Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prosper Joseph Mbena

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:- Ujenzi wa barabara ya kutoka Bigwa - Kisaki upo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM na fedha za ujenzi zitatoka kwenye mpango wa MCC II au Serikalini na nyumba zote zilizomo ndani ya mita 60 zimewekwa alama „X’ tayari kubomolewa katika maeneo ya Ruvu, Kibangile, Kisemu, Mtamba, Nzasa, Kangazi, Kisanzela, Tambau, Mvuha na Magazi hadi Kisaki:- (a) Je, Serikali itakuwa tayari kuwawekea wananchi hao utaratibu wa kuwajengea nyumba bora ili kuachana na utaratibu wa kuwalipa fidia kidogo isiyolingana na mali zao wanazoziacha? (b) Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza ili wananchi waliowekewa alama ya kubomolewa nyumba zao waanze maandalizi ya maeneo ya kuhamia? (c) Je, ni lini Serikali itatengeneza upya madaraja ya Ruvu, Mvuha na Dutuni yaliyomo kwenye barabara hiyo hasa ikizingatiwa kuwa madaraja hayo ni mabovu sana na yamedidimia na yanaweza kusababisha ajali kwa wanaopita hapo?

Supplementary Question 1

MHE. PROSPER J. MBENA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa barabara inayozungumzwa hapa kujengwa kwa kiwango cha lami ni Bigwa - Kisaki na siyo Bigwa - Mvuha ambayo ni sehemu tu ya barabara hii; na kwa kuwa Serikali inazungumzia ufinyu wa bajeti pamoja na kupatikana kwa fedha ndipo ujenzi kamili wa barabara hiyo uanze:-
Je, Serikali ipo tayari kuruhusu ujumbe wa wananchi wa Morogoro Vijijini ukiongozwa na Wabunge wao wa Jimbo la Morogoro Kusini na Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki ili waweze kwenda kumwona Mkuu wa Nchi na kufikisha kilio chao na ikiwezekana waweze kujua kwa nini wafadhali wa MCC II ambao walipangiwa kuutekeleza mradi huu wameuacha na sasa unawaadhibu wananchi wa sehemu hiyo? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa madaraja yaliyotajwa hapo hususan daraja la Ruvu, Mvuha pamoja na Dutuni yanahatarisha sana maisha ya wananchi wanaopita humo barabarani kwa kutumia madaraja hayo:-
Je, Serikali itafanya mara moja matengenezo ya haraka ya kuwawezesha wananchi kupita kwa usalama? Naomba kauli ya Serikali, ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Prosper Joseph Mbena, aliyekuwa Msaidizi wa Rais wa Awamu ya Nne, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kumwona Mheshimiwa Rais, nadhani anafahamu utaratibu kwamba anahitaji kuwasiliana na Viongozi wa Mkoa na kadiri Mkoa utakavyoona kutokana na hoja zitakazoongelewa hilo linaweza kufanyika. Kikubwa ninachomweleza, niliyomjibu hapa ni dhamira ya dhati za Serikali. Kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, barabara hii ya kutoka Bigwa hadi Kisaki, tutaijenga kwa kiwango cha lami kama tulivyoahidi katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Kama ambavyo Viongozi wetu Wakuu wakati wa kampeni na wakati wa misafara mbalimbali wameahidi, tutaitekeleza katika kipindi hiki cha miaka mitano na tunaanzia na nusu yake kutoka Bigwa -Mvuha. Tayari ma-consultant wanafanya kazi tarehe 30 Juni wanakamilisha na baada ya hapo tutaanza kutafuta fedha kujenga hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa swali lake la pili, ni kama nilivyojibu katika swali la msingi kwamba TANROADS Morogoro wataendelea kuyaimarisha madaraja hayo na kuyafanyia matengenezo ili yaweze kupitika kwa usalama wa wananchi wa maeneo hayo.

