Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SHEKIBOKO K.n.y. MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kurasimisha vijana waliopata ujuzi nje ya mfumo rasmi?

Supplementary Question 1

MHE. HUSNA J. SHEKIBOKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, vijana hawa ambao ni mafundi, wamekuwa wakikosa kazi kwenye maeneo tofauti tofauti kwa kigezo cha kukosa cheti, na wale ambao wana vyeti wamekuwa wakichukua hizi kazi na kuwa kama madalali, kazi hizi zinakuwa zinatekelezwa na hawa ambao hawana vyeti.

Je, Serikali haioni sasa umuhimu wa kurasimisha kwa kuwapa vyeti hawa mafundi ujenzi, mafundi seremala, mafundi cherehani ili waweze kuajiriwa katika maeneo mbalimbali?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, pale Lukozi, Wilaya ya Lushoto kuna vijana ambao wanatengeneza maji ya betri kwa ajili ya magari na pikipiki. Lakini jambo hili limezungumzwa mara kadhaa ndani ya Bunge hili lakini bado vijana wale hawajapatiwa namna ya kurasimishwa na kutambulika kama kibaji kipya katika Taifa letu.

Je, Naibu Waziri yupo tayari sasa kutembelea vijana wale na kuwarasimisha?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (MHE. PATROBAS P. KATAMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Husna kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika utoaji wa mafunzo haya ya urasimishaji ujuzi, unaenda sambamba na utoaji wa vyeti pia vya mafunzo ili waweze kutambulika na zaidi ya hapo Serikali ya Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, tunaenda hatua mbali zaidi hao vijana wanaomaliza vyuo vikuu na kurasimishiwa ujuzi, mbali na kuwapa vyeti, tunawakutanisha na halmashauri ili waweze kupewa fedha kwa ajili ya kuanza kama start-up capital katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwapeleka maeneo ya practical placement kwa maana ya sehemu ambazo wanaweza wakajifunza kufanya kazi, lakini pia kuajiriwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunaenda sambamba kwa sehemu kubwa zaidi ya 1,800 wamekwishakupata kazi kwa fedha zilizotolewa mwaka jana wa fedha shilingi bilioni tisa na Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili, nakubaliana naye kwamba nitawatembelea vijana hao na hata wengine walioko nchini kama wana ujuzi na maarifa makubwa kama hayo wanayoyafanya, Ofisi ya Waziri Mkuu iko wazi muda wote kuweza kuwahudumia, tuendelee kupata taarifa lakini tunaendelea kuwatambua na kuwahudumia, lakini kuweza kuhakikisha tunawasaidia. Ahsante.