Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE (K.n.y. MHE. TASKA R. MBOGO) aliuliza:- Sheria ya Mtoto ya Mwaka 2009 inaainisha kuwa, mtu akifika umri wa miaka 18 huyo ni mtu mzima na Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971, Ibara ya 13 inasema umri wa msichana kuolewa ni miaka 15 na mvulana kuoa ni miaka 18:- Je, ni lini Serikali itaifanya marekebisho ya Sheria ya Ndoa, ili watoto wa kike wasiolewe na umri mdogo kama ilivyo sasa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa, suala hili ni nyeti na linagubikwa na mambo mbalimbali ndani ya jamii ikiwemo imani mbalimbali za kidini, mila na desturi. Je, ni lini sasa White Paper hiyo itapitishwa katika makundi mbalimbali ya jamii, ili iweze kupata maoni yake mbalimbali na kuweza kutungwa Sheria inayoweza kumlinda mtoto?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali langu la pili; chini ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi, kwa kuwa, mpaka sasa hivi elimu yetu ya mpaka sekondari ni bure. Je, Serikali sasa haioni kuna umuhimu wa kuongeza elimu ya kidato cha bure ikawa mpaka form six ambayo ni elimu ya lazima, ili tuweze kuvuka ule umri wa miaka 18 ukizingatia sasa hivi watoto wameanza kusoma wakiwa chini ya miaka minne mpaka mitano? Je, Serikali inasema nini kuhusiana na hilo?

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UFUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nashukuru kwa swali alilouliza Mheshimiwa Mbunge, napenda kumjibu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasema kwamba, kila safari tunaanza kwa hatua kwa hiyo, Serikali imeanza kutoa elimu bure na hatua ya kwanza tumeanza na elimu msingi mpaka kidato cha nne. Kuna changamoto ambazo zinajitokeza katika kutekeleza hii, kwa hiyo, tupate nafasi tutatue changamoto, lakini mawazo na mapendekezo ya Mheshimiwa Mbunge ni jambo la msingi ambalo Serikali italiangalia baada ya kuwa tumeweka vizuri hii ambayo tumeanza nayo kwa awamu ya kwanza.

Name

Halima Ali Mohammed

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE (K.n.y. MHE. TASKA R. MBOGO) aliuliza:- Sheria ya Mtoto ya Mwaka 2009 inaainisha kuwa, mtu akifika umri wa miaka 18 huyo ni mtu mzima na Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971, Ibara ya 13 inasema umri wa msichana kuolewa ni miaka 15 na mvulana kuoa ni miaka 18:- Je, ni lini Serikali itaifanya marekebisho ya Sheria ya Ndoa, ili watoto wa kike wasiolewe na umri mdogo kama ilivyo sasa?

Supplementary Question 2

MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Ni lini Serikali italeta marekebisho yaliyoahidiwa na Mheshimiwa Mwakyembe wakati wa bajeti yake ili kuzuia ndoa za watoto wa shule?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nayaunganisha yote mawili kwenye jibu langu hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza mchakato wa white paper toka mwaka 2008 na lengo likiwa ni kutafuta namna ya kuwashirikisha wananchi kwa ujumla wao kwenye kufanya maamuzi juu ya suala hili ambalo limegubikwa na misingi ya dini, lakini pia limegubikwa na misingi ya mila zetu kwenye makabila mbalimbali hapa nchini. Kwa maana hiyo, suala hili Serikali imeonelea isilichukue kwa haraka haraka na ndiyo maana ikaanzisha mchakato wa white paper.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa bahati mbaya mwaka 2010 Mheshimiwa Rais, niseme kwa bahati nzuri pia, aliamua kuanzisha mchakato wa Mabadiliko ya Katiba na ndani yake akidhani kwamba, ile Tume itakapokuwa inakusanya maoni ingewezekana kupata maoni ambayo yangehusisha nia ya wananchi ya kutaka kufanya mabadiliko kwenye sheria mbalimbali ikiwemo Sheria ya Ndoa na Sheria ya Mirathi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati mbaya baada ya mchakato ule kukamilika, maoni yanayohusiana na suala hili hayakuonekana kama ni miongoni mwa mambo ambayo yalipendekezwa na wananchi. Hivyo, sasa hivi Serikali kupitia Wizara ya Sheria na Katiba imeamua kuanza upya jitihada za kuipeleka mbele white paper ili kupata maoni ya wananchi na hatimaye tuweze kuchukua maamuzi kama Serikali.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE (K.n.y. MHE. TASKA R. MBOGO) aliuliza:- Sheria ya Mtoto ya Mwaka 2009 inaainisha kuwa, mtu akifika umri wa miaka 18 huyo ni mtu mzima na Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971, Ibara ya 13 inasema umri wa msichana kuolewa ni miaka 15 na mvulana kuoa ni miaka 18:- Je, ni lini Serikali itaifanya marekebisho ya Sheria ya Ndoa, ili watoto wa kike wasiolewe na umri mdogo kama ilivyo sasa?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona. Nina swali dogo tu, nawaunga mkono wanaharakati wote kuhusu suala hili muhimu, sasa nauliza Serikali, je, itakuwa tayari kuingiza kipengele kwenye sheria ambacho kinazuia kuzaa kabla ya kufikisha miaka 18? Maana wapo watoto wanazaa wana miaka 13 au 14, lakini hawachukuliwi hatua yoyote. Je, Serikali itaweka kipengele kuzuia? Ahsante sana.

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni suala lenye utata kidogo na katika hatua hii kwa kweli, hatujalifikiria hilo. Naomba tuchukue wazo lake tulifanyie kazi tuone kama ni jambo ambalo angalau linaweza hata likafikiriwa kwa sababu lina utata sana.