Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA aliuliza:- (a)Je, ni lini Serikali itaweka ruzuku kwenye pembejeo za kilimo kama vile mbolea ili kuwapunguzia Wakulima ghaarama za uzalishaji? (b)Je, ni lini Serikali itaanzisha Mfuko Maalum wa Zao la Kahawa?

Supplementary Question 1

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Spika, japokuwa swali langu halijajibiwa kifasaha na imekuwa ni mwendelezo wa kukiuka Kanuni namba 46(1) na hii ni kawaida tumeona sijui inamaanisha nini. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza:
Kwanza, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kupunguza bei ya mbolea ili kuwapunguzia wananchi gharama za kilimo?
Pili, ni lini Serikali itapunguza ushuru na tozo mbalimbali katika zao la kahawa ili kuwapunguzia wakulima mzigo maana wakulima wametwishwa mzigo kwa muda mrefu sana. Wamekuwa na tozo nyingi, ushuru mkubwa kwenye kahawa mwisho wa siku hawanufaiki. Sasa ni lini Serikali itapunguza ushuru na tozo mbalimbali katika zao la kahawa ili kuwapunguzia wakulima mzigo?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, kwanzaa kuhusu kupunguza bei ya mbolea, Serikali imejipanga kuhakikisha kwamba inachukua hatua zinazotakiwa ili kuhakikisha kwamba bei ya mbolea inayotumika katika mazao mbalimbali inapungua. Kwa wiki za hivi karibuni Wizara yangu imekuwa ikikutana na wataalam wake kuangalia ni namna gani tunaweza tukaondoa kero mbalimbali zilizopo katika sekta ya kilimo ikiwa ni pamoja na kuondoa kero ya bei ya mbolea ambayo kwa kweli imelalamikiwa na wananchi wengi.
Mheshimiwa Spika, lakini (b) ameulizia kuhusu kuondoa tozo mbalimbali zinazokabili mazao mbalimbali katika sekta yetu ya kilimo. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kuwa Wizara imekuwa ikipitia upya tozo zote zinazotolea ili kuona ni namna gani tunaweza kupunguza.
Mheshimiwa Spika, katika kufanya hivi nafikiri yeye mwenyewe ameshiriki katika Mkutano ambao Mheshimiwa Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi ameuitisha hivi karibuni wa Wabunge wanaotoka maeneo ya mazao haya ili kuangalia changamoto zilizopo lakini vilevile kupata mapendekezo yao ya namna ya kutafuta suluhu. Nimhakikishie tu kwamba, Wizara inapitia upya kuhusu hizo tozo kwa sababu ni kweli wananchi wanalalamikia na muda siyo mrefu tutapata mrejesho kamili kuhusu namna gani Serikali itapunguza au kuondoa moja kwa moja baadhi ya hizo tozo. Nashukuru sana.