Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Mwantum Dau Haji (33 total)

MHE. MWANTUMU D. HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri aliyoyasema Mheshimiwa Waziri, naomba niongeze swali langu la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kuna Askari Polisi ambao kwa maksudi wanafumbia macho masuala ya biashara za madawa ya kulevya katika kuhakikisha mipango ya Serikali ya kudhibiti madawa ya kulevya inafikiwa. Je, kutakuwa na utaratibu gani wa kuwadhibiti Askari ambao hawaendi na kasi ya kupambana na biashara hiyo haramu ya madawa ya kulevya? (Makofi)
MHE. DKT. ABDALLAH S. POSSI - NAIBU WAZIRI, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU: Mheshimiwa Spika, labda niseme tu kutokuchukua hatua kuzuia uhalifu ni kosa la jinai kisheria. Kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Mbunge, Wabunge wote au mwananchi yeyote mwenye taarifa kuhusu Askari ambaye kwa maksudi kabisa hajatimiza wajibu wake, aviarifu vyombo husika na Askari huyo atachukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria. (Makofi)
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pia namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri aliyonipatia, lakini naomba kuuliza swali langu la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Serikali imejipanga vyema kwa ujenzi wa barabara hizo. Je, Serikali ina mpango gani wa kupanua zaidi barabara hizo ili ajali zisitokee?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, upanuzi wa barabara unakwenda sambamba na bajeti. Nadhani Serikali ina mipango mizuri na imefanya kazi kubwa ya kuimarisha mitandao ya barabara nchini na sasa hivi nimesikia kuna mradi wa upanuzi wa barabara ambayo inatokea Dar es Salaam kupitia Chalinze na mbele zaidi. Kwa hiyo, ni mipango ambayo inaendelea kufanyika hatua kwa hatua kadri uwezo wa Serikali utakavyoruhusu.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri swali la nyongeza. Kupitia misaada mbalimbali ambayo Wizara inapokea kutoka kwa wafadhili, haoni kuwa, kuna haja hususan Hospitali ya Mnazi Mmoja, ya kuisaidia Wizara ya Afya ya Zanzibar kwa kuwapatia dawa kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wanaosumbuliwa na magonjwa hayo?
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, katika mambo yaliyopo kwenye Orodha ya Mambo ya Muungano afya si mojawapo. Kwa maana hiyo sisi kama Wizara ya Afya hatuwajibiki moja kwa moja kushughulikia mambo yanayohusu afya kule Zanzibar. Hata hivyo, katika utaratibu na ushirikiano na umoja tulionao tunafanya kazi kwa karibu sana na wenzetu pacha Wizara ya Afya ya kule Zanzibar na hivyo ushirikiano huu tutaendelea kuudumisha.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na namshukuru Waziri kwa masuala yake mazuri aliyonipatia, lakini napenda kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni hatua gani zinachukuliwa kwa wale askari ambao watabainika kuchukua rushwa kwa madereva ambao wametenda makosa?
Na je, madereva wanaojaza abiria kwenye magari kuliko level seat, hawa wanachukuliwa hatua gani?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ambazo askari wanachukuliwa wanapobainika wanajihusisha na vitendo vya rushwa ni kufukuzwa kazi mara moja. Lakini pamoja na kufukuzwa kazi, pia kushitakiwa.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na mimi kwa kuniona. Napenda kumuuliza Mheshimiwa Waziri wa Utamaduni, kuna baadhi ya nyimbo zinazoimbwa katika ma-stage show au zinazooneshwa katika runinga. Nyimbo hizi huwa zinatudhalilisha wanawake kuvaa yale mavazi yao ambayo yanaonesha, je, Serikali inazingatia suala hili au kisheria ni sawa kuimba nyimbo kama zile zinazotudhalilisha sisi wanawake?
NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kuhusiana na nyimbo ambazo zinadhalilisha wanawake ni swali jipya naomba alilete vizuri ili kusudi tuweze kulijibu vizuri zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunavyo vyombo ambavyo vinasimamia kwa kupitia sheria zetu. Tuna Bodi ya Filamu ambayo huwa inaangalia, inapitia maudhui yenyewe kama ni ya filamu au wimbo, lakini pia tuna Kamati ya Maudhui ambayo ipo chini ya TCRA. Kwa hiyo, kwa kutumia sheria zetu tunadhibiti hali kama hii. Vilevile wale ambao wanaona kwamba hali hairidhishi, tunaomba wawasilishe ni wimbo upi au ni filamu ipi ili kusudi hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.
MHE. MWANTUMU D. HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nashukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri aliyoyajibu na naona yametosheleza hasa na wananchi huko watasikia jinsi walivyojipanga. Nina swali langu moja dogo tu la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itakamilisha mradi huu na kuondoa msongamano wa daladala ambazo nyingine ni za kizamani kabisa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumshukuru Mheshimiwa Mwantumu Dau, kwa sababu yeye ni Mjumbe wa Kamati ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ambao wamekuwa wakifanya kazi kubwa sana mpaka kuanza kwa mradi huu.
Naomba niwahakikishie wakazi wa Dar es Salaam kwamba mradi huu awamu ya kwanza umekamilika na sasa tunajiandaa katika mradi wa awamu ya pili kuanzia Mbagala na mradi wa awamu ya tatu kuanzia Gongo la Mboto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mmesikia Mheshimiwa Rais wakati anazindua fly over za Ubungo pale, kwamba fedha zimeshapatikana na muda wowote sasa kazi hii inaweza ikaanza. Lengo kubwa ni kuondoa foleni kabisa na kuondoa haya magari madogo katika Jiji la Dar es Salaam na Serikali kuwahudumia wananchi na kukuza uchumi wake. (Makofi)
MHE. MWANTUM DAU HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Namshukuru Waziri kwa majibu yake mazuri ambayo ameyatoa hapa hivi sasa, lakini nina maswali mawili ya nyongeza nataka kuuliza. Je, Serikali inasema nini katika kuboresha kilimo cha umwagiliaji maji kwa kupitia mito mikubwa, maziwa na mabwawa? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, sambamba na kilimo cha umwagiliaji maji, je Serikali ina mpango gani wa kutoa elimu kwa wakulima juu ya kilimo hicho. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Spika, kama ambavyo tumejibu kwenye swali letu la msingi ambapo Serikali imeweka mipango mikakati ya kuhakikisha kwamba kilimo cha umwagiliaji na hasa pale ambapo tunakuwa na matatizo ya ukame; matatizo ambayo yanasababisha mvua zisijulikane sana. Ndio maana mipango ambayo nimeisema katika majibu yangu ya msingi, inabidi izingatiwe.
Mheshimiwa Spika, vilevile wakulima wanashauriwa katika kilimo hiki cha kutumia maji vizuri, kikiwemo na kilimo hiki ambacho tunaita drip irrigation. Kilimo ambacho kinatumia matone ya maji na hivyo kuweza kuwa na maji mengi kwa ajili ya watumiaji wengine.
Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la pili ambalo ni la elimu kwa wakulima. Ofisi ya Makamu wa Rais kupitia Baraza la NEMC tumekuwa na mikakati mbalimbali ya kuwapa wakulima elimu. Vilevile kwenye Sikukuu ya Wakulima ya Nane Nane tumekuwa tukichapisha majarida mbalimbali; majarida mengine ambayo ninayo hapa ambayo baada ya hapa nitampatia Mheshimiwa Mbunge. Wadau mbalimbali na wakulima wamekuwa wakitembelea mabanda yetu na kupata vipeperushi pamoja na majarida mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, pia mikakati ambayo tumeizungumzia hapa, nitampatia Mheshimiwa Mbunge kuna hii ya National Climate Change Strategy ambayo tumeizungumzia ya mwaka 2012 halafu vilevile tunayo miongozo ambayo ni ya kisera kuhusiana na suala la sekta ya kilimo.
Mheshimiwa Spika, niseme pia kwa faida ya Watanzania wote, masuala ya mazingira ambayo yanaathiri kilimo yameanzia kwenye Biblia ukisoma Mwanzo 10:15 ambapo Mungu alianzisha utaratibu kwenye ile mito minne akamwambia mwanadamu nakuagiza ukalime na kuitunza.
