Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji (41 total)

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia afya njema na kutuwezesha kushiriki kikamilifu katika majadiliano ya Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa miaka mitano, 2016/2017 hadi 2020/2021.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, napenda pia kutoa shukrani zangu za dhati kwako wewe Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kunipa nafasi hii ili kuchangia hoja iliyowasilishwa na Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango tarehe 20 Aprili, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia napenda kuchukua nafasi hii kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa John Pombe Magufuli, kwa kuniamini na kunichagua kuwa Naibu Waziri wa Wizara wa Fedha na Mipango. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile napenda natoa shukrani zangu za dhati kwa wapiga kura wangu wa Jimbo la Kondoa, kwa kuniamini na kunichagua kuwa Mbunge wao. Nawaahidi kwamba sitawaangusha kwa yale yote niliyowaahidi.
Nawashukuru Waheshimiwa Wabunge wote ambao walichangia hoja hii kwa lengo la kuboresha utekelezaji wa Mpango wa kuyafikia malengo tarajiwa. Serikali imepokea ushauri wa Waheshimiwa Wabunge wote na itaufanyia kazi kadri itakavyoonekana inafaa kwa maslahi mapana ya Taifa letu.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja zilizotolewa ni nyingi lakini nitajikita katika kufafanua baadhi ya hoja hizo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya kwanza, uwepo wa vipaumbele vingi na vinavyofanana kwenye Mipango ya Maendeleo tokea uhuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa vipaumbele vingi na vinavyofanana tangia uhuru kumetokana na lengo na nia ya Taifa katika kupunguza umaskini nakufikisha nchi kwenye uchumi wa kati. Hata hivyo Mpango wa Pili wa Maendeleo wa miaka mitano umeainisha maeneo manne ya vipaumbele ambayo ni haya yafuatayo:-
(i) Kukuza Maendeleo ya viwanda;
(ii) Maendeleo ya watu na mabadiliko ya jamii; na
(iii) Kujenga mazingira wezeshi kwa biashara na uwekezaji katika viwanda pamoja na vile vinavyowezesha utekelezaji wa Mpango wenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya pili ilisema Serikali ijikite katika kufadhili miradi ya maendeleo ambayo haiwavutii sekta binafsi kuwekeza. Serikali imedhamiria kutanzua vikwazo vya maendeleo kwa kujenga miundombinu msingi ikiwemo ya nishati, barabara, maji na reli ili kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa sekta binafsi kuwekeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, miundombinu hii ni ya gharama kubwa kama tunavyofahamu na hivyo mara nyingi Serikali inachukua jukumu la kuitekeleza. Mpango wa Kwanza ulianza kutekeleza maeneo haya kama njia muhimu ya kufungua fursa za kiuchumi na Mpango wa Pili unalenga kumalizia pale tulipoishia kwenye Mpango wa Kwanza na kuendelea kutekeleza maeneo mengine manne mapya kama nilivyobainisha hapo juu.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, bado sekta binafsi ina nafasi pia ya kuweza kushiriki katika uwekezaji huu mkubwa maalum utakaowezesha sekta binafsi na wananchi kufaidika.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya tatu ilikuwa Serikali iweke utaratibu mzuri wa kuwaandaa wananchi katika kutumia shilingi milioni 50 kwa kila kijiji na jinsi ya kurejesha fedha hizo. Baraza la Taifa la Uwezeshaji limepewa jukumu la kuandaa mfumo mahsusi utakaotumika katika kugawa na kusimamia fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi na programu mbalimbali za kiuchumi kutegemeana na fursa za vijiji husika. Kazi hiyo inaendelea na kila kijiji kitapatiwa utaratibu na mfumo huo mara utakapokuwa tayari chini ya usimamizi wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja namba nne, uchumi unakua lakini maisha ya watu wa kawaida yanazidi kuwa magumu. Sekta zinazochangia kukua kwa uchumi wa Tanzania kwa kiwango kikubwa ni sekta ambazo zinaajiri idadi ndogo ya watu. Baadhi ya sekta hizo ni ujenzi ambao inakua kwa asilimia 15.9; biashara na matengenezo kwa asilimia 10; usafirishaji na uhifadhi mizigo asilimia 12.5 na fedha na bima asilimia 10.8 kwa takwimu za mwaka 2014. Sekta inayoajiri idadi kubwa ya Watanzania ambayo ni kilimo inakua kwa wastani wa asilimia 3.5 kwa mwaka.
Kiwango hiki cha ukuaji wa sekta ya kilimo ni kidogo hivyo hauwezi kupunguza kiwango cha umaskini kwa haraka. Pia katika kipindi cha zaidi ya miaka 10 iliyopita tuliwekeza zaidi kwenye misingi ya kiuchumi na mazingira rafiki yanayofungua fursa za kiuchumi na kuchochea uwekezaji kama vile elimu na miundombinu ya barabara. Matokeo yanayoakisi uwekezaji huu huonekana baada ya muda mrefu.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, tafiti mbalimbali zinaonyesha kwamba ili kiwango cha umaskini kiweze kupungua kwa kasi wastani wa kiwango cha kukua kwa uchumi katika kipindi cha zaidi ya miaka 10 kinatakiwa kisiwe chini ya asilimia 10 kwa mwaka. Hivyo basi, wastani wa ukuaji wa uchumi wa Tanzania kwa asilimia 6.7 kwa mwaka hautoshi kupunguza kiwango cha umaskini kwa haraka kama ambavyo imekuwa ikielezwa na wadau wengi wa maendeleo.
Mwisho, tunapoangalia viashiria vya kupunguza umaskini hatuangalii kimoja tu cha ukuaji wa uchumi. Pamoja na viashiria vingine, tunaangalia pia kiwango cha ukuaji wa idadi ya watu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa takwimu za sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012; kiwango cha ukuaji wa idadi ya watu ilikuwa ni asilimia 2.7 kwa mwaka. Ukuaji huu wa idadi ya watu ni kubwa na hivyo ni changamoto kwa Taifa hususani pale tunapochukua hatua za kupunguza umaskini.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya tano, Serikali haijawahi kufikia lengo la kutenga asilimia 35 ya mapato yake ya ndani jambo ambalo limeacha miradi mingi kutokamilika kutokana na kutegemea fedha za wahisani ambazo hazitolewi kwa wakati. Katika kipindi chote cha utekelezaji wa Mpango wa Kwanza wa Maendeleo Serikali ilitenga fedha za maendeleo kwa asilimia 27 kwa mwaka ikilinganishwa na lengo la wastani wa asilimia 35 kwa mwaka.
Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa bajeti una changamoto mbalimbali kama tunavyofahamu ikiwa ni pamoja na mapato kuwa chini ya makadirio na sehemu kubwa ya matumizi kuelekezwa kwenye matumizi ya kawaida. Kama Serikali, changamoto hii tumeiona na ndiyo maana kwa bajeti ya mwaka 2016/2017 tumeamua kuongeza bajeti ya maendeleo kutoka asilimia 27 hadi asilimia 40. Ni matumaini yangu kwamba Waheshimiwa Wabunge, mtatuunga mkono uamuzi wetu huu wa Serikali mara tutakapo wasilisha rasmi makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya sita, huduma za masuala ya fedha ni muhimu ziimarike mabenki mengi ya biashara pamoja na Benki ya Kilimo zipo mjini wakati walengwa wako vijiji hakuna huduma. Huduma za mabenki ya kibiashara zimejikita zaidi maeneo ya mjini kufuatia uwepo wa shughuli nyingi za kiuchumi na hivyo kuwa rahisi katika utoaji wa huduma za amana na mikopo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Benki ya Kilimo kilichoanzishwa ni Makao Makuu tu ya benki hii na sasa Serikali inajipanga kuanzisha matawi Mikoani na katika Kanda mbalimbali kulenga wateja walipo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya saba, kilimo kufuatia umuhimu wake kiuchumi, kitaifa na maisha ya kaya na mtu mmoja mmoja kingekuwa ni miongoni mwa maeneo ya kipaumbele ya Mpango. Kwa maana nyingine ni kuwa Mpango unapaswa kuwa na mikakati kamili ya kutekeleza azma ya kuendeleza sekta ya kilimo kuliko kuwa na kauli mbiu zisizotekelezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mpango huu kama ilivyo dhima yake unatilia mkazo maendeleo ya viwanda ili kuchochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya watu.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo ya kipaumbele ya Mpango yamebainisha kwa kuzingatia dhima hii ya mpango yaani kusukuma kasi ya maendeleo ya viwanda kwa maendeleo ya uchumi na maendeleo ya jamii ya Watanzania. Njia pekee ya kufikia azma hii ni kuwa na mfumo wa maendeleo ya viwanda, unaotoa fursa kwa wananchi wengi kushiriki katika maendeleo tarajiwa. Wananchi wengi nchini wanaishi kwa kutegemea kilimo kwa tafsiri pana zikihusisha kilimo cha mazao, ufugaji, misitu na uvuvi.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo haya yote yamebainishwa kuwa kama ya kipaumbele katika ukurasa wa 43 hadi 44 kwa kitabu cha Mpango na umuhimu wa kuhusisha kilimo tunafahamu katika maeneo ya kipaumbele umezingatia yafuatayo: -
(i) Fursa kubwa ya maliasili za uzalishaji kwa maendeleo ya kilimo;
(ii) Uwezekano kwa wananchi waliowengi kushiriki katika ujenzi wa uchumi wa viwanda kama wazalishaji wa malighafi na upatikanaji wa chakula kwa wafanyakazi wa viwandani na wakazi wa mijini; na
(iii) Kupanua soko la ndani kwa bidhaa za viwandani kama walaji, wazalishaji zana za kilimo na pembejeo na pia kupunguza umaskini.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo ili kilimo kiweze kuchangia katika uchumi ni lazima tija ya uzalishaji iongezeke na ili uongezeke Mpango umejielekeza katika kuongeza tija ya kilimo kwa mambo yafuatayo:-
(i) Kubadili kilimo kuwa cha kibiashara;
(ii) Upatikanaji wa mitaji;
(iii) Upatikani rahisi na kwa wakati wa pembejeo;
(iv) Kufungamanisha kilimo na sekta ya viwanda ili kuimarisha soko la ndani la bidhaa za kilimo; na
(v) Kuimarisha huduma za utafiti, ugani, na masoko ya mazao yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa umuhimu wa kipekee niwaombe wadau wote wakiwemo Waheshimiwa Wabunge, kuendelea kutuunga mkono na kushiriki katika jitihada za kujenga na kuimarisha uchumi wetu. Pamoja na mipango mizuri tulionayo ni dhahiri kuwa maendeleo hayapatikani kirahisi wala siyo ya kwenye makaratasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, maendeleo yanahitaji nidhamu katika uwajibikaji kwa kufanyakazi kwa bidii, maarifa, ubunifu na ufanisi katika kufanikisha utekelezaji wa mipango na programu za maendeleo. Tushirikiane sote kwa pamoja katika kutafsiri mapendekezo ya Mpango na bajeti ya Serikali yaliyowasilishwa mbele yetu ili yawe shirikishi na yenye kutekelezeka kwa manufaa ya wananchi wote.
Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge ni wadau namba moja katika ufanisi wa utekelezaji wa Mpango huu wa Pili wa maendeleo uliowasilishwa mbele yetu. Tanzania yenye neema inawezekana chini ya Serikali inayoongozwa na Kiongozi shupavu na mwenye uthubutu kama Dkt. John Pombe Magufuli. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu pia maendeleo ni mchakato na tayari tulishaanza mchakato huu tunaomba mtuunge mkono, tumuunge mkono Mheshimiwa Rais wetu katika utekelezaji wa kauli mbiu ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Hapa Kazi tu!
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema aliyetujaalia neema ya uhai na jioni ya leo tunahitimisha mchakato wa Wizara ya Viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba nikushukuru wewe mwenyewe kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia machache katika Wizara hii. Tatu naomba niseme naunga mkono hoja asilimia mia moja hotuba iliyoletwa na bajeti iliyowekwa mezani na Mheshimiwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji. Naomba nikupe pongezi sana Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yako nzuri ambayo uliiwasilisha vilivyo, hongera sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme masuala machache ambayo yameonekena kwamba yanatakiwa kusemewa na Wizara yangu ya Fedha.
Sehemu ya kwanza kabisa naomba nianze na maoni ya Mwenyekiti wa Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira alipopendekeza kwamba Serikali itoe fedha zinazoidhinishwa na Bunge kwa wakati ili kupelekea utekelezaji wa bajeti zetu katika Wizara zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inakubaliana na wazo hili, inakubaliana kabisa na mapendekezo haya na tunaona umuhimu kama Serikali wa kutoa pesa hizi kwa muda muafaka pale inapohitajika. Pia naomba nilikumbushe Bunge lako Tukufu kwamba utoaji wa fedha za bajeti unategemea upatikanaji wa mapato kwa mwaka husika, hivyo naomba pia tukubali kwamba sote na tunafahamu ni mashahidi kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ya Chama cha Mapinduzi tumedhamiria vilivyo kukusanya mapato, kuziba mianya yote na sote tunaona sasa tunaweza kukusanya zaidi ya asilimia mia moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti katika hilo, Serikali ya Awamu ya Tano pia imedhamiria kwamba Tanzania ya viwanda inawezekana na tunaanza mwaka huu na tumedhamiria kuanza kweli na ndiyo maana tumekuja na asilimia 40 kwa ajili ya bajeti ya maendeleo. Tunaomba sana kama Serikali mtuunge mkono bajeti zetu, tupitishe, tumedhamiria na tumeonesha kwamba tunaweza kukusanya na sasa tunazipeleka pesa katika maendeleo asilimia 40. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja namba mbili ilikuwa ni Serikali na mamlaka zake ipunguze utitiri wa tozo na ushuru ikiwemo kuziondoa zile zisizo na tija. Mapendekezo haya pia tumeyapokea, tumeanza kuyafanyia kazi na kama sote sisi ni mashahidi tulimsikia Mheshimiwa Waziri Mkuu alisema tozo zisizo na tija zote zitaondolewa. Naomba nilithibitishie Bunge lako Tukufu kwamba kikosi kazi kiko kazini na kikao cha kwanza cha kushughulikia tozo hizi zisizo na tija kinafanyika kesho na tuna uhakika mpaka tunaleta bajeti ya Wizara ya Fedha hapa tutakuwa tumeainisha tozo zote zisizo na tija na zote zitafutwa ili tuweze kwenda kwa mwendo unaohusika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawaomba tu Waheshimiwa Wabunge mtuunge mkono pale ambapo tutaleta mapendekezo yetu na muweze kutushauri ili tuweze kwenda mbele kwa ajili ya maendeleo ya watu wetu, maendeleo ya Watanzania na Tanzania kwa ujumla. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya tatu ilikuwa imetoka kwa Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani ambaye aliomba majibu ya kina yatolewe kuhusu ukomo wa bajeti. Akaenda mbele zaidi kuita kwamba uhuni wa Waziri wa Fedha katika kutenga ukomo wa bajeti. Naomba niseme hakuna uhuni hapa, kilicholetwa kama ukomo wa bajeti hakijatoka Wizara ya Fedha peke yake, haya ni maamuzi ya Serikali kwamba asilimia 40 sasa inakwenda kwenye maendeleo na asilimia 60 inakwenda kwenye matumizi ya kawaida. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nilikumbushe Bunge lako Tukufu kwamba ukomo wa bajeti hautolewi na Wizara ya Fedha, unapita katika vikao maalum, tunaanza na vikao vya wataalam, nimewasikia Wabunge wakisema kwamba Mawaziri tunafika pale na tunawadharau wataalam, hapana. Kikao cha kwanza kabisa cha jambo lolote huwa ni wataalam wetu, wanatuletea mapendekezo na mwisho Baraza la Mawaziri linapitisha ili kuleta hapa. Kwa hiyo, hata ukomo wa bajeti haukuwa uhuni, ila ilikuwa ni maamuzi sahihi kabisa na lengo sahihi kabisa la Serikali yetu ya Awamu ya Tano kwamba sasa tunahitaji kuiona Tanzania ikikimbia, Tanzania ya viwanda inawezekana chini ya Dkt. John Pombe Magufuli. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja namba nne pia ilitoka kwa Msemaji wa Kambi ya Upinzani kwamba tupitie upya utaratibu wa kufanya uplifting ya kodi, naomba niseme pia katika tatizo hili, siyo tatizo in such au naweza kuita ni tatizo kwa sababu ya wafanyabiashara au sisi final consumers. Sisi ndiyo tunapelekea kuwa na hii uplifting na mimi siiti ni uplifting kwa sababu tunakwenda kwa standard, tunakwenda kwa sheria, hatuendi tu bila kufikiri, ukadiriaji wa bidhaa zinazoingia nchini, tunafahamu unafanyika chini ya Kifungu cha 122 cha Sheria ya Forodha ya Afrika Mashariki. Hivyo tatizo hii linaonekana kwamba ni kubwa ni kwa sababu tu kama nilivyosema wafanyabiashara wengi au watumiaji wengi wa bidhaa za kutoka nje, huwa wanafanya under invoicing yaani wanapoleta pale hawasemi ukweli bidhaa hii imelipiwa kiasi gani kutoka kule ambako imetoka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo sheria hii niliyoitaja haikutuacha hivi imetupa mwongozo, linapotokea tatizo kama hili sheria inaipa Mamlaka ya Mapato ya Tanzania uwezo sasa wa kuangalia kutoka kwa country of origin ya ile bidhaa, bidhaa ile inauzwa kaisi gani na pia tunaangalia data base ya bidhaa zinazolingana, zinazofanana na bidhaa hiyo ili tuweze kufanya ukadiriaji halisi wa dhamani ya bidhaa ambayo imeingia nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo naomba pia niwaombe Waheshimiwa Wabunge, kwa pamoja tushirikiane hii ni nchi yetu, tuipende nchi yetu, tunahitaji maendeleo siyo maendeleo kwa Chama cha Mapinduzi tu, ni maendeleo kwa ajili ya Taifa letu kwa ujumla na watu wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatutaweza kuendelea kama tusipoweza kulipa kodi husika, kodi ambayo inaendana na bidhaa tunazoingiza nchini, hivyo, kama Mamlaka ya Mapato tutaendelea kusimamia sheria hii, hatuwezi kuwaumiza wateja wetu lakini tunasimamia sheria na pale ambapo mteja anafikisha bidhaa yake, pale kwetu tunafanya uthaminishaji kwa sheria hii na analipa kodi anayostahiili kulipa, hatuna sababu ya kumuumiza mteja wetu katika jambo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia limeongelewa tatizo kwamba kumekuwa na vikwazo kwa wafanyabiashara kutoka Zanzibar kwamba bidhaa zao zinatozwa kodi mara mbili. Naomba nilisemee pia jambo hili. Hakuna kodi zinazotozwa mara mbili kwa bidhaa zinazoingia Zanzibar kuletwa Tanzania Bara, kama mtakumbuka Waheshimiwa Wabunge, nilijibu hapa mbele ya Bunge lako Tukufu kwamba kinachofanyika ni ukadiriaji kwa sababu sheria inayotumika kule upande wa Zanzibar siyo sawa na mifumo tunayoitumia huku Bara, kwa hiyo kinachotokea hapa bidhaa inapoingia Zanzibar inakuwa haijathaminishwa kwa kiwango kile kinachotakiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo inapokuja huku hatutozi kodi mara mbili tunachokifanya sasa ni kuangalia ile tofauti ya kodi iliyotozwa kule thamani ya bidhaa ile Zanzibar na thamani ya bidhaa huku kwa hiyo tunachaji ule utofauti tu wa kodi ile ambayo haikuchajiwa na siyo kodi mara mbili. Serikali inawaangalia wafanyabiashara kutoka Zanzibar kwa jicho chanya kabisa, naomba mtuelewe Serikali ina nia njema na wafanyabiashara wake wa pande zote mbili za Muungano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia iliongelewa tatizo la kwamba Serikali itoe temporary documents kwa magari yanayokuja Tanzania Bara kutoka Zanzibar. Hili pia napenda kulieleza Bunge lako Tukufu ni kwamba hatuna sababu ya kutoa tempoprary documents kwa magari yanayotoka Zanzibar kuja huku Bara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachokifanya, magari yanayolipiwa ushuru wa dola ishirini siyo magari yanayotoka Zanzibar kuingia Tanzania Bara hapana. Ni magari yanayotoka nchi za jirani, nchi tunazopakana nazo kwamba watu wameingia nchini humu na magari yao wanataka kuyatumia na huwa tunawapa muda wa siku sitini, ndani ya muda wa siku sitini hiyo huwa wanalipa dola ishirini. Kwa magari yote yanayotoka Zanzibar kuingia humu nchini, kwa mfano Waheshimiwa Wabunge wamekuja na magari yao huku hakika huwa hawalipi hii dola 20, wanachotakiwa tu wao ni kueleza kwa Mamlaka ya Mapato kwamba ameingia nchini kwa muda upi atakaa hapa nchini, hivyo hakuna tozo yoyote anayotozwa mwenye gari anayetoka Zanzibar.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kinacholalamikiwa kama nilivyosema mwanzo ni kwa gari zinazoingia huku moja kwa moja au zinazoingia huku kutoka Zanzibar kuja kuuzwa huku, kama nilivyosema mifumo yetu ya kodi haifanani kwa hiyo lazima tunafanya uthaminishaji upya kwa sababu hii ni gari inaingia sokoni kwa hiyo na pia kinacholipwa siyo kodi mara mbili kinacholipwa ni utofauti tu wa kodi ambayo ililipwa kule Tanzania Zanzibar na hatimaye inapoingia huku kwetu. (Makofi)
Mheshimiwa Raphael Japhary Michael pia aliongelea kuhusu tuiangalie upya tax regime kwa kupunguza cooperate tax na VAT kwa wafanyabiashara wa ndani, kwa sababu inapelekea compliance kuwa ni ndogo.
Naomba niseme kwamba kodi ya ongezeko la thamani ni kodi inayolipwa na mnunuzi wa bidhaa au huduma na wala siyo kwa mfanyabiashara, hivyo kodi hii wala haipelekei watu kutokulipa kodi au compliance kuwa ndogo hapana, kwa sababu mfanyabiashara ni agent tu wa kodi hii kwa Serikali. Fedha yake huwa inarudishwa kwake pale ambapo anakuwa amerejesha na amelipa kodi husika kule Serikalini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu cooperate tax, ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge, hutozwa kwa faida baada ya kuondoa gharama za uendeshaji kwa mujibu wa sharia, kimsingi pia naomba niseme kodi hii haiathiri gharama za uendeshaji wa kampuni, kwa sababu hii inakuwa ni ile faida ambayo mfanyabiashara ameweza ku-declare kwamba amepata faida ndipo anapolipa cooperate tax. Kwa hiyo, katika kodi hizi mbili pia hazizuii uwekezaji, wala hazisababishi compliance ya kulipa kodi kuwa ndogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mwisho ambalo napenda kuliongelea jioni ya leo ilikuwa ni kutozwa kwa kodi ya VAT kwa transit goods. Jambo hili pia limeleta changamoto kubwa sana na naomba niliambie Bunge lako Tukufu kwamba kwa mujibu wa Sheria ya VAT ya mwaka 2014, mizigo inayopita nchini kwenda nchi za jirani haitozwi kodi ya VAT, hivi haya malalamiko yanayoletwa kinachotozwa kodi ya VAT ni zile tunaita auxiliary services ni zile huduma za msaada kwa ajili ya bidhaa hii kuweza kufika kule nchini. Kwa mfano, tunapokuwa na ulinzi tunapokuwa na storage charges hizi ndizo zinazotozwa VAT na siyo mzigo ule wala transportation yake haitozwi kodi hii. Hivyo naomba pia Waheshimiwa Wabunge, tuwaelekeze wafanyabiashara wetu, tuwaelekeze ma-clearing agency kwamba mizigo ya transit haitozwi kodi ya VAT hapa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa nafasi hii.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 – Wizara ya Fedha na Mipango
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutufikisha hatua hii siku ya leo. Ni hatua muhimu sana kwa taifa letu na naamini ni kwa rehema zake tu tumeweza kufika hatua hii siku ya leo na naamini kwa pamoja Waheshimiwa Wabunge hatuna budi kusema Alhamdulillah. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa mafundisho ya dini yangu baada ya Mwenyezi Mungu huja wazazi wangu. Naomba niwashukuru sana wazazi wangu kwa kunilea vyema na kunifikisha hapa nilipo. Najua kama mtoto wa kike haikuwa rahisi lakini nimeweza kwa sababu walinisaidia, waliniamini na sasa namshukuru Mungu naweza kuwatumikia Watanzania kwa ujumla. Pamoja na wazazi wangu wapo dada zangu, yupo pacha wangu, nawashukuruni sana kwa kuendelea kunipa support. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwashukuru watoto wangu wapendwa, Samira na Abubakar, nasema ahsanteni sana. Naamini bado ni wadogo mnahitaji kuwa na mimi lakini mmeniruhusu na ninaweza kusimama na kuwatumikia Watanzania. Ahsanteni sana na nawapenda sana watoto wangu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee kabisa sasa naomba nimshukuru mume wangu mpenzi. (Makofi/Vigelegele)
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru kwa kipekee kabisa. Safari ya ndoa yetu ilianza mbali tukiwa wanafunzi Chuo Kikuu Mzumbe, tumekwenda pamoja mpaka tunapata PhD yetu, yeye kapata leo na mimi nimepata kesho. Ahsante sana mume wangu. Nakushukuru sana kwa mapenzi yako kwangu, kwa ushauri wako kwangu kama Mchumi, naamini kwa pamoja tutafika salama na nakuahidi mapenzi yangu ya dhati kwako, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda pia kutumia fursa hii kukushukuru wewe binafsi kwa ujasiri wako kama mwanamke, kwa weledi wako katika utendaji wako wa kazi na umetufikisha leo siku hii ya mwisho ya kujadili bajeti ya Serikali yetu. Hongera sana, endelea kusimama imara. Wewe bado mdogo sana, nafasi yako ni kubwa na utafika pakubwa zaidi ya hapo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda pia kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote kwa michango yenu bunifu kabisa, tumeipokea kwa mikono miwili na tutaifanyia kazi. Naamini haitakuwa rahisi kujibu hoja zote hapa mbele lakini naamini tutazijibu zote kwa maandishi. La muhimu zaidi ni kuyafanyia kazi mawazo yenu yote ambayo mmetupatia kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wetu na taifa letu kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa nijibu baadhi ya hoja na hoja ya kwanza ambayo ilisisitizwa na Waheshimiwa Wabunge wengi wakiongozwa na Mheshimiwa Andrew Chenge, namheshimu sana Mheshimiwa Andrew Chenge, nayo ilikuwa ni Serikali itumie mapendekezo yaliyotolewa katika ripoti ya Chenge One ili kuongeza wigo wa mapato na uendelezaji wa sekta ya viwanda. Naomba kulifahamisha Bunge lako Tukufu kwamba Serikali yetu ni sikivu sana, ilizingatia sehemu kubwa ya mapendekezo ya ripoti ya Chenge One tangu ilipotolewa hadi kufikia hivi leo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitasema baadhi tu ya mambo ambayo Serikali yetu imeshayatekeleza. Jambo la kwanza kabisa lilikuwa ni TRA kuyafanyia kazi kwa wakati taarifa za Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA). Napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kwamba Serikali yetu kupitia TRA imekuwa ikitumia ripoti za ukaguzi wa hesabu za TMAA kama nyenzo mojawapo muhimu katika mchakato wa ukaguzi na ugunduzi wa maeneo hatarishi. Tunafahamu Waheshimiwa Wabunge na mmeyasema kwa nguvu zote kwamba katika eneo tunalodanganywa sana ni sekta ya madini. Kwa kushirikiana na TMAA, TRA tumeweza kugundua mambo mengi na tunaendelea kuyafanyia kazi na ndipo mnapoona hata makusanyo ya Serikali yetu yakizidi kuimarika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ya pili ilikuwa ni kuanzisha kodi katika usafirishaji wa fedha kwa njia ya simu za mkononi. Serikali yetu katika hatua hii ilizingatiwa kwenye mapendekezo ya hatua mpya za kodi kwa mwaka 2013/2014. Waheshimiwa Wabunge mliokuwemo kwenye Bunge hili kipindi hicho mliona na katika mwaka huu wa fedha naamini sote tunakumbuka Serikali imewasilisha maboresho ya hatua hii kwa kupendekeza kutoza ushuru wa bidhaa kwa asilimia kumi kwenye ada zinazotozwa na watoa huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge naomba tuelewane. Asilimia kumi hii ni kwa ada zile zinazotozwa na watoa huduma na si kwenye pesa anayoituma Mtanzania kwenda kwa Mtanzania mwingine. Hivyo, naomba tupeleke ujumbe huu kwa wananchi wetu, Serikali ina dhamira nzuri kabisa kwa Watanzania, kuwawezesha kiuchumi waweze kusimama imara, hivyo ada hii haiendi kuwa ni mzigo kwa wananchi bali sasa tunataka na makampuni yale yalipe kodi stahiki. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine katika ripoti ya Chenge One ilikuwa ni kuanzisha ada ya utumiaji wa kadi za simu (sim card). Kama tutakavyokumbuka, hatua hii tuliichukua kipindi kilichopita lakini pamoja na kuichukua na kuiwasilisha hapa Bungeni ilikumbana na vikwazo vingi kutoka kwa wadau na hivyo Serikali kuamua kuchukua hatua ya kuongeza ushuru wa bidhaa kwenye huduma za simu hadi kufikia kiwango cha sasa cha asilimia 17. Naomba tufahamu kwamba unapokua sokoni kwa sisi Wachumi tunafahamu, kunapokuwa na win-lose situation wewe ndiwe utapoteza zaidi hivyo tuliweza kuihamishia kodi hii upande huu na kuthibitisha kwamba ripoti ya Chenge One tunaendelea kuifanyia kazi hatua kwa hatua.
Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lingine lilikuwa ni kuimarisha usimamizi wa utozaji wa kodi katika makampuni ya simu. Serikali yetu sikivu kama kawaida imelifanyia kazi suala hili ambapo mtambo wa telecommunication traffic monitoring system tayari umefungwa na umeanza kutumika. Hivi sasa Serikali inaendelea kuweka mfumo wa kutambua aina na kiasi halisi cha miamala na thamani ya miamala inayofanywa na makampuni ya simu. Aidha, Mamlaka yetu ya Mapato wataendelea kufanya kazi kwa karibu sana na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) ili kukagua hesabu za makampuni ya simu katika kuhakikisha kuwa kodi stahiki zinalipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo tumelifanyia kazi lilikuwa ni pendekezo la kupunguza kiasi cha misamaha ya kodi hatua kwa hatua hadi kufikia asilimia moja ya GDP ambapo tunafahamu misamaha imeendelea kushuka. Kwa historia tu, katika mwaka 2012/2013 misamaha hiyo ilishuka hadi kufikia asilimia 3.5 ya Pato la Taifa, asilimia 2.3 ya Pato la Taifa katika mwaka 2013/2014 na asilimia 1.9 ya Pato la Taifa katika mwaka 2014/2015. Serikali inaendelea na juhudi hii ya kupunguza misamaha hasa ile isiyokuwa na tija na hivyo ifikie walau asilimia moja ya Pato la Taifa katika muda wa kati na mfupi ujao.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuwaeleza Waheshimiwa Wabunge kwamba hadi kufikia Juni 30, 2016 wiki moja ijayo, ni matarajio ya Serikali kwamba misamaha itakuwa chini ya asilimia moja, tutakuwa ndani ya 0.84 ya Pato la Taifa. Hivyo ripoti cha Chenge One Serikali yetu imeendelea kuifanyia kazi vizuri hatua kwa hatua.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme hayo yanatosha katika ripoti ya Chenge One lakini yapo mengi ambayo tumekuwa tukiyafanyia kazi na kwa pamoja tutashirikiana. Kama nilivyosema tutawajibu kwa maandishi na mtaona ni hatua zipi nyingine ambazo zimefikiwa katika kuifanyia kazi ripoti hii ya Chenge One kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu na wananchi wetu kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja nyingine ilikuwa Wizara ya Fedha na Mipango na Benki Kuu ya Tanzania wasimamie na kudhibiti mfumuko wa bei na riba za mikopo. Katika suala la kudhibiti riba za mikopo, Serikali yetu pia inafahamu hili ni tatizo kubwa, linawaumiza wananchi wetu. Pamoja na kuliachia suala hili katika soko lakini pia mkono wa Serikali bado uko pale pale na zifuatazo ni sehemu tu ya hatua tunazochukua kama Serikali kuhakikisha kwamba riba inakuwa si ile inayoumiza wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza, tunaendelea na usimamizi imara wa sera za fedha na bajeti (monitory policy and fiscal policy), tunaendelea kuzifanyia kazi ili kuhakikisha kwamba riba hizi haziendi kuwa ni mzigo kwa wananchi. Jambo la pili, Serikali imeendelea kuhamasisha benki za biashara kutumia takwimu za Credit Reference Bureau kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa taarifa za historia na uaminifu wa wakopaji. Kupitia njia hii ni imani yetu kwamba kama benki hizo za biashara zitaweza kutumia statistics zilizopo katika kitengo hiki itakuwa ni rahisi kufahamu historia ya wateja wao na hivyo haitakuwa jambo jema kuona tena riba ile inapanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kulifikia jambo hili, Serikali pia inaendelea kukamilisha mradi wa vitambulisho vya taifa kwa sababu tunafahamu moja ya kitu kinachosababisha riba iwe kubwa ni pale benki au mkopeshaji hana taarifa sahihi za mtumiaji wa huduma hii. Kwa hiyo, tunaendelea kukamilisha vitambulisho vya taifa, nina imani kubwa sasa kila Mtanzania atajulikana yuko wapi na benki hizi zitakuwa na uhakika wanamkopesha nani na yuko wapi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hili pia Serikali inaendelea kusimamia uandikishwaji wa hati za umilikishwaji wa viwanja kwa Watanzania ili kuwawezesha wananchi kuwa na dhamana wanapohitaji kukopa. Pia Serikali inaendelea kuboresha soko la dhamana za Serikali na soko la jumla la fedha za kigeni ili kuongeza ushindani katika masoko. Pia Serikali yetu inaendelea kuimarisha benki maalum za maendeleo ambazo ni Benki yetu ya Kilimo na Benki ya Maendeleo ya TIB ili ziweze kutoa huduma kwa wahusika na kwa riba ambayo ni sahihi ambayo Watanzania wengi hawataumia. Huo ulikuwa ni mpango wa kudhibiti riba. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kudhibiti mfumuko wa bei, Serikali imeendelea kudhibiti mfumuko wa bei ambapo kwa muda wa kati umebaki kiwango cha wastani wa tarakimu moja. Aidha, kwa mwaka 2015 kiwango kilikuwa wastani wa asilimia 5.6. Pia katika kudhibiti mfumuko huu wa bei Serikali itaendelea kuhakikisha kwanza ujazi wa fedha kwenye uchumi unakuwa sawia na ukuaji wa shughuli za kiuchumi ili upande mmoja usije ukazidi upande mwingine na hatimaye kupelekea madhara yake kwenye mfumuko wa bei.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, Serikali itaendelea kutoa chakula kwa bei nafuu kupitia Hifadhi ya Taifa ya Chakula kwenye maeneo yenye upungufu wa chakula kwa sababu tunafahamu sehemu moja kubwa inayopelekea kuongezeka kwa mfumuko wa bei ni bei ya chakula. Hivyo, tumejipanga vizuri katika suala hili na tuna imani kubwa mfumuko wa bei utaendelea kubaki katika tarakimu moja. Pia Serikali itaendelea kudhibiti bei za nishati ya mafuta na pia kuvutia na kuhimiza uongezaji wa tija katika kila nyanja za uzalishaji na utoaji huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja nyingine ambayo napenda kuitolea ufafanuzi ilisema utajiri wa madini bado haujawanufaisha wananchi hivyo Serikali inapoteza mapato mengi katika transfer pricing na mis-invoicing. Serikali ijenge uwezo wa watumishi kuongeza mapato kwenye sekta ya madini. Katika suala hili Serikali yetu pia imeendelea kulifanyia kazi kwa umakini kuhakikisha kwamba Watanzania wananufaika na sekta hii ya madini. Kama nilivyosema tuna ushirikiano wa karibu kati ya TMAA na TRA na katika hili TRA tumeendelea kuijengea uwezo ambapo TRA ilianzisha Kitengo cha Kodi za Kimataifa (International Taxation Unit) mwisho wa mwaka 2011. Kitengo hiki kimeendelea kujengewa uwezo kupitia mafunzo ya kiutaalam ndani na nje ya nchi yetu. Mafunzo haya yalidhaminiwa na Serikali ya Norway kupitia Norwegian Tax Agency ambapo walitoa fedha ya mafunzo na Serikali ya Marekani kupitia US Treasury ambao wanaendelea kuleta mtaalam wa transfer pricing. Tunawashukuru watu wa Norway pamoja na Serikali ya Marekani kwa kuendelea kutujengea uwezo katika hatua hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia katika kuimarisha uwezo wa kiutaalam kwenye kitengo hiki TRA imenunua haki ya kutumia (transfer pricing data base) itakayowezesha kupata taarifa mbalimbali za kulinganisha, that is comparable data kwa ajili ya upatikanaji wa taarifa na kurahisisha ukokotoaji wa kodi. Vilevile TRA kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha imetengeneza kanuni za transfer pricing pamoja na transfer pricing guidelines kwa ajili ya kutoa mwongozo wa jinsi ya kukokotoa kodi. Hivyo, tuna imani kubwa kabisa kupitia vitengo hivi na jitihada hizi tatizo hili litaondoka na Watanzania wataweza kunufaika na sekta hii ya madini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya wataalam wetu kupata utaalam huu kwa sasa wataalam wa kitengo hiki wanaendelea na ukaguzi katika makampuni matatu ya madini katika eneo hili la transfer pricing. Kazi hii inatajaria kukamilika katika robo ya kwanza ya 2016/2017 na tutaona wazi mbivu na mbichi ni zipi na Watanzania haki yao iko wapi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia TRA imeshajiunga na Shirika la Kimataifa la OECD Global Forum pamoja na Africa Tax Administration Forum na inaendelea na mchakato wa kusaini makubaliano ya kubadilishana habari za kodi. Hii inaturahisishia kujua ni kiasi gani kimetoka Tanzania bila sisi kujua katika black market na tuweze kuelewa nini cha kufanya na jinsi gani ya kupata kodi yetu stahiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika kuhakikisha kuwa maeneo yanayohitaji weledi maalum yanapata wataalam wa aina hii ya kuyasimamia TRA pia hubadilishana uwezo na mamlaka nyingine za mapato na mamlaka za udhibiti nchini zinazohusika na usimamizi wa mapato na taasisi na idara nyingine za Serikali kama vile TCRA, TMAA, Contractors Registrations Board, TANROADS na kadhalika. Hali kadhalika, Serikali inaendelea na jitihada za kukiimarisha kitengo hili ili kuwa na wataalam wengi zaidi kwa ajili ya kukabiliana na changamoto za kikodi zinazoendelea kuibuka katika eneo hili la kodi za kimataifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo napenda kulitolea ufafanuzi ilikuwa Serikali itatumia utaratibu gani kuhakikisha kuwa majukumu ya taasisi zilizokuwa zikijiendesha kwa fedha za retention hayaathiriki. Napenda kulithibitia Bunge lako Tukufu kwamba nia ya Serikali ni njema katika eneo hili, imedhamiria kuhakikisha sasa mapato yote ya Serikali yanatumika kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu. Napenda kulihakikishia Bunge lako kwamba taasisi zote zilizokuwa kwenye utaratibu wa retention zitatakiwa sasa kuwasilisha mahitaji ya bajeti kila mwaka kulingana na kalenda ya uandaaji wa bajeti. Serikali itachambua mahitaji ya taasisi husika na kisha kupangiwa ukomo wa Bajeti. Aidha, Wizara ya Fedha na Mipango itahakikisha kwamba bajeti iliyoidhinishwa kwa ajili ya taasisi hizi na migao ya fedha kutoka Mfuko Mkuu inatolewa bila kuchelewa ili tusikwamishe utendaji kazi wa taasisi zetu hizi. Tunafahamu umuhimu wa majukumu yao na hivyo, hatutachelewesha fedha kuzipelekea taasisi zetu hizi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua hii italeta usawa katika matumizi ya taasisi zetu na kuzuia matumizi yasiyo ya lazima kwa taasisi zote za taifa letu. Nia ya Serikali yetu ni njema kama nilivyosema mwanzo, naomba Waheshimiwa Wabunge muendelee kutuunga mkono. Hii ni tiba sahihi sana ya lile ambalo tulilisikia huko nyuma kwamba zipo taasisi zilizokwenda kufanyiwa mikutano yao ya bodi nje ya nchi, hatuna sababu ya kufanya hivyo. Kama mchumi ukiwa na pesa ambayo unaiona ni nyingi huna matumizi unaweza kutumia vyovyote vile lakini kwa mfumo huu ni imani yangu sasa tutarejesha nidhamu ya matumizi ya pesa za Serikali na pesa hizi ziweze kuleta tija kwa wananchi wetu hasa wa kipato cha chini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja nyingine ilikuwa ni Serikali ilete Muswada wa Sheria ambapo itaanzisha mamlaka ya kusimamia na kudhibiti taasisi ndogo za fedha nchini. Serikali inakamilisha Sera ya Taifa ya Huduma Ndogo za Fedha. Sera hiyo itawezeshwa kutungwa kwa Sheria ya Kusimamia Taasisi Zinazotoa Huduma Ndogondogo za Fedha (The Microfinance Act). Sheria hii itaanzisha Mamlaka za Kusimamia na Kudhibiti Taasisi hizo kwa kutumia madaraja kama, moja, tutakuwa na udhibiti wa taasisi ndogo za fedha zinazopokea amana kwa wananchi (deposit taking microfinance institutions) utakaosimamiwa moja kwa moja na Benki Kuu ya Tanzania. Mbili, tutakuwa na udhibiti wa taasisi za huduma ndogo za fedha zisizopokea amana kutoka kwa wananchi (non deposit taking microfinance institutions). Pamoja na programu na mifuko maalum ya Serikali ya kuwezesha wananchi kiuchumi itakuwa chini ya taasisi hizi na chini ya usimamizi wa Wizara ya Fedha na Mipango.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kutakuwepo na udhibiti wa huduma za fedha zinazotolewa na vyama vya ushirika wa akiba na mikopo chini ya Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania. Mwisho, udhibiti wa huduma za fedha zinazotolewa na vikundi kama vile Village Community Banks (VICOBA), Voluntary Savings Loans Association, Rotating Savings and Credit Association na watu binafsi wanaotoa mikopo na kuweka akiba yaani money lenders and saving collectors chini ya mamlaka ya Serikali za Mitaa. Sheria hii pia itaainisha vigezo na masharti ya ukuaji wa taasisi hizo kutoka daraja moja kwenda daraja lingine ili kuwa na udhibiti imara na ukuaji endelevu wa sekta hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, tulichowaahidi Waheshimiwa Wabunge wakati tunawasilisha bajeti ya Wizara ya Fedha tutamiza ahadi hii ili wananchi wetu waondokane na adha ya usumbufu wa mfumo usio rasmi katika sekta ya fedha. Tunafahamu waathirika wakubwa ni akina mama katika hili na ni imani yangu kubwa tutalisimamia kwa uhakika kabisa ili akina mama waondokane na adha hii ya kukopeshwa bila kuwa mtu yeyote anayeratibu taratibu hizi ili akina mama hawa waondokane na lindi la umaskini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja nyingine ambayo napenda kuitolea ufafanuzi ni kwa nini Serikali hailipi madeni inayodaiwa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii takribani shilingi trilioni 8.942? Waheshimiwa Wabunge kama mnakumbuka nimekuwa nikilisemea jambo hili kwa nguvu zangu zote na tumeji-commit kama Serikali. Naomba tufahamu kwamba katika mapitio ya awali yaliyofanyika, yalionesha kwamba madai ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii yalifikia jumla ya shilingi trilioni 3.89 hadi Juni, 2015. Madai haya yanajumuisha deni la PSPF la kabla ya mwaka 1999 la shilingi trilioni 2.67 na shilingi trilioni 1.22 kwa ajili ya madai ya mifuko yote yaliyotokana na uwekezaji katika miradi mbalimbali ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina nia ya dhati ya kulipa madeni haya yote ili kuimarisha Mifuko yetu ya Hifadhi ya Jamii mara tu baada ya kukamilisha uhakiki wa madai hayo. Tunafahamu tumekuwa na tatizo la wafanyakazi hewa na tumemsikia Mheshimiwa Rais wetu amesema, unapokuwa na wafanyakazi hewa utakuwa na wastaafu hewa pia. Hivyo, tunaendelea kuhakiki hatua kwa hatua tutafika mwisho mzuri na mifuko yetu ya hifadhi ya jamii itaweza kufanyakazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mfano mmojawapo katika hili hadi kufikia Mei, 2016 uhakiki wa madai ya mfuko wa PSPF ulikuwa umekamilika ambapo kiasi kilichokubalika ni shilingi trilioni 2.04 kutoka madai ya awali ya shilingi trilioni 2.67, kuonyesha kwamba kulikuwa na madai hewa katika wastaafu hawa. Hivyo, nawaomba Waheshimiwa Wabunge tuipatie Serikali yetu muda tukamilishe uhakiki huo ambao umeanza kufanywa na Mkuguzi wetu wa Ndani wa Serikali ili tuweze kuondokana na madeni tata na tuweze kulipa kile tunachostahili kukilipa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuhitimisha majibu ya hoja zangu kwa maneno yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika na Bunge lako Tukufu, naomba tufahamu kwamba uchumi wa Tanzania ya viwanda kama alivyosema shemeji yangu Mwijage haupo mikononi mwa vijana wanywa viroba na watafuna mirungi bali mikononi mwa vijana walio tayari kabisa kuingia kwenye uchumi wa kati kiakili na kimwili. Very aggressive to take and tape opportunities that are ahead of us in our country. Kama Wabunge na wawakilishi wa wananchi tuna jukumu la kurejea majimboni mwetu na kuwaandaa vijana wetu wa Tanzania kwa Tanzania ya viwanda iliyo mbele yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, maisha ya vijana wetu hayapo kwenye bangi na pool table, hapana, bali yapo mikononi mwa mama yao Tanzania chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dokta John Pombe Magufuli na Serikali yake ambayo imelenga kwenye ubunifu utakaoleta fursa za kiuchumi kwa vijana wetu. Yapo mikononi mwa Serikali makini ambapo ipo tayari kutengeneza ajira kwa ajili ya watu wake. Serikali yetu ipo tayari kwa hayo yote, naomba tuwaandae Watanzania kuingia kwenye uchumi wa kati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kama mratibu na msimamizi wa sera za uchumi mpana (micro-economic policies), Wizara ya Fedha na Mipango tutafanya kila linalowezekana kuhakikisha tunakuwa na ufanisi katika soko la fedha (Money market), soko la ajira (labor market) na soko la bidhaa (commodity market).
Masoko haya yote matatu yanategemeana, yanatafsiri pia juhudi zetu za kuelekea uchumi wa kati na yanaathiri au yanaathari za moja kwa moja katika maisha ya Watanzania wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, utayari wetu Waheshimiwa Wabunge wa kulipa kodi kwa hiari ni njia pekee ya kutufikisha katika maendeleo endelevu na uchumi wa kati. Hivyo, ni lazima tuangalie kwa umakini rasilimali zetu tulizonazo ndani ya nchi yetu na kuzitumia kwa ufanisi katika kuleta maendeleo ya uchumi jumla (inclusive growth). Hii ni pamoja na kuongeza wigo wa vyanzo vyetu vya mapato ya ndani.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumalizia kwa pongezi kwa Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango kwa ujasiri, uvumilivu na umakini wake katika utendaji wa kazi zake. Naomba nikuambie Mheshimiwa Waziri, mti wenye matunda ndiyo hupigwa mawe, usikate tamaa endelea kwenda mbele. Najifunza mengi kutoka kwako, endelea kunilea na kunijenga, ahsante sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutufikisha hatua hii tuliyofika jioni hii ya leo kama Wizara na kama Serikali. Pili naomba nimshukuru na nimpongeze kwa dhati kabisa Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akiifanya katika kusogeza mbele gurudumu la maendeleo la Taifa letu. Pia naomba nikushukuru wewe mwenyewe Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ujasiri wako, kwa kusimamia haki na kuhakikisha kwamba haki inasimama na nidhamu inarejea ndani ya Bunge letu Tukufu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia, niwashukuru Wabunge wote waliochangia hoja iliyowasilishwa mezani na Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango. Michango yenu tumeichukua ni mingi, tunawashukuru sana na sina uhakika kama tutaweza kuijibu yote hapa, tutajibu machache, lakini kiuhalisia tumechukua na tutawajibu kimaandishi, tunawashukuru sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa naomba kuunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo machache ya utangulizi, naomba sasa nichangie hoja chache ambazo zimejili katika majadiliano ya Waheshimiwa Wabunge katika kujadili na walioleta kwa maandishi pia.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya kwanza, ambayo ningependa kuichangia ni Ucheleweshaji wa Michango ya Mwajiri na nyongeza ya Pensheni kwa Wastaafu wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu kabisa, Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango inawajibika sana kuwasilisha mchango wa mwajiri kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wote wa Umma.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mwaka wa Fedha 2015/2016, Serikali imefanya jitihada kubwa sana katika kuwasilisha michango hiyo. kwa mfano, mchango wa mwajiri uliotarajiwa kuwasilishwa ni Shilingi bilioni 797. 781, hadi kufikia Mei, 2016, Wizara imewasilisha Shilingi bilioni 529.932 kama mchango wa mwajiri kwa Mifuko yote ya Hifadhi ya Jamii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama Wizara na kama Serikali, bakaa ya Shilingi bilioni 267.849 itawasilishwa kabla ya tarehe 1 Julai, 2016. Kwa hiyo, kama Serikali tunatoa Commitment mbele ya Bunge lako Tukufu kwamba, michango yote hii ya waajiri tutaweza kuiwasilisha katika Mifuko yetu yote ya Hifadhi ya Jamii.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, kwa mujibu wa kifungu namba 30(3) na (4) cha Sheria ya Mfuko wa PSPF namba Mbili ya mwaka 1999, Serikali inatakiwa kuwasilisha pia tofauti ya nyongeza ya pensheni kwenye Mfuko wa PSPF. Kuanzia Julai, 2015 hadi Aprili, 2016 Wizara imewasilisha PSPF kiasi cha Shilingi bilioni 75 kati ya Shilingi bilioni 94 zilizotakiwa kuwasilishwa. Pia tunatoa commitment ya Serikali yetu kwamba, bakaa la bilioni 18 tutaweza kuliwasilisha kabla ya tarehe 1 Julai, 2016 ili kuwezesha Mfuko wetu wa PSPF uweze kufanya kazi zake vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama tunavyofahamu Serikali yetu inafanya kazi kwa Cash Budget. Kwa hiyo, michango ambayo hatujamalizia ni kutokana na mapato, ambayo tumekuwa tukikusanya. Hata hivyo, sote sisi ni mashahidi, kupitia Serikali ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, tumeweza kuongeza mapato tangu Serikali yake ilipoingia madarakani na ndiyo maana tunatoa commitment hizi kwamba, tutamalizia bakaa zote zilizobaki katika michango ya hifadhi ya jamii.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa niongelee hoja namba mbili, ambayo ni tatizo la Wizara, Idara na Taasisi mbalimbali za Serikali kutoa takwimu zinazotofautiana juu ya suala moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili ni kweli lipo, lakini kama Serikali hatujakaa kimya, tumeendelea kulifanyia kazi. Ofisi ya Taifa ya Takwimu, tunafahamu ndiyo yenye mamlaka kisheria kuratibu na kusimamia utoaji wa takwimu rasmi zinazotumiwa na Serikali na wadau wengine kwa ajili ya kupanga mipango ya maendeleo ya wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Wizara, Idara na Taasisi za Serikali kutoa takwimu zinazotofautiana, Serikali tumeona tatizo hili na hivyo ilitungwa Sheria ya takwimu ya mwaka 2002; kwa sababu ya kukosa nguvu kisheria ilibadilishwa mwaka jana mwaka 2015 na sasa hivi tunajipanga vizuri zaidi ili kuweza kufika na kuja na takwimu ambazo ni sahihi zitakazoweza kutumika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia Sheria hii, ambayo imeanza kufanya kazi kuanzia mwezi Novemba 2015, Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI na Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika, imeanza kutengeneza Kanzidata ijulikanayo kama e-population register, ambayo itaandikisha watu wote katika Kaya na kuunganisha na masuala ya elimu, hali ya ulemavu, afya, kilimo, kazi na masuala mengine katika jamii.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kanzidata hii ni maelekezo ya kifungu cha 56 cha Sheria za Serikali za Mitaa ya Mwaka 1982 pamoja na Kanuni ya Pili na ya Tano ya taratibu za kazi za Mwenyekiti wa Mtaa au Kitongoji ya mwaka 1993 pamoja na Tangazo la Serikali namba Tatu la tarehe 7 Januari, 1994; ambalo linasisitiza kila Mtaa, Kitongoji kuwa na Register ya wakazi wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa kutambua umuhimu na Mamlaka yake Kisheria, imeanza kutekeleza kazi ya kutengeneza kanzidata ya Taifa, ambayo itasaidia Serikali kuwa One Stop Centre ya Takwimu Rasmi katika sekta zote za katika nchi yetu kwa kutumia takwimu za utawala Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa hivi, mfumo huu unafanyiwa majaribio katika Kata ya Mapinga, Mkoani Pwani na baadaye tutaendelea nchi nzima. Kupitia Ofisi ya Takwimu ya Taifa, kazi ya kuimarisha takwimu za utawala, umetengewa jumla ya Shilingi bilioni 1.6 kwa nchi nzima kwa bajeti ya mwaka 2016/2017.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitumie fursa hii kuwaomba Wananchi wote kupitia sisi Wabunge wao kutoa ushirikiano wa kutosha kwenye zoezi hili kwa ajili ya Taifa letu. Pia Watendaji wa kata, vijiji, vitongoji na mitaa watoe ushirikiano wa kutosha ili tuweze kuwa sasa na takwimu zilizo sahihi kabisa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya tatu, ambayo ningependa kuitolea ufafanuzi ni hoja iliyoletwa na Kambi Rasmi ya Upinzani, kwamba Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali afanye ukaguzi maalum katika Kitengo cha Madeni na Uwekezaji wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.
Mheshimiwa Naibu Spika napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kwamba, Serikali haina pingamizi na mapendekezo haya ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni juu ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kufanya ukaguzi maalum katika Kitengo cha Madeni na Uwekezaji wa Mifuko ya Hifadhi Jamii ili kujiridhisha na usahihi wa taarifa zilizopo. Ni wajibu wa CAG kufanya kazi hiyo na Serikali itampa ushirikiano wa kutosha ili kufanikisha kazi hiyo kwa wakati na kwa kadri Bunge litakavyoelekeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, ushauri wa kutenganisha deni halisi la Taifa na Matumizi mengineyo yanayohusu Mfuko Mkuu wa Hazina pia tutaufanyia kazi kwa kadri itakavyowezekana. Ingawa hakuna ubadhirifu wowote ulioripotiwa katika Mfuko huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja nyingine ilikuwa ni fedha zilizoidhinishwa na Bunge hazitolewi kama zinavyoidhinishwa. Kama nilivyotangulia kusema, tunafahamu mfumo tunaoutumia kutoa fedha za utekelezaji wa bajeti yetu ni mfumo wa Cash Budget. Kwa mfumo wa Cash Budget, fedha za miradi ya maendeleo pamoja na matumizi ya kawaida hutolewa kulingana na mtiririko wa upatikanaji wa fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, ni vyema ikaeleweka kuwa bajeti ni makadirio ya mapato na matumzi, hivyo ni muhimu lakini si lazima bajeti iliyopangwa au kuidhinishwa na Bunge ilingane na matumizi halisi kwa sababu inaangalia uhalisia wa mapato tutakayokusanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, kama nilivyosema mwanzo, Serikali inaendelea na jitihada za kuboresha upatikanaji wa mapato ya kodi na yasiyo ya kodi ili kuweza kutoa fedha kama zinavyoidhinishwa na Bunge. Tunatarajia kabisa kwamba mapendekezo yetu ya bajeti yetu tutaweza kuyafikia kwa kiwango kikubwa kutokana na uboreshwaji wa mapato ambayo Taifa limeyafikia kwa sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja nyingine ilikuwa inasema Serikali iruhusu kutumia fedha za maduhuli badala ya kupelekwa kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali. Kama Serikali, tungependa kufanya hivyo, lakini utaratibu wa fedha za maduhuli kupelekwa Mfuko Mkuu unasaidia kuwepo kwa mgawanyo mzuri wa fedha kwa taasisi au Wizara ambazo hazikusanyi maduhuli, mfano Ofisi yetu ya Bunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya kuruhusu maduhuli yatumike sehemu yanapokusanywa bila kupelekwa Mfuko Mkuu kuna hatari kubwa ya baadhi ya taasisi zetu kutopata fedha na kusababisha kushindwa kutekeleza majukumu yake. Serikali ina vyanzo mbalimbali vya fedha kwa ajili ya kutekeleza bajeti yake. Fedha za maduhuli ni mojawapo ya chanzo cha mapato ya Serikali yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, tukiruhusu fedha hizi za maduhuli zisipelekwe kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali, ipo hatari ya Wizara, taasisi na mikoa isiyokusanya kutopata fedha za kuendesha ofisi, kuendeleza shughuli za maendeleo na kulipa mishahara. Hivyo fedha za maduhuli zinapaswa kupelekwa Mfuko Mkuu ili ziweze kugawanywa katika mafungu mbalimbali kwa ajili ya kutekeleza bajeti iliyoidhinishwa, ambapo makusanyo ya maduhuli ni asilimia 15 ya mapato yote ya ndani. Tunawaomba Waheshimiwa Wabunge mtuunge mkono katika hili ili tuweze kutekeleza bajeti yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja nyingine ilikuwa Serikali iwalipe wastaafu kwa wakati wanapostaafu, ikiwa ni pamoja na kuwalipa pensheni kwa kutumia viwango vyao vya mshahara wa mwisho. Napenda kulihakikishia Bunge lako Tukufu kwamba mishahara ya mwisho kwa watumishi wenye masharti ya ajira ya kudumu na malipo ya uzeeni ndiyo inayotumika kukokotoa kiinua mgongo na pensheni ya watumishi hao mara wanapostaafu.
Mheshimiwa Naibu Spika, wastaafu ambao nyaraka zao za kustaafu zinawasilishwa kwa wakati, yaani angalau miezi mitatu kabla ya mtumishi husika kustaafu na zikiwa hazina kasoro yoyote, wamekuwa wanalipwa mafao yao kwa wakati. Ili kuhakikisha wastaafu wote wanalipwa kwa wakati, waajiri wanashauriwa kuwasilisha nyaraka zote ili tuweze kuwalipa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia napenda kuwaomba waajiri wote, upo mchezo ambao unafanyika mwajiriwa anapokaribia kustaafu, amebakiza miezi miwili kustaafu tayari ameshapeleka nyaraka zake mbalimbali katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, unakuta sasa mwajiriwa huyu ana-collude na mwajiri wake, anapandishwa cheo, kwa hiyo hii ndiyo inayoleta utata. Tayari nyaraka zake zilishapelekwa, sasa inakuwa ni vigumu, umepandishwa cheo mwezi mmoja kabla ya kustaafu inakuwa ni changamoto kushughulikia mafao yako pale ambapo mwajiriwa huyu anapostaafu. Hivyo niwashajihishe waajiri kupeleka nyaraka zote pale miezi mitatu inapokaribia mstaafu huyu anatarajia kustaafu.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja nyingine iliyowasilishwa na ambayo napenda kuitolea maelezo ni kwamba mikopo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo haujasaidia kubadilisha hali ya maisha ya wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba kuna kipindi cha mpito kati ya kukua kwa deni la Taifa linalotokana na mikopo ya miradi ya maendeleo na ustawi wa maisha wa wananchi wetu. Tunafahamu wote ukikopa leo deni linaongezeka leo lakini utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo unachukua muda mrefu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kuna lax period ambayo lazima turuhusu miradi hii inapokuwa imeshatekelezwa, kama miradi mingi ya ujenzi wa barabara, then tutaweza kuona maisha ya wananchi wetu yanaendelea kubadilika. Naomba niliarifu Bunge lako Tukufu kwamba muda si mrefu maisha ya wananchi wetu yataendelea kubadilika na mpaka 2025 tutakuwa ni Taifa la kipato cha kati.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa niongelee tatizo moja ambalo limeongelewa ambalo nalo nimeona Wabunge wengi wameliongelea. Nayo ni marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma ambayo haijajumuishwa katika Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali uliogawiwa kwa Wabunge; wanaomba Serikali iwasilishe marekebisho ya Sheria hiyo haraka iwezekanavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura 410, yatawasilishwa Bungeni kupitia Muswada wa Sheria unaojitegemea kuhusu marekebisho ya sheria hii. Serikali imejipanga kuwasilisha Muswada huu katika Bunge hili la Bajeti linaloendelea sasa hivi. Kwa hiyo, naomba niwape comfort Waheshimiwa Wabunge, marekebisho hayo yatakuja na sheria hii itafanyiwa marekebisho kabla Bunge hili halijafika mwisho. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema haya, naomba nirudie kusema naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango. Nakushukuru sana.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutufikisha hatua hii siku ya leo. Ni hatua muhimu sana kwa taifa letu na naamini ni kwa rehema zake tu tumeweza kufika hatua hii siku ya leo na naamini kwa pamoja Waheshimiwa Wabunge hatuna budi kusema Alhamdulillah. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa mafundisho ya dini yangu baada ya Mwenyezi Mungu huja wazazi wangu. Naomba niwashukuru sana wazazi wangu kwa kunilea vyema na kunifikisha hapa nilipo. Najua kama mtoto wa kike haikuwa rahisi lakini nimeweza kwa sababu walinisaidia, waliniamini na sasa namshukuru Mungu naweza kuwatumikia Watanzania kwa ujumla. Pamoja na wazazi wangu wapo dada zangu, yupo pacha wangu, nawashukuruni sana kwa kuendelea kunipa support. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwashukuru watoto wangu wapendwa, Samira na Abubakar, nasema ahsanteni sana. Naamini bado ni wadogo mnahitaji kuwa na mimi lakini mmeniruhusu na ninaweza kusimama na kuwatumikia Watanzania. Ahsanteni sana na nawapenda sana watoto wangu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee kabisa sasa naomba nimshukuru mume wangu mpenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru kwa kipekee kabisa. Safari ya ndoa yetu ilianza mbali tukiwa wanafunzi Chuo Kikuu Mzumbe, tumekwenda pamoja mpaka tunapata PhD yetu, yeye kapata leo na mimi nimepata kesho. Ahsante sana mume wangu. Nakushukuru sana kwa mapenzi yako kwangu, kwa ushauri wako kwangu kama Mchumi, naamini kwa pamoja tutafika salama na nakuahidi mapenzi yangu ya dhati kwako, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda pia kutumia fursa hii kukushukuru wewe binafsi kwa ujasiri wako kama mwanamke, kwa weledi wako katika utendaji wako wa kazi na umetufikisha leo siku hii ya mwisho ya kujadili bajeti ya Serikali yetu. Hongera sana, endelea kusimama imara. Wewe bado mdogo sana, nafasi yako ni kubwa na utafika pakubwa zaidi ya hapo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda pia kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote kwa michango yenu bunifu kabisa, tumeipokea kwa mikono miwili na tutaifanyia kazi. Naamini haitakuwa rahisi kujibu hoja zote hapa mbele lakini naamini tutazijibu zote kwa maandishi. La muhimu zaidi ni kuyafanyia kazi mawazo yenu yote ambayo mmetupatia kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wetu na taifa letu kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa nijibu baadhi ya hoja na hoja ya kwanza ambayo ilisisitizwa na Waheshimiwa Wabunge wengi wakiongozwa na Mheshimiwa Andrew Chenge, namheshimu sana Mheshimiwa Andrew Chenge, nayo ilikuwa ni Serikali itumie mapendekezo yaliyotolewa katika ripoti ya Chenge One ili kuongeza wigo wa mapato na uendelezaji wa sekta ya viwanda. Naomba kulifahamisha Bunge lako Tukufu kwamba Serikali yetu ni sikivu sana, ilizingatia sehemu kubwa ya mapendekezo ya ripoti ya Chenge One tangu ilipotolewa hadi kufikia hivi leo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitasema baadhi tu ya mambo ambayo Serikali yetu imeshayatekeleza. Jambo la kwanza kabisa lilikuwa ni TRA kuyafanyia kazi kwa wakati taarifa za Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA). Napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kwamba Serikali yetu kupitia TRA imekuwa ikitumia ripoti za ukaguzi wa hesabu za TMAA kama nyenzo mojawapo muhimu katika mchakato wa ukaguzi na ugunduzi wa maeneo hatarishi. Tunafahamu Waheshimiwa Wabunge na mmeyasema kwa nguvu zote kwamba katika eneo tunalodanganywa sana ni sekta ya madini. Kwa kushirikiana na TMAA, TRA tumeweza kugundua mambo mengi na tunaendelea kuyafanyia kazi na ndipo mnapoona hata makusanyo ya Serikali yetu yakizidi kuimarika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ya pili ilikuwa ni kuanzisha kodi katika usafirishaji wa fedha kwa njia ya simu za mkononi. Serikali yetu katika hatua hii ilizingatiwa kwenye mapendekezo ya hatua mpya za kodi kwa mwaka 2013/2014. Waheshimiwa Wabunge mliokuwemo kwenye Bunge hili kipindi hicho mliona na katika mwaka huu wa fedha naamini sote tunakumbuka Serikali imewasilisha maboresho ya hatua hii kwa kupendekeza kutoza ushuru wa bidhaa kwa asilimia kumi kwenye ada zinazotozwa na watoa huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge naomba tuelewane. Asilimia kumi hii ni kwa ada zile zinazotozwa na watoa huduma na si kwenye pesa anayoituma Mtanzania kwenda kwa Mtanzania mwingine. Hivyo, naomba tupeleke ujumbe huu kwa wananchi wetu, Serikali ina dhamira nzuri kabisa kwa Watanzania, kuwawezesha kiuchumi waweze kusimama imara, hivyo ada hii haiendi kuwa ni mzigo kwa wananchi bali sasa tunataka na makampuni yale yalipe kodi stahiki. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine katika ripoti ya Chenge One ilikuwa ni kuanzisha ada ya utumiaji wa kadi za simu (sim card). Kama tutakavyokumbuka, hatua hii tuliichukua kipindi kilichopita lakini pamoja na kuichukua na kuiwasilisha hapa Bungeni ilikumbana na vikwazo vingi kutoka kwa wadau na hivyo Serikali kuamua kuchukua hatua ya kuongeza ushuru wa bidhaa kwenye huduma za simu hadi kufikia kiwango cha sasa cha asilimia 17. Naomba tufahamu kwamba unapokua sokoni kwa sisi Wachumi tunafahamu, kunapokuwa na win-lose situation wewe ndiwe utapoteza zaidi hivyo tuliweza kuihamishia kodi hii upande huu na kuthibitisha kwamba ripoti ya Chenge One tunaendelea kuifanyia kazi hatua kwa hatua.
Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lingine lilikuwa ni kuimarisha usimamizi wa utozaji wa kodi katika makampuni ya simu. Serikali yetu sikivu kama kawaida imelifanyia kazi suala hili ambapo mtambo wa telecommunication traffic monitoring system tayari umefungwa na umeanza kutumika. Hivi sasa Serikali inaendelea kuweka mfumo wa kutambua aina na kiasi halisi cha miamala na thamani ya miamala inayofanywa na makampuni ya simu. Aidha, Mamlaka yetu ya Mapato wataendelea kufanya kazi kwa karibu sana na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) ili kukagua hesabu za makampuni ya simu katika kuhakikisha kuwa kodi stahiki zinalipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo tumelifanyia kazi lilikuwa ni pendekezo la kupunguza kiasi cha misamaha ya kodi hatua kwa hatua hadi kufikia asilimia moja ya GDP ambapo tunafahamu misamaha imeendelea kushuka. Kwa historia tu, katika mwaka 2012/2013 misamaha hiyo ilishuka hadi kufikia asilimia 3.5 ya Pato la Taifa, asilimia 2.3 ya Pato la Taifa katika mwaka 2013/2014 na asilimia 1.9 ya Pato la Taifa katika mwaka 2014/2015. Serikali inaendelea na juhudi hii ya kupunguza misamaha hasa ile isiyokuwa na tija na hivyo ifikie walau asilimia moja ya Pato la Taifa katika muda wa kati na mfupi ujao.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuwaeleza Waheshimiwa Wabunge kwamba hadi kufikia Juni 30, 2016 wiki moja ijayo, ni matarajio ya Serikali kwamba misamaha itakuwa chini ya asilimia moja, tutakuwa ndani ya 0.84 ya Pato la Taifa. Hivyo ripoti cha Chenge One Serikali yetu imeendelea kuifanyia kazi vizuri hatua kwa hatua.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme hayo yanatosha katika ripoti ya Chenge One lakini yapo mengi ambayo tumekuwa tukiyafanyia kazi na kwa pamoja tutashirikiana. Kama nilivyosema tutawajibu kwa maandishi na mtaona ni hatua zipi nyingine ambazo zimefikiwa katika kuifanyia kazi ripoti hii ya Chenge One kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu na wananchi wetu kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja nyingine ilikuwa Wizara ya Fedha na Mipango na Benki Kuu ya Tanzania wasimamie na kudhibiti mfumuko wa bei na riba za mikopo. Katika suala la kudhibiti riba za mikopo, Serikali yetu pia inafahamu hili ni tatizo kubwa, linawaumiza wananchi wetu. Pamoja na kuliachia suala hili katika soko lakini pia mkono wa Serikali bado uko pale pale na zifuatazo ni sehemu tu ya hatua tunazochukua kama Serikali kuhakikisha kwamba riba inakuwa si ile inayoumiza wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza, tunaendelea na usimamizi imara wa sera za fedha na bajeti (monitory policy and fiscal policy), tunaendelea kuzifanyia kazi ili kuhakikisha kwamba riba hizi haziendi kuwa ni mzigo kwa wananchi. Jambo la pili, Serikali imeendelea kuhamasisha benki za biashara kutumia takwimu za Credit Reference Bureau kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa taarifa za historia na uaminifu wa wakopaji. Kupitia njia hii ni imani yetu kwamba kama benki hizo za biashara zitaweza kutumia statistics zilizopo katika kitengo hiki itakuwa ni rahisi kufahamu historia ya wateja wao na hivyo haitakuwa jambo jema kuona tena riba ile inapanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kulifikia jambo hili, Serikali pia inaendelea kukamilisha mradi wa vitambulisho vya taifa kwa sababu tunafahamu moja ya kitu kinachosababisha riba iwe kubwa ni pale benki au mkopeshaji hana taarifa sahihi za mtumiaji wa huduma hii. Kwa hiyo, tunaendelea kukamilisha vitambulisho vya taifa, nina imani kubwa sasa kila Mtanzania atajulikana yuko wapi na benki hizi zitakuwa na uhakika wanamkopesha nani na yuko wapi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hili pia Serikali inaendelea kusimamia uandikishwaji wa hati za umilikishwaji wa viwanja kwa Watanzania ili kuwawezesha wananchi kuwa na dhamana wanapohitaji kukopa. Pia Serikali inaendelea kuboresha soko la dhamana za Serikali na soko la jumla la fedha za kigeni ili kuongeza ushindani katika masoko. Pia Serikali yetu inaendelea kuimarisha benki maalum za maendeleo ambazo ni Benki yetu ya Kilimo na Benki ya Maendeleo ya TIB ili ziweze kutoa huduma kwa wahusika na kwa riba ambayo ni sahihi ambayo Watanzania wengi hawataumia. Huo ulikuwa ni mpango wa kudhibiti riba. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kudhibiti mfumuko wa bei, Serikali imeendelea kudhibiti mfumuko wa bei ambapo kwa muda wa kati umebaki kiwango cha wastani wa tarakimu moja. Aidha, kwa mwaka 2015 kiwango kilikuwa wastani wa asilimia 5.6. Pia katika kudhibiti mfumuko huu wa bei Serikali itaendelea kuhakikisha kwanza ujazi wa fedha kwenye uchumi unakuwa sawia na ukuaji wa shughuli za kiuchumi ili upande mmoja usije ukazidi upande mwingine na hatimaye kupelekea madhara yake kwenye mfumuko wa bei.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, Serikali itaendelea kutoa chakula kwa bei nafuu kupitia Hifadhi ya Taifa ya Chakula kwenye maeneo yenye upungufu wa chakula kwa sababu tunafahamu sehemu moja kubwa inayopelekea kuongezeka kwa mfumuko wa bei ni bei ya chakula. Hivyo, tumejipanga vizuri katika suala hili na tuna imani kubwa mfumuko wa bei utaendelea kubaki katika tarakimu moja. Pia Serikali itaendelea kudhibiti bei za nishati ya mafuta na pia kuvutia na kuhimiza uongezaji wa tija katika kila nyanja za uzalishaji na utoaji huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja nyingine ambayo napenda kuitolea ufafanuzi ilisema utajiri wa madini bado haujawanufaisha wananchi hivyo Serikali inapoteza mapato mengi katika transfer pricing na mis-invoicing. Serikali ijenge uwezo wa watumishi kuongeza mapato kwenye sekta ya madini. Katika suala hili Serikali yetu pia imeendelea kulifanyia kazi kwa umakini kuhakikisha kwamba Watanzania wananufaika na sekta hii ya madini. Kama nilivyosema tuna ushirikiano wa karibu kati ya TMAA na TRA na katika hili TRA tumeendelea kuijengea uwezo ambapo TRA ilianzisha Kitengo cha Kodi za Kimataifa (International Taxation Unit) mwisho wa mwaka 2011. Kitengo hiki kimeendelea kujengewa uwezo kupitia mafunzo ya kiutaalam ndani na nje ya nchi yetu. Mafunzo haya yalidhaminiwa na Serikali ya Norway kupitia Norwegian Tax Agency ambapo walitoa fedha ya mafunzo na Serikali ya Marekani kupitia US Treasury ambao wanaendelea kuleta mtaalam wa transfer pricing. Tunawashukuru watu wa Norway pamoja na Serikali ya Marekani kwa kuendelea kutujengea uwezo katika hatua hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia katika kuimarisha uwezo wa kiutaalam kwenye kitengo hiki TRA imenunua haki ya kutumia (transfer pricing data base) itakayowezesha kupata taarifa mbalimbali za kulinganisha, that is comparable data kwa ajili ya upatikanaji wa taarifa na kurahisisha ukokotoaji wa kodi. Vilevile TRA kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha imetengeneza kanuni za transfer pricing pamoja na transfer pricing guidelines kwa ajili ya kutoa mwongozo wa jinsi ya kukokotoa kodi. Hivyo, tuna imani kubwa kabisa kupitia vitengo hivi na jitihada hizi tatizo hili litaondoka na Watanzania wataweza kunufaika na sekta hii ya madini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya wataalam wetu kupata utaalam huu kwa sasa wataalam wa kitengo hiki wanaendelea na ukaguzi katika makampuni matatu ya madini katika eneo hili la transfer pricing. Kazi hii inatajaria kukamilika katika robo ya kwanza ya 2016/2017 na tutaona wazi mbivu na mbichi ni zipi na Watanzania haki yao iko wapi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia TRA imeshajiunga na Shirika la Kimataifa la OECD Global Forum pamoja na Africa Tax Administration Forum na inaendelea na mchakato wa kusaini makubaliano ya kubadilishana habari za kodi. Hii inaturahisishia kujua ni kiasi gani kimetoka Tanzania bila sisi kujua katika black market na tuweze kuelewa nini cha kufanya na jinsi gani ya kupata kodi yetu stahiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika kuhakikisha kuwa maeneo yanayohitaji weledi maalum yanapata wataalam wa aina hii ya kuyasimamia TRA pia hubadilishana uwezo na mamlaka nyingine za mapato na mamlaka za udhibiti nchini zinazohusika na usimamizi wa mapato na taasisi na idara nyingine za Serikali kama vile TCRA, TMAA, Contractors Registrations Board, TANROADS na kadhalika. Hali kadhalika, Serikali inaendelea na jitihada za kukiimarisha kitengo hili ili kuwa na wataalam wengi zaidi kwa ajili ya kukabiliana na changamoto za kikodi zinazoendelea kuibuka katika eneo hili la kodi za kimataifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo napenda kulitolea ufafanuzi ilikuwa Serikali itatumia utaratibu gani kuhakikisha kuwa majukumu ya taasisi zilizokuwa zikijiendesha kwa fedha za retention hayaathiriki. Napenda kulithibitia Bunge lako Tukufu kwamba nia ya Serikali ni njema katika eneo hili, imedhamiria kuhakikisha sasa mapato yote ya Serikali yanatumika kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu. Napenda kulihakikishia Bunge lako kwamba taasisi zote zilizokuwa kwenye utaratibu wa retention zitatakiwa sasa kuwasilisha mahitaji ya bajeti kila mwaka kulingana na kalenda ya uandaaji wa bajeti. Serikali itachambua mahitaji ya taasisi husika na kisha kupangiwa ukomo wa Bajeti. Aidha, Wizara ya Fedha na Mipango itahakikisha kwamba bajeti iliyoidhinishwa kwa ajili ya taasisi hizi na migao ya fedha kutoka Mfuko Mkuu inatolewa bila kuchelewa ili tusikwamishe utendaji kazi wa taasisi zetu hizi. Tunafahamu umuhimu wa majukumu yao na hivyo, hatutachelewesha fedha kuzipelekea taasisi zetu hizi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua hii italeta usawa katika matumizi ya taasisi zetu na kuzuia matumizi yasiyo ya lazima kwa taasisi zote za taifa letu. Nia ya Serikali yetu ni njema kama nilivyosema mwanzo, naomba Waheshimiwa Wabunge muendelee kutuunga mkono. Hii ni tiba sahihi sana ya lile ambalo tulilisikia huko nyuma kwamba zipo taasisi zilizokwenda kufanyiwa mikutano yao ya bodi nje ya nchi, hatuna sababu ya kufanya hivyo. Kama mchumi ukiwa na pesa ambayo unaiona ni nyingi huna matumizi unaweza kutumia vyovyote vile lakini kwa mfumo huu ni imani yangu sasa tutarejesha nidhamu ya matumizi ya pesa za Serikali na pesa hizi ziweze kuleta tija kwa wananchi wetu hasa wa kipato cha chini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja nyingine ilikuwa ni Serikali ilete Muswada wa Sheria ambapo itaanzisha mamlaka ya kusimamia na kudhibiti taasisi ndogo za fedha nchini. Serikali inakamilisha Sera ya Taifa ya Huduma Ndogo za Fedha. Sera hiyo itawezeshwa kutungwa kwa Sheria ya Kusimamia Taasisi Zinazotoa Huduma Ndogondogo za Fedha (The Microfinance Act). Sheria hii itaanzisha Mamlaka za Kusimamia na Kudhibiti Taasisi hizo kwa kutumia madaraja kama, moja, tutakuwa na udhibiti wa taasisi ndogo za fedha zinazopokea amana kwa wananchi (deposit taking microfinance institutions) utakaosimamiwa moja kwa moja na Benki Kuu ya Tanzania. Mbili, tutakuwa na udhibiti wa taasisi za huduma ndogo za fedha zisizopokea amana kutoka kwa wananchi (non deposit taking microfinance institutions). Pamoja na programu na mifuko maalum ya Serikali ya kuwezesha wananchi kiuchumi itakuwa chini ya taasisi hizi na chini ya usimamizi wa Wizara ya Fedha na Mipango.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kutakuwepo na udhibiti wa huduma za fedha zinazotolewa na vyama vya ushirika wa akiba na mikopo chini ya Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania. Mwisho, udhibiti wa huduma za fedha zinazotolewa na vikundi kama vile Village Community Banks (VICOBA), Voluntary Savings Loans Association, Rotating Savings and Credit Association na watu binafsi wanaotoa mikopo na kuweka akiba yaani money lenders and saving collectors chini ya mamlaka ya Serikali za Mitaa. Sheria hii pia itaainisha vigezo na masharti ya ukuaji wa taasisi hizo kutoka daraja moja kwenda daraja lingine ili kuwa na udhibiti imara na ukuaji endelevu wa sekta hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, tulichowaahidi Waheshimiwa Wabunge wakati tunawasilisha bajeti ya Wizara ya Fedha tutamiza ahadi hii ili wananchi wetu waondokane na adha ya usumbufu wa mfumo usio rasmi katika sekta ya fedha. Tunafahamu waathirika wakubwa ni akina mama katika hili na ni imani yangu kubwa tutalisimamia kwa uhakika kabisa ili akina mama waondokane na adha hii ya kukopeshwa bila kuwa mtu yeyote anayeratibu taratibu hizi ili akina mama hawa waondokane na lindi la umaskini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja nyingine ambayo napenda kuitolea ufafanuzi ni kwa nini Serikali hailipi madeni inayodaiwa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii takribani shilingi trilioni 8.942? Waheshimiwa Wabunge kama mnakumbuka nimekuwa nikilisemea jambo hili kwa nguvu zangu zote na tumeji-commit kama Serikali. Naomba tufahamu kwamba katika mapitio ya awali yaliyofanyika, yalionesha kwamba madai ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii yalifikia jumla ya shilingi trilioni 3.89 hadi Juni, 2015. Madai haya yanajumuisha deni la PSPF la kabla ya mwaka 1999 la shilingi trilioni 2.67 na shilingi trilioni 1.22 kwa ajili ya madai ya mifuko yote yaliyotokana na uwekezaji katika miradi mbalimbali ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina nia ya dhati ya kulipa madeni haya yote ili kuimarisha Mifuko yetu ya Hifadhi ya Jamii mara tu baada ya kukamilisha uhakiki wa madai hayo. Tunafahamu tumekuwa na tatizo la wafanyakazi hewa na tumemsikia Mheshimiwa Rais wetu amesema, unapokuwa na wafanyakazi hewa utakuwa na wastaafu hewa pia. Hivyo, tunaendelea kuhakiki hatua kwa hatua tutafika mwisho mzuri na mifuko yetu ya hifadhi ya jamii itaweza kufanyakazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mfano mmojawapo katika hili hadi kufikia Mei, 2016 uhakiki wa madai ya mfuko wa PSPF ulikuwa umekamilika ambapo kiasi kilichokubalika ni shilingi trilioni 2.04 kutoka madai ya awali ya shilingi trilioni 2.67, kuonyesha kwamba kulikuwa na madai hewa katika wastaafu hawa. Hivyo, nawaomba Waheshimiwa Wabunge tuipatie Serikali yetu muda tukamilishe uhakiki huo ambao umeanza kufanywa na Mkuguzi wetu wa Ndani wa Serikali ili tuweze kuondokana na madeni tata na tuweze kulipa kile tunachostahili kukilipa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuhitimisha majibu ya hoja zangu kwa maneno yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika na Bunge lako Tukufu, naomba tufahamu kwamba uchumi wa Tanzania ya viwanda kama alivyosema shemeji yangu Mwijage haupo mikononi mwa vijana wanywa viroba na watafuna mirungi bali mikononi mwa vijana walio tayari kabisa kuingia kwenye uchumi wa kati kiakili na kimwili. Very aggressive to take and tape opportunities that are ahead of us in our country. Kama Wabunge na wawakilishi wa wananchi tuna jukumu la kurejea majimboni mwetu na kuwaandaa vijana wetu wa Tanzania kwa Tanzania ya viwanda iliyo mbele yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, maisha ya vijana wetu hayapo kwenye bangi na pool table, hapana, bali yapo mikononi mwa mama yao Tanzania chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dokta John Pombe Magufuli na Serikali yake ambayo imelenga kwenye ubunifu utakaoleta fursa za kiuchumi kwa vijana wetu. Yapo mikononi mwa Serikali makini ambapo ipo tayari kutengeneza ajira kwa ajili ya watu wake. Serikali yetu ipo tayari kwa hayo yote, naomba tuwaandae Watanzania kuingia kwenye uchumi wa kati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kama mratibu na msimamizi wa sera za uchumi mpana (micro-economic policies), Wizara ya Fedha na Mipango tutafanya kila linalowezekana kuhakikisha tunakuwa na ufanisi katika soko la fedha (Money market), soko la ajira (labor market) na soko la bidhaa (commodity market).
Masoko haya yote matatu yanategemeana, yanatafsiri pia juhudi zetu za kuelekea uchumi wa kati na yanaathiri au yanaathari za moja kwa moja katika maisha ya Watanzania wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, utayari wetu Waheshimiwa Wabunge wa kulipa kodi kwa hiari ni njia pekee ya kutufikisha katika maendeleo endelevu na uchumi wa kati. Hivyo, ni lazima tuangalie kwa umakini rasilimali zetu tulizonazo ndani ya nchi yetu na kuzitumia kwa ufanisi katika kuleta maendeleo ya uchumi jumla (inclusive growth). Hii ni pamoja na kuongeza wigo wa vyanzo vyetu vya mapato ya ndani.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumalizia kwa pongezi kwa Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango kwa ujasiri, uvumilivu na umakini wake katika utendaji wa kazi zake. Naomba nikuambie Mheshimiwa Waziri, mti wenye matunda ndiyo hupigwa mawe, usikate tamaa endelea kwenda mbele. Najifunza mengi kutoka kwako, endelea kunilea na kunijenga, ahsante sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma kwa kutujaalia sote nafasi na tukaweza kukusanyika katika Bunge hili Tukufu na kuweza kutoa michango yetu katika hoja iliyowasilishwa na Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili naomba niwashukuru na kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wote kwa michango yenu mizuri ambayo mmetupatia sisi Wizara ya Fedha na Serikali yetu ya Awamu ya Tano. Ni imani yangu kubwa kwamba, tumeyasikia mengi mliyoyasema na tutayafanyia kazi, na ninaamini tutakapokuja na mpango kamili mpango huo utakuwa ni mpango mahiri na bajeti yetu itakuwa ni bajeti ionayoonesha michango yenu yote Waheshimiwa Wabunge. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba nichukue fursa hii niweze kuchangia hoja chache sana kulingana na muda wetu tulionao ili tuweze kuahirisha Bunge muda utakapofika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja moja ambayo Waheshimiwa Wabunge wengi wameisema ambayo ningependa kuichambua katika hotuba hii ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha ilikuwa ni kwamba mpango wetu umesahau mambo ya msingi ikiwa ni pamoja na mambo ya kuinua kilimo, mifugo na uvuvi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaamini Waheshimiwa Wabunge wanakazi nyingi wana mambo mengi, lakini mpango wetu umeeleza vizuri sana kuhusu sekta hii ya kilimo, mifugo na uvuvi. Tukienda katika ukurasa wa 56 mpaka 59 umeongelea vizuri sana katika sekta hii ambayo na sisi tunaamini bila kilimo hakuna viwanda Tanzania, bila kilimo Mheshimiwa Mwijage hawezi kugawa viwanda kama alivyofanya hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunathamini sana naomba tusome ndani ya kurasa hizo section ya 6.5 na vipengele vyake, 6.51, 6.52 pamoja na 6.53, vyote hivyo vimeelezwa pamoja na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hii ya kilimo.
Kwa hiyo naomba tusome pale, na bado tunaendelea kuandaa mpango wetu mtakapokuwa mmesoma kama bado mnahoja tunaomba muendelee kutuletea hoja zetu ili tuweze kuandika mpango wetu vizuri zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili au hoja ya pili ambayo ningependa kuitolea maelezo kwa ufupi ilikuwa ni kwamba maisha ya wananchi yanakuwa duni wakati mapato yanaongezeka.
Waheshimiwa Wabunge, naomba niseme kwamba Serikali inakubaliana na hoja hii na hasa iliwasilishwa na Mheshimiwa Waziri Kivuli wa Wizara ya Fedha tunakubaliana naye kwamba mapato yanakuwa, lakini si kwamba hali ni duni kwa wananchi kule, hapana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuimarika kwa hali ya maisha ya wananchi naomba tufahamu jambo moja, haitegemei mapato peke yake, bali hutegemea pia kuimarika kwa huduma za jamii ambazo Serikali yetu ya Awamu ya Tano imekuwa ikizipigania na tukiendelea kutekeleza na ambacho ni kipaumbele chetu kikubwa kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni rai ya Serikali yetu kuwa pamoja na jitihada tunazozichukua kama Serikali tunaomba pia wananchi watumie muda wao mwingi katika shughuli za kiuchumi kwa ajili ya kuboresha maisha yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna maendeleo yanayokuja wala hakuna mabadiliko yanayokuja kwa kuletewa lazima sisi wenyewe tukubali na sisi kama wawakilishi wa wananchi hawa Waheshimiwa Wabunge tuweze kuwaelekeza wananchi wetu nini cha kufanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilimshukuru na nikampongeza ndugu yangu Mheshimiwa Riziki alipotoa aya za Mwenyezi Mungu kutoka katika Kitabu Kitukufu cha Qurani.
Mimi naomba niseme kwa kumjibu katika aya hizo hizo za kitabu cha Qurani kwamba Mwenyezi Mungu anasema hawezi kubadili chochote katika maisha yako mpaka wewe mwenyewe uamue kubadili mwenyewe maisha yako.
Kwa hiyo, hilo ni jambo la msingi sana hatuwezi kuendelea kulaumu Serikali, kulaumu Waheshimiwa Mawaziri, sisi wenyewe tumefanya nini katika kujiletea maendelea ni jambo la msingi sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja nyingine ambayo ningependa kuitolea ufafanuzi ambayo imesemwa kwa nguvu sana, na namshukuru Mheshimiwa Profesa Mbarawa ameweza kueleza nayo ni kuporomoka kwa mizigo ndani ya bandari yetu ya Dar es Salaam. Kwa upande wa Wizara ya Fedha ziliongelewa hoja tatu; ya kwanza ilikuwa ni single customs territory, ya pili ni VAT kwenye transit goods na ya tatu ilikuwa ni wingi wa check points.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe Waheshimiwa Wabunge watutendee haki, wamtendee haki Mheshimiwa Rais wetu. Alipoingia tu madarakani aliondoa check points zote na zimebaki chache sana. Kwa hiyo, katika check points hizi tumtendee haki Mheshimiwa Rais, mtutendee haki na sisi tunaomsaidia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mengi tumekuwa tukiyafanyia kazi na haya machache yaliyobaki ikiwemo single customs territory pamoja na VAT on transit goods tunafahamu faida zake. Kutoka katika ethical point of view siamini sana kama wewe unaweza ukafurahia nyumbani kwako uko salama na kwa jirani yako hakuko salama, haiwezekani. Naamini ilikuwa ni lengo jema la Waheshimiwa Rais wawili, Rais wetu mstaafu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Rais wa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo walipokaa na wakajadili pamoja changamoto hizi na tukaja na hii single customs territory.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa kuwa imepigiwa kelele kwa muda mrefu na sisi kama Wizara ya Fedha hatujakaa kimya tayari timu yetu ya utafiti ipo kazini tutakapokamilisha kuifanya tafiti hii tutawaletea hapa na kwa pamoja kwa sababu tuliipitisha hapa Bungeni tutaleta ili tuoni ni nini cha kufanya. Serikali ni sikivu imesikia na tutalifanyia kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nisemee suala moja, naona kengele imegonga, nayo ni kuhusu TRA kwamba, kwa sasa inakusanya madeni na arrears na siyo kwamba hatukusanyi kodi tunayoistahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme jambo moja, katika hili pia niwaombe Waheshimiwa Wabunge, tunasema no research, no right to speak, kama huna utafiti usiliongelee jambo hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa taarifa ambazo zipo na sisi tunazo kwa sababu ndiyo watendaji katika Wizara hii, tunafahamu kabisa ukusanyaji wa kodi ni suala endelevu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha robo ya kwanza Julai hadi Septemba 2016 TRA wamekusanya shilingi bilioni 3,463.8 katika hizi ni shilingi bilioni 90 tu ambazo ni arrears. Sasa mtutendee haki mnapokuwa mnaleta hoja zenu hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutoka shilingi bilioni 3,000 tuna shilingi bilioni 90 tu ambazo ni arrears na arrears ni kawaida katika maisha yetu hakuna mtu asiyedaiwa, na sisi tunawapa nafasi ya wafanya biashara wetu wanadaiwa muda umefika wa kulipa wanalipa, kwahiyo tulete tu taarifa ambazo ni sahihi tusiwadanganye wananchi wetu kule walipo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimalizie kwa maneno machache kwamba Serikali yetu ina nia njema kabisa na Taifa letu na maendeleo ya watu wake. Mheshimiwa Rais wetu ana nia sahihi kabisa na njema na sisi wasaidizi wake tuna nia njema kabisa ya kumsaidia kuhakikisha Tanzania ya viwanda inapatikana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumejiandaa vizuri, tulichokifanya tumebadilisha tu spending ya Serikali, wanasema the government has shifted its spending pattern from non-productive activities to productive activities ndiyo maana tunapiga kelele. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hilo tulizoea kuona watumishi wakisafiri hata sisi Waheshimiwa Wabunge tukisafiri, na pia namheshimu sana Mheshimiwa Keissy aliyekuwa akisema safari hewa hizi ndizo tulizofuta. Ukifuta hivi vitu lazima tutalalamika, lakini vitu vya msingi, vitu vya kiuchumi, vitu vya kukuza uchumi wetu tunaendelea kuvifanyia kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumezoea kuona Taifa letu likiendeshwa na kodi za wafanyakazi, tumesema hapana. Taifa litaendeshwa na kodi za wafanyakazi pamoja na kodi za wafanyabiashara katika sekta binafsi. Sekta binafsi imesahaulika muda mrefu, alisema vizuri Mheshimiwa Bashe, kwamba kama yalifanyika makosa hivi sasa ni sahihi tuendelee na makosa hayo? Hatuwezi kufanya hivyo. Ndiyo kile nilichosema kutoka kwenye kitabu kitukufu lazima tuwe tayari kujibadilisha sisi kama tunataka na Mwenyezi Mungu atukubalie tunayotaka kubadilisha, hilo ni jambo la msingi sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na katika haya mabadiliko ninaamini Mheshimiwa Waziri wa Fedha ataongea kuhusu mdororo katika sekta ya mabenki. Lakini naomba niwaambie jambo moja mabenki yetu wamekuwa wavivu, benki zote ziko Dar es Salaam, benki zote ziko sehemu zile ambazo kuna taasisi za Serikali, hivi mbona benki hizi haziwafuati wananchi kule walipo? Kule ndiko pesa zilipo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuwaambie mabenki haya, Serikali imechukua pesa yake, Serikali ilikuwa ni mteja kama wateja wengine imechukua pesa zake ili i-invest katika productive economic activities sasa kwa nini tunalalamika? Mdororo uliopo ni ule mabenki yetu yalikuwa mavivu kwamba tunamkopesha mteja wetu hatujui anaenda kufanyia nini pesa tunayomkopesha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajidanganya pesa za Serikali ndani ya benki zetu, Serikali imechukua kama mteja mmojawapo. Wateja wale kwa kuwa walikuwa hawafuatiliwi na sasa hawalipi ndiyo maana tunaona Waheshimiwa wabunge mnasema CRDB ime-register hasara, ni kwa sababu sasa zile pesa walizozoea kutumia zimekwenda kwa mwenyewe na zile ambazo wamekopesha hawana uwezo wa kuzikusanya. Hilo ni jambo la msingi tuseme ukweli, tujitendee haki kama wananchi, tujitendee haki kama Watanzaini na tutaifikisha Tanzania hii salama ndani ya nchi hii na uchumi wa kati tutafika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii na naomba nianze kwa kusema naunga mkono hoja iliyowekwa mezani na Kamati yetu ya Bunge ya Bajeti. Nimpongeze Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati hii, Mheshimiwa dada yangu Hawa Ghasia pamoja na Makamu wake na Wajumbe wote wa Kamati yetu ya Kudumu ya Bajeti kwa kazi nzuri ambayo wamekuwa wakiifanya kwa kutushauri sisi Serikali na kutusimamia. Kwa kweli mnafanya kazi nzuri sana. Hongereni sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme machache kwa sababu muda ni mfupi ambao nimepatiwa, naomba nianze na hili ambalo Waheshimiwa Wabunge wengi wameonesha concern yao kwamba Serikali ipunguze kukopa ndani, tunapunguza mzunguko wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge na Bunge lako Tukufu kwamba, Serikali yetu inakopa katika soko la ndani kwa kuzingatia uwezo wa soko lenyewe na kuhakikisha kuwa haipunguzi uwezo wa Taasisi hizi kukopesha Sekta Binafsi na watu binafsi. Hili naomba lifahamike kuna miongozo, kuna vigezo na lazima tufahamu hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wameihusisha pia na kukopa kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, lakini naomba pia ifahamike kwamba Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ina taratibu na miongozo ya uwekezaji ikiwa ni pamoja na kupanga kiwango au kiasi cha fedha wanazoweza kuweka katika hati fungani na dhamana za Serikali. Kwa hiyo, kama Serikali tuko makini, hatuwezi kabisa kukopa katika Mifuko hii ya Hifadhi ya Jamii mpaka ikafikia kiwango cha kushindwa kulipa wastaafu wetu. Tuko vizuri, tuko imara na mifuko yetu inafuata miongozo kila kitu na wala hamna shida katika hili. Niombe tu kuwajulisha kwamba mikopo ya ndani pia ni njia mojawapo ya kuimarisha Sekta Binafsi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, inapokopesha ina uwezo wa kufanya hivyo. Kwa hiyo, tukizuia na kusema kwamba hapana kwa Serikali tutakuwa tunaiua Sekta yetu Binafsi, tutaua Taasisi zetu ambazo zinaweza kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hilo pia Waheshimiwa Wabunge wameongelea kwamba Mabenki kufanya vibaya kwa sababu hiyo tunakopa, kama nilivyosema mwanzo hapana. Mabenki yetu sasa yanajitathmini yenyewe. Tukumbuke tuliwahi kusema hapa ndani ya Bunge hili kama Serikali yetu kwamba ilifika sehemu mabenki haya yakawa yanatumia pesa ambazo sio za kwake na yakasahau jukumu lao kubwa. Kwanza anapokuja mtu kukopa pale benki anatakiwa afanye tathmini - ilikuwa haifanyiki. Niko Wizara ya Fedha nawasiliana na nafanya vikao na ma-CEO wa mabenki haya, wanaeleza kabisa kwamba sasa mtu aki-apply mkopo wanakwenda kwenye vigezo. Ilifika sehemu wanakopesha bila vigezo na ndiyo maana ya kuongezeka kwa mikopo chechefu. Lazima tuweke uimara katika usimamizi wa sekta yetu ya fedha ili tuweze kutoka vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo ningependa kulitolea ufafanuzi au kuchangia hoja hii ni kuhusu kodi ya majengo kukusanywa na TRA. Katika hotuba hii iliyowasilishwa na Kamati yetu ya Bajeti na data tunazoziona ni kwa quarter ya kwanza na katika quarter ya kwanza, Januari mpaka Septemba, TRA hawakukusanya kodi ya majengo na Halmashauri zilipewa maelekezo waendelee kukusanya kodi hii ya majengo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, performance tunayoiona ni ya Halmashauri zetu kukusanya kodi ya majengo na ndiyo maana Serikali imeona sasa kama Halmashauri zetu zinakusanya katika level hii inaonesha kabisa haziwezi na sasa TRA ichukue kodi hii ili iweze kukusanya. Itakapoletwa taarifa ya nusu mwaka iki-include na quarter ya pili tutaona utofauti mkubwa wa kodi ya majengo ambapo TRA wameanza kukusanya kuanzia mwezi wa Kumi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba tuelewe nia ya Serikali na lengo la Serikali yetu ni jema. Halmashauri zetu zilishindwa kufanya vizuri ndiyo maana kama Serikali tumechukua ukusanyaji huu na mtaona tutakapoleta tathmini yetu ya nusu mwaka, kuna utofauti mkubwa katika hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yako mengi naomba nimalizie kwa kusema katika hili la kufunga biashara nimeona pia Wabunge wengi wameshangilia. Ndugu zangu naomba mfahamu sasa hivi tunarasimisha biashara zetu. Tunaona TRA wanatoa TIN mpya, biashara zilizofungwa ni 4,183, naomba tufahamu katika hili. Biashara mpya zilizofunguliwa ni 1,039,554. Kwa hiyo, naomba niseme katika hili, tutaleta taarifa katika Bunge lako, tunamalizia kufanya tathmini ya ukubwa wa biashara zilizofungwa na ukubwa wa biashara zinazofunguliwa. Kwa hiyo, lazima tuongee tukiwa na data ndugu zangu ili tuweze kuitendea haki Serikali yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, naomba nianze kwa kukushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuweza kuchangia hoja iliyowekwa mezani na Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango na kabla sijaanza kuchangia naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutuwezesha sote kufika hii siku ya leo na kunijalia mimi mwenyewe uzima na nafasi katika kulitumikia Taifa langu.

