Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA (K.n.y MHE. MARWA R. CHACHA) aliuliza:- Kumekuwepo na vifo vyenye utata wa kisiasa lakini inapotokea mpinzani kupoteza maisha havipewi kipaumbele katika upelelezi na hatua zinazochukuliwa:- Je, Serikali inatoa tamko gani juu ya hali hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Spika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Vyama vya Upinzani vimekuwa vikileta vurugu, kutotii amri ya halali za Serikali na Jeshi la Polisi na wakati mwingine kuleta vurugu, kwa mfano, katika Jimbo langu la Ulanga kwenye kijiji cha Iputi - Nambuga walichoma nyumba sita za wananchi. Je, Serikali ina kauli gani kuhusiana na suala hili, ili kutokomeza kabisa tabia hii.
Pili, kumekuwa na Wabunge, wakileta uchochezi wa kisiasa katika maeneo yetu ya makazi. Je, Serikali ina kauli gani kuhusiana na Wabunge kama hawa?(

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba Jeshi la Polisi limekuwa likitekeleza kazi zake kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni kama ambavyo nimeeleza katika jibu la msingi. Kwa maana hiyo basi, katika kutekeleza wajibu wake huo Jeshi la Polisi halibagui mtu yoyote na lina thamini vilevile maisha ya Watanzania wote kwa mujibu wa Ibara ya 14 ya Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na limekuwa likichukua hatua stahiki mbalimbali kwa uhalifu wa aina yoyote iwe kutoka katika Vyama Vya Siasa ama raia wa kawaida.
Kwa hiyo, nilitaka nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mlinga kwamba kuna hatua mbalimbali ambazo zimechukuliwa na viongozi ambao wamekuwa wakitoka katika vyama vya siasa wakishiriki katika vitendo vya uhalifu. Mfano halisi ni katika matukio ambayo yanajitokeza sasa hivi Pemba, miongoni mwa watu ambao wameshikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuchochea vurugu Kisiwani Pemba wapo ambao walikuwa na nafasi kubwa za uongozi katika vyama vya siasa na katika chombo cha kutunga sheria.
Kwa hiyo, hiyo inadhihirisha kwamba Jeshi la Polisi halibagui mtu na atashughulikiwa mtu kwa mujibu wa matendo yake na siyo kwa mujibu wa affiliation yake ya siasa ama rangi, dini, kabila la mtu.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusiana na Wabunge kushiriki katika vitendo vya kihalifu ni kama nilivyozungumza katika swali la nyongeza la mwanzo kwamba iwe Mbunge, mwanachama wa kawaida, kiongozi wa chama cha kisiasa kitakachoamua hatua za kuchukuliwa ni matendo yake na niseme tu kwamba kwa kuwa umegusia suala la Wabunge wao wana haki zao kwa mujibu wa Sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge yanamlinda Mbunge kwa kila ambacho anakisema Bungeni lakini haimlindi Mbunge kwauhalifu wa aina yoyote wa jinai iwe ndani ya Bunge ama iwe nje ya Bunge.
Kwa hiyo, naomba nichukue nafasi hii kuwasihi sana wanasiasa hasa viongozi ikiwemo Wabunge kuwa makini sana na kauli zao na matendo yao kwani yanaweza kuchochea uvunjifu wa amani katika nchi yetu.
Lakini pia nichukue fursa hii kuwanasihi wananchi kuwa makini sana na kauli za wanasiasa ikiwemo viongozi wa siasa katika kuhakikisha kwamba wanafuata misingi ya sheria ya nchi yetu ili waweze kuepuka madhara yanayoweza kuwatokea katika maisha yao.

