitali ile. Kwa hiyo, ni tatizo kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, katika mpango huu wa bajeti ya mwaka huu wa fedha tutahakikisha kwamba, zile shughuli za awali za kuhakikisha kwamba hospitali inasimama, tutajikita nazo hizo. Naomba nimtoe hofu kabisa, tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo. Leo hii asubuhi nilikuwa nafanya mawasiliano na Mkurugenzi kule Shinyanga Vijijini kuona jinsi gani wanajipanga na kuwapa agizo na sisi huku Serikali Kuu tuweke nguvu ya pamoja ili wananchi wa eneo hili waweze kupata huduma ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kiujumla ni kwamba Serikali itajitahidi kwa kadri iwezekanavyo; na katika mchakato wa bajeti nami nitatoa kipaumbele sana kwa sababu nimefika eneo lile, nimebaini changamoto na Mheshimiwa Mbunge muda mrefu alikuwa analipigia kelele eneo hili, lakini kwa bahati nzuri ni ahadi ya Mheshimiwa Rais ambayo wananchi wana imani kubwa katika hilo na kwa kuwa Mheshimiwa Rais ameahidi, lazima litekelezwe. Ni jukumu letu sisi Serikali kuhakikisha tunafanya, tusimwangushe Mheshimiwa Rais, ahadi ile iweze kutekelezeka na wananchi wapate huduma ya afya iliyo bora.
MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali la kuuliza.
Katika Kijiji cha Ushongo kilichopo Wilaya ya Pangani, wakazi wake wamejitahidi kujenga jengo la zahanati kadri ya walivyoweza hadi kufikia kiwango cha lenta, lakini kulikuwa na ahadi kuwa Serikali itamalizia jengo hilo pamoja na kuleta huduma muhimu ikiwemo wahudumu pamoja na dawa, mpaka sasa Serikali bado haijatimiza ahadi hiyo ikiwa ni takriban miaka mitatu sasa. Sasa Serikali itatimiza lini ahadi yake hiyo, hasa ukizingatia kijiji hicho hakina huduma ya usafiri wa umma? Wanatumia boda boda na gari za kukodi. Nashukuru sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme tumesikia suala hili, ndiyo maana hapa katikati tulizungumza kwamba tunafanya tathmini ya maeneo yote kwa majengo ambayo yamejengwa hayajakamilika na katika upande wa zahanati, tuna takribani zahanati 1,358 ambazo ukiangalia tuna bajeti siyo chini ya shilingi bilioni 78 kuweza kumaliza shughuli hizi zote.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikuhakikishie kwamba tulifanya assessment ile ili tuweze kujua nini tunatakiwa tukipange katika mpango wa bajeti tuweze kuondoa haya maboma na kujali juhudi kubwa zilizofanywa na wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Saumu na Waheshimiwa Wabunge wote, katika suala zima la magofu ambayo hayajakamilika yale ya zahanati na vituo vya afya sambamba na hospitali zetu za wilaya, tunaweka mpango mkakati kabambe ambapo tutawaomba Waheshimiwa Wabunge katika mchakato wa bajeti mtuunge mkono ilimradi tuweze kuondoa hivi viporo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naamini tukifanikiwa hata kwa asilimia 60 kwa hivyo viporo ambavyo vipo site huko, tutakuwa tumewezesha kwa kiwango kikubwa kuwapatia wananchi wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania afya bora na miundombinu ya ujenzi wa zahanati. Ahsante.
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza. Nimesikitishwa sana na maelezo ya Mheshimiwa Naibu Waziri pale alivyoeleza kwamba Manispaa ya Mtwara Mikindani imetenga maeneo kama vile Likonde, Mbae na Mjimwema.
Mheshimiwa Naibu Spika, ikumbukwe maeneo haya ni Tarafa mbili tofauti; na siku ya tarehe 21 mwezi wa Nane, Serikali iliweza kubomoa vibanda vidogo vidogo ambavyo vimejengwa katika Kata ya Jangwani, Tarafa ya Mikindani ambapo ni kilometa takribani 10 kwa maeneo aliyoyataja ambapo kuna akinamama wafanyabiashara wadogo wadogo wanauza samaki kihalali kabisa katika maeneo yale. Cha ajabu wale samaki wao wamevunjwavunjwa na kumwagwa. Akinamama wale walikopa pesa kutoka katika mabenki na taasisi mbalimbali za kifedha na mpaka hivi sasa ninavyozungumza hawana uwezo wa kulipa mikopo ambayo wamekopa.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni kwamba, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari hivi sasa afuatane na Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini ambaye anazungumza, aje kuangalia mazingira yale ambayo wale akinamama wamebomolewa maeneo yao ya kuuza samaki ambapo ni mbali takriban kilometa 10 kutoka eneo ambalo amelitaja yeye?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
himiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Maftaha yuko pale site; na hapa nimesema majibu ya msingi ya Serikali ni kwamba lazima Halmashauri zitenge maeneo. Hata hivyo, tumezielekeza Halmashauri kwamba, maeneo watakayotenga lazima waangalie kile kitu kinaitwa accessibility, yaani ni jinsi gani yatafikika? Ndiyo maana Halmashauri mbalimbali tumezielekeza kwamba ziwasiliane na SUMATRA katika maeneo hayo kwamba kuwe na uwezekano hata wa daladala ziweze kufika kwa sababu maeneo mengine unakuta watu wanashindwa kwenda kwa sababu daladala hakuna.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba, jana nilipokuwa nikijibu hapa maswali mbalimbali nikasema Mkoa wa Mtwara ni mkoa wangu wa kipaumbele, ni mkoa wa kwanza. Naomba niseme kwamba nimekubali ombi lake, tutakwenda site, lengo kubwa ni kuwasaidia hawa Watanzania wadogo wanaotaka kujikomboa katika suala la uchumi. Kwa hiyo, hilo, aondoe shaka ndugu yangu, mimi nitafika site, tutakwenda pamoja katika hilo.
MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nami naomba niulize swali dogo la nyongeza. Kutokana na sababu ya msingi kwamba tatizo la Machinga, yaani wafanyabiashara ndogo ndogo pengine linaweza kuwa endelevu, hasa kwenye Halmashauri zenye miji mikubwa ikiwemo Halmashauri ya Jiji la Mwanza ambayo ipo Jimbo la Nyamagana, napenda tu kuiuliza Serikali kwamba, pamoja na utaratibu huu mzuri ambao inaelekeza, Halmashauri zetu zimekuwa na changamoto kubwa ya kifedha. Je, Serikali sasa iko tayari kupitia Wizara ya TAMISEMI kuzisaidia Halmashauri kwa namna moja au nyingine kuweza kuboresha maeneo haya na yawe rafiki kwa hawa wafanyabiashara?
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mabula kwamba siku zote Ofisi ya Rais, (TAMISEMI) iko tayari. Ndiyo maana katika nyakati tofauti tumekuwa tukitoa maelekezo mbalimbali, lakini siyo maelekezo ya maneno peke yake, mpaka ya kiutaalam. Ndiyo maana kuna Halmashauri mbalimbali hivi sasa, wengine wapo katika suala zima la uwekezaji kupitia asasi mbalimbali lakini wanaleta madokezo mbalimbali na miradi yao pale Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), lengo ni kwamba tunayapima, yale ambayo yanaonekana kabisa kama jambo hili litasaidia Halmashauri lakini bila kukwaza Halmashauri hiyo kutokuingia katika mgogoro, tumekuwa tukizisaidia Halmashauri hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Stanslaus kwamba ofisi yetu sisi itashirikiana na Halmashauri zote. Tunajua kwamba zikipata uchumi wa kutosha zitaweza kujiendesha, zitapata own source ya kutosha, akinamama na vijana watapata mikopo, uchumi utabadilika. Kwa hiyo, sisi tupo tayari muda wote kuhakikisha Halmashauri zinafanya kazi zake vizuri.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, Mheshimiwa Jafo, nataka niongezee kwenye swali lililoulizwa na Mheshimiwa Mabula kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali inatambua ukuaji wa miji hii mikubwa na ongezeko la watu wengi wanaokimbilia mijini kwa ajili ya kutafuta riziki, ikiwemo na shughuli hizi zinazofanywa na wafanyabiashara wadogo wadogo. Hata hivyo, Serikali ina programu inayoendelea sasa ya miji mikubwa ya kimkakati ikiwemo na Mwanza ambapo tunatumia kiasi cha karibu shilingi bilioni 350 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kupanga vipaumbele hivyo, Halmashauri walihusishwa na walibainisha maeneo kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu hiyo. Namwomba tu Mheshimiwa Mbunge kwamba wajitahidi sana katika kuhakikisha kwamba watakapowapangia wafanyabiashara wadogo maeneo ya kufanyia biashara, basi wahakikishe kwamba mabasi madogo madogo yanayoweza kupeleka watu yanaweza kufika katika maeneo hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, ni kweli kwamba wamachinga au wafanyabiashara wadogo wadogo ni muhimu sana katika uchumi wa nchi yetu kwa sababu ni wengi na wanafanya shughuli ambazo zinasaidia uchumi wetu. Hata hivyo, niwasihi na niwaombe wajitahidi kufanya biashara katika maeneo yaliyopangwa. Kufanya biashara kwenye kila eneo ikiwemo barabarani na kuziba barabara ili watumiaji wengine wasitumie barabara, inaathiri shughuli nyingine za kiuchumi na kwa hiyo faida yao inakuwa haionekani kwa sababu inazuia shughuli nyingine za watu wengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, busara hii wakiwa nayo, pia busara hiyo hiyo ya wajibu wa Serikali kwa maana ya Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya kwa kushirikiana na Halmashauri zao kuwapangia maeneo mbadala yanayofikika na yanayofaa kwa biashara zao, jukumu hilo ni muhimu sana kufanywa na Serikali za maeneo hayo.
MHE. DEOGRATIUS F. NGALAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini bado tunauliza. Wadau mbalimbali wamekuwa wakichangia michango hii ya maji kwa karibu sana lakini Serikali imekuwa ikusuasua kupeleka hizi hela.
Je, Mheshimiwa Waziri ananithibitishiaje kwamba tutazipata fedha hizi kwa haraka?
Pili, kwa sababu wadau wa maendeleo wamekuwa wakileta ile michango na kazi inakuwa imeshafanyika, kutokana na Serikali kuchelewesha michango yao inakuta kwamba baadhi ya miundombinu inakuwa tayari imeshabomoka.
Je, Serikali inaweza ikagharamia ile miundombinu iliyobomoka kwa sababu ya kucheleweshwa kwa fedha?
NAIBU WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS-TAMISEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumze wazi kwa sababu Serikali kuna commitment ya shilingi milioni 50, na kwa sababu jukumu letu kubwa ni kuhakikisha miradi ya maji iliyotengwa katika kipindi hichi inaweza ikapata msaada wa haraka. Naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Deogratius, ofisi yetu itafanya kila liwezekanalo kuhakikisha tunasukuma pesa hii milioni 50, kama ni matching grands ya kuhakikisha mradi huo unatekelezeka, tutaweza kulifanya hili wala usihofu, mimi mwenyewe naomba nitoe commitment hiyo kama Serikali kuhakikisha jambo hili linakaa vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala zima kwamba miradi mingine imetekelezwa lakini mpaka imechakaa. Je, ni nini kauli ya Serikali kuhakikisha miradi ile sasa inarekebishwa kuweza kufanyakazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Deo kuwa tutakachokifanya kwanza ofisi yetu itawasiliana na Ofisi wa RAS Mkoa wa Njombe, kuangalia ni jinsi gani kama kuna miradi ambayo ina changamoto kubwa na kubainisha ni kitu gani kinatakiwa kifanyike. Kwa sababu mwisho wa siku, mradi kama umetekelezwa lakini mradi saa nyingine umeharibika kabla ya kuwapatia wananchi fursa hiyo ya maji ina maana tutakuwa hatujafikia malengo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Ofisi ya RAS Mkoa wa Njombe naomba niiagize kupitia mkutano huu, kwamba wahakikishe wanafanya follow up katika Jimbo hili la Ludewa kuangalia changamoto iliyokuwepo halafu tuangalie mkakati sasa, tutafanyaje ili mradi miradi hiyo iweze kufanya kazi. Lengo kubwa wananchi wako Mheshimiwa Deo waweze kupata fursa ya maji, na hiyo ndio azma ya Serikali kwamba kuhakikisha inawahudumia wananchi wake.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri hasa eneo la kutoa milioni 50 kwa ajili ya wodi ya watoto, nina maswali madogo mawili ya nyongeza. Swali la kwanza ni lini Serikali itaboresha wodi ya akinamama wajawazito pamoja na sehemu ya kujifungulia hasa ukizingatia hali ya sasa pale hospitalini, akinamama wanakaa katika mazingira magumu na wanalala watatu watatu? (Makofi)
Swali la pili la nyongeza; kama nilivyoeleza kwenye swali la msingi, Hospitali ya Wilaya ya Mbinga inahudumia Halmashauri nne, yaani Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa, Mbinga Vijijini, Mbinga Mjini na sehemu ya Halmashauri ya Songea Vijijini. Gari ambalo limetolewa na waterreed liko kwa ajili ya kitengo cha UKIMWI na linawasaidia wale wagonjwa wa UKIMWI tu, maeneo kama ya Mpepai kwenye zahanati na vituo vya afya Kihungu, Kilimani, Kigonsera, Mkumbi ambao hao wakipata mazingira magumu katika maeneo yao wanahitaji kuletwa katika hospitali ya Wilaya. Ni lini Serikali itatuletea gari la wagonjwa kwa sababu hilo lililosemwa hapa haliko kwa ajili ya kuwasafirisha wagonjwa wa hali ya kawaida, ni wale tu kwenye kitengo cha UKIMWI?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MTAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kujali afya za akinamama na watoto katika eneo hilo, nikiri wazi kwamba kwa umahiri wako nadhani tutafika vizuri. Naomba nimhakikishie katika suala la wodi ya akinamama na watoto kipaumbele cha Serikali hivi sasa ni kuimarisha afya za jamii hasa akinamama na watoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kumbukumbu yangu siyo muda mrefu tulikuwa na mkutano mkubwa sana hapa wa Madaktari wa Mikoa na Wilaya na bahati nzuri mkutano ule alikuwepo Makamu wa Rais wetu kama mgeni rasmi, mambo makubwa sana yameahidiwa pale. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mchakato wa bajeti wa mwaka huu unaokuja tutaangalia jinsi gani tutashirikiana nao kuhakikisha kwamba tunaweka kipaumbele katika wodi ya wazazi katika hospitali yetu ya Mbinga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika suala la gari la wagonjwa, ni kweli nafahamu katika hospitali mbalimbali siyo ya kwake peke yake isipokuwa hospitali nyingi sana changamoto za gari za wagonjwa zimekuwa ni kubwa. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Ofisi yangu itashirikiana naye kutafuta uwezekano wa aina yoyote japokuwa siwezi kuwaahidi hapa sasa, kwa sababu najua jambo kubwa sana linalotukwamisha ni ukomo wa bajeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango mkakati mpana ambao tunauandaa hivi sasa naomba tujadiliane kwa karibu zaidi jinsi gani tutafanya, lengo kubwa ni kuwasaidia wale watu ambao catchment area yake ni kubwa zaidi, tutafanya vipi kama Serikali, tukishirikiana na Mbunge na wadau mbalimbali kuwawezesha wananchi wa eneo hili kufika sehemu za referral ambazo zimekusudiwa katika eneo lake. Ahsante sana
MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza.
Kwa kuwa wananchi wa Kata ya Kitumbeini na Namanga, Wilayani Longido, Mkoa wa Arusha wamekuwa hawapati huduma ya afya, hakuna vituo vya afya imefikia hata wanavuka mipaka kwenda nchi jirani ya Kenya kwa ajili ya kupata matibabu. Je, Serikali ina mpango gani kuwasaidia wananchi hawa waondokane na tatizo hili ukizingatia Wilaya ya Longido haina hata hospitali ya Wilaya.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MTAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika nyakati mbalimbali nilikuwa nikirejea kwamba ni kweli katika vituo vya afya tunavyohitajika kuvipata sasa hivi bado tuna upungufu mkubwa sana.
Katika mpango mkakati wetu sasa hivi tumejielekeza kwamba at least kila Halmashauri tuweze kuwa na hospitali ya Wilaya na katika hili naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, nakumbuka jambo hili muda mrefu sana linapigiwa kelele na kweli haipendezi, katika eneo hili wananchi wanakosa huduma mpaka wanakwenda nchi za jirani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Serikali, lakini kama Halmashauri ya eneo hilo, nitaomba katika mchakato wa bajeti ya mwaka huu unaokuja kwa sababu tumeweka kipaumbele na kila Halmashauri tuna mpango mpana ambao tutakuja kuu-present baadaye hapa, at least tuwe na kituo cha afya katika kila Wilaya kwanza, kituo cha afya kimoja kimoja kwanza na umaliziaji wa magofu. Nadhani Wilaya ya Longido tutaipa kipaumbele hasa katika Kata ambayo ameikusudia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie, Serikali haitawatupa na iko tayari kushirikiana na wananchi wa Longido na kushirikiana na Mbunge ambaye yuko mahiri kutetea eneo hilo.
MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu haya yaliyotolewa na Mheshimiwa Naibu Waziri. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, watoto wa kike wanahitaji faragha na hasa wanapokuwa katika siku zao. Kwa hali hii iliyopo hivi sasa ni tatizo kubwa kwa watoto wa kike. Je, Serikali inachukua hatua gani za dharura kuhakikisha kwamba angalau tunawapatia unafuu watoto wa kike na hasa ukizingatia kwamba shule nyingi pia hazina maji kwa mtoto huyu wa kike inakuwa ni vigumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; je uwiano huu wa 52 kwa 54 na 23 kwa 25 kwa shule za sekondari umezingatia kwa kiasi gani hali ya watoto wenye mahitaji maalum, watoto wenye ulemavu ambao wanalazimika kutambaa katika kinyesi cha watoto wenzao?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MTAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwa sababu ni changamoto kweli hasa watoto wetu wa kike kuna wakati fulani wanataka faragha ya hali ya juu kuwawezesha kusoma katika mazingira rafiki na hili ndiyo maana nimesema kwamba katika yale matundu ambayo tunayajenga 8,991 kwa shule za msingi na yale 1942 kwa shule za Sekondari kipaumbele ni matundu ya vyoo vya kike.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tuna mradi wa MMES II ambao katika shule za sekondari tunajenga takriban matundu yasiyopungua 9,345. Katika haya maelekezo yetu ni kuhakikisha hasa katika shule za sekondari tunaweka nguvu kubwa tuweze kuondoa kabisa tatizo hasa la vyoo vya kike, kwa kujua kwamba, hili jambo ni muhimu sana kwa ajili ya utulivu wa watoto wetu hasa wa kike wanapokuwa katika yale mazingira ambapo hakuna namna lazima wapate mazingira yenye staha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika suala la walemavu ni kweli, katika kipindi cha nyuma kilichopita kwa muda mrefu tulikuwa hatuna kipaumbele cha kutosha katika ujenzi wa miundombinu yetu hasa katika maeneo ya walemavu. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Amina Molel, katika vyoo vyetu vya sasa vyote vinavyojengwa suala la vyoo kwa watu wenye mahitaji maalum ni kipaumbele chetu cha msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa katika maeneo mbalimbali tunakopita na jana nilikuwa katika shule moja ya Chang‟ombe „B‟, tunaenda kujenga karibuni vyoo 20 lakini kipaumbele tumesema katika ujenzi ule ramani zote zinaelekeza watu wenye mahitaji maalum hasa walemavu ili kuhakikisha ujenzi wote unaofanyika sasa hivi uweze kuligusa kundi hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Amina Molel nimhakikishie kundi ambalo analiwakilisha vema humu Bungeni, tutahakikisha tunalipa nguvu ya kutosha na kuhakikisha kwamba haki zao zinapatikana kwa muda wote katika kipindi cha utawala huu.
MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana. Nami naomba niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa, hili tatizo la matundu ya choo hasa shule ambazo ziko pembezoni, shule za vijijini siyo rafiki sana na watoto wa kike pamoja na wanafunzi kwa ujumla. Ni lini Serikali itahakikisha tatizo hili la matundu ya choo linakwisha mara moja?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MTAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la dada yangu Maryam Msabaha Mwanajeshi kutoka kambi ya Bulombora kule Mkoani Kagera kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema awali kwamba mpango mkakati wa Serikali ni kuhakikisha kwamba tunatatua tatizo la vyoo kama Mheshimiwa Molel alivyoanza na swali hili. Nilipopita maeneo mbalimbali kwa mfano takriban wiki moja na nusu nilikuwa katika Wilaya ya Kakonko, Buhigwe na maeneo mengine kule, nilipita katika maeneo hayo nikikagua hata baadhi ya miundombinu ya vyoo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tuna kila sababu, ndiyo maana tuna mpango mkakati mpana sana. Tumetenga fedha karibu bilioni 12, lengo kubwa ni investment katika kuondoa kero hii. Naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge, Serikali kwa umoja wake lakini vilevile na wadau mbalimbali niwashukuru sana, katika kipindi hiki tumeweza kushirikiana vema kwa sababu baada ya kuondoa ajenda ya tatizo la madawati, sasa hivi Serikali na wadau mbalimbali tumejielekeza katika vyoo na vyumba vya madarasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, imani yangu ni kwamba ndani ya muda mfupi tutaona mazingira makubwa sana yamebadilika katika sekta ya elimu katika Jamhuri yetu ya Muungano wa Tanzania.
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwaa Mwenyekiti, nakushukuru. Tatizo la vyoo katika shule zetu za msingi linafanana na tatizo la nyumba za Walimu kwa shule zetu na tatizo hili sasa hivi kama limeachiwa Halmashauri ndiyo watatue tatizo hili, lakini kwa mapato ya Halmashauri nina uhakika mkubwa kwamba tatizo hilo haliwezi kupatiwa ufumbuzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumuuliza Naibu Waziri kwamba Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo hili katika kipindi kifupi kijacho?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MTAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niweke wazi kwamba Serikali kwa sasa imejipanga vema. Imejipanga vema kwanza hata ukiangalia mchakato wa bajeti ya mwaka huu tumemaliza madawati, lakini tumetenga takriban bilioni 13 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba katika shule za msingi na bilioni 11 katika shule za sekondari. Tukishirikiana TAMISEMI na wenzetu wa TEA jambo hili tumekuwa na mkakati mpana sana, lengo siyo nyumba za Walimu peke yake, bali ni madarasa, nyumba za Walimu, maabara na kufanya mpango kabambe wa ukarabati wa shule kongwe. Mwaka huu peke yake, shule kongwe 33, kila shule tunaipatia bilioni moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo letu, Watanzania waone kwamba, Serikali ya Awamu ya Tano, ina lengo la kuweka msukumo wa mbele katika kuboresha elimu yetu ya Tanzania.
MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri sana nina swali dogo tu la nyongeza. Kwa kuwa, yapo maeneo machache viongozi hawa hawashirikishwi kikamilifu kutoa ushauri wa vifungu sahihi kwa matumizi kama ilivyoanishwa kwenye bajeti na kuathiri taarifa za fedha na kutekeleza hoja za ukaguzi. Je, Serikali iko tayari kutoa waraka, kusisitiza ushirikishwaji wa viongozi hawa wanaosimamia rasilimali fedha ili kuleta tija katika matumizi ya vifungu vya bajeti na kuboresha hesabu?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimpongeze kwa namna ambavyo amekuwa akifuatilia matumizi mbalimbali ya rasilimali fedha, lakini niendelee kukumbusha tu kwamba mamlaka za ajira pamoja na menejimenti katika taasisi zote za umma, zinatakiwa kuhakikisha kwamba zinatumia fedha za Serikali kwa mujibu wa taratibu pamoja na sheria mbalimbali za kifedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niendelee kusisitiza kwamba ni lazima waweze kushirikisha wakuu wote wa Vitengo, Wakuu wote wa Idara, katika menejimenti na vikao ili na wenyewe waweze kupata uelewa katika namna ambavyo mipango kazi ya taasisi inavyotekelezwa, pia waweze kutoa ushauri wao ni namna gani wanaweza kuhakikisha kwamba wanatekeleza majukumu yao bila kuathiri taratibu mbalimbali za kifedha na sheria zinginezo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Kwandikwa kwamba, kweli tuko tayari na baada ya kutoka tu hapa tutashauriana na Waziri wa Fedha ili kuona ni kwa namna gani sasa waraka unaweza ukaandaliwa, vilevile kwa upande wa utumishi kuweza kukumbushwa masuala haya.
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, ninashukuru. Nilitaka kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa shilingi bilioni 5.2 ni sawa sawa na mapato ya ndani ya Halmashauri kwa zaidi ya miaka mitatu, na kwa kuwa Halmashauri ya Mji wa Nzega haina uwezo wa kifedha na ndio ilikuwa mantiki ya kumuomba Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete na baadaye Rais John Pombe Magufuli kwamba miradi hii ya ujenzi wa kilometa 10 iende chini ya TANROADS.
Je, sasa Serikali iko tayari kuwaambia wananchi wa Jimbo la Nzega kwamba miradi hii ya kilometa 10 itajengwa chini ya utaratibu wa TANROADS na si kwa kutumia fedha za Halmashauri ya Mji?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli nafahamu Halmashauri ya Mji wa Nzega mapato yake ni madogo, na Mheshimiwa atakumbuka takribani wiki tatu na nusu au wiki nne tulikuwa wote kule Nzega tukihamasisha shughuli za maendeleo. Nipende kumshukuru sana kwa juhudi kubwa anazozifanya katika Jimbo lake
Mheshimiwa Spika, naomba nikuhakikishieni kwamba hii ni commitment ya Serikali na ahadi ya Mheshimiwa Rais. Katika hivi ukiachia hata huo uchache wa mapato, hata ujenzi wa miundombinu katika maeneo mengine tunayoyafanya hivi sasa si kwamba Halmashauri hizo zinauwezo huo.
Mheshimiwa Spika, si muda mrefu tutaanza mchakato hata katika Mji wa Mpwapwa na maeneo mengine mbalimbali hapa nchini. Naomba nisema wazi Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa makusudi imeamua kubadilisha miundombinu ya Manispaa na Majiji ya maeneo mbalimbali, na ndiyo maana utakuta katika miji mikubwa, Manispaa na Halmashauri za Miji sasa hivi mitandao ya barabara imeimarika.
Mheshimiwa Spika, bahati nzuri Mheshimiwa Bashe amepata fursa kubwa, ambapo Mamlaka ya Mji wake vile vile tayari umesha-qualify sasa kuingizwa katika mipango ya ujenzi wa barabara za lami. Kwa hiyo, naomba nimtoe hofu, Serikali itahakikisha ahadi ya Mheshimiwa Rais inatekelezwa, tunajua mapato yenu ni madogo. Lakini pia ni commitment ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI kuhakikisha kwamba miji yote inajengewa barabara za lami. Ondoa hofu Serikali itatekeleza hilo kwa kadiri iwezekanavyo.
MHE. KANALI (MST.) MASOUD ALI KHAMIS : Mheshimwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nilikuwa naomba kuuliza swali la nyongeza.
Je, mabasi haya yana idadi maalum ya kupakia abiria na kama hayana idadi ni kwa nini?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza tuna mabasi ya aina mbili, yale mabasi marefu zaidi na mabasi mafupi, na mabasi haya kila basi lina idadi yake.
Kwa hiyo, nimuondoe shaka Mheshimiwa Mbunge, mabasi haya yana idadi maalumu isipokuwa wakati mwingine katika vituo mabasi yakifika watu huwa wanakimbizana kuingia ndani ya mabasi.
Mheshimiwa Spika, utaratibu umewekwa kuhakikisha kuwa watu wanapanda mabasi hayo kwa kuzingatia idadi yake ili kulinda usalama wa raia katika suala zima la usafiri.
MHE. PROSPER J. MBENA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi hii ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na napenda kumpa taarifa kwamba tayari vikao hivyo vimeshafanyika na tayari mkataba kati ya Kanisa Katoliki pamoja na Halmashauri ya Wilaya Morogoro umeshakamilika na nitampatia nakala ya mkataba huo. Baada ya hatua hiyo kufikiwa. Je, Mheshimiwa Waziri sasa atashughulikia lini? Itachukua muda gani kushughulikia suala la kupatikana kwa watumishi pamoja na kada nyingine zinahitajiwa kwa hospitali hiyo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu kama mchakato huu tayari umeshaanza, basi ina maana kwamba walikuwa mbele ya tukio zaidi. Kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni jukumu la Serikali sasa kwamba mara baada ya mchakato huo kukamilika, sasa ni kuangalia kipi kinachohitajika katika eneo lile hasa tukitoa kipaumbele katika suala zima la watumishi kama alivyozungumza. Kuhusu lini, naomba niseme ni katika kipindi kifupi kijacho. Kwa kuwa lengo letu kubwa ni kuhakikisha kwamba tunaongeza kada katika maeneo mbalimbali, basi Wilaya yake tutaipa kipaumbele hasa katika eneo hili ambapo nami nilifika kule katika Wilaya yake nikaona kwamba ni kweli, wananchi wanaotoka kule Mvuha mpaka kuja Morogoro Mjini ni kilomita nyingi zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tuna kila sababu ya kuiwezesha hospitali hii. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni commitment ya Serikali kuwezesha kituo kile katika vifaa tiba na wataalam. Lengo kubwa ni kwamba wananchi wa eneo lile wapate huduma.
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Changamoto za Morogoro Kusini zinafanana na Changamoto za Jimbo la Karagwe. Katika Hospitali ya DDH Nyakahanga tuna tatizo kubwa la upungufu wa madawa, vifaa tiba na Wauguzi.
Mheshimiwa Naibu Spka, swali langu ni je, Naibu Waziri, Mheshimiwa Jafo kaka yangu, anaweza kuambatana nami baada ya Bunge hili kwenda kusaidiana nami kutatua changamoto za Hospitali ya DDH ya Nyakahanga
pamoja na kuanza mchakato wa kujenga Hospitali ya Wilaya ukizingatia DDH ya Nyakahanga inahudumia Wilaya mbili; Karagwe na Kyerwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri wazi kwamba miongoni mwa Wabunge ambao walikuwa wakinisumbua sana katika Sekta ya Afya ni Mbunge huyu wa Karagwe. Ni kweli kabisa, naomba niseme kuwa, pale ana Daktari wake anaitwa Dkt. Sobo ambaye ni kijana mwenzake; naamini kwamba watashirikiana vya kutosha kuhakikisha mchakato wa Jimbo lile unakaa vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, commitment yetu ni kwamba, katika kipindi hiki nitakuwa na ziara katika Mikoa yetu mitano nikianzia Mkoa wa Tanga, Lindi, Pwani Morogoro pamoja na Mtwara, lakini nitapita Ruvuma. Vile vile Mkoa wa Kagera niliupa kipaumbele kwa zoezi maalum katika kutembelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni imani kwamba kabla ya Bunge lijalo, basi nitajitahidi kwa kadiri iwezekanavyo tufike eneo lile kubaini changamoto za wananchi wa eneo lile la Jimbo la Karagwe ili mwisho wa siku wananchi wa eneo lile waweze kupata huduma bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni commitment ya Serikali, tutajitahidi kwa kadiri iwezekanavyo, hasa nikijua nawe ni mpiganaji mkubwa katika Sekta ya Afya katika eneo lako, tutasukuma kwa kadiri iwezekanavyo wananchi pale wapate huduma bora.
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Miongoni mwa matatizo ambayo tunayapata katika Wilaya ya Babati kwa Hospitali ya Mrara ni ranking ya hospitali hiyo ambapo mpaka sasa inaitwa Kituo cha Afya wakati hospitali hiyo imekuwa ikihudumia watu wa Kondoa na watu wa Babati Vijijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, mara nyingi tumekuwa tukipendekeza kwamba hospitali hii tuipandishe rank iwe Hospitali Teule ya Wilaya, lakini Serikali imekuwa haitupi ushirikiano. Je, sasa wako tayari kutusaidia ili hospitali hiyo ipate dawa na vifaa tiba kuhudumia watu wote hao?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Gekul kwamba Serikali lazima inatoa kipaumbele na ndiyo maana naye anakumbuka juzi juzi tulikuwa pamoja jimboni kwake tukikagua miradi mbalimbali katika Mkoa wa Manyara. Nimeweza kubaini changamoto mbalimbali kimkoa, kiujumla wake kwamba kuna mambo mengi ya kuweka kipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama jambo hili lililetwa kama request Serikalini, lakini bado halijafanyiwa kazi, sasa ni jukumu letu kukumbushana tuone jinsi gani tutafanya ili pale ambapo pamepungua tusukume kwa sababu mwisho wa siku tunataka wananchi wapate huduma.
Kwa hiyo, ni commitment ya Serikali kwamba tutaangalia ni kitu gani kilichokuwa kinakwamisha mwanzo, jambo gani (gap) ambalo inabidi tuliweke vizuri ili tuboreshe eneo na mwisho wa siku wananchi wapate huduma ya afya, kwani ni commitment ya Serikali kuwahudumia wananchi wake.
MHE. DKT. CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii. Naomba kuuliza swali la nyongeza. Nashukuru sana kwa majibu ya Naibu Waziri kwa swali la msingi, lakini ningependa kuuliza kuwa kwa sababu Morogoro Vijijini hatuna mpaka sasa hivi Hospitali ya Wilaya na majibu yametolewa, naomba kuulizia je, inawezekana pia kuboresha Kituo cha Afya cha Dutumi ambacho mpaka sasa hivi na chenyewe kinatumika kwa kutupatia vitendea kazi? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Ishengoma ni Mbunge wa Viti Maalum kule na nimesema kwamba katika ziara yangu nina mpango wa kuja Mkoa wetu wa Morogoro. Lengo ni kutembelea Mkoa mzima wa Morogoro na kubaini changamoto zake.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Ishengoma najua ni mpiganaji wa siku nyingi sana katika eneo hili. Naomba nimhakikishie kwamba katika ziara yangu eneo hili tutakwenda kulitembelea na licha ya kulitembelea na kuangalia mipango ya pamoja jinsi tutakavyofanya, lakini nina maslahi mapana ya Mkoa wa Morogoro kwa sababu najua mkoa ule wananchi wanapata shida, wanatembea mbali, siyo jambo la kufichaficha.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuna kila sababu, kipindi cha ziara yangu tufike eneo hilo, tushauriane kwa pamoja na linalotakiwa kufanywa kwa sasa tutalifanya, lakini linalotakiwa kuwekewa mipango mbadala kwa siku za usoni, tutalijadili kwa pamoja. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Ishengoma kwamba, katika hilo tutashirikiana kwa pamoja Mheshimiwa wangu.
MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Majibu ya Naibu Waziri hayajaniridhisha, ukilinganisha na kwamba vifaa tiba na madawa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa havitoshelezi. Je, ni lini atahakikisha Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara itakuwa na vifaa ambavyo vitakuwa vinatosheleza kwa asilimia mia moja? (Makofi)
Swali la pili; kwa kuwa gari lililopo ni moja ambalo lina uhakika wa kubeba mgonjwa mahututi kumtoa Hospitali ya Rufaa Musoma kumpeleka Mwanza na ile nyingine ni hizi gari ndogo: Je, ni lini atatuletea ambulance nyingine katika Hospitali yetu ya Rufaa ya Mkoa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba nikwambie kwamba najua, kwa sababu wakati nakwenda kufunga Mkutano wa ALAT kule Musoma, nilitembelea mpaka Mkoa wa Mara kuona mpango mkakati wa kujenga Hospitali hii ya Rufaa ya Mkoa wa Mara. Nimetembelea pale, nimeona na tumebadilishana mambo mengi sana na Katibu Tawala wa Mkoa ule. Kwa hiyo, najua kuna changamoto, ndiyo maana katika majibu yangu ya msingi nilisema kweli kuna changamoto katika hospitali hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu ni nini? Ni kuhakikisha kwamba sasa tunasukuma jambo lile. Naomba tushirikiane na Waheshimiwa Wabunge; kama mnavyojua kwamba commitment za afya zina cross cut maeneo mbalimbali nchini. Kwa hiyo, ni imani yangu kwamba, tutaendelea kushirikiana. Commitment ya Serikali, tukiangalia sasa hivi bajeti ambayo imetoka, shilingi milioni 700 mpaka shilingi bilioni 1.8, ni ongezeko la asilimia 61. Hili ni jambo kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kinachofanyika sasa hivi ni nini? Ni kusaidia kusukuma nguvu sasa ili fedha zipatikane na wananchi wapate huduma. Katika mchanganuo wa bajeti katika eneo hilo, ndiyo unagusa katika maeneo mbalimbali ya vifaa tiba na madawa kuiwezesha hospitali hii iweze kufanya vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo Mheshimiwa Mbunge amezungumzia suala la ambulance; ni kweli. Najua kwamba ambulance moja inafanya kazi vizuri, lakini na hizi nyingine zina changamoto kubwa. Sasa naomba nimsisitize Mheshimiwa Mbunge kwa kushirikiana na wadau wengine mbalimbali, katika mchakato huu wa bajeti unaokuja wa 2017/2018, tuweke kipaumbele kinachojiainisha katika upatikanaji wa ambulance. Serikali haitasita kulisukuma hili. Lengo ni kupata ambulance ya maana katika kusaidia wakati wowote emergency inapotokea, wananchi waweze kupata fursa za tiba. Kwa hiyo, nakubali ombi hilo, tutaenda kulifanyia kazi kwa pamoja kama Wabunge na Serikali.
MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tatizo lililopo kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara, linafanana kabisa na tatizo ambalo lipo kwenye Hospitali ya Mkoa wa Tabora ya Rufaa ya Kitete. Kuna tatizo kubwa sana la wagonjwa na hasa akinamama wanapoenda kujifungua, wodi ile ni ndogo na wengi wanalala chini wakiwa hata wale wachache wanakuwa wana-share kitanda kimoja:-
Je, Serikali inajipanga vipi kutatua hili tatizo la muda mrefu la msongamano wa akinamama wanapojifungua pale Hospitali ya Mkoa wa Tabora ya Kitete?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Hospitali ya Kitete pale Tabora ina changamoto kubwa na ndiyo maana ukifanya rejea ya majibu yangu mbalimbali niliyoyatoa hapa Bungeni, tumesema kwamba catchment area ya Mkoa wa Tabora, ukubwa wake na jiografia yake ilivyo ina kila sababu tuweke nguvu. Ndiyo maana katika bajeti ya mwaka huu sitaki kutaja figure hapa exactly, tuna fungu ambalo tumelitenga kwa ajili ya suala zima la ukarabati pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutaangalia ni kipi kilichotengwa katika mwaka huu. Lengo ni kwamba ile fedha ipatikane tu ikafanye kazi na value for money ionekane. Naamini ule ukarabati utaanza mara moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nikuhakikishie kwamba katika majibu yangu ambayo nayakukumbuka hapa Bungeni niliyoyatoa ni suala zima la Hospitali ya Kitete; naomba tuwasiliane kwa karibu zaidi ili tujue ni fungu kiasi gani limetengwa, lakini tuhimize sasa ile fedha ili iweze kufanya kazi vizuri.
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa tatizo la Mara la vifaa tiba pamoja na gari la wagonjwa, ni kama la Rungwe. Napenda kujua commitment ya Serikali kwa Hospitali ya Makandana katika Wilaya ya Rungwe, ni lini watatuletea gari na kutuongezea vifaa tiba kwa ajili ya kuwasaidia wanawake wa Wilaya ya Rungwe katika Hospitali ya Makandana?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikupongeze na niwashukuru sana kwa dua zenu njema. Nakumbuka siku ile nilivyotoka kule baada ya kutoa maagizo kwamba mfumo wa kielectroniki ufanye kazi pale, baada ya muda fulani nikapata ajali, watu wakasema, watu wa huko wamekushughulikia? Nikasema hapana. (Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishukuru sana. Agizo langu nililotoa ndani ya mwezi mmoja lilitekelezeka katika hospitali ile na nilipata mrejesho kwamba makusanyo yamebadilika sana katika hospitali ile ya Makandana. Kwa hiyo, naomba niseme kwamba kweli nilitembelea pale nikakuta gari za wagonjwa hali yake sio nzuri sana. Tulibadilishana mawazo na bahati nzuri wana Mkuu wa Wilaya mzuri sana katika eneo lao.
Mheshimiwa Naibu Spika, nami naomba nilichukue hili kwa sababu kuna vitu vingine tumeshaanza kuvizungumza kuona ni jinsi gani tutafanya kuboresha hospitali ile, tutajadili kwa pamoja ili hospitali hii iweze kupata huduma nzuri, kwa sababu kuna network nzuri ya Waheshimiwa Wabunge katika eneo hilo, mnaofanya kazi kwa pamoja kwa agenda kubwa ya hospitali yenu, basi naamini jambo hili tutalitatua kwa pamoja, kama mawazo shirikishi kuhusu tufanye nini katika mpango wa muda mfupi na mpango wa muda mrefu.
MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tatizo lililoko Mara la ambulance ya kuwachukua wagonjwa, ni sawasawa na tatizo lililopo Wilaya ya Kondoa ambako Kituo cha Afya cha Wilaya ya Kondoa hakina ambulance kwa muda mrefu sasa; iliyopo ni mbovu ya mwaka 2008 na inahitaji matengenezo makubwa sana kiasi kwamba Halmashauri haiwezi kumudu. Je, Serikali iko tayari kutuletea ambulance Wilaya ya Kondoa ili wagonjwa ambao wanatakiwa kupata Rufaa ya kuja Dodoma Mjini wapate usafiri?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tumelisikia suala zima la request katika Wilaya ya Kondoa. Niseme wazi, ukiangalia hata katika database ya mwaka huu, katika Halmashauri ambazo ziliomba kupata ambulance zilikuwa 18, katika kumbukumbu yangu ya karibuni. Hili sina hakika hapa kama tuliweza kuliainisha katika mpango wetu wa bajeti wa Halmashauri ya Kondoa kwa mwaka huu wa fedha, lakini tutaenda kuliangalia. Kama Kondoa haipo, itabidi tujipange kwa pamoja, tuone ni jinsi gani tutafanya katika mchakato wa bajeti ambao utaanza siyo muda mrefu; na mpango wake tumeujadili hapa siyo muda mrefu, tujadili kwa pamoja kwa sababu hii needs assessment inaanzia kutoka katika vikao vyetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutakapolifanya hivi na kwa sababu jambo hili ni pana na ninavyojua, mgonjwa kutoka Kondoa mpaka aletwe Hospital ya General hapa Dodoma ambapo ni mbali sana, tuna kila sababu kuwezesha eneo hilo lipate vifaa vizuri hasa ambulance kuwafikisha wagonjwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Felister Bura kwamba, hili tutaliangalia kwa upana wake, tuone ni jinsi gani tutafanya ili eneo lile lipate huduma bora.
MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu ya Serikali, napenda tu kuiambia Serikali kwamba Halmashauri ya Nsimbo ni moja ya Halmashauri katika nchi yetu ya Tanzania ambayo wananchi kwa kiwango cha chini kabisa wanapata maji safi na salama. Ni asilimia 34 tu. Sasa katika hii bajeti ya milioni 757, kuna miradi ya Kijiji cha Katesunga na Kijiji cha Nduwi ambayo itafadhiliwa na World Bank kama shilingi milioni 273: Je, ni lini fedha hizi zitapatikana ili miradi hii iweze kuanza?
Swali la pili, kutokana na majibu ya Serikali kwamba Mto Ugalla una maji machache kwa kipindi cha kiangazi, lakini wananchi wa pale wamekuwa wakitumia mto ule kwa ajili ya maji kipindi chote na kuna mamba ambao wanahatarisha sana maisha yao: Je, kwa nini Serikali wakati mpango wa muda mrefu; maji kutoa Ziwa Tanganyika ukiwa unafanyika, isitenge fedha ili wananchi wa Kata ya Ugalla na jirani ya Litapunga waweze kupata maji kutoka Mto Ugalla?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali la kwanza kwamba lini fedha zitapatikana; mpango wa upatikanaji wa fedha ni katika mwaka huu wa fedha katika bajeti hii. Ndio maana juzi hapa katika Maswali kwa Waziri Mkuu siku ya Alhamisi, Waziri Mkuu aliongelea suala zima la mtiririko wa fedha na akalihakikishia Bunge hili kwamba kipindi siyo kirefu sana tutaanza kuziona fedha katika Halmashauri zetu; fedha za maendeleo na fedha za OC. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba tuwe na imani kwamba katika mchakato huu wa sasa hivi kabla muda haujapita sana, bajeti hizi zitaanza kutoka ili mradi iweze kutekelezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, kuhusu Mto Ugalla kwamba kwa nini usitumike kwa sasa, kwa sababu mpango uliokuwepo ni wa muda mrefu? Naomba nikiri wazi kwamba Mheshimiwa Richard Mbogo ni Mbunge ambaye nilikuwa naye Jimboni kwake Nsimbo na miongoni mwa miradi tuliyoikagua ni miradi ya maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikiri wazi kwamba nilivyotembelea Jimbo la Nsimbo, ni kweli shida ya maji imekuwa ni kubwa sana. Kwa hiyo, nadhani hili ni wazo jema. Tutalichukua lakini tutawashirikisha na wenzetu kule katika Halmashauri na katika Mkoa, kuona kama ule mradi mkubwa kutoka Ziwa Tanganyika, huenda una gharama kubwa sana, tujue ni kiasi gani, tuweze kuja na mpango mwingine mbadala kusaidia katika Kata hizi ili tusisubiri muda mrefu sana miaka miwili, mitatu au minne kwa wananchi kuendelea kupata shida ya maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimwambie Mheshimiwa Richard Mbogo kwamba jambo hili sasa tutalichukua, tuone ni jinsi gani tutafanya ili kama katika hizo Kata mbili kuna mradi mwingine mbadala tuweze kuufanya. Nadhani jambo hili ni jambo shirikishi sana kwetu Serikali na Halmashauri ya Wilaya. Tutashirikiana na Mheshimiwa Mbunge kwa sababu najua anafuatilia sana ili wananchi katika zile kata mbili wapate fursa ya maendeleo ya maji.
MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Jimbo la Lushoto limezungukwa na vyanzo vingi vya maji: Je, Serikali ina mpango gani ya kuwatua ndoo kichwani akinamama hasa wa Kilole, Kwekanga, Mbwei, Makanya, Ngulwi, Ubiri, Kwemakame na maeneo mengine yaliyobaki katika Jimbo la Lushoto?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika mpango wa maji kwa sasa hivi ambao Waziri wa Maji wakati wote huwa anaelezea hapa, lengo letu kubwa ni kumtua mama ndoo kichwani.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Shekilindi, kwamba, katika ratiba yangu kama tulivyoongea, tarehe 24 mwezi huu wa Novemba, nitakuwa katika Jimbo lake la Lushoto. Naomba tukiwa kule kule site tuweze kubadilishana mawazo. Hivyo vyanzo vilivyoko, lakini vile vile na wenzetu Wizara ya Maji ambao Mheshimiwa Waziri wa Maji yuko makini muda wote kuhakikisha kwamba wananchi wa Tanzania wanapata maji, tutaangalia na kushauri vizuri jinsi gani tutafanya kwa maeneo ya Wilaya ya Lushoto ili wananchi waweze kupata maji. Kwa hiyo, naomba tutumie vizuri ziara yetu ya tarehe 24 kuangalia vyanzo vilivyoko na mambo mengine kuwasaidia wananchi wa Lushoto.
MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri.
Kwa kuwa Jimbo la Lushoto lina kituo kimoja tu cha afya, ambacho kinahudumia takribani Kata saba; je, Serikali haioni sasa kuwa umefikia wakati wa kujenga vituo vya afya hasa katika Kata ya Makanya, Ngwelo, Kilole, Gare, Ubiri, Magamba, Malibwi pamoja na Kwai?
Swali la pili, kwa kuwa wananchi wa Lushoto wamejitolea kujenga zahanati katika vijiji vya Mzalagembei, Bombo, Mavului, Mbwei, Mazumbai, Ilente, Mbelei, Makanka na Kwemachai, lakini zahanati hizi zimebakia kukamilika tu.
Je, Serikali inatoa tamko gani sasa la kumalizia zahanati hizi pamoja na kupeleka watumishi ili wananchi wa Jimbo la Lushoto waondokane na usumbufu wa kutembea umbali mrefu hasa kwa mama zetu na dada zetu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza katika kumbukumbu yangu Mheshimiwa Shekilindi amekuwa akiuliza maswali mengi sana ya sekta ya afya, ofisi yetu inakiri mchango mkubwa wa Mheshimiwa Shekilindi katika Jimbo lake na wananchi wake.
Mheshimiwa Spika, katika kulifanikisha suala hili, Serikali tumeelekeza mpango wetu wa sasa tunaondoka nao, jinsi gani tutafanya katika mwaka huu wa fedha, kuhakikisha kwamba tunajenga vituo vya afya. Mheshimiwa Shekilindi kwa sababu jana nilikujibu hapa kwamba nina mpango wa kuanzia katika Mkoa wako wa Tanga, tena ratiba nimeibadilisha nitaanza siku ya tarehe 21, na Mheshimiwa Shangazi, nitakuwa naye hiyo tarehe 21, tutaangalia jinsi gani tutafanya baada ya kuwa kule site, kutembelea hivyo vituo. Katika mpango wa bajeti inaokuja lengo kubwa ni kuimarisha vituo vya afya, katika ujenzi kwenye maeneo yetu, tumelenga kwamba angalau kila Halmashauri katika mwaka wa fedha tunaoondoka nao tujenge kituo kimoja cha afya.
Mheshimiwa Spika, hali kadhalika katika suala zima la maboma nimesema, tulifanya assessment katika Halmashauri zote, na hili ni agizo la Kamati ya Bajeti, maboma yote ambayo hayajakamilika, tumepata idadi ya maboma. Ndiyo maana nimesema katika bajeti ya mwaka huu unaokuja sasa, ninaomba Waheshimiwa Wabunge, tuungane pamoja kwamba jinsi gani tutafanya mpango mkakati wa kibajeti tuweze kumaliza maboma yale ambayo Mheshimiwa Shekilindi umeyazungumza katika maeneo yako, tukimaliza yale tutakuwa tumesogeza kwa ukaribu zaidi huduma za afya kwa wananchi wetu. Kwa hiyo, nakuunga mkono katika hilo na Serikali imesikiliza kilio chako.
MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi napenda niulize swali la nyongeza.
Katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Vijijini tayari imeshapanua kituo chake cha afya cha Nanguruwe, ambapo pia kinacho chumba cha upasuaji cha kisasa, chenye vifaa na kimeanza kutoa huduma kwa lengo la kuifanya iwe hospitali ya Wilaya, ambapo majengo yote yanayotakiwa yamekamilika.
Je, ni lini Serikali itaibadilishia hadhi kutoka kituo cha afya na kuwa hospitali ya Wilaya baada ya kuwa kila kitu kimekamilika?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli katika mpango wa bajeti tulipokuwa tunajadili na watu wa Mtwara kule Nanguruwe, mwaka huu kwamba wameonesha demand ya kituo hiki, na ni kweli walihakikisha kituo hiki kimekamilisha vitu vyote vya msingi.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Hawa Ghasia, tutawasiliana na wenzetu wa Wizara ya Afya kuangalia zile taratibu za kikawaida kuhakikisha kituo hiki sasa kinapandishwa hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya, tukijua wazi kwamba ikiwa hospitali ya Wilaya hata kasma ya bajeti itabadilika eneo hilo na wananchi wataendelea kupata huduma nzuri baada ya kituo hicho kupanda kuwa Hospitali ya Wilaya.
MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Spika, ahsante.
Kwa kuwa Serikali imeshatoa kibali cha kupeleka wauguzi kule na ukizingatia kwamba hospitali ina upungufu wa wauguzi zaidi ya asilimia 60. Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kupeleka hao wahudumu ukizingatia kwamba hali ya kule siyo nzuri kwa sasa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema wenzetu wa Handeni waliomba kibali. Naomba niseme kwamba ni vibali katika kada mbalimbali zimeombwa, lakini naomba niwahakikishie wazi kwamba, kwa sababu mchakato wa utoaji wa vibali ulishaanza katika sekta ya elimu hasa katika suala zima la walimu wa sayansi, kwa kadri Serikali itakavyoona inafaa tutajitahidi kuhakikisha tunapeleka nguvu na hasa vile vibali ambavyo vimebainishwa.
Ofisi ya Utumishi ikishatoa go ahead katika maeneo mbalimbali, tutashiriki kuona ni jinsi gani tutafanya kuongeza watumishi, tukijua kwamba siyo sekta ya afya peke yake isipokuwa kada mbalimbali zina matatizo makubwa sana na hivyo ni jukumu la Serikali kuhakikisha kwamba tunafanya kila iwezekanavyo ili wananchi waweze kupata huduma inayostahiki. Kwa hiyo, Mheshimiwa Omari naomba ondoa hofu katika hilo.
MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Waziri, lakini ni wazi kwamba kwa miaka mingi sana Serikali haijatoa kipaumbele kwa suala la nyumba za walimu. Kwa mfano, kwenye majibu ya Mheshimiwa Waziri amesema kwamba kwa mwaka wa fedha 2016/2017 Serikali imepanga kujenga nyumba 1,818, ukiangalia nikitumia Mbozi kama case study ya Mkoa wa Songwe, kuna uhaba wa nyumba za walimu 1,432. Je, ni lini sasa Serikali italeta mpango kabambe wa kumaliza tatizo la nyumba za walimu hasa wa vijijini ili iwe kama motisha?
Swali la pili, Mheshimiwa Waziri ambacho nilitaka kufahamu kwamba je, ni lini madeni hayo ya walimu yataanza kulipwa kwa sababu ukisema kwamba yamepelekwa tu Hazina bado haileti tija kwa walimu wa Tanzania. Ninataka kujua kwamba ni lini rasmi madeni hayo yataanza kulipwa?
Mheshimiwa Spika, ninakushukuru.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Spika, najua Mbunge anaguswa sana na sekta ya elimu na nikupongeze sana kwa sababu ukiwa kijana lazima uguswe na elimu.
Mheshimiwa Spika, katika majibu yangu ya msingi na mkakati wa Serikali nimezungumza pale awali. Kwa vile tumebaini changamoto ya nyumba za walimu ndiyo maana Serikali katika bajeti ya mwaka huu tunaoenda nao imetenga takribani shilingi bilioni 13, hii ni kwa ajili ya nyumba za walimu wa shule za msingi peke yake, lakini shilingi bilioni 11 kwa ajili ya shule za sekondari. Hata hivyo, commitment katika mpango mwingine wa MMES II, nimezungumza hapa karibuni nyumba zipatazo140 tumeshazikamilisha.
Mheshimiwa Spika, naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge katika ziara zangu katika Mikoa mbalimbali, miongoni mwa mambo ninayoyatilia kipaumbele sana ni kukagua ujenzi wa nyumba za walimu. Naomba niwapongeze Wabunge wote kwa ujumla wetu katika maeneo yetu nilipopita nimekuta ujenzi wa nyumba za walimu kwa kweli unaenda kwa kasi sana. Kwa vile katika commitment ya Serikali imeshatenga hizi fedha, naomba niwaambie fedha tunaendelea kuzipeleka katika Halmashauri zetu, lengo kubwa walimu waweze kupata mazingira salama ya kuweza kuishi.
Mheshimiwa Spika, katika suala zima la madai ya walimu, nimesema kwamba sasa hivi tumeshahakiki deni la shilingi bilioni 26.04 na haya ni madeni yasiyo ya mshahara. Maana yake Serikali haiwezi kulipa madeni lazima kwanza kuweza kuhakiki, ndiyo maana nimesema zoezi la uhakiki limeisha Oktoba, 2016. Sasa hivi ni mchakato ambao upo katika Wizara ya Fedha kwa utaratibu wa mwisho wa kuweza kulipa. Kwa hiyo, naomba tuwe na subira tu kwa sababu kigezo kikubwa ni kwamba ni lazima deni lihakikiwe na madeni haya yameshahakikiwa na naomba niwaambie walimu wa Tanzania kwamba wawe na subira kipindi siyo kirefu, Hazina kwa kadri inavyojipanga, madeni haya yanaweza kulipwa walimu mbalimbali ili mradi wapate haki zao.
MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa Serikali ningependa ijue kwamba kuna wananchi waliojitolea kwa kujua umuhimu wa walimu kujenga maboma kwa ajili ya nyumba za walimu, pamoja na madarasa.
Je, Serikali itatoa kipaumbele kwa wale wananchi ambao wameonesha umuhimu wa walimu na umuhimu wa elimu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, jibu ni ndiyo Serikali itatoa. Ndiyo maana hivi sasa tumeshaleta fedha karibu awamu mbili za Capital Development Grand, ambapo katika baadhi ya Halmashauri imeshaanza kuweka kipaumbele kumalizia nyumba za walimu. Maeneo niliyofika zile fedha zilizofika, utakuja kuona yale maboma ambayo mwanzo yalibakia sasa hivi utakuta yanakamilishwa. Kwa hiyo, hiyo ndiyo commitment ya Serikali, naomba nikupongeze na hili ni jukumu la kwetu sote Wabunge zile fedha zinavyopita ni lazima tuzisimamie vizuri, tuende tukamalize haya maboma yaliyopo katika maeneo yetu.
MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza linasema kwamba kuna uhaba mkubwa wa watumishi wa kada ya afya, hasa katika Mkoa wa Manyara kwenye zahanati na vituo vya afya. Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kuhakikisha hilo nalo linatatuliwa?
Mheshimiwa Spika, swali la pili tuna upungufu wa dawa hususan Mkoa wa Manyara kwenye hospitali zake zote Je, Serikali ina mpango gani na hili maana afya za wananchi ziko hatiani? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, katika suala zima la watumishi kama tunavyojua ni kwamba maeneo mbalimbali yanakabiliwa na uhaba wa watumishi, hii tumesema ni commitment ya Serikali. Kama nilivyosema katika jibu wakati namjibu Mbunge wa Handeni kwamba Serikali sasa hivi mchakato wa vibali ukikamilika vizuri katika Ofisi ya Utumishi, basi nadhani tutapeleka watumishi kwa kadri maeneo yote yanayowezekana, especially katika Mkoa wako wa Manyara Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Spika, suala zima la upungufu wa dawa ni kweli na naomba kila Mbunge hapa a-pay attention ya kutosha. Nimepita katika Halmashauri mbalimbali Serikali tumeamua kutoa fedha za basket fund awamu mbili zimekamilika, hivi sasa tumeshapeleka fedha za basket fund katika awamu ya tatu, lakini kwa bahati mbaya sana miaka yote uki-track record fedha za basket fund ambayo inakuonesha one third lazima itumike katika kununua madawa na vifaa tiba katika Halmashauri zetu fedha hizo hazitumiki sawasawa.
Mheshimiwa Spika, maeneo mengine utakuta fedha tumezipeleka lakini wakati natembelea juzi, fedha za awamu ya kwanza na fedha za awamu ya pili utafika katika Halmashauri bado fedha za basket fund kwa ajili ya ununuzi wa madawa na vifaa tiba hazijanunuliwa. Ndiyo maana tumetoa maelekezo kwa DMO wote wahakikishe kwamba fedha zilizopelekwa katika maeneo yao zinaenda kutatua matatizo ya wananchi kama tulivyoelekeza.
Mheshimiwa Spika, hili nimhakikishie Mheshimiwa Ester, juzi nilikuwa naongea na Mkurugenzi wako kule wa eneo lile na kumwelekeza kwamba zile fedha aweze kununua na ameniambia ameshanunua dawa nyingine, lakini kuna dawa zingine bado anaziomba kutoka MSD, kuna dawa zingine ameambiwa hazipatikani na nimewaelekeza kwamba, wafanye utaratibu kuzipata dawa hizo lengo kubwa ni wananchi wa maeneo hayo waweze kupata huduma. Kwa hiyo, ni commitment ya Serikali na tunajitahidi kufanya kila liwezekanalo ili kuondoa hili tatizo la dawa nchini kote.
MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nina maswali ya nyongeza, mji umebadilika, je, Serikali haioni haja nayo ibadilike kuleta sheria nyingine?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa baadhi ya watendaji wake wanaokusanya zile shilingi mia moja hamsini, mia mbili wamekuwa na kauli ambazo haziridhishi kwa wananchi, je, anatoa wito gani?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli mji umebadilika lakini kama nilivyosema kwamba Halmashauri ya Jiji kuna sheria ambayo inaongoza utaratibu katika maeneo hayo nayo ni Sheria Ndogo yenye GN Na.60. Naamini kwa sababu kuna wadau mbalimbali na Mheshimiwa Jaku najua ni mdau wa Jiji la Dar es Salaam lakini na Wabunge na Waheshimiwa Madiwani wa maeneo hayo kama wakiona kuna haja ya kurekebisha Sheria Ndogo hiyo basi wafanye hivyo na sisi Ofisi ya Rais - TAMISEMI ambao ndiyo wenye jukumu la kufanya mchakato huu uweze kukamilika tutalishikia bango jambo hili liweze kuwa mahali pazuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala lingine alilosema ni kuhusu kero ya ukusanyaji wa fedha hizo lakini hata uaminifu wa upelekaji fedha zile haupo. Kwa bahati nzuri sasa hivi katika Jiji la Dar es Salaam tuna Mkurugenzi makini sana naamini kwa hizi changamoto ndogondogo zinazobainika tutazisimamia kwa pamoja ili kuzitatua. Lengo ni wananchi wanaoegesha magari yao katika Jiji lile kupata huduma bora bila kupata usumbufu.
MHE. ALLY M. KEISSY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Jiji la Dar es Salaam linashangaza kwani wamechukua kampuni ya kutoka Kenya ili kukusanya fedha za maegesho ya magari Dar es Salaam. Vilevile hawatumii mashine za EFD kukusanya pesa na kupandisha kutoka Sh.300 kwenda Sh.500. Hivi kweli nchi nzima ya watu milioni 50 wamekosa kampuni yoyote katika nchi yetu mpaka kuchukua Kampuni ya Kenya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue concern hii ya Mheshimiwa Keissy lakini ninavyojua katika suala la ukusanyaji Manispaa za Ubungo, Ilala na Kinondoni zinakusanya zenyewe lakini kwa ukubwa wake Manispaa ya Temeke na Kigamboni, Halmashauri ya Jiji yenyewe inasimamia jambo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili suala la kampuni kutoka Kenya kukusanya nadhani huo ni mchakato wao lakini ninavyojua ni kwamba kuna utaratibu maalum kwa Jiji la Dar es Salaam, kila Manispaa kwa maana ya Ilala, Kinondoni na Ubungo zina utaratibu wake wa kukusanya ila Manispaa ya Temeke na Kigamboni Jiji lenyewe linasimamia kwa taarifa nilizokuwa nazo, wanasimamia kama Wakala wa Jiji la Dar es Salaam. Kwa hiyo, Mheshimiwa Keissy kuhusu hii kampuni kutoka Kenya kukusanya fedha hizi ngoja tuzi-cross check zaidi lakini inawezekana ni taarifa za kimagazeti zaidi kuliko uhalisia wake.
MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka nenda, miaka rudi tofauti na kada nyingine za watumishi, kero imekuwa madeni ya walimu, madeni ya walimu. Leo hii mnatuambia kwamba madeni ya walimu yamefikia takribani shilingi bilioni 34 plus. Walimu hawa wanaidai Serikali wengine kama matibabu, likizo, kwa miaka zaidi ya mmoja hadi miwili. Walimu waliopandishwa mishahara miezi 12 iliyopita hadi leo hawajalipwa huo mshahara wanausikia harufu tu. Walimu wengine wamestaafu zaidi ya miezi sita hawajapata mafao yao.
Ningependa kujua kwa kuwa sasa hivi Serikali mnasema mmeshahakiki ni lini, na mnipe tarehe na mwezi hawa walimu watakuwa wamelipwa haya madeni kwa sababu wamechoka kila siku madeni ya walimu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuna walimu waliosimamia mitihani mwaka 2015. Leo hii tunazungumza mwaka 2017, kwa nini hadi leo hawajalipwa na ni lini Serikali itakuwa imewalipa hiyo stahili yao?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema awali, kwanza tuweke kumbukumbu vizuri. Katika kada ambayo Serikali katika njia moja ua nyingine imekuwa ikishiriki vizuri sana katika ulipaji wa madeni ni kada ya walimu. Ukiangalia miaka mitatu mfululizo, trend ya malipo ya madeni ya walimu ambayo tulikuwa tumezungumza hapa katika Bunge kila wakati, kwa kweli Serikali inajitahidi sana. Na ndio maana katika kipindi cha sasa hata ukiangalia katika mwezi wa 11 uliopita huu kuna baadhi ya madeni ya walimu especially katika baadhi ya Wilaya, Halmashauri, kwa mfano kuna Temeke na Halmashauri zingine kulikuwa na outstanding deni karibuni ya shilingi bilioni moja nayo ililipwa vilevile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndio maana katika ulipaji wa madeni mapya mengine; ndio maana Serikali ilikuwa inafanya zoezi zima la uhakiki. Na bahati nzuri, ofisi yetu ya TAMISEMI pamoja na Ofisi ya Hazina ndio ilishiriki, na jambo hili sasa hivi limekamilika. Na ndio maana nimesema hapa siwezi kutoa deadline ni lini, deni hilo litalipwa lakini kwa sababu mchakato wa uhakika umekamilika, hili deni la shilingi bilioni 26 ninaamini sasa hazina si muda mrefu mchakato wa malipo utaanza kuanza.
Naomba Mheshimiwa Mbunge, najua uko makini katika hili lakini amini Serikali yako kwa vile zoezi la uhakiki ambalo lilikuwa ni changamoto limekamilika basi walimu hawa si muda mrefu wataweza kulipwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala zima la deni la kusimamia mitihani na ndio maana nilisema deni hili lilikuwa ni miongoni mwa madeni haya ambayo yaliyohakikiwa ambayo takribani ilikuwa ni shilingi bilioni sita.
Naomba tuondoe hofu walimu wangu katika mchakato wa sasa walimu hawa wote wataendelea kulipwa ili mradi kila mtu haki yake iweze kulipwa, na Serikali haitosita kuhakikisha inawahudumia vyema walimu wake kwa sababu italeta tija kubwa sana katika sekta ya elimu.
MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nina swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, madai ya walimu yasiyo ya mshahara ni pamoja na deni la walimu kwa Serikali juu ya posho na kufundishia yaani teaching allowance ambayo ni ahadi ya Serikali tangu mwaka 2012 ambayo ilitolewa kule Mtwara siku ya Walimu Duniani.
Je, Serikali ina mkakati gani wa ziada kuweza kuwalipa na kuwapatia fedha zao walimu hawa deni wanalolidai, posho la kufundishia yaani teaching allowance kwa haraka inavyowezekana?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA YA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, kwa hali ya sasa tunachokifanya ni kuhakikisha kwa kadri iwezekano kusaidia sekta ya elimu. Ndio maana kabla sijajibu hili swali sasa hivi ukiangalia Serikali yetu kwa kazi kubwa waliyoifanya sasa hivi, mwanzo ukiangalia Walimu Wakuu, hata Waratibu wa Elimu mwanzo walikuwa hawalipwi hizi allowances.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Serikali hivi sasa toka mwaka jana kuanzia Waratibu wa Elimu, Wakuu wa Shule za Msingi na Wakuu wa Shule za Sekondari hivi sasa wote wanalipwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kama kuna madeni mengine yoyote Serikali iko katika michakato mbalimbali kuyalipa madeni haya yote. Naomba niwahakikishie ndugu zangu Wabunge kwamba Serikali yetu jukumu letu kubwa ambalo tunalilenga sasa hivi, kwa sababu tunataka kuhakikisha ubora wa elimu lazima madeni haya yote yatalipwa na kama nilivyosema madeni yote ambayo yamehakikiwa kupitia Hazina yatalipwa madeni hayo. Tunataka walimu wetu wawe na morali ya kufanya kazi katika mazingira yao ya kazi.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano ilipoingia madarakani ilijigamba kwamba itatoa elimu bure na utekelezaji wa elimu bure kwa mujibu wa watafiti wa haki elimu inahitaji takribani shilingi bilioni 700 kwa mwaka mmoja wa fedha. Na hali ilivyo sasa hivi, fedha mnazopeleka ni kidogo tu za fidia ya ada.
Je, mko tayari sasa kuwaambia Watanzania mmeshindwa kutekeleza elimu bure ili Watanzania wachangie suala la elimu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Watanzania wanafahamu. Wakati hatuna programu ya elimu bure, vijana wengi walikuwa wanakosa hata hii elimu ya msingi, wengine walikuwa wanatishwa vitumbua kwenda kuuza barabarani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi juzi nilipita kule katika Mkoa wa Kagera, nilipofika pale Nyakanazi, shule ambayo mwaka huu ime-register wanafunzi wengi zaidi ya wanafunzi 800 wa shule ya msingi peke yake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitendo cha kutoa elimu bure hii kusaidia mitihani, gharama za ada, hata suala zima la posho, ni jambo kubwa sana. Mimi naamini ndio maana kwa rekodi mwaka huu inatuonesha vijana wengi sasa hivi wanaripoti shule za seondari ukilinganisha na kipindi cha mwanzo, kwa sababu mwanzo wazazi walikuwa wanashindwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kikubwa zaidi naomba tuamini kwamba Serikali katika jambo hili imeleta ukombozi mkubwa. Na hili niseme kwa vile Serikali tumejipanga na hili nimelisema sehemu mbalimbali, changamoto yetu inatufanya tunataka tuseme lazima private schools sasa si muda mrefu zitatakiwa zijipange vizuri, kwa sababu tunaenda kwa kasi kubwa ya ajabu. Huku tunakokwenda tutakwenda kupata mafanikio makubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, imani yangu Watanzania wote tutaungana pamoja, hii nchi yote ni ya kwetu, Watanzania wote ni wa kwetu na watoto ni wa kwetu tusaidiane kuhakikisha Tanzania inafika mahali salama katika suala zima la utoaji wa elimu.
MHE.VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, na ameendelea kusema hapa kwamba hii michango tunahitaji kuendelea kuwahamasisha wananchi ili waweze kuchangia. Lakini ukiangalia kwa mapungufu tuliyokuwanayo kwa maana ya madawati, vyumba vya madarasa pamoja na maabara; ni mapungufu makubwa sana na kwa sababu wananchi wengi wanaamini kwamba michango ni hiari kama alivyosema Naibu Waziri, hatuoni kama tutashindwa kutekeleza azma yetu ya kuhakikisha kwamba wanafunzi wote wanaweza kupata elimu bora kwa sababu wanafunzi wengi wataendelea kukosa vyumba vya madarasa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tunatambua kwamba wazazi pamoja na shughuli kubwa wanazozifanya pamoja na kujenga hostel, lakini bado ukiangalia wale wanafunzi wa kike zile gharama zote za kuwasomesha kwenye zile hostel bado ni gharama za wazazi. Ni kwa nini Serikali isikubali kugharimia hizo gharama za hostel baada ya kuwa hizi hostel zimejengwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mathayo kwa sababu katika rekodi pale juzi juzi ameweza kushiriki utoaji wa mifuko 200 ya cement kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika eneo lake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefika pale Musoma Mjini, nimeweza kutembelea nimeona kazi kubwa anayofanya. Kwa hiyo, imani yangu kwa ile kazi unayoifanya na nadhani mnataka mjenge takribani vyumba karibuni 200 vinatakiwa vikamilike ndani ya mwezi Machi, naomba tuwaunge mkono kwa sababu mnafanya kazi njema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa kusema kwa mkakati huu tutashindwa, naomba nikuhakikishie ndio maana mwaka huu tunakamilisha vyumba vingi kwa kutenga karibu shilingi bilioni 29, na ndugu zangu Wabunge naomba niwaambie huku site tunakotoka sasa hivi ukienda huko utakuta kazi kubwa sana ya ujenzi wa madarasa inaendelea. Naamini katika muda huu ambao tuko hapa Bungeni, Mbunge mwingine akirudi katika site kwake atakuta kwamba kuna madarasa mengine katika eneo lake hata alikuwa hajatarajia yameshakamilika. Hii yote ni juhudi ya Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba niwahakikishie Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali tutajitahidi kuhakikisha azma ya Serikali kuwapatia wananchi wake elimu bora inafanikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala zima la zile hostel zilizojengwa changamoto ni kubwa sana, katika suala la vijana hasa watoto wetu wa kike kwamba ikiwezekana kwamba zile hostel zilizojengwa Serikali igharamie. Naomba niseme hili ni wazo ngoja tutalifanyia kazi, kwa sababu kugharamia hostel zote Tanzania ni bajeti kubwa sana na hizi zimejengwa makusudi ni hostel za kata ziko katika maeneo yetu. Lengo ni mtoto anaenda shuleni na kurudi lakini kwa sababu changamoto ya uzito kwa wanafunzi ni vyema tujenge hostel nasema tuendelee na mpango huu wa sasa pale Serikali kwa kushirkiana na wadau mbalimbali itakavyoona kwamba nini tufanye, lengo ni kuboresha wananchi katika kata zetu tutafanya hivyo kwa kadri inavyowezekana.
MHE. NAJMA MURTAZA GIGA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na
majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, bado nina swali moja la nyongeza
ambalo linahusiana na hawa watoto wadogo chini ya umri wa miaka 18 kutumia
huu ulevi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile nilisema sheria hii ya mwaka 1969 ni ya
muda mrefu sasa ni lini Serikali itaweza kujipanga na kuleta ili tuweze kufanyia
marekebisho sheria hii ili tuwabane na hawa watoto wadogo walio chini ya umri
wa miaka 18 kutumia ulevi?
NAIBUWAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA:
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli. Sasa hivi kuna tabia kwenye baadhi ya Mikoa,
utakuta watoto wadogo asubuhi au wakati wa weekend wananyweshwa pombe. Jambo hili kwanza kimsingi ni ukiukwaji wa haki za kibinadamu kwanza
na haki za watoto ambapo mtoto mdogo anatakiwa kuendelezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba tuchukue huu ushauri kwa
sababu sheria hii ni ya muda mrefu sana na kutokana na maoni ya wadau
mbalimbali tutaangalia jinsi gani tutafanya turekebishe, lengo kubwa ni
kuhakikisha kwamba Taifa letu linakuwa Taifa imara kwa sababu lazima tuwalee
hawa watoto kwa kizazi kijacho.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba tuchukue ushauri.
Itakapoonekana pale ina haja, basi wadau mbalimbali wataleta maoni yao na
sisi Wabunge ni miongoni mwa wadau wa kutengeneza hizo sheria. Kwa hiyo, hili
nadhani tutalifanyia kazi vema tuweze kulifanikisha.
MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa
kuwa katika swali la msingi linazungumzia pombe za kienyeji na pombe za
kienyeji katika Taifa letu ni nyingi ikiwemo mbege, kimpumu, ulanzi na pombe
nyinginezo. Ni lini sasa hawa watu wa viwango vya kuandika kilevi kilichoko
kwenye pombe ikiwemo TBS wataingia katika maeneo husika ili kuweza kujua
kwamba ni kiwango gani cha ulevi kinachoruhusiwa katika pombe za kienyeji?
NAIBUWAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA:
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna pombe mbalimbali. Kuna mbege, kuna
ulanzi na nyinginezo, bahati mbaya pombe hizi hazijawekwa katika viwango
stahiki na ndiyo maana maeneo mengine utakuta kuna kesi mbalimbali
zimejitokeza. Baadhi ya watu saa nyingine wamekunywa pombe, pombe ile
imewadhuru na matukio haya tumeona kwamba yametokea maeneo
mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, naamini kwa sababu sasa hivi tuna Wizara
ambayo inafanya kazi vizuri zaidi na hususan suala zima la viwanda na naamini
wenzetu sasa wa TBS watachukua jukumu lao katika maeneo mbalimbali
kuhakikisha ni jinsi gani tunafanya kurekebisha utaratibu mzuri hasa katika hivi
vikundi vidogovidogo vinavyojihusisha na pombe za kienyeji, lengo kubwa ni
kumlinda Mtanzania anywe kitu kinachoridhisha maisha yake lakini na afya yake
ya msingi vilevile.
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nichukue nafasi hii kuwapongeza sana wananchi wa Jimbo la Serengeti kwa kujitahidi kukamilisha vyumba vya maabara kwa asilimia 81.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa wamekamilisha kwa asilimia 81, Mheshimiwa Naibu Waziri uko hapa na umekuja pale Jimbo la Serengeti na umeona hali ilivyo; kwa kuwa wananchi hawa wamejitahidi kwa hali hii. Je, Serikali kupitia hizi fedha za P4R mko tayari kukamilisha hivi vyumba 12 ambayo ni sawa na asilimia 19? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa ujenzi wa maabara ulipaswa pia kuendana na upungufu wa vyumba vya madarasa: Je, kupitia hizi pesa za P4R, mko tayari kupeleka sehemu ya fedha hizi kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa?
Mheshimiwa Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba niwapongeze kwa kazi kubwa waliyoifanya; na kama kuna deficit ya vyumba 12, niseme kwamba Serikali tutashirikiana, siyo na watu wa Serengeti peke yake, isipokuwa jukumu letu kubwa ni kuhakikisha tunapata maabara katika kila sekondari zetu zilizokamilika. Ndiyo maana Mheshimiwa Mbunge nilikwambia hiyo juhudi iendelee, lakini Serikali na sisi tutatia nguvu yetu kuhakikisha maeneo yote yale ya Serengeti yanapata maabara kama tulivyokusudia.
Mheshimiwa Spika, ndiyo maana nimezungumza hapa kwamba tumetenga karibu shilingi bilioni 16. Lengo ni kwamba zile maabara ambazo wananchi wamejitolea kwa nguvu kubwa kuzijenga, lazima ziwe na hivyo vifaa. Kuanzia mwezi Machi mpaka mwisho wa mwaka hapa tutajikuta tumekamilisha suala zima la maabara siyo Serengeti, lakini katika maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, suala zima la ujenzi wa vyumba vya madarasa, ni kweli. Tuna changamoto ya vyumba vya madarasa katika maeneo mbalimbali ikiwepo kwako Serengeti, nami nakupongeza sana, nilikuwa nawe siku ile. Tutajitahidi.
Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka huu ukiangalia katika michakato mbalimbali, tulikuwa na madarasa ambayo yapo katika program ya P4R ambayo tumejenga kwa kiwango kikubwa katika nchi yetu, lakini tulikuwa na madarasa ambayo tulikuwa tunayajenga kwa mpango wa MES II lakini kuna mipango mingine mbalimbali ambayo takriban shilingi bilioni 29 zilitengwa kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vingi vya madarasa, zaidi ya vyumba 3,000.
Mheshimiwa Spika, katika harakati hizi, tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo maeneo ya Serengeti, lakini nchi nzima kwa ujumla kwa hii mipango mipana ya Serikali ili tuondoe changamoto ya madarasa. Lengo kubwa ni wanafunzi wetu wapate maeneo mazuri ya kusomea.


WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA MAFUNZO YA UFUNDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Namshukuru Mheshimiwa Jafo kwa majibu mazuri.
Mheshimiwa Spika, napenda kutumia nafasi hii kuwajulisha Waheshimiwa Wabunge kwamba Serikali imeshanunua vifaa vyenye thamani ya shilingi bilioni 16.9 kwa ajili ya maabara zote nchini zilizokamilika. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tutaanza zoezi la usambazaji wa vifaa hivyo. Kwa hiyo, natoa tu wito kwa Waheshimiwa Wabunge ambao katika maeneo yao maabara hazijakamilika, waendelee kuzikamilisha kwa sababu utaratibu wa Serikali ni kwamba tutakuwa tunapeleka vifaa pale ambapo maabara zimekamilika.
MHE. JORAM I. HONGOLI: Ahsante sana Mheshimiwa Spika. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, naomba niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa sasa tutakuwa na huduma ya upasuaji mdogo katika Kituo cha Afya Lupembe na hatimaye Kichiwa ili kuboresha huduma ya madawa kwa kuwa dawa ni tatizo: Je, Serikali ina mpango gani wa kufungua duka la dawa kwa maana ya MSD katika Kituo cha Afya Lupembe na baadaye Kichiwa? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza lazima nikiri kwamba harakati za Mbunge huyu na watu wa Mkoa wa Njombe kwa ujumla wake tutajitahidi kuziunga mkono. Lengo kubwa ni Mkoa mpya wa Njombe uweze kupata huduma ya afya. Ndiyo maana hata Waziri wangu Mkuu juzi juzi alikuwepo kule kwa ajili ya mipango ya kimkakati katika Mkoa ule mpya.
Mheshimiwa Spika, suala zima la ujenzi wa duka la madawa katika vituo hivyo, siwezi kukiri kwamba katika hivyo Vituo vya Afya tutafanyaje, lakini kwa sababu pale tuna hospitali yetu ya Rufaa ya Mkoa ambayo inajengwa sasa hivi, tutafanya mpango mkakati tufanyeje katika eneo lile tupate duka maalum la MSD. Nia ya Serikali ni watu wa ukanda ule waweze kupata dawa kwa ukaribu zaidi.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, naomba niwahimize Waheshimiwa Wabunge wote, kwa sababu sasa hivi tunaelekeza fedha nyingi sana katika Halmashauri na nashukuru sana, juzi juzi karibu kila Mbunge hapa amepata orodha ya idadi ya fedha kwa ajili ya madawa katika eneo lake, sasa ni kuona jinsi gani twende tukazisimamie.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, nilisema katika siku za nyuma kwamba, tumeelekeza fedha nyingi za basket fund ambazo fedha zile lengo lake ni kwamba one third nikwa ajili ya ununuzi wa madawa na vifaa tiba. Naomba tukasimamie tutatue kero za madawa kwa wananchi wetu, kwa sababu tukifanya hivi, naamini Watanzania wote watafarijika kupata dawa bora katika maeneo yao kwa sababu Serikali sasa hivi imepeleka fedha nyingi sana katika Sekta ya Afya.
MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi hii. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa wepesi wake katika kutatua changamoto tulizonazo kwenye Halmashauri zetu.
Mheshimiwa Spika, chumba cha upasuaji cha Hospitali ya Wilaya ya Bukombe kilikuwa kimejengwa kwa ajili ya kutumika kwa muda baadaye ijengwe theatre. Mheshimiwa Naibu Waziri wa Afya alikuja pale akaona hali halisi ilivyokuwa. Nataka tu kujua commitment ya Serikali, ni lini wataisaidia Hospitali ya Wilaya ya Bukombe na yenyewe ipate chumba cha upasuaji cha kisasa kwa ajili ya kuwapatia huduma wananchi wa Bukombe?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza nikiri wazi kwamba nilifika Jimboni kwa Mheshimiwa Mbunge na ni kweli nimeenda kuitembelea hospitali yetu ya Wilaya angalau pale upasuaji unaendelea. Kwa kuwa eneo lile lina changamoto kubwa sana, ndiyo maana tuna mpango vile vile siyo kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ile peke yake, isipokuwa hata katika Kituo chako cha Afya cha Uyovu kama tulivyoongea.
Mheshimiwa Spika, tutaangalia jinsi gani tutafanya ili tupeleke huduma katika maeneo yale, tupate na back up strategy katika Kituo cha Afya cha Uyovu, tupunguze idadi kubwa ya wagonjwa ambao wataendelea katika Hospitali yetu ya Wilaya. (Makofi)
Kwa hiyo, amini Serikali yako kwa sababu tumekuja kule, tumefanya survey, tumetembelea, tumekutana na wananchi, tumebaini changamoto. Baada ya kubaini changamoto, Serikali tunapanga mkakati wa kuweza kuwasaidia wananchi wa Bukombe.
MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Mimi nina swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa suala la rasilimali watu katika Wizara ya Elimu hasa kwenye vyuo vyetu na hata shule za sekondari bado ni changamoto kubwa na kwa kuwa hali hii inasababisha pia baadhi ya Waratibu wa Elimu kupangiwa masomo ya kufundisha sawasawa na Walimu wengine hali inayopelekea kuona kwamba ni kazi iliyopo nje ya job discription zao. Je, Serikali haioni kwamba kuna haja sasa ya kufikiria kwa kuwa hiyo ni kazi ya ziada basi waweze kupewa posho ya ziada hawa Waratibu wa Elimu kuliko hali ya sasa ambayo wanafundisha kama Walimu wengine lakini hawana nyongeza ya mishahara?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kulitambua hilo ndiyo maana sasa hivi Serikali imeamua kuweka posho ya madaraka ambayo mwanzoni haikuwepo. Kwa kipindi kilichopita tumelipa takribani shilingi bilioni 15 kwa ajili ya posho ya madaraka. Kwa hiyo, jambo hili Serikali tumelizingatia, tunalifanyia kazi na hivi sasa watumishi wale kutokana na jukumu hilo wana posho maalum kila mwezi, kuanzia Walimu Wakuu wa Shule za Msingi, Walimu Wakuu wa Shule za Sekondari halikadhalika Waratibu wa Elimu wa Kata katika maeneo yetu.
Pwani. MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nianze kusema mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Waziri huyu ni mchapakazi, kweli tarehe 5 Januari, ni Waziri wa kwanza aliyefika maeneo ya Delta na nilifanya naye kazi na nikaonesha kweli kauli ya hapa kazi inatekelezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niulize maswali yangu mawili; moja, je, kutokana na barabara hii kwamba kwa sasa ina maeneo mawili ya daraja hayapitiki, je, Serikali haioni kwamba ina kila sababu ya kukarabati madaraja hayo? Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; Barabara ya kutoka Muhoro kwenda Mbwela ina matatizo makubwa hasa kwenye Daraja la Mbuchi, je, Serikali itatusaidiaje katika hilo la Mbuchi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kupokea shukrani zake ndugu yangu Mheshimiwa Ungando, naomba nikiri, kweli nilikuwepo kule na tulitembelea visiwa 40 vya Deltakatika Jimbo lile la Kibiti. Barabara ya kutoka hapa Bunju mpaka Nyamisati kule ndani kwa kweli ina changamoto kubwa sana naomba tulipokee jambo hili kwa sababu katika programu yetu ya uondoaji wa vikwazo tutajitahidi ofisi yetu tufanye kila liwezekanalo kwa sababu tukiwasaidia wananchi wa eneo lile tutakuwa hata tumewasaidia wananchi wa Mafia kwa sababu wanaposafiri kutoka Nyamisati kwenda Mafia lazima watumie barabara ile. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika suala zima la Daraja la Mbuchi, na kwa sababu tulipita kule na vilevile tunajua kuwa tuna harakati ofisi yetu kutengeneza Daraja la Mbwela, tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo kuhakikisha mambo haya yote ofisi yetu inayashughulikia na Mheshimiwa Ungando amini Serikali yako tutakupa ushirikiano kwa sababu jimbo lako ni miongoni mwa majimbo yenye changamoto kubwa.
MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii. Barabara ya Tanga - Pangani - Bagamoyo ni barabara ambayo imekuwa ikitolewa ahadi kila chaguzi kuu zinapofika na Uchaguzi Mkuu uliopita pia ahadi hiyo ilitolewa ya kwamba itaanza kutengenezwa na tayari tunaambiwa upembuzi yakinifu umekwishafanyika, sasa je, ni lini utengenezaji wa barabara hiyo utaanza ikiwa tayari upembuzi yakinifu umekwishafanyika? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara hii nimepita mara kadhaa na juzijuzi nilivyokuwa natembelea Mkoa wa Tanga, ni miongoni mwa barabara niliyoipita kutoka Bagamoyo mpaka pale Pangani na kikubwa zaidi katika kufika pale nilikuta reference ya Waziri wa Miundombinu aliyekuwa akipita pale na kutoa ahadi hiyo ya ujenzi wa barabara hiyo lakini ikiwa sambamba na ujenzi wa daraja lile la pale Pangani. Mheshimiwa Mawenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu ni commitment ya Serikali na kipindi cha sasa kwa sababu ujenzi wa barabara ya lami lazima kwanza upembuzi yakinifu ufanyike na jambo hilo limekamilika, ninaamini suala la barabara hii kwa sababu ni barabara ya kimkakati, kwamba hata kwenda Mombasa ni barabara ya shortcut naamini Serikali hii itafanya kila liwezekanalo ujenzi wa barabara hii uweze kukamilika.
MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la dogo nyongeza. Barabara ya kutoka Mkuranga Mjini mpaka Kisiju Pwani ni miongoni mwa barabara ambayo zimekuwa zikiahidiwa pia kuwekwa lami na Awamu ya Nne na hata Awamu hii ya Tano. Barabara hii inapita katika Makao Makuu ya Wilaya yetu ya Mkuranga lakini pia inapita katika Hospitali yetu Kuu ya Wilaya ya Mkuranga. Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini sasa Serikali itatusaidia kuhakikisha barabara hii inawekwa lami kutoka Mkuranga Mjini kupita Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Hospitali ya Wilaya mpaka Kisiju Pwani?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niweke kumbukumbu sawa, kwanza Mheshimiwa Ulega juzi kwa uchapakazi wake mzuri juzi alikuja ofisini kwetu kwa ajili ya kuhakikisha suala zima la miundombinu ya barabara katika jimbo lake na hii ni miongoni mwa barabara ambayo tulikuwa tukiijadili na Katibu Mkuu wangu pale jinsi gani tutafanya, kwa sababu yale ni Makao Makuu ya Halmashauri na kila Makao Makuu ya Halmashauri lazima angalau barabara ya lami iweze kufikika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Serikali tutaangalia jinsi gani tutafanya lakini nikijua wazi barabara ile ambayo inaenda mpaka Kisiju Pwani ni jambo la mkakati mkubwa sana na kuna barabara nyingine kutoka Kimanzichana inapita katikati kule mpaka inakuja maeneo ya Msanga katika Jimbo la Kisarawe, hizi zote ni barabara za kimkakati kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Mkoa wa Pwani unafunguka, lengo kubwa ni kwamba katika uchumi unaofunguka wa viwanda sasa wananchi waweze kushiriki vizuri katika mchakato wa viwanda. Kwa hiyo, Mheshimiwa Ulega naomba nikuahidi tutakupa ushirikiano wa kutosha kujenga miundombinu yetu ya barabara za lami katika maeneo yetu.
MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza. Mheshimiwa Mwenyekiti, ni fursa kubwa kwa Halmashauri hasa kama ile ya Karatu yenye vivutio vingi vya kitalii na hizi hoteli za kitalii hasa katika kipindi hiki ambacho Halmashauri zetu nyingi zinachechemea katika eneo la mapato ya ndani. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, huoni sasa umefika wakati wa kubadilisha sheria hiyo ili kodi hiyo ya hotel levy ikusanywe na Halmashauri zetu ili iweze kuchangia katika eneo lile la mapato ya ndani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika swali la msingi uliulizwa suala la Serikali inamkakati gani, lakini majibu bado yamerudi kwa Halmashauri ya Karatu kujitangaza pamoja na kwamba kuna kipengele kidogo cha Serikali kusaidia. Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri zetu nyingi hazina mapato ya kutosha ya ndani, je, Mheshimiwa Waziri tunachouliza, ni mkakati wa Serikali wa kutangaza hoteli zile za kisasa ili wale wageni badala ya kulala hata Nairobi waje Karatu ili waondokee pale kwenda Ngorongoro na Manyara? Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, nadhani yote ni mchakato huu wote mpana kwa sisi Waheshimiwa Wabunge kama tukiona kuna haja ya kubadilisha sheria basi nadhani katika mawazo ya pamoja tutafanya hilo kwa pamoja kwa lengo la Halmashauri zetu, lakini hilo ni takwa la kisheria, kwa hiyo, ni sisi wenyewe kufanya maamuzi katika hilo na mchakato huo ukianza inawezekana kila mtu kutakuwa na michango mbalimbali kama ya wadau nini kifanyike. Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili la utangazaji, ni kweli nimezungumza kwamba website ya Karatu lakini kuna mipango mbalimbali ya Serikali na mpango mkubwa sasa hivi hata ukipitia shirika letu la ndege katika suala zima ambalo wenzetu wa Maliasili na Utalii mara nyingi sana wameamua katika shirika letu la ndege liwe miongoni mwa mojawapo kutangaza vivutio mbalimbali vya kitalii. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, katika mpango wa kutangaza vitu mbalimbali vya kitalii hapa kama Serikali ina mipango mipana sana kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii na hilo naomba niseme kwa suala la Karatu tutalipa kama special preference kwa ajili eneo lile lina hoteli nyingi zaidi lakini ni eneo la kimkakati mtu akifika pale anapata faraja anakuwa na sehemu nzuri ya kulala, hana mashaka ya aina yoyote. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi naamini Serikali yetu kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii itaongeza upana wake wa utangazaji wa vivutio vyetu vya utalii, lengo kubwa tuweze kukuza uchumi wa nchi yetu kwa sababu tunategemea kwamba kwa fursa tulizonazo za vyanzo vya kitalii tukitangaza vizuri tutakwenda mbele zaidi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba niungane na hoja yako, kama Serikali tutafanya mpango mpana kuhakikisha mambo yanakwenda vizuri katika nchi yetu.
MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, kwa kuwa huu mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria unaonekana unaendelea kusuasua na hauna uhakika exactly lini utaanza na wananchi wa Tabora wanaendelea kuteseka kwa shida ya maji na sisi pale Tabora Mjini tuna bwawa kubwa la Igombe ambalo lina-access ya maji kwa maana ya lita za ujazo ambazo Serikali kama itaweka mpango mkakati wa kusambaza maji yale ya Igombe na kwa unafuu, Wananchi wa Tabora Mjini watapata nafuu ya tatizo la maji.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba yale maji ya Igombe yaweze kusambazwa kwa bei nafuu kuliko kusubiri huo mradi wa Ziwa victoria ambao haujulikani utaanza lini? Hilo la kwanza
Swali la pili, moja ya tatizo lingine linalosababisha ile Mamlaka ya Maji (TUWASA) Tabora inapata matatizo katika uendeshaji wake ni pamoja na kutolipa deni ambalo Mamlaka ya Uendeshaji ya Maji - TUWASA pale Tabora inaidai Serikali kwa muda mrefu zaidi ya shilingi bilioni 2.3 ambazo zinadaiwa hasa kwenye taasisi zetu za majeshi pamoja na taasisi zingine za Serikali.
Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha TUWASAwanalipwa pesa hizo ili Tabora iweze kupata maji ambayo yatakuwa ni ya uhakika? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka tuweke kumbukumbu sawa. Katika mradi huu wa Tabora-Sikonge ambao katika bajeti yetu mwaka huu nadhani tulipitisha pamoja hapa. Tulitenga takribani shilingi bilioni 29 ukiangalia kitabu cha maendeleo lakini kwa juhudi kubwa zilizofanywa na Serikali kupitia ufadhili kutoka India ndiyo maana nimesema ile figure zaidi ya shilingi bilioni 500 ambayo Serikali imeshaweka commitment hiyo. Hivi sasa mchakato wa manunuzi upo katika hatua mbalimbali na lengo la mradi huu kati ya mwezi Aprili mpaka mwezi Mei mradi huu utakuwa umeanza, kwa hiyo, ndugu yangu, mtani wangu, Mnyamwezi wa Tabora naomba ondoa hofu katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala zima la jinsi gani tutumie bwawa la Igombe, wataalam wetu wameshaanza kufanya tathmini pale. Takribani ule mradi utagharimu shilingi bilioni 1.5 na hili ndiyo maana tumeona kwamba jambo hili kama Ofisi ya Rais - TAMISEMI lakini na kushirikiana na wenzetu ambao ni Wizara mama wa Wizara hiyo tutaangalia jinsi gani tutafanya kwa pamoja katika mchakato wa pamoja wakati tunasubiri mradi mkubwa wa maji wa hizo shilingi bilioni 500, jinsi gani tutafanya hizo back up strategy ya mradi mwingine huu mdogo katika bwawa la Igombe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwahiyo lengo letu kama Serikali ni kuweza kutatua shida ya maji katika Mkoa wa Tabora na ndiyo maana nimesema mradi huu siyo Tabora peke yake, kuna watu wa Tinde pale, kuna watu wa Kahama, kuna watu wa Shinyanga mradi huu utakuja kujibu matatizo ya watu wote wa ukanda ule. Niseme, Wasukuma na Wanyamwezi wa eneo hilo mmepata bahati kubwa sana kwa Serikali kuwaona kwa jicho la karibu kuwatengea takribani shilingi bilioni 580.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hata hivyo, suala zima la bili ya maji; suala la bili ya maji ni kwamba tumetoa maelekezo mbalimbali hapa kwamba bili ya maji kupitia Waziri wa Maji ameshatoa maelezo mbalimbali, sasa naomba niziase taasisi mbalimbali; kila taasisi inayodaiwa deni la maji liweze kulipa deni la maji siyo Tabora peke yake lakini katika maeneo yote ya nchi hii, kama taasisi inayodaiwa na maji, miradi hii ya maji au hizi mamlaka za maji zitashindwa kutupatia maji kwasababu watu wanashindwa kulipa bili za maji.
MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa maji ni kilio cha muda mrefu sana hasa katika Jimbo la Lushoto na ukizingatia Jimbo la Lushoto lina mto mkubwa sana unaitwa Kibohelo, lakini unakuta Lushoto mto ule hautumiki unamwaga tu maji kuelekea bondeni Mombo bila kutumika maeneo yote.
Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuhakikisha maji yale yanaenda hasa katika vijiji vya Dochi, Ngulwi, Miegelo, Kwekanga pamoja na Gare?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Shekilindi anafahamu si muda mrefu sana nilitokea katika Jimbo lake na Jimbo la ndugu yangu Shangazi na kwa bahati nzuri hapa kuna mwalimu wangu hapa kutoka huko huko Lushoto amekuja hapa leo na hili naomba niwahakikishie ni kwamba ni commitment ya Serikali kuangalia jinsi gani tutatumia fursa zote zilizokuwepo kutatua tatizo la maji. Na katika Mpango wa Maji wa Awamu ya Pili, Waziri wa Maji amezungumza hapa mara kadhaa, lengo letu ni kwamba kutumia hizi fursa zilizokuwepo nikwambie ndugu yangu Shekilindi kwa sauti eneo lile nilivyofika kule Lushoto niwaagize wataalam wetu wa maji katika Halmashauri ile waanze michakato ya awali suala zima tufanyeje sasa matumizi halisi ya mto ule uweze kutumika vizuri kwa ajili ya wakazi wa Lushoto.
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele tayari
imeshatimiza masharti yote ya kujenga maabara, ya kujenga mfumo wa maji safi na taka pamoja na matundu nane ya vyoo; na kwa kuwa wananchi wa Wilaya ya Mlele hususan akina mama wa Tarafa ya Inyonga wanapata shida sana kwa ajili ya matibabu yao kwa sababu kile ni kuwa kituo cha afya lakini Halmashauri yao imefanya juhudi kubwa kwa matengenezo yote waliyoweka vigezo Serikali. Je, ni lini sasa Serikali itatoa kibali ili kile kituo cha afya kiweze kuwa Hospitali ya Wilaya?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa yale maeneo ambayo yanajengwa majengo mengine wananchi hawajalipwa fidia zao, wanadai sasa muda mrefu hawajalipwa, ni lini Serikali itawalipa pesa zao ili wananchi wa Wilaya ya Mlele hususan Tarafa ya Inyonga waweze kupata pesa zao?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli na mimi nakumbuka nilitembelea katika Mkoa wetu wa Katavi na
miongoni mwa hospitali nilizokwenda kutembelea ni hiki Kituo cha Afya lakini kipindi kile kilikuwa kinakabiliwa na changamoto kubwa sana ya maji na nilitoa maelekezo pale na nimshukuru sana Mbunge wa Jimbo pale amefanya harakati imepatikana fedha hivi sasa mfumo wa maji
umepatikana. Na bahati nzuri hospitali hii kwa watu wasiofahamu ni kwamba ni kweli miundombinu yote imekamilika, na siku ile nilitoa maelekezo kwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi kwamba sasa kwa sababu eneo lile ndiyo
eneo la kimkakati na Makao Makuu ya Wilaya ya Mlele yako pale Iyonga, nikasema kwa sababu vipaumbele vyote vinavyotakiwa na mahitaji yote yameshakamilika basi waanze mchakato kuhakikisha eneo lile sasa linakuwa rasmi, kituo kile kinakuwa rasmi kuwa Hospitali ya Wilaya ilimradi waweze kukidhi vile viwango vya upataji bajeti inayolingana na hospitali ya Wilaya.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Anna Lupembe naomba
nikuhakikishie kwamba haya yalikuwa maelekezo yangu nilipokuwa kule site kutokana na mahitaji ya maeneo hayo yalivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala zima la wakazi waliokuwa pale; ni kweli, ukiangalia kwamba kuna nyumba nyingi sana zimejengwa katika maeneo yale na bahati mbaya sana kuna watu wanaotaka fidia pale na nilitoa maelekezo katika Halmashauri yetu sasa ipange mkakati jinsi
gani wale watu wataweza kulipwa fidia. Kwa sababu eneo lile likishakuwa hospitali ya wilaya lazima tuwe na eneo la kutosha kwamba wananchi katika eneo lile na hospitali ile iwe na hadhi kwamba maeneo yale sio kuingiliwa na watu na nina imani kwamba katika vipaumbele vya bajeti ya Halmashauri mwaka huu itakuwa imetengwa hiyo. Lengo kubwa ni kuifanya hospitali ile sasa iwe rasmi kuwa Hospitali ya Wilaya.
MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Hospitali ya Wilaya ya Siha inafanana sana na Wilaya ambayo imetangulia kuulizwa hapa, na Mheshimiwa Waziri aliitembelea Hospitali yetu ya Wilaya ya Siha na ameona kwamba tuna wagonjwa wa nje tu, hatulazi lakini juhudi zinaendelea na hata wiki hii wananchi wamejitolea kuchimba msingi kwa ajili ya kuendeleza hospitali yetu na changamoto kubwa tuliyonayo ni watumishi, hospitali yetu haina watumishi na hata tukifikia mahali pa kulaza na kuweza kufanya operation na huduma nyingine
hatutakuwa na watumishi na madaktari.
Je, anatuambia nini kwa sababu ndani ya mwaka
huu tutaanza kulaza na kufanya operation, je, ni mkakati gani wa dharura utafanyika ili hospitali hiyo iweze kupata watumishi wa kutosha na kazi ianze?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nilifika pale Siha na nilivyofika pale licha ya hilo suala la watumishi
lakini nilitoa maagizo. Serikali tumepeleka fedha pale kwa ajili ya kuhakikisha tunamaliza miundombinu katika ile floor ya juu, lakini nilitoa maagizo kwa sababu matumizi ya fedha zile, vikao vilivyokaa kwamba inaonkana fedha zile zilikuwa zinakwenda kutumika isivyo halali. Imani yangu ni kwamba katika eneo la Siha, utawala wa Siha utakuwa umefanya utaratibu mzuri jinsi gani tunaenda kupata value for money jengo lile linakamilika wananchi waweze kupata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la
watumishi sasa, Serikali inasema sio Siha peke yake, isipokuwa katika maeneo yote tuna changamoto sana ya watumishi na hasa katika suala zima la uhakiki tulivyopeleka hivi sasa
kuna watu wengine walikimbia vituo. Kwa hiyo, imani yangu ni kwamba kwa sababu tuna mchakato hivi sasa wa suala zima la ajira nadhani Wizara ya Utumishi itakapokuwa tayari basi kibali kitatoka kuhakikisha kwamba tunapata waajiriwa mbalimbali katika sekta mbalimbali hasa ikiwa sekta ya afya na watakuja kule Siha kuwahudumia wananchi wa Siha.
MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi, naomba kuuliza swali moja dogo la nyongeza.
Kwa kuwa suala la Wilaya ya Mlele linafanana kabisa na suala la Wilaya ya Mvomero na kwa kuwa Wilaya ya Mvomero tayari tumeshajenga Hospitali ya Wilaya ambayo imekamilika kwa asilimia 80 na kwa kuwa kuna fedha ambazo
tunazisubiri kutoka Serikalini ili tukamilishe na wananchi waanze kupata huduma; je, Serikali iko tayari kukamilisha ahadi yake ya kuleta zile fedha na hospitali ile iweze kufunguliwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naam, Serikali iko tayari na ndiyo maana katika kipindi cha sasa katika sekta
ya afya tumekuwa tukipelekeza pesa nyingi sana katika eneo hilo, na ndiyo maana naomba nikuhakikishie sio suala zima la miundombinu hata katika suala zima la madawa tumefanya kazi kubwa sana. Kwa hiyo, Mheshimiwa Murad naomba tukitoka hapa tuwasiliane tuangalie jinsi gani katika bajeti yenu ya mwaka huu kipi kimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo
kuweza kumalizia, lakini jinsi gani tufanye tuweze kusukuma kwamba katika bajeti ya mwaka huu ambayo imetengwa tusukume ilimradi fedha zipatikane suala la ujenzi likamilike ilimradi wananchi wa Mvomero waweze kupata huduma ya afya kama inavyotarajiwa.
MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Na mimi naomba niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa tatizo la Mlele linafanana sana na tatizo la Tabora Manispaa, Uyui pamoja na Kaliua, je, Serikali inasema nini kuhusu kukamilisha au kuandaa mpango wa kukamilisha hospitali ambazo hazipo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, Serikali kama tulivyosema kipaumbele chake ni kuhakikisha huduma ya afya inapatikana na ndiyo maana siwezi ku-disclose
information zote, lakini kuna juhudi kubwa sana inafanyika lakini kiukweli ni kwamba kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, kwanza kipaumbele cha kwanza kinawekwa na Halmashauri, japokuwa mnajua kwamba katika suala zima la cealing ya bajeti wakati mwingine ile cealing ikishaondoka vipaumbele vingine vinakwama, lakini tutaangalia jinsi gani tutafanya, lengo letu kubwa ni kwamba wananchi katika kila
maeneo waweze kupata huduma. Na ndiyo maana tunafanya harakati mbalimbali kufanya marekebisho makubwa katika sekta ya afya lakini imani yangu ni kwamba tutafika mahali pazuri tutasimama vizuri. Kwa hiyo wananchi, ndugu zangu wa Tabora ambao wengi ni watani wangu naomba msiwe na hofu kwamba Serikali yenu iko nanyi kuhakikisha kwamba mambo yanakuwa mazuri.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kama ambavyo Wilaya ya Serengeti inazungukwa na mbuga ya wanyama, vivyo hivyo Wilaya ya Ngorongoro ina changamoto kubwa sana ya kijiografia kutoka tarafa moja kwenda tarafa nyingine ni kilometa nyingi ikiwemo kutoka Tarafa ya Ngorongoro kwenda Tarafa ya Loliondo ambapo kuna takribani kilometa mia na zaidi, na Mheshimiwa Naibu Waziri ulifika umejionea mazingira ya Ngorongoro. Je, Serikali iko tayari sasa, kulingana na ugumu wa jiografia ya Ngorongoro, kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi hao inapatikana?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nilifika Ngorongoro takribani wiki tatu na nusu zilizopita, na ni kweli jiografia ukitoka hapa Karatu wakati unatoka getini pale
mpaka unafika kule Loliondo ni mbali sana na sio hivyo tu, nilifanya jiografia pana sana nikazunguka lile Jimbo la Ngorongoro nikapita mpaka katika Ziwa Natron pale, kweli changamoto ya maji ni kubwa na kama nilivyokuwa kule site niliahidi kwa wananchi kwamba tutafanya kila liwezekanalo kushirikiana na Halmashauri ile ya Ngorongoro kuangalia jinsi gani tutafanya kuhakikisha kwamba tunapata ujenzi wa maji kule kama ni borehole au vyovyote.
Kwa mfano ile Shule ya Sekondari ya Ziwa Natron pale, watoto wako pale lakini na maji yapo pale ila isipokuwa jinsi gani kuyasambaza kufika shuleni. Kwa hiyo, vyote nimeenda kule nimeweza kufanya needs assessment ya eneo lile na naomba nikuhakikishie kwamba kama Serikali na matakwa
yetu ya Kiserikali tutafanya kila liwezekanalo kuwasaidia wananchi wa Ngorongoro.
MHE. PETER A. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
Suala hili la maji kwenye Kijiji changu na Kata ya
Zinginari kuna mradi wa maji ambao unagharimu shilingi milioni 400 umefanywa, muda umeisha lakini mpaka leo maji hayatoki, kimekuwa ni kilio kikubwa sana.
Je, Waziri anafahamu kwamba kuna hii shida na
kama afahamu atakuwa tayari kwenda na mimi kwenye Jimbo langu ili ashuhudie namna ambavyo shilingi milioni 400 hizi zimeliwa na maji hakuna? Nashukuru.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tuna kesi mbalimbali na kuna baadhi ya maeneo mengine kwamba miradi imetekelezwa lakini wakati mwingine maji hayajapatikana na hii ina maana kwamba inatofautiana kutokana na mazingira. Mengine ni suala zima wakati mwingine zimechimbwa borehole ambapo zile borehole wakati mwingine zinakosa maji, lakini sehemu zingine ni suala
zima la usimamizi na uzembe katika usimamizi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kwa kulijua kwa kuona jambo hilo kwasababu ni maeneo ya Kilombero peke yake ambayo nilikuwa bado sijafika katika Mkoa wa Morogoro na ni imani yangu hata katika Bunge hili la Bajeti nitafika kule Kilombero. Basi naomba nikifika kule tuweze
kuangalia jinsi gani tatizo lililoko pale halafu tulipatie tiba halisia kutokana na jinsi tutakavyoliona lengo kubwa ni kwamba Wananchi wa eneo lako waweze kupata huduma ya maji.
MHE. KEMIREMBE J. LWOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ila nina maswali mawili ya nyongeza. Mheshimiwa Naibu Spika wote tunafahamu tatizo la maji na tunajua kabisa maji ni uhai na hakuna Mbunge hata mmoja humu ndani ambaye tutamsimamisha ambaye Jimbo lake halina tatizo la maji.
Mheshimiwa Naibu Spika ifike mahali kama Serikali tuwe na vipaumbele vichache ambavyo tutaweza kuvitekeleza kiuhakika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, katika
mradi huo wa Nyamazugo - Buchosa mradi huo wa maji unapita katika vijiji vya Isenyi, Nyamabanda na Nyanzenda ambapo ndiyo chanzo cha maji kinaanza na unaenda kutekelezwa kwenye vijiji vingine zaidi, swali langu, ni lini Serikali itafikisha maji katika vijiji hivi vichache ambavyo maji yanapita na kwenda kutekelezwa kwenye vijiji vingine?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika Wilaya ya Sumve kwenye vijiji vya Kadashi na Isunga kumekuwepo na mradi wa maji ambao umekaa unasuasua kwa miaka mingi. Je, ni lini Serikali itamaliza mradi huu wa Wilaya ya Sumve? Ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya Mbunge ni kwamba kuna chanzo cha maji lakini kuna vijiji jirani ambapo maji yanatoka kwamba kwa mujibu wa design vijiji
vile vitakosa maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tufanye rejea ya Mheshimiwa Waziri wa maji kwamba na Waziri wa Nishati na Madini kwamba kwa mkakati wa Serikali ya hivi sasa ni kuhakikisha kwamba maeneo yote ambayo vyanzo vinapatikana basi vitapewa kipaumbele jinsi gani kuweka design kama mwanzo vilisahaulika kuweka utaratibu wa
kuweka design nzuri ya kuhakikisha maeneo yale ambayo vyanzo vinapatikana yaweze kupata maji.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba nikuhakikishie kwamba Serikali hii itafanya kila liwezekanalo wananchi wa eneo lako lile lazima wapate maji kutokana kwamba lazima Serikali iweze kuwahudumia wananchi wale, lakini siyo hivyo tu, na wao watasaidia kuweza kulinda vizuri
chanzo cha maji katika eneo lile. Lakini katika eneo la Sumve ni kwamba kuna mradi wa maji lakini mradi huu unaonekana kwamba haujakamilika, ni commitment ya Serikali na
naomba tufahamu, siyo mradi huo peke yake karibu kuna miradi mingi sana ilianza kutekelezwa lakini mingi ilisimama huku nyuma naona flow ya fedha lilikuwa siyo nzuri, lakini hivi sasa kwa Seriakli ilivyojipanga ni kwamba mradi sasa hivi
mkandarasi akikamilisha kazi, aki-submit certificate maana yake certificate inalipwa na mkandarasi anaendelea kufanya kazi. Kwa hiyo, naomba niwahakikishie kwamba Serikali itajitahidi kwa kadri iwezekanavyo miradi yote ambayo ilikuwa ime-stuck sasa wakandarasi waweze kutimiza wajibu wao, wakamilishe ile miradi, wa-raise certificate zitalipwa ilimradi lengo la miradi iweze kukamilika na miradi hiyo iweze
kuwapata wananchi.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Waziri nilitaka kufahamu wakazi wa
Mkoa wa Katavi wamekuwa wakisubiri sana mradi ambao unaendelea kujengwa mradi wa maji wa Ikolongo B, wakazi wa Kata ya Ilembo, Misunkumilo, Kakese pamoja na maeneo mengine mradi huu umepita nyuma ya hizo Kata, lakini wakazi hawa wanakosa maji lakini pia wanatumia maji ambayo ni mchafu ya kutoka kwenye mabwawa pamoja na mito. Sasa naomba unieleze kwamba ni lini mradi huu utakamilika kwa sababu Serikali tayari ilishatenga pesa lakini mradi bado unasuasua? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna baadhi ya sehemu zingine kwamba miradi inasuasua na mnakumbuka kwamba hata Mheshimiwa Rais alivyofika Mkoa wa Lindi aliweza kutoa maelekezo mahususi kwa mkandarasi anaejenga mradi wa maji pale katika Mji wa Lindi na hii ina maana kwamba maana yake ni maeneo mbalimbali kulikuwa na tatizo kubwa hasa baadhi ya wakandarasi wanaoshindwa kutimiza vizuri wajibu wao, wengine wameomba kazi lakini baadae wakienda kule site wanashindwa kutimiza wajibu wao, lakini naomba nikuhakikishie kwamba Serikali hivi sasa inafanya vetting kwa Wakandarasi wote ambao wanashindwa kutimiza wajibu wao, lengo kubwa ni kwamba atakaposhindwa bora atolewe aletwe mkandarasi mwingine aweze kutimiza wajibu wale na Mkandarasi huyu tutaenda ku-assess kazi yake
inaendaje. Lakini hata hivyo ulizungumza ajenda suala zima la kwamba Wananchi wengine ambao wa maeneo yale wanakosa maji, tutafanya mahitaji halisi kuangalia kwa sababu siwezi kuzungumza hapa moja kwa moja kule site
sijaangalia lakini najua suala hilo linamhusu hata ndugu yangu Richard Mbogo, Mbunge wa Nsimbo pale nilivyofika nae ana hoja hiyo hiyo inayolingana ni kwamba tutaangalia kwa kina
tutafanyaje lengo kubwa ni kwamba wananchi wote wa Tanzania kama lengo la Serikali hii kuwatua wakina mama ndoo ya maji liweze kufikia; haliwezi kufikia lazima tupambane wote kwa pamoja, aliyekuwa mzembe tumtoe katika daraja hilo la uzembe awe katika suala zima la sawa sawa wananchi wapate huduma ya maji.
MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Serikali ilikamilisha mradi wa maji wa Ziwa Victoria mwaka 2008 na kwa bahati mbaya kuna baadhi ya vijiji ambavyo bomba limepita kwenye vijiji hivyo vikawa
vimesahaulika na toka mwaka 2014/2015 vijiji kama Kabondo, Mwakuzuka, Matinje, Buluma, Mwaningi ambavyo bomba limepita wala si kilometa 12 bomba limepita kabisa kwenye
vijiji hivyo viliwekwa kwenye mpango kwamba vingepatiwa maji lakini hadi sasa vijiji hivyo havijapata maji kwa sababu fedha hazijatoka.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka kusikia uhakikisho kutoka kwa Waziri kwamba ni lini sasa vijiji hivi vitapata maji kama ilivyokuwa imeahidiwa toka miaka yote niliyoisema?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ajenda inayozungumzia ni suala zima la mradi wa maji wa Ziwa Victoria ambayo hivi sasa hata ukiangalia mradi huu hata watu wa Tabora hujo watakuja kusimama mpaka Sikonge, lakini kuna mpango mkubwa sana wa kuhakikisha kwamba maji haya yanafika mpaka Tabora mpaka Sikonge, lakini kuna changamoto ya baadhi ya vijiji vingine vilivyopitiwa lakini maji havikupata na Mheshimiwa Waziri wa maji alikuwa
akizungumza mara kadhaa hapa Bungeni kwamba lengo kubwa la Serikali ni kuangalia kwa sababu maji yanakwenda kwa utaratibu maalum, lazima yafike katika tanki halafu yaweze kurudi kwahiyo yote inatakiwa ku-design ili iweze kufanyika lakini Waziri hapa alizungumza mara kadhaa kwamba kuangalia jinsi gani watu wote waliopitiwa katika bomba la Ziwa Victoria wataweza kupata maji. Kwa hiyo, naomba nikuhakikishie kwa commitment ya Serikali abayo inaiweka kwa wananchi wa Tanzania na hasa wale wanaopitiwa katika bomba kubwa la Ziwa Victoria
ni kwamba Serikali itafanya kila liwezekanalo kuhakikisha ni jinsi gani maji sasa maji yaweze kuwafikia Wananchi wako na wewe mwisho wa siku ni kwamba tuweze kukuona hapa Bungeni kwa heshima kubwa ya Wasukuma wa kule.
MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante sana, naomba nimuulize bwana Waziri; katika Wilaya ya Kwimba kuna vijiji kumi ambavyo vilipangiwa kupelekewa maji katika mradi wa vijiji kumi, zaidi ya miaka kumi leo,
naomba leo nijue katika hivi vijiji vya Kadashi, Isunga, Shirima na Mhande mkandarasi hayupo site mpaka leo na kwa sababu nilishafanya mawasiliano na Mheshimiwa Waziri wa Maji mwenyewe kwa muda mwingi, nataka leo anipe majibi kazi hii ya miradi hii ya maji katika Wilaya ya Sumve na Kwimba lini itakamilika?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli anachokisema Mheshimiwa Mbunge haongopi na mimi naomba nikiri kwamba nimefika Jimboni kwake kule na miongoni mwa jambo katika taarifa ambayo niliyosomewa ni changamoto ya maji na hali kadhalika suala zima la vijiji kumi katika suala zima la mpango wa World Bank na ni kwa sababu nimesema hapa nyuma kwamba miradi hii ya maji maeneo mengi sana ilisimama na ilisimama kwa sababu hapa nyuma suala zima la kifedha lilikuwa siyo zuri zaidi, lakini
sasa hivi Serikali katika Mfuko wa Maji tumejipanga vizuri kuhakikisha miradi hii inatekelezeka. Lakini jambo lingine utakuta kuna changamoto ya mkandarasi, kwa hiyo kwa sababu taarifa zimeshakuja Serikalini na Waziri wa Maji taarifa hii anayo sasa kwa kina basi nadhani mpango mzuri utafanywa naamini jambo hili
litafanyika vizuri na miradi hii itakamilika na wananchi wa Jimbo lako watapata maji kwa sababu commitment ya Serikali hii kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji.
MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Kwa kuwa Naibu Waziri anayeshughulika na barabara yupo, je, anaweza akalithibitishia Bunge hili kwamba fedha hizi TANROADS
wameshazitenga kweli kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii? Swali langu la pili, je, ni lini madaraja haya yatajengwa, kwa sababu wananchi hawa wa maeneo ya Miesi, Kata za Mkundi na Mpindimbi kwa miaka minne sasa wanapata tatizo kubwa sana baada ya madaraja haya yaliyokuwepo kuzolewa na mafuriko, je, ni lini baada ya bajeti
kazi itaanza?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge sana kwa harakati zake kubwa na kazi kubwa anayofanya katika Jimbo lake kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za maendeleo. Kama tulivyosema, kutokana na kazi hiyo nzuri
ambayo ameifanya ndiyo maana sasa, kwa sababu barabara ile ilikuwa chini ya barabara ya Halmashauri lakini kutokana na msukumo mkubwa ndiyo maana TANROADS imeamua kufanya assessment ya barabara ile na kukubali
kwamba madaraja haya yataweza kujengwa.
Nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge hilo ondoa hofu kwa sababu kwanza imeshafanyika hiyo tathmini na kuona kwamba shilingi bilioni tatu na ofisi ya ujenzi naamini katika harakati za hii bajeti ambayo itakuja hapa tutaona katika jedwali hilo ambalo linaeleza kwa sababu tathmini wameshaifanya tayari.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, suala la ni lini barabara hii itajengwa. Barabara hii itajengwa mara baada ya kutengwa kwa bajeti, kwa hiyo, naomba nikuondoe hofu Mheshimiwa Dismas kwa sababu wananchi wa eneo lile wana umuhimu mkubwa wa barabara hii ambayo ni barabara ya kimkakati kwa suala zima la uchumi wa korosho katika maeneo haya, naomba ondoa hofu. Serikali iko tayari kuhakikisha kwamba itafanya kila liwezekanalo kuhakikisha wananchi wa Lulindi wanapata huduma ya ujenzi wa barabara.
MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika,
ahsante kwa kunipa nafasi hii na mimi niulize swali dogo la nyongeza. Matatizo yaliyoko huko Lulindi yapo katika Jimbo la Manyoni Magharibi, kuna barabara kutoka Idodyandole kwenda Ipangamasasi, kuna tawi la Mto Kizigo imekuwa ni
korofi sana na kwa nguvu ya Halmashauri hatuwezi kujenga;
Je, Mheshimiwa Waziri anaweza akatuahidi angalau kwa maneno kwamba Serikali kupitia TANROADS itatusaidia katika kipande hicho kidogo cha daraja?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba tupewe muda mfupi tu, hatutahitaji muda mrefu tutakuja kutoa taarifa ya barabara ambazo tunapendekeza zipandishwe hadhi na nyingine zikasimishwe kwa TANROADS.
Naomba tu nitoe tahadhari, inaonekana maombi ni mengi sana na tukipeleka barabara nyingi sana TANROADS uwezo wao kwa sababu kifedha haiongezeki sana kulinganisha na mzigo tunaowapa, tusije tukaishia nazo zikawa za sub standard kwa sababu kazi ni kubwa na uwezo
ni mdogo.
Kwa hiyo, nilitaka tu nitoe tahadhari hiyo lakini tutakuja kutoa taarifa hivi karibuni ni zipi zitapandishwa hadhi na zipi zitakasimiwa kwa TANROADS.
Mheshimiwa Spika, naomba tupewe muda kidogo.
MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa Serikali imekuwa ikipeleka fedha kidogo kidogo kwenye Halmashauri hizi ambazo ni mpya. Je, haioni kwamba sasa hakuna sababu ya kuanzisha maeneo mapya ya utawala kabla ya kumaliza maeneo ambayo tayari yameshaanzishwa na uendeshaji wake unasuasua?
Swali la pili, kuendesha Halmashauri ni gharama
kubwa; kunahitaji huduma za afya, miundombinu na
vinginevyo. Je, Serikali iko tayari sasa kuongeza bajeti kwenye
Halmashauri mpya zote nchini ili kuziondoa kabisa katika hali
ambayo sio nzuri sana kwa sasa na kuacha kabisa zoezi la
kuanzisha maeneo mapya ya utawala?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, concern ya Mheshimiwa Juma Suleiman Nkamia tumeipata lakini nikujua uanzishwaji wa Halmashauri hizi mara nyingi sana unaanzia humu Bungeni. Hapa nimekuwa nikijibu maswali kadhaa kwa baadhi ya Wabunge na hasa Malocha anaeniangalia kwa jicho la karibu sana hapa; kila Mbunge kutokana na jiografia jinsi ilivyo anapenda Halmashauri yake iweze kugawanywa au kwa mfano Halmashauri ya Sikonge kule
nilikofika ina square kilometa karibuni 27,000. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ukiangalia kweli kuna maeneo mengine ni kweli kulikuwa kuna haja ya kugawanya lakini vilevile na suala la kuhudumia hizi Halmashauri imekuwa ni changamoto kubwa. Kwa hiyo, sisi kama Serikali tutaangalia kwa kina jinsi gani tutafanya; lengo
kubwa ni wananchi waweze kupata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili jinsi gani hizi Halmashauri ziweze kuongezewa mgao wa fedha. Naomba niseme jambo hili kwamba, kama Serikali tunalichukua ndio maana hata ukiangalia suala la bajeti kidogo linaongezeka.
Changamoto kubwa ni kutokana na mapato yetu
tunayoyapata kama Serikali kwa ujumla. Kikubwa zaidi naomba kuzihamasisha Halmashauri sasa ziweze kuweka mipango mizuri ya jinsi gani itakusanya mapato yake ya ndani kwa sababu mpaka leo hii ukija kuangalia Halmashauri
mbalimbali hata ile bajeti tuliyoitengea mwaka huu zimesua sua katika ukusanyaji wa mapato. Kwa hiyo, naomba nizihamasishe Halmashauri zihakikishe japokuwa tunazigawanya, lakini lazima commitment ya kukusanya mapato iwe ni kipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini concern yake
Mheshimiwa Nkamia naomba tuipokee kama Serikali, kama ni ushauri mpana ili Serikali yetu iweze kwenda vizuri.
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kuna Halmashauri nyingi zilianzishwa kwa misingi ya kisiasa na kuacha Halmashauri ambazo zina hadhi kabisa ya Halmashauri. Vipi Serikali inaonaje kuzifuta mara
moja Halmashauri ambazo zilianzishwa hazina vigezo na kuzipa Halmashauri zenye vigezo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya Mheshimiwa Keissy ndio hoja ile ile ya Mheshimiwa Juma Nkamia. Ndio maana nimesema tukisema kuanzia leo hakuna kugawanya Halmashauri zingine, kuna Halmashauri zingine zina mzigo mkubwa kutokana na jiografia yake ilivyo kubwa kwelikweli. Kwa hiyo, tukisema kuanzia leo ni marufuku nadhani kuna baadhi ya Halmashauri hatutazitendea haki. Hata hivyo, ni kweli kuna Halmashauri zingine sasa hivi ukiziangalia kweli kama inawezekana tuzifute kwa sababu jiografia yake na hata population ya watu bado ni ndogo zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, haya yote ni
mawazo ya Waheshimiwa Wabunge lakini jambo kubwa ni kuijenga vizuri Serikali yetu. Nadhani mawazo yao ngoja tuyachukue na tuone kwa pamoja way forward ni nini, lengo likiwa hapo baadaye Serikali yetu iweze kuendeshwa vizuri.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri niwashukuru Naibu Waziri wa Afya na Naibu Waziri wa TAMISEMI kwa kuja Mbulu na kutembelea baadhi ya Halmashauri za Wilaya ya Mbulu na vituo hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika swali la msingi muuliza swali alitaka pia mpango mkakati wa Serikali kuajiri kada za afya kwa maelezo ya swali la msingi. Je, Serikali ina mkakati gani na ajira ya kada za afya ili kupunguza tatizo
hili?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; ongezeko la asilimia 9.7 ni dogo sana ukilinganisha na tatizo la huduma ya afya hususan dawa na vifaa tiba katika nchi yetu. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kukaa chini na kwenda katika Halmashauri zote nchini kufanya tafiti ili waweze kuleta mpango mkakati wa kuondoa tatizo la
upungufu wa dawa na vifaa tiba katika nchi yetu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza mpango mkakati wa Serikali ni suala zima la ajira kama tulivyosema. Niseme wazi kwamba ajira zilisimama kwa lengo mahususi kutokana na mipango ya Serikali na hapa juzi mnaona kwamba mchakato wa ajira za elimu hasa walimu wa sayansi umeanza lakini sio muda mrefu kwa kadri Ofisi ya Rais, Utumishi itakavyokuwa imejipanga itatoa vibali vya ajira kwa ajili ya sekta ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba tuondoe hofu katika suala hilo kwa sababu tunajua wazi kwamba kweli tuna changamoto ya wahudumu mbalimbali hasa katika sekta ya afya katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la
mpango mkakati ni kweli, kwanza naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge leo hii ukifanya reference katika Halmashauri zetu kuna ma-DMO wengi sana walikuwepo hapa Mkoani Dodoma. Lengo ni kuhakikisha sasa tunatengeneza mipango mizuri na sio ile mipango ya mezani peke yake; tunatengeneza mipango mizuri ya kwenda kujibu matatizo ya afya katika maeneo yetu. Leo hii tumesema fedha zitakwenda moja kwa moja mpaka katika kituo cha afya
na zahanati; tumepata akaunti zote za vituo vya afya katika nchi yetu; huo ni mpango mkubwa kweli.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo naomba
niwaeleze ndugu zangu wakati mwingine tuna tatizo kubwa la usimamizi wa rasilimali fedha. Katika mwaka 2016/2017, mpaka mwezi Julai kuna outstanding fedha ambazo ni za Basket Fund hazijatumika karibu bilioni 20. Katika Mkoa wa Manyara peke yake kuna karibu milioni 500 mpaka mwezi Julai zilikuwa hazijatumika. Mpaka tunapozungumza leo hii bajeti yetu ya mwaka huu Basket Fund ni zaidi ya shilingi bilioni 106.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mpaka mwezi
Desemba fedha zile ambazo zimekuwa accrued ambazo hazijatumika na fedha zilizoingia ni takriban shilingi bilioni 71; kati ya fedha hizo 71, fedha ambazo zimetumika mpaka hivi sasa ni asilimia 55 tu mpaka mwezi Desemba, nini maana
yake? Fedha zipo katika Halmashauri yetu lakini dawa hakuna.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwasihi Waheshimiwa
Wabunge kwamba tuhakikishe katika Halmashauri zetu fedha za Basket Fund tuwabane ma-DMOs na wahasibu wetu tuweze kuzibainisha ziende zikanunue dawa na vifaa tiba; lengo kubwa ni kumwokoa mwananchi wa Tanzania.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Tatizo lililopo Manyara linafanana kabisa na tatizo lililopo Wilaya ya Kakonko. Tatizo ambalo lipo Hospitali ya Wilaya ya Kakonko ambayo ni kituo cha afya haijapata hadhi ya Wilaya ni kupata dawa zenye hadhi ya kituo cha
afya lakini zinatumiwa na wananchi wa Wilaya nzima kama Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Naibu Waziri alitembelea Kakonko akaona hali ya kituo cha afya ilivyo…
MHE. KASUKU S. BILAGO: Ndiyo nauliza hivyo; ni lini sasa Kituo cha Afya Kakonko kitabakia kuwa kituo cha Afya ili iweze kujengwa Hospitali ya Wilaya ya Kakonko?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kweli nikiri kwamba, nimefika pale Kakonko na nimetembelea kile kituo cha afya tukiwa pamoja na Mbunge ni kweli kuna changamoto hizo kubwa lakini tubaini kwamba vipaumbele hivi mchakato wake unaanza kiwilaya. Hata hivyo, Mheshimiwa Bilago anafahamu kwamba pale alikuwa hana ambulance; Serikali imepeleka tayari ambulance kipindi hiki kifupi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika mpango wa bajeti katika Basket Fund yake ana milioni 395, fedha ambayo nimpe taarifa mpaka mwezi wa Saba Halmashauri yake zaidi ya shilingi 197 zilikuwa hazijatumika zimevuka mwaka wakati
wananchi wana matatizo. Kwa hiyo, naomba niseme sisi kama Serikali tutaangalia jinsi gani tutafanya katika mchakato huu ili kwenda pamoja na wenzetu wa Halmashauri, lakini jambo la msingi ni lazima tuwasimamie watendaji wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati mwingine kuna
baadhi ya wengine wanafanya mambo ya hovyo na wananchi wanaendelea kupata shida wakati fedha zipo; Mbunge na watu wengine wanapata matatizo kumbe fedha zipo watendaji wetu wameshindwa kutimiza wajibu wao. Kwa hiyo, tupo pamoja kuhakikisha mambo yanaenda vizuri
katika Halmashauri zetu.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, je, Serikali ina mpango gani wa kuzielekeza Halmashauri kutumia force account ili miradi midogo midogo kama hii iweze kutengenezwa kwa fedha ndogo na iweze kuleta impact?
Swali la pili, kwa kuwa jambo hili linafanana kabisa
na vituo vya afya vilivyoko Jimbo la Magu katika kituo cha afya Lugeye pamoja na Nyanguge. Serikali ina mpango gani wa kuvijengea majengo ya upasuaji ili wananchi waweze kupata huduma karibu? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali hivi sasa si kutoa maelekezo, tayari tumeshatoa maelekezo hivi sasa na Halmashauri mbalimbali zinaendelea kutumia force account na tumepata mafanikio makubwa sana, kwa sababu maeneo mbalimbali unapopita hivi sasa mradi ambao zamani ulikuwa saa nyingine ulikuwa unagharimu shilingi milioni 150 utakuta sasa hivi milioni 70 mradi umekamilika tena upo katika ubora unaokusudiwa.
Kwahiyo Mheshimiwa Kiswaga ni kwamba sasa hivi jambo hilo linaendelea na linaendelea kwa ufanisi mkubwa, na nipende kuwashukuru sana Wenyeviti wa Halmashauri na Wakurugenzi ambao wanasimamia jambo hili kwa uzuri zaidi
na hasa Waheshimiwa Wabunge katika Majimbo yenu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, katika suala zima la Jimbo la Magu ambalo Mheshimiwa Mbunge umesema na ni kweli, katika harakati za Serikali tuna mpango ambao si muda mrefu sana tutakuja kuuanza katika kituo chako kimoja cha afya tutakuja kujenga jengo la upasuaji na kuweka vifaa tiba vyote. Kwa hiyo, naomba nikushauri
Mheshimiwa Mbunge kwamba usiwe na wasiwasi Serikali yako kama kila siku inavyopiga kelele hapa Bungeni itaendelea kushirikiana nanyi na ujenzi huo Mungu akijaalia utaanza hata kabla ya mwezi wa sita.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Katika Mkoa wa Arusha kuna majimbo saba na katika majimbo hayo majimbo mawili yana jiografia ngumu sana
ikiwemo Jimbo la Longido na Jimbo la Ngorongoro. Je, Serikali iko tayari sasa katika bajeti tunayoiendea kutazama majimbo haya kwa mujibu wa jiografia yao ili wananchi wanaoishi
katika maeneo hayo waweze kupata huduma za afya kwa urahisi na kwa wakati?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba Serikali inapeleka nguvu kubwa sana katika eneo hilo, na ndiyo maana juzi juzi nilikuwa katika Wilaya hizo zote mbili;
Wilaya ya Longido pamoja na Wilaya ya Ngorongoro, katika Wilaya ya Ngorongoro siyo muda mrefu sana Mungu akijaalia katika kipindi hiki cha katikati tutakwenda kuwekeza nguvu
kubwa sana kwa kupeleka takribani milioni 700. Lengo kubwa ni kwamba maeneo yale yana jiografia tata sana wananchi waweze kupata huduma kujua kwamba Serikali yao ipo
vitani katika kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma hiyo inayokusudiwa.
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kuna wilaya nyingi mpya ambazo zina matatizo sana ya hata kutokuwa na Hospitali za Wilaya. Na kwa kuwa majibu yake anasema kwamba kuna fedha ambazo zimetengwa, je, Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza kunihakikishia kwamba katika Wilaya ya Busega kituo cha Nasa hizo fedha zitapatikana lini?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Dkt. Chegeni unafahamu na wewe kule kwako umenikaribisha, nakushukuru sana. Hicho kituo cha afya ulichokisema
miongoni mwa maeneo ambayo yana changamoto, na akina mama wanapata shida kubwa sana kupata huduma za upasuaji. Nilikueleza wazi kwamba katika kipindi cha huu
mwaka tutafanya kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba tunajenga jengo la upasuaji kama nilivyosema katika maeneo mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kuwa na imani,
kwamba Serikali kwa kupitia Wizara ya afya tuna mkakati mpana sana kuhakikisha kwamba tunapelekea huduma katika maeneo hayo na Mungu akijaalia kabla ya mwezi wa sita tunaweza tukaenda kuweka jiwe la msingi sawa sawa
na kituo cha afya cha Malya kule kwa ndugu yangu Ndassa.
MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti katika hospitali yetu ya Wilaya ya Siha hatuna hatuna jokofu na imekuwa inaleta usumbufu sana kwenye kuhifadhi miili ya marehemu wetu.
Je, ni lini Serikali itatuletea jokofu kupunguza upungufu huo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Hospitali ya Siha takribani wiki sita zilizopita nilikuwa pale Siha na namshukuru sana Mbunge tulikuwepo pamoja na
tulitembelea hospitali ile na kipindi kilichopita hapa nilitoa maelekezo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilivyofika pale Siha,
kutokana na changamoto tuliyobaini pale, kwamba tumepeleka fedha lakini matumizi yale ya fedha tumeona hayaelekezwi sawa sawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kabla ya jokofu kuanza kuna suala zima la fedha tulizozipeleka pale lazima zitumike vizuri na tumeshatoa maelekezo hayo. Lengo letu ni kwamba lile jengo, floor ya juu iweze kukamilika vizuri lakini hatuachi hapo kwa sababu changamoto kubwa ya pale lazima tuhakikishe hospitali ile inafanya kazi vizuri na Serikali
itaweka nguvu za kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulishapeleka zaidi ya milioni 250, inafanya kazi lakini suala la jokofu litakuwa ni kipaumbele chetu ili kuhakikisha, lengo kubwa hospitali ile inafanya vizuri kwa wananchi wa Siha.
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti
nikushukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.
Kwanza, kwa kuwa michakato hii inachukua muda mrefu sana ambayo inaanzia kwenye ngazi za vijiji mpaka juu kama Naibu Waziri alivyosema.
Je, endapo michakato hii katika ngazi za chini
itakamilika mapema, nini kauli ya Serikali Kuu ili na wao waharakishe na wananachi hawa wapate haki zao?
Swali la pili, kwa kuwa tunapokaribia wakati wa
Uchaguzi Mkuu, Serikali imekuwa na hali ya kugawa kata zetu na vijiji ili kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma kwa karibu. Naomba nifahamu Serikali ina mpango gani
kuanza mchakato huo mapema kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili kuondoa usumbufu na maandalizi pia ya muhimu kwa wananchi hawa ambao maeneo yao ni makubwa na Kata zao ni kubwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA
SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti kwanza katia
sehemu ya kwanza ni kwamba mchakato umekamilika na
Makao Makuu ya Halmashauri imeshathibitishwa ndiyo ile
ambayo imetajwa pale isipokuwa Mheshimiwa Mbunge
alikuwa na utata katika hayo Makao Makuu mapya, kwa
hiyo mchakato huo ulishakamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala zima la kugawa
wakati wa kuelekea kwenye uchaguzi nadhani hii sasa ni
mamlaka zetu katika Ward Council zetu, vikao vyetu vile vya
kisheria kama nilivyovisema, ambapo inaonesha baadaye
jambo hili litaenda katika Tume ya Uchaguzi kupita Ofisi ya
Waziri Mkuu.
Kwa hiyo, hakuna shaka naamini kwamba kila mtu
katika maeneo yake anabaini changamoto zinazokabili eneo
hilo na tutafaya maandalizi ya awali ilimradi kuepusha
ukakasi kwamba maeneo yanagawiwa muda mfupi kabla
ya uchaguzi.
MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Kwa kuwa Wilaya ya Ngorongoro ni kubwa kuliko
Mkoa wa Kilimanjaro, hali inayopelekea jiografia ya Wilaya hiyo kuwa ngumu. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kugawa Wilaya hii ya Ngorongoro au kuweka Halmashauri mbili ili kuwasogezea wananchi wa Ngorongoro huduma kwa karibu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli na Mheshimiwa Mbunge pale wa Jimbo hio la Ngorongoro ambalo Naibu Waziri wa Kilimo na yeye alinialika niweze kufika kule jimboni kwake juzi juzi hapa nilikuwepo kule. Kwa
umbali kweli jiografia ya Ngorongoro ina changamoto kubwa sana kwa sababu ukianzia hapa getini ukitoka hapa Karatu mpaka unafika Makao Makuu kule Loliondo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nilipata fursa ya
kutembelea mpaka Ziwa Natron kwenda shule ya sekondari ya Ziwa Natron. Jiografia ya Ngorongoro kweli ni kubwa zaidi, lakini mara nyingi sana maeneo haya yanagawanywa kutokana na population.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia eneo kubwa la Ngorongoro ni hifadhi, lakini kama kutakuwa na haja ya kuweza kugawanya basi kwa mchako ule ule wa kisheria wananchi wa aeneo hilo watafanya hivyo na Serikali itaangalia kama kuna umuhimu wa kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini inawezekana
tunaweza tukaangalia mbali kwa sababu Ngorongoro na Serengeti ukiangalia jiografia yao ina changamoto kubwa sana. Hili sasa tuwaachie wenye maeneo hayo mkaweza kufanya maamuzi sahihi kama ulivyo Mheshimiwa Catherine Magige unavyokuwa na wazo hilo, basi na Serikali itaangalia nini cha kufanya kwa maamuzi sahihi kwa maslahi mapana kwa wananchi wa Ngorongoro.
MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Pamoja
na majibu mazuri ya Serikali, sote tunajua kazi za Wenyeviti, wamekuwa wanafanya kazi nzuri sana katika mitaa na vijiji vyetu, lakini hakuna hata siku moja wamelipwa posho.
Nataka Serikali iniambie leo ni lini itapanga kiwango cha kuwalipa Wenyeviti hawa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Wenyeviti hawa wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira
magumu sana, wakati huo hawa ndio wasimamizi namba moja wa usalama katika vijiji na vitongoji vyetu, wanatatua migogoro kila siku, watoto wa mitaani wakipotea, wanapelekwa kwenye Wenyeviti, tukigombana usiku break ya kwanza kwa Wenyeviti, sote tunajua kazi za Wenyeviti.
Je, Serikali ipo tayari kuwapa hata usafiri angalau baiskeli za kuwasaidia?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kweli kama anavyosema Mheshimiwa Bupe, Wenyeviti wetu wanafanya kazi kubwa sana katika vijiji, hili jambo halipingiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kusema lini? Naomba nizungumze wazi, kwa sababu tulikuwa na changamoto
kubwa hapa nyuma, hata ukija kuangalia Halmashauri zetu, hata kupeleka zile fedha, Halmashauri nyingine ilikuwa
inaonekana kama ni hisani. Ndiyo maana sasa hivi tunafanya haya marekebisho na muswada huu utaingia Bungeni wakati wowote. Hivi sasa umeshaiva na wadau wameshiriki vya kutosha. Katika Sura ya 290 kifungu cha 54 kinafanyiwa marekebisho na Waziri mwenye dhamana sasa atapewa utaratibu wa kuweka kama misingi ya kisheria, kuzielekeza Halmashauri sasa kupeleka zile fedha. Mwisho wa siku ni kwamba aidha, Halmshauri wataweza kupata hasa Wenyeviti wetu wa vijiji ambao tunatambua kwamba wanafanya kazi kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la usafiri, ni kweli kama nilivyosema ni kwamba utakuta sehemu nyingine
Mwenyekiti wa Kijiji anatoka kitongoji kimoja anakwenda kitongoji kingine, changamoto yake ni kubwa. Vilevile kwa sababu kama tutaweka utaratibu mzuri wa kisheria na hata ukiangalia sheria, sehemu inayozungumza mambo ya expenditure pale, inazungumza kama kuna matumizi ya fedha nyingine zinazoweza kutumika kwa maslahi mapana ya kujenga eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utaratibu huo tukishafanikiwa vizuri, basi tutatoa maelekezo ya kutosha kuona jinsi gani tutafanya, tutaangalia na rasilimali fedha zilizopatikana angalau kama itawezekana baadhi ya vipando hasa baiskeli, lakini maelekezo hayo yatakuja baada ya kurekebisha sheria yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge jambo, lako ni la msingi na Serikali tunalifanyia kazi kama nilivyozungumza.
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya
Mheshimiwa Waziri, Halmashauri nyingi zina mapato kidogo na kwa vile baadhi ya vyanzo vya mapato Serikali Kuu
imevichukua, kwa hiyo, ina maana kwamba baadhi ya Halmashauri hazitaweza kulipa Wenyeviti kwa mujibu wa
majibu ya Mheshimiwa Waziri alivyosema hapa. (Makofi)
Je, Serikali ina mpango gani mbadala kuhakikisha kwamba Wenyeviti wote, regardless wanatoka kwenye
Halmashauri ipi na wenyewe waweze kupata malipo kama haya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna wakati mwingine marejesho yanakuwa siyo rafiki sana, ndiyo maana katika utaratibu wa sasa inawezekana Wabunge wengine watauliza kwamba property tax imechukuliwa imeenda Serikali Kuu, tunafanyaje na haijaridi? Hili hata Waziri wa Fedha baadaye akija ku-table bajeti yake hapa katika mjadala mpana baadaye, itaonekana ni jinsi gani tutafanya. Lengo letu ni kuziwezesha Halmashauri zetu cha kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu changamoto hii hata Waheshimiwa Wabunge wengine wanaweza
wakasimama baadaye wakasema hata Madiwani wengine wamekopeshwa kwenye mabenki, wanataka kupelekewa mahakamani, ndiyo maana nasema katika mchakato huu mpana, mara baada ya kurekebisha sheria, kwa sababu sheria ile itakuja hapa mtaona kwamba Waziri mwenye dhamana atakuwa anapata fursa ya kuhakikisha Halmashauri zinaenda vizuri, kwa sababu zimewekwa kwa mujibu wa Katiba, Ibara ya 145 na utelekezaji wake Ibara ya 146.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Waziri mwenye dhamana amepewa mamlaka hiyo kwa utaratibu wa sheria
za nchi Sura namba 287 na 288 ile ya vijijini na ile ya miji. Kwa hiyo, katika kurekebisha Sheria ya Fedha, itamsaidia sana Waziri mwenye dhamana kufanya maamuzi hayo mwisho wasiku kwa kuangalia jiografia ya Halmashauri hizi ambapo zenyewe zinatofautiana katika nguvu ya kimapato.
Halmashauri ya Ilala huwezi ukafananisha na Halmashauri ya Kakonko kwa mwalimu wangu pale, hizi zinatofautiana. Kwa hiyo, Waziri mwenye dhamana atakuwa anapata nafasi nzuri kuiangalia nchi kwa upana wake na kuangalia hizi Halmashauri, Madiwani na Wenyeviti ili kazi iende vizuri.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na kilio cha muda mrefu cha Madiwani nchini kutokupata nyongeza ya
posho kwa muda mrefu. Ni ukweli usiopingika kwamba Madiwani hawa wamekuwa wakifanya kazi kubwa hasa
kutusaidia sisi Wabunge tukiwa huku Bungeni muda mrefu, lakini Madiwani hawa wamekuwa wanasimamia fedha
nyingi sana zinazopelekwa katika Halmashauri zetu, lakini wameachwa hawana mafunzo, hawana vitendea kazi na
posho zao haziongezeki.
Je, Serikali sasa iko tayari kumaliza kilio cha Madiwani cha muda mrefu katika nchi hii?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli
anavyosema Mheshimiwa Paresso na tukifanya reference ya mwaka 2002 kulikuwa na Tume iliyokuwa inaitwa Tume ya Lubeleje ambaye ni Mbunge senior yuko hapa. Tume hiyo iliundwa na iliweza kubaini mambo hayo. Bahati nzuri katika mikitano yetu ya ALART miwili tuliyofanyia hapa Dodoma na Musoma, jambo hilo vilevile lilijitokeza. Serikali hivi hatuwezi kutoa kauli hapa haraka haraka kwa sababu mchakato huu wa bajeti tutakuja ku-table bajeti na mambo mengine tutajadili kwa pamoja hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kazi ya Madiwani ni kubwa na Serikali inaona hilo, lakini tutajadiliana kwa upana
katika mchakato wa bajeti tuone ni nini tunafanya, way forward katika suala zima la Madiwani wetu katika Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, ninayo maswali
mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tumeleta maombi haya muda mrefu; na vikao hivi vimekaa muda mrefu; na tuna miji miwili ya Dongobesh na Haydom; na kwa kuwa muda umepita, je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari sasa
kutuma wataalamu wake kutoka TAMISEMI ili kushirikiana na wataalamu walioko Wilayani kusaidia vigezo hivi kutimia?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Mheshimiwa Waziri yuko tayari, je, ni lini sasa atawatuma wataalamu hawa ili
kiu ya wananchi wa Mbulu Vijijini itimie?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kama
nilivyosema pale, kwanza elekezo langu ni kwamba naomba niwasihi ndugu zetu wa Mbulu kwamba kwa sababu kazi kubwa na Mbunge umekuwa ukipigania jambo hili sana kwa wakati wote kwamba zile taarifa zipite katika vikao vile vya kisheria sasa zije huku kwetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuwatuma hili jambo, siyo tatizo kubwa sana, kwa sababu hata Mheshimiwa
Flatei kama atakumbuka, kuna team mara ya kwanza ilikuja kule kwa maombi yake vilevile na taarifa tunazo kuhusu Mji huu wa Haydom.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mheshimiwa Mbunge amesema na suala zima la Mji wa Dogobesh. Kama
nilivyosema mwanzo ni kwamba hata Mji wa Dogobesh wakati unataka upandishwe, lazima taratibu hizi za kisheria ziweze kufuatwa ambapo mamlaka haya kuanzishwa kwake, yanatuletea utaratibu wa kisheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Flatei naomba nikutoe hofu kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI, cha kufanya ni kwamba tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo kukupa ushirikiano wote. Ninachokiomba ni kwamba vile vikao vya kisheria viweze kutimiza wajibu wake, tukipata taarifa hizo katika ofisi yetu, nitakupa ushirikiano wote
kuhakikisha Halmashauri yako katika maeneo yako ya Mamlaka Mji Mdogo, basi yaweze kupitiwa na kuweza
kupewa hadhi kama tulivyozungumza.
MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa matatizo yaliyoko huko Mbulu yanafanana kabisa na matatizo yaliyopo Itigi katika Jimbo la Manyoni Magharibi, ni kwamba Itigi ni eneo kubwa sana, lipo katika Wilaya ya Manyoni. Kutoka mwanzo wa Tarafa ya Itigi hadi mwisho kuna zaidi ya kilometa 200 na ni Tarafa moja tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba kuuliza swali dogo tu la nyongeza kwamba Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuigawa Tarafa hii ya Itigi kuwa Tarafa nyingi kwa sababu ya eneo na jiografia ni eneo kubwa sana?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tuko tayari, lakini kwanza lazima mchakato huu uanze katika suala zima la vijiji, itakuja katika vikao vya Ward Council, vitakuja katika vikao vya full council, vitakuja DCC, RCC vitafika kwetu, then Waziri mwenye dhamana, kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa, Sura ya 287 kifungu cha 10 ambacho kinafanya variation ya haya maeneo, atachukua jukumu hilo la kufanya hivyo.
Kwa hiyo, ndugu yangu wa Itigi wala usiwe na hofu katika hilo, anzeni mchakato, sisi Serikali tuko kwa ajili ya
kutekeleza hayo ambayo mtayafanya.
MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nampongeza ndugu yangu Naibu Waziri kwa kazi nzuri anayoifanya na hasa ya kushughulikia matatizo ya wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika tatizo la kule Mbulu hasa kule Haydom, inalingana kabisa na Korogwe Vijijini
katika Mji Mdogo wa Hale na wewe mwenyewe umeshafika pale; je, Serikali Serikali ina mpango gani wa kupandisha hadhi Kijiji cha Hale kuwa Mji mdogo kule Korogwe Vijijini?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tuliweza kufika pale kwa sababu walikuwa na concern ya Mji wa Mombo. Hayo yote, hata timu yetu tuliituma, waliweza kufika kule na kufanya assessment na wataalamu wameshafanya jukumu lao, iko katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI sasa inafanyiwa kazi. Kwa hiyo, mchakato ukikamilika, basi mtapata mrejesho nini kimepatikana katika eneo hilo.
MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Serikali kwamba Halmashauri ya Busokelo haijakidhi vigezo vya kuwa Wilaya, nina maswali mawili kwa Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo vigezo anavyosema haijakidhi sijui ni vipi kwa sababu vigezo ambavyo vinazingatiwa, hasa ni idadi ya watu pamoja na jiografia ya eneo husika, kwetu kwa sababu hii tathmini ilishafanyika tangu miaka 2013 na sasa hivi ni 2017. Hauoni kwamba kuna
umuhimu sasa wa kuanzisha hiyo Halmashauri ya Busokelo iwe inaitwa Wilaya ya Busokelo badala ya sasa ilivyo? Swali la pili, kwa kuwa Mkuu wa Wilaya pamoja na DAS wanafanya kazi nzuri katika Wilaya ya Rungwe, kwa bahati mbaya kwa sababu ya jiografia ya Rungwe ilivyo kuna zaidi ya kata 40 na huyu Mkuu wa Wilaya hawezi kusimamia ama kufuatilia zote kwa wakati mmoja kufuatana na jiografia ilivyo.
Je, hauoni pia ni miongoni mwa sababu ambayo
inaweza ikasababisha ianzishwe Wilaya ya Busokelo na hivyo iweze kuanzishwa haraka iwezekanavyo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwa sababu specification inataka angalau eneo hilo liwe na eneo lisilopungua kilometa za mraba 5,000 nwakati pale kiuhalisia ziko kilometa za mraba 969. Kwa hiyo, hii ilikuwa ni kigezo kimojawapo ambacho kimesababisha isiweze ku-qualify. Kipindi kile idadi ya watu kwa muongozo inatakiwa watu wasiopungua 250,000 lakini katika kipindi kile tathmini ilivyofanyika kulikuwa na watu takribani 96,348.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninafahamu muda mrefu sasa hivi umeshapita kutoka kipindi kile mpaka sasa hivi hii tathmini ukiiangalia huenda population imeongezeka, lakini vilevile hata ukiangalia suala zima la tarafa, vigezo lazima angalao kuwe na tarafa tatu pale ukiangalia ni tarafa moja. Ninafahamu kwamba mlikuwa na juhudi ya kuitenga ile Tarafa moja mpate tarafa nyingine tatu, hii nilidhani kwa sababu Mbunge mnafahamu kama ulivyosema mna kata zipatazo 40, mnaweza mkakaa kwa pamoja sasa na RCC
yenu kuangalia mnaweza kuishauri vizuri nini cha kufanya. Baadae ikionekana vigezo hivi sasa vimekaa vizuri basi Serikali itaona nini cha kufanya na jinsi gani ya kupata eneo hili kuwa eneo la kiutawala la Kiwilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala kwamba Mkuu wa Wilaya ya Busokelo anahudumia eneo kubwa sana, kwa hiyo kuna haja ya kuona hili jambo sasa ikiwezekana Wilaya ile sasa Busokelo iwe Wilaya kamili. Kama nilivyosema pale awali ni kwamba hivi sasa ninyi angalieni jinsi ya kufanya. Nafahamu kwamba ni kweli Mkuu wa Wilaya ya Rungwe anafanya kazi kubwa sana, nilikuwa nae pale site siku ile tulipopata lile tatizo, kweli ni miongoni mwa Wakuu wa Wilaya ambao wanajituma sana katika kazi yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile wote kama Viongozi Wakubwa na Mheshimiwa Naibu Spika uko hapa, nadhani mtaliangalia kwa uzito wenu kwa jinsi gani mtafanya, kama Busokelo, kama Rungwe kwa wakati mmoja ni jinsi gani hata mtafanya mipaka yenu na kila kitu. Lengo kubwa ni kupeleka huduma kwa wananchi na Serikali mkiona kwamba mmekidhi vigezo hivyo, haitasita kufanya maamuzi sahihi.
MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Matatizo yaliyopo huko Busokelo yapo pia katika
Halmashauri ya Wilaya ya Itigi. Katika Wilaya ya Manyoni kuna Halmashauri ya Manyoni na Hamashauri ya Itigi; Halmashauri ya Itigi square kilometer zinakidhi na maombi yamekuwa yakipelekwa kila mara na toka mwaka 1980 Serikali imekuwa ikiwaahidi wananchi wa Itigi kwamba watapatiwa Wilaya kamili.
Je, sasa ni lini Serikali itaipa Halmashauri ya Itigi kuwa Wilaya kamili?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ukiangalia Manyoni, lazima tufahamu juhudi kubwa ya Serikali iliyofanya pale, mwanzo ile yote ilikuwa inaitwa Wilaya na Halmashauri ya Manyoni. Hapa katikati ndiyo tukapata Halmashauri mpya ya Itigi na wewe Mheshimiwa Mbunge unafahamu hata suala zima la upelekaji wa fedha ndiyo kwanza tumepeleka kwa ajili ya kujenga miundombinu ya Halmashauri ile.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili ninafahamu
kwamba, siku ile nilikuwa na Mkuu wa Wilaya pale na alisikitika katika hilo alisema kwamba mafuta anayoyatumia ni kwamba, akiamua kuzunguka eneo lake matufa yanaisha kwa sababu Manyoni ukijumlisha na Itigi ni eneo kubwa sana.
Naomba niseme japokuwa maombi hayo inawezekana mwanzo yalikuja yalidondoka kwa sababu yalishindwa kupata sifa, hizo sifa sasa hivi zikikamilika basi naomba mfanye ile michakato ya kisheria kama inavyokusudiwa kuanzia katika ngazi za Ward DC, Baraza la Madiwani, DCC, RCC na ikifika katika Ofisi ya Rais – TAMISEMI
na Waziri wangu yuko hapa, hawezi kushindwa kufanya maamuzi sahihi kwa kadri anavyoona jambo hilo linafaa kwa maslahi mapana ya wananchi wa Itigi.
MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda yenye majimbo ya Mwibara na Bunda ni majimbo mawili ambayo hayapakani. Jimbo la Bunda liko kwingine na Jimbo la Mwibara liko kwingine, lakini ndiyo yanaunda Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa jambo hili
tulishampelekea Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI, na kwa kuwa Mwibara iliwahi kuwa Jimbo tangu mwaka 1974, lakini tulishapeleka TAMISEMI iwe Wilaya mpaka leo vigezo ilishatimiza lakini hatupatiwi.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri anawaambia nini wana - Mwibara juu ya jambo hili ambalo ni changamoto ya miaka mingi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, wasiofahamu hili Jimbo la Mheshimiwa Kangi Lugola ni sawasawa kama unazungumza kama lile bakuli halafu katikati kuna kile kisahani. Katikati ya kisahani pale unapata Jimbo la Dada yangu Mheshimiwa Ester Bulaya, Jimbo la Bunda Mjini. Ukienda huku utakuta Jimbo la ndugu yangu Mheshimiwa Boniphace Getere na huku unakuta Jimbo la Mwibara, kwa
hiyo anachozungumza ni kweli.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaambie
Waheshimiwa Wabunge, wakati mwingine tunapoenda kufanya maamuzi ya mgawanyo wa haya maeneo wakati mwingine hatuweki mipaka sahihi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, pale hata
ukiangalia ni kama yai, katikati kiini cha yai ndiyo Jimbo la Mheshimiwa Ester Bulaya hata ninaamini inawezekana ukatokea ugomvi mkubwa wa wapi Halmashauri ya Jimbo hilo itajengwa inawezekana ni kutokana na huko mwanzo maamuzi yetu hayakuwa sahihi. Inawezekana ilikuwa ni mihemko ya kisiasa ya kugawanya, jinsi gani tugawanye, hatukufanya maamuzi sahihi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kwamba hili kweli ni changamoto kubwa. Kama Mheshimiwa Kangi Lugola nafahamu kweli changamoto yako ni kubwa na nimefika mpaka kule ziwani siku ile nilivyofika, nimechanginyikiwa kweli Jimbo lako lilivyo. Basi mtajadiliana kwa pamoja kule katika vikao vyenu kuangalia nini cha
kufanya. Jukumu letu kubwa Serikali ni kuona jinsi gani tutafanya ili wananchi waweze kupata huduma. Hivi sasa ninaamini wewe na Mbunge mwenzako ni lazima mkae vizuri la sivyo inawezekana mkapishana wapi Makao Makuu yenu itaenda kujengwa kwa maslahi mapana ya maeneo yenu. Ahsante sana.
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Vilevile katika Wilaya ya Serengeti ni moja ya Wilaya kongwe ambayo kimsingi ni Wilaya ambayo iliizaa Bunda; na ni Wilaya ambayo ina changamoto kubwa sana kijiografia, ni Wilaya ambayo ni kubwa kwa eneo, pia, ni Wilaya ambayo ina kata nyingi kweli.
Je, ni lini Wilaya hii itagawanywa kuwa Wilaya mbili?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba tuweke kumbukumbu sawa, hapa ukiwa unajibu maswali haya lazima kidogo akili yako ikae vizuri. Kwa sababu Wabunge wengine wanasema maeneo yasigawanywe, wengine
wanasema maeneo yagawanywe.
Mheshimiwa Mbunge, nadhani unakumbuka siku ile tulienda wote mpaka usiku tumetoka kule tukiwa Serengeti kwako. Ni kweli Kata zako zimekuwa scattered sana, ndiyo maana nalifananisha Jimbo lako na lile Jimbo la Ngorongoro, ukiingalia jiografia yake ni jiografia yenye changamoto kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutaangalia jinsi gani tutafanya kwa sababu Serikali hii hatuwezi kugawanya kila maeneo tu, ni lazima kuangalia jinsi gani kuweza kuyahudumia yale maeneo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pale kwenye haja na michakato halali na vikao vyetu huko ambako mamlaka tulizopita mamlaka za Wilaya na mamlaka za Mikoa, zikifanya maamuzi hayo basi jambo hilo litakuja katika Ofisi ya Rais TAMISEMI na Waziri wangu ataliangalia, atalipima, pale atakapoona linakidhi basi atafanya maamuzi sahihi, kutokana na uhalisia wa eneo hilo.
MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini niweke wazi tu kwamba vijiji vilivyofaidika mpaka sasa ni vijiji vitatu ambavyo ukilinganisha na jumla ya vijiji 47 vya Jimbo langu ni sawa na asilimia 6.4. Kuna vijiji kama 12 hivi vilikuwa na huduma hii ya maji kabla, vinakuwa vijiji 15 vinavyofaidika ambavyo ni sawa sawa na asilimia 31.9.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu Tanzania tunakimbilia kwenye Tanzania ya Viwanda. Tanzania inayotaka wananchi wafanye kazi kwa bidii, kwa nguvu bila maji, tukijua kwamba, maji ni muhimu katika maisha ya binadamu, tusipopata maji safi na salama uwezekano wa kuwa na magonjwa ya hapa na pale yatakayotufanya tushindwe kufanya kazi inayostahili na kwa hiyo, tushindwe kuipeleka Tanzania katika Tanzania ya Viwanda.
Je, Serikali ina mpango gani kuongeza kasi ya
upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wa Jimbo la Chilonwa?
Swali la pili, je, Serikali haioni kwamba kuna umuhimu sasa siyo lazima kila kijiji kichimbiwe kisima chake au kiwe na chanzo chake, wakati mwingine chanzo kimoja kiweze kuhudumia hata vijiji viwili/vitatu. Serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa kufanya hivyo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu concern ya Mheshimiwa Mbunge ndiyo maana tukiangalia eneo la Wilaya ya Chamwino liko karibu katika Makao Makuu sasa ya nchi yetu. Mheshimiwa Mbunge ndiyo maana unafahamu takribani zipatato wiki Nne nilikuwa katika mradi wa maji wa Wihunze ambao nimeona kwamba Mkandarasi anafanya kazi kwa kusuasua na kutoa maagizo ikifika tarehe Tatu mwezi huu tulioanza nao mradi huo uweze kukamilika na ninasikia hali kidogo inaenda vizuri. Hiyo yote ni juhudi ya Serikali kuangalia jinsi gani tutafanya miradi hiyo ipatikane.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hali hiyo, ndiyo
maana hapa nimezungumza katika majibu yangu ya awali kwamba, mwaka huu tumetenga shilingi bilioni 1.058 kwa ajili ya kupeleka juhudi hii ya maji, hata hivyo naomba nikuhakikishie kwa sababu, eneo la Wilaya ya Chamwino hasa Jimbo lako ni eneo la kimkakati na Ikulu yetu ya Mheshimiwa Rais ndiyo inapojengwa pale. Naomba nikuhakikishie kwamba Serikali itafanya kila liwezekanalo kuhakikisha wananchi wa maeneo yale wanapata huduma ya maji kwa sababu, ndiyo sehemu ambayo ni pumulio la katikati la Jiji la Dodoma, lazima tuweke juhudi za kutosha. Naomba ondoa hofu, Serikali itakuwa na wewe daima kuhakikisha kwamba mambo yanakuwa vizuri katika Jimbo lako.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Wananchi wa Tarafa ya Mikese, Wilayani Morogoro Vijijini, wameahidiwa muda mrefu mradi wa maji, lakini mpaka sasa wanapata taabu sana kwa kupata maji.
Je, ni lini wananchi wa Mikese watapata maji kusudi waondokane na tatizo hilo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niweke kumbukumbu sawa. Mheshimiwa Mama Ishengoma alikuwa
miongoni mwa Wajumbe wa Kamati ya Maji katika Bunge la Kumi na mimi tulikuwa katika Kamati moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri wakati ule Profesa Mark Mwandosya akiwa Waziri wetu wa Maji wa kwanza alikuwa akizungumzia sana suala zima la Mikese. Nadhani hapa tutakapo-table katika Bajeti ya Wizara ya Maji itakapofika, watazungumza jinsi gani Mfuko wa Maji ambao
mwaka huu tunatenga fedha kidogo za kutosha utagusa katika vijiji mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tusubiri Wizara ya Maji itakapokuja kuweka bajeti yake pale, tutajadili kwa upana zaidi jinsi gani tutawasaidia wananchi wa Mikese ambao najua kwamba kweli wana shida kubwa ya maji, lazima wapate mradi wa maji na ahadi ya siku nyingi.
MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante, nakushukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, kwa mujibu wa takwimu tulizopewa kwenye majibu na Mheshimiwa Waziri, asilimia 80 ya waendesha bodaboda hawana leseni, jambo ambalo linawafanya waishi kwenye mzunguko wa kukimbizana na polisi badala ya kuzalisha mali kwa ajili kujenga uchumi wao na uchumi wa Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kumuuliza Mheshimiwa Waziri, je, Serikali iko tayari kuwasaidia kwa kuwawekea ruzuku ya kupunguza walau kwa mara moja kodi ya kulipia leseni angalau kwa nusu ili waweze kupata leseni kama hatua ya kwanza ya kuwasaidia ili tuweze kushirikiana nao kuongelea habari ya kuwahamisha kuwapeleka kwenye ushirika wa SACCOS na mambo mengine?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili; Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuambatana na mimi twende Biharamulo kuziona fursa nyingine zaidi ya kuwaomba tu wajiunge kwenye SACCOS ambazo Serikali Kuu ikishirikiana na sisi tunaweza kuzitumia kuwatoa kwenye yale waliyonayo ili Biharamulo iwe mfano wa kusambaza hatua kama hiyo maeneo mengine ili kundi kubwa la bodaboda nchini tulisaidie liwe la ujasiriamali kweli kweli? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZAA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya Mheshimiwa Mbunge kama ikiwezekana Serikali ifanye uwezeshaji, naomba nikiri wazi kwamba hatuwezi kusema kama Serikali tufanye uwezeshaji kwa watu wote, lakini tunakuwa na mikakati mbalimbali ya kufanya uwezeshaji. Mimi niwapongeze Wabunge wengi humu ndani ambao wamefanya initiatives katika Majimbo yao kuhakikisha vikundi mbalimbali vinahamasishwa na wao wanasaidia ku-chip in humo kwa ajili ya kuwasaidia vijana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo mimi ninajua wazi kwamba kuna baadhi ya Halmashauri nyingine zina mipango mbalimbali yenye lengo la kuwasidia hawa vijana ili hatimaye, kama ulivyofanya Mheshimiwa Mbunge katika Jimbo lako ambapo na sisi tume-recognise shughuli na juhudi kubwa unazofanya katika Jimbo lako, nadhani tukifanya uhamasishaji sisi wengine tutafanya kwa kuangalia fursa zilizopo katika maeneo yetu na hivyo tutaweza kuwasaidia hao vijana kwasababu lengo letu ni kwamba vijana waweze kukomboka katika jambo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kikubwa zaidi kama hatufahamu; bahati nzuri Ofisi ya Mama Jenista Mhagama katika Baraza la Taifa la Uwezeshaji, hata jana nadhani walikuwa wanafunga mafunzo yao, wameona kwamba jinsi vijana wengi wanavyokosa fursa hizi kwa kutokuwa na ufahamu wa kutosha na ndiyo maana wamesema sasa hivi wanataka kuzifanya programu zao kupitia maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika sehemu ya pili naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mimi nipo radhi, nilifika Biharamulo mara ya kwanza, lakini kama kuna jambo lingine mahususi tutakwenda tena ili kuwasaidia vijana wetu waweze kufika mbele katika suala zima la maendeleo.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa
Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Jafo kwa majibu yake mazuri kwenye swali hili la msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge ametaka kuiuliza Serikali ni kwa kiasi gani inaweza ikajipanga kupeleka juhudi za ziada ili kuhakikisha kwamba vijana wa Tanzania, hasa vijana wa kule Biharamulo wanaweza kufaidika na mikopo mbalimbali na kuweza kuwaboreshea shughuli za ujasiriamali wakiwemo vijana wa bodaboda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikuhakikishie kwamba, Mheshimiwa Mbunge ni kati ya Wabunge ambao walihudhuria maonyesho ya mifuko ya uwezeshaji wananchi kiuchumi, na tumeshakubaliana na Mheshimia Mbunge kwamba baada ya shughuli hizi za Bunge kukamilika, Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na timu ya Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi pamoja na yeye Mheshimiwa Mbunge watakuwa na ziara maalum kule Biharamulo ili kuangalia Serikali inaweza ikafanya nini kwa ajili ya maendeleo ya vijana na sekta nyingine.
Nitoe wito kwa Waheshimiwa Wabunge wote, tumefunga maonesho ya mifuko ya uwezeshaji wananchi kiuchumi, tunaomba sana tuendelee kuwasiliana ili fursa zilizopo ndani ya Serikali ziweze kuwafikia Watanzania wengi hasa wakipato cha chini na kipato cha kati wakiwemo vijana na kuweza kuwainua kiuchumi. Nakushukuru
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa Meneja wa TANROADS wa Mkoa ameshaikagua barabara ya kutoka Gulwe – Berege –Chitemo – Mima – Chazima - Igodi Moja – Igodi Mbili mpaka Seluka; na kinachosubiri sasa hivi ni barabara hii ipandishwe hadhi ili iwe barabara ya Mkoa.
Je, Mheshimiwa Waziri anasemaje na kwa ombi hilo Serikali inawaambiaje wananchi wa maeneo hayo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lubeleje, grader la zamani, makali yale yale kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Lubeleje swali hili alikuwa akiliuliza mara kadhaa na hapa umesema kwamba ni kweli. Kwa sababu naamini wenzetu wa Wizara ya Ujenzi jambo hili walishalisikia na ninakumbuka Naibu Waziri wa Ujenzi siku ile alikuwa analizungumza suala hili kwamba jambo hili linafanyiwa kazi. Imani yangu ni kwamba kwa sababu barabara hii ni ya kimkakati nami nakiri wazi kwamba na wewe barabara hii inakuhusu katika eneo lako. Basi naamini Wizara ya Ujenzi itafanya kila liwezekanavyo barabara hii kuipa kipaumbele katika yale matakwa ya wananchi wa eneo hilo.
MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ambayo nimepata kutoka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini ningependa kumweleza kuwa Hospitali ya Wilaya ya Pangani ina magari mawili tu kati ya hayo magari 11 ambayo umeyataja, lakini magari yale ni chakavu mno kiasi kwamba yanapoenda service basi yanalazimika kutengeneza kitu zaidi ya kimoja yaani sio service tu ya kawaida, lazima unakuta na vitu vingine vinakuwa vimeharibika pale.
Mheshimiwa Spika, Serikali pengine haioni umuhimu wa kununua magari mengine mapya badala ya kuacha magari yale chakavu yaendelee kutumikia Hospitali ya Wilaya ya Pangani? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli, na mimi nilivyofika Pangani, Mheshimiwa Mbunge anakumbuka nimefika pale nimeona changamoto hii ya magari. Magari yale ni kweli ni miongoni mwa magari chakavu kama ilivyo katika Halmashauri nyingine. Nikijua wazi kwamba kipaumbele cha kununua magari ya Halmashauri huwa yanafanywa hasa na Halmashauri yenyewe ikianzia katika mchakato wa awali. Hata hivyo, Serikali katika kuimarisha huduma ya afya, tulinunua karibu magari 50 tukapeleka katika maeneo ambayo vipo vifo vingi zaidi. Hata hivyo tuna mkakati mwingine, tukipata gari la ziada tutafanya hivyo.
Mheshimiwa Spika, suala la ununuzi wa magari naomba watu wa Halmashauri ya Pangani tuweke kipaumbele, lakini Serikali haitasita kusaidia wananchi wa Pangani tukijua wazi Jimbo lile na eneo lile jiografia yake iko tata sasa; ukitoka pale Hospitali watu wa Mwela huku na watu wa upande mwingine wana changamoto kubwa sana mpaka kwenda eneo lile.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Serikali tunaliangalia hilo, lakini tutashirikiana vyema na wenzetu wa Pangani kuhakikisha mambo yao yanaenda vizuri. (Makofi)
MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Spika, naomba nami niulize swali moja dogo la nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Waziri umetembelea Wilaya ya Mvomero na umejionea mwenyewe hali halisi ya Wilaya; leo gari la afya ambalo linatumika kwa ajili ya chanjo ndilo linatumika kwa ajili ya kukusanya mapato, lakini Idara ya Ujenzi haina gari, magari yote ni chakavu.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kutusaidia sisi watu wa Mvomero ili tuweze kuendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, anachosema ni kweli. Siku ya Alhamisi tulikuwa Jimboni kwake pale na tulitembelea mpaka Hospitali ya Wilaya na kubaini changamoto na jiografia ya eneo lile kuanzia Turiani na maeneo mengine.
Mheshimiwa Spika, eneo lile ni kweli, hata nilipokutana
na wataalam pale, kuna changamoto ya magari. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama nilivyosema pale awali ni kwamba mchakato wa ununuzi wa magari mara nyingi sana unaanza na kipaumbele cha Halmashauri yenyewe, lakini kwa sababu tuko pamoja hapa na Mbunge siku ile tulikubaliana mambo mengine ya msingi. Tutaendelea kushirikiana vya kutosha kuona ni jinsi gani tutaiwezesha Halmashauri ya Mvomero iweze kufanya vizuri. Ndiyo maana Serikali hata katika suala zima la miundombinu, wewe unafahamu jinsi tunavyowekeza pale hata katika ujenzi wa lami. Lengo kubwa ni kwamba wananchi wa Mvomero wapate matunda mazuri ya Mbunge wao.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itashirikiana naye, pale kwenye mahitaji ya haraka tutafanya kwa ajili ya wananchi wake na watendaji waweze kufanya kazi vizuri katika Jimbo la Mvomero.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kutumia Bunge hili kupiga marufuku magari ya chanjo kutumika kwa shughuli tofauti na chanjo. Kuanzia sasa hivi magari ya chanjo tutayandika herufi kubwa neno “CHANJO” na lisitumike kwa matumizi mengine yoyote. Kwa sababu chanjo ni muhimu kuliko masuala mengine katika Halmashauri.
Mheshimiwa Spika, niliona nitumie Bunge lako kutoa ufafanuzi. Kwa hiyo, ni marufuku Halmashauri ya Mvomero kutumia gari la chanjo kwa ajili ya kukusanyia mapato. Ahsante.
MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, Bukoba Vijijini ni Wilaya ambayo
ina jiografia kubwa na magari ya Bukoba Vijijini yote hasa ya hospitali ni mabovu. Juzi imetolewa ambulance, badala ya kupelekwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Izimbya ikapelekwa kwenye Zahanati ya Kishanji. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri ndivyo mlivyopanga au ni mipango ya Halmashauri?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, tumelisikia hili. Kama alivyosema Mheshimiwa Waziri wa Afya, lengo letu kubwa ni kwamba haya magari ya chanjo yakienda katika maeneo yafanye kazi inayokusudiwa. Sasa kwako wewe kuna scenario tofauti kwamba gari lilitakiwa liende katika hospitali lakini limeenda katika zahanati, lakini ninachoamini ni kwamba kule kuna DMO, viongozi na Mkurugenzi pale, inawezekana kuna jambo ambalo tutaenda kulifanyia kazi tujue nini kilichoendelea.
Mheshimiwa Spika, letu kubwa ni kuhakikisha tunazozipeleka resources na hasa katika sekta ya afya, lazima watu wasimamie mwongozo huu. Gari kama ni la afya litumike kwa ajili ya afya. Ndiyo maana sasa hivi mikoa mingine hata kiwango cha chanjo wanashuka kumbe ni kwa sababu hawazingatii miongozo maalum ya Serikali ambayo tunaelekeza kila siku.
MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza maswali mawili madgo ya nyongeza.
Swali la kwanza, pamoja na jitihada kubwa ambazo zimeshafanywa na Halmashauri yangu ya Jiji la Mwanza, namshukuru sana tu Mkurugenzi kwa jitihada zake anazozifanya kuhakikisha anasaidia wanawake na vijana wa Jiji la Mwanza kujikomboa.
Mheshimiwa Spika, niulize tu kwamba inawezekana haya yanafanyika vizuri kwenye Halmashauri ambazo Wakurugenzi wengi wana utashi wa kusaidia makundi haya. Ni nini sasa mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba fedha hizi zinapaswa kutolewa siyo kwa hiyari, iwe ni kwa lazima kwa mujibu wa makusanyo ya mapato ya ndani ili kuwanufaisha vijana wengi zaidi? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, pili, je, Serikali haioni sasa ni wakati muhimu wa kuongeza asilimia hizi kutoka 10 mpaka 15 kwa sababu ni ukweli usiofichika kwamba vijana na wanawake wanaendelea kuongezeka zaidi hasa katika masuala mazima ya kujitafutia riziki na familia zao pia ili waweze kujikwamua kiuchumi? Nakushukuru. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge anauliza kwamba ni jinsi gani tutaweka uwe kama mkakati wa kisheria; ni kweli ukija kuangalia hata taarifa ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2013/2014, kuna outstanding ya fedha ambazo zilitakiwa zipelekwe karibu shilingi bilioni 37 hazikuweza kupelekwa. Ndiyo maana katika bajeti ya mwaka 2016/2017 tulitoa maelekezo mahususi kwa Wakurugenzi wote kama ndiyo miongoni mwa guideline kutengeneza bajeti ya Halmashauri.
Mheshimiwa Spika, vilevile tuseme kwa kuwa tumeona
kuna changamoto kwa Halmashauri nyingine kutoa hizi fedha, ndiyo maana sasa hivi katika marekebisho yetu ya Sheria ya Serikali za Mitaa Sura ya 290, tumeweka kifungu ambacho kinatoa maelekezo ya kisheria sasa kwamba tunavyoipitisha hapa kwamba Halmashauri sasa haina hiyari isipokuwa ina lazima ya kutekeleza jambo hilo la kisheria.(Makofi)
Mheshimiwa Spika, lengo kubwa ni kuwasaidia vijana
na akina mama na kuzikomesha Halmashauri zote zinazoona kwamba kupeleka ile fedha kama ni hisani, kumbe ni utaratibu. Lazima tunataka tuingize katika utaratibu wa kisheria ambapo nina imani sheria ile ikifika ha Bungeni, Wabunge wote tutashirikiana kwa pamoja kuipitisha kwa sababu ina maslahi mapana kwa wananchi wetu.
Mheshimiwa Spika, katika jambo la pili la kuongeza asilimia 10 mpaka 15; nadhani ukiangalia mgao wa own source, asilimia kumi nadhani tuiweke hapo hapo, kwa sababu hata hizo asilimia kumi Waheshimiwa Wabunge wengine humu walikuwa wanalalamika. Jambo la kuzingatia ni kwamba tuhakikishe ile asilimia kumi inafika.
Mheshimiwa Spika, najua Mheshimiwa Mabula ni mpiganaji wa wananchi wake na mpiganaji wa Machinga pale Mwanza. Na mimi najua tukisimamia vizuri hapa kwa pamoja, jambo hili litawasaidia sana vijana na akina mama katika maeneo mbalimbali kujiingiza katika shughuli za ujasiriamali.
MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.
Pamoja na agizo la Serikali kwenye Halmashauri kuagiza kutenga asilimia kumi kwa vijana na wanawake, kumekuwa na utaratibu wa Halmashauri kugawa pesa hizi kipindi cha Mwenge. Kwa sababu Halmashauri nyingine wanawake wanapata changamoto sana kipindi cha kilimo, Serikali haioni ni hekima au busara kutoa pesa hizi kipindi cha msimu wa kilimo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, nilizungumza mara kadhaa hapa, fedha zile hazitoki kwa Mheshimiwa Dkt. Mpango, fedha zile zinakusanywa katika Halmashauri zetu na Kamati ya Fedha inakaa na kufanya maamuzi fedha zile ziende wapi na kwa akina nani?
Kwa hiyo, jambo hili naomba niseme wazi, kama sisi Wabunge na Madiwani wetu tukiwa committed kuwasaidia wananchi wetu, haitaleta shida kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, najua concern ya Mheshimiwa Mbunge, lakini niwaelekeze sana ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge, twende sasa tukazihakikishe Kamati zetu za Fedha zinapokaa katika ile ajenda ya mapato na matumizi, katika own source, tutenge kabisa pale pale, tuzielekeze kwa vijana na akina mama waweze kujikomboa kwa kadri Serikali ilivyopanga. Huu ndiyo mchakato wa wazi kabisa, kila mtu ataona ni jinsi gani ameshiriki vyema kuhakikisha jamii yake inakwenda vizuri zaidi.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, namshukuru Mheshimiwa Mbunge.
MHE. KHADIJA N. ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa kilimo ndio uti wa mgongo wa Tanzania, ni lini Wizara itaingiza mitaala ya masomo ya kilimo na ufugaji kwenye Sekta ya Elimu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, concern hiyo kweli imejitokeza wazi; na nakumbuka kipindi cha nyuma waliokuwa wanasoma sekondari, kulikuwa na somo moja linaitwa Agricultural Science na mambo ya Nutrition, lakini hapa katikati lilipotea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwanza mitihani ya Form Six na ile ya Form ya Four mwaka 2016, somo hilo sasa limeshaanza kuingizwa. Utaratibu wa Serikali ni kuhakikisha kwamba somo hili la Agricultural Science na masomo mengine, kuhakikisha kwamba suala la kilimo linapatikana limeweza kufanyika hivyo. Nashukuru sana Walimu ambao wamejitokeza, nami nilienda kuwatembelea wakati ule wapo Hombolo wakifanya usahihishaji, wamesema vijana wametoa mwitikio mkubwa sana, inaonekana tunaendelea vizuri. Kwa hiyo, hilo tuondoe shaka, Serikali inalifanyia kazi vizuri.
MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, isipokuwa nina maswali mawili ya nyongeza ya kuuliza. Moja, Mheshimiwa Waziri katika mwaka huu wa fedha 2016/2017, tulitengewa fedha jumla ya sh.82,000,000/= kwa ajili ya ujenzi wa wodi kwenye Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo, lakini mpaka hapa tunapoongea fedha hizi hazijapelekwa katika Halmashauri. Je, Mheshimiwa Waziri atatuhakikishia Bagamoyo kwamba fedha hizi zitaweza kutolewa kabla ya mwaka huu kumalizika ili tuweze kuboresha huduma katika hospitali hiyo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Waziri amenijibu kuhusu ujenzi wa OPD kwa kutumia fedha za (own source) za kwetu wenyewe, lakini OPD hii ni mbovu sana; haina uwezo wa kuhudumia wagonjwa kwa kadri ambavyo ingeweza kutoa huduma ile ambayo wanasema inafaa kwa wananchi wale wa Bagamoyo. Inahitaji ujenzi mpya kabisa. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari ku-commit kiasi cha fedha ili angalau tuweze kuijenga upya OPD hiyo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la commitment ya Serikali katika bajeti ambayo mwaka huu tunaondoka nayo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba bado tuna mwezi mpaka tufike mwezi wa Sita. Lengo letu Serikali ni ile wodi iweze kujengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la OPD, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwanza Bagamoyo tumeingiza katika program maalum ya RBF na hivi sasa tumewapelekea takriban shilingi milioni 150 kutokana na kuwepo kwa zahanati zao 15. Mpango huu utaenda takriban miaka mitatu kwa sababu tume-site kama ni sehemu ya mfano kuanzia na hiyo program.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wakati tunaenda na hizi intervention, kwa sababu lengo letu ni kupandisha vituo vyetu viwe na star. Bahati nzuri Jimbo lake ni miongoni mwa maeneo yaliyofanya vema. Katika vituo 15, vituo 11 vilipata star.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wetu ni nini? Ni kwamba tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo, nami naifahamu OPD yaou pale Bagamoyo jinsi ilivyo, tutashirikiana kwa pamoja nini kifanyike tuhakikishe tunafanya marekebisho makubwa katika OPD ile, kwa sababu wagonjwa wengi sana ukiangalia katika jiografia ya pale wanatibiwa pale. Kwa hiyo, Serikali tutafanya kila liwezekano ili mradi tuweze kuweka mazingira yawe mazuri.
MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Nina swali dogo la nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri. Tatizo la ukosefu wa dawa ni tatizo kubwa katika mahospitali mengi nchini, kuanzia Zahanati na Vituo vya Afya. MSD imeshalipwa zaidi ya shilingi bilioni 80. Sasa Mheshimiwa Waziri naomba atueleze ni kwa nini MSD inashindwa kuagiza dawa wakati wana fedha katika akaunti zao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua kwamba sasa hivi tunapeleka fedha nyingi sana. Kama nilivyosema hapa mara kadhaa katika Bunge letu hili, kupitia ule mfuko (basket fund) peke yake, tuna fedha nyingi ambazo tumezipeleka kule na nimekuwa nikihamasisha Halmashauri mbalimbali wafanye procurement.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tumeweka utaratibu kwamba endapo dawa zinakosekana, kuna prime vendors ambao wanapatikana kwa ajili ya kuhakikisha dawa zinapatikana. Kwa hiyo, endapo dawa zimeonekana miongoni mwa dawa zilizoombwa kutoka MSD zimekosekana, basi tumewaelekeza wataalam wetu katika kanda kwamba waweze kutumia prime vendors ambao wamekuwa identified kabisa na Serikali, kuhakikisha kwamba tuna-fast truck katika suala la upatikanaji wa dawa. Lengo kubwa ni kwamba Hospitali zetu, Zahanati zetu na Vituo vya Afya viweze kupata dawa kwa ajili ya wananchi wetu.
MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami napenda niulize swali la nyongeza. Mikakati ya Serikali ni kuboresha afya katika maeneo yote na kupandisha hadhi baadhi ya Vituo vya Afya kuwa Hospitali. Katika Mkoa wa Mtwara tulikuwa tunapandisha hadhi Kituo cha Afya Nanguruwe na Kituo cha Afya Nanyumbu, kuhakikisha inakuwa Hospitali na tumefikia hatua nzuri ya kufungua kuwa Hospitali. Hata hivyo, Naibu Katibu Mkuu kutoka TAMISEMI alipokuja alisema Vituo vya Afya viendelee kuwa Vituo vya Afya na tuanze ujenzi upya. Sasa nataka kujua ile ni kauli yake au ni kauli ya Serikali? Kwa sababu Serikali siku zote imekuwa ikitusaidia kufikia hapo ili vituo hivyo viwe hospitali. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Kituo cha Afya cha Nanguruwe na Nanyumbu, Mheshimiwa Mbunge anakumbuka nilivyofika pale, Nanguruwe, Kituo cha Afya ambacho kina facilities nyingi sana, kilikuwa na suala zima la ahadi ya Mheshimiwa Rais kuifanya kuwa Hospitali ya Wilaya. Maana yake nini? Naibu Katibu Mkuu wetu alizungumza technically kwamba nini tunatakiwa kufanya? Kwamba tukiwa tuna upungufu wa mambo ya hospitali, lazima tujiwekeze katika suala zima la ujenzi wa hospitali zetu za Wilaya. Siyo kama ni kauli yake, isipokuwa ni kauli ya Serikali sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaposema kwamba tuvi-convert Vituo vya Afya kuwa Hospitali za Wilaya, maana yake tunafifisha baadhi ya juhudi, lakini kuna maeneo mengine yana special preferences. Kwa mfano, pale Nanguruwe, Nanyumbu au maeneo mengine niliyotembelea, unakuta Vituo vya Afya vingine walikuwa katika program ya kufanya kuwa Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana nimesema tuna-treat maeneo mengine case by case. Kwa case kama pale Nanguruwe au Namyumbu ambapo hata Mheshimiwa Rais mstaafu alipopita pale alitoa ahadi, ahadi ile itaendelea kuwepo pale pale. Lengo kubwa ni kuwasaidia wananchi wale na kwa kiwango kikubwa Serikali imesha-invest vya kutosha kukodi na vifaa vingine kuwasaidia wananchi wa eneo lile.
MHE. ROSE K. SUKUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, lakini nina maswai mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri kwamba Afisa Masuhuli anayetumia fedha bila idhini ya TAMISEMI au ya Hazina, hastahili kutumia hizo fedha. Je, ni kwa nini ofisi yake haikutekeleza wajibu huo kwa Maafisa Masuhuli ambao wametumia hizo fedha bila idhini yake au bila idhini ya Ofisi yake pamoja na Hazina? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe mwenyewe umekiri kwamba fedha endapo itabainika imeongezwa, lakini (b) yake umesema kwamba hakuna bajeti inayoidhinishwa ikazidi kupelekwa kwenye Halmashauri: sasa ni ipi tuipokee kutoka kwako endapo fedha zimeongezeka? Unasema kwamba haziongezeki, nami nina uhakika kwamba fedha zinaongezeka; sasa naomba kuuliza. Je, kwa wale ambao wameongezewa fedha na wale ambao wamepunguziwa wanafidiwaje?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Naibu Waziri atupatie majibu ambayo yanastahili.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema hapa kwamba kwa Afisa Masuhuli yeyote ambaye atakiuka utaratibu wa fedha, maana yake atachukuliwa hatua. Kwa sababu, Mheshimiwa Sukum hakunipa mfano halisi, lakini naomba nimhakikishie, kuna maamuzi mbalimbali ya kinidhamu tumeyachukua kwa Watendaji mbalimbali. Hata baadhi ya Wakurugenzi wengine ambao wameenda nje ya system sasa kutokuwa Wakurugenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo ni kwa sababu mwanzo katika njia moja ama nyingine walikiuka utaratibu wa fedha na kufanya ufisadi mkubwa katika fedha hizo na ndiyo maana Serikali ilichukua hatua. Ni kwa sababu hatuwezi ku-publicize hapa kwamba nani na nani, lakini tumechukua hatua mbalimbali kwa baadhi ya Wakurugenzi ambao ni Maafisa Masuhuli, walioko katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake lingine kwamba fedha sehemu nyingine zinaongezeka na nyingine zinapungua, nimezungumza wazi, hapa kila Mbunge akisimama anazungumza kwamba fedha haziji, fedha haziji. Ndiyo nimesema, kwa uzoefu tuliokuwa nao, mara nyingi sana fedha zile tunazozipanga, ndiyo maana hata Mheshimiwa Kawambwa hapa anaomba fedha za wodi yake hazijafika. Uzoefu uliokuwepo ni kwamba fedha zinazokwenda ni chache kuliko kile kilichopangwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kunatokea na special
case kwamba kuna baadhi ya fedha zimeongezeka, ni lazima utaratibu ufuatwe kama nilivyoelekeza katika maelezo yangu ya awali, kwamba lazima atoe taarifa aidha Hazina au Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa Katibu Mkuu kwa ajili ya ufuatiliaji, fedha hizo zirudishwe katika Mfuko Mkuu wa Hazina.
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa, Halmashauri mara nyingi tatizo la fedha ni shida kubwa sana. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza kutuambia ni jinsi gani atahakikisha Ofisi yake inatimiza yale malengo ya fedha iliyoahidi kwenda kwenye Halmashauri?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuhusu usimamizi, aseme
kwa kina atazisimamiaje Halmashauri zake zisifanye ufisadi kwa kuwa, imekuwa ikijirudia mara kwa mara na kutuletea matatizo katika Halmashauri zetu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa tunazungumzia suala zima la fedha na fedha hizi zinatafutwa kwa gharama kubwa kwa ajili ya kuwasaidia wananchi.
Naomba nimhakikishie, nilikuwa nikifanya ziara katika Halmashauri zote na nashukuru Mungu sasa nimebakiza chini ya Halmashauri 10 kuzipitia Tanzania nzima. Ajenda yetu ya kwanza ni suala la uadilifu katika usimamizi wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumewaambia na nimetoa maelekezo katika maeneo yote kwamba Wakurugenzi na Waweka Hazina sasa lazima wanapokwenda katika Kikao cha Kamati ya Fedha ambapo Madiwani na Wabunge ni Wajumbe hapo, lazima watoe taarifa ya transactions katika Halmashauri zao, fedha zilizopokelewa na matumizi yake yalikuwaje. Siyo kupokea lile kabrasha la mapato na matumizi ambapo Mbunge au Diwani anashindwa kujua ndani kilichokuwemo. Kwa hiyo, tumetoa maelekezo haya vya kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba sana Waheshimiwa Wabunge ambao sisi ni Wajumbe wa Kamati ya Fedha kwamba tukiingia katika vikao vyetu, tuweze kuzisaidia Halmshauri hizi kwa sababu sisi ndio wafanya maamuzi ambao tunawawakilisha wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwasihi Wabunge wote kwamba kwa moyo mkunjufu na moyo wa dhati tuzisimamie Halmashauri zetu, compliance iwepo na wananchi wetu wapate huduma na maendeleo.
MHE. KEMILEMBE J. LWOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ila nina swali dogo moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuliona hili na siku ya Mei Mosi ametoa tamko watumishi wote watakaohamishwa vituo vyao walipwe fedha zao kabla ya uhamisho. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna baadhi ya watumishi wengi tu ambao wamehamishwa kwenye vituo vyao vya kazi, wameenda kwingine na hawajalipwa fedha zao za uhamisho mpaka leo. Kuna baadhi ya taasisi hata waliohamishiwa hapa Dodoma Makao Makuu hawajalipwa fedha zao mpaka leo.
Sasa ni lini Serikali italipa fedha za watumishi hawa waliohamishwa na hawajalipwa fedha zao za uhamisho? Nashukuru.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa concern ya Mheshimiwa Mbunge na siku zote maswali yake yamekuwa yakigusa wananchi wake na hasa watumishi, nakupongeza sana Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ofisi yetu ilifanya zoezi la uhakiki wa madeni kwa sababu tuna Halmashauri mpya nyingi sana zimeanzishwa. Kwa mfano, siku nilivyofika pale Busega au kwa mtani wangu Tabora Vijijini kwenye Halmashauri mpya ya Isikizya, nimekutana na watumishi wakilalamikia suala hili la madeni. Ndiyo maana ofisi yetu tukafanya uhakiki wa madeni na tumeyawasilisha Hazina.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tunazunguka maeneo mbalimbali tumekuta baadhi ya Halmashauri tayari madeni haya yameshaanza kulipwa. Kwa hiyo, kwa sababu uhakiki ulishafanyika na taarifa iko Hazina tufanye subira na wengine wameshaanza kulipwa na madeni yao yote yatalipwa kwa sababu Serikali haitaki kuona haki za watu zinadhulumiwa.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Naibu Waziri Mheshimiwa Selemani Jafo kwa majibu mazuri, lakini pia Mheshimiwa Kemilembe kwa swali zuri ambalo kusema ukweli linawagusa watumishi wengi na hasa wa Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tabia za Wakurugenzi wa Halmashauri kuwahamisha na hasa walimu kwa kuwakopa gharama ambazo wangepaswa kuwalipa kwa ajili ya usumbufu na gharama za uhamisho.
Nilisema hapa Bungeni hadi tarehe 30/04/2017 wanapaswa kuwa wamewalipa walimu waliowahamisha. Hili nililisema si kwa madeni ya nyuma sana ya uhamisho maana yale yote tulishayapeleka Wizara ya Fedha kwa ajili ya kulipwa, lakini kuna uhamisho uliofanyika kati ya mwezi Januari hadi Machi wa kupanga ikama za walimu. Deadline imefika na kuanzia sasa Wizara yangu itachukua hatua kwa wale wote ambao hawajawalipa walimu waliowahamisha. Haiwezekani Serikali tunapambana kupunguza madeni lakini wako watu wengine ni viwanda vya kuzalisha madeni yasiyokuwa na sababu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kusema ukweli suala hili tumelitilia msisitizo mkubwa lakini pia Serikali ipo katika mchakato wa kuandaa fedha kwa ajili ya kupanga hizi ikama kwa nchi nzima kwa Halmashauri zote. Zoezi hili litaenda sambamba na malipo ya moja kwa moja kwa watumishi watakaohamishwa kwa sababu ni haki yao ya msingi ya kiutumishi.
MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ambayo yametolewa kuhusiana na suala la kuhamisha watumishi katika Halmashauri zetu lakini suala hili limekuwa sugu sana. Ukiacha hao walimu ambao wamewazungumzia lakini wapo pia wauguzi, watendaji wa kata na vijiji. Mimi kama Mbunge au Diwani naweza kwenda kwa Mkurugenzi nikamuambia Mtendaji huyu simtaki mpeleke katika kijiji au kata nyingine bila kujali stahiki zake. Ni nini sasa kauli ya Serikali kuhusu watumishi hawa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, alichosema Mheshimiwa Sikudhani ni kweli na hili sisi viongozi tunatakiwa tujitathmini kwamba wakati mwingine una interest zako binafsi unasababisha mtu fulani ahame kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine bila kujua kwamba unalimbikiza madeni katika maeneo hayo. Bahati mbaya sana wakati mwingine Mkurugenzi akikataa ndiyo unaanza bifu (kutokuelewana) naye kuanzia hapo kwamba Mkurugenzi huyu hatufai.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme kwamba utaratibu wa kuhamisha kama alivyozungumza Waziri mwenye dhamana Mheshimiwa Boniface Simbachawene ni lazima uendane na bajeti iliyokuwepo. Vilevile si vyema kwa viongozi wowote kuwaweka katika mazingira magumu watumishi hawa na kuwa-frustrate kwa kuwahamisha bila sababu yoyote. Tunasema jambo hilo likome na lisiendelee katika Halmashauri zetu kwa sababu halileti afya kwa watumishi wetu ndani ya nchi yetu.
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuweza kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri
ya Mawaziri na Naibu Waziri, kwa Wilaya ambazo ni mpya na Mheshimiwa Naibu Waziri amezungumzia suala la Busega kwamba alikuta pale matatizo ya watumishi, je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia Wilaya hizi mpya ambazo zimeanzishwa zenye uhaba wa ikama ya watumishi? Vilevile pili baadhi ya watumishi walio wengi hawajalipwa mafao yao. Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu pale awali ni kwamba tutajitahidi Halmashauri hizi mpya ambazo zimeanzishwa na bahati nzuri Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi) amezungumza wazi kwamba tuna hizi ajira mpya ambazo zinakuja lengo kubwa ni kuziba mapengo yote yaliyokuwepo katika maeneo yetu. Ofisi yetu imeshaanza kufanya tathmini ya kujua ni watumishi wangapi wanahitajika katika Halmashauri gani ili kuziba haya mapengo yaliyopo. Kwa hiyo, mtani wangu Mheshimiwa Dkt. Chegeni ondoa hofu zoezi hili litaweza kujibu matatizo ya watumishi katika Jimbo na Halmashauri yako ya Busega.
MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo tu la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Kibaigwa unakua
kwa kasi sana na kwa sasa mji ule ni Mji Mdogo. Hata hivyo, kwa kuwa hatuna watumishi wa kutosha na mji ule haujafanywa kuwa mamlaka, naiomba Serikali sasa ituambie ni lini Mji wa Kibaigwa utapewa mamlaka ili waweze kupanga shughuli za mji wao na kupewa watumishi wa kutosha kuendeleza Mji ule Mdogo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, toka asubuhi nimesema leo kuna utaratibu wa kuhamisha goli katika uwanja. Naomba nikuambie Mheshimiwa Felister Bura kwamba hoja yako imesikika na lengo letu ni kupanga miji hii yetu yote vizuri, kuna Kibaigwa, Kibakwe na maeneo mengine katika Mkoa wako wa Dodoma najua inakua kwa kasi sana. Hata hivyo, wakati tunajielekeza katika mipango ya Mamlaka ya Miji Midogo tutajielekeza jinsi gani tupate watumishi kuweza kuziba nafasi hizo ili wananchi wetu wapate huduma vizuri. Nakushukuru sana.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesimama tena kwa sababu jambo hili limekuwa likiwagusa Waheshimiwa Wabunge wengi na katika maeneo mengi na hasa pale inapoanzishwa Mamlaka za Miji Midogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kiutaratibu mwenye dhamana ya kuendeleza miji hii kuweza kuanza kufanya shughuli zake inapokuwa imeanzishwa Miji hii Midogo ni Halmashauri Mama. Kwa hiyo, inapokuwa Serikali tumekubali kwamba mji huo uanze mipango yote na utaratibu wa uanzishwaji unaanzia kwenye Halmashauri Mama kuijengea uwezo Halmashauri hiyo ya Mji Mdogo ili iweze kufanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwasihi Waheshimiwa Wabunge kwamba mipango yote itapaswa iingie kwenye mipango ya Halmashauri Mama na ndipo sasa kwa yale maeneo ya upungufu wa watumishi Serikali inaweza kuwaleta. Hata hivyo, kama hakuna bajeti au mpango kutoka kwenye Halmashauri Mama sio rahisi kwa Halmashauri hizo za Miji Midogo kuweza kuanza.
MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kutokana
na vitendo vya uhalifu vinavyoendelea ambavyo vinasababisha Kibiti kushindwa kukusanya makusanyo yake ya ndani, je, Wizara itaiangaliaje kwa jicho la huruma ili kuhakikisha wanapata Mwenyekiti wao wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kibiti?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, kutokana
na ukweli kwamba Kibiti ni Halmashauri mpya Mkurugenzi na DC hawana vifaa vya kutendea kazi kama magari. Je, Serikali inaliangaliaje hilo kwa jicho la huruma?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nitoe pole kwa Mheshimiwa Mbunge na wananchi wote wa Kibiti na Rufiji kwa tatizo kubwa linaloendelea pale kwa sababu mpaka hivi sasa tumepoteza Wenyeviti wengi sana na hali hiyo inaogopesha.
Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iko na wananchi wa Kibiti na Rufiji na tutaangalia nini cha kufanya kwa sababu sasa hivi ukiitisha uchaguzi pale hata Wenyekiti wenyewe kujitokeza kugombea nafasi yenyewe wanaogopa.
Kwa hiyo, Serikali inafanya kazi ya kurudisha hali ya utulivu na amani ili hali ya usalama iweze kukaa vizuri. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge amini kwamba Serikali yako itashirikiana na wewe kama inavyofanya hivi sasa ndiyo maana timu ya Mkoa wa Pwani iko kule site kuhakikisha mambo yanakaa sawa. Kwa hiyo, hili jambo tumelichukua kwa moyo wa dhati kabisa na tutashirikiana kupata ufumbuzi wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili la changamoto
ya magari, ni kweli na Mheshimiwa Ungando nikushukuru sana, tulipotembelea vile visiwa 40 vya delta kule tulifanya kazi kubwa sana, tokea asubuhi mpaka tulivyomaliza saa mbili usiku, nimebaini changamoto hizo. Ndiyo maana kipindi kile nilivyorudi haraka tukafanya utaratibu kuwaletea gari moja pale la Road Fund. Hata hivyo, Serikali imeona hili tatizo kwa DC na Mkurugenzi tutajitahidi nini tufanye kwa pamjoa kuisaidia Halmashauri hii mpya ambayo ina changamoto kubwa sana katika suala zima la vitendea kazi.
MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mamlaka ya Mji
wa Lushoto sasa hivi ina zaidi ya miaka nane. Je, Serikali haioni sasa imefikia wakati wa kuipandisha hadhi kuwa Halmashauri ya Mji wa Lushoto ukizingatia Mheshimiwa Jafo alitembelea kule na kuona Mji wetu wa Lushoto jinsi unavyopendeza na ulivyokuwa mkubwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani concern hii Mheshimiwa Mbunge aliileta ofisini kwetu na ndiyo maana Waziri wangu aliniagiza niweze kufika Lushoto kule na nimeweza kufika. Kimsingi wana mambo mengi, kuanzisha hii Mamlaka ya Mji wa Lushoto, suala zima la Halmashauri ya Mlalo, kuna mambo mengi sana yamejitokeza kule. Kwa hiyo, kama Serikali Waziri wangu alituma timu kule ikaenda kufanya assessment na taarifa zile ziko Ofisi ya TAMISEMI katika uchambuzi pale itakapoonekana kwamba vigezo vyote vimekidhi basi hakutakuwa na tatizo. Mheshimiwa Shekilindi naomba vuta subira tu wakati maamuzi yanaenda kufanyika kwa kuangalia kama imekidhi vigezo mbalimbali basi mtapata jibu halisi. Na mimi nimefika pale nimeona ile hali halisi basi tuache michakato iweze kuendelea baadaye tufanye maamuzi sahihi.
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Sitakuwa mbali sana na wanaohitaji miji ipandishwe hadhi. Kwa kuwa kata ya Majimoto sasa imekuwa kubwa kiasi ambacho inatakiwa kupandishwa hadhi na tumekwishaleta maombi katika Wizara inayohusika. Je, ni lini sasa maombi hayo yatashughulikiwa ili kata ya Majimoto iwe Mji Mdogo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kupandisha hadhi na naomba nijibu na Wabunge wengine kwa sababu nimeona wengi wamesimama humu ndani na concern yao wote inafanana na ndiyo maana tuliunda kikosi kazi kwenda kupitia maeneo mbalimbali ikiwemo kwako Majimoto Mheshimiwa Mbunge. Jambo lile sasa liko ofisini kwetu linafanyiwa uchambuzi wa kina, naomba nikutoe hofu kwamba uchambuzi ule wa kina ukishafanyika basi maamuzi sahihi yatafanyika kwa mujibu wa sheria ambapo Waziri mwenye dhamana amepewa mamlaka hayo. Naomba vuta subira tu wakati kazi hii inawekwa vizuri lakini siyo Majimoto peke yake nikifahamu Dongobesh kule na maeneo mengine wote concern yao ni hiyo hiyo, kwa hiyo kama Serikali inafanyia kazi kwa upana wake suala hili.
MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu hayo ambayo hayajaniridhisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba sheria hii haina ubaguzi lakini mimi nasema ina ubaguzi. Kwa sababu iweje sheria ipingane na Katiba? Katiba imetutambua Wabunge wa Viti Maalum na Wabunge wa Majimbo sote ni sawa, tuna haki sawa, tunafanya kazi sawa za kuiletea maendeleo nchi yetu hii iweje leo useme haina ubaguzi?
Je, ni lini sheria hii italetwa hapa Bungeni ili tuirekebishe tupate haki sawa sote, Wabunge wa Majimbo na Wabunge wa Viti Maalum, kwa sababu sote tunafanya kazi sawa?
Pili, kwa kuwa Wabunge wa Viti Maalum tunafanya
kazi zaidi kwa sababu sisi tuna-handle mikoa, lakini Wabunge wa majimbo wanakuwa na majimbo. Jimbo liko ndani ya mkoa, Wabunge wa Viti Maalum tuko kwenye mkoa mzima tunafanya kazi za maendeleo, lakini tunatumia hela zetu za mfukoni tukipata posho, tukipata mshahara, ndiyo tunatumia Serikali haituhurumii?
Je, ni kitu gani chenye kigezo muafaka ambacho amekisema Naibu Waziri kati ya Jimbo na Mkoa upi wenye kigezo ambacho kinakubalika watu wengi, sijui Mkoa ni mkubwa kama alivyosema kuliko Jimbo...
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri anipe kigezo, bado hajaniambia kigezo.(Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa nimesema kwa sababu sijasema mimi kama Jafo, nimesema kwa mujibu wa sheria. Bahati nzuri mnafahamu ndugu zangu kwamba sheria hii ilitungwa humu Bungeni na sheria hii ilipata msuguano mkubwa sana, ndiyo maana ukija kuangalia ni kwamba sheria hii hata suala la vile vigezo vilivyotengwa ndiyo maana inaitwa Sheria ya Mfuko wa Jimbo. Kwa hiyo, kama itaonekana kwamba nini kifanyike hayo sasa ni mawazo mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu lazima tufahamu kuna Wabunge wa Majimbo, kuna Wabunge wa Viti Maalum kutoka Mikoa, kuna Wabunge wengine wanateuliwa na Rais maana yake wanazungumza karibu Tanzania nzima. Kwa hiyo, kama tukitaka tufanye tafakari hiyo na kutakuwa na Wabunge wengine ambao wao wanahudumu Tanzania nzima ndiyo maana nimesema Bunge hili ndiyo lenye dhamana ya kutunga sheria ikionekana jambo hilo linahitajika lifanyike, Bunge litafanya maamuzi sahihi. Tufahamu vilevile hata mkoa hauwakilishwi na Mbunge mmoja. Inawezekana mikoa mingine ina Wabunge wa Viti Maalum saba. Ndiyo maana nimesema jambo hili linatakiwa ifanyike needs assessment kwa ujumla wake kupata maamuzi kama Taifa. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS,TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru Dada yangu Faida Bakar kuna sehemu ya pili alisema Wabunge wanatumia fedha zao. Naomba niwaambie hasa na Wabunge wa Majimbo, fedha za Mfuko wa Jimbo siyo fedha za kwenda kugawa kama zawadi. Fedha za Mfuko wa Jimbo zinapita katika akaunti maalum na zina Wajumbe maalum akiwepo Afisa Mipango ni Katibu wa Mfuko wa Jimbo, fedha ile inaingia mara moja kwa mwaka na Kamati inafanya maamuzi kutekeleza miradi, fedha ile siyo fedha ya kuingia mfukoni kwa mtu kwenda kutoa sadaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, niwatahadharishe Wabunge wa Majimbo kwamba mfahamu fedha hii inakwenda kujibu matatizo ya wananchi. Mlivyopita kuna mahitaji mbalimbali wananchi wameibua sasa katika vikao vyenu mnafanya maamuzi kwenda kujibu matatizo.(Makofi)
MHE. ANDREW J. CHENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii, lakini pia niishukuru sana majibu ya Serikali kwa swali hilo, swali langu la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mgao wa mwisho wa fedha hizi za kuchochea maendeleo ya jimbo, baadhi ya majimbo nchini hapa likiwemo na Jimbo la Bariadi mgao wake wa kisheria ambao umetajwa na Mheshimiwa Waziri katika majibu yake, mgao wake haukuzingatiwa. Majimbo hayo likiwepo na la Bariadi walipewa fedha pungufu kinyume na vigezo hivyo. (Makofi)
Je, Serikali iko tayari kusahihisha dosari hiyo? Ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wangu mwenye dhamana alitoa maelezo hapa katika nyakati mbalimbali suala zima baadhi ya majimbo fedha kuwa pungufu zaidi na hasa katika Mkoa wa Mwanza. Ninafahamu kwamba Mkoa wa Mwanza ulikuwa umeathirika kwa kiwango kikubwa sana lakini mgao ule kipindi kile ulitokea kwa sababu bajeti yetu ilikuwa inalenga bajeti ya majimbo ya mwanzo, kwa hiyo, majimbo mengine yalivyoongezeka kutoka Majimbo 189 mpaka 220 ikasababisha zile fedha zikawa na mgao mdogo, hata hivyo kulikuwa na makosa ya kimahesabu ambayo ofisi yetu ilitoa maelekezo kwa ma-RAS kwamba zile fedha ambazo baaadhi ya majimbo yaliongezewa zirudi kwa ma-RAS wa mikoa, lengo kubwa ni kufanya usahihisho kwa bajeti ile ya mwaka 2016/2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti yetu ambayo tumeipitisha juzi hapa mwaka 2017/2018 ninaamini tumeshafanya marekebisho makubwa na Majimbo yote tarajieni katika bajeti ya mwaka huu unaokuja, imefanya mazingatio ya ongezeko la Majimbo mapya haya ambayo mimi nina imani hatutakuwa na shida tena huko tunakokwenda.
MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Pamoja na majibu hayo mazuri naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ilivyo kwa wananchi
wa Jimbo la Solwa, wananchi wa Jimbo la Msalala nao wameitikia vizuri sana wito wa Serikali kushiriki katika shughuli za maendeleo kwa kuchangia, hivi tunavyozungumza wameshakamilisha maboma 40 ya zahanati, maboma manne ya vituo vya afya na maboma zaidi ya 70 ya nyumba za walimu na vyumba vya madarasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maboma haya ni ya muda mrefu, fedha ambazo zimekuwa zikiletwa mara nyingi zinatosha asilimia 10 hadi 20 ya maboma haya. Nilitaka kujua kwa nini Serikali isiwe na mpango maalum wa kufanya tathmini ya maboma yote na kuleta fedha zinazoendana na maboma ambayo yamekwisha kukamilika ili yaweze kukamilishwa badala ya kuachwa yaanguke?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, moja ya tatizo kubwa ambalo Halmashauri zinapata ni ukosefu wa fedha hasa kutoka vyanzo vya ndani, Halmashauri nyingi za mikoani zimekuwa zikipata shida kupata ushuru wa huduma kutoka kwenye makampuni ya simu. Kwa mfano, Kampuni ya Airtel inalipa zaidi ya shilingi bilioni tano kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, wakati minara yake imetapakaa nchi nzima. Kwa nini Serikali isizisaidie Halmashauri kule ambako minara ipo, ushuru wa huduma ukalipwa kule ili Halmashauri ziweze kupata fedha za nyongeza kutekeleza miradi kama hii?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ulivyosema tunapokea, lakini nilitaka nimshukuru Mheshimiwa Maige kwa sababu kwao kule wamejenga maboma mengi sana lakini kwa kushirikiana na ile Kampuni ya Madini, wameendelea kujenga vituo vya afya. Hata hivyo, kipindi kirefu fedha zilikuwa haziji sasa kuanzia mwaka huu Wizara yetu imesimamia upatikanaji wa fedha na ndio maana mkiangalia kuna maboma mengi sana tunaanza kurekebisha. Bajeti ya mwaka huu tena kama mnakumbuka wakati tunapitisha bajeti hapa tumetenga fedha nyingine kuhakikisha kwamba maboma mbalimbali tunaweza kuyakamilisha katika nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwahakikishie kwamba katika mwaka wa fedha unaokuja kutakuwa na mabadiliko makubwa sana katika umaliziaji wa maboma haya, kwa sababu yote haya tumeshayafanya tathmini Wizara ya TAMISEMI.
MHE. MWANTUMU D. HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nashukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri aliyoyajibu na naona yametosheleza hasa na wananchi huko watasikia jinsi walivyojipanga. Nina swali langu moja dogo tu la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itakamilisha mradi huu na kuondoa msongamano wa daladala ambazo nyingine ni za kizamani kabisa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumshukuru Mheshimiwa Mwantumu Dau, kwa sababu yeye ni Mjumbe wa Kamati ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ambao wamekuwa wakifanya kazi kubwa sana mpaka kuanza kwa mradi huu.
Naomba niwahakikishie wakazi wa Dar es Salaam kwamba mradi huu awamu ya kwanza umekamilika na sasa tunajiandaa katika mradi wa awamu ya pili kuanzia Mbagala na mradi wa awamu ya tatu kuanzia Gongo la Mboto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mmesikia Mheshimiwa Rais wakati anazindua fly over za Ubungo pale, kwamba fedha zimeshapatikana na muda wowote sasa kazi hii inaweza ikaanza. Lengo kubwa ni kuondoa foleni kabisa na kuondoa haya magari madogo katika Jiji la Dar es Salaam na Serikali kuwahudumia wananchi na kukuza uchumi wake. (Makofi)
MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri na ya kutia moyo wananchi wa Nyang’hwale.
Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Kharumwa kilipopandishwa hadhi na kuwa Hospitali ya Wilaya ya Nyang’hwale lakini bado hakijapata watumishi wa kutosha kulingana na hadhi hiyo ya Hospitali ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa kutosha pamoja na vifaa tiba vya kutosha katika Hospitali hiyo ya Wilaya ya Nyang’hwale?(Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kumekuwa na msongamano mkubwa sana katika Hospitali zetu hizi za Rufaa kama vile Bugando na kwingine ukitaka kuonana na Daktari Bingwa; je, Serikali, haioni ni muda muwafaka sasa kuweza kupeleka Madaktari Bingwa wa watoto pamoja na akina mama katika hospitali zetu za Wilaya, ili kuondoa usumbufu huo usiokuwa wa lazima kwa wananchi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge ndiyo maana kwa haja ya Waheshimiwa Wabunge wa Geita hasa ndugu yangu Mheshimiwa Hussein Omar na Mheshimiwa dada yangu Josephine, katika Kituo hiki cha Afya cha Kharumwa kwanza, jambo kubwa tutakalolifanya, licha ya zile bajeti ambazo wenyewe wamezitenga, hivi sasa tutaenda kufanya ukarabati mkubwa wa kituo kile, tutajenga theatre ya kisasa. Lengo kubwa ni kwamba, wale Wasukuma wenzangu wa pale waweze kupata huduma nzuri. Kwa hiyo tutawekeza juhudi hii ya kutosha katika kile, kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge naomba nikutoe hofu katika hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo tunafahamu kwamba changamoto kubwa ni changamoto ya wataalam na bahati nzuri kama ninavyofahamu hata zoezi hili la uhakiki wa watumishi hewa kwenye maeneo mbalimbali tumepata ripoti kwamba idadi ya watumishi hasa katika sekta ya afya, imeathirika sana. Pamoja na watumishi hewa, lakini pia kuna suala zima la ku-forge vyeti. Sasa hivi Serikali iko katika harakati mbalimbali za kuwaajiri watumishi wapya. Naomba nikutoe hofu Mheshimiwa Josephine kwamba tutakapotoa ajira hizi mpya, ambazo si muda mrefu Wizara ya Utumishi watatoa maelekezo nini cha kufanya, tutaelekeza watumishi katika eneo letu hili la Nyang’hwale ili wananchi wa eneo lile waweze kupata huduma nzuri.
Mheshimiwa Spika, kuhusu hoja hii nyingine ya msingi hasa suala zima la madaktari bingwa ni kweli na ndiyo maana leo hii, hasa magonjwa yale ya akinamama, wakati mwingine watu wengi wanatoka mikoani wanaenda Dar es Salaam kwa ajili ya kwenda kuwaona gynecologists. Na kwa sababu hii Serikali yetu inaangalia jinsi gani itafanya ili kuweka uwiano mzuri katika kada mbalimbali zitakazoajiriwa, lakini lazima kuelekeza hawa wataalam katika maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, tukifanya hivyo tutapunguza hii changamoto ya wananchi ambao wengi wao kwenda muhimbili au kwenda sehemu nyingine yoyote ya mbali kwa kujisafirisha inakuwa kazi kubwa. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge nasema hoja yako imekubaliwa, na katika hili Serikali tutafanya kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba tunapeleka watalaam bingwa katika maeneo yetu haya.
MHE. JANET Z. MBENE: Mhehimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Mazingira anayozungumzia Mheshimiwa Chagula hayana tofauti na mazingira mengi ya Wilaya zetu na mikoa yetu ya pembezoni.
Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Ileje ilibahatika kupata fedha kwa ajili ya kujenga Hospitali ya Wilaya ambayo imejengwa na sasa hivi imesimama karibu miaka miwili. Nataka kuomba kuuliza, je, Wizara ya TAMISEMI iko tayari kuimalizia hospitali hiyo kwa sababu ni hospitali kubwa na kwamba kama ingetumika vizuri ingesaidia kiasi kikubwa sana. Sasa hivi wagonjwa wetu wa-referral wanakwenda Malawi. Kwa sababu Mbeya ni mbali zaidi, wanakwenda Malawi kutibiwa sasa hii si sahihi. Mheshimiwa Waziri atuambie, je, itawezekana kututengea fedha bilioni 1.3 kwa ajili ya kumalizia hosptali ile?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba tulichukulie jambo hilo kwa uzito wake na nakumbuka Mheshimiwa Mbunge hata wakati tunajadili mambo mbalimbali hasa katika jimbo lake la Ileje na hata kituo chake cha kimoja cha afya alikuwa akizungumzia suala zima la changamoto ya afya katika Halmashauri ya Ileje. Naomba nikuhakikishie kwamba tutahakikisha tunakamilisha hizo Hospitali za Wilaya ili kupunguza changamoto hizi.
Mheshimiwa Spika, jambo hili liko maeneo mbalimbali, liko Mvomero, Kilolo na maeneo mengine hospitali zime-stack. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge siweze kuthibitisha kwamba by kesho tutatoa fedha, tunachokifanya Serikali kwa sababu tulikuwa na mchakato mpana wa kuhakikisha tunakabati vituo vya afya vipatavyo 100 na zoezi hili la kukarabati vituo vya afya 100 katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania litaanza ndani ya mwezi huu au mwezi ujao.
Mheshimiwa Spika, vilevile tutapeleka maelekezo makubwa kwenye Hospitali za Wilaya ambazo hazijakamilika, na tukimaliza hili tutakuwa tumehakikisha kwamba jukumu la Serikali yetu katika kuwahudumia wananchi litakuwa limefika mahali pazuri.
Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge naomba nikuhakikishie kwamba kwanza katika zile fedha za LGDG ambazo mwanzo zilikuwa sasa hivi tutaelekeza na kuweka nguvu vya kutosha ili fedha zote zipatikane. Vilevile tutazisimamia vizuri ili tuhakikishe kwamba tunamaliza suala hili la miundombinu ili wananchi wetu waweze kupata afya bora.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itashikirikiana nawe katika jimbo lako kuhakikisha sekta ya afya inakwenda vizuri.
MHE. JOHN J. MNYIKA. Mheshimiwa Spika, nashukuru. Inasikitisha majibu yanatoka ya namna hii, hili suala ni la tangu mwaka 2012 kilipovunjwa kituo cha mabasi cha Ubungo; na mwezi Oktoba, mwaka 2014 aliyekuwa Rais, Mheshimiwa Jakaya Kikwete alitamka kwamba kituo kitaanza kujengwa na akatoa mpaka muda mfupi wa kukamilika kwa kituo, lakini majibu mpaka sasa mwaka 2017 yanakuja namna hii.
Sasa swali, ni lini hasa hiki kituo kitakamilika ili kuondoa msongamano ulioko Kituo cha Ubungo ambacho kimeshavunjwa na kiko kwenye hali mbaya?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kituo hiki kinajengwa pembeni ya barabara ya Morogoro, na siku chache zilizopita TANROADS wametoa notice kwa wananchi wote wanaoishi pembezoni ya barabara ya Morogoro mita 121 kutoka katikati ya barabara kila upande. Kuweza ndani ya siku 28 kubomoa majengo yao. Ndani ya siku 28 mita 121 pande zote mbili za barabara kutoka katikati ya barabara. Sasa kwa kuangalia umbali ambao TANROADS umeutaja ni wazi ubomoaji huu utahusu kituo cha sasa cha mabasi ya kawaida ya Mbezi kilichopo. Vilevile kama umbali ni huu wa mita 121 kutoka katikati ya barabara hata hiki kituo kipya kitaguswa.
Mheshimiwa Spika, swali langu kwa Serikali ama Waziri mwenyewe ama Wizara hii ya TAMISEMI ama Wizara ya Ujenzi ijibu; kwa sababu huu umbali utaingilia hiki kituo ni kwa nini Serikali isitengue hili Tangazo lilitolewa na TANROADS la siku 28 ili majadiliano kwanza yafanyike kuhusu huu upana wa barabara sababu ni upana mkubwa sana ambao hauko kwenye barabara yoyote Tanzania? Mita 121 pande zote mbili za barabara kutoka katikati, naomba majibu ya Serikali.
NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: MheshimiwaMwenyekiti, Mheshimiwa Mnyika kwanza umesema kwamba muda umepita sana, ni kweli. Tuelewe kwamba hata suala zima la kituo hiki ni kituo mkakati sana nadhani na wewe liko katika jimbo lako pale. Ni kituo mkakati ambacho ukiangalia sasa hivi hata hizi barabara za kwenda kasi zinaishia pale Mbezi Mwisho. Nashukuru sana tumepata ushauri wa kamati ya TAMISEMI, walipofika kukagua kile kituo wametoa mapendekezo mengi sana.
Mheshimiwa Spika, hata suala hili la la reserve ya barabara waliliona na wakasema ikiwezekana sasa Jiji la Dar es Salaam na kushirikiana na LAPF lifanye mkakati ili kuhakikisha kwamba wenye zile nyumba za jirani wanalipwa fidia ili ni kuongeza kituo. Vilevile wameenda mbali zaidi kwa kusema kwamba kwa uzoefu uliokuwepo maeneo mbalimbali yanapojengwa vituo ili watu watu wakatishe inabidi kutengeneza madaraja ya juu.
Mheshimiwa Spika, Wajumbe wakapendekeza hata ikiwezekana kujengwe tunnel kupitia katika kituo Mbezi cha zamani, kwa hiyo ilikuwa ni ushauri mbalimbali. Hata hivyo jambo hili linaitaji fedha nyingi sana, na kuhusu suala la fedha tunafahamu, wasitani wa shilingi bilioni 28 si jambo dogo; ndiyo maana kuna kitu negotiation kilifanyika kati ya Jiji na wenzetu wa LAPF na jambo hili bahati nzuri tulivyokwenda site siku ile watu wote walikuwepo pale site ili kukubaliana nini kifanyike. Yote hii ni kwa sababu LAPF wameonekeana kwamba wameshafanya mambo mazuri ya mfano. Kwa mfano pale Msamvu wamejenga stand ya kisasa. LAPF wamekuwa commited, wamesema kwamba tunataka tutengeneze stand ambayo hapa Dar es Salaam itakuwa ni stand kubwa ambayo ita-accommodate magari mengi zaidi kwa ajili ya eneo lile.
Kwa hiyo suala la lini mradi utaanza naomba nikuhakikishe, kwa sababu LAPF walishakuwa committed katika utoaji wa fedha, kwa sababu Jiji halitoi fedha; isipokuwa wataingia katika ile joint venture business ambayo itafanyika vizuri na kwa bahati nzuri na wewe Mheshimiwa Mnyika utakuwa miongoni mwa wafaidika kwa sababu stand ile nawe itanufaisha kwenye mapato katika Jiji lako la Dar es Salaam.
Mheshimiwa Spika, suala lingine ni kuhusu uvunjaji, kwamba ikiwezekana tutoe tamko hapa ili suala hili lisitishwe. Mimi niseme kwamba Serikali imesikia hiyo concern yako basi kama Serikali itaangalia nini kifanyike kwa ajili ya maslahi mapana kwa ajili ya Dar es Salaam lakini pia kwa wakazi wa Tanzania. Hata hivyo tumependekeza kwamba wataalam wetu wa detailed design waangalie vya kutosha ili ikiwezekana zile barabara ziweze kusogea mpaka hapa Mbezi Luis Mwisho; kwa sababu hata tukijenga ile stand kubwa pale bila kuitanua ile barabara vya kutosha bado tutakuwa na changamoto kubwa sana kwa sababu magari yatazidi kufungana.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo mambo haya yote kama Serikali inayachukua kwa maslahi mapana kwa mustakabali wa nchini yetu ili kukuza uchumi wetu na wananchi waweze kusafiri vizuri.
MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Napenda sasa katika majibu yake angeweza kufafanua kwa jinsi ambavyo barua ilivyokuwa imeelekeza, kwa sababu tunavyojua katika kikao chetu cha RCC pamoja na uanzishwaji wa Wilaya mpya ya Bukene pia kulikuwa na maombi ya Wilaya mpya ya Manonga.
Kwa hiyo, nilikuwa nafikiria MheshimiwaWaziri atuambie; je, mchakato huo utaenda sambamba pamoja lakini turahisishiwe katika kuanzishiwa Mkoa wetu wa Tabora kwa sababu Mkoa wa Tabora ni mkubwa katika mikoa yote iliyobakia kwa sasa, una kilometa zaidi ya 75,000 na tumeshaona baadhi ya mikoa mingine imegawanywa kama Mkoa wa Mbeya, Arusha na Shinyanga. Naomba sasa Mheshimiwa Waziri atuhakikishie uharakishaji wa kugawa huu mkoa ili kurahisisha kupeleka maendeleo kwa wananchi. Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, alichosema Mheshimiwa Mbunge ni kweli, kwa sababu maombi haya yalivyokuja, lengo kubwa lilikuwa ni kuanzisha Mkoa mpya wa Nzega ambao uliainisha mkoa huo utakuwa na Wilaya nne. Ilipendekezwa kwamba kutakuwa na Wilaya hii mpya ya Bukene, Wilaya kongwe ya Nzega, Wilaya ya Igunga, halikadhalika na Wilaya mpya ya Manonga. Kwa hiyo, huo ndiyo mchakato wenyewe ulivyokuwa katika pendekezo lile. Ndiyo maana nimesema kwamba kulikuwa na mapungufu kadhaa, baadaye sasa ofisi yetu ikapeleka mrejesho kwa Katibu Tawala wa Mkoa na wameshafanyia kazi hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana nimesema kwamba physical verification imeshaenda kufanyika, sasa kilichobakia ni kwamba iko katika mchakato wa kupelekwa kwa Mheshimiwa Rais naye atafanya maamuzi, lakini tukiwa na angalizo kwamba na Mheshimiwa Rais alifika pale Tabora, kuna mazungumzo aliyazungumza. Kwa hiyo, yeye mwenyewe atapima ataona nini kifanyike kuhakikisha kwamba jambo linafanikiwa kwa kadri yeye mwenyewe atakavyoona inafaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imefanya hayo yote ili mradi kufanya jambo hili kwa matakwa yenu na Mheshimiwa Rais aweze kufanya maamuzi.
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Swali la Mheshimiwa Selemani Jumanne Zedi, kwa tatizo lililoko Nzega huko ni sawasawa na tatizo lililoko Serengeti. Sasa namuuliza Mheshimiwa Waziri kwamba Wilaya ya Serengeti kwa ukubwa wake; je, ina-qualify kuigawa kuwa Wilaya mbili?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, qualification ya Wilaya inategemea vigezo kadhaa ikiwepo population ya watu, ikiwepo area size na mambo mengine. Kwa hiyo, kwa sababu ombi hilo hatuna rasmi katika ofisi yetu, maana ingekuwepo limefika, tungeenda kufanya uhakiki kuangalia, je, vile vigezo vyote vya kuanzisha Wilaya mpya vinakidhi au vipi? Ndiyo tungeweza kufanya maamuzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo jambo hili naomba niliache kwa wananchi wa Serengeti wenyewe watafanya maamuzi kwa kadri watakavyoona inafaa na sisi kwa mujibu wa ofisi yetu, itakwenda kufanya tathmini kama hilo litkuja kuangalia kama nini kinafanyika. Ila tufahamu wazi kwamba Serengeti japokuwa eneo ni kubwa lakini idadi ya watu ni wachache, kwa sababu eneo kubwa sana liko katika sehemu ya hifadhi. Kwa hiyo, mambo hayo yote tutayazingatia. Lengo kubwa ni mustakabali wa nchi yetu iwe vizuri.
MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Kwa kuwa Wilaya ya Bunda ni Wilaya kubwa na ina majimbo matatu ya uchaguzi, ikiwemo Bunda, Bunda Mjini na Mwibara; na kwa kuwa tayari Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, miaka saba sasa iliyopita tulishaamua Mwibara iwe Halmashauri ya Wilaya lakini mpaka leo Mheshimiwa Naibu Waziri anatuambia mambo ya uchambuzi na vigezo; je, ni lini mambo ya uchambuzi na vigezo vitafikiwa ili Jimbo la Mwibara sasa miaka saba tangu wananchi wameomba iweze kupatiwa Halmashauri yake?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kangi Lugola amehamisha goli, lakini hakuna matatizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba Mheshimiwa Kangi alivyosema Jimbo la Mwibara, kwanza anafahamu kwamba zamani kwanza walikuwa na majimbo mawili pale, lakini walikuwa na Halmashauri moja, baadaye wakagawanyika tukapata majimbo matatu na Halmashauri mbili; Halmashauri ya Mji na Halmashauri ya Bunda Vijijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto kubwa iliyokuwepo ni kwamba haya majimbo mawili; Jimbo la Mwibara na Jimbo la Bunda Vijijini ukiangalia jiografia yake, haiko sawasawa. Unatoka Jimbo la Mheshimiwa Boniphace Getere, unaenda katika Jimbo la Mheshimiwa Bulaya, halafu unaenda tena Jimbo la Mheshimiwa Kangi Lugola.
Mwenyekiti Mwenyekiti, haya majimbo mawili ambayo ni kwa upande mmoja Magharibi na mmoja Mashariki, katikati kuna Jimbo lingine lakini haya majimbo mawili ni Halmashauri moja. Hili sasa tusema kwamba inawezekana kuna mapungufu yaliyofanyika kule mlipokuwa mnafanya maamuzi kwamba Jimbo hili ligawanyike vipi, ndiyo changamoto kubwa iliyokuwepo hapo. Kwa hiyo, kikubwa zaidi tuseme kwamba mchakato ule ulikwenda lakini tulipata majimbo haya mawili ya Mji na Bunda Vijijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaelekeza, pale itakapoonekana kuna mahitaji ya ziada hasa katika maeneo yale inaonekana kuhudumia Halmashauri ile katika Majimbo mawili ambayo yako sehemu mbili tofauti ni changamoto kubwa, basi mtaleta maombi haya ili tujadili kwa pamoja nini kifanyike. Lengo kubwa ni kuwapatia wananchi huduma ya karibu katika maeneo yao.
MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Ningependa kuuliza maswali mawili ya nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI.
Mheshimiwa Waziri umetuaminisha kwamba mmetupatia shilingi milioni 600 kwa ajili ya kujenga barabara na pia mmetupa shilingi milioni 320 kwa ajili ya kukarabati barabara hizi. Mheshimiwa Waziri barabara ya Phantom-Majengo, ni barabara ya muhimu kweli na barabara hii inachangia pato la Halmashauri kwa asilimia 25. Barabara hii ina urefu wa mita tano na tunasema tunataka tufanye Serikali ya viwanda, kule kuna viwanda vidogo vidogo vya mazao ya mpunga na mahindi.
Mheshimiwa Waziri, hauoni kama kuna umuhimu wa kuingiza barabara hii katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha ili tuweze kutekeleza mpango huu wa Tanzania ya viwanda kwa kuendelea kuzalisha na magari yaweze kupita? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Ushetu, Mheshimiwa Waziri mmetenga shilingi milioni 181 tu kwa ajili ya barabara na tena ni kwa ajili ya ukarabati tu wa barabara, lakini nikufahamishe kwamba kule hakuna barabara hata moja ya lami, barabara zote ni za vumbi na fedha mliyotenga ni kidogo na ile ni Halmashauri mpya. Unawaambia nini Watanzania wa Ushetu, watawezaje kupata barabara nzuri za lami ilihali mmewatengea fedha kidogo namna hii, nini mpango wa Serikali kwa Halmashauri hii mpya?
Mheshimiwa Naibu Spika, nilimaanisha kilometa tano.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, Mji wa Kahama kimkakati tunafahamu na ndio maana hata ninyi katika Mji wa Kahama mlikuwa mnapeleka maombi kwa Mheshimiwa Waziri wa Nchi kwamba Mji ule sasa uwe Manispaa kwa kadri unavyokua. Ukiangalia barabara ya Phantom - Majengo ina kilometa 5.2 ni barabara ya kimkakati ina jukumu kubwa sana, ndiyo maana tumesema mwaka huu tumeanza kutenga fedha hizo. Hata hivyo, unafahamu Mji wa Kahama siyo barabara hii tu ndiyo tunaanza kujenga, kuna miundombinu ya barabara za lami pale zilikuwa zinaendelea na mimi nilifika pale miezi michache iliyopita kuja kukagua.
Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu letu kubwa tunajua kwamba eneo hili ni eneo la mkakati, kama Serikali tutafanya kila liwezekanalo, lakini siyo Mji huu peke yake. Serikali tumejipanga kuna ahadi za Mheshimiwa Rais katika maeneo mbalimbali, hivi sasa ukiangalia katika Halmashauri mbalimbali, juzi Mheshimiwa Rais alikuwa kwa ndugu yangu pale Mheshimiwa Mbowe, alikuwa akiangalia miundombinu ya barabara. Pia nchi nzima hata kwa Mzee Lubeleje kule Mpwapwa kuna ahadi ya Mheshimiwa Rais.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tunachotaka kufanya ni kwamba ndani ya miaka mitano tufanye mabadiliko makubwa sana katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hasa katika ujenzi wa barabara za lami.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaondoe hofu Waheshimiwa Wabunge, siyo kwa Mji wa Kahama peke yake isipokuwa katika miji mbalimbali katika Halmashauri zetu hizi tutahakikisha ujenzi wa barabara za lami hasa kutumia fedha za World Bank ambayo Serikali imechukua commitment ya kutosha kubadilisha miji yake yote iweze kubadilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninyi ni mashahidi mnafahamu sasa hivi, Halmashauri za Miji nyingi sasa hivi na Manispaa zimebadilika katika suala la ujenzi wa barabara za lami TAMISEMI imeamua kufanya hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu eneo la Ushetu kama ulivyosema ni kwamba tunafahamu Ushetu ni Halmashauri mpya na ndiyo maana, ndugu yangu hapa Mheshimiwa Elias Kwandikwa kila siku anapambana na Jimbo lake la Ushetu, kama unavyopambana Mheshimiwa Mbunge hapa. Naomba kuahidi kwamba kwa kutumia Mfuko wa Barabara, nikuahidi tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo tutahakikisha maeneo ya Ushetu na maeneo mengine tutaweka nguvu za kutosha na hasa hizi Halmashauri mpya tutaweza kuzifungua ili wananchi kule waweze kupata huduma wajisikie huru kama wananchi wenzao wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MHE. PETER A. P. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Mheshimiwa Waziri Mji wa Ifakara ni Halmashauri mpya, kutokana na upya wake bado ni changa. Barabara zetu bado ziko katika level ya tope, kutokana na mvua hizi ambazo kule zinanyesha barabara zinaharibika sana. Sisi kama Halmashauri tunajaribu kuziwekea vifusi lakini kwa sababu ni Halmashauri mpya, hatuna fedha za kutosha kuweza kujenga lami.
Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia Halmashauri ya Mji wa Ifakara, Halmashauri ambayo ni mpya ili iweze kuboresha barabara zake, ziweze kuwa katika kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nafahamu Kilombero na maeneo mengine, naomba niwape pole Wabunge wote kwa sababu nikijua wazi kwamba kipindi hiki mvua zinanyesha, barabara nyingi sana katika maeneo yetu zimeharibika vya kutosha. Ndiyo maana katika bajeti yetu ya mwaka huu, tuliyoipitisha tumetenga karibuni shilingi milioni 247 mwaka huu wa fedha 2017/2018 ili kuhakikisha tunafikia maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, hapa sitaki kutoa commitment ya uwongo kusema kesho Kilombero pale Ifakara tutakuja kujenga barabara za lami, itakuwa ni uwongo. Kikubwa zaidi tutaangalia jinsi gani tutafanya kwa bajeti iliyopo sasa, kwa sababu tunakwenda awamu kwa awamu. Tulikuwa na miji mikuu, tumeenda na manispaa, tunaenda katika halmashauri za miji, tunaangalia jinsi gani tutafanya kwa sababu kila barabara zingine zinawekewa kifusi ili barabara iweze kupitika.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba commitment ya Serikali ni kuhakikisha wananchi wake wanaweza kufikiwa, wanaweza kusafirisha mazao yao na hata kusafiri sehemu zingine, hii ni commitment ya Serikali. Hivyo, tutajitahidi kufanya kila liwezekanalo bajeti iliyotengwa katika eneo hilo tutaisimamia vizuri, kwa sababu changamoto kubwa ni usimamizi wa bajeti katika maeneo yetu wakati mwingine.
MHE. FREEMAN A. MBOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu tatizo la Mji wa Kahama kama sahihi kabisa alivyozungumza Mheshimiwa Naibu Waziri linafanana kwa njia moja au nyingine na ahadi za Rais alizotoa wakati wa kampeni, ni kweli Rais wakati wa kampeni alitoa ahadi ya kujengea Halmashauri ya Wilaya ya Hai kilometa tano za lami katika Mji wa Hai katika kipindi chake cha uongozi. Na ni kweli kwamba hivi majuzi Rais alivyokuwa katika ziara kwenye Mkoa wetu wa Kilimanjaro aliulizwa kuhusu ahadi yake na Rais akauliza vilevile Halmashauri imegawiwa fedha kiasi gani katika mwaka huu wa fedha kwa ajili ya Mfuko wa Barabara. Taarifa ambazo Rais alipewa ni fedha ambayo ilikuwa imepangwa kwenye bajeti ambayo ni shilingi bilioni 1.3 lakini hiyo fedha haijapokelewa kwa sababu haijatolewa na Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, natambua kwamba Rais aliagiza kwamba TAMISEMI wakafanye uchunguzi, nakaribisha sana TAMISEMI mkafanye uchunguzi, lakini ukweli ni kwamba fedha pekee ambayo ilishapokelewa ni kama shilingi bilioni 300 ambayo ni lazima mtambue kwamba Wilaya ya Hai ina zaidi ya kilometa 200 za barabara zinazoteleza za milimani ambazo ni lazima zifanyiwe routine maintanace.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sasa Mheshimiwa Naibu Waziri ni wewe kutoa commitment ya kwenda kufuatilizia alichokizungumza Rais, lakini vilevile kukumbushia ahadi ya Rais ya kilometa tano za Halmashauri ya Wilaya ya Hai katika Mji wa Hai, bado ni muhimu sana kwa sababu Mji unakuwa kwa kasi na una zaidi ya wakazi 50,000 ambao kwa kweli hawana hata robo kilometa ya lami katika Mji wa Hai ukiacha barabara ya kwenda Arusha. Mheshimiwa Waziri naomba commitment yako.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA
NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni na hata baada ya kampeni amekuwa akiahidi kufanya mambo mbalimbali hasa anapoona maeneo fulani yana matatizo. Katika eneo la barabara ametoa ahadi maeneo mbalimbali ikiwemo Kasulu kilometa sita na hapa Mheshimiwa Mbowe anasema kilometa tano na hasa barabara za milimani, lakini ameahidi maeneo mengi, Waheshimiwa Wabunge wana ahadi na wana kumbukumbu hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge, kwamba ahadi za Mheshimiwa Rais zitatekelezwa na kwa sababu bado tunao muda na tutaangalia kama utaratibu mzuri ni wa kuzingatia wakati wa bajeti zetu lakini nafahamu mnafahamu kwamba bajeti zetu huwa zina ukomo, kwa hiyo tutajaribu kuangalia namna ya modality nzuri ya kuweza kutekekeleza hili tukimshirikisha aliyeahidi.
Pia nitoe rai tu kwa wenzangu kwamba wakati tunaposimamia ahadi za Mheshimiwa Rais pia tuwe tunakumbuka kuishi naye vizuri na kumheshimu. Ahsante sana.(Makofi)
MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Serikali, naomba tu niipe taarifa Serikali kwamba hiyo fedha imetengwa sh.milioni 220 siyo sahihi ni fedha ambayo ipo kwenye maombi maalum, kwa sababu binafsi nilipitia bajeti ya Halmashauri yote, CDG tulipewa shilingi bilioni 1.24; allocation ya gari la wagonjwa haikuwepo kutokana na fedha kuwa ndogo na mahitaji ya Jimbo la Nsimbo kwa upande wa elimu, afya, na maeneo mengine kuwa na uhitaji zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hilo gari moja lililopo ni msaada ambao Jimbo la Nsimbo lilipata kutoka Shirika la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), tunashukuru kwa mgao huo, kutokana na Jimbo kuwa na makazi ya wakimbizi kwenye Kata ya Katumba.
Je, Serikali haioni ule mpango tuliouleta wa maombi maalum wakachukua kile kipengele tu cha gari la wagonjwa, watuidhinishie ile Halmashauri yetu tuweze kupata gari hilo au laa, hatuna wasiwasi na utekelezaji wa ahadi mbalimbali za Serikali kuhusiana na kujali afya za wananchi wake kwa kutoa magari ya wagonjwa, kama hivi juzi Mheshimiwa Rais ametoa mgari matatu je, Serikali haioni tena kuna umuhimu wa Jimbo la Nsimbo na lenyewe likaangaliwa kupata gari la wagonjwa?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana nimesema kwamba kwanza tumewashukuru wenzetu wa Nsimbo na Mheshimiwa Mbunge naomba nikushukuru sana kwa kuonesha commitment yenu kwamba kulikuwa na hili hitaji ya gari. Ndiyo maana naomba niseme kwamba, kwa kipindi hiki cha Serikali ya Awamu ya Tano, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba, Mheshimiwa Rais na Serikali yake amejipanga sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri umesuhudia hapa kwamba, juzi Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Ally Kessy Mohamed na wenzie Mheshimiwa Rais alitoa magari matatu personally pale, lakini kuna magari mengine 50 yaliweza kupelekwa katika maeneo mbalimbali. Hii yote ni jukumu la Serikali kuwahudumia wananchi. Hivyo, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Richard Mbogo kwamba tutaangalia kile kinachowezekana ili kulisaidia Jimbo lako ambalo liko mpakani kabisa ili suala hili la gari la wagonjwa na yale mambo mengine ya msingi likiwemo suala zima la ujenzi wa kituo cha afya, kufanya ukarabati katika eneo lako tutalifanya. Serikali ya Awamu ya Tano lengo kubwa ni kuwapunguzia adha akina mama na watoto.
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mazingira yaliyopo Nsimbo yanafanana kabisa na mazingira yaliyopo katika katika Jimbo la Kavuu na kupitia initiative ya Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuja kwenye ziara katika Jimbo la Kavuu alituomba tuanzishe Hospitali ya Halmashauri ya Mpimbwe kufuatia kuwepo na kadi za CHF kwa sababu za NHIF hazitumiki kule.
Je, Serikali sasa haioni kuna umuhimu, kutokana na juhudi za wananchi wa Jimbo la Kavuu kuwapatia gari la wagonjwa ambao wamekuwa wakitumia umbali mrefu kutoka Mpimbwe kwenda Mpanda na sasa tutumie katika Jimbo la Kavuu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, mara nyingi sana huwa nazungumza hapa Bungeni kwamba, issue ya gari la wagonjwa ni vema kwanza tukai-allocate katika bajeti zetu za kila mwaka, hilo ni jambo la msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu sana Mheshimiwa Dkt. Kikwembe anavyohangaika kwa Jimbo lake, ndiyo maana hapa juzi alikuwa anahangaika tupeleke huduma za afya pale na ndiyo maana tulimhakikishia pamoja na Waziri wa Afya, na Mheshimiwa Waziri Mkuu alienda pale na akatoa ahadi, tutaenda kufanya ukarabati mkubwa wa kituo chake cha afya kwa kuingiza fedha nyingi ili akina mama na watoto sasa waweze kupata huduma nzuri, hasa huduma ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Dkt. Kikwembe mahitaji yako ambayo umeongea mbele ya Waziri Mkuu, Serikali imeyachukua kwa ujumla wake, hata hivyo, naomba nipendekeze, kwa Wabunge mbalimbali katika suala la ambulance lazima tuliainishe katika bajeti zetu, likishakuwepo katika bajeti tunapata msingi mzuri wa kulifanya jambo hilo katika utekelezaji wake.
MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la gari la wagonjwa Jimbo la Nsimbo ni sawasawa kabisa na tatizo hili linalotukabili Wilaya ya Manyoni. Tunayo Hospitali kubwa ya Wilaya pamoja na vituo viwili vya afya vya Nkonko pamoja na Kintinku. Magari tuliyonayo ni chakavu sana na kumekuwa na matukio mengi ya kubeba wagonjwa na magari yanaharibika njiani mpaka kulala njiani, inabidi utoe gari sasa kutoka Manyoni Mjini kwenda kufaulisha wale wagonjwa.
Je, ni lini Serikali sasa itatupatia nasi angalau gari la wagonjwa kwa Wilaya ya Manyoni ukizingatia hali halisi ya Manyoni pale, kuna ajali nyingi zinatokea kwenye ule mlima wa Saranda Sukamahela?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa lugha ya kwetu sisi, ndiyo maana mwanzo nilianza na kile kitu kinaitwa kingilambago. Nilieleza pale awali kwamba, lazima hili jambo tuliainishe katika suala zima la mpango wetu wa bajeti. Mheshimiwa Mtuka naomba nikuhakikishie kwa sababu nami nilifika pale Manyoni, kwanza nilitoa maelekezo katika hospitali yako kwa sababu, hata hili suala la referral ni lazima maeneo yetu watu wafanye kazi vizuri, niligundua baadhi ya uzembe pale katika watalaamu wetu, nikatoa maelekezo. Jambo hili naomba nikuhakikishie katika mpango wako wa bajeti 2018/2019 naomba liainishwe wazi na likifika kwetu katika Ofisi ya TAMISEMI tutalipa nguvu ili kwamba eneo la Manyoni pale tupate gari la wagonjwa.
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kuna huu utaratibu wa MSD kwenda kwenda vituo vya Afya wamebeba, wanapeleka kondomu na mseto pakiti nane unaenda kwenye zahanati unakuta wamepeleka kondomu na mseto nane, huu utaratibu unasafirisha hivi vitu kutoka Mwanza mpaka kule Serengeti haukubaliki. Je, ninyi kama Wizara mnaona huu utaratibu uendelee?
Swali la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri umekuja pale Serengeti na Serengeti sasa ni Wilaya ya kitalii, tunapata watalii wengi lakini tulikupeleka kwenye ile Hospitali ya Wilaya ukaona umaliziaji wa ile OPD. Wizara mpo tayari kutoa fedha kwa ajili ya kumalizia ile OPD? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala zima la upelekaji wa dawa MSD naomba nitoe ufafanuzi ifuatavyo:-
Ni kwamba dawa zinapofika kule kwanza kuna request ya kawaida inayopelekwa, lakini dawa zinapofika lazima Kamati ya Afya ya kituo husika lazima ihisike katika upokeaji wa dawa, lakini nitoe wito kwa Halmashauri ya Serengeti kwa sababu japo kuwa tumepeleka fedha nyingi pale kuna baadhi ya fedha zingine bado hazijatumika katika ununuzi wa dawa, kwa hiyo nikuombe Mheshimiwa Mbunge najua kwamba kwa sababu pale eneo lako lina changamoto kubwa tushirikiane vema kwamba kuhakikisha tunasukuma MSD dawa ambazo zimebakia karibuni za shilingi milioni 180 zifike pale site, lakini hali kadhalika mnao pesa nyingi zaidi za basket fund bado hazijanunua dawa, nitoe maelekezo hayo kwa Serengeti haraka iwezekanavyo dawa zipatikane kwa sababu tayari Serikali tumepeleka fedha.
Lakini katika suala la pili ni suala zima la hospitali tuliofika, ni kweli na mimi nimefika pale na tulivyoenda kuangalia tukasema ajenda ya Mheshimiwa Rais alipofika pale ni kuahidi kwamba atawahudumia wananchi na ndio maana katika kipindi cha sasa tumefanya commitment zile wodi mbili tutazifanya two wards in one, tutafanya zoezi kubwa pale la kupeleka takribani tutaweka nguvu karibu shilingi milioni 700 lengo kubwa ni kufanya ahadi ya Mheshimiwa Rais katika maeneo mbalimbali iweze kutekelezeka. Kwa hiyo hili ni jukumu la Serikali tunaenda kulitekeleza. (Makofi)
MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipatia fursa ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bima kwa Wote ni utaratibu ambao ungeweza kusaidia sana wananchi wanyonge kuweza kupata huduma nzuri za afya kwa gharama nafuu, lakini vilevile ingesaidia serikali kupata mapato ya kuendesha huduma za afya, sasa nataka kuuliza ni lini Serikali italeta Muswada wa Sheria wa Bima ya Wote (Universal Coverage) kwa ajili ya kujadiliwa hapa Bungeni?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili lipo katika negotiation ambapo wadau mbalimbali wameenda kushiriki na Wizara ya Afya na Wizara yetu inaangalia utaratibu mzuri, naomba niseme kwamba Serikali imejipanga katika hili na si muda mrefu baada ya wataalam kupita katika ngazi mbalimbali basi Serikali itakavyoona kwamba huu muswada sasa umeiva, basi utakuja hapa Bungeni kwa ajili ya kufanya maamuzi hayo.
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa tatizo lililopo Serengeti linafanana kabisa na tatizo lililopo katika Tarafa ya Mtae, Shagayu, Sunga na Rangu, wananchi wamehamasika kuchangia huduma za CHF lakini wanapokwenda kwenye Kituo cha Afya cha Mtae huduma hakuna. Je, Serikali inawambiaje wananchi hawa wa Tarafa Mtae?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niweke rekodi sawa kwamba bahati nzuri tulikuwa na Mheshimiwa Mbunge katika Jimbo lake kipindi kile wakati nilipokwenda kutembelea Wilaya ya Lushoto. Ni kweli kwa sababu tumegundua changamoto ya afya ipo kubwa zaidi ndio maana katika vipaumbele vyetu tumeamua kukiteua hiki Kituo cha Afya cha Mtae ni miongoni mwa vituo ambavyo ndani ya mwezi huu mmoja unaokuja tutaenda kufanya ujenzi wa maternity ward pale na kufanya ukarabati mkubwa lengo kubwa wananchi wa Mtae na maeneo ya jirani waweze kupata huduma nzuri katika eneo lile.
MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Ahsante Mwenyekiti, nipende tu kuuliza swali kwamba Wilaya ya Bunda ina hospitali moja ambao ni Hospitali ya Manyamanyama, na ile hospitali ya Manyamanyama inaitwa Hopsitali ya Wilaya, lakini haina hadhi kama Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Waziri, je, ni lini itakuwa na kiwango kama Hospitali ya Wilaya na dawa zipelekwe kama Hospitali ya Wilaya? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli na tulipofika pale Bunda tulitembelea yale maeneo yote tukaona kwamba kuna changamoto kubwa na hili tulitoa maelezo katika maeneo mbalimbali, hata hivyo kwa ajili ya the backup strategy ya kufanya kwa Bunda na kwa sababu ukiangalia kwa ndugu yangu Kangi Lugola wagonjwa wote wanakuja pale, kwa ndugu Boniphace wagonjwa wote wanakuja pale, ndio maana sasa hivi kwa muda unaokuja na si muda mrefu sana japo tunaweka mikakti ya ile sehemu ya Manyamanyama pale lakini katika eneo la Mgeta tunakwenda kutengeneza kituo cha afya tunakwenda kukiimarisha kwa kiwango kikubwa lengo kubwa ni kupunguza idadi ya wagonjwa wanaokuja pale kuweza kuhakikisha kwamba akina mama na watoto afya zao tunazilinda vizuri.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Sera ya nchi na ya Serikali ni kuhakikisha kwamba kila kijiji na kila kitongoji kuna kuwa na zahanati, na katika mji wa Tunduma katika mtaa wa Makambini eneo la Sogea wananchi wameamua kujenga zahanati katika eneo ambalo lilikuwa limetengwa na Serikali, lakini kutokana na mgogoro uliokuwepo na ambao alikuja kuumaliza Naibu Waziri wa Ardhi, alitoa maelezo kwamba eneo hilo lisianze kujengwa mpaka atakavyotoa ruhusa ya wananchi kuendelea kujenga Zahanati pale. Je, ni lini atatoa ruhusa ili wananchi wa mji wa Tunduma eneo la Makambini waweze kuendelea na ujenzi wa zahanati kama ambavyo sera za nchi zinasema?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nadhani Mheshimiwa Waziri wa Afya alivyopita pale wananchi waliandamana katika suala zima katika kituo kile cha afya nadhani tutafanya utaratibu kupitia ofisi yetu ya TAMISEMI nini kifanyike, lakini kutokana na changamoto ya Tunduma kwa sababu ukipita pale siku niliyopita pale population ni kubwa sana na ndio maana tunaamua kwenda kukiimarisha kituo cha Chipaka na lengo kubwa ni kwamba angalau ile kituo cha afya cha Chipaka kiweze kuwa accommodate wagonjwa wengi na tunakwenda kufanya kazi hizyo muda si mrefu ndani ya mwezi mmoja ujao kwa ajili ya wananchi wa Tanzania lengo letu ni kuboresha maeneo yale.
MHE. ALLY K. MOHAMED:Ahsante sana Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi bima za afya baadhi ya maduka na hospitali zinatumika vibaya, kuzidisha double allocation mtu anaenda kutibiwa anaweza akaandikwa double akaiga saini ya mteja au na zingine zinazidisha bei mara mbili, je, nani anazikagua bima ya afya kabla ya malipo, kwa kuwa zinaendesha wizi wa hali ya juu.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti ni kweli kwa kipindi kirefu sasa hata ukija kuangalia wakati mwingine kuna takwimu na kuna fraud inafanyika katika hizi document hasa za bima ya afya na ndio maana sasa hivi utaratibu wa bima ya afya imeweka sasa hivi document ambayo haijakaa vizuri hawawezi kuilipa, lakini hili sasa naomba niwa sisitize hasa katika wenzetu wa bima ya afya wahakikishe wanaweka mechanisim nzuri ya kuweza kuangalia tuna monitor hizi fomu zinajazwa vizuri, lakini sio kujazwa tu, iangalie ili mradi compliance kwamba fomu iliyojazwa ndio kweli iliyotoa matibabu.
Kwa hiyo Mheshimiwa Keissy naomba tuichukue hoja hii kwa sababu ni hoja ya msingi tunaenda kulinda fedha za wananchi, fedha za serikali tutaenda kulisimamia vizuri kwa kadri iwezekanavyo.
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Ahsante Mheshimiwa Mwenyekiti naomba kwa namna ya kipekee nishukuru kwa sababu suala hili la ulipaji wa maeneo haya fidia hii ni suala la muda mrefu sana kwa kuwa Wizara hii ya TAMISEMI na Wizara ya Ardhi imekubali sasa kulimaliza suala hili tunashukuru kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mtwara Mjini, lakini hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, nilikuwa naomba kujua sheria inatueleza kwamba kwa kuwa maeneo haya yamechukuliwa mwaka 2012/2013 ni muda mrefu hivi sasa wananchi wale wamekosa maeneo ya kulima na kufanya shughuli zao za kimaendeleo, je, Serikali ipo tayari kulipa pamoja na fidia ya nyongeza?
Swali la pili, kwa kuwa ahadi hii ya kuwalipa wananchi hawa Jimbo la Mtwara Mjini ni la muda mrefu, je Mheshimiwa Waziri yupo tayari kulithibitishia Bunge hili kwamba wananchi wa Mtwara Mjini wa maeneo haya ya Mji mwema na Tangira kwamba tarehe hizo walizotaja ni kweli wataenda kulipa fidia? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kulifuatilia hili jambo kwa sababu ni haki za wananchi wako kwa hiyo commitment yako kwa wananchi wako imekuwa vizuri, lakini jambo la pili, utaratibu wa malipo ya fidia ni kwamba mara baada ya tathimini ikishafanyika ikipita miezi sita maana yake malipo yanatakiwa yalipwe ndani ya miezi sita; ikipita miezi sita lazima kuna malipo ya nyongeza yatafanyika. Kwa hiyo, naomba nikuhakikishie kwamba Wananchi haki zao zitalindwa kulingana na muda uliocheleweshwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala la pili kwamba commitment ya Serikali sasa itaenda kulipa hili nimezungumza hapo awali kwamba kilicho chelewesha mwanzo kutokana na Bodi ilikuwa haijaundwa na bahati nzuri sasa bodi imeshaundwa na ndio maana sisi ofisi yetu ina jukumu la kutoa kibali tumeshatoa kibali. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba uondoe hofu kwamba wananchi wa Mtwara leo hii wananisikiliza live kupitia vyombo vya habari kwamba Serikali imejipanga katika hili na itaenda kutekeleza kwa kadri mipango yote ilivyowekwa vizuri kupitia Halmashauri yenyewe.
MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru kwa kunipa nafasi, kwanza naipongeza Serikali kurudisha Ardhi ya Dodoma mikononi mwa wananchi yaani Baraza la Madiwani. (Makofi)
Kwa kuwa CDA imevunjwa na ndio mamlaka iliyokuwa na madaraka juu ya ardhi ya Dodoma na wakati inavunjwa wapo wananchi ambao walishapata barua za kumiliki ardhi, lakini walikuwa hawajaonyeshwa maeneo yao na wapo wananchi ambao wanalipa kidogo kidogo pale CDA, je, Serikali imeweka utaratibu gani wa dharura wa kuhakikishwa kwamba wananchi wa Manispaa ya Dodoma wanahudumiwa wakati taratibu zingine zinaendelea?(Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tunashukuru kwa Mheshimiwa Mbunge ku- recognize kwamba kilio cha wananchi wa Dodoma katika hilo, lakini jambo la pili government works on papers, hakuna haki mtu itayopotea. Kwa hiyo, Serikali itaandaa utaratibu wowote ambao unawezekana na kikosi kazi kwa mujibu Serikali itakavyokuwa imejipanga naomba muondoe hofu kwamba Ofisi ya Rais, Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo jambo hili inaisimamia vizuri tutakuja kutoa taarifa hapa iliyokuwa rasmi juu ya jinsi gani jambo hili linatekelezeka na wananchi wote wa Dodoma wasiwe na hofu kila jambo litakuwa limewekwa vizuri kwa utaratibu wa Kiserikali.

