Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to supplementary Questions by Hon. Japhet Ngailonga Hasunga (CPA) (139 total)

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Pamoja na majibu ya Serikali, ningependa niikumbushe Serikali kwamba wakati Halmashauri ya Wilaya Mpanda inafanya mpango wa matumizi bora ya ardhi ilizingatia mahitaji ya wananchi pamoja na maendeleo yao kwa wakati huo, kwa sasa hivi tunavyozungumza Wilaya ya Mpanda, Mkoa wa Katavi idadi yake ya wananchi imeongezeka. Haya matangazo ya Serikali, Tangazo Na. 447 ya mwaka 1954 Na. 296 ya mwaka 1949 hayaendani na uhalisia na hali ilivyo chini kutokana na ramani hizi kuidhinishwa na Wizara ya Ardhi mwaka 2008 na zilianza kuidhinishwa na ngazi ya Mkoa mpaka na Wizara ya Ardhi kwa Kamishna wa Upimaji na Ramani. Kwa sasa hivi tunaenda kwenye nchi ya viwanda na maeneo mengi yanahitaji wakulima kwa ajili ya kulima mazao mbalimbali na Mkoa wa Katavi tuna mkakati wa kuanzisha zao la korosho. Kulingana na matangazo ya Serikali yanatofautiana na ramani zilivyo, uhalisia na mahitaji ya wananchi. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari hii Kamati ya Ushauri ya Taifa juu ya Misitu iambatane na Mbunge wa Jimbo la Nsimbo baada ya Mkutano huu wa Tisa kwenda kuangalia hali halisi ili waweze kumshauri Waziri na waweze kubadilisha mipaka kwa mujibu wa kifungu cha 29 cha Sheria ya Misitu ya mwaka 2002?
Swali la pili, kutokana na uhitaji mkubwa wananchi kwa maeneo haya na masika tayari imekwishaanza na tunajua Waziri wa Maliasili na Utalii kwa mujibu wa Sheria ya Misitu ya mwaka 2002 yeye ndiye mwenye dhamana ya kutoa kauli. Je, yuko tayari kuwaruhusu wananchi katika Kijiji cha Matandarani na Igongwe Kata ya Isalike waweze kupata maeneo ya kujihifadhi kwa kulima, wakati Kamati ya ushauri ikiendelea kupitia maeneo na kuweza kumshauri Waziri?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tuko tayari baada ya Mkutano huu wa Tisa kumalizika Kamati ya Ushauri itapita maeneo yote ambayo yana migogoro nchi nzima ili iweze kumshauri Mheshimiwa Waziri na aweze kutoa maamuzi sahihi.
Swali la pili, kuhusu kulima ni kweli wananchi wale nimefika katika lile eneo wana matatizo mengi, lakini ninaomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tulipokaa na Mheshimiwa DC pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri walikubali kwamba wametenga eneo la ekari zaidi ya 700 ambalo sasa linatolewa kwa wananchi wale ili waweze kuendelea na hizo shughuli. Kwa hiyo, hatutaweza kuruhusu kwa sasa hivi waendelee na shughuli hizo kwa sababu tayari wameshaondolewa na ukiwaruhusu kupanda zao la korosho ambalo ni la muda mrefu mpaka lije lianze kuvunwa itakuwa ni muda mrefu sana, kwa hiyo tutakachokifanya ni kuwapeleka katika hayo maeneo ambayo tayari yameshatengwa na Serikali ili waendelee na shughuli zao zile ambazo zipo.
MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Swali la kwanza, Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba hiki kitalu kimetolewa kwa ajili mambo ya utafiti wa madini lakini kwa mujibu wa Sheria Na. 5 ya mwaka 2009 ya Wanyamapori inazuia kufanyika kwa utafiti katika maeneo ya hifadhi. Je, ni taratibu zipi ambazo Serikali imetumia kukigawa hiki kitalu ili kifanyiwe mambo ya utafiti wakati sheria hairuhusu?
Swali la pili, kwa kuwa mapori haya yana changamoto mbalimbali, je, Naibu Waziri atakuwa tayari kuambatana na mimi pindi Bunge litakapomaliza shughuli zake ili aweze kuja kuziona hizo changamoto zinazoyakabili haya mapori na kuweza kuzitatua?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Mbunge kwa kazi kubwa amekuwa akifanya katika kuwatetea wananchi wake wa Jimbo la Mbogwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu TANZAM ambaye alipewa kitalu hicho, kwa mujibu wa Sheria Na. 5 ya mwaka 2009 kifungu cha 20(2)kinazuia kabisa shughuli zote za utafiti wa madini ya aina zote kufanyika katika maeneo ya hifadhi. Hata hivyo, kifungu hicho cha 20(3)kinatoa mamlaka kwamba ni aina tatu tu za madini zinaruhusiwa kufanyiwa utafiti, madini hayo ni uranium, gesi na mafuta. Kufuatana na mwekezaji aliyekuwa amepewa hiki kitalu yeye alikuwa anafanya utafiti wa madini ya dhahabu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mkataba pamoja na leseni ya huyu mwekezaji ilimalizika tereha 31 Desember 2014, baada ya kumalizika, tarehe 1 Juni, 2016 Serikali ilimuandikia barua ya kumuomba aondoke katika eneo na aondoe vitu vyote lakini hadi leo bado mwekezaji yule yupo opale na ameweka vifaa vyake wakati hana leseni na ilishapita. Tarehe 28 Aprili, 2017 alikumbushwa juu ya suala hili na mpaka sasa hivi bado hajasema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitumie nafasi hii kutoa siku saba, yule mwekezaji aondoe hivyo vitu vyote, kwa sababu viko pale kinyume na taratibu na sheria iliyopo. (Makofi)
Baada ya kumalizika, tarehe 1 Juni, 2016 Serikali ilimuandikia barua ya kumuomba aondoke katika eneo na aondoe vitu vyote lakini hadi leo bado mwekezaji yule yupo opale na ameweka vifaa vyake wakati hana leseni na ilishapita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 28 Aprili, 2017 alikumbushwa juu ya hili suala na mpaka sasa hivi bado hajasema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitumie nafasi hii kutoa siku saba, yule mwekezaji aondoe hivyo vitu vyote kwa sababu viko pale kinyume na taratibu na Sheria iliyopo. (Makofi)
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza utaratibu huo ambao wa kuwauzia watu binafsi kwa makubaliano kwa asilimia 70 na huu wa asilimia 30 kwa kupeleka kwenye mnada hautumiki kabisa. Labda wanatumia asilimia 100 wanapeleka kwenye mnada. Kitendo hiki kimefanya vile viwanda vidogo vidogo Muheza pale, karibu viwanda kumi vyote vimekufa na ajira ambayo kila kiwanda kilikuwa kinachukua labda watu kutoka 100 – 150 wote kukosa kazi.
Sasa nataka kumuuuliza Mheshimiwa Waziri, kwa nini wasirudishe ule utaratibu ambao ulikuwepo wa hiyo asilimia 70 kwa makubaliano ili wale wenye viwanda vidogo vidogo ambao wanatunza ile misitu(tiki) pale waweze kupata ajira na kuendelea kupata morali ya kuanza kutunza?
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ni kwa nini hata wale ambao wananunua kwa mnada ambao utakuta anakuja tajiri mmoja ananunua mitiki yote pale. Sasa ni kwa nini na yeye asilazimishwe kutengeneza kiwanda cha kukata ile mitiki pale pale Muheza kwa sababu hayo ni madaraka ambayo anayo Waziri kufuatana na regulations ambazo anazitengeneza? Nakushukuru Mheshimiwa Waziri.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba ukiuza kwa njia ya mnada wananchi wengi wanakuwa hawana uwezo wa kushinda ndiyo maana tumeweka utaratibu kwamba ni asilimia 30 ndiyo itakayouzwa kwenye mnada. Asilimia 30 itategemeana na makubaliano binafsi, maana yake tunafuata bei ile iliyokuwa na mnada, tunaangalia viwanda vyote vilivyoko katika eneo husika. Wale wote wanaohitaji wanapeleka maombi na wanapatiwa ili waweze kujijengea uwezo na kuweza kuzalisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili suala la pili ambalo amesema kwamba tumshauri huyu atakayekuwa ameshinda aweze kuwekeza katika eneo husika mimi nafikiri ni ushauri mzuri. Tutalifanyia kazi mara tutakapopata muda husika.Ahsante.
MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ambayo yamekidhi lakini naomba niongeze kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mkoa wa Tabora una historia nyingi sana ukizingatia pia na historia ya Baba wa Taifa, lakini wakati anajibu majibu yake Baba wa Taifa hakuwepo, hawakuongeza, kwa hiyo, niombe Wizara ya utalii iongeze kuitangaza historia ya Baba wa Taifa.
Lakini lingine kuna historia ya miembe ambayo ina umri wa miaka 100 nayo ipo kwenye njia ya watumwa. Kwa hiyo niombe niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Kwa kuwa hivi sasa njia ya utmwa inatambulika, je, Serikali iko tayari kuikarabati ile njia kutoka Tabora hadi Kigoma - Ujiji ili iwarahisishie watalii kupita?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lingine, je, Serikali iko tayari kuwatuma wataalam kuhakikisha vivutio vyote ambavyo vipo katika Mkoa wa Tabora vinaorodheshwa? Ukilinganisha na mapato yaliyopatikana tangu 2013 mpaka 2017 ni milioni mbili, milioni mbili kuna nini? Kwa hiyo nasema kwa uchungu kwamba bado tunahitaji utangazaji wa utalii kwa Mkoa wa Tabora ni muhimu sana naomba izingatiwe, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kukarabati hii njia ambayo inatoka Tabora hadi Kigoma hili tutalifanyia kazi, tutaangalia kadri upatikanaji wa fedha utakavyokuwepo katika bajeti zetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, kuhusu kuorodhesha vituo, ni kweli kabisa Tabora ina historia ndefu sana ikiwa ni pamoja na hiyo aliyoisema ambapo Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliweza kusoma katika Mkoa ule na mambo mengine mengi na mimi mwenyewe nimefika katika yale maeneo, nimetembelea na nimeyaona. Kwa hiyo orodha tuliyonayo ni kubwa na tutaendelea kuifanyia kazi, kuiuhisha ili tuweze kuongeza mapato yatokanayo na utalii katika Mkoa huu wa Tabora.
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu ina vivutio vingi sana vya utalii ukiacha mbuga zetu na mlima na kadhalika, wazee wetu wa zamani, machifu wana vitu vyao ambavyo walikuwa wanatumia. Tuna ngoma zetu na vitu hivi vinaaza kupotea. Sasa Wizara hii ya Maliasili na Utalii ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba vivutio kama hivi, miji yetu kama Mji wa Kilwa vinahifadhiwa kwa ajili ya vizazi vinavyokuja?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nchi yetu na ina vitu vingi ambavyo ni vivutio vya utalii. Ni azma ya Wizara yetu kuhakikisha kwamba hivi vyote vinahifadhiwa ili viweze kutumika na vizazi vijavyo viweze kuvielewa na viweze kufaidika na matunda ya hivyo vitu vyote. Kwa hiyo ni azma ya Wizara yetu, itaendelea kulishughulikia, kuvilinda na kuvihifadhi.
MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nukipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mkoa wa Tabora una vivutio vingi vya utalii ukiwemo uwandaji. Ni lini Serikali itafanya uhakiki wa vitalu vya uwindaji vilivypo Tabora? Kwa sababu kuna taarifa kwamba vitalu vya uwaindaji vilivyopo vinasomeka ni vichache kuliko uhalisia wa vitalu vilivyopo?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kuna vitalu viko vingi katika nchi yetu na kazi yetu kubwa ambayo tunaifanya sasa hivi, tunapitia upya vitalu vyote ili tuweze kuvibaini na kuona vipi vinafaa na vipi havifai. Kwa hiyo badaa ya kukamilisha hilo zoezi ni wazi kabisa Mheshimiwa Mbunge atafahamu ni vitalu vingapi ambavyo vinapatikana katika Mkoa wa Tabora.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ambayo yanatofautiana na swali langu, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimkumbushe kidogo Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba Milima ya Uluguru wanakaa Waluguru, Milima ya Usambaa wanakaa Wasambaa wanaotoka Tanga na Milima ya Udzungwa wanakaa Wadzungwa na Udzungwa iko Wilaya ya Kilolo kwa asilimia 70.
Mheshimiwa Naibu Spika, jibu nililopewa hapa, inaonekana kwamba Kilolo wanapewa kama hisani, siyo haki yao. Kwa hiyo, ninachoomba kwa kuwa tayari yalikuwepo makubaliano ya kuhamisha Makao Makuu ya Udzungwa kwenye Kilolo Udekwa, lifanyike ili wananchi wale wanufaike kwamba ile Udzungwa ni ya Wadzungwa siyo ya Waluguru. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa mara nyingi yamekuwa yakitokea maafa, kwa mfano vijiji vya Msosa, Ikula, Ruaha Mbuyuni, Mahenge na Mtandika wananchi wanauawa na tembo bila kulipwa fidia; na fidia ambayo wanalipwa ni fedha ndogo sana, ni pamoja na uharibufu wa mazao yao.
Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kutunga au kuja kuleta hapa tubadilishe sheria ili wananchi hawa wawe na thamani zaidi ya wanyama ambao ndiyo wanawaua? (Makofi)
NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa ambayo amekuwa akifanya katika Jimbo lake. Amekuwa akifuatilia sana na amekuwa akiwatetea sana wananchi wa Jimbo la Kilolo. Kwa kweli hongera sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba hili suala la kuhamisha Makao Makuu, tutalishughulikia. Yapo mambo mengi ya kuzingatia tunapotaka kuhamisha makao makuu na jitihada sasa hivi zinafanywa katika kuangalia miundombinu kama itawezekana kwenda kufikika katika hayo maeneo ambayo yalikuwa yamekubalika pale awali. Baada ya hilo kukamilika, basi tutalifanyia kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusu fidia ya wananchi ambao wanakuwa wameadhirika na wanyamapori hususan tembo na wanyama wengine, hili suala lipo kwa mujibu wa sheria na kwa mujibu wa tararibu zetu. Ni kweli kabisa taratibu ambazo zipo zinabainisha ni aina gani ya kifuta machozi ambacho kinatolewa kwa wananchi wanaokuwa wameathirika na haya matatizo. Sasa namuomba Mheshimiwa Mbunge kwamba katika hao wananchi ambao amewasema, hiki kiasi japo ni kidogo, hakilingani na thamani ya binadamu anayekuwa amepotea, lakini bado tutaendelea kutoa kwa wakati, nitaomba tuwasiliane nipate hayo majina ili niweze kuyafanyia kazi mara moja. Hilo nitalishughulikia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba nimhakikishie kwamba tuko kwenye harakati ya kuweza kupitia upya sera yetu pamoja na sheria ili tuakikishe kwamba tunahuisha na kuweka viwango vile ambavyo vitakuwa vinatosheleza na vinasaidia katika kupunguza haya matatizo. Nashukuru.
MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Serikali kuhusu tatizo hilo, lakini bado tatizo hili ni kubwa na linaendelea. Mijadala juu ya wapagazi, waongoza watalii na wapishi imekuwa ya muda mrefu baina ya Serikali na waajiriwa hawa, lakini utekelezaji wa makubaliano umekuwa hafifu sana.
Swali la kwanza, je, Serikali haioni kwamba kuna haja kwa sasa kwenda kuonana na waajiriwa kuongea nao ana kwa ana, kujua ni kwa kiwango gani miongozo hii ambayo wameipeleka imetekelezwa na imekuwa na tija kwa hao watu ambao ndio waathirika wa tatizo hili?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kumekuwa na utaratibu kwamba wanaoshughulikia matatizo ya watalii imekuwa ni kampuni ya nje na sio watu wa ndani. Ni kwa nini Serikali haioni haja ya kushirikisha kampuni za ndani kuhakikisha kwamba inasimamia suala la porters na waongoza watalii na inaliacha katika kampuni za nje? Ahsante sana.(Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tunakubaliana kabisa kwamba kuna haja ya kuonana na waajiriwa ili kuweza kubaini kama kweli yale makubaliano tuliyoyafikia pale Arusha yametekelezeka. Na mimi naomba kumwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya kikao hiki cha Bunge tutapanga safari ya kwenda kuonana na wale ili tuweze kuangalia utekelezaji wa hayo mambo yote.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kuhusu matatizo ya hawa wapagazi kwamba yanatatuliwa na kampuni ya nje, hili ni suala ambalo nimelisia sasa hivi, lakini nadhani tutalichukulia hatua na tutahakikisha kwamba matatizo ya Watanzania yanashughulikiwa na Watanzania wenyewe kupitia mifumo iliyowekwa na makampuni yetu yako tayari kabisa kushughulikia hili tatizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge, hili tutalishughulikia na kulifanyia kazi.
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kwa nafasi ya pekee napenda nikipongeze Chama changu cha Mapinduzi kwa kutimiza miaka 41 ya utawala bila kung’oka, na kwa utendaji huu tuna miaka 41 mbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri atakuwa shahidi tangu hili pori lianzishwe ni miaka mingi sasa na watu wameongezeka kwa kiasi kikubwa, sheria hizi zilizoanzisha mapori ndiyo sheria hizi hizi zilizoanzisha vijiji, inapotokea maeneo wanayoishi wananchi yakagundulika madini wananchi wanatolewa, lakini wananchi wanapohitaji kulima maeneo ya mapori wanaambiwa sheria zizingatiwe. Kwa nini sheria ziko bias upande mmoja kwa kuwaonea wananchi ambao ni wanyonge?
(b) Mheshimiwa Waziri tulikuwepo nae Ulanga wiki mbili zilizopita ameona jiografia ya Ulanga ilivyo ngumu maeno yote ya matambalale ambayo wananchi wanaweza wakalima ni Mapori Tengefu, ni Hifadhi na Bonde la mto Kilombero, naomba busara zitumike ili wananchi wapate maeneo ya kilimo kwa sababu wameongezeka kwa kiasi kikubwa.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa wakati tunapata Uhuru idadi ya wananchi wa Tanzania ilikuwa haizidi milioni tisa na ardhi ilikuwa hivi, lakini miaka karibu 56 ya Uhuru wananchi wa Tanzania wameongezeka kwa kiwango kikubwa sana, sasa tuko karibu milioni 52 lakini ardhi haijaongezeka. Kwa hiyo naomba nimuambie Mheshimiwa Mbunge kwamba kutokana na ongezeko la watu ndiyo maana kumekuwa na presha kubwa sana katika maeneo yaliyohifadhiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo naomba nimhakikishie kwamba sheria zilizotungwa sio kwamba ziko bias, sheria ziko vizuri kabisa, sheria zinaainisha maeneo yaliyohifadhiwa, maeneo ambayo yanafaa kwa makazi, maeneo yanayofaa kwa ufugaji, maeneo yanayofaa kwa kilimo kwa hiyo hili lazima tulisimamie ipasavyo. Siyo kwamba sheria zinapendelea labda kitu fulani na Serikali yetu itaendelea kuhakikisha kwamba wananchi wanapatiwa maeneo ya kulima yale yanayostahili na yale yaliyohifadhiwa yaendelee kuhifadhiwa kwa mijibu wa sheria.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali lake la pili ni kweli kwamba tutatumia busara kubwa sana katika kuhakikisha kwamba wananchi wa Jimbo hili la Ulanga wanapata eneo la kulima, kufuatia hatua hiyo na ziara ambayo tumeifanya hivi karibuni kama alivyosema yeye mwenyewe Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii ameunda Kamati ya Wajumbe 22 kwa sababu ya ukubwa wa Bonde lenyewe la Kilombero lilivyo ili kuweza kubainisha, kuweza kupitia maeneo yote na waone ni maeneo gani yahifadhiwe, maeneo gani yatafaa kwa kilimo ili kusudi wananchi wapate kuelekezwa ipasavyo. (Makofi)
MHE. ZUBER M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vya Mpigamiti pamoja na Kikulyungu ni vijiji ambavyo vimepakana na hifadhi ya Selous katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale, lakini kuna mgogoro mkubwa sana wa ardhi kati ya Kikulyungu pamoja na Selous.
Je, ni lini Mheshimiwa Waziri utaweza kutatua mgogoro huu ambao umedumu zaidi ya miaka 10 na watu tayari washapoteza maisha?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika eneo hili kuna migogoro mingi na kuna eneo kubwa ambalo kwa kweli kuna matatizo. Naomba nikuhakikishie hata jana nilikuwa karibu na pori la Selous katika maeneo ya Mbwande nikishughulikia matatizo ambayo yanafanana na namna hii. Kwa hiyo, katika eneo lako hili la Mpigamiti pamoja na Kikulyungu ambako kuna matatizo naomba niseme kwamba ninalichukua tutaendelea kulifanyia kazi na tutashirikiana na wewe ili kuweza kutafuta ufumbuzi wa hili tatizo ambalo limedumu kwa muda mrefu kusudi wananchi wa eneo lako wapate kufaidika na wapate kufurahi. (Makofi)
MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, takribani zaidi ya vijiji 12 vinavyozunguka Pori la Akiba la Mkungunero hawafanyi kazi ya kilimo kwa sababu ya mgogoro mkubwa ambao umedumu zaidi ya miaka 10, kati ya wafanyakazi wa pori la Akiba la Mkungunero na wakulima wanaozunguka pori lile. Suala hili limeshafika Serikalini, lakini hakuna hatua zinazochuliwa. Wabunge wa Majimbo Mheshimiwa Juma Nkamia na Mheshimiwa Dkt. Ashatu wanapata shida sana wakati wa kampeni na hata wakati wa kuwatembelea wananchi wao.
Je, ni lini sasa matatizo haya yatakwisha mpaka halisi wa pori la Mkungunero litabainishwa ili wakulima wale wafanye kazi yao kwa uhuru na kwa amani?(Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kumekuwa na tatizo la muda mrefu la vijiji hivi 12 katika pori la Akiba la Mkungunero ambapo wananchi walikuwa wanagombania mipaka, hili ni mojawapo ya eneo ambalo Kamati ya Kitaifa imeyapitia na wenyewe tumeipitia tumeona kweli kuna mgogoro ambao unatakiwa kutatuliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitumie fursa hii kumuomba Mheshimiwa Felister Bura kwamba katika hili eneo Serikali iliagiza kwamba maeneo yote yenye migogoro yawekewe mipaka na muda wa mwisho ulikuwa ni tarehe 31 Desemba, 2017. Hivi sasa tunafanya tathmini kupitia maeneo yote sio tu katika eneo hili la Mkungunero, katika mapori yote ya akiba na mengine yote kuangalia baada ya kuweka mipaka na vigingi katika haya maeneo ni maeneo yapi ambayo yana migogoro, ni maeneo kiasi gani tunatakiwa tuyaachie ama tuendelee kuyahifadhi na wananchi watafutiwe maeneo mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya haya yote kukamilika basi Waheshimiwa Wabunge watajulishwa na hatimae tutajua kabisa kwamba wananchi sasa watatatuliwa haya matatizo na hili tatizo la Mkungunero na vijiji hivi 12 vyote vitakuwa vimepata ufumbuzi wa kudumu.
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na napenda nipongeze majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, majibu haya yamejikita kuelezea taarifa ambayo siyo sahihi, kwa sababu migogoro mingi imekuwa ikichochewa na uhamishaji wa mipaka na ndiyo malalamiko ya wananchi katika maeneo husika, kwa vile Serikali imekuwa ikihaidi muda mrefu kwamba kuwe na mpango shirikishi kati ya Wizara ya Maliasili na Utalii, TAMISEMI na Wizara ya Ardhi ili kuainisha mipaka vizuri zaidi, kitu ambacho kitaondoa migogoro na migongano iliyopo.
Je, ni lini sasa Serikali kupitia majibu haya, kwa sababu suala hili siyo mara ya kwanza au ya pili kuuliza hapa Bungeni, ni lini Serikali itakaa na wananchi wa maeneo husika ili kutatua mgogoro wa namna hii?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili Mheshimiwa Naibu Waziri aliyekuwepo wakati ule Engineer Ramo Makani alitembelea maeneo husika yaliyotajwa kwa maana kwamba pori la Akiba la Kijereshi kwa wananchi wa kijiji cha Kijereshi, Mwakiloba, Lukungu na Mwamalole na akajione mwenyewe kwamba wananchi wana haki kwa kile wanachokizungumza, vilevile alikwenda Pori la Akiba la Sayanka akajionea mipaka imehamishwa wananchi wamekuwa miaka yote wanalima kabla ya mipaka kuwekwa. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri uko tayari sasa kuja ujionee uhalisia huu na uondokane na taarifa potofu ambazo zinazotolewa na wataalam wako? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kabla ya kujibu naomba niitumie nafasi hii kumpongeza sana kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akiifanya kwa kweli akina Masunga na Hasunga nadhani ni machachari sana, hongera sana Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba nijibu maswali yake. Kuhusu matatizo na migogoro mbalimbali ambayo ipo katika maeneo mengi, ni kweli kabisa tumebaini kwamba kuna migogoro mingi ambayo aidha, imesababishwa na kutokushirikisha vizuri wananchi ama kutokana na sababu mbalimbali ama kuongezeka kwa idadi ya watu katika maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imechukua hatua mbalimbali katika maeneo mengi, kwanza tuliunda Kamati ya Kitaifa shirikishi ambayo ilishirikisha Wizara mbalimbali ambayo sasa imebainisha maeneo mbalimbali yenye migogoro na hivi sasa ipo katika hatua ya mwisho ya kubainisha na kutoa ushauri ili tuweze kufanya uamuzi ni maeneo yapi Serikali iweze kuyaachia kwa wananchi na maeneo yapi yabaki chini ya hifadhi. Baada ya taarifa hiyo kukamilika hivi karibuni nadhani kwamba taarifa hii itatolewa Bungeni na Wabunge wote watapata nafasi ya kuweza kujua.
Kuhusu kukaa na wananchi wa Jimbo la Mheshimiwa Chegeni mimi naomba nimuambie tu kwamba Serikali tuko tayari kukaa na wananchi ili kuweza kupitia mipaka hatua hadi hatua, mimi nimuahidi baada ya Bunge hili tutakaa naye tutapanga kwamba ni lini twende tukawatembelee ili na nijiridhishe kabisa kwamba madai anayoyasema na wananchi wanayoyasema kweli yanahusu hiyo mipaka na kama mipaka imesogezwa basi tuweze kuchukua hatua stahiki katika maeneo haya aliyoyataja. (Makofi)
MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika majibu ya Naibu Waziri amesema Kamati ya Kitaifa iliyoundwa, ninapenda kujua ni lini Kamati hiyo itakamilisha taarifa hiyo na kuileta ndani ya Bunge ili matatizo hayo yaweze kukoma?(Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwamba Kamati ya Kitaifa ambayo ilikuwa inashirikisha zaidi ya Wizara tano iliundwa kupitia maeneo mbalimbali na kupitia nchi nzima kuona migogoro ambayo iko katika maeneo mbalimbali. Kamati hiyo imeshatoa tayari matokeo ya awali ambayo yamebainisha kila kitu ni maeneo gani ambayo yapo kwenye matatizo, baadhi ya maeneo ambayo yamebainishwa ni pamoja na vijiji 366 viko ndani ya hifadhi.
Kwa hiyo, basi juzi tumekaa na hiyo Kamati imetoa tena draft nyingine tumetoa maelekezo ni imani yangu ndani ya kipindi cha miezi miwili, Kamati hiyo itakamilisha kabisa hiyo taarifa na itawasilishwa kwa Waheshimiwa Wabunge na kutoa taarifa kamili.
MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Bunda na Vijiji vya Honyari, Kihumbu, Maliwanda, Sarakwa, Kyandege mpaka wao kati ya pori la Akiba la Gruneti na Mheshimiwa Naibu Waziri amesema hapa kutoka mpaka wa Mto Lubana kwenda kwa wananchi ni mita 500 ningependa kujua kutoka mpaka mto Lubana kwenda porini ni mita ngapi?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa katika hili eneo la Gruneti kuna mipaka ambayo ipo lakini itakuwa ni vigumu sana kumpa taarifa kamili umbali uliopo kati ya huo mto na hilo eneo analolisema. Kwa hiyo naomba nitumie nafasi hii kuwambia kuwa nitakaa nae, tutaenda kutembelea hilo eneo ili tuone kwamba kuna umbali wa mita ngapi ambazo zinahusisha. (Makofi)
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kuna mgogoro kati ya Pori la Akiba la Kimisi na maeneo ya Rweizinga – Mguruka katika Kata ya Bwelanyange, mwaka jana Bunge liliielekeza Serikali iende katika hayo maeneo na kutatua migogoro hii, lakini mpaka hivi sasa Serikali haijafika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kujua ni lini Mheshimiwa Waziri utaambatana na mimi ili tuende kwenye Kata ya Bwelanyange maeneo ya Rweizinga na Mguruka ili kushirikisha wananchi katika kuweka mipaka mipya kati ya pori la Akiba la Kimisi na Kata ya Bwelanyange? Nashukuru.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa katika maeneo aliyoyataja kulikuwa kuna matatizo na wananchi walikuwa na malalamiko kuhusu mipaka na naomba nimhakikishie kwamba niko tayari wakati wowote mwezi wa Machi, mwaka huu nitatembelea katika Mkoa wa Kagera na tutakapokuwa huko basi tutapata nafasi ya kwenda kupitia na kuongea na wananchi juu ya mipaka hiyo yote aliyoitaja katika maeneo ya Bwelanyange na maeneo mengine yote aliyoyataja.
MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tarehe 31Januari, 2018 Waziri wa Maliasili na Utalii, Mheshimiwa Dokta Kigwangala alitoa ilani kwenye kiwanja Namba 4091 kilichopo eneo la Njiro Mkoa wa Arusha kwamba wale watu ni wavamizi, wamejenga eneo la Serikali la kiwanja kinachoitwa kwa jina la Tanzania Tourist Corporation.
Swali langu, kwa nini Mheshimiwa Kigwangalla Waziri wa Maliasili na Utalii asikutane na watu hawa kwa sababu watu hawa pia ni wamiliki halali eneo lile kwa sababu wana hati pia na licha ya hivyo haoni kama huu ni uzembe wa Serikali yenyewe na je, kwa nini wasimtafute aliyehusika kufanya ili kabla hajawahukumu wananchi waliojenga katika eneo lile?(Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii ametoa hilo tamko ametoa siku 30 kwa wale watu waliovamia wajisalimishe waje zile documents halali ili kusudi Serikali iweze kutathmini na kuangalia kama kweli hayo maeneo wameyapata kihalali. Kwa hiyo, siku 30 baada ya hapo ndipo tutafanya uamuzi unaostahili.(Makofi)
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu ya swali hili na niombe kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna nyakati ambazo mlima Kilimanjaro unapata ajali ya moto na kwa sababu hiyo wananchi wanaotokana na halmashauri zinazozunguka mlima wanafanya kazi ya kuzima moto huo, hususan wananchi wa Wilaya ya Rombo na kikubwa wanachoambulia ni nusu mkate. Sasa kwa kuwa kuna utaratibu wa kutoa mrabaha kwa halmashauri ambazo zina madini; je, Serikali haioni kwamba umefika wakati sasa mapato yanayotokana na mlima Kilimanjaro kiasi fulani kitolewa kama mrabaha kwa halmashauri zinazozunguka mlima ili iwe kama incentive na kuwafanya wananchi hao waweze kuulinda mlima wakati majanga ya moto yanapotokea? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kuna vijana wapagazi (porters) ambao wanabeba chakula, maji, gesi na kadhalika kwa ajili ya kuwasaidia watalii kupanda mlima. Vijana hawa wana malalamiko makubwa sana kwamba malipo yao ni ya kinyonyaji. Je, Serikali iko tayari kuchunguza malalamiko haya na kuwasaidia hawa vijana ili waweze kupata stahiki zao?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kuwapongeza wananchi kwa jinsi ambavyo wamekuwa wakishiriki katika kuzima moto pale unapojitokeza katika hifadhi ya Kilimanjaro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la mrabaha hasa kwenye Halmashauri zile ambazo zinazozunguka mlima Kilimanjaro, naomba niseme kwamba hilo tutalifanyia kazi, tutangalia kama hilo linaweza likafanyiwa kazi. Kwa utaratibu uliopo hivi sasa ni kwamba katika bajeti nzima ya hifadhi za Taifa (TANAPA) asilimia tano mpaka saba huwa zinatengwa kwa ajili ya kusaidia miradi mbalimbali inayoibuliwa na wananchi walioko katika maeneo yaliyo jirani na hifadhi mbalimbali. Kwa hiyo, katika hili ambalo amelisema basi tutalifanyia kazi tuone kama nalo linaweza likafanyiwa kama tulivyofanya madini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili la kuhusu wapagazi, kama atakumbuka hapo tulipokuwa tunajibu swali lililokuwa linahusu maslahi wapagazi na waongoza utalii tulisema; katika kikao kilichofanyika Arusha kati Serikali wapagazi na vyama vyao pamoja; katika utatu huo tulikubaliana kabisa viwango ambavyo vimependekezwa na ambavyo tulifikia muafaka. Tukaagiza kwamba sasa wale wote, mashirika yote, taasisi zote, kampuni zote za kitalii lazima ziingie mikataba na hao wapagazi ili angalau kuhakikisha kwamba kwa siku kila mmoja anapata fedha zisizopungua dola elfu kumi kwa siku. (Makofi)
MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa mlima Kilimanjaro ni kivutio kikubwa na kinachoingiza pesa za kigeni kwa kiwango kikubwa kama kilivyotajwa. Je, ni lini sasa Serikali itaboresha miundombinu ya upandwaji wa milima huo kama inavyofanyika katika nchi zingine za Brazil, kule Rio De Janeiro na Cape Town, South Africa kwa kutumia cable ili kuongeza mapato zaidi kupitia mlima huo?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Mahawe kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini tutaboresha miundombinu, tumekuwa tukichukua hatua mbalimbali za kuboresha miundombinu katika hifadhi zetu. Hili alilolipendekeza kuangalia uwezekano wa kuweka labda vitu kama cable car na vitu vinginevyo basi tutaliangalia kwa kadri bajeti itakavyoruhusu pale ambapo tunaweza kutekeleza ili liweze kuwavutia watalii wengi zaisi na kuweza kufanikisha hili jambo.
MHE. ORAN M. NJENZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, napenda vile vile kushukuru majibu ya Serikali na pia nipende kutambua jitihada zinazofanywa na Serikali ya mkoa na TANAPA vile vile kwa kushiriki katika ujenzi wa kituo cha afya pale Ilungu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza kwa vile hii fidia ni ya muda mrefu 1965; je, Serikali inathibitisha kuwa hii fidia itakayolipwa mwaka huu itazingatia thamani na sheria zilizopo sasa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa vile Mji wa Mdogo wa Igoma unakua kwa haraka sana na pale kuna eneo la hifadhi ambalo limezungukwa na mji; je, Serikali itakuwa tayari kuliachia lile ili liweze kutumiwa na shule pamoja na huduma zingine za kijamii? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijajibu hilo swali, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza sana kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akifanya katika kufuatilia fidia hii ya wananchi wake na amefuatilia kwa muda mrefu na taarifa ziko nyingi sana na wananchi wajue kwamba Mheshimiwa Mbunge anafanya kazi nzuri sana hongera sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu fidia, kama nilivyosema kwenye swali la msingi tunafanya tathimini upya mwezi Februari mwaka huu. Kwa hiyo, baada ya tathimini hiyo ni wazi kabisa kwamba tutabaini kwamba mahitaji au fidia inayotakiwa italingana na hali halisi ya leo na si ya mwaka 1965. Kwa hiyo wananchi watapata nafasi nzuri kabisa ya kupata fidia inayostahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu maombi yanayohusu hapa kujenga makao makuu kutokana na ongezeko la watu. Naomba nitoe maelezo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza maeneo mengi yameleta maombi ya namna hiyo yanayofanana, lakini hili ombi ambalo amelileta Mheshimiwa Mbunge nimhakikishie tu nitachukua jukumu la kwenda kwanza kukutana na wananchi wenyewe ili niangalie hilo eneo kama kweli linafaa kutolewa kwa ajili ya huduma za jamii. Hata hivyo, mkazo zaidi utaendelea kusisitizwa kwamba hifadhi ni muhimu kuliko vitu vingine vyote.
MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba amejibu swali ambalo yeye mwenyewe alifika Urambo na kujionea kwamba mpaka uliowekwa na Serikali upo, beacon zilizowekwa na Serikali zipo, lakini cha kushangaza ni kwamba wananchi waliondolewa kwenye eneo ambalo lina mpaka halali wa Serikali. Kwa hiyo, kuwaondoa wananchi kwangu mimi naona ni kwamba hawakutendewa haki kwa sababu waliidhinishwa na mpaka wa Serikali uliokuwepo. Kwa hiyo, kuwaondoa ni kwamba kumewapunguzia eneo lao la kilimo na la ufugaji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza, kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri ulijionea wewe mwenyewe, je, upo tayari kurudi tena na mimi tukakae na wale wananchi tuondoe huu mgogoro ili wananchi waendelee kutumia maeneo yao waliyoyazoea ambayo sasa hivi tunawapa umaskini kutokana na kuwapunguzia eneo la kulima? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Pori la Hifadhi ya North Ugala lina maeneo mengi ya migogoro ya aina hiyo hiyo kutokana na kubadilishiwa mpaka wa awali na kuwawekea wa pili ambao umesababisha upungufu. Sasa swali langu, je, upo tayari kutenga muda wa kutosha tukakae mimi na wewe muda mrefu hasa Urambo umalize migogoro yote katika mpaka huo wa msitu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza sana mheshimiwa Mbunge Margaret Simwanza Sitta kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akifanya katika kuwatetea wananchi wake wa Urambo. Kwa kweli anafanya kazi nzuri sana na ni mwanamke wa Jimbo ambaye kwa kweli anaonyesha mfano wa kuigwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nilishawahi kutembelea katika hili eneo na nilijionea hali yenyewe na tulikaa na wananchi tukatoa elimu tukaelimishana vizuri kabisa na niombe kusema kwamba nipo tayari kurudi tena kwenye eneo lile ili twende pamoja, tuambatane na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi na ambao ndio wenye dhamana ya kuthibitisha mipaka. Tukakae na Wizara ya Wizara ya TAMISEMI, Wizara ya Maliasili na Utalii na wananchi ili tupitie hatua kwa hatua kuweza kumaliza migogoro ambayo ipo katika eneo hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali la pili, nipo tayari pia kutenga muda wa kutosha kabisa kuhakikisha tunapitia miogoro yote ambayo ipo katika Jimbo hilo. (Makofi)
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, kwanza nianze kuwapa pole wananchi wa Kilolo ambao wameunguliwa na shule ya wazazi kule Ukumbi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niulize swali langu moja, kwa kuwa wananchi wa Kilolo moja ya zao kubwa wanalolitegemea ni misitu, tumehamasisha na inasaidia kutunza mazingira. Pia kwa njia ya misitu wanapata mbao ambazo zimesaidia kwa kiwango kikubwa sana kujenga majengo ambayo yamesababisha ofisi nyingi kuhamia Dodoma haraka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo kubwa ambalo lipo sasa ni kwamba wale wananchi wameanza kunyanyasika kusafirisha mbao, watu wa TFS (Wakala wa Misitu) wanawasumbua, TRA wanawasumbua kiasi kwamba wananchi sasa wako tayari kuacha kupasua mbao. Je, Mheshimiwa Waziri utakuwa tayari kwenda kukaa na watu wa TRA kule ili tatizo hili liishe na wananchi wa Kilolo waendelee kufanya biashara zao?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa zao la misitu ni la muhimu sana na limekuwa likitoa mchango mkubwa sana katika uchumi wa nchi yetu, na wananchi wa Kilolo ni mojawapo ambao wmaekuwa wakijishughulisha sana na hili zao, kwa kweli hongera sana kwa kuhamasisha jinsi wanavyojishughulisha na hili suala.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tumeweka utaratibu kwamba mwananchi yeyote mwenye misitu ambaye anataka kujishughulisha na hili zao lazima apate kibali kutoka kwa Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) pamoja na TRA ili ahakikishe kwamba anasafirisha kwa kufuata utaratibu. Na niombe tu kusema kwamba niko tayari kwenda kukaa na TRA pamoja na TFS kuhakikisha kwamba utaratibu mzima unafuatwa pale ambapo wananchi wa Kilolo wanataka kusafirisha mbazo zao.
MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la kukosekana kwa mipaka limeendelea kuleta migogoro na kuwaumiza wananchi wengi hapa nchini. Tatizo hilo limeendelea kuwaumiza wananchi wa Mtaa wa CCT Mkundi pale Manispaa ya Morogoro ambao wamevunjiwa nyumba zao, takribani miaka miwili imepita baada ya kuambiwa kwamba wamejenga kwenye Hifadhi ya Msitu wa Kundi. Hata hivyo wananchi wale walikuwa na vibali halali na walipewa ramani zote na mji kujenga nyumba zao. Je, Serikali ipo tayari kuwalipa fidia wananchi hawa wa Mtaa wa CCT Mkundi?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kulikuwa na matatizo katika msitu wetu ule wa Mkundi ambapo wananchi wengi walikuwa wameondolewa kwa sababu walikuwa wamevamia katika maeneo haya. Kama nilivyokuwa nimesema, hata jana ambapo tumekuwa tukitoa maelezo kwa muda mrefu, kwamba yapo maeneo ambayo yalikuwa yamepimwa katika hifadhi za Taifa, maeneo ni mengi, na jana nilisema kwamba vijiji takribani 366 vimepimwa kwenye hifadhi za misitu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hili eneo pia wananchi hawa kweli walikuwa wamepewa katika hayo maeneo lakini tulipogundua kwamba wamepewa kimakosa ndiyo maana jitihada zikafanyika katika kuwaondoa.
Kuhusu fidia, kwa sababu taratibu zilikuwa zimekiukwa, kwa kweli Wizara tutaangalia kama kweli wanaweza waka-qualify kupata fidia, lakini tunaamini kabisa kwamba kama walivamia na kama Serikali hawakupewa kihalali kwa kupitia, kwa sababu ule ni msitu, basi fidia inaweza isitolewe, lakini kama tutakuta kwamba waliondolewa kimakosa basi tutalitafakari na kuona namna bora ambavyo tunaweza tukalitatua hilo tatizo la wananchi wake.
MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi nipate kuuliza swali dogo tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iliahidi ndani ya Bunge kwamba ingeweza kumaliza migogoro ya wananchi na mapori ya hifadhi mwezi Desemba mwaka jana. Moja kati ya maeneo ambayo yanakabiliwa na mgogoro mkubwa sana ni pamoja na eneo la Swagaswaga katika Wilaya ya Chemba ambako wananchi wamekuwa wakifukuzana na askari wanyamapori kila siku.
Ningeomba kauli ya Serikali, pamoja na kwamba Mheshimiwa Waziri anajiandaa kwenda Urambo, hapa Chemba ni karibu sana, yuko tayari kwenda Chemba pale kabla ya kwenda Urambo?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu katika Pori letu la Swagaswaga na ninaomba nimjibu tu kwamba hivi sasa ninavyoongea, Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii leo hii ameenda kutembelea hilo pori pamoja na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango kwa ajili ya kuangalia huo mgogoro ili waweze kulitatua hili tatizo ambalo limedumu kwa muda mrefu.
MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mgogoro wa misitu na wananchi wa Jimbo la Ukonga Kata ya Vingiziwa, Chanika, Buyuni na Pugu tangu mwaka 1998, mgogoro huu Mheshimiwa Waziri Mkuu anaufahamu, wameshaunda timu huko nyuma.
Ninaomba nipate kauli ya Serikali leo; mgogoro huu unafikia lini mwisho ili wananchi wale wajue kwamba wanaendelea kuishi kwa kufanya maendeleo au wanaondoka na wanakwenda wapi? Naomba nipate majibu hayo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwepo na mgogoro wa muda mrefu katika msitu ule na mimi mwenyewe katika kipindi cha hivi karibuni nimetoka kule nimetembelea mipaka ile na kuangalia, lakini naomba nilitaarifu Bunge lako tukufu kwamba hatua zilichukuliwa na Serikali katika kuwaondoa wananchi wote waliokuwa wamevamia katika yale maeneo na mipaka rasmi imechorwa pamoja na kuweka barabara pembezoni ya mpaka. Kwa hiyo, wananchi wale wote ambao wako ndani wameshaondolewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini yapo maeneo machache ambayo yamebaki ambayo sasa Mheshimiwa Waitara alisema kwamba bado inabidi tukae nao chini na mimi nakubali kwamba baada ya Bunge hili leo hii ntaomba tukutane ili tukae pamoja ili tuweze kutoa tamko la mwisho juu ya wale watu ambao wako katika haya maeneo yaliyobaki.
MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, chanzo cha migogoro hii pia kinatokana na hifadhi ambazo zinatolewa bila utaratibu, tunajua mpaka eneo litangazwe kuwa hifadhi kuna utaratibu ambao unatakiwa kufuatwa. Hivi karibuni kumekuwa na utaratibu wa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kushirikiana na halmashauri kuwaondoa wananchi na kusema maeneo fulani ni hifadhi na wakijua kabisa maeneo hayo hayajatangazwa kwenye Gazeti la Serikali.
Nini tamko la Serikali juu ya Halmashauri ambazo zinaondoa wananchi hao na ikiangalia kabisa hawajafuata taratibu na sheria za nchi yetu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hifadhi za misitu kuna misitu ambayo inasimamiwa na Serikali Kuu, kuna misitu inayosimamiwa na TAMISEMI na kuna misitu inayosimamiwa na Serikali za Vijiji. Kwa hiyo, kama vijiji vimetenga kwamba maeneo hayo ni ya hifadhi basi mamlaka zinazohusika zina wajibu wa kuhakikisha kwamba wananchi hawavamii katika hayo maeneo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo basi, mimi naamini kabisa Wakuu wa Wilaya wamechukua hatua kutokana na maamuzi yaliyokuwa yamefanywa na Halmashauri zinazohusika. Kama kuna maeneo ambayo wananchi wameondolewa bila kufuata taratibu basi ntaomba Mheshimiwa Mbunge anipe hayo maeneo ili tuone na tutafakari ni hatua zipi zilistahili kuchukuliwa. (Makofi)
MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo kubwa la ardhi katika Wilaya ya Sikonge, Mkoa wa Tabora, eneo kubwa ni eneo la hifadhi kuliko eneo ambalo wanaishi binadamu na inabidi wale wanadamu wafanye kazi kwenye eneo la hifadhi.
Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza eneo la hifadhi na kuwapa wananchi ili waweze kufanya shughuli zao za kibinadamu kuliko ilivyo hivi sasa ambapo wananyanyasika, wanadhalilika na kuteseka? Nakushukuru.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli na mimi naomba niungane naye kusema kwamba Mkoa wa Tabora ni mojawapo ya mikoa ambayo ina sehemu kubwa sana ya Hifadhi ya Taifa, kwa kweli hilo Serikali tunakubali na tumeona kabisa juhudi mbalimbali ambazo zimefanywa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli nchi yetu kama tulivyokuwa tunasema kila siku na tumekuwa tukisema, ardhi haiongezeki, idadi ya watu inazidi kuongezeka, shughuli za kibinadamu zimezidi kuongezeka, mambo mengi yamezidi kuongezeka. Kwa kweli mpango wa kupunguza maeneo ya hifadhi hautatusaidia kutatua matatizo, tatizo linaweza kutatuliwa kwa kuwa na mipango bora ya matumizi ya ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiwa na mipango mizuri ya kutumia ardhi iliyopo hiyo itatusaidia kuliko kupunguza hifadhi. Leo hii tutapunguza kesho idadi ya watu itaongezeka zaidi, je tutazidi kupunguza? Mwisho hifadhi zote zitaisha.
Kwa hiyo hatuna mpango wa kuweza kupunguza bali ni kuwashauri wananchi watumie muda wao vizuri wapangilie vizuri ardhi yao ili ile ambayo ipo kwa ajili ya shughuli za kilimo na makazi itumike kama ambavyo imekusudiwa. (Makofi)
MHE. MWANTUM DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri naomba kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa wananchi, wanaendelea kunyanyasika katika maeneo hayo, je, Serikali ina mpango gani wa kutoa muda maalum kwa kumaliza mgogoro huo wa kitaifa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tumekuwa tukitoa majibu kwa muda mrefu kwamba sasa hivi tunayapitia matatizo na changamoto zote zilizopo katika hifadhi zetu, ikiwa nia pamoja na maeneo yale yanayosimamiwa na jumuiya za wananchi, naamini kabisa kwamba baada ya muda mfupi na baada ya Serikali na wadau wengine kukaa kwa pamoja tutaleta ufumbuzi wa suala hili na haya matatizo yatapungua kwa kiwango kikubwa. (Makofi)
MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru. Tatizo hili linafanana kabisa na tatizo la pori tengefu la Loliondo ambalo limedumu kwa kipindi cha miaka 25 sasa au zaidi, tokea nchi hii imepata uhuru ni awamu nne zimepita za uongozi na zote zikiongozwa na Serikali ya CCM. Kila awamu ilikuwa inapeleka uongozi wake kule kwa ajili ya kuongea na wananchi kwa ajili ya mgogoro huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata Waziri Mkuu Mheshimiwa Majaliwa ametoa agizo juzi kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha aunde Kamati ya kwenda kushughulika na tatizo hili. Amepeleka ripoti na Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla amepeleka ripoti lakini mpaka sasa hakuna ambacho kimefanyika;
Naomba kujua je, ripoti hizi, zinasema wananchi wale waendelee kuteseka au ni nini ambacho kiko chini ya carpet ambacho kinasababisha wananchi hawa wasipiwe suluhu, na haki yao kupitia mgogoro huo ambao umeikumba Serikali hii na nchi hii kwa muda mrefu kwa muda wa miaka 25 na zaidi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwa muda mrefu kumekuwa na tatizo na mgogoro huko Loliondo na mgogoro huu umedumu kwa miaka mingi. Hivi sasa Serikali kama ulivyosema mwenyewe imechukua hatua za kuunda kamati mbalimbali ikiwemo kamati ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambayo ilileta mapendekezo na mapendekezo hayo yamepitiwa na Serikali, Serikali imefanya uamuzi ambao tumeufikia ni kutaka kuwa na chombo maalumu kitakachosimamia lile pori la Loliondo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa Serikali inafanya mchakato wa kuanzisha hicho chombo au mamlaka ambayo itahusika na usimamizi wa pori hilo la Loliondo kwa usimamizi na ushirikiano wa wananchi wenyewe wa Loliondo. Hii ndiyo tunaamini kwamba itakuwa suluhu ya tatizo ambalo limedumu kwa muda mrefu katika lile eneo. Kwa hiyo, ni hivi karibuni tu tutaleta huo mwongozo na tutaleta hiyo mamlaka au tutaleta chombo hicho ambacho kitakwenda kusimamia tatizo hilo la Loliondo.
MHE.DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipatia nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri ameongea kuhusu maeneo ya hifadhi ambayo yamekuwa yakihifadhiwa na Serikali lakini pia vyanzo vya maji. Kwa kuwa, wananchi wangu kwa kupitia Halmashauri ya Mpimbwe, Jimbo la Kavuu, wananchi wangu wa Kata ya Itobanilo; vijiji vya Senta Unyenye, Amani na Lunguya wamekuwa wakitumia maji ya Mto Kavuu ambao unapakana na mbuga ya Katavi na askari wa Katavi wamekuwa wakiwanyanyasa wananchi wakati vijiji hivyo hawana maji na tumekuwa na ujirani mwema wa kutumia.
Je, Serikali inasema nini kuhusu hawa watu wa National Park kupiga wananchi hovyo wakiwa wanaenda kutafuta huduma za msingi?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli wananchi wa kata hizo alizozitaja pamoja na hivyo vijiji vimekuwa vikitegemea sana maji ya eneo lile ambalo amelisema karibu na mbuga yetu ile ya Katavi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Sheria zetu za Wanyamapori Sheria Na. 5 ya mwaka 2009 hairuhusu wananchi kuingia katika maeneo ya hifadhi bila kibali. Kwa hiyo, hivi sasa ambacho kinaweza kufanyika ili kunusuru matatizo hayo, kwa sababu tuna sera ile ya ujirani mwema nitaomba tukae na Mheshimiwa Mbunge, tukakae na wananchi wenyewe ili tuweze kuangalia ni namna gani tunawapelekea maji katika maeneo ya vijiji vinavyohusika badala ya kuingia kwenye hifadhi ambapo wanakuwa wanahatarisha maisha yao na pia hali wataharibu hifadhi kitu ambacho ni kinyume na sheria. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge tushirikiane katika kutatua tatizo hili.
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu, baada ya kupata janga la tembo kuharibu mazao ya wananchi wa Serengeti na Bunda nilimwomba chakula, kwa kweli tulipata mahindi nimshukuru sana. Nina maswali mawili ya nyongeza lakini kimsingi swali hili lilikuwa lijibiwe na Wizara ya Maliasili na Utalii. Sasa kwa kuwa Serikali ni moja naomba niulize maswali yafuatayo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2016, baada ya tembo kuharibu mazao sana na kupiga kelele hapa Bungeni ikaonekana hatua haichukuliwi nilimwandikia Spika wa Bunge barua dhidi ya madhara na hatua ambayo wananchi walikuwa wameamua kuichukua. Mheshimiwa Spika akamwandikia Waziri wa Maliasili na Utalii aliyekuwepo, Mheshimiwa Maghembe ambaye tuliondoka naye kwenda naye Serengeti akaona madhara makubwa na akakabidhiwa tathmini ya uharibifu wa mazao na mauaji ambayo yameyosababishwa na tembo.

