Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kemirembe Rose Julius Lwota

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA (K.n.y MHE. STANSLAUS S. MABULA) aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana inahudumia zaidi ya wakazi 300,000 wakiwemo wanaotoka Wilaya za jirani lakini haina vifaa tiba kama vile x-ray, ultrasound na kadhalika huku ikiwepo ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne mwaka 2013 lakini mpaka sasa ahadi hiyo haijatekelezwa. Je, ni lini sasa ahadi hiyo itatekelezwa na kuipatia hospitali hiyo vifaa tiba vya kutosha ili kuokoa maisha ya watu wengi wanaopoteza maisha kwa sababu ya kukosa huduma hizo?

Supplementary Question 1

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante kwa majibu ya Mheshimiwa waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tatizo kubwa la vifaa hivyo kwenye Hospitali hii ya Wilaya ya Nyamagana, na ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais ya mwaka 2013. Sasa je, ni lini vifaa hivi vitaletwa kwenye hospitali ya Wilaya ya Nyamagana?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana inahudumia wananchi zaidi ya 300,000 kwa hiyo inaelemewa na Halmashauri ya Jiji la Mwanza inafika mahala inashindwa kutoa huduma stahiki. Pamoja na hayo, Halmashauri ya Jiji imejitahidi na kuongeza jengo la wodi ya wanaume na watoto ambayo hazikuwepo. Je, Wizara inampango gani wa kutusaidia ili wodi hizi ziweze kukamilika? Ahsante

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nadhani ni mara ya pili Mheshimiwa Kemi anauliza swali la sekta ya afya katika Mkoa wa Mwanza, kwa hiyo nimpongeze sana kwa kuona kwamba suala la afya ni muhimu sana. Lakini katika suala zima la ni lini x-ray italetwa, nimesema hapa kwamba kila kitu ni budgeting na bajeti ya mwaka huu tumetenga karibuni milioni 133. Lengo kubwa ni kwamba x-ray iweze kununuliwa na iweze kufika. Jukumu letu kubwa Ofisi ya Rais - TAMISEMI ni kuhakikisha kwamba pesa hizo mwaka huu wa fedha zinapatikana ili ahadi aliyoweka Mheshimiwa Rais iweze kutimia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kujengwa kwa wodi pale, nipende kusema kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI itashirikiana na ninyi watu wa Mwanza kuhakikisha wodi ile inafanya kazi. Sambamba na hilo nipende kuwashukuru wenzetu wa Vodacom ambapo juzi kupitia vyombo vya habari nimeona wanafanya usaidizi mkubwa sana katika hospitali ya Sekou Toure pale Mwanza. Lengo letu ni kwamba wadau wanaoshiriki kama kama hivi na sisi Serikali tunasaidia kwa kiwango kikubwa kupeleka huduma za afya kwa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Kemi kwamba Serikali itaungana na watu wa Mwanza, itaungana na Bwana Mabula, Mbunge wa Nyamagana na ninyi Wabunge wa Mwanza wote kuhakikisha suala la afya katika mkoa wa Mwanza, kwa sababu ni Jiji kubwa inaimarika vizuri kutokana na population kubwa iliyokuwepo katika eneo hilo.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA (K.n.y MHE. STANSLAUS S. MABULA) aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana inahudumia zaidi ya wakazi 300,000 wakiwemo wanaotoka Wilaya za jirani lakini haina vifaa tiba kama vile x-ray, ultrasound na kadhalika huku ikiwepo ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne mwaka 2013 lakini mpaka sasa ahadi hiyo haijatekelezwa. Je, ni lini sasa ahadi hiyo itatekelezwa na kuipatia hospitali hiyo vifaa tiba vya kutosha ili kuokoa maisha ya watu wengi wanaopoteza maisha kwa sababu ya kukosa huduma hizo?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Naibu Waziri amezungumzia suala la uhaba wa bajeti lakini naomba kuuliza; Benjamin Mkapa Foundation wamejenga vituo vya afya kule mkoa wa Rukwa ambako kuna matatizo makubwa sana; kwa mfano kuna Zahanati ya Kala - Nkasi, Milepa – Sumbawanga, Ngorotwa – Kalambo pamoja na ile ya Kishapu na wamekabidhi kwa Halmashauri toka Juni 2014, lakini mpaka leo havijatumika wakati kuna matatizo makubwa sana, ni kwa nini Serikali haijaweza kuvitumia vituo hivyo?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Pamoja na majibu mazuri naomba nimsaidie Mheshimiwa Naibu Waziri mwenzangu kwamba suala hili ni kwa nini, ni kwa sababu taratibu za makabidhiano bado zinaendelea. Pindi taratibu hizo zitakapokamilika tutakabidhi majengo hayo kwa Halmashauri.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Primary Question