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Ahsante Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa majibu ya nyogeza kwa niaba Waziri wa Ofisi ya Rais -TAMISEMI kuhusiana na swali lililoulizwa na Mheshimiwa Bura kama ifuatavyo:-
Naomba niwahakikishie wananchi wa Dodoma kwamba mbali na kuvunjwa na CDA huduma zote za ardhi zinaendelea chini ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma na watumishi waliokuwa wakifanya kazi sekta ile wapo ambao wataendelea na kazi hiyo na wale ambao walikuwa wamelipia nusu ya maeneo yao wataendelea na utaratibu huo mpaka pale watakapokamilisha kulingana na makubaliano waliopeana awali.
Aidha, wale wote ambao wana zile hati ambao si
hati miliki ambazo tunazitambua kutakuwa na utaratibu wa kubadilishiwa na kupewa zile hati ambazo watapewa muda wa miaka 99 kuanzia pale alipopewa awali. Kwa hiyo, wasiwe na hofu Wizara imejipanga vizuri na kila mmoja atapata haki yake kadri utaratibu wa ofisi ilivyopanga.(Makofi)
MHE. HALIMA ALI MOHAMMED: Ahsante, Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri swali moja.
Mheshimiwa Waziri kwa kuwa suala la Mtwara linafanana sana na suala la Halmashauri ya Kisarawe kata ya Kibongwa, wananchi wamechukuliwa ardhi yao, ikakatwa viwanja, lakini wao hawakupatiwa viwanja wala hawakupatiwa fidia yoyote ile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Mheshimiwa Waziri ni lini wanmanchi wa jimbo lako hili watapatiwa haki yao ya fidia?(Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli viwanja vilipimwa toka mwaka 2005 na ni kweli baadhi ya wananchi walichukuliwa eneo, lakini suala zima la mchakato wa fidia lilikuwa halijalipwa na ndio maana katika kulinda haki za wananchi tulisema hata vile viwanja vya mwanzo watu walitakiwa wapewe na wengine miongoni mwenu ni Wabunge humu ndani, tulivizuia kwamba watu wasipate vile viwanja mpaka wananchi wa pale wapate haki zao.
Kwa hiyo, jambo hili chini ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri linashughulikiwa vizuri na kila mtu atapata haki yake stahiki kwa sababu jambo hili viongozi tumelisimamaia kulinda haki za wananchi wetu.
MHE. LEONIDAS T. GAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake, lakini nataka nimjulishe kwamba Hospitali ya Rufaa hiyo ya Mkoa wa Ruvuma ina msongamano mkubwa sana wagonjwa na hasa akinamama wajawazito na watoto. Kwa mfano, hivi sasa Hospitali ya Mkoa ina vitanda 13 tu kwa ajili ya akinamama wajawazito na watoto. Akinamama hawa kwa wastani wa siku ni wagonjwa 25 mpaka 35 wakitumia vitanda 13.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile lipo tatizo la msingi kweli kweli; pale katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa akinamama wajawazito wananunua dawa, damu, mipira ya kujifungulia na vifaa vingine vyote vya kujifungulia, wananunua wenyewe. Sasa nauliza: Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba huduma zinazotolewa za akinamama wajawazito na watoto zinatolewa katika kiwango kinachotakiwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa vile hivi sasa tunategemea sana Kituo cha Afya cha Mji Mwema ambacho Mheshimiwa Naibu Waziri amesema bado hakijafika mahali kikapandishwa hadhi ya kuwa hospitali kamili. Je, Serikali ni lini italeta gari ya wagonjwa kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wanaofika katika Kituo cha Afya cha Mji Mwema hasa akinamama wajawazito na watoto?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nipokee malalamiko ya Mheshimiwa Mbunge kwamba pale akinamama wananunua dawa, vifaa tiba na mambo mengine; hili Mheshimiwa Mbunge kwa sababu ameshali-cite pale, ina maana jambo hilo lipo. Katika ziara zangu kwa maeneo mbalimbali nilikuwa nikitoa maelekezo kwamba Serikali inapeleka fedha katika Vituo vya Afya hasa katika Halmashauri zetu; lengo kubwa watu wapate dawa na vifaa tiba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimezungumza hapa mara kadhaa kwamba kwa kipindi cha sasa suala la uzembe kwamba Serikali inatoa fedha lakini watu hawazitumii kama inavyokusudiwa (kununua dawa na vifaa tiba), niliwaeleza DMOs wote na Waganga Wakuu wa Mikoa sehemu nilizopita kwamba wahakikishe fedha zinazokwenda lazima ziweze kutumika kama inavyokusudiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nichukue concern hii, lakini hata hivyo, nafahamu kwamba Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alitoa fedha kwa ajili ya kununua vitanda katika Halmashauri zetu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na hivi vitu vimeshakuwa tayari, naomba na yeye avipokee aende akakabidhi mwenyewe pale. Lengo kubwa ni kupunguza changamoto katika maeneo yako. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kwamba hakuna ambulance; mara kadhaa nimekuwa nikitoa ufafanuzi hapa ikiwezekana mchakato uanze katika Halmashauri zetu. Naomba niseme kwamba kilio hiki cha Mheshimiwa Mbunge tumekisikia, japokuwa suala la ambulance lazima lianzishwe katika Halmashauri kuonesha yale mahitaji, lakini tutaangalia nini kifanyike sasa kushirikiana pamoja Serikali Kuu na Halmashauri ya Songea ili tupate ambulance. Wapi itakapotoka, hiyo haijalishi, lakini cha msingi tupate ambulance kwa ajili ya wakazi wengi sana nikijua wazi kwamba hata watu kutoka eneo la Namtumbo wanakuja pale Songea kwa ajili ya kupata huduma ya afya.(Makofi)
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa uzito unaoikabili Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma ni uzito ule ule unaoikabili Hospitali ya Wilaya ya Mbinga hasa ikizingatiwa Wilaya ile inahudumia Halmashauri kubwa tatu, yaani Halmashauri ya Nyasa, Halmashauri ya Mbinga Mjini na Halmashauri ya Mbinga Vijijini, lakini vile vile sehemu ya Halmashauri ya Songea Vijijini: Mheshimiwa Waziri haoni sasa kuna haja ya kutimiza ile ahadi yake aliyoiahidi ya kuiboresha ile hospitali ili kuweza kupunguza mzigo mkubwa kwenda Hospitali ya Mkoa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa Mbunge anakumbuka kwamba tulikuwepo kule Mbinga na tumebaini hizo changamoto, ndiyo maana katika mipango yetu ya sasa, tumeamua kwamba Kituo cha Afya cha Kalembo ambacho ukiangalia mahitaji, sasa yamekuwa makubwa.
Kwanza tuboreshe Kituo cha Afya cha Kalembo ambacho siyo muda mrefu sana tutaenda kufanya ukarabati mkubwa sana wa theater na wodi ya watoto pale; lengo kubwa ni kwamba huduma ziweze kupatikana vizuri zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, ndiyo maana wenzetu kule wa Nyasa tume-cite Kituo cha Afya cha Mkiri ambacho tunaenda kufanyia huduma hiyo hiyo vilevile. Lengo letu kubwa ni katika maeneo hayo mawili, Nyasa na pale Mbinga, tukiweka huduma za kutosha zitasaidia wananchi wa eneo hilo waweze kupata huduma vizuri.
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Hospitali ya Wilaya ya Njombe, Kibena ni hospitali ambayo sasa inasomeka kama Hospitali ya Mkoa na inahudumia watu wengi sana. Pale kuna tatizo kubwa la watoto njiti na hakuna chumba cha kutunzia watoto hawa njiti. Je, Serikali iko tayari kutusaidia kupata chumba cha watoto njiti pale ili tuweze kuokoa maisha ya hawa watoto? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuchukue concern hiyo, kwa sababu Mheshimiwa Mbunge anafahamu tulikuwepo pale Hospitali ya Kibena. Tutajadili kwa pamoja ili tuone nini tufanye ili eneo lile ambalo ni Makao Makuu ya Mkoa pale sasa, japo katika hospitali ile angalau tuweze kupata centre maalum kwa ajili ya watoto njiti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakaa pamoja kujadili nini tufanye kwa ajili ya Hospitali ya Kibena pale iweze kutoa huduma kwa ajili ya wananchi wetu.
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Tatizo la Songea Mjini linafanana sana na tatizo lililopo katika Wilaya ya Mafia. Wilaya nzima ya Mafia haina hata Kituo kimoja cha Afya. Ukizingatia kwamba alipokuja Waziri Mkuu tulimwomba suala hili na mchakato tumeshauanza katika ngazi ya Wilaya. Je, ni lini sasa Serikali itatupatia Kituo cha Afya angalau kimoja pale Kilongwe kwa kuongeza hadhi ile zahanati iliyopo pale?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tulipofika Mafia tulienda katika hicho Kituo cha Afya na nikatoa mapendekezo kadhaa likiwemo suala zima la makazi ya watu katika maeneo yale, lakini tulikubaliana kwamba wafanye mchakato na Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Dau, kwa sababu Mafia jiografia yake lazima tuboreshe huduma ya afya na nilitoa maelekezo pale mbele ya DC na mbele ya Mkurugenzi nini kifanyike kituo kile kiweze kuboreshwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimwambie Mheshimiwa Dau kwamba Serikali imechukua ile, tutafanya kila liwezekanalo hasa eneo la Mafia katika kile Kituo cha Afya ambacho nimekitembelea mwenyewe, tutafanya uboreshaji mkubwa katika kipindi kinachokuja.
MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Halmashauri ya Manispaa ya Moshi imekuwa na maombi ya muda mrefu ya Hospitali ya Wilaya na tulikuwa tayari na majibu ya Serikali kwamba wakati wowote watajibu maombi yetu, lakini mpaka sasa hatuoni mwelekeo wowote. Nini tamko la Wizara ya TAMISEMI katika suala hilo la Hospitali ya Wilaya ya Manispaa ya Moshi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu kweli Halmashauri mbalimbali hazina Hospitali ya Wilaya na siyo Moshi peke yake. Ndiyo maana wakati fulani nilikuwa naongea na dada yangu Mheshimiwa Esther hapa, alileta special request na Mheshimiwa Mbunge najua tupo karibu sana. Tukaona kwamba basi angalau tuongeze suala zima la kimkakati la afya katika eneo hilo, japokuwa tuna hospitali yetu kubwa pale ambayo tunaitegemea, ipo chini ya Kanisa ya KCMC, lakini ni lazima tuboreshe huduma ya afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana tukaona katika kipindi cha sasa tuboreshe kwanza Kituo cha Afya cha Uru Mashariki ambapo siyo muda mrefu, ndani ya miezi miwili tutapeleka fedha za kutosha pale kufanya marekebisho makubwa sana. Tutajenga theater na wodi nyingine pale na vifaa mbalimbali vitawekwa pale. Lengo kubwa ni kupunguza changamoto za wananchi katika eneo lile.
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa wapo wazabuni ambao walitoa huduma hiyo ya kusambaza vyakula na vifaa mbalimbali katika shule zetu zikiwemo na shule za watoto wenye ulemavu, lakini wazabuni hao wengi wao wana miaka zaidi ya mitano hawajaweza kulipwa pesa yao na walio wengi wamekopa benki na wengine nyumba zao zimeuzwa na wengine ziko hatarini kuuzwa. Je, Serikali iko tayari kufanya uhakiki wa madeni hayo ili kuweza kuwalipa wazabuni hao? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa wapo wazabuni wapya ambao walitoa huduma ya kusambaza vyakula shuleni wao wamelipwa lakini wazabuni wa zamani hawajalipwa. Je, Serikali iko tayari kuwalipa wazabuni wa zamani ambao walitoa huduma ya kusambaza vyakula shuleni ambao hawajalipwa lakini wapya wamelipwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la kwanza la kufanya uhakiki wa madeni haya ili walipwe, ndiyo maana nimesema kwamba ni kweli, kuna madeni mbalimbali hasa wazabuni waliotoa vyakula katika shule zetu kabla programu ya elimu bila malipo kuanza. Jambo hili kweli limesababisha wazabuni wengi kupata mtikisiko lakini ndiyo maana ilibidi Serikali kuyapitia madeni haya yote tukijua wazi kwamba lazima kuna mengine siyo sahihi maana katikati hapo tulibaini baadhi ya madeni mengine ni hewa.
Kwa hiyo, Serikali imefanya mchakato wa ku-analyse madeni yote haya ili kutambua deni halisi la Serikali. Naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge na wazabuni wote waliotoa vyakula shuleni kwamba Serikali itafanya kila liwezekanalo kuwalipa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika hii concern kwa nini wazabuni wapya wanalipwa lakini wa zamani hawajalipwa ni kama nilivyosema kwamba utaratibu wa sasa tunapeleka fedha moja kwa moja kule shuleni. Kwa hiyo, kila mwezi mgao wa Serikali ukipeleka kule na fedha ya chakula inakuwepo. Ndiyo maana sasa hivi sitarajii sana kuona kwamba kuna wazabuni watadai kwa sababu fedha zote ambazo zinatakiwa zielekezwe katika ulipaji wa chakula tunazipeleka kila mwezi.
Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali tunalibeba na sisi kama Watanzania na Serikali tutahakikisha kwamba wazabuni wetu wa ndani lazima tuwalinde ili waendelee kufanya biashara yao kwa sababu ndiyo watajenga uchumi wao katika nchi yetu hii.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa wazabuni wanaohudumia chakula Mpwapwa High School, Mazai Girls’ School pamoja na Berege Secondary School form five na six sasa ni zaidi ya miaka miwili hawajalipwa na bado wanahudumia na wamekopa benki. Mheshimiwa Naibu Waziri amefika Mpwapwa sekondari na ameona hali ilivyo na wanataka kukamatiwa nyumba, je, hawa wazabuni watalipwa lini?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lubeleje, Senior MP wa Bunge hili kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli na kwa bahati mbaya kwa Halmashauri ya Mpwapwa siyo kesi ya wazabuni wa chakula peke yake isipokuwa kuna kesi ya wakandarasi mbalimbali ambao wamefanya kazi pale Mpwapwa lakini bado hawajalipwa. Hili napenda hasa nimuelekeze Mkurugenzi wetu wa Halmashauri ya Mpwapwa kwamba madeni mengine ambayo hayajalipwa ni suala la kuangalia Menejimenti ya Kurugenzi yake jinsi gani itafanya kuweza kuyalipa.
Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Lubeleje kwamba Mpwapwa ndiyo maeneo ya priority kwa sababu ofisini kwangu hata watu wa CRDB walifika kulalamikia Halmashauri ya Mpwapwa. Hata hivyo, ukiachia hizo fedha kutoenda lakini kuna mambo mengine ya ziada lazima tuyasimamie. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba tutafanya kila liwezekanalo hasa kwa wazabuni wa Mpwapwa na maeneo mengine ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tuweze kuwalipa fedha hizi ili wasije wakataifishiwa mali zao na mabenki ambazo ziliwekwa kama dhamana wakati wanachukua mikopo. (Makofi)
MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Kwa maelezo ya Mheshimiwa Naibu Waziri inaelekea Serikali haijajipanga kwa ajili ya ujenzi wa vituo hivyo. Kwa kuwa suala la ujenzi wa kituo cha mabasi cha Mbezi Luis ni la miaka mingi na kwa kuwa msongamano uliokuwepo pale Ubungo umekithiri na haileti sura nzuri kwa sababu sasa hivi nchi yetu inatakiwa iwe na kituo chenye hadhi ya Kimataifa. Swali la kwanza, je, ni lini Serikali iko tayari kuanza kujenga kituo cha mabasi katika maeneo ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri ameyataja kwa maana ya mabasi ya Kusini, Kaskazini na yanayotoka Kanda ya Kati na nchi jirani? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa katika maelezo ya Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba kituo cha mabasi ya Kusini kinatarajiwa kujengwa Kongowe na ukiangalia eneo la Kongowe halina nafasi ambayo watajenga kituo bila kutumia pesa nyingi za Serikali.
Je, atakubaliana na mimi kwamba majibu haya hayako sahihi kwa sababu vikao vimeshaanza kufanywa kati ya Wizara ya Maliasili na Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga? Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kuanza kufanya upembuzi yakinifu katika hilo eneo la Vikindu au Mwanambaya huko Mkuranga? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la dada yangu Mheshimiwa Zaynabu Matitu Vulu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano imejipanga sana na ndiyo maana nilisema pale awali mipango yoyote lazima ipangwe katika utaratibu sahihi. Wiki iliyopita nilijibu swali la Mheshimiwa Mnyika linalofanana na swali hili. Kinachotokea ni nini? Serikali kupitia Jiji la Dar es Salaam imeweza kupata eneo la Mbezi Luis. Bahati nzuri Kamati yenye kuhusika ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa iliamua kwenda kujihakikishia na imejiridhisha kuwa ni eneo muafaka. Bahati nzuri sasa LAPF wameshakubali uwekezaji wa kituo hicho cha kisasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pamoja na hayo kuna mambo ya msingi lazima yafanyike. Wiki iliyopita Jiji pamoja na LAPF na wadau wengine walikaa kikao kujadili ujenzi wa kituo hicho ambao utagharimu takribani shilingi bilioni 28. Walikuwa wanajadili katika hicho kituo cha Mbezi Luis daraja litapita juu au chini kwenda katika kile kituo cha mabasi cha kawaida cha daladala. Hiyo haitoshi, tarehe 19 Mei, Kamati hii itakutana tena kufanya mjadala mpana kuona ni jinsi gani kituo hiki kinaenda kujengwa. Kwa hiyo, ndiyo maana nimesema kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano imejipanga sana na tutahakikisha tunajenga vituo katika Jiji la Dar es Salaam ili kusaidia wananchi waweze kupata usafiri mzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kituo cha watu kutoka Kusini ni kweli, Jiji la Dar es Salaam sasa hivi linafanya tafakari kwa sababu yeye anaangalia mipaka yake. Walivyoangalia eneo lililokuwepo la Kongowe waliona kwamba ni lazima kulipa fidia. Kwa hiyo, kwa mkakati unavyokwenda, kwa mfano Kongowe mbele pale Vikindu kuna eneo kubwa, Serikali itaangalia jinsi gani stand ile itaweza kujengwa pale kwa watu wa Kanda ya Kusini na itahakikisha mipango hii yote inafanyika vizuri. Hata hivyo, agenda hii itaenda awamu kwa awamu lakini lazima tumalize kujenga vituo vyote.
Naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba tutaweza kujenga vituo imara kabisa kama tulivyojenga pale Msamvu, Mpanda na maeneo mengine. Lengo kubwa ni wananchi waweze kusafiri vizuri katika nchi yao.
MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa kuwa kituo cha Mbezi Luis kimeshapata mwekezaji LAPF, Serikali inatuambiaje kuhusu kituo cha Boko na cha Temeke, wamewatafuta akina nani watakaosaidia kujenga vituo hivi kwa haraka ili kuondoa msongamano Dar es Salaam? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bulembo, Mbunge Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishukuru sana
swali la Mheshimiwa Mbunge na ndiyo maana nimesema Mbunge Maalum kwa sababu ana hadhi maalum katika nchi hii kutokana na nafasi zake alizokuwa nazo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sasa hivi Serikali tumepata wadau wetu wa LAPF tumeanza na kituo kile lakini hata hivyo tunaenda kutafuta wadau wengine kwa ajili ya kujenga kituo kile katika eneo la Boko na kituo cha Kanda ya Kusini.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, niwaelekeze wenzetu wa Jiji la Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam na wadau wengine hasa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, ikiwezekana wakae na Halmashauri ya Mkuranga, kwa sababu eneo la kimkakati tayari lipo ambalo halina haja ya kulipa fidia kuona ni jinsi gani tuta-fast track hiki kituo ambacho tunaweza tukakijenga eneo la Mkuranga kwa watu wa Kusini ili wakapata unafuu zaidi.
Kwa hiyo, tunachukua mambo yote haya kwa kushirikisha wadau mbalimbali lengo ikiwa ni kujenga vituo ambavyo vitasaidia suala la usafiri katika nchi yetu.
MHE. HALIMA ALI MOHAMMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba nimuulize suala moja Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali inatilia mkazo suala la kukusanya mapato kwa njia ya kielektroniki. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri ana mpango gani wa kuhakikisha katika kituo cha Ubungo wanakusanya mapato kwa njia ya kielektroniki wakati abiria wakiingia na wakati magari yakitoka? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme tumetoa maelekezo kwamba siyo maeneo ya vituo vya mabasi pekee isipokuwa maeneo yote, utaratibu wa Serikali ni kwamba tunaenda kukusanya mapato yote kwa njia ya kielektroniki.
Naomba nisisitize sana na nimuelekeze Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam ambapo eneo lile lipo, kama kuna upungufu kwamba sehemu zingine wamekusanya kwa njia ya kielektroniki na nyingine hawajakusanya washughulikie changamoto hiyo. Naomba niagize na mimi najua kwamba hilo zoezi limeshaanza katika Jiji la Dar es Salaam, kwamba ili kuziba mianya yote ile ya upotevu wa fedha, mifumo yote ya ukusanyaji wa mapato ya Serikali katika vituo ya mabasi, hospitali na maeneo mengine ni kwa kutumia mifumo ya kielektroniki na si vinginevyo.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Majibu ya Mheshimiwa Waziri nadhani hayana uhalisia na mazingira ya Manispaa ya Mpanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi Machi, 2014 Halmashauri ya Mpanda ilitenga shilingi milioni 200 kwa ajili ya ununuzi wa gari la kukusanya taka, gari la kisasa na siyo haya malori mawili ambayo umeyasema.
Kutokana na ubadhirifu ambao umefanyika kwenye Manispaa hii, Serikali inachukua hatua gani kwa huyu mzabuni aliyetumia fedha hizi na mpaka sasa hajarudisha na baadhi ya hao watendaji ambao wamekula pesa hii, wananchi wa Manispaa ya Mpanda hivi tunavyoongea wanashinda na takataka ndani, wanashindwa kuzitoa na Manispaa imeshindwa kukusanya hizi taka kwa wakati. Serikali inamchukulia hatua gani huyu Ndugu Kisira pamoja na watendaji waliokula pesa hizi katika Manispaa ya Mpanda?(Makofi)
Swali la pili, imekuwa ni tabia ya Serikali kuendelea kuhamasisha wananchi kufanya usafi kwenye maeneo yao, lakini kitu kibaya zaidi ni kwamba wananchi hawa wanalazimishwa kufunga maduka, kila siku ya Jumamosi kuanzia saa 1:00 asubuhi mpaka saa 4:00 aasubuhi na siyo Mkoa wa Katavi peke yake au Manispaa ya Mpanda peke yake ni nchi nzima, ikiwepo na maduka ya Dar es Salaam, Kigoma, Mbeya, Mwanza pamoja na Katavi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa tabia hii ya kuendelea kufunga maduka, je, Serikali hamuoni kwamba mnapoteza uchumi wa wananchi wao kuendelea kufunga maduka na huku wakiendelea kufanya usafi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Rhoda tutende haki, swali lako ulilouliza halafu una ajenda, inawezekana swali lako ungeli-frame vizuri lingepata majibu mazuri sana. Kwa sababu swali lako lilikuwa linajenga suala la ubadhirifu wa fedha zilizotengwa, ungelitengeneza vizuri halafu tungeweza kupata majibu mazuri sana katika hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, nimesema kwamba pale kuna magari ya taka mawili, kama kuna suala la ubadhilifu hiyo ni ajenda nyingine, tunachotakiwa kukifanya ni kwamba hatuvumilii ubadhirifu wa aina yoyote, na kama ubadhirifu huo upo, tutaenda kuufanyia kazi tutaenda kufuatilia nini kilichojiri katika Manispaa ya Mpanda kama fedha zilizitengwa lakini hazikutumika vizuri katika suala hilo.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala zima la ajenda kwamba siku ya Jumamosi wananchi wanafunga maduka, kumbukumbu yangu Waziri Mkuu hapa aliulizwa na Mheshimiwa Ulega, Mbunge wa Mkuranga katika suala ya siku ya Jumamosi utaratibu wa kufanya, lengo kubwa ilikuwa usafi ufanyike lakini usizuie shughuli za wananchi katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, agizo hili limeishatolewa kwamba Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya katika maeneo yao tunapofanya utaratibu wa usafi tuangalie modality nzuri usafi ufanyike, lakini kama kuna mambo mengine ambayo saa nyingine yanahusu shughuli mahsusi zinaweza kufanyika. Hapa Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa maelekezo naomba tufanye rejea ile vizuri tusitoe majibu mawili itakuwa ni sub-standard siyo vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niichukue kwamba hoja yako ya usafi ni ajenda yetu ya Kitaifa, lazima kama Wabunge, lazima kama Viongozi tusimame pamoja katika jambo hili. (Makofi)
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa magari ya kunyonya maji machafu na kuzoa taka siyo lazima tu iwe kwenye Manispaa au Majiji, hata Wilaya zetu tunahitaji magari ya kunyonya maji machafu na magari ya kuzoa taka. Je, Serikali ina mpango gani kupeleka gari la kunyonya maji machafu pamoja na kuzoa taka katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI naomba kujibu swali la Mzee wangu Lubeleje, mimi namuita greda la zamani makali yale yale kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya Mzee Lubeleje naomba tuiweke katika vipaumbele vyetu vya Halmashauri, naomba nikusihi Mheshimiwa Lubeleje katika mpango wenu wa Halmashauri hilo jambo mkiliainisha, na sisi katika kupitisha bajeti tutalipa kipaumbele. Ninajua kwamba kweli ni jambo la msingi kufanya usafi na kuwa na mitambo hii ya kuzolea taka na kunyonyea maji, kwa hiyo mkiweka katika kipaumbele, mchakato wa bajeti ujao kama Mpwapwa mtaweka kipaumbele basi sisi hatutasita kuhakikisha jambo hilo tunaliwekea kipaumbele hilo ili Mpwapwa mpate gari la kunyonyea maji taka.
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Takataka zinaweza zikasababisha uchumi mkubwa sana kwa wananchi wetu kwa sababu taka zinaweza zikatengeneza matofali, zinaweza zikazalisha umeme, zinaweza zikatengeneza mbolea nzuri sana na sasa hivi kwa sababu maeneo ya kutupa taka yanaendelea kupungua mwaka hadi mwaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini Serikali isifanye uamuzi wa makusudi, kabisa ikaleta hii teknolojia nchini, ikaanza na majiji yetu ili kuwafanya wananchi wakapata kipato kwa kukusanya takataka na kuzipeleka kwenye maeneo hayo ambayo yanaweza yakazi-process na kuzalisha vitu vingine kwa faida ya Taifa kwa ujumla? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Selasini jambo lako ni zuri sana, ndiyo maana katika ofisi yetu tuna mradi mmoja unaitwa Strategic City Project, katika miji mbalimbali tumetenga utaratibu wa kutengeneza haya madampo ya kisasa, ambapo ukienda Mbeya utayakuta, hapa Dodoma tunajenga na maeneo mbalimbali tunatengeneza madampo kama yale. Lengo letu kubwa ni kwamba taka zitakazozolewa baadaye ziingizwe katika system maalum kuweza ku-convert katika shughuli zingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, sasa hivi tunakaribisha wawekezaji mbalimbali ambao katika njia moja au nyingine watasaidia ukusanyaji wa hizi taka kuweka katika malighafi nyingine, ikiwemo suala zima la utengenezaji wa mkaa.
Kwa hiyo, ni hilo ni jambo zuri Serikali na wadau mbalimbali tushirikiane kwa mustakabali wa nchi yetu ambao mwisho wa siku taka hizi baada ya kuwa uchafu inaweza ikawa malighafi na zitasaidia kujenga uchumi katika nchi yetu. (Makofi)
MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru Serikali kwa hatua hiyo. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; tangu mwaka 2016 mpaka sasa hakuna ongezeko lolote la mshahara kwa watumishi. Serikali inatoa tamko gani kwa watumishi hawa ambao wamekuwa na moyo mkubwa sana wa kujitolea?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; tangu mwaka 2016 mpaka sasa hakuna kupandishwa daraja kwa mtumishi yeyote hususan Mwalimu. Je, Serikali itakuwa tayari sasa kulipa malimbikizo ya mshahara kwa Mtumishi ambaye alistahili kupanda mwaka 2016 mpaka sasa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tukifanya rejea ya takriban siku mbili, Mheshimiwa Waziri anayehusika na mambo ya Utumishi (Waziri wa Utumishi na Menejimenti ya Utumishi wa Umma) alitoa maelekezo hapa kwamba katika hoja yetu ya Bajeti Kuu ilivyokuwa inapita watu walikuwa wanasema kwamba kwa nini sasa fungu hili la mshahara halipo?
Mheshimiwa Naibu Spika, tukumbuke kwamba Mheshimiwa Rais alizungumza wazi alipokuwa katika viwanja vya Mkoa wa Kilimanjaro katika siku ya Mei Mosi. Jambo hili limezingatiwa katika bajeti yetu hii tunayokwenda nayo hivi sasa. Ndiyo maana hata juzi Waziri wa Utumishi wa Umma alikuwa anatoa maelekezo kwamba kuna nyongeza ya fedha hapa ambayo itaenda ku-address jambo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la kupanda madaraja, hali kadhalika eneo hilo madaraja yalisimamishwa kutokana na zoezi maalum la uhakiki hasa wa vyeti feki na watumishi hewa. Vile vile naomba nifanye rejea ya Waziri wetu wa Utumishi wa Umma alipozungumza wazi kwamba suala la kupanda madaraja sasa limewekewa utaratibu mzuri, kila mtu atapanda kwa stahiki yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaambie kwamba kila mtu atapata stahili yake kwa kadri inavyotakiwa na hili Mheshimiwa Waziri amelizungumza wazi kwa sababu yeye ndiyo anahusika na Utumishi kwamba kila mtu atapata stahiki yake na jambo hili sasa hivi linakamilika na kila mtu atapanda daraja kama ilivyokusudiwa. (Makofi)
MHE. MUSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Moja ya matatizo ya Walimu wetu ni kukosa makazi katika maeneo wanayofundishia katika vijiji vyetu. Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba inajenga nyumba za kutosha kwa Walimu wetu ili kuwapa motisha kufundisha vizuri katika maeneo yetu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la kuimarisha miundombinu hasa kwa Walimu, ni kweli tumekuwa na changamoto ya nyumba, ndiyo maana hata baadhi ya Watumishi wengine wakishaajiriwa wanakumbana na changamoto kubwa sana ya makazi. Ndiyo maana toka mwaka 2016 katika Sekta ya Elimu tulitumia fedha nyingi takriban shilingi bilioni 64 kujenga miundombinu ya madarasa, vyoo na nyumba za Walimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, tulifanikiwa katika Shule ya Sekondari; mpango wa MMES II tumejenga nyumba takriban 283. Hata hivyo, naomba nishukuru sana Waheshimiwa Wabunge na wadau mbalimbali. Tumeshiriki kwa pamoja kujenga nyumba katika maeneo mbalimbali, lakini hata hivyo, katika mpango wa Serikali, mwaka huu tutaenda kushirikiana tena na wadau na fungu letu la Serikali kuhakikisha tunaongeza idadi ya nyumba. Lengo kubwa ni Walimu wetu na wataalam mbalimbali ambapo sio kada ya Walimu peke yake, waweze kupata makazi bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, najua hii bado ni changamoto kubwa, lakini naomba tushirikiane kwa pamoja, na Serikali imeweka nguvu za kutosha kuhakikisha kwamba tunajenga nyumba za Walimu na wa kada nyingine katika maeneo mbalimbali.
MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza na ninalo dogo sana. Naomba niseme kwamba Serikali isituambie hapa kama vile inaanza upya.
Mheshimiwa Naibu Spika, taratibu zote hizi za kupandisha vyeo na mengineyo yalikuwepo kabla; lakini sasa hivi kilichotokea kibaya, kuna watu walipandishwa cheo wakalipwa mshahara mpaka miezi mitatu, wakasitishiwa mshahara, wakarejeshwa pale pale. Hivi Mheshimiwa Waziri anatoa kauli gani kuhusu hili? Naomba nijibiwe kwa ufasaha zaidi ili watu waweze kufuatilia.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nashukuru sana maana ningekosa kupata hili swali, roho ya mama yangu Mheshimiwa Riziki ingepata shida sana kwa sababu nilikuwa namwona hapa, hasa nikijua mama yangu ni Mwalimu, kwa hiyo, alikuwa anataka kujua katika kero hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimwambie kwamba; bahati nzuri juzi nilipata viongozi wa Chama cha Walimu kutoka Mkoa wa Rukwa, nilikuwa nao pale ofisini na hiyo ni miongoni mwa concern ambayo waliileta pale ofisini kwetu. Ni kweli kuna watu ambao walipata mishahara ile miezi miwili, lakini baadaye mshahara ukakasitishwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa changamoto kubwa ni kwamba kuna wengine wanaenda kustaafu. Sasa wakistaafu jambo hili linafanyika vipi? Leo hii mtu akistaafu atahesabiwa katika mshahara wa mwanzo wakati alipanda. Ndiyo maana nimesema jambo hili, kama Serikali, tumelichukua kwa uzito wa hali ya juu, tunafanya analysis. Kuna watu wengine ambao watastaafu hivi karibuni. Ina maana tusipo-address vizuri tutakuwa na changamoto kubwa katika hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna watu wengine walipanda, lakini kwa sababu ya utaratibu mzuri uliowekwa naomba niwaondoe hofu Waheshimiwa Wabunge, jambo hili tumelichukua sisi kama viongozi na tumelijua ni tatizo kubwa, lazima tuliweke vizuri. Yalifanyika kwa nia njema kwa sababu huko nyuma hali yetu ilikuwa siyo shwari. Suala zima la watumishi hewa lilikuwa ni jambo kubwa, watumishi takriban 19,000 plus, lilikuwa ni tatizo kubwa sana!
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mpango huu ulikuwa ni mpango mkakati wa Serikali kusaidia kulinda mapato, lakini kupeleka fedha kwa watu wanaostahili . Kwa hiyo, naomba niwatoe hofu wafanyakazi kwamba kila mtu atapata stahili yake na Serikali inafanya kazi kufanya analysis kwa undani zaidi kuondoa hilo tatizo.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa niulize swali la nyongeza. Katika jibu la msingi la Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba Teaching Allowance ipo kwenye mshahara. Sasa tunapata tabu sana tukikutana na Walimu wanapotuambia juu ya kurudisha Teaching Allowance. Je, Serikali itakuwa tayari sasa kutamka ndani ya Bunge hili ili waweze kutambua kwamba Teaching Allowance yao iko kwenye mshahara?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo kubwa tulilokuwa nalo ambalo Waheshimiwa Wabunge wengi sana hapa leo wanalizungumza ni suala zima la maslahi mapana ya watumishi. Ndiyo maana hata hicho kilichokuwepo kama kidogo au kikubwa hakioneshi vizuri ni kwa sababu huenda lile fungu lenyewe, purchasing power imekuwa ni ndogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kupitia Ofisi ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma, juzi juzi kulikuwa na kikao maalum kinafanyika kwa sababu kunaundwa bodi maalum ya kuja kupitia maeneo yote hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukiacha Teaching Allowance, kuna mambo mengine; kuna suala la haki za watu wanaofanya kazi katika mazingira magumu. Kwa hiyo, jambo hili tutakuja kulitamka rasmi sasa baadaye kuhusu mchakato huu unavyokwenda. Hiyo Bodi iliyoundwa sasa kupitia mishahara, siyo kwa Walimu peke yake, isipokuwa watumishi wote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tutaona jinsi gani kila mtumishi atapata stahili yake na nyongeza kwa kiasi gani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hili tutakuja kulitoleaa tamko rasmi hapa baadaye Bungeni likiwa katika utaratibu mzuri baada ya kutoa hii documentation vizuri.
MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kuna shule Shikizi nyingi ambazo zina Walimu wa kujitolea na hawapati posho. Je, ni lini Serikali itaanza kuwalipa posho hawa Walimu wanaofundisha kwenye Shule Shikizi? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, katika jambo hili nadhani kila Halmashauri ina mkakati wake ku-address matatizo ya watumishi katika maeneo mbalimbali; na kuna baadhi ya maeneo mengine utakuta watu wanatumia own source kuonesha jinsi gani wana-address hili jambo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu kuna mambo specific katika eneo la Mheshimiwa Njeza, tutalichukua halafu tuangalie jinsi gani tutafanya kuona nini kimetokea huko ilimradi tuliweke sawa ili kila mtu apate stahiki yake. Kama kuna maeneo mahususi katika Halmashauri husika, basi tutayatoa kwa lengo la kuweka mustakabali mzuri katika maeneo yetu hayo.
MHE. LOLESIA J. M. BUKWIMBA: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu kwa kunipa nafasi niuliza maswali mawili ya nyongeza. Kutokana na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ni kweli kwamba changamoto bado ni kubwa sana katika Mradi huu wa Chankolongo. Pia kutokana na majibu yake na yeye mwenyewe amewahi kufika kwenye huo mradi, mradi huu ni wa muda mrefu sana kiasi kwamba wananchi mpaka sasa hawaelewi kinachoendelea juu ya mradi huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ningependa pia Mheshimiwa Waziri awahakikishie wananchi kwamba, je, ni kweli mwezi Desemba mwaka 2017 mradi huu utakamilika kutokana na changamoto zilizopo?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa mradi huu unakusudia kuvuta maji kutoka Ziwa Victoria na ndani ya Jimbo la Busanda wananchi wana tatizo kubwa sana la maji na maji mengi yanayotumika kwa ajili ya uchenjuaji wa dhahabu ni machafu na wananchi wanapenda kupata maji safai na salama; je, mradi huu utawezesha kufikisha maji na katika Jimbo zima la Busanda?Napenda kupata majibu hayo. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli mimi na yeye Mbunge tulikwenda jimboni kwake ili kuukagua mradi huu na ni kweli mradi huu tumeukuta una changamoto nyingi sana na ndiyo maana kwa hatua tulizozifanya pale na kutoa maelekezo nilipofika site mpaka Engineer pale pamoja na Afisa Manunuzi amesimamishwa majukumu kutokana na mradi huu, kwa hiyo hatukulala kwenye mradi huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, miezi michache iliyopita tulitoa maagizo kwamba choteo liweze kukamilika na mabomba yaweze kupatika. Kwa taarifa nilizozipata juzi ni kwamba lile choteo limekamilika maji yanatoka katika ziwa mpaka yanafika pale katika intake yenyewe, lakini usambaji wa mabomba umekuwa ukisua sua. Ndiyo maana Halmashauri ilivyosukuma, huyu sasa ameingia na hii kampuni nyingine ya Katoma Motor Factors Limited ambayo imefanya commitment ya kuleta mabomba yote bila hata ya kulipwa hata senti tano. Kwa hiyo mabomba yatafikishwa site ndani ya mwezi huu wa saba.
Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa nilizozipata ni kwamba tayari mabomba haya yapo ndani ya meli na kwamba muda wowote yatafika hapa site. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge naomba nikuhakikishie kwamba kwa jinsi nilivyoongea na watendaji katika Halmashauri ya Geita ni kwamba tutasukuma ndani ya mwezi wa 12 mradi huu uweze kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu agenda ya pili, kwamba mradi huu ikiwezekana ufike kwenye maeneo mengine; wazo ni jema lakini naona kwanza jambo la msingi ni kuhakikisha kwamba mradi huu unaweza kukamilika katika vile vijiji vya awali. Jambo hili likishakamilika hapa tutaweka mipango mingine ya namna ya kufanya; kwa sababu chanzo hiki ni kikubwa sana ili kiweze kusaidia wananchi wa Busanda waweze kupata maji kama Mbunge wao anavyohangaika siku zote.
MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa Halmashauri ya Geita DC haina Engineer wa maji na Mheshimiwa Naibu Waziri alishuhudia hilo kwamba Engineer tuliyekuwa naye hakuwa na cheti cha kuwa Engineer wa maji kwenye Halmshauri yetu, na tulimsimamisha mpaka sasa hatuna Engineer, je, Serikali ina mpango gani wa kuleta Engineer wa maji kwenye Halmashauri ya Geita DC?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWAlA ZA MKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kutokana na matatizo yaliyojitokeza pale Geita ilionekana kwamba Injinia yule kipindi kile ilikuwa hatoshi kusimamia miradi ya maji katika Halmashauri ya Geita.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo naomba nimhakikishie kwamba tunafanya harakati. Tumekuwa na changamoto ya mainjinia katika maeneo mbalimbali lakini eneo la Geita tumelipa kipaumbele kwa sababu kuna miradi hii mikubwa ya maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa Serikali katika eneo lile na ukanda ule ni kutumia Ziwa Victoria, kwa hiyo eneo lake tutalipa kipaumbele. Kwa hiyo Mheshimiwa Musukuma naomba avute subira tu kidogo hili jambo tuliweke vizuri, tutapata injinia mzuri ambaye atatusaidia katika miradi ya maji katika eneo lake.
MHE. SALMA M. MWASA: Ahsante Mheshimiwa Naibu Spika, naomba urekebisa kidogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza swali langu lilikuwa ni Hospitali za Wilaya za Ubungo na Kigamboni, lakini hapa naona limekuja la Kigamboni peke yake. Sasa maswali yangu ya nyongeza ni mawili. La kwanza, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya kwenye Wilaya mpya ya Ubungo?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, ni lini Serikali tena itapandisha hadhi kituo cha afya cha Mbezi? Kama huu mchakato wa kujenga Hospitali ya Wilaya utachukua muda basi ipandishe Hospitali ya Mbezi iwe Hospitali ya Wilaya.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli na tunafahamu hizi Kigamboni pamoja na Ubungo ni Wilaya mpya, zimezaliwa kutoka katika Wilaya mama ya Temeke na Wilaya Kinondoni, tukifahamu kwamba Wilaya ya Ubungo ina changamoto hiyo. Kwa hiyo, jambo la msingi ni kwamba, kwa sababu tumegawanyika si muda mrefu sasa niombe Baraza la Madiwani la Ubungo pamoja na timu yote ya Management wafanye utaratibu wa kuandaa hii mipango ya ujenzi wa hospitali mpya ya Ubungo na sisi Serikali katika nafasi yetu tutafanya kila liwezekanalo ili kuhakikisha kwamba eneo la Ubungo linakuwa na hospitali yake kwa sababu tunajua kwamba population ya watu wa Ubungo ni kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo kupandisha hadhi kituo cha Mbezi kwa hivi sasa kiweze kutumika, kikubwa zaidi nimuagize Mkurugenzi pamoja na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kwamba kama wakiona kinatosha waanze kuhakikisha tunaanza harakati za kwanza kukiwezesha kituo hiki kama tulivyofanya kituo cha Vijibweni pale Kigamboni. Tukifanya hivi tutaweza kusaidia kwa kiwango kikubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwasihi hasa Mkurugenzi na DMO wetu, waweze kufanya harakati za haraka na kufanya analysis ya kutosha nini kinaweza kufanyika pale ili kuweza kuongeza tija katika Sekta ya Afya katika wilaya ambayo Mheshimiwa Mbunge anaipigania sana.
MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Baada ya kupandishwa hadhi Zahanati ya Likombe katika Manispaa ya Mtwara Mikindani kuwa Hospitali ya Wilaya kumekuwa na changamoto kubwa sana ya mrundikano wa wagonjwa hasa katika wodi ya wazazi. Je, ni lini Serikali itapanua wodi ile ili akinamama wale waweze kusitirika wakati wanatimiza haki yao ya msingi kama wanawake?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, population ya Mtwara Mikindani sasa hivi imekuwa kubwa kutokana na kuingiliana na mambo ya gesi. Hata hivyo, hivi sasa tunaenda katika harakati za kufanya ukarabati wa vituo vipatavyo 142. Zoezi hili haliishi hapa; Serikali inajielekeza tena kupanua vituo vingine vipya ambako kuna population kubwa. Kituo hiki ambacho Mheshimiwa Mbunge amekizungumzia hapa tutakichukua kama sehemu ya kipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Serikali ya Awamu ya Tano ni kufanya commitment katika kuwahudumia wananchi. Kwa hiyo, hii tutaweka ni sehemu ya kipaumbele kuwahudumia wananchi wa Mikindani ili waweze kupata afya bora katika maeneo yao.
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Changamoto ya huduma ya afya iliyopo Kigamboni na Ubungo inafanana na ile iliyopo Jimbo la Nanyamba ambako hakuna kituo cha afya hata kimoja, hakuna hospitali ya wilaya, hakuna ambulance na hakuna DMO (Mganga Mkuu wa Wilaya). Sasa nataka kujua Serikali ina mpango gani wa muda mfupi wa kutatua changamoto hizi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba Mheshimiwa Chikota tulikuwa wote site na tulifika eneo ambalo wao wameweka kipaumbele kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunakarabati eneo lile ili kupata kituo cha afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na ziara ile nimhakikishie Mheshimiwa Chikota kwamba Serikali imefanya commitment ya kutosha na pale muda si mrefu kuanzia sasa tutawekeza fedha nyingi takribani milioni mia saba katika kile kituo chake ambacho alikiwekea kipaumbele siku tulipofika pale. Kwa hiyo, naomba niwaambie wananchi wa Nanyamba kwamba Mbunge wao amepigana na Serikali imesikia na muda si mrefu tutakwenda kufanya uwekezaji mkubwa sana wa sekta ya afya katika eneo hilo.
MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru nami niulize swali fupi. Hospitali yetu ya Makambako ilipandishwa hadhi tangu 2013 na kuwa hospitali kutoka kituo cha afya, lakini mgao wa dawa mpaka sasa tunapata kama kituo cha afya. Je, Serikali itakuwa tayari sasa kupeleka mgao kama ambavyo ilipandisha kuwa hospitali kwa sababu wataalam, Madaktari wapo na chumba cha kufanyia upasuaji kinaanza mwezi huu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, nilipofika pale jimboni kwake nikiwa naye ni miongoni mwa watu ambao wame-invest pesa zao binafsi kuwasaidia wananchi wao. Mheshimiwa Mbunge hongera sana katika hilo. Changamoto ya mgao wa dawa, kwamba bado unapata kwa mfumo wa kituo cha afya; wakati huo huo ikiwa kwamba Makambako ni center kubwa sana ya watu kutoka katika hizi barabara mbili; ya kutoka Ruvuma na kutoka Mbeya; tunajua ni changamoto kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kwamba eneo lile kwa bajeti ya mwaka huu tutaliangalia vizuri. Tutafanya kila liwezekanalo kumwongezea bajeti kwa sababu tunataka ile center ya upasuaji ifanye kazi vizuri. Hata hivyo, Serikali tutaangalia tufanyeje ili wananchi wa Makambako waweze kupata huduma vizuri. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba niseme kwamba Serikali imelisikia na itakwenda kulifanyia kazi jambo hili.
MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwa kuwa Hospitali ya Wilaya ya Bukoba Vijijini, ni hospitali ya mission na leo hii walivyotoa ambulance imekwenda kwenye Zahanati ya Kishanje. Ni lini Serikali itapandisha hadhi Hospitali ya Mission ambayo tayari wameshakubali kuitoa Serikali, kuwa hospitali ya wilaya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MITAA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tumesikia lile suala la ambulance alilizungumza nadhani hii ni mara ya pili, kwamba maelekezo ilitakiwa iende katika kituo kingine na nimesema kwamba nitafika kule site kufanya verification, maagizo yalikuwaje na hii ambulance imeenda wapi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, kuhusu mchakato wa kuipandisha hii hospitali tutapitia mikataba, tutawasiliana na wenzetu wa Wizara ya Afya kuangalia nini kilichopo na jambo lipi ambalo ni rafiki zaidi tunaloweza kulifanya kwa mustakabali wa wananchi wa Bukoba. Kwa hiyo, tunachukua haya mawazo lakini lazima tufike field pale tuangalie uhalisia wa jambo lilivyo ili tupate majibu muafaka kusaidia wananchi wa Bukoba.
MHE. OMARY A. BADWEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa ni muda mrefu sasa Wenyeviti wa Vitongoji, Vijiji na Mitaa wamekuwa wanadai fadha zao na hawajui ni lini watalipwa malimbikizo haya. Je, sasa Serikali iko tayari kuziagiza halmashauri kupitia Wakurugenzi kuandaa idadi ya fedha ambazo kila halmashauri inadaiwa na viongozi hawa ili Serikali baadaye itoe maelekezo ya namna ya kuwalipa viongozi hawa?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa sina hakika kama katika maelekezo haya ya kuwalipa Wenyeviti wa Vitongoji, Vijiji na Mitaa kama pako mahali panaeleza wanalipwa kiasi gani. Je, Serikali sasa iko tayari kutamka hapa kwamba hizo asilimia 20 ambazo zinapelekwa hao Wenyeviti wa Vitongoji, Vijiji na Mitaa watalipwa kiasi gani kila mmoja kwa mwezi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna halmashauri zingine zinafanya vizuri lakini kuna zingine ni changamoto kubwa. Ukipita huko kwenye halmashauri nyingine utaona kwamba zile asilimia 20 marejesho hayajarudi vijijini. Hata hivyo, tumetoa maelekezo mbalimbali, lakini naomba tutoe maelekezo tena na tutatoa maelekezo kwa waraka maalum kwamba jinsi gani sasa halmashauri hasa Wakurugenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunapokaa katika Kamati ya Fedha katika ajenda ya mapato na matumizi sisi tukiwa wajumbe lazima tuangalie ile compliance ya kurudisha zile fedha katika halmashauri zetu. Bahati mbaya sana katika sehemu nyingine utakuta Ma- DT wanakuwa kama Miungu watu, hawafanyi maelekezo ya Kamati zao za Fedha wanapofanya maamuzi. Kwa hiyo, jambo hili tutatoa maelekezo mengine ya ziada ili asilimia 20 ya fedha hizi ziwewe kurudi vijijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo katika suala zima la kupeleka hizi asilimia 20 mara nyingi zina-differ kutoka halmashauri kwa halmashauri, ndiyo maana tumesema kwamba tunafanya marekebisho ya Sheria ya Fedha ambayo humpa Waziri mwenye dhamana katika kifungu maalum, nadhani katika ibara namba 45, dhamana ya kutoa maelekezo maalum ya namna ya kufanya. Jambo hili lisiwe ni jambo la hiari isipokuwa liwe ni kwa mujibu wa sheria. Lengo kubwa ni kuwasaidia Wenyeviti wetu wa Serikali za Mitaa na Vijiji. (Makofi)
MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Nadhani wote tunatambua umuhimu wa Wenyeviti wa Mitaa na kazi wanazozifanya, lakini kumekuwa na kilio cha muda mrefu sana kuhusiana na maslahi yao kwa kazi kubwa wanayoifanya. Je, Serikali sasa iko tayari kutenga bajeti kwa ajili ya kuwalipa mishahara Wenyeviti wa Mitaa pamoja na Madiwani?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili nililijibu takribani wiki mbili zilizopita na nikasema kwamba kwa jambo la kulipa mishahara utaratibu wa sasa ni kulipa posho. Pale Bunge litakapoamua vinginevyo, tutaangalia jinsi ya kufanya. Kikubwa zaidi ni kwamba tutaendelea na utaratibu huu, lakini tujue kwamba endapo jambo hili litaingia katika mshahara maana yake ni kuwa wage bill lazima itabadilika katika utaratibu wa kiserikali, ambayo vile vile ina changamoto yake. Kwa hiyo lazima tufanye analysis ya kutosha juu ya namna ya kufanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa utaratibu
wa sasa hivi tutaendelea kwa mujibu wa sheria inavyozungumza. Bunge litakapoamua hapo baadaye tutaenda na maamuzi hayo ambayo Bunge litakuwa limeamua hapo baadaye.
MHE. ZITTO Z. R. KABWE: Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma-Ujiji tuliamua kutumia sehemu ya ushuru ambao manispaa inakusanya kwa ajili ya kuongeza fedha za kuwalipa watu hawa, Wenyeviti wa Mitaa pamoja na kuwalipia Bima ya Afya. Hata hivyo, kutokana na hatua ambayo Serikali Kuu imechukua, mmechukua kodi ya majengo, ushuru wa mabango, haya maelekezo mnayoyatoa kwamba halmashauri ziwalipe hawa watu hizi 20 percent zitatoka wapi wakati ushuru wote, mapato yote Serikali Kuu inayachukua? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nasema hiyo ni the best practice ambayo mmeifanya na tunataka innovative idea kama hizo wakati mwingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, suala la kuchukua fedha Serikali kupitia Wizara ya Fedha, Waziri wa Fedha alizungumza wazi, kwamba kinachofanywa na Serikali Kuu ni kukusanya baadaye inarudisha katika halmashauri husika; hii ilikuwa ni wazi kabisa, utaratibu wote ambao Mheshimiwa Waziri wa Fedha alizungumza, kutokana na hamasa nzuri, ndiyo maana leo hii tunaona jinsi ambavyo watu wanapanga foleni TRA kwenda kulipa kodi ya majengo. Kwa hiyo kikubwa zaidi naomba tukubaliane na Serikali, lengo la Serikali ni kusukuma mambo yaende vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunachokihitaji ni kwamba tufike Taifa ambalo linaweza kuamua kufanya mambo vizuri zaidi. Kwa hiyo, tutachukua zile best practice ambazo sehemu mbalimbali zipo. Hata hivyo niseme kwamba Serikali haikuwa na nia ya kunyang’anya authority ya halmashauri katika kuchukua mapato, isipokuwa ni utaratibu tu unawekwa halafu baadaye tutaona nini faida ya jambo hili ambalo ni jipya, lakini ambalo kwetu lina msingi mkubwa sana.
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nina maswali mawili ya nyongeza.
La kwanza tarehe 24 Mei, 2017 wakati Naibu Waziri akijibu swali langu lililokuwa linahusu kupeleka dawa kwenye vituo vya afya niliuliza swali la nyongeza lililokuwa linahusu hospitali hii ya Wilaya. Bahati nzuri Naibu Waziri amefika kwenye hospitali ile akaona, alisema kwamba wametenga shilingi milioni 700 kwenda kumalizia OPD ambayo hiyo ingekuja kabla ya mwaka wa fedha 2016/2017 haujaisha. Mwaka wa fedha 2016/2017 umeisha. Alitamka kwenye Bunge hili, wananchi wa Serengeti walisikia zinaenda shilingi milioni 700 kumalizia OPD. Je, alilidanganya Bunge na wananchi wangu wa Serengeti? Kama siyo kwamba alidanganya, nini kilitokea?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, mantiki ya kupeleka fedha Serengeti ilikuwa siyo kulidanganya Bunge na zoezi hili tutalifanya maeneo mbalimbali. Kama Serikali, tuna mpango na tumezungumza kwamba katika programu ya Serikali kwamba tutafanya katika sekta ya afya hasa vituo vya afya vile ambavyo vimeonekana ni changamoto kubwa katika maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha sasa, takribani vituo 142 tutavifanyia ujenzi huo ambayo ni equivalent pesa yake karibuni shilingi milioni 700 katika kila center kwa ajili ya kutengeneza miundombinu na kupeleka vifaa tiba.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kudanganya Bunge, jambo hilo halipo isipokuwa ni commitment ya Serikali. Kwa hiyo, jambo la msingi ni kwamba watu wa Serengeti wavute subira kwa sababu Serikali ina mipango yake na inatekeleza.
Katika ujenzi huu sehemu nyingine tunafanya bulk procurement kuufanya ujenzi huu tupate mkandarasi wa pamoja kuhakikisha ujenzi huu unaenda sambamba katika maeneo yote na lengo letu kwamba tupate value for money na ubora wa majengo ule unaokusudiwa tuweze kuupata vizuri. Kwa hiyo, ni commitment ya Serikali kuhakikisha kwamba inapeleka huduma za afya kwa wananchi wake wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo lililopo Serengeti linafanana na tatizo lililopo Manispaa ya Moshi na ukizingatia kwamba Manispaa ya Moshi ndiyo Makao Makuu ya Mkoa wa Kilimanjaro na ndiyo eneo ambalo watalii wote wanaoenda mlima Kilimanjaro hupitia pale. Tumekuwa na ombi la muda mrefu la kuomba Hospitali ya Wilaya Serikalini kwa zaidi ya miaka sita au saba hapa. Swali langu, je, Serikali itatusaidia lini kutekeleza ombi letu maalum la kujenga Hospitali ya Wilaya katika Manispaa ya Moshi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli inawezekana kulikuwa na maombi maalum katika vipindi mbalimbali, lakini tufahamu kwamba haya maombi maalum mara nyingi sana siyo kama ile bajeti ya msingi. Kwa hiyo, inategemea kwamba ni jinsi gani Serikali kipindi hicho imepata fedha za kutosha ku-accommodate maombi maalum.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, najua kwamba Moshi kweli hakuna Hospitali ya Wilaya, lakini ukiangalia vipaumbele vya Taifa hili hata ukiangalia katika maeneo mengine kwa mfano kama Serengeti alipokuwa anazungumza ndugu yangu Mheshimiwa Marwa pale, wako tofauti sana na Moshi. Angalau Moshi mna alternative pale, watu wanaweza wakaenda KCMC au sehemu nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutaangalia jinsi tutakavyofanya. Ninyi kama Halmashauri ya Wilaya anzeni kufanya hiyo resource mobilization katika ground level na sisi tutaangalia jinsi gani tulifanye jambo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, ndiyo maana katika kusaidia katika suala zima la Moshi kwa ujumla wake (Moshi Mjini na Vijijini) sasa hivi tunaenda kukiboresha kituo cha Uru Mashariki pale. Lengo kubwa ni kwamba kiweze kusaidiana na hospitali zile ambazo ziko pale kwa lengo kubwa lile lile la kuwasaidia wananchi wa Moshi waweze kupata huduma nzuri ya afya.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri alifika Jimboni kwangu na amekiona Kituo cha Dongobesh na tukaleta ombi la kujengewa theater, je, Mheshimiwa lini sasa theater ile inajengwa ili wananchi wangu wapate matibabu hayo ya upasuaji? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tuliweza kufika Dongobesh na kuweza kufanya tathmini ya changamoto kubwa inayokabili huduma ya afya katika eneo lile.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mpango wa Serikali ndiyo nimezungumza katika vituo 142 kwamba na Dongobesh ni miongoni mwa kituo ambacho tunaenda kukijengea theater; lakini siyo theater peke yake; tutajenga pale theater tutaweka na vifaa lakini halikadhalika tutaweka uboreshaji wa miundombinu kwa bajeti iliyotengwa pale Dongobesh. Kwa hiyo, naomba niwatoe hofu wananchi wa Dongobesh kwamba jambo hili kwa sababu manunuzi yake tumepeleka kwa ujumla, tufanye subira, ni commitment ya Serikali kwamba siyo muda mrefu sana kazi hii itaanza mara moja.
MHE.VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwanza nimpe pongezi kubwa kwa kazi kubwa ambayo ametufanyia pale Kilolo kwa ujenzi wa hospitali, ni kilio cha muda mrefu. Pamoja na hayo, bado shida ipo, tuna tatizo kubwa sana la wagonjwa ambao inabidi waende kutibiwa kwenye Kituo cha Kidabaga lakini kituo kile kiko mbali na kata kama Idete, Masisiwe, Boma la Ng’ombe na Kata nyingine. Tatizo ni kwamba hakipo sawasawa kwa sababu hakuna daktari, hakuna chumba cha upasuaji, hakuna wodi ya akina mama wala hakuna ambulance. Sasa kwa wakati huu tunaposubiria ile hospitali, unasemaje?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika Halmashauri ya Kilolo, kwanza walikuwa hawana Hospitali ya Wilaya, lakini namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge, tulipofika pale tulifanya initiatives za kutosha na walipata karibu shilingi bilioni 2.2. Wao ni miongoni mwa watu wanaojenga hospitali ya kisasa sasa hivi, nawapongeza sana kwa kazi kubwa inayoendelea kufanyika pale. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo najua kwamba kutoka pale kwenda Kidabaga ni mbali sana na ndiyo maana Serikali katika kipindi cha sasa tutaenda kufanya ule ujenzi. Nilishamweleza Mheshimiwa Mbunge kwamba wananchi wa Kidabaga wawe na amani, kituo chao ni miongoni mwa vituo tunaenda kufanyia uboreshaji mkubwa kwa sababu kijiografia eneo lile lina changamoto kubwa sana. Time frame yetu tuliyoweka ni kwamba kabla ya mwezi wa Disemba kituo kile kitakuwa kimekamilika na facilities zake zote. (Makofi)
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa Lamadi ni mji ambao kijiografia unapanuka kwa kasi sana; na kwa kuwa Lamadi hiyo hiyo imeshakidhi vigezo ambavyo Mheshimiwa Waziri amevizungumza hapa, Wizara ya Ardhi imeshapima viwanja pale, miundombinu ya maji ipo, barabara zipo na Mheshimiwa Rais alipokuja alivutiwa sana na mji ule na akasema kwamba angependa uwe mji wa kibiashara, ufanye biashara kwa saa 24 kwa siku.
Je, Serikali haioni kwamba kama kuna kitu kinaitwa
hati ya dharura basi itumike kuufanya Mji wa Lamadi Mji mdogo ili kusudi iweze kuchochea maendeleo kwa wananchi badala ya kuendelea kuuacha hivi hivi ambapo baadaye unaweza ukaleta matatizo makubwa zaidi?
Swali la pili, kwa kuwa ukiangalia katika barabara inayotoka Mwanza kwenda Musoma, mji pekee ambao unakua zaidi ni Lamadi, Serikali haioni kwamba kuendela kuuachia kutangaza Halmashauri ya Mji Mdogo wa Lamadi itazidi kuleta matatizo makubwa zaidi kwa wananchi na kusababisha mpangilio ambao baadaye itakuwa ni tatizo kwa wananchi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Dkt. Chegeni mjukuu wa Mzee Mchengerwa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, alivyosema kupeleka hati
ya dharura kwamba Mji wa Lamadi utangazwe kwa hati ya dharura, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Chegeni tulifika pale kwako Lamadi na mimi najua expansion ya mji ule unavyokua kwa kasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kikubwa zaidi ni kwamba kilio hiki tumekisikia na bahati nzuri Mheshimiwa Rais ameshaweka commitment pale alipokuwa site na bahati mbaya tulivyoangalia kuna baadhi ya changamoto ndogo ndogo ambazo zipo kuufanya mji ule tuutangaze rasmi. Naomba niseme kwamba jambo hili tunalichukua kwa pamoja, baadaye tujadiliane miongoni mwa zile changamoto zilizokuwepo tuziweke sawa ili mradi tuweze kufikia katika mpango ambao unastahiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika jambo lingine kuhusu kuutangaza rasmi, Mheshimiwa Chegeni naomba tutakapokaa baadaye vizuri na bahati nzuri na Mheshimiwa Waziri wangu wa Nchi hapa yupo na amekusikia naye jambo hilo analiangalia kwa karibu zaidi tutafanya utaratibu wa kuona jinsi gani tufanye ili commitment ya Mheshimiwa Rais ameiweka pale basi mwisho wa siku waone kwamba kulikuwa na Dkt. Chegeni amepigania Mji wa Lamadi umeweza kupatikana na kuufanya mji wa kibiashara uweze kuendana na hadhi kwa kadri tutakavyoweza kuutangaza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kilio chako tumekisikia, tutaakaa pamoja, tutajadiliana pamoja nini tufanye sasa cha haraka kwa mustakabali wa Mji wa Lamadi ambao unakua kwa kasi. (Makofi)
MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona. Naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba Mji wa Namanyere ambao unakua pia kwa kasi na unapangwa vizuri, tumeshaomba uweze kupandishwa hadhi na kupata Mamlaka ya Mji wa Namanyere kwa maana ya Halmashauri ya Mji. Kamati ya Kitaifa ilishakuja ikaangalia na ikaona kwamba tuna vigezo vingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua na wananchi wa Namanyere wajue, ni lini Serikali itapandisha hadhi Mji wa Namanyere ili tuweze kunufaika na miundombinu inayopaswa watu wa mjini, wanufaike?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli mwaka 2016 nilikuwa na Wabunge, Mheshimiwa Mipata na Mheshimiwa Keissy pale tulipokuwa tunatembelea katika eneo lile na tumezunguka na ndiyo maana tukaamua kutuma timu. Waziri wangu akatuma ile timu ya haraka kupitia maeneo yote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Naomba niwaambie kwamba timu ile sasa wataalam ndiyo walikuwa wanahakiki kupitia vigezo mbalimbali baadaye mchakato utakavyoenda, utakapofika, basi utaambiwa kwamba Mji wetu wa Namanyere umefikia katika hatua gani.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwahakikishie kwamba lile jambo liko katika ofisi yetu linafanyiwa kazi baada ya ile timu yetu ya uhakiki kwenda kufanya kazi. Kwa hiyo, naomba tuvute subira tu kusubiri mchakato huo ukamilike halafu tutapata mrejesho kwa mustakabali wa Mji wa Namanyere.
MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mji Mdogo wa Mlowo uliopo Wilaya Mbozi, tangu mwaka 2016 umetangazwa kuwa mji mdogo lakini hakuna shughuli yoyote pale inayoendelea kuonesha kwamba ni mji mdogo; bado vitongoji kama kawaida vipo na tayari ile asilimia 80 inayokusanywa na Halmashauri ya Wilaya inaendelea kukusanywa kama kawaida na asilimia 20 inarudi kwenye kijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Mheshimiwa Naibu Waziri naomba nijue ni lini rasmi sasa Mji Mdogo wa Mlowo utaanza kufanya shughuli zake kama Mji Mdogo na kama siyo kijiji kama ilivyokuwa kwa sasa japokuwa tangu mwaka 2016 tumeshapewa kuwa hadhi ya Mji Mdogo lakini shughuli zinazoendelea siyo za Mji Mdogo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, mji anaouzungumzia Mheshimiwa Haonga ni kweli ni mji ambao sasa hivi eneo lake bado lipo katika suala zima la vitongoji, lakini kuna utaratibu ule kwamba vile vijiji tufanye ule uchaguzi wa Serikali za Vitongoji, then wachague Mwenyekiti wa Vitongoji kwa mujibu wa taratibu, then atachaguliwa TEO, then mchakato huu utaenda.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anafahamu katika eneo lake kuna baadhi ya Vitongoji vingi sana havijafanya uchaguzi na hii nakumbuka alikuja ofisini kwangu tulikuwa tunatoa maelekezo kwa Mkurugenzi kwamba aangalie utaratibu wa kufanya yale maeneo ambayo uchaguzi haujafanyika, ziweze kufanya uchaguzi maeneo yote sawa sawa na eneo la Vwawa kule kwa Mbunge wetu wa Vwawa. Maana yake zikifanyika chaguzi zote, basi utaratibu mwingine utafanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo kubwa ni kwamba vile vitongoji vyote viwe na hadhi ya vitongoji na Wenyeviti wake wa vitongoji baadaye wachague Mwenyekiti wao Kitongoji, then achaguliwe TEO, baadaye ule mji sasa unakuwa na mamlaka kamili kufanya kazi yake. Kwa hiyo, ni jambo ambalo tutaendelea kutoa maelekezo kwa Mkurugenzi wetu, waendelee na michakato ile ya kufanya mamlaka ile inaweza kufanya kazi vizuri kama ilivyokusudiwa.
MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Isaka toka miaka ya 1990 imekuwa inajulikana kwamba ni bandari ya nchi kavu, uwekezaji mkubwa sana unafanyika pale na nchi jirani na hivyo ardhi imekuwa ni kitu adimu na uvamizi ni mkubwa. Kwa zaidi ya mwaka sasa wananchi wa Isaka walishaomba eneo hilo liwe mji mdogo na maombi yalishawasilishwa Wizarani lakini kumekuwa na ukimya. Nataka kujua ni hatua gani iliyofikiwa kwa lengo ya kuitangaza Isaka kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesikia maswali mengi na karibu maswali yote yanaomba Miji Midogo. Tunazo Mamlaka za Halmashauri 185 kwa nchi nzima. Tunayo Miji Midogo mingi, mingine inafanya kazi na mingine imeshindikana hata kuanza; lakini pia ndiyo unasikia maswali haya mengi, Bwana Keissy, Mipata wanazungumzia Namanyere, ukimuuliza Mheshimiwa Kikwembe hapa, anazungumzia Majimoto, ukimuuliza Mheshimiwa Edwin Ngonyani anazungumzia kule kwake Namtumbo kule na Lusewa; wengine wanazungumzia Isaka. Kwa hiyo, hapa Waheshimiwa Wabunge wana maswali haya mengi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jibu lake ni hili; ili uweze kuanzisha Mji Mdogo, lazima uangalie kwanza uwezekano wa kuweza kuwa na mapato ya ndani ya kujiendesha. Huanzishi tu halafu Serikali unataka ilete fedha ya kuendesha. Hizi Mamlaka 185 tulizonazo zinashindikana kupata fedha Serikalini kuziendesha; tunapoanzisha mamlaka nyingine tunaleta contradiction, kwa sababu kimsingi hizi mamlaka zinazaliwa na mamlaka mama. Halmashauri mama ndiyo inayozaa Mji Mdogo. Unaposema unaanzisha Mji Mdogo ukapeleka setup ya watumishi pale, maana yake Halmashauri mama ianze kugawana mapato na Halmashauri hii ndogo unayoianzisha ya Mji Mdogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa jambo hili mwanzo wake (genesis) yake ni huko huko kwamba je, hivi tunao uwezo wa kuweza kuanzisha mamlaka hii na ikajiendesha?Je, vyanzo hivi vikichukuliwa na Mji Mdogo, haviathiri Halmashauri mama? Ukimaliza stage hiyo sasa ukaona umejiridhisha, sasa omba.
Mheshimiwa Naibu Spika, cha msingi ninachoweza kushauri Waheshimiwa Wabunge, ili kuweza kwenda na hatua nzuri, hebu twende na stages kama inavyokwenda Lamadi. Kwamba Lamadi wameshafanya Mipango Mji wa ile sehemu; wameipima, lakini wameshajitosheleza katika huduma kama za maji, lakini wamekwenda mbali zaidi wanajenga mpaka barabara za lami; sasa ukifika mahali hapo; kwa mfano, nafahamu kwamba Lamadi sasa wawekezaji wanaojenga mpaka hoteli za kitalii maeneo yale; kwa hiyo, naamini haka kamji kanaweza kakajiendesha.(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge niwasihi, hebu jambo hili twende nalo taratibu. Kama tuliahidi, hebu twende nalo taratibu kwa sababu uamuzi wake utazingatia sana tathmini ya tulikotoka, Miji Midogo tuliyoianzisha imefika wapi na hali ikoje? Ndiyo tufikie uamuzi wa kuamua ku-establish mamlaka hizi ndogo ndogo mpya.
MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Halmashauri ya Nyang’wale imeanzishwa zaidi ya miaka minne na pakatokea kosa la kiuandishi katika GN yake, badala ya kuandikwa Nyang’hwale Makao yake Makuu Karumwa, ikaandikwa Makao Makuu Nyang’hwale na taarifa hii tumeshaileta na tayari leo zaidi ya miaka miwili GN ya Nyang’hwale mpaka sasa hivi hatujaipokea. Je, Mheshimiwa Waziri anatuambia nini sisi Wana-Nyang’hwale, kuna tatizo gani ambalo limekwamisha kuitoa GN hiyo?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli yapo makosa mengi, siyo kwako tu, lakini utaratibu na masahihisho yote yanafanywa na Katibu wa Bunge. Ikishatolewa ile GN, kama kuna marekebisho, inarudishwa na Katibu wa Bunge anaombwa kurekebisha. Bahati nzuri ya kwako iko tayari imerekebishwa na jana ilikuwa ofisini kwangu. Karibu uje uichukue. (Makofi)
MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri juu ya process ya Miji Midogo na kwa kazi nzuri iliyofanywa na Serikali ya kufungua barabara ya lami kwenda Msumbiji inayopita katikati ya Jimbo la Mtama na ile inayokwenda Tunduru mpaka Songea, Miji ya Kiwalala, Mtama na Nyangao kasi yake ya kukua ni kubwa na hizo sifa ambazo Mheshimiwa Waziri alikuwa akizieleza zote tunazo.
Ni lini Serikali itakamilisha sasa mchakato wa kuitangaza miji hii midogo kuwa mamlaka kamili ambayo inajitegemea, badala ya kutaka tujumlishe yote kwa pamoja kama ambavyo Waziri anaeleza, nadhani twende case by case na kwa wale ambao wamekamilisha vigezo wapewe badala ya kusubiri wote kwa ujumla wake?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kama tulivyosema pale awali, concern ya Mheshimiwa Nape ni kwamba ikiwezekana twende case by case, naomba nikuhakikishie kwamba tulivyoenda kufanya tathimini ya maeneo yote, maana yake hata tumefika sehemu nyingine kwa ajili ya watu wametu-invite makusudi kwenda kuangalia hiyo Miji Midogo. Tulipofanya hiyo ziara ndiyo maana tukatuma hiyo timu; na bahati nzuri hiyo timu imefanya kazi kubwa sana. Siyo muda mrefu sana, ile kazi ikikamilika sasa na baada ya kujiridhisha na haya mambo ambayo Mheshimiwa Waziri aliyazungumza kwamba suala zima la kuangalia vigezo vya kiuchumi eneo lile, basi tutatangaza maeneo haya.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tuvute subira tu, kwa sababu kila jambo lina utaratibu wake na mchakato wake, kwa hiyo, tuvute subira tu.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo ambalo alizungumza, ni kweli linakua sana, basi tutaangalia jinsi gani tutafanya maeneo yatakayokuwa tayari, basi yatatangazwa kwa mujibu wa sheria.
MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Upungufu wa walimu umekuwa mkubwa sana kwenye Halmashauri za Wilaya ukilinganisha na Halmashauri za Mji. Je, ni lini Serikali itaweka mgawanyo sawa kwa walimu katika hizi shule zetu za msingi ili kuwe na usawa katika ufaulu wa wanafunzi? Maana yake ilivyo sasa hivi, kuna inequalities. Ukiangalia shule za mjini zinafaulisha vizuri zaidi kuliko za vijijini.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, suala la mgawanyo wa walimu lina mambo mengi, kuna scenario ambayo ipo na hapa tulitoa maelekezo mara kadhaa. Utakuta katika Halmashauri moja hiyo hiyo, walimu wamefika, lakini walimu wengi wanabakia katika vituo vya mijini na hii utakuja kuona sehemu ya vijijini kule walimu wanakuwa hawapo. Ndiyo maana sasa hivi TAMISEMI tunaangalia kwamba kila mikoa tupeleke idadi ya walimu na kila Halmashauri tupeleke idadi ya walimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, napenda kutoa maelekezo mengine tena hapa kwamba Maafisa Elimu wote wa Wilaya wahakikishe wanafanya ile distribution ya walimu katika maeneo mbalimbali, wasiwaache walimu katika kituo kimoja cha mjini. Jambo hilo limejitokeza pale Mbeya. Nilipofika Mbeya, shule moja pale mjini ina walimu mpaka wanabadilishana vipindi, lakini shule nyingine ina walimu wawili peke yake. Hili jambo haliwezekani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hili ni agizo kwa Maafisa Elimu wote wa Wilaya katika Halmashauri zote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wahakikishe wanafanya re-distribution ya Ualimu katika maeneo. Lengo ni kwamba hata kule vijijini walimu waweze kuwepo wanafunzi wapate taaluma inayokusudiwa.
MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Sambamba na hilo, tunajua walimu ni changamoto pamoja na kwamba Serikali imefanya kazi kubwa na nzuri katika jambo hili. Kwenye eneo la shule ya Kimambi; na shule ya Kimambi iko kwenye mpaka wa Liwale na Kilwa. Shule hii ina upungufu sana na walimu na sasa hivi kuna walimu wasiozidi watatu. Hata hivyo walimu wakipangiwa ndani ya Mkoa wa Lindi hasa kwenye vile vijiji wengi hawaripoti na hata wanaporipoti kinachojitokeza ni kutorudi kwenye maeneo yao. Serikali inasemaje juu ya jambo hili? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli shule anayozungumza mama yangu ni kweli shule ambayo kwa kweli ipo mpakani. Na mimi nilipokuwa nikisafiri, nikienda Liwale, nikizunguka Mkoa wa Lindi, ukiangalia kijiografia ni shule ambayo ipo mbali zaidi. Kama taarifa ya sasa, shule ya Kimambi ambayo inaonekana ina walimu watatu, naomba tulichukue hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo naomba niseme kwamba Afisa Elimu wa eneo hili sasa kupitia chombo hiki, leo tuko live, nimwelekeze kuhakikisha kwamba shule ile anaitembelea na by Ijumaa tupate status kwamba amefanya nini kuhakikisha shule hiyo inakuwa na walimu kama katika maeneo mengine yalivyokusudiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili tuondoe sana suala la uonevu katika maeneo mengine, wengine wanaonekana kama hawana thamani kuliko sehemu nyingine, sasa wale tuliowapa dhamana katika Wilaya zetu wahakikishe wanafanya kazi hiyo kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma inayostahiki katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, niwie radhi sana, nilitaka kuongezea kwenye jibu la Naibu Waziri kwamba ni kweli walimu hawa au watumishi hawa tunapowapangia wanakutana pia na changamoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli pia kwamba mazingira ya nchi yetu hayako sawa yote. Yako maeneo yana hali mbaya sana kimazingira, kimiundombinu na huduma nyingine; lakini kubwa ni nyumba za watumishi. Kusema ukweli ni jukumu la mamlaka hizi za Serikali za Mitaa kuangalia mazingira hayo na hata watumishi hao wanaporipoti kuwasaidia kwa kiasi kinachotosheleza ili waweze kukubali kwenda kukaa maeneo yale.
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi tunaweza kuwapangia; lakini unampangia mtu anafika toka siku kwanza mtoto wa kike analia tu mpaka unashangaa amekonda, amepunguza, hata yaani alivyokuja ni tofauti na hawa ni watoto wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tuwe wakweli, Wakurugenzi wetu wakati mwingine wanayoyafanya siyo sawa. Hivi kumpatia usafiri binti mdogo au kijana mdogo anayeanza kazi na Halmashuri ina rasilimali ikampeleka na gari mpaka kile kituo wakampokea vizuri, lakini sehemu nyingine wanafanya na sehemu hawafanyi. Hili jambo ndilo linalopelekea kuwa na upungufu katika baadhi ya maeneo.(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nisisitize na niseme hapa, sisi Wabunge ndio walezi, ndio viongozi kwenye maeneo husika. Tuwe karibu sana; tunaposikia watumishi wamepangwa, tujue hatma yao na mpaka siku watakapokwenda kuripoti kwenye vituo kama jukumu letu kama walezi lakini pia kama tunawajibisha mamlaka husika ili zitekeleze wajibu wao. (Makofi)
MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Waziri japokuwa niseme kwamba majibu haya hayaridhishi na wala hayajatosha.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la msingi nilitaka kujua kwamba Serikali ina mpango gani wa kujenga wodi mpya ya akinamama katika Hospitali hii ya Wilaya ya Mbozi ukizingatia kwamba hospitali hii inahudumia wilaya mbili mpaka sasa. Hali halisi ilivyo pale kuna vitanda 25 tu vya akinamama vya kulala baada ya kujifungua lakini kwa siku wanawake wanaozalishwa katika hospitali hiyo ni wanawake 42 mpaka 50. Kwa hiyo, kukarabati hili jengo hakuwezi kusaidia. Kwa hiyo, swali langu la msingi nataka kujua kwamba Serikali ina mpango gani wa kujenga wodi ya akinamama mpya na kubwa? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, katika
swali langu la msingi pia nataka kujua kwamba Serikali ina mpango gani wa kujenga Hospitali ya Wilaya ya Momba?Hili jambo nimekuwa nikilipigia kelele sana katika Bunge hili kwamba mpaka sasa Wilaya ya Momba hawana Hospitali ya Wilaya. Hali hiyo inapelekea usumbufu sana kwa sababu mara nyingi wanalazimika kuja kutibiwa katika hospitali ya Mbozi ambayo pia nayo jengo lake ni dogo. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Naibu Waziri aniambie ni lini sasa Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya ya Momba? Ahsante.(Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge, haya yote yanatokana na needs za Wabunge wenyewe tunavyokaa katika vikao vyetu. Kwenye vikao vyetu ndipo ambapo tunaweka priority nini kifanyike. Eneo hili priority ya kwanza imeonekana ni lazima tutenge shilingi milioni 180 kwa ajili ya kufanya ukarabati huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba niseme mipango hii yote inaanzia kwetu sisi Wabunge katika maeneo yetu tunapofanya needs assessment au tunapopanga mipango yetu. Hata hivyo, nimhakikishie Mheshimiwa Juliana kwa jinsi anavyopigania haki za akinamama na watoto Serikali tutafanya kila liwezekanalo kuona jinsi gani tutafanya kwa sababu pale Vwawa sasa hivi ndiyo kama Makao Makuu. Licha ya ukarabati huu, lakini tutaangalia nini kingine kifanyike lengo kubwa ni akinamama na watoto hasa wanaozaliwa waweze kuwa katika mazingira salama.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Hospitali ya Momba, niliongea na Mkuu wa Mkoa wetu wa Songwe, Mama Chiku Gallawa wakati tunafanya mikakati ya ukarabati wa vituo vya afya 100, hili jambo aliweka kama priority na aka-identify kwamba Momba haina Hospitali ya Wilaya. Tulibadilishana mawazo tukaona lile eneo la awali ambalo limepangwa kuwa Makao Makuu ya Halmashauri ya Momba kile kituo cha afya cha pale tukiwekee miundombinu ya kutosha ili wananchi wa eneo lile waweze kupata huduma ya kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Juliana kwamba tutafanya kila liwezekanalo kuhusiana na hoja hii na kwamba katika Makao Makuu ya Momba tunaenda kufanya uwekezaji mkubwa sana ndani ya kipindi hiki hiki kabla ya mwezi wa saba. Kilio cha wananchi wa pale ni kwamba wanapata shida na Serikali tumesikia kilio hiki, tutaenda kufanya kazi kubwa na ya kutosha kuwasaidia akinamama na watoto wa maeneo yale. (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Matatizo yaliyopo Momba ni sawa kabisa na matatizo yaliyopo katika Mkoa wa Kigoma ikiwa ni katika Wilaya ya Kakonko na Buhigwe. Wilaya hizo ni mpya na zimekuwa zikipata huduma kutoka kwenye Wilaya Mama. Ni lini Wilaya ya Kakonko na Buhigwe zitapatiwa Hospitali ya Wilaya? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, anavyosema Mheshimiwa Mbunge Genzabuke ni kweli Kakonko wanatumia Kituo cha Afya cha pale Kakonko, hali kadhalika Buhigwe hawana Hospitali ya Wilaya. Kipindi kile nilivyofika Kakonko na Buhigwe tulifanya makubaliano fulani juu ya nini kifanyike kama mipango ya awali kurekebisha hali hii.
Mheshimiwa Naibu Spika,pale Buhigwe kwanza tunaenda kufanya ukarabati mkubwa wa Kituo cha Afya cha Buhigwe kwa kukipatia wodi ya upasuaji na wodi kubwa ya wazazi na vifaa vyote vinavyowezekana. Jambo hili tunalipanga kama Mungu akijalia kabla ya mwezi Agosti tutakuwa tumelitekeleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutashirikiana na wenzetu wa Kakonko kuona ni jinsi gani tufanye, lakini nikifahamu fika kwamba jana nilikuwa naongea na Wabunge wahusika wa maeneo haya na Mheshimiwa Mbunge pia na tuliona hata ikama ya Madaktari walioenda kule ni wachache na katika mchakato ule wa ajira zitakazokuja hapo baadaye tutaongeza idadi ya wataalam kwa sababu ukiachia miundombinu lakini suala la human resources ni jambo la msingi. Haya yote kwa Mkoa wa Kigoma tutayapa kipaumbele ili wananchi wa mkoa huu waweze kupata huduma za afya ya msingi.
MHE. FREEMAN A. MBOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tatizo linalowakabili wananchi wa Mbozi kwenye suala la Hospitali ya Wilaya kwa kiasi kikubwa linafanana na la Hospitali ya Wilaya ya Hai katika Mkoa wa Kilimanjaro. Hospitali hii ya Wilaya ya Hai ilianza kujengwa zaidi ya miaka 10 iliyopita wakati huo Mji wa Hai ukiwa na wakazi wasiofika 10,000 na Mji wa Hai leo ni mji unaokua kwa kasi kuliko miji yote katika Mkoa wa Kilimanjaro ikiwa katika kipindi cha miaka kumi, Mji wa Hai umefikisha zaidi ya wakazi 50,000.
Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali hii imekuwa inajengwa awamu kwa awamu lakini kuna tatizo moja kubwa la msingi ambako wanaume na wanawake wanalala katika wodi moja. Jambo hili nimeli-witness mwenyewe na nimetembelea hospitali hii wiki iliyopita kushuhudia hali hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninachomwomba Naibu Waziri katika hatua ya sasa, kutokana na hali ya unyeti wa hospitali hii na ikiwa vilevile ni hospitali ambayo iko katika barabara kuu ya Arusha-Moshi ambayo inahudumia wagonjwa wote wanaopata ajali katika barabara ile, rai yangu kwa Mheshimiwa Waziri ni kutenga muda wake tuweze kutembelea pamoja hospitali hii kwa pamoja tuone uzito wa tatizo lililopo kisha Serikali itutafutie ufumbuzi wa kudumu kuhusu tatizo hili. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba niseme takriban wiki tisa kama sio kumi zilizopita nilikuwa pale Hai. Nilienda kuitembelea hospitali ile na niliweza kubaini mchakato mkubwa unaofanywa na injinia wetu katika lile jengo la akinamama linalojengwa pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli nimefarijika na nimefurahi sana kwa mkakati uliopangwa. Kwa kutumia hizi Force Account kazi kubwa inafanyika pale. Kwa hiyo, jambo la msingi ni kwamba kama Serikali pale kuna kazi kubwa tunaendelea kuifanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, niseme nimekubali wazo
hilo la kwenda pamoja lakini tayari nimeshakwenda na tumesha-identify na nimeshatoa maelekezo nini wanatakiwa wafanye. Namshukuru sana DMO wetu pale kwa kazi kubwa inayofanywa na menejimenti ya hospitali ile. Hata hivyo, nimetoa maagizo sasa waangalie rasilimali zilizokuwepo kama majengo yaliyokuwepo pale nini kifanyike, wapange mpango mzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi kubwa tunayokwenda kufanya ni kukamilisha lile jengo kubwa linalojengwa ambalo ni la mfano na mimi nimetolea mfano hata nilivyokwenda Siha kule nikawaambia kwamba igeni kwa wenzenu wa Hai kwa kutumia Force Account, kutumia fedha ndogo na kufanya mabadiliko makubwa katika sekta ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeweka nguvu kubwa pale. Hata hivyo, nina mpango wa kwenda Hai na Waziri wangu amepanga hilo kwa sababu Mheshimiwa Rais ameshaelekeza lazima tukahakiki suala zima la matumizi ya fedha na miundombinu ya barabara, kwa hiyo, tutakwenda tuone jinsi gani tutafanya ili hospitali ile iweze kuwahudumia vizuri wananchi wetu wa Hai.
MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Matatizo yaliyopo Mbozi Vwawa yanafanana sana na Kituo cha Afya cha Malya. Kituo cha Afya cha Malya kinahudumia Maswa, Malampaka na Kwimba. Kwa sababu Kituo cha Afya cha Malya kwa sasa kimezidiwa, miundombinu ya majengo na vyumba vya kusaidia wazazi havitoshi, Serikali ina mpango gani sasa wa kuwekeza angalau adha zilizopo pale ziweze kupungua?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, hii sehemu ya Kwimba ina Majimbo mawili, Jimbo la Mheshimiwa Ndassa na Mbunge mwingine lakini ukiangalia hospitali yetu ya wilaya na kule anakosema Malya ni kweli. Ndiyo maana naomba nimshukuru Mheshimiwa Mbunge, katika initiative zake za kutusumbua mimi na Waziri wa Afya alileta Kituo hiki cha Afya cha Malya kiweze kupewa kipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi TAMISEMI tumeshapitisha bajeti yetu na Wizara ya Afya imeshapitisha yao ni kwamba sasa hivi tunaenda kufanya uwekezaji mkubwa katika Kituo cha Afya cha Malya. Naomba nimhakikishie kwamba ombi lake kama Wizara ya Afya na Wizara ya TAMISEMI tumelichukua, tunaenda kufanya ukarabati mkubwa. Katika vile vituo 100 na Malya ni kimojawapo, tunaenda kuwasaidia wananchi wa jimbo lake.
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipatia nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwanza kabisa, napenda nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, suala hili ni la kikatiba kwa maana ya kwamba linahusisha Serikali ya wananchi kwa maana ya Serikali za Vijiji. Kwa kuwa wananchi wamekuwa wakichangia takribani 20% ya maendeleo katika maeneo yao ya vijiji. Je, Serikali sasa inafikiria nini kupeleka pesa za maendeleo kwa wakati ili wananchi hawa waweze kujua sasa ile miradi ni mali yao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli dhana hii inapeleka fursa kwa wananchi na ni kweli tumeshuhudia wananchi katika maeneo mbalimbali wakishiriki vyema katika kutekeleza dhana hii kwa kujitolea katika miradi mbalimbali ya maendeleo. Hata hivyo, naomba nilihakikishie Bunge lako Tukufu kwamba Serikali kwa kipindi cha sasa na nina maana itakapofika mwezi wa Sita mtaona jinsi gani imepeleka nguvu kubwa sana katika eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano katika sekta ya afya mwaka huu peke yake fedha tulizopeleka katika mifuko mbalimbali ikiwepo Basket Fund ni zaidi ya shilingi bilioni 79 na sasa hivi tumeshapeleka fedha za quarter ya nne ambapo tunaenda kukamilisha shilingi bilioni 106, hii ni sekta ya afya peke yake. Tumefanya hivyo pia katika sekta ya elimu na maeneo mbalimbali na juzi juzi hapa tumenunua vifaa vya maabara katika maabara zote zaidi ya 1,000 ambapo vyote vilikuwa vinagharimu shilingi bilioni 16.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kuna fedha nyingine za LDGD ambazo zimeenda moja kwa moja ambazo hazina ukakasi katika kuzitoa kwake. Serikali imepeleka hela za kutosha na ni mara ya kwanza baada ya miaka minne iliyopita tulikuwa hatufanyi hivyo. Kwa hiyo, Serikali itaendelea kuweka nguvu kubwa ya kutosha, lengo kubwa ikiwa ni kuwawezesha wananchi kutekeleza miradi yao.
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Mpango wa Afya ya Msingi (MMAM) muda wake ilikuwa uishe mwaka huu 2017 lakini fedha hizo haziji kwa muda mrefu, takribani kama miaka mitatu nyuma fedha haziji. Ni kwa nini mpango huu wa MMAM ambao ulikuwa unasaidia kujenga zahanati zetu umekwama na anawaambiaje Watanzania kwa sababu maboma/zahanati nyingi bado hazikajamilishwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema hapa sio suala la maboma ya afya peke yake hata maboma ya nyumba za Walimu halikadhalika madarasa. Kipindi fulani hapa takribani miaka mitatu, minne fedha hizi zilikuwa haziendi. Ndiyo maana nimesema kupitia Mfuko ule wa LDGD ambapo kwa sasa mwaka huu kwa mara ya kwanza, namshukuru Mheshimiwa Waziri wangu alilisimamia kwa karibu sana, ndiyo maana hivi sasa Wabunge kama tumepitia katika Kamati zetu za Fedha katika Halmashauri zetu tunaona kuna fedha nyingi zimekuja ambazo zimesaidia kwa kiwango kimoja au kingine kuweza kuhakikisha maboma mengi sana yameweza kujengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeshuhudia hili kwani nilipopita maeneo mbalimbali nilikuwa nikipata taarifa mbalimbali kutoka kwa Wakurugenzi jinsi gani fedha hizi sasa wameweza kuzielekeza katika kuhakikisha zile nguvu za wananchi ambazo wamezitoa hazipotei kwa kukamilisha viporo hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge, naomba tushirikiane kwa pamoja. Lengo kubwa ni kutekeleza mpango wa D-by-D kama alivyosema Mheshimiwa Dkt. Kikwembe, tufanye hili kwa ajili ya mustakabali mzuri kwa kuunganisha nguvu za wananchi katika kuhakikisha Taifa hili linaenda mbele.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nataka tu kumfahamisha Mheshimiwa Gekul kwamba tayari tumeshaanza kuufanyia mapitio Mpango wa Afya ya Msingi (MMAM). Kwa hiyo, tunategemea kabla ya mwisho wa mwaka tutakuwa tumetoa mpango wa pili ambao utatueleza kama, je, ni lazima tuwe na zahanati kila kijiji wakati sasa hivi barabara zinapitika? Je, ni lazima tuwe na kituo cha afya kila kata? Kwa hiyo, hayo maeneo yote tutayaangalia kwa upana wake. Lengo letu ni kuhakikisha tunasogeza huduma bora kwa wananchi. Ahsante sana.(Makofi)
MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na jitihada za Serikali kupeleka fedha za maendeleo, ugatuaji lazima uende sambamba na upelekaji wa resources hususan fedha za OC. Fedha za OC zimekuwa haziendi kwa kiwango kinachokusudiwa matokeo yake imekuwa inaathiri mipango inayopangwa na Halmashauri kwa kutekelezwa kutokana na makusanyo ya ndani. Matokeo yake fedha za makusanyo ya ndani sasa zinatumika kuendeshea ofisi badala ya kuelekezwa kwenye shughuli za maendeleo kama inavyoelekeza ile 50%, ikiwepo 5% ya vijana na wanawake. Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha kwamba inapeleka fedha za OC ipasavyo ili kusudi makusanyo ya ndani yasiathiri utekelezaji wa shughuli za maendeleo, kama ambavyo zimepangwa na Halmashauri zetu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli na nakumbuka kwamba tulipokuwa katika kikao chetu cha ALAT kule Musoma, concern kubwa ilikuwa siyo fedha za OC peke yake hata pesa za maendeleo. Waheshimiwa Wenyeviti wa Halmashauri na Wakurugenzi wali-raise jambo hili katika ofisi yetu na ndiyo maana katika kipindi cha katikati baada ya harakati hizi kufanyika mmeona tumepeleka fedha nyingi sana za maendeleo na pesa za OC.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kama ambavyo Mheshimiwa Waziri wangu siku zote amekuwa akisema definition ya OC maana yake ni Own Source plus zile fedha nyingine zinazotoka Serikali Kuu. Kwa hiyo, sisi Serikali tutajitahidi kwa kadiri iwezekanavyo OC iweze kwenda, lakini niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge katika maeneo yetu vilevile tuhakikishe makusanyo ya ndani haya yanaimarika kwa kiwango kikubwa kwa sababu tumeshuhudia hivi sasa kuna Halmashauri zingine zimefanya vizuri lakini nyingine zinasuasua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hili ni jambo letu sisi sote. Upande wa Serikali tutajitahidi kufanya kila liwezekanalo kuziwezesha Halmashauri zetu ziweze kufanya kazi vizuri kwa sababu bila ya hivyo maana yake utekelezaji wa Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi utakuwa una matatizo. Kwa hiyo, naomba niwahakikishie kwamba Serikali itafanya kila liwezekanalo, tutakusanya mapato lakini tutayapeleka katika Halmashauri zetu ili miradi iweze kutekelezeka vizuri.
MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwa kuwa Hospitali ya Wilaya ya Kibondo ndiyo hospitali vilevile inayotumika kama Hospitali ya Rufaa kwa Wilaya ya Kakonko, lakini inatumika kama Hospitali ya Rufaa kwa wakazi kutoka nchini Burundi, kwa maana ya wakimbizi wapatao laki mbili. Serikali ina mpango gani wa kuongeza majengo kwenye hospitali hiyo ambayo hayajawahi kuongezwa kutoka mwaka 1971?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa sababu hiyo hiyo Serikali ina mpango gani wa kuongeza mgawo wa dawa ili kuweza kukidhi mahitaji ya wananchi wa Wilaya ya Kibondo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hospitali ya Mheshimiwa Mbunge ya kama Kibondo, ni kweli na mimi nilifika tulienda kukagua hospitali ile, kuna changamoto ya miundombinu pale na hata wenzetu wa Kakonko kwa mwalimu wangu pale, mara nyingi sana wanatumia kama ndio referral hospital yao katika eneo lile, changamoto hizo tumeziona. Siku ile nilivyokuwa pale site niliwaambia waangalie upungufu uliokuwepo (needs assessment) maana hata vifaa tiba na X-Ray lilikuwa ni changamoto na nilitoa maelekezo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, imani yangu ni kwamba wenzetu pale Halmashauri watafanya hiyo needs assessment ambapo mchakato utaanza katika vikao vya Halmashauri, tutaangalia nini kwa pamoja kitafanyika kwa ajili ya kuboresha hospitali ile kwa sababu idadi ya wagonjwa niliyoikuta pale ni kubwa sana na ni kweli anachosema Mheshimiwa Mbunge. Kwa hiyo, Serikali inasubiri jinsi gani michakato itawekwa katika kipaumbele cha Halmashauri yenyewe na sisi tutaweka nguvu kwa kadri iwezekanavyo ili hospitali ile iweze kutoa huduma vizuri.
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mkoa wa Kigoma kwa muda mrefu umekuwa haupati watumishi kwa sababu upo pembezoni lakini pia wakimbizi wameingia kwa wingi katika Mkoa wa Kigoma pamoja na kwamba wana hospitali zao kwenye makambi lakini kutokana na binadamu wasivyoweza kuzuiliwa wanaingia kwa wingi katika miji yetu hali inayosababisha wagonjwa kuwa wengi kwenye hospitali zetu. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kulikuwa na suala la concern ya dawa katika Hospitali ya Kibondo ambalo mwanzo nilili-skip. Hata nilivyofika pale site Kibondo nilitoa maelekezo kuhusu matumizi mazuri ya Basket Fund. Maeneo yote nilikopita nimekuta kwamba japokuwa tumepeleka fedha za kutosha kwenye Basket Fund, lakini Waganga wetu wa Wilaya wameshindwa kuhakikisha zile fedha zinatumika kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wetu. Ndiyo maana nimetoa maelekezo kwamba itakapofika mwezi wa Sita, Halmashauri yoyote ambayo Serikali imepeleka fedha lakini zile fedha zimeshindwa kununua dawa na vifaa tiba kuwasaidia wananchi, tutasema kwamba, ma-DMO wao hawatoshi katika maeneo yetu hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala la watumishi, japokuwa tatizo la watumishi ni tatizo kubwa sana, lakini ukiangalia katika mgawanyo wa Madaktari, Kigoma tumepeleka madaktari 10 lakini mikoa mingine imepata madaktari watano. Tunajua japokuwa Madaktari kumi wameenda katika Mkoa mzima wa Kigoma, bado hawatoshi, lakini tutakapokuja katika ajira mpya Mkoa wa Kigoma tutaupa kipaumbele. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba muelewe ndugu zangu, Kibondo pale kwa ndugu yangu Mheshimiwa Nditiye tumepeleka Madaktari watatu, Kasulu tumepeleka Madaktari wawili, halikadhalika Uvinza tumepeleka Madaktari na RAS Kigoma tumepeleka takribani Madaktari wanne. Lengo letu ni kuhakikisha Mkoa wa Kigoma na mikoa mingine ya pembeni iweze kupata…
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutawapa kipaumbele watu wa Kigoma kupata Madaktari wa kutosha.
MHE. ALMASI A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikushukuru sana kuniruhusu kuuliza swali. Kituo cha Afya cha Upuge ndiyo peke yake Hospitali ya Wilaya Jimboni kwangu, hakuna hospitali kabisa isipokuwa Kituo kile cha Upuge na hakina wataalam wa dawa za usingizi, wanaitwa anesthesia kitaaluma, kwa hiyo, hatuwezi kufanya operesheni. Je, Serikali inafikiria nini kupeleka mtaalam wa dawa za usingizi ili operesheni zifanyike? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kituo cha Afya cha mtani wangu pale, katika idadi ya wataalam ambao tutawaajiri hapa katikati kutokana na nafasi nyingi zilizotolewa na Mheshimiwa Rais tutaangalia mahitaji halisi ya kituo hiki then tutawapa kipaumbele ili mradi wampate mtaalam huyo wa usingizi.
MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, je, ni vikundi ngapi zilizochukuliwa hatua mpaka sasa?
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, je, ni vikundi ngapi zilizochukuliwa hatua mpaka sasa?
Mheshimiwa Naibu Spika, samahani ni shule ngapi zilizochukuliwa hatua mpaka sasa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu ameonesha concern kubwa ya suala zima la janga la moto katika maeneo yetu. Hili nimelisema katika jibu langu la msingi takribani shule 29.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la chanzo nani alisababisha imeonekana maeneo mbalimbali ni hitilafu ya umeme, lakini bado hatujabaini hasa watu mahsusi ambao wameshughulika katika suala la kuhujumu miundombinu hii na ndiyo maana tumeunda Kamati hizi shirikishi katika jamii zetu hasa katika ngazi za shule, lengo ni kuzuia baadae watu watakapobainika basi tuweze kuwachukulia hatua katika maeneo hayo.
MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwa nini shule za Serikali hawaweki provision ya kuwa na fire extinguisher ambayo inaweza ikatumika mara tu kama huduma ya kwanza wakati magari ya zimamoto yanaposubiriwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ukiangalia kesi hizi za majanga ya moto na siyo shuleni peke yake hata katika maeneo mbalimbali, ni kwa sababu katika kipindi kirefu tulikuwa tumejisahu kuweka fire extinguisher. Ndiyo maana sasa tumetoa maelekezo katika shule zetu mbalimbali miongini mwa vitu ambavyo tunatakiwa tuviweke viwe vya msingi ni suala la fire extinguisher. Hata hivyo, katika ujenzi wa mabweni yetu, zamani mabweni yalikuwa yakifunguka yanafungukia ndani, hata janga la moto likitokea watoto wanavyogombania kufungua mlango kumbe ndiyo wanazidi kuufunga.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana katika suala la specification tukasema na mabweni yetu sasa hivi yote milango inafungukia kwa nje ili kwamba inapotokea hatari ya moto basi watoto wakiwa wanatoka mlangoni, iwe ni rahisi sana kuweza katoka katika eneo lile pindi janga la moto linapotokea.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni agizo letu na ninaomba niwasihi sana ni waagize Wakurugenzi wote katika Halmashauri zetu kuhakikisha katika maeneo ya shule zetu zote zinakuwa na fire extinguisher as a back up strategy, endapo moto unapotokea, wakati unasubiria kupata magari ya kuzima moto yaje, tuwe na mbinu mbadala wa kuweza kudhibiti moto mapema zaidi.
MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona.
Mkoa wa Arusha ni miongoni mwa Mikoa iliyoathirika na tukio hili la uchomaji wa shule za sekondari, waathirika wakubwa ni wanafunzi. Ningependa tu Waziri atufahamishe kwamba ni hatua gani za haraka zinazochukuliwa na Serikali katika kuhakikisha kwamba wanafunzi wanaendelea na masomo badala ya kuziacha shule hizo kwa muda mrefu pasipo kupewa msaada wowote na badala yake ni wananchi ndiyo wanaojitolea na wasamaria wema. Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mkoa wa Arusha ni miongoni mwa Mikoa ambayo ilipata janga la moto. Tukumbuke kwamba janga hili liliikumba maeneo mbalimbali. Bahati nzuri unafahamu wewe ni mwenyeji wa Mkoa wa Mbeya, shule yetu ya Iyunga, Mbeya kulikuwa na sintofahamu kubwa sana, lakini ni nini tumekifanya katika maeneo mbalimbali. Tulichokifanya kama Serikali si kwamba Serikali ilikuwa inaangalia hivi na kuacha, hapana. Tumefanya harakati maeneo mbalimbali hasa kutumia Halmashauri husika na ngazi Mikoa na Serikali Kuu. Ndiyo maana wanaofahamu kama mashahidi katika Mkoa wa Mbeya, shule ya Iyunga na mimi nilikuwepo site moto ule ulivyokuwa umewaka pale, tumefanya kazi kubwa sana shule yote ya Iyunga pale imebadilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, shule ya Mpwapwa kwa Mzee wangu Mheshimiwa Lubeleje nimefika pale site hivi sasa bweni tunamaliza kulipaua. Pia maeneo mbalimbali harakati hizi zinaendelea, lakini tunaenda awamu kwa awamu, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Amina Mollel kwamba Kamati yetu ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Arusha bahati nzuri wakati moto unawaka Monduli nilikuwepo pale. Nilienda na nilifanya tathmini hiyo, lengo kubwa ni kwamba tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo sehemu yenye mapungufu yote tutashirikiana na jamii husika kuondoa tatizo hili la watoto wetu ili wasikose maeneo ya kukaa.
MHE. AHMED JUMA NGWALI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa fedha za Mfuko wa Jimbo hazijawahi kukaguliwa Zanzibar na kwa kuwa hakuna utaratibu wowote kwa sababu Hazina ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haiwezi kukagua Hazina ya Zanzibar.
Je, fedha za Mfuko huu wa Jimbo zitakaguliwa lini
na kwa utaratibu gani? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, fedha ya Mfuko wa Jimbo uko utaratibu kwamba hizi zinazoingia Bara na zile zinazoingia Zanzibar kupitia Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, hili kuna utaratibu wa wazi kule Ndugu yangu Mheshimiwa Ngwali nadhani tukifanya consultation na wenzetu kutoka Baraza la Wawakilishi tutakuja kuona ni jinsi gani wanafanya kule utaratibu mzima wa usimamizi wa fedha katika eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaamini kwamba Baraza la Wawakilishi litakuwa linafanya kazi yake kwa mujibu wa utaratibu unaotakiwa, ili fedha hizi ziweze kutumiwa kama inavyokusudiwa. (Makofi)
MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza na kwa niaba ya vijana wa Kitanzania ningependa kujua ni lini Serikali itarudisha programu ya michezo katika shule zetu za sekondari na msingi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama alivyozungumza Mheshimiwa Naibu Waziri, kwanza katika suala zima la shule hizi, juzi tumezindua michezo ya UMISETA hapa rasmi, bahati nzuri Kitaifa tumezindulia hapa Dodoma, tuna shule zipatazo 55.
Hata hivyo, tumetoa maelekezo maalum kwa Ofisi
za Mikoa yote sasa programu ya michezo sasa imeishaanza kurudi mashuleni na tumetoa maelekezo kwamba Maafisa Michezo wote waweze kuwezeshwa katika Mikoa yote na katika Halmashauri zote ili kuhakikisha kwamba tunaibua vipaji katika michezo ya watoto wa shule za msingi na watoto wa shule za sekondari.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge naomba nikuhakikishie kwamba Serikali imeshalichukua suala hili na sasa liko katika utekelezaji. Tunawashukuru sana wenzetu wa CocaCola ambao mwaka huu wanafadhili michezo hii ya UMISETA hapa Tanzania, nayo imeishaanza vizuri na tunashukuru sana kwa kweli. (Makofi)
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Wanging’ombe wametumia nguvu kubwa sana kujenga zahanati na vituo vya afya vilivyopo kule Mdandu, Saja, Ilembula na maeneo mengine. Je, Serikali itapeleka lini pesa ili vituo hivyo vya afya na zahanati viweze kumalizika ujenzi?
Swali langu la pili, kule Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Jimbo la Lupembe wananchi wamejitolea ekari 52 za kuweza kujenga hospitali; je, Serikali pia inafikiria lini itaanza ujenzi wa hospitali ndani ya Halmashauri ya Njombe?(Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, kwanza naomba nimpongeze Mbunge kwa initiative kubwa sana ya Mkoa wake wa Njombe. Nafahamu kwamba Wanging’ombe tunatumia Hospitali ya Ilembura kama DDH kwa ajili ya Wananchi kupata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge ndiyo maana katika mwaka huu wa fedha mnafahamu kwamba zile fedha ambazo nyuma zilikuwa hazipatikani za Local Government Development Grants ambazo zilikuwa zinaenda kusaidia hii miradi ya mabomba na ujenzi ulioanza, mwaka huu sasa zimeweza kutoka. Ninashukuru sana Halmashauri mbalimbali wameelekeza fedha hizo hasa katika kumalizia viporo vya zahanati, vituo vya afya, sehemu zingine na madarasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo naomba nimuagize Mkurugenzi wa Wanging’ombe na Baraza la Madiwani kwamba mpaka mwezi wa sita tutaendelea kutoa fedha zingine mpaka ziweze kukamilika katika bajeti yetu ya mwaka huu, zikija kule lazima zingine wazielekeze katika kuhakikisha hizi zahanati na vituo vya afya katika eneo la Wanging’ombe zimefanyiwa kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo katika Halmashauri ya Njombe kama ulivyosema ni kweli jambo hilo limejitokeza mara kadhaa hapa katika Bunge hili na eneo limeshatengwa. Naomba niwahakikishe kwamba Halmashauri kwa kadri itakavyoibua katika bajeti yake mpango wa bajeti wa Serikali katika Halmashauri husika na Ofisi ya TAMISEMI tutashirikiana nao.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu kubwa ni kwamba kila Halmashauri kuwe na hospitali ya Wilaya ili wananchi waweze kuhudumiwa katika eneo hilo. Kwa hiyo, Serikali iko tayari kushirikiana na wananchi wa Njombe kuhakikisha katika mipango yetu hii tunafanikisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Njombe ili wananchi waweze kupata huduma vizuri. (Makofi)
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa Wilaya mpya nyingi hazina Hospitali za Wilaya ikiwemo na Wilaya yangu ya Tanganyika; ni nini mkakati wa Serikali wa kuweza kujenga hospitali sambamba na kuimarisha vituo vya afya wakati inajipanga kujenga hospitali hizo za Wilaya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mheshimiwa Moshi pale kwake wanahudumiwa na Hospitali ya Halmashauri ya Mpanda iko Mpanda Mjini na Makao Makuu ya Wilaya ya Tanganyika Majarila na eneo lingine lote mpaka unaenda ziwani, wananchi wanapata shida kubwa sana. Mheshimiwa Mbunge unakumbuka tulivyokuwa Jimboni kwako tumeenda mpaka katika Makao Makuu ya Halmashauri yako ambayo inatarajiwa kujengwa hivi sasa na miongoni mwa jambo ulilolipendekeza ni kwamba tufanye utaratibu wa kuboresha kile kituo cha afya cha Majarila.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikuhakikishie kwamba, Serikali sasa imetenga takribani shilingi milioni 700 kupeleka katika eneo lako, lengo kubwa ni kuwasaidia wananchi wako ambao wanachangamoto kubwa ya kiafya. Serikali imesikia sana kilio cha wananchi wa Tanganyika na Serikali iko tayari nadhani katika kipindi hiki kuanzia mwezi huu wa Mei mpaka tutakapofika mwezi wa Julai ni imani yangu kubwa tutapeleka nguvu kubwa sana kujenga theatre na kuweka vifaa vyote vya wazazi ili tupunguze vifo vya mama na watoto tuweze kuvipunguza katika eneo lako. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Mji wa Tarime ina Hospitali ambayo ni Hospitali ya Mji, lakini inahudumia Wilaya nzima, ningetaka kujua ni lini Serikali itajenga Hospitali kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Tarime wakati inasubiria kujenga, iipe ile hadhi kama Hospitali ya Wilaya na kuweza kuleta mahitaji kama inavyotakiwa kwa idadi wa watu wa Tarime nzima na siyo Halmashauri ya Mji tu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kesi anayoizungumzia Mheshimiwa Esther hapa inafanana na ya ndugu yangu Mheshimiwa Chumi, tuna Halmashauri zile za Mji na Halmashauri za Wilaya, kwa bahati mbaya ukiangalia Tarime Halmashauri ya Mji ndiyo ina hospitali, Halmashauri ya Wilaya haina hospitali na bajeti mnayopata ni ndogo, hali kadhalika ukiangalia Mufindi na Mafinga, Mafinga kuna Hospitali ya Wilaya bajeti ikienda inakuwa ndogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimepita maeneo mbalimbali niliwapa maelekezo watu, kwa nini maeneo ambayo hakuna Hospitali ya Wilaya kama kuna hospitali zingine zile za mission tunaweka DDH na tunapeleka funds pale kwa nini kunapokuwa kwa mfano katika Halmashauri ya Tarime kuna Hospitali ya Wilaya, kwa nini watu wa Halmashauri ya Wilaya pale, fedha tunazozipeleka ambao wana bajeti kubwa sana wasielekeze fedha zingine kwa ajili ya kununua dawa na vifaa tiba katika Halmashauri ya Mji.
Mheshimiwa Naibu Spika, hili ni jambo nadhani hasa Wakurugenzi wetu katika maeneo husika na viongozi mliopo huko tuangalie haja ya wananchi wetu kuweza kuwahudumia, hili ni jambo kubwa na shirikishi. Kwa hiyo, naomba niagize, katika maeneo ambayo yana scenario kama hii, lazima viongozi mkae muangalie ni jinsi gani tutafanya tuweze kuhudumia eneo hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, nakuunga mkono Mheshimiwa Esther Matiko ni jambo lenye mantiki na lina busara zaidi, naomba maagizo haya yachukuliwe sehemu zote kama ni jambo la kujifunza, nini tufanye tuwasaidie wananchi wetu katika suala la afya. (Makofi)
MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kituo cha afya cha Manonga jengo lake la upasuaji limekamilika; na kwa kuwa mpaka sasa hakifanyi kazi, je, Serikali ni lini, itapeleka vifaa vya upasuaji katika kituo hicho cha afya? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tuna tatizo katika kituo cha afya cha Manonga, pia tulikuwa na tatizo hili katika vituo vya afya mbalimbali ambapo tulivijenga kupitia mradi wa ADB, bahati nzuri tumepata mafanikio katika Mkoa wako katika kituo cha afya cha Itobo na Bukene vimeshaanza kufanya kazi, Manonga pale vifaa vilikuwa bado havijakamilika. Hivi sasa tunaendelea kuangalia ni jinsi gani tufanye kwa sababu pale kulikuwa na mapungufu ambayo yalijitokeza huku, katika suala zima mchakato wa ujenzi ule kuna mambo mengine hayakwenda sawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inalichukua hili tuangalie nini tufanye ili kituo cha afya cha Manonga kiweze kukamilika vizuri kuwa na vifaa pale na wananchi wa eneo lile wajisikie kwamba wana viongozi wao Mbunge wao Mheshimiwa Mwanne Mchemba na Mheshimiwa Gulamali wanawawakilisha huku. Sasa Serikali tumelichukua hili kwa ajili ya kulifanyia kazi. (Makofi)
MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni aibu kwamba Ofisi ya Waziri Mkuu, haijui mipaka ya Jimbo la Kibamba, kwa sababu kati ya kata alizozitaja kwamba ni za Jimbo Kibamba, kata zifuatazo ni za Jimbo la Ubungo. Kata ya Ubungo, kata ya Mburahati, kata ya Kimara na kata ya Makuburi. Kwa hiyo, maana yake Kata tano alizozitaja kwenye jibu siyo za Jimbo la Kibamba na siyo sehemu ya swali nililouliza. Ni aibu zaidi kwamba kasi ya upimaji ni viwanja 186 tu, kwa upande wa kata ya Kibamba. Sasa nina maswali yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu swali la msingi halijajibiwa, je, Serikali iko tayari sasa kuainisha kata kwa kata, mtaa kwa mtaa, kwa upande wa Jimbo la Kibamba, ratiba ya kuharakisha upimaji ili kuepusha sehemu hii ambayo ni Jimbo jipya kabisa nalo kuwa na makazi holela na maeneo mengi yasiyopimwa? (Makofi)
Swali la pili, matatizo haya ya kuchelewa upimaji, na udhaifu katika upimaji yamekwisha leta madhara sasa hivi tunavyozungumza ambapo Serikali imetoa notice na Mheshimiwa Naibu Waziri anafahamu kwa wananchi kutoka Stop Over mpaka maeneo ya Kiluvya mita 121 kutoka katikati ya barabara kwa maana ya mita 240 ukijumlisha pande zote mbili za barabara, wananchi wote hawa wanatakiwa kubomoa nyumba zao hivi sasa tunavyozungumza, lakini ninayo hukumu ya Mahakama ya mwaka 2013 yenye kuonesha kwamba wananchi hao walihalalishwa na hati za vijiji kwenye Kijiji cha Kimara, kijiji cha Mbezi na Kijiji cha Kibamba.
Je, Serikali iko tayari maana hili jambo tumeishauriana muda mrefu, kwa sababu sasa hivi ni dharura hili jambo, kutoa kauli ya kusitisha notice hii ya TANROADS kwanza ili majadiliano yafanyike kuhusu utata huu wa upana wa barabara, maana maeneo mengine yote ni mita 60 lakini hapa peke yake ni mita 121.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba majibu ya Serikali. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mnyika, siyo aibu kwa sababu tunajua nini tunachokifanya. Hapa tulikuwa tunazungumzia matatizo ya Watanzania kama Ofisi ya Rais – TAMISEMI na unafahamu Jimbo lako limegawanywa juzi tu.
Mheshimiwa Mnyika, ukisema aibu na wakati wewe ni Mjumbe wa Baraza la Madiwani na taarifa tunazipata mwaka mzima toka Baraza halijaanza, ndiyo maana mambo mengine ya msingi unashindwa kuyasimamia kwa wananchi wako, hilo ndio jambo la msingi lazima tukubaliane nalo.(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hiyo ndiyo hoja ya msingi kwanza, mipango ya Serikali tumesema nimezungumza maeneo mbalimbali na jinsi Serikali inavyochukua hatua mbalimbali na ndiyo nimekuambia Mheshimiwa Mnyika hii ni politics, haya ni mambo rahisi hata hayataki nguvu haya. Kikubwa zaidi naomba niwasihi Waheshimiwa Wabunge, katika mipango hii ya upimaji katika maeneo yetu tunapaswa wenyewe tuwe karibu jinsi gani tutafanya ili maeneo yetu yapimwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema katika jibu letu la msingi, leo hii ukiaangalia maeneo mengine wamefanya vizuri kwa kutumia wataalam wao mipango shirikishi zaidi na kutumia makampuni mbalimbali, kufanya mipango shirikishi ambayo mwisho wa siku inaweza kujibu jambo hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikuhakikishie kwamba Serikali imesikia kilio chako Mheshimiwa Mbunge, wala usiwe na hofu, itajitahidi kufanya kila liwezekanalo eneo la Jimbo la Kibamba kama nilivyosema, nashukuru sana, kwa sababu timu sasa iko site na Wizara ya Ardhi siku moja ilikuwa inajibu kijumla yake swali la ardhi katika Wilaya ya Ubungo kwa ujumla wake. Naomba nikutoe hofu kwamba, Serikali itashirikiana vema na Baraza la Madiwani kwa kuangalia jinsi tutakavyofanya ili tuweze kupima, ambayo itakuwa ni manufaa makubwa kwa wananchi wako. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la upana wa barabara. Upana wa barabara upo kwa mujibu wa sheria, bahati nzuri wenzetu wa Wizara ya Ujenzi hapa ndiyo wanajua sheria ukianzia ile sanamu pale Posta mpaka unafika Ubungo kuna upana maalum ambao umezungumzwa kisheria, na ukitoka pale mpaka ukija pale Kimara Temboni kuna sheria inaelekeza. Ukitoka pale mpaka unafika maeneo ya karibu na Mto Ruvu sheria inazungumza hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile kuna notice nadhani wenzetu wa Wizara ya Ujenzi wanajua nini wanachokifanya katika eneo lao hilo watatoa maelekezo kwa kadri wanavyoona kwamba inafaa, kutokana na notice iliyotolewa na utaratibu wa kisheria jinsi ulivyo katika eneo lao la kazi. (Makofi)
MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, usimamizi mzuri wa mitihani ni pamoja na kuwalipa stahiki zao wasimamizi wa mitihani wakiwemo walimu pamoja na askari, lakini mwaka 2015 walimu walisimamia mtihani ya kidato cha nne wakakopwa fedha zao, fedha hizo mpaka sasa hawajalipwa. Ninaomba kujua ni lini walimu hao watalipwa fedha zao walizokopwa wakati wanasimamia mitihani? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli mwaka 2015 tulikuwa na deni ambalo walimu walisimamia mitihani walikuwa hawajalipwa na deni lile baada ya uhakiki lilikuwa karibuni shilingi bilioni 6.4. Ninapenda kuzipongeza baadhi ya Halmashauri hasa kuna Halmashauri maalum zingine zilifanya initiative ya kulipa zile fedha karibu shilingi bilioni tatu ziliweza kulipwa, hivi sasa tuna deni ambalo ni outstanding karibuni shilingi bilioni 3.4.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba deni lile tulipeleka Hazina na liko katika hatua ya mwisho kwa wale watu ambao hawajalipwa watalipwa pesa zao.
MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwanza napenda kuipongeza Serikali kwa kuanza kutekeleza Waraka huo wa kuwalipa Posho ya Madaraka Walimu Wakuu wa Shule pamoja na Waratibu. Hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa posho hii kama ilivyoelezwa katika Waraka ni Posho ya Madaraka. Je, Serikali sasa haioni ni wakati muafaka kuanza kulipa posho hii kwa ajili ya viongozi wengine kama vile Afisa Elimu, Afisa Elimu Taaluma pamoja na Afisa Elimu Takwimu na Vifaa? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa kazi ya ualimu ni zaidi ya kufundisha, kuna kufanya maandalio, kufundisha, kusahihisha, kupanga matokeo na mengine mengi tu. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kurejesha ile tulikuwa tunaita Teaching Allowance kwa ajili ya kuwalipa walimu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mbunge kwa sababu swali hili ni concern ya walimu wote na hii kwanza mwanzo ilikuwa inajitokeza na Serikali tuliamua kuitekeleza kama tulivyosema hapo awali. Suala la jinsi gani tuangalie Maafisa Elimu Taaluma, Maasifa Elimu Takwimu watapata posho hii, nadhani vyeo hivi ni vya kimuundo ambavyo viko katika Halmashauri zetu maana yake kuna hao vilevile kuna Maafisa Kilimo na Maafisa mbalimbali. Kwa sasa kwanza tuendelee na utaratibu wa sasa na pale itakapoonekana kuna haja ya kuweza kufanya mabadiliko tutafanya hivyo. Lengo letu kubwa ni kupandisha motivation ya wafanyakazi hasa watendaji wetu katika ngazi mbalimbali waweze kufanya kazi kwa ufanisi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika jambo lingine la Teaching Allowance, hata Mheshimiwa Masoud alisimama hapa hoja yake ilikuwa ni hiyo hiyo, jambo hili tumelichukua. Bahati nzuri Waziri wetu hapa wa Utumishi kutoka Ofisi ya Rais nakumbuka mwezi Mei, 2017 alifanya mkutano rasmi wa uzinduzi wa Bodi hii. Sasa tunakwenda kuangalia suala zima la wafanyakazi katika mazingira mbalimbali maana hatuzungumzii walimu peke yake, tuna Mabwana Shamba, tuna watu wa kada mbalimbali ambao na wenyewe wako katika mazingira hayo magumu. Ndiyo maana Serikali kupitia Ofisi ya Rais, Utumishi inashughulikia jambo hili kwa upana wake lengo kubwa ni kuja na ajenda pana ya Kitaifa ni nini tufanye kutatua matatizo ya wafanyakazi walio katika mazingira mbalimbali ya utendaji wa kazi.
MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Makaimu Watendaji wa Vijiji karibu maeneo mengi ya Tanzania hawapewi posho. Je, Serikali haioni haja ya kuwapa posho Makaimu Watendaji wa Vijiji ili waweze kufanya kazi zao vizuri?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, anachosema Mheshimiwa Mpakate ni kwamba katika maeneo mbalimbali ya vijiji vyetu watu wengi wanakaimu na kuna maeneo mengine walimu ndiyo walikuwa wanakaimu kama Watendaji wa Vijiji na tumetoa maelekezo katika Kurugenzi zetu kuacha kukaimisha Watendaji wa Vijiji hasa wale walimu kwa sababu wanaondoa nguvu kubwa sana ya ufundishaji. Katika jambo hili, kila Halmashauri tumeipa maelekezo na kila Mkurugenzi anajua ana watu wangapi wanakaimu sasa kupitia own source zao wataangalia utaratibu gani wa kufanya lakini lengo kubwa tunataka katika kila kijiji kazi ziweze kufanyika.
MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu ya Naibu Waziri kwanza naishukuru sana Serikali yangu kwa maana ya kwamba iliweza kutatua tatizo la walimu waliokuwa wanapandishwa madaraja lakini hawapati mshahara. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, kwa kuwa taarifa ya uhakiki wa vyeti imeshatolewa na katika Jiji la Mbeya kuna walimu zaidi ya 200 waliobaki. Je, ni lini sasa Serikali itaruhusu marekebisho ya mishahara kwa walimu hao waliokwishapandishwa vyeo vyao kufanyika? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini la pili, kumekuwa na tatizo la watumishi kukaa katika kituo kimoja kwa muda mrefu sana na hivyo kushindwa kuleta changamoto mpya katika kipindi hiki cha Hapa Kazi Tu na kufanya kazi zao kwa mazoea. Nilitaka kujua nini mkakati wa Serikali katika hilo?Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli alichosema Mheshimiwa Dkt. Mary Mwanjelwa, alitaka time frame ni kwamba katika mwaka ujao wa fedha zoezi hili litaanza. Mheshimiwa Mwanjelwa asihofu watumishi wake watapata hiyo stahiki yao inayotakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala la watumishi wengi kukaa kituo kimoja muda mrefu, ni kweli tunafahamu kwamba mtumishi anapokaa miaka 15, 20 hana changamoto mpya ambayo anaweza akaileta katika eneo hilo. Ndiyo maana Ofisi yetu kila mwaka tumekuwa tukifanya utaratibu huo katika maeneo mbalimbali, lengo kubwa ikiwa ni kuleta hii changamoto mpya na tunaendelea kufanya zoezi hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, tuko makini
sana katika kuhamisha watumishi. Kwa mfano, tumetoa maelekezo kwa Wakurugenzi wetu kwamba waangalie jambo hilo, lakini wasihamishe watumishi hivi hivi bila kuwa na pesa yao kuweza kuwalipa. Jambo hili tumelielekeza na bahati nzuri Mheshimiwa Rais siku ya Mei Mosi alilitolea maelekezo maalum kwamba sasa hakuna utaratibu wa kumhamisha mtu kabla ya pesa yake kuwa tayari.
Naomba nimhakikishie kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI tutahakikisha tunakuza utendaji wa kazi na kuangalia mtu kama ame-over stay kwa muda mrefu tutaona namna ya kumhamishia sehemu nyingine ili kuleta changamoto mpya.
MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipatia nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo ambalo linatusikitisha ni kwamba pamoja na kupandishwa madaraja walimu hawa hawalipwi pesa zao suala ambalo linapelekea kila mwaka walimu hao kudai takribani shilingi bilioni 21. Je, Serikali haioni kutokuwapandisha madaraja na kutokuwalipa kunasababisha kulimbikiza madeni yao na ndiyo sababu inafanya walimu kutokuwa na motisha wa kazi? Ni lini sasa Serikali itawalipa fedha zao wanapopandishwa madaraja?(Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, unafahamu tumekuwa tukitoa taarifa mbalimbali ya madeni ya walimu ambayo tumekuwa tukiyalipa na tulisimama kwa ajili ya zoezi la uhakiki. Kwa hili naomba niwaambie, tumezungumza na hapa nilisema katika eneo langu la kwanza kwamba suala la malipo haya yote mwaka huu wa fedha unapokuja kila mtu atapata stahiki yake.
Serikali hii ya Awamu ya Tano lengo lake kubwa ni kuondoa hizi changamoto ndogo ndogo tulizokuwa nazo kwani tunataka tupate wafanyakazi wenye ari ya kutosha. Sisi ambao ni beneficiaries wa utekelezaji wa Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi lazima tuitekeleze, naomba nimhakikishie jambo hilo halina mashaka tutalitekeleza.
MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi ya walimu wamekuwa wakijiendeleza wao wenyewe katika vyuo mbalimbali na kupata vyeti lakini kwa muda mrefu Serikali imekuwa ikivikataa vyeti hivyo, imekuwa haivitambui. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuvitambua hivyo vyeti ili waweze kupandishwa madaraja zaidi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kujiendeleza ni kujiendeleza tu aidha Serikali imekusomesha ama umejiendeleza mwenyewe kinachotakiwa ni kujiendeleza. Ndiyo maana katika jibu la msingi mwanzo nimesema mtu akijiendeleza maana yake ana-submit cheti chake, kinapitiwa na kuhakikiwa na Afisa Utumishi mtu huyo anastahili kupanda daraja na kuwekwa katika nafasi yake anayostahili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama kuna kesi kama hiyo, maana wakati mwingine hatuwezi tukajibu kesi hapa zote kwa ujumla, inawezekana kuna case by case, kama likiwa hilo basi tunaomba tujulishane hiyo kesi imejitokeza wapi tuweze kuifanyia kazi. Mtu yeyote aliyesoma provided kwamba amesoma na ana cheti halali jambo hilo halina mashaka la kuwekwa katika muundo anaostahili. (Makofi)
MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia Serikali kwa maana ya TAMISEMI wametoa muongozo katika makusanyo yale ya Halmashauri kwa maana ya kwamba asilimia 60 zinapaswa kwenda kwenye maendeleo, asilimia 20 zinapaswa kwenda kwenye kata, asilimia 10 zinapaswa kwenda kwa vijana na wakina mama, kwa hiyo Halmashauri inabakia na asilimia 10 peke yake ambayo ndiyo sasa ilipe mishahara na kuendesha Halmashauri. Je, kutokana na hali hiyo ni kwanini sasa hawa Madiwani pamoja na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa wasilipwe moja kwa moja kutoka Serikali Kuu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; ukiwaangalia
hao Madiwani pamoja na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa wanayo majukumu mengi na makubwa kwa hiyo hata wakati mwingine wanashindwa kutekeleza majukumu yao kutokana na tabu walizonazo hasa hasa za usafiri. Je, Serikali sasa imejiandaaje kuhakikisha kwamba nao inawawezesha kupata usafiri ili waweze kutekeleza majuku yao ya kila siku?(Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ni kwamba kwanini sasa hawa Wenyeviti wasilipwe moja kwa moja kutoka Serikali Kuu na msingi umesema kwamba kwa sababu kulikuwa na suala zima la mgawanyo wa zile fedha kwamba asilimia 60 ziende katika maendeleo;
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulipowasilisha bajeti yetu mwaka Mheshimiwa Waziri alitoa ufafanuzi hapa kwa kina kwamba hili limeonekana kwa sababu lilikuwa hoja ya msingi ya Waheshimiwa Wabunge, ndiyo maana tumetoa maelekezo. Mheshimiwa Waziri alizungumza wazi hapa kwamba fedha hizi sasa zitagawanyika tofauti, kwamba kwa baadhi ya Halmashauri hasa zile ambazo uwezo wake ni mdogo, sasa asilimia 60 zitakwenda katika matumizi haya mengine na asilimia 40 itakwenda katika maendeleo, huu ndio ufafanuzi kulingana na bajeti ya mwaka huu tuliyoipitisha hapa Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hata hivyo, lengo letu kubwa katika dhana ya ugatuaji wa madaraka ni kutafuta jinsi ya kufanya katika kuongeza nguvu za Halmashauri za kuweza kukusanya mapato. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mathayo tutaendelea kulisimamia hilo, lakini kubwa na la msingi ni jinsi ya kufanya katika kukusanya vizuri mapato.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hoja ya pili, kuhusu vyombo vya usafiri; ni kweli, tukiangalia viongozi wetu wana changamoto kubwa ya usafiri, kwa sababu kama Madiwani wanafanya kazi kubwa, lakini hili naomba tulichukue sisi Serikali kwa sababu ni jambo ambalo naona ni la msingi hapo baadaye kwa kupitia Halmashauri zetu ni kwa jinsi gani tutafanya kupitia mifuko mbalimbali ili aangalau kuwezesha Waheshimiwa Madiwani waweze kupata vyombo vya usafiri. Hata hivyo jambo hili tutashirikishana vizuri kupitia katika Serikali zetu za Mitaa.
MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kama ilivyoulizwa katika swali la msingi, baadhi ya Madiwani wanaruhusiwa kuingia katika vikao vya Halmashauri husika lakini baadhi ya Wakurugenzi imekuwa vigumu kwao kuwaruhusu, na mfano mzuri ni Mheshimiwa Stella Allex Ikupa ambaye anapaswa kuingia katika Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Ilala, lakini mpaka leo hii imekuwa vigumu kuhudhuria vikao hivyo.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri unatoa kauli gani ili aweze kuingia katika Baraza hilo na kuwatendea haki watu wenye ulemavu katika kuhakikisha kwamba masuala yao yanaingizwa katika bajeti husika?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja hii nadhani kwamba imeshakwisha, kwa hiyo kama kuna ukakasi wa aina yoyote ofisi yetu italifanyia kazi; lengo kubwa ni kwamba mtu aliyepewa dhamana katika eneo hilo aweze kushiriki vizuri hasa lile kundi analoliwakilisha, kundi la walemavu.
MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante na ahsante kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri yetu ya Itilima kwa mwaka wa fedha 2017/2018 tulikaa na kupitisha katika bajeti makadirio ya shilingi bilioni 1.6 na kipaumbele chetu tukaweka shilingi milioni 650 iwe ndiyo sehemu ya ujenzi wa hospitali hiyo. Nataka kumuuliza Mheshimiwa Waziri, ni kigezo gani kilichotumika kutoka kwenye shilingi milioni 600 na kurudi shilingi milioni 179?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa Halmashauri yetu ya Itilima ina changamoto nyingi katika maeneo yetu, na tayari Halmashauri yangu kushirikiana na wananchi eneo tumeshalipata na tayari tumeshafyatua tofali zaidi ya 15,000 na hivi sasa tumekuwa tukitegemea mapato ya ndani yataweza kusaidia kusukuma uendeshaji wa jengo hilo pamoja ikiwa na zina ahadi ya Mheshimiwa Rais? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hoja inayozungumzwa na Mheshimiwa Njalu ni hoja ya msingi, na jambo hili Mheshimiwa Njalu alilizungumza mara kadhaa wakati tulipokuwa tukibadilishana mawazo, lakini jambo hili tulivyokuwa tukilifuatilia ilikuwa ni kuhusu mchakato na ilipofika decision ya mwisho, juzi nilikuwa naongea na Mkurugenzi wa Itilima kwamba nini kilijiri mpaka imefikia hapo; imeonekana kwamba baada ya kikao kile cha mwisho cha Baraza la Madiwani kulikuwa na makubaliano kutokana na fedha iliyotengwa kwamba milioni 169 iliekezwe katika suala hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo ndiyo manaa Serikali Kuu ikaongeza shilingi milioni 200 na zaidi. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge anajua kwamba haja ya suala zima la Hospitali ya Wilaya sisi kupitia Ofisi yetu hata katika commitment tuliyoweka kwa ajili ya eneo lako la Itilima ukiangalia katika maeneo ambayo tunakwenda kuboresha vituo vya afya Itilima nako tutapeleka takribani shilingi milioni 700 Mungu akijaalia kwa lengo tu kubwa la kuhakikisha kwamba wananchi wa Itilima wanapata hospitali.
Kwa hiyo, jambo hili ni la msingi na sisi Serikali tunalichukulia kwa uzito wake mkubwa sana. Jukumu letu kubwa ni kuwasaidia wananchi wako wa Itilima ambao Mheshimiwa Mbunge unawapigania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kuongeza fedha katika kuhakikisha kwamba ujenzi huu ambao unaendelea katika maeneo mbalimbali, kama tulivyosema katika bajeti ya mwaka huu wa fedha 2017/2018 katika fedha zile za CDG tumeziweka katika mafungu ambayo yatamalizia miradi mbalimbali ambayo ime-stuck katika sekta ya afya na sekta ya elimu. Jukumu letu kubwa ni kuweza kuongeza nguvu za wananchi ili hii miradi iliyoanza iweze kumalizika, kwa hiyo, Mheshimiwa Njalu naomba uwe na imani kwamba Serikali yako iko nawe kuhakikisha kwamba maendeleo katika jimbo lako ambalo ni jimbo jipya yanaweza kufanikiwa kama ilivyokusudiwa.
MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana kwa kunipa nafasi hii na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Matatizo yaliyopo huko Itilima yapo pia katika Halmashauri mpya ya Wilaya ya Itigi. Wananchi wa Itigi wanaitegemea sana Hospitali ya Mission ya Mtakatifu Gaspari hawana hospitali ya wilaya. Je, Sasa Serikali iko tayari kusaidia Halmashauri ya Itigi kujenga nayo hospitali ya Wilaya ili iondokane na gaharama kubwa wanazotumia wananchi wake ambao ni wapiga kura wetu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Itigi kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge kuna changamoto, lakini mara nyingi ndugu zangu nilikuwa nikisema hapa kwamba hili suala la ujenzi wa hospitali, ujenzi wa vituo vya afya mara nyingi michakato hii inaanza kule site chini. Hata hivyo niseme kwamba kwa kesi ya Itigi Mheshimiwa unakumbuka kwamba umeuliza swali hili mara kadhaa na ndiyo maana kutokana kwamba umeliuliza swali hili mara kadhaa, hata Serikali sisi kupitia ofisi yetu iliona lazima iipe kipaumbele Itigi kwa sababu hakuna Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulipokwenda kutembelea pale Itigi tulikuta kituo cha afya ambacho hali yake si shwari, tukasema tunaanza na hapa. Ndiyo maana muda si mrefu ujao tutakwenda kujenga centre ya upasuaji kubwa sana na kujenga wodi zingine. Lengo kubwa ni kukiboresha kile Kituo cha Afya cha Itigi angalau kiweze kutoa huduma ambayo inalingana lingana japo na hospitali ili wananchi wa Jimo lako waweze kupata huduma vizuri.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.
Kama ambavyo Halmashauri ya Itilima ilivyokuwa na tatizo la Hospitali ya Wilaya, Wilaya ya Liwale ni Wilaya ya zamani sana na lile jengo lake la Hospitali ya Wilaya limeshachakaa na limezidiwa uwezo. Kwa kutambua hilo Halmashauri yetu ya Wilaya ya Liwale imetenga eneo kama hekari 50 hivi kwaili ya mradi wa hospitali mpya ya Wilaya ya Liwale. Je, Serikali ipo tayari kutuunga mkono katika mradi huu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anafahamu tulikuwa wote site siku ile Liwale na mvua ilikuwa kidogo inanyesha na tumefika Hospitali yake ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wao Liwale pale wana hospitali ya Wilaya, lakini ni hospitali ya muda mrefu sana. Kama wazo hilo zuri lilivyo ambapo mnafikiria kujenga hospitali mpya Serikali haitoshindwa kuungana nanyi, lakini hayo mawazo lazima yaanze kwenu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na ndio maana kwa kuona umuhimu wa Serikali Mheshimiwa Rais alipita kule kutoa ahadi, na kwa sababu hiyo katika kile Kituo cha Afya cha Kibutuka kwa maagizo ya Mheshimiwa Rais, tutakifanyia ukarabati mkubwa Kituo cha Afya cha Kibutuka kwa kujenga theater pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo kubwa ni kwamba
kina mama wanaopatikana katika eneo lile waweze kupata huduma. Kwa hiyo, Serikali itakuwa tayari kushirikiana na mipango mizuri ya pale.
MHE. ELIBARIKI E. KINGU: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya kaka yangu Mheshimiwa Jafo, nilikuwa nataka nipate hakikisho kwa sababu hivi tunavyozungumza mimi na wananchi tumeanzisha ujenzi wa zahanati katika vijiji 19 kwa nguvu zetu.
Mheshimiwa Spika, sasa Mheshimiwa Naibu Waziri atanihakikishia kwamba zahanati hizi za Nkunikana, Puma, Msambu, Unyangwe, Chungu, Kinyampembee, Mpetu, Mayaha, Misake, Maswea, Nsogandogo, Kipunda, German, Mahonda, Iyumbu, Mlandala, Kaugeri, Mduguyu, Mpugizi na Namnang’ana ambazo tumezianzisha kuzijenga ndani ya kipindi cha miaka miwili katika huu mgao, Mheshimiwa Naibu Waziri ananihakikishia kwamba na zenyewe zinakwenda kukamilishwa? Hizi ambazo tumezianzisha sisi.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza kama nilivyosema pale awali, napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Kingu kwa kazi kubwa anayofanya katika ile Wilaya yote ya Ikungi kwa ujumla wake.
Mheshimiwa Spika, katika mpango wa bajeti wa mwaka huu tumetenga karibuni shilingi bilioni 251 katika Local Government Development Grants, lakini katika hizo karibu shilingi bilioni 68 kwa ajili ya kuboresha vituo vya afya na zahanati, yaani yale maboma yaliyojengwa. Katika hizo nilisema pale awali 1.4 billion ni kwa ajili ya Halmashauri ya Ikungi.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba tu Kamati ya Fedha itakapokaa pale, katika vipaumbele vya umaliziaji wa maboma, haya maeneo ambayo tumesema tutawaletea fedha, basi ni vyema katika ule mpango ni lazima tuhakikishe maboma haya yamekamilika kwa sababu Serikali ndiyo imeshafanya jambo lake hilo.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, Mheshimiwa Kingu alileta concern kubwa ya Halmashauri yake kuhusu changamoto ya afya. Ndiyo maana kama Serikali kwa ujumla, hivi sasa tunawapelekea fedha za kwanza, karibu shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya pale Ihanja ambapo tunajua pale kutakuwa na theater kubwa na maabara. Kwa hiyo, eneo lile litabadilika.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kutakuwa na fedha nyingine kwa ajili ya ununuzi wa vifaa. Kwa hiyo, Serikali iko tayari kuhakikisha kwamba wananchi wa Halmashauri yote ya Ikungi inapata huduma nzuri kama tunavyotarajia.
MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Matatizo yaliyoko huko Singida Magharibi yanafanana kabisa na yaliyoko katika Jimbo la Manyoni Magharibi, na sisi tumeanza kujenga zahanati nyingi.
Je, Serikali iko tayari sasa kuiongezea mgao Halmashauri ya Itigi ili iweze kufunika maboma ambayo tayari tumeshayaanza katika vijiji vya Mbugani, Mnazi Mmoja, Tulieni na vijiji vingine vingi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli anachoshuhudia Mheshimiwa Mbunge kwamba tulipofika pale Itigi katika Halmashauri ya Itigi, lakini bahati mbaya wao hawana Hospitali ya Wilaya. Ndiyo maana mpango wa Serikali ni kuhakikisha kwamba Halmashauri ile ambayo kwa jiografia yake mara nyingi wanatumia kile Kituo cha Kanisa kama ndiyo sehemu kubwa ya utoaji huduma ya afya, Serikali hatutasita kutoa ushirikiano.
Mheshimiwa Spika, katika ule mpango ambao fedha ambazo tumetenga; na Halmashauri hiii tutaipa kipaumbele. Kwa hiyo, Mkurugenzi ahakikishe yale maboma yaliyoanzwa kujengwa, yamemilika. Hata hivyo, kuna mpango kwamba, tutaisaidia Itigi as a special case kuona ni jinsi gani wananchi wa Manyoni Magharibi wataweza kupata huduma nzuri.
MHE. DKT. PUDENSIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kumweleza kwamba, pamoja na kwamba Serikali ina nia njema ya kuweka sekondari za wasichana kila tarafa na kwa sasa katika Jimbo langu ama Mkoa wa Katavi kila tarafa bado haijawa bado na Sekondari za form five na six.
Je, haoni sasa kuna umuhimu na ulazima wa hii Shule ya Sekondari ya Mpanda kuanza sasa kwa kidato cha kwanza mpaka cha sita ili tuweze kuzuia mimba za utotoni kama sera na Serikali inavyosema?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kama Serikali, tunaona umuhimu hasa wa kupunguza mimba za utotoni na kwa wasichana ambao Mheshimiwa Mbunge amekuwa akiwapigania hapa.
Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, kama ikiwezekana basi mchakato huo utaanza katika vikao husika kuanzia Baraza la Madiwani then itaenda katika Kamati ya Ushauri ya Mkoa, then itafika kwa Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana ya sekta ya elimu na hapo akiridhia jambo hilo basi litaanza. Kwa hiyo, hili jambo halina mashaka, ni suala zima la kuangalia ni jinsi gani tutafanya.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, tunasisitiza na Serikali inaweka nguvu ya kutosha na kama kuna changamoto kubwa, tutaona jinsi gani tutafanya ikiwa hata kuanzisha shule nyingine mpya zenye ubora unaofanana na ule. Lengo kubwa ni kuhakikisha watoto wetu hasa wasichana waweze kusoma katika mazingira rafiki tupate viongozi na wataalamu wa baadaye.
MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Na mimi napenda kuuliza swali la nyongeza.
Swali ambalo Mheshimiwa Kikwembe ameuliza ni kwamba katika shule nyingi ikiwemo Ndanda Sekondari, Loleza na shule nyingi ambazo zilibadilishwa, zilizokuwa za wasichana na wavulana zikawa za wavulana. Hata hivyo, hizo shule hazijai kwa sababu shule ambayo ilikuwa kidato cha kwanza mpaka cha sita, leo unaifanya ya kidato cha tano tu na cha sita. Mabweni ni mengi. Nenda Loleza, hayajai; Ndanda hayajai; Mtwara Girls na shule nyingine nyingi. Maombi tayari yalishakuwa yamefika TAMISEMI na mchakato wa kufanya tathmini ulishaanza.
Je, ule mchakato ulisimama kwa tatizo gani? Nilichokuwa namuomba Mheshimiwa bado warudi wakalifanyie tathmini suala hilo kwa sababu majengo mengi yako idle na wanafunzi hasa wa kike wanakosa pa kwenda?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa ku-raise concern ambayo na sisi Serikalini tunajaribu kuitafakari. Maamuzi haya yalipofanyika pengine hatukufanya uchambuzi vizuri. Kuna faida kubwa shule inapokuwa na O-level na A- level kwa pamoja kuliko unapoamua A-level wakawa peke yake na O-level wakawa peke yake.
Hata hivyo, tunaendelea kuwasiliana na wenzetu wa Wizara ya Elimu ili tuweze kuona namna ya kurudisha kwa haraka tu, kwa sababu ni suala dogo tu; kurudisha ile miundombinu ipo na pengine maeneo mengine miundombinu imekuwa ikiharibiwa kwa sababu haitumiki. Kwa hiyo, concern ya Mheshimiwa Hawa Ghasia ni ya kweli na tutajaribu kuchambua kwa shule zote nchi nzima tuweze kuona namna ya kuzirudisha shule katika mfumo ule wa zamani ulivyokuwa. (Makofi)
MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, asante sana. Kwanza niipongeze Serikali kwa mpango mzuri wa kunipatia fedha shilingi milioni 18. Nina maswali mawili ya nyongeza. Ukiacha fedha ambayo napewa na Serikali milioni 18 Serikali iliniahidi kunipatia fedha zaidi ya milioni 60 na ikatoa milioni 20 toka 2012 hadi leo hii milioni 40 hawajanipatia. Ni lini ahadi ya Serikali ya milioni 40 ambazo waliniahidi kunipatia ili nimalizie sehemu ya vijiji ambavyo vimebakia vya Kwemshai na Mnungui itatimia?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Shirika Lisilokuwa la Kiserikali liliamua kunipatia fedha na kuchimba visima tisa katika Jimbo langu la Korogwe Vijijini na baadhi ya sehemu Serikali iliamua kuchukua dhamana ya kufunga pampu na kusambaza maji. Katika sehemu hizo Serikali iliamua kwamba katika Kijiji cha Lusanga Mnyuzi, Makuyuni, Kwikwazu pamoja na Kerenge kibaoni kwamba watafunga maji hayo na kuyasambaza. Je, ni lini maji haya yatapelekwa katika vijiji ambavyo Serikali iliamua kwamba watawapelekea maji?
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS - TAMISEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli na niweke rekodi sawa kwamba milioni 81 si milioni 18 ambayo tumeweka katika mpango wa Serikali wa mwaka huu. Mradi ule kutokana na tathmini tuliyofanya tunahitaji karibuni milioni 415. Kwa hiyo hii sisi watu wa Pwani tunasema kama kiingilia mbago tu. Nakumbuka tulipokuwa na Mheshimiwa Rais pale Korogwe Mheshimiwa Mbunge alizungumza hoja hii hasa ya maji katika jimbo lake na Mheshimiwa Rais aliibeba kwa ukubwa wake katika Wilaya nzima ya korogwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie kuwa ni mipango ya Serikali, ukiachana na suala hili la bajeti lakini kwa ahadi ya Mheshimiwa Rais tutafanya kila liwezekanalo ili Wilaya yote ya Korogwe Mjini na Vijijini kama tulivyoelekeza siku ile katika mkutano wetu mambo yatakuwa sawasawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika ajenda nyingine ya wafadhili wetu, tunajua kwamba kuna World Vision kule walifanya kazi na taasisi zingine walifanya kazi kubwa sana. Naomba nimhakikishie, Serikali tumeshaanza kutafuta jinsi ya kufanya ili ahadi ya Serikali juu ya maji iwafikie wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, jana tulisikia kwenye vyombo vya habari, walikuwa wakionesha jinsi wananchi wa jimbo lake walivyokuwa wakishangilia maji kutokana na juhudi kubwa inayofanywa na Waheshimiwa Wabunge wawili katika Wilaya ya Korogwe. Kwa hiyo niwahakikishie kwamba tutatafuta namna ya kufanya ya pamoja kuzishughulikia changamoto tulizobaini kwa kushirikiana na Wizara ya Maji ili ahadi ya Mheshimiwa Rais iweze kutekelezeka na hivyo wananchi wa Korogwe wapate maji safi na salama.
MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitumie fursa hii pia kuishukuru Serikali kwa kutuongezea matenki mawili ya maji katika Kata ya Nalalami na Moita.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, kwa kuwa mradi huu kweli umeanza katika Kata ya Sepeko katika Kijiji cha Lendikinya lakini mradi huu umesimama karibu miezi miwili na miradi mingine minne katika Jimbo la Monduli kwa sababu ya upatikanaji wa fedha ambapo wakandarasi wameandika barua ya kusimamisha mradi na hakuna kazi yoyote inayoendelea kwa sababu Serikali imeshindwa kulipa fedha kwa wakati kwa wakandarasi. Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusu kulipa fedha za wakandarasi ili waweze kurudi site na kuendelea na mradi kwa ajili ya kuwapatia wananchi maji katika kipindi hiki ambacho kiangazi kimeanza?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa tatizo la maji na lenyewe limeendelea kuwa kubwa nchini ni lini Serikali itafanya utafiti wa kutambua ukubwa wa tatizo kwa kila halmashauri katika nchi yetu ili kuleta mipango thabiti ya kuwapatia wananchi maji, kuliko ahadi hizi ambazo zinachua muda kukamilika?
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS - TAMISEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nipokee hii concern kwamba certificate zimeenda lakini bado hazijalipwa. Naomba niweke kumbukumbu sawa; juzi nilitoka Malinyi nilikutana na mradi mkubwa wa maji ambapo tulipata concern kama hiyo. Kwa kushirikiana na Wizara ya Maji tutaziangalia zile certificate ambazo wakandarasi wameshapeleka ambazo zinahitaji malipo zifanyike kwa haraka. Lengo kubwa ni kuwa wakandarasi waendelee na miradi ili ikamilike na wananchi waweze kupata maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kufanya utafiti katika halmashauri zote; nakumbuka, tukifanya rejea katika Bunge la Bajeti, nilizungumza na kuziagiza halmashauri zote zifanye tathmini ya miradi yote inayotengenezwa kwa sababu tunaona kwamba tuna idle project maeneo yote ya nchi na nilitoa deadline siku ile nikiwa hapa Bungeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa bahati nzuri tumeshapata tathmini ya nchi nzima ya miradi yote nini kimekwamisha. Lengo letu ni kujua changamoto zinazoikabili miradi ya maji na nini tufanye. Kwa hiyo mpango huo Mheshimiwa Julius tumeshaenda mbele zaidi, tumeshafanya hilo. Ofisi yetu pale sasa hivi kupitia team ya ma-engineer wetu wanafanya kazi kubwa ya kufanya uchambuzi na kuweka mikakati ambayo italeta majibu ya kuhakikisha miradi hii tunaiwekea mipango sahihi ya kuweza kuitekeleza ili wananchi waweze kupata huduma ya maji kama tunavyokusudia.
MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini maswali mawili ya nyongeza ni kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa Sera ya Afya inasema itajenga zahanati kila kijiji na pia itajenga vituo vya afya kila kata na pia itajenga Hospitali za Wilaya kila wilaya. Je, ni lini sera hii itatekelezwa kikamilifu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa afya ni kipaumbele cha mwanadamu hasa kwa mama na mtoto, je, Serikali haioni umuhimu wa kuupa kipaumbele Mkoa wa Rukwa kwa kuwa hauna Hospitali ya Wilaya hata moja? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli sera yetu inatueleza hivyo na ndiyo maana ukiangalia mchakato wa Serikali kwa kushirikiana na ninyi Waheshimiwa Wabunge, wananchi na wadau mbalimbali mnaona ni jinsi gani tunajitahidi kwa kadri iwezekanavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli naomba nitoe pongezi zangu za dhati, katika maeneo mbalimbali nilikopita nimekuta Wabunge wengi sana na wengine wakitumia Mfuko wa Jimbo na kuungana nguvu na wananchi katika suala zima la ujenzi wa zahanati na vituo vya afya. Nilishawahi kuzungumza hapa siku za nyuma kwamba katika bajeti ya mwaka 2017/2018 tumetenga shilingi bilioni 251 lakini katika hizo shilingi bilioni 68 ni kwa ajili ya ku-top up shughuli hizo za ujenzi wa zahanati huko tunakokwenda kumalizia haya maboma.
Kwa hiyo, mpango wa Serikali ni kuhakikisha kwamba tunafanya kila liwezekanalo sera hii iweze kutekelezwa. Najua kila jambo lina time frame, katika miaka hii mitano mtaona mabadiliko makubwa sana katika sekta ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mahsusi katika Mkoa wa Rukwa, ni kweli kuna changamoto kubwa sana ndiyo maana Serikali tukaona katika Halmashauri zake kutokana na changamoto lazima tuboreshe kwanza vituo vya afya vilivyopo. Leo hii kwa kaka yangu Mheshimiwa Ally Keissy kule Nkasi amepigia kelele sana Kituo chake cha Kirando, tumefanya utaratibu tunaenda kujenga theatre na majengo mengine. Ukienda pale Sumbawanga DC halikadhalika kuna suala la ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mirepa lakini hilo tutafanya kwa kadri iwezekanavyo na ndiyo maana katika Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo hivi sasa tumepeleka karibia shilingi milioni 340 kwa ajili ya zoezi la ujenzi wa Hospitali ya Wilaya.
Kwa hiyo, ni jukumu la Serikali kuhakikisha Mkoa wa Rukwa nao uweze kujengewa miundombinu ili wananchi wa kule waweze kupata huduma nzuri za afya.
MHE. OMARY A. BADWEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ili nami niulize swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Wilaya ya Bahi nayo ni miongoni mwa Wilaya hizo kadhaa ambazo hazina Hospitali ya Wilaya na kumekuwa na matatizo mengi sana, lakini pale Bahi tuna kituo cha afya ambacho hakijafikia level ya upasuaji.
Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kuwaambia wananchi wa Bahi kwamba labda upo mpango wowote mzuri wa kusaidia kile Kituo cha Afya Bahi ili angalau hatua ya upasuaji hasa akina mama na huduma zingine muhimu ziwepo? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nimefika mara mbili kwenye Halmashauri ya Bahi na juzi juzi tulikuwa na Mheshimiwa Mbunge jimboni kwake takribani mwezi mmoja na nusu na bahati mbaya Bahi hawana Hospitali ya Wilaya wala vituo vya vya afya na kile kimoja kiko katika hali mbaya. Kutokana na maombi ya Mbunge tayari tumeshapeleka shilingi milioni 500 ndani ya wiki hii. Tunaenda kukiimarisha Kituo cha Afya cha Bahi, tunakijengea miundombinu ya upasuaji na maabara. Nia yetu ni kwamba Bahi pale huduma zote za msingi ziweze kupatikana kwa ukaribu zaidi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge, ombi lako limekubaliwa na Serikali na tunalifanyia kazi. Lengo letu ni kwamba wananchi wa Bahi wapate huduma nzuri kama wananchi wengine.
MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa ni zaidi ya miaka 53 toka nchi imepata uhuru sehemu yenye hadhi ya mkoa kama Mkoa wa Rukwa hatuna Hospitali ya Wilaya hata moja. Serikali haioni umuhimu sasa wa kuondoa aibu hiyo angalau hata wilaya mbili zipate hospitali ya wilaya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu, Wabunge wote wa Rukwa wakisimama hapa ajenda kubwa ni afya kwa sababu ni kweli siyo jambo la uongo. Ndiyo maana hata nilivyokuwa nikimjibu Mheshimiwa Bupe swali lake lile la msingi la kwanza nilizungumza kwa ujumla wake. Ndiyo maana tumesema mipango ya Serikali katika Halmashauri ya Kalambo sasa hivi kati ya shilingi bilioni 1.4 tuliyoitenga tumepeleka karibu shilingi milioni 340 lakini hili tutalisimamia vizuri katika mwaka huu wa fedha angalau Kalambo ujenzi uende kukamilika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hali kadhalika ukiangalia pale Sumbawanga DC hali ni mbaya vilevile, lakini hivi sasa katika Kituo cha Afya cha Mwimbe tumepeleka fedha karibuni shilingi milioni 500 lakini kule Nkasi tumeshaanza kushughulikia matatizo yake. Jukumu hili lote ni la Serikali. Naomba muwe na imani kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano, commitment yake ile mikoa ambayo ina changamoto kubwa sana tutafanya kila liwezekanalo kuhakikisha wananchi wa mikoa hiyo wanapatiwa huduma.
Kwa hiyo, Mheshimiwa dada yangu naomba nikusihi kwamba Serikali hii iko nanyi Wabunge wa Rukwa wala msiwe na hofu, tutajitahidi kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha huduma ya afya inapatikana vizuri zaidi.
MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. RCC ya Mkoa wa Kagera ilishatoa kibali kuhusu ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Karagwe, lakini suala hilo linakwamishwa na Wizara ya TAMISEMI kwa sababu haitaki kutoa usajili ili hospitali hiyo itengewe bajeti na ujenzi uanze mara moja. Je, ni lini Wizara ya TAMISEMI itaamua kutoa usajili huo ili ujenzi uanze mara moja ili kuokoa akina mama na watoto?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la dada yangu Mheshimiwa Halima Bulembo na kwanza nimpe hongera sana kwa kazi kubwa aliyofanya katika sekta hii ya afya, hongera sana. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, bahati nzuri nimefika Karagwe, bahati nzuri pia anafahamu hata pale Karagwe kulikuwa hakuna DMO. Sisi TAMISEMI ndiyo tukamchukua kijana mmoja anaitwa Sobo tukampeleka pale, ni daktari mzuri sana wa upasuaji. Hata Karagwe pale tulikuwa hatuna centre ya Serikali ya kufanya upasuaji sasa hivi upasuaji pale Karagwe katika kituo cha afya umeanza.
Si hivyo tu, lilivyotokea tetemeko la ardhi, Serikali imefanya juhudi kubwa sana kuboresha kile kituo cha afya na hivi sasa tunapeleka takribani shilingi milioni 500 kufanya wananchi wa Karagwe wanapata huduma nzuri ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwahakikishie kwamba katika ofisi yetu hakuna kibali kitakachokwama isipokuwa wakati mwingine ni changamoto ya bajeti. Tunachukua mawazo yote ya Wabunge wa Karagwe, tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo kutekeleza vipaumbele vyenu mlivyoweka katika mpango wa bajeti maana siyo suala la kibali, kibali sisi hamna tatizo isipokuwa ni pamoja na kuona ni jinsi gani tutenge bajeti kuhakikisha tunajenga hospitali ya wilaya.
Kwa hiyo, ni jukumu la Serikali, tutafanya kila liwezekanalo wananchi wa Karagwe kama tunavyofanya sasa tutaendelea kufanya hivyo ili mradi huduma ya afya ipatikane vizuri katika Wilaya ya Karagwe na Halmashauri yake kwa ujumla. (Makofi)
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Tanganyika ni miongoni mwa wilaya mpya ambazo hazina huduma ya hospitali ya wilaya. Kwa nyakati tofauti, Serikali imekuwa ikiahidi Kituo cha Afya kijiji cha Majalila ambako ni Makao Makuu ya Wilaya. Nilikuwa nataka kujua kauli ya Serikali, je, Kituo kile cha Majalila, ni lini kitaanza kupewa fedha na hatimaye kuanzisha ujenzi wa kituo cha afya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Wilaya ya Tanganyika imegawanyika kutoka Mpanda na mimi Mbunge nafahamu tulifika pale kwake ni kweli kuna tatizo kubwa sana. Kwa mfano wananchi wanaotoka Mwese wakija Mpanda Mjini ni tatizo na tulifika pale Majalila ambapo Makao Makuu ya Wilaya ile inataka ijengwe, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hivi sasa tumetenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya Halmashauri yako ya Wilaya. Juzi nilikuwa naongea na Mkurugenzi wako wa Mpanda DC kuangalia jinsi gani tutafanya.
Kwa hiyo, kuna shilingi milioni 500 tunawaletea na hii sisi tunasema kama ni kingiambago tu, ni fedha ya kwanza tutatoa fedha nyingine kwa ajili ya kununua vifaa ambayo jumla yake itakuwa karibuni shilingi milioni 720. Kwa hiyo, naomba niwahakikishie wananchi wa Tanganyika hili ni jukumu la Serikali kuwafikia watu wote hata ndugu yangu wa Kakonko tulifanya jambo hili kwa sababu siku ile tuliyofika shida ilikuwa kubwa. Hii ni kazi ya Serikali na itafanya kazi kila mahali kwa manufaa ya wananchi wake wa Tanzania.
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, LEKIDIA imekuwa ikishirikiana na wananchi katika kuibua vipaumbele vya maendeleo katika Kata ya Kirua Vunjo Mashariki kwa muda mrefu na kipaumbele cha sasa ni hii barabara ya Uchira - Kisomachi - Kolaria ambao wamejitahidi kuchanga fedha na sasa wana lami pipa 300. Kipaumbele chao ni kwamba hii barabara ijengwe kwa kiwango cha lami.
Je, Serikali ina mpango gani wa dharura wa kusaidia ili lami hii isije ikaharibika kujenga walau hatua kwa hatua kilometa tano na baadaye kilometa nyingine tano ili hatimaye hii barabara iweze kukamilika kwa kiwango lami badala ya kutumia fedha nyingi kwa ukarabati mara kwa mara?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, wananchi wamekuwa wakishiriki sana katika kuchangia maendeleo, wamekuwa wakichangia ujenzi wa zahanati, vituo vya afya, shule na kadhalika. Katika Jimbo langu la Rombo karibu kila kijiji kuna miradi ya maendeleo inayoendelea kwa michango ya wananchi lakini kwa upande wa Serikali fedha zimekuwa haziendi kwa wakati jambo ambalo sasa linawavunja moyo wananchi.
Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusu upelekaji wa fedha za maendeleo jinsi ambavyo zimekubaliwa kwenye bajeti ili kuwatia moyo wananchi hao waendelee kuchangia shughuli za maendeleo ambazo tayari zimeshaanza?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli LEKIDIA wamechanga wamenunua mapipa takribani 340 kwa rekodi niliyokuwa nayo. Ndiyo maana katika jibu langu la msingi nimesema kwa sababu sasa hivi tumeunda Wakala mpya wa TARURA na bahati nzuri tumepata Meneja maalum wa mradi katika Halmashauri ya Rombo na katika Halmashauri zote Tanzania. Meneja hawa jukumu lao sasa ni kufanya needs assessment katika kila Halmashauri. Tuagize Meneja wetu apitie barabara hiyo then ataleta tathmini halafu tutajua nini cha kufanya katika barabara hiyo. Kwa hiyo, ni jukumu kubwa la Serikali kuhakikisha barabara hizi zote zinafanyiwa matengenezo. Kwa hiyo ni commitment yetu Serikali kwa Tanzania nzima, hili jambo tutaenda kulifanya nikitambua juhudi kubwa ya wananchi wanayoendelea kuifanya, lazima tuwaunge mkono. Kwa hiyo, kazi itafanyika baada ya tathmini ya Mameneja wetu walioko site kuangalia kipi kilichopo na kipi kifanyike katika utaratibu gani.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala zima la upelekaji wa fedha, nimesema hapa kwa mfano fedha za barabara tumetenga karibuni shilingi bilioni 263 lakini hizi kuna fedha za barabara zenye vikwazo lakini zingine za road fund na maeneo mbalimbali. Ni jukumu la Serikali kuhakikisha tunapata fedha hizi na bahati nzuri jana tulikuwa na Waziri wa Fedha katika kikao chetu cha mambo ya lishe amesema commitment ya Serikali katika mwaka huu wa fedha ni kuhakikisha fedha zote za maendeleo zinafika katika maeneo husika. Kwa hiyo, ondoa hofu, jukumu letu sasa hivi naomba tuungane mkono wote kwa pamoja tukusanye mapato, tulipe kodi na mwisho wa siku kwamba fedha hizo zitapelekwa katika vijiji vyetu kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma nzuri katika maeneo mbalimbali.
MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu aliyotoa Naibu Waziri, lakini Jimbo langu la Tunduru Kusini vituo vyake vya afya vimechakaa na vina hali mbaya na vina matatizo lukuki pamoja na uhaba wa wafanyakazi,hakuna gari, wala chumba cha upasuaji.
Swali langu, ni lini Serikali itahakikisha vituo hivi vya afya vinapata watumishi wa kutosha ili viweze kuhudumia wananchi wa Tunduru?
Swali la pili, katika kampeni ya uchaguzi mwaka 2010, Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kujenga kituo cha afya katika Mji wa Nalasi ambao una zaidi ya watu 25,000. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hii ya kujenga kituo cha afya pale Nalasi ili kuweza kuwahudumia wananchi wale ambao wako katika vijiji sita katika Mji ule wa Nalasi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, katika suala zima la kuongeza watumishi, Serikali hivi sasa iko katika mchakato wa kuajiri watumishi mbalimbali. Katika hilo Jimbo la Tunduru tutalipa kipaumbele katika suala zima la mgawo wa watumishi kwa sababu Tunduru ina changamoto kubwa sana.
Mheshimiwa Spika, eneo la pili nashukuru Mheshimiwa Mpakate alini-accompany vizuri sana wakati nimeenda katika Jimbo lake. Ni kweli watu wasioijua Tunduru, ukitoka barabarani mpaka Jimbo la Mheshimiwa Mpakate kuna changamoto kubwa sana. Ndiyo maana Mheshimiwa Mbunge alipoleta request, tukaamua kipaumbele cha kwanza twende tukamjengee kurekebisha Kituo cha Afya cha Mkasare.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba leo ninavyozungumza tayari tumeshaingiza shilingi milioni 500 kwa ajili ya kituo kile. Katika kituo kile tutajenga jengo la upasuaji, mortuary, wodi ya wazazi na tutafanya ukarabati mwingine halafu tutawawekea vifaa. Vilevile eneo hili la pili tutaliangalia kwa sababu lengo letu kubwa ni wananchi wa Tunduru waweze kupata huduma nzuri ya afya kwa sababu tunafahamu Wilaya ya Tunduru kwa jiografia yake, changamoto ya afya ni kubwa sana.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mpakate kwamba ahadi na maombi yake tulipokuwa katika mkutano, tumeyatekeleza na tunaendelea kuyafanyia kazi kwa kadri iwezekanavyo.
MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa jibu la Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini napenda tu kujua, maana sasa wamesimamia kwa muda mrefu tangu mwaka 2015/2016 ni muda mrefu sasa.
Je, ni lini sasa uhakiki huu utaweza kukamilika ili walimu waweze kulipwa madai yao? (Makofi)
Swali la pili, katika madai hayo, walimu tu Wilaya yetu ya Geita wanadai zaidi ya shilingi milioni 120, napenda pia kujua ni lini walimu hawa wanaotoka Wilaya yangu ya Geita wataweza kulipwa madai yao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, katika level mbalimbali, mchakato huu wa uhakiki wa deni umeshakamilika. Kwa hiyo, nadhani Hazina sasa hivi wanajipanga, wakati wowote deni hili litaweza kulipwa ili mradi kila mtu haki iweze kupatikana.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo najua Mheshimiwa Bukwimba ni mpiganaji mkubwa sana wa watumishi wake katika jimbo lake, lakini siyo jimbo lake peke yake isipokuwa katika maeneo mbalimbali. Katika eneo la Jimbo lako kwamba lini watalipwa mgao huu wa deni hili ambalo Hazina wanalishughulikia, likilipwa lote litalipwa kwa pamoja.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba tuvute subira kwa sababu Hazina ndiyo walikuwa wanafanya uhakiki wa madeni mbalimbali siyo wa walimu ni mchakato wa kulipa madeni mbalimbali. Jambo hili litakamilika na wananchi wa Busanda kule katika jimbo lako Geita wananchi wa eneo lile watapata hasa hasa watumishi wa Serikali ambao ni walimu watapata madai yao kama ilivyokusudiwa.
MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa muda mrefu sasa Halmashauri nyingi nchini zimekuwa zikipoteza mapato ambayo yamepotea kupitia kampuni mbalimbali za simu kwa kutokulipa hizo service levy katika maeneo mengi nchini.
Je, ni lini sasa Serikali itazibana kampuni hizo ili ziweze kulipa hiyo service levy?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kutokana na Halmashauri nyingi nchini kuwa na vyanzo vichache vya mapato. Je, ni lini Serikali itaweza kufanya mpango wa kuziongezea Capital Development Grants Halmashauri hizo nchini? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI MIKOA: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Ester kwa sababu najua kwamba anaguswa na Halmashauri zake zote ambazo anazisimamia katika mkoa wake. Naomba niwahakikishie kwamba ndiyo maana tumeandaa sheria hii ya fedha, mabadiliko ya Sura Namba 290 kwa lengo la kufanya utaratibu mzuri wa kukusanya hizi kodi.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Ester amezungumzia suala zima la minara ambalo lilikuwa linaleta mkanganyiko mkubwa sana. Katika jambo ambalo litashughulikiwa kwa undani zaidi ni suala zima la ushuru wa minara ambalo tunaliwekea utaratibu kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Spika, nina imani ikifika hapa Bungeni, tutajadili tuone ni utaratibu gani tutafanya. Ninaamini na sheria itakuja siyo muda mrefu, tutaweka utaratibu mzuri ili tuweze kuwabana vizuri hawa wenye makampuni mbalimbali hasa ya simu, waweze kulipa kodi vizuri. Lengo kubwa ni kuziwezesha Halmashauri zetu ziweze kufanya vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, katika mchakato huu wote wa sheria hizi, lengo kubwa la Serikali ni kuziongezea Halmashauri zetu uwezo wa kupata mapato ya kutosha kwa ajili ya kujiendesha.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, katika suala zima la kujiendesha, kuongeza ile Capital Development Grand ni jukumu la Serikali. Ndiyo maana hata ukiachia hilo, ukiangalia ile Local Government Development Grants hata mwaka huu tumeongeza zaidi ya shilingi bilioni 251 kwa lengo tu la ku- facilitate Halmashauri ziweze kufanya kazi yake vizuri.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, eneo hilo tutaangalia nini tufanye Halmashauri zetu ziweze kufanya vizuri tukijua kwamba Halmashauri zikifanya vizuri ndiyo nchi itaenda vizuri katika suala zima la maendeleo.
MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Naomba kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri kukubali kwamba watafanya mazungumzo na mmiliki ambaye ni Chama cha Mapinduzi, shule hii ni muda mrefu sana imefungwa, karibu miaka kumi hamna mwanafunzi anayesoma pale. Ni kwa nini msione sasa ni wakati muafaka wa kuirudisha kwa wananchi ili tuweze kuitumia?
Mheshimiwa Spika, ombi letu la pili, tunaomba shule hii tuitumie kwa ajili ya kidato cha tano kwa sababu Halmashauri ya Wilaya Momba haina shule ya kidato cha tano? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema shule hii inamilikiwa na Chama cha Mapinduzi kupitia Jumuiya yake ya Wazazi. Kwanza naishukuru Jumuiya ya Wazazi kwa sababu imefanya intervention kubwa kwa nchi hii kujenga shule mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa kweli naomba niweke katika kumbukumbu kwamba Jumuiya ya Wazazi kupitia Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, alitusaidia sana kupatikana kwa Shule ya Umumwani, ambayo Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo alikuja kutukabidhi pale na juzi nimeenda kule Kagera watoto wanasoma pale. Kwa hiyo, tunaishukuru sana jumuiya hiyo kwa kazi kubwa sana inayofanya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kama Serikali, hatuwezi kuirudisha tu hivi hivi, isipokuwa kuna utaratibu wa negotiation, pale Jumuiya ya Wazazi itakapoona inafaa, kwa sababu jukumu lake kubwa ni kuwasomesha watoto wa Tanzania kwa mbinu muafaka, basi inawezekana tukaongea na Mwenyekiti pale ambaye nadhani ni Mjumbe wa Kamati Kuu, aangalie nini cha kufanya, aidha kuiboresha mwenyewe ili ichukue watoto ama kuangalia utaratibu kama alivyotusaidia kule Umumwani kwa lengo la kuwasaidia Watanzania. Hili siyo jambo baya sana.
Mheshimiwa Spika, katika suala zima la kuifanya shule hii iwe ya Kidato cha Tano na cha Sita, nadhani hili ni wazo zuri na Jumuiya ya Wazazi pale watakapoona, aidha wenyewe kuifanya na kuiboresha miundombinu yake iwe ya kidato cha tano na cha sita kwa Tanzania, ama kuirudisha Serikalini. Mwenyekiti wa jumuiya hiyo yuko humu, atatuelekeza nini tufanye kwa muktadha wa kusaidia wanafunzi na watoto wa Tanzania.
Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
MHE. ABDALLA M. BULEMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Kabla sijauliza swali, naomba unipe nafasi kidogo niseme maneno mawili kidogo.
Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Silinde kama ameona mali za Chama cha Mapinduzi zinaweza kuja kuombwa Bungeni, nafikiri ni dalili nzuri kwamba naye anaelekea kuja CCM, karibu sana. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu linasema hivi, maombi haya yanayoletwa kwa ajili ya Shule ya Jumuiya ya Wazazi, Wizara naomba iniambie; je, kwa nini msishirikiane na Mbunge mkaimarisha shule nzuri ya Julius Nyerere ambayo inaonekana imeharibika, haifai, haina huduma nzuri, mpaka mwende kutafuta mali za CCM? (Kicheko/Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, nadhani Mheshimiwa Alhaji Bulembo alikuwa anatoa ushauri na mimi napenda kumpongeza sana kwa juhudi kubwa anayofanya katika shughuli zake.
Mheshimiwa Spika, nadhani ushauri huu kama Serikali tumeupokea, kwa sababu Mheshimiwa Alhaji Bulembo wewe ni mlezi wa watoto na ndiyo maana umeamua kujenga shule hizi na kuzisimamia. Kwa hiyo, tutakachokifanya ni kuboresha maeneo mbalimbali ili watoto wetu waweze kusoma kwa kadiri iwezekanavyo.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wetu, hali hii ya makorongo na jiografia inayobadilika kutokana na tabianchi imesababisha jamii yetu hasa akinamama kukosa huduma za afya, watoto na wanafunzi kukosa masomo na kwa kuwa ni tatizo la nchi nzima, je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kuona ni namna gani hata madaraja ya dharura kama yale ya chuma kuwekwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo Halmashauri ya Mji wa Mbulu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, sasa hivi tunabadilika kutoka Watendaji wa Halmashauri na barabara zote zinazohudumiwa na Halmashauri zinapelekwa kwa Wakala wa Barabara za Vijijini. Je, ni kwa namna gani Serikali itatazama suala hili kutokana na kwamba fedha zinazotengwa ni kidogo sana kulingana na fedha za Mfuko wa Barabara kwa zile barabara zilizokuwa zinahudumiwa na halmashauri za wilaya katika maeneo ya vijijini ili fedha zitakazotengwa kwa dharura ziweze kusaidia tatizo hili na jamii ipate huduma stahiki na kwa wakati kuliko sasa ambavyo inapoteza maisha katika hali ya dharura na mvua nyakati za masika? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika nchi yetu kuna maeneo mbalimbali yanaathirika sana, na hasa katika Mkoa ule wa Manyara. Nikiri wazi kwamba eneo lile lina changamoto kubwa sana na wakati mwingine mvua ikinyesha utakuta sehemu nyingine mpaka mito inahama. Hali hiyo inajitokeza hata katika Mkoa huu wetu wa Dodoma na Mkoa wa Morogoro maeneo ya Gairo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kwa suala la upatikanaji wa madaraja ya chuma naomba tu niseme kwamba jambo hilo tumelipokea, japokuwa siwezi kusema kwamba hilo daraja litapatikana lini; lakini kwa haja ya kusaidia wananchi nadhani ngoja tuliweke hilo katika vipaumbele vyetu. Katika maeneo ambayo mwanzo yalikuwepo madaraja hayo, lakini leo hii yametengenezwa madaraja mengine, yale madaraja ambayo ni ya chuma yaliyohamishwa kule, tutaangalia jinsi ya kufanya, kwa kushirikiana na wenzetu wa TANROADS katika maeneo mbalimbali ili kuisaidia jamii yetu hasa kule Mbulu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la TARURA na bajeti; ni kweli katika fedha zinazokwenda za Mfuko wa Barabara; kwa sababu kuna ule mgawanyo wa sheria ambapo sheria ya TANROADS ni tofauti na sheria za halmashauri; lakini tumeunda Wakala mpya ambao una mikakati vile vile.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine linalofanyika ni suala zima la resource mobilization, kutafuta fedha, kwa hiyo naamini; katika kipindi hiki ambacho TARURA inaanza sasa naomba Waheshimiwa Wabunge muwe na imani, kwamba kazi nzuri itafanyika na mtakuja kuona kwamba kuna faida kubwa sana kwa kuanzisha Wakala huu; ambapo iliainishwa wazi katika ilani ya Chama cha Mapinduzi, kwamba lazima katika kipindi hiki Wakala uanzishwe. Sisi jukumu letu ni kuhakikisha kwamba tutasimamia Wakala huu ili uweze kufanya kazi vizuri ili wananchi waweze kupata huduma vizuri
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukurru sana. Naomba tu nimuulize Mheshimiwa Waziri maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nianze na kuipongeza Serikali hii ya Awamu ya Tano kwa kuhakikisha kwamba kaya maskini angalau zinaweza kunufaika na huu mpango wa TASAF na kwa kweli katika mkoa wetu kaya nyingi zimeweza kunufaika na mpango huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa katika Manispaa yetu ya Iringa ambayo ipo Jimbo la Iringa Mjini tuna mitaa 192 na mitaa 98 tu ndiyo ambayo imeweza kunufaika na mpango huu na kuna mitaa 84 ambayo bado haijaweza kufikiwa kabisa na mpango huu wa TASAF; kwa mfano kwenye Kata ya Nduli kuna mitaa ya Kisoeyo, Mikoba, Kilimahewa, Mgongo na Njiapanda na kwenye Kata ya Kituli kuna mtaa wa Hoho; Kata ya Mkwawa kuna mtaa wa Mosi. Je, ni lini Serikali sasa itazifikia kaya hizi maana hali ya kaya katika mitaa hii ni mbaya kuliko hata zile ambazo zimeweza kufikiwa?
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile nina swali lingine la pili. Kwa kuwa zipo kaya ambazo ni maskini na pia zina watoto wenye ulemavu. Kwa mfano katika Mkoa wetu wa Iringa kwenye Jimbo la Kilolo, Kijiji cha Lulanzi, kuna kaya ambayo ina watoto wanne, wote wana ulemavu na baba yao amepooza, mama yao sasa hivi amevunjika mguu. Je, katika mpango huu Serikali inawasaidiaje watu ambao tayari ni maskini na hawawezi kufanya kitu chochote katika kuwasaidia ili waweze kupata miradi? Kwa mfano labda kujengewa/kuwekewa mradi wa kisima ambao wanaweza wakauza maji wakiwa pale pale au wakapewa bajaji ili kuweza kunusuru kaya ambazo ni walemavu halafu ni maskini?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwanza kabisa niseme Serikali inakubali kwamba ni kweli si vijiji vyote, mitaa, kata na shehia nchini mwetu zimeweza kufikiwa na mpango huu wa TASAF. Ni takriban asilimia 70 tu kama nilivyoeleza ya vijiji, kata, shehia 9,989 ndiyo imefikiwa.
Napenda tu kumweleza Mheshimiwa Mbunge kwamba hivi sasa tumeanza taratibu, tunasubiri tu fedha zitakapotoka tuweze kuendelea na zoezi la kuwatambua na kuwaandikisha walengwa liweze kufanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia sasa hivi tuko katika mpango tuliokuwa tunamalizia kipindi cha kwanza cha awamu ya tatu ya TASAf ambayo itamalizika mwaka 2018 kuelekea 2019; na sasa hivi tumeanza kusanifu awamu nyingine na tunaamini pia katika zoezi hilo nalo pia tutaendelea kufanya utambuzi na kujua program itakuwaje.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba pindi tu fedha zitakapopatikana tutaweza kuendelea na zoezi la utambuzi wa walengwa na kuweza kuwaandikisha. Vile vile tutakapoendelea katika kipindi cha pili cha awamu ya tatu ya TASAF tunaamini walengwa wataweza kunufaika.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili amezungumzia kaya za watu ambao ni maskini ambao unakuta ni watu wenye ulemavu. Nipende tu kumweleza Mheshimiwa Mbunge kwamba wakati program hii ya TASAF awamu ya tatu inasanifiwa, suala zima la ulemavu halikuwa kigezo, kigezo kilikuwa ni umaskini lakini pia walikuwa wanaangalia umaskini wa kaya nzima kwa ujumla wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia katika aina za ruzuku ambazo zinatolewa, ruzuku ya kwanza kabisa ambayo inatolewa bila hata masharti ya kuangalia kama familia ina watoto ilikuwa inatolewa kwa kaya nzima. Hata hivyo, nipende kusema, endapo kaya hiyo ina watu wenye ulemavu ambao wako chini ya miaka minane walikuwa wanakuwa treated au wanahesabiwa kama watoto wengine katika familia hiyo kwa mujibu wa ruzuku.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa familia ambazo tumezikuta zina ulemavu wamekuwa wakishirikishwa katika miradi mbalimbali ya ajira ya muda. Hata hivyo, bado kama alivyoeleza yeye tulipata changamoto, ziko familia ambazo unakuta zina watu ambao wamezidi miaka 18, hata wakipewa ajira ya muda wengine ni mpaka wabebwe na hawawezi kufikia katika hiyo miradi mbalimbali. Niseme tu, tumelipokea na sasa hivi tunaposanifu awamu ya tatu ya mradi huu tutaendelea kuliangalia; kwamba katika awamu nyingine ni nini kifanyike kwa ajili ya watu wenye ulemavu lakini pia kwa sasa tunaangalia tunaweza tukawasaidiaje. Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru (Makofi)
MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. TASAF awamu ya pili ilianzisha mradi wa barabara ya Bungurwa-Msunga; leo ni zaidi ya miaka 10 na yapo makalvati yapo tayari zaidi ya 50. Je, ni lini sasa mradi huo au ujenzi wa barabara hiyo utatekelezwa?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kama nitakuwa nimemsikia vizuri; ni kwamba kuna mradi wa makalvati ambao ulikuwa haujamalizika na anataka kufahamu ni lini labda utatekelezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nipende tu kusema kwamba, tulipotekeleza TASAF awamu ya kwanza na awamu ya pili ni kweli iko miradi ambayo haikuweza kukamilika. Hata hivyo kwa maelekezo ambayo Serikali iliyatoa; tulitoa maelekezo kwa halmashauri zetu kuhakikisha kwamba wanaorodhesha miradi yote ambayo walikuwa hawajatekeleza au imeanza kutekelezwa lakini haijakamilika waweze kutengea fedha katika bajeti ili iweze kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge tutafuatilia mradi huo wa kalvati katika Kata ya Misungwi ili tuone ni hatua gani imefikiwa ili mradi huo uweze kukamilika mapema.
MHE. NURU AWADH BAFADHILI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa kuna baadhi ya kaya ambazo ni maskini sana lakini hazikuorodheshwa katika zoezi hili la kuwezeshwa katika mradi huu wa TASAF na kuna wengine wana uwezo lakini vile vile wanapokea pesa hizi za TASAF; je, Serikali inatuambia nini kuhusu hili?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA
BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nipende kusema kwamba ni kweli ziko kaya ambazo zilikuwa ni kaya maskini sana lakini unakuta haijaorodheshwa katika mpango na kinyume chake kaya ambazo si maskini au angalau zina ahueni ziliorodheshwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia katika mchakato huu mzima wa uandikishwaji wa walengwa, ni mikutano yetu mikuu katika kata, kijiji na shehia ambayo inashirikishwa. Kwa kiasi kikubwa baadhi yao katika mikutano mingine mikuu unakuta itikadi za kisiasa zimetumika lakini pia unakuta kuna wengine wameorodheshwa wanaogopa kusema kuwabaini kwamba huyu ameingizwa lakini hastahili.
Mheshimiwa Naibu Spika, nipende tu kutoa rai kwa wananchi wetu pamoja na mikutano mikuu, watakapoona kuna kaya zimeorodheshwa hazistahili basi waweze kutoa ushirikiano na waweze kuziondoa na tunaamini wataweza kufanya hivyo kwa sababu mpaka sasa tumeshaondoa zaidi ya kaya 73,851 na tutaendelea kufanya hivyo. Tunaomba wananchi waweze kutoa ushirikiano ili wawe ni wale tu ambao kweli wanazo sifa ndio waweze kunufaika na mpango huu. Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini naomba kufahamu kwamba kwa maelekezo hayo ambayo Serikali imeyatoa kwa waajiri kutekeleza upandishwaji wa madaraja hayo.
Je, Serikali iko tayari sasa kuratibu suala hilo ili kuhakikisha kwamba tunafanya uhakiki wa walimu wote wenye malalamiko haya ili yapatiwe utatuzi.
Swali la pili, kwa sababu pia yako malalamiko kutoka kwenye Halmashauri zetu kwamba Walimu wanapokwenda kujiendeleza unatokea upungufu wa Walimu kwenye shule wanazotoka.
Je, Serikali iko tayari kutumia vizuri fursa ya Chuo Kikuu Huria ili yenyewe kwa ngazi ya Serikali Kuu iratibu namna ya kuwasaidia Walimu wajiendeleze kwa kupitia Chuo Kikuu Huria bila kuathiri uwepo wao kwenye shule zao? Ninakushukuru.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hoja ya Mheshimiwa Oscar ni kwamba kufanya tathmini ya kuratibu vizuri mchakato huu, naomba tulipokee hili kwa sababu lengo kubwa ni kwamba kama Serikali tuna haja ya watumishi mbalimbali ambao malalamiko yao yapo yaweze kufanyiwa kazi kwa sababu tunajua yakifanyiwa kazi vizuri ndiyo wataweza kufanya kazi vizuri wanapokuwa ofisini mwao.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Mheshimiwa Mukasa nadhani hii ni hoja ya mapendekezo na sisi tutaangalia jinsi gani tuweze kuratibu vizuri ili haki ya mfanyakazi iweze kupatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili katika eneo la pili ni kwamba jinsi gani tufanye kwamba tutoe maelekezo ya watumishi wote kada ya ualimu kutumia Chuo Kikuu Huria. Nadhani tuweke hili dirisha wazi kwa sababu kila mwalimu ana preference yake na kitu gani anachokihitaji, isipokuwa jambo la misngi ni lazima tuweke mipango mizuri lengo ni kwamba walimu watakapoenda kujiendeleza basi tusiwe na mapungufu makubwa katika maeneo yetu. Tunajua kwamba tatizo hili limekabili maeneo mbalimbali lakini hoja hii ni hoja ya msingi nadhani hili sasa katika mamlaka ya Serikali za Mitaa tutatoa maelekezo mahsusi ya kiutawala/kiofisi kwamba nini kifanyike kama walimu wangapi wanatakiwa wakiondoka wengine wabaki, ili watoto wasiathirike.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo katika mchakato wetu ambao tunaufanya hivi sasa lengo kubwa ni kuajiri walimu wapya tunajua kwamba tukiongeza idadi ya Walimu tutaweza kupunguza kwa kiwango kikubwa tatizo hili ambalo liko hivi sasa katika Halmashauri zetu. (Makofi)

