Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuliza:- Serikali ilifanya tathmini na kuona umuhimu wa kujenga daraja kwenye Kata ya Ruhembe kwa shilingi milioni mia sita lakini mpaka sasa shilingi milioni 100 tu zimepelekwa kwenye Halmashauri ya Kilosa. Je, ni lini kiasi cha shilingi milioni 500 kilichobakia kitapelekwa ili kukamilisha daraja hilo na kuwasaidia wananchi wa Ruhembe wanaozunguka umbali mrefu ili kupata mahitaji yao?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza naishukuru sana Serikali kwa kutenga bajeti ya daraja hili la Ruhembe kwenye bajeti ya mwaka 2016/2017. Hata hivyo, kutokana na kilio na mateso makali pamoja na vifo vya watu wa Ruhembe ambao wamekuwa wakilia kwa muda mrefu, Serikali ipo tayari kuleta pesa hizi kule Mikumi katika robo ya kwanza ya mwaka 2016/2017?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nimesema hapa tumetenga shilingi milioni 700 na hii milioni 700 Mheshimiwa Joseph Haule anachosema ni kweli, katika lile daraja tumepoteza watu wengi sana, takribani watu wanane hivi kwa mujibu wa takwimu nilizozipata na mtu mmoja ambaye tumempoteza pale ni mtumishi wa Serikali katika Ofisi yetu ya TAMISEMI.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kwamba, jambo hili sisi wengine tunalifuatilia na tunalijua vizuri sana. Ndiyo maana tumeona katika suala zima la bajeti, mwaka jana waliomba shilingi milioni 600, lakini kilichopitishwa Hazina ilikuwa ni shilingi milioni 300 na ilikuja milioni 100 peke yake. Katika msisitizo mwaka huu tukaona ile milioni 700 lazima irudi katika bajeti kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili linatugusa sana kwa sababu, wananchi pale wakitaka kuvuka kufika ng‟ambo ya pili ni mpaka watembee au wazunguke karibu kilometa 20. Tatizo ni kubwa, ndiyo maana ofisi yetu sasa imefanya harakati za kutosha kuhakikisha tunawasiliana na wenzetu wa TANROAD na hivi sasa nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tunapewa daraja la mudam lile la chuma kupitia ofisi ya TANROAD, si muda mrefu sana angalau liweze kufungwa wakati tukisubiri mpango mrefu kuhakikisha daraja lile linajengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kufanya hivyo sasa angalau tutapunguza kilio cha watu wa eneo lile na imani yangu kubwa ni kwamba, watu wa TANROAD kuanzia wiki hii sasa muda wowote watakwenda kulifunga ili kuondoa tatizo kwa wananchi wa eneo lile.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuliza:- Serikali ilifanya tathmini na kuona umuhimu wa kujenga daraja kwenye Kata ya Ruhembe kwa shilingi milioni mia sita lakini mpaka sasa shilingi milioni 100 tu zimepelekwa kwenye Halmashauri ya Kilosa. Je, ni lini kiasi cha shilingi milioni 500 kilichobakia kitapelekwa ili kukamilisha daraja hilo na kuwasaidia wananchi wa Ruhembe wanaozunguka umbali mrefu ili kupata mahitaji yao?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali ya nyongeza. Kwa kuwa katika kipindi hiki cha mvua barabara nyingi sana zimeharibika, mfano, Wilaya ya Mpwapwa; Kata za Matomondo, Lembule, Mlima, Bereje, Mkanana, Londo, Chamanda, Majami mpaka Nana kule. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari sasa kutenga fungu la kutosha kwa ajili ya ukarabati wa barabara hizo kwa sababu zinapitika kwa shida?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAMISEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi na Mheshimiwa Lubeleje hivi karibuni tumekwenda Wilaya ya Mpwapwa pale kutembelea kuangalia baadhi ya huduma zikiwemo huduma za afya, huduma ya shule, takribani wiki mbili na nusu zilizopita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nimeona changamoto ya barabara katika maeneo yale, lakini nimesema katika kila mgawanyo wa halmashauri una fungu lake. Jukumu letu kubwa ni hii bajeti iliyotengwa, ikishapatikana basi iende kuweka miundombinu, kwa sababu utengaji wa bajeti ni jambo moja na utekelezaji wa bajeti ni jambo lingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sasa hivi Ofisi ya Rais, TAMISEMI tutajielekeza kuhakikisha pesa yote iliyotengwa angalau iweze kufika katika maeneo kwa ajili ya kuhakikisha miundombinu inarekebishwa. Kwa hiyo, Mheshimwa Lubeleje kwa sababu na mimi nilifika kule nimeona hali jinsi gani ilivyo naomba tushirikiane kwa pamoja kuangalia kile kitakachowezekana tuweze kukifanya ili mradi wananchi wa Mpwapwa waweze kupata huduma ya miundombinu ya barabara.