Mheshimiwa Spika, baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu naomba pia niwashukuru wazazi wangu, baba na mama yangu, mimi kama kitinda mimba wao nawashukuru sana kwa kuendelea kuniombea, kuniamini na kunipa radhi yao ili niweze kulitumikia taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba pia nimshukuru sana rafiki yangu wa kudumu na mume wangu mpenzi Dkt. Muhajir Kachwamba ambaye yupo ndani ya Bunge hili, nikushukuru sana kwa kuendelea kuwa rafiki yangu kwa kila hali na katika kila gumu na jema ninalolipitia, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana naomba pia nimshukuru mtoto wangu mwingine ambaye yupo shuleni yuko kidato cha nne, Samira Muhajir; nimuombee kwa Mwenyezi Mungu aweze kufanya vizuri katika maandalizi yake na mtihani wake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda nitoe pongezi; pongezi zangu ziende kwa Mheshimiwa Rais wetu, Mheshimiwa John Pombe Joseph Magufuli kwa uthubutu, ujasiri na ujemedari wake wa kurejesha hadhi ya taifa letu ndani ya Bara letu la Afrika. Tanzania imekuwa mfano na namshukuru sana Mheshimiwa Rais, naendelea kumpongeza na niseme kama Mbunge wa Kondoa, kama alivyosema alipokuwa akiomba kura alipofika Kondoa na sasa anayatekeleza kwa vitendo yale yote aliyowaahidi wapiga kura wetu wa Jimbo la Kondoa. Nimwambie wapiga kura wetu wa Jimbo la Kondoa wapo na yeye asilimia mia moja wanamuunga mkono, aendelee kuchapa kazi kwa niaba yao na kwa niaba ya Watanzania kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nimshukuru na nimpe pongezi sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango. Amekuwa ni kiongozi makini, mwenye dira na asiyetetereka; namshukuru Mwenyezi Mungu kunipa nafasi ya kufanya kazi na Mheshimiwa Dkt. Mpango. Imedhihirika kwenye bajeti hii ya mwaka huu imemuonesha Mpango ni nani katika tasnia ya uchumi, huyu ndiye Dkt. Mpango, katika tasnia ya uchumi wanakufahamu Dkt. Mpango, chapa kazi sisi watumishi tulio wako chini yako tuko na wewe, tutapokea maelekezo yako na tutaendelea kuyatekeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia niwape pongezi watumishi wote wa Wizara ya Fedha na Mipango; naomba niwakumbushe wakati tunaanza vikao vya Kamati ya Bajeti pale mwezi wa pili niliwaambia kama ni siku basi sasa hivi ndiyo alfajiri, ndio saa kumi na moja, mpaka tutakapoelekea. Naomba niwape pongezi sana, wamefanya kazi usiku na mchana bila kupumzika wakipokea maelekezo na wakiyafanyia kazi mpaka saa kumi usiku, hongereni sana chini ya Katibu wetu Mkuu Bwana Doto James. Mmeonesha kwamba Wizara ya Fedha tunaweza na tumeweza kurejesha hadhi na tunaendelea kukimbia, hongereni sana na tupo pamoja na nanyi viongozi wenu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba sasa nichangie baadhi ya hoja ambazo zimetolewa humu ndani, niweze kuzitolea ufafanuzi. Niwashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa kuleta hoja mbalimbali ambazo ni za kuimarisha na pale penye kukosoa mmeweza kukosoa, nawashukuru sana.

Mheshimiwa Spika, hoja ya kwanza ambayo ningependa kuitolea ufafanuzi ipo katika kitabu cha hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani, Msemaji katika Wizara ya Fedha na Mipango, nayo alisemea kuhusu hali ya uchumi wa Taifa na akaendelea kusema ametoa katika taarifa ya Benki ya Dunia. Naomba ninukuu maneno machache yaliyoandikwa kwenye kitabu kile, aliandika yafuatayo:-

“Kukua kwa uchumi kumepungua kutokana na upatikanaji wa fedha kuwa hafifu na kutotabirika/ kutokueleweka kwa Rais Magufuli.”

Mheshimiwa Spika, hoja yake ya pili, aliandika, baadhi ya wawekezaji wa kigeni wameamua au; naomba tuangalie sana hapa ninaposema au kwa sababu anaandika neno halafu analitafutia neno la pili; au wanataka kupunguza shughuli zao na akasema sababu zake ni hizi zifuatazo; alisema moja, ni masharti mapya, magumu na kutozwa kodi kubwa na sababu ya pili katika hilo akatoa reference kutoka PricewaterhouseCoopers Comparative World Studies of Tax Regimes of 2014.

Mheshimiwa Spika, naomba sana Waheshimiwa Wabunge na hasa ndugu zangu wa Kambi Rasmi ya Upinzani tunapojenga hoja zetu tuzijenge tukiwa na uhakika nazo. Umesema mwanzo kabisa kwamba kutotabirika au kutokueleweka kwa Mheshimiwa Rais, Dkt. John Magufuli halafu reference ya 2014, hivi reference ya 2014 Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alikuwa Rais kweli? Kwa hiyo, tuwe na uhakika na nini tunakipeleka.

Mheshimiwa Spika, unasema masharti magumu na kutozwa kodi kubwa; Mheshimiwa Spika wewe ni shahidi na Bunge lako tukufu, ni kodi zipi mpya ambazo zimeongezwa baada ya Serikali ya Awamu ya Tano kuingia madarakani? Anaongelea hizo kodi mpya na kubwa anatoa reference ya mwaka 2014. Hii ni ngumu sana, lazima tuwe na uhakika ni nini tunakifanya na tunalitendea haki Taifa letu kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nimwambie na niwaambie Watanzania kwa ujumla, kwanza waendelee kuamini taarifa iliyowasilishwa na Waziri wa Fedha na Mipango kuhusu hali ya uchumi wa Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, nina kitabu nimekiacha hapa, nitakukabidhi wewe ili ndugu zetu wakifanyie reference. Hiki ni kitabu kilichoandikwa na World Bank alikosema yeye amepata data hizi. Katika kitabu hiki cha taarifa iliyoandikwa na World Bank ni cha tarehe 23 Februari, 2017; chenye kichwa cha habari kinasema United Republic of Tanzania Systematic Country Diagnostic.

Mheshimiwa Spika, katika kitabu hiki ambacho ni very current, cha mwezi wa pili, ndani yake wamesema nini; wamesema, naomba ni-quote maneno yao kwa Kiingereza, wanasema:-

“For the past 10 years the country’s macroeconomic performance has been robust, with GDP growing annually at an average of 6.5 percent-higher than the Sub-Saharan African average and that of many regional peers.” (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tafsiri isiyo rasmi katika hili ni kwamba kwa miaka kumi sasa uchumi wa Taifa letu umekuwa mzuri na umekuwa ukikua kwa zaidi ya wastani wa asilimia 6.5, juu zaidi ya wastani wa ukuaji wa uchumi wa nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara na wenzetu waliotuzunguka katika Ukanda wetu wa Afrika Mashariki. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hizi ndizo taarifa tunazotakiwa kuwapa wananchi wetu, kwa lengo lolote lile ambalo unalo ni vizuri kuzisema kwa umakini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika taarifa hiyo ya Benki ya Dunia ya mwezi wa pili inasema kumekuwa pia na kupungua kwa umaskini kunakoambatana na kupungua kwa utofauti wa kipato kati ya makundi mbalimbali ndani ya jamii. Huu ndio uchumi wa Tanzania na niwaombe Watanzania waendelee kuamini. Kitabu hiki kimetaja sababu ambazo tumekuwa tukizisema hapa kwa nini wamesema hiki wanachokiona na kwa nini taarifa zao zimeonesha hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wamesema taarifa ya kwanza ni kuimarika kwa miundombinu ya barabara na masoko ndani ya nchi yetu. (Makofi)

Waheshimiwa Wabunge, nani si shahidi wa kwamba Nchi yetu imeweza kuunganishwa sasa mkoa kwa mkoa nchi nzima kasoro Mkoa mmoja wa Rukwa. Tuitendee haki nchi yetu, tuwatendee haki viongozi wetu, tumtendee haki Mheshimiwa Rais wetu ambaye kabla ya kuwa Rais alikuwa Waziri wa Miundombinu na Uchukuzi, lazima tumtendee sana haki. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sababu au kiashiria cha pili kilichosababisha conclusion ya taarifa yao na utafiti wao, walisema ni kumiliki kwa vyombo mbalimbali vya mawasiliano na usafiri kwa Watanzania wote. Sisi sote ni mashahidi, kijiji gani utaenda ndani ya nchi hii ukose usafiri dunia ya leo? Hilo ni jambo la msingi sana, utafika popote hata kama kijiji kipo interior kiasi gani utapata usafiri na utafika, naomba ndugu zetu waweze kututendea haki.

Mheshimiwa Spika, naamini sisi sote humu kama Waheshimiwa Wabunge tunawahudumia wapigakura wetu kwa e-payments; hivi kweli sisi ndio wa kusema kwamba uchumi wa nchi yetu haukui? Nani ambaye hatumi M-Pesa, Tigo-Pesa, Airtel-Money kwa wapigakura wake kijiji chochote ndani ya Tanzania? Lazima tujitendee haki na tuwatendee haki Watanzania. Hivi ni baadhi tu ya viasharia vilivyowekwa na taarifa hii, vipo vingi, kama nilivyosema nitakabidhi taarifa hii kwako ili ambaye anataka kufanya reference aje afanye reference ili tuwe na uelewa wa pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimalizie na nukuu chache kuhusu hali ya uchumi wa Taifa letu kutoka kwa wageni mbalimbali waliolitembelea Taifa letu miezi michache iliyopita. Mmoja wao alikuwa Naibu Mkurugenzi wa Benki ya Dunia, Bwana Tao Zhang; akiwa Tanzania, wala hakuwa Washington, alikuwa Tanzania; alisema hivi, nanukuu maneno yake:-

“Uchumi wa Tanzania umebaki kuwa imara kutokana na maboresho ya kisera yanayotekelezwa chini ya uongozi thabiti wa Rais John Pombe Joseph Magufuli.” (Makofi)

Mheshimiwa Spika, akasema hasa katika suala la ukusanyaji wa mapato na vita dhidi ya rushwa na ugaidi. Hao ndio wachumi wa dunia na wanafanya analysis kwa kutumia data ambazo ni credible, naomba tuendelee kuwaamini.

Mheshimiwa Spika, sishangazwi sana na maneno haya yaliyopo kwenye Hotuba hii ya Kambi Rasmi ya Upinzani. Naomba ninukuu pia maneno ya mwekezaji mmoja kutoka China ambaye alikuwa anatafuta taarifa za kwenda kuwekeza katika viwanda vya ngozi na viatu nchini Ethiopia. Mwekezaji huyu kabla hajaenda alikuwa akitafuta taarifa, na haya maneno yake alisema, akasema:-

“Ukiwa nje ya Afrika unapewa picha na baadhi ya watu wakiwemo Waafrika wenyewe kwamba Afrika ni sehemu ya vita, Afrika ni sehemu iliyojaa njaa, Afrika ni sehemu ya magonjwa na kusahau kuwa Afrika ina mchango mkubwa na fursa nyingi katika mchango wa dunia.” (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nanukuu maneno haya ili tu Watanzania watuelewe, kwamba tunachokifanya chini ya uongozi wa jemedari, Dkt. John Pombe Magufuli ni kuimarisha uchumi wa kila Mtanzania (inclusive growth for everyone in Tanzania) hiki ndicho tunachokifanya. Niwaombe Watanzania wapuuze taarifa zilizowasilishwa, niwaombe sana ndugu zangu, Mheshimiwa Bunge lako hili ni Tukufu, litendewe haki kwa kuletewa taarifa ambazo ni haki, taarifa ambazo ni halali, taarifa zenye vyanzo vyenye uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hili, naomba sasa niendelee na baadhi ya hoja nyingine. Hoja ya pili ambayo ninapenda kuielezea ilisemwa na niliitolea maelezo, yawezekana sikuelewa vizuri; ilikuwa ni kuhusu Serikali kutoa maelezo kuhusu utekelezaji wa ahadi ya shilingi milioni hamsini.

Mheshimiwa Spika, wewe umeshuhudia Waheshimiwa Wabunge wakiongea kwa uchungu, wengine kwa kejeli ambazo sio nzuri na hili pia limeandikwa kwa kejeli kubwa sana katika Hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani katika Wizara ya Fedha na Mipango.

Naomba nikumbushe, wakati tuna-conclude Bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango nilisema fedha kwa mwaka wa fedha 2016/2017 zilitengwa shilingi bilioni 59.5, na mwaka huu tumetenga shilingi bilioni 60 chini ya Fungu 21 - Wizara ya Fedha na Mipango. Fedha zimetengwa na hazina wasiwasi kwamba hazipo, zipo fedha hizi. Nikasema kwamba tunachokifanya sasa ni kuhakikisha tunasoma mfumo mzima, tunajifunza kutokana na makosa yaliyotendeka huko nyuma ili tuhakikishe fedha hizi za walipa kodi wa Tanzania zinakuwa na matokeo chanya katika Taifa letu na zinaweza kutekeleza kile ambacho kimesababisha Mheshimiwa Rais aweze kuahidi ahadi hii ya shilingi milioni hamsini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, yapo maswali ambayo tunajaribu kujiuliza kama wataalam wa uchumi, kwamba hivi governance ya hii shilingi milioni hamsini ikoje katika kila kijiji? Hivi tunaposema tunapeleka, tunapeleka shilingi milioni hamsini hizi katika mfumo upi? Tunajiuliza ni njia gani bora tunaweza kumpatia pesa Mtanzania huyu aliyeko kijijini kwangu kule Kalamba. Tunajiuliza, je, baada ya kutambua kijiji kinahitaji kiasi hiki tunawezaje sasa kujua nani anapata nini na kwa kiasi gani na anakwenda kutekeleza mradi gani? Tunaweza kujiuliza na kujibu maswali, je, ni mfumo gani tunataka kuutumia sasa ili kurejesha fedha hizi? Tukumbuke nilisema hapa kwamba fedha hizi si zawadi, fedha hizi ni mkopo. Fedha hizi zinatakiwa zipelekwe zikaimarishe uchumi na hatimaye tuhakikishe zinazunguka kwa Watanzania wote na kila Mtanzania anafaidika na pesa hii na mwisho wa siku pesa hizi zinarudi ndani ya Serikali yetu tukiwa tumeimarisha uchumi wa watu wetu.

Mheshimiwa Spika, naomba niseme kwamba mpaka tulipofika tupo hatua nzuri sana, na pesa kama nilivyosema shilingi bilioni 59.5 zipo, shilingi bilioni 60 tumetenga kwenye bajeti yetu ya mwaka huu, zote tutazipeleka kama ambavyo tuliahidi. Sasa hivi tumefika hatua nzuri, tayari Waraka wa Baraza la Mawaziri umeandaliwa kuhusu utaratibu na maeneo pamoja na mfumo utakaotumika katika kutekeleza programu hii ya uwezeshaji wananchi wetu kiuchumi. Niwaambie tu Waheshimiwa Wabunge kwamba hii ni ahadi ya Mheshimiwa Rais na tumeona kwa pamoja, hakuna ahadi anayoahidi akashindwa kuitekeleza, anatekeleza ahadi zake zote na hili atalitekeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niende kwenye hoja nyingine ambayo imesemwa sana kwamba Serikali inaona kuwa na utaratibu wa kukopa zaidi katika soko la ndani, hali hii kiuchumi si nzuri kwa kuwa taasisi za fedha zinakimbilia kuikopesha Serikali zaidi kuliko sekta binafsi. Katika hili tunafahamu zipo instruments mbalimbali zinatumika kuhakikisha Serikali inakopa na inakopa kwa vigezo, inakopa ikiwa na ukomo kwamba inakopa kiasi gani ili isiathiri utendaji wa sekta binafsi ndani ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama Wizara ya Fedha na Mipango tunafahamu sekta binafsi ndiyo engine ya uchumi, hatuwezi Serikali kufanya kitu chochote kinyume na sekta binafsi. Tunachukua tahadhari ya kutosha katika kulifanya hili na Serikali, kama nilivyosema, imeweka ukomo wa kukopa ndani usiozidi asilimia 1.5 ya Pato la Taifa kwa mwaka ili kuzipa nafasi benki za biashara kuendelea kukopa mikopo kwenye sekta binafsi ambayo ndiyo engine ya uchumi wetu kama nilivyosema. Kwa mwaka huu tumeona kwamba tupunguze kiwango cha kukopa kutoka ndani na mwaka huu tunakopa asilimia moja tu ya Pato la Taifa ili kuipa nafasi sekta binafsi kuchukua mikopo ndani ya benki zetu. (Makofi)

Jambo lingine ambalo limesemewa sana; nililijibu lakini naona nalo halikukaa vizuri au Waheshimiwa Wabunge hawakunielewa ilikuwa ni mikopo kutoka mifuko ya hifadhi ya jamii, kwamba Serikali imekuwa na tabia ya kukopa fedha kutoka Mifuko ya Jamii bila kuzirudisha kwa wakati, nini mpango wa Serikali wa kulipa madeni hayo?

Mheshimiwa Spika, naomba niseme kama nilivyosema kwenye jibu la hoja iliyopita, kukopa ndani ya nchi na hasa kwa mifuko yetu tunaipa nafasi pia mifuko yetu kupata fedha ambazo ni za uhakika. Hata hivyo, katika kulipa madeni haya naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge kwamba katika uchumi malipo ni jambo la muhimu lakini kuhakikisha unalipa nini ni jambo la muhimu zaidi, na hicho ndicho ambacho kimechelewesha malipo haya kwa Mifuko yetu ya Hifadhi ya Jamii. Tumefanya uhakiki; na ninaomba nitoe taarifa chache tu ya kuona ni kwa nini Serikali iliona ni muhimu kufanya uhakiki wa madeni haya, tuchukue mfano mmoja… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Spika, muda umekuwa ni mchache sana lakini naomba niseme kwamba hoja hizi tutaziwasilisha kwa maandishi, na ninaomba niseme kwamba nia na lengo la Serikali yetu ni jema sana la kuhakikisha tunalipa mikopo yote, si ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii tu bali ya wakandarasi, wazabuni pamoja na watumishi. Tunafanya hivyo kuhakikisha Watanzania wanaweza kuimarisha uchumi wao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema haya, naomba nikushukuru sana kwa kunipa nafasi hii na ninaomba niseme naunga mkono hoja hii ya Serikali iliyowekwa Mezani na Waziri wa Fedha na Mipango ambayo imetuhakikishia Serikali yetu ina nia ya dhati ya kuhakikisha uchumi wa viwanda na uchumi wa kati unafika Tanzania kabla ya mwaka 2025.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, naomba nianze kwa kukushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuweza kuchangia hoja iliyowekwa mezani na Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango na kabla sijaanza kuchangia naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutuwezesha sote kufika hii siku ya leo na kunijalia mimi mwenyewe uzima na nafasi katika kulitumikia Taifa langu.

