Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Kila Mtanzania ana haki ya kupata habari wakiwamo wananchi wa Itigi. Je, kwa nini wananchi wa Itigi na maeneo ya jirani wananyimwa haki ya msingi kutokana na Kituo cha Redio Mwangaza kuzuia masafa ya redio nyingine ikiwemo Redio ya Taifa TBC na TBC FM?

Supplementary Question 1

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa ni haki ya kila mwananchi hasa Mtanzania kupitia kodi zao kusikiliza redio ya Taifa hasa TBC. Je, ni lini Serikali sasa itaweka booster yake ya TBC katika Mji Mdogo wa Itigi ili na wananchi wale wasikie redio yao ya Taifa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuambatana na mimi kwenye gari yake yenye redio nzuri ili atakapofika Itigi asikie matatizo yaliyoko pale?

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba usikivu wa redio hasa Redio ya Taifa pale Itigi siyo mzuri lakini hii imetokana na mabadiliko ya teknolojia kutoka Mediam Waves (MW) kwenda FM. TBC kwa sasa inamalizia zoezi la kufanya uchambuzi wa kuangalia mahali ambapo tunatakiwa kuweka booster na maeneo mengine tunalazimika kupeleka mtambo. Sasa ni lini usikivu utaboreka, ni pale utaratibu huu wa kufanya uchambuzi utakapokamilika na ni hivi karibuni kwa sababu tupo mwishoni kabisa, upembuzi ukimalizika tutaamua sasa Itigi tunaweka mtambo au booster.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, mimi kama Waziri wa Habari nipo tayari kuambatana naye na yeye anajua kwamba Singida ni nyumbani kwetu. Najua usikivu pale ni mbovu ndiyo maana tunafanya kila liwezekanalo kazi hii ikamilike mapema tuweze kuongeza usikivu wa Redio ya Taifa kwenye eneo la Mheshimiwa Mbunge.

Name

Savelina Slivanus Mwijage

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Kila Mtanzania ana haki ya kupata habari wakiwamo wananchi wa Itigi. Je, kwa nini wananchi wa Itigi na maeneo ya jirani wananyimwa haki ya msingi kutokana na Kituo cha Redio Mwangaza kuzuia masafa ya redio nyingine ikiwemo Redio ya Taifa TBC na TBC FM?

Supplementary Question 2

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa matatizo ya Itigi ni sawasawa na matatizo ya Wilaya ya Biharamulo hasa msitu tunaokatisha wa Kasindaga Muleba una matatizo ya mawasiliano na pale kuna barrier nyingi za maaskari ambao wanakaa pale saa zote. Ni lini Serikali itaweza kuwawekea mawasiliano pale hata mnara mmoja angalau wa Tigo au Vodacom?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASIALINO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka huu wa fedha wa 2016/2017 Serikali ina mpango wa kupeleka mawasiliano maeneo yote ambayo yana matatizo ya mawasiliano. Moja kati ya eneo hilo ni hilo alilosema Mheshimiwa Mbunge.