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu sahihi na majibu yanayokidhi. Niongezee tu kipengele kile alichosemea kuhusu Wabunge na viongozi wa vyama vya kisiasa kuwa vyanzo vya vurugu na nieleweke wazi kwamba utaratibu ambao tutautumia kuanzia sasa kwa kupima kwamba kila kiongozi anawajibu wa kuhimiza amani katika Taifa hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, ikitokea uchochezi wa aina yoyote ambao na kiongozi yupo tutashughulika na kiongozi aliyewapeleka watu wengine kwenda kwenye matatizo hayo. Kwa sababu mara nyingi viongozi wamekuwa wakiwatanguliza watu wengine na kupata madhara kwa sababu wao hawaguswi na madhara yale. Kwa hiyo, tutakachofanya na nitaaambia vijana wangu kwamba kunapotokea na uchochezi hangaikeni na mzizi wa tatizo ambaye ni kiongozi aliyesababisha watu waende katika matatizo hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nisema kwamba watanzania pamoja na hao ambao hawajasoma vitabu vya historia vinavyoelezea udikteta ni nini wasichanganye udikteta na msimamo wa kusimamia sheria. Mimi niwape taarifa tu kama hawawajui madikteta niwape kwa taarifa zao dikteta huwa hatoi fursa hata ya kuambiwa wewe ni dikteta, huwezi ukamsema mtu wewe ni dikteta na ukaendelea kutembea kwenye disco upo, kwenye unywaji upo, kwenye sherehe upo, yaani kile kitendo kwanza cha kupewa fursa za aina zote zile zinaonyesha kwamba nchi yetu inafuata utawala wa sheria na demokrasia. Wale waliozoea maisha ya deal deal wanatakiwa tu waachane na mambo ya deal deal na wafuate sheria na wataishi kwa usalama.

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri na Mheshimiwa Waziri napenda kuongezea kama Waziri ninayesimamia utawala wa sheria (rule of law) nchi hii kwamba kimsingi swali hili halikutakiwa hata kuwemo kwenye Order Paper kwa kuwa linakiuka masharti ya Kanuni ya 40 ya Kanuni zetu za Kudumu.
Kanuni ya 40 inasema; “Swali lolote la Bunge halitaruhusiwa kuulizwa Bungeni kama (d), limekusudiwa kupata maoni ya kisheria ya kinadharia au kutoa mapendekezo juu ya jambo la kubahatisha tu.”
Mheshimiwa Naibu Spika, hapa ukilisoma hili swali la msingi ni nadharia tupu na hoja zakubahatisha, linasema kumekuwepo na vifo vyenye utata wa kisiasa, vifo vipi hivyo vilivyothibitishwa kitaalamu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nilieleze Bunge lako Tukufu kifo kikitokea, vijana wetu wa polisi wakishirikiana na mamlaka nyingine kama Mkurugenzi wa Mashtaka wanatumia muda mrefu kufikiri hiki kifo kimetokana na nini, wanatafuta ile blameworthy state of mind au unavyopeleka mahakamani kinachotafutwa ni malice aforethought sio tu unakaa kwenye jukwaa unasema hii ni siasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, (b) inasema; linatokana na habari za kubahatisha tu, linasema inapotokea mpinzani kupoteza maisha suala halipewi kipaumbele. Ushahidi upo wapi tuletee huo ushahidi hapa sisi kama Serikali tutajibu, lakini sio maswali generalized, yanaleta tu hisia mbovu katika jamii ya Watanzania.
(f) inasema linaulizwa kwa njia inayoonyesha jibu lake au kutambulisha mkondo fulani wa maoni na hapa unaona bayana mkondo fulani wa maoni. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka kusisitiza tu kwamba Watanzania siasa zisitufikishe huko; kibaka anakamatwa tunaanza kukimbilia kwenda mfukoni ana kitambulisho cha CHADEMA au cha CCM, hatutajenga Taifa hili kwa njia hiyo, ahsante.

