Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Jimbo la Mufindi Kusini linazungukwa na msitu wa Serikali na vijana wanaishi humo hawana ajira. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapa vibali vya kupasua mbao ili kwa kazi hiyo wajiajiri? (b) Je, Serikali haioni haja ya kuwapa vijana hao mtaji ili waanzishe viwanda vidogo vya mbao?

Supplementary Question 1

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Naibu Waziri lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, Mheshimiwa Naibu Waziri alipokuja kule Mufindi hakufika kwenye Jimbo la Mufindi Kusini kuzungumza na wananchi na ukizingatia Jimbo la Mufindi ndilo lililozungukwa na misitu sasa wananchi wanakuuliza, je, utaenda lini ili uweze kuongea na wale wadau wanaozunguka msitu ule? (Makofi)
Swali la pili, kuna makundi ya vijana wameshajiunda tayari ambao wazazi wao waliacha maeneo makubwa sana ambayo yalichukuliwa na watu wa Maliasili na vikundi hivyo Igowole kuna vijana 60, Mninga 60, Kihanga 60, Nzigi 60, Mtwango 60, Sawala 60, Kasanga 60, Mabaoni 60, Kitasengwa 60, Kiyowela 60, Nyororo 60, Kibao 60, Mkalala 60, Mbala Maziwa 60, Malangali 60, Mtambula 60, Ihowanza 60, Logolofu 60 na Luhunga 60. Hawa ni vijana waliojiunga kwenye vikundi tayari na ukitokea moto wanakimbia mbio na bodaboda kwenda kuzima moto katika msitu ule. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa viko vikundi 20 tu na wanaomba kila kikundi kipewe kibali kimoja, Mheshimiwa Naibu Waziri upo tayari mgao huu kuwapatia vibali vyao vijana?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza kuhusu ziara ile niliyoifanya na maelezo kwamba baadhi ya maeneo ambayo yanapakana na shamba la Sao Hill sikuweza kufika. Kwanza ni kweli kutokana na ratiba niliweza kufika tu kwenye baadhi ya maeneo lakini nataka nimthibitishie kwamba bado umuhimu wa kutembelea kwenye maeneo yaliyobaki uko pale pale. Jitihada za Serikali za kuweza kutekeleza Ilani ya CCM, ya kuhakikisha kwamba Hifadhi za Taifa zikiwemo hifadhi za misitu zinawanufaisha wananchi wanaoishi jiraniau wanaopakana nazo iko pale pale na kwa hiyo, napenda tu nimhakikishie na nimpe ahadi tu kwamba nitafika kwenye maeneo hayo na safari hi sitafanya kikao pale Mufindi Mjini nitakwenda kufanya kikao kule kule mashambani porini niweze kuzungumza na wanavijiji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusu vikundi alivyovitaja na idadi ya vijana ambao wako kwenye vikundi hivyo. Kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, nani vyema tukaenda kwa pamoja na Mheshimiwa Mbunge kwanza nikupe pongezi kwa kuwatetea na kuwazungumzia vijana hao na wananchi kwa ujumla katika maeneo hayo. Lakini vilevile niseme kwamba ni nia ya Serikali sasa kwamba hatutasubiri vijana wasubiri tu kunufaika na uvunaji wa mazao ya misitu kutoka kwenye misitu ya Taifa. Lakini sasa mwelekeo ni kuweza kuwafanya vijana na wenyewe waweze kumiliki mashamba yao ndio maana tunagawa mbegu kama vile ambavyo nimesema kwenye jibu la msingi miche karibu laki sita iligawiwa kwenye matukio ya pale awali.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutaendeleza utaratibu wa kuwezesha vikundi hivyo ili baadae viweze kusimama vyenyewe kwa kuwa na mashamba ya kwao ya miti. Nitoe wito na ushauri kwa Halmashauri inayohusika kuweza kuwagawia maeneo vijana hao ili waweze kupata miti, wachukue miche kutoka kwenye Wizara yangu na waweze kupanda katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu maombi yake kwamba katika maombi ya mwaka huu kuweza kuzingatia maombi ya vijana wake kwenye eneo lile ninalichukua nitalifikisha kwa wataalam. Lakini litaenda kutazamwa sambamba na maombi mengine ambayo yamekwishapokelewa kwa mujibu wa muongozo ambayo nimeutaja hapo awali.

Name

Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Jimbo la Mufindi Kusini linazungukwa na msitu wa Serikali na vijana wanaishi humo hawana ajira. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapa vibali vya kupasua mbao ili kwa kazi hiyo wajiajiri? (b) Je, Serikali haioni haja ya kuwapa vijana hao mtaji ili waanzishe viwanda vidogo vya mbao?

