Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Joseph Osmund Mbilinyi (20 total)

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Madiwani na Wabunge wa upande huu wanachangisha watu, isipokuwa wanachangisha kwa hiari siyo kwa kulazimisha na mgambo, naomba hii niliweke clear. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa ku-recognize mawazo yangu kuhusiana na hili suala kwa sababu kuna watu wanachukulia kama tumewa-pre-empty au vitu kama hivyo lakini no. Tunachojaribu kufanya ni kuboresha kwa sababu hata kama Wizara ya Afya wana sera kwa maana ya mipango, huwezi kuwa na mipango halafu fedha anazo mtu mwingine. Unaweza ukampigia simu kwamba bwana njoo na hizo fedha tutekeleze ile mipango katikati akakabwa na zisifike kwa wewe mwenye mipango. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tuna confusion. Nafikiri labda kwa sababu sisi ndiyo Bunge labda ifike mahali sasa turudi tujadili upya kwamba hii system ya afya yote irudishwe kwenye mwamvuli mmoja kwa maana kwamba yote iwe chini ya Waziri wa Afya kwa sababu confusion ni kubwa sana. Ukiangalia hata kwenye ajira za madaktari, wengine wanaajiriwa na TAMISEMI, wengine wanaajiriwa na Wizara ya Afya, wengine wanajiona kwamba ndiyo madaktari wa kweli, wengine siyo madaktari wa kweli na hata linapokuja suala la kudai haki zao, wale walioajiriwa na Wizara ya Afya, Mheshimiwa Kigwangalla anajua, alikuwemo humo katika harakati za madaktari, wale walioajiriwa na Wizara ya Afya wakisema tusimame kidogo, tukaze uzi, Serikali isikilize madai yetu, wale wa TAMISEMI hawagomi. Kwa hiyo, tunaharibu hata umoja wa madaktari. Ili madaktari wawe pamoja inabidi wote wawe chini ya mwajiri mmoja, waongee lugha moja. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nikirudi Mbeya kuna suala la Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, mortuary. Nimepokea malalamiko kutoka kwa wafanyakazi wa mortuary Hospitali ya Mbeya kwamba wanafanya kazi kwenye mazingira magumu sana. Kuna friji 15 lakini kwa zaidi ya miaka miwili sasa friji tisa hazifanyi kazi, zinazofanya kazi ni sita tu kiasi kwamba kama ikitokea ajali na miili mingi ikapelekwa inabidi wana rotate (wanaweka mwili baada ya muda ukipoa wanatoa, wanabadilisha mwingine) that’s too bad for big hospital kama hospitali ya Rufaa ya Mbeya. Hata hivyo, pia hata wale wafanyakazi wanaofanya kazi mle katika mazingira magumu wana malalamiko sana kuhusiana na maslahi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, wananiambia wanatakiwa walipwe 150,000 kwenye postmoterm kwa maana ya daktari mtaalam anaitwa pathologist doctor. Daktari mtaalam anachukua shilingi 100,000 wale wanachukua shilingi 50,000, lakini hata hiyo hela kuipata imekuwa kazi na wale wa hospitali ya Rufaa Mbeya kwa zaidi ya miezi tisa sasa hawapewi ile hela kwa namna mbalimbali, wanaambiwa sijui wamefoji PF3 (zile ripoti za polisi), inafikia mahali wanaambiwa ili kuthibitisha; ndugu wa marehemu wawepo pale waangalie. Sasa wenzetu labda wanaweza, lakini katika utamaduni wetu kukaa pale kuona ndugu yako anapasuliwa moyo, nini kinatolewa sidhani kama ni sahihi. Kwa hiyo, tuangalie utaratibu wa kuthibitisha malipo yao kwa sababu kazi wanayofanya ni muhimu na ngumu.
Mheshimiwa Spika, lakini pia hawa wafanyakazi wa mortuary ifike mahali nao wapewe kozi, kama madaktari wanapewa kozi, manesi wanapewa kozi, na wafanyakazi. Isifike mahali unakwenda kuchukua mlevi tu kwa sababu hana sense, ndiyo umpeleke mortuary akafanye kazi kwa kutumia ile hali. Matokeo yake ndiyo unasikia mwili wa Kilimanjaro umepelekwa Mbeya na mwili wa Mbeya umepelekwa Songea, kunakuwa na mchanganyiko kwa sababu wale watu sio professionals wa ile kazi. Kwa kweli katika nchi za watu, mtu anayefanya kazi katika mazingira haya hata hela yake inakuwa ni nzuri sana kwa sababu tu watu wanatambua umuhimu wa zile kazi wanazofanya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tukienda Hospitali ya Rufaa kuna hili jengo la maabara ya kisasa, linaitwa jengo la mionzi. Jengo hili nimelisemea toka naingia Bunge hili, hiki ni kipindi cha pili sasa. Toka nimeingia Bunge hili ikifikia Wizara ya Afya, nikisimama nalisemea hili jengo. Nikauliza, hivi jengo hili limejengwa na Mzee wangu Mheshimiwa Mwakyusa akiwa Wizara ya Afya, mnataka mpaka tena atokee Waziri kutoka Mbeya ndiyo lile jengo limaliziwe? Hata hivyo, namshukuru Katibu Mkuu sasa hivi anatoka Mbeya labda anaweza akaweka mkazo kidogo kwa sababu haya mambo yapo, hatuwezi kuyakataa, haya mambo yapo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, sasa naomba sasa, naona imetengwa shilingi bilioni tano, ninachoomba ni guarantee ya Waziri, Naibu Waziri na Katibu huko aliko mkimpelekea majibu yatakapokuja, naomba guarantee ya hii shilingi bilioni tano, ni fedha za ndani au za nje zile zilizokataliwa kwa sababu ya uchaguzi wa Zanzibar kuchakachuliwa. Naomba nipate guarantee kujua kwamba hizi fedha zinakuja ili lile jengo limalizike.
Mheshimiwa Spika, naambiwa bilioni tatu ni kukamilisha jengo, shilingi bilioni mbili kwa ajili ya vifaa (CT Scan, MRI Scan), jengo lile likamilike ili sasa ile hospitali iongezeke hadhi na itapunguza hata influx ya wagonjwa kutoka eneo lile kuja Muhimbili na mtapunguza ile hekaheka ya kufunga ofisi, iwe wodi kwa sababu influx ya wagonjwa ni wengi, wengine wanaweza wakaishia huko huko ndugu zangu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kuna suala la Bima ya Afya, Hospitali ya Rufaa Mbeya sasa hivi wanakusanya takriban shilingi 500,000,000 kwa mwezi kutoka shilingi milioni 70 sijui 80 huko nyuma. Shukurani kwa Mkurugenzi aliyepita na aliyepo sasa. Sasa nataka nijue katika hii shilingi milioni 500, ni ngapi inabaki kwa Hospitali ya Rufaa Mbeya kwa ajili ya kuboresha maslahi mbalimbali ya wafanyakazi ikiwemo housing allowance za madaktari kama stahiki yao inavyotaka, ikiwemo on call allowance, daktari amekaa, amekuja kwa Mbunge labda mnaongea masuala mengine tu kama mwananchi wetu wa CHADEMA, lakini anapigiwa simu saa nne usiku kwamba unatakiwa hospitali kuna emergency, akienda kule hakuna malipo yoyote. Sasa nataka kujua hii shilingi milioni 500, ni ngapi inabaki hospitali ya Rufaa Mbeya na hata pia iende kwenye allowance kule mortuary ile ya Mbeya kwa wale wafanyakazi ambao wako frustrated kwa kweli.
Mheshimiwa Spika, mmoja akaniambia, siku moja Waziri alienda pale akamwambia Waziri kwamba hivi ndivyo tunavyolaza wagonjwa kwenye mochwari na bahati mbaya upate ajali, ukifa, ukiletwa hapa ntakulaza chini na wewe ili uone uchungu kama utakuwa na sense zozote.
Sasa kama mfanyakazi anafikia kusema hivyo, hizo ni kauli za mtu aliyekata tamaa na sio vizuri kuwa na wafanyakazi ambao Serikali imewaajiri, waliokata tamaa.
Mheshimiwa Spika, mwisho niseme Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu tulieni, you are vibrant young ones, sister you know energetic, naomba sana tulieni, mshaurini Rais namna ya kutekeleza sekta ya afya iwe bora. Msihofu, msiende kwa mizuka, maana tukisema mnaenda kwa mizuka wengine wanabisha, lakini hivi vitu vipo. Kwa hiyo msihofu, tulieni.
Mheshimiwa Spika, nilisikitika sana mimi binafsi kumwona Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya amebeba stuli, amebeba meza eti anahamisha wakati naamini kwamba huo muda anaofanya hivyo wangeweza kufanya vijana, wako vibarua pale Muhimbili, wangeweza kuhamisha stuli na droo wakati Waziri amekaa ofisini anapitia ripoti mbalimbali zikiwemo ripoti za mortuary ya Mbeya ambayo fridge tisa zimekufa, hazifanyi kazi. Angekuwa amekaa ofisini anafuatilia ripoti za nchi nzima badala ya kutumia muda huo muhimu wa mtu kama Katibu Mkuu msomi kubeba stuli.
Mheshimiwa Spika, ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi lakini nasikitika naenda kuchangia wakati Waziri mwenyewe hayupo; kwa sababu ilibidi hivi vitu avibebe Mheshimiwa Waziri yeye mwenyewe ndio tungeenda sawa zaidi, lakini sio mbaya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze na kuna Wabunge wapya humu wanashangaa suala la sisi kutoka Bungeni sijui tunasaini, sijui tunafanya nini; niwataarifu tu wanatakiwa kabla hujaingia kwenye kitu upate elimu kuhusu utendaji wa hicho chombo au taasisi. Kutoka Bungeni ni suala la kawaida kabisa kwa sababu hata tunavyotoka sio kwamba tunatoka tunakwenda nyumbani; kwa sababu kuna wakati ni heri uwe nje unatumia simu kuongea na watu Jimboni kuliko kukaa humu ndani kusikia watu wanavyo zomea zomea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na niwataarifu tu kwamba tutaendelea kutoka hatua hii mpaka pale kiti anapokaa Naibu Spika aache tendency za udikteta ndani ya Bunge kwa sababu tupo humu tunataka freedom kwa ajili ya masuala yanayohusu hili Taifa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la diplomasia, Wizara hii ni muhimu sana na imefika mahali tunatakiwa tuweke mbele diplomasia ya uchumi; naongea hivi nikiunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Msigwa, Waziri Kivuli kwa sababu tunatakiwa tutoke sasa tuachane na diplomasia ya enzi za cold war. Diplomasia hiyo imepitwa na wakati, lakini unfortunately sisi ndio tunabaki nayo na afadhali hata zamani tulikuwa na misimamo. Sasa hivi hata misimamo hatuna, Wizara ya Mambo ya Nje kazi yake ni pamoja na kusimamia, kuwa MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi lakini nasikitika naenda kuchangia wakati Waziri mwenyewe hayupo; kwa sababu ilibidi hivi vitu avibebe Mheshimiwa Waziri yeye mwenyewe ndio tungeenda sawa zaidi, lakini sio mbaya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze na kuna Wabunge wapya humu wanashangaa suala la sisi kutoka Bungeni sijui tunasaini, sijui tunafanya nini; niwataarifu tu wanatakiwa kabla hujaingia kwenye kitu upate elimu kuhusu utendaji wa hicho chombo au taasisi. Kutoka Bungeni ni suala la kawaida kabisa kwa sababu hata tunavyotoka sio kwamba tunatoka tunakwenda nyumbani; kwa sababu kuna wakati ni heri uwe nje unatumia simu kuongea na watu Jimboni kuliko kukaa humu ndani kusikia watu wanavyo zomea zomea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na niwataarifu tu kwamba tutaendelea kutoka hatua hii mpaka pale kiti anapokaa Naibu Spika aache tendency za udikteta ndani ya Bunge kwa sababu tupo humu tunataka freedom kwa ajili ya masuala yanayohusu hili Taifa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la diplomasia, Wizara hii ni muhimu sana na imefika mahali tunatakiwa tuweke mbele diplomasia ya uchumi; naongea hivi nikiunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Msigwa, Waziri Kivuli kwa sababu tunatakiwa tutoke sasa tuachane na diplomasia ya enzi za cold war. Diplomasia hiyo imepitwa na wakati, lakini unfortunately sisi ndio tunabaki nayo na afadhali hata zamani tulikuwa na misimamo. Sasa hivi hata misimamo hatuna, Wizara ya Mambo ya Nje kazi yake ni pamoja na kusimamia, kuwa Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo ndio diplomasia inayotakiwa kufanyika sasa hivi lakini hatuna rekodi; angalia kama Ethiopia wanavyojaribu kuwashirikisha diaspora yao katika masuala ya uchumi. Walianzisha mradi mkubwa sana wa umeme pale unaitwa Ethiopian Grand Millennium Dam kutokana na mgogoro wa chanzo Nile na support inayopata Egypt baadhi ya mataifa wakakataa kui-support Ethiopia kifedha kwenye ule mradi; walichofanya Serikali ya Ethiopia wakawahusisha watu wao wa diaspora Worldwide, wakawatengenezea bond maalum, wakawawekea utaratibu wale mabwana wanachangia sasa dola kwenye ule mfuko na Ethiopia sasa hivi ule mradi nilikuwa naangalia jana umefikia asilimia 70 ya kutengenezwa, wamebaki asilimia 30 tu kutengeneza bila fedha za nje kwa kutumia fedha za diaspora ya Ethiopia inayoishi North America na Uingereza ndugu zangu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sasa sisi tumekaa tu Ethiopia wanatumia diaspora wanakwenda kuwa na bwawa kubwa, wanaenda kutengeneza historia, wana bwawa kubwa la umeme kuliko yote Afrika kwa kutumia diaspora. Sisi diaspora hatuwashirikishi; huwezi kuwashirikisha watu kwenye uchumi; Watanzania hawa huwezi kuwashirikisha kwenye uchumi wakati hautaki kutambua uraia wao, uzalendo wao na utaifa wao. Hapa nazungumzia diaspora maana yake tunafika mahali tunachanganya mambo, ninyi mnachanganya kati ya utaifa na uraia. Utaifa ni kitu natural, uraia ni kitu cha documentation yaani paper work, kama mimi ningeamua kufanya paper work sasa hivi ningekuwa raia wa Marekani, lakini utaifa ni kitu by nature.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hatuwezi kwenda mbele bila kuwashirikisha hawa watu; mnawadanganya watu mnaenda mnawaambia rudini nyumbani wakirudi nyumbani hawawezi kuacha mambo yao waliyoyatengeneza kule miaka yote eti aache uraia wa Marekani aje hapa akitaka kibali hichi corruption, akitaka hichi corruption na pia aje kama mgeni. Anatakiwa mnatambua mnawapa dual citizenship ili wanavyokuja hapa wanakuja kama Watanzania sio Mtanzania yupo Marekani mmemnyang‟anya utaifa wake kwa sababu ya makaratasi ya uraia halafu anakuja hapa mnamzuia kabisa mnataka awe mwekezaji kama mgeni na sio kama Mtanzania wa hapa, sasa hii ni mbaya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi kwa nini mnaogopa sana diaspora, kwa nini mnaogopa sana dual citizenship mnajua ni hasara kiasi gani mnalipa hili Taifa kwa kutokujua tu remittances zinaingizwa nchini kiasi gani hiyo ni upungufu mkubwa sana na tunaitaka hii Serikali sasa hivi ifanye mkakati walete dual citizenship ili watanzania waliopo nje walete input na sio tu input ya kiuchumi exposure waliyoipata wale mabwana kule hata katika masuala ya utawala tukiwaleta na kuwaingiza katika mfumo wa uendeshaji nchi hivi vitu vidogo vidogo vya uzembe uzembe, rushwa rushwa ndogo ndogo hizi havitakuwepo kwa sababu good governance itaenda kutamalaki pale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa sisi tumekaa, Serikali haiwajali diaspora wakiwa hai na hata wakiwa wamekufa; Watanzania wanauwawa huko kama niki-refer hotuba ya Waziri Kivuli, niende kwenye mauaji ya juzi juzi tu Watanzania wawili katika mwezi mmoja mwezi wa nne wamepigwa risasi hakuna tamko lolote mpaka tupige kelele Bungeni humu ndio Waziri atakuja baadaye atajifanya anatoa tamko wakati alitakiwa walishughulikie hili suala na naunga mkono petition ya Watanzania wanaoishi Marekani ambao wanataka Balozi wa Marekani Washington DC aondolewe mara moja arudishe nyumbani kwa sababu ameshindwa kuwatumikia Watanzania kule Marekani. Ameshindwa kutambua hata pole hajatoa kwenye misiba hii iliyotokea. Umetokea msiba wa Andrew Sanga, Afrika nzima imelia; Serikali haina habari. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Andrew Sanga amepigwa risasi amekufa Serikali hii haina habari; Balozi wa Marekani anapigiwa simu kuna msiba Houston ameacha kwenda kwenye msiba Houston anasema nina udhuru, udhuru wenyewe yupo Dallas, Dallas na Houston ni kama Dar es salaam na Morogoro. Amekwenda Dallas kwenye party ameacha kwenda kwenye msiba ambao umetingisha Marekani nzima na yeye angeenda pale angeenda kuleta harmony kidogo na kuwatuliza wale watu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka Waziri atuambie na aliambie Bunge lako Tukufu Serikali hii imefikia wapi kufuatilia uchunguzi wa mauaji ya Andrew Sanga kwa sababu Marekani usipo-push na wao wana-relax kwa sababu wanajua…
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi muda umemalizika naomba ukae.
Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi, happy new year Waheshimiwa Wabunge wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nitumie fursa hii kuwashukuru Wanambeya kwa kunirudisha tena mjengoni kwa kipindi cha pili na kunifanya niwe Mbunge niliyechaguliwa kwa kura nyingi kuliko wote humu ndani, the most voted MP kwenye election ya 2015. Kama Waziri Mkuu anatokana na Wabunge waliochaguliwa wangeangalia kura nyingi may be mimi ndiye ningekuwa Waziri Mkuu humu ndani . (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme kitu kimoja, tunapanga Mpango wa Maendeleo humu ndani au tunajadili Mipango ya Maendeleo lakini wale wanayoipokea hii Mipango ya Maendeleo sidhani hata kama tayari wako cemented katika mazingira yao. Sina uhakika hata kama tayari mmeshapewa instrument ya kazi na Rais. Rais anapochagua Baraza la Mawaziri anawapa instrument ambayo ndiyo kama job description. Sasa nina wasiwasi kama hawa walishapewa na matokeo yake ndiyo maana wanaenda hovyoovyo tu kwa kufuata mizuka ya Rais. Rais akitumbua majibu huku wao wanatafuta kule kwenda kutumbua, kinachotakiwa siyo kutumbua majipu twende tutumbue mpaka viini. (Kicheko/Makofi)
KUHUSU UTARATIBU
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utaratibu.
MWENYEKITI: Samahani Mheshimiwa Mbilinyi, Waziri wa Nchi.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utaratibu, Kanuni ya 68 pamoja na Kanuni ya 64, mambo yasiyoruhusiwa Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa msemaji aliyekuwa anaongea kwanza ametumia maneno ya kuudhi lakini ametumia maneno ya dhihaka kwa kutaja jina la Rais kwa dhihaka. Kanuni ya 64(d) inasema hatatumia jina la Rais kwa dhihaka katika mjadala kwa madhumuni ya kutaka kulishawishi Bunge kuamua jambo lolote kwa namna fulani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi haya ni maneno kweli yanayostahili heshima ya Rais kusema kwamba anaongozwa kwa mzuka? Mzuka ni kitu gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nafikiri utusaidie kutupa mwongozo wako kama maneno hayo na Kanuni ile ya 64(d) yanaweza kweli kubeba maudhui ya kulitumia jina la Mheshimiwa Rais katika mazingira tuliyonayo hapa. Kwa nini asiyaondoe maneno haya halafu achangie tu hotuba yake kwa staha na watu wote waweze kumwelewa? (Makofi)
MWENYEKITI: Mheshimiwa Joseph, kwa heshima kabisa mdogo wangu naomba ufute maneno hayo.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa tunapambana na changamoto ya generation gap, ndiyo inayomkuta Mheshimiwa Waziri. Mizuka ni neno la Kiswahili lina maana ya hamasa yaani ile amshaamsha kwamba Rais anaamshaamsha na wao kwa sababu hawajapewa job description wanaiga, huyu yuko buchani anaangalia nyama, huyu anafunga mageti, huyu naye sijui anafanya nini, hiki ndiyo kitu wanachokifanya. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mnaozomeazomea niwaonye, wengi wenu waliokuwa wanazomea hawajarudi hapa. Waliorudi ni wajanja kama Dkt. Mwinyi wako kimya tu. Wanaozomeazomea wengi hawajarudi, hamtaonja term ya pili, siyo mchezo, hiyo nawaambia wazi kabisa. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, turudi kwenye mchango…
MWENYEKITI: Samahani Mheshimiwa Mbilinyi, Waziri wa Nchi.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, bado niko pale pale kwenye Kanuni ile ile na naendelea kusisitiza, Mheshimiwa Rais wetu haongozi kwa mzuka, kwa hamasa, anaongoza kwa taratibu, Katiba na sheria, haongozi kwa mzuka au eti kwa hamasa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais ana Ilani, Katiba, sheria, na taratibu anazozitumia kuongoza. Kwa hiyo, huu uongozi wa kufuata generation eti Rais anaongoza kwa mzuka, kwa hamasa, haiwezi kukubalika. Haya ni maneno ambayo yanaudhi na yanataka kudhalilisha jina la Mheshimiwa Rais ndani ya Bunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kauli hiyo ifutwe. (Makofi)
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbunge Mbilinyi!
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tabia imeanza kujitokeza kutaka kufanya kama Rais sijui au huyu Rais wa Awamu ya Tano untouchable, haguswi kwa kauli wala nini, lazima tutasema. Sijasema Rais anaongoza kwa mizuka, nimesema hawa ambao hawajapewa job description ndiyo wanafuata mizuka ya Rais, wanafuata vigelegele, ninyi mnafuata vigelegele. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba unipe nafasi niendelee kuchangia.
MBUNGE FULANI: Mwongozo.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Utapokea Miongozo baadaye, naomba unipe nafasi ya kuchangia. President Magufuli siyo unatouchable ni mhimili mwingine na hili Bunge litajadili bila kumkashifu na bila kumtukana pale atakapokosea, kwamba anapotumbua majipu aende mpaka kwenye viini, anafukuza watu kazi, watu hawapewi nafasi ya kujitetea, halafu tunaongea humu mnataka kusema vitu gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kupata maendeleo bila demokrasia…
MWENYEKITI: Samahani Mheshimiwa Joseph Mbilinyi, naomba unyamaze kimya kwanza. Hii hoja imetolewa na Waziri wa Nchi. Sasa naomba Mheshimiwa Waziri wa Nchi, uendelee.
MBUNGE FULANI: Aendelee nini?
WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, unaongozwa na Kanuni, kama Mheshimiwa Mbilinyi hataki kufuta usemi wake na Kanuni zinaeleza wazi kama Mbunge anaamrishwa hataki kufuta usemi wake, kwa nini usitumie mamlaka yako kwa Kanuni ya 5 ili uweze kufanya maamuzi sahihi? (Makofi)
(Hapa baadhi ya Wabunge walikuwa wakiongea bila mpangilio)
MBUNGE FULANI: Unakifundisha kiti, eeeh!
MBUNGE FULANI: Kwani mzuka maana yake nini?
MWENYEKITI: Samahani, samahani, naomba tusikilizane.
MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi, naomba ufute kauli yako.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, unapoomba unatarajia kupata au kukosa. Katika hili nimekataa kufuta kauli kwa sababu anachokisema nimesema sicho nilichosema. Nenda kwenye Hansard utaona maneno niliyoyaongea kwa ufasaha wake kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo umeamua nyuma, usubiri uende kwenye Hansard utaangalia, kama yakiwa maneno aliyosema Mheshimiwa Mama Waziri…
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi naomba utulie.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Ambaye yupo kwenye tatizo la generation gap basi ningefuta.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi naomba utulie.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Naomba na muda wangu ulindwe lakini.
MWENYEKITI: Sasa kwa sababu umekataa kufuta kauli, nasema tutakwenda kwenye Hansard kuangalia kimezungumzwa nini ili hatua ziweze kuchukuliwa. Tunaendelea, malizia dakika zako chache.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo dakika chache, ni dakika nyingi tu kwa sababu mmenikata wakati nikiwa kwenye dakika moja au moja na nusu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kujadili maendeleo bila demokrasia, bila ya utulivu wa kisiasa kwenye nchi. Rais anasema yeye ni Rais wa vyama vyote, alisema kwenye kampeni mpaka juzi yuko Arusha, naona anaongea na watu, anasema yeye ni Rais wa vyama vyote, lakini Waziri Mkuu wake yule pale anatukataza Wapinzani tusifanye mikutano ya vyama vyetu vya siasa. Demokrasia iko wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kujadili maendeleo bila demokrasia, bila uhuru wa vyombo vya habari, wanafungia magazeti kiholela tu, wanakuja wanazuia wananchi wasiangalie Bunge kwenye TBC ambayo ni Televisheni ya Taifa halafu anakuja Nape anataka kufananisha sisi na Sri Lanka. Hivi toka lini sisi tumewahi kufanya mambo yanayoshabihiana na Sri Lanka? Kwa nini usiige Marekani ambako kuna TV inayoonesha Senate saa ishirini na nne inayoitwa C-Span, iko maalum kwa ajili hiyo, halafu unakwenda kuchagua Weakest link, unaenda Sri Lanka, unaenda Australia, ambako hatushabihiani wala hatushirikiani katika mambo yoyote. Ukifananisha na tunavyoshirikiana na Marekani na tunaweza kuwaiga vitu vizuri kama hivyo wana channel inayoitwa C-Span ambayo inaonesha Bunge la Marekani masaa yote ndugu zangu.
Ndugu zangu katika suala la drugs hatuwezi kujadili maendeleo wakati nguvu kazi inazidi kuharibika. Sasa mimi najiuliza nguvu kazi inazidi kuharibika kwa dawa za kulevya, mmekomaa na ganja (bangi) kama alivyosema yule Mheshimiwa aliyepita, lakini mimi naomba….
MWENYEKITI: Samahani Mheshimiwa Mbilinyi.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Again? I can’t even speak eeh?
TAARIFA
MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.
MWENYEKITI: Mwanasheria Mkuu!
MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Kanuni ya 68(8), si kweli kwamba Mheshimiwa Waziri Mkuu amepiga marufuku vyama vya siasa visifanye shughuli zao za siasa na Mheshimiwa Waziri Mkuu aliifafanua vizuri hiyo hoja siku ya Alhamisi alipoulizwa swali na Kiongozi wa Upinzani hapa Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kutoa taarifa hiyo.
MWENYEKITI: Umeipokea taarifa Mheshimiwa?
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naikataa, Waziri Mkuu anatakiwa afute kauli yake kabisa na aseme vyama viko huru siyo kupindapinda, kwamba niliongea kama Mbunge, sijui niliongea kama nini, aseme kwamba ni ruksa kwa watu kufanya shughuli zao za kisiasa kama kawaida. Hicho ndicho anachotakiwa asema. Ingekuwa ni uongo angekanusha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunajaribu kusema, mnazungumzia dawa za kulevya, Rais Kikwete alimkabidhi Rais Magufuli ripoti ya kazi yake ya miaka kumi yenye kurasa 54. Miaka ya nyuma huko Kikwete alisema anayo majina, je, yale majina kwenye hii ripoti ya kurasa 54 hayakuwepo? Kama hayakuwepo kwenye hii ripoti ya kurasa 54 kulikuwa na nini basi labda wananchi tungeambiwa kwa faida ili tujue nchi inakwendaje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuje kwenye mipango ya maendeleo Kimataifa, safari za nje siyo tatizo. Kuna gharama nzuri na gharama mbaya. Gharama mbaya ni pale kama vile Kikwete alikuwa anaenda sijui anapokelewa sijui na Mkuu wa Shule, Mkuu wa Chuo, sijui anapokelewa na Meya, sijui anapokelewa na Mkuu wa Taasisi gani, lakini ni lazima ili tuende sambamba na dunia, sisi siyo kisiwa, lazima Rais Magufuli aende UN , lazima aende AU kwenye vikao vya Kimataifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kuna Mkutano Davos wa Kimataifa, dunia yote iko kule inazungumzia uchumi, wewe umekaa huku, unasemaje Mipango ya Maendeleo. Kwa hiyo, kuna gharama mbaya na gharama nzuri. Gharama nzuri unakwenda Davos, unakutana kule na dunia, kina Putin na akina nani, mnajadili dunia inavyokwenda masuala ya uchumi, unatangaza na visima vyetu vya gesi kule kwa deal nzuri na vitu vingine kama hivyo ndugu zangu.
Kwa hiyo, gharama nzuri ni pamoja na kwenda Davos, kwenda UN, lakini pia kuangalia delegation iwe ndogo siyo kwenda na delegation ya watu 60, watu 70. Kwa hiyo, President Magufuli he has to go abroad akajifunze. Take a jet brother, he have to take a jet akajifunze dunia inafanya vipi, Marais wanafanya vipi, watu wapo Davos huko akina Putin, akina nani, yeye amekaa hapa. Apunguze delegation tu, aende na watu kama kumi na tano, 10 inatosha, aache kwenda na watu 60, 40.
Mheshimiwa Mwenyekiti, rasilimali watu mnasema mnaboresha wakati wafanyakazi bado wananyanyaswa, wanafukuzwa hovyo. Hapa leo niko Bungeni, tayari huko Mbeya Cement kwangu, kuna wafanyakazi wanapunguzwa. Mtu kafanya kazi miaka nane, anakuja kupewa 180,000/= ndiyo kiinua mgongo huko. Mnaboresha vipi masuala ya wafanyakazi. Umeme, naona hata kazi kuchangia hivi vitu in details kwa sababu miaka mitano nimechangia na mpaka leo bado tuko vilevile, ndiyo maana unaamua kutupia tu kama hivi. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la umeme, Profesa Muhongo, nimeangalia ukurasa wa 41 kwenye mpango wa umeme, nishati. Sijaona mpango wa umeme kutumia chanzo cha joto ardhi (geothermal), ambao dunia nzima inajua ndiyo umeme rahisi, kule Italy kuna kituo cha geothermal toka mwaka 1911 mpaka leo kinafanya kazi, wanabadilisha tu nyembe zile kwa sababau chanzo ni cha uhakika na cha maana zaidi. Katika hili, Serikali hii imeanzisha Kampuni, kuna meneja, kuna management wako kule Mbeya wamekaa hela hamuwapi wanahitaji dola milioni 25 kutuletea umeme huu nafuu, lakini ninyi mnakaa mme-mention hapa kila kitu mambo ya geothermal (joto ardhi) hamna, maana yake nini? Mtakwenda kesho mtawatembelea ofisini, mtasema hawafanyi kazi, mtawafukuza kazi, mnasema mmetumbua majipu wakati hela ya kufanyia kazi hamjawapa ndugu zangu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, nitoe angalizo kwa Mheshimiwa Waziri wa Fedha, nakufahamu siyo sana kwa kukufuatilia weledi wako, wewe ni technocrat, siyo mwanasiasa, usifuate hawa wanasiasa wanazomeazomea, tunaamini kwamba ukitulia, ukatumia nafasi yako kama technocrat ukacha cheap politics, populism, unaweza ukaisaidia nchi pengine na sisi tutaku-support ili twende vizuri. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, I am going to try to be polite today ili nichangie kuona nchi yetu inaenda namna gani. Nitajikita kwenye masuala ya biashara; kubwa, kati na ndogo ambayo yana-reflect kwenye masuala ya ajira kwa namna moja au nyingine. Nitaanza na tatizo lililopo bandarini sasa hivi kwenye suala la mizigo kupungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bandarini mizigo imepungua sana na nashukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu amekuwa mfuatiliaji sana wa namna bandari ya Dar es Salaam inavyokwenda na naamini amebakiza trip mbili kwenda ataitwa Mr. Bandari. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo bandarini ambalo nimelifanyia utafiti baada ya kuingiwa shaka na rafiki yangu mmoja dereva wa malori ya kwenda Congo. Huyu bwana alikuwa hana tatizo, anasafiri, anaishi maisha yake akifika Dar es Salaam ana gari yake, maisha yanaendelea kama kawaida hanisumbui, lakini eventually akaanza tabia ya mizinga. Haipiti siku mbili kaniomba 20,000 nikamwambia naomba tuonane, nikamwambia umefukuzwa kazi? Kasema sijafukuzwa kazi, lakini niko bench nina miezi mitatu toka Januari sijapata mzigo kwenda Congo. Ikabidi nifuatilie kwa namna zangu, nikagundua tatizo ni kitu ambacho kimekuwa introduced bandarini kinaitwa single custom territory hususan kwa mizigo ya Congo upande wa Katanga. Sasa hili limekuwa ni tatizo kwa sababu lina taswira ya siasa za ndani ya Congo.
TAARIFA...
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi, unapokea taarifa hiyo?
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Hapana. Niendelee Mheshimiwa Mwenyekiti?
Mheshimiwa Mwenyekiti, sipokei taarifa yake kwa sababu naishauri Serikali hapa, Waziri Mkuu yupo pale, I am very serious kwa sababu suala lolote linaloleta impact kwenye masuala la ajira lina-affect mitaa na hii ni Serikali za Mitaa; siyo tu kuchagua tu kusimamia vyoo vya stand na kadhalika, masuala ya ajira pia TAMISEMI inahusika direct or indirect.
Kwa hiyo, tunaposimama kuchangia hapa halafu mtu anasimama anataka kupata point kwa sababu Mbunge wa Mbeya Mjini anaongea, that is wrong and very bad for the development of our country. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii single custom territory inaonekana tuliingia kisiasa kwa kuingilia siasa za ndani ya Congo katika masuala ya kukomoana. Jana mmeniona nimekaa muda mrefu na AG pale, nilikuwa najaribu kumpa hii picha kama mshauri wa Serikali ili tuangalie kwamba tunafanyaje kuondoa hili. Kwa sababu kwa kuzuia mizigo ya upande mmoja wa Congo wakati sehemu nyingine ya Congo, Kinshasa na wapi hawajakuwa affected na hii single custom territory, maana yake wale wafanyabiashara wa upande ule wa Katanga wakiona hapa panabana, wanachofanya wanahama bandari. Wamehama bandari, wameenda Beira, wameenda Mombasa; sasa hii ina-affect kwenye ajira ambayo Serikali za Mitaa watu wapo mitaani. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ina-affect namna gani? Kwa hawa wafanyabiashara kuhama na kwenda Bandari za Beira mpaka Soweto - South Africa, kinachofanyika ni kwamba hata Makampuni yetu ya clearing and forwarding ambayo yanaajiri watu around ten thousands nafikiri au kati ya 6,000 na 10,000 hawa wote ajira yao inakuwa shaken. Ajira yao inapata madhara na ndiyo sasa inakuja mpaka kwa madereva wa malori ambao wanaendesha magari ya mizigo kwenda katika maeneo hayo ya Congo. Wanapokosa mizigo ina maana wanakaa bench. Ni familia zile ambazo zinakuwa zimepata madhara kutokana na hiki kitu; halafu mtu anasimama anataka ku-interfere. Malori yakikosa kazi mama ntilie wanakosa kazi humo katika barabara zote. Watarudisha vipi hizo hela za TASAF mnazopeleka mnasema sijui VICOBA wakope; watarudisha vipi kama hizo ajira zao zinakuwa affected?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ukiacha zile direct impact kuna indirect. Mfanyabiashara wa Congo anapokuja kuchukua container zake kumi kutoka China anachofanya, kuna viwanda vyetu local hapa vinatengeneza mafuta ya kula; sisi wenyewe si tunakula mafuta sijui ya Malaysia siku hizi tunanunua supermarket; yale local yanayotengenezwa hapa na viwanda vyetu, akina Zakaria, wale Wacongo, akifuata container zake kumi anachukua na lita kadhaa za mafuta maelfu na maelfu ya mafuta kula anapeleka Congo na michele, viungo na viazi. Utasema utakavyosema. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hawezi kwenda Beira au Mombasa kwenda kufuata container kumi halafu atoke tena kule aje Tanzania kununua mafuta ya kupikia au kuja kufuata viazi au kuja kufuata mchele. Kwa hiyo, haya mambo yana multiply effect kwa watu wetu katika masuala ya ajira. Kwa hiyo, tuangalie hii single custom territory, kwa sababu ninavyosikia katika uchunguzi wangu, ilikuwa ni katika kukomoana tu; siasa za ndani, utawala unataka kukomoa upande mwingine kwa siasa za Urais. Sisi hatutaki kuingia huko Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje unaweza ukalifuatilia hili ukaona unawashauri vipi katika maeneo hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, viwanda vyetu vinadoda, lakini katika biashara nyingine ndogo na za kati pia nyingi zinakufa. Kwa hiyo, wakati tunashughulika huku na big sharks wakubwa wanaoishi kama malaika na wananchi waishi kama shetani. Hawa wanaoishi huku chini wanapata anguko kubwa sana kwa kadri biashara zinavyoanguka. Nitatoa mfano mmoja, juzi nilikuwa niko safarini nakuja Dodoma, nikalala pale Morogoro kwenye hoteli ninayolala. Nitangaze interest, na mimi najaribu kuingia kwenye biashara ya hoteli msije mkasema ndiyo maana. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimelala katika ile hoteli, ina vyumba zaidi ya 45; nafika mimi na dereva wangu, sioni porter, nikasema porter yuko wapi? Wanasema Mheshimiwa tuna hali ngumu, hapa mnapoingia ni ninyi tu ndiyo mnalala humu ndani. Mimi na dereva wangu, nikasema kulikoni? Akasema Morogoro nzima biashara ime-shut down huduma. Sasa Morogoro ilikuwa ni eneo linalotegemea viwanda; viwanda vyote sijui Moproco, Moro Shoes vimekufa, imebaki biashara ya huduma (hospitality) kama hoteli, huduma sijui ya vyakula (restaurant), sasa vile vyote vinakufa pale Morogoro; hata hoteli ya Mzee Makamba Katibu Mstaafu,, itafungwa very soon na watageuza hosteli. Sasa huwezi kugeuza hoteli zote hosteli kwa sababu zile hoteli pia wamechukua mikopo, wale hawajajenga kwa cash, wana mikopo benki. Kwa hiyo, utakwenda ku-affect hata mabenki katika system ya mikopo. Sisi wengine tunaoenda kuchukua mikopo tutapata taabu kupata mikopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hii yote ni kwa ajili ya nini? Eti mmefuta semina, sijui mmefuta warsha; tatizo siyo semina na warsha. Tatizo ni pale Mheshimiwa Waziri unaposahau bahasha Dar es Salaam halafu unaagiza V8 (gari) liilete na dereva na wasaidizi wanakuja Dodoma wanakaa wiki; hilo ndiyo tatizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mnaposema hakuna warsha, hata zile zilizokuwa zinaandaliwa chini ya UNDP sijui na Mashirika mengine watu wanaogopa kuzi-implement; sasa madhara yake ni kwamba siyo tu majadiliano ya uendeshaji nchi hayafanyiki, lakini pia madhara yanakwenda kwenye huduma na moja kwa moja tunapata madhara kwenye ajira za watu wetu. Kama mfano niliotoa wa Morogoro, kwa hiyo, hili tuliangalie kidogo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la TBC halafu nawaona sana Team Lowassa wenzetu wengi tu wanavyojitahidi kunyanyuka nyanyuka, nasikia wameambiwa watashughulikiwa; sasa kila mtu akisimama anasimama na sisi, hatupumui ili kwamba ajisafishe. Kama ulibugi, umebugi tu utashughulikiwa. Maana yake kila mtu akisimama mnamtaja Lowassa leo humu. Aliwaambieni akimaliza siasa anakwenda kuchunga ng‟ombe, mnataka arudi au mnaogopa kivuli? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niseme tu suala la TBC; haya yote niliyoyasema matatizo ya ajira na kadhalika ndiyo kinachoendelea huko chini kama hamwambii Mheshimiwa Rais. Sasa mkiacha sisi humu tuonekane tunawaongelea, wananchi wanapata relief, wanapumua. Wakipumua wanajua hili suala linaongelewa litashughulikiwa hata mkipita miaka mitano tena bila kulishughulikia lakini angalau tunawasaidia, kuwatuliza wananchi kuliko kuwaacha katika sintofahamu; hawajui ndani humu mambo yao yanayojadiliwa ni yapi, matokeo yake huko nje kutakuja kulipuka ndugu zangu. Sitaki kuchafua hali hewa kama mnavyosema. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakuu wa Mikoa aina ya Makonda ndiyo wanafanya nchi iyumbe kiasi kwamba mitaani sasa hivi watu wanasema nchi ina Marais wawili, wanakurupukia mambo. Tumeujenga muziki wa Bongo Fleva kwa zaidi ya miaka 25 mpaka leo unatoa ajira halafu mtu kwa kutaka sifa tu anasimama kwenye podium anavuruga kila kitu kwa muda wa dakika 20. Mheshimiwa Mwenyekiti, vitu kama hivi haviwezi kukubalika na ndiyo maana tunasisitiza umuhimu wa viongozi wote ambao ni presidential nominees wafanyiwe vetting na Bunge. Mtu kama Makonda angepita kwenye Bunge hili kufanyiwa vetting asingepita kwa sababu kwanza hana adabu alimpiga Mzee Warioba, wote tunakumbuka na picha ipo. Mtu aliyempiga Waziri Mkuu Mstaafu na Makamu wa Kwanza wa Rais chini ya Mwalimu Nyerere, anamkunja, leo hii unampa kazi nyeti kama Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ni makosa makubwa sana. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, anatuhumu watu, kama kutuhumu watu yeye Makonda anatuhumiwa kwamba ni mtoto na yeye tumwambie kwamba aende kwa Mganga Mkuu wa Serikali akapimwe marinda. Kwa sababu tufike mahali tuendeshe nchi kwa misingi. Waziri Mkuu upo, Waziri wa Mambo ya Ndani upo, Mawaziri mpo, Waziri wa Sheria upo, Serikali ipo, sasa hii nchi tunaipeleka vipi, tunaiyumbisha. (Makofi/Kicheko) Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, tuliheshimu Bunge ndugu zangu. Bunge liheshimike sana, hatutajenga viwanda kwa kumkamata Mheshimiwa Lissu na kumfunga kila siku na kupata dhamana. Hatutajenga viwanda kwa kumweka Mheshimiwa Lema detention hata kama atakaa kule ndani miaka kumi iko siku atatoka kwa sababu Mandela alikaa kwa miaka 27 na akatoka. Ndugu zangu, hii nchi ni yetu sote, tunaipenda, tunaomba sana tusikilizane, kama walivyosema waliotangulia kwamba sasa mambo ya CHADEMA, CCM yakae mbali tuwatolee macho na tuwakaripie watu kama Makonda, wanakuja hapa wanavurugavuruga nchi wakati nchi ilikuwa inakwenda vizuri. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi sasa ya kuchangia baada ya kususia hotuba kutokana na kubanwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze sijui na Mwenyekiti, sijui Katibu, ni Naibu Katibu, Kiongozi Mstaafu wa UVCCM anayesema kwamba tukiudharau mwenge tutapata taabu sana. Ninyi mmemdharau Mwalimu Nyerere na bado mna- survive, itakuwa sisi kuudharau mwenge! Mmedharau misingi mingi sana ya Mwalimu Nyerere ambayo aliiweka katika nchi hii. Mnalinda mwenge badala ya kulinda Azimio la Arusha ambalo lilikuwa na misingi mizuri kabisa kwa ajili ya kuwa na viongozi bora wa nchi hii. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna mtu anayesimama kwenye Bunge hili, hata wewe uliyekuwa kiongozi wa UVCCM, sijawahi kusikia hata siku moja unamkumbuka Seth Benjamin, shahidi wa Azimio la Arusha. Mnatetea vitu vyepesi vyepesi tu, mnasimama humu ndani. Unasema lazima tukimbize mwenge kwa sababu upo kwenye ngao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye ile ngao kuna jembe na nyundo na pembe ya ndovu. Sasa tuvichengue vyote kuwe na route ya pembe, jembe na kuwe na route ya shoka nazo viwe na mbio zake kwa sababu tu zenyewe nazo zipo kwenye Ngao ya Taifa. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, alichokizungumza Mheshimiwa Lissu ni kitu cha msingi sana. Nembo za Taifa zinaeleweka na tunatakiwa tuziheshimu, tusipotoshe kama tulivyopotosha mambo mengine huko nyuma. (Makofi)