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni kwamba kumekuwepo na uharibifu mkubwa wa mazao na mauaji hauwezi ukaisha mwezi mtu hajauawa na tembo. Mashamba yanaharibiwa kwa kiasi kikubwa na Serikali ilishaahidi kuweka uzio au fence kuzunguka makazi ya wananchi, sasa miaka mitano inaelekea kwisha hakuna hatua yoyote, hakuna chochote kilichofanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeshaweka mpaka fedha kwenye bajeti yake kuweka game posts kwenye maeneo ya makazi ya wananchi ili kuzuia tembo, lakini mpaka leo hakuna chochote kilichofanyika. Nini tamko la Serikali dhidi ya uharibifu unaosababishwa na tembo kwenye mazao ya chakula na mauaji ya wananchi wa Serengeti, Bunda na Tarime na maeneo mengine?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake zuri ambalo ameliuliza. Ni kweli kabisa kumekuwa na matatizo katika maeneo mengi na hilo eneo alilolisema ni mojawapo ya maeneo ambayo kumekuwa na tatizo sana la tembo kuvamia katika mashamba ya watu.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwezi uliopita tarehe 29 na tarehe 30 tulipeleka Maafisa wetu kwenda kufanya tathmini katika yale maeneo ili kuangalia uharibifu mkubwa ambao umefanyika na ili tuone ni hatua gani ziweze kuchukuliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu hili suala ambalo amesema kwamba tuna mpango wa kuweka uzio, naomba nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali bado inafanya jitihada kuhakikisha kwamba tunachukua hatua za tahadhari na kuona ni nini kifanyike katika kuweza kuhakikisha kwamba tunawalinda wananchi wale ambao wanazunguka hifadhi zetu. Kwa hiyo, tutaendelea kulifanyia kazi. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake dogo la nyongeza, lakini kwa niaba pia ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa pongezi alizozitoa naomba nizipokee. Vile vile naomba pia niongezee katika majibu mazuri ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri wa Maliasili amejibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la nyongeza kwa sababu linahusu wakulima, mazao na chakula naomba niseme kabisa kwamba sisi kama Wizara ya Kilimo kwa vile inahusu wakulima na mazao, basi tutashirikiana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, vile vile na Ofisi ya Maliasili na Utalii kuhakikisha kwamba tunahakikisha wakulima wetu wanapewa stahiki zao zinazostahili ili tatizo hili lisiweze kujitokeza tena. Nashukuru.
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Suala la tembo pamoja na uharibifu wake ni suala zito sana. Linaongelewa hapa kwa juu juu lakini madhara yake ni makubwa sana kwa wananchi na hasa wanaozunguka maeneo hayo. Je, unaposema mapitio ya kanuni, ni lini sasa yatakuwa tayari? Swali hilo tu kwa sababu wananchi wana shida kubwa sana.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema kwamba sasa hivi tuko kwenye hatua ya mwisho ya kupitia hizi kanuni upya ili angalau kuweza kuvipitia hivi viwango vyote ambavyo vimekamilika. Kwa hiyo nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mwaka huu hautakwisha hizi kanuni zitakuwa zimeshakamilika.
MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali madogo mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; katika mapato yanayotokana na uwindaji katika hivi vitalu halmashauri zetu ambazo ziko na maeneo haya zinapata asilimia 25 ya mapato, lakini katika hiyo asilimia 25 ni baada ya kutoa zile gharama za uendeshaji. Sasa kumekuwa na changamoto ya ucheleweshaji wa haya makusanyo na kiwango hiki kinachotolewa bado ni kidogo na ukizingatia kwamba halmashauri ndizo ambazo zinasimamia kwa ukaribu maeneo haya. Sasa je, Serikali iko tayari kuongeza kiwango toka asilimia 25 mpaka 30 ili tuweze kukidhi gharama za operesheni katika maeneo hayo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika majibu ya Serikali wameeleza namna bora za kudhibiti hizi nyara za Serikali na tunatambua juhudi ambazo Wizara imefanya kwa kushirikisha vyombo vya ulinzi na usalama, kuboresha kanuni na kuvihusisha kwenye kulinda maliasili hizi za Serikali. Hata hivyo, kuna udhaifu waa kibinadamu, yaani watumishi katika hizi kampuni. Je, Serikali itafanya mkakati gani kuhakikisha kwamba watumishi wa hizi kampuni hawachangii katika udhaifu wa kupoteza nyara za Serikali?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Richard Mbogo kwa swali zuri na kwa jinsi ambavyo amekuwa akifanya kazi katika kutetea wananchi wake wa eneo husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kanuni zinavyoelekeza ni kwamba 25% inayotokana na mapato yote ya uwindaji wa kitalii ndio yanakuwa-calculated na yanaenda kwenye halmashauri, si baada ya kutoa gharama. Hivi sasa tunafanya mapitio ya sheria zote zinazohusu uhifadhi na wanyamapori. Baada ya hizo sheria kukamilika kanuni husika pia zitapitiwa tutaangalia kama hilo walilopendekeza litawezekana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuhusu watumishi ambao wanajihusisha na upotevu wa nyara za Serikali; ni kwamba hivi sasa ofisi yangu tumeunda Kamati ndogo ambayo inapita katika maeneo mbalimbali kubaini makampuni pamoja na watumishi wa ofisi zetu, wale ambao wanakuwa wanahusika na upotevu wa nyara za Taifa. Baada ya Kamati hiyo kukamilisha na mapendekezo kuletwa, hatua stahiki zitachukuliwa kwa watumishi wote wa namna hiyo, kwa sababu tunataka mtumishi afanye kazi yake kwa weledi, kwa kuzingatia kanuni, sheria na maadili ya kazi yake.
MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. La kwanza, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, atakumbuka mnamo mwaka 1981 Serikali ilikitangaza Kisiwa hiki cha Kilwa Kisiwani kuwa Urithi wa Dunia. Hadi kufikia mwaka jana Serikali ilipokea bilioni saba kutoka kwa wafadhili kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa miundombinu iliyopo Kilwa Kisiwani ili kuvutia watalii wengi zaidi.
Mheshimiwa Spika, nitapenda kupata majibu ya Serikali ni kwa nini sasa ujenzi wa miundombinu hii haujafanyika ilhali wameshapokea bilioni saba kutoka kwa wafadhali na pengine Serikali ingeweza kuongeza fedha ili huu ukarabati wa magofu unaoendelea uweze kwenda sambamba na ukarabati wa miundombinu?
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri atakubaliana na mimi, watalii wengi zaidi kutoka nchi mbalimbali duniani wangependa kutembelea urithi huu wa dunia, lakini hadi hivi tunavyozungumza hakuna kivuko cha kueleweka cha kuwavusha watalii kutoka Kilwa Masoko kwenda Kilwa Kisiwani, kitu ambacho kingeweza kuingizia mapato Serikali yetu. Nataka kujua sasa ni lini kivuko hicho kitajengwa kutoka Kilwa Masoko kwenda Kilwa Kisiwani ili kuinua kasi ya uchumi katika sekta hii ya utalii? Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa Kilwa Kisiwani tumepokea fedha zaidi ya bilioni saba kwa ajili ya ukarabati wa majenzi yaani ukarabati wa magofu yote ambayo yapo Kilwa Kisiwani. Naomba nilitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba Kisiwa cha Kilwa Kisiwani kina magofu mengi sana na hizo bilioni saba bado ni kidogo.
Mheshimiwa Spika, hizi tulishaanza kuzifanyia kazi tayari, tumeanza ukarabati na hao vijana ambao wameshapata mafunzo mbalimbali kwa ajili ya kukarabati hayo majenzi wako kazini. Mimi mwenyewe tarehe 9 Machi, nilikuwa kule nikashuhudia jinsi kazi nzuri ambayo inaendelea kufanywa na wale vijana. Kwa hiyo, siyo kwamba zile fedha zimekaa, fedha zile zinaendelea tayari kufanya kazi.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kuhusu kivuko ni kweli kabisa nimeshuhudia katika lile eneo kwamba tukipata kivuko cha kisasa, kizuri kinaweza kikasaidia sana katika kuwavutia watalii ili waweze kufika katika lile eneo. Hivi sasa Serikali inaendelea kujipanga pale hali itakaporuhusu ya kifedha basi tutaweza kupata kivuko hicho ili kiweze ku- promote utalii katika aneo hilo la Kilwa Kisiwani.
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Mkutano wa World Heritage ambao ulifanyika nchini Qatar, Pori la Akiba la Selou na lenyewe lilitangazwa kama urithi wa dunia na nchi mbalimbali zilikubaliana kuisaidia Tanzania takribani dola milioni mbili kwa ajili ya kupambana na ujangili wa tembo. Nataka kujua status ya hali ya ujangili wa tembo katika Pori la Akiba la Selous?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwa kweli kwa sasa hivi hali kidogo ni nzuri, hakuna tena ujangili kama ambavyo umekuwepo na ndiyo maana matukio mbalimbali yale ambayo tulikuwa tunapotelewa na tembo na maeneo mengine yamepungua kwa kiwango kikubwa sana katika hili eneo.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Kutokana na jibu la msingi tumeona namna gani ambavyo migogoro ni mingi hapa nchini. Migogoro hii inapoteza maisha ya Watanzania, migogoro hii inapoteza mali za Watanzania, watu wanafilisiwa mifugo yao, wanaharibiwa nyumba zao, wanachomewa vitu vyao, lakini pia migogoro hii inadumaza uchumi kwa kuwa watu wana - concentrate kwenye migogoro wanashindwa kufanya masuala ya maendeleo.
Mheshimiwa Spika, nilikuwa nategemea Mheshimiwa Waziri baada ya kubaini matatizo haya aje na mpango mkakati, namna gani za haraka kutatua migogoro hii, tofauti anavyosema hapa wataendelea kushirikiana na wadau. Wakati timu zinaendelea kufanya kazi kubaini migogoro hii, bado Watanzania wameendelea kunyanyasika, wakati huu tunapoongea bado watu wanaendelea kunyanyaswa kwenye maeneo ya hifadhi, mipaka, mifugo yao inaendelea kupigwa mnada, vyanzo vinazidi kuharibiwa, nilitegemea wakati Serikali haijaja na mpango wa kutatua matatizo haya, wangesitisha kuendelea kunyanyasa watu ili wenyewe wafanye kazi yao, ndiyo waendelee kushughulikia watu ambao wako ndani ya hifadhi ambapo wamesajiliwa kisheria?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, mwaka 2012/2013, Wizara ya Maliasili na Utalii ilinyang’anya vijiji 26 vyeti vya usajili kutoka Wilaya ya Kaliua kwa madai kwamba vimesajiliwa kinyume na utaratibu wakati walisajiliwa kisheria chini ya Wizara ya TAMISEMI, suala ambalo sasa hivi limeenda kuumiza uchumi wa wananchi wale kwa sababu makampuni ya tumbaku yamesema hayataingia mikataba ya biashara kununua tumbaku kwenye vijiji 26 kwa sababu havina vyeti vya usajili wa vijiji.
Mheshimiwa Spika, naomba Wizara ya Maliasili ituambie itarudisha lini vyeti vya usajili kwa vijiji 26 ambavyo leo wanaenda kuathirika kiuchumi kwa kuwa walisajiliwa kisheria, wanaishi kisheria, kama lilifanyika kosa ni suala la Serikali? Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nitoe taarifa kwamba siyo lengo la watumishi wetu walioko kwenye hifadhi kuwanyanyasa wananchi, kwa mujibu wa kanuni na taratibu hawaruhusiwi kufanya hivyo, kazi yao kubwa ni kuhakikisha wanalinda hifadhi na siyo kuwanyanyasa wananchi wanaozunguka katika maeneo hayo. Kwa hiyo kama kuna kesi kama hizo naomba tuwasiliane na Mheshimiwa Mbunge ili tuweze kuwachukulia hatua stahiki hao ambao wanawanyanyasa wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza kuhusu mpango mkakati nimeeleza kwamba timu hiyo baada ya kukamilisha hilo zoezi Wizara zote zinazohusika zimepewa hii taarifa kwa ajili ya kuanza kuweka mkakati wa makusudi kabisa wa kutekeleza na kutatua migogoro ya namna hiyo. Hiyo kazi imeshaanza na kila Wizara ina mpango wake inatekeleza, sisi kama Maliasili na Utalii tumejipanga kwa ajili ya hiyo.
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ni kwamba, Mheshimiwa Waziri Mkuu alituagiza kuweka mipaka katika maeneo yote yenye migogoro, mipaka ile baada ya kuwekwa sasa Serikali inatathmini ni maeneo yapi yana migogoro, yapi yapo ndani ya hifadhi, yapi tunaweza kuyaachia, yapi lazima tuwape fidia wananchi na yapi tuwaondoe wananchi. Baada ya hiyo yote kukamilika, hatua stahiki zitafanyika na Mheshimiwa Mbunge atapata ule mpango wa Serikali kwa ujumla katika maeneo yote.
Mheshimiwa Spika, kuhusu wananchi ambao Mheshimiwa Mbunge anasema walinyanga’anywa vyeti vyao wa usajili wa vijiji, hiyo taarifa naomba niseme bado sina lakini nitaifuatilia, nitashirikiana na Mheshimiwa Mbunge kuhakikisha kwamba angalau tunapitia na tuone tunashirikiana pamoja na Wizara zingine ili katika hivi vijiji 366 ambavyo viko ndani ya hifadhi tuone kama na hivyo navyo vipo ili kusudi tuone hatua itakayochukuliwa na Serikali, basi itahusu maeneo yote hayo pamoja na vijiji alivyovisema. (Makofi)
MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na nashukuru kwa majibu, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa ni miaka miwili na miezi minne sasa toka Serikali imetamka hilo ililolitamka kuhusu maeneo yaliyopoteza sifa mpaka leo na bado habari ya tathmini inazungumzwa mpaka leo, naomba Kauli ya Serikali kuhusu dhamira ya kukamilisha kazi hii ili tupeleke maendeleo kwa pamoja utalii, kilimo na mifugo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, asilimia 54 ya eneo la Wilaya ya Biharamulo ni maeneo yaliyohifadhiwa. Naomba kujua kutoka kwa Serikali, miongoni mwa maeneo yanayoonesha dalili za kupoteza sifa, yako yale yaliyozunguka Wilaya ya Biharamulo? Nakushukuru.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Oscar kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akiifanya katika kuwatetea wananchi wa Jimbo lake, hongera sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba kweli tathmini ilishakamilika katika hayo mapori tengefu 12 na tulishamaliza kazi. Kazi iliyobaki sasa ni kuhaulisha. Tararatibu za kisheria za kufuta yale maeneo lazima zizingatiwe. Kwa hiyo, huo ndio mchakato ambao bado unaendelea kwa hivi sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuhusu maeneo ambayo yanahusika katika Jimbo la Biharamulo; kwanza, kuna Masasi River, Biharamulo ambalo lina ukubwa wa kilometa 180 lipo kwenye orodha ya hayo mapori tengefu ambayo tunayaangalia. Lakini pia, kuna eneo lingine, Inchwakima nalo ni eneo ambalo bado tunaliangalia katika lile Jimbo la Biharamulo. Kwa hiyo, maeneo haya mawaili ndio yale ambayo yako katika mapori ya akiba ambayo tunayafanyia kazi, ili yaweze kurudishwa kwa wananchi pale ambapo utaratibu utakamilika.
Kwa hiyo, baada ya hapo naamini Mheshimiwa Mbunge utafurahi na wananchi wako watayatumia maeneo hayo vizuri na ipasavyo.
MHE. PROF. NORMAN S. KING: Mheshimiwa Mwenyekiti, inasikitisha kidogo kwa sababu, kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi, ukurasa wa 51 iko bayana, barabara hii imetajwa kwamba ni muhimnu iwekwe kiwango cha lami. Ni lini Serikali itapeleka nguvu kuhakikisha kwamba hili linatekelezwa ili kuboresha miundombinu hii?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, mwaka 2017 Serikali ilikuwa imeahidi kupeleka wanyama kwenye hifadhi hii ili kuongeza vivutio kwenye Hifadhi ya Kitulo. Ni lini mpango wa kupeleka wanyama wasio wakali, ukiacha simba, kwenye hifadhi hii utakamilika?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijajibu maswali hayo naomba nichukue nafasi hii kwanza kumpongeza kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akiifanya, lakini pia nimpongeze kwa jitihada kwamba sasa hivi anaenda kuoa na amesambaza kadi. Kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge wamchangie ili akamilike, aendelee kufanya kazi vizuri. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa hii barabara iko katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwamba itajengwa kwa kiwango cha lami, lakini naomba nimjulishe Mheshimiwa Mbunge tu kwamba hivi sasa barabara ambayo inawekwa lami ni ile ambayo inatoka Njombe hadi Makete, inawekwa lami sasa hivi na bado kuna barabara nyingine ya kutoka Isonje – Makete mpaka Mbeya, nayo iko kwenye feasibility study. Hii barabara ya tatu itakuja kuunganishwa na hizi barabara nyingine mbili ambazo nimezisema na ninaamini kabisa hali itakuwa ni nzuri na Mheshimiwa Mbunge utafurahia baada ya hilo suala kukamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuhusu ni lini wanyama wale ambao tuliahidi kwamba tutawapeleka katika Hifadhi yetu ya Kitulo, Serikali ina mpango wa kupeleka wanyama 25. Ili kuhamisha wanyama kutoka hifadhi moja kwenda hifadhi nyingine kuna taratibu za kisheria ambazo ni lazima zikamilike. Hivi sasa zimeshakamilika na Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii amesharidhia wanyama 25 wahamishiwe katika Hifadhi yetu ya Kitulo kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naamini baada ya muda mfupi utawaona hao wanyama.
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia kuuwawa kwa Ndugu Emmanuel Ernest wa Ilolo na Stefano Ndalu wa Nhinyi na Amani Joseph Sita wa Mvumi Mission kujeruhiwa vibaya na kupata malipo kidogo sana, je, ni lini sasa Serikali itaruhusu vijiji viweze kumiliki silaha kwa ajili ya kujilinda na wanyama hao wakali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, pesa aliyoitaja Mheshimiwa Naibu Waziri kuwa imelipwa kwa watu 27 ukiigawanya ni sawasawa na shilingi 278,518. Sasa Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza kuwatangazia Watanzania kwamba katika nchi yetu tembo wana thamani kubwa kuliko uhai wa watu? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijajibu maswali hayo, naomba nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Livingstone Lusinde kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akiifanya katika kufuatilia na kuwatetea wananchi wake. Kutokana na kazi yake ndiyo maana anajulikana kama kibajaji yaani kwa mambo makubwa anayoyafanya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitumie nafasi hii kuwapa pole wale wananchi wote ambao wameathirika ama wameuwawa na wanyama wakali, nawapa pole sana. Niseme tu kwamba hili suala alilolileta na kupendekeza kwamba tutoe silaha kwa wananchi na hasa katika vijiji kuweza kumiliki silaha, basi pale tutakapokuwa tunapitia sheria, pamoja na kanuni hizi tutaliangalia kama hilo litawezekana ili kusudi tuone kama linaweza kusaidia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili alilouliza ni kwamba kwa mujibu wa Kanuni za Kifuta Jasho na Kifuta Machozi za mwaka 2011 ndiyo vinatoa viwango vile vinavyostahili. Nataka niseme kwamba tunachotoa siyo fidia, ni kifuta machozi na kifuta jasho. Ndiyo maana imeandikwa kabisa kwamba kifuta jasho kama binadamu ameuwawa ni shilingi1,000,000, kama amejeruhiwa ni shilingi 500,000, kama ni mazao yana viwango vyake kufuatana na kilometa. Kwa hiyo, hivi viwango vipo kwa mujibu wa sheria, lakini pale tutakapokuwa tunapitia tutavihuisha na kuona kama kuna haja ya kuvirekebisha ili kusudi vikidhi mahitaji ya wakati uliopo.
MHE. ZAYNAB M. VULU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii na napongeza majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nilitaka kujua, je, ni kwa kiasi gani Serikali imejipanga kuhakikisha inatoa pilipili nyingi ili kuweza kuchoma na kukimbiza tembo hao kwenye maeneo wanayoishi watu hasa ukizingatia kwamba kwanza kuchoma moto misitu ni kuharibu mazingira?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, tulichosema ni kwamba katika maeneo yale yanayozunguka hifadhi zetu au yale ambayo yapo jirani na hifadhi zetu tunajaribu kuwahamasisha wananchi kwamba wapande pilipili na pia pale ambapo pana kinyesi cha tembo tunakichukua kile tunachoma. Nataka niseme kwamba tutaangalia namna na tutazungumza mikakati ambayo tumeiweka katika kuhakikisha kwamba pilipili zinatosha katika maeneo hayo hasa pale tutakapowasilisha bajeti yetu hapo tarehe 21 na 22 Mei.
MHE. JULIUS K. LAIZER. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Tatizo hili la tembo katika nchi yetu limekuwa likiwasababishia Watanzania umaskini mkubwa sana na mkakati wa Wizara hauoneshi kama kuna jitihada nzuri ya kushughulikia jambo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati nauliza swali hili jana usiku tembo wamevamia mashamba ya wananchi zaidi ya ekari 20 na kumaliza kabisa na ni kilomita zaidi ya 20 kutoka eneo la hifadhi. Je, Serikali ina makakati gani wa haraka katika kipindi hiki cha mvua na cha mazao yetu ili kusaidia wananchi kuwaondoa tembo hao waache kuharibu mazao yetu?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kumekuwa na matukio ya tembo katika maeneo mengi hapa nchini na hii imetokana na kuimarika kwa uhifadhi katika maeneo mengi na hivyo tembo wameongezeka. Pale ambapo pametokea tatizo la namna hiyo tunaomba tuwasiliane haraka ili kusudi askari wetu wa doria waweze kwenda na kuchukua hatua na kuwafukuza tembo hao ili warudi katika hifadhi pale ambapo wanastahili.
MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Tatizo la Mtera halina tofauti kabisa na tatizo la kata nzima ya Likuyu Sekamaganga na hususan Kijiji cha Mandela. Walioathirika walishafanyiwa tathmini muda mrefu na hakuna dalili ya kuwalipa hicho kifuta jasho na kifuta machozi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itatoa hicho kifuta jasho na kifuta machozi kwa wale walioathirika katika Vijiji vya Mandela, Likuyu Sekamaganga, Mtonya pamoja na majirani zao wa Mgombasi?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kumekuwa na matukio mengi katika lile Jimbo la Tunduru na maeneo mengine pamoja na kile Kijiji cha Mandela. Naomba nilitaarifu Bunge lako tukufu kwamba matukio haya ya wanyama waharibifu ni mengi sana katika nchi yetu kwa sasa hivi. Hili inatokana na kwamba uhifadhi umeimarika na wanyama wameongezeka lakini pia kuna changamoto nilizozisema nilipokuwa najibu swali la msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa kuna matukio zaidi ya 3,509 ambapo wananchi wamepatwa na matatizo mbalimbali. Jumla ya fedha ambazo zinadaiwa mpaka sasa hivi katika maeneo na wilaya mbalimbali ni zaidi shilingi milioni 828. Kwa hiyo, kazi tunayoifanya sasa hivi ni kutafuta hizi fedha ili kuhakikisha kwamba hao wananchi wote walioathirika na wanyamapori na wanyama waharibifu basi waweze kupata kifuta jasho na kifuta machozi kinachostahili. Baada ya kupata fedha hizo tutafanya hivyo mara moja. (Makofi)
MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniopa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza na vilevile naishukuru Serikali kwa majibu mazuri, lakini pia nimpongeze Waziri kwa kushughulikia mgogoro wa Loliondo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza, tunafahamu awali kulikuwa na tatizo baadhi ya watu na zikiwemo baadhi ya hoteli zilikaidi kukusanya makusanyo haya. Nilitaka tu kujua pamoja na majibu haya mazuri, ni hatua zipi zimechukuliwa kwa wale ambao walikaidi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni hatua zipi zilichukuliwa kwa hoteli ambazo zilikiuka ukusanyaji huu wa kodi hii yaani concession fees?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Amina Mollel kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akiifanya, hasa katika kuwatetea watu wenye ulemavu. Amekuwa akifanya kazi hiyo vizuri sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli wakati tunaanza utekelezaji wa tozo hii baadhi ya hoteli zilikuwa bado hazijapata elimu ya kutosha kwa nini tozo hi imeanzishwa. Kutokana na jitihada ambazo Serikali ilichukua kuwaelimisha wamiliki wa hoteli zote hizo kwa nini tumeanzisha tozo hiyo na kwa nini ni muhimu kulipa na kwa nini tumeachana na mtindo wa zamani, basi hoteli zote hivi sasa zimeelimika na zote zinatekeleza. kwa sababu, zote zina-comply na utaratibu huu mpya basi hakuna hatua ambazo zimechukuliwa. Kwa wale ambao watakaidi ndiyo hapo tutachukua hatua lakini kwa hivi sasa zote zinatekeleza.
MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, inasikitisha sana Watanzania wamekuwa wakilipa Concession Fee sawa na wageni. Je, ni kwa nini Serikali isione umuhimu wa kuwa-charge Concession Fee Watanzania tofauti na wageni?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii kumjibu Mheshimiwa Catherine Magige, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Concession Fees inalipwa katika hoteli za kitalii na ni kwa wageni wanaotoka sana sana nje ya nchi, kwa wenyeji hawatozwi. Katika hilo, zile hoteli ambazo zinamilikiwa na Shirika la Hifadhi ya Taifa hazitozwi hiyo Concession Fee. Kwa hiyo, hii ni specifically kwa zile hoteli za kitalii.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya utalii inachangia takribani 17% ya pato la Taifa na wamiliki wa hoteli hizi za kitalii wamekuwa wakitozwa kodi nyingi au tozo nyingi sana takribani 46 na wamekuwa na malalamiko ya muda mrefu. Je, ni kwa nini Serikali isifikirie utaratibu mwingine wa kuwarahisishia hao wawekezaji kwenye hoteli za kitalii ulipaji wa tozo hizo?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Paresso, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwa na kodi na tozo nyingi ambazo zimekuwepo katika baadhi ya hoteli, lakini jitihada zilizochukuliwa na Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha hizi kodi zote zinahuishwa zinabaki chache. Mwaka jana, kama mtakumbuka, kuna baadhi ya kodi ziliondolewa na mwaka huu hivi sasa kuna kazi inaendelea kwa ajili ya kuhuisha kuangalia hizi kodi ziunganishwe kwa pamoja ili kurahisisha walipaji hao kusudi wasiwe na kodi za hapa na pale. Kwa hiyo, jitihada hizo zinafanyika na Mheshimiwa awe na subira, pale tutakaposoma bajeti yetu atasikia ni hatua gani ambazo tunakusudia kuzichukua.
MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa hali ya utalii kwa sasa hivi imeshuka kutoka asilimia 12.9 na kufika asilimia 3.3 na Mji wa Bagamoyo wanategemea uvuvi na utalii na kuonekanika mahoteli mengi ya kitalii ya Bagamoyo kukosa wageni, je, Serikali ina mikakati gani kuhakikisha inatangaza vituo vya utalii vya Bagamoyo na kuangalia ni tatizo gani lililofanya kushuka kwa asilimia hii ya utalii?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa majengo ya kale ya mji mkongwe wa Bagamoyo yamekuwa yanabomolewa na ramani za majengo yale yanatoweka ambapo yalikuwa ni kivutio sana kwa utalii, lakini ramani zile za kale zinapotea na kujengwa katika miundombinu mingine tofauti, je, Serikali ina mikakati gani kuhakikisha majengo yale yanaboreshwa kurudi katika hali ile ya mji mkongwe?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya utalii kwamba imeshuka kutoka asilimia 12 hadi asilimia tatu katika eneo la Bagamoyo, hii kwa kweli inahitaji labda nipitie takwimu vizuri. Kilichojitokeza zaidi ni kwamba katika hoteli nyingi za kitalii zile za Bagamoyo zilikuwa zinategemea sana uendeshwaji wake wa mikutano, yaani utalii ule wa mikutano ambao ulikuwa unaendeshwa sana Bagamoyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivi sasa mikutano mingi imepungua kutokana na mabadiliko ya hali ya uchumi. Hata hivyo, kutokana na hali hiyo, ndiyo maana Wizara imechukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuamua kuchukua mashirika yetu yaliyoko chini ya Wizara ili yaweze kukabidhiwa hii dhamana ya kutangaza maeneo yote yaliyoko Bagamoyo ikiwemo na ile Hifadhi nyingine ya Saadan kusudi iweze kuvutia watalii zaidi waendelee kuwepo na kuongezeka kule Bagamoyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu majengo ambayo yamekuwa yakiharibiwa na kubomolewa ramani zao zile za awali, ni azma ya Serikali kuendelea kuwahamasisha wananchi wanayoyamiliki hayo majengo kuhakikisha kwamba wanafuata taratibu za kurudishia ujenzi uliokuwepo kabla. Kwa sababu katika eneo lile tunataka majengo yale yaendelee kuwa na ramani na sura iliyokuwa inaonekana toka awali ili iendelee kuwa kivutio kwa upande wa wageni.
MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali kwamba asilimia 40 ifanye kazi ya uhifadhi. Vile vile kwa mujibu wa waraka asilimia 60 inatakiwa iende katika vijiji vinavyopakana na hifadhi ambavyo ni Mwambegwa, Mwanyaina, Mwagwila, Semu, Nyanza, Matale na vingine vingi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka 2016/2017 vijiji vile havikupelekewa hela na asilimia 40 haikufanya kazi ya uhifadhi na hivyo kuipelekea Idara ya Wanyamapori kushindwa kununua silaha kwa ajili ya kukabiliana na wanyamapori. Je, Serikali haioni sasa ipo haja ya zile fedha zikapelekwa moja kwa moja katika vijiji na asilimia 40 ikapelekwa katika Pori la Akiba kuliko kupelekwa Akaunti ya Amana? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, asilimia 44 ya kilometa za mraba ya Wilaya ya Meatu ni hifadhi. Halmashauri imepata ugumu katika kukabiliana na ujangili, uhifadhi wa maliasili na uvamizi wa wanyamapori kwa sababu ina changamoto ya vitendea kazi. Je, Serikali iko tayari kuipatia gari Wilaya ya Meatu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Leah kwa jinsi ambavyo amekuwa akifanya kazi na kufuatilia masuala mbalimbali yanayohusu Jimbo lake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali asilimia 60 zinazobaki kule kwenye Halmashauri kwamba ziende kwenye vijiji kama alivyosema, ni wajibu kila Halmashauri zinazopata mgao huu ile asilimia 60 inatakiwa iende katika vile vijiji vinavyozunguka hifadhi, kwa sababu zinatakiwa zitumike katika kuleta maendeleo ya vijiji vile vinavyohusika. Kwa hiyo, nitumie nafasi hii kuziomba Halmashauri zote nchini kutekeleza hilo agizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili kuhusu maombi ya gari, naomba nichukue nafasi hii kusema kwamba ni kweli kabisa kumekuwa na changamoto katika lile eneo na Wizara yangu inazo taarifa za kutosha. Tutalifanyia kazi maadam amelileta, tutaona pale hali itakaporuhusu kifedha tutawapelekea gari lile ambalo litawasaidia katika shughuli hizo. (Makofi)
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, katika majibu yake amekiri tatizo la tembo linazidi kuongezeka na wananchi wengi sana wanapata madhara makubwa na wanaathirika sana na tatizo hili. Wananchi wa vijiji husika wakiwemo vya Matongo, Mwauchumu, Longalombogo na maeneo mbalimbali hapa nchini wameathirika sana. Nataka tu kujua Serikali sasa inachukua hatua gani za kimkakati, tuache hizi hadithi za kwamba tutafanya, tuko mbioni, ni lini tatizo hizi sasa tutalipatia ufumbuzi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Kikosi dhidi ya Ujangili kimeshajenga kituo pale Lukungu na kituo hiki maana yake ni kusaidia kufukuza wanyama waharibifu wakiwemo viboko. Je, ni lini kituo hiki cha Lukungu kitaanza kufanya kazi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Chegeni. Kwanza kabla sijajibu, naomba nichukue nafasi hii kumpongeza kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia na hii ni mara ya tatu kuliuliza hili swali, hii inaonesha kwamba hili swali ni muhimu sana katika eneo la Jimbo lake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tulivyosema kwenye jibu la msingi kwamba katika maeneo yote haya ambayo kuna matatizo sasa hivi tutachukua hatua za dhati kuanzia tarehe 1 Julai, 2018 wakati bajeti mpya itakapoanza kutekelezwa. Tumejipanga sawasawa kuhakikisha kwamba haya yote tutayatatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu hiki Kituo cha Kupambana na Ujangili (KDU) kwanza kama alivyosema mwenyewe tayari majengo yameshakamilika, tunachosubiri hivi sasa ni kuhakikisha kwamba rasilimali watu pamoja na vifaa vya kutendeakazi vinakamilika ili kusudi kile kituo kianze kufanya kazi katika mwaka wa fedha unaokuja.
MHE. MARGARETH S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Awali ya yote namshukuru Naibu Waziri alifika mwenyewe na kujionea utata uliopo, kati ya mipaka iliyowekwa. Kuna mipaka miwili, wa zamani na wa sasa, ambayo imesababisha wananchi kutolewa kwa nguvu na hata kupoteza mali zao. Swali la kwanza; kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri alifika yeye mwenyewe na kujionea utata uliopo anasemaje kuhusu utata ambao aliuona?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kufuatana na mimi kwenda kukaa kumaliza kabisa utata uliopo pale ili wananchi waendelee na shughuli zao?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nichukue nafasi kumpongeza sana Mheshimiwa Margaret Sitta kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akiifanya katika kuhakikisha kwamba anasimamia uchangishaji wa fedha kwa ajili ya vyoo vya mfano katika shule zetu katika majimbo yote. Nakupongeza sana mama yangu kwa kazi nzuri ambayo umekuwa ukiifanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nitumie nafasi hii kumpongeza kwa jinsi ambavyo amekuwa akilifuatilia hili suala kwa muda mrefu. Nakumbuka mimi mwenyewe nilifika katika lile eneo kweli, tuliangalia utata wa mipaka iliyopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia agizo la Bunge la mwezi wa Sita katika kipindi cha bajeti tulikubaliana kwamba mipaka yote lazima iwekwe kwa ushirikishwaji wa wananchi, viongozi, Wizara ya Ardhi pamoja na Maliasili. Kwa hiyo, nasema tu kwamba, tuko tayari tutashirikiana na Wizara zinazohusika na wadau mbalimbali kuhakikisha utata wa migogoro ya mipaka iliyopo unatatuliwa mara moja na wananchi wanaendelea kufanya kazi zao kwa amani na utulivu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, niko tayari kabisa kufuatana naye lakini wakati nitakapofuatana naye nitaomba kwamba twende pamoja na Waziri wa Ardhi ili tuweze kuhakikisha kwamba wote tunajionea uhalisia uliopo katika eneo hilo.
MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza napenda kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri, alifanya ziara Mkoa wetu wa Lindi kuja kumaliza mgogoro wa mpaka wa Kikulyungu Wilaya ya Liwale lakini na mpaka wa Selous na Wilaya ya Kilwa. Kwa bahati mbaya sana kwa dharura iliyojitokeza Mheshimiwa Naibu Waziri alishindwa kukamilisha ile kazi. Sasa ningependa kujua ni lini Serikali itakuja sasa kumaliza ule mgogoro ili wananchi wa Kikulyungu na wananchi wa Wilaya ya Kilwa waendelee kufanya shughuli zao? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabla ya kujibu naomba niseme kweli kwamba nilikuwa nimeenda kwenye lile eneo hasa katika Wilaya ya Liwale kwa ajili ya kushughulikia ule mgogoro ambao upo katika Kijiji cha Kikulyungu. Bahati mbaya siku ile wakati tunajipanga kuelekea kule ndiyo siku ambapo Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii alipata ajali kwa hiyo nikalazimika kuahirisha ile safari ndiyo maana sikuweza kufika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Kamati ya Ulinzi na Usalama pamoja na Maafisa mbalimbali wa kutoka Wizara ya Ardhi na Wizara ya Maliasili walienda katika eneo husika walikaa na wananchi wakatoa elimu na wananchi wakawapokea na wakawa sasa kwamba wako tayari sasa kushirikiana kwa pamoja ili kuweza kubaini mpaka uliopo na kuondoa huo mgogoro ambao umedumu kwa miaka mingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitumie nafasi hii kusema kwamba, sasa tuko tayari wakati wowote tena tutarudi kuhakikisha kwamba sasa tunashirikiana na wananchi katika kuonesha mipaka ya eneo hilo husika na Mheshimiwa Mbunge utashirikishwa kikamilifu katika hilo suala.
