Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Benki ya Wanawake ni chombo muhimu sana hasa kwa wanawake wa Tanzania:- (a) Je, ni lini litaanzishwa tawi la Benki ya Wanawake katika Mkoa wa Morogoro ili wanawake wa Morogoro wapate kunufaika na benki yao? (b) Je, kuna mkakati gani wa kuanzisha matawi ya Benki ya Wanawake katika Mikoa yote ya Tanzania ili wanawake waweze kukopa kwa urahisi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Licha ya kupata majibu mazuri kutoka kwa Mheshimiwa Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa Mkoa wa Morogoro hauna hata hicho kituo cha kutolea mikopo na mafunzo ya ujasiriamali, je, kuna mikakati gani ya kuanzisha kituo hicho kwenye Mkoa wa Morogoro?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, kituo hicho kitaanzishwa lini? Ahsante

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya 2016/2017, benki imetengewa shilingi bilioni 950. Kwa hiyo, nimuahidi kwamba katika mkoa ambao tutaupa kipaumbele ni Mkoa wa Morogoro ili tuweze kufungua dirisha la kuwawezesha wanaweke kupata mikopo. Hata hivyo, siyo katika Mkoa wa Morogoro tu tumepanga kwamba katika mwaka wa fedha wa 2016/2017 tufungue dirisha maalum ambalo litawawezesha wanawake kupata mikopo yenye riba nafuu angalau kati ya asilimia 10 mpaka 12. Kwa hiyo, hili jambo tutaweza kulianza mara tu utekelezaji wa bajeti ya 2016/2017 utakapoanza.

Name

Azza Hilal Hamad

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Benki ya Wanawake ni chombo muhimu sana hasa kwa wanawake wa Tanzania:- (a) Je, ni lini litaanzishwa tawi la Benki ya Wanawake katika Mkoa wa Morogoro ili wanawake wa Morogoro wapate kunufaika na benki yao? (b) Je, kuna mkakati gani wa kuanzisha matawi ya Benki ya Wanawake katika Mikoa yote ya Tanzania ili wanawake waweze kukopa kwa urahisi?

Supplementary Question 2

MHE. AZZA H. HAMAD: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza. Tatizo la Benki ya Wanawake limekuwa ni kubwa katika mikoa yote, naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri, ni kwanini Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto isikae na kukubaliana na benki ambazo zinapatikana kwa kila mkoa kama NMB, CRDB na NBC ili waweze kuweka angalau dirisha moja kwa kila mkoa kuweza kutoa huduma hizi?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kweli kwa sababu msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Lengo la benki lilikuwa ni kufikisha huduma za mikopo yenye riba nafuu kwa wanawake hasa walio vijijini. Katika jitihada ambazo zimefanyika hatukuweza kwa kweli kufikia lengo hilo ni lazima nikiri hilo. Nimshukuru sana Mheshimiwa Azza kwa wazo zuri tunalipokea na tayari nimeshapata baadhi ya benki ambazo ziko tayari kushirikiana na Benki ya Wanawake ili sasa tuweze kufungua dirisha la Benki ya Wanawake katika benki ambazo ziko katika mikoa na wilaya mbalimbali. Kwa hiyo, kwa kweli naamini ndani ya miezi mitatu tutaweza kuja na suluhisho maalum la kuhakikisha huduma za Benki ya Wanawake zinafika hasa kwa wanawake walio vijijini.

Name

Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Benki ya Wanawake ni chombo muhimu sana hasa kwa wanawake wa Tanzania:- (a) Je, ni lini litaanzishwa tawi la Benki ya Wanawake katika Mkoa wa Morogoro ili wanawake wa Morogoro wapate kunufaika na benki yao? (b) Je, kuna mkakati gani wa kuanzisha matawi ya Benki ya Wanawake katika Mikoa yote ya Tanzania ili wanawake waweze kukopa kwa urahisi?

Supplementary Question 3

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwa umuhimu huohuo wa wanawake wa Mkoa wa Morogoro kupata mikopo kutoka Benki ya Wanawake, Mkoa wetu wa Manyara, wanawake wengi ni wa kutoka jamii ya wafugaji na jamii ya wafugaji hawana elimu pana ya kukopa katika vyombo vya benki hasa tutakapokuwa tumefikiwa na Benki ya Wanawake. Je, Wizara ina mkakati gani kuhakikisha kwamba inaandaa mafunzo ya ujasiriamali pamoja na elimu ya uelewa ili wanawake wa jamii ya kifugaji nao waweze kunufaika na Benki ya Wanawake?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tuna changamoto ya kuwafikia wanawake ambao wako katika jamii za wafugaji lakini pia wanawake wenye ulemavu. Kwa hiyo, ni jambo ambalo tayari nimeshatoa maelekezo kwa Benki ya Wanawake kwamba wakati tunapotoa huduma zetu pia lazima tuwe na huduma maalum kwa wanawake walio pembezoni ikiwemo walio katika jamii za wafugaji. Pia nimeshatoa maelekezo kwa Benki ya Wanawake, tuwe na huduma mahsusi kwa ajili ya wanawake wenye ulemavu na nataka kumthibitisha Mheshimiwa Umbulla na Waheshimiwa Wabunge wanawake wengine ili msiweze kusimama tena kuuliza maswali ya nyongeza kwamba kuwawezesha wanawake kiuchumi ndiyo kipaumbele cha Serikali ya Awamu ya Tano, tunapozungumzia masuala ya usawa wa jinsia, tutajikita tu katika kuwawezesha wanawake kiuchumi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hii imetokea kutokana na takwimu ambazo tunazo kwamba, kwa mfano wanawake ambao wanatumia huduma mbalimbali za benki ni asilimia 51 ukilinganisha na wanaume wanaotumia huduma za benki ni asilimia 63. Kwa hiyo, Mheshimiwa Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan, kwa sababu ni Mjumbe wa High Level Panel on Women’s Economic Empowerment (Jukwa la Kimataifa la Kuwawezesha Wanawake Kiuchumi), ameanzisha jitihada mahsusi za kuhakikisha kwamba wanawake wa Tanzania hasa walio vijijini wanafungua akaunti katika benki mbalimbali nchini, ameanza na akaunti inayoitwa Malaika Account. Lengo la Mama Samia pia ni kutoa elimu kwa wanawake ili waweze kujua masuala mbalimbali ya ujasiriamali na kauli mbiu yake anasema „usinipe samaki nipe nyavu na elimu ili niweze kuvua‟. Kwa hiyo, tunampongeza sana Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan, tunaamini kupitia yeye tutaweza kuwafikia wanawake mbalimbali hasa walio vijijini.