Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amina Nassoro Makilagi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA NASSORO MAKILAGI aliuliza:- (a) Je, Viwanda vinavyozalisha nguo aina ya khanga vipimio vyake na ubora wake vinafaa kwa matumizi ya wanawake wa Kitanzania? (b) Je, upande wa khanga kwa kila kiwanda ni mita ngapi? (c) Je, malighafi gani inayotumiwa kuzalisha khanga kati ya pamba, uzi wa katani, uzi wa nailoni, au uzi wa sufi?

Supplementary Question 1

MHE. AMINA NASSORO MAKILAGI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa khanga hii ni vazi ambalo mwanamke wa Kitanzania analivaa akiwa nyumbani, ni vazi ambalo analivaa akiwa shambani analima, ni vazi ambalo analivaa anapokuwa kwenye shughuli za kijamii kwenye misiba na kwenye shughuli za harusi, ni vazi ambalo mama anakuwa nalo hata anapokwenda leba. Ni vazi ambalo linampokea mtoto hata anapotoka leba. Ni vazi rasmi la Mwanamke wa Kitanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, kanga ambazo zinatengenezwa katika viwanda vyetu vya Tanzania kwa kiwango kikubwa hazikidhi mahitaji ya wanawake wa Tanzania na hasa kwa kuzingatia kwamba vipimo vinavyotumika na ukilinganisha upana na viwango walivyonavyo wanawake wa Tanzania. Wanawake wa Tanzania wanaishi kwa amani na utulivu wako sawa katika afya zao, kanga wanazozivaa haziwatoshi kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna baadhi ya viwanda hata hizi sentimita zilizozungumzwa hawafikii; unakuta urefu ni wa mita 100, sentimita 120 kwa kweli ukiangalia hata wewe mwenyewe haikutoshi hata kwa urefu peke yake. (Kicheko/Makofi)
Sasa swali langu la kwanza, kwa kuwa vazi hili kwa kweli ni vazi la mwanamke wa Kitanzania. Matokeo yake wanawake wameanza kuvaa kanga zinazotoka India na China, wanawake sasa wamehamia kwenye madera, jambo ambalo kwa kweli hawakuzoea, ningependa kujua sasa Serikali inamkakati gani wa kuhakikisha inaielekeza TBS (Shirika la Viwango Tanzania) ili kufuatilia vazi hili, liendane na ubora halisi wa maumbo ya wanawake wa Kitanzania na hasa kwa kuzingatia kwamba kanga hii hata ukiivaa inateleza haifungiki sasa hivi; kwa hiyo hata malighafi wanayoitumia siyo pamba. (Makofi)
Swali la pili, ningependa kujua sasa kwa sababu hili vazi la kanga limekuwa ni dogo, na wanawake wameamua kuachana nalo kwa kuwa na India. Ningependa sasa kujua Serikali ina mkakati gani kwa sababu sasa vazi la dera limekuwa likiwapendeza wakina mama na ni vazi la heshima, ina mkakati gani sasa la kuhamasisha viwanda vya hapa nchini vitengeneze dera badala ya kuwanufaisha mataifa ya mbali? Ahsante sana.

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI (K.n.y. WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Amina Makilagi, Mbunge maalum na machachari kwa akina mama kama ifuatavyo:- (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikiri kama Serikali ni kweli, kwanza nitambue viwanda tulivyonavyo hapa nchini vingi kabisa tulivirithi toka ukoloni na vichache tulivijenga miaka ya 1970 na vingine miaka ya 1980. Viwanda ambavyo tunavyovitambua kama Mwatex, Murutex, Urafiki, ni vya Nida ndiyo vimeongezeka hivi karibuni. Kwa hiyo ni kweli kabisa viwango vyake ni vya chini na hiyo ninakubali.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hatua ambazo Serikali imechukua sasa kwa kutambua mabadiliko ya maendeleo siyo mabadiliko ya uchumi tu hata makuzi ya binadamu. Kwa hiyo ninatambua size za kina mama na hata akina baba, akina baba na nyie mko wapi? Na zenyewe zinakuwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ya kwanza ambayo Serikali imechukua viwango vilivyowekwa na TBS vinavyotumika sasa kwa upande wa nguo za kanga kama nilivyosema ni urefu wa sentimita 165 na upana sentimita 116. Lakini kwa upande wa vitenge urefu wa sentimita 200 na upana wa sentimita 116; lakini ni viwango vya mwaka 2009. Kwa hiyo sasa TBS mkakati wa kwanza kabisa inafanyia maboresho viwango hivyo, akina mama sasa mkae tayari kuvaa viwango vikubwa vya nguo. Viwango vinapitiwa na vitaanza kutumika mwezi Juni, mwakani.
Kwa hiyo akina mama Mheshimiwa Mwakilagi nikupongeze sana; Mheshimiwa Naibu Spika hata wewe nadhani unaendelea kukua utavivaa mwaka 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mpango wa Pili ambao sasa Serikali inafanya, imetenga maeneo maalum kwa ajili ya viwanda vitakavyokuwa vinazalisha sasa nguo aina mbalimbali, vikiwemo vitenge vya kuvaa lakini hata ambavyo vimeshonwa, wametenga hekta 2100 kule TAMCO - Kibaha, pamoja na hekta 431 kule Kigamboni. Kwa hiyo Waheshimiwa akina mama taratibu za kiserikali zinafanyika kuwahakikishia sasa mtavaa nguo bila wasiwasi.
Kuhusiana sasa na madera ni kweli kabisa hata sisi akina baba tunashangaa, unaona akina mama wanavaa madera kila sehemu, kumbe ni kwa sababu hata nguo za kuwabana sasa siyo fashion tena. Sasa hatua za Serikali za makusudi kabisa ambazo imezichukua, sasa hivi vipo viwanda vitatu vinavyozalisha nguo za kuvaa, kiwanda cha kwanza ni cha TUKU ambacho kipo pale Mabibo, lakini viwanda vingine pamoja na Sunflag, pamoja na kile kiwanda cha Mzava karibu na maeneo ya Dar es Salaam.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mavazi aina ya madera Serikali imekaribisha wawekezaji wa Kichina na Kihindi ili waje wawashonee nguo sasa aina ya madera akina mama mnayoyataka. Kwa hiyo Serikali imeshachukua hatua asante sana Mheshimiwa.