Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE (K.n.y. MHE. LUCY S. MAGERELI) aliuliza:- Matatizo ya migogoro ya ardhi na mipango miji ni suala nyeti sana linalohitaji kutazamwa sana katika zama hizi; na hivi karibuni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi aligawa ramani za maeneo ya mitaa ya Jiji la Dar es Salaam lakini zoezi hilo halikufanikiwa kutokana na kukosa mkakati ulioambatana na matumizi ya ramani hizo:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha ramani hizo zinapatikana kwa nchi nzima ili kusaidia kuongoza matumizi ya ardhi katika miji mingi nchini? (b) Waziri Mkuu aliyepita, Mheshimiwa Mizengo Pinda alisema, Serikali ingeuza Government Bond ili kupata fedha za kugharamia mradi huu. Je, agizo hilo limefikia hatua gani katika utekelezaji?

Supplementary Question 1

kwa kunipatia fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa Serikali imeanzisha utaratibu mzuri wa kuwashirikisha Wenyeviti wa Serikali za Mitaa kwa kuwapatia ramani za maeneo husika, je, Serikali itaweza kwenda mbali zaidi na kuwajengea uwezo pamoja na kuwapatia elimu Wenyeviti wa Serikali za Mitaa na Madiwani ili waweze kusimamia maeneo yale ya wazi na ujenzi holela?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Hivi karibuni Serikali imeweka zuio katika Mkoa wa Dar es Salaam kwa watu ambao wamejihamasisha kubadilisha mashamba yao na kupima viwanja ili waweze kujenga na kuuza. Kwa sababu Serikali yenyewe imeshindwa ama kwa kiasi kikubwa haina uwezo wa kukidhi mahitaji ya ujenzi wa viwanja kwa ajili ya wananchi, haioni sasa ni muda muafaka kuweka utaratibu wa jinsi ya kupata kodi badala ya kuweka zuio?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile katika swali lake la kwanza ameishukuru Serikali kwa kutoa ramani kwa Wenyeviti wa Mitaa ili kuweza kulinda na kuhifadhi maeneo yao lakini akataka kujua kama Serikali haioni kwamba kuna haja ya kuwajengea uwezo. Naomba niseme tu kwamba swali lake ni la msingi sana na kama nilivyokuwa naeleza muda mfupi uliopita, watu hawa wanahitaji pia kupewa elimu ya kutosha kuweza kutambua ramani zile na namna ya kuzisimamia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu Wizara imeonyesha dhamira ya dhati kutaka kulinda maeneo ili yasivamiwe kwa kushirikisha elekezi kwa sababau tumeona maeneo kama Kigamboni kuna makampuni zaidi ya matano yamepima maeneo yale lakini kila kampuni ina bei yake ya kiwanja. Kuna wanaouza square meter moja shilingi 25,000/=, kuna wanaouza shilingi 20,000/= na kuna wanaouza kwa shilingi 10,000/=. Ni nani Mtanzania wa kawaida ataweza kununua? Serikali pia huwa inapima lakini gharama zake hazijafikia hata shilingi 10,000/= kwa square meter moja, iweje wao wapime na kuuza katika bei kubwa za namna hiyo?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Serikali imeamua kwa maana ya Wizara kusitisha kwanza zoezi hili na wiki hii bei elekezi itakuwa imeshakamilika na itatoka ili viwanja hivi hata kama wanapima, tunashukuru kwa sababu wanasaidia katika kupanga miji yetu, lakini wapange miji na kuweza kuuza viwanja katika bei ambayo mlaji wa kawaida ataweza kumudu, isiwe ni bei ambazo zinakwenda kubeba wale watu wenye pesa na wasio na pesa watajikuta hawana viwanja. Kwa hiyo, dhamira ya Serikali ni njema na naomba Waheshimiwa Wabunge mtuunge mkono na wiki hii bei elekezi itatoka na viwanja vitaendelea kupimwa kama kawaida lakini kwa maelekezo mazuri ya Wizara. wahusika wenyewe, niwaombe Halmashauri husika kwa sababu Wenyeviti hawa sio wengi sana kwa kushirikiana na Wizara yangu waweze kuweka utaratibu mzuri ili watu hawa waweze kupewa angalau ABCs za kuweza kusoma na kutambua ramani zile ili waweze kufanya kazi yao kwa ufasaha zaidi. Maana tukishawawezesha hawa, kwa sababu pia siyo wote wanaofurahia namna ambavyo miji yao inaharibika, wengi wanachukia, watakuwa katika position nzuri ya kuweza kusimamia jukumu ambalo wamepewa sasa ambalo linastahili kusimamiwa katika maeneo yao. Kwa hiyo, niseme tu Wizara yangu itashirikiana na Halmashauri kuandaa mipango mizuri ili watu hawa waweze kupewa elimu ili waweze kusimamia vizuri maeneo yao kama ambavyo wameelekezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili amezungumzia habari ya zuio la Wizara kwa upimaji unaoendelea katika maeneo mbalimbali. Nawaomba sana Waheshimiwa Wabunge watambue kwamba hatua iliyochukuliwa na Wizara ina lengo zuri na hasa la kutaka kuwalinda walaji wa kawaida kwa maana watu wa kawaida ambao wanatafuta viwanja kwa ajili ya kuweza kupata maeneo yao. Sheria ya Mipangomiji Na. 8 ya mwaka 2007 inaruhusu watu binafsi kupima maeneo hayo lakini kwa kuzingatia taratibu za maeneo hayo.

