Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Katika Halmashauri ya Mbeya kuna mradi wa uchimbaji wa madini unaotarajiwa kuanza kwenye eneo la Mlima Songwe, lakini pia kuna mradi mwingine mkubwa wa joto ardhi kwenye Kata za Swaya, Ijombe na Bonde la Songwe. (a)Je, kwa nini Serikali Kuu haihusishi Halmashauri ya Mbeya katika mradi hiyo ili elimu iweze kutolewa kwa wananchi? (b)Je, wananchi wa Jimbo la Mbeya Vijijini watanufaika vipi na miradi hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana Mwenyekiti, na pia nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini nina maswali madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mradi wa haya madini adimu duniani pamoja na joto ardhi ni muhimu sana kwa uchumi wa viwanda, naomba commitment ya Serikali, moja, je, ni lini wataanza uchimbaji wa joto ardhi ili tuweze kutumia kwenye viwanda vyetu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, na pili, naomba pia commitment ya Serikali pamoja na mradi wa Ziwa Ngozi, je, Serikali imetoa leseni ngapi za uchimbaji na uzalishaji wa madini na nishati ya joto ardhi katika sehemu zingine hapa kwetu Tanzania? Ahsante.

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Answer

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya ni lini tunaanza, utafiti umeshafanyika, unaonesha kwamba ili upate umeme wa joto ardhi unahitaji kuwa na temperature ambayo iko katikati ya nyuzi 180 mpaka 240 celsius. Sasa bahati nzuri hii ya Ngozi iko zaidi ya 240. Kwa hiyo, kinachofuata sasa kwa miezi michache ni kwamba inabidi tuchoronge miamba pale chini tuweze kujua kuna mvuke kiasi gani ambao utaendesha mashine ya kuzalisha umeme wa kiasi gani. Kwa hiyo, tutatoa hiyo tarehe baada ya kujua tuna mvuke wa chini kiasi gani yaani steam.
Mheshimiwa MWenyekiti, na leseni ngapi zimetolewa, ni kwamba tumeshatengeneza ramani ya nchi nzima ambayo inaonesha maeneo yote ambayo tunaweza kuendeleza joto ardhi. Kwa sasa hivi ukiacha ya Ngozi, Mbeya eneo lingine ni la Luhoi kilometa kama 70 Kusini Mashariki mwa Dar es Salaam, halafu na lingine liko sehemu za Kusini mwa Morogoro na Ziwa Natroni kwa hiyo maeneo ni mengi lakini tunaenda hatua kwa hatua.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Katika Halmashauri ya Mbeya kuna mradi wa uchimbaji wa madini unaotarajiwa kuanza kwenye eneo la Mlima Songwe, lakini pia kuna mradi mwingine mkubwa wa joto ardhi kwenye Kata za Swaya, Ijombe na Bonde la Songwe. (a)Je, kwa nini Serikali Kuu haihusishi Halmashauri ya Mbeya katika mradi hiyo ili elimu iweze kutolewa kwa wananchi? (b)Je, wananchi wa Jimbo la Mbeya Vijijini watanufaika vipi na miradi hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. SHABANI O. SHELIKINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa suala la umeme wa REA ni suala la Kitaifa, je, ni lini Serikali itawapatia umeme wananchi wa Makanya, Ngwelo, Kwemashai, Gare na maeneo yote yaliyoba katika Jimbo la Lushoto?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo ya Makanya pamoja na Ngwelo ambayo yalizungumzwa na Mheshimiwa Mbunge ambayo kwa sasa hayajapata umeme, taratibu zinazofanyika sasa ni kukamilisha upatikanaji wa umeme kwenye maeneo ya REA Awamu ya Pili na maeneo aliyoyasema Mheshimiwa Mbunge, maeneo matatu kwa sasa yameshawekwa kwenye orodha ya maeneo ambayo yatapatiwa umeme kwenye REA Awamu ya Tatu inayoanza mwezi Julai mwaka huu.

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Katika Halmashauri ya Mbeya kuna mradi wa uchimbaji wa madini unaotarajiwa kuanza kwenye eneo la Mlima Songwe, lakini pia kuna mradi mwingine mkubwa wa joto ardhi kwenye Kata za Swaya, Ijombe na Bonde la Songwe. (a)Je, kwa nini Serikali Kuu haihusishi Halmashauri ya Mbeya katika mradi hiyo ili elimu iweze kutolewa kwa wananchi? (b)Je, wananchi wa Jimbo la Mbeya Vijijini watanufaika vipi na miradi hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHARLES J. TIZEBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru pia kwa kuniona.
Suala la umeme katika vijiji vingi hapa nchini bado halijawekwa wazi kuhusiana na maeneo ya visiwa. Jimbo langu tu kwa mfano linavyo visiwa 25. Nisizungumzie Jimbo la Mheshimiwa Mwijage huko Gozba, Bumbire na maeneo mengine.
Sasa mimi ningependa tu Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini labda atuambie ni kwa namna gani Wizara au Serikali kwa ujumla imejipanga kufikisha umeme katika maeneo haya ambayo kimsingi si rahisi sana kufikisha umeme wa Gridi ya Taifa?