Mhesimiwa Mwenyekiti, huu mwenge ndiyo maana hata sijauzungumzia kwenye hotuba yangu, hauna hata shughuli ya kufanya; wanavizia miradi. Mbeya Mjini mathalani toka uhuru kulikuwa hakujajengwa madaraja yanayounganisha Jiji la Mbeya na kata za pembezoni kuelekea Mbeya Vijijini, kunazunguka mto. Leo hii chini ya Meya wa CHADEMA, Mheshimiwa Mwashilindi katika kipindi kisichozidi miaka miwili, tumejenga zaidi ya madaraja kumi kuunganisha Jiji la Mbeya na pembezoni. Huko nyuma chini ya Meya wenu hamkujenga, sisi tumejenga halafu eti mnakuja kuleta mwenge kuzindua, ndiyo maana wananchi hawakwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sisi humu ndani pia tunawakilisha wananchi, hatuwezi kuja humu ndani kuzungumza kitu ambacho ni unpopular huko nje. Only people ambao wanaweza kufanya hivyo ni ninyi kwa sababu mnazozijua wenyewe. Mnajua kabisa hiki kitu hakitakiwi na wananchi, lakini mna-impose, mnalazimisha. That is you, sisi hatutafanya hivyo. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wasanii, ifike sehemu sasa sisi wasanii tuache kutumika. Unaangalia move kama ya hawa watu wa filamu ya hivi karibuni, wanaitwa na Bashite. Bashite kakataliwa na jamii zote, mpaka masela wa hip hop wamemkataa, washikaji zake ambao alikuwa nao anafanya naye gym huwaoni tena, wamemkimbia; ameenda kuchukua wanyonge wa bongo filamu, anawakumbatia, anatoa matamko ya ajabu baada ya kukataliwa na vyombo vya habari (media). Wasanii tunaachaje ku-support vyombo vya habari wakati ni wadau wetu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vyombo vya habari ni wadau wetu. Bila wao sisi hatuwezi kufanya sanaa. Ukiona wapo katika movement fulani kudhibiti kitu fulani chenye manufaa kwa nchi, ni lazima sisi wasanii tuunge mkono wanahabari. Wanahabari wamemsusia Bashite, sisi tunaenda tu kukaa pale kwenye makochi ya Serikali kumsaidia kujisafisha na kumnasua. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema wanasiasa tuache kutumia wasanii vibaya, tuache ku-abuse wasanii. Mpaka Wabunge, juzi anasimama humu Mheshimiwa Keissy, huwa na namwita mzee, lakini simwiti mzee, anasimama anasema Msanii Roma kamtukana Rais. Hamjui hata Roma, hajawahi kumwona. Kwanza yeye ni sala tano anavyotuambia, anajuaje mambo ya hip-hop? Hamjui Roma, hajawahi kumwona, anatoka anasema, Roma kamtukana Rais. Wapi? (Kicheko)