Mheshimiwa Spika, baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu naomba pia niwashukuru wazazi wangu, baba na mama yangu, mimi kama kitinda mimba wao nawashukuru sana kwa kuendelea kuniombea, kuniamini na kunipa radhi yao ili niweze kulitumikia taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba pia nimshukuru sana rafiki yangu wa kudumu na mume wangu mpenzi Dkt. Muhajir Kachwamba ambaye yupo ndani ya Bunge hili, nikushukuru sana kwa kuendelea kuwa rafiki yangu kwa kila hali na katika kila gumu na jema ninalolipitia, ahsante sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana naomba pia nimshukuru mtoto wangu mwingine ambaye yupo shuleni yuko kidato cha nne, Samira Muhajir; nimuombee kwa Mwenyezi Mungu aweze kufanya vizuri katika maandalizi yake na mtihani wake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda nitoe pongezi; pongezi zangu ziende kwa Mheshimiwa Rais wetu, Mheshimiwa John Pombe Joseph Magufuli kwa uthubutu, ujasiri na ujemedari wake wa kurejesha hadhi ya taifa letu ndani ya Bara letu la Afrika. Tanzania imekuwa mfano na namshukuru sana Mheshimiwa Rais, naendelea kumpongeza na niseme kama Mbunge wa Kondoa, kama alivyosema alipokuwa akiomba kura alipofika Kondoa na sasa anayatekeleza kwa vitendo yale yote aliyowaahidi wapiga kura wetu wa Jimbo la Kondoa. Nimwambie wapiga kura wetu wa Jimbo la Kondoa wapo na yeye asilimia mia moja wanamuunga mkono, aendelee kuchapa kazi kwa niaba yao na kwa niaba ya Watanzania kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nimshukuru na nimpe pongezi sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango. Amekuwa ni kiongozi makini, mwenye dira na asiyetetereka; namshukuru Mwenyezi Mungu kunipa nafasi ya kufanya kazi na Mheshimiwa Dkt. Mpango. Imedhihirika kwenye bajeti hii ya mwaka huu imemuonesha Mpango ni nani katika tasnia ya uchumi, huyu ndiye Dkt. Mpango, katika tasnia ya uchumi wanakufahamu Dkt. Mpango, chapa kazi sisi watumishi tulio wako chini yako tuko na wewe, tutapokea maelekezo yako na tutaendelea kuyatekeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia niwape pongezi watumishi wote wa Wizara ya Fedha na Mipango; naomba niwakumbushe wakati tunaanza vikao vya Kamati ya Bajeti pale mwezi wa pili niliwaambia kama ni siku basi sasa hivi ndiyo alfajiri, ndio saa kumi na moja, mpaka tutakapoelekea. Naomba niwape pongezi sana, wamefanya kazi usiku na mchana bila kupumzika wakipokea maelekezo na wakiyafanyia kazi mpaka saa kumi usiku, hongereni sana chini ya Katibu wetu Mkuu Bwana Doto James. Mmeonesha kwamba Wizara ya Fedha tunaweza na tumeweza kurejesha hadhi na tunaendelea kukimbia, hongereni sana na tupo pamoja na nanyi viongozi wenu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba sasa nichangie baadhi ya hoja ambazo zimetolewa humu ndani, niweze kuzitolea ufafanuzi. Niwashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa kuleta hoja mbalimbali ambazo ni za kuimarisha na pale penye kukosoa mmeweza kukosoa, nawashukuru sana.

Mheshimiwa Spika, hoja ya kwanza ambayo ningependa kuitolea ufafanuzi ipo katika kitabu cha hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani, Msemaji katika Wizara ya Fedha na Mipango, nayo alisemea kuhusu hali ya uchumi wa Taifa na akaendelea kusema ametoa katika taarifa ya Benki ya Dunia. Naomba ninukuu maneno machache yaliyoandikwa kwenye kitabu kile, aliandika yafuatayo:-

“Kukua kwa uchumi kumepungua kutokana na upatikanaji wa fedha kuwa hafifu na kutotabirika/ kutokueleweka kwa Rais Magufuli.”

Mheshimiwa Spika, hoja yake ya pili, aliandika, baadhi ya wawekezaji wa kigeni wameamua au; naomba tuangalie sana hapa ninaposema au kwa sababu anaandika neno halafu analitafutia neno la pili; au wanataka kupunguza shughuli zao na akasema sababu zake ni hizi zifuatazo; alisema moja, ni masharti mapya, magumu na kutozwa kodi kubwa na sababu ya pili katika hilo akatoa reference kutoka PricewaterhouseCoopers Comparative World Studies of Tax Regimes of 2014.

Mheshimiwa Spika, naomba sana Waheshimiwa Wabunge na hasa ndugu zangu wa Kambi Rasmi ya Upinzani tunapojenga hoja zetu tuzijenge tukiwa na uhakika nazo. Umesema mwanzo kabisa kwamba kutotabirika au kutokueleweka kwa Mheshimiwa Rais, Dkt. John Magufuli halafu reference ya 2014, hivi reference ya 2014 Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alikuwa Rais kweli? Kwa hiyo, tuwe na uhakika na nini tunakipeleka.

Mheshimiwa Spika, unasema masharti magumu na kutozwa kodi kubwa; Mheshimiwa Spika wewe ni shahidi na Bunge lako tukufu, ni kodi zipi mpya ambazo zimeongezwa baada ya Serikali ya Awamu ya Tano kuingia madarakani? Anaongelea hizo kodi mpya na kubwa anatoa reference ya mwaka 2014. Hii ni ngumu sana, lazima tuwe na uhakika ni nini tunakifanya na tunalitendea haki Taifa letu kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nimwambie na niwaambie Watanzania kwa ujumla, kwanza waendelee kuamini taarifa iliyowasilishwa na Waziri wa Fedha na Mipango kuhusu hali ya uchumi wa Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, nina kitabu nimekiacha hapa, nitakukabidhi wewe ili ndugu zetu wakifanyie reference. Hiki ni kitabu kilichoandikwa na World Bank alikosema yeye amepata data hizi. Katika kitabu hiki cha taarifa iliyoandikwa na World Bank ni cha tarehe 23 Februari, 2017; chenye kichwa cha habari kinasema United Republic of Tanzania Systematic Country Diagnostic.

Mheshimiwa Spika, katika kitabu hiki ambacho ni very current, cha mwezi wa pili, ndani yake wamesema nini; wamesema, naomba ni-quote maneno yao kwa Kiingereza, wanasema:-

“For the past 10 years the country’s macroeconomic performance has been robust, with GDP growing annually at an average of 6.5 percent-higher than the Sub-Saharan African average and that of many regional peers.” (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tafsiri isiyo rasmi katika hili ni kwamba kwa miaka kumi sasa uchumi wa Taifa letu umekuwa mzuri na umekuwa ukikua kwa zaidi ya wastani wa asilimia 6.5, juu zaidi ya wastani wa ukuaji wa uchumi wa nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara na wenzetu waliotuzunguka katika Ukanda wetu wa Afrika Mashariki. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hizi ndizo taarifa tunazotakiwa kuwapa wananchi wetu, kwa lengo lolote lile ambalo unalo ni vizuri kuzisema kwa umakini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika taarifa hiyo ya Benki ya Dunia ya mwezi wa pili inasema kumekuwa pia na kupungua kwa umaskini kunakoambatana na kupungua kwa utofauti wa kipato kati ya makundi mbalimbali ndani ya jamii. Huu ndio uchumi wa Tanzania na niwaombe Watanzania waendelee kuamini. Kitabu hiki kimetaja sababu ambazo tumekuwa tukizisema hapa kwa nini wamesema hiki wanachokiona na kwa nini taarifa zao zimeonesha hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wamesema taarifa ya kwanza ni kuimarika kwa miundombinu ya barabara na masoko ndani ya nchi yetu. (Makofi)

Waheshimiwa Wabunge, nani si shahidi wa kwamba Nchi yetu imeweza kuunganishwa sasa mkoa kwa mkoa nchi nzima kasoro Mkoa mmoja wa Rukwa. Tuitendee haki nchi yetu, tuwatendee haki viongozi wetu, tumtendee haki Mheshimiwa Rais wetu ambaye kabla ya kuwa Rais alikuwa Waziri wa Miundombinu na Uchukuzi, lazima tumtendee sana haki. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sababu au kiashiria cha pili kilichosababisha conclusion ya taarifa yao na utafiti wao, walisema ni kumiliki kwa vyombo mbalimbali vya mawasiliano na usafiri kwa Watanzania wote. Sisi sote ni mashahidi, kijiji gani utaenda ndani ya nchi hii ukose usafiri dunia ya leo? Hilo ni jambo la msingi sana, utafika popote hata kama kijiji kipo interior kiasi gani utapata usafiri na utafika, naomba ndugu zetu waweze kututendea haki.

Mheshimiwa Spika, naamini sisi sote humu kama Waheshimiwa Wabunge tunawahudumia wapigakura wetu kwa e-payments; hivi kweli sisi ndio wa kusema kwamba uchumi wa nchi yetu haukui? Nani ambaye hatumi M-Pesa, Tigo-Pesa, Airtel-Money kwa wapigakura wake kijiji chochote ndani ya Tanzania? Lazima tujitendee haki na tuwatendee haki Watanzania. Hivi ni baadhi tu ya viasharia vilivyowekwa na taarifa hii, vipo vingi, kama nilivyosema nitakabidhi taarifa hii kwako ili ambaye anataka kufanya reference aje afanye reference ili tuwe na uelewa wa pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimalizie na nukuu chache kuhusu hali ya uchumi wa Taifa letu kutoka kwa wageni mbalimbali waliolitembelea Taifa letu miezi michache iliyopita. Mmoja wao alikuwa Naibu Mkurugenzi wa Benki ya Dunia, Bwana Tao Zhang; akiwa Tanzania, wala hakuwa Washington, alikuwa Tanzania; alisema hivi, nanukuu maneno yake:-

“Uchumi wa Tanzania umebaki kuwa imara kutokana na maboresho ya kisera yanayotekelezwa chini ya uongozi thabiti wa Rais John Pombe Joseph Magufuli.” (Makofi)

Mheshimiwa Spika, akasema hasa katika suala la ukusanyaji wa mapato na vita dhidi ya rushwa na ugaidi. Hao ndio wachumi wa dunia na wanafanya analysis kwa kutumia data ambazo ni credible, naomba tuendelee kuwaamini.

Mheshimiwa Spika, sishangazwi sana na maneno haya yaliyopo kwenye Hotuba hii ya Kambi Rasmi ya Upinzani. Naomba ninukuu pia maneno ya mwekezaji mmoja kutoka China ambaye alikuwa anatafuta taarifa za kwenda kuwekeza katika viwanda vya ngozi na viatu nchini Ethiopia. Mwekezaji huyu kabla hajaenda alikuwa akitafuta taarifa, na haya maneno yake alisema, akasema:-

“Ukiwa nje ya Afrika unapewa picha na baadhi ya watu wakiwemo Waafrika wenyewe kwamba Afrika ni sehemu ya vita, Afrika ni sehemu iliyojaa njaa, Afrika ni sehemu ya magonjwa na kusahau kuwa Afrika ina mchango mkubwa na fursa nyingi katika mchango wa dunia.” (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nanukuu maneno haya ili tu Watanzania watuelewe, kwamba tunachokifanya chini ya uongozi wa jemedari, Dkt. John Pombe Magufuli ni kuimarisha uchumi wa kila Mtanzania (inclusive growth for everyone in Tanzania) hiki ndicho tunachokifanya. Niwaombe Watanzania wapuuze taarifa zilizowasilishwa, niwaombe sana ndugu zangu, Mheshimiwa Bunge lako hili ni Tukufu, litendewe haki kwa kuletewa taarifa ambazo ni haki, taarifa ambazo ni halali, taarifa zenye vyanzo vyenye uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hili, naomba sasa niendelee na baadhi ya hoja nyingine. Hoja ya pili ambayo ninapenda kuielezea ilisemwa na niliitolea maelezo, yawezekana sikuelewa vizuri; ilikuwa ni kuhusu Serikali kutoa maelezo kuhusu utekelezaji wa ahadi ya shilingi milioni hamsini.

Mheshimiwa Spika, wewe umeshuhudia Waheshimiwa Wabunge wakiongea kwa uchungu, wengine kwa kejeli ambazo sio nzuri na hili pia limeandikwa kwa kejeli kubwa sana katika Hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani katika Wizara ya Fedha na Mipango.

Naomba nikumbushe, wakati tuna-conclude Bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango nilisema fedha kwa mwaka wa fedha 2016/2017 zilitengwa shilingi bilioni 59.5, na mwaka huu tumetenga shilingi bilioni 60 chini ya Fungu 21 - Wizara ya Fedha na Mipango. Fedha zimetengwa na hazina wasiwasi kwamba hazipo, zipo fedha hizi. Nikasema kwamba tunachokifanya sasa ni kuhakikisha tunasoma mfumo mzima, tunajifunza kutokana na makosa yaliyotendeka huko nyuma ili tuhakikishe fedha hizi za walipa kodi wa Tanzania zinakuwa na matokeo chanya katika Taifa letu na zinaweza kutekeleza kile ambacho kimesababisha Mheshimiwa Rais aweze kuahidi ahadi hii ya shilingi milioni hamsini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, yapo maswali ambayo tunajaribu kujiuliza kama wataalam wa uchumi, kwamba hivi governance ya hii shilingi milioni hamsini ikoje katika kila kijiji? Hivi tunaposema tunapeleka, tunapeleka shilingi milioni hamsini hizi katika mfumo upi? Tunajiuliza ni njia gani bora tunaweza kumpatia pesa Mtanzania huyu aliyeko kijijini kwangu kule Kalamba. Tunajiuliza, je, baada ya kutambua kijiji kinahitaji kiasi hiki tunawezaje sasa kujua nani anapata nini na kwa kiasi gani na anakwenda kutekeleza mradi gani? Tunaweza kujiuliza na kujibu maswali, je, ni mfumo gani tunataka kuutumia sasa ili kurejesha fedha hizi? Tukumbuke nilisema hapa kwamba fedha hizi si zawadi, fedha hizi ni mkopo. Fedha hizi zinatakiwa zipelekwe zikaimarishe uchumi na hatimaye tuhakikishe zinazunguka kwa Watanzania wote na kila Mtanzania anafaidika na pesa hii na mwisho wa siku pesa hizi zinarudi ndani ya Serikali yetu tukiwa tumeimarisha uchumi wa watu wetu.

Mheshimiwa Spika, naomba niseme kwamba mpaka tulipofika tupo hatua nzuri sana, na pesa kama nilivyosema shilingi bilioni 59.5 zipo, shilingi bilioni 60 tumetenga kwenye bajeti yetu ya mwaka huu, zote tutazipeleka kama ambavyo tuliahidi. Sasa hivi tumefika hatua nzuri, tayari Waraka wa Baraza la Mawaziri umeandaliwa kuhusu utaratibu na maeneo pamoja na mfumo utakaotumika katika kutekeleza programu hii ya uwezeshaji wananchi wetu kiuchumi. Niwaambie tu Waheshimiwa Wabunge kwamba hii ni ahadi ya Mheshimiwa Rais na tumeona kwa pamoja, hakuna ahadi anayoahidi akashindwa kuitekeleza, anatekeleza ahadi zake zote na hili atalitekeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niende kwenye hoja nyingine ambayo imesemwa sana kwamba Serikali inaona kuwa na utaratibu wa kukopa zaidi katika soko la ndani, hali hii kiuchumi si nzuri kwa kuwa taasisi za fedha zinakimbilia kuikopesha Serikali zaidi kuliko sekta binafsi. Katika hili tunafahamu zipo instruments mbalimbali zinatumika kuhakikisha Serikali inakopa na inakopa kwa vigezo, inakopa ikiwa na ukomo kwamba inakopa kiasi gani ili isiathiri utendaji wa sekta binafsi ndani ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama Wizara ya Fedha na Mipango tunafahamu sekta binafsi ndiyo engine ya uchumi, hatuwezi Serikali kufanya kitu chochote kinyume na sekta binafsi. Tunachukua tahadhari ya kutosha katika kulifanya hili na Serikali, kama nilivyosema, imeweka ukomo wa kukopa ndani usiozidi asilimia 1.5 ya Pato la Taifa kwa mwaka ili kuzipa nafasi benki za biashara kuendelea kukopa mikopo kwenye sekta binafsi ambayo ndiyo engine ya uchumi wetu kama nilivyosema. Kwa mwaka huu tumeona kwamba tupunguze kiwango cha kukopa kutoka ndani na mwaka huu tunakopa asilimia moja tu ya Pato la Taifa ili kuipa nafasi sekta binafsi kuchukua mikopo ndani ya benki zetu. (Makofi)

Jambo lingine ambalo limesemewa sana; nililijibu lakini naona nalo halikukaa vizuri au Waheshimiwa Wabunge hawakunielewa ilikuwa ni mikopo kutoka mifuko ya hifadhi ya jamii, kwamba Serikali imekuwa na tabia ya kukopa fedha kutoka Mifuko ya Jamii bila kuzirudisha kwa wakati, nini mpango wa Serikali wa kulipa madeni hayo?

Mheshimiwa Spika, naomba niseme kama nilivyosema kwenye jibu la hoja iliyopita, kukopa ndani ya nchi na hasa kwa mifuko yetu tunaipa nafasi pia mifuko yetu kupata fedha ambazo ni za uhakika. Hata hivyo, katika kulipa madeni haya naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge kwamba katika uchumi malipo ni jambo la muhimu lakini kuhakikisha unalipa nini ni jambo la muhimu zaidi, na hicho ndicho ambacho kimechelewesha malipo haya kwa Mifuko yetu ya Hifadhi ya Jamii. Tumefanya uhakiki; na ninaomba nitoe taarifa chache tu ya kuona ni kwa nini Serikali iliona ni muhimu kufanya uhakiki wa madeni haya, tuchukue mfano mmoja…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, muda umekuwa ni mchache sana lakini naomba niseme kwamba hoja hizi tutaziwasilisha kwa maandishi, na ninaomba niseme kwamba nia na lengo la Serikali yetu ni jema sana la kuhakikisha tunalipa mikopo yote, si ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii tu bali ya wakandarasi, wazabuni pamoja na watumishi. Tunafanya hivyo kuhakikisha Watanzania wanaweza kuimarisha uchumi wao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema haya, naomba nikushukuru sana kwa kunipa nafasi hii na ninaomba niseme naunga mkono hoja hii ya Serikali iliyowekwa Mezani na Waziri wa Fedha na Mipango ambayo imetuhakikishia Serikali yetu ina nia ya dhati ya kuhakikisha uchumi wa viwanda na uchumi wa kati unafika Tanzania kabla ya mwaka 2025. (Makofi)
Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa
Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili niseme machache katika bajeti hii. Kwanza nianze kwa kuwapongeza Waheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa kazi nzuri ambazo wanazifanya katika kutekeleza majukumu yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwaambia kwamba, tunatekeleza bajeti kulingana na mapato tunayoyapata. Pia lazima tufahamu kwamba katika uchumi tunafahamu mahitaji ni mengi kuliko rasilimali za kutekeleza mahitaji hayo. Kwa hiyo, napenda kusema kwamba uchumi unatufundisha pia kwamba unapokuwa unatenga bajeti, bajeti ni nini? Bajeti is an intelligent guess.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, unaweza kufikiria na ku-plan mipango yako, lakini unapoendelea kuitekeleza bajeti hiyo yapo mengine ya msingi yanayo-emerge na unaweza kuyatekeleza. Ndiyo maana hata Sheria ya Bajeti imetoa nafasi hiyo kwamba, yapo mengine yanayotokea na unaweza kuyatekeleza, lakini ukiwa ndani ya wigo ule wa bajeti ambayo imepitishwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti zilizotekelezwa hakuna jambo lolote lililotekelezwa nje ya bajeti ambayo tumeipitisha. Pia, nilikumbushe Bunge lako Tukufu kwamba, Sheria yetu ya Bajeti, Kifungu cha 41 na Kanuni ya 28 ya Sheria hii ya Bajeti, Namba 11 imempa nafasi Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango kuweza kuhamisha fedha kutoka katika Vote moja kwenda Vote nyingine katika utekelezaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Serikali yetu pia inawasilisha Bungeni Taarifa za kuhamisha matumizi hayo kutoka Vote moja kwenda Vote nyingine na nirudie kusema kwamba, hakuna sehemu ambako tumevuka pale ambapo bajeti yetu ya Serikali tulikuwa tumeipitisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee jambo moja ambalo limesemwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kwamba, ili kutekeleza majukumu yake wamependekeza, Tume ya Pamoja ya Fedha iweze kutekeleza majukumu yake chini ya Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Rais. Katika hili naomba niwaeleze Waheshimiwa Wabunge kwamba, ni muhimu tukaenda katika majukumu ya Tume hii ya Pamoja, majukumu yake ni yapi, ina-deal na mapato kutoka pande zote za Muungano na ndiyo maana ikawekwa chini ya Wizara ya Fedha na Mipango.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tume hii ya Pamoja imefanya ziara katika nchi mbalimbali zenye mfumo huu kama nchi yetu ya Muungano au Shirikisho, kote walikokwenda wamekwenda zaidi ya nchi tisa. Katika nchi hizi ni nchi tatu tu ambazo Tume hii ya Pamoja ya Fedha haiko chini ya Wizara ya Fedha na Mipango, kama ambavyo nimesema turejee kwenye majukumu ya Tume hii kabla hatujapendekeza jambo lingine ili kuweza kuhakikisha kwamba, Tume inafanya kazi kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia kulizungumzia jambo la corporate tax. Jambo la corporate tax lipo kisheria na linatekelezwa kwa Sheria yetu ya Mapato na naomba nilikumbushe Bunge lako Tukufu kwamba, kama alivyosema mchangiaji makampuni hulipa corporate tax kule yalikosajiliwa, lakini tunapoweza kutoa hoja zetu pia tufikirie na tuangalie manufaa ya hiki tunachokipendekeza.
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba nianze kwa kuwapongeza Waheshimiwa Mawaziri wa Elimu kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuhakikisha elimu yetu inakuwa bora na inaweza kwenda mbele.

Ninamshukuru pia Mheshimiwa Rais wetu kwa kuleta elimu bure kwa vitendo na sasa tunaona watoto wote wa Tanzania walioko mijini na vijijini waliokuwa wamekosa nafasi sasa wanaweza kuipata elimu. Nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie point chache ambazo ziliongelewa; kwanza ilikuwa ni kwamba Kamati iliomba Serikai iongeze bajeti ya Wizara ya Elimu hadi kufikia asilimia 10.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jambo hili naomba niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge kwamba tulipoanza mwanzo tulianza Wizara ya Afya tukasema ipewe asilimia 15, leo tunasema Wizara ya Elimu ipewe asilimia 10 na tutakuja Wizara ya Kilimo tutasema kutokana na mikataba mbalimbali ipewe asilimia 10. Tukijumlisha hizi asilimia tunapata asilimia 35 ya bajeti nzima inakwenda kwa Wizara tatu tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sikatai kwamba tumeingia mikataba hii, lakini niwaombe Waheshimiwa Wabunge kwamba tuiamini Serikali yetu, dhamira yake ni ya dhati, tunapotoa bajeti cealing tunaangalia vipaumbele vya Serikali yetu kwa pamoja, kila mmoja apate ili tuweze kuhakikisha kwamba tunaweza kufikisha maendeleo katika sekta zote ndani ya jamii yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge kwamba bajeti ya Wizara ya Elimu imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Kwa mfano, tukichukulia mwaka 2015/2016 bajeti ya sekta ya elimu ilikuwa shilingi bilioni 3870; mwaka 2016/2017 bajeti ya elimu ilipanda na kufika shilingi bilioni 4570 ambayo ni ongezeko la asilimia 22. Kwa hiyo, Serikali ina dhamira ya dhati ya kuhakikisha elimu yetu inapata bajeti ya kutosha na hii inaoneshwa na hizi jitihada ambazo zimekuwa zikiendelea. Tunafahamu umuhimu wa elimu katika maendeleo ya Taifa letu na wananchi wetu kwa ujumla na Serikali yetu ni sikivu, itakuwa inaongeza bajeti ya Wizara ya Elimu pindi uchumi wa Taifa letu unapoimarika na pato la Taifa letu linapokuwa limekaa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili napenda niseme Kamati yetu pia ilipendekeza kwamba iongezwe bajeti katika Bodi ya Mikopo. Naomba kuliambia Bunge lako Tukufu kama nilivyosema mwanzo, azma ya Serikali ni kuhakikisha elimu yetu inakaa vizuri, watoto wetu wanapata elimu tena elimu ambayo ni nzuri, elimu ambayo wananchi wetu wataweza kuifurahia matunda yake. Katika hili naomba nilikumbushe Bunge lako Tukufu kwamba pia katika Bodi ya Mikopo tunafahamu mwaka huu tumeleta bajeti kama ilivyokuwa mwaka jana ya shilingi bilioni 427.55, lakini tusisahau kwamba Bunge letu hili lilipitisha mwaka jana kwamba Wizara yetu ya Elimu pamoja na Wizara ya Fedha tuhakikishe kwamba tunakusanya mikopo ile ambayo walikopeshwa wanafunzi wetu na sasa wapo makazini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuliambia Bunge lako Tukufu kwamba kwa mwezi mmoja sasa tuna uwezo wa kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 13 na pesa zote hizi zinazokusanywa tukizidisha kwa mwaka mzima ni zaidi ya shilingi bilioni 150. Serikali yetu kwa kujua umuhimu wa elimu, pesa zote hizi tumesema ziwe ni Revolving Fund waendelee kukopeshwa wanafunzi wetu wa elimu ya juu. Kwa hiyo, tutaona kwa mwaka mmoja Serikali yetu imeongeza shilingi bilioni 150 kwa Bodi ya Mikopo. Hiki ni kiwango kikubwa na tunayo imani kuwa wanafunzi wetu watazweza kukopeshwa mikopo hii na wataweza kupata elimu kuendelea kuonesha ithibati ya Serikali yetu katika kufikisha elimu iliyo sahihi na kila mwananchi ambaye ana qualify kupata mikopo hii aweze kupata mikopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia kulisemea jambo moja ambalo limesemwa ni kodi nyingi zilizopo katika sekta ya elimu. Tumewaona wenzetu ambao wana shule binafsi wakilisemea kwa kiwango kikubwa. Napenda kuliambia Bunge lako Tukufu kwamba, kodi hizi zilipitishwa na Bunge lako Tukufu. Tukiangalia Sheria ya Kodi ya Mapato, imeletwa hapa tumeipitisha na inatambua kabisa kwa wale ambao hawafanyi elimu kama ni biashara wanapewa msamaha wa kodi nyingi ambazo ziko ndani ya sheria hii, lakini kwa mtu ambaye anafanya biashara ya elimu, anatoa huduma sawa, lakini anatengeneza faida, hivi kweli Waheshimiwa Wabunge tunaweza kuliachia hili kwamba tuwasemehe tu, tuangalie vizuri, tulipitisha sheria hii wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwapa mfano mmoja, hakuna asiyetambua ada zinazotozwa na International School of Tanganyika, lakini katika shule zilizokuwa zikipata msamaha wa kodi ni shule hii. Hivi ndani ya shule hii, kuna mtoto wa maskini nani anayeweza kusoma katika shule hii? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tufikirie kwa mapana tunahitaji kuongeza bajeti yetu ya Wizara ya Elimu, hapo hapo tunataka tupunguze vyanzo vya mapato. Tuwe makini katika mapendekezo yetu tunayoyaleta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya ninakushukuru kwa kunipatia nafasi kusema haya machache.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema, aliyeniwezesha siku ya leo kufika salama na kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu kwa ajili ya kuchangia hoja iliyowasilishwa jana na Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, napenda niwatakie Ramadhani njema na saumu zenye kukubaliwa wale wote wanaofunga mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema naomba sasa nichangie hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango katika baadhi ya hoja zilizopendekezwa na kuchangiwa na Waheshimiwa Wabunge katika Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya kwanza ambayo napenda kuitolea ufafanuzi ni hoja iliyoletwa na Kamati yetu ya Bajeti nayo ilikuwa inapendekeza kwamba ni muhimu kitengo cha kusimamia Deni la Taifa kufanya tathmini ya ulipaji wa deni la Taifa kwa kuzingatia mapato ya ndani badala ya kutumia vigezo vingine kwa lengo la kuifanya Serikali ikope zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hoja hii napenda kusema kwamba, jambo la msingi ambalo tunatakiwa kujiuliza, ni kwa nini tunakopa? Nim-quote mwanafalsafa mmoja alisema; “What matters is not how much you have borrowed, but for what you have borrowed.” Kwa hiyo, hilo napenda tuliseme vizuri kabisa kwamba kinacho-matter zaidi siyo kiwango gani umekopa, lakini umekopa kufanyia nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili napenda kuliambia Bunge lako Tukufu kwamba deni ambalo tunaendelea kulilipa kama Serikali, Serikali yetu ilikopa kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ili kufungua fursa za kiuchumi kwa wananchi wetu na Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi sote ni mashahidi, miundombinu ya Taifa letu inaelekea kuwa mizuri, sasa tunaona Taifa letu limefunguka kwa kiwango kikubwa, ni rahisi sasa kusafiri kutoka mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine bila tatizo lolote. Ni rahisi kusafirisha bidhaa zinazotoka Sumbawanga kufika Dar es Salaam kwa muda wa siku moja au siku moja na nusu. Hii yote ni miradi iliyotekelezwa kupitia mikopo iliyokopwa na Serikali yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, katika hili tunajifunza kwamba uchumi wa Taifa letu unafunguka, ajira zinaongezeka katika Sekta za Kilimo, Sekta za Usafirishaji; na hii ni muhimu sana tuweze kuelewa tunapoliongelea deni letu la Taifa. Katika hili, wachumi wanasema, bottleneck inflation inaondoka kwa sababu sasa bidhaa inayozalishwa kutoka sehemu moja inaweza kusafirishwa na kufika sehemu nyingine ambako bidhaa hizo hazipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiashiria kilichopendekezwa na Kamati yetu ya Bajeti ni sahihi, kinatumika katika kupima kiwango cha uhimilivu wa deni letu la Taifa. Vile vile kuna viashiria viwili vinavyotumika na hiki kilichosemwa ni kimojawapo kati ya hivyo. Kiashiria cha kwanza ni kiashiria ambacho kinapima uwezo wa Taifa letu kuendelea kukopa (solvency indicators). Katika solvency indicators kuna viashiria vidogo vitatu, cha kwanza ni thamani ya sasa ya jumla ya Deni la Taifa kwa Pato la Taifa letu (present values to total public debt) ambayo nayo inaonekana bado tuko vizuri tunaweza kuendelea kukopa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, indicator ya pili ni thamani ya sasa ya deni la nje pekee kwa Pato la Taifa (present value to external debt). Nayo pia tupo katika level nzuri, hatujafika hata nusu ya viashiria ambavyo vimewekwa. Kiashiria kilichopendekezwa na Kamati yetu ya Bajeti ni hiki kiashiria kidogo cha tatu ambacho ni thamani ya sasa ya deni la nje kwa mapato ya ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili kwa sasa hivi tuko asilimia 145.3 ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 250. Kwa hiyo, kwa uhalisia kabisa, bado Taifa letu linaweza kuendelea kukopa kwa sababu viashiria vyote vitatu kwa ajili ya ukopaji vinaruhusu Taifa letu kuendelea kukopa. Katika hili, siyo kwenye kukopa tu, kiashiria cha pili kikubwa ni kiashiria kwa ajili ya uwezo wa Taifa lolote lile kulipa ambayo ni liquidity indicators.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika liquidity indicators kuna viashiria viwili vidogo, kiashiria cha kwanza ni ulipaji wa deni la nje kwa mapato ya ndani ambayo kwa sasa tupo katika asilimia 11.5 ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 20. Kwa hiyo, bado tuna uwezo wa kulipa madeni yetu kama Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiashiria kidogo cha pili, ni ulipaji wa deni la nje kwa kutumia mauzo ya bidhaa nje ambapo Taifa letu tuko katika asilimia 7.8 ukilinganisha na ukomo wa asilimia 20. Kwa hiyo, viashiria vyote vya kukopa na vya kulipa vinaonesha bado Taifa letu la Tanzania tuna uwezo wa kukopa na tuna uwezo wa kulipa bila tatizo lolote kabisa. Hiyo ilikuwa ni hoja ya kwanza ambayo nilipenda kuitolea ufafanuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya pili ambayo pia Waheshimiwa Wabunge wengi wameichangia inahusu hilo hilo Deni la Taifa lakini katika nyanja nyingine, ambapo walisema takwimu zinaonesha kuwa kiasi kikubwa cha mapato ya ndani kinakwenda kulipia Deni la Taifa na hivyo Serikali kushindwa kugharamia masuala mengine ya maendeleo, ukatolewa na mfano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili, napenda kuliambia Bunge lako Tukufu kwamba kama nilivyosema kwenye hoja ya kwanza, Serikali yetu hukopa kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo. Katika hili nilitegemea tupongezwe kwa sababu Serikali imeweza kulipa Deni la Taifa katika kipindi cha mwaka huu kwa kiwango kikubwa kwa kutumia mapato yetu ya ndani. Ndiyo ile niliyosema katika jibu la kwanza kuhusu liquidity indicators.

Kwa hiyo, tuna uwezo mzuri wa kuweza ku-service deni letu bila tatizo lolote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ulipaji wa Deni la Taifa ni wajibu wa kisheria kabisa na hatuwezi kukwepa kama nilivyosema mwanzo, tumekopa kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Tuliingia makubaliano pia ambayo ni ya ukopaji pamoja na umuhimu wa kulipia miradi iliyotekelezwa miaka ya nyuma wakati mikopo hiyo ilipopokelewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ulipaji wa Deni la Taifa kwa kutumia mapato ya ndani ni mojawapo ya sifa kama nilivyosema ya kuonesha uwezo wa kukopa zaidi na uaminifu. Tena tumeweza kulipa kwa mapato yetu ya ndani. Kwa hiyo, tunaonesha kwamba pamoja na kwamba tuna miradi ya maendeleo, lakini kipaumbele chetu ni kulipa ili tuweze kutengeneza sifa nzuri ya Taifa letu. Sisi sote ni wanadamu, tunaishi katika uchumi wetu na tunafahamu ukiwa na deni lazima kulilipa na ndicho ambacho tumekifanya. Kwa uhakika kabisa na miradi yetu ya maendeleo tutaweza kuitekeleza baada ya kuonesha kwamba Taifa letu lina dhamira ya dhati ya kulipa madeni ambayo tumeyakopa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya tatu ambayo ningependa kuitolea ufafanuzi ilikuwa ni kuhusu Serikali kulipa shilingi bilioni 796 kati ya kiasi hicho inachodaiwa na wazabuni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati ya Bajeti nayo ilipendekeza pia kuwa kwamba tuweze kuwalipa Wazabuni, Wakandarasi pamoja na Watumishi wetu. Tumekuwa tukiliambia Bunge lako Tukufu, Serikali yetu ina lengo la dhati kabisa la kulipa wakandarasi, watumishi, wazabuni pamoja na watoa huduma wengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali yetu imekuwa ikilipa madeni haya kulingana na upatikanaji wa mapato kama ambavyo Sheria ya Bajeti Namba 11 kifungu 45(b) kinavyotuelekeza kufanya. Katika bajeti yetu ya mwaka huu wa fedha, tulitenga kiasi cha shilingi bilioni 626 ili kulipa madeni haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi kufikia mwezi Machi, kwa kuonesha dhamira njema ya Serikali yetu, tumeweza kulipa shilingi bilioni 796 zaidi hata ya bajeti tuliyotenga kuonesha kwamba dhamira ya Serikali ni njema, tunataka kulipa madeni haya, tunawathamini wazabuni wetu wanaohudumia Shule yetu, Magereza pamoja na Majeshi yetu mengine. Tumekuwa tukiwalipa mwezi hadi mwezi na kitakwimu tunalipunguza deni hili kulingana na mapato ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuzuia madeni haya yasiendelee kulimbikizwa, Wizara ilitoa angalizo na mwongozo kwa Maafisa Masuuli wote, kwamba hawaruhusiwi sasa kuendelea kulimbikiza madeni haya. Ninavyoongea, kwa mwaka huu wa fedha hakuna deni lolote ambalo tumelimbikiza. Kwa hiyo, hii ni nia njema na lengo bora kabisa la Serikali yetu kuhakikisha kwamba sasa tumejiandaa kuwalipa watu wetu wanaotoa huduma, tunafahamu wanavyosumbuka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwongozo huu uliotolewa na Mlipaji Mkuu wa Serikali, niseme tu kwa Maafisa Masuuli kwamba yeyote atakayekiuka mwongozo huu atakuwa amejifukuzisha kazi mwenyewe, kwa sababu Wizara imekuwa ikipeleka pesa kila mwezi kwa ajili ya malipo ya watoa huduma na wazabuni wetu.

Kwa hiyo, sisi kama moja ya Wajumbe wa Baraza la Madiwani katika Halmashauri tunazotoka, tuhakikishe pesa hizi zinapokuja kwenye Halmashauri zetu, zinatumika vizuri kulingana na maelekezo ambayo yanakuja na pesa hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya nne ambayo ningependa kuitolea ufafanuzi ni utekelezaji wa ahadi ya shilingi milioni 50 kwa kila kijiji, mtaa na shehia. Nimeona jana imesemwa kwa uchungu sana na Waheshimiwa Wabunge wameendelea kuisema. Napenda niseme kwamba hoja hii ilitolewa ufafanuzi pia wakati wa bajeti ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, lakini siyo vibaya mimi kama Naibu Waziri wa Fedha pia nikaweza kuisemea kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo imesemwa na Waheshimiwa Wabunge wengi kwenye hoja hii, ni kwamba kwa mwaka huu wa fedha Serikali yetu ilitenga shilingi bilioni 59.5 kwa ajili ya kuanza utekelezaji katika pilot areas. Wakati tunaendelea kutaka kutekeleza hili, zipo changamoto ambazo zimegundulika na hatuwezi kufanya makosa ambayo yaliwahi kufanyika huko nyuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ambazo zimeonekana ni pamoja na changamoto zilizolikumbuka Taifa letu kutokana na utekelezaji wa JK Fund. Hatutaki tena katika hizi milioni 50 kwa kila kijiji changamoto hii iweze kujirejea. Lazima tujifunze kutokana na makosa yetu na tuweze kuyarekebisha na kuhakikisha kila kinachotolewa kinawafikia walengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya pili ambayo imesababisha tuchelewe kutekeleza hili, ni wananchi kuwa na mtazamo hasi wa fedha hizi kwamba ni fedha za bure. Tunahitaji kufikisha elimu ya ujasiriamali kwa wananchi wetu, wapate elimu waweze kujua fedha hizi siyo za bure. Fedha hizi wanawezeshwa ili atakayewezeshwa leo iwe ni revolving fund aweze kuwezesha na wengine. Kwa hiyo, ni lazima tuandae wananchi wetu ili waweze kuzipokea na kuweza kuzifanyia kazi ambayo ilikusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tumegundua changamoto nyingine kuhusu vijiji vingi kuwa na vikundi ambavyo havijasajiliwa kisheria. Katika hili, vikundi havijasajiliwa kisheria na vipo vingine ambavyo vinasajiliwa specifically ili vipate fedha hii. Kiuchumi hiki ni kitu ambacho hakiwezekani, kwamba kinasajiliwa kikundi, kinasubiri pesa ili waanze utekelezaji, tunategemea nini? Ni kurudia makosa yale yale ambayo yalitokea huko nyuma na hili hatutaki tena liweze kutokea katika shilingi milioni 50 hizi, tunahitaji zionekane zina impact iliyokusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, Waheshimiwa Wabunge ni Madiwani viongozi katika Halmashauri zetu. Katika Halmashauri zetu, tunaona changamoto pia za utekelezaji wa asilimia tano za own source ya Halmashauri zetu kwenda kwa wanawake na asimilia tano kwenda kwa vijana; utekelezaji wake haujakaa vizuri. Kwa hiyo, baada ya kugundua haya yote, Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Ofisi ya Rais, (TAMISEMI) wanaandaa utaratibu mzuri na utakapokuwa umekamilika, fedha zote hizi zitatolewa katika vijiji vyote ambavyo Serikali yetu iliahidi na tutaweza kutekeleza kwa asilimia mia moja ndani ya miaka mitano ya utawala wa Mheshimiwa Rais wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja nyingine ambayo napenda kuitolea ufafanuzi ilikuwa ni ushauri kuhakikisha kuwa pensheni kwa wastaafu inatoka haraka na kwa wakati ili kupunguza usumbufu kwa wazee wetu. Ushauri huu kama Wizara tunaupokea, lakini ninavyofahamu, wastaafu wote wanaolipwa pensheni kupitia Wizara ya Fedha na Mipango, hata baadhi ya mifuko wanalipwa sambamba na mishahara ya wafanyakazi kila mwezi kwenye akaunti zao. Kwa hiyo, hakuna ucheleweshaji wowote ambao unatokea hasa kwenye pensheni ya kila mwezi kwa wastafu wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyowahi kuliambia Bunge lako Tukufu, tulikuwa tukiwalipa miezi mitatu mitatu, wakalalamika na sisi tukafanya analysis ya kutosha tukajiridhisha na sasa tunawalipa kila mwezi na wote wanapata pesa zao siku ambayo mishahara ya Serikali inalipwa. Niseme tu kwamba hili tunalichukua, kama ipo baadhi ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ambayo hailipi pensheni za kila mwezi kwa wakati, tutalifanyia kazi, tutalisimamia vizuri kuhakikisha wazee wetu wanaweza kupata pensheni yao kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, Kamati yetu pia ilishauri kwamba Serikali itimize ahadi yake ya kutoa non cash bond kwa ajili ya shilingi trilioni 2.6 ya mfuko wetu wa PSPF. Katika hili naomba kuliambia Bunge lako Tukufu kwamba nimekuwa nikijibu maswali na nikilieleza Bunge lako Tukufu kwamba Serikali ilikuwa inakamilisha tathmini na sasa tathmini imekamilika kwa ajili ya hii shilingi trilioni 2.6 ambalo ni deni la kabla ya mwaka 1999 pamoja na malipo pia ya mifuko mingine ambayo iligharamia miradi mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, dhamira ya Serikali yetu ni njema kabisa na sasa tuko kwenye hatua za mwisho kuhakikisha kwamba hii non cash bond inaweza kuandikwa na kuanza utekelezaji wake mara moja baada ya uhakiki na tathmini kuwa imekamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja nyingine ilitoka Kambi Rasmi ya Upinzani kwamba Serikali iielekeze Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kuwekeza kwenye miradi yenye faida na ya haraka hususan maeneo yanayochochea ukuaji wa uchumi kama vile reli na bandari. Katika hili naomba kuliambia Bunge lako Tukufu kwamba Serikali yetu kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii imetoa miongozo ambayo imeainisha maeneo ya uwekezaji kwa kuzingatia faida na tija kwa jamii. Mojawapo ya maeneo hayo ni kama ilivyopendekezwa na Kambi Rasmi ya Upinzani kwamba ni ujenzi wa miundombinu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, katika miongozo hiyo, Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii kwa kushirikiana na Benki Kuu inaweka ukomo wa uwekezaji kwa kuzingatia athari za uwekezaji na siyo faida ya haraka. Unaweza ukapata faida ya haraka halafu baadaye uwekezaji ule ukawa siyo endelevu. Hilo haliwezi kutekelezeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutatekeleza lile ambalo ni lenye faida endelevu kwa ajili ya mifuko hii kama tunavyojua wateja namba moja wa mifuko hii ambao ni wastaafu wetu ili waweze kuendelea kulipwa kwa wakati na muda unaotakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna hoja ililetwa kwamba Serikali iweze kutoa taarifa ya hesabu za robo mwaka za kila Mfuko wa Hifadhi ya Jamii. Katika miongozo hii niliyoitaja ina kipengele inayojielekeza mifuko hii kutoa taarifa kwa wateja wao kila robo mwaka. Kwa hiyo, hili lipo na linatekelezwa na mifuko yetu yote ya hifadhi ya jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kulikuwa na mapendekezo pia kwamba Ofisi ya Msajili wa Hazina ichukue usimamizi. Napenda kuliambia Bunge lako Tukufu kwamba Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii pamoja na Msajili wa Hazina na Benki Kuu hushirikiana katika kuisimamia mifuko hii ya hifadhi ya jamii. Kila mmoja ana majukumu yake na kila mmoja anatekeleza majukumu yake kama yalivyowekwa katika sheria na taratibu za nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunaomba watu hawa watatu; Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi Jamii, Msajili ya Hazina na Benki Kuu wote kwa pamoja waendelee kunya kazi yao kwa pamoja ili kuhakikisha mifuko hii ya hifadhi ya jamii inafanya kazi kwa faida, kwa ajili ya wateja wao ambao ni wastaafu wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na hoja kwamba kwa mujibu wa ripoti ya Benki Kuu mfumuko wa bei umepanda kutoka asilimia 5.4 mwezi Machi, 2016 mpaka asilimia 6.4 mwezi 2017.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuliambia Bunge lako Tukufu kwamba mfumuko wa bei uliongezeka kutoka asilimia 5.1 mwezi Aprili, 2016 hadi asilimia 6.4 mwezi Aprili, 2017 ni sahihi na hii sote tunafahamu sababu kuu inayosababisha mfumuko wa bei ni tatizo la bei ya chakula.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sote ni mashahidi, sababu kubwa iliyotokea ni hali mbaya ya hewa katika msimu wa kilimo wa mwaka 2015/2016 kulikosababisha upungufu wa mazao ya chakula katika masoko ndani ya nchi yetu. Hata hivyo, mfumuko wa jumla wa bei umeendelea kudhibitiwa na kubaki katika wigo wa tarakimu mmoja ambapo Serikali yetu imeahidi kwamba ni lazima tutahakikisha mfumuko wa bei unabaki katika tarakimu mmoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliambiwa tuseme na mikakati ambayo tunaitekeleza. Katika hili tunaendelea kuimarisha miundombinu ya masoko yetu na barabara kama nilivyosema mwanzo ili kuwezesha usafirishaji wa chakula kutoka eneo moja kwenda eneo lingine iwe ya urahisi na kuweza kuhakikisha kwamba upungufu wa chakula haupo kwenye maeneo ambayo hayakupata mvua za kutosha. Pia tunaendelea kutoa ruzuku ya pembejeo, kuimarisha huduma za ugani na uimarishaji wa miundombinu ya umwagiliaji ili kupunguza utegemezi wa mvua katika kilimo chetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunaendelea kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na kuimarisha upatikanaji wake katika masoko yetu. Serikali yetu, ni wiki mbili tu zilizopita imeweza kutoa chakula kupeleka katika zile Halmashauri zilizoathirika zaidi na uhaba wa mvua na hii tumepeleka katika lengo hili hili la kuhakikisha stabilization ya bei ya chakula ili kuhakikisha kwamba mfumuko wa bei hauvuki ile digit moja kama nilivyosema mwanzo.

Hoja nyingine zilitoka kwa Waheshimiwa Wabunge mbalimbali, nayo ilikuwa ni kuhusu Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi kuongezewa bajeti pamoja na kuha…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumalizia kwa kusema kwamba nawashukuru Waheshimiwa Wabunge wote waliotoa hoja madhubuti na mijadala mizuri yenye tija kwa ajili ya uboreshaji wa bajeti yetu ya Wizara ya Fedha na Mipango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumalizia kwa kusema, naunga mkono hoja, hoja iliyowekwa mezani na Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango, ahsante sana.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyetuwezesha kufika siku hii ya tano ya mjadala huu muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, napenda na mimi nimshukuru Mheshimiwa Rais wetu kwa kuendelea kuniamini na kuniacha katika nafasi hii ya Naibu Waziri wa Fedha na Mipango ili niweze kuendelea kumsaidia Mheshimiwa Waziri pamoja na yeye Mheshimiwa Rais wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia nikushukuru wewe kaka yangu Job Ndugai kwa kazi nzuri ambayo unaendelea kuifanya ya kuendesha Bunge letu Tukufu. Kwa kweli hongera sana kaka yangu, Mwenyezi Mungu azidi kukubariki ili tuweze kuifanya kazi hii tuliyoaminiwa na Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia niwapongeze Waheshimiwa Wabunge wa Bunge lako Tukufu kwa michango yao mizuri ambayo wametupatia sisi kama Wizara ya Fedha ili kuboresha Mapendekezo ya Mpango na tunapokuja mwezi wa Machi/Aprili na Mpango kamili tuweze kuja na Mpango ambao upo imara. Ninaamini wote kwa pamoja wametimiza wajibu wao Kikatiba wa nini walitakiwa kufanya na niwapongeze sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Wizara tumeyachukua yote, mimi na Mheshimiwa Waziri hatuwezi kujibu michango yote ya Wabunge zaidi ya 100 waliochangia kwa siku 5. Tutazungumzia machache ili tuweze kuendelea mbele kwenda kuandaa Mpango wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa uniruhusu nianze kuchangia hoja hii iliyowekwa Mezani na Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango, kaka yangu, Mheshimiwa Philip Isdor Mpango. Nianze kwa kukupongeza Mheshimiwa Waziri wa Fedha, kazi yako ni njema sana, kazi yako ni nzuri na imeonekana ndiyo maana Mheshimiwa Rais ameendelea kukuamini, hongera sana kaka yangu, simama hivyo hivyo. (Makofi)

Sisi watumishi tulio chini yako wewe ndani ya Wizara ya Fedha na Mipango tunajivunia kufanya kazi na wewe. Kwa wale ambao walikuwa hawajui uchumi sasa wanaufahamu uchumi ndani ya Wizara ya Fedha, nikupongeze sana Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya kwanza ambayo napenda kuitolea ufafanuzi ni hoja ambayo ilisema Serikali ione umuhimu wa kufanya malipo ya wakandarasi ambao wametekeleza miradi mbalimbali ndani ya Taifa letu. Serikali yetu ya Awamu ya Tano inatambua sana umuhimu wa kazi zinazofanywa na wakandarasi, lakini pia umuhimu wa kuwalipa malipo yao kwa muda mwafaka ili waweze kuendelea kufanya kazi zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2016/2017 Serikali imeweza kufanya malipo ya shilingi bilioni 3,358.89 kwa ajili ya wakandarasi, kati ya hizo, shilingi bilioni 1,321.47 zililipwa kama madeni ya wakandarasi waliojenga barabara zetu. Tunalipa lakini la muhimu kama ambavyo tumeendelea kusisitiza lazima uhakiki ufanywe ili tujiridhishe nini tunalipa kama Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya kiasi hicho nilichotaja, shilingi bilioni 1,161.32 kililipwa kwa ajili ya Mfuko wa Reli. Kama ambavyo Serikali yetu imedhamiria kuboresha miundombinu ndani ya Taifa letu na tumeanza kulipa, shilingi bilioni 204.90 zililipwa kwa ajili ya Mfuko wa Maji kwa wakandarasi wetu ambao wamefanya kazi ndani ya Wizara ya Maji. Mwenyekiti hili ulilisema na Waheshimiwa Wabunge walilisema kwa wingi kwamba Mheshimiwa Waziri haangalii ni maswali yapi ambayo yakiulizwa wanasimama Waheshimiwa Wabunge wangapi. Sasa hili naomba kulidhihirishia Bunge lako Tukufu kwamba kama Serikali tumekuwa tukilipa na shilingi bilioni 204 zimelipwa kwa mwaka 2016/2017. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo pia limepigiwa kelele na kama Serikali tunaendelea kulipa na nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Nishati, amesema vizuri na ametoa order nzuri sana na kwa mwaka 2016/2017 tulilipa shilingi bilioni 537.95 kwa ajili ya Mfuko wa Umeme Vijijini kuhakikisha vijiji vyetu vyote vinapatiwa umeme wa kutosha. Shilingi bilioni 133.24 tulilipa wakandarasi walioshughulika na miradi ya viwanja vya ndege. Tumesikia kelele nyingi zikipigwa kwa ajili ya shilingi bilioni 39 tu, hapana, tumelipa zaidi ya hizo kwa sababu zilikuwa ndani ya bajeti yetu ya mwaka husika. Kwa hiyo, nilidhihirishie Bunge lako Tukufu kwamba tumekuwa tukifanya malipo haya kwa ajili ya wakandarasi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika robo ya kwanza ya mwaka huu wa 2018/2019 tumelipa pia shilingi bilioni 562.29 kwa robo ya kwanza tu kwa wakandarasi wanaohusika na miradi mbalimbali ndani ya Serikali yetu. Kwa hiyo, nataka kusema kwamba dhamira ya Serikali yetu ni njema sana katika kuhakikisha kwamba watu wote wanaofanya kazi na Serikali yetu wanalipwa malipo yao yale wanayostahili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jambo hili, liliongelewa pia suala la Serikali kuchukua kodi ya majengo na ni kiasi gani ambacho tumeweza kukusanya kwa Mamlaka ya Mapato na hili aliliongelea vizuri sana kaka yangu Mheshimiwa Lubeleje.

Napenda kusema kwamba katika ukusanyaji wa Kodi ya Mapato niliambie Bunge lako Tukufu kwamba hatukunyang’anya Halmashauri zetu chanzo chake cha mapato. Nasema hivyo kwa sababu moja kubwa, dhamira ya Serikali ya kuchukua chanzo hiki ilikuwa ni kuongeza ufanisi wake ili sasa tuone ni jinsi gani tutaweza kuzirejesha pesa hizi katika Halmshauri zetu. Kwa mwaka 2016/2017 kwa Halmashauri 30 tu tumeweza kukusanya shilingi bilioni 34.09 ukilinganisha na shilingi bilioni 28 ambazo zilikusanywa na Halmashauri husika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisema dhamira ilikuwa ni kuongeza ufanisi na ufanisi tumeuongeza zaidi ya asilimia 20 lakini ukiangalia Mamlaka ya Mapato Tanzania ilianza kukusanya kodi hii mwezi Oktoba. Kwa hiyo, nilidhihirishie Bunge lako Tukufu kwamba kwa mwaka huu ambao tumeanza tangu mwezi Julai, mapato yetu kutoka Kodi ya Majengo yatakuwa ni mazuri sana. Mifumo yetu imekamilika, tumeanza kufanya kazi kwa umakini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ambalo lilikuwa linaulizwa kuhusu hili ni kwamba zimerejeshwa kiasi gani? Kama nilivyosema, dhamira kuu ilikuwa kuongeza ufanisi lakini kuhakikisha pesa hizi zinarejea kwa wananchi kwenda kufanya kazi. Baada ya kuzikusanya shilingi bilioni 34.09 pesa zote zilirejeshwa kulingana na bajeti za Halmashauri zetu kama Sheria yetu ya Fedha tuliyopitisha ilivyotuelekeza. Kwa hiyo, katika hili pia napenda kulieleza Bunge lako Tukufu kwamba hayo ndiyo mambo ambayo Serikali yetu ya Awamu ya Tano inayafanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja nyingine ambayo napenda kuitolea ufafanuzi ilikuwa ni kuhusu Serikali kutounga mkono sekta binafsi kwa kuwa Mapendekezo ya Mpango hayaongelei sekta hiyo wala kuainisha miradi ambayo Serikali itashirikiana na sekta binafsi katika kuitekeleza. Nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Viwanda amelielezea suala hili lakini pia niwaombe Waheshimiwa Wabunge ni muhimu wanapokuja kuchangia wawe wamepitia Mpango kuanzia page ya kwanza mpaka ya mwisho kuliko kuja kutuhumu bila kuwa na facts wakizifahamu. Hilo ni jambo la msingi sana. Nilichoki-note, watu wanasoma hotuba ya Mheshimiwa Waziri halafu wanakuja kuchangia Bungeni, hapana, hotuba ya Mheshimiwa Waziri ni summary ya kitabu kizima cha Mapendekezo ya Mpango, kwa hiyo wakipitie kwa umakini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema hivi? Nasema hivi kwa sababu ndani ya Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa mwaka 2018/2019 tumeainisha sekta binafsi itahusika na miradi ipi na katika awamu ipi. Tumeonesha waziwazi kabisa ukurasa wa 26 hadi 28 wa Mapendekezo ya Mpango, tumeonesha sekta binafsi ilivyoshirikiana na Serikali kutekeleza bajeti yetu ya 2017/2018. Tukatoka hapo, ukurasa wa 58 hadi 59 tukaainisha sasa kwa haya Mapendekezo ya Mpango tunayokwenda nayo, Mpango wetu unaokuja tunataka sekta binafsi ishiriki katika miradi ipi. Kwa hiyo, ndiyo maana nimesema wawe wanapitia kitabu kile tulichokileta Bungeni kwa ajili ya kujadili hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali yetu kwa kutambua umuhimu wa sekta binafsi katika kuleta maendeleo, hatukuishia tu kuainisha baadhi ya miradi lakini tumekwenda mbele na kuainisha na mikakati ni jinsi gani sekta binafsi na Serikali zitashirikiana ili tuweze kufanya kazi pamoja. Kwa hiyo, niombe sana hilo lifanyike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika hoja hiyo liliongelewa pia suala zima la kwa nini Serikali inawekeza kwenye miradi mikubwa ya maendeleo ikatolewa mfano mradi wa reli yetu ya kati (Standard Gauge Railway), ukatolewa mfano pia mradi wa Stiegler’s Gorge kwa ajili ya kuzalisha nishati ya umeme. Katika hili, naomba niseme jambo moja, ipo katika dunia nzima katika uchumi kwa nchi ambazo zimeendelea na sisi tunaendelea kuendelea, miradi hii ya miundombinu huwa ina sifa zake kuu tatu au nne ambazo ndizo zinazotoa mwelekeo kwamba ni nani atawekeza katika miradi ya miundombinu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe Waheshimiwa Wabunge hasa waliosema katika jambo hili, waende wakasome The Economics of Infrastructure Projects ili waweze kuelewa. Katika economics of infrastructure projects, Maprofesa wabobezi wa uchumi wanasema miradi yote ya miundombinu ambayo ni ya kimkakati duniani kote huwa ina hatua zake tatu. Hatua ya kwanza, huwa ni planning phase, hatua ya pili huwa ni construction na hatua ya tatu huwa ni operation. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika planning phase wabobezi wa uchumi wanasema miradi hii, naomba ku- quote, sifa moja katika planning phase ni nini kilichopo. Wanasema; many strategic infrastructure projects generate cash flows after many years, and the initial phase of this project is subject to high risks. Hii ina maana kwamba miradi yetu hii ya miundombinu ya kimkakati katika initial phase huwa ina risk kubwa sana na risks hizi hakuna kampuni yoyote ya binafsi ambayo iko tayari kuchukua risk hii katika initial phase ya miradi hii. Ndicho ambacho Serikali yetu imeona nini cha kufanya, lazima uoneshe nia wewe kama Serikali. Tunaihitaji miradi hii, tunahitaji Standard Gauge Railway, nani wa kuwekeza kwa sifa hizi, hayupo, except the government itself. Katika hili, tumeanza vizuri na imeanza Serikali yetu at the initial phase, the planning phase, we planned, sasa hivi tuko kwenye construction phase, tunafanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sifa ya pili ya miradi hii ya kimkakati, hasa ya miundombinu, wachumi wabobezi wanasema; even though the direct payoffs to an owner of an infrastructure project may cover its costs, the indirect externalities include beneficial for the economy as a whole. Nini maana yake? Inamaanisha kwamba sawa gharama zake ni kubwa na risks zake ni kubwa lakini miradi hii ya miundombinu ina faida nje ya ile sekta husika. Sasa hivi tulikuwa tukilalamika mahindi yanayozalishwa Sumbawanga hayawezi kusafiri, Serikali ime-invest kwenye miundombinu ya barabara sasa mahindi yetu yanaweza kusafiri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kaka yangu Mheshimiwa Lubeleje, amelalamika asubuhi kwamba mahindi kule kwake Mpwapwa hayapo. Kwa infrastructure zilizowekezwa na Serikali ndugu zangu wa Mpwapwa watapata mahindi kwa bei nafuu. Ndiyo maana ya Serikali kuwekeza katika infrastructure projects kubwa kama standard gauge katika initial phase na construction phase lazima Serikali iweke mkono wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, faida hizi ni kubwa kama nilivyosema. Kwa hiyo, la msingi, tunapokwenda kwenye operational phase ambapo sasa tayari miradi hii itaanza ku- generate revenue, cash flow inaingia, ndipo utakapoyaona makampuni binafsi yanaingia ili sasa kuweka mabehewa mazuri kwa ajili ya kusafirisha wananchi wetu na bidhaa zao. Hakuna kampuni au mfanyabiashara ambaye anakuja kuwekeza akijua ataishi yeye, atakufa, ataishi mtoto wake atakufa halafu awekeze mtaji, hilo halipo. Ni Serikali tu kwa sababu ya faida pana ya mradi husika kwenye uchumi, tunataka kujenga nini, uchumi wa viwanda, bila standard gauge hatuna uchumi wa viwanda. Ndiyo maana Serikali yetu imefanya hicho ambacho tumekifanya. Niwaombe Waheshimiwa Wabunge waendelee kutu-support ili tuweze kufanya kazi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala hilo, naungana kabisa asilimia 100 na kaka yangu, Mheshimiwa Bashe, aliposema economics is not a rocket science, we agree a hundred percent. Economics is not a rocket science but economics is a social science, you need to understand the agency you are dealing with, the behavioral economics, unafanya kazi na watu gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wifi yangu anasema nirudie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema naungana na Mheshimiwa Bashe aliposema economics is not a rocket science, that’s quite right lakini economics is a social science, unahitaji nini, unahitaji kuelewa the social actors you are dealing with. Unakaa chini unaendelea kusubiri Stiegler’s Gorge tangu alivyouanzisha Mheshimiwa Baba wa Taifa letu, Mwalimu Nyerere mpaka leo hakuna mwekezaji aliyejitokeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii Serikali imeanza kuwekeza Stiegler’s Gorge, tutakapoanza initial phase, the construction phase, operational phase, tutapata wawekezaji na uchumi wetu utaruka, that’s where now the rocket science will come, not at the initial phase. Niwaombe sana na mimi napenda kusema katika jambo hili sababu tunayo, nia tunayo, dhamira tunayo na uwezo tunao wa kuwekeza katika miradi mikubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema dhamira tunayo, sababu tunayo na uwezo tunao kwa sababu bado hatujafika asilimia zaidi ya 40 ya kukopa kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania. Tukope, tuwekeze ili Watanzania wafikiwe na maendeleo kule walipo. Kama tungekuwa tunakopa na kulipana posho tungeweza kuogopa, lakini tunakopa tunawekeza kwenye standard gauge tusafirishe bidhaa zetu. Tunakopa tuwekeze kwenye Stiegler’s Gorge tuzalishe umeme wa kutosha viwanda vya shemeji yangu, Mheshimiwa Mwijage, vifanye kazi, hatuna sababu ya kuogopa. Mheshimiwa Waziri wa Fedha, niko na wewe nitafanya kazi pamoja na wewe katika jambo hili, naamini hilo limeeleweka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niende kwenye hoja nyingine ambayo ilisemwa na Kambi Rasmi ya Upinzani, wakasema kwamba Serikali inafanya matumizi ya fedha ambazo hazikuidhinishwa na Bunge kinyume na utaratibu wa Sheria ya Fedha ya Matumizi ya Umma ya 2011. Napenda kwanza kukanusha hiki kilichosemwa na Watanzania wafahamu Serikali yao ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Chama cha Mapinduzi iko makini katika kutekeleza sheria zake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatujafanya jambo hilo, hata siku moja. Kitu ambacho wanasahau ndugu zetu hawa na kuja kudanganya wananchi, Mheshimiwa Waziri wa Fedha kapewa mamlaka ya kufanya uhamisho kutoka kifungu kimoja kwenda kwenye kifungu kingine, amepewa hiyo dhamana. Mheshimiwa Silinde, sikiliza nikufundishe uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri wa Fedha amepewa hayo mamlaka, anayo mamlaka, labda kama mnataka kumpoka lakini anayo hayo mamlaka. (Makofi)
Anafanya reallocation kutoka kifungu kimoja kwenda kifungu kingine ndani ya bajeti ya Serikali iliyopitishwa na Bunge lako.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, naomba nim-quote kaka yangu Jafo alivyosema wanaanza kupata kiwewe kwamba hawezi kutukamata wapi tunakwenda. Hii speed siyo ya kawaida hakuna wa kutusogelea ndugu zangu. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee kutoa darasa, Sheria ya Bajeti kifungu cha 48 kinampa mamlaka hiyo Waziri wa Fedha, kikisomwa pamoja na Kanuni zake, Kanuni ya 26(1) inamwelekeza Mheshimiwa Waziri wa Fedha nini cha kufanya. Kanuni ya 26(2) inamwelekeza aweze kufanya reallocation kwa kiwango gani, ndicho ambacho amekuwa akifanya Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Serikali yetu haijawahi kutumia fedha hizi nje ya bajeti iliyopitishwa na Bunge lako Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja hiyo inaunganishwa na naona ndicho wanachokitafuta lakini wanashindwa kufika, kwamba Serikali sasa ilete Bungeni adjustment ya bajeti kwa sababu wamesahau mamlaka haya ya Waziri. Naomba niseme jambo moja, nini maana ya bajeti ya nyongeza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhamisha kifungu hiki, kupeleka kifungu hiki siyo bajeti ya nyongeza ndugu zangu. Maana ya bajeti ya nyongeza ni kwamba Serikali ndani ya mwaka husika imekusanya mapato ya ziada ambayo hayakupitishwa na Bunge lako Tukufu na sasa inataka kuyafanyia matumizi. Hiyo ndiyo bajeti ya nyongeza ambayo Mheshimiwa Waziri wa Fedha kama anataka kutumia hayo mapato ya ziada tutalazimika kuja kwenye Bunge lako lakini kwa reallocation of funds between votes tunatakiwa tu tunapokuja hapa katika mid year review tu-report nini tumefanya, wala siyo kuleta bajeti ya ziada, hatuna bajeti ya ziada ndugu zangu. Tuko ndani ya bajeti iliyopitishwa na Bunge, ndani ya matumizi husika, tunatumia katika miradi yetu ya kipaumbele ndani ya Serikali yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vizuri tukawa na uelewa wa pamoja wa Sheria tunazopitisha sisi wenyewe halafu tunaposimama tuseme kwa Watanzania nini Serikali inafanya kwa niaba yao. Hilo ni jambo la msingi sana nilitaka kuliomba Bunge lako Tukufu tukubaliane na hiki ambacho kiko ndani ya Sheria iliyopitishwa na Bunge lako Tukufu na siyo kuja hapa na kuwadanganya Watanzania kwamba Mheshimiwa Rais anatoa order, hawezi kutoa order bila kujua hiyo pesa ipo na ilipitishwa na Bunge lako Tukufu. Hilo ni jambo la msingi sana katika utekelezaji wa shughuli za Serikali yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja nyingine ambayo iliongelewa kwa uchungu na kwa sauti kali ilikuwa ni kwamba Mipango ya Maendeleo ya mwaka 2016/2017, 2017/ 2018 na 2018/2019 yote inafanana. Nianze kwa kukuomba kwamba tuwe tunapitia vitabu hivi ili tuweze kujua lakini tusisahau msingi wa mipango hii mitatu na sasa tumebakisha mipango mingine miwili ni Mpango wa Pili wa Maendeleo wa miaka mitano. Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano ndiyo unatupa sisi base ya miradi ipi itekelezwe, kwa kiwango kipi na imeelekezwa kabisa. Ukichukua Mpango ule wa Miaka Mitano mimi nausoma vizuri sana na baada ya kusikia hili nilienda nikarudia kusoma mara mbili, mara tatu kuna nini? Nikagundua miradi mingi iliyopo kwenye Mpango wa wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano inatekelezwa kwa kipindi cha kuanzia miaka mitatu mpaka mitano, nini maana yake? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2016/2017 tulileta mradi ule ukiwa katika initial phase, mwaka 2017/2018 tumeleta mradi ule katika hatua zake za mwanzo za utekelezaji, mwaka 2018/2019 tunaleta sasa wapi tumefika baada ya kufika nusu ya utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano, miradi ni ile ile. Tofauti ya miradi hii inayoripotiwa ni utekelezaji wake hatua moja kwenda hatua nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tukianza ku-crash miradi ambayo ipo kwenye Mipango yetu ya Maendeleo ya mwaka mmoja tunawambia nini Watanzania? Hatukuwa makini kupitisha Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano kwa sababu hakuna sehemu Waziri wangu wa Fedha anaweza kwenda kuchukua mradi ambao hauko kwenye Mpango wa Pili wa Maendeleo.