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nataka kuweka msisitizo tu kwamba msimamo wa Serikali kuhusu wanafunzi kujiunga na vyuo vikuu ni kwamba mwanafunzi anachagua mwenyewe mahali ambapo anataka kusoma, kwa hiyo utaratibu huo unawahusu watarajiwa wote wa vyuo vikuu ikiwa ni pamoja na walimu. Kwa hiyo, Serikali itaendelea kuweka tu mazingira mazuri ili wanafunzi waweze kuendelea kuwa na fursa ya kwenda mahali wanapotaka lakini Serikali haiwezi ikampangia mtu kinyume na matakwa yake. (Makofi)
MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na tabia kwenye Halmashauri wanapokwenda masomoni baadhi ya watumishi kwenye Halmashauri, Halmashauri zinakuwa zinagharamia hususan wale walioko kwenye ngazi ya pale Halmashauri. Lakini si kwa kada za ualimu na kada zingine.
Je, nini kauli ya Serikali kwamba Halmashauri zinagharamia masomo kwa wale watumishi waliopo ndani ya Halmashauri pale pale au kwa watumishi wa Halmashauri nzima? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu ni kwamba kuna utaratibu wa mapendekezo ya watu kuonyesha preference yao kwamba watu wanataka kwenda kusoma, hili mara nyingi sana huwa inawekwa katika mchanganuo wa kibajeti katika kila Idara, kwamba kila Idara ina utaratibu na mipango yake kwamba mwaka huu kuna watu wangapi wataenda kusoma. Kwa hiyo, jambo hili sio wale wa Makao Makuu peke yake hapana, jambo hili maana yake ni kwa Halmashauri nzima, kama kuna Halmashauri ambayo inafanya kuwapa upendeleo maalum wale waliopo Makao Makuu peke yake, hilo ni kosa na halikubaliki.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, utaratibu ni kwamba mpango wa bajeti wanapopanga bajeti wanapanga mwaka huu Idara fulani tutapeleka watu fulani kusoma katika level fulani ambayo inaingizwa katika bajeti, then unaweka hilo open door policy katika hiyo Idara, kila mtu aweze ku-apply kuangalia nani ata-qualify katika kipindi hicho kuweza kupata fursa ya masomo, kwa sababu mkate huo ni mkate wa Halmashauri nzima siyo watu maalum katika Makao Makuu ya Halmashauri.
MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naomba kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, walimu wengi walipata fursa ya kwenda kujiendeleza na waliweza kujiendeleza, pale wanapokuwa wanafanya hayo masomo yao katika ngazi ya shahada wanapokwenda kwenye ile Block Teaching Practice walimu hawa wanapangiwa kwenye shule za sekondari na wanapomaliza bado walimu hawa wanarejeshwa kwenye shule za msingi. Wanaporejeshwa kwenye shule za msingi, yale waliyosomea hayapo kwenye shule za msingi bali yapo kwenye shule za sekondari.
Serikali hapa ina utaratibu gani wa kubadilisha au wa kutengeneza mitaala kuhusiana na shule za msingi ili wakitoka kule warudi kule kule walikotoka? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani Mama yangu Salma Kikwete anazungumzia changamoto za jinsi gani tuweze kuboresha elimu yetu kwa watu walioko katika vyuo wanapoenda kwenye katika zile field practical na wanapoenda kufundisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, hili ni wazo kwa sababu bahati nzuri Mheshimiwa ni mwalimu anajua changamoto gani zipo na vipi tuziboreshe. Mimi naomba tulichukue hili kama wazo jema, kwamba nini tufanye hasa katika suala zima la mitaala kiujumla wake, hata hivyo, tuangalie ni jinsi gani wanafunzi wetu wanapokuwa katika masomo, kile kitu ambacho anaenda kufanyia field practical na iwe best practice akienda kwenye kazi. Kwa hiyo, nasema huu ni ushauri mzuri, Serikali tumeuchukua, tunachukua mawazo mazuri, kwa sababu tuko katika mchakato wa kuboresha elimu yetu iwe elimu shindani tunachukua mawazo haya kwa ajili ya kuyafanyia kazi vizuri. (Makofi)