MHE.SUZAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu ya Naibu Waziri. Mheshimiwa Waziri, amezungumzia suala la Malinyi na Ulanga, swali langu lilijikita zaidi Jimbo la Mlimba lenye kata 16 na kuna kata zisizopungua 14 ambazo zinatakiwa ziende zikafanyiwe marekebisho; na jibu lake limejikita kwenye kata tatu tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa pamoja na mpango huo wa Serikali kutaka kuhifadhi hilo eneo, wananchi hatukatai, lakini kuna barua zimeshasambazwa kwamba, wananchi wanatakiwa waondoke, wafugaji na wakulima mwisho tarehe 30 mwezi Agosti. Zoezi la uelimishaji kweli limefanyika katika vijiji hivyo saba na imeundwa timu ya watu 15, lakini kiangazi ndiyo hiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, waliahidi tangu mwezi Agosti watamaliza hilo zoezi kwenye hizo kata 14, ona, wamefikia kata tatu hata kata tatu wameunda tu timu lakini hawaenda kuweka vigingi. Je, lini sasa Serikali itaenda kuweka vigingi kwa kisababisho kwamba hamna hela? Kwa nini wanatufanyia hivi jamani? Lini watakwenda, hilo swali la kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa wananchi hawana uhakika wa maeneo haya kama yataenda kwenye hifadhi ama watabaki nayo, katika kata zote 14 wananchi wanagoma kuchangia maendeleo ya kujenga shule na zahanati kwa sababu hawajui hatima yao katika maeneo hayo. Sasa Serikali kwa nini wanaleta kigugumizi hawapeleki hela? Wanatunyang’anya maeneo lakini wanasema hawana hela za kwenda kuweka mipaka na kiangazi ndio hiki je, ikifika wakati wa mvua watakwenda huko?
Mheshimiwa Mwenyekiti, wako tayari kwenda lini waniahidi hapa jamani? Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kumpongeza kwa kuamua kushirikiana vizuri kabisa na Serikali kwamba kuna haja ya kuweka hivyo vigingi ili mipaka ieleweke kwa wananchi kusudi waendelee kushughulika na shughuli zao na maeneo ambayo yamehifadhiwa yaendelee kuhifadhiwa, nampongeza sana kwa msimamo huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuweka vigingi ni kweli kabisa kwamba tulisimamisha kwa sababu ya mgogoro uliokuwepo, lakini kuna hatua kadhaa ambazo tulikuwa tumezichukua. Hatua ya kwanza tuliunda Kamati ya watu 22 wa kupitia wilaya zote tatu ili waweze kutoa ushauri kwa Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, namna bora ya kuhakikisha kwamba vile vingingi vinawekwa na kupunguza migogoro ambayo ilikuwepo. Kamati hiyo tunatarajia kwamba itamaliza kazi yake na italeta ripoti wiki mbili zijazo kuanzia leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kwenda kutenga fedha naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba fedha zimetengwa, fedha zipo; na nitumie nafasi hii kweli kuungana naye kwamba ni kipindi muafaka kwa sababu mvua zikianza itakuwa ni vigumu sana kwenda kuweka mipaka katika lile eneo hasa kipindi cha mvua, lakini kipindi hiki ndio kipindi muafaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tutahakikisha kwamba ndani ya mwezi huu wa 10 mipaka hiyo inawekwa na nitaagiza taasisi zinazohusika zihakikishe kwamba hili zoezi linakamilika na wananchi wanashirikishwa na yeye mwenyewe Mbunge anashiriki kikamilifu katika hilo zoezi ili kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawasawa.
MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Suala la migogoro ya ardhi, misitu, maliasili na wananchi inazidi kuongezeka kila siku hapa nchini hali ambayo inaipatia Serikali hasara kubwa ya kuweka ulinzi katika maeneo hayo, halikadhalika wananchi wanaathirika sana kwa kuchomewa majumba yao na mali zao kuharibiwa kutokana na zoezi hilo. Sasa inaonekana hii dhana ya ushirikishi inayotumika hapa labda inatumika vibaya au hawajashirikishwa kwa dhati. Je, Mheshimiwa Waziri na Serikali yake wako tayari sasa kuja Zanzibar kujifunza mbinu walizotumia katika haya na wakafanikiwa?
NAIBU WAZIRI WIZARA YA MALIASILI NA UTALII:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba niseme kwamba tuko tayari kabisa kwenda kujifunza mbinu bora za kuhakikisha migogoro hii haipo. Kama walivyofanya Zanzibar basi na sisi tungependa tutumie mbinu hizo hizo kuhakikisha kwamba huku migogoro yote inamalizika.
MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na majibu ya Waziri naomba niulize maswali ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa majibu ya Waziri, utunzwaji wa Faru Fausta umewezesha kulitumikisha taifa kwa gharama kubwa kuliko wazee wa Tanzania waliofanyakazi ya kuleta haki na amani katika Taifa hadi Faru Fausta kuonekana ni wa muhimu ni kwa ajili ya amani iliyopatikana kwa wazee hawa. (Makofi)
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali haioni ni wakati sasa wa kuhakikisha wazee wa taifa hili wanatunzwa kama vile gharama zote anavyotunzwa faru Fausta ili waweze kuleta amani katika nchi hii?
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa kuwa kwa majibu ya Waziri amesema anahifadhiwa na ana ulinzi mkali, hivyo hata watalii hawamuoni, hizo fedha za kigeni zinazopatikana zinatokana na nini na wakati amehifadhiwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niweke record vizuri kwa dada yangu Mheshimiwa Mbunge kwamba wanyama wana haki sawa kama binadamu wengine na huyu mnyama kutokana na uadimu wake, na kwamba ni moja ya wanyama ambao wapo hatarini kutoweka ndiyo maana tumemweka kwenye ulinzi maalum. Kutokana na umuhimu wake huo na kutokana na jinsi ambavyo ameliingizia Taifa fedha nyingi za kigeni na kutokana na kwamba watu wengi wanataka kujua maisha yake kwamba ataishi miaka mingapi, maana mpaka sasa hivi ana miaka 53 ndio maana tumeamua kumweka kwenye ulinzi huo sawa na binadamu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilo Ilani ya Chama cha Mapinduzi inasema Wazee wote sasa hivi tunawatambua ili kutengeneza sera nzuri ya kuweza kuwasaidia na kuwalipa pensheni. Kwa hiyo, watalipwa sambamba na faru huyu, Faru Fausta ambaye ndiyo sera inavyosema ya Chama cha Mapinduzi, nashukuru. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii naomba niongeze maelezo kidogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sera ya Afya ya mwaka 2017 Serikali inatambua mchango na kuthamini mchango wa wazee na tumeweka utaratibu wazee wote ambao wako zaidi ya miaka 60 watapata matibabu bure.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeweka mkakati sasa hivi kuhakikisha kwamba wazee wanatambuliwa na kupewa vitambulisho vya kupewa matibabu na tumeweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba, katika vituo vyetu vyote vya kutolea huduma za afya wazee wanapewa kipaumbele cha kwanza. (Makofi)
Kwa hiyo pamoja na majibu yote ambayo ametoa Naibu Waziri mchango huu ambao unapatikana katika mapato ya utalii katika sekta hii ya utalii ndio haya yanayoingia kwenye Mfuko Mkuu wa Taifa na kwenda kuwahudumia wazee hawa. (Makofi)
MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nianze kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri katika Bunge lililopita aliniahidi kuja Lindi kutembelea maeneo haya na kwa kweli alikuja na aliambatana na viongozi wa Mkoa na Wilaya katika kutembelea na kujionea maeneo haya ya mgogoro wa ardhi. Napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza, mwaka 1974 mpaka huu ulikuwa Mto Matandu lakini mwaka 2010 katika marejeo ya mpaka, mpaka huu ulikuwa katika Bwawa la Kihurumila, Kijiji cha Kikulyungu. Napenda kujua ni kwa nini Serikali iliamua kuhamisha mpaka huu kutoka katika Mto Matandu na ukafika katika Bwawa hili la Kihurumila?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili napenda kujua sasa baada ya ziara yake na kujionea mwenyewe, nini sasa Serikali itafanya katika kumaliza mgogoro huu wa mipaka kati ya Serikali kupitia Selous na Serikali ya Wilaya ya Kilwa lakini na mpaka wa Wilaya ya Liwale na Selous?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii kuwashukuru Wabunge wote kwa maombi makubwa ambayo mmekuwa mkiyatoa kwa sababu siku ambapo tulikuwa tutatue hili tatizo ndiyo siku ambayo Mheshimiwa Waziri alipata ajali na hivyo ikalazimika kwamba tukatishe ile ziara na tuende kumhudumia Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaarifu Bunge lako tukufu kwamba Mheshimiwa Waziri jana ametolewa hospitalini na sasa yupo nyumbani, kwa hiyo, tunawashukuru sana kwa maombi yenu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge, kweli kwa muda mrefu amekuwa akilifuatilia tatizo hili na sisi kama Serikali ndiyo maana tuliamua kwamba hili tatizo sasa lifike mahali lifikie mwisho. Naomba nijibu maswali yake mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, si kweli kwamba Serikali ilisogeza mpaka ilitokana tu na tafsiri. Tafsiri ya mpaka iliyoandikwa kwenye GN ya mwaka 1974 ndiyo wataalam walipotafsiri wakaona mpaka unapita wapi. Hata hivyo mwaka 2010 wananchi hawakuridhika ndiyo maana tukaamua kwamba kwa sasa hivi tufanye tena upya kwa kutumia wataalam.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba kutokana na hiyo ziara na maagizo ambayo tulikuwa tumeshayatoa tumeamua kwamba Kamati rasmi kutoka Wizara ya Ardhi iko tayari inapitia mpaka wa Ruangwa na Kilwa ili kurekebisha ile mipaka na baada ya hapo tarehe 18 Septemba wataenda katika Kijiji cha Kikulyungu ambapo wataangalia mpaka wa Kijiji cha Kikulyungu pamoja na mpaka wa Selous. Kwa hiyo, ni imani yangu kwamba baada ya hapo tatizo hili litakuwa limekwisha kwa sababu wananchi wameahidi kushirikiana vizuri kabisa na hiyo Kamati. Naomba tu ushirikiano na Mheshimiwa Mbunge awe na subira.
MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kunipa nafasi. Niipongeze Serikali kwanza kwa kazi nzuri iliyofanyika kwenye mapori ya hifadhi ya wanyamapori Kimisi, Burigi na Biharamlo kwa kuondoa mifugo na sasa hifadhi hizo zimepanda hadhi kuwa National Parks. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna tatizo hususani kwa Maafisa ya Wanyamapori ambao siyo waaminifu ambao sasa wanaenda vijijini na kuswaga mifugo kuingiza kwenye pori la hifadhi kwa lengo la kutengeneza mazingira ya rushwa. Serikali inachukua hatua gani kwa maafisa hawa ambao sio waamini? Hili limetokea Ngara na ushahidi upo. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Gashaza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza na ni kweli kabisa kwamba Serikali imepandisha mapori matano katika eneo lile kuwa sasa ni Hifadhi ya Taifa. Naomba nitumie nafasi hii kumjulisha tu kwamba baada ya kupandisha hayo mapori sasa hakuna shughuli yoyote ya kibinadamu au uwindaji wowote unaoruhusiwa katika maeneo hayo kwa mujibu wa Sheria ya Hifadhi za Taifa. Kwa hiyo naomba tu tuendelee kushirikiana na kuhakikisha kwamba hayo hayatokei.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kwamba wafanyakazi wetu wanakamata mifugo na kuiingiza kwenye hifadhi halafu ndiyo wanaomba rushwa, naomba nitumie fursa hii kusema kwamba kwanza wafanyakazi hawaruhusiwi kufanya hivyo na pale ambapo inabainika wafanyakazi wetu wanakiuka maadili ya kiutumishi basi tunaomba taarifa wananchi watusaidie kututajia kwamba kuna mfanyakazi huyu na huyu anaomba rushwa nasi tutachukua hatua zinazostahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, katika maeneo yote ya mapori nchini hairuhusiwi mifugo wala kilimo kuingia katika maeneo hayo. Kwa hiyo, nitumie nafasi hii kuwaombeni hakuna mwananchi yeyote anayeruhusiwa kuingiza mifugo ikiingizwa itataifishwa na hivyo ndiyo sheria inavyoelekeza. Kwa hiyo, naomba ushirikiano na wananchi wote.
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kuna mgogoro unataka kufukuta katika Jimbo langu kwenye Kata ya Nyatwali inayojumuisha wakazi zaidi ya 11,000. Lile sio Pori la Akiba ni maeneo yao ambayo wanaishi, inasemekana Serikali inataka kuwahamisha haijawashirikisha, hawajui wanaenda wapi na wanalipwa nini. Nini tamko la Serikali kuondoa hili tatizo kwa sababu mna migogoro mingi msitengeneze migogoro mingine na Bunda hatutakubali.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nampongeza kwa jinsi ambavyo anawateea wananchi wake. Niseme tu kwamba mpaka sasa hivi hatuna taarifa rasmi kwamba tunataka kuihamisha hiyo Kata ya Nyatwali. Kwa hiyo, kama kuna fununu za namna hiyo lazima zitazingatia taratibu na sheria zote zilizopo kuhakikisha kwamba wananchi wanashirikishwa kikamilifu na viongozi wote wanashirikishwa ndipo hapo wananchi wanaweza kuhamishwa. Kama wananchi watakuwa waliingia kinyume na taratibu hapo ndiyo lazima nguvu zitatumika lakini kama siyo hivyo nikuhakikishie tu kwamba wananchi watashirikishwa vizuri kabisa ili kuhakikisha kwamba sheria inazingatiwa.
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa vile sasa kuna mgogoro mwingine umeanza kuzuka kati ya wananchi na wanyama waharibifu kama tembo na viboko. Je, Serikali inasaidiaje wananchi ambao wanaishi kando kando ya hifadhi hizi pamoja na ziwa kuepukana na mgogoro huu ambapo sasa tembo wanajeruhi watu na kuharibu mali za watu pamoja na kuuwa watu lakini viboko wanafanya uharibifu mkubwa sana wa mazao ya wananchi. Serikali ina mpango gani sasa kuwasaidia wananchi hawa kuondokana na mgogoro huu?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Raphael Chegeni, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kumekuwa na changamoto ya wanyama wakali na waharibifu katika maeneo mengi nchini lakini Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kuhakikisha kwamba inawaelimisha wananchi ipasavyo kuhakikisha kwamba wanakabiliana na hao wanyamapori pamoja na kuweka maafisa katika kila wilaya kuhakikisha kwamba wanashirikiana na wananchi na wale wa vijiji kuhakikisha kwamba wanawadhibiti hao wanyama wakali na waharibifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia kwa kutumia Kikosi chetu cha Kupambana na Ujangili (KDU) na katika maeneo yale ambayo imeoneka kwamba wanyama wale wamezidi tumekuwa tukichukua hatua za kufungua kituo katika hilo eneo ili kuhakikisha askari wetu wanakuwepo hapo kwa muda mrefu na ili kuwadhibiti hao wanyama wakali na waharibifu. Kwa hiyo, naomba tu tuendelee kushirikiana tuhakikishe kwamba tunapambana na hao wanyama wakali na waharibifu.
MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Wakati katika baadhi ya maeneo kumekuwa na migogoro baina ya Serikali na hayo maeneo ya mbuga za wanyama, lakini kuna maeneo mengi ya utalii kwa mfano maeneo ya kihistoria kama kule Iringa Isimila kuna maeneo yana maporomoko ya maji ambayo pia ni kivutio cha utalii na kuna maeneo yana misitu na ndege wazuri ambapo ni vivutio vya utalii. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuwekeza nguvu kutangaza vivutio hivyo ili walao kupunguza pressure huko kwenye mbuga za wanyama?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa nchi yetu imebahatika kuwa na maeneo mengi ya vivutio vya utalii ikiwemo misitu, malikale, maeneo ya historia na mambo mengine. Hivi sasa Serikali imetengeneza mkakati mkubwa wa kuhakikisha kwamba vivutio vyote vinatangazwa ipasavyo ili kuhakikisha utalii wa ndani na utalii wa nje unaongezeka katika maeneo yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tumechukua hatua kuhakikisha kwamba Mikoa ya Kusini tunapanua utalii ili kupunguza pressure kubwa upande wa Kaskazini. Tunaamini jitihada hizi zitazaa matunda makubwa na kuhakikisha kwamba vivutio vyote vinafahamika na watalii wengi wanaongezeka zaidi nchini.
MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa background information nzuri sana. Kimsingi nioneshe tu masikitiko yangu kwamba ukiangalia muktadha wa swali hili, itoshe tu kusema kwamba bado Mheshimiwa Waziri hakuweza kulitendea haki swali hili.
Mheshimiwa Spika, swali liliuliza; je, ni lini Serikali itafanya marekesho ya bei hizi katika kuimarisha uchumi wa Taifa hili na hususan wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro? Ingekuwa swali linauliza je, Serikali ina mkakati gani? Ndipo jibu lilipaswa kuwa hili. Kwa sababu jibu la Mheshimiwa Naibu Waziri linasema Serikali imejinga kukutana na wadau. Ni kweli, lakini swali lililenga kujua ni lini hasa?
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, ni kweli kwamba moja ya kuinua mapato ya Serikali kupitia kivutio hiki cha Mlima wa Kilimanjaro ni pamoja na kuboresha mpango mkakati wa soko la utalii duniani. Nilipenda Mheshimiwa Naibu Waziri atuambie, je, kupitia uwekezaji wa Shirika la Ndege la Tanzania ni kwa nini Serikali haikuona umuhimu wa kurudisha nembo ya Mlima wa Kilimanjaro katika ndege hizi za Shirika la Ndege ili basi kwa muktadha huo tuweze kuinua soko la utalii kwa nchi ya Tanzania? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nichukue nafasi hii kumpongeza. Najua yeye ni mdau mkubwa sana katika huu mlima na amekuwa akitushauri sana katika masuala mengi. Kuhusu maswali yake yote mawili ambayo ameuliza, suala la kuuliza ni lini? Labda nilitaarifu Bunge lako tukufu kwamba kupitia Kamati ya Kudumu ya Bunge tumeshakutana na wadau mbalimbali katika kuzungumza masuala mbalimbali zikiwemo changamoto pamoja na gharama kubwa ambazo wanatozwa watu mbalimbali wanaopanda Mlima Kilimanjaro. Tumeshakaa tumezungumza, lakini kama Serikali tunataka kujiridhisha. Tunataka tukutane na wadau wengi zaidi kuliko wale wa vyama vyao ili tuone kama kuna haja ya kupunguza au hakuna haja ya kupunguza.
Mheshimiwa Spika, suala la kwamba ni lini? Basi niseme tu kwamba kati ya kipindi cha sasa mpaka mwezi Desemba, hili suala tutakuwa tumeshafikia muafaka kama tupunguze au tuongeze. Kwa hiyo, siyo suala la kupunguza tu.
Mheshimiwa Spika, swali la pili kwamba kulikuwa na nembo kwenye Shirika la Ndege zetu la Kilimanjaro, nadhani tulikuwa na alama kwa ajili kutangaza Mlima wetu Kilimanjaro. Ilikuwemo kwenye nembo hiyo na bado itaendelea kuwemo. Mpaka sasa hivi tumeweka zaidi, lakini siyo tu kutangaza Mlima Kilimanjaro, bali tunaangalia na vivutio vingine vingi ambavo vipo, ndiyo maana ndege zetu sasa hivi tunaweka vitu vingi na alama nyingi zaidi ambazo zinaendelea kulitambulisha Taifa letu. Bado tutakaa na wadau mbalimbali kuona kama kuna haja ya kurudisha ile alama iwepo pale kama alama ya utambulisho. (Makofi)
MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Aaah, ni mimi bwana.
Nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Nakubaliana na Mheshimiwa Waziri kwamba gharama za kupanda Mlima Kenya haziwezi kulingana na Mlima Kilimanjaro kwa sababu ya unique tuliyonayo katika mlima wetu. Tumezungumza na tour guides ambao wanafanya hiyo kazi, wanasema hiyo siyo sababu; sababu ni kuongezeka kwa 18 percent ya VAT katika gharama ambayo inamgusa moja kwa moja mtalii.
Je, Serikali lini sasa itakaa kuona kwamba hili ni tatizo na kuonda 18 percent kwa wageni wanaokuja ili waje kwa wingi na tukusanye kwa wingi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, ni kweli kabisa kwamba Serikali ilianzisha VAT katika huduma mbalimbali za kitalii ambazo zinatolewa, ni karibu takribani miaka miwili sasa imepita toka kuanzishwa kwa VAT.
Mheshimiwa Spika, sasa hivi tuliagizwa tufanye utafiti mpana zaidi tuone kama kweli hii VAT imeleta athari. Sasa katika kipindi kifupi ni vigumu sana kuweza kujua kama VAT imeleta athari au haijaleta athari. Kwa hiyo, sasa hivi ambacho tunakifanya, tunataka tufanye study kubwa, lakini pia tuone ni maeneo gani ambayo tunaweza kuyatumia ambayo tunaweza kupanua wigo wa kupata mapato mengi zaidi badala ya kutegemea tu suala la VAT.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hili tutalifanyia kazi na tunaomba tuendelee kupata maoni zaidi na mawazo namna ya kuboresha huduma zetu hizi za utalii.
MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali madogo mawili ya nyongeza pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, tofauti ya majibu haya kwamba kuna asilimia 60 na 70 na kuna asilimia 30, wadau hawa wanapita katika njia moja na wanachukua vibali sehemu moja na wakaguzi wa vizuia, wanakagua bila kujua huyu katoka kwenye mashine ya kisasa au mashine ya kizamani. Kwa mpango huo, inamaanisha kwamba kuna mwanya mkubwa sana wa rushwa, kuna mtu atatoka na asilimia 60 na mwingine asilimia 30. Je, sasa Serikali inakuja na mkakati gani uliobora kabisa kuepusha watumishi ambao sio waaminifu kufanya kazi ambayo imenyooka kwa dhamira iliyopo sasa ya Awamu hii ya Tano kwamba tunataka wananchi watendewe haki?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni lini sasa Serikali itaona njia bora zaidi ya kusaidia wadau hawa wajasiriamali, wale ambao wana mashine za kizamani waweze kuwezeshwa na kupata mashine hizi za kisasa ili kuondoa mkanganyiko huu ambao unasababisha mwanya mkubwa wa rushwa?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Omary Massare, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza kwa sababu yeye ni mdau mkubwa sana wa mazao yatokanayo na misitu na kwa kweli amekuwa akifanya kazi nzuri sana na amekuwa mshauri mzuri sana katika masuaa mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mkakati ambao Wizara imeweka, Serikali kwa kweli imeweka mkakati mkubwa wa kuhakikisha tunawahamasisha wananchi wote wahakikishe wanapata teknolojia za kisasa, mashine ambazo ni bora kwa sababu hizi mashine zingine kwa kweli zinafanya upotevu mkubwa sana na hasara ni kubwa. Katika suala hilo ndiyo maana tumeweka mkazo kwamba wale wote ambao wanakuwa na zile mashine ambazo zinapoteza sana kwa kweli hawaruhusiwi. Pale ambapo itabainika kwamba baadhi ya watumishi wetu katika maeneo kadhaa wanaruhusu hizo mashine zitumike kwa rushwa basi tunaomba mtusaidie kututajia majina ili hatua kali ziweze kuchukuliwa kwa watumishi wa aina hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu namna ya kuwasaidia Watanzania hawa, kwa kweli ziko njia nyingi za kuwasaidia Watanzania lakini nitumie nafasi hii kuwahamasisha kwamba wajaribu kutafuta mikopo ya aina mbalimbali. Kuna aina nyingi za mikopo sasa hivi, kuna ile mikopo inayotolewa na Halmashauri, kuna mifuko mingi inatoa mikopo basi wachukue mikopo ili waweze kupata mashine ambazo ni bora ambazo zitawafanya wapate mazao mengi zaidi kuliko mashine ambazo ziko hivi sasa. (Makofi)
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kumekuwa na kauli ya Serikali kwamba kila Halmashauri wapande miti 1,500,000 kwa ajili ya kuhifadhi mazingira yetu. Nafahamu Wizara hii, Wizara ya TAMISEMI pamoja na Mazingira wanahusika na hawa wana mbegu za miti mbalimbali. Kwa nini msione umuhimu wa kutoa miti katika Halmashauri zetu hiyo 1,500,000 ili tuipande na kuhifadhi mazingira kwa sababu mkitegemea Halmashauri watoe fedha, wanunue hiyo miti Halmashauri zetu hazina fedha, kwa nini msitupe hiyo miti 1,500,000 tupande?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Pauline Gekul, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa ni sera ya Serikali kuhakikisha kwamba Halmashauri zote nchini zinapanda miti angalau kila Halmashauri 1,500,000 lakini kumekuwa na upungufu wa miche ya kupanda. Hivi sasa kama Serikali tumechukua hatua kwa kutumia Wakala wetu wa Misitu kuhakikisha kwamba wanashirikiana na Halmashauri kwanza kwa kuwapatia mengi lakini katika maeneo mengi kuwapa miche ile ambayo tayari tumeshaiotesha ili kusudi zile Halmashauri ziende kufanya kazi ile ya kupanda katika maeneo mbalimbali. Siyo tu suala la kupanda lakini baada ya kupanda pia Halmashauri zihakikishe kwamba zinailinda ile miti na kuhakikisha kwamba kweli inakua sio tu inapandwa halafu inaachwa.
MHE. YUSSUF HUSSEIN SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, kidogo nimeguswa hapa. Huyu papa ni papa mmoja na hadhuru mwanadamu na mara nyingi kwa kule kwetu sisi huwa mwezi Desemba wanatoka Somalia wanakuja zao mpaka wanakuja kupiga kambi Minai – Zanzibar wanakuwa kwa wingi sana na huyu papa huwa anawafuata wale dolphins. Mara nyingi huwa anawafuata wale dolphins, swali langu kwa Mheshimiwa Waziri, kipindi cha Desemba mpaka Februari wanakuja na kurudi ni kipindi ambacho tunaweza tukafanya utalii mkubwa sana katika eneo letu la kuanzia mpakani na Kenya Duga mpaka Zanzibar. Je, Wizara yako imejipangaje sasa kutumia fursa hii ambayo wale dolphins na huyu papa wanatangaza nchi yetu wenyewe, sisi tutumie tu hiyo fursa. Lini tutatumia hiyo fursa ya kujenga hoteli katika ukanda huo. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba katika kipindi hiki hawa potwe wanakuwa wengi sana katika maeneo haya au wanakuja katika maeneo haya. Pia kuna vivutio vingi sana ambavyo vipo katika ukanda wa bahari yetu hasa katika fukwe zetu hizi za bahari ambazo tunaweza tukafanya na ndiyo maana Serikali sasa hivi iko mbioni katika kuhakikisha kwamba tunaanzisha mamlaka ya kusimamia fukwe zote za bahari kusudi tuweze kufaidika na huu utalii wa baharini ambao tulikuwa hatujautumia kwa muda mrefu sana. Kwa hiyo, naamini katika hizi jitihada, pale ambapo zitakuwa zimekamilika na sheria itakapokuwa imeletwa hapa Bungeni basi hizi jitihada zitakuwa zimekwenda sambamba na hilo wazo la Mheshimiwa Mbunge. Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)
MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali madogo ya nyongeza kama yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, buffer zone inayozungumziwa hapa katika Bonde la Kilombero ni pana sana, linaanzia kilometa tatu mpaka 12. Mheshimiwa Rais aliahidi angalau kuwasaidia wananchi hawa kipande kidogo tu cha hii buffer zone.
Mheshimiwa Mwenyekiti, zoezi hili la uwekaji wa mipaka limeshakamilika kwa Wilaya ya Malinyi lakini bado kuna malalamiko mengi yamejitokeza na busara alizotumia Mheshimiwa Waziri wa Maliasili, ameunda tume lakini hata hiyo tume haiwashirikishi kabisa wananchi.
Swali langu, kwa nini sasa Serikali wasione busara kuanzisha upya tena mipaka hiyo kama walivyoanza mwaka 2016 kwa dhana ya kuwashirikisha wananchi kwa kikamilifu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi hawa sasa wanatoka kule kwenye buffer zone wanarudi kwenye ardhi ya vijiji, ardhi ya vijiji ndiyo vyanzo vya mito ambayo inatiririsha maji kwenye Mto Kilombero.
Sasa, je, Serikali ina mpango gani mahusus (commitment) kupitia taasisi zake za TAWA au TANAPA kuwezesha Wilaya ya Malinyi kutengeneza schemes za umwagiliaji kwa ajili ya kilimo na mifugo katika eneo hili ili kuendeleza ustawi wa hilo Bonde la Kilombero? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kumshukuru na kumpongeza kwa jinsia ambavyo amekuwa akilifuatilia hili suala na ambavyo amekuwa akishirikiana na Serikali katika kutafuta ufumbuzi wa tatizo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ushirikishwaji wa wananchi ni suala pana na ni suala ambalo pengine bado linahitaji ufafanuzi; lakini tuna lengo kubwa kwamba lazima wananchi wote wa maeneo yote kwenye migogoro washirikishwe kikamilifu kupitia wananchi, viongozi wao, Serikali kwa ujumla na wadau wengine wote lazima washirikishwe na hilo ndiyo tumekuwa tukilifanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitatoa mfano, katika Wilaya ya Malinyi wakati tunaweka mipaka tulifanya vikao 27 na wananchi wakaelimishwa kwa nini tunahitaji kuhifadhi eneo lile na kwa nini lazima kuwe na buffer zone. Katika hivyo vikao tukafanya mikutano 12 na wananchi na katika hao wananchi walioshiriki katika hilo walikuwa ni 1,382; kwa hiyo, kwa ujumla walishirikishwa kwa mapana na marefu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kama kuna upungufu, namuomba Mheshimiwa Mbunge basi tutakaa tena tuangalie kama kunahitaji ushirikishwaji wa zaidi ya hapo basi tutafanya kama alivyoomba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la scheme ya umwagiliaji; ni kweli kabisa kwamba kumekuwa na matumizi mabaya ya maji katika eneo lote zima katika Ramsar Sites.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tunataka tuhakikishe kwamba lazima kuwe na matumizi endelevu ya maji katika lile bonde kwa sababu pale ndipo vyanzo vya maji ya Mto Kilombero ambao ndiyo utaenda kuzalisha umeme mkubwa kule Stiegler’s Gorge, kwa hiyo, lazima tuhifadhi vizuri na tuhakikishe kwamba wananchi wanaelimishwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutekeleza hilo basi tutashirikiana na wananchi, Serikali, Wizara ya Maji na Umwagiliaji na Wizara ya Kilimo na kuona ni aina gani ya scheme zianzishwe katika maeneo yale ya juu kusudi wananchi wale waweze kunufaika na ule mradi. Zaidi ya hapo tutashirikiana pia na Bodi ya Bonde la Mto Rufiji ambayo ipo kule kwa ajili ya kuhamasisha na kuhakikisha kwamba wananchi hawaharibu vile vyanzo vya maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo ninaamini wananchi watafaidika na huu mpango wa scheme ambao Mheshimiwa Mbunge anapendekeza.
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize maswali ya nyongeza. Kwanza kabisa nianze kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri ambayo amenipatia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa Serikali imefungua mradi wa REGROW ambao utafanya kazi ya kukuza utalii wa ukanda wa Kusini ukiwemo Mkoa wa Iringa; je, Serikali ina mkakati gani wa kujengea uwezo wananchi waliopo katika mkoa wetu ili watumie vizuri fursa hiyo kujiajiri na kuweza kujipatia kipato? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa nje ya maeneo ya utalii kuna historia kubwa za machifu akiwemo Mtwa Mkwawa, lakini kuna Kituo cha Kalenga, eneo la Mlambati ambapo Mwalimu Nyerere aliweka jiwe la msingi mwaka 1998 kama ukumbusho wa miaka mia moja.
Je, ni lini Serikali itachukua ya kuyaboresha kwa ajili ya kuvutia watalii na kuhakikisha kwamba pesa inayopatikana katika maeneo hayo, inawasaidia wananchi wanaozunguka eneo hilo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, kabla sijajibu haya maswali nichukue nafasi hii kwanza kumpongeza kwa jinsi ambavyo amesimama imara katika kuupigania Mkoa wa Iringa, lakini pia alipigania sana kuhakikisha kwamba Kituo cha Utalii kinajengwa pale Kihesa, Kilolo. Kwa kweli nampongeza sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maswali yake ameuliza; je, tuna utaratibu gani wa kuhakikisha tunawajengea uwezo? Naomba nichukue nafasi hii kusema kwamba katika mradi mkubwa ambao tunaenda kuutekeleza Mikoa ya Kusini unaohusu hifadhi nne yaani Udzungwa, Mikumi, Ruaha pamoja na Selous ya Kaskazini, tuna utaratibu wa kuimarisha miundombinu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili wananchi wa Mkoa wa Iringa waweze kufaidika na huu mradi, ni lazima wajengewe uwezo ili waelewe umuhimu wa kuuendeleza utalii na wawe tayari kuwakarimu watalii watakaokuwa wanatembelea katika Mkoa wa Iringa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hivi sasa tuna mpango kabambe wa kuhakikisha kwamba, kwanza tunawaelimisha namna ya kuanzisha makampuni ya kitalii ya kuongoza watalii, lakini pili, namna watakavyowakarimu pamoja na kuwaonyesha mambo mbalimbali ambayo yapo katika Mkoa wa Iringa ukiwemo utamaduni wa Iringa na tatu, ni pamoja na kuwapokea na kuwakarimu katika hoteli mbalimbali. Kwa hiyo, hii mipango yote tutaitekeleza katika mwaka wa fedha huu unaoanza Julai. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu kile Kituo cha Kalenga, kama alivyosema kweli kabisa miundombinu bado haitoshelezi. Hivi sasa tuna mpango kabambe wa kuhakikisha barabara ya lami inajengwa kutoka Iringa hadi kwenye lango kuu la Ruaha. Wakati tutakapokuwa tunajenga ile barabara, tutaangalia uwezekano wa kuimarisha ile miundombinu, kuchepusha pale kupeleka katika hiki Kituo cha Kalenga kwa sababu ni karibu ili tuhakikishe kwamba nako panafikika kiurahisi. (Makofi)
MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa niweze kuuliza swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa Mkoa wa Mbeya una vivutio vya asili kama ulivyo Mkoa wa Iringa na vivutio hivyo vya asili ni kama Mlima Rungwe, Mlima Kejo, Ziwa Nyasa na maeneo mengine kama Maziwa ya Masoko, Kingururu, Iramba pamoja na Daraja la Mungu.
Je, Serikali ina mpango gani kuvitangaza vivutio hivi ili wananchi wanaoishi maeneo hayo waone umuhimu wa uwepo wa vivutio hivyo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kweli kabisa Mkoa wa Mbeya una vivutio vingi sana kama ulivyo Mkoa wa Iringa na kama ilivyo mikoa mingi. Hivi sasa kama nilivyosema, tunayo mikakati kabambe ya kuhakikisha kwamba vivutio vyote nchi nzima vinatangazwa. Nimesema tutaanzisha studio ya kutangaza na tutaanzisha channel ya utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, katika mikakati hii, maeneo yote yenye vivutio vya utalii Mkoa wa Mbeya nayo yataingizwa katika huo mpango kabambe wa kutangaza ili kusudi watalii mbalimbali waweze kujua Tanzania na Mkoa wa Mbeya kuna nini? Nina uhakika Mheshimiwa Mbunge atafaidika sana hasa baada ya kuanza kutangaza maeneo haya. (Makofi)
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.
Kwa kuwa Mkoa wa Mtwara una vituo vingi sana vya kitalii, kwa mfano, ile beach ya Msimbati ambayo inaweza kuendesha gari, kuna Shimo la Mungu kule Newala, lakini vilevile Newala kuna Kituo cha Utamaduni wa Kimakonde na Mji maarufu wa asili Mikindani.
Je, Serikali ina mpango gani maalum wa kutangaza vivutio hivi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa katika sehemu za Newala pamoja na Mikindani na maeneo mengine ya Mtwara yana vivutio vingi vya asili, maliasili na vitu vingi kwa kweli, hivi sasa naomba niseme tu kwamba tumechukua jitihada za kuhakikisha tunatangaza vyote kwa kushirikiana na Halmashauri zilizopo katika Mkoa wa Mtwara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutatangaza maeneo yote hayo na Mji wa Mikindani tutahakikisha kwamba tunautangaza ipasavyo kwa sababu una historia ndefu na nzuri ambayo nina uhakika watalii wengi watavutiwa kwenda kutembelea katika hilo eneo. (Makofi)
MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa Mikoa ya Singida, Simiyu, Tabora na Shinyanga pia ina vivutio vyake; ukienda utakutana na akina Mtemi Chenge, Chifu Mayenga, Mtemi Gerege na wengine wengi.
Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kutembea mikoa hiyo ili tumwonyeshe vivutio hivyo aweze kuviingiza kwenye ramani ya utalii kwenye mikoa hiyo? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa katika mikoa yote aliyoitaja ina vitu vingi na ina historia ndefu ya utamaduni wa Mtanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie kwamba nipo tayari wakati wowote kuongozana kwenda kutembelea mikoa hiyo na nitaomba wakati naenda tuongozane naye ili kusudi aweze kunionesha maeneo yote hayo na Serikali iweze kuyachukua na kuyatangaza ipasavyo. (Makofi)
MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi.
Kwa kuwa Jiji la Dar es Salaam lina vivutio vingi vya utalii kama vile Daraja la Kigamboni, Hospitali ya Ocean Road, Uwanja wa Uhuru, Magomeni pale kuna Nyumba ya Mwalimu Nyerere, Karimjee Hall na Makumbusho ya Taifa. (Makofi)
Je, Serikali imejipanga vipi katika kulisaidia Jiji la Dar es Salaam ambao wameanza zoezi hilo la kutangaza vivutio vya utalii kulipa nguvu ili waweze kufanya vizuri zaidi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa Dar es Salaam nayo ni miongoni mwa mikoa ambayo ina vivutio vingi vya utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua hilo, ndiyo maana tulianza na mkakati wa kuhakikisha kwamba Dar es Salaam inatangazwa na tunaanzisha vituo vya utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshirikiana na Mkoa kuhakikisha kwamba tunaanzisha basi maalum ambalo litakuwa linatembelea vituo vyote, kuanzia pale Makumbusho, Magomeni na maeneo mengine yote aliyoyataja kwamba yanatangazwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi, tutaendeleza hizi jitihada ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba lile daraja letu la Kigamboni sasa linatumika kama mojawapo ya kivutio cha utalii. (Makofi)
MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Moshi Vijijini Kata ya Mbokomu, tumekuwa tukizungumza mara nyingi kwamba kuna mti mkubwa sana ambao ni kivutio cha utalii pale; lakini Serikali haijachukua jitihada zozote kwenda kuutangaza mti ule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa napenda kujua Mheshimiwa Waziri ana mkakati gani wa kuhakikisha wanautangaza mti ule uwe ni moja ya kivutio cha utalii katika Mkoa wa Kilimanjaro?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli nilikuwa sina taarifa kama kuna mti mkubwa wa namna hiyo, lakini naamini kabisa kama kuna mti mkubwa wa namna hiyo, basi itakuwa ni kivutio kizuri sana cha utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tutachukua hatua za kuhakikisha kwamba kwanza nautembelea, lakini la pili, tuweze kuutangaza kusudi wananchi waweze kujua kwamba kuna mti mkubwa ambao ni kivutio kizuri sana katika Mkoa wa Kilimanjaro na katika eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ambalo naomba niliseme, nchi ya Tanzania ni nchi tajiri sana ambayo ina vivutio vingi sana. Tukiwekeza, tutaweza kuivusha nchi hii na tutaweza kuisogeza mbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tushirikiane Wabunge wote kuhakikisha vivutio vyote tunavitangaza kwa pamoja ikiwemo…
kwenye Instagram na Facebook mlizonazo muweke picha cha utalii. (Makofi)
MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya mipaka kati ya Vijiji vya Kata ya Buger na TANAPA, pia Vijiji vya Lositete, Upper kitete, Silahamo na Endamagang na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imekuwa migogoro ya muda mrefu ambayo haipati utatuzi.
Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari baada ya Bunge hili kuja Karatu ili kuongoza majadiliano ya kumaliza mgogoro huo?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba katika lile eneo kuna baadhi ya migogoro ambayo imejitokeza na imekuwepo kwa muda mrefu, ninaomba niseme tu kwamba niko tayari pale ambapo tutapanga ratiba vizuri mimi na wewe tuende tukaangalie, tukawasikilize wananchi ili tuone ni namna gani tunaweza kutatua hiyo migogoro iliyopo.
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, urithi mkubwa wa Taifa letu unapotea. Ngoma zetu zinapotea, lugha zetu za asili zinapotea, vyakula vyetu vinapotea. Wewe ni Chifu, unafahamu hazina kubwa ambayo Machifu walikuwa nayo, mavazi yao, vyombo vyao vya nyumbani, samani zao na vyote hivi vinaweza vikavutia utalii kwa kiwango kikubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ni kwa nini usiwepo mkakati wa kila Halmashauri au kila Wilaya kujenga jumba la makumbusho na kwa sababu hiyo Viongozi wa Halmashauri na Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa kuhamasisha wananchi ili vitu vyote vya asili vikakusanywa, kwanza kwa ajili ya elimu ya watoto wetu, lakini kwa ajili pia ya kuvutia utalii ikiwa ni pamoja na kuleta mashindano ya ngoma za asili ambazo zina mafunzo mengi sana kwa Taifa letu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Roman Selasini, Mbunge mzuri sana ambaye amekuwa akifuatilia sana mambo ya utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli niseme tu kwamba kama ulivyosema ni kweli kabisa tunayo mikakati mingi ambayo tunataka kuitekeleza. Lakini kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson, kwa utaratibu wake aliyoanzisha wa kuhakikisha kwamba anashindanisha ngoma za asili, na hili ndilo tunalolitaka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na sisi katika mkakati wa kuhakikisha kwamba hili tunalitekeleza, tumeamua kwamba mwezi wa Septemba kila mwaka, nchi ya Tanzania Mikoa yote, Halmashauri zote, zitakuwa zinasherehekea Mwezi wa Urithi wa Utamaduni wetu. Kwa hiyo, ngoma mbalimbali zitashiriki katika Kanda, katika Mikoa, kuhakikisha Watanzania wanakumbuka utamaduni wao. Nami ninaamini kabisa tukitekeleza hili kwa pamoja basi vitu vyote vile, mali kale zote zitaweza kubainishwa na kuweza kuelimishwa na wananchi wote wataweza kuvibaini vizuri kabisa. (Makofi)
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa; Serikali imetoa matangazo na kuweka vibao kuhalalisha masoko ya mazao ya misitu maeneo ambayo hakuna mashamba ya misitu, wakijua kabisa kwamba misitu inayovunwa wale wavunaji wanavuna visivyo halali. Kwa mfano, ukitoka Dodoma ukiwa unaelekea Morogoro kuna vibao kwamba kuna masoko halali, lakini wale watu kule hakuna mashamba ya misitu, wanavuna kwenye maeneo ambayo siyo halali na hawana namna nyingine, hawajaelimishwa namna gani wapande misitu ili wavune mazao ya misitu kwenye maeneo ambayo yamepandwa. Je, Serikali haioni kwamba, kuweka masoko ya mazao ya misitu maeneo ambayo hakuna mashamba ya misitu ni kuhalalisha kuendelea kuhakikisha kwamba misitu iliyopo ya asili inateketea?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la la pili; kwa kuwa kwenye majibu ya msingi Mheshimiwa Waziri anasema kwamba misitu imepandwa. Kuna baadhi ya misitu ya uoto wa asili imepandwa lakini tumeshuhudia kazi wanayofanya Maafisa Misitu maeneo yetu, ikiwepo Kaliua ni kupiga mihuri magogo, kupiga mihuri mbao na kutoa vibali kwa ajili ya uvunaji usio halali kiasi kwamba speed ya kuvuna misitu baada ya kuwepo kwa TFS imeongezeka tofauti ya ilivyokuwa mwanzoni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nauliza, je, Serikali haioni kwamba kuna sababu ya kukaa na Maafisa wao wa Misitu ili sasa waanze kazi ya uhakika ya kurejesha uoto wa asili ikiwepo maeneo mbalimbali kwa sababu Kaliua kuna misitu mingi lakini hakujapandwa mti hata mmoja kuhakikisha kwamba tunarejesha uoto wa asili maeneo ambayo yameharibika? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, naomba nikiri kabisa kwamba kweli kumekuwa na matumizi mabaya ya misitu yetu katika maeneo mengi na vituo vingi vipo katika maeneo ambayo kwa kweli hakuna misitu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kuwepo kwa sehemu ya kituo hata kama hakuna msitu siyo tatizo, tatizo ni kwamba ule mkaa unaouzwa katika lile eneo je, una kibali na umepatikana katika taratibu zilizowekwa. Kama haujapatikana kwa mujibu wa utaratibu hilo ndilo linakuwa tatizo kubwa lakini kama vibali vipo na mkaa umesafirishwa kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine maadam una vibali hilo linakuwa siyo tatizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hilo tutaendelea kulifuatilia pale ambapo watu wanafungua vituo wanaweka masoko bila vibali maalum Serikali itachukua hatua zile zinazostahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuhusu hawa Maafisa Misitu ambao wapo maeneo mengi na wamekuwa hawatekelezi labda majukumu yao sawasawa na kama ulivyosema wamekuwa labda wanagonga mihuri tu zile mbao, kwa kweli naomba nitumie nafasi hii kuwaagiza Maafisa Misitu wote kuhakikisha wanasimamia hifadhi zetu zote zilizoko katika maeneo yao, mihuri inayotakiwa kutolewa ni pale ambapo wale wavunaji wamevuna katika ile misitu wanayoisimamia, kwa mujibu wa taratibu kwa mujibu wa sheria na kanuni tulizojiwekea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo wakiwa wamefuata hizo taratibu na wakigonga haina shida, shida inakuwa pale wanapopita njiani humu halafu wanagonga hiyo mihuri wakati wao wenyewe hawajui hizo mbao zimetoka sehemu gani. Kwa hiyo, Serikali itaendelea kuchukua hatua zinazostahili, kwa wale ambao watakuwa wanakiuka hizi taratibu ili kusudi hifadhi zetu ziendelee kuwepo hapa nchini. (Makofi)
MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa hii na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa, katika Mkoa wa Tabora kumekuwa na kero kubwa ya kuwapiga, kuwanyang’anya baiskeli zao, kuwajeruhi, kuwanyang’anya simu zao na pesa walizonazo mfukoni wanaobeba mkaa kutoa vijijini kuleta mjini. Je, Mheshimiwa Waziri ni haki mtu anapofanya kosa kuchukuliwa hatua kupigwa hapo hapo bila kupelekwa kwenye vyombo vya sheria? (Makofi)
NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kumekuwa na changamoto hizo, katika maeneo mengi nchini, watu wamekuwa wakinunua mkaa na wamekuwa wakisafirisha kwa baiskeli, wamekuwa wakisafirisha kwenye bodaboda na vyombo vingine ambavyo kwa mujibu wa sheria za usalama barabarani haviruhusiwi kufanya hivyo. Pale ambapo wanakuwa wamekiuka hizo taratibu wanatakiwa wakamatwe, wapelekwe katika vituo, wapelekwe katika mikondo ya sheria siyo kuwapiga. Wale ambao wanaowapiga wananchi bila ya kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria, ni ukiukaji wa taratibu na ukiukaji wa sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwaombe watendaji wote kokote waliko nchini wahakikishe wanazingatia sheria na kanuni na miongozo iliyopo na wahakikishe wanawatendea haki wananchi ili kusudi wasinyanyaswe na kupigwa. (Makofi)
MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimwombe Mheshimiwa Waziri kwenye swali langu la (a) amejibu kitu tofauti kabisa na swali ambavyo nilivyoliuliza. Pamoja na hayo, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; hivi karibuni tumemwona Mheshimiwa Rais wetu akitoa maelekezo kwenye Wizara hii ya Maliasili kugawa baadhi ya maeneo ya Hifadhi kwa ajili ya wakulima na wafugaji, kwa mfano Kagera Nkanda, Mheshimiwa Rais alitoa maelekezo kwa wananchi wa Kagera Nkanda, Wilaya ya Kasulu wapewe eneo ndani ya hifadhi kwa ajili ya kulima na kufuga. Kwa nini sasa Mheshimiwa Waziri asitoe maelekezo yale yale yaliyotumika kuwagawia wananchi wa Kagera Nkanda awagawie sasa na wananchi wanaouzunguka maeneo ya Pakunda, Pachambi na maeneo ya Ipuguru?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; kwa kuwa tunafahamu kwamba utaratibu wa uwekaji wa vigingi unatakiwa ufuate sheria. Kijiji cha Kalilani na Kijiji cha Sigwesa kimesajiliwa kwa mujibu wa sheria. Je, Mheshimiwa Waziri akija akigundua kwamba GN hivi vigingi vilivyowekwa kwenye Kijiji cha Kalilani na Kijiji cha Sigwesa hakikufuata taratibu atakuwa yuko tayari kuondosha vile vigingi na kuviweka nyuma ili kupunguza migogoro iliyopo baina ya Vijiji vya Sigwesa na kijiji cha Kalilani? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza kwa jinsi ambavyo ameeleza, inawezekana kweli labda maeneo mengine majibu tuliyoyatoa hayajafikia, hayajawa katika kile kiwango alichokusudia, nimuahidi tu kwamba mimi nitapata nafasi ya kwenda kutembelea katika eneo hilo, ili niende kutembelea kijiji hadi kijiji na kitongoji hadi kitongoji kusudi tuweze kubaini kama kweli kuna upungufu wa namna hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuwagawia maeneo ya hifadhi naomba nimshauri Mheshimiwa Mbunge kwamba kwanza utaratibu wa kugawa hifadhi kwa sasa jinsi ulivyo, kwa kweli kuna kazi kubwa sana. Hata hivyo, kama pale ikionekana kweli wananchi wa Jimbo husika wana matatizo ya ardhi na hawana mahali pa kulima, hawana mahali pa kufugia mifugo yao na mambo mengine, basi namuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri aangalie, afanye mchakato na awasiliane na Wizara ya Maliasili na Utalii ili tuangalie katika yale maeneo ambayo yanahifadhiwa chini ya Serikali za Vijiji, kama yanaweza yakamegwa na wananchi wakaweza kupatiwa hilo eneo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, kuhusu kuondoa vigingi pale ambapo itaonekana kuna makosa. Tuko tayari kabisa pale ambapo itaonekana vigingi vimewekwa katika maeneo ambayo siyo sahihi, tuko tayari kabisa kwamba tutaviondoa na tutaviweka katika maeneo ambayo yanastahili pale ambapo mipaka kisheria inatakiwa kuwekwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua kuna matatizo hayo Nchi nzima, na ndiyo maana tuliahidi mbele ya Bunge hili tutakwenda kila eneo kuhakikisha kwamba vigingi vinawekwa katika maeneo yale yanayotakiwa. (Makofi)
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa muda mrefu sana katika Wilaya ya Kasulu, eneo la Kagera Nkanda wananchi walikuwa wakizuiliwa kulima. Mwaka jana tarehe 21 Mheshimiwa Rais alipokuja Wilaya ya Kasulu wananchi walimpokea kwa nderemo na vigelegele akawaruhusu kwenda kulima katika pori la Kagera Nkanda, lakini hivi sasa ninavyoongea tarehe 21 mwezi huu, wananchi wameambiwa waondoe mazao katika eneo hilo la Kagera Nkanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kauli ya Serikali, ni kwa nini wananchi waliruhusiwa na Mheshimiwa Rais kulima katika eneo hilo na leo wanaondolewa kwa kutaka kupigwa ndani ya wiki moja? Naomba kauli ya Serikali. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Mheshimiwa Rais alitoa maagizo kwamba lile eneo ligawiwe kwa wananchi ili waweze kulitumia katika shughuli zingine za kibinadamu za uzalishaji. Naomba nimhakikishie tu kwamba agizo la Mheshimiwa Rais alilolitoa linatekelezeka na lazima liheshimike, kama kuna mtu analikiuka hilo tutashughulika nae. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa ambacho kinatakiwa sasa hivi kufanyika ni kuhakikisha kwamba baada ya Rais kutoa lile eneo, taratibu za kisheria ya kuondoa na kuweka mipaka mipya lazima zifanyike. Kwa hiyo, wale Watendaji ambacho tunakifanya sasa hivi ni kuhakikisha kwamba sasa tunarekebisha ile mipaka, ili kusudi yale maeneo yaliyogawiwa kwa wananchi yabaki kwa wananchi na yale mengine ambayo yanatakiwa kubaki kama hifadhi yaendelee kubaki kama hifadhi.
MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tatizo lililoko Kigoma Kusini linafanana kabisa na tatizo lililoko kwenye Jimbo la Ndanda hasa maeneo ya Namajani na Mahinga ambako mipaka kati ya Jeshi la Magereza pamoja na wananchi haieleweki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna tatizo kama hilo kwenye Kata ya Chingulungulu, Kijiji cha Misenjesi kati ya Hifadhi ya Taifa pamoja na wananchi. Sasa nataka kufahamu, ni lini Serikali itakwenda kutoa ufafanuzi mzuri na kuweka mipaka hii sahihi kati ya Mbuga ya Misenjesi na wanakijiji wa Kijiji cha Chingulungulu kwa sababu pametokea matatizo makubwa ya kutoelewana maeneo hayo? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kama nilivyosema kwenye nchi nzima kuna maeneo ambayo yana matatizo ya mipaka na kama alivyosema mwenyewe kwenye Jimbo lake kuna maeneo hayo. Nataka nimhakikishie tu kwamba, tuko tayari sasa hivi, tunapitia mipaka yote nchi nzima na tutakwenda huko pia kuangalia huo mpaka ili tuone kwamba ni nani ameingia nani hajaingia kusudi tuweze kurekebisha matatizo hayo na migogoro yote iweze kumalizika, hiyo tutaifanya karibu nchi nzima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Mbunge awe na uvumilivu kidogo, baadaye tatizo lake hilo litamalizika. (Makofi)
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa majibu haya inaonesha kabisa dhahiri kwamba Mheshimiwa Waziri amedanganywa na uhalisia wa wananchi wa Jimbo la Mpanda Vijijini, kutokana na swali hili kwa sababu imekuwa ni mara ya tatu nauliza swali hili, lakini pia Serikali imeshindwa kutatua migogoro pamoja na mauaji yanayoendelea katika kata hizi, Kata ya Kapalamsenga, Ikola, Isengule, Iteteme pamoja na Kalema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vijiji hivi wananchi wamekuwa wanateswa na askari wa Wanyamapori na mwaka jana wamekufa zaidi ya vijana wawili kwa kupigwa risasi na askari wa wanyamapori. Ni nini tamko la Serikali kutokana na vifo na manyanyaso yanayoendelea katika Jimbo hili la Mpanda Vijijini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika majibu haya ndiyo maana nikasema kwamba Mheshimiwa Waziri, amedanganywa. Hakuna ushirikishwaji wowote kati ya Vijiji, Vitongoji pamoja na wananchi. Ni kwa nini Serikali inatumia nguvu wakati wananchi wanatakiwa wapewe elimu, washirikishwe kuliko kulazimishwa kupeleka hizo GN kwenye maeneo ambayo vijiji hawajapewa ramani husika kujua na kutambua mipaka yao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme tu kwamba siyo azma ya Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wake wanateswa, hiyo haturuhusu. Haturuhusu kabisa, lakini pale ambapo wananchi wale ambao wanaenda kuingia katika maeneo ya hifadhi bila kufuata taratibu, hatua za kisheria lazima zichukuliwe. Kuchukuliwa siyo kuwatesa wala kuwapiga, lazima wanakamatwa wanapelekwa katika mikondo ya sheria na hapo wanashitakiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kwenye maeneo ya Mheshimiwa kuna tatizo la namna hiyo, basi nitaomba tuwasiliane baadae ili unipe baadhi ya watu ambao wamepata matatizo hayo, kusudi tuweze kuwachukulia hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wote tunafahamu tunapoenda katika mipango ya matumizi bora ya ardhi hasa katika vijiji lazima mipango iwe shirikishi kwa sababu wanaotakiwa kupanga ni wananchi wenyewe wote wanahusika, sasa akiniambia kwamba wananchi hawakushirikishwa kwa kweli nashindwa kuelewa. Huo mpango lazima upitishwe na mkutano wa Kijiji. Sasa ulipitishwaje kama wananchi hawakushirikishwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama kuna changamoto hizo, basi nitakapokwenda katika hilo eneo basi tukae wote kama Serikali pamoja na wananchi tuone kama kweli hawakushirikishwa au kuna tatizo lingine la mahitaji ya ardhi. (Makofi)
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Migogoro kati ya hifadhi zetu na wananchi itaendelea kwa muda, kwa sababu wananchi wanaongezeka, wanyama wanaongezeka, ardhi iko pale pale. Wanyama hawawezi kufanya uzazi wa mpango, lakini sisi tunaweza. Je, ni lini Serikali yetu itakuja na sera na mpango kabambe wa uzazi wa mpango kwa wanadamu ili tuweze kudhibiti ongezeko hili la watu ambalo linaweza likaathiri hata shughuli nyingine za kiuchumi kama afya, elimu na kadhalika? (Kicheko)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba idadi ya wananchi imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Wakati tunapata uhuru mwaka 1961 idadi ya Watanzania walikuwa ni milioni 10.3, sasa hivi mwaka 2018 idadi ya Watanzania tunakadiriwa kufika milioni 54.2. Kwa hiyo utakuta kwamba sasa idadi imeongezeka kwa kiwango kikubwa wakati ardhi imebaki vilevile haijaongezeka. Kwa hiyo na hii ina maana gani, ina maana tuje na mipango madhubuti ya kuhakikisha moja, tunadhibiti idadi ya ongezeko la watu lakini la pili, matumizi bora ya ardhi yetu tuliyonayo, ndiyo maana tumeweka mkazo katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hili wazo la mpango wa uzazi wa mpango, naomba nilichukue kama Serikali tutalifanyia kazi kuhakikisha kwamba tunawahimiza Watanzania wote tuwe na uzazi wa mpango ili kusudi tuzae idadi ya watoto inayolingana na ardhi ile tuliyonayo. (Makofi)
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa majibu haya inaonesha kabisa dhahiri kwamba Mheshimiwa Waziri amedanganywa na uhalisia wa wananchi wa Jimbo la Mpanda Vijijini, kutokana na swali hili kwa sababu imekuwa ni mara ya tatu nauliza swali hili, lakini pia Serikali imeshindwa kutatua migogoro pamoja na mauaji yanayoendelea katika kata hizi, Kata ya Kapalamsenga, Ikola, Isengule, Iteteme pamoja na Kalema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vijiji hivi wananchi wamekuwa wanateswa na askari wa Wanyamapori na mwaka jana wamekufa zaidi ya vijana wawili kwa kupigwa risasi na askari wa wanyamapori. Ni nini tamko la Serikali kutokana na vifo na manyanyaso yanayoendelea katika Jimbo hili la Mpanda Vijijini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika majibu haya ndiyo maana nikasema kwamba Mheshimiwa Waziri, amedanganywa. Hakuna ushirikishwaji wowote kati ya Vijiji, Vitongoji pamoja na wananchi. Ni kwa nini Serikali inatumia nguvu wakati wananchi wanatakiwa wapewe elimu, washirikishwe kuliko kulazimishwa kupeleka hizo GN kwenye maeneo ambayo vijiji hawajapewa ramani husika kujua na kutambua mipaka yao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme tu kwamba siyo azma ya Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wake wanateswa, hiyo haturuhusu. Haturuhusu kabisa, lakini pale ambapo wananchi wale ambao wanaenda kuingia katika maeneo ya hifadhi bila kufuata taratibu, hatua za kisheria lazima zichukuliwe. Kuchukuliwa siyo kuwatesa wala kuwapiga, lazima wanakamatwa wanapelekwa katika mikondo ya sheria na hapo wanashitakiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kwenye maeneo ya Mheshimiwa kuna tatizo la namna hiyo, basi nitaomba tuwasiliane baadae ili unipe baadhi ya watu ambao wamepata matatizo hayo, kusudi tuweze kuwachukulia hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wote tunafahamu tunapoenda katika mipango ya matumizi bora ya ardhi hasa katika vijiji lazima mipango iwe shirikishi kwa sababu wanaotakiwa kupanga ni wananchi wenyewe wote wanahusika, sasa akiniambia kwamba wananchi hawakushirikishwa kwa kweli nashindwa kuelewa. Huo mpango lazima upitishwe na mkutano wa Kijiji. Sasa ulipitishwaje kama wananchi hawakushirikishwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama kuna changamoto hizo, basi nitakapokwenda katika hilo eneo basi tukae wote kama Serikali pamoja na wananchi tuone kama kweli hawakushirikishwa au kuna tatizo lingine la mahitaji ya ardhi. (Makofi)
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Migogoro kati ya hifadhi zetu na wananchi itaendelea kwa muda, kwa sababu wananchi wanaongezeka, wanyama wanaongezeka, ardhi iko pale pale. Wanyama hawawezi kufanya uzazi wa mpango, lakini sisi tunaweza. Je, ni lini Serikali yetu itakuja na sera na mpango kabambe wa uzazi wa mpango kwa wanadamu ili tuweze kudhibiti ongezeko hili la watu ambalo linaweza likaathiri hata shughuli nyingine za kiuchumi kama afya, elimu na kadhalika? (Kicheko)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba idadi ya wananchi imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Wakati tunapata uhuru mwaka 1961 idadi ya Watanzania walikuwa ni milioni 10.3, sasa hivi mwaka 2018 idadi ya Watanzania tunakadiriwa kufika milioni 54.2. Kwa hiyo utakuta kwamba sasa idadi imeongezeka kwa kiwango kikubwa wakati ardhi imebaki vilevile haijaongezeka. Kwa hiyo na hii ina maana gani, ina maana tuje na mipango madhubuti ya kuhakikisha moja, tunadhibiti idadi ya ongezeko la watu lakini la pili, matumizi bora ya ardhi yetu tuliyonayo, ndiyo maana tumeweka mkazo katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hili wazo la mpango wa uzazi wa mpango, naomba nilichukue kama Serikali tutalifanyia kazi kuhakikisha kwamba tunawahimiza Watanzania wote tuwe na uzazi wa mpango ili kusudi tuzae idadi ya watoto inayolingana na ardhi ile tuliyonayo. (Makofi)
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa majibu haya inaonesha kabisa dhahiri kwamba Mheshimiwa Waziri amedanganywa na uhalisia wa wananchi wa Jimbo la Mpanda Vijijini, kutokana na swali hili kwa sababu imekuwa ni mara ya tatu nauliza swali hili, lakini pia Serikali imeshindwa kutatua migogoro pamoja na mauaji yanayoendelea katika kata hizi, Kata ya Kapalamsenga, Ikola, Isengule, Iteteme pamoja na Kalema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vijiji hivi wananchi wamekuwa wanateswa na askari wa Wanyamapori na mwaka jana wamekufa zaidi ya vijana wawili kwa kupigwa risasi na askari wa wanyamapori. Ni nini tamko la Serikali kutokana na vifo na manyanyaso yanayoendelea katika Jimbo hili la Mpanda Vijijini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika majibu haya ndiyo maana nikasema kwamba Mheshimiwa Waziri, amedanganywa. Hakuna ushirikishwaji wowote kati ya Vijiji, Vitongoji pamoja na wananchi. Ni kwa nini Serikali inatumia nguvu wakati wananchi wanatakiwa wapewe elimu, washirikishwe kuliko kulazimishwa kupeleka hizo GN kwenye maeneo ambayo vijiji hawajapewa ramani husika kujua na kutambua mipaka yao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme tu kwamba siyo azma ya Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wake wanateswa, hiyo haturuhusu. Haturuhusu kabisa, lakini pale ambapo wananchi wale ambao wanaenda kuingia katika maeneo ya hifadhi bila kufuata taratibu, hatua za kisheria lazima zichukuliwe. Kuchukuliwa siyo kuwatesa wala kuwapiga, lazima wanakamatwa wanapelekwa katika mikondo ya sheria na hapo wanashitakiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kwenye maeneo ya Mheshimiwa kuna tatizo la namna hiyo, basi nitaomba tuwasiliane baadae ili unipe baadhi ya watu ambao wamepata matatizo hayo, kusudi tuweze kuwachukulia hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wote tunafahamu tunapoenda katika mipango ya matumizi bora ya ardhi hasa katika vijiji lazima mipango iwe shirikishi kwa sababu wanaotakiwa kupanga ni wananchi wenyewe wote wanahusika, sasa akiniambia kwamba wananchi hawakushirikishwa kwa kweli nashindwa kuelewa. Huo mpango lazima upitishwe na mkutano wa Kijiji. Sasa ulipitishwaje kama wananchi hawakushirikishwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama kuna changamoto hizo, basi nitakapokwenda katika hilo eneo basi tukae wote kama Serikali pamoja na wananchi tuone kama kweli hawakushirikishwa au kuna tatizo lingine la mahitaji ya ardhi. (Makofi)
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Migogoro kati ya hifadhi zetu na wananchi itaendelea kwa muda, kwa sababu wananchi wanaongezeka, wanyama wanaongezeka, ardhi iko pale pale. Wanyama hawawezi kufanya uzazi wa mpango, lakini sisi tunaweza. Je, ni lini Serikali yetu itakuja na sera na mpango kabambe wa uzazi wa mpango kwa wanadamu ili tuweze kudhibiti ongezeko hili la watu ambalo linaweza likaathiri hata shughuli nyingine za kiuchumi kama afya, elimu na kadhalika? (Kicheko)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba idadi ya wananchi imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Wakati tunapata uhuru mwaka 1961 idadi ya Watanzania walikuwa ni milioni 10.3, sasa hivi mwaka 2018 idadi ya Watanzania tunakadiriwa kufika milioni 54.2. Kwa hiyo utakuta kwamba sasa idadi imeongezeka kwa kiwango kikubwa wakati ardhi imebaki vilevile haijaongezeka. Kwa hiyo na hii ina maana gani, ina maana tuje na mipango madhubuti ya kuhakikisha moja, tunadhibiti idadi ya ongezeko la watu lakini la pili, matumizi bora ya ardhi yetu tuliyonayo, ndiyo maana tumeweka mkazo katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hili wazo la mpango wa uzazi wa mpango, naomba nilichukue kama Serikali tutalifanyia kazi kuhakikisha kwamba tunawahimiza Watanzania wote tuwe na uzazi wa mpango ili kusudi tuzae idadi ya watoto inayolingana na ardhi ile tuliyonayo. (Makofi)
MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu haya ambayo ameyatoa japokuwa hayaoneshi dhamira ya dhati ya kutaka kumaliza mgogoro huo. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza, mgogoro huu umekuwa wa muda mrefu sana, lakini kwa majibu ya Serikali hayakuonesha hapa ni lini watakutana na viongozi wa Mkoa ili kumaliza huu mgogoro. Kwa sababu umesema tu watakaa lakini haisemi ni lini. Kwa sababu huu mgogoro ni wa muda mrefu kwa hiyo, ningeomba Serikali ituambie ni lini watadhamiria kumaliza huu mgogoro?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali langu la pili, kuna mgogoro pia kwenye Serikali ya Wilaya ya Kilwa na Wizara kuhusiana na mpaka huu wa Selous. Kwa hiyo, nayo Mheshimiwa Waziri ningependa aniambie ni lini mgogoro huu watamaliza ili kuepukana na vurugu ambazo zinaweza zikatokea katika kugombania mipaka hii katika maeneo haya?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hi kumpongeza sana kwa sababu amekuwa ni mdau mzuri sana wa mambo ya utalii katika eneo la kusini, kwa kweli tutaendelea kushirikiana naye. Sasa kuhusu lini tutakutana naomba nimhakikishie tu kwamba kati ya mwezi wa saba na wa tisa kabla ya Bunge la mwezi tisa tutafanya jitihada za kuhakikisha kwamba tunakutana na viongozi wa Lindi na tutashughulikia migogoro yote inayohusiana na hilo Pori la Akiba la Selous.
MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri lakini naomba niulize swali kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ipo migogoro inayoendelea baina ya vijiji vyetu na hifadhi zetu, ikiwemo Hifadhi hiyo ya Selous ambayo muuliza swali ameizungumza, lakini pia ipo migogoro baina ya kijiji na kijiji, hii inapelekea wananchi wengi kukosa amani.
Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kumaliza migogoro hii katika nchi yetu ili wananchi waendelee kuishi kwa amani? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kumekuwa na changamoto, kumekuwa na migogoro mbalimbali katika maeneo mbalimbali yanayopakana na hifadhi. Lakini naomba nitumie nafasi hii kumueleza Mheshimiwa Mbunge kwamba kuanzia mwaka wa fedha 2018/2019 yaani Julai, Wizara kwa kushirikiana na taasisi zetu za Hifadhi za Taifa tutahakikisha kwamba vijiji vyote vinavyozunguka maeneo ya hifadhi vinapimiwa na vinaondokana na matatizo ambayo yapo katika yale maeneo. Kwa sababu tumetenga fedha kwa ajili ya hiyo kazi kwa hiyo vijiji vyote vitapitiwa.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vilivyotajwa na Mheshimiwa Waziri kwamba, ndiyo vinavyochangia katika Wilaya ya Liwale kwa Selous, vijiji hivi ndivyo vilivyoanzisha mgogoro kwa sababu vijiji hivi vimepakana na Selous kwa Mto wa Matandu. Kwa nini Kikulyungu peke yake ndio ambayo imeonekana kwamba imeondoka Matandu na ndio maana wanakijiji Wakikulyungu waligoma. Sasa Mheshimiwa Waziri ninachotaka kujua je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kufuatana na Mheshimiwa Waziri wa Ardhi muende mkatafsiri GN ambayo inaitambua Pori la Akiba la Selous ukiachana na hii tangazo la mwaka 1974?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba tuko tayari kuongozana na Mheshimiwa Waziri pamoja na viongozi wengine wa Mkoa wa Lindi ili tushughulikie migogoro yote inayohusu mpaka wetu kule. (Makofi)
MHE. BONNAH M. KALUWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nilitaka nimuulize Mheshimiwa Waziri pale Segerea kuna pori moja linaitwa Msitu wa Nyuki, walikuwa wanafuga nyuki zamani lakini naona Wizara imeshaachana na huo mpango wa kufuga nyuki.
Sasa Wizara ina mpango gani na hilo pori maana yake wameliacha tu, na kama hawana mpango nalo kwa nini wasitupe sisi Manispaa ya Ilala ili tuweze kulitumia katika matumizi ya soko na mambo mengine ya huduma za kijamii? (Makofi)
NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba tuna msitu katika lile eneo ambalo lilikuwa linatumika kwa ajili ya kufuga nyuki, lakini si kwamba lile pori tumeliacha tu, kuliacha tu bado linaendelea kuhifadhi ule uoto wa asili.
Kwa hiyo, bado ni pori linalotambulika vizuri kabisa na bado tutaendeleza jitihada za kufuga, lakini pia inasaidia sana katika kuweza kupunguza carbon dioxide ambayo inatokea katika viwanda mbalimbali pale Dar es Salaam. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, lile eneo tutaendelea kulihifadhi na litaendelea kuhifadhia na kuendelezwa.
MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Swali la kwanza, Tanzania tunalenga kujiondoa kwa watalii 1,300,000 kwa mwaka na pia kujiondoa kwenye mchango wa utalii katika pato la Taifa kwa asilimia 17.5 na pia kufikia ajira milioni mbili zinazotokana moja kwa moja na utalii. Je, Serikali haioni kiwango cha diploma na certificate ni kidogo kwa sasa na kwamba tuende kwenye degree? Ni lini Serikali inajipanga kuongeza hadhi chuo hicho kiwe na uwezo wa kutoa degree?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, injini ya kutawala sekta ya utalii ni elimu na ujuzi katika eneo la menejimenti. Je, ni lini Serikali inapanga kuwezesha Chuo hicho cha Utalii kutoa course ya juu ya menejimenti ili kuondoa wageni kutawala sekta hii katika eneo la menejimenti? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Ally Saleh, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba mpaka sasa hivi tumekuwa tukitoa stashahada na astashahada lakini hivi sasa Serikali ina mpango wa kuanzisha degree katika maeneo hayo kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Columbia kutoka Canada. Baada ya kukamilika mitaala na ikishapitishwa, basi tutaanza kutoa hizo degree ambazo zitawaandaaa vijana wetu katika hizo fani ambazo Mheshimiwa Mbunge ameuliza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kuhusu masuala ya mafunzo ya menejimenti, ni kweli kabisa tumekuwa na changamoto kubwa katika mafunzo na course zinazotolewa kwa ajili ya menejimenti kuwaandaa vijana kuweza kushika nyadhifa mbalimbali katika hoteli zetu na katika maeneo mbalimbali. Hivi sasa Wizara kuanzia mwaka wa fedha 2018/ 2019 tunategemea kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa watu mbalimbali, ambayo yatahusu watu zaidi ya 800 katika maeneo ya menejimenti ili kuwaandaa na kuweza kushika nyadhifa mbalimbali na nafasi katika utumishi katika maeneo ya utalii.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Najua nia ya Serikali ya kuanzisha vyuo hivi ni pamoja na kukuza utalii na kuingiza pato la letu la ndani na nje.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa tembo wametoka kwenye Hifadhi ya Udzungwa National Park wameshambulia katika Vijiji vya Mailindi, Maghana kwenye Kata ya Mahenge, wananchi wako kwenye hali mbaya na jambo hili limekuwa likijitokeza kila mwaka. Naomba tu Mheshimiwa Waziri aende akaone hali jinsi ilivyo lakini pia ahakikishe kwamba kituo kidogo cha askari wa wanyamapori kinafunguliwa pale. Tatizo hili ni la kila mwaka, namwomba sana Mheshimiwa Waziri.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Balozi Venance Mwamboto, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mwamoto, amekuwa akifuatilia sana hili suala na tumekuwa tukizungumza ni hatua gani ambazo tunaweza kuzichukua. Naomba nimhakikishie kwamba nitakuwa tayari kwenda kuangalia hali halisi katika Kata hiyo ya Mahenge ili kuona ni hatua gani zichukuliwe na Serikali. Moja ya hatua ambazo tunategema kuzichukua ni pamoja na kujenga out post katika lile eneo ili wasaidiane na wananchi na Halmashauri ile katika kudhibiti hao tembo ambao wamekuwa wakizagaa katika maeneo mbalimbali.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, hawa wabeba mizigo kwenye milima yetu ambao wanatembeza Wazungu wamekuwa hawapewi mafunzo na wanafanya kazi hii kwa uzoefu Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wanapatiwa mafunzo haya lakini na maslahi yao kwa ujumla yanatazamwa?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso ambalo kwa kweli anataka kujua kwamba ni mpango gani tulionao katika kutoa mafunzo kwa hawa wanaobeba mizigo. Naomba nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tumejiandaa vya kutosha katika mwaka huu wa fedha unaoanza Julai mwaka 2018, tunategemea kutoa mafunzo mafupi kwa hao watu wote pamoja na wale wanaongoza utalii katika eneo la Mlima Kilimanjaro ili kusudi waweze kutoa zile huduma ambayo wateja wetu wanazitarajia. Kwa hiyo, awe na subira, baada ya mwaka kuanza ataona matunda na mabadiliko makubwa yatakayojitokeza.
MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nimsahihishe Naibu Waziri, amesema Msitu wa Mkussu; siyo Mkusu ni Mkuzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa misitu ya Wilaya ya Lushoto iliyoungua tokea mwaka 2004 ni takribani miaka 14 sasa, lakini mpaka sasa hivi miti ile ya asili haijaota, imebaki vichaka tu. Je, nini commitiment ya Serikali juu ya kurudisha haraka uoto wa asili uliopotea kwa kupanda miti katika maeneo ya misitu iliyoungua pamoja na sehemu za maporoko? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Wilaya ya Lushoto ina vijana wengi wamejiunga kwenye vikundi, je, Serikali ipo tayari kuwapa miche ya miti ya asili bure ili kurudisha haraka uoto wa asili uliopotea kwa muda mrefu sasa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shabaani Shekilindi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nachukue nafasi hii kumpongeza sana kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia sekta ya misitu na kwa jinsi ambavyo amekuwa akitoa ushauri kwa namna mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, eneo lolote lile ambalo ni misitu ya asili, ukienda kuanza kupanda miti mingine utaharibu ule uoto wa asili. Tunachofanya sisi ni kuliacha lile eneo kama lilivyo. Tukishaliacha kama lilivyo, ikifika kipindi ile miti itaota yenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, natambua kabisa kwamba katika lile eneo ambalo Mheshimiwa Mbunge anasema imechukua muda mrefu haijaota, lakini hivi sasa Wakala wa Taifa wa Misitu Tanzania wanafanya utafiti ili wapate mbegu na miche bora ile ya asili iliyokuwepo katika lile eneo ili tuone kama tunaweza tukaipanda katika eneo lile kusudi kurudisha ule uoto wa asili.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusu miche hii ya asili ambayo inaweza ikapandwa katika eneo hili na wale vijana waweze kupata ajira, kama nilivyosema Wakala wa Taifa wa Misitu anafanya utafiti. Tukishakamilisha, tukabaini mbegu au miche mizuri ya asili katika eneo lile, basi tutaenda kuhakikisha kwamba inapandwa katika lile eneo na wale vijana watapata ajira.
MHE. HAMIDA M. ABDALLAH. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu haya ya Serikali. Swali la kwanza, maeneo haya ni yale ambayo walikaa wakoloni wa mataifa haya makubwa ambayo leo hii wanasaidia. Je, Serikali imesaidia kwa namna gani katika kuendeleza miundombinu ya Kilwa Kisiwani na Msongo Mnara ili kuendeleza utalii wa maeneo haya? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili la nyongeza, napenda kujua Serikali inasaidiaje katika kuhakikisha Kilwa Kisiwani na Msongo Mnara tunaendeleza utalii, maana hali ya kule ni mbaya sana, miundombinu ni mibovu, watalii sasa wanapungua kwa sababu hakuna hoteli, hakuna vifaa vya kuwawezesha watalii kuvuka kwenda Kilwa Kisiwani na Kilwa Msongo kuona haya magofu ya ukoloni? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Hamida Abdallah, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nachukua nafasi hii kutambua mchango wake ambao amekuwa akiutoa katika hii sekta ya utalii kule Lindi. Kwa kweli amekuwa akifanya kazi nzuri sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa katika lile eneo mimi mwenyewe nimefika Machi na nimeona jinsi miundombinu ambavyo iko kwenye hali mbaya. Hiyo inasababisha watalii wengi washindwe kufika katika lile eneo. Hivi sasa tumeandaa mkakati maalum kwa ajili ya kuboresha ile miundombinu katika vile Visiwa vya Kilwa pamoja na Songo Mnara ili kuhakikisha ile miundombinu inapitika wakati wowote; iwe ni kipindi cha masika au kipindi cha kiangazi, kusudi watalii waweze kufika.
Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya changamoto kubwa ambayo iko pale ni pamoja na kutafuta boti ya kisasa itakayokuwa inawavusha watalii kuwapeleka kule katika Kisiwa. Sasa hili tunashirikiana na Wizara ya Uchukuzi ili tuone namna ambavyo tunaweza tukapata boti nzuri ya kuweza kusaidia katika shughuli hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, kuhusu namna ya kuimarisha utalii katika eneo lile, mpango mkubwa ambao tunao kama Wizara ni pamoja na kuunganisha na Pori la Akiba la Selous. Tunataka iwe ni circuit moja, watalii wanapokwenda kutembelea Selous katika upande ule, basi tuunganishe na hii circuit ya Kilwa Kisiwani pamoja na Songo Mnara kusudi vyote kwa pamoja iwe package moja. Hiyo tunaamini itasaidia sana katika kuimarisha utalii katika lile eneo.
MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwa sababu yapo maeneo mengine ambayo yanaweza na yenyewe kuwa ni urithi wa dunia, kama vile magofu ya Mjerumani ya Mkalama. Wizara inafanya juhudi gani kuyaweka katika orodha hiyo na kuona namna ya kuyaboresha? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Allan Kiula, Mbunge wa Mkalama, rafiki na kaka yangu ambaye tunalingana urefu, hongera sana. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kweli kabisa katika maeneo yale kuna magofu yaliyoachwa na Mjerumani. Katika utaratibu ambao Wizara sasa imeamua kuchukua, tumeamua kuangalia mali kale zote zilizopo na kuziboresha. Ili tuweze kuziboresha, hatua ambazo tumechukua, tumeamua kushirikisha hizi taasisi zilizo chini ya Wizara zenye uwezo kidogo wa kifedha na kuwakabidhi hayo maeneo ili waweze kutengeneza miundombinu mizuri iweze kusaidia katika kuboresha na kuyatangaza na kuvutia watalii katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika jitihada hizi, nina imani kabisa yale maeneo ya magofu yatapata ufadhili mzuri sana na hivyo yataimarika vizuri sana na kuweza kuvutia watalii.
MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali madogo ya nyongeza. Pamoja na kuwa na doria za pamoja kati ya halmashauri na hifadhi hizo na pamoja na kuwa na hivyo vituo vilivyotajwa bado kasi ya wanyama waharibifu na wakali kutoka ndani ya hifadhi na kwenda nje kwenye makazi ya wananchi, imeendelea kuwa kubwa mno.
Mheshimiwa Spika, changamoto kubwa ambayo tunayo kwenye Halmashauri zetu ni Halmashauri hazina usafiri kwa ajili ya kuwafukuza wanyama hao, Halmashauri hazina silaha stahiki kwa ajili ya wanyama hao, lakini pia, bajeti ndogo ambazo Halmashauri tunazo, pia, uchache wa watumishi wa sekta hiyo ya wanyamapori.
Mheshimiwa Spika, hapa imesemwa kuna magari mawili yamenunuliwa kwa ajili hiyo. Magari hayo mawili naamini yako Ngorongoro hayako Karatu huku ambako tatizo lilipo. Sasa Mheshimiwa Waziri anaweza akaongea na watu wake wa Ngorongoro ili angalau gari moja liwekwe Halmashauri, wale Maofisa wa Halmashauri pindi tatizo linapotokea waweze kwenda kushughulika?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, fedha hizi za kifuta jasho au kifuta machozi, pamoja na kwamba, ni ndogo sana lakini pia, zinachelewa sana kuwafikia...
Mheshimiwa Spika, swali; kwa nini fedha hizi zisilipwe kwenye hifadhi husika badala ya mlolongo ambao sasa hivi zinalipwa kutoka Wizarani? Mheshimiwa Spika, ninakushukuru. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kumekuwa na changamoto hizi za kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu katika maeneo mengi. Changamoto ziko katika upande wa usafiri, watumishi, pamoja na vifaa vile vinavyotakiwa kutumika katika kupambana na hao wanyamapori.
Mheshimiwa Spika, sasa niombe kusema tu kwamba, kama nilivyosema kwenye swali la msingi, magari mawili yameshanunuliwa na tayari kweli yako pale. jitihada ambazo tutafanya ni kulingana na jinsi ambavyo amependekeza Mheshimiwa Mbunge, kuhakikisha angalau gari moja linakuwepo katika maeneo yale kusudi pale linapotokea tukio basi gari hilo liweze kusaidia katika juhudi hizo za kupambana na wanyama wakali.
Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili, kuhusiana na fedha za kifuta jasho na kifuta machozi kwamba, ziwe zinatolewa na hifadhi inayohusika, ni suala ambalo labda tutaliangalia wakati tunapitia upya hizi sheria ambazo tutaona kama kweli, inafaa. Kwa hivi sasa ilivyo tuna mfuko maalum ambao unatumika kwa ajili ya kifuta jasho na kifuta machozi.
Mheshimiwa Spika, huu mfuko bado unakabiliwa na changamoto ya kuwa na fedha za kutosha. Kwa hiyo, katika pendekezo analolileta nafikiri tutaliangalia, tutaona kama linafaa, tunaweza tukalichukua. (Makofi)
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Changamoto ambazo zinakabili vijiji hapa nchini vinavyopakana na hifadhi za wanyama zimekuwa ni changamoto za muda mrefu kwamba, wanyama wanaingia na kuharibu mazao na kuuwa watu, lakini ukiangalia nchi mbalimbali zilizoendelea duniani wanaweka electrical fence, ili kudhibiti moja kwa moja tatizo hili. Je, Serikali kwa nini isianze kwa awamu kutekeleza na kuweka hizo electrical fence, ili angalau kukomesha kabisa tatizo hili? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Paresso, dada yangu ambaye amekuwa akifuatilia kwa karibu sana matukio mbalimbali na amekuwa alifanya kazi nzuri sana, hongera sana.
Mheshimiwa Spika, sasa kuhusu electrical fence kuwekwa katika hifadhi zetu zote ni suala zuri, lakini uwezo wa kifedha ndiyo changamoto. Ukiangalia ukubwa wa hifadhi tulizonazo kwamba, zote tutaweka electrical fence kwa kweli, inaweza ikachukua muda mrefu sana. Sitaki kutoa commitment ya Serikali, lakini tutaendelea kulifanyia kazi ili tuone kwamba, kama litawezekana, kama pale ambapo bajeti itaruhusu basi tunaweza kulitekeleza.
MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, niwapongeze Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kunipa gari la kusaidia kufukuza wanyama waharibifu kwenye maeneo yangu, lakini pia, najua wana mpango wa kupeleka fedha za kifuta jasho katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa, sasa ni miaka 15 Vijiji vya Hunyali, Kihumbu, Maliwanda, Salakwa, Kyandege, Tingilima, wamekuwa ni wahanga wakuu wa wanyama waharibifu wa mazao, sasa Serikali ina mpango gani sasa mbadala ikiwepo kupima vijiji hivyo ili kupata Hati Miliki za Kimila na kuendesha maisha ya wananchi wa makazi hayo?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa sasa kuona ni kuamini na kuamini ni kuona, ni lini sasa Wizara au Waziri atatembelea maeneo haya, ili kujihakikishia hali halisi ya uharibifu huo? Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, kwanza ni kweli kabisa kwamba, sasa hivi Wizara ina mpango mkubwa mahususi wa kuhakikisha kwamba vijiji vyote ambavyo vinazungukwa na Hifadhi za Taifa vinakuwa na mpango bora wa matumizi ya ardhi. Hili tunalifanya kuanzia mwaka wa fedha unaoanza Julai mwaka huu. Katika kutekeleza hilo tunashirikiana na Wizara ya Ardhi, ambapo ndiyo wamepewa hizi fedha kwa ajili kusaidia kupima vijiji vyote hivi ili wawe na mpango mzuri na kuhakikisha matumizi yanaeleweka vizuri kabisa.
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, kuhusu kwenda kutembelea na kujionea hali halisi, naomba nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tuko tayari wakati wowote mara baada ya Mkutano huu wa Bunge kumalizika tutapanga ni lini tunaweza kufika kule ili tujionee hali halisi ilivyo huko.
MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri bado kidogo ayajaniridhisha kwa sababu mimi nilitembelea Mikumi pale 2016 na majibu niliyopewa ni haya haya kwamba mwekezaji amepatikana na ukarabati unaendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa namwomba Mheshimiwa Naibu Waziri anihakikishie hapa huu ukarabati utamalizika lini ili tuweze kupata mapato ya uhakikika? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili ni kwamba mbuga hii ya Mikumi ipo katikati ya barabara ambayo inaenda mikoani na nje ya Tanzania. Kulikuwa na mpango wa kuanzisha road toll ili kuweza kupata mapato zaidi katika mbuga hii ambayo inakumbana na changamoto nyingi, miundombinu na hata magari ya kuzuia ujangili.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua, ni lini Serikali itaanzisha ushuru huu kwa sababu mchakato ulishaanza, sasa kuna kigugumizi gani? Hii itasaidia mbuga hii iweze kupata mapato na kukabiliana na changamoto ili iweze kuboresha na kuongeza mapato zaidi? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia na ni kweli kabisa kwamba mwaka 2016 alifika pale kuangalia ni namna gani hoteli zinaweza kuongezeka katika lile eneo ili kukabiliana na hii changamoto ya uhaba wa vyumba vya watalii kulala pale Mikumi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie kwamba ni kweli kabisa kwamba yule mwekezaji alipatikana siku nyingi toka mwaka 2016, lakini baada ya kupatikana, kwa mujibu wa taratibu za uwekezaji, lazima kwanza EIA ifanyike ili aweze kuendelea na huo mradi. Huo mradi baada ya kufanya hiyo tathimini ya mazingira, imekamilika mwezi Novemba, 2017. Baada ya kukamilika, mwezi Februari, 2018 ndipo mwekezaji amekabidhiwa rasmi lile eneo.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kukabidhiwa lile eneo, sasa hivi ametoa mpango kazi, na mimi mwenyewe nilienda pale nikaona, sasa hoteli yenyewe inategemea kukamilika mwezi Novemba mwaka ujao yaani mwaka 2019. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kuweka road toll kule Mikumi, ni kweli hili suala limekuwepo na tumekuwa tukiliangalia ndani ya Serikali kuona kama kweli linaweza likatusaidia na kama linaweza likafanya kazi. Bado tuko kwenye hatua za majadiliano na kuona namna bora ya kuweza kulitekeleza hilo ili kusudi tusilete usumbufu kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, wazo la Mheshimiwa Mbunge ni zuri na ninaomba niseme kwamba Serikali bado inaendelea kulifanyia kazi.
MHE. MBAROUK SALIM ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu nyingi ambazo zina vivutio vya utalii utakuta miundombinu yake ni mibovu sana. Hii ndiyo sababu kubwa ambayo inasababisha wawekezaji warudi nyuma na washindwe kuwekeza katika maeneo ambayo yana vivutio na hivyo kushusha utalii.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba wanaboresha miundombinu katika maeneo hayo ya utalii? Nashukuru. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kumekuwa na maeneo ya namna hiyo na bado kumekuwa na changamoto ya uwekezaji. Kazi kubwa tunayoifanya kama Serikali ni kuhakikisha kwamba tunaboresha kwanza mazingira ya uwekezaji na kuwahamasisha wawekezaji ili kusudi waweze kuwekeza katika maeneo yote hayo na yaweze kuchangia katika shughuli mbalimbali za utalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme tu kwamba tutakaa na Mheshimiwa Mbunge ili tuone namna gani tunaweza tukafanya hiyo kazi ili kusudi wananchi wa eneo lile waweze kufaidika na matunda ya hiyo kazi.
MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, sekta ya utalii ni sekta ambayo ina fursa nyingi sana na kubwa za kulisaidia Taifa kimapato. Suala la Mikumi kama ambavyo limejibiwa sasa hivi, tunapoteza fursa kubwa sana. Mikumi ilikuwa ni kivutio katika vivutio vya mwanzo kabisa vya utalii nchi hii. Ilikuwa inatoa fursa kubwa sana kwa utalii wa ndani hasa kwa vijana, wanafunzi na taasisi mbalimbali wanaotaka kwenda kuangalia mambo ya utalii. Jinsi ilivyo sasa hivi imekwama kwa muda mrefu na hii sawa na sehemu nyingine nyingi tu.
Je, Serikali sasa hivi iko tayari kuja na mkakati mahususi unaohakikisha kuwa sehemu zote za kitalii zinaendelezwa kwa kutumia sekta binafsi? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba Mikumi ilikuwa ni moja ya hifadhi ambayo ilikuwa inatoa mchango mkubwa sana katika pato la Taifa, lakini kumekuwa na changamoto ya hivi karibuni kwamba mchango ule kidogo umeshuka sana kutokana na mambo mbalimbali. Ndiyo maana kwa kutambua hilo, Serikali tumekuja na mradi mkubwa wa kuboresha utalii Kusini. Katika mradi huo, moja ya maeneo ambayo yamepewa uzito ni pamoja na hifadhi ya Mikumi, kwa sababu ule mradi wa kukuza utalii wa Kusini, tunahudumia Selous upande wa Kaskazini, Udzungwa, Mikumi na Ruaha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, katika huo mradi tunaboresha miundombinu yote, tutatangaza ipasavyo kuhakikisha kwamba tunawavutia watalii mbalimbali wa ndani na nje ya nchi ili waweze kuingiza mapato na Serikali iweze kupata mapato ya kutosha na kuweza kuendeleza nchi yetu.
MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza Swali la nyongeza. Kama ilivyo Morogoro kwamba kuna vivutio kwa watalii ndivyo ilivyo kwa Mkoa wa Dodoma ambako Wilayani Kondoa kuna michoro ambayo haipo Tanzania na michoro ile iko katika mapango ya Kolo na Pahi, lakini vivutio vile havijawahi kutangazwa na Serikali.
Je, Serikali ina mkakati gani? Pamoja na Wabunge wa Kondoa kuhangaika kuleta watalii, lakini bado haitoshelezi kama Serikali haitatia mkazo kutangaza vile vivutio.
Je ni lini sasa au Serikali ina mkakati gani kutangaza michoro ile ya mapango ya Kolo, Pahi na maeneo mengine katika Wilaya ya Kondoa?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba nichukue nafasi hii kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Felister Bura na Wabunge wote wa Mkoa wa Dodoma kwa jinis ambavyo wamekuwa wakilifanyia kazi hili suala. Hivi sasa tunajua kabisa kwamba Dadoma ndiyo Makao Makuu ya nchi na kweli lazima tuziimarishe hizi hifadhi zetu na maeneo maengine ya Utalii ili kuweza kuvutia watu mbalimbali kuja kuwekeza katika Mkoa huu wa Dodoma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kitu ambacho tunategemea kukifanya katika kutangaza yale maeneo ya michoro ya Miambani kule Kondoa; yaani Kolo na pale Pahi; jitihada ambazo tunaweka kuanzia tarehe 1 Julai, 2018 tunategemea kuanzisha studio ya kutangaza utalii yaani kutangaza vivutio vyote nchi nzima. Hiyo ni pamoja na hilo eneo, tutalitangaza vizuri sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, tunategemea kuanzisha channel maalum kupitia TBC ambayo itakuwa inahusiana na masuala ya utalii. Kwa kutumia hilo basi, tunaamini kwamba basi matangazo, wananchi wengi wa ndani na wa nje wataweza kupata fursa ya kuweza kujua vivutio vyote tulivyonavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, la tatu, tunategemea kutumia viongozi mbalimbali mashuhuri pamoja na mambo mengine mengi kutangaza ndani ya nchi na nje ya nchi kwa kutumia mitandao ya facebook, twitter na mambo mengineyo ili kusudi vivutio vyote vieleweke kwa watanzania lakini kwa watu wote walioko nchi za nje waweze kuijua Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitumie nafasi hii niseme kwamba sasa hivi Tanzania tumepata taarifa kwamba sasa imekuwa ni nchi inayoongoza kwa safari Afrika kupitia Serengeti. Kwa kweli huu ni ufahari mkubwa na Dodoma nayo itafaidika sana na haya mambo ambayo tunakwenda kuyafanya.
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa naibu Spika, ahsante sana. Kuhusu Hoteli ya Kitalii ya Mikumi: Je, Mheshimiwa Naibu Waziri anafahamu kwamba mwekezaji wa kwanza alifanya hujuma makusudi baada ya kuchukua shilingi bilioni nne na mpaka leo akaichoma hoteli ile?
Je, Serikali imechukua hatua gani kwa yule mwekezaji wa kwanza? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli kama Serikali hatuna taarifa kama kweli ile ilichomwa kama hujuma, lakini tunachojua ni kwamba ilipata janga la moto mwaka 2009 na ikaungua yote. Yule aliyekuwa amekabidhiwa baada ya hapo, alishindwa kuendeleza. Baada ya kuona ameshindwa kuendeleza, ndiyo maana Serikali tukaamua tena kuchukua hatua kuhakikisha kwamba tunamtafuta mwekezaji mwingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwekezaji huyu sasa liyepatikana amekuja na michoro mizuri sana na design nzuri sana ambazo ninazo hata baaadaye Mheshimiwa Keissy naweza nikamwonyesha hapa jinsi ilivyo ambapo tunategemea itakapofika mwaka 2019 hoteli yenyewe itakuwaje? Kwa hiyo hilo tunalo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hilo la kusema kwamba alifanya hujuma, hizo taarifa hatunazo kama Serikali.
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto za miundombinu katika hifadhi ya Serengeti zinafanana na changamoto za Hifadhi mpya ya Kimisi na Burigi.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweka miundombinu katika hifadhi mpya ya Kimisi na Burigi ili hifadhi hii iweze kuchangia mapato katika Halmashauri zetu za Wilaya zilizopo katika Mkoa wa Kagera pamoja na kuchangia pato la Taifa?
Swali la pili, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kuambatana na mimi kwenda kwenye Kata za Bweranyange, Rugu, Nyakasimbi, Nyakabanga na Nyakakika ili kutatua migogoro ya mipaka kati ya vijiji kwenye Kata hizi na Hifadhi? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue nafasi hii kuwapongeza sana Wabunge wa Mkoa wa Kagera kwa jinsi ambavyo wameshirikiana na Serikali kuhakikisha kwamba maeneo yale yanapandishwa hadhi na sasa Burigi na Kimisi yatakuwa ni mojawapo ya Hifadhi za Taifa. Kwa hiyo, itakuwa ni hadhi ya juu kabisa ya uhifadhi katika nchi yetu. Kwa kweli hongereni sana.
Mheshimiwa Spika, sasa baada ya kupandisha hadhi maeneo hayo, hatua inayofuata sasa ni kuhakikisha kwamba miundombinu ya maeneo yote yale inaimarishwa, barabara zipitike wakati wote ili kusudi watalii waweze kutembelea katika yale maeneo na Serikali iweze kupata fedha nyingi zinazotokana na mapato ya utalii. Kwa hiyo, hilo litafanyika.
Swali la pili, kuhusu kuambatana naye kwenda katika maeneo hayo, naomba nimhakikishie tu kwamba mara baada ya Mkutano huu wa Bunge tutaambatana pamoja, kwa sababu tunataka kwenda kuangalia sasa baada ya kupandisha hadhi mapori yetu yote yale matano, tuone je, nini kinatakiwa kufanyika? Tufanyeje kuhakikisha kwamba utalii sasa unakua katika ile Kanda ya Magharibi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli hilo lote, tutalifanya vizuri kabisa na ninaomba tushirikiane ili tuweze kufanyakazi vizuri zaidi.
MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Kutokana na swali la msingi la ubovu wa barabara ya Serengeti, Wizara ya Maliasili inaniambiaje; kwa sababu barabara zimekuwa mbovu, Hoteli ya Seronera, Lobo, Ngorongoro na Lake Manyara zilikuwa ni hoteli katika nchi hii katika Hifadhi ya Serengeti? Leo hii watalii wakienda, wanabebewa maji kwenye ndoo. Wizara inayajua hayo? Inazirudisha lini hoteli hizi Serikalini? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba tulikuwa na hoteli ambazo zilikuwa zinamilikiwa na Serikali katika miaka ya nyuma na hoteli hizi nyingi zilibinafsishwa. Kati ya hoteli 17 ambazo zilikuwa zimebinafsishwa ilionekana karibu hoteli 11 zilikuwa hazifanyi vizuri ikiwemo hizi hoteli chache ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tumeliona hilo, tumeanza kufuatilia kupitia mikataba ile ambayo walipewa ili kuhakikisha kwamba kama tumeona kwamba hawakufanya yale waliyostahili kuyafanya na uwekezaji waliotakiwa kuufanya, Serikali iweze kuzichukua hizo hoteli na kuwapa wawekezaji wengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baadhi ya hoteli sasa hivi zimechukua hatua, zinaboresha huduma zao. Hili analolisema la maji, kwa kweli sasa litaendelea kupungua hasa baada ya kuanza kutekeleza miradi mbalimbali ya kuhakikisha maji yanakuwepo katika maeneo hayo. (Makofi)
MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Katika Mkoa wetu wa Rukwa tumejaaliwa kuwa na maporomoko ya Kalambo ambayo kama Mkoa sisi tumejipanga.
Sasa napenda kujua katika Wizara ya Maliasili na Utalii mmejipangaje katika kutengeneza mazingira rafiki ili kuweza kuwavutia watalii?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba katika Mkoa wa Rukwa tunalo eneo lile la maporomoko ya Kalambo ambayo ni maporomoko ya aina yake ambayo tena ni urithi wa dunia. Kwa kweli lile eneo ni zuri sana. Baada ya kuona hivyo, mimi mwenyewe nimefika pale kuangalia mazingira yalivyo, tumechukua hatua ya kuanza kujenga ngazi kubwa ambayo inatoka kule juu kushuka kule chini ambayo ni mita karibu 230. Tunatarajia lile daraja litasaidia sana katika kuboresha na kuvutia watalii kuweza kutembelea yale maporomoko.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ya pili, tumewaagiza Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) kuhakikisha kwamba wanawekeza katika lile eneo; wanaweka hoteli ambayo itakuwa ndiyo kivutio kizuri cha kuwavutia watalii katika lile eneo kusudi waweze kutumia muda mrefu wa kukaa katika lile eneo. Ni tofauti na sasa hivi ambapo unakuta kwamba wenzetu wa Zambia wameweka hoteli upande wao, lakini upande wetu huduma hizi zimekuwa hazipo. Hivyo tumekuwa tukikosa watalii. Nina imani baada ya kuchukua hizi hatua, sasa watalii wataongezeka sana kwa upande wa Tanzania kwa sababu ndiyo sehemu pakee unayoweza ukaiona Kalambo vizuri kuliko maeneo mengine.
MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa nafasi. Changamoto zilizopo maeneo ya Serengeti na kwingine, zinafanana kabisa na Mbuga yetu ya Katavi ambayo inakosa watalii kutokana na miundombinu mibovu.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ndani ya Mbuga ya Katavi ili kuvutia watalii?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba tunayo hifadhi kubwa ya Katavi ambayo ina wanyama wa kila aina.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa Setikali imechukua hatua mbalimbali za kuhakikisha kwamba kwanza tunaboresha miundombinu iliyopo ndani ya ile hifadhi ili tuweze kuwavutia watalii wengi kutoka maeneo mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua nyingine ni kwa sababu ule uwanja wa Ndege wa Katavi umekuwa mzuri kabisa na tunaamini katika hizi jitihada ambazo Serikali imechukua za kuongeza ndege, basi safari za ndege zikianza kutumia uwanja ule wa Katavi basi ina maana watalii wataongezeka sana katika lile eneo na hivyo miundombinu ikiwa inapitika, watalii wengi sana wataweza kuvutiwa na kutembelea katika ile mbuga ya Katavi.
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Waziri, wananchi wa vijiji vya Merenga, Machochwe, Nyamakendo, Mbalibali, Tamkeri, Bisarara, Mbilikili, Bonchugu, Miseke na Pakinyigoti wamenituma nimwombe Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli aende akawasikilize matatizo yao, lakini Mheshimiwa Rais, Dkt. Magufuli wa Wizara ya Maliasili na Utalii ni Mheshimiwa Waziri.
Je, uko tayari baada ya Bunge hili kuambatana na mimi kwenda kusikiliza matatizo yao? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Wananchi wa vijiji vilivyopo kando kando ya Hifadhi ya Serengeti, mapori ya akiba ya Ikorongo na Gurumeti pamoja na Ikoo na WMA kazi yao kubwa ilikuwa ni uwindaji, ufugaji na kilimo. Uwindaji sasa hivi hawawindi, maana wakienda kuwinda hawarudi; mifugo yao imetaifishwa; mazao yao ya kilimo tembo wanakula; ninyi kama Wizara, nini mbadala mnaowasaidia wananchi wa maeneo haya ili waweze kujikimu kiuchumi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba kwanza naomba nimhakikishie tu kwamba niko tayari wakati wowote pale ambapo muda utaruhusu tutapanga, lazima twende tukatembelee katika yale maeneo. Hiyo inatokana na kwamba sasa hivi tuna mpango kabambe wa kuhakikisha kwamba maeneo yote yanayopakana na Hifadhi za Taifa, lazima vijiji vyote vile vipimwe vizuri, tuweke mipaka vizuri lakini pia tuimarishe ule ulinzi katika yale maeneo hasa kule ambako kumekuwa na changamoto nyingi ambapo wanyamapori wamekuwa wakiharibu mazao na shughuli za wananchi wanazofanya katika yale maeneo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, pia tutaweka minara, pamoja na kutumia ndege zisizokuwa na Rubani. Kwa hiyo, mambo mengi tutayafanya kuhakikisha kwamba haya yanafanyika. Ili kufanya hayo, lazima tufike na tuone kwamba wananchi wanaondokana na hizi changamoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu hatua mbadala; sasa hivi tunatoa elimu ni nini kinaweza kufanyika katika yale maeneo yaliyo jirani na hifadhi? Kwa sababu ukipanda yale mazao ambayo wanyamapori wanayapenda, ni wazi kabisa kwamba yataliwa na wanyamapori. Ukipanda yale mazao ambayo wanyamapori hawayapendi, wanayaogopa, basi kidogo hii itasaidia.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutakwenda kukaa pamoja na Mheshimiwa Mbunge na wananchi kwa pamoja, tutashauriana kuona ni aina gani ya mazao ambayo wananchi wa maeneo yale watashauriwa kwamba wayapande ili kuondokana na hii migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza katika hayo maeneo. (Makofi)
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza naishukuru Serikali kwa kutoa kifuta machozi takribani milioni nane kwa ajili ya wananchi waliopoteza maisha yao na wale walioathiriwa na wanyama wakali.
Mheshimiwa Naibu Spika, mnamo mwaka 2016 Serikali iliahidi kufanya ziara katika Tarafa ya Daudi na Tarafa ya Ndekoti kwa ajili ya wananchi ambao mali zao na mazao yameharibiwa na wanyama wakali, lakini hadi sasa Serikali haijatimiza ahadi yake hiyo kwa kuwa wale waliokuwa kwenye Wizara walibadilishwa.
Je, ni lini Serikali itafanya ziara katika Tarafa ya Daudi na Tarafa ya Ndekoti kwa ajili ya wananchi ambao mali zao zimeathiriwa na wanyama ikiwemo mazao na hawajapata kufidiwa hadi sasa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba inawezekana kulikuwa na ahadi ya kwamba viongozi wa Kitaifa wataenda kutembelea katika lile eneo.
Naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hata kama viongozi wa kitaifa hawajafika, bado wapo Watendaji wetu ambao lazima wafike katika yale maeneo na wahakikishe kwamba wanahakiki mali zilizopotea, wanahakiki uharibifu uliofanyika kusudi wale wananchi wanaostahili kupewa kile kifuta jasho au kifuta machozi, waweze kulipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa nafasi hii, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba leo hii nitawaagiza watendaji wafike katika lile eneo ili wakutane na hao wananchi, wafanye tathmini na tuone ni kiasi gani wananchi wale wanastahili kulipwa kwa mujibu wa kanuni zetu tulizonazo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu utayari, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakuwa tayari, tutakuja pia kuhakikisha kwamba haya yote yanatekelezeka na wananchi waweze kuona kwamba Serikali yao inawajali vizuri. (Makofi)
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa matatizo yaliyopo katika Jimbo la Serengeti yanafanana kabisa na matatizo yaliyopo katika Jimbo la Kavuu hasa katika Kata za Chamalendi, Mwamapuli, Majimoto na vitongoji vyake; kumekuwa na matatizo ambayo wananchi hasa wafugaji wamekuwa wakisukumizwa na askari wa wanyamapori ndani ya Mbuga ya Katavi na wamekuwa wakipotea na mara nyingi wakiwa wakitafutwa na ndugu zao ni nguo tu zinapatikana:-
Je, Serikali inasema nini sasa kwa ujumla kuhusu askari wote wa wanyamapori wanaofanya kazi katika mbuga zote za National Park katika kuhakikisha usalama wa wale wanaowaita majangili wakati sio majangili? Kwa sababu tu wanakuwa wameingia kwenye mbuga, kwa hiyo, wataitwa majangili.
Je, Serikali inasema nini kuhusu Askari hao ambao wamekuwa wakiwateka wananchi na kuwapora ng’ombe zao na mali…
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba niseme tu kwamba sina taarifa kamili kwamba askari wetu wamekuwa wakiwakamata watu na kuwaingiza kwenye hifadhi halafu wanapotea moja kwa moja. Hizo taarifa hatunazo kama Serikali na kama Mheshimiwa Mbunge anazo na anao ushahidi wa namna hiyo, basi nitaomba nikae naye ili aweze kunipa hayo majina ya watu ambao wamepotea kusudi Serikali iweze kuchukua hatua zinazostahili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu namna ya kuboresha yale maeneo, naomba nitumie nafasi hii kuwaomba wananchi wote wanaopakana na hifadhi zetu kuhakikisha kwamba wanazingatia taratibu, sheria, kanuni na miongozo iliyopo. Hawaruhusiwi kuingia bila kibali kwenye hifadhi. Kwa kawaida ukiingia kwenye hifadhi bila kibali, ni vigumu sana kujua yupi ni jangili, yupi sio jangili. Kwa hiyo, ili kuweza kuondokana na hilo, ni kuwaomba wananchi kutoingia katika maeneo ya hifadhi ili kusudi tuondokane na hilo tatizo.
MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba nimuulize Naibu Waziri maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, pamoja na Serikali kutoa elimu katika sekta hii ya vyuo vya utalii, lakini wamekuwa wakichukua wanafunzi ambao wamefeli au wanapata division four na kutofanya vizuri katika vyuo vingi na kusababisha hoteli nyingi za kitalii kuajiri wafanyakazi kutoka nje. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha vyuo vya utalii ili kuhakikisha wanachukua wale wanafunzi ambao wanafanya vizuri ili sekta hii iweze kufanya vizuri katika anga za kimataifa na hapa nchini? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa wenzetu Kenya, kwa mfano unatokea London unafika Airport ya Kenya, watalii wengi wanashuka sana Kenya na unaona ni namna gani wenzetu wamejitangaza katika sekta hii ya utalii na kupunguza tozo katika suala la utalii. Nauliza Serikali, je, haini sasa kuna umuhimu wa kupunguza kodi katika sekta hizi za utalii ili tuweze kufanya vizuri na kuingiza Pato la Taifa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba kumekuwa na upungufu wa wataalam katika Sekta hii ya Utalii na ndiyo maana kwa kuliona hilo, Serikali imechukua hatua ya kuhakikisha kwamba kwanza tunakiimarisha chuo chetu cha utalii ili kiweze kutoa mafunzo. Kwa hivi sasa kilikuwa kinatoa mafunzo katika ngazi ya stashahada na astashahada, lakini kuanzia mwaka 2019 kwa ushirikiano pamoja na chuo cha Canada (Vancouver) tumeamua kwamba sasa tuanzishe programme ya kutoa degree, degree hizo zitasaidia kuandaa wataalam mbalimbali ambao watashiriki katika sekta ya utalii. Baadhi ya degree ambazo tunategemea kuzianza ni hizi zifuatazo:-
(i) Digrii ya ukarimu (degree in hospitality operations) ;
(ii) Digrii ya Utalii (degree in travel and tourism management) na
(iii) Digrii ya Utaratibu wa Matukio (degree in events management)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo katika hizi degree tatu zitakapoanza ni imani yetu kwamba tutakuwa tunaweza kupata wataalam wale ambao sasa watakuwa wanatoka hapa hapa nchini na kuweza kuhudumia vizuri sekta hii ya utalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo pia tunawahamasisha wawekezaji katika vyuo vingine vya binafsi waweze kuwekeza katika eneo hili kwa sababu sasa hivi mahitaji bado ni makubwa na wataalam bado ni wachache.
Mheshimiwa Naibu Spika, hili la kwamba tunachukua wale waliofeli, si kweli. Kwa mujibu wa taratibu zilizopo katika nchi hii, watu wote waliomaliza hata kama yuko division four kama ana ‘D’ nne na kuendelea anaruhusiwa kujifunza na ngazi ya cheti (astashahada) na akifaulu anaendelea katika ngazi ya stashahada. Kwa hiyo, nadhani kwamba mkakati huu bado hatuchukui wale ambao ni failure, tunachukua wale ambao wana sifa za kujiunga na hivi vyuo.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili kuhusu kupunguza kodi katika huduma mbalimbali za utalii; ni azma ya Serikali ya Awamu ya Tano kuhakikisha kwamba kodi hizi zinapunguzwa ili wawekezaji na watu mbalimbali waweze kushiriki katika hizi shughuli za utalii; na mmesikiliza katika hatua mbalimbali ambazo tumechukua. Hivi sasa bado tunaendelea kutazama ni aina gani za kodi ambazo zinaweza zikapunguzwa zaidi ili kusudi hii sekta iweze kuimarika zaidi nchini. (Makofi)