Kwa hiyo, Mheshimiwa Mwakyembe ulienda kukaa na mtu aliyemtukana Rais wako pale kwenye press? Halafu watu mnapiga makofi, mnashangilia. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema, mtu kama Mheshimiwa Keissy nampuuza. Kwanza Bunge lililopita miaka mitano yote alikuwa anatetea bangi humu ndani; nashangaa hajaulizwa. Miaka mitano yote alikuwa anatetea bangi. Alinifuata mimi, bwana tutetee hoja ya bangi; nikamwambia bwana, mimi hayo mambo siyajui, wala sijawahi kuyagusa. Utajijua mwenyewe huko. (Kicheko/ Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi namtaka Roma Mkatoliki, msanii wa muziki ambao nimeuasisi, atoke sasa aongee kwa uwazi, in details kilichomkuta ni nini? Public ikishajua, inaweza ikasaidia kujua ni nani waliomteka yeye na wenzake na walitumwa na nani, full stop. Vinginevyo tutaendelea kuwa na debate kama za Ben Saanane hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ripoti ya Nape, naomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kujibu atuambie kabisa kiuweledi what made you deny ripoti ya Waziri aliyekutangulia Mheshimiwa Nape? Huyu mtu Bashite ameenda kuvamia kituo cha redio na tv mpaka studio na watu wana bunduki, machineries, polisi wamesema hawawajui wale watu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni nani wale watu walioenda kuvamia kituo cha Clouds fm? Kuna watu wananiambia, Sugu ulikuwa na bifu na Clouds miaka yote, sasa hivi unawatetea. Nilikuwa na bifu na Clouds kwa sababu ya haki. Haki ni haki, iwe dhidi yangu, iwe ni dhidi ya Clouds na mtu yeyote, nitatetea. Hata kama ninyi huko nikiona Waziri yeyote hatendewi haki, nitamtetea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu mtu ripoti imewekwa wazi kwamba amefanya makosa, kwa nini analindwa? Analindwa kwa maagizo ya nani Bashite? Maagizo ya nani yanafanya eti waseme hatuwezi kuchukua hatua kwa sababu Bashite hakusikilizwa? Hakusikilizwa wakati Tume imeenda imekaa ofisini kwake masaa matano, sita, saba, nane, akatokea mlango wa uani! Sasa yeye ni bingwa wa kuwaambia watu tukutane central police, tukutane mahakamani; yeye anaitwa kwenye vyombo halali vya sheria, chombo kilichoundwa na Waziri, anaingia mitini, he is a coward.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bashite is a coward, ni jambazi, thug, ni criminal ni fraud. Bashite ni fraud kwa sababu ame-forge vyeti. Halafu Serikali inatoka inasema ooh, hatukuwagusa wanasiasa. Ma-RC na ma-DC siyo wawakilishi wa wananchi. Sisi hapa ndiyo tunaweza kuingia kwenye uongozi kwa kusoma na kuandika, lakini siyo RC wala DC. Wale wanatakiwa lazima wawe na level fulani ya elimu na hili suala linajulikana wazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zaidi, suala la Bashite siyo kwamba ana elimu gani? Suala ni ku-forge. He is a fraud! Amefanya forgery, anatakiwa kusimama mahakamani, ndipo sehemu anapotakiwa kusimama. Sasa kinachomfanya azuiwe asichukuliwe hatua hizo …

KUHUSU UTARATIBU....

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sasa Serikali kupitia Waziri wa TAMISEMI inaanza kutupa mwanga wa Bashite ni nani, kwa sababu inaleta mjadala sana katika Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, huyu mtu ni fraud. Tunaonea watu wadogo, watu wanalazwa, watu wanazimika, eti nchi hii wanasema dereva wa Mkuu wa Mkoa anatakiwa awe na cheti cha form four, lakini Mkuu wa Mkoa hata kama ameishia darasa la pili, akiweza kusoma na
kuandika that is a big joke! Ilibidi mje na maelezo yanayonyooka. Tanzania hii nawaambia kila siku, watu wameamka, siyo kama Tanzania ile ya zamani unaamka tu unasema kwamba kiongozi fulani fikra zake zimeota; ameota au amefanya nini ndiyo maono sahihi kwa asilimia mia moja. Hata wakati huo, kulikuwa na mijadala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge la wakati ule mimi nikiwa mdogo, tulikuwa hatuoni kwenye tv, tunasikiliza kwenye redio, kuna watu walikuwa wanaitwa akina Tuntemeke Sanga na Mohamed Nandonde, huwaoni kwa sura lakini lazima usikilize Bunge ukisia kwamba anadai barabara ya Mtwara wakati ule. Halafu sasa hivi mnakuja mnasema tu tumefanya hivi, tumefanya hivi, mnasahau watu waliofanya kazi, mnamsahau Rashid Kawawa na Mwalimu Nyerere. Hata mtoto wa Kawawa juzi mmemnyima Ubunge hapa wa Afrika Mashariki, halafu mnajidai mnaenzi watu. Mtoto wa Nyerere pia mmemnyima Ubunge wa East Africa hapa, halafu mnasema mnaenzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii cybercrime naona imeanzishwa kwa ajili ya UKAWA tu. Wakati vijana wa UKAWA kutoka akina Mdude Nyagali kutoka Mbozi mpaka hao tunaozuiwa tusiwataje, akina Ben Saanane wanapata matatizo, wanakamatwa na kunyanyaswa kwa kutoa maoni yao kwenye mitandao, vijana wa CCM wanatukana Viongozi wa Upinzani mpaka matusi ya nguoni lakini hakuna mtu ambaye anawakamata wala kuwachukulia hatua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vitu hivi mnaweza mkaona ni vitu vyepesi sana, lakini niwambieni mna… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kutuhakikishia juzi wakati unafungua tunaanza Bunge ulituhakikishia kuwa tusiwe na wasiwasi safari hii tuko salama tukiwa Dodoma.

Sasa naiomba na excutive nao watuhakikishie usalama tunapokuwa kwenye maeneo mengine mbalimbali ya nchi kwa sababu ni uwazi dunia yote sasa inajua Wabunge wa Upinzani na watu wengine wenye mawazo mbadala hawako salama. Sasa hatuwezi kujadili mipango katika mazingira ambayo sio salama, so please don’t shoot me, natoa ushauri, mawazo maoni yangu kwa Serikali, tubishane hoja na sio bullets, mfano tunazungumzia mipango ya kubana matumizi, lakini ukiangalia Baraza la Mawaziri limeongezeka, Mawaziri wameongezeka Makatibu Wakuu wameongezeka. Viongozi wa kawaida wana ulinzi wa kupita kiasi, Naibu Spika ana walinzi wawili, wasaidizi ambao akisafiri nao nje wote wanalipiwa business class zile ni fedha ambazo zinakatwa tiketi. (Makofi)

Mheshimiwa Menyekiti, nakumbuka Mheshimiwa Spika wakati ule ukiwa Naibu Spika nilikuwa nakuona unatembea na Katibu tu na gari moja. Lakini leo hii unakuta Naibu Spika ana motorcade ya magari kibao, Bashite ana motorcade, ana walinzi kuliko hata Waziri Mkuu. Sasa unajiuliza gharama zote hizi zinazotumuka kwa Bashite ulinzi motorcade kuliko Waziri Mkuu, ni majukumu gani aliyopewa ambayo yanalazimika apewe ulinzi wa gharama kiasi hicho?

T A A R I F A ....

MHE.JOSEPH O. MBILINYI: Hiyo sio taarifa hilo ni swali na hiki siyo kipindi cha maswali, kipindi cha maswali kimeshakwisha. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumzia mipango, lakini mipango bila utaratibu haiwezi kuwa mipango. Sasa watu wanawaka sana tukizungumza kuhusiana airport ya Chato, hamna mwenye tatizo na airport ya Chato, lakini tatizo ni namna ilivyokuja na bajeti yake na utaratibu wake ndiyo tatizo lililopo. Sasa ukiangalia kama project kama hizi inanikumbusha enzi ya Mobutu Sese Seko Kuku Ngbendu Wa Za Banga wa Zaire alikwenda kijijini kwake Gbadolite akajenga Ikulu ya ya vyumba zaidi ya 100. Akaja na project ya airport ya kimataifa, lakini leo vyote vile kwa sababu vilikuja/vilizuka bila mipango ya nchi vinakaliwa na popo na panya. Kwa sababu ndege gani itaenda kutua Chato Mheshimiwa Rais atakapomaliza muda wake, mnakosa muda wa kwenda Butiama kwa Baba wa Taifa mtaenda Chato? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunachozungumza hapa its not personal ni principals, mipango. Tunajisifu kupanda kwa bei ya korosho zao moja tu ambalo mazingira yake wote tunajua ni kama mazingira yaliyopandisha kahawa enzi za Mrema, Mrema akawa anatafuta credit miaka yake yote kwa kupanda bei ya kahawa, kumbe tatizo lilikuwa kwamba kulitokea ugonjwa wa kahawa huko Brazil kahawa ikawa inahitajika. Kwa sababu kama korosho imepanda bei kwa mipango vipi mipango ya kupandisha bei ya kunde, choroko, mbaazi, tunasikia sasa hivi mbaazi bei imekuwa mpaka shilingi 100. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama suala ni mipango na mikakati ya kutafuta masoko ya mazao basi tutumie maarifa tuliyopandisha bei ya korosho kufika shilingi 4,000 na mbaazi nayo ifike hata shilingi 1,500 au 2,000 ili kuondoa kilio hiki cha wakulima wa mbaazi, tumbaku, choroko na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakwenda sasa hivi tuna zunguka kuzindua barabara, lakini barabara zote ni za Mzee Kikwete, flyovers za Mzee Kikwete, Daraja la Kigamboni Mzee Kikwete Awamu ya Tano barabara pekee tunayoijua ya approve ni ile kutoka Mwenge mpaka Morocco ambayo wali-divert fedha za sherehe ya uhuru ikaenda kujenga kile kipande cha barabara, lakini barabara zote tunazozindua sasa hivi ni za Mzee Kikwete mwana dipromasia aliyetukuka Mungu ampe maisha marefu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwasihi Mawaziri hasa hawa wapya achene kushindana kwa matamko, mshaurini Rais maana yake kila siku matamko mara tunataka viwanda 100 kila Mkoa halafu ilo jukumu unampa Mkuu wa Mkoa ambaye hata allowances zile anazostahili kupelekewa azipelekwi hazitoshi kabisa. OC hamna, Halmashauri hamna fedha, leo unamwambia anajukumu la kusimamia ujenzi wa viwanda 100 huu sio upangaji wa mipango, huku ni kudanganyana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwaombe sana Mawaziri wapya hasa vijana be humble, cool down, show your talent, will recognize and appriciate you, acheni misifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hili suala la makinikia naona hamna anayelizungumza hili ni suala nyeti ambalo kama Taifa tulikuwa tunalifuatilia sana, lakini kuna dillema nyingi sana katika taarifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tuliambiwa tuna tarajia kupata trilioni 400 plus kutoka kwa hawa mabwana waliokuwa wanatuibia kwamba kila Mtanzania angeweza kupata Noah moja na mafuta tungejua sisi wenyewe namna ya kupata, lakini kila mtanzania angeweza kupata noa moja. Lakini baadaye baada ya muda tunaambiwa kwamba wezi wamekubali kulipa bilioni 700 tu kutoka trilioni
400 plus na baadaye tunaanza kusikia tena jamaa wamegoma kwamba hawawezi hiyo kutoa. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo hamna taarifa we turned to be the wealth laughing stock, dunia nzima inatucheka International media zina tuandika vibaya, zinamwandika vibaya Rais wetu kutokana na vitu kama hivi. Huyu mtu kama msemaji wa Serikali badala ya kukaa kusemea mambo kama haya yeye amekalia tu kufungia magazeti kwa vifungu ambavyo ni wrong. Mtu anakuja anafunga gazeti kwa kutumia kifungu namba 54(1) cha sheria mpya ya habari ya mwaka 2016 wakati ile sheria straight and direct inasema adhabu ni kifungo au faini kwa mtu a person, sio gazeti lakini Msemaji Mkuu wa Serikali anatoka anafungia gazeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, anafungia magazeti kwa kifungu ambacho ni wrong anafikiri watu ni wajinga, watu wanatafuta sheria hata kwenye mitandao wanaenda wanasoma kile kifungu ndiyo maana wanaharibu sifa ya Mtukufu Rais wa Awamu ya Tano mpaka watu wanamuita dikteta kwa sababu ya watu kama huyu Msemaji wa Serikali kwa sababu udiktekta ni ku-dictate, ni kulazimisha, unalazimisha sheria ambayo aihusiani kuchukua hatua ambayo haihusiani which is very wrong.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ni jukumu la hili Bunge sasa kuwaambia hawa Mawaziri mnapokaa kwenye Baraza la Mawaziri muangalie Rais usoni na mumshauri, yule ni binadamu kama nilivyosema alikuwa anakaa kiti cha pale mi nilikuwa nakaa kiti cha pale havipiti hata viti sita/saba kutoka nilipokuwa nakaa. Tulikuwa tunaandikiana nae vinoti humu tukiwa na ishu mbalimbali, ninyi mnashindwaje kumshauri kwamba this is wrong, this right. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu inafika mahali sasa Watanzania hawaamini tena kauli za Serikali inakuwa flip-flop, Rais anasema hivi, Waziri anakuja nasema vile matokeo yake mnabaki kuwa defensive wakati mlikuwa kwenye position ya ku-offensive, tulivyoanza anza apa sisi Bunge hili kama Kambi ya Upinzani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, amekuja hapa Waziri wa Elimu, majukwaani mnasema Rais anaenda vizuri sasa hivi hakuna tena migomo wala maandamano ya wanafunzi, juzi tumeona mgomo, leo Waziri wa Elimu anakuja hapa anapiga longolongo, karatasi nyingi unamaliza miti tu, kutengeneza karatasi unaleta jangwa unamaliza miti, maelezo mengi. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala ni kwamba watoto wanaangaika mikopo juzi wameandamana na ninyi mlikuwa mnasema kwamba maandamano hakuna, mnatengaje fedha za wanafunzi 30,000 wakati projection ni wanafunzi 61,000 wanafunzi 31,000 wote waende wape waende mitaaani wakatukabe hii haiwezekani, kwa hiyo, lazima tuwe realistic kwenye mipango yetu. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, tulivyofika hapa tulivyoanza hili Bunge mambo tukasema mpaka wapinzani ni ukweli tulikuwa tunasema dah, bwana sasa huyu jamaa aliyekuja tutakuwa na hoja gani mnaleka hoja wenyewe Rais hayumo humu ninyi ndo mnatakiwa mje na vitu ambavyo vita-reflect uongozi wa Awamu Tano sisi tukose hoja lakini mnaleta hoja wenyewe tukisema mnashindwa kujibu hoja, mnatusubiri tutoke nje ya geti wakati mnaingia kwenye nyumba zetu mtupige pyuu pyuu, that is wrong, that is very wrong. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo ulisema tusiulize tena…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi huo nao ni Mpango pia? (KIcheko)

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: ...za kata halafu ukiuliza unawauliza wahusika unawaambia kwamba aah, mmeanza mambo gani tena ya ku-shoot, wanakuambia aah, usijali we haumo, nani yumo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nakushuru sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza naomba niwashukuru sana Wanambeya wenzangu kwa kusimama na mimi nilipofungwa kisiasa kwenye Gereza Kuu la Luanda, Mbeya, pia nawapa pole kwa wao kufungwa kisaikolojia. Nawashukuru pia Watanzania wote ndani na nje ya Tanzania kwa kulaani kufungwa kwangu kiholela. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niwashukuru sana Wabunge wote hasa wa Upinzani, kwa support kubwa waliyotoa, lakini pia hata upande wa CCM, japo kuwa mliogopa kuja kuniangalia lakini salamu zenu nilizipata; na source ya hofu yenu wote tunaelewa, lakini nimshukuru mzee, Profesa Mark Mwandosya, aliwawakilisha upande wa CCM kwa kuja kunitembelea jela. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nami niwapongeze Mheshimiwa Stephen Masele na Mheshimiwa Mboni Mhita kwa nafasi walizochaguliwa kwenye Bunge la Afrika. Bunge letu limejiunga kwenye Vyama vya Kibunge vya kimataifa kama CPA, PAP, ACPEU, IPU na kadhalika, lakini wote tunafahamu ni kwamba hatushiriki vyema na tatizo sijajua ni nini. Hata hivyo, kama hatujui umuhimu mbona tunafurahia matunda ya ushindi wa Mheshimiwa Masele na Mheshimiwa Mboni Mhita wakati wote tunajua hata kwenda huko walijigharamia wenyewe? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niende kwenye hoja, na nitaanza na masuala ya sera za mambo ya nje (foreign policy). Mheshimiwa Waziri wakati anaanza kuchangia alisisitiza sana kwamba mwelekeo wetu wa foreign policy hatutakubali kuingiliwa wala kuchaguliwa marafiki. Naomba nimhakikishie na kumkumbusha Mheshimiwa Waziri, najua ana weledi katika nyanja za kimataifa, kwamba sisi kama Tanzania hatujawahi kuburuzwa wala kuchaguliwa marafiki tangu enzi ya Mwalimu Nyerere na ndiyo maana tulikuwa member wa nchi zisizofungamana na upande wowote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika ile Non-Aligned Organization (movement) sisi tulikuwa ni member muhimu sana na tulitambulika kimataifa. Tanzania ilikuwa inaheshimika kimataifa kwa mambo kadhaa. Kwanza na muhimu tulikuwa na sera ya kutetea wanaokandamizwa duniani; mfano South Africa, Mozambique, tuliwasaidia sana mpaka kufikia kujiondoa katika makucha ya apartheid na wale Mozambique kupata uhuru wao kutoka kwa Wareno.

Mheshimiwa Naibu Spika, sera hizo hizo tulizokuwa nazo dhidi ya South Afrika na Mozambique ndizo tulisimamia Sera yetu ya Mambo ya Nje kwa Palestina na Sahara ya Magharibi. Mwalimu Nyerere alifuta uhusiano wa kibalozi na Israel kwa ku-support struggle ya Wapalestina kudai uhuru. Sasa tujiulize leo hii tunaenda kufungua Ubalozi Israel, je, ile course ya Mwalimu ku-support uhuru wa Palestina imefikia wapi?

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivi kwa sababu ukiangalia ni kwamba hali imezidi kuwa mbaya Wapalestina ndani ya Gaza na maeneo mengine yanayokaliwa kimabavu wanazidi kuuawa kila siku kadri Israel inavyoongeza uwezo wake wa kijeshi.

Mheshimiwa Naibu Spika, halikadhalika Mwalimu Nyerere na sisi kama Taifa tulifuta uhusiano na Morocco kwa ku-support kudai haki kwa Sahara ya Magharibi chini ya POLISARIO. Sasa leo tumeacha sera zetu dhidi ya Morocco kwa ahadi ya kujengewa uwanja wa mpira stadium, tunajivunjia heshima kwa ahadi ya kujengewa uwanja wa mpira ambao Mheshimiwa Mkapa amejenga pale Dar es Salam uwanja wa mpira kwa support ya Wachina bila kuuza nchi wala bila kukiuka misimamo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina uhakika Mheshimiwa Waziri na Bunge hili Mwalimu Nyerere Baba wa Taifa huko alikolala kaburini Mwitongo anageuka geuka kwa jinsi Taifa hili linavyokwenda sasa hivi katika sera ya mambo ya nchi za nje. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, diaspora; naomba sana Mheshimiwa Waziri tuache siasa kwenye maisha ya Watanzania wenzetu. Ni lini Serikali itatambua Watanzania wanaoishi nje ya nchi (diaspora)? tuache kutoa ahadi kila tena nasikia mwakilishi yuko hapa, I hope amekuja ile straight hakuja kisiasa kwa sababu wenzake anaowawakilisha wanalia sana kule, sisi tumekaa kule, tuna mawasiliano kule, tunajua kilio chao, hata hapa kwenye simu nina mawasiliano ya kutoka diaspora baada ya wao kujua kwamba leo kinaenda kuzungumzwa nini, wametoa nao changamoto zao wanataka tuzizungumze humu.

Mheshimiwa Naibu Spika, wanachotaka watu wa diaspora ni kuruhusiwa uraia pacha, kama ambavyo uraia pacha uko katika nchi nyingine. Wapewe uraia pacha ili waweze kushiriki kujenga uchumi na si tu makongamano mara kuwaalika Zanzibar, mara kuwaalika wapi. Wakati umefika turuhusu sasa uraia pacha ili watu hawa waweze kushiriki katika uchumi wa nchi. Hawa watu wa diaspora sasa wanaanzisha kitu kinachoitwa Tanzania Global Diaspora Council (TGDC). Sasa tusije sisi na mawazo yetu tunataka kuwasaidia vipi sijui kuwashirikisha vipi, wale wana exposure wamefunguka, wanajua wanachokitaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa itakiwa tutambue na Serikali iniambie imejipangaje kufanya kazi hiki chombo cha diaspora cha Tanzania Global Diaspora Council ambacho kinaenda kuanzishwa na hawa Watanzania wenzetu katika kusaidia kuji-integrate kwenye masuala ya nchi yao ambayo wanaipenda. Kwa sababu, otherwise mtu kama ameshapata uraia wa wapi anaweza akaamua kuendelea na maisha na kusaidia kuleta maendeleo kwenye yale maeneo wakati tungewapa fursa wangeweza kafanya hivyo katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hatuna ajenda ya pamoja kwa diaspora. Mheshimiwa Mzee Kikwete alipokuwa anaenda nje aliwashawishi experts wa Tanzania huko nje warudi kujenga nchi yao; lakini utawala huu uliofuata ukawageuka na kuanza kuwanyanyasa mfano ni yule mama Julieth Kairuki wa TIC. Mheshimiwa Dkt. Kikwete alikwenda kumshawishi South Afrika ameacha kazi yake nzuri, ameacha kila kitu kilicho kizuri kinachoendana na weledi wake amekuja nyumbani kusaidia kujenga nchi, lakini leo unamwambia kwamba hatuwezi kukulipa huo mshahara mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi alikuja kwa makubaliano gani kutoka South Afrika anakuja hapa tunakuja tunawageuka? Wengine waliambiwa warudi kujenga nyumbani na kuwekeza wakaanza kurudi kwa wingi wakajenga majumba, wakafungua biashara. Leo hii Waziri wa Ardhi hawa si raia halali, kwa hiyo mali zao zitataifishwa tunawatia woga Watanzania wezetu hawa wakati walikuwa wangeweza kushiriki vizuri sana katika masuala yetu ya uchumi na kujenga nchi.

T A A R I F A . . .

