Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Barabara inayounganisha vijiji vya Msanga na Kawawa ni muhimu sana kiuchumi kwa kata ya Msanga na Wilaya ya Chamwino na pia kuna mazao mengi ya uhakika kutoka Kawawa na vitongoji vyake, lakini barabara hiyo ni korofi sana kwa sababu ya mbuga iliyoko kati ya vijiji hivyo viwili na zaidi, daraja kubwa lililopo limevunjika kabisa kiasi kwamba halipitiki kabisa wakati wa mvua na wakati wa kiangazi hupitika kwa taabu sana. Je, Serikali ina mpango gani wa kurekebisha barabara hiyo na kulijenga daraja husika ili kuboresha mawasiliano ya vijiji hivi viwili na masuala ya usafirishaji?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa Jimbo la Chilonwa na Jimbo la Mpwapwa yanapakana, na kwa kuwa matatizo ya barabara ya Jimbo la Chilonwa ni sawa kabisa na matatizo ya Jimbo la Mpwapwa, Kibakwe na Kongwa.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri utatusaidiaje wananchi wa Jimbo la Mpwapwa kuhusu barabara ya kutoka Lupeta - Bumila - Makutupa kwenda Mbori - Mang‟weta - Mlali mpaka Pandambili. Barabara hii iko chini ya TANROADS, lakini ni muda mrefu sasa haijatengenezwa, pamoja na barabara ya Mkanana – Majami pamoja na Nana. Nakuomba Mheshimiwa Naibu Waziri Serikali itoe tamko kuhusu barabara hii, ni lini itaanza kuzikarabati?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema wiki iliyopita kwamba greda ni la zamani lakini makali yale yale.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii anayosemea Mheshimiwa Mbunge ni kwamba ukitoka huku baada ya kuvuka Kibaigwa unafika sehemu inaitwa Pandambili, unapita ile barabara ambayo ni ndefu sana, inapita Mlali, inapita Cha Mkoroma, inapita Makutupa, katikati inapitia Mang‟weta mpaka unafika pale Mpwapwa Mjini ni barabara ndefu kwa kweli. Kijiografia ni barabara ambayo watu hawa zamani walikuwa wakipitia barabara ya Kibaigwa kuzunguka huku walikuwa na tatizo kubwa sana, kufunguka kwa barabara ile kwa kiwango kikubwa imesaidia sana watu wa eneo hilo. Barabara ile takribani mwezi uliopita niliipita mimi mwenyewe kwa gari yangu, nimeiona na kiufasaha ni kwamba ukiangalia katika vitabu yenyewe imejiainisha katika barabara za TANROADS kwamba ni miongoni mwa barabara zitakazofanyiwa matengenezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu kubwa ni kwamba Mheshimiwa Lubeleje, barabara hiyo itaendelea kutengezwa ili watu wa maeneo yale ambao najua suala zima la uchumi wa eneo lile unakua kutokana na ujenzi wa barabara ile, basi naamini kabisa Serikali kwa sababu imetenga katika bajeti ya mwaka huu wa fedha ukarabati wa barabara ile, ukarabati huo utaendelea kufanyika kama ilivyokusudiwa.

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Barabara inayounganisha vijiji vya Msanga na Kawawa ni muhimu sana kiuchumi kwa kata ya Msanga na Wilaya ya Chamwino na pia kuna mazao mengi ya uhakika kutoka Kawawa na vitongoji vyake, lakini barabara hiyo ni korofi sana kwa sababu ya mbuga iliyoko kati ya vijiji hivyo viwili na zaidi, daraja kubwa lililopo limevunjika kabisa kiasi kwamba halipitiki kabisa wakati wa mvua na wakati wa kiangazi hupitika kwa taabu sana. Je, Serikali ina mpango gani wa kurekebisha barabara hiyo na kulijenga daraja husika ili kuboresha mawasiliano ya vijiji hivi viwili na masuala ya usafirishaji?