Kwa hiyo, lazima tulifahamu hilo, twende tusome content of the document not what the Minister has presented in the Parliament, tutapata content na tutaelewa sasa wapi tupo na miaka mwili inayobaki nini tutafanya, je, tutaweza kutimiza kile tulichodhamiria? Hicho ndicho kilichopo, ukisoma tu bila kubeba jicho la planning ndani ya mipango hii utagundua hatuna utofauti ndani ya mipango yetu lakini ukiweka jicho la planning (the planners) utaona nini kilichopo ndani ya mipango yetu na wapi tunaelekea sasa katika kuhakikisha Tanzania ya viwanda tunaifikia kabla ya mwaka 2020. Dhamira yetu ni moja tu, kabla ya mwaka 2025 tunahitaji kuona Watanzania wenye kipato cha kati, kabla ya mwaka 2020 tunadhamiria kuona Watanzania wa Tanzania ya viwanda, hilo ndiyo jambo la msingi na ndiyo kazi tunayoifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya niseme jambo lingine ndogo ambalo liliongelewa katika ile ile hoja ya kupotosha Watanzania na nini Serikali yetu inafanya. Ilikuwa ni hoja kwamba Serikali imeendelea kudharau mamlaka ya Bunge lako Tukufu kwa kuacha kuleta sheria ya kusimamia mipango tunayopitisha ndani ya Bunge lako. Naomba kusema Serikali yetu ni sikivu sana hasa Serikali ya Chama cha Mapinduzi inayoongozwa na Mheshimiwa John Pombe Magufuli. Ni Serikali sikivu sana na hatuna ujanja huo wa kulidharau Bunge lako. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kusema kwamba, katika hili turejee kwenye Sheria ya Bajeti Na.11 ya mwaka 2015, kwa nini ilitungwa Sheria ya Bajeti, ni kusimamia mipango na bajeti tunayopitisha humu ndani. Tunahitaji sheria nyingine ipi na kufanya lipi? Pia kwa kila mwaka tuna Appropriation Act kwa ajili ya kusimamia matumizi ya Mpango tunaojadili leo, sasa tunahitaji sheria nyingine kufanya nini? Hatuhitaji sheria nyingine. Tunayo Sheria ya Bajeti na tunayo Appropriation Act ya kila siku. Sheria ya Bajeti inatuwezesha kubainisha kisheria majukumu na mipaka ya kiutendaji ya wahusika wakuu katika mchakato mzima wa kibajeti na kimpango. Sheria ya Bajeti inaweka uwiano kati ya mipango yetu, mapato yetu na matumizi yetu, tunahitaji sheria nyingine ya kufanya nini? Sheria ya Bajeti pia inaweza kutueleza na sisi tukatambua mzunguko wa kisheria wa kibajeti nini kilichopo, tungekaa tukaisoma vizuri wala tusingefika sehemu ya kuja na personal issues za kumtuhumu Waziri wa Fedha hata siku moja, turejee tu kwenye sheria tunazozipitisha sisi wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, naomba nikushukuru kwa kupata nafasi hii. Kama nilivyosema mwanzo yako mengi tutayafanyia kazi kwa umakini yote kwa pamoja na tutakuja na Mpango unaoakisi mapendekezo mazuri yaliyotolewa na Wabunge hasa wa Chama changu, Chama cha Mapinduzi walioongea mengi kwa ajili ya kuboresha Mpango wetu. Yale machache ya upande wa pili tutayachukua yale mazuri, yale mabaya naomba tuyaache humu humu tunapotoka tutoke na ushirikiano wetu na udugu wetu ili tuweze kutekeleza azma ya Serikali yetu na Hapa Kazi Tu itafanikiwa. Ahsante sana.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019; na Mapendekezo ya Serikali Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia fursa hii. Kabla sijaanza kuchangia hoja hii ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema aliyetujalia sote fursa hii ya kuwepo katika jengo lako hili Tukufu kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, pia baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu, kama ilivyo kawaida, napenda niwashukuru wazazi wangu wawili, Mzee Kijaji na Mke wake Mama Aziza Abdallah, nawashukuru sana kwa malezi yao kwangu yaliyonifikisha hapa nilipo siku hii ya leo.

Mheshimiwa Spika, napenda kumshukuru Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kwa kazi kubwa anayoifanya katika Taifa hili kwa kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo alizunguka Taifa hili kuinadi ilani hiyo. Nampongeza sana Mheshimiwa Rais wetu, hakika yuko makini anatekeleza kile ambacho aliwaahidi Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nampongeza pia, Mheshimiwa Mama yetu Mama Samia Suluhu Hassan, mama wa mfano kwa Taifa la Tanzania. Amekuwa ni mama yetu wa mfano, sisi wanawake tunajivuna kuwa na mama kama yeye, aendelee kupambana sisi wanawake wenzake tuko naye sambamba kuhakikisha tunayatenda kwa ajili ya watoto wa kitanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimshukuru na nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miongozo yake kwetu sisi tulio chini yake. Kwa kweli, ni kiongozi imara, ni kiongozi makini, busara zake zinatuwezesha kufika hapa tulipo siku hii ya leo.

Mheshimiwa Spika, naomba nikushukuru wewe pia, kaka yangu, Mheshimiwa Spika Job Yustino Ndugai, kwa uongozi wako imara kwa Bunge letu Tukufu na Waheshimiwa Wenyeviti na watendaji wote wa Bunge letu Tukufu. Naomba niseme kwamba, najivunia na najisikia faraja kuwa ni Mbunge kutoka moja ya Majimbo ya Dodoma ambako wewe ni mlezi wetu, najivunia sana Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba sasa nimshukuru Mheshimiwa Waziri wangu wa Fedha. Kwa mara ya kwanza niliposimama ndani ya Bunge hili, miaka miwili iliyopita, tukiwa tunawasilisha bajeti ya Serikali kama hivi, nilimwambia Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwamba, najivunia kufanya kazi chini yake. Miongozo yake, ushauri wake kwangu kwa kweli, ameweza kunifanya nisimame na kuwa ni mmoja wa Manaibu Waziri imara kabisa.

Mheshimiwa Spika, ulisema huwezi kujisifu mwenyewe, lakini naomba nijisifu mwenyewe na sijafika hapa ni kwa sababu, Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango ananipa nafasi ya kutenda haya ninayoyatenda. Nakushukuru sana Mheshimiwa Waziri na nakuombea kwa Mwenyezi Mungu azidi kukuimarisha, busara yako inatungoza sisi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia, niwapongeze sana watendaji wote ndani ya Wizara ya Fedha na Mipango wakiongozwa na Katibu Mkuu Mheshimiwa Dotto James. Niliwaeleza tulipoanza mchakato huu mwezi Machi nikawaambia, kama ni siku basi ilikuwa alfajiri ule mwezi wa Machi na leo hii tarehe 26 mwezi Juni basi ni saa 12.00 jioni. Naomba niwaambie siku yetu tumeikamilisha kwa ufanisi mkubwa, Watendaji wote wa Wizara ya Fedha najisikia faraja sana kufanya nanyi kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nianze kusema na kama ilivyo kawaida yangu naomba ni-site Aya mbili ndani ya Kitabu Kitukufu cha Mwenyezi Mungu, Quran na hii naomba iende kwa Mheshimiwa Rais wetu. Mheshimiwa Rais namwambia maneno haya ya Mwenyezi Mungu kutoka Surat Al-qalam, Aya ya 7 - 8; Mwenyezi Mungu anasema katika Aya ya 7 kwamba:

“Falaatutwiil-mukadhdhibina, waddu lautudihinu fayudihinuun” Mwenyezi Mungu anasema hivi, wala usiwatii wale wanaokadhibisha yale unayoyatenda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, namwambia Mheshimiwa Rais, asiwatii hata kidogo wale wanaokadhibisha jitihada zake anazozifanya kwa ajili ya wananchi wanyonge wa Tanzania. Dunia inaona, jamii inaona, Watanzania wanaona, Watanzania wanasema. Pia nimwambie Mheshimiwa Rais wangu kwamba, hii yote Aya ya pili niliyosema, Mwenyezi Mungu anasema, hao wanaokadhibisha wanatamani ulegeze japo kwa sekunde moja, ili waweze kutulia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, namwambia Mheshimiwa Rais aendelee kupambana. Sisi tunaona, Watanzania wanaona na Mwenyezi Mungu akipenda 2019 haya ninayoyasema yatadhihirika ndani ya Taifa la Tanzania. Kwa hiyo, Mheshimiwa Rais endelea kuchapa kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba sasa niseme machache katika hoja ambazo zimewekwa mezani na Waheshimiwa Wabunge wamesema. Hoja ya kwanza nayo imekuwa ni kuhusu Serikali ya Awamu ya Tano kuelekea kuziua halmashauri zetu. Jambo hili limesemwa kwa uchungu na msisitizo mkubwa na Waheshimiwa Wabunge ndani ya Bunge lako Tukufu. Naomba niseme yafuatayo:-

Mhesimiwa Spika, limesemwa jambo hili kwa kisingizio cha kwamba, Serikali ya Awamu ya Tano imechukua makusanyo ya property tax, lakini pia makusanyo ya ushuru wa mabango. Tulipitisha sheria ndani ya Bunge lako Tukufu na ndipo tulipoanza kutekeleza hili ambalo linalalamikiwa leo.

Mheshimiwa Spika, na sheria tuliyoipitisha, Sheria ya Fedha ya Mwaka 2017 ilituruhusu kukusanya mapato haya kwenye halmashauri zetu zote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Serikali siku zote ni sikivu na hasa Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi, ni Serikali sikivu; ilisikiliza maoni yaliyotolewa katika ripoti ya Kamati yako Maalum, maarufu kama Chenge One. Chenge One katika taarifa ile walisisitiza kwamba, Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato ya Tanzania ikusanye kodi ya majengo, ikusanye na kodi ya mabango na Serikali iko sikivu tukaanza kuyatenda haya.

Mheshimiwa Spika, kwa nini tumefanya hivyo? Tumefanya hivyo, ili kama ilivyoshauriwa ndani ya Chenge One ni kuimarisha makusanyo ya mapato hayo, ili tuweze kuyapeleka kwa Watanzania kwa Taifa zima. Nimshukuru sana na niwashukuru Waheshimiwa Mawaziri waliosema kabla yangu, wale waliokema ile kuligawa Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, nilisema mwaka jana wakati nachangia Bajeti ya Wizara ya Fedha kwamba, tuko kwenye hatari kubwa ya kuligawa Taifa hili vipandevipande, ule umimi tuuache ndugu zangu. Tunachokifanya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuyakusanya mapato haya na kuhakikisha tunayarejesha kwenye halmashauri zetu kulingana na bajeti za halmashauri husika na ndicho ambacho tumekuwa tukikifanya Serikali ya Awamu ya Tano.

Mheshimiwa Spika, niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge waelewe hiyo dhamira njema ya Serikali yetu, tumekuwa tukifanya hivyo, hakuna halmashauri ambayo imekosa bajeti ya maendeleo, wala bajeti ya matumizi ya kawaida katika utendaji wetu ndani ya miaka mitatu iliyopita. Katika kudhihirisha haya Serikali yetu imekuja na mpango wa kuziwezesha halmashauri zetu kuweza kuja na mipango imara, mipango mikakati kwa ajili ya kuongeza mapato ya halmashauri.

Mheshimiwa Spika, hili napenda kulisema, tuelewane jambo moja, Wakurugenzi wa Halmashauri ni watendaji wakuu wa halmashauri zetu. Hawa wanaitwa ni CEO wa halmashauri zetu zote na misingi ya mafanikio ya mtendaji yoyote wa taasisi haijawahi kubadilika kati ya sekta binafsi na sekta ya umma. Ndio maana sasa Serikali imekuja na mpango huu kwamba, tunataka kupima ubunifu wa watendaji wetu, ili tuweze kuwawezesha kuwapa pesa, ili waweze kutekeleza mipango ya maendeleo, lakini yenye tija kwa wananchi wanaowaongoza. Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge sisi ni madiwani katika halmashauri zetu.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Kaka yangu Jafo tulifanya kikao tarehe 14 Mei, pale Wizarani tukisaini mikataba ya shilingi bilioni 131.5 kwa ajili ya halmashauri zile zilizoonesha ubunifu wa kubuni miradi ya maendeleo itakayoleta tija kwa wananchi wao, itakayoleta tija kwa halmashauri zao kujiongezea kipato.

Mheshimiwa Spika, naomba niwasifu sana Wakuu wa Mikoa wafuatao: Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nawasifu Wakuu hawa wa Mikoa kwa sababu, wana-vision, wana ndoto ndani ya mikoa yao. Wamekaa na watendaji wao baada ya sisi kutoa mwongozo wa kuja na mikakati hii kwa ajili ya kuongeza mapato ya halmashauri, Wakurugenzi wao wakaja na maandiko mazuri ambayo yamepata fedha hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, juzi Jumamosi nilikuwa Mkoani Simiyu. Wengi wakanishangaa, unakwenda kuhitimisha bajeti kesho kutwa, umefikaje Simiyu leo? Nikawaambia niko Simiyu kwa sababu, ni utekelezaji wa bajeti tunayoipitisha. Nilikwenda Simiyu kuangalia viwanda vilivyoanzishwa ndani ya Mkoa wa Simiyu na Halmashauri za Wilaya ndani ya Mkoa wa Simiyu. Nikawa namuuliza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Maswa, nikamwambia baada ya kuanzisha kiwanda hiki cha chaki kwa mwaka mmoja unakusanya mapato kiasi gani?

Mheshimiwa Spika, akaniambia ndio wameanza, wanakusanya zaidi ya milioni 600 kwa mwaka kwa kiwanda hicho kimoja. Nikamwambia una sababu sasa wewe na Baraza lako la Madiwani la kwenda kusimama kusubiri mapato ya kusubiri mtu anayetoka kujisaidia chooni kwamba, unakusanya mapato? Akaniambia hana sababu kwa sababu, ana miradi ambayo inamuongezea mapato na hana sababu ya kulalamika hajapata mapato kutoka Serikali Kuu.

Mheshimiwa Spika, hili napenda lieleweke na liende kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri zote 185 kwamba, Serikali iko tayari. Mkoa wa Simiyu peke yake mikataba tuliyosaini juzi wamepata shilingi bilioni 8.2 kwa ajili ya viwanda vidogo vidogo na ndio maana nimekuwa
nikisema tatizo la Serikali ya Awamu ya Tano sio pesa, tatizo unataka pesa ukafanye nini. Hilo ni jambo la msingi sana, lazima tukae pamoja tuelewane kama viongozi, ili tujue ni nini tunakwenda kufanya na Watanzania tunaenda kuwapa nini.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo hili niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge hili la kulalamikia mapato haya yaliyokusanywa yamekusanywa yanakwenda wapi?Yamekusanywa halafu yanarejeshwa kwenye halmashauri kulingana na bajeti.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, ukiacha hiyo ya kurejeshewa hiyo tumekuja na mkakati wa kuongeza mapato ya halmashauri. Kwa nini tusikae na Wakurugenzi wetu tukaelekezana, wakaandaa maandiko, tukatekeleza, Serikali haijazuia kuanzisha viwanda vidogovidogo.

Mheshimiwa Spika, naomba sisi tuwe wa kwanza kutenda maono ya Mheshimiwa Rais, tuwe sisi ni wa kwanza kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi, iliyosema 2025 Tanzania itakuwa ni Tanzania ya viwanda. Mwaka 2025 Tanzania itakuwa ni Tanzania ya watu wenye kipato cha kati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hayawezekani haya kama tusipokuwa wabunifu sisi viongozi na tukawaelekeza wananchi wetu, tukaainisha fursa zilizomo ndani ya maeneo yetu katika kutenda ili kuja kuiona Tanzania ya viwanda na Tanzania ya uchumi wa pato la kati. Haya yanawezekana, mikoa niliyoitaja wameonesha dhamira hii kwa kuanza kutenda, wengine tuige ili tuweze kufanya kazi kwa pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hoja ya pili ambayo ningependa kuitolea ufafanuzi, naomba niziseme hizi mbili tu, najua muda sio rafiki, ilikuwa ni Serikali ya Awamu ya Tano kuvunja Katiba na Sheria kwa kukusanya pesa za Mifuko Maalum na kuziingiza kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali bila kuzipeleka kwenye matumizi yaliyokusudiwa.

Mheshimiwa Spika, naomba nirudie hili, hakuna Serikali inayoheshimu Katiba, Serikali inayoheshimu sheria zilizotungwa na Bunge lako kama Serikali ya Awamu ya Tano. Nasema haya kwa sababu tunaielewa Katiba, Ibara ya 135 (1) na (2), Ibara ya 136(2), Ibara ya 143(2)(a) na (b) tunaifahamu kama Wizara ya Fedha na tunaifahamu Sheria ya Bajeti iliyotungwa na Bunge lako Tukufu. Hatuko tayari kuvunja Katiba yetu wala kukiuka sheria zilizotungwa.

Mheshimiwa Spika, nasema haya kwa sababu kwanza mapato ya Serikali yako ya aina mbili, hayo yanayokusanywa kwenda Mfuko Mkuu wa Serikali ambayo yametajwa katika Katiba 135(1) na (2), ambayo hayo yakikusanywa kutoka kwenye Revenue Collection Account ya TRA moja kwa moja huenda katika Mfuko Mkuu wa Hazina yakisubiri kupangiwa matumizi ili yapelekwe yanakotakiwa. Aina ya pili ni haya yaliyotajwa 135(2) na 136(2) ambayo ni mapato yenye Mifuko Maalum, matumizi yake ni maalum.

Mheshimiwa Spika, naomba kuliambia Bunge lako Tukufu, tunailinda Katiba, tunatekeleza Sheria. Hakuna mapato yoyote kutoka kwenye vyanzo maalum yanayoingia katika Mfuko Mkuu wa Hazina. Mapato haya yakishakusanywa kutoka kwenye Petroleum Levy Deposit Collection Account yanakwenda moja kwa moja kwenye mifuko husika. Naomba kusema yafuatayo kwa data zifuatazo:-

Mheshimiwa Spika, Mfuko wetu wa Nishati Vijijini, mpaka kufikia tarehe 30 Mei, tulishakusanya shilingi bilioni 309.209. Nini tumepeleka kwenye Mfuko wa REA? Tumepeleka zaidi ya shilingi milioni 333.528 zaidi ya asilimia 108 ya tulichokikusanya kwenye kipindi hiki cha miezi 11. Kwa nini zimezidi hizi asilimia nane? Zimezidi kwa sababu huwa kuna lag period. Zinazokusanywa Juni, huwa zinakwenda kwenye REA Account mwezi Julai.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ndiyo maana mnaona hii 8% inayozidi. Ndiyo maana napenda kuliambia Bunge lako Tukufu kwamba tuko tayari, tuliapa kuilinda Katiba na kuisimamia Sheria. Hatuko tayari kuvunja Katiba wala Sheria.

Mheshimiwa Spika, huo ulikuwa ni Mfuko wa REA. Tukienda kwenye Mfuko wa Barabara, mpaka tarehe 30 Mei, 2018 tumekushanya zaidi ya shilingi milioni 740,655. Nini tumepeleka kwenye Mfuko wa Road Fund? Tulichokipeleka ni shilingi milioni 783,141 zaidi ya asilimia
100 imezidi 6%. Kwa hiyo, hakuna sehemu ambako fedha hizi za Mifuko Maalum zinakwenda kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina, hapana. Tutalinda sheria na pia tutaisimamia.

Mheshimiwa Spika, tukienda kwenye Mfuko wa Maendeleo ya Reli, mpaka tarehe 30 Mei, 2018 tumekusanya shilingi milioni 203,974 na tumepeleka shilingi milioni 221,971 zaidi ya asilimia 109.

Mheshimiwa Spika, najua ni kengele ya pili, yako mengi ya kusema, lakini nataka kusema haya yanayoonesha image ya Wizara ya Fedha kwamba tunavunja Katiba na Serikali yetu, nasema hapana, hatuvunji Katiba. Tuko tayari kufanya kazi kwa ubunifu wa hali ya juu, kuhakikisha Taifa hili linasimama kiuchumi, tunafikisha maendeleo kule kwa wananchi wetu.

Mheshimiwa Spika, kile nilichomwambia Mheshimiwa Rais wangu nilipoanza kusema hapa, naomba nimwambie Mheshimiwa Waziri wangu wa Fedha kwamba Falatutwii-l-mukadhdhibina, waddu Lautudihinu, fayudihinuun. Wala usigeuke nyuma, utageuka jiwe Mheshimiwa Waziri. Chapa kazi, tuko tayari kukusaidia kufanya kazi yako. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana na naunga mkono hoja.
Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kabla sijaanza kuchangia hoja iliyowekwa mezani na Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kuunga mkono hoja hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda kuanza kwa kumshukuru sana Mwenyezi Mungu aliyetuwezesha kufika siku hii muhimu sana kwa Taifa letu kwa Wizara yetu ya Fedha na Mipango. Pia nawashukuru sana viongozi wetu wakuu, Mheshimiwa Rais wetu kwa miongozo yake kwetu ambayo amekuwa akituongoza ili tuweze kuhakikisha kwamba Taifa letu linakuwa ni Taifa la kipato cha uchumi wa kati hata kabla ya mwaka 2025. Nampongeza sana Mheshimiwa Rais katika jambo hili, amesimama imara na tunaliona Taifa letu kweli linasogea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, namshukuru pia mama yetu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa miongozo yake kwetu, kwa ushauri wake kwetu na kututakia mema katika utekelezaji wa majukumu yetu. Pia namshukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu, kiongozi wetu wa shughuli za Serikali ndani ya Bunge letu tukufu, naye kwa miongozo yake, yote haya tunayatenda kwa pamoja, namshukuru sana. Kwa pamoja, niwatakie afya njema viongozi wetu wa Taifa.

Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Waziri wa Fedha na Mipango, Mheshimiwa Dkt. Philip Isdori Mpango kwa kuendelea kufanya kazi hii kwa moyo wake wote kwa kujitolea usiku na mchana. Hakika nasema na Mheshimiwa Waziri naomba nikwambie kwamba najivunia kufanya kazi nawe kama msaidizi wako. Usichoke kunipa miongozo yako, niko tayari kwa muda wowote kulitumikia Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote kwa mijadala ambayo ni yenye afya kabisa ndani ya Bunge lako tukufu. Hii yote haiwezekani, bali ni uongozi wako makini, uongozi wako hodari kabisa ndiyo unasababisha Bunge letu liendelee kuwa na afya. Nakupongeze sana kaka yangu kwa uongozi huu. Endelea kusimama imara na kwa pamoja tutalifikisha Taifa letu kule ambako dira yetu ya maendeleo inatuelekeza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba sasa nichangie baadhi ya hoja ambazo Waheshimiwa Wabunge wamezisema ndani ya Wizara yetu ya Fedha. Nianze na hoja ambayo ilikuwa ni kuhusu malipo ya madeni mbalimbali ambayo Serikali yetu inadaiwa na watoa huduma, watumishi wetu na wazabuni wetu.

Mheshimiwa Spika, nawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge katika hoja hii, wameisema vizuri sana. Nawashukuru kwa kipekee wale waliotuunga mkono kwenye zoezi zima la uhakiki kuhakikisha kwamba kile kinachoenda kulipwa kinalipwa kile ambacho Watanzania walipokea huduma. Nawapongeze sana Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Spika, naomba niseme kwamba, Serikali yetu iko committed kabisa kuhakikisha kwamba madai yote ambayo Serikali inadaiwa na Watanzania na wasiokuwa Watanzania yanalipwa. Nasema hivi kwa sababu, mwaka huu 2017/2018, bajeti kwa ajili ya kulipa madeni haya ilikuwa ni shilingi trilioni moja kamili ndani ya bajeti ambayo Bunge lako tukufu iliipitisha.

Mheshimiwa Spika, ninapoongea leo, tayari tumeshalipa zaidi ya bajeti iliyopitishwa na Bunge lako tukufu. Tulipitisha shilingi trilioni moja na leo tayari tumeshalipa shilingi 1,167,753,620,321. Hii ni dhamira njema ya Serikali yetu kuhakikisha kila kinachohakikiwa katika madeni tunayodaiwa kinalipwa kwa Watanzania na wasiokuwa Watanzania.

Mheshimiwa Spika, hii shilingi trilioni 1.167 ambayo tumeshalipa tayari imelipwa kwa akina nani? Maana imesemwa kwamba Serikali inadharau, walimu hawalipwi, hapana. Tumelipa madeni haya kwa watu wote. Kama tutakumbuka Waheshimiwa Wabunge, mwezi wa pili Serikali yetu ililipa madeni ambayo yameshahakikiwa kwa watumishi peke yao zaidi ya shilingi bilioni 43. Katika hizi shilingi bilioni 43 zililipwa kwa ajili ya watumishi 27,389. Kati ya watumishi 27,389 walimu walikuwa ni 15,919. Hii ni commitment ya hali ya juu sana kwamba yote tuliyoyahakiki, tuna uhakika nayo, yanalipwa kabisa kama inavyotakiwa. Walimu wetu tunawakumbuka, tunatambua mchango wao kwamba bila wao sisi sote tusingekuwa hapa tulipo.

Mheshimiwa Spika, madeni haya ambayo tunayalipa, tunalipa, kama nilivyoanza kusema, baada ya uhakiki kukamilika. Naomba hili liweze kueleweka. Katika hizi trilioni moja ambazo tumeshalipa tayari, ni madeni yaliyohakikiwa hadi Juni, 2016. Tulihakiki, kwa nini tunahakiki?

Mheshimiwa Spika, sisi sote ni Watanzania, tunafahamu tulikotoka, tumepigwa vya kutosha. Haikuwa ajabu kusikia mwalimu anaidai Serikali zaidi ya shilingi milioni 500. Unaweza ukajiuliza, haya ni madai ya nini kwa mtumishi mmoja wa umma kuidai Serikali? Anakwambia ni madai kwa ajili ya likizo yake. Ni likizo gani hiyo mtumishi wa umma ataidai Serikali zaidi ya shilingi milioni 500? Kwa hiyo, hili liweze kukaa sawa sawa na haya yote tunafanya kwa dhamira njema kama nilivyosema.

Mheshimiwa Spika, kifungu cha 10 cha Sheria ya Bajeti, namba 11 ya mwaka 2015 na kifungu cha 5 cha Sheria ya Fedha za Umma namba 6 ya mwaka 2001, pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2004 vinampa mamlaka Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango kusimamia matumizi ya fedha za Umma, ndicho kinachofanyika.

Mheshimiwa Spika, pia vifungu vya 12 na Kifungu cha 68 vya Sheria yetu ya Bajeti, namba 11 ya mwaka 2015 vinampa mamlaka Mlipaji Mkuu wa Serikali kusimamia matumizi bora ya fedha za umma kwa taasisi za umma, lakini pia kufanya marejeo ya mapato na matumizi ya taasisi za umma. Kwa hiyo, hiki tunachokifanya kinafanywa kwa msingi imara kabisa wa sheria, hakuna sheria yoyote inayovunjwa katika hili.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza, ni commitment ya hali ya juu ya Serikali yetu kuhakikisha kwamba madeni haya yote yanalipwa lakini baada ya uhakiki.

Mheshimiwa Spika, napenda kuliarifu pia, Bunge lako tukufu kwamba yapo madeni ambayo ni Juni, 2017. Madeni haya tunaendelea kuyahakiki. Tunataraji uhakiki wa madeni ya mpaka Juni, 2017 yafike mwisho wake, mwisho wa mwezi huu wa sita. Tutakapokuwa tumejiridhisha tayari sasa tutaanza kuyalipa. Kwa hiyo, hii ni sahihi na niwaombe sana watumishi wetu, Maafisa Masuhuli na watu wote walioihudumia Serikali yetu watusaidie sana kwenye zoezi hili.

Mheshimiwa Spika, tunapambana na changamoto kubwa, unakwenda sehemu unakuta hupati zile nyaraka halisi na Maafisa Masuhuli hawataki kushiriki. Watoa huduma ukiwaambia tunaomba nyaraka zako zile original ambazo unasema unaidai Serikali, hawataki kutupatia. Sasa tukibaki tu tunalalamika wakati tunatenda jambo hili kwa ajili ya dhamira njema hatutafika na tutaendelea kulalamika. Nawaomba sana watu wote wanaoidai Serikali yetu waweze kutoa nyaraka hizi.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa pia na malalamiko mengine kwenye jambo hili kwamba madeni yaliyolipwa ya watumishi mwezi wa pili, kama nilivyosema yalilipwa kwa kiwango kidogo.

Mheshimiwa Spika, madeni haya yaliyolipwa ndiyo yaliyogundulika ni halali kulingana na nyaraka zote zilizohitajika. Hatukatai yalikuwa submitted madeni ya shilingi bilioni 66.92, yaliyokuwa halali ni shilingi bilioni 43.39 na Serikali ikasema kwa yule ambaye anaona hajalipwa na ana nyaraka halali, azilete sisi tutazipokea, tuhakiki, tukijiridhisha na madeni yote haya ya shilingi bilioni 66 kama yatagundulika ni halali, basi Serikali yetu itaweza kuyalipa.

Mheshimiwa Spika, naomba pia niseme jambo ambalo limesemwa kwa kiwango kikubwa linalohusiana na malipo haya, kwamba, katika Wizara ambazo zinavunja sheria za nchi yetu ni Wizara ya Fedha na Mipango.

Mheshimiwa Spika, kwa masikitiko makubwa tumelisikiliza, lakini tunapenda kuwaambia kwa ujasiri wa hali ya juu, katika Wizara tunazofuata sheria ni Wizara ya Fedha na Mipango. Hatuko tayari kuona tunavunja aidha, Katiba yetu wala sheria zetu ambazo Bunge lako tukufu limetunga. Nasema haya kwa sababu yalisemwa pia kwamba pesa za Mifuko Maalum zinakusanywa na zinawekwa kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali na kazi hazifanyiki.

Mheshimiwa Spika, tunasema kwa ujasiri mkubwa Wizara ya Fedha kwamba jambo hili halipo. Kwa sababu katika mtiririko wa makusanyo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania zipo aina mbili za makusanyo. Makusanyo ambayo siyo ya mifuko maalum na makusanyo ya mifuko maalum. Makusanyo ambayo siyo ya mifuko maalum yanaingia katika Revenue Collection Deposit Account ya Mamlaka ya Mapato Tanzania. Pesa hizi zikishaingia hapa, ndiyo zinakwenda moja kwa moja kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali, lakini vyanzo vyenye mapato maalum vinaingia katika mfuko maalum ambao huu unakusanya pesa zote hizi zenye vyanzo maalum inaitwa ni Fuel Levy Collection Deposit Account na jina lake linajieleza.

Mheshimiwa Spika, katika hizo, ziko fedha za Mfuko wa Reli, zina akaunti yake. Zikishaingia katika Deposit Account zinakwenda kwenye mfuko specific. Fedha za Mfuko wa Barabara zikishaingia kwenye Deposit Account hiyo zinakwenda kwenye Account ya Mfuko wa Barabara na fedha za Mfuko wa Umeme Vijijini zikishaingia katika Deposit Account hiyo zinakwenda kwenye Account ya REA.

Mheshimiwa Spika, nini kinafanyika na inaonekana kwamba, tunazuia fedha hizi kama Wizara ya Fedha? Wakati tunajadili bajeti za Wizara mbalimbali, tulisikia Waheshimiwa Wabunge wakilalamika ndani ya Bunge lako tukufu kwamba fedha nyingi za maji zimepelekwa, lakini ukifuatilia miradi ya maji, hakuna miradi inayofanya kazi. Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Jemedari wetu, Dkt. John Pombe Magufuli, tumesema hili hatutaki litokee. Hatutaki liweze kutokea. Tutafuatilia kuanzia mwanzo wa miradi hiyo, tutajiridhisha na mchakato mzima mpaka tutakapopeleka pesa. Watakapoanza kutekeleza miradi hiyo, kama Wizara tuliopewa mamlaka ya kufuatilia makusanyo na matumizi ya fedha za Serikali, tutakwenda kwenye miradi kukagua na kujiridhisha kama kweli pesa hiyo inafanya kazi hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ndipo tulipo na siku zote Waheshimiwa Wabunge niwaambie, kwenye transformation yako machungu ndani yake, lakini machungu yenye dhamira ya dhati ya kwamba tukimaliza hapa, tutakwenda kwa mfumo sahihi wa kuhakikisha kwamba sasa Taifa linakimbia na pesa za Watanzania masikini zinatumika kama ilivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hiki tukifanyacho ni jambo ambalo limesemwa hata kwenye vitabu vitukufu vya dini zetu. Kwa wale Waislamu naomba mwende kwenye Surat Israa, naomba msome. Mheshimiwa Khatib kwa hili naomba nisikilize, katika Surat Israa nenda aya ya 27, aya ya 28, aya ya 30 inasema nini katika mapato na matumizi ya pesa za mtu yeyote na za Serikali yetu. Ndicho tunachokifanya.

Mheshimiwa Spika, mwisho wa aya hii ya 30 ya Surat Israa, ndugu zangu, Mwenyezi Mungu anatuambia kwamba hicho mnachokifanya muwe na hofu kwa Mungu kwa sababu wanaofanya ubadhirifu hao ni marafiki wa shetani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Tano haitaki kuwa marafiki wa shetani. Serikali ya Awamu ya Tano inataka kutenda kwa ajili ya Mungu. Tutafanya kazi hiyo, niwaombe sana tushirikiane kuhakikisha hili linafanya kazi na Taifa letu linapata maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, naona na Mheshimiwa Khatib kapiga makofi, naamini hiyo, imeingia vizuri. Anasema imekuja vizuri kwa hiyo, ndiyo maana kapiga makofi. Tunafanya hayo kwa utukufu wa Mungu aliyetuamini na kutuweka kwenye mjengo huu, nashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la tatu ambalo ningependa kulisemea, nalo ni kuhusu Serikali yetu kuchukua vyanzo vya mapato vya Halmashauri zetu. Naomba nitumie neno alilolitumia mtani wangu Mheshimiwa Msigwa kwamba tumezi-ground Halmashauri, hapana, siyo sahihi hata kidogo. Nasema hili kwa sababu moja kubwa, nimesema dhamira ya Serikali kwenye kusimamia mapato na matumizi ya Serikali yetu, jambo tunalolifanya kwenye property tax nilieleza Bunge lililopita nikasema, tulileta mabadiliko ya sheria tukabalidisha wote kwa pamoja hapa ndani ya Bunge lako tukufu.

Mheshimiwa Spika, tulichokibadilisha, tukasema, pesa hizi zitakusanywa halafu zitarejeshwa kwenye Halmashauri zetu kulingana na bajeti za Halmashauri husika. Hicho kipengele cha mwishio naona kinasumbua sana; “kulingana na bajeti za Halmashauri husika,” ndicho tunachokifanya Serikali ya Awamu ya Tano. Tunakusanya na tunapeleka katika Halmashauri zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niliambie Bunge lako tukufu, tumepitisha bajeti hapa ya Wizara ya Afya, kila Mbunge alisimama ana zaidi ya vituo viwili au vitatu kwenye Jimbo lake. Hizo ndiyo pesa zinazokusanywa na Serikali ya Awamu ya Tano. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi sote ni mashahidi, mvua imenyesha ya kutosha, ikaharibu miundombinu, sasa hivi kila Mheshimiwa Mbunge jimboni kwake wakandarasi wameshafika wanarekebisha miundombinu iliyoharibika. Ndiyo bajeti tunayoirejesha Halmashauri hii, haiwezi kusema kwamba zinaweza kutoka sehemu nyingine, hapana.

Mheshimiwa Spika, wapo wanaobeza elimu bure, hapana. Ndiyo bajeti tunayoikusanya, tunarejesha na inamfikia kila mtoto wa maskini wa Taifa hili. Hilo ndilo jambo la msingi na hii ndiyo Serikali ya Awamu ya Tano. Tunatenda kwa vitendo na wananchi wanaona haya tunayoyafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hilo ndilo jambo la msingi, hii ndiyo Serikali ya Awamu ya Tano tunatenda kwa vitendo na wananchi wanayaona haya tunayoyafanya.

Mheshimiwa Spika, niwakumbushe jambo moja, Mamlaka ya Mapato Tanzania ndiyo mamlaka pekee kisheria ambayo imepewa jukumu la kusimamia sheria zote za kodi zilizoainishwa katika jedwali la kwanza la Sheria ya Mamlaka ya Mapato Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza jukumu hili sheria hii inabainisha katika Ibara ya 5(1)(a) kuwa TRA itakadiria, itakusanya na kuhasibu mapato husika, ndicho ambacho Serikali yetu ya Awamu ya Tano inafanya. Kwa mujibu wa Ibara ya 5(1)(c) cha Sheria Mamlaka ya Mapato kinatuambia Mamlaka ya Mapato inawajibika kusimamia makusanyo ya tozo na maduhuli yote ya Serikali yanayokusanywa na Wizara pamoja na Idara mbalimbali za Serikali.

Mheshimiwa Spika, pia naomba nilikumbushe Bunge lako tukufu kwamba turejee historia ya Chenge One na mapendekezo yake. Nini Chenge One ilisema? Tunachofanya kama Serikali tunatekeleza haya yote ambayo Bunge lako liliagiza Serikali yetu, Serikali ya Chama cha Mapinduzi ni sikivu sana. Kwa hiyo tumeanza kutekeleza hatua kwa hatua kuhakikisha hili linafanyika.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niseme kwamba Bunge lako Tukufu liliridhia marekebisho madogo ya sheria ikiwa ni utekelezaji wa mapendekezo ya Chenge One, hivyo hatupaswi Waheshimiwa Wabunge kujitoa katika suala hili kwa kuwa mapendekezo ya awali ni ya Bunge tukufu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tunachokifanya ni kutekeleza tu yale ambayo Bunge hili lilipitisha.

Mheshimiwa Spika, naomba kusema pia kidogo katika dhamira ile ya kuhakikisha tunawafikia Watanzania kule walipo baada ya kukusanya mwezi wa Aprili, 2018 na Waheshimiwa Wabunge walikuwepo wakati tunazindua mkakati kwa ajili kuongeza mapato katika Halmashauri zetu. Waheshimiwa Wabunge wengi walikuwepo, Halmashauri nyingi za Mkoa wa Dar es Salaam zilipata pesa za kutosha siku ile wakati tunazidua mkakati huu, dhamira ni nini? Ni kuhakikisha kila taasisi ndani ya Serikali yetu wanakuwa ni wabunifu kuhakikisha tunatafuta vyanzo vya mapato. Kwa hiyo, tutengeneze tuongee na Wakurugenzi wetu kwenye Halmashauri zetu. Tuweze kuandika miradi bunifu kwa ajili ya kuongeza mapato ya Halmashauri zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali ina pesa, tatizo siyo pesa tatizo tunakwenda kuzitumiaje, hilo ndilo jambo la msingi sana. Halmashauri nyingi zimepata fedha hizi kwa ajili ya kwenda kutekeleza miradi itakayoongeza mapato kwenye Halmashauri husika. Niwaombe sana kwa pamoja tushirikiane katika jambo hili ili tuweze kufikisha huduma kwa wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la nne ambalo ningependa kulitolea ufafanuzi katika mchango wangu, ni hoja ya ndugu yangu Mheshimiwa Kombo aliyohoji pamoja na Wabunge wengine waliohoji kuhusu majukumu ya Tume ya Pamoja na Fedha. Waliohoji kwa nini wanapewa bajeti?

Mheshimiwa Spika, napenda kuliambia Bunge lako tukufu kwamba majukumu ya Tume hii ya Pamoja ya Fedha yapo kwa mujibu wa Katiba, ambayo nayo ni pamoja na kuchambua mapato na matumizi yanayotokana na au yanayohusu utekelezaji wa mambo ya Muungano. Ndani ya wiki iliyopita nilijibu swali kuhusu Tume hii ya Pamoja ya Fedha, nikasema tayari nini Tume ya Pamoja na Fedha imefanya katika kipindi chake uhai wake. Imefanya mambo makubwa ifanya study za kutosha na sasa katika bajeti hii ya mwaka 2018/2019 Tume ya Pamoja ya Fedha pamoja na mambo mengine inakwenda kupanga na kufanya mapitio ya study ya usimamizi wa Deni la Taifa kwa ajili ya kuhuisha taarifa kufanya mapitio na takwimu zilizotumika katika study za awali iliyowasilishwa Serikalini.

Mheshimiwa Spika, Tume hii pia itaendelea kufanya uchambuzi wa mapato na matumizi na utekelezaji wa mambo ya Muungano kwa lengo la kuwa na kanzidata ya taarifa sahihi za fedha zinazohusu mambo ya Muungano. Vilevile Tume imepanga kufanya kazi nyingine zikiwemo kutoa elimu kwa wadau wa Tume hii kuhusu uhusiano wa kifedha baina ya Serikali ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Hili la kutoa elimu ni muhimu sana ili kwa pamoja tuweze kuelewa ni nini tunafanya hata ule mjadala niliyosema wiki iliyopita mbele ya Bunge lako tukufu naamini tukishapata elimu ya kutosha mjadala ule utafikia maafikiano mazuri na tutaenda kutekeleza majukumu haya Kikatiba kama yalivyopitishwa.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo ningependa kulisemea nalo ilikuwa hoja ya kwamba kwa nini bidhaa zinazoingia Tanzania Bara kutoka nje ya nchi kupitia Zanzibar zinatozwa kodi mara mbili. Napenda kuliambia Bunge lako tukufu na Watanzania kwa ujumla kwamba hakuna bidhaa inayotozwa kodi mara mbili. Bidhaa tunachokifanya ni kufanya assessment (uthamini) upya wa bidhaa iliyopitia Zanzibar kutoka nchi jirani na katika hili iliunganishwa kwamba bidhaa kutoka Zanzibar haziruhusiwi kuuzwa Tanzania Bara, hakuna zuio hilo.

Mheshimiwa Spika, bidhaa zote zinazozalishwa Zanzibar zinaruhusiwa kuuzwa Tanzania Bara lakini zifuate mfumo wa kiforodha. Hilo ni jambo la muhimu sana lazima tuhakikishe nini kinaingia na kimetoka wapi. Katika moja kwa nini Serikali yetu inafanya hivyo, tunafanya haya kwa sababu jambo kubwa tuko kwenye soko huria na tunahitaji kuweka mazingira mazuri, mazingira sawa sawa, mazingira, sawia ya kufanya biashara kati ya Tanzania yetu yote. Tunahitaji fair and competitive environment kwa ajili ya ufanyaji wa biashara. Tunataka haya siyo kwamba tunahitaji maana yake ilisemwa kwamba mfumo huu umeletwa ili kuiua bandari ya Zanzibar hapana! Tunachokihitaji ni hii fare and competitive environment ya kufanya biashara. Mtu awe na choice yeye mwenyewe, kwa nini apitie bandari ya Zanzibar na asipitie Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, hilo ni jambo la msingi lakini tukifanya upande mmoja kodi inayotozwa kwamba ni ndogo kulinganisha na upande wa pili halafu bidhaa zinazopita kodi ndogo ziingie upande wa pili. Hapa hakuna fare and competitive environment kwenye jambo hilo, kwa hiyo, hapo tutakuwa tume-declare moja kwa moja kwamba tulichokifanya ni kuilinda bandari ya Zanzibar na kuja kuiua bandari ya Dar es Salaam si sahihi hata kidogo. Yeyote atakayekwenda tufanye tu assessment ya kawaida.

Mheshimiwa Spika, katika hili naomba niseme jambo moja, Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa sasa inatumia mfumo wa TANCIS. Ndugu zetu wa ZRB wanatumia mfumo wa ASYCUDA na Serikali zetu mbili kwa sababu lengo letu ni kulinda muungano wetu kuhakikisha muungano huu unakwenda sawia tuko kwenye majadiliano na majadiliano haya muda mfupi tutafika conclusion kuhakikisha Watanzania wote wanafaidika na Utanzania wao katika jambo hili. Niombe sana liweze kueleweka hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika jambo lililohusiana na jambo hili pia ilikuwa ni magari yanayotoka Zanzibar kuja huku Tanzania Bara. Tukichukulia nilikoanzia mifumo yetu ya kodi haiko sawia kinachotendeka sasa maana yake tuliambiwa hapa na niombe Waheshimiwa Wabunge tuwe tunasema ukweli ili tuweze kuwaongoza wananchi waliotuamini katika njia sahihi. Nalisema hili kwa sababu magari yote yanayotoka katika nchi za SADC, magari yote yanayotoka katika nchi za East Africa na magari yote Zanzibar ambayo ni Tanzania wote wanapewa muda wa miezi mitatu wanapoingia nchini. Tunafanya hayo ili kujiridhisha ili kujiridhisha gari hili kweli linaingia Tanzania Bara kwa ajili ya matumizi au kwa ajili ya biashara. Maana yake mtu anaweza akapitisha Zanzibar gari kwa sababu kodi yao iko chini kutokana na mfumo wao, ikija huku tutaua soko la huku hatutakuwa na fair competition kwenye soko letu.

Mheshimiwa Spika, niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge sote kwa pamoja tushirikiane dhamira ni njema, dhamira yetu ni moja kuwatumikia Watanzania maskini na hakuna maendeleo bila kodi lazima kodi zikusanywe na kwa hilo tutasimama imara kuzisimamia kuhakikisha kodi zote zinakusanywa kulingana na sheria zetu ambazo Serikali yetu imezipitisha.

Mheshimiwa Spika, jambo jingine ambalo napenda kulisemea ni kuhusu TRA kuwa Mawakala wakukusanya nimeligusia. Naamini hii ni kengele ya pili naomba nirejee kusema nakushukuru sana kunipa nafasi hii ya kuweza kutoa mchango wangu kidogo kwa ajili ya maendeleo ya Taifa hili na Waheshimiwa Wabunge tushirikiane tushikamane tumpe moyo Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango ili kazi yake iweze kuwa rahisi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo napenda kurejea naunga mkono hoja hii, ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa fursa hii. Nianze kwa kuwapongeza sana kaka yangu Mheshimiwa January, Waziri, pamoja na Naibu Waziri kaka yangu Mheshimiwa Sima kwa kazi kubwa ambayo wanaendelea kuifanya kwenye Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme mambo machache sana baada ya pongezi, kwenye hotuba hii na hoja hii iliyowekwa mezani na Mheshimiwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na jambo la kwanza ambalo limeonekana kwenye vitabu vyote vitatu, kitabu cha Upinzani, kitabu cha Kamati zote mbili za Kudumu za Bunge walipoongelea fedha ambazo zimetolewa, hasa fedha za maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha hizi hutolewa kulingana na jinsi zinavyopatikana, kwa hiyo zikipatikana then mgao unafanyika nani apate nini kulingana na majukumu ya Ofisi husika na kama ilivyooneshwa kwenye vitabu hivi bajeti ilipitishwa na sisi hasa hii sehemu ya kujenga na kufanya ukarabati wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Luthuli, Tunguu na Wete-Pemba. Tumetoa kiwango hiki cha fedha shilingi milioni
538.4 ndizo ambazo zimetolewa kwa ajili ya ukarabati wa Ofisi hii, lakini ninachoomba kusema hapa ni pale ambapo vitabu vyote vimesisitiza kwamba fedha hii iliyotolewa ni fedha ya nje hakuna fedha ya ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeanza kwa kusema tunatoa fedha hizi kulingana na upatikanaji wa fedha husika. Katika hili mkononi mwangu nimebeba kitabu cha hotuba ya bajeti ya Serikali nzima aliyoisoma Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango. Ndugu zangu tunapojadili jambo hili tusioneshe kwamba kuna mtu ambaye hapewi kwa sababu ya aina fulani ya Wizara yake, hapana. Vyanzo vya mapato vya bajeti kuu wa Serikali vimetajwa kwenye kitabu hiki. Moja ya vyanzo vya mapato kama ilivyoelezwa, tuna mapato ya ndani na tuna mapato ya nje ambayo kwenye mapato ya nje tuna misaada na mikopo nafuu, tuna misaada na mikopo nafuu kwa ajili ya miradi ya maendeleo, tuna misaada na mikopo nafuu ya kisekta kwa hiyo tunapoongelea jambo hili tuiongelee bajeti ya Serikali kama ilivyowasilishwa na vyanzo vyake vya mapato kuliko kusema fedha za ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zinapopatikana kwenye kapu, Mfuko Mkuu wa Hazina zinapoingia fedha hizi zinagawiwa kutokana na mgao ambao kwahiyo haingii akilini tunaposema kwamba huyu apewe fedha za ndani wakati tayari ana fedha za nje na Wizara nyingine haina fedha za nje, kwa hiyo kwa kuwa tu tunataka na huyu aonekane ana fedha za ndani basi tulazimishe hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niliombe Bunge lako Tukufu liweze kuzingatia yanayowasilishwa na tunayoyapitisha ndani ya Bunge lako Tukufu. Hiyo ilikuwa hoja ya kwanza ambayo nilikuwa napenda kusema kuhusu mapato ya Serikali na jinsi gani tunavyoyapeleka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo ningependelea kulitolea maelezo hapa ni kuhusu Akaunti ya Fedha ya Pamoja. Nakumbuka vizuri sana mwaka jana tulitoa ahadi kama Serikali kwamba jambo hili linaendelea kufanyiwa kazi. Tunafahamu, Serikali ina ngazi zake za kufanya maamuzi, tayari watalaam wetu wameshamaliza kulifanyia kazi jambo hili na sasa tulipo kikao kilifanyika tarehe 9 Februari, 2019 chini ya Mwenyekiti wa Kamati hii ambaye ni Makamu wetu wa Rais anafanya kazi nzuri sana mama yetu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli nimpongeze sana Mama Samia amesimama imara kuhakikisha Muungano wetu unakuwa imara na unaendelea kudumu tofauti na inavyowekwa hapa kwenye Bunge lako Tukufu kwamba Chama cha Mapinduzi, tukumbuke ni Chama cha Mapinduzi ndicho kilichoasisi Muungano huu. Ni viongozi wa vyama hivi viwili kwa dhamira njema ya pande zote mbili za Muungano. Ndiyo maana nataka kumpongeza kwa dhati ya moyo wangu Mheshimiwa Makamu wa Rais. Angekuwa na moyo kama wa hao wanaotaka kupotosha Watanzania kwenye Bunge lako Tukufu tusingetoka. Serikali ina dhamira njema ya kuhakikisha jambo hili tunafika muafaka ambapo tutakapoanza kuja kwenye migao halisi sasa ya fedha hizi pande zote mbili za Muungano ziwe zimeridhika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemsikiliza kaka yangu Mheshimiwa Jaku anasema, Zanzibar wakati wanaungana walikuwa wachache, hivyo Watanzania Bara wakati tunaungana tulikuwa milioni 55? Kwa hiyo tuangalie hoja hizi, base yetu ni nini ya kuleta hoja hizi. Kwa hiyo tunaposema 4.5 ni ndogo umechukua kigezo gani kusema 4.5 ni ndogo inayopelekwa Zanzibar? Kwa hiyo tarehe 9 Februari, 2019, kikao kilichofanyika hapa Dodoma maamuzi yalifanyika. Kama tulivyokuwa tuna-report siku zote kwamba Serikali inayafanyia kazi pale ambapo hatujaelewana na sasa tumeelewana na unaandaliwa Waraka wa Baraza la Mawaziri ili kwenda kufanya maamuzi ya mwisho na jambo hili liweze kufika mwisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kombo amesema tutoe commitment, commitment ndiyo hiyo. Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kikao hili ameshaelekeza na tayari waraka umeanza kuandaliwa, anataka commitment nyingine ipi Mheshimiwa Kombo? Kwa hiyo Serikali ya Chama cha Mapinduzi imedhamiria kuona Muungano huu unaendelea kuwa imara, Muungano huu unaendelea kuwa na faida na pande mbili zote za Muungano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo limeongelewa ni kuhusu kodi mara mbili. Nimekuwa mimi na naomba niwe shahidi ndani ya Bunge lako Tukufu, nimekuwa nikisema siku zote hakuna kodi, hakuna bidhaa yoyote inayotozwa mara mbili. Kinachotokea nimesema hapa na jambo hili ni katika mambo ambayo yapo kwenye Waraka ulioandaliwa wa Baraza la Mawaziri kwamba valuation system zetu kati ya Zanzibar na Tanzania Bara siyo moja. Watalaam wetu wamemaliza kuandaa taarifa yao ya kitaalam, wameshaileta tayari inaingia kwenye Waraka huu unaoshughulikia kero za Muungano ili sasa tuweze kulitatua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuko kwenye dunia huru ambayo tunafanya boiashara. Haiwezekani jirani yako akaingiza bidhaa kutoka kwa jirani mwingine kwa bei ya chini halafu bidhaa hiyo useme uilete nyumbani kwako ili uweze kufanya biashara. Hiyo haitowezekana, ni ngumu sana, kama kweli sisi ni Taifa moja, ni lazima tuwe na valuation system moja yenye manufaa mapana kwa Watanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea kulikumbusha Bunge lako Tukufu hakuna maendeleo bila kodi. Lazima kodi ilipwe na lazima ilipwe katika rate zilizokubalika. Tunachikifanya Mamlaka ya Mapato Tanzania tuna-adopt international system…

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tume-adopt international system ambayo…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Jaku kaa chini please.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tume-adopt international system, tuna international database sasa huwezi ukajifungia chumbani ukasema mimi siangalii kinachotokea duniani, mimi nataka nilinde watu wangu, unalinda watu wako ukiwa na nini mkononi? Kwa hiyo ni lazima tukubaliane na dunia inakwenda vipi, global business inakwenda vipi ili kwa pamoja tuweze kuwaletea maendeleo Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mgao wa Mashirika ya Umma; nilijulishe Bunge lako Tukufu kama ambavyo wamesema Waheshimiwa Wabunge hapa, Benki Kuu tunapeleka na tayari tarehe Mosi Februari, 2019 tumepeleka zaidi ya shilingi bilioni 15 ambazo ulikuwa ni mgao kutoka gawiwo la Benki Kuu. Kwa Mashirika mengine yaliyosalia tunaendelea kuyafanyia kazi na ni moja ya mambo yanayoshughulikiwa kwenye kero za Muungano ili kwa pamoja Mashirika haya yaweze nayo gawiwo waliloanza kutoa, kwanza lazima, tukumbuke Mashirika haya yalikuwa hayafanyi vizuri, Serikali imefanya jitihada kubwa Mashirika haya yameanza kufanya vizuri kwa sasa tunalishughulikia ili kama linavyoingia gawiwo la Benki Kuu, moja kwa moja…

MWENYEKITI: Nakuongezea dakika moja malizia.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa hiyo tunakwenda kumalizia na mashirika mengine likiingia tu gawiwo lile kwenye Mashirika haya iende moja kwa moja asilimia 4.5 kwenda Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Benki yetu TPB; hii huwa tunagawana kulingana na hisa ulizonazo kwenye Benki hii. Kwa hiyo hili halina changamoto yoyote, limekuwa likitendeka miaka yote ya Muungano na tangu TPB Bank ilipoanza kutengeneza faida.