MHE. JOSEPH. O MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ilifaa kabisa kubakisha ubalozi wetu pale Cairo, Egypt, kwa sababu ule ubalozi ulikuwa neutral na ulikuwa unaweza ku-harmonize pande zote yaani Palestina na Israel mpaka mambo yao yatakapokaa sawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais ni top diplomat wa nchi, suala la kusafiri bado ni muhimu, labda kama ana tatizo la kiafya. Tena anapokwenda nje anaweza kutumia lugha ya Kiswahili kwa sababu Rais wa Xi Jinping wa China kila anakokwenda anaongea Kichina japokuwa ni msomi aliyesomea Marekani. Yeye amesomea chuo kikuu na elimu zake za juu Marekani anazungumza Kiingereza vizuri, lakini kila anapokwenda anazungumza lugha ya Kichina; kwa hiyo tena tutakuwa tunaitangaza na lugha yetu ya Kiswahili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na kama tatizo ni gharama mbona anatuma delegations? Mara Makamu wa Rais, mara Waziri Mkuu nao wanatumia gharama kwa sababu hawaendi kule kwa miguu.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hatuendi UN, hatuendi Davos, hatuendi Common Wealth. Common Wealth ni Mkutano wa Wakuu wa Nchi (Head of States), lakini sisi tunatuma wawakilishi wakati kule kuna fursa za kiuchumi na biashara. Rais Uhuru Kenyatta ametumia vizuri sana fursa za kiuchumi na kibiashara kwa nchi alipokwenda Common Wealth, hali kadhalika Rais Ramaphosa wa South Afrika pia alitumia huo kukutana na investors wa kutosha aka-archive miradi ya takribani Rand trilioni 1.2 kwa ajili ya nchi yake; ndizo faida ya majukwaa haya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Rais kusafiri haiepukiki, ni muhimu na kama alivyonukuliwa mzee Kikwete Rais aliyepita kwamba kusafiri kulimsaidia sana, mkaa bure si sawasawa na mtembea bure; hii alisema wazi. Kwa hiyo kusafiri ni muhimu sana, kwa sababu Mabalozi tunaowachagua huko hawatusaidii kwa sababu tunachagua Mabalozi wetu kisiasa bila kuangalia weledi. Aidha, tunawapa ubalozi watu kama zawadi au kuwa- control.

Mheshimiwa Naibu Spika, Dkt. Slaa tumempa zawadi kwa kazi aliyoifanya 2015 katika uchaguzi, tumempa ubalozi, lakini Dkt. Emmanuel Nchimbi tumempa ubalozi Brazil kum- control ili awe mbali kudhibiti ushawishi wake ndani ya Chama cha Mapinduzi. Haya ni mambo ambayo yako wazi na yanaeleweka kabisa. Sasa hawa ni shida sana kusimamia diplomasia ya uchumi, watakuwa wanaleta siasa pekeyake na iko hivi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilisimamishwa kidogo. Diplomasia ya uchumi bila stability ni shida. Tunawatisha wawekezaji, tunapiga risasi Wabunge, tunafunga ovyo Wabunge. Wawekezaji wa nje walifuatilia haya mambo. Wakifuatilia haya mambo inakuwa wanasita sasa kuja kuwekeza kwa sababu hakuna mwekezaji anayetaka kuweka kwenye nchi ambayo haiko stable, haina amani na usalama.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia. Kwanza niungane na Bajeti Mbadala ya Kambi ya Upinzani na pia ni- endorse statement ya KUB, Mheshimiwa Freeman Aikaeli Mbowe kwamba Awamu hii ya Tano imekuwa na bajeti hewa endelevu ikiwemo bajeti hii. Bajeti hii ni hewa kwa sababu haifikii malengo.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2016/2017 malengo yalikuwa trilioni 29 zilipangwa, lakini only trilioni 20 zilitoka. 2017/2018, trilioni 31 lakini only trilioni 21 zilitoka. Makisio wanaweka makubwa kuliko uhalisia wa vyanzo vya mapato, kwa hiyo wanaleta makisio hewa na wanajua kabisa kwamba ni hewa kwa sababu haliwezi gap lile likawa linajirudia kila mwaka.

Mheshimiwa Spika, Serikali hii inafanya matumizi nje ya bajeti iliyopitishwa na Bunge lako. Kwa mfano ujenzi wa ukuta Mererani, hosteli za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ujenzi wa airport Chato, suala la kuhamia Makao Makuu Dodoma, haya yote yanaweza yakawa mambo mazuri, lakini ili yakamilike katika uendeshaji wa nchi yalitakiwa lazima yapite kwenye Bunge lako Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata Sera ya Viwanda ni hewa kwa sababu kila siku tunaskia mnazindua viwanda vipya na kuhesabu idadi imeongezeka, mara viwanda 3,000 tayari siku mbili unasikia kuna viwanda 4,000, hatuoneshwi ujenzi tunaoneshwa uzinduzi. Hii maana yake ni nini; maana yake ni kwamba hawa jamaa wanazindua viwanda ambavyo vipo toka zamani. Kwa mfano kulikuwa na kiwanda kimoja Mwanza, sitaki kukitaja, kilishazinduliwa toka mwaka 2013 huko na marehemu Kigoda, Waziri wa Viwanda, lakini juzi naangalia kwenye taarifa ya habari naona Waziri Mkuu anakwenda kuzindua tena kiwanda kile kile ambacho mimi taarifa zake za uzinduzi nilikuwa nazo. Kwa hiyo tunakwenda na vitu hewa.

Mheshimiwa Spika, sasa mimi nabaki najiuliza; huyu Mheshimiwa Dkt. Mpango alikuwa ametoka, alikuwa ni Katibu wa Tume ya Mipango kwenye Awamu ya Nne chini ya Dkt. JK na nchi ilikuwa inakwenda, sasa hivi wamemweka juu zaidi, ni Waziri kwenye Awamu ya Tano, lakini mambo hayaendi kiasi kwamba najiuliza kweli hii mipango ni ya kwake au kuna mtu anapanga wana-impose tu kwenye makabrasha yake aje kusema humu Bungeni? Hivyo ndivyo vitu ninavyojiuliza, nina uhakika kabisa mipango hii siyo ya Mheshimiwa Dkt. Mpango, kuna mtu anapanga hii mipango sasa sijui anatumia vigezo gani.

Mheshimiwa Spika, sababu zinajulikana, otherwise Wabunge wa CCM hususani wamejaa unafiki. Asilimia 98/99 ya Wabunge wa CCM wanalalamika pamoja na sisi mambo yanavyokwenda, hawaridhiki na hali inavyokwenda katika Awamu hii ya Tano lakini hawasemi hadharani. Sasa sisi tukisema nje wanatulaumu, wanasema sasa ninyi tunawaambia halafu mkifika ndani… (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Mbilinyi, ukisema Wabunge wa CCM ni wanafiki unajua unamsema na Spika pia?

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Hapana, wewe uko exempted kwa sababu hata sasa hivi umeonesha kidogo unanyoosha Kiti kusema ukweli, kwa hiyo tunakupa tano zako. Wakifanya vizuri tunawasifia, wakikosea tunakosoa na tunapokosoa hatuna chuki, no personal vendetta against anybody. Tunapochangia na kukosoa, yote ni kwa ajili ya Taifa hili tukiamini kwamba Taifa hili ni letu sote.

Mheshimiwa Spika, sasa hawa wenzetu wanalalamika nje; kwenye korido huko, kwenye chai na ukisema wanasema kwamba ninyi tunawaambia mkifika ndani tena mnatutoa nishai. Of course lazima tuseme ili nchi iende, wanataka tukae navyo sisi moyoni na sisi tupate presha, presha bakini nazo ninyi wenyewe.

Mheshimiwa Spika, hawa watu wanaokaa kimya ni hatari zaidi kuliko sisi tunaosema. Niseme, mtu kama Mheshimiwa Bashe, Mheshimiwa Nape, Mheshimiwa Alhaji Bulembo hawa siyo tatizo ndani ya CCM kwa sababu hawa angalau wanaongea, tatizo ni ninyi msiosema halafu mnalalamika kwenye makorido (corridors). (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunatakiwa tujue kitu kimoja; katika Taifa la watu almost 55,000,000, sisi tuliomo humu 300 plus, sisi tuko privileged to serve, sasa tusije tukatumia hii privilege to serve kusaliti wananchi; huku unasema hivi huku unasema vile. Halafu kitu kimoja nimefanya utafiti nimegundua, you guys don’t love President Dr. Magufuli, ninyi CCM hamumpendi Dkt. Magufuli. Hamumpendi Rais wetu wala hamlipendi hili Taifa kwa sababu mtu unayempenda lazima umwambie ukweli mambo yanapokuwa hayajakaa sawasawa na hili tunalisema kila siku.

Mheshimiwa Spika, hamuwezi kukaa mnalalamika na sisi, mnasema mambo hayaendi lakini mkifika kwenye floor hapa hamsemi ukweli halafu kila mtu akisimama mnam- personalize, mpaka Mheshimiwa Dkt. Mpango anakuja kumfananisha na madikteta wa North Korea kwa ajili ya kupitiliza upambe, yaani unakuwa mpambe mpaka tajiri ananuna, anaona hapa unaharibu, unanifananisha na watu ambao sitaki kufananishwa nao. Kwa hiyo you guys don’t love our president, mngempenda lazima mngemwambia ukweli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niseme, kama nilivyosema, penye ukweli tunapongeza penye tatizo tunasema. Nampongeza sana Rais Magufuli kwa kum-demote, kumtumbua Mkurugenzi Msaidizi wa Usalama wa Taifa TIS, kutoka kuwa Deputy Director mpaka kuwa RAS kwa sababu toka Mheshimiwa Rais amefanya kitendo kile hali ya nchi imetulia kidogo, hatusikii sana mambo ya kuokota watu kwenye viroba, hatusikii watu kupotea toka yule Deputy amekuwa demoted kuwa RAS haya mambo hatuyasikii. Kwa hili nampongeza Rais na aendelee kuchukua mawazo yetu yeye sisi tutampa kwa sababu wao hawataki kutoa mawazo wanafanya unafiki dhidi ya Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nchi hii sasa Mheshimiwa Mbunge kila Taasisi imekuwa kama polisi. Tumetoka kuongea hapo unaona Maafisa wa Wizara wanaanza kutembea na rula kupima samaki, sasa dagaa utapima kwa rula gani, inabidi watutengenezee rula za kupimia dagaa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, BASATA nao hawako nyuma kila Taasisi imegeuka kuwa kama polisi, kazi ni kamata, fungia sijui nini. Mimi jana wamefungia nyimbo yangu, inaitwa namba 219, wakati nyimbo hata sijaitoa upambe huo.

Mheshimiwa Spika, na- declare interest mimi ni msanii pia na ni msanii nguli wa hip pop Afrika na duniani na ndiyo nilikotokea na nimetoa mchango mkubwa sana katika sanaa ya muziki wa kizazi kipya, bongo fleva mpaka hapa ilipofikia. Hilo Serikali inatakiwa ilitambue sana na isikilize sana tunapozungumzia masuala ya wasanii na namna inavyotengeneza ajira.

Mheshimiwa Spika, sasa wewe unafungia nyimbo ambayo sijatoa, nyimbo ime-link katika katika industry ya music ku-link kupo, mimi najiandaa kushuti video nyimbo ime- link, BASATA hawajaniita kunihoji, pengine ndiyo nilikuwa nawapelekea hiyo nyimbo waisikilize; wao wanatoa tu statement wanafungia nyimbo ya msanii wakati hawajawahi kuingia studio hata siku moja, hawajui hata mihangaiko ya studio, hawajui hata gharama wanakurupuka tu kufungia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumeijenga hii sanaa miaka mingi mpaka imekuwa ajira, wanataka sisi wote tuimbe mapenzi. Sisi siyo kila mtu lazima aimbe mapenzi, sisi tunaimba masuala ya kijamii…

T A A R I F A . . .

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, kama alivyosema ni kaka yake, kwanza naomba mlinde muda wangu, ningempiga lakini kwa hali dada yangu naomba nimwache, tumsubiri mjomba, sitampiga namheshimu. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, ila tu ninachomwambia mimi siyo Roma wala mimi siyo Diamond, naiburuza BASATA Mahakamani kwa suala hili na ndiyo watajua namna gani nchi inatakiwa iendeshwe kwa kufuata utawala bora na sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimeshasema nyimbo imevuja, nyimbo sijaitoa rasmi, wimbo...

(Hapa walijibizana bila kutumia kipaza sauti)

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Ahsante sana Mheshimiwa Waziri Mwakyembe unalielewa suala hili, wimbo umevuja, kwa hiyo BASATA nawasiliana na Mawakili wangu sita ili niwaburuze BASATA Mahakamani, ndiyo watanyooka waache kuchezea kazi za wasanii. Huyo dada yangu Mheshimiwa Shonza mwenyewe hajawahi kuingia hata studio ku-record halafu anakuja anafungia nyimbo za watu kiholela.

Mheshimiwa Spika, nikiacha na hayo ujumbe umeshafika, niombe tu Mheshimiwa Waziri tuondoe siasa kwenye masuala ya uchumi na biashara, nikitangaza interest mimi pia ni mfanyabiashara mchanga ninayeanza.

Mheshimiwa Spika, toka nimeanza kabiashara kangu hawa jamaa wameingiza siasa mara, sijui TRA wamefanya nini, wanakuja wanakuta clear, wanaenda sijui kwenye Taasisi gani wanakuja wanakuta clear, mwisho RSO Afisa Usalama wa Taifa Mkoa anaenda benki iliyonikopesha kuhoji ku-check anakuta kweli mimi nimekopeshwa. Anauliza toka lini mmeanza kukopesha wapinzani? Jamaa akamwambia, Joseph Mbilinyi Mkurugenzi wa kampuni fulani hajaja hapa kama Mbunge, hajaja hapa kama mwanasiasa, amekuja hapa kama mfanyabiashara na mpaka sasa hivi analipa marejesho yake vizuri. (Kicheko/ Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Mheshimiwa Waziri Mpango tuache kutumia TRA, tuache kutumia Taasisi zingine ku-discourage wafanyabiashara wachanga kama sisi.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba iende kwenye rekodi pia, hata kukata hotuba za upinzani ni shambulio dhidi ya uhuru wa habari. Ni kuwazuia wananchi kupata mawazo mbadala yanayotoka upande mwingine. Hii inatuharibu sana kama Taifa. Jana nilikuwa naangalia kipindi cha The Stream kwenye Al-jazeera, topic ilikuwa uhuru wa habari na demokrasia Tanzania. Dunia imeanza kutumulika na tunatia aibu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niendelee ku-stress kwamba, kigezo cha kuwa na magazeti sijui 200 plus, kwamba ni uhuru wa habari, hiyo si hoja ni hoja mfu, kwa sababu hatutaki quality tunataka quantity. Haina maana kuwa na magazeti 216 ambayo waziri au Dkt. Abbasi anaweza akaamuka tu asubuhi kwa strike ya pen au penseli akayafuta yote kwa dakika moja tukawa tuko tumerudi kwenye zero. (Makofi)

Kwa hiyo, tatizo la uhuru wa habari katika hii nchi, ni very serious…

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Antony Komu.

T A A R I F A

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpe taarifa msemaji kwamba ni kweli kuwa na idadi kubwa ya vyombo vya habari si kigezo peke yake cha kuwa na uhuru wa habari. Hii ni kwa sababu hata kule Zaire wakati Mobutu anatawala na dunia nzima ikipiga kelele kwamba hakuna demokrasia na uhuru wa habari kulikuwa na vyama vingi vya siasa vikifika 400 kuliko mahali pengine popote duniani. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Joseph Mbilinyi, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, naipokea na ni hatari sana kwa sababu mambo kama haya angalia Zaire walivyofanya na mwisho wao na sasa hivi angalia Sudan na mwisho wa Al-Bashir…

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Nakuambia vile. Jana Ali Bashir amehamishwa kutoka house arrest alipokuwa amezuiwa amepelekwa kwenye gereza kuu la Khartoum ambako alikuwa anawafunga wapinzani wa kisiasa. Leaders beware. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana niwapongeze sana MCT, LHRC na THRDC kwa hatua yao ya kupeleka Mahakamani baadhi ya vifungu vibovu vilivyopitishwa vya Sheria ya Habari ya mwaka 2016. Hawa walienda kwenye Mahakama ya Afrika Mashariki na imetoa hukumu kwamba vifungu vile vinazuia haki ya watu kupata habari au vinazuia uhuru wa habari. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tujiulize sisi Wabunge tunakaa humu ndani tunawawakilisha watu, tunatunga sheria inaenda inapingwa Mahakamani halafu inatupiliwa mbali si tunaonekana mapoyoyo. Tunatia aibu kimataifa kwa sababu nchi za East Africa zamani zilikuwa zinaiangalia Tanzania kwenye maeneo mbalimbali ya kidemokrasia na kadhalika, Mheshimiwa Kikwete alituweka vizuri sana lakini leo hii Mahakama za nje zinatengua, zinatuambia kwamba Bunge la Tanzania lilitunga sheria ya kukandamiza uhuru wa habari, hawalaumu hata Serikali, sasa hivi vitu ni vibaya sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mashambulio haya yalianza toka Awamu ya Tano ilivyoingia. Shambulio la kwanza la uhuru wa habari lilikuwa ni kuzuia Bunge live, tena nakumbuka Naibu Spika ndiyo ulikuwa umekalia Kiti siku hiyo, nakumbuka vizuri sana. Sasa unazuia Bunge live kwamba watu wafanye kazi lakini leo Mkuu kila siku yuko kwenye TV asubuhi, mchana, jioni, usiku mbaya zaidi unakuta Wakuu wote wa Taasisi za…

KUHUSU UTARATIBU

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, Kuhusu Utaratibu.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Joseph Mbilinyi, kuna kanuni inavunjwa, Mheshimiwa Jenista.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu utaratibu, ninazo Kanuni mbili ambazo Mheshimiwa Mbunge mchangiaji anakokwenda anakwenda kuzivunja. Kanuni ya kwanza ni Kanuni ya 53(8), inasema, Mbunge yeyote hataruhusiwa kufufua jambo lolote ambalo Bunge lilikwishakuliamulia katika Mkutano huu uliopo ama mikutano iliyokwishakupita. Hiyo ni kanuni ya kwanza ambapo anapoendelea kuzungumza na kuchangia Mheshimiwa Mbunge maamuzi yote ya Bunge live na taratibu nyingine zote zilishafanyiwa maamuzi kwenye mikutano iliyopita na jambo hili lilikwishaondolewa katika mijadala yetu kwa kuwa lilishafanyiwa maamuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Kanuni nyingine aidha wewe ulikaa kwenye Kiti ama hukukaa kwenye Kiti lakini Bunge lilishakwishafanya maamuzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kanuni nyingine tunaposhughulikia masuala ya utendaji kazi wa Mheshimiwa Rais, kwanza yanasimamiwa na Katiba kama Kiongozi Mkuu wa nchi inamlinda kufanya kazi kwa sheria ambazo zinatumika kusimamia utendaji kazi na mwenendo wa Rais. Kwa hiyo, suala la kujadili mwenendo wa shughuli Rais kwa mujibu wa Katiba, hata akitaka kuwa na TV, akitaka kutangazwa saa 24, hili siyo suala la Bunge ni la Kikatiba na la mhimili wa Urais. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kwenye Kanuni yetu ya 64(1)(e) inatukataza pia kuzungumzia mwenendo na utendaji kazi wa viongozi wanaotoa maamuzi na mwenendo hasa wa Mheshimiwa Rais. Kwa hiyo, kama mchangiaji ana hoja kuhusu vyombo na uhuru wa habari, uhuru wa habari huo usimwingize Mheshimiwa Rais katika utendaji wake wa kazi kwa mujibu wa Katiba na kwa mujibu wa Kanuni tulizonazo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nirudi kusema Kanuni ya 53(8) ni lazima Waheshimiwa Wabunge yale ambayo yalikwishakufanyiwa maamuzi hayatakiwi kuwa tena ni part ya mjadala mpya ndani ya Bunge letu.

Mheshmiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, amesimama Mheshimiwa Jenista akiomba kuhusu utaratibu wa Kiti kwa Kanuni ambazo amezirejea kwamba zilikuwa zinavunjwa. Ameanza na Kanuni ya 53(8) inayozungumzia kuhusu jambo ambalo lilikwishaamuliwa na Bunge katika mikutano iliyokwisha ama katika mkutano huo unaohusika. Pia ametupeleka kwenye Kanuni ya 64(1)(e) inayokataza kuzungumzia mwenendo wa Rais.

Waheshimiwa Wabunge, sikusudii kurejea kwenye mchango wa Mheshimiwa Mbilinyi na ambao Mheshimiwa Jenista ameona kwamba unazigusa hizi Kanuni mbili. Huwa siku zote tunakumbushana kufuata utaratibu ule ambao tumejiwekea wenyewe kwa ajili ya majadiliano humu ndani.

Waheshimiwa Wabunge, Kanuni ya 53 inakataza kuzungumzia jambo ambalo lilikuwa limekwishaamuliwa isipokuwa kama unaleta hoja mahsusi ili Bunge liweze kuliangalia upya jambo ambalo liliamuliwa. Jambo ambalo kwa sasa hivi hakuna hoja inayozungumzia Bunge kuliangalia upya jambo ambalo lilikwishaamuliwa. Nadhani kwenye hilo linazungumzia maelezo ya Mheshimiwa Mbilinyi kuhusu uamuzi si hata wa Bunge, uamuzi wa Serikali kutokuonesha tena moja kwa moja mijadala inayoendelea Bungeni.

Waheshimiwa Wabunge, kwa hiyo, kama Bunge lilihojiwa kuhusu jambo hilo ilikuwa ni hoja ambayo ililetwa ili Bunge lifanye maamuzi. Kwa sababu ililishapita ni vizuri kuzingatia masharti ya Kanuni zetu. Kama jambo hilo bado linaleta tabu miaka mitatu au minne baada ya uamuzi huo, Kanuni zetu zinatoa fursa kwa Mheshimiwa Joseph Mbilinyi ama mtu mwingine yeyote kufanya hivyo.

Waheshimiwa Wabunge, Kanuni ya 64 kuhusu mchango wa Mheshimiwa Mbilinyi pia ambao Mheshimiwa Jenista ametupeleka kwenye fasili ya (1)(e) kutokuzungumzia mwenendo wa Rais. Ni vizuri kukumbushana kwamba Kanuni hii inazungumzia mambo yasiyoruhusiwa Bungeni na hilo ni mojawapo isipokuwa ikiwa hoja iliyoko Mezani imeletwa mahsusi kwa ajili ya kuzungumzia mwenendo wa Rais, jambo ambalo silo lililoko Mezani sasa. Kwa hiyo, niwaombe tuzingatie Kanuni zetu tulizojiwekea ili majadiliano yetu yawe yanaenda vizuri bila kukatisha kila wakati kwa kuvunja hizi Kanuni.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbilinyi utakuwa umepata mwongozo wa mambo haya yote mawili katika dakika zako zilizobaki uendelee kuchangia hoja iliyoko Mezani na siyo hoja ambayo kwanza ilifanyiwa maamuzi lakini pili usizungumzie mwenendo wa Rais ama mtu mwingine yeyote ambaye siyo hoja iliyoko mezani sasa. Mheshimiwa Mbilinyi.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninachogundua watu wamejaa hofu na kujipendekeza, mimi hakuna sehemu hata tukienda kwenye Hansard nimesema Rais, nimesema Mkuu. Sasa haya ndiyo mambo tunayosema mnajiongeza mpaka mnaharibu mpaka Rais anawaambiwa kwamba Watanzania siyo wajinga kwa sababu hata hili watalifuatilia kwenye mitandao na watajua tofauti yangu na yenu katika hoja hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia jambo mnaweza mkawa mmesema ninyi humu ndani kwamba...

