Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. FREEMAN A. MBOWE) aliuliza:- Mfumo wa Vyama Vingi vya Siasa huwapa wananchi fursa ya kuchagua kiongozi na chama wanachotaka sambamba na Ilani za Vyama husika katika kila ngazi ya uchaguzi kuanzia ya Mtaa/Kijiji, Kata, Jimbo na Taifa:- (a) Je, ni kwa nini Serikali ya CCM hupuuza ukweli huu na kulazimisha Ilani ya Chama chao kutekelezwa nchi nzima kila ngazi bila kujali matakwa ya wananchi kupitia uchaguzi? (b) Je, katika mazingira ya Manispaa au Halmashauri za Wilaya palipo na uongozi wa Chama tofauti na CCM ni ipi mipaka ya Wakuu wa Wilaya na Mikoa kutoa amri au maelekezo ya kiutendaji? (c) Je, Serikali haioni kuwa sasa ni wakati muafaka kuweka utaratibu wa kisheria na kikanuni ili kuondokana na mfumo huu kandamizi ambao ni urithi na ukiritimba wa mfumo wa chama kimoja cha siasa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali madogo mawili. Kwa kuwa Chama cha Mapinduzi kinaongoza kwa kuwa na utaratibu unaoeleweka na wa kidemokrasia ndani ya chama chake tofauti na baadhi ya vyama ambavyo vimekuwa havina uongozi wa demokrasia iliyoshamiri. Je, Serikali kupitia kwa Msajili wa Vyama anaweka utaratibu gani ili kuhakikisha demokrasia ndani ya vyama inatekelezwa?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa nchi yetu iko kwenye vyama vingi na baadhi ya wanasiasa wanagomea mijadala ndani ya Bunge kitu ambacho ni kuwanyima haki wananchi ambao wamewachagua ili waje kuwawakilisha ndani ya Bunge. Je, Bunge hili linazidi kuchukua hatua gani dhidi ya kitendo hiki cha kutowatendea haki wananchi hawa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza limeulizwa, Serikali kupitia Msajili wa Vyama vya Siasa inahakikisha vipi demokrasia inakuwepo katika vyama vya siasa. Vyama vya siasa vipo kwa mujibu wa sheria ambayo imevianzisha lakini vilevile vyama hivi vinasimamiwa na Msajili wa Vyama ambaye kazi yake kubwa ni kuratibu shughuli zote za vyama na amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba vyama vyote vinatii sheria ambayo imeviunda lakini na Katiba ya nchi ambayo inaelekeza masuala mbalimbali ya kiuongozi katika vyama hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kwa nafasi ya Msajili wa Vyama vya Siasa yeye siku zote ndiye amekuwa mlezi wa vyama hivi na popote pale ambapo kumekuwa kuna shida ya masuala ya kidemokrasia ndani ya vyama amekuwa akichukua hatua stahiki kwa maana ya kukutana na wadau na kuweka mambo sawasawa katika vyama hivi. Kwa hiyo, tunaendelea kuamini kwamba kwa nafasi ya Msajili ataendelea kuvilea vyama hivi na kuhakikisha demokrasia inakuwepo katika vyama vya siasa kama ambavyo vimeanzishwa kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili limeulizwa kwamba kama Serikali tunachukua hatua gani sasa kwa namna ambavyo hali inaendelea hapa Bungeni ambapo baadhi ya wenzetu wanatoka nje na hivyo wananchi kukosa uwakilishi kupitia uongozi wao humu ndani. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari jambo hili lilishatolewa ufafanuzi mara nyingi sana na wewe Naibu Spika ulishatoa maelekezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nisirudie maneno mazuri ambayo umekwishayatoa, lakini msimamo unafahamika kwamba wote tumeingia humu ndani kwa ajili ya kutetea na kuwasilisha maslahi ya watu wetu. Kwa hiyo, ndugu zangu Watanzania wenzetu huko nje wanaona ambao wamebaki kutetea maslahi yao na ambao wametoka.