Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Baadhi ya mambo ambayo yanamkosesha mkulima wa tumbaku mapato stahiki ni pamoja na tozo za pembejeo zinazoingizwa nchini na kuzifanya kuwa ghali, kuwepo wanunuzi wachache wa tumbaku na hivyo kudumaza ushindani wa bei na uwezo mdogo wa kifedha wa Bodi ya Tumbaku:- (a) Je, Serikali imefikia hatua gani katika kuondoa utitiri wa tozo za pembejeo? (b) Je, hadi sasa Serikali imevutia wanunuzi wangapi kutoka China na kwingineko? (c) Je, kuanzia msimu wa 2016/2017 Serikali imeiongezea Bodi ya Tumbaku kiasi gani cha fedha katika bajeti yake ili iendeshe masoko ya tumbaku kwa ufanisi?

Supplementary Question 1

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, masoko ya tumbaku yanayumba au kwa lugha nyepesi yanasuasua kutokana na uwezo mdogo wa kifedha wa Bodi ya Tumbaku ambayo ndiyo inapaswa kulipa wale ma-classifiers wanaopanga tumbaku lakini pia na kuajiri ma-classifiers. Je, Serikali katika mwaka huu wa fedha 2016/2017, imeiongezea Bodi ya Tumbaku kiasi gani ili ifanye kazi ipasavyo masoko yaende kama inavyopaswa?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Serikali inafahamu kwamba makato mbalimbali yako kwenye pembejeo lakini pia katika bei anayopangiwa mkulima kodi ni nyingi. Lini Serikali itakuja hapa na orodha ya kodi ambazo zimeondolewa ili mkulima apate mapato anayostahili?

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba masoko ya tumbaku yanayumba na siyo kwamba yanayumba Tanzania peke yake bali yanayumba dunia nzima mahali tumbaku inakozalishwa kwa sababu ya bei ya tumbaku kidunia imeshuka. Kwa hivyo, hilo jambo linasababisha hata soko letu hapa ndani na lenyewe liyumbe hivyo hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, sababu kubwa ni hiyo, lakini sababu zingine ni hizi za kwetu za ndani kama hivyo Bodi yenyewe kutokuwa na pesa za kutosha kuendesha shughuli zake kikamilifu. Ndiyo maana mwaka wa fedha uliopita pamoja na kwamba walikuwa wanapata ruzuku ya Serikali kuendesha Bodi yao, ukaanzishwa huo ushuru kwa wanaosafirisha nje tumbaku ili kuisaidia kukidhi mahitaji yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili kwamba kodi ni nyingi ni kweli kodi ni nyingi kama nilivyosema katika jibu langu la msingi. Ndiyo maana Serikali imechukua hatua hii ya kuunda Kamati ya Makatibu Wakuu wapitie hizi kodi za mazao yote siyo zao la tumbaku peke yake ili kuona zile kodi ambazo ni kero na ambazo zinaweza zikafutwa au kuondolewa mara moja ziondolewe na zile ambazo zitakuwa zinaathiri bajeti za Halmashauri zetu au Serikali Kuu basi hizi zitakuja kufutwa katika mwaka wa fedha ujao.

Name

Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Baadhi ya mambo ambayo yanamkosesha mkulima wa tumbaku mapato stahiki ni pamoja na tozo za pembejeo zinazoingizwa nchini na kuzifanya kuwa ghali, kuwepo wanunuzi wachache wa tumbaku na hivyo kudumaza ushindani wa bei na uwezo mdogo wa kifedha wa Bodi ya Tumbaku:- (a) Je, Serikali imefikia hatua gani katika kuondoa utitiri wa tozo za pembejeo? (b) Je, hadi sasa Serikali imevutia wanunuzi wangapi kutoka China na kwingineko? (c) Je, kuanzia msimu wa 2016/2017 Serikali imeiongezea Bodi ya Tumbaku kiasi gani cha fedha katika bajeti yake ili iendeshe masoko ya tumbaku kwa ufanisi?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba na mimi kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa wakulima wa eneo langu Manyoni Mashariki eneo la Makuru, Heka na Mkwese wana kilio kikubwa sana cha mapunjo ya bei ya tumbaku kutokana na hawa wapangaji wa madaraja (classifiers) kutokuwa waaminifu na pia kutokana na utitiri/wingi wa madaraja ya tumbaku, yapo 72. Waziri anatoa tamko gani kusimamia hawa classifiers vizuri kwa maana ya kutoa elimu kwa wakulima?
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili, ni lini Serikali…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mtuka swali la nyongeza huwa ni moja, Mheshimiwa Waziri.
MHE. DANIEL E. MTUKA: Naomba majibu tafadhali.