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nimependa niongeze majibu ya nyongeza kutokana na majibu mazuri aliyoyatoa Mheshimiwa Naibu Waziri kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na jitihada tunazofanya za kuongeza kozi ambazo zinatolewa kwenye Chuo chetu cha Utalii lakini pia tunatambua kwamba sekta ya utalii pamoja na kwamba inaajiri watu zaidi ya 1,500,000 Chuo chetu cha Utalii toka kimeanza kimetoa wahitimu wasiozidi 5,000. Kwa maana hiyo wanaofanya kazi kwenye hoteli si lazima kwamba wanatoka kwenye chuo chetu cha utalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua hilo na kwa kutambua kwamba kuna wadau wengine ambao wanatoa taaluma ambazo zinatumika kutoa huduma kwenye sekta ya utalii kama VETA na vyuo vingine ambavyo vimesajiliwa na NACTE, tumeona tuanzishe mtihani wa Kitaifa ambao utaweka standard pamoja zote kwa usawa ili kila anayehitimu atoke kokote kule anakotoka afanye huo mtihani, aingie katika vigezo ambavyo vitakuwa vinatambulika kitaifa na sasa ndiyo aende kuajiriwa kwenye sekta ya utalii. Kwa sababu tunaamini, ili tuweze kupata watalii wengi, ni lazima tuongeze ubora wa huduma tunazotoa ili watalii wapate experience nzuri na wanapoenda kule kwao warudi tena kutalii lakini pia waseme maneno mazuri kwa watu wengine katika cycles of influence zao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo pamoja na jitihada hizo, tumetunga kanuni za kufanya certification ya professionals wanaotaka kuajiriwa kwenye sekta ya utalii, lakini pia tunaanzisha mafunzo ya Uanagenzi katika hoteli na maeneo yote ya utalii ili ku-boost kidogo quality ya watoa huduma kwenye Sekta ya Utalii. (Makofi)
MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kw akunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Manyoni hususan Jimbo la Manyoni Mashariki tunavyo vivutio vingi sana vya utalii. Kwa mfano, tunazo kumbukumbu ya kituo kikubwa cha msafara wa watumwa wa njia ya kati kuanzia Ujiji, Unyanyembe kwenda Bagamoyo, lakini pia tunayo kumbukumbu ya ngome kuu ya Wajerumani iliyotumika kupambana na Mtemi Mkwawa wa huko Uheheni; lakini pia tuna jiwe la picha ya Bikira Maria kule Iseke. Je, Serikali iko tayari kusaidia kutangaza vivutio hivi ili kuinua kiwango cha ajira? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa, mimi mwenyewe juzi Jumamosi nilikuwa kule Wilaya ya Manyoni na nimetembelea katika maeneo yote aliyoyataja na kuona utajiri mkubwa ambao Wilaya ya Manyoni inao hasa katika haya maeneo ambayo ameyataja.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ambazo tunategemea kuchukua kama Wizara ni kwamba tutakwenda tutatangaza sasa vivutio vyote vile pamoja na historia nzuri ambayo ipo pale. Kuna jiwe moja ambali linajulikana kama jiwe la mjusi lakini zaidi ya hapo tumefika sehemu ambayo tunaita ndipo kitovu cha nchi hii yaani katikati ya Tanzania. Kuna maeneo mengi sana yenye vivutio vizuri sana kule Manyoni ambayo tutayatangaza sanjari na hatua ambazo tunazichukua katika kutangaza utalii katika maeneo yote nchini. (Makofi)
MHE. RISALA S. KABONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa wamiliki wengi wa hoteli za kitalii wanatumia wanafunzi waliopo kwenye mafunzo ya vitendo kufanya kazi za kuhudumia watalii na baada ya muda huo hawaajiriwi. Mchezo huu unasababisha ukosefu wa ajira kwa wahitimu kwa muda mrefu na kuikosesha Serikali mapato. Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua taizo hili? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza yeye mwenyewe ni mhifadhi mzuri sana, kwa hiyo nampongeza sana kwa kuwa mhifadhi mzuri na naamini atatumia taaluma yake vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kwamba, hoteli nyingi zimekuwa kweli zinawapokea vijana wanaotoka katika vyuo mbalimbali kwa ajili ya kupata field yaani kupata uzoefu ili waweze kwenda kuajirika katika maeneo mbalimbali. Hii ni hatua nzuri. Kwa hiyo, nafikiri hii ni ya kui- encourage zaidi ili kusudi hoteli nyingi zipokee hao vijana wetu, wafundishwe namna ya kufanya kazi kwa vitendo ili wanapoajiriwa pale waweze kutumia taaluma zao vizuri na waweze kufanya kazi ya kutoa huduma ile ambayo inastahili.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili, kuhusu ajira, ni kwamba tutaendelea kuhamasisha wawekezaji na hoteli mbalimbali ili ziweze kuwapokea vijana wetu ambao wamehitimu katika vyuo mbalimbali ili waweze kuajiriwa na waweze kutoa ile huduma nzuri. Pamoja na yale majibu ambayo Mheshimiwa Waziri ameshayatoa, basi jitihada hizi tunaamini kabisa kwamba zitasaidia sana katika kuboresha suala la ajira hapa nchini. (Makofi)
MHE. ALFREDINA A. KAHIGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa Serikali iko pamoja na Halmashauri ya Wilaya kudhibiti wanyama hawa waharibifu, je, Serikali haioni umuhimu wa kuhakikisha kuwa inawapatia vifaa vya kutosha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tunaelewa kuwa wanyama hawa ni waharibifu, je, hakuna njia nyingine ya kuwadhibiti wanyama hawa badala ya kuwauwa? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Alfredina Apolinary Kahigi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza kwa jinsi ambavyo amekuwa akishirikiana na Serikali katika kufuatilia masuala haya. Niseme tu kama nilivyokuwa nimesema kwenye swali la msingi, tumechukua hatua kadhaa katika kuhakikisha tunawadhibiti wanyamapori wakali na waharibifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ambayo ipo, ni kweli kabisa vifaa vya kudhibiti bado havitoshi hata hivyo tunaendelea kujipanga vizuri kuhakikisha kwamba tunapata vifaa vya kisasa vitakavyosaidia kuwadhibiti wanyamapori wakali na waharibifu katika maeneo yote ikiwa ni pamoja na kutumia zile ndege zisizowakuwa na rubani lakini pia kufanya shughuli nyingine ambazo zitawafukuza wale wanyamapori kusudi wasilete uharibifu ule ambao umekuwa ukijitokeza katika maeneo mengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, ni kweli kabisa hatupendekezi na hatushauri watu kuwaua wanyamapori, kwa sababu wanyamapori wanayo haki ya kuishi katika nchi hii kama Mungu alivyofanya uumbaji yeye mwenyewe kwamba lazima viwepo hapa duniani. Kwa hiyo, hizi ni maliasili ambazo lazima zilindwe. Hata hivyo, pale inapoonekana kwamba wamekuwa wengi tunafanya uvunaji endelevu ndipo hapo tunaweza kuwaua. Ngedere wakizidi ndiyo tunawaua otherwise tunakuwa na idadi ambayo lazima iendelee kuwepo na hatushauri viongozi wetu au wafanyakazi wetu kuwaua wanyama hao.
MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wengi katika Wilaya ya Urambo wanateseka kutokana na migogoro iliyopo kwenye mapori ya hifadhi. Nichukue nafasi hii kumshukuru Naibu Waziri ambaye anajibu maswali sasa hivi alikuja kumaliza migogoro ile lakini haikuwezekana kutokana na muda mfupi uliokuwepo. Je, anatuambia nini sisi wananchi wa Urambo atakuja kumaliza migogoro iliyopo Runyeta ambako walichomewa nyumba zao na mazao yao, Tevera katika Kata ya Uyumbu na Ukondamoyo ambayo bado kuna mchuano mkubwa sana ambapo wananchi wamekosa mahali pa kulima kutokana na migogoro ya misitu?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Sitta, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza kwa jinsi ambavyo amefanya kazi nzuri ya kuhamasisha wadau mbalimbali kuhakikisha fedha zinapatikana kwa ajili ya ujenzi wa vyoo katika shule zetu. Hongera sana mama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa nilishafika katika eneo lile, nilikutana na wananchi na tukajadiliana juu ya mgogoro uliopo na Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii atatembelea eneo lile ili aweze kukutana na wananchi na kuhakikisha kwamba sasa ule mgogoro ambao ulikuwepo muda mrefu unaisha mara moja. Kwa hiyo, naomba asubiri kidogo Waziri ataenda katika eneo hilo na sasa watakaa pamoja kulitafutia uvumbuzi wa kudumu tatizo hilo.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Mwaka 2015/2016 wanyama wakali walipoteza maisha ya wananchi watano katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu. Hivi sasa Halmashauri ya Mbulu toka ianzishwe mwaka 2015 haina Maafisa wa Wanyamapori. Je, ni lini Serikali yetu itatusaidia kutupatia Askari wa Wanyamapori katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zacharia Issaay, Mbunge wa Mbulu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kumekuwa na upungufu wa wafanyakazi katika maeneo mengi ikiwemo Maafisa Wanyamapori. Katika jitihada ambazo zinafanyika sasa hivi tumeweka kwenye bajeti inayokuja kuangalia kama tunaweza kupata wafanyakazi wachache ambao tutawasambaza katika wilaya mbalimbali hapa nchini. Naomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira hilo likikamilika tutafikiria Wilaya ya Mbulu ili waweze kupata wafanyakazi hao.
MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Awali ya yote, nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kufanya ziara Jimboni kwangu Mikumi, pindi ambapo simba walivamia zizi la mwanakijiji wetu pale Kikwalaza na akaweza kuzungumza na wananchi. Pia alifanikiwa kwenda Ruhembe, bahati mbaya sana ni kwamba Mheshimiwa Naibu Waziri hakuwasiliza wananchi bali alisikiliza haya ambayo anaambiwa na viongozi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza niseme tu, kama kweli tunaipenda nchi yetu, sisi tunajua kwamba kuwa na Hifadhi ya Taifa ya Mikumi siyo laana bali ni baraka kutoka kwa Mungu, lakini ukweli ni kwamba wananchi wa Kata ya Ruhembe, Kijiji cha Kitete Msindazi na Kielezo wanateseka sana kwa sababu ya kunyimwa haki zao za msingi za kuishi maeneo yale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwambie tu Mheshimiwa Naibu Waziri, pamoja na ziara aliyoifanya, yale yote aliyoyazungumza kule hakuna hata kimoja kilichotekelezwa. Nimwombe asiwasikilize hawa wanaomwandikia hivi vitu, aje awasikilize wananchi wa Kata wa Ruhembe wamwambie A, B, C na vitu vingine vyote. Kwa hiyo, hiyo ndiyo rai yangu kwake kwamba namkaribisha tena Mikumi, azungumze na wananchi hawa viongozi wanaomwambia yote yamekamilika na kwamba kuna amani, wanafanyakazi yake iwe ngumu sana kwa kutokuwa na amani katika Kata yetu na Jimbo la Mikumi kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, sasa hivi wananchi wa Mikumi, napata ukakasi kusema kama wanapotea au wanachukuliwa na watu wasiojulikana, kuna watu wanatoka Usalama na TANAPA wananchi wa Mikumi wanakufa na wanapotea na wengine wanarudi wakiwa vilema kwa sababu tu wanaonekana kuchukuliwa katika hali ambayo haipo na tukiwatafuta katika Vituo vya Polisi hatuwapati, tunaambiwa wamepelekwa Dar es Salaam. Je, Serikali inasemaje kuhusu wananchi wa Mikumi wanaopotea? Mpaka sasa takribani wananchi 40 kutoka Kata za Muhenda, Ruhembe, Kidodi wamepotea hatujui wako wapi. Serikali inataka kutuambia nini kuhusu hawa ndugu zetu? Tumechoka kuzika nguo na ndugu zetu hatuwaoni? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Joseph Leonard Haule, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa nimeshatembelea eneo hilo na ni kweli kabisa nilikaa na wananchi tukaweza kuzungumza na wakabainisha mambo mengi na tuliyawekea mkakati wa namna ya kuyatatua. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kipindi kati ya sasa na mwezi Septemba, tena wakati nakwenda Kilombero, nitapita kwenye eneo hilo ili tuweze kukutana na hao wananchi ili tuone kama kweli matatizo yao yanaendelea kuwepo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu hao wananchi ambao anasema kwamba wanapotea bila sisi kujua, nadhani hizi taarifa kama Serikali hatunazo. Kama Mheshimiwa Mbunge anayo majina na anasema wananchi karibu 40 wote wamepotea, nadhani ni wakati muafaka tupatie hayo majina ili nasi Serikali tuweze kushirikiana na wananchi kubaini hao wananchi wote watakuwa wamekwenda wapi. Ni msimamo wetu kama Serikali kwamba kazi yetu ni kulinda wananchi na kuhakikisha wanaendelea kuishi vizuri na kufanya shughuli zao.
MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Maliasili ndani ya Jimbo la Mlimba wamepeleka barua kwamba wananchi wakulima na wafugaji mwezi Julai waondoke wakati wa mipaka ya bonde hilo haijafanyiwa kazi na Waziri aliunda timu, kwenda kurekebisha mipaka ya Ramsar. Nini kauli ya Serikali kuhusu vitisho kwa wananchi hawa ambao hata mazao yao hawajavuna?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Susan Kiwanga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa mnamo mwaka jana tulitembelea bonde lote na tukazungumza na wananchi. Wananchi waliomba badala ya kuhama katika kipindi kile wapatiwe muda wa kutosha wa kujiandaa na waweze kuvuna mazao yao ndipo wahame. Ndipo Serikali ikatoa agizo kwamba ifikapo mwisho wa mwezi Agosti, 2018 wananchi hao wote wawe wamehama na wamevuna mazao yao yote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kama unaniambia kwamba wameambiwa wahame mwezi wa Julai, ni kinyume na agizo tulilokuwa tumelitoa awali. Agizo la Serikali tulisema wananchi wale waachwe, wavune mazao yao lakini ikifika tarehe 31 Agosti, 2018, wananchi wote wawe wameshahama katika eneo hilo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Susan na wananchi wake waendelee kutulia, wavune kwa utaratibu ili kusudi wahamie katika yale maeneo ambayo watakuwa wameelekezwa na Serikali.
MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Ni lini Serikali itatatua mgogoro wa muda mrefu wa mpaka kati ya Hifadhi ya Uwanda na Vijiji vya Ilambo, Mpande, Kilangawana, Legeza, Kapenta, Mkusi na Iwelamvua ili kuondoa manyanyaso ambayo wananchi wanapata kwa kunyang’anywa mazao, vifaa vyao vya kilimo na kuwapiga na mwaka juzi mtu mmoja aliuwawa? Ni lini Serikali itatatua mgogoro huu?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Malocha, Mbunge machachari kweli kweli, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba kumekuwepo na changamoto ya mgogoro ambayo imekuwepo katika eneo lile. Hivi sasa tumejipanga katika kipindi hiki, Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii atakwenda kuona eneo hilo. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane ili kusudi apate ratiba kamili ni lini atakuja, mtatembelea maeneo ya vijiji vyote hivyo na kuona ni hatua gani zichukuliwe kuhakikisha kwamba hiyo migogoro ambayo imedumu muda mrefu basi yote inatatuliwa kwa kipindi hiki.
MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Awali ya yote, nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kufanya ziara Jimboni kwangu Mikumi, pindi ambapo simba walivamia zizi la mwanakijiji wetu pale Kikwalaza na akaweza kuzungumza na wananchi. Pia alifanikiwa kwenda Ruhembe, bahati mbaya sana ni kwamba Mheshimiwa Naibu Waziri hakuwasiliza wananchi bali alisikiliza haya ambayo anaambiwa na viongozi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza niseme tu, kama kweli tunaipenda nchi yetu, sisi tunajua kwamba kuwa na Hifadhi ya Taifa ya Mikumi siyo laana bali ni baraka kutoka kwa Mungu, lakini ukweli ni kwamba wananchi wa Kata ya Ruhembe, Kijiji cha Kitete Msindazi na Kielezo wanateseka sana kwa sababu ya kunyimwa haki zao za msingi za kuishi maeneo yale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwambie tu Mheshimiwa Naibu Waziri, pamoja na ziara aliyoifanya, yale yote aliyoyazungumza kule hakuna hata kimoja kilichotekelezwa. Nimwombe asiwasikilize hawa wanaomwandikia hivi vitu, aje awasikilize wananchi wa Kata wa Ruhembe wamwambie A, B, C na vitu vingine vyote. Kwa hiyo, hiyo ndiyo rai yangu kwake kwamba namkaribisha tena Mikumi, azungumze na wananchi hawa viongozi wanaomwambia yote yamekamilika na kwamba kuna amani, wanafanyakazi yake iwe ngumu sana kwa kutokuwa na amani katika Kata yetu na Jimbo la Mikumi kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, sasa hivi wananchi wa Mikumi, napata ukakasi kusema kama wanapotea au wanachukuliwa na watu wasiojulikana, kuna watu wanatoka Usalama na TANAPA wananchi wa Mikumi wanakufa na wanapotea na wengine wanarudi wakiwa vilema kwa sababu tu wanaonekana kuchukuliwa katika hali ambayo haipo na tukiwatafuta katika Vituo vya Polisi hatuwapati, tunaambiwa wamepelekwa Dar es Salaam. Je, Serikali inasemaje kuhusu wananchi wa Mikumi wanaopotea? Mpaka sasa takribani wananchi 40 kutoka Kata za Muhenda, Ruhembe, Kidodi wamepotea hatujui wako wapi. Serikali inataka kutuambia nini kuhusu hawa ndugu zetu? Tumechoka kuzika nguo na ndugu zetu hatuwaoni? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Joseph Leonard Haule, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa nimeshatembelea eneo hilo na ni kweli kabisa nilikaa na wananchi tukaweza kuzungumza na wakabainisha mambo mengi na tuliyawekea mkakati wa namna ya kuyatatua. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kipindi kati ya sasa na mwezi Septemba, tena wakati nakwenda Kilombero, nitapita kwenye eneo hilo ili tuweze kukutana na hao wananchi ili tuone kama kweli matatizo yao yanaendelea kuwepo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu hao wananchi ambao anasema kwamba wanapotea bila sisi kujua, nadhani hizi taarifa kama Serikali hatunazo. Kama Mheshimiwa Mbunge anayo majina na anasema wananchi karibu 40 wote wamepotea, nadhani ni wakati muafaka tupatie hayo majina ili nasi Serikali tuweze kushirikiana na wananchi kubaini hao wananchi wote watakuwa wamekwenda wapi. Ni msimamo wetu kama Serikali kwamba kazi yetu ni kulinda wananchi na kuhakikisha wanaendelea kuishi vizuri na kufanya shughuli zao.
MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Maliasili ndani ya Jimbo la Mlimba wamepeleka barua kwamba wananchi wakulima na wafugaji mwezi Julai waondoke wakati wa mipaka ya bonde hilo haijafanyiwa kazi na Waziri aliunda timu, kwenda kurekebisha mipaka ya Ramsar. Nini kauli ya Serikali kuhusu vitisho kwa wananchi hawa ambao hata mazao yao hawajavuna?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Susan Kiwanga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa mnamo mwaka jana tulitembelea bonde lote na tukazungumza na wananchi. Wananchi waliomba badala ya kuhama katika kipindi kile wapatiwe muda wa kutosha wa kujiandaa na waweze kuvuna mazao yao ndipo wahame. Ndipo Serikali ikatoa agizo kwamba ifikapo mwisho wa mwezi Agosti, 2018 wananchi hao wote wawe wamehama na wamevuna mazao yao yote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kama unaniambia kwamba wameambiwa wahame mwezi wa Julai, ni kinyume na agizo tulilokuwa tumelitoa awali. Agizo la Serikali tulisema wananchi wale waachwe, wavune mazao yao lakini ikifika tarehe 31 Agosti, 2018, wananchi wote wawe wameshahama katika eneo hilo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Susan na wananchi wake waendelee kutulia, wavune kwa utaratibu ili kusudi wahamie katika yale maeneo ambayo watakuwa wameelekezwa na Serikali.
MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Ni lini Serikali itatatua mgogoro wa muda mrefu wa mpaka kati ya Hifadhi ya Uwanda na Vijiji vya Ilambo, Mpande, Kilangawana, Legeza, Kapenta, Mkusi na Iwelamvua ili kuondoa manyanyaso ambayo wananchi wanapata kwa kunyang’anywa mazao, vifaa vyao vya kilimo na kuwapiga na mwaka juzi mtu mmoja aliuwawa? Ni lini Serikali itatatua mgogoro huu?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Malocha, Mbunge machachari kweli kweli, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba kumekuwepo na changamoto ya mgogoro ambayo imekuwepo katika eneo lile. Hivi sasa tumejipanga katika kipindi hiki, Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii atakwenda kuona eneo hilo. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane ili kusudi apate ratiba kamili ni lini atakuja, mtatembelea maeneo ya vijiji vyote hivyo na kuona ni hatua gani zichukuliwe kuhakikisha kwamba hiyo migogoro ambayo imedumu muda mrefu basi yote inatatuliwa kwa kipindi hiki.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa, kila mwaka wananchi wa Monduli wamekuwa wakipoteza mali lakini pia kupoteza maisha kutokana na uharibifu huu; na Mheshimiwa Naibu Waziri kutokana na takwimu ulizoziwasilisha hapa si kweli kwamba ni vijiji vyote vimelipwa. Kuna vijiji vya Moita, Naiti, Mswakini, Makuyuni na Isilalei wananchi hawa hawajalipwa fidia kwa mwaka 2014/2015, 2015/2016, 2016/2017. Je, ni lini sasa Serikali mtawalipa wananchi hao ambao wamepata uharibifu mkubwa na wamesubiri kwa muda mrefu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Kanuni hii ya Kifuta Jasho na Kifuta Machozi ambayo imekuwa ikitumika kwa wananchi ambao kwa namna moja ama nyingine mazao yao au mali zao zimeharibiwa na wanyamapori katika nchi hii imepitwa na wakati na kwa kweli imewaletea wananchi usumbufu mkubwa sana kwa sababu wananchi hao mali zao zinaharibika kwa kiwango kikubwa na wanachokuja kulipwa hakilingani na uhalisia. Je, Serikali sasa haioni ni wakati mwafaka kuendana na hali ya sasa na thamani ya fedha ya sasa kubadili kanuni hii ili kulipa uhalisia wa uharibifu unaofanywa na wanyamapori?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba si vijiji vyote ambavyo vimeshalipwa fidia. Hivi sasa naomba nilitaarifu Bunge lako tukufu kwamba madai ambayo yamepokelewa kutoka katika wilaya mbalimbali hapa nchini yalifika takribani 15,370 na madai ambayo yameshalipwa tayari ni 6,185. Kwa hiyo, utaona kwamba kuna madai karibu 9,562 ambayo bado hayajahakikiwa na bado hayajalipwa, hivi sasa zaidi ya shilingi milioni 828 zinadaiwa. Kwa hiyo, baada ya zoezi la uhakiki kukamilika vijiji vyote hivyo vitapata fidia na kifuta machozi hicho ambacho tumekisema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia kulitaarifu Bunge lako tukufu kwamba hivi sasa tunafanya mapitio ya Kanuni za Kifuta jasho na Kifuta Machozi za Mwaka 2011. Mara tu zitakapokamilika kupitiwa na kuidhinishwa, basi haya masuala yote ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyasema yataangaliwa. Ahsante sana.
MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, nimshukuru kwanza Naibu Waziri kwa majibu mazuri sana, lakini kwa ujumla niwashukuru watu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Waziri na viongozi wake wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo hili la wanyama waharibifu, hasa tembo, katika Jimbo la Bunda na kwa kata tatu ambazo zina vijiji 18 ni kubwa sana. Nikiangalia toka tuanze kulipa haya malipo ya fidia, ni mabilioni ya hela yanaenda na nimeona hapa tumekuwa na mikakati mingi, kuweka ukuta, kuweka pilipili na kuchimba mitaro na wengine huko vijijini kwenye Jimbo la Bunda wanasema tembo hawa hawana uzazi wa mpango, mnasema tembo wamepungua lakini ni wengi sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuuliza, ni lini sasa mikakati halisi ya Serikali itakuwepo ya kuzuia mnyama tembo ili kutoleta umaskini kwenye maeneo ya kwetu? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba katika eneo la Serengeti, na hasa katika Jimbo la Bunda kumekuwa na matatizo hayo na changamoto hizo ambazo zimekuwa zikijitokeza. Suala ni lini hasa tutakuja na mipango, sasa hivi tunakuja na mpango mkakati ambao tutausema tutakapokuwa tunawasilisha bajeti yetu ya mwaka 2018/2019, ni hatua gani ambazo tunategemea kuchukua katika maeneo mbalimbali ya Hifadhi za Taifa na maeneo mengine ya mapori ya akiba ili kukabiliana na changamoto hizi za wanyama waharibifu.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba tu aendelee kutusubiri, pale tutakapowasilisha bajeti yetu basi atuunge mkono ilia one hizo hatua ambazo tunakwenda kuchukua ambazo ndizo zitakazokuwa suluhu ya changamoto mbalimbali.
MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri sana. Kwanza niishukuru Serikali kwa kutengeneza hilo greda ambalo sasa kwa kweli litasaidia sana katika utengenezaji wa barabara kule kwenye Mapori yetu ya Akiba ya Kigosi Moyowosi. Sasa niombe kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, je, Serikali ina mpango gani wa kuipatia mapori haya ya akiba pesa kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya barabara katika mwaka ujao wa fedha ujao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kwa kuwa gari la Grand Tiger sasa hivi limeharibika na mapori haya mawili ni makubwa sana, je, Serikali iko tayari sasa kuyapatia haya mapori magari mawili kwa ajili ya kufanya doria na utawala katika maeneo hayo?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze kwa kazi kubwa ambayo umekuwa ukiifanya. Nakumbuka mwaka jana swali hilihili aliuliza na amekuwa akilifuatilia kwa karibu sana, hongera sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sababu tumeshalitengeneza lile greda sasa hivi tumeshatenga fedha za kutosha kwa ajili ya kukarabati na kutengeneza miundombinu mbalimbali katika ile hifadhi. Kwa hiyo, pale bajeti itakapowasilishwa ataona ni kiasi gani tutakuwa tumetenga katika hilo eneo kwa ajili ya kufanya hiyo kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu maombi ya gari; ni kweli kabisa hili gari ambalo nimesema kwamba tunaendelea kulitengeneza bado lina changamoto na tutalifufua. Lakini kwa nyongeza zaidi naomba nikuahidi kwamba tutakuongezea gari lingine moja ili yakiwa hayo mawili basi yataweza kufanya kazi nzuri sana katika hilo eneo. (Makofi)
MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa Pori la Hifadhi ya Swagaswaga ambalo lipo karibu na Dodoma lina wanyama wengi na kwa kuwa Dodoma sasa ni Makao Makuu ya nchi. Je, Wizara haioni sasa ipo haja ya kuliimarisha pori hili ili liwe sehemu ya kivutio kikubwa cha utalii kwa wageni wanaokuja katika Mkoa wa Dodoma?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juma Nkamia...(Kicheko) Kama ifuatavyo; samahani nimekosea jina lako.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba pori hili la Swagaswaga ni pori muhimu sana katika Mkoa huu wa Dodoma na hasa kwa kuzingatia kwamba sasa hizi hapa imekuwa ni Makao Makuu ya nchi. Kwa hiyo, tutachukua hatua mbalimbali za kuimarisha ili iwe ni kivutio cha utalii katika hili eneo na kuliwekea mikakati ya kutosha kusudi wananchi wengi ambao wanaishi katika Jiji hili la Dodoma waweze kutembelea katika hili eneo. Nikuhakikishie, kesho nitaenda kutembelea lile Pori la Mkungunero. Nikipata muda Jumapili nitapitia kwenye hilo eneo lingine ili tuone ni mikakati gani inaweza kufanyika tuweze kuimarisha utalii katika hili eneo.
MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mimi narudi kwenye swali la msingi. Ikolojia ya Kigosi Moyowosi inategemea sana uwepo wa Mto Malagarasi. Mto huu uko kwenye kitisho kikubwa cha kukauka kwa sababu mifugo imekuwa ni mingi. (Makofi)
Je, Wizara mnafanya nini kuokoa chepechepe (wetland) ya Mto Malagarasi ambayo imevamiwa na ng’ombe wengi na mpaka leo kuna ng’ombe zaidi ya 100,000 kwenye wetland ya Mto Malagarasi?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa swali la Mheshimiwa Daniel Nsanzugwanko. Naomba nimhakikishie tu kwamba katika lile eneo la Mto Malagarasi ni eneo muhimu sana kwa ajili kutoa maji na kusambaza katika maeneo muhimu kama ulivyokuwa umesema wewe mwenyewe. Ni kweli kabisa sasa hivi tunaweka jitihada, limevamiwa lile pori, kuna wanyama wengi, kuna mifugo mingi emeenda katika lile eneo, lakini lile eneo ni mojawapo ya maeneo ambayo yako kwenye Ramsar sites.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hivi sasa tunakuja na mkakati wa kutosha kabisa wa kuweza kuhakikisha kwamba hatua ya kwanza ilikuwa ni kuweka vigingi katika mipaka yetu ile Ramsar site. Bado zoezi halijakamilika, litakapokamilika naamini kabisa tutakuwa tumekuja na ufumbuzi kidogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ya pili, nitumie fursa hii kabisa kwamba mifugo hairuhusiwi katika maeneo ya hifadhi zozote kwa mujibu wa sheria. Ndiyo maana tukikamata hiyo mifugo, kwa kweli tunaipeleka mahakamani na hatua kali zitachukuliwa kwa watu wa namna hiyo.
Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutachukua hatua za makusudi za kuhakikisha kwamba mifugo yote katika eneo hilo inaondolewa mara ili kuhakikisha huo mto unaendelea kuwepo na uendelee kutusaidia katika matumizi mbalimbali.
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Katika hifadhi Serengeti National Park pamoja na Ngorongoro, hali ya barabara siyo mzuri na hususan kwenye kipande cha barabara kuanzia Ngorongoro getini mpaka lango la Serengeti National Park kuna udongo wa Volcano ambao hata watengeneze vipi, kwa muda mfupi unakuta ule udongo unaharibika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali haina mpango wowote wa kutengeneza ile barabara hata kwa kiwango cha zege ili kuondoa shida kubwa ambayo tunaipata watu tunaopita kwenye hiyo barabara?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampa hongera sana, amekuwa ni mdau mkubwa sana kwa sababu maeneo mengi, maliasili na hifadhi nyingi ziko katika eneo lake. Nafikiri nitakapokwenda kule, nitajua maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba sasa hivi Serikali inapitia maombi mbalimbali, inapitia utaratibu wa kuweka barabara ya kudumu ambayo inaanzia Karatu kupitia Ngorongoro mpaka Serengeti. Mara baada ya taratibu hizo kukamilika na clearance zote kufanyika, kwa sababu ni maeneo ya hifadhi, kumekuwa na mabishano makubwa juu ya aina ya barabara ambayo inatakiwa ijengwe.
Sasa hivi tumefikia hatua nzuri, makubaliano yanakuja na ninaamini kabisa kwamba baada ya muda mfupi tutaanza kuweka barabara ya kudumu ambayo ndiyo suluhu ya hilo tatizo ambao Mheshimiwa Mbunge amelisema.
MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Tumeshuhudia namna ambavyo Naibu Waziri anasisitiza kwa ukali kabisa kuchukuliwa hatua watu wanaoingiza mifugo hifadhini jambo ambalo ni sawa. Lakini anaongea kwa sauti ya chini na unyonge inapofikia kufidia mwananchi anayeharibiwa mazao na wanyama. Sasa kwa sababu Biharamulo asilimia 50 karibu ya eneo ni hifadhi na kwa sababu vijiji zaidi ya 15 kila mara wanaharibiwa mazao yao, yuko tayari twende tutathimini? Inawezekana akiona hali ile atajua namna Serikali ikae kutafuta namna ya kubadilisha approach ili tuwafidie wananchi badala ya kuwapa kifuta jasho? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa katika maeneo yale ya Biharamulo sehemu kubwa ni hifadhi na kumekuwa na changamoto mbalimbali hasa zikiwemo hizo za mifugo pamoja na uharibifu na uvamizi katika maeneo haya ya vijiji. Naomba nimhakikishie tu kwamba niko tayari wakati wowote tupange twende tukaangalie tuone ni maeneo gani na tuone mikakati gani tunaweza tukaifanya kwa kushirikiana na Serikali tuone hatua za kuchukua. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. ANNA J. GIDARYA: Mheshimiwa Spika, asante, nasikitika majibu ya Serikali kwa asilimia 90 ni uongo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, wananchi hawa walikaa kwenye hilo eneo miaka 20 iliyopita, fidia wanayosema ya kifuta jasho katika yale mabanda au tuseme zile nyumba waliwathaminishia TANAPA bila kuwashirikisha, kila mmoja fidia haikuzidi shilingi 300,000.
Mheshimiwa Spika, muda wote huo bila kuangalia riba wananchi walikaa mitaani na watoto wao waliathirika walikosa na masomo kwa sababu walifukuzwa watoto wakawa wanakaa kwenye nyumba za watu baki. Leo hii Serikali inasema imelipa, siamini katika hili. Mheshimiwa Waziri upo tayari kwenda Babati kwa ajili ya kuhakikisha kama mgogoro upo au haupo? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, TANAPA imelazimisha kuweka mipaka ya kudumu bila kuwashirikisha wahusika wenyewe wa mgogoro. Mkurugenzi anayezungumziwa kwamba amelipa, walienda kutoa amri yeye na Mkuu wa Wilaya mipaka ikawekwa, wananchi hawakushirikishwa, mgogoro huo haukuisha mpaka sasa. Lakini ni kwa nini sasa Serikali katika maeneo yenye migogoro ya hifadhi wamekuwa wakatili kupitiliza, wananchi hawa ni Watanzania au sio Watanzania?
Mheshimiwa Spika, tunaomba majibu ya Serikali ili tusiumane umane hapa kila siku tunarudia suala la Ayamango na Gedamar, ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia kuhusu haya maeneo na mgogoro huu, amekuwepo mstari wa mbele sana, hongera sana. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyosema, mgogoro huu umekuwepo kwa muda mrefu, lakini kilichokuwepo mwanzoni, hata hifadhi yenyewe ilikuwa bado haijajua mipaka yake na ndiyo maana mwaka 2004 walipoenda kuhakiki mipaka ilibainika kwamba hata baadhi ya maeneo ya hifadhi yalikuwa yako nje kwa sababu hata hifadhi yenyewe ilikuwa haijui. Lakini waliofanya uhakiki ilikuwa ni Wizara ya Ardhi ambayo ndiyo yenye mamlaka ya kuhakiki mipaka, ndio waliofanya. Sisi hatuhakiki, Wizara ndiyo wanatuonesha mipaka kwa ramani hii kuwa mipaka ni hapa na hapa, kwa hiyo, naamini kabisa kwamba walifanya kazi yake vizuri.
Mheshimiwa Spika, kuhusu kwenda kuongozana naye, naomba nimhakikishie niko tayari baada ya Kikao cha Bunge tuongozane twende tukaangalie hali halisi iliyopo ili tuone kama bado mgogoro upo tuweze kuutatua kwa pamoja na wananchi waweze kushirikishwa katika utatuzi wa huu mgogoro. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii. Napenda tu kulihakikishia Bunge lako kwamba migogoro ya mipaka hasa katika maeneo ya hifadhi tayari Wizara kwa kushirikiana na TANAPA, tunavyo vijiji vipatavyo 427 katika hifadhi nane ambavyo hatua za uhamasishaji kwa ngazi ya mkoa na wilaya zimeanza, baadaye zitashuka kwenye ngazi ya vijiji na kote huko kutapimwa ili kuweza kupanga pia matumizi bora ya ardhi katika maeneo hayo na tayari pesa, shilingi bilioni nne, zimeshatolewa katika Kitengo chetu kile cha Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi, kwa hiyo, tuna imani na Tarangire ipo, itakwenda kufanyiwa kazi ili kuondoa utata wa mipaka. (Makofi)
MHE. JOSHUA S. NASSARI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Spika, kwanza ni-declare interest, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Bunge hili ya Ardhi, Maliasili na Utalii na unakumbuka ulikuja Meru wewe, siku mimi nimeoa wewe ulikuja Meru ukimwakilisha Mama Makinda, na kwenye harusi ulizungumza ukasema miongoni mwa vilio ambavyo Mbunge wenu Nassari amekuwa akipigia kelele kwenye Bunge ni suala la ardhi.
Mheshimiwa Spika, Kata ya Ngarenanyuki ambayo inapakana na Hifadhi ya Taifa ya Arusha, hususan Kitongoji cha Momela, wamekuwa na mgogoro wa muda mrefu sana na Serikali na Wizara kwa sababu ya shamba namba 40 na shamba namba 41 yaliyoachwa na walowezi, walowezi ambao watu wa Meru hawa walichomewa nyumba miaka ya 1950, mwaka 1952 wakamtuma mtu UN, leo 2018 tumezungumza kwenye Bunge, aliyekuwa Naibu Waziri wa Wizara hii Mheshimiwa Engineer Ramo Makani akakubali kuondoka hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nikiwa masomoni Uingereza Mheshimiwa Mzee Mbatia huyu wakazungumza na wakakubaliana kwenda Meru kuniwakilisha kunisaidia kumaliza mgogoro. Amefika Wilayani Arumeru kasimamishwa na Mkuu wa Wilaya kutokwenda kwenye mgogoro, Mheshimiwa Mzee Mbatia akarudishwa kutoka kijijini kule ameshatoka Moshi. Huyo Mkuu wa Wilaya ndio aliyekwenda kuweka vigingi bila kushirikisha wananchi na imagine Wizara ya Ardhi hii imetoa hati mwaka huu mwezi wa pili, mwezi wa tatu maaskari wamekwenda kupiga risasi ng’ombe wa wananchi kwenye shamba namba 40 na shamba namba 41. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwenye Kamati mimi nimetaka kulia, mwanaume nikajizuia, sasa swali langu, Naibu Waziri wewe uko tayari baada ya kikao hiki kuongozana na mimi twende ili tukauangalie mgogoro huu na ili tuweze kujenga mahusiano mema kati ya hifadhi na watu wa Momela? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mgogoro huu umedumu kwa muda mrefu na viongozi waliotangulia walishafika katika yale maeneo na wakaona hali halisi na mimi niko tayari kuongozana naye ili twende tukaangalie nijionee mwenyewe ili tuweze kufanya uamuzi unaostahili.
Mheshimiwa Spika, lakini kwa kuongeza tu ni kwamba, kama tulivyosema, Serikali iliunda Kamati ya Kitaifa ya kubaini aina yoyote ya migogoro nchini na Kamati hiyo imeshamaliza kazi yake na imeleta mapendekezo Serikalini ambayo Wizara zinazohusika zinayafanyia kazi na kufikia uamuzi, tukishafikia uamuzi nina imani kabisa tatizo hili la Meru litakuwa nalo ni mojawapo ambalo litaisha kabisa.
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante, mgogoro uliopo Manyara unafanana na mgogoro uliopo Ulanga kati ya Selous Game Reserve na wananchi wa Kata za Ketaketa, Ilonga na Mbuga, Mheshimiwa Waziri analifahamu vizuri. Sasa wananchi wameendelea kukamatwa na kupigwa, huku siyo tu kuwachokoza wananchi, ni kunichokoza hata na mimi mwenyewe.
Mheshimiwa Spika, sasa naomba majibu ya Mheshimiwa Waziri, lini yuko tayari kwenda kwa ajili ya kumaliza huu mgogoro kati ya Selous Game Reserve na wananchi wa hizi kata?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, niko tayari kuongozana naye kwa sababu tulishakubaliana kwamba baada ya wiki hii Jumamosi inayofuata twende tukaangalie hali halisi katika eneo lile ambako kuna mgogoro. Kwa hiyo, tutakwenda, tutabainisha na tutakaa na wananchi ili tuone kwamba tatizo ni nini na tulipatie ufumbuzi.
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.
Kwanza Mheshimiwa Naibu Waziri mambo mengi wamekuongopea humu, siyo Wilaya wala Halmashauri ya Mji ambayo imewahi kunufaika na chochote kutokana na Mbuga ya Serengeti. The way walivyokujibu kama Bunda, kuna Halmashauri moja. Hivi vijiji vyote viko kwenye Halmashauri ya Mji na asubuhi nimetoka kuongea na Mkurugenzi na Mhasibu hatujawahi kupata hata shilingi moja. Ni lini sasa tutapata hii asilimia 25 ya tozo za uwindaji? Swali la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi wanaozunguka Mbuga ya Serengeti katika Jimbo langu wamekuwa wakipata tatizo kubwa sana la tembo kuharibu mali zao na Mheshimiwa Jenista ameshajionea uharibifu huu. Takribani wananchi 880…
...kati ya hao waliolipwa ni 330 tu, bado watu 550 hawajalipwa kifuta jacho japo kidogo. Ni lini sasa watalipwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme kwamba ni kweli kabisa Wilaya ya Bunda ina Halmashauri mbili na haya majibu sisi tunayoyatoa tunatoa katika Wilaya, siyo katika Halmashauri. Tunatoa katika Wilaya nzima, tunazungumzia Wilaya. Kama ingekuwa kwamba labda inatakiwa tuangalie kwenye Halmashauri, basi majibu hayo yengefanana. Hayo majibu niliyoyasema na hizo fedha ambazo nimezisema ni zile zilizoletwa katika Wilaya nzima ya Bunda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nijibu maswali yake kama ifuatavyo; kwa asilimia 25 na kwa kuwa Halmashauri yake ya Mji ina vijiji vinavyopakana na haya Mapori ya Akiba na hizi fedha nilizosema zimeshapelekwa, kama bahati mbaya Halmashauri yake haijapata mgao, basi tukitoka hapa nitafuatilia kuhakikisha ule mgawanyo unakwenda katika vijiji vyote vinavyohusika. Kwa hiyo, hilo nitalifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, naomba nirekebishe kidogo takwimu, kwa takwimu sisi tulizonazo Mheshimiwa Mbunge, katika Wilaya ya Bunda, kifuta jasho kilicholipwa ni kwa wahanga 1,127 ambao jumla ya shilingi 186,333,350 zimelipwa kama kifuta jasho. Shilingi milioni moja zililipwa kama pole kwa mhanga mmoja ambaye alipoteza maisha.
Kwa hiyo, suala la kusema kwamba hazijatolewa, zimetolewa na katika list niliyonayo mpaka sasa hivi nimeangalia kama Bunda kuna wahanga ambao wanadai, bado sinayo. Kwa hiyo, kama wapo ambao bado wanadai, naomba hiyo list tuipate ili tuweze kuifanyia kazi kusudi waweze kulipwa mara moja. (Makofi)
MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Meatu inapaswa kunufaika na miradi ya maendeleo inayotokana na ujirani mwema, Outreach Department kutokana na Serengeti National Park na Ngorongoro Conservation; lakini ni zaidi ya miaka kumi haujawahi kutekelezwa mradi wowote.
Je, ni lini sasa Halmashauri ya Meatu italetewa miradi ya maendeleo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba taasisi zetu zote zinazohusika na masuala ya uhifadhi zinao mpango madhubuti kabisa wa kuhakikisha kwamba zinachangia katika miradi mbalimbali ya vijiji vile vinavyozunguka katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Wilaya ya Meatu nina uhakika kabisa kwamba imetengewa kiasi cha fedha ambazo zitatekeleza miradi mbalimbali ya vile vijiji vinavyozunguka katika maeneo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge, tumekuwa tukifanya hivyo, kwa mfano, takribani kuanzia mwaka 2004 mpaka 2016 jumla ya shilingi bilioni 17.2 zimetumika katika kutekeleza miradi mbalimbali ya vijiji vinavyozunguka hifadhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nina uhakika na Wilaya ya Meatu ni mojawapo ambayo imefaidika na itaendelea kufaidika. Na mimi naomba tuwasiliane baadae ili tuone kwamba imetengewa kiasi gani katika mwaka unaofuata.
MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Mkoa wa Kilimanjaro umezungukwa na vijiji 88 ambavyo ni vya ujirani mwema, lakini kwa miaka kumi iliyopita mapato ya mlima huu ilikuwa ni shilingi bilioni 471.5 lakini vijiji vinavyozunguka vimepata shilingi bilioni 2.28 tu ambayo ni chini ya asilimia 0.48 wakati sera ni asilimia 7.5.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali haioni umuhimu ili vijiji hivi vipate haki yake badala ya kupata shilingi bilioni 2.6 kwa mwaka, wapate shilingi bilioni 40, TANAPA waweze kukaa na Halmashauri husika za Rombo, Moshi na Hai ili waweke utaratibu ili waweze kupata haki yao inavyostahili? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa vijiji vingi vinapakana kabisa na ile hifadhi yetu ya Mlima Kilimanjaro na niseme tu kwamba katika utaratibu wa sera ya ujirani mwema, tunachokifanya sisi katika bajeti nzima ile ya TANAPA tunatenga kati ya asilimia tano mpaka asilimia saba kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ile ya ujirani mwema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatukusema kwamba basi hizi zote asilimia saba ndiyo ziende katika vile vijiji, katika lile eneo husika. Maadam Mheshimiwa Mbatia ameleta haya mapedekezo, tutakaa chini, tutayaangalia na nitaiagiza TANAPA wakae na hizo Halmashauri ili kuona namna gani wanaweza kufaidi zaidi katika huo mradi. (Makofi)
MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza pamoja na maelezo mazuri ya Serikali itakumbukwa kwamba siku nne tano zilizopita Mheshimiwa Waziri Mkuu alikiri kwamba zoezi la uhakiki limegubikwa na vitendo vya rushwa. Sasa ni hatua gani zimechukuliwa na Serikali kuwachukulia hatua wale ambao wameshiriki zoezi hili na kujihusisha na vitendo vya rushwa, ambayo kwa kweli kwa sehemu kubwa ndiyo imevuruga zoezi hili na kulikosesha maana na matokeo yake wakulima wameathirika sana.
WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, awali ya yote kabla ya kujibu hili swali, naomba nichukue nafasi hii kwanza kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kwa kuniteua katika nafasi hii na kuniamini kwamba naweza kufanya kusaidia katika maendeleo.