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Sugu, kwani Mkuu ni nani? Ni Mheshimiwa Mbowe?

(Hapa baadhi ya Wabunge walizngumza bila kufuata utaratibu)

NAIBU SPIKA: Siyo nikija Mbeya tu hata sehemu nyingine lakini usiendeleze jambo ambalo nimekwishalitolea ufafanuzi hapa mbele. Malizia mchango wako ukiwa umeondoa hayo ambayo tumesema yanavunja Kanuni.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Katibu, dakika ngapi zimebaki nijue kabisa?

NAIBU SPIKA: Huwezi kumwongelesha Katibu Mheshimiwa Mbilinyi, wewe si ni Mbunge mzoevu, wewe mwenyewe umesimama kwa kuwa mimi nimekuruhusu ili uzungumze. Unapomuuliza Katibu yeye anazungumza humu ndani? Mheshimiwa Mbilinyi, tafadhali.

MBUNGE FULANI: Maliziamalizia Jimbo la Mbeya linaondoka hilo.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, unajua mimi nawaambia, don’t go personal on me, I am just doing the job for this country. Tukiendelea hivi tunakubali kuingizwa kwenye giza, tutajikuta kama North Korea ambapo wameelekezwa mpaka namna ya kupiga makofi. Nchi nzima wanatakiwa kupiga makofi kwa inchi tatu, kutoka hapa kuja hapa, paa, paa, paa, sasa mnataka hili Taifa lifike huko.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunajizuia kwenye kila eneo la uwazi, hebu angalia hivi ni sababu gani iliyofanya tujitoe OGP (Open Government Partnership), huu mkataba wa kimataifa? Mkataba huu unataka nchi wanachama kukuza uwazi katika uwajibikaji na utendaji wa Serikali. Serikali hii inajinasibu kwamba inapenda uwazi, inataka kila kitu kiwe wazi, kwa nini sasa tunajitoa katika vyombo ambavyo vinatu- endorse kwamba sisi ni watu ambao tunataka uwazi. Halafu tukisema mnatutafutia mbinu mbadala, mnatuvizia, matokeo yake mnaleta Taifa katika mtanziko mkubwa kwa kufanya mambo bila kushirikisha Wabunge kama mlivyofanya kwenye vitambulisho vya wajasiriamali. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, mmekaa huko wenyewe, mmepeana vitambulisho, Mbeya Mjini mmeleta vitambulisho 45,000 wakati Wamachinga hawafiki hata 3,000. Watendaji wanalia kule na kwa sababu hawana uwazi hawawezi kutoka na kuitisha press kusema hiki kitu hakiwezekani wanalia chinichini, huku ndiko mnakolipeleka Taifa. Uhuru wa habari, uhuru wa kupata taarifa, uhuru wa kutoa taarifa hakuna, wanabaki kunong’ona tu. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiriakwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbilinyi, muda wako umekwisha.

(Hapa Mhe. Joseph O. Mbilinyi aliendelea kuongea bila kutumia kipaza sauti)
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi kuchangia mpango huu. Lazima tukubalien kwamba hakuna mpango wa maendeleo bila Utawala Bora na Demokrasia na wakati naendelea kuchangia naomba tu ikumbukwe kwamba, nadhani wote tunakumbuka kwamba mwaka jana nilifungwa Gerezani kwa takribani miezi mitano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kulitaarifu Bunge lako kwamba Mahakama Kuu ilitengua hukumu ile na ilisema kwamba mashitaka yalikuwa batili, mwenendo wa kesi ulikuwa batili na hukumu ilikuwa batili na hivyo kuthibitisha kwamba nilikuwa nimefungwa kisiasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kukipongeza sana Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Mwenyekiti wake, Kamati kuu yake pamoja na Viongozi wote kwa uamuzi wa busara waliofikia jana kujitoa kwenye uchaguzi ambao badala ya kuwa uchaguzi uligeuka kuwa uchafuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mbeya tuna Mitaa 181 hawa jamaa wametuengua wote wamebakiza wagombea 11 tu, Mitaa 181 halafu unasema eti wakakate rufaa na wapo wanajaribu kukata rufaa unakwenda unakuta Ofisi zimefungwa. Angalia sasa vipingamizi wanavyowawekea au sababu za kuwaengua; ukijaza na pen nyeusi wanasema ulitakiwa ujaze na blue, ukijaza na pen ya blue wanasema ulitakiwa ujaze na pen nyeusi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu ya kazi, mtu akiandika mkulima wanasema ulitakiwa uandike kilimo, akiandika kilimo wanasema ulitakiwa uandike mkulima sasa you guys are joke! You are a joke yaani mnafanya vitu vya ajabu kabisa na nawahakikishia mnachokitafuta mtakipata. Leteni Muswada Bungeni tunawaambia kabisa Serikali kwa sababu Bunge hili sijawahi kuona Mbunge ameleta Muswada halafu u-proceed. Serikali leteni Muswada Bungeni, Mheshimiwa Kangi wewe ndiyo kimbelembele wa kuleta utemi sijui uko wapi, walete Muswada mfute vyama vingi tuwe chama kimoja, kwani kuna shida gani? kwasababu ndiyo kitu mnachokitaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na katika hili nimeona Wabunge wengi wa CCM waliomakini hawajafurahia, tunaongea nao nje hapo. Yaani unaona kabisa hata psychologically, facial expressions, body language unaona na kwa kauli zao unaona kabisa Wabunge wengi waliomakini kwa upande wa Chama cha Mapinduzi hawajafurahia ukiachia wale kama jamaa yangu Mheshimiwa Waitara ambaye anatetea mkate. Hata ningekuwa mimi labda kwa sababu si kapinduka halafu kapewa mkate lazima alinde mkate vinginevyo anakatwa na Makonda kaanza kumuingilia kule Ukonga kwa hiyo, lazima dish liyumbe kidogo, ayumbeyumbe ajaribu kutetea mkate. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini unawawezaje watu…

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: …unawezaje kuacha…

MWENYEKITI: Mheshimiwa hebu taarifa.

T A A R I F A

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nimpe taarifa Mheshimiwa Sugu Ndugu yangu na taarifa ya kwanza ni kwamba Sugu ubunge wake ana jasho langu nimemtengeneza mwenyewe…

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Weee mavi yako! Pumbavu wee! [Maneno Haya Siyo Sehemu ya Taarifa Rasmi za Bunge]

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): ….nimefanyakazi kabla hujawa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo la pili, unasikia maneno hayo naamini kwamba utachukua hatua lakini nimpe taarifa kwamba uchaguzi huu una Kanuni na viongozi wa CHADEMA walipewa taarifa mapema, CCM walijipanga, wao hawakujipanga kuandaa watu wao kwa hiyo kutueleza habari iliyojazwa, amejaza mtu mwingine Sugu anazungumza humu ndani shule inamsumbua pia kwasababu aliyejaza form ndiyo anatakiwa a-clarify hicho ambacho anakisema humo ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimpe taarifa kwamba Mheshimiwa Sugu kwamba sisi tunaendelea na mchakato na Kanuni zipo…

MWENYEKITI: Taarifa moja tu.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): …na utaratibu wa nchi hii ni kufuata Kanuni zilizopo.

MWENYEKITI: Ahsante.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Kwa hiyo, maneno mengine yote yale hayatafuta utaratibu wa Kanuni na Sheria zilizopo.

MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa kabla sijakuhoji kuhusiana na taarifa hiyo, Mheshimiwa Sugu nakuheshimu sana, nakuomba ufute kauli ya neno uliyotumia, naomba tu ulifute naamini ulimi umeteleza tu.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua humu ndani sisi tuna-discuss issue serious za hii nchi…

MWENYEKITI: Naelewa.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: …halafu hawa watu…

MWENYEKITI: Hapana.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: …wanaleta mambo ya kulinda mkate, nafuta kwa heshima ya Kiti…

MWENYEKITI: Ahsante sana.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: …lakini vinginevyo hawa watu wana nanihii sana…

MWENYEKITI: Ahsante

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: …wanakera, we are very serious humu ndani…

MWENYEKITI: Unasemaje kuhusu na taarifa yake?

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: …mtu anakaa tu Ubunge, Ubunge, hivi Sugu asipokuwa Mbunge wa Mbeya ndiyo hii Nchi itananihii…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Sugu.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: …itakamilisha mambo yao yote?

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi unasema kuhusiana na taarifa unaikubali, unaikataa?

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Siwezi kupokea taarifa hiyo haina maana kabisa.

MWENYEKITI: Haya endelea kuchangia sasa.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tusiangalie tulipoanguka…

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: …tusiangalie tulipo…

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri hebu kaa tu, kaa tu, Mheshimiwa Waziri hebu kaa tu.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, natumaini dakika zangu zinatunzwa, natumaini dakika zangu zinatunzwa.

Hebu tuwe wakweli, Attorney General yupo hapa, Waziri wa Utawala Bora hayuko lakini Naibu Waziri wa Utawala Bora yuko pale.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Changia tu hoja Mheshimiwa.

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Changia tu hoja.

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Taarifa.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Nalihutubia Bunge linafanya fujo, kwa hiyo kwanza atolewe kwanza aliyefanya fujo yule…

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: …kama tunavyotolewaga sisi.

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mollel hebu kaa.

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni muhimu taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa kaa chini usibishane na mimi. Changoa hoja yako Mheshimiwa.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Kama Messi, everybody anataka, utafikiri Messi niko uwanjani. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu turudi kuwa serious kidogo kwenye mambo ya nchi tusiangalie tulipoanguka, tuangalie tulipojikwaa. Yanayotokea haya kwa heshima zote, yanayotokea haya kwenye uchaguzi huu ni matokeo ya kauli ya Rais kwamba Mtendaji atakayemtangaza mpinzani wakati amempa gari, amempa mshahara, amempa sijui nyumba, sijui amempa nini atamfuta kazi, ndiyo matokeo haya. Unajua kauli ya Rais ni agizo. Kwa hiyo, ili twende sawa sawa… [Maneno Haya Siyo Sehemu ya Taarifa Rasmi za Bunge]

MWENYEKITI: Mheshimiwa Sugu hayo maelekezo ya Rais unayotaka kuiaminisha Kamati unaweza ukanipatia mimi sasa hivi ukaniletea hapa?

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Of course, najua utaratibu siwezi kuyaleta sasa hivi lakini ukinipa muda nitayaleta yapo.

MWENYEKITI: Kwa hiyo una-insist kwamba unayo?

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Yapo, naweza kuyaleta.

MWENYEKITI: Sasa Mheshimiwa mimi nakushi usiende kwenye territory hiyo, changia umalize mchango wako.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: I hope dakika zangu zinatunzwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kitu kimoja, humu ndani kwa trend, utaratibu ulivyo, utamaduni, mazoea wanaorudi humu ni asilimia 30 tu, asilimia 70 tunabaki nje na huko nje hali ni mbaya kuliko mnavyoweza kufikiria. Kwa hiyo, mnayo nafasi ya kurekebisha wakati mkiwa humu ndani kuinyoosha Serikali. Msipoirekebisha 70 percent/80 percent mtabaki nje au niseme tutabaki nje tutakuwa hatuna tena pa kusemea kwa sababu ukisema nje unakamatwa unafungwa, angalau humu Bungeni tunayo nafasi ya kusema, hatutaki kusema sasa hivi. Kazi yetu sisi iwe kushauri siyo kusifia bila sababu. Unamsifia mtu kwa kitu ambacho hajafanya mpaka mwenyewe anashangaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais amekuja kule Mbeya wanamsifia kwa jengo la radiolojia ambalo nimepambania mimi Mbunge kwa Katibu Mkuu wa Wizara.

MBUNGE FULANI: Taarifa.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: …ili Bunge litenge fedha na Bunge likatenga fedha wanakuja wanamshukuru mtu mwingine badala…bajeti zinapitishwa humu ndani ya Bunge…

MWENYEKITI: Mheshimiwa...

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: …kodi za wananchi…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Sugu.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: …hizi fedha za nchi hii zinazonunua ndege, zinazofanya nini…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Sugu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ukisoma Katiba yako na kwenye eneo zima la bajeti ambayo tunaanza mapendekezo haya mpaka itakapofikia kilele mwezi Juni, bajeti hiyo anayeanzisha mchakato kupitia mamlaka aliyoipa ni Rais. Mipango hii ambayo tunaiongelea yote inawezesha pesa hiyo ije kwenye hicho chumba cha radiology ulichokisemea ni pesa ya Watanzania ambayo Rais amefanya kwahiyo anaposifiwa ni yeye, wewe ni catalyst tu ya kwenda kuhakikisha pesa inatumika vizuri. Kwa hiyo, unapokuja kusema kwamba wanampa sifa ambazo siyo zake wewe mwenyewe ulipaswa umpe sifa kama walivyompatia wananchi wengine. Na Rais ni muungwana nilisikia siku ile alivyokupa nafasi ya kuongea kwa wananchi wa Mbeya kama Mbunge wao, heshima kubwa. Ahsante sana. (Makofi)

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Kwa kweli yaani sina tatizo na Rais, nina tatizo na hawa wapambe kwa sababu gani, Rais hata mimi nilimuunga mkono…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana muda wako umekwisha.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nami naunga mkono Taarifa ya Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii ambayo mimi ni member. Tuko vizuri chini ya Mwenyekiti wetu, Mheshimiwa Serukamba, ingawa kuna muda anakuwa very partisan badala ya kuwa bipartisan tunapokuwa kwenye vikao, anakuwa na mambo ya uchama sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitagusia kwenye afya na habari. Kwenye afya tunajisifu kwa kujenga majengo mengi ya Zahanati, Vituo vya Afya na hata Hospitali. Hii lazima tuelewane, hata mimi najenga kupitia Mfuko wa Jimbo, na kadhalika; najenga Zahanati, natoa bati kwenye Vituo vya Afya na kadhalika, lakini tuna tatizo la madawa na vifaa tiba kwenye maboma tunayojenga. Kwa hiyo, yale maboma maana yake bila vifaa vya matibabu yanaweza yakawa hata guest house. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunajisifu kujenga majengo lakini hatuna watumishi wa kutosha wa afya. Kwa mujibu wa study pungufu ni takribani asilimia 52; tuna asilimia 48 tu ya Watumishi wa Afya wakiwemo Madaktari, kwa sababu hatuajiri kabisa. Kinachoshangaza, graduates wapo wengi sana kwenye kada ya afya wakiwemo Madaktari ambao wako mitaani hawana kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, yupo kijana mmoja Daktari, amemaliza Udaktari, amesajiliwa na Baraza la Madaktari, lakini yuko pale Uyole mpigakura wangu anauza vocha za kurusha. Daktari ambaye ame-graduate, amesajiliwa na Baraza yuko mtaani anauza vocha kwa sababu hakuna ajira. Kwa hiyo, hili ni tatizo sana. Inabidi tuangalie namna gani tunaongeza nguvu ya kuajiri.

Mheshimiwa Naibu Spika, mbaya sasa hata wale wachache waliopo, hiyo asilimia 48, maslahi yao ni duni sana bado, kama ilivyo kwa watumishi wengine wa Serikali au wa Umma. Sasa hivi kwa takribani miaka mitano Madaktari na Watumishi wengine wa Umma hawajaongezewa mshahara hata shilingi mia ndani ya miaka mitano. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Madaktari walikuwa vocal, wanaongea na kugoma, sasa hivi hamsikii wanagoma mnafikiri kwamba wameridhika; sisi tunakutana nao kwenye Kamati, hawajaridhika. Ni kwamba sasa hivi kidogo mambo yako chini ya iron fist, hard kidogo! Hawawezi, wanaogopa kuishia kule ambako tunaishia wengine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, awamu yote hawajaongezwa mshahara hata shilingi mia, hali inayosababisha tudhani labda hawa watu wanafanya kazi chini ya mgomo baridi. Kwa sababu haiwezekani, hata hili suala la kwenda kutibiwa nje, nafikiri hili suala tunasema kwamba hatuendi tena nje kisiasa, lakini kiuhalisia (practically) bado tunahitaji kupeleka baadhi ya wagonjwa nje kwa ajili ya matibabu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano ni Mheshimiwa Lwakatare, my brother hapa, amekaa Hospitali ya Muhimbili, hospitali kuu kabisa ya Tanzania takribani miezi mitatu hajanyanyuka. Amepelekwa India, amekaa siku tano, siku ya sita amerudi, siku ya saba tuko naye Bungeni. Huu ni ushahidi kwamba bado kuna vitu tuna-miss; kama siyo vifaa, basi wataalam. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la matibabu kwa wananchi masikini ni gharama mno. Ni gharama sana! Sasa nashauri, wakati tunajipanga vyema na masuala ya Bima ya Afya na kadhalika, tusiache watu wafe, tuwatibu. Uzuri ni kwamba ninyi mnajipambanua kama ni wajamaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi tuko mlengo wa kati, huku ubepari huku nini, soko huria ndiyo msimamo wetu. Ninyi mnasema ni wajamaa; wajamaa gani mnaacha kutibu watu? Kwa sababu hata Uingereza ambao ni mabepari wanatibu watu bure chini ya mfumo wa NHS (National Health Services). Nashangaa sana, hivi mnawezaje kutoa elimu bure mshindwe kutoa matibabu bure? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbilinyi subiri kidogo. Mheshimiwa Ummy, taarifa.

T A A R I F A

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpe taarifa mzungumzaji. Kwanza Sera ya Serikali, lakini pia ndiyo uhalisia, hakuna Mtanzania anyehitaji matibabu ambaye amekosa kupata matibabu. Ndiyo maana taarifa ya Kamati imeonesha, tukichukua Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma kwa kipindi
cha Julai hadi Desemba, zaidi ya shilingi milioni 800 zimetumika kuwalipia wagonjwa wasio na uwezo wa kulipia. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, Mheshimiwa Sugu anapotosha, hatujasema hatupeleki kabisa wagonjwa nje. Ninyi ni mashahidi, watu wa mafua, Malaria na magonjwa madogo madogo wote walikuwa wanakwenda nje. Tumewapunguza kutoka 600 mpaka 53. Kwa hiyo, ni kweli hatupeleki nje kwa magonjwa ambayo tuna uwezo wa kuyatibu ndani ya nchi na tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais, tumefanya vizuri. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Joseph Mbilinyi, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, hapana. Halafu asimwingize Rais, hapa tunaongea na ninyi ambao mmetumwa na Rais kufanya hizi kazi. Kwa hiyo, msimwingize Rais kwenye mijadala yetu humu, maana yake mnajificha kwenye kichaka cha Rais. Nini watu!
Wewe Mheshimiwa Waziri, ninyi mnasema kwamba hamjakosa fedha za kutibu Mtanzania, ninyi mnashikilia maiti za Watanzania kwa sababu wamekosa fedha za matibabu! Eeh! (Makofi)

MBUNGE FULANI: Hawalipi!

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuna Watanzania; nenda Muhimbili, nenda Hospitali zote za Serikali, Mtanzania mwalimu mshahara wake shilingi 300,000/= au shilingi 400,000/=, anaumwa ugonjwa serious, analazwa miezi mitatu, minne, bili inakuja shilingi milioni saba, shilingi milioni nane, shilingi milioni tisa; anafariki dunia, hawa wanashikilia maiti. Mnashikilia maiti za Watanzania ninyi. Wanawanyima fursa Watanzania ya kwenda kufanya ibada za maziko. Wanawanyima Watanzania fursa...(Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbilinyi, kuna taarifa nyingine. Mheshimiwa Kandege.

T A A R I F A

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naheshimu sana mchango wa Mheshimiwa Mbunge, lakini siyo vizuri akapotosha. Kwa sababu hakuna mtumishi wa Serikali hata mmoja ambaye hayuko kwenye insurance. Sasa anasema mwalimu ambaye ana mshahara wa shilingi 300,000/= anashindwa kutibiwa wakati yuko fully covered na insurance! Siyo sahihi. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Joseph Mbilinyi, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, haya basi, tufanye siyo walimu, tufanye Watanzania wa kawaida kama yule ambaye alimwomba Mheshimiwa Rais shilingi milioni tano ili agomboe maiti yake. Sasa ni wangapi ambao wanamwona Rais mpaka wapate huo msaada? Mpaka Watanzania wengine wachangie ili kumfanya Mheshimiwa Rais afanye shughuli zake. Ninyi, msimwingize Rais kwenye haya mambo ya humu Bungeni. Tukae na ninyi.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, hiyo itakuwa taarifa ya mwisho kwa Mheshimiwa Mbilinyi. Mheshimiwa Dkt. Ndugulile.

T A A R I F A

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, namheshimu sana Mheshimiwa Mbilinyi, ni rafiki yangu sana, lakini kwa kweli kile anachokisema hapa ni upotoshaji wa hali ya juu sana na akiwa ni Mjumbe wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi ndani ya Wizara na kupitia hospitali zetu tumeweka utaratibu mzuri sana; na ni fursa hii ya kuwaelekeza Waheshimiwa Wabunge. Tuna Dawati la Social Welfare ambalo kama kuna mwananchi ambaye amepata matibabu ya aina yoyote ile na akashindwa kugharamia aidha amepona au mgonjwa wake amefariki anakwenda katika Dawati hili la Social Welfare pale, watamfanyia assessment.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi hatuna maiti ambayo tunaishikilia kama Serikali. Ndiyo maana lile ambalo alikuwa anasema Mheshimiwa Waziri hapa, tunatumia fedha nyingi sana, zaidi ya shilingi milioni 800 katika hospitali zetu nyingi kwa ajili ya kugharamia haya matibabu mengine ya watu ambao hawana uwezo.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbilinyi, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, hapana. Ndiyo tunachosema, kwa sababu kama dawati lipo, halafu wananchi hawalijui na ninyi mpo, mpaka mwananchi anakurupuka kwenda kumwomba Mheshimiwa Rais shilingi milioni tano, tuna tatizo! Ndiyo maana tunasema hapa kuna tatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, matibabu ni gharama sana kwenye kila eneo. Twende kwa akina mama kwenye huduma za uzazi, kujifungua; hospitali za Serikali sasa gharama ni balaa. Ni gharama kubwa mno! Hospitali ya Wazazi Meta Mbeya kujifungua ni mpaka shilingi 300,000/= kwa operation, kujifungua kawaida mpaka shilingi 150,000/=, shilingi 200,000/=. Hii ni Hospitali ya Rufaa ya Wazazi Meta, Maternity Hospital pale Mbeya Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa najiuliza, wakati wa Mheshimiwa Dkt. Kikwete na Mheshimiwa Mkapa huko nyuma wazazi walikuwa wanaambiwa waende hospitali na kanga, pamba, nyembe, sijui sindano na vitu vidogo vidogo, mambo mengine yote wanayakuta huko huko; inakuwaje? Ni nini kimesababisha Sera ile ya Afya Bure, Matibabu Bure kwa Wazazi Wajawazito Pamoja na Watoto Mpaka Miaka Mitano, ile sera imekwenda wapi? Au kama ndiyo matokeo ya sanctions ambazo tumeanza kuwekewa, basi mtuambie ili tufunge mkanda na tujiandae kwamba tuko katika stage gani. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbilinyi kengele ya pili imeshagonga.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Kweli!

