Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafufua Shule za Msingi za Ufundi Wilayani Hai na kurejesha mfumo wa wanafunzi kufanya mitihani na kupewa vyeti?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshiiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali.

Mheshimiwa Spika, swali hili niliwahi kuuliza likiwa linafanana hivi kwenye maswali ya papo kwa papo kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Majibu yaliyotolewa na Serikali na haya yanayotolewa sasa hivi yanapishana. Sasa napenda kufahamu msimamo wa Serikali kuhusu shule hizi, kwa mfano shule ya Mshara, Sare na Mroma. Shule hizi zina majengo, vifaa na walimu: Je, Serikali inatoa msimamo gani kuhusiana na shule hizo?

Swali la pili; Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha Ufundi VETA ndani ya Jimbo la Hai ilhali tayari tumeshapanga eneo maalum kwa ajili ya ujenzi wa chuo hiki? (Makofi)

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Saashisha, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tuna shule za msingi 123 hapa nchini ambazo zilikuwa zinatakiwa zitoe mafunzo ya ufundi pamoja na elimu ya msingi, lakini shule zote hizo sasa hivi hazitoi mafunzo hayo kwa sababu ya uhaba wa walimu. Vyuo ambavyo vilikuwa vinatoa mafunzo kwa mfano Chuo cha Ualimu cha Mtwara ambacho kazi yake kubwa ilikuwa ni kuwafundisha walimu elimu ya ufundi kwa ajili ya shule za msingi, imeacha kufanya kazi hiyo kwa sasa hivi.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza katika kujibu swali la msingi, sasa hivi tunapitia mitaala yote ya shule za msingi, sekondari na vyuo vya ufundi na lengo lake kubwa ni kuhakikisha kwamba tunaingiza ufundi na ujuzi katika shule zote ikiwa ni pamoja na hizi shule 123 na hizi shule za Jimbo la Hai kama alivyoeleza Mheshimiwa Saashisha. Tunatarajia kwamba tutamaliza shule za mitaala mwisho wa mwaka huu, hivyo tutaweza kuanza sasa kuhakikisha kwamba tunafundisha wanafunzi katika ngazi zote hizo.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu VETA, ni nia ya Serikali kuhakikisha kwamba tunajenga vyuo vya VETA kila Wilaya hapa nchini na juhudi hizo zinaendelea. Kwa yale maeneo ambayo tayari Wilaya zimeshatenga maeneo na hasa maeneo yale ambayo Wilaya na Halmashauri na Wabunge wameanza juhudi za kukusanya fedha kwa ajili ya ujenzi, tutajitahidi kuhakikisha kwamba tunaenda kuongeza nguvu za Serikali ili kukamilisha azma hii ya kuwa na VETA katika kila Wilaya ikiwa ni pamoja na Jimbo la Hai kwa Mheshimiwa Saashisha.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafufua Shule za Msingi za Ufundi Wilayani Hai na kurejesha mfumo wa wanafunzi kufanya mitihani na kupewa vyeti?

Supplementary Question 2

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Swali langu ni: Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba tunashirikiana na nchi nyingine ambazo zimeendelea katika sekta hii ya ufundi stadi hasa kwa masuala ya Exchange Program kuwapeleka watoto wetu Internship ili waweze kujifunza zaidi ufundi?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nashukuru sana kwa swali la Mheshimiwa Jesca kwa sababu pamoja na swali alilouliza hapa, tunafanya jitihada pamoja kuhakikisha kwamba tunaunganisha nguvu kupeleka vijana kwenda kusoma nchi za nje ikiwa ni pamoja na nchi ya Uturuki ambapo wameendelea vizuri sana katika masuala ya ufundi stadi na elimu ya ufundi.

Mheshimiwa Spika, Serikali inakusudia kuhakikisha kwamba tunaanzisha taratibu kwanza za kuwa na staff exchange ya walimu wetu wa ufundi kwenda nchi nyingine kuangalia wanafundishwa vipi na kuleta walimu kutoka nje kuja kukaa kwa muda katika vyuo vyetu ili kuboresha elimu ya ufundi. Vile vile kupeleka wanafunzi wetu katika nchi ambazo zimeendelea vizuri zaidi katika elimu za ufundi ikiwa ni pamoja na Uturuki. Namwahidi Mheshimiwa Jesca kwamba jitihada ambazo ameshazianza tutazifanya pamoja mpaka tutazikamilisha. Ahsante sana.