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. FREEMAN A. MBOWE) aliuliza:- Mfumo wa Vyama Vingi vya Siasa huwapa wananchi fursa ya kuchagua kiongozi na chama wanachotaka sambamba na Ilani za Vyama husika katika kila ngazi ya uchaguzi kuanzia ya Mtaa/Kijiji, Kata, Jimbo na Taifa:- (a) Je, ni kwa nini Serikali ya CCM hupuuza ukweli huu na kulazimisha Ilani ya Chama chao kutekelezwa nchi nzima kila ngazi bila kujali matakwa ya wananchi kupitia uchaguzi? (b) Je, katika mazingira ya Manispaa au Halmashauri za Wilaya palipo na uongozi wa Chama tofauti na CCM ni ipi mipaka ya Wakuu wa Wilaya na Mikoa kutoa amri au maelekezo ya kiutendaji? (c) Je, Serikali haioni kuwa sasa ni wakati muafaka kuweka utaratibu wa kisheria na kikanuni ili kuondokana na mfumo huu kandamizi ambao ni urithi na ukiritimba wa mfumo wa chama kimoja cha siasa?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa kuwa nafasi za Wakuu wa Mikoa na Wakuu Wilaya zipo kisheria na zipo ndani ya Katiba, Serikali inasemaje kwa baadhi ya vyama ambavyo vimekuwa vikiwapuuza, vikiwadharau na kutotii amri zao pale wanapotakiwa kufanya hivyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Katiba yetu na sheria mbalimbali zimeunda nafasi ya Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya. Katika utaratibu wa Katiba yetu ukisoma katika Ibara ya 64 inaelekeza wazi kabisa kwamba Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya ni wawakilishi wa Serikali katika eneo husika kwa maana ya Rais. Kwa hiyo, wako pale kwa niaba ya Serikali na ndiyo maana kazi yao kubwa ni kuhakikisha wanasimamia na kuelekeza yale matakwa na mambo yote ambayo Serikali imekuwa ikiyataka yafanyike katika maeneo husika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa mujibu wa Sheria ya Utawala wa Mikoa, Sura ya 97, katika kifungu kile cha 14(1)-(3) imeelezea wazi pia kazi ya Wakuu wa Wilaya. Kwa hiyo, niwaombe tu wanasiasa wenzangu ikifika masuala ya utendaji, viongozi hawa wako kwa mujibu wa sheria na Katiba hawajajiweka wenyewe. Kwa hiyo, amri zao, maelekezo yao ni lazima yazingatiwe kwa sababu wako pale kwa niaba ya Mheshimiwa Rais na kwa niaba ya Serikali.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. FREEMAN A. MBOWE) aliuliza:- Mfumo wa Vyama Vingi vya Siasa huwapa wananchi fursa ya kuchagua kiongozi na chama wanachotaka sambamba na Ilani za Vyama husika katika kila ngazi ya uchaguzi kuanzia ya Mtaa/Kijiji, Kata, Jimbo na Taifa:- (a) Je, ni kwa nini Serikali ya CCM hupuuza ukweli huu na kulazimisha Ilani ya Chama chao kutekelezwa nchi nzima kila ngazi bila kujali matakwa ya wananchi kupitia uchaguzi? (b) Je, katika mazingira ya Manispaa au Halmashauri za Wilaya palipo na uongozi wa Chama tofauti na CCM ni ipi mipaka ya Wakuu wa Wilaya na Mikoa kutoa amri au maelekezo ya kiutendaji? (c) Je, Serikali haioni kuwa sasa ni wakati muafaka kuweka utaratibu wa kisheria na kikanuni ili kuondokana na mfumo huu kandamizi ambao ni urithi na ukiritimba wa mfumo wa chama kimoja cha siasa?