Supplementary Question 2

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kama ilivyo kwenye vijiji vya Msanga, Kawawa na kadhalika katika Jimbo la Chilonwa, ndivyo ilivyo katika Wilaya ya Mkalama kwenye kata ya Msingi pamoja na kata ya Kinyangiri, vijiji vya Ishinsi pamoja na Kidi na Lelembo, vijiji hivi mvua inaponyesha vinakuwa ni kama kisiwa kwa sababu vimezungukwa na mito ambayo haina madaraja, hivyo wagonjwa wanapougua wakibebwa kwenye machela hawawezi kuvuka na matokeo yake wengine wanaweza wakapoteza maisha.
Je, Serikali inasemaje kuhusu kuwawekea madaraja ya kuvuka wakati wote vijiji hivi nilivyovitaja? Ahsante

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kwamba kwanza tumelipokea ombi hili, bahati nzuri ni kwamba siku ya tarehe 25 Juni, Mbunge wa Mkalama amenialika kwenda Jimboni kwake kwa ajili ya kukabidhi madawati.
Mheshimiwa Naibu Spika, hii maana yake ninazungumza ni Jumamosi hii inayokuja, nitakapofika kule Mkalama, miongoni mwa maeneo ya kuyatembelea baada ya kuhakikisha tunazindua baadhi ya ile miradi ambayo Mbunge amekusudia ikiwepo madawati na mambo mengine, lakini tutakwenda kutembelea maeneo haya ikiwezekana tuweze kubaini nini kinatakiwa kifanyike ili wananchi wa Jimbo la Mkalama waendelee kupata huduma.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Barabara inayounganisha vijiji vya Msanga na Kawawa ni muhimu sana kiuchumi kwa kata ya Msanga na Wilaya ya Chamwino na pia kuna mazao mengi ya uhakika kutoka Kawawa na vitongoji vyake, lakini barabara hiyo ni korofi sana kwa sababu ya mbuga iliyoko kati ya vijiji hivyo viwili na zaidi, daraja kubwa lililopo limevunjika kabisa kiasi kwamba halipitiki kabisa wakati wa mvua na wakati wa kiangazi hupitika kwa taabu sana. Je, Serikali ina mpango gani wa kurekebisha barabara hiyo na kulijenga daraja husika ili kuboresha mawasiliano ya vijiji hivi viwili na masuala ya usafirishaji?

Supplementary Question 3

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nataka kuuliza swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa Wizara ya TAMISEMI pamoja na Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano ni Wizara ambazo zinashabihiana katika utekelezaji kwenye maeneo ya Wilaya yetu; na kwa kuwa kuna baadhi ya maeneo ambayo hakuna barabara wala hakuna mawasiliano. Kwa mfano, Kata ya Mahenge katika Kijiji cha Ilindi Namagana, Kata ya Ruaha Mbuyuni katika Kijiji cha Ikula na Kata ya Nyanzwa katika Kijiji cha Nyanzwa hakuna mawasiliano, hakuna barabara, sasa Serikali inasemaje kuboresha maeneo hayo ili wale wananchi nao wahisi kwamba wapo Tanzania?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, analozungumzia Mheshimiwa Mwamoto ni jambo la msingi, na kama Serikali naomba niseme kwamba ni haki ya Serikali kusikiliza kwanza, nikijua kwamba ujenzi wa barabara una vipaumbele vyake kutokana na Sera za Barabara.
Mheshimiwa Naibu Spika, watu wengine wanaweza wakashangaa kwa nini barabara kutoka Airport kila wakati inakarabatiwa ni kwa sababu barabara ikiwa bora lazima ikarabatiwe kwanza, lakini barabara ikiwa korofi inawekwa kipaumbele cha mwisho.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ambayo haijafunguliwa maana yake inakuwa kipaumbele cha mwisho kabisa. Kwa hiyo jambo la msingi ukiangalia hata Mfuko wa Barabara maana yake hautoelekeza katika kufungua hizo barabara mpya. Ni lazima tubuni mipango mikakati mingine jinsi gani tutafungua barabara hii.
Mheshimiwa Mwamoto najua kwamba tarehe 18 Julai, nitakuwa Jimboni kwako kutembelea, naomba tufike maeneo hayo tubainishe kwa pamoja. Katika ziara yangu naanzia Mkoa wa Iringa katika Jimbo la Kilolo, tutakaa pamoja kama nilivyokuahidi, tutatembelea kubaini nini tufanye kwa pamoja, ni mkakati gani tutafanya ili wananchi wa maeneo hayo waweze kupata huduma inayokusudiwa, na kwamba wakiri kwamba Mwamoto aliyekuwa DC sasa ni Mheshimiwa Mbunge katika Jimbo la Kilolo anafanyakazi.