Pia nichukue nafasi kuwashukuru viongozi wengine wote wanaomsaidia Mheshimiwa Rais lakini pia, wewe Mwenyewe Mheshimiwa Spika kwa malezi mazuri, ambayo ndiyo yamenifanya nifikie katika nafasi hii.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naomba nimjibu Mheshimiwa Nape Nnauye kama ifuatavyo, ni kweli kabisa kwamba wakati tunaendelea na hili zoezi la uhakiki katika maeneo mengi kumekuwa na maneno katika baadhi ya maeneo kwamba baadhi ya viongozi na baadhi ya wafanyakazi ambao wako kwenye Kamati za uhakiki wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya rushwa. Sisi kama Wizara tuliposikia tu hatukusubiri tupate ushahidi, tuliposikia baadhi ya wafanyakazi wanashiriki kwenye rushwa tumechukua hatua na naomba niliarifu Bunge lako Tukufu kwamba kwenye upande wa Wizara na bodi zake.

Mheshimiwa Spika, wafanyakazi wanne tumeshawachukulia hatua tumeshawasimamisha na hivi sasa tunakusudia kuwapeleka Mahakamani kutokana na kudhihirika kwamba wamejihusisha na vitendo vya rushwa. Lakini pia kuna baadhi ya wafanyakazi ambao wako TAMISEMI ambao tunawasiliana ndani ya Serikali ili nao waweze kuchukuliwa hatua zinazokusudiwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nataka kusema kwamba Serikali haitavumilia wafanyakazi wote ambao watakuwa wanajihusisha na vitendo vya rushwa na pale ambapo Waheshimiwa Wabunge mnazo takwimu au mmepata taarifa kwamba mfanyakazi wetu yeyote anajihusisha na rushwa tunaomba mtupatie hizo taarifa na kama Serikali tutachukua hatua mara moja. Ahsante.
MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa katika jibu la msingi la Serikali kwenye suala la pembejeo tunakiri kwamba moja ya sababu ya kupanda na kuongezeka kwa gharama ni kwa sababu pembejeo zinaagizwa kutoka nje. Katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM, katika Mpango wa Serikali, kulikuwa na ujenzi wa Kiwanda cha Mbolea Kilwa Mkoani Lindi. Serikali imefikia wapi kukamilisha ahadi hii ya Ilani ya Uchaguzi ili kusaidia upatikanaji wa pembejeo?
WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Naomba nijibu kidogo swali la nyongeza la Mheshimiwa Nape kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi tuliweka ahadi ya kuhakikisha kwamba tunajenga kiwanda cha kuzalisha mbolea pale Kilwa. Naomba nimhakikishie tu kwamba hatua za ujenzi wa kiwanda hicho tuko katika hali nzuri sana. Mpaka sasa hivi wiki mbili zilizopita wataalam kutoka Pakistan, Ujerumani na Morocco wamekuja kwa ajili ya kuangalia na kufanya tathmini ya mwisho na kufanya mazungumzo na Serikali ili kuhakikisha kwamba kiwanda hiki cha mbolea kinajengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni matumaini yetu kwamba baada ya muda mfupi, kiwanda hiki kitaanza kujengwa sambamba na maeneo mengine ya viwanda ambavyo vitajengwa ili kuweza kupunguza gharama za pembejeo hapa nchini. Nashukuru.
MHE. CECIL D. MWAMBE:Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, suala hili la chai, linafanana kabisa na suala ambalo liko kwenye mikoa inayolima korosho.