Mheshimiwa Spika, hivyo, vyanzo vya maji ni asili yake kwenye Biblia. Hii ndio maana na sisi kwa kutunga Sheria hii namba 20 ya 2004, vilevile tumechukua kipengele hicho tukaweka kifungu cha sita (6) ambacho kinatoa wajibu wa kisheria kwa kila mtanzania kutunza na kuhifadhi mazingira.
Mheshimiwa Spika, Ahsante sana. (Makofi)
MHE. MWANTUM DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri naomba kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa wananchi, wanaendelea kunyanyasika katika maeneo hayo, je, Serikali ina mpango gani wa kutoa muda maalum kwa kumaliza mgogoro huo wa kitaifa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tumekuwa tukitoa majibu kwa muda mrefu kwamba sasa hivi tunayapitia matatizo na changamoto zote zilizopo katika hifadhi zetu, ikiwa nia pamoja na maeneo yale yanayosimamiwa na jumuiya za wananchi, naamini kabisa kwamba baada ya muda mfupi na baada ya Serikali na wadau wengine kukaa kwa pamoja tutaleta ufumbuzi wa suala hili na haya matatizo yatapungua kwa kiwango kikubwa. (Makofi)
MHE. MWAMTUMU D. HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi kwa kuniona. Kwa kuwajengea uwezo watu wenye ulemavu kwenye suala la ubakaji, je, Serikali imejipanga vipi kuhusu suala hili?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. STELLA I. ALEX): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikihakikisha ulinzi kwa watu wenye ulemavu kila iitwapo leo. Kwa hiyo, niseme kwamba hata hili la ubakwaji kwa watoto wenye ulemavu Serikali itaendelea kuhakikisha kwamba inawapatia ulinzi. Hata hivyo si hilo tu, mtu ambaye atabainika kwamba amefanya kitendo hicho kwa mtu mwenye ulemavu atachukuliwa hatua kali na hatua stahiki kama inavyostahili ahsante.
MHE. MWANTUM DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri sana na yenye msingi, nampongeza sana. Hata hivyo, nina maswali yangu mawili ya nyongeza hapa. Swali la kwanza, kwa kuwa ubakaji umekithiri hapa nchini na hasa wanaume ndio chanzo kikuu cha masuala hayo; je, Serikali itachukua hatua gani za kimkakati ili wananchi watokwe na hofu na suala hili?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, Serikali ina mpango gani wa kutunga sheria kali ili kudhibiti ubakaji na udhalilishaji? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jibu langu la msingi nimeeleza mikakati ambayo Serikali inaifanya kuhakikisha kwamba tunapunguza sana matukio haya ya udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto na mikakati naomba niirudie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ni kuuhakikisha kwamba mpango mkakati ule ambao tumeuandaa tunausimamia vizuri; Pili, tumeendelea kushirikiana na vyombo vya dola na kuanzisha madawati mbalimbali; Tatu, kuanzisha one stop centre; Nne, ni kutoa elimu kwenye jamii. Tunatambua kwamba matukio mengi ya udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto yanafanya karibu sana na wanafamilia. Niendelee kutoa rai kwa jamii kuhakikisha kwamba tusifumbie macho matukio kama haya na tusimalizane nayo katika ngazi ya familia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, linahusiana na kwa nini tusitunge sheria kali; sheria tulizokuwa nazo za mwenendo wa adhabu na Sheria ya Mtoto na Sheria ya Masuala ya Kujamiiana zinajitosheleza kabisa na hatua zilizokuwepo pale zinatosha kabisa kuchukua hatua kwa wale wote ambao wanafanya matukio kama haya.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Namshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri aliyoyatoa hivi sasa. Kwa kuwa hakuna ucheleweshwaji wa mishahara, napenda kuuliza maswali yangu mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Serikali inasema nini kuhusu uongezaji wa mishahara kwa watumishi hao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali inasema nini kuhusu upandishaji wa madaraja mbalimbali kwa watumishi wa umma?
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza ameuliza Serikali inasema nini kuhusu uwekezaji wa mishahara ya wafanyakazi. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba mshahara ni mali halali ya mfanyakazi mwenyewe hivyo kuhusu uwekezaji ni mfanyakazi mwenyewe anaamua mshahara wake nini aufanyie, akitaka kuuwekeza wote yuko huru kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu upandishwaji wa madaraja, Serikali yetu siku zote imekuwa ikiwatendea haki wafanyakazi wetu kwenye upandishaji wa madaraja na kila mwaka wafanyakazi hupandishwa madaraja.
MHE. MWATUM DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri aliyoyatoa yenye kila aina ya vinjonjo. Napenda kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa programu hizi katika sekta ya kilimo linahusiana na suala la kuhimili mabadiliko ya tabianchi; je, Serikali ina mkakati gani kutoa elimu kwa wakulima ili waende sambamba na mabadiliko ya tabianchi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nampongeza Mheshimiwa Mwatum ambaye amekuwa akifuatilia sana masuala ya mazingira na hasa mambo haya ya mabadiliko ya tabianchi. Namhakikishia kwamba pamoja na mipango hii ambayo Serikali tumekuwa tukiifanya, hata kule Unguja na Pemba tunashirikiana na Taasisi za Kimataifa USAID pamoja na FAO katika miradi ya kilimo ya kuhimili mabadiliko ya tabianchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa kutoa elimu, nimhakikishie Mheshimiwa Mwantum tayari mpaka sasa Serikali ilishatoa mwongozo pamoja na mafunzo kwa watu wapatao 192 wakiwemo Maafisa Kilimo, Maafisa Uvuvi, Maafisa Mifugo pamoja na Maafisa Mipango kutoka kwenye Halmashauri za Wilaya na kuwaelekeza kwamba katika mipango wanayoipanga Wilayani pamoja na bajeti waweze kushirikisha mipango hiyo ya kilimo himilivu cha mabadiliko ya tabianchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, elimu hii tayari tulishaipeleka kwa wananchi na bado tunaendelea katika mpango huu tuliosema endelevu wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi, ni element ambayo pia inahusishwa. Pamoja na kwamba Mheshimiwa Rais alizindua juzi hapa ASDP II, vilevile kuna element ya kutoa mafunzo ya kilimo himilivu kutokana na mabadiliko ya tabianchi.
MHE. MWATUM DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa jibu lake zuri ambalo alilolitoa hapo, lakini naomba kuuliza swali la langu la nyongeza. Tunaelewa kuwa Serikali inawajibika vilivyo katika kushughulikia na kutatua matatizo hayo. Je, ni lini hasa Serikali itafikia ukomo wa suala hili kwa kuwa imekuwa ni kero kubwa kwa Askari wetu, kwani kufanyiwa hivyo pia kunawanyima haki zao na vilevile itawapelekea kutokufanya kazi kwa ufanisi na uadilifu? Ahsante.
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi ni kwamba Maofisa, Wakaguzi pamoja na Askari wa vyeo mbalimbali wa Jeshi la Polisi na hata vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama vilivyoko chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi mishahara yao inaendelea kurekebishwa. Hata hivyo, pale ambapo kutorekebishwa kwa mshahara kwa askari yeyote kutatokana na uzembe wa makusudi kwa Afisa ambaye anashughulika na mishahara ya Askari nimeshatoa maelekezo kwamba ifikapo mwezi wa Tano mwaka huu asiwepo Askari, wala Afisa wala Mkaguzi anayelalamikia stahiki yake. Pia nimewaelekeza kwamba wasicheze na maslahi na stahiki za Askari. Kufanya hivyo ni sawa na kushika mboni ya Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nishukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, suala alilosema Naibu Waziri ni suala zuri sana wala halina mjadala, lakini sasa Serikali haioni ni wakati sasa wa kufanya matibabu yakawa bure nchini hasa kwa wale waliokuwa hawana bima?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Waziri ametoa rai kwamba watu waende kwenye mazoezi, kuhusu suala la mlo na mambo mengine, ni kweli lakini napenda kuishauri Serikali, je, ni kwa nini haitoi elimu kwa jamii namna ya kujikinga na magonjwa yasiyoambukizika hasa haya ya pressure, sukari na shinikizo la damu? Ahsante.