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TAKNOLOJIA:
Mheshiwa Naibu Spika, ahsante sana. nampongeza Mheshimiwa kwa majibu mazuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuongezea tu kwamba lengo la kufanya mafunzo kwa vitendo ni kutoa fursa kwa wanafunzi kuweza kufanya kwa vitendo kile ambacho wanajifunza. Katika teaching practice jambo kubwa ambalo linaangaliwa ni ule mfumo wa ufundishaji yaani kwa kingereza tunaita pedagogical skills, jinsi ambavyo mwalimu anaweza akalihimili darasa, anaweza akafanya yale ambayo yanatakiwa kumudu darasa lake. Kwa hiyo, mwalimu ambaye anajifunza mafunzo ya sekondari principal za darasani kwenda kujifunza, hata akienda kufanya katika shule za msingi hakuna jambo lolote ambalo linaharibika. Ndio maana wapo walimu wa sekondari wanapangiwa kwenda kufundisha shule za msingi kwa sababu kinachoangaliwa ni ule uwezo wa mwalimu kufanya ule ufundishaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na nini anachokifundisha, ukiangalia maudhui ya mtaala katika elimu ya msingi ni ya kiwango cha chini kuliko ya sekondari. Kwa hiyo, ni dhahiri kwamba mwalimu ambaye ana uwezo wa kufundisha sekondari atakuwa ni mwalimu mzuri sana katika kufundisha shule za msingi. (Makofi)
MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana vilevile nishukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna kazi zilizokuwa zinaendelea zilizokuwa zinafanywa na Halmashauri na hizo zimehamishiwa kwenye TARURA sasa hivi. Je, ni lini TARURA wataanza na kuendeleza hizo kazi?
Swali la pili, kama ilivyo katika Mji Mdogo wa Rujewa vilevile Mheshimiwa Rais aliahidi kumalizia ujenzi wa kituo cha mabasi cha Mbalizi katika Mji Mdogo wa Mbalizi.
Je, ni lini kazi hiyo ya kujenga kituo cha mabasi cha Mji Mdogo wa Mbalizi kitaanza? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tumekuwa na kipindi cha mpito ambapo kazi za ujenzi wa barabara katika Halmashauri zilikuwa zikisimamiwa ndani ya Halmashauri zetu, lakini chini ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Sasa hivi tumeunda Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini ambao unaitwa TARURA sasa umeshaanza kuchukua majukumu hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, tunafahamu wazi kwamba kulikuwa na mikataba mingine na kazi mbalimbali zilikuwa zinaendelea na tulitoa maelekezo katika ofisi yetu kwamba zile kazi zote kutokana na mikataba iliyokuwa inaendelea ambazo ziliingiliwa na Halmashauri kazi zile zilipaswa kuendelea, isipokuwa taratibu za malipo ndio zilikuwa zinafanyiwa utaratibu maalum. Tulitoa maelekezo haya kwa Mameneja wa TARURA katika nchi nzima katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata hivyo, wakati mwingine kulikuwa na uelewa tofauti katika baadhi ya maeneo, baadhi ya maeneo kazi zilikuwa zinaendelea vizuri lakini sehemu zingine kazi zilisimama, kazi kubwa iliyofanyika ni kuhamisha zile akaunti ziweze kufanya kazi vizuri ili utaratibu uendelee kufanyika kama ilivyokusudiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na concern yako Mheshimiwa Oran naomba niiagize Halmashauri yako Meneja kama kuna changamoto ambayo ameipata katika ofisi yake tuwasiliane na ofisi na hasa na Mtendaji Mkuu wa TARURA ampe maelekezo ya kutosha nini kifanyike, ili kazi kule site isiendelee kukwama, ziendelee kufanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala zima la ujenzi wa stendi hii ya Mbarali, naomba nilichukue hili halafu nijue kwamba kuna kitu gani kilichokubaliwa na imefikia hatua gani? Changamoto iko wapi? Hili naomba niwahakikishie ofisi yangu itasimamia kwa sababu ahadi ya Mheshimiwa Rais lazima itekelezwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nilichukue jambo hili tutaenda kulifanyia kazi haraka iwezekanavyo, kuangalia nini tufanye ili kuhakikisha ile stendi inatengenezwa.(Makofi)
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, TARURA imepokea kazi hizi za barabara katika Halmashauri zetu, sasa katika masuala haya ya barabara katika Halmashauri tulikuwa tunakarabati barabara hata katikati ya msimu, inaweza ikatokea mvua nyingi ikasomba barabara, Halmashauri ikatoa lori, wananchi wanashiriki kujenga ile barabara.
Je, katika kipindi hiki cha TARURA, wataendelea kufanya hiyo Kazi? Kwa sababu sasa TARURA haina malori, Halmashauri ina malori haina mafungu ya barabara, lakini TARURA wana mafungu hawana malori. Hapa huu utaratibu wa kurekebisha hizi barabara utakuwaje? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, hili jambo wala kwanza halina mashaka, kwa sababu jukumu hili sasa liko chini ya TARURA. Lakini ufahamu siyo Halmashauri yako peke yake, kuna Halmashauri mbalimbali wengine wana greda. Nafahamu magreda haya au malori haya sio kwamba yatakuwa yanafanya kazi peke yake lakini inawezekana ni kitega uchumi cha kwenu ninyi kama Halmashauri. Wakati TARURA inafanya kazi yake, wakati inatekeleza kupitia Meneja wa TARURA katika ngazi husika lazima kama utaratibu wa kukodi malori utafanywa katika utaratibu ule usiokuwa na kikwazo. Kwa hiyo, kama mna malori yenu, mna magreda yenu ambayo nanyi ni sehemu ya kitega uchumi kwenu barabara zitakapokuwa zinajengwa katika maeneo yale kama mtakuwa na utaratibu wa kukodisha jukumu kubwa ni kwamba TARURA itemize wakibu wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mwalongo naomba usihofu kila kitu kitaenda vizuri, ni kipindi cha mpito tu kina mashaka kwa sababu ni jambo jipya lakini jambo hili litakuwa halina matatizo ya aina yoyote, tutafika muda mtaona kila kinaenda vizuri katika Halmashauri zetu.
MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la miundombinu ya barabara katika Mji Mdogo wa Rujewa linafanana kabisa na ubovu wa miundombinu ya barabara katika Mji Mdogo wa Mloo, Jimbo la Mbozi.
Je, nini ahadi ya Mheshimiwa Waziri kwa wananchi wa Mloo kuhusu miundombinu mibovu ya barabara ambayo ni tatizo la muda mrefu sana?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Haonga unapozungumza suala la Mloo nafahamu kwamba changamoto kubwa ya Wabunge wengi humu ni suala zima la miundombinu ya barabara katika Halmashauri zetu. Ndiyo maana nawashukuru sana katika Mpango ule wa bajeti mwaka huu mmeona tumetenga bajeti kubwa karibuni ya shilingi bilioni 263. Lengo kubwa ni kwamba barabara za vijijini zenye vikwazo na zile barabara nyingine tuweze kuzihudumia.
Kwa hiyo, naomba niseme kwamba katika eneo la kwako ulilozungumza na kwa sababu tumeshawaajiri watu tena tunawapa performance contract ya jinsi gani kila meneja katika Halmashauri anapoenda kule afanye kazi yake na tutaipima na meneja atakaposhindwa ku-deliver maana yake hatokuwa na hiyo nafasi atapewa mtu mwingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba ondoa hofu ni kwamba tutakuwa katika mkakati wa kutofanya kazi tena kimazoea katika utaratibu wa sasa, na kwa sababu jambo hili liliahidiwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi lazima tuwe na TARURA tutaenda kutekeleza kwa nguvu zote, naomba ondoa hofu katika eneo la Mloo tutalifanyia kazi haraka iwezekanavyo. (Makofi)
MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Wakati wa kampeni Mheshimiwa Rais alitembelea Namanyere na akatoa ahadi kwamba akipita tutapata kilometa tano za barabara ya lami. Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo amekuwa akilisema mara kwa mara lakini mpaka sasa halijatekelezwa.
Nataka kujua Serikali ina mpango gani kutekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli na hata nilipotembelea Namanyere Mheshimiwa Keissy alizungumza katika mkutano nilipokuwa ninaongea na Watumishi kuhusu ahadi hiyo sambamba na ahadi ya maji ambapo bwawa lilikuwa linaendelea kujengwa.
Mheshimiwa Mipata kwa sababu nafahamu pale Namanyere ndiyo Makao yenu Makuu ya Mji kwa ahadi hii ya Serikali na sisi ametupa dhamana kuhudumu katika ofisi yake, tutafanya kila liwezekanalo katika kipindi hiki cha miaka mitano, ahadi ya Mheshimiwa Rais kupitia TARURA tutaitekeleza, tutakapofika mwaka 2020 tusiwe na changamoto nyingine yoyote katika suala la hiyo kilometa tano Mheshimiwa Rais alizoziahidi. (Makofi)
MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafsi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile vikao halali vya Halmashauri ya Wilaya ya Songea vilishamaliza jukumu la kihalmashauri kuhusu matumizi ya eneo hili la ardhi; na kwa vile katika mazungumzo na ufuatiliaji Wizara ya Kilimo walishaelekeza kwamba sasa Mkoa ukabidhi sehemu ya eneo la shamba hilo kwa wananchi ili waweze kuendelea na shughuli za kilimo; na kwa vile msimu wa kilimo umekaribia sana na wananchi hawana sehemu ya kulima mazao ya chakula, na kwa vile wafugaji tayari wameanza kufuga katika eneo hilo.
Je, Serikali ipo tayari sasa kutoa maelekezo kwa Serikali ya Mkoa kuhusu kutekeleza jukumu hili haraka iwezekanavyo?
Pili, iwapo zoezi hili litaendelea kuchelewa kutekelezwa, je, Serikali ipo radhi sasa kuruhusu wananchi wa Ngadinda na kwa vile mipaka inafahamika, kuiagiza Serikali ya kijiji iweze kuanza kushirikiana na wananchi kuwatengea maeneo hayo waweze kuanza kuzalisha?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa hizo initiative zote walizozifanya mpaka wamefikia hapo. Mimi nafahamu kwamba kama hatua nyingi za msingi zimeshafanyika kikubwa zaidi ni sehemu yetu ya Mkoa. Nichukue fursa hii kuiagiza Ofisi ya Mkoa wa Ruvuma iangalie jinsi gani ya kufanya kama mijadala yote imeshakamilika iende haraka kurekebisha jambo hili ili wakulima na wafugaji tusiwe na mgogoro tena katika eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunajua wazi kwamba jambo hili likiwa na ukakasi wake mwisho wa siku tunakuja kuzalisha matatizo makubwa sana ya uvunjivu wa amani. Kwa hiyo, nitumie fursa hii kuiagiza timu ya Mkoa wetu wa Ruvuma iende ikalifanyie kazi jambo hilo haraka iwezekanavyo na ikiwezekana mpaka mwezi wa Kumi jambo hilo liwe limekamilika na ofisi yetu ya TAMISEMI tupate taarifa ya jinsi gani jambo hilo limekamilishwa kwa sababu vikao vyote halali kwa taarifa niliyoipata kutoka kwa Mbunge zimeshakamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la pili kwamba kukiruhusu kijiji kwenda kuhakikisha kwamba wanaenda kugawa hilo eneo, naomba tuvute subira kwanza, timu ya Mkoa ifanye kazi yake vizuri baadaye tukishapata taarifa tutajua nini kifanyike. Lengo kubwa kama unavyowapigania wananchi wako Serikali itaingilia kati kwa nguvu zote sisi tukishirikiana na Wizara ya Kilimo tutafanya kila liwezekanalo eneo lile liwe katika utaratibu mzuri, wananchi wa eneo lile waweze kupata ardhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ondoa hofu Mheshimiwa Mbunge tunalifanyia kazi jambo hili.(Makofi)
MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu wananchi wa Madaba wameonesha kuhamasika sana kulima tangawizi, hata mimi ninalima tangawizi Madaba. Je, Serikali haioni kwamba kiwanda cha Mamba Miamba ambacho kitakuwa tayari by March next year, kitahitaji tangawizi nyingi sana siyo kutoka Same tu pamoja na Madaba.
Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapatia wananchi wa Madaba ardhi ya uhakika ili walime tangawizi kwa wingi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tuchukue kilio cha mama vilevile kama kilio cha Mheshimiwa Joseph Mhagama. Serikali inaona umuhimu huo na tutafanya kila liwezekanalo kuhakikisha mambo pale yanakaa sawasawa wananchi walime tangawizi waje, kulisha katika kiwanda cha Mama Anne Kilango Malecela. (Makofi
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru kwa fursa hii.
Tatizo la mgogoro wa shamba la Madaba linafanana sana na tatizo la shamba la Kigomani na Utumaini lililopo Wilayani Mafia.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari kuja Mafia kukaa na wadau wa Halmashauri pamoja na Viongozi wengine kutatua tatizo hilo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Mbunge na lile deni letu tumeshatoa shilingi milioni 50 tumemaliza kituo cha afya, hongera sana Mheshimiwa Mbunge kwa ujenzi wa theatre. Hata hivyo, katika jambo hili mimi naomba nilichukue, lakini kabla mimi sijaja kule nimuagize Mkuu wa Wilaya ya Mafia kwanza aende akalishughulikie jambo hili na ikiwezekana tupate taarifa amelishughulikia vipi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitakapopata hiyo taarifa jinsi gani limeshughulikiwa jambo hili na mgogoro huo haukuisha, na mimi nitaona jinsi gani ya kufanya, lakini kwamba nitatumia vyombo vyangu vya chini kule kwanza, Mkuu wa Wilaya ya Mafia aanze kuifanya kazi hiyo harka iwezekanavyo kumaliza hilo tatizo na ofisi yetu ipate taarifa ndani ya mwezi mmoja, jinsi gani mgogoro huo umeshughulikiwa kwa kadiri iwezekanavyo. (Makofi)
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwanza utaratibu wote umeshafuatwa, vijijji vimekaa, Kamati ya Maendeleo ya Kata imekaa, Full Council imekaa na mpaka kwenye Kamati ya Ushauri ya Mkoa na ni ombi la muda mrefu sana. Wananchi wa Mkanana wanapata shida, kwanza hakuna mawasiliano ya barabara kabisa na ninakuomba tukimaliza Bunge tuende kule upite ile njia uone kama inapitika.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, kwa kuwa kwenye swali langu limetaja kuna umbali kutoka Mkanana, Chibwegele mpaka Chitemo ni kilometa 45 ndipo wananchi wanafuata usafiri. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, utakuwa tayari kukubali ombi langu tufuatane na wewe sasa baada ya Bunge hili, ukawaone watu wa Mkanana, Chibwegele, wanavyopata shida?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza nikiri nipokee kama taratibu zote mpaka katika ngazi ya mkoa zimekamilika tutafanya ufuatiliaji kuangalia utaratibu umefanyika lini. Kama sio yale maombi ya zamani ambayo mwanzo yalikuwa hayakukizi vigezo, kama haya mapya, ofisi yangu nadhani inafanya uchambuzi wa maeneo mbalimbali katika maeneo haya mapya.
Mheshimiwa Spika, lakini katika jambo lingine la pili, Mheshimiwa mbunge ameomba ikiwezekana twende pamoja, naomba nikueleze wazi na mimi niko pamoja kwa sababu, najua Mheshimiwa Mzee Lubeleje watu, wanahistoria hawafahamu kwamba Mpwapwa yote ilikuwa Jimbo moja wakati huo, baadaye ikagawanyika na Jimbo lingine la Kongwa. Kwa hiyo, alifanya juhudi hizi miaka mingi sana katika michakato mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba niwahakikishie Wana-Mpwapwa, Wana-Kongwa na sehemu uliyosema, tutafika pale tutabaini miongoni mwa mambo hayo, lakini hasahasa tatizo la barabara katika Wilaya ya Kongwa na Wilaya ya Mpwapwa, nini tufanye kwa pamoja kuwasaidia wananchi hawa ambao kwa kiwango kikubwa wameisaidia sana Serikali hii katika mambo mbalimbali.
MHE. ALPHAXARD K. LUGOLA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri alishuhudia mgawanyo wa majimbo mawili ya Bunda na Mwibara kutokutana ndani ya Halmashauri moja. Na kwa kuwa, Mheshimiwa Waziri wa wakati huo, Mheshimiwa Simbachawene alikuja kushuhudia na kuamua kwamba, wabadilishe mipaka Jimbo la Bunda lirudi Bunda Mjini wawe Halmashauri moja na Mwibara ibaki yenyewe iwe halmashauri wakatuahidi watatoa Government Notice muda si mrefu na ilikuwa mwezi wa saba. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, hiyo GN imefikia hatua gani, Wana-Mwibara wanataka kusikia?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli analozungumza Mheshimiwa Mbunge hapa hazushi na bahati nzuri mimi nimepata fursa ya kutembelea majimbo haya yote matatu, Jimbo la Mwibara, Jimbo la Bunda Vijijini, hali kadhalika Jimbo la Bunda Mjini. Mgawanyiko wake kwa kweli, ulikuwa una changamoto kubwa sana na bahati nzuri harakati hizi zimeshaanza.
Naomba nichukue ombi lako hili Mheshimiwa Kangi, twende tukalifanyie kazi kwa undani kujua kwamba, hili jambo limefikia wapi na hasa taratibu zilizofuatwa pale, baadaye tutaweza kutoa maamuzi sahihi, lakini sitaki kutoa commitment ya moja kwa moja hapa, tunalifahamu hili jambo tutaenda kulifanyia kazi kwa maslahi mapana ya hizi halmashauri zetu ambazo ziko kule.
MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri na kwa sababu hiyo naomba niwe na swali moja tu la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, baada ya barabara hii sasa kutengenezwa na kuwa inapitika angalau kwa uzuri, magari makubwa na yanayobeba mzigo mzito sasa yanaitumia barabara hiyo kiasi kwamba eneo la kama kilometa moja limetengeneza tifutifu kubwa sana ambayo kama isiposhughulikiwa kipindi hiki, mvua itakaponyesha itakuwa shida sana kupitika. Mheshimiwa Naibu Waziri anasema nini kuhusu kuirekebisha sehemu hiyo kipindi hiki kabla mvua haijanyesha ili isije ikakosa kupitika tena? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, anachosema Mheshimiwa Mbunge ni kweli, bahati nzuri nimeenda kui- survey barabara ile na lile eneo moja kati ya Kijiji cha Msanga na Kawawa pale katikati hali imeharibika sana. Uharibifu ule ni kutokana na kwamba katika ujenzi wa Ikulu Ndogo ya Chamwino, malori ya TBA yanatumia barabara ile.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, tumeongea na Mkurugenzi, bahati nzuri watu wa TBA wamekubali kufanya marekebisho katika barabara ile.
Mheshimiwa Spika, niwashukuru sana TBA kwa sababu sasa hivi nao wanachonga barabara ya kilometa tano kutoka pale Kawawa kwenda maeneo ya Matelu ambayo ni mafanikio makubwa.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge, Ofisi yetu ya Chamwino chini ya Mkurugenzi tumeshafanya hiyo harakati na watu wa TBA wamekubali wataona jinsi gani ya kufanya ili mradi kurekebisha eneo lile liweze kupitika kwa wananchi wa Chamwino.
MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mweyekiti, ahsante. Nasikitika sana kwa majibu ya Waziri ambayo yamekuwa ni hayo hayo yakijirudia. Tumeona wenzetu wa Kahama na Shinyanga wananufaika kwa kiasi kikubwa sana na mradi huu wa maji kutoka Ziwa Victoria. Ni kwa nini Serikali imeviacha vijiji hivi ambavyo viko karibu kabisa na Ziwa Victoria kuvipatia maji muda mrefu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, zoezi la usanifu limekuwa likichukua muda mrefu sana kabla miradi kuanza kutekelezwa. Je, ni lini usanifu wa mradi huu utakamilika? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu concern ya Mheshimiwa Mbunge kwa changamoto hii ya maji na ame-compare na mradi wa maji unaokuja Kahama sasa hivi unakwenda Tabora mpaka Sikonge. Ni kweli, katika nchi yetu na maeneo mbalimbali kuna changamoto ya maji lakini siyo kwamba watu wa vijiji vile wamesahaulika ndiyo maana katika jibu langu nilizungumzia mpango wa maji katika Ziwa Victoria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipofika Musoma jambo ambalo tulielekezana na wataalam ni kwamba siyo vyema watu wa mji kwa mfano ukianzia hapa Bunda mpaka unafika kule Musoma ambako ukiangalia wana utajiri mkubwa wa Ziwa Victoria halafu wakaendelea kupata shida ya maji. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika Programu ya Uendelezaji wa Sekta ya Maji Awamu ya Pili ni commitment ya Serikali katika kipindi hiki cha miaka hii, tutahakikisha usanifu unakamilika lakini siyo usanifu peke yake bali mradi mkubwa huu wa maji lengo ni kuwasaidia wananchi wa eneo lile kwa sababu wakikosa maji hata huduma za uchumi zinakwama.
MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba niiulize Serikali, katika Wilaya ya Kwimba visima 188 vimeharibika, havifanyi kazi kutokana na kuzeeka lakini vingine vimechakaa na vimekauka.
Sasa naomba kuuliza, kwa sababu wananchi wa Kata za Mwabomba na hasa Nkalalo pale center wanashida kubwa sana ya maji kutokana na visima hivi kuharibika, je, Serikali sasa ina mpango gani wa kusaidia ili visima hivyo viweze kufanya kazi wakati tunasubiri mradi mkubwa wa maji ya Ziwa Victoria? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hoja ya Mheshimiwa Ndassa inakwenda katika maeneo mbalimbali na tumekuwa na changamoto kubwa sana katika visima vya maji na ndiyo maana tumekuwa tukitoa maelekezo maeneo mbalimbali kwamba hivi visima vya maji recharging capacity wakati mwingine inashuka kutokana na uharibifu wa mazingira. Hata hivyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Ndassa kwamba katika mpango wa Serikali wa sasa hivi kuna mashindano maalum tumeyatoa kwa kila Halmashauri ya jinsi gani mipango yao mikakati watakavyozindua kuhakikisha miradi ambayo mwanzo ilikuwa haifanyi vizuri wanafanya ukarabati wa visima hivyo na kuweza kuvisimamia. Kuna mpango maalum ambao tumepata fedha kutoka World Bank ambapo zinasaidia sana katika suala zima la kuongeza nguvu za Halmashauri. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba kupitia Halmashauri zetu, ni mpango siyo wa Halmashauri ya Kwimba peke yake isipokuwa ni katika Halmashauri mbalimbali tumewaelekeza wataalam wetu wahakikishe sasa wanavikarabati visima mbalimbali viweze kutoa maji, lakini hata hivyo kuweza kusimamia vizuri kwa sababu baada ya kufanya hivyo watapata fedha nyingine zaidi kwa ajili ya kuhakikisha wanakarabati vituo vyao vya maji. Kwa hiyo, naamini Wilaya ya Kwimba itafanya hili ili wananchi wa maeneo yale waweze kuondokana na shida ya maji katika maeneo yao.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu mazuri, niipongeze sana TASAF kwa kazi nzuri, sasa nina maswali mawili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza ni kwamba kazi hii kweli imeanza Mheshimiwa Naibu Waziri lakini bado haijakamilika katika vijiji ulivyotaja. Ni lini kazi hii itakamilika ili maeneo haya yaweze kupata huduma ya maji kwa sababu kuna shida kubwa sana ya maji?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali ina mpango gani wa kuongeza vijiji katika mpango wa kuchimbiwa mabwawa, katika vijiji vya Kisisi, Ngalamilo, Iwondo pamoja na Nana kwa sababu hawa nao wana matatizo makubwa sana ya maji. Ni lini wataanza shughuli hizi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lubeleje, Senior MP kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, lini miradi hii itakamilika na kuweza kutoa huduma ya maji, kwanza naomba nimuahidi katika Bunge hili la bajeti linaloendelea nitaomba mimi na Mheshimiwa Lubeleje twende katika miradi hii tukaiangalie kwanza halafu tushauriane vizuri tukiwa site kwa sababu najua Wilaya ya Mpwapwa ina tatizo kubwa sana la maji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vijiji vingine ambavyo ameviorodhesha ni kweli, nafahamu maeneo kwa mfano hata kule Tambi hali ya maji ni mbaya mpaka wanakuja huku Chamkoroma kutafuta maji. Kwa hiyo, tuna kila sababu kuhakikisha kwamba Wilaya ya Mpwapwa tunaipa kipaumbele. Pia katika ziara yangu hii nikiwa na Mheshimiwa Mbunge tutaambatana na wataalam kutoka kwenye Halmashauri tuweze kufika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na Makutupa ambako Mheshimiwa alikuwa anapigia kelele sana muda mrefu jinsi gani tutafanya kuweka mipango sahihi kusaidia shida ya maji katika Wilaya yetu ya Mpwapwa.
MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana na nashukuru pia kwa majibu mazuri ya Serikali kuhusiana na barabara hizi, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kuna madaraja makubwa matatu kwenye barabara hizi ambazo Mheshimiwa Naibu Waziri amezitaja na Halmashauri ya Wilaya ya Itilima imekuwa ikileta bajeti yake ili iweze kuyajenga madaraja haya matatu lakini TAMISEMI wanapunguza bajeti hiyo kiasi kwamba Halmashauri imeshindwa kujenga haya madaraja matatu. Je, Serikali inasema nini juu ya madaraja haya kwa sababu yasipojengwa ni kikwazo kikubwa kwa usafiri kwa wananchi wa Wilaya ya Itilima?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuna ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kujenga daraja la Mwabasabi, ni ya mwaka juzi. Serikali inasema nini juu ya ujenzi wa daraja hilo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli wakati mwingine bajeti zinakuja lakini kutokana na ukomo wa bajeti mapendekezo mengine ya Halmashauri yanakuwa yamekwama. Katika mchakato wa bajeti ya mwaka huu tulivyokuwa tukipitisha hapa, tuliona ni jinsi gani Ofisi ya Rais, TAMISEMI itahakikisha inaangalia vipaumbele katika maeneo korofi hasa kuondoa vikwazo na ndiyo maana tumepitisha bajeti ya shilingi bilioni 247.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutajitahidi kuangalia katika mpango wetu wa kuondoa vikwazo maeneo mbalimbali pale ambapo kuna vikwazo vya msingi katika ujenzi wa madaraja tutatoa kipaumbele. Naomba niwasihi wataalam wetu kule site waanze kufanya designing na needs assessment katika maeneo mbalimbali ili kuonyesha ni gharama kiasi gani zinahitajika katika ujenzi wa madaraja haya ambayo yatahusika. Kwa hiyo, naomba niseme kwamba kama Serikali tunalichukua hili lakini katika mpango wetu wa kuondoa vikwazo tutatoa kipaumbele katika maeneo haya. Lakini suala la ahadi ya Mheshimiwa Rais, naomba niwahakikishie lengo kubwa la Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha kwamba ahadi hizi zote zinatekelezeka. Naomba nimhakikishie kwamba katika kipindi hiki cha utekelezaji wa Ilani 2015 - 2020 daraja hili ni miongoni mwa maeneo ambayo tunaenda kuyajenga, lengo kubwa ni ili ahadi ya Mheshimiwa Rais iweze kutekeleza katika maeneo hayo.
MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa barabara ya Kichangani - Tubuyu katika Manispaa ya Morogoro ambayo ina urefu wa kilometa nne imejengwa kwa kilometa moja kwa shilingi bilioni tatu yaani kilometa nne imejengwa kwa shilingi bilioni 12. Je, Serikali iko tayari kupeleka wataalam kwenda kubaini ubadhirifu wa ujenzi wa barabara hii ambayo imejengwa kwa Mfuko wa Benki ya Dunia? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepata concern hii kutoka kwa Wabunge hasa wa Mkoa wa Morogoro na hasa barabara hizi zinazojengwa under Strategic Cities Project pamoja na barabara zingine ambazo zinajengwa katika Manispaa. Bahati nzuri kwa taarifa za Morogoro tunazifanyia kazi, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaenda kufanya verification kuangalia value for money katika eneo lile lakini zoezi hilo tutalifanya maeneo mbalimbali ikiwemo katika Mji wa Hai, Mkoa wa Kilimanjaro. Lengo letu ni kwamba thamani ya fedha ipatikane ili wananchi waweze kupata huduma inayolingana na thamani ya fedha. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge kilio chake kimesikika tutaenda kulifanyia kazi eneo hili.
MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Waziri kwa majibu mazuri naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa mwaka jana tuliomba fedha kwa ajili ya ukarabati Hospitali yetu ya Rufaa takribani shilingi bilioni 1.7 na tumekwishapata shilingi bilioni moja, je, fedha iliyobaki itakuja lini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili, nimuombe Mheshimiwa Waziri aseme kama atakuwa tayari kuambatana nami kwenda kuangalia hali ya Hospitali yetu ya Rufaa ya Mkoa na Kituo cha Afya cha Sokoine. Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika mpango wa bajeti ilitengwa karibuni shilingi bilioni 1.7 na ndiyo maana kwa mujibu wa Serikali kwa sababu mipango yake ni kuhakikisha miradi hii inatekelezeka tayari tumeshapeleka shilingi bilioni moja. Nishukuru sana wakati naongea na Sekretarieti ya Mkoa mwezi mmoja uliopita walikuwa katika michakato ya kuona ni jinsi gani fedha zile ziweze kutumika vizuri zaidi kuhakikisha kwamba jengo lile linakamilika. Hata hivyo, ni mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba hospitali hii inakamilika. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutajitahidi kadri iwezekanavyo fedha zipatikane, mpango ule wa ujenzi wa Hospitali yetu ya Rufaa ya Mkoa wa Singida iweze kukamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la pili kwamba ikiwezekana tuweze kuongozana, nimwambie Mheshimiwa Mbunge tujipange ikiwezekana hata kesho mchana, tutoke hapa mara moja tukafanye kazi turudi tuendelee na kazi za Bunge kwa sababu ni lazima tuhakikishe kwamba tunawafikia wananchi kuweza kuwahudumia kwa karibu zaidi.
MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tabora Manispaa mara mbili tulitenga pesa kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya, tulianza majengo hayo miaka mitatu iliyopita, lakini na mwaka huu wa fedha tumetenga tena bajeti hiyo ya shilingi milioni 120 kwa ajili ya kuendeleza majengo hayo.
Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kutupa pesa ili tuweze kumalizia Hospitali hiyo ya Wilaya ili tuweze kutatua kero kubwa inayoikabili Hospitali yetu ya Rufaa kwa population kubwa iliyopo Tabora Manispaa ili wananchi waanzie kwenye Hospitali yao ya Wilaya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimhakikishie Mheshimiwa Munde kwa sababu muda mwingi sana amekuwa ukipigia kelele Mkoa wake wa Tabora na ndiyo maana kwa mapenzi makubwa mpaka Mheshimiwa Rais akaona amkabidhi ambulance kwa ajili ya wananchi wake wa Tabora katika sekta ya afya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hili, naomba nimhakikishie kwamba mwaka wa fedha bado haujaisha, japokuwa tumepeleka fedha za Local Government Development Grants katika Halmashauri mbalimbali waweke vipaumbele tutaangalia kwa Tabora nini kimewekezwa. Naomba nimhakikishie kwa sababu mwaka haujaisha tutajitahidi kwa kadiri iwezekanavyo bajeti ile iweze kufika ili mpango wa bajeti wa Manispaa ya Tabora uweze kukamilika kama ulivyokusudiwa katika ujenzi wa Hospitali ya Wilaya.
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa swali la msingi linafanana kabisa na tatizo tulilonalo katika Hospitali yetu ya Mkoa, karibu asilimia 85 ya Madaktari wa Hospitali ya Mkoa wa Iringa wanaishi nje kabisa ya hospitali ile na kusababisha wagonjwa kupata matatizo makubwa wanapokuja usiku kwa ajili ya matibabu. Tatizo kubwa lililoko katika Hospitali ya Mkoa kuna mwingiliano wa Magereza na Hospitali. Tulishauri mara nyingi kwamba Waziri wetu wa Afya pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani waweze kukaa pamoja waone kwamba lile gereza liweze kutoka ili madaktari wengi waweze kukaa karibu na Hospitali ile ya Mkoa ili kusaidia wagonjwa wanaofika hata usiku.
Je, ni lini sasa ombi hilo la Mkoa litaweza kutekelezeka ili wananchi wa Iringa waweze kupata haki ya kupata madaktari wakati wote?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Kabati kwa sababu wiki mbili zilizopita tulikuwa pale Iringa tukaenda mpaka Kilolo na miongoni mwa mambo tuliyopitia katika sekta ya afya kipindi cha nyuma tulifika mpaka Hospitali ya Frelimo kwa ajili ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma. Kwa jambo hili, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa sababu Waziri wa Afya na Waziri wa Mambo ya Ndani wameshakaa tayari ku-discuss jambo hilo, usihofu kila kitu kitaenda vizuri lengo kubwa ni tuweze kuwapatia huduma wananchi wetu vizuri. Kwa hiyo, hilo jambo ondoa hofu kila kitu kitaenda vizuri Serikali itashughulikia.
MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa tatizo la nyumba hizi za kukaa wahudumu wa afya hasa maeneo ya vijijini hasa Mikoa ya Lindi na Mtwara na Jimbo la Mtama ni kubwa sana. Pamoja na kazi nzuri sana inayofanywa na Taasisi ya Benjamin Mkapa ya ujenzi wa nyumba katika maeneo mbalimbali, Serikali haioni sasa umefika wakati wa kuanzisha mfuko maalum kwa ajili ya kulishughulikia tatizo hili ili kusogeza huduma za afya karibu na wananchi wetu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mkoa wa Lindi ni miongoni mwa maeneo ambayo yana changamoto kubwa sana ya afya. Mheshimiwa Nape ni shahidi kwamba katika jambo ambalo amekuwa akilipigia kelele sana ni hili la sekta ya afya na nimpongeze sana katika utekelezaji wa Ilani last week alienda kukabidhi ile ambulace, nadhani wananchi wa Mtama wana-appreciate kazi kubwa anayoifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili alilotoa ni wazo zuri kwa sababu sasa hivi tunatumia fedha za Local Government Development Grants kwa ajili ya kuhakikisha miradi mingi hasa viporo inakamilika hasa katika ujenzi wa majengo mbalimbali ya afya na elimu. Ndiyo maana katika mpango wa bajeti ya mwaka huu tumetenga karibuni shilingi bilioni 251.18, lengo kubwa ni kuwezesha upatikanaji wa makazi kwa wataalamu wetu.
Kwa hiyo, jambo la kuanzisha mfuko, nadhani kwa sasa tutumie huu mfumo tuliokuwa nao lakini wazo ni zuri tutalifanyia kazi kama Serikali kuona nini tufanye, lengo kubwa tuweze kutatua matatizo ya afya kwa Watanzania wote kwa ujumla wetu.
MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwanza naomba niweke rekodi sawasawa. Cha kwanza, Wilaya ya Mkalama haina Hospitali ya Wilaya, pili mapato ya ndani ni kidogo ukilinganisha na mahitaji ya Wilaya mpya zote Tanzania na tatu ni kwamba gari lililopo lilirithiwa kutoka Wilaya ya Iramba na uzoefu unaonyesha mgawanyo wa mali unapofanyika Wilaya mpya zinapata yale magari mabovu mabovu, hilo gari lipo tu kwenye vitabu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, ni lini Serikali itatoa magari mapya na ya uhakika kwa Wilaya zote mpya Tanzania ikiwepo Mkalama? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali pamoja na kujenga Kituo cha Afya ina mpango gani wa kunusuru vifo hasa vya akina mama na watoto katika mazingira ya kutokuwepo na gari la wagonjwa? Mheshimiwa Naibu Waziri ameshafika Mkalama na Naibu Waziri wa Afya naye alishafika Mkalama na kuona jiografia ile, hapa nilipo wananchi wangu wanalia kila siku msiba.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa Mbunge Jimbo lake limegawanyika kutokana na lile Jimbo alilokuwa Mheshimiwa Mwigulu Mchemba. Tulivyofika pale miongoni mwa changamoto kubwa sana katika Jimbo lake, kwanza kweli hawana Hospitali ya Wilaya lakini ndiyo maana jambo kubwa tulilolifanya kutokana na shida kubwa iliyopatikana pale, Mheshimiwa Mbunge alinipeleka pale na tukaweza kuangalia kwa pamoja tukaweka katika mpango wao wa sasa kuhakikisha kwamba tunakikarabati kile Kituo cha Afya ili waweze kuwa na theater kabisa ya upasuaji wa watoto na Mungu akijalia tutapeleka mradi wa takribani shilingi milioni 700.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la lini gari la wagonjwa litapatikana, naomba nisitoe commitment ni lini litapatikana. Kama nilivyosema awali katika majibu yangu ya msingi kwamba jambo kubwa hili tuanzie katika needs assement ya Halmashauri yetu. Naomba niseme kwamba Serikali imesikia kilio cha Mheshimiwa Allan na tutaangalia uwezekano wowote utakaowezekana, tukipata fursa tutatoa kipaumbele kwa Jimbo la Mkalama kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma ya kutosha.
Mheshimiwa Mweyekiti, hata hivyo, niseme kwamba kama Serikali kwa umoja wake inajua kwamba wananchi wa Mkalama wana shida kubwa sana, tutajadiliana kwa pamoja kwa mawazo mapana zaidi. Kwa sababu licha ya kutokuwa na vituo vya afya…
Hata miundombinu ya barabara kuwasaidia wagonjwa kufika hospitalini ni shida tutalifanyia kazi.
MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwa kuwa Ukerewe inaundwa na visiwa na kwa kuwa yanapotokea matatizo ya dharura kiafya inakuwa kazi ngumu sana kuwawahisha wagonjwa kupata huduma ya ziada.
Je, sasa Serikali haioni umuhimu wa kutoa ambulance boat kuweza kusaidia kuokoa maisha ya wananchi wa Ukerewe?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshiniwa Mwenyekiti, najua kwamba tulipeleka ambulance kule ya kawaida katika kipindi cha kati, lakini na mahitaji ya kwamba watu wa Ukerewe wapate ambulance boat, naomba Serikali tuchukue kwa mawazo yenu mapana. Kama Mbunge anavyofahamu tuliongea naye private kwamba tutafika Ukerewe baada ya Bunge hili, tukifika kule tutajadiliana kwa mapana na pamoja nini tutawasaidia wananchi wa Ukerewe. Pia jambo hili tutaangalia jinsi gani tuliweke katika kipaumbele kama Serikali kwa kuweka mawazo ya pamoja kwa upana wake.
MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Chemba ni kati ya Wilaya mpya katika Mkoa wetu wa Dodoma. Ukitoka Kondoa kwenda Chemba ni zaidi ya kilomita 50 na ukitoka Dodoma Mjini kwenda Chemba ni zaidi ya kilomita 100 lakini Kituo cha Afya kilichopo pale hakikidhi mahitaji na Kituo cha Bahi ambacho kinahesabika kama Hospitali ya Wilaya bado kina upungufu makubwa. Je, lini Serikali itaungana na wananchi wa Chemba kuhakikisha kwamba Makao Makuu ya Wilaya inapata hospitali ya Wilaya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini ni kwamba mpango wa Serikali wa mwaka huu imetengwa shilingi milioni 23 ambayo ni kwa ajili ya kuhakikisha tunafanya maandalizi ya awali lakini tumeshaingiza katika mpango mwingine na vilevile wenzetu wa Chemba wako katika mchakato wa kushirikisha National Health Insurance Fund katika jambo hilo. Kwa hiyo, naomba tuseme kwamba mipango hii yote itaenda kwa pamoja kusaidia Chemba iweze kupata kituo cha afya. Hata hivyo, ndiyo maana tunaamua kufanya ukarabati mkubwa katika Kituo kimoja cha Afya cha Chemba na Bahi tupunguze referral system ili kusaidia wananchi kupata huduma za upasuaji wakiwa katika maeneo yao.
MHE. WILLIAM M. NGELEJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza naishukuru sana Serikali kwa ufafanuzi wa swali ambalo limeulizwa na Mheshimiwa Kemirembe lakini nilitaka tu kupata commitment ya Serikali kwa sababu kwa kuwa ombi letu la Halmashauri ya Sengerema la huo mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Serikali lipo Serikalini kwa zaidi ya miaka mitatu sasa.
Je, ni lini Serikali itaunganisha nguvu na Halmashauri ya Sengerema kutekeleza mradi huu kwa sababu ombi letu lipo pale na Serikali inafahamu? Nachotaka kujua sasa hivi ni lini Serikali itatuwezesha kupitia kasma ambayo tumeiomba ukijumlisha na kasma ambayo tumeitenga sisi Sengerema ili tutekeleze mradi huo? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itafanya jambo hilo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, ndiyo maana nimesema katika commitment yetu katika bajeti inayokuja tumetenga shilingi bilioni 251.18 ambapo katika fedha hizo miongoni mwa mambo tunayoenda kufanya ni suala zima la ujenzi wa vituo vya afya na hospitali katika maeneo mbalimbali. Nina uhakika Sengerema waliweka jambo hili kama priority yao katika mpango wa Halmashauri basi halina shaka tutashirikiana na ofisi yetu ya TAMISEMI lengo kubwa ikiwa ni wananchi kupata huduma ya afya.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru sana kwa kunipa nafasi ili na mimi niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa mwaka 2015 wakati wa kampeni Mheshimiwa Rais alituahidi kilomita10 Mpwapwa Mjini na kwa kuwa bajeti iliyopita tumepewa kilomita moja tu, hata Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Jafo analifahau hilo. Je, Mheshimiwa Waziri ataahidi wananchi wa Mji wa Mpwapwa kwamba hizo kilomita 10 zitakamilika?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Naibu wangu kwa ufafanuzi mzuri wa maswali ya awali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika swali la Mheshimiwa Lubeleje, ni kweli anachozungumza na mimi na yeye tulikuwa pamoja pale Mpwapwa Mjini kukagua barabara na ndiyo maana tumempelekea injinia mzuri sana kupitia TARURA na injinia yule wakati tunafanya ukaguzi wa Shule ya Sekondari ya Mpwapwa nilimpa maelekezo maalum.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimtoe hofu Mheshimiwa Lubeleje ule ujenzi wa lami unaoendelea pale Mpwapwa Mjini tutaukamilisha na itakapofika 2020 Mheshimiwa Lubeleje awe na uhakika kwamba ahadi ya Mheshimiwa Rais itakuwa imekamilika na kuthibitisha kwamba Mbunge wao amefanya vyema kusimamia eneo hilo. Ahsante sana.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Hizi kilomita 10 Mheshimiwa Rais aliahidi maeneo mengi sana. Nashauri data zote za kilomita 10 ambazo Mheshimiwa Rais aliahidi ili wamkumbushe kwa sababu kwa Jiji langu la Mbeya aliahidi pia kilomita ikiwemo barabara ya Mapelele, Kata ya Ilemi lakini mpaka leo hatuoni mchakato wowote na hatujapata nafasi ya kumuuliza Mheshimiwa Rais kwa sababu hajawahi kuja Mbeya toka amechaguliwa zaidi anarudi tu Kanda ya Ziwa. Mara ya mwisho ilikuwa aje Mbeya juzi kwenye ALAT, lakini waka-cancel siku mbili kabla ya siku ya ALAT kufanyika…
Kwa hiyo, tunamwomba sana Mheshimiwa Rais aje Mbeya pia.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la rafiki yangu Mheshimiwa Sugu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tunazo takwimu zote za nchi nzima za ahadi za Mheshimiwa Rais za ujenzi wa miundombinu ya lami lakini na maeneo mengine. Mheshimiwa Sugu anafahamu pale katika Jiji la Mbeya kupitia Ofisi yetu tumepata investment kubwa ya kujenga barabara za lami katika Jiji la Mbeya. Siyo barabara za lami peke yake tumefanya uboreshaji, zile barabara zote tunazifunga taa na kujenga damp za kisasa kupitia mradi wa Strategic City Project.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, jambo hili ni commitment ya Serikali na tumefanya vizuri Jiji la Mbeya, Tanga na Arusha na niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba ahadi zote ambazo Mheshimiwa Rais alizizungumza katika Halmashauri mbalimbali tutazitekeleza kupitia miradi yetu na kuhakikisha kwamba ikifika 2020 viporo hivi tutakuwa tumevimaliza hakuna shida ya aina yoyote.
MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kuna barabara ambazo upembuzi yakinifu ulishakamilika toka mwaka 2015/2016. Kwa mfano, barabara ya kutoka Nyororo - Igohole mpaka Mtwango upembuzi yakinifu ulishafanyika. Ni lini sasa Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga barabara ile kwa kiwango cha lami?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kigola anafahamu tulipokuwa Wilayani kwake tulizunguka maeneo mbalimbali na barabara anayoizungumzia ilikuwa ni barabara ya TANROADS na kulikuwa na barabara zingine za Halmashauri ambazo TARURA itashughulikia na zile barabara za Kimkoa ambazo TANROADS itashughulikia. Najua wazi kwamba mazoezi ya upembuzi yakinifu katika maeneo mbalimbali yanafanyika na kwa vile ile ilikuwa katika ahadi na Ilani ya Chama cha Mapinduzi, naomba nimhakikishie kwamba Serikali ni moja, tutahakikisha jukumu la Serikali tunalifanya ili barabara ile ya Nyororo iweze kujengwa kwa kadri iwezekanavyo.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa lengo la Serikali kuchukua vyanzo vingi vya Halmashauri za Wilaya ilikuwa ni kusaidia ruzuku ya kutosha kwenye Halmashauri hizi. Lakini kwa kuwa ruzuku inayotolewa haitoshelezi kabisa kwa Halmashauri hizi kujiendesha.
Sasa swali langu, naishauri Serikali kwamba je, Serikali inaweza kurudisha baadhi ya vyanzo vya mapato kwa Halmashauri ili nazo ziweze kujiendesha badala ya kusubiri ruzuku na ruzuku yenyewe inachelewa sana?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu wangu katika swali la msingi nilipenda kujibu swali la Mheshimiwa Lubeleje ambapo mimi ninamuita greda la zamani makali ya yale yale. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna vyanzo mbalimbali vilichuliwa na Serilkali Kuu. Hata hivyo, kwa mamlaka tuliyopewa tutafanya namna ili kuhakikisha kwamba mapato, hata hayo ya vyanzo vilivyobaki yaweze kukusanywa vizuri.
Mheshimiwa Spika, ilikuwa kwamba hata miongoni mwa vyanzo tulivyokuwa navyo ukusanyaji ulikuwa na changamoto kubwa na ndiyo maana katika program zetu hivi sasa tunafanya namna ili tuweze kutumia mifomu ya electronic kwa ajili ya uongezaji wa mapato.
Mheshimiwa Spika, naomba niwahakikishieni kwamba sasa hivi Wizara ya Fedha imefanya commitment kwamba fedha zote zilizokusanywa zipelekwe na ndiyo maana mpaka leo hii ninavyozungumza katika quarter ya kwanza zaidi ya shilingi trilioni moja imechukuliwa katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa katika OC na miradi ya maendeleo.
Kwa hiyo, ni imani yangu kwamba kutokana commitment ya Serikali katika ukusanyaji wa mapato jambo hili litakwenda vizuri; na hatimaye Mamlaka za Serikali za Mitaa zitaweza kutimiza wajibu wake kama inavyokusudiwa.
MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niuliza kwamba Wilaya ya Siha inafanana sana na Nyamagana tuna hospitali mpya ya Wilaya ambayo Waziri wa TAMISEMI Mheshimiwa Jafo alikuja akashirikiana na sisi kufanya kazi nzuri ya kuhakikisha hospitali hiyo inaweza
kulaza na kufanya upasuaji. Lakini sasa tuna changamoto, pamoja na vifaa lakini tuna upungufu wa asilimia 74 ya watumishi. Je, Waziri atakuwa tayari tukae na yeye kujadili kwa namna ya dharura namna ya kusaidia hospitali hiyo? (Makofi
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mollel kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nilifika Siha na ni kweli hata takriban wiki moja na nusu nilikuwa naongea na Mkuu wa Wilaya yako ya Siha na bahati nzuri katika kazi kubwa tunayoenda kuifanya katika umaliziaji wa hospitali tatu za awali ikiwepo Mvomero na Hospitali ya Siha na maeneo mengine tunaenda kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, jambo hilo hata bila kukaa tumeshalimaliza tayari kwa ajili ya maslahi mapana ya wananchi wa Tanzania. (Makofi)
MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, wakati fulani ni vizuri haya majibu nayo tukawa tunayaona vizuri kwa sababu, Mheshimiwa Mbunge anauliza Daraja la Mto Mori, Rorya. Majibu ya matumaini yanakuja Daraja la Mto Mori, Tarime inakuwa inapoteza ile ladha ya swali na hasa mtu anapokuwa ameuliza swali kwa muda mrefu katika Bunge hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka kujua Halmashauri hazina uwezo wa kujenga hili daraja ndio maana zimeomba Serikali Kuu isaidie kwa maana ya TAMISEMI. Ni lini sasa Serikali Kuu itatoa fedha za kusaidia daraja hilo kwa sababu Halmashauri ya Wilaya ya Rorya uchumi wake ni mdogo haiwezi kujenga hilo daraja?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika Jimbo la Bunda ambalo natoka mimi kuna daraja la Mto Chamtikiti ambalo limeharibika muda mrefu na hivi karibuni tumesikia kwamba kuna fedha ilitoka kwa ajili ya kutengeneza daraja, lakini mpaka leo mvua inanyesha wanafunzi hawaendi shuleni kwa sababu ya hilo daraja. Ni lini Waziri atakuja Bunda kuliona hilo daraja kwa ajili ya kusaidia hali hiyo?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niseme ni kweli nafahamu na mimi Mheshimiwa Getere unafahamu nilikuwa kule Rorya na pale changamoto ni kubwa. Na ni kwamba Halmashauri tunafahamu wazi kwamba kwa sasa haitaweza isipokuwa ni kwa kupitia mamlaka yetu tuliyoiunda ya TARURA.
Kwa hiyo, naomba niwahakikishie kwamba, suala zima la daraja hili na kwa sababu eneo hili ni eneo la kipaumbele, nitawaagiza wataalam wangu wafike katika daraja hilo, lakini na eneo lingine ambalo Mheshimiwa Getere ulilizungumza, lengo kubwa ni kwamba waende kufanya tathmini tujue thamani ya kazi halafu tutaangalia tutalitengeneza kwa kifungu gani. Aidha, kupitia DFAD kwamba eneo hilo saa nyingine ni eneo la vikwazo au kupitia Mfuko wa Barabara kwa kadiri itakavyoonekana inafaa, lakini nikuhakikishie kwamba, nitawatuma wataalam wangu wataenda kufanya study ya kutosha, lengo kubwa kuwasaidia wananchi katika maeneo hayo.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa Mheshimiwa Rais aliahidi maeneo mengi hasa wakati wa kampeni katika Jimbo la Mbulu Vijijini aliahidi ujenzi wa barabara kilometa tano katika Mji wa Haydom na Dongobesh kilometa mbili. Je, ni lini sasa ahadi hizi za Mheshimiwa Rais zitatekelezwa?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilizungumza hapa siku za nyuma zilizopita kwamba kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu kwamba uratibu wa ahadi zote za Mheshimiwa Rais umefanyiwa kazi na nikuhakikishie Mheshimiwa Flatei kwamba commitment yetu ni kwamba, tutakapofika mwaka 2020 tuhakikishe kwamba, zile ahadi zote za barabara hizi ambazo zimelengwa ziweze kukamilika. Na kupitia Wakala wetu wa TARURA tumewapa hayo maelekezo kwamba, wahakikishe kwanza jambo la kwanza wana-identify ahadi za Mheshimiwa Rais na ahadi za viongozi wakuu katika maeneo hayo lengo kubwa kwamba waweke mpango kazi jinsi gani tutafanya tukifika mwaka 2020 maeneo hayo yote tuwe tumeweza kukamilisha jambo hili.
MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupewa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Jimbo la Lupembe, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe
ni moja ya Halmashauri ambayo haina Hospitali ya Wilaya na tuna vituo vya afya vinne, kituo cha afya kimoja cha Lupembe ni cha zamani, hivi karibuni tumefungua chumba cha upasuaji tayari operation zinaendelea pale. Tuna Kituo cha Kichiwa ambacho tunatarajia pia tuwe na theater ili kuwahudumia akina mama wasitembee umbali mrefu kwenda Kibena.
Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kujenga au kuanzisha chumba cha upasuaji ili akina Mama katika Kituo cha Afya cha Kichiwa ili akina Mama wasisafiri umbali mrefu kwenda hospitali ya Kibena ambayo ipo mbali sana na wanapoishi ambapo Jimbo la Lupembe lipo. Ahsante.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA
NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Lupembe kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kituo cha afya cha Kichiwa kumbukumbu zangu katika programu yetu ya vile vituo vya afya vya kwanza 172, katika vituo vile kuna fedha ambazo tulipata kutoka Canada, fedha zile zimeshaendelea katika maeneo mbalimbali na baadhi ya vituo sasa hivi wameshafika level ya renta, lakini kuna zile fedha kutoka World Bank ni kwamba upelekaji wake wa fedha utakamilika ndani ya wiki hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni kwamba wananchi wako watarajie kwamba jinsi gani waweze kushiriki kazi lakini fedha zile tutatumia force account. Niwasihi hasa viongozi wetu huko katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa, zile fedha zinapokuja lazima wazisimamie vizuri tupate value or money na wananchi waweze kupata huduma. (Makofi)
MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Halmashauri ya Kibiti ni Halmashauri moja ambayo imetoka Wilaya ya Kibiti na kituo chake kikubwa cha afya Kibiti lakini hivi sasa kimezidiwa kutoa huduma.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Hospitali
ya Wilaya ya Kibiti? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hoja anayoizungumza Mheshimiwa Ungando ni hoja ya kweli na kwa sababu nilikuwa naye katika vile visiwa 40 vya Delta kwa kutwa nzima na changamoto ya afya kule ni kubwa sana, ndiyo maana katika kipindi cha sasa tumepeleka fedha katika kituo cha afya kimoja ambacho mimi na Mheshimiwa Mbunge tulizunguka mpaka usiku pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala zima la progamu ya uanzishaji wa Hospitali ya Wilaya ya Kibiti, naomba nikusihi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutashirikiana kwa pamoja kwa sababu lengo letu kubwa zile Wilaya zote zilizokosa hospitali sasa tuweze kuwa na progamu maalum kwa ajili ya kujenga hospitali. Kwa hiyo, Mheshimiwa Ungando naomba nikupe faraja kwamba tutashirikiana kwa pamoja tuangalie way forward tunafanyaje tupate Hospitali ya Wilaya ya Kibiti kwa sababu population ya watu pale ni kubwa hasa ukiangalia barabara ya Kilwa lazima tuhakikishe kwamba tunafanya jambo hilo kwa haraka. (Makofi)
MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniruhusu niulize swali la nyongeza.
Kwa vile matatizo haya ya afya katika Wilaya ya Kakonko yanafanana sana na ukosefu wa Hospitali ya Wilaya ya Uyui na Wilaya ya Uyui tumejitahidi kupitia Halmashauri kujenga hospitali lakini tumeishia kwenye OPD na tungeomba Serikali ituambie; je, inaweza kutuongezea hela ili tuweze kumalizia OPD yetu?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli pale hawana Hospitali ya Wilaya na wameanza programu ya ujenzi wa OPD, lakini sasa hivi tunafanya needs assessment katika maeneo yote ambayo majengo yalianza bado hayajakamilika. Ndiyo maana katika harakati zetu sasa hivi tunakamilisha Kilolo, Mvomero lakini tunaenda kule Siha ninaamini kwamba Uyui. Naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mchakato tunaofanya hivi sasa na wataalam wangu pale ofisini tutaangalia nini tufanye, lengo kubwa tuikamilishe hospitali yetu ya Uyui na wale Wanyamwezi wa Tabora pale waweze kupata huduma kama Wanyamwezi wengine hapa Tanzania. (Makofi)
MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.
Katika suala la elimu bure, moja ya changamoto ni pamoja na utoro unaowakabili hasa watoto wa kike. Sasa ningependa kujua Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba Serikali sasa ina mpango gani kuhakikisha ya kwamba watoto wa kike wanaoingia shuleni wanabaki shuleni kwa kumaliza, kwa Serikali kuweka pesa za ruzuku kwa ajili ya sanitary pads (vifaa vya hedhi) kuziongeza katika capitation fund ili kuweza kupunguza suala la utoro mashuleni. Sasa Serikali ina mkakati gani katika bajeti ijayo kuongeza pesa hizo ili watoto wetu waweze kupata pedi hizo bure mashuleni? Ahsante. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA
NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika makubaliano ya Jumuiya ya East Africa nadhani ni miongoni mwa jambo ambalo lilikuwa likijadiliwa sana hasa tatizo kubwa la watoto wasichana wanapokosa hivi vifaa kwa ajili ya kujikimu wakiwa shuleni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tulichukue hili kwa sababu ni jambo la msingi basi tukifika kwenye mchakato wa bajeti sisi sote tushirikiane kwa pamoja tuangalie nini tufanye ili mradi kuhakikisha kwamba tuweze kusaidia vijana wetu watulie masomoni na wapate elimu vizuri. Kwa hiyo, tunalichukua kama mchango mzuri katika mchakato tutakuja tutaijadili. (Makofi)
MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jibu la msingi Waziri amezungumzia kwamba baadhi ya Halmashauri tayari wameshamaliza ujenzi wa maabara katika shule za sekondari na mojawapo ya Halmashauri hii ni Halmashauri ya Malinyi tumeshamaliza karibu asilimia 90 ya maabara ya masomo ya sayansi katika shule za sekondari na baadhi ya majengo haya sasa hivi yanaanza kuharibiwa na wadudu wau ndege aina ya popo.
Je, ni lini Serikali watakamilisha utaratibu wa kupeleka vifaa ili maabara hizo zianze kutumika rasmi.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwamba tuliweza kununua vifaa kwa ajili ya maabara zaidi ya 1,000, tumeweza kuvisambaza. Ninafahamu Mheshimiwa Dkt. Mponda hata tulivyofika kule kwako Malinyi tuliona kweli ulitoa concern hiyo.
Kwa hiyo, tutafanya kila liwezekanalo kuona jinsi ya upelekaji wa vifaa. Hata hivyo, katika ile shule ambayo ulisema ina changamoto kubwa, kabla ya mwezi wa pili nadhani tutafanya kazi kubwa kuhakikisha kwamba shule ile tunaiboresha, wananchi wa Malinyi ambao wana changamoto kubwa sana waweze kupata elimu vizuri.(Makofi)
MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante na mimi napenda kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Mtwara Vijijini, Kata ya Mambo Pacha Nne na Kata ya Tangazo, Kijiji cha Kilambo, wameanza mchakato wa kujenga vituo vya afya na michango ya wananchi inaenda kwa kasi kubwa.
Je, Serikali itatusaidiaje katika kukamilisha ujenzi wa vituo vya afya katika Kata ya Tangazo, Kijiji cha Kilambo na Kata ya Mango, Pacha Nne?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa sababu, miongoni mwa maeneo ambayo alileta kama request katika Jimbo lile la Mtwara ni eneo hilo kwa sababu liko linapakana na Msumbiji.
Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, katika vipaumbele vyetu vya sasa katika programu tunayoanza nayo kabla ya mwezi wa pili, maeneo yale tumeyapa kipaumbele na tumeyaingiza katika mpango wetu wa bajeti ya muda katika hizi funds ambazo tunazipata kutoka kwa wafadhili mbalimbali. (Makofi)
MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii. Serikali iliahidi kupeleka fedha za kutosha kwa ajili ya ukarabati na kuviwezesha vituo vya afya karibu sehemu yote ya nchi. Mojawapo ni kituo cha afya cha Ulyankulu. Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kutupa status ya utumaji wa fedha hizo kwenye vituo vya afya kote nchini?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS – TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri wangu kwa ufafanuzi mzuri wa swali la awali. Hata hivyo, napenda kutoa status ya suala la ujenzi wa vituo vya afya ambavyo tumesema ni ukarabati mkubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, tulifanikiwa kupata fedha kutoka mifuko miwili. Fedha kutoka World Bank ambapo lengo letu ni kukarabati vituo vya afya 100, lakini nyingine tulipata fedha kutoka Ubalozi wa Canada tumeshazipeleka katika kila kituo takriban shilingi milioni 500. Hali ya ujenzi mpaka sasa, wengine wako katika stage ya lenta na wengine wanapauwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, fedha zilizotoka Mfuko wa World Bank, fedha zile zilichelewa kidogo ambapo ndani ya wiki hii fedha hizo ndio zitafika vituoni, japokuwa tulitoa deadline kwamba, tarehe 30 mwezi wa 12 vituo vyote viwe vimeweza kukamilika, kwa sababu hizi fedha kutoka Mfuko wa World Bank zilichelewa kufika vituoni tuta-extend huo muda angalau tufike mwishoni mwa mwezi Januari. Hali halisi hivi sasa fedha za Canada zimeshafika, lakini za World Bank ndiyo wiki hii zinafika vituoni. (Makofi)
MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kupata nafasi hii. Napenda tu kumuuliza Mheshimiwa Waziri ni lini Kituo cha Bunda Mjini kitapewa hadhi ya hospitali ya Wilaya?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS – TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la mchakato wa kupandisha kituo cha afya kuwa hospitali ni utaratibu. Mchakato huo unaanzia katika Halmashauri kwenye Baraza la Madiwani linafanya hivyo and then inaenda DCC, RCC, baadaye inafika kwa Waziri mwenye dhamana wa sekta ya afya; atakapoona kwamba kituo hiki kimekidhi na inafaa kufanya hivyo, basi atafanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani kama mchakato huo umeshaanza basi, jukumu hilo litakuwa chini ya Ofisi ya Waziri wa Afya, atakapoona kwamba vigezo vimekamilika na inabidi kufanya hivyo basi atafanya hivyo bila tatizo. (Makofi)
MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Matatizo ya upungufu wa Madaktari, watumishi wengine wa afya na vifaa tiba yaliyoko hospitali ya Mkoa wa Geita ni sawa kabisa na yale yaliyoko kwenye Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe, Hospitali ya Nansio. Serikali iko tayari sasa kuangalia visiwa vya Ukerewe kwa upendeleo maalum na kutusaidia kuondoa tatizo hili ili kupunguza vifo vya akinamama na watoto visiwa vya Ukerewe?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli. Mheshimiwa Mbunge anakiri kwamba, nilipata fursa ya kwenda na tuliweza kufika mpaka kule Ukerewe na ni kweli changamoto ya afya katika visiwa vile imekuwa ni kubwa zaidi. Ndiyo maana katika vipaumbele vyetu sasa hivi hata ukiangalia idadi ya Madaktari ambao juzi tu tumewaajiri, tumeajiri Madaktari takribani 2,058, tumepeleka vijana kule kwa ajili ya kusaidia suala la changamoto inazozipata.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, kuna fedha vilevile tunaenda kuboresha kile kituo cha afya kama alivyopendekeza Mheshimiwa Mbunge na hatutasita kuendelea. Tunafanya juhudi ya kutosha hasa kwa sababu tunajua kwamba eneo la Ukerewe lazima tuboreshe miundombinu ili hata watumishi tunaowapeleka kule wawe na hamasa ya kufanya kazi baada ya kuboresha mazingira yao. Kwa hiyo, jukumu hili tumelichukua sisi Serikali kwa ajili ya maslahi mapana ya wananchi wa Ukerewe.
MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Hospitali ya Geita ambayo sasa hivi ni Hospitali Teule ya Mkoa ilikuwa Hospitali ya Wilaya. Hata baada ya kuipandisha hadhi na kuwa hospitali ya mkoa imeendelea kupata huduma kutoka Serikali Kuu kama hospitali ya wilaya. Je, ni lini Serikali itaipatia huduma kama hospitali ya mkoa?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kwamba, kwa sababu imepandishwa, tunalifanyia kazi. Hata hivyo juhudi tuliyofanya kubwa kama Serikali ni kuhakikisha tunaanza hospitali ile kubwa ya Rufaa ya Mkoa, juzi Naibu Waziri wangu nimemtuma kuna kazi kubwa imeshaanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwahakikishie wananchi wa Geita kwamba Serikali tumejipanga kuboresha sekta ya afya katika Mkoa wa Geita kwa ujumla wake ili kuimarisha hospitali yetu ya Rufaa ya Mkoa na hospitali ya Mkoa na hali kadhalika vituo vya afya, tukijua kutokana na uchimbaji wa madini population imekuwa kubwa katika maeneo hayo. Kwa hiyo, kama Serikali tumelichukua, tutalifanyia kazi kuhakikisha tunapata idadi ya dawa zinazohitajika katika hospitali. (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Kwa kuwa, Mheshimiwa Naibu Waziri ametoa majibu mazuri ya kueleweka katika maswali haya na katika majibu yake ya msingi. Je, yupo tayari sasa kuandika maelekezo haya yaende kwenye Halmashauri yetu ili hizi Community Centers zifanye kazi yake iliyokusudiwa? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze ndugu yangu Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile kwa umahiri wake wa kwenda vizuri katika eneo hilo la afya na maendeleo ya jamii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwa muda mrefu sana Maafisa Maendeleo ya Jamii walikuwa wanatumika kama spare tyre. Matumizi yao mara nyingi sana katika Halmashauri zetu walikuwa hawatumiki vizuri, lakini kuanzia sasa ndiyo maana last week tulikuwa na training kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii yaliyodumu kwa siku tano mfululizo. Licha kutoa mafunzo hayo tuliwapa terms of reference nini wanatakiwa kufanya katika kazi zao. Namshukuru sana Mheshimiwa Jenista Mhagama, Waziri wa Afya na Waziri wa Viwanda, tuliwapa mwongozo maalum kwa ajili ya kwenda kusimamia katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa nimewaagiza Wakurugenzi wote kwa sababu Maafisa Maendeleo ya Jamii ndio agent of change katika maendeleo ya Halmashauri zetu. Sasa wawatumie na wawawezeshe kwa rasilimali fedha hali kadhalika kuwafanya kwamba kazi zao zifanyike vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge naomba niwahakikishie kuanzia sasa mtaona mwenendo tofauti wa Maafisa Maendeleo ya Jamii chini ya Wizara ya Afya na chini ya TAMISEMI ambao ndio tunawasimamia kwa karibu zaidi kama waajiri wao. (Makofi)
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza tatizo la uhaba wa vyumba vya madarasa na vyumba na uhaba wa nyumba za walimu limekuwa tatizo kubwa sana na Jimbo langu ni miongoni mwa matatizo ambayo yanawakabili katika shule ya Busongola, Bulamata, Vikonge, Mchangani, Kapanga na Kafishe ambako kuna vyumba viwili tu vya madarasa lakini zipo darasa saba. Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo la uhaba wa vyumba vya madarasa na uhaba wa nyumba za walimu?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Naibu wangu Mheshimiwa Kandege kwa clarification nzuri kwa maswali yote yaliotangulia.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tuna changamoto kubwa sana ya vyumba vya madarasa na ndio maana kwa Serikali kipindi hiki cha sasa tulifanya tulitumia takribani shilingi bilioni 21 kuhakikisha tunaongeza vyumba vya madarasa katika shule za sekondari 85 na shule za msingi 19. Lakini hata hivyo kipindi cha muda mfupi uliopita tumetumia takribani shilingi bilioni 16 kufanya uwezeshaji mkubwa katika shule za sekondari 65 na shule za msingi 56 lakini hata hivyo naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge katika fedha tulizozitenga takribani shiling bilioni 246 kwa ajili ya kusaidia kwamba yale maboma yaliyojengwa kuhakikisha tunayakamilisha naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge tushirikiane vya kutosha na wizara ya fedha, fedha ziweze kutoka ziende katika halmashauri zetu kwa lengo la kumalizia viporo na kujenga maeneo mengine lengo kubwa wanafunzi wetu wapate mahali pa zuri pa kusomea.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kunipa nafasi mimi ni kwa namna gani Serikali itoe utaratibu wa jamii, Halmashauri na Serikali Kuu kuweza kuweka nguvu pamoja kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu hivi sasa maboma yaliyo mengi katika Halmashauri zetu yamechukua miaka mingi ningeomba basi Mheshimiwa Waziri atume wataalamu kwa baadhi ya maeneo machache ili kunyambulisha ni gharama gani zitakazotumika katika ujenzi wa nyumba hizi za walimu na tuwe na lengo kwa kila Halmashauri kwa zile nyumba ambazo ziko katika lenta ili tuweze kukamilisha kuungana na wananchi. Nashukuru.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba kumpongeza Mheshimiwa Issaay nadhani swali lake limejenga katika kujenga suala zima la ushauri na kiufupi kwamba ushauri huu tumeuchukua ndio maana tuliongeza bajeti katika mwaka huu wa fedha kutoka shilingi bilioni 150 npaka kufika shilingi bilioni 246 kwa lengo kubwa kuweza kuhakikisha eneo hilo tunalifanyia kazi. Lakini tunafanya kazi hilo katika maeneo yote sekta ya afya na sekta ya elimu ambapo Mheshimiwa Issaay ndio ulikuwa umejenga hoja ya msingi kipindi cha Bunge lililopita.
Kwa hiyo, naomba niseme tutalichukua hili naamini kwa pamoja tukishirikiana lakini hata hivyo nipende kuwapongeza Wabunge hasa wanaotumia Mfuko wa Jimbo na kwa kushirikiana na maeneo yao ambapo katika tembea yangu nimekuta miradi mingi ambayo Wabunge kupitia Mfuko wa Jimbo wameingiza fedha kuhakikisha nyumba za walimu na madarasa yanafanyika hivyo, kwa hiyo nawapongeza sana kwa hali hiyo.
MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuru. Pamoja na mikataba ya bodaboda na bajaji, mikataba ni fursa za hawa vijana kufanya kazi katika miji. Sera ya MKURABITA ni mkakati wa kurasimisha biashara za wanyonge ziwe rasmi. Bodaboda na bajaji hizi baada ya mikataba hii wanapata tabu sana kufanya biashara katika miji na hasa kwenye barabara kubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa kutambua na kuwajali wafanyabiashara wadogo wadogo, lakini Mamlaka za Halmashauri bado zinazuia vijana hawa wasifanye biashara kwa uhakika na kuwatia hasara sana. Yako malalamiko, madalali wanaokamata bajaji na bodaboda wanaruhusu bodaboda zao tu ziingie mjini.
Je, Serikali sasa kwa kutambua sera MKURABITA wanaonaje sasa hili jambo liruhusiwe na hawa vijana wapate uhalali wa kufanya biashara katika miji yetu? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, haya mambo yanatofautiana, ni case by case Mikoa kwa Mikoa na Wilaya kwa Wilaya, lakini Mheshimiwa Zungu ame-raise jambo la msingi sana. Naomba Ofisi yangu ilichukue jambo hili kwa ajili ya kuliwekea utaratibu mzuri tuangalie jambo gani lifanyike katika eneo gani ili mradi tufikie muafaka kwa ajili ya vijana wetu. (Makofi)
MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijauliza swali la nyongeza, naomba kuchukua fursa hii kukushukuru sana wewe kwa ushiriki wako mkubwa kutafuta fedha za kujenga Hospitali ya Wilaya ya Namtumbo kupitia Selous Marathon na hivi karibuni tutakuwa na chakula cha jioni kule Dar es Salaam, nakushukuru sana. Wananchi wa Namtumbo wataenzi sana kazi hiyo unayoifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, hivi Serikali hususani Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na TAMISEMI haioni umuhimu wa kuongeza bajeti ya kuendeleza ujenzi wa jengo la upasuaji kutoka milioni 100 zilizotajwa kwa mwaka ujao wa fedha hadi walau bilioni moja ili kweli ujenzi ufanyike?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa kuwa aliyekuwa Naibu Waziri wa Afya Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla alishafika Lusewa, Makao Makuu ya Mji Mdogo wa Sasawala na kujionea umbali ulivyo kutoka pale Lusewa hadi maeneo ambayo yanaweza yakapatikana huduma za upasuaji na hivyo akajionea kabisa hatari ambayo akina mama wajawazito wanaipata.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi Waziri wa TAMISEMI atatusaidiaje kuteleleza ahadi ambayo Naibu Waziri huyo aliitoa ya kuhakikisha Kituo hiki cha Afya cha Lusewa kinakamilika na kuanza kutoa huduma ndani ya mwezi mmoja wakati akijua kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo haina fedha kabisa?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Ngonyani kwa kazi kubwa anayofanya ya kuwalilia wananchi wake. Bahati nzuri mimi nimeweza kufika kule Namtumbo na Naibu Waziri wakati huo sasa hivi Waziri wa Maliasili, ni kweli changamoto ni kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue hoja ya Mheshimiwa Mbunge kwa ujumla wake na ndiyo maana kutokana na changamoto ya eneo hili ukiachia kile Kituo cha Afya cha Namtumbo tulichopeleka takribani shilingi milioni 400 mwezi Desemba na kazi tume-target mpaka tarehe 30 Aprili, zote ziwe zimekamilika lakini tumeanza juhudi tena kubwa zingine kuhakikisha tunaongeza vituo vya upasuaji katika Kituo cha Afya cha Msindo na Mkongo ambapo tunaenda kuweka thearter maalum kwa ajili ya upasuaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali tumesikia kilio chake, tutafanya kila liwezekanalo na timu yangu hapa chini ya Naibu Mawaziri wangu kuhakikisha kwamba mambo haya yanaenda kwa kasi na ndiyo maana kutokana na jiografia ya Wilaya ile jinsi ilivyo leo hii tuna zoezi tena la vituo vya afya viwili. Ahsante.
MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mkoa wa Morogoro wenye Wilaya saba na Halmashauri tisa ina Hospitali za Wilaya mbili tu ambazo ni Ulanga na Kilosa. Kwa kuwa katika bajeti ya mwaka huu, Serikali imetenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Wilaya ya Morogoro hususani katika Halmashauri ya Morogoro Vijijini katika Kata ya Mvuha.
Je, ni lini Serikali italeta hizi shilingi milioni 500 ili tuanze ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Mvuha?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Naibu Waziri, napenda kujibu swali hili la Mheshimiwa Omary Mgumba, ni kweli na mimi nilipata fursa ya kufika Mvuha nikiwa na Mbunge mwenyewe jiografia na hali ya pale tunatakiwa tufanye kila liwezekanalo kuhakikisha tunaimarisha huduma ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wengine wote ni jukumu la Serikali kuhakikisha kwamba tunaboresha sekta ya afya ndiyo maana leo hii tunaboresha vituo vya afya 212 kwa awamu ya kwanza kihistoria.
Mheshimiwa Mgumba naomba nikuambie, nilifika pale na tumebaini changamoto na Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi itafanya kila liwezekenalo kuwasaidia wananchi wa Morogoro Vijijini na wananchi wengine katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, rai yangu moja kubwa ni kwamba tunafanya ujenzi wa vituo vya afya 212 then vituo vya afya vingine 70 vipya vitakuja, niwaombe Waheshimiwa Wabunge tushirikiane kusimamia matumizi mazuri ya fedha, lengo kubwa ni kwamba ikifika tarehe 30 Aprili, tuwe tume- launch vituo vya afya visivyopungua 212 katika historia ya nchi yetu hii.
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, wabheja sana.
Kwa kuwa Jimbo la Kishapu lenye watu shapu na Mbunge shapu, ni moja ya Majimbo ama Jimbo lililotekeleza kwa kiwango cha juu sana mpango wa huduma za afya. Tunayo hospitali ya kisasa kabisa katika Wilaya yetu ya Kishapu, tuna vituo vinne vya afya vya kisasa kabisa ambavyo vimekamilika na vinatoa huduma bora katika Jimbo la Kishapu, lakini katika vijiji 118, takribani asilimia 50 mpango wa zahanati katika Jimbo la Kishapu unaendelea vizuri na miongoni mwa vituo hivyo vya zahanati vinatoa huduma bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu je, ndugu yangu, wajina Mheshimiwa Suleiman Jafo na dada yangu Mheshimiwa Ummy, kutokana na malumbano ama tatizo kubwa la mpango wa afya ambalo ni dhahiri limeelezeka na wewe umekiri kuwa watu wengi wanahitaji kuuliza maswali katika jambo hili la afya na kwa kuwa Kishapu tumekwishajitahidi tumepiga hatua…
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Kwa kuwa Kishapu tumepiga hatua kubwa, je, Wizara ya Afya na Ofisi ya TAMISEMI kwa maana ya Wizara hawaoni sasa watoe kipaumbele kwa Jimbo la Kishapu ili kuiweka kuwa ni ajenda maalum na kipaumbele cha kumaliza tatizo hili ili Kishapu iwe mfano katika Wilaya zote nchini kwa kumaliza kabisa tatizo hili kwa kutuongezea michango?
AZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge Nchambi kwa kazi kubwa ya ujenzi wa vituo vya afya na zahanati na shughuli kubwa wanayofanya ya uhamasishaji katika eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mbunge kwamba tutamuunga mkono na ajenda ya kwanza ni kwamba Ofisi yangu itafanya utaratibu wa ziara maalum kama ya kiheshima kwenda kule Kishapu ku-recognize juhudi kubwa inayofanywa kule. Baadaye tutaangalia way forward tunafanyaje kwa pamoja kwa lengo kubwa la kuwasaidia wananchi wa Kishapu kwa juhudi hiyo waliyoifanya.
MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Chalinze Wilayani Mdaula, kuna zahanati ambayo wananchi kwa nguvu zao wamekuwa wanaijenga tangu mwaka 2012. Wamejenga, wameweka plasta, wameweka madirisha, lakini bado wanasuasua kwa sababu uchumi siyo mzuri. Sasa swali langu kwa Serikali, ni lini sasa Serikali itaongeza nguvu ya Serikali kuwasaidia wananchi ile zahanati imalizike kusudi wananchi waweze kupata mahali pa kwenda kupata tiba? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Naibu Waziri wangu kwa ufafanuzi mzuri wa maswali yote ya awali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunafahamu Mdaula na maeneo mengine kuna changamoto, wananchi wamefanya juhudi kubwa na ndiyo maana azma ya Serikali yetu ni kuhakikisha kwamba tunaunga mkono juhudi za wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hilo, sasa hivi tunafanya uwezeshaji wa kuangalia jinsi gani tutafanya kuhakikisha maboma yote yaliyojengwa katika Halmashauri zetu tunayakamilisha. Tutatumia takribani shilingi bilioni 69 ambapo jambo hili maeneo ya Mdaula pale, hasa Halmashauri ya Chalinze tutawaelekeza wahakikishe katika umaliziaji wa maboma hayo, ile Zahanati ya Mdaula iweze kutengewa fedha katika hizo fedha ambazo tutazitoa kuhakikisha kwamba wananchi wa eneo lile wanapata huduma za afya, kama azma ya Serikali ilivyokusudia.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, toka tumeanzisha Wakala wa Barabara (TARURA) katika Mkoa wa Songwe na Wilaya ya Momba hakuna barabara yoyote ambayo inajengwa sasa hivi kwenye bajeti ya mwaka 2017/2018, je, kazi hii ya TARURA itaanza kutekelezwa lini na hasa barabara ya kutoka Kakozi - Ndalambo kuelekea Kapele? Barabara ni mbaya sana na sasa haipitiki. Ahsante sana.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli na kama tunavyofahamu, ni kwamba tarehe 7 Julai, 2017 ndiyo Wakala huu umeanza kufanya kazi rasmi katika mwaka huu wa fedha tunaoendelea nao. Huu ni Wakala mpya na lengo lake ni kuhakikisha kwamba zile kazi zilizokuwa zinafanywa na Halmashauri zetu, sasa zitafanywa na Wakala huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati nzuri mwezi uliopita nilikuwa na kikao na Watendaji wote wa TARURA wa Nyanda za Juu Kusini pale Mjini Mbeya na kuwapa maelekezo mbalimbali, lakini zoezi hilo lilikuwa limekamilisha semina na maelekezo mbalimbali kwa wataalam wote wa TARURA nchi nzima. Baada ya kufanya zone zote nne, tulianza Bagamoyo tukaenda Tanga, tukaenda Mwanza na tukamalizia kule Mbeya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wakala huu sasa uko katika mchakato wa stage mbalimbali. Ndiyo maana wale wanafahamu mikoa mbalimbali hivi sasa. Sasa kandarasi zinaanza kutoa mikataba kwa wakandarasi wa aina mbalimbali na mingine kutokana na zile bajeti zake zilizopita ziko kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nikuhakikishie kwamba mchakato huu unaenda na maeneo yote ya Tunduma na mikoa yote hivi sasa itashughulikiwa kwa kadri kandarasi hizo zilizotangazwa. Naomba niwahakikishie kwamba katika hili hatutakuwa na masihara katika usimamizi hasa wa ukandarasi utakaofanyika kule site, lengo letu ni kwamba Halmashauri zipate barabara bora kwa lengo kubwa la kuwasaidia wananchi wetu.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Kwa kuwa Kituo hiki cha Afya kinahudumia maeneo makubwa katika eneo la Ilemela, Usagara Wilaya ya Misungwi, pamoja na Jimbo la Sumve na ni Kituo cha Afya ambacho kiko highway, wakati wowote watu wanapata matatizo wanaposafiri wanahitaji huduma hii kubwa. Kwa kuwa sera ya mwaka 2007 ni kama imepitwa na wakati ukilinganisha na mazingira:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kubadilisha ili angalau kulingana na mazingira ya Kituo hiki cha Afya cha Kisesa, kiweze kupandishwa hadhi na kuwa hospitali ya wilaya ili kiweze kuhudumia maeneo makubwa?
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
6
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali iko hatua za mwisho, mkataba wa kujenga jengo la X-ray, jengo la upasuaji, limeanza mwaka 2013. Kama ni hatua za mwisho, leo ni miaka mitatu. Serikali haioni kwamba hii ni aibu, miaka mitatu inajenga majengo haya bila kukamilika na yanasubiri tu shilingi milioni 77 ili yaweze kukamilika? Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kuniambia hizi shilingi milioni 77 zikipatikana hata kesho ili huduma hizi zianze kutolewa, yuko tayari kunipa fedha hizi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikiri wazi, kituo cha Kisesa, junction yake ukiiangalia na ukubwa wake sasa hivi wa population ya pale, kweli ni eneo ambalo lina-capture watu wengi sana. Ukiangalia hata Kata jirani wanategemea sana Kituo cha Afya cha Kisesa. Kubwa zaidi, kwa mujibu wa sera siwezi kusema hapa kwamba tutabadilisha sera hii, kwa sababu nyie mnafahamu, lengo letu ni kuzifikia kila Halmashauri kupata hospitali za wilaya. Hivi sasa mnaona tuna deficit na tunaenda kwa kasi ili mradi angalau sasa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tuna wilaya zipatazo 139 na Halmashauri 181. Lengo letu ni kwamba kila Wilaya angalau ipate hospitali ya wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu kubwa ni kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi, tutafanya juhudi kituo hiki kiweze kukamilika na suala la upasuaji liweze kuendelea na huduma nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili ni kwamba, X-ray kwa muda mrefu imesuasua katika kituo hiki. Kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa sababu yeye alikuwa ni Mwenyekiti wa Halmashauri hii ya Magu ambayo naizungumza hivi leo. Kwa hiyo, hata mambo yanayoendelea huko, naye alichangia kwa kiwango kikubwa mpaka kufanikisha ujenzi huo unaendelea, naye anajua wazi tunaendaje. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mikakati iliyofanyika katika hicho kituo, sasa hivi tuko katika hali ya mwisho. Kwa sababu najua juhudi ya Mheshimiwa Mbunge aliyokuwa anaifanya hata nilipokuwa Jimboni kwake kule mwezi wa Kwanza katika harakati kubwa za kuboresha huduma ya afya hiyo na hata alikuwa anaomba hata ingewezekana watu walioasisi mifumo mizuri ya afya, Dkt. Pembe arudi Magu kwa ajili ya kuhakikisha afya inakwenda vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo kubwa ni kuhakikisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI kama tulivyofanya mawasiliano na Mkurugenzi kule, tutaweka nguvu ili ikifika mwezi wa Sita jengo lile liweze kukamilika na wa Kisesa waweze kupata huduma kama ilivyokusudiwa.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa upandishaji hadhi wa vituo vya afya nchini umekuwa na urasimu sana kwa sababu vibali lazima vitolewe na Serikali Kuu: Je, Serikali sasa haioni kwamba kuna umuhimu wa upandishaji hadhi wa vituo tu vya afya ukarudi kwenye Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kuliko kusubiri iende Serikali Kuu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kuna jambo moja hapa, kwa sababu katika mchakato wa upandishaji wa vituo vya afya, siyo Serikali tu inaamua. Jukumu kubwa ni kuhakikisha kwamba kuna vikao halali ambavyo vinakaa na mwisho wa siku yale maamuzi yote yaliyopitishwa mpaka katika Baraza la Madiwani yanakwenda Wizara ya Afya. Baadaye wakaguzi wanakuja kuangalia na mwisho kile kituo kinapandishwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima kurudisha katika Serikali za Mikoa; katika Mikoa kwa mujibu wa sera za afya, tuna Wakaguzi wa Kanda za Afya. Ni kwa nini zinafika mpaka Wizarani? Lengo ni kupata wataalam ambao watahakikisha quality control inafanyika na kituo kile kinakidhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni mawazo mazuri, huko mbele au siku za usoni tutaangalia ni jinsi gani tutafanya, ikiwezekana katika ku-decentralize, tukaweka timu za kufaa katika ngazi za mikoa ambapo wakati mwingine tunaweza tukafanya jambo hilo likaendeshwa katika huko, lakini kwa sasa hivi huo ndiyo utaratibu, lakini wazo ni zuri, huko siku za usoni inawezekana tukalifanyia kazi.
MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD: Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza;
Swali la kwanza, zahanati ya Mafiga inahudumia kina mama wengi lakini haina madawa kwa ajili ya akina mama na pia haina ultra sound machine ya akina mama.
Je, lini Serikali itaipatia zahanati ya Mafiga vifaa hivi?
Swali la pili, hospitali ya Mkoa wa Morogoro ambayo ipo njia panda ya barabara ya Morogoro inayokwenda Mikoa mingine yote ya Bara na ajali nyingi zinatokea, lakini haina mashine ya X-Ray, mashine iliyopo sasa hivi haifanyi kazi vizuri.
Je, Serikali haioni kama kuna uharaka wa kuipatia hospitali ya Mkoa wa Morogoro mashine ya X-Ray?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika maeneo yangu ambayo nimetembelea ni Morogoro, na jambo ambalo nimeshuhudia pale ni kwamba kama Mheshimiwa Mbunge pale kwa kweli kwa kutumia, licha ya ushawishi wakati mwingine anatumia resources zake mwenyewe kwa ajili ya wananchi wake. Naomba nikuhakikishe kwamba katika hii zahanati ya Mafiga uliyoisema ambayo changamoto kubwa ni madawa pamoja na vifaa tiba especially ultra sound na nimesema katika maelezo yangu ya awali. Katika research tuliyofanya haraka haraka vitu vingine vingekuwa vinaweze kupatikana kwa ukaribu sana lakini tatizo kubwa tulilokuwa nalo mwanzo ni kutokana na ile management ya fedha zilizokuwa zinapatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia idadi ya wanaofika katika zahanati ya Mafiga pale lakini collection ilikuwa ni changamoto kubwa sana. Ndiyo maana tulitoa maelekezo ya kutosha licha ya kufanya juhudi zingine za upatikanaji wa dawa na vifaa tiba, changamoto kubwa ni kwamba tukienda kukusanya mapato yetu vizuri ambayo katika njia moja au nyingine unakuta kwamba baada ya kutumia mifumo ya electronic, collection imeenda zaidi ya asilimia 800. Watu waliokuwa wanakusanya shilingi laki moja leo wanakusanya shilingi milioni moja, unaona kwamba jinsi gani pesa hizi zikikusanywa vizuri zitaenda kusaidia katika suala zima la madawa na vifaa tiba.
Kwa hiyo Mheshimiwa Abood naomba nikuambie ninakuhakikishia kabisa kwamba katika zahanati ya Mafiga mimi na wewe kwa sababu tumeshaahidi kwamba tutaenda Morogoro, hii ni sehemu ya kwanza kwenda kubaini kuwa tatizo la msingi ni nini, na tutafanyaje kuondoa tatizo la madawa, kwa sababu mwanzo watu hata mwongozo walikuwa hawaufuati, pesa hata zikikusanywa haziendi katika madawa na vifaa tiba, isipokuwa watu wanagawanya kwa per diem na vikao vingine visivyokuwa na maana yoyote.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo nimhakikishie Mheshimiwa Abood kwamba, hapa tutafanya ukatabati mkubwa ili utendaji wa zahanati hii na nyinginezo zinafanya kazi vizuri kwa ajili ya wananchi wa Morogoro.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la hospitali ya Morogoro ni kweli na mimi nikuambie kwamba miongoni mwa field practical zangu wakati nilipokuwa Chuo Kikuu mwaka 1998, nilifanya research zangu pale na field practical nilifanyia pale Morogoro, naifahamu vizuri hospitali ya Mkoa wa Morogoro. Ni kweli inapokea wagonjwa wengi sana na wakati mwingine hata ajali zikitokea watu wengi ni sehemu ya kimbilio, wanaotoka Iringa, Dodoma na sehemu mbalimbali pale ni kimbilio. Tunajua X-Ray machine ipo lakini haifanyi kazi vuziri, tuna mpango mpana sasa hivi wa Serikali hasa kwa ajili ya hospitali zetu za Mikoa na hospitali zetu za Kanda. Mpango huo sasa kwa Serikali ya Tanzania kwa kushirikana na Serikali ya Uholanzi tutahakikisha kwamba tunapeleka vifaa tiba katika hospitali zetu za Kanda na hospitali za Mkoa. Ninaamini na hospitali yetu ya Mkoa wa Morogoro tutaipa kipaumbele kutokana na strategic area yake ya kijiografia, lazima tuipe nguvu wananchi wa Morogoro waweze kupata huduma, ili wanufaike na huduma njema ya Serikali yao ya Awamu ya Tano ambayo inafanya kazi kwa maslahi ya Watanzania.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, kuhusu suala la uhaba wa dawa katika vituo vyetu vya afya, ningependa kuwafahamisha Waheshimiwa Wabunge kwamba tunapitia upya vigezo vya kugawa fedha za dawa. Kwa sababu kwa kweli tumeona hakuna uwazi, unakuta kituo kingine kina wananchi wengi lakini mgao wa dawa fedha ya dawa ni ndogo. Kwa hiyo, nataka kuwathibitishia Waheshimiwa Wabunge tunaangalia upya vigezo kama ni hospitali ya Mkoa wanatakiwa kupata shilingi ngapi na taarifa hizi tutazitoa kwa kila Mbunge ajue kituo chake cha afya kinapata shilingi ngapi, hospitali yake ya Wilaya inapata shilingi ngapi na hospitali ya Mkoa inapata shilingi ngapi. Kwa hiyo, tunataka kuwa wawazi zaidi katika mgao wa fedha za dawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.
Katika Hospitali yetu ya Wilaya ya Geita ambayo imepandishwa hadhi kuwa hospitali ya Mkoa kuna msongamano mkubwa sana wa watu kiasi kwamba kwa kweli changamoto ni kubwa sana. Ningependa hasa kujua kwa sababu tunatakiwa tujengewe Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa.
Ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi rasmi katika hospitali ya Mkoa ambayo itakuwa ni Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Mheshimiwa Bukwimba tulikuwa na Mheshimiwa Makamu wa Rais tulifungua hospitali ile ya Geita, kweli kuna msongamano mkubwa, na pale ni kipaumbele, nadhani mchakato wa Serikali tutafanya mambo haya kwa haraka kuangalia bajeti ya mwaka wa fedha unaokuja, tuweke mipango ya pamoja ya Kiwilaya na Kimkoa na mwisho wa siku tujenge hospitali yetu ya rufaa ya Mkoa wa Geita.
MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa kwa mujibu wa jibu lake la msingi Mheshimiwa Naibu Waziri, ameonesha kuna bakaa ya fedha ambazo zimebaki hazijawasilishwa kwenye Halmshauri ya Wilaya ya Msalala, kiasi kwamba itapelekea miradi kutokamilika kwa wakati. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, anaweza kulihakikishia Bunge hili kabla ya mwaka wa fedha mpya haujaanza miradi ile itakamilika na Serikali itapeleka fedha?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa swali la msingi limeelekeza changamoto ya upelekaji wa fedha za maendeleo ambalo ni changamoto inayoikabili karibu nchi nzima kwa mwaka huu wa fedha, hususani, Halmashauri zetu za Mkoa wa Pwani. Je, Naibu Waziri yupo tayari kutoa maelekezo kwa Wakurugenzi kwa miradi ambayo ni viporo hasa ya Sekta ya Afya, wawasilishe taarifa haraka ili Serikali iweze kuikalimisha katika Halmashauri mbalimbali za Mkoa wa Pwani?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, bajeti pale mpaka mwezi Desemba, nimesema zilikuwa hazijafikia shilingi bilioni 3.1 zilizokuwa zimepelekwa, lakini mpaka mwezi Mei, hivi sasa fedha ambazo zimepelekwa katika ile bajeti imefika bilioni mbili (2), lakini fedha zingine za nje zimeongezeka na zimefikia karibu bilioni 1.9 mwezi uliopita. Kwa hiyo, jukumu kubwa ni nini? Tunaona kwamba kuanzia mwezi Desemba, mpaka hivi sasa kuna fedha nyingine za Serikali zimezidi kupelekwa na hapa maana yake Serikali itajitahidi kwa kadiri iwezekanavyo ili miradi iliyokusudiwa iweze kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, isipokuwa katika hili, ni lazima wataalam wetu, wakati mwingine ule uwezo wa utumiaji wa fedha za miradi kwa watendaji wetu umekuwa ni udhaifu zaidi. Kwa mfano, hapa tunapozungumza fedha nyingi zimeshapelekwa kule Msalala, basi nawaomba watendaji wetu waweze kuhakikisha kwamba, fedha zilizofika za maendeleo zitumike ilimradi wananchi waweze kupata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni jinsi gani tutafanya kwa Mkoa wa Pwani. Kikubwa zaidi naomba niwaagize kama nilivyosema, ni kwamba Wakurugenzi wote wa Mkoa wa Pwani na mikoa mingine yote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wahakikishe kwambam kwanza wanaandaa zile changamoto zilizokuwepo katika Sekta ya Afya na miradi mingine, lakini tubainishe kwamba hata hizo fedha zilizofika ziweze kutumika kwa ajili ya maslahi ya wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hili, naomba nitoe onyo kwa Wakurugenzi mbalimbali, kipindi cha mwaka unapofika siku hizi za mwisho, watu wamekuwa wakifanya mambo ya ajabu sana katika matumizi ya fedha za Serikali, wakijua kwamba mwaka unakwisha. Wakati mwingine fedha zinapelekwa sehemu ambazo hata zisizohusika, ambazo haziendi kuwagusa wananchi. Kwa mwaka huu naomba nikiri wazi kwamba, Mkurugenzi yeyote ambaye atacheza na fedha za Serikali, naamini Waziri wangu ataamua kuchukua fimbo kubwa sana kuhakikisha kwamba watu hawa wanawajibishwa. Lengo kubwa kuhakikisha wananchi wetu wanapata huduma kutokana na kazi kubwa inayofanywa na Serikali yao ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Pamoja na majibu mazuri ya namna ambavyo Serikali imejipanga katika kuhakikisha wafanyabiashara ndogo ndogo, machinga, mama lishe na wengine wanaofanana na biashara hizo wanatengenezewa mazingira mazuri ya kibiashara; lakini tungependa hasa kufahamu kwa mfano, habari za uwezeshaji wa mitaji inawezekana ikawa ni njia rahisi sana ya kuwa-contain machinga hawa pamoja na maeneo wanayopewa ili waweze kufanya biashara zao kwa uhakika kwa sababu tayari wanakuwa na kipato kizuri? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa sababu matatizo ya haya ya Dar es Salaam yanafanana sana na matatizo yaliopo Jiji la Mwanza, Wilayani Nyamagana, ambako pia kumekuwa na changamoto kubwa sana. Pamoja na maeneo mengi kupangwa, lakini Halmashauri zimefika sehemu zinakuwa zinabeba mzigo mzito kuona namna ya kuwawezesha hawa wafanyabiashara ndogo ndogo. Yako maeneo mengi yamepangwa, lakini uwezo wa wafanyabiashara hawa kwenda kule kutokana na miundombinu ambayo inakuwa siyo rafiki sana, maana Halmashauri inaweza ikatengeneza eneo vizuri, lakini miundombinu mingine ili iweze kufikika sawasawa inahitaji nguvu ya ziada.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini Serikali na Wizara inatuhakikishia kwamba iko tayari kushirikiana na Halmashauri hizi kuwatengenezea wafanyabiashara ndogo ndogo, machinga na mama lishe ili waweze kupata kipato na maeneo yao yawe sahihi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabla sijajibu swali hili, napenda kumpongeza kwanza Mheshimiwa Stanslaus Mabula na Mheshimiwa Angelina Mabula. Siku sita zilizopita, nilikuwa Mkoani Mwanza, lakini jukumu langu kubwa kule lilikuwa ni suala zima la kuwa cheque ya karibu shilingi milioni 900 wajariamali wa Mwanza ambao wamejiunga pamoja kwa ajili ya kuhakikisha kwamba katika makampuni yao walioyaanzisha yalikuwa takribani 24 waweze kufanya kazi vizuri. Mheshimiwa Mabula naomba niwapongeze sana, mmefanya kazi kubwa sana! (Makofi)
MheshimiwaNaibu Spika, sasa katika suala la mitaji, naomba niseme kwamba mitaji hii malengo yetu katika Serikali ya Awamu ya Tano itatoka katika maeneo tofauti. Eneo kubwa kwanza la mtaji katika hivi vikundi vidogo vidogo, tulisema hata katika bajeti yetu ya TAMISEMI kwamba mwaka huu tumeelekeza asilimia tano ya vijana na asilimia tano ya akina mama ambao takriban kuna karibuni shilingi bilioni 56.4. Imani yangu ni nini? Imani yangu ni kwamba, kama Halmashauri zetu zitahakikisha zile own source, ile ten percent ambayo tano kwa akina mama na tano kwa vijana, tukizielekeza vizuri shilingi bilioni 56.4, zitaleta mafanikio makubwa sana katika Halmashuri zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hili ni eneo moja la mtaji. Sambamba na hilo katika Ofisi ya Waziri Mkuu, kuna suala zima la uwezeshaji. Eneo hili nalo litaweza kufanya kazi kubwa kuwawezesha vijana waweze kuwa na skills za kutosha katika suala zima la uwekezaji katika maeneo yao.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba, Serikali imejipanga na juzi tulikuwa na Benki moja inaitwa Covenant Bank, ambayo iko tayari kushirikiana na wadau mbalimbali. Lengo kubwa ni kukuza mitaji kwa watu wa eneo la chini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nikiri kwamba, sasa tunahakikisha kwamba hii mitaji sasa, wananchi wapate fursa, lakini sambamba na kupata elimu ilimradi waweze kupata mitaji kuweka uchumi wao.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini eneo la pili, kwa suala zima la kuboresha miundombinu. Ni kweli, maeneo mengine miundombinu inakuwa ni changamoto kubwa.
Kwa hili, nawaomba Waheshimiwa Wabunge wote, lakini nawapongeza wale ambao tayari wameshajenga masoko kuhakikisha kwamba wanawa-accommodate wafanyabiashara mbalimbali. Sambamba na hilo, tubainishe; inawezekana kweli maeneo mengine masoko yapo, lakini hayapitiki vizuri, barabara siyo rafiki na hata maeneo ya mama ntilie hayajakuwa sawa sawa. Basi naomba tuibue mambo haya katika Halmashauri zetu, tushirikiane kwa pamoja, bajeti zetu zinazokuja tuweke kipaumbele jinsi gani tutafanya hawa akina mama ntilie, wauza mitumba na watu wa kada mbalimbali waweze kupata fursa kwa ajili ya uchumi wa nchi yao na maendeleo yao binafsi.
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Hii Awamu ya Tano, kila siku namsikia Mheshimiwa Rais anazungumza haya mambo, kwamba ukinunua kitu dukani omba risiti; ukienda hotelini, omba risiti, je, Serikali imejipangaje kuhusu hawa wauza mitumba na wanaotembeza mali (machinga) na mama ntilie kwa ajili ya kutoa risiti ili tupate kodi ya Serikali yetu? Serikali imejipangaje hapo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Keissy, kwa nyakati tofauti amekuwa akihimiza sana suala la ulipaji kodi. Naomba tukiri kwamba hii nchi haitaweza kwenda bila watu kulipa kodi. Namshukuru sana Mheshimiwa Rais, 2015 ametudokeza sehemu moja, mfanyabiashara mmoja anaingiza karibu shilingi milioni saba kila dakika. Kwa hiyo, kuna watu wakubwa wanakwepa kodi na wadogo wakati mwingine kodi hazikusanywi vizuri.
Mheshimiwa Keissy naomba nikuhakikishie, Ofisi ambayo inaongozwa na kaka yangu, Mheshimiwa Dkt. Mpango imejipanga vizuri kuhakikisha kwamba inafanya utaratibu mzuri, kila mtu atalipa kodi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nisisitize tena; na sababu ni kwamba katika kada zote, kila mtu atawekewa utaratibu mzuri ilimradi kodi tupate shilingi trilioni 29.54 kutimiza matakwa ya bajeti yetu. Naomba tushirikane na Serikali kwamba wale wenye sheli za mafuta waweke mashine za mafuta na kila mtu atumie mashine za EFD katika Halmashauri zote, tutumie elektroniki na kila utaratibu, kwamba Mheshimiwa Dkt. Mpango ametuwekea utaratibu kuona jinsi gani tutafanya tukusanye kodi kila mtu alipe kodi bila kukwepa kodi.
MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Tatizo la kusumbuliwa akina mama lishe limekuwa kubwa sana katika maeneo mbalimbali ndani ya nchi yetu. Siyo siri, tunapozungumzia mama lishe, sana tunawagusa akina mama na wale wajasiriamali wadogo wadogo. Wewe, mimi na Waheshimiwa Wabunge wote tutakuwa mashahidi kwamba hawa akina mama ndio wapigakura wa Chama cha Mapinduzi. Ni nini sasa agizo la Serikali kuhakikisha hawa akina mama lishe wanatengewa maeneo maalum ya kufanyia biashara zao katika Halmashauri zote ndai ya nchi yetu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli akina mama lishe wakati mwingine wanapata changamoto kubwa sana. Kibaya zaidi ni pale utakapoona Mgambo anakwenda kuchukua jungu la mama lishe halafu wanakusanyika pembezoni wanakwenda kula kile chakula cha mama lishe. Hili jambo linakera sana! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana siku moja nilipokwenda katika Soko lile la Ilala pale nilitoa maelekezo kwamba tuone jinsi ya kuwarasimisha vizuri tuwaweke katika utaratibu mzuri. Hilo ni moja.
Sehemu nyingine hata wakati mwingine kunaweza kuwa na utaratibu mzuri, Halmashauri zimejenga vibanda kwa akina mama lishe, lakini kuna baadhi ya watumishi wasiokuwa waadilifu, wanatumia vile vibanda wanakodisha akina mama lishe kwa pesa kubwa sana. Jambo hili tumelikemea pale Ilala na sehemu mbalimbali, lakini suala la upangaji wa haya maeneo ni kama nilivyosema. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nawaomba ndugu zangu, Waheshimiwa Wabunge, tushirikiane na Halmashauri zetu, tutenge haya maeneo, tuyaweke vizuri ilimradi kwanza wale akina mama waliokuwa wanafanya kazi zao katika maeneo ya jua; waliokuwa wanafanya kazi zao katika maeneo yasiyo rafiki; bajeti zile zikifika katika mwaka huu wa fedha tutakaokuja nao, katika Ofisi ya Rais TAMISEMI ambao ndiyo jukumu letu kubwa kuzisaidia Halmashauri, hatutasita kuipa mipango ili kipaumbele ilimradi hawa akina mama waweze kupata fursa ya kufanya kazi zao katika mazingira rafiki; kwa sababu hata katika suala zima la afya itasaidia kupambana na magonjwa ya kipindupindu.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Sikudhani, naomba nikwambie kwamba nitashirikiana na wewe na ninajua kwamba Tunduru ndiko unakotoka, kule bainisheni hilo, tutaweka kipaumbele ilimradi wananchi waweze kupata fursa na akina mama wapate fursa nzuri za kiuchumi.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Pamoja na jitihada nzuri za Mheshimiwa Rais wetu; na pia pamoja na harakati kubwa ya kuwajengea Watanzania nia njema ya kulipa kodi; kwa kuwa Mheshimiwa Rais wakati wa Uchaguzi na katika Kampeni zake aliahidi kuondolewa kwa tozo ndogo ndogo kutokana na wafanyabiashara wadogo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali haioni kuwa ina kila sababu ya kutazama upya Ilani ya Chama cha Mapinduzi na makundi gani yanasamehewa katika hizo tozo ndogo ndogo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, katika vipindi tofauti, Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais na timu zote tulipokuwa tukinadi ilani na Mheshimiwa Rais aliahidi kundoa hizi tozo ndogo ndogo ambazo zimekuwa kero kwa wananchi; kwamba mboga mboga, nyanya nini imekuwa ni kero kubwa zaidi. Kwa sababu kodi hizi zinatozwa kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa Sura Na. 290, ndiyo maana tumefanya maelekezo sasa; kuna mchakato unakwenda kwa ajili ya kurekebisha sheria zetu tuone ni jinsi gani sasa tutakusanya katika kodi zile kama crop cess na maeneo mengine lakini kuondoa usumbufu kwa wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hili lipo katika mchakato na wadau mbalimbali ndiyo wanaweka maoni yao sawasawa na mwisho wa siku sheria hiyo itakuja katika Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; tuipitishe sisi sote kwa pamoja, tufanye amendments, tushauri, turekebishe, mwisho wa siku ni kwamba mwananchi wa kawaida atakuwa ameguswa na matamko ya Mheshimiwa Rais alipokuwa akinadi na Ilani ya Chama cha Mapinduzi kama tulivyoelekeza.
MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba tu kutoa ufafanuzi tena kwamba Wilaya ya Bunda ina Majimbo matatu. Kuna Mwibara ya Mheshimiwa Kangi Lugola; kuna Bunda Mjini kwa Mheshimiwa Ester Bulaya na kuna Jimbo la Bunda kwa Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Namshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri lakini naomba Mawaziri au Manaibu Waziri wanapokuwa wanapata hayo majibu kutoka kwenye Halmashauri wawe wanayatazama vizuri kwa sababu majibu ninayoyaona hapa yanahusu mpango wa Halmashauri siyo swali la Boniphace Mwita kwenye Jimbo la Bunda.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mimi nimeuliza mambo ya malambo unaniambia kuna gharama za kujenga mnada, sasa hainiletei faida kwenye swali langu hili. Naomba kujua tu, ni lini hizi shilingi milioni 90, shilingi milioni 200 na shilingi milioni 110 ambazo Naibu Waziri amezitaja kwamba zitatumika kukarabati na kujenga malambo hayo zitapelekwa Bunda na zitatoka chanzo gani?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, naomba kujua, malambo hayo sita ya kukarabati ambayo Naibu Waziri ameyataja hapa na matano ya kujengwa, yatajengwa vijiji gani? Maana naona kama hii ni jumla ya Wilaya ya Bunda yote.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala kwamba lini pesa hizo zitapelekwa ni kama nilivyosema katika jibu langu la msingi. Mheshimiwa Getere pia lazima akubali kwamba kama alivyosema awali kwamba Bunda ina Majimbo matatu, Bunda la Mjini, halikadhalika na Jimbo la Mwibara la kaka yangu pale Mheshimiwa Kangi Lugola, mipango yote ya fedha maana yake ninyi mnapokaa katika Halmashauri yenu ndiyo mnafanya maamuzi sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, haiwezekani Jimbo likatengeneza bajeti yake kama Jimbo isipokuwa kama Halmashauri ambayo ina Majimbo matatu ndiyo inapanga hivyo vipaumbele. Ndiyo maana katika jibu langu la msingi nimeainisha jinsi gani mlipanga mipango ya miaka mitatu katika ukarabati na ujenzi wa yale malambo mengine matano. Kwa hiyo, lini fedha hizo zitakwenda, ndiyo maana nimesema katika mwaka huu wa fedha mlianza kutenga bajeti ambayo kuanzia Julai ndiyo mwaka wa fedha huwa unaanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la pili kuweza kusema vijiji specific, Mheshimiwa Mbunge naomba niweze kusema wazi kwamba kwa hapa itakuwa vigumu kwa sababu Halmashauri imepanga mpango wake huu na kuainisha vijiji, nadhani tuwasiliane baadaye tuone jinsi gani tutafanya. Vilevile tuangalie na ninyi kule katika Halmashauri mpango mlioupanga mlisema mtatekeleza mradi huu katika vijiji gani.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie kwamba kilio cha Wanajimbo lake la Bunda kimesikika. Jukumu letu kubwa ni kuhakikisha sasa Wanabunda katika Jimbo lake wanapata mahitaji yale ambayo wanayakusudia. Mwisho wa siku kama wananchi wa kawaida au kama wafugaji wa kawaida basi waweze kupata maji kwa ajili ya malisho yao na matumizi mengine ya nyumbani.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa muda wa kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Serikali imefanya feasibility study (upembuzi yakinifu) kwenye malambo mengi na kwa kuwa swali la msingi la Bunda linafanana na Mbulu Vijijini na Mbulu Mjini, je, Serikali ina mpango gani kuyajenga malambo hayo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli huwezi kufanya jambo lolote katika mradi mkubwa bila kufanya upembuzi kwanza kuangalia jinsi utakavyotekeleza mradi huo. Kama alivyosema katika eneo lake kuna maeneo ambayo wamefanya feasibility study kujua gharama ya ujenzi itakuwaje na anataka kujua ni lini sasa kazi hii itafanyika. Naomba niseme wazi kwamba katika mchakato huu wa bajeti kila Halmashauri imetengewa bajeti yake kutokana na vipaumbele vilivyowekwa na bahati mbaya tulikuwa na ukomo wa bajeti.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, inawezekana feasibility study imeshafanyika lakini mradi haujionyeshi katika mwaka huu wa fedha. Lengo kubwa ni ndani ya kipindi cha miaka mitano mradi ule uweze kutekelezwa. Imani yangu kubwa ni kwamba kama feasibility study imefanyika, kama fedha hiyo haijatengwa specific katika Jimbo lake katika mwaka huu wa fedha, basi katika mchakato wa bajeti ya mwaka unaokuja itakuwepo ili malambo yajengwe wananchi wapate huduma ya maji.
MHE. ANDREW J. CHENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Napenda niiulize Serikali, kwa sababu tatizo hili ni kubwa katika maeneo mengi nchini na nichukue tu kwa upande wa Jimbo langu la Bariadi na Jimbo la jirani la Itilima, malambo kama la Sakwe, Igegu, Sapiwi, Matongo, Mwamapalala na Mwamoto yote haya yameshambuliwa na magugu maji na maeneo mengi nchini najua hali ni hii.
MHE. ANDREW J. CHENGE: Na Malya. Je, Serikali haiwezi ikaja na mpango kabambe kama ilivyofanya kwa Ziwa Victoria miaka ya 1990 wakati limeshambuliwa na magugu maji ili kunusuru malambo haya hasa katika maeneo ambayo tuna pressure kubwa sana ya population kuliko kuziachia Halmashauri kwa mtindo huu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Chenge amezungumzia suala la mpango kabambe wa kushughulikia tatizo la magugu maji lakini kuhakikisha kwamba huduma ya maji inapatikana kwa wananchi. Nadhani Waziri wa Maji katika bajeti yake alizungumzia suala la kukamilika kwa mpango wa maji wa awamu ya kwanza sasa tunaendelea katika mpango wa maji wa awamu ya pili.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa maji wa awamu ya pili maelekezo yake ni nini? Maelekezo yake ni kwamba tutabainisha fursa mbalimbali, kwa mfano, ukiacha watu wa Kanda ya Ziwa wanaopata fursa ya maji kutoka Ziwa Victoria lakini na maeneo mbalimbali kuona ni jinsi gani wataweza kupata maji. Ndiyo maana nikimkumbuka au nikim-quote Waziri wa Maji alisema tutaangalia fursa zote zilizokuwepo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna maeneo mengine yamechimbwa visima virefu (bore holes) lakini vimekosa maji. Ndiyo maana ya maelekezo haya kwamba kila Halmashauri angalau kwa mwaka mmoja itenge fedha kwa ajili ya ujenzi wa lambo moja. Huo ni mpango mdogo wakati mpango mkubwa ni kwamba katika miaka hii mitano inayokuja ya ya programu ya maji ya kuhakikisha tunamtua ndoo mama kichwani tutahakikisha tunatumia fursa mbalimbali ikiwemo mito mikubwa, malambo na hata maziwa ya jirani ili mradi wananchi wa maeneo husika wapate maji. Kwa hiyo, napenda kumjulisha Mheshimiwa Chenge kamba jambo lake Serikali imelisikia na ndiyo mkakati mpana wa Serikali katika kuhakikisha tunamtua ndoo mama kichwani kama tulivyoahidi katika Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi.
MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa mwaka 2015 niliuliza hapa Serikali imejipanga vipi kupambana na magugu maji kwenye lambo la Kabainja ambalo liko Wilaya ya Bunda Jimbo la Mwibala na Serikali hii ikaahidi Bunge hili kwamba malambo yote ambayo yana magugu maji na malambo yote ambayo yalichakachuliwa kwa maana kwamba hayakukamilika itatenga fedha na kuanzisha mpango maalum ambao nadhani Mheshimiwa Chenge alikuwa anashauri. Je, kwa nini Serikali sasa haizungumzii mpango huu ambao waliuzungumzia mwaka 2015 sasa wanaanza kutupa majibu mengine mapya kana kwamba ndiyo wanataka wajipange upya? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, haya siyo majibu mapya ni mpango ule ule wa Serikali unaendelea. Nimjulishe Mheshimiwa Kangi Lugola lengo letu ni nini. Maana suala la magugu maji ni jambo moja lakini malambo mengine tukiyafanyia utafiti kuna mengine yanakufa kutokana na shughuli za kijamii ambazo zinazunguka malambo hayo. Kwa hiyo, mpango wa Serikali katika kuhakikisha tunapambana na magugu maji uko pale pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, sitaenda kwenye detail ya kila Halmashauri kuonyesha imejipanga vipi katika kushughulikia suala hilo lakini tunaendelea vilevile na suala la kutoa elimu maana kuna maeneo ambapo malambo yanakufa siyo kwa sababu ya magugu maji bali ni kutokakana na kazi za kijamii hasa kilimo. Watu wanapofanya shughuli za kilimo na mifugo kuzunguka haya malambo mwisho mvua inaponyesha udongo unasombwa unajaza malambo na kusababisha yafe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tuna mpango mpana, licha ya suala la magugu maji lakini elimu katika maeneo mbalimbali inaendelea kutolewa kwa wananchi. Lengo kubwa ni kuhifadhi vyanzo vya maji ili visije vikafa kabla ya muda uliokadiriwa. Hili limekuwa ni tatizo kubwa hasa malambo mengi kujaa matope na mchanga ukiachia magugu maji ambapo ndani ya muda mfupi yanakufa lakini inasababishwa na wakazi wenyewe wa maeneo haya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama Serikali tumeendelea kutoa elimu na tunaomba sana ushirikiano wa Waheshimiwa Wabunge wote. Agenda hii ni yetu sote, lazima tupambane nayo. Mwisho wa siku ni kuhakikisha kila mwananchi anapata maji katika maeneo yake.
MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Waziri amekiri kwamba kwa sasa Mfuko wa Barabara unatoa asilimia chache sana ambazo ni asilimia 30 kwa barabara za vijijini ambazo ni nyingi kuliko barabara zinazohudumiwa na TANROADS na TANROADS zinapata asilimia 70. Je, ni lini Waziri sasa ataleta mabadiliko ya sheria hii katika Bunge hili ili tuweze kunusuru barabara ambazo zinatumiwa na wananchi wengi ambao ni maskini?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Waziri ameona suluhisho la kudumu ni kuanzisha Wakala wa Barabara zinazohudumiwa na Serikali za Mitaa kama ilivyo kwa TANROADS. Je, ni lini hasa Wakala huu utaanzishwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwamba ni kweli kwa mujibu wa sheria yetu ni kwamba asilimia 30 inaenda Halmashauri Serikali za Mitaa na asilimia 70 inaenda TANROADS, hili nadhani ni takwa la kisheria na siwezi kutoa commitment hapa leo kwamba ni lini sheria italetwa, kwa sababu jambo hili ni mpango mpana.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Miundombinu ambayo ndiye mmiliki mkubwa wa sheria hii, tutaangalia jinsi gani tutafanya. Kama Watanzania tunajua jinsi gani tuna changamoto na ukifanya rejea katika mijadala mingi sana ya Wabunge jambo hili wamelijadili kwa kina. Kwa hiyo, Serikali tulichukue halafu tuone ni jinsi gani tutafanya, lengo kubwa ni wananchi wetu wapate huduma.
Mheshimwa Naibu Spika, Serikali za Mitaa zinafanya mikakati mingine mbadala ya kuhakikisha tunapata fedha nyingi sana. Ndiyo maana hata juzi nilikuwa nikipita katika mikoa mbalimbali kuangalia zile barabara ambazo TAMISEMI tunazihudumia kupitia fedha kutoka World Bank, ndiyo maana Miji yetu mikubwa yote ukianzia Arusha, Mbeya, Dodoma, Iringa na maeneo mengine tunajenga hizi barabara za Serikali za Mitaa kwa kutumia njia zingine mbadala, tuna source fund ili maeneo yetu yaweze kupitika vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kuanzisha Mfuko wa Barabara katika Serikali za Mitaa hili nimesema, mchakato sasa unaendelea katika ofisi yetu. Naamini wataalam wetu wa sheria watakamilisha zoezi hili na siyo muda mrefu inawezekana tuka-table kwa mara ya kwanza. Lengo kubwa ni kwamba, Wabunge tujadili kwa pamoja kwa maslahi mapana ya nchi yetu. (Makofi)
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza naomba nitoe pole kwa wananchi wangu wa Ipanko, usiku wa leo kuvamiwa na Polisi na kupigwa sana na kuumizwa. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa sasa hivi taasisi za kifedha zimeleta ugumu kukopesha taasisi za Serikali kwa sababu ya ugumu wao wa kulipa haya madeni. Je, sasa Serikali haioni kuwa inahitajika ifanye mpango wa dharura kwa ajili ya kutengeneza barabara za vijijini?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli anachozungumzia kwamba Serikali kufanya mpango mbadala ndiyo maana mwanzo nimesema, katika kuhakikisha tunafanya mpango mbadala Ofisi ya Rais, TAMISEMI inafanya mambo makubwa sana. Leo hii ukitembea katika Manispaa zetu maeneo mbalimbali tunatengeneza barabara za kiwango cha lami tumeanza katika miji mikubwa, tumekuja katika Manispaa baadaye tunakwenda katika Halmashauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu kubwa takribani miaka mitano itakayokuja tutaona mabadiliko makubwa sana ya miundombinu ndiyo maana mwaka huu ukiangalia zile fedha tulizotenga katika maeneo mbalimbali takribani bilioni 200 zitaenda kupakwamua sehemu korofi ambazo barabara zetu za Halmashauri zimekuwa hazipitiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili la Mheshimiwa Goodluck niseme kwamba huu ni mpango wa Serikali na naomba nikwambie kwamba tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo kama ombi lako linavyosema tutaendelea kuweka mkazo ili wananchi wapate huduma.
MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa, Halmashauri ya Moshi imeshatenga bajeti kwa ajili ya kujinunulia mitambo, naomba niulize kama Serikali itakuwa tayari kuji-commit kushirikiana na sisi ili tuweze kufanya hizo njia mbadala za kupata mitambo kukwepa zile gharama za mara kwa mara za kukarabati barabara kutokana na ukosefu wa mitambo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Komu nadhani sitoweza kusema commitment kwa sababu lazima kama ofisi yetu ione andiko hilo linasemaje. Kwa sababu kama kuna andiko linakuja katika Ofisi ya Rais lazima tuliangalie, needs assessment inafanyika lakini hizo fedha zinapatikana wapi. Lengo kubwa ni mwisho wa siku baada ya kufanya hilo inawezekana tunaisaidia hata Halmashauri yenyewe kwa sababu unaweza ukafanya jambo ukaingia commitment hapa, baadaye linaweza likaleta athari kubwa sana kwa wananchi wa eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, imani yetu kubwa ni kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI itapokea mawazo mazuri yote na tutayafanyia kazi. Mambo kama hayo yakija kwetu maana yake tutafanya, kwa sababu ni sehemu ya utalii lazima miundombinu yake iwe rafiki. Kwa hiyo, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, mlango wake utakuwa wazi kujadiliana na kushauri vizuri, mwisho wa siku tupate mipango mizuri katika nchi yetu.
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo hili la Muheza liko sawa na sisi watu wa Rungwe Magharibi, katika Hospitali ya Makandana tuna shida ya watumishi wa afya, vile vile na usafiri kwa ajili ya wagonjwa hususan wanawake. Je, ni lini Serikali itawatazama wananchi hawa kuweza kutuletea wataalam ikiwa pamoja na gari jipya la wagonjwa kama mlivyofanya kwa watu wa Muheza? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli anavyosema Mheshimiwa Mbunge, siku ya Jumatatu nilikuwa katika Hospitali ya Makandana pale katika Wilaya ya Rungwe, nilitembelea Hospitali na nilibaini miongoni mwa changamoto mbalimbali katika Hospitali ile na kwa pamoja tukaangalia jinsi gani tutafanya kama Serikali kuweza kutatua changamoto zile. Ndiyo maana hata katika maagizo yangu niliwaeleza kwamba hospitali ile licha kwanza suala la madawa lakini suala la gari la wagonjwa na hata suala la ukusanyaji wa mapato katika hospitali ile haliko sawasawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimekuta pale wanatumia mifumo ya analog, kutumia risiti ambayo kwa kiasi kikubwa inapoteza fedha nyingi za Serikali, ndiyo maana nimeagiza mwisho wa mwezi huu lazima wahakikishe wanatumia mifumo ya electronic. Kwa hivyo, haiwezekani hospitali kubwa kama ile wanakusanya sh. 3,000,000 kwa mwezi wakati kituo cha afya cha Kaloleni kinakusanya sh. 40,000,000 kwa mwezi!
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tunalifanyia kazi kwa upana wake. Kuhusu suala zima la miundombinu tumetembelea miundombinu, nina hakika maelekezo tuliyopeana siku ya Jumatatu tutaendelea vizuri na mwisho wa siku tutapata gari la wagonjwa ili hospitali yetu iwe katika mazingira mazuri na wananchi wa eneo lile waweze kupata huduma bora ya afya.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa, tatizo la Hospitali Teule ya Muheza linafanana na tatizo la Hospitali ya Wilaya ya Mbinga Mjini, mapema mwaka huu Waziri Mkuu alipofanya ziara yake Mkoa wa Ruvuma aliahidi kwamba Hospitali ya Wilaya ya Mbinga itaboreshwa katika maana ya theatre, nyumba ya kuhifadhia marehemu pamoja na kuhakikisha kwamba Madaktari wanaongezeka na gari ya wagonjwa. Ni lini ofisi yako itahakikisha hizo ahadi za Waziri Mkuu zinatekelezwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Pius Mapunda kwanza kwa kushiriki pamoja na Waziri Mkuu katika ziara yake, vilevile kwa sababu Waziri Mkuu ameshatoa ahadi hii haina negotiation, kinachotakiwa ni kwamba katika mpango wa fedha kwa sababu sasa hivi bajeti imeshapita na Waziri Mkuu lengo lake ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika ofisi yetu ya Rais, TAMISEMI tutahakikisha mchakato wa mwaka wa fedha wa 2017/2018 vipaumbele ambavyo Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuja pale aliviona, lazima tuviweke kama ni vipaumbele vya awali. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge katika mipango yao ya Bajeti kule wanapoanzisha lazima ionekane wazi na ikifika katika ofisi yetu nitaweza kuipa nguvu ili mambo haya yaweze kutekelezeka na wananchi katika eneo lake waweze kupata huduma kama Mheshimiwa Waziri Mkuu alivyokusudia.
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Hospitali nyingi teule hapa nchini zinamilikiwa na mashirika ya dini na katika mikataba kati ya wamiliki na Serikali, Serikali inasaidia madawa pamoja na wafanyakazi. Hata hivyo, hospitali hizi nyingi zimekuwa chakavu na zimekuwa ni mzigo mkubwa sana kwa hawa wamiliki. Je, Serikali iko tayari kuandaa mpango maalum au wa kurekebisha ile mikataba au wa kuweka fungu maalum la fedha ili kusaidia kuhuisha hizi hospitali ziweze kufanya kazi vizuri zaidi ya kuhudumia wananchi wetu, kwa mfano ile hospitali ya Huruma pale Rombo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikia Mheshimiwa Selasini na ni kweli. Katika kazi zetu, sana tunafanya kazi na taasisi mbalimbali hasa katika sekta ya afya, lakini sitaki kutoa commitment hapa isiyokuwa na uhakika, nikijua wazi hapa nimetoka kujibu swali kuhusu Hospitali yetu ya Mukandana kule Rungwe hata ukiangalia changamoto katika miundombinu hizi hospitali za Serikali zenyewe vilevile bado tunatakiwa tuziwekee nguvu, isipokuwa tunathamini mchango wa taasisi hizi.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo kubwa ni kwamba sehemu ambayo ni ya makubaliano yetu kwa mfano kutoa fedha kwa ajili ya madawa, kwa ajili ya watumishi, lazima kwanza tutekeleze kwa kiwango kinachoridhisha. Naamini tutakapofanya hivi vizuri hata taasisi za dini wataangalia na nguvu zao watafanya jinsi gani ili kuboresha hili suala zima la miundombinu, lakini sitaki kutoa commitment hapa, kusema kwamba kesho na keshokutwa tutafanya hili. Litakuwa ni jambo la uwongo na uwongo siyo jambo jema kama binadamu.
MHE. SILVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali na kwa niaba ya wananchi wa Kibaha nishukuru kwa kutupatia hiyo 1.4 bilioni katika upanuzi wa hospitali hii, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, hospitali ya Tumbi inapokea takribani asilimia nane hadi 10 ya majeruhi wote Tanzania. Licha ya miundombinu hafifu katika chumba cha kupokelea majeruhi hospitali hii imekuwa ikijitahidi kupokea majeruhi na kuwatibia na kwa mujibu wa taratibu majeruhi hutibiwa bila kutozwa chochote na hatimaye Serikali inapaswa kurejesha fedha hizi kwa hospitali ikiwa pamoja na Hospitali ya Tumbi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa takribani miaka mitano fedha hizi hazijarejeshwa katika hospitali hii, jambo ambalo limepelekea huduma kuwa hafifu na za kubabaisha. Je, Serikali sasa itarejesha lini fedha hizi ikiwa ni pamoja na special package kulingana na idadi kubwa ya majeruhi yanayokwenda katika hospitali hii?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kituo cha afya mkoani ambacho kinahudumia takribani wakazi 150,000 wa Mji wa Kibaha kina miundombinu hafifu, wagonjwa wanalala chini jambo ambalo linapelekea hata wagonjwa wengine kupewa rufaa pasipostahili kwa ajili ya kukosa miundombinu ya kutolea huduma.
Je, Serikali sasa ina mpango gani wa kupandisha hadhi kituo hiki ikiwa ni pamoja na kukipatia miundombinu na vifaa tiba ili kiweze kukabili na kuwahudumia wananchi wa kibaha ambao ni mji unaokua kwa kazi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli maswali yake Mheshimiwa Koka ni maswali ya msingi. Hospitali ya Kibaha ni hospitali ambayo iko pembeni mwa Barabara Kuu ya Morogoro, na karibuni katika kipindi kirefu sana tumeshuhudia ajali nyingi zikijitokeza katika maeneo haya. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge unalolizungumza ni jambo la kweli kabisa. Katika swali lako la kwanza Serikali tutafanya analysis ili kuisaidia hospitali hii iweze kufanya vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la special package ya kusaidia hospitali hii, nadhani Serikali nayo itafanya kwa kina ili jambo hili liweze kwenda vizuri ili Hospitali hii ya Tumbi iweze kutoa huduma kwa wananchi kama inavyokusudiwa. Naamini si wananchi wa Mkoa wa Pwani au wa Kibaha peke yake, hapana, ni wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao wengi wao wakipata ajali hospitali hiyo ndiyo limekuwa kimbilio la karibu zaidi kabla mtu mgonjwa hajafikishwa katika Hospitali ya Muhimbili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili, juu ya kituo cha afya cha mkoani; ni kweli na mimi niliweza kufika kituo kile mwaka jana mwanzoni. Sasa hivi mgonjwa yeyote hataruhusiwa kwenda Hospitali ya Tumbi mara baada ya Hospitali hii kupandishwa. Kila mgonjwa wa Kibaha Vijijini lazima atibiwe katika kituo hiki ndipo apewe referral na yule wa Kibaha Mjini atibiwe kituoni pale ndipo apewe referral; lakini kituo kile cha afya kina changamoto kubwa sana. Bahati nzuri watu kutoka Wizara ya Afya walikuja pale kufanya analysis kuangalia ni jinsi gani kinaweza kupandishwa hadhi kuwa hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati mbaya pale awali ilionekana ina upungufu mkubwa, ikiwepo wodi ya wazazi, lakini Mbunge nikushukuru sana kwa juhudi kubwa uliyofanya na wananchi wako na viongozi wako, wodi ya wazazi sasa hivi pale imejengwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo ni kwamba katika bajeti ya mwaka huu wa fedha, licha ya kujengwa ile wodi ya wazazi, lakini mmetenga karibu 700,000,000. Katika milioni 700 karibu milioni mia mbili arobaini na, ni kwa ajili ya ukarabati, mtajenga theatre ambapo kabla hospitali hii haijapandishwa kuwa hospitali ya Wilaya lazima kuwe na theatre room na bajeti ya mwaka huu pia mmetenga bajeti hiyo, lakini mmetenga bajeti ya kununua standby generator.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba niseme kwamba katika bajeti ya mwaka huu naamini kwamba tutasukuma kwa kadri iwezekanavyo ili pesa hizi ziweze kupatikana ili miundombinu ile ikamilike ili Kituo cha Afya cha Mkoani kiwe na hadhi ya Hospitali ya Wilaya ili wananchi wa Kibaha waweze kupata huduma bora katika maeneo haya. Ahsante sana.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Hospitali ya Tumbi ni hospitali ambayo ilikuwepo tangu enzi za Nordic countries, wakati huo ikiwa chini ya Nordic countries kama chini ya shirika. Ilikuwa inatoa huduma nzuri sana, lakini mpaka sasa hivi huduma yao imefifia, je, Serikali ina mpango gani wa kufuatilia huduma za Hospitali ya Tumbi ambayo inatolewa kwa wananchi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tukumbuke kwamba, Mheshimiwa Mbunge alikuwa Mkuu wa Mkoa ule wa Pwani kipindi hicho na naamini kwamba anaijua vizuri hospitali hiyo ndiyo maana swali lake limekuwa la msingi sana juu ya kuiboresha hospitali hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba mwanzo ilikuwa inatoa huduma nzuri zaidi, lakini tukikumbuka zamani population ya watu waliokuwa wakitibiwa katika hospitali hiyo ni tofauti na hivi sasa. Hivi sasa takriban wagonjwa kati ya 300 mpaka 500 wanafika pale kila siku na wengine wanaolazwa. Kwa hiyo, idadi ya watu wanaotibiwa kwa sasa hivi ni kubwa zaidi kuliko hapo mwanzo na ndio maana sasa hivi Serikali imehakikisha inashirikiana na wadau mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kumshukuru Mbunge wa Kibaha Mjini na Serikali kwa ujumla, katika harakati zilizofanyika angalau sasa hivi kuna mashirika mbalimbali kama wenzetu kutoka Korea na taasisi zingine wametusaidia vifaa mbalimbali kwa lengo la kuboresha hospitali ile.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la awali ni kwamba, mwaka huu tumetenga shilingi bilioni 1.4, lakini tutaendelea kuhakikisha tunafanya kila liwezekanalo hadhi ya Hospitali ya Tumbi iweze kuwa nzuri zaidi kwa sababu sio Wanapwani wanaotibiwa pale peke yake isipokuwa wananchi wote ambao wanapita katika ukanda wa barabara hiyo, wakipata matatizo hospitali ya Rufaa ya Tumbi ni Hospitali ya karibu ambayo ni kimbilio la wananchi wengi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge, naomba nikuahidi kwamba Serikali inalitazama kwa macho ya karibu zaidi jambo hilo na ndiyo maana Waziri wetu wa Afya, Naibu Waziri, walikwenda pale na Waziri wangu wa nchi alifika pale katika kutembelea Shirika la Elimu Kibaha kuangalia changamoto za pale. Katika mwaka huu wa fedha tutapambana kwa kadri iwezekanavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka uliopita ilitengwa milioni 700 haikuweza kupatikana, tutapambana mwaka huu ili bajeti iweze kupatikana ili hadhi ya Hospitali ya Tumbi iwe kama vile ilivyokuwa pale awali.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri naomba kuuliza swali dogo. Kwa kuwa sasa kuna wimbi kubwa la ujenzi wa vituo vya afya katika ngazi za kata, kwa mfano, Wilaya yetu ya Mbulu ina tarafa tano, ni kwa nini Serikali isifanye utaratibu wa kupitia tarafa zote hizo tano na kuona ni kituo gani cha afya chenye mahitaji madogo ya fedha ili iweze kutoa huduma kwa kutengewa fedha za kutosha? Kwa mfano tarafa zote zina vituo vingi lakini hakuna kituo kinachotoa huduma stahiki? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wa Mheshimiwa Mbunge tumeupokea kwanza na ndiyo maana wiki iliyopita kamati ya Bunge ya Bajeti, Wizara ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI pamoja na Wizara ya Afya tulikuwa tuna kikao cha pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kikao kile kililenga kubaini kwanza maboma yaliyokuwepo yote kabla hayajakamilishwa. Najua Mheshimiwa Mbunge una-concern kubwa ya maboma katika maeneo yako. Tumefanya tathmini ya maboma yote yaliyojengwa, lakini hayajakamilika, pia tathmini ya zahanati na tathmini ya vituo vya afya vina hali gani. Lengo letu ni kuwa na kituo cha afya ambacho mtu hata huduma za operation ziweze kufanyika vizuri katika maeneo husika. Kwa hiyo, jambo hilo sasa tumelifanya kwa pamoja na Kamati ya Bunge imeelekeza. Lengo kubwa ni kupata fedha za kuboresha huduma ya afya katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo ni kwamba kinachotakiwa kufanyika ni wataalam wetu na Wabunge wetu kutushauri, kwamba ikiwezekana tu-review ramani za majengo yetu. Wakati mwingine inaonekana kujenga kituo cha afya gharama yake inakuwa kubwa kumbe inawezekana kwamba, isiwe friendly kwa mazingira husika. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge ni kwamba, Serikali tunalifanyia kazi na kwamba tutateua baadhi ya vituo, tuviweke katika hadhi nzuri ili viweze kutoa huduma bora na viwe kimbilio ya wananchi katika maeneo yao.
MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Na mimi nina swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wanawake wa Simiyu wamehamasika vizuri sana na wanafanana kabisa na wanawake wa Mvomero na wanawake wa Sumve.
Je, Waziri atatueleza ni lini sasa katika suala zima la maendeleo zile shilingi milioni 50 zitakwenda Sumve na Mvomero kwa sababu wanawake wale wameshajiunga kwenye vikundi na vikundi vile vimeshasajiliwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimwambie wanawake wa Mvomero na wale Wasukuma wa kule hawawezi kufanana, hilo ni jambo la kwanza. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, naomba nimtoe shaka, najua Mheshimiwa Murad ni mpiganaji mkubwa sana, Serikali itahakikisha watu wa Mvomero, Bariadi, Sikonge na wa maeneo yote fedha zile zinapatikana na zinawafikia wananchi ili mradi wahakikishe wanajihusisha katika shughuli za ujasiriamali. Suala hili Serikali imelisikia ndiyo maana imeweka katika bajeti yake ya mwaka huu wa fedha.
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Ni ukweli usiopingika kwamba wanawake katika nchi hii ndiyo wanaolisha Taifa hili kwa sababu akina mama wengi wanajishughulisha na kilimo na biashara ndogo ndogo. Ni kweli pia kwamba katika baadhi ya Halmashauri akina mama wengi wananyanyasika sana na biashara zao kwa kutozwa kodi mbalimbali ambazo hazina tija.
Je, ni lini Serikali itatoa tamko kwa Halmashauri zote ikiwepo Halmashauri yangu ya Rombo waache kuwatoza akina mama zile kodi ambazo zinawaletea bugudha na hivyo kushindwa kuendesha biashara zao kwa ufanisi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika kufanya hili nadhani tunafanya rejea, hata Mheshimiwa Rais alipokuwa akizunguka sehemu mbalimbali alikuwa akisema kwamba akina mama hawa wasinyanyaswe.
Naomba niseme wazi kwamba kutokana na agizo hilo la Mheshimiwa Rais, Ofisi ya Rais, TAMISEMI tunaandaa marekebisho ya Sheria ya Serikali za Mitaa inayohusiana na mambo ya Kodi, Sura Namba 290 na hivi sasa ipo katika mchakato wa mwisho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo ni kuondoa zile kero mbalimbali siyo za akina mama peke yake bali ni pamoja na walemavu na makundi mbalimbali. Katika mchakato huu tutakwenda kuhakikisha tunaondoa kero hii siyo kwa akina mama na vijana tu, lakini na group la walemavu lazima wawezeshwe na Halmashauri.
Hata hivyo, watakapowezeshwa kitafanyika nini ili mitaji yao iende vizuri, ndiyo hiyo sheria inakuja sasa hivi. Imani yangu ni kwamba Wabunge wote kwa pamoja sheria ile itakapokuja hapa tutashirikiana kuipitisha kwa sababu jambo hili lina maslahi mapana sana kwa wananchi wetu lakini kikubwa zaidi lina maslahi katika uchumi wa nchi yetu.
MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza, lakini pamoja na maswali mawili ya nyongeza, nikiri kwamba sijaridhishwa kabisa na majibu ya Mheshimiwa Waziri na wala sikubaliani nayo kwa sababu za msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sote tunafahamu, Nyamagana ndiyo kitovu cha Mkoa wa Mwanza na ni mji unaokua kwa kasi sana, barabara hii haijasemwa leo, imesemwa sana, sasa tukisema mwaka 2017/2018 ndiyo tuanze upembuzi yakinifu tunakuwa hatuwatendei haki wananchi wa Jimbo la Nyamagana.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nimwombe Naibu Waziri na akumbuke kwamba iko sasa hivi mikakati ya kuboresha miji ukiwemo Mji wa Mwanza, barabara hii itakuwa muhimu sana kwa mkakati wa Serikali wa ukusanyaji mapato, ni lini watakuwa tayari kutumia fedha za dharura kuhakikisha hii shughuli ya kufanya upembuzi yakinifu inafanyika kwa mwaka huu na mwaka ujao barabara hii ianze kujengwa? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, kwa sababu zilezile kwamba Mji wa Mwanza ni mji unaokua kwa kasi na mara nyingi tumekuwa tukitumia fedha nyingi wakati wa dharura, tunaposubiri mvua nyingi zinanyesha na kuharibu barabara. Je, ni lini sasa fedha hizi za dharura zitatumika kuimarisha barabara ikiwemo barabara ya kutoka Mkuyuni kwenda Nyangurugulu kutokea Mahina, Buzuruga, lakini ya kutoka Mkolani kwenda Saint Augustine University kupitia Luchelele na Nyegezi Fisheries?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nataka nimjulishe Mheshimiwa afanye rejea katika maeneo ambayo tunafanya mikakati kama Serikali kuboresha barabara zetu likiwepo na Jiji la Mwanza. Kupitia mpango wetu wa strategic cities Mwanza ni eneo ambalo tunajenga miundombinu hiyo ikiwa sambamba na Shinyanga, Arusha, Iringa, Mbeya na maeneo mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, najua kwamba barabara hii ni kweli haijakamilika, lakini nimesema kila jambo lina mpango na Mheshimiwa Mabula, anafahamu Mheshimiwa Rais alivyokwenda pale alisema siyo hizo barabara za eneo la Mwanza isipokuwa hata kujenga daraja katika Ziwa Victoria, nalo linafanyika katika Jiji la Mwanza, mpango mkakati huo unapoenda maana yake kutakuwa na uboreshaji wa hizo barabara.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba najua, amesema ni muda mrefu, lakini anakumbuka huko nyuma alikotoka wapi na hivi sasa yeye yuko wapi. Naamini uwepo wake sasa utasukuma mambo haya yaende vizuri zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba Serikali imejipanga ile ring road itatengenezwa. Kwa mujibu wa Serikali ilivyojipanga ring road tutatengeneza na isitoshe na yeye anafahamu kule site kuna watu sasa hivi wanaboresha barabara za Jiji la Mwanza, naomba niwahakikishie watu wa Mwanza, Mheshimiwa Rais alivyotoa kwamba kujenga barabara mpaka kupeleka airport baada ya kuvunja sherehe maana yake hiyo ni commitment ya Serikali ili baadaye Watanzania wote wanufaike, amesema kwamba tuelekeze eneo hili kwa sababu ni eneo la mkakati, ni azma ya Serikali kuboresha miundombinu hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, naomba nimwambie kwamba katika kipindi cha sasa Serikali ilivyojipanga tutaboresha barabara za aina mbalimbali na katika hilo la kwamba kwa kutumia fedha za dharura tutafanya nini. Juzijuzi nilikuwa katika Jimbo la Mheshimiwa Mabula kule Ilemela, kuna baadhi ya barabara tumefanyia ukarabati.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia afuate rejea yangu ya kipindi kilichopita, kwamba tutafanya kila liwezekanalo barabara zilizoharibika kwa kadri rasilimali fedha itakavyopatikana tutaendelea kuiboresha. Kwa hiyo, nimwambie mtani wangu, asihofu, awaambie watu wa Mwanza kwamba wamempata jembe lakini Serikali itamsaidia kuboresha Jiji la Mwanza. (Makofi)
MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Ipo ahadi pia ya Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika Mji wa Biharamulo ya kuweka kilometa nne za lami wakati akituomba kura. Kwa kuwa sisi habari ya kilometa nne haina mambo makubwa yanayojumuisha mpaka habari ya vivuko kwenye Ziwa Victoria, Naibu Waziri anatuambia nini kuhusu utekelezaji wa haraka na wa siku za karibuni wa ujenzi huo wa ahadi ya Rais?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba niwape pole watu wa Kagera kwa msiba mkubwa uliotupata na najua sio hilo tu, maana yake maeneo mbalimbali kule yatakuwa yameathirika hasa miundombinu ya barabara. Naomba nimhakikishie, kwa sababu ahadi hii ni ahadi ya Mheshimiwa Rais na ndiyo maana Mheshimiwa Rais amejielekeza katika ukusanyaji wa mapato ili mradi kuhakikisha ahadi zake zimetekelezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu, kama mwenyewe anavyosema na kama Serikali yake inavyoonesha jinsi gani ukusanyaji wa mapato ulivyo, tutahakikisha barabara hii inatengenezwa, lakini sitaki kukwambia commitment ya tarehe, kwamba lini tutafanya hivyo, lakini katika kipindi hiki naamini itatengenezeka kwa sababu nguvu kubwa inaelekezwa kuhakikisha ahadi za Rais na utekelezaji wa ilani unatekelezeka katika kipindi hiki.
MHE. JUMA H. AWESO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya kumuuliza. Mimi kama Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Pangani sikubaliani na majibu ya Mheshimiwa Waziri ya kusema kwamba mazungumzo yanaendelea, ilhali wananchi wangu wakitaabika. Tunapozungumzia suala la X-Ray, tunazungumzia uhai wa wananchi wa Jimbo langu la Pangani. Leo wananchi wanatoka Muhungulu, Mkalamo wanafuata huduma ya X-Ray Tanga Mjini.
Sasa nataka nijue ni nini nguvu ya Serikali katika kuhakikisha kwamba inatupatia fedha za dharura ili X-Ray hii ipatikane kwa haraka?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, pamoja na changamoto ya ukosefu wa X-Ray bado Hospitali yetu ya Wilaya imekuwa na changamoto lukuki za ukosefu wa dawa pamoja na vifaa tiba. Je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kuongozana na mimi baada ya Bunge kuhakikisha kwamba, tunaenda kukabiliana na changamoto ambazo Hospitali yetu ya Wilaya inakabiliana nazo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lolote haliwezi kukamilika bila ya mazungumzo, ndiyo maana halmashauri pale imefanya utaratibu wa kupata hii milioni 70 kutoka NHIF.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mbunge kwamba, utaratibu uliowekwa na halmashauri yake na yeye mwenyewe akiwa mjumbe wa Baraza la Madiwani; na nikijua kwamba yeye ni kijana mahiri anapambana sana juu ya suala la afya katika eneo lake; sisi tuta-fast track hiyo process ya kupata X-Ray haraka ili wananchi wa Pangani ambao kwa muda mrefu anawapigania waweze kupata huduma ya afya, lakini nimpongeze sana katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kuongozana na Mheshimiwa Mbunge, naomba nimwambie kwamba, niko tayari. Baada ya Bunge, mpango wangu ni kutembelea Mikoa ya Tanga, Lindi, Mtwara, Pwani na Mkoa wa Morogoro. Kwa hiyo, nimhakikishie tu kwamba, tutafika Pangani na tutakagua eneo hilo. Hali kadhalika tutakagua kituo cha afya ambacho wanaendelea kukijenga ili tuone namna ya kukusanya nguvu za pamoja za kuhakikisha kwamba, wananchi wa Wilaya ya Pangani wanapata huduma ya afya.
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Naomba kuuliza swali dogo tu la nyongeza. Kwa kuwa Hospitali yetu ya Manispaa ya Iringa ilifunguliwa ili kupunguza msongamano mkubwa sana uliopo katika Hospitali ya Mkoa, lakini mpaka leo hii Hopsitali hii haina mashine ya X-Ray wala Ultra Sound. Pia hospitali hii imekuwa ikihudumia mpaka wagonjwa wanaotoka Kilolo kwa sababu Kilolo pia Hospitali yao ya Wilaya imekaa vibaya kiasi kwamba wagonjwa wanaotoka kule Kilolo wanakuja kuhudumiwa katika hospitali hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua kwamba, kama mashine hizi zingekuwepo zingeweza pia kuingiza pesa ili kuzisaidia ziweze kujiendesha. Je, Serikali sasa inaisaidiaje hospitali hii iweze kupata hizi mashine ili iweze kuhudumia wananchi waliopo katika Manispaa ya Iringa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nasema ngoja nilichukue hili kwa sababu katika kuangalia kwa haraka haraka sikuweza kufahamu kwamba mpaka hivi vifaa vya X-Ray bado vina changamoto kubwa, lakini naomba tulichukue hili kwa ajili ya kulifanyia kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitembelea kule Kilolo, nilijua kwamba watu wa Kilolo wote wanakuja kupata huduma pale na nilijua kwamba vifaa vyote vimekamilika. Jambo hili tutalifanyia kazi kwa pamoja ili Hospitali hii ya Manispaa iweze kutoa huduma bora kwa wananchi wote kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Iringa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba niseme kwamba tutashirikiana kwa pamoja na Mheshimiwa Ritta Kabati pamoja na Wabunge wengine wa huko ili hospitali ile ambayo ni centre kubwa sana ya magari makubwa yanayopita kutoka nchi za jirani kuja Tanzania iwe na uwezo wa kuwahudumia watu kwa kiwango kikubwa.
MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini kwanza naomba niseme, mimi nikiwa ni Mbunge wa Jimbo la Nsimbo, nina masikitiko makubwa sana kuhusiana na uongozi wa Wilaya na Mkoa kwamba katika kutekeleza majukumu yao, hawaangalii haki za msingi. Tarehe 24 wamefanya operation ya kuondoa watu kwenye Hifadhi ya Kijiji ambao walipewa na uongozi wa Kijiji kwa kuwachomea nyumba, mvua zinanyesha, wanakosa pa kulala. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hii imekuwa ni tofauti na kauli ya Mheshimiwa Makamu wa Rais aliyotoa mwaka 2016 kwamba endapo watu wako katika maeneo ya hifadhi, wanatakiwa watafutiwe maeneo mengine na ndiyo wapelekwe. Kutokana na hilo, naomba kuuliza, je, Wizara husika iko tayari kuwafuta machozi wananchi wa Kitongoji cha Kamini, Kaumba katika Kijiji cha Katambike, Kata ya Ugala?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ilitolewa taarifa hapa kwamba imeundwa tume ambayo inashirikisha Wizara karibu tatu kushughulikia kero za migogoro ya ardhi. Sasa tunaomba majibu ya hiyo tume, yamefikia wapi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa ya kwamba Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na Mkoa ilifanya uchomaji wa nyumba kwa sababu hii taarifa kwetu sisi ni mpya, ni ngeni, naomba tulichukue hili kwanza kwa ujumla wake kwa sababu jambo hili maana yake ni haki za binadamu ambao saa nyingine wameathirika. Kwa hiyo, kama Ofisi ya TAMISEMI tunasema kwamba habari hii kwanza tumeipata, tutaifanyia kazi kwanza, lakini suala zima la ulipaji wa fidia kwa wale walioathirika kwa Wizara yenye dhamana kwa sababu jambo hili, sijajua, ni jambo mtambuka. Je, iliyohusika ni Wizara ya Maliasili na Utalii au Ofisi ya Rais - TAMISEMI?
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana nimesema jambo hili kwanza lazima lifanyiwe tafiti ya kina kujua nini kilichojiri kule katika eneo hilo. Pia kuna suala zima la kikosi kazi kilichoundwa na Wizara takriban nne, je, kimefikia wapi?
Mheshimiwa Naibu Spika, naamini kazi ile inaendelea hivi sasa, tukijua kwamba tuna changamoto kubwa sana nchini mwetu. Leo hii mikoa mbalimbali, ukiangalia Mkoa wa Morogoro, Mkoa wa Pwani na karibu katika maeneo yote kuna tatizo hilo kubwa sana. Ninaamini kabisa kikosi hicho kinaendelea na kazi hiyo na pindi taarifa hiyo itakapokuwa imekamilika ambapo aliyehitaji jambo hilo lifanyike ni Waziri Mkuu mwenyewe, basi tutapata taarifa rasmi ya Kiserikali kuhusiana na jambo hili linavyoshughulikiwa katika maeneo mbalimbali, lakini kujua ukubwa wake maana yake tunataka kuokoa Taifa hili kwa sababu sasa hivi janga la mauaji limekuwa kubwa sana, na huu ndiyo suluhu ya jambo hili kwa sababu kila eneo sasa hivi lina shida kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Richard Mbogo naomba tuvute subira tu, taarifa hii ikikamilika itatolewa rasmi hapa katika Bunge letu.

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Naibu Waziri wa TAMISEMI kwa majibu yake mazuri, lakini nilipenda tu kuongeza jibu kwa hoja ya msingi aliyokuwa ameuliza kwenye swali la nyongeza kwamba ile Kamati iliyoundwa mpaka sasa hivi imefanya kazi wapi na wapi?
Mheshimiwa Naibu Spika, ile Kamati mpaka sasa imeshakwenda mikoa minne; imekwenda Geita, Kagera, Morogoro na Tabora. Wakimaliza hapo, wanaelekea Kaskazini. Kwa hiyo, ile Kamati tayari imeshaanza kazi yake, lakini pia sisi ndani ya Wizara tumeshaanza kazi hiyo katika kufuatilia. Ni juzi tu nilikuwa Kusini na Waziri wangu alikuwa Kaskazini. Kwa hiyo, tunaendelea na kazi hiyo.
MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Naibu Waziri, kwa kuwa Serikali imekiri kwamba kuna Kamati Maalum iliyoundwa kwa ajili ya kushughulikia matatizo hayo na wakati huo huo Kamati inavyoendelea na kazi yake, Serikali imeendelea kuwaondoa wafugaji na kutaifisha mifugo yao, je, haioni ni wakati muafaka wa kusubiri Kamati hiyo imalize kazi yake ili waje na suluhu ya kudumu juu ya jambo hili?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama tulivyosema, Kamati iko site, lakini sijajua kwa sababu wakati mwingine kuna case by case.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna maeneo mengine haya mambo yanatofautiana mazingira kwa mazingira; na kwa sababu katika maeneo mbalimbali tuna Wakuu wetu wa Mikoa ambao wapo; na ni viongozi Wakuu wa Kamati za Ulinzi na Usalama wa Mikoa hiyo, hali kadhalika na Wakuu wa Wilaya, mambo haya wakati Kamati inafanya kazi wao watapima uzito wa maeneo haya na kuona jinsi gani ya kufanya ili utaratibu uende vizuri. Lengo kubwa ni kumsaidia Mtanzania katika mazingira yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naamini kwa sababu tuna Kamati za Ulinzi na Usalama za Mikoa na Wilaya na Kamati inaendelea kufanya kazi, nawaomba Wakuu wa Wilaya kuratibu mambo haya katika maeneo yetu na mikoa yetu. Jambo kubwa ni kuwalinda wananchi wetu waweze kuishi kwa usalama ili kujenga uchumi wa nchi yetu.
MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru kwa kunipa nafasi tena naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili la kupandishwa
hadhi kituo hiki limekwisha kujadilikwa katika mamlaka zilizopo pale wilayani na hata mkoani, kwa hiyo kama ni suala la mamlaka iliyobaki kushughulikia jambo hili ni mamlaka iliyoko juu ya hizo mbili. Je, ni lini sasa timu hiyo ya ukaguzi
itatumwa ili upandishwaji hadhi wa kituo hiki uweze kukamilika?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa safari ya kuelekea kupata Hospitali ya Wilaya ya Karatu imeanza, Mheshimiwa Waziri yuko tayari sasa kutenga fedha katika bajeti ya kuanzia mwaka huu na kuendelea ili miundombinu michache iliyobakia iweze kukamilika? Ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nili-cross check mpaka jana kuangalia taarifa hizi status zikoje, lakini kwa
taarifa nilizozipata kule inaonekana mchakato ulikuwa haujakamilika vizuri. Kwa hiyo, naomba tushauriane tu, tutaangalia jinsi gani tutafanya ili wenzetu wa Halmashauri ili kama lile jambo limekwama halijafika katika mamlaka husika, hasa katika Wizara ya Afya waweze kufanya hivyo ili
Waziri wa Afya aweze kufanya maamuzi, nadhani jambo hilo litakuwa halina shida kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Wizara kuweza
kutenga fedha, ni kweli, na unakumbuka nilikuja pale jimboni kwako na nilitoa maelekezo kadhaa ambapo nilikua sijaridhika na kufika pale nilikuta watu wamefunikwa mablanket ambayo yametolewa store baada ya kusikia Naibu Waziri anakuja pale; kwa hiyo nimegundua changamoto
mbalimbali pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mchakato wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya tutaendelea kufanya hivyo. Naomba niwasihi hasa ndugu zetu wa Halmashauri, anzeni mpango huo sasa kuanzia bajeti zenu za Halmashauri ikifika kwetu sisi
Wizarani jambo letu kubwa liwe ni ku-compile vizuri na kufanya taratibu vizuri ili mchakato wa ujenzi wa hospitali ufanyike. Hoja yako ni hoja ya msingi na bahati nzuri eneo lile ni eneo la kitalii lazima tuwekeze vya kutosha tuwe na hospitali yenye maana pale hata mgeni akija aweze kupata
huduma nzuri.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti nashukuru kunipa nafasi ili na mimi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti tatizo la Karatu linafanana
na tatizo la Korogwe Mjini. Korogwe Mjini haina hospitali, kwa maana ya Halmashauri ya Mji, na Wilaya yetu tumeamua kwa makusudi kabisa kujenga kwanza kituo cha afya ambacho tutakifanya kiwe hospitali.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuweza kutusaidia kutupiga jeki kwa sababu tunajenga kituo cha afya chenye ghorofa tatu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niweke kumbukumbu sawa ni kwamba nipende kumshukuru Mama Mary Chatanda, Profesa Maji Marefu pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Korogwe kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya ambapo nimetembelea mara kadhaa katika eneo lile. Nilivyofika pale nimekuta initiative mbalimbali wanazozifanya hasa katika suala zima la sekta
ya elimu na sekta aya afya na bahati nzuri wanatumia hospitali ya ndugu yangu Profesa Maji Marefu, iko vijijini lakini obvious kijiografia iko mjini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kwa sababu
mmeanza harakati za ujenzi, na kile kituo cha afya ni kituo cha afya makini inaonekana kuna viongozi makini eneo lile, Serikali itachukua wazo lile jema kuangalia wapi mmeishia, tukishirikiana nanyi kwa pamoja tufanyeje, kwa kuangalia resource tulizo nazo tusukume ili eneo la pale ambalo ni katikati; watu wanaotoka Arusha hata ikipatikana ajali
lazima watakimbizwa pale, tuweze le tuweze kushirikiana kwa pamoja tujenge Hospitali ya Wilaya pale.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa
Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nianze kwanza kwa kuishukuru Serikali kwa kusikiliza kilio cha
watu wa Kilolo kwa ujenzi wa hospitali. Pamoja na hiyo, Mheshimiwa Waziri, itachukua muda mrefu hiyo hospitali kuweza kuisha. Lakini tatizo ambalo lipo ni kwamba Wagonjwa inabidi wapelekwe Kituo cha Afya Kidabaga ambacho hakijakamilika, hakina wodi ya watoto, wodi ya wazazi wala upasuaji, lakini inabidi sasa wasafirishwe waende
kwenye hospitali ambayo iko zaidi ya kilometa 120. Tatizo hakuna gari Mheshimiwa Naibu Waziri kwa hiyo utatusaidiaje ilituweze either kukarabatiwa vizuri kituo cha Kidabaga au tupate gari?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anafahamu tulifanya ziara pamoja na tukakuta hospitali yao ya Wilaya pale iko taabani. Tukafanya mawazo ya pamoja, na bahati nzuri ndani ya muda mfupi wakapaa shilingi bilioni 1.2. Lakini, kama hiyo haitoshi niwapongeze; kwasababu wameshafanya harakati na ujenzi unaendelea kule site na Mungu akitujaalia ndani ya wiki mbili hizi wakati tuko Bungeni nitakwenda kutembelea ili kuona ni jinsi gani ujenzi unaendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Kituo cha Afya cha Kidabaga nadhani unafahamu kwamba Serikali tutaweza kuweka nguvu kubwa pale kwa sababu tukiangalia jiografia yake ni tata sana, tutaangalia namna ya kufanya. Tutapeleka fedha kwa ajili ya kujenga theatre ikiwezekana na wodi ya wazazi. Lengo kubwa wananchi wa eneo lile waweze kupata huduma bora.
MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Hospitali nyingi za Wilaya zina mkataba kati ya Serikali na mashirika hasa ya dini, Hospitali ya Kilema ikiwa moja wapo. Tunajenga maabara ya kisasa, nini commitment
ya Serikali katika hospitali ya Kilema ili iweze ikatoa huduma zilizo bora katika Taifa hili?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme ujenzi wa maabara ni jambo jema sana na sisi Seriali tunaappreciate
hiyo juhudi kubwa inayofanyika na ukiona hivyo
maana yake tunasaidia juhudi za Serikali jinsi gani iweze kusaidia wananchi wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya commitment ya
Serikali katika hilo naomba tuangalie jinsi gani tutafanya katika suala zima la mikataba hata suala zima la watendaji; kwa sababu wakati mwingine tunaweza tukawa na maabara lakini tukawa na watu ambao hawawezi kuendesha vizuri ile maabara. Kwa hiyo, commitment ya Serikali ni kuangalia jinsi gani tutafanya ili maaabara ikikamilika tuweze ku-deploy watu wazuri pale wa kuweza kufanya analysis ya maabara, wananchi wetu wakienda pale waweze kupata huduma bora hata magonjwa yao yaweze kudundulika vizuri zaidi.
MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, nina swali moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo cha afya ambacho
kiko katika kijiji cha Mwera, Kata ya Mwera ni kituo ambacho kwa muda mrefu sana kimepandishwa hadhi ya kuwa kituo cha afya; lakini kituo kile hakina huduma zinazokidhi kuwa
kaama kituo cha afya. Hakina gari la wagonjwa, lakini pia vipimo vya damu salama bado havipo katika hospitali ile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kujua ni lini
Serikali itakipa hadhi sahihi kituo kile ya kuwa kituo cha afya katika Wilaya ya Pangani?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kusema lini kwanza naomba tuweke rekodi sawa za Mheshimiwa Mbunge kwamba kipindi kile mlinialika na Mheshimiwa Aweso tumefika pale Mwera na nikatoa maagizo kwamba
kituo kile kutokana na yule mwekezaji pale japo anawekeza aweze kujenga theatre.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwashukuru kwa sababu wodi ya wazazi imeedelea kujengwa, lakini hata hivyo Serikali kuufanya kuwe kituo cha afya lazima miundombinu ikamilike vizuri, ndiyo maana tukaona sasa hivi tujenge jengo la theatre pale kubwa lakini pia kujenga na wodi zingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na ndiyo maana
nikamuelekeza Mheshimiwa Aweso kwamba awaambie watu waiandae mapema ile BOQ. Tuta deploy pesa pale, kwa sababu watu wa pale wakikosa huduma, suala la kuvuka Mto Pangani ni changamoto kubwa sana na usiku vivbuko hakuna. Kwa ajili ya kuwaokoa Watanzania
tumeamua kuweka nguvu kubwa za kutosha, fedha za kutosha kujenga jengo lile litakamilika huenda kabla ya mwezi wa saba mwaka huu ujenzi utakuwa umeshaanza.
MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa dawa za kurefusha maisha kwa waathirika hawa wa UKIMWI zimekuwa zikitolewa kwenye vituo vya afya na kwenye zahanati chache. Kwa nini sasa Serikali isitoe huduma hizi kwenye zahanati zote ili kuwapunguzia wananchi hawa ambao wameathirika kutembea umbali mrefu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, waathirika hawa
au hawa watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI wanaoishi vijijini sehemu kubwa ndiyo waathirika pia kwa maana ya umaskini. Kwa nini sasa Serikali isiweke utaratibu wa kuwakopesha waathirika hawa kwenye vikundi mikopo midogo midogo ili waweze kupata fedha waweze kufanya shughuli ndogo ndogo kama vile kilimo, kufuga na bustani ili kuwainua kiuchumi au kuweza kupata fedha za kuweza kujikimu kwa maana ya kuwasaidia kuishi vizuri kwa kupata mahitaji madogo madogo? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, concern ya Mheshimiwa Mbunge ni kwamba ikiwezekana hizi dawa zitolewa katika zahanati zote, naomba niseme sasa hivi tumeanzisha zile center maalum na tutambue kwanza zoezi hili lilipoanza tulikuwa tunafanya katika Hospitali za Wilaya lakini tuka-scale up hii programu sasa imeenda katika vituo vya afya mpaka zahanati.
Kwa hiyo, tunachukua hoja hii ya msingi lengo kubwa ikiwa ni jinsi gani tutafanya tuwasaidie wananchi wetu waweze kupata huduma kwa karibu.
Kwa hiyo, tutashirikiana na wenzetu Wizara ya Afya, kuangalia tufanyeje mambo yetu ya kisera ili wananchi wetu wa Tanzania ambao wameathirika na janga la UKIMWI waweze kupata tiba kwa maeneo ya karibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili amesema kwamba hawa waathirika wengi wao ni maskini, ni kweli na ndiyo maana ukiangalia mipango ya Serikali hivi sasa hata ule mpango wa TASAF, lengo kubwa ni zile kaya maskini ambazo upatikanaji wa fedha inakuwa ni tatizo tunaziingiza katika mpango wa TASAF ziweze kupata fedha kuweza kujikimu katika maisha yao.
Hata hivyo, nizielekeze Halmashauri zote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa vile tunakuwa na mpango maalum wa kuziwezesha familia zetu hasa za wanawake na vijana ambapo asilimia tano ni kwa vijana na asilimia tano ni kwa wanawake, tuangalie kama tuna watu ambao wameathirika basi familia hizi tuzipe kipaumbele katika suala zima la mikopo ili waweze kushiriki katika suala la uchumi ili kujikomboa na umaskini.
MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Katika swali la msingi muuliza swali Mheshimiwa Joram Hongoli alisema kwamba wamekuwa wakipoteza maisha kule Njombe kutokana na kutembea umbali mrefu bila kupata matibabu.
Pia kule Njombe na maeneo mengine ya karibu kuna tatizo au tabia ya kurithiana wajane na wagane pale ambapo mmoja amefariki bila kupimwa vizuri afya zao. Wengine wamekwenda mbali zaidi, kumekuwa na tabia ya kwenda katika mapango jambo ambalo linaongeza matatizo ya VVU na UKIMWI na viongozi ndani ya Halmashauri wamekuwa wakilifahamu suala hili.
Je, Serikali ina mkakati gani wa ziada ili kuhakikisha kwamba tabia ya kurithiana wajane na wagane na matambiko katika mapango unakomeshwa katika maeneo hayo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala analozungumzia Mheshimiwa Masoud ni kweli ni jambo halisia na lipo. Miongoni mwa sababu kubwa zinazosababisha hili janga la UKIMWI liweze kuongezeka ni ile tabia ya kwamba mtu amefariki halafu mtu mwingine anamrithi, lakini kuna visababishi mbalimbali. Jukumu letu kubwa hapa sisi kama Serikali ni kutoa elimu kwa wananchi ni vitu gani ambavyo vinasababisha ongezeko la UKIMWI katika maisha yetu. Katika suala hili zima la kurithiana, Serikali imekuwa ikitoa elimu mara kwa mara kwamba utaratibu ule wa zamani wa kimila kwamba mtu amefariki bila kujua afya zao zikoje basi shemeji au mtu mwingine anamrithi si utaratibu mwema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaelekeza maeneo mbalimbali hasa katika Halmashauri zetu kwa sababu Serikali za Mitaa ziko kwenye maeneo yote kuendelea kutoa elimu hii. Ni vyema wananchi wote sasa wajue kwamba programu ya upimaji wa afya zetu ni jambo la msingi kwa sababu sio wagane peke yake hata katika hali ya kawaida katika suala zima la ndoa ajenda ya kupima afya zetu ni jambo la msingi ili kuzilinda familia zetu na watoto watakaozaliwa.
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Kibena katika Jimbo la Njombe Mjini ndiyo inayotumika kama Hospitali ya Mkoa wa Njombe lakini haina kipimo cha x-ray.
Je, Serikali ipo tayari kutuwezesha wananchi wa Jimbo la Njombe Mjini mashine ya x-ray ili iweze kusaidia wananchi wote wa Mkoa wa Njombe?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme kwamba amehamisha goli, goli limehama kutoka katika swali la msingi, hii ni kwa sababu Mheshimiwa Mbunge anaguswa na wananchi wa Njombe. Ni kweli pale hakuna x-ray na tulivyofika pale ilibainika kweli changamoto kubwa pale ni x-ray. Hata hivyo, tulitoa maelekezo kwa Halmashauri katika mipango yao ya bajeti kuhakikisha wanapata x-ray, aidha, kwa kupata mikopo kutoka NHIF au kutumia mikakati yoyote kupata funds.
Napenda nimtaarifu Mbunge kwamba suala hili tumelichukua na tutakaa pamoja naye kuangalia tufanye nini ili tuwaokoe wananchi wa pale Njombe wanaohudumiwa na Hospitali ya Kibena kupata x-ray kwa sababu mtu akiumia inakuwa shida. Tunatambua eneo hilo imepita barabara kubwa ya magari yanayotoka Songea, kwa hiyo, ajali zikitokea pale lazima waweze kupimwa na vipimo hivyo vya x-ray. Kwa hiyo, nitaomba tukae pamoja kuona ni jinsi gani tutakuwa na mpango mkakati, Halmashauri na Serikali tubadilishane mawazo ya jinsi ya kupata x-ray katika Hospitali ya Njombe.
MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Wilaya ya Kilema inahudumia zahanati zaidi ya 13; lakini zahanati hizo zina upungufu mkubwa wa vifaa tiba pamoja na watumishi ambapo zahanati ya Miwaleni imefungwa kabisa kwa kukosa watumishi. Ni nini tamko la Serikali kuhusu watumishi hawa kwenye zahanati zote 13?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka Mheshimiwa Mbatia ali-raise concern hii nadhani wiki iliyopita kuhusu hospitali hii. Mimi nafahamu wazi hata katika zoezi letu hili la uhakiki wa watu walioghushi vyeti, katika sekta ya afya tutakuwa na changamoto kubwa sana ya kukosa wataalam. Ndiyo maana Mheshimiwa Rais juzi alitoa maelekezo kwamba tutakuwa na ajira takribani 52,000 lakini miongoni mwao watakuwa ni wa kada ya madaktari, wahudumu wa afya pamoja na wauguzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimtoe shaka Mheshimiwa Mbunge kwamba katika ajira mpya tutaipa kipaumbele zahanati yake kwa sababu tunajua kuna vifaa vingi vimewekezwa ni lazima tupate wataalam wa kufanya ile. Kwa hiyo, tutalichukulia kwa umakini mkubwa ili kuwasaidia wananchi wa Vunjo waweze kupata huduma.
MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa suala la umbali linalowakabili wagonjwa wa UKIMWI kule Njombe ndilo hilo hilo ambalo linawakabili akina mama wajawazito wa Jimbo la Mwibara. Kutoka katika Kituo cha Afya cha Kasiguti pamoja na Kisorya kwenda Hospitali ya Misheni ni takribani kilometa 40. Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari baada ya Bunge hili la bajeti kuambatana na mimi ili twenda kwenye Kituo cha Afya cha Kisorya na Kasuguti ajionee namna ambavyo wananchi wametumia nguvu zao kujenga wodi ili Serikali iweze kutusaidia kukabiliana na changamoto ya umbali mrefu inayowakumba akina mama wajawazito?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi pamoja na Waziri wangu Mheshimiwa Boniface Simbachawene tumekuwa na mkakati mkubwa sana wa kuyafikia maeneo mbalimbali. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya hapa tutaangalia tufanye utaratibu gani ili tuweze kufika katika maeneo yake, lakini siyo hapo peke yake tutafika mpaka Rorya pamoja na Tarime kule kwa sababu kuna changamoto mahsusi katika Mkoa wa Mara ambazo lazima twende tukazifanyie kazi.
MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nifanye masahihisho kidogo ni Kata ya Katumba siyo Mtumba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haya maeneo ambayo ilikuwa ni makazi ya wakimbizi yalikuwa yanapata ufadhili wa Shirika la Wakimbizi Duniani (UNHCR) katika huduma mbalimbali za jamii ikiwemo elimu, maji na barabara. Ningependa kujua Serikali ina mpango gani wa kuhusisha UNHCR kwa kuwa makambi yanaenda kuvunjwa, msaada gani ambao watautoa ili kuboresha miundombinu mbalimbali ambayo sasa hivi imekuwa ni hafifu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema pale awali kwamba maeneo haya uchaguzi bado haujafanyika, japo uchaguzi haujafanyika jukumu kubwa la Serikali ni kuhakikisha katika maeneo hayo, wanaendelea kupata huduma za kijamii kwa ufanisi kama kawaida. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI jambo hilo tunaliangalia kwa karibu zaidi na kwa kuanza changamoto yetu kubwa ni kuisukuma bajeti hii ambayo sasa hivi imepitishwa kuhakikisha kwamba Halmashauri hii inafanya uchaguzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo ni kuhakikisha kwamba, kwanza tunajua katika maeneo hayo huduma za kijamii nyingi zilikuwa zinatolewa na Shirika la Wakimbizi Duniani, sasa hivi ni jukumu la Serikali. Hili ni jukumu letu kubwa na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutapeana ushirikiano wa kutosha ili wananchi wa pale waweze kupata huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo miundombinu ya barabara, huduma ya elimu, huduma ya afya na ifike muda na wao wajione kwamba ni wananchi kama wananchi wengine wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MHE. MWANNE I. NCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naitwa Mwanne Ismail Nchemba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, tatizo la Wakimbizi wa Katumba linafanana na tatizo la Wakimbizi wa Ulyankulu na kwa kuwa hawakufanya uchaguzi wa Madiwani. Je, Serikali inasema nini, ni lini utafanyika uchaguzi wa Madiwani katika Jimbo la Ulyankulu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa sababu hao ni wananchi wake, akiwa Mbunge wa Viti Maalum ana kila sababu ya kuona maeneo hayo yanafanyika uchaguzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka swali hili nilijibu katika Mkutano wetu wa Bunge uliopita, nilisema pale kuna takribani Kata tatu uchaguzi haujafanyika kwa sababu za msingi, bado suala zima la utengamano linaendelea na pale sasa hivi bado Jeshi na Wizara ya Mambo ya Ndani wanaendelea kumiliki eneo lile. Utararibu utakapokamilika jukumu letu kubwa watu wa TAMISEMI baada ya ule mtangamano kuwa vizuri zaidi na eneo lile sasa rasmi likishakuwa chini ya TAMISEMI, mchakato wa uchaguzi sasa utaendelea ili watu wa pale wajikute nao wana Serikali yao halali iliyowekwa kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi Namba 292
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Ahsante. Kwa kuwa Waziri amekiri kwamba bajeti iliyopita walitenga milioni 870, lakini ni milioni 157 tu ndiyo zimepelekwa. Je, haoni umuhimu wa kuhakikisha pesa iliyobaki inapelekwa.
Swali la pili, kwa kuwa Halmashauri ya Rungwe imepata mafuriko na uharibifu wa barabara umekuwa mkubwa sana, naomba Wizara hii itutumie pesa za haraka kwa ajili ya emergency kwa ajili ya vijiji kama tisa zaidi ya kilometa 40; kama Kijiji cha Kyobo, Ikuti na sehemu za Lupepo. Je, Serikali haioni umuhimu wa kupeleka pesa hizo haraka kwa ajili ya kusaidia barabara na madaraja yaliyoharibika?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika majibu yangu ya msingi nilisema bajeti ilikuwa ya shilingi milioni 870, zilizopelekwa mpaka sasa ni shilingi milioni 157, jibu hili nimekuwa nikilitoa kila mahali katika vipindi mbalimbali. Nilisema wazi, ukiachia changamoto ya ujenzi wa barabara, lakini kuna miradi mingi kipindi kilichopita ilikuwa haiendi vizuri. Nilitolea mifano miradi ya maji na miradi mingineyo kwamba upelekaji wa pesa ulikuwa ni tatizo kubwa sana, lakini kulikuwa na sababu zake za msingi. Katika mwaka uliopita pesa nyingi sana zilienda katika matukio makubwa ambayo yalikuwa yamejitokeza kama suala la uandikishaji na uchaguzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mchakato wa hivi sasa, Serikali imejielekeza zaidi katika ukusanyaji wa mapato, ndiyo maana hivi sasa hata ukiangalia kwa mara ya kwanza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imevunja rekodi katika ukusanyaji wake wa mapato. Nilisema kwamba hata miradi iliyokuwepo mwanzo imesimama, lakini hivi karibuni miradi hiyo inapelekewa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nia yetu ni kwamba, katika kipindi hiki cha bajeti kilichobakia nina imani Serikali itajitahidi kupeleka fedha katika miradi yote iliyosimama nikijua wazi katika maeneo hayo mengine wakandarasi ambao ni wa ndani na wengine wa nje wanaendelea kudai. Kwa hiyo, suala hili tunaweka kipaumbele siyo kwa ajili ya maeneo hayo tu isipokuwa kwa Tanzania nzima kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mafuriko na kuharibu miundombinu ya barabara, hili nilisema ni kweli. mwaka huu ukiangalia maeneo mbalimbali tumekuwa na changamoto ya mvua kubwa iliyonyesha. Nimetolea mfano kule Rungwe, ukienda Kyela, ukienda Kilosa na maeneo mbalimbali, yote yameathirika kwa ajili ya mvua na ndiyo maana tulipeleka utaratibu kwamba kila Halmashauri ianishe uharibifu wa miundombinu mara baada ya mvua ile kunyesha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jukumu letu kubwa ni kuangalia sasa kile ambacho tunaweza kusaidia kwa kipindi cha sasa. Kwa hiyo, baada ya uharibifu huo, Serikali itachukua jukumu la kusaidia siyo maeneo ya Rungwe peke yake, isipokuwa maeneo mbalimbali ambayo yameathirika na nafahamu hata maeneo ya Morogoro hali ilikuwa mbaya sana na maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MHE. CHARLES J. TIZEBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona. Kwa kweli, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri ningependa tu kujua baada ya Halmashauri zetu kuleta haya maombi na ilikuwa katika matarajio yetu kwamba uharibifu huu usikutane na msimu mwingine wa mvua kwa sababu uharibifu utakuwa mkubwa zaidi na bajeti tuliyoipitisha inaweza ishindwe kukidhi hayo mahitaji. Sasa, labda ni lini tu Mheshimiwa Waziri watatuona kabla mvua hazijaanza tena hasa sisi tunaotoka kwenye maeneo ya misimu miwili ya mvua?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini naomba niseme kwamba hapa siwezi kusema kesho au keshokutwa, kwa sababu tunachofanya ni needs assessment. Tuna Halmashauri zipatazo 181, kila Halmashauri ina changamoto yake ya jinsi gani miundombinu ya barabara imeharibika. Kwa hiyo, wataalam wetu wanalifanyia assessment katika maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikopita maeneo mengine ni kweli huo uharibifu umekuwa wa kiwango kikubwa sana. Hivi sasa wananchi wengine wanashindwa hata kufika katika maeneo mbalimbali. Kwa hiyo, jukumu letu kubwa ni ku-fast truck hii process ili angalau kitakachopatikana kidogo tuweze kugawana ili wananchi waweze kupata huduma kwa kipindi hiki cha sasa.
MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mbunge wa Rungwe Mheshimiwa Saul Henry Amon, Mji wa Tukuyu ni miongoni mwa miji mikongwe katika nchi hii hata utaitwa Tokyo. Lakini mradi wa Masoko aliousema Mheshimiwa Naibu Waziri una changamoto nyingi na hadi umepelekea Mkandarasi wa mara ya kwanza walipelekeana Mahakamani pamoja na Halmashauri na hata sasa amepatikana Mkandarasi mwingine, lakini Mkandarasi huyu wa pili bado naye hajalipwa fedha zake na wanakoelekea inawezekana ikawa kama Mkandarasi wa kwanza. Je, Serikali inatoa kauli gani ili akinamama ambao wanatoka mabondeni na maeneo mengine mbalimbali tuwatue ndoo kichwani ili huyu Mkandarasi aweze kulipwa fedha zake.
Swali la pili, Mji wa Tukuyu una milima, mabonde pamoja na mlima Rungwe, tuna maji ya kutosha. Hatuna sababu yoyote Serikali kutopeleka maji kule kwa sababu hata maji ya gravity tu yanatosha kwa ajili ya wananchi waweze kupata maji. Serikali inatoa kauli gani ili wananchi wa eneo hilo waweze kupata maji? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nirejee, siku ya Jumatatu nilikuwa Rungwe, miongoni mwa mambo ambayo tulijadili na Mwenyekiti wa Halmashauri, DC na Kaimu Mkurugenzi ni suala zima la mradi huu wa maji mkubwa ambao katika njia moja au nyingine ukiweza kukamilika utasaidia watu wa Mji wa Tukuyu kupata maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wanaotumia pale Tukuyu ni mradi ambao ulibuniwa miaka ya nyuma, wakati huo population ilikuwa ndogo sana, lakini sasa hivi idadi imekuwa kubwa sana, ndiyo maana katika kurudi kwangu hapa tulichokubaliana ni kwamba nitawasiliana na wenzetu wa Wizara ya Maji ili kuangalia tutafanya jinsi gani kwa sababu changamoto kubwa ya mradi wa Masoko ni suala zima la fedha. Hata Mheshimiwa Atupele aliposema kwamba Mkandarasi wa kwanza alikoma na wa pili hivi sasa, ni kweli!
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi hata kazi pale site imesimama changamoto kubwa sana ni fedha, ndiyo maana siku zote tunasikilizana humu katika Bunge letu, katika kipindi cha sasa Serikali inaona miradi mingi ya maji ambayo mwanzo ilikuwa imesimama, sasa inatekelezeka kwa sababu kwamba nguvu kubwa ya Serikali imewekwa katika ukusanyaji wa mapato. Imani yangu kubwa baada ya hii nitampa reference nilichokipata kule juzi, Waziri wa Maji, tutaangalia kwa pamoja jinsi gani tutafanya mpango mkakati mpana kuhakikisha watu wa Tukuyu ule mradi unakamilika, ili kutoa ile kadhia kwa akinamama katika Mji wa Tukuyu.
Mheshimiwa Naibu Spika, agenda ya pili ni kweli. Tukuyu nilipopita juzi nimeona maeneo mengi sana kuna maji ya chemichemi, lakini katika mipango ya Serikali hapa na Wizara ya Maji ilizungumza katika Bajeti yake kwamba tutajielekeza katika vile vyanzo rafiki vilivyopo kuhakikisha kwamba vyanzo vilivyopo vinatumika vizuri. Imani yangu kwa sababu Mji wa Tukuyu ni takribani miezi miwili tu wanakosa mvua, tutatumia vyanzo hivi vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutashauriana na Serikali yetu kwa ujumla, TAMISEMI na Wizara ya Maji, lengo kubwa ni kwamba Mji na Wilaya kongwe ile ya Rungwe uweze kunufaika na suala zima la maji na vilevile katika Jimbo la Busokelo ambako ndugu yangu Mheshimiwa Fredy Atupele anapatikana kule.
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ningeomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri maswali mawili madogo ya nyongeza.
Kwa kuwa tatizo la Itobo linafanana kabisa na tatizo la Kata ya Lusu kuwepo kwa kituo cha afya ambacho kilijengwa na ADB chenye vifaa na vitendea kazi vya namna hiyo. Je, Serikali haioni wakati umewadia wa kuhakikisha wanapeleka Wataalam na katika kituo cha afya cha Lusu ili kuweza kutatua tatizo linalowakabili wananchi wa Lusu kwa sababu wanatembea zaidi ya kilometa 20?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kituo cha afya cha Zogolo kilichopo katika Kata ya Nzega ndogo ambacho majengo yake yamekamilika na baadhi ya majengo kwa ajili ya wodi kwa akinamama na theatre yanahitaji kumaliziwa na kituo cha afya kilichopo Kata ya Mbogwe ambacho hutumika kwa ajili ya kuhudumia Kata zaidi ya saba, je, Serikali haioni wakati umewadia wa kutenga fedha kwenda kusaidia nguvu za wananchi katika vituo hivi vya afya vya hizi Kata mbili cha Zogolo na Mbogwe ili wananchi wa maeneo hayo waache kusafiri masafa marefu kwenda kufuata huduma katika hospitali ya Wilaya ya Nzega?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna vituo hivi vilivyojengwa na ADB, kuna kule Itobo, Bukene na kituo cha Lusu. Si hivyo tu hata nilivyofika Masasi nilikuta kuna vituo vimejengwa. Changamoto kubwa ya vituo hivi ni kwamba vina vifaa vizuri sana, tatizo lake ni katika suala zima la wataalam.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumejielekeza, pamoja na Waziri wa Afya, kuona ni jinsi gani tutafanya katika ajira itakayokuja katika maeneo haya ambayo yana upungufu hasa wa Wataalam wale wa upasuaji na dawa za usingizi ili tukiwapata wataalam hawa tuweze kuwapeleka kwenye vituo hivyo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Hussein Bashe kwamba, Mkoa wa Tabora ni miongoni mwa mikoa ambayo tumeiwekea kipaumbele na hasa kutokana na vituo hivi kuwa na vifaa vyenye thamani kubwa sana, tusipovitumia kwa sasa vinaweza vikaharibika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, jambo hili katika mchakato huu unaokuja sasa hivi maeneo yale yote na maeneo mengine ambayo nimetembelea ambapo vituo vile vimejengwa, vitapewa kipaumbele katika upatikanaji wa Wataalam wanaokidhi kwa matumizi ya vile vifaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mchakato utakaokuja maeneo yale yote na maeneo mengine ambayo nimetembelea ambako vituo vimejengwa vitapewa kupaumbele katika upatikanaji wa wataalam wanaokidhi matumizi ya vifaa vile.
Mheshimiwa Naibu Spika, juu ya suala la kituo cha Zogolo pamoja na Mbogwe, nimesema awali, katika bajeti ya mwaka huu watu walikuwa na malalamiko kwa kusema kwamba hawaoni jinsi gani Wizara ya TAMISEMI imekwenda kuhakikisha kwamba ukarabati umefanyika. Tulisema kwamba kupanga bajeti hizi za kumalizia inaanzia katika ngazi za Halmashauri. Ndiyo maana nimesema pale awali kwamba wiki iliyopita, Wizara ya Afya na TAMISEMI na Kamati ya Bajeti imekaa pamoja kubaini upungufu kama huo. Lengo letu kubwa ni kuja na mpango mkakati mpana zaidi ili kuhakikisha vituo hivi ambavyo vina suasua tutaweza kuvikamilisha wananchi wapate huduma bora.
MHE. DKT. CHARLES J. TIZEBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri yanakubaliana na ukweli kwamba viko vituo vingi vya afya vyenye vyumba vya upasuaji nchini lakini havifanyi kazi kwa sababu mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, Benjamin Mkapa Foundation wamejenga vituo vingi karibu 20 Mkoa wa Rukwa vyenye vyumba vya upasuaji na havifanyi kazi kwa sababu ya kukosa wataalam. Huko Buchosa kuna kituo cha Mwangika, planning international wamejenga hakina Wataalam wa usingizi. Sasa nimwombe tu Waziri, kwamba labda wanaweza kuchukua takwimu kutoka Halmashauri zote ili kabla ya Bunge hili kuahirishwa tujue ni vituo vingapi ambavyo vina theatres na bado hazifanyi kazi kwa sababu ya upungufu wa Wataalam hawa wa usingizi.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba ushauri wa Tizeba japokuwa tumeshakuwa na current data lakini tutazifanyia kazi bila shaka.
MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza linalofanana kabisa na swali la msingi la Mheshimiwa Zedi. Hakuna jambo linalosikitisha kama pale ambapo majengo ya Serikali ambayo yameanza kujengwa halafu yanaachwa nondo zinaoza na kusababisha hasara kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, Serikali inasema nini kuhusu jengo la upasuaji lililoanza kujengwa katika Wilaya ya Urambo ambayo mpaka sasa haijakamilika wakati huo jengo la upasuaji katika kituo cha Usoke halijakamilika, jengo la kliniki ya akinamama wajawazito katika Kata ya Usisya na Isongwa yote nondo zinaoza. Serikali inasema nini kuhusu uharibifu huu unaoendelea wakati wananchi wanahitaji huduma katika Wilaya ya Urambo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema hapa mwanzo, nikasema kwanza kuhusu majengo ambayo hayajakamilika wakati mwingine tunakuwa na makosa wakati wa budgeting. Wakati mwingine tunapanga bajeti, jengo halijakamilika na mwaka mwingine tunatenga bajeti bila kuangalia mradi uliopita. Kwa hiyo, kwanza katika vikao vyetu vya awali vya Halmashauri ni jambo la msingi kubainisha miradi ambayo haijakamilika na kuitengea fedha katika bajeti, kwa sababu bajeti hiyo ikishathibitishwa ndipo majengo hayo huweza kumalizika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana nampongeza Mheshimiwa Mama Sitta kwa sababu ana-concern kubwa kwa akinamama. Ndiyo maana nimesema kwamba kwa kuona umuhimu wa jambo hilo tumeelekeza Halmashauri zote na barua tumeshaiandika imeenda katika Halmashauri zote; kwamba kila Halmashauri ilete mchanganuo wa majengo ambayo hayajakamilika ili tuweze kupanga kwa pamoja. Jambo hili lilifanywa na Kamati ya Bajeti ya Bunge kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais, TAMISEMI wiki iliyopita.
Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu letu kubwa ni kupata mpango mkakati wa namna ya kufanya ili kuondoa haya maboma ambayo tangu mwaka 2007 – 2010 yalianzishwa na hadi sasa hayajakamilika. Kwa hiyo, Mheshimiwa Sitta nikuhakikishie kwamba mpango wetu uliokuwepo ni mpango wa pamoja baina ya Bunge na Wizara za Serikali kuhakikisha kwamba huduma za afya, ukamilishaji wa majengo unakamilika ili wananchi waweze kupata huduma bora.
MHE: STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa matatizo ya vyumba vya upasuaji yako pia kwenye Wilaya ya Nyamagana hasa, kwenye Hospitali yetu ya Sekou Toure ambayo Miundombinu yake ya theatre iliyopo sasa iko mbali kutoka kwenye Jengo ambalo ni labour ward. Pale kwenye jengo la labour ward tayari kuna jengo ambalo lilishaandaliwa lakini halina vifaa kabisa. Ni lini Serikali itakuwa tayari kupeleka vifaa vya upasuaji kwenye jengo hilo ambalo liko karibu sana na chumba wanachojifungulia akinamama, tukiamini kupatikana kwa vifaa hivi kutasaidia kuokoa maisha ya mama na mtoto yanajitokeza hasa wakati wa kujifungua?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, huyu Mbunge anayeuliza hivi kwanza tuelewe kwamba yeye ni Msukuma, kwa hiyo lugha yake lazima tuielewe vizuri. Najua kwamba Mbunge huyu yuko makini katika Jimbo la Nyamagana kwa sababu kazi aliyoifanya akiwa kama Mwenyekiti, Meya wa Jiji lile tunaitambua wazi. Kwa hiyo, nimthibitishie, hata maamuzi waliyofanya kufuma mifumo ya electronic mpaka sasa hivi wanakusanya kutoka 150,000 mpaka milioni tatu kwa siku, ni mchakato mkubwa sana ambao Mbunge huyu ameufanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kama Serikali tunasema kwamba, kwanza mimi mwenyewe nilimwambia nilipoongea naye hapo awali kwamba nitakwenda Mwanza, tutatembelea Sekou Toure, tutapanga kwa pamoja jinsi gani tutafanya ili vifaa tiba vipatikane. Vitapatikana wapi, tutajua katika mpango wa pamoja tutakapokaa pamoja, lakini nitakwenda kule Mwanza kubainisha kwanza mapato yao ya ndani wanayoyapata, lakini pia kuangalia fursa zipi nyingine tutakazozitumia ili wananchi wa Mwanza waweze kupata huduma bora.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili na mimi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa katika mipango yote ya kujenga shule za sekondari, shule za msingi, zahanati, vituo vya afya tunasahau sana huduma za maji, umeme pamoja na afya. Sasa nataka niulize swali kwa Mheshimiwa Waziri na bahati nzuri sana Mheshimiwa Jafo, Waziri wa TAMISEMI Mpwapwa anaifahamu vizuri sana. Katika bajeti ya mwaka 2018/2019; je, Serikali itakuwa tayari kutenga fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba vituo vya afya, zahanati, shule za msingi, sekondari zote Jimbo la Mpwapwa zinapata huduma ya maji, umeme na afya?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri wangu kwa majibu mazuri sana aliyoyatoa hapo awali. Pia naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lubeleje kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli ukiangalia hali halisi ya Jimbo la Mpwapwa changamoto hizo alizozungumza Mheshimiwa Mbunge ni kweli, lakini hata hivyo tunachokifanya ni kuhakikisha kwamba tunawapatia huduma ya maji. Nafahamu kwamba Jimbo la Mpwapwa, Wilaya ya Mpwapwa ina changamoto kubwa. Tumeweza kuhakikisha kwamba; kwa mfano ile miradi sita na Mzee Lubeleje anafahamu tulivyokuwa kule Mima pamoja katika ujenzi wa Kituo cha Afya, mtandao wa maji ambao kwa muda mrefu wakandarasi walikuwa mradi huo walikuwa hawajaanza sasa wakandarasi wote sita wako site.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jukumu letu kubwa ni kwamba maji yale yatakapotoka katika jamii kuna water points tutazipeleka katika taasisi hizi za Umma kwa ajili ya kuhakikisha kwamba vituo hivyo vinapata maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mpango wa REA mnafahamu kwamba Wizara ya Nishati imezungumza wazi katika mpango wa REA Awamu ya Tatu kwamba itahakikisha katika sehemu zote za umma hasa vituo vya afya, shule pamoja na taasisi za dini zote zitapatiwa umeme kupitia katika mpango wa REA III. Isipokuwa katika hili niwaombe Waheshimiwa Wabunge katika ajenda hiyo lazima tuanze maandalizi ya awali ya kuweka wiring katika maeneo hayo, kwa sababu umeme ukishafika hapo ni lazima taasisi yenyewe iwe imeshafanya wiring ili kuhakikisha kwamba huduma hiyo inapatikana vizuri. Ahsante sana.
MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa tatizo lililopo katika jimbo la Kibiti linafanana na baadhi ya maeneo katika mji wa Dodoma, kwamba baadhi ya mitaa mfano Nkuhungu, Ilazo, Makole barabara zake za mitaa zipo katika hali duni sana. Je, Serikali itarekebisha lini barabara hizi ukizingatia kwamba sasa hivi Dodoma ni Makao Makuu? Ahsante.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu wazi hoja anayozungumza Mheshimiwa Fatma Toufiq kwamba ni kweli ni hoja halisia. Hii ni kwa sababu mji wetu wa Dodoma sasa hivi kwa maamuzi sahihi yaliyofanywa Serikali ni Makao Makuu yetu. Hata hivyo kupitia miradi yetu ambayo tunaendelea nayo hapa Dodoma, sawasawa na miradi ambayo tunaendelea nayo katika miji saba katika ile Strategic City Project; kazi hii inaendelea awamu kwa awamu. Wabunge nadhani mnakuwa ni mashahidi. Wabunge waliofika mwaka 2010 hapa Dodoma wakifanya ulinganifu na hali ilivyo hivi sasa ni tofauti sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo tutaendelea kujenga miundombinu hii. Sasa hivi kuna ring road karibuni zitakuwa tatu. Kuna hii ambayo hata ukifika kule inakatisha, vilevile tuna barabara zetu za mitaa na wataalam wetu wanaendelea na kazi hiyo. Lengo letu ni kwamba tukifika mwaka 2020 Jiji la Dodoma litakuwa ni tofauti sana kwa sababu mpango wetu huo ambao unaenda mpaka mwaka 2020 utahakikisha mji wa Dodoma wote mitaa yake yote itakuwa na kiwango cha barabara za lami.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo si lami peke yake isipokuwa tutapeleka na mataa pamoja na mifereji yote ya kuondoa maji kuhakikisha jiji hili linakuwa jiji la mfano ambao ndio mpango hasa wa Serikali yetu ilivyoamua.
MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, walimu wa shule zote za Wilaya ya Songea walisimamishwa wakati Wilaya zingine wamepandiswa madaraja na maslahi yao yameongezeka, walimu wa Songea Vijijini hawakufanyiwa hivyo kwa sababu taarifa kutoka kwa Mkurugenzi zilichelewa kuifikia Wizara. Suala hili limefuatiliwa kwa miaka miwili sasa na walimu hawa hawajapata stahiki zao mpaka sasa.
Je, Serikali inatoa tamko gani kwa walimu waliopo Songea, kwa maana ya Songea Vijijini na Halmashauri ya Wilaya ya Madaba kuhusu madai na malalamiko yao? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna kesi za aina mbalimbali, na hata jana nilipata kesi inayofanana na hiyo kutoka kwa Mheshimiwa Kanyasu. Nimewaelekeza wataalam wetu wafanye tathmini maeneo mbalimbali yenye changamoto, nikifahamu kwamba lengo letu kubwa ni kuhakikisha kwamba watumishi wetu wanafaya kazi kwa amani. Maeneo mengine wamefanya vizuri, maeneo mengine bado hawajafanya vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimewaelekeza wataalam wangu waweze kufanya kufanya tathmini maeneo mbalimbali yenye changamoto ili tuwasaidie watumishi wote ambao wana changamoto mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tuweze kubaini utendaji wa kazi wa baadhi ya watu tuliowapa mamlaka. Wale wataonekana kwamba wamekuwa ni kikwazo basi ni vyema tukaweza tukawachukulia hatua za kinidhamu kwa sababu katika njia moja au nyingine wanaweza wakasababisha Serikali ikalaumiwa kumbe kutokana na uzembe wa watu wachache.
Kwa hiyo jambo hili tumelichukua na toka jana timu yangu inafanyia kazi jambo hilo kwa sababu lilitoka vile vile katika Mkoa wa Geita. Maeneo mbalimbali kuna kesi kama hizo, kwa hiyo Serikali tunaichukulia yote kwa ujumla wake na kuyafanyia kazi. (Makofi)
MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto ilihamisha walimu 210 kwa wakati mmoja, lakini mpaka sasa hivi walimu wale hawajalipwa stahili zao.
Je, ni lini walimu wale wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto watalipwa pesa zao za uhamisho?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza tulichukue hilo tujue kwa nini kwa sababu kuna fedha maalum tulizitoa kwa EPforR kwa ajili ya kuhakikisha walimu wanahamishwa katika maeneo mbalimbali na stahili zao zinapatikana. Kesi kama hiyo tumeshaanza kuishughulikia katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa ambako nadhani kuna maeneo mbalimbali imejitokeza kesi kama hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaangalia nature ya uamisho huo ulikuwaje na kwa nini watu walikuwa hawajalipwa, na kama walikuwa hawajalipwa ikiwa tayari Serikali ilishatoa pesa kwa EPforR tutaangalia nini tufanye.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Shekilindi naomba tulichukue hilo kama Serikali kwa concern ya eneo la Lushoto pamoja na maeneo mbalimbali ambayo yatakuwa na kesi kama hiyo. Tutaweza kuratibu vizuri jinsi gani ya kuondoa tatizo hili ambalo hatimaye kama nilivyosema awali tunataka walimu waweze kuhama kwenye maeneo ya kazi wakiwa wamefanya kazi kwa amani kama inavyokusudiwa. (Makofi)
MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Vijiji vya Kasu, Milundikwa, Katani, Kisula pamoja na Malongwe, Kata ya Kandanse wameamua kujenga Kituo chao cha Afya Kasu na wadau mbalimbali wameonesha kuwachangia ikiwepo Mfuko wa Jimbo. Je, Serikali ipo tayari kuwaunga mkono juu ya juhudi zao hizo za kupata Kituo cha Afya? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ninafahamu Mheshimiwa Mipata na mwenzake Mheshimiwa Keissy katika Wilaya yao kule wamefanya kazi kubwa sana ya kuhamasisha ajenda ya afya na ndiyo maana nilipofika pale nimeona jiografia ya Wilaya ya Nkasi ina changamoto kubwa sana. Hii ndiyo maana katika kipaumbele chetu, kwa kuunga mkono wananchi wa Kasu, tumehakikisha kwamba katika kipindi cha hivi karibuni tutawezesha Kituo cha Afya cha Kasu na Wampembe kuhakikisha kwamba vile vituo vya afya viwili vya maeneo hayo viweze kupata huduma ya upasuaji kwa lengo kubwa kwamba population iliyopo kule na wengine kutoka nchi jirani muweze kuhakikisha mnawa- manage vizuri katika sekta ya afya. Kwa hiyo, hilo tumeliangalia na tunalipa kipaumbele. (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Kakonko ni kati ya wilaya mpya na mpaka sasa Wilaya hiyo haina Hospitali ya Wilaya. Eneo hilo la Kakonko limepakana na Mkoa wa Kagera na wananchi wengi wanakuja kutibiwa katika Kituo cha Afya cha Kakonko kwa kuwa hawana hospitali jirani yao. Serikali iliahidi kupeleka shilingi milioni 500, mpaka sasa shilingi milioni 500 hizo hazijapelekwa katika Wilaya ya Kakonko. Nilitaka kujua, je, ni lini Serikali itapeleka milioni 500 ili wananchi wa Kakonko waweze kupata huduma ya matibabu? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Kakonko ni sehemu yenye changamoto kubwa na Mheshimiwa Mbunge nakumbuka hata tulivyokuwa kule kipindi kile tumeona idadi kubwa ya watu kutoka Burundi wakitibiwa pale katika kituo kile cha afya.
Ni kweli tumetenga shilingi milioni 500 na nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba fedha zile zilikuwa zinaenda awamu kwa awamu. Ni imani yangu kwamba sasa hivi kwa muda huu ninapozungumza katika ile batch ya mwisho zitakuwa zimefika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ondoa hofu ndani ya kipindi hiki nina amini, lakini nita-cross check leo hii kwa nini hazijafika kwa sababu tumeshazitengea zile fedha ziende Kakonko kwa ajili ya uboreshaji wa kituo kile cha afya. (Makofi)
MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwepo changamoto kubwa sana ya barabara kutokana na mitandao ya maji na hasa katika kata mbalimbali za Jimbo la Segerea ikiwemo Kata ya Vingunguti; je, ni kutokana na ubovu wa mabomba ndiyo maana tunazidi kuona maji yanazidi kutiririka hovyo katika maeneo haya?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, changamoto hiyo ipo. Kama tunavyokumbuka, wakati nilipotembelea barabara ya Kwa Mnyamani kutoka hapa Buguruni barabara ya Kwa Mnyamani kwenda Vingunguti, barabara ile muda mwingi sana maji yamejaa barabarani’ Tatizo kubwa ni kwamba yale mabomba yanapasuka kwa hiyo yanajaa barabarani na barabara inaharibika.
Mheshimiwa Naibu Spika, na ndiyo maana nilitoa agizo pale kwamba Manispaa yetu ya Ilala, TARURA pamoja na DAWASCO waweze kukaa pamoja kuangalia ile miundombinu yote ambayo iko barabarani iwekwe vizuri. Bahati nzuri zoezi hilo limekamilika, hivi sasa linaendelea vizuri, niwashukuru sana DAWASCO, pia niwashukuru Manispaa ya Ilala kwa kazi kubwa waliyofanya, na hivi sasa hata ile barabara tunaiboresha, sasa itakuwa kwa kiwango cha lami yote kuanzia hapa Buguruni tunapoingilia mpaka unafika Vingunguti.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili limefanyika shirikishi, kwamba maeneo hayo sasa yawe yanapitika vizuri, vilevile na mitandao ile ya maji ambayo inachanganyana sana wataalam nimewaagiza waiweke vizuri kuhakikisha kwamba tunalinda barabara zetu hizi. (Makofi)
MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwa namna inavyofanya maendeleo nchini, lakini nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI kwa namna yeye na timu yake wanavyohangaikia maendeleo katika nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikia Mheshimiwa Waziri akisema juu ya barabara za lami na mabomba kuanzia Buguruni kwenda Vingunguti, sikumsikia akisema kwenye eneo ambalo kodi ndiko zinakokusanywa, kuanzia Buguruni kurudi mjini. Je, maeneo haya ya Buguruni kurudi mjini barabara za lami na maji vipi Mheshimiwa Waziri?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli jambo la maji na barabara ni mtambuka lote kwa pamoja nafahamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Zungu kwanza kuhusu suala la hiyo mitandao ya barabara na maji tumetoa maelekezo, lakini hata hivyo tukija katika upande wa barabara, Mheshimiwa Zungu ofisi yetu itafanya kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba Jimbo lile la Ilala kupitia Mradi wa DMDP jimbo lako litaweza kuwa linang’ara zaidi kwa sababu hili ni jukumu la ofisi yetu, na kwa vile unapigana sana kwa wananchi wako, jambo hili tunalibeba na tunalisimamia kwa nguvu zote kwa kipindi hiki.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo langu la Tunduma na Wilaya yetu ya Momba kulikuwa na majengo ambayo yalikuwa yanatumika na Kampuni ya CC iliyokuwa inajenga barabara ya kutoka Tunduma kwenda Sumbawanga. Majengo hayo yaliteuliwa kwamba yangeweza kutumika kama Hospitali ya Wilaya, lakini sasa hivi inaonesha kuna mabadiliko. Waziri anawaambia nini wananchi wa Mji wa Tunduma kuhusiana na majengo yale kwa sababu aliwahakikishia kwamba itakuwa Hospitali ya Wilaya?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza nitaenda kufanya follow up kujua kwamba ni Waziri gani alitoa commitment hiyo.
Jambo la pili, nafahamu wazi kwamba kuna maeneo mengi sana majengo yaliyokuwa yakitumika na wenzetu wa Wizara ya Ujenzi, hasa yale makampuni, majengo yale mengi sana yameombwa kwa ajili ya ama vituo vya afya au maendelezo ya Hospitali za Wilaya. Ninafahamu wazi kwamba Tunduma kuna changamoto kubwa kwa sababu idadi ya watu pale ni kubwa na ndiyo maana tunaanza ule ujenzi wa kituo cha afya, japokuwa umekuwa ukisuasua lakini tutasimamia kwa karibu ili uweze kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo hilo ndugu yangu Mheshimiwa Mwakajoka naomba niseme kwamba tunalichukua kwenda kulifanyia tathmini kuona nini kimekwamisha, kwa sababu hatimaye tunataka wananchi wa Tunduma wapate huduma vyema kabisa. Kwa hiyo tutalifanyia kazi Serikali kwa ujumla wake wote.
MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, Hospitali ya Wilaya ya Mbozi ambayo pia inatumika kama Hospitali ya Mkoa wa Songwe akina mama ambao hujifungua pale ni wastani wa akina mama 18 hadi 20 kwa siku, lakini kwa bahati mbaya sana hospitali ile haina wodi ya wazazi.
Je, ni lini Serikali itajenga wodi ya wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi ambayo hutumia kama Hospitali ya Mkoa kwa sasa?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la ndugu yangu, comrade wangu hapa kuhusu swali la Hospitali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu kuna changamoto kubwa ya wodi ya wazazi na jukumu la Serikali yetu ni kuhakikisha kwamba hizi Hospitali za Wilaya zote tunahakikisha tunaziimarisha vizuri zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tunachukua hoja hiyo halafu kwenda kufanya analysis kupitia wataalam wetu kwenda pale kuangalia mapungufu yaliyokuwepo ili tuboreshe hospitali ile na hatimaye wananchi wa eneo lile waweze kupata huduma nzuri. Kwa hiyo, nalichukua hili kwa ajili ya kuhakikisha tunalifanyia kazi.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Kwanza napongeza TARURA kwamba wameanza kazi vizuri hususani katika Mji wangu wa Korogwe, lakini napenda kujua je, Wizara ina mpango gani sasa wa kuwawezesha hawa TARURA hususani kwenye hizi Halmashauri za Miji pamoja na kwamba wanawapa fedha za kujenga barabara zile kwa kiwango cha changarawe, sasa wapewe fedha za kutengeneza ile mifereji kwa kiwango cha kutumia mawe ili kusudi wasiweze kurudia mara kwa mara kutengeneza zile barabara? Wana mpango gani wa kuwatengea fedha ili Miji hii iweze kuwa na barabara zilizo imara kwa kupitia kuweka mawe misingi yao? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri yote ya msingi ya mwanzo yaliyoweza kutolewa. Naomba nimpongeze mama Mary Chatanda ni miongoni mwa Wabunge ambao tulipambana sana katika ujenzi wa barabara na stendi yake ya pale Korogwe Mjini.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa utengenezaji katika Halmashauri za Mji kwanza tunatumia mradi wa UGLSP ambao tunagusa takribani Manispaa na Halmashauri zote za Mji. Kwa hiyo, naomba niwahakikishie Wabunge wote ambao wako katika Halmashauri za Miji na Manispaa mpango wetu mkakati ni kuhakikisha maeneo haya tunayabadilisha kwa ajili ya ujenzi katika maeneo haya kwa tabaka la lami. Huu ndiyo mpango wa Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, katika ile Miji Mikuu Saba ambayo nimezungumza tutaaendelea kuboresha suala la mifereji, suala la barabara kwa kiwango ambacho tunajua kwamba barabara zetu tunataka guarantee ya miaka 20 ndiyo tuweze kuzifanyia service, ndiyo maana hatuko katika supervision ya hali ya juu.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, naomba nikiri kwamba TARURA tuna mtandao wa barabara takribani kilometa 108,000 ambao ni matandao mkubwa sana, lakini ukiangalia kutokana na suala la kisera la mgawanyo wa Mfuko wa Barabara ambao asilimia 30 inakuja TARURA na asilimia 70 inaenda TANROAD, eneo hili ndilo lina changamoto kubwa. Baadaye tutaangalia nini cha kufanya, lengo letu kubwa ni kwamba Halmashauri zote ziweze kupitika kwa sababu wananchi huko ndiko uchumi unapojengeka. (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa Serikali imekiri kwamba Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wanafanya kazi nzuri na imekuwa ikiwategemea kwenye kazi zote na hata kualika mikutano yote ya Wabunge, Madiwani na kufanya kazi kubwa, asilimia 20 ambayo Mheshimiwa Waziri ameitaja katika majibu yake ya msingi haijawahi kupelekwa hata siku moja.
Je, kwa nini sasa Serikali isilete namna nzuri ya kuwalipa moja kwa moja hawa Wenyeviti kwa sababu, ni viongozi ili pasiwe na utaratibu huu wa asilimia ambayo haijawahi kupelekwa tangu wameanza kazi hizi mpaka sasa? (Makofi)
Swali la pili, kwenye swali langu la msingi nilieleza habari ya Madiwani. Madiwani kimsingi wanapata posho ndogo ya shilingi 300,000 na kitu kama sikosei. Je, ni lini sasa mnaongeza posho hizi ili walau basi wafanye kazi nzuri katika chini ya Halmashauri zetu huko Wilayani? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nafahamu concern ya Mheshimiwa Flatei, lakini jambo hili sio la Mheshimiwa Massay peke yake, naamini Wabunge wengi sana wanaguswa na jambo hili. Na ndio maana unaona Mheshimiwa Massay alivyosimama hapa watu wengi sana, kila mtu alismama kutaka kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndugu zangu naomba niseme ni kweli, kuna baadhi ya Halmashauri hizi posho hazirudi, lakini Halmashauri nyingine zinafanya vizuri katika urejeshaji wa posho hii ya asilimia 20. Ndiyo maana sasa tumesema katika mpango wetu wa kufanya marekebisho ya Sheria ya Fedha ya Serikali za Mitaa, Sura Namba 290, tumeweka kifungu maalum ambacho kinampa Waziri mwenye dhamana na jambo hilo kuweka suala zima la regulation maalum ya kulilazimisha suala hili sasa liwe suala la kisheria sio suala la kihiyari.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni kwamba utaratibu wetu katika jambo hili mimi ninaamini si muda mrefu sheria hiyo ya fedha itakuja hapa, tutaifanyia marekebisho, sasa itakuwa ni muarobaini na katika hili naomba niwasihi kwa hali ya sasa hasa Wakurugenzi wetu wote kwamba asilimia 20 kupeleka kila kijiji sio jambo la hiyari ni jambo la lazima sasa tulipeleke ili wananchi wetu kule chini waweze kufanya kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika ajenda ya posho ya Madiwani, ninakumbuka kwamba tulikuwa na Tume Maalum hapa ilikuwa maarufu kama Tume ya Lubeleje ambayo ilipitia maeneo mbalimbali na bahati nzuri Mheshimiwa Mzee Lubeleje amerudi tena Bungeni kama Senior MP, ilipendekeza mapendekezo mbalimbali, ndio maana tumesema kwa nyakati mbalimbali kwamba, Serikali inaangalia jambo hili na jinsi gani utaratibu wetu wa mapato utakuwa vizuri basi tutafanya marekebisho kwa kadri itakavyowezekana. (Makofi)
MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Na mimi niseme tu kwamba mimi ni miongoni mwa Wenyeviti wa Tanzania wa Serikali ya Mtaa wa Vodacom Kata ya Chanji kwa hiyo, ninaloliuliza ninalijua na changamoto zake.
Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ya Serikali inayotengwa watekelezaji wa kwanza ni Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji, kauli hii ya kwamba wataanza kulipwa posho sio mara ya kwanza ndani ya Bunge hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba time frame ni lini sheria italetwa hapa ili Wenyeviti waanze kulipwa posho kwa sababu sio hisani wanafanya kazi kubwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Dada yangu, Mheshimiwa Aida, Mbunge wa Viti Maalum, lakini Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji, kama walivyokuwa Wenyeviti wengine wa Jimbo la Ukonga kule nikifahamu hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama nilivyosema hapa kwamba kwanza kulikuwa na uzembe. Naomba niseme kwamba hata ile asilimia 20 kama kungekuwa na commitment ya kurudi vizuri katika Halmashauri zetu, maana sasa hivi tunapozungumza kuna Halmashauri nyingine zinafanya vizuri katika hilo. Tuna baadhi ya ushahidi kuna Halmashauri nyingine Wenyeviti wake wa vijiji wanalipwa vizuri kutokana na kwamba wameweka commitment ya asilimia 20 lazima irudi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la time frame ni kwa sababu ni suala la sheria ni suala la kimchakato na taratibu zote sheria hii imeshapitia hivi sasa inaenda nadhani katika Baraza la Mawaziri kupitia katika vifungu mbalimbali, ikishakamilika itakuja humu Bungeni. Sasa niwaombe Waheshimiwa Wabunge sheria ikija humu tunawaomba tushiriki wote kwa pamoja vizuri kwa sababu, ina vifungu vingi sana vinazungumzia suala la mapato katika Serikali za Mitaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni imani yangu kwamba tutajadili kwa kina tuje kuangalia jinsi gani tutafanya marekebisho mazuri ambayo yataenda kuwagusa Wenyeviti wetu wa Serikali za Vijiji kuweza kupata ile posho yao kwa kadiri inavyostahiki. (Makofi)
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nishukuru sana kwa majibu ya Serikali ambayo yana matumaini ya ujenzi ya Hospitali ya Wilaya.
Swali la kwanza, kwa kuwa Serikali iliahidi na mipango yake inachukua muda mrefu, je, Serikali ina mpango gani wakati inajipanga kuweza kukiboresha kituo cha afya cha Hamai ili kiweze kutoa huduma nzuri sambamba na kuchimba kisima ambacho ni tatizo kwenye eneo la kituo hicho cha afya?
Swali la pili, kwa kuwa matatizo ya Halmashauri ya Wilaya ya Chemba ni sawa na tatizo lililoko kwenye Wilaya ya Tanganyika na Naibu Waziri analifahamu hili. Serikali iliahidi kujenga kituo cha afya Majalila. Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga kituo hicho cha Majalila?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika Halmashauri ya Chemba tunao huu mpango wa kuhakikisha tunajenga Hospitali ya Wilaya. Kwa vile changamoto ya Jimbo la Chemba ni kubwa ndiyo maana Serikali katika mpango wake wa kuboresha vile vituo vya afya 100, kituo cha afya cha Hamai ni miongoni mwa vituo vya afya ambacho tunaenda kukiwekea ufanisi mkubwa wa ujenzi wa miundombinu ambapo imani yangu ni kwamba si muda mrefu mchakato huo utaanza.
Kwa hiyo, naomba nikuhakikishie kwamba kwa wananchi wa Chemba na hili tumeshaongea na Mheshimiwa Nkamia kwamba tutafanya kila liwezekanalo katika kipindi kifupi kijacho tutaenda kukiboresha kile kituo cha afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la Wilaya ya Tanganyika Mheshimiwa Mbunge unafahamu tulikuwa wote Tanganyika nilivyokuja Jimboni kwako. Tulitembelea Makao Makuu yako na Wilaya yako ya Tanganyika ambayo ni mpya, ndiyo maana tumepanga katika mpango wa kuboresha Wilaya hii katika eneo la Majalila kile kituo cha afya ambacho kinasuasua sana tutamekiingiza katika mpango wa vituo vya afya 100.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba nikuhakikishe kwamba wananchi wa Tanganyika wawe na imani kwamba Serikali inaenda kufanya investment kubwa eneo lile ili wananchi wa Tanganyika wapate huduma nzuri za afya.
MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, kwa kuniona.
Matatizo yanayowakabili wananchi wa Wilaya Chemba kwa kukosa huduma za Hospitali za Wilaya yanalingana kabisa na ya Wilaya ya Malinyi ambapo wananchi hawana Hospitali ya Wilaya. Halmashauri ya Malinyi imeweka utaratibu kuomba TAMISEMI kuifanya Hospitali ya Lugala ambayo inamilikiwa na taasisi ya kidini kuwa Hospitali ya Wilaya, lakini ombi hilo na utaratibu huu TAMISEMI wamesimamisha.
Je, Serikali ina utaratibu gani wa haraka wa kuwasaidia wananchi wa Wilaya ya Malinyi kupata hospitali ya Wilaya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ukiangalia Ulanga, Malinyi wana changamoto kubwa ya sekta ya afya. Katika mpango wa haraka Mheshimiwa Mponda, naomba nikuhakikishie kwamba kuna kituo cha afya cha Mtimila ambacho tumekiwekea kipaumbele tunakuja kukiwekea miundombinu muda si mrefu, kuanzia huu mwezi wa sita kwenda mwezi wa saba inawezekana mchakato huo utaanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwahakikishe wananchi wa Malinyi kwamba Serikali imewaona, tutaenda kufanya kazi kubwa pale ambayo mtakuja kuona ikifika mwezi wa nane hapo Mungu akijalia, inawezekana hali ikawa ni tofauti wananchi watakwenda kupata huduma nzuri sawa sawa na kituo cha afya cha Lupilo katika Jimbo la Ulanga (Makofi)
MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuwa hii hospitali ya Wilaya ya Kondoa inahudumia Halmashauri tatu; na kwa kuwa imepata ufinyu mdogo sana wa bajeti na kuleta changamoto katika madawa na vifaa tiba. Sasa Serikali inaona lini wakati inafikiria kuwapatia watu wa Chemba hospitali yao, hospitali hii ikaongezewa bajeti ili kuweza kuhudumia vyema Wilaya hizi tatu? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Kondoa changamoto ni kubwa na ndiyo maana ukiangalia kuna Majimbo matatu tofauti ambayo ni Chemba, Kondoa Vijijini na Kondoa Mjini lakini hospitali inayotumika sasa hivi ni Hospitali ile ya Kondoa na ukiangalia population mpaka watu wengine kutoka katika wilaya especially kama Wilaya ya Hanang’ walioko mpakani wengine wanakuja hapa Kondoa.
Kwa hiyo, jambo hili ni kubwa na tumeliona ndiyo maana katika mpango wetu wa bajeti wa mwaka huu sasa hasa ukiangalia basket fund tumebadilisha utaratibu wa basket fund tumeongeza bajeti katika eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu ni kuangalia ni jinsi gani tutafanya ili wananchi wapate huduma. Hata hivyo tumetoa maelekezo maeneo mbalimbali, kwa mfano tuna Halmashauri ya Kondoa Mji na Halmashauri ya Kondoa Vijijini lakini hospitali ni moja. Nimewahitaji Wakurugenzi wa maeneo yale waangalie katika suala zima la basket fund katika Halmashauri ambapo ile hospitali iko na jinsi gani kufanya kwa kuweka utaratibu wa kusaidia ile hospitali angalau kwa hali ya sasa iweze kufanya vizuri kwa sababu wananchi wote wanaohudumiwa ni watu kutoka maeneo hayo ambapo ni hospitali yetu lazima tutakuja kuweka nguvu wananchi wapate huduma nzuri. Kwa hiyo, nikushukuru sana Serikali inaifanyia kazi jambo hili.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nataka kuongeza kwenye swali la Mheshimiwa Sware.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kugawanya fedha kwa ajili ya dawa, vifaa na vifaa tiba tunazingatia vigezo vikuu vitatu. Kigezo cha kwanza ni idadi ya walengwa wanaopewa huduma katika hospitali hiyo (service population) ambapo inachukua asilimia 70, kigezo cha pili ni hali ya umaskini katika eneo husika ambacho kinabeba asilimia 15 na kigezo cha tatu ni hali ya vifo vya watoto chini ya miaka mitano. Kwa hiyo, nilikuwa namuomba Mheshimiwa Sware Halmashauri hizi tatu ambazo zinatumia Hospitali ya Wilaya ya Kondoa wakae pamoja watuletee mapendekezo yao Wizara ya Afya kwamba hospitali hii inahudumia Halmashauri tatu na sisi tutazingatia katika kuwaongezea bajeti ya dawa. Ninakushukuru sana. (Makofi)
MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, asante kwa kuwa swali la msingi linafanana kabisa na Wilaya mpya za Mkalama pamoja na Ikungi na wanatimiza vigezo vyote ambavyo Waziri amevitaja hapa.
Je, Serikali ni lini sasa italeta huduma za hospitali za Wilaya katika Wilaya hizo za Mkalama na Ikungi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mkalama ni Halmashauri mpya na imegawanyika kutoka Halmashauri ya Iramba, tunaenda kuhakikisha tunaboresha kile kituo cha afya cha Inimbila kwa sasa lengo kubwa ni kwamba kiweze kuwa na suala zima la upasuaji kuondoa haya mambo ya referral system, ambapo tunajua kwamba jambo hili tukilifanya litasaidia sana wananchi wa Jimbo la Mkalama kuweza kupata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, hali kadhalika katika kituo cha afya cha Ikungi tunaenda kuweka uboreshaji mkubwa wa miundombinu ya afya ambayo kwa wananchi wa eneo lile wataweza kupata huduma mzuri hivi sasa ambapo kama nilivyosema awali tumeingiza katika mpango ule wa vituo vya afya 100 ambao Serikali iko katika hatua za mwisho kwa sababu kila kitu kimeshakamilika, tegemeeni Waheshimwa Wabunge katika maeneo hayo Serikali imewasikia na itafanya mambo hayo kwa kadri iwezekanavyo. (Makofi)
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru. Mheshimiwa Naibu Waziri ulifika Babati ukaona hospitali yetu ya Mrara na tukakueleza kwamba tunapata wagonjwa kutoka Kondoa ambalo ndiyo swali la msingi siku ya leo. RCC tulishakaa kwamba hospitali yetu ipandishwe hadhi kutoka kituo cha afya kwenda hospitali ya Wilaya naomba nifahamu Mheshimiwa Naibu Waziri ni lini pendekezo letu hilo la RCC mtalifanyia kazi maana hospitali ya Mrara ina hali mbaya na wagonjwa ni wengi tunashindwa kuwahudumia?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nimefika na Mheshimiwa Mbunge tuliambatana pamoja siku ile tukitembea. Ni kweli wanachangamoto kubwa sana ni kwa vile utaratibu wa upandishaji wa vituo uko kwa mujibu wa sheria na utaratibu ambao ninyi mmeshakamilisha jambo hilo lote na hivi sasa liko Wizara ya Afya katika final stages, nadhani Wizara ya Afya itakapokamilisha hilo jambo mtapata mrejesho, kwa sababu dhamira ya Serikali ni kuwahudumia wananchi wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, kama mambo yote katika Mkoa yamekamilika naamini Wizara ya Afya ita- finalizes hilo jambo lengo kubwa ni kuwasaidia wananchi wa Babati waweze kupata huduma vizuri. (Makofi)
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa wapo watoto walemavu wa aina mbalimbali wanaokosa kupata elimu kutokana na uchache wa shule maalum kwa watoto hawa na hasa kwa Mkoa wa Tabora ambao una shule moja tu ya mission; kwa hiyo, watoto wengi wa Kaliua na maeneo mbalimbali wanakosa kupata elimu kutokana na kwamba kile kituo kina idadi maalum ya watoto walemavu.
Je, Serikali ina mpango gani maalum wa kuhakikisha kwamba kila mkoa, hasa Mkoa wa Tabora kunajengwa shule maalum ili watoto wenye ulemavu wa aina mbalimbali waweze kupata elimu sawa na watoto wengine? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli swali hili ni la msingi sana na Serikali tumeliona hili. Ndiyo maana katika Ofisi yetu ya Rais, TAMISEMI hivi sasa tuna Mkurugenzi maalum anayehusika na Dawati la Ulemavu. Lengo kubwa ni kuhakikisha tunafanya hilo vizuri. Hata hivyo, nataka nilijulishe Bunge lako hili Tukufu leo hii, Mheshimiwa Waziri Mkuu leo hii anapokea vifaa mbalimbali vikiwemo vya maabara, sambamba na vifaa vyote vya kielimu katika makundi ya walemavu. Tukio hilo linafanyika pale Lugalo na Shule moja ya Uhuru Mchanganyiko itaenda kupatiwa majira ya saa 7.00 mchana, kuona commitment ya Serikali katika hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, nini tunatakiwa kukifanya? Maana tutaelekeza katika Mikoa yetu. Lengo letu ni kwamba watu wenye ulemavu waweze kupata elimu kama watu wengine kwa kadri inavyokusudiwa. Kwa hiyo, ni commitment ya Serikali na hili tunaweza kulifanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namuomba dada yangu Mheshimiwa Magdalena Sakaya wala asiwe na shaka katika hilo, ni commitment ya Serikali kwamba sasa tunaenda kwa kasi katika suala zima la sekta hiyo hasa kwa watu wenye mahitaji maalum.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimshukuru Mheshimiwa Dada Magdalena Sakaya kwa swali lake zuri, lakini nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria Namba 9 ya mwaka 2010 ambayo ndiyo inatupa mwongozo wa namna nzuri ya kuwashirikisha wenzetu wenye ulemavu katika nchi yetu ya Tanzania ili waweze kupata haki zao zote, inatupa pia maelekezo kwamba msingi wa elimu tutakaouweka katika kuwahudumia wenzetu wenye ulemavu katika nchi yetu ya Tanzania kwa sasa tunaupeleka katika mtazamo wa ujumuisho. Shule zote zitakuwa inclusive. Hatutataka kuwa na shule ambazo zitawatenga wenye ulemavu wasome wao peke yao tu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, dhana hiyo tumeona kwamba haiwasaidii, inawafanya wajisikie ni watu wasiojiweza. Kwa hiyo, tunapotengeneza mfumo huu sasa wa elimu jumuishi kwa kuzingatia Sheria Namba 9 ya mwaka 2010, unawasaidia na wao kujiona wana uwezo, wanaweza kushindana na wanaweza wakafanya mambo kama wanavyofanya watu wengine ambao hawana ulemavu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kupitia Sheria hiyo Namba 9 ya mwaka 2010 tutajitahidi kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri kuboresha miundombinu, vifaa vyao kwa ajili ya kujifunzia kama vile programu nzito sana ya leo ya kukabidhiwa vifaa, inayofanywa na Mheshimiwa Waziri Mkuu kule Dar es Salaam.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunawaomba sana Waheshimiwa Wabunge tuwe pamoja kuhakikisha wenye ulemavu wanakuwa ni part ya maisha ya kawaida ya Watanzania wote.
MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na namshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Kwa kuwa Nyakanazi ni eneo lililokaa kimkakati kwa maana ni njia panda ya kuelekea Kigoma, Kahama na nchi za jirani za Rwanda na Burundi na kwa kuwa hivi karibuni kulingana na mipango ya Serikali iliyopo, kutakuwa na reli inatoka Isaka kwenda Rwanda.
Je, Naibu Waziri haoni kwamba sambamba na mchakato unaopaswa kufanywa na kijiji kupitia Halmashauri na Mkoa, Serikali Kuu nayo ina wajibu wa kuingia kwenye mchakato huo ili nguvu hizo zikutane kupaboresha zaidi kwa sababu panaendelea kuwa sehemu ya mkakati ikiwekwa reli?
Swali la pili, je, Mheshimiwa Naibu Waziri yupo tayari kuambatana nami atakapopata fursa ili twende kuona kwa pamoja na kufanya maandalizi ya kifikra kabla hata mchakato wa vikao haujaanza? Nakushukuru sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba niungane na Mheshimiwa Mbunge kwamba pale Nyakanazi ukiangalia kijiografia, ndiyo unapata njia ya kwenda Kakonko kule, lakini inaondoka Rwanda na huku tena inaenda Bukoba yaani ni junction pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, pale kweli ukuaji wake ni mkubwa sana, ndiyo maana hata mwaka huu katika usajili wa watoto peke yake, inaonekana darasa la kwanza tumesajili zaidi ya wanafunzi 1,000 na kitu katika shule ya Nyakanazi. Kwa hiyo, mahitaji ni makubwa, lakini baada ya kuongea na viongozi pale, kuna mpango mkakati kama alivyozungumza Mheshimiwa Mbunge siku nilivyofika pale, ni kwamba wanataka kuifanya kuwa hub fulani ya kibiashara kubwa sana kwa ajili ya kufanya mji ule kuwa chemchem.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, suala la kuungana na wananchi wa pale, kama Serikali Kuu tumesema kwamba kama hilo litafanyika vizuri na Waziri mwenye dhamana hapa kuhusu Maliasili na Utalii watakapoona jambo hilo na kuangalia assessment pale hali ikoje, nadhani Serikali itafanya maamuzi sahihi kutokana na taratibu zinavyokwenda. Kwa hiyo, hilo naomba Mheshimiwa Oscar aondoe hofu kuhusu ushiriki wa Serikali Kuu katika jambo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kuambatana, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tulikubaliana kuna mambo na changamoto mbalimbali kwamba mara baada ya Bunge la Bajeti tutapanga ratiba maalum kwa ajili ya kufika Biharamulo. Vilevile licha ya changamoto ya pale Nyakanazi, kuna mambo mengine ya msingi uliyazungumza katika siku za nyuma tutakuja kuyajadili pamoja katika Jimbo lako la Biharamulo Magharibi.
MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia wajawazito wanaofika kliniki na kugundulika kuwa wameathirika na maradhi haya ya UKIMWI, je, Serikali ina utaratibu gani wa kuwapatia dawa pamoja na lishe bora ili waweze kupata afya bora? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, dawa zote za kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI kwa makundi yote wakiwemo wa akina mama wajawazito zinatolewa bure kwa gharama za Serikali. Dawa za kuongeza virutubisho mwilini wakati mwingine zinaweza zikawa hazipatikani lakini zikipatikana pia kwa akina mama wajawazito zinakuwa ni bure.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuwapa lishe, hatujaanza utaratibu wa kutoa lishe kwa kundi hili la akina mama wajawazito wala kwa kundi lolote lile kwa sababu tunaamini hilo ni jukumu la kawaida tu la kila siku la kifamilia. Kuna miradi kutoka katika NGOs mbalimbali ambazo zinafanya kazi kwa ukaribu na Wizara yetu, wanafanya hivyo kwa baadhi ya maeneo nchini lakini sisi kama Serikali hatujaanza kutekeleza mpango wa kutoa chakula kwa akina mama wajawazito ambao wana maambukizi ya virusi vya UKIMWI.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la Mheshimiwa Kadutu la Ulyankulu linafanana kabisa na Tarafa ya Mima ambayo imeshatangazwa kwamba imeanzishwa kuwa Tarafa ya Mima, lakini mpaka sasa hakuna majengo, hakuna watumishi. Naomba Mheshimiwa Naibu Waziri, ni lini mtajenga majengo, mtaleta watumishi ili kweli ile Tarafa ya Mima ianze kufanya kazi mara moja maana sasa inatamkwa tu Tarafa ya Mima?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Kata za Matomondo pamoja na Mlembule ni kata kubwa sana na zina vigezo vyote kuwa tarafa, je, Mheshimiwa Naibu Waziri, unasemaje kuhusu hili? Ni lini mtaanzisha Tarafa hizi Kata mbili, Mlembule na Matomonda?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Senior MP Mheshimiwa Lubeleje ambaye mimi namuita grader la zamani makali yale yale kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika Tarafa ya Mima ambayo kwa mujibu wa utaratibu Mheshimiwa amesema kwamba imeshaanzishwa lakini majengo ni bado. Basi mimi naomba nielekeze katika Halmashauri husika kwa sababu nadhani wakati tunafanya mchakato wa kuanzisha tarafa hizi ni lazima tutakuwa tumejipanga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge nafahamu kwamba unafanya juhudi kubwa, lakini niwasihi wenzetu kule, kwa sasa hivi iangalie namna ya kufanya katika mipango ile ikiwezekana ya Kihalmashauri na Kiwilaya. Katika maana hiyo tuanze michakato ya kuanzisha majengo kwa kuangalia suala zima la ki-bajeti. Jambo hili linaanzia kule kule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo wakati wa mchakato wa bajeti na sisi tutaunga mkono suala la watumishi; ambayo ndiyo mamlaka yetu kupeleka watumishi kama Serikali. Nikuhakikishie Mheshimiwa Lubeleje kwamba jambo hili tutalifanya kwa kadiri taratibu za Serikali zinavyokwenda sasa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuanzishwa tarafa mpya katika Kata ya Matomondo na. Najua kwamba michakato hii iko vile vile kwa mujibu wa Sheria za uanzishwaji wake. Kwa sababu hiyo basi nishauri Baraza la Madiwani kwamba jambo hili likionekana linakidhi sasa katika Halmashauri yetu ya Mpwapwa basi liweze kufanyika katika ile michakato ya kimsingi ambayo inaanzia katika vijiji inakuja katika vikao vya Ward C, na Halmashauri ya Wilaya then DCC ya wilaya na Mkoa, baadaye inakuja Ofisi ya Rais (TAMISEMI) kwa maamuzi zaidi.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Lubeleje naomba nikuhakikishie kwamba mkianza mchakato huo Ofisi ya Rais TAMISEMI itasikiliza kilio chenu na kuweza kukifanyia kazi kwa kadri inavyoona inafaa.
MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mchakato wa uanzishwaji wilaya ni wa muda mrefu na hili swali sasa ni la mara nyingi tunauliza; kwa kuwa Ulyankulu ilikuwa na makazi ya wakimbizi, na ambao wapo mpaka sasa, na kwamba vile vile wapo wakimbizi ambao wamepewa uraia na kusababisha kuongezeka kwa idadi ya watu na kuwa na watu wengi.
Je, Serikali haioni hilo? je, ni lini sasa inaweza ikaamua kwa maksudi kuhakikisha kwamba wilaya ile sasa inakuwepo baada ya kukamilisha vigezo vyote tulivyovileta. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema pale awali, mapendekezo ya kwanza yalivyokuja ikaonekana kuna mapungufu ya idadi ya watu, hii ndiyo iliyokuwa miongoni mwa vigezo ambavyo vilifanya isi-qualify kipindi kile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge amekiri hapa kwamba kuna baadhi ya makazi ya wakimbizi, nadhani takriban kata tatu, zimesababisha kuwepo kwa sasa idadi kubwa sana ya watu katika maeneo hayo ambayo sasa wamesajiliwa kuwa kama raia wa Tanzania. Hata hivyo utaratibu ni ule ule kwa sababu lile jambo la mwanzo lilidondoka haliku--qualify. Kwamba kama tunaona idadi sasa hivi inatosha twende na michakato ile ile kama nilivyosema awali, kwamba ipitishwe katika vikao vya kisheria ambavyo katika Ward C, DCC pamoja na RCC.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vikifika kwetu sisi, tutawatuma wataalam kuja kufanya verification, iki-qualify biashara imekwisha. Kwa hiyo mama Mwanne Mchemba naomba nikutoe shaka katika hilo, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) itasikiliza jambo hili na kwa kupitia document zote zilizotumwa kutoka kwenu tutalifanyia kazi jambo hili. (Makofi)
MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo yaliyopo huko Wilaya ya Ulyankulu yanafanana kabisa na matatizo yaliyoko katika Jimbo langu la Manyoni Magharibi. Jimbo la Manyoni Magharibi ni Tarafa ya Itigi ambayo ina upana mkubwa, eneo moja mpaka eneo lingine ni kilometa 219, ni jimbo kubwa kuliko majimbo mengi. Tumeshapeleka na kupitia taratibu zote hadi RCC kuiombea Itigi kuwa Wilaya lakini hadi leo Serikali imekuwa kimya. Je, Serikali inasema nini kuhusu jambo hili la Wilaya ya Itigi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli. Kwanza awali hata hili eneo la Itigi tulikuwa hatujapata Halmashauri kamili na ndiyo maana mchakato wa kwanza ulikuwa ni kupata Halmashauri. Suala hili najua Mheshimiwa Massare umelizungumza mara nyingi tangu uchaguliwe kuwa Mbunge. Naomba nikuhakikishie kwamba tutafanya verification katika ofisi yetu kuona hizi document ziko katika process gani. Kama hali haijawa sawa sawa tutatoa maelekezo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni kwamba ikamilishe zile taratibu ningine zote ambazo zitakuwa zimepungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nakumbuka kwamba Mheshimiwa Mbunge tulifika pale Itigi na kweli ukiangalia jiografia hata aliyekuwa Mkuu wa Wilaya wa kule ambaye sasa hivi ndiye Mkurugenzi wetu Mkuu wa TIC alikuwa anapata changamoto kubwa sana kui-manage ile Wilaya ya Manyoni. Kwa hiyo, Mheshimiwa Massare naomba nikuhakikishie kwamba mambo haya yote yakikamilika, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) itakapojiridhisha, haitasita kufanya maamuzi kwa maslahi mapana ya eneo lako husika.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa nia kubwa ya kugawa maeneo ni kusogeza huduma kwa wananchi na kwa kuwa Mheshimiwa Waziri baada ya sisi wananchi wa Kilolo kupige kelele kutokana na ukubwa wa Wilaya yetu, uliridhia na kutupa Halmashauri ya Mji Mdogo sasa ni muda mrefu na ulifika na kuona kwamba sasa tunastahili kupata Halmashauri kamili. Je, ni lini sasa Mheshimiwa? Hebu tupe jibu ili wananchi wakusikie.
NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli. Mwaka jana tulikwenda na Mbunge tukafika mpaka jimbo lake, tukatembea. Kijiografia jimbo lile ni kubwa sana, linapakana na ndugu yangu Profesa Jay, linapakana na Waziri wangu Simbachawene huku Kibwakwe, ni jimbo ambalo liko tata kweli kweli. Hata hivyo tulivyofika pale Ilula tumekutana na wananchi wa Ilula ambao mapendekezo yao yametufikia, na bahati nzuri baada ya ile ziara nikatuma timu kwenda kufanya verification.
Mheshimiwa Mwenyekiti, verification imeshafanyika na hivi sasa tuko katika mchakato wa kufanya maamuzi ambapo kwa jambo hili mwenye kufanya maamuzi ni Mheshimiwa Rais mwenyewe mwenye dhamana katika eneo hilo, atakaporidhia basi Mheshimiwa Mwamoto naomba usiwe na hofu, ni kweli Serikali imefanya process zote na sasa tuko katika final stage katika kufanya maamuzi. (Makofi)
MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Wilaya ya Arumeru ina Halmashauri mbili kwa maana kwamba Halmashauri ya Meru na Arusha DC. Wilaya hii eneo lake ni kubwa kiasi kwamba hata wakati mwingine huduma kuzifikia jamii inakuwa ni vigumu. Je, ni lini sasa Serikali (kwa sababu tayari ilikwishaanza mchakato siku za nyuma) itaendelea na mchakato huo kuhakikisha kwamba inagawanya wilaya hii inakuwa wilaya mbili ili huduma za kijamii ziweze kuwafikia wananchi kwa haraka? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la dada yangu Amina Mollel Mbunge ambaye anawakilisha hasa kundi la walemavu kwa umakini zaidi humu Bungeni kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Wilaya ya Meru ni kubwa sana, ina Arusha DC na Meru. Ukiangalia, bahati mbaya Halmashauri ile iko kama mbalamwezi fulani hivi, kwamba Jiji la Arusha liko katikati halafu ile wilaya imezunguka hivi. Kwa hiyo hata management yake inakuwa ni ngumu zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili kama nilivyosema katika maeneo mbalimbali, kwanza naamini michakato mbalimbali imeanza huko lakini wakati mwingine inawezekana taarifa zikawa zimekuja lakini vigezo havikukidhi. Kwa hiyo, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge Amina Mollel kwamba tutakapopata taarifa za vikao vya RCC kutoka Mkoa wa Arusha na Mkuu wetu wa Arusha akishajipima kule akiona kwamba jambo hilo limeridhia, na likishafika kwetu na sisi tutalifanyia kazi kufanya taratibu zote za kisheria zinazohitajika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ikionekana kwamba inafaa sasa kuigawanya zile wilaya mbili, Serikali itaona jinsi gani ya kufanya katika hilo. Kwa hiyo naomba nikuhakikishie, ni kwamba utaratibu ni ule ule wa kisheria tu, kama unavyosema ugawanyaji wote wa maeneo unasemaje. Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana wa eneo hilo akiridhia, basi mchakato utakamilika hatimaye mtapata wilaya mpya.
MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, amekiri wazi kwamba Serikali ina mpango wa kuanzisha shule ya kidato cha tano na cha sita katika maeneo ya Mkula tofauti na maeneo yanayotumika kwenye majengo yaliyoachwa na Kampuni ya Group Sogesca.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza; itambulike kuwa shule hii ambayo ameizungumzia kwamba ni ya kutwa iko kwenye mgogoro baina ya wananchi pamoja na Kampuni ya SK iliyoko mjini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro huu Mheshimiwa Waziri Mkuu anaujua. Alipokuja kwenye ziara tarehe 2 mwezi wa tatu mwaka wa jana aliukuta mgogoro huu wa wananchi, kwamba shule hii iko kwenye majengo ambayo yana mgogoro. Nataka kusikia kauli ya Serikali, Waziri Mkuu aliagiza kuwa majengo yale yarudi kwenye mikono ya wananchi ili shule ile iweze kuendelea vizuri. Sasa nataka kuuliza, nini kauli ya Serikali kuhusu shuke iliyoko kwenye majengo yenye mgogoro?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa kipaumbele cha Serikali ni masomo ya sanyansi. Mkoa wa Simiyu walimu wa masomo ya sayansi ni changamoto kubwa sana hususan shule iliyoko Wilayani Itirima, shule ya Mwarushu ina mwalimu mmoja tu wa masomo ya sayansi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kusikia sauti ya Serikali ni nini mkakati wa Serikali kupeleka walimu wa sayansi katika maeneo hayo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Dada yangu Gimbi Dotto, kumbe alikuwa anataka aniingize katika choo kisichokuwa na jinsia maalum, kwamba shule kumbe ina mgogoro halafu tuanzishe kidato cha tano na cha sita. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna mgogoro lakini nadhani Naibu Waziri wa Ardhi atazungumzia hasa katika suala hili la mgogoro jinsi gani Serikali imejipanga mara baada ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kutoa maagizo; Serikali inayafanyia kazi hayo yote kwa pamoja na nikuhakikishie Mheshimiwa Gimbi kwa sababu najua wewe ni mpiganaji mpaka umeniletea walimu ambao walikuwa na matatizo katika eneo lako kule. Siku zote unaniletea taarifa ofisini kwangu pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba tutashughulikia matatizo katika Mkoa huu wa Simiyu kwa kadri iwezekanavyo ili mambo ya elimu yaende vizuri. Kuhusu shule ambayo haina walimu wa sayansi, naomba tuseme kwamba katikati tulipeleka walimu wa sayansi lakini si kwamba tumeziba gap zote za walimu wa sayansi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa tunaendelea kupeleka walimu wa sayansi. Tutaichukulia hii shule ambayo unaisemea kuwa ni kipaumbele, tutafanya kila liwezekanalo ili kuhakikisha kwamba tunapeleka walimu wa sayansi wa kutosha. Lengo la Serikali ni kuhakikisha kwamba watoto wanapata elimu vizuri. Kwa hiyo naomba uendelee na hizo juhudi zako nzuri za kuwawakilisha vizuri wananchi wako wa kule.