Mheshimiwa Spika, mlolongo huu wa kuongeza thamani ya mazao na mwaka kama utakumbuka Mheshimiwa Waziri alipokuja kwenye Kamati yetu ya viwanda na bishara walileta pale ndani wakasema wanafanya utafiti namna ya kuongeza thamani kwenye kochoko ambayo inazalisha nipa ili kuwaongezea mapato wakulima kwa maana ya gongo…

SPIKA: Kochoko ndiyo nini?

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, kochoko ni zile washi zinazotokana baada ya mavuno ya korosho, wakulima huwa wanazitupa lakini wengine huwa wanaziuza na wanatengeneza gongo na inafahamika na kwamba kongo si pombe haramu isipokuwa namna inavyotengenezwa.

Sasa nataka nimuulize Mheshimiwa utafiti huo ambao ulikuwa unafanywa na Chuo cha Kilimo cha Naliendele umefikia wapi mpaka sasa hivi ili wakulima waweze kujipatia kipato cha ziada kutokana na mazao yao ya shambani? Ahsante.
WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Naibu Waziri kwa majibu mazuri aliyoyatoa, pia nichukue nafasi hii kumpongeza ndugu yangu Mheshimiwa Mwambe kwa jinsi ambavyo ameendelea kufuatilia suala hili la korosho.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa Chuo chetu kupitia tawi letu la Naliendele tumefanya utafiti wa kina na tumebaini kwamba kuna mazao mengi tunayoweza kuzalisha kutokana na korosho ikiwemo juice na ikiwemo mvinyo maalum ambao unatokana na haya mabibo ya korosho na tumetoa maagizo kwenye tawi letu sasa hivi kujenga kinu cha kuweza kuchakata hiyo ili tuweze kuzalisha mvinyo pamoja na juice ambayo tutaiuza hapa nchini na hivi itaongeza thamani na kuongeza mapato yanayotokana na zao la korosho.

Mheshimiwa Spika,kwa hiyo Mheshimiwa Mwambe awe na subira baada ya muda mfupi tu atakiona kile kiwanda kikiwa kimejengwa pale na kuweza kuchakata hiyo, ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Awali ya yote nitoe pole kwa wananchi wa nchi nzima hii ambao wamepata adha ya mafuriko hasa wa Wilaya yangu ya Liwale na Mkoa wa Lindi. Nawapa pole sana Mwenyezi Mungu aendelee kuwapa nafuu wakati huu wanahangaika na makazi yao.

Mheshimiwa Spika, suala la kilimo hakuna mtu ambaye hajui kwamba nchi yetu asilimia 75 ni wakulima lakini naona Serikali usimamizi wa kilimo wameachia Vyama vya Ushirika ambavyo havina uwezo wa kulisimamia. Mfano kwa suala la kuagiza vifaa au pembejeo wameachiwa Vyama vya Ushirika ambapo wao ndiyo wanaoingia mikataba na suppliers wa pembejeo hata kwenye mauzo. Kama Serikali mtaamua kuviachia Vyama vya Ushirika kusimamia kilimo basi tutendelea kusuasua kwenye kilimo.

Mheshimiwa Spika, mfano mzuri mwaka huu kwenye zao la korosho tumechelewa msimu tumekuja kuanza msimu mwezi wa kumi na moja wakati korosho wakulima wameshaanza kuzivuna tangu mwezi wa nane. Jambo hili mliliachia kwenye Vyama vya Ushirika matokeo yake tumechelewa kuanza msimu toka mwezi wa Novemba mpaka leo wakulima bado wana korosho.

SPIKA: Sasa swali.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Je, Serikali ipo tayari kusimamia mazao haya badala ya kuviachia Vyama vya Ushirika?
WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza si kweli kwamba tumeachia Vyama vya Ushirika kusimamia mazao. Mazao mengi hasa ya kimkakati yanasimamiwa na Bodi za Mazao ikiwemo Bodi ya Korosho na Vyama Ushirika vimekuwa vinakusanya hayo mazao na kuyapeleka sokoni kwa ajili ya kuuza kwa niaba ya wanachama si kwamba vinasimamia uzalishaji na hili tutaendelea kulifanyia kazi na tutaendelea kulisimamia.

Mheshimiwa Spika, lakini nilitaka kusema tu kwamba kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri tunataka mazao yote, pembejeo zote, kuanzia mbegu, mbolea viuadudu, hivi vyote vitakuwa vinasambazwa na sekta binafsi katika maeneo yote. Tunataka Watanzania watumie fursa hii kuona kwamba sasa ni wakati mwafaka kuna fursa ya kupeleka viuadudu vya korosho, pamba, kahawa na katika mazao yote tunataka sekta binafsi isambaze vitu vyote hivyo badala ya kutegemea Serikali. Serikali sisi tutasimamia kuratibu maendeleo ya zao na namna ya kutafuta masoko lakini siyo kusambaza pembejeo ni fursa kwa Watanzania.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niwaombe tu Mheshimiwa Kuchauka na Watanzania wote wanaotaka kusambaza sulphur huko kwenye zao la korosho, wanaotaka kupeleka viuadudu huko kwenye pamba, wanaotaka kupeleka kwenye kahawa, kwenye tumbaku sio Vyama vya Ushirika ni sekta binafsi. Sisi tutasimamia ubora wa usambazaji wa vitu hivyo ili viwafikie wakulima.

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana na niwaombe Watanzania watumie nafasi hiyo.
MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Pamoja na kwamba Serikali ya Awamu ya Tano inahimiza sana kilimo.

Je, Serikali inasemaje kutokana na zoezi linalowavunja moyo wakulima wa Urambo la wakulima kunyang‟anywa mali zao, nyumba zao na wengine mpaka wamekimbia miji yao kutokana na madai kwamba waliuza isivyotakiwa kwa mauzo ya tumbaku ya mwaka 2016/2017. Serikali inatoa kauli gani kuhusu hili zoezi linalowavunja moyo wakulima wa Urambo? (Makofi)
WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Margaret Sitta, Mbunge wa Urambo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kumekuwa na changamoto mbalimbali katika maeneo mbalimbali hapa nchini ikiwemo eneo la Urambo kwa baadhi ya viongozi wa Vyama vya Ushirika waliingia kwenye matatizo kwa sababu waliuza tumbaku ya wananchi bila kufata taratibu na wali-collude na wafanyabiashara na hivyo kuathiri bei ile ambayo ingetokana na soko.

Mheshimiwa Spika, kutokana na hali hiyo, tulikabidhi taarifa kamili ya ukaguzi TAKUKURU ili wawafuatilie viongozi mbalimbali wale ambao walikiuka maadili ya viongozi na ambao hawakusimamia mazao sawasawa wakasababisha hasara kwa wananchi na kwenye Vyama vya Ushirika. Hilo zoezi linaendelea nchi nzima wale viongozi wote wanakamatwa na TAKUKURU.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa kuwa amesema wananchi wanakamatwa, TAKUKURU sidhani kama wanakamata wananchi ambao hawakuvunja hizi taratibu, ila kama kuna tatizo kama hilo, sisi tutafuatilia sasa hivi, tutaongea na viongozi wa TAKUKURU ili watuambie ni kitu gani kinachoendelea kwa wananchi wa Urambo ili tuweze kuhakikisha kwamba tunashirikiana na TAKUKURU na kuchukua hatua kwa wale ambao ni wabadhirifu badala ya wananchi wa kawaida wale ambao ni wakulima, ahsante.
MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Changamoto ya ununuzi wa tumbaku inafanana sana na changamoto wanayokabiliana nayo wakulima wa zao la mahindi. Hivi sasa ni msimu wa mavuno, ningependa kujua kwa Serikali imejipangaje kwa mwaka huu juu ya ununuzi wa zao hili la mahindi?
WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa katika msimu uliopita tulikuwa na changamoto ya masoko ya zao la kilimo, lakini kama sote tunavyojua, Serikali imekuwa ikihakikisha kwamba inatafuta masoko na muda huu tunapoongea tumepata masoko makubwa sana ya mahindi katika nchi za Kusini. Hivi sasa Rwanda wanahitaji zaidi ya tani 100,000; Burundi wanahitaji zaidi ya tani 100,000; lakini nchi ya Zimbabwe wanahitaji tani 800,000 za mahindi na nchi nyingine nyingi zinahitaji mahindi kwa wingi.

Kwa hiyo, ninachotaka kusema ni kwamba sasa hivi soko la mahindi ni kubwa sana, wakulima wote wenye mahindi tunaomba wajitokeze watuambie wana kiasi gani, washirikiane na Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuanzia wiki taasisi zetu ikiwemo NFRA pamoja na CPB wanaanza kununua mahindi na kukusanya mahindi kutoka kwa wakulima mbalimbali pamoja na wafanyabiashara, lakini pia taasisi nyingine ambayo tumeipa jukumu la kupeleka mahindi Zimbabwe nayo inaanza kununua mahindi wiki hii.

Kwa hiyo wakulima wakae mkao kila mahali wenye mahindi sasa hivi ni wakati wa kula mkate mzuri, nakushukuru. (Makofi)
MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kupata nafasi ya kuuliza swali.

Mheshimiwa Spika, sasa tunaelekea kwenye msimu ujao wa zao letu la korosho na nilitaka nipate maelezo kutoka Serikalini, mpaka hivi sasa wakulima hawajapata taarifa zozote juu ya uwepo na lini na bei elekezi ya pembejeo. Kwa hiyo, ningeomba Serikali itoe maelezo ili kuhakikisha wakulima wanapata ufahamu juu ya uwepo wa pembejeo lakini bei elekezi itatolewa lini, lakini pia ni lini itasambazwa?(Makofi)
WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ni kweli sasa hivi ni msimu wa kilimo cha zao la korosho hasa katika kupulizia madawa ikiwemo sulfur na maeneo mengine. Sasa hivi Serikali tumejipanga tumehakikisha kwamba sulfur ipo ya kutosha katika maeneo yote tumeshapaleka na bado tunajaribu kufanya tathmini kuangalia kama kuna sehemu tuna upungufu ili tuhakikishe kwamba hayo madawa yanakuwepo. Sambamba na hilo tumeanza kujiandaa kabisa katika msimu unaokuja ikiwa ni pamoja na uteuzi wa Bodi ya Korosho ambayo tayari tumeshaiteua kwa ajili ya kuanza kazi na kuweza kupanga mikakati mbalimbali ya kuendeleza hili zao la korosho.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge avute tu muda ni kwamba kila tumejipanga na kitakwenda vizuri na nina uhakika wakulima wa korosho watafurahi sana, ahsante.