NAIBU SPIKA: Sina saa mimi jamani, Makatibu wananiongoza hapa.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, wamekula sana dakika zangu!
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa hii ni bajeti ya mwisho katika miaka mitano. Naomba nimpongeze sana Mwenyekiti wa CHADEMA na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Mheshimiwa Mbowe kwa Uongozi wake imara wa kujenga upinzani credible na sio upinzani magumashi pamoja na yote anayokutana nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia nawapongeza Wabunge wenzangu wote wa CHADEMA tuliovuka, ambao hatukuunga mkono kwa sababu tumevumilia sana miaka mitano hii Awamu ya Tano haikuwa rahisi, siasa zilikuwa zinahusika na magereza kushambuliwa, kupigwa risasi na mambo mengine mengi tu ambayo tumeweza ku-survive mpaka hapa tulipofika kwa kweli nawapongeza sana Wabunge wenzangu kwa kuvuka uvuli wa mauti. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa suala la Corona lipo chini ya Waziri Mkuu, naomba nianzie huko. Kwanza lazima tuelewane hapa, suala la Corona sio suala la kiimani ni suala la sayansi. Na ndio maana hata Papa mwenyewe, mimi ni

mkatoliki amefunga Vatican na Italy yote hawaendi kanisani hata St. Peters Basilika ambapo kila jumapili maelfu kwa makumi ya maelfu ya watu duniani kote na Waitaliano wanasali pale juzi Papa amesali peke yake kwa sababu ya kuchukulia umakini wa suala hili. Hili suala sio la kiimani na imani tunayo kwa mfano sisi Wakatoliki tuna imani lakini tunaamini sayansi na ndio maana kila unapokuta Kanisa Katoliki lazima utakuta shule ya Chekechea na Zanahati kwa sababu tunaamini katika Sayansi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Corona ni pandemic, wakishasema kuna epidemic, ilianza kama epidemicsaa hizi inaitwa pandemic hakuna suala la kutishana hapa, ni suala la ku-discuss kwa kina. Corona inaua na itaua mamilioni, ndivyo wanasayansi wanasema hivyo tusipochukua hatua. Tushirikiane kukabili na hili, tusilete siasa kwenye hili na niwapongeze sana Zanzibar kwenye hili Zanzibar wamechukua hatua sana wamefanya vizuri sana, unamuona pale yule Waziri wa Afya, yupo on point kila time kujaribu ku update hali ya mambo inavyokwenda. Corona sio tatizo la Ummy Mwalimu na Wizara ya Afya, maana yake watu Ummy, Ummy, Waziri wa Fedha anahusika, Waziri wa Biashara anahusika Waziri wa Uwekezaji anahusika kwa sababu biashara zinakufa.

Mheshimiwa Spika, BOT wako kimya tu kwa hiyo tunaangalia tu upande wa vitanda matibabu tutakufa ni kweli huko tupo ovyo lakini njia pekee ya kuidhibiti korona kwa nchi maskini kama sisi Tanzania ni kudhibiti isisambae. Sasa nyinyi mnasema mbona hamwagi nini ile hamsanitize miji, kama Arusha, mgonjwa wa kwanza tulitakiwa tuone hata yale magari ya polisi basi yale ya washawasha, wekeni dawa yamwage maji mitaani, mnasubiri mpaka muwamwagie maji CHADEMA wazee! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, m-sanitize miji angalau ile ambayo imeanza kupata shida ndugu zangu, hiyo ndio njia ya pekee ya ku-contain ili isisambae sana, Ikisambaa sana hatuwezi ventilators tunazo mia moja na hamsini tu. Tunavyoambiwa tunazo mia moja na hamsini tu, wakati Jiji la New York wanahangaika zifike laki moja na nusu, sisi kama Taifa la watu milioni hamsini na saba tunazo mia moja hamsini tu, Itakuwa balaa hapa. Spain wanafikia time wanasema wazee wa miaka themanini wasipewe vitanda vya ICU kwa sababu vitanda vimeisha hapa tutatumia vigezo gani au kukata, shika laki mtoe Sugu muweke Mheshimiwa Jenista na kadhalika, kwa sababu tutafanyaje. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hili suala la korona ni serious, hata kama sisi sio UK hata kama sisi sio Italy, hata kama sio US lakini tuangalie wenzetu wa sub-Sahara wanafanya nini, sub-sahara in Africa, Kenya. Basi tusiwaambie wenye nyumba wasitoze kodi kwamba nyumba nyingi hapa ni za watu binafsi na ni masikini wanategemea hizo kodi kusomesha watoto. Lakini watoto si hawaendi shule, elimu si bure, okay tusifike huko tuweke unafuu kwenye yale ya Serikali, hii Serikali si ina hela hii mara ya mwisho Mheshimiwa katuambia tuna akiba ya dola za kutumia miezi sita. Where is that money, bring that money tupange bajeti hela ya bajeti ya Mwenge, bajeti ya Mwenge haitoshi kwenye corona. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haitoshi watu wanapanga bajeti za kufa mtu, bajeti kubwa na mikakati. Kenya Serikali inatoa miongozo, umeme, maji hivyo ni vya Serikali. Mseme bwana tuko vizuri nchi hii tajiri umeme, maji iwe bure kwa wananchi ili kuwaletea unafuu kuanzia sasa ili pale anapopanga ule mchango wa LUKU, mchango wa maji usiwepo tutakuwa tumewapa unafuu wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini mabenki Kenya yamesitisha marejesho ya mikopo kwa biashara na makampuni. Hili sio suala la wananchi maskini, hili suala ni la kitaasisi, Mheshimiwa Dkt. Mpango this is yours na BoT, sitisheni wekeni breki kwenye marejesho kwa sababu bila hivyo hizi biashara zitakufa Corona inakuja kupita Mungu anatusaidia tutashindwa kunyanyuka kwa sababu hakuna biashara itakayonyanyuka na Serikali haiwezi kuajiri watu wote na itakuwa shida sana kwetu sisi sote.

SPIKA: Mheshimiwa Sugu naona kila jambo una copy and paste from Kenya.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, hapana nitakupa mfano wa Ghana Serikali ipo serious, Ghana imesema wananchi kuanzia Jumapili hii wote wakae ndani Taifa zima linaenda kupimwa kwa sababu huwezi kujua ukubwa wa tatizo bila vipimo. Hii hapa mnasema eti tuko ishirini, ishirini tupime humu tu Bungeni hata mimi mwenyewe sioni kama niko guarantee na niko salama.

SPIKA: Tunaposema Mheshimiwa Sugu, hiyo unayosema Ghana wanasema watu wote wakae ndani ili Serikali ya Tanzania unayosema watu wote wakae ndani ili Oktoba uchaguzi kule Mbeya uhairishwe, hiyo sasa ndio tunasema haiwezekani.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, kwenye uchaguzi nakuja, naomba tu utunze muda wangu.

SPIKA: Muda wake muutunze. (Makofi/Kicheko)

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Muutuze muda wangu, kwenye uchaguzi nakuja, tuko vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi naongea habari hizi serious sana, nyakati kama hizi zinaitwa defining moments. Nyakati kama hizi ndio leadership inapimwa, tutoke tuonyeshe leadership watanzania wanatuangalia. Kwa sababu hawa watu wanatushangaa kwamba aaah korona wanasema tunanii mbona wao wapo Bungeni eeeh! Kwa hiyo, lazima humu ndani tuwaonyeshe kwa nini tuko Bungeni, tujadili vitu vya kuokoa maisha yao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Rais kwa kauli yake kuwa uchaguzi utakuwa huru na wa haki, umezungumzia uchaguzi nakuja huko. Uchaguzi uwe huru na wa haki Mungu atupunguzie makali ya Corona ili tufike salama Oktoba, Mungu atusaidie. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini ili kutuhakikishia kwamba uchaguzi huu uwe huru na wa haki Rais achukue hatua chanya ku-support kauli zake. La msingi kabisa ili wadau wa uchaguzi, wa ndani, wa nje, wa kimataifa maana yake uchaguzi ni suala la wote, wadau wawe na imani nae wawe na imani na kauli yake kwa kuanza kabisa tunataka Tume huru. Tume ambayo watendaji wake watawajibika kwa tume na sio kwa mteuzi ambaye ni Rais. Tume ambayo yenye kinga na ulinzi wa kikatiba ya ajira za wale watendaji wa Tume kama ilivyo kwa majaji, kama ilivyo kwa CAG. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Isiwe rahisi kumchomoa Mtendaji Mkuu wa Tume hajatangaza tu hajamtangaza Sugu kesho hawi Mwenyekiti wa Tume, that isvery bad. Kuhusu Mbeya na Uchaguzi Mkuu kule tunasema hivi, Tume huru bila Tume huru lazima tutoboe mradi wananchi wametupa kura. (Makofi))

Mheshimiwa Spika, by the way Mbeya mimi hamjawahi kunipa kwenye silver plat. Uchaguzi wangu wa 2010 alikufa mtu mmoja kwa ajili ya kulinda kura, uchaguzi wa 2015 vilema watatu wengine mpaka leo nawahudumia. Uchaguzi huu na maisha yalivyokuwa magumu sijui mtatuzika wangapi Mbeya hata Corona inaweza ikawa na nafuu lakini sio kuchakachua uchaguzi huu kwa kigezo chochote kile. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, maana yake nawaona tu sasa hivi hawasemi tena kama kule Mbeya, hawasemi tena Sugu hashindi wanasema Sugu hatatangazwa, utafikiri nimewahi kutangazwa wakati nimelala nyumbani. (Makofi/Vicheko)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunataka Tume huru, yenye uwezo wa kuteua wasimamizi na watumishi wake yenyewe isiteuliwe, na haya maelezo yote haya tumeiweka kwenye hotuba ya KUB lakini pia yamo kwenye barua yetu tuliyomuandikia Mheshimiwa Rais kumpa mapendekezo ya tunaenda vipi Oktoba baada ya sisi kutoka Mwanza kwenda kuonesha kitambaa cheupe kwamba tupo tayari kwa maridhiano nilikuwepo kwenye ile…

SPIKA: Mheshimiwa Sugu, samahani kidogo kuna taarifa nadhani ni Naibu Spika au ni nani taarifa, malizia Mheshimiwa Sugu. (kicheko)

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, kama chama tumeandika barua kwa Mheshimiwa Rais mpaka leo haijajibiwa kutoa mapendekezo yetu, tunaenda vipi kwa amani kwenye uchaguzi wa Oktoba. Msisitizo wake na msingi ukiwa Tume huru. Kama Tume huru na haki basi turuhusiwe katika sehemu ya hizo haki turuhusiwe kupinga matokeo ya Rais Mahakamani. Mbona matokeo ya Mbunge tunapinga, ile mwaka 2010 yule alinipinga nikamtuliza na Mahakamani mwaka 2015, hakupinga kabisa kwa sababu kura zilikuwa ni nyingi mno. Mwaka 2020 hata njia ya Mahakamani hamtaiona nyinyi kwa Mbeya Mjini,hamtaiona hata njia ya Mahakamani. (Makofi/Kicheko)

MBUNGE FULANI: Taarifa Mheshimiwa Spika.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunataka tume huru tunataka sheria, Marekebisho ya Sheria za Uchaguzi, tunataka marekebisho ya Sheria za Uchaguzi…

SPIKA: Kengele imeshagonga tayari Mheshimiwa Sugu.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI:…ili Rais nae akichakachua tumshitaki Mahakamani kwamba amechakachua uchaguzi. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi. Kwanza naomba niwapongeze Wabunge wenzetu wa upande wa pili ambao walioneka kwamba wamesimama na kutetea hizi hoja zilizopita siku mbili kama Mheshimiwa Hussein Bashe na wengine, nawaomba waendelee hivyo na kesho kwenye Muswada wa Sheria ya Habari kwa sababu nao ni disaster kwa Taifa. Kwa hiyo, nawashukuru sana na tuendelee kuwa pamoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wamarekani wanasema uchumi ni mahesabu (arithmetic’s) hautaki maneno maneno, mara uchumi umekua kwa 7.9%, mara 7.2%, uchumi ni arithmetic’s (mahesabu). Humu ndani katika retreat ya kwanza kabisa nilisema, I was scared of the future, now this is the future I was scared about ambayo wote tunaijadili. Nilikuwa mtu wa kwanza kuongelea in detail matatizo ya bandari yaliyotokana na Single Custom Territory. Nikafanya consultation mpaka na Waziri Mkuu maana alikuwepo, lakini mpaka sasa hivi hakuna kilichotoa majibu zaidi ya kusema hata meli moja ikija bandarini haina tatizo. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia niendelee kusisitiza kwamba we should take jets kwa sababu lazima tuwe na international interactions. Nashukuru Mkulu ameanza kutoka, juzi alikuwa Nairobi, nafikiri ataongeza mileage kwenye ndege. Kwa sababu hata Wabunge wanaposhindwa kusafiri kwenda kwenye vyombo ambavyo ni vya makubaliano ya Kimataifa, hatuwezi kwenda SADC, PAP, tunasikia hata Spika ananyimwa kibali cha kusafiri, sasa hii nchi tukijifungia ndani humu tutapata vipi maarifa, tutabadilishana vipi mawazo na wenzetu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata Marekani ambao wana kila kitu bado Obama anasafiri anakuja mpaka Kenya na Tanzania kwa sababu international interactions zinakuwa ni kwa maslahi mapana. Watu hawawezi kuwa wanakuja kwetu tu, Wabunge wanakuja kwetu, delegation zinakuja kwetu na sasa hivi naona Rais anapokea delegation nyingi nyingi lakini sisi hatutoki, wataacha kuja watasema hawa tunawatembelea wao hawatutembelei, acha wajifungie humo humo ndani watajijua wenyewe, sasa hii itakuwa mbaya zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nisisitize, hatuwezi kuwa na mipango bila sera. Nataka Waziri wa Fedha aniambie leo ni nini sera yetu kuhusu misaada kutoka nje? Maana tunasikia kauli nyingi za majigambo, tuna wa-criticize Wamarekani, Wazungu kwamba wenyewe hawajafanya hiki na kile, hatuhitaji misaada tuko tayari kujitegemea, lakini eventually tunaishia kuomba msaada Morocco ambao ni third world wenzetu! Morocco ni dunia ya tatu wenzetu tunaomba msaada sijui watujengee uwanja na vitu gani sijui. Labda pengine tukiangalia ngozi nyeupe tunajua kila mtu mweupe ni Mzungu na ana hela, lakini Morocco ni third world ndugu zangu na wao wanahitaji misaada kama sisi, wale ilitakiwa tuongee mambo yao mengine tu kwa sababu yule bwana ni rafiki mzuri sana wa Puff Daddy wa Marekani na hata picha zimeonesha lifestyle yake. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanasema uchumi unakua uchumi unakua kwa nani? Biashara zinakufa, Mpango inabidi ubadilishe jina kwa sababu you have to live your name, kama wewe ni Mpango basi uwe na mipango. Mimi Sugu hata ukiangalia nikikomaa na kitu nakomaa nacho kama sugu, Iam living my name. Kwa hiyo, unatakiwa Mheshimiwa Mpango uishi kwa jina lako. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimuulize, fedha hamna, hivi ni yeye Mpango alimshauri Rais kwamba wachapishe noti mpya kwamba watu wanaficha fedha? Watu wakificha fedha hawawezi kuficha fedha hizi ambazo zinashuka thamani kila siku, wakificha fedha wataficha dola na kadhalika. Tatizo linalotokea ni kwamba wamekusanya fedha zote za Serikali kutoka kwenye mabenki wamepeleka BoT wakati wao hawazungushi fedha wanakaa tu. Rudisheni zile fedha CRDB, NMB, NBC wale ndiyo wanaofanya biashara waendelee kukopesha, watu waendelee kufanya biashara na kutanua mambo yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye ukurasa wa 14 wanasema misingi ya mpango wa bajeti kwa mwaka wa 2017/2018, halafu namba nne wanasema, katika mikakati inayotarajiwa kuweka bajeti ni kusubiri bei za mafuta katika soko la dunia zinavyoendelea kuimarika. Sisi hatuchimbi mafuta, bei ya mafuta inaposhuka ni faida kwetu. Juzi nilikuwa naangalia Waziri wa Fedha wa India anasema uchumi wa India una-boom, construction zinaendelea, viwanda vinajengwa, tunachukua advantage ya kushuka kwa soko la mafuta kwa sababu sisi hatuchimbi mafuta.
Mheshimiwa Mwenyekiti, watasema mafuta tunayo yatapatikana leo? Hiyo gesi imeshaanza kuchimbwa lakini bado hatuoni hata manufaa yake, mpaka leo ukienda Mtwara watu wanachoma vitumbua, watu wamechoka wanategemea korosho wakati gesi ipo na ndiyo maana hata Mheshimiwa Mwambe amechoka kugombea gesi, humsikii anasema gesi, yeye anazungumzia korosho tu. Hata watu wa Mtwara ukiwaambia gesi wanakwambia ninayo tumboni, wanaleta utani, they joke about it kwa sababu they don’t believe about it. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sisi leo hatuwezi kusema kwamba eti bajeti yetu itatengemaa kutegemea kuimarika kwa bei ya mafuta duniani. Kuimarika kwa bei ya mafuta duniani ni disaster kwetu. Faida kwetu sisi tena msimu huu ambao tunasema tunataka kujenga viwanda ni kukomaa kipindi hiki kuanzisha hivyo viwanda kwa sababu nishati ya mafuta bei iko chini na hamna namna nyingine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanasema mipango, tutapeleka milioni 50 kila kijiji, za nini? Hii ni mentality ya rushwa wakati wa uchaguzi! Ndiyo maana story zinaendelea, milioni 50 kila kijiji, milioni 10 Wabunge, sijui milioni ngapi za nini, tena mnasema mtapeleka cash wafanyie nini? (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashauri angalau wangesema kila kijiji kije na proposal kulingana na mazingira yake, kwa bajeti ya milioni 50 mtafanya nini? Mfano kijijini unasema sisi tunataka tuimarishe kilimo, tuna vijana hapa wanasoma mambo ya ugani kwenye vyuo vya kilimo, fedha hizi zikija sisi tutanunua maksai na plau. Kijana akirudi kutoka masomoni badala ya kulia anatafuta kazi tunamkabidhi plau halafu yule ng’ombe wa maksai anakuwa ni wa kijiji, unampa eneo anaendelea kulima pale organic food halafu ninyi mnatafuta soko la kuuza hizi organic food nje ya nchi kwa sababu zina soko sana kuliko hivi vyakula vya mbolea. Nyie mmeng’ang’ana na viwanda wakati mtaji hamna! Ooh sijui General tyre itarudi, Mbeya ZZK, nimechoka hata kuiulizia mpaka leo imebaki kuwa ghala tu la pombe ndugu zangu. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mnasimama hapa mnasema tumenunua ndege (Bombadier), nataka niulize ni nani aliyepanga nauli za ndege hii kwa sababu highlight ya nauli wametoa. Sasa hizo Bombardier highlight ya nauli eti kwenda Mwanza Sh.160,000, kwenda Mbeya Sh. 305,000, kuja Dodoma Sh.3 00,000, hivi Mwanza na Dodoma mbali wapi au mnataka kumfurahisha ngosha? Tena huyu anatakiwa kutumbuliwa! Huwezi kusema nauli ya kwenda Mwanza ni Sh.160,000 ambako ni kilometa elfu moja na zaidi halafu kwenda Mbeya ambako ni kilometa 800 unasema Sh. 300,000…
MWENYEKITI: Malizia Mheshimiwa Mbilinyi muda wako umekwisha.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Ni inayounganika, nimetoka kuongea na Waziri Mkuu pale, sasa hivi kuna disaster diaspora. Serikali mmetoa tamko kwamba watu wote wa diaspora wenye passport za nje ambao wamejenga nyumba hapa zinataifishwa. Hii kauli imetolewa na Waziri wa Ardhi, Mheshimiwa Lukuvi and this is very bad na nimeongea na Waziri Mkuu, lakini naongea hapa….
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi muda wako umekwisha.
Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tano, okay, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kwanza kabisa na kwa umuhimu, nimetumwa na wafanyabiashara wa Mbeya kuja kuiambia Serikali kwamba wanaiomba Serikali kwa level ya Mheshimiwa Waziri waende Mbeya mkae nao kikao kwa ajili ya kujadili masuala ya ulipaji kodi. Kwa sababu kumekuwa na vikwazo vingi sana kiasi kwamba Mbeya tunashindwa kuzalisha wafanyabiashara mabilionea wa kutosha kama ilivyokuwa kwenye majiji mengine ikiwemo Dar es Salaam, Arusha na Mwanza kutokana na sintofahamu zinazotokana na TRA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mathalani unakuta mtu ana-declear labda mapato mwaka huu shilingi milioni kumi, mwakani ana declear milioni kumi again, mwaka unaofuata watatu aki declear milioni 30 wana back date wanamlazimisha kwamba wewe ulidanganya itakuwa hata kwa miaka mitatu, minne yote ulikuwa unaingiza milioni 30. Kwa hiyo, wana impose kinguvu kodi tofauti na mapato ambayo yule mfanyabiashara ame-declear. Hili ni tatizo kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mheshimiwa Waziri Dkt. Mpango mfanyabiashara wa Mbeya akijenga nyumba nzuri inakuwa na madhara kwa sababu wanaenda ku double kodi kwenye biashara yake kwamba ulipata wapi hizi hela za kujengea hii nyumba. Ndio maana Mbeya tumechelewa kuwa mansion na mpaka leo hatuana mansion yako machache machache ndio kwanza yanaanza ukifananisha na majiji mengine na hii haiwezekani kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali hii inasababisha wafanyabiashara wakifikia lengo level fulani ya mtaji inabidi wahame Mbeya waende kwenye miji mingine ili waweze kupata ustawi wa kibishara, lakini wakikaa Mbeya inakuwa migogoro na watu wa TRA.

Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri kwa level ya Waziri wafanyabiashara wa jiji la Mbeya wamenituma kwamba wanataka wanahitaji uende mkakae ili mjadiliane na haya mambo kwa sababu yamekuwa hivi maiaka nenda miaka rudi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu bajeti, naunga mkono maoni ya upinzani, kodi ikiwa kero inachotakiwa ni kuiondoa sio kuibadilisha kiujanja ujanja kama mlivyofanya kwenye masuala ya road licence kupeleka kwenye mafuta kiasi kwamba unawapa mzigo wananchi ambao wengine hawana magari kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ni sahihi kwa mujibu wa Kambi ya Upinzani fedha hii ipelekwe katika maeneo hii shilingi 40 kama inalazimika kuongeza shilingi 40 kwa kila lita basi twende tuipeleke kwenye maji. Tukimaliza maji twendwe kwenye miundombinu ya elimu; yaani tunafanya vitu kwa miaka kwa series, miaka mitano maji, miaka mitano tunakuja kwenye miundombinu ya elimu ikiwepo nyumba za walimu na hata vyoo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa katika Bunge hili na Taifa hili viongozi wakubwa wa Serikali wanazungumzia masuala ya kununua nini hizi boeing mpya jetliner sijui ziende wapi, lakini wanafunzi wetu wa shule za msingi hawana vyoo, wanakunya nje. Kwa hiyo hivi vitu vidogo vidogo ndio tunatakiwa tuviangalie kwanza kabla hatujaangalia mambo mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu madini na mimi nasema mikataba iletwe si ya madini tu, madini, gesi mikataba ya kununua ndege bombardier, nyumba za Serikali zilizouzwa mikataba yote iletwe ndani ya Bunge hili ili tuipitie upya. Tukisema mnasema tunampinga Rais hatumpingi tuko tayari kumsaidia na kumshauri lakini kwa sharti moja kama mimi binfsi Mjumbe wa Kamati Kuu sitaki uteuzi. Sitaki u-DC, sitaki sijui Ukuu wa Mkoa, sitaki Uwaziri ninachotaka afanye Mheshimiwa Rais ni kufungua mijadala atuache atusikilize mawazo yetu na ayafanyie, kazi hicho ndio kitu kibwa tunachokifanya, yaani sisi tunaweza tukamsaidia vizuri Mheshimiwa Rais tukiwa huku kuliko kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kirimanjaro au kuwa Katibu Mkuu wa Wizara fulani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunamuomba sana Mheshimiwa Rais achie mijadala tujadili vyanzo vya matatizo kwa kina, asitubane, hata kama matatizo hayo yatakuwa yamesababishwa na watu ambao sasa hivi ni Marais wastaafu wacha tujadili, ambaye yuko clean atabaki kuwa clean ambaye ana mawaa basi Sheria itachukua mkondo wake ili tutengeneze presidence kama inavyotakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mwisho katika hizi dakika tano ni chache nikupongeze Dkt. Mpango, Mwakajoka amekuchana kiutendaji kazi, lakini mimi kwa tabia una-smile kidogo sasa hivi. (Makofi/Kicheko)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana nakushukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, wakati unaingia uliona kulikuwa na makelele kidogo ilitokana na Mheshimiwa Ali King kututukana na kutuita Mbwa. Sasa kiti kitaangalia namna ya kumrekebisha lakini kama rafiki yangu namsamehe kwa sababu ni rafiki yangu tunakunywa naye pombe na tunakula nae kitimoto Sheikh Ali King. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni mtu wangu wa karibu nakula naye sana kitimoto.

T A A R I F A . . .

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, nashukuru hajakanusha kwamba tunakula naye kitimoto ile yeye hapendi ya mafuta. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, naomba sasa nijiekeleze kwenye kuchangia kwa mara nyingine niwashukuru sana wana Mbeya kwa namna walivyosimama na mimi nilipofungwa gerezani. Nawashukuru sana wana Mbeya na sitaacha kuwashukuru kwa sababu katika changamoto ile waliweza kunipa projection ya mbele tunaendaje na wanaendelea vipi na Mbunge wao. Wakati niko gerezani nilisoma na nilipata taarifa kwamba uliagiza Wabunge wa upinzani tupewa Ilani za CCM ili tuzisome. Sasa sina uhakika kama agizo lako lilitekelezwa, lakini naomba nikuhakikishie sio tu tuna Ilani ya Chama chenu lakini pia tuna list ya ahadi zenu za mwaka 2015. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu hatuwezi kukaa na kuongea mapungufu yenu wakati hatuwafuatilii kwa hiyo tunawafuatilia. Mfano wa list ya ahadi zenu ni laptop kwa kila mwalimu ni hewa, lakini kuna hili suala la shilingi milioni 50 kila kijiji na kila mtaa ni hewa, mmeng’ang’ana na suala


la elimu bure lakini wote tunajua elimu bure ni disaster, ni kitu kizuri ambacho hakijapangwa. Kuna watu wanasema kwamba mlirukia ajenda ya CHADEMA kwenye suala la elimu bure kwa namna mnavyotekeleza inaonekana kama ni kweli hili suala mlilirukia tu. Kwa hiyo, tunachoomba kwa msisitizo kwa leo kwa Wizara hii ya Fedha Waziri Mpango atakaposimama au Naibu wake atuambie ni lini utekelezaji wa shilingi milioni 50 kila kijiji na kila mtaa zitaanza kupelekwa kule kwenye mitaa kwa sababu kuna mitaa 181 Jiji la Mbeya ambalo wanasubiri hizi shilingi milioni 50 kila mtaa tuna kazi ya kuzifanyia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu hii ni nchi yetu wote tunapozungumza tuwe serious katika masuala kuna masuala tunaongea kiutani utani tu mfano ni ujenzi wa hosteli za Chuo Kikuu cha Da es Salaam maarufu kama Hosteli za Magufuli, Mheshimiwa Rais. Tunaambiwa mnasema na mnang’ang’ania kwamba ujenzi wa zile hosteli ni shilingi bilioni 10 tu majengo 10 ina maana kila jengo moja lenye ghorofa nne ni shilingi milioni 500. Kama ingekuwa kweli hivyo hata mimi ningejitolea kujenga majengo mawili pale. Lakini niko kwenye Kamati ya Maendeleo na Huduma ya Jamii ambayo masuala ya elimu yako chini yetu tumeshakwenda pale kutembelea ule ujenzi ukweli ni kwamba pale zimetumika shilingi bilioni 54 plus na sio shilingi biloni 10 zilizotumika. Lakini nashangaa sijaona ripoti ya CAG katika suala hili, sijui ni nini au ni nani au ni maagizo kutoka juu ndio yamezuia hili suala watu wanang’ang’ana shilingi bilioni 10 wakati kitu ni uwazi kabisa hesabu zinasema shilingi bilioni 54 plus ndio zimetumika kujenga ule ujenzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa najiuliza hivi tunamdanganya nani hii nchi yetu sote tunamdanganya nani? Kama ni fedha, hizo fedha ni zetu sisi kama Taifa sio mali ya mtu binafsi. Sasa kwa nini tunapeleka mambo namna hii niliwahi kusema katika Bunge hili numbers don’t lie, women lie, men lie but numbers don’t lie na bahati mbaya tunapozungumza masuala ya fedha ni namba sio maneno maneno, fedha ni namba; shilingi bilioni 10 na shilingi bilioni 54 ni namba mbili tofauti. Tunakwenda masuala ya fedha


hizi fedha ni zetu wote sio fedha za mtu binafsi. Tunahoji kuhusu shilingi trilioni 1.5 ambazo matumizi yake hayajulikani hatujasema kwamba mmeiba tunasema tunata kujua zimeenda wapi? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, hakuna sehemu sisi tumesema kwamba mmeiba hizi hela sasa nyinyi mnasimama mnasema fulani! Simama eti! Kweli hela zimeibiwa? Hazijaibiwa Mheshimiwa! Hakuna mtu aliyesema kwamba hizi fedha zimeibiwa ila tunahoji kwamba hizi fedha shilingi trilioni 1.5 ziko wapi please explain shilingi trilioni 1.5 zimekwenda wapi hiki ndio kitu ambacho tunahitaji sisi kwa sababu hii nchi ni yetu sote na nchi sio sebule ya familia kwamba tu tunapelekana tu. Hii nchi mambo madogo yanatushinda, hili ni Taifa ambalo linashindwa kushonea uniform hata askari wake magereza pamoja na wafungwa, hili ni Taifa ambalo linashindwa kulisha na kutibu wafungwa wake, watu wanakufa kiholela na ukitaka kupima umaskini wa Taifa chunguza magereza zake, ukiingia katika magereza zetu utakuta taswira halisi ya umaskini wa Tanzania kupitia maisha yanayoendelea mle ndani. Watu hawana chakula, watu hawana madawa, mtu kafungwa unamwambia alete bima ya afya wakati haruhusiwi hata kutembea na shilingi 1,000 mle ndani, bima ya afya ataitoa wapi? Tunashindwa na mambo madogo sana . (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, nchi hii leo tumefika mahali eti kubeba ndoo ya samaki kutoka Mwanza kuja Dar es Salaam na maeneo mengine lazima uwe na kibali kweli mboga! Kitoweo! Na hii halafu mnasema mnakuza ajira. Kwa sababu unavyozuia ile biashara ya wale kina mama wengi wao wakiwa wajane pale Mwanza wanauza ndoo za samaki. Mheshimiwa Jenista wakati ule ukiwa Mwenyekiti wangu kwenye Kamati, tulikuwa tunakumbushana sana kubeba samaki tukitoka ziara Mwanza na Mara kubeba samaki kwenye ndoo. Lakini hii Serikali yako ambayo wewe ni Chief Whip inakataza inasema kwamba marufuku kubeba samaki hata watatu/wanne/watano ni lazima uwe na kibali kubeba Samaki wa Mboga kutoka Mwanza. Kweli Mheshimiwa tumefika hapo? (Makofi/Kicheko)


Mheshimiwa Spika, kulipa kodi ni wajibu, nashauri TRA iwe rafiki wa walipa kodi, iache kufanya utafikiri yenyewe ni polisi. TRA inafanya kazi kama polisi na sometimes inatumika kisiasa. Angalia walichomfanyia Kakobe. Kakobe katoa mawazo yake kama raia, Mtanzania na kiongozi wa waumini. Mara wamemwita, mara wanahoji kodi, mara sijui wanahoji nini, matokeo yake wamekosa kile walichokuwa wanakitafuta kwa Askofu Kakobe, wanakuja wanasema ooh, hana tatizo lolote na yeye hana hela ila Kanisa lake lina shilingi bilioni nane. Who asked you? Nani amekuuliza Kanisa la Full Gospel lina kiasi gani benki? Wanaingilia na kutoa ripoti za fedha za taasisi za watu bila kuulizwa na bila utaratibu. Kwa sababu kanisa sio Kakobe, kwa nini kama ulitaka kumchunguza Kakobe na umekuta hana kitu, unaanza kutoa taarifa za Taasisi ya watu?

Mheshimiwa Spika, sasa hayo mambo ya TRA yako mengi sana na tumeelezwa mengi sana. Mbeya Songwe…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Naomba dakika moja tu, wanakata sana dakika hao. Hii ni namba yangu ya mfungwa jela, ambayo nitaendelea kuivaa kadri nitakavyojisikia. Kuhusu suti wewe unanijua, ni kawaida yangu kupiga suti kali.

Mheshimiwa Spika, mambo haya ya kuingiza siasa kwenye uchumi, TRA wanasababisha Mbeya na Songwe tumechoka. Sasa hivi tunapoongea, wafanyabiashara wa Tunduma wanahama, wanaenda kufanya biashara upande wa Zambia. Wanafanya biashara Zambia wanakuja kulala Tanzania. Hapa ndiyo tulipofikia na sisi yetu ni macho, lakini hii ngoma ishakwama inaonekana wazi kabisa.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi. Katika kujadili mpango naomba kwanza Dkt. Mpango aniambie toka Awamu ya Tano imeingia kuna FDIs ngapi zimeshakuja nchini, naomba anipe takwimu, FDIs ni Foreign Direct Investiments. Naomba kujua ni ngapi toka Awamu ya Tano iingie madarakani, zimeshakuja nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia napenda nijue toka Awamu ya Tano kwenye Arbitration Courts, kwenye Mahakama za nje kuna migogoro na kesi ngapi dhidi yetu? Maana tunasikia tu ACACIA wameenda Mahakamani, mara Pan African Energy wako Mahakamani kutudai kwa hiyo, tunaomba tujue pamoja na gharama ya fedha ambazo wanataka tuwalipe kupitia hizo mahakama? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu katika haya mambo no one is perferct. Na sisi kazi yetu kushauri humu ndani na ninyi huko mnatakiwa Mawaziri mnatakiwa mumshauri Rais msimuogope, tunarudia kusema hiki kitu. Na ndio maana kwa sababu, hakuna mtu perfect, even the President can not be perfect every time na ndio maana pamoja na mbwembwe zote tukasubiri Baraza la Mawaziri kachukua time sana kutangaza Baraza la Mawaziri, lakini mpaka leo bado ameshatumbua Mawaziri 11. Kwa hiyo, kama angekuwa perfect wale aliochelewa kuwateuwa ina maana wangekuwa sawasawa na angeenda nao mpaka leo, lakini mpaka sasa hivi 11 wameshatumbuliwa, hii inamaanisha kwamba no one is perfect na muendelee kumshauri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana nimuunge mkono my friend, Mheshimiwa Lusinde katika Bunge lililopita 2010/2015 alikuwa na hoja yake anapenda sana kuisema Bungeni kwamba, viongozi tupimwe afya ya akili. Hili alilisema sana Mheshimiwa Lusinde wakati ule sikumuelewa, lakini kwa trend ya mambo yanavyokwenda sasa hivi katika hii nchi kwa kweli, naomba ni … halafu nimuunge mkono Mheshimiwa Lusinde ile hoja yake kwamba kuanzia sasa viongozi wote kuanzia chini Serikali ya Mtaa, Diwani, Mbunge, Rais, hakuna kuchaguliwa kama hajaenda kupimwa afya ya akili kwa sababu mambo yanavyokwenda sio sawasawa kabisa, angalia wanachofanya ma-DC…

KUHUSU UTARATIBU . . .

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Kanuni haiwezi kuzidi Katiba. Mambo mengine ni matakwa ya kikatiba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu sikum-cite mtu, individual, nimezungumzia mfumo wa uteuzi. Ndio kitu nilichozungumzia hapa, mfumo wa uteuzi kwamba, tunavyoteuwa kuanzia Diwani, Mbunge kwenda juu, pengine hata Mwenyekiti wa Kiti na Spika nao inabidi wapite katika huo mchakato, lakini ninyi kwa sababu mtakuwa mmeshachekiwa kama Wabunge kwa hiyo, mtakuwa safe kukaa kwenye hicho kiti kwa hiyo, it is not personal.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi natumaini unanitunzia dakika zangu ili nifanye kazi yangu ya Kibunge kwa sababu hii nchi tunafika hapa, tunafunganafungana hovyo, tunapiganapigana risasi hovyo kwa sababu ya unafiki, watu hawataki kusema ukweli. Angalia walichokifanya wale Maprofesa wa Chuo Kikuu juzi pale Mlimani, Nkrumah Hall ni sehemu ya tafakuri ya Taifa. Hayati Mwalimu Nyerere alikuwa anaenda pale kukutana na wasomi ku-discuss mustakabali wa nchi, leo hii maprofesa watu wazima kabisa wanamuita pale kiongozi wanaanza kumsifia, sio vibaya kusifia, lakini wange-balance wamwambie na mapungufu yake kwa maslahi ya nchi hii, hicho ndio tulichotakiwa kufanya, hakuna anayemwambia ukweli kiongozi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Taifa nje watu wanalia, na mimi najua, Mheshimiwa Msigwa anajua, Mhesimiwa Jesca anajua, Mheshimiwa Mhagama unajua, AG unajua, Waziri Mkuu unajua, nje watu wanalia we are not happy, the nation is in sombre … the nation is not happy. Tuambiane ukweli, ili tusonge mbele. Unaona sisi mnatufunga tunatoka tunatabasamu ni kwa sababu ya Taifa hili. Kwa sababu ya mslahi ya Taifa hili na si vinginevyo, lakini tungetoka tumenuna tungezidi…

T A A R I F A . . .

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepokea Taarifa ya Mheshimiwa Bwege.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Taifa lina uwoga ndugu zangu, Taifa lina woga, sasa hatuwezi kujadili maendeleo kwenye uwoga.

T A A R I F A . . .

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu naye ndio anasababisha hoja yangu kwamba nobody is perfect kwamba hata wale waliochaguliwa kwa mbwembwe wametumbuliwa, huyu ni mmoja wa waliotumbuliwa katika wale 11, unaona. Huyu ni mmoja wa waliotumbuliwa katika wale 11. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo we are serious here. Hapa ndugu zangu tuko serious, we love this country. Sisi wengine mnavyotuona tumetokea mtaani mpaka hapa tulipofika tunaona Mheshimiwa Kikwete alipotufikisha na mapungufu yake yote alipotufikisha, lakini at least tulikuwa tunaona mwanga, sasa mnatuingizaje kwenye giza na mmekaa tu hapa jamani mnasema tujadili mipango? Tunajadilije mipango polisi wanauwa watu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, polisi wanatuhumiwa kuuwa watu kila kona. Tukisema kwamba uchunguzi ufanyike mnatukamata badala ya kutuomba ushirikiano tuwape information. Jijini Mbeya kwangu mimi, watoto wawili, vijana wawili wamekufa mikononi mwa polisi, Allen Mapunda wa Kata ya Ihyela amekufa mikononi mwa polisi, Kijana Kapange mpaka leo maiti yake iko mortuary kwa zaidi ya siku 160 kwa sababu familia imegoma inasema tunataka uchunguzi huru, sio polisi wajichunguze, tunataka uchunguzi huru. Mpaka leo maiti ya kijana siku 160 iko imelala mortuary, hili Taifa gani? Halafu mnasema kwamba watu wanafuraha katika Taifa kama hili? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu hawana furaha ndugu zangu. Polisi wanatuhumiwa kuuwa watu with impunity, hakuna mtu anayeingia, hakuna tunachofanya, angalia afya, nilikuwa namuuguza mama pale Hospitali ya Taifa…

K U H U S U U T A R A T I B U. . .

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kangi is my friend, my brother. Yeye mwenyewe ni mhanga wa sintofahamu za Awamu ya Tano, alipigwa kesi ya rushwa sijui iliishia wapi? (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, alipigwa kesi, hawa ndio walikuwa ni wahanga wa mwanzo kabisa wa vurugu match. Alipigwa kesi ya rushwa sijui imeishia wapi, kwa hiyo Waheshimiwa... (Kicheko)
Hapa tunaongea masuala ya afya, tunaongea masuala ya mpango wa nchi, lakini mambo hayaendi, kwenye afya tumekazana kujenga majengo, wataalam hatuna, nilikuwa pale Muhimbili, mama anahitaji huduma moja inaitwa vascular surgery naambiwa daktari yuko mmoja tu halafu hayupo ameenda Hijja. Hijja ni kitu kizuri huwezi kumzuia yeye kwenda Hijja, lakini jukumu lenu ni ninyi kuhakikisha kuwa kuna watalaam wa kutosha kwa sababu hilo hitaji ni kaja kugundua ni wagonjwa wengi sana wako lined up na wanapoteza maisha na vile na kila kitu kwa sababu ya kukosa wataalam.

Sasa wewe mtaalam wa vascular surgery Taifa kama hili yuko mmoja, halafu mnasema tunaenda vizuri afya, tunaenda nini tunafanya vipi mnakazana kusema kwamba bajeti ya dawa imeongezeka iko bilioni mbili.

Mimi nitasikia raha mkiniambia bajeti ya dawa imepungua na hiyo bilioni 200, 300 pelekeni kwenye maji na vyanzo vingine sehemu nyingine ambazo ni chanzo cha magonjwa ili bajeti ya dawa ipungue na sio kuongeza bajeti ya dawa halafu kudhani kama ni sifa. Mnasema sasa hivi ni bilioni 200 mwakani mtasema bilioni 400, mwaka unaofuata mtasema bilioni 600 kwenye madawa sio sifa, sifa ni kupunguza bajeti ya madawa maana yake kwamba Taifa lina afya watu hawaugui na si vinginevyo ndugu zangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiongozi unatakiwa kuishi kwa mfano, wewe umetajwa kabla watu hawajatajwa, leo hii wenzako wanatajwa mwaka mmoja, miaka miwili baadae halafu unaanza kuwa-harass na kuwafanya hivi wakati... (Makofi/Kicheko)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba kwa unyeyekevu kabisa nianze kwa kumpongeza…

SPIKA: Dakika 10 eeh.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, sawa na ahsante sana. Naomba nianze kwa kumpongeza sana Chief Whip wa Opposition, Mheshimiwa Tundu Antiphas Mughway Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki na Rais Mstaafu wa Tanganyika Law Society – TLS. Nampongeza kwa ziara zake za kimataifa kuelezea hali halisi ya kinachoendelea nchini kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Lissu alimiminiwa risasi 38 na 16 ziliingia mwilini. Katika hali ya kawaida ilibidi alegee na kurudi nyuma, lakini pamoja na kwamba, bado yuko kwenye matibabu amechukua jukumu la kuzunguka na kupaza sauti ili dunia ijue kwamba… (Makofi)

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Mbilinyi walikuwa wanauliza ukurasa wa ngapi wa taarifa?

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, kama wao wanavyoanza na pongezi tu kwa mtukufu. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Spika, muda wangu. Kwa hiyo, kwa mtu ambaye risasi 16 zimeingia ambaye alitakiwa alegee, lakini amenyanyuka na anazunguka kuilezea dunia kwamba, Tanzania, Tanzania ambayo ilikuwa ni kitovu cha amani Kusini mwa Jangwa la Sahara, hivi sasa imekuwa ni authoritarian regime. Tuelewane kitu kimoja, Serikali siyo Taifa kuikosoa Serikali siyo kulichafua Taifa na kuikosoa Serikali siyo kuitukana Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa niende kwenye hoja, kwanza naunga mkono ripoti ya Kamati yetu ya Huduma na Maendeleo ya Jamii. Nianze na habari na utawala bora. Kwanza Mungu atuondolee kabisa balaa la pepo la kuongeza muda wa utawala, ni tabia na mawazo ya kidikteta moja kwa moja, iwe kwenye Ubunge au kwenye Urais. Maana naona hii trend mlianza kama utani lakini sasa hivi mnakuwa serious, naamini mnahitaji maombi na tutapiga magoti tuwaombee ili msiliingize Taifa huko mnakotaka kulipeleka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwapongeze CCM Habari kwa kumilikishwa Chanel Ten na Magic FM. Naamini kwa hatua hii sasa mtaiacha TBC ibaki kuwa TV ya umma.

T A A R I F A

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, siipokei taarifa yake, actually alichoniambia Keissy ni kwamba anataka ni m-support hoja yake ya kutaka bangi iruhusiwe na nimemkatalia na hii anayo toka Bunge lililopita. Kwa hiyo, hiyo taarifa yake siichukui. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, naipongeza CCM kwa kukabidhiwa Channel Ten na Magic FM. Sijui mmepewa, mmenunua na kwa utaratibu gani kwa sababu najua makampuni yanapouzwa upo utaratibu lakini tumeona tu ghafla watu wanakabidhiwa vyombo vya habari. Tunaamini sasa mtaiacha TBC ibaki kuwa TV ya umma ili mbaki na vyombo vyenu ambavyo mnavyo hivi sasa, muiache TBC kuwa televisheni ya umma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimemuona Mwenyekiti wa Taifa katoa shilingi milioni 200 kuboresha Channel Ten na Magic FM, wananchi wa Mbeya Mjini wananipigia wanasema Mheshimiwa hizo fedha shilingi milioni 200 zilizotoka ni fedha za CCM, fedha za Serikali Hazina au zinatoka wapi? Tunavyofahamu Mwenyekiti wa CCM Taifa kazi yake ya Urais mshahara wake ni shilingi milioni 9 tu. Sasa wananchi wanajiuliza anatoa wapi mamilioni anayoyagawa kila sehemu anakopita wakati mchahara wake Rais mnyonge ni shilingi milioni 9 tu. (Makofi)

T A A R I F A

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, walisema ni Rais katoa, kwa hiyo, kama ni Mwenyekiti ndiyo mnanipa taarifa basi naelewa sasa kumbe ni hela za Chama cha Mapinduzi na siyo hela za mtu binafsi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye afya, ripoti inaonyesha kwamba rufaa za nje zimepungua kutoka 114 takribani kwa mwaka mpaka 38. Kwangu mimi na nilivyofuatilia kwenye Kamati hii siyo success story kwa sababu watu wanakufa sana. Hivi sasa Madaktari wanaogopa kutoa rufaa kwa sababu ya kuangalia mtazamo wa kisiasa unataka nini kwamba hatutaki kupeleka watu nje. Lazima tukubali kwamba hatuna mabigwa wala hatuna vifaa vya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sometime, narudia tena sametime Muhimbili pale nimekaa zaidi ya mwezi mmoja na nusu hata mtungi wa gesi oxygen inabidi ibadilishwe yaani kuna mgonjwa hapa amelala, amewekewa mtungi, mgonjwa mwingine kule anataka kuwekewa mtungi inabidi watu wamkatie nurse ili mtungi uhamishwe wanasema huyu amepumua kidogo tutamletea tena baadaye. Kwa hiyo, katika hali kama hiyo huwezi….