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa ya kujibu swali dogo la nyongeza ambalo limeulizwa. Ninamshukuru pia Mheshimiwa Naibu Waziri ambaye amejibu swali lake vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nimfahamishe Mbunge pengine wakati mwingine ni muhimu pale ambapo Serikali inachukua hatua tuwe tunaweza kuweka kumbukumbu zetu vizuri. Mgogoro huu anaouzungumzia tayari Serikali ilishaumaliza, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mheshimiwa Lukuvi alishakwenda kule na yule Bwana alinyang’anywa title yake na Mheshimiwa Rais alishaifuta, kwa hiyo hakuna mgogoro pale na SK Investment si mmiliki tena wa eneo lile kwa sababu Serikali imeshafuta umiliki wake na ilitangazwa kwenye vyombo vya habari, naomba tuwe tunafuatilia vizuri ili tusiwe tunachanganya haya mambo. (Makofi)
MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino ilianzishwa zaidi ya miaka Kumi iliyopita na Halmashauri hii Makao yake Makuu yako karibu sana na Chamwino Ikulu. Kwa hiyo, nilitegemea Serikali ingeliangalia hili suala kwa jicho la kipekee kabisa. Idara za Halmashauri hii zimetawanyika, ukitoka Ofisi ya Mkurugenzi hadi Ofisi ya Ardhi ni kilometa tano.

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukitoka Ofisi ya Mkurugenzi hadi Idara nyingine ambazo nyingine ziko kwenye shule za msingi, nyingine ziko kwenye nyumba za watu binafsi kwa hiyo, ufanyaji kazi na huduma kwa wananchi uko katika hali ngumu kabisa kutokana na jengo lile kutokamilika. Halmashauri waliwafuata TBA wakafanya tathmini wakaona kwamba, zinahitajika shilingi…

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, sawa shilingi bilioni 2.3 na Serikali imetenga shilingi milioni 600 tu kukamilisha lile jengo.
Je, ni lini sasa Serikali itatoa fedha za kutosha kwa ajili ya lile jengo la Halmashauri na likamilike kwa wakati, japo floor ya chini, ili watumishi wahamie wakafanye kazi pale?
Swali la pili, Halmashauri ya Chemba iliomba shilingi milioni 950 kwa mwaka huu wa fedha na wamepata shilingi milioni 450 tu. Je, shilingi milioni 500 zilizobaki watapata lini ili waendelee na ujenzi wa jengo la Halmashauri?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, watumishi wa Halmashauri ya Chamwino wanapata shida kubwa sana na hili tunalijua wazi. Ninajua kwamba mkataba wa kwanza wa mkandarasi wa kwanza umevunjwa lakini commitment ya Serikali iko pale pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema awali mpaka hivi asubuhi na-cross check pale tumeshapeleka shilingi milioni 750 hivi sasa. Kama ulivyosema tathmini iliyofanywa na TBA imeonekana kumaliza lile eneo la ground floor peke yake karibu ni shilingi bilioni mbili. Hata hivyo, nimeongea nimeongea na Kaimu Mkurugenzi pamoja na Engineer leo wafike ofisini kwangu kuangalia way forward tunafanyaje kwa sababu tathmini iliyofanywa gharama yake ni kubwa, lakini Engineer na timu yake wanasema kwa kutumia wao utaalamu wao pale ile shilingi milioni 750 wataweza kumaliza ile ground floor na hivi sasa tunajielekeza kuangalia jinsi gani fedha zitumike vizuri.
Kwa hiyo, nimemuagiza Kaimu Mkurugenzi na Engineer leo hii wanakuja kukutana na wataalam katika ofisi yetu tuangalie tufanye nini ili tumalize ile ground floor.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la ujenzi pale Chemba, ni kweli tumepeleka shilingi milioni 500 mpaka hivi sasa, tunachotaka kufanya ni kuhakikisha kwamba, fedha tunazipeleka maeneo haya na maeneo mengine tofauti, lengo kubwa ofisi hizi ziweze kukamilika na watumishi wetu wapate maeneo mazuri ya kufanya kazi. (Makofi)

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lililopo Chamwino ndiyo tatizo lililopo Manispaa ya Tabora. Ofisi mpya ya Halmashauri imekwama kwa muda mrefu sasa kukamilika kwa sababu ya ukosefu wa fedha. Kwa kuwa ombi maalum kupitia Hazina Serikali iliahidi kutoa shilingi bilioni mbili ili kuweza kukamilisha ujenzi huo pamoja na kumlipa mkandarasi anayedai karibu shilingi bilioni moja Masasi Construction.
Je, Serikali ni lini italeta pesa hiyo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Tabora ili jengo hili liweze kukamilika? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli lilikuwa ombi maalum, lakini tutaenda kulifanyia kazi. Siwezi kutoa commitment hapa lakini tutaenda kulifanyia kazi tuangalie kwamba lile ombi la awali limefikia wapi halafu tutapeana mrejesho nzuri na Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu najua ni kweli Manispaa ya Tabora wanapata shida.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tutakwenda kuangalia jinsi gani tutafanya.
MHE. MUSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la Halmashauri ya Chamwino linafafana na tatizo la Halmashauri ya Tabora Uyui. Tuna zaidi ya miaka kumi tumeamia Isikizya, lakini jengo la Halmashauri yetu lina zaidi ya miaka mitano halijakamilika kutokana na kutoletewa pesa.
Je, ni lini Serikali itatusaidia ili kumalizia ujenzi wa jengo hilo. Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema mwanzo ni kwamba maombi haya ya Halmashauri yako katika maeneo mbalimbali na ni kweli Mheshimiwa Mbunge nimefika kwako Uyui tulikuwa pamoja siku ile, kikubwa zaidi tutaangalia kipindi hiki kutokana na bajeti zilizotengwa katika mahali ambapo pesa ambazo hazijapelekwa basi tutafanya harakati ziwezekanazo mradi tuweze kupeleka fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niweze kusema kwamba commitment ya Serikali ni kuhakikisha kwamba kama tulivyofanya mwaka huu hivi sasa tumepeleka takriban bilioni 30 kwa Halmashauri mpya na Halmshauri mbalimbali kwa hiyo tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo kuwezesha mpango huu wa Serikali ambao tumeupanga katika bajeti zetu. (Makofi)
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niipongeze Serikali kwa kutenga hiyo milioni 250 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya. Kutenga fedha ni jambo moja na kulipeleka ni jambo lingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ikumbukwe kwamba mwaka wetu wa bajeti unaanza mwezi Julai, unaisha mwezi Juni, kuchelewa kuipeleka hiyo pesa kwa namna yoyote ile kutaathiri ujenzi wa hilo jengo hasa ikizingatiwa gharama zinaweza zikabadilika.
Je, Serikali inawahakikishia vipi wananchi wa Mbinga kwamba pesa hii itakwenda kwa wakati na ndani ya mwaka wa bajeti wa 2017/2018 jengo likatakamilika? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge mwenyewe na wananchi wa Mbinga, kwa sababu Mbunge unakumbuka ulikuja mpaka ofisini kwangu kwa shida kubwa sana za Jimbo lako na eneo lako. Mwaka huu umepambana mpaka umepata shilingi milioni 250 ambayo kutokana na maombi yako tumeiweka katika bajeti ya mwaka huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni commitment ya Serikali, kwamba tutakapofika mwezi wa Saba mpaka kipindi ambacho tutakachoenda nacho hicho sasa nikuhakikishe kwamba Serikali itajitahidi kwa kadri iwezekanavyo In Shaa Allah, tutajitahidi fedha zitaenda na nikuombe kwamba usimamizi uwe karibu kama ulivyokuwa makini jengo hilo liweze kukamilika kwa ajili ya wananchi wa Mbinga.
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Mheshimiwa Mwwenyekiti, Serikali inapochelewesha kupeleka fedha ambazo ziko kwenye bajeti kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi mbalimbali za Serikali kama Ofisi za Wakuu wa Wilaya na za Halmashauri inasababisha variation katika ujenzi wa ofisi hizi na kwa sababu hiyo Serikali inaingia katika matumizi makubwa zaidi katika kumalizia.
Je, kwa nini Serikali isitoe kwa mkupuo fedha hizo ofisi hizo zikamalizika zote kwa pamoja ili Halmashauri pamoja Wilaya hizo zikawa na ofisi na Serikali ikaokoa kiasi kikubwa cha fedha kwa njia ya variation?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo la Mheshimiwa Selasini ni wazo zuri na ndiyo maana nimesema mwaka huu tumetoa karibu shilingi bilioni 30 kwa ajili ya ujenzi huo, lakini unaangalia jinsi gani kila sehemu ina eneo lake la kimkataba la ujenzi. Ndiyo maana hapa tukusema kila Mbunge ataanza kupinga kelele.
Kwa hiyo, ni wazo zuri tutaenda kulifanyia kazi lengo kubwa ni kwamba tumalize haya matatizo yote ya ofisi wananchi na wataalam wetu waweze kupata huduma kwa hiyo ni wazo zuri na Serikali tunaendelea kupeleka fedha kwa kadri tunavyokusanya na mimi naamini kwamba utafika muda ofisi nyingi zitakamilika na Watendaji wetu watakuwa katika mazingira mazuri ya kufanya kazi.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kaliua haina Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Wilaya anatumia Ofisi ya Tarafa ambayo ina hali mbaya na ni chumba kimoja kidogo wanajibana pale. Ofisi ya Wilaya imeanza kujengwa tangu mwaka 2012 na imesimama mwaka 2014 mpaka leo haijaendelezwa. Naomba kujua Serikali ina mpango gani wa kutoa fedha ya kutosha ili Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ikamilike na Mkuu wa Wilaya aweze kufanya kazi kwa ufanisi zaidi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, alichosema Mheshimiwa Sakaya ni kweli na ndiyo maana nimesema kwamba sasa hivi tunajitahidi kupeleka fedha na hata katika Halmashauri yake anafahamu tumeshapeleka milioni 700 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Halmashauri Kaliua. Hiyo ni commitment ya Serikali kwa Kaliua. Angalia kipindi hiki cha muda mfupi tumepeleka shilingi milioni 700 lakini najua Ofisi ya DC bado haijakamilika. Hii tunalichukua kuangalia jinsi gani tumefanya allocation ya funds niangalie kama Kaliua katika suala la jengo la Mkuu wa Wilaya hali ikoje halafu tutasukuma ili jengo liweze kukamilika. Ofisi hizi zilisimama muda mrefu na sasa hivi nimetoa commitment kubwa ya Serikali kupeleka kwa ajili ya umaziaji wa majengo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo usiwe na mashaka Dadangu tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo.
MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kuuliza swali ndogo tu la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jengo la Mkuu wa Wilaya ya Maswa limeshajengwa lakini limebakia umaliziaji. Mheshimiwa Naibu Waziri alishafika hapo na kuliona sasa anaweza kutuhakikishiaje kwamba mwaka unaoanza wa fedha, fedha kidogo kwa ajili ya umaliziaji zimetengwa ili Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Maswa aweze kuhamia kwenye jengo hilo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge mwaka huu wa fedha unaokuja tutamaliza lile jengo la Mkuu wa Wilaya, tuna kila sababu kuhakikisha Wakuu wa Wilaya wetu majengo yao yote yanakamilika na tumejipanga katika hilo, Mheshimiwa Ndaki wala usihofu tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo ile kazi kubwa iliyobakia pale tuweze kuiimaliza ili Mkuu wetu wa Wilaya afanye kazi katika mazingira rafiki. (Makofi)
MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa shule nyingi zimekuwa na matatizo ya kutokuwa na Walimu hasa shule zile za A-level zenye michepuo ya sayansi. Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha kwamba shule hizi ambazo zina michepuo ya sayansi zinakuwa na Walimu wa kutosha ili wanafunzi hawa waweze kusoma vizuri na kuweza kumudu masomo yao vizuri.
Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa kuwa imekuwa ni kawaida kwa shule za Serikali kuongeza tahasusi kwenye shule hizi za A-level ambavyo huenda sambamba na ongezeko la wanafunzi. Katika shule hizi za A-level utakuta wanafunzi ni wengi na miundombinu haitoshi ukilinganisha na idadi ya wanafunzi. Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha kwamba ongezeko la wanafunzi linaenda sambamba na ongezeko la miundombinu kwa maana ya madarasa, mabweni na miundombinu mingine? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli tumekuwa na changamoto ya Walimu hasa wa sayansi katika shule zetu na ndiyo maana hapa katikati tuliomba kibali kutoka Ofisi ya Rais, Utumishi na tulipata kibali cha kuajiri Walimu na Walimu wale sasa hivi tumewaajiri kuwapeleka sehemu mbalimbali. Hata hivyo, bado hatujaweza ku-fill hiyo gaps yote iliyonanii na hii ni kutokana na jinsi hali ilivyo huko katika soko.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, tutaendelea kufanya kila liwezekanalo, hivi sasa tuko katika mchakato kwa lengo kwamba tukipata wale Walimu wengine ambao maombi yao yalikuwa hayajakamilika vizuri, tuweze kuongeza kupeleka katika shule zetu ili tupate Walimu wa sayansi kwa ajili ya kufundisha vijana wetu wanaojiunga na kidato cha tano na cha sita.
Mheshimiwa Spika, katika eneo la pili kuhusu suala zima la miundombinu, ni kweli tumeliona hilo ndiyo maana ukiangalia hivi sasa hata wanafunzi waliofaulu na kukidhi vigezo hatukuweza kuwachagua wote kutokana na suala la miundombinu, wengine tutawachagua katika second selection.
Mheshimiwa Spika, Serikali sasa hivi imeweza kufanya harakati na kupata takribani shilingi bilioni 21 ili kuweka miundombinu katika shule zipatazo 85, ambazo tunajua tukifanya hivi itasaidia sana kuhakikisha vijana wetu watafika shuleni na kusoma katika mazingira salama na mwisho wa siku waweze kupata elimu bora kama Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inavyokusudia.
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri kuna maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa kama tunavyofahamu Jiji la Dar es Salaam linazidi kupanuka na maeneo ya pembezoni zipo sekondari nyingi ambazo mwisho wake ni kidato cha nne; na kwa kuwa katika Jimbo la Segerea hasa katika eneo la Kinyerezi na Kipawa, bado hakuna Sekondari za kidato cha tano na sita. Je, Serikali haioni kwamba ni wakati sahihi sasa wakupeleka hizi shule za kidato cha tano na sita katika maeneo ya pembezoni?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa swali hili linafanana kabisa na kule Lushoto, hasa Jimbo la Mlalo. Tunazo Tarafa tano katika Halmashauri yetu ya Lushoto, lakini ni Tarafa nne pekee ndio zenye sekondari ya kidato cha tano. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka Tarafa ya Umba na Mlola nazo zipate sekondari za kidato cha tano? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge kwamba Jiji la Dar es Salaam linapanuka, na shule nyingi nyingine zimejengwa pembeni mwa Jiji la Dar es Salaam especial maeneo ya kule Mbondole, Zingiziwa na maeneo mengine. Kwa hiyo nimesema kama ni ile mikakati wa Kiserikali, kwa sababu Halmashauri wenyewe wana mkakati wa kujenga takribani shule sita mpya za sekondari. Sisi Serikali katika hilo tutawaunga mkono shule hizi, na mara baada ya kukamilishwa kwake tutaweza kuzisajili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo kubwa vijana wetu ambao wanapata nafasi baada ya kumaliza kidato cha nne waweze kupata nafasi ya kidato cha tano na sita. Kuhusu suala la shule za kule Mlalo, Mheshimiwa Shangazi kama mtakuwa mmeianzisha hii mipango kule Mlalo katika Halmashauri yenu ya Lushoto, naomba nikuhakikishie kwamba Serikali haitosita kushirikiana nanyi. Kwa sababu hata nilipokuwa ziarani kule mlinipeleka shule moja ya sekondari ambayo mmeniambia kwamba watoto wanafaulu kwa kiwango kikubwa sana. Kwa hiyo Serikali itaungana na ninyi, lakini ni mara tu baada ya kuanza michakato hii mliyoianza ya ujenzi wa sekondari za kidato cha tano na sita. Serikali tutaungana na hilo ili kuwafanikisha wananchi wa Mlalo na Wilaya ya Lushoto kwa ujumla ili waweze kupata fursa hii ya elimu ya kidato cha tano na cha sita. (Makofi)
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, kwa kuwa Serikali inakiri kwamba kuna baadhi ya Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa wamekuwa wakiitumia sheria hii vibaya.
Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuleta mabadiliko ya Sheria hii hapa Bungeni?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuna baadhi ya Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa wamewasimamisha baadhi ya Wenyeviti wa Vijiji na Mitaa ambao wamechaguliwa kihalali kwa muda mrefu na kukaimisha nafasi hizo kwa watu wengine, jambo ambalo linakwenda kinyume kabisa na sheria, kanuni na taratibu bora za uendeshaji wa Serikali za Mitaa. Je, Serikali inatoa kauli gani dhidi ya jambo hili? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema awali, hivi sasa sheria hii inajitosheleza. Changamoto kubwa ni matumizi ya ile sheria. Ndiyo maana tumesema kwamba ofisi yetu na kupitia Waziri wangu hapa, aliitisha kikao maalum cha kupeana maelekezo ya jinsi ya kutekeleza vizuri sheria hii. Lengo kubwa ni kwamba makusudio ya sheria hii yaweze kufikiwa kama vilivyo.
Kwa hiyo ukiangalia, muktadha wa sheria yenyewe haina matatizo isipokuwa katika implementation ya sheria. Ndiyo maana tumesema kwamba maelekezo maalum yametolewa na sasa hivi hatutarajii kwamba kama kutakuwa na mapungufu yoyote mara baada ya maelekezo hayo ambapo ofisi yetu imefanya kazi kubwa sana katika eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la Wenyeviti wa Vijiji kusimamishwa na baadhi ya Wakuu wa Wilaya, naomba ikiwezekana tupate taarifa ya eneo specific, liko wapi, halafu tuangalie kesi gani ambayo imejitokeza katika eneo husika tuweze kuangalia tatizo gani limesababisha kusimamishwa. Hata hivyo tuna imani kwamba Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya jukumu lao kubwa ni kuhakikisha kwamba utaratibu wote unasimamiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na wakati mwingine inawezekana baadhi ya vijiji kuna baadhi ya Wenyeviti wa Vijiji huenda wameuza ardhi ya kijiji au kufanya jambo lingine ambalo lilikuwa tofauti na utaratibu, ndiyo maana utakuta Mkuu wa Wilaya au Mkuu wa Mkoa anafanya taratibu za kisheria. Lakini kama kuna jambo ambalo limekiukwa basi naomba ofisi yetu tupate taarifa hizo tuweze kulifanyia kazi kwa misingi ya kisheria.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Sheria hii ya Mikoa inatoa mamlaka kwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kuweza kumkamata mtu katika mazingira ambayo wanaamini kwamba mtu huyo ama anatenda kosa la jinai, ama kwa ufahamu wao ametenda kosa la jina, ama anafanya kitendo chochote kinachovunja amani na utulivu, ama anaona mtu huyu anatarajia kutenda au kuhatarisha amani, hivyo ndio tafsiri ya sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jukumu hili wamepewa hawa kwa sababu ya ku-maintain law and order. Utaiona leo hii inapokuwa ipo kinyume na wewe kama mbaya, lakini ikiwa inakusaidi katika wakati ambapo amani yako, haki yako au jinai dhidi yako inataka kutokea, mkuu huyu anapochukua zile hatua ndipo utakapoona msingi wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa ni wenyeviti wa Kamati za Ulinzi na Usalama, mamlaka haya yanatokana na nguvu kubwa waliyonayo katika msingi wa Katiba. Halikadhalika, mtu yoyote anayo haki ya kuomba mtu mwingine ambae anaweza kutenda kosa la jinai dhidi ya mtu fulani au ya watu fulani kuomba wakamatwe.
Kwa hiyo haki hii sio tu wamepewa hawa peke yao, ukisoma vizuri sheria nyingine tulizonazo pia zinakupa wewe nguvu ya kusema wewe hapana, Simbachawene mimi naona huyu anatarajia au anahatarisha amani au anataka kutenda kosa, akakamatwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, isipokuwa cha msingi ni pale tu ambapo inapaswa kutumika kwa kuzingatia sheria. Mtu huyo awe ana mtarajio ya kupelekwa mahakamani immediately baada ya kukamatwa na baada ya muda ule kupita. Isikamatwe kwa ajili ya show off tu, asikamatwe mtu kwa ajili ya ku-show, asikamatwe kwa ajili tu ya kuonesha kwamba wewe una madaraka. Lazima akamatwe mtu huyo kama kweli kitendo chake kinahatarisha amani na utulivu. Hapa ndipo ninapotaka nisisitize kwamba Wakuu wetu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kwa kutumia sheria hii, wawe makini na kuhakikisha kwamba wanaitumia kama vile sheria inavyotaka. (Makofi)
MHE. JAMAL KASSIM ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Issa Mangungu na wananchi wa Mbagala nitakuwa na maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vile Serikali katika mwaka unaokuja 2017/2018 wamepanga kutoa ajira za walimu. Je, ni walimu kiasi gani ambao wamepangwa kwenda kuajiriwa katika Wilaya ya Temeke hususan katika jimbo la Mbagala, katika shule za sekondari za Kingugi, Mbande, Charambe, Toangoma na Mbagala Kuu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali katika mwaka huu imeajiri walimu wengi wapya, je, ni lini sasa Serikali itawapatia stahiki zao walimu hawa wapya na pia kuwapatia makazi ili kuwawesha kufanya kazi yao kwa ufanisi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema pale awali kwamba tuna mpango wa kuajiri walimu, lakini katika hili sasa hivi tunafaya vile vile na tathmini ya idadi ya walimu ambao wametoka katika system ya kiserikali mara baada ya vyeti fake. Kwa hiyo, tutaleta taarifa rasmi hapa baadaye kwamba idadi ya walimu ambao wamekutana na vyeti fake ambapo hivi sasa kuna deficit ambayo itakuwepo, lakini na idadi ya walimu wapya. Kwa hiyo, tutaleta taarifa rasmi ya idadi ya walimu. Hata hivyo naomba nikuhakikishe Mheshimiwa Jamal kwamba kwa Mkoa wa Dar es salaam maeneo ya Temeke na mimi nafahamu sana Temeke ilivyogawanyika mpaka kwenda kule ndani maeneo ya Toangoma tutaangalia ni jinsi gani tutafanya ili maeneo hayo kama ambavyo umeainisha tuweze kuwapeleka walimu wa kutosha ili vijana wetu wanaokwenda kujiunga, waweze kupata elimu hiyo inayokusudiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika upande wa pili wa swali lako nadhani Mheshimiwa Jamal, nimesahau kidogo kipengele cha pili.
MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na swali la msingi kwa kuwa Ilani ya Chama cha Mapinduzi imesema watoto wote wasome bure, katika jimbo la Kaliua shule ya msingi Ushokola walimu wanafundishia nje na walimu hawatoshi. Ni lini Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi itaona hili tatizo la Kaliua kuongezea walimu wa shule za msingi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Bulembo, Senior MP, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la bwana Bulembo bahati nzuri siku nne zilizopita nilikuwa na viongozi kutoka katika Wilaya ya Kaliua, walifika ofisini kwangu pale lakini ili kujadili ajenda za kimaendeleo. Ninasema Senior MP kwa sababu mwanzo alikuwepo na hivi sasa mnajua kazi zake kubwa anazozifanya katika nchi hii na juzi alikuwepo kule Mkoa wa Tabora nadhani ndio maana ameweza kufanya verfication ya tatizo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kikubwa zaidi nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge; nilikubaliana na viongozi waliotoka Kaliua kwamba nitafika Kaliua. Naomba nikuhakikishie kwamba nitatembelea shule ile ili kubaini mahitaji halisi. Hata hivyo Serikali tutaweka mpango, namna ya kufanya ili tuweze kujenga miundombinu na kuwapatia walimu ili vile vile wananchi wa eneo lile wapate fursa ya kusema tulitembelewa na mjumbe wa Kamati Kuu ambaye anasimamia suala zima la utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi. (Vicheko/Makofi)
MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa vile swali langu ni sawa sawa na hali halisi iliyoko Mbagala, ningependa nimuulize Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI kwamba jimbo la Same Mashariki limekuwa na shida sana ya walimu, tuna kata moja ya Bwambo, shule ya Changuruwe imekuwa na walimu wawili tangu darasa la kwanza mpaka la saba kwa muda mrefu sana na kilio hiki hakijaweza kusikilizwa na kufanyiwa kazi. Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kunisaidia ni lini atanipa walimu tuongezee hii shule ambayo wanabidii sana lakini kwa walimu wawili hata ungefanya nini hawawezi kutosheleza kusaidia wanafunzi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Mbunge nikupe pole katika hilo. Nilivyofika katika Mkoa wa Kilimanjaro, miongoni mwa Mikoa ambayo ina walimu wengi ni Mkoa wa Kilimanjaro. Kwa hiyo, nitumie fursa hii sasa kumuagiza Afisa Elimu wa Mkoa, haiwezekani walimu wote wakajazana Moshi Mjini, wakati wananchi wa Same hawana walimu. Nimuagize Afisa Elimu wa Mkoa wa Kilimanjaro, shule zinapofunguliwa ahakikishe shule ambayo Mheshimiwa Mbunge ameianisha katika Halmashauri ya Same amepeleka walimu wa kutosha, la sivyo tutamuona kwamba hatoshi kusimamia eneo hilo la elimu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante sana kwa kupata fursa hii. Kama ilivyoshida ya walimu katika jimbo la ndugu zangu wa Mbagala na sisi watu wa Mkuranga tunashida kubwa ya upungufu wa walimu. Serikali inanipa ahadi gani ya kuhakikisha kwamba upungufu ule wa walimu unapungua? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Ulega, kama alivyokuwa makini kusimamia shughuli za maendeleo katika jimbo lake, naomba nimuhakikishie kwamba katika mchakato huu wa sasa wa kuelekea kuajiri walimu Mkuranga tutaipa kipaumbele, na nikijua kwamba jimbo lako lile limetawanyika sana, tutakupa kipaumbele ili elimu kwa wananchi wa Mkuranga iweze kupanda na hatimaye waweze kupata mafanikio mazuri ya Serikali yao.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri napenda niongezee sehemu kidogo tu. Waheshimiwa Wabunge ni karibu maeneo mengi yana upungufu wa walimu na hasa kwenye shule zetu za msingi. Pamoja na jitihada za Serikali kuwapeleka walimu ambao wanaonekana wamezidi katika baadhi ya maeneo lakini baadhi ya shule bado walimu hao ni wachache, kwa sababu ya changamoto za miundombinu zilizopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapopokea mipango ya Halmashauri na vipaumbele vyao inasikitisha kuona wakati mwingine mipango hiyo, na kwa sababu utawala wa nchi hii unatoka chini kwenda juu na si juu kwenda chini na ndio maana bajeti inaanza kupangwa kutoka chini baadaye juu tunakuja kumalizia, tungelitegemea vipaumbele viwe nyumba za walimu na miundombinu kama hiyo inayotegemea kujenga mazingira bora ya watumishi hawa kwenda kufanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, anachokizungumza Mheshimiwa Mbunge aliyeuliza swali la msingi inaonekana ni mazingira magumu ya kule milimani ya kule Same ndiyo maana walimu hawakai, hivyo ukijiuliza hakuna nyumba na hata walimu hawa wakifika uongozi tu wenyewe kuwapokeana kujenga mazingira mazuri ni vigumu sana, hawashughuliki nao, na ndiyo maana kuna upungufu.
Kwa hiyo niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge, sisi ndio tunaoshiriki kwenye vikao vya maamuzi makubwa, sisi tunashiriki kwenye vikao ambavyo vinapanga mipango na bajeti. Tupange mipango hiyo inayotatua kero za nyumba za walimu ndipo tutakapoweza kuwa-retain walimu hawa katika shule zetu.
MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii kuipongeza sana Serikali kwa majibu mazuri lakini nina swali la nyongeza.
Pesa hizi zilizokuwa zinakusanywa na Halmashauri zilikuwa zinasaidia kazi ndogo ndogo kwenye zile Halmashauri. Namuomba Mheshimiwa Naibu Waziri atuambie Serikali imepanga vipi kuhakikisha inaziba hilo gap?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Halmashauri mwanzo zilikuwa zinajielekeza kwa kukusanya tozo hizi ambazo zilikuwa zinasaidia katika kuendesha Halmashauri. Nadhani hiki kilikuwa ni kilio cha Watanzania wote, ambao Watanzania wadogo wadogo kule chini ilikuwa inapigwa kelele sana ndio maana Serikali sasa imeomua kulichukua hili na Wizara ya Fedha hapo alipoweka hotuba yake hapa nilizungumza hili wazi. Kwa hiyo, naomba tukifika katika Finance Bill mtaona jinsi gani Serikali imejipanga na ku-address jambo hilo vizuri kwa mustakabali wa Halmashauri zetu unavyoenda.
MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mweyekiti, nakushukuru, pamoja na Serikali kuamua kuondoa tozo hizo tayari Halmashauri zilishaweka kwenye bajeti zao. Je, Serikali inatoa tamko gani ama wata-review hizo bajeti au itakuwaje? Hiyo ndiyo shida yangu ahsante na shida kwenye Halmashauri zetu.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani hii ni hofu ya Wabunge wengi humu ndani, na hata juzi Wabunge wengi walikuwa wananiuliza kule kwamba jinsi gani tunavyokuja. Na ndiyo maana naomba niwaambie kuwa Serikali itakachokifanya sasa hivi ndiyo maana nimesema tukifika katika Finance Bill tutaona jinsi gani mchanganuo utakavyokwenda. Lengo kubwa kwa sababu Halmashauri zimeshatenga bajeti yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia bajeti ya Halmashauri ilivyotengwa kuna tofauti sasa na kama ambavyo vingine viliwekwa kama ni vyanzo vya mapato katika Halmashauri hiyo. Ndiyo maana Wizara ya Fedha itakapohitimisha mijadala hii tutaona ni jinsi gani mafungu hayo yatawekwa vizuri. Lengo kubwa bajeti ya Halmashauri kama property tax ilivyowekwa katika suala la majumba, kwa hiyo, msihofu katika hili.
MHE. HASSAN S. KAUNJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri nina maswali mawili ya nyongeza.
La kwanza Serikali ya Awamu ya Nne ilitoa ahadi ya kujenga kituo cha Afya katika kata ya Mnazi Mmoja. Ahadi hii ilikuwa ina inataka kutekelezwa na Serikali Kuu, mpaka tunapozungumza hakuna chochote kinachoendelea ikiwa ni mwaka wa saba sasa. Nini kauli ya Serikali kuhusu jambo hilo?
Swali la pili, wananchi wa Lindi tuliwahamasisha waanze kujenga vituo vya afya katika kata zao. Wamepata maelekezo kutoka TAMISEMI ya kwamba vituo hivyo visimame kujengwa kwa muda mrefu mpaka sasa. Nini kauli za Wizara dhidi ya watu wale ambao wameamua kujitolea kuweza kujenga vituo vile vya afya? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi ya Serikali kama zilivyo ahadi zingine na nikifahamu sehemu ya Mnazi Mmoja ni juction ya population kubwa na imetolewa ahadi hii takriban miaka saba, nikijua kwamba kuna juhudi zimeshaanza pale. Naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali naomba ihamasishe Halmashauri yako muanze kuibua jambo hili vizuri halafu na sisi tutaliratibu vizuri. Naomba nikuambie Serikali itakupa ushirikiano wa kutosha lengo letu ni kwamba commitment ya Serikali ya ahadi zote zilizotolewa na viongozi wetu wa Kitaifa tunaenda kuzitekeleza.
Kwa hiyo, naomba nikusihi Mheshimiwa Mbunge katika mchakato huu bajeti utakao kuja sasa tuliweke hili vizuri ili na sisi tutalipa nguvu, lengo kubwa kituo cha afya tuweze kukitengeneza katika eneo lile. Jambo la hivi vituo vya afya vingine ambavyo wananchi wameanza ujenzi nikijua kwamba commitment ya Serikali ni kuwahamazisha wananchi katika suala zima la ujenzi wa afya. Kama vituo hivyo ni vipya vinaendelea basi naomba niseme kwamba tutaendeleza kuvihakikisha tunavipa nguvu. Lakini nikijua kwamba kuna utaratibu ambao wakati mwingine umejitokeza kuna utaratibu wa kubadilisha zahanati kuwa kituo cha afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana Ofisi yetu sasa ilitoa maelekezo kama hizi zahanati tuziache ziwe zahanati lakini tujenge vituo vipya viwe vya afya. Lakini kwa sababu Bwana Kaunje jambo hili umelileta hapa naomba nikuhakikishie kwamba ofisi yetu itakupa ushirikiano wakutosha kuangalia scenario ipi iliyoko kwenye Manispaa ya Lindi tuweze kusaidiana kwamba wananchi waweze kupata huduma kutokana na hali halisi ilivyo pale kwako Lindi.
MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa katika jitihada za kupunguza mzigo mkubwa unaobebwa na Hospitali ya Lindi, Serikali iliingia makubaliano na hospitali za mission kwa mfano Hospitali ya Nyangao pale Jimbo la Mtama kwa ajili ya kusaidiana nao katika kutoa huduma za afya ili tupunguze mzigo mkubwa katika Hospitali ya Lindi. Lakini utekelezaji wa makubaliano hasa upelekaji wa fedha na watumishi kwa ajili ya kufanya kazi katika hospitali hizi ambazo mmekubaliana nazo hautelekezeki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali sasa itaanza kupeleka pesa kama walivyokubaliana pamoja na watumishi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Nape, naomba tulichukue hilo kwa sababu kuna hizi ahadi najua kwamba katika hospitali mbalimbali zinatekelezeka na nikijua kwamba kweli kuna shida kubwa na ndiyo maana kutokana na kesi ile ya kwako tumeona kwamba pale Kituo cha Nyangarapa ambao kituo cha afya kwenda kukiboresha zaidi kama tulivyokubali pale mwanzo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tutaenda kukiboresha kituo hiki lakini suala zima la commitment za hizi taasisi ambazo za dini au vituo mbalimbali vya dini au vituo mbalimbali binafsi ambao Serikali imeingilia nazo, kama kuna scenario ambayo kwa Wakilindi iko tofauti kidogo upelekaji wa fedha hauko vizuri tunakwenda kuufuatilia kuangalia jinsi gani tuuboreshe wananchi waweze kupata huduma vizuri.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Majibu ya Mheshimiwa Waziri nadhani hayana uhalisia na mazingira ya Manispaa ya Mpanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi Machi, 2014 Halmashauri ya Mpanda ilitenga shilingi milioni 200 kwa ajili ya ununuzi wa gari la kukusanya taka, gari la kisasa na siyo haya malori mawili ambayo umeyasema.
Kutokana na ubadhirifu ambao umefanyika kwenye Manispaa hii, Serikali inachukua hatua gani kwa huyu mzabuni aliyetumia fedha hizi na mpaka sasa hajarudisha na baadhi ya hao watendaji ambao wamekula pesa hii, wananchi wa Manispaa ya Mpanda hivi tunavyoongea wanashinda na takataka ndani, wanashindwa kuzitoa na Manispaa imeshindwa kukusanya hizi taka kwa wakati. Serikali inamchukulia hatua gani huyu Ndugu Kisira pamoja na watendaji waliokula pesa hizi katika Manispaa ya Mpanda? (Makofi)
Swali la pili, imekuwa ni tabia ya Serikali kuendelea kuhamasisha wananchi kufanya usafi kwenye maeneo yao, lakini kitu kibaya zaidi ni kwamba wananchi hawa wanalazimishwa kufunga maduka, kila siku ya Jumamosi kuanzia saa 1:00 asubuhi mpaka saa 4:00 aasubuhi na siyo Mkoa wa Katavi peke yake au Manispaa ya Mpanda peke yake ni nchi nzima, ikiwepo na maduka ya Dar es Salaam, Kigoma, Mbeya, Mwanza pamoja na Katavi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa tabia hii ya kuendelea kufunga maduka, je, Serikali hamuoni kwamba mnapoteza uchumi wa wananchi wao kuendelea kufunga maduka na huku wakiendelea kufanya usafi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Rhoda tutende haki, swali lako ulilouliza halafu una ajenda, inawezekana swali lako ungeli-frame vizuri lingepata majibu mazuri sana. Kwa sababu swali lako lilikuwa linajenga suala la ubadhirifu wa fedha zilizotengwa, ungelitengeneza vizuri halafu tungeweza kupata majibu mazuri sana katika hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, nimesema kwamba pale kuna magari ya taka mawili, kama kuna suala la ubadhilifu hiyo ni ajenda nyingine, tunachotakiwa kukifanya ni kwamba hatuvumilii ubadhirifu wa aina yoyote, na kama ubadhirifu huo upo, tutaenda kuufanyia kazi tutaenda kufuatilia nini kilichojiri katika Manispaa ya Mpanda kama fedha zilizitengwa lakini hazikutumika vizuri katika suala hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala zima la ajenda kwamba siku ya Jumamosi wananchi wanafunga maduka, kumbukumbu yangu Waziri Mkuu hapa aliulizwa na Mheshimiwa Ulega, Mbunge wa Mkuranga katika suala ya siku ya Jumamosi utaratibu wa kufanya, lengo kubwa ilikuwa usafi ufanyike lakini usizuie shughuli za wananchi katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, agizo hili limeishatolewa kwamba Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya katika maeneo yao tunapofanya utaratibu wa usafi tuangalie modality nzuri usafi ufanyike, lakini kama kuna mambo mengine ambayo saa nyingine yanahusu shughuli mahsusi zinaweza kufanyika. Hapa Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa maelekezo naomba tufanye rejea ile vizuri tusitoe majibu mawili itakuwa ni sub-standard siyo vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niichukue kwamba hoja yako ya usafi ni ajenda yetu ya Kitaifa, lazima kama Wabunge, lazima kama Viongozi tusimame pamoja katika jambo hili. (Makofi)
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa magari ya kunyonya maji machafu na kuzoa taka siyo lazima tu iwe kwenye Manispaa au Majiji, hata Wilaya zetu tunahitaji magari ya kunyonya maji machafu na magari ya kuzoa taka. Je, Serikali ina mpango gani kupeleka gari la kunyonya maji machafu pamoja na kuzoa taka katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI naomba kujibu swali la Mzee wangu Lubeleje, mimi namuita greda la zamani makali yale yale kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya Mzee Lubeleje naomba tuiweke katika vipaumbele vyetu vya Halmashauri, naomba nikusihi Mheshimiwa Lubeleje katika mpango wenu wa Halmashauri hilo jambo mkiliainisha, na sisi katika kupitisha bajeti tutalipa kipaumbele. Ninajua kwamba kweli ni jambo la msingi kufanya usafi na kuwa na mitambo hii ya kuzolea taka na kunyonyea maji, kwa hiyo mkiweka katika kipaumbele, mchakato wa bajeti ujao kama Mpwapwa mtaweka kipaumbele basi sisi hatutasita kuhakikisha jambo hilo tunaliwekea kipaumbele hilo ili Mpwapwa mpate gari la kunyonyea maji taka.
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Takataka zinaweza zikasababisha uchumi mkubwa sana kwa wananchi wetu kwa sababu taka zinaweza zikatengeneza matofali, zinaweza zikazalisha umeme, zinaweza zikatengeneza mbolea nzuri sana na sasa hivi kwa sababu maeneo ya kutupa taka yanaendelea kupungua mwaka hadi mwaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini Serikali isifanye uamuzi wa makusudi, kabisa ikaleta hii teknolojia nchini, ikaanza na majiji yetu ili kuwafanya wananchi wakapata kipato kwa kukusanya takataka na kuzipeleka kwenye maeneo hayo ambayo yanaweza yakazi-process na kuzalisha vitu vingine kwa faida ya Taifa kwa ujumla? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Selasini jambo lako ni zuri sana, ndiyo maana katika ofisi yetu tuna mradi mmoja unaitwa Strategic City Project, katika miji mbalimbali tumetenga utaratibu wa kutengeneza haya madampo ya kisasa, ambapo ukienda Mbeya utayakuta, hapa Dodoma tunajenga na maeneo mbalimbali tunatengeneza madampo kama yale. Lengo letu kubwa ni kwamba taka zitakazozolewa baadaye ziingizwe katika system maalum kuweza ku-convert katika shughuli zingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, sasa hivi tunakaribisha wawekezaji mbalimbali ambao katika njia moja au nyingine watasaidia ukusanyaji wa hizi taka kuweka katika malighafi nyingine, ikiwemo suala zima la utengenezaji wa mkaa.
Kwa hiyo, ni hilo ni jambo zuri Serikali na wadau mbalimbali tushirikiane kwa mustakabali wa nchi yetu ambao mwisho wa siku taka hizi baada ya kuwa uchafu inaweza ikawa malighafi na zitasaidia kujenga uchumi katika nchi yetu. (Makofi)
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali kwamba uchumi ukiwa nzuri tutaongeza, ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwa kuwa majibu yanaonesha kwamba kila baada ya miaka miwili Serikali ilikuwa ikiongeza posho za Waheshimiwa Madiwani mpaka 2015 na leo tuko 2017 tayari miaka miwili. Je, Serikali haioni kwamba kulingana na mazingira wanayofanyia kazi Waheshimiwa Madiwani pamoja na kupanda kwa maisha, sasa ni muda muafaka wa kuongeza posho angalau kidogo ili waweze kumudu maisha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa mikopo hii wanayokopa kwenye mabenki ni kutokana na posho yao, Serikali haioni kwamba hizi fedha ni ndogo zaidi, hawawezi hata kupeleka kwenye usafiri. Je, Serikali kwa nini isiweke ruzuku kama inavyotoa kwa Waheshimiwa Wabunge nusu ili Waheshimiwa Madiwani waweze kumudu usafiri? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kwamba kwa wastani wa miaka miwili posho ya Madiwani inaongezeka; naomba nikiri kwamba Madiwani wetu wanafanya kazi kubwa sana. Mheshimiwa Kiswaga na Waheshimiwa Wabunge naomba niwaambie kwamba kwa bahati nzuri nilipata fursa ya kukaa na Madiwani katika vikao vya ALAT kule Musoma na hapa Dodoma na hii imekuwa ni concern yao kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni kweli na sasa hivi limewasilishwa katika mamlaka husika na kwamba sasa linafanyiwa kazi na linachambuliwa vizuri. Mambo yakikamilika vizuri basi watapata mrejesho kwamba Serikali imeamua vipi katika jambo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la ruzuku kwa vyombo vya usafiri nadhani ni wazo zuri naomba tulichukue, na Serikali itaangalia ni jinsi gani itafanya kwa sababu Madiwani wanafanya kazi kubwa, lakini siwezi kutoa commitment kutoka hapa kwamba nini kinafanyika kwa sasa.
MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri hapa amesema wataongeza kipato kwa Madiwani ikiwa mapato ya Serikali yataongezeka; lakini kwa mwaka sasa Serikali imekuwa ikitangaza kuongezeka kwa mapato, yaani makusanyo yamekuwa makubwa, ninachokitaka badala tu ya kuwalipa posho kwa nini sasa Madiwani wasilipwe mishahara kama tunavyolipwa sisi Wabunge ili wafanye kazi hiyo kwa moyo. Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Menyekiti, Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo la kulipwa mshahara na posho; kwa sababu kuna nafasi mbalimbali zimetengwa kwa utaratibu wake; kwa utaratibu Madiwani wanalipwa posho sawasawa na Wenyeviti wa Vijiji, kwamba kuna posho ile ya asilimia 10 kwa Wenyeviti wa Vijiji, lakini kuna posho maalum ya Madiwani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu wazo la mshahara, hili tuseme ni wazo tu ambalo Wabunge wanatoa kuona jinsi gani jambo hili linaboreshwa. Hata hivyo, mara nyingi Serikali inafanya tathmini katika maeneo mengi zaidi na hasa kuangalia wage bill ya Serikali itakuwaje baadaye endapo Madiwani wataingizwa katika eneo hilo kwa wakati mmoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwa hiyo nasema kwamba ni mawazo au chemchem ambayo inasaidia kuboresha ili unapofika wakati tuangalie jinsi ya kufanya; lakini kwa sasa hivi utaratibu tunaokwenda nao ni utaratibu wa posho kwa mujibu sheria.
MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Huko nyuma Serikali ilikuwa ikitoa mafunzo kwa Madiwani ambapo mafunzo hayo yaliwajengea uwezo mkubwa ikiwa ni pamoja na kufahamu mipaka yao. Je, ni lini Serikali itarejesha mafunzo haya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba, kwa kipindi cha nyuma kulikuwa na mafunzo ya Madiwani ambayo yalikuwa yakitolewa ili kuwajengea uwezo waweze kufanya kazi yao vizuri kwa sababu wao ndio wanafanya maamuzi katika Mabaraza yetu ya Madiwani katika halmashauri zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, hapa katikati mafunzo kidogo yalisimama. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mchakato huu wa mafunzo umeanza katika maeneo mbalimbali na mafunzo haya yataweza kuwafikia Madiwani, lengo kubwa ni kujenga uwezo wao kwa kadri itakavyoonekana kwamba itafaa.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali moja dogo. Bahati nzuri mimi nimekuwa Diwani kwa miaka kumi na tano na Mwenyekiti wa Halmashauri. Kazi ya Udiwani zamani ilikuwa mikutano tu, unakuja kuitwa kwenye kikao unarudi nyumbani; lakini kwa kuwa sasa hivi Udiwani ni kusimamia miradi, ikianza kujengwa darasa mpaka jioni uko pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Mheshimiwa Naibu Waziri atakubaliana nami kwamba mtekeleze yale maagizo au maelekezo ya Tume ya Lubeleje ya kushughulikia maslahi ya Madiwani, muwalipe Madiwani posho ya kutosha ili nao waweze kumudu maisha kwa sababu wanashinda kwenye miradi mpaka jioni?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mbunge wa siku nyingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri wazi kwamba kuna Tume iliundwa ambayo Mheshimiwa Lubeleje ambaye ni Mbunge; ndiyo maana namwita Senior MP alikuwa ndiye Mwenyekiti wa Tume ile. Tume ile ilitoa mapendekezo mbalimbali na miongoni mwa mapendekezo hayo yaliyotolewa katika Tume ya Lubeleje ndiyo haya yaliyosababisha kufanya maboresho ya hata hivi viwango tunavyoviona hivi sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kikubwa zaidi na tukiri wazi kwamba Madiwani ndio wenye jukumu kubwa sana la kusimamia kazi za kule site. Ndiyo maana nimesema kwamba Serikali inalitazama hili kwa upana wa hali ya juu; kwamba nini tufanye. Kwa hiyo, hali itakapokuwa imeridhisha na maamuzi yakifanyika naamini kwamba posho ya Madiwani itaongezeka. Lengo ni kuwawezesha kufanya vizuri katika usimamizi wao wa kazi kwani wanafanya kazi kubwa na hakuna mtu anayebeza katika hili.
MHE. KANGI A.LUGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Waheshimiwa Wabunge hapa kila tukigusa maombi ya fedha kwenye miradi ya maji, barabara na afya tunaambiwa pale hali ya uchumi itakapokuwa nzuri. Leo pia tunagusa suala la posho za Madiwani tunaambiwa hali ya fedha itakapokuwa nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Taarifa ya Hali ya Uchumi ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwenye bajeti hii anasema hali ya uchumi ni nzuri na kwenye ukurasa wa tatu wa taarifa ya Benki, hii hapa ninayo, wanasema uchumi umekuwa kwa asilimia saba, ni kiwango kikubwa sana cha kimataifa. Sasa je, hii hali ya uchumi wanayotaka ni asilimia ngapi ndiyo hali ya uchumi itakayokuwa nzuri? Mimi nashindwa kuelewa.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumza hali ya uchumi itakapokuwa nzuri; ni kweli tunakwenda vizuri, lakini malengo ya Serikali hii ya Awamu ya Tano ni kwenda mbali zaidi na ndiyo maana najua suala hili la posho si kwa Madiwani peke yake ni hata Walimu pamoja na watumishi wengine, kila mtu anataka angalau mshahara wake uweze kuongezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana tumesema kwamba acheni Serikali kwanza ijipange vizuri katika hili. Tunajua tuna vipaumbele vyetu vingi sana ambavyo ni lazima vyote tuvitekeleze. Ngoja tujipange vizuri, lakini kila kundi litaweza kufikiwa kwa kadri Mheshimiwa Rais alivyojipanga na Serikali yake ya Awamu ya Tano na hatimaye kila mtu ata-realize kwamba kweli hatukufanya makosa katika kupanga mipango muafaka kwa ajili ya nchi yetu.
MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Pamoja na posho za Madiwani, Wenyeviti ya Vijiji na Vitongoji kuwa ndogo, lakini bado halmashauri nyingi zimekuwa zinawakopa viongozi hawa posho hizi kiasi kwamba wana muda mrefu hawalipwi. Sasa Serikali iko tayari kutoa kauli yenye muda maalum kuhakikisha kwamba viongozi hawa wanalipwa madeni yao ya posho zao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, juzi nilipokea concern kutoka Buchosa kwamba Madiwani wamekopwa takribani miezi minane, hili halikubaliki hata kidogo. Wakati mwingine utagundua kwamba ni uzembe tu wa usimamizi nzuri. Watu wanafanya collection lakini wakati mwingine katika suala la kuwalipa Madiwani wanaona kama ni hisani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nitoe maelekezo kwamba halmashauri mbalimbali tunafanya makusanyo, makusanyo yale yanakusanywa na Madiwani ndio wanaofanya maamuzi, lazima mwende mkalipe posho za Madiwani kwa kadri iwezekanavyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Madiwani wanafanya kazi kubwa lakini posho zao hazilipwi na wakati huo huo shughuli nyingine zinaendelea ambazo Madiwani hao ndio waliosimamia kupata fedha hizo, haitokubalika. Tutaenda kufuatilia halmashauri moja hadi nyingine. Naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba tuta-cross check na halmashauri mbalimbali ambazo kwa makusudi kabisa wamekataa kuwalipa madiwani either kwa kiburi au kwa jambo lingine lolote.
MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, siridhiki kabisa na majibu aliyotoa Mheshimiwa Naibu Waziri, na huu ndio mzaha ambao hatupendi Wabunge. Milioni 20 mimi ninazo mfukoni hapa, si ningetengeza bwawa hilo? Halitengelezeki kwa milioni 20 bwawa hilo, Bwawa kubwa na limepasuka. Nataka kujua na alisema kwamba itatokana na ruzuku, nani anatoa ruzuku, hatujui; lakini hela zinakwenda kwa nani, hatujui; mkandarasi nani atafanya hiyo kazi hatujui, jibu hili si sahihi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sitaki tena kuomba mwongozo baadaye lakini ningependa Waziri anijibu vizuri, kwamba hizo hela zitatoka wapi na hela hizo hazitoshi, lakini je, lini hela zitapatikana? Hiloni swali la kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tangu mwaka 2014/2015, 2016/2017, leo miaka mingapi? Barabara imejaa miti iliyoota, nani atatengeneza hiyo barabara ya kwenda kwenye bwawa kwa sababu haipitiki? Nataka kujua pia je, barabara ile itatengenezwa na nani?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu milioni ishirini; mara nyingi kila mtu ana taaluma yake. Maana yake ma-engineer kama wamefanya assessment; kwa sababu ni ile sehemu iliyobomoka tu. Kama Mbunge anahisi kama shilingi milioni ishirini haitoshi; katika hili naomba niseme kwamba; kwa sababu bwawa limevunjika katika spillways; ngoja tupeleke hizo fedha halafu tuone nini kitaendea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakapofanya assessment; kama mtaalam wa maji, mabwawa, engineer amefanya assessment na amesema ni milioni ishirini, lakini Mheshimiwa Mbunge anasema haitoshi, aah, tutaangalia maana huyo mtu inawezekana qualifications zake hazimtoshi kukaa katika nafasi hiyo, ndiyo maana ameleta assessment ya milioni ishirini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili maana yake si kwa sababu yuko Jafo hapa; kwa sababu kuna mtu alifanya designing na assessment ya bwawa lilivyopasuka na amesema milioni ishirini. Isipotosha maana yake watu hawa ndio watakaokuwa wanakwamisha shughuli za maendeleo katika maeneo yetu, hatutaweza kuvumilia. Naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwa sababu nina safari ya kwenda Kaliua na Urambo nitapita kwenda kutembelea bwawa hilo na kuangalia hali halisi ikoje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini fedha hizi zitatoka katika Local Government Capital Development Grant kutoka TAMISEMI, naomba asihofu fedha hizo zitakwenda. Kuhusu suala la barabara kufika katika eneo lile naomba niseme kwamba hiki ni kipaumbele cha Halmashauri yenyewe kadri inavyosema kwamba bajeti yake inajenga barabara katika eneo gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu naamini kwamba tutafika site tutakwenda kuiona hiyo barabara, basi waweke kipaumbele kama barabara hiyo ambayo haipo katika mpango lazima iwekwe katika mpango ili wananchi waweze kufika katika eneo hilo.
MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo tu la nyongeza. Matatizo yaliyoko huko Uyui yapo pia katika Jimbo la Manyoni Magharibi. Halmashauri ya Wilaya ya Itigi kuna mabwawa madogo yale malambo madogo ambayo yamepasuka na mengine yamefukiwa na maji likiwemo la Kaskasi stesheni, Mkalamani Itigi Majengo, pamoja na la Muhanga. Je, Serikali iko tayari na sisi kutusaidia fedha kidogo katika Mfuko huo ili na sisi kama halmashauri tuweze kurekebisha mabwawa haya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu Mheshimiwa Mbunge ame-pose hilo swali hapa sasa hivi na hatujui kwamba mabwawa hayo assessment imefanyika na inahitaji gharama kiasi gani na hatujui kama Halmashauri imeweka kipaumbele gani katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme tu kwamba kwa sababu suala la mabwawa hayo ni jambo la msingi; naomba tuwaagize wenzetu wa Halmashauri ya Itigi, kwamba sasa wataalam wa maji waweze kwenda katika eneo hilo wafanye tathmini ya mabwawa hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni kwa sababu mabwawa haya yakijengwa yataisaidia jamiii katika eneo letu; tujue kwamba kama Serikali tunajipanga vipi kurekebisha mabwawa hayo mara baada ya kupata bajeti halisi na tuweze kuliweka katika mipango ya maendeleo ya bajeti katika Halmashauri ya Itigi.
MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Matatizo yaliyopo Uyui kwenye miradi inayosimamiwa na TASAF na TAMISEMI yanafanana kabisa na matatizo yaliyopo katika Jimbo la Ndanda hasa kwenye Kata ya Mwena.
Mheshimiwa Mwenyekit, kwenye hii TAMISEMI phase III ambayo imekuwa ikishirikisha wananchi. Kuna miradi pale ya mabomba ambayo Mheshimiwa Diwani kwa kushirikiana na watendaji wamekuwa hawatekelezi wajibu wao; kwa maana ya thamani ya pesa haionekani kwenye miradi. Sasa Mheshimiwa Waziri tunaomba atuleze badala ya kusubiri mpaka haya mambo yaharibike kabisa ndipo Wizara yake ikachukue hatua, je, hawaoni kuna haja ya kufuatilia utoaji na matumizi ya pesa ya TASAF katika maeneo mbalimbali kadiri siku zinavyokwenda?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme wazi kwamba jambo la kusimamia fedha (value for money) katika maeneo yetu naomba tulipe kipaumbele sana. Mheshimiwa Cecil nakumbuka tumetembelea mpaka kwenye bwawa lake pale chini. Kama fedha lakini usimamizi si mzuri na kama fedha imekwenda wengine wanatengeneza caucus kule kwa ajili ya kula ile fedha, jambo hilo halikubaliki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe Waheshimiwa Wabunge kwa sababu wao ni Wajumbe wa Kamati ya Fedha, wasikubali kupitisha mradi wa aina yoyote katika site na Majimbo yao ambayo wanaona katika njia moja au nyingine, mradi huu baadhi ya watu wanahujumu kwa makusudi. Tukifanya hivi ndipo tutalinda fedha hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sasa naomba nitoe maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Masasi, kwamba aangalie kwanza nini kilichotokea katika mradi huo ambao tunasema kwamba lengo ni kuweza kuwasaidia wananchi halafu tupate taarifa. Nitaenda kufanya follow up ya haraka ili fedha zinapokwenda kule site lazima fedha zile ziweze kuleta matunda makubwa sana kwa manufaa ya wananchi.
MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Naomba niulize swali la nyongeza. Kutokana na mvua zilizonyesha, barabara yetu ya kutoka Mbwela kwenda Muholo imeharibika zaidi. Je, Wizara yake ina mkakati gani wa kutukarabatia barabara hiyo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, najua Mheshimiwa Ungando amehamisha goli lakini ngoja nimjibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, anachosema Mheshimiwa Mbunge ni kweli, ile barabara kwanza ni korofi na Mheshimiwa Mbunge anakumbuka siku ile tulikuwa delta mpaka usiku saa mbili ndipo tulirudi kwa kuwa barabara iliharibika sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu tumepitisha fedha za barabara za vikwazo na barabara hiyo tumeiweka basi nimhakikishie Mheshimiwa Ungando kwamba kwa sababu bajeti tumeipitisha jana na yeye amepiga kura ya ndiyo, bajeti hii sasa itakapoanza kufanya kazi katika eneo lake lile tutalipa kipaumbele ili barabara ile tuirekebishe sambamba na ujenzi wa yale madaraja ambayo yanakwamisha sana kuwapitisha wananchi wa Kibiti.
MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa mabwawa yameendelea kupasuka katika nchi hii na kwa kuwa katika Wilaya ya Monduli, Kata ya Esilalei, bwawa la Josho na Oltukai, tulishaleta mpaka kwa Waziri Mkuu kuomba Serikali iweze kukarabati mabwawa yaliyopasuka mwaka 2015. Je, ni lini Serikali itakuja kukarabati mabwawa haya ambayo Serikali ilishahaidi kuyakarabati?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa ukiangalia kila mtu anazungumza kuhusu bwawa lililopasuka na nimetoa maangalizo, kwamba mabwawa haya yanapasuka huenda kandarasi haikusimamiwa vizuri, ile spillway (utoro wa maji) haukuwa vizuri au ile embarkment haikushindiliwa vizuri au utaalam wenyewe uliotumika huenda haukutumika sawasawa; kwa hiyo hapa inawezekana kila mtu atazungumza bwawa lake limepasuka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe maelekezo kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri zote wafanye tathmini ya mabwawa yote yaliyopasuka ili Serikali tuone kwamba tuna tatizo kiasi gani tuweze kulipangia mpango na tulirekebishe na hatimaye mabwawa haya yawasaidie wananchi katika mifugo, maji ya kunywa na matumizi mengine. (Makofi)
MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya wanawake na vijana hususan wa Mkoa wa Mwanza napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza. La kwanza, kwa kuwa kumekuwa na tabia ya baadhi ya Halmashauri za Wilaya kutokutoa asilimia kumi kwa wanawake na vijana kikamilifu na nyingine kutokutoa kabisa; je, Serikali inachukua hatua gani juu ya Halmashauri hizi zinazokaidi agizo hili la Serikali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa vikundi vya maendeleo vya wanawake na vijana vimekuwa ni vingi sana na fedha hii imekuwa ikinufaisha vikundi vichache; je, ni lini Serikali itaongeza asilimia hii ili iweze kunufaisha vikundi vingi na ukizingatia kwamba ikifanya hivyo itakuwa imepunguza kwa asilimia kubwa tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Mbunge kwa harakati zake kama kijana na kama mwanamke kugombea na kupambana kwa haki za wanawake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kuhusu suala la asilimia kumi, kwamba Halmashauri nyingine hazitengi; katika bajeti ya mwaka wa 2016/2017, tulipotenga bilioni 56.8 tulitoa maelekezo kwa Wakurugenzi wote kwamba commitment ya bajeti ya Serikali katika 10 percent, yaani five ya vijana na five ya akinamama lazima itekelezwe. Katika hili tumeona kwamba mpaka mwezi Machi tumetoa bilioni kumi na saba, lakini mpaka juzi wakati tunafuatilia ina maana fedha zinaongezeka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba niwasihi hasa Waheshimiwa Wabunge, sisi ni wajumbe katika Mabaraza yetu, fedha zile zinakusanywa wala haziendi kwa Mpango haziendi Hazina, zinaishia katika Halmashauri zetu. Lazima kila kinachokusanywa kila mwezi tunapoingia katika Kamati ya Fedha tusikubali kupitisha ile bajeti, fedha zimekusanywa pale, lazima tutenge moja kwa moja five percent ya vijana na five percent ya akinamama ili tuwasaidie watu wetu kule site.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili Wakurugenzi wote ambao tumekubaliana lazima walitekeleze na tarehe 30 mwezi wa sita tutafanya assessment ya Wakurugenzi wote ambao wameshindwa ku-meet commitment hii ambayo ilikuwa ni guideline na maelekezo ya Kamati ya TAMISEMI ya Bunge hili wakati tunapitisha bajeti. Kwa hiyo wakurugenzi wote lazima wajiandae, hiyo ni miongoni mwa assessment tutakayoifanya katika performance ya kufanya kazi zao katika maeneo yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, kuongeza ten percent; naomba nimwambie dada yangu, hii ten percent yenyewe inatosha kwa sababu fedha zile kuna nyingine zinakwenda katika maendeleo, posho za Madiwani na posho ya vijiji. Asilimia kumi kinachotakiwa ni compliance tu, kama kila Halmashauri itaweza kutoa kweli asilimia kumi tutaweza kufanya vizuri zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme kwamba asilimia kumi inatosha, isipokuwa sasa lazima wajue tumetoa maelekezo kwamba katika ile asilimia kumi lazima watenge asilimia mbili kwa ajili ya walemavu katika Halmashauri zetu. (Makofi)
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Naomba niulize swali moja dogo la nyongeza. Kwa kuwa vijana wanaohitimu elimu ya sekondari katika nchi yetu ni kama 400,000 hivi na wanaokwenda kidato cha tano ni kama vijana 90,000, zaidi ya vijana 300,000 wanabaki. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuanzisha kambi maalum ili kusudi sasa vijana hawa waweze kupata misaada ya kutosha ya utaalam wa kilimo na ufugaji?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo ni zuri, hata hivyo Serikali imesha-take initiatives za kutosha katika eneo hilo, ndiyo maana Serikali inashirikiana na wadau mbalimbali, na hivi sasa mikoa mbalimbali wameshaanzisha kambi za vijana katika jitihada za kujenga ujasiriamali, ujasiri na uzalendo. Jambo hilo limetokea katika Mkoa wa Tabora pamoja na Pwani na mikoa mingine na zoezi hilo linaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tuwashukuru wenzetu wa taasisi binafsi hasa shirika la Plan International ambalo kupitia mikoa mbalimbali kama vile Mkoa wa Morogoro, Lindi, Mtwara, Dar es Salaam, Pwani na mikoa mingine wameanza kupitisha programu maalum ya vijana kwa ajili ya kuwawezesha katika fani mbalimbali za ufundi. Hili limetoa mafanikio makubwa, zaidi ya vijana 9,500 wamepata skills hizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba Serikali itawatumia wadau mbalimbali na nguvu za Serikali lakini na Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya nawashukuru sana, wameshaanza ku- take hiyo initiative kwa kufanya mabadiliko hayo makubwa; naamini tukifanya hivi tutawasaidia sana vijana wetu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Halmashauri zilizo nyingi zinashindwa kutenga hii asilimia kumi kwenye Mfuko wa Vijana na Wanawake na hii inathibitishwa na ripoti mbalimbali za CAG, na ni ukweli kwamba tuna Mifuko karibu 19 ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Je, Serikali haioni sasa iko haja ya kupunguza Mifuko hii angalau kati ya miwili mpaka mitano ikiwemo hii iunganishwe kuwe Mfuko mmoja ili kuwe na ufanisi na iwafikie kweli wananchi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ku- harmonize hii Mifuko tuwe na Mfuko mmoja nadhani ni suala la kuzungumzika, tutafanya tathmini ya kina. Hata hivyo katika Mfuko wa asilimia kumi kuna maelekezo sasa hivi tunayatoa. Sasa hivi zile fedha katika ten percent zinaingia katika deposit account kama unaingiza katika dust bin mwishowe hata assessment hatuwezi kufanya vizuri; ndiyo maana sasa hivi tunaangalia jinsi gani tutafanya; kama ikiwezekana tuwe na akaunti maalum ya Mfuko katika Halmashauri ili tuweze kui-monitor vizuri; ili zikiingia zinazorudi kutoka kwa watakaokopa tuweze kuisimamia vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni wazo zuri tutaendelea kuchukua yote haya ili hatimaye tuboreshe Mifuko hii iweze kuwasaidia vijana na akinamama na hatimaye tutatengeneza ajira kwa wananchi wetu.
MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona. Kwa kuwa uwezo wa Halmashauri unatofautiana na Halmashauri nyingine ni duni kabisa hazina kipato zikiwepo Halmashauri za Hai, Siha, Rombo na kwingineko; je, Serikali ina mpango gani sasa wa kufanya top up ili nia yao njema ya kuwezesha wanawake na vijana ifanane Tanzania nzima?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo la mama ni zuri, Halmashauri zingine pato lake ni dogo lakini kutokana na wazo hilo zuri ndiyo maana Serikali ina mifuko mingine ya ku-top up. Kuna Mfuko kutoka katika empowerment programu yetu ambayo inasaidia na tuna fedha nyingi sana hapa, takribani kuna Mifuko 17.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo ni wazo zuri lakini Serikali imeshachukua initiative tayari, Mifuko hiyo ipo, isipokuwa jamii yetu wakati mwingine hawana taarifa sahihi kuhusu mifuko hiyo. Ndiyo maana sasa wakati programu hii inaendeshwa hapa Dodoma takribani mwezi mmoja uliopita uwezeshaji huo umeshatolewa na tumewaelekeza sasa Maafisa wetu wa Maendeleo ya Jamii waweze kushuka katika grassroot ili kuweza kuwaelimisha wananchi ni wapi watapata hizi fedha na uwezeshaji ili kujiinua kiuchumi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni wazo zuri na Serikali hivi sasa inaendelea ku-top up isipokuwa Maafisa Maendeleo ya Jamii wafanye kazi yao sasa kuhakikisha jamii sasa inapata uelewa wa kutosha juu ya mifuko hii ili waweze kupata uwezeshaji wa kutosha.
MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri. Hivi vituo vilianza miaka mingi sana, sasa hivi ni miaka tisa bado havijakamilika na mimi swali langu nimesema ni lini sasa Serikali itamaliza ujenzi huu kwa sababu umechukua muda mrefu sana? Hilo ni swali la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imesema itapeleka Sh.35,500,000 na imeshapeleka Sh.8,000,000 tu, bado Sh.24,000,000 bado. Je, ni lini Serikali sasa itapeleka hii fedha Sh.24,000,000 ili ujenzi ule ukamilike? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge, tulipokuwa kule site; miongoni mwa maeneo tuliyotembelea ni Sekta ya Afya katika Jimbo lake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli hivi sasa imepelekwa shilingi milioni nane, bado takriban shilingi milioni 24. Hata hivyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge; hivi leo asubuhi nilikuwa naongea na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, Bwana Shemdoe. Katika mambo ambayo tumekubaliana ni kwamba atenge fedha kwa kadri inavyowezekana kuhakikisha vituo hivi vinakamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua wazi kwamba Jimbo la Mufindi Kusini ni miongoni mwa Halmashauri tajiri ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Rasilimali walizonazo zikisimamiwa vizuri tutaweza kufanya vitu vingi zaidi. Kwa hili Mkurugenzi amenipa commitment leo hii asubuhi wakati naingia getini, amesema kwamba atashirikiana na Waheshimiwa Wabunge ahakikishe miradi yote ambayo bado haijakamilika watumie fedha, own source, wakamilishe miradi yote wasiwe na viporo tena vinavyoendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itasimamia vizuri, lakini kwa sababu na wao wamejipanga vizuri, yeye na Mheshimiwa Mgimwa, nadhani hakuna kitu kitakachoharibika katika Halmashauri yao kwa sababu ni miongoni mwa Halmashauri tajiri, own source yao ni kubwa kuliko jambo lingine lolote.
MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Nami naomba kuuliza swali dogo la nyongeza. Hospitali ya Mji wa Mafinga inahudumia Halmashauri mbili za Wilaya ya Mufindi na Mji wa Mafinga. Hata hivyo, katika fedha za Basket Fund, Halmashauri ya Mji wa Mafinga inapokea kiasi kidogo kiasi kwamba inaathiri utendaji wa Hospitali ya Mafinga ambayo inahudumia Halmashauri zote mbili. Je, ni lini Serikali itaongeza fedha za Basket Fund kwa ajili ya Hospitali ya Mji wa Mafinga ambayo inahudumia halmashauri zote mbili? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, anachosema Mheshimiwa Chumi, siyo jambo la uongo. Ni kweli Halmashauri ya Mafinga pale ukiangalia ule Mji, wananchi wa Mufindi wote wanakuja kutibiwa pale Mafinga. Bahati mbaya ukifanya comparison; ulinganifu wa Basket Fund ya Mafinga na Mufindi, Mafinga Basket Fund yao ni ndogo, lakini wagonjwa wote wanakuja kutibiwa Mafinga. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, scenario hiyo iko sambamba na kule Tarime, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Halmashauri ya Tarime nanii, kwamba ya Mji ina fedha kidogo, lakini Halmashauri hii ina fedha nyingi lakini ha-top up nanii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge, maeneo ambayo Halmashauri haina Hospitali ya Wilaya lakini kuna hospitali mfano ya Taasisi ya Dini, wanatumia kituo kile kama DDH na wanapeleka fedha. Sasa tujiulize, kama watu wa Mufindi hawana hospitali, wanatumia Hospitali ya Mafinga na kama wangekuwa hawana Mafinga, maana yake kungekuwa na hospitali ya private pale ya DDH, wangeitumia kama hivyo na kupeleka fedha. Kwa nini hapa msikae sasa kufanya harmonization ya jambo hilo kulifanya liwe vizuri?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuseme kwamba jambo hili tumelichukua na nitalikabidhi katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa dada yangu Mheshimiwa Ummy Mwalimu, tutaangalia nini tufanye. Lengo kubwa ni kwamba mwisho wa siku, Halmashauri ya Mafinga na Hospitali ya Mafinga iweze kujiendesha vizuri kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wale. (Makofi)
MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kama lilivyo swali la msingi, kwenye Jimbo langu la Kyerwa, wananchi wameanzisha vituo ambavyo wameshaanza ujenzi, wamefika kwenye kumalizia boma. Kwa mfano, kama Kata yangu ya Kimuri, kuna wananchi ambao wamejenga boma limefikia kwenye lenta na wameweza kujenga maboma zaidi ya kumi. Maboma haya yamekaa karibu miaka saba. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha maboma haya? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka nikupe taarifa, Mheshimiwa Bilakwate anapoishi kwake pale wakati mwingine ninapofika pale hata mtandao wa simu anapata nchi ya Rwanda. Bahati mbaya hana Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, licha ya suala hili la maboma, kutokana na ombi lake tumeamua kujenga theater sasa na sehemu ya kupasulia wagonjwa pamoja na kupata huduma nyingine katika Kituo chake cha Afya cha Mulongo. Tumefanya hivi ili eneo lake liweze kupata huduma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tumefanya assessment ya maboma yote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, jinsi gani tutayamalizia, yale ya Vituo vya Afya na Zahanati, takriban shilingi bilioni 950 zinahitajika. Katika mwaka huu wa bajeti tumeshatenga karibu shilingi bilioni takriban 95. Lengo kubwa ni kuhakikisha tunamalizia hivi viporo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Local Government Capital Development Grant, tumetenga karibu shilingi bilioni 251, karibu one third ya fedha hizo zinakwenda katika suala zima la umaliziaji wa maboma. Kwa hiyo, nawaagiza Wakurugenzi wote wakiwemo na wa Halmashauri yake; inapofika ile fedha, naomba tuweke mgawanyo mzuri wa jinsi gani tutakavyomalizia maboma haya na siyo ya afya peke yake, hata katika Sekta ya Elimu. (Makofi)
MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Mheshimiwa Naibu Waziri, mapema mwaka huu alifanya ziara katika Mkoa wa Arusha hususan katika Jimbo la Monduli na akatembelea Vituo vya Afya vya Makuyuni na Kigongoni. Vituo hivyo vilianza kujengwa kwa nguvu za wananchi na kufikia kwenye lenta na aliahidi kuvimalizia mapema mwaka huu au mwaka kesho. Naomba maoni ya Mheshimiwa Waziri, je, ni lini atatoa fedha hizo za kumalizia Vituo hivyo vya Afya vya Jimbo la Monduli? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli siku ile nilifika Arusha, nikafika Monduli na priority yetu ni kwamba tumeitenga pale na commitment tuliyoifanya ni kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Mto wa Mbu ambapo tumezungumza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, nimewapongeza wananchi kwa juhudi kubwa wanayoifanya katika suala zima la ujenzi wa Vituo vya Afya. Kwa hiyo, ni commitment ya Serikali na tuko katika michakato ya aina mbalimbali, tutaweza kukamilisha mambo haya kwa kadri inavyowezekana.
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Katika Jimbo la Serengeti, Vituo vya Afya vya Iramba na Nata vimetengewa fedha kwenye mwaka huu wa bajeti pamoja na Hospitali ya Wilaya ambayo imetengewa shilingi milioni 700. Leo ni tarehe 21, tarehe 30 mwaka wa fedha huu tulionao unaisha; na Mheshimiwa Waziri alipokuja pale Jimbo la Serengeti, alituhakikishia kwamba fedha zitakuja. Nini tamko lake kuhusu fedha hizi kutokufika mpaka sasa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nilikuwa na Mheshimiwa Ryoba Jimboni kwake na tulitembelea ile Hospitali ya Wilaya, nami nilikuwa najua kwamba jana ndiyo angeunga mkono Bajeti ya Serikali kwa sababu ndiyo fedha zenyewe hizi zinazopelekwa kwa wananchi. Sasa tunapokuja site pale tunakubaliana fedha ziweze kwenda, tunapokuja huku katika kupitisha mafungu wenzetu mnasusa hamtaki kupitisha, sio jambo zuri. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Serikali, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Ryoba, tumekwenda pale tumeona matatizo ya wananchi. Sawa! Suala la fedha tutakwenda kulitekeleza na kama tulivyoongea kwa kirefu zaidi, pale ukiangalia kupitia Ofisi yetu na Wizara ya Afya katika lile jengo la pale Mugumu tunafanya ile two in one sword, tutafanya lile na wananchi watapata huduma. (Makofi)
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Jimbo la Buyungu, Wilaya ya Kakonko tumepata ufadhili wa kujengewa vituo vya kisasa vya baba, mama na mtoto kutoka Bloomberg, USA. Ni vituo vya kisasa kabisa. Sasa nataka commitment ya Serikali, vituo vile vinawekewa vifaa vya kisasa na vinahitaji wataalam wa kisasa. Je, Serikali iko tayari kuleta wataalam baada ya vituo hivyo kukamilika?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli Kakonko ni eneo ambalo linapata changamoto kubwa sana. Ndiyo maana siku ile nilivyokuwa naongea na watumishi wetu pale Kakonko mpaka kama binadamu unajisikia huzuni kwa cost load waliyokuwa nayo, ni kubwa zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie, kwa sababu Serikali ipo katika mpango wa kuajiri watumishi wengi; na najua katika Mkoa wa Kigoma tumepeleka watumishi wapatao takribani tisa au 12, kati ya hapo tu kwa Mkoa mzima wa Kigoma, lakini mahitaji ni makubwa zaidi. Ngoja mchakato huu sasa wa ajira hizi mpya utakapotoka tutaangalia jinsi gani tusaidie wananchi wa Kakonko pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili siyo kwa Kakonko peke yake na Mkoa wa Kigoma wote kwa ujumla kwa sababu kuna changamoto kubwa ya wakimbizi, kwa hiyo, huduma inakuwa ni tight sana. Kwa hiyo, lazima tutalichukua jambo hilo; Kasulu, Kakonko, Kibondo, Uvinza na sehemu nyingine, kutoa kipaumbele kwa Mkoa wa Kigoma. (Makofi)
MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru Serikali kwa hatua hiyo. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; tangu mwaka 2016 mpaka sasa hakuna ongezeko lolote la mshahara kwa watumishi. Serikali inatoa tamko gani kwa watumishi hawa ambao wamekuwa na moyo mkubwa sana wa kujitolea?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; tangu mwaka 2016 mpaka sasa hakuna kupandishwa daraja kwa mtumishi yeyote hususan Mwalimu. Je, Serikali itakuwa tayari sasa kulipa malimbikizo ya mshahara kwa Mtumishi ambaye alistahili kupanda mwaka 2016 mpaka sasa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tukifanya rejea ya takriban siku mbili, Mheshimiwa Waziri anayehusika na mambo ya Utumishi (Waziri wa Utumishi na Menejimenti ya Utumishi wa Umma) alitoa maelekezo hapa kwamba katika hoja yetu ya Bajeti Kuu ilivyokuwa inapita watu walikuwa wanasema kwamba kwa nini sasa fungu hili la mshahara halipo?
Mheshimiwa Naibu Spika, tukumbuke kwamba Mheshimiwa Rais alizungumza wazi alipokuwa katika viwanja vya Mkoa wa Kilimanjaro katika siku ya Mei Mosi. Jambo hili limezingatiwa katika bajeti yetu hii tunayokwenda nayo hivi sasa. Ndiyo maana hata juzi Waziri wa Utumishi wa Umma alikuwa anatoa maelekezo kwamba kuna nyongeza ya fedha hapa ambayo itaenda ku-address jambo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la kupanda madaraja, hali kadhalika eneo hilo madaraja yalisimamishwa kutokana na zoezi maalum la uhakiki hasa wa vyeti feki na watumishi hewa. Vile vile naomba nifanye rejea ya Waziri wetu wa Utumishi wa Umma alipozungumza wazi kwamba suala la kupanda madaraja sasa limewekewa utaratibu mzuri, kila mtu atapanda kwa stahiki yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaambie kwamba kila mtu atapata stahili yake kwa kadri inavyotakiwa na hili Mheshimiwa Waziri amelizungumza wazi kwa sababu yeye ndiyo anahusika na Utumishi kwamba kila mtu atapata stahiki yake na jambo hili sasa hivi linakamilika na kila mtu atapanda daraja kama ilivyokusudiwa. (Makofi)
MHE. MUSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Moja ya matatizo ya Walimu wetu ni kukosa makazi katika maeneo wanayofundishia katika vijiji vyetu. Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba inajenga nyumba za kutosha kwa Walimu wetu ili kuwapa motisha kufundisha vizuri katika maeneo yetu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la kuimarisha miundombinu hasa kwa Walimu, ni kweli tumekuwa na changamoto ya nyumba, ndiyo maana hata baadhi ya Watumishi wengine wakishaajiriwa wanakumbana na changamoto kubwa sana ya makazi. Ndiyo maana toka mwaka 2016 katika Sekta ya Elimu tulitumia fedha nyingi takriban shilingi bilioni 64 kujenga miundombinu ya madarasa, vyoo na nyumba za Walimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, tulifanikiwa katika Shule ya Sekondari; mpango wa MMES II tumejenga nyumba takriban 283. Hata hivyo, naomba nishukuru sana Waheshimiwa Wabunge na wadau mbalimbali. Tumeshiriki kwa pamoja kujenga nyumba katika maeneo mbalimbali, lakini hata hivyo, katika mpango wa Serikali, mwaka huu tutaenda kushirikiana tena na wadau na fungu letu la Serikali kuhakikisha tunaongeza idadi ya nyumba. Lengo kubwa ni Walimu wetu na wataalam mbalimbali ambapo sio kada ya Walimu peke yake, waweze kupata makazi bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, najua hii bado ni changamoto kubwa, lakini naomba tushirikiane kwa pamoja, na Serikali imeweka nguvu za kutosha kuhakikisha kwamba tunajenga nyumba za Walimu na wa kada nyingine katika maeneo mbalimbali.
MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza na ninalo dogo sana. Naomba niseme kwamba Serikali isituambie hapa kama vile inaanza upya.
Mheshimiwa Naibu Spika, taratibu zote hizi za kupandisha vyeo na mengineyo yalikuwepo kabla; lakini sasa hivi kilichotokea kibaya, kuna watu walipandishwa cheo wakalipwa mshahara mpaka miezi mitatu, wakasitishiwa mshahara, wakarejeshwa pale pale. Hivi Mheshimiwa Waziri anatoa kauli gani kuhusu hili? Naomba nijibiwe kwa ufasaha zaidi ili watu waweze kufuatilia. Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nashukuru sana maana ningekosa kupata hili swali, roho ya mama yangu Mheshimiwa Riziki ingepata shida sana kwa sababu nilikuwa namwona hapa, hasa nikijua mama yangu ni Mwalimu, kwa hiyo, alikuwa anataka kujua katika kero hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimwambie kwamba; bahati nzuri juzi nilipata viongozi wa Chama cha Walimu kutoka Mkoa wa Rukwa, nilikuwa nao pale ofisini na hiyo ni miongoni mwa concern ambayo waliileta pale ofisini kwetu. Ni kweli kuna watu ambao walipata mishahara ile miezi miwili, lakini baadaye mshahara ukakasitishwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa changamoto kubwa ni kwamba kuna wengine wanaenda kustaafu. Sasa wakistaafu jambo hili linafanyika vipi? Leo hii mtu akistaafu atahesabiwa katika mshahara wa mwanzo wakati alipanda. Ndiyo maana nimesema jambo hili, kama Serikali, tumelichukua kwa uzito wa hali ya juu, tunafanya analysis. Kuna watu wengine ambao watastaafu hivi karibuni. Ina maana tusipo-address vizuri tutakuwa na changamoto kubwa katika hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna watu wengine walipanda, lakini kwa sababu ya utaratibu mzuri uliowekwa naomba niwaondoe hofu Waheshimiwa Wabunge, jambo hili tumelichukua sisi kama viongozi na tumelijua ni tatizo kubwa, lazima tuliweke vizuri. Yalifanyika kwa nia njema kwa sababu huko nyuma hali yetu ilikuwa siyo shwari. Suala zima la watumishi hewa lilikuwa ni jambo kubwa, watumishi takriban 19,000 plus, lilikuwa ni tatizo kubwa sana!
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mpango huu ulikuwa ni mpango mkakati wa Serikali kusaidia kulinda mapato, lakini kupeleka fedha kwa watu wanaostahili . Kwa hiyo, naomba niwatoe hofu wafanyakazi kwamba kila mtu atapata stahili yake na Serikali inafanya kazi kufanya analysis kwa undani zaidi kuondoa hilo tatizo.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa niulize swali la nyongeza. Katika jibu la msingi la Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba Teaching Allowance ipo kwenye mshahara. Sasa tunapata tabu sana tukikutana na Walimu wanapotuambia juu ya kurudisha Teaching Allowance. Je, Serikali itakuwa tayari sasa kutamka ndani ya Bunge hili ili waweze kutambua kwamba Teaching Allowance yao iko kwenye mshahara?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo kubwa tulilokuwa nalo ambalo Waheshimiwa Wabunge wengi sana hapa leo wanalizungumza ni suala zima la maslahi mapana ya watumishi. Ndiyo maana hata hicho kilichokuwepo kama kidogo au kikubwa hakioneshi vizuri ni kwa sababu huenda lile fungu lenyewe, purchasing power imekuwa ni ndogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kupitia Ofisi ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma, juzi juzi kulikuwa na kikao maalum kinafanyika kwa sababu kunaundwa bodi maalum ya kuja kupitia maeneo yote hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukiacha Teaching Allowance, kuna mambo mengine; kuna suala la haki za watu wanaofanya kazi katika mazingira magumu. Kwa hiyo, jambo hili tutakuja kulitamka rasmi sasa baadaye kuhusu mchakato huu unavyokwenda. Hiyo Bodi iliyoundwa sasa kupitia mishahara, siyo kwa Walimu peke yake, isipokuwa watumishi wote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tutaona jinsi gani kila mtumishi atapata stahili yake na nyongeza kwa kiasi gani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hili tutakuja kulitoleaa tamko rasmi hapa baadaye Bungeni likiwa katika utaratibu mzuri baada ya kutoa hii documentation vizuri.
MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kuna shule Shikizi nyingi ambazo zina Walimu wa kujitolea na hawapati posho. Je, ni lini Serikali itaanza kuwalipa posho hawa Walimu wanaofundisha kwenye Shule Shikizi? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, katika jambo hili nadhani kila Halmashauri ina mkakati wake ku-address matatizo ya watumishi katika maeneo mbalimbali; na kuna baadhi ya maeneo mengine utakuta watu wanatumia own source kuonesha jinsi gani wana-address hili jambo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu kuna mambo specific katika eneo la Mheshimiwa Njeza, tutalichukua halafu tuangalie jinsi gani tutafanya kuona nini kimetokea huko ilimradi tuliweke sawa ili kila mtu apate stahiki yake. Kama kuna maeneo mahususi katika Halmashauri husika, basi tutayatoa kwa lengo la kuweka mustakabali mzuri katika maeneo yetu hayo.
MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kuuliza swali dogo tu la nyongeza. Kwa kuwa, pesa hizi za Mfuko wa Barabara zinapelekwa kidogo kidogo, kwa mwezi au baada ya miezi kadhaa. Je, Serikali haioni kuna sababu sasa ya kupeleka fedha hizi kwa mkupuo ili Halmashauri iweze kupangilia vizuri ujenzi na ukarabati wa barabara zake kwa umakini zaidi kuliko hivi sasa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo ni zuri lakini kama mnavyofahamu tunakwenda kwa utaratibu wa cash budget, kadri tunavyopata, tunavyokusanya pesa hizi za barabara ndiyo tunazipeleka hivyo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba aondoe hofu Serikali itajitahidi kwa kadri iwezekaavyo na kwa sababu tumejielekeza vizuri katika makusanyo ya mapato, nina imani katika Jimbo lake na najua kwamba katika Mji wake wa Mwasa ana ahadi ya ile barabara ya Mheshimiwa Rais ya kilometa tatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka huu barabara hiyo tumeiingiza katika mpango wa bajeti barabara ile ya one point something billion itaingia pale. Kwa hiyo, naomba niwahakikishie kwamba tutajitahidi kukusanya fedha na kuhakikisha kwamba commitment zote za Serikali tulizoziweka ziweze kutekelezeka katika Majimbo.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza. Swali hili linafanana kabisa na vituo vya afya vya Mima na Mbori ambavyo havijakamilika sasa ni zaidi ya miaka 10 lakini naishukuru Serikali kwamba mmetenga fedha kwa ajili ya kukamilisha vituo hivyo. Sasa Mheshimiwa Waziri utakuwa tayari kutembelea kuona ujenzi wa kituo cha afya - Mima na kituo cha afya cha Mbori?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa kuna mpango wa kujenga kituo cha afya Chunyu na eneo la Chunyu lina idadi ya watu wengi, je, mpango huu umefikia wapi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lubeleje, greda la zamani makali ya yale yale kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, niko tayari kutembelea kituo cha afya Mima na Mbori, tumekubaliana na Mheshimiwa Mbunge licha ya vituo hivi vya afya, tutakwenda kutembelea na miundombinu ya barabara katika Jimbo lake ambalo kwa kweli lina mtandao mkubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, katika kituo cha afya hicho ambacho ameuliza kwamba mpango ukoje, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tukishafika site sasa japo tutatembelea vituo hivi vya afya viwili, lakini ni vema tutembelee na kituo cha afya hiki kipya ambacho kiko katika mpango wa ujenzi halafu pale tutajadiliana kwa pamoja nini tufanye ili wananchi wa kituo hiki kiweze kujengwa na wananchi wa eneo lile waweze kupata huduma.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri swali moja dogo la nyongeza. Kwa kuwa, wananchi wa Kata ya Usinge Wilaya ya Kaliua wanakwenda Nguruka kwa sababu Kata ya Usinge ambayo ni kubwa sana ina wananchi wengi na ni center ya biashara haina kituo cha afya, ina Zahanati moja ndogo kiasi ambapo inasababisha watu waende kule Nguruka ambapo ni mbali sana karibu kilometa 40 kwenda pale Nguruka. Je, Serikali ina mpango gani sasa kuhakikisha ule mpango wake wa kujenga kituo cha afya Kata ya Usinge unaanza haraka ili kupunguza msongamano wa wananchi wanaokwenda kuhudumiwa katika Kata ya Nguruka? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Kata ya Usinge ina changamoto kubwa na ukiangalia population pale ni kubwa sana, wakati ukitoka Kigoma pale ukipita unaona kweli kuna haja. Naomba niseme kwamba Serikali tumelichukua hili, tutahakikisha tunafanya kila liwezekanalo eneo lile kujenga kituo cha afya ili wananchi waweze kupata huduma.
MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kuna mpango wa kujenga vituo vya afya 100 ambao tumeusikia kwa muda mrefu sana na mojawapo ni kituo cha kwangu cha Mgeta. Sasa ningependa kujua ni kigugumizi gani kipo mpaka sasa vituo vile havijaanza kujengwa wakati hela imetoka muda mrefu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tuna mpango wa ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya na miongozi mwa vituo hivyo ni Kituo cha Afya cha Mgeta. Naomba niwaambie kwamba mchakato sasa uko katika suala zima la evaluation, tulikuwa katika tendering process kwa sababu tuna vituo vingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge katika kipindi hiki cha mwezi wa Julai wataona ujenzi unaendelea katika maeneo mbalimbali ya vituo vile 100; then tutakuwa na program nyingine ya ujenzi wa vituo vipatavyo 42. Kwa hiyo, kuanzia mwezi wa Julai wananchi wa Mgeta watarajie kwamba, ujenzi katika eneo lao utaanza mara moja.
MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa kituo cha afya cha Manonga kimekamilika na kwa kuwa mpaka sasa vifaa havijapelekwa. Je, ni lini sasa Mheshimiwa Waziri watapeleka vifaa hivyo kwa ajili ya wodi ya upasuaji?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kituo cha afya cha Manonga kimekamilika na nakumbuka vituo vile vilikuwa ni miongozi mwa vituo ambavyo tumetengeneza kwa African Developmnet Bank na vituo vile tulitengeneza pale Bukene katika Mkoa wake, hali kadhalika hapa Itogo, lakini bahati mbaya Manonga vifaa vilikuwa havijafika, hata kwa ndugu yangu Mheshimiwa Cecil Mwambe pale kulikuwa na kazi tumefanya katika kituo cha Chiwale, vinafanana katika kesi kama hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Manonga kulikuwa na kesi maalum kwamba vifaa havikufika na kwa sababu jambo lile lilikuwa na bajeti yake maalum, naomba niseme kwamba tunalichukua na tutalifanyia kazi kwa haraka sana kwa sababu bajeti yake ilikuwepo ili vifaa vile viweze kufika, wananchi wa Manonga waweze kupata huduma kama ilivyokusudiwa katika mradi ule.
MHE. GIBSON B. OLE MEISEYEKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nirekebishe jina langu tu naitwa Gibson Blasius Ole Meiseyeki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni kulikuwa na zoezi la ubomoaji uliofanyika katika shamba la Mheshimiwa Mbowe katika Wilaya ya Hai. Je, ofisi yako ilibariki tukio hili?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa, Arumeru Magharibi kuna mashamba mengi ya wawekezaji ambayo kiuhalisia yamejengwa kwenye maeneo ambayo pia ni vyanzo vya maji na wananchi wanakusudia kwenda kuisaidia Serikali kuondoa mashamba hayo ambayo kimsingi yanaharibu vyanzo vyetu vya maji. Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusiana na nia hii ya wananchi ya kuyaondoa mashamba yote ambayo yako kwenye maeneo ambayo hayaruhusiwi kwa mujibu wa taratibu. (Makofi.) Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais –TAMISEMI naomba kujibu swali la ndugu yangu Gibson, naomba niishie hapo hapo huko mbele majina ya kimasai yasije yakanichanganya zaidi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama suala la kubariki zoezi lililofanyika Katamba katika shamba la Mheshimiwa Mbowe, kwa sababu hili jambo ni specific sana na sijajua harakati za pale, sitaki kulitolea comment katika hilo. Naomba nizungumze hapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu wananchi wapo tayari sasa kushirikiana na Serikali, kuhakikisha kwamba inashirikiana vizuri kwenda kuondoa wale wananchi au mashamba yaliyopo katika eneo husika. Tukifanya rejea jana kulikuwa na mkutano mkubwa sana wa Waziri wa Mazingira na wadau kule katika Mkoa wa Iringa. Bahati nzuri niwashukuru baadhi ya Wabunge hasa katika Mkoa wa Iringa walikuwa katika mkutano ule, kuna mambo mahsusi yalijadiliwa katika suala la hivi vyanzo vya maji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, maelekezo yangu ni kwamba Wakurugenzi wote wameelekezwa utaratibu wa kufuata sasa katika vyanzo hivi vya maji. Imani yangu kubwa wazo hilo lake lililokuwa jema na kwa sababu tuna timu kule katika ngazi ya Mkoa na katika ngazi za Halmashauri, ukichukua na combination ya mawazo mazuri ya mkutano wa jana uliofanyika katika Mkoa wa Iringa, naamini litaenda kufanyika jambo sahihi kwa mujibu wa taratibu jinsi hali halisi ilivyo kule katika Mkoa wa Arusha hasa Arumeru.
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria inasema mwambao wa Ziwa Tanganyika ni mita 60, lakini kuna upendeleo wa hali ya juu hasa kwenye Kijiji cha Kilando, wanavunjiwa watu na baadhi hawavunjiwi ambao wako chini ya hiyo kiwango cha mita 60. Je, Mheshimiwa Waziri anatoa tamko gani kuhusu wananchi wanaokaa mwambao mwa Ziwa Tanganyika kuacha upendeleo, kuvunjiwa baadhi ya watu na wengine kuachwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hii sheria au utaratibu huu kwanza lengo lake kubwa ni kuhakisha tunalinda vyanzo vyetu vya maji. Leo hii katika nchi yetu maeneo mbalimbali, maeneo chepechepe, maeneo oevu, yote yanatoweka kwa sababu kuna uvamizi mkubwa sana na ndio maana tunakumbwa na janga kubwa na ukosefu wa maji katika maeneo yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, imani yangu kwamba, sheria itafuatwa hasa na Watendaji wetu wa chini, tusifanye double standard katika maeneo mbalimbali. Lazima kama tunafuata sheria utekelezaji wa sheria kwa sababu tunasema sheria ni msumeno, lazima ufuate hakuna kusema kumwonea mtu huyu na unamuacha mtu huyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo naomba nimhakikishie Mheshimiwa Keissy kwamba wataalam wetu tutawaelekeza kwamba wanapokwenda kutekeleza sheria, lazima waache utaratibu wa double standard ili sheria itekelezwe kwa haki katika nchi yetu.
MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa lengo la Serikali ni kufanya vyanzo vya maji viendelee, lakini wanapowazuia wananchi kutolima kwenye vyanzo vya maji Serikali haiwapi mkakati wala kutengeneza eneo mbadala la kulima vyakula hivyo ikiwemo Mkoa wa Rukwa. Je, ni nini mkakati wa Serikali kabla haijawazuia kuwaandalia eneo mbadala la kuendelea na mazao hayo wanayolima? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli nafahamu, Mheshimiwa Aida ametoka Ziwa Rukwa, katika nchi yetu miongoni mwa Maziwa ambayo yapo hatarini kutoweka zaidi ni katika Ziwa letu Rukwa ambalo linaonekana sasa, wataalam wetu wanasema ukifanya tathmini miaka ishirini iliyopita na hivi sasa hali iko tofauti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa Serikali jambo la kwanza ni kuhakikisha kwamba tunatoa elimu. Maana leo hii tunapozungumza wengine ndio wanaenda kuvamia vyanzo vya maji, kwa hiyo mkakati wa kwanza ni kutoa elimu. Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili tutawaelekeza wataalam wetu hasa jinsi gani wafanye, kuwabainisha wananchi waweze kutafuta fursa nzuri kwa sababu nchi yetu bado kuna maeneo na fursa kubwa katika suala zima la kilimo. Kwa hiyo jambo hili naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutalifanya, lakini kwanza ni elimu, watu wafahamu nini maana ya chanzo cha maji na nini athari yake chanzo cha maji kinapoharibika.
MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na namshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Serikali imekiri kwamba kuna dhuluma sana miongoni mwa wananchi wetu, ni lini sasa Serikali itachukua hatua kwa sababu kuna matukio mengi sana ambayo siwezi kuyaorodhesha hapa, yako kule kwenye Jimbo la Igunga ambapo wananchi wengi sana wamedhulumiwa. Ni lini sasa Serikali itachukua hatua hizo badala ya kutoa onyo tu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa kwenye Kijiji cha Lugubu, kijiji kiliamua kutenga eneo moja kuwa eneo la hifadhi, lakini kwa bahati mbaya baadhi ya watendaji waliwaruhusu wananchi wawili waingie kwenye hilo eneo na kukazuka mgogoro mkubwa sana wa ardhi ambao Mahakama ya Ardhi na Mahakama ya Mwanzo wameshindwa kuurekebisha huo mgogoro. Je, ni lini sasa Serikali itatusaidia jambo hili ili tuweze kutenga eneo katika Kijiji hicho cha Lugubu? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwamba lini tutaanza kuchukua hatua naomba nikuhakikishie kwanza naomba ikiwezekana atupe orodha sasa hivi, kama kuna watu wa aina hiyo basi tuanze kuelekeza mara moja jinsi gani watu ambao wanakwamisha haki za watu ambao wanadhulumu kwa makusudi na wao wamepewa dhamana tuweze kuwachukulia hatua. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba nimsihi kama ana orodha sasa hivi naomba aikabidhi kwangu tuweze kuifanyia kazi haraka iwezekanavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo lingine katika Kijiji cha Lugugu ambalo amezungumza kwamba kuna eneo la kijiji limetengwa lakini kuna watu wawili wamekabidhiwa eneo hilo, eneo ni mali ya kijiji, kwa kweli inatia huzuni. Katika hili naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutalifanyia kazi. Naomba nimwelekeze Mkuu wetu wa Wilaya ya Igunga aweze kufanyia uchunguzi wa haraka katika eneo hilo kipi kinachojili ili mradi mwisho wa siku haki ya wananchi iweze kupatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, jambo hilo halitavumilika hata mara moja na kwa vile nimekubaliana na Wabunge wa Mkoa wa Tabora kwamba nitakwenda Mkoa wa Tabora lakini nitakuwa na interest ya kufika eneo hilo kwenda kujua ni ubadhirifu gani unaofanyika ambao unanyima haki za watu, lengo kubwa tuhakikishe wananchi wanapata huduma inayotakiwa. (Makofi)
MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwa kuwa kukosa fedha za kuendeshea shughuli za Mabaraza ya Ardhi ya Kata ni kichocheo kikubwa sana cha rushwa kinachopelekea wananchi wengi kunyimwa haki zao za msingi. Sasa Serikali haioni sababu na umuhimu sasa itoe ruzuku kwa Mabaraza haya ili yaweze kuendesha shughuli zake na kuondoa uwezekano wa kuchukua rushwa? Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwa kesi kubwa nyingi sana kuja kuziangalia hata maamuzi mengine yanakuwa yanasababishwa na baadhi ya wale ambao wako katika Mabaraza ya Kata. Wakati mwingine inaonekana kwamba mtu aliyenacho ndiyo huyo ambaye haki inamwendea, hili ndiyo maana Serikali ilikuwa inafanya tathimini kwa kina sana kuangalia nini kifanyike katika suala zima katika uendeshaji wa Baraza la Kata.
Mheshimiwa Naibu Spika, wazo la Mheshimiwa Mbunge tunalichukua lakini kuna mchakato mpana tunaufanya kuona jinsi gani tutaboresha haya Mabaraza ya Kata yaweze kufanya kazi vizuri zaidi kulinganisha na hivi sasa kwa sababu haki nyingi za watu zinapotea kwa sababu haki haisimamiwi vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, wazo hili tunalichukua, lakini tunajumuisha miongoni mwa mambo ya kufanya restructuring tuifanyeje, lengo kubwa la Mabaraza hayo yaweze kufanya vizuri, kwa hiyo, ni wazo zuri tunalichukua kama Serikali kulifanyia kazi kwa mpango.
MHE. ALHAJ ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kama alivyojibu mjibu swali, kwa kuwa hawa Wazee wa Mahakama wanalipwa nafikiri Sh.5,000/= au Sh.7000/=. Je, huo mchakato wanaoufanya wanajiandaa kuongeza kiwango cha hawa Wazee kwa sababu ni kazi ya hiyari? Isije kuwa wanashindwa kwenda Mahakamani ndiyo maana haki inachelewa kupatikana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema hapa Mheshimiwa Bulembo kwamba tunachokifanya ni kufanya tathmini ya kina jinsi gani tutafanya kuhakikisha wananchi wanapata haki. Siwezi kusema kwamba kiwango hiki kitaongezeka kwa sababu kuna mambo mengi ndani yake yanaendelea hapa, isipokuwa kwamba tuamini Serikali inafanya kazi na mwisho wa siku ni kwamba miongoni mwa kuondoa kero nyingi za wananchi ni kushughulikia Mabaraza ya Kata, ili kulinda haki za watu kwa kuyashughulikia na kuyaunda vizuri Mabaraza ya Kata.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Serikali inafanya kazi hii hatima yake itakapofika, basi tutapata mwelekeo maalum wa Serikali wa jinsi gani jambo hili tunaenda kuli- handle vizuri kwa maslahi mapana ya wananchi.
MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa, sababu mojawapo ya utendaji mbovu wa Mabaraza ya Ardhi ni kwa sababu hawana weledi na mafunzo ya kutosha; na kwa kuwa pia Halmashauri ndiyo yenye jukumu la kuwapa mafunzo Wajumbe wa Mabaraza ya Ardhi na Halmashauri hizi hazina pesa, Serikali inaonaje kupiga marufuku Mabaraza ya Ardhi ambayo hayajapata mafunzo ya kutosha kufanya kazi yake mpaka hapo yanapokuwa yamepata mafunzo ya kutosha?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kupiga marufuku kwamba Mabaraza yasifanye kazi jambo hilo naomba niseme kwamba hatuwezi kupiga marufuku hapa, isipokuwa tunachotaka kufanya ni kwamba niwasihi hasa Wakurugenzi wa Halmashauri zetu zote 185 ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pale inapobainika kwamba kuna Mabaraza ya Kata ambayo uelewa wao ni mdogo katika utaratibu tunaokwenda nao katika kuyaboresha kipindi hiki cha mpito, lazima wahakikishe wanatumia ile staffing yao iliyokuwa katika Halmashauri kuona watafanyaje kuhusu capacity building kwa watu hawa, lengo kubwa waweze kutoa haki stahili.
Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni hoja ya msingi, kwa hiyo, hatuwezi kusitisha hivi sasa, lakini tutaendelea kuwasihi Wakurugenzi wetu wa Halmashauri zetu wafanye capacity building kwa kushirikiana na Wanasheria tuliokuwa nao, lengo kubwa likiwa, Mabaraza haya yaweze kufanya kazi kwa mujibu wa sheria.
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Niulize sasa maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa msimamizi wa mradi huu aliyejenga mradi wa maji wa Kijiji cha Ngomalusambo alijenga chini ya kiwango, ikiwa ni pamoja na kufunga pampu ya kusukuma maji ambayo haina uwezo na haikuwa stahili iliyokuwa imelengwa. Je, Serikali inachukua hatua gani kwa Mkandarasi na Msimamizi aliyejenga mradi huu chini ya kiwango na kuipotezea Serikali kiasi kikubwa cha fedha?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, miradi mingi ya maji imekuwa na tatizo ya usimamizi mbovu kiasi kwamba miradi inayoelekezwa haitengenezwi vizuri. Mfano pale Kijiji cha Majalila kulikuwa na mradi mkubwa wa maji ambao Serikali imetoa fedha nyingi lakini ilipangiwa kujengewa vituo vya maji 28 vikajengwa 12. Je, msimamizi wa mradi huu wanachukua hatua gani ili aweze kuwajibishwa.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika mradi wa Ngomalusambo kwamba imefungwa mashine ambayo iko chini ya kiwango siwezi kulizungumza hapa sasa, lakini kwa taarifa nilizozipata ni kwamba ule mradi ulianza lakini charging capacity yake kile kisima imekuwa kidogo, kwamba pampu inafungwa lakini ikisukuma maji sasa hivi wanasukuma takribani masaa 18 wanavyotumia diesel maana yake gharama inakuwa kubwa zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hizi ni taarifa ambazo nilizipata kwa wataalam wangu. Hata hivyo, concern aliyozungumza Mheshimiwa Mbunge naomba tuifanyie kazi, kwenda kufanya uchunguzi je, ni kweli kisima kimepoteza uwezo au pampu iliyofungwa haina uwezo. Maana yake mpango uliopo sasa hivi katika Halmashauri ya Mpanda ni kwenda kuchimba kingine kuhamisha ile mitambo iendelee kufanya vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kama Mbunge anasema pampu iliyofungwa haina uwezo basi hili maana yake ni jambo kubwa sana lazima tukalifanyie kazi na ikiwezekana tuunde Tume maalum kwenda kuchunguza kwamba kipi kinachojili katika eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hali kadhalika katika mradi wa Majalila na Mbunge anakumbuka siku ile tulivyofika pale tulikuta ule mradi upo idle pale katika Wilaya Tanganyika haufanyi kazi. Nikatoa maelekezo na nimepata taarifa mradi ule umeshaanza kufanya kazi, lakini inaonekana kwamba kuna changa la macho, badala ya vituo vya maji 24 vimefungwa 12 maana yake hapo kuna tatizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa matatizo hayo yote, kama hali ipo hivyo, Ofisi ya TAMISEMI hatuwezi kuridhika na hali hiyo. Naomba nimhakikishie tutaunda Tume maalum kutoka ofisini kwangu kwenda kufanya uchunguzi wa miradi hiyo miwili, lakini siyo hiyo miradi miwili na ile miradi mingine minne inayoendelea, kuweza kubaini kwamba ni tatizo gani linaendelea lengo kubwa tuweze kulinda fedha za Serikali na kuhakikisha wananchi wanapata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilio cha Mheshimiwa Mbunge kimesikika, tunaenda kukifanyia kazi kama tulivyofanya kazi Mkoa wa Geita na maeneo mengine.
MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Miradi ya World Bank, miradi ya maji mikubwa ya World Bank Kijiji cha Rungu, Wilaya ya Mbozi lakini pia kuna mradi mwingine Kijiji cha Ihanda tangu imezinduliwa na Mwenge miradi hii haijawahi kutoa maji. Sasa naomba niulize kwa nini miradi inazinduliwa na mwenge lakini haitoi maji?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, hapa hoja siyo miradi ya kuzinduliwa na Mwenge haitoi maji, nafikiri hoja ya msingi ni kwa nini mradi umezinduliwa lakini hautoi maji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika,i naomba niwasihi Wabunge sisi ni Wajumbe wa Kamati za Fedha, Wajumbe wa Baraza la Madiwani. Tusikubali hata siku moja, mradi ambao tunasimamia katika Kamati ya Fedha watu wanakuja kufanya kanyaboya, mradi unazinduliwa hautoi maji na wewe Mbunge upo, niseme kwamba jambo hili ni la kwetu sote. Mheshimiwa Haonga naomba niseme kwamba hili la kwetu sote hatuwezi tukakubali katika jambo hili, kama mradi huo hautoi maji na kwa vile tumekubaliana kwamba baada ya Bunge hili tunakwenda kupiga kazi ngumu Mkoa wa Songwe, tupitie huo mradi twende tukabaini kitu gani kinachoendelea hapo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho wa siku tulinde fedha hizi ambazo wananchi wana shida kubwa ya maji hatuwezi kukubali, sio mbio za mwenge peke yake isipokuwa kiongozi yoyote au mradi wowote unaozinduliwa ni lazima ufanye kazi kama unavyokusudiwa. Kwa hiyo, naomba nimsihi nikifika pale, hata kama ratiba yangu haijawekwa huko naomba aniambie kwamba Mheshimiwa Naibu Waziri ule mradi uko hapa, lazima tufike hapo site twende kuangalia nini kinaendelea.
MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo lililopo Ngomalusambo Wilayani Mpanda la mradi wa maji kukamilika lakini hautoi maji halina tofauti na mradi wa maji uliopo Wilayani Tunduru Kijiji cha Nandembo. Mradi ule ulitumia mamilioni mengi ya shilingi lakini mpaka hivi tunavyozungumza wananchi wale hawapati maji. Napenda kujua ni nini kauli ya Serikali katika kuhakikisha sasa huduma hiyo inapatikana ipasavyo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kuna sababu inawezekana mradi mwingine kwa mfano juzi juzi nilikuwa na ndugu yangu Kibajaji hapa katika Kijiji chake cha Manzase mradi umekamilika lakini tatizo kubwa lilikuwa ni suala zima la power, kwamba nishati ya aina gani iweze kutumika, kwa hiyo case by case hii miradi haitoi maji kwa sababu maalum. Inawezekana sehemu nyingine pampu hazijakamilika, hazijanunuliwa au mradi haufanyi kazi vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa case ya Mheshimiwa Mbunge, sifahamu mradi huo ukoje. Jambo ninalotaka kulifanya tukitoka hapa naomba anipe takwimu halisi ni kitu gani kinachoendelea pale tutoe maelekezo ya stahili nini kinachotakiwa kufanyika, kwa sababu najua miradi hii inakwama katika maeneo mbalimbali. Kwa hiyo Mheshimiwa Sikudhani naomba anijulishe baadaye kuna kitu gani pale kinachoendelea, tutoe maagizo mahsusi katika suala zima la mradi tuweze kuwasaidia wananchi wake waweze kupata maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo nilimwona Mheshimiwa Musukuma hapa akisimama kwa ajili ya mradi wake wa Changorongo, naamini alitaka kusimama kwa hoja hiyo. Mheshimiwa Msukuma kwa sababu tumekubaliana hapa miongoni mwa jambo tunalotaka kwenda kulifanya baada ya Bunge kutembelea ile shule ya msingi tutafika hapo kwa ajili ya kujibu lile swali kwa ajili ya wananchi wa Geita pale ambao muda mrefu tumewapigia kazi waweze kupata huduma inayostahili.
MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa tatizo la maji la Mpanda Vijijini linalingana kabisa na tatizo la mradi wa maji wa World Bank katika kata ya Mkako, Wilayani Mbinga lakini pia katika Kata ya Litola, Wilayani Namtumbo na Kata ya Luwiko, Wilayani Songea Mjini, naomba kujua kwamba miradi hii imeonesha tayari imekamilika kwa mujibu wa taarifa, lakini haitoi maji hata kidogo, kiasi ambacho inaleta tafrani kwenye maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasanaomba nijue kwamba je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuongozana na mimi katika Mkoa wangu wa Ruvuma kwenye maeneo haya niliyoyataja ili kuona hali halisi ya miradi hiyo na kuweza kuikamilisha ili wananchi, wanawake wote wa Mkoa wa Ruvuma kwenye maeneo hayo wapate maji?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kumjibu kwa haraka tu kwamba mimi nipo tayari. Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naomba…

