Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza:- Je, ni kwa nini bei ya kuunganisha umeme katika Kijiji cha Lwamgasa ni shilingi 321,000 tofauti na vijiji vingine?

Supplementary Question 1

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza kwa vile taarifa za TAMISEMI hazikuwa sahihi je, Serikali iko tayari kuwarejeshea wananchi pesa ambazo zimezidi kutoka shilingi 27,000 hadi 321,000 baada ya taarifa yetu kujulikana kwamba siyo sahihi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, zoezi la kubaini vijiji mji ambavyo vimetajwa hapa kwenye swali la msingi litakamilika lini ili wananchi wenye uwezo mdogo kwenye vijiji vyetu waweze kupata umeme ikiwemo Kaduda, Chibingo, Ibondo na vingine vingi? Naomba kuwasilisha.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya nyongeza mawili ya Mheshimiwa Tumaini Mbunge wa Busanda kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niweke taarifa sahihi kwamba tunaamini kabisa taarifa za TAMISEMI zilikuwa sawa kwa mujibu wa Sheria ya Mipango Miji. Isipokuwa kinachogomba ni ile hali ya kwamba watu wanatambuliwa kuwa wako mjini lakini wao wanajiona hawako Mjini na kwa sababu tumelibaini hilo tumeona ni vema sasa sisi Wizara ya Nishati twende site na kubaini hata kama eneo ni la mji, lakini je, uhalisia wa maisha ya wakazi wa maeneo yale ni wa namna gani? kwa sababu Sheria ya Mipango Miji imeweka maeneo na mazingira ya masharti kama kuna maduka, kama kuna vituo vya afya, kama kuna barabara za lami na nini hayo ndiyo maeneo ya mji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niseme tu taarifa ya TAMISEMI kwa mujibu wa sheria ilikuwa sawa. Lakini maeneo hayo yanawakazi wenye vipato tofauti na hivyo sisi tunafanya utafiti na upembuzi yakinifu kuona ni kiasi gani kilipwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo hapo niseme kwamba anaposema turudishwe kwa wananchi namuomba asielekee huko. Kwa sababu Serikali ya Awamu ya Sita inaweka ruzuku kwenye gharama za kuunganisha umeme kwa kulingana na maeneo mbalimbali yalivyo. Kwa hiyo Serikali iliweka ruzuku hata hii 320,000 bado ni ruzuku imewekwa ili wananchi waweze kupata umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa shughuli ikikamilika ambayo ameuliza kwenye eneo la pili ni lini? Tunaendele, tunafanya kazi hii ni kubwa tulimaliza awamu ya kwanza tukaona kuna maeneo hatukufika tumerudi. Tunaomba yeye na Waheshimiwa Wabunge wawe wavumilivu ili zoezi litakapokamilika tuweze kuja kutoa taarifa sahihi na kuweza kutangaza gharama sahihi kila eneo.

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza:- Je, ni kwa nini bei ya kuunganisha umeme katika Kijiji cha Lwamgasa ni shilingi 321,000 tofauti na vijiji vingine?

Supplementary Question 2

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza. Nataka tu nijue Serikali inatumia kigezo gani? tofauti ya 27,000 na shilingi 300,000 ni kubwa mno je, Serikali haioni hebu ije na mkakati wa kuona kiwango fulani ambacho kitakuwa kina rationale nzuri kwa wote wanaokaa mjini na wale wa vijijini? Ahsante sana.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, huko nyuma kuliwahi kuwa na viwango tofauti tofauti vya kuunganisha umeme. Sasa kwa maneno machache niseme tulipata kipindi fulani mradi wa kupeleka umeme vijijini na ulikuwa unafanyika bure kwa watanzania wote waliyokuwa wanakidhi vigezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ule mradi ulikuwa wa mfadhili na mfadhili akasema hawezi kutoa bure, kwa hiyo, tutakubaliana kwamba basi mwananchi alipie VAT ambayo kipindi hicho VAT ilikuwa ni shilingi 27,000 ndiyo genesis ya shilingi 27,000 ilipoanzia. Kwa hiyo, tumekwenda nayo kwa utaratibu huo mpaka sasa na Serikali sasa ndiyo inafanya mchakato na upembuzi mpana zaidi ili kuona kama tunaweza tukawa tuna viwango tofauti tofauti kwa misingi tofauti tofauti kama hii 27,000 ilikotokea kipindi hicho ilikuwa kuunganisha, ilikuwa 150,000 nadhani sasa asilimia 18 au 20 nadhani VAT ilikuwa asilimia 20 ikawa ni shilingi 27,000 ndiyo genesis ya shilingi 27,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, gharama halisi ni shilingi laki saba, laki sita mpaka laki saba. Kwa hiyo, inapungua kwenda laki tatu kulingana na ruzuku ambayo inayotolewa na Serikali kwenye maeneo ya mijini na maeneo ya vijijini au kwenda shilingi 27,000. Nashukuru.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza:- Je, ni kwa nini bei ya kuunganisha umeme katika Kijiji cha Lwamgasa ni shilingi 321,000 tofauti na vijiji vingine?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru Kijiji cha Luganga na Kijiji cha Kilolo ndipo yalipo Makao Makuu ya Wilaya lakini hivi ni vijiji vilivyosajili. Je, Serikali ipo pia tayari kuangalia hivi vijiji kwa sababu wamepewa kulipa zaidi ya shilingi 300,000 ambayo ni tofauti na 27,000 kwenye vijiji vingine?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuhakikishie Mheshimiwa Nyamoga kwamba maeneo yote yatafikiwa na upembuzi huu unafanyika nchi nzima kwenye maeneo yote ili kuweza kubaini uhalisia wa kila eneo.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza:- Je, ni kwa nini bei ya kuunganisha umeme katika Kijiji cha Lwamgasa ni shilingi 321,000 tofauti na vijiji vingine?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama navyofahamu wafugaji hawaishi mjini sasa vijiji vya Kisimani na Kilimani pale Himo viliingizwa kwenye Mji mdogo wa Himo na hivyo kukosa fursa ya kufurahia umeme wa REA. Je, mnatoa kauli gani kuhusu hilo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Kimei kwamba azma na nia ya Serikali ya Awamu ya Sita ni kuhakikisha kila Mtanzania popote alipo anapelekewa huduma ya umeme na tayari tumeshaanza kufikisha kwa kila kijiji. Lakini hatua kubwa inayofuata ni ya kupeleka kwenye vitongoji ambavyo hata juzi kwenye bajeti tumevisema na tunatarajia pesa kubwa tutaipata kwenye mwaka wa fedha ule mwingine unaofuata ili vitongoji vyote maana yake wananchi wote waweze kupata huduma ya umeme popote walipo.