Supplementary Question 2

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi.
Kwa kuwa asilimia kubwa ya wanawake hapa Tanzania wako kwenye vikundi vya ujasiriamali hususani Mkoa wangu wa Iringa na changamoto kubwa ya hivi vikundi havina miradi endelevu ambayo ingekuwa msaada mkubwa sana kuwasaidia hawa akinamama kuendelea kupambana na hizi changamoto zao wanazopambana nazo kila siku.
Sasa Mheshimiwa Waziri huoni hii ni fursa kubwa pamoja na kazi nzuri ambayo mmewasaidia vijana. Huoni hii ni fursa nzuri sasa kuwasaidia akina mama wote sio tu wale wanaozunguka ule msitu bali akina mama wote wa Mkoa wa Iringa na Wilaya zote, Iringa Mjini, Iringa Vijijini, Kilolo na Mufindi ili waweze kunufaika na msitu huu? Ahsante sana.

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nakubaliana naye kabisa na huo ndiyo mwelekeo wa Serikali kuongeza ajira miongoni mwa vijana, lakini pia kuongeza ajira miongoni mwa akina mama. Sasa misitu ni eneo moja ambalo Serikali inaweza kufikia malengo yake ya kuweza kufanya vijana na akina mama wakaweza kupata ajira. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na mwelekeo wa Serikali nitoe wito kwa Halmashauri zinazohusika katika Mkoa wa Iringa, baada ya akina mama kuwa wamejiunga katika vikundi basi waweze kupewa maeneo, halafu baada ya pale kwa shughuli zile za kiutaalam na utoaji wa mbegu na pia hata usimamizi wa kutoa utaalam na kuhakikisha kwamba mashamba hayo yanastawi vizuri wataupata kutoka Wizarani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kuanzia sasa tuwe na mwelekeo wa kuhakikisha kwamba sekta ya misitu ichangie sana kwenye lengo la Serikali kuweza kutoa ajira za kutosha upande wa akina mama na kwa vijana.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Jimbo la Mufindi Kusini linazungukwa na msitu wa Serikali na vijana wanaishi humo hawana ajira. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapa vibali vya kupasua mbao ili kwa kazi hiyo wajiajiri? (b) Je, Serikali haioni haja ya kuwapa vijana hao mtaji ili waanzishe viwanda vidogo vya mbao?

Supplementary Question 3

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa Wilaya ya Lushoto ina misitu ya Shume Magamba na mingine midogo midogo na vijana walio wengi Lushoto hawana ajira, je, Serikali haioni sasaimefikia wakati wa kuwapatia vijana hao vibali ili na wao waweze kuwa na ajira?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi na kama nilivyojibu kwenye maswali ya nyongeza yaliyotangulia, ni kweli kwamba, kama Taifa sasa tunakwenda kuhakikisha kwamba tunapunguza kwa kiwango kikubwa na kwa kadri itakavyowezekana jinsi jitihada zinavyozidi kuendelea ni nia ya Serikali ikiwezekana kumaliza kabisa changamoto hii ya ajira nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, na nimesema kwamba Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia sekta zilizoko chini ya Wizara hii na sekta ya misitu ikiwa ni mojawapo tunaweza kutoa mchango mkubwa na ndio mwelekeo kwamba tunaenda kutoa mchango mkubwa wa kuweza kutoa ajira kwa ajili ya makundi mbalimbali nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kusubiri vibali kwa ajili ya kuvuna misitu ya Taifa haliwezi peke yake likawa ni suluhisho la ajira katika Taifa, isipokuwa kupitia vibali hivyo vidogo au vichache vikundi vinaweza vikapata mitaji. Lakini kutokana na vyanzo vingine vikundi hivyo baada ya kujiunga viweze kujenga uwezo wa kuwezesha kuweza kupata mikopo kutoka kwenye benki mbalimbali ili waweze kujiunga na kuweza kuanzisha mashamba yao.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na mashamba yao wenyewe wataweza kuwa na misitu ambayo itakuwa ni mikubwa, lakini pia wataweza kutokana na biashara ya misitu hata wakaanzisha viwanda vidogo vidogo vya mbao (saw mills). Kama nilivyosema kwenye majibu ya msingi na baada ya pale ajira itakuwa ni ya uhakika kwa ajili ya wao wenyewe kwenye vikundi lakini pia wanaweza kuajiri hata wengine ambao watakuwa wako jirani nao.