Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to supplementary Questions by Hon. Subira Khamis Mgalu (169 total)

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwanza nionyeshe masikitiko yangu makubwa kwa majibu ya Serikali, lakini natambua ugeni wa Mheshimiwa Naibu Waziri na nimhakikishie kwamba hayo majibu ambayo umeandaliwa yana mapungufu makubwa.
Je, utakuwa tayari kwenda field kutembelea ukajionee hali halisi iliyopo katika mradi huu kwa sababu sio kweli kwamba umekamilika?
Mheshimiwa Spika, la pili, kumekuwa na matatizo makubwa ya kukatikakatika kwa umeme na hasa kunapokuwa na dalili za mvua au mvua inaponyesha. Je, tatizo hili la kukatikakatika kwa umeme litakwisha lini katika Halmashauri ya Temeke?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mimi mwenyewe binafsi Jumapili nilifanya ziara ya kutembelea miradi hii na nilipita pamoja na TANESCO. Tulikuwa na Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Umeme (TANESCO) na Meneja wa TANESCO Mkoa wa Temeke tuliitembelea. Katika majibu yangu ya msingi nimeainisha miradi ambayo haijakamilika na mradi ambao haujakamilika ulikuwa Masista Magogo Na. 2 na Na. 3 ambao utakamilika Disemba 2017.
Mheshimiwa Spika, kwahiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba miradi hiyo kwa kweli nimeiona lakini changamoto kubwa iliyopo ni kwamba wakati miradi inakuwa designed scope yake na tunatambua maeneo ya Mbagala na Wilaya ya Temeke na Kigamboni ujenzi wa makazi unaongezeka kwa kasi, kuna maeneo yameongezeka wananchi wengi wamejenga. Kwa hiyo, scope ile imewaacha nje kwa hiyo unaona kwamba mahitaji yameongezeka kuliko ambavyo scope ilizingatiwa. Kwa hiyo, nimthibitishie. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge ameuliza tatizo la kukatikakatika kwa umeme kwa Wilaya ya Temeke litaisha lini. Ni kweli kuna tatizo la kukatikakatika kwa umeme maeneo ya Temeke, Mbagala, Yombo Dovya, Buza na Kigamboni. Serikali kupitia TANESCO imekuwaikitekeleza miradi mbalimbali, hata mwaka huu wa fedha imetenga kiasi cha shilingi bilioni 3.2.
Mheshimiwa Spika, sambaba na hilo kuna ujenzi wa miradi inayoendelea chini ya Mradi wa TEDAP (Tanzania Energy Development and Access Expansion Project). Miradi hiyo inahusisha ujenzi wa msongo wa KVA 232 unaotoka Gongolamboto mpaka Mbagala na ujenzi wa kituo kikubwa cha kupoozea umeme chenye MVA 50.
Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo pia kuna ujenzi wa msongo wa umeme wa kilovoti 132 ambao unatoka Mbagala unaelekea Kigamboni, ujenzi wa msongo wa umeme unaotoka Kurasini kuelekea Kigamboni. Kwa hiyo, jitihada zote hizo na tatizo linasababishwa na kuongezeka kwa mahitaji ya umeme Mbagala na ndio maana unakatikakatika. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kutokana na kazi zitakamilika Desemba 2017 na kuanzia Disemba, 2017 nakuthibitishia kwamba tatizo la kukatikakatika kwa umeme kwa Wilaya ya Temeke litakuwa limepungua na litaisha kabisa. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Pamoja na majibu ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Pwani, tangu alama ya X zilivyowekwa Serikali haijarudi kutoa mrejesho kwamba kitu gani kinaendelea na wananchi wale kujua tathmini hiyo watalipwa kiasi gani. Je, ni lini watarejesha mrejesho kwa wananchi ili waweze kujua malipo yao yatakuwa kiasi gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Serikali iliweka alama za X mwaka 2015 na sasa hivi tunaelekea 2018. Wananchi wanauliza watalipwa kwa tathmini ile au uthamini utafanywa mwingine? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza ameuliza ni lini Serikali itapeleka mrejesho, naomba nimtaarifu muda si mrefu Serikali itapeleka mrejesho wa namna ambavyo malipo haya ya bilioni 21.6 kwa wakazi wa maeneo haya inakojengwa msongo huu wa kilovoti 400. Kwa kuwa mimi na yeye ni Wabunge tunaotoka Mkoa wa Pwani na niwataarifu pia Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Koka na Mheshimiwa Ridhiwani maana nao wamekuwa wakifuatilia, kwa hiyo muda si mrefu tutawapelekea mrejesho na taarifa wataipata. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge ameuliza kwamba kwa kuwa tathmini ilifanyika mwaka 2015 na tunaelekea mwaka 2018, naomba tu nimtaarifu kwamba malipo ya fidia yatalipwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo. Ahsante. (Makofi)
MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Hoja ya kulipa fidia watu wanaopisha mradi wa TANESCO inafanana na watu ambao walichomewa moto mashamba yao wakati wa ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam katika Kijiji cha Kilangala. Bahati TPDC kwa kushirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Lindi waliunda Tume ya kwenda kuhakiki yale madai ya kuunguziwa moto mashamba yao mwaka 2013.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari tathmini imeshafanyika na kinachosubiriwa ni kulipwa tu lakini tuliahidiwa wananchi wale wangelipwa mwezi wa Julai. Naomba commitment ya Serikali, ni lini wananchi wa Kilangala watalipwa hizi fedha zao ambazo zilitokana na wao kuchomewa moto mashamba yao? Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni kweli tathmini ilifanyika na naomba nimtaarifu kwamba wananchi wa Kijiji cha Kilangali watalipwa kwa mujibu wa sheria na taratibu. Ahsante.
MHE. BONNAH M. KALUWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami nilitaka nimuulize Mheshimiwa Waziri. Wananchi wa Jimbo la Segerea, Kata ya Kinyerezi, Mtaa wa Kifulu nao pia walitoa maeneo yao kwa ajili ya kuipisha TANESCO na mpaka sasa hivi hawajalipwa tangu Machi, 2016. Nataka nimuulize Mheshimiwa Waziri ni lini wananchi wa Kinyerezi watalipwa pesa hizo kwa ajili ya maeneo yao waliyotoa?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bonnah Kaluwa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tathmini ya maeneo ya Kinyerezi ambapo maeneo yao yametolewa kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa Kinyerezi imekamilika na kiasi cha Sh.10,475,603,000 zinahitajika. Kwa hiyo, naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge na wananchi wake kwamba fidia hii italipwa kwa bajeti zinazokuja. Ahsante.
MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwepo na kilio kikubwa sana cha mahitaji ya umeme Kata ya Mkange pale Chalinze ukizingatia kuwa sehemu hii inachangia kwenye uchumi wetu wa Taifa hususan katika Wilaya ya Bagamoyo, pia na Halmashauri ya Chalinze na Tanzania kwa ujumla hususan katika viwanda pamoja na utalii.
Je, Serikali inajipangaje kusaidia wananchi pamoja na wawekezaji wa viwanda umeme ili kupunguza ukali wa maisha wa eneo hili la Kata ya Mkange? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi mkubwa wa Stiglers Gorge unadhamiria kuikomboa nchi yetu katika umeme hususan katika viwanda vinavyojengwa pamoja na treni hii ya umeme.
Je, Serikali inawaachaje wananchi wa Jimbo la Rufiji ambao wametunza bwawa hili pamoja na Mto Rufiji kwa miaka mingi sana hususan wakazi wa Kata ya Mwaseni, Kipugira, Ngorongo na Mkongwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru kwa maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge Mchengerwa na naomba nimpongeze kwa jitihada zake za kufuatilia changamoto mbalimbali za nishati katika jimbo lake pamoja na muuliza swali la msingi. Ameuliza swali juu ya mahitaji ya umeme kwenye Kata ya Mkange iliyoko Jimbo la Chalinze na ni kweli Kata hii ya Mkange imepakana na Mbuga ya Saadani.
Naomba nimtaarifu kwamba katika mradi ambao unaendelea waUrban Peri Urban Edification Project of Coast Region na Kigamboni – Kata ya Mkange itapata umeme kupitia Miono. Kwa hiyo, naomba nimtaarifu kwamba Serikali imezingatia na kwa kuwa ina dhamira kwamba kila kijiji ifikapo 2020/2021 kipate umeme kwa hiyo Kata ya Mkange itapata umeme kupitia Miono.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ameulizia suala la Stiglers Gorge. Naomba nilitaarifu Bunge lako Tukufu ni kweli Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli imedhamiria kwa dhati kuongeza upatikanaji wa nishati nchini kwetu na imedhamiria kwa dhati kutekeleza mradi huu ambao utaongeza megawati 2100, tender imeshatangazwa na zaidi ya makampuni…
Mheshimiwa Mwenyekiti, na nimtaarifu tu Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa mradi huu unatekelezwa katika maeneo ya Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Pwani eneo la Rufiji Kata alizotaja Mwaseni na Ngorongo ni Kata ambazo ni kweli zimetunza bwawa hili na zitafaidika kwanza kupitia upatikanaji wa nishati hii ya umeme lakini pia kupitia ajira ambazo zitapatikana kipindi cha ujenzi wa bwawa hili, lakini tatu, Wilaya hii ya Rufiji imekuwa ikikumbwa na mafuriko ya mara kwa mara. Kupitia ujenzi wa bwawa hili ni dhahiri kwamba ule uhifadhi wa maji utasaidia kuzuia masuala ya mafuriko katika maeneo haya.
…lakini langu lingine pia ujenzi wa bwawa hili litasaidia shughuli za kilimo cha umwagiliaji kwa maeneo yale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba Watanzania muamini mradi huu unatekelezwa kwa pesa za ndani za nchi yetu. (Makofi/Vigelegele)
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Pamoja na majibu hayo naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Kalenga pamoja na kazi nzuri inayofanyika wakandarasi hawa wanapeleka umeme lakini hawafikishi kwenye Taasisi za umma kama zahanati shule.
Je, Serikali inatoa msisitizo gani na kuwafariji hawa wanchi wa Kalenga juu ya utekelezaji wa mradi huo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika Jimbo ya Njombe Mjijini yupo mkandarasi anayetekeleza mradi wa Makambako - Songea. Mradi hule ulikuwa-designed miaka mingi sana, matokeo yake ni kwamba mitaa imepanuka na maeneo yamepanuka na yule anatumia mchoro wa miaka mingi iliyopita.
Je, Serikali inatusaidiaje sasa ili kusudi mradi ule wa Makambako - Songea inaopisha umeme katika vijiji, umeme ule uweze kufika vitongoji vyote na taasisi za umma?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza lilijielekeza kwenye taasisi za umma ambazo hazifikiwi na Mradi wa REA unaoendelea. Ningependa kumtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba kwenye Mkoa wa Iringa kuna mradi wa densification unaotekelezwa kwa ajili ya maeneo ambayo yalirukwa kwenye Awamu wa Pili. Inaangalia maeneo ya umma, taasisi mbalimbali, iwe hospitali, ziwe shule za msingi na kadhalika. Kwa hiyo nimuhakikishie kwamba mradi wa densification unafanya hiyo kazi katika Mkoa wa Iringa na mkandarasi anaendela na kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, aliulizia juu ya mradi wa Makambako - Songea. Naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwamba katika mradi huu wa Makambako Songea ujenzi wa laini wa msongo wa KV 220 kwanza kazi inaendela vizuri lakini pia swali lake alikuwa anauliza je maeneo ambayo vijiji vinavyopitiwa na msongo huo usambazaji wa umeme ukoje. Nimthibitishe Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi ya kusambaza umeme itaendelae na maeneo ambayo yataachwa REA III itaendelea kuya-cover kwasababu mpango wa Serikali ya Awamu Tano ni kuhakikisha kwamba vijiji vyote vinapata umeme ifikapo 2020/2021. (Makofi)
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mradi wa REA III tayari umeanza na vijiji vingi vimepimwa, lakini sasa hivi kuna baadhi ya vijiji ambavyo vilisahaulika na baadaye tukaleta kuomba tena viingizwe.
Sasa Serikali inatuambiaje hasa katika Wilaya ya Kilolo, je, vijiji ambavyo vilisahaulika vitaongezwa?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kama nilivyosema, mradi wa REA una awamu mbili, na lengo lake ni kuvifikia vijiji 7,823. Awamu ya kwanza vijiji 3,559 na awamu ya pili vijiji 4,313. Nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba vijiji vyote vitafikiwa umeme ifikapo mwaka 2020/2021. (Makofi)
MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, maeneo ya Kakelege na eneo la uwanja wa ndege Kata ya Nkilizia yapo katikati ya mji wa Nansio. Lakini maeneo haya yamerukwa na huduma ya umeme, jambo linalofanya wananchi wa maeneo haya waone kama wametengwa. na Mheshimiwa Waziri nimekuwa namuwasilishia tatizo hili mara kwa mara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali langu nataka kujua Serikali imefikia hatua ipi kuhakikisha kwamba maeneo haya yaliyo katikati ya mji wa Nansio yote yanapata huduma za umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika maelezo yangu ya awali Serikali inatekeleza mradi pia wa densification ambao sasa hivi Awamu ya Kwanza na ni kwa Mikoa sita. Baada ya kukamilika kwa mikoa hiyo Serikali itaendelea pamoja na wafadhili wa Norway kutekeleza awamu ya pili. Nia ya mradi huu ni kusambaza umeme katika maeneo kaya, vitongoji na taasisi za umma zilizorukwa. Kwa hiyo, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba Awamu ya Pili ya mradi huu itafikiwa katika maeneo ambayo ameyataja.
MHE. DUNSTAN. L. KITANDULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Serikali ilihaidi kwamba Kata ya Mwakijembe ambayo iko mpakani na Kenya vijiji vyake vilisahaulika lakini kuna umuhimu wa kiulinzi vijiji vile kupata umeme. Serikali ilihaidi kwamba kabla mkandarasi hajaondoka kufanya survey wataagizwa ili jambo hilo lifanyike. Je, ni lini jambo hili litakamilika?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kata anayoitaja Mheshimiwa Mbunge ya Mwakijembe ni kata ambayo iko mpakani, laikini kama alivyosema aliliwasilisha ombi lake hilo. Kwa kutambua umuhimu wa maeneo ambayo yako mpakani suala lake linashughulikiwa na mkandarasi wa Mkoa wa Tanga katika maeneo ambao Wilaya ya Mkinga na Wilaya zinginezo ni Delimiki Electric Company Limited yupo site anaendelea na hiyo kazi. Kwa hiyo nimtoe wasi wasi Mheshimiwa Mbunge, kwamba Serikali inashughulikia. Na kwa kuwa nia yetu ni kusambaza umeme katika maeneo yetu hilo jambo litafanikiwa, ahsante.
MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza, pamoja na kupita bomba la gesi katika maeneo mengi ya Mtwara na Lindi, bado vijiji na mitaa mingi haina mtandao wa umeme. Je, ni lini REA III itamaliza tatizo hili kwa mikoa ya kusini? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, mkandarasi aliyepewa kusambaza mtandao wa umeme Mtwara yupo slow sana. Je, Serikali inachukua uamuzi gani kwa mkandarasi huyo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge ameuliza; ni lini REA III itamaliza tatizo la kusambaza umeme katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mtwara. Nataka nimfahamishe Mheshimiwa Mbunge kuwa Mkandarasi wa Mkoa wa Mtwara ni JV Radi Service Limited na ameshalipwa asilimia kumi na yupo Mkoani Mtwara akiendelea na kazi ya upimaji wa njia ya umeme, na kwa kuwa Wizara tumetoa maelekezo kwamba vifaa vyote vya mradi huu REA III vipatikane ndani ya nchi, wakandarasi wanachoendelea nacho sasa ni namna ya kutafuta vifaa vyote na kuagiza ndani ya nchi, na nimhakikishie kazi hii itafanyika kwa mujibu wa ratiba iliyopangwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili anaulizia hatua gani zitachukuliwa dhidi ya mkandarasi huyu. Naomba nimwambie ratiba ya REA iko awamu mbili, awamu ya kwanza ni 2017 hii Julai mpaka 2019, kwa hiyo mkandarasi huyu yupo ndani ya muda. Na kwa kuwa amelipwa asilimia 10 na ameanza kazi, nimthibitishie tu zoezi la upelekaji umeme katika Mtwara kwa mkandarasi huyu JV Radi Service itakamilika kwa wakati.
MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa
Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi.
Kwa kuwa chanzo cha umeme pale Somanga Fungu kinashindwa kufanya kazi vizuri na kupelekea matatizo makubwa ya umeme kwa Wilaya ya Kilwa na Rufiji kwa sababu ya mitambo ile kuchelewa kufanyiwa ukarabati na kwa kuwa sasa tatizo hilo linaendea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itatuunganisha watu wa Kusini na Gridi ya Taifa kwasababu sasa umeme imeshafika pale Kilwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge Ngombale kwamba mitambo ya Somanga Fungu inatarajia kufanyiwa ukarabati hivi karibuni na kampuni ya RENCO ya Italy. Na Serikali kupitia TANESCO wameshasaini mkataba na ukarabati huo utakamilika Desemba, 2018 ambapo mitambo itakuwa na uwezo wa kuzalisha megawati 7.5 na matumizi ya Kilwa ni megawati tatu. Kwa hiyo naomba nimtaharifu kwamba hilo linafanyiwa kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ameuliza ni lini…
MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, wasiwasi wangu katika swali langu la msingi ni viwango vya miundombinu hii hasa nguzo. Wamesema kwamba TANESCO wana zoezi la kukagua nguzo kabla ya matumizi. Swali langu liko hapa: wanachukua hatua gani wanapogundua kwamba nguzo hizi ziko chini ya viwango? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Juma Othman Hija, kwa swali lake la nyongeza. Kama ambavyo jibu langu la msingi limesema, Shirika la TANESCO hufanya ukaguzi kwanza wa vifaa hivi kabla havijatumika kwenye miradi hii. Kwa hiyo, endapo inagundulika nguzo hizi hazina ubora, nguzo hukataliwa na wanaotekeleza miradi miradi hiyo huelekezwa kutimiza vigezo na hasa vile viwanda ambavyo vinatengeneza hizi nguzo. Ahsante sana.

MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Chilonwa, Vijiji vya Bwawani, Kata ya Kamanchali na Vijiji vya Mlebe, Kata ya Msamalo nguzo zilikuwa zimeshapelekwa kwa ajili ya kuweka umeme na mashimo yakachimbwa, lakini baadae nguzo hizi zikaja kuhamishwa.
Je, Serikali ina mpango gani sasa kuona umuhimu wa kuvipa vipaumbele vijiji hivi ambavyo vilikuwa vimeshapelekewa nguzo na kuondolewa ili katika awamu ya tatu visije vikawa vijiji vya mwisho tena? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Makanyaga, Mbunge wa Jimbo la Chilonwa kwa swali lake zuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakiri kwamba ni kweli vipo baadhi ya vijiji ambavyo vilipelekewa miundombinu ya hizi nguzo, lakini baadae zikahamishwa kwa kuwa havikuwepo kwenye mpango wa utekelezaji wa kupeleka umeme vijijini REA Awamu ya Pili. Nimdhibitishie kwamba kwenye hii REA Awamu ya Tatu ambayo inaendelea kwa round hii ya kwanza, vile vijiji vyote ambavyo kwa bahati mbaya, kwamba vilipelekewa nguzo halafu zikaondolewa, miradi hiyo itatekelezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba vijiji vyote nchi nzima vitapata miundombinu ya umeme kwa kipindi hiki ambacho kinaendelea. Ahsante sana.
MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi niulize maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya kuridhisha ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali madogo mawili. Swali la kwanza, miradi ya umeme ya REA III imezinduliwa karibu nchi nzima katika kila Mkoa, lakini utekelezaji wake mpaka sasa hivi haupo, isipokuwa ipo katika mipango kama hivi ambavyo inaonesha. Nini ambacho kinasababisha au kimesababisha kucheleweshwa kwa miradi ya REA III kuanza kukamilika tofauti na iliyopo katika maandishi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili ni kwamba pamoja na majibu yake, Miradi ya REA tuliiwekea zuwio la fedha, yaani tuli-ring fence fedha zake ambazo zilitakiwa zisiguswe, lakini mpaka sasa hivi miradi hii haitekelezeki kwa sababu hizi fedha hazieleweki mahali ziliko.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu nataka niulize je, hizi fedha ambazo tumezi-ring fence kwa ajili ya utekelezaji wa hii miradi, kwa nini hazitumiki kutekeleza mradi ikizingatiwa kuna fedha ambazo tunakata katika mafuta shilingi 50 kwenye kila lita ya mafuta? Kwa nini zinashindwa kutumika kwa ajili ya kumalizia hii miradi? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli miradi hii ya umeme vijijini ilizinduliwa mwezi wa Sita mwaka 2017. Naomba nimhabarishe Mheshimiwa Mbunge kwamba wakandarasi wote ambao waliteuliwa takribani 27 tulikutana nao tarehe 13 Januari, 2018 hapa Dodoma.
Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa miradi una kazi mbalimbali. Kwanza, walikuwa wana-survey na mnakumbuka Waheshimiwa Wabunge wengi mlileta mapendekezo, maombi ya vijiji mbalimbali, kwa hiyo, lazima survey ifanyike.
Pili, baada ya survey lazima kuwe na michoro, lakini nimthibitishie kwa Mkoa wake wa Songwe na Wilaya yake ya Momba, mkandarasi wake ameshaagiza vifaa na kesho tarehe 31 Januari na tarehe 01 TANESCO wanaenda Mkoa wa Arusha kuangalia zile transfoma. Kwa hiyo, ni wazi kwamba miradi hii inatekelezeka, lakini zipo hatua mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, niongezee kwa kusema pia, vipo vijiji ambavyo vimeshawashwa umeme REA hii ya III. Kwa hiyo, inategemea Mkandarasi na huo muda. Kwa mfano, Geita kuna vijiji vimewaka; Mwanza Halmashauri ya Bumbuli pia umeme umewaka REA hii ya III. Kwa hiyo, miradi inaendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili alikuwa anasema kwamba, vipi kuhusu pesa zake za miradi hii ya umeme vijijini? Ni kweli nalishukuru Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Bunge hili iliwekwa tozo maalum kwenye mafuta na mfuko huo kweli umelindwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niishukuru Wizara ya Fedha kwamba pesa zimekusanywa, zimewasilishwa na mpaka sasa tumeshapata shilingi bilioni 170.
Kwa hiyo, pesa kwenye miradi hii siyo tatizo. Tatizo ambalo lipo, changamoto tuliyokuwa tunaiona ni hawa wakandarasi kujipanga kwa mujibu wa wakati na ratiba wanavyozipanga. Ndiyo maana baada ya kuona hilo tatizo, tumekutana nao hapa Dodoma na tumewapa maelekezo kwamba mwisho tarehe 28 Februari, wakandarasi wote waanze kazi. Siyo kazi ya survey, kazi ya kuweka nguzo na miundombinu mingine ili miradi itekelezeke.
Mheshimiwa naibu Spika, nilithibitishie Bunge lako, miradi hii muda wake, hii awamu ya kwanza hii ni kipindi hiki mpaka Aprili, 2019.
Kwa hiyo, niwatoe hofu. Kwa kuwa pia tumeweka usimamizi mzuri, kila mkoa tumemtaka engineer mmoja asimamie, kila Wilaya kuwe na engineer mmoja kwa ajili ya miradi ya REA tu. Kwa hiyo, ninaamini, hata kasoro ambazo zilijitokeza kwa miradi ya REA awamu nyingine, kwa Awamu hii ya III itaenda vizuri na itakamilika kwa wakati. (Makofi)
MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ina vijiji 12 tu ambavyo vimepata umeme wa REA, lakini vijiji 22 bado havijaingizwa kwenye mpango huu wa REA III. Naomba kujua ni lini sasa Serikali itaingiza hivi vijiji 22 vyote ili waweze kupata umeme wa REA? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Hongoli kwamba vijiji vyake 22 vilivyosalia vyote vitaingizwa kwa Awamu ya Tatu round ya pili ambavyo vinahusika vijiji 4,314. Kama ambavyo nimejielekeza tangu mwanzo, lengo la Serikali hii ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha vijiji vilivyosalia 7,873 vyote vinafikiwa na miundombinu ya umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, awamu hii tumeanza na vijiji 3,559 vinasalia vijiji 4.314. Kwa hiyo, ndani yake kuna vijiji 22,000 vya Jimbo lake la Njombe. Kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote na Watanzania wote, Serikali ya Awamu ya Tano inaenda kufanya mapinduzi ya nishati vijiji vyote. (Makofi)
MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake. Wizara ya Nishati imesema mara nyingi ndani na nje ya Bunge kwamba katika vijiji ambavyo vinahusika na mradi wa REA watu wote walioko kwenye vijiji hivyo, hata wale ambao nyumba zao ni za majani watapewa umeme. Hata hivyo, katika utekelezaji wa miradi hii Awamu ya Kwanza na Pili katika Wilaya ya Mwanga ni familia chache sana zilizokuwa zimejitayarisha kupewa umeme ambazo zimefungiwa umeme huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeambiwa kwamba nia yake ni kuipa TANESCO biashara ya kuzifungia kaya hizo umeme kwa Sh.177,000/= baada ya mradi kukamilika. Je, sera hii tuliyotangaziwa hapa imefutwa lini ikaja hii ya TANESCO kuchagua watu wachache kuwapa umeme na wengine kuwaacha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tuliambiwa kwamba, mkandarasi huyu ambaye ameshindwa kazi ya kusambaza umeme pale awali hawezi tena kupewa kazi katika Wizara ya Nishati na Madini, hasa kazi ileile ambayo yeye alifukuzwa kwa kushindwa kutekeleza. Sasa katika Wilaya ya Mwanga aliyekuwa anatekeleza mradi huu kwa niaba ya SPENCON alikuwa bwana mmoja anaitwa Mrs. Njarita & Company Limited. Sasa Njarita huyo huyo amepewa kazi ya kutekeleza mradi huo kwa jina lingine la Octopus. Je, inatuambia nini au inawezaje kututhibitishia kwamba, huyu aliyeshindwa kutekeleza huu mradi huko nyuma, sasa ataweza kutekeleza round hii? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mheshimiwa Profesa Jumanne Abdallah Maghembe kwa maswali yake mawili ya nyongeza, lakini na kwa kazi nzuri anayofanya katika kufuatilia mahitaji ya nishati katika Jimbo lake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa kwenye ziara wiki iliyopita katika Jimbo la Mheshimiwa Maghembe, kukagua maeneo mbalimbali ambako mradi huu wa REA Awamu ya Pili haukufanyika vizuri, lakini utakubaliana na mimi kwamba, ni kweli kuna mahitaji makubwa na kwa kuwa, hizi kazi zinatekelezwa kwa mujibu wa scope na kwamba, scope ile inakuwa haikidhi mahitaji, lakini Serikali ya Awamu ya Tano kwa kutambua hilo imekuja na Mradi Mpya wa Ujazilizi (densification).
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu unatekelezwa katika mikoa sita ya awali ya mfano. Ilipofika Mkoa wa Kilimanjaro na wao Mkandarasi Mshauri Elekezi yupo ndani ya mkoa ule kujaribu kufanya feasibility study kwa ajili ya mradi huu, densification kwa maeneo ambayo au kwa kaya ambazo hazijaguswa au taasisi za kijamii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimthibitishie Mbunge hakuna ukweli wowote kwamba, zile kaya ambazo hazijaunganishwa nia ya kwamba, iipe kazi TANESCO.
Mheshimiwa Mwenyekiti, TANESCO ni Serikali ambayo nayo ina kazi ya kusambaza umeme, lakini kwa utaratibu mwingine, lakini si kweli kwamba, kaya hazifikiwi kwa sababu ya kuipa kazi TANESCO. TANESCO itaendelea na kazi ya kusambaza umeme, lakini kama umeme vijijini na ndio maana Serikali imetambua uwepo wa ukubwa wa mahitaji imekuja na huo Mradi wa densification. Kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge zile kaya ambazo hazijaunganishwa, zile taasisi za umma ambazo hazijaunganishwa, zitaunganishwa kupitia mradi huu wa densification ambao umefanya vizuri katika Mikoa ya Songwe, Mbeya, Pwani, Arusha, Tanga, Iringa na Mara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ameeleza kwamba mbona mkandarasi yuleyule ndio amepewa kazi na kwamba, Wizara itathibitishaje kwamba kazi zitafanyika. Ni kweli kazi ilifanywa na Kampuni ya SPENCON ambayo ndio ilikuwa main contractor. Huyu Kampuni ya Njarita Octopus walikuwa Sub Contractor. Uchunguzi uliofanyika na Serikali na Wakala wa Umeme Vijijini ulithibitisha kwamba, tatizo lilikuwa kwa main Contractor mwenyewe ambaye ni Spencon si hawa Sub Contractor.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilo nilipokuwa katika ziara tulikuwa na Mkandarasi huyu Njarita na sisi tumempa maelekezo na masharti, ndani ya miezi sita kazi zile zilizoshindwa kufanywa zimalizike na zikamilike.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati nzuri nilipokuwa eneo la tukio mkandarasi alikuwa ameshaanza kazi na niliwaomba viongozi wa maeneo hayo, Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya, Waheshimiwa Wenyeviti wa Halmashauri, pia nilizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mama yangu Anna Mghwira kwamba Ofisi yetu au Wizara yetu itasubiria taarifa za mara kwa mara za Mkandarasi huyu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wakandarasi hawa waliopewa kazi hii tutawafuatilia kwa kila hatua kuona kwamba, makosa yaliyojitokeza awamu zilizopita hayajitokezi tena. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza niipongeze Serikali chini ya Wizara ya Nishati kwa kazi nzuri wanayofanya ya usambazaji wa umeme vijijini, hasa hii REA Awamu ya Tatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwamba, kwa kuwa gharama za kuunganisha umeme wakati mradi unaendelea katika eneo ni Sh.27,000 na mradi ukishapita ni Sh.177,000; na kwa kuwa idadi nzuri na kubwa ya watumiaji wa umeme ni biashara nzuri kwa TANESCO, kwa nini sasa bei hii isiwe moja hiyohiyo ya 27,000 badala ya bei kupanda baada ya mradi kwisha? Kama haiwezekani, basi REA hawa waendelee na kazi ya usambazaji wa nguzo na miundombinu na TANESCO wafanye kazi moja tu ya kupeleka umeme na kukusanya kodi yao baada ya kupeleka umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa na namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge, Kaka yangu Nape Nnauye. Ni kweli bei ya kusambaza umeme ya vijijini ni Sh.27,000 kipindi cha mradi na hii ni hatua ya Serikali yetu ya Awamu ya Tano kwamba, imegharamia gharama zote za uunganishwaji kwa umeme huu na kwamba mwananchi yeye gharama yake ni analipia VAT.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu wazo alilolisema kwamba, mara baada ya mradi kukamilika na miundombinu kukabidhiwa TANESCO ni kweli wananchi wanaunganishwa kwa bei ya Sh.177,000, lakini hata hivyo niseme hata hii bei pia, Sh.177,000 nayo ina mchango wa Serikali kwa sababu, mijini kwa bei hii wanaunganishwa kwa Sh.321,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, wazo alilosema linapokelewa na litafanyiwa kazi na ni la msingi kwa sababu, Wizara yetu na Shirika letu la TANESCO na wadau wengine wa nishati kwamba, tunauza bidhaa ya umeme. Kwa hiyo, ni vema zaidi kwamba, tunapoiuza tupate wateja wengi, ili tupate mapato na kuendesha shughuli mbalimbali na uwekezaji mpya wa maeneo ya nishati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, nimelipokea na Serikali itaona utaratibu gani wa kufanya ili iweze kurahisisha. Ahsante sana.
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikiahidi mara nyingi sana kulipa fidia wananchi ambao maeneo yao yanapitiwa na umeme wa KV400. Miongoni mwa maeneo hayo ni Mkoa wa Manyara na katika Jimbo langu la Babati Mjini, wameahidi zaidi ya mara tatu na ahadi ya mwisho ni tarehe 17 Disemba, kwamba, mngewalipa. Hata hivyo, mpaka sasa Mheshimiwa Naibu Waziri mmekuwa mkisema kwamba, Wizara ya Fedha haiwapi pesa na Waziri wa Fedha yuko hapa. Naomba awatangazie wananchi wa Jimbo langu la Babati Mjini kwamba, ni lini wanawalipa fidia hiyo kwa sababu, wamechoka kusubiri?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Pauline Gekul kwa swali lake zuri, lakini naomba niseme haijapata kutokea Wizara yetu ya Nishati ikasema Wizara ya Fedha haijatupa pesa, kwa sababu Serikali inafanya kazi kwa pamoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ambayo ilijitokeza ni kwamba tulipata jedwali la thamani ya fidia. Wizara yetu ya Fedha kazi yake yeye hata inapoleta pesa ni kuangalia malipo yanafanyika kwa walengwa na kwa viwango sahihi. Kwa hiyo kulikuwa na changamoto ndogo ndogo tu za kumalizia kwa ajili ya kuthibitisha uhalali, kiwango na walipwaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimwambie Mheshimiwa Mbunge mradi huu wa KV400 msongo huu ni muhimu ambao unaunganisha na nchi ya jirani ya Kenya kwa kusafirisha umeme kwa maeneo mbalimbali. Kwa hiyo nimthibitishie kwamba fidia ya wananchi wa maeneo hayo italipwa muda si mrefu, ndani ya mwaka huu wa fedha na maandalizi yanaendelea vizuri. Ahsante sana.
MHE. SULEIMAN S. MURAD: Mheshimiwa Mwenyekiti, na yeye apewe maelekezo afike kwenye kaya zote. Na Mheshimiwa Naibu Waziri nakukaribisha Mvomero karibu sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Murad kwa swali lake la nyongeza na kazi anazoendelea kufanya za kufuatilia miradi ya umeme. Nakubaliana na yeye kwamba, huyu Mkandarasi MDH kwa kweli hakufanya vizuri na hakuwa mkandarasi katika mkoa wake tu, lakini alikuwa mkandarasi pia katika Mkoa wa Pwani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo sisi tumetoa maelekezo kwa REA kwa sababu, wakandarasi wote wa Miradi ya REA Awamu ya Pili ni Mikoa miwili tu Tanga na Arusha ambao wametimiza vigezo na wamemaliza kipindi cha uangalizi. Kwa hiyo mikoa mingi ina changamoto, Singida, Mbeya, Mikoa ya Kanda ya Ziwa. Kwa hiyo, tumetoa maelekezo na tumewataka REA wafanye tathmini na tutachukua hatua na kwamba, maelekezo ni kwamba, awamu ya tatu isiruke kitongoji chochote wala taasisi ya umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niliahidi Bunge lako Tukufu kwamba, nimesema tangu awali kwamba, upungufu wa awamu ya pili tumeubaini, tathmini imefanyika, awamu ya tatu tumejipanga vizuri kuhakikisha kwamba, umeme huu au miradi hii inatimiza lengo lililotarajiwa na maelekezo ya Serikali kwamba, kila kitongoji kisirukwe. Ahsante sana.
MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwanza kabisa namshukuru Waziri wa Wizara hiyo kwa sababu alifika na alifanya kazi mpaka saa mbili usiku na akanyeshewa na mvua alifika Ibaga. Pia Waziri aliacha maagizo ya kwamba umeme uende nyumba kwa nyumba usivuke na nguzo ziletwe zaidi ya 20. Nguzo zilizokuja ni 20 na umeme umekwishawaka lakini umetengeneza ubaguzi kwa sababu ziko taasisi za dini hazijapata, misikiti na baadhi ya wananchi. Kwa hiyo, umeme umewaka lakini bado umeleta matatizo. Je, ni lini agizo la Waziri litatekelezwa la kuongeza nguzo, umeme uwake katika maeneo hayo ili tatizo hilo liwe limekwisha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi wa Mkalama wako tayari kutekeleza sera ya viwanda inayoasisiwa na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Je, yupo tayari baada ya Bunge kutembelea na kuwathibitishia wananchi kuwaka kwa umeme kupitia REA III kwa Vijiji vya Mwanga, Kidarafa, Kikonda, Ipuli, Isanzu na maeneo mengine ya Mkalama ambayo yana uzalishaji mkubwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa hii. Kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Allan Kiula kwa namna ambavyo amekuwa akifuatilia utekelezaji wa miradi hii, nimepokea shukrani za Mheshimiwa Waziri wangu kwa ziara yake. Napenda nisisitize agizo lake la Mheshimiwa Waziri la kuagiza kwamba, zifike nguzo za kutosha katika maeneo ambayo miradi Awamu ya Pili haikukamilika katika Mkoa wa Singida litekelezwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimtaarifu kwamba, katika utaratibu huo mkandarasi mpya ambaye amepewa kazi ya kukamilisha miradi ambayo iliachwa na Mkandarasi wa awali Spencon, tumemwelekeza kwamba, maeneo yote nguzo zifike kwa wakati na ni nyingi na wananchi wote wa maeneo yale ambao wamekaa muda mrefu kusubiria umeme wa REA Awamu ya Pili wapatiwe huduma na pasiwepo kitongoji ambacho kimerukwa wala taasisi za jamii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili; umekuwa utaratibu wa Wizara yetu kwa kuwa, tunatambua miradi hii inatekelezwa vijijini kufanya ziara, wilaya kwa wilaya, kata kwa kata na kijiji kwa kijiji ambako miradi inatekelezwa. Kwa hiyo, nimuahidi kwamba, ziara katika Mkoa wa Singida katika maeneo aliyoyataja ikiwemo Ipali, Mwanga na Isanzu itafanyika kama ambavyo ilivyokuwa kawaida ya Wizara yetu. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la REA linahusu pia, Kata ya Soga, Kibaha Vijijini ambapo katika Kijiji cha Zogowale umeme ulifika kwa ajili ya ku-pump maji mpaka umefika Shule ya Waamuzi, Sekondari. Wananchi wa Kijiji cha Msufini walihamasishwa kutoa mazao na kutoa ardhi kwa ajili ya kupitisha umeme wa REA, huu ni mwaka wa tatu na hiyo kazi haijafanyika. Je, Wizara ina mpango gani kuhakikisha wale wananchi ambao wameshatoa mimea yao na wametoa ardhi zile nguzo za umeme zipite mpaka ufike Msufini pale Kata ya Soga na vijiji vya karibu?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na napenda nimshukuru Mheshimiwa Mbunge mwenzangu wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani. Nimthibitishie maeneo aliyoyataja Zogowale na hapo Kijiji cha Msufini kwamba, maeneo haya yamezingatiwa katika Mradi wa Peri Urban ambapo kwa kweli Serikali baada ya kuona kuna maeneo ni vijiji ambavyo vimekuwa na ongezeko la makazi na vimekuwa vikubwa, Serikali ikaja na Mradi wa Peri Urban ambao ni nje ya REA Awamu ya Tatu. Kwa hiyo, nimtaarifu na nimthibitishie vijiji hivyo vipo katika mradi huu Mpya wa Peri Urban ambako kazi ilitangazwa na mchakato wa kumtafuta mkandarasi sasa unaendelea. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, tatizo la REA II katika vijiji vingi umeme umepita bila kugusa maeneo ya wananchi. Je, nini Kauli ya Serikali kwamba, vijiji vyote ambavyo vilipitiwa na REA II na haujafika kwa wananchi vinarekebishwa ili wananchi waendelee kupata umeme kuliko umeme umepita katika vijiji lakini haujawagusa wananchi?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Namshukuru Mheshimiwa Julius kwa swali lake zuri na kwa kuwa, swali lake limejielekeza kwamba, utekelezaji wa miradi ya REA II kwamba kuna baadhi ya wananchi hawakufikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimtaarifu pamoja na Bunge lako Tukufu kwamba Serikali baada ya kuliona hilo kwamba, kuna maeneo yanatakiwa yafikiwe na miundombinu ya umeme ilikuja na mradi mpya densification, maana yake ujazilizi. Mradi huu unajielekeza kwenye maeneo ambako miundombinu ya umeme mkubwa imepita, lakini zipo kaya, vipo vitongoji, zipo taasisi za kijamii ambazo hazijafikiwa, kwa hiyo, huu mradi wa densification ambao umeanza kwa majaribio Mikoa Nane ikiwemo Mkoa wa Arusha, Tanga, Kilimanjaro, Mara, Songwe, Iringa pamoja na Pwani umeonesha mafanikio na katika maeneo hayo kazi zinaendelea na wamefikia hatua sasa ya kufunga transformer.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mradi huu ambao umelenga vijiji 305 na kuunganisha wananchi elfu 53, kwa kuwa, Serikali imeona mradi huu una mafanikio mradi, nataka nilitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba, hii densification sasa itaendelea na mikoa mingine. Hata sasa Mshauri Mwelekezi yuko katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya kutathmini na kuona namna ambavyo tutatekeleza mradi huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimtaarifu tu Bunge lako kwamba, kwa kweli, wananchi wasiwe na wasiwasi, Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Uongozi wa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli itakamilisha miradi hiyo.
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mheshimiwa Naibu Waziri sambamba na Waziri mwenye dhamana wamekuwa mara kadhaa wakijibu maswali hapa na kuahidi kwamba, visiwa vidogo vyote nchi nzima vitapatiwa umeme wa solar. Sasa ningependa kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri. Je, ni lini umeme wa solar utakwenda katika Visiwa vya Jibondo, Chole, Juani na Bwejuu? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Dau, Mbunge wa Mafia kwa swali lake zuri na tunatambua Mafia nako ni Wilaya ambayo ina visiwa vingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nisisitize kwamba, hii miradi tunayosema, huu mradi kabambe wa REA awamu ya tatu tunaoutekeleza, vijiji ambavyo vimetamkwa 7,873 vinahusisha pia na vijiji ambavyo tunaviita off grid. Kwa hiyo, nimthibitishie mchakato wa kuwapata Wakandarasi wanaopeleka umeme katika maeneo ambayo si rahisi kufika miundombinu ya kawaida unaendelea. Kwa mfano, Mkuranga kuna visiwa ambavyo tulipeleka umeme kupitia REA hii na utaratibu unaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo niseme siyo Mafia tu, lakini katika maeneo mbalimbali ambayo ni magumu kufikika kwa miundombinu ya kawaida, mradi huu wa REA Awamu ya Tatu ambapo vipindi vyake ni hii 2017/2018, 2018/2019 na 2019/2020 vijiji hivyo vitapatiwa. Hakuna kijiji ambacho kitaachwa kwa sababu tu ya mazingira yake. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
MHE. AISHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Tatizo lililoko Iramba Mashariki halina tofauti na tatizo lililoko Singida Kaskazini, Manyoni Magharibi, pamoja na Jimbo la Ikungi. Je, ni lini sasa Serikali itapeleka umeme kwa vijiji vilivyobaki ambavyo vilikuwa katika mpango wa REA II, ukizingatia sasa tuko mpango wa REA III, ili wananchi wa maeneo hayo waweze kunufaika na Sera ya Viwanda? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na nampongeza sana Mheshimiwa Aisharose kwa swali lake zuri. Naomba nimtaarifu tu katika maeneo ambayo ameyataja, Singida Kaskazini, Manyoni Magharibi, Ikungi, Mkandarasi ambaye anaenda kufanya kazi hizi zilizoachwa na Mkandarasi Spencon ameshateuliwa ambaye ni Emek Engineering and Dynamic na System Company Limited. Kwa hiyo, wako katika mchakato wa kumalizia tu masuala ya manunuzi ya kutoa Performance Bond, lakini kazi itaanza muda siyo mrefu na kwamba vijiji vyote ambavyo viliachwa awamu ya pili vitapatiwa umeme. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona niulize swali dogo la nyongeza. Matatizo yaliyopo Iramba Mashariki yanafanana kabisa na matatizo yaliyopo Wilaya ya Ngara. Vijiji vingi vya Wilaya ya Ngara, hasa Tarafa ya Lulenge, havina umeme. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme katika vijiji hivyo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami niungane nawe kuwapongeza Wabunge Viti Maalum na Wabunge wote ambao kwa kweli Bunge zima hili leo ni ushuhuda kwamba, limekuwa likifuatilia miradi ya nishati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Oliver kwa swali lake zuri ameuliza kwamba, Vijiji vya Wilaya ya Ngara ni lini vitapatiwa nishati ya umeme. Nataka nimjibu kwamba, kama ambavyo tumekuwa tukitoa taarifa ndani ya Bunge lako na si taarifa tu kwamba labda ni porojo ni kweli, Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli inatekeleza huu mradi kabambe wa kupeleka umeme katika vijiji vilivyosalia 7,873.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe pia ni shahidi. Jana wakati tunahitimisha taarifa ya Kamati yetu ya Nishati na Madini, Mheshimiwa Waziri wangu wa Nishati alitoa taarifa kuwashwa kwa umeme katika vijiji 24 katika utaratibu huu wa REA awamu ya tatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wilaya ya Ngara Mkandarasi yupo anafanya kazi. Ameanza zile kazi za awali za upembuzi na kadhalika lakini kwa sasa Wakandarasi wote nchi nzima wana-mobilise vifaa na wengine wako site wanaendelea na kazi mbalimbali. Nataka nilitibitishie Bunge, ile awamu ya kwanza ambavyo ni vijiji 3,559 tumesema mpaka Juni, 2019 viwe vimekamilika halafu tunaanza safari nyingine ya kumalizia vijiji vingine. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Mji wa Tunduma uko mpakani mwa Zambia na Tanzania na ni Mji ambao unahudumia Mataifa zaidi ya Nane yanaotumia Mpaka wa Tunduma, lakini kumekuwa na tatizo kubwa sana la umeme kukatika mara kwa mara na kusababisha usalama wa wageni pamoja na Wakazi wa Mji wa Tunduma kuwa hatarini. Je, ni lini Serikali itaweka umeme wa uhakika, kama ambavyo wenzetu wa Zambia pale ng’ambo walivyoweka umeme wa uhakika? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi hii na napenda nimshukuru Mheshimiwa Frank kwa swali lake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme Wilaya ya Tunduma ipo katika Mkoa wa Songwe, Mkoa ambao awali ulikuwa Mkoa mmoja wa Mbeya, kwa hiyo line zote zinazopeleka umeme katika Mkoa mpya wa Songwe zinatokana na Mkoa wa Mbeya. Kwa hiyo ni wazi njia ndefu ya kupeleka umeme katika Mkoa wa Songwe inasababisha kukatikakatika kwa umeme katika maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali kwa sasa pia ni kujenga Sub Station kubwa Tunduma ili kuwezesha upatikanaji wa umeme vizuri. Kwa sasa pia kuna mpango wa kujenga line ya kV 400 ambayo inaanzia maeneo ya Tunduma mpaka Mbeya inaenda mpaka Sumbawanga kwa ajili ya kurahisisha usafirishaji wa umeme katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge Serikali ya Awamu ya Tano inatambua hilo tatizo, lakini mipango hii ipo na itatekelezeka na baada ya muda umeme utakuwa ume-stabilize katika Mkoa Mpya wa Songwe. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Waziri katika Jimbo la Njombe Mjini kuna vijiji ambavyo vimepitiwa na mradi wa Makambako - Songea na mradi huu haujaingia kwenye vitongoji, haujaingia kwenye zahanati, shule ikiwemo shule ya sekondari ya Anne Makinda; na kwa kuwa mradi huu ni wa muda mrefu sana na vijiji vinaendelea kupanuka.
Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika vijiji hivi vilivyopitiwa na mradi wa Makambako - Songea?
Swali langu la pili, Jimbo la Lupembe lina vijiji 45, kati ya vijiji 45, vijiji 34 havina umeme ikiwemo Kijiji cha Ninga na kwa kuwa wananchi wa Kijiji cha Ninga wameamua kuunga mkono sera ya viwanda kwa kununua mashine ya kusaga yenye uwezo wa kusaga sembe zaidi ya tani 12 kwa siku, kwa nia ya kuanzisha kiwanda.
Je, Serikali itapeleka lini umeme katika vijiji hivi hususani Kijiji cha Ninga ili ndoto yao ya kiwanda chao kiweze kufanya kazi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu maswali mawili ya nyongeza.
Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge Neema pamoja na Wabunge wa Viti Maalum kwa namna ambavyo wanauliza maswali katika sekta yetu ya nishati.
Swali lake la kwanza amerejea kwamba mradi unaoendelea wa ujenzi wa msongo wa KV 220 Makambo - Songea; kwanza awali ya yote nimshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kutuwekea jiwe la msingi katika mradi huu. Mradi huu unaendelea vizuri mpaka sasa umefikia asilimia 70, na utaunganisha vijiji 120 katika Mikoa ya Njombe na Ruvuma.
Mheshimiwa Naibu Spika, Katika maeneo ambayo ameyataja Mheshimiwa Mbunge Neema na naomba nimtaarifu mpaka sasa Vijiji vitano katika Mkoa wa Njombe vimeshawasha umeme kupitia mradi huu na kwamba katika maeneo ambayo ameyataja hayajafikiwa na mradi huu, nataka nimwambie tu pia Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa densification na kwa mkoa wa Njombe peke yake mpaka sasa hivi vijiji 12 vimeshaunganishwa.
Kwa hiyo nataka nimwambie maeneo ambayo yatakakuwa mradi huo haukuyafikia yatafikiwa na miradi ambayo inaendelea REA Awamu ya Tatu pamoja na densification ambavyo kama nilivyosema na kama ambavyo Serikali imekuwa ikitoa maelekezo, taasisi za umma ikiwemo shule ya sekondari na hapa amerejea sekondari ya Mama Anne Makinda viunganishwe katika miradi hii inayoendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili amekitaja Kijiji cha Ninga, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kama alivyosema Jimbo la Lupembe lina vijiji 34 kati ya vijiji hivyo, vijiji 24 vipo katika mradi wa REA Awamu ya Tatu pamoja na kijiji ambacho amekitaja, na naomba niwapongeze vijiji vyote ambavyo vinatekeleza sera ya viwanda na kwa kuwa Serikali yetu ya Awamu ya Tano imedhamiria kutekeleza mapinduzi ya viwanda, nishati ya umeme itafika katika Kijiji cha Ninga pamoja na vijiji vingine kwa Awamu ya Tatu ambayo inaendelea. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa uzinduzi wa REA Awamu ya Tatu kimkoa wa Geita ulifanyika kwenye Wilaya ya Nyangh’wale, Kijiji cha Nijundu, mwenzi wa sita mwaka jana, lakini cha ajabu mpaka leo hii hata kijiji kimoja kati ya vijiji 35 vya Wilaya ya Nyangh’wale havijapelekewa nguzo.
Je, ni lini sasa Serikali itaanza kupeleka nguzo hizo katika hivyo vijiji ambavyo tumepewa vijiji 35?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Amar kwa swali lake zuri, katika Mkoa wa Geita mkandarasi wake ni JV White Service Limited ambaye ameshaanza kazi, na kwa kuwa ameeleza kwamba mpaka sasa katika Wilaya yake, nataka niseme wakandarasi hawa walipoteuliwa unakuta Mkoa mmoja una mkandarasi mmoja, na Mkoa huo unaweza ukawa na Wilaya mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maelekezo ya hivi karibuni katika Mkoa wa Geita mkandarasi alikuwa ameshaagiza nguzo takribani 3,000 na tulimpa maelekezo aende kila Wilaya. Kwa hiyo, kama mkandarasi mpaka sasa hivi hajafika katika Wilaya ya Nyang’wale naomba nimuelekeze na nimpe agizo kwamba kama vile tulivyotoa maelekezo tulivyokutana kikao cha tarehe 13 Januari, wakandarasi wote wafanye miradi Wilaya zote, wasijielekeze katika Wilaya moja.
Kwa hiyo, ninamuagiza mkandarasi JV White wa Mkoa wa Geita aelekee kwenye Wilaya zote na afanye kazi ya kuunganisha kupeleka hii miundombinu ya umeme kama ambavyo tulikubaliana katika Kikao cha tarehe 13 Januari, 2018.
MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi kuuliza maswali ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; kwa kuwa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki tulipata vijiji 17 kati ya vijiji 64 katika miradi ya umeme ya REA Awamu ya Kwanza na REA Awamu ya Pili, na kwa kuwa katika awamu zote hizo utekelezaji wake wa miradi hiyo kuna taasisi za umma kama vile shule, zahanati, vituo vya afya na nyumba za ibada na vijiji na vitongoji vingi kwa mfano, Kijiji cha Tomondwe, Mfumbwe, vitongoji vya Misala vilirukwa.
Je, Serikali huu mradi wa densification utafika lini Morogoro hususan katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki ili vijiji na vitongoji hivi vilivyorukwa vipatiwe umeme? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, pamoja na majibu hayo nataka niweke kumbukumbu sawa. Swali kama hili niliuliza katika Bunge lililopita katika swali la nyongeza na swali la msingi Bunge lingine lililopita. Serikali ilinipa majibu katika jimbo langu wamenipa vijiji 20 na si 14; mpaka sasa hivi huyo mkandarasi ameshafika na amefanya survey ya vijiji vyote 20. Hata hivyo kwa kuwa amefanya vijiji saba amepata mkataba wa kufanya survey pamoja na kujenga miundombinu ya umeme. Lakini vijiji 13 ameambiwa tu afanye survey ukizingatia ndani ya vijiji hivyo ndiko kunakojengwa kiwanda kikubwa cha sukari ambacho kitaanza ujenzi mwaka huu pamoja na Bwawa la Kidunda.
Je, Serikali imejipanga vipi ili kumalizia na ujenzi katika vijiji hivi 13 na vijiji vile vingine vya Tomondo na sehemu zingine? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza Mheshimiwa Mgumba amejielekeza kwenye utekelezaji wa miradi ya REA Awamu ya Kwanza na REA Awamu ya Pili ambako yako maeneo mbalimbali yalirukwa.
Napenda nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba maeneo ambayo yalirukwa katika awamu ya kwanza na ya pili Serikali yetu imekuja na mpango wa densification, kwa maana ya ujazilizi katika maeneo ambayo taasisi za umma, vijiji na kaya mbalimbali. Kwa kuwa densification imetekelezwa katika mikoa nane ya awali kama ambavyo tumepata kusema ndani ya Bunge lako Tukufu, awamu inayofuata sasa Serikali kupitia Wakala wa Umeme Vijijini imeajiri mshauri elekezi ambaye ni Multconsult ASA kutoka Norway pamoja na NORPLAN ya Tanzania kwa ajili ya kufanya verification ya maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali pia kupitia Wakala wa Umeme Vijijini imeomba ufadhili kutoka Norway, Sweden na Ufaransa kwa ajili ya densification ya awamu ya pili. Nilitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba maeneo mbalimbali na mikoa mbalimbali yataanza kufikiwa na densification ya awamu ya pili ikiwemo Mkoa wa Morogoro.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili Mheshimiwa Mgumba amejielekeza kwenye maeneo yale ambayo kama ambavyo amerejea jibu letu Bungeni la Mkutano wa Tisa kwamba katika vijiji vyake 20, vijiji saba vimefanyiwa survey na hivyo 13. Kama tunavyotambua jimbo hilo miradi mikubwa ya kimkakati inatekelezwa ikiwemo ujenzi wa Kiwanda cha Sukari pia na ujenzi wa Bwawa la Kidunda. Nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge nia yetu sisi kama Wizara ya Nishati ni kuwezesha sekta zingine. Kwa hiyo ni wazi kabisa kwamba vile vijiji 13 ambavyo vipo katika maeneo ambayo miradi mikubwa inapita tumemuelekeza mkandarasi ambaye ni State Grid maeneo yote ambayo amefanya upembuzi yakinifu amalizie kuendelea na ujenzi wa miundombinu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nimtoe hofu Mheshimiwa Mgumba kwamba maeneo yote ambayo ameyataja, hivyo vijiji 20 lakini pia kwa kutambua umuhimu wa maeneo hayo pia tumemuongezea vijiji nane vikiwemo vijiji viwili katika Kata ya Mkulazi ambako mradi mkubwa wa ujenzi wa kiwanda cha sukari unafanyika na Bwawa la Kidunda. Pamoja na kwamba maagizo ya Serikali pia yameelekeza kwamba maeneo ambayo kuna miundombinu mikubwa ya umeme iliyopita katika kata yake mojawapo ambayo ameitaja Tomondo pia tumempa vijiji vinne kwa sababu iko karibu na Kata ya Kiloka na Mikese ambako kuna miundombinu ya umeme. Kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kuwa Wizara inafanya kazi pamoja naye. Ahsante sana.
MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kusimama katika Bunge lako Tukufu naomba nimshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunipa nafasi hii, na niwashukuru sana wana-CCM na Chama changu cha Mapinduzi na hasa wananchi wa Jimbo la Singida Kaskazini kwa kuniwezesha kuwa mwakilishi wao hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hayo yaliyozungumwa katika Jimbo la Morogoro Kusini yanafanana sana na Jimbo la Singida Kaskazini. Jimbo la Singida Kaskazini wakati unaongelea usambazaji wa umeme REA Awamu ya Tatu tulipata Mradi wa REA Awamu ya Pili katika vijiji vya Mrama, Makhandi, Mitula, Merya, Mipilo, Magojoha, Msange, Madasenga, Njia Panda, Mohamo, Mwamba na Mgori. Hata hivyo, mwaka 2016 mwishoni mkandarasi huyo alifilisika wa SPENCON na kazi hiyo ilisimama tangu mwaka 2016 na hadi sasa mradi huo haujaendelea mpaka.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nilikuwa nataka nimuulize Mheshimiwa Waziri atuambie Serikali inatueleza ni lini mkandarasi mwingine atapatikana kwa sababu mkandarasi huyu aliyekuwepo tunaambiwa hawezi kuomba tena kazi hiyo ya kuendeleza shughuli hiyo ya REA Awamu ya Pili, atapatikana mkandarasi mwingine na kumalizia shughuli hiyo ili wananchi wa Jimbo la Singida Kaskazini waendelee nao kunufaika na nishati ya umeme? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu swali hili la nyongeza la Mheshimiwa Monko. Na mimi niungane na Waheshimiwa Wabunge wengine kuendelea kumpongeza Mheshimiwa Monko kwa kuaminiwa na wananchi wa Jimbo la Singida Kaskazini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tumepata kusema ndani ya Bunge, na tumeweza kuwapa pole wananchi wa Mikoa ya Singida na Kilimanjaro baada ya kutokea matatizo ambayo hayakutarajiwa ya mkandarasi SPENCON ambaye kwa kweli alifanya kazi kama asilima 65 na akashindwa kumalizia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyopata kusema pia, Serikali kwa kuliona hilo ikachukua hatua stahiki kupitia Wakala wa Umeme Vijijini na kuanza harakati za kutafuta mkandarasi mpya kwa ajili ya kumalizia kazi zilizosalia katika Jimbo la Singida Kaskazini pamoja na majimbo mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mchakato huu ambao umefanyika na Wakala wa Umeme Vijijini tumefanikiwa kumpata mkandarasi katika Mkoa wa Kilimanjaro ambaye ameshaanza kazi na mimi nimejiridhisha, nilienda nikamuona, lakini katika Mkoa wa Singida mchakato unaendelea kwa sasa kwa wakandarasi wale watarajiwa kuwasilisha performance bond na baada ya hapo mkataba wa awali ambao wameuwasilisha kwenye Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa mapitio na tunatarajia mwezi Machi mwaka huu kazi zianze.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, na baada ya kikao hiki cha Bunge lako tukufu naomba tuonane naye kwa ajili ya kumweleza kazi zitakazofanyika na vijiji ambavyo vitafikiwa ili aweze kuwaambia wananchi wake. Nakushukuru. (Makofi)
MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini mahitaji ya umeme katika maeneo mengi hasa katika Vitongoji vya Halmashauri ya Jimbo la Chalinze imekuwa ni muhimu sana. Kwa mfano, kule Msinune, Kiwangwa bado umeme haujafika na ahadi ya Serikali ni kwamba umeme hautaruka Kitongoji chochote.
Je, Serikali imejipangaje katika kuhakikisha kwamba inawapelekea umeme wananchi wanaoishi katika vitongoji hivyo vikiwemo vile ambavyo vipo katika Kata ya Vigwaza na Mbwewe na maeneo mengine ya Halmashauri yetu? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza nami niwe mmoja wa kumtakia heri katika siku yake ya kuzaliwa Mbunge wetu wa Chalinze, Mheshimiwa Ridhiwani Jakaya Kikwete.
Mheshimiwa Ridhiwani atakumbuka kwamba mwezi wa Kumi na Mbili tulifanya ziara pamoja naye na Waheshimiwa Wabunge wengine wa Mkoa wa Pwani kwenye majimbo yao; tulipita katika maeneo ya Kata ya Kiwangwa, Msinune na Bago na Mheshimiwa Mbunge atakumbuka pia tuna mradi wa densification unaoendelea kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Chalinze.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, maeneo ambayo ameyataja ya Msinune na Bago ni maeneo ambayo yapo katika mradi wa REA Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza. Kwa hiyo, nimthibitishie Mhesimiwa Mbunge Serikali ya Awamu ya Tano kwa kweli kupitia miradi yake hii inayoendelea itapeleka umeme katika vitongoji mbalimbali ambavyo vina changamoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana kwa kazi yake ya kufuatilia hasa upatikanaji wa nishati ya umeme Jimboni Chalinze. Ahsante. (Makofi)
MHE. SILVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Rais na Serikali yake kwa miradi mikubwa ya maendeleo inayoendelea ikiwa ni pamoja na hii ya umeme, pia Waheshimiwa Mawaziri kwa kazi kubwa wanayofanya kufuatilia miradi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo la kulipa fidia ni kuwawezesha wananchi wanaoathirika na miradi hii mikubwa ya maendeleo ili waweze kupata fedha za kuweza kufanya shughuli nyingine mbadala za kiuchumi wanapopisha maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, fidia zimekuwa zikichelewa sana, wakati mwingine takribani mpaka miaka mitano huku wananchi hawa wakitaabika bila kuweza kufanya shughuli mbadala.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali mawili ya nyongeza. nafahamu uhakiki wa tathmini na hususan katika maeneo ya Kibaha Mjini, Vijijini na mpaka Chalinze ulikwishakamilika toka 2017.