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:- Ujenzi wa barabara ya kutoka Bigwa - Kisaki upo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM na fedha za ujenzi zitatoka kwenye mpango wa MCC II au Serikalini na nyumba zote zilizomo ndani ya mita 60 zimewekwa alama „X’ tayari kubomolewa katika maeneo ya Ruvu, Kibangile, Kisemu, Mtamba, Nzasa, Kangazi, Kisanzela, Tambau, Mvuha na Magazi hadi Kisaki:- (a) Je, Serikali itakuwa tayari kuwawekea wananchi hao utaratibu wa kuwajengea nyumba bora ili kuachana na utaratibu wa kuwalipa fidia kidogo isiyolingana na mali zao wanazoziacha? (b) Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza ili wananchi waliowekewa alama ya kubomolewa nyumba zao waanze maandalizi ya maeneo ya kuhamia? (c) Je, ni lini Serikali itatengeneza upya madaraja ya Ruvu, Mvuha na Dutuni yaliyomo kwenye barabara hiyo hasa ikizingatiwa kuwa madaraja hayo ni mabovu sana na yamedidimia na yanaweza kusababisha ajali kwa wanaopita hapo?

Supplementary Question 2

MHE.DKT. PUNDECIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi nami niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali yetu ina lengo jema la kuunganisha barabara za mikoa ili kuharakisha maendeleo katika nchi yetu yote; na kwa kuwa ujenzi wa barabara nyingi umekuwa ukikumba nyumba nyingi zinazokuwa pembezoni mwa barabara ambazo zinawekewa „X’ kwa mfano, kutokea Ilalangulu kwangu kule mpaka Kasansa na fidia mara nyingi wanatathmini pale ambapo pesa zinakuwa hazijapatikana lakini pindi zinapopatikana wanakuja kuwalipa wananchi fidia ile ya mwanzo:-
Je, Serikali inasema nini kufikiria namna ya kutathimini upya fidia za wananchi mara ujenzi unapoanza?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Fidia ile ya zamani na hata ya sasa ya mwaka 1999 imeeleza wazi kwamba baada ya kufanyiwa tathmini na kama fidia itachelewa kulipwa kuna penalty zimewekwa. Kwa hiyo, malipo yanalipwa zaidi na kuna utaratibu, malipo yanaongezeka kwa kadri muda unavyoongezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani hiyo sheria tuliiweka kwa makusudi kabisa tukijua wakati mwingine uwezo wa Serikali wa kulipa kwa pamoja ni mdogo, maana miradi mingi inaihusu Serikali. Kwa hiyo, katika kuwafidia wale ambao wanacheleweshwa kulipa, kuna utaratibu huo wa kufanya mahesabu mapya kwa kuzingatia kipindi ambacho amecheleweshwa kulipwa. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge hili litatekelezwa pindi tutakapoanza kupata nguvu ya kulipa fidia katika eneo husika.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:- Ujenzi wa barabara ya kutoka Bigwa - Kisaki upo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM na fedha za ujenzi zitatoka kwenye mpango wa MCC II au Serikalini na nyumba zote zilizomo ndani ya mita 60 zimewekwa alama „X’ tayari kubomolewa katika maeneo ya Ruvu, Kibangile, Kisemu, Mtamba, Nzasa, Kangazi, Kisanzela, Tambau, Mvuha na Magazi hadi Kisaki:- (a) Je, Serikali itakuwa tayari kuwawekea wananchi hao utaratibu wa kuwajengea nyumba bora ili kuachana na utaratibu wa kuwalipa fidia kidogo isiyolingana na mali zao wanazoziacha? (b) Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza ili wananchi waliowekewa alama ya kubomolewa nyumba zao waanze maandalizi ya maeneo ya kuhamia? (c) Je, ni lini Serikali itatengeneza upya madaraja ya Ruvu, Mvuha na Dutuni yaliyomo kwenye barabara hiyo hasa ikizingatiwa kuwa madaraja hayo ni mabovu sana na yamedidimia na yanaweza kusababisha ajali kwa wanaopita hapo?