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Je, Serikali haioni sasa kuwaondolea matibabu yakawa bure nchini hasa kwa wale wasio na bima?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali langu la pili, Mheshimiwa Waziri ametoa rahi hapa kwamba watu waende kwenye mazoezi, kuhusu suala la mlo na mambo mengine, ni kweli lakini napenda kuishauri Serikali. Serikali haitoi elimu kwa jamii namna ya kujikinga na magonjwa yasiyoambukizwa hasa haya ya pressure, sukari na shinikizo la damu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mwantumu Dau kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka nianze kumpa tu maelezo ya awali kuhusiana na swali lake la kwanza ambalo ameliongelea. Magonjwa haya yasiyoambukizwa ni magonjwa ambayo yana gharama sana na ni magonjwa ya kudumu. Naomba nitoe mfano, mgonjwa wa tatizo la figo ili kusafisha damu kwa wiki anahitaji kati ya laki saba na nusu mpaka milioni moja; na upandikizaji wa figo kwa sasa nchini tunafanya kwa takribani milioni 20.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mgonjwa wa kisukari anahitaji kati ya shilingi 50,000 mpaka 100,000 kutokana na idadi ya dawa; vivyo hivyo kwa mgonjwa ambaye ana shinikizo la damu. Kwa hiyo tumekuwa tunaona ongezeko kubwa sana na ndiyo maana utaona kwamba sisi kama Serikali tumeweka msisitizo mkubwa sana na tunataka kuanzisha program ya kitaifa; lengo ni kuanza kupambana kwasababu mwanzoni tulikuwa tunapambana na magonjwa ya kuambukiza. Unapomtibu malaria mtu leo hatorudi tena katika kituo chetu cha huduma za afya labda baada ya mwaka mmoja. Lakini mgonjwa ambaye anatatizo la kisukari, pressure na saratani, huyu anaingia katika mfumo wetu wa kudumu wa kupata huduma za afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwahiyo gharama za matibabu haya ni kubwa, na sisi kama Serikali ili kutoa nafuu kwa wananchi ndiyo sasa tunataka tuelekee katika mfumo wa bima ya wananchi wote na mwezi Septemba tunataka tulete Muswada huo ambao utaweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba kila mwananchi anakuwa na bima ya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika kipindi hiki cha awali msisitizo mkubwa ambao tunaendelea nao ni kutoa elimu. Tunatoa elimu kupitia Wizara, na ndiyo maana tuliona hata tumepiga marufuku matumizi ya tv zetu katika vituo vya afya ili viweze kutoa elimu kwa umma. Tunaongea na wenzetu wa SUMATRA ili hata katika vyombo vya usafiri elimu ya afya kwa umma.