MHE. SILVESTRY F. KOKA: Je, ni lini sasa kwa uhakika wananchi hawa watalipwa fedha zao?
Swali la pili, Serikali sasa haioni kwamba kuna haja ya kufanya maandalizi ya malipo haya mapema ili tathmini ikishafanyika wananchi waweze kupata malipo yao mapema bila kupata usumbufu na malalamiko makubwa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, Koka. Kwanza napenda kumshukuru sana na kumpongeza kwa namna ambavyo amekuwa akifuatilia miradi yetu kwenye sekta ya nishati na hususan katika suala hili la fidia kwa mradi huu wa Kinyerezi hadi Arusha, pia tumepokea pongezi zake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kumthibitishia Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo swali letu la msingi limesema kwamba fidia hii ya shilingi bilioni 21.56 zimetengwa kwa mwaka huu wa fedha 2017/2018. Ni matarajio yetu kwa kuwa uhakiki wa fidia hii umekamilika na matarajio yetu kwamba mwisho wa mwaka huu wa fedha, pesa hizi zitalipwa na naomba niendelee kuwashukuru wananchi wa maeneo ya Kisarawe, Kinyerezi yenyewe, Kibaha, Chalinze kwa uvumilivu wao. Napenda niwathibitishie Serikali italipa fidia hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili; tunapokea huo ushauri na Serikali ya Awamu ya Tano kwa kweli nia ni hiyo ya kuona kwamba maeneo wanayochukua kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mikubwa, wananchi wanawezeshwa. Ndiyo maana wakati wa bajeti tutaomba atuunge mkono. Tumetenga kabisa kiwango kikubwa tu cha fidia kwa miradi mikubwa ambayo inatarajiwa kutekelezwa kwa mwaka wa fedha huo 2018/2019 na kuendelea. Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa umeme wa 400KV ni mkubwa sana na unahitaji transfoma zenye ubora wa hali ya juu. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kutumia transfoma zetu za kiwanda cha TANELEC cha Arusha ambazo zina ubora wa hali ya juu?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa na ninamshukuru sana Mheshimiwa Catherine na ninampongeza pia kwa kufuatilia masuala ya nishati akiwa pia ni Mjumbe wetu wa Kamati ya Nishati na Madini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba umeme unaosafirishwa kwa njia hii ya msongo wa 400KV ni mkubwa na kwa kuwa ni mkubwa, Wizara yetu ya Nishati ilishatoa maelekezo kwamba kuanzia sasa vifaa vyote vinavyotumika kwenye miradi ya umeme vinatakiwa kutoka kwenye viwanda vyetu vya ndani na kimojawapo ni Kiwanda na TANALEC-Arusha. Mara kadhaa takribani kama zaidi ya mara mbili Mheshimiwa Waziri amefanya ziara katika kiwanda kile. Kiwanda hicho kina uwezo wa kuzalisha transfoma kama 10,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niendelee kutoa wito kwa Wakandarasi wote wanaotekeleza miradi ya umeme nchini pamoja na Shirika la umeme, TANESCO kwamba bado agizo letu liko pale pale, vifaa vyote vitoke ndani ya nchi na viwanda vyetu vina uwezo na mara kadhaa tumekutana navyo na vimetuthibitishia. Ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza; wakati wa upanuzi wa Kiwanda cha Umeme cha Liwale wakati wanapanua ile plant yao, walichukua mashamba ya wananchi ambapo mpaka leo hii zaidi ya miaka mitano wananchi wale hawajui hatima ya malipo yao. Nini kauli ya Serikali namna ya kuwalipa wale wananchi mashamba yao?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Namshukuru Mheshimiwa Kuchauka kwa swali la nyongeza na ninampongeza pia kwa kazi zake, lakini nataka niseme kwamba suala la fidia kwa mashamba ambayo yamechukuliwa kwa upanuzi wa kituo cha kuzalisha umeme Liwale, naomba kwa kuwa kwa takwimu kwa sasa hivi sina, naomba nilichukue.
Naomba tu nimpe Mheshimiwa Mbunge taarifa ya nyongeza kwamba kwa sasa kutokana na kukamilika kwa ujenzi wa laini ya msongo wa Kv 132 inayotoka Kituo cha Kuzalisha Umeme Mozambique, nataka nimthibitishie na jitihada ambazo zinaendelea za Wizara kuhakikisha Mikoa ya Kusini, Lindi na Mtwara inapata umeme kutoka Gridi ya Taifa kwamba kwa hivi karibuni Wilaya ya Liwale itapata umeme kupitia kituo hicho na kwamba hata yale matumizi ya mafuta ya kuzalishia umeme Wilaya ya Liwale yatapungua na umeme utapatikana kwa uhakika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la fidia nitalichukua, baada ya Bunge hili tutalifanyia mchakato wa kupata taarifa ya uhakika. Ahsante. (Makofi)
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Kwanza napenda nipongeze majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri pamoja na kazi inayofanywa na Wizara hii ya Nishati katika kuwapatia umeme Watanzania. Hata hivyo, nina maswali madogo mawili:
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; pamoja na jitihada hizi kuna vijiji 10 vimesahaulika, Vijiji hivi ni kama Mwamigongwa, Rwangwe, Ilumya, Igabulilo, Mwamalole, Mwabayanda, tayari tulishaongea na Wizara kwamba kuna vijiji ambavyo katika mzunguko huu vimerudiwa kutajwa majina tena, tukasema wafanye substitution; Je, Wizara inalifanyaje suala hili ili kusudi vijiji hivi ambavyo vimerudiwa visirudiwe tena na ambavyo havina umeme viweze kupatiwa umeme? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa umeme unasambazwa na moja ya agizo ni kwamba Taasisi za Serikali ziweze kupata umeme huu ikiwemo zahanati, shule na kadhalika na kuna baadhi ya maeneo ambayo umeme hu unasambazwa kwa mitaa michache. Je, nini kauli ya Serikali kuhakikisha kwamba umeme unasambazwa kulingana na mahitaji ya watumiaji? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa. Kwanza nimpongeze sana kwa kazi nzuri ya kufuatilia miradi ya nishati katika Jimbo lake, lakini la pili amevitaja vijiji kumi ambavyo kwa maelezo yake vimesahaulika na ameunganisha hapo na vijiji ambavyo vimetajwa kwenye REA Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza ambapo inaonekana vina miundombinu ya umeme.
Mheshimiwa Spika, msimamo wetu wa Wizara ni kwamba vijiji vyote vyenye miundombinu ya umeme ambavyo vipo kwenye Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza vifanyiwe marekebisho na vijiji ambavyo havina miundombinu ya umeme. Kwa kuwa, amevitaja vijiji vyake kumi na kwa kuwa ameshafanya mawasiliano na Wizara na REA kwamba nia ya mradi huu wa Awamu ya Tatu ni kupeleka umeme kwenye maeneo ambayo hakuna miundombinu. Kwa hiyo, nataka niwaelekeze REA kwamba wafanye substitution kwa sababu ni jambo la kawaida na tumekuwa tukifanya katika maeneo mengine.
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, ametaka tamko la Serikali juu ya maeneo ya Taasisi za Umma, ni kweli tumetoa tamko, tulitazama upungufu wa REA awamu zilizopita kwamba Taasisi nyingi za umma ikiwemo miradi ya maji, ikiwemo zahanati, vituo vya afya zilirukwa. Kwa hiyo, mradi wa REA Awamu ya Tatu tuliona tusirejee changamoto za REA awamu zilizopita.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naendelea kusisitiza agizo la Wizara na Serikali kwamba maeneo ya Taasisi za Umma yapatiwe vipaumbele katika kupeleka miundombinu ya umeme. Naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo hili la Busega na maeneo yote kwamba hilo ndiyo tamko la Serikali ya Awamu ya Tano. Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)
MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Wizara. Nikiri kweli kuwa wamefanya kazi nzuri ila katika haya majibu kuna Kijiji cha Mbuyuni bado hakijapata umeme pamoja na kuwa kimeorodheshwa kuwa kimo kwenye orodha ya vilivyopatiwa umeme.
Mheshimiwa Spika, tatizo lingine ni umeme uliokwenda Idunde umeruka Vijiji vya Rukwa na Kapalala; Je, ni lini Serikali itahakikisha hivi vijiji vilivyobaki vya Kapalala, Mbuyuni na Rukwa vitapatiwa umeme ikiwa ni pamoja na vijiji vya Kata ya Ikukwa ambayo ni karibu sana na Jimbo la Songwe navyo vitapatiwa umeme?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, nakiri kuwa Serikali imefanya kazi nzuri ya kupeleka umeme vijijini, lakini kwa mazingira ya vijijini wanahitaji vilevile huduma kutoka TANESCO; Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kuwa kutakuwa na huduma kwa wateja ambazo zitakuwa karibu huko vijijini ili waweze kupata huduma pamoja na hii huduma nzuri iliyofanyika kwa mpango wa REA? Mheshimiwa Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na namshukuru sana Mheshimiwa Njeza kwa maswali yake mawili ya nyongeza. Nampongeza pia kwa kazi nzuri kwenye Jimbo lake.
Mheshimiwa Spika, katika maswali yake la kwanza amejielekeza kwenye Kijiji cha Mbuyuni ambacho anasema kiko kwenye orodha ya vijiji vyenye umeme, lakini pia hakina umeme. Naomba hili nilichukue ili tuweze kufuatilia takwimu hii na nitampa majibu ya uhakika.
Mheshimiwa Spika, pia, katika swali lake hilo alielekeza vijiji ambavyo vimerukwa ikiwemo vijiji vya Kata ya Ikukwe. Naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi vijiji vyote vilivyosalia 7,873 nchi nzima vitapata miundombinu ya umeme kwa mizunguko. Mzunguko wa kwanza na mzunguko wa pili.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, vile 3,559 vya mzunguko wa kwanza kazi inaendelea mpaka Julai, 2019 kisha tunaanza mradi wa REA awamu ya tatu mzunguko wa pili. Kwa hiyo naomba nimthibitishe Mbunge maeneo ambayo yaliyosalia yatapatiwa miundombinu ya umeme kupitia REA awamu ya tatu mzunguko wa pili.
Mheshimiwa Spika, ameuliza suala la namna gani wananchi wa maeneo ya vijijini watapata huduma ya TANESCO. Naomba nilithibitishie Bunge lako Tukufu kuwa, kazi ya kupeleka miundombinu ya umeme inahusu vijiji vyote na tunatambua baadhi ya vijiji viko mbali na ofisi zetu za TANESCO ambazo ziko kila Wilaya, tumeielekeza TANESCO kufungua ofisi ndogo ndogo kwenye miji mikubwa na miji ambayo iko karibu na maeneo ya vijijini.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nikuthibitishie hilo linafanyika na tumeshapokea orodha ya ofisi za TANESCO ndogondogo mpya ambazo zingine zitajengwa lakini pia tumeomba pale ambapo, maana yake ujenzi ni suala la muda mrefu, lakini pale ambapo kuna maeneo ya vijiji kwenye Kata kuna Ofisi za Watendaji wa Kata, basi kipindi ambacho wataanza kuunganisha wateja tumeomba TANESCO waende kutumia hizo ofisi kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi wetu na nia ni kurahisisha utoaji wa huduma hizi kwa wananchi wa vijijini. Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)
MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, Mheshimiwa Naibu Waziri katika majibu yake anasema kwamba REA Awamu ya Tatu lengo lake kubwa ni kupeleka umeme katika vijiji ambavyo havina miundombinu ya umeme, lakini kosa lile lile lililofanyika katika REA I na II, kuruka Vitongoji na Vijiji tumeliona tena katika REA hii ambayo inatekelezwa. Kwa mfano, sasa hivi kimepewa Kijiji cha Bagilo ambapo vimerukwa Vijiji vya Hewe, Mgozo na Tegetero, lakini pia...
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kijiji cha Kidunda kimepewa, vimerukwa vijiji vya Mkulazi na Chanyumbu; je, Serikali ina mpango gani wa kuvipatia vijiji hivyo ambavyo vimerukwa katika REA III ili tusirudie kosa lile la REA I na II?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba mradi huu umeanza. Ni kweli umeanza, lakini mkandarasi huyu ana miezi sita sasa tangu alipokuja kufanya tathmini tu, hajarudi site mpaka leo. Baada ya kumfuatilia inaonekana kwamba hajapewa advance wala letter of credit ya kuanza kazi. Katika majibu yake Mheshimiwa Naibu Waziri anasema mradi huu unatakiwa ukamilike Julai, 2019, mpaka leo kazi haijaanza. Je, ni lini Serikali itaweza kutoa letter of credit kwa mkandarasi huyu ili aweze kuanza kupata vifaa na vitendea kazi ili aweze kuanza mradi na kutekeleza ndani ya wakati? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza lazima nimpongeze Mheshimiwa Mgumba kwa kazi anayoifanya. Ndani ya kipindi kifupi amkeshauliza zaidi ya maswali manne ya Sekta ya Nishati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza alijielekeza kwenye changamoto zilizojitokeza katika REA ya I na REA II ya urukwaji wa vijiji. Naomba nikiri kweli changamoto hiyo ilikuwepo, lakini pia naomba niseme kupitia mradi huu wa REA Awamu ya Tatu, baada ya kupokea maombi mbalimbali ya Waheshimiwa Wabunge, awali mpango ulikuwa ni vijiji 3,559 lakini baada ya kupokea malalamiko ya kurukwa kwa vijiji, vitongoji na taasisi za umma tumefanya tathmini nyingine na upembuzi yakinifu, tumepata vijiji kama 1,541 ambavyo vinatakiwa viongezeke awamu hii tunapoendelea kutekeleza mzunguko huu wa kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge vijiji alivyovitaja ni miongoni mwa vijiji 1,541 ambavyo vitaongezeka kwenye vijiji 3,559 na vitakuwa vijiji 5,100 kwa awamu ya kwanza ambavyo vitapelekewa miundombinu ya umeme. Pamoja na kwamba nakiri, lakini gharama zitaongezeka. Pia kwa kuwa kazi ya Bunge hili ni kuidhinisha bajeti kwa miradi hiyo na uhitaji unaonekana ni mkubwa, sina mashaka kwamba Bunge litatimiza wajibu wake na kwamba vijiji ambayo tumeviona lazima viongezeke ili kutimiza lengo ambalo limekusudiwa kwamba tusirudie makosa ya awamu nyingine, litatimia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, amejielekeza kwamba ni kweli Mkandarasi wa Mkoa huu wa Morogoro, State Grid alifanya tathmini na kwamba hajalipwa advance. Nataka niseme wakati wa malipo ya advance kulikuwa na masharti na sharti mojawapo lilikuwa malipo lazima wa-submit performance bond. Bahati mbaya mkandarasi huyu haku-submit kwa wakati, lakini nakiri mpaka sasa hivi Wakandarasi wote wamesha-submit, utaratibu wa malipo unaendelea kwenye Wizara ya Fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, utaratibu wa ufunguaji wa letter of credit, tunashukuru tumepokea barua wiki iliyopita kwamba sasa tunaweza tukaendelea na utaratibu huo. Kwa hiyo, tunajipanga pamoja na Wakala wa Nishati Vijijini ili kuifanya kazi hiyo kwa haraka na miradi hii itekelezeke kwa haraka. Ahsante. (Makofi)
MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza na mimi nipongeze Wizara kwa speed nzuri wanayochukua ya kusambaza umeme vijijini. Hata hivyo nina suala moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maeneo ambayo Mheshimiwa Wazairi ametueleza pia kuna taasisi za Serikali ambazo Mheshimiwa Waziri hakuzitaja. Je, nini mikakati ya kuziunganishia taasisi za Serikali, umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa. Kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Hija kwa pongezi zake kwenye swali lake; la nyongeza ameuliza mkakati wa Serikali wakusambazia umeme taasisi za Kiserikali. Kama nilivyosema kwenye jibu langu la mzingi katika utekelezaji wa REA I na II kulikuwa na mapungufu ya kuruka baadhi ya maeneo na hususani Taasisi za Kiserikali utekelezaji wa REA III kama Serikali tumetoa maelekezo kwamba taasisi zote za Serikali zipatiwe kipaumbele na napenda kuwashukuru wakandarasi wote wamekuwa wakitekeleza maelekezo haya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo napenda nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwa sasa kwa makandarasi wameendelea kuunganisha maeneo ya Kiserikali iwe ya zahanati, miradi ya maji, vituo vya afya na hospitali. Nakushukuru.
MHE. ZAINABU M. AMIRI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kutokana na kugundulika kwa gesi nchini mwetu, je, ni lini Serikali itasitisha uingizaji wa gesi ili tuweze kutumia gesi yetu hapa nchini?
(Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, pilot project iliyofanyika ni Mikocheni Dar es Salaam, je, ni vigezo gani vimezingatiwa katika project hiyo na isiwe kule ilikotoka gesi Mtwara? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zainabu Mndolwa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza ameuliza ni lini Serikali itasitisha uagizaji wa gesi kutoka nje ya nchi. Ni kweli ugunduzi wa gesi asilia iliyogunduliwa hapa nchini ni gesi zaidi ya mita za ujazo trilioni 55,000. Nataka nimwambie Mheshimiwa Mbunge matumizi ya gesi yapo mengi kama nilivyoeleza kwenye swali la msingi ikiwemo kwenye uzalishaji wa umeme, matumizi ya viwanda na matumizi ya majumbani.
Mheshimiwa Spika, sasa hivi kuna mipango mbalimbali ambayo inafanywa na Serikali ikiwemo pia ujenzi wa kiwanda cha kusindika gesi asilia Mkoani Lindi. Kwa hiyo, baada ya kiwanda hiki kukamilika na hizi fursa mbalimbali za usambazaji gesi na miundombinu mbalimbali ya kusambaza gesi kwa ajili ya matumizi ya majumbani na viwandani itakapokamilika, Serikali itatafakari kwa kina namna ambavyo inaweza kusitisha uagizaji wa gesi hiyo nchini. Kwa sasa bado tuna mahitaji na kwa kuwa mipango inaendelea, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itatafakari na kuchukua hatua pale ambapo tutakuwa tumejiridhisha na soko na uhitaji wa gesi asilia ndani ya nchi na kwa matumizi ya nchi. (Makofi)
Mheshimwia Spika, swali lake la pili alikuwa anauliza kuhusu vigezo vilivyotumika kwa maeneo ya kusambaza gesi kwa matumizi ya majumbani na ameuainisha Mkoa wa Mtwara. Nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kuna miradi na tafiti zinazoendelea katika Mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Morogoro, Dodoma, Mwanza na Tanga chini ya Mradi wa JICA ili kuona mahitaji ya matumizi ya gesi ya kupikia ili kuanza mradi wa usambazaji wa gesi katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Spika, nimthibitishie katika Mkoa wa Mtwara kwa mwaka huu wa fedha kiasi cha shilingi milioni 140 zimetengwa kuendelea na study hiyo na kwamba mkoa huo utapatiwa usambazaji wa gesi kwa matumizi ya nyumbani. Nakushukuru.
MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, kufuatia ugunduzi wa gesi, Serikali ya CCM iliwahakikishia Watanzania na wananchi wa Mtwara kwamba maisha yetu kwa kiwango kikubwa yatabadilika. Ikumbukwe kwamba bomba la gesi lilijengwa kwa mkopo usiopungua shilingi trilioni 1.5 kwenda shilingi trilioni 2. Hivi tunavyozungumza na kwa taarifa za Serikali inaonesha kwamba tunatumia asilimia 5 tu ya gesi katika bomba husika. Nataka tu Serikali ituambie, Deni la Taifa linakua, tulikopa tukajenga bomba tukajua kwamba tunapata suluhu lakini sasa hivi tunatumia bomba asilimia 5, ni nini kimetokea hapo katikati kilichopelekea kushindwa kulitumia kwa asilimia 95 ? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tunaambiwa tena kuna mpango Stigler’s Gorge wa kuzalisha umeme. Sasa mtuambie bomba la gesi limekwamia wapi katika uzalishaji wa umeme na hii Stiegler’s Gorge inaanzia wapi ili kama Taifa tuwe na taarifa, maana tunaona tunapelekwapelekwa tu. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu swali la Mheshimiwa Halima Mdee, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali ilitekeleza mradi mkubwa huu wa ujenzi wa bomba la gesi la Mkoa wa Mtwara. Kama alivyoeleza kwenye swali lake, kwa sasa matumizi ya kusafirisha gesi kwa kupitia bomba hili kwa mwaka huu unaoendelea imefika lita za ujazo milioni 175 kutoka milioni 145 za mwaka 2016/2017, ni wazi ongezeko linatokana na mahitaji makubwa.
Mheshimiwa Spika, naomba nimthibitishie tulipokuwa tunajenga bomba hili na ahadi tulizotoa kwa wana Mtwara, ahadi zile ni sahihi kwa sababu kuna miradi mbalimbali ambayo inayoendelea. Kwa mfano, Mtwara peke yake tunajega mradi wa kuzalisha umeme wa megawatts 300 kwa kutumia gesi asilia ya Mkoa wa Mtwara. Sambamba na hilo, pia kuna mpango wa kujenga mradi wa kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia Somanga Fungu, kwa kuzalisha megawatts 330 kwa kutumia gesi hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nchi yoyote lazima izalishe umeme kwa vyanzo mbalimbali, huwezi kutumia gesi asilia peke yake ukatosheleza mahitaji ya nchi nzima. Ndiyo maana tunazalisha umeme kwa kutumia maji na gesi. Sasa hivi zaidi ya asilimia ya 50 megawatts zinazozalishwa zinatumia gesi. Kwa hiyo, ni wazi kwamba gesi ambayo iligundulika Mtwara imeleta tija katika uzalishaji wa umeme. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini kama tunavyofahamu umuhimu wa kuzalisha umeme kwa kutumia vyanzo vingine, Serikali imetafakari, kwa sababu lengo la Serikali ni kuzalisha umeme wa bei nafuu na kumfikia mtumiaji kwa bei nafuu. Ndiyo maana Serikali imekuja na mradi wa Stiegler’s Gorge utakaozalisha megawatts 2,100. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nimewahi kusema ndani ya Bunge lako Tukufu kwamba uzalishaji wa umeme kwa kutumia maji una unafuu zaidi, unatumia shilingi 36 ukilinganisha na gesi ambayo ni shilingi 147. Kwa nchi inayotarajiwa kujenga viwanda nchi nzima na kazi inayoendelea lazima tuzalishe umeme kwa wingi. Kwa kuwa lengo la Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli ni kuzalisha megawatts 5,000 mradi wa Stiegler’s Gorge ndiyo wakati wake muafaka. Mheshimiwa Spika, nashukuru. (Makofi)
MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri yenye kutia moyo wananchi wa Jimbo la Manyoni Magharibi, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kijiji cha Kalangali kimepitiwa na umeme ukaenda kutua kijiji cha pili cha Mkoa wa Tabora, Kijiji cha Kipili. Wananchi wa Kalangali wanasononeka sana na kupitwa na umeme huu. Je, sasa Wizara hii iko tayari kuingiza kijiji hiki katika mzunguko huu wa kwanza, Awamu ya Tatu ya REA?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Waziri wa Wizara hii alipokuwa Naibu Waziri alikuja Itigi na alifanya mkutano mzuri sana na wananchi. Sasa yuko tayari kwenda kufanya mkutano na wananchi wa Rungwa kuwahakikishia kwamba Awamu ya Tatu mzunguko wa pili umeme utaenda hadi Rungwa?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza lilihusu Kijiji cha Kalangali ambapo kwa maelezo yake kijiji hiki kimepitiwa na miundombinu ya umeme ambayo imeelekea Mkoa wa Tabora na wananchi wa kijiji hiki hawajapa umeme huo.
Napenda nikubali maelezo ya Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kuwa kuna maelekezo ya Serikali maeneo yote yaliyopitiwa na miundombinu ya umeme mkubwa na ambayo hayajapata umeme yapatiwe. Kwa kuwa kazi katika kijiji hiki ni kushusha transfoma na kuwaunganisha wateja, napenda nimthibitishie nitatoa maelekezo kwa mkandarasi na REAwafanyie kazi kijiji hiki na kipatiwe umeme katika awamu hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ombi la Mheshimiwa Waziri kufanya ziara katika Wilaya ya Itigi, Kijiji cha Rungwa, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ombi hilo limekubaliwa na ziara itafanyika kama ilivyo utaratibu wetu kutembelea maeneo mbalimbali. Ahsante.
MHE. ISSA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Waziri na Mheshimiwa Naibu Waziri kwa ushirikiano walioutoa kwa wananchi wa Mbagala mpaka mradi huu kukamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa kuwa baada ya kukamilika substation ya Mbagala, Mbagala ni eneo ambalo lina viwanda; je, wana mkakati gani sasa kuvishawishi viwanda vilivyopo Mbagala kutumia gesi asilia ili kupunguza low voltage ambayo tunaipata kutokana na matumizi ya viwanda vile?
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itafanya eneo la Mbagala (District) kuwa Mkoa kwa sababu ina wateja wengi na TANESCO imeelemewa kule Mbagala kiasi kwamba inashindwa kupaleka umeme katika maeneo ya Toangoma, Vigozi, Mponda na maeneo mengine?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri tumepokea pongezi zake, nasi kwa kweli tunamshukuru sana kwa ushirikiano alioufanya kwa kipindi chote cha utekelezaji wa mradi huu Jimboni kwake Mbagala.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge ameeleza mkakati wa Serikali wa kuvishawishi viwanda kutumia gesi asilia. Naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge Wizara yetu kupitia TPDC tuna mkakati wa kusambaza gesi asilia kwa matumizi ya viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata kwa mwaka huu wa fedha ambao utaanza 2018/2019 TPDC imeshaingia makubaliano ya awali ya kusambaza gesi katika maeneo mbalimbali ya viwanda yaliyopo Mkuranga, kwa mfano Kiwanda cha Bakhressa, Loth Steel cha Mkuranga na pia hata Kiwanda cha Biku na Cocacola Kwanza, Dar es Salaam.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, wazo lake hilo linafanyiwa kazi na viwanda tunavihamasisha vitumie gesi kwa sababu gesi ipo na ya kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, ameuliza ni lini tutaifanya Mbagala kuwa Mkoa? Naomba nilichukue hili suala na linajadilika ndani ya Wizara, tunaweza tukalifanyia kazi. Ni kweli Mbagala ina wateja na watumiaji wengi wa umeme. Naomba hili tulichukue. Ahsante. (Makofi)
MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Singida Kaskazini lina Kata 21 na Vijiji 84. Kata za Muhunga, Ngimu, Itaja, Makulo na Ughandi hazina kijiji hata kimoja ambacho kimepitiwa na miradi ya umeme wa REA II na REA III. Je, ni lini wananchi hawa watapata fursa hiyo ya kupata umeme ambao ni muhimu sana katika shughuli za maendeleo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mradi wa REA Awamu ya Tatu ambao umeshaanza sasa yapo maeneo ya wananchi ambayo tayari wameshajiandaa pamoja na taasisi ambayo yanarukwa na umeme, katika mpango wa upatikanaji wa umeme huu ambao unaendelea sasa. Serikali ina kauli gani kwa wananchi katika maeneo hayo ambayo tayari wameusubiri umeme huu kwa muda mrefu na wako karibu na njia za umeme? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Napenda nimpongeze sana Mheshimiwa Monko, ni Mbunge mgeni lakini kwa kipindi kifupi cha kuchaguliwa kwake amefanya kazi kubwa ya kufuatilia miradi ya nishati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kiti chako pia kimekuwa kikiagiza mara kwa mara kupitia Mheshimiwa Spika na Waheshimiwa Wenyeviti na Naibu Spika, naomba niliarifu Bunge lako tukufu kwa miradi yote ya REA kwa ujumla yake, kulikuwa na agizo la kufuatilia ufunguaji wa Letter of Credit.
Naomba niliarifu Bunge lako tukufu na niishukuru Kamati ya Bajeti, Wizara ya Fedha na Benki Kuu na nikutaarifu kwamba mpaka sasa Wizara ya Nishati kupitia REA tumefanikiwa kufungua Letter of Credit kwa makampuni 14 yenye jumla ya shilingi bilioni 220. Hii maana yake nini? Maana yake ni kwamba kuanzia sasa utekelezaji wa miradi ya REA Awamu ya Tatu itapata kasi kubwa. Niwathibitishie Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote kwamba wategemee sasa miradi kushika kasi kubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nijielekeze kwa maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, swali lake la kwanza ametaja Kata kadhaa ambazo amesema amesema hakuna hata Kijiji kimoja ambacho kina umeme katika REA zote zilizopita mpaka sasa. Nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kweli kwa mradi huu unaoendelea wa REA awamu ya tatu, mzunguko wa kwanza na mzunguko wa pili yatafikiwa maeneo yote. Kwa hiyo, maeneo na kata ambazo amezitaja zitapatiwa umeme katika mzunguko wa pili utakaoanza Julai, 2019 na kukamilisha Juni, 2021. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, katika maeneo ambayo Mradi wa REA umeanza, Mheshimiwa Mbunge amesema zipo taasisi za umma zimerukwa na yapo maeneo ambayo wananchi wamepitiwa na umeme mkubwa lakini hawana dalili za kupata umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara ya Nishati imetoa maelekezo kwa wakandarasi wote nchi nzima. Hapa namwomba mkandarasi wa Mkoa wa Singida na wakandarasi wote; na kama nilivyosema sasa mambo ni mazuri, wahakikishe kazi inakwenda kwa mujibu wa scope na yale maeneo ambayo yameainishwa yapate huduma hii. Ahsante. (Makofi)
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, maeneo mengi nguzo zimeshapelekwa katika vijiji hususani Mkoa wangu wa Manyara, kinachokosekana ni zile conductor na nyaya kwa ajili ya kuunganisha zile nguzo na umeme uwake na Mkandarasi wetu wa Mkoa wa Manyara ameagiza hizo conductors na nyaya muda mrefu viwandani na hili halijafanyika huenda hili tatizo lipo maeneo mengine. Naomba nifahamu ni lini sasa hizo conductors na nyaya zitatoka ili umeme uwake kwenye maeneo na vijiji vyetu ambavyo nguzo zimeshafikishwa?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, naomba nitambue jitihada kubwa ambazo zimefanywa na Wizara hii, wamelipa shilingi milioni 102 kwa fidia ya wananchi wa Haraa kwa ajili ya umeme huu wa REA, Naibu Waziri anafahamu tulilishughulikia kwa karibu sana. Nitambue jitihada za KV400 ambazo zimefanyika na hivi navyoongea katika Mkoa wangu wa Manyara pale TANESCO Babati …
Mheshiwa Spika, ahsante. Jitihada hizi zinaendelea isipokuwa Mheshiwa Naibu Waziri kuna tatizo moja limejitokeza la variation kati ya Wizara ya Fedha na Wizara ya Nishati kwa baadhi ya wananchi ambao wanadai fidia hii ya KV400. Naomba nifahamu, hili tatizo la variation na reconciliation kujua hawa wanastahili kiasi gani linamalizwa lini kabla hawajaondoka Babati waweze kupata fedha hizo? Mheshimiwa Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Pauline Gekul, Mbunge Babati Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kwanza kwa niaba ya Serikali tunapokea shukrani za Mheshimiwa Pauline kutokana na jitihada mbalimbali ambazo zimefanyika katika miradi hii ya REA. Amekiri na kutambua kwamba nguzo zimefika katika maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, kwenye suala la vifaa vya conductors na nyaya, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge ni kweli hivi vifaa kwa mfano conductors wanaagiza nje ya nchi, lakini kwa kuliona tatizo la ucheleweshaji ndiyo maana baadhi ya vifaa katika mradi huu tulitoa maelekezo viwanda vyetu vya ndani vizalishe na wakandarasi waagize. Kwa hiyo, suala hili la vifaa hususani nyaya, viwanda vinavyohusika ni ni East African Cable pamoja na Kilimanjaro Cable, jambo ambalo limejitokeza wakandarasi wengi wanapenda kuagiza kwa mtu mmoja.
Mheshimiwa Spika, tumetoa rai kwamba kwa kuwa Serikali ilivyotoa maagizo ya kuviwezesha viwanda vya ndani kusambaza vifaa vya utekelezaji wa miradi hii, wakandarasi wote waone namna gani ya ku-order hivi vifaa wasirundike order kwa mtu mmoja. Kwa hiyo, naomba nilichukue hili tuende tukashulighulikie kwa kuwa nguzo zimefika maeneo mengi, basi vifaa vilivyosalia vifike ili kazi ikamilike na wananchi wapate huduma ambayo imekusudiwa.
Mheshimmiwa Spika, swali lake la pili nami nimshukuru kwa kufuatilia malipo ya fidia kwa wananchi wake na maeneo mbalimbali hususani katika mradi huu wa ujenzi wa njia ya umeme KV400 unaotoka Singida mpaka Namanga. Katika Wilaya yake kama alivyosema Serikali imeanza kulipa fidia, niishukuru sana Wizara ya Fedha kwa kutekeleza ahadi hiyo lakini amesema kuna variation. Naomba baada ya kikao hiki tukutane naye Mheshimiwa Mbunge ili tuweze kushughulikia suala ambalo amelisema. Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Spika, pamoja na kusahisha jina la eneo la Kitungule badala ya Kitungule isomeke Kilungule.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Ali Mangungu anaishukuru sana Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa kazi kubwa iliyoifanya katika kipindi hiki cha mwaka mmoja na kwa kweli wanaomba yale maeneo yaliyobakia yakamilishwe, kwa hiyo, eneo la kwanza ni ombi.
Mheshimiwa Spika, pili, ndugu zao wa Namtumbo wanaomba kuna vijiji 70 na miji midogo miwili. Katika miji midogo miwili mji mdogo mmoja tu mitaa yake ina umeme, vinginevyo vijiji vyote 70 pamoja na mitaa ya Mji Mdogo wa Lusewa havina umeme. Pamoja na kwamba dalili zinaonekana lakini muda unapita na hakuna dalili ya umeme kupatikana katika Wilaya hiyo nzima ya Namtumbo.
Ni lini Serikali itawasha umeme katika Wilaya ya Namtumbo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, swali la kwanza tumepokea pongezi za Mheshimiwa Mbunge Mheshimiwa Issa Ali Mangungu na Serikali tunampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia maendeleo ya nishati katika Jimbo lake la Mbagala na ombi lake tumelipokea katika maeneo yaliyosalia kama nilivyosema mradi umekamilika kwa asilimia 90 basi asilimia 10 ndani ya muda mfupi itakamilika.
Swali lake la pili la ndugu wa kutoka Jimbo la Namtumbo. Kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema naomba nilitaarifu Bunge lako tukufu na niwapongeze Wabunge wote wa Mkoa wa Ruvuma na Mkoa wa Njombe kwa kuiunga mkono Serikali katika utekelezaji wa mradi mkubwa wa ujenzi wa line ya kusafirisha umeme Makambako - Songea yenye urefu kilometa 250. Napenda nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge tarehe 01 na tarehe 02 tulifanya ziara kukagua mradi huo na kimsingi mradi umekamilika.
Mheshimiwa Spika, ujenzi wa substation tatu Madaba, Songea - Makambako umekamilika, ujenzi wa line umekamilika, kinachoendelea sasa hivi ni usambazaji umeme katika maeneo ya vijiji 122, vijiji 60 ni Mkoa wa Ruvuma, na vilivyosalia ni Mkoa wa Njombe. Katika Jimbo lake la Namtumbo takribani vijiji 35 vitapata umeme kupitia mradi huu mkubwa wa ujenzi wa line ya Makambako - Songea.
Mheshimiwa Spika, naomba nilitaarifu Bunge lako mwezi huu Septemba tarehe 25 au 26 mradi huu utazindua rasmi na sasa hivi kinachoendelea ni test mbalimbali zinazoendelea katika line hii. Kuanzia tarehe 15 Septemba tutasafirisha umeme kwa mara ya kwanza kwenye Gridi ya Taifa kuelekea Songea Mkoa wa Ruvuma. Nawashukuru sana wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kwa kutuunga mkono na kwa kweli mambo mazuri. Ahsante sana.(Makofi)
MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, mahitaji ya umeme kwa Kyerwa ni makubwa sana, yako maeneo mengi ambayo hayafikiwa kabisa kama Kata ya Bugomola, Kibale, Businde na Bugara na maeneo mengine mengi hayajafikiwa. Ni kwa nini Wizara isiruhusu TANESCO, REA wanapomaliza kupitisha line kuu, Wizara isiruhusu TANESCO wakaanza kuwafungia umeme wananchi ambao wanahitaji umeme?
Swali la pili, REA Awamu ya Pili ambayo kwetu Kyerwa ni REA Awamu ya Kwanza kwa sababu ndipo umeme ulipopelekwa huyu Mkandarasi amesuasua sana mpaka sasa ameshindwa maeneo mengi, wako wananchi wengi ambao wamelipia mpaka sasa hawajafungiwa miaka miwili.
Je, ni hatua zipi zinachukuliwa kwa Mkandarasi huyu ambaye inaonekana ameshindwa kufanya kazi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bilakwate naye pia nimpongeze kwa namna ambavyo amefuatilia masuala la nishati katika Jimbo lake.
Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza lilijielekeza kwenye mahitaji ya umeme, kwa nini TANESCO isiendelee kuwaunganisha wananchi wa maeneo hayo wanaopenda umeme. Napenda nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba ni kweli katika Mkoa wa Kagera, Mkoa ambao pia ulikuwa haujaunganishwa kwenye gridi ya Taifa tumeunganisha Wilaya za Ngara mpaka Muleba na tunatarajia kukamilisha mpaka Bukoba Mjini.
Mheshimiwa Spika, kutokana na uunganishwaji wa gridi ya Taifa katika maeneo hayo kumejitokeza mahitaji na tumeendelea kuwapa maelekezo TANESCO kwamba inapotokea fursa siyo lazima kusubiri miradi ya REA Awamu ya Tatu. Kwa hiyo, kama kweli wapo wananchi wa Wilaya ya Kyerwa wanahitaji umeme na wao hoja siyo kusubiri umeme wa REA ambapo una bei nafuu wako tayari kulipia hata gharama za kuunganishwa umeme na TANESCO, naielekeza TANESCO ifanye upembuzi yakinifu na iwapelekee umeme wananchi hao kwasababu wao kwao umeme hawaangalii hoja kwamba ni wa REA au ni umeme kupitia TANESCO.
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, natambua Kata alizozitaja Mheshimiwa na ni kweli mpaka sasa hivi hazijasambaziwa umeme. Natambua uwepo wa Mkandarasi Makuroi katika Mkoa wa Kagera, lakini ni ukweli nakiri kwamba katika Wilaya zingine mkandarasi yule hajafanya vizuri, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tulimuita Makuroi kwa sababu anafanya pia na Mkoa wa Rukwa, na mimi nilipata fursa ya kutembelea Mkoa wa Rukwa nikaona ni namna gani anavyolegalega lakini kwa sasa ameshaagiza magari na nimeyathibitisha ana magari mengi tu ya kusambaza nguzo na tulithibisha order ambazo amezitoa katika viwanda mbalimbali vya nguzo vya Mkoa wa Iringa, kwa sasa hivi kwa kweli tumemuelekeza na wakandarasi wote wa miradi hii kwamba lazima kila Wilaya kuwe na genge lake na wasijielekeze sehemu moja.
Kwa hiyo, naomba nimthibitishe Mheshimiwa Mbunge baada ya jibu au baada ya kikao hiki tukutane ili tuendelee na mikakati yakuwasimamia wakandarasi wote. Ahsante.
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Spika, Jimbo la Tarime Mjini, Kata za Nkende, Kenyemanyori, Kitare, Nyamisangura na Turwa pamoja na Nyandoto hazina umeme kabisa, Bunge lililopita niliuliza swali kama hili na Naibu Waziri akaahidi atatembelea Tarime ili kuweza kuona wakandarasi wa REA ambao tangu mwaka 2016 walitakiwa watekeleze huu mradi, lakini mpaka leo ni Kata ya Nyandoto ndiyo tumeona sasa wameanza kufanyakazi.
Je, ni kwa nini Naibu Waziri hukuweza kutekeleza ile ahadi ambayo uliahidi kwa wana Tarime ili waweze kupata huu umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru kwa kutambua kwamba kazi imeanza ka Kata ya Nyandoto kama alivyoitaja, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kuwa ahadi yangu ya kutembelea Jimbo la Tarime Mjini na Mkoa wa Mara iko pale pale ila kutokana tu muingiliano wa ratiba, lakini kwa kuwa kazi zetu ziko site naomba nimthibitishie baada ya Bunge hili nitatembelea Wilaya hiyo ya Tarime na Wilaya zingine za Mkoa wa Mara kuhamasisha na kukagua miradi hii na kuwapa shime wakandarasi wafanyekazi kwa haraka na kama inavyokusudiwa. Ahsante.
MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Spika, nami naomba niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Kigoma tuko off grid, kuna mradi wetu mkubwa sana wa Malagarasi ambao tuliambiwa ungeanza quarter hii ya kwanza ya financial year hii. Ningependa kujua kutoka kwa Waziri ni lini mradi sasa wa Malagarasi mini-hydro utaanza ili tuanze kuwa na chanzo cha uhakika cha umeme katika Mkoa wa Kigoma?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Ameuliza ni lini mradi huu wa Malagarasi utaanza. Kama ambavyo tuliwasilisha kwenye bajeti yetu ya Bunge hili na ikaidhinishwa na Bunge lako tukufu kwamba mradi huu utaanza kwa mwaka huu wa fedha 2018/2019, lakini jambo kubwa hapa amelizungumzia kwamba Mkoa huu upo off grid, naomba nilitaarifu Bunge lako tukufu, hivi karibuni Benki ya Dunia imetoa pesa kwa ajili ya ujenzi wa line inayotoka Iringa – Mbeya - Sumbawanga lakini pia kipande cha Nyakanazi - Kigoma kimepata ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, kwa hiyo, kwa vyovyote vile Mkoa huu tunaanza kuingia kwenye gridi kutokana na miradi hiyo, wananchi wa Kigoma niwathibitishie kwamba kwa kweli Serikali ya Awamu ya Tano inafanyakazi kuhakikisha Mkoa huu unaingia kwenye Gridi ya Taifa. Ahsante. (Makofi)
MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na nitoe pongezi kwa mkandarasi ambaye amepangwa kwenye Jimbo langu la Mufindi Kusini kwa kazi nzuri anayoifanya. Tulikuwa tuna tatizo la transfoma pale Ihowanza baada ya kumpa taarifa nimepata taarifa kwamba ameshaipeleka na pale Mbalamaziwa tulikuwa tuna tatizo la transfoma ameshaipeleka na sasa hivi mkandarasi yupo site. Kwa kazi hiyo nzuri, naipongeza sana Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali langu la kwanza kuna vitongoji vingi sana kwenye Jimbo langu la Mufindi Kusini ambavyo havikufanyiwa survey na tulikuwa tumeandika hata majina tukapeleka pale TANESCO, je, vile vitongoji ambavyo vilikuwa vimerukwa mara ya kwanza na vyenyewe vitapewa umeme?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ningemuomba Waziri kama atapata nafasi kwa sababu kwenye Jimbo langu la Mufindi Kusini hawajaja, je, atakuja sasa kufanya mkutano akielezea vizuri matumizi haya ya umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tumepokea pongezi za Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo miradi ya REA III inavyoendelea katika Wilaya ya Mufindi hususani katika jimbo lake. Namshukuru kwa kulithibitishia Bunge lako kama mkandarasi yupo anaendelea vizuri na kweli mkandarasi Sengerema ni miongoni wa wakandarasi ambao wanafanya kazi zao vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia nimpongeze yeye mwenyewe Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia masuala ya nishati katika jimbo lake, anafanya kazi vizuri. Ndiyo maana katika maswali yake ya nyongeza amekiri kwamba kulikuwa na tatizo la transfoma kwenye kata alizozitaja na kutokana na maelekezo ya Mheshimiwa Waziri transfoma hizo zimeshafika katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake moja ameuliza ni lini vitongoji ambavyo havijafikiwa na umeme vitapata? Nataka nilitaarifu Bunge lako Tukufu na Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inaendelea kufanya upembuzi yakinifu kwenye Mradi wa densification II baada ya kufanikiwa kwa densification I, ambayo itahusisha mikoa 17 pamoja na Mkoa wa Iringa na katika vitongoji ambavyo vitasalia vitapatiwa umeme katika mradi wa ujazilizi awamu ya pili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu kutembelea katika Jimbo lake la Mufindi Kusini na hususan Wilaya ya Mufindi, nataka nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya Bunge hili kwa kweli tutatembelea Mkoa wa Iringa kwa sababu mpaka sasa hivi tuna vijiji takribani 20 vinatakiwa kuwashwa umeme lakini pia kuna mradi ambao unaendelea wa BTIP ambao kwa kweli umefanya vizuri. Hivyo, nataka nilitaarifu Bunge ipo kazi ya kufanya katika huo Mkoa wa Iringa na Jimbo lake la Mufindi Kusini, kwa hiyo, tutakuja. Ahsante sana.
MHE. TUNZA I. MALAPO: Pamoja na majibu hayo ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Kwa kuwa Serikali imekiri kwamba mitambo ni michakavu na ni kweli ni ya muda mrefu; je, imejipangaje kununua mitambo mipya ulizingatia kuna ongezeko kubwa la mahitaji ya umeme katika mikoa hiyo ya Lindi na Mtwara?
Swali la pili; ni lini Serikali itaunganisha mfumo wa gesi asilia ili uweze kutumika katika majumba ya Mkoa wa Lindi na Mtwara ukizingatia kwamba kule ndiko gesi inakozalishwa? Nakushukuru.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Mheshimiwa Tunza Malapo kwa kufuatilia masuala ya umeme katika Mkoa wa Mtwara. Kama nilivyojibu kwenye majibu yangu ya swali la msingi; kwanza, Serikali baada ya kuona uchakavu wa mitambo hii tisa ya Kituo cha Mtwara, imenunua mitambo miwili mipya. Hivi ninavyozungumza, kazi ya ufungaji wa mitambo hii inaendelea ambayo itazalisha megawati nne.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua Mikoa ya Mtwara na Lindi mahitaji yanaongezeka, Serikali imekuja na mpango wa kujenga mitambo mingine ya kuzalisha umeme megawati 300 kwa kutumia gesi na mpaka sasa Kampuni ya JICA imeendelea na upembuzi yakinifu. Kama ambavyo tumesema kwenye bajeti yetu mradi huu utaanza kutekelezwa mwaka 2018/2019.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimtoe wasi wasi Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeliona hilo na kwamba mradi huu mkubwa wa megawati 300 utatatua matatizo yote katika Mikoa hiyo ya Kusini na pia itaupeleka umeme katika Gridi ya Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ameeleza ni lini mpango wa kusambaza…
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Tunza ameulizia ni lini mpango wa kusambaza gesi asilia majumbani katika Mkoa wa Mtwara utaanza? Napenda nimthibitishe Mheshimiwa Mbunge kwamba kama ambavyo ameona hivi karibuni tumezindua mpango wa kusambaza gesi asilia katika Mkoa wa Dar es Salaam, lakini Mkoa wa Dar es Salaam unakwenda sambamba na Mikoa ya Mtwara na Lindi. Kwa hiyo, hii kazi itafanyika katika mwaka 2018/2019, tutasambaza gesi katika maeneo mbalimbali kwa matumizi ya majumbani kwa Mikoa hiyo. Ahsante.
MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la kukatika katika kwa umeme liko vilevile kwenye Jimbo la Kibamba kwenye Kata za Kibamba, Kwembe, Msigani, Mbezi, Saranga na Goba ambako kuna tatizo vilevile la kupungua kwa umeme (low voltage). Sasa ni hatua gani ambazo Serikali inachukua kuhakikisha kwamba hili tatizo la kukatika katika na kupungua kwa umeme linamalizika?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mnyika juu ya suala la kukatika katika kwa umeme kwa maeneo ya Jimbo lake la Kibamba pamoja na Kata alizozitaja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mnyika, Serikali kupitia Shirika la TANESCO lina mpango wa kujenga kituo kikubwa cha kupokea na kupoozea umeme maeneo ya Kibamba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo anafahamu katika Mkoa wa Dar es Salaam kulikuwa na ukarabati wa miundombinu ya umeme na ujenzi wa vituo mbalimbali hasa baada ya kuongezeka kwa mahitaji; na ilionekana ile njia ya msongo wa KV132 inayotoka Ubungo kupeleka umeme katika maeneo mbalimbali imezidiwa, hivyo baada ya kukamilika kwa vituo vya Gongo la Mboto, Kipawa, Mbagala na Kurasini, Serikali sasa kupitia TANESCO imejielekeza katika ujenzi wa kituo hicho cha Kibamba.
Kwa hiyo, naomba niendelee kuwahimiza watu wa TANESCO wafanye haraka huo mradi uanze ili uweze kutatua matatizo ya kukatika katika kwa umeme na low voltage katika Jimbo la Kibamba na Kata alizozitaja. Nakushukuru. (Makofi)
MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Tatizo la kukatika kwa umeme katika Mji wa Mtwara limefanana kabisa na Moshi Manispaa. Moshi umeme huwa unakatika sana na hata ukirudi, unarudi mdogo sana.
Je, ni lini sasa Serikali itahakikisha Moshi inapata umeme wa uhakika ukizingatia Moshi ni Mji wa viwanda?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge Lucy Owenya wa Viti Maalum swali lake kuhusu kukatika katika kwa umeme kwa maeneo ya Moshi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme wakati mwingine sababu zinazopelekea kukatika kwa umeme ni uchakavu wa miundombinu ya kusafirishia umeme. Kwa kuliona hilo, Serikali kupitia ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, umekuja na mradi wa ujenzi wa njia ya Msongo wa KV 400 unaotoka Singida mpaka Namanga ambao huo pia utatumika kusafirishia umeme ambao utakuwa wa kutosha kufika maeneo ya Moshi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, tuna ujenzi pia wa njia ya msongo wa KV 400 ambao utatoka Kinyerezi – Kibaha – Chalinze – Segera na Moshi. Kwa hiyo, nataka nimthibitishe Mheshimiwa Mbunge kwamba hilo suala limeonekana kwa kuwa mahitaji ya umeme kwa ajili ya viwanda yameongezeka sana Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro, ndiyo maana Serikali inataka kutekeleza hiyo miradi ili umeme unaozalishwa kwa wingi usafirishwe na uweze kutumika. Ahsante.
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Tatizo lililopo Mtwara linafanana kabisa na tatizo lililopo Mkoa wa Kagera. Umeme ukatika mara kwa mara hasa Bukoba Mjini, Bukoba Vijijini, Muleba, Missenyi na Karagwe. Je, ni lini tatizo hili la kukatika umeme litakwisha?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Oliver naye ameuliza ni lini Mkoa wa Kagera suala la kukatika kwa umeme litapungua kama siyo kumalizika kabisa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni kweli tunatambua Mkoa wa Kagera ambao kwanza wanapata umeme kutokea Uganda, tunanunua kama megawati 10 kutoka Uganda ambazo tunazisambaza katika maeneo yale, lakini Serikali pia kwa kuliona hilo, ndiyo maana sasa imejitahidi kuunganisha Wilaya za Ngara na Biharamulo kwenye Gridi ya Taifa. Mkakati huo unaendelea na pia tuna mpango wa kujenga transmission line ili umeme ambao utazalishwa katika maeneo ya Rusumo ambao tumeingiza megawati 80 tuweze kusambaza katika maeneo ya Mkoa wa Kagera na kuweza kutatua tatizo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namshukuru Mheshimiwa Mbunge na ninampongeza kwa ufuatiaji wake na Wabunge wote wa Viti Maalum ambao wanafuatilia sekta ya nishati, nawashukuru sana.
MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa tatizo lililopo katika Mkoa wa Mtwara linafanana na kukatika kwa umeme katika eneo la Kigogo Mkoani Dar es Salaam tena bila taarifa; je, Serikali ina mkakati gani wa kukabiliana na kadhia hii? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mheshimiwa Toufiq amekuwa akifuatilia mara kwa mara suala hili la kukatika kwa umeme kwa maeneo ya Kigogo. Kupitia mpango wa Serikali na Shirika lake la TANESCO, tunajenga sub-station maeneo ya Mburahati ambapo sub-station hiyo itasaidia kumaliza kabisa tatizo la kukatika kwa umeme maeneo ya Kigogo. Nakushukuru.
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Tatizo la kukatika kwa umeme Mkoani Mtwara linafanana sana na tatizo la kukatika kwa umeme katika Kisiwa cha Mafia. Kisiwa cha Mafia kinapata umeme kutoka kwenye majenereta manne makubwa ya dizeli. Kwa kuwa Mheshimiwa naibu Waziri amesema Mkoa wa Mtwara una majenereta 11 yakiwemo mawili mapya; je, haoni sasa ni muhimu tuchukue yale majenereta mawili mapya ya Mtwara na kuyapeleka mafia?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiwa shahidi, Mheshimiwa Mbaraka Dau ameshauliza maswali zaidi ya mawili kwa tatizo la umeme la Mafia. Naomba nimthibitishie kwamba Serikali kama ambavyo imepata kumjibu ndani ya Bunge, tunalishughulikia kwa karibu tatizo la upatikanaji wa umeme katika Wilaya ya Mafia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hilo swali alilosema kwamba tupeleke mashine mbili, naomba nimwombe kaka yangu, nami pia ni Mbunge wa maeneo hayo kwamba hili suala aje Ofisini tulizungumze, lakini kwa sasa zile mashine lazima zitumike Mtwara na Mafia tutafanya utaratibu mwingine. Ahsante sana.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nitoe ombi, Hospitali ya Haydom umeme unakatika mara nyingi sana. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Waziri atafute namna mbadala ya kusaidia umeme wa Haydom.
Swali sasa kwanza, nimshukuru Mheshimiwa Waziri alifika katika Jimbo la Mbulu Vijijini na kuahidi kwamba umeme utafika Endagichan Masieda, Endagichan Endamila, Yaeda Chini na Eshkeshi; je, ahadi hiyo bado ipo na umeme utafika vijiji hivyo?
Swali la pili; kwa kuwa Hospitali ya Haydom inatumia shilingi milioni 12 kwa ajili ya jenereta za dizeli kwenye vyanzo vya maji, je, Serikali ina mpango gani wa haraka ili kuisaidia hospitali ile kujihudumia vizuri kwa umeme kufika pale katika vyanzo vya maji?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini.
Kwa kweli nampongeza kufuatia ziara aliyofanya Mheshimiwa Waziri katika Jimbo lake tarehe 9 Mei, 2018 na kama mwenyewe alivyosema Mheshimiwa Waziri alipofika katika Jimbo lake alitoa ahadi ya kuongezeka kwa vijiji 22 kwa kuwa Jimbo hili lina vijiji vingi. Kwa hiyo, namthibitishia Mheshimiwa Mbunge, vijiji alivyovitaja ni miongoni mwa vijiji ambayo Mheshimiwa Waziri aliahidi na tumeshaviwasilisha REA kwa ajili ya taratibu za awali za upembuzi yakinifu.
Swali lake la pili kuhusu Hospitali ya Haydom, Mheshimiwa Waziri kupitia ziara yake ya tarehe 9 Mei, 2018 alitoa maelekezo kwa TANESCO kukamilisha ukarabati wa miundombinu ili wananchi wa Mkoa wa Manyara wapate umeme wa uhakika kwa wakati wote. Kwa hiyo, naomba niwahimize TANESCO wakamilishe hiyo kazi mwisho wa mwezi huu. Ahsante.
MHE. AISHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lililopo Mbulu Vijijini Iinafanana kabisa na tatizo lililopo Iramba Mgharibi. Vijiji 13 vya Jimbo la Iramba Magharibi hadi sasa havijapatiwa umeme. Baadhi ya vijiji hivyo ni Kisua, Tieme B, Kisonso, Makunda, Twinke, Tulya, Meli na Kisiriri.
Je, ni lini sasa Serikali itapeleka umeme katika vijiji hivyo ili kuyawezesha makundi ya wanawake na vijana kujiajiri?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aisharose Matembe kuhusu masuala ya REA katika vijiji vyake 13. Kwanza naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mkoa wake wa Singida umepata vijiji 150 kwa REA hii Awamu ya Tatu, mzunguko wa kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, vijiji hivi kama ambavyo nimekuwa nikirejea kwenye majibu ya msingi, mpango wa Serikali ni kupeleka vijiji vyote umeme. Kwa hiyo, vijiji 13 vipo katika mpango wa REA mzunguko wa kwanza na ninawaomba Waheshimiwa Wabunge wote wafanye ufuatiliaji wa karibu na kwa kweli nafarijika kuona Wabunge wa Viti Maalum wanachangamkia miradi hii ya REA. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Wizara hii imekuwa ikijitahidi sana kwenye suala zima la usambazaji wa umeme katika maeneo mbalimbali kupitia miradi ya REA pamoja na taratibu nyingine.
Je, Wizara hii iko tayari sasa kuweza kuwasaidia wananchi wetu wa Wilaya ya Shinyanga Mjini na hasa Jimbo langu la Shinyanga ambako natoka ambapo tunakabiliwa na tatizo kubwa sana la kukatika sana sana kwa umeme; kwa taarifa nilizonazo ni kwamba kituo cha kusambazia umeme cha Ibadakuli kimezidiwa nguvu.
Je, Serikali ipo tayari sasa kuweza kusaidia kituo hiki kukiongezea nguvu ili umeme wa uhakika uweze kupatikana? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii. Ni kweli kufuatia utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa msongo wa KV 400 kutoka Iringa mpaka Shinyanga, mradi ule una taratibu za upanuzi wa vituo vya kupokea na kupoozea umeme kimojawapo ikiwa ni Ibadakuli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kituo kile pamoja na kuzidiwa, mradi huu wa kukikarabati na kukiwezesha kutoka kwenye KV 220 na kufika KV 400 utakwenda kutatua tatizo la wananchi wake wa Shinyanga ambako amekuwa akifuatilia sana mahitaji wa umeme. Ahsante.
MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniruhusu nami niulize swali la nyongeza kuhusu REA. REA haikupita kabisa katika vijiji vya Kanyenye, Majengo, Ikongolo, Kiwembe, Zumbuka na Igulawima, tukategemea kwamba REA Namba Tatu itatusaidia hilo, lakini sasa mkandarasi haonekani. Lini mkandarasi ataonekana katika vijiji hivyo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Almas juu ya lini Mkandarasi atafika katika maeneo yake kutekeleza mradi katika vijiji alivyotaja?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme, kwa kweli Wakandarasi kwa sasa hivi wako site na kwa kuwa kupitia Bunge lako na kupitia Wizara ya Fedha na Benki Kuu kwamba zile pesa shilingi bilioni 268 Letter of Credit zimefunguliwa pamoja na dola milioni 52. Kwa hiyo, nataka niseme wakandarasi wote hawana kisingizio tena waende site, wafanye kazi ili miradi hii ikamilike kwa wakati na hakutakuwa na msalie Mtume. Ahsante. (Makofi)
MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Kwanza na mimi nampongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kazi nzuri anayoifanya na kwa majibu yake mazuri.
Kwa kuwa umeme wa REA kwa sehemu kubwa inapopita katika Wilaya zetu za Mkoa wa Manyara zikiwepo Mbulu vijijini, zinapita katika barabara kuu na kuacha pembeni taasisi muhimu kama shule, zahanati na nyinginezo:-
Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba umeme huu sasa ujaribu kwenda vijijini zaidi ili iweze kunufaisha shule za sekondari, zahanati na taasisi nyingine muhimu na huko ambako kuna wananchi walio wengi zaidi?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Umbulla ambapo kwa kweli ameuliza swali la msingi, lakini tangu mwanzo baada ya kubaini changamoto ya REA I na REA II tumetoa maelekezo. REA Awamu ya Tatu taasisi zote za Umma alizozitaja ziwe zipaumbele. Kwa hiyo, naomba niendelee kusisitiza kwa wakandarasi, wasimamizi wa miradi yote, Mikoa na Wilaya walitekeleze hilo kwa wakati na kwa usimamizi wa hali ya juu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili ili Wabunge wasiendelee kuuliza swali kama hili, ni kwamba densifications awamu ya pili inaanza hivi karibuni katika mikoa 11. Densification hii maana yake ni ujazilizi, yale maeneo ambayo yamerukwa yatapatiwa umeme katika awamu inayoanza mwaka 2018/2019. Nawashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa sababu mmeshapitisha bajeti, msiwe na wasiwasi.
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto katika utekelezaji wa mradi wa REA pia ni upatikanaji wa nguzo. Katika Jimbo la Bunda Mjini ni lini sasa nguzo zitafika katika maeneo ya Bunda Store, Nyamswa, ambapo katika Kitongoji cha Zanzibar pamoja na Nyabeu Sazila ili wananchi wahakikishiwe kupata umeme wa uhakika kwa sababu tatizo kubwa la maeneo hayo ni nguzo? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Bunda Mjini, Mheshimiwa Esther Bulaya, juu ya masuala ya upatikanaji wa nguzo katika maeneo ambayo ameainisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme Mkandarasi DEM yuko site anaendelea na kazi. Kama changamoto ilikuwa ufunguaji wa Letter of Credit kwa ajili ya kuagiza vifaa kwa wingi, tumeshawafungulia Wakandarasi wote; na kwa kuwa pia viwanda vya kuzalisha nguzo ambavyo viko ndani ya nchi, tumekutana navyo na nguzo zipo. Kwa mfano, hapo Kuwaya Iringa, Saw Mill Iringa na tumefanya uhakiki kwamba nguzo za kutosha zipo. Rai yangu kwa wakandarasi wote, waagize hivyo vifaa kwa wakati ili kusiwe na visingizio. Nakushukuru.
MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Waziri hizi pesa za REA ni pesa ambazo ziko ring fenced, lakini mpaka sasa ninavyozungumza kwenye Jimbo langu mradi wa densification haujafanyika hata mmoja kwenye maeneo ya Nyamorege, Nyabitocho, Kyoruba, Pemba na Matongo ambayo ni maeneo makubwa yenye watu wengi. Kwa mfano, Nyamorege ina watu zaidi ya 20,000 wenye uwezo wa kutumia umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nauliza, ni lini mkandarasi atakwenda pale? Kwa sababu mnasema pesa zipo, lakini yeye anasema hajalipwa pesa; lini anakwenda kuwekea watu wa Tarime umeme hasa Kata ya Susuni ambayo haina umeme kabisa kata nzima na ina watu wengi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Heche ameeleza kwamba kuna mradi wa densification, haoni maendeleo yoyote. Nataka niseme hii miradi iko tofauti. Densification kwa kweli hela zake zipo na unafadhiliwa na Serikali ya Norway pamoja na Serikali ya Tanzania na ni shilingi bilioni 62. Sasa labda baada ya kipindi hiki cha maswali na majibu, namwomba Mheshimiwa Mbunge tukutane ili tuongee na mkandarasi nijue tatizo lake ni nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa densification hauna matatizo kabisa na kwa kuwa Mkoa wa Mara uko katika mikoa ile nane ya awali na sasa hivi matarajio yetu ni mwezi Mei miradi yote ya densification iwe imekamilika ili tuanze na densification awamu ya pili. Kwa hiyo, namuomba Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane baada ya hapa ili tuweze kuona tatizo ni nini ili niweze kulishughulikia.
MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi.
Naomba niulize swali moja la nyongeza. Tarafa ya Wampembe yenye Kata nne za Kala, Wampembe, Kizumbi na Ninde iko kwenye mpango wa REA. Ninavyosema hivi, hakuna harakati zozote zinazoendelea katika kupeleka umeme katika maeneo haya. Je, ni lini Serikali itapelekea wananchi umeme katika maeneo haya?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mipata juu ya lini Serikali itapeleka umeme katika Tarafa ya Mwampembe; na ameainisha kwamba iko katika mpango wa REA. Napenda nimthibitishie kwamba Mkandarasi Nakuroi Investment yupo anafanya kazi katika Mkoa wa Rukwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimwelekeze Mkandarasi na tumetoa maelekezo kwamba wasifanye kazi kujielekeza kwenye eneo moja. Kwa kuwa hakuna changamoto nyingine ya kuagiza vifaa, nawaomba Wakandarasi wote wa miradi ya REA wawe na magenge ya kutosha katika Majimbo yote na Wilaya zote ili kazi zitekelezeke kwa wakati na kwa speed ambayo tunaitarajia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tatizo ni hilo, nitaongea na Wakandarasi wote nchi nzima. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Waziri amezungumza vizuri sana kuhusiana na habari ya kupeleka umeme katika Jimbo Busanda, lakini vijiji hivi ambavyo amevitaja bado hatujamwona mkandarasi, hajafika. Napenda kujua ni lini sasa mkandarasi ataanza rasmi kufanya kazi katika vijiji hivyo vya Ntono na Bugogo ambavyo amevitaja katika jibu la msingi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, sera ya nchi ni kwamba mahali popote ambapo nguzo zinapita na nyaya juu, lazima wananchi waweze kupata umeme. Kwenye Jimbo la Busanda kuna vijiji ambavyo vimepitiwa na nguzo; kwa mfano, Nyaruyeye pamoja na vijiji vingine sehemu za Busaka vimepitiwa na nguzo juu lakini havina umeme. Ndiyo maana nilimfuata Mheshimiwa Waziri ofisini nikapeleka vijiji 30 vya nyongeza kwa ajili ya kupatiwa umeme, lakini hapa sijavisikia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujua sasa Wizara inasemaje kuhusu kuvipatia umeme vijiji 30 ambavyo nimeongea na Mheshimiwa Waziri?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Mheshimiwa Bukwimba kwa kufuatilia masuala ya umeme katika Jimbo lake akiwa Mbunge mwanamke wa Jimbo pia. Ameulizia ni lini mkandarasi ataripoti katika Jimbo lake?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nirejee kama nilivyosema awali, tutakutana nao wakandarasi tena kwamba maelekezo ni yale yale, mkandarasi asikae sehemu moja. Kwa hiyo, pengine kama yuko katika maeneo mengine, tumesema wawe na magenge na kila Wilaya wakandarasi kazi ionekane imeanza kwa sababu hakuna kikwazo tena.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kutokana na changamoto iliyokuwepo ya uwepo wa vijiji ambavyo vimepitiwa na miundombinu ya umeme na umeme hakuna, imekuja densification ya awamu ya pili ambapo Geita ni Mkoa mmojawapo katika densification ya awamu ya pili pamoja na mikoa mingine, jumla 11.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba la hilo, vijiji vyake 30 tumeviwasilisha REA kwa ajili ya mchakato na ninamthibitishia vitakuwepo katika hiyo orodha kama ambavyo amefuatilia Mheshimiwa Mbunge. Nakushukuru.
MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa Dodoma ni Mji Mkuu, pia ni Jiji, lakini kukatika kwa umeme ni jambo la kawaida.
Je, nini kinachosababisha hata kukatika kwa umeme Sengia na Site Two kuwa ni jambo la kawaida? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba nijibu swali la mama yangu Mheshimiwa Fakharia kwamba kukatika kwa umeme kwa Mkoa wa Dodoma naomba nilichukue na tunalishughulikia, lakini wakati mwingine ni kutokana na kubadilisha tu nguzo ambazo zimeoza, nyaya na kadhalika, lakini kwa kuwa ni Jiji kwa kweli tunalifanyia kazi kwa karibu. Ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Utekelezaji wa REA Awamu ya Tatu kwenye Mkoa wa Lindi tumepata Mkandarasi ambaye uwezo wake ni mdogo sana. Mpaka sasa hivi awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi huu ishafika nusu ya wakati wake lakini bado yuko kwenye Wilaya moja tu ya Ruangwa. Ni lini mkandarasi huyu ataweza kufika Liwale?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Kuchauka juu ya changamoto za utekelezaji wa miradi hii ya REA Awamu ya Tatu na mkandarasi. Lazima nikiri kwamba mkandarasi wa Mkoa wa Lindi State Grid kuna matatizo ambayo yanaendelea kufanyiwa kazi.
Kwa hiyo, nimthibitishie tu, hivi karibu Mkandarasi huyu zitakapoisha changamoto hizi atafanya kazi kama ilivyokusudiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapa tukutane na Mheshimiwa Mbunge na wote wa Mkoa wa Lindi ili tuweze kujadili suala hili. Ahsante.
MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru, Jimbo la Mchinga halina Mamlaka ya Mji Mdogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua tu kwa Mheshimiwa Waziri, ni kigezo gani kinachotumiwa na TANESCO Lindi kuwalipisha watu wa Mchinga fedha nyingi ya kuunganisha umeme tofauti na vijiji vingine wakati Mchinga yenyewe ni kijiji kama maeneo mengine?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, uunganishwaji wa umeme katika maeneo ya vijijini bei yake ni shilingi 177,000, umeme ambao unaunganishwa kupitia TANESCO na ile shilingi 27,000 ni kwa umeme vijijini. Kwa hiyo, naomba nimthibitishie Mbunge kwamba hakuna tofauti, ila mijini ni shilingi 377,000 na vijijini ni shilingi 177,000. Kama wanakuwa-charged zaidi ya hizo, naomba tuonane ili niweze kulishughulikia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba radhi kwa Waheshimiwa Wabunge kwa tatizo lililojitokeza sasa hivi. Ahsante. (Kicheko/Makofi)
MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa niulize swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa Tabora Manispaa mpaka leo hii kuna baadhi ya Kata hazina umeme na Serikali ilituahidi hapa Bungeni kuanzia mwaka 2013 itatuletea umeme wa REA, lakini cha kushangaza Makao Makuu ya Kata hizo yote yamewekewa umeme wa REA ambapo vijiji vyake mpaka leo hii havijawekewa umeme wa REA. Umeme wa REA umewekwa Itonjala, Ifucha, Kalunde, Ntalikwe, Tetemia, Misha, Kakola na baadhi ya Makao Makuu ya Kata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nimuulize Mheshimiwa Waziri, ni lini sasa Serikali itatuletea umeme wa REA kwenye baadhi ya vijiji ambavyo mpaka leo hii havijawekewa umeme wa REA ukizingatia ile ni Manispaa?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Munde Abdallah Tambwe swali lake la msingi linahusu maeneo ambayo tulipeleka umeme kwenye Makao Makuu ya Kata na bado vijiji. Naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo alipata kuja ofisi akaelezea na ninampongeza kwamba vitongoji na vijiji vya Kata zile vitapata umeme kupitia mradi wa densification awamu ya pili. Mkoa wa Tabora ni miongoni mwa mikoa 11 ambapo mradi huu utaanza mwaka 2018/2019.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama nilivyoomba Wabunge wote wa Viti Maalum kwa sababu ni wahanga, ni wafaidika wa umeme kwa kuwa wanawake wakipata umeme wamefaidika wote, waendelee kufuatilia ili umeme upatikane katika maeneo yote. Ahsante. (Makofi)
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru. Mwaka 2016 mwezi wa kumi, Mkoa wa Mara ndiyo walizindua REA Awamu ya Tatu na densification. Mpaka naongea sasa hivi, Jimbo la Tarime Mjini maeneo mengi, maeneo ya Kanyamanyori, Kata ya Nyandoto, Kitale na Nkende mradi huu haujaanza na ni kwa asilimia 90 hawa watu hawana umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujua sasa ni lini Serikali itaenda kuelekeza maana imepita takribani miaka miwili ili miradi iweze kufanyika kwa ufanisi na wananchi waweze kupata umeme? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nijibu swali la Mheshimiwa Esther Matiko kuhusu masuala ya umeme katika Mkoa wa Mara hususan katika Jimbo lake, kwanza, kwa kuwa nimeona ndani ya Bunge bado changamoto za wakandarasi kuanza kuendelea na kazi, inaonekana Wabunge wengi hawaridhiki kwamba speed inaonekana ni ndogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, mara baada ya kutupitishia bajeti yetu, sisi tunaendelea na ziara. Ndiyo maana leo Mheshimiwa Waziri hayupo, ameshafanya ziara pia katika Mkoa wa Mara. Kutokana na tatizo hili, naomba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba nitafanya ziara Mkoa wa Mara tena ili kuona kwa nini wakandarasi mpaka sasa hivi wanasuasua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawaomba wakandarasi hili ni onyo la mwisho kwa kweli kama speed itaendelea Serikali ya Awamu ya Tano itasita kuvunja mikataba nao kKwa sababu miezi iliyobaki ni michache na tumeshawapa hela kwa nini inashindikana. Nashukuru ahsante.
MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na kumshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu haya ambayo ametupa nina maswali mawili ya nyongeza.
Mhshimiwa Spika, kwanza, katika kipindi hichohicho kampuni ya Dodsal imefanya utafiti wa gesi na mafuta katika Kata ya Vigwaza, Wilaya ya Bagamoyo. Napenda kujua nini matokeo ya utafiti huo?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, napenda kujua ni maeneo gani katika Mkoa wa Pwani ambapo gesi imegundulika kwa kiwango cha kibiashara?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Jumanne Shukuru Kawambwa. Namshukuru sana ameuliza swali katika Kata yetu ya Fukayosi.
Mheshimiwa Spika, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni kweli Kampuni hii ilifanya utafiti pia katika maeneo ya Vigwaza, Kwala na Ruvu. Kazi inayoendelea sasa hivi ni kukusanya data na kuzichakata zile takwimu za mitetemo ambazo zinaitwa 3D. Kwa hiyo, kazi hiyo inaendelea ili kubaini kiwango cha gesi asilia kilichopo katika mashapo ambayo gesi imegundulika katika maeneno hayo.
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ameuliza ni maeneo gani katika Mkoa wa Pwani mpaka sasa gesi imegundulia. Kwa kweli ni maeneo hayo kama ambavyo nimesema katika jibu hili la nyongeza, ni Kwala, Ruvu na Vigwaza ambapo utafiti unaendelea. Sasa hivi data ambazo wanazikusanya za mitetemo hiyo ya 3D wanaendelea kuzifanyia michakato ili kubaini kiwango cha gesi na kuweza kutathmini kama kinafaa katika vigezo mbalimbali vya kiuchumi. Nakushukuru sana.
MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Serikali imekuwa na utaratibu wa kupeleka wanafunzi katika vyuo vya nchi za nje kwa ajili ya kupata utaalam kwenye masuala ya gesi na mafuta. Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba wanafunzi hawa baada ya masomo wanapata ajira kwenye makampuni haya ambayo yanafanya tafiti kwenye Taifa letu ili waweze kuonyesha uwezo wao, experience yao na uzalendo wao katika makampuni ya utafiti? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu swali la nyongeza. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jesca Kishoa linalohusu masuala ya namna gani Serikali imejipanga kutumia utaalam wa vijana ambao wamekuwa wakipelekwa nchi mbalimbali kupata mafunzo katika eneo la mafuta na gesi. Ni kweli kwamba utaratibu huo upo na hata mwaka huu wa fedha unaoendelea tumepokea nafasi 20 kutoka katika nchi ya China kwa ajili ya kupeleka vijana wetu.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa utelekezaji wa miradi ya gesi na mafuta unayoendana na ubia baina ya Taasisi yetu ya TPDC na kampuni hizo ya kimataifa, ni wazi kabisa kwamba mpango wa Serikali ni kuona vijana wale wakihitimu wanafanya kazi katika maeneo haya. Kwa vyovyote vile, kwa kuwa baada ya kuhitimu wanakuwa wamepata teknolojia na wanatosha katika mazingira hayo, wengi wamekuwa wakipata ajira katika kampuni hizi za kimataifa zinazofanya utafiti ndani ya nchi yetu lakini Serikali itaendelea na utaratibu huo. Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Spika, naomba niongeze majibu kidogo kwenye suala hili la msingi sana la kuweza kuwawezesha Watanzania kushiriki katika uchumi unaojengwa kwenye nchi yetu ya Tanzania.
Mheshimiwa Spika, baada ya kuona kwamba mageuzi makubwa ya kiuchumi yanafanyika na hasa uwepo wa miradi mikubwa ya kimkakati katika nchi yetu, Serikali imefanya kwa makusudi marekebisho ya sheria mbalimbali, lakini vilevile imetunga kanuni mbalimbali za kuhakikisha Watanzania ambao wana uwezo na weledi katika sekta hizo wanapewa kipaumbele cha ajira kwenye maeneo husika.
Mheshimiwa Spika, suala hili limeshafanikiwa, kanuni zimeshatengenezwa kwenye suala la mafuta na gesi na wenzetu wa Wizara ya Madini wameshatengeneza kanuni za kuhakikisha Watanzania wanaajirika kwenye maeneo hayo. Vilevile Ofisi ya Waziri Mkuu inatengeneza sasa mfumo mzuri wa local content wa kuhakikisha bidhaa na huduma za Watanzania zinaweza kutumika na zikashiriki katika ujenzi wa uchumi wetu kupitia miradi mikubwa ya kimkakati katika nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)
MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, ili kuondokana na uharibifu wa mazingira kwa kukata miti hovyo ikiwemo matumizi ya nguzo za umeme za miti. Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kutumia nguzo za chuma badala ya nguzo za miti katika kusambaza umeme vijijini na mijini? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mndolwa. Ni kweli kuna mpango huo wa kuhama kutoka kwenye matumizi ya nguzo zinazotokana na miti, na kwenda nguzo zinazotokana na zege.
Mheshimiwa Spika, kwanza Shirika letu la TANESCO limeunda kampuni tanzu kwa ajili ya kuzalisha nguzo za zege. Pili kama Wizara pia tumehamasisha wadau wa ndani kuanzisha viwanda vya kutengeneza nguzo za zege na tayari kuna viwanda Bagamoyo, Kibaha na Mbeya na hiki nilikitembelea.
Mheshimiwa Spika, kinachofuata sasa ni taratibu za manunuzi, tumewaelekeza TANESCO kwamba miradi inayoendelea ya umeme vijijini kupitia REA na kupitia hata miradi yao, tuanze kuhama kutoka kwenye nguzo hizi za miti ambazo zinadumu kwa muda mfupi sana ndani ya miaka mitano, sita wakati hizi nguzo za zege zinaweza kudumu zaidi ya miaka 20 na kuendelea. Kwa hiyo, ni wazi tutakapotimiza azma yetu ya kutumia nguzo za zege tuta-save pesa nyingi zinazotumika kwenye ukarabati wa nguzo hizi za kawaida ambazo zinachukua muda mfupi na zinaoza. Nakushukuru.
MHE. ALFREDINA A. KAHIGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nyingine. Nina maswali mawili ya nyongeza, naomba kuyauliza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, katika Wilaya yetu ya Bukoba Vijijini kuna baadhi ya kata nitazisema japokuwa ni nyingi. Katika Kata ya Rubafu -Kijiji cha Bwendangabo, Kata ya Buma - Kijiji cha Bushasha, Kata ya Bwendangabo - Kijiji cha Kashozi, Kata ya Nyakato - Kijiji cha Ibosa; hizo ni baadhi ya Kata ambazo nimezitaja, lakini ni kata nyingi sana katika Wilaya yetu ya Buboka Vijijini au niseme Mkoa mzima wa Kagera tuna shida ya umeme.
Je, Serikali inaona umuhimu wa kuwapa kipaumbele cha kuweza kuwawekea umeme haraka iwezekanavyo? Hilo ni swali la kwanza.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, wananchi wa kata hizo hizo nilizozitaja wamenunua solar. Solar hizo tayari zimeshaharibika. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakiki hizo solar kabla hazijaingia sokoni? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza, amezitaja kata mbalimbali katika Wilaya yake ya Bukoba Vijijini na amewakilisha Mkoa mzima na ameeleza ni namna gani Serikali itaweka kipaumbele. Nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kuwa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkoa huo wa Kagera kwa awamu hii ya tatu inayoendelea jumla ya vijiji 141 vitapatiwa umeme. Katika Wilaya yake ya Bukoba Vijijini, Kijiji cha Burugo kimeshasambaziwa nguzo na kazi zinaendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kuwa Kata zile alizozitaja na vijiji alivyovitaja, kwa awamu hii ya kwanza vijiji kwa Bukoba vijijini ni 22, lakini kwa awamu ambayo itaendelea mzunguko wa pili unaoanza Julai vijiji vyote vilivyosalia vitapatiwa umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, ameuliza masuala ya sola ambazo zimewekwa katika maeneo hayo ya Bukoba Vijijini na maeneo mengine ya Mkoa wake kwamba nyingi zimeharibika. Serikali ina utaratibu ndani ya Serikali na kwa Taasisi mbalimbali. Kwa mfano, kuna masuala ya TBS yanavyoangalia viwango na taasisi nyingine za kiserikali za kuangalia bidhaa zinazoingia ndani ya nchi zisiwe bidhaa ambazo kwa kweli ni fake.
Mheshimwia Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali yetu itaendelea kuziimarisha zile taasisi zinazohusika na kuzuia bidhaa feki ndani ya nchi ili kujiridhisha na vifaa hususani vya masuala ya nishati viingie vifaa bora na wananchi wapate huduma bora. (Makofi)
Mheshimwia Naibu Spika, nakushuruku Mheshimiwa. (Makofi)
MHE. JORAM A. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la umeme lililopo Wilaya ya Kagera linafanana kabisa na tatizo la umeme mradi ule wa Makambako - Songea. Ule mradi umepita katika Kata tatu; Kata ya Kichiwa, Kata ya Igongoro na Kata ya Ikuna. Kwenye maeneo hayo kuna baadhi ya maeneo yana huduma muhimu kama shule, zahanati na vituo vya afya umeme haujapelekwa huko. Nini kauli ya Serikali kwa mkandarasi aliyesambaza umeme kwenye maeneo haya, kuhakikisha kwamba umeme unaenda kwenye maeneo yenye huduma muhimu? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Katika mradi unaoendelea Makambako - Songea kwa kweli tunarajia mwezi Septemba mradi ule utakamilika na kuzinduliwa rasmi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi inayoendelea ya kusambaza umeme katika maeneo ambayo yameainisha, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kuwa miradi hii ya kupeleka umeme vijiji ipo ya aina mbalimbali, kuna mradi wa Makambako - Songea ambao unalenga vijiji 121, lakini sambamba na hilo kuna mradi ambao unaendelea wa densification kwa maeneo ya Mkoa wa Njombe na Mkoa wa Iringa.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mradi huu, densification ya awamu ya kwanza ina vijiji kama 305 na mradi umekamilika umefikia asilimia 98.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, maeneo ambayo hajasalia kama ambavyo tunafahamu mradi wa REA Awamu ya Tatu unaendelea na maeneo yale na maelekezo yetu kama Serikali, tumesema taasisi za umma iwe shule, iwe zahanati, iwe miradi ya maji na taasisi zote kwamba kipaumbele kwa wakandarasi waelekeze kwenye maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama Serikali tunaendelea kusisitiza hayo maelekezo na yaendelee kutekelezwa na Wakandarasi wote. Nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, kwa kweli kwa awamu inayoendelea, changamoto hizi hazitakuwepo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Katika Jimbo la Mbulu Mjini kuna maporomoko ya Haino katika Tarafa ya Nambisi, Kata ya Nambisi. Maporomoko hayo ambayo wataalam kutoka Serikalini na taasisi mbalimbali zisizo za Serikali wameendelea kuyatembelea; na kwa kuwa, tuna mahitaji makubwa ya uzalishaji wa umeme nchini, je, ni lini Mheshimiwa Waziri na Wizara yake watatembelea maporomoko ya Haino ili yaweze kutoa mchango wake katika sekta ya umeme kwa nchi nzima na hususan Jimbo la Mbulu Mjini?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Issaay, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Serikali tunatambua uwepo wa maporomoko haya ambayo kwa mujibu wa tafiti mbalimbali yana uwezo hata wa kuzalisha Megawati 5,000. Kupitia Serikali na TGDC tuna mpango wa kuhakikisha kwamba tunazalisha Megawati 200 kupitia maporomoko mbalimbali ambayo yataleta nishati ya joto ardhi ifikapo 2025, naomba nimkubalie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama Serikali kupitia Wizara ya Nishati tutafanya ziara katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyosema Mheshimiwa Waziri kwenye jibu lake kwamba kwa mwaka huu kuna maeneo kama 50 ambayo yatafanyiwa tafiti likiwemo eneo la maporomoko hayo katika Jimbo la Mbulu Mjini. Ahsante sana.
MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuuliza maswali ya nyongeza.
Kwanza napenda nitumie nafasi hii kuwapongeza kabisa Wizara hii inafanya kazi kubwa na ya kutukuka, lakini ni ukweli unaojulikana kwamba sisi katika Mkoa wa Kigoma na Katavi na hasa wananchi wangu wa Buhigwe umeme umechelewa kufika. Hivyo kwa commitment hii sasa ya Serikali kwamba ule mgogoro mtakuwa mmeumaliza kwamba Mei Mkandarasi atakuwa site. Kwanza kwa hatua hiyo kwa niaba ya wananchi wa Buhigwe na Mkoa wa Kigoma tunawapongeza sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali mawili ya nyongeza, swali la kwanza; viko vijiji kama ulivyovitaja mwenyewe Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba vimeshapatiwa umeme lakini kwenye vitongoji umeme bado haujaenda. Nataka kufahamu mkandarasi huyu atakayeenda kupeleka umeme kwenye vijiji vilivyobaki je, atapeleka kwenye vitongoji, kwenye vijiji ambavyo tayari vimeshapewa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, nini commitment ya Serikali kwa sababu sisi mmetucheleweshea umeme kwa muda mrefu na wananchi wangu wanahitaji umeme kwenye vijiji vyao. Je, mkandarasi hamtaweza kumkwamisha kwamba hamna hela? Naomba commitment ya Serikali.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niwape pole wakazi wa Mikoa ya Kigoma na Katavi, lakini niwashukuru sana Wabunge wa maeneo hayo ya Mkoa wa Kigoma, Jimbo la Buhigwe, Kasulu, Uvinza pamoja na Kigoma Vijijini pamoja na majimbo ya Mkoa wa Katavi kwa namna ambavyo wamekuwa wakifuatilia suala hili na kuwa na matumaini na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati pia nimepokea pongezi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali yake yalikuwa mawili ambalo moja lilijielekeza vijiji ambavyo vimepatiwa umeme kama ambavyo jibu langu la msingi limesema, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika maeneo ambayo Serikali inatambua yapo maeneo ya vijiji yalipata umeme lakini vipo vitongoji havikupata huduma hiyo na ndiyo maana Serikali imekuwa ikitekeleza mradi wa densification yaani ujazilizi na kwa sasa kwa mwaka unaokuja wa fedha 2018/2019 Serikali imeandaa mpango wa densification awamu ya pili ambayo itaenda kwenye mikoa mbalimbali ikiwemo Mkoa huu wa Kigoma. Kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi ambao wote vitongoji ambavyo havina umeme kwenye vijiji vyenye umeme vitapatiwa huduma hiyo kupitia mradi wa densification.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge mkandarasi huyu atakapoanza kazi Mei, 2018 hatakwamishwa kwa sababu Serikali kupitia Wizara ya Fedha mpaka sasa imeshatoa pesa zaidi ya shilingi bilioni 221 ambavyo imetokana na chanzo hiki cha umeme (REA) ambao umetokana na tozo ya mafuta. Kwa hiyo, nimthibitishie Mbunge kwamba tatizo la pesa halipo, asante. (Makofi)
MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, tarehe 13 Julai, 2017 aliyekuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini ambaye sasa ni Waziri wa Nishati alikuja kuzindua Mradi wa REA III katika Kijiji cha Nyamatala, Kata ya Ngula lakini hadi leo ni miezi saba hakuna hata eneo moja umeme umeshawaka. Nataka nipate majibu ya Serikali miezi saba sio Kitongoji, Kijiji wala Kata na uzinduzi huo ulikuwa kimkoa. Nataka nipate majibu ya Serikali tatizo hasa ni nini na umeme huu utaanza kuwaka lini.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba ni kweli katika Mkoa wa Mwanza mkandarasi wa Nippo Group Limited yupo kazini na ninaomba nimfahamishe baada ya uzinduzi ule kazi ambazo ziliendelea ni pamoja na tathmini, uchambuzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia niliarifu Bunge lako kipindi kile ambapo miradi inazinduliwa yapo mahitaji mbalimbali ambapo yalijitokeza kutoka kwa Wabunge kutokana na uhitaji wa nishati hii Vijijini. Kwa hiyo, tathmini ya ilivyokuwa inaendelea kufanyika na maeneo mbalimbali ambako wakandarasi walikuwepo, vipo Vijiji pia vya nyongeza pia vimeongezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimtaarifu kwamba kwa Mkoa wa Mwanza mpaka sasa mkandarasi yule ameshawasha Vijiji sita lakini naomba nimwelekeze Mkandarasi Nippo tulitoa maelekezo kwa wakandarasi wote wafanye kazi katika Wilaya zote, wawe na magenge ya kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, pengine changamoto inayojitokeza mkandarasi huyu yupo katika Wilaya zingine hajafikiwa katika Jimbo lake. Lakini naomba nimthibitishie na wizara kwa awamu hii imepanga kufanya ziara katika Jimbo lake na kazi zitaendelea na kwa sababu mikataba hii inaonyesha na muda wa kazi ni kuanzia kipindi hiki mpaka Novemba, 2019 ndio zinakamilika, naomba nimtoe wasiwasi yeye Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Jimbo lake kwamba huduma hii ya umeme vijijini kama ilivyozinduliwa itapatikana kwasababu mkandarasi yupo ndani ya wakati, asante sana.