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Naomba nitoe maelekezo mahsusi kwamba karibu maeneo mengi miradi hii ina matatizo. Naomba niwaagize Wakurugenzi wote wa Halmashauri zote 185 by tarehe 20 mwezi Julai tupate takwimu za miradi yote iliyokamilika ipi inatoa maji na ipi haitoi maji tuje na suluhisho la kusaidia wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, endapo tutaona kwamba, tumepata takwimu hiyo, baadaye tunaona kwamba, Mbunge analalamikia mradi fulani, lakini katika orodha haupo, tutajua kwamba, mradi ule umehujumiwa makusudi na Halmashauri husika. Kwa hiyo, hatutosita kuchukua hatua stahiki kwa watu wote ambao kwa njia moja au nyingine wameshiriki kuhujumu hii miradi, mwisho wa siku wananchi wanashindwa kupata huduma hii ya maji. (Makofi)
MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza kabisa napenda kutoa pongezi kwa Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri. Nina maswali mawili tu madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba ujenzi unaendelea, lakini unaendelea kwa kasi ndogo sana.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba wanatoa fedha kwa wakati na kuhakikisha ujenzi huo unaendelea kwa haraka ili ukamilike, kwa sababu watumishi wanapata shida sana kusafiri kutoka Bariadi hadi Ligangabilili?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, Serikali ina mpango gani juu ya kuikaribisha National Housing (Shirika la Nyumba la Taifa) kwenye Mkoa wa Simiyu kuweza kujenga nyumba za National Housing katika mkoa nzima yaani katika wilaya zake zote tano ili kuweza kuwasaidia wafanyakazi kupata makazi mazuri ya kuweza kuishi? Ahsante sana.
NABU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwa ajenda ya kasi ndogo ya utendaji wa kazi naomba nichukue concern hiyo, tutafanya follow up kuangalia ni kinachoendea. Nilifika pale Itilima, ni kweli changamoto kubwa ilikuwa ni tatizo la fedha. Tukaja kufanya uhangaikaji katika ofisi yetu ndiyo maana tukapata zile fedha nyingine zikaenda kule, ili kuweza kuongeza speed ya ufanyaji wa kazi pale. Vilevile tutawasiliana na wenzetu wa Itilima ili kuangalia kuna kitu gani ambacho kinakwaza. Nia ni kuongeza speed ya utendaji wa kazi ili hatimaye wananchi na hasa watumishi wa Itilima waweze waweze kukaa katika mazingira rafiki.
Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la National Housing kuweza kukaribia katika Mkoa wa Simiyu kwa ajili ya kujenga nyumba; ni wazo nzuri, na niwashukuru sana wenzetu wa National Housing wamekuwa wakishiriki ujenzi wa nyumba katika maeneo mbalimbali. Hata hivyo ninaamini kwamba tutapata maelekezo vizuri juu ya nini cha kufanya kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, ambayo ni Wizara yenye dhamana katika eneo hilo, hasa katika Mkoa wa Simiyu.
Mheshimiwa Spika, mara nyingi sana wanaambiwa kwamba watenge maeneo maalum kwa ajili ya kuwakaribisha National Housing. Hata hivyo kuna maeneo mengine National Housing walijenga nyumba lakini matumizi ya zile nyumba imekuwa ni changamoto kubwa na sana katika Halmashauri zetu.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tuchukue kama ni challenge nyingine katika upande wetu vilevile, kwamba endapo National Housing wanakuja kuwekeza basi lazima nisiamasishe Halmashauri tuwe tayari kuhakikisha kwamba tunazitumia nyumba hizo, kwa sababu fedha hizi zisipotumika vizuri tutatengeneza gharama kubwa kwa Serikali yetu. Kwa hiyo, ni wazo zuri Mheshimiwa Nyongo na mimi kama TAMISEMI nitalichukua jambo hili, nitaongea na dada yangu Mheshimiwa Angelina, Naibu Waziri wa Ardhi tuangalie namna ya kufanya ili wananchi wa Simiyu waweze kufanya kazi kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wa Simiyu.

NAIBU WAZIRI WA ARDHI:
Mheshimiwa Spika, Ahsante sana. Napenda kujibu swali la nyongeza na kumshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri alivyojibu majibu yake mazuri kuhusiana na suala la National Housing.
Kwa Mkoa wa Simiyu tayari National Housing wana maeneo waliyopewa katika Wilaya mbili, Wilaya ya Busega pamoja na Wilaya ya Bariadi. Tatizo lililoko katika wilaya zingine ni kwamba bado hawajawa tayari kutenga maeneo.
Mheshimia Spika, kwa maelekezo ambayo pia Mheshimiwa Rais alitoa kwamba National Housing ili waweze kujenga na waweze kutoa nyumba zao kwa bei nzuri lazima Halmashauri husika iwe imeshatenga eneo ambalo halina changamoto kwa maana kwamba litahitaji fidia, litahitaji miundombinu. Kwa hiyo, wao wafanye maandalizi tayari viwanja waweke National Housing watakwenda kujenga. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, la pili pia, kuna Wilaya zaidi ya 30 ambazo National Housing wamejenga na nyumba zile zinaharibika, ikiwemo Mkoa wa Rukwa, nyumba zimejengwa lakini watu hawajaingia wala hawajapanga. Kwa hiyo, wakati mwingine ku-pull up resources katika maeneo mengine inakuwa ni ngumu; na katikati hapa walisimama kwa ajili ya kuendeleza eneo la Iyumbu. Kwa hiyo halmashauri yoyote itakayokuwa tayari National Housing wataweza kuja, lakini tuwaombe pia mfanye maandalizi yale ya msingi ili National Housing waweze kushiriki.
MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi nipate kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa watumishi wengi wa Serikali wamehamishiwa Mkoa wa Dodoma, je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha watumishi wote wa Serikali wanapata nyumba na waache kuhangaika hangaika mitaani kwa sababu nyumba za National Housing hazitoshi kwa watumishi wa Serikali waliohamishiwa Dodoma?
NABU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la mate wangu wa Bulombora dada yangu Mheshimiwa Maryam Msabaha kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kwanza ni kweli, ni nia njema Serikali. Tumesema kwamba Serikali ya Awamu ya tano si mlimila dole, kwamba inatekeleza kile ilichokiahidi; imesema tunaamia Dodoma na tumehamia sasa hivi Dodoma. Naomba niwahakikishie kwamba Serikali imeweka mipango vizuri kupitia nyumba za TBA, National Housing na CDA. Mkiangalia kule kama mnapita Iringa Road zimekarabatiwa, lengo lake kubwa ni kwamba kuweza kuwa-accommodate watumishi wote wa Serikali.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tunashukuru sana kwa suala hili zuri, Serikali imeweka mpango vizuri. Niwaahakikishie watumishi wote kwamba msiwe na hofu mtakapokuja Dodoma, Serikali inapanga mipango mizuri, na ndiyo maana hata National Housing sasa wanajenga huu mji mpya pale. Hii yote ni kwa ajili ya kuhakikisha kwamba kwenye mchakato huu wa Mji Mkuu wa Serikali kuhamia Dodoma, Dodoma iweze ku-accommodate watumishi hawa wanaokuja hapa.
MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Spika, swali langu dogo tu la nyongeza ni kwamba kwa kuwa masharti ya mikopo kwenye mabenki na SACCOS nyingi ambazo kwa kweli watu wengi wamekopa na wameshindwa kulipa madeni na yamewasababishia umaskini mkubwa. Je, hamuoni kwamba kuna haja Serikali sasa mkatazama namna nyingine ya kuwapatia walimu hawa mikopo ya masharti nafuu ili waweze kujenga nyumba zao za kudumu? Swali la kwanza.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, mna mpango gani wa kuiwezesha Halmashauri ya Maswa kama tulivyoongea siku za nyuma, kwamba Halmashauri na zenyewe ziwe na uwezo au zijengewe uwezo wa kuchukua mikopo ili mikopo hiyo kupitia halmashauri iwasaidie walimu hao kujenga nyumba zao za bei nafuu? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli mikopo mingine inayotokana na taasisi za benki ina changamoto nyingi sana, lakini kwa utaratibu wa sasa wa kuwasaidia wafanyakazi kuna suala la mortgage financing ambalo Bunge hili hili lilipitisha sheria humu ndani kuwawezesha watumishi mbalimbali waweze kupata fursa ya mikopo kupitia fedha wanazochangia katika mifuko yao ya Hifadhi ya Jamii.
Mheshimiwa Spika, katika hili naomba niwapongeze Utumishi Housing ambao wamefanya kazi kubwa sana katika maeneo mbalimbali hivi sasa. Tunaona wazi kwamba matangazo yao yametoka, sasa naomba tuwaambie watumishi wa Serikali, tutumie dirisha hili vizuri ili tuweze kupata nyumba katika maisha yetu.
Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la kuziwezesha Halmashauri mbalimbali hasa Halmashauri ya Maswa, kupata mikopo kwa ajili ya kuhakikisha kwamba inafanya uwekezaji; kuhusiana na jambo hili mara nyingi sana ofisi yetu huwa inapokea vibali mbalimbali vya kutaka halmashauri kufanya uwekezaji katika eneo fulani. Hata hivyo mara nyingi sana ofisi yetu huwa inapitia haswa yale maombi kuangalia ili jambo likishapitishwa, likapatiwa kibali ambapo lisije likawa mzigo mkubwa sana kwa Halmashauri hiyo kiasi cha kushindwa kujiendesha.
Kwa hiyo, mawazo mazuri yanakaribishwa, na ofisi yetu ina wataalam watafanya analysis lile jambo linalofanyika basi Halmashauri hiyo haitawekwa nyuma kuhakikisha kwamba inapewa kibali ili ifanye uwekezaji katika halmashauri yake.
MHE. ROSE K. SUKUM: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana kwa kunipa fursa hii ya kuweza kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naomba unipe fursa niweze kumuelezea Mheshimiwa Waziri alivyodanganywa na waliomjibia maswali haya.
Mheshimiwa Spika, uchunguzi umeshafanyika Wilaya ya Hanang na uchunguzi huo umefanywa na timu ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara kwa ajili kujua ubadhirifu wa fedha hizo, sio tu fedha za chakula bali ni fedha nyingine pia zipo za shilingi bilioni moja.
Mheshimiwa Spika, nasikitika Mheshimiwa Waziri, nimekuletea document hizi za uchunguzi uliofanyika ndani ya ofisi yenu, leo unakuja kujibu kirahisi kiasi hiki ina maana kwamba wewe umedanganywa, haya si majibu yaliyotakiwa. Fedha hizi zimetumika, shilingi milioni 100 unazozisema hizo zimetumika ni fedha za SEDEP ziko kwenye uchunguzi hii na nitakukabidhi sasa hivi. Hizi za SEDEP zimetumika kwenda kununua magodoro na kadhalika kwenye hayo mabweni. Kwa hiyo ni kosa moja wapo lilitumika la kutumia fedha ambazo hazistahili kutumika.
Mheshimiwa Spika, la pili taarifa ya Mkaguzi wa Ndani imeeleza Aprili 15 zikisema matumizi mabovu ya hizi fedha, fedha hizi hazikutumiwa na halmashauri zimetumiwa na mtu mmoja au watu wachache ndani ya Halmashauri. Sasa iweje Halmashauri irudishe hizi fedha ili kuweza kulipia deni la mtu ambaye amekula hizo hela? Pia kwa taarifa uliyosema majibu ya Mkurugenzi kwamba amesimamishwa, Mkurugenzi yuko kazini anafanya kazi yuko ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara, na hawa watumishi wengine wako Wilaya ya Hanang wanafanya kazi.
Mheshimiwa Spika, naomba unisaidie, ni kwa nini hawa watumishi hawakuchukuliwa hatua mpaka sasa hivi na taarifa hii iko ofisini kwako?
La pili, kama kweli inatakiwa ithibitike, utatumia hatua gani kuwezesha uchunguzi maalum ufanyike kwa ajili ya kujua ubadhilifu wa fedha za Wilaya ya Hanang? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza wizi ni wizi hakuna wizi mdogo hakuna wizi mkubwa; wizi ni wizi. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Sukum kwamba japokuwa hapa tulikuwa tunaeleza ule mchakato wa zile fedha maalum lakini kilichokuwepo kutokana na specific questions ambazo umeuliza ni kwamba inaonekana Halmashauri ya Hanang si hiyo, kuna lidudu likubwa liko katika Halmashauri ya Hanang. Ndiyo maana nimesema wizi ni wizi hauna mjadala.
Mheshimiwa Spika, naomba nikuhakikishie, haya yote aliyosema Mheshimiwa Sukum kwamba tutafanyaje, nimesema hapa tumechukua hatua. Kama kuna ubabaishaji wa aina yoyote katika zile hatua tulizochukua naomba nikuhakikishie kwamba by this week ambapo leo Ijumaa, by next week ofisi yetu itatuma special investigation team. Lengo lake kubwa ni kwenda kujiridhisha ni kitu gani kimejificha ndani ya boksi; kwenda kutatuta tatizo la msingi la fedha ambazo inawezekana zimetumika kinyume cha taratibu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, na hili naomba nimhakikishie Mheshimiwa Sukum; katika jambo hili Serikali ya Awamu ya Tano haitavumilia uzembe wa mtu yoyote wa aina yoyote. Hili naomba niseme kwamba kwa concern aliyozungumza Mheshimiwa Rose Kamil Sukum, tunaiagiza timu yetu ya investigation and follow up kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, si kutoka ofisi ya Mkoa, kutoka katika ofisi yetu; iende ikafanye uchunguzi wa haraka, by next week tuweze kupata majibu halisia. Lengo kubwa tulinde fedha za walipa kodi wa Tanzania na hatimaye ziweze kusaidia wananchi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba kuyajibu maswali yake kwa pamoja kwa muktadha wa namna hiyo.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri yaliyotolewa na Naibu Waziri Jafo, lakini concern iliyooneshwa na Mheshimiwa Mbunge ni kubwa na kwa sababu hiyo basi kwa kuwa pia taarifa zetu zinakuwa tofauti na alizonazo, nimuombe baada ya kipindi cha maswali aje ofisini kwetu tuweze kupata taarifa zaidi, kwa sababu jambo hili ni la muda mrefu na bahati mbaya yule Mkurugenzi aliyekuwa pale sasa hayuko pale, lakini kesi ipo na inaendelea. Pengine kwa hatua hii sasa tunahitaji kwenda kwa haraka zaidi kulingana na concern aliyoonesha Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, ni kweli kwamba kumekuwa na maamuzi mabaya kwenye Halmashauri yenye lengo la kutaka kuzitafuna fedha fulani kama zipo ambayo chanzo chake huwa ni kubadilisha matumizi. Waheshimiwa Wabunge mimi napenda niwasihi sana, mabadiliko ya matumizi ya fedha za miradi zinazoletwa kwenye Halmashauri yanafanywa na Waheshimiwa Madiwani na vikao vile vinaridhia. Kupitia mwanya huo basi yanayotokea ni mambo ya ajabu. Kuna watu wamebadilisha hela ya mradi ambayo fedha inatolewa na World Bank wamekwenda kufanya yao, wamegawana posho, wamelipana vitu vya ajabu na wamepeana safari.
Mheshimiwa Spika, sasa kuanzia sasa uamuzi tulioufanya sisi kama Wizara ni kwamba mabadiliko ya matumizi ya fedha yoyote itabidi na Katibu Mkuu - TAMISEMI aridhie. Kwa sababu yanayofanywa huko ni mambo ya ajabu sana, kuna watu wanabadili fedha lakini kubadili huko ni kwa lengo la kwenda kutaka kuzitafuna. Kwa hiyo, sisi Serikali ya Awamu ya Tano hatutakubali jambo hilo liendelee kutokea. Niwasihi Waheshimiwa Wabunge mtusaidie kwa sababu na ninyi mnakuwepo kwenye vikao hivyo. (Makofi)
MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwanza nitashukuru sana kama TAMISEMI itakwenda kujua ukweli ni nini. Swali langu ni kwamba shule zile zilizotajwa za Katesh, Gendabi, Balangdalalu na Bassodesh sasa hivi kwa muda mrefu hazijapewa hela za chakula na ni shule za bweni. Taarifa hizo nimezifikisha kwa Mawaziri, nataka kujua, je, watoto waendelee kukaa bila chakula au kuna hatua ambazo zimechukuliwa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli siku ya Mei Mosi tulikuwepo pale Katesh na Mama Mary Nagu na alilileta tena jambo. Hata hivyo alilifikisha ofisini kwetu na ofisi ya Naibu Katibu Mkuu Elimu ilikuwa inashughulikia jambo hili. Kwa hiyo Mama Mary Nagu naomba vuta subira, tunadhani jambo hili linafikishwa mahali pazuri. Nadhani tutahakikisha kwamba watoto wale wanaweza kupata huduma kama ulivyopeleka katika maombi yale. (Makofi)
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, tarehe 30 Desemba, 2017, Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Jafo alitembelea Kijiji cha Mima na kuona barabara ya Mima ilivyo mbaya na nilimwonyesha ni barabara ya kwenda Mkanana, ile barabara kilometa 26 zote ni mawe matupu wala hakuna udongo kule, yote ni mbaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Mheshimiwa Naibu Waziri anaposema anatengeneza eneo korofi, hili eneo lote kubwa linalobaki atatengeneza nani na wananchi wa Mkanana, Kibwegele wana shida? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri alipotembelea Mpwapwa tarehe 30 Desemba alikakuga barabara ya lami kilometa moja Mjini Mpwapwa na aliwaahidi wananchi wa Mji wa Mpwapwa kwamba kilometa zote 10 watazijenga kwa kiwango cha lami. Mbona sijaiona bajeti hii ya kujenga barabara za lami Mpwapwa Mjini kilometa 10? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Lubeleje, senior MP, ambaye mimi huwa napenda kumuita greda la zamani makali yaleyale kutokana na kazi yake kubwa anayoifanya kule Mpwapwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nikiri wazi kwamba nilikuwa na Mheshimiwa Lubeleje katika Jimbo lake na ni kweli barabara ile ina changamoto kubwa na hata siku ile tulivyoenda kukagua kituo cha afya cha Mima tulitumia muda mrefu sana kutokana na changamoto za barabara ile. Hata hivyo, niliwaagiza wataalam kwamba wafanye uchambuzi wa kutosha nini kifanyike katika barabara ile, maana ukiangalia wigo wake, siyo hiyo peke yake, barabara hizo zote ambazo anazizungumzia Mzee Lubeleje ziko katika hali mbaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, japokuwa bajeti iliyokuwepo hapa ni ndogo lakini kupitia Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) tunaziweka katika mpango wa utekelezaji maalum kwa kuzitafutia fedha kwa sababu eneo lile lina changamoto kubwa. Kwa hiyo, naomba nimwombe Mheshimiwa Lubeleje avute subira kwani ofisi yetu inafanya kazi kwa sababu wataalam nimewatuma kufuatilia kazi ile.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu barabara za Mji wa Mpwapwa, ni kweli, mpango uliokuwepo pale ni takribani kilometa tano lakini mtandao wote wa barabara ya lami ni karibu kilometa 10 Mjini Mpwapwa. Hivi sasa wakandarasi wanaendelea na kazi na katika mpango wa bajeti ya mwaka huu, majibu ya Naibu Waziri alipokuwa anazungumza hapa ambayo ni mazuri sana yalikuwa yakijibu suala zima la Mtanana lakini suala la mtandao wa barabara za lami katika mpango wa bajeti ya mwaka huu Mheshimiwa Lubeleje ataona jinsi gani Serikali imejipanga kutekeleza mpango ule wala asiwe na hofu.
MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa wananchi wa Yulansori, Lelembo wanapata shida kubwa ya barabara na Halmashauri haina uwezo kama ilivyo kwa wananchi wa Mpwapwa na kwa bahati nzuri Waziri wa TAMISEMI alishatembelea maeneo hayo, je, Serikali ina kauli gani kuwasaidia wananchi hawa ambao ni wazalishaji wakubwa wa mazao ya mahindi, alizeti na vitunguu?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nilifika maeneo yale mimi na Mbunge tumetembelea barabara ile yenye kilometa 25.2. Kwa sababu changamoto za barabara ile ni kubwa kwani mmomonyoko umekuwa mkubwa kwa bajeti ya kawaida imekuwa ni jambo kubwa sana. Tuliwaelekeza wataalam wafanye upembuzi yakinifu wa barabara ile na inaonekana kuna madaraja na ukibadilisha kuweka tabaka la kifusi, bahati nzuri taarifa hizo zipo katika Ofisi yetu na katika mpango wa bajeti wa mwaka 208/2019 barabara ile ni miongoni mwa barabara za kipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mwaka huu unaokuja barabara ile tunaenda kuishughulikia. (Makofi)
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa barabara inayounganisha Mkoa wa Iringa na Morogoro ni moja tu inapitia Kitonga; na kwa kuwa hoja hii nilishawahi kuileta kwamba siku itakapotokea barabara ya Kitonga imefunga kwenda Zambia na Afrika ya Kusini itabidi watu wazunguke Dodoma. Kwa kuwa wananchi wa Kilolo wa Kata ya Muhanga, Masisiwe, Idete, Itonya, Kimala wameanza kwa makusudi kabisa kupasua barabara ambayo Serikali ilishaahidi kuunganisha Mkoa wa Morogoro na kutokea kwa Mheshimiwa Susan Kiwanga, wamefanya jitihada kubwa, je, Mheshimiwa Waziri atakubali kuitembelea na kutuunga mkono ili wananchi waweze kupata nguvu na kuimalizia barabara hiyo? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, nilivyofika katika Halmashauri na Jimbo la Kilolo, Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Kilolo walizungumzia concern ya barabara hiyo. Kwa sababu jukumu letu kama Serikali ni kubwa ni kutoa huduma kwa wananchi, nami nilieleza wazi kwamba ni jukumu la Serikali kushughulikia barabara hii. Kwa sababu barabara hii itadondokea kwa wenzetu wa TANROARD, lakini ni Serikali yetu yote kwa ujumla, tutaangalia nini cha kufanya kwa ajili ya kuipa kipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli pia siku ile wananchi walisema endapo barabara ile ikijifunga watashindwa kusafiri lakini hatuwezi kutoa ahadi ya moja kwa moja hapa. Niseme Serikali tumelichukua kwa ujumla wake na kuliweka miongoni mwa mipango mikakati ili siku za usoni barabara ile ikiwezekana tuiboreshe kwa huduma pana ya wananchi wa Tanzania lakini hata nchi jirani.
MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa matatizo yaliyoko kule Manyamanyama hayana tofauti sana na matatizo yaliyoko kwenye Jimbo la Geita. Mwaka jana mwezi Machi, Waziri wa Afya alikipandisha Kituo cha Afya Nzela na kuwa hospitali ya wilaya kwa kuwa Wilaya ya Geita haina hospitali ya wilaya lakini kumekuwa na mkanganyiko kati ya TAMISEMI na Wizara ya Afya na Waziri hajawahi kutembelea eneo lile akaliona pengine akawa na huruma kama alivyopata huruma ya Waziri wa Afya. Je, ni lini Waziri wa TAMISEMI ataambatana na mimi kwenda kuona kituo kile kilichopandishwa hadhi na majengo na ubora ulioko pale ili aweze kuridhia na mambo yaende mbele? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nipongeze majibu mazuri ya Naibu wangu, Mheshimiwa Kandege aliyoyatoa katika maswali ya awali yaliyojitokeza, hata hivyo, naomba kujibu swali la mtani wangu Mheshimiwa Musukuma, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kuambatana, namwomba Mheshimiwa Mbunge kwanza aondoe hofu, kama tulivyokwenda katika Jimbo lake na katika Mkoa wa Geita mara nyingi na kufanya kazi kubwa sana, nimwambie mara baada ya Bunge hili la bajeti nitaomba twende kwa ziara maalum kwa sababu Mkoa wa Geita miongoni mwa mambo tunayokwenda kuyafanya ni ujenzi wa hospitali zingine za wilaya katika mkoa huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nina kila sababu kufika Geita kuangalia maeneo muafaka wapi tutajenga hospitali hizo kwa manufaa mapana ya watani zangu Wasukuma wa Mkoa wa Geita ili waweze kupata huduma nzuri ya afya. Kwa hiyo, Mheshimiwa Musukuma asihofu tutaondoka pamoja. (Makofi)
MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Tunaishukuru sana Serikali ya Awamu ya Tano kutupa fedha kwa ajili ya upanuzi wa Kituo cha Afya cha Bahi. Kituo hiki kinawahudumia wananchi wengi sana kwa sababu mji ule unaendelea kupanuka kila siku.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo tulilonalo, upanuzi unafanyika lakini hatuna vitendea kazi, watumishi walioko pale ni Manesi wanne tu na yuko Daktari mmoja na Matabibu wachache sana ambao hawakidhi mahitaji ya wagonjwa wanaokwenda katika kituo kile cha afya. Ni lini sasa Serikali italeta watumishi na vitendea kazi vya kutosha kwa ajili ya huduma za Kituo cha Afya cha Bahi?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, naomba nimshukuru Mheshimiwa Bura kwa sababu yeye amekuwa Msemaji wa Mkoa wa Dodoma kwa nafasi yake ya Viti Maalum na anautendea haki sana mkoa huu. Naomba ku-declare interest, jengo ambalo tumemaliza hivi sasa katika Hospitali ya General, amefanya kazi kubwa sana kuhakikisha tumepeleka pesa na hivi sasa tumepeleka karibuni shilingi bilioni mbili hospitali ile inapata huduma. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, eneo la Bahi kweli tumeboresha kituo kile cha afya lakini siyo hivyo tu kwa kelele zake na za Mbunge wa Bahi mwaka huu tunakwenda kuanza ujenzi wa hospitali mpya za Wilaya za Bahi, Chemba pamoja na Chamwino. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hilo, wenzetu kupitia Utumishi kabla ya Juni, kuna mpango mkakati kupata watumishi wapya katika sekta ya elimu na sekta ya afya. Pia kwa vile tunajua Bahi ni pumulio la makao makuu yetu ya nchi kwa maana ya hapa Dodoma tutajitahidi kuhakikisha tunawapeleka watumishi wa kutosha ikiwa lengo kubwa ni wananchi wa eneo lile waweze kupata huduma vizuri. (Makofi)
MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Pamoja na mikakati mizuri ambapo Wizara inahakikisha tunatokomeza hivi vitendo vya ubakaji nadhani Walimu wana nafasi kubwa ya malezi ya watoto wetu. Kwa nini tusiweke kipengele maalum kwenye mitaala yao jinsi ya kubaini na kuwafanyia counseling hawa watoto mara wanapobaini kuwa wamebakwa? Nakushukuru sana.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli jambo hili kwanza linakera na linaudhi lakini si muda mrefu tulikuwa na kikao cha Maafisa Elimu wote wa Mikoa na Wilaya na jambo hilo tumeliwekea msisitizo hasa katika suala zima la kuhakikisha kwamba, watoto wa kike wanalindwa. Hata hivyo, ushauri wa Mheshimiwa ni mzuri, Serikali tumeuchukua na tutakwenda kuufanyia kazi kwa kadri tutakavyoona inafaa.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniruhusu niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa swali hili la Ndanda la Bwawa la Lukuledi linafanana kabisa na bwawa lililopo Mbulu Vijijini, Bwawa la Mangisa ambalo linahudumia Kata ya Yaeda Ampa, Bashay na Gidihim na hali yake kwa kweli inaelekea kuisha kabisa kwa sababu linakauka.
Je, Serikali itatusaidiaje ili hili Bwawa la Mangisa liweze kupatiwa ufumbuzi ili vijiji nilivyovitaja viendelee kupata huduma ya maji?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kufanya clarification vizuri katika maswali yote.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la Mbulu kweli kuna changamoto kubwa ya hili bwawa ambalo Mheshimiwa Flatei analizungumzia, lakini naomba nikiri wazi kwamba miundombinu ya mabwawa katika maeneo mbalimbali imeendelea kuathirika siku hadi siku na kushindwa kuhakikisha uwezo wake unapotea.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hali hiyo changamoto kubwa ni suala zima ambalo hata Naibu Waziri hapa amezungumza, uharibifu mkubwa wa mazingira katika vyanzo vya maji, watu wanapenda katika maeneo ya mabwawa kuweka mashamba, kinachotokea ni kwamba mvua inavyonyesha udongo unatiririka kutoka mashambani unaenda kujaza katika mabwawa na mabwawa haya yanakufa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Flatei tumeisikia hoja yako tutawatuma wataalam kwenda kufanya uhakiki kuangalia nini kinachotakiwa kufanyika pale. Hata hivyo, naomba niwasihi viongozi wote katika maeneo mbalimbali hasa katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa, wahakikishe kwamba katika suala la vyanzo vya maji hasa mabwawa kuzuia vitendo vya shughuli za kibinadamu hasa kilimo, kwa sababu jambo hilo linaharibu miundombinu ya mabwawa katika nchi yetu. (Makofi)
MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Miongoni wa vitu vya afya ambavyo vilipangiwa kupatiwa pesa Mkoani Ruvuma ni pamoja na Kituo cha Afya Namtumbo na Mkasali. Naishukuru Serikali vituo hivyo vimepata pesa. Hata hivyo, kipo Kituo cha Afya cha Matemanga ambacho kilipangiwa kupatiwa pesa kwa ajili ya ukarabati, lakini pesa ile mpaka sasa haijaenda. Ni nini kauli ya Serikali kuhusiana na hiyo pesa ya ukarabati wa vituo vya afya? Ahsante. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri yale ya awali. Naomba kumpa comfort kwanza mtani wangu Mnyamwezi. Mheshimiwa Ntimizi wiki iliyopita alikuja ofisini kwetu pale kwa ajili ya vituo vya afya vitano vilivyoanzishwa katika mchakato wa ujenzi wa na tumewapa commitment kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI itahakikisha kwamba ina- support ndani ya mwaka huu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kuhusu suala la Matemanga, tayari naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ndani ya wiki hii tu-cross-check accounts zetu kule katika halmashauri yetu, tutakuwa tumeshaingiza hizo fedha tayari kwa ajili ya kuhakikisha kituo kile kinakamilika. (Makofi)
MHE. ALFREDINA A. KAHIGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Wilaya ya Bukoba Vijijini tuna tatizo la ma-engineer wa ujenzi na tulitengewa fedha za force account shilingi milioni 900 kwa ajili ya kutujengea Kituo cha Afya katika kata mbili, kata za Kishanje na Rubafu, lakini hatuna ma-engineer wa ujenzi. Tunajenga chumba cha mama na mtoto, mortuary na chumba cha Mganga katika kata hizo mbili.
Je, ni lini Serikali itatusaidia ma-engineer wa ujenzi? Ahsante. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikupongeze kwa Tulia Marathon mmefanya vizuri sana. Hongera sana. (Makofi)
Pia nampongeza sana Mheshimiwa Mama Kahigi kwa sababu amekuwa mfuatiliaji mzuri sana tokea alipokuwa Mjumbe wa Kamati ya TAMISEMI. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tumesikia kilio hiki kwa sababu tunajua kwa Mkoa wa Kagera tulikuwa hatuna hospitali zile za Wilaya na ninyi mmeleta concern hizo kubwa na ndiyo maana mwaka huu wa fedha tunaenda kujenga hospitali tatu mpya kule Karagwe, Kyerwa pamoja na Bukoba Vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunapeleka infrastructure nyingi sana katika eneo hilo na suala zima la kupata wataalam tutaweka kipaumbele chetu, lengo kubwa ni kwamba vile vituo vya afya na hospitali ambazo tunaenda kuzijenga tuwe na wataalam wa kutosha kwa ajili ya kuweza kusimamia. Kwa hiyo, tunalichukua kwa ajili ya kwenda kulifanyia kazi. (Makofi)
MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Lengo la kutenga pesa hii lilikuwa ni kuwainua vijana na wanawake jambo ambalo limekuwa ni kinyume na lengo ambalo lilikusudiwa hasa pale zinapotolewa kipindi cha Mwenge. Serikali haioni kuna umuhimu wa kupeleka pesa hizi kulingana na mahitaji hasa kwa wale ambao wanajishughulisha na kilimo ikatolewa kipindi cha msimu wa kilimo? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri sana kwa maswali yale ya awali. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la dada yangu Mheshimiwa Aida, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, tumetoa maelekezo maalum kwa fedha hizi na niwasihi Waheshimiwa Wabunge, siku zote tunasema kwamba fedha hizi zinaishia katika halmashauri hata kule Hazina hazifiki. Ni jukumu la Kamati ya Fedha kila mwezi wanapofanya collection wahakikishe kama wamepata shilingi milioni 100, asilimia kumi ya shilingi milioni 100 maana yake ni shilingi milioni kumi zitolewe kwa wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni imani yangu kwamba Kamati za Fedha zote, dada yangu Mheshimiwa Aida nimepata concern yako, zihakikishe wanatenga fedha hizi. Ndiyo maana katika Finance Bill ya sasa hivi tunafanya mabadiliko ya sheria katika Sheria ya Fedha ya Serikali za Mitaa, Sura ya 290 ili kuhakikisha kwamba Waziri mwenye dhamana anasimamia vizuri eneo hilo.
Mheshimiwa Spika, naomba niwaambie wazi kwamba mtu yeyote atakaye-temper na fedha hizi ambapo kwa mwaka huu wa fedha tumetenga zaidi ya shilingi bilioni 61, kwa kweli hatutakuwa na ajizi ya aina yoyote. Hata hivyo, niwasihi Wabunge tunapokaa katika Kamati ya Fedha tuweze kuzisimamia vizuri fedha hizi kwa sababu ni jukumu letu wananchi wetu hasa vijana na akina mama waweze kupata mikopo hii.
MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati huu ni Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi, ni sera, sheria na kule kwenye halmashauri zetu lisipotekelezwa ni hoja ya ukaguzi lakini bado kuna changamoto za utekelezaji. Je, ni lini sasa Serikali itatoa waraka mkali kabisa ambao utaelekeza halmashauri zote zitekeleze na zisipotekeleza ziweze kuwajibishwa?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la rafiki yangu Mbunge wa Kondoa Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, jambo hili tumelitolea maelezo hapa mara kadhaa na hata tukifanya rejea wakati nawasilisha bajeti yetu ya mwaka wa fedha 2018/2019 tulisema wazi kwamba katika ajenda hii ya mikopo ya akina mama na vijana sasa suala hili linakuwa si la hiari tena. Nimesema wazi mara kadhaa kwamba jamani fedha hizi hazifiki Hazina zinaishia katika halmashauri zetu. Jukumu letu kubwa sisi kuhakikisha tunasimamia katika Kamati za Fedha ili fedha hizi ziweze kufika kwa vijana na akina mama, hilo ndilo jambo la msingi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ndiyo maana katika Finance Bill ya mwaka huu tumeleta kifungu maalum kwa ajili ya enforcement ya jambo hilo. Ni imani yangu kwamba baada ya Sheria hiyo ya Fedha kufika hapa, Wakurugenzi wote, lakini niwatake Madiwani wote na Wabunge wote katika halmashauri zetu tuweze kuwa imara kuhakikisha utaratibu wa fedha hizi ambazo zinatengwa na katika bajeti ni lazima zitengwe, ziweze kuwafikia vijana na akina mama wetu. Kwa hiyo, hili ni jambo letu sisi sote na si jambo la mtu mmoja na kwa vile sheria inakuja nadhani hapa itakuwa hakuna suala la negotiation, tutakwenda kwa mujibu wa sheria itakavyotuongoza. (Makofi)
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Manispaa ya Iringa ni moja ya Manispaa ambazo zinatekeleza kwa ukamilifu na kwa uaminifu suala hili la asilimia 10 kwa vijana na akina mama. Na kwa kuwa Serikali imekuwa ikichelewa wakati fulani kuleta pesa zinazotoka Serikali Kuu kwa ajili ya maendeleo, Wizara haioni ni muhimu sasa kuziona halmashauri kama Manispaa ya Iringa ambazo zinafanya vizuri ili ziwape kipaumbele kupeleka hela za kimaendeleo kwa sababu zinatekeleza wajibu wake?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la rafiki yangu, Mheshimiwa Mchungaji Msigwa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, naomba nikiri wazi kuna manispaa nyingi sana zafanya vizuri hapa nchini kwetu katika miradi mbalimbali ya maendeleo. Miongoni mwa manispaa inayofanya vizuri vilevile ni Manispaa ya Kinondoni ukiachana na Iringa na juzi juzi waliweza kutoa fedha zaidi ya shilingi bilioni 2 kwa ajili ya mikopo ya akina mama na vijana. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini katika suala zima la upelekaji wa fedha za maendeleo tumejipanga na ndiyo maana hapa katikati unaona jinsi tunavyojitahidi kwa kadri iwezekanavyo na tuna matarajio kwamba kabla mwaka huu wa fedha haujafika, si Halmashauri ya Iringa peke yake isipokuwa manispaa zote na halmashauri zote kuhakikisha zinapata fedha na especially kwa ajili ya kwenda kukamilisha yale majengo yetu ya hospitali na madarasa. Tunawasiliana na wenzetu wa Hazina ikibidi tutatumia force account kuhakikisha kiwango kikubwa cha fedha kinapatikana katika halmashauri zetu ili miradi hii ya maendeleo iweze kutekelezeka katika eneo yetu.
MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri anasema kwamba anaiagiza Tume ya Taifa ya Walimu kutatua changamoto za walimu, lakini Serikali iliwaahidi walimu kuwapatia posho ya kufundishia (teaching allowance)ili iwe motisha kwao lakini hadi sasa Serikali imekuwa na kigugumizi, fedha hizo (teaching allowance) bado hawatoi kwa walimu.
Je, sasa Serikali inataka ituambie mliwadanganya walimu au mna nia ya kutoa teaching allowance iwe kama ni motisha?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niwapongeze Naibu Mawaziri wote kwa majibu mazuri sana ya awali na ufafanuzi na ningependa kujibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Masoud kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mjuavyo kwamba Serikali kwa kubaini kwamba kuna changamoto nyingi, si kwa walimu pekee isipokuwa kwa watumishi wa kada mbalimbali; kupitia Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma iliunda bodi maalum kwa ajili ya kupitia swala zima la kazi mbalimbali za mazingira magumu. Sehemu nyingine posho nyingine huwa zinaingizwa katika mishahara kwa kadiri itakavyoonekana inafaa.
Kwa hiyo, Serikali imeangali kwa ujumla wake ndiyo maana kwa upande wa walimu, kwanza ilianza baadhi ya kada mbalimbali hasa katika Walimu Wakuu wa Sekondari na Msingi na hali kadhalika kwa Maafisa wale wetu wa Kata wa Elimu (Waratibu wa Elimu) kwa ajili ya kuwapatia responsibility allowance. Kwa hiyo, ni jukumu la Serikali kuangalia nini cha kufanya kwa ajili ya kuboresha si maslahi ya walimu peke yake isipokuwa kwa watumishi wote wa umma kwa kadiri itakavyoona inafaa kwa ajili ya kuboresha maisha yao.
MHE. OMARY A. BADWEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, kwa kunipa nafasi na mimi ya kuuliza swali ndogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa maelekezo ya Serikali sasa ni kujenga zahanati katika kila kijiji na bahati nzuri wananchi katika maeneo mbalimbali wameitikia ujenzi wa zahanati hizo na wako katika hatua mbalimbali. Hata hivyo kwa bahati mbaya sana zaidi ya miaka minne, mitano baadhi ya vijiji wamejenga hizo zahanati na wamefika hatua mbalimbali hakuna fedha ya Serikali ambayo imekwenda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni kama alivyosema Mheshimiwa Waziri Serikali ilitoa maelekezo kwa Wakurugenzi kupitia upya bajeti ya fedha za CBG ili kupata miradi michache ambayo itakuwa na matokeo ya haraka na baadhi ya sehemu hizo katika Wilaya ya Bahi kwa mfano Kijiji cha Chonde tumezitengea fedha hizo lakini mpaka sasa fedha hizo hazijaja na mwaka unakwisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Serikali inawaambia nini Watanzania na Bunge hili kwamba ni lini sasa fedha hizi za CBG ambazo zimefanyiwa marekebisho zitakuja kwenye Halmashauri zetu na kuweza kufanya kazi ambayo imekusudiwa?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwanza niwapongeze Wabunge wengi wametumia mfuko wa Jimbo kwa ajili ya kusaidia kwa kuungana na wananchi katika ujenzi wa zahanati na vituo vya afya, hii ni pongezi kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo tunafahamu kwamba ni kweli, tulikuwa na kikao maalum ambacho kilihusisha Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Mipango, watu wa manunuzi especially na baadhi ya Wenyeviti wa Halmashauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikiri wazi kwamba takribani wiki mbili zilizopita niliwasiliana na wenzangu, nilikuwa na kikao cha watu watatu, mimi hapa, Mheshimiwa Jenista Mhagama na Waziri wa Fedha kuhusu upatikanaji wa hizo fedha kwa ajili ya kwenda kumalizia hiyo miradi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo imani yangu kubwa ni kwamba kabla hatujafunga mwaka huu; kwa sababu pesa zile tunaenda kujenga kwa kutumia force account jambo hili litakamilika vizuri. Lengo kubwa miundombinu hii twende tukalimalize katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa. (Makofi)
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Lushoto yenye tarafa tano ina Vituo vya Afya katika Tarafa ya Mlola, Mlalo, Mnazi pamoja na Lushoto Mjini; je, ni lini sasa Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Tarafa pekee iliyobaki ya Mtae?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Naibu Waziri kwa majibu mazuri sana ya maswali yote ya awali. Mheshimiwa Shangazi alishafika ofisini kwetu mara kadhaa kuhusu kituo hiki na ndiyo maana tumeanza katika awamu hii kupeleka pale Mnazi. Naomba nimhakikishie kwa sababu wananchi wa Mtae wanapata shida, katika kipindi kinachokuja tutafanya kila liwezekanalo, kuhakikisha eneo lile tunalipatia Kituo cha Afya. Lengo letu ni kupunguza vifo vya mama na watoto. (Makofi)
MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Jimbo la Bagamoyo kata zake zote isipokuwa moja tu ndiyo ina kituo cha afya ambacho ni kipya. Je, ni nini mpango wa Serikali kuweza kutupatia angalau kituo kimoja au viwili zaidi kwa Jimbo zima la Bagamoyo? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Wilaya ya Bagamoyo ina changamoto kubwa na hivi sasa tuliimarisha katika Kituo cha Afya cha Kerege. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kadri iwezekanavyo na tukijua kwamba jiografia ya Bagamoyo na mahitaji yake yalivyo, nadhani kabla hatujafika mwezi wa saba, hapa katikati, tutafanya jambo katika kituo kimoja cha afya ambacho yatapendekeza kutoka Wilaya ya Bagamoyo. (Makofi)
MHE. ALMAS. A MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naipongeza sana Serikali kwa fedha ambazo imetupatia kwa ajili ya Kituo cha Upuge na fedha ambazo zinapelekwa kwenye zahanati hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo naomba niseme ukweli kwamba methali ya kwamba mzigo mzito mpe Mnyamwezi, hatuitaki tena kwa sababu inatukandamiza. Tunasema mzigo mzito punguza, beba mwenyewe. Kwa sababu tumegundua kwamba kumbe mzigo mzito ni kutokuwa na vituo vya afya, kutokuwa na barabara huko kwetu, hatutaki tena.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunataka Bunge hili lielewe kwamba Wilaya yote ya Uyui ina kituo kimoja tu cha afya, sidhani kama kuna Wilaya nyingine hapa Tanzania iko namna hiyo, lakini vilevile hakuna tena hospitali ya Wilaya katika Wilaya nzima. Kwa hiyo, vituo vya afya vilivyopo, zahanati hizi ndiyo tunazoomba zipanuliwe ziweze kuwa vituo vya afya. Kwa hiyo, wananchi wa Kata ya Usagari, wamechanga shilingi milioni 50 wakiwa na lengo la kupanua kituo kile kiwe kituo cha afya na maeneo yapo. Tunaona ni bora kuongezea kuliko kujenga upya…
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali, je, Serikali iko tayari kubadili msimamo wake ili hela za wananchi, shilingi milioni 50 na Mfuko wa Jimbo wa shilingi milioni 10 watuongezee tupanue kituo kile kiwe kituo cha afya? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, samani swali langu la pili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; kwa kujua hali ilivyo kule Jimboni kwangu kwamba hakuna kituo cha afya, hakuna zahanati bora zaidi ya hiyo ya Migungumalo; je, Serikali iko tayari kutusaidia kujenga kupandisha Zahanati za Ilolanguru na Ufuluma ili vitumike kwa muda kama vituo vya afya?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la mtani wangu Mnyamwezi wa Tabora kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepata maombi yake Mheshimiwa Maige. Hata hivyo naomba nikiri wazi kwamba Mbunge huyu amekuwa mpiganaji sana wa eneo lake. Hata siyo muda kwa kazi kubwa anayofanya, hata jina la Halmashauri yake muda si mrefu sana litabadilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu kwamba kutokana na changamoto, ndiyo maana tuliwapa fedha kuimarisha Kituo cha Afya cha Upuge ambacho sasa hivi kinaenda vizuri, lakini hata katika bajeti ya mwaka 2018/2019 kutokana na shida kubwa waliyokuwa nayo tumewapa takriban shilingi bilioni 1.5 watajenga Hospitali ya Wilaya. Vilevile kabla ya tarehe 15 mwezi wa saba katika Jimbo la Igalula tutapeleka fedha nyingine kwa ajili kuimarisha kituo cha afya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba wananchi wa jimboni kwako tutafanya kila liwezekanalo ili kama kuna vituo ambavyo vinatakiwa tuvipe hadhi, tutaangalia nini tufanye, lengo letu kubwa kama Serikali ni kuhakikisha kwamba Wanyamwezi wa Tabora wanapata huduma ya afya vizuri kama wengine. (Makofi)
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza kabisa naishukuru Serikali kwa kutupatia fedha milioni mia tano kujenga Kituo cha Afya cha Ihalula, lakini naomba kuiuliza Serikali; je, lini sasa watatupatia fedha kwa ajili kukarabati Hospitali ya Halmashauri ya Mji Njombe Kibena?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mwalongo kwa sababu juzi nilienda kukagua kituo kile wamejenga vizuri sana. Nilipokuwa Mkoani Njombe nilitembelea vituo mbalimbali, miongoni mwa kituo ambacho wametumia taaluma vizuri ya Force Account, Mheshimiwa Mwalongo mmefanya vizuri. Hata hivyo tunafahamu katika ujenzi, hasa changamoto ya miundombinu, kama Serikali, tunachukua hili tunaweka katika mipango yetu. Lengo kubwa ni kwamba isiwe kwa hospitali yako peke yake, lakini hospitali mbalimbali za Wilaya ambazo zinachangamoto lazima tulirekebishe ili wananchi wapate huduma vizuri. (Makofi)
MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naipongeza sana Serikali katika kuhakikisha inaboresha miundombinu ya sekta ya afya. Hata hivyo, je, Serikali iko tayari kwenda sambamba na uongezaji wa watumishi katika maeneo hayo? Kwa sababu sasa hivi changamoto kubwa sana ni watumishi katika zahanati zetu na vituo vya afya pamoja na hospitali.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumemsikia Mheshimiwa Hawa Ghasia, ninafahamu kwamba siyo muda mrefu tutaimarisha kituo chake cha Mahulunga pale katika Jimbo lake ambalo najua kwamba changamoto ya watumishi itakuwa kubwa. kwa bahati nzuri Naibu Waziri alishasema awali kwamba tunaajiri watumishi 6,180.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutawapa kipaumbele katika miundombinu hii wananchi waweze kupata huduma ya afya katika Jimbo la Mtwara DC.
MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kituo cha Afya Endabash katika Tarafa ya Endabash inahudumia kata nne, lakini kituo hicho kina upungufu mkubwa ikiwemo jengo la mama na mtoto, maabara na mortuary. Ni lini Serikali itatoa fedha ili miundombinu hiyo iliyobaki ikamilike ili kituo hicho kitoe huduma stahiki?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninafahamu Endabash ni sehemu yenye changamoto kubwa. Tukijua wazi kwamba Wilaya yetu ya Karatu ni center kubwa ya watalii, ndiyo maana katika mipango mikakati yetu kwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI tunataka kuangalia tuone ni jinsi gani tutafanya tu upgrade kituo kimoja. Mimi naamini kwamba kwa sababu ya ajenda kubwa ya utalii, jukumu langu kubwa ni kuhakikisha unajipanga vizuri na watu wako, ikifika kabla ya mwezi Disemba kituo hicho kiwe kimekamilika kwa ajili ya kuwatumikiwa wananchi wa eneo hilo.
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Wanging’ombe kuna Kituo cha Afya cha Makoga. Kituo hiki ni cha kimkakati, kinahudumia wananchi wa Tarafa ya Imalinyi na Mdandu. Tuseme ni theluthi mbili ya wananchi wa Wilaya ya Wanging’ombe wanapata huduma katika Kituo cha Afya hicho cha Makoga, lakini hali yake ya miundombinu ni mibaya sana. Je, ni lini Serikali itatoa pesa ili kuweza kukarabati Kituo kile cha Afya cha Makoga?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumpongeza Mheshimiwa Neema Mgaya na Wabunge wa Njombe wote kwa ujumla wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi tulikuwepo kule tukifanya harambee na tulipata shilingi milioni mia moja na thelathini na saba. Namshukuru Mheshimiwa Neema, Mheshimiwa Lwenge na Waheshimiwa Wabunge wote. Hii tulifanyia pale Makoga na kweli changamoto yake ni kubwa. Hata hivyo tulitembelea Kituo kingine cha Afya cha Palangawano ambacho kinajengwa. Kwa hiyo, kama Serikali tumeweka kipaumbele katika maeneo haya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini kabla ya mwezi wa 12 kati ya vituo hivyo viwili tutaweza kukiboresha kituo kimojawapo. Hata hivyo priority ya Makoga na Palangawale lazima tuikamilishe kwa ajili ya wananchi wa Wanging’ombe waweze kupata huduma vizuri. (Makofi)
MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza nimshukuru Waziri kwa majibu yake mazuri na kueleza mkakati, lakini naomba niulize swali moja la nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hizi hospitali 67 ambazo zitajengwa, je, Wilaya ya Songea Mjini ipo? Kwa sababu kuna wakazi 300,000, Kata 21 na hakuna Hospitali ya Wilaya na kuna kituo hata kimoja tu cha afya. Je, Wilaya ya Songea Mjini ambapo Jimbo la Songea Mjini lipo itapata hizo hospitali 67?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Damas Ndumbaro, Mbunge wa Songea Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, tukumbuke nilipo-table budget speech yangu mwaka huu tarehe 14, niliainisha hospitali hizo ambapo kwa mara ya kwanza tunakwenda kuweka historia katika nchi yetu. Katika Mkoa wa Ruvuma tunakwenda kujenga hospitali Namtumbo, Songea DC pamoja na Nyasa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niseme wazi kwamba kwa Songea Mjini bado hatujatenga bajeti yake kwa sababu pale tuna Hospitali ya Mkoa. Hata hivyo, namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge tumewasiliana mara kadhaa. Tulichokifanya ni nini? Hapa katikati tutafanya resource mobilization kusaidia watu wa Songea Mjini waweze kupata japo kituo kingine acha afya as a backup strategy kupunguza idadi ya wagonjwa ambao wengi wanakwenda katika hospitali ya mkoa. Kwa hiyo, tutakwenda kulifanyia kazi suala hili katika kuimairisha vituo vya afya.
MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Hivi karibuni katika kuboresha shughuli za afya nchini, Serikali ilitoa ahadi kwamba itatoa pesa kwa ajili ya kuboresha Kituo cha Afya cha Wampembe pamoja na kile kinachojengwa na wananchi cha Kasu. Nataka kuuliza, ni lini pesa hizi zitatolewa ili wananchi waweze kunufaika na huduma hizo?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mipata, Mbunge wa Nkasi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tumesema wazi kwamba tunajenga, tunaboresha vituo vya afya kwa mara ya kwanza 208 na tutatumia takribani shilingi bilioni 156 pamoja na kuimarisha miundombinu mingine hasa ya wahasibu. Hata hivyo, naomba nikiri wazi, juzi juzi tumeweka katika ile batch ya mwisho ya vituo 25 na muda siyo mrefu hapa nilikuwa naongea na Mheshimiwa Nkamia kuhusu fedha hizo. Kwa hiyo, tuta-cross checks vizuri ili katika maeneo yote tuliyoyapa kipaumbele fedha ziweze kufika.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika halmashauri ya Mheshimiwa Mbunge ambapo kulikuwa na changamoto ya ukosefu wa Hospitali ya Wilaya, katika mpango wetu wa Serikali wa kujenga hospitali 67 na wilaya yake tunakwenda kuipatia Hospitali ya Wilaya. Ni kwa imani yangu kubwa kwamba wananchi wa Nkasi kwa ujumla wake watapata huduma nzuri za afya katika maeneo yao.
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Changamoto za huduma za afya zilizopo Rorya zinafanana na Jimbo la Nanyamba. Naishukuru Serikali imetupa ujenzi wa vituo vitatu na kituo kimoja cha Dijecha ujenzi umekamilika. Je, ni lini Serikali italeta watumishi kwa sababu kituo kile kina watumishi saba na mahitaji ya sasa ni watumishi 41?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ridhaa yako, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Chikota, Mbunge wa Nanyamba, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nimepata concern hii na kwa sababu tunajenga hivi vituo vya afya vipya 208 au tunaviboresha lengo letu kubwa ni ili viweze kufanya huduma ya upasuaji, tunajua tuna mahitaji makubwa ya wataalam. Hata hivyo, takribani wiki mbili zilizopita tumeshatangaza ajira zipatazo 6,180. Lengo kubwa ni kwamba watu wale tutakapowaajiri tuwapeleke katika vituo hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, imani yangu Mheshimiwa Chikota wala asihofu kwa sababu Nanyamba vilevile ni miongoni mwa eneo ambalo tunalenga kuja kujenga Hospitali ya Wilaya tunajua mahitaji yatakuwa ni makubwa zaidi. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba ni mpango wa Serikali wale watumishi 6,180 tutawagawanya maeneo mbalimbali lakini hata hivyo hatutaishia hapo itabidi tuongeze watumishi wengine kwa lengo la kuwasaidia Watanzania.
MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa nafasi. Hospitali au Kituo cha Afya cha Sinza maarufu kama Hospitali ya Palestina ilipandishwa hadhi na kuwa Hospitali ya Wilaya lakini bado iko katika mazingira madogo sana yaani eneo lake ni dogo sana na hata bajeti yake inakwenda kwenye masuala ya kituo cha afya. Je, ni lini sasa Serikali itatoa bajeti ya kutosha lakini vilevile kupanua mazingira yake ili wananchi wa Sinza na Ubungo kwa ujumla waweze kupata huduma stahiki? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la dada na mama yangu Mheshimiwa Susan Lyimo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, anachokisema Mheshimiwa Susan ni kweli. Wiki tatu zilizopita nilikuwa katika Kituo hicho cha Palestina, nilikwenda kukagua ujenzi, hasa miundombinu. Pale kulikuwa na ukarabati unafanyika lakini ukarabati ule nilipata mashaka kama value for money ipo? Nimekwenda kuangalia pale na population niliyoikuta pale ilikuwa ni kubwa sana. Ndiyo maana mpango wa Serikali kwa Wilaya ya Ubungo, kwanza yenyewe haina Hospitali ya Wilaya. Kile Kituo cha Afya hata ukiangalia mazingira yake siyo rafiki zaidi kupandishwa kuwa hospitali ya wilaya. Ndiyo maana mwaka huu sasa katika Jiji la Dar es Salaam tunakwenda kujenga hospitali tatu kuanzia Kigamboni, Ilala maeneo ya Kivule pamoja na Ubungo lakini wenyewe wata-decide wapi hospitali hizo zitakwenda kujengwa. Kwa hiyo, ni jukumu letu kuboresha huduma za afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, nimemweleza pale Mkurugenzi kwamba ukusanyaji wa mapato sikuridhika nao. Leo hii Kituo kile cha Palestina, thamani ya fedha inayokusanywa hailingani na idadi ya watu. Kwa hiyo, maana yake kuna mianya mikubwa ya upotevu wa mapato. Kwa hiyo, nilitoa maagizo, imani yangu kubwa ni kwamba eneo lile marekebisho yatafanyika kwa maslahi mapana ya wakazi wa Ubungo.
MHE. ANNA J. GIDARYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mazingira yaliyopo Kondoa yanafanana na mazingira yaliyopo Babati Vijijni. Zahanati ya Galapo ni Zahanati ya muda mrefu, imepandishwa kuwa Kituo cha Afya, lakini mpaka sasa hatuna jengo la upasuaji. Kwa nguvu za wananchi tumejitahidi mpaka tumepaua hilo jengo. Mpaka sasa tuna vifaa vya hicho chumba cha upasuaji lakini tuna changamoto ya kumalizia hilo jengo ili litumike. Ni lini sasa Serikali itapeleka pesa za kumalizia hilo jengo? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeze dada yangu Mheshimiwa Anna kwa swali zuri, lakini nawapongeza Wabunge wa Babati na kaka yao Mheshimiwa Jitu Soni kwa pamoja. Nafahamu Babati Vijijini ina changamoto kubwa ya afya na ndiyo maana kwa Zahanati ya Galapo ambayo imepandishwa lakini kwa sasa kipaumbele chetu kwamba tumeanza na vituo viwili vya afya, kile ni cha kwanza na sasa hivi tunaenda katika Kituo cha Magugu, kwa sababu tunajua pale Magugu ni center kubwa sana gari nyingi zinapita.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hilo tumeweka kipaumbele na hata hivyo ni mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba Kituo cha Afya cha Galapo tutafanya kila liwezekanalo kwa mipango ya Serikali tuweze kukiimarisha kwa ajili ya wananchi wa Babati Vijijini waweze kupata huduma vizuri. (Makofi)
MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa matatizo yaliyoelezwa na Waheshimiwa Wabunge wenzangu ni sawa kabisa na matatizo yaliyoko Jimboni kwangu. Jimbo la Geita Vijijini lenye population ya watu kama 1,000,000 halina kabisa Kituo cha Afya hata kimoja, baada ya Kituo cha Afya Nzela kupanda hadhi na kuwa Hospitali ya Wilaya. Je, Wizara haioni umuhimu wa kutusaidia pesa ili tuweze kujenga kituo kwa wananchi walioko Ibisabageni na Rubanga kuliko na umbali wa kilometa 80 mpaka kukipata Kituo cha Afya kilichopandishwa hadhi ya kuwa Hospitali ya Wilaya? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kweli tunafahamu changamoto kubwa ya afya kule Geita Vijijini na hata hivyo namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu kwa pamoja tumeshirikiana kuhakikisha Kituo cha Afya cha Nzela kile cha kwanza kimekuwa ni cha kisasa zaidi. Hata hivyo, kwa vile tunajua changamoto ni kubwa, ndiyo maana Geita DC sasa hivi tunaenda kuipa Hospitali ya Wilaya rasmi sasa katika bajeti yetu ya mwaka 2018/2019.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, katika Mpango wa Serikali wa sasa, nia yetu ni kwamba kabla ya mwezi wa Tisa mwishoni kuelekea mwezi wa Kumi tutakuwa tumeweka miundombinu ya kisasa katika Kituo cha Afya cha Nyarugusu, nadhani ni Zahanati lakini tutai-upgrade. Lengo kubwa ni kwamba wachimbaji ambao ni population kubwa ya eneo lile waweze kupata huduma nzuri sana ya afya na kuwahudumia wananchi wa Geita kwa ujumla wake. (Makofi) Mheshimiwa Spika, nashukuru.
MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa hii adimu. Wilaya ya Hanang’ ina Kituo cha Afya kimoja ambacho ndicho kinakarabatiwa sasa lakini kuna Wilaya kubwa haina Kituo cha Afya kingine. Nilimwomba Mheshimiwa Waziri Kituo cha Afya cha Basotu na Kituo cha Afya cha Endasak ambako kuna watu wengi ambao wanategemea huduma hiyo, atusaidie. Je, anaweza kutuambia ni lini ukarabati huo utaanza ili watu wa Endasak na Basotu waweze kunufaika na huduma ya afya? Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba nikiri kwamba Mheshimiwa Mary Nagu, tena alikuja na wananchi wake tukiwa getini alileta hiyo hoja. Nakiri wazi pia kwamba Endasak na Basotu ni changamoto kubwa na ina population kubwa. Nia na mpango wa Serikali ni kwamba Mungu akijaalia kabla ya mwezi wa Tisa tutakuwa tumeshaanza ujenzi pale Basotu kwa kadri kama tulivyokubaliana siku ile. (Makofi) Mheshimiwa Spika, nashukuru.
MHE. RITA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi, ili niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa katika Manispaa yetu ya Iringa kuna Daraja la Igumbiro, daraja ambalo limekuwa likileta maafa kila mwaka na ambalo limechukua muda mrefu sana kumalizika. Je, ni lini sasa Serikali itatoa pesa ili Daraja lile la Tagamenda liweze kukamilika?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maeneo ambayo tunafanya uwekezaji mkubwa wa miundombinu ni pamoja na Manispaa ya Iringa. Serikali ya Chama cha Mapinduzi imeamua kuboresha miundombinu katika Manispaa hiyo ya Iringa na hivi sasa tumekamilisha barabara kadhaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Ritta Kabati kwamba wataalam wangu wataenda kufanya tathmini katika eneo hilo ambalo limebakia linaonekana lina changamoto. Lengo letu kubwa ni ili tuhakikishe kama hiyo kazi ina upungufu wa aina yoyote tuweze kuurekebisha ili wananchi wa Iringa wawe katika mazingira mazuri ya kuweza kusafiri.
MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Suala la kupitika barabara ni suala muhimu sana kwa ajili ya uchumi na maendeleo ya wananchi; na kwa kuwa, Madaraja ya Mipande, Mtengula, Chawara hadi kule Buyuni, lakini pia Daraja la Mwitika Maparawe ni madaraja ambayo yamezolewa na mafuriko kutokana na mvua kubwa. Je, nini kauli ya Wizara ya TAMISEMI katika kuhakikisha madaraja haya yanarudishwa ili kuwe na mawasiliano ya usafiri?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Bwanausi, kwanza kwa kufuatilia madaraja hayo, kwa sababu nikiri wazi kwamba alifika ofisini kwangu na nilimwelekeza aende akakutane na Mkurugenzi wetu wa Barabara Vijijini, Ndugu Digaga na amefanya hivyo. Ofisi yangu sasa hivi wanakwenda kufanya tathmini ya kina ya nini kifanyike kwa sababu wananchi wa eneo hilo wamekwama sana katika suala la usafiri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kama alivyofika kwangu na kama nilivyomwelekeza kufika TARURA, ofisi yetu italifanyia kazi kwa nguvu zote eno hilo.
MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kata za Rhotia na Mbulumbulu Wilayani Karatu ni maarufu sana kwa uzalishaji wa mazao ya chakula. Hata hivyo barabara za kuelekea kwenye kata hizo zinazounganisha Makao Makuu ya Wilaya ya Karatu zina hali mbaya sana kwa kukosa matangenezo ya mara kwa mara lakini pia kutokana na mvua zilizonyesha mwaka huu; je, ni nini kauli za Serikali kwa Meneja wa TARURA Mkoa ili barabara hizo ziweze kutengenezwa ili wananchi waweze kufika kwenye masoko?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze kaka yangu Mbunge wa Karatu. Kubwa zaidi ni kwamba maelekezo yetu si kwa Meneja wa TARURA wa Mkoa wa Arusha peke yake, isipokuwa ni maelekezo yetu kwa Mameneja wa TARURA wote katika mikoa yote 26, kwamba wafanye needs assessment ya barabara zetu zote zilizoharibika. Lengo letu kubwa ni kwamba kile kichache tutakachokuwa nacho kwa ajili ya ukarabati tuweze kurekebisha maeneo hayo. Kwa hiyo ni maelekezo yangu kwa meneja wa TARURA wa Mkoa wa Arusha na hali kadhalika Mkoa wa Babati, Wilaya ya Karatu wafanye hivyo haraka iwezekanavyo watupe taarifa.
MHE. MUSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Katika mkakati wa kupunguza vifo vya mama na mtoto Jimboni Igalula tumeanzisha ujenzi wa vituo vya afya vitano kwa nguvu za wanachi na Mbunge ambapo tumefikia katika hatua ya boma. Je, Serikali ina mpango gani kusaidia nguvu hizi za wananchi ukizingatia hatuna kituo hata kimoja cha afya katika Jimbo la Igalula? Ahsante sana. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri sana, yale ya wali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali hili la Mheshimiwa Ntimizi, kwanza naomba nimpongeze Mbunge huyu, katika kazi ambayo ameifanya ni kuhamasisha wananchi wake kujenga vituo vya afya vipya lakini bado havijajengwa. Nikiri wazi kwamba amefika ofisini kwangu na kuweza kuweka kipaumbele katika suala zima la Jimbo lake. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama tulivyoongea ofisini kwetu jinsi gani tutafanya ofisi yetu isaidie katika suala zima maeneo yale tupate vituo vya afya hasa tukianza na vituo vya afya viwili, jambo hili ni commitment ya Serikali, tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo ili wananchi wa eneo lile la Jimbo la Igalula waweze kupata huduma ya afya.
MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kupunguza vifo vya akina mama wajawazito ni pamoja na uwepo wa vifaa vya kujifungulia katika hospitali zetu lakini mpaka hivi tunavyozungumza, ziko hospitali, zahanati na vituo vya afya akina mama wanatakiwa waende na mabeseni na mipira kwa ajili ya kujifungua. Ni lini tatizo hili litarekebishwa na Serikali yetu? Ahsante. (Makofi
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la dada yangu Mheshimiwa Sikudhani Chikambo, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Ruvuma, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tuna changamoto ya vifaa mbalimbali lakini lazima tumshukuru Mheshimiwa Rais, tukumbuke hapa katikati aliweza kutoa vifaa kwa karibu Halmashauri zote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na uboreshaji wa vituo hivi vya afya 208 tunavyovijenga ambavyo jumla yake pamoja na vifaa itagharimu karibu shilingi bilioni 156, naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge wote siyo muda mrefu sana vituo hivi vinavyokamilika, vifaa hivi tutavisambaza maeneo mbalimbali. Ni imani yangu kubwa kwamba tutapunguza kero kubwa sana katika suala zima la vifaa vya kujifungulia katika vituo vyetu vya afya na zahanati zetu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza kabisa, takwimu zinaonesha kwamba katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa ikiwemo Geita kuna changamoto kubwa sana ya vifo vya akinamama wakati wa kujifungua; na kwa sababu hiyo wengi inatokana na kwamba wakati wa kujifungua, pale wanaposhindwa kuwapeleka hospitali ya rufaa ya Mkoa inakuwa ni vigumu kwa sababu hakuna usafiri. Kwa hiyo, ni muhimu sana kituo cha afya cha Bukoli kipatiwe kwa kweli gari la wagonjwa. Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kuona umuhimu huo wa kupatiwa gari la wagonjwa katika kituo cha afya cha Bukoli? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, vile vile sambamba na gari la wagonjwa kuna upungufu mkubwa sana wa watumishi, hasa katika vituo hivi vya afya ikiwemo cha Bukoli pamoja na kituo cha Katoro, Chikobe, vyote hivyo. Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kuhakikisha kwamba inapunguza tatizo hili?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote naomba nimshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu mazuri yale ya awali. Nafahamu changamoto kubwa inayolikabili Jimbo la Busanda hali kadhalika Mkoa mzima wa Geita.
Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ombi lake tunalichukua, pale inapopatikana fursa tutaangalia nini cha kufanya kwa ajili ya kuweza kulishughulikia eneo hilo.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kwa ajili ya kupunguza hili tatizo la vifo vya akinamama na watoto; na hasa tuna kesi kubwa sasa hivi ya akinamama wengi kupata fistula kwa sababu ya kuwapeleka maeneo mbalimbali kwa kuwa referral system inapatikana mbali; ndiyo maana tumejielekeza katika kuimarisha vituo hivi vya afya.
Mheshimiwa Spika, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba Serikali yetu imejipanga; na mpango mkakati wa hivi sasa ni kwamba tunatarajia kukamilisha vituo vya afya 350 kwa lengo kubwa la kupunguza tatizo hili. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wote kwamba Serikali itafanya kila liwezekanalo; hata kule sehemu ya Songambele na sehemu ya Mkoka jambo hili lipo katika kipaumbele chetu kuhakikisha wananchi wanapata huduma vizuri.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Jafo; lakini nimesimama kwa sababu ya hoja ya Mheshimiwa Lolesia Bukwimba, kwamba Geita ni moja ya mikoa yenye idadi kubwa ya vifo vitokanavyo na uzazi. Kwa hiyo nakubaliana, nataka tu kuongeza majibu ya Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI.
Mheshimiwa Spika, sambamba na ujenzi au ukarabati wa vituo vya afya tunajikita pia katika kuboresha huduma ambazo akinamama wajawazito wanapatiwa. Kwa mfano tumeifanya tathmini, wanawake ambao wanakwenda katika vituo vya kutoa huduma za afya hawapimi, hawafanyiwi vipimo muhimu; kwa mfano wingi wa damu, labda mkojo na shinikizo la damu. Hivi leo Mheshimiwa Makamu wa Rais anazindua kampeni ya Kitaifa ya kuhimiza uwajibikaji katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi; na kipaumbele tumeweka Geita, Kigoma, Kagera na mikoa yote ya Kanda ya Ziwa.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, suala la kupunguza vifo halitamalizika kwa kujenga majengo tu, pia tunataka kusimamia ubora wa huduma anazopewa mama mjamzito pamoja na vitoto vichanga. Tunasema jiongeze tuwavushe salama.
Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)
MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Wilaya ya Karatu ina zaidi ya umri wa miaka 20 na haina hospitali ya wilaya badala yake wananchi wamekuwa wakipata huduma hiyo katika vituo vya afya binafsi na hata vile vya chini. Tayari kama Halmashauri tumeshatenga eneo la kutosha la kujenga Hospitali ya Wilaya. Je, ni lini Serikali sasa itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la kaka yangu, Mheshimiwa Mbunge wa Karatu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, licha ya ujenzi wa vile Vituo vya Afya 350 ambavyo tunaendelea navyo kama tunavyofahamu mpango wa Serikali katika mwaka huu wa fedha tunajenga hospitali mpya 67. Hata hivyo, mwaka huu wa fedha tena 2019/2020 bajeti tunayoenda nayo tutachukua maelekezo jinsi gani tufanye zile wilaya ambazo hazina hospitali za wilaya twende tukamalize tatizo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu Mkoa wa Arusha tulielekeza nguvu kazi kule maeneo ya Ngorongoro na
Longido hata hivyo katika bajeti ya mwaka huu ambao tunaenda kuipanga, si muda mrefu Aprili, 2019 tuka-take consideration ya maeneo hayo. Lengo ni kwamba wananchi wote wapate huduma kama inavyokusudiwa.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nina swali moja.Kwa kuwa ujenzi wa Kituo cha Afya Mboli ambapo hata Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI Jafo anakifahamu maana ndiyo barabara yake ya kwenda Chamkoroma kule. Na kwa kuwa kituo hiki hakijakamilika wamejenga wananchi, nilikwishawaomba shilingi milioni 500 TAMISEMI ili wakamilishe kituo kile.
Je, Serikali inasemaje kuhusu kutoa shilingi milioni 500 ili tuweze kukamilisha kituo kile ili wananchi wa Kata ya Matomondo, Kata ya Mlembule, Kata ya Chamkoroma na Kata ya Tubugwe waweze kupata huduma?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nikiri wazi kwamba nishukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri kwa maeneo yale ya Mheshimiwa Mgimwa ambayo ndiyo Serikali imejipanga katika utaratibu huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti,kwa swali la Mheshimiwa Lubeleje ambaye mimi namwita greda la zamani makali yale yale, si muda mrefu nilikuwa naye kule Wilayani Mpwapwa takribani wiki tatu zilizopita tulikuwa Mpwapwa. Hata hivyo kutokana na mchango mkubwa wa Mzee Lubeleje sasa hivi tunakamilisha Kituo cha Afya cha Mima na ndiyo maana siku ile alitoa hoja ya Kituo cha Afya cha Mboli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jukumu la Serikali kuhakikisha wananchi wa maeneo mbalimbali watapata huduma. Kwa hiyo, Mheshimiwa Lubeleje uwe na amani kwamba ni mpango wa Serikali kuboresha vituo vya afya na miongoni mwa vituo vya afya tutakavyoviimarisha ni Kituo cha Afya cha Mboli. (Makofi)
MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye majibu ya msingi ya Mheshimiwa Naibu Waziri ametuhamasisha Waheshimiwa Wabunge tuwahamasishe wananchi ili waweze kujenga shule za sekondari kwenye Kata ambazo hazina sekondari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Jimbo langu la Kigoma Kusini tunazo shule mbili za sekondari; tunayo Shule ya Basanza na Shule ya Mwakizega, lakini kinachosikitisha ni kwamba tangu hizi shule wananchi wamejenga wameweka madarasa kumi, ofisi za walimu na sasa hivi wanakimbizana na maabara. REO Mkoa wa Kigoma na Ukaguzi hawataki kabisa kuzisajili hizi shule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini TAMISEMI na Wizara ya Elimu hawakai pamoja na kuona ni jinsi gani shule ambazo mnatuhamasisha tuwaambie wananchi wajenge muwe pia mnazipa kipaumbele katika usajili? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimhakikishie dada yangu, Mheshimiwa Hasna kwamba TAMISEMI na Wizara ya Elimu tunafanya kazi kwa vizuri zaidi, ndiyo maana mimi na pacha wangu, Mheshimiwa Profesa Ndalichako tunakwenda vizuri, lakini hata hivyo naomba niwahakikishie kwamba tumefanya hamasa kubwa sana watu wajenge hizi shule kwa ajili ya kupunguza umbali wa watoto kusafiri na hasa kesi ya mimba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na inawezekana kuna maeneo mengine kuna case by case, naomba niichukulie kesi hii ya Mkoa wa Kigoma, Uvinza kuona kuna nini kinachoendelea. Lakini hata hivyo, naomba nitumie fursa hii kumuagiza Mkurugenzi wangu wa Elimu pale Ofisi ya Rais, TAMISEMI kufuatilia jambo hilo haraka iwezekanavyo ili mradi kwamba kama vigezo vyote vimekamilika kuweka mchakato wa haraka kuhakikisha shule hizo zinasaidiwa haraka iwezekanavyo.

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimshukuru Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa majibu mazuri ambayo ameyatoa na nimesimama hapa kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge kwamba Wizara yangu ndiyo inayohusika na usajili wa shule na hakuna urasimu wowote katika kusajili shule. Kinachotakiwa ni kwamba wanapoomba usajili vigezo na masharti viwe vimekamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu shule ambazo Mheshimiwa Mbunge, dada yangu, amezisema, bahati nzuri hizo shule nazifahamu na ukaguzi ulishafanyika. Kuna mapungufu ambayo yameonekana na hatua iliyopo sasa hivi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza ameshaji- commit kwamba ndani ya miezi mitatu, ifikapo Disemba, 2018 atakuwa amekamilisha mapugufu yaliyopo na timu yangu itarudi kukagua na kama viko vizuri usajili utatolewa kwa sababu tuko hapa kwa ajili ya kuwezesha juhudi za wananchi watoto wakasome.
MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ilivyo kwa Bagamoyo, Mji Mdogo wa Mbalizi ulianza mchakato wa kuomba iwe ni Halmashauri ya Mji kwa muda mrefu sana. Je, ni lini Serikali itaipa Mbalizi kuwa na hadhi ya Halmashauri ya Mji? Ahsante.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama wanavyofahamu Wabunge wengi sana humu, kuna mapendekezo mbalimbali ya maeneo mbalimbali kuanzisha mamlaka mpya lakini najua kwamba Mbalizi ni miongoni mwa maeneo ambayo yalikuwa katika mchakato wa kupandishwa hadhi, lakini nimuombe Mheshimiwa Mbunge kwamba tuvute subira kwa sababu mpango wa Serikali wa sasa hivi wa maelekezo ni kutoanzisha mamlaka mpya lakini kwa vile jambo hili liko katika subira tuvute subira pale hali itakapokuwa sasa imekaa vizuri Mji wa Mbalizi ni miongoni mwa miji ambayo itapewa kipaumbele cha kwanza katika upandishaji wa hadhi. (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Jimbo la Mbulu Vijijini lina kituo kimoja tu cha afya, je wananchi wa Maretadu wamejenga sana kituo cha afya cha Maretadu, je, Mheshimiwa Waziriy uko tayari kutusaidia fedha ya kumalizia kituo cha afya Maretadu?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeza Naibu Waziri kwa majibu mazuri yote ya kwanza. Namfahamu Mheshimiwa Flatei Massay na katika Jimbo lake kulikuwa na changamoto kubwa sana ya afya na ndio maana katika kelele zake nyingi sana kwa kuwaombea wananchi wake tulimpelekea hospitali ya Wilaya na kituo cha afya cha Dongobeshi. Hata hivyo, tunalichukua ombi hilo tutalifanyia kazi kwa sababu lengo letu na mkakati wetu wananchi wote wapate huduma ya afya, kwa hiyo jambo hili tutalichukua, tutaangalia jinsi gani ya kulifanyia kazi.
MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa ipo zahanati ya Kijiji cha Kigarama ambayo jengo la OPD limejengwa kwa nguvu ya wananchi mpaka kukamilika, lakini zahanati hiyo takribani miaka miwili haijaweza kufanya kazi kwa sababu hakuna nyumba ya watumishi na choo hakijakamilika. Upo uwezekano wa kupata nyumba ya kupanga kwenye center hiyo ya karibu ambapo ni rahisi Mganga kuweza kuhudumia akitokea hapo. Je, Wizara iko tayari kutoa kibali ili zahanati hiyo iweze kufunguliwa kuondoa adha ya akinamama wanaokwenda kujifungua kutembea umbali mrefu zaidi ya kilomita 30 wakati tayari wameshatoa mchango kwa ajili ya ujenzi wa zahanati hiyo?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kwa kauli yako naomba nimwagize Mganga Mkuu wetu wa Mkoa wa Kagera aende akafanye ufuatiliaji wa zahanati hiyo, kama imekamilika kweli lazima wahakikishe nguvu za wananchi ambao lengo lao wapate huduma kuhakikisha kwamba wanaipata. Kwa hiyo namwagiza Mganga wetu Mkuu wa Mkoa wetu wa Kagera aende akafanye kazi ili na Mheshimiwa Mbunge apate kibali na wananachi wapate huduma.
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na hayo, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, wananchi wanajenga katika maeneo mbalimbali ambayo Serikali inasema hayaruhusiwi kwa sababu ya uhaba wa ardhi lakini wakati huohuo maeneo hayo yana viongozi na baada ya kujenga wanapelekewa maji, umeme na kadhalika. Nataka kujua, Serikali inawachukulia hatua gani watendaji au viongozi wa maeneo kama hayo ambao wanawaacha wananchi wanajenga wakishakamilisha ndiyo wanaingia kwenda kuwaondoa na kwa sababu hiyo kuharibu mali zao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, suala la kuchukua madaraka vibaya kwa baadhi ya Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa bado linaendelea nchini. Natambua juhudi za Waziri wa Nchi, Mheshimiwa Jafo na Waziri Mheshimiwa George Mkuchika na hatua mbalimbali ambazo baadhi ya Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa wamechukuliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kuna wilaya nyingine kwa mfano Wilaya ya Hai, Mkuu wa Wilaya bado anaendelea na vitendo vya kuwakamata hovyo wawekezaji, wananchi na kushinikiza baadhi ya wanasiasa kwa kutumia vikosi vya askari wahame kwenye vyama vyao, hata Mkuu wa Mkoa wa Iringa…

MWENYEKITI: Uliza swali Mheshimiwa.

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Tulikuwa naye kwenye kikao juzi hapa tukamwambia ajirekebishe, akatoka akaenda ku- tweet kwamba sasa atakwenda speed kilometa 120 badala ya 80 alizokuwa anaenda nazo, sasa hii ni insubordination kwa Serikali. Baada ya matamko yote ya Mawaziri, Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa ambao bado wanaendelea ku-insubordinate Serikali ni hatua zipi ambazo Serikali imepanga kuchukua?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimshukuru Mjumbe wa Kamati yangu ya TAMISEMI, kaka yangu Mheshimiwa Selasini kwa maswali yake mawili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tumeshatoa maelekezo mbalimbali; jambo la kwanza watu wasivamie maeneo ambayo siyo halali kwa ujenzi, lakini jambo la pili tumetoa maelekezo kwa viongozi wetu kwa sababu wao tumewapa dhamana wahakikishe wanasimamia maeneo hayo. Kitendo cha wananchi hata kujenga sehemu isiyoruhusiwa halafu tunawaangalia mwisho wa siku kuja kuwabomolea sio jambo sawasawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, maelekezo hayo tumeshayatoa. Ndiyo maana Mheshimiwa Rais ametoa maelekezo katika baadhi ya vijiji na kuna Kamati Maalum inaongozwa na ndugu yangu Mheshimiwa Lukuvi inafanya kazi hiyohiyo lakini na maelekezo mengine ya Kiserikali tunayafanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili la kwamba baadhi ya Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wanaendelea kufanya mambo ambayo siyo sawasawa, ni kweli Mheshimiwa Mbunge unafahamu kwamba tulipotoka hali ilikuwa ni mbaya sana. Tulikuwa na idadi kubwa sana ya Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya hali kadhalika Wakurugenzi wa Halmashauri, hasahasa Wakuu wa Wilaya walikuwa wakifanya mambo sivyo lakini kazi kubwa iliendelea kufanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi ndani tunafanya tathmini hali imebadilika sana lakini katika tabia za binadamu tuna case by case ambazo tunazishughulikia na hata mambo unayozungumzia hivi sasa mengine yako katika utaratibu wa kushughulikiwa. Kwa hiyo, tuvute subira siyo kila kitu ni kutangaza publically lakini kuna mambo kama Serikali tunayafanyia kazi kwa sababu lengo letu ni utii wa sheria bila shuruti uweze kufanyika lakini kufuata utaratibu, sheria na kanuni kwa viongozi na wananchi wote. Ahsante.
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ukiacha Wakuu wa Wilaya ambao wanafanya vibaya wako Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa wanaofanya vizuri. Kwa mfano, kwa Wakuu wa Mikoa yupo Salum Hapi wa Iringa amekuwa mbunifu kupita kiasi, Ndugu Alexander Mnyeti, Ndugu Mrisho Gambo na Ndugu Paul Makonda... (Makofi/Kicheko)

MWENYEKITI: Mheshimiwa, uliza swali Mheshimiwa Mlinga.

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Swali langu ni hili, je, Wizara ina mkakati gani wa kuwaandalia motisha ama tuzo kwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya hawa ambao wanafanya kazi vizuri?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama nilivyosema hapo awali mwanzo tulikuwa na matatizo mengi sana, sasa hivi matatizo haya kwa kweli kwa kiwango kikubwa yamepungua sana. Ni kweli nikiri wazi kwamba kuna Wakuu wa Mikoa hivi sasa wanafanya kazi nzuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano, tulianzisha programu ya ujenzi wa viwanda, katika kila mkoa viwanda 100, matarajio yetu ni kupata viwanda 2,600 lakini tumepata viwanda 4,877 ni outstanding performance, lakini kazi hii imesimamiwa na Wakuu wa Mikoa.

Kwa hiyo, agenda ya kuwapa appreciation baadhi ya Wakuu wa Mikoa tumeshaanza kuifanya katika vikao vyetu na juzi-juzi baadhi ya Wakuu wa Mikoa tumeshawakabidhi vyeti vyao kwa jinsi walivyoshiriki katika kuhakikish mambo ya Serikali yanaenda vizuri. Kwa hiyo, hilo tutaendelea kulifanyia kazi, ahsante.
MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona. Si Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya tu ambao hawafanyi vizuri, wapo pia ma-RPC ambao hawafanyi vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, RPC anapotangaza kwamba wananchi wakiandamana atawapiga hadi wachakazwe, hivi kazi ya msingi ya Jeshi la Polisi kwa wananchi wanaolipa kodi ili walipwe mishahara, ni kuchakaza wananchi?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru sana swali la dada yangu Mheshimiwa Devotha Minja. Nadhani kitu kikubwa kama Taifa, jambo la kwanza tuweke ushirikiano katika kila eneo. Nadhani vyombo vingine vinaongozwa kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni hasa katika suala zima la mambo ya ndani na sitaki kuviingilia. Kwa hiyo, imani yangu ni kwamba wananchi wote tutafuata utaratibu wa utii wa sheria bila shuruti kwa ajili ya kuepuka migongano mingine ambayo inawezekana siyo ya lazima kwa afya ya Taifa letu.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Korogwe Mji tumekabidhiwa Hospitali ya Wilaya Magunga kutoka Korogwe Vijijini. Kwa bahati mbaya sana ina wodi moja tu ambayo wanalala wajawazito pamoja na wale waliojifungua. Je, Serikali itakuwa tayari kusaidia tupate fedha angalau tuweze kujenga wodi ya wajawazito na watoto?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri sana ya ndugu yangu Mheshimiwa Shekilindi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri wazi kwamba tumefika katika Hospitali ile anayoizungumzia Mheshimiwa Mama Chatanda mara kadhaa licha ya upungufu wa wodi lakini hospitali ile imekuwa ya wahenga sana, imekuwa kongwe. Kwa hiyo, ni mpango wetu kuhakikisha tunafanya maboresho ya hospitali za zamani. Nimhakikishie Mheshimiwa Chatanda kwamba licha ya wodi hizo lakini tutaangalia kwa jicho lingine jinsi gani tufanye hospitali ile ifafanane sasa na Halmashauri ya Mji wa Korogwe.
MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, pamoja na ujenzi wa hospitali na Vituo vya Afya lakini bado kuna upungufu mkubwa sana wa watumishi wa afya hapa nchini. Je, Serikali haioni sasa huu ni muda muafaka wakati wanajenga Vituo vya Afya, lakini pia watoe ajira mpya kwa watumishi wa afya na pia walipe stahiki za wale watumishi wa afya wengine ili kuongeza morali na tija?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Jimbo la Mikumi lina jiografia mbaya sana na tuna Vituo vinne vya Afya vya Kidodi, Mikumi, Ulaya na Malolo ambacho wananchi wanajenga kwa nguvu zao wenyewe. Je, Serikali haioni sasa huu ni muda muafaka ili kuokoa Watanzania wa Mikumi tuweze kupatiwa magari ya wagonjwa kusaidia akina mama na watoto ambao wanapata matatizo katika maeneo hayo? Ahsante sana.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mheshimiwa Haule katika ziara kadhaa nilizofanya tulikuwa pamoja kule Jimboni kwake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mpango wa Serikali, kama tunavyofahamu kwamba Mheshimiwa Rais na Serikali kwa ujumla imefanya mchakato wa ujenzi wa Vituo vya Afya 352hivi karibuni, Hospitali zetu za Wilaya 67 na mwaka huu tumeongeza 27 mpya, jambo hili linataka human resources kwa ajili ya kuweza kufanya kazi vizuri.

Kwa hiyo, ni mpango wa Serikali tutaangalia nini kifanyike. Licha kwamba mwanzo tuliajiri takribani watumishi wasiopungua 11,000; wale wa Serikali za Mitaa na Serikali Kuu lakini tutaangalia nini kifanyike kwa ajili ya kuongeza idadi ya watumishi katika vituo vyetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Mikumi suala zima la kuongeza miundombinu, nikushukuru, lakini Mbunge hapa kwanza unge-appreciate kazi kubwa iliyofanyika pale Mikumi, nadhani na wewe unakumbuka, ilikuwa ni ya kusuasua sana. Serikali tumeenda tumefanya kazi kubwa na hivi sasa imekuwa ni miongoni mwa Kituo bora sana cha Afya katika eneo lile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo tutaendelea kuangalia nini kifanyike kwa maeneo mbalimbali yenye changamoto kubwa, siyo Mikumi peke yake. Ni mpango wa Serikali kuangalia nchi nzima tunahakikisha wananchi wanaopata shida ya huduma ya afya sasa inakuwa ni historia. Ahsante sana.
MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Lupembe katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ina vituo vinne lakini haijawahi kupata fedha kwa ajili ya uboreshaji wa vituo hivi na jiografia ya Jimbo lile ni mbaya sana. Tunashuruku kwamba mmetupatia Hospitali ya Wilaya lakini wananchi wanataka kujua ni lini Halmashauri ya Wilaya ya Njombe itapata fedha kwa ajili ya uboreshaji wa Vituo vya Afya vya Kichiwa, Sovi, Lupembe na Ikuna ambacho ujenzi wake karibia unakamilika? Naomba tupate majibu.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, binafsi naomba nimpongeza Mheshimiwa Hongoli kwa vile nafahamu wazi na yeye anafahamu mpaka jana takribani saa tatu na nusu usiku tulikuwa tunaongea naye kuhusu suala zima la sekta ya afya. Hii inaonyesha jinsi gani anajali wananchi wake na kufuatilia masuala ya afya. Ndiyo maana katika awamu ya kwanza tulimpatia Hospitali ya Wilaya na najua katika mpango wa bajeti ya mwaka huu tumemtengea Kituo kimoja cha Afya lakini bado hali siyo nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana nilikuhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba ni commitment yetu sisi Serikali na Mungu akijalia huenda kabla hata mwezi Julai haujafika, tutafanya kila liwezekanalo tukupatie Kituo kingine cha Afya bora zaidi ili wananchi wa Jimbo lile la Njombe DC waweze kupata huduma vizuri.
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo hili linafanana sana na Hospitali ya Frelimo Mjini Iringa. Hospitali yetu ya Frelimo inatoa huduma kubwa kwa maeneo mengi ukizingatia kwamba Iringa Mjini ndiyo kitovu na maeneo mbalimbali wanakuja kutibiwa pale. Katika mpango wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa mmekuwa mkitoa pesa za vifaa kwenye hospitali mbalimbali lakini cha kushangaza mwaka jana kwenye Hospitali yetu ya Frelimo hamkutoa mkiona kwamba ni Kituo cha Afya wakati ni hospitali. Nilitaka nipate majibu ni kwa nini hamkutoa vile vifaa kama hospitali zingine kwenye Hospitali yetu ya Frelimo ambayo kwa kweli inasaidia wagonjwa wengi sana katika Manispaa yetu ya Iringa Mjini?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mheshimiwa Msigwa na Mheshimiwa Msigwa anafahamu nimefika pale Flerimo mara kadhaa na nakumbuka tulikuwa na Mbunge pacha wako Mheshimiwa mama Kabati. Hospitali ile inachukua watu wengi sana na mimi nimefika pale nimeona. Naomba niwapongeze Madaktari wa pale wanafanya kazi vizuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni commitment yetu sisi Serikali, naomba nikuhakikishie kwamba eneo lile tutaenda kuliboresha zaidi. Nilivyofika pale nimeona kuna kila sababu ya kufanya maboresha na rasilimali ni chache lakini lazima tutazigawanya. Kwa hiyo, ni mpango wa Serikali tutafanya kila liwezekanalo ili wananchi wa Iringa waweze kupata huduma vizuri katika Hospitali ya Frelimo.
MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Kituo cha Afya cha Endasak na Basotu nilishaongea na Mheshimiwa Waziri atusaidie kuboresha ili vionekane kama ni vituo kwa sababu havina hata wodi na havijafikia hadhi ile lakini vinajulikana na wananchi kama ni Kituo cha Afya. Naomba nijue Mheshimiwa Waziri anasema nini kuhusu vituo hivi viwili vya Hanang?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumshukuru mama yangu Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu senior MP katika Bunge hili. Ni kweli niliongea na Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu na bahati nzuri nimefika kule Hanang, ni mpango wa Serikali naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu kama tulivyozungumza ni commitment ya sisi Serikali tunatafuta fedha tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo vituo vile viweze kupata huduma kama tunayokusudia, kwa hiyo, hilo ondoa hofu Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu.
MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Ili uweze kwenda chuo kikuu ni lazima uwe na ufaulu unaostahili na ufaulu huu unategemea jinsi ambavyo wanafunzi wametengenezwa, wanafunzi wamejengwa kuanzia ngazi ya Msingi hatimaye Sekondari, A-Level na O- Level.

Mheshimiwa Spika, hali ya ufaulu ndani ya Mkoa wa Lindi ni mbaya, ni mbaya! Mkoa wa Lindi bila kuzungusha, umekuwa wa mwisho katika ufaulu. Kwa misingi hii, kuwa wa mwisho si tatizo, unaweza ukawa wa mwisho katika mazingira ya kufanya vizuri, lakini unaweza kuwa wa mwisho katika mazingira ya kufanya vibaya.

Mheshimiwa Spika, sasa kwa kuwa, Lindi tumekuwa wa mwisho katika mazingira ya kufanya vibaya, Je, Serikali ina mpango gani wa kuangalia changamoto zilizojitokeza ndani wa Mkoa wa Lindi mpaka kuwa wa mwisho? Na hii itapelekea kwamba kama Mheshimiwa Waziri husika akija na kuangalia nini changamoto zinazokabili Mkoa wa Lindi kuwa wa mwisho? Naomba Mheshimiwa Waziri, atengeneze ziara ili aje atambue changamoto zinazokabili Mkoa wa Lindi, pamoja wana Lindi wenyewe wameshakaa vikao vya mkakati kuangalia changamoto hizo. Ahsante. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimpongeze mama yetu Mama Salma Kikwete, hakika amekuwa mama mpambanaji sana kuhakikisha elimu inasonga mbele kwa wato wote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nilichukue jambo hili na ni kweli, Lindi imekuwa haifanyi vizuri na ndiyo maana hapa kipindi cha katikati, Ofisi ya Rais TAMISEMI kuona hivyo, niliweza kumtuma Naibu wangu Waziri Waitara alikwenda Mkoani Lindi kwa ajili ya kutembelea miongoni mwa shule mbalimbali na mambo mengine.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo lengo letu kubwa ni kuboresha shule zile kwanza mazingira yawe rafiki zaidi na ndiyo maana maombi ambayo Mama Kikwete naye aliyaomba hasa katika shule mfano kama ile Lindi Sekondari. Ndiyo maana hata katika kipindi cha sasa hivi hapa, tutakwenda kuifanyia ukarabati shule yote ya Lindi Sekondari, lakini siyo Lindi Sekondari, isipokuwa kuzipitia shule za Lindi kuziweka katika mazingira rafiki.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, mwenyewe nitafanya ziara maalumu Mkoani Lindi kwa ajili ya kuhakikisha jinsi gani tunafanya kuufanya mkoa huu sasa uinuke kielimu na ndiyo maana hata katika mgao wa walimu, kipaumbele chetu sasa hivi tunaona kwamba jinsi gani hata badaye tupeleke walimu wa kutosha na hata uhamisho wa walimu katika Mkoa wa Lindi hivi sasa tumesimamisha kaika mkoa ule kwa lengo kubwa kwamba mkoa huu tuweze kuu-promote uwe katika hali nzuri.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa mama yangu Salma Kikwete. Kwanza nimpongeze sana mama Salma Kikwete kwa kazi nzuri ambayo anaifanya katika kuhakikisha kwamba elimu inasonga mbele na hasa kwa mtoto wa kike.

Mheshimiwa Spika, na kuhusiana na swali lake, pamoja na majibu mazuri ambayo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI ameyazungumzia kuangalia miundombinu, nami nimuahidi Mheshimiwa Mama Salma Kikwete kama Wizara ya Elimu, ambayo kazi yetu ni kuweka Sera ya Elimu na kuhakikisha kwamba viwango vya elimu vinafikiwa, tutafanya ukaguzi maalum katika Shule za Mkoa wa Lindi, ili tuweze kubaini changamoto ambazo zinapatikana na tuweze kuchukua hatua mahususi kuhakikisha kwamba Mkoa wa Lindi unainuka katika ufaulu kwa wanafunzi ambao wanasoma katika shule za sekondari na shule za msingi.
MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, suala hili la upungufu wa madarasa limekuwa likijirudia mara kwa mara na Waziri anasema wana takwimu. Mwaka juzi wanafunzi 133,000 walifaulu lakini wakashindwa kuchanguliwa kwa sababu ya madarasa, lakini mwaka huu tena zaidi ya wanafunzi 58,000 wamefaulu darasa la saba lakini wamekosa madarasa.

Mheshimiwa Spika, swali langu, ni kwa sababu gani Serikali kama ina projection na inajua ni wanafunzi wangapi wanaweza kufaulu na wako darasa la saba, ni kwa sababu gani hawana mpango mahususi kuhakikisha kwamba kila mwaka wanatenga fedha kwa ajili ya madarasa ili angalau kwa miaka mitano tuhakikishe kwamba tatizo hili sugu limekwisha na wanafunzi wetu wanapomaliza darasa la saba wanakwenda shuleni kama wengine. Kwa sababu tunavyozungumza leo kuna Wanafunzi Dar es Salaam na Mikoa mingine wamefaulu darasa la saba lakini watakwenda kuanza mwezi wa tano, haoni kwamba hili ni tatizo? Ahsante sana.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimshukuru dada yangu Mheshimiwa Susan Lyimo kwa sababu amekuwa na mchango mkubwa sana katika elimu.

Mheshimiwa Spika, Serikali inafanya kila liwezekanalo na kwa mfano, mwaka huu tulikuwa na wanafunzi takribani 759,000 waliofaulu na hii inaonekana kutokana na juhudi kubwa ndiyo maana mwaka huu ufaulu umepanda kwa wastani wa asilimia 3.7 ambayo ni mafanikio makubwa sana yaliyowahi kutokea.

Mheshimiwa Spika, ndiyo maana licha ya ufaulu huo ulikuwa mkubwa lakini zaidi ya asilimia 92 na wanafunzi wote tuliowachangua katika awamu ya kwanza tulibakisha wanafunzi 58,000 ambao hata hivyo wanafunzi wote hivi sasa tumeshawachangua na hivi sasa kuna shughuli kubwa sana ya umaliziaji baadhi ya madarasa 1,080 ambayo naomba niwahakikishie Watanzania kwamba ukiona juhudi wanafunzi wanafaulu ni impact kubwa ya Serikali ya uwekezaji iliyosababisha mpaka wanafunzi waweze kufaulu zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tushikamane kwa pamoja kuona ufaulu mkubwa kwetu sisi iwe ni mafanikio makubwa kwamba Tanzania inasonga mbele katika suala zima la kuhakikisha kila Mtanzania anapata elimu. Ahsante.
MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, nilitaka kujua; kwa kuwa gharama ya kutumia asphalt yaani kujenga lami kama zinavyoonekana ni ya ghali na kwa kuwa ahadi za Mheshimiwa Rais ikiwemo barabara za Himo Mjini, Kahe na ya kwenda Kilema kwenye maeneo ya mwinuko zinahitajika zijengwe ili zipitike wakati wote. Nataka kujua, Serikali imefikia wapi kupitia wataalam kuja na teknolojia nyingine ya kutumia calcium oxide na moram ambayo ni rahisi kuliko hii ya asphalt ili ziweze zikatumike kwenye barabara zote nchi nzima na barabara zote ziweze kupitika kwa sababu ziko kwenye hali mbaya sana?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kijibu swali la kaka yangu James Mbatia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli gharama ya kutumia asphalt ni kubwa lakini mara nyingi sana mahitaji ya barabara aina gani ya teknolojia ijengwe ni kutokana na jinsi gani ya ile barabara mahitaji yake yalivyo. Ndiyo maana ukiangalia katika ofisi yetu sasa hivi kuna barabara tunazijengwa kwa double surface dressing na hizi cost yake unaona kwamba ina- range katia ya shilingi milioni 300 mpaka milioni 500 lakini barabara ya asphalt inakwenda mpaka one billion per kilometer.

Sasa unakuja kuona ukiangalia hizi barabara ambazo sasa hivi tunazijenga katika miji mbalimbali tunatumia asphalt kwa sababu mizigo inayopita huko na kwa sababu tunalenga katika ajenda ya kiuchumi lazima tutengeneze barabara ambazo zitaweza kupitisha magari mazito kuhakikisha tunachochea uchumi wa eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, ushauri uliozungumza katika kitengo chetu cha ofisi yetu kuna watu wanafanya research maalum kwa aina mbalimbali ya barabara ya madaraja na ndiyo maana hata ukienda kule Kigoma tumeamua sasa hivi kuna teknolijia nyingine tumetoa Belgium ya ujenzi wa madaraja, kwa hiyo hiyo yote ni juhudi ya Serikali kuangalia nini tufanye katika maeneo gani, lengo kubwa ni kuhakikisha Wanancho wote waweze kufika.

Kwa hiyo, ushauri wako unachukiliwa lakini naamini kwamba Serikali inafanya juhudi kubwa kuhakikisha Wananchi wanapata huduma nzuri ya barabara. Ahsante.
MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mtama niishukuru sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa kutupa bilioni 1.5 kwa ajili ya kujenga Hospitali ya Wilaya. Pamoja na shukrani hizi mwaka 2017 Waziri Mkuu alifanya ziara jimboni Mtama katika Kata ya Mtama na majengo ambayo ina idadi ya watu wengi sana na mpaka sasa tuna zahanati alitoa ahadi ya kujenga kituo cha afya. Sasa je, Serikali haioni umefika wakati wa ahadi hii ya Mheshimiwa Waziri Mkuu itekelezwe?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Nape Nnauye na wananchi wake wa Mtama kwa kazi kubwa waliyoifanya ya uimarishaji wa kituo cha Afya cha Mnazi Mmoja na hali kadhalika ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ambayo tumewapelekea fedha. Lakini tukijua wazi kwamba Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa ahadi sehemu hii ni jukumu letu la Serikali kwamba tutafanya kila liwezekanalo maeneo yote ambayo viongozi wetu wa kitaifa wametoa ahadi tutaweza kuyashughulikia. Sambamba na hilo hata kule mkoani Kigoma kwa Peter Serukamba kuna scenario kama hiyo zote tunaenda kufanyia kazi kwa kadri tutakavyokuwa tumejipanga, hakuna shaka.
MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana ni kwa nini Kituo cha Afya Nemba ambacho ni kipya na ujenzi umekamilika hakianzi kutoa huduma?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba kule kwake kulikuwa na changamoto kubwa sana na ndio maana tulianza na ujenzi wa kituo kile cha afya cha Yakanazi lakini kazi kubwa inaendelea ujenzi wa hospitali sasa wilaya.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo tumejenga vituo vya afya 352 na vituo hivi tumeshaanza kuwakilisha kwamba vingine vinapata vifaa na hivi sasa tunawasiliana na wenzetu MSD katika vile vituo vyote ambavyo vimekamilisha vifaa viweze kupatikana na kupeleka wataalam wetu, na lengo kubwa ni vituo hivi viweze kufunguliwa. Kwa hiyo, nikuhakikishie Mheshimiwa Oscar wala usiwe na hofu kituo kile kitafanya kazi vizuri kama ulivyopigania humu Bungeni na wananchi wako watapata huduma vizuri bila mashaka ahsante sana.
MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipa fursa hii ya kuuliza swali moja la nyongeza na nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri. Kwa kutambua kwamba tangu mwaka 2005 miaka 14 sasa wakati ambapo Bagamoyo ilipewa hadhi ya mamlaka ya Mji Mdogo uongozi na wananchi wa Bagamoyo wameendelea kupambana kutekeleza vigezo 12 vya kupandisha hadhi mji ule kuwa halmashauri ya mji. Mpaka hivi sasa imebaki vipengele hivyo viwili kimoja cha master plan kingine cha upimaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tutaendelea kupambana na hiki cha master plan lakini upimaji wa ardhi ni suala ambalo linahitaji gharama kubwa. Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo haina vitendea kazi vya upimaji wa ardhi hivi sasa havina vyombo kwa ajili ya upimaji wa ardhi. Je, Serikali ina kauli gani kuweza kuisaidia halmashauri hii ambayo imepambana miaka 15 sasa kwa ajili ya kuweza kupata hadhi?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Dkt. Jumanne Shukuru Kawambwa yeye na viongozi wake na wenzake na Mwenyekiti wa Halmashauri waliweza kufika ofisini mara kadhaa katika jambo hilo. Tunafahamu kwamba juhudi kubwa inafanyika na ni azma yetu kuhakikisha kwamba maeneo yote ambayo yana kipaumbele tuweze kuyafanyia kazi. Katika jambo hili naomba niseme wazi kweli tumekuwa na changamoto katika suala zima la upatikanaji wa vifaa lakini hata hivyo niwashukuru sana wenzetu wa Wizara ya Ardhi kwa ushirikiano mkubwa tunaoendelea kuufanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa halmashauri mbalimbali zitaweza kupata vifaa hivi kwa ajili ya kuhakikisha kwamba hivi vifaa vya upimaji vinaweza vikapatikana na tukumbuke wazi hata katika bajeti ya Wizara ya Ardhi jambo hili waliainisha wazi. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Jumanne Shukuru Kawambwa kwamba Serikali inalichukua hili kwa uzito mkubwa sana kuhakikisha halmashauri zetu zinawezeshwa kuhakikisha zinapima maeneo yao kwa urahisi zaidi ahsante.
MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kabla ya maswali yangu mawili ya nyongeza, napenda kutoa pongezi kwa Serikali kwa kukamilisha ujenzi wa barabara kati ya Mafinga na Igawa, ambayo ilikuwa imeharibika na kiasi cha kuwa chanzo cha ajiali nyingi ambazo zilipoteza maisha ya watu wengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, barabara zinazopitika mwaka mzima Mafinga ni wastani wa asilimia 24 tu; na Mafinga ni kitovu cha shughuli za kiuchumi za Wilaya ya Mufindi kutokana na mazao ya misitu na hivyo kuwa na mchango mkubwa sana katika uchumi wa Taifa letu. Je, Serikali, iko tayari kuiangalia Mafinga kwa jicho la huruma na kuiongezea fedha TARURA Mafinga ili angalau barabara hizi ziweze kupitika kwa mwaka mzima? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa mujibu wa hotuba ya Waziri ukurasa wa 83, TARURA inasimamia wastani wa barabara zenye urefu wa kilomita 100,000 na zaidi na katika hizo, lami haizidi kilometa 1,500, changarawe haizidi kilometa 24,000, za udongo hazizidi kilometa 85,000, madaraja zaidi ya 2,000 na makalavati zaidi ya 50,000. Je, Serikali iko tayari kuiangalia TARURA na kuiongezea fedha ama kupitia mfuko wa barabara ama kutafuta chanzo chochote? Kwa sababu ndiyo ambayo inasimamia barabara nyingi zinazobeba uchumi mkubwa wa kubeba mazao, malighafi na bidhaa kutoka vijijini kwenda highway?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kumpongeza bwana Chumi kwa sababu amekuwa mpiganaji mkubwa sana wa Mafinga katika kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma bora za maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, ukiangalia Mji wa Mafinga sasa unakua na eneo kubwa sana la uchumi. Ndiyo maana katika majibu yangu au majibu yetu, Naibu Waziri alizungumza kwamba Mafinga, Kasulu, Nzega na maeneo mengine ambako ile miji imechipua hivi sasa ambayo haikuwepo katika mpango wa kwanza, tunaliwekea mpango maalum. Kwa hiyo, Mheshimiwa Chumi nikuhakikishie kwamba Serikali itafanya tathmini ya kutosha nini kifanyike kwa Mafinga? Lengo ni kusaidia Mji wa Mafinga unaokua ambao vilevile unachangia uchumi hasa wa Taifa letu hili kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuongeza financing katika suala zima la TARURA, ni kweli. TARURA mwanzo tulifanya tathmini, mtandao wa barabara ulikuwa ni kilomita 108,000 lakini sasa hivi tathmini ya juzi, imefika kilomita 135,000, kwa hiyo, package yake ni kubwa. Kwa kuliona hili, Serikali hivi sasa kupitia Mfuko wa Barabara inaendelea kufanya tathmini, nini kifanyike kwa lengo la kuangalia jinsi gani tuboreshe kwa ajenda kubwa ya kusaidia TARURA iweze kufanya kazi vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tunaendelea kufanya resources mobilization kutafuta vyanzo vingine vya mapato na hasa kupitia wadau wetu wa maendeleo. Hapa niwashukuru DFID pamoja na USAID kwa kazi kubwa tunayoendelea kuifanya hivi sasa. Imani yangu ni kwamba kwa mkakati wa Serikali tunaoenda nao, huko mbele ya safari, tutahakikisha TARURA inafanya kazi vizuri kwa maslahi mapana ya Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Mji wa Tunduma ni sawa na Mji wa Mafinga na mji huu uko mpakani mwa Tanzania na Zambia na ni sura ya nchi ya Tanzania ambayo inapitiwa na Mataifa zaidi ya nane.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango huu wa uboreshaji wa miji hasa kwenye miundombinu ya barabara, unatakiwa ufanyike pia katika Mji wa Tunduma: Je, Serikali imejipanga namna gani kuhakikisha kwamba Mji wa Tunduma unapata barabara bora katika mpango huu ambao utaanza mwaka 2020.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru ndugu yangu kwa swali zuri la Tunduma. Nami nikiri wazi kwamba Tunduma ni miongoni mwa miji inayokua na hata katika kutembea kwetu pale, tulitembelea maeneo ya hospitali kuangalia miradi ya maendeleo, ni kweli kuna maeneo yana changamoto kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kama nilivyosema awal kwamba ni mpango wa Serikali, kwa sababu kuna ile miji ambayo ilianzishwa baada ya mpango kuanza, ambapo tulikuwa tumepata dola za Kimarekani karibu milioni 254, lakini pia kupitia mradi wa TSP tumetumia karibu milioni 840. Kwa hiyo, katika mpango wa sasa ni kwamba tutaweka Tunduma na maeneo yote yale ambayo mwanzo hayakuhusishwa katika ule mpango wa awali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo kubwa ni kwamba, kama tulivyofanya katika miji yetu mikuu sasa hivi ukienda Mbeya, Tanga, Arusha, Dodoma, ukienda Babati, Iringa, Musoma, Tabora, kokote unakopita tumefanya uwekezaji mkubwa wa kujenga barabara za kisasa, kuimarisha miundombinu na tutaendelea katika hiyo miji mipya ambayo ipo Tunduma hapo baadaye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Adha iliyopo Urambo ya Hospitali ya Wilaya kuhudumia population nje ya eneo linalohitajika ni sawa na ile ya Hospitali ya Mji wa Tarime ambayo kwa kweli na nimeshaongea mara nyingi sana hapa Bungeni, inahudumia watu nje ya population ya Mji wa Tarime, wanatoka Shirati, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na Serengeti.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Kata ya Kinyemanyoli waliamua kujenga kituo cha afya ili kupunguza ile population ambayo inaenda kupata huduma ya Halmashauri ya Mji wa Tarime na nilishauliza hapa akaahidi kwamba angeweza kupeleka fedha. Nataka kujua sasa ni lini Serikali itapeleka fedha ku-support nguvu za wananchi ili tuweze kuwa na kituo cha afya Kinyemanyoli kupunguza adha wanayopata wajawazito na watoto?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri kwa maswali yaliyoulizwa hapo awali.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu Mkoa wa Mara umekuwa na changamoto mbalimbali za sekta ya afya lakini tumefanya investment kubwa katika mkoa huo na tukifahamu kwamba eneo la Tarime Mji napo kuna changamoto hizo. Ni jukumu la Serikali kuangalia nini kifanyike katika maeneo hayo kama tulivyofanya kazi katika Mkoa mzima wa Mara. Kwa mfano, kwa sasa hivi tunajenga Hospitali za Wilaya takriban tatu na kuimarisha vituo vya afya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Esther Matiko kwamba tunaifahamu changamoto zilizopo kule na tunazishughulikia. Kikubwa zaidi naomba nimuagize Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara kwenda kufanya tathmini na kutuletea taarifa ili katika mchakato wetu wa bajeti unaokuja mwezi wa tano tuangalie jinsi gani tutaweza ku-address matatizo ya maeneo hayo kwa sababu lengo letu kubwa ni kuhakikisha kwamba wananchi wa Tarime Mji wanapata huduma vizuri. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Hospitali ya Mji wa Kondoa inahudumia takriban Halmashauri sita. Tunazungumzia Kondoa Vijijini, Chemba, Kiteto, wakati mwingine mpaka Hanang’ na Babati. Bajeti tunayopata ni shilingi milioni 45 kati ya milioni 160 ambayo tunahitaji kutoka Basket Fund. Nimelizungumzia sana suala hili Bungeni hapa.