T A A R I F A

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri anafahamu vizuri ana struggle na hapa tunachofanya ni kumsaidia kwa sababu yeye hawezi kutamka haya tunayotamka atatumbuliwa. It is not about you Madam Minister it is about the Nation, hatukusaidii wewe tunalisaidia Taifa hapa, hakuna vifaa na wataalam wa kutosha, watu wakufa.

T A A R I F A

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, nilindie muda wangu vinginevyo sasa mimi katika hili Bunge nitakuwa sichangii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haya mambo tunaongea tuko serious, kama Mzee Kingunge angepelekwa nje kutibiwa pengine leo hii tungekuwa na Mzee Kingunge. Huwezi kumweka Mzee Kingunge mwezi mzima hospitali ya rufaa, ukishamweka wiki moja hajapata nafuu ujue kuna tatizo mpeleke kwenye weledi wa juu zaidi. Mpaka leo mnashindwaje kumpeleka Mheshimiwa Salim Mohamed Salim, Waziri Mkuu Mstaafu, Makamu wa Pili wa Rais, unashindwaje kumpeleka kutibiwa nje pamoja na wananchi wengine wenye mahitaji? (Makofi)

T A A R I F A

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, niwaombe sana hawa wanaosimama kutoa taarifa, hii nchi siyo ya baba yao wala hili Bunge siyo la mama yao, hili Bunge ni la Taifa na hapa tunajadili suala la Taifa.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Spika,
kuhusu utaratibu.

SPIKA: Mheshimiwa Mbilinyi, nakuomba sana u-withdraw hayo uliyoyasema.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU): Kabisa.

SPIKA: Kwa Wabunge wenzako, ndugu zako na Waheshimiwa wenzako.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, kwa sababu tunaheshimiana I am withdrawing this lakini ujumbe umeshafika, habari ndiyo hiyo.

SPIKA: Ahsante sana. Tunaendelea na Mheshimiwa Ritta Kabati.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Muda wangu haujaisha hata kengele ya pili katika mustakabali wako haujaisha Mheshimiwa.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi nami niweze kuchangia hotuba hii. Kuna msemo unasema Conversation rules the Nation. Ni two ways game; ukipenda kusikilizwa, basi lazima ujue na kusikiliza pia. Leo nitajikita kwenye maeneo mawili, kupongeza na kushauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwanza kwa kumpongeza CAG, Profesa Assad kwa uzalendo mkubwa aliouonesha, kwa sababu katika nchi hii watu walianza kutokwa na imani na wasomi wakiwemo maprofesa wetu, lakini kwa hatua alizochukua Prof. Assad recently kwa kweli amerudisha imani kwa wananchi kwamba kunao bado maprofesa ambao wana mapenzi na Taifa hili na wana misimamo yanapokuja masuala ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, napenda nimpongeze Rais kwa kukubali mwaliko wa wafanyakazi Mei Mosi, kuja Mbeya kuwa mgeni rasmi. Pamoja na kwamba anakuja kwenye shughuli ya Kitaifa ya Mei Mosi, lakini Mbeya wanamsubiri sana kwa sababu ni sehemu ambazo alikuwa hajakanyaga kabisa toka awe Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaase wanaoshughulika na ile protocol ya Mheshimiwa Rais wajaribu kuwazuia Chama cha Mapinduzi wasitake au kujaribu kutumia ujio wa Mheshimiwa Rais ambayo ni ziara ya kiserikali kwa maslahi ya chama chao kwa sababu wanaweza wakavuruga ziara ya Mheshimiwa Rais kwa sababu Mbeya ni Cosmopolitan kisiasa, imechanganyika sana. Kuna vyama vyote vinatamalaki pale na viko vyama ambavyo vinazidi idadi ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi, hususan Jijini Mbeya.

MHE. GOOLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utaratibu.

KUHUSU UTARATIBU

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi, kuhusu utaratibu.

MHE. GOOLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Menyekiti, nasimama kwa mujibu wa Kanuni ya 68 kuhusu utaratibu, nikisoma Kanuni ya 64(1) (c) nikisoma pamoja na Kanuni ya 53(8), kuwa Mheshimiwa Mbunge hatazungumzia suala ambalo tayari Bunge lilishafanyia maamuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tangu asubuhi alianza Mheshimiwa Ally Saleh kuongelea suala la CAG, akaja Mbunge mwingine akaongelea tena suala la CAG na sasa hivi Mheshimiwa Sugu. Sisi suala la huyu mtu tayari tulishaliongea kama Bunge na tulishafanya maazimio, lakini bado tu wamekuwa wakijaribu kulifukua kitu ambacho ni kinyume na kanuni zetu. Kwa hiyo, nilikuwa naomba hilo.

MWENYEKITI: Mheshimiwa umeeleweka. Mheshimiwa Selasini.

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Kanuni aliyotumia siyo. Kanuni ya Utaratibu ni ya 64. Pili, imekuwa ni mazoea Mheshimiwa Mlinga ku-interrupt wasemaji wa Kambi hii kila wanapozungumza na kwa vitu vya ovyo kabisa, kupoteza muda tu. Sasa ningependa kujua, huu ndiyo utaratibu? Au Kambi hii ya Chama cha Mapinduzi imemu-assign yeye ku-interrupt wazungumzaji wa Kambi hii kila wakati?

MWENYEKITI: Mheshimiwa Jenista.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utaratibu. Twende tu kwa utaratibu, kwa heshima na Bunge litatuelewa. Yote yanaweza kuwa ni mambo mema, tunataka kupata mfumo mzuri wa kujadiliana hapa ndani, lakini maneno pia anayoyatumia Chief Whip mwenzangu katika kueleza, umesikia sitaki kurudia lile neno alilolitamka hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nafikiria pia tutumie lugha nyepesi, ambazo ni za kibunge, zitatusaidia tu kufuata kanuni na utaratibu utaenda vizuri. Tupunguze kutumia lugha ambazo siyo nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nafikiria lugha ya Chief Whip mwenzangu, hebu apunguze kidogo na ikiwezekana tuiondoe, sitaki kuirudia.

MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, naomba tuelewane. Mheshimiwa Mlinga alirekebisha kanuni; alianza 68 lakini baadaye akarudia 64(1); kwa hiyo, alikwenda kwenye utaratibu, lakini jambo ambalo linazungumzwa, Chief Whips wote wawili mko sahihi, tunatakiwa twende kwa mujibu wa utaratibu. Lugha pia tuwe nazo nzuri.

Kuhusu suala la CAG lililozungumzwa, ikiwa mtu anajadili taarifa; na ikiwa mtu anajadili jambo ambalo limeshazungumzwa Bungeni, ni jambo lingine.

Kwa hiyo, twende kwenye utaratibu. Kama tunazungumzia taarifa, tuzungumzie taarifa, lakini tusizungumzie masuala ambayo yamepita Bungeni. Kwa hiyo, tuendelee na utaratibu huo.

Mheshimiwa Mbilinyi naomba uendelee.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, almost naanza hapa, kwa sababu niliongea kwa sekunde 20, kwa hiyo, kwa kuwa nina dakika 10 na nili-keep my watch, nina dakika tisa kama na sekunde kama 40 hivi, ukiondoa tano hizi ambazo nimeongea sasa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kutoa statement ya ukaribisho kwa Mheshimiwa Rais Jijini Mbeya na hali ya siasa, niendelee kumpongeza na niseme kwamba leo nimesema nitapongeza na kushauri. Masikio ya wafanyakazi na familia zao yote yatakuwa Mbeya Mei Mosi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Wafanyakazi wa Mbeya ambao mimi ni Mbunge wao na Wafanyakazi wa nchi nzima, naomba sasa with respect, nimshauri Mheshimiwa Rais atakapokuwa Mbeya mwaka huu Mei Mosi, atangaze ongezeko la mshahara kwa wafanyakazi. Kwa sababu toka ameingia madarakani huu ni mwaka wa tatu mishahara haijaongezeka hata ndururu na wafanyakazi wana hali mbaya sana katika maeneo yote ya nchi hii na ngazi zote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia aangalie suala la wastaafu. Wako wengi sana wamestaafu, wengine mwaka wa pili sasa lakini hawajalipwa mafao yao katika Idara mbalimbali wakiwemo wastaafu kwenye Idara za ulinzi na usalama kama Magereza, Polisi, wamestaafu miaka miwili sasa na hili nilishalisema bado wako kwenye Police Quarter hawaondoki, hawana hata nauli za kubebea mizigo kurudi hata makwao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama suala la mishahara haliko kwenye bajeti, Waheshimiwa Mawaziri, naomba safari hii mrudi mezani mwangalie namna gani mtafanya ili basi Mheshimiwa Rais atakapokuja Mbeya atangaze ongezeko la mishahara kwa wafanyakazi wetu nao wapate unafuu wa maisha kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naunga mkono kauli ya Mheshimiwa Rais kuwa Watanzania sio wajinga. Aliongea wakati anamwapisha Mheshimiwa Balozi aliyekuwa anakwenda Cuba. Ni kweli kabisa Watanzania siyo wajinga; na ukitaka kupima, angalia jinsi walivyolipokea suala la CAG baada ya CAG kufanya Press Conference jana Dar es Salaam. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ujinga aliousema Mheshimiwa Rais kwamba Watanzania sio wajinga, aka-cite suala la MO Dewji kutekwa na maelezo yake ya nini kilitokea, Polisi, uchunguzi ulikwendaje, hewa; hivyo hivyo Watanzania wanajiuliza kuhusu Mheshimiwa Tundu Lissu, wanajiuliza kuhusu Ben Saanane, wanajiuliza kuhusu Azori na watu wengine wote waliopotea. Kwa hiyo, naungana mkono kabisa na Mheshimiwa Rais kwamba Watanzania sio wajinga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niungane na ahadi ya Mheshimiwa Rais aliposema kwamba baada ya kumaliza miaka kumi iwapo atashinda mwakani hataongeza hata saa moja Ikulu. Hili namuunga mkono na asiwasikilize wapotoshaji wanaoleta njaa kwenye masuala ya uongozi wa nchi kwa kumperemba na kutaka kumwingiza chaka kwa sababu Afrika hiyo imeshapita na mifano ipo, nitaisema mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, itapendeza zaidi kama akiahidi kwamba atakuwa tayari kukabidhi madaraka kwa amani mwakani iwapo atashindwa kwenye uchaguzi wa 2020 mwakani. Atoe kauli na siyo tu aahidi kwa maneno, aahidi kwa vitendo kwa kutusaidia kuifumulia mbali Tume ya Uchaguzi kwa sababu Tume ya Uchaguzi iliyokuwepo haikidhi, imejaa makada wa wazi kabisa wa Chama cha Mapinduzi, chama tawala watu wanaovaa uniform za chama kesho wanaenda kusimamia uchaguzi. Uchaguzi huo utavurugika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bila Tume Huru, tutaingiza nchi hii kwenye machafuko ya kiuchaguzi kama ilivyotokea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Kenya mwaka 2017. Take my word, wakati tunaanza hili Bunge nilisema humu ndani kwenye briefing, I was worried about the future; I was scared of the future, mkacheka cheka hapa lakini leo everybody sees future imetukaliaje. Sasa tunayo nafasi ya kujirekebisha kuokoa mambo mabaya yanayokwenda kutokea yasitokee. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, uchaguzi wa mwaka 2020 itakuwa siyo mchezo, kwa sababu wananchi wanakwenda kuchagua kati ya taabu na nafuu. Sasa watu wanaochagua kati ya taabu na nafuu, huwezi kuwaletea mchezo. Maisha yamekuwa magumu; wafanyabiashara hoi, wafanyakazi hoi. Huu ni mwaka wa tatu sasa President Dr. Magufuli yuko Ikulu lakini bado analalamika na kutumbua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi nimemwangalia kwenye tv akiwa Namtumbo, bado mpaka leo hii nchi hii Rais anakwenda ku-question ujenzi wa shilingi milioni 60 wa zahanati sijui jengo gani kule wakati ameweka timu, ameweka Wakuu wa Wilaya; wote kazi yao ni kumvizia Sugu wamkamate wamweke ndani masaa 48, halafu wanashindwa kusimamia kazi ambazo Mheshimiwa Rais amewachagua wao kufanya hizo kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa huu ni mwaka wa tatu Mheshimiwa Rais analalamika, bado anatumbua, timu haijakaa sawa na sasa tunaenda dakika ya 85 kuelekea dakika ya 90. Msaidieni sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nishauri tubadili approach. Masuala ya ukali hayasaidii, turudi sasa kwenye lile suala kama aliloongea Mheshimiwa Japhary…

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHES. JOSEPH O. MBILINYI: …Meya Mstaafu wa Arusha aliposema kwamba…

MWENYEKITI: Taarifa.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Tunahitaji kujenga taasisi imara

MHE. MARWA R. CHACHA: Kaa chini.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi, taarifa.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: …na siyo kujenga mtu imara.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi, Mheshimiwa Mbilinyi subiri kidogo, taarifa. Mheshimiwa Chacha.

T A A R I F A

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumpa taarifa, mwongeaji anasema Tume ya Uchaguzi siyo huru. Liliundwa Bunge la Katiba lililokuwa linaunda Tume, wakaunda chombo kinaitwa UKAWA wakaondoka Bungeni. Leo wanataka Tume huru, ipi? (Makofi)

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, yule nampuuza. Ila acha niseme neno moja, kwa nini Bunge linafika hapa? Angalia hoja muhimu zinazoletwa humu Bungeni, halafu angalia Wabunge wa sasa upande wa CCM wanaochangia. Huwezi kuona Mheshimiwa Chenge kasimama au Mheshimiwa Mwinyi au hata Mheshimiwa Jenista mwenyewe hawezi kusimama kuchangia vitu vya msingi. Wanawaachia mapoyoyo kama yule wavuruge Bunge tu kwa style ya namna hii. (Makofi/Kicheko)[Maneno Haya Siyo Sehemu ya Taarifa Rasmi za Bunge]

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee. (Makofi/Kicheko)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kuhusu Utaratibu.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi umeyatafuta haya. Mheshimiwa Jenista.

Mheshimiwa Mbilinyi subiri, Mheshimiwa Jenista.

KUHUSU UTARATIBU

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kanuni ya 64(1) (f) na (g), inakataza kabisa kutumia lugha ya kuudhi na inayodhalilisha watu wengine na hairuhusu kutumia lugha zinazofanana na lugha ya matusi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kanuni zinatutaka humu ndani unapom-address Mbunge mwenzako, utatumia jina lake kwa kumwita Mheshimiwa. Mheshimiwa Mbilinyi anamwita Mbunge mwenzake poyoyo. (Kicheko/Makofi)

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Jenista, malizia.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba sana hii siyo lugha ya Kibunge. Katika tafsiri ya lugha za Kibunge tulizonazo, hii siyo lugha ya Kibunge. Ni lugha ya kudhalilisha na kuudhi. Tunaomba lugha hiyo aifute na aiondoe kwenye Hansard ya leo.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbilinyi, hilo neno hata mimi maana yake siijui, naomba ulifute tu.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba uzingatie dakika zangu, bado saba hata kengele ya kwanza haijapiga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tupo kwenye shida kidogo. Angalia ma-RC na ma-DC…

MWENYEKITI: Naomba ufute lile neno.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeshafuta. Poyoyo! Nimeshafuta, nitalitumia nje. (Kicheko/ Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, angalia state tuliyokuwepo ma–RC, ma–DC ni vituko kabisa. Angalia yule RC wa Tabora, Mheshimiwa Aggrey Mwanri. Namheshimu sana my brother; anakaa anasema, yeye atamwomba Mungu, Mungu amshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli kwa kazi nzuri. Kweli! That is blasphemy. Hiyo ni blasphemy inaitwa, maana yake kwa Kiswahili ni kufuru. katika baadhi ya maeneo ambayo wako serious na Mungu, Mheshimiwa Aggrey Mwanry sasa hivi angekuwa mahali pabaya sana kwa kufanya blasphemy.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais wetu ni Mkristo, tunamwona Kanisani kila siku, nashangaa hata Mheshimiwa Msigwa, mwandishi wake wa habari hajalaani kitendo kile. Tunaliingiza hili Taifa kwenye laana, namwomba Mungu alihurumie hili Taifa kwa kauli za watu kama akina Mheshimiwa Aggrey Mwanri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mko busy sana kuzuia maandamano. Maandamano ni haki ya Kikatiba watu ku- express, yatawasaidia ninyi wenyewe kujua joto likoje. Hamwezi kuzuia maandamano kwa kutumia Polisi. Yakifika hayazuiliki. Omar Al-Bashir saa hizi siyo Rais. Jana amelala Rais, leo siyo Rais. Amezuia shughuli za vyama vya siasa, amezuia maandamano, amefuta vyama vya siasa kwa miaka 30 akiwa Ikulu ya Khartoum, Sudan. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini bei ya mkate tu, mwaka 2018 mwishoni kapandisha bei ya mkate tu, watu wameingia barabarani, vyama vya siasa hakuna, haoni mtu wa ku-negotiate naye, ameishia ku-negotiate na Jeshi, Jeshi limemwambia kaa barracks, hatuwezi kupiga risasi watu, imetosha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mtafanya mbinu kuzuia maanadamano, mtafanya nini; yatakapofika mama! Kumbuka Algeria. Yule jamaa, yule mzee na ni wapambe tu. Mzee wa watu, Bouteflika, ana miaka 82, amechoka yuko kwenye wheel chair, wapambe wanalazimisha aongeze muda, agombee ili wao wabaki kwenye nafasi, kama wanavyofanya baadhi ya watu hapa sasa hivi kuanza kumwambia President Dr. Magufuli, eti aongeze muda sijui aongeze miaka saba kwa maslahi yao binafsi. Hiyo Afrika imepita, tutapata taabu sana. Namwomba sana Mheshimiwa Rais asisikilize huo upuuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, moja kwa moja nitakwenda ku-stress kwenye suala la utalii Southern circuit (Ukanda wa Kusini) naona mkazo bado kabisa. Wakati Mheshimiwa Waziri anazungumzia mafanikio ya watalii milioni 1.5 kwa mwaka jana waliotembelea Tanzania ningependa aniambie katika hao milioni 1.5 ni watalii wangapi walikwenda kwenye ukanda wa Kusini ikiwemo Kitulo, Ruaha, Katavi, Selous na hata Mbeya kama Mbeya tuna maeneo kama Lake Ngozi, Lake Kisiba, tuna Matema beach, tuna Ngonga beach yote hayo ni maeneo ya vivutio vya watalii kwenye eneo lile la Southern circuit. Kwa hiyo, nilitaka kujua kwamba katika 1.5 million ni wangapi walikwenda kutembelea kule.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuipongeza Wizara kwa ile branding ya “Tanzania unforgettable” it is a super thing. Nilivyoiona tu ile kitu nikasema sasa Dkt. Kigwangala yuko kazini lakini take it international; CNN, BBC na kwenye platform zingine za Kimataifa na wewe mwenyewe pia brother safari nenda Mamtoni, nenda Ulaya, nenda Marekani ukajue watalii wanataka nini ili uje uwaandalie hayo mazingira huko. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenda wewe mwenyewe tu kutalii Serengeti, kwenda wapi haisaidii kuvutia watalii wa KImataifa ni sisi tu ambao tunakuwa na Instagram na maeneo mengine. Kwa hiyo brother utoke, uende Ulaya, uende Marekani ukajue watalii wanataka wanataka nini halafu sasa hii Tanzania unforgettable itakuwa imekaa sawa sawa na siyo ile channel yetu ya TBC ambayo tumeianzisha kutangaza utalii ambayo badala ya kutangaza utalii unakuta wanaonyesha miradi iliyofadhiliwa na TANAPA ya ujenzi wa vyoo na madarasa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hiyo inasaidia vipi katika kutangaza utalii tunasema wkamba tumeanzisha ile channel kwa ajili ya kutangaza utalii ile inasaidia vipi kuonyesha kwamba TANAPA wako pale? Au unaonyesha madaktari wa wanyama wanachoma Tembo sindano. Kuna watu ni waoga hawapendi kuona hata vidonda vya wanyama ukiwaonyesha vile unawaogopesaha hata kwenda tena kutalii kwahiyo tuonyesheni vitu vizuri, tuonyesheni wanyama, tuonyesheni Ngorongoro, tuonyesheni Serengeti kupitia hii Tanzania unforgettable na siyo vinginevyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu tozo kwenye biashara; nitangaze interest kidogo, kwenye biashara za hoteli kama alivyoongea Mheshimiwa Lucy Uwenya jana tozo zimekuwa nyingi sana, unakaa mtu anapiga hodi mimi ni idara fulani nataka tozo, huyu anapiga hodi hatuwezi kwenda. Na tena ilitakiwa hoteli hizi mpya zinazoanza muwape nao kama miaka mitatu au at least miaka miwili ya task hizi tozo ili wakue kibiashara na hoteli zikikaa standard wakikua kibiashara huduma zikikaa sawasawa hao watalii mnaowavutia kuja watakuwa na sehemu sasa nzuri za kufikia, sehemu nzuri za kulala na si vinginevyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana kwa sababu Mheshimiwa Waziri Mkuu jana amesema kwamba hizi tozo zitaondolewa naomba niiombe Serikali iondoe hizi tozo haraka sana kwa sababu matozo haya yamejazana katika biashara, sio tu biashara za hoteli hata biashara nyingine tofauti tozo zimezidi saba nchi hii ndio maana biashara hazikui, tuondoe tozo katika hizi biashara watu waajiri wakishaajiri hata wale wafanyakazi wanalipa kodi income task, wanalipa nini nayo ni njia nyingine ya kulipa kodi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hizi kampuni au hizi biashara zinanunua bidhaa mbalimbali zinalipa kodi. Brother Mheshimiwa Dkt. Kigwangala concentrate kwenye kazi kwa sababu vitu vingine sometime unakuwa kama unaenda off step unavunja bodi halafu Mheshimiwa Rais siku mbili baadaye anakuja anairudisha vitu kama vile havitakiwi inakuwa ni kama political movies. Nakujua una potential yaani probably katika watu wanaokujua katika hili jengo na uwezo wako na potential wako mimi niko kwa kule tulikotoka forget about political issues, zile petty issues za politics, concentrate kwenye kutuongezea watalii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi kama Malaysia kwa mwaka wana watalii 25 milioni brother yaani wana watalii wengi kuliko population. Population ni 20 milioni lakini wanakuwa wana wataalii kwa mwaka 25 milioni ukiuliza vivutio hawana. Kuna siku nilikwenda Malaysia nikwauliza vivutio vyenu ni nini wakasema tuna maghorofa sijui ghorofa gani limejengwa kwa vyuma, tuna daraja gani, tuna beach na vyakula yaani mpaka vyakula wameviweka kama sehemu ya kivutio cha watalii. Sisi tuna madude yote haya kuanzia Ngorongoro, kuanzia Serengeti, kuanzia sijui Ruaha, kuanzia wapi kwa kweli tulitakiwa tuwe na watalii hata angalau milioni 10,15 kwa uwezo wetu wa kujitangaza, ahsante sana. (Makofi)