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri katika swali la Mheshimiwa Ndassa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Mheshimiwa Ndassa kwa kweli wakati tunakwenda kuzindua alifanya kazi kubwa sana, lakini nimpe taarifa katika Jimbo lake tayari wakandarasi wapo katika Kijiji cha Nyamatara na Nyambiti; na Nyambiti na Nyamatara kesho wanawasha umeme. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge awasiliane na Mheshimiwa Katibu wake na jana tuliwasiliana naye pale Nyamatara wameshasimika nguzo, transfoma wamepeleka juzi na kesho na keshokutwa wataendelea kuwasha kwenye vijiji viwili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vya Nguge pamoja na Nipo katika Mkoa wa Mwanza pia wameshawasha umeme lakini pamoja nahayo nitawasiliana na Mheshimiwa Ndassa tukae naye vizuri ili maeneo mengine vipaumbele tuweze kuwapelekea umeme haraka iwezekanavyo.
MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza naomba nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri alifanya ziara katika Jimbo la Ukonga na tukafanya mikutano mpaka saa moja usiku, namshukuru sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa tu nijue kwamba Jimbo la Ukonga lina shida kubwa ya umeme ambayo Mheshimiwa Waziri na Naibu wake wanafahamu. ningependa nijue katika hii mipango ya REA ambayo inaendelea Ukonga nao wategemee nini? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa. Na mimi naomba nimpongeze Mbunge Mheshimiwa Waitara ni kweli tulifanya mikutano zaidi ya sita katika Jimbo lake na nimthibitishie baada ya mikutano ile kwa mwaka wa fedha unaokuja 2018/ 2019 Serikali inakuja na mpango wa Peri-urban kwa maeneo ya Mkoa wa Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani na kisha itaendelea Peri-Urban II. Ahsante.
MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Kwa kuwa Serikali inafanya vizuri sana kwenye umeme vijijini lakini bado tuna tatizo kubwa kwenye umeme mjini ikiwemo Singida Mjini yapo maeneo ambayo hayana umeme. Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kutuletea umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge Sima. Pamoja na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini tulifanya ziara katika Mkoa wa Singida na katika Wilaya ya Singida Mjini tuliona hilo tatizo. Kwa hiyo, nataka niseme ni kweli Serikali inatambua tatizo la uwepo wa ukuaji wa maeneo ya mijini na changamoto ya upatikanaji wa nishati kwa hiyo, inakuja na mpango wa Peri-Urban ambao utapeleka umeme katika miji inayokua kuanzia mwaka wa fedha 2018/2019.
MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa niweze kuuliza swali moja la nyongeza.
Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kuweza kupata nafasi ya kuja katika Jimbo langu la Busokelo, lakini nina swali moja tu kwamba ulivyokuja wana Busokelo tulikuomba kwamba vijiji vyote ambavyo vipo kwenye scope ya REA III na kwa bahati mbaya sana hivi vijiji baadhi yao vina nyumba za nyasi lakini hii leo ninavyouliza swali kwako Mheshimiwa Waziri ni kwamba vile vijiji vimerukwa. Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya Vijiji 8 ambavyo vimerukwa kwenye scope ambayo ipo sasa kwa REA III? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Atupele, tulifanya ziara pamoja katika Jimbo lake na kwa kweli katika Jimbo la Busokelo vijiji takribani 50 vipo katika REA hii ya Awamu ya Tatu na mkandarasi Stag International tulimwelekeza afanye tathmini katika maeneo yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hyo, naomba nimthibitishie vile vijiji nane ambavyo vipo kati ya vijiji 50 ambavyo vitapatiwa umeme katika REA awamu hii mzunguko wa kwanza tunamwelekeza mkandarasi vyote avifanyie tathmini na kwa kuwa Serikali imeelekeza nyumba yoyote iwe ya tembe au kawaida zote zinapatiwa umeme na tumeshuhudia mara kadhaa tukizindua umeme na nyumba hizi ambazo zimewekewa umeme. Kwa hiyo, nataka niseme hakuna nyumba mbayo itabaguliwa na mkandarasi atavifikia vile vijiji vinane, asante sana. (Makofi)
MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hangamoto ya umeme iliyopo manispaa ya Tabora inafanana kabisa na ile ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga katika Kata ya Tambani, Mwandege na vijiji vyake. Je, ni lini sasa umeme utawaka kwenye Kata hizi ikizingatiwa mradi wa REA I na REA II tayari ulishapita? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nikiri kwa kweli kwa Mbunge wa Mkuranga, Mheshimiwa Ulega pamoja na Mheshimiwa Mchafu wamekuwa wakifuatilia sana masuala ya nishati ya umeme katika Wilaya ya Mkuranga. Na ninaomba nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge, mkandarasi wa Mkoa wa Pwani Sengerema tumezungumza naye na Jumapili hii atapeleka nguzo kwa ajili ya maeneo hayo ya Tambani, Mwandege ambapo pana ongezeko kubwa la wananchi na hususani Kijiji cha Mlamleni katika Wilaya ya Mkuranga. Nataka nimthibitishie kazi kuanzia Jumamosi hii nguzo zitafika na itaendelea katika Mradi huu wa REA Awamu ya Tatu. Ahsante sana.
MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, Jimbo la Mbozi lenye kata 11 kuna kata mbili ambazo karibu vijiji 14 havina umeme kabisa. Sasa naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, ni lini sasa hizi kata mbili za Magamba na Kata ya Bara zitapatiwa umeme wa REA? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme mpango wa Serikali ni kupeleka umeme katika maeneo yote ambayo yamesalia, vijiji 7,873. Kwa hiyo, kwa kuwa swali lake limejielekeza kwenye kata mbili ambazo zina vijiji 14 na hakuna umeme kabisa, nataka nimuarifu kwa kipindi hiki cha 2018/2019 – 2019/2020 Serikali itakamilisha upelekaji wa umeme katika maeneo ya hizo kata mbili na vijiji vyake kwa mradi huu kabambe wa REA Awamu ya Tatu unaoendelea kutekelezwa ndani ya mwaka huu wa fedha na unaoendelea. Ahsante.
MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza REA kwa kazi nzuri, lakini hata hivyo katika Wilaya yetu ya Hanang kuna changamoto nyingi ambazo tunaziona, kwa mfano kuna taasisi ambazo hazijapata umeme pale ambapo umeme umeletwa, kuna maeneo yanarukwa njiani wanakwenda kwingine, je, Waziri atakubali kuja kutembelea Hanang ili tuone changamoto hizo ili tuzisahihishe na kama anaweza kumtuma mkandarasi kuja kuona changamoto hizo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru mama yangu, Mheshimiwa Dkt. Nagu na tumekubali huo mwaliko wa kutembelea kwa kuwa sisi Wizara yetu pamoja na Mheshimiwa Waziri na viongozi mbalimbali tumekuwa tukifanya ziara kwa kuwa miradi hii inatekelezwa vijijini. Kwa hiyo, naomba nimuagize pia mkandarasi Angelic, tuliwapa maelekezo wakandarasi wote taasisi muhimu za umma zipatiwe huduma hii ya umeme na maelekezo ya Serikali kupitia Mheshimiwa Rais pia mwenyewe kwamba vijiji visirukwe. Kwa hiyo, naomba nisisitize maelekezo haya yako palepale na tutafanya ziara katika maeneo yote likiwemo Jimbo la Hanang.
MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, kwanza nianze kwa kumpongeza Waziri na Naibu Waziri kwa ziara walizozifanya kwenye Halmashauri ya Mbeya. Naibu Waziri alitembelea kata ambazo hazina umeme kabisa lakini zinalizunguka Jiji la Mbeya kama Kata za Swaya na Maendeleo. Je, ni lini hizi kata mbili nazo zitapewa umuhimu wa kupewa umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tukushukuru sana kwa namna ambavyo umetambua mahitaji ya nishati na kuwapa fursa Waheshimiwa Wabunge kuuliza maswali mengi. Umenipa fursa ya kujibu maswali ya Mheshimiwa Njeza, Mheshimiwa Mwamoto pamoja na Mheshimiwa Frank.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Njeza na Mheshimiwa Mwamoto maswali yao yanalingana kwa sababu yamehusisha masuala ya umeme vijijini. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Njeza, tulifanya ziara Mbeya, pamoja na kwamba Jimbo lake ni Mbeya Vijijini, hapa amezisemea kata ambazo zipo ndani ya Jiji la Mbeya, na kama nilivyosema, Serikali imetambua ukuaji wa maeneo katika Miji, Manispaa na Majiji na ndiyo maana tumekuja na mradi huu unaoitwa Peri-Urban. Niliombe Bunge lako tukufu, tutakapowasilisha bajeti yetu ya mwaka 2018/2019 ituunge mkono katika miradi mbalimbali ukiwemo Mradi huu wa Peri- Urban kuupitisha kwa kishindo kisha tufanye kazi ya kupeleka umeme katika maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilo, Mheshimiwa Mwamoto, ni kweli tulifanya ziara tena kwa mara ya kwanza Mawaziri wawili, Mheshimiwa Waziri mwenyewe na mimi Naibu Waziri tulikuwa kwenye kata hiyo aliyoitaja. Nataka niseme sisi lengo letu ni kupeleka nishati kwenye maeneo yenye uhitaji ikiwemo mojawapo ya maeneo ambayo kweli yanahitaji nishati ni eneo la viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwapongeze Mheshimiwa Mbunge na vijana hao kwa kutenga eneo la viwanda vidogo vidogo na kwa gharama za Serikali umeme utafika katika maeneo hayo na nitoe rai tu wao waendelee kujipanga kuunganisha lakini umeme utafika kama ambavyo tumeahidi katika ule mkutano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la mwisho la Mheshimiwa Frank, ni kweli Mji wa Tunduma ni mji ambao umekuwa na upo mpakani. Nataka niseme Mji wa Tunduma upo katika Mkoa mpya wa Songwe na wakati huo umeme katika Mkoa wa Songwe ulikuwa unatoka katika njia ya kusafirisha umeme ni ndefu kutoka Mbeya. Serikali ina mpango wa kujenga sub-station palepale Tunduma kwa ajili ya kuufanya Mkoa mzima wa Songwe upate nishati ya uhakika na wakati wote. Kwa hiyo, nimthibitishe Mjumbe kwa kuwa yeye Mheshimiwa Mbunge ni Mjumbe wa Kamati yetu ya Nishati na yeye pia atuunge mkono katika bajeti yetu ili mradi huu wa ujenzi wa sub-station pamoja na line ambayo inatoka Mbeya inayoenda Sumbawanga - Mpanda – Kigoma - Nyakanazi ya KV 400 ambayo yote kwa pamoja itachangia kwa upatikanaji wa umeme wa uhakika. Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana, ahsante sana.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri alifika Kilolo, tena Kijiji cha Kihesa Mgagao, Kata ya Ng’uruwe, na kuwaahidi vizuri wananchi wa Kilolo kuhusu umeme; na kwa kuwa sasa baadhi ya vijana wameshatenga maeneo kwa ajili ya viwanda vidogo vidogo. Je, ni nani haswa anayepaswa kusogeza umeme kwenye maeneo ambayo vijana tayari wameshatengewa maeneo, ni gharama za nani? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tukushukuru sana kwa namna ambavyo umetambua mahitaji ya nishati na kuwapa fursa Waheshimiwa Wabunge kuuliza maswali mengi. Umenipa fursa ya kujibu maswali ya Mheshimiwa Njeza, Mheshimiwa Mwamoto pamoja na Mheshimiwa Frank.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Njeza na Mheshimiwa Mwamoto maswali yao yanalingana kwa sababu yamehusisha masuala ya umeme vijijini. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Njeza, tulifanya ziara Mbeya, pamoja na kwamba Jimbo lake ni Mbeya Vijijini, hapa amezisemea kata ambazo zipo ndani ya Jiji la Mbeya, na kama nilivyosema, Serikali imetambua ukuaji wa maeneo katika Miji, Manispaa na Majiji na ndiyo maana tumekuja na mradi huu unaoitwa Peri-Urban. Niliombe Bunge lako tukufu, tutakapowasilisha bajeti yetu ya mwaka 2018/2019 ituunge mkono katika miradi mbalimbali ukiwemo Mradi huu wa Peri- Urban kuupitisha kwa kishindo kisha tufanye kazi ya kupeleka umeme katika maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilo, Mheshimiwa Mwamoto, ni kweli tulifanya ziara tena kwa mara ya kwanza Mawaziri wawili, Mheshimiwa Waziri mwenyewe na mimi Naibu Waziri tulikuwa kwenye kata hiyo aliyoitaja. Nataka niseme sisi lengo letu ni kupeleka nishati kwenye maeneo yenye uhitaji ikiwemo mojawapo ya maeneo ambayo kweli yanahitaji nishati ni eneo la viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwapongeze Mheshimiwa Mbunge na vijana hao kwa kutenga eneo la viwanda vidogo vidogo na kwa gharama za Serikali umeme utafika katika maeneo hayo na nitoe rai tu wao waendelee kujipanga kuunganisha lakini umeme utafika kama ambavyo tumeahidi katika ule mkutano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la mwisho la Mheshimiwa Frank, ni kweli Mji wa Tunduma ni mji ambao umekuwa na upo mpakani. Nataka niseme Mji wa Tunduma upo katika Mkoa mpya wa Songwe na wakati huo umeme katika Mkoa wa Songwe ulikuwa unatoka katika njia ya kusafirisha umeme ni ndefu kutoka Mbeya. Serikali ina mpango wa kujenga sub-station palepale Tunduma kwa ajili ya kuufanya Mkoa mzima wa Songwe upate nishati ya uhakika na wakati wote. Kwa hiyo, nimthibitishe Mjumbe kwa kuwa yeye Mheshimiwa Mbunge ni Mjumbe wa Kamati yetu ya Nishati na yeye pia atuunge mkono katika bajeti yetu ili mradi huu wa ujenzi wa sub-station pamoja na line ambayo inatoka Mbeya inayoenda Sumbawanga - Mpanda – Kigoma - Nyakanazi ya KV 400 ambayo yote kwa pamoja itachangia kwa upatikanaji wa umeme wa uhakika. Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana, ahsante sana.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Tunduma uko mpakani mwa Zambia na Tanzania na ni mji ambao unapokea wageni wengi wanaotoka nchi za Kusini mwa Afrika lakini huduma ya umeme kwenye Mji wa Tunduma ni haba sana na umeme unakatikakatika mara kwa mara na kusababisha usalama wa wageni na wananchi wa Tunduma kuwa hatarini. Je, ni lini Serikali itahakikisha kwamba inaweka umeme wa uhakika katika Mji wa Tunduma?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tukushukuru sana kwa namna ambavyo umetambua mahitaji ya nishati na kuwapa fursa Waheshimiwa Wabunge kuuliza maswali mengi. Umenipa fursa ya kujibu maswali ya Mheshimiwa Njeza, Mheshimiwa Mwamoto pamoja na Mheshimiwa Frank.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Njeza na Mheshimiwa Mwamoto maswali yao yanalingana kwa sababu yamehusisha masuala ya umeme vijijini. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Njeza, tulifanya ziara Mbeya, pamoja na kwamba Jimbo lake ni Mbeya Vijijini, hapa amezisemea kata ambazo zipo ndani ya Jiji la Mbeya, na kama nilivyosema, Serikali imetambua ukuaji wa maeneo katika Miji, Manispaa na Majiji na ndiyo maana tumekuja na mradi huu unaoitwa Peri-Urban. Niliombe Bunge lako tukufu, tutakapowasilisha bajeti yetu ya mwaka 2018/2019 ituunge mkono katika miradi mbalimbali ukiwemo Mradi huu wa Peri- Urban kuupitisha kwa kishindo kisha tufanye kazi ya kupeleka umeme katika maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilo, Mheshimiwa Mwamoto, ni kweli tulifanya ziara tena kwa mara ya kwanza Mawaziri wawili, Mheshimiwa Waziri mwenyewe na mimi Naibu Waziri tulikuwa kwenye kata hiyo aliyoitaja. Nataka niseme sisi lengo letu ni kupeleka nishati kwenye maeneo yenye uhitaji ikiwemo mojawapo ya maeneo ambayo kweli yanahitaji nishati ni eneo la viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwapongeze Mheshimiwa Mbunge na vijana hao kwa kutenga eneo la viwanda vidogo vidogo na kwa gharama za Serikali umeme utafika katika maeneo hayo na nitoe rai tu wao waendelee kujipanga kuunganisha lakini umeme utafika kama ambavyo tumeahidi katika ule mkutano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la mwisho la Mheshimiwa Frank, ni kweli Mji wa Tunduma ni mji ambao umekuwa na upo mpakani. Nataka niseme Mji wa Tunduma upo katika Mkoa mpya wa Songwe na wakati huo umeme katika Mkoa wa Songwe ulikuwa unatoka katika njia ya kusafirisha umeme ni ndefu kutoka Mbeya. Serikali ina mpango wa kujenga sub-station palepale Tunduma kwa ajili ya kuufanya Mkoa mzima wa Songwe upate nishati ya uhakika na wakati wote. Kwa hiyo, nimthibitishe Mjumbe kwa kuwa yeye Mheshimiwa Mbunge ni Mjumbe wa Kamati yetu ya Nishati na yeye pia atuunge mkono katika bajeti yetu ili mradi huu wa ujenzi wa sub-station pamoja na line ambayo inatoka Mbeya inayoenda Sumbawanga - Mpanda – Kigoma - Nyakanazi ya KV 400 ambayo yote kwa pamoja itachangia kwa upatikanaji wa umeme wa uhakika. Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana, ahsante sana.
MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Mwambe nina maswali mawili ya nyongeza.
La kwanza, kuna taarifa kwamba mkandarasi ambaye amepewa kazi ya kukamilisha miradi hii ya REA katika Mkoa wa Mtwara, hasa Wilaya ya Masasi yenye Jimbo la Ndanda pamoja na Nanyumbu ana matatizo ya kiusajili.
Je, Serikali haioni ni wakati mwafaka wa kuachana na mkandarasi huyu na kumtafuta mwingine ambaye atakamilisha kazi hii kwa wakati? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, umeme ni huduma, lakini pia umeme ni biashara. Inakuaje mji mpya unapoanzishwa watu wamekaa wanahitaji huduma ya umeme lakini hawaipati kwa wakati? Serikali mnahujumu shirika hili? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tunza kwa niaba ya Mheshimiwa Cecil Mwambe na swali lake la kwanza limejielekeza kwa Mkandarasi anayefanya Mradi huu wa REA Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza ambaye kwa mujibu wa jibu langu la msingi nimemtaja, JV RADI Services.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maelezo ya Mheshimiwa Mbunge, nataka nimthibitishie kwamba mkandarasi huyu siyo kwamba ana tatizo la usajili, ni utaratibu wa kawaida wa kuhakiki ambao upo ndani ya Serikali. Kuna jumla ya Wakandarasi sita katika Mradi huu wa REA Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza ambao uhakiki wao unaendelea kwa vyombo mbalimbali.
MheshimiwaMwenyekiti, kwa hiyo, naomba wakazi wa Mtwara wavute subira kwamba hivi karibuni tu uhakiki huo utakamilika na ataendelea na kazi. Sambamba na hilo, pamoja na uhakiki huo, huyu mkandarasi alipewa mkataba kwa mujibu wa taratibu, lakini pia ameanza kazi. Kuna vijiji kama vitatu Mtwara Vijijini amewasha umeme, anaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, kwa maeneo ya miji ambayo inakua, Mheshimiwa Mbunge ameeleza kwamba upatikanaji wa umeme au uunganishwaji wa miundombinu ya umeme unakuwa ni shida.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge na kama ambavyo tumewasilisha bajeti yetu jana, kuna miradi mbalimbali ambayo Serikali imeona ianze kutekeleza ili kukidhi mahitaji ya umeme katika miji inayokua. Mfano, kuna mradi unaokuja peri-urban Awamu ya Kwanza utakaoanza mwaka wa fedha 2018/2019. Pia hata densification ya awamu ya pili ambayo ni kwa mikoa 11 ikiwemo Mtwara, Dodoma, Kagera, Singida, Lindi, Kilimanjaro, itaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, Serikali imeliona hilo kwa kuwa kazi ni nyingi na tumeona tuisaidie hilo liweze kuendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)
MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kusisitiza kwamba Awamu ya Tatu ya REA ni awamu ya kuwasha Tanzania nzima na kwamba umeme utakapokwenda vijijini hakuna hata kaya itarukwa. Ni ukweli kwamba usambazaji huu unapofanyika vipo vitongoji au vijiji coverage inakuwa ni ndogo sana. Mfano Kijiji cha Gwangali kule Karatu, kati ya vitongoji vitano, ni vitongoji viwili tu ndiyo umeme umevifikia. Nini kauli ya Serikali juu ya wakandarasi hawa ambao hawazingatii maelekezo ya Serikali?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Karatu, ambaye ameuliza nini kauli ya Serikali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu jana kupitia hotuba ya bajeti yetu ya Wizara ya Nishati, tumesema kinagaubaga kwamba mkakati wa Serikali ni kuhakikisha vijiji na vitongoji vinafikiwa na huduma ya umeme. Kwa hiyo, tumetoa rai kwa wakandarasi. Kwa mujibu wa hotuba yetu, tumesema kutokana na mpango huo na ndiyo maana kuna vijiji vya nyongeza 1,541 ambavyo tunavifanyia uhakiki. Kwa hiyo, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, nia ya Serikali ni kufikisha umeme kadri inavyowezekana. (Makofi)
MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi, naomba kuuliza swali dogo la nyongeza.
Pamoja na kazi nzuri ambayo inafanywa na Wizara ya Nishati katika kusambaza umeme vijijini, lakini zipo taarifana hali halisi ndivyo ilivyo kwamba REA Awamu ya Tatu inasuasua sana kwa madai kwamba wakandarasi hawajalipwa pesa zao. Sasa ni lini Serikali itawalipa pesa zao ili wakandarasi hawa waongeze kasi ya kusambaza umeme kama ambavyo Serikali imeahidi hapa ndani ya Bunge?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na napenda nimthibitishie Mheshimiwa Nape kwamba wiki mbili zilizopita Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Benki Kuu ilifungua Letter of Credit kwa makampuni zaidi ya 18 kiasi cha shilingi bilioni 260. Naomba nilithibitishie Bunge lako tukufu kwamba kuanzia sasa miradi ile itashika kasi kwa sababu tatizo la ufunguaji wa Letter of Credit limekwisha na Benki Kuu imefanya kazi yake na ninapenda niishukuru sana. Ahsante. (Makofi)
MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Mikumi ni Jimbo la kitalii na kuna wawekezaji wengi sana wamejenga mahoteli kule katika Jimbo la Mikumi katika maeneo ya Kikwalaza, Tambukareli pamoja na kule Msimba, lakini mpaka leo wanatumia majenereta na hawana umeme. Je, Serikali haioni umuhimu wa kupeleka umeme maeneo hayo ili kuwawezesha wawekezaji wetu waweze kuwekeza katika sekta hii muhimu ya utalii?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii, kama ambavyo nakumbuka naye Mheshimiwa Haule anakumbuka, Bunge lako hili hili aliuliza swali la msingi kuhusu upelekaji wa umeme katika Jimbo lake. Napenda nimthibitishie kwamba majibu tuliyotoa ya upelekaji wa umeme wa Awamu ya Tatu na kwa maeneo aliyotaja ambayo yanahusiana na masuala ya utalii, Serikali ya Awamu ya Tano italifanyia kazi. Namwomba aiunge mkono bajeti yetu leo, tuendelee kufanya kazi. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri wa Nishati alifanya ziara katika Jiji la Arusha tarehe 18 Machi na alifanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Mkonoo, Kata ya Terat na kuwaahidi hadi kufikia mwezi Aprili, umeme wa REA utakuwa umeshaanza kushughulikiwa, lakini sasa ni Mei hakuna chochote kinachoendelea, je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake kwa wananchi hawa wa Mkonoo, Kata ya Terat? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa, ni kweli Mheshimiwa Waziri alifanya ziara katika Kata hiyo ya Terat na kwa kuwa Mkoa wa Arusha Mkandarasi wake NIPO ambaye anafanya kazi vizuri alitoa maelekezo hayo na kwa kuwa mkandarasi NIPO ni mmojawapo wa Wakandarasi ambao wamefunguliwa Letter of Credit na ameagiza vifaa, ninaamini kwamba kazi itafanyika. Kwa hiyo, napenda nimwagize Mkandarasi NIPO wa Mkoa wa Arusha atekeleze agizo la Mheshimiwa Waziri na kwamba mwezi huu wa tano unaoendelea mpaka mwezi wa sita umeme uwe umewaka katika maeneo haya ambayo yameainishwa. Nampongeza sana Mheshimiwa Catherine. (Makofi)
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Mheshimiwa Naibu Waziri anasema mshauri elekezi ataanza kazi mwezi Julai na itachukua kama miezi saba. Sasa nataka atuhakikishie watu wa Mafia, baada ya miezi saba ya mshauri kumaliza kazi, je, ujenzi rasmi wa hizi hybrid utaanza lini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa sasa hivi kuna tatizo kubwa sana Mafia la kukatikakatika umeme na vyanzo ni vya mafuta, hivyo vimekuwa havitoshelezi na kwa kuwa Mikoa ya Lindi na Mtwara imeshaingizwa kwenye Gridi ya Taifa na kuna majenereta pale kama manane hivi ya two megawatts, je, Mheshimiwa Naibu Waziri haoni sasa kwa kipindi hiki cha mpito wakati tukisubiri hizo jitihada nyingine kuwa tayari, tupatiwe angalau majenereta mawili yale ya Lindi na Mtwara?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa. Mheshimiwa Mbaraka Dau, swali lake la kwanza ameuliza baada ya upembuzi yakinifu kuanza na kukamilika, nimthibitishie kwamba ni kweli mradi huo utaanza ndani ya hiyo miezi saba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumweleza Mheshimiwa Dau kwamba kwa mujibu wa swali langu la msingi tumesema kabisa kwamba Benki ya Maendeleo ya Ufaransa imeonesha nia ya kufadhili mradi huu na kinachosubiriwa ni upembuzi yakinifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa eneo tumelipata na kazi itaanza mwezi wa saba, naomba nimthibitishie kwamba kwa kudra za Mwenyezi Mungu kwa kipindi cha miezi saba hiyo na kwa kuwa tunayo benki tayari imeonesha nia, kazi hiyo itaanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, ameuliza kwamba sasa baada ya mafanikio makubwa ya kuunganisha Mikoa ya Mtwara na Lindi kwenye Gridi ya Taifa, amewasilisha ombi kwa niaba ya wananchi wake na naomba nimpongeze, ni lini kwamba tunaweza tukapeleka yale majenereta?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme kama Serikali tumelipokea hilo jambo lake na linazungumzika, lakini kwa sasa tunajaribu kwa sababu uzinduzi wenyewe wa kuunganisha umeme wa gridi umefanyika tu juzi, tunajaribu kuangalia upatikaji wa umeme baada ya kuunganisha mikoa hii kwenye gridi, lakini hapo baadaye tutakapoona umeme umetulia unapatikana kwa ukamilifu, basi nalo linazungumzika na tutalipokea. Ahsante. (Makofi)
MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusu umeme kupelekwa Mafia, naomba kujua nini harakati na mkakati wa Serikali wa kupeleka umeme katika Visiwa vya Jibondo, Chole na Jiwani huko huko Mafia? Kwa sababu Jibondo, Chole na Jiwani vyote hivyo ni visiwa ndani ya Kisiwa kikuu cha Mafia. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa, kwa kuwa REA kupitia miradi ya kupeleka umeme vijijini upo mradi wa kupeleka umeme katika maeneo ya off-grid ikiwemo visiwa; visiwa alivyovitaja Jibondo, Jiwani na Chole vipo katika mkakati huo na kama miezi minne iliyopita REA ilifanya tathmini katika maeneo mbalimbali ya visiwa vikiwemo Visiwa vya Kibiti, Mkiongoroni, Mbuchi, Salale, Saninga, Koma na maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka nimthibitishie mradi huo upo na bahati nzuri wafadhili ambao ni Serikali ya Norway pamoja na Sweden wapo ku-support maeneo yote ya visiwa ikiwemo hata Visiwa vya Ukerewe na maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilithibitishie Bunge lako tukufu kwamba mradi huo upo. (Makofi)
MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE: Mheshimiwa Spika, kwanza naishukuru sana Wizara na Waziri wa Nishati na Madini, kwa jibu zuri sana ambalo ametupatia.