Mheshimiwa Mwenyekjiti, baada ya kusema haya, nirejee kuwapongeza Waheshimiwa Mawaziri Wizara hii na naunga mkono hoja. (Makofi)
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango napenda kutoa shukurani za dhati, kwako wewe binafsi, Mheshimiwa Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge kwa kusimamia vema mjadala wa hoja iliyowasilishwa mnamo tarehe 5/11/2019 na Waziri wa Fedha na Mipango ambayo ni Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa na Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti kwa mwaka 2020/2021.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia kuwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wote waliochangia ama kwa maandishi au kwa kuzungumza. Jumla ya Waheshimiwa Wabunge 111 wamechangia katika mjadala huu, ambapo Wabunge 95 wamechangia kwa kuzungumza na Wabunge 16 kwa maandishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ulivyotangulia kusema, lengo la wasilisho la Waziri wa Fedha na Mipango mbele ya Bunge lako Tukufu lilikuwa ni kuomba maoni na ushauri wa Waheshimiwa Wabunge wakiwasilisha mawazo na maoni ya wananchi kuhusu maendeleo ya nchi yao na mgawanyo wa rasilimali fedha ili yazingatiwe katika hatua inayofuata ya kuandaa Mpango wa Maendeleo wa Taifa na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka ujao wa Fedha, mwaka 2020/2021.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Serikali nakiri kuwa lengo hili limefanikiwa kwa kiwango cha hali ya juu sana na narudia kusema, ahsanteni sana kwa michango yenu Waheshimiwa Wabunge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na kutoa maoni na ushauri kuhusu Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 2020/2021, Waheshimiwa Wabunge wametoa pia pongezi nyingi sana kwa Serikali yetu ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Jemedari wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, kwa kufanikisha kwa kiwango cha juu utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa na Bajeti tangu Serikali yetu ya Awamu ya Tano iingie madarakani Novemba, 2015.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa moyo mkunjufu na kwa unyenyekevu mkubwa sana, napenda kupokea pongezi hizi za Waheshimiwa Wabunge kwa niaba ya Serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa heshima na taadhima napenda kuwashukuru kwa moyo wa dhati kabisa Viongozi wetu Wakuu wa Kitaifa wakiongozwa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Makamu wa Rais Mama yetu Mama Samia Suluhu Hassan na Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutuamini katika kusimamia majukumu ya Wizara ya Fedha na Mipango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakika pongezi hizi zilizotolewa na Kamati yako ya Mipango ni matokeo ya miongozo na maelekezo yao ambayo wamekuwa wakitupatia kwa lengo la kuliletea Taifa letu maendeleo. Kwa niaba ya Waziri wangu, pamoja na Wizara ya Fedha na Mipango, napenda kuwaahidi kwamba hatutawaangusha, kwani heshima na dhamana mliyotukabidhi kwa niaba ya Watanzania ni kubwa sana na yenye utukufu ndani yake nasema ahsanteni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipekee napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Waziri wa Fedha na Mipango, Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango kwa kuniamini na kunipa jukumu la kutoa ufafanuzi kwa niaba yake, wa hoja za Waheshimiwa Wabunge siku hii ya leo. Nitumie pia fursa hii kuwashukuru kwa dhati watendaji na watumishi wote wa Wizara ya Fedha na Mipango, wakiongozwa na Katibu Mkuu, Bwana Doto Mgosha James, kwa kuchambua na kutafuta takwimu na taarifa zilizohitajika kutolea ufafanuzi wa hoja mbalimbali zilizotolewa na Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba uniruhusu kutambua mchango wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa Mashimba Mashauri Ndaki, Mbunge wa Maswa Magharibi. Kamati ilitupatia ushauri wa msingi na wa mwanzo ambao Waziri wa Fedha na Mipango alieleza kwa ufupi wakati akiwasilisha hoja hii mbele ya Bunge lako tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile, tumepokea mchango uliotolewa na Mheshimiwa David Ernest Silinde, Mbunge wa Momba, kwa niaba ya msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu hoja iliyombele yetu. Aidha, nakushukuru sana Mheshimiwa Mwenyekiti wewe binafsi kwa mchango wako kama Spika na miongozo yako ambayo umetupatia ndani ya kipindi hiki cha siku tano, lakini pia mchango wako kama Mbunge unayewakilisha wananchi wa Jimbo la Kongwa nasema ahsante sana tumepokea mchango wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majadiliano ya hoja iliyowasilishwa mbele ya Bunge lako Tukufu, Serikali imepokea maoni mengi sana kwa uchache tumejitahidi kuyachambua na kuyaweka katika makundi yafuatayo:-

(i) Kundi la kwanza ambapo mchango umewekwa nguvu na Waheshimiwa Wabunge ni kuweka msukumo thabiti kwenye sekta ya kilimo, hususan kuwa na uhakika wa upatikanaji wa pembejeo, mbegu na zana bora, huduma za ugani, mikopo na mitaji, miundombinu ya umwagiliaji na utafiti ili kuongeza uzalishaji, tija, ubora na uhakika wa masoko na bei ya masoko ya wakulima wetu; (Makofi)

(ii) Eneo la pili ni kwamba Serikali ichukue hatua ya kuboresha uratibu na usimamizi wa utekelezaji wa miradi ya maji ili thamani halisi ya fedha inayopelekwa kwenye miradi ya maji iweze kuonekana na hatimaye kufikia malengo ya kutatua changamoto ya muda mrefu ya ukosefu wa maji safi na salama kwa wananchi wetu;

(iii) Kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya kimkakati kama vile umeme, reli na barabara ili kuvutia uwekezaji mahiri na hivyo kuchochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi na kijamii ndani ya Taifa letu;

(iv) Kuwekeza na kutumia kikamilifu rasilimali za bahari na maziwa (the blue economy), hususan uvuvi wa bahari kuu;

(v) Kuboresha mazingira ya kufanya biashara ndani ya Taifa letu; na

(vi) Kuimarisha mfumo wa uratibu, usimamizi na ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Serikali, naahidi kuwa, wakati wa kuandaa Mpango wa Maendeleo wa Taifa na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2020/ 2021 tutazingatia ipasavyo maoni na ushauri uliotolewa na Bunge lako Tukufu lilipokaa kama Kamati ya Mipango kwa sekta zote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kazi ya Wizara yetu ya Fedha katika siku hizi tano ilikuwa ni kupokea maoni na ushauri, ambao sasa tunakwenda kuutafakari kama serikali nzima na kuufanyia kazi hatimaye kuja na mpango wetu wa maendeleo na bajeti kwa mwaka ujao wa fedha naomba nisiseme mengi sana. Hata hivyo, kama ilivyo ada naomba uniruhusu nitoe ufafanuzi kwa baadhi tu ya hoja zilizotolewa na Waheshimiwa Wabunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya kwanza na naamini wengi watashangaa nisipoongelea kuhusu Serikali yetu kuwekeza katika kilimo ili sekta ya kilimo ambayo imepewa msukumo mkubwa na hoja ya kwanza ni Serikali iwekeze zaidi katika sekta ya kilimo ikiwezekana kutenga 10% ya bajeti kama Azimio la Maputo na Azimo la Malabo linavyotuelekeza ili kuiwezesha kukua kwa 6% kama Azimio la Malabo pia linavyotuelekeza na hivyo kuchangia kwa kiwango kikubwa kwenye pato la Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Serikali tunafahamu umuhimu wa sekta ya kilimo na mchango wake mkubwa kwenye ukuaji wa uchumi wetu na pato la Taifa. Lakini ni vizuri kama watanzania tukafahamu kuwa ili sekta ya kilimo iweze kukua na kutoa mchango mkubwa kwenye pato la Taifa ni muhimu sana serikali yetu kuwekeza kimkakati katika maeneo makuu yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la kwanza ni mafunzo, utafiti pamoja na ugavi. Eneo la pili ni usalama wa chakula, uhifadhi na lishe. Eneo la tatu masoko kwa ajili mazao kwenye soko letu la kilimo. Eneo la nne upatikanaji wa mikopo yenye riba nafuu, eneo la tano miundombinu na elimu ya kuongeza thamani ya mazao yetu. Eneo la sita upatikanaji na usambazaji wa pembejeo na zana za kilimo, na eneo la saba ni kuwa na miundombinu wezeshi kama vile umeme, maji na umwagiliaji, barabara, reli, madaraja, vivuko na meli pamoja na mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali yetu inatambua sana na imekuwa ikitenda mengi katika maeneo haya na ninaomba niseme machache ambayo Serikali yetu ya Awamu ya Tano imekuwa ikiyatekeleza ili kuhakikisha ukuaji wetu wa sekta ya kilimo unakua kama tulivyosaini maazimio mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la kwanza Serikali yetu imeanza utekelezaji wa Programu ya ASDP II ambapo shilingi bilioni 25.19 ambazo ni fedha za ndani na shilingi trilioni 1.37 fedha za nje zimetumika kati ya mwaka wa fedha 2016/ 2017 na robo ya kwanza ya mwaka 2019/2020 katika kutekeleza kazi zifuatazo;-

(i) Serikali imefadhili jumla ya wanafunzi 3,897 kama yalivyo malengo yetu kwenye program hii ASDP II katika ngazi ya Astashahada na Stashahada ili kuhakikisha tunakuwa na maafisa ugani wa kutosha;

(ii) Tumewekeza pia kwenye Utafiti ambapo tumefanikiwa jumla ya miche 37,816 ya korosho kuzalishwa na kusambazwa nchini katika mikoa ile ambayo ina potential kubwa ya uzalishaji wa korosho. Lakini pia mbegu bora 14 zimegunduliwa na TARI na aina 11 ya mbegu mpya za mpunga zimegunduliwa na kutambulishwa katika skimu 40.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema akiba ya chakula ni jambo la muhimu sana taifa letu limeona na sisi ni mashahidi tunaona Taifa letu limekuwa na akiba ya chakula ya kutosha kwa sababu ya uwekezaji ambayo serikali ina wekeza. Tumeweza kufikia tani 68,124.69 na ukarabati wa maghala 105 yenye uwezo wa kuhifadhi tani 31,500 umekamilika ili kuhakikisha chakula chetu kinakuwa salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia tumefanyika ukarabati na ujenzi wa skimu za umwagiliaji. Ambapo skimu 5 zimekamilika ikiwa ni pamoja na barabara za kuingia na kutoka zenye urefu wa kilomita 15 na mafunzo kwa wajumbe 311 wa umoja wa umwagiliaji katika Wilaya za Mvomero, Kilosa na Kilombero.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maelezo ya kina niwaombe Waheshimiwa Wabunge wa utekelezaji wa ASDP II yanapatikana katika ukurasa wa 65 - 66 wa Mapendekezo ya Mpango wa 2020/2021 na ukurasa wa 259 – 277 wa Taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kwa kipindi cha mwaka 2016/2017 hadi robo ya kwanza ya mwaka 2019/2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali yetu haikuishia hapo kwenye utekelezaji wa ASDP II peke yake, tumekuwa pia na utekelezaji wa mpango wa kuendeleza wa kuendeleza kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania. Baadhi ya kazi zilizotekelezwa kati ya 2016/2017 na 2019/2020 kwa fedha za ndani ni pamoja na kuendeleza kongano sita zakuongeza tija katika uzalishaji, thamani ya mazao, usambazaji wa mbolea, masoko na watoa huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia hekta 38,477 za mazao zimelimwa kwa kutumia teknolojia ya kisasa. Tumeendelea kutenda mambo mengi ambapo pia tumeweza kufufua vinu vya kusaga nafaka NMC Dodoma na Mwanza. Ambapo kwa kinu cha Dodoma kimekamilika na kinu cha Mwanza kimefikia 80% ili kuhakikisha sasa tunaweza kuongeza thamani ya mazao ya wakulima wetu na tumetumia shilingi bilioni 15.53 katika kufufua vinu hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali yetu pia imetoa jumla ya shilingi bilioni 9.92 kwa ajili ya kufufua kiwanda cha Ngozi Karanga – Moshi. Kazi ya kutengeneza na kusimika mashine inaendelea hii yote ni katika kuhakikisha mipango yetu ya kuinua kilimo chetu mazao yetu ya kilimo inafikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali yetu pia imetekeleza programu ya uendelezaji wa mifumo ya masoko na Huduma za Fedha Vijijini ambapo tumetumia shilingi bilioni 114.28 fedha za nje zimetumika kuboresha miundombinu ya masoko vijijini, kuwajengea uwezo wakulima wapato 83,988 katika vikundi 2,408, taasisi 10 za fedha na vyama vya ushirika vya akiba na mikopo 720 pia vimefikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kulieleza Bunge lako Tukufu yameelezwa mengi kwamba Serikali yetu haitoi kipaumbele kwenye kilimo chetu haya nayaeleza na yameandikwa kwenye document ambazo tayari tunazo tuweze kuzipitia ili tuwafikishie watanzania ujumbe kwamba nini kinafanyika na Serikali yetu ya Awamu wa Tano kuhakikisha kilimo chetu kinakuwa imara na kinatekelezeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja hii iliunganishwa na ukuaji wa sekta hii ya kilimo. Lakini Waheshimiwa Wabunge naomba kwa unyenyekevu mkubwa tupitie vitabu yetu. Kitabu chetu cha Taarifa ya Hali ya Uchumi kwa mwaka 2017, ukurasa 20. lakini pia taarifa ya hali ya uchumi kwa mwaka 2018 ukurasa 20 pia utaona kwamba, sekta ya kilimo ilikua kwa asilimia 5.6 kati ya mwaka 2014 hadi mwaka 2018 tofauti na ambavyo Waheshimiwa wabunge wengi wamesema sekta hii imekuwa kwa chini ya asilimia tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwango hiki kinakaribiana na lengo la Malabo ambapo nilisema tulisaini azimio hili la Malabo la kuhakiksha sekta yetu ya kilimo inakuwa kwa angalau la asilimia 6 sisi tupo asilimia 5.6 na taarifa zetu mbalimbali tunazozisambasa na ambazo watanzania wanatakiwa kufikishishwa na kuzisoma zinaeleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa jitihada nilizozieleza tunaendelea kupiga hatua katika nyanja ya uwekezaji, kaika sekta ya kilimo na sekta wezeshi, hususan katika Awamu ya Tano ya uongozi wa Jemedari wetu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Hivyo basi, ni matarajio yetu kuwa, tutavuka lengo hili la Malabo la asilimia sita ndani ya muda mfupi ujao tunachohitajika ni kuisapoti serikali yetu kuongea na watanzania kuongea na wakulima na wafugaji wetu ili wazione fursa zinaletwa mbele yao na serikali yao tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende kwenye hoja namba mbili, hoja na mbili ambayo ningependa kuitolea maelezo kidogo ni ile ambayo Waheshimiwa Wabunge wengi pia wamesema Serikali iangalie uwezekano wa kukopa kupitia export credit ili kukamilisha Mradi wa Reli ya Kisasa kwa pamoja badala ya kujenga kidogo kidogo ili kuona matokeo chanya na yenye tija ya uwekezaji huu. Hoja hii ni muhimu sana na kama Serikali tunaipokea lakin lazima tufahamu dhamira njema ya Serikali yetu ya Awamu ya Tano ya kutekeleza mradi huu wa Reli yetu ya Kisasa kwa awamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunavyofahamu Awamu ya kwanza ya ujenzi inafanyika kwa kutumia mapato ya ndani na Awamu ya pili inagharimia kwa fedha za mkopo utakaopatikana kwa utaratibu wa Export Credit Agency ambao masharti yake ni nafuu tofauti na ilivyodaiwa na Waheshimwa wabunge kwamba tunakopa kwa masharti ya kibiashara hapana tunakopa mikopo naafuu ili tuweze kutekeleza mradi wetu huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uamuzi wa kutekeleza mradi huu kwa awamu unatokana na tathmini ya kitaalam iliyofanyika kuhusu upatikanaji na gharama za mikopo, uwezo wa Serikali wa kuhudumia deni bila kuathiri utekelezaji wa bajeti ya maeneo ya kipaumbele pamoja na uhimilivu wa deni la Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wamekuwa wakisisitiza sana kuhusu uhimilivu wa deni la Serikali na katika hili naomba niliombe Bunge lako Tukufu lifahamu kwamba kwa mujibu wa sheria ya mikopo, dhamana na misaada sura 134, tunatakiwa kukopa kwa kuzingatia tathimini ya uhimilivu wa deni yaani debt sustainability analysis na ukomo wa kawaida ni kati ya dola za kimarekani milioni 800 hadi dola Kimarekani 1,000 kwa mwaka. Hivyo basi, uamuzi wa kukopa fedha za mradi mzima kwa wakati moja tutakwenda kuvunja sheria tuliyoitunga wenyewe lakini pia tutakwenda kupata usumbufu kwenye kuli-manage deni letu la Taifa. Naomba tuendelee kuiamini serikali yetu dhamira yake ni njema katika kuhakikisha mradi wetu unakamilika kwa wakati lakini utekelezwe kwa awamu kama ambavyo Bunge lako tukufu limeletewa mbele yako.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya tatu ambayo ningependa kuisemea kwa ufupi ni hoja iliyosemwa kwamba utekelezaji wa miradi mikubwa mitatu ya kimkakati ambayo ni mradi wa wa reli ya standard gauge, kufua Umeme katika Mto Rufiji na ununuzi wa Ndege za Serikali imechukua shilingi trilioni 4.42 ambayo ni sawa na asilimia 36 ya fedha zote za miradi ya maendeleo. Lakini hoja hii ikasemwa zaidi kwamba miradi hii haina faida za moja kwa moja katika uchumi wa nchi yetu. Hii inatokana na ukweli kwamba malighafi inayotumika kujenga reli yetu ya kisasa ambayo ni chuma na cement karibu zote zinatoka nje ya nchi na hivyo fedha zinaondoka katika mzunguko wa ndani na kupelekwa nje kwa ajili ya ununuzi wa malighafi hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa watanzania wafahamu ukweli kuhusu miradi hii na faida ambayo inapatikana wakati wa utekelezaji wa miradi hii na baada ya kukamilika kwa miradi hii. Ni vizuri watanzania wasipotoshwe ukiaacha faida za moja kwa moja kwenye uchumi wetu zitakazopatikana baada ya miradi hii kukamilika, zipo faida ambazo zimeshaonekana tayari kwenye Taifa letu tangu kuanza kwa utekelezaji wa miradi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa uchache na ufupi, naomba niseme kwa kila mradi nini Taifa letu limepata? Nianze na mradi wa reli yetu ya kisasa (Standard Gauge Railway). Hadi Septemba, 2019 Serikali yetu tunafahamu kwenye mradi huu imetoa shilingi trilioni 2.52 lakini mradi huu umezalisha ajira kwa Watanzania takribani 13,117. Hawa ni Watanzania ambao hawakuwa na ajira. Wamepata ajira kwenye mradi huu na wanaendelea kulipwa kutokana na utekelezaji wa mradi huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu pia umefungua fursa kwa Wakandarasi na Wazabuni wa ndani zaidi ya 640. Hawa walikuwa hawana kazi. Kupitia mradi huu Wakandarasi hawa wamepata kazi kupitia mradi huu na fedha wanazolipwa zinabaki ndani ya Taifa letu tofauti na ambavyo imesemwa fedha nyingi inaondoka kwenda nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zabuni za Wakandarasi hawa 640 zina thamani ya shilingi bilioni 664.7. Tunaweza kuangalia kwa asilimia, ni kiwango kikubwa cha pesa kinachobaki ndani ya Taifa letu kutokana na utekelezaji wa mradi huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa mradi huu pia unakadiriwa kutumia cement mifuko milioni tisa na nondo za madaraja kilogramu milioni 115 kwa kipande cha Dar es Salaam hadi Makutupora tu. Malighafi hizi zinatoka ndani ya Taifa letu. Hakuna cement inayonunuliwa nje ya nchi kuja kutekeleza mradi huu. Kwa hiyo, viwanda vyetu vinaendelea kuzalisha cement kwa kiwango kikubwa katika utekelezaji na fedha hizi zinaendelea kubaki ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia mradi huu utaendelea kutekelezwa kwa kuzingatia masharti ya mkataba ambapo asilimia 30 ya gharama za mradi itatumika katika ununuzi wa huduma na bidhaa kutoka nchini. Kwa hiyo, Serikali yetu chini ya Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, iko makini katika kila mradi unaotekelezwa kuhakikisha Taifa letu linafaidika na utekelezaji wa mradi huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kukamilika kwa mradi huu, tunafahamu ni mengi tutafaidika nayo, lakini dogo tu ambalo Taifa hili limekuwa likiumia kwa muda mrefu ni gharama za matengenezo ya barabra zetu, tutaokoa takribani kwa mwaka mmoja zaidi ya shilingi bilioni 6.7. Ndiyo dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano, ndiyo dhamira ya Chama cha Mapinduzi, ndiyo dhamira ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kuhakikisha kuwa mradi huu unatekelezwa kwa wakati, fedha zake zinatafutwa kwa wakati na ndiyo maana tulijibana na kuhakikisha awamu ya kwanza ya mradi huu inatekelezwa na fedha za Watanzania wenyewe, fedha za walipakodi wa Tanzania wenyewe. Nawashukuru sana Watanzania kwa kuendelea kulipa kodi kwa hiari, kwa kuendelea kujitolea kusimamia miradi yao ya maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa niende kwenye mradi wa pili ambao nao tumeambia kwamba fedha zote zinaondoka hazibaki nchini. Ni mradi wa uzalishaji wa umeme kwa nguvu za maji wa Julius Nyerere. Mradi huu hadi Oktoba, 2019, nao pia umetusaidia kuzalisha ajira za Watanzania ambao walikuwa hawana ajira zaidi ya 1,456. Mradi huu pia umeongeza fursa kwa Wakandarasi wa Kampuni zetu za ndani. Kampuni 10 za Kitanzania hadi Oktoba 2019, zimepata kazi kwenye mradi huu wa uzalishaji umeme kwa nguvu ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia mradi huu tumeona kuna ongezeko la ununuzi wa bidhaa za ndani, mfano, cement, nondo, kokoto, mchanga pamoja na vyakula vya aina mbalimbali ambavyo vinatusaidia kuchochea ukuaji wa sekta yetu ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunavyofahamu, Tanzania tunayoiendea na Tanzania tuliyopo ni Tanzania ya viwanda. Hakuna Tanzania ya viwanda bila ya kuwa na umeme wa uhakika, hakuna Tanzania ya viwanda bila ya kuwa na umeme wa bei nafuu. Tunatarajia tutakapokamilisha mradi huu, bei ya umeme itashuka na kwa uhakika tutaweza kuiona Tanzania ya Viwanda ambayo Watanzania wameisubiri kwa muda mrefu. Nitoe tu rai yangu kwa Waheshimiwa Wabunge, tuendelee ku- support miradi hii kwa dhamira njema kabisa ili kuwapa fursa Watanzania wenzetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mradi wa Shirika la Ndege; mradi huu pia umesaidia sana katika kuzalisha ajira za Watanzania zaidi ya 436 hadi kufikia Septemba 2019. Mradi huu pia umerahisisha huduma ya usafiri ambapo njia 11 za ndani ya nchi; na sita nje ya nchi zimeanzishwa hadi kufikia mwezi Oktoba, 2019. Tunaona mapato yetu yakiongezeka tukiweza kukusanya kutokana na utekelezaji wa uboreshaji huu wa Shirika letu la Ndege, lakini pia kuongezeka kwa idadi ya watalii ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ilikuwa no hoja ya pili ambayo ningependa kuitolea maelezo kidogo ili tuondoke tukiwa na ufahamu. Yote ambayo yamependekezwa na Kamati yako ya Mipango juu ya miradi hii tutakwenda kuitekeleza tunapoanza kuandaa Mpango wetu wa Maendeleo wa Mwaka 2020/2021 lakini tukizingatia pia hatuvunji sheria tunapotekeleza miradi yetu hii ya maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya nne ambayo ningependa kuisemea kidogo ni fedha za kutosha kwa ajili ya TARURA. Hili limesemwa karibu na Wabunge wote ndani ya Kamati yako ya Mipango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali yetu inatambua sana umuhimu wa kuboresha barabara za mijini na vijijini ili kuboresha huduma ya usafiri na usafirishaji hususan katika maeneo ya vijijini. Katika kutekeleza azma hii, Serikali yetu imeongeza bajeti ya TARURA kwa mwaka wa fedha 2019/ 2020 kutoka shilingi bilioni 272.6 mwaka 2018/2019 hadi Shilingi bilioni 285.2 mwaka 2019/2020 ikiwa ni ongezeko la shilingi bilioni 12.6.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali inafanya mapitio ya mtandao wa barabara nchini ili kubaini mtandao wa barabara za TANROADS na zile za TARURA na hatimaye kufanya maamuzi juu ya mgawanyo wa fedha za Mfuko wa Barabara. Tunatambua uhitaji huu na tunakwenda kushughulika nalo tunapokwenda kuanda Mpango wetu wa Maendeleo wa mwaka 2020/2021.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya tano ambayo ningependa pia kuitolea maelezo kidogo ni hoja ambayo pia imesemwa na angalau na Wabunge zaidi ya asilimia 80, nayo ni kuhusu utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo kwa njia ya ubia kati ya Sekta Binafsi na Sekta ya Umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali yetu ina dhamira njema sana ya kuona Sekta Binafsi inashiriki katika utekelezaji wa miradi yetu mikubwa ya maendeleo na ndiyo maana tulileta sheria hapa, tukafanya marekebisho ya Sheria yetu ya Ubia, Sura 103 na kwa mujibu wa Kanuni ya 29(1) ya Sheria ya Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi kama ilivyorekebishwa mwaka 2018 kwa dhamira njema kabisa, miradi yote inayoibuliwa inatakiwa kutangazwa inapofikia hatua ya ununuzi kwa kumpata mbia wa kuwekeza. Kanuni hii imeainisha kuwa miradi hiyo itatangazwa katika vyombo mbalimbali vya habari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpendekezo ya Mpango wetu wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2020/ 2021 ukurasa wa 74, tumeainishwa jumla ya miradi nane ya ubia. Kati ya miradi hiyo ambayo inatarajiwa kutangazwa kwa mwaka 2019/2020 na utekelezaji wake kuanza 2020/ 2021:-

(i) Mradi wa uendeshaji wa huduma ya usafiri wa mabasi yaendayo haraka Jijini Dar es Salaam awamu ya kwanza;

(ii) Mradi wa Kuzalisha Dawa za Binadamu (General Pharmaceuticals), kiwanda tunachotarajia kitajengwa Pwani;

(iii) Mradi wa Kuzalisha Bidhaa za Pamba za Hospitali (Medical Cotton Products) ambacho kinatarajiwa kujengwa Mwanza; na

(iv) Mradi wa Kuzalisha Maji Tiba (IV fluids) kinachotarajiwa kujengwa kule Jijini Mbeya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ushahidi huu, siyo kweli kwamba Serikali haitaki kutekeleza miradi ya maendeleo kwa mfumo wa ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi. Serikali ipo tayari kwa kuanza na miradi hii huku tukiendelea kuandaa miradi mingine kama sheria inavyotuelekeza. Nitoe wito kwa Waheshimiwa Wabunge wote na Watanzania kwa ujumla kwamba, yeyote mwenye Mwekezaji mwenye dhamira njema wawalete wawekezaji hao na Serikali yetu ipo tayari kufanyanao kazi kwa mujibu wa Sheria na kanuni zilizopo na kwa maslahi mapana ya Taifa letu. Tuko tayari kabisa, tuaomba mtuletee wawekezaji na tutafanyanao kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya sita ambayo pia napenda kuitolea maelezo kidogo, ambayo nayo karibu asilimia 98 ya Waheshimiwa Wabunge wameigusia ni hoja ya mapendekezo kwamba Mpango huu tunaoupendekeza unakuja na mkakati gani wa kutatua tatizo la maji ifikapo mwaka 2020/2021?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mapendekezo ya Mpango wetu huu yanalenga kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama, kusimamia vyanzo vya maji, kudhibiti matumizi ya fedha za maji, ikiwa ni pamoja na ubora wa miradi ya maji. Aidha, Mapendekezo ya Mpango wetu yanalenga pia kuongeza kiwango cha upatikanaji maji mijini na vijijini kutoka hali ya sasa ambapo Jiji la Dar es Salaam limefikia asilimia 85, mikoa mingine asilimia 80, Miji Midogo ni asilimia 64 na vijijini ni asilimia 64.8.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuongeza kiwango cha upatikanaji wa maji pamoja na ubora wa miradi ya maji, Mpango tunaoupendekeza mbele ya Bunge lako Tukufu umeainisha kufanya yafuatayo ambapo kama Serikali tumekuwa tukiyarudiarudia na tunakwenda kuyasimamia:-

(i) Tunakwenda kuendelea na usimamizi wa matumizi endelevu ya maji;

(ii) Kuimarisha uratibu, ufuatiliaji na tathmini katika miradi ya maji nchi nzima;

(iii) Kuongeza kiwango cha upatikanaji wa maji vijijini na mijini kwa kukamilisha miradi inayoendelea na kuanza miradi mipya ambayo itapendekezwa ndani ya Mpango tunaokuja nao; na

(iv) Tunakwenda kuimarisha Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira vijijini, yaani RUWASA pamoja na shughuli za mfuko wa maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya yote tumeyaeleza katika mapendekezo ya Mpango na tunapokwenda sasa kuandaa Mpango wetu, tunakwenda kuainisha kazi zote zinazokwenda kutekelezwa ndani ya mwaka ujao wa fedha ili kuhakikisha Watanzania wanapata huduma bora ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja nyingine ambayo ningependa kuisemea kidogo ni ile ambayo Waheshimiwa Wabunge pia wameiongelea na kuomba Serikali ifanye marejeo ya vipaumbele vya Kitaifa hususan kwa kuzingatia Sekta ya Maji, Sekta ya Afya na miundombinu ya barabara hasa barabara za vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maji, afya na miundombinu kama ambavyo Waheshimiwa Wabunge wetu wamependekeza ni miongoni mwa vipaumbele vya awali kabisa vilivyoainishwa katika Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano yaani Mwaka 2016/2017 hadi 2020/ 2021 na Serikali yetu imekuwa ikiwezekeza fedha nyingi kwenye sekta hizi. Maeneo hayo kama ilivyopendekezwa na Waheshimiwa Wabunge yataendelea kuwa ya kipaumbele kwa Taifa kutokana na umuhimu wake katika kuboresha maisha ya wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, maeneo hayo yameainishwa vizuri kabisa pia katika kitabu cha Mapendekezo ya Mpango tunaokwenda kujanao ukurasa wa 69. Kinachokosekana ni kazi zinazokwenda kufanyika ambazo zitakwenda kuainishwa baada ya kuwa tayari tumeshapokea maoni na ushauri wa Kamati yako ya Mipango tunapokwenda kuandaa Mpango wetu wa Maendeleo wa Mwaka 2020/2021, tutauleta mwezi wa Tatu kwenye Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja nyingine ambayo Waheshimiwa Wabunge wameisema kwa nguvu ni ukamilishaji wa maboma yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi; maboma katika Sekta ya Elimu na Sekta ya Afya. Serikali yetu inatambua nguvu za wananchi zilizowekezwa katika ujenzi wa maboma haya na ndiyo maana kila mwaka tunatenga bajeti na kuitekeleza kwa asilimia kubwa kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma yaliyojengwa na wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, kati ya Julai, 2018 na Oktoba, 2019, Serikali yetu imetoa jumla ya shilingi bilioni 104 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa maboma ya huduma za jamii katika Sekta ya elimu na Afya. Kati ya fedha hizi, shilingi bilioni 38.9 zilitolewa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa maboma 96 ya Vituo vya Afya na shilingi bilioni 29.9 zilitolewa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa maboma ya madarasa 2,392 ya shule zetu za sekondari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile, Serikali kupitia Programu ya Lipa Kulingana na Matokeo, katika Sekta ya Elimu ilitoa shilingi bilioni 35.2 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa maboma ya vyumba vya madarasa 2,760 na matundu ya vyoo 670 kwenye shule zetu za msingi. Tunaendelea kutekeleza bajeti hii kwa mwaka huu wa 2019/2020 ili kuhakikisha maboma yote yanafunikwa na wananchi wetu wanaanza kupata huduma kwenye maeneo haya ambapo waliweka nguvu zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja nyingine ambayo napenda kuisemea kwa ufupi sana ni hoja ambayo karibu asilimia 100 ya Waheshimiwa Wabunge wa upande wa Upinzani walisema kuhusu fedha za miradi ya maendeleo katika Sekta ya Kilimo ambazo zimetolewa kwa asilimia mbili na asilimia 98 hazikuweza kutolewa. Hili naomba nilisemee ili Watanzania waelewe uhalisia, nini Serikali yao inafanya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema wakati najibu hoja ya kwanza kabisa kazi nyingi ambazo zimefanyika katika Sekta ya Kilimo; ni vizuri tukatambua kwamba, bajeti ya Sekta ya Kilimo inajumuisha fedha zinazotengwa kwenye Fungu 43 - Wizara ya Kilimo, Fungu 64 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Fungu 99 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi, upande wa Mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bajeti ya mwaka 2018/ 2019, bajeti iliyotengwa kwa ajili ya Sekta ya Kilimo ilikuwa shilingi bilioni 108.4 na kiasi kilichotolewa siyo shilingi bilioni mbili kama ilivyosemwa na Waheshimiwa Wabunge wengi wa upande wa Upinzani. Kiasi kilichotolewa ni shilingi bilioni 66.2 ambayo ni sawa na zaidi ya asilimia 61 ya fedha yote ambayo ilitengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naendelea kusisitiza kwamba ni muhimu tukawa na takwimu sahihi ili tunaposimama kwenye Bunge lako Tukufu tuweze kuwaleleza Watanzania dhamira njema ya Serikali yao ya kuweza kukiinua kilimo chetu ili kiendelee kuchangia katika ukuaji wa pato letu la Taifa. Tunatambua sana umuhimu wa Sekta ya Kilimo na kama Serikali tutaendelea kuweka nguvu yetu kubwa huko.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikia kengele imegonga lakini niseme pia hoja ya mwisho ya Waheshimiwa Wabunge ambao wamesema ni vizuri tukafanya tathmini, yaani tufanye tathmini tunapokwenda kukamilisha utekelezaji wa Mpango wetu wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano. Tayari Serikali yetu imeanza zoezi hili la kufanya tathmini ya utekelezaji ya Mpango wetu wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano wakati tunaanza kuandaa Mpango wetu wa Tatu wa Maendeleo katika utekelezaji wa Dira yetu ya Taifa mwaka 2020/2025.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna tunaloliogopa kwa sababu tunajua tumetekeleza mengi katika sekta zote na tuko tayari kama Taifa kuwaeleza Watanzania, dhamira yetu ilikuwa ni kuiondoa Tanzania kutoka kwenye Taifa la kipato cha chini kwenda kwenye Taifa la kipato cha kati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vizuri Watanzania wakajua kwamba katika taarifa iliyotolewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika Juni, 2019 inaainisha nchi nne ambazo zimechangia kukua kwa uchumi wa Bara la Afrika. Naomba nizitaje hizo nchi nne mbele ya Bunge lako Tukufu. Nchi ya kwanza ni Djibouti, nchi ya pili ni Ethiopia, nchi ya tatu ni ya Rwanda na ya nne ni taifa letu la Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetenda mengi makubwa, wananchi wanajua, Watanzania wanaelewa na walioko nje ya taifa letu wanaona mengi makubwa yanayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano, na tumekuwa ndani ya nchi nne zilizochangia ukuaji wa asilimia 6.5 wa Pato la Bara letu la Afrika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa miradi mikubwa tunayotekeleza naomba niwaambie Watanzania wasiwe na wasiwasi, tumejipanga tunaweza kukusanya mapato yetu wenyewe, tu natekeleza miradi mingi. Miradi ya afya tunatekeleza; zaidi ya hospitali 67 tumejenga, hii ni kwa ajili ya wananchi wenyewe. Zaidi ya vituo vya afya 352 tumevijenga. Mwaka huu tunakwenda kujenga zaidi ya hospitali nyingine 19 za halmashauri zetu. Hii yote ni kuwafikia Watanzania, ni kuhakikisha kwamba Watanzania wanafikiwa na maendeleo kama ambavyo sisi viongozi wao na viongozi wetu wa kitaifa wanavyotuelekeza kuyatenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie na jambo moja ambalo tumekuwa tukilisisitiza kwa muda mrefu lakini linarudiwa rudiwa sana kutamkwa katika Bunge lako tukufu. Hoja yenyewe ni pale ambapo Kambi Rasmi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba dakika moja.

MWENYEKITI: Malizia tu Mheshimiwa, nakuongezea dakika tano.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni pale ambapo Kambi Rasmi ya Upinzani inaposema Seriakli yetu inavunja Katiba kwa kutokuleta sheria ya kusimamia utekelezaji wa mpango. Leo nimeongea taratibu sana na nimekuwa mpole sana ili niweze kueleweka vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili naomba niseme, Serikali yetu imekuwa ikiheshimu Ibara inayotajwa na Kambi Rasmi ya Upinzani, Ibara ya 63 (3) (c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 iliyoweka sharti ya kutunga sheria ya kusimamia utekelezaji wa mpango wa maendeleo kwa kufanya yafuatayo;

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza, tunalishukuru Bunge lako Tukufu, mwaka 2015 Bunge letu lilipitisha Sheria ya Bajeti Sura 439 ambayo inasimamia uandaaji, uidhinishaji, utekelezaji, tathmini na utoaji wa taarifa za utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Serikali. Kwa hiyo, hiyo ni sheria ya kwanza inayosimamia utekelezaji wa Mipango ya muda mrefu na Mipango ya muda mfupi inayopangwa na Serikali yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kila mwaka Serikai yetu huwasilisha kwenye Bunge lako Tukufu Muswada wa Sheria ya Fedha unaobainisha vyanzo mbalimbali vya mapato vitakavyotumika kugharamia Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa mwaka husika. Naomba tutambue mpango wa maendeleo unatafsiriwa kwenye bajeti ya mwaka husika. Kwahiyo sheria zinazoletwa kwenye kutekeleza bajeti ya mwaka husika ndiyo sheria zinazosimamia utekelezaji wa mpango ule wa mwaka husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kila mwaka Serikali yetu bila kukaidi tumekuwa tukiwasilisha mbele ya Bunge lako Tukufu Muswada wa Sheria ya Kuidhinisha Matumizi ya Serikali kwa Mwaka Unaofuata kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Maendeleo. Kwahiyo naomba niseme nikisimama kwa nguvu zote kifua mbele kwamba hatujavunja Katiba wala sheria yoyote ndani ya nchi yetu kwa sababu tunasema yale yote tuliyoelekezwa na taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kusema kwa Waheshimiwa Wabunge waliotueleza kwamba mpango wetu mapendekezo haya hayakuainisha deliverables au outcomes. Haya ni mapendekezo, tumechukua maoni, tunakwenda kuyafanyia kazi, tutakapokuja na Mpango wetu tutaeleza. Nitoe mfano ambao ulitolewa wakati wa kuchangia kwamba Sekta ya kilimo na likatajwa zao la pamba kwamba hatuna deliverables kama Serikali yaani tunakwenda tu hatujui tunaelekea wapi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukichukua Mpango wa Maendeleo wa mwaka huu tunaoutekeleza ukienda ukurasa wa 86 kwenye kilimo cha kahawa na pamba imeainishwa wazi wazi wapi tupo na wapi tunaelekea. Kwahiyo naomba niseme tumejipanga vizuri, Serikali ya Awamu ya Tano inaongozwa kiuadilifu kabisa na tunaandaa mipango yetu inayotakiwa kwa ajili ya utekelzaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nihitimishe tena kwa kutoa shukrani zangu za dhati kwa Waheshimiwa Wabunge wote waliochangia hoja hii ya Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2020/2021 na Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2020/2021. Aidha nawaomba sana Waheshimiwa Wabunge kwa ujumla wetu tusisite kuendelea kutoa maoni na ushauri wa kuboresha Mpango wetu huu kwani sasa kazi ndiyo imeanza; tunaenda kutekeleza yale yote ambayo mmetuelekeza. Siku zote kama Wizara/ Serikali tunathamini sana maoni, ushauri na mapendekezo yenu. Tuko tayari kuyapokea muda wowote. Kama nilivyoainisha hapo awali, Serikali itazingatia maoni na ushauri wenu wote lakini bila kuvunja sheria na kanuni za nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe wito kwa Waheshimiwa Wabunge wote kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katika dhamira yake ya kujenga Tanzania mpya, Tanzania ya kipato cha Kati, Tanzania ya viwanda. Yanawezekana, tumeanza kuyaona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mambo mengine, nawaomba sana Waheshimiwa Wabunge kuendelea kuwahimiza wananchi wetu kushiriki katika shughuli za maendeleo ili kujiletea mabadiliko chanya katika maisha yao na Taifa letu kwa ujumla lakini bila kusahau kwamba hakuna taifa ambalo liliwahi kuwa huru bila kuwa na mapato yake imara ya ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe sana Watanzania wanaponunua waombe risiti na wale wanaouza waweze kutoa risiti ili tuendelee kukusanya mapato ya Taifa letu. Aidha, mwisho kabisa natoa wito kwa Watanzania wote kushiriki kwa amani na salama kabisa katika uchaguzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa tarehe 24, Novemba 2019 kwani uchaguzi wa Serikali za Mitaa ndio msingi imara wa uchaguzi Mkuu ujao mwaka 2020 japo umeshaonesha kuna green light kwa chama kile kile cha kijani kuendelea kufanya vizuri. Tuendelee kusimama imara tunakwenda kuwatumikia Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema maneno haya naomba nikushukuru tena na naomba kuwasilisha. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Fedha na Mipango
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kunipa fursa hii ya kuchangia hoja hii ya hotuba ya makadirio ya bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa mwaka 2019/2020 kama ilivyowasilishwa na Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango.

Mheshimiwa Spika, naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupatia fursa tena ya kukutana katika Bunge lako tukufu kwa ajili ya jambo hili kubwa kwa ajili ya Taifa letu na Watanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wetu Mheshimiwa Makamu wa Rais na Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi kubwa wanayoifanya kwa niaba ya Watanzania, kwani waliwaamini na sisi tunaona na Watanzania wanaona utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi unavyotekelezwa kwa kasi kubwa kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nikushukuru na wewe binafsi pamoja na Mheshimiwa Naibu Spika, Wenyeviti wote wa Bunge kwa miongozo yenu mnayotupa tunapokuwa kwenye Bunge hili Tukufu ili tuweze kuwatumikia Watanzania kwa ujumla wake tunawashukuruni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nimshukuru sana, Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango Kaka yangu Dkt. Philip Mpango kwa kazi kubwa anayoifanya kwa ajili ya Watanzania kwenye Wizara hii ngumu kama ambavyo imeelezwa na Waheshimiwa Wabunge huu ndiyo moyo wa Serikali yetu, ndiyo roho ya Taifa letu hakika nakupongeza sana Dkt. Philip Mpango kwa kazi kubwa unayoendelea kuifanya na mimi nakutia moyo uendelee kulitumikia Taifa letu wala usirudi nyuma kwamba lazima apatikane Mtanzania wa kulibeba hili kwa kipindi hiki na Mtanzania aliyechaguliwa, Mtanzania aliyeaminiwa, Mtanzania aliyeteuliwa na Mwenyezi Mungu ni wewe kwa ajili ya Taifa letu, usikate tamaa endelea kusimama imara naamini mishale yote inapiga lakini naamini bado uko imara, endelea kusimama imara Mheshimiwa Waziri wangu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema maneno hayo, naomba pia niwapongeze sana, watendaji wetu ndani ya Wizara ya Fedha na Mipango na wao pia naomba niwatie moyo, waendelee kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu wa hali ya juu, wameipata nafasi ya kuwatumikia Watanzania, wawatumikie Watanzania kwa moyo wote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya maneno hayo ya utangulizi naomba sasa niseme maneno machache kwenye hoja ambazo zimechangiwa na Waheshimiwa Wabunge na nianze na hoja ya kwanza ambayo ilisema makusanyo ya kodi yameshuka sana kipindi hiki cha Serikali ya Awamu ya Tano.

Mheshimiwa Spika, naomba niseme jambo hili siyo la kweli hata kidogo, siyo la kweli kwa sababu Watanzania wanaona, Watanzania wanaona yanayotendeka ndani ya Taifa lao, ni kupitia makusanyo ya kodi haya ambayo leo tunaambiwa yameshuka.

Mheshimiwa Spika, kama makusanyo ya Kodi yameshuka, tungeweza wapi kuanza utekelezaji wa mradi wa reli ya kisasa, isingewezakana hata kidogo, isingewezekana leo hii Stiegler’s Gorge kule Rufiji, mradi ule umeanza kutekelezwa kama makusanyo yangekuwa ni ya chini kama inavyodaiwa kwenye Bunge hili tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwaombe Waheshimiwa wabunge, tuwape moyo watumishi wetu wanaoshughulika na kazi hii ngumu ya ukusanyaji wa mapato ya Taifa letu, wanaifanya kazi katika mazingira magumu, wanaifanya kazi hii kwa kujitolea maisha yao, ni kazi ngumu, ni kazi yenye viahatarishi vingi lakini wanaifanya kwa nguvu zao zote.

Mheshimiwa Spika, nimeanza kusema kwamba siyo kweli makusanyo yamepungua kwa sababu ukiangalia kwa miaka mitano mfululizo, tukianza mwaka 2014/2015 makadirio ya ukusanyaji wa Kodi yalikuwa ni shilingi trilioni 11.9, kipi kilikusanywa mwaka 2014/2015.

Mheshimiwa Spika, kilichokusanywa ilikuwa ni trilioni 10.66 hicho ndicho kilichokusanywa 2014/2015 kabla Serikali ya Dkt. John Pombe Magufuli ya Awamu ya Tano haijaingia madarakani, leo tunapoongea mwaka 2017/2019 kipi kimekusanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi ya Awamu ya Tano.

Mheshimiwa Spika, makadirio yalikuwa shilingi trilioni 17.3 haya ni ya kodi, na nini kilikusanywa, kilichokusanywa ilikuwani trilioni 15.25 ukilinganisha haya mambo mawili unaweza ukaelewa, ni kweli mapato yamepungua, makusanyo yamepungua, taarifa hizi bahati nzuri, takwimu za kikodi huwa hazijawahi kudanyanya na hili naomba Waheshimiwa Wabunge tuwatendee haki Watanzania.

Mheshimiwa Spika, Kwa sababu wao ni mashahidi wanaona, wao ni mashahidi wanadhihirisha kile ambacho kinatendwa na Serikali yao waliyoiamini.

Mheshimiwa spika, limeunganishwa jambo hili na jambo la pili kwamba tunaangalia sasa kati ya uwiano, kati ya mapato ya Kodi na Pato la Taifa. Wanasema kwamba limepungua ni kweli uwiano wa Kodi dhidi ya Pato la Taifa kutoka asilimia 13.2 mwaka 2016/2017 hadi imefika Pato la Taifa asilimia 12.8 kwa mwaka 2017/2018.

Mheshimiwa Spika, nini kimetokea? Kilichotokea hii ndiyo naomba Watanzania waelewe, calculations hizi zimefanyika kwa kufuata rebasing ambayo ni marekebisho yaliyofanywa kwenye takwimu za Pato la Taifa, kwamba yamefanywa mabadiliko, na kama tusingetumia rebasing mabadiliko ya takwimu za Pato la Taifa, mchango, uwiano wa kodi dhidi ya Pato la Taifa ilikuwa ni asilimia 3.6. Kwa hiyo kama tungetumia mwaka wa kizio wa 2017, uwiano huu usingekuwa umepungua.

Kwa hiyo, hili linadhihirisha kwamba mapato haya hayajapungua, mapato yako vizuri tukiangalia makadirio yameongezeka na makusanyo halisi yameongezeka, kwa hiyo, tuwatendee haki Watanzania, tuwaeleze ukweli kile ambacho Serikali yao waliyoiamini kipi Serikali inafanya.

Mheshimiwa Spika, naomba niseme kuhusu jambo la pili nayo ni kuhusu Ofisi ya Msajili wa Hazina kwamba ofisi hii bado haijaonyesha uimara wake kwenye kusimamia kampuni na mashirika ya umma. Naomba kulihakikishia Bunge lako tukufu kwamba Ofisi ya Msajili wa Hazina kwa sasa, ni imara sana, na sisi sote ni mashahidi tunaona utendaji mzuri wa watumishi wetu kwenye ofisi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nasema hili kwa sababu tunaiona Ofisi ya Msajili wa Hazina ikiendelea kufanya tathmini na ufuatiliaji ili kuimarisha usimamizi na ufanisi wa mashirika ya umma pamoja na kampuni ambazo Serikali yetu imekeza huko, tunafatilia kwenye hisa chache, lakini pia kule ambako Serikali yetu ina hisa nyingi.

Mheshimiw Spika, matokeo ya hili tumeona kabisa kwamba hata mapato yaliyokusanywa kutoka kwenye gawio, kutoka kwenye kampuni hizi na mashirika ambapo Serikali yetu ina hisa yameongezeka kwa kiwango kikubwa sana.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, kwa mwaka huu wa 2018/2019 ambapo hadi tarehe 30 Aprili, 2019 Ofisi ya Msajili wa Hazina ilikuwa imekusanya shilingi bilioni 602.64 ikilinganishwa na ilichokuwa kimetarajiwa kukusanywa ambayo ilikuwa ni shilingi bilioni 597.77 hii tunaiona ni zaidi ya asilimia 101 na hii ni tarehe 30 Aprili; je, tukienda mpaka tarehe 30 Juni, 2019 tunaiona Ofisi ya Msajili wa Hazina ikiwa inafanya kazi yake vizuri katika kipindi hiki.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Msajili wa Hazina inaendelea pia kushughulikia ukaguzi maalum katika taasisi ambazo Serikali yetu ina hisa chache ambapo tayari mpaka tarehe 30 tulishakagua taasisi 33 na tayari tumeona mapungufu yaliyokuwa yamebainika na mapungufu hayo yanaendelea kufanyiwa kazi ili sasa tuweze kuona taasisi hizi na mashirika haya yakifanya kazi kwa tija kwa ajili ya Watanzania.

Mheshimiwa Spika, Serikali yetu pia imechukua hatua mbalimbali, haya yote yasingewezekana kama Serikali isingeimarisha Ofisi hii ya Msajili wa Hazina na Serikali inaendelea na mambo mbalimbali kuhakikisha Ofisi hii inaendelea kuwa imara ili tuweze kupata faida kwenye taasisi na mashirika haya ambayo tumewekeza, kwa mfano, Serikali tayari imeandaa Waraka wa Baraza la Mawaziri wenye lengo la kurekebisha Sheria ya Ofisi ya Msajili wa Hazina ili kuendelea kuiimarisha zaidi, ili iweze kufanya kazi kwa tija zaidi kwa ajili ya Watanzania wote, lakini pia tumeona Serikali yetu imeongeza Bajeti ya kutosha kwenye Bajeti ya maendeleo kwenye Ofisi hii ya Msajili wa Hazina hadi kufikia shilingi bilioni
2.3 kwa mwaka wa fedha 2019/2020 kutoka bilioni 1.6 tu zilizokuwa za mwaka 2018/2019.

Mheshimiwa Spika, hii yote inalenga kuimarisha mifumo ya usimamizi ya kielektoniki ili tuweze kuyafatilia mashirika na taasisi ambazo tumewekeza kama Serikali yetu.

Mheshimiwa Spika, kuhusu utendaji wa Ofisi ya Msajili wa Hazina, liko jambo ambalo limehojiwa nalo ni malipo ya mafao ya wastaafu 1071 wa TAZARA yamefikia wapi.

Mheshimiwa Spika, napenda kuliambia Bunge lako tukufu kwamba kundi la kwanza ni la wastaafu 1172 walioacha kazi baada ya muda wao wa kustaafu kutimia kama ambavyo ilivyoainishwa katika makubaliano ya pamoja kati ya TAZARA na watumishi hao.

Mheshimiwa Spika, hivyo basi, kwa kuwa wastaafu hawa hawakustahili kulipwa kiinua mgongo kwa sababu walikuwa wametimiza vigezo vya kupata malipo ya pensheni ambayo yanaendelea kulipwa kila mwezi. Pia kulikuwa na kundi la pili ambalo kundi la pili la wastaafu hawa wanastahili kulipwa ambapo Serikali imeridhia kuwalipa kama ifuatavyo na hatua za malipo zimefikia katika hatua mbalimbali, kundi la kwanza ilikuwa ni Shauri la S. Dagaa na wenzake 271 kesi namba 88 ya mwaka 2009 hawa Serikali imeridhia baada ya kesi kuisha waweze kulipwa shilingi trilioni 1.422.

Mheshimiwa Spika, kundi la pili lilikuwa ni Shauri la Kiobya na wenzake ambapo Serikali inatakiwa kulipa jumla ya shilingi bilioni 41.549; Shauri la tatu ambalo ni kundi la tatu wanaostahili kulipwa ilikuwa ni Shauri la Kassim Mshana na wenzake 79 ambapo jumla ya shilingi 814,695,000 zinatakiwa kulipwa kwa ajili ya Kassim Mshana na wenzake 79.

Mheshimiwa Spika, kundi la nne, ilikuwa ni Shuari la Kaduma na wenzake 130 ambapo wanatakiwa kulipwa jumla ya shilingi bilioni 8.042, Ofisi ya Msajili wa Hazina inaendelea kushughulikia malipo yao kwa makundi haya niliyoyataja na muda siyo mrefu basi watalipwa mafao yao kama ambavyo imeelekezwa na mahakama.

Mheshimiwa spika, jambo lingine ambalo limeelezwa kwa urefu na ambalo limekuwa likirudia mara kwa mara nayo ilikuwa ni malipo ya wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Spika, malipo kwa ajili ya wastaafu hawa Serikali ilishayamaliza, hii ni kwa mujibu wa hati ya makubaliano yaani deed of settlement ya tarehe 20 Septemba, 2005 na kuthibitishwa na mahakama kama hukumu tarehe 21 Septemba, 2005 Serikali tayari ilishawalipa stahiki zao wastaafu hawa waliokuwa 31,788 wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyovunjika tarehe 30 Juni, 1977.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema haya, naomba nirejee kusema naunga mkono hoja hii ya Wizara ya Fedha na Mipango na nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata fursa hii ya kuchangia hoja ambazo zimewekwa mezani. Kwanza kabisa nami nianze kwa kutoa pole kwa familia ya Marehemu Mzee wetu, Mzee Kingunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nitoe hongera sana kwa Wenyeviti wote watatu kwa kuwasilisha vizuri kabisa hoja za Kamati zao mbele ya Bunge lako Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie katika suala hili na moja kubwa ambalo nataka kuanza nalo ni hiki ambacho kinaelezwa kama mkanganyiko wakati hakuna mkanganyiko wowote ambacho ni kuhusu Kodi ya Majengo. Naomba niiseme vizuri na ikiwezekana nitumie dakika zangu zote saba na Waheshimiwa Wabunge naomba mnisikilize kwa umakini na kwa pamoja tunapofanya maamuzi tufanye

maamuzi tukiwa tunaelewa nini tunafanya ndani ya Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, imesemwa vizuri mwaka 2016/2017, Serikali ilikuja hapa Bungeni na Sheria ya Fedha ya mwaka huo na tukaleta ndani ya sheria kodi hii ikusanywe na Mamlaka ya Mapato Tanzania lengo likiwa ni ufanisi. Tulipoleta tulifungua na akaunti maalum kwa ajili ya kuweka pesa hizi za Kodi ya Majengo katika Benki Kuu ya Tanzania. Tulifungua akaunti hiyo tukiwa na dhamira ya dhati ya kukusanya na kuzirejesha kule zilivyo na ndicho tulichokifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kutokana na historia ambayo sio njema, imesemwa hata jana wakati Kamati ya LAAC na PAC walipowasilisha taarifa zao humu ndani kuhusu matumizi yasiyo mazuri kwenye Halmashauri zetu. Pesa za miradi zinazopelekwa hutumika ndivyo sivyo. Kama Serikali na Wizara ambayo tumepewa mamlaka ya kusimamia mambo ya fedha hatuwezi kuacha haya yanaendelea kutendeka ndani ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kKwa umakini mkubwa wa Serikali yetu ya Awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli anayechukia ufisadi, anayechukia ubadhirifu wa fedha za umma, ikaja ndani ya Bunge lako Tukufu na tukaleta hoja kwamba pesa hizi zikusanywe na Mamlaka ya Mapato na zitarejeshwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niisome sheria tuliyoipitisha, baada ya kukusanywa kwa ufanisi tukasema, the apportionment and disbursement of the proceeds collected under this section shall be made to a Local Government Authority based on its budget. Nini tunabishana ndani ya Bunge lako Tukufu, sheria iko wazi na ndicho tunachokifanya kama Wizara, ndicho tunachokifanya kama Serikali. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala hili, kwanza naomba nitoe caution kwa Bunge lako Tukufu, tumwogope kama ukoma mtu anayetaka kuligawa Taifa hili vipande vipande. Tumekusanya tumeonesha ufanisi, matumizi sio mazuri na nini tumefanya baada ya kukusanya, tunazirejesha kulingana na sheria ilivyotuelekeza, according to the budget of the Local Government Authority, ndicho sheria inavyosema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, waambie tu watulie, tuwafundishe ili waweze kufahamu, hiki haiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa leo tukisema kule Geita wakusanye kodi kutoka kwenye madini ibaki Geita na kule Manyara Mererani wakusanye kodi inayotokana na Tanzanite ibaki Mererani hatutokuwa na Taifa na Dar es Salaam wachukue kodi yote inayotoka bandarini wapi Taifa hili linakwenda? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe mfano mmoja ambao umesemwa hapa bajeti ya maendeleo kwa fedha za ndani kwa Mkoa wa Dar es Salaam ni shilingi bilioni 14.2, nini Serikali tumefanya kwa pesa za ndani kwa Mkoa wa Dar es Salaam? Tumepeleka shilingi bilioni 11 ambayo ni asilimia 79, tunapeleka kwa Mkoa wa Dar es Salaam. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepeleka shilingi bilioni 11, nini tumekusanya kwenye Kodi ya Majengo Mkoa wa Dar es Salaam. Kwenye Kodi ya Majengo Mkoa wa Dar es Salaam tumekusanya shilingi bilioni 10 na sisi tushapeleka shilingi bilioni 11, hii ndiyo Kodi ya Majengo tunayoulizwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wapi tunataka kuelekea? Jambo la msingi kabisa tunalotaka kulielewa hapa, tuwaulize hao wa Kinondoni wanaosema wao wakikusanya ni mradi upi Halmashauri ya Kinondoni iliwahi kutelekeza kupitia Kodi ya Majengo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, watutajie tu mradi mmoja na kwenye bajeti ya mwaka huu, ndiyo maana nasema watulie, watueleze bajeti item iliyosema tutakusanya Kodi ya Majengo kiasi hiki na itakwenda kujenga kitu fulani twende kwenye bajeti ya Halmashauri ya Kinondoni. Kwa hiyo, tusiwadanganye Watanzania, tukalikatakata Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe mfano mwingine mdogo kwenye kodi hii ili Waheshimiwa Wabunge tuelewane na tufanye maamuzi sahihi. Nini kimekusanywa Halmashauri ya Kinondoni kwa mwaka elfu mbili, Mheshimiwa Halima analidanganya Bunge lako, Halmashauri ya Kinondoni mwaka 2014/2015 ilikusanya shilingi bilioni tano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukapeleka kwenye maendeleo zaidi ya shilingi bilioni tisa, Kinondoni peke yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe Wabunge wanaopenda haki, wanaotaka Taifa letu liendelee kuwa Taifa moja kama tulivyoapa, tushikamane kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba nianze kwa kumshukuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema aliyetufikisha katika hatua hii asubuhi hii ya leo ikiwa ni kuhitimisha hotuba ya bajeti ya nne ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba pia niwashukuru sana wazazi wangu wawili kwa kuendelea kuniweka kwenye maombi mtoto wao ili niweze kuwatumikia Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba pia nimshukuru sana Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuendelea kuniamini kwa mwaka wa nne huu nikiwa ndani ya Wizara ya Fedha na Mipango, hakika imani hii ni kubwa kwangu na naomba kumhakikishia kwamba sitamuangusha yeye wala Wanakondoa walioniamini kunileta katika Bunge hili tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba pia nikushukuru sana wewe kama kiongozi wa Bunge hili Tukufu kwa jinsi unavyoliendesha Bunge hili kwa viwango na kwa jinsi ambavyo upo imara kusimamia maendeleo ya Taifa letu. Nikushukuru sana ukiwa kama kaka yangu kutoka Mkoa wa Dodoma kwa miongozo na malezi yako kwangu hakika unaendelea kunijenga. Nakushukuru sana na nakuombea kwa Mwenyezi Mungu baraka tele na afya njema. Ahsante sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba pia shukrani hizi nizielekeze kwa kiongozi wetu wa Serikali ndani ya Bunge lako Tukufu Mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa kwa miongozo na maelekezo yake anayoendelea kutupatia kama Wizara na kama Serikali. Nina hakika Watanzania wanaiona kazi nzuri unayoifanya Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mwenyezi Mungu aendelee kukujalia busara na afya njema ili uendelee kuwatumikia Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba pia nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, kwangu mimi kufanya kazi na huyu Mheshimiwa Waziri ni fursa kubwa sana, najifunza mengi, mazuri kutoka kwake. Hakika naendelea kuwa mwanafunzi mzuri kwake na namwahidi kuendelea kuwa msaidizi wakw wa karibu ili aweze kutekeleza majukumu yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia niwashukuru sana familia yangu, mume wangu Dkt. Muhajiri Kachwamba na rafiki yangu wa karibu kwa miaka 20 sasa. Hakika nafasi aliyonipa ni kubwa sana kwenye maisha yake na mchango wake kwenye mafanikio yangu ni mkubwa sana. Namshukuru sana kwa kuendelea kuniamini, kuendelea kunisaidia niweze kutenda majukumu yangu. Kwa watoto wangu pia nawashukuru sana, najua wamekuja likizo, lakini mama anarudi saa tano, saa sita usiku wanaendelea kunivumilia, nasema waendelee kunivumilia kwa sababu niliiomba nafasi ya kuwatumikia Watanzania na nimeipata nafasi hii waendelee kunivumilia, nitarejea kukaa nao pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, shukrani zangu za mwisho lakini si kwa umuhimu, ni kwa wapiga kura wangu wa Jimbo la Kondoa, hakika waliniamini mwaka 2015, wakiwa wananijua kidogo sana, lakini sasa wamenijua kwa utendaji wa kazi katika Jimbo la Kondoa, lakini kwa kuwatumikia Watanzania. Naomba niwaambie Watanzania, Wanakondoa kwamba, sitawaangusha, nitaendelea kulisimamia Jimbo la Kondoa, liko imara na nawahakikishia Chama cha Mapinduzi mwaka 2019 Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa tutashinda kwa asilimia 100 na mwaka 2020, mimi Mbunge wao nitarejea ndani ya Bunge hili kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba sasa nianze kuchangia hotuba hii iliyowekwa mezani na Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango na naomba nianze kwa kulisemea jambo la biashara, hali ya biashara ndani ya Taifa letu, ambalo yalisemwa maneno makali sana dhidi ya Waziri wa Fedha na Mipango, dhidi yangu mimi msaidizi wake kwamba sisi tunashangilia ufungwaji wa biashara ndani ya Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, tukaambiwa, Kariakoo imekufa kwa sababu ya Waziri wa Fedha na Mipango na Naibu wake kwa sababu tumeshindwa kusimamia. Pia ikasemwa kwamba, kwa nini tumechelewa kufanya maamuzi ya kuzuia ufungaji wa biashara, hadi mwaka wa nne ndiyo Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango anakuja kuzuia ufungaji wa biashara.