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA (K.n.y MHE. MARWA R. CHACHA) aliuliza:- Kumekuwepo na vifo vyenye utata wa kisiasa lakini inapotokea mpinzani kupoteza maisha havipewi kipaumbele katika upelelezi na hatua zinazochukuliwa:- Je, Serikali inatoa tamko gani juu ya hali hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. KANGI. A. LUGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.
Kwa mujibu wa Ibara ya 14 ya Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kila raia wa nchi hii anayo haki ya kuishi na katika Ibara hiyo haikuainisha haki ya kuishi kwa kutumia vigezo vya itikadi za vyama, wala kigezo cha ukabila, wala kigezo cha udini, wala kigezo cha umri.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatoa kauli gani kwa Watanzania na hata Wabunge ambao wamekuwa na tabia ya kuhusisha kila vifo vinavyotokea na masuala ya itikadi za kisiasa ili liwe fundisho kwa wananchi wenye tabia hiyo kwa sababu maswali kama hayo yanaleta uchochezi na yanaweza yakasababisha maafa na hata uhasama wa kudumu kati ya koo ambazo yule mwananchi amekufa? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake zuri na niseme kitu hiki na Watanzania wasikie na wapokee.
Moja, Mtanzania hawi na madaraja kutokana na chama chake, dini yake ama kabila lake. Hakuna nusu Mtanzania kwa sababu ya chama alichonacho na hakuna Mtanzania daraja la pili kutokana na chama alichonacho. Watanzania wote ni Watanzania daraja la juu na wana haki sawa za kuishi na viongozi wanaowagawa Watanzania na kuwatengenezea chuki hata wakadhuriana kwa misingi ya kisiasa wanapaswa kupuuzwa na ndio maana sisi tukiona kiongozi anayefanya vitu vya aina hiyo tunachukua hatua.
Kwa hiyo, wao kwa watanzania maeneo popote pale walipo wasije wakagawanywa kwenye misingi hiyo na niliwahi kuisema eneo moja na ninarudia tena wasije wakaenda kwenye kuuana kwa misingi ya vyama ile hali sisi ambao tunakuwa viongozi huku na wakati mwingine tunawasukuma kufanya hivyo tukija huku wakishatuchagua tunagongesha glass za juice marazote tunapoonana hapa ili hali wao kule wameshasababisha yatima, wajane na kusababisha matatizo katika familia. Kwa maana hiyo nitoe rai kwa Watanzania na nitoe rai kwa kila mmoja wetu kuhakikisha kwamba tunalinda Utanzania wetu na undugu wetu ambao tumeachiwa na hawa waasisi wetu na ili Taifa letu liweze kupata heshma inayolinda utu.

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA (K.n.y MHE. MARWA R. CHACHA) aliuliza:- Kumekuwepo na vifo vyenye utata wa kisiasa lakini inapotokea mpinzani kupoteza maisha havipewi kipaumbele katika upelelezi na hatua zinazochukuliwa:- Je, Serikali inatoa tamko gani juu ya hali hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. ANGELINA A. MALEMBEKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi nilikuwa naomba kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-
Kwa kuwa Jeshi la Polisi pamoja na kazi nyingine kazi yake kubwa ni kulinda mali na raia, nilitaka kufahamu kuna ukweli gani kuhusiana na raia kupigwa na polisi huko Pemba? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Niabu Spika, sio kweli kwamba polisi wamekuwa wakipiga raia huko Pemba na ninaomba nichukue fursa hii mbele ya Bunge lako Tukufu kutoa mfano halisi ambao ulijitokeza siku za hivi karibuni kule Pemba kwa kitendo cha maigizo na usaniii kilichofanywa na watu kutoka chama cha upinzani cha kisiasa kwa makusudi kabisa ili kupotosha jamii na dunia kwa ujumla wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati polisi imefanya kazi yake ya kuwakamata wahalifu ambao wanafanya vitendo vya uhalifu Pemba kuna mhalifu mmoja alijifanya kwamba amekufa na amepigwa na baada ya kuhojiwa na polisi alikimbia na kukamatwa, mtu ambaye amekufa anawezaje kukimbia.
Kwa hiyo, huo ni ushahidi wa usanii ambao unafanywa kwa kulipaka matope jeshi la polisi. Naomba dunia na Watanzania watambue kwamba polisi hata siku moja hawezi kufanya kazi kinyume na sheria, maadili yake na weledi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kauli hiyo sio kweli kinachofanyika ni kwamba kuna raia ambao wamefanya vurugu za makusudi na polisi inachukua jitihada za kuwakamata na kupeleleza na baadae kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nimalizie tukwa kuendelea kutoa wito kwamba tuendelee kuhakikisha kwamba tunalinda amani ya nchi yetu lakini vilevile tusitumie kauli ama vitendo vilivyokuwa sio vya kweli kulipaka matope Jeshi la Polisi na kuipaka matope nchi yetu mbele ya Watanzania na mbele ya Jumuiya za Kimataifa.