Mheshimiwa Spika, nina maswali madogo mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, katika maeneo ambayo tayari yamepatiwa umeme kule vijijini, wako wananchi wengi sana ambao bado hawajapatiwa umeme kinyume na ahadi ambazo tumepewa hapa Bungeni kwamba kila mmoja atakayepitiwa na nguzo au waya za umeme na yeye atapata umeme. Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba hawa watu ambao wamepitwa bila kufungiwa umeme wanafungiwa umeme kama wenzao waliofungiwa awali?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika Tarafa yetu ya Jipe ambayo ina urefu wa kilomita 70 kuanzia mwanzo mpaka mwisho, viko vijiji viwili ambavyo bado havijahudumiwa na mradi wa REA ambavyo ni Vijiji vya Kwanyange na Karambandea. Serikali ina mpango gani wa kuvihudumia vijiji hivi na kuvipatia umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza napenda nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri anayofanya katika Jimbo lake. Nilifanya ziara mwaka jana mwezi kama huu niliona namna ambavyo anashughulika na kero za Nishati katika Jimbo lake.

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza ni kwenye maeneo ambayo yamepitiwa na miundombinu ya umeme mkubwa lakini baadhi ya wananchi hawajapata kuunganishiwa umeme, napenda nimtaarifa Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imepanga Mradi wa Ujazilizi Awamu ya Pili baada ya mafanikio ya Mradi wa Ujazilizi Awamu ya Kwanza.

Mheshimiwa Spika, Mradi huu wa Ujazilizi Awamu ya Pili ambao utaanza Machi, 2019 unahusisha mikoa tisa ya awali ikiwemo Mkoa wa Kilimanjaro lakini baadaye mwezi Julai, 2019 tutaanza Awamu ya Pili katika mikoa iliyosalia. Kwa hiyo, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wananchi ambao hawajapata umeme katika vijiji ambavyo miundombinu ya umeme imefika kupitia Mradi wa Ujazilizi watafikiwa na huduma hii ya nishati.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili linahusiana na vijiji katika Tarafa ya Jipe ambapo Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe, Mbunge wa Jimbo la Mwanga anasema bado havijafikiwa na miundombinu ya umeme. Nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba licha ya Mradi wa Ujazilizi, Serikali pia kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza Mradi wa REA Awamu ya Tatu mzunguko wa pili ambapo upembuzi yakinifu umeanza na hivyo vijiji viwili vitafikiwa na miundombinu ya umeme baada ya mradi huo kuanza. Ahsante.
MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Hadi sasa Wilaya ya Mbogwe ni vijiji 28 tu ambavyo tayari vina umeme na REA awamu ya tatu inajumuisha vijiji 28 pia. Sasa hapa nataka kuuliza Serikali kama vile vijiji vya REA awamu ya tatu na vyenyewe vitahusishwa katika hii Densification?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, vijiji 31 haviko kabisa katika mpango wa REA awamu ya tatu: Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba vijiji 31 vya Wilaya ya Mbogwe ambavyo havijapata umeme vinapatiwa umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu maswali ya nyogeza ya Mheshimiwa Masele. Maswali yake mawili yalijielekeza kwanza kwenye mradi unaendelea wa REA awamu ya tatu katika vijiji 28. Alikuwa anauliza je, huu mradi wa ujazilizi utafika katika maeneo hayo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge ametaja kwamba katika Jimbo lake kuna vijiji 28 vina umeme na anaamini katika vijiji hivyo vipo Vitongoji ambavyo havikuguswa katika miradi ya REA awamu ya kwanza na awamu ya pili. Kwa hiyo, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba mradi wa ujazilizi utaelekea kwenye maeneo yale ya vijiji 28 ambapo kuna Vitongoji havikufikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge ameulizia vijiji 31 katika Jimbo lake ambavyo havina umeme. Nataka nilitaarifu Bunge lako Tukufu na wananchi wa Jimbo la Mbogwe ambapo Mheshimiwa Mbunge anafanyia kazi nzuri kwamba vijiji 31 vitaingia kwenye mradi wa REA awamu ya tatu mzunguko wa pili na sasa kazi hiyo imeanza na ameshapokea hiyo orodha na mchakato unaendelea na mradi huu unatarajia kuanza mwezi Julai, 2019 ahsante.
MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Naibu Spika, asante sana. Kwanza nioneshe masikitiko yangu makubwa sana kwa Jimbo lenye chanzo kikubwa cha umeme kama Kidatu lakini pia ni Jimbo la Utalii kuwa na vijiji kama 57 lakini ni 16 tu ambavyo vina umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la kwanza, ni kweli mkandarasi kweli State Grid yuko kule site na kwa muda mrefu ameonekana kuchimba mashimo na sasa hivi hajaonekana kwa sababu anasema kwamba ana tatizo la
nguzo. Je, ni lini maeneo haya ya Zombo, Ulaya, Muhenda, Tindiga, Vidunda, Uleling’ombe, Kilangali na Mwinsagala wataweza kupata umeme?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali na mbili, kwa kuwa kuna maeneo ambayo kuna nguzo na umeme umepita lakini maeneo hayo hayajapata umeme, mfano maeneo ya Ruaha Darajani, Kikwalaza, Mshimba lakini pia maeneo ya Ruhembe na Tambuka Reli, Kipekenya na maeneo ya Malolo. Je, ni lini serikali itawapatia umeme wananchi wa maeneo hayo kama ilivyofanya kwenye maeneo ya Nyanda za Juu Kusini.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Mheshimiwa Mbunge kwenye swali lake la kwanza la nyongeza amejielekezea katika kazi zinazoendelea katika Jimbo lake kupitia mkandarasi State. Amesema mkandarasi alionyesha kuna tatizo la nguzo, naomba nimtaarifu mkandarasi huyo nimewasiliana naye asubuhi hii na kwamba kweli kulikuwa na tatizo la nguzo. Lakini Serikali kupitia Mheshimiwa Waziri Mkuu na uongozi wa Mkoa wa Iringa ulifanya kikao kikubwa na ulifikia makubaliano na sasa wakandarasi wote nchi nzima wanapata nguzo na ninavyozungumza takribani nguzo 4000 zimeshaenda katika maeneo mbalimbali ikiwemo katika eneo la Mkoa wa Morogoro.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, kwamba mkandarasi yupo katika Mkoa wa Morogoro na anaendelea na kazi na Mheshimiwa Mbunge amekiri na kwa kweli kwa kuwa nguzo zimeruhusiwa na hivi asubuhi nilivyokuwa nawasiliana naye, mkandarasi ametoa taarifa ya kwamba anaendelea kwenye maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge umeyataja kwenye swali lako la msingi na kwamba pia alikuwa ameagiza mita takribani 3000 na karibu zinafika mwezi wa pili Dar es Salaam. Kwa hiyo, kazi ya uunganishaji katika vijiji hivyo itaendelea vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili umejielekeza katika maeneo ambapo kuna miundombinu ya umeme kwa mfano Ruaha Darajani, lakini wananchi hawajaunganishiwa umeme. Nataka nikutaarifu Mheshimiwa Mbunge Serikali yetu ya Awamu ya Tano imekuja na mradi mwingine wa ujazilizi awamu ya pili ambao utaanza Machi, 2019 kwa gharama ya shilingi bilioni 197 na wafadhili wa Norway, Sweden na Serikali ya Ufaransa pamoja na Serikali ya Tanzania na mradi huu unaanza Machi kwa mikoa yote 26.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka nitoe wito kwa TANESCO na REA kubainisha vitongoji zaidi ya 1000 na vijiji ambavyo vimepitiwa na miundombinu ya umeme mkubwa lakini hawajaunganishiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, nichukue fursa hii pia kutoa wito kwa wananchi wote ambao miradi imekamilika ya Densification Awamu ya Kwanza ya Mradi wa BTIP Iringa – Shinyanga na mradi wa Makambako – Songea kulipia shilingi 27,000 na kuunganishwa umeme. Kwa sababu taarifa ambazo tunazo inaonekana wananchi wa maeneo hayo wengi bado hawajalipia na miradi ile inakaribia kukamilika. Kwa hiyo, nitoe wito walipie mapema ili kuepuka gharama wakati miradi itakapokabidhiwa TANESCO.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali, ila nina maswali mawili ya nyongeza. moja ya Kampuni zilizoomba kujenga mtambo wa kuchenjua shaba pale Mbesa ni Metalicca Commodities Corporation ya Marekani ikishirikiana na Minerals Access System Tanzania (MAST) lakini ni muda mrefu toka wameomba na majibu hayatolewi kutokana na kuchelewa kwa mwongozo. Je, Serikali mpaka sasa imefikia wapi kutengeneza mwongozo mzuri ukizingatia shaba ina tabia tofauti na madini mengine ili kuwezesha wawekezaji hao walioomba kupata kibali cha kuweza kujenga mitambo yao?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kumekuwa na leseni nyingi sana za utafiti zilizotolewa na Serikali kwa kampuni tofauti mbalimbali kwa muda mrefu na wamekuwa wanakaa kwa muda mrefu bila kuweza kuendeleza maeneo hayo:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwanyang’anya au kufuta leseni zile za utafiti kwa yale makampuni ambayo yamekaa muda mrefu na badala yake maeneo yale kupewa wachimbaji wadogo ili waweze kujikimu na kujitafutia riziki kwa njia ya kuchimba madini katika maeneo hayo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kwamba Serikali imetoa mwongozo na mwongozo wenyewe umetoka tarehe 25, Januari, unaoonesha aina zote za madini yanaweza yakachenjuliwa katika kiwango gani na baada ya kuchenjuliwa yanapewa sasa ruhusa (permit) kwa ajili ya kusafirisha kupeleka nje ya nchi. Kwa hiyo, kwa kila aina ya madini tumetoa mwongozo huo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge afuatilie tu na aone kwamba sasa wale wawekezaji wanaokuja ambapo sisi tumejipanga kutafuta mwekezaji ambaye kweli yuko serious na kampuni zimekuja zaidi 11 wameonesha nia ya kuwekeza kwenye smelter, tunataka tuwawekee kampuni ambazo tuna uhakika nazo kwamba zinaweza kuwekeza kwenye kuchenjua au kuyeyusha zile shaba kwa maana ya smelter.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kuhusu hizi leseni za utafiti za makampuni mbalimbali, ni kwamba mpaka sasa hivi, katika meza zetu tunapitia leseni zote ambazo zinaonesha ni leseni zilizotolewa mwaka gani. Tunataka kuangalia status zake zikoje? Tunapitia leseni ambazo zinafanyiwa kazi; lakini zile leseni ambazo ni za PL walipewa makampuni mbalimbali, wengi tumeona wameshikilia maeneo na hawafanyi kazi yoyote. Sasa hivi Wizara yetu tunapitia leseni zote. Kwa kampuni ambayo haifanyi chochote katika leseni ambazo tumewapatia, tunakwenda kuzifuta.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kwa leseni ambazo tumewapa watu kwa ajili ya uchimbaji kwa maana ya Primary Mining License, Mining License, Special Mining License na zenyewe tunaangalia kwa mujibu wa sheria na taratibu. Kama umekuwa na leseni huwezi kuifanyia kazi, sisi Wizara ya Madini muda siyo mrefu tutawapa default notice na tunakwenda kuzifuta leseni zote.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
MHE. AUGUSTINO V. HOLLE: Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa kama Mkoa bado hatujaunganishwa kwenye Grid ya Taifa na kumekuwa na tatizo kubwa sana la kukosa nishati hii muhimu na kupelekea mkoa wetu kuwa miongoni mwa mikoa maskini; sasa je, Wizara ya Nishati imejipangaje vipi kuhakikisha kwamba inakamilisha kwa haraka na kwa ufanisi mradi wa REA awamu ya tatu katika Mkoa wa Kigoma ambao kimsingi umezinduliwa muda umeenda sana katika Kijiji au Kata ya Lusese? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri ya kufuatilia changamoto ya nishati. Ni kweli Mkoa wa Kigoma pamoja na Mkoa wa Katavi kazi za upelekaji umeme kupitia mradi wa REA awamu ya tatu mzunguko wa kwanza zilichelewa kutokana na matatizo ambayo yalikuwa nje ya uwezo wa Wizara yetu ya Nishati pamoja na Wakala wetu Vijijini. Hata hivyo mradi huo umeshazindua rasmi na mkandarasi anaendelea na kazi ya survey na watakamilisha hivi karibuni.
Mheshimiwa Spika,aomba niwatoe hofu wakazi wa Mkoa wa Kigoma pamoja na Katavi kwamba kwa kweli kwa maelekezo ya Serikali na mkandarasi aliyeteuliwa ana uwezo na hivyo atafanya kazi kwa haraka iwezekenavyo nakushukuru. (Makofi)
MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kwanza kabisa ya kuuliza swali katika Bunge hili Tukufu.
Mheshimiwa Spika, nawashukuru sana wana-CCM wote popote walipo kwa kunikaribisha Chama cha Mapinduzi. Nawashukuru wananchi wa Ukonga kuendelea kuniamini, pia namshukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini kwa kuchukua baadhi ya maeneo ya Jimbo la Ukonga kuingiza kwenye umeme wa peri-urban; eneo la Mbondole, Kitonga, Chanika, Kibanguro, Viwege, Zingiziwa na Buyuni, Mgeule na Mgeule Juu vimeingizwa kwenye peri-urban. Sasa ningependa nijue, ni lini sasa maeneo hayo muhimu katika Jimbo la Ukonga kwa kuwaheshimu watu waliounga mkono juhudu za CCM watapata umeme haraka iwezekanavyo? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwita, Mbunge wa Jimbo la Ukonga kupitia Chama Cha Mapinduzi na nimpongeze sana kwa kushinda kwa kishindo katika uchaguzi huo. Kwanza ameishukuru Wizara yetu kwa namna ambavyo tumeingiza maeneo ya Jimbo lake la Ukonga kwenye mradi wa peri-urban.
Mheshimiwa Spika, lakini Mheshimiwa Mwita Waitara atakubaliana na mimi tulifanya ziara katika maeneo hayo katika maeneo mbalimbali ambayo ndiyo imekuwa kivutio cha kuipigia kura Chama cha Mapinduzi katika uchaguzi uliopita. Sasa kazi imeanza ya kupeleka umeme katika maeneo hayo kupitia TANESCO na kwa kupitia mradi wa peri-urban tuko katika hatua za kumpata mkandarasi na hivi karibuni kazi ambazo zimesalia katika maeneo mbalimbali zitakamilika. Hata baada ya Bunge hili pamoja na Mheshimiwa Mbunge tutawasha umeme katika maeneo ya Zingiziwa, Buyuni na Mbondole kutokana na kazi nzuri inayofanywa na Shirika la Umeme la TANESCO. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati, ninayo maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, dhamira ya wananchi lakini dhamira ya Serikali ya kupeleka umeme vijijini kwa maana ya REA utekelezaji wake umekuwa mdogo na unasuasua sana. Katika Jimbo langu kuna vijiji vya Kashangu, Jeje, Idodyandole, Ipangamasasi, Mbugani, Agondi, Mabondeni, Kitopeni, Ipande, Muhanga, Damwelu, Kitalaka, Kaskazi Station, Kintanula na Rungwa havina umeme. Je, nini kauli ya Serikali kwa wananchi wa vijiji hivi wategemee lini kupelekewa umeme? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa umeme wa Mkoa wa Singida unakwenda hadi katika Wilaya ya Manyoni pamoja na Itigi lakini hatuna substation ipo station moja tu kubwa kule Singida. Je, Serikali iko tayari sasa kuweka substation Itigi kwa ajili ya kuboresha miundombinu hii ya umeme? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Massare, Mbunge wa Jimbo la Manyoni Magharibi. Kwanza, nimpe pole kwa ajili ambayo aliipata na namwombea kwa Mwenyezi Mungu ampe afya njema. Pamoja na changamoto hiyo ya afya Mheshimiwa Massare ameendelea kulitumikia Jimbo lake hususani katika sekta ya nishati.