Mheshimiwa Spika, naomba kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, kuanzia hotuba ya bajeti ya mwaka wa kwanza, Mheshimiwa wa Fedha aliyewasilisha ndani ya Bunge lako tukufu, mwaka 2016/2017, aliwaelekeza watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, ni marufuku kufunga biashara ya mfanyabiashara yeyote yule bila kufuata utaratibu na sheria zinazowaelekeza hivyo.

Mheshimiwa Spika, mambo hayo yalisemwa ndani ya Bunge lako Tukufu, kwa hiyo kuja leo kumlaumu Mheshimiwa Waziri wa Fedha, siyo sahihi hata kidogo na amechukua jitihada za kutosha Mheshimiwa Waziri wa Fedha kuhakikisha biashara hazifungwi kwa sababu tu ni watumishi wa Mamlaka ya Mapato wanataka kufunga, hapana, zipo sheria zinazowaelekeza kufanya hivyo.

Mheshimiwa Spika, lakini niseme jambo la pili, katika soko huria, moja ya sifa za uchumi wa soko huria ni uhuru wa kuanzisha biashara na uhuru wa kufunga biashara, yaani tunasema kuna free entry and exit from the market. Kwa hiyo, tukiangalia sana wengi waliofunga biashara siyo kwa sababu wamelazimishwa kufunga biashara na watumishi wetu wala na viongozi wa Serikali yetu wala na Waziri wa Fedha na Mipango.

Mheshimiwa Spika, kwenye uchumi wa soko huria ambao Taifa letu lipo, ifahamike kwamba biashara pia zinaweza kufungwa kwa sababu mbalimbali. Sababu ya kwanza, yaweza kuwa ni kubadilisha aina ya biashara, mfanyabiashara ambayo amekuwa akiifanya, lakini pia yaweza kuwa kwa sababu ya ushindani mkali katika biashara husika, hiyo inaweza kupelekea pia mfanyabiashara akabadilisha biashara yake. Vile vile yawezekana, ni kushindwa kuisimamia biashara yake husika, lakini yawezekana pia biashara ambayo wamekuwa wakiifanya, walikuwa kwenye shareholding na wameshindwa kuelewana, wanaamua kui-dissolve biashara yao ili waweze kufanya biashara nyingine.

Mheshimiwa Spika, katika sababu hizi, haijaachwa nje pia hata sababu ya kwamba mfanyabiashara huyu ana mzigo mkubwa wa madeni, aidha kwenye benki za biashara au kwenye taasisi zozote za kibenki, lakini pia hata yawezekana ana madeni ya kikodi na kama tunavyofahamu, kodi hukusanywa kwa kufuata sheria.

Mheshimiwa Spika, hizi zaweza kuwa ni sababu zilizopelekea baadhi ya biashara kufungwa. Nipende kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, zipo tafiti ambazo zimefanyika duniani na zote zikabainisha kwamba, zaidi ya asilimia 50 ya biashara za ukubwa wa kati na ukubwa mdogo, hufa kabla ya kusherekea birthday yao ya mwaka wa tano. Kwa hiyo, yawezekana hii pia ikawa ni hali ile ya kawaida ya biashara hizi za saizi ya kati na saizi ya ukubwa mdogo ambazo zinaweza kuwa zinakufa ni kwa sababu ya sababu hizi nilizozitaja na hii si kwa Tanzania tu, hii ni kwa dunia nzima kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge, kwamba, nilituhumiwa pia kwamba nimekuwa nikijisifu kwa kuzifunga biashara hizi ndani ya Taifa letu. Naomba nikiri ndani ya Bunge lako Tukufu, kitu ambacho nimekuwa nikikisimamia kama Naibu Waziri wa Fedha na Mipango ni kuhakikisha sheria zinafuatwa ndani ya Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, nikitoa mfano, wakati nachangia hotuba ya Viwanda na Biashara, liliongelewa sana tatizo la kufungwa kwa biashara na zikatolewa takwimu ambazo siyo sahihi ndani ya Bunge lako Tukufu. Ilinilazimu kueleza ukweli, kuwaeleza Watanzania, nini uhalisia ndani ya Taifa lao ili waweze kufahamu.

Mheshimiwa Spika, ukiniruhusu naombakunukuu nilichokisema. Siku ya tarehe 15 mwezi wa tano mwaka 2019 nilisema maneno yafuatayo:-

“Kwamba ni kweli zipo biashara zinazofungwa na zipo biashara zinazofunguliwa. Nikasema, kwa Tanzania kwa mwaka huu mmoja biashara zilizofungwa ni 16,252 na biashara zilizofunguliwa ni 147, 817.”

Mheshimiwa Spika, nililazimika kutoa takwimu hii kwa sababu ilihojiwa ndani ya bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara. Hata hivyo, siyo sahihi, tukiangalia takwimu hizi siyo sahihi kusema ndani ya Taifa letu biashara nyingi zinafungwa kuliko zinazofunguliwa. Kisayansi kinachotakiwa kufanyika, baada ya kujiridhisha na biashara zinazofungwa na kufunguliwa, ni kwenda kufanya utafiti sasa wa kisayansi, tuweze kujiridhisha biashara zinazofunguliwa ni za ukubwa gani, ni katika sekta zipi na sababu zipi zinazopelekea kufungwa kwa biashara hizi. Wizara ya Fedha na Mipango kupitia Kitengo chake cha Utafiti na Sera kinaendelea kufanya utafiti huu ili tuweze kujiridhisha, nini kinasababisha biashara hizi kufungwa na ni zipi zinazofunguliwa na sababu zinazosababisha zifunguliwe ili tuweze kama Serikali kuzilea biashara hizi.

Mheshimiwa Spika, pia nilisema kwenye Bunge lako Tukufu siku hiyohiyo kwamba, ni muhimu tukajiuliza maswali, kama kweli yanayosemwa, tunayotaka kuamisha Watanzania, kwamba biashara nyingi zinafungwa kuliko zinazofunguliwa, nilihoji maneno yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, nilisema na leo naomba nirudie kuyahoji maswali haya; swali la kwanza nikasema; kama ni kweli biashara nyingi zinafungwa, je Serikali ingeweza wapi kuongeza ukusanyaji wa mapato tangu Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani, kwa mwezi kwa zaidi ya asilimia 75, kama biashara kweli zinafungwa? Tumetoka shilingi bilioni 870 kwa mwezi na sasa tunakusanya trilioni 1.3, kama biashara zinazofungwa ni nyingi zaidi kuliko zinazofunguliwa wapi tungeyapata mapato haya.

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili la kujiuliza, kama kweli biashara nyingi ambazo ni chanzo kikubwa cha mapato ya Serikali yetu, Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi ya Awamu ya Tano, isingiweza kulipa mishahara ya watumishi wetu ndani ya tarehe 20 kila mwezi zaidi ya bilioni 580 kila mwezi, kama kweli chanzo hiki cha mapatao kimefungwa, wapi tunazipata fedha hizi.

Mheshimiwa Spika, vile vile nikasema, ni vizuri tukajiuliza, zaidi ya asilimia 85 ya bajeti iliyokwenda kwenye miradi ya maendeleo kwa mwaka huu wa fedha, ni fedha zetu wenyewe za ndani. Kama biashara zinafungwa, Serikali ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli inatoa wapi fedha hizi kwenda kugharamia zaidi ya asilimia 85 ya miradi ya maendeleo inayotekelezwa!

Mheshimiwa Spika, ni vizuri pia tukafahamu kwamba Wiraza ya Fedha na Mipango, hatuwezi kukaa kimya tunapoona watumishi wetu wanaendelea kuvunja sheria na hatuwezi kukataa, wapo baadhi ya watumishi wetu, ambao siyo waaminifu wakishirikiana pamoja na wafanyabiashara ambao siyo waaminifu kulinyima Taifa letu mapato. Hili hatuwezi kulivumilia, tunapogundua mfanyabiashara anakwepa kodi kwa makusudi, hatuwezi kulivumilia, kwa sababu tumeaminiwa ili kuhakikisha Taifa hili linapata mapato yake, lazima tusimame imara.

Mheshimiwa Spika, nitoe mfano mmoja wa jinsi tunavyoshughulikia, kwa mfano, kati ya mwezi Mei, 2017 hadi mwezi Aprili, 2019, zaidi ya watumishi 30 wa Mamlaka ya Mapato Tanzania walisimamishwa kazi kutokana na utovu wa nidhamu katika kazi zao za kila siku, hili hatuwezi kulivumilia, tutasimamia kwa watumishi wa Mamlaka ya Mapato, tutasimamia kwa wafanyabiashara ambao siyo waaminifu kuhakikisha kwamba biashara zinaendelea kufanywa, biashara halali kwa ajili ya mapato halali ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitoe mifano miwili ili tuweze kuelewa na Watanzania waielewe Serikali yao ya Chama cha Mapinduzi nini inataka. Tarehe 19 Aprili, nilipokea wageni ofisini kwangu, walikuwa ni vijana watatu wakiwa wametoka Mkoa wa Kagera na kutoka Mkoa wa Mwanza, wamekuja ofisini kwangu wakija kulalamika, wanakuja kulalamika kwamba wamepewa assessment kubwa ya kodi.

Mheshimiwa Spika, nilianza kuifuatilia ile kesi, nilipoifuatilia ile kesi yaliyojiri, ndiyo maana nasema, tunao baadhi ya watumishi wetu ambao siyo waaminifu na baadhi ya wafanyabiashara ambao siyo waaminifu. Kilichojiri, zilikuwa ni malori manne ya tani 10 yaliyobeba vitenge vilivyotoka China, maroli haya manne yalikuwa yametoka wapi, maroli manne haya yalikuwa yamepita Bandari ya Dar es Salaam yakiwa ni transit, ni mizigo inayokwenda nchi jirani. Malori yale yanaonekana yamepita mpaka katika mpaka wetu wa Mtukula, yalipopita Mtukula hayakwenda Uganda yakageuza kurudi Tanzania tena. Yalipofika mpakani tukawa tumepata taarifa hizi, yakasimamishwa, kuangalia hawana document hata moja inayoonyesha malori hayo yamekwenda Uganda na kwa nini yanarudi Tanzania.

Mheshimiwa Spika, kuja kufuatilia, tayari kuna mfumo, kati ya watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania kutoka Bandari ya Dar es Salaam, Makao Makuu na mipaka yote mpaka yalipoingia Uganda. Walipokuja wale vijana, hawakuwa wenye mizigo, wale vijana waliokuja walikuwa ni madalali ambao wanakusanya kodi halali kutoka wa wafanyabiashara, lakini wao madalali wanalipa kiwango kidogo sana cha fedha waki-collude na watumishi wetu. Kwa jambo kama hili, hakika tumeaminiwa, lazima tulismamie, lazima walipe kodi na lazima mfanyabiashara wa aina hii kulingana na sheria, zile lori zote nne zilitaifishwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo hili lazima tulisimamie, kwa sababu tunahitaji mapato ili tuweze kuwahudumia Watanzania, kwenye afya zao, Watanzania kwenye shule zao na Watanzania kwenye, watoto wetu kulipiwa ada na Serikali yao.

Mheshimiwa Spika, kama hilo ndilo linalotafsiriwa, Ashatu anakuja kushangilia kufungwa kwa biashara, hilo naomba nimwambie Rais wangu, nitaendelea kusimamia. Hilo naomba niwaambie Watanzania, sitoruhusu waibiwe, nikiwa Naibu Waziri wa Fedha, sitofanya hivyo. Lazima nitasimama imara na kodi zote zitakusanywa kulingana na sheria tulizozipitisha ndani ya Bunge lako Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba sasa niende kwenye hoja ya pili, hoja ya pili ambayo ningependa kuisema mbele ya Bunge lako tukufu, nikiwa nachangia hotuba hii ya Bajeti Kuu ya Serikali, ni kuhusu kufutwa kwa kodi ya ongezeko la thamani kwenye taulo za kike.

Mheshimiwa Spika, hata nisipo-declare interest mimi ni mwanamke, mimi ni mwanamke na mimi nina mchango wangu kwenye kila kinacholetwa na Waziri wa Fedha ndani ya Bunge lako Tukufu. Yameongelewa maneno magumu sana, ambapo, nikamwambia Mheshimiwa Waziri wa Fedha jambo hili naomba nilibebe mwenyewe. Naomba niwaeleze Watanzania, mimi nikiwa kama mwanamke, naijua adha hii na halipendezi hata kidogo Waheshimiwa Wabunge, naomba tu niseme, haipendezi hata kidogo kwa maneno aliyoelezwa Waziri wa Fedha ndani ya Bunge hili Tukufu na lazima tufahamu Waheshimiwa Wabunge, Waziri wa Fedha anapoleta hoja hapa ndani ya Bunge hili, inakuwa ni hoja ya Serikali, siyo hoja ya Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunapotoa tuhuma hizi, hasa zile ambazo ni personal attack, naomba tufahamu ana moyo, hakuondolewa nyongo Mheshimiwa Waziri wa Fedha, anaumia kama mwanadamu, lazima tujitafakari, lazma tuvae viatu vyake, lazima tujiulize ningekuwa ni mimi nikaelezwa maneno haya ningejisikiaje. Inakera na inaumiza, lakini naomba niwaambie Watanzania, dhamira ya Serikali yao ni njema sana. Kama ambavyo nimekuwa nikisema siku zote kwenye Bunge hili Tukufu, kodi ina mchango mdogo sana kwenye bei ya mwisho ya bidhaa. Hili limejidhihirisha, Bunge lako Tukufu kwa dhamira njema, kama ambavyo Serikali yetu ilileta ndani ya Bunge lako Tukufu, tulipitisha kuondolewa kwa kodi hii ya ongezeko la thamani kwenye taulo za kike.

Mheshimiwa Spika, yamesemwa maneno mengi sitaki kuyasikia, kwamba bajeti hii is gender insensitive! Nikasema nirudi pale ofisini kwangu nikaangalie, hivi ni kipi kinachosababisha bajeti ya Serikali, Serikali iliyoaminiwa na wananchi kuliongoza Taifa hili, kwamba iambiwe bajeti yake ni insensitive, hivi kweli, ni taulo ya kike ya Sh.2,500 tu! Nikajiuliza maswali mengi, nikarudi kuangalia what is gender budgeting. Gender budgeting haimaanishi item moja na item hii mchango wake ni upi katika uchumi wa mwanamke, katika uchumi wa Taifa.

Mheshimiwa Spika, nikarudi kikasema nianze na afya ya mwanamke, Serikali ya Awamu ya Tano imefanya nini, Serikali ya Awamu ya Tano imefanya makubwa kwenye afya ya mwanamke. Nikisema kwa mikoa michache, nikianza na vituo vya afya, hospitali za wilaya tulizojenga katika mikoa yetu, tunakwenda kum-target mwanamke. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikiongelea Mkoa wa Simiyu peke yake tumepeleka bilioni 4.5 kwa ajili ya kujenga hospitali kwenye halmashauri zake ili wanawake waweze kupata huduma bora za afya.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Geita tumepeleka bilioni tatu; hii ni kwa mwaka mmoja tunaangalia afya ya mwanamke.

Mheshimiwa Spika, tukiichukua Kanda ya Ziwa yote tumepeleka kwa mwaka mmoja bilioni 22.5 kwa ajili ya afya ya Watanzania ambapo mtu wa kwanza tunayemwangalia ni mwanamke wa Kitanzania.

Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge wanajua; katika vitabu vya Wizara ya TAMISEMI vya bajeti tulionesha nini tumepeleka. Serikali ya Chama cha Mapinduzi inamjali sana mwanamke, na sisi kwa pamoja tumekiri hapa mwanamke wa Tanzania akiwa kijiji, akiwa mjini ndiye anayelilisha taifa hili. Nikajiuliza sana, kwamba huyu Mwanamke anayelilisha taifa ndiye anashindwa kuwa na shilingi 3,000 kwa ajili ya kununua taulo ya kike kwa mwezi? Hili lazima tuliangalie katika uwanda mpana ili tuweze kuelewa kwa pamoja.

Mheshimiwa Spika, naomba niseme, baada ya kuwa tumeondoa kodi hii ya ongezeko la thamani kwenye taulo hizi za kike nini kimetokea; Serikali yetu haikukaa kimya tukasema tulifuatilie jambo hili, kwamba je, kuna athari yoyote iliyokwenda kwa wanawake? Ikafanywa study katika Wizara ya Viwanda na Biashara, Mamlaka ya Mapato Tanzania na Fair Competition Commission. Nini kilijiri mpaka leo tuje tuseme kwamba bajeti hii haikumuangalia mwanamke kwa jicho la pekee? Kilichojiri ni kwamba tuligundua kwamba kuondolewa kwa kodi hii; kwanza wanawake wengi hawajui kama kodi hi imeondolewa. Hili lilikuwa jambo la kwanza.

Mheshimiwa Spika, kwenye Bunge lako ikasemwa wapo kwamba watu walioalikwa mpaka mikutano ya kimataifa kwenda kupongezwa kwa ajili ya kuondolewa kwa kodi hii; unapongezwa kwa ajili ya jambo gani?

Mheshimiwa Spika, nilishaona watu wanapewa tuzo kwa ajili ya wanawake lakini unaulizwa umefanya nini kupewa tuzo hiyo? Unaitwa kwenda mataifa mbalimbali kwenda kupongezwa wakati ndani ya taifa lako hujasimama kuwaambia wanawake kwamba kodi hii imeondolewa kwa ajili yenu. Kwahiyo hili lazima tiliangalie kwa jicho pana ili tuweze kuelewa.

Mheshimiwa Spika, baada ya kujua wanawake wengi hawajui pia tukakuta jambo la pili. Kwamba athari iliyopatikana bei haijapungua kule ambako tulidhamiria bei ipungue. Bado taulo iliyouzwa shilingi 2,500 leo hii bado inauzwa shilingi 2,500, taulo iliyouzwa 5,000 bado leo hii inauzwa shilingi 5,000.

Mheshimiwa Spika, badaa ya kuondolewa kwa kodi hii nini kilitokea kwenye viwanda vyetu vya ndani? Kilichotokea kwa viwanda vyetu vya ndani ni viwanda vyetu vya ndani kupunguza uzalishaji wa bidhaa hii. tunapopunguza uzalishaji nini tunajifunza? Tukipunguza uzalishaji tunakwenda kuondoa ajira za vijana walioajiriwa kwenye viwanda hivi vya ndani. Hizi ni athari hasi baada ya kuondoa kodi hii ya ongezeko la thamani kwenye taulo za kike.

Mheshimiwa Spika, Serikali yetu haikuishia hapo; tukakaa chini tukatafakari nini cha kufanya? Tukasema jambo la la kwanza ni kuendelea kuodoa asilimia 10 ya import duty (ushuru wa forodha) kwenye mali ghafi zote zinazozaloisha taulo za kike. Hii iliondolewa tangu mwaka 2012, lakini ilisemwa kwenye Bunge hili kwamba haijaondolewa. Naomba niwaambie Watanzania tunawajali sana wanawake. Tuliondoa uhuru huu wa forodha wa asilimia 10 tangu mwaka 2012.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili tukasema; ukiangalia bidhaa hii ya taulo za kike ni bidhaa ya muhimu ambayo whether bei imepanda au haijapanda lazima itatumika tu. Unapokuwa na bidhaa ya namna hii wachumi tunaiita ni necessity goods, haiwezi kutibiwa kwa ajili ya measures za kikodi peke yake. Unapokuwa na bidhaa ya aina hii lazima uwe na measures za kikodi lpamoja na measures za kibajeti na measures nyingine za kiutawala ili uweze kuwasaidia hawa wanaotakiwa kutumia bidhaa hii.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali ya Chama cha Mapinduzi inamjali mwanamke wa Tanzania, baada ya kuondoa asilimia 10 ya ushuru wa forodha tukasema tunaondoa asilimia tano ya kodi ya mapato ya viwanda vipya vitakavyoanzishwa kwa ajili ya kutengeneza taulo hizi za kike.

Mheshimiwa Spika, hii tumeiondoa kwa muda wa mika miwili. Hata hivyo, Bunge lako Tukufu na Waheshimiwa Wabunge wakasema hii haitoshi na Serikali yenu ya Chama cha Mapinduzi inawasikiliza, imekubali kwamba tunaondoa tena asilimia tano kwa ajili ya kodi ya mapato kwa viwanda vya ndani vinavyozalisha bidhaa hii kwa miaka miwili mfululizo. Kwahiyo mwanzo tulisema viwanda vingine hatuna uhakika kama vitakuja lakini sasa tunaondoa kwa viwanda vya ndani ambavyo tayari vinazalisha, tunawapunguzia asilimia tano ili waweze kuionyesha kama ina athari hiyo.

Mheshimiwa Spika, nimsema measures za kikodi pake yake haziwezi kujibu jambo hili. Serikali yenu ya Chama cha Mapinduzi iliyoaminiwa na Watanzania tumekuja na suluhisho pia la aina nyingine, nayo ni kuanzishwa viwanda vinavyotumia PPP ambavyo vimefika kwenye hatua kubwa ambayo tunaamini ndani ya mwaka huu wa fedha viwanda hivyo vitakuwa vimekamilika.Ni kiwanda kinachojengwa katika Mkoa wa Simiyu ambacho kinajengwa na NHIF na kinajengwa na Workers compensation pale Bariadi-Simiyu ili kiweze kuzalisha taulo hizi za kike. Kitakapozalisha taulo hizi za kike kwa sababu Serikali ina mkono wake, Serikali sasa itakuwa na uwezo wa ku-control bei za bidhaa inayozalishwa na kiwanda hiki.

Mheshimiwa Spika, tukiweza ku-control bei nini maana yake; hata wazalishaji wengine sasa wakiona viwanda vyetu hivi vimezalisha bidhaa za kutosha nao watashusha bei. Hiyo ni Serikali ya Chama cha Mapinduzi ikiwa inawaangalia Watanzania wote kwa ujumla wake pamoja na kuangalia makundi mbalimbali ili yaweze kufanya majukumu yao ya kimaendeleo.

Mheshimiwa Spika, tukiacha kiwanda hiki cha Simiyu kuna kiwanda kingine kinajengwa Pwani. Kiwanda hiki kinajengwa Pwani na MSD ambao nao wako katika hatua ya mwisho na mkataba unasainiwa ndani ya siku hizi mbili. Ndani ya mwaka huu mmoja kiwanda hiki pia kitakuwa kimeanza kuzalisha bidhaa hii na hatimaye tutaiuza kwa bei ya chini na tutamfikia mwanamke kule alipo.

Mheshimiwa Spika, haya ndiyo ambayo tumesema tuyaseme kama Serikali kwa ajili ya bidhaa hii kwa kuwa sisi ni wasikivu tumesikia na tunakuja na suluhisho za aina tatu ili kiukweli tuweze kuwasaidia Watanzania.

Mheshimiwa Spika, naomba niseme jambo moja la mwisho nalo ni kuhusu miradi ya PPP, kwanini Serikali haitaki kutekeleza;

Mheshimiwa Spika, Serikali inalishukuru Bunge lako tukufu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Malizia Mheshimiwa Waziri, dakika moja.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, Serikali inalishukuru Bunge lako Tukufu kwa kuwa iliruhusu kufanya mabadiliko kwenye Sheria ya PPP na tukisoma kwenye mipango yetu ya maendeleo, Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano na pia Mpango wa Maendeleo wa Mwaka Mmoja, Serikali iko tayari kushirikiana na wadau binafsi katika kuwekeza kwenye maeneo muhimu kwa ajili ya uchumi wa taifa letu.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema haya naomba niseme naunga mkono hoja na nashukuru kwa kunipa fursa hii.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo
MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, naunga mkono hoja na naomba stakabadhi ghalani kwa Dodoma tuondoleeni, ni usumbufu mkubwa. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara
WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mnamo tarehe 6 Mei, 2022 niliwasilisha katika Bunge lako Tukufu hotuba ya bajeti ya Wizara yangu ikiainisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara kwa mwaka, 2022/2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kukushukuru, Mheshimiwa Spika pamoja na Mheshimiwa Naibu Spika, kwa namna ambavyo mmeongoza na kusimamia vyema majadiliano ya bajeti ya Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara. Nawashukuru pia Waheshimiwa Wabunge wote kwa michango yao waliyotoa kwa njia ya kuzungumza na maadhishi pia, maoni na ushauri wenu tumeuchukua kwa ajili ya kuufanyia kazi ili tuweze kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme kuwa ninatambua na kuthamini dhamira na nia njema iliyotawala mjadala huu ambao kimsingi ulilenga kuboresha mikakati na mbinu za kisekta, zitakazotekelezwa katika mwaka 2022/2023 na hata kuelekea mbele zaidi na hivyo kutoa mchango unaotakiwa kwa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuishukuru sana Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile Mbunge wa Mufindi Kusini na Makamu Mwenyekiti wetu Eric James Shigongo Mbunge wa Buchosa, pamoja na Waheshimiwa Wajumbe wote wa Kamati kwa maoni na ushauri mzuri waliotupatia kwa ajili ya kuboresha utendaji kazi ndani ya Wizara yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Martha Nehemia Gwau Mjumbe wa Kamati, kwa kuwasilisha vema Taarifa ya Kamati kwa niaba ya Mwenyekiti, hongera sana. Aidha, napenda kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote ambao wamechangia kuanzia mwanzo mpaka mwisho na kipekee kabisa, naomba pia nimshukuru Kaka yangu Mheshimiwa Mohamed Hussein Bashe Waziri wa Kilimo kwa kuchangia hoja hii na kutoa ufafanuzi wa hoja ambazo zimeibuliwa na Waheshimiwa Wabunge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipekee kabisa napenda kumshukuru Naibu Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Mheshimiwa Exaud Silaoneka Kigahe Mbunge wa Mufindi Kaskazini, kwa kutoa ufafanuzi wa baadhi ya hoja za Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ninawashukuru Watendaji wote ndani ya Wizara yetu wakiongozwa na Katibu Mkuu kwa kuweza kufanya kazi usiku na mchana, hadi leo tunaelekea kuhitimisha mjadala huu wa hotuba ya Bajeti ya Wizara yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepokea pongezi nyingi za utendaji wa Wizara na Taasisi zake kutoka kwa Waheshimiwa Wabunge nasi tunaahidi kuendeleza mafanikio yaliyopatikana kwa ari zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, tumepokea michango mingi ambayo ni chachu katika kuleta maendeleo ya uchumi wa nchi yetu, hususani kupitia sekta yetu ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara. Napenda kuwahakikisha Waheshimiwa Wabunge kuwa maoni na ushauri wenu na maelekezo ya Bunge hili katika kujadili bajeti ya sekta hii tutayazingatia kuyafanyia kazi ikiwemo kutoa mrejesho wa utekelezaji. Aidha, kutokana na muda mfupi tulionao hadi kuhitimisha hotuba hii, maelezo na majibu ya kina ya michango mbalimbali yameandaliwa na tutayawasilisha kwa maandishi kwa Ofisi ya Bunge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwatambua Waheshimiwa Wabunge waliochangia hotuba ya bajeti ya Wizara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, jumla ya Waheshimiwa Wabunge waliochangia ni Wabunge 29 na kati ya hawa Waheshimiwa Wabunge 23 wamechangia kwa kuzungumza hapa Bungeni na Waheshimiwa Wabunge Sita wamechangia kwa maandishi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maelezo hayo ya utangulizi naomba sasa nitoe ufafanuzi wa baadhi ya hoja zilizoibuliwa na Waheshimiwa Wabunge katika kujadili hoja hii niliyowasilisha kama ifuatavyo: - (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ridhaa yako niruhusu nijikite katika hoja moja au mbili ambazo ni msingi mkubwa wa mjadala huu wa siku hizi mbili za kujadili hotuba ya bajeti yetu. Hoja yenyewe inaweza kuwa imebeba michango yote ya Waheshimiwa Wabunge nayo ni hoja iliyosemwa na Waheshimiwa Wabunge wengi kuhusu hali ya sekta ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara, lakini ikiunganishwa na hali inayoendelea duniani hali ya mfumuko wa bei katika bidhaa mbalimbali na mwishoni ikionekana kama Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi inaendeshwa bila maono wala dira naomba niseme yafuatayo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna nchi duniani iliyofikia hatua ya juu ya maendeleo bila kuwa na mageuzi ya uchumi wa viwanda. Hata hivyo, nadharia ya maendeleo ya kiuchumi (Theory of Economic Development) inabainisha kwamba ipo misingi muhimu misingi mikuu ambayo nchi ama Taifa hutakiwa kuwanayo ili kufikia hatua yoyote ile ya maendeleo. Misingi hiyo ni uwepo wa miundombinu wezeshi kwa ajili ya shughuli endelevu za maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukirejea kwenye nadharia ya uchumi wa miundombinu (The Economics of Infrastructure) inatueleza miundombinu hii wezeshi uwekezaji wake ni mkubwa na hakuna Taasisi ama Sekta binafsi yoyote yoyote ambayo ipo tayari kuwekeza kwenye miundombinu, lazima miundombinu hii wezeshi iwekezwe na Serikali yenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miundombinu hii wezeshi ni pamoja na miundombinu ya barabara ni pamoja na miundombinu ya usafirishaji wa reli, usafirishaji wa anga, miundombinu ya afya, miundombinu ya elimu yote hii lazima iwepo kama tunataka kuona matokeo makubwa ya uchumi wa viwanda ndani ya Taifa lolote duniani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nchi yetu Tanzania ilikuwa ni muhimu sana tulipopata uhuru mwaka 1961 kuwa na mipango ya muda mrefu na mipango ya muda mfupi. Nichukue fursa hii, kuwapongeza sana Viongozi wetu wa Serikali ambao wote wametokea Chama cha Mapinduzi kuanzia Serikali ya Awamu ya Kwanza Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere nampongeza kwa dhati ya nafsi yangu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mzee wetu Alhaji Ali Hassan Mwinyi nampongeza kwa dhati ya nafsi yangu alifanya makubwa kuhakikisha, nadharia hizi za uchumi zinafikiwa na Taifa letu linanufaika na mapinduzi ya viwanda. Nampongeza sana Mzee wetu Hayati Mkapa alifanya makubwa. Nampongeza sana Rais wetu mstaafu wa Awamu ya Nne Jakaya Mrisho Kikwete alifanya makubwa kuhakikisha Taifa letu linanufaika na uchumi wa viwanda.

Nampongeza sana Hayati Dkt. John Pombe Magufuli amefanya makubwa na sasa nampongeza sana Mama mlezi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anafanyakazi kubwa kuhakikisha yale yote yaliyofanywa na watangulizi wake yanazaa matunda yanayotakiwa. Pongezi nyingi na niliombe Bunge lako Tukufu tusimkatishe tamaa Rais wetu anafanyakazi kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ipi ilikuwa dira yetu baada tu ya kupata uhuru. Baada ya kupata uhuru dira yetu ilikuwa ni kuwa na Taifa huru katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kisiasa. Hivyo, ili tuweze kufika huko kama Taifa ilitulazimu tuanze hatua moja kwenda hatua nyingine na ndipo aliposema Mheshimiwa Waziri wa Kilimo viwanda vilijengwa katika Serikali ya Kwanza ni sahihi kabisa, lakini kuna kiwanda kilichojengwa eneo moja la nchi unazalisha bidhaa ambazo hakuna miundombinu ya kupeleka sokoni unakwenda kuzalisha tunachokiita botanic inflation. Kwa hiyo, kifo kile kilikuwa ni kifo cha kiuchumi na wala hatutakiwi kujilaumu na kwa sababu tuna Serikali makini, ndio maana tukarudi kwenye nadharia zote za kiuchumi na sasa tuko sehemu sahihi ya kunufaika na mapinduzi ya nne ya viwanda ambayo dunia nzima ipo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yalisemwa sisi watanzania kweli tulalamike kuhusu mafuta kutoka Ukraine, mafuta kutoka Malaysia ambayo yameshindwa kufika nchini ni sahihi. Kwa sababu, tulianza na utekelezaji wa mipango mingine huko nyuma, naomba nianzie na Mpango wa kwanza wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano tulioanza kuutekeleza mwaka 2011/2012 hadi mwaka 2015/2016. Mpango huu ulilenga kufungulia fursa fiche za ukuaji wa uchumi baada ya kuwa tumesoma tumerudi kwenye Structural Adjustment tumeona haifanyikazi, wachumi wa Taifa hili wakafanya kazi yao na sasa tukaanza mwelekeo sawasawa wa kwenda kunufaika na mapinduzi ya viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango huu ulitaka kuhakikisha kuwa Taifa letu linakuwa na miundombinu sahihi kwa ajili ya kuwezesha shughuli zingine za maendeleo kuelekea kwenye uchumi wa kati na wa juu. Ni katika kipindi hiki ndipo tulipoona kazi kubwa iliyofanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliona ukarabati wa reli ya kati yenye urefu wa kilomita 2,707 ambapo huko nyuma tuliona matatizo makubwa ya miundombinu hii lakini tulikarabati na mwendo ukaendelea. Tukahakikisha kuna jengo la kukarabati kilomita 2,775 za barabara za lami kwa mara ya kwanza ndani ya Taifa letu tukielekea kuufungua uchumi wa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukaona maboresho makubwa katika Bandari ya Dar es Salaam ambako uwezo wa kuhudumia shehena ya mizigo uliongezeka kwa kiwango kikubwa. Tukaona kuongezeka kwa uzalishaji wa umeme kutoka megawati 900 mwaka 2010 hadi megawati 1,246 mwaka 2015.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukazalisha chakula cha kutosha hadi asilimia 125 ya chakula kikazalishwa. Tukaona miundombinu ya elimu shule za kata zikajengwa kwenye kila Kata ndani ya Taifa letu. Tukaimarisha miundombinu ya afya na lishe katika ngazi zote kwa wakazi wote wa Mijini na Vijijini. Huwezi kuwa na Tanzania ya viwanda kama huna jamii ambayo iko imara kiafya na ambayo imeelimika. Hii ilikuwa ni mpango wa kwanza wa maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mpango wa Pili wa Maendeleo ambao ulisemwa hapa Serikali ya Awamu ya Tano ilikuwa ya viwanda; viko wapi viwanda? Viwanda tunavyo na nimetaja kwenye hotuba ya bajeti yangu. Mpango wa Pili wa Maendeleo ulikuwa na dhima ya kujenga uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuzi ya uchumi na maendeleo ya watu. Lengo kuu la pili lilikuwa ni kurekebisha mapungufu yote ya mpango wa kwanza ili tuweze kuendelea kutembea mguu sawa kuelekea mapinduzi ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwenye mpango huu ndipo tulipoona Serikali ya Awamu ya Tano ya Chama cha Mapinduzi ikiongozwa na Hayati Dkt. John Pombe Magufuli na msaidizi wake Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan, tukianza ujenzi wa reli ya kisasa ili kuhakikisha sasa viwanda vyote vilivyojengwa vikizalisha bidhaa ichukue muda mfupi bidhaa hizo kufika bandarini na kusafirishwa nje ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona mradi mkubwa wa kuzalisha umeme. Huwezi kuwa na viwanda kama huna umeme wa kujitosheleza. Tunao mradi mkubwa wa umeme unaokwenda kuzalisha megawati 2,115 ambao hatuna muda mrefu mradi huu unakamilika. Ni maandalizi ya uchumi wa viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi kwenye ziara ya Mheshimiwa Rais wetu, Mama Samia Suluhu Hassan, moja ya hati za makubaliano tulizosaini ni mkataba wa kibiashara kati ya Jiji ya Dallas na nchi yetu ya Tanzania. Jiji la Dallas liwe kama lango la biashara ya bidhaa zinazozalishwa Tanzania kwenda kuuzwa katika Bara la Amerika yote Kaskazini na Kusini, lakini Tanzania kiwe kama kituo kikuu cha biashara kwa Afrika ya Mashariki, kwa Afrika ya Kusini na Nchi za Afrika ya Kati. Biashara zote zinazotoka duniani zipite Bandari ya Dar-es-Salaam. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ndiyo tunayoyafanya kuelekea uchumi wa viwanda na kupitia utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Maendeleo tukaona mradi wa kufufua Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) inafanya kazi ndani ya nchi na nje ya nchi. Huwezi kuingia mikataba ya biashara na wenzako, wenzako wakaleta ndege zao wewe usifanye hivyo, hapana. Moja ya kipengele kwenye mkataba huu ni kuwa na mkataba mwingine mdogo (Open Skies Agreement), niishukuru Wizara ya Uchukuzi inahitimisha mkataba huo ili sasa na sisi ndege zetu ziweze kuruka kuelekea duniani kupitia Dallas. Haya yote yamewezekana kwa sababu tumetekeleza mpango wa pili wa maendeleo tukifungua zile fursa fiche, miundombinu wezeshi kwa ajili ya uchumi wa viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuendelea na ujenzi wa miundombinu ya msingi, Mpango huu wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano pia ulijikita katika kujenga viwanda vinavyotumia malighafi zinazopatikana nchini, hususan katika sekta za kilimo, madini na gesi asilia na uzuri takwimu huwa zinaongea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika sekta ya viwanda utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Maendeleo tulifikia asilimia 105 ya malengo tuliyokuwa tumejiwekea. Kwa mara ya kwanza tukaona mchango wa sekta ya viwanda kwenye pato la Taifa ukifikia asilimia 25.1, ni mafanikio makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kasi ya ukuaji wa shughuli za uzalishaji iliongezeka kutoka asilimia 5.2 hadi asilimia 8.5, huku tukiona mchango wa sekta ya madini ukikua kwenda kufikia asilimia 12.6 kutoka asilimia 6.9. Hii ni kwa sababu miundombinu wezeshi yote ilishafanya kazi yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunatekeleza Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano tulioanza kuutekeleza mwaka 2021/2022 na tunakwenda kuhitimisha mwaka 2025/2026, ambao ni muendelezo wa Mpango wa Kwanza na wa Pili na lengo lake kuu sasa ni kujenga uchumi shindani na viwanda kwa maendeleo ya watu wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge mmesema vizuri sana, lazima viwanda hivi vitambue watu wetu nini walichonacho. Ndio maana sasa baada ya kuona miundombinu wezeshi yote imekamilika nchi yetu imefunguka kwa miundombinu. Bidhaa itakayozalishwa kwenye kona yoyote ya Taifa letu ina uwezo wa kusafiri kwenda eneo lingine lolote ndani ya Taifa letu kwa muda mfupi. Ndani ya mpango huu ndio tunamwona kiongozi wetu makini, jasiri, Mama Samia Suluhu Hassan, Rais wetu, anaelekeza bajeti kwenda kwenye sekta za uzalishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru sana Mheshimiwa Bashe, amesema vyema. Hotuba ya bajeti yake inakwenda kuongezeka kwa kiwango kikubwa. Hiyo yote ni kuwezesha viwanda vyetu vipate malighafi tayari kwa uzalishaji ili tuweze kusafiri salama kwenye safari ya maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu imefunguka kama nilivyosema kwa miundombinu yote ya msingi kuelekea uchumi shindani na wa viwanda. Pongezi nyingi kwa Serikali yetu ya Awamu ya Sita na Serikali nyingine zote ambazo zimeongozwa na wazalendo wa Taifa letu waliojua vipaumbele vya Taifa letu kuelekea kwenye nchi ya maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kisiasa. Ndio maana tunaona sasa jitihada kubwa anayoifanya Mheshimiwa Rais wetu ni kuueleza ulimwengu Taifa letu liko tayari sasa kwa safari ya kimaendeleo. Tuko tayari na wawekezaji tumefungua milango ili waje kuwekeza kwenye maeneo yote ya kiuchumi ndani ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona mikataba ambayo tumesaini, hati zote za makubaliano 44 zote zinawaelekeza wawekezaji kuja kuwekeza katika sekta za uzalishaji, katika sekta za viwanda. Ndio maana mpaka kufika mwaka 2025 tutakuwa hatuna tena upungufu wa sukari nchini Tanzania, tutazalisha kutoka Tanzania, kutoka kwenye viwanda vidogovidogo na viwanda vikubwa na jitihada hiyo ni pamoja na uwekezaji kwenye eneo la Mkulazi ambalo Waheshimiwa Wabunge wamesema na tayari mwekezaji yuko site anafanya kazi yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunakwenda kutumia teknolojia zote, teknolojia za kati, teknolojia za juu, ili kuhakikisha viwanda vidogovidogo, vya kati na vikubwa vinawekezwa. Ndio maana tuna kongani za viwanda kule Kitaraka, Manyoni, lakini tuna kongani za viwanda pale Kwala, Kibaha na tuna kongani za viwanda hapa Nala, Dodoma. Tunachotaka kufanya ni kuihudumia dunia kutoka Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge ambao wametusemea kwamba, tuongezewe fedha, lakini wamekiri sisi ni Wizara inayoratibu uwekezaji na viwanda. Uwekezaji na viwanda hivi upo kwenye sekta nyingine za kiuchumi na tunafanya kazi kwa karibu zaidi na sekta zote; sekta ya madini, sekta ya kilimo, sekta ya fedha tunafanya kazi kwa karibu kuhakikisha haya yote yanafanikiwa. Tuko kwenye majadiliano na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuona viwanda vilivyopo kwenye mifugo na uvuvi tunavipaje kipaumbele ili vinufaike na mafanikio makubwa haya. Kwa hiyo, niwatoe hofu tunafanya kazi hii kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo niseme tu Taifa letu lina dira ya muda mrefu na lina dira ya muda mfupi. Mipango yote hiyo inapitishwa na Bunge lako Tukufu kwa ajili ya utekelezaji. Kikubwa niwaombe Waheshimiwa watuunge mkono ili tuweze kuyatimiza haya yote mazuri tunayoyapanga kwenye sekta hii ya uwekezaji, viwanda na biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisema nianze na jambo hili na moja dogo la pili ambalo napenda kulisemea kabla muda wangu haujaisha ni mradi wa kimkakati wa Liganga na Mchuchuma. Tumesikia Bunge lako limesema na limekiri ni mradi wa muda mrefu. Tunafanya kazi kwa karibu na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuona tunapohitimisha mjadala na mwekezaji wetu Taifa letu linaendelea kuwa salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze timu yetu ya kitaifa ya majadiliano imefanya kazi yake nzuri na sasa jambo hili liko mikononi mwa Waziri wa Uwekezaji na Mwanasheria Mkuu wa Serikalim. Tunaliahidi Bunge lako Tukufu tunakwenda kulihitimisha. Nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Ludewa, ndugu yangu Mheshimiwa Kamonga, alitahadharisha kuhusu mgongano wa sheria mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali inafanya kazi kuona hakuna mgongano wa sheria hizi mbili, Sheria ya Ardhi pamoja na Sheria ya Uthamini ili tuweze kufika hatua njema kwa ajili ya wananchi wetu na wananchi wetu waweze kufanikiwa. Jambo ambalo naweza kuahidi ni kwamba, Wizara yangu pamoja na Mthamini Mkuu wa Serikali tutafanya ziara na kuongea na wananchi wa vijiji hivyo viwili ili tuweze kuhitimisha jambo hili kwa mafanikio makubwa kati ya Serikali, wananchi wetu, pamoja na mwekezaji wetu. Hivyo, nimtoe shaka Mbunge, tuko tayari na muda mfupi mradi huu utaanza utekelezaji wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema maneno haya, kabla ya kuhitimisha hoja yangu, napenda tena kuwashukuru kwa dhati Waheshimiwa Wabunge wote waliochangia hoja hii. Niwaombe tu tuendelee kushirikiana katika kuwatumikia Watanzania katika kuwaletea maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jitihada zinazofanywa na Serikali yetu kupitia Mheshimiwa Rais wetu, Mama Samia Suluhu Hassan, zinatuhusu sisi sote. Tumemsikia jana Mheshimiwa Rais akisema ametusemea vizuri Watanzania; sisi ni wakarimu, wawekezaji wamemsikia wanakuja kwa wingi. Naomba tuwapokee na tushirikiane nao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wakati sasa, kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge mmoja, wa kutengeneza mabilionea kutoka ndani ya Watanzania waongezeke zaidi na wanaanza na sisi Waheshimiwa wawakilishi wa wananchi. Sisi Wabunge tushiriki, Taifa letu limefunguka na tunasema Tanzania is ready to take off, lazima na sisi tuwe ndani ya safari hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwahakikishie pia kuwa, Wizara yangu itaendelea kuilea na kuisimamia sekta binafsi ya Tanzania. Hakuna Taifa lililofanikiwa bila sekta binafsi. Ndio maana viwanda vingi kwa asilimia 90 vinashikiliwa na sekta binafsi.

Mimi nasafiri na sekta binafsi kama Waziri mwenye dhamana. Mheshimiwa Rais wetu kwenye safari zake zote anasafiri na sekta binafsi ili sekta yetu binafsi ishindane ndani na nje ya Taifa letu. Hivyo, tusafiri kwa pamoja kwenye safari hii ya maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema maneno haya, naomba kutoa hoja. Ahsante sana. (Makofi)

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naafiki.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara
WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii na kwa ridhaa yako nianze kwa aya moja ndani ya kitabu kitukufu cha Mwenyezi Mungu, inayosema, “Rabbi-rishirahii swadri, wayassirli amri, weahlul-ukudata minlisani yafqahu kauli.” (Makofi)

Mheshimiwa Spika, maana yake; nimemuomba Mwenyezi Mungu aunyooshe ulimi wangu ili niweze kuyasema yale ambayo Waheshimiwa Wabunge wameongea kwa dhamira njema kabisa ya kujenga uchumi wa Taifa hili ili niyaseme na yaeleweke, ndio maana ya aya hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii kukushukuru sana wewe kwa uongozi wako madhubuti, lakini pia wasaidizi wako Mheshimiwa Naibu Spika pamoja na Wenyeviti wa Kamati zetu kwa namna ambavyo mmeongoza na kusimamia vyema majadiliano ya bajeti ya Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara kwa mwaka 2023/2024.

Nawashukuru pia Waheshimiwa Wabunge wote kwa uchangiaji wenu makini mlioufanya kwa maandishi na kwa kuzungumza moja kwa moja katika Bunge hili Tukufu. Naomba niseme kuwa ninatambua na kuthamini dhamira na nia njema iliyotawala mjadala huu ambayo kimsingi ililenga kuboresha mikakati na mbinu za kisekta zitakazotumika kutekeleza malengo tuliyopanga kwa mwaka 2023/2024 na hivyo kutoa mchango unaotakiwa kwa Taifal letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee naishukuru sana Kamati yetu ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile, Mbunge wa Mufindi Kusini na Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Mariam Ditopile Mzuzuri, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma na Waheshimiwa Wajumbe wote wa Kamati kwa namna ambavyo wanajenga hoja na kushauri ipasavyo kuhusu uendelezaji wa sekta ya uwekezaji, viwanda na biashara hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya viongozi wenzangu na watumishi wa Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara na taasisi zake naomba kupokea pongezi nyingi za utendaji zilizotolewa na Waheshimiwa Wabunge hasa kwa Mheshimiwa Rais wetu na kwetu sisi viongozi wa Wizara. Aidha, tunaahidi kuendeleza mafanikio yaliyopatikana kwa ari zaidi. Vilevile tumepokea ushauri na michango mingi ambayo ni chachu na changamoto muhimu katika kuleta maendeleo ya mipango ya uchumi yenye mchango kwa sekta ya uwekezaji, viwanda na biashara.

Mheshimiwa Spika, mawasilisho hayo yanatambua na kuzingatia pia hoja mbalimbali za sekta hii zilizojitokeza wakati wa kujadili na kupitisha bajeti za Ofisi ya Waziri Mkuu, Ofisi ya Rais na Makamu wa Rais na pia Wizara zilizonitangulia kuwasilisha bajeti zao hapa Bungeni kwani Wizara yangu ni Wizara mtambuka ambayo tunashughulika na Wizara zote.

Napenda kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge kuwa ushauri wenu na maelekezo ya Bunge hili katika kujadili bajeti ya Wizara hii tutayazingatia na kuyafanyia kazi ikiwemo kutoa mrejesho wa utekelezaji wake. Aidha, kutokana na muda mfupi nilionao katika kuhitimisha bajeti hii, maelezo na majibu ya kina ya michango mbalimbali yameandaliwa na yatawasilishwa kwa maandishi.

Mheshimiwa Spika, kabla sijajielekeza katika kujibu na kufafanua hoja mbalimbali zilizojitokeza naomba kuwatambua Waheshimiwa Wabunge 39 waliochangia katika majadiliano ya hotuba ya bajeti ya Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara. Kati yao Waheshimiwa Wabunge 35 wamechangia kwa kuongea hapa Bungeni na Waheshimiwa Wabunge wanne wamechangia kwa maandishi.

Mheshimiwa Spika, na kati yao, naomba uniruhusu niseme hili, kati ya Wabunge hao Wabunge 23 wamechangia kuhusu suala la Twiga Cement na Tanga Cement. Inaonesha ni kwa kiwango gani ambavyo Waheshimiwa Wabunge wanaguswa na uwekezaji na biashara ndani ya Taifa letu. Kwa shabaha ya kumbukumbu orodha hiyo itawasilishwa na kuwekwa katika Kumbukumbu Rasmi za Bunge.

Mheshimiwa Spika, naomba pia niwashukuru Waheshimiwa Mawaziri wenzangu ambao wamechangia hoja hii na kutoa ufafanuzi wa hoja mbalimbali akiwemo Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango, Mheshimiwa Naibu Waziri wangu, Mheshimiwa Exhaud Kigahe na Mheshimiwa Patrobas Katambi, nawashukuru sana kwa kutoa majibu kwa hoja za Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Spika, hoja na mipango iliyotolewa na Waheshimiwa Wabunge katika kujadili hotuba yangu inaonesha nia thabiti ya ushirikiano wenu na Wizara hii katika kuziendeleza sekta ya uwekezaji, viwanda na biashara na kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya Taifa letu. Nimehamasika na jinsi mlivyonitia nguvu kwa kukubaliana nami katika mambo ya msingi na kutetea kwa nguvu zenu zote maslahi mapana na yenye maslahi makubwa ya Taifa na wananchi wetu tunaowawakilisha hapa Bungeni. Kwa ujumla wake hoja na michango mingi iliyotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo pamoja na Waheshimiwa Wabunge wote waliozungumza na kuchangia kwa maandishi zinashabihiana katika maeneo mengi na zimelenga maeneo mbalimbali ambayo sasa napenda kujielekeza kujibu na kutoa ufafanuzi wake.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyotangulia kusema, hoja kubwa ilikuwa ni jambo la Twiga na Tanga Cement, nami nitajielekeza huko baada ya kuwa nimeongeza mchango kidogo kwenye majibu ya hoja za Waheshimiwa Wabunge yaliyotolewa na Mheshimiwa Naibu Waziri; nayo ni kuhusu suala la Liganga na Mchuchuma. Nawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge mliotambua kwamba Serikali hii imejipanga kuleta maendeleo kwa wananchi wake, kuwafikia kulekule waliko.

Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge wanakumbuka ni Bunge hilihili mwaka jana lilielekeza fidia hii ikalipwe. Nampongeza sana kwa dhati ya moyo wangu, Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan, bila kusita ametoa bilioni 15.4 kwa ajili ya malipo ya fidia ya wananchi wetu wote kwenye mradi huu wa Liganga na Mchuchuma. Hii ni dhamira ya dhati sana. Na niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge maelekezo yenu kama ilivyosema Kamati yetu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo tunayatekeleza kwa asilimia kubwa. Sasa hivi timu ile ya majadiliano inaendelea na kazi yake ya kujadiliana, kama ambavyo Serikali ilitoa maelezo yake hapa Bungeni; kwamba tunatamani kumalizana na mwekezaji yule wa mwanzo ambaye tayari tulishasainiana mikataba kwa wema na kuondokana naye ili Taifa letu lisiingie kwenye migogoro na gharama nyingine ambazo hazina msingi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kulihakikishia Bunge lako Tukufu kwamba taarifa yetu tuliyoitoa mwezi wa 11, kwenye Bunge la mwezi wa 11 hapa Bungeni kwamba, tulipata taarifa rasmi kutoka Serikali ya China, mwekezaji yule amefilisika, ni kweli, amefilisika. Pamoja na taarifa ile ya kufilisika ile ni kampuni inayojitegemea, lazima tushughulikenayo kwa kufuata kanuni na taratibu na sheria zetu, ili kuliepusha Taifa letu kuingia katika migogoro ambayo haina maana.

Mheshimiwa Spika, aliyefilisika ni yeye, lakini bado ana mikataba na sisi; na kama ambavyo Wabunge walitahadharisha huko nyuma wakasema ni wakasema tumuite tuje tuongee naye. Huko nyuma, miaka sita iliyopita, nililieleza Bunge lako Tukufu, tulimuita hakuwahi kutokea na sasa tumemuita amekuja, yupo mezani. Tunajadiliana naye na bahati nzuri na yeye amekiri kweli amefilisika. Amefilisika, lakini bado ana mkataba na sisi lazima tuhitimishe naye vizuri, hicho ndicho ninachokisema. Kazi mliyotutuma tunaendelea kuifanya kwa kiwango cha hali ya juu kwa uharaka, lakini kwa uzalendo mkubwa wa Taifa letu ili sasa mradi huu uanze kutekelezeka, uondoke kwenye miradi ya historia, miradi ambayo ni simulizi ndani ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya maneno haya, nilimsikia Mheshimiwa Neema Mgaya alisema anataka kuleta hoja binafsi. Nilitamani sana kwamba Bunge tumpongeze Mheshimiwa Rais kwa kuonesha njia ya kutaka jambo hili liishe sasa na kuwapelekea ujumbe wawekezaji wetu kwamba Tanzania ni salama. Ameweza kuja tumeanza mchakato huu, tumpe nguvu Mheshimiwa Rais wetu ili tulihitimishe jambo hili kwa wakati na tuweze kuona athari chanya ya mradi huu ambao umekuwa ni historia kwa Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, hoja ya pili ambayo nilitamani niitolee maelezo inaunganishwa na hoja kubwa ambayo ningetamani nichukue muda wangu mwingi kuieleza. Nayo ni kufutwa, kuondolewa kwenye usajili kwa Kampuni ya Chalinze Cement Company Limited. Kwa nini imeondolewa? Ni jukumu letu kuzisajili, ni jukumu letu kuwawekea masharti, ili watekeleze.

Mheshimiwa Spika, msajili analo jukumu la kuhakikisha daftari linakuwa na taarifa sahihi na za uhakika na Sheria ya Kampuni imempatia mamlaka msajili kufuta kampuni yoyote ambayo wakati wa usajili iliwasilisha taarifa za uongo.

Mheshimiwa Spika, msajili anaendelea na zoezi la upekuzi wa taarifa zilizomo kwenye daftari la kampuni ambapo zoezi hili ni endelevu kwa lengo la kuhakikisha kampuni zisizokidhi vigezo zinaondolewa zote. Katika zoezi hilo msajili alibaini kuwa Chalinze Cement Company Limited iliwasilisha taarifa za uongo wakati wa usajili, kama ifuatavyo: -

Moja; anuani ya kampuni iliyosajiliwa haipo kwenye usajili popote pale ndani ya Taifa hili. Kwa hiyo, kwanza anuani ya kampuni ni ya uongo kwa hiyo, ukitaka kumfikia huwezi kumfikia, yuko wapi.

Pili; anuani za wana-hisa alizozisajili hazipo kwenye sajili zozote ndani ya Taifa letu. kwa hiyo, nayo pia hata hao wanahisa ni wa kufikirika.

Mheshimiwa Spika, mawasiliano ya simu ya mkononi yaliyosajiliwa kwetu sisi si ya mwanahisa aliyetajwa kwenye usajili huo. Aidha, kwa mujibu wa sheria msajili alitoa notice ya kusudio la kufuta Kampuni ya Chalinze Cement Company Limited ambapo wakurugenzi wake walipewa siku 30 kuanzia tarehe 19 Januari, 2023 kuwasilisha maelezo kwa nini kampuni hiyo, isiondolewe kwenye daftari la kampuni kwa kuwasilisha taarifa za uongo wakati wa usajili.

