Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Bwawa la Kalemawe lilijengwa mwaka 1959 na kumekuwepo na makubaliano baina ya Serikali, UNCDF na wadau wengine juu ya ukarabati wa Bwawa hili. Je, kazi ya ukarabati itaaza lini ili Wafugaji na Wakulima waondokane na shida ya uchakavu wa bwawa hilo?

Supplementary Question 1

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza ni kwamba hili bwawa lilitengenezwa maalum kwa ajili ya wafugaji kutokana na kwamba walihamishwa kutoka mbuga ya wanyama ya Mkomazi, na kazi ya pili ilikuwa uvuvi, ya tatu ilikuwa yale maji yanayo-spill over ndiyo yaende kwa wakulima. Tatizo ni kwamba huu mradi wote umegeuzwa kwamba unalenga wakulima zaidi kuliko wafugaji, matokeo yake nina wasiwasi kwamba hata Mtaalam (Consultant) mwingine akipatikana wa kutengeneza huu usanifu atakosea, kama alivyokosea mara ya kwanza ambapo huu mradi ulipotangazwa zile Terms of Reference hazikueleweka. Matokeo yake yalivyoenda UN Capital Development Fund, yakarudi kwamba haikukidhi matakwa ya ule mradi ungetengenezwaje. Sasa ninavyoliona hapa litarudia tena, because focus pia imebadilika kutokana na majibu ya Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Spika, swali langu ni hivi huoni ni wakati muafaka sasa mradi huu ukasimamiwa na Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ili pia tupate technical assistance ya kusaidia ku- frame huu mradi vizuri? Because kuharibika kwa huu mradi, I mean kujaa tope ni kwamba wafugaji walikuwa wanaleta ng‟ombe kwenye bwawa na hili bwawa ni kubwa sana, square kilometer kuna takwimu mbili, inaonesha 32 square kilometers, nyingine inaonesha square kilometers 24, ni mradi mkubwa sana. Kwa hiyo, ninachoomba au ninachoshauri ni kwamba huu mradi haionekani kwamba unatakiwa uendeshwe au usimamiwe na Wizara ya kilimo ili uweze kupata technical assistance inayotakiwa?
Swali la pili, sasa hivi wananchi wanapata shida sana, wanaolima hapa, licha ya kwamba mbolea na msaada wa kitaalam unakosekana, lakini ndege aina ya kweleakwelea, wanavamia sana mashamba ya wakulima na sasa hivi ndiyo kipindi ambacho mpunga wa eneo lote hilo la kwanzia Maore, Ndungu, Kihurio mpaka Bendera, linavamiwa na hawa ndege waharibifu. Je, Serikali inaweza kusema nini kuhusu kutatua tatizo la kuua hawa ndege waharibifu? Ahsante.

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, ombi lake ni kwamba anataka bwawa lile lisimamiwe na Serikali Kuu badala ya Halmashauri. Naomba niwahakikishie, mwaka jana kwenye Bunge la Kumi tulipitisha Sheria ya Umwagiliaji na tukaanzisha Tume ya Umwagiliaji, Tume hii ndiyo itakayosimamia ujenzi wa mabwawa yale makubwa ambayo yataongeza eneo la umwagiliaji. Kwa hiyo, nikuhakikishie Mbunge suala la utaalam lipo katika Wizara ya Maji na Umwagiliaji kuhakikisha mabwawa haya yatatengenezwa inavyotakiwa, kwa hiyo usiwe na wasiwasi.
Swali la pili kuhusu ndege, hilo nafikiri labda Waziri wa Kilimo yupo hapa, anaweza akajibu. Ahsante sana.

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, hilo swali la ndege waharibifu nimeshalipokea pia swali la aina hii kutoka kwa Mheshimiwa Elibariki Kingu, Mbunge makini wa kutoka Jimbo la Singida Magharibi, kuna ndege waharibifu wa aina hiyo hiyo. Niwaambie tu Waheshimiwa Wabunge kwa maeneo hayo ambayo yamepata uharibifu wa aina hiyo, nimewaelekeza wataalam wangu ili waweze kutumia utaratibu ambao Serikali huwa inatumia wa kutumia ndege kwenda kushughulika na ndege waharibifu wa mazao katika maeneo hayo husika.
Kwa hiyo, kama kuna eneo lingine ambalo Wabunge hawakupata fursa ya kuuliza lina matatizo ya aina hiyo, naomba baada ya kuahirisha Bunge nipate taarifa za aina hiyo ili niweze ku-communicate na wataalam wangu waweze kuchukua hatua zinazostahili.