Mheshimiwa Naibu Spika, maswali yake mawili ya nyongeza, la kwanza lilijielekeza katika utekelezaji wa mradi huu wa REA III. Katika Wilaya ya Manyoni REA III, mzunguko wa kwanza kuna vijiji 30 na Jimbo lake lina vijiji 10.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge mkandarasi yupo anaendele na kazi katika maeneo ya Manyoni Mashariki katika Vijiji vya Majengo, Selia, lakini kwa kuwa, yeye Mheshimiwa Mbunge katika Jimbo lake la Manyoni Magharibi ameuliza utekelezaji, nataka nimtaarifu hata asubuhi hii nimeongea na mkandarasi, ameshaanza kupeleka vifaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka pia, nilitaarifu Bunge lako Tukufu kutokana na utatuzi wa changamoto ambazo zilikuwa zinaukabili mradi. Mradi vizuri, sasa hivi unaendelea vizuri kwa sababu, mpaka sasa tunavyozungumza mpaka Januari vijiji takribani 5766 vimeshapata umeme kutokana na utekelezaji wa mradi huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge ameulizia juu ya ujenzi wa substation katika eneo la Itigi Manyoni:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba, Singida tuna substation. Kutokana na mipango ya Serikali na ujenzi ulioanza wa line ya Kv 400 kutoka Singida mpaka Namanga, Serikali ina mpango wa ku-upgrade Kituo cha Singida. Kwa hiyo, nataka nimtaarifu kwamba, kutokana na matengenezo yatakayoendelea tutakipandisha hadhi Kituo cha Singida, ili kuhimili umeme mkubwa utakaosafirishwa mpaka Namanga, hivyo ni wazi kwamba, Mkoa mzima wa Singida kuhusu changamoto ya labda pengine usafirishaji wa umeme haitakuwpo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namwomba tu Mheshimiwa Mbunge aendelee tu kuiunga mkono Serikali, mipango ya kupandisha hadhi substation ya Singida inaendelea. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Naomba kujua mara nyingi nimekuwa naongea Vijiji vya Manispaa ya Mtwara Mjini nimekuwa nikivitaja vijiji hivi katika Bunge hili miaka yote mitatu na Serikali ikiwa inaahidi kwamba, inatekeleza suala la kupeleka umeme. Vijiji hivi ni Mkangara ambako Naibu Waziri alishaenda kule na akaona hali halisi, Naulongo, Mkunjanguo, Namayanga na maeneo…

NAIBU SPIKA: Uliza swali Mheshimiwa Maftah, uliza swali.

MHE. MAFTAH A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujua kwa nini Serikali haitaki kutenga bajeti ili kupeleka umeme katika vijiji hivi au mitaa hii?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maftaha kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo yeye mwenyewe amekiri kwenye swali lake la nyongeza kwamba, mimi hata pamoja na Waziri wa Nishati tumeshafanya ziara zaidi ya mara mbili katika Mkoa wa Mtwara. Maeneo ambayo ameyataja ikiwemo Mkangara, Chipuputa na Mheshimiwa Mbunge atakubaliana na mimi hata TANESCO Mkoa wa Mtwara imekuwa ikijitahidi kufanya miradi. Nilipofanya ziara mwaka jana zaidi ya mitaa saba TANESCO imefanya miradi, lakini kwa eneo maalum ambalo ni maeneo aliyoyataja yameshaingia kwenye mpango wa utekelezaji wa mradi wa ujazilizi unaoanza Machi, 2019.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, hata alipofanya ziara Mheshimiwa Waziri wa Nishati pia ametoa maelekezo yale ambayo tuliyaelekeza siku za nyuma na kwa kuwa Mtwara imepitiwa na bomba la gesi na Serikali ilitoa punguzo kwa ajili ya kuwasambazia umeme wananchi wa maeneo ya gesi na mitaa mingi ipo katika Mtwara Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge ambaye amekuwa akifuatilia mara kwa mara kwamba, vijiji, mitaa aliyoitaja na vijiji katika Manispaa ya Mtwara Mikindani na maeneo ya Mtwara vitapatiwa umeme na kazi zinaendelea na mradi wa ujazilizi utaanza mwezi Machi, 2019. Ahsante sana.
MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, ripoti ya UNDP inatahadharisha kwamba vita nyingine ya ulimwengu katika siku zinazokuja itakuwa ni maji, pamoja na chakula na kwa sababu, umeme unaotumia mionzi ya jua umethibitika kote ulimwenguni kwamba ni umeme muafaka, ni kwa nini Serikali sasa isi-concentrate kwenye umeme huu, ambao katika Taifa letu la maeneo mengi sana, ambao ni almost…

MWENYEKITI: Swali Mheshimiwa Lema.

MHE. GODBLESS J. LEMA: Swali langu ni kwa nini Serikali isi-concentrate sasa, kwenye umeme huu na ikaachana na umeme wa maji ambao sehemu kubwa inakwenda kuleta uharibifu wa mazingira.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Godbless Lema kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake, amejielekeza, kwa nini Serikali isijielekeze zaidi kwenye umeme huu, unaotokana na jua, kwenye jibu letu la msingi tumeainisha jitihada ambazo Serikali imefanya. Tumesema kutokana na Power System Master Plan yetu kwamba tunatakiwa tuzalishe zaidi ya MW 350 kwenye Power System Master Plan na nikaeleza kwamba hata kazi yenyewe imeanza, TANESCO wametangaza Tender kwa ajili ya MW zaidi ya 200 kwenye upepo na 150 kwenye jua, lakini ukiacha mradi huu wa Kishapu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, Serikali imejielekeza kuhakikisha kwamba nishati jadidifu ina mchango mkubwa katika kuzalisha umeme, licha tu ya kwamba umeme wa jua, lakini kuna umeme wa makaa ya mawe ambao tumetangaza wa MW 600, licha ya huo pia umeme unaotokana na jotoardhi, tunatarajia kuzalisha MW 200, katika kipindi hiki, hii Power System Master Plan.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile amesemea kwenye miradi ya maji, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, tafiti zimefanyika za kina kuainisha sustainability ya miradi yote ya umeme inayotokana na miradi ya maji, lakini kwa kutambua miradi ya umeme, inayozalishwa kwa maji na gharama nafuu, zaidi zinatumika shilingi 36 kulinganisha na umeme wa upepo ambao ni shilingi 103; umeme wa jua, shilingi 103 kwa per unit kilowatts; lakini pia umeme unaotokana na makaa ya mawe 108. Kwa hiyo masuala haya ni zaidi kulinganisha gharama kwa sababu nia ya Serikali ni kumpatia Mtanzania umeme wa gharama nafuu na wa uhakika. Ahsante sana.
MHE. LUCY S. MAGERELI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amekiri mwenyewe kwamba tatizo hili lipo Kigamboni na ni kubwa. Katika majibu yake unaona anaeleza kabisa kwamba umeme unaopatikana Kigamboni unakidhi kuhudumia wateja 12,000 tu, wakati wakazi wa Kigamboni ni zaidi ya 300,000.

Mheshimiwa Spika, nimekuwa nikifuatilia suala hili tangu mwaka 2016 Mheshimiwa Muhongo akiwa Waziri wa Nishati, majibu ni haya haya. Mheshimiwa Mgalu yeye ni shahidi, nimeshakutana naye mara kadhaa tukijadiliana suala hili hili na majibu yamekuwa ni haya haya. Je Serikali ina nia thabiti ya kuondoa tatizo hili Kigamboni kweli?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika majibu yake Mheshimiwa Waziri ameonesha kwamba kuna ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha Kurasini cha KVA 132, ambacho anaeleza kwamba kinakamilika mapema Aprili, 2019. Tunavyozungumza leo ni mapema Aprili, 2019, je, kituo hiki kimekwishakamilika?
NAIBU WAZIRI NISHATI: Mheshimiwa Spika, katika swali lake la kwanza la nyongeza, Mheshimiwa Mbunge amesema kwamba majibu ni yale yale na nini mkakati wa Serikali. Nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge majibu si yale yale kwa sababu zipo hatua zinazoendelea na tatizo la kukatikakatika kwa umeme hususan siyo Kigamboni tu katika Jiji la Dar es Salaam, ni kutokana na kuongezeka kwa mahitaji na kuzidiwa kwa kituo cha Ubungo cha jumla. Nini Serikali imefanya; yapo matengenezo makubwa pia yanaendelea pale Ubunge ambapo kwa sasa kituo kile ambacho kilikuwa na uwezo wa kusafirisha umeme wa megawati 635 kwa ujumla kwa Mkoa wa Dar es Salaam na mahitaji yake ni megawati 500 lakini inapotokea kwa mfano kituo cha Songas, kituo cha Tegeta, kinapotokea matengenezo ya mtambo mojawapo lazima kunakuwa na upungufu wa umeme katika maeneo mbalimbali ikiwepo Kigamboni.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kwenye jibu langu la msingi nimesema kwamba hatua zilizochukuliwa zaidi ya bilioni 16 zimewekezwa katika kituo cha Dege; zaidi ya bilioni 1.5 zishatumika. Kwa hiyo, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge nia ya dhati ipo na si kwa Kigamboni tu, bali kwa maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Dar es Salaam na maeneo mengine.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge dada Lucy anaulizia kwamba ujenzi wa hiki kituo ambacho nimekitaja Dege nimesema mapema Aprili, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kituo hiki mpaka ifikapo tarehe 30 mwezi wa Aprili kitakuwa kimeanza kufanya kazi. Pia alisema kwamba umeme katika kituo cha Kigamboni kinahudumia watu 12,000, nataka nimtaarifu kituo cha Mbagala pia kinahudumia wakazi wa Kigamboni na umeme mwingine ambao unatokea Ubungo. Ahsante sana.
MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Naomba niulize swali dogo la nyongeza; kwa kuwa matatizo ya Wilaya ya Kigamboni yanafanana kabisa na matatizo ya Wilaya ya Mvomero; kwa kuwa katika Wilaya ya Mvomero, Kata ya Kibati kuna tatizo kubwa sana la msongo wa umeme na hivi ninapozungumza leo hapa Bungeni hakuna umeme Kibati kutokana na transfoma ya Kibati kuungua kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa na wananchi wa Kibati wako gizani.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kufanya ziara na mimi Kibati ili kuondoa tatizo hili ambalo wananchi wanateseka?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Murad Saddiq, Mbunge wa Mvomero kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza tumepokea hiyo changamoto ambayo anasema katika Kata ya Kibati transfoma imeharibika, si tu kwamba inahitaji nifanye ziara bali inatakiwa wananchi hawa wapate huduma haraka, kwa hiyo naiagiza TANESCO Mkoa wa Morogoro suala la kuharibika kwa transformer halisubiri ziara, inatakiwa wafanye matengenezo haraka iwezekanavyo ili huduma iendelee.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, nataka nilisemee kwa ujumla; nimesema kwamba kuna matengenezo makubwa yanafanyika Mkoa wa Dar es Salaam kituo cha Ubungo ambacho kinapokea umeme kutoka Kidatu kwa njia ya msongo kilovoti 220 ambao unafika Morogoro unapoozwa unapelekwa Dar es Salaam. Kwa hiyo, matengenezo ya Dar es Salaam kwa kweli yana athari za moja kwa moja na upungufu wa Mkoa wa Morogoro, Mkoa wa Pwani na Mkoa wa Tanga; nichukue fursa hii kuwapa pole wakazi wa mikoa hii na kuwaomba radhi, lakini tuvumilie mwezi Aprili, mwaka huu 2019 yakikamilika matengenezo yale makubwa ambapo yamegharimu zaidi ya bilioni 32 hali itatulia.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Tatizo la kukatika kwa umeme limekuwa linajitokeza sana kwenye Visiwa vya Ukerewe hali inayoathiri shughuli za kiuchumi na hasa shughuli za utoaji wa huduma za afya kwenye hospitali yetu ya Wilaya ya Nansio.

Ningependa kupata kauli ya Serikali, ni mkakati gani uliopo kuondoa tatizo hili na kufanya Visiwa vya Ukerewe vipate umeme bila shida ya kukatikakatika kwa umeme kwenye maeneo hayo. Nashukuru sana.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mkundi Mbunge wa Ukerewe kupitia Chama cha Mapinduzi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Mheshimiwa Mbunge aliwasilisha hilo leo asubuhi kwamba kuna tatizo hilo katika Visiwa vya Ukerewe na hapa nilipo nishatoa maelekezo kwamba kwa sababu umeme wa Ukerewe unatokea katika maeneo ya Bunda na kwa changamoto ambayo nimeipata hivi asubuhi baada ya kuwasiliana na Meneja kwamba kuna tatizo la changamoto ya nguzo, ndiyo maana Serikali imefanya maamuzi ya kuhama sasa itumie nguzo za zege.

Kwa hiyo, tumetoa maelekezo ifanyike utafiti wa kina changamoto ni nini ili ifanyiwe kazi, kwa hiyo namwomba Mheshimiwa Mbunge baada ya kutoka hapa tufanye mazungumzo ili kuweza kumpa mikakati ambayo Serikali imepanga. Ahsante.
MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mbunge wa Jimbo la Kibiti Mheshimiwa Ally Seif Ungando na wananchi wa Kibiti, napenda kuipongeza na kuishukuru Serikali kwa juhudi ilizofanya, lakini pamoja na hayo, nina maswali mawili. Kwa kuwa umeme umeshafikia hatua hiyo ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri ameielezea, ningependa kujua ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye maeneo ya Nyatanga, Kingwira, Zimbwini, Runyozi na Makaoni?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa Serikali iliahidi kaya 90 katika eneo la Kitembo na katika kaya hizo 90, kaya 40 bado hazijapata umeme, ningependa kujua Serikali imejipangaje katika hilo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge Zainab Vullu, Mbunge mwenzangu wa Viti Maalum wa Mkoa wa Pwani.

Katika maswali yake mawili ya nyongeza, amepongeza kwa niaba ya Mheshimiwa Mbunge Ally Seif Ungando na mimi nimepokea kwa niaba ya Wizara, kwa kazi ambayo inaendelea katika maeneo ya Wilaya ya Kibiti na katika maeneo mbalimbali, lakini ameulizia maeneo ya Nyatanga, Zimbwini, yatapata lini umeme. Nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge mama Vullu kwamba katika REA III mzunguko wa pili unaoendelea, maeneo haya yameingizwa katika orodha na kazi inatarajiwa kuanza 2019 mwezi wa Saba. Nalitarajia Bunge hili wakati wa kuwasilisha Bajeti yetu ituunge mkono ili kazi ya kumaliza vijiji ambavyo vimesalia katika mradi wa REA III mzunguko wa kwanza viweze kufanyiwa kazi.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, ameelezea eneo la Kitembo nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na kumshukuru kwa sababu ni moja ya maeneo ambayo tunayatembelea kwenye ziara mimi pamoja na yeye Kitembo tumewasha umeme kama anavyosema, tumeshawaunganishia kaya 50, hizi kaya 40 kwa sababu mradi unakuwa na wigo wa wateja wa awali. Mradi unakuwa na kazi za awali, kaya zinazobaki TANESCO inaendelea na kazi yake ya kusambaza umeme. Kwa hiyo, naomba nielekeze TANESCO kuzingatia kwamba mradi unapokamilika na kukabidhiwa waendelee kuwasambazia umeme wananchi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali inaongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli imefanya uamuzi wa kisera, kwamba kwa sasa umeme utakaosambazwa na TANESCO, REA na wadau wowote, bei ya kuunganisha ni shilingi 27,000/=. Kwa hiyo hakuna kikwazo kingine kwamba kutakuwa na bei nyingine pengine shilingi 177,000/=, bei ni moja shilingi 27,000/=; kwa hiyo TANESCO waendelee na kazi ya kusambaza umeme katika maeneo mbalimbali ambao mradi wa REA umekamilika. Ahsante.
MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwenye Kata ya Kolo, Jimbo la Kondoa Mjini tulipata ufadhili mkubwa sana wa wenzetu wa MKAJI kwa ajili ya kukarabati Zahanati kwa lengo la afya ya mama na mtoto, na waliweka lengo kubwa sana mkazo mkubwa kwenye huduma ya maji, kimekarabatiwa kisima kirefu, kimemalizika sasa hivi takriban miezi mitatu. Kinachokwamisha ni supply ya umeme pale ili huduma hiyo iweze kuanza kutumika. Tumewaomba TANESCO Wilaya, TANESCO Mkoa mpaka sasa hivi bado tunasubiria. Je, ni lini sasa wenzetu wa TANESCO watatuletea ule umeme ili zoezi zima la wenzetu wa MKAJI lianze kuleta tija?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sannda, Mbunge wa Kondoa Mjini, kwamba hili swali lake ni zuri linahitaji utekelezaji, nimwahidi Mheshimiwa Mbunge baada ya kipindi cha maswali na majibu na ratiba ya Bunge tukutane na pia nitafanya ziara maalum na wataalam wa TANESCO katika maeneo hayo ili kuhakikisha kisima hiki kinapata huduma hii ili dhamira iliyotarajiwa kwa ujenzi wa zahanati na ukarabati hiyo iweze kufikiwa, ili iweze kupata maji na huduma iweze kutolewa. Ahsante.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri na kazi nzuri ambayo Wizara ya Nishati na Madini inafanya, sasa naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu ulianza toka mwaka 1998, mpaka leo ni takribani miaka 20. Namwomba Mheshimiwa Naibu Waziri, kama atakuwa tayari sasa kuambatana na Mheshimiwa Profesa Norman King Sigalla ili kwenda kujionea mwenyewe hali inayoendelea ili wananchi wa Makete ambako kumekuwa na matatizo mengi kule yanatokea na barabara hawana, waweze kuwa na imani na Serikali yao.

Swali la pili linalohusu umeme; kwa kuwa kilio na hamu ya Watanzania ni kuona umeme unapita kila sehemu: Je,
sasa, Mheshimiwa Naibu Waziri aliwahi kutoa ushauri kwamba sehemu ambako kuna miradi mikubwa na hakuna umeme, umeme uweze kupelekwa; kikiwepo Kijiji cha Iyai, ambako Mheshimiwa Naibu Waziri ulifika, Kijiji cha Kising’a, Winome, Nyanzwa, Ilindi, Msosa, Kitimbo na Ikula? Je, ni lini sasa Serikali itahakikisha hizo ambazo ilitoa ahadi yenyewe umeme unafika ili wananchi wale waweze kupata umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ya Mheshimiwa Mwamoto ameuliza kwa niaba ya Mheshimiwa Profesa Norman, kwamba ni lini nitakuwa tayari kutembelea Jimbo la Makete? Nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba tulifanya ziara Jimbo la Makete mwaka 2018 mwezi Desemba. Katika mambo mbalimbali ambayo nilishuhudia ni uwepo wa uhitaji wa umeme, lakini uwepo wa vyanzo vingi vya kuzalisha umeme hususan vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana Serikali kupitia agizo la Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, kwamba sasa mchakato wa ujenzi wa bwawa la Lumakali uanze na kwa hatua za awali tumepata mfadhili ambaye ni World Bank ambaye ana-support hatua hizi za kurudia tena upembuzi yakinifu kwa sababu ulichukua muda mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimthibitishie tu Mheshimiwa Mbunge kama jibu langu la msingi lilivyosema, kwamba mradi huu utaanza kama ilivyokusudiwa, mapema mwezi Januari, 2021, kwa sababu Serikali ina dhamira ya dhati ya kuongeza uzalishaji wa umeme kupitia chanzo hiki cha maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, Mheshimiwa Mbunge ameyataja maeneo. Ni kweli tumefanya ziara katika Jimbo la Kilolo zaidi ya mara tatu. Mwezi Machi, 2018, mwezi Novemba, 2018 na hivi karibuni tulikuwa na Kamati ya Bunge katika Jimbo lake katika maeneo ya Dinganayo, Ikuvala, lakini maeneo hayo pia tumewasha umeme na wiki hii tutawasha umeme katika maeneo ya Ngelango, Itungi na Mlavu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ameeleza jambo la msingi, kwamba kwa kuwa Serikali tulitoa maelekezo, maeneo yote ambako miradi hii ya umeme vijijini yanaunganishiwa, taasisi za Umma na hasa maeneo ya viwanda yapewe kipaumbele. Naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge, mara baada tu ya kujibu swali hili, naomba tukutane naye, tuelekee ofisini tuone namna ya kufuatilia na kwa kuwa amekuwa mfuatiliaji mzuri sana wa miradi ya nishati vijijini na hasa hili eneo la viwanda ambalo amelitaja, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, kabla ya mwaka huu wa fedha haujaisha, eneo hilo litakuwa limepatiwa umeme ili wananchi wale wapate ajira na pia Serikali ipate mapato kupitia vile viwanda. Ahsante sana.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza nafasi kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la umeme limekuwa na kasi na hali ni mbaya katika Jimbo la Mbulu Vijijini na Mheshimiwa Naibu Waziri amefika na vile vijiji alivyoahidi mpaka sasa umeme haujapatikana: Je, atatusaidiaje angalau umeme uweze kupatikana kwenye vijiji alivyoahidi Mbulu Vijijini?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nilitaarifu Bunge lako, kwamba miradi inayoendelea ya kupeleka umeme vijijini, miradi hii inachukua miezi 24. Kwa mujibu wa taratibu na kwa kuwa hizi LC (Letter of Credit) zilifunguliwa mwezi wa Saba mwaka 2018, naomba niwatie moyo Waheshimiwa Wabunge kwamba tunao muda wa kutekeleza huu mradi na kasi inaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Flatei amekuwa mfuatiliaji mzuri, msimamizi mzuri, nimeshafanya ziara kwenye Jimbo lake, Mheshimiwa Waziri ameshaenda, tutamsimamia karibu Mkandarasi ambaye anafanya mradi katika maeneo hayo na miradi itakamilika kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Mimi nina mambo mawili, la kwanza ni ombi, la pili ni swali.

Mheshimiwa Naibu Waziri, kwanza naipongeza Serikali. Hivi ninavyoongea leo, tangu siku ya Ijumaa na leo asubuhi Jumatatu watu wa KV 400 wako Babati eneo la Singu wakilipa wananchi fidia zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ombi langu kwa Serikali, kwa kuwa kuna sintofahamu kati ya wananchi na Mwekezaji katika shamba la Singu, wananchi walikuwepo tangu miaka ya 1970, mwekezaji amepewa hati mwaka 2011 na wananchi wanalipwa asilimia 34 leo ya ardhi. Hebu niiombe Wizara ya Ardhi, ilitazame hili jambo upya, waone kati ya wananchi na mwekezaji, ni nani mvamizi, ili haki itendeke wale wananchi walipwe asilimia 100 ya ardhi.

Swali sasa kwa Wizara ya Nishati. Mheshimiwa Naibu Waziri, siyo wananchi wote wanaolipwa, leo wanalipwa tu Sigino pale, lakini mtaa wa Sawe, Maisaka Kati, Kijiji cha Kiongozi na Malangi, wao cheki zao hazijaandaliwa mpaka sasa. Naomba nifahamu, ni lini Wizara ya Fedha na Mipango nao watamaliza kukamilisha cheki hizi ili na hao wananchi waweze kulipwa? Maana mazao yao yameshafyekwa na mradi unaendelea. Ni lini cheki zao zitafika?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo umesema, swali la kwanza ni ombi; lakini kabla sijaendelea, naomba nitoe pole kwa wakazi wa Mkoa wa Manyara, kufuatia kifo cha Meneja wa TANESCO wa Mkoa huo wa Manyara, pamoja na Meneja wa TANESCO wa Wilaya ya Mbulu ambao walifariki siku za hivi karibuni.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, napenda nijibu hili swali la pili, ambalo Mheshimiwa Pauline Gekul ameuliza Mitaa ya Sawe, Mwaisaka Kati, Kiongozi, lini watalipwa fidia zao? Kwa kuwa Wizara ya Fedha ilifanya uhakiki na kukabainika baadhi ya changamoto na ikapelekea sasa kupeleka watathmini wengine ambao walifanya mapitio; hivi ninavyosema, jedwali jipya ambalo linawasilishwa kwa Ofisi ya Mtathimini Mkuu wa Serikali, limeshafika Dodoma na Mtathimini Mkuu wa Serikali yuko katika hatua za mwisho za kusaini na kisha malipo yataandaliwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wake wa hili suala mara kwa mara, pamoja na wananchi wake. Nimwahidi tu kwamba, hili suala kwa kweli kwa kuwa amesema na yeye na sisi tumepokea pongezi, malipo yameanza kwa wakazi wa maeneo hayo ya Sawe, Mwaisaka Kati, Kiongozi, kwamba malipo yatafanyika siyo muda mrefu kuanzia sasa kama ambavyo jibu letu la msingi limesema. Ahsante.
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Tatizo la fidia lililopo Babati linafanana kabisa na tatizo la fidia lililopo katika mradi wa umeme wa Rusumo Wilaya ya Ngara. Je, ni lini wananchi wa Kata ya Mlukulazo na Mtobee watalipwa fidia kwa maeneo yao yaliyoathiriwa na mradi wa Rusumo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Oliver la masuala ya fidia katika mradi wa bwawa la kuzalisha umeme la Rusumo la megawati 80 pamoja na njia yake ya Msongo wa KV 220 kutoka Rusumo - Nyakanazi. Kwanza Mheshimiwa Mbunge Oliver nimpongeze kwa kufuatilia suala hili la malipo ya fidia; lakini kwa kuwa mradi umeanza na fidia ililipwa pengine wapo wananchi ambao wana malalamiko au bado hawajalipwa, naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge, baada ya hapa tu nitalifuatilia kuona wakazi wa Kata ya Mlukulazo na Kata nyingine ambayo ametaja kwamba wanalipwa stahiki zao kwa sababu mradi ule unaendelea mpaka sasa ambao una manufaa makubwa katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu ya Serikali ambayo yanaonekana kuchupachupa kwa baadhi ya mambo, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ni community based, kwa kuwa research ni suala la Muungano na 2018 ilifanywa research kule Zanzibar nzima, ndani ya harakati za wale vijana kufanya research waliwaharibia wananchi wetu mazao yao. Je, ukizingatia research ni suala la Muungano Serikali ya Jamhuri ya Muungano ina namna gani ya kurejea nyuma angalau kuwapa mkono wa pole wale waliowaharibia mazao yao?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Serikali imesema kwamba wamekubaliana mafuta na gesi kila upande ufanye kwa kutumia taasisi zake. Pamoja na Azimio ambalo limepitishwa na Baraza la Wawakilishi kule Zanzibar lakini bado suala la mafuta linabaki ni la Muungano. Je, hatuoni sasa ni wakati mwafaka sheria hii ambayo imo ndani ya Katiba ya Muungano kwamba mafuta ni suala la Muungano tukalitoa sasa ili kurahisisha uwekezaji kule Zanzibar?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Muhammed Amour Muhammed, Mbunge wa Bumbwini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa maswali mazuri. Swali lake la kwanza ameulizia namna gani Serikali ya Muungano inaweza ikawalipa fidia wananchi ambao mazao yao yaliharibiwa wakati wa utafiti. Kama lilivyosema jibu langu la msingi, utafiti huu ulifanyika kwa ajili ya masuala ya mafuta au gesi; na kwa kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Zanzibar kwa nia njema ilipofika mwaka 2015 Bunge hili lilipitisha Sheria ya Mafuta na kifungu cha 2 kilianisha kabisa mamlaka ambazo zitatumika katika suala zima la utafutaji mafuta ni kwa pande zote mbali na ni kwa nia njema ya kupunguza urasimu. Kwa kuwa shughuli hizi za utafiti za mafuta na gesi zilifanyika upande wa Zanzibar ambao wana mamlaka na walipitisha Sheria ya Mafuta ya mwaka 2015 labda nilichukue na kwa sababu tuna ushirikiano mzuri tutawasiliano na Wizara ya upande wa pili wa Muungano Zanzibar kuona hili jambo wanalifanyia kazi vipi lakini nia ilikuwa njema.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ameuliza kwa kuwa suala hili lilifanyika kwa nia njema kwa nini lisifanyiwe marekebisho. Jambo la kufanya marekebisho katika Katiba limeundiwa utaratibu wake ndani ya Katiba hiyo hiyo lakini kwa sasa kwa nia njema Bunge hili hili liliridhia kupitisha Sheria ya Mafuta ya mwaka 2015 na Baraza la Wawakilishi wakapitisha Sheria yao ya Mafuta ya mwaka 2016 kwa sasa shughuli zinaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nilitaarifu Bunge lako walikuwa mashahidi tarehe 23 Oktaba, 2018, Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar ilitiliana saini mkataba wa kugawana faida itakayopatikana wakati wa kuchimba mafuta au gesi na Kampuni ya RAK Gas kutoka nchi ya Ras Al Khaimah. Kwa hiyo, ni wazi kwamba tangu waingie mkataba huo kazi inaendelea na hakujatokea mgongano. Hata hivyo, hili naomba niliachie mamlaka zingine na Bunge hili kama itaona inafaa. Ahsante sana.
MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mbunge wa Jimbo husika Mheshimiwa Lijualikali anakubali kwamba ni kweli kazi inafanyika, lakini changamoto iliyopo ni kwamba umeme unawekwa kwa kurukaruka. Wakishafikisha kwenye centre vitongoji vingine havipati na kutoka kwenye centre kwenda kwenye vitongoji vingine kuna umbali mpaka wa kama kilomita sita mpaka kilomita nane, suala ambalo baadaye litakuwa gumu kwa wananchi kupeleka umeme katika hivyo vitongoji vingine.

Swali lake ni kwamba: Je, Serikali haioni umuhimu wa kuboresha usambazaji wa umeme kuhakikisha kwamba wanapopeleka kwenye kijiji basi wasambaze katika maeneo yote na vitongoji vyote vya kijiji hicho?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, naomba pia niulize kwa niaba ya wananchi wa Halmashauri ya Geita Mjini ambako mimi natoka. Serikali ilituahidi ndani ya Bunge kwamba kuna maeneo ambayo yamekuwa mitaa sasa na zamani yalikuwa ni vijiji, lakini kiuhalisia bado yana mazingira kama ya vijiji hivi; Serikali iliahidi kwamba bado wale wananchi ingawa wanaishi kwenye mitaa ingewapa umeme kwa kupitia mradi wa REA. Maeneo hayo ni katika Kata za Ihanamilo; baadhi ya mitaa; Kata ya Kasamwa, Kata za Kanyara na Kata za Burela.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini sasa Serikali itatusaidia kupeleka umeme katika maeneo hayo na katika kata hizo kwa kupitia mradi huu wa REA kama ilivyoahidi ndani ya Bunge? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu maswali mawili ya nyongeza. Kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kushuruku kwamba Mheshimiwa Mbunge Lijualikali ametambua kazi mbalimbali ambazo zinaendelea katika Jimbo la Kilombero kuhusu mradi wa REA awamu ya tatu, mzunguko wa kwanza. Ametoa ushauri kwamba ni namna gani Serikali inaweza ikaboresha zaidi katika usambazaji wa umeme inapofika kwenye eneo fulani.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge, Serikali yetu ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli imeliona hilo kwamba, kwa kuwa miradi hii ngazi yake kwanza ni ngazi ya kijiji, imetambua vijiji zaidi ya 3,559 kwa awamu hii ya kwanza, REA awamu ya tatu mzunguko wa kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vina vitongoji. Kwa hiyo, Serikali ilibuni mradi ambao ilifanya majaribio ya ujazilizi kwa mikoa minane ambapo uligusa vitongoji 305 na iliwaunganisha wananchi kama 25,000 na mradi ule ulifanyika kwa mafanikio makubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuwa na mafanikio hayo, tutakuja na mradi mwingine densification awamu ya pili katika Bunge hili la Bajeti linaloendelea. Kwa hiyo tutaomba mtuidhinishie, lakini mradi huu unakwenda kutatua tatizo la vitongoji vinavyoachwa. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine, hilo linatambulika.

Mheshimiwa Naibu Spika, niendelee kuamini kwamba gharama za kupelekea umeme kwenye kijiji kimoja; kilimeta moja tu ni shilingi milioni 50. Kwa hiyo, Serikali ambayo inafanya mambo mengi ya kimaendeleo lazima kwenda hatua kwa hatua. Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge waendelee kutuunga mkono na vitongoji vingine vitafikiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge Upendo Peneza, ameelezea masuala ya Halmashauri ya Geita. Kwanza kata zote ambazo alizitaja, bahati nzuri na Mheshimiwa Mbunge mwenyewe wa Jimbo naye amelizungumzia, Mheshimiwa Naibu Waziri wa Maliasili, lakini naye nimpongeze pia amelielezea.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba maeneo yote ambayo yako katika Halmashauri za Miji na tunatambua kwamba bado yapo katika pia katika maeneo ya vijijini, kuna mradi unakuja peri-urban ambako maeneo ya kata ambazo zimetajwa zitashughulikiwa na bei ni ile ile shilingi 27,000/=. Kwa hiyo, niwatoe hofu wakazi wa maeneo yote ya miji na mitaa, mradi wa ujazilizi na mradi wa wa peri-urban utakuja kutatua tatizo ambalo limebaki.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
MHE. SILYVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na nichukue fursa hii kwa dhati kabisa kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kazi kubwa anayoifanya katika miradi ya umeme na hususan mradi mkubwa wa Stiegler’s gorge ambao unakwenda kutuondolea gharama kubwa ya umeme hakika ni neema. Nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri ameshatutembelea zaidi ya mara tatu katika Jimbo langu, anachapa kazi na kwa pamoja Serikali ya Chama cha Mapinduzi inafanya vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza. La kwanza, pamoja na kuchukua muda mrefu katika fidia hii, lakini wananchi wa Kibaha wana taarifa kwamba wenzao wa Arusha na Singida walikwishakupata malipo, kama hivi ndivyo, je, wanapata malipo kwa ubaguzi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika miradi ya ujazilishaji katika Mji wa Kibaha yaani densification Mitaa ya Muheza, Mbwate, Lumumba, Sagale, Mkombozi, Mbwawa Hekani, Kumba na Mtakuja miradi hii bado haijaanza utekelezaji kama ilivyokuwa imeahaidiwa. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha miradi hii ambayo wananchi wanaisubiri kwa hamu ili waweze kupata umeme na kukidhi mahitaji yao ya kiuchumi?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Silvestry Koka, ndugu yangu kutoka Jimbo la Kibaha Mjini kuwa kwanza tumepokea pongezi na nichukue fursa hii kumpongeza yeye binafsi Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini pamoja na Waheshimiwa Wabunge wenzake wa Mkoa wa Pwani ambao wanapitiwa na mradi huu akiwemo Mheshimiwa Mbunge wa Kibaha Vijijini, Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Chalinze pamoja na dada yangu Mheshimiwa Bonnah, Mbunge wa Jimbo la Segerea kwa kazi ya kuwasemea wananchi wao na kufuatilia masuala ya fidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama alivyosema nimefanya ziara katika maeneo yao mbalimbali, lakini nataka niseme moja ya jambo ambalo limejitokeza baada tu ya Serikali yetu ya Awamu ya Tano chini ya Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kuja na mapinduzi ya kutaka kutekeleza mradi wa Rufiji Hydro Power Stiegler’s, njia hii ya msongo wa kilovoti 400 ilikuwa inaitwa Kinyerezi – Chalinze - Tanga. Kwa hiyo baada ya kuja na ule mradi ilikuwa lazima sasa kuwe na line ya kilovoti 400 kutoka Rufiji mpaka Chalinze ambayo inaunganishwa na Dodoma na kimsingi kwa ajili pia ya kuwezesha treni yetu ya umeme ambayo kama maelezo yalitolewa inatarajia kuanza kazi Novemba, 2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na wananchi, nami mwenyewe pia ni muhanga kwa sababu nawakilisha wanawake wa Mkoa wa Pwani. Nataka niseme kwa kweli kwa kuwa mradi huu wa ujenzi wa njia hii ya msongo wa kilovoti 400unaanza kutekelezwa Januari, 2020, hatuwezi kuanza mradi huu bila kuwalipa wananchi fidia. Kwa hiyo kiwango kilichotajwa kwenye jibu langu la msingi cha bilioni 36 na kwamba ndio wakati wake muafaka sasa wa kulipa kwa sababu hata fidia inayolipwa maeneo ya Singida, maeneo ya Mkoa wa Manyara kwa ajili ya njia ya msongo wa kilovoti 400 kutoka Singida mpaka Namanga ni kwa sababu mradi umeanza kutekelezwa na ndio maana lazima ulipe fidia maana yake ni moja ya masharti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa maeneo haya niliyoyataja, tunawashukuru na tunawaomba radhi kwamba wamechukua muda mrefu lakini wamekuwa na subira, waendelee na kwamba sasa kwa kweli mchakato wa malipo upo mbioni kukamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, ametaja maeneo ya Muheza, Lumumba, Madina, Mtakuja, Mbwawa kote huku mimi na Mheshimiwa Mbunge tulifanya ziara pamoja, nataka niwathibitishie wananchi kwa kazi ambayo Mheshimiwa Mbunge alikuwa anafanya kwamba maeneo haya tuliahidi kuyapelekea umeme kwa mradi wa Peri-urban na huo mradi wa Peri-urban pia unagusa Jimbo ya Ukonga kwa ndugu yangu Mheshimiwa Waitara pia kwa ndugu yangu Mheshimiwa Naibu Waziri wa Afya maeneo ya Kigamboni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme kwa hatua iliyofikiwa, mradi huu unaanza mwezi wa Nne kwa sababu taratibu zote za manunuzi zimekamilika na kwa sasa wakandarasi wale au wale ambao wametenda ipo hatua ya post qualification. Kwa hiyo Serikali imedhamiria kwa dhati kabisa maeneo ambayo yanakua kwa kasi kupelekea mradi wa Peri-urban. Naomba tu waendelee kuvumilia mwezi wa Nne mwishoni utaanza huu mradi. Ahsante sana.
MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona swali hili la Mheshimiwa Koka, tena hili la juzi, lakini katika Jimbo la Mlimba kuna mradi mkubwa wa umeme mkubwa ulikuwa unapelekwa kutoka Kihansi Jimboni Mlimba kwenda Wilaya ya Malinyi, katika mwaka 2014 na mpaka 2016 TANESCO ikakubali kwamba wale watu wanatakiwa walipwe, lakini mpaka leo unavyozungumza wengine wameshakufa, wengine wameshazeeka hawajalipwa hata senti tano. Je, ni lini sasa Serikali itawalipa hawa wananchi au kwa vile wako mbali sanahakuna barabara jamani kosa, letu nini wananchi wa Mlimba?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Susan, Mbunge wa Jimbo la Mlimba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nipokee hii changamoto ambayo ameielezeaMheshimiwa Suzana na nikitambua kwamba kwa kipindi cha Bunge hili la Kumi na Moja, awamu ya kwanza alihudumu Kamati ya Nishati na Madini na nimwahidi kwamba tutaenda kufuatilia kwa sababu maeneo haya anayoyataja na kwa kuwa mradi mkubwa wa Kihansi unaozalisha umeme zaidi ya megawati 180 ni ya wananchi wa maeneo hayo, hivyo tunawategemea sana na wamekuwa watunzaji wazuri wa mazingira na mpaka sasa hivi hatujawahi kupata changamoto yoyote ya kusema labda maji yamepungua katika uzalishaji wa umeme. Kwa hiyo nimwahidi Mheshimiwa Mbunge baada tu ya hapa naomba tufuatilie, kwa sababu hata jana aliniambiakuhusu hili suala ili kuona fidia imefikia wapi, lakini nihakikishe kwamba kama haki hiyo ipo na tahmini ilifanyika Serikali ya Awamu ya Tano inalipa fidia. Ahsante sana.
MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nataka kuuliza kuhusu suala la fidia; wananchi wa Mkuranga, Kibiti na Rufiji wanadai fidia zaidi ya miaka mitatu kutoka TANESCO. Sasa kutokana na mradi huu wa umeme wa Kinyerezi, je, ni lini wananchi hawa watalipwa hizo fidia?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mama yetu Mheshimiwa Mama Salma Kikwete, Mbunge wa kuteuliwa na Mheshimiwa Rais, lakini anahudumu Mikoa ya Pwani na Lindi kama ambavyo ameuliza masuala ya fidia ya mradi wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Somangafungu Kinyerezi. Kimsingi mradi huu fidia yake inalipwa na TANESCO na maeneo ambayo yalipitiwa na mradi huu kuanzia Kilwa, Kibiti, Rufiji, Mkuranga na maeneo ya Mbagala na Ilala Dar es Salaam, nataka nikiri kwamba kutokana na mradi huu takribani gharama yake kama isiyopungua bilioni 50 hivi, lakini TANESCO mpaka sasa hivi wamelipa zaidi ya bilioni 30.