Mheshimiwa Mwneyekiti, na mimi niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge, magonjwa haya ya kuambukiza yanazidi kukua; nitoe rai ya kuhakikisha kwamba tunatunza afya zetu na kutunza afya zetu ni kuhakikisha kwamba tunakula mlo sahihi tunafanya mazoezi na tuhakikishe kwamba tunakuwa na matumizi ya wastani ya vileo ikiwa ni pamoja na pombe na sigara.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri wa Mazingira kwa suala lake zuri ambalo alilolitoa hivi sasa hivi hapa. Lakini pia nimpongeze kwa suala langu la Bunge lililopita wakaja Zanzibar wakaja kutuhimiza ahadi yake ya kuja kuangalia mambo ya hali ya hewa ya mmomonyoko wa ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali mawili ya nyongeza, kwa kuwa mikoko ina mchango mkubwa wa kunusuru mazingira nini mpango wa Serikali katika kuhakikisha inaotesha mikoko ambayo inauwezo wa kunusuru maji chumvi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili bila maji baridi hatima ya kilimo na uhai wa binadamu viko hatarini. Je, kuna tafiti zozote za kuyalinda kuhakikisha upatikanaji endelevu wa maji baridi ahsante? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ridhaa yako nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji Mbunge wa Viti Maalum ni kweli amekuwa mstari wa mbele na sasa hivi amekuwa mwana mazingira tunamtumia sana hasa kwenye eneo hili la Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru kwa maswali yake mawili; moja, tunao mkakati maalum na unaendelea kwa kushirikisha wenzetu wa Serikali za Mitaa hasa kwenye halmashauri zetu kuhakikisha wanaweka miche kwa ajili ya mikoko ambayo itatumiwa kwenye maeneo hayo tuliyoyaeleza ya Pwani pembezoni mwa bahari. Na mkakati huo unaendelea na miche ipo ya kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namba mbili, utafiti zinaendelea na mpaka sasa tupo na utafiti unaendelea na wakati wowote tutaweka suala hili katika utaratibu ambao tutahakikisha maeneo haya kunakuwepo na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwenye kila eneo ambalo kuna mwambao wa bahari ahsante sana.
MHE. MWANTUM DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu ya kina kuhusu swali langu hili, nampongeza sana, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, yamekuwepo matukio ya ongezeko la kina cha bahari kiasi cha kuwepo kwa tishio la kimazingira katika baadhi ya maeneo. Je, Serikali inasema nini kuhusiana na suala hilo katika Visiwa vya Unguja na Pemba?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tatizo hili ni la muda mrefu kweli, toka lilivyogundulika kuhusu mazingira katika Visiwa vyetu vya Pemba na Unguja. Mheshimiwa Naibu Waziri atakuja lini sasa Zanzibar kuangalia maeneo yaliyoathirika katika Visiwa vya Pemba na Unguja? Nataka unihakikishie utakuja lini Zanzibar mbele ya Bunge letu hili.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mwantum Dau Haji kwani amekuwa mdau mzuri wa eneo hili la mazingira. Nimhakikishie tu kwamba katika miradi ambayo inaendelea na kama nilivyosema kwamba tunashirikiana vizuri na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar sasa tunaifanyia tathmini. Katika tathmini ile ambayo tunaifanya kila baada ya miezi mitatu maana yake sasa nitakuja rasmi baada ya Bunge hili, walau siku mbili hivi kwa ridhaa ya Mwenyekiti, ili tukishirikiana nawe na Wabunge wengine kwenye maeneo ya Pemba kuyaona hayo maeneo vizuri na kuhakikisha tunayapatia ufumbuzi wa kudumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri na yenye tija ndani yake na pia nakiri kwamba katika kituo cha Dunga ni kweli tayari hili jengo liko katika kukamilisha mwisho wake kuwa zuri sana na lifanye kazi. Niseme maswali yangu mawili ya nyongeza, kwa kuwa jengo la Makunduchi la muda mrefu na mwaka 2015 waliamua polisi kuweka foundation pale ili wapate kituo chao cha uhakika, je sasa swali langu liko hapa; Serikali itamaliza ujenzi huu lini? Swali langu la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwamba eneo la Makunduchi ni eneo la utalii. Kila mwaka kule Makunduchi kunakuwa kunafanywa Mwaka Kogwa, na ukizingatia hata mwaka jana Mheshimiwa Waziri wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alikuwa yeye ndiyo mgeni rasmi alikwenda kule. Swali langu lipo hapa, Serikali ina mpango gani wa kuweka ulinzi katika eneo lile hasa sambamba na ujenzi wa vituo vya polisi? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nikianza na swali lake la kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika maeneo ambayo tunayaangalia kwa karibu pale ambapo bajeti itakapokaa vizuri tuweze kumaliza ni hilo jengo ambalo amelizungumza la kituo cha polisi Makunduchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kuimarisha ulinzi hasa ukizingatia eneo la Makunduchi ni sekta ya utalii, nimhakikishie kwamba sasa hivi tunavyozungumza tuna mkakati kabambe wa kuimarisha usalama katika maeneo hususan Ukanda wa Pwani wa Zanzibar maeneo ambayo yamekuwa yanatumika kiutalii ili tuweze kuongeza imani ya watalii na wawekezaji katika ukanda huo. Kwa hiyo, tutakapokamilisha mkakati huo, sehemu ya Makunduchi ni moja katika maeneo ambayo yatafaidika.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba nimjibu maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Naibu Spika, je, katika bajeti ya mwaka huu wa fedha kumetengwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa ofisi hiyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili. Je, Mheshimiwa Naibu Spika uko tayari kuambatana ili twende ukajionee katika eneo hilo mwenyewe kwa macho yako hali halisi ya kusaidia kuhamasisha wananchi wako wa Mkoa wa Kusini Unguja, ili na wao wajue kwamba, wewe Naibu wao unafanya kazi vizuri? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimeeleza kwenye jibu langu la msingi, kukwama kwa kituo hiki kulikuwa kunasababishwa na upungufu wa fedha ambao sasa unatokana na ufinyu wa bajeti. Je, naulizwa, katika bajeti hii tumeingiza hiyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwambie kwamba, katika bajeti hii haikuingizwa, lakini nimuahidi tu kwamba, katika bajeti ijayo tutajitahidi hii Ofisi ya OCD Wilaya ya Kusini Unguja na ofisi nyingine na maeneo mengine ambayo yana uhitaji wa vituo hivi tutajitahidi tuhakikishe kwamba, tunapeleka au tunaendeleza ujenzi. Hasa ule ujenzi ambao umekwama wa vituo vya polisi katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali jingine je, nipo tayari kuambatananaye mama yangu?