Supplementary Question 3

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Chama cha Mapinduzi ndicho kilichoshinda katika uchaguzi mkuu uliokwisha hivi karibuni mwaka 2015; na kwa kuwa Serikali iliyoko madarakani sasa inatakiwa kutekeleza Ilani ya Uchaguzi iliyojinadi kwa wananchi wake; na kwa kuwa ziko nchi ambazo uchaguzi ukishamalizika vyama vya siasa vingine havipaswi kwenda kufanya mikutano ya hadhara, je, hatuoni sasa ni wakati muafaka wa kufanya marekebisho ya sheria ili chama kilichoko madarakani kiweze kuachiwa nafasi ya kuendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi?

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri na kuendelea kuwakumbusha wanasiasa kwamba madaraka ya Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa yako kwa mujibu wa Katiba na waendelee kutii madaraka na pale wanapovunja sheria, sheria zitaendelea kuchukua mkondo wake. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Mheshimiwa Mary Chatanda ameleta ushauri kwa Serikali na ninachoweza kusema kwa niaba ya Serikali ni kwamba, kwa kuwa Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sheria mbalimbali zilizowekwa ndizo zinazofuatwa kwa sasa kuongoza misingi ya utawala bora na hasa pale chama kinaposhinda kuendelea kutekeleza Ilani yake ya Uchaguzi, hivyo ndivyo ilivyo sasa. Kwa hiyo, kama nchi hii itaona kwamba kunatakiwa kufanya mabadiliko na michakato ya Katiba inaendelea, basi mambo hayo mengine mapya yanaweza kuzingatiwa katika michakato ya Katiba inayoendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa tunaendelea kuwakumbusha Watanzania wote chama kilichoshinda na kushika hatamu ya kuendesha nchi hii kwa mujibu wa Ilani ya Uchaguzi ni Chama cha Mapinduzi na Watanzania
wote wataendelea kushughulikiwa kupitia Ilani ya Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi, sheria na Katiba iliyopo sasa.

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. FREEMAN A. MBOWE) aliuliza:- Mfumo wa Vyama Vingi vya Siasa huwapa wananchi fursa ya kuchagua kiongozi na chama wanachotaka sambamba na Ilani za Vyama husika katika kila ngazi ya uchaguzi kuanzia ya Mtaa/Kijiji, Kata, Jimbo na Taifa:- (a) Je, ni kwa nini Serikali ya CCM hupuuza ukweli huu na kulazimisha Ilani ya Chama chao kutekelezwa nchi nzima kila ngazi bila kujali matakwa ya wananchi kupitia uchaguzi? (b) Je, katika mazingira ya Manispaa au Halmashauri za Wilaya palipo na uongozi wa Chama tofauti na CCM ni ipi mipaka ya Wakuu wa Wilaya na Mikoa kutoa amri au maelekezo ya kiutendaji? (c) Je, Serikali haioni kuwa sasa ni wakati muafaka kuweka utaratibu wa kisheria na kikanuni ili kuondokana na mfumo huu kandamizi ambao ni urithi na ukiritimba wa mfumo wa chama kimoja cha siasa?

Supplementary Question 4

MHE. KAPT. GEORGE H. MKUCHIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ni taratibu dunia nzima katika mfumo wa vyama vingi Ilani ya Chama kilichoshinda uchaguzi ndiyo inayotekelezwa. Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba elimu hiyo au uelewa huo unawafikiwa viongozi wa vyama vyote vilivyosajiliwa katika nchi hii?

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijajibu swali la Mheshimiwa Mkuchika, naomba nimpongeze sana kwa kushinda kesi yake ya uchaguzi na kuwabwaga wale wapinzani ambao walikuwa wanafikiri kwamba Mheshimiwa George Mkuchika hakushinda kihalali. Kwa hiyo, naomba nimpongeze sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Gerge Mkuchika ameomba kujua ni kwa kiasi gani Serikali itajitahidi kuhakikisha inatoa elimu na hasa kwa vyama ili viweze kutambua umuhimu wa kutii na kuamini kwamba Katiba inayotutawala inaelekeza ilani inayotekelezwa katika nchi ni Ilani ya chama kilichoshinda.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka sasa kadri tunavyoendelea katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya Serikali, Serikali imeendelea kuwafahamisha Watanzania wote, vyama vya siasa vilikuwa vikipata elimu hiyo kabla ya uchaguzi na hata baada ya uchaguzi kwamba waendelee kuamini chama kilichoshinda ndicho kitakachotekeleza Ilani yake ya Uchaguzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie Bunge hili lako Tukufu kuendelea kuvikumbusha Vyama vyote vya Siasa vipitie Sheria ya Uchaguzi, vipite Katiba na vilevile viendelee kusikiliza na kupata maelekezo yanayotolewa na viongozi mbalimbali tukiendelea kusisitiza kwamba chama kilichoshinda, Chama cha Mapinduzi ndicho chenye Ilani ya Uchaguzi na Serikali itapanga mipango kwa kuzingatia Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi na siyo vinginevyo.