Mheshimiwa Mwenyekiti,natambua kwamba zipo changamoto za baadhi ya wananchi wachache na hata hivi karibuni tulipanga na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Mkuranga kufanya kikao na Menejimenti ya TANESCO ili kuweza kutambua mpango wao mkakati wa kumalizia malipo ambayo yamesalia. Kwa hiyo, nimshukuru kwamba na tunamwalika Mheshimiwa Mbunge, Mama yetu Mama Salma Kikwete na Mheshimiwa Mbunge wa Rufiji na Mheshimiwa Mbunge wa Kilwa katika kikao hiko ili kutambua akina nani wamelipwa, akina nani hawajalipwa kwa sababu zipo changamoto pia katika suala zima la wanaojitokeza. Hata hivyo, nimwahidi kabisa kwamba TANESCO kwa kweli wamejipanga kulipa kwa sababu mradi huu ni lazima utajengwa kutokana na uwekezaji unataka kufanyika Mkoa wa Mtwara wa ujenzi wa mtambo wa kuzalisha megawati 300 na Somangafungu yenyewe wa ujenzi wa mtambo wa kuzalisha megawati 330. Kwa hiyo nimshukuru na kumpongeza kwa swali lake zuri hili. Ahsante sana.
MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa nini Serikali haitaki kuwapa gesi wawekezaji wa kiwanda cha mbolea ambao wako tayari kujenga Msangamkuu, Mkoani Mtwara vijijini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, miongoni mwa manufaa ya gesi kwa wananchi wa Mkoa wa Mtwara ni pamoja na kupelekewa umeme lakini mpaka sasa baadhi ya maeneo hakuna umeme Mkoani Mtwara. Naomba kujua kwa nini Serikali haipeleki umeme maeneo mengi ya Mkoa wa Mtwara?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Shamsia, wifi yangu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Mbunge ameuliza kuna mwekezaji, ni kweli wapo wawekezaji kampuni ya WD capital ya Egypt pamoja na Oman Petra Chemical ya Oman na LMG ya Ujerumani ambayo iliingia makubalino na Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani kuwekeza kiwanda cha mbolea katika Mji wa Msangamkuu ambayo itatumia malighafi ya gesi asilia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme sio sahihi sana kwamba walikataliwa kupewa gesi, lakini kikwazo kilikuwa bei ya gesi ambao wawekezaji wetu walikuwa wanaitaka. Kwa mfano, sambamba na huyo pia kuna mradi wa Kampuni ya Ferrestal ambayo waliingia ubia na Kampuni yetu TPDC lakini wote hao walikuwa bei yao ya awali ambayo walikuwa wanaitaka ni iwe USD 2.26 ambako gharama za uzalishaji wa gesi hizi kwa mujibu wa EWURA ni USD 5.6. Kwa hiyo utaona gape yake lakini Serikali yetu ya Awamu ya Tano inayovutia wawekezaji ili kupitia maagizo ya Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli iliridhia tuanze mchakato wa mazungumzo. Kupitia mchakato wa mazungumzo ambao ulihusisha TIC ambayo yalifanyika mwezi Machi mwaka huu 2019, tumefikia bei ambayo wenzetu wawekezaji hawa wamerejea ili kuitafakari na baada ya wiki mbili walisema watarejea tena na bei hiyo ni kama USD 3.36 ambayo tunaamini pengine hiyo inaweza sasa ikafanikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka niwathibitishie wakazi wa maeneo ya Kilwa ambako Ferrestal na TPDC watajenga kiwanda hicho na wakazi wa maeneo ya Msangamkuu Mkoani Mtwara kwamba, fursa ya ujenzi wa viwanda vya mbolea ambao faida kubwa itatoa ajira na mapato bado ipo na Serikali hii ya Awamu ya Tano kupitia hata Ofisi ya Waziri Mkuu Uwezeshaji na hata Taasisi ya TIC na taasisi zingine tutahakikisha kwamba fursa hii itafanyika kwa ufasaha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, ameulizia kwa nini Mkoa wa Mtwara kwa kuwa unatoa gesi haujapelekewa umeme kwa kiwango ambacho Mheshimiwa Mbunge ameulizia. Nataka niseme ni kweli Mkoa wetu wa Mtwara tunautegemea sana kwa gesi megawati 1,600, zinazozalishwa sasa asilimia 52 inatokana na gesi. Pia Mkoa wa Mtwara kwa REA awamu ya tatu inaendelea ina vijiji 167, lakini Manispaa ya Mtwara Mikindani baadhi ya maeneo hata mimi niliyatembelea Mkangaula, Mkanalebi na pale maeneo ya mjini na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo tulikuwa naye pamoja na amekuwa wakiliulizia mara kadhaa hapa ndani ya Bunge kwa kazi nzuri ya kufuatilia miradi hii nimhakikishie tu ujazilizi awamu ya pili unaendelea na utaugusa Manispaa ya Mtwara Mikindani na maeneo mengine na hata Mkoa wa Lindi kwa sababu bado tunatarajia gesi kutoa mchango mkubwa katika kuzalisha umeme ahsante sana.
MHE. ALFREDINA A. KAHIGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuulizia swali la nyongeza. Je, ni vigezo gani ambavyo vimepelekea kupeleka gesi ya bei nafuu majumbani Mkoani Dar es Salaam, sehemu za Mikocheni badala ya kuipeleka Mtwara mahali ambako gesi inaanzia. Ahsante?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Kahigi, kwanza nimpongeze kwa kutambua utanzania uliopo kwa sababu yeye anatokea Mkoa wa Kagera, lakini ameuliza swali linalohusiana na masuala ya gesi, kwa nini kwa watu wa Mtwara hawakuunganishiwa hii gesi ya majumbani. Nataka nimthibitishie kupitia Serikali yetu na TPDC kwa sasa na Mheshimiwa Waziri wetu wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Merdad Kalemani alizindua mradi wa usambazaji gesi majumbani Mkoa wa Mtwara na Dar es Salaam na ni kweli kwamba Dar es Salaam tuna takribani viwanda zaidi ya 20 ambavyo vimeunganishiwa, tuna nyumba nyingi lakini ndio utaratibu za kuunganisha zaidi zinaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimthibitishie Mheshimiwa Kahigi kwamba hata sasa hivi tunasubiri tu vifaa na kuanzia mwezi wa Nne wakazi wa Mkoa wa Mtwara kwenye nyumba za maeneo ya railway pale wataunganishiwa gesi, Chuo cha ufundi Mtwara Technical kitaunganishiwa gesi, pia na maeneo ya Mkuranga viwanda vyaGypsum nao wote wataunganishiwa gesi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho niseme, miradi hii ya kusambaza gesi asilia majumbani ni mradi ambao unahitaji mtaji mkubwa. Tunaishukuru sana Wizara ya Fedha kwa kuridhia kwamba TPDC waendelee na mchakato wa kuhuisha sekta binafsi katika uwekezaji wa mradi huu ambao unatarajia kutumia takriban bilioni 200 katika Mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Morogoro, Dodoma na Tanga na pia kuna mpango wa kujenga bomba la gesi kuelekea Uganda, zote ni kutumia hizo fursa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nithibitishe kwamba kwa kweli Serikali yetu ya Awamu ya Tano inatambua matumizi ya gesi asilia ukiacha kuzalisha umeme lakini kwa viwandani na majumbani ili kulinda mazingira yetu kwa wananchi kuacha kukata miti, watumie gesi mbadala. Ahsante sana.
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Nimemsikiliza vizuri sana Mheshimiwa Naibu Waziri, dada yangu akijibu hili swali, nami naliona ni jambo la muhimu sana kwa sababu uharibifu wa mazingira katika nchi hii umekuwa mkubwa sana na kwa sababu nchi yetu inatumia pesa nyingi sana za kigeni kuagiza mafuta kwa ajili ya magari na mitambo. Je, ni lini Serikali italeta hapa Bungeni mpango mkakati wa namna gesi yetu itakavyotumika majumbani na kwenye magari na mitambo mingine ili kuweza kuokoa pesa nyingi za kigeni ambazo zinatumika kwa ajili ya kuagiza mafuta kutoka nje?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Selasini,
kaka yangu na Mbunge wa Jimbo la Rombo ambalo ameuliza ni lini Serikali italeta mpango mkakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme Serikali kupitia TPDC ina mpango mkakati wa matumizi ya gesi, tangu gesi ilivyogunduliwa na kwa kuwa tuna gesi nyingi zaidi ya trilioni 55 Cubic feet, gesi hii imepangiwa mkakati wa matumizi yake. Kuna gesi ya kutumia kwenye masuala ya uzalishaji wa umeme, kuna kiwango cha gesi cha kutumia kwa ajili ya viwanda, kuna kiwango cha gesi cha kutumia kwa ajili ya majumbani, kuna gesi ya kiwango cha kutumia kwa ajili ya magari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, swali lake aliloliuliza ni kwamba huo mkakati tunaowasilisha upo wa kimaandishi kabisa, Gas System Master Plan ambayo imeainisha matumizi yake na kiwango kimepangwa kabisa hadi 2035. Nachotaka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge, ndiyo maana nimesema mchakato wa matumizi yote haya hata sasa hivi kipo kituo Dar es Salaam pale Ubungo, unaweza ukabadilisha gari lako kutoka matumizi ya mafuta ya kawaida diesel kwenda kwenye matumizi ya gesi. Tunachofanya sasa ni kutaka kuongeza vituo vingi zaidi ili huduma hiyo ipanuke, kwa hiyo, jambo hilo lipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimesema hapa kwenye swali la nyongeza la mama yangu Mheshimiwa Mama Kahigi kwamba mipango yote inahitaji uwekezaji wa kutosha. Tunafurahi kwamba Serikali yetu kwa kuungwa mkono, Serikali ya Oman ilikuja hapa na kulikuwa na MoU tumeshaisaini lakini zaidi inataka kuisaidia sekta hii ya gesi hasa usambazaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba tunatambua hilo na umuhimu wa utunzaji wa mazingira pia. Ndiyo maana sasa hivi hii gesi ya LPG inayotoka nje ya nchi tumeona tuipangie mkakati kwa muda kwamba lazima nayo iingie kwenye bulk procurement kusudi iingie kwa wingi kwa madhumuni ya kushusha bei na kutumika kwa wingi wakati tunasubiri utekelezaji wa mkakati wa muda mrefu wa kuhakikisha gesi hii yetu ya asilia tunaisambaza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nimalizie hata mradi wa LNG wa Lindi wa kusindika gesi ili kurahisisha usafirishaji wake, sasa hivi mazungumzo yameanza tunatarajia utaanza 2024. Mradi huu ukishaanza tutakuwa na uwezo wa ku-export gesi zaidi na kusambaza ndani ya nchi na kujenga miundombinu ya kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana, ahsante.
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwa kutimiza ahadi yake kupeleka gesi kwenye Kiwanda chetu cha Saruji cha Dangote. Pamoja na pongezi hizi, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, pamoja na kupeleka gesi kwenye Kiwanda chetu cha Dangote, kuna viwanda vingine Mkoani Mtwara hususan viwanda vya kubangua korosho. Je, Serikali imejipangaje kupeleka gesi kwenye viwanda hivyo ili itumike katika shughuli za uzalishaji katika viwanda hivyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili ni kuhusu usambazaji wa gesi majumbani kwa sababu gesi inayozalishwa ni nyingi lakini matumizi ni kidogo. Je, Serikali imejipangaje kuongeza idadi ya watu watakaotumia gesi majumbani kwa Wilaya ya Nanyamba, Newala, Masasi na Mikoa mingine ili tutumie gesi yetu ipasavyo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abdallah Chikota, Mbunge wa Nanyamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nipokee pongezi zake kwa niaba ya Wizara baada ya kukamilisha ahadi yetu ya kumpelekea gesi Kiwanda hiki kikubwa cha Dangote kinachozalisha saruji. Pili, nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge Chikota kwa kazi nzuri anayofanya katika kufuatalia matumizi ya gesi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali yake mawili ya nyongeza anauliza ni lini Serikali itasambaza gesi katika viwanda ambavyo viko Mkoani Mtwara ikiwemo vya kubangua korosho. Napenda nimtaarifu Serikali yetu inatambua umuhimu wa gesi katika kuwezesha viwanda kuzalisha malighafi kwa kutumia gesi na ina mpango kabambe wa kusambaza gesi katika maeneo ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka sasa tuna viwanda zaidi ya 27 ambavyo vinatumia gesi na sasa hivi kuna mradi ambao unatekelezwa wa kusambaza gesi majumbani na viwandani na hasa maeneo ya Mtwara na Mkuranga. Hivi ninavyozungumza tayari TPDC imeshakamilisha mazungumzo na mkataba wa mauziano ya gesi ya viwanda vya KNAUF Gypsum Mkuranga na Lodhia Mkuranga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye viwanda vya kubangua korosho, naomba niwataarifu wawekezaji wetu wote wenye viwanda katika ukanda huo ambao bomba la gesi limepita kutoka Mtwara kwamba fursa hiyo ipo, waje tu tuzungumze na TPDC. Serikali imejipanga katika uwekezaji huo na hata katika Mpango wa Matumizi ya Gesi kiasi cha trilioni 8 cubic fit zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya viwanda tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili alikuwa anauliza ni lini usambazaji wa gesi asilia majumbani utafanyika. Nataka nimtaarifu sasa hivi hata Waziri wetu Mheshimiwa Dkt. Medard Kalemani alizindua Mradi wa Usambazaji wa Gesi Asilia katika Mkoa Mtwara na Dar es Salaam. Kazi inayoendelea ni ununuzi wa vifaa mbalimbali na mpaka sasa vimeshanunuliwa vifungashio, vifaa vya kupunguza mgandamizo wa gesi, vifaa vya kupimia gesi majumbani. Vifaa vyote hivi vitakamilika ifikapo Mei, 2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kazi ya kusambaza gesi katika Mikao ya Mtwara, Lindi na Dar es Salaam inaendelea. Ahsante sana.
MHE. AJALI R. AKBAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kuna taarifa ambazo ni rasmi, kwamba pamoja na kwamba Dangote amepatiwa gesi hii na baadhi ya viwanda vilivyopo Mkuranga, sasa vile viwanda vimeshindwa kutumia ile gesi katika kiwango ambacho ni tarajiwa. Ina maana wanatumia gesi pungufu na vingine vimetoa notice ya kufungwa.

Je, ni lini sasa Serikali itapunguza bei ya gesi hii ili viwanda hivi visifungwe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, (b) nina taarifa rasmi vilevile kwamba kuna wawekezaji ambao walikuwa wametoka mashariki ya mbali; China na Uturuki, wapatao wanne ambao waliokuwa wamekusudia kuja kuwekeza hapa nchini. Ikumbukwe kwamba faida ya gesi siyo kwamba ni kwa kuuza tu, lakini vile viwanda vingeweza kulipa kodi, kutoa ajira na faida nyingine ambazo Taifa lingeweza kupata tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inaonekana kwamba bei ya gesi yetu ni Dola 5.5 per metric tones wakati katika Soko la Dunia ni Dola 3.7 per metric tones. Sasa je, Serikali ina mkakati gani na kwa nini sasa isifanye sub…

MWENYEKITI: Swali, swali swali!

MHE. AJALI R. AKBAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali ni kwamba, naomba kwamba Serikali ipunguze bei ili wawekezaji hawa wasikimbie ili tupate faida nyingine zitokanazo na viwanda hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu maswali mwili ya nyongeza ya Mheshimiwa Akbar, Mjumbe wa Kamati yetu ya Nishati na Madini. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri anayoifanya katika ushiriki wake kwa Kamati yetu inayosimamia Sekta yetu ya Nishati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali mawili aliyojielekeza; la kwanza Mheshimiwa Mbunge ameeleza namna ambavyo viwanda vilivyounganishiwa gesi ikiwemo Dangote na viwanda vya Mkuranga kwa mfano Goodwill, kwamba vinaona bei ya gesi ni kubwa; nataka nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba hilo suala limewasilishwa Wizarani; na kwa kuwa wapangaji wa gesi hii ni wa bei ya gesi asilia (EWURA) pamoja na Taasisi ya PURA ambayo ina- regulate Sekta ya Nishati upande wa gesi kuhusu masuala ya upstream, ni kwamba ndani ya Serikali jambo hili limepokelewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kupitia EWURA kwa kuwa ni kazi yao kupanga hizi bei za gesi itafanyia kazi kuangalia mchakato mzima. Pia ni lazima nikiri kwamba gharama ya uzalishaji wa gesi hapa nchini hii gesi ambayo inatumika ni zaidi ya shilingi USD 5.36. Kwa hiyo, utaona, lakini nia ya Serikali ni kuwezesha viwanda kutumia gesi na kuzalisha malighafi. Kwa hiyo, hili jambo limepokelewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili Mheshimiwa Mbunge ameulizia kwamba kuna wawekezaji kutoka nchi mbalimbali ambao wameonesha nia ya kuwekeza, sisi kama Serikali ya Awamu ya Tano kwa kweli imeandaa mazingira ya kukaribisha uwekezaji katika maeneo mbalimbali hasa viwanda vya mbolea katika Mkoa wa Mtwara na eneo la Kilwa. Hata sasa iliundwa Kamati ya Wataalam kufanya mapitio ya gesi hasa katika suala zima la kuwezesha viwanda hivi na wawekezaji katika kuwekeza kwenye suala la mbolea. Kwa hiyo, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge suala hili limefanyika, sasa hivi kinachofuata ni kikao baina ya wawekezaji na tangu mwezi wa Nne pia kilifanyika kwa ajili ya kupanga bei na kukubaliana. Hata wale wawekezaji kwa mfano Kampuni ya Helm na AG ya WD ya Egypt walishapewa mwelekeo na namna ya kufanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimthibitishie tu kwamba Serikali ipo tayari kuwakaribisha wawekezaji na waje tu na mazungumzo yanaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Jimbo la Singida Kaskazini lina miradi ya REA II, REA III, phase I pamoja na umeme wa backborne kwenye vijiji 54. Hadi sasa ni vijiji 13 tu ndiyo ambavyo vimekwishakufikiwa na umeme na vingine mpaka sasa bado. Je, Mheshimiwa Waziri wa Nishati yuko tayari kuambatana nami kutembelea Jimbo la Singida Kaskazini kujionea changamoto zilizopo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Monko kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Monko amerejea Mradi wa REA awamu ya pili ambapo kwa kweli kama Serikali tuliwaomba radhi wakazi wa Mkoa wa Singida na Kilimanjaro baada ya makosa ambayo yalitendeka katika Mradi wa REA awamu ya pili na tukafanya kazi na kumweka Mkandarasi mpya ambaye anaendelea na kazi kwa kushirikiana na REA.

Mheshimiwa Spika, swali lake ameulizia utayari wetu wa kuambatana naye; nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge nipo tayari mimi pamoja na Waziri kwa wakati tofuati kutembelea Jimbo lake kama ambavyo tulishafanya mwezi wa Nane tulitemebelea Jimbo lake ikiwemo Kijiji cha Iddi Simba na tuliwasha umeme pia aliwakilishwa na Mheshimiwa Mbunge Aisharose Matembe. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge niko tayari muda wowote kutembelea eneo lake na kuendelea kuwasha umeme na kukagua kazi inavyoendelea. Ahsante sana.
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kwa sasa tunajua kwamba tuna mradi wa REA ambao ndiyo umejielekeza kupeleka umeme vijijini. Katika Kijiji cha Sazira katika Jimbo la Bunda Mjini ambalo lina Vitongoji vitatu cha Nyamungu, Wisegere na Kinamo havijawahi kupitiwa na mradi huu wa REA phase I, phase II na hata phase III. Sasa ningependa kujua hawa wananchi wa Kijiji cha Sazira ni lini watapatiwa umeme ili na wenyewe waweze kupata umeme katika shughuli zao za kimaendeleo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; katika Mji wa Tarime pia tumepitiwa na umeme wa REA ambao unapita kwenye aidha Kijiji sehemu ndogo tu au kata. Ningependa kujua maeneo ambayo yana Taasisi kama sekondari, zahanati au vituo vya afya na shule ya msingi kama vile Kitale tuna Kijiji cha Nkongole ambacho kina hizo Taasisi zote, Kenyamanyori Senta tuna Kibaga ambayo ina mgodi pale haijapitiwa na umeme wa REA. Ni lini sasa Serikali itahakikisha kwamba inapeleka huu umeme wa REA kwenye yale maeneo ambayo hayajaguswa kabisa na Mheshimiwa Naibu Waziri aliniahidi kwamba ungeweza kwenda Tarime kujihakikishia hayo maeneo ambayo kila siku nayauliza hapa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther Matiko, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza ameulizia Kijiji cha Sazira ambacho kipo Bunda Mjini ambacho kina vitongoji vitatu na hakina umeme. Kama ambavyo tumepata kujibu maswali hapa ya msingi kwamba mpango wa Serikali ni kupeleka umeme vijiji vyote. Kwa sasa tuna mradi huu unaoendelea wa REA awamu ya tatu ambao unahusisha vijiji 3,559 lakini ukichanganya na miradi mingine yote ya Ujazilizi, BTIP tunatarajia kufikisha umeme ifikapo Julai, 2020 kwa vijiji 9,299.

Kwa hiyo kijiji ambacho amekitaja kwenye Wilaya ya Bunda Mjini hapo vipo katika mpango wa REA awamu ya tatu, mzunguko wa pili ambao utaanza Julai, 2019 na kukamilika 2021. Kwa hiyo niwatoe hofu tu wananchi wote nchi nzima, mpango wa Serikali ya Awamu ya Tano ni kupeleka umeme katika vijiji vyote nchi nzima.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ameulizia suala la Jimbo lake la Tarime; ni kweli niliahidi kutembelea Jimbo hilo kama utaratibu wetu ndani ya Wizara, lakini nitazingatia angalizo lako kwamba kwa ruhusa ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, lakini nimtoe hofu tu Mheshimiwa Esther kwamba katika maeneo ambayo ameyataja na hasa Taasisi za Umma, Wizara imetoa maelekezo mahususi na naendelea kurejea hayo maelekezo kwamba Taasisi za umma ni moja ya kipaumbele katika kuzipelekea umeme iwe shule ya msingi, sekondari, kituo cha afya au miradi ya maji.

Kwa hiyo naomba niwaelekeze Wakandarasi kuzingatia maelekezo hayo na Mameneja wote wa TANESCO na wasimamizi wa miradi hii ya REA kwamba umeme ufikishwe kwenye Taasisi za Umma ili kuboresha utoaji wa huduma ambazo zinatokana na hizo Taasisi za umma.

Mheshimiwa Spika, katika haya maeneo aliyoyasema Mheshimiwa kwanza mojawapo lipo katika REA awamu ya tatu, mradi unaoendelea na Mkandrasi Derm yupo, anaendelea vizuri na ni moja wa Wakandarasi ambao kwa kweli wanafanya kazi vizuri na nimhakikishie tu mpaka Juni, 2019 hii miradi itakuwa imekamilika. Ahsante.
MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake pamoja na majibu hayo naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati utafiti wa awali unafanyika kuhusu maeneo yanayofaa kwa ajili ya mradi huu waliokuwa wakifanya utafiti walifika pia Isaka na Igusule kama ambavyo jibu limesema na baada ya maamuzi kufanyika kwamba mradi huu unajengwa Igusule walisema bado kuna miundombinu muhimu ya Isaka ambayo itatumika ikiwa ni pamoja na Ofisi za TRA, Bandari ya Nchi Kavu, Reli, Umeme pamoja na ofisi zingine za Kiserikali.

Sasa nilitaka kufahamu kwa sababu pia walisema wataweka transit yard pale Isaka nilitaka kujua hatua gani imefikiwa kwa ajili ya upataji wa eneo hilo la transit yard na maandalizi ya wananchi wa Isaka kwa ajili ya kushiriki katika huo mradi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa kuwa mradi huu unatoa fursa za kibiashara na ajira kwa wananchi waliowengi sana wa maeneo hayo. Je, ni maandalizi gani ya kiujumla ambayo yamefanyika kwa ajili ya kuandaa wananchi hawa wa Isaka pamoja na Igusule ili waweze kushiriki katika kunufaika na mradi huo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI (K.n.y. WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana kwa namna ambavyo amekuwa akifuatilia mradi huu wa Bomba la Mafuta kutoka Hoima Uganda na namna gani wananchi wake hususan wa Jimbo la Msalala watakavyoweza kufaidika na maswali yake mazuri ya nyongeza na mara baada ya kukubali uamuzi wa wabia wa mradi huu wa eneo la kujenga kiwanda iwe Igusule.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa kuwa maswali yake ya nyongeza yamehusiana na miundombinu mingine ni kweli tafiti mbalimbali zimeendelea kufanyika kuhuisha miundombinu mbalimbali ikiwemo reli, ikiwemo ofisi mbalimbali za kiserikali itakavyotumika katika mradi huu na nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika eneo la Isaka hapo pia vitajengwa ofisi ya mradi huu ya EACOP na miundombinu mingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia wananchi wake na yeye mwenyewe anajua eneo la Igusule ni kama kilometa 5 tu kutoka Isaka. Kwa hiyo, ni wazi kabisa wananchi wa maeneo ya Isaka na maeneo mengine ya Mkoa wa Shinyanga pamoja na Mkoa wa Tabora watapata fursa mahususi kabisa katika mradi huu ikiwemo ajira na masuala mengine ya kibiashara na mpaka sasa mradi huu umeajiri takribani watanzania 229 kwa hizi hatua za awali lakini kuna makampuni nane yanatoa huduma mbalimbali katika mradi huu lakini pia faida zake mojawapo ni utoaji wa ajira utakapoanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikutaarifu tu kwa sasa mazungumzo yanaendelea na kwamba hatua ambayo imefikiwa sasa hivi ni tumefika mbali na tunatarajia mradi huu kuanza mwezi septemba 2019. Kwa hiyo, utakapoanza utaleta tija kubwa na faida kwa wananchi wa mikoa nane iliyopitiwa na bomba hili, wilaya 24, kata 134 na vijiji 280.

MHE. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana yaliyosemwa na Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niwadhibitishie Waheshimiwa Wabunge Serikali kwa kutambua umuhimu wa mradi wa bomba hilo la mafuta na jinsi litakavyoweza kukuza ajira na uchumi wa Taifa letu, Ofisi ya Waziri Mkuu imeandaa programu maalum ya local content na tumeanza mafunzo maalum katika mikoa hiyo yote nane ili kuwahabarisha wananchi katika mikoa hiyo ni namna gani wanaweza wakatumia fursa mbalimbali ambazo zitapatikana katika mradi huo muhimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe wito kwa Wabunge wote ambao wanatoka katika mikoa ambayo inapitiwa na bomba hilo tuweze kuwasiliana ndani ya Ofisi ya Waziri Mkuu ili kuwaweka pamoja wananchi wao waweze kufaidika na mradi wa bomba la mafuta katika fursa mbalimbali zitakazopatikana.
MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, hili eneo la Sojo Kata ya Igusule ambako pameamliwa kujengwa kiwanda hiki liko jimboni kwangu na wananchi wametoa hekari 400 ili kupisha ujenzi wa kiwanda hichi muhimu. Na kwa kuwa majibu ya Mheshimiwa waziri wamesema mwezi wa tisa ambayo ni miezi minne tu kutoka sasa mkandarasi anakabidhiwa eneo.

Je, nilitaka kujua kwamba Serikali inaweza kutoa commitment kwamba ndani ya kipindi hichi cha miezi minne kabla mkandarasi hajapewa hilo eneo wananchi wote waliotoa hekari 400 watakuwa wamelipwa fidia zao?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI (K.n.y. WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza na yeye pia nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia mradi huu mkubwa wa ujenzi wa bomba hili la mafuta na tija yake kwa wananchi wa maeneo yake hayo, kwa eneo ambalo limechaguliwa kujenga kiwanda cha kuunganisha mabomba.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimdhibitishie Mheshimiwa Mbunge moja ya kazi muhimu ambayo imefanyika ni kutambua mkuza ambako bomba litapita na tunatambua bomba hili ambalo litakuwa na urefu wa kilometa 1445 na zaidi ya kilometa hizo 1147 ziko upande wa Tanzania, Serikali yetu kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi na TPDC imetambua ule mkuza na imeshafanya tathimini ya mali mbalimbali ambazo ziko katika huo mkuza ikiwemo eneo hilo la ujenzi wa kiwanda hichi cha courtyard.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimthibitishie tathmini imekamilika na kwa kuwa tupo katika hatua nzuri ya mazungumzo ya Host Government Agreement baada ya hapo tutaenda Share Holders Agreement na kasha kufanya maamuzi ya investment decision na hatua zote hizi zipo katika mchakato wa miezi hii ambayo imesalia.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimthibitishie tu Mheshimiwa Mbunge na kwa utashi wa viongozi wetu Marais wan chi mbili hizi, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli na Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museven wa Uganda kwamba mwezi wa tisa utakapoanza mradi huu wananchi wote watakaopisha mkuza huu wa bomba watakuwa wamefidiwa kwa sababu tathmini ile imekamilika na sasa yapo tu mapitio ya mwisho ambayo yanafanywa baina ya Wizara ya Nishatu wataalamu, TPDC, Wizara ya Ardhi, Maendeleo Nyumba na Makazi na taasisi nyingine za Kiserikali. Nikushukuru sana.
MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, swali la kwanza kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Pwani especially sehemu hizo zilizotajwa, walisitishiwa tangu 2014 wakati wa Awamu ya Nne, na anasema kwamba watalipa fidia kwa uthamini wa 2018 watu hawa walikuwa wanajenga wakaacha ujenzi na gharama zimepanda.

Je, Serikali iko tayari kulipa hasara ambayo maongezeko ya gharama za ujenzi watakapokuwa wanalipa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa kuwa Serikali imekaa kimya muda wote huu. Je Waziri yuko tayari kufuatana na mimi baada ya Bunge ili akaweze kuongea hayo ambayo ameyaeleza hapa wananchi waweze kumuelewa kwa urahisi?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru kwa kufuatilia ili suala hili ni swali lake la pili, lakini pamoja naye niwashukuru Waheshimiwa Wabunge wa Majimbo ya Kibaha Mjini, Kibaha Vijijini na Chalinze kwa kufuatilia hili swali kwa karibu.

Mheshimiwa Spika, lakini nataka nimueleze Mheshimiwa Mbunge na na wananchi wa Mkoa wa Pwani wakati wa mwaka 2014/2015 Serikali ilipo design mradi huu wa Kinyerezi, Chalinze, Segera Tanga ulikuwa kabla haujafanywa maamuzi ya ujenzi wa mradi mkubwa wa Rufiji Hydro Power.

Kwa hiyo, Serikali ya Awamu ya Tano ilipoingia madarakani na kuamua kutekeleza mradi huu kwa nia ya kufanya nchi iwe na umeme wa kutosha ilibidi ifanye utaratibu wa kuuisha upembuzi yakinifu kwa sababu mradi huu sasa wa Rufuji Hydro Power kuna njia mpya ambayo itajengwa ya KV 400 kutoka Rufiji, Chalinze ambayo inaelekea Dodoma.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ndiyo suala ambalo limepelekea fidia hii kuchelewa kwa sababu lazima iuishwe, lakini tunatambua fidia inalipwa kwa mujibu Sheria na Kanuni. Kwa hiyo, malipo ya fidia hii kwa wananchi wa Mkoa wa Pwani yatazingatia Sheria na Kanuni za nchi ambazo zinapeleka malipo haya ya fidia.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili amesema je, nipo tayari?, nataka nimualifu Mheshimwa Mbunge na mimi pia ni mdau ni Mbunge wa Mkoa wa Pwani hivi karibuni tu nilifanya ziara Kata ya Pera Jimbo la Chalinze na niliongea na wananchi suala hili.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo namkubalia kwamba baada ya Bunge hili au wakati wowote tunaweza tukafanya ziara katika maeneo ya Kibaha, maeneo ya Jimbo la Segerea, maeneo ya Kibaha Vijijini, maeneo ya Chalinze kuzungumza na wananchi na kwamba kwa kweli kama nilivyosema wakati wa bajeti yetu wataona tumedhamilia kabisa kulipa hii fidia kwa sababu mradi huu unaanza mapema Julai, 2020 na kukamilika Desemba, 2022, ahsante sana.
MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, mradi wa kuchakata gesi wa LNG Likong’o Lindi. Ni muda mrefu sana wananchi wa eneo la Likong’o hawafanyi shughuli zao za kilimo ili kujipatia mahitaji yao ya msingi na kuongeza uchumi wao binafsi na mradi huu ni muhimu sana kwa wananchi wa Lindi kwa ajili ya kuongeza uchumi wao, lakini si hilo tu bali ni Taifa kwa ujumla kwa sababu ni mradi mkubwa sana, Mheshimiwa Waziri.

Je, ni lini wananchi hawa wa Lindi hasa Likong’o watalipwa fidia zao kwa ajili ya kuinua vipato vyao na kuacha eneo hilo liendelee na kazi iliyokusudiwa?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu swali la Mheshimiwa mama Salma Kikwete Mbunge wa kuteuliwa na Mheshimiwa Rais juu ya suala la fidia la eneo la Likong’o ambalo tunatarajia kutekeleza mradi mkubwa wa kujenga kiwanga cha kuchakata gesi asilia ambayo imegundulika kwa wingi katika Mikoa ya Mtwara kwa kiasi cha trilioni cubic feet 55.

Mheshimiwa Spika, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge mama Salma na wananchi wa Mkoa wa Lindi Serikali inatambua umuhimu wa mradi huu na ndiyo maana Mheshimiwa Rais alitoa maelekezo ya kukwamua mkwamo ambao uliokuwepo kwa Wabia wale wa mradi wa kutaka kila mmoja tuzungumze naye kwa wakati tofauti na mazungumzo hayo yameanza kati ya kampuni ya BP SHELL pamoja na STATOIL ambayo kwa sasa hivi inajulikana kama equinor.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mazungumzo haya yameanza kwa kwa kuwa sasa hivi kuna kila dalili ya mradi huu kufanyika na taratibu zinaendelea na Kamati ya Wataalam wameshakaa suala la fidia kwa eneo hili limeshafanyiwa kazi na naomba nimualike Mheshimiwa Mama Salma Kikwete na Wabunge wote wa Mkoa wa Lindi kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati kwenye mkutano wa tarehe 21 mwezi huu wa 5 wa ku-raise awareness ya mradi huu na ambapo pia taarifa na uhakika wa ulipaji wafidia baada ya tathimini kukamilika itatolewa.

Mheshimiwa Spika, tunawashukuru wananchi wa Mkoa wa Lindi kwa uvumilivu wao tunakuja tarehe 21 na kwamba kila kitu Serikali imekiweka vizuri, ahsante sana.
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kwanza nichukue nafasi, nimshukuru Mheshimiwa Waziri, na Naibu wake Waziri wanafanya kazi nzuri sana, na ni kazi ambayo itaisaidia sana CCM 2020 tunakoenda kwenye uchaguzi.

Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili ya nyongeza, swali la kwanza Mheshimiwa Waziri wa Nishati alipokuja Serengeti mwaka huu mwanzoni alihaidi maeneo ya yafuatayo yatapa umeme; shule ya Sekondari Inagusi ilipo Kata ya Isenye, Kijiji cha Nyamatoke na Mosongo vilivyopo Kata ya Mosongo pamoja na Kiyakabari Kata ya Stendi Kuu.

Ni lini maeneo haya yatapata umeme ambao ulihaidiwa na Mheshimiwa Waziri?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, ni lini TANESCO au REA watapeleka umeme Kata ya Morotonga katika Vitongoji vya Mutukura na Romakendo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza tupokee pongezi zake, lakini naamini pongezi ni kuhitaji zaidi huduma. Kwa hiyo, tumepokea kwa ahadi kwamba tutaendelea kufuatilia hiyo miradi. La pili pia nimpongeze yeye Mheshimiwa kwa namna ambavyo anavyofuatilia masuala ya nishati katika Jimbo lake na sekta mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, lakini masuala yake mawili yamejielekeza kwanza kwenye ziara ambayo imefanywa na Mheshimwia Waziri wa Nishati katika Jimbo la Serengeti na ahadi aliyoitoa katika shule ya Sekondari Nagusi na maeneo ya Kiyabakari. Nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Mheshimiwa Waziri wa Nishati alipotoa ahadi hii alikuwa na uhakika wa utekelezaji wa mradi wa REA Awamu ya III mzunguko wa kwanza unaoendelea na kwamba mkandarasi Derm wa Mkoa wa Mara ni miongoni mwa wakandarasi wanaofanya vizuri tulivyo wa-rank na kwamba inatarajiwa itakamilisha kazi kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, maeneo aliyoyataja mara tu Julai 2019 mradi wa REA Awamu ya III unaanza na kazi ndiyo itafanyika. Kwa hiyo nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwa kipindi hiki cha kuendelea 2019 maeneo haya yote ataiona kazi inaanza na nguzo zitapelekwa na ninaomba nimuelekeze mkandarasi Derm azingatie maelekezo ya Mheshimiwa Waziri pamoja na Meneja wa TANESCO wa Mkoa wa Mara na msimamizi wa mradi wa REA katika Mkoa wa huo.

Mheshimiwa Spika, swali la pili Mheshimiwa Mbunge ameulizia masuala la kwa mfano Marotonga na eneo ambalo umelitaja Mgumu Mjini, yanaonyesha haya maeneo ni ya ujazilizi. Kama nilivyosema kwenye jibu la msingi Mheshimiwa Agnes Serikali baada ya kuona pana changamoto baada ya miradi ya REA kukamilika na kwa kuwa lengo lake Serikali ni kusambaza umeme palikuwa na changamoto ya gap ya usambazaji wa umeme. Na ndiyo maana ikabuni mradi wa ujazilizi na bahati nzuri Mkoa wa Mara ulikuwemo katika ujazilizi Awamu ya kwanza ambao ulikuwa kama mradi wa majaribio.

Mheshimiwa Spika, na Serikali imekuja na mradi wa ujazilizi Awamu ya pili, Awamu ya II(a) ambayo itakuwa na Mikoa tisa na Awamu ya II(b) itakuwa na Mikoa 16, ikiwemo Mkoa wa Mara na kwa kweli tunauhakika Awamu ya II(a) utafadhiliwa na Serikali za Norway, Sweden na Umoja wa Ulaya na hela zake tunazo bilioni 197 na Awamu ya II ya ujazilizi two (b) itafadhiliwa na Serikali ya Ufaransa mpaka sasa tunauhakika wa kiasi cha bilioni 270 kati ya bilioni 400 ambazo zitaanzia kazi na mchakato tupo hatua ya manunuzi na mradi huu utaanza 2019/20 kwa ajili ya kufikisha umeme katika maeneo ya Vitongoji ili kuweza kusambaza umeme, nikushukuru sana.
MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa tena nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Namshukuru Naibu Waziri alishafika maeneo hayo na kesho Mheshimiwa Waziri atakuwa yuko Mkalama kwa suala hili hili.

Maswali mawili ya nyongeza; katika suala zima la mradi wa ujazilizi hasa katika vijiji vya Iguguno, Kinyangiri, Nduguti, Gumanga, Iyambi, Nkalakala, wananchi wameshaelimishwa? Kwa sababu wananchi wanalalamika. Sasa REA wamechukua hatua gani kuwaelimisha wananchi kwamba ujazilizi unakuja?

Swali la pili. Ziko sehemu ambazo umeme umeshawaka, lakini kumekuwa na maeneo ambayo yamerukwa na Naibu Waziri anafahamu na alifika. Ni lini umeme utawaka kwenye Kanisa la TAG Ibaga, Mkalama Kituo cha Afya, Matongo, Kijiji cha Kidi na Kitongoji kimoja cha Gumanga?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza sana kwa kazi nzuri anayoifanya. Ni kweli tuliambatana pamoja katika maeneo ya Nkito kama ambavyo nimeyataja katika swali langu la msingi, Ibaga na tukawasha umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika maswali yake mawili, ameulizia mradi wa ujazilizi. Kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, ni kwamba Mradi wa Ujasilizi awamu ya pili unaanza Julai, 2019 kwa gharama za shilingi bilioni 197 kwa mikoa tisa ikiwemo Singida Tabora, Shinyanga, Dodoma, Kilimanjaro, Tanga, Pwani na maeneo mengine.

Kwa hiyo nataka nimthibitishie katika huu ujazilizi ya awamu ya pili katika Vijiji alivyovitaja ikiwemo cha Iguguno na Ibagala vitapatiwa umeme na nataka niielekeze REA pamoja na TANESCO ifanye uhamasishaji katika maeneo haya na kwamba TANESCO Mkoa wa Singida ijipange sasa kwa ajili ya vitongoji vyote ambavyo vinatakiwa viingie katika mradi wa ujazilizi, awamu ya pili, mzunguko wa kwanza na mikoa mingine 16 itapatiwa mradi wa ujazilizi, awamu ya pili, mzunguko wa pili, ambao utagharimu zaidi ya bilioni 460 na mazungumzo yanaendelea na Serikali ya Ufarasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ameuliza katika maeneo Mbaga na Mkalama kikiwemo na kituo cha afya, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge, kwa kuwa katika Wilaya ya Mkalama kwa mradi wa REA awamu ya tatu imegusa vijiji 30 na mradi wa REA awamu ya kwanza vilikuwa vijiji 14 na kwa kuwa wilaya yake ina vijiji takribani 70, ni wazi vijiji 26 vitaingia katika rea awamu ya tatu, mzunguko wa pili ambao pia unaanza sambamba mwezi Julai, 2019.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi inayoendelea sasa hivi katika Wakala wa Nishati Vijijini ni kuandaa makabrasha kwa ajili ya kutangaza zabuni na kuwapata wakandarasi wa kuanza mradi huu ili iwezeshe nchi yetu ifikapo 2020/2021 Juni, tuwe tumemaliza vijiji vyote nchini ambavyo havikuwa na umeme. Ahsante sana.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Lumuma inayotoka Wilaya ya Kilosa ni mashuhuri sana kwa kilimo cha vitunguu, lakini kata hii haina umeme na inategemea umeme kutoka Wilaya ya Mpwapwa ambayo ipo kwenye mkoa mwingine wa Dodoma. Je, kata hii ni lini itapatiwa huduma ya umeme ili iweze kupata huduma ya umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa mama yangu Dkt. Christine Ishengoma kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naye pia naomba nimpongeze kwa kufanya kazi nzuri kama Wabunge wengine wa Viti Maalum kufuatilia sekta mbalimbali. Katika swali lake hili la nyongeza ameuliza hii Kata ya Lumuma ambayo ipo jirani kabisa na Wilaya ya Mpwapwa nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge hata Diwani wa Kata ile mwanamama amekuwa akifuatilia na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kilosa naye nataka nimtaarifu Mheshimiwa na wananchi wote wa Kata ya Lumuma kwamba, tunatambua changamoto hii na kwa kuwa wapo karibu na Wilaya ya Mpwapwa tumeiagiza TANESCO, yapo maeneo tumeamua kuwapa TANESCO ili wasambaze umeme vijijini na mpaka sasa zaidi ya maeneo 200 yametwaliwa na TANESCO ili isaidie REA katika kusambaza umeme vijiji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuahidi mama Mheshimiwa Dkt. Ishengoma tutaambatana katika ziara kwenye kata hii ya Lumuma kuelezea ujumbe huu pamoja na TANESCO na REA na kwamba watapatiwa umeme katika nyakati za kuanzia mwezi Julai, 2019 na kuendelea. Ahsante sana.
MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Nimeongea na Waziri mara nyingi na akaniahidi kwamba kwenye mradi wa REA ambao sasa hivi upo field kwenye Kata ya Idete, Shule ya Sekondari Matundu Hill na Shule ya Sekondari Kamwene ambapo mradi unapita pembeni kidogo anasema maeneo haya ni muhimu kupeleka, lakini mpaka leo hakuna jitihada za Serikali.

Je, ni lini sasa Shule ya Sekondari Matundu Hill Idete na Shule ya Sekondari Kamwene watapatiwa umeme ili wanafunzi wa sekondari waweze kujisomea na kupata ufaulu mzuri?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nijibu swali la Mheshimiwa Kiwanga Susan kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru kwa swali lake zuri, nami nimewahi kufika Idete; katika Idete pale ikiwemo Gereza la Idete limeunganishiwa umeme kwa kutumia ile umeme wa low cost design. Kwa hiyo nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge ahadi ya Mheshimiwa Waziri na hapa nitoe malekezo kwa Shule za Sekondari Kamwene na Matundu Hill Idete nimwagize mkandarasi State Grid wa Mkoa wa Morogoro atekeleze maagizo ya Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, agizo hili sio kwa mkandarasi wa Morogoro peke yake na wakandarasi wote nchi nzima, watekeleze agizo la Serikali la kuhakikisha wanapofikisha umeme katika maeneo mbalimbali kama pana taasisi za umma iwe kituo cha afya, iwe mradi wa maji, iwe sekondari waunganishe. Tuliwaeleza variation ya namna hiyo inakubalika na Serikali hii ya Awamu ya Tano haiwezi kushindwa kulipa gharama kama inagharimu mradi mzima wa REA awamu ya tatu zaidi ya takribani trioni moja na bilioni mia moja. Kwa hiyo, nawaomba wakandarasi watii maelekezo ya Serikali. Ahsante sana.
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Tarehe 10 Agosti, 2018, Waziri wa Nishati alizindua mradi wa REA III katika Mkoa wa Kigoma katika Kijiji cha Lusesa, Kata ya Lusesa na akaahidi kwamba baada ya mwezi mmoja umeme utawaka katika kata hiyo na viunga vyake vinavyozunguka kata hiyo, lakini mpaka leo umeme haujawaka. Nataka nijue ni lini Serikali itaagiza wanaohusika na umeme waweze kuwasha umeme katika kata hiyo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la dada yangu Mheshimiwa Josephine Genzabuke kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze kwa kweli kwa kazi kama Mbunge wa Viti Maalum kufuatilia masuala ya sekta ya nishati mkoani kwake. lakini kama ambavyo amesema uzinduzi katika Kata ya Lusesa ulifanyika mwaka 2018 mwezi Agosti, ni wazi kabisa kulikuwa na changamoto ya mkandarasi katika Mikoa ya Kigoma na Katavi na niwashukuru Wabunge wa mikoa hiyo pamoja na wananchi kwa subira yao namna ambavyo waliliridhia. Hata hivyo, nataka niseme mkandarasi huyu wa CCCE Etern anaendelea na kazi. Hata hivi karibu Mheshimiwa Waziri amewasha vijiji kama vitatu katika Wilaya ya kibondo.

Kwa kuwa Mheshimiwa Mbunge amesema katika Kata ya Lusesa ambapo imezinduliwa na ahadi ilitolewa na kwamba mpaka sasa hivi bado vijiji vya Kata hiyo ya Lusesa havijawashwa, naomba nilichukue ili niwasiliane na Meneja wa TANESCO wa Mkoa wa Kigoma pamoja na mkandarasi, kwa vile uzinduzi ulifanyika kwa kata hii na ni wazi lazima ilikuwa kazi ifanyike kwa haraka na umeme uwake, pamoja na kwamba mkandarasi hana muda mrefu.