Mheshimiwa Naibu Spika, nikwambie. Kwa ridhaa kabisa niko tayari kuambata na Mheshimiwa Mbunge tuende huko tukaangalie hilo eneo. Na itakuwa vizuri kwa sababu, tukifika huko tutawakusanya wananchi…

MBUNGE FULANI: Sio wewe.

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: …lakini
pia tutakaa na wadau ili kuhakikisha kwamba, tunawashajihisha kujenga kituo hiki, ili wananchi wa maeneo hayo, hasa maeneo ya Makunduchi, Kizimkazi, Mtende, Bwejuu, Paje na Jambiani na maeneo ya karibu waweze kupata huduma za ulinzi na usalama kama wanavyopata wananchi wengine. Nakushukuru.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri naomba kutoa maswali yangu mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, jamii iliyo kuwa inawaona watu wenye ulemavu hawawezi kufanya kazi ikiwemo ujasiriamali. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha watu wenye ulemavu nao wajaikwamue kimaisha?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, Waziri yuko tayari kuambatana na mimi kwenda Zanzibar kwenda kuwaona watu wenye ulemavu jinsi wanavyojikita kuhusu suala la ujasiriamali? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WATU WENYE ULEMAVU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji. Amekuwa akifuatilia kwa ukaribu sana masuala yetu ya watu wenye ulemavu.

Niseme kwamba suala hili la watu kuwaona watu wenye ulemavu kama wanabaguliwa na hawawezi kufanya shughuli, nataka nimwambie tutaendelea kutoa elimu lakini kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu tutaendelea kuwasaka wale wote wanaowanyanyapaa na kuwatumikisha watu wenye ulemavu ili kuchukua hatua stahiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile tutaendelea kuwajengea uwezo watu wenye ulemavu wao wenyewe waweze kujiamini na waone wana mchango katika Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba niko tayari tuambatane naye baada ya kukamilika kwa bajeti hii na twende Zanzibar tukafanye kazi. Ahsante. (Makofi)
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Kwanza napenda kuipa shukrani Serikali yangu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jinsi inavyofanya kazi zake katika Wizara hii ya Maji, inatekeleza kwa hali na mali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi sasa hivi ni mkazi wa Dodoma nakaa maeneo ya Mkalama. Eneo lile la Mkalama maji yapo mengi sana lakini mabomba yanakuwa yanapasuka sana maji yanatoka na hovyo. Mimi mwenyewe binafsi nakuwa nahisi huruma. Kwa hiyo nimwambie Mheshimiwa Waziri, kama Serikali imeliona suala hili kule sehemu ya Mkalama basi ifanye kazi zake kwenda kuyaziba yale mabomba ili maji yasitoke hovyo. Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza kutoka kwa Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nipende kupokea pongezi kwa namna ambavyo ameridhishwa na utekelezaji wetu. Sasa kuhusiana na tatizo la maji kumwagika baada ya mabomba kupasuka maeneo ya Mkalama nipende kusema kwamba Meneja wa Maji Mkoa wa Dodoma Engineer Aron anafanya kazi usiku na mchana. Lengo ni kuona anakwenda kufanyia kazi mapungufu yote haya yanayoendelea kujitokeza. Siyo tu eneo la Mkalama hata wale wenzetu wanaotoka Ilazo taarifa za matatizo ya maji pale tunazo na tunazifanyia kazi. Tayari tumempa mtu kazi ya kuweza ku-supply mabomba.

Kwa hiyo mabomba haya yakifika, tunatarajia wiki hii yatafika, tunakuja kufanya ukarabati na marekebisho maeneo yote ambayo yana matatizo ya kupasuka na kumwaga maji mitaani.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kuuliza maswali yangu mawili ya nyongeza. Kwanza, nishukuru Serikali yangu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na mama Samia Suluhu Hassan jinsi anavyo chapa kazi mwanamama, kweli kinamama tunaweza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Naibu Waziri na Serikali yake inatambua uchakavu huu wa majengo ya polisi ya Makunduchi pamoja na makazi na wametenga jumla ya shilingi milioni kumi na moja na tisini na tatu mia nne, ambazo fedha hizi zinatakiwa ziende zikafanye ukarabati katika majengo haya na vituo vya polisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, vituo hivi vimechakaa sana, binafsi ukizingatia Makunduchi ni sehemu ya utalii hususan kila mwaka tunakwenda kule kukoga mwaka na viongozi wetu wakubwa wakubwa wanakwenda kule Makunduchi.

Kwa hiyo, je, Serikali lini itakwenda kuyatengeza majengo haya ili tuondoe kadhia hii ya majengo haya machakavu?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala langu la pili, namuomba Mheshimiwa Naibu Waziri tena nasema tena, Mheshimiwa Naibu Waziri aende mwenye Makunduchi akayaone jinsi yale majengo pamoja na zile nyumba zilivyochakaa. Tuoneeni huruma jamani, tunaona vibaya? Ahsante sana naomba kuwasilisha. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NAMBO YA NDANIYA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba kujibu masuala mawili mazuri sana ya nyongeza yaliyoulizwa na Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Kusini Unguja, Mwantumu Dau Haji nayajibu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, moja miongoni mwa azma kubwa ya Serikali hasa kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kupitia Jeshi la Polisi ni kuhakikisha kwamba inaboresha na inatengeneza vituo vyote vya polisi vilivyopo nchini pamoja na nyumba za makaazi za maafisa hawa wa polisi na familia zao. Kwa hiyo, kubwa ni mwambie tu Kituo cha Makunduchi ni moja miongoni mwa kituo ambacho tumeshakipanga na tayari fedha hizi tumo mbioni kuzitafuta na kupitia mwaka wa fedha ujao tutahakikisha kwamba kituo hiki tunakipa kipaumbele ili kijengwe na shughuli za kitalii na mambo mengine yaweze kuendelea vizuri na shughuli za ulinzi na usalama.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo pia, nipo tayari kwenda Makunduchi kwenda kuona hilo eneo ili kuona namna ambavyo tunaweza tukashauri na tukaweza kupata fedha kwa ajili ya kukarabati hicho kituo. Nakushukuru.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, lakini napenda kumuuliza maswali yangu mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia soko lenye uhakika na tija nchini?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; je, Serikali ina mpango gani wa kuwaunganisha akinamama kwenye mitandao ya wafanyabiashara duniani? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Mwantumu kwa vile ambavyo anawasemea sana akinamama ili kuhakikisha nao wanajikomboa katika kufanyabiashara katika mazingira mazuri. Lengo la Serikali, kwanza ni kuhakikisha wafanyabiashara wote wakiwemo akinamama wanazalisha bidhaa zao katika ubora. Kwa hiyo, la kwanza tunalofanya kuhakikisha tunawapa mafunzo ili kuhakikisha wanazalisha bidhaa zenye tija.

