Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata ya Mwabuki?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana Mheshimiwa kwa majibu mazuri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, moja, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata za Mtambula, Luhunga na Mninga kule Mufindi Kusini?

Mheshimiwa Spika, pili, ni lini Serikali itakamilisha miradi ya maji ya Malangali, Nambalamaziwa na Igohole ambayo tayari Serikali imeshaanza kutenga fedha?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kihenzile, Mbunge wa Mufindi Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, la kwanza, Serikali imejipanga hivi sasa katika kata zile tatu alizozitaja inafanya utafiti wa kupata vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Spika, la pili, tayari taratibu za manunuzi zimekwisha kukamilika na mnano mwezi Desemba utekelezaji wa mradi utaanza.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata ya Mwabuki?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Miradi mingi ya maji ikiwemo ya Jimbo la Ukerewe inasuasua kukamilika kwa sababu ya mchakato mrefu wa kupata msamaha wa kodi. Nini mkakati wa Serikali kupunguza urasimu kwenye kupata misamaha ya kodi ili miradi hii ya maji iweze kukamilika haraka? Nashukuru. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Mkundi, Mbunge wa Ukerewe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli na hivi sasa Serikali inaendelea na jitihada, Wizara ya Maji kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha kufanya utaratibu wa kuhakikisha kwamba misamaha yote ya kodi inayohusu sekta ya maji iweze kupitiwa na kupatikana suluhu mapema ili kuweza kuwanufaisha wananchi.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata ya Mwabuki?

Supplementary Question 3

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi, mkakati wa kutoa maji Ziwa Tanganyika ni mkakati wa muda mrefu. Nataka kujua mkakati wa muda mfupi wa kuwasaidia zile kata tano za Wilaya ya Nkasi, Kata ya Namanyele, Nkomoro, Majengo pamoja na Isunta kuepusha hiki kipindi ambacho wanakipitia kigumu?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge wa Nkasi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, jumla ya fedha shilingi bilioni 657 zimetengwa na iko miradi 381 mipya. Ninayo imani kwamba katika hii miradi 381, miradi hii ya Nkasi ni miongoni mwao. Kwa hiyo, Mheshimiwa Aida uendelee kufuatilia katika kuhakikisha kuwa wananchi wa Nkasi na wenyewe wanapata faida hii ya maji safi na salama.