Name

Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE (K.n.y. MHE. LUCY S. MAGERELI) aliuliza:- Matatizo ya migogoro ya ardhi na mipango miji ni suala nyeti sana linalohitaji kutazamwa sana katika zama hizi; na hivi karibuni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi aligawa ramani za maeneo ya mitaa ya Jiji la Dar es Salaam lakini zoezi hilo halikufanikiwa kutokana na kukosa mkakati ulioambatana na matumizi ya ramani hizo:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha ramani hizo zinapatikana kwa nchi nzima ili kusaidia kuongoza matumizi ya ardhi katika miji mingi nchini? (b) Waziri Mkuu aliyepita, Mheshimiwa Mizengo Pinda alisema, Serikali ingeuza Government Bond ili kupata fedha za kugharamia mradi huu. Je, agizo hilo limefikia hatua gani katika utekelezaji?

Supplementary Question 2

MHE. ISSA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Mheshimiwa Naibu Waziri amesema katika jibu lake hapa kwamba Halmashauri zijitahidi kuweza kuwapa semina au mafunzo Wenyeviti wa Serikali za Mitaa na Maafisa wengine. Hata hivyo, Wizara yake inadaiwa na Halmashauri, kwa mfano, Halmashauri ya Manispaa ya Temeke tunadai gawiwo la asilimia 30 ya shilingi bilioni moja kutokana na gawiwo la kodi ya ardhi. Tangu mwaka 2014 tunadai na tunauliza hawatujibu, hawaoni kwamba juhudi za Halmashauri kuweza kupanga, kutoa elimu zinakwamishwa na Wizara yenyewe kwa kutokurejesha ile asilimia 30?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