Supplementary Question 3

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nami naomba niulize swali la nyongeza ambalo linalingana kabisa na lile la Morogoro Vijijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara za kutoka Njombe – Mdandu - Iyayi na kutoka Njombe - Lupembe -Madeke, zilishafanyiwa upembuzi na usanifu miaka miwili, mitatu iliyopita:-
Je, ni lini sasa barabara hizi zitaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Sanga kama ilivyo kwa Mheshimiwa Prosper Mbena pamoja na Mheshimiwa Dkt. Kikwembe ni wafuatiliaji sana wa masuala haya ya barabara na fidia katika maeneo yao. Nawapongeza sana kwa hilo na nawaomba waendelee na juhudi hizo kwa sababu kwa kufanya hivyo wanatuunga mkono sisi tulio katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ambayo dhamira yetu pekee ni kuwajengea wananchi miundombinu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ambazo ameziongelea Mheshimiwa Sanga katika bajeti ambayo wameshaipitisha kuna mafungu ambayo yametengwa kwa ajili ya kuanza kujengwa kwa lami. Namhakikishia Mheshimiwa Sanga kwamba katika zile fedha zilizotengwa katika barabara hizo mbili, ikiwa na ile ya kwenda Madeke na hii ya kwenda Iyayi tutazisimamia kuhakikisha zinaanza kutumika kujenga barabara hizo kwa kiwango cha lami kama ambavyo viongozi wetu wa kitaifa waliahidi.

Name

Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:- Ujenzi wa barabara ya kutoka Bigwa - Kisaki upo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM na fedha za ujenzi zitatoka kwenye mpango wa MCC II au Serikalini na nyumba zote zilizomo ndani ya mita 60 zimewekwa alama „X’ tayari kubomolewa katika maeneo ya Ruvu, Kibangile, Kisemu, Mtamba, Nzasa, Kangazi, Kisanzela, Tambau, Mvuha na Magazi hadi Kisaki:- (a) Je, Serikali itakuwa tayari kuwawekea wananchi hao utaratibu wa kuwajengea nyumba bora ili kuachana na utaratibu wa kuwalipa fidia kidogo isiyolingana na mali zao wanazoziacha? (b) Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza ili wananchi waliowekewa alama ya kubomolewa nyumba zao waanze maandalizi ya maeneo ya kuhamia? (c) Je, ni lini Serikali itatengeneza upya madaraja ya Ruvu, Mvuha na Dutuni yaliyomo kwenye barabara hiyo hasa ikizingatiwa kuwa madaraja hayo ni mabovu sana na yamedidimia na yanaweza kusababisha ajali kwa wanaopita hapo?

Supplementary Question 4

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii nami niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Manyoni kuna barabara ya kutoka Manyoni kwenda Sanza. Tatizo la Mto Sanza ni sawa kabisa na tatizo lililoko kule Morogoro Kusini. Daraja hili ni kubwa, linaunganisha Manyoni na Dodoma kwa jirani yangu Mheshimwa Badwel. Daraja hili lilijengwa mwaka 2014 na kukamilika lakini mwaka 2015 mvua iliponyesha likabomoka na sina mawasiliano na jirani yangu hasa wakati mvua zikinyesha:-
Je, ni lini Serikali itatujengea daraja hili?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge ambaye ni kati ya Wabunge wa Mkoa wa Singida walio…
MHE. DANIEL E. MTUKA: Manyoni Mashariki.
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Wa Mkoa wa Singida, Jimbo la Manyoni Mashariki ambaye ni makini kama walivyo Wabunge wengine katika kufuatilia masuala ya wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nami kwa kweli nichukue nafasi hii kumpongeza kwa kazi kubwa anayoifanya ya kufuatilia mahitaji ya wananchi wa Manyoni Mashariki. Kwa kweli huwa anaenda mbali zaidi, anafika hata maeneo ya Bahi yale ambayo yanaungana na maeneo yake na Manyoni Magharibi, yeye pamoja na Mheshimiwa Mama Mlata. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana na kwa kweli nawapongeza sana kwa juhudi hizi zote wanazozifanya. Nawaombeni muendelee kutuunga mkono katika dhamira yetu ya kuwajengea Watanzania miundombinu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, hivi ninavyoongea CEO wa TANROADS Taifa, Ndugu Patrick Mfugale, ananisikia na atahakikisha anawasiliana na wasaidizi wake wa mikoa hii miwili; Dodoma na Singida ili waweze kuangalia hili eneo ambalo kwa taarifa ya Mheshimiwa Mbunge mawasiliano yamekatika. Nilisema kwamba baada ya mvua kukatika, mkazo wetu mkubwa kwa sasa ni kurudisha mawasiliano katika maeneo yale yaliyokatika. Kwa hiyo, eneo hili ni mojawapo kama ambavyo amelisema; hao viongozi wa TANROADS nawataka walishughulikie haraka sana ili warudishe mawasiliano na wananchi waendelee kupata huduma za usafiri.