Mheshimiwa Spika, pili, kupitia taasisi zetu tunawaunganisha kwenye masoko mbalimbali kupitia maonesho ambayo yanaandaliwa na TANTRADE. Pia kwenye kuhakikisha wanaingia kwenye mtandao wa wafanyabiashara duniani kwa kupitia chamber ya wafanyabiashara wanawake Tanzania Women Chamber of Commerce tumekuwa tukiandaa kwa kushirikiana na Serikali, ziara kwenye Maonyesho ya Kimataifa ikiwemo ile iliyofanyika mwaka 2018 kule China ili angalau kuwapa uelewa mpana kwa wafanyabiashara wetu akinamama katika masoko ya kimataifa.

Mheshimiwa Spika, pia zaidi sasa tumeanzisha biashara mtandao kupitia TANTRADE na Posta ili iwasaidie kufanya biashara kwenye mtandao na hivyo kujiongezea kipato. Nakushukuru sana.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kutoa maswali yangu mawili ya nyongeza.

Kwa kuchelewa kuonekana TB Serikali ina mkakati gani ili kuepukana na masuala ya maambukizi? (Makofi)

Je, kuna mpango gani wa kutoa elimu kwa umma juu ya ugonjwa huu kwa kupitia warsha, semina au kongamano? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mwantumu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza anasema kwa sababu ugonjwa wa TB unachelewa kuonekana Serikali ina mpango gani wa kusaidia wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja ni utafiti, tayari nchi yetu kwa kushirikiana na vyuo vikuu mbalimbali duniani umefanyika utafiti kwenye Hospitali ya Kibong’oto iliyoko Wilayani Siha ambao ulitizama vinasaba vya TB ambavyo huko nyuma TB ilichelewa kugundulika sana kwa sababu wakati mwingine ukipima unamuona mtu ana TB, lakini ni TB mfu, sasa imegundulika kupitia Hospitali yetu ya Kibong’oto technic ambayo inatumia RNA kwa kutumia watafiti wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja ni kwenye kutambua haraka, sasa hivi kuna vipimo ambavyo vimegundulika madaktari wazalendo wa Kitanzania kwa kushirikiana na Wamarekani wamegundua vinaweza kutambua mapema vimelea. Lakini ya pili, tunapeleka huduma chini sasa kwa bajeti ya mwaka huu kuna vituo 1,859 vinakwenda kuwezeshwa kuweza kupima, kuna ambulance na x-ray digital ambazo ni movable zinakwenda kuzungushwa kwenye nchi nzima ambavyo kila mkoa itakuwa na ya kwake kwa ajili kuzunguka kwenye jamii kusaidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, amesema warsha na kutoa semina, sasa hivi Serikali imenunua malori ambayo ni hospitali inayotembea ambayo ina x- ray yenye artificial inteligency ambayo inatembea kila mkoa na kutoa semina na kwenda kwa kongamano, kila mikutano na kuitisha wananchi, kupima pale pale na tiba kutolewa eneo lile lile. (Makofi)
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nimpongeze Waziri kwa majibu yake mazuri ambayo yanatia moyo na vile vile niwapongeze Mawaziri wangu hawa wa Utumishi kwa jinsi wanavyofanya kazi, wanafanya kazi sana katika hasa masuala haya ya TASAF wanafanya kazi kutoka hapa Tanzania Bara mpaka Zanzibar.

Mheshimiwa Spika, nina swali moja tu la nyongeza, pamoja na jitihada hizo Serikali inasema nini katika kuhakikisha wanaofikiwa ni walengwa zaidi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI
WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumeboresha kwanza mifumo ya namna ya kuweza kuwapata walengwa na tumeenda kidigitali zaidi, wale waandikishaji wanatumia teknolojia, kwa kutumia tablets (vishikwambi), kuwaingiza walengwa katika mfumo wa TASAF.

Mheshimiwa Spika, vile vile kuna mfumo mwingine ambao umeongezwa wa malalamiko kwa wale ambao wanaona huenda walistahili kuwemo kwenye mpango wa TASAF, lakini waliachwa, basi kuna mfumo wa malalamiko na yale malalamiko yao yakiwekwa huwa yanapitiwa na wataalam wa TASAF na kuweza kuwarejea kuwahakiki tena na kuona kama wanastahili.

Mheshimiwa Spika, niseme tu kwamba mfumo uliowekwa wa namna ya kuwapata walengwa wa kaya maskini huwa hauanzii juu kwenda chini, mfumo ule unaanzia chini kwenda juu kwa maana Serikali ya Kijiji na wananchi hukutana katika mikutano ya kijiji na wanaanza kwa kutambuana wao kwamba fulani ni kaya maskini fulani si kaya maskini. Kwa hiyo, mfumo ule umeanza toka kijijini kuja mpaka juu sasa tayari Serikali imechukua hatua hizo lakini tunazidi kusisitiza wale wanaoenda kuandikisha kule kwa kushirikiana na Watendaji wetu wa Vijiji na Kata kuwa wakweli na kuhakikisha haonewi mtu katika wale wanaostahili kuingia katika mpango wa TASAF, basi waingizwe katika mpango wa TASAF nao waweze kuwa katika walengwa ambao wananufaika na mradi huu.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana; pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa shehia yangu ya Fuoni ina matatizo makubwa katika eneo hilo, matatizo ya wizi na vibaka pamoja na wabakaji, maana kuna vibaka na wabakaji masuala mawili hayo muyaone.