Kwa hiyo nitoe maelekezo kwamba agizo la Mheshimiwa Waziri litekelezwe katika Kata hii ya Lusesa, vijiji hivyo ambavyo vimeanishwa viwashwe na nimwahidi Mheshimiwa Mbunge, baada ya hili Bunge la Bajeti, tutafanya naye ziara katika Mkoa wa Kigoma. Ahsante sana.
MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa wananchi wa Kibiti wanategemea sana nishati yao ya mkaa na kuni, je, ni lini sasa wataunganishiwa hii gesi asilia katika Miji ya Kibiti, Bungu na Jaribu?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Serikali sasa inajenga mradi mkubwa wa umeme kule Mloka wa Stiegler’s, je wananchi wa Kibiti ambao kwa kiasi kikubwa wanategemea kukata kuni na mkaa wanaweza wakapatiwa upendeleo wa kupata vibarua?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuruku kwa kunipa nafasi ya kujibu swali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ally Seif Ungando, Mbunge wa Kibiti kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeza kwa kazi nzuri anayofanya katika Jimbo la Kibiti, hususan katika sekta hii ya nishati. Maswali yake ya nyongeza kwanza ameuliza ni lini sasa Serikali itasambaza gesi katika Wilaya hii ya Kibiti, katika jibu letu la msingi tumesema katika kipindi hiki cha muda wa kati kati ya mwaka 2010 mpaka 2020 tumekuwa tukutekeleza miradi ya muda wa kati na muda mfupi wa kusambaza gesi katika maeneo mbalimbali. Mpaka sasa Mheshimiwa Waziri wa Nishati wiki mbili zilizopita amezindua uunganishaji wa gesi nyumba mpya 26. Matarajio yetu mpaka ifikapo Septemba, 2019 kuunganisha nyumba kama 333 katika Mkoa wa Mtwara na Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Mkoa wa Lindi na Pwani, Serikali kupitia TPDC imekuja na mradi mkubwa kabambe wa kusambaza gesi asilia. Mradi huu utafanywa na mashirikiano baina ya sekta binafsi na Serikali na kwa sasa hatua ambao imefikia tumeshampata Mshauri Mwelekezi, anaandaa makabrasha na kufanya feasibility study ya mradi mzima, matarajio yetu mwezi wa Tano mwakani kuwapata wakandarasi wa sekta binafsi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri niwakaribishe sekta binafsi katika maeneo mbalimbali ili kujumuika na Serikali katika mradi mkubwa wa kusambaza gesi asilia kwa matumizi ya majumbani na viwandani na hususan katika Wilaya ya Kibiti kwa kuwa nayo imepitiwa na bomba la gesi hususan katika maeneo ambayo ameyataja Jaribu, Kibiti maeneo ya Nyamwimbe, Kata ya Mlanzi, maeneo ya Mangwi, Kata ya Mchukwi na maeneo mengine kama ambavyo anafahamu Mheshimiwa Mbunge, kwa hiyo nimwaidi hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge ameuliza mradi wa Stiegler’s Gorge Rufiji Hydro Power unaotekelezwa katika Kata ya Mwaseni, Kijiji cha Mloka. Ni kweli mradi ule una matarajio makubwa ya kutoa ajira na kwa kuwa maelekezo ya Serikali ya Awamu ya Tano kupitia Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, utekelezaji huu wa miradi hii mikubwa ya mikakati, lengo kubwa ni kuzalisha ajira na katika maeneo ambayo mradi unatekelezwa na kwa Watanzania wote kwa ujumla. Kwa hiyo nimwahidi na hata yeye anafahamu, hata zile kazi za awali za madereva zilizotangazwa, zimetangazwa kupitia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kibiti na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Rufiji na Wakuu wa Wilaya wa Mkoa wa Morogoro. Kwa hiyo ni wazi kabisa kipaumbele kwa watakaokuwa na sifa wanaostahili, lakini zipo kazi za kawaida za vibarua mbalimbali, watapata wananchi wa Kibiti na wananchi wa Wilaya ya Rufiji na wa maeneo ya Mkoa wa Morogoro. Kwa hiyo hilo kwa kweli halina mjadala, ndivyo ambavyo tumelipangilia. Ahsante sana.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Baada ya Mtwara kupatikana kwa gesi Mheshimiwa Waziri akatangaza kwamba Liwale nao tutapata umeme wa gesi kutoka Mtwara. Wakati ambapo Mheshimiwa Waziri anatangaza nikamwomba nikamwambia kwa umeme ule wa Mtwara nafuu Liwale wakatuachia umeme wetu wa mafuta, lakini jambo hilo halikutekelezwa, matokeo yake sasa Liwale umeme unapatikana kwa shida sana.

Je, Mheshimiwa Waziri anatuahidi nini sisi watu wa Liwale shida hii tunayoipata mwisho lini? Maana sasa hivi umeme haupatikani kabisa, unawaka masaa mawili au matano.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuruku kwa kunipa nafasi ya kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale kupitia Chama cha Mapinduzi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Kuchauka ameelezea katika swali lake la nyongeza kwamba tulitoa ahadi ya kuunganisha Wilaya ya Liwale katika umeme wa gesi, lakini kwa sasa nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge ni kweli kuwa Wilaya ya Liwale kwa mara ya kwanza imeunganishwa na grid ya Taifa kupitia Kituo cha Maumbika, lakini tunatambua changamoto iliyojitokeza katika maeneo mbalimbali ambapo tumeunganisha grid ya Taifa lakini inatokana na umbali wa kusafirisha umeme huyo kufikia katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Shirika la TANESCO lipo katika hatua ya manunuzi ya kifaa ambacho kitakuwa na uwezo wa kurekebisha hali hiyo ili isiendee. Kwa hiyo niwathibitishie wakazi wa Wilaya ya Liwale, wakazi wa mikoa ya Lindi na Mtwara ambao wameunganishwa kwenye grid ya Taifa, wakazi pia wa Mkoa wa Ruvuma na wakazi wa Biharamulo, Ngara kwamba tatizo ni muda na limepatiwa ufumbuzi na kwamba likishashughulikiwa wataona faida ya umeme wa uhakika ambao unatokana na grid ya Taifa, kuliko huu ambao ni wa mafuta ambao kwa kweli umelisaidia shirika kuokoa kiasi cha pesa na kuweza kuendelea kuwekeza katika maeneo mengine. Kwa hiyo nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na kwa kuwa hivi karibuni kwenye tarehe 21 nitafanya ziara katika jimbo lake, nitatoa hayo maelezo. Ahsante sana.
MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupewa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza nipende tu kuwashukuru Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri, waliweza kufanya ziara katika Jimbo la Mbeya Vijijini na katika ziara hiyo waliahidi kuwa wangepeleka umeme katika Kata za Maendeleo, Itawa na Shizuvi, ikiwa ni pamoja na vijiji vinavyolizunguka Jiji la Mbeya. Sasa je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye Kata za Maendeleo, Itawa na Shizuvi?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oran Njeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tulitembelea Mkoa wa Mbeya, hususan Jiji la Mbeya na si chini ya mara mbili na kuwaahidi wananchi wa Kata za Maendeleo na Kata ambayo ameitaja ya Itawa, kwamba tutawapatia umeme na hususan katika mradi unaoendelea wa ujazilizi awamu ya pili, mzunguko wa kwanza, ambao hatua za manunuzi zimeshakamilika na kiasi cha shilingi bilioni 169 zimetengwa. Mkoa wa Mbeya ni miongoni mwa mikoa tisa ambayo itapata fursa ya ujazilizi awamu ya pili, mzunguko wa kwanza kama ambavyo imepata fursa ya ujazilizi awamu ya kwanza kutokana na mahitaji makubwa. Kwa hiyo nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na nimuahidi kwamba maeneo haya yatapatiwa umeme katika mradi ambao utaanza Julai, 2019. Ahsante sana.
MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Serikali katika REA awamu ya pili ilichukua umeme kutoka Mjini Sumbawanga na kupitisha katika jimbo langu kupeleka Mkoa wa Katavi maeneo ya Kibaoni bila kushusha umeme katika Vijiji vya Mbwilo, Mnazi, Kalumbaleza, Mpete, Mtapenda, Mfinga na Kizungu. Je, ni lini Serikali itashusha umeme katika maeneo hayo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Malocha, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze kwa kazi nzuri anayofanya kwenye jimbo lake na yeye mwenyewe anathibitisha tulishafanya ziara pia katika Mkoa wa Rukwa na Jimbo lake zaidi ya mara mbili. Nataka nimwarifu maeneo hayo ambayo ameyataja ambapo umeme ulipita wakati unaelekea Mkoa wa Katavi kwamba tumeshatoa maelekezo maeneo hayo yaingie kwenye REA awamu ya tatu, mzunguko wa pili unaoanza Julai, 2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo Mkandarasi Nakuroi anaendelea na kazi katika Mkoa wa Rukwa na hususan katika jimbo lake na maeneo ambayo tulitembelea pamoja yanaendelea na kazi vizuri na yatawashwa umeme kwa kipindi kinachoendelea. Kwa hiyo kwa maeneo haya na kwa kuwa umeme ulipita na nafurahi leo ninaposimama hapa pia kama ambavyo mnafahamu Rais wa Benki wa Dunia ameshatoa fursa ya mradi wa kusafirisha umeme katika msongo wa KV 400 ambao unaelekea Sumbawanga, Mpanda, Nyakanazi, Kigoma, kwa hiyo kutakuwa na uhakika wa umeme katika maeneo aliyotaja Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naishukuru Serikali kwa majibu mazuri. Pamoja na majibu yao mazuri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; sasa hivi ni takribani miaka 53 toka tumepata uhuru na majiko haya yamekuwa yakitumika pamoja na athari zake. Je, Serikali iko tayari sasa kuanzisha kampeni mahususi ya kutokomeza matumizi ya majiko ya mafiga matatu katika shule za sekondari, vyuo, primary na kote huko ili kuondoa athari hizo kama ilivyofanya kampeni ya kuboresha maabara na kuleta madawati kwa shule zote hizo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kuna makampuni binafsi ambayo yanasambaza gesi hizo za kupikia (liquid gas) na pia kwenye mitungi midogo ambayo ni affordable ikiwemo Mihan na Oryx. Sasa Serikali iko tayari kushirikiana na makampuni hayo ili kupunguza athari za moshi unaowaumiza sana akina mama walioko vijijini na kwingineko na bado hawajapata elimu ya matumizi ya majiko hayo kwamba wanaumia ili waweze kupatiwa majiko hayo kwa bei nafuu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa mama yangu Shally Raymond. Kwanza nimpongeze kwa kazi nzuri anayoifanya kwenye eneo lake la Mkoa wa Kilimanjaro hususan kwa masuala ya wanawake na inadhihirisha kwa swali hili ambalo ameliuliza linalohusiana na masuala ya majiko ya mafiga matatu.

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza la nyongeza ameulizia kama Serikali ipo tayari kuanzisha kampeni ya kuondokana na majiko haya hususan katika shule za sekondari na msingi.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, tunatambua kwamba majiko haya ya mafiga matatu yana athari ya kimazingira na kiafya lakini kwa kuwa tumelitambua hilo, Serikali pia ina mpango wa usambazaji wa gesi asilia katika mikoa mbalimbali ambapo imeanza na mikoa saba ikiwemo Mkoa wa Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara, Tanga, Dodoma na Morogoro lakini sambamba na hilo, Serikali pia imekuwa iki-support makampuni yanayohusiana na gesi ya LPG.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, kwa kuwa hatua hizi zinaendelea katika kuhakikisha kwamba kwanza gesi asilia inasambazwa katika maeneo mbalimbali ambayo ina bei nafuu, lakini pili kwa kushirikiana na makampuni yanayoingiza nchini LPG ili iweze kushusha bei, nina uhakika kwamba tutafikia hatua hiyo ya kupeleka nishati hii ambayo itatumika katika shule za sekondari.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, pia kuna makampuni mbalimbali ambayo yanashirikiana katika suala zima la usambazaji wa nishati jadidifu katika maeneo mbalimbali. Kwa hiyo, nitoe wito tu katika makampuni hayo kuendelea kuiunga mkono Serikali ili iweze kufikia hatua ya kutangaza hiyo kampeni na ni jambo jema. Namwomba yeye pamoja na Wabunge wote wa Viti Maalum, Wabunge wote na wananchi mbalimbali tuhamasishe utunzaji wa mazingira na utumiaji wa nishati mbadala hasa katika kupikia ili kupunguza uharibifu wa mazingira.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, ni kweli yapo makampuni kama nane ambayo yanahusika na masuala ya uingizaji wa gesi ya LPG ikiwemo Oil Gas Tanzania Ltd, Taifa Gas, Mount Meru Gas lakini pamoja na hayo kuna Lake Gas, Oilcom na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, nini Serikali imefanya? Tumeona kwa kuwa kiwango cha matumizi ya LPG kimeongezeka kutoka kwa mfano tani 90,000 mwaka 2016 mpaka tani 147,000 mwaka 2018. Kwa hiyo, ni wazi matumizi yameongezeka, kwa hiyo, tulichofanya, tunatafakari namna ambavyo gesi ya LPG inaweza ikaingizwa kwa mfumo wa uagizwaji wa pamoja. Tupo katika mazungumzo na wadau wa makampuni haya na taasisi mbalimbali ili kuwezesha kuweka mazingira wezeshi ambayo yataisaidia hata EWURA kuweza kupanga bei ambayo inaweza ikawasaidia watanzania kutumia gesi hii ili kulinda mazingira yetu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nitoe wito kwa makampuni ambayo yanaagiza; kwanza nawapongeza kwa uwekezaji wanaofanya, waendelee kujenga miundombinu katika mikoa mbalimbali ili hii gesi ya LPG iweze kuwafikia Watanzania wote. Serikali itaendelea kuandaa mazingira wezeshi ili kuwezesha huduma hii ipatikane kwa urahisi.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)
MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kumekuwa na tatizo kubwa sana la kukatika kwa umeme wakati mwingine kwa siku nzima au hata zaidi ya siku kwenye visiwa vya UKerewe kila wakati mvua inaponyesha. Ningeomba Mheshimiwa Waziri awaambie wananchi wa Ukerewe ni lini tatizo hili litakoma ili wafurahie huduma ya umeme kama yalivyo maeneo mengine nashukuru sana?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli eneo la Ukerewe kwa mwezi mmoja uliopita umeme ulikuwa umekatika sana umesababishwa na sababu moja tu, wavuvi wanaovua kutoka eneo la Kisolia ambapo ni mwanzo wa kuingilia kutoka Bunda kuelekea Lugenzi wamekuwa mara nyingi sana wakikata nyaya wakati wa uvuvi. Lakini nyaya zile zimekuwa zikitikiswa pia wakati wa mvua inapoambatana na upepo, kwa hiyo, ni kweli maeneo ya Ukerewe yamekuwa yakipata changamoto kwa kukatika kwa umeme kipindi hiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hatua tulizochukua kwa niaba ya Mheshimiwa Mbunge na wananzegwa wananchi wa Ukerewe ni kwamba kwanza tumeanza kujenga kebo ya kutoka Kisolia kwenda Lugenzi ambapo ni kilomita nne na tume-commit shilingi bilioni 375 na ujenzi umeanza tutafunga kebo tutaipitisha juu ili wavuvi waache kuzigusa na hivyo kutakuwa na umeme muhimu sana kwa maeneo hili. Kwa hiyo, wananchi wa Ukerewe wavumilie kipindi cha wiki mbili zinazofuata mradi utakamilika ili umeme uwe ni uhakika zaidi kwa maeneo ya UKerewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, nipe nafasi kidogo kwa sababu ni suala la Ukerewe nitoe tangazo kwa wananchi sio wa Ukerewe peke yake ingawa Mheshimiwa Mbunge hajaliuliza, kumekuwa na changamoto kwa wananchi wa Ukerewe hasa watumiaji wadogo wa umeme kutozwa shilingi 2500 kwa unit kinyume na utaratibu na sheria ya umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nitoe tangazo kwa wananchi wa Ukerewe wasikubali kutoa shilingi 1000 kwa unit kwa sababu wananchi wote wa Ukerewe ni sawa na Watanzania wengine ambao wanatumia unit 75 ambao wanatakiwa walipe shilingi 100 per unit badala ya 2500 per unit.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitoe tangazo hili Mheshimiwa Mbunge anifikishie, lakini nimuombe Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe alisimamie na Meneja wa TANESCO alisimamie ili mwananchi yoyote atakayepatikana akitozwa hivyo kupitia kwa mkandarasi basi atoe taarifa mara moja na Serikali ichukue hatua dhidi ya watu ambao sio wazalendo kwa kitendo hicho ahsante. (Makofi)
MHE. WILLY Q. QAMBALO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, mkandarasi Nipol group anayefanya usambazaji wa umeme katika Mkoa wa Rushu hususani Wilaya ya Karatu kazi yake ya usambazaji ni ndogo sana, hivi sasa pamoja na kwamba muda wake wa ukandarasi unakaribia kuisha lakini bado vijiji vingi vya Kata za Bugeri, Kansai Endamarieki havijafikiwa na umeme. Nini kauli ya Serikali juu ya mkandari huyo ambaye anasuasua?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kazi za ujenzi wa mradi wa REA Awamu ya III mzunguko wa kwanza zinaendelea na mkandarasi Nipol anafahamu kabisa hivi karibuni tulifanya kikao cha wakandarasi wote na kwamba tumewaambia kwamba ifikapo tarehe 30 Juni, 2020 mradi utakuwa umekamilika na watakabidhi vijiji vyote vitakuwa vimejengewa miundombinu ya umeme na kazi ya kuwasambazia wateja itaendelea.

Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge baada ya kipindi cha maswali na majibu tuonane ili tuweze kuzungumza zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimthibitishie tu usimamizi umeimarishwa na ni muagize mkandarasi Nipol kwa niaba ya Waziri wa Nishati kwamba azingatie dead line iko pale pale na aitaongezwa muda wowote kwa wakandarasi wote nchini lazima wakamilishe tarehe 30 Juni, 2020 ili uunganishaji pamoja na miundombinu. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kabla sijauliza maswali ya nyongeza, nitumie fursa hii kuwashukuru sana Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa kuja kutembelea Jimbo la Ulyankulu na kuona changamoto zetu. Sasa nina maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, katika vijiji ambavyo vimeshapitiwa na umeme, kumekuwa na upungufu mkubwa sana wa nguzo kiasi kwamba maeneo mengi hayatapata umeme. Je, Serikali inasema nini kuhusu suala hili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, umeme kuupeleka kwenye Mgodi wa Silambo, kuna njia mbili. Je, mkandarasi anaweza kuelekezwa umeme kuelekea katika Mgodi wa Silambo ukapitia eneo la Ikonongo badala ya kupita Uyoa kutoka Kaliua?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kadutu. Nami nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Kadutu na Wabunge wote wa Mkoa wa Tabora kwa kazi nzuri zinazoendelea katika majimbo yao, hususani katika kufuatilia Mradi wa REA Awamu ya Tatu unaoendelea. Nawashukuru kwa ushirikiano wao kupitia ziara zetu tunazofanya katika majimbo yao, mara zote tunawakuta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa katika maswali yake ya nyongeza, swali lake la kwanza ameeleza kuhusu vijiji ambavyo vinapatiwa umeme na akasema nguzo ni chache, nataka nilitaarifu Bunge lako Tukufu kupitia swali hili la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Kadutu kwamba kwa kweli hii miradi ya umeme kwa kila kijiji inapokwenda kunakuwa na wigo, kilometa na wateja wa awali lakini kazi ya kuunganisha inaendelea. Ndiyo maana kwa kurahisisha zoezi hilo, tumeielekeza TANESCO na wao wataendelea kusambaza kwa bei ileile ya REA ya Sh.27,000. Kwa hiyo, nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge Kadutu kwamba kazi hiyo itaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, nimtaarifu tu Mkoa wa Tabora ni miongoni mwa mikoa tisa ya awali ambayo Mradi wa Awamu ya Pili ya Ujazilizi unatarajiwa kuanza hivi karibuni na taratibu za manunuzi zinaendelea na kiasi cha shilingi bilioni 169 zimetengwa na Bunge lako Tukufu kwa ajili ya kazi ya ujazilizi. Kwa hiyo, maeneo ya vijiji ambapo kuna vitongoji havikufikiwa vitafikiwa kupitia Mradi huu wa Ujazilizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili Mheshimiwa Kadutu ameulizia kama tunaweza tukatoa maelekezo ya kupeleka umeme kwenye Mgodi wa Silambo kupitia njia ya kutoka Ikonongo. Nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kuwa ametoa wazo hilo nilichukue na baada ya kipindi cha maswali na majibu tukutane na tuweze kufanya mawasiliano na TANESCO na REA tuone uwezekano huo ambao pengine hautaathiri kilometa ambazo zimetajwa katika mradi wa kupeleka umeme katika mgodi alioutaja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)
MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Dodoma ni Jiji ambalo lina vijiji na lina vijiji 34 ambavyo tulikwishapeleka ombi kwa Wizara na Mbunge wa Jimbo hili aliwahi kutembelea maeneo hayo pamoja na Waziri mhusika na tuliomba kupatiwa umeme wa REA. Naomba wananchi wajue ni lini sasa vile vijiji 34 ambavyo tuliviombea umeme wa REA vitapata umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la mama yangu, Mheshimiwa Felister Bura kuhusu vijiji 34 vya Jiji la Dodoma ambavyo vinahitaji umeme wa REA. Kwanza nimpongeze yeye mwenyewe kwa kazi nzuri ya kuwasemea wanawake wa Dodoma lakini pia nimpongeze Mbunge wa Jimbo naye Mheshimiwa Mavunde amekuwa akifuatilia na tumefanya ziara katika Jimbo lake hili la Dodoma Mjini, Mheshimiwa Waziri na mimi mwenyewe tumetembelea Jimbo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme tu hivi vijiji 34 vipo katika Mpango wa Ujazilizi Awamu ya Pili. Mkoa wa Dodoma ni miongoni mwa mikoa tisa na tunakamilisha taratibu za manunuzi na kuanzia kipindi hiki cha mwezi wa Septemba na Oktoba tutakuwa tumeshawapata wakandarasi na kuwakabidhi site.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nilitaarifu Bunge lako kwa kuwa Dodoma sasa imekuwa ni Jiji na ni Makao Makuu ya Serikali, kwa kweli moja ya mikoa ambayo iko katika kipaumbele cha kusambaza miundombinu ya umeme Mkoa wa Dodoma nao upo. Hata tulivyowaelekeza TANESCO kuendelea kuwaunganisha wananchi kwa bei ya Sh.27,000, Mkoa wa Dodoma nao mpaka sasa zaidi ya wananchi 4,000 wameunganishwa hususani katika maeneo ambayo ni pembezoni mwa mji. Kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge Dodoma ni kipaumbele na tutaendelea kufanya kazi hiyo kwa kasi zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Napenda nami nimuulize Naibu Waziri swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kata zaidi ya sita pale Jimboni kwangu Tarime Vijijini ambapo nguzo zimesimamishwa huu ni mwezi wa nne lakini bado hakuna nyaya wala activity yoyote inayoendelea. Sasa sijui ni nini kinachoendelea na napenda awaambie wananchi ni lini sasa nyaya zitapitishwa pale ili waanze kupata umeme wa REA?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Heche, Mjumbe wetu wa Kamati ya Nishati na Madini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ameulizia kuhusu kata sita kwenye jimbo lake ambapo amesema nguzo zimesimama lakini hakuna kinachoendelea. Nimwombe tu Mheshimiwa Heche baada ya kipindi hiki cha maswali na majibu tukutane ili niweze kufuatilia kwa karibu kwa nini mkandarasi DERM ambaye anaendelea na kazi katika Mkoa wa Mara hafanyi vizuri kwa sababu tunaamini mkandarasi yule ni miongoni mwa wakandarasi sita wanaofanya vizuri. Kwa hiyo, tukutane ili nijue kwa nini katika maeneo hayo bado nyaya hazijasambazwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwatoe hofu tu wakazi wa Mkoa wa Mara na nchi nzima, miradi hii tunatarajia mpaka Desemba kazi ya ujenzi wa miundombinu iwe imekamilika, ibaki kazi ya uunganishaji wa wateja ambapo kwa mujibu wa mkataba Mradi wa REA Awamu ya Tatu utakamilika Juni, 2020. Kwa hiyo, niendelee kuwatoa hofu lakini kweli kuna umuhimu wa kuongeza kasi zaidi, tutalifuatilia kwa pamoja ili kujua ni nini kimekwamisha kazi hiyo. Pia napenda kumjulisha Mheshimiwa Mbunge kwamba hivi karibuni baada ya Bunge hili nina ziara ya Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa katika eneo la Ilazo, Extension C katika Jiji hili la Dodoma, wananchi wanajenga nyumba zao kwa bidii sana lakini tatizo linakuja kwenye umeme. Wananchi wamefika TANESCO wameambiwa nguzo hakuna na anayetaka nguzo kuanzia nguzo mbili ni Sh.600,000 na kuanzia nguzo tatu na kuendelea inakuwa ni Sh.2,000,000. Hili suala linakuwaje kwa sababu kazi ya Serikali ni kusambaza miundombinu kama walivyofanya Idara ya Maji wamepeleka maji, barabara zimechongwa lakini hili la umeme linakuwaje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kujibu swali la nyongeza la mama yangu, Mheshimiwa Nuru. Ameulizia suala la maeneo ya Ilazo hususani swali lake limelenga kwamba wananchi wanakwenda TANESCO wanaambiwa walipie gharama ya nguzo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali hili ni zuri, nataka pia nirejee maelekezo na maagizo ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Medard Kalemani kwamba nguzo zote ni bure na kwa nini tumetoa agizo hilo? Gharama ya kupeleka umeme ina vitu vingi; kuna masuala ya transfoma, waya na kadhalika, lakini imekuwa tu ni mazoea kwa Shirika letu la TANESCO kutanguliza kipaumbele cha nguzo wakati ni sehemu tu ya gharama ya kuwaunganishia umeme Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niendelee kusisitiza agizo la Waziri wa Nishati lipo palepale, wananchi waendelee kuhudumiwa kwa TANESCO yenyewe kujiandaa na mpango wa manunuzi wa nguzo kwa sababu zile nguzo zinakuwa mali ya TANESCO. Kwa hiyo, nataka nilichukue suala hili la kulisimamia baada ya kutoka hapa. Kweli nimepokea salamu nyingi sana za wananchi kuhusu kuendelea kwa lugha ya Mameneja kusema nguzo hakuna, kuwachaji wananchi gharama za nguzo na kuwarudisha wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka tuendelee kusisitiza, tumesema Meneja ambaye hayupo tayari kupanga mipango ya kuwaunganishia wananchi kwa kutumia ubunifu wake kwa gharama za nguzo za Serikali, Meneja huyo atupishe ili tuwape Mameneja wengine mamlaka ili waendelee kuwaunganishia umeme wananchi. Kwa sababu yapo maeneo wanaweza kuunganisha kama kuna maeneo wanaona wanashindwa kutekeleza agizo hili la Serikali yetu ambayo imeamua kuwapunguzia gharama wananchi atupishe tu ili wengine waendelee kufanya kazi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba kusisitiza hili agizo lipo na yeyote anayeona hawezi basi atupishe ili tumteue mtu mwingine aweze kupanga mipango ya kuwaunganisha wananchi umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijauliza maswali yangu mawili ya nyongeza, naomba nichukue fursa hii kumpongeza Waziri kwa namna anavyojibu maswali hapa pamoja na kazi yake. Nafanya hivi sina hiyana kwa sababu imekuwa ni desturi ya Mawaziri kuwasifia Wabunge wa Chama cha Mapinduzi na sisi huku kukaa kimya na mimi nichukue nafasi hii kujisifu, nafanya kazi nzuri jimboni kwangu. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa maswali, swali la kwanza, swali hili limekuja ni mara ya pili sasa na Chuo cha Ufundi Arusha kimeonesha nia ya kutaka kufanya kazi hii. Kwa nini kuchukua mzunguko mrefu kuwapa TANESCO kufanya upembuzi yakinifu wasiachie tu hiki chuo kikafanya hii kazi kikamaliza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kama nilivyosema nafanya kazi nzuri sana kwenye Jimbo lango, kuna Kata za Reha, Nanjara, Kitirima, Kingachi, Mrao Keryo, Katangara Mrere ambako kuna vijiji umeme haujafika na kuna nguzo ambazo ziko chini. Ukweli ni kwamba kuna matatizo makubwa ya nguzo jimboni kwangu. Je, Waziri sasa yuko tayari kutoa maagizo maalum ili TANESCO kule Rombo wasiniharibie kazi yangu nzuri nayofanya ili kazi hii ikafanyika mara moja?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Baba Paroko, Mbunge wa Jimbo la Rombo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tupokee pongezi zake lakini na sisi tunakiri kweli mara kwa mara amekuwa akifuatilia changamoto mbalimbali za jimbo lake kwenye sekta ya nishati na hata kupitia ziara zetu tumekuwa tukishirikiana naye vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali yake ya nyongeza mawili ameuliza kwamba kwa nini inachukua mzunguko mrefu kuihusisha TANESCO. Kwa mujibu wa sheria kwa kweli mwenye mamlaka na masuala mazima ya sekta ya nishati, hususani masuala ya umeme, ni TANESCO ambaye ndiyo mzalishaji, msafirishaji na msambazaji. Kwa hiyo, labda nilichukue hili ili tuone namna gani tutafanya uharaka kati ya TANESCO na hicho Chuo cha Ufundi Arusha kwa ajili ya kuona huu upembuzi yakinifu unaotarajiwa kufanyika ufanyike kwa haraka ili tuone fursa zilizopo wakati wa kutekeleza ule mradi, aina ya maporomoko ya maji na uwezo wa kuzalisha hizo megawati, kwa hiyo, nilichukue hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili la nyongeza kuna kata amezitaka ikiwemo Nanjara akiainisha kwamba kuna nguzo ziko chini na vijiji vingine kazi ya kusambaza umeme haijamalizika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka nimtaarifu, kwenye Jimbo lake la Rombo ni vijiji nane tu ambavyo havina umeme. Mkoa wa Kilimanjaro mzima una Kata 148 zote zina umeme na vijiji 519 ni Vijiji 453 vina umeme. Kwa hiyo, bado vijiji 66 tu. Kazi iliyopo, tuna matarajio Mkandarasi ambaye yupo, ni kweli alikuwa na changamoto, lakini tumekaa naye Dodoma hapa kutaka kujua mpango kazi wake. Tuna matarajio mpaka Desemba vijiji 35 vitakuwa vimekamilika, vitabakia Vijiji ambavyo kwa kweli kama Vijiji 26 ambavyo naomba niwathibitishie wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro vitakuwa vimekamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto iliyopo Kilimanjaro, wanahitaji ujazilizi na kwa awamu ya pili ya ujazilizi inayoendelea Mkoa wa Kilimanjaro ni miongoni mwa Mikoa tisa. Kwa hiyo, maeneo ambayo ni ya Vijiji alivyotaja Mheshimiwa Mbunge yataingia kwenye ujazilizi, vitongoji na maeneo kadhaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepata message nyingi sana za wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro ikiwemo na Wilaya yako na Rombo na kazi nzuri pia inayofanywa pale na Mkuu wa Wilaya ya Rombo. Kwa hiyo, nataka nikuthubitishie kwamba tutashirikiana ili ujazilizi ukidhi mahitaji kwamba tumalize Mkoa wa Kilimanjaro wote kwamba uwe umewekewa umeme kwa miradi inayoendelea.

Mheshimiwa Mwenyemiti, ahsante sana.
MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nchi yetu ya Tanzania tumebahatika kuwa na vyanzo vingi vya umeme ikiwemo umeme wa upepo, Joto ardhi, maji, solar na vinginevyo. Sasa Serikali ina mkakati gani shirikishi na endelevu ifikapo mwaka 2030 kutekeleza kikamilifu lengo la saba la malengo endelevu ya dunia la kuwa na affordable and clean energy?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali zuri la nyongeza la Mheshimiwa Mbatia akiuliza mkakati wa Kiserikali ambapo kufikia mwaka 2020 inaweza ikatekeleza lengo la millennium ambalo amelitaja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza mkakati wa Serikali yetu ya Awamu ya Tano tulivyojipanga ifikapo mwaka 2025 tuna matarajio ya kuzalisha megawatts 10,000. Megawatts 10,000 hizi zitatokana na vyanzo mbalimbali ambavyo amevitaja ikiwemo maji, gesi, nishati jadidifu, joto ardhi, solar na masuala ya upepo. Hivi tunavyozungumza, kwa kutambua umuhimu wa kuwa na energy mix ya uhakika ambapo kuzalisha umeme kutokana na vyanzo mbalimbali kupitia TANESCO, Serikali imetangaza tenda kwa ajili ya kuzalisha megawatts 950 ikiwemo megawatts 600 ya Makaa ya Mawe, megawatts 200 kupitia upepo na megawatts 150 kupitia jua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, kuhusu masuala ya joto ardhi, Serikali kupitia tafiti mbalimbali na Taasisi yake ya joto ardhi, imetambua uwepo wa vyanzo vya kuweza kuzalisha umeme kupitia joto ardhi na sasa mpango unaoendelea, tunaishukuru Wizara ya Fedha imeiwezesha Tasisi ya joto ardhi kiasi cha pesa takribani shilingi bilioni 28 kwa ajili ya ununzi wa mashine za kuchoronga visima kwa ajili ya utafiti unaoendelea. Matarajio yetu, tutaanza kuzalisha megawatts 30 kutoka kwenye joto ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbatia kwamba kwa kweli Serikali inatambua na kuona umuhimu wa kuwa na energy mix ya kutosha kupitia vyanzo mbalimbali na ndiyo maana imejielekeza kwenye umeme wa maji, imejielekeza kwenye umeme wa gesi na miradi mbalimbali inayoendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimthibitishie tu kwamba tulivyojipanga, hilo lengo la millennium litafikiwa na tutakuwa na umeme wa kutosha ambao utaiwezesha nchi yetu pia kusaidia nchi za jirani, nchi za ukanda wa SADC na nchi za ukanda wa Afrika Mashariki. Tumejipanga sasa hivi ujenzi wa njia za kusafirisha umeme unaendelea vizuri katika maeneo hayo ili kuweza kuuza umeme katika nchi za jirani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)
MHE. MARY P. CHATANDA Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipa nafas niulize swali la nyongeza. Nichukue nafasi hii kuishukuru Wizara ya Nishati kupitia Waziri, Naibu Waziri pamoja na watendaji wa TANESCO Mkoa na Wilaya ya Korogwe kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya sasa ya kuhakikisha kwamba vijiji vinapata umeme wa REA katika maeneo yale ambayo yalikuwa yamekosa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la nyongeza ni kwamba; kwa kuwa adha hii imekuwa ni ya muda mrefu na majibu aliyoyatoa Naibu Waziri ni mazuri, yanaridhisha:

Je, ni lini sasa ukarabati huu utakamilika? Maana unaweza ukasema unaendelea kukarabati, halafu inaweza ikawa mwaka mzima unafanyika ukarabati. Ni lini sasa watakamilisha ukarabati huu ili kusudi wananchi waondokane na adha hii ambayo wanaipata sasa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimepokea kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri shukrani zake, lakini kipekee nampongeza Mheshimiwa Chatanda kwa kazi nzuri anayofanya kwenye Jimbo lake, lakini kwa ushirikiano wake pamoja na ofisi yetu ya TANESCO ya Mkoa na Wilaya ya Korogwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye jibu letu la msingi ni kwamba kwanza ukarabati huu ni mkubwa, unahusisha nguzo zaidi ya takriban 920 na unagharimu shilingi bilioni 1,400. Mpaka sasa zaidi ya nguzo 500 zimesharekebishwa, zimeondolewa zile mbovu na zimewekwa hizo mpya. Nataka nimwambie, matarajio yalikuwa tukamilishe mwezi huu Januari mwishoni na huu wa Pili unaoendelea, lakini kwa kuwa mvua zinaendelea, tumeongea na TANESCO tukiwaelekeza kwamba pamoja na changamoto ya mvua, lakini waendelee kufanya haraka kukamilisha nguzo takribani 400 zilizobaki ili wananchi wa Korogwe vijijini na mjini wapate umeme wa uhakika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Mama Chatanda amekuwa akiambatana na TANESCO Wilaya katika maeneo hayo na mwenyewe amejionea. Kwa hiyo, niendelee tu kuwapa pole wananchi wa Korogwe, lakini dhamira ya Serikali kupitia Shirika la
TANESCO ni kuhakikisha umeme unapatikana wa uhakika na muda wote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni wiki iliyopita tu tumepta taarifa ya kuvuja kwa bomba la gesi, suala ambalo ni la hatari lakini ni kudra za Mwenyezi Mungu hakuna madhara yaliyojitokeza. Sasa licha ya juhudi za Serikali kuunganisha viwanda na gesi, nini hatua wanazochukua kunusuru hali ya namna hiyo isijitokeze kwa ajili ya kunusuru maisha ya wat? Swali la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika utawala wa Awamu ya Nne kazi kubwa ilifanyika ya kuhakikisha gesi inazalishwa na kusambazwa viwandani kama njia au nishati mbadala, lakini kwa sasa tunaona nguvu kubwa imewekwa kwenye Stiegler’s na miradi mingine ya umeme wa maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali; Kwa kuwa mradi wa gesi ulikuwa haujatumika kwa asilimia mia moja na tunaona tumehamia mradi mwingine, ni nini mkakati uliopo kuhakikisha mradi wa gesi unazalishwa na unatumika kwanza katika full capacity kabla ya kuhamia miradi mingine? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Anatropia katika swali lake la kwanza ameeleza namna ambavyo taarifa ilitolewa rasmi na TPDC kuhusu kuvuja kwa gesi kwenye maeneo ya Somanga Fungu. Kama anavyofahamu tangu imeanza kujengwa miundombinu ya gesi, tangu gesi imeanza kutumika kwa mara ya kwanza 2004 mpaka sasa ni tukio la kwanza. Kwa hiyo, ni wazi kabisa miundombinu iliyojenga taratibu zote za precaution juu ya masuala ya bomba yalizingatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, taarifa rasmi imetolewa, wataalam wa SONGAs wakishirikiana na TPDC na Wizara ya Nishati walikuwa eneo la tukio na kila kitu kilifanyiwa kazi na kwa sasa kwa kweli hali imetengamaa na tutaendelea kuchukua hatua stahiki kuhakikisha kwamba matukio kama haya hayajitokezi na kama ambavyo inaonesha ni mara ya kwanza. Kwa hiyo, nataka nimtaarifu kwamba hatua zote zitachukuliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ameulizia namna gani tutaendelea kuwekeza katika miradi ya gesi na amehusisha kwamba Serikali ya Awamu ya Tano imejielekeza kwenye mradi wa Mwalimu Nyerere Hydro Power. Naomba nimtaarifu Mheshimiwa Anatropia kwamba katika suala zima la uwekezaji wa masuala ya nishati hususan ya umeme, vipo vyanzo mbalimbali; Serikali yoyote lazima itumie vyanzo mbalimbali mbadala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaposema masuala ya gesi, umeme wa maji, umeme wa makaa ya mawe, umeme wa upepo na umeme wa nishati mbadala pia. Kwa hiyo, Serikali ilipoamua kujielekeza kwenye mradi huu wa Mwalimu Nyerere Hydro Power, ni kuhakikisha kwamba lengo la uzalishaji wa megawatt 10,000 ifikapo 2025 linafikiwa kwa mradi huu mkubwa ambao utazalisha megawatt 2,115.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tumepata kusema ndani ya Bunge chanzo hiki cha kuzalisha umeme wa maji kina nafuu, kinagharimu shilingi 36 tu kwa unit, lakini pia Serikali inaendelea na uwekezaji wa miradi ya kuzalisha umeme kwa gesi. Kwa mfano, hata sasa hivi kuna mradi wa kuzalisha umeme wa gesi Mtwara wa Megawatt 300 lakini pia upo Mradi wa Somanga Fungu Megawatt 330.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri Mkuu alifanya ziara nchini Japan, aliambatana na Maafisa kutoka TPDC akiwepo Mkurugenzi Mtendaji lakini pia hivi karibuni ametoka Urusi, kote kule wamezungumza na wawekezaji mbalimbali na amewaalika kwa niaba ya Serikali kuja nchini Tanzania hapa kuwekeza katika miradi ya gesi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kujielekeza kwenye miradi ya gesi na miradi mingine yoyote ili kupata energy mix ya uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)
MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa matumizi ya gesi asilia siyo kwa viwandani tu, bali hata majumbani:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba unapeleka gesi asilia kwenye majumba katika maeneo ya Ubungo, Manzese, Vingunguti, Mbagala, Gongolamboto, Tandika, Mwananyamala na Tandale; maeneo ambayo yana wakazi wengi ili kuwasaidia akina mama kupata nishati ya gesi kwa bei nafuu; pia katika kupunguza gharama za mkaa na uhifadhi wa mazingira?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mheshimiwa Mariam Kisangi anapozungumzia masuala ya usambazaji wa gesi majumbani, anamzungumzia mwanamke ambaye ndio mtumiaji mkubwa wa rasilimali ya gesi majumbani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nimtaarifu kwamba ni mkakati wa Serikali kwamba kwanza mpaka sasa zaidi ya kaya 500 zimeshasambaziwa gesi asilia katika Mikoa ya Dar es Salaam na Mtwara. Kazi inayoendelea sasa kwa mwaka 2019/2020 tuna matarajio ya kaya zaidi ya 1,000 kuzifikia na kazi inaendelea na mpaka sasa vifaa vyote vya kuunganishia yakiwemo mabomba, mita za matumizi ya gesi vimeshafika na vimeshafungwa na vipo katika nyakati za majaribio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, maeneo aliyoyataja ikiwemo Tandale, Mwananyamala, Mbagala na maeneo ambayo Mbunge anawakilisha, nataka nimthibitishie kwamba Serikali imedhamiria na ndiyo maana imetenga katika mpango mzima matumizi ya gesi, kiasi cha futi za ujazo trilioni 0.7 kwa ajili ya matumizi ya majumbani ili kuokoa mazingira pia. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Swali la msingi lilikuwa linaulizia mradi wa LNG wa Lindi. Napenda kufahamu kutoka Serikalini, ni lini Serikali italipa fidia wakazi wa Likong’o, Mto Mkavu na Mchinga ambao wapo tayari kupisha mradi huu?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bobali, Mbunge wa Mchinga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ameuliza lini fidia italipwa kwa wakazi wa maeneo ya Likong’o, Mchinga na Mitwelo Mkoani Lindi ambao wamepisha eneo kwa ajili ya Mradi huu mkubwa wa LNG. Napenda nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba mwezi uliopita wataalamu wa TPDC na Wizara ya Fedha na Mipango walikuwa ziara katika Mkoa wa Lindi kuhitimisha zoezi zima la tathmini. Matarajio yetu ifikapo Disemba 2019 zoezi la kuanza kulipa fidia kwa wakazi wa maeneo hayo litaanza na litaendelea na hatimaye kukamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwathibitishie wakazi wa Mkoa wa Lindi ambao kwa kweli kwa muda mrefu wamekuwa wakiulizia fidia hiyo, Serikali ya Awamu ya Tano sasa iko tayari kuwalipa. Fidia iliyotengwa ni kiasi cha shilingi bilioni 56 na mambo yote yamekamilika na itaanza kulipwa na wakati huo sisi Serikali na wawekezaji tunaendelea na mazungumzo. Ahsante.
MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, awali ya yote napenda niipongeze Wizara ya Nishati hasa Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya kuifanya Tanzania inayomeremeta. Umeme ni maendeleo, umeme ni uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini kwenye Kata ya Kitumbikwela ambapo kuna Kijiji cha Sinde na Mnali itapatiwa umeme wa REA na maeneo mengine yote yaliyosalia hapa nchini?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa mama yangu Salma Kikwete, Mbunge wa Kuteuliwa na Mheshimiwa Rais.

Kwanza nimpongeze kwa kazi nzuri anayoifanya kutokana na heshima aliyopewa na Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkoa wa Lindi na Mkoa wa Pwani, lakini swali lake limejielekeza kuulizia Kata ya Kitumbikwela, Vijiji vya Sinde na Mnali ni lini vitapata mradi wa REA. Nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mama Salma, natambua hii ni changamoto ambayo aliwasilishiwa alipofanya ziara lakini tumefanya mawasiliano na TANESCO kwa kuwa tuliwapa maelekezo ya kubaini maeneo ambayo yanaweza yakapelekewa miundombinu ya umeme kupitia kwao TANESCO na wamebaini maeneo 754. Moja ya maeneo ambayo wamebaini ni eneo la Kitumbikwela na kwa bajeti ya TANESCO ya mwaka 2019/2020 eneo hilo na vijiji ambavyo amevitaja ikiwemo Mnali vitapatiwa umeme katika kipindi hiki.

Kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge na maeneo ambayo Lindi yamesalia kati ya vijiji 150, Mkandarasi State Grid anaendelea na kazi na tutaratajia ifikapo Disemba, 2019 kazi itakamilika. Kwa hiyo niwape moyo Wananchi wa Mkoa wa Lindi na Waheshimiwa Wabunge wote akiwemo Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mbunge wa Jimbo la Ruangwa kwamba kazi ya mkandarasi inaendelea na tutamsimamia vizuri ili akamilishe. Ahsante sana.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Rais wetu na Serikali nzima, Waziri, Naibu Waziri na Watendaji wote kwa kazi kubwa wanayofanya katika nchi yetu hususani Jimbo la Mbulu Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali yangu madogo ya nyongeza ni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa mahitaji ya umeme katika Jimbo la Mbulu Mji ni makubwa; na kwa kuwa Jimbo la Mbulu Mji sehemu nyingi zilikosa umeme wakati wa REA I na II. Je, sasa Serikali inachukua hatua gani kwa wale wananchi ambao hadi sasa wameendelea kuachwa na umeme umeshapita kwenye maeneo yao na maombi yao hayajibiwi na Ofisi yangu ina orodha kubwa sana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa mahitaji ni makubwa sana ya chombo kinachoitwa UMETA (Umeme Tayari) na kwa kuwa majengo mengi katika Jimbo la Mbulu Mjini yako mbalimbali kwa maana ya nyumba za wananchi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta chombo hiki cha UMETA kwa kiasi kikubwa ili kuwapatia wananchi umeme ambao wana uhitaji mkubwa sana?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zacharia, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Mjini. Nampongeza kwa kazi nzuri anayoifanya katika Jimbo lake hususani katika kufuatilia sekta ya nishati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, ameuliza Serikali ina mpango gani kwa kuwa mahitaji ya umeme ni makubwa na kwa maeneo mbalimbali ambayo hayajafikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba kupitia Serikali yetu kuna Mradi wa Ujazilizi Awamu ya Pili B ambapo Mkoa wa Manyara ni miongoni mwa mikoa 16 ambayo itahudumiwa. Kwa sasa Mshauri Elekezi Multiconsult na Norplan wanaendelea kuhakiki vitongoji katika maeneo mbalimbali. Mradi huu utafadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Ufaransa kwa Euro milioni 100 na unatarajiwa kuanza mapema mwakani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sambamba na miradi ya REA III ambayo itaendelea kupitia TANESCO, nimthibitishie tu Mheshimiwa Mbunge kwa jitihada hizi na huu Mradi wa Ujazilizi kwenye maeneo ambayo umepita vitongoji vimeachwa, Jimbo lake la Mbulu Mjini nalo litazingatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ameulizia masuala ya kifaa kinachoitwa UMETA. Kwanza Serikali kupitia utekelezaji wa Mradi wa REA III, Mzunguko wa Kwanza vimetoa UMETA 250 kwa kila mkandarasi ambapo vinagaiwa bure kwa makundi maalum. Sambamba na hilo, kwa kuwa tumeona uhitaji ni mkubwa Shirika la TANESCO na REA wanaendelea na mchakato wa kuhakikisha UMETA inapatikana kwa bei nafuu ambayo ni Sh.36,000 ambapo kila mwananchi ana uwezo wa kumudu.

