Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Hospitali ya Kibena inakabiliwa na uchakavu pamoja na upungufu wa madawa:- Je, Serikali itakarabati hospitali hiyo pamaja na tatizo la upungufu wa dawa?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri na naipongeza pia Serikali kwa kutambua umuhimu wa kuipandisha hadhi Hospitali ya Kibena kuwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.
Swali langu la nyongeza, Mheshimiwa Naibu Waziri, Serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa kujenga Hospitali ya Wilaya mpya ndani ya Wilaya ya Wanging‟ombe, ukizingatia kwamba Wilaya hii ni mpya na iko ndani ya Mkoa mpya?
Vilevile swali la pili la nyongeza, Serikali haioni kwamba tatizo la ukosefu wa madawa na uchakavu wa majengo ya Hospitali lipo pia katika Wilaya ya Ludewa na lini Serikali itatafutia ufumbuzi suala hilo.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, hoja ya Mheshimiwa Mbunge ni kwamba Hospitali ile ilikuwa ya Wilaya ya Njombe, sasa maana yake itaenda kupandishwa kuwa hospitali ya Mkoa, watakuwa hawana hospitali ya Wilaya, hiyo ndiyo hoja ya Mheshimiwa Mbunge. Naomba tulichukue hili, kwanza, kwa sababu matatizo makubwa ya hospitali hii hivi sasa ya Kibena imekuwa ni kwa sababu mwanzo ilikuwa ni hospitali ya Wilaya na kwa vile ni hospitali ya Wilaya hata ule mgao wake unaenda kiwilaya Wilaya, ndiyo maana Serikali imeona sasa ni vema hospitali hii kuipandisha daraja kuwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa.
Mheshimiwa Spika, kitendo cha kuifanya kuwa hospitali ya Mkoa, maana hata catchment area yake inakuwa tofauti na hivi sasa ilivyo. Maana yake ni nini, wananchi wa Mkoa wa Njombe watakuwa na fursa kubwa ya kupata matibabu mazuri zaidi kulinganisha na pale mwanzo.
Mheshimiwa Spika, kwa nini sasa tusihakikishe tunajenga hospitali ya Wilaya nyingine mpya, hili kama Ofisi ya TAMISEMI kwa kushirikiana na halmashauri husikia tutafanya hiyo kazi. Naomba niseme kwamba hapa sasa hivi ukiangalia hata kwa ndani kuna mgogoro, ukiangalia wale wanaosema kwamba hii hospitali yetu ikiwa ya Mkoa tutakuwa hatuna hospitali ya Wilaya. Nadhani sasa hivi tushikamane kwa pamoja tupate Hospitali ya Mkoa, mikakati mingine mipana iende katika suala zima la upataji wa hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Spika, naomba nilichukue hili Suala la Ludewa kwa sababu yote ni maeneo ambayo yanatakiwa yatafanyiwa kazi na wewe najua ni Mbunge wa Viti maalum wa Mkoa wa Njombe tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo. Mkoa wa Njombe ni Mkoa mpya, wananchi wake waweze kunufaika na huduma za afya ya Serikali yao, asante sana.