Je, Serikali haioni haja kujenga Kituo cha Polisi katika eneo hilo? (Makofi)

Je, ni lini Serikali itaanza huo ujenzi katika maeneo hayo? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwantumu Dau, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, umuhimu wa kujenga Vituo vya Polisi kwa kweli unaanzia kwa wananchi na mamlaka zao za Serikali za Mitaa. Kwa maana ya uwepo wa matukio ya wizi, udokozi kwenye shehia aliyoibainisha, nimwombe Mheshimiwa Mbunge kwamba katika vikao vya Kamati za Usalama watakapojadili na kuona umuhimu wa kujenga Kituo cha Polisi, basi sisi Polisi Makao Makuu kwa maana ya IGP atatenga fedha kwa ajili ya kusaidiana na nguvu za wananchi kujenga vituo hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kama Kamati ya Usalama ya Wilaya na Mkoa wataona umuhimu tuko tayari kuungana nao. Ni lini? Wakati wowote tutakapopata maombi hayo tutatekeleza mpango wa ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi kwa kuniona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumuuliza Mheshimiwa Waziri, kwamba siyo utapeli wa simu za nje tu lakini pia kuna utapeli wa kiholela wa kuongezewa au kupandishwa vyeo humu nchini. Utapigiwa simu umeambiwa umepandishwa cheo kwa hiyo usubiri barua yako. Kwa hiyo na hili pia linatumika katika njia za simu. Je, Serikali ina mpango gani kuhusu suala hili?
NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA
YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, utapeli unakuja kwenye picha tofauti tofauti. Kuna picha ya kutafutiwa kazi, picha ya kupandishwa vyeo kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema, lakini sana sana tunachokiomba tu kwa Watanzania ni kwamba pale wanapopokea changamoto kama hizi basi waweze kuwasiliana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ili tuweze kuchukua hatua stahiki nasi tukiwa tunaendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kupitia kitengo chao cha Cyber Crimes Act. Kwa hiyo, tunaamini kabisa kwa ushirikiano huu basi tutaweza kuhakikisha kwamba changamoto hizi zinadhibitiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vita dhidi ya matapeli siyo vita dhidi ya Serikali peke yake, ni vita dhidi ya umma na kwa pamoja tukifanya kazi kwa pamoja tutahakikisha kweli tumetokomeza changamoto kama hii. Nakushukuru sana.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nimshukuru Waziri kwa majibu yake mazuri sana ambayo ameyatoa sasa hivi. Nilikuwa na kitu kwanza kidogo kabla sijampa maswali yangu ya nyongeza mawili niliyonayo.

Nashukuru kwamba mwezi wa Ramadhani wenzetu wa jamii, wenzetu humu Bungeni walituheshimisha sana, wote walikuwa wanavaa mashungi na wanaume walikuwa wakivaa kanzu pamoja na koti, hilo kwanza niwashukuru sana na Mwenyezi Mungu awajaalie wazidi kutufuata sisi wenzetu Waislam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali mawili ya nyongeza, zipo nchi zimefanikiwa kujenga daraja za umbali mrefu, kwa nini tusipate uzoefu kutoka kwao?

Swali langu la pili, je, kwa nini usitumike mpango wa ubia na sekta binafsi PPP kwa ajili ya ujenzi huo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, upande wa Zanzibar na upande wa Tanzania Bara, wahusika tayari wameshakutana kwamba hili suala linazungumzika na lipo linachakatwa, bado yatokanayo na hilo hayajapatikana ikiwa ni pamoja na kulifanyia kazi lile alilosema Mheshimiwa Mbunge kupata uzoefu kutoka sehemu mbalimbali ambazo wenzetu wameshajenga madaraja mengine marefu kama haya, ndiyo maana tunasema yatokanayo na hayo bado lakini suala hilo lipo linafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la pili kuhusu PPP, ni kweli kabisa kwamba siyo mpango kwa maana ya Serikali ichukue fedha zake ijenge na hata hao walioonesha nia ni sekta binafsi. Kwa hiyo, tunaamini daraja hili kama litajengwa, litajengwa kwa mtindo wa PPP kama alivyoshauri Mheshimiwa Mbunge. Ahsante.
MHE. MWATUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa kujibu maswali yangu yenye kina na ambayo mimi mwenyewe nimeyaelewa. Napenda kumuuliza swali langu hivi, je, ni lini sasa hizo milioni 15 ambazo zimekisiwa kwenda kununuliwa mapikipiki pamoja na hayo magari katika wilaya nyingine pamoja na Mikoa, lini sasa Serikali itapeleka pesa hizo ili zifanyike kununulia magari hayo? (Makofi)
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwatum Dau Haji, Mbunge wa Viti Maalum, kama Ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, shilingi bilioni 15 sehemu ya fedha hiyo tayari imekwisha tolewa na gari hizo tayari zimekwishaagizwa. Tunatarajia mwezi Agosti, 2023 tuweze kupokea magari hayo utaratibu wa Serikali ambao tunanunua magari hayo kupitia GPSA. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba sehemu ya fedha hizo tayari zimeshatolewa na sehemu ya magari hayo yamekwishaagizwa na mara yatakapowasili basi tutaanza utaratibu wa kuyagawa katika wilaya kama ambavyo tumepanga.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ambayo ameegemea zaidi kwenye mtazamo wa Sheria badala ya hali halisi ilivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Je, ni lini mmechukua hatua kwa meli zilizozidisha abiria na kusababisha vifo vingi zaidi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania inavyombo vingapi? Vinavyotoa huduma za abiria na mizigo baharini na maziwa makuu? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, Mwantumu Dau Haji, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kuna baadhi ya vyombo huwa vinakiuka sheria kwa kuzidisha uzito wa abiria na mizigo. Kupitia TASAC tunatoa elimu kwa wamiliki wa vyombo hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spaka, pili; sheria inatutaka kwa yeyote atakayezidisha uzito kulipa faini na kabla meli haijaondoka kuna Maafisa ambao wanahakikisha mstari wa ujazo haujazidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, faini hizo zinatofautiana kulingana na urefu wa chombo na chombo. Chombo chenye urefu wa mita zaidi ya 24 wanalipa faini ya shilingi laki nne na chombo chenye urefu chini ya mita 24 wanalipa faini ya shilingi laki mbili lakini ikithibitika pia huyo mmiliki ameshindwa kulipa faini hiyo anapelekwa Mahakamani.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ameuliza idadi ya vyombo tulivyonavyo hapa nchini. Kwa Sensa ambayo ilifanywa na TASAC mwaka 2021 kwa kushirikiana na Ofisi ya Mtakwimu wa Taifa (NBS) inaonesha vyombo vyote tulivyonavyo hapa nchini kwa ukanda wa bahari, maziwa makuu yote, mito na maziwa madogo ni 52,189; hii ndiyo takwimu iliyofanyika mwaka 2021. Na kati ya vyombo hivyo asilimia 53.6 vipo Ziwa Victoria, asilimia 13.4 vipo Bahari ya Hindi, asilimia 10.2 vipo Ziwa Tanganyika, asilimia 7.6 vipo Ziwa Nyasa na asilimia 15.2 vipo maeneo ya Maziwa Madogo pamoja na Mito. Ahsante.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nimshukuru waziri kwa majibu yake mazuri sana aliyoyatoa hapa hivi sasa, lakini nina maswali yangu mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa suala hili ni la muda mrefu, je, Serikali inaweza kutuambia nini hali halisi kwa sasa pamoja na mifano?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; kwa kuwa ongezeko la thamani, mazao yetu hapa nchi kuna maboresho ya mazao yetu, je, Serikali iko tayari kutengeneza viwanda vidogovidogo katika wilaya zetu?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hali halisi ya upatikanaji wa masoko ya mazao yetu. Nataka nikiri mbele ya Bunge lako kwamba hivi sasa katika baadhi ya mazao hasa mazao ya nafaka soko la mazao haya limekuwa ni kubwa ndani na nje ya mipaka ya Tanzania na hivyo kuwawezesha wakulima wetu wengi kuwa na masoko ya uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hivyo katika matunda na mbogamboga pia na kwenyewe tunafanya vizuri hivi sasa parachichi letu limepata nafasi ya kwenda katika masoko ya Hispania, China, Marekani, pamoja na Afrika ya Kusini hii ni ishara njema kuonesha kwamba kuna kazi imefanyika kwenye kutangaza mazao yetu, lakini pia kwenye kahawa na korosho na mazao mengine pia tunafanya vizuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili la kuongeza thamani, ni mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba tunaendelea kuongeza thamani ya mazao yetu ya kilimo. Mkakati uliopo hivi sasa ni kuhakikisha kwamba tunajenga uwezo kwa uanzishaji wa viwanda vidogovidogo kuanzia kule katika eneo la korosho na mazao mengine ya nafaka. Hivi sasa bodi ya mazao mchanganyiko yenyewe tu imeshaendelea kuwekeza katika vinu vingi vya kusaga mazao ya nafaka ili kuongeza thamani ya mazao yetu. Hii ni hatua ya Serikali lakini pia na sekta binafsi wanatuunga mkono.
MHE. MWANTUMU DAU. HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante. Nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake ya Serikali aliyoyatoa. Nina maswali yangu mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa kilimo BBT kwa vijana, Serikali ina mpngo gani wa kuja na BBT kwa wanawake wasiyosijiweza? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili je, Serikali haina umuhimu wa kuhakikisha mikopo hii inawafikia wanawake hao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwantumu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli moja ya changamoto tulizonazo ni kuona namna gani ya kuwawezesha wanawake wawe na kesho nzuri kama ambavyo kuna programu hii ya kesho nzuri kwa vijana kwenye sekta ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani hili ni wazo zuri ili kuona namna gani tunawasaidia wanawake ambao ndio wana mchango mkubwa sana katika uchumi wa nchi hii. Nadhani kama Serikali tunachukua hili ili tuweze kuja na programu maalum yenye mlengo huo kwa ajili ya kuhakikisha wanawake wanakuwa na kesho nzuri kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la pili, ni dhahiri kweli Serikali tumeshaona changamoto zilizojitokeza kwenye mifuko mbalimbali ikiwemo ile 10% ilikuwa inatengwa na Halmashauri kwamba ilikuwa haiwafikii walengwa wakiwemo wanawake kutokupata kwa wakati na mambo mengine mengi. Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshatoa maelekezo tupitie upya namna ya kuhakikisha mifuko hii inawasaidia na hasa wanawake waweze kupata fedha zile kwa wakati, lakini kulingana na mahitaji yao. Sasa tunaangalia kwa namna ya pekee zaidi wanawake wasiojiweza ili waweze kupata mikopo au uwezeshaji huu kwa wakati kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameshauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwanza napenda kushukuru Serikali yangu sikivu kwa jitihada zake inazozifanya kuibua miradi ya vituo vya Polisi nchini.