Kwa hiyo, niendelee kutoa maelekezo kwa niaba ya Waziri wa Nishati, TANESCO na REA kuendelea kusambaza UMETA hasa kwenye taasisi za umma ambazo hazina mahitaji makubwa na wananchi wa kawaida. Ahsante.
MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoka na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika utekelezaji wa miundombinu ya Dar es Salaam na ukatikaji wa umeme, TANESCO imekuwa haitoi taarifa ya kuwepo kwa tatizo la ukatikaji wa umeme katika baadhi ya maeneo ambayo miundombinu hiyo inatekelezwa, jambo ambalo linasabisha kuleta usumbufu mkubwa kwa wananchi wanaotumia umeme, lakini hasa katika maeneo ya umma, ikiwemo hospitali ya Sinza Jijini Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha kwamba miundombinu ya TANESCO haiathiriki ya umeme kutokana na utengenezaji wa barabara zinazotengenezwa katika eneo hilo la Dar es Salaam?

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, katika baadhi ya maeneo ya Dar es Salaam, ambayo hayapati umeme wa kutosha, ni pamoja na katika Jimbo la Mheshimiwa Mwita Mwaikwabe Waitara, Jimbo la Ukonga, Mheshimiwa Ndugulile Jimbo la Kigamboni, Mheshimiwa Kubenea mwenyewe Jimbo la Ubungo na Majimbi mengine likiwemo la Kibamba.

Sasa Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha Jiji la Dar es Salaam, ambalo ndiyo kitovu cha biashara, linapata umeme wa kutosha na wakati wote bila usumbufu wowote na hasa ukizingatia kwamba, mradi mkubwa wa umeme wa gesi uko Kinyerezi?

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Mheshimiwa Kubenea ameulizia taarifa, endapo, pindi umeme unapokatikatika. Nataka nimtaarifa Mheshimiwa Kubenea, kwamba Serikali kupitia TANESCO tulitoa maelekezo ya kutumia maendeleo ya teknolojia katika kuhakikisha wananchi inawafikia taarifa haraka na maendeleo hayo ni kupitia pia uundwaji wa ma-group mbalimbali na katika Mkoa wa Dar es Salaam, Kanda zote zimeundiwa ma-group na hata mimi mwenyewe nipo kwenye group la Kibamba la utoaji taarifa za huduma ya TANESCO na mikoa yeto ina ma-group ya whatsapp.

Mheshimiwa Naibu Spika, na sambamba na hilo pia, hata katika kikao cha maafisa habari nchi nzima kilichofanyika Mwanza, Shirika la Umme TANESCO na Wizara ya Nishati ni miongoni mwa taasisi na Wizara zilizofanya vizuri katika kuwahabarisha wananchi taarifa mbalimbali zinazohusiana na sekta ya nishati. Kwa hiyo, nataka niwape, pengine kama Mheshimiwa Mbunge hajaungwa kwenye haya ma-group nataka nielekeze kwamba Mbunge wa Ubungo sambamba na Wabunge wengine wote waungwe kwenye ma-group na viongozi wote ili iwe kiungo katika kutoa taarifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia ameulizia namna ya uboreshaji wa miundombinu ya usafiri wa umeme katika Mkoa wa Dar es Salaam. Nataka nimtaarifu Mheshimiwa Kubenea, katika Mkoa wa Dar es Salaam, kwanza kuna mradi mkubwa wa upanuzi wa Kituo cha Ubungo, kituo hiki kinapokea umeme kutoka mitambo ya Kidatu kwa msongo wa kilo vote 220 na inapoza kwenye mashine za MVA 125 na inafanya kwamba, megawatts 200 kusambaza katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sambamba na hilo, kituo hiki kinapokea umeme kutoka mitambo ya SONGAS megawatts 189, mitambo ya Ubungo ll megawatts 129 na Kituo cha Tegeta megawatts 45. Mahitaji ya Mkoa wa Dar es Salaam ni megawatts 500, lakini Kituo cha Ubungo kina uwezo wa megawatts 655. Lakini lazima niseme kwamba mitambo hii inafanyiwa ukarabati, wakati mwingine inafikia ukomo, inatakiwa ibadilishwe vipuli, kwa hiyo, inapotokea hiyo, ndiyo maana changamoto ya kukatikakatika umeme kwa Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanya nini? Serikali ya awamu ya tano kupitia TANESCO inaendelea na upanuzi wa Kituo cha Ubungo, imeshaagzia na imefika mashine ya MVA 300 ambayo itaongeza megawatts 240 kwenye msongo wa kilovoti 132 na kufanya Mkoa wa Dar es Salaam kuwa na upatikanaji mkubwa wa megawatts za kutosha kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ameyataja Majimbo ya Ukonga, ametaja Jimbo la Kigamboni, kwamba lina changamoto. Nataka nimtaarifu, Waheshimiwa Wabunge wa Majimbo haya, akiwemo Mheshimiwa Waitara, Mheshimiwa Ndugulile, wamefanya jitihada kubwa ya kufuatilia maeneo ambayo hayana umeme na ndiyo maana Serikali ikabuni mradi wa Peri-urban na imetenga bilioni 86 na sasa hivi hatua iliyokuwepo ile mikataba ya wakabdarasi ilishafikishwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Kwa hiyo, niwatoe hofu wakazi wa maeneo ya Ukonga, ambako mimi mwenyewe nimefanya ziara kata sita, ikiwemo Zingiziwa, Buyuni, Kivule, lakini pia maeneo ya Somangila, maeneo ya Pembamnazi, maeneo ya Kisarawe ll, maeneo ya Msonga, maeneo ya Buyuni, yote hayo yametengewa bajeti na mradi utafanyika na kwa gharama za REA elfu 27. Wakazi wa Dar es Salaam wakae mkao wa tayari, Serikali ya Chama cha Mapinduzi imejipanga kutekeleza miradi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)
MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la ngongeza.

Tatizo la umeme lililopo Kibamba linafanana kabisa na tatizo la umeme lililopo katika Jimbo la Lupembe Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Tuna vijiji 22 havina umeme, lakini tangu Januari, 2019 mkandarasi wa REA amesambaza umeme katika vijiji viwili kwenye vijiji hivyo viwili amesambaza kitongoji kimojakimoja. Kwa hiyo, nini kauli ya Serikali sasa kuhakikisha kwamba hivi vijiji 22 vinapelekewa umeme na kuhakikisha kwamba mkandarasi huyu anasambaza umeme kwa kasi ili vijiji vyote 22 viweze kupata umeme? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Hongoli atakuwa shahidi, tulifanya ziara pamoja naye katika jimbo lake na nimpongeze kwa kazi nzuri anayoifanya, lakini nataka nimthibitishie mkandarasi JV Mufindi anaendelea na kazi, lakini nataka niwathibitishie Wabunge wote kwa sababu yapo maswali mengi ya Mradi wa REA, kwamba Mradi wa REA bado mudo upo, inatarajiwa ikamilike Juni, 2020.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kama Wizara Mhesimiwa Waziri wa Nishati ametoa maelekezo, miradi ikamilike ifikapo Septemba, 2019. Naomba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge, tutaendelea kumsimamia mkandarsi kwa karibu na ukizingatia sasa hivi wakandarasi karibu wote wameshafanikiwa kupata vifaa vyote vya mradi. Kwa hiyo, nimtoe hofu tu kwamba vijiji 22 vitakalika na kasha tutaanza tena REA Awamu ya III mzunguko wa pili kwa vijiji vyake vyote vilivyosalia, ili kulifanya jimbo lake ifikapo 2021 yote iwe imemeremeta. Ahsante sana.
MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Nataka nipate tu maelezo ya Serikali ni lini mtapeleka umeme katika vile vijiji ambavyo vilishapitishwa kwenye mradi wa REA II vijiji vya Ruvu na Dimba katika Jimbo la Mchinga?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge ameulizia vijiji vyake viwili ambavyo viko kwenye mpango wa kupelekewa umeme katika REA III mzungunguko wa kwanza, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge na tulikutana Lindi nikamuahidi baada ya Bunge hili la Bajeti tutatembelea Jimbo lake na Mkandarasi State Grid kupitia ziara ambayo alifanya Mheshimiwa Waziri katika Wilaya ya Luwangwa, Wilaya ya Nachingwea na Jimbo la Mtama Lindi vijijini ameonesha kupata kasi zaidi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nilitaka nimtaarifu tu kwamba kazi inaendelea katika vijiji alivyovitaja na baada ya Bunge hili kwa ruksa ya Mheshimiwa Waziri tutaambatana naye tukague na tuwashe umeme katika vijiji vyake asiwe na wasiwasi ahsante sana. (Makofi)
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona niweze kuuliza swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa kabla ya kuuliza swali naomba kutoa pole nyingi kwa Wananchi wa Mkoa wa Kagera kwa mafuriko kwa ajili ya mvua nyingi zinazoendelea kunyesha. Mimi Mbunge wao na Serikali tuko pamoja, nawapa pole sana Ndugu zangu wa Mkoa wa Kagera.

Mheshimiwa Spika, sasa swali la nyongeza, changamoto iliyopo Rungwe inafanana kabisa na changamoto iliyopo Wilaya ya Ngara katika Kata ya Mlusagamba, Kata ya Bukiriro na Mganza. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika kata hizo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Mbunge Oliver na kumpongeza, hii ni mara yake ya tatu anasimama ndani ya Bunge hili kuulizia masuala ya nishati katika Jimbo la Ngara. Hizo kata alizozitaja ikiwemo Msagamba, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwa miradi ya REA inayoendelea kata hizi zimeingia kwenye REA Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Pili, ambao unaanza tarehe 01Julai, 2019, tuko katika hatua za kuandaa makabrasha ya zabuni. Kwa hiyo, nimtoe hofu tu kwamba, na Wananchi wakazi wa Ngara kwamba, Serikali yetu ya Awamu ya Tano imedhamiria ifikapo 2020/21 maeneo yote, vijiji vyote vikiwemo vijiji vya Wilaya ya Ngara viwe vimewaka umeme. Kwa hiyo, nimtoe tu wasi Mheshimiwa Mbunge aendelee kushirikiana na sisi katika kufuatilia hayo maeneo yake, asante sana.
MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nashukuru sana:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ile ya Awamu ya Pili ilipeleka umeme katika Mji Mdogo wa Laela, lakini haikushusha umeme katika sekondari ya Lusaka na Sekondari ya Kaengesa. Je, ni lini Serikali itashusha umeme katika sekondari hizo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Malocha amejielekeza kwenye utekelezaji wa REA II ambapo Mji wa Raela nao ulifikiwa, lakini ameeleza Sekondari za Kaengesa kwamba, hazijapatiwa umeme. Nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwanza nimpongeze kwa kazi nzuri, tuliambatana kwenye ziara katika jimbo lake mpaka Kilyamatundu, lakini tulitoa maelekezo kwamba, Mradi wa Ujazilizi Awamu ya II ambao unaanza tarehe 01Julai, 2019 na tuko hatua za mwisho za kuwapata wakandarasi maeneo ya Raela na hususan vitongoji ambavyo havijafikiwa na hizi sekondari.

Mheshimiwa Spika, namuagiza Meneja TANESCO wa Mkoa ahakikishe maeneo haya yanaingizwa kwenye Mradi wa Ujazilizi Awamu ya Pili, ili waendelee kusambaziwa umeme na maeneo menginebya taasisi za umma katika Mkoa wa Rukwa kwa kuwa upo katika orodha ya mikoa 26 ambayo itafikiwa na Mradi wa Ujazilizi Awamu ya II. Ahsante sana.
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa jinsi Waziri na Naibu wake wanavyojibu haya maswali inaonekana kwamba, kazi yao ni nzuri, wanazunguka sana kwenye hii nchi na wana data za kutosha. Nawapongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa katika Jimbo la Rombo kuna Kata za Reha, Nanjara, Kitirima, Mraokerio, Kwandele, ambazo vijiji kadhaa bado havijapata huduma ya umeme na mradi wa ujazilizi bado haujaanza kufanya kazi vizuri. Je, ni lini kata hizi na vijiji vyake sasa mradi wa kuwapelekea umeme utakamilika? Asante.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru sana na yeye pia kwenye jimbo lake tumewahi kufanya ziara, lakini kwa kweli, nikiri katika Mkoa wa Kilimanjaro kulikuwa na changamoto ya utekelezaji wa mradi wa REA II na Serikali ilichukua hatua na ikaitangaza ile kazi tena na mkandarasi yuko site anaendelea. Katika maeneo aliyoyataja ikiwemo Kata ya Nachara na vijiji ambavyo havijapatiwa miundombinu ya umeme Mheshimiwa Mbunge ameulizia masuala ya mradi wa ujazilizi:-

Mheshimiwa Spika, nataka nimtaarifu Mkoa wa Kilimanjaro ni miongoni mwa mikoa 9 ya ujazilizi ambayo itapata mradi wa ujazilizi Awamu ya II, mzunguko wa kwanza. Kwa hiyo, nataka nimtaarifu kwa kweli, vitongoji vyote vilivyosalia katika Mkoa wa Kilimanjaro vitapate umeme na huo mradi kama nilivyosema kwenye maswali ya awali kwamba, uko hatua za kuwapata wakandarasi. Ahsante sana.
MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza. La kwanza vijiji nilivyovitaja vya Katani, Sintali, Nkana na Nkomachindo niseme na Malongwe pamoja na Wapembe nimeuliza kwenye swali la msingi ni lini hasa vitapata umeme? Hapa amesema viatapata kwenye mzunguko wa pili ambao utaisha mwaka 2021 na utaanza mwezi Julai mwaka huu. Sasa ni lini hasa nataka kujua kwa sababu wananchi wa maeneo haya wamezungukwa na maeneo ya umeme?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili vijiji vya Kipande, Kundi kuna sekondari zetu lakini sekondari zote hazijaunganishwa na umeme, pia Kijiji cha Ntemba ambako kuna umeme unapelekwa safari hii hatua chache kama kilometa nne kuna Chuo cha Ufundi cha Mvima na kuna pia Kituo cha Afya cha Mvima. Mheshimiwa Naibu Waziri alipokuja walitoa ombi la kuunganishiwa umeme na hadharani tulikubali kwamba tutawaunganishia umeme. Ni lini katika maeneo haya huduma za jamii yatapata umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nilifanya naye ziara katika Jimbo la Nkasi Kusini na maeneo aliyoyataja hayo tulitembea kwa pamoja. Lakini nataka niseme kwamba katika swali lake la msingi kwa vijiji alivyovitaja ikiwemo cha Wampembe anaulizia ni lini hasa umeme utawaka. Kama ambavyo tumejieleza katika jibu la msingi kwamba mradi wa REA awamu ya tatu mzunguko wa pili unatarajiwa kuanza tarehe 01 Julai, 2019 na kwa kuwa leo ni bajeti yetu nimwombe Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako tukufu liridhie bajeti hii ili tuanze kutekeleza mradi huu na kwa kuwa hatua za awali zimeshafanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili anaulizia umeme ambao unapelekwa katika Kijiji cha Ntemba ambako mita chache kuna Kituo cha Ufundi na Kituo cha Afya, ni kweli nilivyofanya ziara katika eneo lake jambo hili lilijitokeza na kwa kuwa ni sera ya Serikali ya Awamu ya Tano kwamba maeneo yote ya huduma za jamii ikiwemo vyuo, shule za sekondari na vituo vya afya vipatiwe umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee kusisitiza ahadi hii ipo na kwamba eneo hili litapatiwa umeme na kama alivyosema Mheshimiwa Waziri katika majibu ya nyongeza kwamba tumeelekeza TANESCO kufikisha umeme katika taasisi mbalimbali na kazi hiyo inaendelea. Ahsante.
MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ni kwamba Serikali imesema kwamba hakuna fidia katika miradi hii ya umeme wa REA. Ningependa kujua sasa kwamba je, Serikali ipo tayari kuwaelimisha wananchi kujua kwamba hakuna fidia kabla miradi ile haijaanza kutekelezeka? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa kuna vijiji vingi sana hapa Tanzania ambavyo vimepitiwa na nguzo juu lakini umeme haujashuka kwenye vijiji vile na katika nchi yetu ya Tanzania pia hata katika Jimbo langu limeshuhudia kuna vijiji mpaka sasa mradi wa umeme ulipita tangu mwaka 2014, nguzo zimepita juu lakini wananchi hawajashushiwa umeme.

Je, Serikali ipo tayari sasa kuangalia vijiji hivyo vyote Tanzania nzima na kuhakikisha kwamba vijiji hivi vinapatiwa umeme vikiwemo vile vya Jimbo la Busanda ambavyo vipo vingi Nyaruyeye na Busaka hawajapata umeme? Niombe Serikali iweze kunijibu. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Lolesia kwa kazi nzuri anayoifanya lakini maswali yake amejielekeza kwenye namna gani Serikali itaelimisha wananchi. Nichukue fursa hii kwanza kuwashukuru Watanzania wote kwa maeneo mbalimbali ambapo miradi hii ya REA inatekelezeka, kwa kweli Serikali, REA,TANESCO hata na Wizara yenyewe ya Nishati haijapata changamoto kubwa ya madai ya fidia.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwanza Watanzania wenyewe wapo tayari, lakini sisi tutaendelea kuelimisha kadiri tutavyopata fursa kwenye ziara mbalimbali za Mikoa na Wilaya ikiwemo kwenye Jimbo lake la Busanda kwamba wananchi kwa kweli kwa kuwa Serikali inalipia gharama zote na wao wanalipia VAT tu shilingi 27,000 na haijawahi kuwa kikwazo, tutaendelea kutekeleza mradi huu na tunawaomba watupe nafasi zaidi na waiunge mkono Serikali yetu ya Awamu ya Tano yenye nia ya kuhakikisha ifikapo mwaka 2021 vijiji vyote 12,268 vinapata umeme.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ameuliza katika vijiji ambavyo vimepitiwa na umeme wa msongo mkubwa lakini havijashushiwa umeme, nikiri kweli tatizo hilo lipo na hivi karibuni Mheshimiwa Waziri wa Nishati alivyofanya ziara katika maeneo mbalimbali ya hapa Dodoma, maeneo ambayo miundombinu ya umeme mkubwa imepita lakini hawajashushiwa, wametoa maelekezo kwa TANESCO kwamba ifikapo Desemba 2019 maeneo yote yaliyopitiwa na miundombinu ya umeme haijashushwa umeme, ishushwe kwa sababu katika maeneo hayo kinachofanyika ni ujenzi wa line ndogo LV na kuweka transfoma na kuwaunganishia wananchi umeme kwa bei ileile ya shilingi 27,000. Kwa hiyo, nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge ikiwemo vijiji alivyota kwenye Jimbo lake la Busanda, Mkoa wa Geita na mikoa mingine yote nchini kwamba tatizo hilo kwa kweli tunaliona na tumeshaliwekea mikakati kama miradi ya Quiq Wins katika kupelekea utekeezaji wa mradi huo. Nakushukuru sana.
MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona na kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza kwenye Wizara hii ya Nishati.

Mheshimiwa Spika, sisi katika Wilaya ya Longido na hata Monduli pia, tumepitiwa na umeme wa msongo mkubwa na napenda kuishukuru Serikali kwa sababu wameshalipa fidia kwa watu wale ambao walistahili kufidiwa, lakini pia naomba kuuliza kwa sababu vijiji vilivyopitiwa katika Wilaya yangu ya Longido ni vitano; Eorendeke, Kimokorwa, Oromomba, Ranchi na Engikaret kuna maeneo mahsusi ambayo jamii iliyatenga kama maeneo ya wazi wakitarajia kwamba fidia yake itakwenda kurudishwa ndani ya kijiji waweze kufanyia miradi ya maendeleo kama kujenga shule, zahanati na kuboresha miundombinu mbalimbali ambayo ni pungufu sana ikiwa ni pamoja na barabara katika vijiji vile.

Mheshimiwa Spika, je, ni lini Wizara itarejesha hizo fedha za maeneo ambayo jamii iliyatenga kama maeneo ya wazi kwa vijiji husika au halmashauri ili tuweze kufanyia hayo maendeleo ambayo tayari wananchi wameshabainisha? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa na nimpongeze kwa kufuatilia masuala ya nishati hususan fidia ya wananchi wake.

Mheshimiwa Spika, ni kweli maeneo aliyoyataja ikiwemo Wilaya ya Longido yamepitiwa na njia ya msongo wa KV 400 kutoka Singida – Namanga na tumeshalipa fidia takribani kama shilingi bilioni 44 na maeneo aliyosema ambayo yalikuwa ya maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli za jamii, thamani yake ya fidia ni kama shilingi bilioni 10, utaratibu unaendelea wa kuweza kuyalipa katika maeneo mbalimbali ili pesa hizo ziweze kuchangia shughuli za maendeleo, nakushukuru.
MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, awali napenda tu nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri aliyefanya ziara yake tarehe 16 Mei ambayo imesaidia sana hasa kwenye Mradi wa REA III.

Mheshimiwa Spika, Kata ya Mgori ambayo ina shule ya kidato cha tano na sita pamoja na Kituo cha Afya cha Mgori pamoja mgodi wa dhahabu pekee tulionao Jimboni wa Mpitipi katika Kata ya Mudida ambavyo vyote vipo katika umeme wa REA II havijapata umeme hadi sasa. Mgodi huu upo kilometa tatu tu kutoka ulipo umeme wa REA mpaka sasa.

Je, Waziri anawaambia nini wananchi kwamba maeneo haya yatapatiwa umeme lini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili Kata ya Kinyeto yenye Kijiji cha Kinyeto, Mkimbii, Ntunduu na Minyaa pamoja na Kata ya Muhama yenye Kijiji cha Muhama na Msikii vipo katika umeme wa backbone. Vijiji hivi havijapata umeme mpaka sasa kwa sababu wanahitaji ku-upgrade kutoka umeme wa kilovolti 11 kwenda kwenye kilovolti 33.

Je, Mheshimiwa Waziri anatuahidi ni lini zoezi hili la upgrade litafanyika ili wananchi hawa waweze kupata umeme, ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Monko na nimshukuru na yeye na kumpongeza sana kwa kazi nzuri na kama alivyosema Mheshimiwa Waziri wa Nishati alifanya ziara katika Mkoa wa Singida tarehe 16 Mei na kutoa msukumo mpya wa kasi ya miradi hii.

Mheshimiwa Spika, maswali yake mawili yalijielekeza kwanza kwenye Kata ya Mgori ambayo ipo chini ya REA II ambapo kwa kweli kulikuwa na changamoto katika Mkoa wa Singida na Kilimanjaro na ndiyo maana Serikali ilichukua hatua za haraka za kusitisha mkataba na kumpa mkandarasi mwingine na mpaka sasa hivi kazi zinazoendelea katika mradi wa REA II wa mkandarasi EMEC ni vijiji vinne vimeshawashwa kati ya 16.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba maeneo haya aliyoyataja yakiwemo na Mgori na kwenye mgodi huo kwa kuwa kazi inaendelea na kulikuwa na changamoto ya vifaa, Mheshimiwa Waziri aliielekeza REA iwasilishe vifaa mapema. Nimthibitishie tu kwa kipindi ambacho tunaelekea mpaka mwezi wa tisa, vijiji 12 vilivyosalia ikiwemo vya Kata ya Mgori vitapata umeme kutokana na jitihada zake za usimamizi na kufuatilia.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ameulizia suala la Kata ya Kinyeto ambapo ipo katika mradi wa backbone na katika Jimbo hili, mradi huu unahusisha vijiji tisa na mpaka sasa hivi vijiji sita vimeshawashwa bado vijiji vitatu ambavyo Mheshimiwa Mbunge ndiyo ameviulizia hapa. Na kwa kuwa tatizo ni ku-upgrade tu kutoka KV 11 mpaka 33, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge mara baada ya kutoka hapa tufanye mawasiliano na REA na kwa kuwa siyo changamoto kubwa na transfoma za aina hii zipo, ni kwamba ndani ya mwezi tu mmoja mpaka mwisho wa mwezi wa sita huu vijiji vilivyosalia ni vitatu na viwake. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, tatizo la miradi hii ya REA ambapo unakuta mradi umefika kwenye eneo kama kijiji lakini unakuta nyumba, taasisi za kidini, taasisi kama shule, zahanati, pampu za maji zimeachwa bila kuunganishiwa umeme, ni tatizo ambalo lipo pia Jimboni kwangu Bukene na Wilaya ya Nzega yote.

Mheshimiwa Spika, sasa ninachotaka kujua ni kwamba pamoja na kwamba Waziri alifanya ziara na akatoa maelekezo maalum kwa Mkandarasi wa Wilaya ya Nzega ambaye ni POMI Engineering kuhakikisha maeneo yaliyoachwa yanaunganishwa, lakini mpaka sasa mkandarasi huyu inaonekana ameshindwa kabisa kupata vifaa vya kuunganishia maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, sasa nilitaka kujua je, Serikali iko tayari kutoa maelekezo maalum au kumsaidia huyu mkandarasi ili aweze kupata hivi vifaa; waya, nguzo ambavyo inaelekea kabisa kumpata…

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. SELEMANI J. ZEDI:...ili aweze kufanya kazi ya kuunganisha maeneo hayo yaliyoachwa. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zedi, Mbunge wa Bukene kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze pia Mheshimiwa Zedi kwa kazi nzuri ndani ya Jimbo lake, wiki moja iliyopita tulikuwa katika ziara ya Jimbo lake na nilifanya pia ziara katika Wilaya ya Nzega. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, umelisema kwa jumla pia suala hili la vifaa, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Zedi na Wabunge wote, kweli zipo changamoto za hapa na pale kuhusu vifaa, lakini tukitathmini mchango wa sekta ya nishati kwenye viwanda vya ndani, kwa sababu changamoto hii imejitokeza baada ya kutoa agizo vifaa vyote vinavyotumika katika mradi huu vizalishwe ndani ya nchi na agizo hili limesababisha kuwezesha viwanda zaidi ya tisa vipya vinavyozalisha nguzo, viwanda zaidi ya vinne vya mita na viwanda zaidi ya vitano vya waya havikuwepo nchini, vyote hivi vimetokana na agizo la kuhakikisha kwamba vifaa vyote vinavyotumika kwenye miradi hii vizalishwe ndani ya nchi ili vilete ajira lakini pia mapato kwa wananchi lakini pia mapato kwa wanaoajiriwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Zedi mimi nikuthibitishie tu sisi kama Wizara tunaendelea kusimamia kuhakikisha changamoto hii inapungua na kama nilivyosema katika majibu mbalimbali ndani ya Bunge lako tukufu, imeendelea kupungua na ndiyo maana leo tunajivunia zaidi ya vijiji 1,400 tumeshaviwasha kwenye REA III mzunguko wa kwanza ukiacha na awamu zingine.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nitoe wito kwa wakandarasi pamoja na ma-supplier kwa kuwa wanategemeana, wakae pamoja ili kuondoa vikwazo mbalimbali ambavyo vinaonesha kwamba vinachangia kutokuwepo kwa vifaa kwa wakati katika maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niwaombe tu Wabunge muendelee kutuunga mkono katika hili ili mradi huu unaotumia shilingi trilioni moja na bilioni 200 uchangie uchumi wa taifa kwa kutekeleza Sera ya Viwanda, asante sana. (Makofi)
MHE. ANNE K. MALECELA:Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kupata nafasi hii. Jimbo la Mheshimiwa Mnzava ni mpakani na kijiji changu cha Kongei ambako nimezaliwa na umeme kwenye kijiji hiki umefika muda mrefu, lakini kuna Vitongoji vya Mabambara, Ihindi na Idurundi, huenda vimesahauriwa kabisa. Mheshimiwa Waziri unaniambia nini katika hili?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda nijibu swali moja la Mheshimiwa Mama yangu Anne Kilango Malecela na nimshukuru sana kwa kazi nzuri ya kufuatilia sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya nishati na kwa kuwa swali lake la nyongeza ameulizia katika usambazaji wa umeme kwenye vitongoji vilivyosalia katika Kijiji chake cha Kongei.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimtaarifu kwamba Mkoa wa Kilimanjaro ni miongoni mwa mikoa tisa ambayo mradi wa ujazilizi awamu ya pili ambao upo hatua za kumpata mzabuni, Mkoa huu wa Kilimanjaro umo kwenye mikoa hiyo tisa na nimwagize Meneja wa TANESCO Mkoa wa Kilimanjaro na wa Wilaya ya Same azingatie vile vijiji ambavyo vimepatiwa umeme kikiwemo Kongei, lakini vipo vitongoji ambavyo havina umeme ili waendelee kusambaza kupitia umeme wa ujazilizi awamu ya pili ambapo Bunge letu mmetupitishia takribani shilingi bilioni 169 na tunawashukuru sana. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi, katika Wilaya ya Chunya, Kijiji cha Itumbi, ni sehemu ambayo Wizara ya Madini imetenga vitalu vya wachimbaji wadogo wadogo kwa Wilaya nzima na Wizara ya Madini ni sehemu ambapo inajenga kituo cha ushauri kikubwa kwa wachimbaji wadogo wadogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini REA Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza, kijiji hiki hakijapitiwa. Je, Serikali inatoa tamko gani kwenye kijiji hiki cha muhimu sana?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nimpongeze sana Mheshimiwa Mwambalaswa katika swali lake la nyongeza.

Kwanza ningependa sana nimshukuru katika mambo mawili, la kwanza, alituletea maeneo yote ambako kuna uchimbaji wa madini, na sisi kutpitia Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) tumeshaainisha Kijiji cha Itumbi kwa sababu ni kijiji cha mfano kwa wachimbaji wadogo na tumeshatenga transfoma mbili za kVA 315 kila kijiji, kikiwemo Kijiji cha Itumbi. Kwa hiyo, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Kijiji cha Itumbi kitapelekewa umeme kwa sababu tunajua umuhimu wa wachimbaji wadogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, na mpango huu tumeuanza kwa nchi nzima, tumemaliza kufunga transfoma tatu katika Mgodi wa Nyakafuru, tumewasha mwezi uliopita na sasa hivi tunahangaika na kuwasha kwa wachimbaji wadogo eneo la Kidirifu na Itumbi, pamoja na K9 kule Geita, pamoja na Kidirifu na Society kule Katavi. Kwa hiyo, ni wananchi wote ambako kuna migodi, shuguli za uchimbaji tunazithamini sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, wiki iliyopita nilikwenda Mwakitoryo, Mwakitoryo nao watafungiwa transifoma ya kVA 315 Ijumaa wiki hii. Kwa hiyo, maeneo yote ya migodi likiwemo eneo la Itumbi, Mheshimiwa Mbunge yatafungiwa umeme natutakuja kuwasha umeme wenyewe hapo Itumbi kwa wachimbaji wadogo. (Makofi)
MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na kwa kweli nitumie fursa hii kumpongeza sana Waziri kwa sababu katika Wilaya ya Monduli vijiji vilivyokuwa vimepatiwa umeme peke yake vilikuwa 16 na sasa karibu vijiji vyote 64 vitaingizwa kwenye awamu ya tatu. Lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, tatizo kubwa la REA katika maeneo mengi ni kwamba umeme unafika kwenye kijiji lakini vitongoji na maeneo mengi ya wananchi umeme ule haufiki.

Je, nini mkakati madhubuti wa Serikali kuhakikisha kwamba maeneo yote ambayo umeme haujafikia japo inaonekana kijiji kimefikiwa umeme unaweza kupelekwa kwa wananchi kuliko kuwa na umeme ambao umefika kijijini lakini wananchi hawajapata umeme?

Mheshimiwa Spika, swali la pili katika Kata ya Engaruka katika Shule ya Oldonyolengai tayari laini kubwa imefika ni kazi ya kuunganisha tu katika shule ya msingi Engaruka Juu na katika zahanati ya Oldonyolengai. Je, nini kauli ya Serikali kwa mkandarasi aliyoko site ili aweze kuunganisha umeme katika maeneo hayo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Julius na kwa niaba yake napokea pongezi zake kwa kazi nzuri aliyoifanya katika Mkoa wa Arusha na maeneo mbalimbali na pia nimpongeze Mheshimiwa Julius kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya katika jimbo lake la Monduli.

Mheshimiwa Spika, kama alivyouliza na nakiri ndani ya Bunge lako kweli miradi hii ya umeme inayoendelea REA awamu ya tatu au na REA awamu mbalimbali kazi yake ya msingi ya kwanza ni kufikisha miundombinu ya umeme mkubwa katika baadhi ya maeneo kwenye vijiji.

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua hilo na ndio maana Serikali yetu ya Awamu ya Tano imebuni mradi wa ujazilizi awamu ya kwanza ambao ulifanyika katika mikoa 8 na tumepata mafanikio makubwa wateja takribani 30 wamepatiwa umeme katika vijiji 305. Mpango unaoendelea sasa hivi ni Ujazilizi Awamu ya Pili A kwenye mikoa tisa ikiwemo Mkoa wa Arusha pia Mkoa wa Mwanza, manispaa za Ilemela na Nyamagana na maeneo mbalimbali. Sambamba na hilo katika mradi huu wa REA wa Ujazilizi Awamu ya Pili takribani Bunge lako tukufu limetupitishia pesa shilingi bilioni 169 ambayo inaenda kuwezesha wateja wa awali 60,000 kuunganishiwa umeme.

Kwa hiyo, nimtaarifu tu Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa bajeti imeshapita tunawaahidi kwamba tutaendelea kuisimamia ili vitongoji vyote viendelee kuunganishwa lakini kwa kweli kazi kubwa kwanza ni kufikisha umeme katika maeneo ya makao makuu ya vijiji kasha usambazaji ni jambo endelevu. Pia naomba niseme taarifa ya ziada tumeielekeza TANESCO wamebaini maeneo 754 ambayo yamepitiwa na miundombinu ya umeme mkubwa na pale kazi kubwa itakuwa ni kuweka transfoma na kushusha huo umeme na kwa kuwa tumeamua TANESCO, REA yote ishambulie na ndio maana Serikali imefanya maamuzi ya makusudi ya kisera kufanya kwamba bei ya kuunganishia umeme 27,000.

Mheshimiwa Spika, naomba nikutaarifu na Bunge lako juzi tulikuwa na mkutano mkubwa na tutaanza kuzindua wateja wanaounganishwa kwa bei shilingi 27,000 na tunaanza Wilaya ya Kondoa wameshaunganishwa wananchi 500 baada ya uamuzi wa Serikali. Kwa hiyo, niwatoe hofu wananchi wote na vitongoji ambavyo hawajaguswa.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, ameelezea masuala ya kwa kuwa laini kubwa imefika katika Kata ya Engaruka, ameuliza; Serikali inatoa maelekezo gani kwa mkandarasi ambaye ni NIPO Group aliyeko katika Mkoa wa Arusha. Juzi mkutano wetu baina ya REA na TANESCO tumeendelea kutoa msisitizo umuhimu wa kuunganisha taasisi za umma katika miradi inayoendelea.

Kwa kuwa TANESCO tumeipa mamlaka sasa na wao kuendelea kusambaza umeme vijijini kwa bei ya shilingi 27,000 na kwa kuwa imetenga shilingi bilioni 40 na Bunge mmeidhinisha ni wazi maeneo haya ya taasisi za umma yatafikiwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, REA na TANESCO wataendelea kushambulia maeneo mbalimbali ili kukamilisha na watanzania wapate fursa ya kutumia umeme kwa bei nafuu ikiwa ni azma ya Serikali yetu ya Awamu ya Tano. Ahsante sana.
MHE. ALLY SEIF UNGANDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, nina maswali mawili ya nyongeza, moja kwa kuwa sasa wananchi hawa wa Delta wamesubiri sana kwa muda mrefu umeme wa solar; Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuwapelekea hata taa katika wakati huu mfupi ili waweze kujipatia huduma kwenye vituo vya afya na shule?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa wananchi wa Lungungu, Nyamatanga, Lwaluke, Kikale, Mtunda, kuna laini kubwa ambayo imepita na tayari kazi imekamilika. Je, lini umeme utakwenda kuwashwa kwenye maeneo hayo?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI Mheshimiwa Naibu Spika, kiukweli nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge Ungando hii ni mara ya tatu anawaulizia wananchi wa Visiwa vya Delta, kwa kuwa ni Mbunge wa Mkoa wa Pwani natambua Visiwa hivyo na nimefanya ziara kimoja hadi kimoja vyote pamoja naye Mheshimiwa Mbunge Ally Seif Ungando.

Mheshimiwa Naibu Spika, atakubaliana na mimi kwamba kwa kuwa Serikali yetu ina nia ya kufikisha umeme vijiji vyote nchini, na kwa kuzingatia yapo maeneo kama 89 hivi ambayo yako Visiwani na wao lakini wana haki ya kupata umeme. Ndiyo maana kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Serikali iliamua kufanya upembuzi yakinifu kuainisha mahitaji na kumpata mzabuni mkandarasi ambaye atafanya kazi hiyo na mchakato huo unakamilika tarehe 26 Juni, 2019.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza ameainisha kwa kuwa huu muda wa mchakato mpaka mkandarasi, inawezekana ikachukua muda mrefu anauliza namna gani Serikali inaweza ikatumia mkakati wa muda mfupi wa kuwezesha hususan taasisi za umma ikiwemo kituo cha afya cha Mbwera. Tunaishukuru sana Serikali kwa mara ya kwanza kutupatia fedha za kujenga kituo cha afya Mbwera, kinapatiwa umeme mara baada ya kuanza shughuli zake.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimtaarifu tu Mheshimiwa Mbunge hilo tumelipokea na Wakala wa Nishati Vijijini katika maeneo ya Kiongoroni, Kiechuru, Kiasi na Mbwera itafanya kupeleka mfumo wa taa kwa ajili ya taasisi za umma ili zitoe huduma kabla mradi huu wa kupeleka nishati ya solar katika maeneo hayo kwa ajili ya matumizi ya wananchi na wa taasisi za umma.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, Mheshimiwa Mbunge ameyaulizia maeneo ya Lungungu, maeneo ya Rwaluke, maeneo ya Nyamatanga, maeneo ya Mtunda. Maeneo haya kulikuwa na mradi wa REA Awamu ya Pili na mkandarasi hakufanya vizuri lakini Serikali hii inayoongozwa na Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli iliamua kuanza tena mchakato na maeneo yale ambayo kazi haikukamilika ilipewa TANESCO na baada ya kupewa TANESCO wameendelea na kazi. Nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge ajiandae ili twende tukazindue kuwasha umeme kuanzia Jumatano wiki ijayo mara baada ya kuhitimisha bajeti yetu ya Serikali. Tutafanya sherehe kubwa sana katika maeneo haya kwa kuwa wamesubiri muda mrefu. Kwa hiyo, niwataarifu wakati wa Kibiti kwamba maeneo haya ambayo mmesubiri Serikali imefanya kazi na tutawasha umeme kwa kishindo. Ahsante sana.
MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nimesikiliza majibu ya Serikali kwa namna zoezi hili linavyokwenda kwa kusuasua hivi, Serikali itafanya juhudu gani za ziada ili ifikapo Juni, 2020 kama alivyosema Naibu Waziri kwamba umeme huo umefika katika Vijiji vya Ipungusa, Msolwa, Kalengakule, Miembeni, Iduindembo, Ipungusa, Matema, Lumumwe, Uchindile, Kitete, Idandu na Mgwasi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika Manispaa ya Morogoro zipo kata ambazo hazina umeme licha ya kuwepo mjini, kata hizi ni Kauzeni Juu, Kiegea, maeneo ya Mkundi, Magadu Juu, katika Kata ya Tungi maeneo ya Paranganyiki, Kambi A, na B; Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwa wananchi hao?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Devotha Minja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza Mheshimiwa Devotha Minja ameulizia ni namna gani Serikali itafanya kuhakikisha ifikapo Juni, 2020 kwamba umeme maeneo hayo yaliyotajwa katika swali la msingi yanapatiwa umeme. Naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge, ni kweli kulikuwa na kusuasua kwa mkandarasi State Grid katika Mkoa wa Morogoro lakini hivi ninavyosimama ndani ya Bunge naomba nimtaarifu kwamba kwa wiki ijayo kwanza kwa sasa alishawasha vijiji 18 kati ya 150 katika Mkoa Morogoro; na kwa kuwa kulikuwa na tatizo la nguzo, alikuwa na nguzo zaidi ya 900 ambazo zilivyopimwa zilionekana kama haizifai. Ninapozungumza ndani ya Bunge zaidi ya nguzo 700 zimeonekana zinafaa sasa zinaweza zikaendelea na mradi na wiki ijayo anapokea nguzo 2,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, wiki ijayo atawasha vijiji 16 vikiwemo 6 vya Wilaya ya Kilombero vikiwemo alivyovitaja ambavyo ni Kilama, Kalengakelu, Matema, Iduendemo, Miembeni na Msolwa. Vijiji hivi vitawashwa wiki ijayo na mimi natarajia kufanya ziara katika Mkoa wa Morogoro, tutamwalika Mheshimiwa Mbunge tuambatane pamoja. Sambamba na hilo, kwa hiyo nithibitishe tu kwamba kwa kweli kama tulivyojipanga na kwa kuwa tumejitahidi kutatua changamoto zinazojitokeza na zipo bado zinaendelea lakini tunakaa vikao mara kwa mara. Tuna uhakika mpaka ifakapo Juni, 2020 tutakamilisha mzunguko wa kwanza REA Awamu ya Tatu.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ameulizia kwenye Manispaa ya ya Morogoro, naomba nimtaarifau Mheshimiwa Mbunge mwenyewe nimeshatembelea Manispaa ya Morogoro kama mara mbili nikiwa na Mheshimiwa Aboud. Moja wapo ya maeneo ambayo tuliwasha ni maeneo ya Tungi, ni kweli maeneo ni mengi na kwa kuwa Mkoa wa Morogoro una kua sana katika ujenzi wa makazi. Maeneo haya kwa kuwa tumelitambua hilo, kama nilivyosema hapa Bungeni tuliona kwamba licha tu ya Wakala wa Nishati Vijijini kuendelea na kazi ya kusambaza umeme vijijini lakini pia tuitake TANESCO nayo ifanya kazi hiyo hiyo na kwa kuwa tumesema bei ya kuunganisha iwe 27,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kulitambua hilo katika mpango mkakati wa ndani ya TANESCO na kwa kuwa tumeona tuna umeme wa ziada unaosalia kama Megawatts 300, TANESCO kwa mwaka wa fedha 2019 itajielekeza kwanye miradi ya distribution (usambazaji wa umeme). Takribani milioni 400 zimeidhinishwa na Bunge lako Tukufu kwa ajili ya kusambaza umeme katika maeneo ambayo yanakuwa kwa kasi yakiwemo Majiji na Manispaa, ikiwemo Manispaa ya hapa Dodoma, Manispaa ya Morogoro, Jiji la Tanga, Jiji la Mwanza, Jiji la Mbeya na maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimthibitishie tu Mheshimiwa Mbunge jana nilikuwa Kondoa kukagua haya maelekezo yalivyoanza. Kweli TANESCO wameanza kazi ya kupeleka vijijini umeme na kwa kuunganisha wateja 27,000. Nimehakikisha kweli jana tu wateja zaidi ya 500 wameunganishwa baada ya maelekezo ya Serikali ya Awamu ya Tano kwamba TANESCO sasa kazi kubwa ni kutafuta wateja na ipunguze bei ya kuunganisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nilithibitishie Bunge lako tunatambua mahitaji, tumejipanga vizuri na tutaendelea kusimamia na kupambana ili lengo hili lifikie. Ahsante sana.
MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Pia nichukue fursa hii kuwapa hongera sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa juhudi kubwa wanayoweka katika utekelezaji wa miradi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nina swali moja la nyongeza. Kijiji cha Kondo katika Kata ya Zinga ambacho kilikuwa kwenye mradi wa REA II, mpaka kufikia Juni 2016 kijiji hicho hakikutekelezewa mradi wake na Mheshimiwa Waziri akaahidi vijiji vyote ambavyo havikutekelezewa miradi yao katika REA II basi vitapewa kipaumbele katika REA III. Huu ni mwaka 2019 kijiji hicho ambacho kiko katika Kata ya Zinga na humo ndani kuna Shule ya Msingi ya Kondo na jirani kuna Shule ya Sekondari ya Zinga, sehemu zote hizo hazina umeme mpaka hivi sasa. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri ana kauli gani kuhusu kukipatia umeme Kijiji hiki cha Kondo na miundombinu ya Shule ya Sekondari Zinga na Shule ya Msingi Kondo mapema iwezekanavyo? Ahsante sana. (Makofi)
WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya kwenye swali la msingi la Mheshimiwa Mbunge. Nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Kawambwa kwa kazi nzuri anayofanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabla sijajibu swali, Mheshimiwa Mbunge katika Jimbo lake vijiji vyote sasa vimeshapata umeme kwa sababu ya kazi anayoifanya anavyofuatilia, kilichobaki ni vitongoji. Kwa hiyo nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge, kati ya wilaya ambazo sasa hivi vijiji vyake ambavyo vimeshapata umeme ni pamoja na Jimbo la Bagamoyo, kwa hiyo Mheshimiwa hongera sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, alishughulika sana na Shule ya Sekondari ya Fukayosi mwaka jana, ilikuwa na changamoto ya umeme na imejengwa na Korea Kusini, tunampongeza sana ina umeme sasa hivi na inakwenda vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna vitongoji 169 katika Jimbo la Mheshimwa Mbunge; vitongoji 161, vitongoji 100 vyote vina umeme bado vitongoji 69 na Kati ya vitongoji 69 ambavyo havina umeme ni pamoja na Kitongoji cha Kondo. Kwenye Kijiji cha Kondo kuna vitongoji vitatu; vitongoji viwili tayari vina umeme isipokuwa Kondo Kati anayozungumza Mheshimiwa Mbunge.

Kwa hiyo nimpe tu imani Mheshimiwa Mbunge kwamba nimeshawaelekeza wakandarasi kwa kushirikiana na TANESCO wameshaanza kupeleka umeme kwenye Kitongoji cha Kondo na watakamilisha tarehe 12 mwezi ujao. Wanapeleka kwenye Kitongoji cha Kondo pamoja na Shule ya Msingi ya Kondo, lakini pamoja na Shule ya Sekondari ya Zinga. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge wala asiwe na wasiwasi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niongeze kidogo kwa Jimbo la Bagamoyo na Chalinze, mkandarasi aliyeko kule anapeleka umeme kwenye vitongoji vyote na Peri urban inaanza tarehe Mosi mwezi ujao kujumuisha vitongoji vyote vya Bagamoyo pamoja na Chalinze. Chalinze kuna kijiji kirefu sana cha Msigi pamoja na Magurumatare cha kilomita 28 na chenyewe kinapelekewa umeme. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa chanzo cha umeme cha maji cha Tulila kipo katika Kata ya Mpepai na miundombinu yake inapitia katika Kitongoji cha elfu mbili na vijiji vya Kata za Mapendano kuelekea Songea, Serikali haioni umuhimu wa kuvipatia Vijiji vya Kata za Mpepai na Kihungu umeme kwanza kabla ya vijiji vingine hasa ukizingatia vijiji hivyo hulinda na kuitunza miundombinu hiyo na hivyo kuwafanya wananchi wa Mpepai kupata hisia za kuwa wametengwa na kubaguliwa kwenye huduma hiyo ya umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ni kweli miundombinu ya umeme kutoka katika chanzo cha maji cha Tulila inapita katika Kata za Mpepai na Kihungu. Katika Kata ya Kihungu kuna Vijiji vya Pachasita na Kihungu ambavyo tayari vimeunganishwa na huduma ya umeme. Kijiji kimoja cha Lipembe kitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA III unaoendelea.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika jibu la msingi kuwa kupitia utekelezaji wa mradi wa REA III, Mzunguko wa pili, vijiji vyote vya Kata ya Mpepai ambavyo ni Lipilipili, Luhangai, Mtua, Mpepai na Ruvuma chini vitapatiwa umeme.