Je, ni lini sasa Serikali itakubaliana na uhalisia wa mahitaji hayo na kutuongezea bajeti yetu kukidhi mahitaji ya wananchi wa maeneo hayo?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sannda, Mbunge wa Kondoa Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, tuna changamoto katika maeneo ya miji ukiachia ile Halmashauri ya Mji wa Kondoa lakini kwa dada yangu Mheshimiwa Esther Matiko pale Tarime na hali kadhalika kwa Mheshimiwa Chumi pale Mafinga. Ndiyo maana tumewaagiza wataalam wetu sasa hivi wanafanya analysis kuangalia changamoto kubwa ya idadi ya watu na mgawanyo wa fedha ili tuweze ku-regulate vizuri ili mradi maeneo hayo yaweze kupata huduma vizuri. Kwa hiyo, naomba tuwe na subira kidogo, wataalam wetu wanafanya kazi hiyo, naamini katika Mpango wa Bajeti yetu ya mwaka wa fedha 2020/2021 jambo hilo tutali-address vizuri kwa maslahi mapana ya wananchi wetu.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini ahadi hizi ni za muda mrefu kwamba Serikali ina mpango na mkakati wa kujenga daraja hili la Manamba kwenda Kijiji cha Tambi. Hapa anazungumzia kuhusu usanifu, je, ni lini sasa daraja hili litajengwa? Daraja hili ni upana wa mita 100 na wanafunzi wanashindwa kuvuka, ni lini sasa atajenga daraja hili?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa wanafunzi wa shule ya msingi na sekondari wanashindwa kuvuka mto huu kwenda shule ya sekondari na kwenda shule ya msingi na ni kero kubwa sana. Ni lini sasa pamoja na kutathmini mtajenga daraja hilo? Hata Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI analifahamu.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Seneta wetu Mheshimiwa Mzee Lubeleje ambapo mimi huwa napenda kumuita grader la zamani makali yale yale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli anayosema Mheshimiwa Lubeleje. Daraja lenyewe linaunganisha maeneo ya Mseta na Nambi lakini daraja lile ni kubwa kidogo na sasa hivi kuna korongo hata Mheshimiwa Mbunge anafahamu juzi juzi nilikuwa pamoja naye kule, ukiangalia tuna kazi kubwa ya kufanya. Tulikuwa na fedha kutoka DFID ambapo tulianza katika maeneo ili kuondoa vikwazo, tumekamilisha katika baadhi ya maeneo lakini pale lazima iwe fedha ya kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika tathmini inayofanyika lengo ni kutafuta fedha kwa sababu daraja lile siyo la shilingi millioni 300 au 4000, ni daraja kubwa linalotaka zaidi ya bilioni 2. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunalifahamu daraja hilo na nimuagize Mtendaji wetu Mkuu, watu wameshafanya design pale afike yeye mwenyewe Mhandisi Seif akaangalie ili katika mpango wa bajeti tuweke vipaumbele kwa sababu eneo lile lina watu wengi lazima tuweze kuwaokoa. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Lubeleje kwamba jambo lile tunalifanyia kazi kwa nguvu zote.
MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Matatizo ya kukosekana kwa madaraja na kusababisha watu kushindwa kuvuka yapo vilevile kwenye Kata ya Goba hasa Mtaa wa Kulangwa na kwenye mitaa kadhaa. Kwa sababu Serikali inalifahamu suala hili na Mheshimiwa Waziri wakati anajibu swali alisema kuna fedha maalum wanazitafuta. Je, watakapotafuta fedha maalum ni pamoja na Kata ya Goba ili kwenda kuondoa matatizo ya madaraja Mtaa wa Kulangwa na mitaa mingine? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la ndugu yangu Mheshimiwa Mnyika, Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunafahamu maeneo yenye changamoto mbalimbali ikiwepo katika Jimbo a Kibamba na tukifahamu wazi kwamba katika eneo la Dar es Salaam kuna maeneo mengi tumeanza kuya-address kupitia mradi wa DMDP lakini hata hivyo kuna maeneo mengine bado hasa katika Wilaya ya Kigamboni na baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Ubungo. Siwezi kutoa commitment ya moja kwa moja hapo kwa sababu mimi sitaki kuzungumza biashara ya uongo lakini kama Serikali tunaichukua changamoto hii na kuhakikisha wataalam wetu wanapitia maeneo hayo halafu kuangalia kipi kiwekwe kwenye kipaumbele cha kwanza ili kuwasaidia wananchi wetu waweze kusafiri na kutekeleza kufanya huduma zingine za kijamii. Ahsante.
MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Kutoka Mogitu kwenda Basotu na Haydom, kuna barabara ambayo inawafikisha watu hospitali wanapougua lakini kwa bahati mbaya kutokana na mvua maji mengi kutoka ukuta wa bonde la ufa yamekuwa yakiharibu ile barabara mpaka imefungwa na watu wawili kufia pale. Je, Waziri anasema nini kuhusu barabara hii? Nitashukuru watu wa Hanang wakisikia ili wawe na moyo wa kuendelea kuishi.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze mama yangu Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu kwa kazi kubwa sana anayofanya katika Jimbo la Hanang. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ni miongoni mwa barabara ambazo nimezipita mara kwa mara na nimepita mpaka Dongobesh. Ni kweli kuna changamoto kubwa na juzi juzi alinipa taarifa ya barabara hii na nyingine. Kubwa zaidi niseme siku ileile tuliyoongea niliweza kuwasiliana na Mtendaji wetu Mkuu wa TARURA kuhakikisha wanafanya tathmini ikiwa ni pamoja na barabara za Kilindi Mkoani Tanga. Imani yangu watu wangu wako site hivi sasa ama wanaelekea site ili tupate jawabu halisia nini tufanye tuweze kuwasaidia. Ni kweli najua kweli kuna changamoto katika eneo hilo. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa napenda kuishukuru Serikali kwa namna ambavyo imekuwa ikitukimbilia pale shule yetu imekuwa na majanga ya moto zaidi ya mara mbili. Tunaishukuru sana Serikali.

Mheshimiwa Spika, lakini la pili nishukuru kwa majibu mazuri niliyopewa na Waziri.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, katika huu mpango wa pili ambapo watakuwa wametafuta fedha, je, Shule ya Korongwe Girls itapewa kipaumbele cha kwanza hasa ikizingatiwa kwamba pia ina watoto wenye ulemavu ili walimu wale wawe na moyo wa kuendelea kufanya kazi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa tunazo shule za kata katika Halmashauri zetu kwa nchi nzima ambapo tulikuwa tumeweka mipango kwa ajili ya ujenzi wa maabara lakini kwa bahati mbaya sana Halmashauri nyingine zimeshindwa kukamilisha mahabara hizo. Je, mtakuwa tayari sasa kuweka mpango wa kukamilisha zile maabara zilizoko kwenye Halmshauri zetu ili watoto waweze kupata elimu iliyo bora kuliko bora elimu?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la mama yangu Mheshimiwa Mary Chatanda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Mary Chatanda maana kwa vipindi tofauti tumefanya ziara jimboni kwake Korogwe na awamu ya mwisho tulienda naye katika shule yetu ya Sekondari Korongwe na kuongea na wanafunzi na kubainisha changamoto mbalimbali. Nafahamu kwamba juzijuzi hapa shule ilipata madhara ya bweni kuungua na ndiyo maana nimetuma wataalamu ili bweni lile tulikarabati haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Spika, katika programu hii ya kukarabati, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Chatanda tutakapoanza awamu hii shule ya Korongwe tutaiweka katika awamu ya kwanza bila kigugumizi chochote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hali kadhalika mpango wa kuhakikisha tunamalizia maabara, kama mnavyokumbuka kwamba hapa katikati tulitoa zaidi ya shilingi bilioni 32.5 kwa lengo la kuhakikisha kwamba tunamalizia maboma mbalimbali. Tunajua fika fedha hii haitoshi kwani kuna mabweni mengine hayajakamilika.

Mheshimiwa Spika, ni azma ya Serikali hata katika mpango wa bajeti ya mwaka 2019/2020 tutahakikisha katika maeneo mbalimbali tunakamilisha ujenzi wa maabara na vifaa. Juzijuzi tumetumia zaidi ya shilingi bilioni 17 ili tupate vifaa vya maabara vijana waweze kufanya practically katika maeneo ya shule.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali kupitia Waziri, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa hospitali ya Mji wa Mbulu inategemewa na kata zinazopakana kutoka Wilaya ya Babati, Karatu na hata upande wa Jimbo la Mbulu Vijijini; na kwa kuwa hospitali hii inakabiliwa na upungufu mkubwa wa fedha za uendeshaji hali inayopelekea wagonjwa kujigharamikia wakati wa rufaa na ukosefu mkubwa sana wa dawa. Mheshimiwa Waziri ameshafika mara kadhaa na sasa hivi tuko kwenye mpango wa bajeti wa 2020/2021. Je, Serikali ina mkakati gani wa kusaidia hospitali ya Mji wa Mbulu kwa kuiongezea fedha za uendeshaji?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa Vituo vya Afya ya Daudi na Tlawi tayari vimeanza kutoa huduma, tunaishukuru sana Serikali. Pia nia ya Serikali ni njema kujenga Kituo cha Afya katika Tarafa ya Nambis ambapo vijiji vyake baadhi vina umbali wa kilomita 30 mpaka 40 kwenda hospitali wa Mji wa Mbulu. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka maombi niliyowasilisha ya gari la ambulance kutafutwa haraka ili wananchi wa kata hizo za Nambis na maeneo mengine ya pembezoni wapate huduma ya usafiri haraka kwenda kupata matibabu? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Zacharia Paul Issay, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge na pacha wake Mheshimiwa Flatei Massay hapa karibuni tulienda kufanya ziara katika Halmashauri hizi mbili na niwapongeze Wabunge hawa wamefanya kazi kubwa sana ya kusimamia miundombinu kwa fedha ambazo tumepeleka kule.

Mheshimiwa Spika, ni kweli hospitali ya Mheshimiwa Mbunge siyo suala la mgao wa fedha peke yake hata hali ya majengo haipendezi. Ndiyo maana kwa ombi la Mheshimiwa Mbunge nilipendekeza na nilielekeza kwamba zile shilingi milioni 500 sasa zianze kuibadilisha Hospitali ya Mbulu kwa sababu tunajua itakapokuwa na mazingira mazuri hata suala zima la ukusanyaji wa mapato litaongezeka. Hata hivyo, ni azma ya Serikali Mheshimiwa Mbunge wala usihofu tutaangalia nini kifanyike kuhakikisha mgao wa dawa katika eneo lile ambapo tunajua fedha nyingi sana zinaenda vijijini kuwasaidia Halmashauri ya Mbulu Mjini kuweza kuongeza ule mfuko wao wa dawa ili waweze kupata huduma vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ajenda ya upatikanaji wa ambulance, naomba nimhakikishie tutashirikiana na dada yangu Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya pale tutakapopata gari aina yoyote tutawapelekea. Kwa kweli nimefika kule na nimeona changamoto kubwa katika eneo hilo lazima tupate usafiri.
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, tarafa ya Mtae katika Halmashauri ya Lushoto ambayo ina kata tano ndiyo pekee mpaka sasa hivi haijapata kituo cha afya. Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kujenga kituo cha afya katika Tarafa ya Mtae?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la ndugu yangu Mheshimiwa Rashid Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hili amelileta kwa muda na alikuwa na changamoto pale Mnazi na Mtae na ndiyo maana tukaona tuanze katika eneo lingine lakini hii eneo la Mtae lipo katika mpango kazi wetu. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ajenda yetu ipo palepale katika mgao wa fedha tutakaoupata tutahakikisha suala la Mtae linapata kituo cha afya. Kwa hiyo, wala asiwe na hofu, ni jukumu letu kutatua changamoto kwenye maeneo mbalimbali. Kwa hiyo, Mheshimiwa Shangazi wala asihofu suala hilo liko katika mpango wetu wa kazi.
MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba sasa niulize maswali yangu mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, katika Mkoa wa Kagera, Halmashauri ya Bukoba na hasa Jimbo la Bukoba Vijijini ni mahali ambapo hawafanyi vizuri kielimu katika matokeo na hasa darasa la saba lakini pamoja mambo mengine ni ukosefu wa walimu na ni tatizo la muda mrefu. Kutokana na jibu la msingi bado kuna mahitaji ya walimu zaidi ya 500. Je, Serikali inalichukuliaje jambo hili na kuhakikisha walimu wanapatikana ili Bukoba Vijijini na yenyewe iweze kwenda mbele kielimu?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, yapo maeneo mengine katika Halmashauri mbalimbali za Tanzania ambapo yako mbali kabisa yaani tuseme ni remote areas ambapo walimu wakipelekwa hawaendi. Je, Serikali ina mpango gani kufanya uwiano kwa kuhakikisha walimu wanaenda katika maeneo hayo ili Watanzania wote waweze kufaidika na mfumo wa elimu uliopo katika nchi?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la mama yangu Mheshimiwa Conchesta Rwamlaza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema ni kwamba tutaendelea kufanya kila liwezekanalo na hasa katika mpango wa kuajiri walimu. Naomba nimhakikishie kwamba tutaweka kipaumbele katika Mkoa wetu wa Kagera tukijua kwamba mkoa huu ni miongoni mwa mikoa ya pembezoni na tunajua kwamba lazima tufanye juhudi ya kutosha. Kwa hiyo, katika mipango ya baadaye suala la walimu katika Halmashauri ya Bukoba tutalifanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, lakini suala la nini Serikali inafanya kuhakikisha usambazaji wa walimu unafanyika, kutokana na changamoto hiyo, tulichokifanya kupitia mpango wa PforR tumehakikisha tunafanya msawazo wa walimu. Tulipeleka fedha katika maeneo mbalimbali kuhakikisha walimu wanatawanya na tuliwaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri wahakikishe wale walimu waliojazana mijini wanahamishwa kwenda maeneo ya pembezoni kwa kupewa posho maalumu za kuwahamisha walimu ili hata watu wa pembezoni wafaidike na programu hii ya elimu bila malipo ambapo ni jambo jema kwa ajili ya vijana wetu. Kwa hiyo, suala hili tunalifanyia kazi kwa nguvu zote Mheshimiwa.
MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Kwanza naomba nitoe pongezi zangu na niwatakie kheri wanafunzi wote wa kidato cha pili kote nchini kwa kuanza mitihani yao ya taifa leo hii.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, nataka nijikite kwenye swali la msingi. Kwenye Halmsahauri ya Lindi Vijijini sasa hivi ni Halmshauri ya Lindi Mjini kwenye Jimbo la Mchinga, Kata ya Mpingo kuna shule shikizi. Bahati nzuri hiyo shule shikizi wananchi wamejitahidi, wamejenga na kule kuna wafugaji huenda mwakani ikaanza. Tatizo letu ni vifaa vya vitakavyotumika kwa ajili ya wanafunzi wale kujifunza na kujifunzia.

Je, Serikali itatusaidiaje kwenye tatizo hili kwa ajili ya wale wafugaji waliopo kule? Ahsante.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la mama yangu Mheshimiwa Salma Kikwete ambapo namuita kama Balozi wa Elimu katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nasema hivyo kwa sababu Mheshimiwa mama Salma amechukua muda wake mwingi sana ku-invest kusaidia watoto wa Kitanzania wapate elimu. Kwa hiyo, mama tunakushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, eneo hili ambalo amelizungumzia ni eneo la wafugaji, ni shule shikizi, kwa heshima ya mama yetu, naomba nimuagize Mkurugenzi wangu wa Elimu amuagize Afisa Elimu Mkoa atembelee haraka Shule hiyo Mpingo kwenda kufanya needs assessment kuona kuna jambo gani la haraka linatakiwa kurekebishwa mapema ili itakapofika Januari watoto waweze kupata matunda mazuri ya swali hili.

Kwa hiyo, namuagiza Mkurugenzi wangu aweze kufanya kazi hiyo haraka iwezekanavyo.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, sasa naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Jimbo la Kilolo na Wilaya ya Kilolo ni kubwa sana na Mheshimiwa Waziri anajua; na kwa kuwa Halmashauri ya Mji Mdogo wa Kilolo ambayo ni Ilula ilianzishwa muda mrefu, zaidi ya miaka mitano, kwa kigezo kwamba ili kupunguza ukubwa wa wilaya na jimbo ili kuwafikia wananchi. Je, sasa haoni ni wakati muafaka sasa wa kuipa hadhi ya kuwa halmashauri kamili kwa sababu vigezo vyote vilivyotajwa hapa vimekamilika?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Wilaya ya Kilolo ina ukubwa na sifa zote zinazokubalika; na kwa kuwa vikao vingi vimeshakaliwa, je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kufika Wilaya ya Kilolo na kujionea mwenyewe jinsi mambo yalivyo tayari kwa kugawa kutupa halmashauri kamili?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya kaka yangu, Mheshimiwa Venance Mwamoto, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, suala la Mji wa Ilula nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge, ziara yetu ya kwanza ambayo nilifanya mimi na yeye ambayo impact yake ndiyo maana Kilolo leo hii imepatikana hospitali ya wilaya ya kisasa. Licha ya ziara ile, jambo lingine kubwa tulitembelea eneo la Ilula na maeneo mbalimbali na ni kweli; Halmashauri ya Kilolo ni kubwa sana maana inapatikana mpaka huku na Kibakwe, ukiangalia jiografia yake ni kubwa sana. Kwa hadhi ya eneo lile, hasa Ilula, inapaswa kuwa halmashauri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, maelekezo ya Serikali ya hivi sasa kwamba status quo inabakia kwamba mpaka pale Serikali ijipange kwa sababu maeneo yote sasa hivi yamesimamishwa kupandishwa hadhi, lakini japo kuwa hadhi inastahili lakini kwanza kipindi cha sasa itasubiri kwanza mpaka hizi halmashauri ambazo zimeshapandishwa tuweze kuziwekea infrastructure za kutosha.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo jambo hilo naomba nimwambie kwamba lipo katika pending issue pale ambapo sasa tukipewa go ahead na utaratibu utakapokwenda vizuri tutalifanyia kazi wala Mheshimiwa Venance Mwamoto asihofu.

Mheshimiwa Spika, ajenda ya ukubwa wa halmashauri yake kama nilivyosema awali mimi na yeye tumeshatembea sana mpaka katika yale madaraja yaliyokuwa hayapitiki. Nimhakikishie kwamba tumefanya kazi kubwa, Mheshimiwa Venance Mwamoto asihofu, pale muda utakaporuhusu jambo hilo Serikali italiangalia kwa jicho la karibu sana.
MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri lakini kwa kuwa wananchi hawa wa maeneo ya Mipande na Mtegula, lakini pamoja na Mwitika - Maparawe, wamekuwa wanapata adha kubwa sana kutokana na kukosekana kwa madaraja haya makubwa; na kwa kuwa Mheshimiwa Rais alishahaidi kuyashughulikia madaraja haya, naomba Serikali itoe kauli ni lini madaraja haya ya Mtengula - Mipande na Mwitika - Maparawe yatajengwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kwa kuwa madaraja haya ambayo Mheshimiwa Rais aliahidi jumla ni manne na tayari daraja la Shaurimoyo na Nanjocha yalishajengwa kwa kutumia TANROADS. Je, Serikali haioni umuhimu TANROADS kumaliza madaraja haya mawili yaliyobaki? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Jerome Dismas Bwanausi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli madaraja haya yamekuwa na kadhia kubwa sana na nikiri wazi Mheshimiwa Bwanaus alikuja pale mpaka nikamkabidhi kwa Mkurugenzi wetu wa TARURA Bwana Seif wakaweza kuongea vya kutosha na ndiyo imewezesha sasa hivi usanifu unafanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kutokana na shida iliyo pale na hili ni agizo la Mheshimiwa Rais na Serikali imeshakamilisha kile kipande kingine cha madaraja, jukumu kubwa sasa ni kwamba usanifu huu utakapokamilika tutaangalia ni wapi fedha zitapatikana. Mimi na kaka yangu Kamwelwe tunashirikiana kwa karibu zaidi na baada ya usanifu tutashirikiana kuona jinsi gani tutafanya ikiwezekana wenzetu wa TANROADS waweze kusaidia katika eneo lile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Lulindi kwamba kama Mheshimiwa Rais alivyoelekeza madaraja haya yatajengwa ili wananchi hawa wanaopata shida kwa kipindi kirefu waweze kuondokana na adha hii inayowakabili.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa madaraja katika maeneo mengi nchini ikiwemo Jimbo la Mbulu Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Daraja la Gunyoda katika Jimbo la Mbulu Mjini linahitaji zaidi ya shilingi milioni 700 na hadi sasa ni mwaka wa nane (8) Serikali ikiombwa kujengwa daraja hilo. Je, Serikali haioni umuhimu mkubwa wa kuja na mpango mkakati kupitia TARURA na TANROADS ili kuainisha baadhi ya madaraja ambayo yanakwamisha huduma za jamii ili kuweza kutatua tatizo hili kwa nchi nzima?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Zacharia Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikiri wazi kwamba Mheshimiwa Issaay tumeshafika Jimboni kwake takribani mara kadhaa na mwezi mmoja na nusu uliopita nilikuwa kule na kweli wana changamoto hizo. Nadhani kwa juhudi yake aliyoifanya na mwenzake kule Mheshimiwa Flatei walikuwa na changamoto kubwa la Daraja la Magara ambapo leo hii Serikali imeshasikia na kuweza kujenga lile daraja la Magara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii maana yake ni nini? Ni mpango wa Serikali maeneo yote yenye vikwazo aidha kupitia TARURA au kupitia TANROADS kuondoa changamoto zilizopo na mpaka sasa kazi kubwa imefanyika maeneo mbalimbali. Nimtoe hofu Mheshimiwa Zacharia ni mpango wa Serikali kupitia TARURA na TANROADS kuhakikisha tunaondoa vikwazo kwa wananchi ambao wanashindwa kusafiri katika maeneo hayo.
MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tatizo la daraja linawakumba pia wananchi wa Mbagala – Nzasa – Kilungule
- Mwanagati - Buza. Eneo hilo maji yanapojaa katika Mto Mzinga wananchi wanashindwa kuvuka na hata watoto wanashindwa kwenda shuleni mpaka wananchi wamejijengea daraja lao la miti. Je, Serikali lini itajenga daraja hilo ili kuwasaidia wananchi hao?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la mama yangu Mheshimiwa Kisangi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, ukiangalia maeneo ya Mbagala yote yalikuwa na changamoto kubwa sana na ndiyo maana Serikali tumeanza awamu kwa awamu. Mheshimiwa Kisangi unakumbuka kulikuwa na changamoto kubwa kati watu wa Mbagala Kuu na Kibada kupitia Twangoma. Serikali imekalisha ujenzi wa daraja kubwa maeneo yale kwa mabilioni ya fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, nafahamu changamoto iliyopo katika Mto Mzinga na mimi mwenyewe nimeshatumia barabara ile kwa kutumia pikipiki mara kadhaa, nalifahamu eneo hilo. Nimhakikishie kwamba ni jukumu la Serikali eneo lote la Jiji la Dar es Salam miundombinu ambayo ilikuwa ina changamoto kubwa kupitia mpango wa awamu kwa awamu maeneo yote tutaweza kuyaunganisha ili wananchi waweze kusafiri kutoka eneo moja mpaka eneo lingine.
MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba niulize swali, barabara ya kutoka Igunga - Itumba - Loya madaraja yake pamoja na barabara yenyewe imeharibika sana na ilipata fedha kwenye bajeti iliyopita lakini mchakato wa kumpata mkandarasi umechukua muda mrefu sana. Nimeongea na TARURA hata Makao Makuu bado sasa ni miezi sita. Je, ni lini barabara hii itakarabatiwa kwa sababu fedha ipo?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Dalaly Peter Kafumu, Mbunge wa Igunga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tuseme kwamba kulikuwa na changamoto kwako na Nzega kule kwa Mheshimiwa Bashe, tumepeleka hela kwa pamoja daraja kule kwa Mheshimiwa Bashe limekamilika lakini kwako Mheshimiwa Dalaly bado kuna changamoto kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kueleza maneno mafupi, nimuagize Mtendaji Mkuu wa TARURA, Bwana Victor Seif ahakikishe kwamba ndani ya mwezi mmoja nipate matokeo nini kinafanyika eneo hilo kwa sababu fedha zipo hatuna sababu ya kuchelewa. Kwa hiyo Mheshimiwa Kafumu haya ni maelekezo yangu ndani ya mwezi mmoja nipate status ya ujenzi huo na ndiyo maana namuagiza Mtendaji wangu Mkuu wa TARURA afuatilie eneo hilo.
MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa ni miaka 19 tangu mgogoro uanze na wananchi wale hawafanyi mwendelezo wowote, walijenga majengo yao wakasimamishwa. Je, Serikali ipo tayari kuwalipa fidia ya hasara ambayo wameipata kwa muda wote huo?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la mama yangu Mheshimiwa Mary Muro, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli ni muda mrefu na kwenye taarifa yangu hapa nimesema. Hata hivyo, kila kitu lazima kina win-win situation na ndiyo maana nimesema kwamba kuna mkakati unaendelea. Kikubwa zaidi nimuelekeze Mkurugenzi wetu wa Halmashauri ya Kibaha aende akakae na wananchi wakubaliane nini kifanyike kwa ajili ya eneo hilo ili kuondoa mgogoro huu ambao umedumu kwa muda mrefu lakini mwisho wa siku kila mwananchi awe na furaha.

Kwa hiyo, Mheshimiwa mama Muro achukue maelekezo yangu haya kwamba namuelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri yetu aende kukaa na wananchi pamoja na timu yote na ikiwezekana Kamati ya Fedha, on site meeting, wakubaliane nini kifanyike ili mradi kuondoa dukuduku za aina yoyote kwa wananchi wetu wa Kibaha Vijijini.
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali ninayo maswali mawili ya nyongeza.

(i) Je, Serikali itapeleka lini fedha ilizoahidi kwa ajili ya kujenga mabweni na maktaba pale Bugene Sekondari ambao ni A-level peke yake ya Serikali kwenye wilaya ya watu laki tatu na tisini?

(ii) Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kuambatana na mimi pamoja na Mbunge wa Jimbo Mheshimiwa Bashungwa ili ukajionee mlundikano wa wanafunzi Bugene Sekondari kwa sababu ya upungufu wa mabweni?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza naomba nianze kujibu swali la pili kwa kwanza nipo tayari tutaambatana pamoja hakika tutaenda kufanya kazi nzuri tu kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kifupi niseme nimpongeze sana Mheshimiwa Oliver, kwa sababu yeye na Mbunge Mheshimiwa Innocent wamekuwa wakipambana sana kuhakikisha Halmashauri ya Karagwe inafanya vizuri. Eneo hili ndio maana hata ile shule ya kwanza tuliyoipatia shilingi 190 ni kwa ajili ya maombi yao waliyoyaleta ofisi kuhakikisha tunasaidia wazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na upande wa Bugene sekondari tunajua ni wazi kweli idadi ya wanafunzi ni wengi, naomba nikuhakikishie Serikali itafanya kila liwezekanalo kuhakikisha tunaongeza fedha pale kwa ajili miundombinu ile iweze kuimarika vizuri tuweze kupokea watoto ambao tunatarajia si muda mrefu tutawatangaza. Kwa hiyo, hii ni commitment ya Serikali tutafanya kila liwezekanalo tutaongeza fedha kuimarisha miundombinu ya pale.
MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali, katika jimbo langu la Bunda kuna maboma ya maabara na hasa katika Shule ya Sekondari Salama. Mheshimiwa Waziri hatudhuliani ni ndugu yangu, katika ile shule kumekuwepo na maboma mawili ambayo kuna mabati na mbao zinaenda kuonza ni muda mrefu, wananchi hali yao ni mbaya wamekuwa na michango mingi kwenye maeneo mbalimbali. Nakuomba Waziri hili ni ombi rasmi nakuomba Waziri unisaidie kunipelekea milioni 30 tu kwenye shule ya sekondari salama ahsante.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue ombi la Mbunge Boniphace kwa sababu nikifahamu eneo lake lile kwa kweli kuna changamoto nyingi mbalimbali na nikiri wazi kwamba eneo hilo lazima tulipe kipaumbele kwa sababu kuna fedha tu kidogo zinahitajika tutaangalia mfuko ukoje halafu tutashirikiana mimi na wewe kuangalia jinsi gani tutafanya kuhakikisha hiyo miundombinu ambayo wananchi wamejitolea isiweze kuharibika.
MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru shule ya wasichana Nyalanja yenye kidato cha tano na sita ina mchepuo mmoja tu lakini inayo madarasa sita zaidi ya miaka mitano hayatumiki.

Je, Serikali haioni haja ya kutupatia bweni kwa ajili ya kuongeza mchepuo mwingine?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kuna miundo mbinu kama hiyo, naomba nilichukue jambo hilo kwa sababu hivi sasa ukingalia tuna vijana wengi sana ambao kwa kweli ufaulu umeongezeka. Kwa mfano mwaka huu tuna vijana zaidi laki moja plus ambao wote wanatakiwa wape nafasi kwa ajili ya kidato cha tano na kuendelea. Kwa hiyo, kama kuna fursa kama hiyo ya madarasa yapo tutaangalia nini tufanye ikiwezekana tukatafute fedha kwa haraka tuongeze pale bweni kwa ajili kuhakikisha kwamba tunaongeza mchepuo mwingine vijana wengi wa kitanzania waweze kupata nafasi.
MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo wanafunzi wengi wa kike wamekuwa wakipata mimba katika mazingira magumu.

Je, Serikali ina mikakati gani kujenga hostel za watoto wa kike ili wapate kujistiri waondokane na vishawishi vya barabarani?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli ndio maana azma ya Serikali juzi juzi mwezi wa tatu Serikali imetoa takribani shilingi bilioni 54.6 ambayo katika hili lengo lake ni kujenga madarasa takribani 988 lakini mabweni mapya 210 kwa hiyo ni commitment ya Serikali kuhakikisha jinsi gani mabweni haya yanjengwa.

Kwa hiyo, Mheshimiwa dada yangu naomba nikuhakikishie kwamba tutafanya kila liwezekano tutaangalia nini tufanye licha tunaanza kujenga mabweni 210 katika maeneo mbalimbali lakini juhudi ya Serikali itaendelea kuhakikisha vijana hawa wa kike tunawaondoa katika hali hatalishi zaidi hasa kwa watu ambao wana nia mbaya kuhakikisha wanaharibu future ya watoto wa kike. Kwa hiyo, tunaendelea kulichukua kwa ajili ya Serikali kulifanyia kazi.
MHE. SEBASTIANA S. KAFUPI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru pamoja na majibu mazuri ya Serikali Mkoa wa Katavi ni kati ya mkoa ambayo haijafunguka kwa maana ya kuunganishwa na mikoa mingine. Kitendo cha kupewa kilomita hizo chache kinafanya mkoa huu uendelee kujifunga. Serikali inasema nini katika hilo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo kama haitoshi kigezo cha idadi ya magari yanayopita katika barabara ni tunda la uzuri wa barabara. Serikali inasema nini kwenda kuboresha barabara ili baadaye idadi ya magari iongezeke?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nami ni shahidi kwa sababu nimefika Mkoa wa Katavi mara kadha na Mheshimiwa Kapufi anafahamu, na ndio maana Serikali hata katika Manispaa yake pale tunawekeza fedha nyingi sana kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu wa barabara za lami. Lakini hata hivyo ni kweli vigezo hivi vimewekwa kwa mujibu wa utaratibu kama pale itakapobidi tutaangalia nini kifanyike kuhakikisha kwamba Mkoa wa Katavi unapatiwa fedha za kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo naomba nikuhakikishie kwamba jukumu la wizara yetu yale maeneo yenye changamoto kubwa tutahakikisha kwamba kama maoni yako ulivyotoa hayo tutahakikisha jinsi gani tunaipa nguvu. Na ndio maana hata katika addition finance ya sasa hivi ambayo bado hatua disclose tumeweka kipaumbe kwa ajili ya kuongeza katavi kupata fedha nyingi za ziada nini kifanyike katika eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hata hivyo katika suala nzima la traffic ya magari kama ulivyosema ni jukumu la Serikali sisi tunahakikisha kwamba tunaimarisha miundombinu ya barabara hizo lengo kubwa ni kwamba barabara zikifunguka magari mengi yatapita. Kwa hiyo, ni jukumu la Serikali kwa hiyo Mheshimiwa Kapufi usihofu Serikali ipo kwa ajili yakuwahudumia wananchi.
MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Halmashuri ya Uvinza ni halmashauri ambyao kijiografia na kimuundo imekaa katika mazingira magumu sana. Lakini kwenye mgao wa bajeti Halmashauri ya Uvinza imekuwa ikipata pesa dogo, na huku inashindwa kutekeleza miradi ya kimaendeleo katika halmashauri yake. Mheshimiwa Waziri ni shahidi aliona ukubwa wa jimbo na mazingira jinsi yalivyo na alituahidi kutuongezea fedha katika mgao wa bajeti.

Je, Mheshimiwa Waziri katika bajeti ya 2019/2020 umezingatia kuongeza pesa za maendeleo katika Halmashauri ya Uvinza?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nami nilikuwepo Uvinza mara kadhaa na juzi juzi nilikuwanae Mheshimiwa Mbunge. Na ni kweli ukitoka makao Makuu ya uvinza mpaka unafika kule kalya karibu kilomita 300 na jimbo kweli ni kubwa, kwa hiyo, jukumu la Serikali tutafanya kila liwezekanalo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndio maana katika bajeti ya mwaka huu kuna fedha kidogo tumeiongeza Mheshimiwa Mbunge na hata katika kipaumbele tukaona hata pale mjini kidogo japo angalau tuongeze na tabaka la lami.

Kwa hiyo, kuna bajeti ya kuweka tabaka lami pale mjini lakini hata hivyo tunajua kwamba changamoto kubwa ipo katika Uvinza kwa siku za usoni tutaendelea kwa kuifanyia kazi eneo hili kwa sababu kasungura kenyewe kadogo tutajitahidi kufanya kila liwezekano lengo kubwa ni kuimarisha Uvinza iende vizuri.
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri pale Mtwara Mjini Manispaa ya Mtwara mjini nimekuwa naulizia barabara kwa muda mrefu barabara ya kutoka Mikindani, Lwelu mpaka Dimbuzi lakini barabara ya kutoka kata ya ufukoni, Mbaye mpaka Mbawala chini. Lakini barabara ya kutoka Mtawanya mpaka Namayanga. Barabara hizi nimekuwa nikizungumza ndani ya Mbunge hapa kwa muda mrefu na hivi sasa TARURA imekuwa inasuasua kuzitengeneza barabara hizi ambazo ni muhimu kwa wananchi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuzitengeneza barabara hizi kwa kiwango cha lami?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuchukue jambo hili kama ulivyosema Mheshimiwa Mbunge. Lakini naomba kuweka takwimu sawa kwamba katika maeneo ambayo tumeyapa kipaumbele sana ni Mtwara Mikindani. Katika mpango wetu wa miji mikakati, miji ile ambayo nane ambayo inahusisha Tanga, Dar es Salaam, Arusha, Dodoma, Ujiji lakini vilevile Mikindani ipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ndio maana leo ukiangalia ya miaka mitano iliyopita na Mtwara ya leo ni vitu tofauti. Lakini huwezi ukafanya mambo yote kwa siku moja, imani yangu Serikali tutaendelea kupambana lengo kubwa ni kuwahudumiwa wananchi hasa wa Mtwara mikindani na maeneo mengine waweze kuhakikisha barabara zao zinapitika kwa wakati wote.
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize maswali ya nyongeza. Kwa kuwa Mkoa wetu wa Iringa ni mkoa ambao kwa kweli una baridi sana na wanafunzi wengi wamekuwa wakisoma kwa shida kutokan ana uchakavu mkubwa uliopo wa shule zetu za msingi. Na shule zetu nyingi za msingi toka zimejengwa hazijawahi kukarabatiwa, nishukuru baadhi ya wazazi wa Mkoa wa Iringa wamekuwa wakisaidia katika ukarabati na Mheshimiwa Waziri nafikiri alikuja akaona baadhi ya shule ambazo tumeanza kuzikarabati.

Je, Serikali iko tayari sasa kusaidia angalau kidogo baadhi ya shule ule ukarabati ambao wazazi wanafanya na Serikali ikasaidia japo kidogo ili tuweze kukarabati shule nyingi za Iringa?

Mheshimiwa Spika, swali letu la pili, kwa kuwa pia sambamba na hilo, shule nyingi za sekondari maabara nyingi hazijakamilika na wanafunzi wengi sana wamekuwa wakifanya mitihani bila kusoma vizuri kwa sababu ya kutomalizika kwa maabara.

Je, Serikali sasa inasemaje kuhusiana na kumalizia maabara ambazo bado hazijaisha ili wanafunzi wetu wa Iringa waweze kusoma na kufaulu vizuri?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya dada yangu, Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mkoa wa Iringa pamoja na mikoa mingine ina changamoto hizo za uchakavu wa miundombinu. Lakini naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu safari zangu za Mkoani Iringa tulivyofika pale katika Manispaa ya Iringa alienda kunionesha akiwa na timu yake pale, miongoni mwa shule ambazo yeye mwenyewe na wadau wenzake waliweza kushiriki katika ukarabati.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, lengo la Serikali yetu ni kuhakikisha tunafanya kila liwezekanalo kufanya ukarabati wa shule hizi ndiyo maana juzijuzi Serikali yetu imetoa zaidi ya shilingi bilioni 35.5 kwa lengo la kuhakikisha kwamba tunaongeza nguvukazi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kubadilisha miundombinu hiyo.

Mheshimiwa Spika, lakini hata hivyo, nikiri wazi kwamba katika suala zima la maabara kweli kuna changamoo kubwa, kama lengo la Serikali lilivyo kwamba agenda yetu kwa mfano katika bajeti ya mwaka 2019/2020 ambayo nimeiwasilisha hapa Bungeni siku chache zilizopita, zaidi ya shilingi bilioni 90.08 tunazielekeza katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, lakini karibuni bilioni 58 kati ya hizo zinaenda katika elimu ya sekondari na lengo letu kubwa ni kuhakikisha kwamba maabara tunaziimarisha katika maeneo yetu na ndiyo maana juzijuzi tumetoa fedha zaidi ya shilingi bilioni 16 ambazo tunakwenda kununua vifaa vya maabara kwa vijana wanapokuwa sekondari waweze kusoma vizuri masomo yao.
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, High School ya Kirando tumejenga maabara leo miaka minne, na mlileta vifaa vya maabara vinakaa chini vinaliwa na mchwa. Lini Serikali itapeleka pesa kumaliza majengo matatu ambayo yako tayari yameshapigwa bati lakini yamekaa kama vichaka vya kuchezea panya ndani?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Keissy na DC wake wa Wilaya ya Nkasi, ndugu yangu Saidi Mtanda, katika wilaya ambazo zinafanya kazi kubwa sana ya ujenzi wa miundombinu ni Wilaya ya Nkasi.

Mheshimiwa Spika, na niseme juhudi iliyofanywa na wananchi katika eneo hilo, hasa ujenzi wa hiyo maabara, juzijuzi kama nilivyosema tulipeleka fedha ili wabainishe yale maboma, nadhani hilo ni miongoni mwa maboma. Nimuagize Mkurugenzi katika vile vipaumbele ambavyo tumepeleka fedha hizi za maboma hilo liwe sehemu mojawapo, sasa sijui kama watakuwa hawajaingiza. Lakini tutafuatilia, kuhakikisha ofisi yetu maabara hiyo inakamilika, maabara iweze kufanya kazi, Mheshimiwa Keissy usiwe na hofu.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwa kazi kubwa iliyofanya ya ujenzi wa Vituo vya Afya vya Daudi na Tlawi. Hata hivyo, katika swali langu la msingi nilikuwa nimeomba kituo hiki kwa ajili ya tarafa kwa sababu Jimbo la Mbulu Mjini lina tarafa tatu, tarafa mbili zimeshapata vituo vya afya ambavyo ni vituo pekee katika Jimbo la Mbulu Mjini.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa Tarafa ya Nambis ambayo iko pembezoni kama sehemu ya vijijini haina kituo cha afya na ina zahanati mbili tu katika kata hizo nne. Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kutafuta fedha za dharura ili walau zahanati moja katika zile mbili kwenye tarafa hiyo ikapandishwa hadhi na kuongezewa majengo na miundombinu mingine ya huduma ili wananchi hao wapunguziwe adha ya kusafiri mbali na huduma bora zaidi za afya?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; katika mpango wa awali wa vituo viwili vya afya; Kituo cha Afya Tlawi na Kituo cha Afya Daudi, Serikali ilikuwa na nia njema ya kupeleka vifaatiba na vitendeakazi vya milioni 440. Je, ni lini sasa Serikali yetu itakamilisha upelekaji wa vifaa hivi vya milioni 440 katika Vituo vya Afya Daudi na Tlawi ili kuweza kuboresha huduma ya afya?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, nikiri wazi kwamba Mheshimiwa Zacharia amekuwa ni mfuatiliaji sana na hata wiki iliyopita tulikuwa pamoja kujadili mambo mbalimbali katika jimbo lake.

Mheshimiwa Spika, saula la jinsi gani tupate fedha za haraka, naomba Mheshimiwa Mbunge nikuahidi kwa sababu kwanza ufahamu kwamba juzijuzi tulikuwa twende wote pamoja kule Jimboni Mbulu lakini kulikuwa na mkutano ule wa Ma-DC ambao ulikuwa unafanyika tumeshindwa kwenda. Kwa hiyo, ahadi yetu tunatarajia Mwezi wa Sita tutaenda hata ikiwezekana site hiyo tutaweza kufika. Lakini kikubwa zaidi tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo tutafute fedha kuisaidia hilo eneo ambalo umezungumza kwa lengo kubwa la kuwahudumia wananchi.

Mheshimiwa Spika, agenda ya vifaatiba ni kweli tumejenga vituo takribani 352 na katika vituo hivyo vituo 44 vya kwanza vimeshapata vifaa lakini vituo vingine bado vifaa vinakuja. Kwa hiyo, tutafanya kila liwezekanalo vituo vyote 352 ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambavyo Mheshimiwa Rais amevijenga vyote vitapata vifaa kwa lengo kubwa wananchi waweze kuhudumiwa vizuri. Kwa hiyo, usipate shida Mheshimiwa Issaay, tunalifanyia kazi.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la msingi lipo kwenye Jimbo la Mbulu Mjini na mimi nipo Jimbo la Mbulu Vijijini. Jimbo la Mbulu Vijijini kuna kata 18, Mheshimiwa Waziri umefika umekuta kituo kimoja cha afya kama mke wa Mkristo; unaonaje ndugu yangu? Maretadu wamejenga kituo cha afya wamefika lenta; utatupatia fedha ili walau tuwe na kituo cha pili cha afya?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kweli nimefika Mbulu na ni kweli ni changamoto kubwa ndiyo maana Serikali katika eneo lile kutokana na shida kubwa tulianza na ujenzi wa Kituo cha Afya cha Dongobesh. Lakini hata hivyo tuliamua kutoa fedha zaidi ya shilingi 1.5 billion kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbulu Vijijini.

Mheshimiwa Spika, nafahamu Mbulu jinsi ilivyo kuna maeneo wengine wako katika Bonde la Ufa na wengine wako juu. Tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo kama maombi Mheshimiwa Mbunge alivyoyaacha mara kadhaa ofisini kwetu tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo wale watu wa kata zingine kule za mbali tuangalie jinsi gani tutafanya tupate fedha kuwasaidia ujenzi wa kituo cha afya.
MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, Tarafa ya Bashnet iliyopo Babati Vijijini haina kituo cha afya hata kimoja na kilichopo kinatoa huduma sawasawa na zahanati. Je, ni lini Serikali itakumbuka Tarafa ya Bashnet? Ahsante.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, tunatambua changamoto ya Mkoa wa Manyara kwa ujumla wake na ndiyo maana Serikali tulitoa 3.9 billion kwa ajili ya vituo vya afya vile vyote na tumetoa takribani shilingi bilioni 3 kwa ajili ya hospitali za wilaya. Lakini hata hivyo, nafahamu Babati Vijijini ina changamoto kubwa ndiyo maana tulianza na Kituo cha Afya cha pale Magugu na kituo cha afya kingine, lakini mwaka huu tumewapatia ujenzi wa hospitali ya wilaya katika bajeti ya mwaka huu ambayo nimeisoma si muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, lakini eneo hilo Mheshimiwa Mahawe alilolizungumza tutalichukua kulifanyia kazi, nini kifanyike kwa haraka kwa mpango wa Serikali kuwahudumia wananchi wa Babati Vijijini, tunafahamu wengine wanatoka mbali na huduma hizi ni huduma za msingi kuokoa maisha ya akina mama wajawazito. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mahawe naomba ondoa hofu, kama upiganaji wako ulivyo wa kawaida kwa Mkoa mzima wa Manyara, kilio chako kimesikika tutakifanyia kazi.
MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Spika, ahsante, nianze na hapa kwenye huu Mkoa wako wa Dodoma. Niko maeneo ya katikati hapo Mjini, baa hizi zimekuwa kero kwa wananchi ambao wamejenga maeneo karibu na hizi bar.

Mheshimiwa Spika, isitoshe, wamekuwa wanatoka wanawake mbalimbali, wengine wanatoka Dar es Salaam, wanatoka Morogoro, wanatoka mikoa mbalimbali wanakuja hapa kwenye Jiji hili la Dodoma kwa sababu ni Makao Makuu ya Serikali. Tatizo kubwa bar hizi zinapiga miziki na matusi makubwa sana kwa jamii, imekuwa ni kero kubwa sana kwa jamii.

Je, ni lini Serikali itahakikisha inafanya msako maalum kwa Mkoa huu wa Dodoma, hasa ukichangia maeneo ya Mjini niliyoyataja Mheshimiwa Waziri?

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuna hawa akinamama ambao hawataki kufanya kazi wanajiingiza kwenye haya masuala yasiyokuwa ya stahiki za kijamii yaani kama tukisema kama Marekani wao wana tozwa kodi, Uholanzi wanatozwa kodi, sasa hawa wanawake askari wa Dodoma wamekuwa mara kwa mara askari kanzu wamekuwa wakiwachukua mara kwa mara lakini wanarudi tena kwenye maeneo haya haya wanakuwa wanafanya matukio ambayo hayaendani na jamii ya Kitanzania na maadili.

Je, Serikali ina mikakati gani kuhakikisha inawachukua wanawake wote hawa ambao wanafanya biashara haramu ambazo hazina stahiki na kuangalia hata wanawapeleka kwenye mashamba ya JKT wakafanye kazi? Naomba jibu la Serikali.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Msabaha, meti wangu wa kambi yetu ya Bulombola kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kilio hiki cha Dodoma kikubwa zaidi nini mkakati wa Serikali? Nimuelekeze Mkuu wa Mkoa kwa sababu akiwa kama Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama ya Mkoa, na Mkuu wake wa Wilaya kuhakikisha kwamba vile vitendo vya hovyo vyote ambavyo vinakiuka utaratibu waweze kuvisimamia kwa sababu Jeshi la Polisi hapa lipo waangalie nini kinachofanyika kuhakikisha hadhi ya Jiji la Dodoma linabakia kama lilivyo badala ya kuchafuliwa.

Mheshimiwa Spika, mkakati hawa watu ambao hii kauli nyingine uliyoizungumza ya watu inawezekana wanafanya biashara zisizo sawasawa, ndiyo maana Serikali mnakumbuka mwaka jana hapa tulipitisha sheria asilimia 10 iende katika vikundi ya vijana, akinamama na walemavu. Imani yetu ni kwamba kwa vile ukiangalia Dodoma pato lao ni kubwa mpaka juzi juzi wamekusanya zaidi ya shilingi bilioni 55 own source collection. Kwa hiyo ukichukua hapo asilimia nne yake maana yake ni fedha nyingi sana, kwa hiyo vikundi hivi ninaimani kwamba viongozi wetu watendaji wetu hasa maafisa maendeleo ya jamii chini ya Mkurugenzi wakiweka utaratibu mzuri wa kuwawezesha hawa akinamama tutawatoa katika suala zima hatarishi walilokuwepo nalo kwa wao kwamba kujiingiza katika shughuli halali za kiuchumi za Taifa letu hili.
MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwenye awamu ya tatu nyumba za Serikali ziliuzwa na nyingi zilikuwa zile za Shanti Town kule Moshi, Oysterbay Dar es Salaam, Gangilonga na Wilolasi Iringa na hapa Kilimani Dodoma na kwingineko. Nyumba hizo zilikuwa ni za makazi na zilikuwa ni eneo tulivu sana zikiitwa uzunguni. Lakini nyumba hizo ndiyo zimegeuka sasa ni Bar, ni maeneo ya kuoshea magari kule Moshi Shanti town zinasumbua wananchi na watoto hawalali. Ni lini sasa Serikali italeta sheria hapa Bungeni kama zile sheria za awali hazifuatwi ili zikatazwe kabisa?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli hii ni kero kubwa sana mpaka hivi leo asubuhi nilikuwa naongea na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kwamba ukiangalia kuna jengo la sinema karibu ya Shule ya Sekondari ya Arusha Girls na Shule ya Sekondari nyingine katikati, inaonekana badala ya kuweka jengo la sinema la kawaida sasa imekuwa sehemu ya night club na mambo vuruguvurugu hata hivyo kuhatarisha hasa madhara makubwa kwa wanafunzi wetu.

Mheshimiwa Spika, lakini maeneo hayo uliyoyazungumza ni kweli mkakati wa Serikali nadhani sheria ipo isipokuwa ni enforcement ya hizi sheria tu ndiyo inatakiwa. Kikubwa zaidi niwaelekeze viongozi wetu katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa ambao ni Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya palepale ninaimani wakizingatia vizuri eneo hili la kusema kuleta utulivu katika maeneo yao ninaamini kwamba jambo hili halitokuwa na mashaka. Kwa hiyo, niwaagize wakuu wa mikoa wote sasa waanze kufanya ufuatiliaji wa karibu kukomesha vitendo hivi vya hovyo vinavyotokea katika mazingira yetu ambao siyo jambo jema katika Taifa letu.
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru hizi bar zinamilikiwa na watu wakubwa sana na wenye fedha hata miongoni mwetu vilevile kuna baadhi ambao tuna hizi bar, na ni kutokana na mipango miji kutozingatiwa. Sasa ni kwanini Serikali isitoe tu tamko kwamba kuanzia sasa bar hizi zinazojengwa hovyo hovyo ni marufuku na atakayetoa kibali hatua zitachukuliwa?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema na Mheshimiwa Mbunge amesema wamiliki wa hizo bar wengine ni wakubwa inawezekana wengine wako humu ndani, kikubwa zaidi sheria ipo. Jambo kubwa linalotakiwa kufanywa sasa hivi ni kufanya usimamizi wa sheria, ndiyo maana hapa nimezungumza siwezi kutoa matamko tu hivi hivi kwa sababu sheria tayari ipo ni lazima tuzingatie tunasema STK – Sheria, Taratibu na Kanuni.

Mheshimiwa Spika, nina imani viongozi wangu wote wa ngazi za chini huko chini hasa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya naomba wawe wakali hasa kuona haya mambo yasiyokuwa sawasawa wayasimamie kuondoa hii kero ambayo Mheshimiwa Selasini hapa ameizungumza.
MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi kwa kiasi kikubwa swali langu linafanana na Mheshimiwa Njeza kumekuwepo confusion ya kuongeza maeneo na kupandisha hadhi. Mkoa wa Shinyanga tulishamaliza mchakato wa kupendekeza mji wa Kahama uwe manispaa na sifa zote tunakidhi na kigezo kikubwa kimekuwa ni suala la mapato ambayo halmashauri ya Manispaa ya Kahama ina uwezo wa kujiendesha kwa hiyo si changamoto kwa Serikali. Pia Mji wa Isaka na tulishafikisha wizarani je, ni lini Wizara kwa mtazamo maalum inaweza ikaruhusu Halmashauri ya Mji wa Isaka pamoja na Halmashauri ya Manispaa ya Kahama itaanza?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Naibu wangu kwa ufafanuzi mzuri sana. Katika swali hili lakini tunafahamu kwamba nishukuru Mheshimiwa Maige kwa concern yake; tuna maeneo makubwa matatu kwanza, kuna Halmashauri ya Mji wa Geita, Kahama, pamoja na Halmashauri ya Mji wa Kibaha ambao sasa iko katika suala la kufanya tathmini ya kuhakikisha kuzipandisha katika hadhi ya manispaa. Kwa hiyo lakini kuna utaratibu sasa hivi ambao tunaendelea kuufanya kwanza kutoanzisha maeneo mapya lakini hilo suala zima la hadhi tutalifanyia kazi pale jambo litakapoiva vizuri mtapata mrejesho Waheshimiwa Wabunge.
MHE. AZZA H. HAMAD: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza maswali ya nyongeza. Awali ya yote niipongeze sana Serikali kwa kazi kubwa ambayo inaifanya katika kuhakikisha inaboresha miundombinu katika shule zetu. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; Je, Serikali iko tayari sasa kuhakikisha inajenga mabweni katika shule zetu zilizoanzishwa kimkakati zaidi katika shule ya sekondari Samuye, Kizumbi, Isagenhe na Ukenyenge zilizopo katika Mkoa wa Shinyanga kwa sababu Wanafunzi wamekuwa wakitembea umbali mrefu na hivyo kukumbana na vishawishi vingi barabarani na kupelekea kupanga mitaani?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Je, Serikali hamuoni sasa ni wakati muafaka wa kuweza kufikiria kutokuwapangia shule zilizoko mbali wanafunzi hawa kwa kuwa kila Kata sasa hivi ina shule?

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kwanza nikiri, Mheshimiwa Azza takribani wiki mbili au tatu zilizopita alikuwa akinijulisha suala zima la changamoto ya miundombinu ya elimu katika Mkoa ule wa Shinyanga na nilimuhakikishia kwamba Serikali tutafanya kila liwezekanalo, lile linalowezekana tutaenda kulifanyia kazi alichanganye pamoja na ajenda hiyo ya elimu pamoja na ajenda ya afya.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo naomba niseme kwamba Serikali tutaangalia kila kinachowezekana katika maeneo uliyoyaainisha lile litakalowezekana kwa sasa tutaweza kulifanya. Lakini ni azma ya Serikali kuhakikisha tunapambana miundombinu inaimarika kama tulivyofanya pale sekondari ya Tinde ambapo Mbunge tumeenda wote pamoja pale kwa ajili ya kuona eneo gani lazima tufanye hilo.

Mheshimiwa Spika, suala la kutowapangia mbali kwa vile kila Kata sasa ina shule, jambo hili ndiyo kielelezo chetu ni kwamba kama katika Kata hasa zile zetu ambapo kama kuna vijana wamefaulu katika eneo lile ni vyema sasa watoto wakapangiwa kwa karibu zaidi kuepusha usumbufu huo mabao Mheshimiwa Mbunge ulizungumza. Kwa hiyo, tumelichukua Serikali na tutalitolea maelekezo katika maeneo mbalimbali.
MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, pamoja na juhudi za Serikali kuhakikisha kwamba wanajenga mabweni, utakubaliana nami kwamba baadhi ya mabweni hayo yamekuwa yakiungua mara kwa mara na hivi karibuni shule ya Ashira mabweni yake mawili ya wasichana yameungua.

Je, Serikali mna utaratibu gani wa kuhakikisha kwamba kunakuwa na ulinzi katika shule hizo ili hii rasilimali kubwa ambayo imeshatumika ya fedha kujenga mabweni hayo iweze kulindwa?

Mheshimiwa Spika, ahsante.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Dada yangu Susan.

Mheshimiwa Spika, ni kweli na niwape pole Wananchi wote wa Tanzania kwa sababu watoto wale, juzi nilikuwepo Ashira ile shule wkeli imeungua lakini ukija kuangalia taarifa ya awali inaonyesha kwamba ni hujuma tu kwa sababu yale mabweni mawili hayaungani na siyo kwamba kulikuwa na short ya umeme.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni kweli inawezekana maeneo mengine kuna hujuma na nawaomba niwaeleze Serikali juzi nilisha-deploy timu yangu ya Mainjinia iko pale tokea jana inafanyakazi na leo hii haraka iwezekanavyo ndani ya wiki mbili, tatu tuanze ukarabati wa yale majengo kwa sababu siyo muda mrefu vijana wa form five wengine tutawaingiza katika maeneo yale. Kwa hiyo, tutafanya ukarabati wa shule ile yote kwa ujumla wake kuhakikisha inarudi Ashira katika hali yake ya kawaida.

Mheshimiwa Spika, lakini hata hivyo ni maelekezo yetu sasa kipaumbele suala zima la walinzi na hasa kuangalia usalama wa shule zetu nini kifanyike kwa sababu tunatumia fedha nyingi sana, haiwezekani watu wenye nia mbaya wakahujumu juhudi hii kubwa ya Serikali na Wananchi wake kwa ujumla.
MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii, na mimi niulize swali dogo la nyongeza kwenye swali hili la msingi mwaka wa fedha 2017/ 2018 Serikali ilitenga shilingi bilioni 251 kwa ajili ya kumalizia majengo ya zahanati, maboma pamoja na maboma ya shule za msingi, lakini fedha hizo katika mwaka huu hawakutoa kitu na mwaka wa fedha uliofuatia 2018/2019 ambao tupo Serikali ilitoa shilingi bilioni 69 kwa ajili ya shughuli kwa maana shilingi bilioni 39 kwenye majengo ya zahanati na shilingi bilioni 28 kwenye majengo ya shule za msingi.

Sasa nataka kujua commitment ya Serikali ya shilingi bilioni 184 zilizobaki za fedha za ndani kwenda kumalizia maboma hayo ya zahanati katika nchi zetu ikiwemo Jimbo la Momba? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kama tunavyofahamu kwamba ukiangalia katika kipindi cha karibuni Serikali imefanya investment kubwa sana katika maeneo hayo na hasa katika upande ule wa Maboma kuna takribani shilingi bilioni 38 kwanza zilitoka kwa ajili ya sekta ya afya awamu ya kwanza, lakini juzi juzi mwezi wa tatu hapa zilitoka karibuni shilingi bilioni 29.9 kwa ajili ya sekta ya elimu.

Mheshimiwa Spika, lakini, naomba nikuhakikishie kwamba mwezi wa nne hapa katikati tumetenga tena karibuni shilingi bilioni 35.6 kwa ajili ya kuhakikisha kwamba suala la sekta ya elimu kuhakikisha maboma mbalimbali yanatekelezeka.

Mheshimiwa Spika, Kwa hiyo naomba nikutoe hofu Mheshimiwa Silinde kwamba Serikali ni nia yake kubwa kwamba kuhakikisha maeneo yote yenye changamoto yanaweza kufanyiwa kazi kwa lengo kubwa Watanzania wapate huduma vizuri. (Makofi)
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize maswali mawili ya nyongeza pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, barabara hii ninayoizungumzia kutoka Mima – Nkanana – Chibwegele eneo korofi siyo kilomita 5 ni zaidi ya hapo. Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga fedha za kutosha kwa sababu shilingi milioni 42 hazitoshi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili nakushukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kutambua kwamba barabara ya kutoka Gulwe – Berege - Mima - Chitope inahitaji shilingi bilioni 1.6 ili ipate matengenezo makubwa. Sasa ni lini fedha hizi zitatafutwa ili barabara hiyo iweze kufanyiwa ukarabati? Bahati nzuri Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI ameshapita barabara hiyo. Ahsante.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niwapongeze Naibu Mawaziri wawili kwa majibu mazuri kwa maswali ya awali.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Lubeleje ambaye mimi namwita greda la zamani makali yaleyale siku zote ni Mbunge ambaye anafuatilia jimbo lake, ni kweli tulipokwenda ziarani jimboni kwake tumebaini changamoto kubwa, si barabara hiyo tu hata kwenda Nambi, Tubugwe na maeneo mbalimbali kuna changamoto kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana ukiangalia katika bajeti ya mwaka huu na Mheshimiwa Lubeleje anafahamu kwamba kwa kuwepo na kipaumbele kwanza, sababu changamoto yake kubwa hata pale mjini tumeamua mwaka huu tutaenda kuwawekea barabara za lami lakini ile barabara ambayo ina changamoto kubwa, siku ile tulipita katika mazingira magumu sana, naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba awe na amani kwamba tutafanya kila liwezekanalo barabara hii ambayo kwa kweli haipitiki na shilingi milioni 42 ili kuifanya marekebisho makubwa. Hata hivyo, nimhakikishie kwamba ni commitment ya Serikali na hasa katika Jimbo la Mpwapwa na Wilaya nzima ya Mpwapwa tutafanya kila liwezekanalo ili wananchi wa Mpwapwa wafaidi matunda mazuri ya Mbunge wao ambaye ni senior MP katika Bunge hili.
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, napenda kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, je, ni kwa nini miji inapopanuliwa maeneo ya mashamba ya mazao marefu yasiachwe mijini kama ilivyo katika nchi nyingine kama Malaysia ambapo kilimo cha michikichi na mazao mengine kinaendeshwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, sheria hiyo haihusishi baadhi ya Mikoa kama Kagera, Kilimanjaro na Arusha ambako wakulima wanaendelea kulima mijini mazao marefu?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ritta Enespher Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kama nilivyotoa majibu ya swali la msingi, Serikali huwahamisha wakulima wa mazao ya aina zote kwenye maeneo ya mijini yaliyoiva kwa ajili ya ukuaji au uendelezaji wa miji kwa kuzingatia Sheria ya Mipango Miji, Na. 8 ya 2007 (Kifungu cha 7 na Kifungu cha 28 na Kanuni zake za mwaka 2008. Sheria hii hutumika kwa pamoja na Sheria ya Utwaaji wa Ardhi, Na. 47 ya 1967; Sheria ya Ardhi, Na. 4 ya 1999 na Sheria ya Upimaji na Ramani, Sura ya 324 ya mwaka 2002.

Mheshimiwa Spika, hivyo, sheria za nchi yetu zinazohusika na usimamizi wa uendelezaji wa miji haziruhusu uwepo wa mashamba ya mazao marefu mijini isipokuwa sheria hizo zinaruhusu kilimo cha mijini (urban farming) cha mazao mafupi yasiyozidi urefu wa mita moja hususan kilimo cha mboga mboga.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, sheria tajwa katika majibu niliyoyatoa katika swali la kwanza la nyongeza hapo juu zinatumika katika maeneo yote ya nchi yetu ya Tanzania na hivyo sheria hizi hazitumiki kwa kubagua baadhi ya mikoa fulani ya Tanzania. Sehemu kubwa ya mazao marefu yanayolimwa katika Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Kagera ambayo ni kahawa, migomba na miparachichi yana sifa ya kuhifadhi mazingira na kupendezesha mandhari ya miji na makazi kama ilivyo kwa miti ya vivuli na matunda.
MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, je, ni lini Serikali itaifanyia ukarabati miundombinu ya Hospitali ya Wilaya ya Tunduru yakiwemo majengo yake (wodi, vyumba vya upasuaji, majengo ya mapokezi na kadhalika kwani miundombinu hiyo ni chakavu kutokana na umri mrefu tangu uhuru?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Sera ya Afya inafafanua kuhusu hitaji la uwepo wa Kituo cha Afya kwa kila Kata. Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Nampungu ambayo ni mojawapo ya kata tatu za Tarafa ya Nampungu yenye kata tatu na hakuna Kituo cha Afya hata kimoja?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Engineer Ramo Matala Makani, Mbunge wa Tunduru Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi kuwa, Serikali inaendelea na mpango wa uboreshaji wa Hospitali ya Wilaya ya Tunduru ambapo wodi mbili ziko katika hatua ya ukamilishaji kwa gharama ya Shilingi milioni 140 na Hospitali imewezeshwa kufungua duka la dawa na kupatiwa mashine ya Ultrasound. Serikali itaendelea kuikarabati, kuipanua na kuiboresha Hospitali ya Halmashauri ya Tunduru kwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Aidha katika Hotuba itakayowasilishwa na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutatoa ufafanuzi kuhusu mpango wa ujenzi na ukarabati wa hospitali kwa mwaka wa fedha 2020/2021. Mheshimiwa Mbunge anaombwa kuvuta subira mpaka wakati wa uwasilishaji wa Bajeti ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI.

Mheshimiwa Spika, pili, Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya kutolea huduma za afya ya msingi nchini kwa kukarabati miundombinu iliyopo, kukamilisha maboma na kujenga miundombinu mipya. Hadi Machi, 2020 vituo vya kutolea huduma za afya 400 ikiwemo Hospitali za Halmashauri mpya 98 zimepokea fedha kwa ajili ya ukarabati na ujenzi.

Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza hili, Serikali imetoa kipaumbele kwa maeneo ambayo yana uhitaji mkubwa wa huduma za afya kwa kuzingatia vigezo vya wingi wa watu, umbali na maeneo ambayo ni magumu kufikika. Serikali inaendelea kutekeleza Sera na Mpango huu kwa awamu kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.
MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ambayo hayajaniridhisha, naomba niseme kwamba shule ile ilifungwa kwa sababu alizozitaja lakini mpaka dakika hii Shule ya Sekondari Ulyankulu imefurika wanafunzi mpaka wamehamishiwa Shule ya Sekondari Mkindo ambayo sio ya bweni.

Je, Serikali haioni sasa kuna haja ya kuwarudisha wale wanafunzi ambao wanatembea umbali mrefu na kuwaongezea wazazi gharama ambazo hazihitajiki?

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili, shule ile imefungwa sasa hivi haifanyi kazi ya aina yoyote imekuwa ni makazi ya ngedere na nyani, hali ambayo inasababisha wananchi na Serikali waone kwamba walitupa nguvu zao za bure na za rasilimali fedha pasipokuwa na sababu ya maana.

Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kuirudisha tena kwa sababu mahitaji yamekuwa ni makubwa? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Naibu Waziri wangu kwa kujibu vizuri maswali yote yaliyokuja hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kuchukua fursa hii kumpongeza dada yangu Mheshimiwa Rehema Migilla kuwa Mbunge wa Ulyankulu, dada yangu hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini jambo lake tumelichukua kwa sababu tunafahamu eneo lile lilikuwa la wakimbizi, lakini wewe ndiyo uko site kule unaona mahitaji yote ya msingi. Hivi sasa namuagiza Afisa Elimu wetu wa Mkoa wa Tabora aende akafanye tathmini ya haraka atuletee majibu ya haraka ili kuhakikisha kwamba tunawasaidia watoto wa eneo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo siyo shule hiyo pekee, hata ile shule ambayo juzi katika ziara tulipokuwa na Mheshimiwa Rais tumetoa melekezo, shule hizo zifanyiwe harakati za haraka kama ikiwezekana tuzifungue haraka.

Lengo letu kubwa ni Watanzania waweze kupata huduma vizuri. Ahsante sana.
MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mradi huu katika mapendekezo ya awali ulikuwa ufike kwenye eneo la Pugu na kwa kuwa sasa mji umekua kwa kasi na wote mnafahamu Mkoa wa Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani vimeungana, je, Serikali haioni ni wakati muafaka sasa kutekeleza mradi huu mpaka eneo la Pugu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kutumia historia ama matokeo ya mradi wa awamu ya kwanza kutoka Kimara mpaka Kariakoo na Posta wakati miundombinu imejengwa na sasa wafanyabiashara ndogo ndogo wanafanya biashara kwenye miundombinu hii mipya, je, Serikali haioni ni wakati muafaka sasa kuunganisha miundombinu ya mradi huu wa mabasi yaendayo haraka na masoko yatayoingiza wafanyabiashara kwenye maeneo haya ya vituo mlisho vya Banana, Mombasa na Gongolamboto? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali ndugu yangu Mheshimiwa Jerry Silaa, Mbunge wa Ukonga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mawazo ni mazuri na tukifahamu kwamba Jiji la Dar es Salaam linazidi kutanuka, lakini design ya kwanza ilikuwa inatuelekeza tunaishia mahali fulani. Si hivyo tu, tulifikiria hata sehemu ya barabara inayoenda Mbagala, sasa hivi inaishia pale Mbagala Rangi Tatu, tulikuwa tunafikiria jinsi gani tutafanya tufike mpaka pale mbele ya Kongowe.

Kwa hiyo, haya yote ni mawazo mazuri, wataalam wetu wataendelea kuyafanyia kazi, lakini tuna phase one ya design, kama tutakuwa na variation yoyote tunaweza tukaifanya katikati ya kazi yetu lakini lengo letu ni kuhakikisha kwamba Watanzania wanapata huduma vizuri, hasa hii ya mwendokasi.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili la kuhakikisha haya mabasi yanapita katika vituo vya kutoa huduma; ni kweli na hata ukiangalia katika ujenzi wa soko letu la Kisutu pale Dar es Salaam, Ilala moja ya jambo kubwa ni kutengeneza daraja linalounganisha mwendokasi na kutengeneza soko. Wataalam wetu wa TANROADS na wale ambao wanafanya ujenzi walikuwa wanaendelea na kazi hiyo. Kwa hiyo, hilo jambo ni kipaumbele chetu kwa sasa.

Mheshimiwa Spika, siyo hivyo tu, hata kuwa na pack maalum kwamba mtu akiondoka sehemu fulani anaweza akaacha gari lake na kuweza kusafiri. Hayo yote ni mambo ambayo tunayafanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika awamu hii tutaenda kufanya maboresho makubwa kwa lengo kubwa miundombionu hii na usafiri wetu huu unakuwa safi na salama kwa wasafiri wote wa Jiji la Dar es Salaam.
MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Name naomba nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa miradi hii ya kimkakati ambayo tunaizungumzia imekuwa na msaada mkubwa sana kwenye Halmashauri zetu na hasa kuisaidia TARURA kwenye kuhakikisha miradi inafanikiwa zaidi, tunao mradi mwingine mkubwa wa Tacticambao Serikali imeshauanzisha ikiwemo Jiji la Mbeya pamoja na Jiji la Mwanza na Manispaa nyingine.

Je, ni nini sasa mpango wa Serikali kuhakikisha mradi huu unaanza haraka ili tuone matokeo yake makubwa kama TSCP?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya maswali ya awali. Pia naomba nimpongeze ndugu yangu, mtani wangu Mheshimiwa Stanslaus Mabula Bin Jongo wa kutoka Pwani kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika Jiji ambalo tumefanya kazi kubwa sana ni Jiji la Mwanza. Kwa hili, nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa waliyofanya kwa kushirikiana na TAMISEMI kubadilisha Jiji la Mwanza kuonekana katika sura iliyokuwepo. Hata hivyo, mpango wetu kama nilivyosema wakati natoa budget speech yangu katika mwaka uliopita kwa mwaka wa Fedha 2021, kwamba tumekuwa na ile miradi ya Tactic, ambapo matarajio yetu makubwa ni kwamba tutakwenda kugusa maeneo 45 zikiwepo Halmashauri za Miji, Mafinga ikiwa ni mojawapo, Nzega, Kasulu, Handeni Mjini na maeneo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge wawe na subira tu, kazi inakwenda vizuri. Ni imani yetu kwamba mradi huu unakwenda kubadilisha kabisa nchi yetu. Katika miaka mitano ijayo, Tanzania miji yake yote itakuwa ni ya ajabu kutokana na kazi kubwa tunayokwenda kuifanya. Kwa hiyo, msihofu, kazi inafanyika vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Mikopo hii inahusu watu wenye ulemavu; na swali langu ni kwamba, inapotokea mtu mwenye ulemavu ambaye hawezi kufanya shughuli yoyote, lakini ana mlezi ambaye anamlea. Je, Serikali sasa haioni kuna sababu ya kumkopesha yule mtu ambaye anamlea mtu mwenye ulemavu ili aweze kufanya shughuli itakayomwezesha yule mtu kuweza kumlea vizuri yule mtu mwenye ulemavu? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nawashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa michango yao mikubwa mpaka tulipofikia hapa. Tukumbuke kihistoria kwamba Mfuko huu ulikuwa haufanyi vizuri, lakini kwa taarifa tuliyoitoa mwaka 2020, zaidi ya shilingi bilioni 124 ziliweza kuelekezwa katika makundi haya. Mpaka leo taarifa yetu ya miezi sita mpaka mwezi Desemba, zaidi ya shilingi bilioni 22.45 zimeelekezwa katika makundi hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, nazishukuru Kamati za Bunge hasa Kamati ya TAMISEMIna Kamati ya LAAC katika kutoa ushauri wa uboreshaji wa Kanuni na hasa makundi ya watu wenye ulemavu. Hivi sasa tume-review kanuni zetu za kuhakikisha, hata kama mlemavu ni mmoja, aweze kupata mkopo ambapo hayo yalikuwa ni maelekezo ya Bunge. Hata hivyo, tumeenda katika suala zima la uboreshaji katika eneo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika na Waheshimiwa Wabunge, nia yetu ni kwamba Mfuko huu uende kufanya vizuri. Kwa hiyo, Mheshimiwa Dada Malapo, hilo ni jambo ambalo Serikali hivi sasa inalifanyia kazi, lengo likiwa, walemavu waweze kushiriki vizuri katika shughuli za kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)
MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii kuuliza swali la nyongeza.

Ningependa kujua, kwasababu wamesema kwamba wananchi wale ambao walikuwa wanalima katika mlima ule walikuwa wanaharibu mazingira na bado magereza ambao wanapewa eneo lile wameendeleza kilimo kama walivyokuwa wanafanya wananchi. Sasa ningependa kujua kilimo cha wale waliopewa Magereza wao hawaharibu mazingira au wananchi ndio wanaharibu mazingira?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ningependa kujua kama Mlima Nkongole ndio pekee ambao Serikali imeona kwamba uhifadhi lakini ukienda maeneo kama Mwanza wananchi wanaishi mlimani.

Je, ni mlima Nkongole peke yake ndiyo imeonekana ni hifadhi au iutumie au kwa milima yote ambayo ipo katika nchi hii ndiyo inayohifadhiwa na Serikali? Ahsante.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwita, Mbunge wa Tarime Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, ajenda ya uharibifu wa mazingira, haijalishi mtu ama taasisi kama watu binafsi wanaharibu mazingira, kama Jeshi la Magereza linaharibu mazingira ama taasisi yoyote inaharibu mazingira wote ni waharibifu wa mazingira. Kwa haina excuse ya aina yoyote na kutokana na jibu la msingi Naibu Waziri, Ofisi ya Rais - TAMISEMI alivyokuwa akijibu hapa alieleza wazi kama eneo hilo lipo katika mchakato katika maeneo lindwa. Sio eneo hilo peke yake, isipokuwa kuna maeneo mengine ya fukwe na maeneo mengine ambayo sisi Serikali tumeona kwamba kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004 sasa kuna mchakato wa kuainisha maeneo hayo yote.

Kwa hiyo, tuseme kama Jeshi la Magereza licha ya kukabidhiwa wanaharibu mazingira maana yake jambo hilo halifai na ofisi yetu inasema jambo hilo tutaendelea kulisimamia kwa karibu zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa nini maeneo mengine watu bado wanaendelea kujenga nyumba. Tumesema sasa hivi tutakuwa nimetoa maelekezo mahasus katika upande wa mazingira na ndio maana katika suala zima ambalo tutalizindua siku ya tarehe 5 Juni, 2021 Kampeni Kabambe ya Kimazingira miongoni mwa mambo hayo tutakayokwenda kuyaainisha ni suala zima la utoaji elimu katika suala zima la utunzaji wa mazingira.

Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge sote tushirikiane pamoja katika ajenda kubwa ya kulinda mazingira hususan kuilinda nchi yetu. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, Serikali imejipangaje kutoa elimu ya namna ya kutenga takataka kulingana na makundi yao kwa sababu kuna zile takataka ambazo zinaoza kwenye mazingira, lakini kuna nyingine kama pastiki na hizo chuma chakavu haziwezi kuoza inabidi zifanyiwe recycling zirejeshwe tena naomba kupata mkakati wa Serikali imejipangaje?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la dada yangu Mheshimiwa Tunza Malapo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli changamoto ya takataka ambazo zimechanganyika imekuwa ni jambo kubwa sana hata ukienda katika madampo yetu ya kisasa ambayo yanapaswa kutenganisha zile taka unaona kwamba tumekuwa na changamoto kubwa sana katika kupitia hilo ndiyo maana tarehe 3 Juni tuliwaita hapa Maafisa Mazingira wote kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa na Mikoa yote kwa lengo la kuwapa utaratibu mzima jinsi gani wataweza kutoa elimu katika Mamlaka za Serikali za Mitaa na ngazi za mikoa kwa ajenda kubwa kwamba mamlaka hizo zikishirikiana na taasisi yetu ya NEMC ziweze kuhakikisha nchi yetu iko salama.

Kwa hiyo Mheshimiwa Tunza Malapo swali lako ni swali muafaka kabisa na hivi sasa Serikali imeshaliwekea maelekezo na mpango huo unaanza mara moja.
MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa kuna taasisi tatu hapa nchini za NEMC, Wizara ya fedha pamoja na TAMISEMI, zimeanza mchakato karibu miaka sita mapaka kumi iliyopita, na mpaka leo hazijaweza kukamilisha utaratibu wa kuweza accredited.

Je, Wizara au Ofisi Makamo wa Rais Mazingira, ina mpango gani wa kuweza kuzihamasisha na kuzijengea uwezo taasisi hizi ziweze kukamilisha mchakato huu na kuweza kufaidika na fedha hizi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kwa vile Zanzibar hakuna taasisi hata moja ambayo imeanza mchakato huu. Je, kuna utaratibu gani au mikakati gani ambayo imepangwa na Ofisi ya Makamo wa Rais Mazingira, kuweza kuzijengea uwezo taasisi za Zanzibar na kuzihamasisha ziweze kuanzisha mchakato wa kujiunga na mfuko huu wa taibanchi. Ahsant sana. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS
(MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali na Mhesimiwa Soud Mohammed Jumah kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa mwenyekiti, ni kweli katika hizi fedha za mifuko hii miwili ya Adaptation na Green fund, hizi mara nyingi sana tushindwa kuzi – access kwa muda mrefu, hata hivyo Ofisi ya Makamo wa Rais Muungano na Mazingira, imeweza kuhakikisha kwamba katika kipindi cha hivi karibuni imejitahidi kufanya kazi yake kubwa vya kutosha, na tushukuru sasa hivi, kwa mfano, NEMC imefanikiwa kupata fedha kutoka mfuko wa Adaptation Funds, ambao ni wastani wa shilingi billion 6 ambazo hizi tupo katika mchakato na Wizara ya fedha kuweza kuzi – access vizuri ili ziweze kufanyakazi nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tunaendelea kuzijengea uwezo taasisi hizo. Tunafahamu kwamba TAMISEMI walianza mchakato takriban miaka mitatu, na bado kuna suala la capacity tunaendelea kulifanyia kazi. Kwa upande huu wa Zanzibar, juzi tulikuwa na ziara kule Zanzibar (Unguja na Pemba) na jana tulimaliza. Miongoni mwa jambo kubwa sana tulokubaliana nalo ni suala zima la kuangalia jinsi gani tutafanya kazi kwa pamoja katika upande wa kimazingira, kwa sababu jambo la mazingira linakata maeneo yote mawili.

Mheshimiwa mwenyekiti, hili naomba nikuhakikishie Mheshimiwa mbunge, mimi na dada yangu kule Mheshimiwa Saada Mkuya, ambae anahusiana na upande wa Mazingira kwa upande wa Zanzibar, tutafanya kila liwezekanalo kwa umoja wetu. Na hivi sasa Mkurugenzi wetu wa Mazingira anaitwa Dkt. Andrew Komba hivi muda huu ninayozungumza yuko Zanzibar akifanya kikao na wakuu wa Mikoa kule Pemba, katika ajenda kubwa ya kuangalia jinsi gani tutafanya ajenda ya pamoja ya mazingira ndani ya nchi yetu.
MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mbali na majibu mazuri yaliyojibiwa na Mheshimiwa Waziri, lakini bado nilikuwa na maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; kama ni hivyo ndivyo, je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuhakikisha kwamba katika hayo mashindano ambayo mnaenda kuyaandaa yanaenda kuwaunganisha vijana wa kike na wa kiume moja moja kwa moja au asilimia 50 ya wanawake na asilimia 50 ya wanaume katika hayo mashindano? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kama hivyo ndivyo, Mheshimiwa Waziri ni lini mashindano hayo yataanzishwa kwa sababu tayari tulishaona katika mpango kazi mmetuambia kwamba hayo mashindano yataanza. Nahitaji commitment ya Serikali, ni mwaka gani hayo mashindano yataanza? Ahsante sana. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Naibu Waziri wangu kwa majibu mazuri, lakini nimpongeze dada yangu Latifa kwa sababu miongoni mwa vijana ambao wamewakilisha Tanzania mwaka huu katika mjadala wa siku ya Muungano, Latifa alikuwa mmojawapo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika hilo, suala zima la kuhakikisha wanawake na wanaume wanashiriki kwa uzuri zaidi, tutalifanyia kazi. Na bahati nzuri kama unavyofahamu Serikali ya Awamu ya Sita imejielekeza huko kuhakikisha mchanganyiko wa jinsia zote mbili zinashiriki vizuri. Wasiwasi wangu ni kwa wanaume tusijetukajikuta kwamba idadi ya wanaume ikawa ndogo kuliko idadi ya wanawake katika michezo hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika upande wa commitment jambo hili kwa sababu suala zima la uratibu na Wizara ya Michezo kule Zanzibar na Wizara ya Michezo hapa Bara tutalifanya, baadae tutatoa taarifa rasmi katika suala zima la mchakato wa michezo hiyo, ahsante sana. (Makofi)
MHE. JULIANA D. MASABURI: Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini nina swali moja la nyongeza. Inasemekana samaki na dagaa za Ziwa Victoria zina madini ya zebaki: -

Je, Serikali imefanya tafiti juu ya hili? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote naomba kumpongeza sana dada yangu Mheshimiwa Juliana, kwa kweli yeye ni mwanamazingira mzuri sana. Katika upande huo kuhusu samaki na dagaa wanaopatikana katika Ziwa Victoria kwamba inasemekana wana madini ya zebaki, jambo hilo tuseme kwamba si sawasawa kwa sasa hivi, kwa sababu tunafahamu kwamba tuna-export samaki wengi nje ya nchi na samaki hao wamekuwa wakinufaisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wataalamu wetu hivi sasa wanaendelea kufanya kazi kubwa ya kuhakikisha kwamba katika suala la kanda ya ziwa matumizi mbalimbali ya kemikali yanadhibitiwa, lakini hata hivyo mpaka hivi sasa tafiti mbalimbali zimefanyika na hazijaonyesha kwamba samaki hawa wanaathirika.

Kwa hiyo, kikubwa zaidi tuwaombe wananchi katika maeneo mbalimbali kuendelea kuzingatia masuala mahususi ya kimazingira kwa lengo kubwa la kuendelea kulinda Taifa letu kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)
MHE. ASYA MWADINI MOHAMMED: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Changamoto hizi za uchafuzi wa kimazingira ambazo zinatokea katika maziwa mbalimbali vile vile hutokea katika fukwe za bahari yetu. Nataka kujua: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kudhibiti uchafuzi huu wa kimazingira kwenye fukwe ukizingatia fukwe hizi tunazihitaji zaidi katika vivutio vyetu vya utalii?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la dada yangu Mheshimiwa Asya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, jambo la kwanza kama Serikali tumeweza kutoa miongozo na hasa kuona jinsi gani tunafanya uratibu wa kufanya recycling process wa taka zote zinazoingizwa baharini. Hata hivyo, mnakumbuka hivi karibuni tuliweza kutoa baada ya kuona pale kuna changamoto kubwa licha ya kuzuia mifuko ya plastic, lakini imeonekana kwamba katika recycles vile vifuniko vya chupa havirejesheki na hivyo mara nyingi sana vimekuwa vikisababisha changamoto kubwa hasa katika samaki baharini.

Mheshimiwa Spika, hivyo, ndiyo maana tumetoa miongozo mbalimbali ya kuhakikisha tunalinda mazingira. Kubwa zaidi tumesisitiza ajenda ya usafi katika maeneo ya miji yote inayozunguka ufukwe wa bahari. Tulitoa maelekezo tulipokuwa pale Kinondoni kwamba maeneo yote yanayozunguka ufukwe wa bahari, Maafisa Mazingira katika maeneo hayo kuhakikisha kwamba ajenda ya usafi kwa wakazi wote inaendelea kwa lengo la kuhakikisha kwamba tunakuwa na mazingira rafiki kwa ajili ya utalii. Ahsante.
MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri yaliyojibiwa na Mheshimiwa Waziri, lakini nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa ujumla, jibu lake linaonesha kwamba hii mifuko haifanyi kazi Zanzibar na inafanya kazi Tanzania Bara, lakini wapo Watanzania Bara wanaoishi Zanzibar ambao nao walipaswa kunufaika na mifuko hii; ambao hawana sifa ya kunufaika kwenye mifuko kama hii wakiwa Zanzibar. Hawa wananufaikaje? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la rafiki yangu sana Mheshimiwa Ramadhan Suleiman Ramadhan. Ni kwamba kwa wote wanaoishi Bara na kufanya shughuli zao huku Bara, kwa zile fursa zinazohusika na mambo ya Bara zinawagusa huku upande wa bara na wale wote wanaoishi kule Zanzibar na fursa zinazohusika katika mifuko mbalimbali ya Zanzibar, wanapata fursa hiyo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, katika jambo hilo halina shida yoyote, kwa sababu siyo suala la kimuungano. Kwa hiyo, turidhie tu utaratibu wa sasa. Bahati nzuri kule kuna Wizara Maalum inafanya michakato hiyo. Ninaamini, kama kuna maeneo kidogo yanataka uboreshaji, basi inawezekana kwa ushauri mzuri wa upande wa pili, kufanyika uboreshaji wa ziada. Kwa hiyo, hiyo ndiyo hali iliyopo sasa.

Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu hoja yake ni nzuri, inachochea kuona pande zote za Muungano zikiwa na vitu mbalimbali ambavyo vinaweza vikasaidia wananchi katika maeneo haya. Ahsante sana.
MHE. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa biashara ya gesijoto imeshamiri sana duniani na imekuwa inaendelea kwa miaka mingi; na nchi nyingi zimefaidi kwa kuuza gesijoto ambayo inahifadhiwa kwenye misitu; na Tanzania yenyewe hii tunayo misitu mingi iliyohifadhiwa ambayo mojawapo ni ule wa KINAPA na ni mkubwa; naomba nijue mkakati wa Serikali wa kuingia kwenye biashara hii ya carbon trading kwa sababu itatupa fedha kule kwenye vijiji vyetu. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kwa sababu aliyeuliza swali ni mtu mzito katika Kamati ya Mazingira, licha ya kumwomba alete swali hili kama swali la msingi, kwa faida kubwa ni kwamba tuna success story ndani ya nchi yetu katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika. Jambo hili, watu wa Tanganyika zaidi ya 3.2 billion wanakusanya kutokana na Carbonate Hydrates Program.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nadhani jambo hili tutaenda kulichakata vizuri, lakini litakapokuja katika swali la msingi tutalifanyia kazi vizuri kwa heshima ya Mheshimiwa Mbunge. Ahsante.
MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa majibu, lakini pamoja na majibu mazuri nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, pamoja na mambo mengine Wabunge kutoka Zanzibar, pamoja na majukumu mengine tunatakiwa kuwaeleza wananchi wa Zanzibar juu ya umuhimu na faida za Muungano wetu. Kwa kujua hilo, je, Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar haioni ipo haja ya kuwashirikisha Wabunge kutoka Zanzibar katika uibuaji wa vipaumbele vya miradi inayotokana na fedha za Muungano?

Pili, Mheshimiwa Waziri katika Mkutano wa Nne aliniahidi kwenda Jimboni kwangu kutembelea vijiji vya Mjini Wingwi na Sizini.

Je, ananiahidi ni lini tutakwenda kutekeleza ahadi hiyo?Ahsante. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omar Issa Kombo, Mbunge wa Wingwi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nikiri wazi kwamba kwa kweli Wabunge kutoka Zanzibar wamekuwa na kipaumbele sana cha kushughulikia changamoto za wananchi wa Zanzibar akiwemo ndugu yangu Omar. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwamba niliahidi kwenda ni kweli, bahati nzuri nilishafika Zanzibar mpaka Jimbo la Nungwi, Jimbo la Amani na maeneo mengine, lakini nikuhakikishie kwamba ahadi yangu ya kufika katika eneo lako la kazi lipo pale pale tutaenda kuchapa kazi ondoa hofu katika hilo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kushirikisha Wabunge wa Zanzibar naomba niwashukuru, hata hii ajenda ukiangalia fedha za Covid, Wabunge wa Zanzibar mlileta fedha mahsusi hapa wakati mchakato wa barabara ulipokuwa ukifanyika ndiyo maana hata suala zima la fedha za Covid unaona kwamba zaidi ya shilingi bilioni 231 zimeenda upande wa Zanzibar lengo ni kuona kwamba hisia za Wabunge wa Zanzibar zimeonekana kuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba yale Wabunge wanayoyachangia humu katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo lazima iwe shirikishi.

Mheshimiwa Spika, hiyo, hilo jambo ni zuri, tutaendelea kuboresha zaidi jinsi gani Wabunge watashiriki vizuri katika kuibua hoja mbalimbali. (Makofi)
MHE. SIMAI HASSAN SADIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa masuala ya badiliko ya tabianchi si masuala ya ki-Muungano lakini masuala ya mikataba ya kimataifa na masuala ya mikataba ya kikanda ni masuala ambayo yanahusika moja kwa moja na masuala ya kimuungano je mtaishirikisha vipi Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika matayarisho ya mfuko huo wa mazingira?
WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimia Mwenyekiti, kwanza pamoja na majibu mazuri sana aliyoyatoa Comrade Chillo, Naibu Waziri wangu naomba kujibu swali la nyongeza la ndugu yangu Simai, kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli suala la mazingira si suala la Muungano. Hata hivyo, katika kipindi chote, kwa sababu mazingira hayajali mipaka, tumehakikisha kutekeleza miradi mbalimbali upande wa Tanzania Bara na upande wa Visiwani. Ndiyo maana leo hii tuna mradi mkubwa wa ujenzi wa ukuta kule Wete Pemba, hali kadharika Kaskazini A kuna mradi unaendelea. Hata hivyo katika mradi wetu, na juzi mmeona tulikuwa na tukio kubwa sana la kupokea Mwana Mfalme katika nchi yetu katika mradi wa carbon credit, na kwenye jambo hili tumeshirikiana kwa kizuri zaidi. Kwa hiyo huku tunakokwenda sasa ushirikiano wetu unakuwa mkubwa zaidi; na hata katika vikao hivi vya awali ambavyo tumeendelea kuvifanya vyote tunashiriki kwa umoja na Ofisi ya Makamu wa Kwanza Zanzibar kule, kwa lengo la kuhakikisha kwamba mazingira tunayashughulikia wote kwa upana wake katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, siku za karibuni kupitia vyombo vya habari tumeshuhudia mama mmoja ambaye alifika Zanzibar akiwa na ndizi na alipigwa faini, akatakiwa arudi na bidhaa hiyo upande wa Bara. Lakini wote tunaelewa kwamba Tanzania ni nchi moja.

Ni nini kinasababisha kwamba bidhaa kama hizo zikienda upande wa pili zinarudishwa na nini kauli ya Serikali kwenye hili?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nishukuru kwa busara yako njema ya kuongoza Bunge letu hili tukufu.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la dada yangu Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Dada Paresso alizungumza suala zima la kuzuiliwa kwa ndizi za mama mmoja wiki iliyopita ambapo Watanzania walishuhudia jambo lile likitokea katika mitandao ya kijamii. Na kweli mimi mara baada ya kuona jambo lile kwa sababu ninahusika na dhamana ya Muungano wetu, lakini nikifahamu kwamba Muungano wetu katika mambo tunafanya vizuri katika upande wa Muungano maeneo yote mawili. Ililazimu ofisi yangu kwa haraka sana kuwasiliana na ofisi ya mwenzangu, Mheshimiwa Hamza, Waziri Ofisi ya Makamu wa Pili Zanzibar, kumuuliza kulikoni ninachokiona katika mitandao?

Mheshimiwa Spika, Waziri mwenzangu alinijibu ya kwamba jambo hilo ni kweli limetokea, lakini ni kwa sababu kufuatia Tangazo la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambalo limetolewa kwa mujibu wa Sheria Namba 9 ya mwaka 1997, Sheria ya Uhifadhi wa Mimea, na tangazo hilo limetokana na hivi karibuni imebainika kuna ugonjwa wa mnyauko wa migomba ambao unaitwa Banana Xanthomonas Campestris.

Mheshimiwa Spika, kutokana na hilo sasa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iliamua kutoa tangazo maalum la kuzuia mazao yote ya migomba ikiwemo ndizi, mimea na majani kwa lengo la kuepusha ugonjwa huo usisambae katika maeneo mbalimbali, lakini wakatoa maelekezo katika maeneo yote ya kuingilia vyombo mbalimbali kuzuia mimea hiyo isiweze kuingia.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa mujibu wa Sheria hiyo Namba 9 ya mwaka 1997; endapo kosa hilo litabainika kuna adhabu zake tatu, jambo la kwanza aliyehusika kuingiza mimea hiyo anapaswa kuiteketeza kwa gharama zake mwenyewe; ahabu ya pili ni kwamba anaweza akapewa fine ya 50,000 kulipa ama zaidi ya hapo na adhabu ya tatu, anaweza akaelekezwa ya kwamba adhabu yake ni kifungo cha miezi sita kwenda gerezani miezi sita ama adhabu zile mbili kwa pamoja. Hii ni kwa mujibu wa Sheria Namba 9 ya mwaka 1997.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tangazo hili lilikuwa limetoka na kuwekwa katika maeneo yote ya kuingilia kwa mipaka ile. Tunafahamu kwamba kila nchi duniani ina utaratibu au kila maeneo mamlaka zina taratibu zake za kulinda.

Kwa hiyo, hili lilikuwa ni suala zima la udhibiti, lakini kwa bahati mbaya mama yule alikuwa hafahamu kwamba kuna lile tangazo lilitoka kabla. Kwa hiyo, ndio maana tulipofuatilia tulipata majibu hayo kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na ni kweli tangazo lile lilitoka kwa kuziia suala zima la ugonjwa wa mnyauko wa migomba usiingie katika upande wa Zanzibar.

Mheshimiwa Spika, sisi katika hilo tukaona basi ni vyema tangazo lile likatolewa kwa uwazi zaidi. Lengo kubwa ni kwamba watu wasiofahamu kwamba kuna zuio la kuingiza mazao ya migomba basi kila Mtanzania aweze kulipata kwa ajili ya kuchukua tahadhari hizo.

Mheshimiwa Spika, na hicho ndicho kilichojiri kule Zanzibar. Kwa hiyo, mpaka hivi sasa tangazo lile ni tangazo halali la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, limewekwa kwa ajili ya kuzuwia mimea hasa mazao ya migomba, ndizi zake, migomba na majani yasiingie kwa ajili ya kuzuia suala zima la uambukizaji wa ugonjwa wa mimea hii ya ndizi.

Mheshimiwa Spika, huu ndio mustakabali wa jambo hili. Kwa hiyo, hili wenzetu wameli-treat hivyo, lakini ni kwa mujibu wa Sheria ya Quarantine kule utaratibu wa kuhifadhi mimea katika eneo hilo. Naomba kuwasilisha. (Makofi)
MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kupata hii nafasi. Matukio ya kudhoofisha Mlima Kilimanjaro yanatupunguzia pride ya sisi Watanzania kwa sababu Mlima Kilimanjaro ni pride kwa nchi yetu. Hivi Serikali hamuoni kwamba kuna umuhimu wa kuweka uzito mkubwa kuyaangalia hayo matukio yanayotokea mara kwa mara ili kuurudisha mlima wetu katika hali ambayo sio ulivyo sasa? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri kwa ufafanuzi mzuri na majibu mazuri ya awali lakini Mlima Kilimanjaro ni kweli ni fahari yetu sisi Watanzania na kwa mfano mwaka jana tulipokuwa na kesi ya uwakaji wa moto Mlima Kilimanjaro, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira ilifanya kazi kubwa sana na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa sababu Mlima ule upo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tulienda pale kama timu na kupanga mikakati mbalimbali chini ya KINAPA. Kwa hiyo, ni kweli jambo hili la Uwakaji wa moto kwa sababu tuliunda timu kwa ajili ya kufanya utafiti nini sababu ya kuwaka moto, je ni hujuma ama ni nini? Lakini jambo hilo nadhani Serikali tunaendelea vizuri na nikuhakikishie Mama Anne Kilango Malecela, sisi dhamira yetu ya dhati ni kuhakikisha Mlima Kilimanjaro unaendelea ku-survive vizuri zaidi. Lakini niwaombe sana wanachi wa Mkoa Kilimanjaro wakati tunapanda karibuni mita 3,700 pale tumegundua kuna watu wanafanya shughuli mle ya ukati wa miti na uchomaji yaani ni changamoto kubwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niwaombe wananchi wote kwamba suala la kuutunza Mlima Kilimanjaro ni jukumu la kwetu sote sisi Watanzania kwa sababu linatuletea uchumi wa hali ya juu kubwa kwa hiyo tuna kila sababu kuulinda fahari hii sote kwa pamoja kwa ajili ya nchi yetu Tanzania. Ahsante sana.
MHE. BONIPHANCE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Wilaya ya Kishapu ni moja kati ya Wilaya ambazo zipo katika mkakati na mapambano ama kampeni za mabadiliko ya tabia nchi katika Kata ya Alagana pamoja na Kata ya Kiloleli, ipo miradi iliyotekelezwa hasa ya mabwawa ya mifugo ambayo kimsingi miradi hiyo imetekezwa chini ya kiwango.

Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kuambatana na mimi kwenda Jimboni kwangu kujenga miradi hiyo na kushauri namna bora amna namna gani ya kuweza kuirudia na kuitekeleza upya? (Makofi)
WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kumshukuru kaka yangu Mbunge wa Kishapu, nadhani swali lake lilikuwa linaendena na lile swali la kwanza la EBA, kwa sababu tuna Mradi wa EBA umetekelezwa katika halmashauri tano ikiwepo na Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu sasa kwa vile swali hili lilikuwa linaenda katika upande ule wa Saasisha swali la Mlima Kilimanjaro.

Mheshimiwa Spika, kiufupi niseme ni kwamba Mheshimiwa Mbunge nitaambatana na wewe tuende tukafanye kuangalia kama kuna mapungufu ya aina yoyote kuweza kuyafanyia kazi kama Serikali, ni jukumu letu kulifanya. Lakini binafsi naomba niwashukuru hawa Wabunge wa Kishapu, Wabunge wa Nzega, Wabunge wa Mkalama, Wabunge wa Mvomero na Mpwapwa katika mradi huo wameutendea haki sana kusimamia vizuri katika maeneo mbali mbali tumepata mafanikio makubwa. Kwa hiyo, Mbunge this is my commitment kwamba tutaenda pamoja kutembelea. (Makofi)
MHE. JOSEPH A. TADAYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali ninapenda kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo hilo la magugu maji katika Ziwa Jipe limedumu zaidi ya miaka 20 sasa, na imekuwa ni ahadi ya Serikali kila wakati ya kuondoa magugu maji hayo. Pamoja na shukrani kwa Mheshimiwa Rais kupitia kwa Mheshimiwa Waziri alimtuma Naibu Waziri akaja kuwapa ahadi hiyo wananchi, lakini Serikali haioni sasa kwamba umefika wakati kwa vile tatizo hili limekuwa kwa muda mrefu sana, ziko mashine hizi aquatic wild harvesters nyingi sana China na kila mahali ambazo thamani yake haizidi hata dola laki tano, ambazo zinaweza zikafanya kazi hii kwa namna endelevu kidogo kidogo ili kuzuia kuendelea kwa uharibifu wa mazingira na pia kuwawezesha wananchi wa Mwanga kuendelea kufaidi matunda ya lile Ziwa wakati Serikali inaendelea na mpango mkubwa huo wa mabilioni ya fedha ambao tunausubiri kwa hamu, ahsante.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Joseph Tadayo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninapenda kushukuru sana Mheshimiwa Mbunge amekuwa akielezea hoja hii mara nyingi sana na ndiyo maana takribani wiki nne zilizopita nilimtuma Naibu wangu, Mheshimiwa Chilo alienda kule kwa ajili ya kuangalia uhalisia ulivyo. Kama nilivyosema ni kwamba tunaendelea na mchakato huu na andiko letu hili ni kwa ajili ya Ziwa Jipe na hali kadhalika Ziwa Chala lakini maoni ya Mheshimiwa Mbunge naomba niseme kwamba Ofisi yetu imeyachukuwa, lengo letu ni kwamba kuhakikisha tunatumia mbinu zote zinazowezekana, hili itaangalia fursa zote zinazopatikana hata tukipata mradi kidogo wa muda mfupi, nini kifanyike lakini jambo kubwa la pale litaendelea kufanyika katika mradi huu lakini lile wazo la kwanza lakini wazo lako tunalichukua kwa ajili ya kulifanyia kazi Mheshimiwa Mbunge.
MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ziwa Victoria mwaka jana lilichafuka sana na likasababisha Samaki wengi wakafa hasa wale watu waliokuwa wametengeneza Vizimba wakapata hasara kubwa, Serikali ilipotuma wataalam waliweza kusema kwamba ni kwa sababu ya vinyesi vya mifugo kwa maana ya ng’ombe ndiyo vimesababisha hali hiyo imetokea, yale majibu hakuna yeyote aliyekubaliana nayo.

Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba hali hiyo haijitokezi tena ili wananchi wanaoishi Kanda ya Ziwa wasiendelee kupata hasara?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mathayo, Mbunge wa Musoma kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tulipata changamoto sana katika Ziwa Victoria, changamoto hii ilisababishwa na suala zima la mkondo wa Mto Mara ulikuwa unashuka kule, hili kama tulivyosema ni kwamba lengo letu ni kwamba hatuhitaji wananchi waweze kupata hasara na katika hili ndiyo maana msisitizo wetu mkubwa ulikuwa ni jinsi gani wananchi kupewa elimu ya utunzaji wa mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maeneno mbalimbali tulivyoona miongoni mwa changamoto kubwa inayotokea ni uhalibifu wa mazingira. Leo hii hatuzungumzii Ziwa Victoria peke yake hata Ziwa Babati hivi karibuni, unaona kwamba ongezeko la magugu maji. Ndiyo maana Ofisi ya Makamu Wa Rais, Muungano na Mazingira ilichokifanya ni nini hivi sasa? Ilichokifanya sasa hivi ni kuandika maandiko mengi kwa pamoja na siyo linalozungumzia suala la Ziwa Jipe peke yake lakini sasa hivi tuna suala zima la Ziwa Babati, na eneo lote la Ziwa Victoria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jukumu letu ni kuona jinsi gani tutafanya tupate mbinu mbadala ya kuhakikisha maeneo haya yote tunayatunza kwa lengo la kuwasaidia wananchi na uchumi wao. Ahsante sana.
MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa mabadiliko ya tabianchi yanasababisha mvua kunyesha pasipo utaratibu na mafuriko pia. Je, Serikali imejipanga vipi katika kukabiliana na hali hiyo ya njaa pamoja na mfumuko wa bei katika nchi yetu? (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Mariam Kisangi hilo swali lako hapo mwishoni hebu litengeneze lirudi kwenye hoja yako kwa sababu mfumuko wa bei sasa utaelekea Wizara nyingine.

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, mabadiliko ya tabianchi yanaathiri sana wakulima pamoja na makazi ya watu. Je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na hali hiyo? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba kumpongeza Naibu Waziri kwa majibu mazuri yote yaliyopita, lakini swali la Mama Mariam Kisangi ni swali la msingi sana.

Mheshimiwa Spika, Wataalam wa Idara ya Hali ya Hewa wanatuambia hivi sasa kiwango cha mvua maeneo mengine kimeshuka. Inaonesha wastani wa mita 1,500 sasa imefika mpaka mita 750, lakini tunakumbuka hivi karibuni tumekumbana na changamoto kubwa sana ya ukame katika Mikoa mbalimbali hasa Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Manyara. Katika hili ndiyo maana Serikali tumejielekeza kuelekeza suala zima la utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi, Ibara ya 238(L) kinachosema kwamba kila Halmashauri ipande miti milioni 1.5.

Mheshimiwa Spika, ninawashukuru Wabunge hawa na Watanzania na wadau wengine hatuna jinsi yoyote ya kupambana na hali hii, ni lazima tupande miti kwa kiwango kikubwa sana. Ninawaomba Watanzania wote tushirikiane na Serikali katika kulinda mazingira kupambana na mabadiliko ya tabianchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. (Makofi)
MHE. ASYA MWADINI MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Nina swali moja la nyongeza.

Kwa kuwa, kuna kero Saba ambazo bado hazijapatiwa ufumbuzi na kuna kero nyingine ambazo wameanza kuzipatia ufumbuzi. Je, ni nini mpango wa Serikali kuhusiana na utoaji wa taarifa wa kero hizi ili wananchi waweze kujua tathmini na ufuatiliaji wa kero ngapi ambazo zimetatuliwa na ngapi ambazo hazijatatuliwa kwa maslahi mapana ya Taifa? Ahsante.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali zuri la Dada yangu, Mheshimiwa Asya, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli safari yetu ya utatuzi wa hoja za muungano kama mnavyokumbuka tulikuwa na hoja 25, katika hoja hizo mwaka 2010 tulitatua hoja Mbili, mwaka 2020 tukatatua hoja Tano. Katika kipindi hichi cha mwaka mmoja chini ya Kiongozi Mama Samia Suluhu Hassan na Mheshimiwa Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi tulitatua hoja 11. Kwa hiyo, tumefanikisha kumaliza kutatua hoja 18 za Muungano kati ya hoja 25, kwa hiyo tumebakiwa na hoja Saba. Utaratibu wetu ni kwamba tarehe 23 Agosti, 2021 jambo kubwa lililofanyika Zanzibar ilikuwa ni kuitisha vyombo vya habari na kuwaeleza wananchi kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo tumejipanga kupitia vikao mbalimbali ndiyo maana katika bajeti tuliyopitisha mwaka huu tumetoa maelekezo ya kina na kutenga bajeti maalum ya kutoa elimu ya upana kwa suala la muungano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo jambo hili linaendelea kuwapa wananchi katika taarifa mbalimbali kupitia runinga, vyombo vya habari mbalimbali, magazeti hali kadhalika redio zetu ikiwa ni pamoja na zile local radio zetu.
MHE. NAJMA MURTAZA GIGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa tafsiri ya kamusi ya Kiswahili – English, kero maana yake ni a noise, a noise ni kama maudhi ambayo ndiyo hizo kero zenyewe. Maudhi yakiendelea hata kwenye ndoa inaweza kusambaratika. Je, Serikali haioni umuhimu wa kubadilisha hili neno na kuweka japo changamoto tukizingatia kwamba hizi changamoto ni endelevu kila siku zinakuja na zingine zinaondoka?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Dada yangu, Mheshimiwa Najma Giga, ambaye ni Mbunge machachari sana na Mwenyekiti wetu wa Kamati ya Bunge hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli ushauri wake ni mzuri na ndiyo maana sasa hivi tunavyopeleka taarifa sasa hivi tunaita ni hoja za Muungano siyo kero za Muungano. Kwa vile mafanikio ni makubwa zaidi kulikoni hizi hoja, kwa hiyo jambo hili Mheshimiwa Mbunge tumelichukua na tunaendelea kulifanyia kazi na hakika ninawaomba Watanzania kwa ujumla, sasa tuendelee kuhubiri zaidi mafanikio zaidi katika utekelezaji wa mambo Katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MHE. MOHAMED SULEIMAN OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili nyongeza. Kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majawabu yake haya mazuri.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza ningeomba tu kuuliza katika asilimia hizi alizozotaja karibu majimbo mengi ya Zanzibar tayari yameongezwa ukubwa wa eneo na kwa maana hiyo idadi ya watu pia imeongezeka, lakini hata ile hali ya uchumi ya wananchi kwenye majimbo hayo pia hayako vizuri.

Je, Serikali haioni sasa ndio muda muafaka wa kupitia upya vigezo hivi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili ni ushauri tu kwamba kiongezwe kifungu cha kuangalia gharama ya matumizi ya hizi fedha kwenye maeneo husika kwa sababu sisi kwa kule Zanzibar kama hizi fedha zinatumika kwenye miradi labda ya shule au madarasa vifaa vya ujenzi viko juu sana katika manunuzi yake. Kwa hiyo tungeomba kigezo hiki pia kiongezwe. Nashukuru sana. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la ndugu yangu Mohamed Suleiman Omar kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kweli majimbo mengi sasa hivi idadi ya watu imeongezeka na hili si kwa upande wa Zanzibar peke yake isipokuwa kwa nchi nzima na ndio maana mwaka huu kuna umuhimu mkubwa sana. Katika sensa yetu ya watu na makazi, ni vyema watu wakajitokeza tukapata idadi halisi ya wananchi katika maeneo husika, hata projection zozote za masuala ya miradi ya maendeleo iweze kuakisi uhalisia wa watu. Kwa hiyo jambo hilo ni jambo la msingi sana, ni imani yangu kubwa baada ya sensa yam waka huu tutapata takwimu halisi ya kila eneo.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo ndio maana pale Naibu Waziri hapa alizungumza katika bajeti yetu ya mwaka huu wa fedha tumeona ongezeko hili sasa limeongezeka kutoka shilingi bilioni 11 kwa majimbo yote mpaka shilingi bilioni 15.99, hay ani mafanikio makubwa na tuna kila sababu kumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa utashi wake wa kuona majimbo haya lazima yaongezewe fedha.

Katika suala lingine la kuangalia au utaratibu mwingine wa kuboresha hili ni jukumu letu kama Serikali na hasa kuangalia masuala ya mipaka na mambo mengine. Naomba nikuahidi Mheshimiwa Mbunge na kama unavyofahamu kwamba jukumu langu kubwa hata nikija kule Zanzibar kwa kuchechua issue mbalimbali za kuhusu maeneo ya Zanzibar ambayo mimi nimepewa jukumu la kulisimamia, lengo letu ni kwamba wananchi wanaotarajia katika Mfuko wa Jimbo waweze kunufaika katika miradi ile inayogusa katika maeneo ya majimbo yao, ahsante sana.
MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, masuala mazima ya Mfuko wa Jimbo kwa wananchi wetu ni katika nia ya kuongeza maendeleo na mipango mizima ya kuinua uchumi wa wananchi wetu. Lakini Mheshimiwa Waziri katika Wizara yako kama utakumbuka Novemba mwaka jana Mheshimiwa Rais alipokuwa Glasgow alihutubia nchi tajiri na akaziomba kuongeza ufadhili wa fedha kwa nchi maskini ili kuweza kusaidia masuala mbalimbali ya kulinda mazingira. Fedha hizi zimekuwa nyingi sana, zimetolewa nyingi sana, lakini mbona Wizara hii iko kimya kutoa idhibaki (accreditation) kwa taasisi za Serikali na zisizo za Serikali kwa sababu tunafahamu kwamba nchi hii ikipata pesa hizi maendeleo yatapatikana.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimshukuru sana dada yangu Lucy Mayenga kwa ufatiliaji wake na kwa kweli katika mkutano uliofanyika mwezi Novemba mwaka jana kule Glasgow, Scottish; Mheshimiwa Rais alizungumza mambo makubwa sana. Naomba niwaambie Watanzania katika mkutano ule hii image ya Tanzania imekuwa kubwa sana kwa Rais wetu katika kushughulikia masuala mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini jambo alilouliza halihusiani na Mfuko wa Jimbo isipokuwa kama Serikali katika masuala ya miradi ya maendeleo ndio maana pale ofisini kwetu sasa hivi tunafanya kazi kubwa ya uandishi wa miradi. Na mtakumbuka mwaka huu itakapofika tarehe 5 Juni tutazindua mpango mkakati wa kutekeleza maeneo mbalimbali ambao mpango huo ndani yake una jinsi gani tunafanya resource mobilization ya upatikanaji wa fedha kushughulikia changamoto za kimazingira katika maeneo mbalimbali ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na mimi nina swali langu la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kisheria wahusika wakuu wa mfuko wa jimbo kwa upande wa Bara na Wizara inayohusiana na masuala ya Serikali za Mitaa, lakini kwa upande wa Tanzania Zanzibar wasimamizi wakuu ni Wizara ya Muungano inayohusika na masuala ya Muungano.

Swali langu je, ni sababu zipi fedha za Mfuko wa Jimbo kupelekwa katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais zisizimamiwe kupitia Ofisi ya inayoshughulikia masuala ya Muungano? Ahsante sana.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, naomba kujibu swali la kaka yangu; ni kwamba Wizara yetu ni Wizara ya Muungano, lakini katika masuala ya uratibu kwa upande wa Zanzibar ofisi inayohusiana na masuala ya uratibu yote ni Ofisi ya Makamu wa Pili na hata hivi asubuhi nilikuwa naongea na pacha wangu, ndugu yangu Hamza katika masuala mbalimbali ya kimaendeleo. Kwa hiyo, jambo hili halina mashaka, isipokuwa ni kwamba jambo kubwa linahitajika ni jinsi gani tutafanya kama kulikuwa na changamoto mbalimbali ya utekelezaji wa miradi lengo letu sisi kubwa kuweza kuingilia.

Mheshimiwa Spika, ndio maana nishukuru sana hata hapa nyuma Bwana Abdulwakil pale nilienda mpaka jimboni kwake wakanieleza masuala mbalimbali ya changamoto na tukaanza kuyatatua. Na mimi niwashukuru sana Wabunge wa Zanzibar baada ya kuibua changamoto mbalimbali za fedha za Mfuko wa Jimbo sasa ninaamini japo kama inawezekana matatizo bado yapo lakini naamini sasa hivi angalau kidogo speed ya utekelezaji imebadilika sana ukilinganisha na miaka ya nyuma iliyopita. Kwa hiyo tunaamini kwamba suala la uratibu linaenda vizuri mpaka sasa.
MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri; je, Serikali ina mpango gani wa kuwatumia vijana waliohitimu masomo ya environmental science katika kusaidia kueneza elimu hii ya kupunguza hii hewa ya ukaa?
WAZIRI WA NCHI. OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la mama yangu, Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara kutoka Mkoa ule wa Ruvuma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli sasa hivi tuna vijana wengi sana wamehitimu environmental science katika vyuo mbalimbali ikiwepo Dar es Salaam, SUA pamoja na University of Dodoma na vyuo vingine.

Mheshimiwa Spika, na ndiyo maana katika ajenga hiyo kikubwa zaidi tunachokifanya ni kwamba si rahisi Serikali ikaajiri watu wote, lakini tumeweka suala zima la kuleta hamasa katika makundi mbalimbali hasa kutumia vijana hawa na hasa wakati fulani nilipokuwa katika mkutano pale Dar es Salaam, mkutano unaohusiana na masuala ya mabadiliko ya tabia nchi tulitoa maelekezo katika NGOs mbalimbali sasa zifungue milango kwa vijana waliosoma environment science. Hata kuwapa internship au mikataba ya muda mfupi kwa lengo kubwa vijana hawa waweze kutumia kiupana zaidi kwa ajili ya Taifa letu hili.

Mheshimiwa Spika, imani yangu maelekezo yale tuliyoyatoa katika taasisi mbalimbali wenzetu wataenda kuyazingatia kwa lengo kubwa vijana hawa waweze kutumika kwa mustakabali wa nchi yetu katika utunzaji wa mazingira.
MHE. ASYA MWADINI MOHAMMED: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi; kwa kuwa utunzaji wa misitu iwe ya mikoko ama ya kawaida husaidia sana katika utunzaji wa mazingira.

Swali langu kwa Serikali; je, Serikali ina mpango gani wa kuvitambua vikundi vyote vinavyojitolea kwa maksudi katika utunzaji wa mikoko hasa kwa upande wa Zanzibar?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la dada yangu Asya, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Zanzibar, kama ifuatavyo:-

Kwanza nipongeze vikundi vyote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bara na Visiwani wanajihusisha katika ajenda ya mazingira jambo hilo ni jambo jema sana na sisi kama Serikali jukumu letu kubwa ni kuwatambua. Lakini si kuwatambua peke yake, juzi juzi tulikuwa na mkutano kule Belgium katika miradi maalum inayosemwa miradi ya hewa ukaa na miongoni mwa ajenda kubwa jinsi gani vikundi hivi vidogo vidogo vinavyochipua katika ajenda ya mazingira baadaye vifanyiwe utaratibu maalum wa uwezeshaji kwa ajili ya ajenda ya kulinda mazingira, lakini ajenda ya kiuchumi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo jambo hilo ni jukumu letu Ofisi ya Makamu wa Rais tutaendelea kulifanya na kama mnavyoona bajeti yetu iliyopita imelenga vilevile katika suala zima la capacity building katika makundi na vikundi mbalimbali hilo ni jukumu letu tutaenda kulifanya kwa upana mkubwa zaidi ikiwemo Zanzibar. Ahsante sana.
MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru; katika Kata ya Kimara na Kata ya Idete yupo mwekezaji ambaye ni Kampuni inaitwa Odzungwa Corridor na yeye anafanyakazi ya kupanda miti kwa ajili kuja kuvuna hewa ya ukaa miaka ijayo.

Sasa je, Serikali haioni umuhimu wa kuzungumza naye ili aweze pia kushirikisha misitu iliyopo tayari ili huo uvunaji uweze kuanza na malipo yaweze kufanywa kwa sababu ipo miti ambayo iko tayari?

Lakini swali la pili; moja kati ya lengo la kuwepo kwa misitu kimsingi ni hifadhi ya mazingira na hivi karibuni bei za mazao ya misitu hususan mbao imeshuka sana na kama inakatisha tamaa wakulima kuendelea kulima miti na baadaye tutapata madhara makubwa.

Ni nini kauli ya Serikali kuhusu tatizo hili ambalo linaweza likawa na matatizo makubwa baadaye? Ahsante.
WAZIRI WA NCHI. OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la ndugu yangu, Mheshimiwa Justin Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-

Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa sababu kwa mara kadhaa alikuwa akizungumzia hoja ya upandaji wa miti wa kibiashara hususan katika wilaya yake ya Kilolo na Mkoa mzima wa Iringa pamoja na Mkoa wa Njombe wanavyojihusisha na upandaji wa miti.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ajenda ya huyu mkulima ambayo analima hii miti ni kama tunavyosema kwamba tumeandaa mwongozo sasa, mwongozo huu uta-address suala zima la uhifadhi wa mazingira na watu mmoja mmoja mara baada ya mwongozo huu watapewa maelekezo jinsi gani ya kushiriki vyema kwa ajili ya kupata utajiri mkubwa kupitia suala la misitu. Kwa hiyo, afanye subira tu nadhani kwa malengo yake yanaendana pamoja na mkakati wa Serikali tunaoendelea nao.

Mheshimiwa Spika, lakini suala zima misitu, thamani ya miti inashuka, basi niseme kwamba katika hilo kwetu sisi upande wa Mazingira tuseme kwamba hiyo ni fursa sasa kwa wale ambao wanaopanda miti ambao kesho na keshokutwa biashara hii hewa ya ukaa itapokuwa kubwa tutaenda kufanya mambo mawili; kwanza kutunza mazingira, lakini jambo la pili vilevile kuhakikisha kwamba tunakabiliana na mabadiliko ya tabianchi lakini kikubwa zaidi kuhakikisha tunapeleka utajiri wa mtu mmoja mmoja kupitia ajira ya misitu, ahsante.
MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza; kwenye majibu yake Mheshimiwa Waziri amekiri kwamba wapo kuandaa mwongozo utakaoruhusu wawekezaji kuja kuwekeza kwenye kupunguza makali ya hewa ya ukaa; ni lini mwongozo huo utakamilika?
WAZIRI WA NCHI. OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, ni kwamba kwanza nimshukuru Mheshimiwa Ramadhan na nilijua kama ni miongoni wa vijana machachari na hata mwaka huu wanawezekana wakaenda kutuwakilisha kule Misri katika ajenda ya mabadiliko ya tabia nchi.

Mheshimiwa Spika, katika upande huo Serikali ni kama nilivyosema ni kwamba mwongozo huu uko katika hatua za mwisho, takriban mwezi mmoja uliopita tulikuwa katika kile kituo cha Carbon Tanzania ambacho sisi tumeki-center pale University of Sokoine Morogoro, tulikuwa na kikao hicho imani yetu ni kwamba mwanzoni mwa mwaka wa fedha unaokuja maana yake kuanzia Julai kwenda hapa mbele si muda mrefu mpango huo utaweza kukamili ili mradi kwamba watu waweze kushiriki katika ajenda hii kubwa ya kibiashara.
MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana mimi nilitaja kujua tu kwamba je, Wizara hii ya Muungano na Mazingira ni kwa kiasi gani inashirikiana na Wizara ya Makamu wa Kwanza wa Rais ambayo pia nayo inashughulikia masuala ya mazingira katika kukabiliana na suala hili la changamoto ya gesi ukaa au hewa ukaa?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kama tunavyofahamu kwamba Ofisi ya Makamu wa Rais ina deal na masuala ya Muungano Bara na Visiwani, Lakini masuala ya mazingira upande wa Zanzibar ni chini ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais. Hata hivyo tunafahamu kwamba ajenda ya mazingira ni ajenda mtambuka haina mipaka, ndiyo maana muda wote tumeweza kushirikiana vya kutosha kabisa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais na ndiyo maana hata ukiangalia miradi mingine tunayoiandika katika bajeti yetu Madam Maryam pale Mbunge wa Pandani anafahamu kwamba katika jambo tulijadili katika kikao chetu katika Kamati yetu ya Bunge, miongoni mwa mambo jinsi gani miradi mbalimbali inaenda mpaka kule Zanzibar na hata hivyo ndiyo maana leo hii tuna miradi Kaskazini A, na hata mradi wa Sepwese pale tunaenda kujenga ukuta pale hii yote ni suala zima la mpango wa pamoja jinsi gani tunashughulika na ajenda ya mazingira katika maeneo yetu.
MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mie kuuliza swali moja la nyongeza.

Kwa kuwa misitu mingi ipo katika Serikali Kuu na Serikali za Mitaa; je, kuna utaratibu gani wa Serikali kuzihamasisha taasisi za Serikali kuweza kushiriki katika biashara hii ya hewa ukaa?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Soud, mimi namuita encyclopedia ya mambo ya mazingira kwa sababu amebobea sana katika mambo ya mazingira katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni kwamba kama tulivyosema ni kwamba katika kushirikisha taasisi hizi hata sasa hivi ukiangalia kwa mfano TFS wana misitu mingi sana, lakini bado hawajanufaika katika hewa ya ukaa, ni halmashauri ya Katavi peke yake na kule kama tulivyosema Simanjiro ambao wao kwa mwaka ile own source collection katika hewa ya ukaa ni kubwa zaidi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ndiyo maana tumeweka mwongozo kwa lengo kubwa ni kwamba taasisi kwa mfano TFS, vijiji vyetu, halmashauri zetu na watu binafsi waweze kushiriki vizuri katika hewa ya ukaa. Kwa hiyo ndiyo jambo ambalo tuliona kulikuwa na gap hapo tunaenda kuya-address gap hii kwa lengo kubwa ni kwamba kujenga uchumi wa nchi yetu katika suala zima la hewa ya ukaa.
MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mafuriko katika Mto wa Kanoni ulio katika Manispaa ya Bukoba umewatesa watu kwa miaka mingi na sasa hivi naishukuru Serikali kwa kuweza kukubaliana na ombi la Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba na sasa wanauingiza mto huu katika mradi wa TACTIC.

Je, kuna mvua za vuli zitaanza mwaka huu za mwezi Oktoba mpaka Januari; Serikali inaweza ikaongezea fedha kiasi kwenye ile milioni sita inayotengwa na Halmashauri ili kusudi angalau wakafanya ukarabati wa awali isije ikatokea tena mafuriko mwaka huu?

Swali la pili; ili kuweza kuondoa mafuriko kabisa katika mto huu, inabidi mto upanuliwe, kina kiongezwe, kuta zijengwe za mto huu kutoka kwenye Kata ya Kagondo, Rwamishenye, Amgembe, Gireye, Bakoba hadi kuingia kwenye Ziwa Victoria. Je, katika huu mradi unaokuja wa TACTIC haya maeneo yote yatazingatiwa?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la mama yangu Mheshimiwa Mushashu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru sana Mama Mushashu kwa sababu katika kumbukumbu yangu ni Mbunge mwana mazingira muda mrefu sana na hili analozungumza ni utashi kutoka katika moyo wake kabisa na nikiri wazi kwamba Manispaa imeanza kufanya kazi na Serikali kila muda tunafanyakazi, na Mama Mushashu anakumbuka kupitia mradi wa UGLSP pale katika Manispaa ya Bukoba hata mwanzo tulianza kufanya kazi hii kale kamfereji kadogo kalikokuwa kanaenda pale mpaka katika ziwa.

Kwa hiyo, tumetenga milioni sita hata hivyo tutaangalia pale itapobainika kwamba ile milioni sita ina changamoto tutaona nini cha kufanya kwa upande wa Serikali kwa ujumla wake. Lakini katika hizi kata zingine je, zitahusika vipi? Kama nilivyosema ni kwamba lengo letu ni kwamba kuondoa changamoto ya mafuriko na kama ulivyosema kweli katika kata hizi zote zinakabiliwa na mafuriko haya mto unapotokea jambo hili.

Tutaangalia katika ujenzi wa kuta katika mto huu jambo hilo lote litazingatiwa na hata kama kutatakiwa additional financing ya kuhakikisha maeneo mengine yote tuyaboreshe tutalifanya Mheshimiwa Mbunge bila shaka aina yoyote.
MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi; je, Serikali ina mpango gani wa kuokoa Ziwa Babati kwa kuondoa magugu yanayozidi kukua kwa kasi?

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la dada yangu Asia, Mbunge wa Manyara Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Ziwa Babati limekuwa na changamoto na magugu sambamba na maeneo mengine. Serikali tumeandaa mpango maalum hivi sasa kubainisha juhudi tulizonazo juu ya mpango huo lengo kuangalia maeneo ya changamoto mbalimbali. Kwa hiyo, tuko katika stage ya kutafuta fedha siyo Ziwa Babati peke yake lakini na maziwa mengine yanayokabiliana na magugu katika maeneo mbalimbali.

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Wilaya ya Same Jimbo la Same Mashariki kuna mito mikubwa mitatu ambayo inatitirisha maji bondeni ili wananchi watumie katika umwagiliaji wa mpunga kwenye Kata za Maore, Ndungu na ...

SPIKA: Swali?

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Tatizo hii mito imejaa magugu imejaa magogo. Je, Serikali iko tayari kusaidia mito hii isafishwe ili maji yatiririke kwa urahisi? Ahsante.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, ni jukumu la Serikali kusaidia maeneo mbalimbali na hata eneo hilo kifupi ni kwamba niwatume wataalam wangu kwenda kuangalia kufanya need assessment ya eneo lile, lengo ni kwamba tunapoenda kutafuta mipango ya kutafuta fedha na eneo hilo tuweze kulishughulikia maana yake sambamba na Ziwa Jipe ambalo liko katika Wilaya ya Mwanga kule katika Mkoa wa Kilimanjaro.