Mheshimiwa Spika, baada ya siku 30 zilizotolewa kumalizika bila ya Wakurugenzi kutoa maelezo yoyote, Msajili aliendelea na hatua inayofuata kwa mujibu wa kifungu cha 400A(3) cha Sheria ya Kampuni na kuifuta Chalinze Cement Company Limited. Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge, naomba waelewe dhamira njema ya Serikali yetu. Tunahitaji wawekezaji, lakini wawe wale wenye dhamira njema na Taifa letu, siyo wawekezaji wanaokuja kutuchezea Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunabaki na orodha ya makampuni mengi ambayo hayapo, makampuni hewa, lakini kibaya zaidi taarifa zote alizozisema wakati anasajili ni za uongo. Kwa hiyo, naomba hilo Watanzania wajue, mtu huyu alishughulikiwa na sheria iliyotungwa na Bunge hili hili Tukufu, hakuna sehemu yoyote ambapo Serikali ilikosea.

Mheshimiwa Spika, jambo la Tanga na Twiga Cement; nimepokea maelekezo ya Bunge lako na kama utaridhia, sisi kama Wizara tuko tayari kutoa semina kwa Wabunge wote kuhusu utendaji wa Tume ya Ushindani pamoja na Baraza la Ushindani la Taifa ili sote kwa pamoja tuwe na uelewa wa pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na hoja na Waheshimiwa Wabunge kama nilivyosema 23, zaidi ya asilimia 50 ya Wabunge waliochangia hotuba ya bajeti hii kuhusu jambo hili na ilianza kuambiwa kwa nini FCC imeruhusu. FCC ndugu zangu ni Tume yetu ya Ushindani; kwa nini imeruhusu muungano wa Kampuni za Twiga Cement na Tanga Cement ambazo hapo awali ulizuiwa na Baraza la Ushindani.

Mheshimiwa Spika, jibu sahihi la hoja hii kwa Waheshimiwa Wabunge ni kwamba Tume ya Ushindani haikushughulika na ombi la muungano wa kampuni mbili ambao ulizuiwa na Baraza la Ushindani; hilo ni jibu la kwanza. Haikushughulika na ombi lile lililozuiwa na Baraza la Ushindani. Tunaheshimu sheria zote za nchi hii na hasa zile mimi Waziri wa Uwekezaji niliyebeba Katiba ya Taifa letu, nikabeba kitabu kitukufu kuapa, nimeapa kuzilinda na nitazilinda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kilichofanyika na Wizara yetu inapenda kusema na kulijulisha Bunge letu Tukufu kwamba mnamo tarehe 22 Desemba, 2022 Scancem International DA ambayo inamiliki asilimia 69 pale Twiga Cement ilileta ombi la kununua asilimia 68.33 ya hisa za AfriSam Mauritius ndani ya Kampuni ya Tanga Cement.

Mheshimiwa Spika, tarehe 22 Desemba, 2022 ndiyo tulipokea maombi hayo. Taratibu zote za kisheria zilifuatwa katika kuwasilisha na kuchambua ombi hili. Kwa mujibu wa kifungu cha 11(2) cha Sheria ya Ushindani kinachosomeka sambamba na Kanuni ya 33 ya Kanuni za Ushindani za Mwaka 2018 na Kanuni ya 2(1) ya Kizingiti cha Uwasilishaji wa Maombi ya Miungano ya Makampuni za Mwaka 2017 (The Threshold for Notification of a Merger) kinatoa wajibu kwa kampuni ambazo zinataka kuungana na zimekidhi vigezo vilivyowekwa chini ya vifungu tajwa hapo juu kuwasilisha maombi yao bila kujali kama kusudio lao la awali lilikataliwa au kukubaliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vigezo hivi ni pamoja na ununuzi wa hisa au mali za kampuni inayonunuliwa, kizingiti cha mtaji wa kampuni zote mbili kama unafikia au kuzidi kiasi cha shilingi bilioni 3.5 na kubadilika kwa uwezo wa kiutawala (change of control) imebadilika?

Mheshimiwa Spika, hivyo napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kuwa, ombi hili lililoruhusiwa ni ombi jipya kutokana na vifungu nilivyovitaja kabla, ni ombi jipya ambalo tulilipokea kwa barua yenye kumbukumbu namba CDC127359/144 lililotolewa mbele ya Tume ya Ushindani kwa kuzingatia takwimu za hali ya soko la saruji kwa mwaka 2022. Kwa sababu ombi hili tulilipokea mwaka 2022 hatukuwa na sababu ya kutumia takwimu za mwaka 2020, tutatumia takwimu za mwaka 2022. Natamani sana Watanzania watuelewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ombi hili jipya lililoruhusiwa na Tume yetu ya Ushindani ni tofauti na lile la awali lenye kumbukumbu Na. CDC127359/136 lililowasilishwa tarehe 2 Novemba, 2021. Kwa hiyo, tuna maombi mawili; la kwanza la mwaka 2021 na ambalo lilitumia takwimu za Desemba, 2020 kwa sababu hatukuwa na takwimu nyingine katikati hapo.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya hoja za Waheshimiwa Wabunge, ombi hili lililowasilishwa tarehe 2 Novemba, 2021, liliruhusiwa kwa masharti tarehe 6 Aprili, 2022 kwa kuzingatia kigezo cha uwezo uliosimikwa. Amelieleza vizuri Mheshimiwa Naibu Waziri Patrobass Katambi, kisheria maana yake nini.

Mheshimiwa Spika, tuliruhusu kwa sababu utawala wa soko wa kampuni mbili zilizoomba kujiunga kutumia installed capacity ulikuwa unafikia asilimia 31.53 ambazo ni chini ya asilimia 35 ambayo ni threshold ya mwisho ya kuruhusiwa kwa kampuni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kutokana na sheria inavyosema, haijasema tutumie installed capacity wala sales volume, kwa sababu Sheria ya Tume ya Ushindabni is an economic act (sheria ya kiuchumi). Sheria ya kiuchumi ina-deal na behaviour za wateja wake walioko kwenye eneo lile lililopo, it’s a behavioral act, inabadilika wakati kwa wakati. Wamesema vizuri Wabunge kwamba mazingira yanabadilika na yalibadilika kweli.

Mheshimiwa Spika, kwa nini FCC waliamua ombi ambalo lilizuiwa na FCT hapo mwanzo? Nimeshalieleza wazi, ombi tuliloliamua ni jipya kabisa, wala siyo lile la zamani.

Mheshimiwa Spika, napenda pia kutoa taarifa kwamba mchakato wa kupokea, kuchambua na kutoa maamuzi ya muungano wa kampuni kama nilivyosema unaongozwa na nadharia za kiuchumi na kibiashara. Nadharia hizi na viashiria vyake, market variables, lazima viangaliwe na hivyo basi, kutokana na ukweli huu, viashiria kutoka mwaka 2020 mpaka mwaka 2022 vilibadilika na hapo tunatoa picha kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba hata huko nyuma imewahi kutokea ndani ya Taifa letu, kampuni ziliomba kuungana kwa mazingira ya kwanza wakanyimwa kwa sababu mazingira hayakuwa yanaruhusu na waliporejea mazingira yakawa yanaruhusu na wakaruhusiwa kuungana, nayo wala siyo miaka mingi iliyopita.

Mheshimiwa Spika, FCC mnamo tarehe 10 Juni, 2021 iliendelea kuzuia ombi la Kampuni ya Toyota Tshusho, zote ziko ndani ya Taifa letu kuinunua Kampuni ya CFAO Motors kama ambavyo ombi hilo lilivyozuiliwa na FCC na baadaye kuafikiwa na Baraza la Ushindani (FCT) mwaka 2013. Ya kwanza ilikuwa 2012 na sasa ni 2013, wakaruhusiwa ndani ya Taifa letu kupitia Tume ya Ushindani na Baraza la Ushindani hili hili ambalo tena leo tunasema watumishi wetu wamekwenda ndivyo sivyo na Waziri wamenisisitiza nisimamie haki na niliapa kusimamia haki na nitaisimamia.

Mheshimiwa Spika, siyo ndani ya Taifa letu tu, Nchi ya Afrika Kusini ambao wote tupo kwenye SADC, mwaka 2019 ilizuia muunganiko wa Africa Forest Fund Limited na Guka Forest Holding kwa sababu mazingira wakati huo mwaka 2019 hayakuwa yanaruhusu. Mwaka 2021 kampuni zilezile zikaomba kuungana kwa sababu ya mabadiliko ya hali ya uchumi ndani ya Taifa na mwaka 2021 baada ya mamlaka za ushindani nchini Afrika ya Kusini kuridhika na mabadiliko na muundo wa soko, kampuni hizi mbili ziliruhusiwa. Kwa hiyo, siyo jambo jipya, ni jambo ambalo lipo kwa majirani zetu, ni jambo ambalo lipo ndani ya Taifa letu na kilichofanyika ni kitu cha kawaida kabisa.

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na hoja nyingi kwenye jambo hili, naomba niseme tu kidogo, maana yake imesemwa pia kwamba hakukuwa na uwazi kwenye jambo hili.

Mheshimiwa Spika, kuhusu hoja hii ya kutokuwa na uwazi katika ununuzi wa hisa za AfriSam Mauritius ndani ya Kampuni ya Tanga Cement, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, mara baada ya ombi hilo kuletwa Tume ya Ushindani ulifanyika mchakato wa uwazi ambapo kwa mujibu wa Kanuni ya 49 ya Kanuni za Ushindani za Mwaka 2018 tunatakiwa kutoa tangazo kwa Taifa na kwa dunia kwamba kuna mchakato huu unaendelea.

Mheshimiwa Spika, tangazo hilo tulilitoa kwenye magazeti ya Daily News na Habari Leo ya tarehe 11 Februari, 2023 ili kuutaarifu umma juu ya jambo hili tena kwamba tumeanza nalo. Hatukupokea malalamiko kwa yeyote na kikao cha wadau ambacho kilihusisha kampuni zote za uzalishaji saruji ndani ya Taifa letu, taasisi ya kuwatetea walaji ndani ya Taifa letu walikuwemo kwenye kikao, hawakupinga wakasema wameridhika mchakato uendelee. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, huyo anayekuja kinyumenyume nani? Siri yake ni ipi? Kwa nini asiiseme wazi basi tukajua? Wakati haya yote yakiendelea, nimewahi kuwaandikia barua hawa Chalinze Cement, mimi mwenyewe Waziri kwamba, nataka kwenda kuwatembelea kwenye kiwanda chenu. Mpaka leo sijawahi kupata jibu niende au nisiende. Chalinze Cement ni nani? Ni mdudu gani ndani ya Taifa letu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Chalinze Cement amesajiliwa baada ya ombi la kwanza la Twiga na Tanga kuungana, hakuwepo huko nyuma. Tumefanya kikao cha wadau, Chalinze Cement hakuwepo. Tumemaliza michakato yote anaibuka kuja kusajiliwa na sisi kama ilivyo jukumu letu la kusajili tukamsajili, si mtu ameleta documents, ametuletea tumemsajili. Sasa tumfuatilie, Waziri mwenyewe nimemwita, kama hutaki nije kwako njoo tuongee, niletee malalamiko yako. Mpaka hapa nilipo hajawahi kuja kwangu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nawashukuru Waheshimiwa Wabunge wenye dhamira njema ya kulinda jitihada za Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuita wawekezaji kutoka nje na kuwalinda wawekezaji wa ndani ambao tayari walishawekeza; nawashukuru sana. Wapo walioniambia na wengine wamenionesha mpaka picha ya watu hao wakizunguka kwa Wabunge kuwaeleza wasaidie kupinga jambo hili. (Makofi) [Maneno Haya Siyo Sehemu ya Taarifa Rasmi za Bunge]

Mheshimiwa Spika, naomba Waheshimiwa Wabunge tuchukue tahadhari ya hali ya juu na watu wasiolitakia mema Taifa letu. Mheshimiwa Rais amefanya kazi kubwa sana kui-brand Tanzania. Wawekezaji wengi wanakuja, nimesema kwa mwaka mmoja tuna wawekezaji 240, hawakuwahi kutokea katika historia ya miaka 60 ya Taifa letu, yametokea sasa, tusitumike. [Maneno Haya Siyo Sehemu ya Taarifa Rasmi za Bunge]

Mheshimiwa Spika, kuna watu ambao wanataka kusimama mbele ya Mheshimiwa Rais kumwambia hapana Mheshimiwa Rais na Mheshimiwa Rais amesema hapana na mimi nimeapa kulinda sheria zote zilizopo ndani ya Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara na nitasimamia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitumie podium hii kumwomba Chalinze Cement aje tumsaidie. Tunajua yako mengi yaliyowakwamisha wenzake, sasa aje tumsaidie kama kweli anataka kuwekeza ndani ya Taifa la Tanzania. Mimi niko tayari, wasaidizi wangu wote wako tayari, waje tuwekeze kwa pamoja na tuwahudumie Watanzania wote kwa pamoja.

Mheshimiwa Spika, baada ya maneno haya, naomba kuhitimisha kwa kuwashukuru tena Waheshimiwa Wabunge wa Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kupitia kwao, nimesimama mbele yao najiamini ni mzalendo na naiamini imani yangu, nimeapa kulinda Katiba ya Taifa hili, nimeapa kulinda sheria zinazoongoza Wizara ya Uwekezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunaomba sana mtupitishie bajeti ya Wizara yetu kwa mwaka 2023/2024, ili tuendelee kulinda jitihada za Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuita wawekezaji, kuwawezesha wafanyabiashara wetu na hatimaye Taifa letu liweze kuhudumia Afrika kutoka hapa tulipo, liweze kuhudumia dunia kutoka hapa tulipo. Uwezo huo tunao chini ya Serikali ya Awamu ya Sita ya Chama cha Mapinduzi inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya maneno haya, naomba kutoa hoja.

WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naafiki.
Azimio la Bunge kuhusu Mapendekezo ya Kuridhia Itifaki ya Biashara ya Huduma ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika ya Mwaka 2012
WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kumshukuru tena Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema ambaye ametuwezesha kujadiliana kwa upendo wa hali ya juu lakini na wivu wa maendeleo kwa Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwashukuru sana wajumbe wa Kamati yetu ya Viwanda, Biashara, Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa kazi kubwa waliyoifanya wakati tunajadiliana jambo hili kwenye kamati, tuliifanya kazi hii kwa uzalendo wa hali ya juu na Kamati yetu wametushauri tukiwa ndani ya kamati na tumechukua ushauri wao na tutaendelea kuufanyia kazi kama Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati yetu imesema hapa ikatoa maoni na ushauri kwa Serikali wakati wakiwasilisha taarifa yetu hapa ili ilipowasilishwa na Makamu Mwenyekiti wetu mdogo wangu Mheshimiwa Mariam Ditopile. Niwashukuru sana na nikushukuru mno kwa usomaji mzuri na nia uliyoitanganza. Sisi kama Wizara tumekuelewa, na naamini na wajumbe wote wa Kamati tumekuelewa, basi tunakwenda kutenda jambao nakupongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze pia Mheshimiwa Kihenzile kwa kutuongoza vyema kwenye Kamati yetu, tangu ilipokuwa Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira, na hata ilipobadilioshwa na kuwa Kamati ya Viwanda, Biashara, Kilimo, Mifugo na Uvuvi aliifanya kazi yake kwa uzalendo wa hali ya juu na kwa weledi wa hali ya juu, na hatimaye Mheshimiwa Rais ameweza kumteua na kuwa Naibu Waziri, nampongeza sana. Sisi kama Wizara tunatambua kazi yake njema aliyoifanya kwetu kwa jinsi aliyotushauri. Kama Wizara mawazo yake tutaendelea kuyafanyia kazi pamoja na wajumbe wote wa Kamati yetu. Hakika sisi kama Wizara tunawashukuru sana na tunatambua mchango wenu mwema wa utendaji wa Wizara yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikushukuru wewe kwa jinsi ulivyoliongoza Bunge letu tukufu siku hii ya leo na siku zote ambazo umekuwa ukituongoza kwenye majadiliano ndani ya Bunge letu hili. Nikushukuru na nikupongeze sana. Tumeyapokea yote yaliyosemwa na Waheshimiwa Wabunge, tumepokea hoja, ushauri pamoja na maelekezo kutoka kwa Waheshimiwa Wabunge nane waliochangia jambo letu hili ambalo tumeliweka mezani. Nawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge kwa kuweza kutushauri sisi kama Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema wakati nawasilisha hoja hii pale mwanzoni, kwamba tayari Serikali yetu ilikuwa inaendelea kushiriki kwenye majadiliano, kwenye utekelezaji wa itifaki hii. Tulikuwa tunashiriki kwa sababu sisi ni wajumbe kwenye Jumuiya yetu ya Maenedeleo Kusini mwa Afrika, lakini tulikuwa hatuna uwezo wa kwenda kutekeleza kile ambacho kilikuwa kinajadiliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo leo hii Waheshimiwa Wabunge tumelileta mbele yenu, tunawaomba sana muweze kuridhia. Na niwashukuru Wabunge wote nane mliochangia, mmekubali kuridhia itifaki hii ili kama Taifa sasa twende kunufaika nalo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maelezo haya ya awali naomba nimpongeze sana Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa utayari wake wa kuona Taifa letu linashiriki kule duniani kupitia diplomasia ya uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huwezi kushirirki vizuri kule duniani kama na majirani zako bado hamjajiimarisha ushirikiano hasa ushirikiano huu wa kibiashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais wetu alituelekeza na ametoa maelekezo kwa itifaki zetu zote zinazohusu biashara kwenye ukanda wetu, zote ziweze kufanyiwa kazi na tuziridhie. Ni kwa sababu ya utayari wake, wa kuona Watanzania wananufaika na uwepo wa Taifa letu na uwepo wa benefits zote tulizonzo ndani ya Taifa letu, comparative advantage tuliyokuwa nayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, amesema na amekuwa akisema siku zote, tusiendelee kuongelea comparative advantages tulizonazo kama Taifa tu na badala yake lazima tuzitumie hizo sasa kunufaisha Taifa letu. Na moja ya utekelezaji wake huu ni kuletwa kwa Itifaki hii leo ya Biashara ya huduma, ili Watanzania washiriki kwa pamoja kunufaika na uwepo wa Taifa letu kijiografia hapa tulipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri, amejibu baadhi ya hoja mabazo Waheshimiwa Wabunge wamezisema, na mimi wala siwezi kuzisema zote. Naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge wenzangu kwamba hoja zote mlizozitoa zinatuwezesha sisi tunapoingia kwenye majadiliano kule kwenye utekelezaji wa Itifaki hii kwenye Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, tuweze kupeleka hoja za wananchi kupitia nyinyi Waheshimiwa Wabunge. Kwa hiyo sina sababu ya kuzijibu zote hapa, Mheshimiwa Naibu Waziri wangu amesema, kwa hiyo mimi nawashukuru sana mmetupa nguvu mmetupa hoja ya Kwenda kuendeleea kuzisimamia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizisemee mbili tu. Hoja ya kwanza niliyoulizwa ni kwamba, kwa nini tumechukua zaidi ya miaka kumi na tatu hadi leo ndio tunaleta Itifaki hii ndani ya Bunge letu tukufu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge nilianza kulijibu jambo hili tukiwa tunajadiliana hapa. Moja ya sababu ambayo tumechukua muda huu mrefu ilikuwa ni kuwaandaa Watanzania ili tunapoingia waweze kunufaika kwa asilimia kubwa na kuingia kwetu kwenye utekelezaji wa Itifaki hii. Serikali yetu baada ya Mheshimiwa Rais wetu kusaini mwaka 2012 tulitafuta Mshauri Mwelekezi ambaye ni Mtanzania, akazunguka kwenye sekta zote akakaa na wafanyabiashara wetu na hata sekta hizi ambazo tumeweza sasa kuingia tumeona sekta za mwanzo sita ilikuwa zimetoka kwa wadau wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Watanzania ambayo ni sekta binafsi imeshirikishwa kwa asilimia 100. Kwa hiyo hii ilikuwa sababu ya kwanza kwa nini tangu mwaka 2012 hatujaleta itifakii hii ndani ya Bunge letu tukufu, tulikuwa tunawaandaa Watanzania ili waweze kunufaika na itifaki hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili lilosababisha tuchukue kipindi chote hiki ni kuandaa miundombinu wezeshi ya kwenda kunufaika na itifaki hii ya Azimio la Biashara ya Huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeandaa Taifa letu miundombinu ya barabara. Taifa letu sasa linaunganishwa na nchi zote tulizopakana nazo, kwa hiyo hii ilikuwa ni mojawapo tuhakikishe tumeungana na mataifa yote kupitia barabara zetu, tumekamilisha. Sasa tuna zaidi ya magari 36,000 yanayopita on transit kupitia barabara zetu ambayo ni moja ya miundombinu muhimu ya kuhakikisha huduma zinafika kwenye nchi nyingine. Kwa hiyo ya kwanza ilikuwa ni maandalizi haya ya miundombinu husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge mmeongelea kuhusu uwekezaji kwenye Bwawa la Mwalimu Nyerere kuhusu upatikanaji wa nishati ya umeme. Tunaridhia tukiwa sasa tuko tayari; asilimia 95 ya bwawa letu limekamilika tunaenda kuwa na umeme wa ziada tunaziambia nchi za jirani zetu, nchi zetu tulizonazo kwenye Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, tuko tayari sasa kuwafikishia huduma ya nishati ya umeme. Hiyo yote ilikuwa ni kuwaandaa Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali yetu kuanzia Serikali ya Awamu ya Tatu, Serikali ya Awamu ya Nne, Serikali ya Awamu ya Tano na sasa Serikali ya Awamu ya Sita tumewekeza kwa kiwango kikubwa kwenye Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa. Ni wiki mbili zilizopita Mheshimiwa Rais amezindua mkongo mwingine To Africa 5G, zile si za kubaki Tanzania. Tunufaike Watanzania lakini tuwaambie nchi za Kusini mwa Afrika kwamba sasa tuko tayari kuwahudumia kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano. Miundombinu imewekwa vizuri sasa tunapeleka huduma, tunaridhia leo Watanzania tukiwa sote tuna uwezo wa kuwahudumia kwenye sekta zote tulizo nazo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba niwatoe hofu Waheshimiwa Wabunge na ndugu zangu Watanzania, kwamba hatujachelewa. Tumesema theluthi mbili ya nchi za Kusini mwa Afrika zilizotakiwa kuridhia ili utekelezaji huu uanze zimefikiwa mwaka 2022, Januari, ni mwaka jana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo sisi hatuko nyuma kwa hiyo tuko tayari kuingia sasa. Na kama ilivyo kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekuwa akisisitiza, kwamba tunapokwenda kujiunga na kanda hizi za kiuchumi na kibiashara tusiingie kama wasindikizaji. Hili pia ninyi Waheshimiwa Wabunge mmesema, kwamba tuingie kama washindani, na ndilo lengo lililokuwa la Serikali yetu. Mazingira sasa ni mazuri, mazingira yameandaliwa tuendelee kunufaika sasa na uwepo wetu kwenye Jumuiya hii ya Maendeleo Kusini mwa Afrika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimalizie jambo moja la mwisho. Nimshukuru sana Mheshimiwa dada yangu Jenista Mhagama kwa kusema, Serikali tunajiratibu. Na hata leo tunapohitimisha hapa ushauri elekezi niliousema mwanzo alishaainisha sera, sheria na kanuni ambazo zitaonekana kama vikwazo tunapoelekea kule kufanya biashara hii ya huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari Ofisi ya Waziri Mkuu walishaanza kuturatibu kupitia kitengo alichokitaja Mheshimiwa Waziri; kwa hiyo tumeanza kuzifanyia kazi hizo kwa uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu. Niwatoe hofu Waheshimiwa Wabunge, Serikali tuko tayari, sisi mmesema kama waratibu wa biashara ndani ya Taifa letu tunafanya kazi kwa ukaribu sana na Ofisi ya Waziri Mkuu. Yote tunayaainisha tunamkabidhi Mheshimiwa Waziri Mkuu, na yeye anakaa na sisi kama Serikali; tunaweza kuyashughulikia moja baada ya jingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, zipo sera, nimetaja moja, Sera ya Biashara ya Mwaka 2003, zipo hatua za mwisho katika kupitishwa na Serikali yetu ili iweze kuchukua yote mliyoyasema Waheshimiwa Wabunge, tupo hatua za mwisho na tunaendelea kuifanya kazi. Niwatoe hofu Serikali yetu imeweka miundombinu wezeshi na mizuri, ufanyaji biashara ndani ya Taifa letu umerahisishwa kwa kiwango kikubwa. Mmesemea issue ya leseni Serikali tulishaiona tunaendelea kuifanyia kazi, na kupitia Bunge letu Tukufu tuna imani matamanio ya wafanyabiashara wetu wa ndani ya nchi, yatafikiwa lakini pia wafanyabiashara wetu ambao watatoka nje ya nchi kuja kutuletea teknolojia zilizo kule kwenye nchi zao pia nazo tutaendelea kuzishughulikia hatua baada ya hatua.

Mheshimiwa Mwenyekiti baada ya kusema maneno haya naomba sasa kuleta kwenye Bunge lako Tukufu Itifaki hii ya Biashara ya Huduma ya SADC, Ili Bunge letu liweze kuridhia kama Sheria yetu na Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 163, Ibara ndogo ya 3(e) inavyotuelekeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja.

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, naafiki.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
NAIBU WAZIRI FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi naomba nianze kwanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais wetu kwa kazi nzuri anayofanya hasa katika sekta hii ya elimu. Pia niwapongeze sana Mheshimiwa Profesa Ndalichako na mtani wangu Mheshimiwa Ole Nasha kwa kazi njema ambayo mnaifanya katika sekta hii. Mimi naamini mnaandika historia na historia itawakumbuka, mnafanya kazi njema sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa sababu ya jambo ambalo linabezwa humu ndani la elimu bila malipo au elimu bure. Hili ni jambo kubwa kabisa ambalo alianza nalo Mheshimiwa Rais wetu na tukaanza kwa kupeleka shilingi bilioni 18.77 tulipoanza Serikali ya Awamu ya Tano. Tumeongeza tukaenda shilingi bilioni 20.24 leo tunapoongea kwa kila mwezi tunapeleka zaidi ya shilingi bilioni 23.876. Hii ni dhamira njema ya Serikali ya Awamu ya Tano kwamba inataka kuwaondoa watoto wa maskini, wale ambao walikuwa hawaendi shule sasa waende shule wasome bila tatizo. Si vizuri sana tukabeza kila jambo kwa sababu tu mimi ni mpinzani, mimi ni vile lakini hapana, tutende haki katika jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ambalo ningependa kulisemea katika dakika hizi chache ni mchango wa sekta binafsi kwenye sekta hii ya elimu. Kama Serikali tunathamini sana mchango wa sekta binafsi katika sekta ya elimu na ndiyo maana mwaka jana katika mapendekezo waliyotuletea sekta binafsi tuliondoa tozo nne kwa sekta binafsi katika elimu. Hii ni dhamira ya dhati ya Serikali yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Watanzania tumekumbwa na tatizo moja kwamba huwa tunaweza kuongelea zaidi matumizi bila kujiuliza mapato yanapatikana wapi. Hili tukiweza kulielewa vizuri kwamba tuondokane sasa na matumizi tuanze kufikiria mapato, mapato yetu yanatoka wapi. Tunaposema tuondoe hiki na kile na sheria na kanuni zetu zimeweka wazi unapopendekeza ondoa kodi hii lete mbadala basi tulete kodi ipi ili iweze kufidia yale mapato ambayo yameondoka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, dhamira ya Serikari ya Awamu ya Tano ni njema kabisa, tulianza na tunaendelea kutekeleza. Tayari task force ipo kazini, juzi tulikuwa think tank meeting kwa ajili ya kupitia maombi mbalimbali yaliyoletwa na wadau wetu mbalimbali ya kikodi na ushuru mbalimbali, tunaendelea kuyafanyia kazi. Nakiri tumepata maombi pia kutoka kwa ndugu zetu hawa wa sekta binafsi kwenye elimu na sisi tunaendelea kufanyia kazi lazima tushirikiane kwa pamoja kuona maendeleo ya Taifa letu yanapelekwa vipi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho ambalo napenda kulisemea kwa uchache kwa siku ya leo ni hili pia ambalo linabezwa ndani ya Bunge lako tukufu kwamba Serikali haiwathamini na haiwajali walimu, siyo sahihi na nasema hili kwa sababu moja tu. Baada ya kuingia madarakani tulikuwa na tatizo kubwa la watumishi hewa, tumefanya kazi vizuri wameweza kuondoka watumishi hewa. Tumefanya uhakiki wa madai ambayo watumishi wote walikuwa wanadai tumemaliza na sisi sote Waheshimiwa Wabunge ni mashahidi mwezi wa pili Serikali yetu imelipa madai ya shilingi 43,005,747,874 na tumelipa deni hili kwa watumishi wote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tusikilizane tuelewe nini Serikali inafanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika shilingi bilioni 43 tulizolipa zilikuwa ni kwa ajili ya watumishi 27,118. Kati ya watumishi hao walimu walikuwa 15,593. Kwa hiyo, tuiangalie hii ratio kabla ya kutafuta cheap popularity kwamba Serikali haiwajali walimu si sahihi hata kidogo. Lazima twende kwa takwimu tuieleze vizuri tuweze kujua nini Serikali ya Awamu ya Tano inafanya. Niwaambie walimu tuko pamoja na ndiyo maana Serikali imeongeza kufikia shilingi bilioni 23 kwa sababu tunakwenda kuwalipa walimu pesa yao ya madaraka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba sana walimu wetu waendelee kuchapa kazi Serikali ya Magufuli ya viwanda, tunatambua mchango wao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kutufikisha hatua hii.

Pia nichukue fursa hii kuwapongeza Mawaziri wa Wizara hii, Mheshimiwa Waziri, Dkt. Tizeba, pamoja na Naibu wake, kwa kazi nzuri ambayo wamekuwa wakiifanya ndani ya Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kwa kusema machache katika mambo yaliyoonekana yako ndani ya Wizara yetu ya Fedha. Nianze na jambo la kwanza kabisa kusema kwamba kama Wizara ya Fedha tunatambua umuhimu wa Wizara ya Kilimo kwenye ukuaji wa uchumi wa taifa letu na tumekuwa tukiipa kipaumbele cha kutosha kabisa Wizara hii ya Kilimo kama ambavyo bajeti yetu imeonesha, kwa dhati kabisa tunatambua mchango wake na tutaendelea kuwekeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirejee tu kusema Waheshimiwa Wabunge, jambo la msingi tunalotakiwa kuelewa; katika mchakato wa kibajeti na katika theory ya uchumi ambayo ni ya kawaida kabisa, tunatambua mahitaji yako mengi kuliko rasilimali (resources) tulizonazo. Tukilitambua jambo hili tutaweza kwenda sambamba na bajeti ambayo Serikali imependekeza, la msingi tuweke nguvu kwenda kwenye utekelezaji wa bajeti tuliyonayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa niende specific kwenye hoja, nayo ilisema ni asilimia kumi, Maputo Declaration au Malabo Declaration kwamba Serikali ifike huko. Nimeanza kusema kuwa resources ziko chache kuliko mahitaji tuliyonayo. Sote kwa pamoja tuko hapa tumeanza kupitisha bajeti hizi, tulianza na bajeti ya afya tukasema iongezwe, bajeti ya maji iongezwe, lakini la msingi tukubali tu kwamba Serikali inatambua umuhimu na inawapa kipaumbele cha uzito wa juu sana wakulima wetu wa taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili tunafahamu kabisa kuwekeza katika sekta ya kilimo ni jambo la kwanza, lakini pia uhalisia uliopo. Sekta ya kilimo ni nani wawekezaji? Wawekezaji kwenye sekta ya kilimo ni wawekezaji binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siamini sana kama Mheshimiwa Dkt. Tizeba ana mashamba ya kupeleka pesa moja kwa moja. Tunachokifanya kama Serikali kuiwezesha sekta hii ni kuziwezesha sekta nyingine ambazo zinafanya kazi pamoja na sekta hii ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge tunasema Serikali ya vitu badala ya Serikali ya watu, si sahihi hata kidogo. Niliwahi kusema ndani ya Bunge lako tukufu kwamba barabara zetu zimewezesha sasa hivi chakula kinaweza kutembea kwenye mkoa unaozalisha kwenda kwenye mkoa ambao hauzalishi, na ndiyo maana limesemwa pia hili, kwamba tunazuia kuuza mahindi nje, na Mheshimiwa Waziri atalisemea vizuri ili ku-control mfumuko wa bei, hapana, mfumuko wa bei una-attributes zake ambazo zinachangia kwenye mfumuko wa bei, chakula ni sehemu moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa nini chakula ndani ya Tanzania kinachangia kwa kiwango kikubwa, ni kwa sababu Taifa letu limeweza kufunguka kwa miundombinu ambayo Serikali ya Chama cha Mapinduzi imewekeza kwa kiwango kikubwa. Unaweza ukasafiri kutoka Mbeya ukafika Arusha ndani ya siku moja kwa sababu ya miundombinu. Kwa hiyo, twende tu kwa pamoja tuelewe uchumi unafanya vipi kazi ili tuweze kwenda wote kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati yetu ya Kilimo ilisema kuhusu uwekezaji kwenye Benki yetu ya Kilimo (TADB). Tulianza kuwekeza shilingi bilioni 60 na mpaka sasa hivi niwapongeze uongozi wa Benki ya TADB, katika shilingi bilioni sitini waliyokuwa nayo, sasa hivi wana shilingi 66,785,790,000 wameweza kuongeza kiwango hiki katika utendaji wao wa kazi. Vilevile kama Serikali pia hatukuiacha wazi, tumechukua mkopokutoka TADB na kuonesha tunathamini wakulima wetu, bilioni mia mbili na sita zote tumezipeleka kwenye benki yetu ya kilimo. Dhamira ni ileile moja, kuwawezesha wakulima wa Tanzania ili waweze kufikiwa na benki yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kama ambavyo nimekuwa nikiliambia Bunge lako tukufu kwamba Benki ya Kilimo inajiandaa mwezi huu wa tano inafungua tawi hapa Dodoma, mwezi wa sita inakwenda kufungua tawi Mbeya, mwezi wa tisa inafungua tawi Mwanza. Dhamira yetu ni ya dhati, kuwafikia wakulima wetu kule walipo ili waweze kupata huduma hii. Pia katika benki zinazofanya kazi na wakulima ni Benki yetu ya Kilimo. Popote mkulima alipo akishaonesha interest anahitaji mkopo anatembelewa kule alipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kengele imegongwa, naomba nilisemee jambo moja, nalo ni kuhusu Bodi ya Korosho na pesa ambazo zipo. Ni sahihi, pesa ipo na Serikali iko tayari kuitoa lakini lazima tukubali itolewe kwa mfumo upi na inakwenda kufanya nini, hilo ni jambo la msingi sana. Tunalalamika hapa kuhusu utendaji mbovu wa watendaji wetu, lazima tusimame imara wote kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetoa shilingi bilioni kumi kwa sababu tumejiridhisha zinakwenda kufanya kazi ya Bodi ya Korosho, zilizobaki kama Wizara tunaendelea kuzihakiki, na kwa sababu tulishawapa Bodi ya Korosho mwongozo wa nini cha kufanya, wametuletea mahitaji yao na sisi tunaendelea kuhakiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwape mfano tu ndugu zangu umuhimu wa hiki ambacho Serikali yetu inafanya, umuhimu wake ni huu, katika maombi tuliyoyapokea kutoka Bodi ya Korosho, nichukulie kipengele kimoja cha pesa za utafiti. Katika pesa za utafiti walikuwa wameomba shilingi bilioni 7.2, katika shilingi bilioni 7.2 kwa ajili ya utafiti, ndani ya pesa hizi kulikuwa na pesa ambazo haziendi kufanya kazi ya utafiti, sasa ni jambo la ajabu kusema kwamba Serikali tuachie, tupeleke tu kwa sababu sheria inatuelekeza hivyo. Tumepewa dhamana ya kuangalia pesa za nchi yetu. Mfano wa hizi shilingi bilioni 7.2 maombi yalikuwepo na shilingi bilioni 2.8 zinazokwenda kuwalipa honorarium watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo dhamira ya pesa ya utafiti kutumia shilingi bilioni 2.8 kwenda kuwalipa honoraria watumishi, lazima tumeaminiwa na Serikali yetu kusimamia rasilimali fedha ya taifa letu. Tujiridhishe, hii honorarium inayoenda kulipwa, kila mtumishi kwa honorarium hii anakwenda kulipwa shilingi milioni 19 kwa mwaka kwa ajili ya honorarium tu, hapana, tujiridhsihe anakwenda kufanya kazi gani ya ziada inayomuwezesha kulipwa. Tulianza kubana matumizi na mafanikio ya kubana matumizi tunayaona kwenye maendeleo ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme jambo moja nalo ni kuhusu malipo ya watu wa pembejeo. Waheshimiwa Wabunge wamesema vizuri sana; mchanganyiko wanaousema wao ndio ambao Serikali tuliupata, na ili kuondokana nao nani kaiibiwa Serikali katika maombi haya? Vyombo vya uchunguzi vipo kazini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Waheshimiwa Wabunge, sisi kama wasimamizi wa rasilimali za taifa hili tusimame wote kwa pamoja. Vyombo vya uchunguzi vifanye kazi yao. Mheshimiwa Kunti, vyombo vya uchunguzi ni muhimu sana, kama ni watumishi wa Serikali waweze kujulikana nani aliongeza sifuri kwenye shilingi milioni 20 ikawa shilingi bilioni mbili, lazima tuweze kukubaliana na hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, TAKUKURU ikijiridhisha, tukipata taarifa yao, Serikali iko tayari. Pesa si tatizo kwa Serikali ya Awamu ya Tano, tutatoa pesa tutawalipa wote ambao wanaidai Serikali yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa kumshukuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema aliyetufikisha hapa tulipo leo na Serikali ya Dkta John Pombe Magufuli mbele ya Watanzania inaendelea kuthibitisha kwamba ni safi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia na napenda sana kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa kazi anazoendelea kuzifanya, nampongeza sana. Aendelee kukaza kamba, Watanzania wamemuelewa na sisi tutaendelea kutenda kwa ajili ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeanza kuyasema haya ili tuweze kuwa na uelewa wa pamoja kwa sababu yamesemwa hapa kulikuwa na Special Audit, hivi hata kusoma kawaida tu hatujui? Special Audit, nini kilichoandikwa ndani ya taarifa ya Mkaguzi Mkuu na nini kilichoandikwa ndani ya hotuba ya Mwenyekiti na Kamati yake? Mheshimiwa Mwenyekiti nikupongeze sana na Kamati yako kwa kuendelea kusimama imara, hukutikisika hata pale ulipotikiswa na ukahakikisha Watanzania wanakuwa na taarifa sahihi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishukuru sana wachangiaji wote waliochangia, nimshukuru sana Waziri wa Kilimo ile sehemu ya kwanza niliyotaka kuisema ameisema, sasa naomba niende kwenye sehemu ya pili. Tukichukua taarifa hii tukaisoma vizuri, hii ya Mwenyekiti wa Kamati na Kamati ya PAC, tunakwenda kwenye hadidu za rejea kwa nini CAG alitakiwa kufanya uhakiki (verification). Alitakiwa kufanya uhakiki huu na Bunge lako Tukufu kwa sababu, kwanza, siyo kwamba yeye alikuwa na hoja ya upotevu wa shilingi trilioni 1.5. Taarifa zake za mwanzo alizowasilisha mbele ya Mheshimiwa Rais, alizozikabidhi Bungeni hazikuwa na hiyo hoja lakini watu wasiolitakia mema Taifa hili, wasioitakia mema Serikali ya CCM ya Awamu ya Tano wakaja na hoja hii ya upotevu wa shilingi trilioni 1.5. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hata Serikali tulipotoa kauli hapa tarehe 20 Aprili, bado waliendelea kusema na kwa sababu Serikali ya Chama cha Mapinduzi ni sikivu, tulisikia na tukaruhusu na tukatoa vielelezo vyote hata vya ziada vilivyotakiwa ili waambiwe kuna wizi au hakuna wizi. Nashangaa leo wanaposimama wale wale wanasema kwamba anayetakiwa kuthibitisha siyo CAG, mnakula matapishi yenu leo? Kwa hiyo, lazima tu tuseme ukweli, tuseme wazi ndicho walichokihitaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda kwenye taarifa ya Kamati ukurasa wa 18, aliyejibu hakuwa PST, hakuwa Paymaster General alikuwa ni Msaidizi wa CAG. Alisema: “... The difference of Tanzania Shillings 1.515.18 resulted from factors such as differences in information reviewed and adjustments passed by management...”. Mimi tarehe 20 mbele ya Bunge lako Tukufu nilisema wazi kwamba haya yamesababishwa na Ofisi ya CAG kutumia budget execution report ambayo haina adjustments. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndicho nilicholiambia Bunge lako Tukufu kwa kuwa nilikuwa naamini wataalam wangu ndani ya Wizara ya Fedha na Mipango wako makini, hawana tatizo lolote kuhakikisha rasilimali za Taifa hili zinasimamiwa ipasavyo. Naomba niwaambie Watanzania waendelee kumuamini Dkt. John Pombe Magufuli, waendelee kumuamini Dkt. Philip Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango, waendelee kuwaamini watumishi wote wa Wizara ya Fedha na Mipango wakiongozwa na Katibu Mkuu Bwana Dotto James. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi sina wasiwasi wa kuaminika mbele ya Watanzania, wananchi wa Jimbo la Kondoa waliniamini. Kwa hiyo, naamini naaminika sina tatizo. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuondoka hapo tunakwenda kwenye hadidu za rejea. Mheshimiwa Catherine, shika hadidu za rejea kwenye taarifa uliyoitumia kutudanyanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda kwenye taarifa ya Kamati, twende kwenye aya 2.2.2.2, ukurasa wa 26, nini Kamati imesema, naomba kunukuu: “CAG alifanya hitimisho kuwa utekelezaji wa awali na wa sasa unafanana” Watanzania mnajua nini kilikuwa kinatafutwa kwenye hili? Walikuwa wanatafuta kuthibitisha rumors zao mitaani kwamba kuna pesa zinazotumika bila kufuata kanuni na taratibu na Katiba ya Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, anawathibitihia hapa CAG na ili tuweze kumuelewa vizuri, CAG page ya 20 kwa wale wenye taarifa yake someni kaandika nini. Tangu Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani, Katiba ya nchi haijavunjwa kwenye matumizi ya fedha za Serikali. Hicho ndicho kinachotafutwa na sasa wamedhihirishiwa wanakuja na hoja zisizo na mantiki yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukienda kwenye 2.2.2.3, page hiyo hiyo ya 26, nini kilisemwa na conclusion ni nini? Kwa nini tuondoke kwenye hoja? Nilisema asubuhi reallocation between vote siyo kazi ya CAG, ni kazi ya Waziri wa Fedha na Mipango kisheria. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nini CAG ameandika, ukurasa wa 16, Mheshimiwa Zitto fungua, recommendation, alichokisema: We also recommend that, the Treasury ensure that the Minister’s approval, it is the approval of the Minister not of the CAG, not of the Bunge. Kwa hiyo, haya yote yamekwenda ku-cancel uongo wote mtaani leo tunarudi na 2.4 ambayo haipo popote kwenye taarifa ya CAG, haipo popote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, limeongelewa jambo moja hapa la warrant and exchequer issue notification. Hili kwa kuwa Mheshimiwa Hassunga hakulisema naomba nitoe darasa. Liko hivi, exchequer issue warrant ni nini? Exchequer issue warrant ni nyaraka inayoandaliwa na Mhasibu Mkuu wa Serikali kwenda kwa Governor wa Benki Kuu ya Tanzania baada ya idhini ya Mlipaji Mkuu ili ahamishe fedha kutoka akaunti ya mapato kwenda kwenye akaunti ya matumizi. Inapoingia kwenye akaunti ya matumizi kama yule ambaye aliiandika hii pesa kwenye bajeti yake hajatuletea taarifa inayothibitisha kutumia pesa hii hawezi kupelekewa exchequer issue notification. Mhasibu Mkuu wa Serikali anapoandaa exchequer issue reports hii haiwezi kuingia kwenye ripoti yake kwa sababu haijatumiwa na mtu anayetakiwa kutumia. Kwa hiyo, hili lieleweke wazi, tuwaachie wenye CPA zao waongee kuhusu CPA zao lakini wakiwa na uhakika wa nini kinachotakiwa kufanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema haya nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. (Makofi/Vigelegele)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana, kwa kunipa nafasi hii, naomba nichangie Taarifa ya Kamati ya PIC kwa machache yaliyosemwa. Lakini naomba nianze hapa alikoishia Mheshimiwa Hasunga, ndugu zangu Katiba, Sheria wala Kanuni yoyote ndani ya Taifa hili, haipo iliyozuia Taifa hili kufanya biashara ndio maana PIC Mwenyekiti wake anatueleza Serikali kwamba tuendelee kusimamia mashirika yetu ili yaendelee kufanya vizuri. Sasa hiki mnachokisema kwamba Serikali ilinunua korosho elfu tatu na mia ngapi, imeuza bei hii halafu yote ipelekwe kwa mwananchi that is not a business analysis. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo hilo, nilitaka nianze kulisema hivyo, naomba tu tulie ili tuweze kusikilizana na na tuelewe nini Serikali inafanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na jambo moja muhimu ndani ya Kamati yetu ya PIC na niishukuru sana Kamati ya PIC kwa kuendelea kutoa ushirikiano/kutoa ushauri na hata nilipopitia kitabu chenu, maazimio yote, mmeshauri Serikali iwe iendelee kufanya improvement katika maeneo mbalimbali, nakushukuru sana kwa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika tangu nimeingia ndani ya Bunge hili, na ndani ya Wizara ya Fedha, jambo kubwa ambalo Kamati hii ilikuwa inaongelea ilikuwa ni kuimarisha na kuboresha ofisi ya Msajili wa Hazina. Kama Serikali tulilipokea kwa mikono miwili, tukafanyia kazi Maazimio haya ya Bunge na leo hii napenda kumpongeza Msajili wa Hazina na watu wake, wanafanya kazi nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nayasema hayo wanafanya kazi nzuri kwa sababu gawio lililotolewa na Taasisi haijawahi kutokea katika historia ya Taifa hili, tuliona wenyewe Taasisi zimetoa gawio kwa sababu ya uimara wa Ofisi ya Msajili wa Hazina.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili la TEHAMA ambalo Kamati imesema napenda kusema kwamba tayari tumeanza na sasa hivi mfumo, wa TEHAMA wa Ofisi ya Msajili wa Hazina upo katika kufanyiwa majaribio na kati ya taasisi za Serikali, taasisi 27 tayari zimeshafanyiwa majaribio na tayari zimeshazipata mafunzo ya jinsi ya kutumia mfumo huo, mfumo wenyewe unaitwa Financial Analysis Reporting System ambayo ndiyo kazi kubwa ya Ofisi ya Msajili wa Hazina. Kwa hiyo, kama ambavyo Waheshimiwa Wabunge wamependekeza, kama ambavyo Kamati imependekeza tumesikia kama Serikali na sasa tunaifanyia kazi hii sasa itatupa nafasi popote pale alipo Msajili wa Hazina popote pale alipo Katibu Mkuu wa Hazina ataweza kuona Taasisi zote za Serikali zinafanyaje kazi. Hili ni azimio lilikuwa la Bunge na sisi kama Serikali tunaanza kufanyika kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utendaji wa Ofisi ya Msajili wa Hazina na hii ndiyo maana siku zote tunapenda kusema, lazima tuwe na hofu ya Mungu, tunapoongea ndani ya Bunge hili lazima tuwe na hofu ya Mungu. Ndugu yangu, rafiki yangu Mheshimiwa Ester Bulaya uliposema kwamba Ofisi ya Msajili wa Hazina haijawahi kuwasilisha taarifa kwenye Kamati hii, hakuna aliyekataa, ni maoni ya Kamati lakini wewe, kipo ulichokiongezea kwamba taarifa hii Wizara ya Fedha na Mipango ndio inaishikilia taarifa ya Msajili wa Hazina na kuizuia kwamba isiletwe katika Bunge hili Tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme hapana, Maazimio ya Kamati ambayo yaliletwa na sasa, tunayafanyia kazi ilikuwa ni kuhakikisha Ofisi ya Msajili wa Hazina inaongezewa Bajeti na ndicho ambacho Wizara ya Fedha na Serikali imefanya na sasa hivi ndicho walichokisema Msajili wa Hazina kwenye Kamati, wameongea na Ofisi ya Bunge kuona utaratibu na ni lini wawasilishe taarifa yao kwenye Bunge letu tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa ratiba waliyopewa kufika Aprili, 29 taarifa ya Msajili wa Hazina, itakuwa imewasilishwa katika Bunge lako tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi hii na naunga mkono hoja za Kamati zote mbili, ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa hii. Naomba nianze kwa pongezi kwa Waziri, Mheshimiwa Kakunda na Mheshimiwa Eng. Stella Manyanya kwa kazi kubwa wanayoifanya kwenye Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie machache sana katika Wizara hii, mambo mawili au matatu. La kwanza, nianze na alilolisema Mheshimiwa Dkt. Chegeni jana kwamba mimi Naibu Waziri wa Fedha mwaka jana nililidanganya Bunge kwa kutoa takwimu ambazo siyo sahihi kwa biashara zinazofungwa na zinazofunguliwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuliambia Bunge lako Tukufu, sina sababu ya kudanganya kwa sababu niko field, mimi nafahamu kinachotokea, biashara zinazofungwa tunazijua, biashara zinazofunguliwa tunazijua. Nimpe tu taarifa Mheshimiwa Dkt. Chegeni kwamba kwa mwaka huu kuanzia Julai, 2018 hadi Aprili, 2019 biashara zilizofungwa nchi nzima ni 16,252 lakini biashara zilizofunguliwa ambazo ni mpya ni 147,818. (Makofi)

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, huo ndiyo ukweli, huo ndiyo uhalisia. Kama biashara zingekuwa zimefungwa bila kufunguliwa nyingine tungewezaje kukusanya kodi inayokusanya Mamlaka ya Mapato Tanzania?

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, hili lazima tulielewe, kwa sababu sehemu ambako biashara inafungwa tu hiyo wachumi tunaita it is a dormant economy, Tanzania is not a dormant economy na hatujawahi kufika huko, tunaendelea kusisitiza. Kwa hili, nimpongeze sana Dkt. John Pombe Magufuli, Watanzania halali wamemuelewa na wanaendelea kufanya biashara halali. (Makofi)

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, Watanzania wanaendelea kufanya biashara…

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mtulie, kwani wakati mnaongea si tulikuwepo.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tusikilizane na kuna wengine mkianza kutajwa majina huwa mnajisikia vibaya sana. Kwa hiyo, tusifanye fujo ambazo ukitajwa hapa mbele unaanza kujisikia vibaya, tumuache Mheshimiwa anachangia kama wewe ulivyopata fursa ya kuchangia, muache atoe ufafanuzi amalize.

Mheshimiwa Naibu Waziri, zungumza na mimi tu wala hawa wasikupe taabu.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba niendelee kusema uchumi wetu uko imara na makini, tunaendelea kutenda kwa ajili ya Watanzania. Hili ni jambo la msingi sana na ndiyo maana hatujawahi kushuka kwenye makusanyo tangu ameingia Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli madarakani chini ya trilioni moja kukusanya kila mwezi. Huu ndiyo uhalisia na ndiyo tunayoyajua ambao tuko field.

Mheshimiwa Naibu Spika, niende kwenye suala la pili ambalo napenda kuchangia, nalo ni hili ambalo limesemwa hapa kwamba kwa nini waagizaji wa mizigo kutoka nje wanaombwa original documents. Sheria inasema nini? Kifungu cha 234 cha Sheria ya Forodha ya Afrika Mashariki kinamtaka mteja kuleta nyaraka halisi za uingizaji wa mizigo, sheria inatuelekeza hivyo. Kwa mujibu wa sheria hii mzigo wa kuthibitisha muamala wowote ule upo kwa muingizaji wa muamala huo hapa nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sheria inatuambia a burden of proof of any import transaction rests on the shoulder of the importer or the authorities of the exporting country. Tunachokifanya kwa sasa, nimesema Watanzania halali wanafanya biashara halali wamemuelewa Dkt. John Pombe Magufuli na hii lazima tuelewe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni mwaka jana tu kipindi kama hiki ombwe kama hili la mafuta lilitokea, tujiulize swali la kwanza, kwa nini huwa wana-target kipindi kama hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani? Lazima tuelewe scenario nzima kabla hatujasimama kuwatetea, kwa nini wana-target kipindi kama hiki? Sheria inasema hivyo, hiki ni chakula, unapotuletea tuoneshe umeitoa nchi gani kwa original document, hiki ni chakula. Sisi tuliopewa mamlaka haya ya kusimamia tunataka Watanzania walindwe kwa kila hali na lazima tulisimamie jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niyasemee mafuta haya. Mafuta yaliyopo bandarini yalikuja metric tons 14,400. Katika mafuta haya yapo ambayo hawajafanya declaration mpaka leo, yako bandarini lakini hawajafanya declaration, kipi kinafichwa kwenye hilo? Lazima tujiulize ndugu zangu Watanzania. Waheshimiwa Wabunge tuelewe dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni njema sana. Kwa hiyo, lazima kabla hatujabebwa tu tuelewe nini kilichopo kwenye mzigo huo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hawaja-declare mpaka leo, yapo mengine wame-declare ndiyo hayo ambayo hawajaleta original documents na sisi hatutotoa bila kuleta original documents…

MBUNGE FULANI: Sawasawa.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, hatuwezi kutoa mpaka tuweze kutekeleza sheria. Original documents ziletwe tujiridhishe ni crude oil au siyo crude oil kwa sababu crude oil inalipiwa kodi kutoka kwenye country of origin. Kama imelipiwa kule watuletee tujue thamani yake ili tuweze kuwapelekea Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mafuta hayohayo yapo mengine yameondolewa. Mwanzo walisema yanatumika ndani ya nchi lakini wameyaondoa wameyapeleka nchi jirani, lipi linafichwa hapo?

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Kijaji, muda umekwisha lakini inavyoonekana una hoja nyingi sana za kujibu hapo, maliza hoja zako ndani ya dakika moja ninayokuongezea.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nimalizie kwa kusema tunaendelea kusisitiza Watanzania waendelee kumuelewa Dkt. John Pombe Magufuli, biashara halali ziendelee kufanyika na tunaendelea kulinda afya ya Watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2019
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa fursa hii adhimu kwa Wizara yetu na sisi kuweza kuchangia kuhusu hoja iliyowasilishwa Mezani na Waheshimiwa Wenyeviti. Na nitajikita zaidi kwenye hoja zilizowasilishwa na Mwenyekiti wa PAC, Mheshimiwa Kaboyoka.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kumshukuru sana Mwenyekiti yeye pamoja Kamati yake kwa kazi kubwa waliyoifanya na kuleta taarifa hii muhimu sana ndani ya Bunge letu Tukufu. Niseme tu kama ambavyo wamekiri ndani ya taarifa yao hoja zote ambazo ziliwasilishwa mwezi Februari mwaka 2019 tunazifanyia kazi kama ambavyo wamekiri, zimebaki chache sana ambazo tunaendelea kuzishughulikia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niende kwenye hoja ambayo imeonekana imevuta hisia kubwa ya Waheshimiwa Wabunge, nayo ni kuhusu Uchambuzi wa Taarifa ya CAG kwa Hesabu za Serikali kwa Mafungu ya Serikali Kuu na Mashirika ya Umma, hasa hali halisi ya ufanisi katika utendaji wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Kamati ilipendekeza, kama tulivyosikia na kuona wote kwa pamoja kwamba, Serikali iziboreshe na kuziongezea uwezo Bodi za Rufaa za Kodi na Baraza za Rufaa za Kodi kwa kuteuwa Wenyeviti, Makamu Wenyeviti na wajumbe wa kutosha, ili kuziwezesha taasisi hizi kufanya vikao vyake vya kusikiliza na kuhitimisha kesi za kodi kwa wakati, lakini pia kamati ikapendekeza Serikali iweze kutoa bajeti ya kutosha kwa ajili ya taasisi hizi, ili zifanye kazi zake kwa wakati na kwa ufanisi:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa Bodi hizi za Rufaa za Kodi Mheshimiwa Rais ameweza kuteuwa Mwenyekiti na Makamu Wenyeviti pamoja na wajumbe wote wa bodi hizi mbili. Kwa hiyo, hilo ni jambo la kwanza kabisa ambalo kama Wizara tulikuwa tunaliomba na ambalo lilikuwa linachelewesha utendaji kazi wa taasisi hizi mbili muhimu sana katika ukusanyaji wa mapato. Kwa hiyo, sasahivi bodi hizi zina wajumbe wake wote pamoja na Wenyeviti na Makamu Wenyeviti kama ambavyo sheria ilivyopitishwa na Bunge letu Tukufu.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kupata wajumbe hawa bodi hizi zimeanza kufanya kazi vizuri kabisa na tumeweza kwa mwaka 2019 bodi imeweza kushughulikia jumla ya kesi 652 zenye thamani ya shilingi trilioni 2.073 na Dola za Kimarekani 81,644,013. Tuishukuru pia Ofisi ya CAG kwa kuweza kuyasema haya kwenye taarifa yake ya mwaka 2017/2018; imetusaidia na tumeanza kufanyia kazi yote haya na sasa tunaendelea kumalizia machache yaliyobaki.

Mheshimiwa Naibu Spika, niliambie pia Bunge lako Tukufu kwa kesi za mwaka 2017 zote zimeshashughulikiwa na taasisi zetu hizi mbili, hatuna kesi hata moja ambayo imebaki ya mwaka 2017. Kesi za mwaka 2018 zimebaki kesi 13 tu na sasa hivi bodi hizi zinashughulikia kesi zilizofunguliwa mwaka 2019. Kwa hiyo, tumefuta kabisa baklog ambayo taasisi hizi mbili ziliikuta na sasa tunafanya kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niweze kulitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba, bajeti pia, taasisi hizi zinapatiwa bajeti ya kutosha na kwa kesho tu, kesho siku ya Alhamisi zitatolewa hukumu kwa kesi zaidi ya 10. Kuna Makamu Wenyeviti wako Arusha na baadhi ya wajumbe wanaendelea kuendesha kesi hizi. Mwenyekiti yuko Dar es Salaam anaendelea na kesi na baadhi ya wajumbe na Makamu Mwenyekiti wa pili yuko Mwanza na baadhi ya wajumbe wote wanaendelea kuzishughulikia kesi hizi. Ni dhamira ya Serikali yetu kwamba, mpaka kufikia mwezi Juni, 2020 kesi zote za mwaka 2019 ziwe zimekwisha, ili tuanze kushughulika na kesi za mwaka 2020. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya pili ambayo ningependa kuitolea ufafanuzi nayo ilikuwa ni mapendekezo ya Kamati kwamba, Serikali iongeze wataalamu, lakini pia wataalamu waongezewe uwezo wa kufanya kazi katika maeneo yao husika:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuliarifu Bunge lako tukufu kwamba, Serikali yetu kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania imeendelea kuwajengea uwezo watumishi wetu wa Mamlaka ya Mapato katika masuala mbalimbali ya usimamizi wa kodi ikiwa ni pamoja na weledi katika sheria za kodi, ukaguzi na ukadiriaji kupitia mafunzo ya ndani na mafunzo ya muda mfupi na muda mrefu pia. Mafunzo haya hutolewa na chuo chetu cha kodi (Institute of Tax Administration) ambacho kinafanya kazi kubwa sana katika eneo hili kutuandalia wataalam wetu, ili waweze kufanya kazi hizi kwa ufanisi wa hali ya juu.

Mheshimiwa Naibu Spika, na hii tunaiona kwa pamoja kama Taifa. Ni kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa mwezi Juni, kuanzia mwezi Julai, 2019 hadi mwezi Disemba, 2019 Mamlaka ya Mapato walitarajiwa kukusanya shilingi trilioni
9.45 na kwa sababu sasa tunawawezesha wataalam wetu kufanya kazi hii kwa weledi mkubwa Mamlaka ya Mapato kwa miezi hii sita imeweza kukusanya zaidi ya shilingi trilioni 9.1 ambayo ni sawasawa na 96.3%. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni ufanisi wa hali ya juu, tuendelee kuwapa moyo wataalam wetu, lakini pia Watanzania kwa ujumla tuendelee kulipa kodi kwa hiyari tusisubiri kulazimishwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni muhimu sana tukafahamu mengi makubwa yanayotendwa na Serikali yetu ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli yanatendwa kwa sababu ya makusanyo mazuri ya mapato. Kwa hiyo, niwaombe Watanzania kwa pamoja tujitolee kwa hiyari yetu kila mmoja kulipa kodi yake ile anayostahili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilishukuru pia Bunge lako Tukufu walipotupitishia sheria yetu ya fedha ya mwaka jana na mwaka huu tunayoitekeleza pale tulipoleta hoja ya Tax Amnest, imetusaidia sana pia kuweza kukusanya kodi. Hii yote ni mikakati mbalimbali ambayo Serikali inakaa na kutafakari na kuona ni jinsi gani ya kupeleka unafuu kwa walipa kodi, lakini pia Serikali yetu iweze kupata kodi yake inavyotakiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema maneno haya naomba niwapongeze tena Wenyeviti na wajumbe wa kamati zote mbili ambazo zimewasilisha taarifa zao mbele ya Bunge lako Tukufu. Kama Wizara tunasema kwa niaba ya Serikali tutaendelea kuyafanyia kazi yote yaliyopendekezwa na Kamati kwa sababu, tayari tumeshayaanza na ufanisi wake tunauona.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa fursa hii ya kutoa mchango wangu kwenye hoja hizi. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba nianze kwa kuunga mkono hoja na kuwapongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Mawaziri wake wawili kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuhakikisha kilimo chetu kinanyanyuka.