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli wako classifiers ambao siyo waaminifu, lakini katika kumwajiri mtu huwezi ukajua mara moja kwamba huyu siyo mwaminifu ni mpaka pale anapoingia kazini ndiyo tabia zake za hovyo hovyo zinaanza kuonekana.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali na Wizara ilichokifanya sasa hivi ipo katika utaratibu na imekwishatoa idhini au kibali cha ajira kwa Bodi ya Tumbaku iajiri classifiers wengine 35 katika mwaka huu wa fedha unaokwisha ili kuongeza idadi ya classifiers hawa wafike kwenye maeneo mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya jambo ambalo limekuwa linasababisha kufanya vitu ambavyo siyo vya kiadilifu katika kukagua madaraja ya tumbaku ni kwa sababu classifier wanakuwa wachache, anahitajika maeneo mengi kwa hivyo anaanza kutumia ule uhaba wao kufanya mambo ya kuomba kitu hiki au kingine. Kwa maana hiyo, hawa watakapokuwa wameajiriwa tunatarajia kwamba angalau hilo zoezi la kutambua madaraja ya tumbaku litakwenda bila vikwazo au tabia hizo za kuomba rushwa kwa wenye tumbaku.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Baadhi ya mambo ambayo yanamkosesha mkulima wa tumbaku mapato stahiki ni pamoja na tozo za pembejeo zinazoingizwa nchini na kuzifanya kuwa ghali, kuwepo wanunuzi wachache wa tumbaku na hivyo kudumaza ushindani wa bei na uwezo mdogo wa kifedha wa Bodi ya Tumbaku:- (a) Je, Serikali imefikia hatua gani katika kuondoa utitiri wa tozo za pembejeo? (b) Je, hadi sasa Serikali imevutia wanunuzi wangapi kutoka China na kwingineko? (c) Je, kuanzia msimu wa 2016/2017 Serikali imeiongezea Bodi ya Tumbaku kiasi gani cha fedha katika bajeti yake ili iendeshe masoko ya tumbaku kwa ufanisi?

Supplementary Question 3

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kama lilivyo swali la msingi, naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais wakati yupo kwenye kampeni aliahidi kuondoa tozo mbalimbali ambazo zinamdidimiza mkulima wa kahawa. Mpaka sasa Serikali bado haijaondoa hizo tozo. Je, Serikali ipo tayari kuwaruhusu wananchi wale wanaolima kahawa waweze kuuza kahawa sehemu nyingine ambapo watapata bei nzuri?

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Answer

shimiwa Rais wakati wa kampeni aliwaahidi Watanzania kwamba huu msururu wa kodi utatafutiwa utaratibu wa kuziondoa zile ambazo hazistahili kutozwa au zenye kuleta kero kwa wananchi. Pamoja na nia hiyo nzuri ya Mheshimiwa Rais bado mazao haya tunayahitaji hapa nchini. Serikali hii imeweka kipaumbele cha kuwa nchi ya viwanda na hivi viwanda vitahitaji malighafi ipatikane hapa hapa nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, halitakuwa jambo la busara leo tukisema kwa sababu tuna tatizo hili la kodi ndogo ndogo zenye kero, basi tuachie malighafi kwa ajili ya viwanda vyetu ianze kuuzwa nje. Utaratibu tunaoufanya ni kuchukua hatua za dharura kuhakikisha kwamba bei zinakuwa nzuri na masoko yanakuwa mazuri ili kutowapa shida wananchi wakati wa kuuza mazao yao.