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA (K.n.y MHE. STANSLAUS S. MABULA) aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana inahudumia zaidi ya wakazi 300,000 wakiwemo wanaotoka Wilaya za jirani lakini haina vifaa tiba kama vile x-ray, ultrasound na kadhalika huku ikiwepo ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne mwaka 2013 lakini mpaka sasa ahadi hiyo haijatekelezwa. Je, ni lini sasa ahadi hiyo itatekelezwa na kuipatia hospitali hiyo vifaa tiba vya kutosha ili kuokoa maisha ya watu wengi wanaopoteza maisha kwa sababu ya kukosa huduma hizo?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa tatizo hili la kifaa cha x- ray katika Hospitali ya Nyamagana ambalo Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI amelijibu na sisi katika Hospitali yetu ya Wilaya ya Mkuranga linatusumbua; je, Serikali inaweza kutuhakikishia kwamba katika mgao huo wa vifaa tiba hivi hospitali ya Wilaya ya Mkuranga itakuwa ni miongoni mwa hospitali zitakazopata kifaa hiki cha x-ray ili kuwaondoa wana Mkuranga na adha ya kusafiri umbali mrefu mpaka Dar es Salaam katika Hospitali ya Temeke? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Hospitali ya Mkuranga haina x-ray, hali kadhalika na Hospitali ya Mafia na maeneo mengine yote. Lakini katika harakati zilizofanyika sasa hivi wenzetu wa Mafia angalau kupitia Mbunge Mheshimiwa Dau sasa wamepata x-ray, nadhani wiki iliyopita walinijulisha kwamba Mafia inapata x-ray.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la Mkuranga vilevile tunajua kweli hakuna. Nimuombe Mheshimiwa Mbunge tukae pamoja, kwa sababu katika bajeti ya mwaka huu nadhani haikutengwa, lakini tutakaa kwa mikakati ya pamoja tuangalie jinsi gani tutafanya kuwashirikisha wadau mbalimbali ambao katika njia moja au nyingine wanaweza kutusaidia kupata x-ray kwa sababu kifaa hiki ni muhimu sana ukiangalia au ukizingatia suala zima la ajali za pikipiki zinazotokea maeneo mbalimbali ambapo lazima mtu apimwe aangaliwe jinsi gani amepata majeruhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile nilipenda kuongezea yale majibu, kwamba vile vifaa havijafunguliwa katika hospitali nyingine. Kweli mimi nimepita maeneo mbalimbali, nilipita mpaka Bukene kwa rafiki yangu Mheshimiwa Zedi kuona center ambazo hazijafunguliwa; na tumetoa maagizo, ndiyo maana hata juzi hapa nimezungumza kwa ukali sana juu ya suala zima la Hospitali ya Singida. Lakini nimesikia, na leo nimekutana na Mbunge wa Singida amesema lile jambo limeshashughulikiwa sasa, hata vile vitanda havihami kutoka katika Hospitali ya Rufaa ya Singida.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, katika ziara zangu ambazo natarajia kuzifanya, lengo langu ni kufika katika Nyanda za Juu Kusini kuhakikisha kwamba kwa sababu tunapeleka madaktari wapya maeneo mbalimbali hizi zahanati ambazo hazijafunguliwa; ambapo tunawashukuru sana wenzetu wa Mkapa Foundation, wamefanya kazi kubwa sana; center hizi zinafunguliwa ili wananchi wapate huduma katika maeneo yao ya karibu zaidi.

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa majibu ya nyongeza kwenye maswali yote yanayohusu vifaa tiba kama x-ray hapa nchini kwamba Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaendesha mradi mkubwa wa vifaa tiba unaoitwa ORIO. Mradi huu utahusisha ununuzi wa vifaa mbalimbali vya kufanyia uchunguzi wa magonjwa kama MRI, CT Scan, x-ray, ultrasound na vifaa vingine na kuvitawanya nchi nzima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati nzuri Hospitali ya Mkuranga kwa mujibu wa kumbukumbu zangu ni mojawapo ya vituo ambavyo vitapatiwa mashine ya x-ray.