Mheshimiwa Spika, naomba niseme mambo mawili makubwa, na jambo la kwanza ni ambalo limesemwa kwa kiwango kikubwa na Waheshimiwa Wabunge wengi, lile la kufikia asilimia 10 ya bajeti yetu kupelekwa kwenye kilimo.

Mheshimiwa Spika, Serikali yetu inatambua sana umuhimu wa sekta ya kilimo katika kufikia dhima ya mpango wetu wa pili wa maendeleo wa miaka mitano. Hakuna viwanda bila kuwa na malighafi na hakuna malighafi bila kuwa na kilimo.

Mheshimiwa Spika, nimeanza kwa kuwapongeza Waheshimiwa Mawaziri, mchango wa kilimo chetu, kwenye uchumi wetu wa taifa unaonekana sasa na unaendelea kukua; mwaka huu ime-register ukuaji mzuri tu na mimi nawapongeza sana. Hiyo yote imetokana na Serikali kuwekeza katika kilimo chetu. Ndiyo maana pamoja na mambo mengi ambayo Serikali inayo ya kufanya, kwa mfano tunaangalia uhalisia wa mapato yetu kwa mwaka husika ukilinganisha na mahitaji ya lazima yanayohitajika ili mambo mbalimbali yaweze kutendeka. Kwa mfano ulipaji wa Deni letu la Taifa ambalo lilitumika kwa kiwango kikubwa kwa ajili ya miradi yetu ya maendeleo. Vilevile tunatakiwa kuhakikisha watumishi wetu wanalipwa mishahara yao kwa wakati, jambo ambalo Serikali yetu inatenda sasa tangu imeingia madarakani.

Mheshimiwa Spika, pia Waheshimiwa Wabunge tusisahau kwamba tunavyowekeza kwenye kilimo siyo ile pesa inayokwenda moja kwa moja kwenye Wizara ya Kilimo. Tunaweza tukapeleka pesa nyingi kwenye kilimo lakini kama hatuna miundombinu hatutaweza kuleta athari chanya kwenye kilimo chetu, na ndiyo maana Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli tangu akiwa Waziri wa Ujenzi aliimarisha sana miundombinu. Mikoa yetu yote imeunganishwa na sasa tunaenda kukamilisha Mkoa wetu wa Kigoma kuunganisha na mikoa mingine.

Mheshimiwa Spika, lakini pia tunataka kuhakikisha tumbaku inayozalishwa Tabora, pamba inayozalishwa Mwanza inasafirishwa kwa siku moja kufika Dar es Salaam. Hata kama ni viwanda vyetu vya nguo vinavyoenda kuanzishwa kule Bariadi – Simiyu, tunataka kuhakikisha nguo zile zinafika ndani ya siku moja Dar es Salaam. Tunaenda kuwekeza kwenye SGR ili kuhakikisha kilimo chetu kinaleta tija kwa wakulima wetu.

Mheshimiwa Spika, tunaposema Tanzania ya Viwanda, nimesema huwezi kuwa na viwanda bila kuwa na malighafi. Moja ya malighafi ni umeme wa bei nafuu ambao upo unapatikana kwa wakati wowote, ndicho Serikali ya Awamu ya Tano inafanya, kuhakikisha kilimo chetu kinaleta tija katika mnyororo mzima wa thamani wa mazao yetu ya kilimo.

Mheshimiwa Spika, pamoja na mambo hayo, hatujaisahau Wizara ya Kilimo na bajeti nzima ya maendeleo, ndiyo maana mwaka huu tukiangalia kitabu hiki cha bajeti ya kilimo kwenye bajeti ya maendeleo tumeongeza bajeti ya maendeleo kwa asilimia 46. Hii ni kwa sababu tunajali na tunathamini kilimo chetu kwenye mnyororo mzima kuanzia uzalishaji mpaka kwenye mazao yake ya mwisho.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ambalo ningependa kulisemea mchana wa leo ni kuhusu VAT refund. VAT refund sote tunafahamu kwamba Taifa letu liliumizwa kwa kiwnago kikubwa, tunaendelea kulipa madeni haya ya VAT refund…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Malizia Mheshimiwa Waziri.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nashukuru, naomba niseme tu kwamba tayari deni la bilioni 20.8 limeshahakikiwa na linalipwa ndani ya mwezi huu na bilioni 28.8 nalo pia tunamalizia uhakiki wake tunaenda kuwalipa Watanzania na ambao wanatudai ndani ya Serikali yetu.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema haya naomba nirejee kusema naunga mkono hoja na nashukuru sana kwa nafasi hii. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa kukushukuru kwa kunipa fursa hii ili nami nichangie hoja iliyowekwa mezani na Mhehimiwa Waziri Maliasili na Utalii. Nianze kwa kuunga mkono hoja hii, lakini pia kuwapongeza sana Waheshimiwa Waziri na Naibu Waziri wake kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa muda ni mchache naomba niseme hili suala kikodi na tozo kama ambavyo nimekuwa nikisisitiza siku zote nashukuru tumelipokea, tumelisikia wamesema, lakini niendelee kuomba tusiwahishe shughuli, tusubiri muda wa shughuli hii ukifika tutaongelea kuhusu tozo na kodi mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili ambalo ningependa kulitolea maelezo machache ni hili kwamba Serikali ilikataa ofa iliyotolewa na Serikali fulani kwa ajili ya utekelezaji wa mradi mbadala wa mradi wa kuzalisha umeme wa Mto rufiji. Naomba niseme yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kulingana na Sheria ya Misaada, Mikopo na Dhamana, ni Wizara ya Fedha pekee inayoshughulikia mikopo, dhamana na msaada kutoka sehemu yoyote ndani ya dunia hii na wanaposimama Mheshimiwa Mbunge kusema kwamba Serikali ilipata offer na ikakataa tuwe tunajitathimini, kujitafakari nini tunakisema na lengo letu la kusema jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapopata taarifa ya aina hiyo sisi kama Wizara rasmi huwa tunapeleka kwenye Kamati yetu ya Taifa ya Madeni kufanyia analysis ya huo unaoitwa msaada au offer. Tukishamaliza kwenye Kamati ya Madeni, wanamshauri Mheshimiwa wa Fedha. Sasa unapofika kwenye conclusion, unasimama kwenye Bunge Tukufu kuwadanganya Watanzania dhamira yako ni ipi? Hilo lazima tulielewe. Sisi kama wenye Wizara yenye mamlaka ya kushughulika na misaada, mikopo na dhamana hatujawahi kupata formal letter yoyote kutoka sehemu yoyote ndani ya dunia hii kwa ajili ya utekelezaji wa mradi mbadala.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niwaambie Watanzania weendelee kumpuuza Mheshimiwa Mbunge huyu ambaye amesimama akiwa amepewa dhamana kuja kuwadanganya Watanzania. Dhamira ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ni njema sana. Tunakwenda kwenye Tanzania ya viwanda, tunatekeleza Mpango wa Pili wa Maendeleo, Dira ya Taifa letu 2025, kujenga uchumi wa viwanda utakaoleta mabadiliko kwa wananchi wetu, lazima tuwe na umeme wa bei nafuu, lazima tutekeleze mradi huu na naomba niseme tuko tayari na tumeanza kutenda.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia amesema Mhehimiwa Mbunge huyu kwamba Serikali haina uwezo, naomba nimwambie tumejipanga, tumejiandaa na tupo tayari kutekeleza mradi huu na utakamilika kwa wakati na Watanzania waweze kufaidi matunda ya Taifa lao. Ni jambo dogo la kawaida la kujiuliza amesema vizuri Mheshimiwa Dkt. Mollel. Daktari Mollel alipoulizwa ni wao taifa hilo hilo ambalo walisema miaka hiyo kama ungetekelezwa mradi huo ungekuwa ni chanzo kikubwa cha maendeleo ya Taifa lao. Leo kuna nini Watanzania tunatekeleza wenyewe?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tusikubali kutumika bila kuwa na sababu ya msingi, sisi ni Taifa huru, tumesimama na mradi huu tutautekeleza na naomba niliambie Bunge lako Tukufu tayari tumshapeleka Sh.688,650,898,267 kama fedha ya kuanza utekelezaji wa mradi huu na pesa yake ipo wala hatuhitaji kwenda kukopa au kuomba, ipo kwa ajili ya mradi wa umeme wa Mto Rufiji.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la mwisho…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na narejea kusema naunga mkono hoja hii.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nianze kwa kuunga mkono hoja hii na kuwapongeza sana Mheshimiwa Waziri kaka yangu Dkt. Mendrad Kalemani na dada yangu Mheshimiwa Subira Mgalu kwa kazi kubwa wanayoifanya, hakika Taifa linaona na wananchi wetu wanaona na naamini wako kwenye mikono salama sana kwa hiyo waendelee kuchapa kazi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia hoja hii kwa maneno mafupi sana. La kwanza ni kuhusu mradi wetu wa Rufiji Hydro Power Project. Nimesema wiki iliyopita wakati nachangia hapa nikasema Serikali yetu imejiandaa vizuri hatuna wasiwasi na malipo yoyote kuhusu Mradi huu wa Rufiji Hydro Power Project na ndio maana tumeshalipa shilingi bilioni 723, sio kwamba tumefanya makosa, hapana.

Mheshimiwa Spika, Serikali ilikuwa inafahamu kabisa kwamba bajeti uliyotupitishia hapa na Bunge lako Tukufu ilikuwa ni shilingi bilioni 700 kamili lakini mpaka sasa tumelipa bilioni 723.598 ni kwa sababu ya umuhimu wa mradi huu na Waheshimiwa Wabunge wamehoji kwamba zimetoka wapi pesa nyingine, hizi bilioni 23.

Mheshimiwa Spika, naomba kulikumbusha Bunge lako Tukufu kwamba mamlaka ya kufanya uhamisho wa Mafungu kutoka Fungu moja kwenda Fungu lingine ni mamlaka ya Waziri wa Fedha na Mipango. Kunapokuwa na jukumu muhimu, jukumu la msingi ambalo halitakiwi kusubiri mamlaka hiyo Bunge lako Tukufu kupitia Sheria ya Bajeti na kanuni zake alipewa Mheshimiwa Waziri wa Fedha, anafanya uhamisho wa fedha kutoka Fungu moja kwenda Fungu lingine. Hii bilioni 23.598 Mheshimiwa Waziri amehamisha kutoka Fungu 21 - Hazina kwenda Fungu 58 ili mradi huu uweze kutekelezwa na Taifa letu liweze kupata faida iliyokusudiwa.

Mheshimiwa Spika, asubuhi wakati najibu swali hapa niliona kulikuwa na mshangao na mshangao wenyewe ni kwamba kodi haichangii kwenye bei ya bidhaa yoyote inayozalishwa. Kwa Tanzania kwa sasa hivi gharama kubwa kwenye viwanda vyetu ni umeme, umeme wetu ni wa bei ya juu na ndio maana Mheshimiwa Rais wetu alipobeba Ilani ya Chama cha Mapinduzi aliahidi ndani ya miaka mitano, bei ya umeme itashuka na haiwezi kushuka, hakuna miujiza ya kushuka kama hatutotekeleza Rufiji Hydro Power Project, naye Mheshimiwa Rais kwa sababu aliahidi ni mtekelezaji na sasa tunatekeleza. Naomba nimwambie Mheshimiwa Spika na Bunge lako Tukufu tuko tayari Serikali ya Chama cha Mapinduzi kutekeleza mradi huu bila kuchelewa.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ambalo ningependa kulisemea ni kuhusu deni la TPDC na Waheshimiwa Wabunge wamesema kwamba Serikali imeiachia TPDC kulipa deni hili. Uhakika wa suala hili na ukweli wake ni kwamba deni hili kwa sasa linalipwa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi siyo TPDC, ni Serikali kuu ndio inayolipa deni hili na deni lenyewe ni deni la mkopo kwa ajili ya kujenga Bomba la gesi na kuna deni kwa ajili ya mkopo wa Mnazibay. Madeni haya yalichukuliwa kutoka katika Benki ya Exim Bank China na yote haya tumeanza kuyalipa Serikali Kuu.

Mheshimiwa Spika, cha msingi tu tunachotakiwa kufahamu, mkopo huu ulikopwa na Serikali kupitia TPDC kwa makubaliano kwamba miradi hii itakapotekelezwa TPDC itairejeshea Serikali fedha hizi. Hii kwa sababu ni mradi wa maendeleo ambao lazima ulete faida ndani ya Taifa letu, ndio maana Serikali ikasema kwa sababu miradi hii haijaanza kuzalisha vizuri Serikali inalipa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na naunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI: Mheshimiwa Spika, naomba nianze kwa kumshukuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia kufika hatua hii kama Bunge letu Tukufu. Lakini pia, kwa kutupitisha Taifa letu katika mtihani mzito tuliopita, lakini tumepita salama kama Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba pia, kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kuchangia kwenye Bunge hili, niwashukuru sana wapiga kura wangu wa Jimbo la Kondoa kwa kuniamini tena kwa mara nyingine na kunirejesha Bungeni kwa kura za kishindo. Wale waliojaribu kuchezea jimbo lile waliona moto walioupata na naomba wasiendelee kusogelea lile jimbo niko imara na wananchi wananiamini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa hotuba yake aliyowasilisha, wakati akiwasilisha makadirio ya bajeti ya ofisi yake pamoja na Taasisi zilizo chini ya ofisi yake. Ninapompongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu natambua usaidizi mkubwa anaoupata kwa wasaidizi wake hasa dada yetu, mimi binti yangu Mheshimiwa Jenista Mhagama, hongera sana mwanangu unachapa kazi vizuri, unatuheshimisha wanawake hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni dakika chache naomba niseme mambo machache sana nayo ni; kwa nini Tanzania tumeingia uchumi wa kati miaka mitano kabla ya muda tuliojipangia? Tumeingia uchumi wa kati kwasababu ya uwekezaji mkubwa uliofanywa na Taifa letu, chini ya uongozi makini wa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais wetu amefanya uwekezaji kwenye miradi mikubwa na ukisoma taarifa ile ya Benki ya Dunia wameeleza wazi ni kwanini Taifa letu tumeweza kupiga hatua hii kubwa? Kwa hiyo, nitoe wito kwa Serikali yetu na nitoe pongezi sana, kwa Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mwongozo sahihi kwamba, miradi yote mikubwa inakwenda kutekelezwa mpaka ikamilike, pongezi sana kwa Serikali yetu. Nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa usimamizi mkubwa anaoufanya kwenye eneo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninapopongeza hili niombe sana sana, watanzania tuwe makini na tunachokiongea katika muda huu. Tunapoanza kubeza miradi iliyowekezwa na Serikali yetu ya awamu ya tano tunamuudhi Mwenyezi Mungu. Naomba tusimame kwa pamoja na tutambue kwamba wapo wenzetu ambao walifanikiwa kuvuka kutoka kwenye level ndogo ya uchumi kwenda kwenye level kubwa ya uchumi lakini walianguka na wakarudi kwenye uchumi wa chini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati Taifa letu tunapanda kuingia kwenye uchumi wa kipato cha kati, tulishuhudia dunia kuna nchi tatu zilishuka kutoka uchumi wa juu kuja uchumi wa chini, makosa yaliyofanyika ni haya tunayoyaona watanzania tunafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge sisi ni viongozi, tuonyeshe mshikamano dhahiri, mshikamano wa kuyaendeleza yote mazuri ambayo yalianzishwa na Serikali yetu ya Awamu ya Tano. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika mengi mazuri yaliyotendwa na Serikali yetu ya Awamu ya Tano, ni kuleta makao makuu kwa vitendo Jijini Dodoma. Niombe sana tunapokwenda sasa kuanza utekelezaji wa bajeti yetu hii, tuone miradi mikubwa iliyokuwa inaletwa Dodoma na Serikali ya Awamu ya Tano inakamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais wetu, Mama Samia Suluhu Hassan ametoa muelekeo, uwanja wa ndege wa Msalato utekelezwe kwa haraka. Tumenunua ndege nyingi… (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana, dakika tano zimeisha

MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maji
MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishukuru kwa kunipatia fursa hii niweze kuchangia katika sekta hii muhimu kwa wananchi wa Tanzania. Naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri mdogo wangu Aweso, kwa kazi kubwa anayoifanya kwenye Wizara hii na nimuambie, kwa utu wake kwa wema wake Mwenyezi Mungu atakusimamia na utatenda maajabu kwenye Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa kunukuu maneno ya Mheshimiwa Rais mama Samia Suluhu Hassan, aliyoyasema tarehe 22 April, 2021 wakati akihutubia Bunge lako Tukufu, alisema maneno yafuatayo nanukuu: “Licha ya mafanikio yaliyopatikana katika miaka mitano iliyopita, tatizo la maji bado ni kubwa kwenye maeneo mengi nchini. Hali hii inachangiwa na usimamizi usioridhisha wa miradi na vile vile, matumizi mabaya ya fedha zinazotengwa, kwa ajili ya upatikanaji wa maji safi na salama.” (Makofi)

Mheshima Naibu Spika, naomba pia nimnukuu na nikupongeze sana Mheshimiwa Aweso kwa kutambua mchango wa watangulizi wako, Mheshimiwa Eng. Kamwele, Mheshimiwa Prof. Mbarawa. Mheshimiwa Prof. Mbarawa Waziri wa Maji wa Serikali ya Awamu ya Tano mwaka 2020 wakati akihitimisha hotuba ya Wizara yake alisema maneno yafuatayo nanukuu pia: “Tatizo ndani ya Wizara ya Maji sio upatikanaji wa fedha bali ni usimamizi wa fedha zinazopelekwa sekta ya maji.” (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimetanguliza maneno haya ili kumwambia Mheshimiwa Waziri kwamba, anatakiwa atengeneze kitengo chake imara cha usimamizi na ufuatiliaji wa miradi yote ya maendeleo ndani ya sekta yake husika. Hapo ndipo Taifa letu linapoteza fedha nyingi kwasababu, nimemsikia mtanguliza wangu Mheshimiwa Subira Mgalu akisema ukawazingue waliotajwa kwenye vitabu vya CAG. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunakwenda kuwazingua watu ambao wameshawaumiza watanzania faida yake ni nini! Jambo la kwanza, tunatakiwa kwanza tuimarishe usimamizi, sifa ya mradi ina mwanzo na mwisho wa utekelezaji wa mradi husika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na katika Serikali ndani ya Afrika zilizowekeza kwenye mifumo mingi ya kiteknolojia ni Taifa letu la Tanzania. Zipo software ambayo unaweza uka- install ndani ya ofisi yako popote ulipo, kwenye simu yako, ukafanya monitoring and evaluation ya miradi yako yote iliyopo kwenye sekta yako husika. Na hii itatuondoa kwenda kwenye post valuation, watanzania wanaumia wameshapelekewa fedha za kutosha hawapati matokeo chanya, hapana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, twendeni kimkakati miradi yote inayopelekewa fedha siku ya kwanza ujue inaanza tarehe 1 mwezi Julai inamaliza tarehe 1 mwezi wa Septemba, nenda nayo kila siku na utaokoa fedha za kutosha za watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa nijielekeze jimboni kwangu Kondoa, sisi wana Kondoa tunabahati kubwa tuna chanzo cha maji cha Mto Moko. Chanzo cha maji cha Mto Moko umekieleza ukurasa wa 27 kwenye kitabu chako. Ulipoeleza chanzo hiki Mheshimiwa Waziri kule ambako chanzo cha maji kipo, ni vijiji viwili tu vinavyopata maji kutoka kwenye chanzo hiki cha maji. Vijiji vyote vinavyopata maji kutoka kwenye chanzo hiki cha maji vinakwenda Wilaya ya Chemba. Kwa nini mradi huu usihujumiwe na kule ambako mabomba yanapita? Wananchi wanaona maji yanakwenda Chemba lakini wao hawana maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri nilishafika ofisini kwako nikakuambia, nimeona wananchi wametoboa bomba linalopeleka maji Chemba nikawauliza kwa nini wanafanya hivi? Wanasema maji yanatoka kwetu sisi hatuna maji, tunahangaika na maji tunaangalia maji yanakwenda sehemu nyingine hapana. Basi naomba Mheshimiwa Waziri nipendekeze, mnapotekeleza miradi ya maendeleo tekelezeni sera ya maji ya mwaka 2002, inayoelekeza kila Kijiji ambako miundombinu ya maji inapita, basi wao wapate maji kwanza kabla ya kule mnakowapelekea. Hii itawezesha miradi yetu na miundo mbinu yetu ya maji iweze kuwa ya kudumu kwa sababu, walinzi wa kwanza wa kudumu watakuwa ni wanavijiji ambayo mabomba yale yanapita kwenye vijiji vyao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye ukurasa wa 27 wa kitabu cha Mheshimiwa Waziri anapendekeza pia vijiji 11 vya Wilaya ya Chemba vinakwenda kupata maji kwenye bwawa la kimkakati la Kisangaji ambalo linajengwa Wilaya ya Kondoa. Kwa hiyo, vijiji 11 vipo Chemba, bwawa lipo Kondoa, hakuna Kijiji hata kimoja cha Kondoa kinachokwenda kupata maji. Wanakondoa wamekukosea nini Mheshimiwa Waziri? Naomba sana mtekeleza Sera ya Maji wapatieni maji pale Bwala la Kisangaji lilipo vijiji vyote vilivyozunguka bwala hilo viweze kupata maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimalizie kwa kumwambia Mheshimiwa Waziri kwamba akiimarisha Kitengo cha Tathmini na Ufuatiliaji miradi yote, mfano mradi uliopo katika Kijiji cha Sauna Kisese ingekuwa ya kuendelea mpaka leo sasa miundombinu imechoka kwa sababu hatufuatilii, fedha nyingi zimewekezwa, wananchi wanakosa maji. Vijiji vya Busi, Sambwa na Pahi wana miundombinu ya maji inahitajika fedha kidogo sana lakini Wizara haifuatilii na haijui nini kinaendelea tutakuja kuwekeza fedha nyingine nyingi ambazo hazitakuwa na msaada tena maana miundombinu ile itakuwa imeshachoka na imeoza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema maneno haya nimalizie kumtakia kila la kheri Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ameanza vizuri na amesema tatizo la maji ni la kwake analibeba kwa kuwa ni mama. Nina uhakika kwa uchapakazi wa Mheshimiwa Waziri atamtendea haki mama yetu, atawatendea haki Watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa fursa hii. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo
MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia kwenye Wizara hii muhimu kwa maendeleo ya watu wetu.

Mheshimiwa Spika, naomba nianze kwa pongezi kwa Mheshimiwa Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan kwa mwongozo wake sahihi alioutoa na hasa kusababisha mfumo wa stakabadhi ghalani kusitishwa kwenye Mkoa wa Dodoma mwaka huu, 2021. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni uongozi makini na sina wasiwasi na uongozi wa Profesa Mkenda, nimefanya naye kazi ni kiongozi makini, nina uhakika atatuvusha Watanzania. Lakini pia Mheshimiwa Naibu Waziri, kaka yangu Bashe nikupongeze sana tumeanza mbali tangu tukiwa wanafunzi. Nafahamu uwezo wako, simama kwenye haki na Mwenyezi Mungu atakusimamia utatenda vyema. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimepongeza kwa kufutwa kwa stakabadhi ghalani au kusitishwa kwa mwaka huu 2021. Lakini Wanakondoa wamenituma niulize kwa Serikali, je ni mwaka huu tu 2021? Au mfumo huu kwa mikoa ambayo hatuna mfumo ambao ni strong wa ushirika, hauruhusiwi tena kufanya kazi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimetumwa kuuliza suala hili kwa sababu mwaka jana Mkoa wa Dodoma na hasa Kondoa tulipita kwenye mazingira magumu sana. Nilimsikiliza vizuri Mheshimiwa Mbunge wa Songwe jana Mheshimiwa Mulugo akiongea mpaka kufikia kutishiwa kwa ajili ya kutetea wananchi wake. Mheshimiwa Mulugo, mwenzako Kondoa mwaka jana ilikuwa ni zaidi ya kuuwawa, sasa sijui zaidi ya kuuwawa ni nini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni hatari mno, unaposimama na wananchi unawaeleza mfumo wa stakabadhi ghalani ni nini? Mfumo wa stakabadhi ghalani hauji kwenye masoko peke yake. Tunapoongelea kwenye masoko hapa tunaukuta mfumo wa stakabadhi ghalani na TMX, hapa ni climax. Lazima uwe umeshaanza kufanya kazi kuanzia kwenye uandaaji wa mashamba ya wananchi. Wananchi wanaandaje mashamba? Wanapataje mbegu bora na sahihi? Wananchi hao wanatunzaje mazao yao? Wananchi hawa, je wana vyama vya msingi kwenye maeneo yao? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wewe unatoka Dodma, nimekusikia jana umesema na wewe unashukuru mwaka huu kusitishwa lakini wananchi wetu wameumia. Wapo wananchi wameamua kuacha kulima zao la ufuta kwa sababu ya mfumo huu wa stakabadhi ghalani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa Mheshimiwa Waziri, Profesa Mkenda kaka yangu nikuombe sana hebu angalia huo mfumo. Kwanini wananchi wanaupigia kelele? Yaani Serikali inasema unamsaidia mwananchi halafu mwananchi anapiga kelele? Hapa mbona ni vitu viwili ambavyo havieleweki. Unakuja kufuta mfumo wa stakabadhi ghalani tayari wakulima wameacha kulima ufuta, umetusaidia kweli? Hebu tunaomba tuanzie mwanzo tusimame imara tuone ni jambo gani tunatakiwa kufanya. Kwanini mfumo wa stakabadhi ghalani?

Mheshimiwa Spika, walikuja pamoja, stakabadhi ghalani pamoja na TMX, na kwa hili naomba niishauri Serikali yangu tukufu. Soko lile la bidhaa TMX wamewekeza kiwango kikubwa kwenye miudnombinu ya TEKBOHAMA. Mifumo ile iliyowekezwa tusi--justify kwa kuumiza wananchi wanyonge, hapana. Kwa hiyo, jambo la msingi kwenye mfumo ule wa TMX soko la bidhaa kwanza Serikali iangalie pale ambapo ipo Wizara ya Fedha ni sehemu sahihi ya kuweka soko la bidhaa? Soko la bidhaa linatafuta masoko. Masoko yanatafutwa na Wizara ya Viwanda na Biashara, inakuwaje TMX ina-hang kwenye Wizara ya Fedha. Inakuja inajiunganisha na Wizara ya Kilimo hapa katikati kuna kitu kinakosekana. Kwa hiyo, tusiende kuwaumiza wananchi wetu kwa sababu ya vitu ambavyo hatujavifanyia kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nim-quote Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika. Alisema maneno yafuatayo; the future millionaires and billionaires of Afrika will come initially from agriculture. Kilimo…

SPIKA: Ahsante sana.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022
MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kukushukuru wewe kwa kunipatia fursa hii ya kuchangia hoja ya mawasilisho matatu yaliyofanywa na Mheshimiwa Waziri wa Fedha kuhusu Hali ya Uchumi wa Mwaka 2020, Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha pamoja na watumishi wote wa Wizara ya Fedha na taasisi zake zote kwa kutuandalia bajeti nzuri ya kimkakati kwa maendeleo endelevu ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee kabisa naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Naomba kumuita kwa jina hili; the Tanzanite super woman of our time. (Makofi/ Vigelegele)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais wetu ameanza vizuri uongozi ndani ya Taifa letu kama Rais wa Serikali ya Awamu ya Sita. Bajeti iliyowasilishwa siku ya tarehe 10, Juni, 2021 inadhihirisha umakini, ujasiri na weledi wake katika eneo la uchumi wa Taifa letu; pongezi nyingi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia bajeti hii inathibitisha msemo wa wahenga unaosema mama ni nguzo na mlezi wa familia. Nayasema haya kwa sababu kuu mbili kwa siku hii ya leo kwa sababu ya muda; sisi sote Watanzania ni mashahidi kwamba chini ya uongozi thabiti wa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli na msaidizi wake namba moja mama Samia Suluhu Hassan, Taifa letu limehimili mtikisiko na mdororo wa uchumi wa athari ya Ugonjwa wa Korona (UVIKO-19) kwa mwaka 2020.

Mheshimiwa Naibu Spika, nalisema hili kwa sababu katika taarifa iliyowasilishwa, Taifa letu ni miongoni mwa mataifa 11 tu kati ya Mataifa 45 yaliyo Chini mwa Jangwa la Sahara ambayo uchumi wetu umekuwa kwa ukuaji chanya wa asilimia 4.8. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mataifa 43 yaliyo chini ya Jangwa la Sahara ukuaji wao wa uchumi umekuwa kwa ukuaji hasi, na mataifa mawili yameona ukuaji wao wa uchumi ni sifuri. Hakika tunastahili kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wetu kwa kuweza kuhimili mtikisiko huu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, uhimilivu huo wa uchumi wetu haujaletwa na jambo jingine bali ni ujasiri, uthubutu wa viongozi wetu wakuu na sasa tukiongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati Hayati Dkt. John Pombe Magufuli alipotuambia Watanzania tufanye kazi wapo wenzetu walitukimbia humu Bungeni tuache kupitisha bajeti, lakini kwa umakini wa viongozi wetu tulisimama imara bajeti tuliyoipitisha ndiyo hii leo inatueleza zile mbinu zote na mikakati mbalimbali tuliyoitekeleza imewezesha Taifa letu kuwa moja ya nchi chache zilizoweza kuhimili mtikisiko huu wa uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ambalo limesababisha nimsifu Mheshimiwa Rais wetu, katikati ya kipindi hiki kigumu cha Corona mwaka 2020 tuliona Taifa letu likiingia katika kundi la nchi zenye hadhi ya uchumi wa kipato cha kati, miaka mitano kabla ya kipindi tulichojiwekea Watanzania kwenye Dira yetu ya Maendeleo ya Taifa. Hili nalo jambo tunasema ni jambo ambalo limeishangaza dunia tumewezaje kama Taifa, tumeweza kwa sababu tuna viongozi jasiri na sasa tuna mwanamama shupavu anayetupa miongozo ya kutenda yaliyo makubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sababu moja kubwa iliyofanikisha Taifa letu tuweze kuingia katika nchi zenye hadhi ya uchumi wa kipato cha kati ni uwekezaji kwenye miradi mikubwa ya kielelezo. Ukisoma bajeti iliyowasilishwa pamoja na Mpango wa Pili wa Maendeleo, tunaona commitment kubwa ya Serikali yetu ya kwenda kuikamilisha miradi hii ya kielelezo ambayo itaendelea kutuwezesha kufanya uchumi wetu uendelee kuwa imara. Pongezi nyingi sana kwa Rais wetu na Serikali yake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, commitment hii ya Mheshimiwa Rais inadhihirisha nadharia ya uwekezaji kwenye miundombinu (theory of economics of infrastructure investment) inayotuambia kwamba uwekezaji kwenye miradi mikubwa hasa ya miundombinu lazima ifanywe na Serikali yenyewe. Jambo ambalo tulisimama imara Serikali ya Chama Cha Mapinduzi tukasema tunakwenda kuwekeza kama Serikali kwa sababu tunahitaji kuona matokeo chanya ya uwekezaji wetu huu ambao tunaufanya na ambao tayari tumeshaona matumaini makubwa ndani ya uchumi wetu ulio imara kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya pongezi hizo naomba sasa niishauri Serikali yangu. Nianze kwa kupongeza kwa kupeleka asilimia zaidi ya 37 ya bajeti nzima kwenda kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa mwaka huu 2021/2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili thamani halisi ya fedha zetu asilimia 37 zaidi ya trilioni 13 tunazozipeleka kwenye Miradi ya Maendeleo iweze kuonekana kwenye maisha halisi ya wananchi wetu naomba kushauri mambo yafuatayo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, naomba Serikali yetu sikivu iimarishe Idara ya Mipango ya Kitaifa; Idara ya Mipango ya Kitaifa iwezeshwe ili iweze kufanya kazi yake ya tathmini na ufuatiliaji wenye tija kwa ajili ya Taifa letu. Idara hii inapendekeza iwezeshwe katika maeneo makuu matatu; eneo la kwanza iwezeshwe kwenye eneo la Rasilimali fedha, eneo la pili iwezeshwe kwenye eneo la Rasilimali watu na eneo la tatu iwezeshwe kwenye eneo la rasilimali teknolojia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni imani yangu tukiiwezesha Idara hii ya Mipango ya Taifa inaweza kufanya kazi kubwa ya kufuatilia miradi mbalimbali ya maendeleo na fedha nyingi zinazowekezwa na Serikali yetu kwenye miradi ya maendeleo. Tatizo kubwa la ndani ya Taifa letu siyo upelekaji wa fedha bali ni usimamizi, ufuatiliaji na kufanya tathimini ya fedha zile tunazozipeleka kwenye miradi ya maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ambalo ningependa kushauri katika idara hii, pia niombe sana tunahitaji kufanya kubadilisha mfumo wa kitaasisi wa jinsi kazi ya ufuatiliaji na tathimini inayofanyika ndani ya Serikali yetu. Wizara ya Fedha na Mipango naomba sana muweke nguvu kwenye neno Mipango ndani ya Wizara yenu hapa ndipo kwenye kupanga mipango kwenye ufuatiliaji kuhakikisha kwamba tunahakikisha tunapata thamani halisi ya fedha inayopelekwa kwenye eneo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hili ni eneo muhimu sana kwa sababu mara nyingi tumeona tukifanya ufuatiliaji baada ya miradi kukamilika. Hili jambo linapelekea fedha nyingi za Serikali kupotea, nipendekeze ikiwapendeza Serikali yetu tuwe na real time monitoring and evaluation ya miradi yote tunayopeleka fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa tuanze kufuatilia…

NAIBU SPIKA: Kengele ya pili imeshagonga Mheshimiwa, ahsante sana.

MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sekunde thelathini.

Mheshimiwa Naibu Spika, napendekeza kwamba kabla fedha haijapelekwa idara hii ya mipango ya kitaifa ikajiridhishe na eneo ambalo tunakwenda kuwekeza, lakini mchakato mzima wa manunuzi ukoje kwa sababu miradi mingi tunaona wanachelewesha katika eneo la manunuzi, fedha nyingi za Serikali zinapotea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukifanya pia ufuatiliaji wakati wa utekelezaji naamini alichokisema Mheshimiwa Rais jana pale wakati anazindua jengo la Benki Kuu pale Mwanza, kwamba pesa iliyowekezwa ni kubwa kuliko jengo linaloonekana hatutoweza kusikia kauli hizi tena kwa sababu idara hii itafanya kazi yake inayotakiwa na thamani halisi ya fedha itaonekana.

NAIBU SPIKA: Haya ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naunga mkono hoja. (Makofi)
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo kwa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024
WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nami nianze kwa kukushukuru kwa kunipa nafasi hii ili nami nichangie kwenye wasilisho hili la Mheshimiwa Waziri wa Fedha. Pili naomba niseme Waheshimiwa Wabunge kama Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara tumewasikia, maoni yenu tumepokea na tunakwenda kuyafanyia kazi ili tunapokuja sasa na mpango wa maendeleo kwa mwaka 2023/2024 uwe umebeba maaoni ya wananchi kwa sababu Wabunge ni wawakilishi wa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wetu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya hasa kwa kufungua Taifa letu, kwa kutuletea wawekezaji na kutuletea wafanyabiashara wa kutosha pia kuwapeleka wafanya biashara wa Tanzania kulifikia soko la Dunia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yamesemwa mengi kama nilivyosema tumepokea naomba nisemee moja tu nalo ni kuhusu Bagamoyo Special Economic Zone. Tunapoiongelea eneo maalum la kiuchumi la Bagamoyo lina miradi kadhaa ambayo bandari ni sehemu mojawapo ya miradi hiyo iliyopo kwenye eneo hili. Kwa hiyo, ningeomba sana Waheshimiwa Wabunge na nashukuru mmesema mawazo mema na mazuri ambayo kama Serikali tumeendelea kuyafanyia kazi na niwashukuru sana Viongozi wetu wa Taifa hili kuanzia Rais wetu Mstaafu wa awamu ya Tatu aliliona na likawekwa kwenye Dira ya Taifa ya Maendeleo ambayo imeanza kutekelezwa mwaka 2000 mpaka 2025.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nampongeza sana Mheshimiwa Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne akalibeba na kuanza utekelezaji wake, Mheshimiwa Rais wetu Hayati Dkt. John Pombe Magufuli naye kwenye Awamu ya Tano alilifanyiakazi na ikafika alipolifikisha. Namshukuru sana Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amelibeba jambo hili na ameliondoa kwenye mkwamo uliokuwepo. Kwa sababu mwanzo ilikuwa inaongelewa bandari peke yake, Mheshimiwa Samia suluhu Hassan amesema tukijenga bandari peke yake bila miundombinu mingine wezeshi hiyo bandari haitofanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukijenga bandari peke yake bila kuwa na Mji wa viwanda pale Bagamoyo tutakuwa hatujafika dhamira njema iliyowekwa kwenye Dira ya Taifa ya Maendeleo. Katika hili ukijenga bandari bila kuwa na logistic hub utakuwa hujafanya lolote. Mheshimiwa Rais ametoa maelekezo na nikushukuru sana wewe Mheshimiwa Mwenyekiti na Bunge lako Tukufu lilitupitishia bajeti na sasa tunahitimisha kufanya mapitio ya mpango kabambe wa eneo zima la Bagamoyo ambalo tunahitimisha Tarehe 15/11/2022 tukishakuwa na master plan mpya itatueleza sasa ni kipi cha kufanyika kwenye eneo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, iliulizwa pia kuhusu eneo hili kuhusu fidia wapi tumefikia. Niseme kwa historia nilioitoa yapo maeneo ambayo tayari yalishalipiwa fidia na yako maeneo ambayo yalikuwa hayajalipiwa fidia. Eneo lote ambalo lilitarajiwa enzi hizo kujengwa bandari lote la hekta 800 lilishalipiwa fidia, lakini eneo lote ambalo lilikuwa lijengwe Chuo cha Teknolojia tayari lilishalipiwa fidia nalo ni eneo la hekta 179.7.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lote pia ambalo lilikuwa lijengwe Chuo cha Uongozi ambalo ni hekta 198 lililipiwa fidia, eneo lililobaki lilikuwa halijalipiwa fidia kwa sababu kulikuwa na changamoto ndani yake na ndiyo maana ya Serikali kuelekeza sasa turejee kwenye mpango kabambe mpya ili eneo hili sasa tuhitimishe na tuwalipe fidia wale waliotakiwa kulipwa, lakini wapo Watanzania wenye maeneo yao kwenye eneo hili ambao wako tayari kuwekeza hatutakiwi kuwalipa fidia kwa sababu wanawekeza kulingana na mpango kabambe. Kwa hiyo, hili tunalibeba tunakwenda nalo niwahakikishie wananchi wa Bagamoyo, niwahakikishie Watanzania tuko tayari kwa ajili ya eneo hili. Ahsante sana. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022
WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nami naomba nianze kwa kuwapongeza sana Wenyeviti wa Kamati ambao wamewasilisha taarifa siku hii ya leo. Kipekee kabisa naomba nimpongeze Mheshimiwa Kihenzile kwa kazi njema anayoifanya pamoja na Wajumbe wa Kamati yetu ya Viwanda, Biashara na Mazingira. Kwa kweli, niwashukuru sana kwa maelekezo, kwa mashauriano, lakini ushirikiano mwema ambao tumekuwa nao ndani ya Kamati yetu katika utendaji wetu wa kazi. Niwaombe sana tuendelee kushirikiana kwa maslahi mapana ya Taifa letu kwani tunatambua uchumi wa Taifa letu unajengwa kwenye msingi wa viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema haya, naomba pia, niseme sisi kama Wizara kwa niaba ya Serikali tumepokea maoni yote, lakini pamoja maelekezo yaliyotolewa na Kamati yetu ndani ya wasilisho lao siku hii ya leo. Ushauri wao tumeupokea, kama ilivyo kawaida tutaendelea kushirikiana katika kuufanyia kazi. Tutaendelea kukumbushana wapi tuimarishe zaidi ili tuweze kusafiri salama katika safari ya maendeleo ndani ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya utangulizi huo, naomba niseme mambo mawili tu. Moja, ni lile tuliloanzanalo, mradi unganishi wa Liganga na Mchuchuma. Kamati yetu imekuwa na maelekezo mazuri tu ambayo kama Serikali tumeendelea kuyafanyia kazi na tulikofika ni sehemu nzuri. Niombe tu Kamati yetu, kama ambavyo wametuelekeza tuharakishe ili tuweze kufanikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua umuhimu wa chuma, tunatambua umuhimu wa makaa ya mawe katika uchumi wa dunia kwa sasa, yalipigwa marufuku, lakini walewale waliopiga marufuku wameyarejea kunyumenyume makaa ya mawe na bei yake imeongezeka duniani. Tunatambua kama Serikali na tunakwenda pamoja katika milima yetu ile ya Liganga na Mchuchuma tufanye kazi kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyotangulia kusema asubuhi dhamira ya Serikali ni njema katika kuhakikisha rasilimali hizi za Taifa ambazo tumebarikiwa na Mwenyezi Mungu ziweze kulinufaisha Taifa letu. Tunapoongelea jambo hili niwashukuru pia, nirejee Mheshimiwa Ole-Sendeka na Mheshimiwa Nyongo, walisema vema kuhusu mkataba ule ambao tunakiri Serikali iliusaini,tunakiri wala hakuna anayepinga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapokuwa tumeusaini ule mkataba na ikagundulika kuna makosa yalifanyika, ni wazi kosa moja haliwezi kuzalisha kosa la pili. Lazima turekebishe ili tusafiri pamoja na mradi huu uweze kuwa wa mafanikio kwa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapoendelea kulifanya jambo hili niwaombe, sisi kama wawakilishi wa wananchi, tuitambue dhamira hiyo njema ya Serikali yetu kuhakikisha miradi yetu yote ya msingi inalinufaisha Taifa letu. Tumefika pazuri, kama nilivyosema, tunafanya kazi vizuri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili kuhakikisha mkataba huu ambao tuliusaini tunapouvunja tusije tukaliingiza Taifa letu kwenye mgogoro mwingine. Kwa hiyo, ndio maana nimesema tumepokea maelekezo ya Kamati tutakwenda nayo kwa umakini ili tuhitimishe vyema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kidogo tu niseme, Mheshimiwa Askofu Josephat Gwajima amesema vyema kabisa wala hakukosea, lakini nimkumbushe Mheshimiwa Gwajima, tulisema kwenye Kamati mwekezaji huyu hatukatai tulisaini mkataba, lakini baada ya kusaini mkataba tumegundua tatizo, tumemwita njoo tuongee. Ameitwa zaidi ya mara tano na Serikali, hakuwahi kutokea, sasa huyo tutasema kweli bado tumbebe ni mwekezaji? Hapana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maslahi mapana ya Taifa tutasema hapana, kama kweli ni mwekezaji aje mezani tukae tuongee kwa pamoja. Pale palipofanyika makosa tuparekebishe, tuendelee kama kweli yuko serious na mkataba huu. Kama ataendelea kugoma na sisi kama Serikali tunaendelea kukusanya taarifa kutoka kulekule nchini kwake, tumtambue sawasawa kama bado kweli ni mwekezaji, then Serikali itafanya maamuzi sahihi ambayo hayataliumiza Taifa wala mwekezaji mwenyewe hataumizwa kwa sababu, tumeshampa nafasi ya kutosha ya kumwita tukae mezani, lakini amekuwa hatokei. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, juu ya hili nisisitize tu maelekezo ya Kamati yako. Walituelekeza kwa sababu, tumechelewa muda mrefu, mwaka jana tumeelekezwa, ni vizuri basi tuendelee mbele kuwalipa fidia wananchi wa eneo lile. Serikali ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ni sikivu, tumepokea na kabla ya kulipa tukakubaliana humu humu Bungeni lazima tukafanye uhuishaji wa taarifa ile ya uthamini kwa sababu, ilifanyika mwaka 2015 ili tusivunje sheria tunapowalipa wananchi wetu.

Mheshimiwa mwenyekiti, tumekamilisha kazi ya uhuishaji wa taarifa ile ya uthamini ambayo mpaka sasa Serikali iko tayari ndani ya miezi hii miwili tunakwenda kuwalipa wananchi wetu baada ya uhuishaji wa taarifa yao.

WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya uhuishaji wa taarifa yetu hii ya uthamini wa wananchi wetu, tunatambua kama Serikali na bajeti tunayo. Bajeti tuliyonayo ni Shilingi 15,979,788,646.50. Hii ndiyo thamani sasa tunayokwenda kuwalipa wananchi wetu ili hata tutakapotaka kwenda kuingia kwenye majadiliano na mwekezaji yeyote tuwe eneo lile hatuna tena mgogoro na wananchi. Ni Serikali ya Mama inayosikiliza wananchi wake, na tayari kazi hii tumeshaihitimisha. Niwahakikishie wanakamati pamoja na Bunge letu Tukufu tuko makini, tutahakikisha miradi yetu yote ambayo ipo kwenye rasilimali za Taifa letu ziweze kuwanufaisha wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo napenda kulisemea, imeongelewa Kampuni moja ya SICPA. Kampuni hii ina mkataba, ninavyotambua kule Mamlaka ya Mapato, namwachia Mheshimiwa Waziri wa Fedha ataiongelea, lakini kampuni hii isichanganywe. Kampuni hii ilipokuwa na mkataba na Serikali ambapo ikimaliza kazi yake ituachie Watanzania, ilikuwa ni kwenye uzalishaji wa vinasaba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye uzalishaji wa vinasaba, kampuni ilimaliza mkataba wake na tuliwaongezea mwaka mmoja na bei ilipungua kutoka kwenye kinasaba kimoja ambacho kinawekwa kwenye lita 1000 za mafuta kutoka Dola nane mpaka Dola mbili kwa mkataba wao wa mwaka mmoja. Kwa nini tuliongeza mwaka mmoja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliongeza mwaka mmoja kwa sababu ilikuwa watufundishe sisi TBS tuweze kuzalisha kinasaba chetu wenyewe. Tayari hatua ya kwanza kinasaba cha TBS kimeshapitishwa na taasisi zote za viwango na ndani ya miezi sita tunahitimisha na tunafunga mkataba na SICPA kwenye uzalishaji wa vinasaba. Ni Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara na ubunifu uko ndani yetu, tumeshazalisha kinasaba chetu. Hatutaingia tena mkataba na kampuni hii kwenye uzalishaji wa vinasaba vinavyowekwa kwenye mafuta yanayoingia ndani ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa mwenyekiti, kwa hiyo, naomba tusichanganye mambo haya mawili. Maana kampuni hii imeitwa ni wezi; hapana ndugu zangu, tulipotoka tusirudi. Twendeni tufanye kazi na Kampuni zetu. Kampuni haziwezi kuwa mwizi kama sisi hatujawa wezi. Kwa hiyo, kama sisi tumekubali kuukataa wizi na makampuni yetu ya kibiashara hawawezi kuwa wezi. Nasi tumeamua, Serikali ya Awamu ya Sita tumeanza na kinasaba chetu, tuko tayari. Ndani ya miezi sita tuko sokoni na wala hatuhitaji tena kuingia mkataba na yeyote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitamani niseme hayo mawili. Nakushukuru sana kwa fursa hii. Naiomba Kamati yetu, ushirikiano wetu ndiyo mafanikio yetu ndani ya Wizara na Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)
Azimio la Bunge Kuhusu Pendekezo la Kuridhiwa Mkataba Baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Dubai kwa Lengo la Kuanzisha Ushirikiano wa Kiuchumi na Kijamii katika Uendelezaji wa Maeneo ya Bandari Nchini
WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nami nakushukuru sana kwa kunipa fursa niweze kuchangia kwenye hoja iliyowekwa mezani na Mheshimiwa Profesa Mbarawa kuhusu azimio hili.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumshukuru sana Mwenyezi Mungu ambaye ametufikisha hapa tulipo kuanzia pale safari yetu ilipoanzia kwenye jambo hili. Naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi yake njema anayoifanya kwenye eneo la uwekezaji. Mheshimiwa Rais yeye ameamua kulifungua Taifa letu na tumeona uwekezaji tunaoupokea na wawekezaji tunaowapokea ndani ya Taifa letu sasa ni zaidi ya asilimia 100 ya miaka ya nyuma ambayo ilikuwepo. Kwa hiyo, kwa kweli Mheshimiwa Rais tunampongeza sana, hata jambo hili lilikoanzia ni kwenye maonesho ya Dubai Expo 2020 ambayo yalifanyika mwaka 2022. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata Mheshimiwa Rais alipoamua kwenda kwenye maonesho yale wapo waliosema kwa nini anakwenda. Kwa hiyo, hili ya kuongea huko nje wala Mheshimiwa Rais naamini halimpi shida kwa sababu ameyazoea, cha muhimu ni kuona anatekeleza malengo yale aliyoapa kuyakeleza kwa niaba ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye siku ya kilele cha maonesho ya Expo siku ya Tanzania tarehe 28 Februari, 2022 Mheshimiwa Rais aliona mikataba 37 ikisainiwa yenye thamani ya shilingi za Kitanzania trilioni 20.5 ambayo kwenye mikataba hiyo 37 tunataraji kutengeneza ajira za vijana wa Kitanzania 205,500. Moja ya mikataba ile 37 ni huu ambao umepelekea kuja na azimio hili, ndio maana nimeanza kwa kumpongeza sana, sana Mheshimiwa Rais wetu kwa kazi njema anayoifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwapongeze pia Wabunge mmesema vyema kama kuna Mtanzania hajatuelewa basi huyu ameamua mwenyewe kutokuelewa, lakini elimu iliyotolewa hapa kuanzia alipoanza Profesa Kitila Mkumbo mpaka wa mwisho Mheshimiwa Kigwangalla elimu imefika kwa Watanzania, cha muhimu hapa ni kuunga mkono twende tukatekeleze mkataba huu. (Makofi)

Naomba pia kuongeze pale kwenye hizo hofu ambazo zinasemwa huko nje, bandari yetu imeuzwa, bandari yetu imebinafsishwa, naomba niwaambie Watanzania kuwa bandari yetu iko salama, haijauzwa na haijabinafsishwa; kilichofanyika ni kutafuta mwekezaji kati ya wawekezaji wengi tunaowahitaji kwenye Bandari ya Dar es Salaam, huyu ni mmoja kati ya wawekezaji wengi tunaowahitaji kwenye Bandari ya Dar es Salaam. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niwakumbushe Watanzania tulipofanya kongamano kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya tarehe 3 Februari, 2023, tulisaini hati za makubaliano nyingine sita na wawekezaji mbalimbali kwa ajili ya uwekezaji kwenye Taifa letu. Moja ya mkataba tuliosaini siku ile ni hati ya makubaliano kati ya Mamlaka ya Bandari ya Tanzania na Bandari ya Antwerp ya nchini Ubelgiji na lengo lake lilikuwa ni kuimarisha ushirikiano katika uboreshaji wa utoaji huduma wa Bandari ya Dar es Salaam. Kwa hiyo, kama bandari imeuzwa Serikali imeingia hati ya makubaliano nyingine na mwekezaji mwingine ni jambo sio kweli.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, bandari yetu ni salama, bado ipo mikoni mwa Watanzania na bado tunawahitaji wawekezaji wengine waje wawekeze kwenye Bandari ya Dar es Salaam na bandari nyingine zote tulizonazo ndani ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nilitamani sana hilo niwaambie Watanzania kwamba bandari yetu ni salama na bado tunahitaji wawekezaji wengine. Profesa Mbarawa na timu yako endelea kututafutia wawekezaji na kuwapokea wawekezaji wetu kwa ajili ya bandari zetu zote na tuweze kufanya vizuri ndani ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 3) wa Mwaka 2018
NAIBU WAZIRI FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii ili nami niweze kuchangia hoja hii iliyoko mezani iliyowekwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumpongeza sana Mwanasheria Mkuu wa Serikali na wataalam wake pamoja na Mheshimiwa Waziri wa Katiba na Sheria kwa kazi nzuri waliyoifanya katika kutuletea hoja hii iliyoko mezani. Imekuja kwa wakati muafaka kabisa, kwa kweli nawapongeza sana kwa kazi nzuri ambayo wameifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia machache katika hoja hii. Nianze na hoja ya kwanza ambayo imeongelewa sana hasa kuhusu marekebisho katika Sheria yetu ya Takwimu, Sura 351, ambapo wanasema kwamba sheria inajikita katika kudhibiti tafiti zitakazokuwa zinafanyika hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba marekebisho ya sheria hii ni msaada mkubwa sana wa hao tunaowadanganya tunawatetea leo. Kwa nini nasema hivyo? Marekebisho haya yanamtaka kila mtu au taasisi inayofanya utafiti kwa ajili ya matumizi ya kupanga sera au kupanga mipango ya maendeleo, afuate utaratibu ili matokeo ya tafiti yake yatumike katika kufuatilia na kutathimini mipango ya maendeleo iliyowekwa. Hiyo ndiyo dhana halisi ya marekebisho haya tunayoleta.

Mheshimiwa Spika, katika hili ambalo Serikali inapendekeza, Taifa letu limekuwa katika ombwe kubwa la kutokuwa na takwimu ambazo siyo sahihi. Nitoe mfano mmoja, mwaka 2012 nilikuwa nafanya research yangu ya Personnel Economics, nikiwa natoka Chuo Kikuu cha Agdal, nimekuja Tanzania kufuatilia taarifa rasmi, sikuzipata, nikaenda kuzipata taarifa za Tanzania kutoka South Africa. Kwa nini ilitokea hiyo? Ni kwa sababu hakukuwa na marekebisho haya ya sheria ambayo yangewasaidia watu wenye takwimu zao ambazo sasa zitakuwa ni takwimu sahihi, kwa hiyo, ndicho ambacho sheria hii inapendekeza.

Mheshimiwa Spika, tunachokifanya ni kutoa wigo mpana zaidi kwa watafiti wetu hasa katika kutumia kanuni na taratibu za ukokotoaji wa taarifa za kitakwimu ili kuziba pengo hili ambalo takwimu za Tanzania hazipatikani Tanzania, zinakwenda kupatikana sehemu nyingine. Tuna watafiti wengi, sasa hao watafiti tunataka kuwasaidia tu. Kwa hiyo, NBS wanachotaka kukifanya ni kuhakikisha kila tafiti inayofanyika inakuwa formalized na inatumika kwa ajili ya kupanga mipango mbalimbali ya maendeleo ndani ya Taifa letu. Hicho ndicho ambalo tunataka kufanya. Kwa hiyo, hiki kinachosemwa kwamba tunaenda kudhibiti, hapana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hoja hii inachanganywa na kwamba Ofisi yetu ya Taifa ya Takwimu inakwenda kudhibiti hata research zinazofanyika kwenye vyuo vyetu vya elimu ya juu. Siyo sahihi hata kidogo. Tafiti zinazofanyika kwenye vyuo vyetu zina taratibu zake, wala Ofisi ya Taifa ya Takwimu haihusiani na tafiti za kwenye vyuo vyetu. Kwa hiyo, hili tusiwadanganye Watanzania, tuwaeleze ukweli dhamira ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi ya Awamu ya Tano, nini tunataka kufanya. Tuwaeleze ukweli Watanzania waelewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, umetolewa mfano wa TWAWEZA, hivi leo unaweza ukamwambia TWAWEZA akasema ile tafiti yake ni official statistic, kwa kuwa amefuata nini? Hata methodology aliyotumia haifahamiki. Anawezaje kusema kwamba ile ni takwimu sahihi sasa, kwamba itumike katika kupanga mipango ya maendeleo? Siyo sahihi. Tuwasadie Watanzania, tuwaeleze ukweli na hao TWAWEZA waje tukae pamoja ili tuweze kuwa na takwimu sahihi za kupanga maendeleo sahihi ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hoja ya pili ambayo napenda kuisemea ni ile inayosema kwamba mtafiti yeyote kabla ya kutoa matokeo, ni kile kifungu kinachopendekezwa cha 24A(2). Kinachoongelewa hapa, lengo la kifungu hiki ni kuhakikisha kuwa tunatoa nafasi ya majadiliano ya kitaalam baina ya mtafiti na jopo letu la wataalam katika sekta husika.

Mheshimiwa Spika, nimetangulia kusema kwamba tunataka kupata formalized takwimu ndani ya Taifa letu. Kwa hiyo, lazima tukae pamoja, wewe mtafiti unayesema umefanya research yako kuonyesha kwamba hali ya umaskini ni kiwango fulani tukae pamoja basi utujuze, umetumia methodology gani? Sample uliyochukua kuja ku-generalized matokeo ya takwimu yako umetumia watu wangapi? Huwezi kufanya research ya watu watano halafu ukatuambia Watanzania wanasema, Watanzania hawawezi kuwa ni watu watano. Research zina taratibu zake na ndicho ambacho tunapendekeza katika kifungu cha 24A. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini yako mapendekezo mengine kwamba kifungu cha 24B kifutwe kwa kuwa maudhui yake yameelezwa katika kifungu cha 24A. Napenda kuliambia Bunge lako Tukufu kwamba kifungu cha 24A(1) kinahusu mtu ambaye amepewa takwimu na hapa ndiyo nataka tuelewane, kifungu hiki kinamwongelea mtu ambaye amepewa takwimu na Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa ajili ya kufanya uchambuzi wa kina, yaani further analysis. Kwa hiyo, hapa kwanza amepewa takwimu, ndicho kifungu hiki kinachoongelea, anakwenda kufanya further analysis. Sasa wewe umepewa takwimu na mtu aliyekusanya, anajua amejua ametumia methodology gani kukusanya takwimu zake, kabla hujatoa matokeo, ukiambiwa urudi tuweze kukubaliana kama kweli ulielewa nini kilikusanywa, unalalamika, hii siyo sawa hata kidogo. Naomba tuweze kuelewana. Kwa hiyo, kifungu hiki kama Serikali tunapendekeza kiendelee kuwepo kwa sababu kinaongelea mtu aliyechukua takwimu kutoka Ofisi ya Takwimu ya Taifa.

Mheshimiwa Spika, kifungu cha 24B(2) nacho kinapendekezwa kifutwe. Nimesema hiki cha kwanza nilichokiongelea, mtafiti huyu kapewa takwimu na Ofisi ya Taifa ya Takwimu. Hiki cha 24B kinaongelea taarifa za kitakwimu ambazo zimekusanywa sasa na mtafiti mwenyewe. Kwa hiyo, ni vifungu viwili tofauti vinavyooongelea maana tofauti, ndiyo maana Serikali yetu imependekeza ili tuweze kuwasaidia. Huyu aliyekuja kuchukua taarifa kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu afanye kazi yake, afanye further analysis ili turudi mezani tukae kwa pamoja kwa maana tu ya kuelewana nini ameelewa na nini amepata kutoka kwenye takwimu ambazo zimekusanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu? Hiki cha pili kinamwongelea anayekwenda kukusanya taarifa zake yeye mwenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ni vizuri tukaelewana. Nawashukuru Waheshimiwa Wabunge wengi wamesema hapa, kwamba kumekuwa na ombwe la kila mmoja kuja na taarifa zake. Ofisi ya Taifa ya Takwimu inasema mfumuko wa bei wa mwezi Agosti, ni asilimia 3.3, anaibuka mtu mwingine anakwambia mfumuko ni asilimia 2.2 bila kueleza kwa undani amekusanyaje taarifa zake kumfikisha kwenye hayo matokeo anayotueleza. Ndiyo lengo la kifungu hiki, tuelewane kwa pamoja, tutoke kwa pamoja kama Taifa, lengo likiwa ni maendeleo kwa Watanzania. Tusitoe takwimu ambazo kila mmoja akiamua basi atamchanganya tu Mtanzania na tushindwe kukaa chini na kufanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niseme jambo la mwisho…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja, ahsante sana.