Makazi, majibu mafupi.
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nimesema hapa kwamba Halmashauri zishiriki katika suala zima la kuwajengea uwezo Wenyeviti hawa lakini kwa kushirikiana pia na Wizara. Maana ya kujenga uwezo ni kwa kutumia mapato ya ndani ya Halmashauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la asilimia 30 kutorudi kwenye Halmashauri, naomba niseme tu kwamba, tunapokusanya mapato haya, yanakwenda kwenye kapu moja la Serikali ambapo tunakwenda kugawana keki wote kwa pamoja na pale pesa hizo zinaporudi Wizarani mara moja zinakwenda katika maeneo husika. Tunatambua wazi kwamba Halmashauri nyingi zinadai lakini katika kudai pia kuna Halmashauri nyingi pia Wizara inazidai ambazo walikopeshwa pesa kwa ajili ya kupima viwanja. Kwa hiyo, pesa wakati mwingine inapoingia Wizara inakata katika kufidia madeni ambayo imetoa ili pesa ile iweze ku-generate na kuweza kuwapa Halmashauri nyingine lakini Halmashauri nyingi zaidi zinadai.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwahakikishie tu kwamba tumekwishachukua takwimu sahihi za madai yanayodaiwa kwa asilimia 30. Kwa hiyo, mara tutakapopokea fedha kutoka Hazina na sisi tutazituma moja kwa moja. Nia na dhamira ya Serikali ni nzuri ya kuweza kuhakikisha mpango unakwenda vizuri kwa kushirikisha pande zote. Kwa hiyo, zitakapokuja hizi fedha tutazileta na tunajua zitasaidia.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe tahadhari pia, tuna malalamiko likiwepo lalamiko kutoka Halmashauri ya Magu kwamba pesa hizi zikirudi Wakurugenzi wanazipangia shughuli nyingine na idara husika haipewi. Kwa hiyo, tuseme pesa hizi zikirudi kule zinatakiwa zirudi kwenye idara husika ili zifanye shughuli ya utawala wa ardhi na siyo kuzipangia matumizi mengine. Naomba sana Wakurugenzi ambao wanazitumia ndivyo sivyo, basi tunakwenda kufanya uhakiki ili tuweze kuona ni namna gani pesa hizi zitafanya kazi iliyokusudiwa.

Name

Ali Salim Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mwanakwerekwe

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE (K.n.y. MHE. LUCY S. MAGERELI) aliuliza:- Matatizo ya migogoro ya ardhi na mipango miji ni suala nyeti sana linalohitaji kutazamwa sana katika zama hizi; na hivi karibuni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi aligawa ramani za maeneo ya mitaa ya Jiji la Dar es Salaam lakini zoezi hilo halikufanikiwa kutokana na kukosa mkakati ulioambatana na matumizi ya ramani hizo:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha ramani hizo zinapatikana kwa nchi nzima ili kusaidia kuongoza matumizi ya ardhi katika miji mingi nchini? (b) Waziri Mkuu aliyepita, Mheshimiwa Mizengo Pinda alisema, Serikali ingeuza Government Bond ili kupata fedha za kugharamia mradi huu. Je, agizo hilo limefikia hatua gani katika utekelezaji?

Supplementary Question 3

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Ni lini Wizara itakuja Wilaya ya Mkalama kutugawia ramani mpya Wabunge na viongozi husika na kutuonyesha mipaka ya Wilaya kwa Wilaya ili kuepusha migogoro inayoendelea sasa na inayosababisha uvunjifu wa amani kama ambavyo imejitokeza katika Jiji la Dar es Salaam?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimwa Allan ametaka kujua ni lini Wizara itagawa ramani kama ilivyofanya Dar es Salaam ili kuweza kuepusha uvamizi katika maeneo hayo? Naomba nirudie tena kusema kwamba zoezi hili limefanywa na Wizara kwa kuanzia Dar es Salaam lakini lengo la kufanya kwa kila Mkoa na kila Halmashauri inao wajibu wa kutoa ramani hizi kwa Wenyeviti wake ili waweze kulinda maeneo yao siyo kwamba Wizara itakwenda katika kila Halmashauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nirudie tena kusema kupitia katika Bunge lako hili kwamba Halmashauri zote zinatakiwa kusimamia zoezi hili na hasa katika maeneo ambayo migogoro imekuwa mingi katika maeneo ya mjini ambapo viwanja vimevamiwa ovyo ovyo ili waweze kuona ni jinsi gani wataweza kutawanya ramani hizo ili watu waweze kulinda maeneo yao. Kama kuna tatizo pengine katika uelimishaji wa kusoma zile ramani basi Wizara inaweza ikasaidia kutoa wataalam kwenda kushirikiana na Halmashauri kuwafanya hawa watu waweze kusoma ramani vizuri na kuweza kuyalinda maeneo yao. Kwa hiyo, nizitake tu Halmashauri ziweze kufanya kazi hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, anasema ni lini tutakwenda kwa ajili ya kubainisha mipaka ambayo ipo…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, swali la nyongeza lazima liwe moja, kama yalikuwa mawili, basi umeshamaliza kujibu hilo moja. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Ndiyo Mheshimiwa Naibu Spika.