Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuondoa changamoto za biashara za mpakani hasa utitiri wa tozo?

Supplementary Question 1

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Waziri uko tayari kuja Kigoma baada ya Bunge hili ili uweze kuongea na wafanyabiashara wa Wilaya zote zinazopakana na nchi ya Congo na Burundi?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Felix kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kawaida mtoto hufuata kichogo cha mlezi wake. Kwa kuwa Mheshimiwa Rais mara nyingi anawasikiliza wafanyabiashara na hata Kariakoo alimtuma na kumwelekeza Mheshimiwa Waziri Mkuu akaenda kusimama kwa zaidi ya masaa sita kusikiliza wafanyabiashara, kwa hiyo na mimi niko tayari kwenda Buhigwe na mipakani kuwasikiliza wafanyabiashara. (Makofi)

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuondoa changamoto za biashara za mpakani hasa utitiri wa tozo?

Supplementary Question 2

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Mpaka wa Mutukula ambao ni mpaka wa Tanzania na Uganda ndani ya Wilaya ya Misenye ni mpaka ambao kiuchumi unakusanya mapato makubwa, lakini wafanyabiashara wa pale wanakabiliwa na utitiri wa tozo ambazo kama mazingira mazuri ya kiwekwa biashara hiyo itakua…

SPIKA: Swali lako.

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Spika, ni lini sasa Serikali itaboresha mazingira ya biashara katika mpaka wa Mutukula?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ipo katika jitihada za kuweka mazingira mazuri ya kibiashara, kwa hiyo, siyo tu sehemu ambayo ameitaja Mheshimiwa Mbunge, sehemu zote ambazo ziko mipakani na ambazo sio za mipakani tutajitahidi kuondoa changamoto hiyo ya biashara. (Makofi)

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuondoa changamoto za biashara za mpakani hasa utitiri wa tozo?

Supplementary Question 3

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru; tatizo sio tozo peke yake kuna utitiri wa vituo bubu vya ukaguzi wa bidhaa barabarani; je, na hivyo vitaondoka lini?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kajege kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ndio inawezekana lakini naomba hili tulichukue tulifanyie utafiti tuone kama zipo changamoto hizo ambazo zinakwamisha harakati za biashara tuweze kuzipunguza ama kuziondoa kabisa.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuondoa changamoto za biashara za mpakani hasa utitiri wa tozo?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, ni lini mtahakikisha mnaondoa askari polisi kujihusisha na ukusanyaji wa kodi kwenye mipaka? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni lini tutaondoa askari polisi? Askari polisi ni chombo cha usalama, usalama wa mali na usalama wa wananchi. Hatuwezi kuwaondoa sehemu za mipakani, kwa hiyo, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutafuatilia nini kinatokea huko katika biashara hiyo ya mipakani. (Makofi)