Mheshimiwa Spika, kituo cha Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, kilianza kujengwa toka mwaka 2016, hadi hii leo 2022 kituo hicho bado hakijamalizwa. Kilijengwa kikapigwa plasta baadhi ya vyumba, chooni bado, nje hakijapigwa plasta hadi hii leo Polisi wapo Wilaya ya Kati wameazimwa eneo la vitambulisho ndiko wanakofanyia kazi zao. Je, Serikali itamaliza lini Kituo hiki cha Polisi cha Dunga, ili Polisi waweze kufanya kazi kama kawaida?(Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wake makini juu ya kituo hiki na juhudi zilizofanywa na wananchi katika kujenga kituo hiki mpaka hatua iliyofikiwa, ulituelekeza siku moja hapa na mimi nikajibu kwamba Wizara inaandaa mpango wa kumalizia vituo na kujenga maeneo ambayo hayana vituo kabisa. Kipaumbele kitawekwa kwenye maeneo ambayo tayari wameshajenga vituo kama hawa wa Dunga. Kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, katika mwaka ujao tutafanya kila liwezekanalo ili ukamilishaji wa kituo hicho uweze kuanza.

Mheshimiwa Spika, ninashukuru sana.(Makofi)
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwanza napenda kushukuru Serikali yangu sikivu kwa jitihada zake inazozifanya kuibua miradi ya vituo vya Polisi nchini.

Mheshimiwa Spika, kituo cha Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, kilianza kujengwa toka mwaka 2016, hadi hii leo 2022 kituo hicho bado hakijamalizwa. Kilijengwa kikapigwa plasta baadhi ya vyumba, chooni bado, nje hakijapigwa plasta hadi hii leo Polisi wapo Wilaya ya Kati wameazimwa eneo la vitambulisho ndiko wanakofanyia kazi zao. Je, Serikali itamaliza lini Kituo hiki cha Polisi cha Dunga, ili Polisi waweze kufanya kazi kama kawaida?(Makofi)

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wake makini juu ya kituo hiki na juhudi zilizofanywa na wananchi katika kujenga kituo hiki mpaka hatua iliyofikiwa, ulituelekeza siku moja hapa na mimi nikajibu kwamba Wizara inaandaa mpango wa kumalizia vituo na kujenga maeneo ambayo hayana vituo kabisa. Kipaumbele kitawekwa kwenye maeneo ambayo tayari wameshajenga vituo kama hawa wa Dunga. Kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, katika mwaka ujao tutafanya kila liwezekanalo ili ukamilishaji wa kituo hicho uweze kuanza.

Mheshimiwa Spika, ninashukuru sana.(Makofi)