Name

Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Answer

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli kwamba visiwa vyetu vinahitaji kupata umeme na cha kwanza vilivyopata umeme ni visiwa vya Zanzibar ambapo tumejenga cable chini ya bahari. Wao wana megawati 100 lakini mahitaji ya Zanzibar ni megawati 50, kwa hiyo wanayo 50 zaidi. Na Mheshimiwa Tizeba yeye mwenyewe anafahamu kisiwa cha kwanza kabisa katika Ziwa Victoria kupata umeme ni kisiwa chake ambacho kwa mara ya kwanza tumepitisha cable chini ya Ziwa Victoria, na tumemuomba Waziri Mkuu akazindue huo umeme kwa sababu ni wa kipekee kabisa. Na hivi sasa Kisiwa cha Ukara vilevile wamepatiwa umeme na ni mtu binafsi aliyewekeza umeme pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti na Wabunge wote ni kwamba hivi visiwa vingi vidogo vidogo hatutaweza kujenga cable kwa kila kisiwa, ila umeme watakaoupata ni umeme wa jua.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Katika Halmashauri ya Mbeya kuna mradi wa uchimbaji wa madini unaotarajiwa kuanza kwenye eneo la Mlima Songwe, lakini pia kuna mradi mwingine mkubwa wa joto ardhi kwenye Kata za Swaya, Ijombe na Bonde la Songwe. (a)Je, kwa nini Serikali Kuu haihusishi Halmashauri ya Mbeya katika mradi hiyo ili elimu iweze kutolewa kwa wananchi? (b)Je, wananchi wa Jimbo la Mbeya Vijijini watanufaika vipi na miradi hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri kuhusu mpango wa umeme vijijini. Mimi nina kata 15 lakini nina kata tatu ambazo zimepata umeme na ni vijiji vitatu vimepata umeme, je, Kata zifuatazo zitapata umeme katika mpango huu? Kata ya Bukwimba, Nyugwa, Busolwa, Shabaka, Nyijundu, Nyabulanda, Kafita, Kakola, Mwingilo, Kaboha, Nyabulanda na Izunya, je, serikali katika mpango wake wa mwaka huu tutapata umeme katika Jimbo la Nyang’hwale Kata zote hizo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa katika Jimbo la Nyang’hwale ni kata tatu tu ambazo zimepata umeme kwa mpango wa REA Awamu ya Pili, lakini REA Awamu ya Tatu pamoja na tathmini inayofanyika sasa katika REA Awamu ya Pili, vijiji vyote na kata zote zilizobaki za Nyang’hwale pamoja na vijiji alivyovitamka vimeingizwa kwenye mpango wa REA unaoendelea utakaonza mwezi Julai mwaka huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kadhalika kama nilivyosema bado TANESCO wanaendelea na kazi za kuunganisha umeme katika maeneo yote na maeneo ya Nyang’hwale ambayo hayatapitiwa yataingizwa kwenye mpango wa TANESCO ili vijiji vyote na kata zote za Nyang’hwale zipate umeme mwaka 2017/2018.

Name

Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Katika Halmashauri ya Mbeya kuna mradi wa uchimbaji wa madini unaotarajiwa kuanza kwenye eneo la Mlima Songwe, lakini pia kuna mradi mwingine mkubwa wa joto ardhi kwenye Kata za Swaya, Ijombe na Bonde la Songwe. (a)Je, kwa nini Serikali Kuu haihusishi Halmashauri ya Mbeya katika mradi hiyo ili elimu iweze kutolewa kwa wananchi? (b)Je, wananchi wa Jimbo la Mbeya Vijijini watanufaika vipi na miradi hiyo?

Supplementary Question 5

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona.Ningependa kupata jibu, kwakuwa masuala ya madini hasa yale ambayo si ya kawaida yapo hata katika Mkoa wa Songwe; tuna migodi ya marumaru hususan Mbozi, Ileje, Chunya, yote haya bado hayajaendelezwa kwa kiasi ambacho yangeweza kuleta tija, je, Wizara ya Nishati na Madini itafanya lini utafiti wa kuja kutuletea na sisi uchimbaji wa migodi hii kwa sababu ina faida sana. Badala ya kuagiza tiles nje tungeweza kutumia za kwetu na ubora wake ni mzuri kuliko ule wa nje?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile, je, mgodi wa Kiwira ambao uko Ileje na haujawahi kuifaidia Ileje utazinduliwa lini? Ahsante sana

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa katika Mkoa wa Mbeya pamoja na maeneo ya Songwe na Ileje kuna madini ya aina nyingi sana mbali na dhahabu. Na madini mengi yaliyoko katika maeneo yale ni madini ya viwandani. Kama nilivyosema kwenye swali langu la msingi, madini ya niobium yanapatikana kwenye Mkoa wa Mbeya na hasa kwenye maeneo ya Songwe karibu na Gereza la Songwe. Madini haya ya niobium ni adimu sana, na ni madini ya kwanza kupatikana kwa Tanzania na Afrika Mashariki. Kama nilivyosema madini haya yatatumika sana kwa shughuli za viwandani na hasa baadaye kwa kutengeneza computer, engine za ndege pamoja na rocket,, kwa hiyo ni madini ambayo yanapatikana sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti niongeze tu, kwamba sasa madini mengine yaliyoko pale utafiti unafanyika. Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) linaendelea na kufanya utafiti ili kubaini madini mengine ambayo yanapatikana kwenye maeneo ya Songwe, Mbeya Vijijini pamoja na Ileje ili na yenyewe yaweze kuchimbwa kwa faida.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nije sasa kwenye mgodi wa Kiwira. Kama mnavyojua Mgodi wa Kiwira unatarajiwa kabisa kwa kuanza kuzalisha umeme, lakini kwa shughuli za uchimbaji wa Mgodi wa Kiwira sasa hivi kinachofanyika ni kukamilisha detail design na taratibu za kumpata mkandarasi. Na kwa utaratibu ambao kwenye bajeti yetu tutakayoisoma Alhamisi wiki hii tutawaeleza, taratibu za kuanza ujenzi huu zitaanza mwaka 2018 na mgodi huu utachukua takribani miaka 20 na kuendelea.